Isaya
26 Katika siku hiyo+ wimbo huu utaimbwa+ katika nchi ya Yuda:+ “Tuna jiji lenye nguvu.+ Yeye anaweka wokovu kuwa kuta na boma.+ 2 Fungueni malango,+ ili taifa la uadilifu linaloshika mwenendo wa uaminifu liingie.+ 3 Mwelekeo ambao umetegemezwa vema utaulinda katika amani ya kudumu,+ kwa sababu huyo hufanywa akutegemee wewe.+ 4 Mtegemeeni Yehova,+ kwa nyakati zote, kwa maana katika Yah Yehova kuna Mwamba+ wa mpaka nyakati zisizo na kipimo.
5 “Kwa maana amewashusha chini wale wanaokaa juu ya kilele,+ mji ulioinuliwa.+ Yeye anaushusha, anaushusha mpaka duniani; anauleta kwenye mavumbi.+ 6 Mguu utaukanyagia chini, miguu ya mwenye kuteseka, nyayo za watu wa hali ya chini.”+
7 Pito la mwadilifu ni unyoofu.+ Kwa kuwa wewe ni mnyoofu, utaifanya njia ya mwadilifu kuwa laini.+ 8 Ndiyo, kwa ajili ya njia ya hukumu zako, Ee Yehova, tumekutumaini wewe.+ Tamaa ya nafsi imekuwa kwa ajili ya jina lako na kwa ajili ya ukumbusho wako.+ 9 Nimekutamani wewe kwa nafsi yangu usiku;+ ndiyo, ninaendelea kukutafuta kwa roho yangu ndani yangu;+ kwa sababu, wakati kunapokuwa na hukumu kutoka kwako kwa ajili ya dunia,+ wakaaji wa nchi yenye kuzaa hakika watajifunza uadilifu.+ 10 Hata mwovu akionyeshwa kibali, yeye hatajifunza uadilifu.+ Atatenda isivyo haki katika nchi ya unyoofu,+ naye hatauona ukuu wa Yehova.+
11 Ee Yehova, mkono wako umeinuliwa juu,+ lakini wao hawauoni.+ Wataona na kupata aibu+ kutokana na bidii kwa ajili ya watu wako. Ndiyo, moto+ kwa ajili ya adui zako utawateketeza wao. 12 Ee Yehova, utatuhukumia amani,+ kwa sababu umetenda kazi zetu zote kwa ajili yetu.+ 13 Ee Yehova Mungu wetu, mabwana wengine mbali na wewe wamekuwa wamiliki wetu.+ Ni kwa msaada wako wewe peke yako tutalitaja jina lako.+ 14 Wao wamekufa; hawataishi.+ Wakiwa ni wasiojiweza katika kifo,+ hawataamka.+ Kwa hiyo umeelekeza fikira zako ili uwaangamize na kuharibu majina yao yote.+
15 Umeliongezea hilo taifa; Ee Yehova, umeliongezea hilo taifa;+ umejitukuza mwenyewe.+ Umeieneza mbali mipaka yote ya nchi hiyo.+ 16 Ee Yehova, wakati wa taabu wamekuelekezea fikira zao;+ wametoa mnong’ono wa sala walipopata nidhamu+ yako. 17 Kama vile mwanamke mwenye mimba anapokaribia kuzaa, anavyopata maumivu, hulia akiwa katika maumivu yake ya kuzaa, ndivyo tumekuwa kwa sababu yako, Ee Yehova.+ 18 Tumepata mimba, tumekuwa na maumivu ya kuzaa;+ ni kana kwamba sisi tumezaa upepo. Hatutimizi wokovu wowote ulio halisi kuhusiana na nchi,+ wala hakuna wakaaji wowote wa nchi yenye kuzaa wanaoanguka katika kuzaliwa.+
19 “Wafu wako wataishi.+ Maiti wangu—wataamka.+ Amkeni, pigeni vigelegele kwa shangwe, enyi mnaokaa mavumbini!+ Kwa maana umande+ wako ni kama umande wa miholi,+ na dunia itawaacha hata wale wasiojiweza katika kifo waanguke katika kuzaliwa.+
20 “Nendeni, watu wangu, ingia katika vyumba vyako vya ndani, na ufunge milango nyuma yako.+ Jifiche kwa kitambo kidogo mpaka hukumu itakapopita.+ 21 Kwa maana, tazama! Yehova anakuja kutoka mahali pake ili kulitoza hesabu kosa la mkaaji wa nchi juu yake,+ na nchi hakika itafunua umwagaji wake wa damu+ wala haitawafunika tena watu wake waliouawa.”+