Sefania
Sefania
1 Neno la Yehova lililomjia Sefania mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana wa Hezekia katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni+ mfalme wa Yuda:
2 “Bila shaka nitakimaliza kila kitu kutoka katika uso wa nchi,” asema Yehova.+
3 “Nitammaliza kabisa mtu wa udongo na mnyama.+ Nitamaliza kiumbe kinachoruka cha mbinguni na samaki wa baharini,+ na vikwazo pamoja na waovu;+ nami nitamkatilia mbali mwanadamu kutoka katika uso wa nchi,”+ asema Yehova. 4 “Nami nitaunyoosha mkono wangu juu ya Yuda na wakaaji wote wa Yerusalemu,+ nami nitakatilia mbali mabaki ya Baali kutoka mahali hapa,+ jina la makuhani wa miungu ya kigeni pamoja na makuhani,+ 5 na wale wanaoliinamia jeshi la mbinguni+ juu ya madari, na wale wanaoinama,+ wakifanya viapo rasmi kwa Yehova+ na kufanya viapo rasmi kupitia kwa Malkamu;+ 6 na wale wanaorudi nyuma wasimfuate Yehova,+ ambao hawakumtafuta Yehova wala kuuliza habari kutoka kwake.”+
7 Kaa kimya mbele za Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova;+ kwa maana siku ya Yehova iko karibu,+ kwa maana Yehova ametayarisha dhabihu;+ amewatakasa+ watu wake walioalikwa.
8 “Na itatukia katika siku ya dhabihu ya Yehova kwamba nitakaza fikira kwa wakuu, na wana wa mfalme,+ na wale wote wanaovaa mavazi ya kigeni.+ 9 Nami nitakaza fikira kwa kila mtu anayepanda jukwaani siku hiyo, wale wanaojaza nyumba ya mabwana zao jeuri na udanganyifu.+ 10 Na kutatokea siku hiyo,” asema Yehova, “sauti ya kilio kutoka katika Lango la Samaki,+ na mayowe kutoka eneo la pili,+ na mshindo mkubwa kutoka vilimani.+ 11 Pigeni mayowe,+ ninyi wakaaji wa Makteshi, kwa maana watu wote walio wafanya-biashara wamenyamazishwa;+ wale wote wanaopima fedha wamekatiliwa mbali.
12 “Na itatukia wakati huo kwamba nitapekua Yerusalemu kwa uangalifu kwa kutumia taa,+ nami nitakaza fikira kwa watu wanaoganda juu ya machicha yao,+ wanaosema moyoni mwao, ‘Yehova hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.’+ 13 Na mali yao itakuwa ya kunyakuliwa na nyumba zao zitakuwa mahame yenye ukiwa.+ Nao watajenga nyumba, lakini hawatakaa humo;+ nao watapanda mashamba ya mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.+
14 “Ile siku kuu+ ya Yehova iko karibu.+ Iko karibu, nayo inaharakisha sana.+ Sauti ya siku ya Yehova ni chungu.+ Hapo mwanamume mwenye nguvu anatoa kilio.+ 15 Siku hiyo ni siku ya ghadhabu, siku ya taabu na ya maumivu makali,+ siku ya dhoruba na ya ukiwa, siku ya giza na ya weusi,+ siku ya mawingu na ya weusi mzito, 16 siku ya baragumu na ya king’ora,+ juu ya majiji yenye ngome na juu ya minara mirefu ya pembeni.+ 17 Nami nitawataabisha wanadamu, nao watatembea kama vipofu;+ kwa sababu wamemtendea Yehova dhambi.+ Na damu yao itamwagwa kama mavumbi,+ na matumbo yao kama mavi.+ 18 Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwakomboa katika siku ya ghadhabu ya Yehova;+ bali dunia yote itateketezwa kwa moto wa bidii yake,+ kwa sababu atafanya maangamizi, yenye kutisha kwelikweli, ya wakaaji wote wa dunia.”+