Luka
23 Kwa hiyo umati huo ukasimama, wote pamoja, na kumpeleka kwa Pilato.+ 2 Ndipo wakaanza kumshtaki,+ wakisema: “Tulimkuta mtu huyu akipindua+ taifa letu na kuwakataza watu wasimlipe Kaisari kodi+ na kusema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo mfalme.”+ 3 Sasa Pilato akamuuliza: “Je, wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Akamjibu, akasema: “Wewe mwenyewe unasema.”+ 4 Ndipo Pilato akawaambia wakuu wa makuhani na ule umati: “Mimi sioni uhalifu wa mtu huyu.”+ 5 Lakini wao wakaanza kusisitiza, wakisema: “Yeye huwachochea watu kwa kufundisha katika Yudea yote, hata kuanzia Galilaya mpaka hapa.” 6 Aliposikia hilo, Pilato akauliza kama mtu huyo alikuwa Mgalilaya, 7 na, baada ya kuhakikisha kwamba alikuwa wa kutoka eneo la utawala wa Herode,+ akampeleka kwa Herode, ambaye yeye mwenyewe pia alikuwa katika Yerusalemu siku hizo.
8 Herode alipomwona Yesu alishangilia sana, kwa maana kwa muda mrefu alikuwa akitaka kumwona+ kwa sababu alikuwa amesikia+ juu yake, na alikuwa akitumaini kuona ishara fulani kutoka kwake. 9 Sasa akaanza kumuuliza maswali kwa maneno mengi sana; lakini yeye hakumjibu.+ 10 Hata hivyo, wakuu wa makuhani na waandishi wakaendelea kusimama na kumshtaki kwa ukali.+ 11 Ndipo Herode pamoja na askari-jeshi wake walinzi wakamfedhehesha,+ naye akamdhihaki+ kwa kumvika vazi jangavu na kumrudisha kwa Pilato. 12 Wote wawili Herode na Pilato+ sasa wakawa marafiki siku ileile; kwa maana kabla ya hapo walikuwa na uadui kati yao wenyewe.
13 Ndipo Pilato akawaita pamoja wakuu wa makuhani na watawala na watu 14 na kuwaambia: “Mliniletea mtu huyu kama mtu anayewachochea watu waasi, na, tazameni! mimi nilimhoji mbele yenu lakini sikupata katika mtu huyu msingi+ wa mashtaka mnayoleta juu yake. 15 Kwa kweli, wala Herode hakupata, kwa maana alimrudisha kwetu; na, tazama! hajafanya lolote linalostahili kifo.+ 16 Kwa hiyo nitamwadhibu+ na kumfungua.” 17 —— 18 Lakini wakiwa pamoja na umati, wao wote wakapaaza sauti, wakisema: “Mwondolee mbali huyu,+ lakini tufungulie Baraba!”+ 19 (Huyo ni mtu aliyekuwa ametupwa gerezani kwa sababu ya uchochezi wa uasi fulani uliotukia katika jiji na kwa kuua.) 20 Tena Pilato akawapaazia sauti, kwa sababu alitaka kumfungua Yesu.+ 21 Ndipo wakaanza kupiga kelele, wakisema: “Mtundike mtini! Mtundike mtini!”+ 22 Mara ya tatu akawaambia: “Kwa nini, ni jambo gani baya alilofanya mtu huyu? Mimi sikuona jambo lolote linalostahili kifo ndani yake; kwa hiyo nitamwadhibu na kumfungua.”+ 23 Ndipo wakaanza kufanya haraka-haraka, kwa sauti zilizo kubwa, wakidai kwamba atundikwe mtini; na sauti zao zikaanza kushinda.+ 24 Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu ili dai lao litimizwe:+ 25 akamfungua+ yule mtu aliyekuwa ametupwa gerezani kwa uchochezi wa uasi na kuua na ambaye wao walikuwa wakidai, lakini akamtia Yesu mikononi mwao wamtendee wanavyopenda.+
26 Sasa walipokuwa wakimpeleka, walimshika Simoni, mzaliwa wa Kirene, akija kutoka mashambani, nao wakamtwika mti wa mateso aubebe nyuma ya Yesu.+ 27 Lakini kulikuwa na umati mkubwa wa watu na wa wanawake ambao walimfuata waliokuwa wakijipiga-piga kwa huzuni na kumwombolezea. 28 Yesu akawageukia wanawake hao na kusema: “Binti za Yerusalemu, acheni kunililia. Badala yake, jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu;+ 29 kwa sababu, tazameni! siku zinakuja ambapo watu watasema, ‘Wenye furaha ni wanawake walio tasa, na matumbo ya uzazi ambayo hayakuzaa na maziwa ambayo hayakunyonyesha!’+ 30 Ndipo watakapoanza kuiambia milima, ‘Tuangukieni!’ na vilima, ‘Tufunikeni!’+ 31 Kwa sababu ikiwa wao wanafanya mambo haya wakati mti ni mbichi, itakuwaje utakapokuwa umekauka?”+
32 Lakini watu wengine wawili, watenda-maovu, walikuwa pia wakipelekwa wakauawe pamoja naye.+ 33 Nao walipofika mahali panapoitwa Fuvu la Kichwa,+ huko wakamtundika mtini yeye na wale watenda-maovu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.+ 34 [[Lakini Yesu alikuwa akisema: “Baba, wasamehe,+ kwa maana hawajui wanalofanya.”]] Zaidi ya hayo, ili kugawa mavazi yake, wakapiga kura.+ 35 Na wale watu wakasimama wakitazama.+ Lakini wale watawala walikuwa wakicheka kwa dharau, wakisema:+ “Aliwaokoa wengine; mwacheni ajiokoe mwenyewe, ikiwa huyu ndiye Kristo wa Mungu, Yule Aliyechaguliwa.”+ 36 Hata wale askari wakamdhihaki,+ wakija karibu na kumpa divai kali+ 37 na kusema: “Ikiwa wewe ndiye mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.” 38 Kulikuwa pia na maandishi juu yake: “Huyu ndiye mfalme wa Wayahudi.”+
39 Lakini mmoja wa wale watenda-maovu waliotundikwa akaanza kumwambia kwa maneno ya matusi:+ “Wewe ndiye Kristo, sivyo? Jiokoe mwenyewe na sisi.” 40 Yule mwingine akamjibu, akamkemea na kusema: “Je, wewe humwogopi Mungu hata kidogo, kwa kuwa sasa umo katika hukumu ileile?+ 41 Nasi, kwa kweli, tuko hivyo kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kwa ukamili kile tunachostahili kwa mambo tuliyofanya; lakini mtu huyu hakufanya jambo lolote lisilofaa.”+ 42 Naye akaendelea kusema: “Yesu, unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”+ 43 Naye akamwambia: “Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami+ katika Paradiso.”+
44 Basi, kufikia sasa ilikuwa karibu saa sita, na hata hivyo kukawa na giza juu ya dunia yote mpaka saa tisa,+ 45 kwa sababu nuru ya jua ilikosekana; ndipo pazia+ la patakatifu likapasuka katikati.+ 46 Na Yesu akaita kwa sauti kubwa na kusema: “Baba, ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako.”+ Alipokuwa amesema jambo hilo, akakata pumzi.+ 47 Kwa sababu ya kuona lililokuwa limetukia yule ofisa-jeshi akaanza kumtukuza Mungu, akisema: “Kwa kweli mtu huyu alikuwa mwadilifu.”+ 48 Na umati wote uliokuwa umekusanyika pamoja hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoyaona mambo yaliyotukia, wakaanza kurudi, wakipiga-piga vifua vyao. 49 Zaidi ya hayo, wale wote waliojuana naye walikuwa wamesimama umbali fulani.+ Pia, wanawake, waliokuwa wamemfuata pamoja kutoka Galilaya, walikuwa wamesimama wakiona mambo haya.+
50 Na, tazama! mwanamume aliyeitwa Yosefu, ambaye alikuwa mshiriki wa Baraza, mtu mwema na mwadilifu+— 51 mtu huyu hakuwa amepiga kura katika kuunga mkono mbinu yao na tendo+—alikuwa wa kutoka Arimathea, jiji moja la Wayudea, naye alikuwa akiungojea ufalme wa Mungu;+ 52 mtu huyu alimwendea Pilato na kuomba apewe mwili wa Yesu.+ 53 Naye akaushusha+ na kuufunga katika kitani bora, naye akamlaza katika kaburi+ lililochongwa katika mwamba, ambamo hakuna mtu aliyepata kulazwa.+ 54 Sasa ilikuwa ni siku ya Matayarisho,+ na nuru ya jioni ya siku ya sabato+ ilikuwa ikikaribia. 55 Lakini wale wanawake, waliokuwa wamekuja pamoja naye kutoka Galilaya, wakafuata, wakalitazama kaburi+ na jinsi mwili wake ulivyolazwa;+ 56 nao wakarudi kutayarisha manukato na mafuta yaliyotiwa marashi.+ Lakini, bila shaka, walipumzika siku ya sabato+ kulingana na amri.