Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Wakolosai 1:1-4:18
  • Kwa Wakolosai

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Wakolosai
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Kwa Wakolosai

Kwa Wakolosai

1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu,+ na Timotheo+ ndugu yetu 2 kwa watakatifu na ndugu waaminifu katika muungano+ na Kristo walioko Kolosai:

Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.+

3 Sikuzote sisi humshukuru+ Mungu Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo tunaposali kwa ajili yenu,+ 4 kwa kuwa tulisikia juu ya imani yenu kuhusiana na Kristo Yesu na upendo mlio nao kwa watakatifu wote+ 5 kwa sababu ya tumaini+ ambalo linawekwa akiba kwa ajili yenu mbinguni.+ Tumaini hili mlilisikia hapo mbele kupitia kutangazwa kwa ile kweli ya habari njema+ 6 ambayo imejitokeza kwenu, kama inavyozaa matunda+ na kuongezeka+ katika ulimwengu+ wote kama vile inavyofanya pia katikati yenu, tangu siku mliposikia na kujua kwa usahihi fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu katika kweli.+ 7 Hivyo ndivyo mmejifunza kutoka kwa Epafra+ mtumwa mwenzetu mpendwa, aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yetu, 8 ambaye pia alitufunulia upendo+ wenu katika njia ya kiroho.

9 Hiyo ndiyo sababu sisi pia, tangu siku tuliposikia juu ya jambo hilo, hatujaacha kusali kwa ajili yenu+ na kuomba kwamba mjazwe ujuzi sahihi+ wa mapenzi yake katika hekima+ yote na utambuzi wa kiroho,+ 10 ili mtembee kwa kumstahili+ Yehova+ kwa kusudi la kumpendeza yeye kikamili mnapoendelea kuzaa matunda katika kila kazi njema+ na kuongezeka katika ujuzi sahihi+ wa Mungu, 11 mkifanywa kuwa na nguvu kwa nguvu zote kwa kadiri ya uwezo wake wenye utukufu+ ili kuvumilia+ kikamili na kuwa wenye ustahimilivu pamoja na shangwe, 12 mkimshukuru Baba aliyewafanya ninyi mfae kushiriki urithi+ wa watakatifu+ katika nuru.+

13 Yeye alitukomboa kutoka katika mamlaka+ ya giza, akatuhamisha+ na kutuingiza katika ufalme+ wa Mwana wa upendo wake,+ 14 ambaye kwa njia yake tunaachiliwa huru kupitia fidia, kusamehewa dhambi zetu.+ 15 Yeye ndiye mfano+ wa Mungu asiyeonekana,+ mzaliwa wa kwanza+ wa viumbe vyote; 16 kwa sababu kwa njia yake+ vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani, vitu vinavyoonekana na vitu visivyoonekana, hata viwe ni viti vya ufalme au utawala au serikali au mamlaka.+ Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia yeye+ na kwa ajili yake. 17 Pia, yeye ni wa kabla ya vitu vingine vyote+ na kwa njia yake vitu vingine vyote vilifanywa kuwapo,+ 18 naye ndiye kichwa cha mwili, kutaniko.+ Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,+ ili yeye awe ndiye wa kwanza+ katika vitu vyote; 19 kwa sababu Mungu aliona ni vema ujazo+ wote ukae katika yeye, 20 na kupitia yeye apatanishe+ tena kwake mwenyewe vitu vingine vyote+ kwa kufanya amani+ kupitia damu+ aliyomwaga juu ya mti wa mateso,+ hata kama ni vitu vilivyo duniani au vitu vilivyo mbinguni.

21 Kwa kweli, ninyi ambao hapo zamani mlikuwa mmetengwa,+ nanyi mlikuwa adui kwa sababu akili zenu zilikuwa zimekazwa juu ya matendo maovu,+ 22 yeye sasa amewapatanisha+ tena kwa njia ya mwili wenye nyama wa huyo kupitia kifo chake,+ ili awatoe ninyi mkiwa watakatifu na wasio na dosari+ na bila shtaka+ lolote mbele zake, 23 bora tu, bila shaka, mwendelee katika imani,+ mkiwekwa imara juu ya msingi+ na mkiwa thabiti+ na bila kuondoshwa kwenye tumaini la ile habari njema mliyoisikia,+ na ambayo ilihubiriwa+ katika uumbaji wote+ ulio chini ya mbingu. Mimi Paulo, nilikuja kuwa mhudumu wa hii habari njema.+

24 Ninashangilia sasa katika mateso yangu kwa ajili yenu,+ nami, kwa upande wangu, ninajazia kinachopungua cha dhiki+ za Kristo katika mwili wangu kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kutaniko.+ 25 Mimi nilikuja kuwa mhudumu+ wa kutaniko hili kwa kupatana na usimamizi-nyumba+ kutoka kwa Mungu niliopewa kwa faida yenu ili kulihubiri neno la Mungu kwa ukamili, 26 siri takatifu+ iliyokuwa imefichwa tangu mifumo ya mambo+ iliyopita na tangu vizazi vilivyopita. Lakini sasa imefunuliwa+ kwa watakatifu wake, 27 ambao Mungu amependezwa kuwajulisha ule utajiri wenye utukufu+ wa hii siri takatifu+ katikati ya mataifa. Ni Kristo+ katika muungano na ninyi, tumaini la utukufu wake.+ 28 Yeye ndiye tunayemtangaza,+ tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu katika hekima yote,+ ili tumtoe kila mtu akiwa kamili+ katika muungano na Kristo. 29 Kwa kusudi hili kwa kweli ninafanya kazi kwa bidii, nikijikaza+ kulingana na utendaji+ wake na ambao unafanya kazi ndani yangu kwa nguvu.+

2 Kwa maana nataka mjue jinsi nilivyo na shindano+ kubwa kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walio katika Laodikia+ na wale wote ambao hawajauona uso wangu katika mwili, 2 ili mioyo yao ifarijiwe,+ ili waunganishwe pamoja kwa upatano katika upendo+ na kufikia utajiri wote wa uhakikisho kamili wa uelewaji+ wao, kufikia ujuzi sahihi wa siri takatifu ya Mungu, yaani, Kristo.+ 3 Hazina zote za hekima na za ujuzi zimefichwa kwa uangalifu ndani yake.+ 4 Ninasema jambo hili ili mtu yeyote asiwadanganye ninyi kwa hoja zenye kushawishi.+ 5 Kwa maana ingawa sipo katika mwili, hata hivyo mimi nipo pamoja nanyi katika roho,+ nikishangilia na kuona utaratibu+ wenu mzuri na uthabiti wa imani+ yenu kumwelekea Kristo.

6 Kwa hiyo, kwa kuwa mmempokea Kristo Yesu aliye Bwana, endeleeni kutembea katika muungano+ na yeye, 7 mkiwa mmetia mizizi+ na kujengwa+ katika yeye na kuimarishwa katika imani,+ kama vile mlivyofundishwa, mkijawa kabisa na imani katika kutoa shukrani.+

8 Mjihadhari: labda kuna mtu ambaye atawachukua+ ninyi kama windo lake kupitia falsafa+ na udanganyifu mtupu+ kulingana na pokeo la wanadamu, kulingana na mambo ya msingi+ ya ulimwengu na si kulingana na Kristo; 9 kwa sababu ni katika yeye kwamba ujazo+ wote wa sifa+ ya Mungu+ hukaa kimwili. 10 Na kwa hiyo ninyi mna ujazo kwa njia yake, ambaye ni kichwa cha serikali yote na mamlaka.+ 11 Kwa uhusiano+ pamoja naye ninyi pia mlitahiriwa+ kwa tohara iliyofanywa bila mikono kwa kuuvua mwili wenye nyama,+ kwa tohara ambayo ni ya Kristo, 12 kwa maana mlizikwa pamoja naye katika ubatizo wake,+ na kwa uhusiano pamoja naye mlifufuliwa+ pia pamoja kupitia imani+ yenu katika utendaji+ wa Mungu, aliyemfufua huyo kutoka kwa wafu.+

13 Zaidi ya hilo, ingawa mlikuwa wafu katika makosa yenu na katika hali ya kutotahiriwa ya mwili wenu, Mungu aliwafanya ninyi kuwa hai pamoja naye.+ Yeye alitusamehe kwa fadhili makosa yetu yote+ 14 na kuifuta+ kabisa ile hati iliyoandikwa kwa mkono+ kutupinga, iliyokuwa na amri+ na iliyokuwa ikitupinga sisi;+ na Yeye ameiondoa njiani kwa kuipigilia misumari+ juu ya mti wa mateso.+ 15 Kwa njia ya huo, kwa kuzivua na kuziacha uchi serikali na mamlaka,+ alizionyesha hadharani zikiwa zimeshindwa,+ akiziongoza katika maandamano yenye shangwe ya ushindi.+

16 Kwa hiyo mtu yeyote asiwahukumu+ ninyi katika kula na kunywa+ au kuhusu sherehe+ au kuhusu kushika mwezi mpya+ au sabato;+ 17 kwa maana mambo hayo ni kivuli+ cha mambo yanayokuja, bali uhalisi+ ni wa Kristo.+ 18 Msiache mtu yeyote awanyang’anye+ tuzo+ mwenye kupendezwa na unyenyekevu wa kujifanya na namna ya ibada ya malaika, “akichukua msimamo juu ya” mambo ambayo ameona, akijivuna bila sababu inayofaa kutokana na hali yake ya akili ya kimwili, 19 lakini yeye hakishiki imara kile kichwa,+ yeye ambaye kutokana naye mwili wote, ukiandaliwa na kuunganishwa pamoja+ kwa upatano kwa njia ya viungo na kano zake, huendelea kukua kwa ukuzi ambao Mungu hutoa.+

20 Ikiwa mlikufa+ pamoja na Kristo kuelekea mambo ya msingi+ ya ulimwengu,+ kwa nini ninyi, kana kwamba mnaishi katika ulimwengu, mnazidi kujitiisha chini ya amri hizi:+ 21 “Usishike, wala usionje,+ wala usiguse,”+ 22 kuhusu mambo ambayo yote yamekusudiwa kuharibiwa kwa kutumiwa, kulingana na amri na mafundisho ya wanadamu?+ 23 Kwa kweli, mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima katika namna ya ibada ya kujitwika mwenyewe na unyenyekevu wa kujifanya, kuutendea mwili kwa ukali;+ lakini hayana thamani yoyote katika kuzuia kuutosheleza mwili.+

3 Hata hivyo, ikiwa mlifufuliwa+ pamoja na Kristo, endeleeni kutafuta mambo yaliyo juu,+ ambako Kristo ameketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu.+ 2 Endeleeni kukaza akili zenu juu ya mambo yaliyo juu,+ si juu ya mambo yaliyo duniani.+ 3 Kwa maana mlikufa,+ na uhai wenu+ umefichwa pamoja na Kristo katika muungano+ na Mungu. 4 Wakati Kristo, aliye uhai wetu,+ atakapofunuliwa, ndipo ninyi pia mtakapofunuliwa+ pamoja naye katika utukufu.+

5 Kwa hiyo, viueni+ viungo vya mwili+ wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono,+ tamaa yenye madhara, na kutamani,+ ambako ni ibada ya sanamu. 6 Kwa sababu ya mambo hayo ghadhabu ya Mungu inakuja.+ 7 Ninyi, pia, mlitembea wakati mmoja katika mambo hayo, mlipokuwa mkiishi katika hayo.+ 8 Lakini sasa, kwa kweli, yaondoleeni mbali mambo haya yote kutoka kwenu,+ ghadhabu, hasira, ubaya, matukano,+ na maneno machafu+ kutoka kinywani mwenu. 9 Msiwe mkiambiana uwongo.+ Uvueni utu wa zamani+ pamoja na mazoea yake, 10 na mjivike utu mpya,+ ambao kupitia ujuzi sahihi unafanywa kuwa mpya kulingana na mfano+ wa Yule aliyeuumba, 11 ambapo hakuna Mgiriki wala Myahudi, tohara wala kutotahiriwa, mgeni, Msikithe, mtumwa, mtu huru,+ bali Kristo ni kila kitu na katika vitu vyote.+

12 Basi, kama waliochaguliwa wa Mungu,+ watakatifu na wapendwa, jivikeni upendo mwororo wenye huruma,+ fadhili, unyenyekevu wa akili,+ upole,+ na ustahimilivu.+ 13 Endeleeni kuvumiliana na kusameheana kwa hiari+ ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika+ juu ya mwingine. Kama vile Yehova alivyowasamehe ninyi+ kwa hiari, nanyi fanyeni vivyo hivyo pia. 14 Lakini, zaidi ya mambo haya yote, jivikeni upendo,+ kwa maana huo ni kifungo kikamilifu+ cha muungano.

15 Pia, acheni amani+ ya Kristo itawale mioyoni mwenu,+ kwa maana ninyi, kwa kweli, mliitiwa hiyo katika mwili mmoja.+ Na mjionyeshe kuwa wenye shukrani. 16 Neno la Kristo na likae ndani yenu kwa wingi katika hekima yote.+ Endeleeni kufundishana+ na kuonyana kwa zaburi,+ sifa kwa Mungu, nyimbo za kiroho+ kwa neema, mkimwimbia Yehova+ mioyoni mwenu. 17 Na lolote lile mnalofanya kwa neno au kwa tendo,+ fanyeni kila jambo katika jina la Bwana Yesu,+ mkimshukuru+ Mungu Baba kupitia yeye.

18 Enyi wake, jitiisheni+ kwa waume zenu, kwa kuwa inafaa katika Bwana. 19 Enyi waume, endeleeni kuwapenda wake zenu+ nanyi msiwakasirikie kwa uchungu.+ 20 Enyi watoto, watiini+ wazazi wenu katika kila jambo, kwa maana hilo linapendeza vema katika Bwana. 21 Enyi akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu,+ ili wasivunjike moyo. 22 Enyi watumwa, watiini katika kila jambo wale ambao ni mabwana zenu katika maana ya kimwili,+ si kwa matendo ya utumishi wa macho, kama wenye kupendeza wanadamu,+ bali kwa unyoofu wa moyo, kwa kumwogopa Yehova.+ 23 Lolote mnalofanya, lifanyeni kwa nafsi yote+ kama kwa Yehova,+ na si kama kwa wanadamu, 24 kwa maana mnajua kwamba mtapokea kutoka kwa Yehova+ thawabu inayofaa ya urithi.+ Mtumikieni Bwana, Kristo.+ 25 Hakika yule anayetenda kosa atapokea malipo+ kwa lile kosa alilotenda, na hakuna ubaguzi wowote.+

4 Enyi mabwana, endeleeni kuwapa watumwa wenu yaliyo ya uadilifu na ya haki,+ mkijua kwamba ninyi pia mna Bwana mbinguni.+

2 Endeleeni kudumu katika sala,+ mkikaa macho katika hiyo pamoja na kutoa shukrani,+ 3 na wakati huo pia mkisali kwa ajili yetu,+ ili Mungu afungue mlango+ kwa ajili ya neno letu, ili tuseme siri takatifu+ juu ya Kristo, ambayo kwa ajili yake mimi niko katika vifungo vya gereza;+ 4 ili niifunue kama ninavyopaswa kusema.+

5 Endeleeni kutembea kwa hekima kuelekea wale walio nje,+ mkijinunulia wakati unaofaa.+ 6 Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote,+ yenye kukolezwa chumvi,+ ili mjue jinsi mnavyopaswa kumjibu+ kila mtu.

7 Tikiko+ ndugu yangu mpendwa na mhudumu mwaminifu na mtumwa mwenzangu katika Bwana, atawajulisha ninyi mambo yangu yote. 8 Namtuma yeye kwenu kusudi mjue mambo yetu na ili awafariji mioyo yenu,+ 9 pamoja na Onesimo,+ ndugu yangu mwaminifu na mpendwa, ambaye ni wa kutoka kati yenu. Watawajulisha ninyi mambo yote ya hapa.

10 Aristarko+ mateka mwenzangu anawatumia ninyi salamu zake, na pia Marko+ binamu ya Barnaba, (ambaye mlipokea amri kumhusu yeye ili mkamkaribishe+ ikiwa atakuja kwenu,) 11 na Yesu anayeitwa Yusto, hawa wakiwa ni kati ya wale waliotahiriwa. Ni hawa tu walio wafanyakazi wenzangu kwa ajili ya ufalme wa Mungu, na hawa ndio wamekuwa msaada wenye kunitia nguvu. 12 Epafra,+ ambaye ni kutoka kati yenu, mtumwa wa Kristo Yesu, anawatumia ninyi salamu zake, sikuzote akijikaza kwa ajili yenu katika sala zake, ili mwishowe msimame mkiwa kamili+ na kwa usadikisho imara katika mapenzi yote ya Mungu. 13 Kwa kweli namtolea yeye ushahidi kwamba anajitahidi sana kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walioko Laodikia+ na wale walioko Hierapoli.

14 Luka+ tabibu mpendwa anawatumia ninyi salamu zake, na pia Dema.+ 15 Wapeni salamu zangu ndugu walioko Laodikia na pia kwa Nimfa na kutaniko lililo katika nyumba yake.+ 16 Na mtakapokuwa mmesomewa barua hii, pangeni isomwe+ pia katika kutaniko la Walaodikia, nanyi pia msome ile ya kutoka Laodikia. 17 Pia, mwambieni Arkipo+ hivi: “Endelea kuangalia huduma ambayo uliikubali katika Bwana, ili uitimize.”

18 Hii hapa ni salamu yangu, ya Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe.+ Endeleeni kuvikumbuka akilini vifungo vyangu vya gereza.+ Fadhili zisizostahiliwa ziwe pamoja nanyi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki