Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Wafilipi 1:1-4:23
  • Kwa Wafilipi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Wafilipi
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Kwa Wafilipi

Kwa Wafilipi

1 Paulo na Timotheo, watumwa+ wa Kristo Yesu, kwa watakatifu wote katika muungano na Kristo Yesu walio katika Filipi,+ pamoja na waangalizi na watumishi wa huduma:+

2 Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.+

3 Namshukuru Mungu wangu sikuzote kila mara ninapowakumbuka ninyi+ 4 katika dua zangu zote kwa ajili yenu nyote,+ ninapoendelea kutoa dua yangu kwa shangwe, 5 kwa sababu ya mchango+ ambao mmeutoa kwa ajili ya habari njema tangu siku ya kwanza mpaka sasa. 6 Kwa maana nina uhakika juu ya jambo hili, kwamba yeye aliyeanza kazi njema katika ninyi ataiendeleza mpaka aikamilishe+ kufikia siku+ ya Yesu Kristo. 7 Ni sawa kabisa kwangu kufikiri hili kuwahusu ninyi nyote, kwa sababu ya mimi kuwa nanyi katika moyo wangu,+ ninyi nyote mkiwa washiriki+ pamoja nami katika fadhili zisizostahiliwa, katika vifungo vyangu vya gereza+ na katika kutetea+ na kuithibitisha kisheria+ habari njema.

8 Kwa maana Mungu ni shahidi wangu kuhusu jinsi ninavyowatamani sana ninyi nyote kwa namna ya upendo mwororo+ kama alio nao Kristo Yesu. 9 Na hili ndilo ninaloendelea kusali, kwamba upendo wenu uwe mwingi+ hata zaidi na zaidi pamoja na ujuzi sahihi+ na utambuzi kamili;+ 10 kwamba mhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi,+ ili muwe bila kasoro+ na msiwe mkiwakwaza+ wengine mpaka siku ya Kristo, 11 na mjazwe matunda ya uadilifu,+ ambayo ni kupitia Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa kwa Mungu.+

12 Basi nataka mjue, akina ndugu, kwamba mambo yangu yamegeuka na kuwa yenye kuendeleza mbele habari njema+ badala ya kuwa kinyume, 13 hivi kwamba vifungo vyangu+ vimejulikana kwa watu wote+ kwa kushirikiana na Kristo kati ya Walinzi wote wa Mfalme na wale wengine wote;+ 14 na walio wengi kati ya akina ndugu katika Bwana, wakihisi uhakika kwa sababu ya vifungo vyangu vya gereza, wanaonyesha uhodari hata zaidi kulisema neno la Mungu bila woga.+

15 Ni kweli, wengine wanamhubiri Kristo kwa wivu na kushindana,+ lakini wengine pia kwa nia njema.+ 16 Hao wa mwisho wanamtangaza Kristo kutokana na upendo, kwa maana wanajua kwamba mimi nimewekwa hapa kwa ajili ya kutetea+ habari njema; 17 lakini wale wa kwanza hufanya hivyo kutokana na ugomvi,+ si kwa kusudi safi, kwa maana wanataka kuchochea dhiki+ juu yangu katika vifungo vyangu vya gereza. 18 Nini basi? Si kitu, isipokuwa tu kwa kila njia, kama ni kwa unafiki+ au ni kwa kweli, Kristo anatangazwa,+ nami nashangilia katika jambo hilo. Kwa kweli, nitaendelea pia kushangilia, 19 kwa maana najua hilo litatokeza wokovu wangu kupitia dua+ yenu na gawio la roho ya Yesu Kristo,+ 20 kwa kupatana na tarajio langu lenye hamu+ na tumaini+ kwamba sitaona aibu+ kwa njia yoyote, bali kwamba katika uhuru wote wa kusema,+ Kristo, kama sikuzote hapo mwanzoni, atatukuzwa hivyo sasa kwa njia ya mwili wangu,+ iwe ni kupitia uzima au ni kupitia kifo.+

21 Kwa maana kwa habari yangu kuishi ni Kristo,+ na kufa+ ni faida. 22 Basi ikiwa ni kuendelea kuishi katika mwili, hilo ni tunda la kazi yangu+—na bado jambo la kuchagua silifanyi lijulikane. 23 Niko chini ya mkazo kutokana na mambo haya mawili;+ lakini kile ninachotamani ni kule kufunguliwa na kule kuwa pamoja na Kristo,+ kwa maana hili, kwa hakika, ni bora zaidi.+ 24 Hata hivyo, mimi kubaki katika mwili ni lazima zaidi kwa sababu yenu.+ 25 Kwa hiyo, nikiwa na uhakika juu ya hili, najua nitabaki+ nami nitakaa pamoja na ninyi nyote kwa ajili ya ninyi kuendelea mbele+ na shangwe ya imani yenu, 26 ili furaha yenu ifurike katika Kristo Yesu kwa sababu yangu kupitia kuwapo kwangu tena pamoja nanyi.

27 Ila tu jiendesheni kwa namna inayostahili+ habari njema juu ya Kristo, ili, kama nitakuja na kuwaona ninyi au kama sitakuwapo, nisikie juu ya mambo yanayowahusu ninyi, kwamba mnasimama imara katika roho moja, kwa nafsi moja+ mkikazana pamoja kwa ajili ya imani ya habari njema, 28 nanyi msiwaogope hata kidogo wapinzani+ wenu. Jambo hili ni uthibitisho wa uharibifu kwao, lakini wa wokovu kwenu;+ na ishara hii inatokana na Mungu, 29 kwa sababu ninyi mlipewa pendeleo kwa ajili ya Kristo, si muwe tu na imani+ katika yeye, bali pia mteseke+ kwa ajili yake. 30 Kwa maana ninyi mna pambano lilelile kama mlivyoona kunihusu mimi+ na kama mnavyosikia sasa kunihusu mimi.+

2 Basi, ikiwa kuna kitia-moyo chochote katika Kristo,+ kukiwa na faraja yoyote ya upendo, kukiwa na ushirika wowote wa roho,+ kukiwa na upendo mwororo+ na huruma zozote 2 fanyeni shangwe yangu ijae kwa kuwa mna akili ileile+ na mna upendo uleule, mkiunganishwa pamoja katika nafsi, mkishika wazo moja akilini,+ 3 bila kufanya jambo lolote kwa ugomvi+ au kwa kujisifu,+ bali kwa unyenyekevu wa akili mkiwaona wengine kuwa ni bora+ kuliko ninyi, 4 mkiendelea kuangalia, si faida za kibinafsi za mambo yenu wenyewe tu,+ bali pia faida za kibinafsi za wengine.+

5 Iweni na mtazamo huu wa akili ndani yenu ambao ulikuwa pia ndani ya Kristo Yesu,+ 6 ambaye, ingawa alikuwa katika umbo la Mungu,+ hakufikiria kufanya unyakuzi, yaani, kwamba yeye awe sawa na Mungu.+ 7 Hapana, bali alijiondolea mwenyewe hali yake na kuchukua umbo la mtumwa+ na kuwa kama wanadamu.+ 8 Zaidi ya hayo, alipojikuta katika umbo la mwanadamu,+ alijinyenyekeza naye akawa mtiifu mpaka kifo,+ ndiyo, kifo juu ya mti wa mateso.+ 9 Kwa sababu hii pia Mungu alimpandisha kwenye cheo cha juu zaidi+ na kumpa kwa fadhili jina lililo juu ya kila jina lingine,+ 10 ili katika jina la Yesu kila goti lipigwe la wale walio mbinguni na wale walio duniani na wale walio chini ya nchi,+ 11 na kila ulimi ukiri+ waziwazi kwamba Yesu Kristo ni Bwana+ kwa utukufu wa Mungu Baba.+

12 Kwa hiyo, wapendwa wangu, kwa jinsi ambavyo mmekuwa mkitii sikuzote,+ si wakati wa kuwapo kwangu tu, bali kwa utayari zaidi sasa wakati wa kutokuwapo kwangu, endeleeni kuufanyia kazi wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa+ na kutetemeka; 13 kwa maana Mungu ndiye ambaye, kwa ajili ya mapenzi yake mema, anatenda ndani yenu+ ili ninyi muwe na nia na kutenda pia.+ 14 Endeleeni kufanya mambo yote bila kunung’unika+ na kubishana,+ 15 ili mje kuwa bila lawama na wasio na hatia,+ watoto+ wa Mungu wasio na dosari katikati ya kizazi kilicho kombo na kilichopotoka,+ ambao kati yao mnaangaza kama mianga katika ulimwengu,+ 16 mkiendelea kulishika sana neno la uzima,+ ili niwe na sababu ya kufurahi katika ile siku ya Kristo,+ kwamba sikukimbia bure wala kufanya kazi kwa bidii bure.+ 17 Hata hivyo, hata ikiwa ninamiminwa kama toleo la kinywaji+ juu ya dhabihu+ na utumishi wa watu wote ambako imani imewaongoza ninyi,+ mimi nafurahi na kushangilia+ pamoja nanyi nyote. 18 Basi katika njia hiyohiyo ninyi wenyewe furahini pia na kushangilia pamoja nami.+

19 Kwa upande wangu ninatumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo kwenu upesi, ili nafsi yangu ichangamke+ nitakapojua kuhusu mambo yenu. 20 Kwa maana sina mtu mwingine yeyote aliye na mwelekeo kama wake atakayejali+ kwa unyoofu mambo yenu. 21 Kwa maana wengine wote wanatafuta faida zao wenyewe,+ wala si zile za Kristo Yesu. 22 Lakini ninyi mnaujua uthibitisho alioutoa juu yake mwenyewe, kwamba kama mtoto+ na baba yake yeye alitumika pamoja nami katika kuendeleza habari njema. 23 Basi, huyu ndiye mtu ninayetumaini kumtuma mara tu nikiisha kuona jinsi mambo yalivyo kunihusu mimi. 24 Kwa kweli, nina uhakika katika Bwana kwamba mimi mwenyewe pia nitakuja upesi.+

25 Hata hivyo, naona ni lazima nimtume kwenu Epafrodito,+ ndugu yangu na mfanyakazi mwenzi+ na askari-jeshi mwenzi,+ lakini mjumbe wenu na mtumishi wa kibinafsi kwa ajili ya uhitaji wangu, 26 kwa kuwa yeye anatamani kuwaona ninyi nyote naye amehuzunika kwa sababu mlisikia alikuwa mgonjwa. 27 Ndiyo, kwa kweli, alikuwa mgonjwa karibu kufa; lakini Mungu alimwonea rehema,+ kwa kweli, hakumwonea rehema yeye peke yake, bali mimi pia, ili nisipate huzuni juu ya huzuni. 28 Kwa hiyo ninamtuma kwa haraka zaidi, ili mtakapomwona, mshangilie tena nami nipunguziwe huzuni. 29 Kwa hiyo mkaribisheni+ kama ilivyo desturi katika Bwana kwa shangwe yote; nanyi mwendelee kuwaheshimu sana watu wa namna hiyo,+ 30 kwa sababu alikaribia sana kufa kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiihatarisha nafsi+ yake, ili ajazie kikamilifu kutokuwapo kwenu hapa ili kunitolea mimi utumishi wa kibinafsi.+

3 Mwishowe, ndugu zangu, endeleeni kushangilia katika Bwana.+ Hainitaabishi mimi kuendelea kuwaandikia ninyi mambo yaleyale, bali ni usalama kwenu.

2 Mjihadhari na hao mbwa,+ mjihadhari na wale wanaotenda madhara, mjihadhari na wale wanaoukata mwili.+ 3 Kwa maana sisi ndio wenye tohara ya kweli,+ ambao tunatoa utumishi mtakatifu kwa njia ya roho+ ya Mungu nasi tunajisifu katika Kristo Yesu+ na hatuna uhakika wetu katika mwili,+ 4 ijapokuwa mimi, kama kuna mtu yeyote, nina sababu za kuwa na uhakika pia katika mwili.

Mtu mwingine yeyote akifikiri ana sababu za kuwa na uhakika katika mwili, mimi ni zaidi:+ 5 nilitahiriwa siku ya nane,+ kutoka katika ukoo wa familia ya Israeli, wa kabila la Benyamini,+ Mwebrania aliyezaliwa kwa Waebrania;+ kwa habari ya sheria, Farisayo;+ 6 kwa habari ya bidii, nikilitesa kutaniko;+ kwa habari ya uadilifu ulio kwa njia ya sheria, mtu aliyejionyesha kuwa bila lawama. 7 Lakini vitu vilivyokuwa faida kwangu, hivyo nimeviona kuwa hasara kwa sababu ya Kristo.+ 8 Kwa hiyo, kwa kweli naviona vitu vyote kuwa hasara kwa sababu ya thamani bora zaidi ya kumjua Kristo Yesu Bwana wangu.+ Kwa sababu yake nimekubali hasara ya vitu vyote nami naviona kuwa takataka nyingi,+ ili niweze kumpata Kristo 9 na nipatikane katika muungano naye, nikiwa, si na uadilifu wangu mwenyewe, ambao hutokana na sheria,+ bali ule ambao ni kupitia imani+ katika Kristo, uadilifu unaotoka kwa Mungu kwa msingi wa imani,+ 10 ili kumjua yeye na nguvu za ufufuo wake+ na kushiriki katika mateso yake,+ nikijitiisha kwenye kifo kama chake,+ 11 ili kuona kama nitaufikia kwa vyovyote ule ufufuo+ wa mapema kutoka kwa wafu.

12 Si kwamba tayari nimelipokea au tayari nimefanywa kuwa mkamilifu,+ bali ninafuatilia+ ili kuona kama pia ninaweza kulishika+ lile ambalo kwa ajili yake pia mimi nimeshikwa+ na Kristo Yesu. 13 Akina ndugu, bado mimi mwenyewe sijioni kwamba nimekwisha kulishika hilo; lakini kuna jambo moja kulihusu: Nayasahau mambo ya nyuma+ na kujinyoosha kwenda mbele kuelekea mambo yaliyo mbele,+ 14 ninafuatilia kuelekea ule mradi+ kwa ajili ya tuzo+ la mwito wa Mungu wa kwenda juu+ kwa njia ya Kristo Yesu. 15 Basi, kadiri wengi wetu walivyo wakomavu,+ na tuwe na mtazamo huu wa akili;+ na mkiwa na mwelekeo wa akili ulio tofauti na huo kwa jambo lolote, Mungu atawafunulia ninyi mtazamo huo ulio hapo juu. 16 Kwa vyovyote, kwa kadiri ambavyo tumefanya maendeleo, na tuendelee kutembea kwa utaratibu+ katika kawaida hiyohiyo.

17 Kwa muungano, iweni waigaji+ wangu, akina ndugu, na endeleeni kuwaangalia wale wanaotembea katika njia inayolingana na kielelezo ambacho sisi tuliwawekea ninyi.+ 18 Kwa maana kuna wengi, nilikuwa nikiwataja mara nyingi lakini sasa nawataja pia nikilia, wanaotembea kama adui za mti wa mateso wa Kristo,+ 19 na mwisho wao ni uharibifu,+ na mungu wao ni tumbo lao,+ na utukufu wao uko katika aibu+ yao, nao wamekaza akili zao juu ya vitu vilivyo duniani.+ 20 Lakini sisi, uraia+ wetu uko mbinguni,+ ambako kutoka huko pia tunamngojea+ mwokozi kwa hamu, Bwana Yesu Kristo,+ 21 ambaye ataufanya upya mwili wetu wa hali ya chini+ ili uwe kama mwili wake wenye utukufu+ kulingana na utendaji+ wa nguvu alizo nazo, ndiyo, kuvitiisha+ vitu vyote kwake mwenyewe.

4 Kwa hiyo, ndugu zangu wapendwa na wanaotamaniwa, shangwe yangu na taji+ langu, simameni imara+ katika njia hii katika Bwana, wapendwa.

2 Namhimiza Euodia nami namhimiza Sintike wawe na akili moja+ katika Bwana. 3 Ndiyo, nakuomba wewe pia, mwenzangu halisi katika nira,+ endelea kuwasaidia wanawake hawa ambao wamekazana pamoja nami+ katika habari njema pamoja na Klementi na vilevile wale wafanyakazi wenzangu+ wengine, ambao majina+ yao yamo katika kitabu cha uzima.+

4 Shangilieni sikuzote katika Bwana.+ Mara nyingine tena nitasema, Shangilieni!+ 5 Usawaziko wenu+ na ujulikane kwa watu wote. Bwana yuko karibu.+ 6 Msihangaike juu ya kitu chochote,+ bali katika kila jambo kwa sala na dua+ pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu;+ 7 na amani+ ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo+ yenu na nguvu zenu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.

8 Mwishowe, akina ndugu, mambo yoyote yaliyo ya kweli, mambo yoyote yaliyo ya hangaiko zito, mambo yoyote yaliyo ya uadilifu, mambo yoyote yaliyo safi kiadili,+ mambo yoyote yaliyo ya kupendeka, mambo yoyote yanayosemwa vema, wema wa adili wowote ulioko na jambo lolote la kustahili sifa lililoko, endeleeni kuyafikiria mambo hayo.+ 9 Mambo mliyojifunza na vilevile mkayapokea na kuyasikia na kuyaona kuhusiana nami, mzoee kuyafanya hayo;+ na Mungu wa amani+ atakuwa pamoja nanyi.

10 Nashangilia sana katika Bwana kwamba sasa mwishowe mmeamsha fikira zenu kwa ajili yangu,+ jambo ambalo kwa kweli mlikuwa mkilifikiria, lakini mkakosa nafasi. 11 Si kwamba ninasema kwa habari ya kuwa katika uhitaji, kwa maana nimejifunza kuwa mwenye kujitosheleza katika hali zozote nilizo nazo.+ 12 Kwa kweli najua jinsi ya kupungukiwa na vyakula,+ kwa kweli najua jinsi ya kuwa na wingi. Katika mambo yote na katika hali zote nimejifunza siri ya jinsi ya kushiba na pia jinsi ya kuwa na njaa, jinsi ya kuwa na wingi na pia jinsi ya kupatwa na uhitaji.+ 13 Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yeye anayenipa nguvu.+

14 Hata hivyo, mlitenda vema kwa kuwa washiriki+ pamoja nami katika dhiki yangu.+ 15 Kwa kweli, ninyi Wafilipi, mnajua pia kwamba mwanzoni mwa kutangaza habari njema, nilipoondoka Makedonia, hakuna kutaniko hata moja lililoshiriki pamoja nami katika jambo la kutoa na kupokea, isipokuwa ninyi peke yenu;+ 16 kwa sababu, hata katika Thesalonike, mlinitumia kitu fulani mara moja na vilevile mara ya pili kwa ajili ya uhitaji wangu. 17 Si kwamba ninatafuta hiyo zawadi+ kwa bidii, bali ninatafuta kwa bidii matunda+ yanayoleta faida zaidi kwenye hesabu yenu. 18 Hata hivyo, mimi nina vitu vyote kwa ukamili nami nina wingi. Nimejaa, kwa kuwa sasa nimepokea kutoka kwa Epafrodito+ vitu vilivyotoka kwenu, harufu tamu,+ dhabihu yenye kukubalika,+ inayompendeza Mungu vyema. 19 Naye Mungu wangu+ ataujaza kikamilifu uhitaji wenu wote+ kwa kadiri ya utajiri+ wake katika utukufu kwa njia ya Kristo Yesu. 20 Sasa kwa Mungu na Baba yetu kuwe na utukufu milele na milele.+ Amina.

21 Mpeni kila mtakatifu salamu+ zangu katika muungano+ na Kristo Yesu. Ndugu walio pamoja nami wanawatumia ninyi salamu zao. 22 Watakatifu wote, lakini hasa wale wa nyumbani mwa Kaisari, wanawatumia ninyi salamu zao.+

23 Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo ziwe pamoja na roho mnayoonyesha.+

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki