Luka
19 Naye akaingia Yeriko+ na akawa akipita. 2 Sasa kulikuwa na mwanamume anayeitwa Zakayo; naye alikuwa mkuu wa wakusanya-kodi, na alikuwa tajiri. 3 Basi, alikuwa akitafuta kuona+ Yesu huyu ni nani, lakini hangeweza kwa sababu ya umati, kwa sababu alikuwa mfupi. 4 Kwa hiyo akakimbia mbele na kupanda mforsadi-tini kusudi amwone, kwa sababu alikuwa karibu kupitia njia hiyo. 5 Sasa Yesu alipofika hapo, akatazama juu na kumwambia: “Zakayo, shuka haraka, kwa maana leo lazima nikae katika nyumba yako.” 6 Ndipo akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa shangwe. 7 Lakini walipoona hilo, wote wakaanza kunung’unika,+ wakisema: “Ameingia apate kukaa pamoja na mwanamume mtenda-dhambi.” 8 Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana: “Tazama! Nusu ya mali zangu, Bwana, mimi nitawapa maskini, na chochote nilichomnyang’anya mtu yeyote kwa shtaka la uwongo+ nitarudisha mara nne.”+ 9 Ndipo Yesu akamwambia: “Leo wokovu umekuja kwenye nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Abrahamu.+ 10 Kwa maana Mwana wa binadamu alikuja kutafuta na kuokoa kilichopotea.”+
11 Walipokuwa wakisikiliza mambo hayo akatoa mfano kwa kuongezea, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu nao walikuwa wakiwazia kwamba ufalme wa Mungu ulikuwa ukikaribia kujionyesha mara moja.+ 12 Kwa hiyo akasema: “Mtu fulani wa ukoo mashuhuri alisafiri mpaka nchi ya mbali ili ajipatie mamlaka ya kifalme kwa ajili yake mwenyewe na kurudi.+ 13 Akaita kumi kati ya watumwa wake akawapa mina kumi na kuwaambia, ‘Fanyeni biashara mpaka nije.’+ 14 Lakini raia zake wakamchukia+ na kutuma baraza la mabalozi kumfuata, na kusema, ‘Hatumtaki mtu huyu awe mfalme juu yetu.’+
15 “Mwishowe aliporudi baada ya kupata mamlaka ya kifalme aliamuru watumwa hao ambao alikuwa amewapa fedha waitwe, ili ahakikishe kile walichokuwa wamepata faida kwa biashara.+ 16 Ndipo wa kwanza akajitokeza, akisema, ‘Bwana, mina yako ilipata faida ya mina kumi.’+ 17 Kwa hiyo akamwambia, ‘Vema, mtumwa mwema! Kwa sababu katika jambo dogo sana umejionyesha mwenyewe kuwa mwaminifu, uwe na mamlaka juu ya majiji kumi.’+ 18 Sasa wa pili akaja, akisema, ‘Mina yako, Bwana, ilileta mina tano.’+ 19 Akamwambia huyu pia, ‘Wewe, pia, usimamie majiji matano.’+ 20 Lakini mwingine akaja, akisema, ‘Bwana, hii hapa mina yako, ambayo niliitunza ikiwa imehifadhiwa katika kitambaa. 21 Unaona, nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu; wewe huchukua kile ambacho hukuweka akiba nawe huvuna kile ambacho hukupanda.’+ 22 Akamwambia, ‘Ninakuhukumu kutoka kinywani mwako mwenyewe,+ mtumwa mwovu. Ulijua, sivyo, kwamba mimi ni mtu mgumu, ambaye huchukua kile ambacho sikuweka akiba na kuvuna kile ambacho sikupanda?+ 23 Kwa hiyo kwa nini hukutia fedha zangu katika mahali pa kutunzia akiba? Kisha wakati ambapo ningefika ningezichukua pamoja na faida.’+
24 “Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama kando, ‘Chukueni hiyo mina kutoka kwake mkampe yule aliye na mina kumi.’+ 25 Lakini wakamwambia, ‘Bwana, huyo ana mina kumi!’— 26 ‘Ninawaambia ninyi, Kila mtu aliye na kitu, ataongezewa; lakini yule ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.+ 27 Zaidi ya hayo, hao adui zangu ambao hawakutaka niwe mfalme juu yao waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’ ”+
28 Kwa hiyo, alipokuwa amesema hayo, akaanza kwenda, akipanda kwenda Yerusalemu.+ 29 Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima unaoitwa Mlima wa Mizeituni,+ akatuma wawili kati ya wanafunzi,+ 30 akisema: “Nendeni mkaingie katika kijiji mnachokiona mbele yenu, na ndani yake baada ya kuingia mtamkuta mwana-punda akiwa amefungwa, ambaye hakuna yeyote kati ya wanadamu ambaye amewahi kuketi juu yake. Mfungueni mkamlete.+ 31 Lakini mtu yeyote akiwauliza ninyi, ‘Kwa nini mnamfungua?’ Mwambieni hivi, ‘Bwana anamhitaji.’ ”+ 32 Kwa hiyo wale waliotumwa wakaondoka wakakuta sawa na vile alivyowaambia.+ 33 Lakini walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe wakawaambia: “Kwa nini mnamfungua huyo mwana-punda?”+ 34 Wakasema: “Bwana anamhitaji.”+ 35 Nao wakampeleka kwa Yesu, nao wakayatupa mavazi yao ya nje juu ya huyo mwana-punda na kumweka Yesu juu yake.+
36 Alipokuwa akisonga+ mbele wakawa wakitandaza mavazi yao ya nje barabarani.+ 37 Mara tu alipokaribia barabara ya kushuka Mlima wa Mizeituni umati wote wa wanafunzi wakaanza kushangilia na kumsifu Mungu kwa sauti kubwa juu ya matendo yote yenye nguvu ambayo walikuwa wameona,+ 38 na kusema: “Aliyebarikiwa ni Yule anayekuja akiwa ndiye Mfalme katika jina la Yehova!+ Amani mbinguni, na utukufu katika mahali palipoinuka juu zaidi!”+ 39 Hata hivyo, baadhi ya Mafarisayo kwenye umati wakamwambia: “Mwalimu, wakemee wanafunzi wako.”+ 40 Lakini akajibu akasema: “Ninawaambia ninyi, “Kama hawa wangekaa kimya, mawe+ yangepaaza sauti.”
41 Naye alipokaribia hapo, akalitazama jiji na kulililia,+ 42 akisema: “Kama wewe, naam, wewe, ungalikuwa umefahamu+ leo mambo yanayohusiana na amani—lakini sasa yamefichwa kutoka machoni pako.+ 43 Kwa sababu siku zitakuja juu yako wakati adui zako watakapojenga kukuzunguka ngome+ yenye miti iliyochongoka+ nao watakuzunguka+ na kukutaabisha+ kutoka kila upande, 44 nao watakuangusha chini wewe na watoto wako walio ndani yako,+ nao hawataacha jiwe juu ya jiwe+ ndani yako, kwa sababu hukufahamu wakati wa kukaguliwa kwako.”+
45 Naye akaingia katika hekalu na kuanza kuwafukuza nje wale waliokuwa wakiuza,+ 46 akiwaambia: “Imeandikwa, ‘Na nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’+ lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”+
47 Zaidi ya hayo, akawa akifundisha kila siku katika hekalu. Lakini wakuu wa makuhani na waandishi na wakuu kati ya watu walikuwa wakitafuta kumwangamiza;+ 48 na bado hawakufanikiwa, kwa maana watu wote walikuwa wakishikamana sana naye ili wamsikie.+