Isaya
33 Ole wako wewe unayepora, bila wewe mwenyewe kuporwa, na wako wewe unayetenda kwa hila, bila wengine kukutendea kwa hila!+ Mara tu utakapokuwa umemaliza kupora, wewe nawe utaporwa.+ Mara tu utakapokuwa umemaliza kutenda kwa hila, wao watakutendea kwa hila.+
2 Ee Yehova, tuonyeshe kibali.+ Tumekutumaini wewe.+ Uwe mkono+ wetu kila asubuhi,+ ndiyo, wokovu wetu wakati wa taabu.+ 3 Vikundi vya watu vimekimbia kwa sababu ya sauti ya machafuko.+ Mataifa yametawanywa wakati uliposimama.+ 4 Na nyara+ yenu kwa kweli itakusanywa kama wakati mende wanapokusanyika, kama mmiminiko wa makundi ya nzige unaomiminika juu ya mtu.+ 5 Yehova hakika atainuliwa juu,+ kwa maana yeye anakaa kileleni.+ Ataijaza Sayuni haki na uadilifu.+ 6 Na kutegemeka kwa nyakati zako kutakuwa mali ya wokovu+—hekima na ujuzi,+ kumwogopa Yehova,+ ambazo ni hazina yake.
7 Tazama! Mashujaa wao wenyewe wamepaaza kilio barabarani; wajumbe wa amani+ watalia kwa uchungu. 8 Njia kuu zimefanywa ukiwa;+ mwenye kutembea juu ya njia amekoma.+ Amelivunja agano;+ ameyadharau majiji;+ hamhesabu kuwa kitu mwanadamu anayeweza kufa.+ 9 Nchi imeomboleza, imenyauka.+ Mlima Lebanoni umefedheheshwa;+ umeoza. Sharoni+ imekuwa kama nchi tambarare ya jangwani; na Bashani na Karmeli inakung’uta majani yao.+
10 “Sasa nitasimama,”+ asema Yehova, “sasa nitajikweza;+ sasa nitajiinua juu.+ 11 Ninyi mnachukua mimba ya majani makavu;+ mtazaa majani makavu. Roho yenu wenyewe, kama moto,+ itawateketeza ninyi.+ 12 Na vikundi vya watu vitakuwa kama miteketezo ya chokaa. Watawashwa moto kama miiba iliyokatwa.+ 13 Sikieni, ninyi mlio mbali, jambo nitakalofanya!+ Na jueni, ninyi mlio karibu, nguvu zangu.+ 14 Watenda-dhambi wamekuwa na hofu katika Sayuni;+ mtetemeko umewashika waasi-imani:+ ‘Ni nani kati yetu anayeweza kukaa kwa muda na moto unaoteketeza?+ Ni nani kati yetu anayeweza kukaa kwa muda wowote pamoja na mioto inayodumu muda mrefu?’+
15 “Kuna yule anayetembea katika uadilifu+ wenye kuendelea na kusema jambo la unyoofu,+ anayekataa pato lisilo la haki kutoka kwa wapunjaji,+ anayetikisa mikono yake kabisa kukataa rushwa,+ anayeziba sikio lake lisisikilize umwagaji wa damu, na anayefunga macho yake ili yasione jambo baya.+ 16 Yeye ndiye atakayekaa juu katika vilele;+ kilele chake kilicho salama kitakuwa mahali penye miamba ambapo ni pagumu kufikiwa.+ Hakika atapewa mkate wake;+ chemchemi yake ya maji haitaisha.”+
17 Macho yako yatamwona mfalme katika uzuri wake;+ yataona nchi iliyo mbali.+ 18 Moyo wako utatoa maelezo kwa sauti za chini+ juu ya jambo lenye kuogopesha: “Mwandishi yuko wapi? Anayetoa malipo yuko wapi?+ Anayehesabu minara yuko wapi?”+ 19 Hutaona watu wenye dharau, watu wenye lugha ngumu mno kuweza kuisikiliza, wenye ulimi ulio na kigugumizi usiweze kuuelewa.+ 20 Tazama Sayuni,+ mji wa pindi zetu za sherehe!+ Macho yako mwenyewe yataliona Yerusalemu likiwa makao yasiyo na usumbufu, hema ambalo hakuna atakayelikunja.+ Vigingi vyake vya mahema havitang’olewa kamwe, wala hata kamba yake moja haitakatwa.+ 21 Lakini huko Mwenye Utukufu,+ Yehova, atakuwa kwetu mahali pa mito,+ pa mifereji mipana. Kundi lolote la merikebu halitapita juu yake, wala hakuna meli yenye utukufu itakayopita juu yake. 22 Kwa maana Yehova ni Mwamuzi+ wetu, Yehova ni Mpaji-sheria+ wetu, Yehova ni Mfalme+ wetu; yeye mwenyewe atatuokoa.+
23 Kamba zako zitalegea; hazitashika mlingoti wake usimame imara; hawakutandaza tanga.
Wakati huo nyara kwa wingi zitagawanywa; vilema nao kwa kweli watachukua nyara kubwa.+ 24 Na hakuna mkaaji atakayesema: “Mimi ni mgonjwa.”+ Watu wanaokaa katika nchi hiyo watakuwa wamesamehewa kosa lao.+