Methali
20 Divai ni mdhihaki,+ kileo husababisha msukosuko,+ na kila mtu anayepotezwa nacho hana hekima.+
2 Kuogopesha kwa mfalme ni mngurumo kama ule wa mwana-simba mwenye manyoya shingoni.+ Mtu yeyote anayejiletea hasira yake anaitendea dhambi nafsi yake mwenyewe.+
3 Ni utukufu kwa mtu kuepuka kugombana,+ lakini kila aliye mpumbavu atatumbukia humo.+
4 Kwa sababu ya majira ya baridi kali mvivu hatalima;+ atakuwa akiombaomba wakati wa mavuno, lakini hapatakuwa na chochote.+
5 Shauri moyoni mwa mtu ni kama kilindi cha maji,+ lakini mtu mwenye utambuzi ataliteka.+
6 Wanadamu wengi hutangaza fadhili zao wenyewe zenye upendo,+ lakini ni nani anayeweza kumpata mtu mwaminifu?+
7 Mwadilifu anatembea kwa utimilifu wake.+ Wanawe watakuwa na furaha baada yake.+
8 Mfalme anaketi juu ya kiti cha hukumu,+ akitawanya ubaya wote kwa macho yake.+
9 Ni nani anayeweza kusema: “Nimeusafisha moyo wangu;+ mimi nimekuwa safi kutokana na dhambi yangu”?+
10 Aina mbili za mawe ya mizani na aina mbili za vipimo vya efa+—vyote viwili ni chukizo kwa Yehova.+
11 Kwa matendo yake, mvulana hujitambulisha kama utendaji wake ni safi na mnyoofu.+
12 Sikio lenye kusikia na jicho lenye kuona—Yehova ndiye aliyevifanya vyote viwili.+
13 Usipende usingizi, usije ukaingia katika umaskini.+ Fungua macho yako; ushibe mkate.+
14 “Ni kibaya, ni kibaya!” asema mnunuzi, naye aenda zake.+ Kisha anajisifu.+
15 Kuna dhahabu, pia kuna wingi wa marijani; lakini midomo ya ujuzi ni vyombo vyenye thamani.+
16 Ikiwa mtu amemwekea mgeni dhamana, lichukue vazi lake;+ na ikiwa amejihusisha na mwanamke mgeni, chukua rehani kutoka kwake.+
17 Mkate unaopatikana kwa udanganyifu humpendeza mtu,+ lakini baadaye kinywa chake kitajaa changarawe.+
18 Kwa shauri mipango yenyewe hufanywa imara,+ na kwa mwongozo stadi endeleza vita vyako.+
19 Anayezunguka-zunguka akiwa mchongezi anafunua mazungumzo ya siri;+ wala usishirikiane na mtu anayeshawishiwa na midomo yake.+
20 Mtu yeyote anayemlaani baba yake na mama yake,+ taa yake itazimwa giza linapokaribia.+
21 Urithi hupatikana kwa pupa mwanzoni,+ lakini wakati wake ujao hautabarikiwa.+
22 Usiseme: “Nitalipiza uovu!”+ Mtumaini Yehova,+ naye atakuokoa.+
23 Aina mbili za mawe ya mizani ni chukizo kwa Yehova,+ na mizani ya kudanganya si nzuri.+
24 Hatua za mwanamume hutoka kwa Yehova.+ Naye mtu wa udongo anaweza kutambuaje njia yake?+
25 Ni mtego wakati mtu wa udongo amepaaza sauti kwa haraka, “Ni kitakatifu!”+ na baada ya kuweka nadhiri+ ndipo anaelekea kufanya uchunguzi.+
26 Mfalme mwenye hekima anawatawanya watu waovu,+ naye huzungusha gurudumu juu yao.+
27 Pumzi+ ya mtu wa udongo ni taa ya Yehova, inayochunguza kwa uangalifu sehemu zote za ndani kabisa za tumbo.+
28 Fadhili zenye upendo na ukweli—hizo humlinda mfalme;+ na kwa fadhili zenye upendo amedumisha kiti chake cha ufalme.+
29 Uzuri wa vijana ni nguvu zao,+ na utukufu wa wazee ni kichwa chao chenye mvi.+
30 Vidonda vya mapigo ndivyo huondolea mbali ubaya;+ na mapigo, sehemu za ndani kabisa za tumbo.+