ESTA
1 Katika siku za Ahasuero,* yaani, Ahasuero aliyetawala mikoa 127*+ kuanzia India mpaka Ethiopia,* 2 siku hizo Mfalme Ahasuero alipokuwa akiketi kwenye kiti chake cha ufalme katika ngome ya* Shushani,*+ 3 katika mwaka wa tatu wa utawala wake aliwafanyia karamu wakuu na watumishi wake wote. Jeshi la Uajemi+ na Umedi,+ watu mashuhuri, na wakuu wa mikoa* walikuwa mbele yake, 4 na kwa siku nyingi, siku 180, akawaonyesha utajiri wa ufalme wake wenye utukufu, na pia ukuu, heshima, na fahari yake. 5 Baada ya siku hizo kwisha, mfalme akawafanyia karamu kwa siku saba watu wote waliokuwa katika ngome ya* Shushani,* wakubwa kwa wadogo, katika bustani ya jumba la mfalme. 6 Kulikuwa na vitambaa vya kitani, pamba bora, na vitambaa vya bluu vilivyofungwa kwa kamba za kitambaa laini, sufu ya zambarau iliyofungwa kwa pete za fedha, nguzo za marumaru, na makochi ya dhahabu na fedha kwenye sakafu ya mawe mekundu, lulu, na marumaru nyeupe na nyeusi.
7 Walipewa divai katika vikombe vya* dhahabu; kila kikombe kilikuwa tofauti na vikombe vingine, na divai ya kifalme ilikuwa nyingi sana, kulingana na mali ya mfalme. 8 Walikunywa kulingana na sheria ya kwamba hakuna mtu aliyelazimishwa,* kwa maana mfalme alikuwa amepanga na maofisa wa jumba la mfalme kwamba kila mtu afanye kama alivyopenda.
9 Pia, Malkia Vashti+ akawafanyia wanawake karamu katika nyumba ya kifalme ya* Mfalme Ahasuero.
10 Siku ya saba, moyo wa mfalme ulipokuwa umechangamka kwa sababu ya divai, akawaambia Mehumani, Biztha, Harbona,+ Bigtha, Abagtha, Zethari, na Karkasi, maofisa saba wa makao ya mfalme waliokuwa wahudumu wake binafsi, 11 wamlete Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa na taji la* malkia, ili awaonyeshe watu na wakuu urembo wake, kwa maana alikuwa mrembo sana. 12 Lakini Malkia Vashti akaendelea kukataa kuja, hakutii agizo la mfalme alilopewa na maofisa wa makao ya mfalme. Basi mfalme akakasirika sana, na ghadhabu yake ikawaka.
13 Kisha mfalme akazungumza na wanaume wenye hekima waliokuwa na ujuzi kuhusu desturi* (kwa maana hivyo ndivyo habari za mfalme zilivyoletwa kwa wale wote walioifahamu sheria na kesi za kisheria, 14 na watu waliokuwa karibu zaidi na mfalme walikuwa Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena, na Memukani, wakuu saba+ wa Uajemi na Umedi, walioingia kwa mfalme na waliokuwa na vyeo vya juu zaidi katika ufalme). 15 Mfalme akauliza: “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewaje kwa sababu hajatii agizo la Mfalme Ahasuero aliloambiwa na maofisa wa makao ya mfalme?”
16 Ndipo Memukani akajibu hivi mbele ya mfalme na wakuu: “Malkia Vashti hajamkosea mfalme peke yake,+ bali pia amewakosea wakuu wote na watu wote walio katika mikoa yote ya* Mfalme Ahasuero. 17 Kwa maana jambo alilofanya malkia litajulikana kwa wanawake wote walioolewa, nao watawadharau waume zao wakisema, ‘Mfalme Ahasuero aliamuru Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini akakataa kuja.’ 18 Leo hii mabinti wa wakuu wa Uajemi na Umedi wanaojua jambo alilofanya malkia, watawaambia wakuu wote wa mfalme, na hilo litasababisha dharau na hasira nyingi. 19 Basi mfalme akipenda, na atoe amri ya kifalme itakayoandikwa katika sheria za Uajemi na Umedi, zisizoweza kubadilishwa,+ kwamba Vashti asije tena kamwe mbele ya Mfalme Ahasuero, na mfalme ampe cheo chake cha umalkia mwanamke aliye bora kuliko yeye. 20 Na amri hiyo itakaposikiwa katika milki yake yote kubwa, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mkubwa mpaka mdogo zaidi.”
21 Pendekezo hilo likamfurahisha mfalme na wakuu, naye mfalme akafanya kama alivyosema Memukani. 22 Basi akatuma barua kwa mikoa yote ya ufalme,*+ kila mkoa* kwa mwandiko wake wenyewe* na kwa kila kikundi cha watu katika lugha yao wenyewe, kwamba kila mume awe bwana mkubwa* wa nyumba yake mwenyewe na azungumze lugha ya watu wake mwenyewe.
2 Baada ya mambo hayo, hasira kali ya Mfalme Ahasuero+ ilipopungua, akakumbuka kosa la Vashti+ na uamuzi uliofanywa kumhusu.+ 2 Ndipo wahudumu binafsi wa mfalme wakasema: “Mfalme atafutiwe wasichana warembo mabikira. 3 Na mfalme ateue wajumbe katika mikoa yote ya* milki yake+ ili wawakusanye pamoja na kuwaleta wasichana wote warembo walio mabikira kwenye nyumba ya wanawake* katika ngome ya* Shushani.* Watatunzwa na Hegai+ towashi wa mfalme aliye mlinzi wa wanawake, nao watarembeshwa.* 4 Msichana atakayependwa zaidi na mfalme atakuwa malkia badala ya Vashti.”+ Na pendekezo hilo likamfurahisha mfalme, naye akafanya hivyo.
5 Kulikuwa na mwanamume fulani Myahudi aliyeishi katika ngome ya* Shushani;*+ aliitwa Mordekai+ mwana wa Yairi mwana wa Shimei mwana wa Kishi, Mbenjamini,+ 6 aliyekuwa miongoni mwa watu waliopelekwa uhamishoni kutoka Yerusalemu pamoja na Mfalme Yekonia*+ wa Yuda, ambaye Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alimpeleka uhamishoni. 7 Alikuwa mlezi* wa Hadasa,* yaani, Esta binti ya ndugu ya baba yake,+ kwa maana Esta hakuwa na baba wala mama. Msichana huyo alikuwa mrembo na mwenye umbo zuri, na baba na mama yake walipokufa, Mordekai alimchukua na kumlea kama binti yake. 8 Amri na sheria ya mfalme ilipotangazwa na wasichana wengi kukusanywa kwenye ngome ya* Shushani* chini ya utunzaji wa Hegai,+ Esta pia alipelekwa kwenye nyumba ya* mfalme chini ya utunzaji wa Hegai mlinzi wa wanawake.
9 Basi msichana huyo alimpendeza Hegai na kupata upendeleo wake,* basi Hegai akapanga mara moja arembeshwe*+ na kupewa chakula cha pekee, pia akampa wasichana saba waliochaguliwa kutoka kwa nyumba ya mfalme. Vilevile akamhamisha Esta na wale wasichana na kuwapeleka mahali bora zaidi katika nyumba hiyo ya wanawake.* 10 Esta hakusema lolote kuhusu watu wake+ wala watu wake wa ukoo, kwa maana Mordekai+ alikuwa amemwagiza asimwambie yeyote.+ 11 Siku baada ya siku Mordekai alikuwa akipita mbele ya ua wa nyumba ya wanawake* ili ajue hali ya Esta na mambo yaliyokuwa yakimpata.
12 Kila msichana alikuwa na zamu ya kwenda mbele ya Mfalme Ahasuero baada ya kurembeshwa kwa kipindi cha miezi 12 walichopangiwa wanawake, kwa maana huo ndio uliokuwa utaratibu wa kurembeshwa*—miezi sita kwa mafuta ya manemane+ na miezi sita kwa mafuta ya zeri+ na mafuta mbalimbali ya urembo.* 13 Kisha msichana angekuwa tayari kwenda mbele ya mfalme, naye alipewa chochote alichoomba alipoondoka katika nyumba ya wanawake* kwenda kwenye nyumba ya mfalme. 14 Msichana angeingia kwa mfalme jioni, na asubuhi angerudi kwenye nyumba ya pili ya wanawake* iliyosimamiwa na Shaashgazi, towashi wa mfalme,+ mlinzi wa masuria. Hangerudi kwa mfalme tena isipokuwa iwe mfalme alipendezwa naye kwa njia ya pekee na kumwita kwa jina.+
15 Ilipofika zamu yake ya kuingia kwa mfalme, Esta binti ya Abihaili ndugu ya baba ya Mordekai, aliyemchukua na kumlea kama binti yake,+ hakuomba chochote ila vitu alivyopendekeza Hegai towashi wa mfalme, aliyekuwa mlinzi wa wanawake. (Wakati wote huo kila mtu aliyemwona Esta alipendezwa naye.) 16 Esta akapelekwa kwa Mfalme Ahasuero katika nyumba yake ya kifalme mwezi wa kumi, yaani, mwezi wa Tebethi* katika mwaka wa saba+ wa utawala wake. 17 Naye mfalme akampenda Esta kuliko wale wanawake wengine wote, akapata upendeleo na kibali* machoni pa mfalme kuliko wale mabikira wengine wote. Basi akamvika taji la* malkia na kumfanya kuwa malkia+ badala ya Vashti.+ 18 Naye mfalme akaandaa karamu kubwa kwa ajili ya wakuu wake wote na watumishi wake wote, karamu ya Esta. Kisha akatangaza msamaha kwa mikoa,* naye akatoa zawadi kulingana na mali ya mfalme.
19 Sasa mabikira*+ walipokusanywa mara ya pili, Mordekai alikuwa ameketi katika lango la mfalme. 20 Esta hakusema lolote kuhusu watu wake wa ukoo na watu wa taifa lake,+ kama Mordekai alivyokuwa amemwagiza; Esta aliendelea kutii maneno ya Mordekai, kama alivyofanya alipokuwa akimlea.+
21 Siku hizo Mordekai alipokuwa akiketi katika lango la mfalme, Bigthani na Tereshi, maofisa wawili wa makao ya mfalme, walinzi wa milango, walikasirika na kupanga njama ya kumuua Mfalme Ahasuero. 22 Lakini Mordekai akajua jambo hilo, na mara moja akamwambia Malkia Esta. Naye Esta akazungumza na mfalme kwa jina la* Mordekai. 23 Basi jambo hilo likachunguzwa na mwishowe likathibitishwa, na wale wanaume wawili wakatundikwa mtini; na mambo hayo yote yakaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati mbele ya mfalme.+
3 Baada ya mambo hayo Mfalme Ahasuero alimpandisha cheo Hamani+ mwana wa Hamedatha Mwagagi+ na kumkweza juu ya wakuu wengine wote katika utawala wake.+ 2 Watumishi wote wa mfalme waliokuwa katika lango la mfalme walikuwa wakimwinamia na kumsujudia Hamani, kwa maana mfalme alikuwa ameamuru atendewe hivyo. Lakini Mordekai alikataa kumwinamia au kumsujudia. 3 Basi watumishi wa mfalme waliokuwa katika lango la mfalme wakamuuliza Mordekai: “Kwa nini unapuuza amri ya mfalme?” 4 Ingawa siku baada ya siku walimuuliza hivyo, hakuwasikiliza. Kisha wakamjulisha Hamani ili kuona kama tabia ya Mordekai ingevumiliwa;+ kwa maana Mordekai alikuwa amewaambia kwamba yeye ni Myahudi.+
5 Sasa Hamani alipoona kwamba Mordekai amekataa kumwinamia na kumsujudia, alikasirika sana.+ 6 Lakini alichukizwa na wazo la kumuua Mordekai peke yake, kwa maana alikuwa ameambiwa kuhusu watu wa Mordekai. Hivyo, Hamani akaanza kutafuta njia ya kuwaangamiza Wayahudi wote katika milki yote ya Ahasuero, watu wote wa Mordekai.
7 Katika mwezi wa kwanza, yaani, mwezi wa Nisani,* mwaka wa 12+ wa utawala wa Mfalme Ahasuero, wakapiga Puri+ (yaani, Kura) mbele ya Hamani ili kuamua siku na mwezi, nayo ikaangukia mwezi wa 12, yaani, Adari.*+ 8 Kisha Hamani akamwambia Mfalme Ahasuero: “Kuna watu fulani waliotawanyika na kusambaa kati ya watu+ katika mikoa yote ya* milki yako,+ ambao sheria zao ni tofauti na za watu wengine wote, nao hawatii sheria za mfalme, na wakiachwa watamletea mfalme hasara. 9 Mfalme akipenda, amri ya kuwaangamiza Wayahudi na iandikwe. Nitawapa maofisa talanta 10,000 za fedha* ili waziweke katika hazina ya mfalme.”*
10 Ndipo mfalme akavua pete yake ya muhuri+ kutoka mkononi mwake, akampa Hamani+ mwana wa Hamedatha Mwagagi,+ aliyekuwa adui wa Wayahudi. 11 Mfalme akamwambia Hamani: “Umepewa fedha na pia watu hao ili uwatendee upendavyo.” 12 Kisha waandishi wa mfalme+ wakaitwa siku ya 13 ya mwezi wa kwanza. Wakaandika+ maagizo yote ya Hamani kwa maliwali wa mfalme, magavana wa mikoa,* na wakuu wa vikundi mbalimbali vya watu, kila mkoa* kwa mwandiko wake wenyewe* na kila kikundi cha watu kwa lugha yao wenyewe. Maagizo hayo yaliandikwa katika jina la Mfalme Ahasuero na kutiwa muhuri kwa pete ya mfalme.+
13 Wajumbe wakapeleka kwenye mikoa yote ya* mfalme barua zilizokuwa na agizo la kuangamiza, kuua, na kuwafutilia mbali Wayahudi wote, vijana kwa wazee, wanawake kwa watoto, katika siku moja, siku ya 13 ya mwezi wa 12, yaani, mwezi wa Adari,+ na kuchukua mali zao.+ 14 Nakala ya agizo hilo ilipaswa kutolewa iwe sheria katika kila mkoa* na watu wote watangaziwe, ili wajitayarishe kwa ajili ya siku hiyo. 15 Wajumbe wakaondoka haraka+ kulingana na agizo la mfalme; sheria hiyo ilitolewa katika ngome ya* Shushani.*+ Kisha mfalme na Hamani wakaketi ili kunywa, lakini kulikuwa na hali ya wasiwasi katika jiji la Shushani.*
4 Mordekai+ alipojua mambo yote yaliyofanywa+ akayararua mavazi yake, akavaa nguo za magunia na kujimwagia majivu. Kisha akaenda katikati ya jiji, akilia kwa sauti kubwa na kwa uchungu. 2 Akaenda karibu na lango la mfalme, kwa maana hakuna mtu aliyepaswa kuingia katika lango la mfalme akiwa amevaa nguo za magunia. 3 Katika kila mkoa*+ ambako neno la mfalme na amri yake ilifika, kulikuwa na maombolezo makubwa miongoni mwa Wayahudi, pia walifunga,+ wakalia, na kuomboleza. Wengi wao walilala chini katika majivu wakiwa wamevaa nguo za magunia.+ 4 Watumishi wa kike na matowashi wa Esta walipokuja na kumwambia habari hiyo, Malkia alifadhaika sana. Akaagiza Mordekai apelekewe mavazi ili avae badala ya nguo za magunia, lakini Mordekai akayakataa. 5 Ndipo Esta akamwita Hathaki, mmoja wa matowashi wa mfalme, aliyechaguliwa na mfalme kumhudumia Esta, naye akamwagiza amuulize Mordekai maana ya jambo hilo na kilichokuwa kikiendelea.
6 Basi Hathaki akatoka na kwenda kwa Mordekai kwenye uwanja wa jiji mbele ya lango la mfalme. 7 Mordekai akamwambia yote yaliyompata na kiasi kamili cha pesa+ ambacho Hamani alikuwa ameahidi kulipa katika hazina ya mfalme ili Wayahudi waangamizwe.+ 8 Pia akampa nakala ya amri iliyoandikwa na kutolewa Shushani*+ kwamba waangamizwe. Hathaki alipaswa kumwonyesha Esta na kumfafanulia+ na kumwambia aende kwa mfalme kumwomba kibali na kumsihi moja kwa moja kwa niaba ya Wayahudi.
9 Basi Hathaki akarudi na kumwambia Esta mambo yote aliyosema Mordekai. 10 Kisha Esta akamwambia Hathaki amwambie hivi Mordekai:+ 11 “Watumishi wote wa mfalme na watu wa mikoa ya* mfalme wanajua kuna sheria moja tu kwa mwanamume au mwanamke yeyote atakayeingia katika ua wa ndani wa mfalme+ bila kuitwa: Mtu huyo anapaswa kuuawa; ataishi ikiwa tu mfalme atamnyooshea fimbo yake ya ufalme ya dhahabu.+ Nami sijaitwa kuingia kwa mfalme kwa siku 30 sasa.”
12 Mordekai alipopata ujumbe wa Esta, 13 akamjibu hivi Esta: “Usidhani kwamba kwa kuwa unaishi katika makao ya mfalme unaweza kuokoka kati ya Wayahudi wengine wote. 14 Kwa maana ukikaa kimya wakati huu, Wayahudi watapata msaada na ukombozi kutoka chanzo kingine,+ lakini wewe na nyumba ya baba yako mtaangamia. Ni nani ajuaye ikiwa umepata cheo cha umalkia kwa ajili ya wakati kama huu?”+
15 Kisha Esta akamjibu hivi Mordekai: 16 “Nenda, wakusanye Wayahudi wote walio Shushani* na mfunge+ kwa ajili yangu. Msile wala kunywa kwa siku tatu,+ usiku na mchana. Mimi pia pamoja na watumishi wangu wa kike tutafunga. Kisha nitaingia kwa mfalme, jambo ambalo ni kinyume cha sheria, na ikiwa nitaangamia, acha niangamie.” 17 Basi Mordekai akaenda zake na kufanya mambo yote ambayo Esta alimwagiza afanye.
5 Siku ya tatu+ Esta akavaa mavazi yake ya kifalme na kusimama katika ua wa ndani wa nyumba ya* mfalme, sehemu iliyotazamana na nyumba ya mfalme, naye mfalme alikuwa ameketi kwenye kiti chake cha ufalme ndani ya nyumba ya mfalme akitazama langoni. 2 Mara tu mfalme alipomwona Malkia Esta akiwa amesimama kwenye ua, akafurahi kumwona, naye mfalme akamnyooshea Esta fimbo yake ya ufalme ya dhahabu+ iliyokuwa mkononi mwake. Basi Esta akakaribia na kuigusa ncha ya fimbo hiyo.
3 Mfalme akamuuliza: “Malkia Esta, kuna nini? Niambie unachotaka. Hata ukiomba nusu ya ufalme wangu utapewa!” 4 Esta akajibu: “Mfalme akipenda na aje leo pamoja na Hamani+ kwenye karamu ambayo nimemwandalia.” 5 Basi Mfalme akawaambia watumishi wake: “Mwambieni Hamani aje haraka, kama Esta anavyoomba.” Basi, mfalme na Hamani wakaenda kwenye karamu ambayo Esta alikuwa ameandaa.
6 Karamu ya divai ilipokuwa ikiendelea, mfalme akamwambia Esta: “Una ombi gani? Utapewa utakachoomba! Na unataka nini? Hata ukiomba nusu ya ufalme wangu, utapewa!”+ 7 Esta akamjibu: “Hili ndilo ombi langu na jambo ninalotaka, 8 Ikiwa nimepata kibali chako Ee mfalme, nawe mfalme ukipenda kutimiza ombi langu na kunipa ninachotaka, naomba mfalme uje pamoja na Hamani kwenye karamu ambayo nitawaandalia kesho; na kesho nitafanya kama unavyosema mfalme.”
9 Siku hiyo Hamani aliondoka akiwa na shangwe na uchangamfu moyoni. Lakini Hamani alipomwona Mordekai katika lango la mfalme na kutambua kwamba hakusimama wala kutetemeka alipomwona, Hamani alimkasirikia sana Mordekai.+ 10 Hata hivyo, Hamani akajizuia na kwenda nyumbani kwake. Kisha akawatuma watu wawaite marafiki zake na pia Zereshi+ mke wake. 11 Hamani akajigamba kuhusu utajiri wake mwingi, wanawe wengi,+ na jinsi mfalme alivyompandisha cheo na kumkweza juu ya wakuu na watumishi wa mfalme.+
12 Hamani akaendelea kusema: “Isitoshe, Malkia Esta hakumwalika mtu mwingine yeyote isipokuwa mimi nimsindikize mfalme kwenye karamu aliyoandaa.+ Kesho pia amenialika mimi ili niwe naye pamoja na mfalme.+ 13 Lakini mambo hayo yote hayaniridhishi ninapoendelea kumwona Mordekai Myahudi akiwa ameketi kwenye lango la mfalme.” 14 Ndipo Zereshi mke wake na marafiki zake wote wakamwambia: “Agiza mti wenye kimo cha mikono 50* usimamishwe. Kisha asubuhi umwambie mfalme kwamba Mordekai anapaswa kutundikwa juu yake.+ Halafu uende na mfalme kujifurahisha kwenye karamu.” Pendekezo hilo likampendeza Hamani, kwa hiyo akaagiza mti huo usimamishwe.
6 Usiku huo mfalme hakupata usingizi.* Hivyo, akaagiza kitabu cha historia ya nyakati kiletwe,+ nacho kikasomwa mbele yake. 2 Wakapata kwamba kilikuwa kimeandikwa habari ambazo Mordekai alitoa kuhusu Bigthana na Tereshi, wale maofisa wawili wa makao ya mfalme, walinzi wa milango, waliopanga njama ya kumuua Mfalme Ahasuero.+ 3 Mfalme akauliza: “Mordekai amepewa heshima na shukrani gani kwa tendo hilo?” Ndipo watumishi binafsi wa mfalme wakasema: “Hajafanyiwa jambo lolote.”
4 Baadaye mfalme akauliza: “Ni nani aliye katika ua?” Basi Hamani alikuwa amekuja katika ua wa nje+ wa nyumba ya* mfalme ili azungumze na mfalme kuhusu kumtundika Mordekai juu ya mti aliokuwa ameutengeneza kwa ajili yake.+ 5 Watumishi wa mfalme wakamjibu: “Ni Hamani+ aliyesimama kwenye ua.” Mfalme akasema: “Mwambieni aingie.”
6 Hamani alipoingia, mfalme akamwambia: “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme angependa kumheshimu?” Hamani akajiambia moyoni: “Mfalme angependa kumheshimu nani isipokuwa mimi?”+ 7 Basi Hamani akamwambia mfalme: “Mtu ambaye mfalme angependa kumheshimu, 8 na aletewe mavazi ya kifalme+ ambayo mfalme huvaa na farasi ambaye humbeba mfalme, farasi mwenye taji la kifalme kichwani. 9 Kisha mmoja wa wakuu wa cheo cha juu wa mfalme apewe hayo mavazi na yule farasi, nao wanapaswa kumvisha mtu ambaye mfalme angependa kumheshimu, na wamtembeze katika uwanja wa jiji akiwa juu ya farasi. Kisha wanapaswa kutangaza kwa sauti mbele yake: ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme angependa kumheshimu!’”+ 10 Mara moja mfalme akamwambia Hamani: “Fanya haraka! Chukua mavazi na farasi, nawe umfanyie Mordekai kama ulivyosema, yule Myahudi anayeketi katika lango la mfalme. Usikose kumfanyia lolote kati ya mambo uliyosema.”
11 Basi Hamani akachukua mavazi hayo na farasi, akamvisha Mordekai+ na kumtembeza katika uwanja wa jiji akiwa juu ya farasi na kutangaza kwa sauti mbele yake: “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme angependa kumheshimu!” 12 Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme, lakini Hamani akaenda haraka nyumbani kwake, akiomboleza akiwa amefunika kichwa chake. 13 Hamani alipomsimulia Zereshi mke wake+ na marafiki zake wote mambo yaliyompata, watu wake wenye hekima na Zereshi mke wake wakamwambia: “Ikiwa Mordekai ambaye umeanza kuanguka mbele yake ni wa uzao wa Kiyahudi,* hutaweza kumshinda; kwa hakika utaanguka mbele yake.”
14 Walipokuwa wakizungumza naye, maofisa wa makao ya mfalme wakaja na kumchukua Hamani na kumpeleka haraka kwenye karamu ambayo Esta alikuwa ameandaa.+
7 Basi mfalme na Hamani+ wakaja kwenye karamu ya Malkia Esta. 2 Mfalme akamuuliza tena Esta siku ya pili wakati wa karamu ya divai: “Malkia Esta, una ombi gani? Utapewa unachoomba. Unataka nini? Hata ukiomba nusu ya ufalme wangu utapewa!”+ 3 Malkia Esta akajibu: “Ikiwa nimepata kibali chako, Ee mfalme, nawe mfalme ukipenda, naomba uuokoe uhai wangu,* na pia uhai wa watu wangu.+ 4 Kwa maana tumeuzwa,+ mimi na watu wangu, tuangamizwe, tuuawe, na kufutiliwa mbali.+ Kama tungeuzwa tuwe watumwa wa kiume na wa kike, ningekaa kimya. Lakini msiba huu haufai, kwa sababu utamletea mfalme hasara.”
5 Ndipo mfalme Ahasuero akamuuliza Malkia Esta: “Ni nani huyo, na yuko wapi mwanamume aliyethubutu kufanya jambo hilo?” 6 Esta akasema: “Mpinzani na adui ni huyu Hamani mwovu.”
Hamani akaogopa sana kwa sababu ya mfalme na malkia. 7 Mfalme akasimama kwa hasira na kutoka kwenye karamu ya divai, akaenda kwenye bustani ya jumba la mfalme, lakini Hamani akasimama ili kumsihi Malkia Esta auokoe uhai wake,* kwa maana alijua mfalme alikuwa ameazimia kumwadhibu. 8 Mfalme aliporudi kutoka kwenye bustani ya jumba la mfalme na kuingia katika nyumba ya karamu ya divai na kumwona Hamani akiwa amejiangusha kwenye kochi, mahali alipokuwa Esta. Mfalme akasema: “Je, sasa anataka kumbaka malkia katika nyumba yangu mwenyewe?” Mara tu maneno hayo yalipotoka kinywani mwa mfalme, wakaufunika uso wa Hamani. 9 Harbona,+ mmoja wa maofisa wa makao ya mfalme akasema: “Pia Hamani alitengeneza mti kwa ajili ya Mordekai+ aliyetoa habari iliyomwokoa mfalme.+ Mti huo wenye kimo cha mikono 50* umesimamishwa nyumbani kwa Hamani.” Ndipo mfalme akasema: “Mtundikeni juu yake.” 10 Basi wakamtundika Hamani kwenye mti aliokuwa ameutengeneza ili kumtundika Mordekai juu yake, na hasira ya mfalme ikatulia.
8 Siku hiyo Mfalme Ahasuero akampa Malkia Esta nyumba* ya Hamani+ aliyekuwa adui ya Wayahudi;+ naye Mordekai akaja mbele ya mfalme, kwa maana Esta alikuwa amemfunulia kuhusu uhusiano wao wa kifamilia.+ 2 Kisha mfalme akavua pete yake ya muhuri+ aliyokuwa amempokonya Hamani, akampa Mordekai. Naye Esta akamweka Mordekai kuwa msimamizi wa nyumba ya Hamani.+
3 Zaidi ya hayo, Esta akazungumza tena na mfalme. Akaanguka chini miguuni pake, akalia na kumsihi mfalme akomeshe madhara ya Hamani Mwagagi na njama aliyopanga dhidi ya Wayahudi.+ 4 Mfalme akamnyooshea Esta fimbo ya ufalme ya dhahabu,+ naye Esta akainuka na kusimama mbele ya mfalme. 5 Esta akasema: “Ukipenda Ee mfalme na ikiwa nimepata kibali chako, na ikiwa ni jambo jema kwako mfalme, nawe umependezwa nami, acha agizo liandikwe la kufuta barua za njama ya Hamani+ mwana wa Hamedatha Mwagagi,+ alizoandika ili kuwaangamiza Wayahudi katika mikoa yote ya* mfalme. 6 Kwa maana ninawezaje kuvumilia kuona msiba utakaowapata watu wangu, na ninawezaje kuvumilia kuona watu wangu wa ukoo wakiangamizwa?”
7 Basi Mfalme Ahasuero akamwambia Malkia Esta na Mordekai Myahudi: “Tazama! Nimempa Esta nyumba ya Hamani,+ naye Hamani ametundikwa mtini,+ kwa sababu alipanga njama ya kuwashambulia* Wayahudi. 8 Sasa andikeni katika jina la mfalme jambo lolote mnaloona linafaa kwa niaba ya Wayahudi nanyi mlitie muhuri kwa pete ya mfalme, kwa maana agizo lililoandikwa katika jina la mfalme na kutiwa muhuri kwa pete ya mfalme haliwezi kufutwa.”+
9 Ndipo waandishi wa mfalme wakaitwa wakati huo katika mwezi wa tatu, yaani, mwezi wa Sivani,* siku ya 23, wakaandika mambo yote ambayo Mordekai aliwaamuru Wayahudi, na pia maliwali,+ magavana, na wakuu wa mikoa*+ kuanzia India mpaka Ethiopia, mikoa* 127, kila mkoa* kwa mwandiko wake wenyewe* na kila kikundi cha watu kwa lugha yao wenyewe na kwa Wayahudi katika mwandiko wao wenyewe* na lugha yao.
10 Aliandika agizo hilo katika jina la Mfalme Ahasuero na kulitia muhuri kwa pete ya mfalme,+ kisha akatuma barua za agizo hilo kupitia wajumbe walioendesha farasi; farasi hao wenye mbio walitumiwa kusafirisha barua, nao walizalishwa kwa ajili ya utumishi wa mfalme. 11 Katika barua hizo mfalme aliwaruhusu Wayahudi katika majiji yote wakusanyike ili walinde uhai wao* na kuangamiza, kuua, na kuharibu jeshi lolote la taifa lolote au mkoa* ambao huenda ungewashambulia wao, kutia ndani wanawake na watoto wao, na kuchukua mali zao.+ 12 Wangefanya hivyo siku ileile katika mikoa yote ya* Mfalme Ahasuero, siku ya 13 ya mwezi wa 12, yaani, mwezi wa Adari.*+ 13 Maandishi* ya agizo hilo yalipaswa kutangazwa kuwa sheria katika mikoa yote.* Watu wote walipaswa kutangaziwa agizo hilo, ili Wayahudi wajitayarishe siku hiyo kulipiza kisasi dhidi ya maadui wao.+ 14 Wajumbe walioendesha farasi wa kusafirisha barua waliotumiwa katika utumishi wa mfalme wakaondoka haraka na kwa kasi kulingana na agizo la mfalme. Sheria hiyo ilitangazwa pia katika ngome ya* Shushani.*+
15 Naye Mordekai akatoka mbele ya mfalme akiwa amevaa mavazi ya kifalme ya rangi ya bluu na nyeupe, taji kubwa la dhahabu, na joho la kitambaa bora cha sufu ya zambarau.+ Na jiji la Shushani* likapiga kelele kwa shangwe. 16 Wayahudi wakapata kitulizo,* wakafurahi, wakashangilia, na kupata heshima. 17 Na katika mikoa yote* na majiji yote, popote ambapo agizo la mfalme na sheria yake ilifika, Wayahudi walifurahi na kushangilia, wakafanya karamu na kusherehekea. Watu wengi wa mataifa yaliyokuwa nchini walikuwa wakijitangaza kuwa Wayahudi,+ kwa maana waliwaogopa Wayahudi.
9 Siku ya 13 ya mwezi wa 12, yaani, mwezi wa Adari,*+ wakati ambapo agizo na sheria ya mfalme ilipaswa kutekelezwa,+ siku ambayo maadui wa Wayahudi walitarajia kuwashinda, mambo yaligeuka, Wayahudi wakawashinda wote waliowachukia.+ 2 Wayahudi wakakusanyika pamoja katika majiji yao kwenye mikoa yote ya* Mfalme Ahasuero+ ili kuwashambulia wale waliotaka kuwadhuru, na hakuna mtu aliyeweza kuwazuia, kwa sababu mataifa yote yaliwaogopa sana.+ 3 Na wakuu wote wa mikoa,* maliwali,+ magavana, na watu waliofanya kazi za mfalme waliwaunga mkono Wayahudi, kwa sababu walimwogopa Mordekai. 4 Sasa Mordekai alikuwa na mamlaka+ katika nyumba ya* mfalme, na umaarufu wake ulikuwa ukienea kotekote katika mikoa yote,* kwa sababu mamlaka ya Mordekai yalizidi kuongezeka.
5 Wayahudi waliwashambulia kwa upanga maadui wao wote, wakawaua na kuwaangamiza; waliwatendea walivyotaka wale waliowachukia.+ 6 Katika ngome ya* Shushani,*+ Wayahudi waliwaua na kuwaangamiza wanaume 500. 7 Pia, waliwaua Parshandatha, Dalfoni, Aspatha, 8 Poratha, Adalia, Aridatha, 9 Parmashta, Arisai, Aridai, na Vaizatha, 10 wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedatha, adui ya Wayahudi.+ Lakini baada ya kuwaua, hawakuwapora chochote.+
11 Siku hiyo, mfalme alijulishwa idadi ya watu waliouawa katika ngome ya* Shushani.*
12 Mfalme akamwambia Malkia Esta: “Katika ngome ya* Shushani* Wayahudi wamewaua watu 500 na pia wana kumi wa Hamani. Unafikiri wamewaua watu wangapi katika mikoa mingine ya* mfalme?+ Sasa una ombi gani? Utapewa unachotaka. Unataka nini kingine? Kitatimizwa.” 13 Esta akajibu: “Ukipenda Ee mfalme,+ Wayahudi walio Shushani* waruhusiwe kesho pia kutekeleza sheria ya leo;+ agiza wana kumi wa Hamani watundikwe mtini.”+ 14 Basi mfalme akaagiza jambo hilo lifanywe. Sheria ikatangazwa Shushani,* na wana kumi wa Hamani wakatundikwa.
15 Wayahudi waliokuwa Shushani* wakakusanyika pamoja tena siku ya 14 ya mwezi wa Adari+ na kuwaua watu 300 huko Shushani,* lakini hawakuwapora chochote.
16 Wayahudi wengine wote waliokuwa katika mikoa ya* mfalme, wakakusanyika pamoja pia ili kulinda uhai wao.*+ Wakawaangamiza maadui wao,+ wakawaua watu 75,000 kati ya wale waliowachukia; lakini hawakuwapora chochote. 17 Mambo hayo yalitukia siku ya 13 ya mwezi wa Adari, wakapumzika siku ya 14 ya mwezi huo na kuifanya kuwa siku ya karamu na kushangilia.
18 Wayahudi waliokuwa Shushani* wakakusanyika pamoja siku ya 13+ na ya 14,+ wakapumzika siku ya 15 na kuifanya kuwa siku ya karamu na kushangilia. 19 Ndiyo sababu Wayahudi wa mashambani walioishi katika majiji ya wilaya zilizo mbali waliifanya siku ya 14 ya mwezi wa Adari iwe siku ya karamu na kushangilia, siku ya kusherehekea,+ na siku ya kupeana mafungu ya vyakula.+
20 Mordekai+ akaandika matukio hayo kisha akatuma barua rasmi kwa Wayahudi wote waliokuwa katika mikoa yote ya* karibu na ya mbali ya Mfalme Ahasuero. 21 Akawaagiza waadhimishe siku ya 14 ya mwezi wa Adari, na pia siku ya 15, kila mwaka, 22 kwa sababu katika siku hizo Wayahudi walipumzika kutokana na usumbufu wa maadui wao, na mwezi huo huzuni yao ikageuzwa kuwa shangwe, na maombolezo yao+ kuwa siku ya kusherehekea. Walipaswa kuadhimisha siku hizo zikiwa siku za karamu na kushangilia, za kupeana mafungu ya vyakula, na za kuwapa maskini zawadi.
23 Na Wayahudi wakakubali kuendelea kufanya sherehe waliyoanzisha na kufanya mambo waliyoandikiwa na Mordekai. 24 Kwa maana Hamani+ mwana wa Hamedatha Mwagagi,+ adui ya Wayahudi wote, alikuwa amepanga njama ya kuwaangamiza Wayahudi,+ na alikuwa amepiga Puri,+ yaani, Kura, ili kuwatisha na kuwaangamiza. 25 Lakini Esta alipokuja mbele ya mfalme, mfalme alitoa agizo lililoandikwa hivi:+ “Njama yake mbaya dhidi ya Wayahudi+ na irudi juu ya kichwa chake mwenyewe”; nao wakamtundika yeye pamoja na wanawe mtini.+ 26 Ndiyo sababu waliziita siku hizo Purimu, kutokana na jina la ile Puri.*+ Kwa hiyo, kwa sababu ya mambo yote yaliyoandikwa katika barua hiyo na yale waliyoona kuhusiana na tukio hilo na mambo yaliyowapata, 27 Wayahudi pamoja na wazao wao na wote waliojiunga nao wakajitwika wajibu wa+ kusherehekea siku hizo mbili bila kukosa na kutekeleza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu siku hizo, wakati uliowekwa kila mwaka. 28 Siku hizo zilipaswa kukumbukwa na kuadhimishwa na kila kizazi, katika kila familia, kila mkoa,* na kila jiji; na Wayahudi hawakupaswa kuacha kuzikumbuka siku hizo za Purimu wala wazao wao kuacha kuziadhimisha.
29 Kisha Malkia Esta, binti ya Abihaili, na Mordekai Myahudi wakaandika kwa mamlaka kamili ili kuthibitisha barua ya pili kuhusu Purimu. 30 Mordekai akawatumia barua rasmi Wayahudi wote waliokuwa katika mikoa 127+ ya* milki ya Ahasuero,+ kwa maneno ya amani na kweli 31 ili kuthibitisha kuadhimishwa kwa siku za Purimu katika nyakati zilizowekwa, kama walivyoagizwa na Mordekai Myahudi na Malkia Esta+ na kama walivyojitwika wajibu, wao na wazao wao,+ pamoja na kufunga+ na kutoa dua.+ 32 Na amri ya Esta ilithibitisha mambo hayo kuhusu Purimu,+ nayo ikaandikwa katika kitabu.
10 Mfalme Ahasuero akaamuru watu wafanye kazi ya kulazimishwa katika nchi na katika visiwa vya bahari.
2 Na matendo yake yote makuu na yenye nguvu, na pia habari kamili kuhusu ukuu wa Mordekai+ ambao mfalme alimpa alipomkweza,+ je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati+ za wafalme wa Umedi na Uajemi?+ 3 Kwa maana Mordekai Myahudi ndiye aliyekuwa wa pili kwa cheo kutoka kwa Mfalme Ahasuero. Alikuwa mkuu* miongoni mwa Wayahudi na aliheshimiwa na ndugu zake kwa ujumla,* naye aliwasaidia watu wake na kutetea masilahi ya* wazao wao wote.
Inaaminiwa kwamba ni Shasta wa Kwanza, mwana wa Dario Mkuu (Dario Histaspisi).
Au “wilaya 127 za utawala.”
Au “Kushi.”
Au “jumba la mfalme lililokuwa.”
Au “Susa.”
Au “wilaya za utawala.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “vyombo; bilauri za.”
Au “aliyezuiwa.”
Au “jumba la kifalme la.”
Au “kilemba cha.”
Au “taratibu.” Tnn., “nyakati.”
Au “wilaya zote za utawala za.”
Tnn., “wilaya zote za utawala za mfalme.”
Au “wilaya ya utawala.”
Au “mtindo wake wenyewe wa kuandika.”
Au “mkuu.”
Au “wilaya zote za utawala za.”
Au “nyumba ya harimu.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “watakandwa.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Anaitwa Yehoyakini kwenye 2Fal 24:8.
Au “mtunzaji.”
Maana yake “Mhadasi.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “jumba la.”
Au “upendo wake mshikamanifu.”
Au “akandwe.”
Au “katika nyumba ya harimu.”
Au “nyumba ya harimu.”
Au “kukandwa.”
Au “na kukandwa kwa wanawake.”
Au “nyumba ya harimu.”
Au “nyumba ya pili ya harimu.”
Angalia Nyongeza B15.
Au “upendo mshikamanifu.”
Au “kilemba cha.”
Au “wilaya za utawala.”
Au “wasichana.”
Au “kwa niaba ya.”
Angalia Nyongeza B15.
Angalia Nyongeza B15.
Au “wilaya zote za utawala za.”
Talanta ilikuwa sawa na kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Au labda, “Nitalipa talanta 10,000 kwenye hazina ya mfalme kwa ajili ya wale watakaofanya kazi hiyo.”
Au “wilaya za utawala.”
Au “wilaya ya utawala.”
Au “mtindo wake wenyewe wa kuandika.”
Au “wilaya zote za utawala za.”
Au “wilaya ya utawala.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “Susa.”
Au “wilaya ya utawala.”
Au “Susa.”
Au “wilaya za utawala za.”
Au “Susa.”
Au “jumba la.”
Karibu mita 22.3 (futi 73). Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “usingizi wa mfalme ulitoweka.”
Au “jumba la.”
Tnn., “anatokana na mbegu ya Wayahudi.”
Au “nafsi yangu.”
Au “nafsi yake.”
Karibu mita 22.3 (futi 73). Angalia Nyongeza B14.
Au “mali yote.”
Au “wilaya zote za utawala za.”
Tnn., “aliunyoosha mkono wake kwa nguvu dhidi ya.”
Angalia Nyongeza B15.
Au “wilaya za utawala.”
Au “wilaya za utawala.”
Au “wilaya ya utawala.”
Au “mtindo wake wenyewe wa kuandika.”
Au “mtindo wao wenyewe wa kuandika.”
Au “nafsi zao.”
Au “wilaya ya utawala.”
Au “wilaya zote za utawala za.”
Angalia Nyongeza B15.
Au “Nakala.”
Au “wilaya zote za utawala.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “Susa.”
Tnn., “wakaona nuru.”
Au “wilaya zote za utawala.”
Angalia Nyongeza B15.
Au “wilaya zote za utawala za.”
Au “wilaya za utawala.”
Au “jumba la.”
Au “wilaya zote za utawala.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “wilaya nyingine za utawala za.”
Au “Susa.”
Au “Susa.”
Au “Susa.”
Au “Susa.”
Au “wilaya za utawala za.”
Au “kutetea nafsi zao.”
Au “Susa.”
Au “wilaya zote za utawala za.”
Neno “Puri,” linamaanisha “Kura.” Neno hilo katika wingi ni “Purimu,” nalo lilianza kutumiwa kurejelea sherehe ya Wayahudi inayosherehekewa mwezi wa 12 wa kalenda takatifu. Angalia Nyongeza B15.
Au “wilaya ya utawala.”
Au “wilaya 127 za utawala za.”
Au “Alithaminiwa sana.”
Tnn., “umati wa ndugu zake.”
Tnn., “kuzungumza kuhusu amani kwa niaba ya.”