Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Wimbo wa Sulemani 1:1-8:14
  • Wimbo wa Sulemani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wimbo wa Sulemani
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Wimbo wa Sulemani

Wimbo wa Sulemani

1 Wimbo ulio bora,+ ambao ni wa Sulemani:+ 2 “Na anibusu kwa busu za kinywa chake,+ maana maonyesho yako ya mapenzi ni bora kuliko divai.+ 3 Maana harufu ya mafuta yako+ ni nzuri. Kama mafuta yanayomiminwa, ndivyo lilivyo jina lako.+ Hiyo ndiyo sababu wanawali wamekupenda. 4 Nivute nyuma yako;+ na tukimbie. Mfalme ameniingiza katika vyumba vyake vya ndani!+ Na tufurahi na kushangilia katika wewe. Na tutaje maonyesho yako ya mapenzi kuliko divai.+ Wamekupenda inavyostahili.+

5 “Mimi ni msichana mweusi, lakini mwenye kupendeza, enyi binti za Yerusalemu,+ kama mahema ya Kedari,+ tena kama vitambaa vya mahema+ ya Sulemani. 6 Msinitazame kwa sababu mimi ni mweusi, kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mama yangu mwenyewe walinikasirikia; waliniweka kuwa mtunzaji wa mashamba ya mizabibu,+ ijapokuwa sikulitunza shamba langu mwenyewe la mizabibu.

7 “Niambie, ewe ambaye nafsi yangu imekupenda,+ mahali unapochunga,+ mahali unapolaza kundi katikati ya mchana. Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefungwa nguo za maombolezo kati ya makundi ya wenzako?”

8 “Ikiwa wewe mwenyewe hujui, ewe uliye mrembo zaidi kati ya wanawake,+ nenda mwenyewe katika nyayo za kundi uchunge wana-mbuzi wako kando ya maskani za wachungaji.”

9 “Nimekufananisha na farasi-jike wangu katika magari ya Farao,+ ewe msichana mwenzi wangu.+ 10 Mashavu yako yanapendeza kati ya nywele zilizosukwa, shingo yako katika mkufu wa shanga.+ 11 Tutakufanyia vitaji vya dhahabu,+ pamoja na vifungo vya fedha.”

12 “Maadamu mfalme yupo penye meza yake ya mviringo, marashi+ yangu mwenyewe ya nardo yametoa harufu+ yake nzuri. 13 Kwangu mimi mpenzi wangu ni kama mfuko wa manemane;+ katikati ya maziwa+ yangu atalala usiku kucha. 14 Kama kishada cha hina+ ndivyo alivyo mpenzi wangu kwangu, kati ya mashamba ya mizabibu ya En-gedi.”+

15 “Tazama! Wewe ni mrembo, ewe msichana mwenzi wangu.+ Tazama! Wewe ni mrembo. Macho yako ni kama ya njiwa.”+

16 “Tazama! Wewe ni mrembo,+ mpenzi wangu, pia mwenye kupendeza. Pia kitanda+ chetu ni cha majani. 17 Nguzo za nyumba yetu kuu ni mierezi,+ maboriti yetu ni miberoshi.

2 “Mimi ni zafarani+ tu ya nchi tambarare ya pwani,+ yungiyungi la nchi tambarare za chini.”+

2 “Kama yungiyungi katikati ya magugu yenye miiba, ndivyo alivyo msichana mwenzi wangu katikati ya mabinti.”+

3 “Kama mtofaa+ katikati ya miti ya msituni, ndivyo alivyo mpenzi wangu katikati ya wana.+ Kivuli chake nimekitamani sana, na hapo nimekaa chini, na matunda yake yamekuwa matamu kinywani mwangu. 4 Alinileta ndani ya nyumba ya divai,+ na bendera+ yake juu yangu ilikuwa upendo.+ 5 Enyi watu niburudisheni kwa keki za zabibu,+ nitegemezeni kwa matofaa; kwa maana mimi nimelewa mapenzi.+ 6 Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu; nao mkono wake wa kuume unanikumbatia.+ 7 Nimewaapisha ninyi,+ enyi binti za Yerusalemu, kwa swala-jike+ au kwa paa+ wa porini, kwamba msijaribu kuamsha au kuwasha upendo ndani yangu mpaka wenyewe utake.+

8 “Sauti ya mpenzi wangu!+ Tazama! Anakuja,+ akipanda juu milimani, akiruka juu vilimani. 9 Mpenzi wangu anafanana na swala+ au mtoto wa paa. Tazama! Anasimama nyuma ya ukuta wetu, akichungulia madirishani, akitazama kupitia pazia.+ 10 Mpenzi wangu amejibu na kuniambia, ‘Simama, ewe msichana mwenzi wangu, mrembo wangu,+ twende zetu.+ 11 Kwa maana, tazama! msimu wa mvua+ umepita, mvua kubwa imekwisha, imekwenda zake. 12 Maua yametokea katika nchi,+ wakati wa kukata matawi ya mizabibu+ umefika, na sauti ya njiwa-tetere+ imesikiwa katika nchi yetu. 13 Mtini+ nao umepevusha rangi ya tini zake za mapema;+ nayo mizabibu imechanua, imetoa harufu yake nzuri. Simama, njoo, ewe msichana mwenzi wangu,+ mrembo wangu, twende zetu. 14 Ewe njiwa wangu+ katika makimbilio ya mwamba, katika mahali palipofichika pa njia yenye mwinuko mkali, nionyeshe umbo lako,+ acha nisikie sauti yako, kwa maana sauti yako ni tamu na umbo lako ni lenye kupendeza.’”+

15 “Tukamatieni mbweha,+ wale mbweha wadogo wanaoharibu mashamba ya mizabibu, kwa maana mashamba yetu ya mizabibu yamechanua.”+

16 “Mpenzi wangu ni wangu nami ni wake.+ Anachunga+ katikati ya mayungiyungi.+ 17 Mpaka mchana uvumishe upepo mtulivu na vivuli viwe vimekimbia, geuka, ewe mpenzi wangu; uwe kama swala+ au kama watoto wa paa juu ya milima ya kutenganisha.

3 “Nyakati za usiku kitandani mwangu nimemtafuta yeye ambaye nafsi yangu imempenda.+ Nilimtafuta, nisimpate. 2 Tafadhali niache niamke, niende kuzunguka jijini;+ barabarani na katika viwanja vya watu wote,+ niache nimtafute yeye ambaye nafsi yangu imempenda. Nilimtafuta, nisimpate. 3 Walinzi+ waliokuwa wakizunguka jijini walinikuta, ‘Je, mmemwona yeye ambaye nafsi yangu imempenda?’ 4 Punde tu baada ya kuwaacha nikampata yeye ambaye nafsi yangu imempenda. Nikamkamata, nisimwachilie, mpaka nilipokuwa nimemleta katika nyumba ya mama yangu na katika chumba cha ndani cha yeye aliyekuwa amenichukua mimba. 5 Nimewaapisha+ ninyi, enyi binti za Yerusalemu, kwa swala-jike au kwa paa wa porini,+ kwamba msijaribu kuamsha au kuwasha upendo ndani yangu mpaka wenyewe utake.”+

6 “Ni nini hiki kinachokuja kutoka nyikani kama nguzo za moshi, kikiwa kimetiwa harufu ya manemane na ubani,+ pamoja na kila namna ya poda ya marashi ya mfanya-biashara?”+

7 “Tazama! Ni kitanda chake, kile cha Sulemani. Wanaume 60 wenye nguvu wamekizunguka, kutoka kati ya wanaume wenye nguvu wa Israeli,+ 8 wote wana upanga, wamefundishwa vita, kila mmoja na upanga wake pajani mwake kwa sababu ya hofu wakati wa usiku.”+

9 “Ni kitanda ambacho Mfalme Sulemani amejifanyizia

kwa miti ya Lebanoni.+ 10 Nguzo zake amezifanya kwa fedha, vitegemezo vyake kwa dhahabu. Kiti chake ni cha sufu iliyotiwa rangi ya zambarau, ndani yake binti za Yerusalemu wamekipamba vifaa kwa upendo.”

11 “Enyi binti za Sayuni, nendeni nje mtazame Mfalme Sulemani akiwa na shada+ ambalo mama yake+ alimfumia siku ya arusi yake na siku ya moyo wake kushangilia.”+

4 “Tazama! Wewe ni mrembo,+ ewe msichana mwenzi wangu. Tazama! Wewe ni mrembo. Macho yako ni kama ya njiwa,+ nyuma ya ushungi wako.+ Nywele zako ni kama kundi la mbuzi+ ambao wameruka chini kutoka eneo lenye milima la Gileadi.+ 2 Meno yako ni kama kundi la kondoo-jike waliokatwa manyoya hivi karibuni+ ambao wamepanda kutoka kuoshwa, wote wanazaa mapacha, wala hakuna yeyote kati yao amepoteza watoto wake. 3 Midomo yako ni kama tu uzi mwekundu, na maneno yako yanakubalika.+ Kama kipande cha komamanga ndivyo yalivyo mashavu yako nyuma ya ushungi wako.+ 4 Shingo yako+ ni kama mnara+ wa Daudi, uliojengwa kwa mistari ya mawe, ambao juu yake hutungikwa ngao elfu, ngao zote za mviringo+ za wanaume wenye nguvu. 5 Maziwa yako mawili+ ni kama watoto wadogo wawili, mapacha ya swala-jike, ambao wanalisha katikati ya mayungiyungi.”+

6 “Mpaka mchana uvume upepo mtulivu+ na vivuli viwe vimekimbia, nitakwenda zangu kwenye mlima wa manemane na kwenye kilima cha ubani.”+

7 “Wewe ni mrembo kabisa,+ ewe msichana mwenzi wangu, wala hamna kasoro ndani yako.+ 8 Na uje pamoja nami kutoka Lebanoni, ewe bibi-arusi,+ uje pamoja nami kutoka Lebanoni.+ Ushuke kutoka kilele cha Milima ya Anti-Lebanoni, kutoka kilele cha Seniri,+ naam, Hermoni,+ kutoka katika matundu ya simba, kutoka katika milima ya chui. 9 Umefanya moyo wangu upige, ewe dada yangu,+ bibi-arusi wangu,+ umefanya moyo wangu upige kwa moja la macho yako,+ kwa kidani kimoja cha mkufu wako. 10 Jinsi yalivyo mazuri maonyesho yako ya mapenzi,+ ewe dada yangu, bibi-arusi wangu! Jinsi maonyesho yako ya mapenzi yalivyo bora kuliko divai na harufu nzuri ya mafuta yako kuliko namna zote za manukato!+ 11 Midomo yako inadondosha asali ya sega,+ ewe bibi-arusi wangu. Asali+ na maziwa viko chini ya ulimi wako, na harufu nzuri ya mavazi yako ni kama harufu nzuri+ ya Lebanoni. 12 Dada yangu,+ bibi-arusi wangu, ni bustani iliyowekewa boma, bubujiko lililofungwa kwa kutiwa muhuri. 13 Ngozi yako ni paradiso ya makomamanga, yenye matunda bora kabisa,+ mimea ya hina pamoja na mimea ya nardo;+ 14 nardo+ na zafarani,+ kane+ na mdalasini,+ pamoja na namna zote za miti ya ubani, manemane na udi,+ pamoja na manukato yote yaliyo bora zaidi;+ 15 na bubujiko la bustani, kisima cha maji safi,+ na vijito vinavyotiririka kutoka Lebanoni.+ 16 Amka, ewe upepo wa kaskazini, ingia, ewe upepo wa kusini.+ Vuma juu ya bustani yangu.+ Manukato yake na yatiririke.”

“Mpenzi wangu na aje katika bustani yake, ale matunda yake yaliyo bora kabisa.”

5 “Nimeingia katika bustani yangu,+ ewe dada yangu,+ bibi-arusi wangu.+ Nimechuma manemane+ yangu pamoja na manukato yangu. Nimekula sega langu la asali pamoja na asali yangu;+ nimekunywa divai yangu pamoja na maziwa yangu.”

“Kuleni, enyi wapenzi! Kunyweni, mlewe maonyesho ya mapenzi!”+

2 “Mimi nimelala, bali moyo wangu umeamka.+ Kuna sauti ya mpenzi wangu akipiga hodi!”+

“Nifungulie,+ ewe dada yangu, msichana mwenzi wangu, njiwa wangu, wangu asiye na lawama!+ Maana kichwa changu kimejaa umande, mashungi ya nywele zangu yamejaa matone ya usiku.”+

3 “‘Nimevua kanzu yangu. Naweza kuivaaje tena? Nimeosha miguu yangu. Naweza kuichafuaje?’ 4 Mpenzi wangu alirudisha nyuma mkono wake kutoka kwenye tundu la mlango, na tumbo+ langu likawa na msukosuko ndani yangu. 5 Mimi mwenyewe nikasimama nimfungulie mpenzi wangu. Mikono yangu ikadondoka manemane na vidole vyangu manemane ya majimaji, juu ya matundu ya kufuli. 6 Mimi mwenyewe nikamfungulia mpenzi wangu, kumbe mpenzi wangu alikuwa amegeuka, alikuwa amepita. Nafsi yangu ilikuwa imenitoka alipoongea. Nikamtafuta, nisimpate.+ Nikamwita, asiniitikie. 7 Walinzi+ waliokuwa wakizunguka jijini wakanikuta. Wakanipiga, wakaniumiza. Walinzi wa kuta+ wakanivua kifuniko changu kipana.

8 “Nimewaapisha+ ninyi, enyi binti za Yerusalemu,+ kwamba, mkimpata mpenzi wangu,+ mwambieni kuwa mimi nimelewa mapenzi.”+

9 “Jinsi gani mpenzi wako ni bora kuliko mpenzi mwingine yeyote,+ ewe uliye mrembo zaidi kati ya wanawake?+ Jinsi gani mpenzi wako ni bora kuliko mpenzi mwingine yeyote, hata ukatuapisha kwa kiapo cha namna hii?”+

10 “Mpenzi wangu anametameta na ni mwekundu, mwenye kuvutia zaidi kati ya elfu kumi.+ 11 Kichwa chake ni dhahabu, dhahabu safi. Mashungi ya nywele zake ni vishada vya tende. Nywele zake nyeusi ni kama kunguru. 12 Macho yake ni kama njiwa kando ya mifereji ya maji, ambao wanaoga katika maziwa, wakiwa wameketi ndani ya vyombo vya mviringo. 13 Mashavu yake ni kama eneo dogo la bustani ya manukato,+ minara ya mimea yenye harufu tamu. Midomo yake ni mayungiyungi, inadondosha manemane ya majimaji.+ 14 Mikono yake ni mianzi ya dhahabu, imejazwa krisolito. Tumbo lake ni bamba la pembe ya tembo lililopambwa kwa yakuti. 15 Miguu yake ni nguzo za marumaru zinazokalia vikalio vya dhahabu safi. Sura yake ni kama Lebanoni, bora kama mierezi.+ 16 Kinywa chake ni utamu mtupu, na kila kitu kumhusu ni chenye kupendeza kabisa.+ Huyo ndiye mpenzi wangu, na huyo ndiye mvulana mwenzi wangu, enyi binti za Yerusalemu.”

6 “Mpenzi wako amekwenda wapi, ewe mwanamke mrembo zaidi kati ya wanawake?+ Mpenzi wako amegeukia upande gani, ili tumtafute pamoja nawe?”

2 “Mpenzi wangu ameshuka kwenda katika bustani yake,+ katika eneo dogo la bustani ya manukato,+ kuchunga+ katikati ya bustani, na kuchuma mayungiyungi. 3 Mimi ni wa mpenzi wangu, naye mpenzi wangu ni wangu.+ Anachunga+ katikati ya mayungiyungi.”

4 “Wewe ni mrembo, ewe msichana mwenzi wangu,+ kama Jiji la Kupendeza,+ unavutia kama Yerusalemu,+ unatisha kama vikosi+ vilivyokusanyika kuzunguka bendera.+ 5 Geuzia mbali macho yako+ kutoka mbele yangu, kwa kuwa yamenishtua mimi. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi ambao wameruka chini kutoka Gileadi.+ 6 Meno yako ni kama kundi la kondoo-jike ambao wamepanda kutoka kuoshwa, wote wanazaa mapacha, na kati yao hakuna yeyote aliyepoteza watoto wake.+ 7 Kama kipande cha komamanga ndivyo yalivyo mashavu yako nyuma ya ushungi wako.+ 8 Huenda kuna malkia 60 na masuria 80 na wanawali wasio na hesabu.+ 9 Lakini kuna mmoja ambaye ni njiwa wangu,+ wangu asiye na lawama.+ Kuna mmoja ambaye ni wa mama yake. Yeye ndiye aliye safi wa yule aliyemzaa. Binti wamemwona, nao wakamtangaza kuwa mwenye furaha; malkia na masuria, nao wakaanza kumsifu,+ 10 ‘Mwanamke+ huyu ni nani, anayetazama chini kama mapambazuko,+ mrembo kama mwezi mpevu,+ mwenye kutakata kama jua linaloangaza,+ mwenye kutisha kama vikosi vilivyokusanyika kuzunguka bendera?’”+

11 “Nilikuwa nimeshuka kwenda katika bustani+ ya milozi, nione matumba katika bonde la mto,+ nione kama mzabibu ulikuwa umechipuka, kama mikomamanga ilikuwa imechanua.+ 12 Kabla sijajua, nafsi yangu mimi ilikuwa imenitia katika magari ya watu wangu wenye kujitoa kwa kupenda.”

13 “Rudi, rudi, ewe Mshulami! Rudi, rudi, ili tukutazame!”+

“Mnaona nini kwa Mshulami?”+

“Kitu kama dansi ya kambi mbili!”

7 “Jinsi hatua zako zimekuwa nzuri katika viatu vyako,+ ewe binti mwenye kujitoa kwa kupenda!+ Mikato ya mapaja yako ni kama mapambo,+ kazi ya mikono ya fundi. 2 Kitovu chako ni bakuli la mviringo. Divai iliyochanganywa+ isikosekane ndani yake. Tumbo lako ni rundo la ngano, lililozungushiwa ua wa mayungiyungi.+ 3 Maziwa yako mawili ni kama watoto wawili, mapacha ya swala-jike.+ 4 Shingo yako+ ni kama mnara wa pembe ya tembo. Macho yako+ ni kama vidimbwi katika Heshboni,+ kando ya lango la Bath-rabimu. Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni, ambao unaelekea Damasko. 5 Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli,+ na mashungi+ ya nywele za kichwa chako ni kama sufu iliyotiwa rangi ya zambarau.+ Mfalme amenaswa na mining’inio ya nywele zako.+ 6 Jinsi ulivyo mrembo, na jinsi unavyopendeza, ewe msichana mpendwa, katikati ya furaha tele!+ 7 Hiki kimo chako kinafanana na mtende,+ na maziwa yako+ kama vishada vya tende. 8 Nimesema, ‘Nitapanda juu ya mtende, nikamate vitawi vya matunda yake ya tende.’+ Tafadhali, maziwa yako na yawe kama vishada vya mzabibu, na harufu nzuri ya pua yako kama matofaa, 9 na kinywa chako kama divai bora+ zaidi ambayo inashuka kwa ulaini+ kwa ajili ya mpenzi wangu, ikitiririka taratibu juu ya midomo ya wenye kulala usingizi.”

10 “Mimi ni wa mpenzi wangu,+ na tamaa yake imenielekea mimi.+ 11 Njoo, ewe mpenzi wangu, twende shambani;+ tukae katikati ya mimea ya hina.+ 12 Na tuamke mapema, twende katika mashamba ya mizabibu, tuone kama mzabibu umechipuka,+ kama ua limechanuka,+ kama mikomamanga imechanua.+ Huko nitakupa wewe maonyesho yangu ya mapenzi.+ 13 Dudai+ zimetoa harufu yake nzuri, na kando ya maingilio yetu kuna namna zote za matunda bora kabisa.+ Mapya na ya zamani vilevile, ewe mpenzi wangu, nimekuwekea hazina.

8 “Laiti ungekuwa kama ndugu yangu,+ ukinyonya maziwa ya mama yangu!+ Ningekukuta nje, ningekubusu.+ Watu hawangenidharau mimi. 2 Ningekuongoza, ningekuleta ndani ya nyumba ya mama yangu,+ aliyekuwa akinifundisha. Ningekupa kinywaji cha divai iliyotiwa vikolezo,+ maji safi ya makomamanga. 3 Mkono wake wa kushoto ungekuwa chini ya kichwa changu; nao mkono wake wa kuume ungenikumbatia.+

4 “Nimewaapisha ninyi, enyi binti za Yerusalemu kwamba msijaribu kuamsha au kuwasha upendo ndani yangu mpaka wenyewe utake.”+

5 “Mwanamke+ huyu ni nani, anayepanda kutoka nyikani,+ akimwegemea mpenzi wake?”+

“Chini ya mtofaa nilikuamsha. Hapo mama yako alikuwa na uchungu wa kukuzaa. Hapo yeye aliyekuwa akikuzaa alipata uchungu.+

6 “Nitie kama muhuri juu ya moyo wako,+ kama muhuri juu ya mkono wako; kwa maana upendo una nguvu kama kifo,+ msisitizo juu ya kujitoa kikamili+ ni wenye kudai kama Kaburi.* Miwako yake ni miwako ya moto, mwali wa moto wa Yah.+ 7 Maji mengi hayawezi kuuzima upendo,+ wala mito haiwezi kuufagilia mbali.+ Kama mtu angetoa vitu vyote vyenye thamani vya nyumba yake kwa ajili ya upendo, hakika watu wangevidharau.”

8 “Tunaye dada mdogo+ ambaye hana maziwa yoyote. Tutamfanyia nini dada yetu siku atakapochumbiwa?”

9 “Kama akiwa ukuta,+ tutajenga juu yake mnara wa fedha; lakini akiwa mlango,+ tutamzuia kwa ubao wa mwerezi.”

10 “Mimi ni ukuta, na maziwa yangu ni kama minara.+ Basi nimekuwa machoni pake yeye kama msichana anayepata amani.

11 “Kulikuwa na shamba la mizabibu+ ambalo Sulemani alikuwa nalo katika Baal-hamoni. Aliwapa watunzaji+ hilo shamba la mizabibu. Kila mmoja alikuwa akileta vipande elfu moja vya fedha kwa ajili ya matunda yake.

12 “Shamba langu mwenyewe la mizabibu liko chini ya mamlaka yangu. Nawe, Ee Sulemani una elfu na wale wanaotunza matunda yake wana mia mbili.”

13 “Enyi mnaokaa katika bustani,+ hao wenzi wanasikiliza kwa makini sauti zenu. Acheni niisikie.”+

14 “Kimbia, mpenzi wangu, ujifanye kama swala au kama mtoto wa paa juu ya milima ya manukato.”+

[Maelezo ya Chini]

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki