Isaya
1 Maono+ ya Isaya+ mwana wa Amozi aliyoyaona kuhusu Yuda na Yerusalemu katika siku za Uzia,+ Yothamu,+ Ahazi+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda:+
2 Sikieni,+ enyi mbingu, utege sikio, Ee dunia, kwa maana Yehova mwenyewe amesema: “Nimelea na kukuza wana,+ lakini wao wenyewe wameniasi.+ 3 Ng’ombe anamjua vema mnunuzi wake, na punda anaijua hori ya bwana wake; Israeli mwenyewe hakujua,+ watu wangu mwenyewe hawakujiendesha kwa uelewaji.”+
4 Ole wake taifa lenye dhambi,+ watu walio na kosa zito, uzao unaotenda maovu,+ wana wenye kuharibu!+ Wamemwacha Yehova,+ wamemvunjia heshima Mtakatifu wa Israeli,+ wamegeuka kuelekea nyuma.+ 5 Ni wapi pengine mtakapopigwa tena,+ kwa kuwa mnazidisha maasi?+ Kichwa chote kimo katika hali ya ugonjwa, na moyo wote ni mnyonge.+ 6 Kuanzia wayo wa mguu mpaka kwenye kichwa hakuna mahali pasipo na kasoro.+ Majeraha na machubuko na mapigo ya hivi karibuni—hayakufinywa yatoe usaha wala kufungwa, wala kulainishwa kwa mafuta.+ 7 Nchi yenu ni ukiwa,+ majiji yenu yameteketezwa kwa moto;+ udongo wenu—mbele ya macho yenu wageni+ wanaula,+ na ukiwa huo ni kama maangamizi yaliyofanywa na wageni.+ 8 Na binti Sayuni+ ameachwa akiwa amebaki kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama kijumba cha mlinzi ndani ya shamba la matango, kama jiji lililozingirwa.+ 9 Kama Yehova wa majeshi hangalituachia waokokaji wachache tu,+ tungalikuwa kama Sodoma, tungalifanana na Gomora.+
10 Sikieni neno la Yehova,+ enyi madikteta+ wa Sodoma.+ Tegeni sikio kwa sheria ya Mungu wetu, ninyi watu wa Gomora. 11 “Dhabihu zenu nyingi zina faida gani kwangu?” asema Yehova. “Nimetosheka na matoleo mazima ya kuteketezwa+ ya kondoo-dume+ na mafuta ya wanyama waliolishwa vizuri;+ nami sikupendezwa na damu+ ya ng’ombe-dume wachanga na wana-kondoo na mbuzi-dume.+ 12 Ninyi mnapoendelea kuingia ili kuona uso wangu,+ ni nani ambaye ametaka hilo kutoka mkononi mwenu, kuzikanyaga-kanyaga nyua zangu?+ 13 Acheni kuleta ndani matoleo zaidi ya nafaka yasiyo na thamani.+ Uvumba—ni chukizo kwangu.+ Mwezi mpya+ na sabato,+ kuita mkusanyiko+—siwezi kuvumilia matumizi ya nguvu za uchawi+ pamoja na kusanyiko kuu. 14 Nafsi yangu imechukia miezi yenu mipya na majira yenu ya sherehe.+ Zimekuwa mzigo kwangu;+ nimechoka kuzibeba.+ 15 Nanyi mnaponyoosha mikono yenu,+ mimi huficha macho yangu kutoka kwenu.+ Hata mjapotoa sala nyingi,+ mimi sisikilizi;+ mikono yenu imejaa umwagaji wa damu.+ 16 Jiosheni;+ jisafisheni;+ ondoeni ubaya wa matendo yenu mbele za macho yangu;+ acheni kutenda mabaya.+ 17 Jifunzeni kutenda mema;+ tafuteni haki;+ mrekebisheni mkandamizaji;+ fanyeni hukumu kwa ajili ya mvulana asiye na baba;+ teteeni masilahi ya mjane.”+
18 “Sasa, njooni, nasi tunyooshe mambo kati yetu,” asema Yehova.+ “Hata dhambi zenu zikiwa nyekundu, zitafanywa kuwa nyeupe kama theluji;+ hata zikiwa nyekundu kama kitambaa chekundu; zitakuwa kama sufu. 19 Ninyi mkionyesha utayari na kusikiliza, mtakula mema ya nchi.+ 20 Lakini mkikataa+ na kwa kweli muwe waasi, mtaliwa na upanga; kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hayo.”+
21 Lo! Jinsi mji mwaminifu+ umekuwa kahaba!+ Ulikuwa umejaa haki;+ uadilifu ulikuwa ukikaa ndani yake,+ lakini sasa ni wauaji.+ 22 Fedha yako imekuwa takataka.+ Pombe yako ya ngano imechanganywa na maji.+ 23 Wakuu wako ni wakaidi na rafiki za wezi.+ Kila mmoja wao ni mwenye kupenda rushwa+ na mwenye kufuatilia zawadi.+ Hawamtendei hukumu mvulana asiye na baba; na hata kesi ya mjane haiwafikii.+
24 Kwa hiyo Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli,+ asema hivi: “Aha! Nitajiondolea wapinzani wangu, nitajilipizia kisasi+ juu ya adui zangu.+ 25 Nami nitaugeuza mkono wangu juu yako, nitayeyusha takataka yako kana kwamba kwa sabuni, nitaondoa uchafu wako wote.+ 26 Nami nitawarudisha tena waamuzi kwa ajili yako kama hapo kwanza, na washauri kwa ajili yako kama pale mwanzoni.+ Kisha wewe utaitwa Jiji la Uadilifu, Mji Mwaminifu.+ 27 Sayuni atakombolewa kwa haki,+ na watu wake wanaorudi, kwa uadilifu.+ 28 Na anguko la waasi na la wenye dhambi litakuwa kwa wakati uleule mmoja,+ na wale wanaomwacha Yehova watafikia mwisho wao.+ 29 Kwa maana wataona aibu kwa sababu ya miti yenye nguvu ambayo ninyi mliitamani,+ nanyi mtafedheheka kwa sababu ya bustani ambazo mmechagua.+ 30 Kwa maana mtakuwa kama mti mkubwa ambao majani yake yananyauka,+ na kama bustani ambayo haina maji. 31 Na mwanamume mwenye nguvu kwa hakika atakuwa kitani,+ na matunda ya kazi yake yatakuwa cheche; na vyote viwili hakika vitateketezwa katika miali ya moto kwa wakati uleule mmoja, bila kuwa na yeyote wa kuzima.”+
2 Jambo ambalo Isaya mwana wa Amozi aliona katika maono kuhusu Yuda na Yerusalemu:+ 2 Na itatukia katika siku za mwisho+ kwamba mlima wa nyumba+ ya Yehova utawekwa imara juu ya kilele cha milima,+ nao utainuliwa juu ya vilima;+ na mataifa yote yatamiminika huko.+ 3 Na vikundi vingi vya watu hakika vitaenda na kusema: “Njooni,+ twendeni juu kwenye mlima wa Yehova, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo; naye atatufundisha njia zake, nasi tutatembea katika mapito yake.”+ Kwa maana sheria itatoka katika Sayuni, na neno la Yehova katika Yerusalemu.+ 4 Naye hakika atafanya hukumu kati ya mataifa+ na kunyoosha mambo+ kuhusu vikundi vingi vya watu.+ Nao watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu.+ Taifa halitainua upanga juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.+
5 Enyi watu wa nyumba ya Yakobo, njooni tutembee katika nuru ya Yehova.+
6 Kwa maana umewaacha watu wako, nyumba ya Yakobo.+ Kwa maana wamejaa vitu vya kutoka Mashariki,+ nao ni wenye kufanya uchawi+ kama Wafilisti, nao wamejawa na wana wa wageni.+ 7 Na nchi yao imejaa fedha na dhahabu, na hakuna kikomo kwa hazina zao.+ Na nchi yao imejaa farasi, na hakuna kikomo kwa magari yao.+ 8 Na nchi yao imejaa miungu isiyo na thamani.+ Wao huinamia kazi ya mikono ya mtu, kile ambacho vidole vya mtu vimetengeneza.+ 9 Na mtu wa udongo huinama, na mwanadamu hushuka, nawe huwezi kuwasamehe.+
10 Ingia ndani ya mwamba, ujifiche katika mavumbi kwa sababu ya hofu ya Yehova, na kutoka mbele ya ukuu wake wa fahari.+ 11 Macho yenye majivuno ya mtu wa udongo yatashushwa, na kiburi cha wanadamu kitainama;+ na Yehova peke yake atainuliwa juu siku hiyo.+ 12 Kwa maana hiyo ni siku ya Yehova wa majeshi.+ Iko juu ya kila mtu aliyejikweza na aliye juu sana na juu ya kila mtu aliyejiinua juu au aliye chini;+ 13 na juu ya mierezi yote ya Lebanoni+ ambayo ni mirefu na iliyoinuliwa juu na juu ya miti yote mikubwa sana ya Bashani;+ 14 na juu ya milima yote mirefu na juu ya vilima vyote ambavyo vimeinuliwa juu;+ 15 na juu ya kila mnara mrefu na juu ya kila ukuta wenye ngome;+ 16 na juu ya meli zote za Tarshishi+ na juu ya mashua zote zenye kutamanika. 17 Na majivuno ya mtu wa udongo yatainama, na kiburi cha wanadamu kitashushwa;+ na Yehova peke yake atainuliwa juu katika siku hiyo.+
18 Na miungu isiyo na thamani itapitilia mbali kabisa.+ 19 Na watu wataingia ndani ya mapango ya miamba na ndani ya mashimo ya mavumbi kwa sababu ya hofu ya Yehova na kutoka mbele ya ukuu wake wenye fahari,+ atakaposimama ili dunia ipatwe na mitetemeko.+ 20 Katika siku hiyo mtu wa udongo atatupia panya-sange na popo miungu yake ya fedha ya ubatili na miungu yake ya dhahabu isiyo na thamani ambayo walikuwa wamemfanyia yeye ili ainame mbele yake,+ 21 ili aingie ndani ya mashimo katika miamba na ndani ya mipasuko ya miamba, kwa sababu ya hofu ya Yehova na kutoka mbele ya ukuu wake wenye fahari,+ atakaposimama ili dunia ipatwe na mitetemeko. 22 Kwa ajili yenu wenyewe, jiepusheni kutoka kwa mtu wa udongo, ambaye pumzi yake iko katika mianzi ya pua yake,+ kwa sababu yeye atafikiriwa kwa msingi gani?+
3 Kwa maana, tazama!+ Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi, anaondoa katika Yerusalemu+ na katika Yuda kitegemeo na tegemeo, kitegemeo kizima cha mkate na kitegemeo kizima cha maji,+ 2 mwanamume mwenye nguvu na shujaa wa vita, mwamuzi na nabii,+ na mwaguzi na mwanamume mzee,+ 3 mkuu wa watu 50+ na mwanamume mwenye kuheshimiwa sana na mshauri na mjuzi wa ufundi wa uchawi, na mchawi stadi.+ 4 Nami hakika nitawafanya wavulana kuwa wakuu wao, na nguvu za kidhalimu zitatawala juu yao.+ 5 Na watu kwa kweli wataoneana, kila mmoja na mwenzake.+ Watashambulia, mvulana juu ya mwanamume mzee,+ na mwenye kupuuzwa juu ya mtu aliye wa kuheshimiwa.+ 6 Kwa maana kila mmoja atamshika ndugu yake ndani ya nyumba ya baba yake, akisema: “Wewe una nguo ya kujitanda. Unapaswa kuwa dikteta+ kwetu, na hili rundo la mabomoko lililoharibiwa linapasa kuwa chini ya mkono wako.” 7 Yeye atapaaza sauti yake siku hiyo, akisema: “Mimi sitakuwa mfunga-majeraha; na nyumbani mwangu hamna mkate wala nguo ya kujitanda. Msiniweke kuwa dikteta juu ya watu.”
8 Kwa maana Yerusalemu limejikwaa na Yuda imeanguka,+ kwa sababu ulimi wao na matendo yao yanapingana na Yehova,+ katika kujiendesha kwa uasi machoni pa utukufu wake.+ 9 Sura ya nyuso zao kwa kweli hushuhudia dhidi yao,+ nazo zinaeleza kuhusu dhambi yao kama ile ya Sodoma.+ Hawajaificha. Ole wa nafsi yao! Kwa maana wamejiletea wenyewe msiba.+
10 Semeni kwamba itakuwa vema kwa mwadilifu,+ kwa maana watakula matunda ya matendo yao.+ 11 Ole wake mtu mwovu!—Msiba; kwa maana matendo yaliyotendwa kwa mikono yake mwenyewe atalipwa yeye!+ 12 Na kuhusu watu wangu, wagawa-kazi wao wanatenda vikali, na wanawake kwa kweli hutawala juu yao.+ Enyi watu wangu, wale wanaowaongoza wanawapoteza ninyi,+ nao wameivuruga njia ya mapito yenu.+
13 Yehova anasimama ili kushindana, naye amesimama ili kukata hukumu juu ya vikundi vya watu.+ 14 Yehova mwenyewe ataingia katika hukumu pamoja na wazee wa watu wake na wakuu wao.+
“Nanyi wenyewe mmeliteketeza kwa moto shamba la mizabibu. Vitu vilivyochukuliwa kwa unyang’anyi kutoka kwa mwenye kuteseka vimo ndani ya nyumba zenu.+ 15 Ninyi mnamaanisha nini kwa kuwa mnawaponda watu wangu, na kwa kuwa mnazisaga nyuso za wenye kuteseka?”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.
16 Na Yehova anasema: “Kwa sababu binti za Sayuni wamekuwa na majivuno, nao wanatembea shingo zao zikiwa zimenyooshwa na kutupa macho yao kwa kutamani, wanatembea kwa hatua fupifupi, na kwa miguu yao wanatoa milio ya kengele,+ 17 Yehova pia atafanya utosi wa binti za Sayuni kuwa na vigaga,+ na Yehova mwenyewe atafunua wazi paji la uso wao.+ 18 Katika siku hiyo Yehova ataondolea mbali uzuri wa bangili na tepe za kichwani na mapambo yenye umbo la mwezi,+ 19 herini na vikuku na shungi,+ 20 vitambaa vya kichwani na mafurungu na mavazi ya kifuani+ na ‘nyumba za nafsi’ na kauri zenye kuvuma za mapambo,+ 21 pete za vidole na pete za pua,+ 22 na kanzu za fahari na kanzu fupi za nje na kanzu na vikoba, 23 na vioo vya mkononi+ na mavazi ya ndani na vilemba+ na shungi+ kubwa.
24 “Na itatukia kwamba badala ya mafuta ya zeri+ kutakuwa na harufu tupu ya kuoza; na badala ya mshipi, kamba; na badala ya nywele zilizosukwa kwa mpangilio wa usanii, upara;+ na badala ya vazi lenye thamani, kuvaa nguo za magunia;+ kutiwa alama+ mwilini badala ya urembo. 25 Wanaume wako wataanguka kwa upanga, na nguvu zako kwa vita.+ 26 Na milango yake italazimika kuomboleza na kuhuzunika,+ naye hakika ataachwa ukiwa. Atakaa chini kwenye udongo.”+
4 Na wanawake saba kwa kweli watamkamata mwanamume mmoja siku hiyo,+ wakisema: “Tutakula mkate wetu wenyewe na kuvaa nguo zetu wenyewe; ila tu sisi na tuitwe kwa jina lako ili kuiondoa shutuma yetu.”+
2 Katika siku hiyo kile ambacho Yehova anachipusha+ kitakuwa kwa ajili ya pambo na kwa ajili ya utukufu,+ na mazao ya nchi yatakuwa kitu cha kujivunia+ na kitu kizuri kwa ajili ya wale wa Israeli walioponyoka.+ 3 Na itatukia kwamba wale waliobaki katika Sayuni na wale waliosalia katika Yerusalemu watasemwa kuwa ni watakatifu kwake,+ kila mtu aliyeandikwa kwa ajili ya uzima katika Yerusalemu.+
4 Yehova atakapokuwa ameosha kinyesi cha binti za Sayuni+ naye atausafisha+ umwagaji wa damu+ wa Yerusalemu kutoka ndani yake kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza,+ 5 pia juu ya kila mahali palipofanywa imara pa Mlima Sayuni+ na juu ya mahali pake pa mkusanyiko hakika Yehova ataumba wingu wakati wa mchana na moshi, na mwangaza wa moto unaowaka+ wakati wa usiku;+ kwa sababu kutakuwa na kificho juu ya utukufu wote.+ 6 Na kutakuwa na kibanda kwa ajili ya kivuli wakati wa mchana kutokana na joto kavu,+ na kwa ajili ya kimbilio na kwa ajili ya maficho kutokana na dhoruba na kutokana na mvua.+
5 Tafadhali, acha nimwimbie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi wangu kuhusu shamba lake la mizabibu.+ Palikuwa na shamba la mizabibu ambalo mpenzi wangu alikuwa nalo kando ya kilima chenye kuzaa sana. 2 Naye akalilima na kuliondoa mawe na kulipanda mzabibu bora mwekundu, na kujenga mnara katikati yake.+ Na pia kulikuwa na shinikizo la divai ambalo alichimba ndani yake.+ Naye akaendelea kulitumaini lizae zabibu,+ lakini mwishowe likazaa zabibu-mwitu.+
3 “Na sasa, enyi wakaaji wa Yerusalemu nanyi watu wa Yuda, tafadhali hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.+ 4 Kuna kitu gani ambacho bado sijalifanyia shamba langu la mizabibu, ambacho bado sijafanya ndani yake?+ Kwa nini nilitumaini lizae zabibu, lakini mwishowe likazaa zabibu-mwitu? 5 Na sasa, tafadhali, acheni niwajulishe ninyi kitu nitakacholifanyia shamba langu la mizabibu: Ukigo wake utaondolewa,+ nalo halitakosa kuteketezwa kwa moto.+ Ukuta wake wa mawe utabomolewa, nalo halitakosa kuwa mahali pa kukanyaga-kanyaga.+ 6 Nami nitaliweka kuwa kitu kilichoangamizwa.+ Nalo halitapunguzwa matawi, wala halitalimwa.+ Nalo litamea vichaka vya miiba na magugu;+ nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua yoyote juu yake.+ 7 Kwa maana shamba la mizabibu+ la Yehova wa majeshi ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ndilo shamba alilolipenda.+ Naye akaendelea kutumaini hukumu+ ifanywe, lakini, tazama! ikawa ni kuvunjwa kwa sheria; kutumaini uadilifu ufanywe, lakini, tazama! ikawa ni kilio.”+
8 Ole wao wanaounganisha nyumba na nyumba,+ na wale wanaounganisha shamba na shamba hata nafasi isiwepo tena+ nanyi mmefanywa mkae peke yenu kabisa katikati ya nchi! 9 Yehova wa majeshi ameapa masikioni mwangu kwamba nyumba nyingi, ingawa ni kubwa na nzuri, zitakuwa kitu cha kushangaza kabisa, bila mkaaji.+ 10 Kwa maana hata ekari kumi+ za shamba la mizabibu zitazaa kipimo kimoja tu cha bathi,+ na hata kipimo kimoja cha homeri ya mbegu kitazaa kipimo kimoja tu cha efa.+
11 Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema ili watafute tu kileo,+ wanaokawia mpaka giza la jioni sana hivi kwamba divai inawawasha!+ 12 Na kutakuwa na kinubi na kinanda, tari na filimbi, na divai katika karamu zao;+ lakini hawauangalii utendaji wa Yehova, wala hawakuiona kazi ya mikono yake.+
13 Kwa hiyo watu wangu watalazimika kwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ujuzi;+ na utukufu wao utakuwa ni watu wenye njaa,+ na umati wao utakaushwa kwa kiu.+ 14 Kwa hiyo Kaburi* limeipanua sana nafsi yake nalo limekipanua kinywa chake kwa kupita mipaka;+ na kilicho cha fahari ndani yake, pia umati wake na ghasia yake na mwenye kufurahi, hakika wataingia ndani yake.+ 15 Na mtu wa udongo atainama, na mwanadamu atashuka, na hata macho ya walio juu yatashuka.+ 16 Na Yehova wa majeshi atakuwa juu kupitia hukumu,+ na Mungu wa kweli, aliye Mtakatifu,+ hakika atajitakasa kupitia uadilifu.+ 17 Na wana-kondoo dume kwa kweli watalisha kana kwamba katika malisho yao; na mahali penye ukiwa pa wanyama waliolishwa vizuri pataliwa na wakaaji wageni.+
18 Ole wao wanaovuta kosa kwa kamba zisizosema kweli, na dhambi kana kwamba ni kwa kamba za gari la kukokotwa;+ 19 wale wanaosema: “Kazi yake na iharakishe; hiyo na ije upesi ili tuione; nalo shauri la Mtakatifu wa Israeli likaribie na kuja, ili tupate kulijua!”+
20 Ole wao wanaosema kwamba wema ni ubaya na ubaya ni wema,+ wale wanaoweka giza badala ya nuru na nuru badala ya giza, wale wanaoweka uchungu badala ya utamu na utamu badala ya uchungu!+
21 Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, walio na busara mbele ya nyuso zao wenyewe!+
22 Ole wao walio na nguvu katika kunywa divai, na wanaume walio na nguvu za kuchanganya kileo,+ 23 wale wanaomtangaza mtu mwovu kuwa mwadilifu kwa kufikiria rushwa,+ na wanaomwondolea mwadilifu hata uadilifu wake!+
24 Kwa hiyo kama mwali wa moto unavyoteketeza majani makavu+ na kama majani matupu yanavyoingia ndani ya miali ya moto, ndivyo kisiki chao kitakavyokuwa kama harufu ya kuoza,+ na ua lao litaenda juu kama mavumbi, kwa sababu wameikataa sheria ya Yehova wa majeshi,+ nao wamelidharau neno la Mtakatifu wa Israeli.+ 25 Ndiyo sababu hasira ya Yehova imewaka juu ya watu wake, naye atanyoosha mkono wake juu yao na kuwapiga.+ Na milima itatetemeka,+ na maiti zao zitakuwa kama takataka katikati ya barabara.+
Kwa sababu ya hayo yote hasira yake haijarudi nyuma, bali mkono wake bado umenyooshwa. 26 Naye ameliinulia ishara taifa kubwa lililoko mbali,+ na amelipigia mluzi kwenye mwisho wa dunia;+ na, tazama! likiwa na haraka litaingia upesi.+ 27 Hakuna yeyote aliyechoka wala hakuna yeyote anayejikwaa katikati yao. Hakuna yeyote anayesinzia wala hakuna yeyote anayelala. Na mshipi ulio viunoni mwao hakika hautafunguliwa, wala kamba za viatu vyao hazitakatwa vipande viwili; 28 kwa sababu mishale yao imenolewa na pinde zao zote zimepindwa.+ Kwato za farasi wao zitahesabiwa kuwa jiwe,+ na magurudumu yao kama upepo wa dhoruba.+ 29 Kunguruma kwao ni kama kule kwa simba, nao hunguruma kama wana-simba wenye manyoya shingoni.+ Nao watanguruma na kuyakamata mawindo na kuyapeleka salama, wala hapatakuwa na mkombozi.+ 30 Nao siku hiyo watanguruma juu yake na mngurumo kama wa bahari.+ Na mtu kwa kweli ataiangalia nchi, na, tazama! kuna giza lenye kutaabisha;+ na hata nuru imetiwa giza kwa sababu ya matone yanayoanguka juu yake.
6 Katika mwaka ule aliokufa Mfalme Uzia,+ mimi, hata hivyo, nilimwona Yehova,+ akiwa ameketi juu ya kiti cha ufalme+ kilicho juu na kilichoinuliwa, na pindo za nguo yake zilikuwa zimelijaza hekalu.+ 2 Maserafi walikuwa wamesimama juu yake.+ Kila mmoja alikuwa na mabawa sita. Aliufunika uso wake kwa mawili,+ na kwa mawili aliifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka huku na huku. 3 Na huyu akamwita yule na kusema: “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova wa majeshi.+ Utukufu wake umejaa katika dunia yote.” 4 Na viegemeo+ vya milango vikaanza kutetemeka kutokana na sauti ya yule aliyekuwa akiita, na mwishowe nyumba ikajaa moshi.+
5 Nami nikasema: “Ole wangu! Kwa maana ni kama nimenyamazishwa, kwa sababu mimi ni mtu asiye na midomo safi,+ nami ninakaa katikati ya watu wasio na midomo safi;+ kwa maana macho yangu yamemwona Mfalme, Yehova wa majeshi, mwenyewe!”+
6 Ndipo mmoja wa maserafi akaruka kunijia, na katika mkono wake kulikuwa na kaa+ linalowaka ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka kwenye madhabahu.+ 7 Naye akakigusa kinywa+ changu na kusema: “Tazama! Hili limeigusa midomo yako, na kosa lako limeondoka na dhambi yako imefanyiwa upatanisho.”+
8 Nami nikaanza kuisikia sauti ya Yehova akisema: “Nitamtuma nani, na ni nani atakayeenda kwa ajili yetu?”+ Nami nikasema: “Mimi hapa! Nitume mimi.”+ 9 Naye akaendelea kusema: “Nenda, nawe uwaambie watu hawa, ‘Sikieni tena na tena, lakini msielewe; na mwone tena na tena, lakini msipate ujuzi wowote.’+ 10 Fanya moyo wa watu hawa kuwa mgumu,+ na uyafanye masikio yao kuwa magumu,+ na ushikanishe macho yao pamoja, ili wasione kwa macho yao na kwa masikio yao wasisikie, na ili moyo wao usielewe na ili kwa kweli wasigeuke na kujiponya.”+
11 Ndipo nikasema: “Ni mpaka wakati gani, Ee Yehova?”+ Kisha akasema: “Ni mpaka majiji yabomoke, yawe bila mkaaji, na nyumba ziwe bila mtu wa udongo, na nchi iharibiwe iwe ukiwa;+ 12 na kwa kweli Yehova aondolee mbali watu wa udongo, na hali ya ukiwa ienee sana katikati ya nchi.+ 13 Na bado ndani yake patakuwa na sehemu ya kumi,+ nayo itakuwa tena kitu cha kuteketezwa, kama mti mkubwa na kama mti mnene sana ambapo, inapokatwa,+ kuna kisiki;+ uzao mtakatifu utakuwa kisiki chake.”+
7 Sasa ikawa katika siku za Ahazi+ mwana wa Yothamu mwana wa Uzia, mfalme wa Yuda, kwamba Resini+ mfalme wa Siria na Peka+ mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli, walikuja Yerusalemu ili kupiga vita juu yake, naye hakuweza kupiga vita juu yake.+ 2 Na habari ikapelekwa kwa nyumba ya Daudi, kusema: “Siria imeegemea Efraimu.”+
Na moyo wake na moyo wa watu wake ukaanza kutetemeka, kama kutetemeka kwa miti ya msituni kwa sababu ya upepo.+
3 Na Yehova akamwambia Isaya: “Tafadhali ondoka, uende kukutana na Ahazi, wewe na Shear-yashubu+ mwana wako, kwenye mwisho wa bomba+ la kidimbwi cha juu kando ya njia kuu ya uwanja wa mfuaji wa nguo.+ 4 Nawe umwambie, ‘Jiangalie na uendelee kukaa bila wasiwasi.+ Usiwe na hofu, wala usiache moyo wako uogope+ kwa sababu ya ncha mbili za mkia za hivi vipande vya mti vinavyotoa moshi, kwa sababu ya hasira kali ya Resini na Siria na mwana wa Remalia,+ 5 kwa sababu Siria pamoja na Efraimu na mwana wa Remalia wamekata shauri la jambo baya juu yako, wakisema: 6 “Na tupande juu ya Yuda na kuirarua, tuichukue iwe yetu kupitia mashambulizi; nasi tumfanye mfalme mwingine atawale ndani yake, mwana wa Tabeeli.”+
7 “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Halitasimama, wala halitatokea.+ 8 Kwa maana kichwa cha Siria ni Damasko, na kichwa cha Damasko ni Resini; na katika muda wa miaka 65 tu Efraimu itavunjwa vipande-vipande ili isiwe kikundi cha watu.+ 9 Na kichwa cha Efraimu ni Samaria,+ na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia.+ Ninyi msipokuwa na imani, basi hamtadumu muda mrefu.”’”+
10 Na Yehova akaendelea kumwambia Ahazi, akisema: 11 “Jiombee ishara kutoka kwa Yehova Mungu wako,+ ifanye kuwa yenye kina kirefu kama Kaburi* au uifanye kuwa ndefu kama maeneo ya juu.” 12 Lakini Ahazi akasema: “Sitaomba, wala sitamjaribu Yehova.”
13 Naye akasema: “Tafadhali, sikiliza, Ee nyumba ya Daudi. Je, ni jambo dogo kwenu kuwachosha wanadamu, kwamba pia mmchoshe Mungu wangu?+ 14 Kwa hiyo Yehova mwenyewe atawapa ninyi ishara: Tazama! Mwanamwali+ kwa kweli atapata mimba,+ naye atazaa mwana,+ naye hakika atamwita jina lake Imanueli. 15 Atakula siagi na asali kufikia wakati atakapojua jinsi ya kukataa lililo baya na kuchagua lililo jema.+ 16 Kwa maana kabla ya mvulana huyo kujua jinsi ya kukataa lililo baya na kuchagua lililo jema,+ nchi ya wale wafalme wawili mnaowahofu na kuchukizwa kwa sababu yao itaachwa kabisa.+ 17 Yehova ataleta juu yenu+ na juu ya watu wenu na juu ya nyumba ya baba yako siku ambazo hazijaja tangu siku ile Efraimu alipoondoka kando ya Yuda,+ yaani, mfalme wa Ashuru.+
18 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba Yehova atawapigia mluzi nzi walio katika mwisho wa mifereji ya Nile ya Misri na nyuki+ walio katika nchi ya Ashuru,+ 19 nao wote hakika wataingia na kutua, juu ya mabonde ya mito yenye maporomoko na juu ya mipasuko ya miamba na juu ya miti yote yenye miiba na juu ya mahali pote pa kunyweshea.+
20 “Katika siku hiyo, kwa kutumia wembe uliokodiwa katika eneo la ule Mto,+ kwa kumtumia mfalme wa Ashuru,+ Yehova atakinyoa kichwa na nywele za miguu, nao utafagilia mbali hata ndevu.+
21 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba mtu mmoja atahifadhi hai ng’ombe mchanga wa mifugo na kondoo wawili.+ 22 Na itatukia kwamba, kutokana na wingi wa kutokezwa kwa maziwa, atakula siagi; kwa sababu siagi na asali+ ndivyo vitu atakavyokula kila mtu aliyebaki katikati ya nchi.
23 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja, yenye thamani ya vipande elfu moja vya fedha,+ patakuwa—kwa ajili ya vichaka vya miiba na kwa ajili ya magugu.+ 24 Atakuja hapo akiwa na mishale na upinde,+ kwa sababu nchi yote itakuwa vichaka vitupu vya miiba na magugu. 25 Na milima yote ambayo ilikuwa ikiondolewa mimea misumbufu kwa jembe—wewe hutakuja hapo kwa kuogopa vichaka vya miiba na magugu; napo hakika patakuwa mahali pa kufungulia ng’ombe na nchi ya kukanyagwa na kondoo.”+
8 Na Yehova akaniambia: “Jichukulie bamba kubwa+ na uandike juu yake kwa kalamu ya mwanadamu anayeweza kufa, ‘Maher-shalal-hash-bazi.’ 2 Nami nipate ushuhuda+ kwa ajili yangu mwenyewe kwa mashahidi waaminifu,+ Uria kuhani+ na Zekaria mwana wa Yeberekia.”
3 Ndipo nikamkaribia yule nabii wa kike, naye akapata mimba na baada ya muda akazaa mwana.+ Yehova sasa akaniambia: “Mwite jina lake Maher-shalal-hash-bazi, 4 kwa maana kabla mvulana huyo hajajua jinsi ya kuita,+ ‘Baba yangu!’ na ‘Mama yangu!’ mtu fulani atachukulia mbali mali za Damasko na nyara za Samaria mbele ya mfalme wa Ashuru.”+
5 Na kwa mara nyingine tena Yehova akaniambia, akisema: 6 “Kwa sababu kikundi hiki cha watu kimeyakataa+ maji ya Shiloa+ yanayotiririka polepole, na kuna kumfurahia+ Resini mwana wa Remalia;+ 7 kwa hiyo, tazama! Yehova analeta juu yao+ maji yenye nguvu na yaliyo mengi ya ule Mto,+ mfalme wa Ashuru+ na utukufu wake wote.+ Naye hakika atakuja juu ya sakafu zake zote za vijito na kwenda juu ya kingo zake zote 8 na kusonga mbele kupitia Yuda. Kwa kweli yeye atafurika na kuvuka.+ Atafika mpaka shingoni.+ Na kunyooshwa kwa mabawa+ yake kutatokea ili kuujaza upana wa nchi yako, Ee Imanueli!”+
9 Fanyeni madhara, enyi vikundi vya watu, na mvunjwe vipande-vipande; na tegeni sikio, enyi nyote mlio katika sehemu za mbali za dunia!+ Jifungeni mshipi,+ na mvunjwe vipande-vipande!+ Jifungeni mshipi, na mvunjwe vipande-vipande! 10 Pangeni hila, nayo itavunjwa!+ Semeni neno lolote, nalo halitasimama, kwa maana Mungu yupo pamoja nasi!+ 11 Kwa maana Yehova ameniambia hivi kwa nguvu za mkono, ili anigeuze kando niache kutembea katika njia ya kikundi hiki cha watu, kusema: 12 “Ninyi msiseme, ‘Ni hila!’ kuhusu yale yote ambayo kikundi hiki cha watu huendelea kusema, ‘Ni hila!’+ na kitu wanachokiogopa ninyi msikiogope, wala msikitetemekee.+ 13 Yehova wa majeshi—yeye Ndiye mnayepaswa kuona kuwa mtakatifu,+ naye ndiye anayepaswa kuwa kitu cha kuogopwa nanyi,+ na Yeye ndiye anayepaswa kuwatetemesha ninyi.”+
14 Naye atakuwa kama mahali patakatifu;+ lakini kama jiwe la kujigonga juu yake na kama mwamba wa kujikwaa+ juu yake kwa nyumba zote mbili za Israeli, kama mtego na kama mnaso kwa wakaaji wa Yerusalemu.+ 15 Na wengi kati yao hakika watajikwaa na kuanguka na kuvunjwa, na kunaswa na kukamatwa.+
16 Funga ule ushuhuda,+ tia muhuri kwenye sheria kati ya wanafunzi wangu!+ 17 Nami nitaendelea kumtarajia Yehova,+ ambaye anauficha uso wake kutoka kwa nyumba ya Yakobo,+ nami nitamtumaini yeye.+
18 Tazama! Mimi na watoto ambao Yehova amenipa+ ni kama ishara+ na kama miujiza katika Israeli kutoka kwa Yehova wa majeshi, anayekaa katika Mlima Sayuni.+
19 Nao wakiwaambia ninyi: “Toeni maombi kwa wenye kuwasiliana na pepo+ au kwa wale wenye roho ya kubashiri wanaonong’oneza+ na kusema maneno kwa sauti za chini,” je, kundi lolote la watu halipaswi kutoa maombi kwa Mungu wake?+ Je, maombi yatolewe kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?+ 20 Kwa sheria na kwa ushuhuda!+
Hakika wataendelea kusema yanayolingana na neno hili+ ambalo halitaona nuru ya mapambazuko.+ 21 Na kila mtu hakika atapita kati ya nchi akiwa na mkazo sana na njaa;+ na itatukia kwamba kwa sababu ana njaa naye amejitia ghadhabu, kwa kweli atamlaani mfalme wake na Mungu+ wake naye hakika atakaza macho kuelekea juu. 22 Naye ataiangalia dunia, na, lo! taabu na giza,+ weusi, nyakati ngumu na weusi bila mwangaza.+
9 Hata hivyo, weusi huo hautakuwa kama wakati nchi ilipokuwa na mkazo, kama wakati wa kwanza mtu alipoidharau nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali+ na wakati wa baadaye mtu alipofanya iheshimiwe+—njia iliyo kando ya bahari, katika eneo la Yordani, Galilaya ya mataifa.+ 2 Watu waliokuwa wakitembea katika giza wameona nuru kuu.+ Kwa habari ya wale wanaokaa katika nchi yenye kivuli kizito,+ nuru imewaangazia.+ 3 Umelifanya hilo taifa kuwa na watu wengi;+ umefanya kuwe na shangwe kuu kwa ajili yake.+ Wameshangilia mbele zako kama kwa shangwe ya wakati wa mavuno,+ kama wale walio na shangwe wakati wanapogawana nyara.+
4 Kwa maana nira ya mzigo wao+ na fimbo iliyo juu ya mabega yao, fimbo ya yule anayewalazimisha kwenda kazini+ umezivunja vipande-vipande kama katika siku ya Midiani.+ 5 Kwa maana kila kiatu cha mtu anayekanyaga+ kwa mitetemeko na nguo ya kujitanda iliyoviringishwa katika damu vimekuwa kwa ajili ya kuteketezwa kama vile chakula kwa ajili ya moto.+ 6 Kwa maana kuna mtoto ambaye amezaliwa kwetu,+ kuna mwana ambaye tumepewa;+ na utawala wa ukuu utakuwa juu ya bega lake.+ Naye ataitwa jina Mshauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele,+ Mkuu wa Amani.+ 7 Hakutakuwa na mwisho kwa habari ya wingi wa huo utawala wa kifalme+ na kwa amani,+ juu ya kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake ili kuufanya imara+ na kuutegemeza kwa njia ya haki+ na kwa njia ya uadilifu,+ kuanzia sasa na kuendelea mpaka wakati usio na kipimo. Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.+
8 Kuna neno ambalo Yehova alituma juu ya Yakobo, nalo likaanguka juu ya Israeli.+ 9 Na watu hakika watalijua,+ wote, Efraimu na mkaaji wa Samaria,+ kwa sababu ya majivuno yao na kwa sababu ya dharau lao la moyo kwa kusema:+ 10 “Matofali yameanguka, lakini tutajenga kwa mawe yaliyochongwa.+ Mikuyu+ imekatwa, lakini tutaweka mierezi badala yake.” 11 Na Yehova ataweka wapinzani wa Resini kuwa juu yake, naye atawachochea adui za yule,+ 12 Siria kutoka mashariki+ na Wafilisti kutoka nyuma,+ nao watamla Israeli kwa kinywa kilicho wazi.+ Kwa sababu ya hayo yote hasira yake haijarudi nyuma, bali mkono wake bado umenyooshwa.+
13 Na watu hawakurudi kwa Yeye anayewapiga,+ nao hawakumtafuta Yehova wa majeshi.+ 14 Na Yehova atakatilia mbali kutoka katika Israeli kichwa+ na mkia,+ chipukizi na kitete, katika siku moja.+ 15 Mwenye kuzeeka na mwenye kuheshimiwa sana ndiye kichwa,+ na nabii anayetoa mafundisho ya uwongo ndiye mkia.+ 16 Na wale wanaowaongoza watu hawa ndio wanaowapoteza;+ na wale kati yao wanaoongozwa, ndio wanaovurugwa.+ 17 Ndiyo sababu Yehova hatashangilia hata juu ya wanaume wao vijana,+ naye hataonyesha rehema juu ya wavulana wao wasio na baba na juu ya wajane wao; kwa sababu wote ni waasi-imani+ na watenda-maovu na kila kinywa kinasema kwa kukosa akili. Kwa sababu ya hayo yote hasira yake haijarudi nyuma, bali mkono wake bado umenyooshwa.+
18 Kwa maana uovu umewaka kama moto;+ utateketeza vichaka vya miiba na magugu.+ Nao utashika moto katika vichaka vya msitu,+ navyo vitachukuliwa juu kama moshi unaopaa.+ 19 Nchi imewashwa moto katika ghadhabu ya Yehova wa majeshi, na watu watakuwa kama chakula kwa ajili ya moto.+ Hakuna yeyote atakayemwonyesha huruma hata ndugu yake.+ 20 Na mtu atakata upande wa kuume naye hakika atakuwa na njaa, na mtu atakula upande wa kushoto, nao hakika hawatashiba.+ Kila mmoja wao atakula nyama ya mkono wake mwenyewe,+ 21 Manase atamla Efraimu, na Efraimu atamla Manase. Wote pamoja watapigana na Yuda.+ Kwa sababu ya hayo yote hasira yake haijarudi nyuma, bali mkono wake bado umenyooshwa.+
10 Ole wao wanaotunga masharti yenye kudhuru+ na wale ambao, wakiandika sikuzote, wameandika taabu tupu, 2 ili kuwasukuma mbali watu wa hali ya chini kutoka kwenye kesi na kuwanyang’anya haki wale wanaoteseka kati ya watu wangu,+ ili wajane wawe nyara yao, na ili hata wapore wavulana wasio na baba!+ 3 Nanyi mtafanya nini katika ile siku ya kukaziwa uangalifu+ na wakati wa uharibifu, utakapokuja kutoka mbali?+ Je, mtamkimbilia nani kupata msaada,+ nanyi mtauacha wapi utukufu wenu,+ 4 isipokuwa iwe kwamba mtu atainama chini ya wafungwa na kwamba watu wataendelea kuanguka chini ya wale ambao wameuawa?+ Kwa sababu ya hayo yote hasira yake haijarudi nyuma, bali mkono wake bado umenyooshwa.+
5 “Aha, Mwashuru,+ fimbo ya hasira yangu,+ na kijiti kilicho mkononi mwao kwa ajili ya shutuma yangu! 6 Nitamtuma yeye juu ya taifa lenye kuasi imani,+ nami nitampa amri juu ya watu wa ghadhabu yangu,+ ili kuchukua nyara nyingi na kuchukua uporaji mwingi na kuwafanya kuwa mahali pa kukanyaga kama udongo wa barabara.+ 7 Ingawa huenda asiwe hivyo, atakuwa na mwelekeo; ingawa huenda moyo wake usiwe hivyo, atapanga hila, kwa sababu kuangamiza kumo moyoni mwake,+ na kukatilia mbali mataifa yasiyo machache.+ 8 Kwa maana yeye atasema, ‘Je, wakuu wangu si wafalme vilevile?+ 9 Je, Kalno+ si kama tu Karkemishi?+ Je, Hamathi+ si kama tu Arpadi?+ Je, Samaria+ si kama tu Damasko?+ 10 Popote ambapo mkono wangu umezifikia falme za mungu asiye na thamani ambaye sanamu zake za kuchongwa ni nyingi kuliko zile zilizo katika Yerusalemu na katika Samaria,+ 11 je, haitakuwa kwamba kama vile nilivyolitendea Samaria na miungu yake isiyo na thamani,+ ndivyo nitakavyolitendea Yerusalemu na sanamu zake?’+
12 “Na itatukia kwamba Yehova atakapokomesha kazi yake yote katika Mlima Sayuni na katika Yerusalemu, ndipo nitakapotoza hesabu kwa ajili ya matunda ya dharau la moyo wa mfalme wa Ashuru na kwa ajili ya kujihesabia makuu kwa majivuno ya macho yake.+ 13 Kwa maana yeye amesema, ‘Kwa nguvu za mkono wangu hakika nitatenda,+ na kwa hekima yangu, kwa maana nina uelewaji; nami nitaiondoa mipaka ya vikundi vya watu,+ nami hakika nitavipora vitu vyao vilivyowekwa akiba,+ nami nitawashusha wakaaji kama mwenye nguvu.+ 14 Na kana kwamba ni kiota, mkono wangu+ utafikia mali+ za vikundi vya watu; na kama mtu anapokusanya mayai ambayo yamebaki, ndivyo nitakavyoikusanya hata dunia yote, na hakika hakuna yeyote atakayetikisa mabawa yake wala kufungua kinywa chake wala kunong’oneza.’”
15 Je, shoka litajiinua juu ya mtu anayekata akilitumia, au msumeno kujitukuza juu ya mtu anayeusogeza mbele na nyuma, kana kwamba fimbo iliwasogeza mbele na nyuma wale wanaoiinua juu, kana kwamba fimbo ilimwinua juu yeye ambaye si mti?+ 16 Kwa hiyo Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi, ataendelea kupeleka ugonjwa unaodhoofisha juu ya watu wake wanono,+ na chini ya utukufu wake mteketezo utaendelea kuteketeza kama mteketezo wa moto.+ 17 Na Nuru+ ya Israeli atakuwa moto,+ na Mtakatifu wake mwali wa moto;+ nao utawaka na kuteketeza magugu yake na vichaka vyake vya miiba+ katika siku moja. 18 Na Yeye atakomesha utukufu wa msitu wake na shamba lake la matunda,+ kuanzia kwenye nafsi mpaka kwenye nyama kabisa, na itakuwa kama kuyeyuka kwa mtu anayeugua.+ 19 Na ile miti mingine ya msitu wake—itakuwa ni hesabu ambayo mvulana mdogo ataweza kuiandika.+
20 Na itatukia hakika katika siku hiyo kwamba yale mabaki ya Israeli+ na wale walioponyoka wa nyumba ya Yakobo hawatamtegemea tena kamwe yule anayewapiga,+ nao hakika watamtegemea Yehova, Mtakatifu wa Israeli,+ katika ukweli.+ 21 Mabaki wachache watarudi, mabaki ya Yakobo, kwa Mungu Mwenye Nguvu.+ 22 Kwa maana hata kama watu wako, Ee Israeli, wangekuwa kama chembe za mchanga wa bahari,+ ni mabaki wachache kati yao ndio watakaorudi.+ Maangamizi+ yaliyoamuliwa yatakuwa yakifurika katikati kwa uadilifu,+ 23 kwa sababu Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, atakuwa akifanya katikati ya nchi yote maangamizi na uamuzi imara.+
24 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi, amesema hivi: “Msiogope, enyi watu wangu mnaokaa katika Sayuni,+ kwa sababu ya Mwashuru, aliyekuwa akiwapiga kwa fimbo+ na aliyekuwa akiinua fimbo yake juu yenu kama Misri alivyofanya.+ 25 Kwa maana bado muda kidogo sana—na shutuma+ ile itafika mwisho, na hasira yangu iwafanye wachakae.+ 26 Na Yehova wa majeshi hakika atatikisa juu yake mjeledi+ kama ule wakati wa kushindwa kwa Midiani kando ya mwamba wa Orebu;+ na fimbo yake itakuwa juu ya bahari,+ naye hakika ataiinua juu kama alivyotendea Misri.+
27 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba mzigo wake utaondoka juu ya bega lako,+ na nira yake itaondoka juu ya shingo yako,+ na nira hakika itavunjwa+ kwa sababu ya mafuta.”
28 Amekuja juu ya Aiathi;+ amevuka katika Migroni; anaviweka vyombo vyake katika Mikmashi.+ 29 Wamevuka kivuko, Geba+ ni mahali pao pa kukaa usiku, Rama+ limetetemeka, Gibea+ la Sauli limekimbia. 30 Paaza sauti yako kwa vilio vikali, Ee binti Galimu.+ Kaza uangalifu, Ee Laisha. Ee mwenye kuteseka, Anathothi!+ 31 Madmena amekimbia. Wakaaji wa Gebimu wameenda kujikinga. 32 Kungali ni mchana kutua Nobu.+ Yeye anatikisa mkono wake kwa kutishia mlima wa binti Sayuni, kilima cha Yerusalemu.+
33 Tazama! Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi, anakata matawi kwa mshindo wa kutisha;+ na wale walio na ukuzi mrefu wanakatwa, na walio juu wanashuka.+ 34 Naye amepiga vichaka vya msitu kwa chombo cha chuma, na kwa mkono wa mwenye nguvu Lebanoni utaanguka.+
11 Na tawi+ litatoka katika kisiki cha Yese;+ na kutoka katika mizizi yake chipukizi+ litazaa.+ 2 Na roho ya Yehova itatua juu yake,+ roho ya hekima+ na ya uelewaji,+ roho ya shauri na ya nguvu,+ roho ya ujuzi+ na ya kumwogopa Yehova;+ 3 naye atakuwa na shangwe katika kumwogopa Yehova.+
Na hatahukumu kulingana na sura inayoonekana kwa macho yake tu, wala kukaripia kulingana tu na jambo lililosikiwa na masikio yake.+ 4 Naye atawahukumu kwa uadilifu watu wa hali ya chini,+ atakaripia kwa unyoofu kwa ajili ya watu wapole wa dunia. Naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake;+ na kumuua mwovu kwa roho ya midomo yake.+ 5 Na uadilifu utakuwa mshipi wa viuno vyake,+ na uaminifu mshipi wa viuno vyake.+
6 Na mbwa-mwitu kwa kweli atakaa pamoja na mwana-kondoo+ kwa muda fulani, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi, na ndama na mwana-simba mwenye manyoya shingoni+ na mnyama aliyelishwa vizuri wote pamoja;+ na mvulana mdogo atakuwa kiongozi juu yao. 7 Na ng’ombe na dubu watakula pamoja; watoto wao watalala pamoja. Na hata simba atakula majani kama ng’ombe.+ 8 Na mtoto anayenyonya hakika atacheza juu ya shimo la nyoka;+ na mtoto aliyeachishwa kunyonya atatia mkono wake juu ya tundu la kupitishia nuru la nyoka mwenye sumu. 9 Hawatasababisha madhara+ yoyote wala kusababisha uharibifu wowote katika mlima wangu wote mtakatifu;+ kwa maana dunia hakika itajawa na kumjua Yehova kama vile maji yanavyoifunika bahari.+
10 Na itakuwa katika siku hiyo+ kwamba patakuwa na mzizi wa Yese+ ambao utakuwa unasimama kuwa ishara kwa ajili ya vikundi vya watu.+ Mataifa yatamtafuta yeye ili kuuliza habari zake,+ na mahali pake pa kupumzikia patakuwa patukufu.+
11 Na itatukia katika siku hiyo kwamba Yehova atatoa tena mkono wake, mara ya pili,+ ili kuchukua mabaki ya watu wake watakaobaki kutoka Ashuru+ na kutoka Misri+ na kutoka Pathrosi+ na kutoka Kushi+ na kutoka Elamu+ na kutoka Shinari+ na kutoka Hamathi na kutoka visiwa vya bahari.+ 12 Naye hakika atainua ishara kwa ajili ya mataifa na kukusanya watu wa Israeli waliotawanywa;+ na watu wa Yuda waliotawanywa atawakusanya pamoja kutoka miisho minne ya dunia.+
13 Na wivu wa Efraimu utaondoka,+ na hata wale wanaomwonyesha Yuda uadui watakatiliwa mbali. Efraimu hatamwonea Yuda wivu, wala Yuda hatamwonyesha Efraimu uadui.+ 14 Nao wataruka juu ya bega la Wafilisti upande wa magharibi;+ wakiwa pamoja watawapora wana wa Mashariki.+ Watanyoosha mkono wao juu ya Edomu na Moabu,+ na wana wa Amoni watakuwa raia zao.+ 15 Na Yehova hakika ataukata ulimi wa bahari ya Misri,+ na kuutikisa mkono wake juu ya Mto+ katika mng’ao wa roho yake. Naye ataupiga katika mito yake saba, naye atawafanya watu watembee wakiwa wamevaa viatu vyao.+ 16 Na kutakuwa na njia kuu+ kutoka Ashuru kwa ajili ya mabaki+ ya watu wake watakaobaki,+ kama ilivyokuwapo njia kwa ajili ya Israeli siku ile alipokuwa akiondoka katika nchi ya Misri.
12 Na katika siku hiyo+ hakika wewe utasema: “Nitakushukuru, Ee Yehova, kwa maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako ilirudi nyuma mwishowe,+ nawe ukanifariji.+ 2 Tazama! Mungu ni wokovu wangu.+ Nitakuwa na tumaini wala sitakuwa na hofu;+ kwa maana Yah Yehova ni nguvu+ zangu na uwezo+ wangu, naye alikuwa wokovu wangu.”+
3 Ninyi hakika mtateka maji katika mabubujiko ya wokovu mkiwa na furaha.+ 4 Na katika siku hiyo hakika mtasema: “Mpeni Yehova shukrani!+ Liitieni jina lake.+ Tangazeni matendo yake kati ya vikundi vya watu.+ Semeni kwamba jina lake limeinuliwa juu.+ 5 Mpigieni Yehova muziki,+ kwa maana ametenda makuu.+ Hilo limetangazwa duniani kote.
6 “Paaza sauti na upige kelele kwa shangwe, Ee mwanamke mkaaji wa Sayuni, kwa maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu katikati yako.”+
13 Tangazo juu ya Babiloni+ ambalo Isaya mwana wa Amozi+ aliona katika maono: 2 “Simamisheni ishara+ juu ya mlima wa miamba mitupu. Wapaazieni sauti, tikiseni mkono,+ ili waingie katika milango ya watu wenye vyeo.+ 3 Mimi mwenyewe nimetoa amri kwa watu wangu waliotakaswa.+ Pia nimewaita watu wangu wenye nguvu kwa ajili ya kuonyesha hasira yangu,+ watu wangu wenye kufurahi kwa njia yenye kutokeza. 4 Sikilizeni! Umati katika milima, kitu kama kikundi cha watu wengi sana!+ Sikilizeni! Ghasia za falme, za mataifa yaliyokusanyika pamoja!+ Yehova wa majeshi anakusanya jeshi la vita.+ 5 Wanakuja kutoka katika nchi iliyo mbali,+ kutoka katika mwisho wa mbingu, Yehova na silaha za shutuma yake, ili kuivunja dunia yote.+
6 “Pigeni mayowe,+ kwa maana siku ya Yehova iko karibu!+ Itakuja kama uporaji kutoka kwa Mweza-Yote.+ 7 Ndiyo sababu mikono yote itaanguka, na moyo wote wa mwanadamu anayeweza kufa utayeyuka.+ 8 Na watu wamekuwa na wasiwasi.+ Utungu na uchungu wa kuzaa zimewashika; wana uchungu kama mwanamke anayezaa.+ Wanatazamana kwa mshangao. Nyuso zao ni nyuso zilizowaka.+
9 “Tazama! Siku ya Yehova inakuja, ikiwa na ukali pamoja na ghadhabu na pamoja na hasira inayowaka, ili kuifanya nchi iwe kitu cha kushangaza,+ na ili kuwaangamiza watenda-dhambi wa nchi kutoka ndani yake.+ 10 Kwa maana nyota za mbinguni na makundi-nyota yake ya Kesili+ hazitatoa nuru yake; jua litakuwa na giza linapochomoza, na mwezi hautatoa nuru yake. 11 Nami hakika nitaleta ubaya wake juu ya nchi yenye kuzaa,+ na kosa lao wenyewe juu ya waovu. Nami kwa kweli nitakifanya kiburi cha wenye kimbelembele kikome, na majivuno ya waonevu nitayashusha.+ 12 Nitamfanya mwanadamu anayeweza kufa kuwa haba kuliko dhahabu safi,+ na mtu wa udongo kuwa haba kuliko dhahabu ya Ofiri.+ 13 Ndiyo sababu nitaifadhaisha mbingu,+ na dunia itatikisika itoke mahali pake kutokana na ghadhabu ya Yehova wa majeshi+ na katika siku ya hasira yake inayowaka.+ 14 Na itatukia kwamba, kama swala aliyefukuzwa na kama kundi ambalo halina mtu wa kulikusanya pamoja,+ watageuka, kila mmoja kwenda kwa watu wake mwenyewe; nao watakimbia, kila mmoja kwenda katika nchi yake.+ 15 Kila mtu atakayepatikana atachomwa kwa silaha, na kila mtu atakayekamatwa katika mfagio huo ataanguka kwa upanga;+ 16 na watoto wao watavunjwa vipande-vipande mbele ya macho yao.+ Nyumba zao zitaporwa, na wake zao watalalwa kinguvu.+
17 “Tazama, ninawaamsha Wamedi+ juu yao, ambao hawaioni fedha kuwa kitu na ambao, kwa habari ya dhahabu, hawapendezwi nayo. 18 Na pinde zao zitawavunja vipande-vipande hata vijana.+ Nao hawatauhurumia uzao wa tumbo;+ macho yao hayatawasikitikia wana. 19 Na Babiloni, lile pambo la falme,+ uzuri wa fahari ya Wakaldayo,+ litakuwa kama wakati Mungu alipoangamiza Sodoma na Gomora.+ 20 Hatakaliwa kamwe,+ wala hatakuwa na makao kwa kizazi baada ya kizazi.+ Na hapo Mwarabu hatapiga hema lake, na hakuna wachungaji watakaoruhusu makundi yao kulala hapo. 21 Na hapo wakaaji wa maeneo yasiyo na maji hakika watalala, na nyumba zao zitajaa bundi-tai.+ Na hapo mbuni watakaa, na roho waovu wenye umbo la mbuzi watarukaruka hapo.+ 22 Na mbwa-mwitu watapiga mayowe katika minara yake ya makao,+ na nyoka mkubwa atakuwa katika majumba ya mfalme yenye furaha tele. Na majira yake yamekaribia kuja, na siku zake hazitakawishwa.”+
14 Kwa maana Yehova atamwonyesha Yakobo+ rehema, naye bado hakika atachagua Israeli;+ na kwa kweli atawapa pumziko juu ya udongo wao,+ na mkaaji mgeni ataungana nao, nao watajiunga na nyumba ya Yakobo.+ 2 Na vikundi vya watu kwa kweli vitawachukua na kuwaleta mahali pao wenyewe, na nyumba ya Israeli watajichukulia hao wawe urithi juu ya udongo wa Yehova wakiwa watumishi wanaume na wakiwa wajakazi;+ nao watawateka+ wale wanaowashika mateka, nao watawatiisha wale waliokuwa wakiwalazimisha kwenda kazini.+
3 Na itatukia katika siku ile ambapo Yehova atakupa pumziko kutokana na maumivu yako na kutokana na msukosuko wako na kutokana na utumwa wako mgumu ambao kwa huo ulifanywa mtumwa,+ 4 kwamba utapaaza neno hili la kimethali juu ya mfalme wa Babiloni na kusema:
“Lo! Jinsi yule anayewalazimisha wengine kufanya kazi amefikia kikomo, ukandamizaji ukafikia kikomo!+ 5 Yehova ameivunja fimbo ya waovu, fimbo ya wanaotawala,+ 6 yeye anayevipiga vikundi vya watu katika ghadhabu kwa mapigo bila kukoma,+ yeye anayeyatiisha mataifa katika hasira kali pamoja na mateso yasiyo na kizuizi.+ 7 Dunia nzima imepumzika,+ imekuwa huru kutokana na usumbufu. Watu wamechangamka kwa vigelegele vya shangwe.+ 8 Hata miberoshi+ imekushangilia pia, mierezi ya Lebanoni, ikisema, ‘Tangu ulale, hakuna mkataji yeyote wa miti+ anayekuja juu yetu.’
9 “Hata Kaburi*+ chini limetetemeka kwa sababu yako ili likupokee wakati wako wa kuingia. Na kwa sababu yako limewaamsha wale wasiojiweza katika kifo,+ viongozi wote wa dunia walio kama mbuzi.+ Limewafanya wafalme wote wa mataifa wasimame kutoka kwenye viti vyao vya ufalme.+ 10 Wote wanaanza kusema na kukuambia, ‘Je, wewe pia umedhoofishwa kama sisi?+ Je, umefananishwa na sisi?+ 11 Kiburi chako kimeshushwa mpaka katika Kaburi,* kelele za vinanda vyako.+ Chini yako, funza wametandikwa kama kitanda; na wadudu ni kifuniko chako.’+
12 “Lo! Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni,+ ewe mwenye kung’aa, mwana wa mapambazuko! Jinsi ulivyokatwa ukaangushwa kwenye dunia,+ wewe uliyekuwa ukiyaondolea mataifa uwezo!+ 13 Kwa habari yako, wewe umesema moyoni mwako, ‘Nitaenda juu mbinguni.+ Nitakiinua kiti changu cha ufalme+ juu ya nyota+ za Mungu, nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano,+ katika sehemu za mbali zaidi za kaskazini.+ 14 Nitaenda juu ya mahali palipo juu pa mawingu;+ mimi nitajifananisha na Aliye Juu Zaidi.’+
15 “Hata hivyo, utashushwa chini mpaka katika Kaburi,*+ katika sehemu za mbali zaidi za shimo.+ 16 Wale wanaokuona watakukazia macho; watakuchunguza kwa makini, wakisema, ‘Je, huyu ndiye yule mtu aliyekuwa akiifadhaisha dunia, aliyekuwa akizitikisa falme,+ 17 aliyeifanya nchi yenye kuzaa iwe kama nyika na aliyeyapindua majiji yake,+ ambaye hakuwafungulia wafungwa wake njia ya kwenda nyumbani?’+ 18 Wafalme wengine wote wa mataifa, ndiyo, wote, wamelala katika utukufu, kila mmoja katika nyumba yake mwenyewe.+ 19 Lakini wewe, umetupiliwa mbali bila kaburi kwa ajili yako,+ kama chipukizi lenye kuchukiwa, umevikwa watu waliouawa, waliochomwa kwa upanga ambao wanashuka mpaka katika mawe ya shimoni,+ kama mzoga uliokanyagiwa chini.+ 20 Hutaungana nao katika kaburi, kwa sababu uliiharibu nchi yako mwenyewe, uliwaua watu wako mwenyewe. Uzao wa watenda-maovu hautatajwa mpaka wakati usio na kipimo.+
21 “Tayarisheni ubao wa kuwachinjia wanawe kwa sababu ya kosa la mababu zao,+ ili wasije wakasimama na kuimiliki dunia na kuyajaza majiji juu ya uso wa nchi yenye kuzaa.”+
22 “Nami nitasimama kupigana nao,”+ asema Yehova wa majeshi.
“Nami nitakatilia mbali kutoka katika Babiloni jina+ na mabaki na watoto na wazao,”+ asema Yehova.
23 “Nami nitamfanya kuwa makao ya nungunungu na madimbwi ya maji yenye matete, nami nitamfagia kwa ufagio wa maangamizi,”+ asema Yehova wa majeshi.
24 Yehova wa majeshi ameapa,+ akisema: “Hakika kama vile nilivyoazimia, ndivyo itakavyokuwa, na kama vile nilivyotoa shauri, hivyo ndivyo itakavyotimia,+ 25 ili kumvunja Mwashuru katika nchi yangu+ na ili nimkanyagie chini juu ya milima yangu mwenyewe;+ na ili nira yake iondoke juu yao na ili mzigo wake uondoke juu ya bega lao.”+
26 Hili ndilo shauri ambalo limeamuliwa juu ya dunia yote, na huu ndio mkono ambao umenyooshwa juu ya mataifa yote. 27 Kwa maana Yehova wa majeshi mwenyewe ametoa shauri,+ na ni nani anayeweza kulivunja?+ Na mkono wake umenyooshwa, na ni nani anayeweza kuurudisha nyuma?+
28 Katika ule mwaka ambao Mfalme Ahazi alikufa+ tangazo hili lilitolewa: 29 “Usishangilie,+ Ee Ufilisti,+ yeyote kati yenu, ati kwa sababu fimbo ya yule anayewapiga imevunjwa.+ Kwa maana kutoka katika mzizi wa nyoka+ atatoka nyoka mwenye sumu,+ na tunda lake litakuwa nyoka wa moto anayeruka.+ 30 Na wazaliwa wa kwanza wa watu wa hali ya chini hakika watakula, na maskini watalala katika usalama.+ Nami nitauua mzizi wako kwa njaa, na kile kitakachobaki kwako kitauawa.+ 31 Piga mayowe, Ee lango! Paaza kilio, Ee jiji! Ninyi nyote mtavunjika moyo, Ee Ufilisti! Kwa maana moshi unakuja kutoka kaskazini, wala hakuna yeyote anayejitenga na vikosi vyake.”+
32 Na mtu yeyote atasema nini kwa kuwajibu wajumbe+ wa taifa lile? Kwamba Yehova mwenyewe ameuweka msingi wa Sayuni,+ na kwake wenye kuteseka wa watu wake watapata kimbilio.
15 Tangazo juu ya Moabu:+ Kwa sababu limeporwa wakati wa usiku, Ari+ la Moabu limenyamazishwa. Kwa sababu limeporwa wakati wa usiku, Kiri+ la Moabu limenyamazishwa. 2 Ameenda mpaka juu kwenye Ile Nyumba na mpaka Diboni,+ mpaka mahali pa juu, kwenye kilio. Moabu inapiga mayowe juu ya Nebo+ na juu ya Medeba.+ Pana upara+ juu ya vichwa vyote ndani yake; ndevu zote zimenyolewa. 3 Wamevaa nguo za magunia+ katika barabara zake. Katika madari+ ya huko na katika viwanja vya watu wote vya huko kila mtu huko analia, anashuka huku akilia.+ 4 Na Heshboni na Eleale+ yanalia. Sauti yao imesikika mpaka Yahazi.+ Ndiyo sababu watu wenye silaha wa Moabu wanaendelea kupaaza sauti. Nafsi yake imetetemeka ndani yake.
5 Moyo wangu unamlilia Moabu mwenyewe.+ Wakimbizi wa huko wamefika mbali mpaka Soari+ na Eglath-shelishiya.+ Kwa maana kwenye mpando wa Luhithi+—kila mmoja anaupanda akilia; kwa maana katika njia ya kwenda Horonaimu+ wanapaaza kilio kuhusu ule msiba. 6 Kwa maana maji ya Nimrimu+ yanakuwa ukiwa mtupu. Kwa maana majani mabichi yamenyauka, majani yamefika mwisho; hakuna chochote ambacho kimekuwa kijani kibichi.+ 7 Ndiyo sababu masalio na mali zao zilizowekwa ghalani ambazo wameweka, wanaendelea kuzibeba na kuzivusha kwenye bonde la mto la mierebi. 8 Kwa maana kilio kimezunguka eneo la Moabu.+ Mayowe ya huko yamefika mpaka Eglaimu; mayowe ya huko yamefika mpaka Beer-elimu, 9 kwa sababu maji ya Dimoni yamejaa damu. Kwa maana nitaweka vitu zaidi juu ya Dimoni, kama vile simba kwa ajili ya wale wa Moabu watakaoponyoka na kwa ajili ya mabaki wa nchi hiyo.+
16 Pelekeni kondoo-dume kwa mtawala wa nchi,+ kutoka Sela kuelekea nyikani, kwenye mlima wa binti Sayuni.+
2 Na itatukia kwamba, kama vile kiumbe chenye mabawa kinachokimbia, kilichofukuzwa kutoka katika kiota chake,+ ndivyo watakavyokuwa binti za Moabu kwenye vivuko vya Arnoni.+
3 “Leteni shauri, tekelezeni uamuzi.+
“Fanya kivuli chako kama usiku katikati ya mchana.+ Wafiche waliotawanywa;+ usimsaliti yeyote anayekimbia.+ 4 Watu wangu waliotawanywa na wakae wakiwa kama wageni ndani yako, Ee Moabu.+ Uwe maficho kwao kwa sababu ya mporaji.+ Kwa maana mkandamizaji ameufikia mwisho wake; uporaji umekoma; wale wanaowakanyaga wengine wamemalizwa kutoka duniani.+
5 “Na kiti cha ufalme hakika kitafanywa imara kwa fadhili zenye upendo;+ na mtu ataketi juu yake katika ukweli ndani ya hema la Daudi,+ akihukumu na kutafuta haki na kuwa mwenye haraka kufanya uadilifu.”+
6 Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu, kwamba yeye ana kiburi sana;+ majivuno yake na kiburi chake na ghadhabu yake+—maneno yake matupu hayatakuwa hivyo.+ 7 Kwa hiyo Moabu atampigia mayowe Moabu; naam, yote itapiga mayowe.+ Waliopigwa wataomboleza kwa sababu ya keki za zabibu kavu za Kir-haresethi,+ 8 kwa sababu matuta ya Heshboni+ yamenyauka. Mzabibu wa Sibma+—wamiliki wa mataifa wamekata matawi yake mekundu. Wamefika mpaka Yazeri;+ walikuwa wametanga-tanga nyikani. Machipukizi yake yalikuwa yameachwa yatoe majani; yalikuwa yamevuka mpaka baharini.
9 Hiyo ndiyo sababu nitalia kwa kilio cha Yazeri juu ya mzabibu wa Sibma.+ Nitakulowesha wewe kwa machozi yangu, Ee Heshboni+ na Eleale,+ kwa sababu kupaaza sauti kumeanguka juu ya kiangazi chako na juu ya mavuno yako.+ 10 Na kushangilia na shangwe zimeondolewa katika shamba la matunda; na hakuna vigelegele vya shangwe katika mashamba ya mizabibu, hakuna sauti inayopaazwa.+ Mwenye kukanyaga hakanyagi divai yoyote itoke katika mashinikizo.+ Nimekomesha kupaaza sauti.+
11 Ndiyo sababu matumbo yangu yana msukosuko kama kinubi juu ya Moabu,+ na sehemu yangu ya ndani juu ya Kir-haresethi.+
12 Na ikatukia kwamba ilionekana kuwa Moabu alichoshwa akiwa juu ya mahali pa juu;+ naye akaja katika patakatifu pake kusali,+ naye hakuweza kutimiza lolote.+
13 Hili ndilo neno ambalo Yehova alisema kuhusu Moabu hapo zamani. 14 Na sasa Yehova amesema hivi: “Katika muda wa miaka mitatu, kulingana na miaka ya mfanyakazi wa kukodiwa,+ utukufu+ wa Moabu utafedheheshwa pia kwa fujo nyingi za kila aina, na wale watakaobaki watakuwa wachache mno, wasio na nguvu.”+
17 Tangazo juu ya Damasko:+ “Tazama! Damasko limeondolewa lisiwe jiji, nalo limekuwa rundo, bomoko linaloharibika.+ 2 Majiji ya Aroeri+ ambayo yameachwa yamekuwa mahali pa makundi, ambapo kwa kweli yanajilaza, pasipo mtu yeyote wa kuyatetemesha.+ 3 Na jiji lenye ngome limekomeshwa kutoka katika Efraimu,+ na ufalme kutoka katika Damasko;+ na wale waliobaki wa Siria watakuwa tu kama utukufu wa wana wa Israeli,” asema Yehova wa majeshi.+
4 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba utukufu wa Yakobo utakuwa wa hali ya chini,+ na hata unono wa nyama yake utakondeshwa.+ 5 Na itatukia kwamba mvunaji anapokusanya nafaka inayosimama na mkono wake unapovuna masuke ya nafaka,+ atakuwa kama mtu anayeokota masalio ya masuke ya nafaka katika nchi tambarare ya chini ya Refaimu.+ 6 Na lazima ndani yake pabaki masalio kama kunapokuwa na upigaji wa mzeituni: zeituni mbili au tatu zilizoiva juu ya tawi; nne au tano juu ya matawi yanayozaa matunda hapo,” asema Yehova Mungu wa Israeli.+
7 Katika siku hiyo mtu wa udongo atatazama juu kwa Mtengenezaji wake, na macho yake yatamtazama Mtakatifu wa Israeli.+ 8 Naye hatazitazama madhabahu,+ kazi ya mikono yake;+ naye hatatazama kile ambacho vidole vyake vimetengeneza, kwenye miti mitakatifu wala kwenye vinara vya uvumba.+ 9 Katika siku hiyo majiji yake yenye ngome yatakuwa kama mahali palipoachwa kabisa katika mwitu, hata lile tawi ambalo wameliacha kabisa kwa sababu ya wana wa Israeli; napo lazima pawe mahame yenye ukiwa.+ 10 Kwa maana umemsahau+ Mungu wa wokovu wako;+ nawe hukumkumbuka Mwamba+ wa ngome yako. Ndiyo sababu unapanda mashamba makubwa yenye kupendeza, nawe unayaweka chipukizi la mgeni. 11 Wakati wa mchana unaweza kulijengea ua shamba lako kwa uangalifu, nawe unaweza kuichipusha mbegu yako wakati wa asubuhi, lakini hakika mavuno yatakimbia katika siku ya ugonjwa na maumivu yasiyoweza kuponywa.+
12 Lo, fujo za vikundi vingi vya watu, ambao wana mchafuko kama mchafuko wa bahari! Nazo kelele za vikundi vya taifa, wanaofanya kishindo kama kelele za maji yenye nguvu!+ 13 Vikundi vya taifa+ vitafanya kishindo kama kelele za maji mengi. Na Yeye atavikemea,+ navyo vitakimbia na kufukuzwa kama makapi ya milima mbele ya upepo na kama mgurumo wa mbaruti mbele ya upepo wa dhoruba.+ 14 Wakati wa jioni, kumbe, tazama! kuna tisho la ghafula. Kabla ya asubuhi—halipo tena.+ Hilo ndilo fungu la wale wanaotuteka, na kura ya wale wanaotupora.+
18 Lo, nchi ya wadudu wenye kuvuma walio na mabawa, iliyoko katika eneo la mito ya Ethiopia!+ 2 Hiyo ndiyo inayotuma wajumbe+ kwa njia ya bahari, na kwa njia ya vyombo vya mafunjo juu ya uso wa maji, ikisema: “Nendeni, enyi wajumbe wepesi, kwa taifa lenye watu warefu na walio laini, kwa watu wenye kuogopesha kila mahali, taifa lenye nguvu zinazodumu na lenye kukanyaga-kanyaga, ambalo mito imeifagilia mbali nchi yake.”+
3 Enyi wakaaji wote wa nchi yenye kuzaa+ nanyi wakaaji wa dunia, mtaona maono kama wakati ishara inapoinuliwa juu ya milima,+ nanyi mtasikia sauti kama wakati baragumu inapopigwa.+ 4 Kwa maana Yehova ameniambia hivi: “Nitakaa bila usumbufu na kupatazama mahali pangu palipofanywa imara,+ kama joto linalometameta pamoja na nuru,+ kama wingu la umande katika joto la mavuno.+ 5 Kwa maana kabla ya mavuno, wakati ua linapofikia ukamilifu na ua linapokuwa zabibu inayoiva, lazima mtu pia akate vitawi kwa miundu na kuviondoa vikonyo, lazima avikate.+ 6 Wote pamoja wataachiwa ndege mwenye kuwinda wa milimani na mnyama wa dunia.+ Na juu yao ndege mwenye kuwinda atakaa wakati wa kiangazi, na juu yao kila mnyama wa dunia atakaa wakati wa mavuno.+
7 “Katika wakati huo zawadi italetwa kwa Yehova wa majeshi,+ kutoka kwa watu warefu na walio laini,+ kutoka kwa watu wenye kuogopesha kila mahali, taifa lenye nguvu zinazodumu na lenye kukanyaga-kanyaga, ambalo mito imeifagilia mbali nchi yake, kwenye mahali pa jina la Yehova wa majeshi, Mlima Sayuni.”+
19 Tangazo juu ya Misri:+ Tazama! Yehova amepanda juu ya wingu jepesi+ na anakuja kuingia Misri. Na miungu ya Misri isiyo na thamani hakika itatetemeka kwa sababu yake,+ na moyo wa Misri utayeyuka katikati yake.+
2 “Nami nitawachochea Wamisri juu ya Wamisri, nao hakika watapigana kila mmoja na ndugu yake, na kila mmoja na mwenzake, jiji juu ya jiji, ufalme juu ya ufalme.+ 3 Na roho ya Misri lazima itatanishwe katikati yake,+ nami nitavuruga shauri lake.+ Nao hakika wataenda kwa miungu isiyo na thamani+ na kwa wachawi na kwa wenye kuwasiliana na pepo na kwa wajuzi wa kubashiri matukio.+ 4 Nami nitaitia Misri katika mkono wa bwana mgumu, na mfalme atakayetawala juu yao atakuwa mwenye nguvu,”+ asema Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi.
5 Na maji hakika yatakauka kutoka baharini, na mto utakuwa mkavu na kwa kweli utakauka.+ 6 Na lazima mito itoe harufu mbaya; mifereji ya Nile ya Misri lazima ishuke na kukauka.+ Matete+ na vitete lazima vioze. 7 Mahali palipo wazi kando ya Mto Nile, penye kinywa cha Mto Nile, na kila udongo wa kupanda mbegu wa Mto Nile zitakauka.+ Hakika zitafukuziwa mbali, nazo hazitakuwapo tena. 8 Na wavuvi watalazimika kuomboleza, na wale wote wanaotupa ndoano ndani ya Mto Nile lazima wahuzunike, na hata wale wanaotandaza nyavu za kuvulia juu ya uso wa maji kwa kweli watadhoofika.+ 9 Na wafanyakazi wa kitani+ kilichochambuliwa lazima waone aibu; pia wafumaji wa nguo wa vitambaa vyeupe. 10 Na wafumaji+ wake lazima wapondwe, wafanyakazi wote wa kulipwa wawe na huzuni katika nafsi.
11 Wakuu wa Soani+ ni wapumbavu kwelikweli. Na kwa habari ya wenye hekima wa washauri wa Farao, shauri lao ni kitu kisicho cha akili.+ Ninyi mtamwambiaje Farao: “Mimi ni mwana wa wenye hekima, mwana wa wafalme wa kale”? 12 Basi, wao wako wapi—watu wenu wenye hekima+—ili sasa wawaambie ninyi na ili wajue yale ambayo Yehova wa majeshi ameshauri kuhusu Misri?+ 13 Wakuu wa Soani wametenda kwa upumbavu,+ wakuu wa Nofu+ wamedanganywa, wakuu wa makabila+ yake wamesababisha Misri iende huku na huku. 14 Yehova mwenyewe amechanganya katikati yake roho ya mvurugo;+ nao wamesababisha Misri kwenda huku na huku katika kazi yake yote, kama mtu aliyelewa anavyogaagaa katika matapiko yake.+ 15 Na Misri haitakuwa na kazi yoyote ambayo inaweza kufanywa na kichwa wala mkia, chipukizi wala tete.+
16 Katika siku hiyo Misri itakuwa kama wanawake, nayo hakika itatetemeka+ na kuingiwa na hofu kwa sababu ya kutikiswa kwa mkono wa Yehova wa majeshi ambao anautikisa juu yake.+ 17 Na nchi ya Yuda itakuwa kisababishi cha kuyumba-yumba kwa Misri.+ Kila mtu anayeambiwa juu yake ameingiwa na hofu kwa sababu ya shauri la Yehova wa majeshi ambalo anashauri juu yake.+
18 Katika siku hiyo kutakuwa na majiji matano katika nchi ya Misri+ yanayosema lugha ya Kanaani+ na kuapa+ kwa Yehova wa majeshi. Jiji moja litaitwa Jiji la Kubomoa.
19 Katika siku hiyo kutakuwa na madhabahu kwa Yehova katikati ya nchi ya Misri,+ na nguzo kwa Yehova kando ya mpaka wake. 20 Nayo itakuwa ni ishara na ushahidi kwa Yehova wa majeshi katika nchi ya Misri;+ kwa maana watamlilia Yehova kwa sababu ya wakandamizaji,+ naye atawapelekea mwokozi, aliye mkuu, ambaye kwa kweli atawakomboa.+ 21 Na Yehova hakika atajulikana kwa Wamisri;+ na Wamisri lazima wamjue Yehova katika siku hiyo, nao watatoa dhabihu na zawadi+ nao watamwekea Yehova nadhiri na kuitimiza.+ 22 Na Yehova hakika ataipiga Misri.+ Kutakuwako kupigwa na kuponywa;+ nao lazima warudi kwa Yehova,+ naye atakubali kusihi kwao na kuwaponya.+
23 Katika siku hiyo kutakuwa na njia kuu+ kutoka Misri kwenda Ashuru, na Ashuru kwa kweli watakuja kuingia Misri, na Misri kuingia Ashuru; nao hakika watatoa utumishi, Misri pamoja na Ashuru. 24 Katika siku hiyo Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na pamoja na Ashuru,+ yaani, baraka katikati ya dunia,+ 25 kwa sababu Yehova wa majeshi atakuwa amewabariki,+ akisema: “Wabarikiwe watu wangu, Misri, na kazi ya mikono yangu, Ashuru,+ na urithi wangu, Israeli.”+
20 Katika mwaka ule ambao Tartani+ alikuja Ashdodi,+ wakati Sargoni mfalme wa Ashuru alipomtuma,+ naye akapigana vita na Ashdodi na kuliteka;+ 2 wakati huo Yehova alisema kwa mkono wa Isaya mwana wa Amozi,+ akisema: “Nenda,+ ukavue nguo ya gunia kutoka viunoni mwako;+ nawe uvue viatu vyako kutoka miguuni pako.”+ Naye akafanya hivyo, akitembea akiwa uchi na miguu wazi.+
3 Na Yehova akaendelea kusema: “Kama vile Isaya mtumishi wangu alivyotembea akiwa uchi na miguu wazi kwa miaka mitatu ili kuwa ishara+ na dalili juu ya Misri+ na juu ya Ethiopia,+ 4 hivyo ndivyo mfalme wa Ashuru atakavyoliongoza kundi la mateka wa Misri+ na wahamishwa wa Ethiopia, wavulana na wanaume wazee, wakiwa uchi na miguu wazi, na matako yakiwa wazi, uchi wa Misri.+ 5 Nao hakika wataingiwa na woga na kuona aibu juu ya Ethiopia ambayo ni tumaini lao walilotazamia+ na juu ya Misri ambayo ni uzuri wao.+ 6 Na mkaaji wa nchi hii ya pwani atakuwa na hakika kusema siku hiyo, ‘Tumaini letu tulilolitazamia liko hivyo, tulilokimbilia kupata msaada, ili kukombolewa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru!+ Na sisi wenyewe tutaokoka jinsi gani?’”
21 Tangazo juu ya nyika ya bahari:+ Kama kusonga mbele kwa pepo za dhoruba+ upande wa kusini, jambo linakuja kutoka nyikani, kutoka katika nchi yenye kuogopesha.+ 2 Kuna maono magumu+ ambayo nimeambiwa: Mwenye kutenda kwa hila anatenda kwa hila, na mporaji anapora.+ Nenda juu, Ee Elamu! Zingira, Ee Umedi!+ Nimekomesha kuugua kote kunakosababishwa naye.+ 3 Ndiyo sababu viuno vyangu vimejaa maumivu makali.+ Utungu umenishika, kama utungu wa mwanamke anayezaa.+ Nimevurugika hivi kwamba sisikii; nimeingiwa na wasiwasi hivi kwamba sioni. 4 Moyo wangu umepigapiga; kutetemeka kumeniogopesha. Gizagiza la jioni ambalo nililipenda limefanywa likawa kwangu kitu cha kutetemesha.+
5 Meza na ipangwe, viti vipangwe, kuwe na kula, kunywa!+ Simameni, enyi wakuu,+ itieni ngao mafuta.+ 6 Kwa maana Yehova ameniambia hivi:
“Nenda, weka mlinzi, ili aseme yale tu anayoyaona.”+
7 Naye akaona gari la vita pamoja na jozi ya farasi wa vita, gari la vita la punda, gari la vita la ngamia. Naye akasikiliza kwa makini, na kukaza fikira sana. 8 Naye akaita kama simba:+ “Ee Yehova, juu ya mnara wa mlinzi ninasimama sikuzote wakati wa mchana, na kwenye kituo changu cha ulinzi ninasimama kila usiku.+ 9 Na, tazama, sasa, linakuja gari la vita la watu, pamoja na jozi ya farasi wa vita!”+
Naye akaanza kusema: “Ameanguka! Babiloni ameanguka,+ na sanamu zake zote za kuchongwa za miungu yake amezivunja na kuziangusha chini!”+
10 Enyi watu wangu waliopurwa na mwana wa uwanja wangu wa kupuria,+ nimewaletea ninyi habari za yale ambayo nimeyasikia kutoka kwa Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli.
11 Tangazo juu ya Duma: Kuna mtu anayeniita kutoka Seiri:+ “Mlinzi, kuna habari gani za usiku? Mlinzi, kuna habari gani za usiku?”+ 12 Mlinzi akasema: “Lazima asubuhi ije, na usiku pia. Ikiwa ninyi mnataka kuuliza, ulizeni. Njooni tena!”
13 Tangazo juu ya nchi tambarare ya jangwani: Mtakaa usiku katika msitu katika nchi tambarare ya jangwani, enyi misafara ya watu wa Dedani.+ 14 Leteni maji ili mkampokee mwenye kiu. Enyi wakaaji wa nchi ya Tema,+ mpokeeni mtu anayekimbia mkiwa na mkate kwa ajili yake. 15 Kwa maana wamekimbia kwa sababu ya panga, kwa sababu ya upanga uliochomolewa, na kwa sababu ya upinde uliopindwa na kwa sababu ya ukali wa vita.
16 Kwa maana Yehova ameniambia hivi: “Katika muda wa mwaka mmoja, kulingana na miaka ya mfanyakazi wa kukodiwa,+ utukufu wote wa Kedari+ utafikia mwisho wake. 17 Na wale waliobaki kati ya hesabu ya wapiga-upinde, wale wanaume wenye nguvu wa wana wa Kedari, watakuwa wachache,+ kwa maana Yehova mwenyewe, Mungu wa Israeli, amesema hivyo.”+
22 Tangazo la bonde la maono:+ Una nini wewe, basi, hata nyote mkaenda juu ya paa?+ 2 Ulijaa machafuko, jiji lenye msukosuko, mji wenye furaha.+ Watu wako waliouawa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.+ 3 Madikteta+ wako wote wamekimbia kwa wakati mmoja.+ Wamechukuliwa kuwa wafungwa bila kuhitaji upinde. Watu wako wote ambao wamepatikana wamechukuliwa kuwa wafungwa pamoja.+ Walikuwa wamekimbia kwenda mbali.
4 Ndiyo sababu nimesema: “Msinitazame. Nitaonyesha uchungu katika kulia.+ Ninyi msisisitize juu ya kunifariji kwa sababu ya kuporwa kwa binti ya watu wangu.+ 5 Kwa maana ni siku ya kuvurugika+ na ya kukanyagiwa+ chini na ya kufadhaisha+ ambayo Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, anayo katika bonde la maono. Kuna mbomoaji wa ukuta,+ na kilio kitaenda kwenye mlima.+ 6 Na Elamu+ imelichukua podo, katika gari la vita la mtu wa udongo, pamoja na farasi wa vita; na Kiri+ imeifunua ngao. 7 Na itatukia kwamba nchi zako tambarare za chini zilizo bora zaidi zitajaa magari ya vita, na farasi wa vita lazima wajiweke katika lango, 8 na mtu atakiondoa kisitiri cha Yuda. Na siku hiyo utatazama kulielekea ghala la silaha+ la nyumba ya msitu,+ 9 nanyi hakika mtayaona yale matundu ya ukuta wa Jiji la Daudi, kwa maana kwa kweli yatakuwa mengi.+ Nanyi mtayakusanya maji ya kidimbwi cha chini.+ 10 Nanyi kwa kweli mtazihesabu nyumba za Yerusalemu. Nanyi pia mtazibomoa nyumba ili kuufanya ukuta+ usiweze kufikiwa. 11 Nanyi lazima mfanye beseni kati ya hizo kuta mbili kwa ajili ya kukusanya maji ya kidimbwi cha kale.+ Nanyi hakika hamtamtazama Mtengenezaji Mkuu wake, na yeye aliyeifanya zamani za kale hakika hamtamwona.
12 “Na Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi, atataka katika siku hiyo kuwe kilio+ na maombolezo na upara na kuvaa nguo za magunia.+ 13 Lakini, tazama! furaha na shangwe, kuchinja ng’ombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa divai,+ ‘Na tule na tunywe, kwa maana kesho tutakufa.’”+
14 Na Yehova wa majeshi amejifunua masikioni mwangu:+ “‘Kosa hili halitafanyiwa upatanisho+ kwa ajili yenu mpaka mtakapokufa,’+ Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, amesema.”
15 Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, amesema hivi: “Nenda, ingia kwa huyu msimamizi-nyumba, kwa Shebna,+ aliye juu ya nyumba,+ 16 ‘Hapa kuna nini ambacho ni haki yako, na hapa kuna nani ambaye ni haki yako, hata ukajichimbia hapa kaburi?’+ Anachimba kaburi lake juu ya kilele; anajichongea makao katika mwamba. 17 ‘Tazama! Yehova anakutupa chini kwa mtupo wenye jeuri, Ee mwanamume, na kukushika kwa nguvu. 18 Bila shaka atakufunga imara, kama mpira kwa ajili ya nchi pana. Utakufa huko, na huko magari ya utukufu wako yatakuwa aibu ya nyumba ya bwana wako. 19 Nami nitakusukuma utoke katika cheo chako; na mtu atakuondoa katika cheo chako rasmi.+
20 “‘Na lazima itatukia katika siku hiyo kwamba nitamwita mtumishi wangu,+ yaani, Eliakimu+ mwana wa Hilkia.+ 21 Nami nitamvika kanzu yako, nitamfunga imara ukumbuu wako,+ nitaitia mkononi mwake mamlaka yako; naye lazima awe baba kwa mkaaji wa Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.+ 22 Nami nitauweka ufunguo+ wa nyumba ya Daudi juu ya bega lake, naye atafungua bila mtu yeyote kufunga, atafunga bila mtu yeyote kufungua.+ 23 Nami nitampigilia kama kigingi+ mahali panapodumu, naye lazima awe kama kiti cha ufalme cha utukufu kwa nyumba ya baba yake.+ 24 Nao wataning’iniza juu yake utukufu wote wa nyumba ya baba yake, wazao na machipukizi, vyombo vyote vya aina ndogo, vyombo vya aina ya bakuli na vilevile vyombo vya mitungi mikubwa.
25 “‘Katika siku hiyo,’ asema Yehova wa majeshi, ‘kile kigingi+ ambacho kimepigiliwa mahali panapodumu kitang’olewa,+ nacho kitakatwa na kuanguka, na mzigo ulio juu yake utakatiliwa mbali, kwa maana Yehova mwenyewe amesema hayo.’”+
23 Tangazo la Tiro:+ Pigeni mayowe, enyi meli za Tarshishi!+ kwa maana imeporwa isiwe bandari tena, isiwe mahali pa kuingia.+ Wamefunuliwa habari kutoka katika nchi ya Kitimu.+ 2 Kaeni kimya, enyi wakaaji wa nchi ya pwani. Wanabiashara kutoka Sidoni,+ wale wanaovuka bahari—wamekujaza. 3 Na mbegu ya Shihori+ imekuwa juu ya maji mengi, mavuno ya Nile, mapato yake; nayo yakaja kuwa faida ya mataifa.+
4 Ona aibu, Ee Sidoni;+ Ee ngome ya bahari, kwa sababu bahari imesema: “Sijapata uchungu wa kuzaa, nami sijazaa, wala sijalea vijana, wala kulea mabikira.”+ 5 Kama vile wakati wa ile habari juu ya Misri,+ ndivyo watu watakavyokuwa na maumivu makali wakati wa ile habari juu ya Tiro.+ 6 Vukeni mpaka Tarshishi; pigeni mayowe, enyi wakaaji wa nchi ya pwani. 7 Je, hili ndilo jiji lenu lililokuwa na furaha tangu siku za kale, tangu nyakati zake za zamani? Miguu yake ilikuwa ikimpeleka mbali kukaa kama mgeni.
8 Ni nani ambaye ametoa shauri hili+ juu ya Tiro, mwenye kuvika watu mataji, ambaye wanabiashara wake walikuwa wakuu, ambaye wafanya-biashara wake walikuwa watu wenye vyeo wa dunia?+
9 Yehova wa majeshi mwenyewe ametoa shauri hili,+ kutia unajisi kiburi cha uzuri wote,+ kuwatendea kwa dharau watu wote wenye vyeo wa dunia.+
10 Vuka juu ya nchi yako kama Mto Nile, Ee binti Tarshishi.+ Hakuna tena kiwanda cha meli.+ 11 Ameunyoosha mkono wake juu ya bahari; amezifadhaisha falme.+ Yehova mwenyewe ametoa amri juu ya Foinike, ya kuziangamiza ngome zake.+ 12 Naye asema: “Usifurahi kamwe tena,+ ewe uliyekandamizwa, bikira binti Sidoni.+ Simama, vuka mpaka Kitimu.+ Hata huko hakutakuwa na utulivu kwako.”
13 Tazama! Nchi ya Wakaldayo.+ Hiki ndicho kikundi cha watu—Ashuru+ hakujionyesha kuwa hicho—walimweka awe msingi kwa ajili ya wakaaji wa jangwani.+ Wamesimamisha minara yao ya kuzingira;+ wameivua minara yake ya makao;+ mtu amemweka kuwa bomoko linaloharibika.+
14 Pigeni mayowe, enyi meli za Tarshishi, kwa maana ngome yenu imeporwa.+
15 Na itatukia katika siku hiyo kwamba Tiro lazima lisahauliwe kwa miaka 70,+ sawasawa na siku za mfalme mmoja. Mwishoni mwa ile miaka 70 itakuwa kwa Tiro kama katika wimbo wa kahaba: 16 “Chukua kinubi, lizunguke jiji, Ee kahaba uliyesahauliwa.+ Fanya kila unaloweza kupiga vinanda; fanya nyimbo zako ziwe nyingi, ili upate kukumbukwa.”
17 Na itatukia kwamba mwishoni mwa miaka 70 Yehova atakaza fikira zake juu ya Tiro, naye atarudia malipo+ yake na kufanya ukahaba na falme zote za dunia zilizo juu ya uso wa nchi.+ 18 Na faida yake na malipo+ yake lazima viwe kitu kitakatifu kwa Yehova. Havitawekwa akiba, wala kurundikwa, kwa sababu malipo yake yatakuja kuwa ya wale wanaokaa mbele za Yehova,+ kwa ajili ya kula na kushiba na kwa ajili ya mavazi yenye fahari.+
24 Tazama! Yehova anaifanya nchi kuwa tupu na kuifanya ukiwa,+ naye amepotoa uso wake+ na kuwatawanya wakaaji wake.+ 2 Na itakuwa kwa watu kama vile ilivyo kwa kuhani; itakuwa kwa mtumishi kama vile ilivyo kwa bwana wake; itakuwa kwa mjakazi kama vile ilivyo kwa bimkubwa wake; itakuwa kwa mnunuzi kama vile ilivyo kwa muuzaji; itakuwa kwa mkopeshaji kama vile ilivyo kwa mkopaji; itakuwa kwa mchukua-faida kama vile ilivyo kwa mlipa-faida.+ 3 Hakika nchi itafanywa kuwa tupu, na hakika itaporwa,+ kwa maana Yehova mwenyewe amesema neno hilo.+ 4 Nchi imeomboleza,+ imefifia. Nchi yenye kuzaa imenyauka, imefifia. Wakuu wa watu wa nchi wamenyauka.+ 5 Nayo nchi imechafuliwa chini ya wakaaji wake,+ kwa maana wamezivunja sheria,+ wamelibadili sharti,+ wamevunja agano linalodumu mpaka wakati usio na kipimo.+ 6 Ndiyo sababu laana imeila nchi,+ na wakaaji wake wamehesabiwa hatia. Ndiyo sababu wakaaji wa nchi wamepungua hesabu, na wanadamu wanaoweza kufa walio wachache sana ndio wamebaki.+
7 Divai mpya imeomboleza, mzabibu umenyauka,+ wote wenye furaha moyoni wameanza kuugua.+ 8 Furaha ya matari imekoma, kelele za waliosisimuka sana zimekoma, furaha ya kinubi imekoma.+ 9 Wanakunywa divai bila wimbo wowote; kileo kinakuwa kichungu kwa wale wanaokinywa. 10 Mji uliohamwa umebomolewa;+ kila nyumba imefungwa isiingiwe. 11 Kuna kilio barabarani kwa sababu ya upungufu wa divai. Shangwe yote imepitilia mbali; furaha ya nchi imeondoka.+ 12 Hali ya kushangaza imeachwa nyuma katika jiji; lango limebomolewa na kuwa tuta tupu la mabomoko.+
13 Kwa maana itakuwa hivyo katikati ya nchi, katikati ya vikundi vya watu, kama kupigwa kwa mzeituni,+ kama masalio wakati ukusanyaji wa zabibu umemalizika.+ 14 Wao wenyewe watapaaza sauti yao, watapiga vigelegele kwa shangwe. Hakika watapaaza vilio vya shangwe kutoka baharini kwa ukuu wa Yehova.+ 15 Ndiyo sababu katika eneo la nuru+ watamtukuza Yehova,+ katika visiwa vya bahari jina la Yehova,+ Mungu wa Israeli. 16 Kuna muziki ambao tumesikia kutoka mwisho wa nchi:+ “Pambo kwake Aliye Mwadilifu!”+
Lakini nasema: “Mimi nimekonda,+ mimi nimekonda! Ole wangu! Wanaotenda hila wametenda kwa hila.+ Wanaotenda hila wametenda kwa hila.”+
17 Hofu na shimo na mtego ziko juu yako, wewe mkaaji wa nchi.+ 18 Na itatukia kwamba yeyote anayeikimbia sauti ya kitu kinachotia hofu ataanguka katika shimo, na yeyote anayetoka ndani ya shimo atakamatwa katika mtego.+ Kwa maana milango ya maji ambayo iko juu itafunguliwa,+ na misingi ya nchi itatikisika.+ 19 Nchi imepasuka kabisa, nchi imetikiswa kabisa, nchi imeyumbishwa-yumbishwa kabisa.+ 20 Nchi inasonga kwa kuyumba-yumba kabisa kama mlevi, nayo imeyumba huku na huku kama kijumba cha mlinzi.+ Na makosa yake yamekuwa mazito juu yake,+ nayo itaanguka, hivi kwamba haitasimama tena.+
21 Na itatukia katika siku hiyo kwamba Yehova ataelekeza fikira zake juu ya jeshi lililo juu mahali pa juu, na juu ya wafalme wa nchi juu ya nchi.+ 22 Nao hakika watakusanywa kama kukusanywa kwa wafungwa ndani ya shimo,+ na kufungiwa ndani ya gereza la shimoni;+ na baada ya siku nyingi watakaziwa fikira.+ 23 Na mwezi mpevu umefedheheka, na jua linaloangaza limeona aibu,+ kwa maana Yehova wa majeshi amekuwa mfalme+ katika Mlima Sayuni+ na katika Yerusalemu na mbele ya wanaume wake wazee kwa utukufu.+
25 Ee Yehova, wewe ni Mungu wangu.+ Ninakutukuza,+ ninalisifu jina lako,+ kwa maana umetenda mambo ya ajabu,+ mashauri+ kutoka nyakati za kale, kwa uaminifu,+ kwa kutegemeka.+ 2 Kwa maana umefanya jiji kuwa fungu la mawe, mji wenye ngome kuwa bomoko linaloanguka, mnara wa makao ya wageni usiwe jiji, ambalo halitajengwa upya mpaka wakati usio na kipimo.+ 3 Ndiyo sababu wale ambao ni kikundi cha watu wenye nguvu watakutukuza wewe; mji wa mataifa yenye kuonea, watakuogopa.+ 4 Kwa maana umekuwa ngome kwa mtu wa hali ya chini, ngome kwa maskini katika taabu aliyo nayo,+ kimbilio kutokana na dhoruba ya mvua, kivuli+ kutokana na joto, wakati mlipuko wa wenye kuonea ni kama dhoruba ya mvua juu ya ukuta. 5 Kama joto katika nchi isiyo na maji, unazitiisha kelele za wageni, joto kwa kivuli cha wingu.+ Muziki wa watu wenye kuonea unanyamazishwa.+
6 Na Yehova wa majeshi hakika atavifanyia vikundi vyote vya watu,+ katika mlima huu,+ karamu ya vyakula vinono vilivyotiwa mafuta,+ karamu ya divai iliyowekwa kwenye machicha, ya vyakula vinono vilivyotiwa mafuta vilivyojazwa urojorojo,+ ya divai+ iliyowekwa kwenye machicha, iliyochujwa.+ 7 Na katika mlima huu hakika ataumeza uso wa kifuniko kinachovifunika vikundi vyote vya watu,+ na mfumo uliofumwa kwa kusokotana juu ya mataifa yote. 8 Yeye kwa kweli atameza kifo milele,+ na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote.+ Na shutuma ya watu wake ataiondoa katika dunia yote,+ kwa maana Yehova mwenyewe amesema hayo.
9 Na katika siku hiyo hakika mtu atasema: “Tazama! Huyu ndiye Mungu wetu.+ Tumemtumaini yeye,+ naye atatuokoa.+ Huyu ndiye Yehova.+ Tumemtumaini yeye. Na tuwe na shangwe na kushangilia katika wokovu wake.”+
10 Kwa maana mkono wa Yehova utatua juu ya mlima huu,+ na Moabu atakanyagwa chini+ katika mahali pake kama fungu la majani linavyokanyagwa chini katika mahali penye mbolea.+ 11 Naye atapiga mikono yake katikati yake kama mwogeleaji anavyoifanya mikono yake, naye atashusha majivuno+ yake kwa mwendo wa udanganyifu wa mikono yake. 12 Na lile jiji lenye ngome, pamoja na kuta zako ndefu za usalama, atalilaza chini; atalishusha, ataliangusha chini kwenye dunia, kwenye mavumbi.+
26 Katika siku hiyo+ wimbo huu utaimbwa+ katika nchi ya Yuda:+ “Tuna jiji lenye nguvu.+ Yeye anaweka wokovu kuwa kuta na boma.+ 2 Fungueni malango,+ ili taifa la uadilifu linaloshika mwenendo wa uaminifu liingie.+ 3 Mwelekeo ambao umetegemezwa vema utaulinda katika amani ya kudumu,+ kwa sababu huyo hufanywa akutegemee wewe.+ 4 Mtegemeeni Yehova,+ kwa nyakati zote, kwa maana katika Yah Yehova kuna Mwamba+ wa mpaka nyakati zisizo na kipimo.
5 “Kwa maana amewashusha chini wale wanaokaa juu ya kilele,+ mji ulioinuliwa.+ Yeye anaushusha, anaushusha mpaka duniani; anauleta kwenye mavumbi.+ 6 Mguu utaukanyagia chini, miguu ya mwenye kuteseka, nyayo za watu wa hali ya chini.”+
7 Pito la mwadilifu ni unyoofu.+ Kwa kuwa wewe ni mnyoofu, utaifanya njia ya mwadilifu kuwa laini.+ 8 Ndiyo, kwa ajili ya njia ya hukumu zako, Ee Yehova, tumekutumaini wewe.+ Tamaa ya nafsi imekuwa kwa ajili ya jina lako na kwa ajili ya ukumbusho wako.+ 9 Nimekutamani wewe kwa nafsi yangu usiku;+ ndiyo, ninaendelea kukutafuta kwa roho yangu ndani yangu;+ kwa sababu, wakati kunapokuwa na hukumu kutoka kwako kwa ajili ya dunia,+ wakaaji wa nchi yenye kuzaa hakika watajifunza uadilifu.+ 10 Hata mwovu akionyeshwa kibali, yeye hatajifunza uadilifu.+ Atatenda isivyo haki katika nchi ya unyoofu,+ naye hatauona ukuu wa Yehova.+
11 Ee Yehova, mkono wako umeinuliwa juu,+ lakini wao hawauoni.+ Wataona na kupata aibu+ kutokana na bidii kwa ajili ya watu wako. Ndiyo, moto+ kwa ajili ya adui zako utawateketeza wao. 12 Ee Yehova, utatuhukumia amani,+ kwa sababu umetenda kazi zetu zote kwa ajili yetu.+ 13 Ee Yehova Mungu wetu, mabwana wengine mbali na wewe wamekuwa wamiliki wetu.+ Ni kwa msaada wako wewe peke yako tutalitaja jina lako.+ 14 Wao wamekufa; hawataishi.+ Wakiwa ni wasiojiweza katika kifo,+ hawataamka.+ Kwa hiyo umeelekeza fikira zako ili uwaangamize na kuharibu majina yao yote.+
15 Umeliongezea hilo taifa; Ee Yehova, umeliongezea hilo taifa;+ umejitukuza mwenyewe.+ Umeieneza mbali mipaka yote ya nchi hiyo.+ 16 Ee Yehova, wakati wa taabu wamekuelekezea fikira zao;+ wametoa mnong’ono wa sala walipopata nidhamu+ yako. 17 Kama vile mwanamke mwenye mimba anapokaribia kuzaa, anavyopata maumivu, hulia akiwa katika maumivu yake ya kuzaa, ndivyo tumekuwa kwa sababu yako, Ee Yehova.+ 18 Tumepata mimba, tumekuwa na maumivu ya kuzaa;+ ni kana kwamba sisi tumezaa upepo. Hatutimizi wokovu wowote ulio halisi kuhusiana na nchi,+ wala hakuna wakaaji wowote wa nchi yenye kuzaa wanaoanguka katika kuzaliwa.+
19 “Wafu wako wataishi.+ Maiti wangu—wataamka.+ Amkeni, pigeni vigelegele kwa shangwe, enyi mnaokaa mavumbini!+ Kwa maana umande+ wako ni kama umande wa miholi,+ na dunia itawaacha hata wale wasiojiweza katika kifo waanguke katika kuzaliwa.+
20 “Nendeni, watu wangu, ingia katika vyumba vyako vya ndani, na ufunge milango nyuma yako.+ Jifiche kwa kitambo kidogo mpaka hukumu itakapopita.+ 21 Kwa maana, tazama! Yehova anakuja kutoka mahali pake ili kulitoza hesabu kosa la mkaaji wa nchi juu yake,+ na nchi hakika itafunua umwagaji wake wa damu+ wala haitawafunika tena watu wake waliouawa.”+
27 Katika siku ile Yehova,+ akiwa na upanga wake mgumu na wenye nguvu,+ ataelekeza uangalifu wake juu ya Lewiathani,*+ yule nyoka anayenyiririka,+ juu ya Lewiathani, yule nyoka mpotovu, na hakika yeye atamuua huyo mnyama mkubwa wa baharini+ aliye ndani ya bahari.
2 Katika siku ile mwimbieni huyo mwanamke:+ “Shamba la mizabibu+ la divai yenye kutoa povu! 3 Mimi, Yehova, ninamlinda yeye.+ Nitamnywesha maji kila wakati.+ Ili yeyote asielekeze fikira zake kupigana naye, nitamlinda usiku na mchana.+ 4 Mimi sina ghadhabu.+ Ni nani atakayenipa vichaka vya miiba+ na magugu katika pigano? Nitavikanyaga hivyo. Nitaviwasha moto kwa wakati mmoja.+ 5 Kama sivyo na ashike ngome yangu, na afanye amani pamoja nami; na afanye amani pamoja nami.”+
6 Katika siku zinazokuja Yakobo atatia mizizi, Israeli+ atachanua maua na kwa kweli achipuke; na kwelikweli wao watajaza matunda juu ya uso wa nchi yenye kuzaa.+
7 Je, ni lazima mtu ampige kwa pigo kama la mtu anayempiga? Au, je, ni lazima auawe kwa mauaji kama ya watu wake waliouawa?+ 8 Utashindana naye kwa mlio wa kushtua utakapokuwa ukimfukuza. Lazima yeye atamfukuza huyo kwa mlipuko wake, ulio mkali katika siku ya upepo wa mashariki.+ 9 Basi kwa njia hii kosa la Yakobo litafanyiwa upatanisho,+ na haya ni matunda yote wakati anapoiondoa dhambi yake,+ wakati anapofanya mawe yote ya madhabahu kama mawe ya chokaa ambayo yamepondwa, hivi kwamba miti mitakatifu+ na vinara vya uvumba havitasimama.+ 10 Kwa maana jiji lenye ngome litakuwa peke yake, uwanja wa malisho utaachwa peke yake na kuachwa kama nyika.+ Ndama atalisha hapo, naye atalala hapo; naye kwa kweli atakula matawi yake.+ 11 Vitawi vyake vitakapokuwa vimekauka, wanawake wanaoingia watavivunja, na kuviwasha.+ Kwa maana wao ni kundi la watu lisilo na hamu ya uelewaji.+ Ndiyo sababu Mtengenezaji wake hatalionyesha rehema, na Mfanyizaji wake hatalionyesha kibali.+
12 Na itatukia katika siku ile kwamba Yehova atayapiga matunda,+ kuanzia kijito kinachotiririka cha ule Mto+ mpaka kwenye bonde la mto la Misri,+ na basi ninyi mtaokotwa mmoja baada ya mwingine,+ enyi wana wa Israeli. 13 Na itatukia katika siku ile kwamba baragumu kubwa itapigwa,+ na wale wanaoangamia katika nchi ya Ashuru+ na wale waliotawanyika katika nchi ya Misri+ hakika watakuja na kumwinamia+ Yehova kwenye mlima mtakatifu katika Yerusalemu.+
28 Ole wake taji lenye utukufu la walevi wa Efraimu,+ na ua linalonyauka la pambo lake la uzuri lililo juu ya kichwa cha bonde lenye rutuba la wale ambao divai imewashinda nguvu! 2 Tazama! Yehova ana mtu mwenye nguvu na aliye hodari.+ Hakika atatupa chini kwa nguvu kama dhoruba ya mawe yenye mngurumo,+ dhoruba yenye kuangamiza, kama dhoruba yenye mngurumo ya maji yenye nguvu, yanayofurika.+ 3 Mataji yenye utukufu ya walevi wa Efraimu yatakanyagiwa+ chini kwa miguu. 4 Na ua linalonyauka+ la pambo lake la uzuri lililo juu ya kichwa cha bonde lenye rutuba litakuwa kama tini ya mapema+ kabla ya wakati wa kiangazi, ambayo, wakati mwonaji anapoiona, ikiwa bado mkononi mwake, yeye huimeza.
5 Katika siku hiyo Yehova wa majeshi atakuwa kama taji la pambo+ na kama shada la urembo+ kwa wale wanaobaki+ kati ya watu wake, 6 na kama roho ya haki kwa yule anayeketi katika hukumu,+ na kama nguvu kwa wale wanaogeuzia mbali pigano kutoka katika lango.+
7 Na hawa pia—kwa sababu ya divai wamepotea na kwa sababu ya kileo wametanga-tanga. Kuhani na nabii+—wamepotea kwa sababu ya kileo, wamevurugika kutokana na divai, wametanga-tanga+ kutokana na kileo; wamepotea katika kuona kwao, wameyumba-yumba kuhusu uamuzi. 8 Kwa maana meza zote zimejaa matapiko machafu+—hakuna mahali ambapo hayapo.
9 Mtu atamfundisha nani ujuzi,+ na mtu atamfanya nani aelewe yale ambayo yamesikiwa?+ Je, ni wale ambao wameachishwa kunyonya, wale walioondolewa kwenye maziwa?+ 10 Kwa maana ni “amri juu ya amri, amri juu ya amri, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, hapa kidogo, pale kidogo.”+ 11 Kwa maana kwa njia ya wale wanaogugumiza kwa midomo yao+ na kwa lugha tofauti+ yeye atasema na watu hawa,+ 12 wale ambao amewaambia: “Hapa ndipo mahali pa kupumzika. Mpeni pumziko yeye aliyechoka. Na hapa ndipo mahali pa starehe,” lakini ambao hawakuwa tayari kusikia.+ 13 Na neno la Yehova hakika litakuwa kwao “amri juu ya amri, amri juu ya amri, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia,+ hapa kidogo, pale kidogo,” ili waende na hakika wajikwae kuelekea nyuma na kwa kweli wavunjwe na kunaswa na kukamatwa.+
14 Kwa hiyo sikieni neno la Yehova, ninyi wenye kujigamba, ninyi watawala+ wa watu hawa walio katika Yerusalemu: 15 Kwa sababu mmesema: “Tumefanya agano pamoja na Kifo;+ nasi tumetekeleza maono pamoja na Kaburi;*+ lile furiko la ghafula linalofurika, ikiwa litapita katikati, halitatufikia, kwa maana tumefanya uwongo kuwa kimbilio+ letu nasi tumejificha katika jambo lisilo la kweli”;+ 16 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninaweka katika Sayuni+ jiwe+ kuwa msingi, jiwe lililojaribiwa,+ jiwe la pembeni+ lenye thamani la msingi imara.+ Yeyote anayeonyesha imani hataingiwa na wasiwasi.+ 17 Nami nitaifanya haki kuwa kamba ya kupimia+ na uadilifu+ kuwa timazi; na mvua ya mawe+ itafagilia mbali lile kimbilio la uwongo,+ na maji yatafurika mahali pa maficho.+ 18 Na lile agano lenu pamoja na Kifo hakika litavunjwa,+ na yale maono yenu pamoja na Kaburi* hayatasimama.+ Lile furiko la ghafula linalofurika, wakati linapopita katikati+—ninyi pia mtakuwa mahali pa kukanyagwa-kanyagwa nalo.+ 19 Kila mara linapopita katikati, litawachukua ninyi,+ kwa sababu litapita katikati asubuhi baada ya asubuhi, wakati wa mchana na wakati wa usiku; nalo litakuwa sababu ya kutetemeka+ ili kufanya wengine waelewe yale ambayo yamesikiwa.”
20 Kwa maana kitanda kimekuwa kifupi mno mtu asiweze kujinyoosha juu yake, na shuka iliyofumwa ni nyembamba mno mtu anapojifunika. 21 Kwa maana Yehova atasimama kama katika Mlima Perasimu,+ atafadhaika kama katika nchi tambarare ya chini karibu na Gibeoni,+ ili afanye tendo lake—tendo lake ni la ajabu—na ili afanye kazi yake—kazi yake si ya kawaida.+ 22 Na sasa msijionyeshe kuwa wenye kudhihaki,+ ili pingu zenu zisiwe na nguvu, kwa maana kuna maangamizi, jambo lililoamuliwa, ambalo nimelisikia habari zake kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi, kwa ajili ya nchi yote.+
23 Tegeni sikio, na mwisikilize sauti yangu; kazeni uangalifu na mlisikilize neno langu. 24 Je, mkulima hulima mchana wote+ ili kupanda mbegu, na kuchimbua na kuvunja udongo wake?+ 25 Anapokuwa ameufanya udongo wake kuwa laini, je, hatawanyi bizari nyeusi na kuinyunyiza bizari,+ na je, hatii ndani ngano, mtama,+ na shayiri mahali palipochaguliwa,+ na kusemethi+ kuwa mpaka wake?+ 26 Na mtu humrekebisha+ kulingana na lililo sawa. Mungu wake mwenyewe humfundisha.+ 27 Kwa maana bizari nyeusi haisagwi kwa kifaa cha kupuria;+ wala gurudumu la gari la kukokotwa halizungushwi juu ya bizari. Kwa maana kwa kawaida bizari nyeusi hupigwa kwa fimbo,+ na bizari kwa fimbo ya mkono. 28 Je, kwa kawaida unga wa mkate hupondwa? Kwa maana mtu haendelei kuukanyaga+ bila kuacha kamwe.+ Na lazima yeye aanze kuzungusha gurudumu la gari lake la kukokotwa, na farasi zake, lakini yeye haupondi.+ 29 Na haya pia yametoka kwa Yehova wa majeshi mwenyewe,+ ambaye amekuwa wa ajabu katika shauri, ambaye amefanya kwa njia kuu kazi yenye matokeo.+
29 “Ole wa Arieli,+ wa Arieli, mji ambapo Daudi alipiga kambi!+ Ongezeni mwaka juu ya mwaka; sherehe+ na zikamilishe zamu. 2 Nami itanipasa kufanya mambo yawe magumu+ kwa Arieli, na kutakuwako kilio na maombolezo,+ naye atakuwa kwangu kama jiko la madhabahu ya Mungu.+ 3 Nami nitapiga kambi pande zote juu yako, nami nitakuzingira kwa ngome na kusimamisha juu yako mazingiwa.+ 4 Nawe utashuka hivi kwamba utasema kutoka chini, na neno lako litakuwa la sauti ya chini kama kutoka mavumbini.+ Na kama vile mwenye kuwasiliana na pepo sauti yako itatoka chini, na kutoka mavumbini neno lako litatoa mlio kama wa ndege.+ 5 Na umati wa wale walio wageni kwako utakuwa tu kama vumbi laini,+ na umati wa waonevu+ kama tu makapi yanayopitilia mbali.+ Na hilo litatokea mara moja, kwa ghafula.+ 6 Mtakaziwa fikira kutoka kwa Yehova wa majeshi kwa mngurumo na kwa tetemeko na kwa sauti kubwa, upepo wa dhoruba na tufani, na mwali wa moto unaoteketeza.”+
7 Na itakuwa tu kama katika ndoto, katika maono ya usiku, kuhusu ule umati wa mataifa yote yanayopiga vita juu ya Arieli,+ wale wote wanaopiga vita juu yake, na minara ya kumzingira na wale wanaofanya mambo yawe magumu kwake.+ 8 Ndiyo, itakuwa tu kama wakati mtu aliye na njaa anapoota ndoto, na, tazama, anakula, naye huamka kumbe nafsi yake ni tupu;+ na kama tu wakati mtu aliye na kiu anapoota ndoto, na, tazama, anakunywa, naye huamka, na, tazama, amechoka nayo nafsi yake imekauka; hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa ule umati wa mataifa yote yanayopiga vita juu ya Mlima Sayuni.+
9 Kawieni, na mshangae;+ jitieni upofu, na mtiwe upofu.+ Wamelewa, lakini si kwa divai;+ wametembea kwa kuyumba-yumba, lakini si kwa sababu ya kileo.+
10 Kwa maana Yehova amemwaga juu yenu roho ya usingizi mzito;+ naye anafunga macho yenu, manabii,+ naye amefunika vichwa vyenu,+ waonaji.+ 11 Na kwenu ninyi maono ya kila jambo yanakuwa kama maneno ya kitabu ambacho kimefungwa kwa muhuri,+ ambacho wao wanampa mtu anayejua kuandika, wakisema: “Tafadhali, soma hiki kwa sauti,” naye analazimika kusema: “Siwezi, kwa maana kimefungwa kwa muhuri”;+ 12 na kile kitabu kinapewa mtu asiyejua kuandika, mtu fulani akisema: “Tafadhali, soma hiki kwa sauti,” naye analazimika kusema: “Sijui kabisa kuandika.”
13 Na Yehova anasema: “Kwa sababu watu hawa wamekaribia na vinywa vyao, nao wamenitukuza kwa midomo yao mitupu,+ nao wameupeleka moyo wao mbali nami,+ na woga wao kwangu ni amri ya wanadamu inayofundishwa,+ 14 kwa hiyo, tazama, mimi hapa, yule Mmoja atakayekitendea tena kikundi hiki cha watu kwa njia ya ajabu,+ kwa njia ya ajabu na kwa jambo la ajabu; na hekima ya watu wao wenye hekima itaangamia, na uelewaji wa watu wao wenye busara utajificha.”+
15 Ole wao wanaojizamisha ndani sana katika kuficha shauri kutoka kwa Yehova,+ na ambao matendo yao yamefanyika mahali penye giza,+ huku wakisema: “Ni nani anayetuona, na ni nani anayejua habari zetu?”+ 16 Upotovu wenu! Je, mfinyanzi ahesabiwe kama udongo?+ Kwa maana, je, kitu kilichofanywa kiseme hivi kumhusu mwenye kukifanya: “Yeye hakunifanya”?+ Na je, kitu ambacho kimefanywa kwa kweli kiseme kumhusu mwenye kukifanya: “Hakuonyesha uelewaji”?+
17 Je, si muda kidogo sana bado na Lebanoni itafanywa kuwa shamba la matunda+ na shamba hilo la matunda litahesabiwa kuwa kama msitu?+ 18 Na katika siku hiyo viziwi hakika watasikia maneno ya kitabu,+ na kutoka katika mahali penye weusi na kutoka katika giza macho ya vipofu yataona.+ 19 Na wapole+ hakika wataongeza kushangilia kwao katika Yehova, na hata maskini kati ya wanadamu watashangilia katika Mtakatifu wa Israeli,+ 20 kwa sababu mwonevu ataufikia mwisho wake,+ na mwenye kujigamba atakwisha,+ na wale wote wanaokaa macho ili kutenda madhara+ watakatiliwa mbali, 21 wale wanaomwingiza mtu ndani ya dhambi kwa neno lake,+ na wale wanaotega mtego kwa ajili ya yule anayekaripia langoni,+ na wale wanaomsukuma kando mwadilifu kwa mabishano matupu.+
22 Kwa hiyo Yehova amesema hivi kwa nyumba ya Yakobo, yeye aliyemkomboa Abrahamu:+ “Yakobo sasa hataona aibu, wala uso wake sasa hautabadilika rangi;+ 23 kwa maana wakati anapowaona watoto wake, kazi ya mikono yangu, katikati yake,+ watalitakasa jina langu,+ nao hakika watamtakasa Mtakatifu wa Yakobo,+ nao watamheshimu Mungu wa Israeli.+ 24 Na wale wanaokosea katika roho yao kwa kweli watakuja kuujua uelewaji, na hata wale wanaonung’unika watajifunza mafundisho.”+
30 “Ole wao wana wakaidi,”+ asema Yehova, “wale walio na mwelekeo wa kutekeleza shauri, lakini si la kutoka kwangu;+ na kumimina toleo la kinywaji, lakini si kwa roho yangu, ili kuongeza dhambi juu ya dhambi;+ 2 wale wanaojitayarisha kushuka kwenda Misri+ na ambao hawakuuliza kutoka kinywani mwangu,+ ili kupata kinga katika ngome ya Farao na kupata kimbilio katika kivuli cha Misri!+ 3 Na ngome ya Farao itakuwa kwenu sababu ya kuona aibu,+ na kimbilio katika kivuli cha Misri sababu ya kufedheheka.+ 4 Kwa maana wakuu wake wamekuja kuwa katika Soani,+ na wajumbe wake wamefika hata Hanesi. 5 Kila mtu hakika atakionea aibu kikundi cha watu ambacho hakimletei mtu faida, ambacho hakina msaada wala hakileti faida, lakini husababisha aibu na pia husababisha shutuma.”+
6 Tangazo juu ya wanyama wa kusini:+ Katika nchi ya taabu na hali ngumu,+ ya simba na chui anayenguruma, ya kipiri na nyoka wa moto anayeruka,+ juu ya mabega ya punda wakomavu wanabeba mali zao, na akiba zao juu ya nundu za ngamia.+ Havitakuwa na faida kwa ajili ya watu. 7 Na Wamisri ni ubatili mtupu, nao watasaidia bure tu.+ Kwa hiyo nimemwita huyu: “Rahabu+—kazi yao ni kuketi tuli.”
8 “Sasa njoo, iandike juu ya bamba pamoja nao, na uiandike katika kitabu,+ ili itumike kwa ajili ya siku ya baadaye, kuwa ushahidi mpaka wakati usio na kipimo.+ 9 Kwa maana wao ni watu waasi,+ wana wasiosema kweli,+ wana ambao hawataki kuisikia sheria ya Yehova;+ 10 ambao wamewaambia wale wanaoona, ‘Msione,’ na wale wanaopata maono, ‘Msione maono ya mambo manyoofu kwa ajili yetu.+ Tuambieni mambo laini; oneni maono ya mambo ya udanganyifu.+ 11 Geukeni kando kutoka njiani; ondokeni katika pito.+ Mkomesheni Mtakatifu wa Israeli kwa ajili yetu.’”+
12 Kwa hiyo Mtakatifu wa Israeli amesema hivi: “Kwa sababu ya ninyi kulikataa neno hili,+ na kwa kuwa mnategemea upunjaji na yaliyo ya hila na ninyi mnajitegemeza juu yake,+ 13 kwa hiyo kosa hili litakuwa kwenu kama sehemu iliyovunjika ambayo inakaribia kuanguka, uvimbe katika ukuta ulioinuliwa juu sana,+ ambao kubomoka kwake kunaweza kuja kwa ghafula, mara moja.+ 14 Na hakika mtu atauvunja kama vile mtungi mkubwa wa wafinyanzi unavyovunjwa,+ kupondwa vipande-vipande bila mtu kuuachilia, hivi kwamba kati ya vipande vyake vilivyopondwa hakuwezi kupatikana kigae kinachoweza kutumiwa kukusanya moto jikoni wala kuteka maji kutoka eneo lenye matope.”+
15 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Mtakatifu wa Israeli,+ amesema hivi: “Mkirudi na kupumzika mtaokolewa. Nguvu zenu zitakuwa tu katika kukaa bila usumbufu na katika kutegemea.”+ Lakini hamkutaka.+ 16 Nanyi mkasema: “Hapana, bali tutakimbia juu ya farasi!”+ Ndiyo sababu mtakimbia. “Nasi tutapanda juu ya farasi wepesi!”+ Ndiyo sababu wale wanaowafuatilia ninyi watajionyesha kuwa wepesi.+ 17 Watu elfu moja watatetemeka kwa sababu ya kemeo la mmoja;+ mtakimbia kwa sababu ya kemeo la watano mpaka mtakapokuwa mmebaki kama mlingoti juu ya kilele cha mlima na kama ishara juu ya kilima.+
18 Na kwa hiyo Yehova ataendelea kutarajia kuwaonyesha ninyi kibali,+ na kwa hiyo atasimama ili kuwaonyesha ninyi rehema.+ Kwa maana Yehova ni Mungu wa hukumu.+ Wenye furaha+ ni wale wote wanaoendelea kumtarajia.+ 19 Wakati watu walio katika Sayuni+ watakapokaa katika Yerusalemu,+ wewe hutalia kwa vyovyote.+ Yeye hakika atakuonyesha kibali unapotoa sauti ya kilio chako; mara tu atakapokisikia kwa kweli atakujibu.+ 20 Na Yehova hakika atawapa ninyi mkate kwa namna ya taabu na maji kwa namna ya ukandamizaji;+ na bado Mfundishaji wako Mkuu hatajificha tena, na macho yako yatakuwa macho yanayomwona Mfundishaji Mkuu wako.+ 21 Na masikio yako yatasikia neno nyuma yako likisema: “Hii ndiyo njia.+ Tembeeni ndani yake,” iwe mtakwenda upande wa kuume au iwe mtakwenda upande wa kushoto.+
22 Nanyi mtakitia unajisi kifuniko cha sanamu zenu za kuchongwa za fedha+ na kifuniko kinachobana cha sanamu yenu ya kuyeyushwa+ ya dhahabu.+ Utazitawanya.+ Kama mwanamke mwenye hedhi, utaiambia hivi: “Uchafu mtupu!”+ 23 Naye hakika ataleta mvua kwa ajili ya mbegu yako unayoipanda katika udongo,+ na mkate kuwa mazao ya udongo, ambao utakuwa mnono na wenye mafuta.+ Mifugo yako italisha katika siku hiyo katika malisho mapana.+ 24 Na ng’ombe na punda wakomavu wanaolima udongo watakula chakula kilichokolezwa kwa mboga chungu, ambacho kilipepetwa kwa sepetu+ na kwa uma. 25 Na juu ya kila mlima mrefu na juu ya kila kilima kirefu kutakuja kuwa na vijito,+ mitaro ya maji, katika siku ile ya mauaji makubwa wakati minara itakapoanguka.+ 26 Na nuru ya mwezi mpevu itakuwa kama nuru ya jua linaloangaza; na ile nuru ya jua linaloangaza itaongezeka mara saba,+ kama nuru ya siku saba, siku ile Yehova atakapofunga mvunjiko+ wa watu wake na kuliponya+ jeraha kali linalotokana na pigo kutoka kwake.
27 Tazama! Jina la Yehova linakuja kutoka mbali, likiwaka kwa hasira+ yake na kwa mawingu mazito. Na midomo yake imejaa shutuma, na ulimi wake ni kama moto unaoteketeza.+ 28 Na roho yake ni kama mto unaofurika ambao hufika mpaka shingoni,+ ili kuyarusha mataifa huku na huku kwa kichujio+ cha ubatili; na lijamu+ inayomfanya mtu kwenda huku na huku itakuwa katika taya za vikundi vya watu.+ 29 Ninyi mtakuwa na wimbo+ kama ule wakati wa usiku ambapo mtu hujitakasa kwa ajili ya sherehe,+ na kushangilia kwa moyo kama kule kwa mtu anayetembea akiwa na filimbi+ ili kuingia katika mlima wa Yehova,+ kwa Mwamba wa Israeli.+
30 Na Yehova hakika atafanya utukufu wa sauti+ yake usikiwe naye atafanya kushuka kwa mkono wake kuonekane,+ katika kuwaka kwa hasira+ na mwali wa moto unaoteketeza+ na tufani ya mvua na dhoruba ya mvua+ na mawe ya mvua.+ 31 Kwa maana Ashuru itaingiwa na woga kwa sababu ya sauti ya Yehova;+ yeye ataipiga kwa fimbo.+ 32 Na kila pigo la fimbo yake ya kutia adabu ambayo Yehova atafanya itue juu ya Ashuru hakika litakuwa pamoja na matari na vinubi;+ naye kwa kweli atapiga vita juu yao kwa mtikiso wa silaha za vita.+ 33 Kwa maana Tofethi+ yake imepangwa kuanzia majuzi; pia imetayarishwa kwa ajili ya mfalme mwenyewe.+ Yeye amefanya fungu lake liwe na kina kirefu. Kuna moto na kuni kwa wingi. Pumzi ya Yehova, kama mto wa kiberiti, inawaka juu yake.+
31 Ole wao wanaoshuka kwenda Misri kutafuta usaidizi,+ wale wanaotegemea farasi+ ambao si kitu, na wanaotegemea magari ya vita,+ kwa sababu ni mengi, na kutegemea farasi wa vita, kwa sababu wana nguvu sana, lakini ambao hawakumtazama Mtakatifu wa Israeli wala kumtafuta Yehova mwenyewe.+ 2 Na yeye pia ana hekima+ na ataleta msiba,+ naye hakuyatangua maneno yake;+ na hakika yeye atasimama kushindana na nyumba ya watenda-maovu+ na kushindana na usaidizi wa wale wanaozoea kufanya mambo yenye kudhuru.+
3 Hata hivyo, Wamisri ni watu wa udongo,+ wala si Mungu; na farasi wao ni nyama,+ wala si roho. Na Yehova mwenyewe atanyoosha mkono wake, na yeye anayetoa usaidizi atajikwaa, na yeye anayesaidiwa ataanguka,+ nao wote watafikia mwisho wakati mmoja.
4 Kwa maana Yehova ameniambia hivi: “Kama simba anavyonguruma, mwana-simba mwenye manyoya shingoni,+ juu ya mawindo yake, wakati hesabu kamili ya wachungaji wanapokusanywa kupigana naye, na ijapokuwa sauti yao yeye haingiwi na woga na ijapokuwa kelele zao yeye hatainama; vivyo hivyo Yehova wa majeshi atashuka ili kupiga vita juu ya Mlima Sayuni na juu ya kilima chake.+ 5 Kama ndege wanaoruka, vivyo hivyo Yehova wa majeshi atamlinda Yerusalemu.+ Atamlinda, yeye pia hakika atamkomboa.+ Atamwokoa, pia atamponya.”
6 “Rudini+ kwake Yeye ambaye wana wa Israeli wamemwasi kabisa.+ 7 Kwa maana katika siku hiyo watakataa kila mmoja miungu yake ya fedha isiyo na thamani na miungu yake ya dhahabu isiyo na thamani,+ ambayo mikono yenu imewafanyizia ninyi kuwa dhambi.+ 8 Na Mwashuru ataanguka kwa upanga, si ule wa mwanadamu; na upanga, si ule wa mtu wa udongo, utamla.+ Naye atakimbia kwa sababu ya upanga, na wanaume wake vijana watafanyishwa kazi ya kulazimishwa. 9 Na mwamba wake mwenyewe utapitilia mbali kwa sababu ya woga mtupu, na kwa sababu ya ishara+ wakuu wake wataingiwa na woga,” asema Yehova, ambaye nuru yake iko katika Sayuni na ambaye tanuru+ yake iko katika Yerusalemu.
32 Tazama! Mfalme+ atatawala kwa ajili ya uadilifu;+ nao wakuu+ watatawala wakiwa wakuu kwa ajili ya haki. 2 Na kila mmoja atakuwa kama mahali pa kujificha kutokana na upepo na mahali pa kujificha kutokana na dhoruba ya mvua,+ kama vijito vya maji katika nchi isiyo na maji,+ kama kivuli cha mwamba mzito katika nchi iliyochoka.+
3 Na macho ya wale wanaoona hayatafungamanishwa pamoja, na masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.+ 4 Na moyo wa wale walio na haraka kupita kiasi utafikiria ujuzi,+ na hata ulimi wa wenye kigugumizi utasema upesi mambo yaliyo wazi.+ 5 Mtu asiye na akili hataitwa tena mkarimu; naye mtu asiye na msimamo hatasemwa kuwa ni mheshimiwa;+ 6 kwa sababu mtu asiye na akili atasema upumbavu mtupu,+ na moyo wake utatenda madhara,+ utatenda uasi-imani+ na kusema juu ya Yehova mambo mapotovu, utasababisha nafsi ya mwenye njaa kushinda bila kula,+ naye anasababisha hata mtu mwenye kiu ashinde bila maji ya kunywa. 7 Naye mtu asiye na msimamo, vyombo vyake ni vibaya;+ yeye ametoa shauri kwa ajili ya matendo ya mwenendo mpotovu,+ kuwavunja wenye kuteseka kwa maneno ya uwongo,+ hata maskini anaposema jambo lililo haki.
8 Naye mtu mkarimu, ametoa shauri kwa ajili ya mambo ya ukarimu; naye atasimama kwa ajili ya mambo ya ukarimu.+
9 “Enyi wanawake mnaostarehe, simameni, sikilizeni sauti yangu!+ Enyi binti msiojali, litegeeni sikio neno langu! 10 Katika muda wa mwaka mmoja na siku fulani ninyi msiojali mtafadhaika,+ kwa sababu uvunaji wa zabibu utakuwa umefikia mwisho lakini hakuna mavuno ya matunda yatakayoingizwa ndani.+ 11 Tetemekeni, enyi wanawake mnaostarehe! Fadhaikeni, enyi msiojali! Vueni nguo na kuwa uchi, na kuvaa nguo za magunia viunoni.+ 12 Jipigeni vifua katika kuomboleza+ juu ya mashamba yenye kutamanika,+ juu ya mzabibu wenye kuzaa matunda. 13 Juu ya udongo wa watu wangu inatokea miiba mitupu,+ vichaka vyenye miiba, kwa maana viko juu ya nyumba zote zenye furaha, ndiyo, mji uliochangamka sana.+ 14 Kwa maana mnara wa makao umeachwa,+ kelele za jiji zimeachwa; Ofeli+ na mnara wa mlinzi umekuwa nyika, kwa wakati usio na kipimo furaha ya punda-milia, malisho ya makundi; 15 mpaka roho itakapomiminwa juu yetu kutoka juu,+ na nyika itakuwa imekuwa shamba la matunda, na shamba la matunda lihesabiwe kuwa msitu halisi.+
16 “Na katika nyika haki itakaa, nao uadilifu utakaa katika shamba la matunda.+ 17 Na kazi ya uadilifu wa kweli itakuwa amani;+ na utumishi wa uadilifu wa kweli utakuwa utulivu na usalama mpaka wakati usio na kipimo.+ 18 Na watu wangu watakaa katika makao yenye amani na katika makao ya uhakika kamili na katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.+ 19 Na hakika kutanyesha mvua ya mawe wakati msitu utakaposhuka+ na jiji kuteremka katika hali ya kushushwa.+
20 “Wenye furaha ni ninyi mnaopanda mbegu kando ya maji yote,+ mkiifungua miguu ya ng’ombe na ya punda.”+
33 Ole wako wewe unayepora, bila wewe mwenyewe kuporwa, na wako wewe unayetenda kwa hila, bila wengine kukutendea kwa hila!+ Mara tu utakapokuwa umemaliza kupora, wewe nawe utaporwa.+ Mara tu utakapokuwa umemaliza kutenda kwa hila, wao watakutendea kwa hila.+
2 Ee Yehova, tuonyeshe kibali.+ Tumekutumaini wewe.+ Uwe mkono+ wetu kila asubuhi,+ ndiyo, wokovu wetu wakati wa taabu.+ 3 Vikundi vya watu vimekimbia kwa sababu ya sauti ya machafuko.+ Mataifa yametawanywa wakati uliposimama.+ 4 Na nyara+ yenu kwa kweli itakusanywa kama wakati mende wanapokusanyika, kama mmiminiko wa makundi ya nzige unaomiminika juu ya mtu.+ 5 Yehova hakika atainuliwa juu,+ kwa maana yeye anakaa kileleni.+ Ataijaza Sayuni haki na uadilifu.+ 6 Na kutegemeka kwa nyakati zako kutakuwa mali ya wokovu+—hekima na ujuzi,+ kumwogopa Yehova,+ ambazo ni hazina yake.
7 Tazama! Mashujaa wao wenyewe wamepaaza kilio barabarani; wajumbe wa amani+ watalia kwa uchungu. 8 Njia kuu zimefanywa ukiwa;+ mwenye kutembea juu ya njia amekoma.+ Amelivunja agano;+ ameyadharau majiji;+ hamhesabu kuwa kitu mwanadamu anayeweza kufa.+ 9 Nchi imeomboleza, imenyauka.+ Mlima Lebanoni umefedheheshwa;+ umeoza. Sharoni+ imekuwa kama nchi tambarare ya jangwani; na Bashani na Karmeli inakung’uta majani yao.+
10 “Sasa nitasimama,”+ asema Yehova, “sasa nitajikweza;+ sasa nitajiinua juu.+ 11 Ninyi mnachukua mimba ya majani makavu;+ mtazaa majani makavu. Roho yenu wenyewe, kama moto,+ itawateketeza ninyi.+ 12 Na vikundi vya watu vitakuwa kama miteketezo ya chokaa. Watawashwa moto kama miiba iliyokatwa.+ 13 Sikieni, ninyi mlio mbali, jambo nitakalofanya!+ Na jueni, ninyi mlio karibu, nguvu zangu.+ 14 Watenda-dhambi wamekuwa na hofu katika Sayuni;+ mtetemeko umewashika waasi-imani:+ ‘Ni nani kati yetu anayeweza kukaa kwa muda na moto unaoteketeza?+ Ni nani kati yetu anayeweza kukaa kwa muda wowote pamoja na mioto inayodumu muda mrefu?’+
15 “Kuna yule anayetembea katika uadilifu+ wenye kuendelea na kusema jambo la unyoofu,+ anayekataa pato lisilo la haki kutoka kwa wapunjaji,+ anayetikisa mikono yake kabisa kukataa rushwa,+ anayeziba sikio lake lisisikilize umwagaji wa damu, na anayefunga macho yake ili yasione jambo baya.+ 16 Yeye ndiye atakayekaa juu katika vilele;+ kilele chake kilicho salama kitakuwa mahali penye miamba ambapo ni pagumu kufikiwa.+ Hakika atapewa mkate wake;+ chemchemi yake ya maji haitaisha.”+
17 Macho yako yatamwona mfalme katika uzuri wake;+ yataona nchi iliyo mbali.+ 18 Moyo wako utatoa maelezo kwa sauti za chini+ juu ya jambo lenye kuogopesha: “Mwandishi yuko wapi? Anayetoa malipo yuko wapi?+ Anayehesabu minara yuko wapi?”+ 19 Hutaona watu wenye dharau, watu wenye lugha ngumu mno kuweza kuisikiliza, wenye ulimi ulio na kigugumizi usiweze kuuelewa.+ 20 Tazama Sayuni,+ mji wa pindi zetu za sherehe!+ Macho yako mwenyewe yataliona Yerusalemu likiwa makao yasiyo na usumbufu, hema ambalo hakuna atakayelikunja.+ Vigingi vyake vya mahema havitang’olewa kamwe, wala hata kamba yake moja haitakatwa.+ 21 Lakini huko Mwenye Utukufu,+ Yehova, atakuwa kwetu mahali pa mito,+ pa mifereji mipana. Kundi lolote la merikebu halitapita juu yake, wala hakuna meli yenye utukufu itakayopita juu yake. 22 Kwa maana Yehova ni Mwamuzi+ wetu, Yehova ni Mpaji-sheria+ wetu, Yehova ni Mfalme+ wetu; yeye mwenyewe atatuokoa.+
23 Kamba zako zitalegea; hazitashika mlingoti wake usimame imara; hawakutandaza tanga.
Wakati huo nyara kwa wingi zitagawanywa; vilema nao kwa kweli watachukua nyara kubwa.+ 24 Na hakuna mkaaji atakayesema: “Mimi ni mgonjwa.”+ Watu wanaokaa katika nchi hiyo watakuwa wamesamehewa kosa lao.+
34 Njooni karibu, enyi mataifa, ili msikie;+ nanyi vikundi vya taifa,+ kazeni uangalifu. Dunia na vyote vilivyomo na visikilize,+ nchi yenye kuzaa+ na mazao yake yote.+ 2 Kwa maana Yehova ana hasira juu ya mataifa yote,+ na ghadhabu juu ya jeshi lao lote.+ Yeye atawaangamiza; atawatoa wauawe.+ 3 Na watu wao waliouawa watatupwa nje; na harufu mbaya ya mizoga yao itapaa;+ na milima itayeyuka kwa sababu ya damu yao.+ 4 Na wale wote wa jeshi la mbingu wataoza. Na mbingu zitakunjwa,+ kama vile kitabu cha kukunjwa;+ na jeshi lao lote litanyauka, kama vile majani yanavyonyauka na kuanguka kutoka kwenye mzabibu na kama tini iliyonyauka na kuanguka kutoka kwenye mtini.+
5 “Kwa maana upanga+ wangu hakika utaloweshwa mbinguni. Tazama! Utashuka juu ya Edomu,+ na juu ya watu ambao nimewatenga ili niwaangamize+ katika haki. 6 Yehova ana upanga; nao utajazwa damu;+ utalainishwa kwa mafuta, kwa damu ya wana-kondoo dume na mbuzi-dume, kwa mafuta+ ya figo za kondoo-dume. Kwa maana Yehova ana dhabihu katika Bosra, na machinjo makubwa katika nchi ya Edomu.+ 7 Na ng’ombe-mwitu+ watateremka pamoja nao, na ng’ombe wachanga pamoja na wenye nguvu;+ na nchi yao itajaa damu, na mavumbi yao yatapakwa mafuta.”+
8 Kwa maana Yehova ana siku ya kisasi,+ mwaka wa malipo kwa ajili ya kesi juu ya Sayuni.+
9 Na mito yake itabadilishwa iwe lami, na mavumbi yake yawe kiberiti; na nchi yake itakuwa kama lami inayowaka.+ 10 Haitazimwa wakati wa mchana wala wakati wa usiku; moshi wake utaendelea kupaa mpaka wakati usio na kipimo.+ Atakauka kutoka kizazi hata kizazi;+ milele na milele hakuna atakayevuka katikati yake.+ 11 Na mwari na nungunungu watammiliki, na bundi wenye masikio marefu na kunguru watakaa ndani yake;+ na yeye atanyoosha juu yake kamba ya kupimia+ ya utupu na mawe ya ukiwa. 12 Watu wake wenye vyeo—hakuna yeyote hapo watakayemwita kwenye ufalme, na wakuu wake wote watakuwa si kitu.+ 13 Miiba itatokea kwenye minara yake ya makao, upupu na magugu yenye miiba katika mahali pake penye ngome;+ naye atakuwa makao ya mbwa-mwitu,+ ua kwa ajili ya mbuni.+ 14 Na wakaaji wa maeneo yasiyo na maji watakutana na wanyama wanaopiga mayowe, na hata roho mwovu mwenye umbo la mbuzi+ atamwita mwenzake. Ndiyo, hapo babewatoto atastarehe na kujipa mahali pa kupumzika.+ 15 Nyoka-pili ametengeneza kiota chake hapo na kutaga mayai, naye atayaangua na kuyakusanya pamoja chini ya kivuli chake. Ndiyo, ndege-mbua+ watajikusanya hapo, kila mmoja na mwenzake.
16 Mjitafutie wenyewe katika kitabu+ cha Yehova na msome kwa sauti: hakuna hata mmoja wao amekosekana;+ kwa kweli kila mmoja wao hakosi kuwa na mwenzake, kwa maana kinywa cha Yehova ndicho kimeamuru,+ na roho yake ndiyo imewakusanya pamoja.+ 17 Na ni Yeye amewapigia kura, na mkono wake mwenyewe umewagawia mahali hapo kwa kamba ya kupimia.+ Wataimiliki mpaka wakati usio na kipimo; watakaa ndani yake kizazi baada ya kizazi.
35 Nyika na nchi isiyo na maji itafurahi;+ na nchi tambarare ya jangwani itakuwa na shangwe na kuchanua maua kama zafarani.+ 2 Itachanua maua+ bila shaka, nayo itashangilia kwa shangwe na kwa kilio cha furaha.+ Itapewa utukufu wa Lebanoni,+ fahari ya Karmeli+ na ya Sharoni.+ Kutakuwa na wale watakaouona utukufu wa Yehova,+ fahari ya Mungu wetu.+
3 Tieni nguvu mikono iliyo dhaifu, na myaimarishe magoti yanayolegea-legea.+ 4 Waambieni wale wanaohangaika moyoni:+ “Iweni na nguvu.+ Msiogope.+ Tazameni! Mungu wenu atakuja na kisasi,+ Mungu akiwa na malipo.+ Yeye mwenyewe atakuja na kuwaokoa ninyi.”+
5 Wakati huo macho ya vipofu yatafunguliwa,+ na masikio ya viziwi yatazibuliwa.+ 6 Wakati huo kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya,+ na ulimi wa bubu utapaaza sauti kwa furaha.+ Kwa maana maji yatakuwa yamebubujika katika nyika, na mito katika nchi tambarare ya jangwani. 7 Na nchi iliyokaushwa na joto itakuwa kama dimbwi lenye matete, na nchi yenye kiu kama mabubujiko ya maji.+ Katika makao ya mbwa-mwitu,+ mahali pao pa kupumzika, patakuwa na majani mabichi na matete na mimea ya mafunjo.+
8 Na hakika kutakuwa na njia kuu hapo,+ ndiyo, njia; nayo itaitwa Njia ya Utakatifu.+ Asiye safi hatapita juu yake.+ Nayo itakuwa kwa ajili ya yule anayetembea katika njia hiyo, wala hakuna wapumbavu watakaotembea huku na huku juu yake. 9 Hakuna simba atakayekuwa hapo, na wanyama-mwitu wenye kunyafua hawatakuja juu yake.+ Hakuna yeyote atakayepatikana hapo;+ na waliokombolewa watatembea hapo.+ 10 Na wale hasa waliokombolewa na Yehova watarudi+ na kuja Sayuni kwa vigelegele vya shangwe;+ na kushangilia kutakuwa juu ya kichwa chao mpaka wakati usio na kipimo.+ Watafikia furaha na kushangilia, na huzuni na kuugua zitakimbia kabisa.+
36 Sasa ikawa katika mwaka wa kumi na nne wa Mfalme Hezekia kwamba Senakeribu+ mfalme wa Ashuru+ akapanda kuja juu ya majiji yote yenye ngome ya Yuda na kuyateka.+ 2 Na mwishowe mfalme wa Ashuru akamtuma Rabshake+ kutoka Lakishi+ kwenda Yerusalemu,+ kwa Mfalme Hezekia, akiwa na jeshi kubwa, naye akasimama tuli kando ya lile bomba+ la kidimbwi cha juu+ kwenye njia kuu ya uwanja wa mfuaji wa nguo.+ 3 Ndipo Eliakimu+ mwana wa Hilkia, aliyekuwa juu ya hiyo nyumba, na Shebna+ mwandishi na Yoa+ mwana wa Asafu+ karani,+ wakatoka nje, wakamjia.
4 Basi Rabshake akawaambia: “Tafadhali, mwambieni Hezekia, ‘Mfalme mkuu,+ mfalme wa Ashuru,+ amesema hivi: “Ni tumaini gani hili ambalo umelitegemea?+ 5 Wewe umesema (lakini hilo ni neno la midomo), ‘Kuna mashauri na nguvu kwa ajili ya vita.’+ Sasa umeweka tegemeo katika nani, hivi kwamba ukaniasi mimi?+ 6 Tazama! Umetegemea usaidizi wa tete hili lililopondeka,+ Misri,+ ambalo, mtu akiliegemea, hakika litaingia mkononi mwake na kuuchoma. Hivyo ndivyo Farao+ mfalme wa Misri alivyo kwa wote wanaomtegemea.+ 7 Nawe ukiniambia, ‘Tumemtegemea Yehova Mungu wetu,’ je, yeye siye ambaye mahali pake pa juu+ na madhabahu zake Hezekia ameondoa,+ huku akiwaambia Yuda na Yerusalemu, ‘Mnapaswa kuinama mbele ya madhabahu hii’?”’+ 8 Basi sasa, tafadhali, mpeni dhamana+ bwana wangu mfalme wa Ashuru,+ nami niwape farasi elfu mbili tuone ikiwa mnaweza kuweka wapanda-farasi juu yao.+ 9 Unawezaje, basi, kugeuza nyuma uso wa gavana mmoja wa watumishi wadogo zaidi wa bwana wangu,+ na huku wewe unategemea Misri kwa ajili ya magari na kwa ajili ya wapanda-farasi?+ 10 Na sasa, je, nimekuja juu ya nchi hii ili kuiharibu bila kupewa mamlaka kutoka kwa Yehova? Yehova mwenyewe aliniambia,+ ‘Nenda juu ya nchi hii, nawe lazima uiharibu.’”+
11 Ndipo Eliakimu+ na Shebna+ na Yoa+ wakamwambia Rabshake:+ “Tafadhali, sema na watumishi wako katika lugha ya Kisiria,+ kwa maana tunasikia; wala usiseme nasi katika lugha ya Wayahudi+ masikioni mwa wale watu walio juu ya ukuta.”+ 12 Lakini Rabshake akasema: “Je, bwana wangu amenituma kusema maneno haya kwenu na kwa bwana wenu? Je, si kwa wale watu ambao wameketi juu ya ukuta, ili wale mavi yao wenyewe na kunywa mkojo wao wenyewe pamoja nanyi?”+
13 Na Rabshake akaendelea kusimama+ na kuita kwa sauti kubwa katika lugha ya Wayahudi,+ naye akaendelea kusema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru.+ 14 Mfalme amesema hivi, ‘Msiache Hezekia awadanganye ninyi,+ kwa maana hawezi kuwakomboa.+ 15 Wala msiache Hezekia awafanye ninyi mkamtegemee Yehova,+ na kusema: “Hakika Yehova atatukomboa.+ Jiji hili halitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 16 Msimsikilize Hezekia, kwa maana mfalme wa Ashuru amesema hivi: “Salimuni amri kwangu,+ mtoke nje mje kwangu, mle kila mtu kutokana na mzabibu wake mwenyewe na kila mtu kutokana na mtini+ wake mwenyewe na mnywe kila mtu maji ya tangi lake mwenyewe,+ 17 mpaka nije na kuwachukua ninyi na kwa kweli niwapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe,+ nchi yenye nafaka na divai mpya, nchi yenye mkate na mashamba ya mizabibu; 18 ili Hezekia asiwashawishi ninyi,+ akisema, ‘Yehova mwenyewe atatukomboa.’ Je, kila mmoja wa miungu ya mataifa ameikomboa nchi yake mwenyewe kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?+ 19 Iko wapi miungu ya Hamathi+ na Arpadi?+ Iko wapi miungu ya Sefarvaimu?+ Na je, imekomboa Samaria kutoka mkononi mwangu?+ 20 Ni miungu gani kati ya miungu yote ya nchi hizi ambayo imeikomboa nchi yao kutoka mkononi mwangu+ hivi kwamba Yehova akomboe Yerusalemu kutoka mkononi mwangu?”’”+
21 Nao wakaendelea kukaa kimya wala hawakumjibu neno lolote,+ kwa maana amri ya mfalme ilisema: “Hampaswi kumjibu.”+ 22 Lakini Eliakimu+ mwana wa Hilkia, aliyekuwa juu ya hiyo nyumba,+ na Shebna+ mwandishi na Yoa+ mwana wa Asafu karani wakaja kwa Hezekia, mavazi yao yakiwa yameraruliwa,+ wakamwambia maneno ya Rabshake.+
37 Na ikawa kwamba mara tu Mfalme Hezekia aliposikia, mara moja akayararua mavazi yake, akavaa nguo za magunia,+ akaingia ndani ya nyumba ya Yehova.+ 2 Na zaidi ya hayo, akamtuma Eliakimu,+ aliyekuwa juu ya hiyo nyumba, na Shebna mwandishi+ na wanaume wazee wa makuhani+ wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa Isaya+ nabii, mwana wa Amozi.+ 3 Nao wakamwambia: “Hezekia amesema hivi, ‘Leo ni siku ya taabu+ na ya kemeo na ya dharau yenye dhihaka,+ kwa maana wana wamefika mpaka kwenye mlango wa tumbo la uzazi, na hakuna nguvu za kuzaa.+ 4 Pengine Yehova Mungu wako atayasikia maneno ya Rabshake,+ ambaye mfalme wa Ashuru bwana wake alimtuma ili kumdhihaki+ Mungu aliye hai, naye kwa kweli atamtoza hesabu kwa ajili ya maneno ambayo Yehova, Mungu wako, ameyasikia.+ Nawe uinue sala+ kwa ajili ya mabaki ambao wanapatikana.’”+
5 Basi watumishi wa Mfalme Hezekia wakaingia kwa Isaya.+ 6 Ndipo Isaya akawaambia: “Mwambieni bwana wenu, ‘Yehova amesema hivi:+ “Usiogope+ kwa sababu ya maneno uliyosikia ambayo watumishi+ wa mfalme wa Ashuru wamesema vibaya kunihusu. 7 Tazama, ninatia roho+ ndani yake, naye atasikia habari+ na kurudi katika nchi yake mwenyewe; nami hakika nitamwangusha kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.”’”+
8 Baada ya hapo Rabshake+ akarudi na kumkuta mfalme wa Ashuru akipigana na Libna,+ kwa maana alikuwa amesikia kwamba ameondoka Lakishi.+ 9 Sasa alisikia ikisemwa hivi kumhusu Tirhaka+ mfalme wa Ethiopia: “Amekuja kupigana nawe.” Aliposikia hayo, akatuma wajumbe+ mara moja kwa Hezekia, na kusema: 10 “Mwambieni hivi Hezekia mfalme wa Yuda, ‘Usiache Mungu unayemtegemea akudanganye,+ na kusema: “Yerusalemu halitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 11 Tazama! Wewe mwenyewe umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru walizitendea nchi zote kwa kuziangamiza,+ na je, wewe mwenyewe utakombolewa?+ 12 Je, miungu+ ya mataifa ambayo mababu zangu waliharibu imeyakomboa,+ naam, Gozani+ na Harani+ na Resefu na wana wa Edeni+ waliokuwa katika Tel-asari? 13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi+ na mfalme wa Arpadi+ na mfalme wa jiji la Sefarvaimu+—wa Hena na wa Iva?’”+
14 Ndipo Hezekia akaichukua ile barua kutoka mkononi mwa wale wajumbe, akaisoma,+ kisha Hezekia akaenda katika nyumba ya Yehova, akaitandaza mbele za Yehova.+ 15 Na Hezekia akaanza kusali kwa Yehova,+ akisema: 16 “Ee Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli,+ unayeketi juu ya makerubi, wewe peke yako ndiye Mungu wa kweli wa falme zote za dunia.+ Wewe mwenyewe umezifanya mbingu na dunia.+ 17 Tega sikio lako, Ee Yehova, usikie.+ Fungua macho yako,+ Ee Yehova, uone, na uyasikie maneno yote ya Senakeribu+ ambayo ametuma ili kumdhihaki Mungu aliye hai.+ 18 Ee Yehova, ni kweli kwamba wafalme wa Ashuru wameziharibu nchi zote, na nchi yao wenyewe.+ 19 Na miungu yao iliteketezwa kwa moto,+ kwa sababu hiyo haikuwa miungu,+ bali kazi ya mikono ya mwanadamu,+ miti na mawe, hivi kwamba wakaiharibu.+ 20 Na sasa, Ee Yehova Mungu wetu,+ utuokoe kutoka mkononi mwake,+ ili falme zote za dunia zijue kwamba wewe, Ee Yehova, ndiye Mungu peke yako.”+
21 Naye Isaya mwana wa Amozi akatuma habari kwa Hezekia, na kusema: “Yehova, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Kwa sababu umesali kwangu kumhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru,+ 22 Yehova amesema neno hili juu yake:
“Bikira, binti Sayuni, amekudharau, amekudhihaki.+
Binti Yerusalemu ametikisa kichwa chake nyuma yako.+
23 Umemdhihaki+ nani na kusema vibaya+ juu yake?
Nawe umepaaza sauti+ yako juu ya nani
Na kuinua macho+ yako juu?
Ni juu ya Mtakatifu wa Israeli!+
24 Umemdhihaki Yehova kupitia watumishi wako, nawe unasema,+
‘Kwa wingi wa magari yangu ya vita, mimi mwenyewe+—
Mimi hakika nitapanda vilele vya maeneo yenye milima,+
Sehemu za mbali zaidi za Lebanoni;+
Nami nitaikata mierezi yake iliyotukuka, miberoshi yake iliyo bora.+
Nami nitaingia katika kilele chake cha mwisho, msitu wa shamba lake la matunda.+
25 Mimi hakika nitachimba na kunywa maji,
Nami nitaikausha mifereji yote ya Nile+ ya Misri kwa nyayo za miguu yangu.’+
26 Je, hujasikia?+ Tangu nyakati za zamani za kale ndilo nitakalofanya.+
Tangu siku zilizopita nimelifanya.+ Sasa nitalitimiza.+
Nawe utafanya majiji yenye ngome yawe ukiwa kama marundo ya mabomoko.+
Watakuwa kama majani ya shambani na majani mabichi yaliyo laini,+
28 Nami najua vema kuketi kwako kimya na kuondoka+ kwako na kuingia kwako,+
Na kujichochea kwako juu yangu,+
29 Kwa sababu kujichochea kwako juu yangu+ na kunguruma kwako kumepanda mpaka ndani ya masikio yangu.+
Nami hakika nitatia kulabu yangu puani mwako na lijamu yangu katikati ya midomo yako,+
Nami hakika nitakurudisha kupitia njia ile uliyoijia.”+
30 “‘Na hii itakuwa ndiyo ishara kwa ajili yako: Mimea inayochipuka kutokana na mbegu zilizoanguka+ italiwa mwaka huu, na katika mwaka wa pili nafaka inayochipuka yenyewe; lakini katika mwaka wa tatu pandeni mbegu, mvune, na mpande mashamba ya mizabibu na kula mazao yake.+ 31 Na wale watakaoponyoka wa nyumba ya Yuda, wale wanaobaki,+ hakika watatia mizizi kwenda chini na kuzaa matunda kwenda juu.+ 32 Kwa maana mabaki+ watatoka katika Yerusalemu na wale wanaoponyoka katika Mlima Sayuni.+ Bidii ya Yehova wa majeshi itatenda hayo.+
33 “‘Kwa hiyo Yehova amesema hivi kumhusu mfalme wa Ashuru:+ “Hataingia katika jiji hili+ wala hatapiga mshale humo, wala kulikabili kwa ngao, wala kujenga juu yake boma la kulizingira.”’+
34 “‘Atarudi kupitia ile njia aliyoijia, naye hataingia ndani ya jiji hili,’ asema Yehova.+ 35 ‘Nami hakika nitalilinda+ jiji hili ili kuliokoa kwa ajili yangu mwenyewe+ na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.’”+
36 Na malaika+ wa Yehova alitoka, akapiga na kuwaua watu 185,000 katika kambi ya Waashuru.+ Watu walipoamka asubuhi na mapema, tazama, wote walikuwa mizoga iliyokufa.+ 37 Basi Senakeribu+ mfalme wa Ashuru akaondoka, akaenda, akarudi,+ akaanza kukaa katika Ninawi.+ 38 Na ikawa kwamba alipokuwa akiinama nyumbani mwa Nisroki+ mungu wake,+ Adrameleki na Shareza, wanawe mwenyewe, wakampiga na kumuua kwa upanga,+ nao wakakimbia, wakaenda katika nchi ya Ararati.+ Na Esar-hadoni+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
38 Katika siku hizo Hezekia akawa mgonjwa kufikia hatua ya kufa.+ Basi Isaya+ mwana wa Amozi nabii akaingia kwake na kumwambia: “Yehova amesema hivi, ‘Wape amri watu wa nyumba yako,+ kwa maana wewe hakika utakufa wala hutaishi.’”+ 2 Ndipo Hezekia akageuza uso wake kuelekea ukuta,+ akaanza kusali kwa Yehova+ 3 na kusema: “Nakuomba, Ee Yehova, tafadhali ukumbuke+ jinsi nilivyotembea+ mbele zako kwa ukweli+ na kwa moyo mkamilifu,+ nami nimetenda yaliyokuwa mema machoni pako.” Na Hezekia akaanza kulia sana.+
4 Sasa neno+ la Yehova likamjia Isaya, kusema: 5 “Nenda, umwambie Hezekia, ‘Yehova, Mungu wa Daudi babu yako+ amesema hivi: “Nimeisikia sala yako.+ Nimeyaona machozi yako.+ Tazama, naongeza miaka kumi na mitano juu ya siku zako;+ 6 nami nitakukomboa wewe pamoja na jiji hili kutoka katika mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitalilinda jiji hili.+ 7 Na hii ndiyo ishara kwa ajili yako kutoka kwa Yehova kwamba Yehova atatenda neno hili ambalo amesema:+ 8 Tazama, ninafanya kivuli cha vipandio ambacho kilikuwa kimeshuka juu ya vile vipandio vya ngazi ya Ahazi kwa sababu ya jua+ kirudi nyuma vipandio kumi.”’”+ Na jua likarudi nyuma polepole vipandio kumi juu ya vipandio vya ngazi ambavyo lilikuwa limeshuka.+
9 Haya ni maandishi ya Hezekia mfalme wa Yuda, aliposhikwa na ugonjwa+ kisha akapona ugonjwa wake.+
10 Mimi nilisema: “Katikati ya siku zangu nitaingia katika malango+ ya Kaburi.*
Nitanyimwa mabaki+ ya miaka yangu.”
11 Nimesema: “Sitamwona Yah, ndiyo, Yah, katika nchi ya walio hai.+
Sitawaona wanadamu tena—pamoja na wakaaji wa nchi ya kukoma.
12 Makao yangu yameng’olewa+ na kuondolewa kwangu kama hema la wachungaji.
Nimeukunja uhai wangu kama mfumaji wa nguo;
Mtu fulani ananikatilia mbali+ kutoka kwenye nyuzi za mtande.
Tangu mapambazuko mpaka usiku unaendelea kunitoa.+
Tangu mapambazuko mpaka usiku wewe unaendelea kunitoa.+
15 Nitasema nini, na kwa kweli yeye ataniambia nini?+
Yeye ametenda pia.+
Ninaendelea kutembea kwa unyamavu miaka yangu yote katika uchungu wa nafsi yangu.+
16 ‘Ee Yehova, kwa sababu hiyo wanaendelea kuishi; na kama ilivyo kwa kila mtu, ndivyo na uhai wa roho yangu.+
Nawe utanirudishia afya na hakika kunihifadhi hai.+
17 Tazama! Kwa ajili ya amani nilipata jambo chungu, ndiyo, chungu;+
Nawe mwenyewe umeshikamana na nafsi yangu na kuizuia kutokana na shimo la uharibifu.+
Kwa maana umezitupa dhambi zangu zote nyuma ya mgongo wako.+
18 Kwa maana Kaburi* haliwezi kukusifu;+ kifo hakiwezi kukusifu.+
Wale wanaoshuka shimoni hawawezi kuutumaini ukweli wako.+
19 Aliye hai, aliye hai, ndiye anayeweza kukusifu,+
Kama vile mimi ninavyoweza leo hii.+
Baba anaweza kuwapa wanawe ujuzi+ kuhusu ukweli wako.
20 Ee Yehova, chukua hatua ya kuniokoa,+ nasi tutapiga nyimbo zangu za kinanda nilizochagua+
Siku zote za maisha yetu katika nyumba ya Yehova.’”+
21 Naye Isaya akasema: “Acha wachukue keki ya tini kavu zilizoshinikizwa na mlipake lile jipu,+ ili apone.”+ 22 Wakati huo Hezekia akasema: “Kuna ishara gani kwamba nitapanda kwenda katika nyumba ya Yehova?”+
39 Wakati huo Marodak-baladani+ mwana wa Baladani mfalme wa Babiloni+ alimtumia Hezekia barua na zawadi,+ baada ya kusikia kwamba alikuwa mgonjwa lakini amepata nguvu tena.+ 2 Basi Hezekia akaanza kushangilia juu yao+ naye akawaonyesha nyumba yake ya hazina,+ fedha na dhahabu na mafuta ya zeri+ na mafuta mazuri na ghala lake lote la silaha+ na vyote vilivyokuwa katika hazina zake. Hakuna kitu chochote ambacho Hezekia hakuwaonyesha katika nyumba yake+ na katika mamlaka yake yote.+
3 Baada ya hapo Isaya nabii akaingia kwa Mfalme Hezekia na kumwambia:+ “Watu hawa walisema nini, nao walitoka wapi wakaja kwako?” Kwa hiyo Hezekia akasema: “Walitoka katika nchi ya mbali kuja kwangu, kutoka Babiloni.”+ 4 Akaendelea kusema: “Waliona nini ndani ya nyumba yako?”+ Naye Hezekia akasema: “Waliona kila kitu kilicho ndani ya nyumba yangu. Hakuna chochote ambacho sikuwaonyesha katika hazina zangu.” 5 Sasa Isaya akamwambia Hezekia:+ “Sikia neno la Yehova wa majeshi, 6 ‘Tazama! Siku zinakuja, na vyote vilivyo ndani ya nyumba yako na ambavyo mababu zako wameweka akiba mpaka leo hii kwa kweli vitachukuliwa kwenda Babiloni.’+ ‘Hakuna chochote kitakachobaki,’+ Yehova amesema. 7 ‘Na baadhi ya wana wako mwenyewe watakaotoka kwako ambao utawazaa, watachukuliwa+ na kuwa maofisa wa makao ya mfalme+ katika jumba la mfalme wa Babiloni.’”+
8 Ndipo Hezekia akamwambia Isaya: “Neno la Yehova ambalo umesema ni jema.”+ Naye akaendelea kusema: “Kwa sababu amani na kweli+ zitaendelea kuwapo katika siku zangu.”+
40 “Wafarijini, wafarijini watu wangu,” asema Mungu wenu.+ 2 “Semeni na moyo wa Yerusalemu+ na kumwambia kwamba utumishi wake wa kijeshi umetimizwa,+ kwamba kosa lake limelipwa.+ Kwa maana kutoka mkononi mwa Yehova amepokea hesabu kamili kwa ajili ya dhambi zake zote.”+
3 Sikilizeni! Mtu fulani anaita nyikani:+ “Fungueni njia ya Yehova!+ Nyoosheni njia kuu kwa ajili ya Mungu wetu katika nchi tambarare ya jangwani.+ 4 Kila bonde na liinuliwe,+ na kila mlima na kilima kishushwe.+ Na nchi yenye matuta itakuwa nchi tambarare, na nchi yenye mawemawe itakuwa nchi tambarare ya bondeni.+ 5 Na utukufu wa Yehova hakika utafunuliwa,+ na wote wenye mwili watauona pamoja,+ kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hayo.”+
6 Sikiliza! Mtu anasema: “Ita!”+ Na mtu akasema: “Niite nini?”
“Wanadamu wote ni majani mabichi, na fadhili zao zote zenye upendo ni kama ua la shambani.+ 7 Majani mabichi yamekauka, ua limenyauka,+ kwa sababu roho ya Yehova imepuliza juu yake.+ Hakika watu ni majani mabichi.+ 8 Majani mabichi yamekauka, ua limenyauka;+ lakini kwa habari ya neno la Mungu wetu, litadumu mpaka wakati usio na kipimo.”+
9 Panda juu ya mlima mrefu,+ wewe mwanamke unayeleta habari njema kwa ajili ya Sayuni.+ Paaza sauti yako kwa nguvu, wewe mwanamke unayeleta habari njema kwa ajili ya Yerusalemu.+ Ipaaze. Usiogope.+ Yaambie majiji ya Yuda: “Tazameni Mungu wenu.”+ 10 Tazama! Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atakuja kama mtu mwenye nguvu, na mkono wake utakuwa ukitawala kwa ajili yake.+ Tazama! Thawabu yake iko pamoja naye,+ na mshahara anaolipa uko mbele zake.+ 11 Atalichunga kundi lake mwenyewe kama mchungaji.+ Atawakusanya pamoja wana-kondoo kwa mkono wake;+ naye atawabeba katika kifua chake.+ Wale wanaonyonya atawaongoza kwa uangalifu.+
12 Ni nani ambaye amepima maji katika mkono wake,+ na kupima vipimo vya mbingu kwa shubiri+ na kuweka katika kipimio mavumbi ya dunia,+ au kupima milima kwa kipimio, na vilima katika mizani? 13 Ni nani ambaye ameipima roho ya Yehova, na ni nani kama mtu wake wa mashauri anayeweza kumjulisha jambo lolote?+ 14 Alishauriana na nani ndipo mtu amfanye aelewe, au ni nani anayemfundisha katika njia ya haki, au kumfundisha ujuzi,+ au kumjulisha njia ya ufahamu wa kweli?+
15 Tazama! Mataifa ni kama tone kutoka katika ndoo; nayo yamehesabiwa kuwa kama mavumbi membamba juu ya mizani.+ Tazama! Anaviinua visiwa+ kama mavumbi membamba tu. 16 Hata Lebanoni hautoshi katika kuendeleza kuwaka kwa moto, na wanyama-mwitu+ wake hawatoshi kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.+ 17 Mbele zake mataifa yote ni kama kitu ambacho hakipo;+ kwake yeye yamehesabiwa kuwa si kitu na kuwa ni ubatili.+
18 Nanyi mnaweza kumfananisha Mungu na nani,+ nanyi mnaweza kuweka kando yake mfano gani?+ 19 Fundi ametengeneza tu sanamu ya kuyeyushwa,+ na fundi wa chuma huifunika kwa dhahabu,+ naye anafua minyororo ya fedha.+ 20 Yeye huchagua mti fulani uwe mchango, mti ambao haujaoza.+ Hujitafutia fundi stadi, ili kutayarisha sanamu ya kuchongwa+ isiyoweza kufanywa iyumbe-yumbe.+
21 Je, ninyi hamjui? Je, hamsikii? Je, hamjaambiwa hilo tangu mwanzo? Je, hamjatumia uelewaji tangu kuwekwa misingi ya dunia?+ 22 Kuna Yeye anayekaa juu ya mviringo wa dunia,+ ambayo wakaaji wake ni kama panzi, Yeye anayetandaza mbingu kama shashi bora, anayezitandaza kama hema la kukaliwa ndani,+ 23 Yeye anayewafanya maofisa wakuu wasiwe kitu, ambaye amewafanya waamuzi wa dunia wawe ubatili mtupu.+
24 Bado hawajapandwa kamwe; bado hawajapandwa mbegu kamwe; bado kisiki chao hakijatia mizizi kamwe duniani.+ Na mtu anahitaji kupuliza tu juu yao nao wanakauka;+ na dhoruba ya upepo itawachukulia mbali kama majani makavu.+
25 “Lakini ninyi mnaweza kunifananisha na nani ili nipate kuwa sawa naye?” asema aliye Mtakatifu.+ 26 “Inueni macho yenu juu, mwone. Ni nani ameviumba vitu hivi?+ Ni Yeye anayelileta jeshi lake kulingana na hesabu, ambaye zote anaziita kwa jina.+ Kutokana na wingi wa nguvu zenye msukumo,+ yeye pia akiwa hodari katika nguvu, hakuna hata moja kati ya hizo inayokosekana.
27 “Kwa sababu gani unasema, Ee Yakobo, na kusema, Ee Israeli, ‘Njia yangu imefichwa kutoka kwa Yehova,+ na haki kwa ajili yangu humkwepa Mungu wangu’?+ 28 Je, hujajua au, je, hujasikia?+ Yehova, Muumba wa miisho ya dunia, ni Mungu mpaka wakati usio na kipimo.+ Yeye hachoki wala hazimii.+ Haiwezekani kuchunguza kikamilifu uelewaji wake.+ 29 Yeye anampa nguvu mtu aliyechoka;+ naye huzijaza nguvu kamili kwa mtu asiye na nguvu zenye msukumo.+ 30 Wavulana watachoka na pia kuzimia, na vijana hakika watajikwaa, 31 lakini wale wanaomtumaini+ Yehova watapata nguvu mpya.+ Wataruka juu kwa mabawa kama tai.+ Watakimbia wala hawatazimia; watatembea wala hawatachoka.”+
41 “Nyamazeni mbele zangu, ninyi visiwa;+ na vikundi vya mataifa+ vipate nguvu mpya. Na wakaribie.+ Na waseme wakati huo. Na tuje karibu pamoja kwa ajili ya hukumu.+
2 “Ni nani ambaye amemwamsha mtu kutoka mashariki?+ Ni nani ambaye katika uadilifu alimwita miguuni pake Yeye, ili kumpa mataifa mbele yake, na ili kumfanya atiishe wafalme?+ Ni nani ambaye aliendelea kuwatoa kama mavumbi kwa upanga wake, hivi kwamba kwa upinde wake wamefukuzwa huku na huku kama majani makavu?+ 3 Ni nani aliyeendelea kuwafuatilia, aliyeendelea kupita kwa amani kwa miguu yake juu ya njia ambayo hakuijia? 4 Ni nani ambaye amekuwa akitenda+ na kufanya hayo, akiviita vizazi tangu mwanzoni?+
“Mimi, Yehova, Yule wa Kwanza;+ na kwa wale wa mwisho mimi ni yuleyule.”+
5 Visiwa+ viliona na kuanza kuogopa. Miisho ya dunia ilianza kutetemeka.+ Walikaribia na kuendelea kuja. 6 Wakawa wakimsaidia kila mmoja mwenzake, na mtu akawa akimwambia ndugu yake: “Uwe na nguvu.”+ 7 Kwa hiyo fundi akamtia nguvu fundi wa chuma;+ yeye anayelainisha kwa nyundo ya chuma akamtia nguvu yeye anayefua kwenye fuawe, akisema hivi kuhusu ile lehemu: “Ni nzuri.” Mwishowe mtu akaipigilia misumari ili isiweze kuyumba-yumba.+
8 “Lakini wewe, Ee Israeli, ni mtumishi wangu,+ wewe, Ee Yakobo, ambaye nimemchagua,+ uzao wa Abrahamu+ rafiki yangu;+ 9 wewe, ambaye nimekushika kutoka miisho ya dunia,+ na wewe, ambaye nimekuita kutoka sehemu zake za mbali.+ Na basi nikakuambia, ‘Wewe ni mtumishi wangu;+ nimekuchagua wewe,+ nami sikukukataa.+ 10 Usiogope, kwa maana mimi nipo pamoja nawe.+ Usitazame huku na huku, kwa maana mimi ni Mungu wako.+ Nitakutia nguvu.+ Nitakusaidia kwelikweli.+ Nitakushika kwelikweli kwa mkono wangu wa kuume+ wa uadilifu.’+
11 “Tazama! Wale wote wanaowaka hasira juu yako wataona aibu na kufedheheshwa.+ Watu wanaogombana nawe watakuwa si kitu na kuangamia.+ 12 Utawatafuta, lakini hutawapata, wale watu wanaopambana nawe.+ Watakuwa kama kitu ambacho hakipo na kama si kitu,+ wale watu wanaokupiga vita. 13 Kwa maana mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika mkono wako wa kuume,+ Mwenye kukuambia, ‘Usiogope.+ Mimi mwenyewe nitakusaidia.’+
14 “Usiogope, wewe Yakobo uliye mdudu,+ ninyi watu wa Israeli.+ Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Yehova, Mkombozi+ wako, Mtakatifu wa Israeli. 15 “Tazama! nimekufanya kuwa chombo cha kupuria,+ kifaa kipya cha kupuria kilicho na meno yenye makali kuwili. Utaikanyaga milima na kuiponda; na vilima utavifanya kuwa kama tu makapi.+ 16 Utawapepeta,+ na upepo utawachukulia mbali,+ na dhoruba ya upepo itawasukuma kwenda njia mbalimbali.+ Nawe mwenyewe utashangilia katika Yehova.+ Utajisifu katika Mtakatifu wa Israeli.”+
17 “Wenye kuteseka na maskini wanatafuta maji,+ lakini hakuna yoyote. Ulimi wao umekauka+ kwa sababu ya kiu.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nitawajibu wao.+ Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha wao.+ 18 Nitafungua mito juu ya vilima vitupu, na mabubujiko katikati ya nchi tambarare za bondeni.+ Nitaifanya nyika kuwa dimbwi la maji lenye matete mengi, na nchi isiyo na maji kuwa chemchemi za maji.+ 19 Katika nyika nitaweka mwerezi, mshita na mhadasi na mfuta.+ Nitaweka mberoshi katika nchi tambarare ya chini ya jangwani, mtidhari na mvinje wakati uleule;+ 20 ili watu waone na kujua na kusikiliza na kuwa na ufahamu wakati uleule, kwamba ni mkono wa Yehova umefanya hayo, na ni Mtakatifu wa Israeli aliyeumba hilo.”+
21 “Leteni mbele kesi yenu ya ubishi,”+ asema Yehova. “Toeni hoja zenu,”+ asema Mfalme wa Yakobo.+ 22 “Leteni na kutuambia mambo ambayo yatatendeka. Mambo ya kwanza—yalikuwa ni nini—semeni, ili tuyatie moyoni mwetu na kujua wakati wake ujao. Au, tufanyeni tuyasikie mambo yanayokuja.+ 23 Semeni mambo ambayo yatakuja baadaye, ili tujue kwamba ninyi ni miungu.+ Ndiyo, mnapaswa kutenda mema au kutenda mabaya, ili tutazame huku na huku na kuyaona wakati uleule.+ 24 Tazama! Ninyi ni kitu ambacho hakipo, na mafanikio yenu si kitu.+ Mtu yeyote anayewachagua ninyi ni chukizo.+
25 “Nimemwamsha mtu kutoka kaskazini, naye atakuja.+ Kutoka mashariki+ ataliitia jina langu. Naye atakuja juu ya watawala-wasaidizi kana kwamba wao ni udongo+ na kama vile mfinyanzi anayekanyagia chini chombo kibichi.
26 “Ni nani ambaye amesema jambo lolote tangu mwanzo, ili tujue, au kutoka nyakati za zamani, ili tuseme, ‘Yeye anasema sawa’?+ Kwa kweli hakuna yeyote anayesema. Kwa kweli hakuna yeyote anayemfanya mtu asikie. Kwa kweli hakuna yeyote anayeyasikia maneno yenu.”+
27 Kuna mmoja kwanza, anayeambia Sayuni: “Tazama! Wako hapa!”+ na kuambia Yerusalemu nitawapa mletaji wa habari njema.+
28 Nami nikaendelea kuona, na, tazama, hapakuwa na mtu; na kutoka kwao waliokuwa hapo hapakuwa pia na yeyote aliyekuwa akitoa shauri.+ Nami nikaendelea kuwauliza, ili watoe jibu. 29 Tazama! Wote ni kitu ambacho hakipo. Kazi zao si kitu. Sanamu zao za kuyeyushwa ni upepo na ubatili.+
42 Tazama! Mtumishi wangu,+ ambaye ninamshika sana!+ Mchaguliwa wangu,+ ambaye nafsi yangu imemkubali!+ Nimetia roho yangu ndani yake.+ Yeye atawatolea mataifa haki.+ 2 Hatapaaza kilio wala kupaaza sauti yake, naye hataacha sauti yake isikike barabarani.+ 3 Hataponda tete lililovunjika;+ wala hatazima utambi wa kitani unaofifia. Ataleta haki katika ukweli.+ 4 Hatafifia wala kupondwa mpaka atakapoweka haki duniani;+ navyo visiwa vitaendelea kuingojea sheria yake.+
5 Mungu wa kweli, Yehova, Muumba wa mbingu+ na Mkuu anayezitandaza;+ Yeye anayeitandaza dunia+ na mazao yake,+ Yeye anayewapa pumzi+ watu walio juu yake,+ na roho wale wanaotembea ndani yake, amesema hivi:+ 6 “Mimi mwenyewe, Yehova, nimekuita katika uadilifu,+ nami nikakushika mkono wako.+ Nami nitakulinda na kukutoa kuwa agano la watu,+ kuwa nuru ya mataifa,+ 7 ili wewe uyafungue macho yenye upofu,+ umtoe mfungwa katika gereza la shimoni,+ uwatoe katika nyumba ya kizuizini wale wanaoketi gizani.+
8 “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu;+ nami sitampa mwingine yeyote utukufu wangu mwenyewe,+ wala sitazipa+ sanamu za kuchongwa sifa yangu.+
9 “Mambo ya kwanza—tazama, yamekuja,+ lakini ninayatangaza mambo mapya. Kabla hayajaanza kutokea, mimi huwafanya ninyi myasikie.”+
10 Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+ sifa yake kutoka mwisho wa dunia,+ ninyi mnaoshuka kwenda baharini+ na kwa vyote vilivyomo ndani yake, ninyi visiwa na ninyi mnaokaa ndani yake.+ 11 Nyika+ na majiji yake na yapaaze sauti yao, makao ambayo Kedari hukaa.+ Wakaaji wa mwamba+ na wapaaze kilio kwa shangwe. Watu na walie kwa sauti kubwa kutoka katika vilele vya milima. 12 Nao wamhesabie Yehova utukufu,+ nao watangaze sifa zake katika visiwa.+
13 Yehova mwenyewe atatokea kama mwanamume mwenye nguvu.+ Ataamsha bidii kama shujaa wa vita.+ Atapaaza sauti, ndiyo, atapiga kelele za vita;+ atajionyesha kuwa mwenye nguvu zaidi juu ya adui zake.+
14 “Nimenyamaza kimya kwa muda mrefu.+ Niliendelea kukaa kimya.+ Niliendelea kujizuia.+ Nitakoroma kama mwanamke anayezaa, nitahema, na kutweta wakati uleule.+ 15 Nitaharibu+ milima na vilima, nami nitakausha majani yake yote. Nami nitaibadili mito iwe visiwa, nitayakausha madimbwi yenye matete mengi.+ 16 Nami nitawafanya vipofu watembee katika njia ambayo hawakuijua;+ nitawafanya wakanyage katika barabara ambayo hawakuijua.+ Nitabadili mahali penye giza mbele yao pawe nuru,+ na nchi ya mawemawe iwe nchi tambarare.+ Hayo ndiyo mambo ambayo nitafanya kwa ajili yao, nami sitawaacha.”+
17 Watarudishwa, wataona aibu sana, wale wanaoitegemea sanamu ya kuchongwa,+ wale wanaoiambia sanamu ya kuyeyushwa: “Ninyi ni miungu yetu.”+
18 Sikieni, ninyi viziwi; na tazameni ili mwone, ninyi vipofu.+ 19 Ni nani aliye kipofu, ikiwa si mtumishi wangu, na ni nani aliye kiziwi kama mjumbe wangu ninayemtuma? Ni nani aliye kipofu kama yule aliyepewa thawabu, au kipofu kama mtumishi wa Yehova?+ 20 Jambo lililohitajika ni kuona mambo mengi, lakini wewe hukuendelea kuangalia.+ Jambo lililohitajika ni kufungua masikio, lakini wewe hukuendelea kusikiliza.+ 21 Yehova mwenyewe, kwa ajili ya uadilifu wake,+ amependezwa kuitukuza sheria+ na kuifanya iwe na utukufu. 22 Lakini ni kikundi cha watu walioporwa na kunyakuliwa,+ wote wakiwa wamenaswa katika mashimo, nao wameendelea kufichwa katika nyumba za kizuizi.+ Wamekuwa kwa ajili ya kuporwa bila mkombozi,+ kwa ajili ya kunyakuliwa bila yeyote wa kusema: “Rudisha!”
23 Ni nani kati yenu atakayetega sikio asikie jambo hili? Ni nani atakayekaza uangalifu na kusikiliza kwa ajili ya nyakati za baadaye?+ 24 Ni nani ambaye amemtoa Yakobo kwa ajili ya kunyakuliwa tu, na Israeli kwa waporaji? Je, si Yehova, Yeye ambaye tumemtendea dhambi, na ambaye hawakutaka kutembea katika njia zake na ambaye hawakuisikiliza sheria yake?+ 25 Kwa hiyo Yeye aliendelea kumwaga ghadhabu juu yake, hasira yake, na nguvu za vita.+ Nayo ikaendelea kumteketeza pande zote,+ lakini hakuangalia;+ nayo ikaendelea kuwaka juu yake, lakini akawa haweki lolote moyoni.+
43 Na sasa Yehova, Muumba+ wako, Ee Yakobo, na Mfanyizaji+ wako, Ee Israeli, amesema hivi: “Usiogope, kwa maana nimekukomboa.+ Nimekuita kwa jina lako.+ Wewe ni wangu.+ 2 Ukipita katikati ya maji,+ nitakuwa pamoja nawe;+ na katikati ya mito, haitafurika juu yako.+ Ukitembea katikati ya moto, hutaungua, wala mwali wa moto hautakuchoma.+ 3 Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wako, Mtakatifu wa Israeli Mwokozi wako.+ Nimetoa Misri kuwa fidia kwa ajili yako,+ Ethiopia+ na Seba badala yako. 4 Kwa sababu umekuwa mwenye thamani machoni pangu,+ umeonwa kuwa mwenye kuheshimika, na mimi mwenyewe nimekupenda.+ Nami nitawatoa watu badala yako, na vikundi vya mataifa badala ya nafsi yako.+
5 “Usiogope, kwa maana nipo pamoja nawe.+ Kutoka mashariki nitauleta uzao wako, nami nitakukusanya pamoja kutoka magharibi.+ 6 Nitaiambia kaskazini,+ ‘Toa!’ na kusini, ‘Usizuie. Walete wanangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka mwisho wa dunia,+ 7 kila mtu ambaye anaitwa kwa jina langu+ na ambaye nimemuumba kwa ajili ya utukufu wangu,+ ambaye nimemfanya, ndiyo, ambaye nimemfanyiza.’+
8 “Leteni kikundi cha watu ambao ni vipofu ingawa macho yapo, na walio viziwi ingawa wana masikio.+ 9 Mataifa yote na yakusanywe mahali pamoja, na vikundi vya mataifa vikusanywe pamoja.+ Ni nani kati yao anayeweza kutangaza haya?+ Au, je, wanaweza kutufanya tusikie mambo ya kwanza?+ Na watoe mashahidi wao,+ ili watangazwe kuwa waadilifu, au wasikie na kusema, ‘Ni kweli!’”+
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,”+ asema Yehova, “mtumishi wangu ambaye nimemchagua,+ ili mjue+ na kuwa na imani katika mimi,+ na ili mwelewe kwamba mimi ni Yeye yuleyule.+ Kabla yangu hakuna Mungu yeyote aliyefanyizwa,+ na baada yangu hapakuendelea kuwapo yeyote.+ 11 Mimi—mimi ni Yehova,+ na zaidi ya mimi hakuna mwokozi.”+
12 “Mimi mwenyewe nimetangaza na kuokoa na kufanya lisikiwe,+ wakati hapakuwa na mungu yeyote mgeni katikati yenu.+ Basi ninyi ni mashahidi wangu,”+ asema Yehova, “nami ni Mungu.+ 13 Pia, wakati wote mimi ni Yeye yuleyule;+ na hakuna yeyote anayekomboa kutoka katika mkono wangu.+ Nitatenda,+ na ni nani anayeweza kuurudisha nyuma?”+
14 Yehova, Mkombozi wenu,+ Mtakatifu wa Israeli,+ amesema hivi: “Nitatuma ujumbe huko Babiloni kwa ajili yenu na kuyashusha mapingo ya magereza,+ na Wakaldayo katika meli kwa vilio vyao vya kulalamika.+ 15 Mimi ni Yehova Mtakatifu wenu,+ Muumba wa Israeli,+ Mfalme wenu.”+
16 Amesema hivi Yehova, Yeye anayefanya njia katikati ya bahari na barabara katikati ya maji yenye nguvu,+ 17 Yeye anayetoa gari la vita na farasi, jeshi na wenye nguvu wakati uleule:+ “Watalala chini.+ Hawataamka.+ Hakika watazimwa.+ Watazimwa kama utambi wa kitani.”+
18 “Msiyakumbuke yale mambo ya kwanza, wala msiyafikirie yale mambo ya zamani. 19 Tazama! Ninafanya jambo jipya.+ Sasa litachipuka. Ninyi mtalijua, sivyo?+ Kwa kweli, nitaweka njia kupitia nyikani,+ kupitia mito ya jangwani.+ 20 Mnyama wa mwituni atanitukuza,+ mbwa-mwitu na mbuni;+ kwa sababu nitakuwa nimewapa maji hata katika nyika, mito katika jangwa,+ ili kuwafanya watu wangu, mchaguliwa wangu,+ wanywe, 21 watu ambao nimejifanyia, ili wasimulie sifa zangu.+
22 “Lakini wewe hukuniita mimi, Ee Yakobo,+ kwa sababu umechoka nami, Ee Israeli.+ 23 Hukuniletea kondoo wa matoleo yako mazima ya kuteketezwa, wala hukunitukuza kwa dhabihu zako.+ Mimi sikukulazimisha unitumikie na zawadi, wala sikukuchosha na ubani.+ 24 Hukuninunulia kwa pesa yoyote kane tamu;+ wala hukunijaza mimi kwa mafuta ya dhabihu zako.+ Kwa kweli umenilazimisha kutumikia kwa sababu ya dhambi zako; umenichosha kwa makosa yako.+
25 “Mimi—mimi ndiye Yeye anayefuta+ makosa+ yako kwa ajili yangu mwenyewe,+ na dhambi zako sitazikumbuka.+ 26 Nikumbushe; na tujiweke hukumuni pamoja;+ toa masimulizi yako kuhusu jambo hilo ili uwe upande wa haki.+ 27 Baba yako, yule wa kwanza, ametenda dhambi,+ na wasemaji wako wamenikosea.+ 28 Kwa hiyo nitawatia unajisi wakuu wa mahali patakatifu, nami nitamtoa Yakobo awe mtu wa kuangamizwa na kumtoa Israeli kwa ajili ya matukano.+
44 “Na sasa sikiliza, Ee Yakobo mtumishi wangu,+ na wewe, Ee Israeli, ambaye nimekuchagua.+ 2 Yehova, Mtengenezaji+ wako na Mfanyizaji+ wako, ambaye aliendelea kukusaidia tangu tumboni,+ amesema hivi, ‘Usiogope,+ Ee mtumishi wangu Yakobo, na wewe, Yeshuruni,+ ambaye nimekuchagua. 3 Kwa maana nitamimina maji juu ya mwenye kiu,+ na vijito vinavyotiririka juu ya mahali pakavu.+ Nitaimimina roho yangu juu ya uzao wako,+ na baraka yangu juu ya wazao wako. 4 Nao watachipuka kama katikati ya majani mabichi,+ kama mierebi+ kando ya mitaro ya maji. 5 Huyu atasema: “Mimi ni wa Yehova.”+ Yule naye atajiita kwa jina la Yakobo,+ na mwingine ataandika juu ya mkono wake: “Mali ya Yehova.” Na mwingine atajiita kwa jina la Israeli.’+
6 “Yehova, Mfalme wa Israeli+ na Mkombozi wake,+ Yehova wa majeshi, amesema hivi, ‘Mimi ndiye wa kwanza na mimi ndiye wa mwisho,+ na zaidi yangu hakuna Mungu.+ 7 Na ni nani aliye kama mimi?+ Na aite, ili alitangaze na kulileta kwangu.+ Tangu wakati nilipowachagua watu wa zamani za kale,+ mambo yanayokuja na vilevile mambo yatakayoingia na wayatangaze. 8 Msiwe na hofu, wala msishangazwe.+ Je, tangu wakati huo mimi sikuwafanya ninyi mmoja mmoja myasikie na kuyatangaza?+ Nanyi ni mashahidi wangu.+ Je, kuna Mungu zaidi ya mimi?+ Hapana, hakuna Mwamba.+ Sikumtambua yeyote.’”
9 Wanaofanya sanamu ya kuchongwa wote ni ubatili,+ na vipenzi vyao hawatakuwa na faida yoyote;+ na wakiwa mashahidi wao hawaoni lolote wala hawajui lolote,+ ili waone aibu.+ 10 Ni nani ambaye amefanya mungu au kutengeneza sanamu ya kuyeyushwa?+ Imekuwa isiyo na faida yoyote.+ 11 Tazama! Wenzake wote wataona aibu,+ na hao mafundi ni kutoka kati ya watu wa udongo. Wote watajikusanya pamoja.+ Watasimama tuli. Watakuwa na hofu. Wataona aibu wakati uleule.+
12 Naye mfuaji wa chuma kwa kutumia tezo, amekuwa akishughulika kufanya hivyo kwa kutumia makaa; naye anaitengeneza kwa nyundo, naye anaendelea kushughulika kufanya hivyo kwa mkono wake wenye nguvu.+ Pia, ameona njaa, na kwa hiyo hana nguvu. Hajanywa maji; kwa hiyo anachoka.
13 Naye mchongaji wa mti, ameinyoosha kamba ya kupimia; huinakili kwa chokaa nyekundu; huitengeneza kwa chombo kinachoparuza mbao; naye huendelea kuinakili kwa bikari, na hatua kwa hatua huifanya kuwa kama mfano wa mtu,+ kama urembo wa mwanadamu, ili iketi ndani ya nyumba.+
14 Kuna mtu ambaye kazi yake ni kukata mierezi; naye huchukua aina fulani ya mti, mti mkubwa, naye huuachilia uwe na nguvu kwa ajili yake mwenyewe kati ya miti ya msituni.+ Aliupanda mlaurusi, na mvua inayonyesha huendelea kuufanya uwe mkubwa. 15 Nao umekuwa kitu cha kutumiwa na mwanadamu ili kufanya moto uendelee kuwaka. Basi yeye huchukua sehemu yake ili aote moto. Kwa kweli yeye huota moto na kuoka mkate. Yeye pia hutengeneza mungu ili apate kumwinamia.+ Ameutengeneza kuwa sanamu ya kuchongwa,+ naye huisujudia. 16 Nusu yake kwa kweli anaiteketeza ndani ya moto. Juu ya nusu yake yeye huchoma vizuri nyama ambayo yeye hula, naye hushiba. Yeye pia huota moto na kusema: “Aha! Nimeota moto. Nimeona nuru ya moto.” 17 Lakini mabaki yake huyafanya kuwa mungu, kuwa sanamu yake ya kuchongwa. Huisujudia na kuinama na kuitolea sala na kusema: “Nikomboe, kwa maana wewe ni mungu wangu.”+
18 Hawajajua,+ wala hawaelewi,+ kwa sababu macho yao yamechafuliwa ili yasione,+ moyo wao ili usiwe na ufahamu.+ 19 Na hakuna mtu anayekumbuka moyoni mwake+ wala kujua wala kuelewa,+ kusema: “Nusu yake nimeiteketeza motoni, nami nimeoka mkate juu ya makaa yake; ninachoma nyama na kula. Lakini je, niyatengeneze mabaki yake yawe chukizo?+ Je, nisujudie ubao wa mti uliokauka?” 20 Anajilisha majivu.+ Moyo wake ambao umedanganywa umempotosha.+ Naye haikomboi nafsi yake, wala hasemi: “Je, hamna uwongo katika mkono wangu wa kuume?”+
21 “Kumbuka mambo haya, Ee Yakobo,+ na wewe, Ee Israeli, kwa sababu wewe ni mtumishi wangu.+ Mimi nimekufanya.+ Wewe ni mtumishi wangu. Ee Israeli, mimi sitakusahau.+ 22 Nitayafutilia mbali makosa yako kana kwamba ni kwa wingu,+ na dhambi zako kana kwamba ni kwa wingu kubwa. Rudi kwangu,+ kwa maana nitakukomboa.+
23 “Pigeni vigelegele kwa shangwe, ninyi mbingu,+ kwa maana Yehova amechukua hatua!+ Pigeni kelele za ushindi,+ ninyi sehemu za chini kabisa za dunia!+ Changamkeni, ninyi milima,+ kwa vigelegele vya shangwe, Ee msitu nanyi miti yote mlio ndani yake! Kwa maana Yehova amemkomboa Yakobo, naye anaonyesha uzuri wake juu ya Israeli.”+
24 Yehova, Mkombozi+ wako na Mfanyizaji wako tangu tumboni, amesema hivi: “Mimi, Yehova, ninafanya mambo yote, mimi peke yangu ninazitandaza mbingu,+ na kuitandaza dunia.+ Ni nani aliyekuwa pamoja nami? 25 Ninazitangua ishara za wenye kuongea maneno matupu, na ni mimi anayewafanya waaguzi watende kiwazimu;+ Yule anayewageuza watu wenye hekima warudi nyuma, na Yule anayeugeuza ujuzi wao kuwa upumbavu;+ 26 Yule anayelitimiza neno la mtumishi wake, na Yule anayelitekeleza kikamilifu shauri la wajumbe wake;+ Yule anayesema kuhusu Yerusalemu, ‘Atakaliwa,’+ na kuhusu majiji ya Yuda, ‘Yatajengwa upya,+ nami nitapainua mahali pake palipofanywa ukiwa’;+ 27 Yule anayekiambia kilindi cha maji, ‘Kauka; nami nitaikausha mito yako yote’;+ 28 Yule anayesema kumhusu Koreshi,+ ‘Yeye ni mchungaji wangu, naye atatenda kikamilifu mapendezi yangu yote’;+ neno langu kuhusu Yerusalemu, ‘Atajengwa upya,’ na kuhusu hekalu, ‘Msingi wako utawekwa.’”+
45 Yehova amemwambia hivi mtiwa-mafuta wake,+ Koreshi, ambaye mkono wake wa kuume nimeushika,+ ili kuyatiisha mataifa mbele yake,+ hivi kwamba nivifungue viuno vya wafalme; nifungue mbele yake milango yenye pande mbili, hivi kwamba hata malango hayatafungwa: 2 “Mimi nitaenda mbele yako,+ nami nitayanyoosha matuta ya nchi.+ Nitavunja vipande-vipande milango ya shaba, nami nitayakata na kuyaangusha mapingo ya chuma.+ 3 Nami nitakupa wewe hazina zilizo katika giza na hazina+ zilizofichwa katika maficho, ili ujue kwamba mimi ni Yehova, Yule anayekuita kwa jina lako,+ Mungu wa Israeli. 4 Nilikuita wewe kwa jina, kwa ajili ya mtumishi wangu Yakobo na kwa ajili ya Israeli mchaguliwa wangu;+ nilikupa jina la heshima, ijapokuwa hukunijua mimi.+ 5 Mimi ni Yehova, na hakuna mwingine yeyote.+ Zaidi ya mimi hakuna Mungu.+ Nitakulinda kwa ukaribu, ingawa hukunijua mimi, 6 ili watu wajue kutoka mashariki na kutoka magharibi ya kuwa hakuna yeyote mwingine zaidi yangu.+ Mimi ni Yehova, na hakuna mwingine yeyote.+ 7 Kufanyiza nuru+ na kuumba giza,+ kufanya amani+ na kuumba msiba,+ mimi, Yehova, ninafanya mambo hayo yote.+
8 “Ninyi mbingu, sababisheni mtiririko kutoka juu;+ na anga zenye mawingu zitiririshe uadilifu.+ Dunia na ifunguke, nayo izae wokovu, nayo ichipushe uadilifu+ wakati uleule. Mimi mwenyewe, Yehova, nimeiumba.”+
9 Ole wake yeye ambaye ameshindana na Mfanyizaji wake,+ kama kigae cha udongo na vigae vingine vya udongo! Je, udongo+ umwambie mfanyizaji wake: “Wewe hutengeneza nini?” Na kitu ulichotengeneza kiseme: “Yeye hana mikono”? 10 Ole wake anayemwambia baba: “Wewe umezaa nini?” na kumwambia mke: “Una uchungu wa kuzaa nini?”+
11 Yehova, Mtakatifu wa Israeli+ na Mfanyizaji+ wake, amesema hivi: “Niulizeni hata mambo ambayo yanakuja+ kuwahusu wanangu;+ na kuhusu utendaji+ wa mikono yangu ninyi mnapaswa kuniamuru. 12 Mimi mwenyewe nimeifanya dunia+ nami nimemuumba mwanadamu juu yake.+ Mimi—mikono yangu mwenyewe imezitandaza mbingu,+ nami nimeliamuru jeshi lake lote.”+
13 “Mimi nimemwamsha mtu katika uadilifu,+ na njia zake zote nitazinyoosha.+ Yeye ndiye atakayelijenga jiji langu,+ na watu wangu walio uhamishoni atawaacha waende zao,+ si kwa bei+ fulani wala kwa rushwa,” Yehova wa majeshi amesema.
14 Yehova amesema hivi: “Wafanyakazi wa Misri+ wasiolipwa na wanabiashara wa Ethiopia na Wasabea,+ watu warefu,+ watakujia wewe, nao watakuwa wako.+ Watatembea nyuma yako; watakuja wamefungwa pingu,+ nao watakuinamia wewe.+ Watasali kwako, wakisema, ‘Kwa kweli Mungu ameungana na wewe,+ na hakuna mwingine yeyote; hakuna Mungu mwingine.’”+
15 Kwa kweli wewe ni Mungu anayejificha,+ Mungu wa Israeli, Mwokozi.+ 16 Hakika wote wataona aibu na kufedheheshwa.+ Watengenezaji wa maumbo ya sanamu watatembea kwa kufedheheka pamoja. 17 Naye Israeli hakika ataokolewa kwa kuwa katika muungano na Yehova+ apate wokovu mpaka nyakati zisizo na kipimo.+ Ninyi hamtaona aibu,+ wala hamtafedheheshwa+ mpaka nyakati zisizo na kipimo za milele.
18 Kwa maana Yehova, Muumba wa mbingu,+ Yeye Mungu wa kweli,+ Mfanyizaji wa dunia na Mtengenezaji wake,+ Yeye aliyeifanya imara,+ ambaye hakuiumba tu bila sababu, ambaye aliiumba ili ikaliwe na watu,+ amesema hivi: “Mimi ni Yehova, wala hakuna mwingine.+ 19 Sikusema katika mahali pa maficho,+ mahali penye giza pa dunia; wala sikuuambia uzao wa Yakobo, ‘Nitafuteni mimi tu bila sababu.’+ Mimi ni Yehova, ninayesema lililo la uadilifu, ninayetangaza lililo la unyoofu.+
20 “Jikusanyeni na kuja.+ Njooni karibu pamoja, ninyi wenye kuponyoka kutoka katika mataifa.+ Wale wanaochukua miti ya sanamu yao ya kuchongwa hawajapata ujuzi wowote, wala wale wanaotoa sala kwa mungu ambaye hawezi kuokoa.+ 21 Toeni habari zenu na ripoti yenu.+ Ndiyo, na washauriane pamoja kwa umoja. Ni nani ambaye amefanya hili lisikiwe tangu zamani za kale?+ Ni nani ambaye ametoa habari zake tangu wakati huo?+ Je, si mimi, Yehova, ambaye hakuna Mungu mwingine zaidi yangu;+ Mungu mwadilifu na Mwokozi,+ kukiwa hakuna mwingine isipokuwa mimi?+
22 “Geukeni mje kwangu mkaokolewe,+ ninyi nyote mlio katika miisho ya dunia; kwa maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine yeyote.+ 23 Nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe+—neno limetoka kinywani mwangu katika uadilifu,+ hivi kwamba halitarudi+—kwamba kila goti litapigwa mbele zangu,+ kila ulimi utaapa,+ 24 ukisema, ‘Hakika kuna uadilifu kamili na nguvu katika Yehova.+ Wale wote wanaomwakia hasira watakuja kwake moja kwa moja na kuona aibu.+ 25 Uzao+ wote wa Israeli utaonekana kuwa sawa+ katika Yehova na watajisifu.’”+
46 Beli+ ameinama,+ Nebo amejikunja; sanamu+ zao zimekuwa za wanyama-mwitu na za wanyama wa kufugwa, mizigo yao, vifurushi, mzigo wa kulemea wanyama waliochoka. 2 Watajikunja; wote watainama pamoja; hawawezi kwa vyovyote kuuponyosha+ mzigo, bali nafsi yao wenyewe itaenda utekwani.+
3 “Nisikilize mimi, Ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote mnaobaki wa nyumba ya Israeli,+ ninyi niliowachukua tangu tumboni, ambao mmechukuliwa toka tumbo la uzazi.+ 4 Hata uzeeni mwa mtu mimi ni Yeye yuleyule;+ na hata wakati wa kichwa chenye mvi cha mtu nitaendelea kubeba.+ Mimi mwenyewe hakika nitatenda,+ ili mimi mwenyewe nichukue na ili mimi mwenyewe nibebe na kuponyosha.+
5 “Ninyi mtanifananisha na nani+ au kunifanya kuwa sawa na nani au kunilinganisha na nani ili tuwe sawasawa?+ 6 Kuna wale wanaotoa dhahabu kwa wingi katika kikoba, nao hupima fedha kwa mizani. Wanamwajiri fundi wa chuma, naye huifanya kuwa mungu.+ Wanasujudu, ndiyo, wanainama.+ 7 Wao huichukua begani,+ huibeba na kuiweka mahali pake ili isimame tuli. Hiyo haisongi kutoka mahali pake inaposimama.+ Mtu hata huililia, lakini haijibu; haimwokoi mtu kutoka katika taabu yake.+
8 “Kumbukeni hili, ili mjipe moyo. Liwekeni moyoni,+ ninyi wakosaji.+ 9 Kumbukeni mambo ya kwanza ya zamani za kale,+ kwamba mimi ni Mungu+ wala hakuna Mungu mwingine,+ wala yeyote kama mimi;+ 10 Yeye anayetangaza tangu mwanzo ule mwisho,+ na kutoka zamani za kale mambo ambayo hayajafanywa;+ Yeye anayesema, ‘Shauri langu mwenyewe litasimama,+ na kila jambo ambalo ni mapenzi yangu nitafanya’;+ 11 Yeye anayemwita ndege mwenye kuwinda kutoka mashariki,+ kutoka nchi ya mbali mtu atakayetekeleza shauri langu.+ Mimi nimesema hilo; pia nitalitimiza.+ Nimelifanyiza, pia nitalitenda.+
12 “Nisikilizeni, ninyi wenye moyo mkaidi,+ ninyi mlio mbali na uadilifu.+ 13 Nimeuleta karibu uadilifu wangu.+ Hauko mbali,+ na wokovu wangu hautachelewa.+ Nami nitaleta wokovu katika Sayuni, na kwa Israeli uzuri wangu.”+
47 Shuka uje uketi mavumbini,+ Ee binti ya Babiloni+ uliye bikira. Keti chini mahali ambapo hakuna kiti cha ufalme,+ Ee binti ya Wakaldayo.+ Kwa kuwa hutaona tena kwamba watu wanakuita wewe mwororo na aliye laini.+ 2 Chukua jiwe la kusagia la mkononi,+ usage unga. Vua shela+ yako. Vua rinda lenye kuning’inia.+ Funua mguu.+ Vuka juu ya mito. 3 Unapaswa kufunua uchi wako.+ Pia, shutuma yako inapaswa kuonekana.+ Nitalipiza kisasi,+ nami sitakutana na mtu yeyote kwa njia ya fadhili.
4 “Kuna Yeye anayetukomboa.+ Yehova wa majeshi ni jina lake,+ Mtakatifu wa Israeli.”+
5 Keti kimya,+ uingie gizani,+ Ee binti ya Wakaldayo;+ kwa kuwa hutaona tena watu wakikuita Bimkubwa+ wa Falme.+ 6 Nilikuwa na ghadhabu kuwaelekea watu wangu.+ Niliutia unajisi urithi wangu,+ nami nikawatia mkononi mwako.+ Hukuwaonyesha rehema zozote.+ Uliifanya nira yako kuwa nzito sana juu ya mzee.+ 7 Nawe uliendelea kusema: “Mpaka wakati usio na kipimo mimi nitakuwa Bimkubwa,+ milele.” Hukuweka mambo haya moyoni mwako; hukukumbuka mwisho wa jambo hilo.+
8 Na sasa sikia jambo hili, wewe mwanamke mwenye kupenda raha, unayeketi katika usalama,+ unayesema moyoni mwako: “Mimi ndiye, wala hakuna mwingine yeyote.+ Sitaketi kama mjane, wala sitajua inavyokuwa kupoteza watoto.”+ 9 Lakini mambo haya mawili yatakujia wewe kwa ghafula,+ katika siku moja: kupoteza watoto na ujane. Yatakuja juu yako kwa kipimo chake kamili,+ kwa ajili ya wingi wa ulozi wako, kwa ajili ya nguvu kamili za maapizo yako—kwa kuzidi mno.+ 10 Nawe uliendelea kuutegemea ubaya wako.+ Wewe umesema: “Hakuna anayeniona.”+ Hekima yako na ujuzi wako+—mambo hayo ndiyo yamekupotosha; nawe unaendelea kusema moyoni mwako: “Mimi ndiye, wala hakuna mwingine yeyote.” 11 Na msiba utakuja juu yako; hutajua uchawi wowote wa kufanya juu yake. Na shida itaanguka juu yako;+ hutaweza kuiepuka. Na uharibifu utakuja juu yako kwa ghafula,+ ambao kwa kawaida huujui.
12 Simama tuli, sasa, na maapizo yako na wingi wa ulozi wako,+ mambo ambayo umeyafanyia kazi ya taabu tangu ujana wako; ili labda uweze kufaidika, ili labda uwatie watu hofu. 13 Umechoka kwa wingi wa washauri wako. Na wasimame, sasa, na kukuokoa, wanaoabudu mbingu, watazamaji wa nyota,+ ambao kwenye miezi mipya wanajulisha habari za mambo yatakayokuja juu yako. 14 Tazama! Wamekuwa kama majani makavu.+ Moto hakika utawateketeza.+ Hawataikomboa nafsi+ yao kutoka katika nguvu za mwali wa moto.+ Hakutakuwa na kuwaka kwa makaa ili watu wajipashie moto, wala nuru ya moto ya kuketi mbele yake. 15 Ndivyo hakika watakavyokuwa kwako, wale ambao umefanya kazi pamoja nao kama wachawi+ wako tangu ujana wako. Kwa kweli watatanga-tanga, kila mmoja kwenda katika eneo lake mwenyewe. Hakutakuwa na yeyote wa kukuokoa.+
48 Sikieni hili, enyi nyumba ya Yakobo, ninyi mnaojiita wenyewe kwa jina la Israeli+ na ambao mmetoka katika maji ya Yuda,+ ninyi mnaoapa kwa jina la Yehova+ na mnaomtaja Mungu wa Israeli,+ si katika kweli na si katika uadilifu.+ 2 Kwa maana wamejiita kuwa wametoka katika jiji takatifu,+ nao wamejitegemeza juu ya Mungu wa Israeli,+ Yehova wa majeshi ni jina lake.+
3 “Mambo ya kwanza nimeyatangaza tangu wakati ule, nayo yalitoka katika kinywa changu mwenyewe, nami nikaendelea kuyafanya yasikiwe.+ Kwa ghafula nilitenda, na mambo yale yakafika.+ 4 Kwa sababu nilijua kwamba wewe ni mgumu+ na kwamba shingo yako ni kano ya chuma+ na paji la uso wako ni shaba,+ 5 mimi pia niliendelea kukuambia tangu wakati ule. Kabla halijaingia, mimi nilikufanya ulisikie,+ ili usiseme, ‘Sanamu yangu mwenyewe imeyafanya, na sanamu yangu ya kuchongwa na sanamu yangu ya kuyeyushwa zimeyaamuru.’+ 6 Wewe umesikia.+ Yatazame yote.+ Na kwa habari yenu, je, hamtalitangaza?+ Nimekufanya usikie mambo mapya tangu wakati huu, hata mambo yaliyohifadhiwa, ambayo hukuyajua.+ 7 Kwa wakati huu yataumbwa, wala si tangu wakati ule, hata mambo ambayo kabla ya leo hukuyasikia, ili usiseme, ‘Tazama! Tayari nimeyajua.’+
8 “Na zaidi ya hayo, wewe hukusikia,+ wala hukujua, wala tangu wakati ule na kuendelea sikio lako halikufunguliwa. Kwa maana najua vema kwamba bila shaka uliendelea kutenda kwa hila,+ nawe umeitwa ‘mkosaji tangu tumboni.’+ 9 Nitaizuia hasira yangu kwa ajili ya jina langu,+ na kwa ajili ya sifa yangu nitajizuia kukuelekea ili usikatiliwe mbali.+ 10 Tazama! Nimekusafisha, lakini si kwa namna ya fedha.+ Nimekuchagua katika tanuru ya kuyeyushia ya mateso.+ 11 Nitatenda kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe nitatenda,+ kwani mtu angewezaje kujiachilia mwenyewe atiwe unajisi?+ Nami sitampa mwingine yeyote utukufu wangu mwenyewe.+
12 “Nisikilize mimi, Ee Yakobo, na wewe Israeli mtu wangu niliyemwita. Mimi ni Yeye yuleyule.+ Mimi ndiye wa kwanza.+ Na zaidi ya hayo, mimi ndiye wa mwisho.+ 13 Na zaidi ya hayo, mkono wangu mwenyewe uliuweka msingi wa dunia,+ na mkono wangu mwenyewe wa kuume ulizitandaza mbingu.+ Ninaziita, ili ziendelee kusimama pamoja.+
14 “Kusanyikeni pamoja, ninyi nyote, msikie.+ Ni nani kati yao ameyatangaza mambo haya? Yehova mwenyewe amempenda.+ Atafanya mapendezi yake juu ya Babiloni,+ na mkono wake mwenyewe utakuwa juu ya Wakaldayo.+ 15 Mimi—mimi mwenyewe nimesema. Na zaidi ya hayo, nimemwita yeye.+ Nimemleta, na njia yake itafanikishwa.+
16 “Njooni karibu nami. Sikieni hili. Tangu mwanzo sikusema kutoka katika mahali pa maficho hata kidogo.+ Tangu wakati wa kutokea kwake mimi nimekuwa pale.”
Na sasa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova mwenyewe amenituma, ndiyo, roho yake.+ 17 Yehova, Mkombozi wako,+ Mtakatifu wa Israeli,+ amesema hivi: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe,+ Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake.+ 18 Laiti ungesikiliza amri zangu!+ Ndipo amani yako ingekuwa kama mto,+ na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.+ 19 Na uzao wako ungekuwa kama tu mchanga, na wazao kutoka tumboni mwako wangekuwa kama chembe zake.+ Jina lake halingekatiliwa mbali wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”+
20 Tokeni katika Babiloni!+ Kimbieni kutoka kwa Wakaldayo.+ Tangazeni kwa sauti ya vigelegele vya shangwe, fanyeni hili lisikiwe.+ Lifanyeni liende mpaka mwisho wa dunia.+ Semeni: “Yehova amemkomboa mtumishi wake Yakobo.+ 21 Nao hawakupata kiu+ alipokuwa akiwatembeza kupitia mahali palipo ukiwa.+ Alitiririsha kwa ajili yao maji kutoka katika mwamba, naye aliupasua mwamba ili maji yatiririke.”+
22 “Hakuna amani,” Yehova amesema, “kwa waovu.”+
49 Nisikilizeni, enyi visiwa,+ na kazeni uangalifu, enyi vikundi vya mataifa vilivyo mbali.+ Yehova mwenyewe ameniita+ tangu tumboni.+ Amelitaja jina langu tangu tumbo la mama yangu.+ 2 Naye akakifanya kinywa changu kuwa kama upanga mkali.+ Amenificha katika kivuli+ cha mkono wake.+ Naye hatua kwa hatua akanifanya kuwa mshale ulionolewa. Alinificha katika podo lake. 3 Naye akaniambia: “Wewe ni mtumishi wangu, Ee Israeli,+ wewe ambaye kwako nitaonyesha uzuri wangu.”+
4 Lakini mimi nikasema: “Nimefanya kazi ya kutaabika bure.+ Nimemaliza nguvu zangu kwa ajili ya jambo lisilo la kweli na la ubatili.+ Kwa kweli hukumu yangu ina Yehova,+ na malipo yangu yana Mungu wangu.”+ 5 Na sasa Yehova, Yeye aliyenifanya tangu tumboni niwe mtumishi wake,+ amesema kwamba nimrudishe Yakobo kwake,+ ili Israeli akusanywe kwake.+ Nami nitatukuzwa machoni pa Yehova, na Mungu wangu atakuwa nguvu zangu. 6 Naye akasema: “Limekuwa si jambo dogo kwako kuwa mtumishi wangu ili kuyainua makabila ya Yakobo na kuwarudisha hata waliolindwa wa Israeli;+ mimi pia nimekutoa uwe nuru ya mataifa,+ ili wokovu wangu ufike katika sehemu ya mwisho ya dunia.”+
7 Yehova, Mkombozi wa Israeli,+ Mtakatifu wake, amemwambia hivi yeye ambaye amedharauliwa katika nafsi,+ yeye ambaye amechukiwa na taifa,+ mtumishi wa watawala:+ “Wafalme wataona na hakika watasimama,+ na wakuu, nao watainama, kwa sababu ya Yehova, ambaye ni mwaminifu,+ Mtakatifu wa Israeli, anayekuchagua.”+
8 Yehova amesema hivi: “Katika wakati wa nia njema nimekujibu,+ na katika siku ya wokovu nimekusaidia;+ nami nikaendelea kukulinda ili nikutoe uwe agano kwa ajili ya watu,+ kuitengeneza upya nchi,+ kuyafanya mafungu ya urithi yaliyofanywa ukiwa yamilikiwe tena,+ 9 kuwaambia wafungwa,+ ‘Tokeni nje!’+ kuwaambia wale walio gizani,+ ‘Jifunueni!’+ Watalisha kando ya njia, na malisho yao yatakuwa kwenye mapito yote yaliyokanyagwa.+ 10 Hawatakuwa na njaa,+ wala kuwa na kiu,+ wala joto kali na jua halitawaunguza.+ Kwa maana Yeye anayewahurumia atawaongoza,+ naye atawaelekeza karibu na mabubujiko ya maji.+ 11 Nami nitaifanya milima yangu yote kuwa njia, na njia zangu kuu zitakuwa juu ya mwinuko.+ 12 Tazama! Hawa watakuja kutoka mbali,+ na, tazama! hawa kutoka kaskazini+ na kutoka magharibi,+ na hawa kutoka katika nchi ya Sinimu.”
13 Toeni kilio cha furaha, ninyi mbingu,+ na uwe na shangwe, Ee dunia.+ Milima na ichangamke kwa kilio kikuu cha furaha.+ Kwa maana Yehova amewafariji watu wake,+ naye anawaonyesha huruma watu wake walioteseka.+
14 Lakini Sayuni akaendelea kusema: “Yehova ameniacha,+ na Yehova mwenyewe amenisahau.”+ 15 Je, mke anaweza kumsahau mtoto wake anayenyonya hivi kwamba asimhurumie mwana wa tumbo lake?+ Hata hawa wanawake wanaweza kusahau,+ lakini mimi mwenyewe sitakusahau wewe.+ 16 Tazama! Nimekuchora juu ya mikono yangu.+ Kuta zako ziko mbele zangu sikuzote.+ 17 Wana wako wamefanya haraka. Walewale wanaokubomoa na kukuangamiza watatoka kwako. 18 Inua macho yako pande zote, uone. Wote wamekusanywa pamoja.+ Wamekujia. “Kama ninavyoishi,” asema Yehova,+ “utajivika hao wote kana kwamba ni kwa mapambo, nawe utajifunga hao kama bibi-arusi.+ 19 Ingawa kuna mahali pako palipoharibiwa na mahali pako palipofanywa ukiwa na nchi ya mabomoko yako,+ ingawa sasa umesongamana mno kuweza kukaliwa, na wale wanaokumeza wamekuwa mbali,+ 20 bado wana wa hali yako ya kufiwa watasema hivi masikioni mwako,+ ‘Mahali hapa pamesongamana mno kuweza kukaliwa nami.+ Nipe nafasi, ili nipate kukaa.’+ 21 Nawe hakika utasema moyoni mwako, ‘Ni nani amekuwa baba ya hawa kwa ajili yangu, kwa kuwa mimi ni mwanamke aliyefiwa na watoto na ni tasa, aliyeenda uhamishoni na kufungwa?+ Na kwa habari ya hawa, ni nani amewalea?+ Tazama! Mimi mwenyewe nilikuwa nimeachwa nyuma peke yangu.+ Hawa—wamekuwa wapi?’”+
22 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama! Nitayainulia mataifa mkono wangu,+ nami nitaviinulia vikundi vya watu ishara yangu.+ Nao wataleta watoto wako katika kifua, nao watawabeba binti zako juu ya bega.+ 23 Na wafalme watakuwa watunzaji kwa ajili yako,+ na binti zao wa kifalme watakuwa wanawake wenye kutunza kwa ajili yako.+ Watakuinamia wewe kifudifudi, nao watayaramba mavumbi ya miguu yako;+ nawe utajua kwamba mimi ni Yehova, ambaye wale wanaonitumaini mimi hawataona aibu.”+
24 Je, wale waliokwisha kuchukuliwa wanaweza kuchukuliwa kutoka kwa mwanamume mwenye nguvu,+ au, je, kundi la mateka wa mwonevu linaweza kuponyoka?+ 25 Lakini Yehova amesema hivi: “Hata kundi la mateka la mwanamume mwenye nguvu litachukuliwa,+ na wale waliokwisha kuchukuliwa na mwonevu wataponyoka.+ Nami nitashindana na mtu yeyote anayeshindana nawe,+ nami nitawaokoa wana wako.+ 26 Nami nitawafanya wale wanaokutendea vibaya waile nyama yao; nao watalewa kwa damu yao kana kwamba ni kwa divai tamu. Na wanadamu wote watajua kwamba mimi, Yehova,+ ni Mwokozi+ wako na Mkombozi+ wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+
50 Yehova amesema hivi: “Basi, kiko wapi cheti cha talaka+ cha mama yenu, ambaye nilimfukuza?+ Au ni nani kati ya wakopeshaji wangu ambaye nimewauza ninyi kwake?+ Tazama! Mmeuzwa kwa sababu ya makosa+ yenu wenyewe, na mama yenu amefukuzwa kwa sababu ya makosa yenu wenyewe.+ 2 Kwa nini basi, nilipoingia, hapakuwa na mtu yeyote?+ Nilipoita, hakuna aliyejibu?+ Je, kweli mkono wangu umekuwa mfupi mno kwamba hauwezi kukomboa,+ au je, ndani yangu hamna nguvu za kukomboa? Tazama! Mimi huikausha bahari+ kwa kemeo+ langu; mimi huifanya mito kuwa nyika.+ Samaki wao hunuka kwa sababu ya maji kukosekana, nao hufa kwa sababu ya kiu.+ 3 Mimi huzifunika mbingu weusi,+ nami hufanya nguo ya gunia iwe kifuniko chake.”+
4 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amenipa ulimi wa waliofundishwa,+ ili nijue jinsi ya kumjibu neno yeye aliyechoka.+ Yeye huamka asubuhi baada ya asubuhi; huliamsha sikio langu ili lisikie kama wale waliofundishwa.+ 5 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova mwenyewe amelifungua sikio langu, nami kwa upande wangu sikuwa mwasi.+ Sikugeuka upande ulio kinyume.+ 6 Mgongo wangu niliwapa washambuliaji, na mashavu+ yangu nikawapa wale wenye kung’oa nywele. Uso wangu sikuuficha kutoka kwa mambo yenye kufedhehesha na mate.+
7 Lakini Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova mwenyewe atanisaidia.+ Ndiyo sababu sitalazimika kufedheheka. Ndiyo sababu nimeufanya uso wangu kama jiwe, nami najua kwamba sitatiwa aibu.+ 8 Yeye anayenitangaza mimi kuwa mwadilifu yupo karibu.+ Ni nani anayeweza kushindana nami? Na tusimame pamoja.+ Ni nani aliye mpinzani wangu katika kesi?+ Na anikaribie.+ 9 Tazama! Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova mwenyewe atanisaidia. Ni nani anayeweza kunitangaza mimi kuwa mwovu?+ Tazama! Wote, kama vazi, watachakaa.+ Nondo atawala wao.+
10 Ni nani kati yenu anayemwogopa+ Yehova, akiisikiliza sauti ya mtumishi wake,+ ambaye ametembea katika giza+ lenye kudumu na ambaye kwa ajili yake kumekuwa hakuna mwangaza? Na alitegemee jina la Yehova+ na kujitegemeza juu ya Mungu wake.+
11 “Tazama! Ninyi nyote mnaowasha moto, mnaowasha cheche, tembeeni katika nuru ya moto wenu, na katikati ya cheche ambazo mmeziwasha moto. Hakika mtapata hili kutoka mkononi mwangu: Mtalala katika maumivu matupu.+
51 “Nisikilizeni mimi, ninyi mnaofuatilia uadilifu,+ ninyi mnaotafuta kumpata Yehova.+ Uangalieni mwamba+ ambao mlichongwa kutoka ndani yake, na tundu la shimo ambalo mlichimbwa kutoka ndani yake. 2 Mwangalieni Abrahamu+ baba yenu+ na Sara+ ambaye hatua kwa hatua aliwazaa ninyi kwa uchungu wa kuzaa mtoto. Kwa maana alikuwa mmoja nilipomwita,+ nami nikambariki na kumfanya kuwa wengi.+ 3 Kwa maana Yehova hakika atamfariji Sayuni.+ Hakika atafariji mahali pake pote palipoharibiwa,+ naye ataifanya nyika yake kuwa kama Edeni+ na nchi yake tambarare ya jangwani kama bustani ya Yehova.+ Furaha na kushangilia zitapatikana ndani yake, kutoa shukrani na sauti ya muziki.+
4 “Nikazieni uangalifu mimi, enyi watu wangu; nanyi kikundi changu cha taifa,+ nitegeeni sikio. Kwa maana sheria itatoka kwangu,+ nami nitaustarehesha uamuzi wangu wa hukumu kama nuru kwa vikundi vya watu.+ 5 Uadilifu wangu uko karibu.+ Wokovu+ wangu hakika utatoka, na mikono yangu itavihukumu vikundi vya watu.+ Visiwa vitanitumaini mimi,+ navyo vitaungojea mkono wangu.+
6 “Inueni macho yenu kuzielekea mbingu,+ na mwitazame dunia chini. Kwa maana mbingu zitatawanywa vipande-vipande kama moshi,+ nayo dunia itachakaa kama nguo,+ na wakaaji wake watakufa kama chawa. Lakini wokovu wangu utadumu mpaka wakati usio na kipimo,+ na uadilifu wangu mwenyewe hautavunjwa.+
7 “Nisikilizeni mimi, ninyi mnaoujua uadilifu, watu ambao sheria yangu imo moyoni mwao.+ Msiogope shutuma ya wanadamu wanaoweza kufa, wala msiingiwe na hofu kwa sababu tu ya maneno yao mabaya.+ 8 Kwa maana nondo atawala wao kana kwamba ni vazi, na nondo wa nguo atawala wao kana kwamba ni sufu.+ Lakini kuhusu uadilifu wangu, utakuwa ni wa mpaka wakati usio na kipimo, na wokovu wangu mpaka vizazi visivyo na hesabu.”+
9 Amka, amka, jivike nguvu,+ Ee mkono wa Yehova!+ Amka kama katika siku za zamani za kale, kama katika vizazi vya nyakati zilizopita zamani.+ Je, si wewe uliyemvunja Rahabu+ vipande-vipande, uliyemchoma kwa silaha yule mnyama mkubwa wa baharini?+ 10 Je, si wewe uliyeikausha bahari, maji ya kilindi kikubwa?+ Uliyevifanya vilindi vya bahari kuwa njia ili watu waliokombolewa wavuke?+ 11 Ndipo watu wa Yehova waliokombolewa watarudi na kuja Sayuni kwa vigelegele vya shangwe,+ na kushangilia kutakuwa juu ya kichwa chao mpaka wakati usio na kipimo.+ Watapata furaha na shangwe.+ Huzuni na kuugua hakika zitakimbia kabisa.+
12 “Mimi—mimi mwenyewe ndiye Yule anayewafariji ninyi.+
“Wewe ni nani kwamba umwogope mwanadamu anayeweza kufa ambaye atakufa,+ na mwanadamu ambaye atafanywa kuwa majani mabichi tu?+ 13 Na kwamba umsahau Yehova Mtengenezaji wako,+ Yeye anayezitandaza mbingu+ na kuweka msingi wa dunia,+ hivi kwamba ulikuwa na hofu sikuzote mchana kutwa kwa sababu ya ghadhabu ya mtu anayekusonga,+ kana kwamba alikuwa amejitayarisha kukuangamiza?+ Na iko wapi ghadhabu ya yule anayekusonga?+
14 “Yeye anayeinama katika minyororo hakika atafunguliwa haraka,+ ili asiende katika kifo shimoni+ na ili mkate wake usikosekane.+
15 “Lakini mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayeichafua bahari ili mawimbi yake yachafuke.+ Yehova wa majeshi ni jina lake.+ 16 Nami nitayatia maneno yangu katika kinywa chako,+ na hakika mimi nitakufunika kwa kivuli cha mkono wangu,+ ili kuzipanda mbingu+ na kuuweka msingi wa dunia+ na kuuambia Sayuni, ‘Ninyi ni watu wangu.’+
17 “Amka, amka, simama, Ee Yerusalemu,+ wewe ambaye umekunywa mkononi mwa Yehova kikombe chake cha ghadhabu.+ Bilauri, kikombe kinachosababisha kuyumba-yumba, umekunywa, umemaliza.+ 18 Hakuna mmoja wa wanawe+ wote aliozaa aliyemwongoza, wala hakuna mmoja wa wanawe wote aliolea aliyemshika mkono wake.+ 19 Hayo mambo mawili yalikuwa yakikuangukia.+ Ni nani atakayekusikitikia?+ Uporaji na mvunjiko, na njaa na upanga!+ Ni nani atakayekufariji wewe?+ 20 Wana wako mwenyewe wamezimia.+ Wamelala chini kichwani pa barabara zote kama kondoo-mwitu katika wavu,+ kama wale ambao wamejaa ghadhabu ya Yehova,+ kemeo la Mungu wako.”+
21 Kwa hiyo tafadhali, sikiliza jambo hili, Ee mwanamke+ aliyeteseka na kulewa, lakini si kwa divai.+ 22 Bwana wako, Yehova, Mungu wako, anayewashindania+ watu wake, amesema hivi: “Tazama! Nitakichukua kutoka mkononi mwako kile kikombe kinachosababisha kuyumba-yumba.+ Ile bilauri, kikombe changu cha ghadhabu—hutarudia kukinywea tena.+ 23 Nami nitakitia mkononi mwa wale wanaokuudhi,+ ambao wameiambia nafsi yako, ‘Inama chini ili tuvuke,’ hivi kwamba ulikuwa ukiufanya mgongo wako kama dunia, na kama barabara kwa ajili ya wale wanaovuka.”+
52 Amka, amka, vaa nguvu zako,+ Ee Sayuni! Vaa mavazi yako mazuri,+ Ee Yerusalemu, jiji takatifu!+ Kwa maana mtu asiyetahiriwa na mtu asiye safi hawataingia ndani yako tena.+ 2 Jitikise uwe huru kutoka mavumbini,+ simama, chukua kiti, Ee Yerusalemu. Jifungue pingu za shingo yako, Ee binti Sayuni uliye mateka.+
3 Kwa maana Yehova amesema hivi: “Ninyi mliuzwa bure,+ nanyi mtakombolewa bila pesa.”+
4 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Watu wangu waliteremka kwenda Misri hapo kwanza ili kukaa wakiwa wageni;+ nayo Ashuru ikawakandamiza bila sababu.”
5 “Na sasa, nina faida gani hapa?” asema Yehova. “Kwa maana watu wangu walichukuliwa bure.+ Wale waliokuwa wakiwatawala waliendelea kupiga mayowe,”+ asema Yehova, “na sikuzote, mchana kutwa, jina langu lilikuwa likivunjiwa heshima.+ 6 Kwa sababu hiyo watu wangu watalijua jina langu,+ kwa sababu hiyo katika siku hiyo, kwa sababu mimi ndiye Yule anayesema.+ Tazama! Ni mimi.”
7 Jinsi inavyopendeza juu ya milima miguu+ ya yeye anayeleta habari njema,+ yeye anayetangaza amani,+ yeye anayeleta habari njema za jambo bora,+ yeye anayetangaza wokovu,+ yeye anayeuambia Sayuni: “Mungu wako amekuwa mfalme!”+
8 Sikiliza! Walinzi+ wako mwenyewe wamepaaza sauti yao.+ Wanaendelea kupiga pamoja vigelegele kwa shangwe; kwa maana wataona jicho kwa jicho+ wakati Yehova atakapokusanya Sayuni tena.+
9 Changamkeni, pigeni pamoja vigelegele kwa shangwe, enyi mahali palipoharibiwa pa Yerusalemu,+ kwa maana Yehova amewafariji watu wake;+ amekomboa Yerusalemu.+ 10 Yehova ameweka wazi mkono wake mtakatifu mbele ya macho ya mataifa yote;+ na miisho yote ya dunia itauona wokovu wa Mungu wetu.+
11 Geukeni, geukeni, tokeni humo,+ msiguse kitu chochote kilicho najisi;+ tokeni katikati yake,+ jiwekeni safi, ninyi mnaovichukua vyombo vya Yehova.+ 12 Kwa maana hamtaondoka na wasiwasi, wala hamtaenda kwa kukimbia.+ Kwa maana Yehova atakuwa akienda mbele yenu,+ na Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi wenu wa nyuma.+
13 Tazama! Mtumishi wangu+ atatenda kwa ufahamu.+ Atakuwa na cheo cha juu na hakika yeye atainuliwa na kutukuzwa sana.+ 14 Kwa kadiri ambavyo wengi wamemtazama kwa mshangao+—sura yake ilikuwa imeharibika sana+ kuliko ya mwanadamu mwingine yeyote na umbo lake lenye fahari+ kuliko lile la wana wa binadamu— 15 vivyo hivyo atayashtua mataifa mengi.+ Wafalme watafunga kinywa chao mbele yake,+ kwa sababu kwa kweli wataona yale ambayo hawakuwa wamepata kusimuliwa, nao watafikiria mambo ambayo hawakuwa wamepata kusikia.+
53 Ni nani aliyeliamini jambo ambalo tumesikia?+ Na kwa habari ya mkono wa Yehova,+ umefunuliwa kwa nani?+ 2 Naye atapanda kama tawi+ mbele ya mtu, na kama mzizi kutoka katika nchi isiyo na maji. Yeye hana umbo la fahari,+ wala utukufu wowote; nasi tutakapomwona, hana sura ili kwamba tumtamani.+
3 Alidharauliwa na kuepukwa na wanadamu,+ mtu aliyekusudiwa maumivu na kuzoeana na ugonjwa.+ Na ilikuwa kana kwamba uso ulifichwa kutoka kwetu.+ Alidharauliwa, nasi tulimhesabu kuwa asiye na maana.+ 4 Kwa kweli yeye mwenyewe aliyachukua magonjwa yetu;+ na kwa habari ya maumivu yetu, yeye aliyabeba.+ Lakini sisi tulimhesabu kama aliyepata mapigo,+ aliyepigwa na Mungu+ na kuteswa.+ 5 Lakini alikuwa akichomwa kwa silaha+ kwa ajili ya ukosaji wetu;+ alikuwa akipondwa kwa ajili ya makosa yetu.+ Adhabu iliyokusudiwa kuleta amani yetu ilikuwa juu yake,+ na kwa sababu ya majeraha+ yake sisi tumeponywa.+ 6 Sisi sote tumeenda huku na huku kama kondoo;+ sisi tumegeuka kwenda kila mmoja kwenye njia yake; na Yehova amefanya kosa letu sote likutane na huyo.+ 7 Alikazwa sana,+ naye alijiachilia ateswe;+ ingawa hivyo hakufungua kinywa chake. Alikuwa akiletwa kama kondoo machinjioni;+ na kama kondoo-jike ambaye amekuwa bubu mbele ya wakataji-manyoya wake, yeye pia hakufungua kinywa chake.+
8 Kwa sababu ya kizuizi na hukumu yeye aliondolewa mbali;+ na ni nani atakayejishughulisha na habari za kizazi chake?+ Kwa maana aliondolewa+ katika nchi ya walio hai.+ Alipata pigo kwa sababu ya ukosaji wa watu wangu.+ 9 Naye atafanya kaburi lake liwe pamoja na waovu,+ na pamoja na jamii ya matajiri katika kifo chake,+ ingawa yeye hakuwa amefanya jeuri+ wala hapakuwa na udanganyifu kinywani mwake.+
10 Lakini Yehova alipendezwa kumponda;+ alimfanya kuwa mgonjwa.+ Ukiifanya nafsi yake kuwa toleo la hatia,+ atauona uzao wake,+ ataongeza siku zake,+ na mapendezi+ ya Yehova yatafanikiwa mkononi mwake.+ 11 Kwa sababu ya taabu ya nafsi yake yeye ataona,+ atatosheka.+ Kupitia ujuzi wake mtu mwadilifu, mtumishi wangu,+ atawaletea watu wengi msimamo wa uadilifu;+ naye mwenyewe atayachukua makosa yao.+ 12 Kwa sababu hiyo nitampa fungu katikati ya wengi,+ naye atagawa nyara pamoja na wenye nguvu,+ kwa sababu aliimwaga nafsi yake mpaka kufa,+ naye alihesabiwa pamoja na wakosaji;+ naye mwenyewe aliichukua dhambi ya watu wengi,+ aliingilia kati kwa ajili ya wakosaji.+
54 “Piga vigelegele kwa shangwe, wewe mwanamke tasa ambaye hukuzaa!+ Changamka kwa vigelegele vya shangwe na upaaze kilio kikali,+ wewe ambaye hukuwa na maumivu ya kuzaa mtoto,+ kwa maana wana wa aliye na ukiwa ni wengi kuliko wana wa yule mwanamke aliye na mume,”+ Yehova amesema. 2 “Fanya mahali pa hema lako pawe na nafasi kubwa zaidi.+ Nao wanyooshe hema la maskani yako kuu. Usizuie. Refusha kamba za hema lako, na uvitie nguvu vigingi vya hema lako.+ 3 Kwa maana utapasua kwenda upande wa kuume na wa kushoto,+ na uzao wako mwenyewe utayamiliki hata mataifa,+ nao watakaa hata katika majiji yaliyoachwa ukiwa.+ 4 Usiogope,+ kwa maana hutaaibishwa; wala usifedheheke,+ kwa maana hutakatishwa tamaa.+ Kwa maana utaisahau hata aibu ya wakati wa ujana wako,+ nawe hutaikumbuka tena shutuma ya ujane wako wenye kuendelea.”
5 “Kwa maana Mtengenezaji Mkuu+ wako ni mume wako,+ Yehova wa majeshi ndilo jina lake;+ na Mtakatifu wa Israeli ni Mkombozi wako.+ Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote.+ 6 Kwa maana Yehova alikuita kana kwamba wewe ni mke aliyeachwa kabisa na kuumizwa katika roho,+ na kama mke wa wakati wa ujana+ ambaye alikuja kukataliwa,”+ Mungu wako amesema.
7 “Kwa maana nilikuacha kabisa kwa muda kidogo,+ lakini nitakukusanya kwa rehema nyingi.+ 8 Nilificha uso wangu kutoka kwako kwa muda kidogo kwa furiko la ghadhabu,+ lakini nitakuonyesha rehema kwa fadhili zenye upendo mpaka wakati usio na kipimo,”+ Mkombozi+ wako, Yehova, amesema.
9 “Jambo hili kwangu ni kama tu siku za Noa.+ Kama vile ambavyo nimeapa kwamba maji ya Noa hayatapita tena juu ya dunia,+ vivyo hivyo nimeapa kwamba sitakuwa na ghadhabu tena kukuelekea wewe wala kukukemea.+ 10 Kwa maana huenda milima ikaondolewa, na huenda vilima vikayumba-yumba,+ lakini fadhili zangu zenye upendo hazitaondolewa kwako,+ wala agano langu la amani halitayumba-yumba,”+ Yehova, Yule anayekuonyesha rehema,+ amesema.
11 “Ewe mwanamke uliyeteseka,+ uliyerushwa na tufani,+ usiyefarijiwa,+ tazama, ninayaweka mawe yako kwa saruji ngumu,+ nami nitauweka msingi wako+ kwa yakuti.+ 12 Nami nitaifanya minara yako kwa zabarijadi, na malango yako kwa mawe yanayowaka moto,+ na mipaka yako yote kwa mawe yenye kupendeza. 13 Na wana wako wote+ watakuwa watu waliofundishwa na Yehova,+ na amani ya wana wako itakuwa nyingi.+ 14 Utafanywa imara katika uadilifu.+ Utakuwa mbali sana na ukandamizaji+—kwa maana hutaogopa yeyote—na jambo lolote lenye kutia hofu, kwa maana halitakuja karibu nawe.+ 15 Mtu yeyote akishambulia, haitakuwa kwa maagizo yangu.+ Yeyote atakayekushambulia ataanguka kwa sababu yako.”+
16 “Tazama! Mimi mwenyewe nimemuumba fundi, yeye anayepuliza+ moto wa makaa+ na kutokeza silaha kama ufundi wake. Mimi mwenyewe pia nimemuumba mtu mharibifu+ kwa ajili ya kazi ya kuvunja-vunja. 17 Silaha yoyote itakayofanywa juu yako haitafanikiwa,+ na ulimi wowote utakaoinuka juu yako katika hukumu wewe utauhukumu.+ Hilo ndilo fungu la urithi la watumishi wa Yehova,+ na uadilifu wao ni kutoka kwangu,” asema Yehova.+
55 Haya, ninyi nyote mlio na kiu!+ Njooni kwenye maji.+ Na wale wasio na pesa! Njooni, mnunue mle.+ Ndiyo, njooni, mnunue divai+ na maziwa+ bila pesa na bila bei.+ 2 Kwa nini mnaendelea kulipa pesa kwa ajili ya kitu ambacho si mkate, na kwa nini kazi yenu ni kwa ajili ya kitu ambacho hakishibishi?+ Nisikilizeni kwa makini, na mle yaliyo mema,+ na nafsi yenu ipate furaha tele katika unono.+ 3 Tegeni sikio+ mnijie.+ Sikilizeni, na nafsi yenu itaendelea kuwa hai,+ na bila kusita mimi nitafanya pamoja nanyi agano linalodumu mpaka wakati usio na kipimo+ kuhusu fadhili zenye upendo kwa Daudi ambazo ni za uaminifu.+ 4 Tazama! Nimemtoa+ kuwa shahidi+ kwa vikundi vya mataifa,+ kuwa kiongozi+ na kamanda+ kwa vikundi vya mataifa.
5 Tazama! Utaliita taifa ambalo hulijui,+ na watu wa taifa ambao hawakukujua watakimbia wakija kwako,+ kwa ajili ya Yehova Mungu wako,+ na kwa ajili ya Mtakatifu wa Israeli,+ kwa sababu atakuwa amekurembesha.+
6 Mtafuteni Yehova, wakati anapoweza kupatikana.+ Mwiteni akiwa bado yupo karibu.+ 7 Mtu mwovu aiache njia yake,+ na mtu mwenye madhara ayaache mawazo yake;+ naye arudi kwa Yehova, ambaye atamwonyesha rehema,+ na kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.+
8 “Kwa maana mawazo yenu si mawazo yangu,+ wala njia zangu si njia zenu,”+ asema Yehova. 9 “Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu kuliko dunia,+ ndivyo njia zangu zilivyo juu kuliko njia zenu,+ na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.+ 10 Kwa maana kama vile mvua inayonyesha hushuka, na theluji, kutoka mbinguni nayo hairudi mahali pale, mpaka kwa kweli iwe imeinywesha dunia na kuifanya izae na kuchipuka,+ na mbegu kweli iwe imepewa mpandaji na mkate kupewa anayekula,+ 11 ndivyo litakavyokuwa neno langu linalotoka katika kinywa changu.+ Halitarudi kwangu bila matokeo,+ bali hakika litatenda yale ambayo yamenipendeza,+ na hakika litafanikiwa katika yale ambayo nimelituma.+
12 “Kwa maana ninyi mtaenda kwa kushangilia,+ nanyi mtaingizwa ndani kwa amani.+ Milima na vilima vitachangamka mbele yenu kwa vigelegele vya shangwe,+ nayo miti ya porini itapiga makofi yake.+ 13 Badala ya kichaka cha miiba mberoshi utatokea.+ Badala ya upupu wenye kuwasha mhadasi utatokea.+ Na litakuwa jambo lenye sifa kwa Yehova,+ ishara mpaka wakati usio na kipimo+ ambayo haitakatiliwa mbali.”
56 Yehova amesema hivi: “Shikeni haki,+ na mfanye yaliyo ya uadilifu.+ Kwa maana wokovu wangu unakaribia kuingia,+ na uadilifu wangu kufunuliwa.+ 2 Mwenye furaha ni yule mwanadamu anayeweza kufa ambaye hufanya jambo hili,+ na mwana wa binadamu anayelishika,+ anayeishika sabato ili asiitie unajisi,+ na kuuzuia mkono wake ili asitende ubaya wa aina yoyote.+ 3 Na mgeni ambaye amejiunga na Yehova asiseme,+ ‘Bila shaka Yehova atanitenga na watu wake.’+ Wala towashi+ asiseme, ‘Tazama! Mimi ni mti mkavu.’”
4 Kwa maana Yehova amewaambia hivi wale matowashi wanaozishika sabato zangu na ambao wamechagua lile ambalo nimependezwa nalo+ na ambao wanalishika agano+ langu: 5 “Nitawapa ukumbusho+ na jina+ katika nyumba yangu+ na katika kuta zangu, jambo lililo bora kuliko wana na mabinti.+ Nitawapa jina mpaka wakati usio na kipimo,+ ambalo halitakatiliwa mbali.+
6 “Na wageni ambao wamejiunga na Yehova ili kumhudumia+ na kulipenda jina la Yehova,+ ili kuwa watumishi wake, wale wote wanaoishika sabato ili wasiitie unajisi na kulishika agano langu,+ 7 mimi pia nitawaleta katika mlima wangu mtakatifu+ na kuwafanya washangilie ndani ya nyumba yangu ya sala.+ Matoleo yao mazima ya kuteketezwa+ na dhabihu+ zao zitapata kibali juu ya madhabahu yangu.+ Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya vikundi vyote vya watu.”+
8 Neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ambaye anawakusanya waliotawanyika wa Israeli,+ ni hili: “Nitawakusanya pamoja kwake wengine mbali na wale walio wake ambao tayari wamekusanywa.”+
9 Ninyi nyote wanyama wa mwituni, njooni mle, ninyi nyote wanyama-mwitu walio msituni.+ 10 Walinzi wake ni vipofu.+ Hakuna hata mmoja wao ambaye ameona.+ Wote ni mbwa walio bubu; hawawezi kubweka,+ wanahema, wanalala chini, wanapenda kusinzia.+ 11 Wao ni mbwa wenye nguvu katika tamaa ya nafsi;+ hawakujua kushiba hata kidogo.+ Wao pia ni wachungaji ambao hawakujua jinsi ya kuelewa.+ Wote wameiendea njia yao wenyewe, kila mmoja kwa mapato yake yasiyo ya haki kutoka katika mpaka wake mwenyewe:+ 12 “Njooni! Acheni nichukue divai kidogo; na acheni tunywe kileo kupindukia.+ Na kesho hakika itakuwa tu kama leo, sikukuu yenye kupita kiasi.”+
57 Mwadilifu ameangamia,+ lakini hakuna anayeweka jambo hilo moyoni.+ Na watu wa fadhili zenye upendo wanakusanywa kwa wafu,+ hali hakuna anayetambua kuwa ni kwa sababu ya msiba kwamba mwadilifu amekusanywa.+ 2 Yeye huingia katika amani;+ wao hupumzika+ vitandani+ mwao, kila mmoja anayetembea kwa unyoofu.+
3 “Na kwa habari yenu, njooni karibu hapa,+ ninyi wana wa mwanamke mwenye kubashiri,+ uzao wa mzinzi na wa mwanamke anayefanya ukahaba:+ 4 Mnajifurahisha juu ya nani?+ Mnaendelea kufungua wazi kinywa, na kutoa ulimi,+ juu ya nani? Je, ninyi si watoto wa ukosaji, uzao wa uwongo,+ 5 wale wanaojiwasha tamaa kati ya miti mikubwa,+ chini ya kila mti wenye majani mengi,+ wakiwaua watoto katika mabonde ya mito chini ya mipasuko ya miamba?+
6 “Fungu lako lilikuwa pamoja na mawe laini ya bonde la mto.+ Hayo—hayo yalikuwa kura yako.+ Zaidi ya hayo, uliyamwagia toleo la kinywaji,+ ulitoa zawadi. Je, nitajifariji kwa mambo hayo?+ 7 Uliweka kitanda chako juu ya mlima mrefu na ulioinuka.+ Ulienda hapo pia kutoa dhabihu.+ 8 Nawe uliweka ukumbusho wako nyuma ya mlango na ya mwimo wa mlango.+ Kwa maana uliniacha, ukajifunua na kupanda juu; ulikipanua kitanda chako.+ Nawe ukafanya agano pamoja nao kwa ajili yako. Ulipenda kuwa nao kitandani.+ Ulikitazama kiungo cha uume. 9 Nawe uliteremka kumwendea Meleki ukiwa na mafuta, na ukaendelea kufanya marhamu yako kuwa mengi.+ Nawe ukaendelea kuwatuma mbali wajumbe wako, hivi kwamba ukashusha mambo mpaka katika Kaburi.*+ 10 Umefanya kazi katika wingi wa njia zako.+ Hukusema, ‘Hakuna matumaini!’ Umepata kitu cha kuhuisha nguvu zako.+ Ndiyo sababu hujawa mgonjwa.+
11 “Ulimhofu na kuanza kumwogopa nani,+ hivi kwamba ukaanza kusema uwongo?+ Lakini wewe hukunikumbuka mimi.+ Hukuweka moyoni mwako jambo lolote.+ Je, mimi sikuwa nikinyamaza kimya na kuficha mambo?+ Kwa hiyo hukuniogopa mimi.+ 12 Mimi mwenyewe nitatangaza uadilifu+ wako na kazi+ zako, kwamba hazitakupa faida.+ 13 Wakati unapotoa kilio cha kuomba msaada vitu vyako ulivyokusanya havitakukomboa,+ bali upepo utavichukulia mbali vyote.+ Pumzi itaviondolea mbali, lakini yule anayenikimbilia+ atairithi nchi naye ataumiliki mlima wangu mtakatifu.+ 14 Na hakika mtu atasema, ‘Fanyeni matuta, fanyeni matuta! Fungueni njia.+ Ondoeni kipingamizi chochote katika njia ya watu wangu.’”+
15 Kwa maana Yeye Aliye Juu na Aliyeinuka Sana,+ anayeishi milele+ na ambaye jina lake ni takatifu,+ amesema hivi: “Mimi ninakaa kileleni na katika mahali patakatifu,+ pia pamoja na mtu aliyepondwa na mwenye roho ya unyenyekevu,+ ili kuipa uhai roho ya watu wa hali ya chini na kuupa uhai moyo wa wale wanaopondwa.+ 16 Kwa maana sitashindana mpaka wakati usio na kipimo, wala sitakuwa na ghadhabu daima;+ kwa maana roho itafifia+ kwa sababu yangu, viumbe vinavyopumua ambavyo mimi mwenyewe nimevifanya.+
17 “Nilikuwa na ghadhabu kutokana na makosa ya pato lake lisilo la haki,+ nami nikampiga, nikiuficha uso wangu,+ nilipokuwa na ghadhabu. Lakini yeye aliendelea kutembea akiwa mwasi+ katika njia ya moyo wake. 18 Nimeziona njia zake; nami nikaanza kumponya+ na kumwelekeza+ na kumlipa yeye malipo kwa faraja+ na watu wake wanaoomboleza.”+
19 “Mimi ninaumba matunda ya midomo.+ Kutakuwa na amani yenye kuendelea kwa yule aliye mbali na kwa yule aliye karibu,”+ Yehova amesema, “nami nitamponya.”+
20 “Lakini waovu ni kama bahari inayorushwa-rushwa, wakati ambapo haiwezi kutulia, ambayo maji yake yanaendelea kurusha juu magugu-maji na matope. 21 Hakuna amani,” Mungu wangu amesema, “kwa waovu.”+
58 “Ita kwa sauti kamili kutoka kooni; usizuie.+ Paaza sauti yako kama baragumu, uwaambie watu wangu maasi+ yao, na nyumba ya Yakobo dhambi zao. 2 Ingawa hivyo siku baada ya siku waliendelea kunitafuta mimi, nao wakawa wakionyesha kupendezwa kuzijua njia zangu,+ kama taifa lililoendeleza uadilifu na ambalo halikuwa limeiacha haki ya Mungu wao,+ kwa kuwa waliendelea kuniomba hukumu za uadilifu, wakimkaribia Mungu ambaye walipendezwa naye,+
3 “‘Kwa nini tulifunga nawe hukuona,+ tukazitesa nafsi+ zetu nawe ukawa huangalii?’+
“Kwa kweli ninyi mlikuwa mkipata upendezi katika siku ile ya kufunga kwenu, wakati kulipokuwa na wafanyakazi wenu wote ambao mliendelea kuwalazimisha kwenda kazini.+ 4 Kwa kweli mlikuwa mkifunga kwa kusudi la kugombana na kupambana,+ na kwa kusudi la kupiga kwa ngumi ya uovu.+ Je, hamkuendelea kufunga kama katika siku ile ya kufanya sauti yenu isikike kileleni? 5 Je, kufunga ambako ninachagua kunapasa kuwa hivi, kama siku ya mtu wa udongo kuitesa nafsi yake?+ Kwa kuinamisha kichwa chake kama kitete, na kwamba atandike nguo ya gunia na majivu kuwa kitanda chake?+ Je, hilo ndilo unaloliita kuwa ni kufunga na siku inayokubalika kwa Yehova?+
6 “Je, huku siko kule kufunga ambako mimi nachagua? Kufungua pingu za uovu,+ kufungua vifungo vya nira,+ na kuwaachilia huru wale waliopondwa,+ na kwamba ninyi mkate kila nira iwe vipande viwili?+ 7 Je, si kumgawia mwenye njaa mkate wako,+ na kwamba uwaingize nyumbani kwako watu wanaoteseka, wasio na makao?+ Kwamba, ukimwona mtu aliye uchi, umfunike,+ na kwamba usijifiche kutoka kwa watu wenye damu moja nawe?+
8 “Kama ingekuwa hivyo nuru yako ingetokea kama mapambazuko;+ na kupona kungetokea haraka kwa ajili yako.+ Na uadilifu wako hakika ungetembea mbele yako;+ utukufu wa Yehova ungekuwa ulinzi wako wa nyuma.+ 9 Kama ingekuwa hivyo wewe ungeita, na Yehova mwenyewe angejibu;+ ungelilia msaada, naye angesema, ‘Mimi hapa!’
“Ukiondoa katikati yako nira,+ kunyoosha kidole+ na kusema mambo yenye madhara;+ 10 nawe ukimpa mwenye njaa tamaa yako ya nafsi,+ ukiishibisha nafsi ambayo inateseka, nuru yako pia hakika itamulika hata gizani, na giza lako litakuwa kama katikati ya mchana.+ 11 Na Yehova hatakosa kukuongoza+ sikuzote+ na kuishibisha nafsi yako hata katika nchi yenye kukauka,+ naye ataitia nguvu mifupa yako;+ nawe utakuwa kama bustani iliyonyweshwa maji vizuri,+ na kama chemchemi ya maji, ambayo maji yake hayaishi. 12 Na kwa mwongozo wako hakika watu watajenga mahali palipoharibiwa muda mrefu;+ utaisimamisha misingi ya vizazi vyenye kufuatana.+ Na wewe kwa kweli utaitwa mrekebishaji wa tundu,+ mtengenezaji wa barabara za kukaa kando yake.
13 “Ikiwa kwa ajili ya sabato utarudisha nyuma mguu wako kuhusiana na kuyafanya mapendezi yako mwenyewe katika siku yangu takatifu,+ na kwa kweli uiite sabato kuwa ni furaha tele, siku takatifu ya Yehova, inayotukuzwa,+ nawe kwa kweli uitukuze badala ya kufanya njia zako mwenyewe, badala ya kutafuta kinachokupendeza na kusema neno; 14 ndipo utakapopata furaha tele katika Yehova,+ nami nitakupandisha mahali pa juu pa dunia;+ nitakufanya ule kutokana na fungu la urithi la Yakobo babu yako,+ kwa maana kinywa chenyewe cha Yehova kimesema hayo.”+
59 Tazama! Mkono wa Yehova haujawa mfupi mno kwamba usiweze kuokoa,+ wala sikio lake halijawa zito mno kwamba lisiweze kusikia.+ 2 Hapana, bali makosa yenu ndiyo mambo yanayosababisha mgawanyiko kati yenu na Mungu wenu,+ na dhambi zenu zimesababisha kufichwa kwa uso wake kutoka kwenu ili asisikie.+ 3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu,+ na vidole vyenu kwa kosa. Midomo yenu imesema uwongo.+ Ulimi wenu uliendelea kunong’ona ukosefu wa uadilifu.+ 4 Hakuna anayeita katika uadilifu,+ wala hakuna yeyote ambaye ameenda mahakamani katika uaminifu. Jambo lisilo la kweli limetegemewa,+ na ubatili umesemwa.+ Taabu imetungwa mimba, na madhara yamezaliwa.+
5 Wameangua mayai ya nyoka mwenye sumu, nao wakaendelea kufuma utando wa buibui.+ Yeyote aliyekula sehemu ya mayai yao alikufa, na yai lililovunjwa likawa likiangua nyoka mwenye sumu.+ 6 Utando wao wa buibui hautatumika kama vazi, wala hawatajifunika kwa kazi zao.+ Kazi zao ni kazi zenye madhara, na matendo ya jeuri yako mikononi mwao.+ 7 Miguu yao huendelea kukimbia kuelekea ubaya mtupu,+ nao wanafanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia.+ Mawazo yao ni mawazo yenye madhara;+ uporaji na mvunjiko zimo katika njia kuu zao.+ 8 Wameipuuza njia ya amani,+ wala hakuna haki katika mapito yao.+ Wamejipotoshea wenyewe barabara zao.+ Hakuna yeyote anayetembea humo atakayejua amani.+
9 Ndiyo sababu haki imekuwa mbali sana nasi, na uadilifu hautufikii. Tunaendelea kutumainia nuru, lakini, tazama! giza; kutumainia mwangaza, lakini tukazidi kutembea katika weusi unaoendelea.+ 10 Tunaendelea kupapasa tukiutafuta ukuta kama vipofu, nasi tunaendelea kupapasa kama wale wasio na macho.+ Tumejikwaa katikati ya mchana kama katika giza la jioni; kati ya wenye nguvu sisi ni kama wafu tu.+ 11 Tunaendelea kuugua, sisi sote, kama dubu; nasi tunaendelea kulia kwa huzuni kama njiwa.+ Tuliendelea kutumaini kupata haki,+ lakini hapakuwa na yoyote; kutumaini kupata wokovu, lakini umekaa mbali nasi.+ 12 Kwa maana maasi yetu yamekuwa mengi mbele zako;+ nazo dhambi zetu, kila moja imeshuhudia juu yetu.+ Kwa maana maasi yetu yapo pamoja nasi; nayo makosa yetu tunayajua vema.+ 13 Kumekuwa na ukosaji na kumkana Yehova;+ na kulikuwako kurudi nyuma kutoka kwa Mungu wetu, kusema ukandamizaji na maasi,+ kutunga na kunong’ona maneno ya uwongo kutoka moyoni.+ 14 Na haki ililazimishwa kusonga nyuma,+ nao uadilifu uliendelea kusimama mbali.+ Kwa maana kweli imejikwaa hata katika kiwanja cha watu wote, na lililonyooka haliwezi kuingia.+ 15 Na kweli haipo,+ na mtu yeyote anayeacha ubaya anaporwa.+
Na Yehova akaona, na ikawa vibaya machoni pake kwamba haki haikuwapo.+ 16 Naye alipoona kwamba hapakuwa na mtu, akaanza kushangaa kwamba hapakuwa na yeyote anayeingilia kati.+ Na mkono wake ukaokoa kwa ajili yake, na uadilifu wake mwenyewe ndilo jambo lililomtegemeza.+ 17 Ndipo akavaa uadilifu kama vazi la chuma,+ na kofia ya chuma ya wokovu juu ya kichwa chake.+ Zaidi ya hayo, alivaa nguo za kisasi kama mavazi+ na kujifunga kwa bidii kana kwamba ni koti lisilo na mikono.+ 18 Atatoa thawabu kulingana na matendo,+ ghadhabu kwa adui zake, atawatendea adui zake kama vile inavyostahili.+ Atavilipa visiwa tendo linalostahili.+ 19 Nao wataanza kuliogopa jina la Yehova kutoka magharibi,+ na kutoka mashariki utukufu wake,+ kwa maana ataingia kama mto wenye kutaabisha, ambao roho ya Yehova imeuendesha.+
20 “Naye Mkombozi+ hakika atakuja Sayuni,+ na kwa wale wanaouacha ukosaji katika Yakobo,”+ asema Yehova.
21 “Lakini mimi, hili ndilo agano langu pamoja nao,”+ Yehova amesema.
“Roho yangu iliyo juu yako+ na maneno yangu ambayo nimetia kinywani mwako+—hayataondolewa kinywani mwako wala kinywani mwa uzao wako wala kinywani mwa uzao wa uzao wako,” Yehova amesema, “tangu sasa mpaka wakati usio na kipimo.”+
60 “Simama,+ Ee mwanamke, toa nuru,+ kwa maana nuru yako imekuja+ na utukufu wa Yehova umeangaza juu yako.+ 2 Kwa maana, tazama! giza+ litaifunika dunia, na weusi mzito utavifunika vikundi vya mataifa; lakini Yehova ataangaza juu yako, na utukufu wake utaonekana juu yako.+ 3 Na hakika mataifa yataenda kwenye nuru yako,+ na wafalme+ kwenye mwangaza wa mwanga wako.+
4 “Inua macho yako pande zote, uone! Wote hao wamekusanywa pamoja;+ wamekuja kwako wewe.+ Wana wako wanaendelea kuja kutoka mbali, na binti zako ambao watatunzwa wakiwa ubavuni.+ 5 Wakati huo utaona na hakika ung’ae,+ na moyo wako kwa kweli utatetemeka na kupanuka, kwa sababu mali za bahari zitajielekeza kwako; mali za mataifa zitakuja kwako.+ 6 Wingi unaosukasuka wa ngamia utakufunika, ngamia-dume wachanga wa Midiani na wa Efa.+ Wale wote kutoka Sheba+—watakuja. Watabeba dhahabu na ubani. Nao watatangaza sifa za Yehova.+ 7 Makundi yote ya Kedari+—yatakusanywa pamoja kwako. Kondoo-dume wa Nebayothi+—watakuhudumia.+ Wakiwa na kibali watakuja juu ya madhabahu yangu,+ nami nitairembesha nyumba yangu ya urembo.+
8 “Ni nani hawa wanaokuja wakiruka kama wingu,+ na kama njiwa kwenye matundu yao ya ndege? 9 Kwa maana visiwa vitaendelea kunitumaini,+ meli za Tarshishi+ pia kama pale mwanzoni, ili kuwaleta wana wako kutoka mbali,+ wakiwa na fedha yao na dhahabu yao,+ kwa ajili ya jina+ la Yehova Mungu wako na kwa Mtakatifu wa Israeli,+ kwa maana atakuwa amekurembesha.+ 10 Na wageni kwa kweli watazijenga kuta zako,+ na wafalme wao wenyewe watakuhudumia;+ kwa maana nitakuwa nimekwisha kukupiga katika ghadhabu yangu,+ lakini katika nia yangu njema hakika nitakuwa nimekuonyesha rehema.+
11 “Na malango yako kwa kweli yataachwa wazi sikuzote;+ hayatafungwa wakati wa mchana wala wakati wa usiku, ili kukuletea mali za mataifa,+ na wafalme wao watakuwa wenye kuongoza.+ 12 Kwa maana taifa lolote na ufalme wowote ambao hautakutumikia, utaangamia; nayo mataifa yataharibiwa bila shaka.+
13 “Utukufu wa Lebanoni utakuja kwako wewe, mberoshi, mtidhari na mvinje wakati uleule,+ ili kuparembesha patakatifu pangu;+ nami nitapatukuza mahali pangu pa miguu.+
14 “Na wana wa wale wanaokutesa watakuja kwako, wakiwa wanainama;+ na wale wote wanaokuvunjia heshima watainama penye nyayo za miguu yako,+ nao watakuita wewe jiji la Yehova, Sayuni+ wa Mtakatifu wa Israeli.
15 “Badala ya wewe kuwa aliyeachwa kabisa na kuchukiwa, bila kuwa na yeyote anayepita katikati,+ nitakuweka kuwa kitu cha fahari mpaka wakati usio na kipimo, furaha kwa kizazi baada ya kizazi.+ 16 Nawe kwa kweli utanyonya maziwa ya mataifa,+ utanyonya matiti ya wafalme;+ nawe utajua hakika kwamba mimi, Yehova,+ ni Mwokozi+ wako, na Mwenye Nguvu+ wa Yakobo ni Mkombozi+ wako. 17 Badala ya shaba nitaingiza dhahabu,+ na badala ya chuma nitaingiza fedha, na badala ya miti, shaba, na badala ya mawe, chuma; nami nitaweka amani kuwa waangalizi+ wako na uadilifu kuwa wagawa-kazi wako.+
18 “Jeuri haitasikiwa tena katika nchi yako, uporaji na mvunjiko ndani ya mipaka yako.+ Na hakika wewe utaziita kuta zako Wokovu+ na malango yako Sifa. 19 Kwa maana kwako wewe jua halitakuwa tena nuru wakati wa mchana, na mwezi hautakupa tena mwangaza kuwa nuru. Na Yehova atakuwa kwako nuru+ inayodumu mpaka wakati usio na kipimo, na Mungu wako kuwa urembo wako.+ 20 Jua lako halitatua tena, wala mwezi wako hautafifia; kwa maana Yehova atakuwa kwako nuru+ inayodumu mpaka wakati usio na kipimo, na siku za kuomboleza kwako zitakuwa zimemalizika.+ 21 Na kwa habari ya watu wako, wote watakuwa waadilifu;+ mpaka wakati usio na kipimo wataimiliki nchi,+ chipukizi nililolipanda,+ kazi ya mikono yangu,+ ili mimi nirembeshwe.+ 22 Mdogo atakuwa elfu, na mnyonge atakuwa taifa lenye nguvu.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nitaharakisha jambo hilo kwa wakati wake.”+
61 Roho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova iko juu yangu,+ kwa sababu Yehova amenitia mafuta+ niwatangazie wapole habari njema.+ Amenituma kufunga majeraha ya waliovunjika moyo,+ kutangaza uhuru kwa wale waliochukuliwa mateka+ na kufunguliwa kabisa kwa macho hata kwa walio wafungwa;+ 2 kutangaza mwaka wa nia njema upande wa Yehova+ na siku ya kisasi upande wa Mungu wetu;+ kuwafariji wote wanaoomboleza;+ 3 kuwapa wale wanaoomboleza kwa ajili ya Sayuni, kuwapa vazi la kichwani badala ya majivu,+ mafuta ya furaha+ badala ya maombolezo, nguo ya kujitanda ya sifa badala ya roho iliyovunjika;+ nao wataitwa miti mikubwa ya uadilifu,+ bustani ya Yehova,+ ili yeye arembeshwe.+ 4 Nao watajenga upya mahali palipoharibiwa kwa muda mrefu;+ watasimamisha mahali palipofanywa ukiwa pa nyakati za kale,+ nao hakika watajenga upya yale majiji yaliyoharibiwa,+ mahali palipofanywa ukiwa kwa kizazi baada ya kizazi.
5 “Na wageni kwa kweli watasimama na kuchunga makundi yenu,+ na watu wa nchi nyingine+ watakuwa wakulima wenu na watunza-mizabibu wenu.+ 6 Nanyi mtaitwa makuhani wa Yehova;+ itasemekana ninyi ni wahudumu wa Mungu wetu.+ Ninyi mtakula mali za mataifa,+ nanyi mtasema kujihusu ninyi wenyewe kwa kuchangamka katika utukufu wao.+ 7 Badala ya aibu yenu kutakuwa na fungu mara mbili,+ na badala ya fedheha watapiga vigelegele kwa shangwe juu ya fungu lao.+ Kwa hiyo watamiliki fungu mara mbili+ katika nchi yao. Watakuwa na shangwe mpaka wakati usio na kipimo.+ 8 Kwa maana mimi, Yehova, napenda haki,+ nachukia unyang’anyi pamoja na ukosefu wa uadilifu.+ Nami nitatoa malipo yao katika ukweli,+ nitafanya kwao agano linalodumu mpaka wakati usio na kipimo.+ 9 Na uzao wao kwa kweli utajulikana katika mataifa, na wazao wao katikati ya vikundi vya watu.+ Wale wote wanaowaona watawatambua,+ kwamba wao ni uzao ambao Yehova amebariki.”+
10 Hakika nitafurahi katika Yehova.+ Nafsi yangu itakuwa na shangwe katika Mungu wangu.+ Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu;+ amenivika koti lisilo na mikono la uadilifu,+ kama bwana-arusi ambaye, kama kuhani, anavaa vazi la kichwani,+ na kama bibi-arusi anayejipamba kwa vitu vya mapambo yake.+ 11 Kwa maana kama vile dunia inavyotoa chipukizi lake, na kama vile bustani inavyochipusha vitu vilivyopandwa ndani yake,+ ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atakavyotoa chipukizi la uadilifu+ na la sifa mbele ya mataifa yote.+
62 Sitanyamaza kwa ajili ya Sayuni,+ nami sitakaa kimya kwa ajili ya Yerusalemu+ mpaka uadilifu wake utoke kama mwangaza,+ na wokovu wake kama mwenge unaowaka.+
2 “Na mataifa hakika yatauona uadilifu wako,+ Ee mwanamke,+ na wafalme wote utukufu wako.+ Na hakika wewe utaitwa kwa jina jipya,+ ambalo kinywa cha Yehova kitalichagua. 3 Nawe utakuwa taji la urembo mkononi mwa Yehova,+ na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako. 4 Haitasemekana tena kuwa wewe ni mwanamke aliyeachwa kabisa;+ na nchi yako haitasemekana tena kuwa imeachwa ukiwa;+ lakini wewe mwenyewe utaitwa jina Upendezi Wangu Umo Ndani Yake,+ na nchi yako itaitwa jina Inamilikiwa Kama Mke. Kwa maana Yehova atakuwa amependezwa na wewe, na nchi yako itamilikiwa kama mke.+ 5 Kwa maana kama vile kijana anavyomchukua bikira awe mke wake, ndivyo wana wako watakavyokuchukua wewe uwe mke wao.+ Na Mungu wako atakufurahia+ kama vile bwana-arusi anavyomfurahia bibi-arusi.+ 6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu.+ Mchana kutwa na usiku kucha, sikuzote, wasikae kimya.+
“Ninyi mnaomtaja Yehova,+ msinyamaze kimya,+ 7 wala msiache anyamaze mpaka aweke imara, ndiyo, mpaka aweke Yerusalemu kuwa sifa katika dunia.”+
8 Yehova ameapa kwa mkono wake wa kuume+ na kwa mkono wake wenye nguvu:+ “Sitawapa tena adui zako nafaka yako iwe chakula,+ wala wageni hawatakunywa divai yako mpya,+ ambayo umeifanyia kazi. 9 Lakini wale wanaoikusanya wataila, nao hakika watamsifu Yehova; na wale wanaoikusanya watainywa katika nyua zangu takatifu.”+
10 Tokeni nje, tokeni nje kupitia malango. Fungueni njia ya watu.+ Fanyeni matuta, fanyeni matuta kwa ajili ya njia kuu. Ondoeni mawe juu yake.+ Inueni ishara kwa ajili ya vikundi vya watu.+
11 Tazama! Yehova amefanya isikiwe mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia:+ “Mwambieni binti Sayuni,+ ‘Tazama! Wokovu wako unakuja.+ Tazama! Yeye anayo thawabu anayotoa,+ na malipo anayotoa yako mbele zake.’”+
12 Na hakika watu watawaita wao kuwa watu watakatifu,+ wale waliokombolewa na Yehova;+ na wewe mwenyewe utaitwa Aliyetafutwa, Jiji Ambalo Halikuachwa Kabisa.+
63 Ni nani huyu anayetoka Edomu,+ aliye na mavazi yenye rangi zinazong’aa kutoka Bosra,+ huyu ambaye ana nguo zenye kuheshimika, anayetembea katika wingi wa nguvu zake?
“Ni mimi, Yeye ambaye husema katika uadilifu,+ Yeye ambaye ni mwingi wa nguvu za kuokoa.”+
2 Kwa nini nguo zako ni nyekundu, na mavazi yako ni kama yale ya mtu anayekanyaga ndani ya shinikizo la divai?+
3 “Mimi mwenyewe nimelikanyaga pipa la divai,+ kulipokuwa hakuna mtu yeyote pamoja nami kutoka katika vikundi vya watu. Nami niliendelea kuwakanyaga katika hasira yangu,+ niliendelea kuwakanyagia chini katika ghadhabu yangu.+ Na damu yao inayobubujika ikaendelea kutawanyika juu ya mavazi yangu,+ nami nimezichafua nguo zangu zote. 4 Kwa maana siku ya kisasi imo moyoni mwangu,+ na ule mwaka wa watu wangu waliokombolewa umekuja. 5 Nami niliendelea kutazama, lakini hapakuwa na msaidizi; nikaanza kushangaa, lakini hapakuwa na yeyote aliyetegemeza.+ Kwa hiyo mkono wangu ukanipa wokovu,+ na ghadhabu+ yangu ndiyo iliyonitegemeza. 6 Nami katika hasira yangu niliendelea kuvikanyagia chini vikundi vya watu, na katika ghadhabu yangu nikaendelea kuwalewesha+ na kuimwaga chini damu yao inayobubujika.”+
7 Nitazisema fadhili zenye upendo za Yehova,+ sifa za Yehova, kulingana na yote ambayo Yehova ametutendea,+ wema mwingi kwa nyumba ya Israeli+ ambao amewatendea kulingana na rehema+ zake na kulingana na wingi wa fadhili zake zenye upendo. 8 Naye aliendelea kusema: “Hakika wao ni watu wangu,+ wana ambao hawataonekana kuwa waongo.”+ Basi akawa Mwokozi+ wao. 9 Wakati wa taabu zao zote hilo lilimtaabisha.+ Na mjumbe wake binafsi akawaokoa.+ Katika upendo wake na katika huruma yake yeye mwenyewe aliwakomboa,+ naye akawainua na kuwachukua siku zote za zamani za kale.+
10 Lakini wao wenyewe waliasi+ na kuihuzunisha roho yake takatifu.+ Sasa alibadilika akawa adui+ yao; yeye mwenyewe alipiga vita juu yao.+ 11 Na mtu akaanza kuzikumbuka siku za zamani za kale, Musa mtumishi wake: “Yuko wapi Yeye aliyewapandisha kutoka katika bahari+ pamoja na wachungaji wa kundi lake?+ Yuko wapi Yeye aliyetia ndani yake roho Yake takatifu?+ 12 Yeye aliyeufanya mkono+ Wake mzuri uende upande wa mkono wa kuume wa Musa; Yeye aliyegawanya maji kutoka mbele yao+ ili kujifanyia mwenyewe jina linalodumu mpaka wakati usio na kipimo;+ 13 Yeye aliyewatembeza kupitia katikati ya maji yenye kututumuka hivi kwamba, kama farasi nyikani, hawakujikwaa?+ 14 Kama vile mnyama anavyoteremka ndani ya nchi tambarare ya bondeni, ndivyo roho ya Yehova ilivyowapumzisha.”+
Hivyo uliwaongoza watu wako ili ujifanyie mwenyewe jina zuri.+
15 Tazama kutoka mbinguni,+ uone kutoka katika makao yako yaliyoinuliwa ya utakatifu na uzuri.+ Iko wapi bidii+ yako na nguvu zako kamili, msukosuko wa sehemu zako za ndani,+ na rehema+ zako? Zimejizuia kunielekea.+ 16 Kwa maana wewe ni Baba yetu,+ ingawa huenda iwe Abrahamu mwenyewe hakutujua na huenda iwe Israeli mwenyewe asitutambue, wewe, Ee Yehova, ni Baba yetu. Mkombozi wetu wa zamani za kale ni jina lako.+ 17 Kwa nini, Ee Yehova, unaendelea kutufanya tutange-tange kutoka katika njia zako? Kwa nini unafanya moyo wetu uwe mgumu ili usikuogope?+ Rudi kwa ajili ya watumishi wako, makabila ya fungu lako la urithi.+ 18 Kwa muda kidogo watu wako watakatifu+ walikuwa na miliki. Adui zetu wenyewe wamepakanyaga patakatifu pako.+ 19 Kwa muda mrefu tumekuwa kama watu ambao hukutawala juu yao, kama wale ambao jina lako halikuwa limeitwa juu yao.+
64 Laiti ungezipasua mbingu, ushuke chini,+ ili milima itetemeke kwa sababu yako,+ 2 kama wakati moto unapowasha vichaka, na moto kuyachemsha maji, ili kuwajulisha adui zako jina lako,+ ili mataifa yafadhaike kwa sababu yako!+ 3 Ulipofanya mambo yenye kuogopesha+ ambayo hatungeweza kuyatumaini, ulishuka chini. Milima ilitetemeka kwa sababu yako.+ 4 Na kutoka zamani za kale hakuna aliyesikia,+ wala hakuna aliyetega sikio, wala hakuna jicho lililomwona Mungu, isipokuwa wewe,+ unayetenda kwa ajili ya mtu anayeendelea kumtarajia huyo.+ 5 Umekutana na yule anayefurahi na kutenda uadilifu,+ wale wanaoendelea kukukumbuka katika njia zako mwenyewe.+
Tazama! Wewe ulikuwa na ghadhabu,+ huku sisi tukiendelea kutenda dhambi+—katika hizo muda mrefu, na je, sisi tuokolewe?+ 6 Nasi tunakuwa kama mtu asiye safi, sisi sote, na matendo yetu yote ya uadilifu ni kama vazi la vipindi vya hedhi;+ nasi tutafifia kama majani,+ sisi sote, na makosa yetu yatatuchukua kama upepo.+ 7 Na hakuna yeyote anayeliitia jina lako,+ hakuna yeyote anayeamka ili akushike; kwa maana umeuficha uso wako kutoka kwetu,+ nawe unatuyeyusha+ kwa nguvu za kosa letu.
8 Na sasa, Ee Yehova, wewe ni Baba yetu.+ Sisi ni udongo,+ nawe ni Mfinyanzi+ wetu; nasi sote ni kazi ya mkono wako.+ 9 Usiwe na ghadhabu kupindukia,+ Ee Yehova, wala usilikumbuke milele kosa letu.+ Tazama, sasa, tafadhali: sisi sote ni watu wako.+ 10 Majiji yako matakatifu+ yamekuwa nyika. Sayuni+ umekuwa nyika tupu, Yerusalemu limekuwa mahame yenye ukiwa.+ 11 Nyumba yetu ya utakatifu na uzuri,+ ambayo ndani yake mababu zetu walikusifu wewe,+ imekuwa kitu cha kuteketezwa motoni;+ na kila kimoja cha vitu vyetu vyenye kutamanika+ kimeharibika. 12 Mbele ya mambo hayo yote, je, utaendelea kujizuia,+ Ee Yehova? Je, utanyamaza na kutuacha tuteseke kupindukia?+
65 “Wale ambao hawakuwa wameniuliza+ nimewaacha wanitafute.+ Wale ambao hawakuwa wamenitafuta nimewaacha wanipate.+ Nimesema, ‘Mimi hapa, mimi hapa!’+ kwa taifa ambalo halikuwa linaliitia jina langu.+
2 “Nimewanyooshea watu wakaidi+ mikono yangu mchana kutwa, wale ambao wanatembea katika njia ambayo si nzuri,+ wakifuata mawazo yao;+ 3 watu ambao washiriki wake ni wale wanaonitia uchungu+ mbele za uso wangu daima, wakiwa wanatoa dhabihu katika bustani+ na kufukiza moshi wa dhabihu+ juu ya matofali, 4 wakiwa wameketi katikati ya makaburi,+ ambao pia wanalala usiku kucha katika vijumba vya kukeshea, wakiwa wanakula nyama ya nguruwe,+ mchuzi wa vitu vichafu+ ukiwa katika vyombo vyao; 5 wale wanaosema, ‘Kaa peke yako. Usinikaribie, kwa maana hakika nitakupa utakatifu.’+ Hawa ni moshi katika mianzi ya pua yangu,+ moto unaowaka mchana kutwa.+
6 “Tazama! Imeandikwa mbele zangu.+ Sitakaa kimya,+ lakini nitatoa thawabu;+ nitatoa thawabu vifuani mwao,+ 7 kwa ajili ya makosa yao wenyewe na kwa ajili ya makosa ya mababu zao wakati uleule,”+ Yehova amesema. “Kwa sababu wamefukiza moshi wa dhabihu juu ya milima, nao wamenishutumu+ juu ya vilima,+ mimi pia nitapima kwanza kabisa malipo yao vifuani mwao.”+
8 Yehova amesema hivi: “Kama vile divai mpya+ inavyopatikana katika kishada na mtu husema, ‘Usikiharibu,+ kwa sababu baraka imo ndani yake,’+ ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu ili nisimharibu kila mtu.+ 9 Nami nitaleta uzao kutoka katika Yakobo+ na mrithi wa milima yangu kutoka katika Yuda;+ na wachaguliwa wangu wataumiliki,+ na watumishi wangu wenyewe watakaa huko.+ 10 Na Sharoni+ utakuwa uwanja wa malisho kwa ajili ya kondoo+ na nchi tambarare ya chini ya Akori+ mahali pa kupumzikia ng’ombe, kwa ajili ya watu wangu ambao watakuwa wamenitafuta.+
11 “Lakini ninyi ndio wale watu wanaomwacha Yehova,+ wale wanaousahau mlima wangu mtakatifu,+ wale wanaoandaa meza kwa ajili ya mungu wa Bahati Njema+ na wale wanaojaza divai iliyochanganywa kwa ajili ya mungu wa Majaliwa.+ 12 Nami nitawaandikia ninyi upanga,+ nanyi nyote mtainama ili kuuawa;+ kwa sababu niliita,+ lakini hamkuitika; nilisema, lakini hamkusikiliza;+ nanyi mliendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pangu,+ mlichagua jambo ambalo halikunipendeza.”+
13 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama! Watumishi wangu watakula,+ lakini ninyi mtakuwa na njaa.+ Tazama! Watumishi wangu watakunywa,+ lakini ninyi mtakuwa na kiu.+ Tazama! Watumishi wangu watashangilia,+ lakini ninyi mtaona aibu.+ 14 Tazama! Watumishi wangu watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya hali nzuri ya moyo,+ lakini ninyi mtalia kwa sababu ya maumivu ya moyo nanyi mtapiga mayowe kwa sababu ya mvunjiko kabisa wa roho.+ 15 Nanyi hakika mtaweka jina lenu kuwa kiapo kwa wachaguliwa wangu, na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova kwa kweli atawaua ninyi mmoja mmoja,+ lakini watumishi wake atawaita kwa jina lingine;+ 16 ili kwamba yeyote anayejibariki duniani atajibariki kwa Mungu wa imani,+ na yeyote anayetoa ahadi yenye kiapo duniani ataapa kwa Mungu wa imani;+ kwa sababu taabu za zamani kwa kweli zitasahauliwa na kwa sababu kwa kweli zitafichwa kutoka machoni pangu.+
17 “Kwa maana, tazama, mimi ninaumba mbingu mpya+ na dunia mpya;+ na mambo ya zamani hayatakumbukwa akilini,+ wala hayataingia moyoni.+ 18 Lakini furahini,+ na muwe na shangwe milele katika hivi ninavyoumba.+ Kwa maana tazama, mimi ninaumba Yerusalemu kuwa sababu ya kushangilia na watu wake kuwa sababu ya kufurahi.+ 19 Nami nitashangilia katika Yerusalemu na kufurahi katika watu wangu;+ na ndani yake haitasikika tena sauti ya kulia wala sauti ya kilio cha huzuni.”+
20 “Hapatakuwa tena kutoka mahali hapo mtoto anayenyonya anayeishi siku chache,+ wala mzee ambaye hatimizi siku zake;+ kwa maana mtu atakufa akiwa mvulana tu, ingawa ana umri wa miaka mia moja; na kuhusu mtenda-dhambi, ingawa ana umri wa miaka mia moja yeye atalaaniwa.+ 21 Na hakika wao watajenga nyumba na kukaa ndani yake;+ na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.+ 22 Hawatajenga na mtu mwingine akae ndani yake; hawatapanda na mtu mwingine ale. Kwa maana siku za watu wangu zitakuwa kama siku za mti;+ na watu wangu waliochaguliwa wataitumia kazi ya mikono yao wenyewe kikamilifu.+ 23 Hawatafanya kazi ya bure,+ wala hawatazaa kwa ajili ya kupata usumbufu;+ kwa sababu wao ni uzao wa watu wa Yehova waliobarikiwa,+ na wazao wao pamoja nao.+ 24 Na kwa kweli itakuwa kwamba kabla hawajaita mimi mwenyewe nitajibu;+ wakiwa bado wanasema, mimi nitasikia.+
25 “Mbwa-mwitu+ na mwana-kondoo watalisha kama kitu kimoja,+ na simba atakula majani kama ng’ombe;+ na kuhusu nyoka, chakula chake kitakuwa mavumbi.+ Hawatadhuru+ wala kufanya uharibifu wowote katika mlima wangu wote mtakatifu,”+ Yehova amesema.
66 Yehova amesema hivi: “Mbingu ni kiti changu cha ufalme,+ na dunia ni kiti cha miguu yangu.+ Iko wapi, basi, nyumba ambayo ninyi mnaweza kunijengea,+ na pako wapi, basi, mahali pa kupumzika kwa ajili yangu?”+
2 “Sasa mikono yangu imefanya hivi vyote, hivi kwamba hivi vyote vikaja kuwako,”+ asema Yehova. “Basi, nitamtazama huyu, yeye anayeteseka na kujuta rohoni+ na kutetemeka kwa ajili ya neno langu.+
3 “Yeye anayemchinja ng’ombe ni kama yeye anayemuua mwanadamu.+ Yeye anayemchinja kondoo ni kama yeye anayevunja shingo ya mbwa.+ Yeye anayetoa zawadi ni kama yeye anayetoa damu ya nguruwe!+ Yeye anayetoa ukumbusho wa ubani+ ni kama yeye anayebariki akitumia maneno ya uchawi.+ Wao pia ndio wamechagua njia zao wenyewe, na nafsi yao imependezwa na machukizo yao.+ 4 Mimi nami nitachagua njia za kuwatendea vibaya;+ nami nitaleta juu yao mambo yanayowatia hofu;+ kwa sababu niliita, lakini hakuna aliyejibu; nilisema, lakini hakuna aliyesikiliza;+ nao waliendelea kutenda yaliyokuwa mabaya machoni pangu, walichagua jambo ambalo sikupendezwa nalo.”+
5 Sikieni neno la Yehova, ninyi mnaotetemeka kwa ajili ya neno lake:+ “Ndugu zenu wanaowachukia,+ ambao wanawatenga ninyi kwa sababu ya jina langu,+ walisema, ‘Yehova na atukuzwe!’+ Yeye pia atatokea pamoja na shangwe kwa ajili yenu,+ nao ndio watakaotiwa aibu.”+
6 Kuna sauti ya ghasia kutoka jijini, sauti kutoka hekaluni!+ Ni sauti ya Yehova akiwalipa adui zake yale yanayostahiliwa.+
7 Kabla mwanamke hajawa na uchungu wa kuzaa, alizaa.+ Kabla ya kushikwa na uchungu wa kuzaa, alijifungua mtoto wa kiume.+ 8 Ni nani amesikia jambo kama hili?+ Ni nani ameona mambo kama haya?+ Je, nchi+ itazaliwa kwa uchungu katika siku moja?+ Au, je, taifa+ litazaliwa wakati uleule mmoja?+ Kwa maana Sayuni ameshikwa na uchungu wa kuzaa naye vilevile amezaa wanawe.
9 “Nami, je, nitasababisha kupasuka wala nisisababishe kuzaliwa?”+ asema Yehova. “Au, je, mimi ninasababisha kuzaliwa na kwa kweli ninasababisha kufunga uzazi?” Mungu wako amesema.
10 Shangilieni pamoja na Yerusalemu na muwe na shangwe pamoja naye,+ ninyi nyote mnaompenda.+ Furahini sana pamoja naye, ninyi nyote mnaoendelea kuomboleza juu yake;+ 11 kwa sababu mtanyonya na hakika mshibe kutokana na titi la faraja zake kamili; kwa sababu mtakunywa na kupata furaha tele kutokana na titi la utukufu wake.+ 12 Kwa maana Yehova amesema hivi: “Tazama, mimi ninampa amani kama mto+ na utukufu wa mataifa kama mto unaofurika,+ nanyi hakika mtanyonya.+ Mtachukuliwa mkiwa ubavuni, nanyi mtapakatwa juu ya magoti.+ 13 Kama vile mtu ambaye mama yake mwenyewe anaendelea kumfariji, ndivyo mimi nitakavyoendelea kuwafariji ninyi;+ na kuhusiana na Yerusalemu ninyi mtafarijiwa.+ 14 Nanyi hakika mtaona, na moyo wenu hautakosa kufurahi,+ na mifupa+ yenu itachipuka kama majani mororo.+ Na mkono wa Yehova hakika utajulishwa kwa watumishi wake,+ lakini yeye kwa kweli atawashutumu adui zake.”+
15 “Kwa maana, tazama, Yehova anakuja kama moto,+ na magari yake ni kama upepo wa dhoruba,+ ili kulipa hasira yake kwa ghadhabu tupu na kemeo lake kwa miali ya moto.+ 16 Kwa maana, kama moto, Yehova atabishana na wote wenye mwili, ndiyo, akiwa na upanga wake;+ na waliouawa wa Yehova hakika watakuwa wengi.+ 17 Wale wanaojitakasa na kujisafisha kwa ajili ya bustani+ zilizo nyuma ya mtu katikati, wakila nyama ya nguruwe+ na kitu chenye kuchukiza, panya anayeruka,+ wote wataufikia mwisho wao pamoja,” asema Yehova. 18 “Na kuhusu kazi+ zao na mawazo+ yao, mimi ninakuja ili kuyakusanya mataifa yote na lugha zote pamoja;+ nao itawapasa kuja na kuuona utukufu wangu.”+
19 “Nami nitatia ishara katikati yao,+ nami nitawapeleka baadhi ya wale walioponyoka kwenda kwenye mataifa,+ Tarshishi,+ Pulu, na Ludi,+ wale wanaouvuta upinde, Tubali na Yavani,+ visiwa vilivyo mbali,+ ambao hawajasikia habari kunihusu mimi wala kuuona utukufu wangu;+ nao hakika watatangaza juu ya utukufu wangu kati ya mataifa.+ 20 Nao kwa kweli watawaleta ndugu zenu wote kutoka katika mataifa+ yote kuwa zawadi kwa Yehova,+ wakiwa juu ya farasi na ndani ya magari na ndani ya magari ya kukokotwa yaliyofunikwa na juu ya nyumbu na juu ya ngamia-jike+ wepesi, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu,+ Yerusalemu,” Yehova amesema, “kama vile wana wa Israeli wanavyoleta zawadi katika chombo safi ndani ya nyumba ya Yehova.”+
21 “Nami kutoka kwao pia nitachukua baadhi yao kwa ajili ya makuhani, kwa ajili ya Walawi,” Yehova amesema.
22 “Kwa maana kama vile mbingu mpya+ na dunia mpya+ ninazozifanya zinavyosimama mbele zangu,”+ asema Yehova, “ndivyo uzao wenu+ na jina lenu litakavyoendelea kusimama.”+
23 “Na hakika itatukia kwamba kutoka mwezi mpya mpaka mwezi mpya na kutoka sabato mpaka sabato wanadamu wote wataingia ili kuinama mbele zangu,”+ Yehova amesema. 24 “Nao kwa kweli wataenda na kuitazama mizoga ya wale watu waliokuwa wakinikosea;+ kwa maana funza walio juu yao hawatakufa na moto wao hautazimwa,+ nao watakuwa chukizo kwa wanadamu wote.”+
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Pengine mamba.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.