Yeremia
1 Maneno ya Yeremia+ mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani waliokuwa katika Anathothi+ katika nchi ya Benyamini;+ 2 ambaye neno la Yehova lilimjia katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni,+ mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wake.+ 3 Nalo likaendelea kuja katika siku za Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, mpaka kumalizika kwa mwaka wa kumi na moja wa Sedekia+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, mpaka Yerusalemu lilipoenda uhamishoni katika mwezi wa tano.+
4 Na neno la Yehova likaanza kunijia, na kusema: 5 “Kabla sijaanza kukuumba ndani ya tumbo+ nilikujua,+ na kabla hujatoka ndani ya tumbo la uzazi nilikutakasa.+ Nilikufanya uwe nabii kwa mataifa.”
6 Lakini nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tazama, mimi hakika sijui jinsi ya kusema,+ kwa sababu mimi ni mvulana tu.”+
7 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Usiseme, ‘Mimi ni mvulana tu.’ Lakini kwa wale wote nitakaokutuma kwao, unapaswa kwenda; na kila jambo nitakalokuamuru, unapaswa kusema.+ 8 Usiogope kwa sababu ya nyuso zao,+ kwa maana ‘mimi niko pamoja nawe ili kukukomboa,’+ asema Yehova.”
9 Basi Yehova akanyoosha mkono wake na kunigusa kinywa+ changu. Ndipo Yehova akaniambia: “Tazama, nimeyatia maneno yangu katika kinywa chako.+ 10 Tazama, nimekupa utume leo ili uwe juu ya mataifa na juu ya falme,+ ili kung’oa na kubomoa na kuangamiza na kuangusha,+ ili kujenga na kupanda.”+
11 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: “Unaona nini, Yeremia?”
Basi nikasema: “Ninaona chipukizi la mlozi.”
12 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Umeona vema, kwa maana niko macho kuhusu neno langu ili kulitimiza.”+
13 Na neno la Yehova likanijia mara ya pili, na kusema: “Unaona nini?”
Basi nikasema: “Ninaona chungu cha kupikia chenye mdomo mpana ambacho kinapuliziwa, na mdomo wake umeinama kutoka kaskazini.”
14 Ndipo Yehova akaniambia: “Msiba utafunguliwa kutoka kaskazini juu ya wakaaji wote wa nchi.+ 15 Kwa maana ‘tazama, ninaziita familia zote za falme za kaskazini,’ asema Yehova;+ ‘nao hakika watakuja na kuweka kila mmoja kiti chake cha ufalme kwenye mwingilio wa malango ya Yerusalemu,+ na juu ya kuta zake zote kuzunguka pande zote na juu ya majiji yote ya Yuda.+ 16 Nami nitasema nao hukumu zangu juu ya ubaya wao wote,+ kwa kuwa wameniacha+ nao wanaendelea kufukizia miungu mingine+ moshi wa dhabihu na kuinamia kazi za mikono yao wenyewe.’+
17 “Nawe unapaswa kufunga mshipi viunoni mwako,+ na kusimama na kuwaambia kila jambo ambalo mimi ninakuamuru. Usiwe na hofu yoyote kwa sababu yao,+ ili mimi nisikutie hofu mbele yao. 18 Lakini mimi, tazama, leo nimekufanya wewe kuwa jiji lenye ngome na nguzo ya chuma na kuta za shaba+ juu ya nchi yote,+ kuwaelekea wafalme wa Yuda, kuwaelekea wakuu wake, kuwaelekea makuhani wake na kuwaelekea watu wa nchi hii.+ 19 Nao hakika watapigana nawe, lakini hawatakushinda,+ kwa maana ‘Mimi niko pamoja nawe,’+ asema Yehova, ‘ili nikukomboe.’”+
2 Na neno la Yehova likanijia,+ na kusema: 2 “Nenda, ukaite masikioni mwa Yerusalemu, ukisema, ‘Yehova amesema hivi:+ “Ninakumbuka vema fadhili zako zenye upendo wakati wa ujana wako,+ upendo wako wakati ulipochumbiwa ili kuolewa,+ ulivyotembea kunifuata nyikani, katika nchi ambayo haipandwi mbegu.+ 3 Israeli alikuwa kitu kitakatifu kwa Yehova,+ zao la kwanza kwake Yeye.”’+ ‘Watu wowote waliomrarua walikuwa wakijiingiza katika hatia.+ Msiba ulikuwa ukija juu yao,’ alisema Yehova.”+
4 Lisikie neno la Yehova, Ee nyumba ya Yakobo,+ nanyi nyote familia za nyumba ya Israeli.+ 5 Yehova amesema hivi: “Baba zenu walipata jambo gani ndani yangu ambalo halikuwa la haki,+ hivi kwamba wakasimama mbali sana nami,+ nao wakaendelea kufuata sanamu ya ubatili+ na wao wenyewe wakawa ubatili?+ 6 Nao hawakusema, ‘Yehova yuko wapi, Yeye aliyetupandisha kutoka katika nchi ya Misri,+ Yeye aliyetutembeza kupitia nyikani, kupitia nchi tambarare ya jangwani+ na shimo, kupitia nchi isiyo na maji+ na yenye kivuli kizito,+ kupitia nchi ambayo mwanadamu yeyote hakupita ndani yake na ambayo hakuna mtu wa udongo aliyekaa ndani yake?’
7 “Nami mwishowe nikawaleta ninyi katika nchi yenye mashamba ya matunda, ili mle matunda yake na vitu vyake vyema.+ Lakini mkaingia na kuitia unajisi nchi yangu; nanyi mkaufanya urithi wangu kuwa chukizo.+ 8 Makuhani wenyewe hawakusema, ‘Yehova yuko wapi?’+ Na wale wanaoshughulika na sheria hawakunijua;+ na wachungaji wenyewe walinikosea,+ na hata manabii walitoa unabii kupitia Baali,+ nao wakawafuata wale ambao hawangeweza kuleta faida yoyote.+
9 “‘Kwa hiyo nitapambana zaidi nanyi,’+ asema Yehova, ‘nami nitapambana na wana wa wana wenu.’+
10 “‘Lakini vukeni mpaka nchi za pwani za Kitimu,+ mkaone. Ndiyo, tumeni watu Kedari+ nanyi mfikirie kwa njia ya pekee, mkaone ikiwa jambo lolote kama hili limetendeka.+ 11 Je, taifa limebadili miungu,+ kwa ajili ya ile ambayo si miungu?+ Lakini watu wangu mwenyewe wameubadili utukufu wangu kwa ajili ya kitu ambacho hakiwezi kuleta faida yoyote.+ 12 Tazameni kwa mshangao, enyi mbingu, jambo hili; na nywele zisimame kwa woga mkubwa sana,’ asema Yehova,+ 13 ‘kwa sababu kuna mambo mawili mabaya ambayo watu wangu wamefanya: Wameniacha mimi,+ niliye chemchemi ya maji yaliyo hai,+ ili wajichimbie matangi ya maji, matangi yaliyovunjika, ambayo hayawezi kutunza maji.’
14 “‘Je, Israeli ni mtumishi,+ au ni mtumwa aliyezaliwa nyumbani? Kwa nini amekuwa kitu cha kuporwa? 15 Wana-simba wenye manyoya shingoni wananguruma+ juu yake; wametoa sauti zao.+ Nao wakaifanya nchi yake kuwa kitu cha kushangaza. Majiji yake yamewashwa moto, hivi kwamba hakuna mkaaji.+ 16 Hata wana wa Nofu+ na Tahpanesi+ waliendelea kujilisha juu yako kwenye utosi wa kichwa.+ 17 Je, hilo silo jambo ulilojifanyia mwenyewe kwa kumwacha Yehova Mungu+ wako wakati alipokuwa akikutembeza njiani?+ 18 Na sasa kwa nini ujishughulishe na njia ya Misri+ ili kunywa maji ya Shihori?+ Na kwa nini ujishughulishe na njia ya Ashuru+ ili kunywa maji ya ule Mto? 19 Ubaya wako unapaswa kukurekebisha,+ na matendo yako mwenyewe ya kukosa uaminifu yanapaswa kukukaripia.+ Jua, basi, na kuona kwamba kumwacha Yehova Mungu wako ni jambo baya na lenye uchungu,+ nawe hujaingiwa na hofu yangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi.
20 “‘Kwa maana zamani nilivunja nira yako vipande-vipande;+ nilizikata pingu zako. Lakini ulisema: “Mimi sitatumikia,” kwa maana ulikuwa umelala huku umejinyoosha+ juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi,+ ukifanya ukahaba.+ 21 Lakini mimi nilikuwa nimekupanda kama mzabibu bora mwekundu,+ wote ukiwa mbegu ya kweli. Basi ni jinsi gani umebadilika kunielekea ukawa machipukizi yaliyoharibika ya mzabibu wa kigeni?’+
22 “‘Lakini hata ukijiosha kwa magadi na kujichukulia kiasi kikubwa cha sabuni,+ kosa lako hakika lingekuwa doa mbele zangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 23 Jinsi gani unaweza kusema, ‘Mimi sikujitia unajisi.+ Sikufuata Mabaali’?+ Ona njia yako katika bonde.+ Angalia lile ambalo umefanya. Ngamia-jike mchanga aliye mwepesi ambaye anakimbia huku na huku bila mwelekeo katika njia zake; 24 punda-milia+ aliyezoea nyika, wakati wa tamaa ya nafsi yake, akiupumua upepo;+ wakati wake wa kupandwa, ni nani anayeweza kumgeuza? Wale wote wanaomtafuta hawatajichosha. Watampata katika mwezi wake. 25 Zuia mguu wako usiwe mguu wazi, na koo yako isiwe na kiu.+ Lakini ulisema, ‘Hakuna matumaini!+ Hapana, lakini mimi nimewapenda wageni,+ nami nitawafuata.’+
26 “Watu wa nyumba ya Israeli wameona aibu kama ile ya mwizi ambaye amekamatwa,+ wao, wafalme wao, wakuu wao na makuhani wao na manabii wao.+ 27 Wanauambia mti, ‘Wewe ni baba yangu,’+ na jiwe, ‘Wewe ulinizaa.’ Lakini mimi wamenigeuzia sehemu ya nyuma ya shingo badala ya uso.+ Na wakati wa msiba wao watasema, ‘Simama utuokoe!’+
28 “Lakini iko wapi miungu yako ambayo umejifanyia?+ Na isimame ikiwa inaweza kukuokoa wakati wa msiba wako.+ Kwa maana miungu yako imekuwa kama hesabu ya majiji yako, Ee Yuda.+
29 “‘Kwa nini mnaendelea kushindana nami?+ Kwa nini nyote mmenikosea?’+ asema Yehova. 30 Nimewapiga wana wenu bila matokeo.+ Hawakushika nidhamu yoyote.+ Upanga wenu umewala manabii wenu, kama simba anayeangamiza.+ 31 Enyi kizazi, oneni wenyewe neno la Yehova.+
“Je, nimekuwa nyika tupu kwa Israeli+ au nchi yenye giza zito? Kwa nini hawa, watu wangu, wamesema, ‘Tumeenda huku na huku. Hatutakuja kwako tena’?+ 32 Je, bikira anaweza kuyasahau mapambo yake, na bibi-arusi mavazi yake ya kifuani? Lakini watu wangu mwenyewe—wamenisahau mimi kwa muda wa siku zisizo na hesabu.+
33 “Kwa nini wewe, Ee mwanamke, unaboresha njia yako ili kutafuta upendo? Kwa hiyo pia umefundisha njia zako mambo mabaya.+ 34 Pia, alama za damu za nafsi+ za maskini wasio na hatia+ zimepatikana katika pindo za nguo zako. Sikuzipata katika tendo la kuvunja na kuingia, lakini ziko juu ya hizo zote.+
35 “Lakini unasema, ‘Nimebaki bila hatia. Hakika hasira yake imeondoka juu yangu.’+
“Tazama, ninaingia katika ugomvi pamoja nawe kwa sababu unasema, ‘Sikutenda dhambi.’+ 36 Kwa nini unaona kubadili njia yako kuwa jambo dogo sana?+ Utaona aibu kwa ajili ya Misri,+ kama vile ulivyoona aibu kwa ajili ya Ashuru.+ 37 Kwa sababu hiyo pia utaenda mikono yako ikiwa juu ya kichwa chako,+ kwa sababu Yehova amevikataa vitu vyako ambavyo una uhakika ndani yake, nawe hutapata mafanikio katika hivyo.”
3 Kuna msemo: “Mwanamume akimwacha mke wake na mke huyo aondoke kwake na kuwa wa mwanamume mwingine, je, mwanamume huyo anapaswa kurudi kwake tena?”+
Je, nchi hiyo haikutiwa unajisi hakika?+
“Nawe mwenyewe umefanya ukahaba pamoja na rafiki wengi;+ na je, unapaswa kurudi kwangu mimi?”+ asema Yehova. 2 “Inua macho yako kuelekea mapito yaliyokanyagwa, ukaone.+ Ni wapi ambapo hawakukulala kinguvu?+ Umekaa kando ya njia kwa ajili yao, kama Mwarabu nyikani;+ nawe unaendelea kuitia nchi unajisi kwa matendo yako ya ukahaba na kwa ubaya wako.+ 3 Kwa hiyo manyunyu mengi yamezuiwa,+ na hata mvua ya masika haikunyesha.+ Nawe umekuwa na paji la uso la mke anayefanya ukahaba. Umekataa kufedheheka.+ 4 Je, umeniita kutoka sasa na kuendelea ‘Baba yangu,+ wewe ni rafiki wa karibu wa ujana wangu!+ 5 Je, mtu anapaswa kufungia kinyongo mpaka wakati usio na kipimo, au kuendelea kuangalia jambo milele?’+ Tazama! Umesema, nawe ukaendelea kufanya mambo mabaya na kupata ushindi.”+
6 Na Yehova akaniambia katika siku za mfalme Yosia:+ “‘Je, umeona lile ambalo Israeli asiye mwaminifu amefanya?+ Anaenda juu ya kila mlima mrefu+ na chini ya kila mti wenye majani mengi,+ ili afanye ukahaba huko.+ 7 Na baada ya yeye kufanya mambo hayo yote niliendelea kusema kwamba arudi kwangu, lakini hakurudi;+ na Yuda akaendelea kumtazama dada yake mwenye hila.+ 8 Nilipoona jambo hilo, kwa sababu Israeli asiye mwaminifu alikuwa amefanya uzinzi, nilimfukuza+ nami nikampa cheti chake cha talaka kamili,+ ingawa hivyo Yuda, dada yake anayetenda kwa hila, hakuogopa, bali yeye mwenyewe pia akaanza kwenda na kufanya ukahaba.+ 9 Na ukahaba wake ulifanyika kwa sababu ya maoni yake ya kipuuzi, naye aliendelea kuitia nchi unajisi+ na kufanya uzinzi pamoja na mawe na pamoja na miti;+ 10 na hata ijapokuwa hayo yote Yuda dada yake mwenye hila hakurudi kwangu kwa moyo+ wake wote, ila kwa uwongo,’+ asema Yehova.”
11 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Israeli asiye mwaminifu ameonyesha nafsi yake kuwa yenye uadilifu kuliko Yuda anayetenda kwa hila.+ 12 Nenda, nawe uitangazie kaskazini+ maneno haya na kusema:
“‘“Rudi, Ee Israeli mwenye kuasi,” asema Yehova.’+ ‘ “Sitawatazama ninyi kwa hasira,+ kwa maana mimi ni mshikamanifu,”+ asema Yehova.’ ‘ “Sitaendelea kufungia kinyongo mpaka wakati usio na kipimo.+ 13 Ila uangalie tu kosa lako, kwa maana umemkosea Yehova Mungu wako.+ Nawe umeendelea kutawanya njia zako kwa wageni+ chini ya kila mti wenye majani mengi,+ lakini ninyi hamkuisikiliza sauti yangu,” asema Yehova.’”
14 “Rudini, enyi wana waasi,’+ asema Yehova. “Kwa maana mimi nimekuwa mume wenu;+ nami nitawachukua, mmoja kutoka katika jiji moja na wawili kutoka katika familia moja, nami nitawaleta ninyi Sayuni.+ 15 Nami nitawapa wachungaji wenye kupatana na moyo wangu,+ na hakika wao watawalisha ninyi kwa ujuzi na ufahamu.+ 16 Na itatukia kwamba mtakuwa wengi nanyi hakika mtazaa matunda katika nchi siku hizo,” asema Yehova.+ “Hawatasema tena, ‘Sanduku la agano la Yehova!’+ wala halitaingia moyoni, wala hawatalikumbuka+ au kulitamani, nalo halitafanywa tena. 17 Wakati huo wataita Yerusalemu kuwa kiti cha ufalme cha Yehova;+ na mataifa yote yataletwa pamoja+ kwake kwa jina la Yehova katika Yerusalemu,+ nao hawataufuata tena ukaidi wa moyo wao mbaya.”+
18 “Katika siku hizo watatembea, nyumba ya Yuda ikiwa kando ya nyumba ya Israeli,+ nao pamoja+ watatoka katika nchi ya kaskazini na kuingia katika nchi ambayo niliwapa mababu zenu kuwa fungu la urithi.+ 19 Nami mwenyewe nimesema, ‘Lo! jinsi nilivyokuweka kati ya wana na kukupa nchi yenye kutamanika,+ fungu la urithi la pambo la majeshi ya mataifa!’ Nami nikasema tena, Ninyi mtaniita ‘ “Baba yangu!”+ nanyi hamtarudi mwache kunifuata.’ 20 ‘Kwa kweli kama mke anavyomwacha mwenzake kwa hila,+ ndivyo ninyi, enyi nyumba ya Israeli, mlivyonitendea kwa hila,’+ asema Yehova.”
21 Sauti imesikika katika njia zilizokanyagwa, kulia, kusihi kwa wana wa Israeli. Kwa maana wameipotosha njia yao;+ wamemsahau Yehova Mungu wao.+
22 “Rudini, ninyi wana waasi.+ Nitaiponya hali yenu ya uasi.”+
“Sisi hapa! Tumekuja kwako, kwa maana wewe, Ee Yehova, ni Mungu wetu.+ 23 Kwa kweli vilima na pia machafuko juu ya milima+ ni uwongo.+ Kwa kweli wokovu wa Israeli uko katika Yehova Mungu wetu.+ 24 Lakini jambo la aibu+ limekula kazi ya mababu zetu tangu ujana wetu, makundi yao na mifugo yao, wana wao na binti zao. 25 Tunalala katika aibu+ yetu, na fedheha yetu inaendelea kutufunika;+ kwa maana tumemtendea dhambi+ Yehova Mungu wetu, sisi na baba zetu tangu ujana wetu na kuendelea mpaka leo hii,+ nasi hatukuitii sauti ya Yehova Mungu wetu.”+
4 “Kama ukitaka kurudi, Ee Israeli,” asema Yehova, “unaweza kurudi kwangu mimi.+ Nawe ukiondolea mbali machukizo yako kwa ajili yangu,+ basi hutakwenda ukiwa kama mkimbizi. 2 Na hakika wewe ukiapa,+ ‘Kama anavyoishi Yehova katika kweli,+ katika haki na katika uadilifu!’+ ndipo kwa kweli mataifa yatajibariki katika yeye, nayo yatajisifu katika yeye.”+
3 Kwa maana Yehova amesema hivi kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Jilimieni udongo unaofaa kwa kilimo, na msiendelee kupanda kati ya miiba.+ 4 Tahiriweni kwa ajili ya Yehova, na kuondoa magovi ya mioyo yenu,+ ninyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu; ili ghadhabu yangu isitoke kama moto, na hakika iteketeze bila yeyote wa kuizima, kwa sababu ya ubaya wa matendo yenu.”+
5 Tangazeni jambo hilo katika Yuda, na kulihubiri hata katika Yerusalemu,+ na mliseme, na kupiga baragumu katika nchi yote.+ Iteni kwa sauti na kusema: “Jikusanyeni pamoja, nasi tuingie katika majiji yenye ngome.+ 6 Inueni ishara kuelekea Sayuni. Andaeni mahali pa kukimbilia usalama. Msisimame tuli.” Kwa maana kuna msiba ambao ninaleta kutoka kaskazini,+ mshindo mkubwa. 7 Amepanda kama simba kutoka katika kichaka chake,+ na yule anayeyaangamiza mataifa ameondoka;+ ametoka mahali pake ili kuifanya nchi yako kuwa kitu cha kushangaza. Majiji yako yatabomoka hivi kwamba hakutakuwa na mkaaji.+ 8 Kwa sababu hiyo vaeni nguo za magunia.+ Pigeni vifua vyenu na kupiga mayowe,+ kwa sababu hasira ya Yehova inayowaka haijaondoka juu yetu.+
9 “Na itakuwa katika siku hiyo,” asema Yehova, “kwamba moyo wa mfalme utaangamia,+ pia moyo wa wakuu; na hakika makuhani wataingiwa na mshangao, nao manabii watastaajabishwa.”+
10 Nami nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Kwa kweli umewadanganya kabisa watu+ hawa na Yerusalemu, kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’+ na upanga umefika mpaka kwenye nafsi.”
11 Na wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa hivi: “Kuna upepo unaokausha wa mapito ya nyikani+ kwenye njia ya kwenda kwa binti ya watu wangu;+ si wa kupepeta, wala wa kusafisha. 12 Upepo unaovuma kwa nguvu kamili unatoka kwao kuja kwangu. Sasa mimi mwenyewe pia nitasema hukumu nao.+ 13 Tazama! Atakuja kama mawingu ya mvua, na magari yake ni kama upepo wa dhoruba.+ Farasi zake ni wepesi kuliko tai.+ Ole wetu, kwa sababu tumeporwa! 14 Osha moyo wako uwe safi kutokana na ubaya mtupu, Ee Yerusalemu, ili upate kuokolewa.+ Fikira zako zenye makosa zitakaa ndani yako mpaka wakati gani?+ 15 Kwa maana sauti inasema kutoka Dani+ nayo inatangaza jambo lenye kudhuru kutoka eneo lenye milima la Efraimu.+ 16 Ndiyo, tangazeni jambo hilo, kwa mataifa. Lihubirini dhidi ya Yerusalemu.”
“Walinzi wanakuja kutoka katika nchi ya mbali,+ nao wataipaaza sauti yao juu ya majiji ya Yuda. 17 Wamekuwa kama walinzi wa shamba juu yake pande zote,+ kwa sababu ameniasi hata mimi,”+ asema Yehova. 18 “Njia yako na matendo yako—wewe utalipwa hayo.+ Huu ndio msiba ulio juu yako, kwa maana ni mchungu; kwa sababu umefika mpaka moyoni mwako.”
19 Ee matumbo yangu, matumbo yangu! Nina maumivu makali katika kuta za moyo wangu.+ Moyo wangu umechafuka ndani yangu.+ Siwezi kunyamaza kimya, kwa maana nafsi yangu imesikia sauti ya baragumu, king’ora cha vita.+ 20 Mshindo juu ya mshindo umetangazwa, kwa maana nchi yote imeporwa.+ Ghafula mahema yangu yameporwa,+ na katika muda mfupi vitambaa vya mahema yangu. 21 Nitaendelea kuona ishara, kusikia sauti ya baragumu, mpaka wakati gani?+ 22 Kwa maana watu wangu ni wapumbavu.+ Hawanijali mimi.+ Wao ni wana wasio na hekima; nao si wale walio na uelewaji.+ Wana hekima ya kutenda mabaya, lakini kwa kweli hawajui kutenda mema.+
23 Niliiona nchi, na, tazama! ilikuwa tupu na ukiwa;+ na katika mbingu, na, tazama! nuru yake haikuwapo.+ 24 Niliiona milima, na, tazama! ilikuwa ikitikisika, na vilima vyote vilitetemeshwa.+ 25 Niliona, na, tazama! hapakuwa na mtu wa udongo yeyote, na viumbe vyote vinavyoruka vya mbinguni vilikuwa vimekimbia.+ 26 Niliona, na, tazama! shamba la matunda lilikuwa nyika, na majiji yake yote yalikuwa yamebomolewa.+ Ilikuwa kwa sababu ya Yehova, kwa sababu ya hasira yake inayowaka.
27 Kwa maana Yehova amesema hivi: “Nchi yote itakuwa mahame yenye ukiwa,+ na je, mimi sitafanya maangamizi kamili?+ 28 Kwa sababu nchi hiyo itaomboleza,+ na mbingu juu hakika zitakuwa na giza.+ Ni kwa sababu nimesema, nimefikiria, wala sikujuta, wala sitarudi nyuma kutoka katika jambo hilo.+ 29 Kwa sababu ya sauti ya wapanda-farasi na wapiga-upinde jiji zima linakimbia.+ Wameingia vichakani, nao wamepanda kuingia ndani ya miamba.+ Kila jiji limeachwa, na hakuna mtu anayekaa ndani yake.”
30 Sasa kwa kuwa umeporwa, utafanya nini, kwa sababu ulikuwa ukivaa nguo nyekundu, kwa sababu ulikuwa ukijipamba kwa mapambo ya dhahabu, kwa sababu ulikuwa ukipanua macho yako kwa kujipaka wanja?+ Ulikuwa ukijirembesha kwa ubatili tu.+ Wale wanaokutamani wamekukataa; wanaendelea kuitafuta nafsi yako.+ 31 Kwa maana nimeisikia sauti kama ya mwanamke mgonjwa, taabu kama ya mwanamke anayezaa mtoto wake wa kwanza,+ sauti ya binti Sayuni ambaye anaendelea kuvuta pumzi kwa nguvu. Anaendelea kuinyoosha mikono yake:+ “Ole wangu, sasa, kwa maana nafsi yangu imechoka kwa sababu ya wauaji!”+
5 Nendeni huku na huku katika barabara za Yerusalemu na mwone, sasa, na mjue, nanyi mjitafutie katika viwanja vyake vya watu wote ikiwa mnaweza kumpata mwanadamu,+ ikiwa kuna yeyote anayetenda haki,+ yeyote anayetafuta uaminifu,+ nami nitamsamehe. 2 Hata wakisema: “Kama anavyoishi Yehova!” watakuwa wanaapa kwa uwongo mtupu.+
3 Ee Yehova, je, macho yako hayaangalii uaminifu?+ Umewapiga,+ lakini hawakuwa wagonjwa.+ Uliwaangamiza.+ Walikataa kukubali nidhamu.+ Walizifanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba.+ Walikataa kurudi.+ 4 Hata kama mimi mwenyewe nikisema: “Hakika wao ni wa tabaka ya chini. Walitenda kwa upumbavu, kwa maana wameipuuza njia ya Yehova, hukumu ya Mungu wao.+ 5 Nitashika njia kwenda kwa wakuu na kusema nao;+ kwa maana wao lazima waliiangalia njia ya Yehova, hukumu ya Mungu wao.+ Hakika wao wote pamoja lazima waliivunja nira; lazima wawe walizikata pingu.”+
6 Ndiyo sababu simba kutoka msituni amewashambulia, mbwa-mwitu wa nchi tambarare za jangwani anaendelea kuwapora,+ chui anakaa macho kwenye majiji yao.+ Kila mtu anayetoka humo anararuliwa vipande-vipande. Kwa maana makosa yao yamekuwa mengi; matendo yao ya kukosa uaminifu yamekuwa mengi sana.+
7 Nawezaje kukusamehe kwa ajili ya jambo hili? Wana wako wameniacha, nao wanaendelea kuapa+ kwa kitu ambacho si Mungu.+ Nami niliendelea kuwashibisha,+ lakini wakaendelea kufanya uzinzi,+ nao wanaenda katika nyumba ya mwanamke kahaba wakiwa makundi-makundi. 8 Wamekuwa farasi walioshikwa na nyege, wenye mapumbu yenye nguvu. Kila mmoja wao analia kwa ajili ya mke wa mwenzake.+
9 “Je, nisitoze hesabu kwa sababu ya mambo haya?” asema Yehova.+ “Au, je, nafsi yangu isijilipizie kisasi juu ya taifa ambalo liko hivyo?”+
10 “Njooni juu ya mistari yake ya mizabibu na kuharibu,+ lakini msiangamize kabisa.+ Chukueni machipukizi yake yenye kutoa majani mengi, kwa maana hayo si ya Yehova.+ 11 Kwa maana nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda hakika zimenitendea kwa hila,” asema Yehova.+ 12 “Wamemkana Yehova, nao wanaendelea kusema, ‘Yeye hayuko.+ Na hakuna msiba utakaokuja juu yetu, nasi hatutaona upanga wala njaa.’+ 13 Nao manabii wanakuwa upepo, na lile neno halimo ndani yao.+ Hivyo ndivyo watakavyotendewa.”
14 Kwa hiyo Yehova, Mungu wa majeshi, amesema hivi: “Kwa sababu ninyi mnasema jambo hilo, tazama, nayafanya maneno yangu kinywani mwenu kuwa moto,+ na watu hawa watakuwa kuni, nao hakika utawateketeza.”+
15 “Tazama, ninaleta juu yenu taifa kutoka mbali,+ enyi nyumba ya Israeli,” asema Yehova. “Ni taifa linalodumu. Ni taifa la zamani za kale,+ taifa ambalo lugha yake hamwijui, nanyi hamwezi kusikia na kuelewa yale wanayosema. 16 Podo lao ni kama kaburi lililo wazi; wote ni wanaume wenye nguvu.+ 17 Hakika wao pia watakula mavuno yako na mkate wako.+ Watu hao watakula wana wako na binti zako. Watakula makundi yako na mifugo yako. Watakula mzabibu wako na mtini wako.+ Watavunja-vunja kwa upanga majiji yako yenye ngome unayoyategemea.”
18 “Na hata katika siku hizo,” asema Yehova, “Sitawaangamiza ninyi.+ 19 Na itakuwa kwamba mtasema, ‘Kwa sababu gani Yehova Mungu wetu ametutendea mambo haya yote?’+ Nawe utawaambia, ‘Kama mlivyoniacha mimi, kwenda kumtumikia mungu wa kigeni katika nchi yenu, ndivyo mtakavyowatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.’”+
20 Tangazeni jambo hili katika nyumba ya Yakobo, na kulitangaza katika Yuda, mkisema: 21 “Sikieni jambo hili, sasa, enyi watu wasio na hekima ambao hawana moyo wa ufahamu:+ Wana macho, lakini hawawezi kuona;+ wana masikio, lakini hawawezi kusikia.+ 22 ‘Je, hata hamniogopi mimi,’+ asema Yehova, ‘au, je, hata hamna maumivu makali kwa sababu yangu,+ ambaye nimeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari, sharti linalodumu mpaka wakati usio na kipimo kwamba haiwezi kuvuka? Ingawa mawimbi yake husukasuka, bado hayawezi kushinda; na ingawa huchafuka, bado hayawezi kuuvuka.+ 23 Lakini hawa watu wamekuwa na moyo mgumu na wenye kuasi; wamegeuka kando nao wanaendelea kutembea katika mwendo wao.+ 24 Lakini hawakusema moyoni mwao: “Sasa, na tumwogope Yehova Mungu wetu,+ Yeye anayenyesha mvua kubwa na mvua ya vuli na mvua ya masika katika majira yake,+ Yeye anayetulindia majuma yaliyoamriwa ya mavuno.”+ 25 Makosa yenu wenyewe yameyafukuzia mbali mambo hayo, na dhambi zenu wenyewe zimewazuilia ninyi mema.+
26 “‘Kwa maana watu waovu wamepatikana kati ya watu wangu.+ Wanaendelea kukaza macho, kama wakati wawindaji wa ndege wanapochutama.+ Wameweka mtego wenye kuharibu. Wao wanawanasa watu. 27 Kama tundu lilivyojaa viumbe vinavyoruka, ndivyo nyumba zao zilivyojaa udanganyifu.+ Ndiyo sababu wamekuwa wakuu nao wanapata utajiri.+ 28 Wamenenepa;+ wameng’aa. Pia wamejaa kabisa mambo mabaya. Hawakutetea kesi yoyote,+ hata kesi ya mvulana asiye na baba,+ ili wapate mafanikio;+ nao hawakuifuatilia hukumu ya maskini.’”
29 “Je, nisitoze hesabu kwa sababu ya mambo hayo,” asema Yehova, “au, je, nafsi yangu isijilipizie kisasi juu ya taifa ambalo liko hivyo?+ 30 Hali yenye kushangaza, ndiyo, jambo lenye kuchukiza sana, limetokezwa katika nchi:+ 31 Manabii wenyewe kwa kweli wanatoa unabii kwa uwongo;+ nao makuhani wanakandamiza kulingana na nguvu zao.+ Na watu wangu wamependa mambo yawe hivyo;+ nanyi mtafanya nini mwisho wake?”+
6 Kimbilieni usalama, enyi wana wa Benyamini, kutoka katikati ya Yerusalemu; nanyi mpige baragumu+ katika Tekoa.+ Na mwinue ishara ya moto katika Beth-hakeremu;+ kwa sababu msiba umetazama chini kutoka upande wa kaskazini, mshindo mkubwa.+ 2 Binti Sayuni amefanana kweli na mwanamke mwenye kupendeza na aliye laini.+ 3 Wachungaji na makundi yao walimjia. Walisimamisha mahema yao pande zote juu yake.+ Kila mmoja alilisha sehemu yake.+ 4 Wametakasa vita juu yake:+ “Simameni, na acheni tupande katikati ya mchana!”+
“Ole wetu, kwa maana mchana umepungua, kwa maana vivuli vya jioni vinaendelea kurefuka!”
5 “Simameni, twende wakati wa usiku, tukaiharibu minara ya makao yake.”+
6 Kwa maana Yehova wa majeshi amesema hivi: “Kateni miti+ na mjenge boma la kuzingira+ Yerusalemu. Yeye ni jiji ambalo lazima litozwe hesabu.+ Yeye ni ukandamizaji mtupu katikati yake.+ 7 Kama tangi linavyoweka maji yake yakiwa baridi, ndivyo yeye alivyouweka ubaya wake ukiwa baridi. Jeuri na uporaji zimesikiwa ndani yake;+ ugonjwa na tauni ziko mbele za uso wangu sikuzote. 8 Urekebishwe,+ Ee Yerusalemu, ili nafsi yangu isije ikaondoka kwako ikiwa imechukizwa;+ ili nisije nikakuweka uwe mahame yenye ukiwa, nchi isiyokaliwa.”+
9 Yehova wa majeshi amesema hivi: “Bila shaka wataokota mabaki ya Israeli kama mzabibu.+ Rudisha mkono wako nyuma kama mtu anayekusanya zabibu juu ya vikonyo vya mzabibu.”
10 “Nitasema na nani na kumpa nani onyo, ili wasikie? Tazama! Sikio lao halijatahiriwa, hivi kwamba hawawezi kusikiliza.+ Tazama! Neno la Yehova limekuwa shutuma+ kwao, na katika neno hilo wao hawawezi kupendezwa.+ 11 Nami nimejawa na ghadhabu ya Yehova. Nimechoka kujizuia.”+
“Imwage wakati uleule juu ya mtoto aliye barabarani+ na juu ya kikundi cha vijana walio rafiki za karibu; kwa maana wao pia watakamatwa, mwanamume pamoja na mke wake, mzee pamoja na mtu mwenye siku nyingi.+ 12 Na nyumba zao hakika zitapewa wengine ili wazimiliki, na mashamba na wake vilevile.+ Kwa maana nitanyoosha mkono wangu juu ya wakaaji wa nchi,” asema Yehova.+
13 “Kwa maana kuanzia aliye mdogo zaidi kati yao mpaka aliye mkubwa zaidi kati yao, kila mmoja anajipatia pato lisilo la haki;+ na kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa uwongo.+ 14 Nao wanajaribu kuponya kijuujuu kuvunjika kwa watu wangu,+ wakisema, ‘Kuna amani! Kuna amani!’ wakati hakuna amani.+ 15 Je, waliona aibu kwa sababu jambo walilokuwa wamefanya lilikuwa chukizo?+ Jambo moja ni kwamba hakika wao hawaoni aibu yoyote; jambo lingine ni kwamba hawajapata kujua hata jinsi ya kufedheheka.+ Kwa hiyo wataanguka katikati ya wale wanaoanguka;+ watajikwaa wakati nitakapowatoza hesabu,” Yehova amesema.
16 Yehova amesema hivi: “Simameni tuli katika njia, na kuona, na kuuliza juu ya barabara za zamani za kale, mahali ambapo sasa pana njia nzuri;+ na mtembee ndani yake,+ na kustarehesha nafsi zenu.”+ Lakini waliendelea kusema: “Hatutatembea.”+ 17 “Nami nilisimamisha walinzi juu yenu,+ ‘Isikilizeni sauti ya baragumu!’”+ Lakini waliendelea kusema: “Hatutaisikiliza.”+ 18 “Kwa hiyo sikieni, enyi mataifa! Nawe ujue, Ee kusanyiko, jambo litakalokuwa katikati yao. 19 Sikiliza, Ee dunia! Tazama, ninaleta msiba juu ya watu+ hawa kama matunda ya fikira zao,+ kwa maana hawakuyasikiliza maneno yangu; na sheria yangu—pia waliendelea kuikataa.”+
20 “Ina faida gani kwangu kwamba mnaleta ubani kutoka Sheba+ na kane nzuri kutoka katika nchi ya mbali? Matoleo yenu mazima ya kuteketezwa hayaleti furaha,+ na dhabihu zenu hazikunipendeza mimi.”+ 21 Kwa hiyo Yehova amesema hivi: “Tazama, ninawawekea watu hawa vikwazo,+ nao hakika watajikwaa juu yake, akina baba na wana pamoja; jirani na mwenzake—wataangamia.”+
22 Yehova amesema hivi: “Tazama! Kikundi cha watu kinakuja kutoka nchi ya kaskazini, na kuna taifa kubwa litakaloamshwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+ 23 Watashika upinde na mkuki.+ Ni katili, nao hawatakuwa na huruma. Sauti yao itavuma kama bahari,+ nao watapanda juu ya farasi.+ Limejipanga katika utaratibu wa vita kama mwanamume wa vita juu yako, Ee binti Sayuni.”+
24 Tumesikia habari zake. Mikono yetu imelegea.+ Taabu imetushika, maumivu ya kuzaa kama ya mwanamke anayezaa.+ 25 Usiende nje shambani, wala usitembee njiani; kwa maana kuna upanga wa adui, kuna woga pande zote.+ 26 Ee binti ya watu wangu, vaa nguo ya gunia+ na ugaegae katika majivu.+ Omboleza kama kumwombolezea mwana wa pekee, kilio cha uchungu;+ kwa sababu mporaji atakuja juu yetu kwa ghafula.+
27 “Nimekufanya wewe kuwa mpimaji wa madini katikati ya watu wangu, mtu anayefanya uchunguzi kamili; nawe utaangalia nawe utaichunguza njia yao.+ 28 Wote ni watu wakaidi zaidi,+ wanaotembea wakiwa wachongezi+—shaba na chuma. Wote ni wenye kuharibu.+ 29 Mivukuto+ imeunguzwa. Risasi inatoka ndani ya moto wao.+ Mtu ameendelea kusafisha sana kwa ubatili tu, na wale wabaya hawakutengwa.+ 30 Hakika watu watawaita fedha iliyokataliwa,+ kwa maana Yehova amewakataa.”+
7 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema: 2 “Simama katika lango la nyumba ya Yehova, nawe utangaze hapo neno hili,+ na kusema, ‘Sikieni neno la Yehova, ninyi nyote wa Yuda, mnaoingia katika malango haya ili kumwinamia Yehova. 3 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Fanyeni njia zenu na matendo yenu kuwa mema, nami nitaendelea kuwakalisha mahali hapa.+ 4 Msiyategemee maneno ya uwongo,+ mkisema, ‘Hekalu la Yehova, hekalu la Yehova, hili ni hekalu la Yehova!’ 5 Kwa maana ikiwa hakika mtazifanya njia zenu na matendo yenu kuwa mema, ikiwa hakika mtatenda haki kati ya mtu na mwenzake,+ 6 ikiwa hamtamkandamiza mkaaji mgeni, mvulana asiye na baba na mjane,+ nanyi hamtamwaga damu isiyo na hatia mahali hapa,+ hamtaifuata miungu mingine ili kujiletea wenyewe msiba,+ 7 mimi, nami, hakika nitaendelea kuwakalisha mahali hapa, katika nchi ambayo niliwapa mababu zenu, kutoka wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo.”’”+
8 “Tazama, mnayategemea maneno ya uwongo—hakika haitakuwa na faida yoyote kamwe.+ 9 Je, inawezekana kuwe wizi,+ uuaji+ na uzinzi+ na kuapa kwa uwongo+ na kumfukizia Baali moshi+ wa dhabihu na kuifuata miungu mingine ambayo hamkuijua,+ 10 nanyi mje na kusimama mbele zangu katika nyumba hii ambayo jina langu limeitwa juu yake,+ na kusema, ‘Hakika tutakombolewa,’ huku mkiyafanya machukizo haya yote? 11 Je, nyumba hii ambayo jina langu limeitwa juu yake,+ imekuwa pango tu la wanyang’anyi machoni penu?+ Tazama, mimi mwenyewe pia nimeona jambo hilo,” asema Yehova.+
12 “‘Hata hivyo, nendeni, sasa, mahali pangu palipokuwa katika Shilo,+ ambapo nilifanya jina langu likae hapo pale mwanzoni,+ na kuona nilivyopafanya kwa sababu ya ubaya wa watu wangu Israeli.+ 13 Na sasa kwa sababu mliendelea kufanya kazi hizi zote,’ asema Yehova, ‘nami nikaendelea kusema nanyi, nikiamka mapema na kusema,+ lakini hamkusikiliza,+ nami nikaendelea kuwaita, lakini hamkujibu,+ 14 nitaitendea pia nyumba ambayo jina langu limeitwa juu yake,+ ambayo mnaitegemea,+ na mahali ambapo niliwapa ninyi na mababu zenu, kama nilivyotendea Shilo.+ 15 Nami nitawatupa ninyi nje kutoka mbele za macho yangu,+ kama nilivyowatupa nje ndugu zenu wote, uzao wote wa Efraimu.’+
16 “Nawe usisali kwa ajili ya watu hawa, wala usipaaze kilio cha kusihi kwa ajili yao wala sala wala kuniomba,+ kwa maana sitakusikiliza.+ 17 Je, wewe huoni yale wanayofanya katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?+ 18 Wana wanaokota kuni, na akina baba wanawasha moto, na wake wanakanda unga ili kumfanyia ‘malkia wa mbingu’ keki za dhabihu;+ na miungu mingine inamiminiwa matoleo ya kinywaji+ kusudi wanitie uchungu.+ 19 ‘Je, wananitia mimi uchungu?’ asema Yehova.+ ‘Je, si wao wenyewe, kusudi watie nyuso zao aibu?’+ 20 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama! Hasira yangu na ghadhabu yangu zinamwagwa juu ya mahali hapa,+ juu ya mwanadamu na juu ya mnyama wa kufugwa, na juu ya mti wa shambani+ na juu ya mazao ya udongo; nayo itateketeza, wala haitazimwa.’+
21 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Ongezeni hayo matoleo yenu mazima ya kuteketezwa kwenye dhabihu zenu na kula nyama.+ 22 Kwa maana sikusema na mababu zenu, wala sikuwaamuru wao katika siku nilipowatoa katika nchi ya Misri, kuhusu mambo ya toleo zima la kuteketezwa na dhabihu.+ 23 Lakini niliwaamuru neno hili, nikisema: “Tiini sauti yangu,+ nami nitakuwa Mungu wenu,+ nanyi mtakuwa watu wangu; na mtembee katika njia+ yote ambayo nitawaamuru ninyi, ili iwe vema kwenu.”’+ 24 Lakini hawakusikiliza, wala hawakutega sikio lao,+ bali wakatembea katika mashauri kwa ukaidi wa moyo wao mbaya,+ hivi kwamba wakawa watu wa kuelekea nyuma wala si mbele,+ 25 tangu siku ile mababu zenu walipotoka katika nchi ya Misri mpaka leo hii;+ nami niliendelea kuwatumia ninyi watumishi wangu wote manabii, nikiamka mapema kila siku na kuwatuma.+ 26 Lakini hawakunisikiliza, nao hawakutega sikio lao,+ bali waliendelea kufanya shingo yao kuwa ngumu.+ Walitenda vibaya zaidi kuliko mababu zao!+
27 “Nawe utawaambia maneno haya yote,+ lakini hawatakusikiliza; nawe utawaita, lakini hawatakujibu.+ 28 Nawe utawaambia, ‘Hili ndilo taifa ambalo watu wake hawakuitii sauti ya Yehova Mungu wake,+ nao hawakushika nidhamu.+ Uaminifu umeangamia, nao umekatiliwa mbali kutoka katika kinywa chao.’+
29 “Nyoa nywele zako ambazo hazijakatwa na kuzitupilia mbali,+ na kuimba wimbo wa huzuni+ juu ya vilima vilivyo wazi, kwa maana Yehova amekikataa+ naye atakiacha kizazi ambacho amekighadhibikia.+ 30 ‘Kwa maana wana wa Yuda wamefanya mambo mabaya machoni pangu,’ asema Yehova. ‘Wameyaweka machukizo yao katika nyumba ambayo jina langu limeitwa juu yake, ili kuitia unajisi.+ 31 Nao wamejenga mahali pa juu pa Tofethi,+ palipo katika bonde la mwana wa Hinomu,+ ili kuwateketeza wana wao na binti zao katika moto,+ jambo ambalo sikuamuru wala halikuingia moyoni mwangu.’+
32 “‘Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘wakati halitaitwa tena Tofethi na bonde la mwana wa Hinomu, bali bonde la uuaji;+ nao watazika katika Tofethi bila ya kuwa na nafasi ya kutosha hapo.+ 33 Na maiti za watu hawa zitakuwa chakula cha viumbe vinavyoruka vya mbinguni na cha wanyama wa dunia, pasipo mtu yeyote wa kuwatetemesha.+ 34 Nami nitaikomesha sauti ya kufurahi na sauti ya kushangilia kutoka katika majiji ya Yuda na kutoka katika barabara za Yerusalemu sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi;+ kwa maana nchi itakuwa mahali palipofanywa ukiwa.’”+
8 “Wakati huo,” asema Yehova, “watu wataleta pia mifupa ya wafalme wa Yuda na mifupa ya wakuu wake na mifupa ya makuhani na mifupa ya manabii na mifupa ya wakaaji wa Yerusalemu kutoka katika makaburi yao.+ 2 Nao kwa kweli wataitandaza mbele ya jua na mbele ya mwezi na mbele ya jeshi lote la mbingu ambalo wamelipenda na ambalo wamelitumikia na ambalo wamelifuata+ na ambalo wamelitafuta na ambalo wameliinamia.+ Haitakusanywa, wala haitazikwa. Itakuwa kama mbolea juu ya uso wa nchi.”+
3 “Na hakika wale mabaki wa wale wote wanaobaki kutoka katika familia hii mbaya watachagua kifo badala ya uzima+ katika mahali pote pa wale wanaobaki, ambapo nitakuwa nimewatawanya,”+ asema Yehova wa majeshi.
4 “Nawe uwaambie, ‘Yehova amesema hivi: “Je, wataanguka na wasiamke tena?+ Mtu akirudi, je, yule mwingine hatarudi pia?+ 5 Kwa nini watu hawa, Yerusalemu, wanakosa uaminifu kwa ukosefu wa uaminifu unaodumu? Wameshika udanganyifu;+ wamekataa kurudi.+ 6 Nimetega sikio,+ nami niliendelea kusikiliza.+ Jinsi walivyoendelea kusema haikuwa sawa. Hakuna mtu yeyote aliyekuwa akitubu ubaya wake,+ akisema, ‘Nimefanya nini?’ Kila mmoja anarudi katika mwendo unaopendwa na wengi,+ kama farasi anayekimbia kwenda vitani. 7 Hata korongo juu mbinguni—anajua vema nyakati zake zilizowekwa;+ na njiwa-tetere+ na barawai na teleka—huangalia vema wakati wa kila mmoja wao kuingia. Lakini watu wangu hawajaijua hukumu ya Yehova.”’+
8 “‘Ninyi mnawezaje kusema: “Sisi tuna hekima, nasi tuna sheria ya Yehova”?+ Hakika, sasa, kalamu+ ya uwongo ya waandishi imefanya kazi ya uwongo mtupu. 9 Wenye hekima wameona aibu.+ Wameingiwa na woga nao watashikwa. Tazama! Wamelikataa neno la Yehova, nao wana hekima gani?+ 10 Kwa hiyo nitawapa wanaume wengine wake zao, mashamba yao kwa wale wanaoyamiliki;+ kwa maana, kuanzia aliye mdogo zaidi mpaka aliye mkubwa zaidi, kila mmoja anajipatia pato lisilo la haki;+ kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa uwongo.+ 11 Nao wanajaribu kuponya kijuujuu kuvunjika kwa binti ya watu wangu,+ wakisema: “Kuna amani! Kuna amani!” wakati hakuna amani.+ 12 Je, waliona aibu kwa sababu walikuwa wamefanya chukizo?+ Jambo moja ni kwamba hakika hawakuweza kuona aibu; jambo lingine ni kwamba hawakujua namna ya kufedheheka.+
“‘Kwa hiyo wataanguka katikati ya wale wanaoanguka. Katika wakati wa kuwakazia fikira,+ watajikwaa,’ Yehova amesema.+
13 “‘Nitakapokuwa nikikusanya, nitawamaliza,’ asema Yehova.+ ‘Hakutakuwa na zabibu juu ya mzabibu,+ wala hakutakuwa na tini juu ya mtini, na hakika majani yatakauka. Na vitu ninavyowapa vitapita kando yao.’”
14 “Kwa nini tunaketi tuli? Jikusanyeni pamoja, nasi tuingie katika majiji yenye ngome+ na tunyamaze humo. Kwa maana Yehova Mungu wetu ametunyamazisha,+ naye anatupa sisi maji yaliyotiwa sumu tunywe,+ kwa sababu tumemtendea Yehova dhambi. 15 Amani ilitumainiwa, lakini hakuna mema yaliyokuja;+ wakati wa kuponywa, lakini, tazama! hofu!+ 16 Kukoroma kwa farasi zake kumesikiwa kutoka Dani.+ Kutokana na sauti ya kulia kwa farasi-dume zake nchi nzima imeanza kutikisika.+ Nao wanaingia na kuila nchi na vyote vilivyomo, jiji na wakaaji wake.”
17 “Kwa maana tazama, ninawatuma nyoka katikati yenu, nyoka wenye sumu,+ wasioweza kutumbuizwa,+ na hakika wao watawauma ninyi,” asema Yehova.
18 Huzuni isiyoweza kutibiwa imeniingia.+ Moyo wangu ni mgonjwa. 19 Tazama, kuna sauti ya kilio cha kuomba msaada cha binti ya watu wangu kutoka katika nchi ya mbali:+ “Je, Yehova hayumo Sayuni?+ Au, je, mfalme wake hayumo ndani yake?”+
“Kwa nini wamenitia uchungu kwa sanamu zao za kuchongwa, kwa miungu yao ya kigeni ya ubatili?”+
20 “Mavuno yamepita, kiangazi kimeisha; lakini sisi hatukuokolewa!”+
21 Nimevunjwa-vunjwa+ kwa sababu ya kuvunjika kwa binti ya watu wangu.+ Nimehuzunika. Mshangao kamili umenishika.+ 22 Je, hakuna zeri katika Gileadi?+ Au, je, hakuna mponyaji humo?+ Kwa nini, basi, kupona+ kwa binti ya watu wangu hakujatokea?+
9 Laiti kichwa changu kingekuwa maji, na macho yangu yangekuwa chemchemi ya machozi!+ Ndipo ningelia usiku na mchana kwa ajili ya waliouawa wa binti ya watu wangu.+
2 Laiti ningekuwa na mahali pa kukaa wasafiri+ katika nyika! Ndipo ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa maana wote ni wazinzi,+ kusanyiko kuu la wanaofanya hila;+ 3 nao wanapinda ulimi wao uwe upinde wao katika uwongo;+ lakini katika uaminifu hawajaonyesha kuwa ni wenye nguvu katika nchi.
“Kwa maana walienda kutoka ubaya mpaka ubaya, nao walinipuuza hata mimi,”+ asema Yehova.
4 “Jihadharini kila mmoja na rafiki yake,+ wala msimtegemee ndugu hata kidogo.+ Kwa maana kila ndugu hakika atanyakua mahali pa mwingine,+ na kila rafiki atatembea huku na huku akiwa mchongezi,+ 5 nao wanaendelea kumchezea kila mmoja rafiki yake;+ nao hawasemi ukweli hata kidogo. Wameufundisha ulimi wao kusema uwongo.+ Wamejichosha tu katika kufanya kosa.+
6 “Unaketi katikati ya udanganyifu.+ Kupitia udanganyifu wamekataa kunijua mimi,”+ asema Yehova.
7 Kwa hiyo Yehova wa majeshi amesema hivi: “Tazama, ninawayeyusha, nami lazima niwachunguze,+ kwa sababu nitatendaje vinginevyo kwa ajili ya binti ya watu wangu?+ 8 Ulimi wao ni mshale unaoua.+ Huo umesema udanganyifu. Kwa kinywa chake, mtu anaendelea kusema amani pamoja na mwenzake; lakini ndani yake anaweka mavizio yake.”+
9 “Kwa sababu ya mambo hayo, je, nisiwatoze wao hesabu?” asema Yehova. “Au, je, nafsi yangu isijilipizie kisasi juu ya taifa ambalo liko hivyo?+ 10 Nitapaaza kilio na maombolezo juu ya milima, na wimbo wa huzuni+ juu ya viwanja vya malisho; kwa maana vitakuwa vimeteketezwa+ hivi kwamba hakuna mwanadamu anayepita katikati na kwa kweli watu hawataisikia sauti ya mifugo.+ Kiumbe kinachoruka cha mbinguni na mnyama watakuwa wamekimbia; watakuwa wameenda.+ 11 Nami nitafanya Yerusalemu kuwa rundo la mawe,+ mapango ya mbwa-mwitu;+ na majiji ya Yuda nitayafanya kuwa mahame yenye ukiwa, bila mkaaji.+
12 “Ni mwanadamu yupi ambaye ana hekima, ili aelewe jambo hili, yule ambaye kinywa cha Yehova kimesema naye, ili aseme jambo hili?+ Kwa nini nchi iangamie, kwa kweli iteketezwe kama nyika bila yeyote wa kupita katikati?”+
13 Na Yehova akasema: “Kwa sababu wameiacha sheria yangu ambayo nilitoa iwe mbele yao, na kwa sababu hawakuitii sauti yangu wala kutembea ndani yake,+ 14 lakini waliendelea kufuata ukaidi wa moyo+ wao na sanamu za Baali,+ ambazo baba zao walikuwa wamewafundisha;+ 15 kwa hiyo Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Tazama, mimi ninawafanya wao, yaani, watu hawa, kula pakanga,+ nami nitawafanya kunywa maji yaliyotiwa sumu;+ 16 nami nitawatawanya kati ya mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuyajua,+ nami nitatuma upanga uwafuate mpaka nitakapowaangamiza.’+
17 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Jiendesheni kwa uelewaji, na kuwaita wanawake wanaoimba nyimbo za huzuni,+ ili waje; na iteni wanawake stadi, ili waje,+ 18 na ili wafanye haraka na kufanya maombolezo juu yetu. Macho yetu na yatiririke machozi, macho yetu yanayong’aa na yatiririke maji.+ 19 Kwa maana ni sauti ya maombolezo ambayo imesikiwa kutoka Sayuni:+ “Jinsi tulivyoporwa!+ Jinsi tulivyoona aibu! Kwa maana tumeiacha nchi; kwa maana wameyatupilia mbali makao yetu.”+ 20 Lakini lisikieni neno la Yehova, enyi wanawake, na sikio lenu lichukue neno la kinywa chake. Kisha mwafundishe binti zenu maombolezo,+ na kila mwanamke amfundishe mwenzake wimbo wa huzuni.+ 21 Kwa maana kifo kimekuja kupitia madirisha yetu; kimeingia ndani ya minara ya makao yetu, ili kumkatilia mbali mtoto kutoka barabarani, vijana kutoka katika viwanja vya watu wote.’+
22 “Sema, ‘Yehova asema hivi: “Maiti za wanadamu zitaanguka kama mbolea juu ya uso wa uwanja na kama mafungu ya nafaka iliyokatwa hivi karibuni nyuma ya mvunaji, bila yeyote wa kukusanya.”’”+
23 Yehova amesema hivi: “Mtu mwenye hekima asijigambe kwa sababu ya hekima yake,+ wala mwanamume mwenye nguvu asijigambe kwa sababu ya nguvu zake.+ Mtu tajiri asijigambe kwa sababu ya utajiri wake.”+
24 “Lakini yule anayejigamba na ajigambe kwa sababu ya jambo hili, kuwa na ufahamu+ na kuwa na ujuzi kunihusu mimi, kwamba mimi ni Yehova,+ Yeye anayeonyesha fadhili zenye upendo, haki na uadilifu duniani;+ kwa maana mimi hupendezwa na mambo hayo,”+ asema Yehova.
25 “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitamtoza hesabu kila mtu aliyetahiriwa lakini ambaye bado yumo katika hali ya kutotahiriwa,+ 26 juu ya Misri+ na juu ya Yuda+ na juu ya Edomu+ na juu ya wana wa Amoni+ na juu ya Moabu+ na juu ya wote wenye nywele zilizokatwa kwenye vipaji vya nyuso wanaokaa nyikani;+ kwa maana mataifa yote hayakutahiriwa, na nyumba yote ya Israeli hawakutahiriwa moyoni.”+
10 Sikieni neno ambalo Yehova amesema juu yenu, enyi nyumba ya Israeli. 2 Yehova amesema hivi: “Msijifunze njia ya mataifa hata kidogo,+ wala msiingiwe na hofu kutokana na ishara za mbinguni, kwa sababu mataifa yanaingiwa na hofu kutokana nazo.+ 3 Kwa maana desturi za vikundi vya watu+ ni pumzi tu, kwa sababu ni mti+ tu ambao mtu amekata kutoka msituni, kazi ya mikono ya fundi mwenye tezo.+ 4 Na kwa fedha na dhahabu mtu huzifanya zipendeze.+ Huzifunga kwa misumari na kwa nyundo, ili yoyote isiyumbe-yumbe.+ 5 Hizo ni kama sanamu ya kufukuza ndege ya shamba la matango, nazo haziwezi kusema.+ Nazo hakika hubebwa, kwa maana haziwezi kupiga hatua zozote.+ Zisiwatie woga, kwa maana haziwezi kufanya jambo lolote lenye kuleta msiba, na zaidi ya hayo, haziwezi kufanya wema wowote.”+
6 Kwa vyovyote hakuna yeyote aliye kama wewe, Ee Yehova.+ Wewe ni mkuu, na jina lako ni kuu katika nguvu.+ 7 Ni nani ambaye hapaswi kukuogopa,+ Ee Mfalme wa mataifa,+ kwa maana inafaa kwako; kwa sababu kati ya wote wenye hekima wa mataifa na kati ya falme zao zote kwa vyovyote hakuna yeyote aliye kama wewe.+ 8 Na wakati uleule wao hawatumii akili na ni wajinga.+ Mti huchochea kufuatilia ubatili tu.+ 9 Fedha iliyofuliwa ikawa mabamba ndiyo inayoletwa kutoka Tarshishi,+ na dhahabu kutoka Ufazi,+ kazi ya fundi na ya mikono ya fundi wa chuma; mavazi yao ni uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau. Vyote ni kazi ya watu stadi.+
10 Lakini kwa kweli Yehova ni Mungu.+ Yeye ndiye Mungu aliye hai+ na Mfalme mpaka wakati usio na kipimo.+ Kwa sababu ya ghadhabu yake dunia itatikisika,+ na hakuna mataifa yatakayostahimili shutuma yake.+ 11 Ninyi mtawaambia hivi: “Miungu+ ambayo haikuzifanya mbingu na dunia ndiyo itakayoangamia kutoka katika dunia+ na kutoka chini ya mbingu hizi.” 12 Yeye ndiye Mtengenezaji wa dunia kwa nguvu zake,+ Yeye anayeifanya imara nchi yenye kuzaa kwa hekima yake,+ na Yeye aliyezitandaza mbingu kwa uelewaji wake.+ 13 Kutokana na sauti yake yeye huleta machafuko ya maji mbinguni,+ naye husababisha mivuke ipande kutoka mwisho wa dunia.+ Hata ameyafanya malango kwa ajili ya mvua,+ naye huuleta upepo kutoka katika maghala yake.+
14 Kila mtu amejiendesha kwa kukosa sana kutumia akili asiweze kujua.+ Hakika kila fundi wa chuma ataona aibu kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+ kwa maana sanamu yake ya kuyeyushwa ni uwongo,+ na hamna roho ndani yake.+ 15 Hizo ni ubatili, kazi ya mzaha.+ Zitaangamia siku zitakapokaziwa fikira.+
16 Yeye aliye Fungu la Yakobo+ si kama vitu hivyo, kwa maana yeye ndiye Mfanyizaji wa vitu vyote,+ na Israeli ndiyo fimbo ya urithi wake.+ Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+
17 Kusanya kifurushi chako kutoka chini,+ Ee mwanamke anayekaa chini ya mkazo.+ 18 Kwa maana Yehova amesema hivi: “Tazama, ninawatupa nje kwa kombeo wakaaji wa dunia pindi hii,+ nami nitawataabisha ili wapate kujua.”+
19 Ole wangu kwa sababu ya kuvunjika kwangu!+ Pigo langu limekuwa na ugonjwa. Nami nimesema: “Hakika huu ni ugonjwa wangu, nami nitauchukua.+ 20 Hema langu limeporwa, na kamba zangu zote za mahema zimekatwa vipande viwili.+ Wanangu wameondoka kwangu, nao hawapo tena.+ Hakuna yeyote anayetandaza tena hema langu wala kuinua vitambaa vyangu vya mahema. 21 Kwa maana wachungaji wamejiendesha bila kutumia akili,+ wala hawakumtafuta Yehova.+ Ndiyo sababu hawakutenda kwa ufahamu, na wanyama wao wote waliolishwa wametawanywa.”+
22 Sikiliza! Habari! Tazama imekuja, pia mshindo mkubwa kutoka katika nchi ya kaskazini,+ ili kuyafanya majiji ya Yuda kuwa mahame yenye ukiwa, mapango ya mbwa-mwitu.+
23 Ninajua vema, Ee Yehova, kwamba njia ya mtu wa udongo haimo katika uwezo wake. Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.+ 24 Hata hivyo, Ee Yehova, nirekebishe mimi kulingana na hukumu;+ si katika hasira yako,+ usije ukanimaliza.+ 25 Mwaga ghadhabu yako juu ya mataifa+ ambayo yamekupuuza,+ na juu ya familia ambazo hazikuliitia jina lako.+ Kwa maana wamemla Yakobo.+ Ndiyo, wamemla, nao wanaendelea kumwangamiza;+ nao wameyafanya makao yake kuwa ukiwa.+
11 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema: 2 “Sikieni maneno ya agano hili!
“Nawe uyaseme+ kwa watu wa Yuda na kwa wakaaji wa Yerusalemu, 3 nawe uwaambie, ‘Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi: “Amelaaniwa mtu yule ambaye hayasikilizi maneno ya agano hili,+ 4 ambayo niliwaamuru mababu zenu siku ile niliyowatoa katika nchi ya Misri,+ kutoka katika tanuru ya chuma,+ nikisema, ‘Tiini sauti yangu, nanyi mfanye mambo kulingana na yote ninayowaamuru;+ nanyi hakika mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu,+ 5 kwa kusudi la kutimiza kiapo nilichowaapia mababu zenu,+ kuwapa nchi inayotiririka maziwa na asali,+ kama ilivyo leo hii.’”’”
Nami nikajibu na kusema: “Amina, Ee Yehova.”
6 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Tangaza maneno haya yote katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu,+ ukisema, ‘Sikieni maneno ya agano hili, nanyi lazima myafanye.+ 7 Kwa maana niliwaonya mababu zenu siku ile niliyowatoa katika nchi ya Misri+ na mpaka leo hii, nikiamka mapema na kuwaonya, nikisema: “Tiini sauti yangu.”+ 8 Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao,+ bali wakaendelea kutembea kila mmoja katika ukaidi wa moyo wake mbaya;+ na kwa hiyo nikaleta juu yao maneno yote ya agano hili nililowaamuru kufanya, lakini hawakufanya.’”
9 Na zaidi, Yehova akaniambia: “Hila imepatikana kati ya watu wa Yuda na kati ya wakaaji wa Yerusalemu.+ 10 Wamerudi kwenye makosa ya mababu zao,+ wale wa kwanza, waliokataa kuyatii maneno yangu, lakini ambao wenyewe wameifuata miungu mingine ili kuitumikia.+ Nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda zimevunja agano langu nililofanya pamoja na mababu zao.+ 11 Kwa hiyo Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta juu yao msiba+ ambao hawataweza kuondoka ndani yake;+ nao hakika wataniomba msaada, lakini sitawasikiliza.+ 12 Na majiji ya Yuda na wakaaji wa Yerusalemu wataenda na kuiomba msaada miungu ambayo wanaifukizia moshi wa dhabihu,+ lakini ambayo hakika haitawaletea wokovu wowote katika wakati wa msiba wao.+ 13 Kwa maana miungu yako imekuwa mingi kama majiji yako, Ee Yuda;+ nanyi mmeweka madhabahu nyingi kama barabara za Yerusalemu kwa ajili ya kile kitu cha aibu,+ madhabahu za kumfukizia Baali moshi wa dhabihu.’+
14 “Nawe usisali kwa ajili ya watu hawa, wala usipaaze kilio cha kusihi wala sala kwa ajili yao,+ kwa maana sitawasikiliza wakati watakaponiomba kuhusu msiba wao.+
15 “Mpendwa wangu ana kazi gani ndani ya nyumba yangu,+ hivi kwamba wengi wao wafanye jambo hili,+ hii mbinu ya uovu?+ Na kwa nyama takatifu, je, wao watafanya jambo hilo lipite kutoka juu yako,+ msiba wako utakapokuja? Je, wewe utafurahi wakati huo?+ 16 ‘Mzeituni wenye majani mengi, wenye kupendeza kwa kuwa na matunda na kwa umbo,’ ndivyo ambavyo Yehova amekuita jina lako.+ Kwa sauti ya mngurumo mkubwa, amewasha moto juu yake, nao wamevunja matawi yake.+
17 “Na Yehova wa majeshi, Mpandaji wako,+ ametangaza msiba juu yako kwa sababu ya ubaya wa nyumba ya Israeli+ na nyumba ya Yuda ambao wametenda kwa upande wao ili kunitia uchungu kwa kumfukizia Baali moshi wa dhabihu.”+
18 Na Yehova amenijulisha ili nijue. Wakati huo ulinionyesha matendo yao.+ 19 Nami nilikuwa kama mwana-kondoo dume, mtulivu, ambaye huletwa machinjioni,+ nami sikujua kwamba walipanga hila juu yangu:+ “Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali kutoka katika nchi ya walio hai,+ ili jina lake lisikumbukwe tena.” 20 Lakini Yehova wa majeshi anahukumu kwa uadilifu;+ anachunguza figo na moyo.+ Lo! acha nione kisasi chako juu yao, kwa maana ni kwako wewe nimeifunua kesi yangu.+
21 Kwa hiyo Yehova amesema hivi juu ya watu wa Anathothi+ wanaoitafuta nafsi yako, wakisema: “Usitoe unabii katika jina la Yehova,+ usije ukafa mkononi mwetu”; 22 kwa hiyo Yehova wa majeshi amesema hivi: “Tazama, mimi ninakaza fikira zangu juu yao. Vijana watakufa kwa upanga.+ Wana wao na binti zao watakufa kwa njaa.+ 23 Nao hawatakuwa hata na mabaki, kwa sababu nitaleta msiba juu ya watu wa Anathothi,+ mwaka wa kuwakazia fikira.”+
12 Wewe ni mwadilifu,+ Ee Yehova, ninapokuletea lalamiko langu, kwa kweli ninaposema nawe hata kuhusu mambo ya hukumu. Kwa nini njia ya waovu ndiyo imefanikiwa,+ kwamba wale wote wanaofanya hila ndio hawana wasiwasi? 2 Umewapanda; nao pia wametia mizizi. Wanaendelea kusonga mbele; nao pia wamezaa matunda. Wewe upo karibu katika kinywa chao, lakini mbali na figo zao.+ 3 Nawe, Ee Yehova, unanijua mimi vema;+ unaniona, nawe umeuchunguza moyo wangu katika muungano na wewe.+ Waweke peke yao kama kondoo wa kuchinjwa,+ na kuwatenga kwa ajili ya siku ya kuuawa. 4 Nchi itaendelea kunyauka+ mpaka wakati gani, na majani ya uwanja wote kukauka?+ Kwa sababu ya ubaya wa wale wanaokaa ndani yake wanyama na viumbe vinavyoruka vimefagiliwa mbali.+ Kwa maana wamesema: “Yeye hauoni wakati wetu ujao.”
5 Kwa sababu umekimbia pamoja na watu wanaoenda kwa miguu, nao wakakuchosha, basi, unawezaje kushindana mbio na farasi?+ Na je, wewe una uhakika katika nchi ya amani?+ Basi utatendaje kati ya vichaka vyenye fahari kando ya Yordani?+ 6 Kwa maana hata ndugu zako mwenyewe na nyumba ya baba yako, hata wao wenyewe wamekutendea kwa hila.+ Hata wao wenyewe wameita nyuma yako kwa sauti kubwa. Usiwe na imani nao hata kidogo, eti kwa sababu wanakuambia mambo mema.+
7 “Nimeiacha nyumba yangu;+ nimeuacha urithi wangu;+ nimemtia mpendwa wa nafsi yangu mkononi mwa adui zake.+ 8 Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba msituni. Yeye amepaaza sauti yake juu yangu. Ndiyo sababu nimemchukia.+ 9 Urithi+ wangu kwangu ni kama ndege mwenye kuwinda wa rangi nyingi;+ ndege wenye kuwinda wamezunguka pande zote juu yake. Njooni, kusanyikeni pamoja, ninyi nyote wanyama wa mwituni; waleteni ili wale.+ 10 Wachungaji+ wengi wameliharibu shamba langu la mizabibu;+ wamelikanyaga fungu langu.+ Fungu langu linalotamanika+ wameligeuza kuwa nyika ya mahame yenye ukiwa. 11 Limefanywa kuwa mahame yenye ukiwa;+ limenyauka; limefanywa kuwa ukiwa kwangu.+ Nchi yote imefanywa kuwa ukiwa, kwa sababu hakuna mtu ambaye amelitia jambo hilo moyoni.+ 12 Waporaji wamekuja kwenye mapito yote yaliyokanyagwa sana. Kwa maana upanga wa Yehova unakula kutoka mwisho mmoja wa nchi mpaka mwisho ule mwingine wa nchi.+ Hakuna amani kwa yeyote mwenye mwili. 13 Wamepanda ngano, lakini wamevuna miiba.+ Wamefanya kazi mpaka wakawa wagonjwa; hawatakuwa na faida yoyote.+ Nao hakika wataona aibu kwa ajili ya mazao yenu kwa sababu ya hasira ya Yehova inayowaka.”
14 Yehova amesema hivi juu ya jirani zangu wote wabaya,+ wanaogusa fungu la urithi ambalo niliwamilikisha watu wangu, Israeli:+ “Tazama, ninawang’oa kutoka katika nchi yao;+ na nyumba ya Yuda nitaing’oa kutoka katikati yao.+ 15 Na itatukia kwamba baada ya kuwang’oa hakika tena nitawaonyesha rehema+ na kuwarudisha, kila mmoja kwenye fungu la urithi wake na kila mmoja kwenye shamba lake.”+
16 “Na itatukia kwamba ikiwa kwa hakika watajifunza njia za watu wangu katika kuapa kwa jina langu,+ ‘Kama anavyoishi Yehova!’ kama walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa Baali,+ wao pia watajengwa katikati ya watu wangu.+ 17 Lakini wasipotii, mimi pia nitaling’oa taifa lile, nitaling’oa na kuliharibu,”+ asema Yehova.
13 Yehova ameniambia hivi: “Nenda, ujipatie mshipi wa kitani uutie kiunoni mwako, lakini usiutie ndani ya maji yoyote.” 2 Basi nikauchukua mshipi kulingana na neno la Yehova, nikautia kiunoni mwangu. 3 Na neno la Yehova likanijia mara ya pili, na kusema: 4 “Uchukue ule mshipi uliopata, ulio kiunoni mwako, nawe usimame, uende Efrati,+ na kuuficha hapo katika mpasuko wa mwamba.” 5 Basi nikaenda, nikauficha kando ya Efrati, kama Yehova alivyoniamuru.
6 Lakini ikawa baada ya siku nyingi kwamba Yehova akaniambia: “Simama, nenda Efrati na kuchukua kutoka huko ule mshipi niliokuamuru uufiche huko.” 7 Basi nikaenda Efrati, nikachimba na kuuchukua ule mshipi kutoka mahali ambapo niliuficha, na, tazama! mshipi ulikuwa umeharibika; haukufaa kwa jambo lolote.
8 Ndipo neno la Yehova likanijia, na kusema: 9 “Yehova amesema hivi, ‘Ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda+ na kiburi kingi cha Yerusalemu. 10 Watu hawa wabaya wanaokataa kuyatii maneno yangu,+ wanaotembea katika ukaidi wa moyo+ wao na wanaoendelea kufuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiinamia,+ pia watakuwa kama mshipi huu ambao haufai kwa jambo lolote.’ 11 ‘Kwa maana kama vile mshipi unavyoshikamana na kiuno cha mtu, ndivyo nilivyoifanya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda kushikamana nami,’+ asema Yehova, ‘ili wawe kwangu kikundi cha watu+ na jina+ na sifa na kitu kizuri; lakini hawakutii.’+
12 “Nawe uwaambie neno hili, ‘Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi: “Kila mtungi mkubwa hujazwa divai.”’+ Nao hakika watakuambia, ‘Je, hatujui hakika kwamba kila mtungi mkubwa hujazwa divai?’ 13 Nawe uwaambie, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama, ninawajaza ulevi wakaaji wote wa nchi hii na wafalme wanaoketi kwa ajili ya Daudi+ juu ya kiti chake cha ufalme na makuhani na manabii na wakaaji wote wa Yerusalemu.+ 14 Nami nitawagonganisha mmoja na mwingine, akina baba na wana, wakati uleule,”+ asema Yehova. “Sitaonyesha huruma, wala kuwa na majonzi, nami sitakuwa na rehema ya kujizuia kuwaharibu.”’+
15 “Sikieni na mtege sikio. Msiwe na majivuno,+ kwa maana Yehova amesema.+ 16 Mpeni Yehova Mungu wenu utukufu,+ kabla hajaleta giza+ na kabla miguu yenu haijagongana juu ya milima wakati wa jioni.+ Nanyi hakika mtaitumaini nuru,+ naye kwa kweli ataifanya iwe kivuli kizito;+ ataigeuza iwe giza zito.+ 17 Lakini msiposikia jambo hilo,+ nafsi yangu italia na kutoa machozi katika mahali pa maficho kwa sababu ya kiburi nayo hakika itatoa machozi; na jicho langu litatiririka machozi,+ kwa sababu kundi+ la Yehova litakuwa limekwisha kuchukuliwa mateka.
18 “Mwambie mfalme na malkia,+ ‘Ketini mahali pa chini,+ kwa maana hakika taji lenu la urembo litashuka kutoka juu ya vichwa vyenu.’+ 19 Majiji ya kusini yamefungwa, hivi kwamba hakuna anayeyafungua. Yuda yote imepelekwa uhamishoni. Imepelekwa uhamishoni kabisa.+
20 “Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini.+ Liko wapi kundi ambalo ulipewa, kundi lako zuri?+ 21 Utasema nini wakati mtu anapokukazia fikira zake,+ wakati wewe umewafundisha kama rafiki zako kando yako tangu pale mwanzoni?+ Je, uchungu wa kuzaa hautakushika wewe, kama wa mwanamke anayezaa?+ 22 Na utakaposema moyoni mwako,+ ‘Kwa nini mambo haya yamenipata?’+ kwa sababu ya wingi wa makosa yako marinda yako yameondolewa yasiwe kifuniko;+ visigino vyako vimetendewa kijeuri.
23 “Je, Mkushi+ anaweza kuibadili ngozi yake? au, chui madoa yake?+ Ninyi pia mngeweza kufanya mema, watu waliofundishwa kutenda mabaya.+ 24 Basi nitawatawanya+ kama majani makavu yanayopita katika upepo kutoka nyikani.+ 25 Hii ndiyo kura yako, fungu lako lililopimwa kutoka kwangu,”+ asema Yehova, “kwa sababu umenisahau+ nawe unaendelea kuutegemea uwongo.+ 26 Nami pia nitainua marinda yako juu ya uso wako, na hakika aibu yako itaonwa,+ 27 matendo yako ya uzinzi+ na milio yako,+ mwenendo wako mpotovu katika ukahaba. Juu ya vilima, katika mashamba, nimeyaona machukizo yako.+ Ole wako, Ee Yerusalemu! Huwezi kuwa safi+—baada ya muda gani zaidi?”+
14 Hili ndilo neno la Yehova lililomjia Yeremia kuhusiana na mambo ya ukame:+ 2 Yuda imeomboleza,+ na malango yake yamefifia.+ Yamehuzunika mpaka chini,+ na hata kilio cha Yerusalemu kimeenda juu.+ 3 Na watu wao walio mashuhuri wamewatuma watu wao walio wanyonge walete maji.+ Wamekuja kwenye mitaro. Hawakupata maji.+ Wamerudi vyombo vyao vikiwa vitupu. Wamepatwa na aibu+ na kukata tamaa, nao wamekifunika kichwa chao.+ 4 Kwa sababu ya udongo ambao umepasuka-pasuka kwa maana hakujakuwako mvua juu ya nchi,+ wakulima wameona aibu; wamekifunika kichwa chao.+ 5 Kwa maana hata paa aliye porini amezaa, lakini akamwacha mtoto, kwa sababu hapakuwa na majani mororo. 6 Na punda-milia+ wamesimama tuli juu ya vilima vitupu; wamevutavuta upepo kama mbwa-mwitu; macho yao hayaoni sawasawa kwa sababu hakuna majani.+ 7 Hata makosa yetu yakishuhudia juu yetu, Ee Yehova, tenda kwa ajili ya jina lako;+ kwa maana matendo yetu ya kukosa uaminifu yamekuwa mengi;+ sisi tumekutendea dhambi.+
8 Ewe tumaini la Israeli,+ Mwokozi wake+ wakati wa taabu,+ kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi, na kama msafiri ambaye amegeuka kando ili alale usiku?+ 9 Kwa nini unakuwa kama mtu aliyeshangazwa, kama mwanamume mwenye nguvu ambaye hawezi kuokoa?+ Na bado wewe upo katikati yetu,+ Ee Yehova, na jina lako limeitwa juu yetu.+ Usitukatishe tamaa.
10 Yehova amesema hivi kuwahusu watu hawa: “Hivyo wamependa kutanga-tanga;+ hawakuzuia miguu yao.+ Basi Yehova hakuwafurahia.+ Sasa atalikumbuka kosa lao naye atazikazia fikira dhambi zao.”+
11 Na Yehova akaniambia: “Usisali kwa ajili ya watu hawa wapate mema yoyote.+ 12 Wakati wanapofunga, mimi sisikilizi kilio chao cha kusihi;+ na wanapotoa toleo zima la kuteketezwa na toleo la nafaka, mimi siyafurahii;+ kwa maana nitawamaliza kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni.”+
13 Ndipo nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tazama, manabii wanawaambia, ‘Hamtaona upanga, wala hakutakuwa na njaa kwenu, bali nitawapa amani ya kweli mahali hapa.’”+
14 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Manabii wanatoa unabii wa uwongo katika jina langu.+ Mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru wala kusema nao.+ Maono ya uwongo na uaguzi na kitu kisicho na thamani+ na udanganyifu wa moyo wao ndiyo mambo wanayowaambia ninyi kwa njia ya unabii.+ 15 Kwa hiyo Yehova amesema hivi kuwahusu wale manabii wanaotoa unabii katika jina langu na ambao mimi sikuwatuma na ambao wanasema kwamba hakuna upanga wala njaa itakayokuja katika nchi hii, ‘Hao manabii watamalizwa kwa upanga na kwa njaa.+ 16 Na watu walewale ambao wao wanawatolea unabii watakuwa watu waliotupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga, bila yeyote wa kuwazika—wao, wake zao na wana wao na binti zao.+ Nami nitamwaga juu yao msiba wao.’+
17 “Nawe uwaambie neno hili, ‘Macho yangu na yatiririke machozi usiku na mchana wala yasitulie,+ kwa maana bikira, binti ya watu wangu, amevunjwa kwa mavunjiko makuu+ kwa pigo lenye ugonjwa.+ 18 Kwa kweli nikienda nje shambani, tazama, sasa, wale waliouawa kwa upanga!+ Na kwa kweli mimi nikija ndani ya jiji, tazama, pia, magonjwa yaliyoletwa na njaa!+ Kwa maana nabii na kuhani vilevile wamezunguka kwenda katika nchi ambayo hawakuijua.’”+
19 Je, umeikataa Yuda kabisa,+ au, je, nafsi yako imechukia Sayuni?+ Kwa nini umetupiga, hivi kwamba hakuna maponyo kwa ajili yetu?+ Amani ilitumainiwa, lakini hakuna mema yaliyokuja; na wakati wa kuponywa, na, tazama! hofu!+ 20 Tunakubali, Ee Yehova, uovu wetu, kosa la mababu zetu,+ kwa maana tumekutendea dhambi.+ 21 Usitutendee bila heshima kwa ajili ya jina lako;+ usikidharau kiti chako cha ufalme chenye utukufu.+ Ukumbuke; usivunje agano lako pamoja nasi.+ 22 Je, kati ya sanamu za ubatili+ za mataifa kuna yoyote inayoweza kunyesha mvua, au, je, hata mbingu zinaweza kutoa manyunyu?+ Je, si Wewe, Ee Yehova Mungu wetu?+ Nasi tunakutumaini wewe, kwa maana wewe mwenyewe umeyatenda mambo hayo yote.+
15 Na Yehova akaniambia: “Kama Musa+ na Samweli+ wangekuwa wamesimama mbele zangu, nafsi yangu haingewaelekea watu hawa.+ Wangefukuzwa mbele za uso wangu, ili watoke waende.+ 2 Na itakuwa kwamba ikiwa watakuambia, ‘Tutoke twende wapi?’ wewe pia uwaambie, ‘Yehova amesema hivi: “Yeyote aliyekusudiwa tauni yenye kufisha, aende kwenye tauni yenye kufisha! Na yeyote aliyekusudiwa upanga, aende kwenye upanga! Na yeyote aliyekusudiwa njaa, aende kwenye njaa!+ Na yeyote aliyekusudiwa kwenda utekwani, aende utekwani!”’+
3 “‘Nami nitaweka juu yao familia nne,’+ asema Yehova, ‘upanga wa kuua, na mbwa wa kukokota, na viumbe vinavyoruka vya mbinguni+ na wanyama wa dunia ili wale na kuangamiza. 4 Nami nitawafanya kuwa kitu cha kutetemesha falme zote za dunia+ kwa sababu ya Manase mwana wa Hezekia, mfalme wa Yuda, kwa sababu ya yale aliyofanya Yerusalemu.+ 5 Kwa maana ni nani atakayekuhurumia, Ee Yerusalemu, na ni nani atakayekusikitikia,+ na ni nani atakayegeuka kando ili kuuliza juu ya hali yako?’
6 “‘Wewe mwenyewe umeniacha,’+ asema Yehova. ‘Unaendelea kutembea kwa kurudi nyuma.+ Nami nitaunyoosha mkono wangu juu yako na kukuangamiza.+ Nimechoka kujuta.+ 7 Nami nitawapepeta kwa uma+ katika malango ya nchi. Hakika mimi nitawaua watoto wao.+ Nitawaangamiza watu wangu, kwa kuwa hawajageuka kuziacha njia zao.+ 8 Machoni pangu wajane wao wamekuwa wengi sana kuliko chembe za mchanga wa bahari. Nitamleta mporaji juu ya mama, juu ya kijana, katikati ya mchana.+ Nitaangusha ghafula juu yao wasiwasi na masumbufu.+ 9 Mwanamke anayezaa watoto saba amedhoofika; nafsi yake imepambana ili kupata pumzi.+ Jua lake limetua wakati kungali mchana;+ limeona aibu na kufedheheka.’ ‘Nami nitaupa upanga mabaki yao mbele ya adui zao,’+ asema Yehova.”
10 Ole wangu,+ Ee mama yangu, kwa sababu umenizaa mimi, mtu wa ugomvi na mtu wa kuzozana na dunia yote.+ Sikutoa mkopo, nao hawakunipa mkopo. Wote wananilaani.+
11 Yehova amesema: “Hakika nitakuhudumia upate mema.+ Hakika nitakutetea wakati wa msiba na wakati wa taabu,+ juu ya adui.+ 12 Je, mtu anaweza kuvunja chuma vipande-vipande, chuma kutoka kaskazini, na shaba? 13 Mali yako na hazina zako nitazitoa ziporwe,+ si kwa sababu zimelipiwa bei yake, bali kwa sababu ya dhambi zako zote, katika maeneo yako yote.+ 14 Nami nitawavusha wao pamoja na adui zako kuingia katika nchi ambayo wewe hukuijua.+ Kwa maana moto umewashwa katika hasira yangu.+ Umewashwa juu yenu.”
15 Wewe mwenyewe umejua.+ Ee Yehova, nikumbuke+ na unikazie fikira zako na kulipiza kisasi juu ya watesaji wangu.+ Usiniondolee mbali katika upole wako wa hasira.+ Angalia kwamba ninachukua shutuma kwa ajili yako.+ 16 Maneno yako yalipatikana, nami nikayala;+ na neno lako linakuwa kwangu furaha na kushangilia+ kwa moyo wangu;+ kwa maana jina lako limeitwa juu yangu,+ Ee Yehova Mungu wa majeshi.+ 17 Sikuketi katika kikundi cha rafiki wanaofanya utani+ na kuanza kufurahi.+ Kwa sababu ya mkono wako nimeketi mimi peke yangu,+ kwa maana wewe umenijaza shutuma.+ 18 Kwa nini maumivu yangu yamekuwa yenye kudumu+ na pigo langu haliponi?+ Limekataa kupona. Hakika wewe unakuwa kwangu kama udanganyifu,+ kama maji yasiyotegemeka.+
19 Kwa hiyo Yehova amesema hivi: “Ukirudi, basi nitakurudisha.+ Utasimama mbele zangu.+ Na ukileta kilicho cha thamani kutoka katika vitu visivyo na thamani, utakuwa kama kinywa changu. Wao wenyewe watarudi kwako, lakini wewe mwenyewe hutarudi kwao.”
20 “Nami nimekufanya wewe kuwa ukuta wa shaba wenye ngome kwa watu hawa;+ nao hakika watapigana nawe, lakini hawatakushinda.+ Kwa maana mimi niko pamoja nawe, ili kukuokoa na kukukomboa,”+ asema Yehova. 21 “Nami nitakukomboa kutoka katika mkono wa watu wabaya,+ nami nitakukomboa kutoka katika mkono wa wenye kuonea.”
16 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Usijichukulie mke, wala usiwe na wana na mabinti mahali hapa.+ 3 Kwa maana Yehova amesema hivi kuhusu wana na mabinti wanaozaliwa mahali hapa, na kuhusu mama zao wanaowazaa na kuhusu baba zao wanaowazaa katika nchi hii,+ 4 ‘Watakufa vifo vya magonjwa.+ Hawataombolezewa,+ wala hawatazikwa.+ Watakuwa kama mbolea juu ya uso wa nchi;+ nao watamalizwa kwa upanga na kwa njaa,+ na maiti zao kwa kweli zitakuwa chakula kwa viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kwa wanyama wa duniani.’+
5 “Kwa maana Yehova amesema hivi, ‘Usiingie katika nyumba ya karamu ya mwombolezaji, nawe usiende kuomboleza wala kuwasikitikia.’+
“‘Kwa maana nimeondoa amani yangu kwa watu hawa,’ asema Yehova, ‘hata fadhili zenye upendo na rehema.+ 6 Na hakika wao watakufa, wakubwa kwa wadogo, katika nchi hii. Hawatazikwa,+ wala watu hawatajipiga-piga kwa ajili yao, wala hakuna yeyote atakayejikata-kata+ wala kujitia upara kwa ajili yao.+ 7 Nao hawatawapa mkate wowote kwa sababu ya kuomboleza ili kumfariji mtu juu ya waliokufa;+ wala hawatawapa kikombe cha faraja ili kunywa kwa sababu ya baba ya mtu na kwa sababu ya mama ya mtu.+ 8 Nawe usiingie kamwe katika nyumba ya karamu kuketi pamoja nao ili kula na kunywa.’+
9 “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Tazama, ninaikomesha kutoka mahali hapa mbele ya macho yenu sauti ya furaha na sauti ya kushangilia, sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi.’+
10 “Na itakuwa kwamba, utakapowaambia watu hawa maneno haya yote na kwa kweli wao wakuambie, ‘Kwa sababu gani Yehova amesema juu yetu msiba huu wote ulio mkubwa, nasi tuna kosa gani na dhambi gani ambayo tumemtendea Yehova Mungu wetu?’+ 11 ndipo wewe pia utakapowaambia, ‘ “Kwa sababu baba zenu waliniacha,”+ asema Yehova, “nao wakaendelea kuifuata miungu mingine na kuitumikia na kuiinamia.+ Lakini wakaniacha mimi, nao hawakuishika sheria yangu.+ 12 Na ninyi katika matendo yenu mmetenda vibaya zaidi kuliko baba zenu,+ na, tazama, kila mmoja wenu anaufuata ukaidi+ wa moyo wake mbaya kwa kutonitii mimi.+ 13 Nami nitawatupa ninyi nje ya nchi+ hii mpaka ndani ya nchi ambayo hamkuijua ninyi,+ wala baba zenu, na humo mtaitumikia miungu mingine+ mchana na usiku, kwa sababu mimi sitawapa kibali chochote.”’
14 “‘Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,’+ asema Yehova, ‘wakati haitasemwa tena: “Kama anavyoishi Yehova aliyewaleta wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri!”+ 15 bali: “Kama anavyoishi Yehova aliyewaleta wana wa Israeli kutoka katika nchi ya kaskazini na kutoka katika nchi zote ambako alikuwa amewatawanya!” na hakika mimi nitawarudisha kwenye nchi yao, niliyowapa mababu zao.’+
16 “‘Tazama, ninawaita wavuvi wengi,’ asema Yehova, ‘na hakika wao watawavua; na baadaye nitawaita wawindaji wengi,+ na hakika wao watawawinda wao kutoka katika kila mlima na kutoka katika kila kilima na kutoka katika mipasuko ya miamba.+ 17 Kwa maana macho yangu yako juu ya njia zao zote. Hawakufichwa kutoka mbele zangu, wala kosa lao halikufichwa kutoka mbele za macho yangu.+ 18 Na, kwanza kabisa, nitalipa kiwango kamili cha kosa+ lao na cha dhambi yao, kwa sababu waliitia nchi yangu unajisi.+ Walikuwa wameujaza urithi wangu mizoga ya machukizo yao na vinyaa vyao.’”+
19 Ee Yehova nguvu zangu na ngome yangu, na kimbilio langu katika siku ya taabu,+ kwako wewe mataifa yote yatakuja kutoka miisho ya dunia,+ nao watasema: “Kwa kweli mababu zetu walikuja kumiliki uwongo mtupu,+ ubatili na vitu ambavyo ndani yake havina faida yoyote.”+ 20 Je, mtu wa udongo anaweza kujifanyia miungu wakati hiyo si miungu?+
21 “Kwa hiyo, tazama, ninawafanya wajue; wakati huu mmoja nitawafanya waujue mkono wangu na nguvu zangu,+ nao watajua kwamba jina langu ni Yehova.”+
17 “Dhambi ya Yuda imeandikwa kwa kalamu ya chuma.+ Imechongwa kwa ncha ya almasi juu ya bamba la moyo wao,+ na juu ya pembe za madhabahu zao,+ 2 wakati wana wao wanapokumbuka madhabahu zao na miti yao mitakatifu kando ya mti wenye majani mengi, juu ya vilima virefu,+ 3 juu ya milima porini. Mali zako, hazina zako zote, nitazitoa ziporwe tu+—mahali pako pa juu kwa sababu ya dhambi katika maeneo yako yote.+ 4 Nawe unafungua, kwa kupenda kwako mwenyewe, kutoka katika fungu la urithi wako ambalo nilikuwa nimekupa.+ Mimi pia nitakufanya uwatumikie adui zako katika nchi ambayo hukuijua;+ kwa maana ninyi mmewashwa kama moto katika hasira yangu.+ Utaendelea kuwashwa mpaka wakati usio na kipimo.”
5 Yehova amesema hivi: “Amelaaniwa yule mtu hodari anayemtegemea mtu wa udongo+ na kwa kweli kuufanya mwili wa nyama kuwa mkono wake,+ na ambaye moyo wake unamwacha Yehova.+ 6 Na hakika yeye atakuwa kama mti ulio peke yake katika nchi tambarare ya jangwani wala hataona wakati mema yatakapokuja;+ lakini atakaa mahali pakavu katika nyika, katika nchi yenye chumvi ambayo haikaliwi.+ 7 Amebarikiwa yule mtu hodari anayemtegemea Yehova, na ambaye Yehova amekuwa uhakika wake.+ 8 Na hakika yeye atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, unaopeleka mizizi yake kando ya mto; naye hataona joto linapoingia, bali kwa kweli majani yake yatakuwa mengi.+ Na katika mwaka wa ukame+ hatahangaika, wala hataacha kuzaa matunda.
9 “Moyo ni wenye hila kuliko kitu kingine chochote nao ni hatari.+ Ni nani anayeweza kuujua? 10 Mimi, Yehova, ninauchunguza moyo,+ ninazikagua figo,+ ili kumpa kila mmoja kulingana na njia zake,+ kulingana na matunda ya matendo yake.+ 11 Kama kwale ambaye amekusanya kile ambacho hakutaga ndivyo alivyo mtu anayekusanya utajiri, lakini si kwa haki.+ Katikati ya siku zake atauacha,+ na mwisho wake ataonekana kuwa hana akili.”+
12 Kuna kiti cha ufalme chenye utukufu kilicho juu tangu mwanzo;+ ndicho patakatifu petu.+ 13 Ee Yehova, tumaini la Israeli,+ wale wote wanaokuacha watapatwa na aibu.+ Wale wanaoniasi+ wataandikwa katika mavumbi, kwa sababu wameiacha chemchemi ya maji yaliyo hai, Yehova.+ 14 Uniponye, Ee Yehova, nami nitapona.+ Uniokoe, nami nitaokoka;+ kwa maana wewe ni sifa yangu.+
15 Tazama! Kuna wale wanaoniambia: “Neno la Yehova liko wapi?+ Na liingie, tafadhali.” 16 Lakini mimi sikufanya haraka kuacha kuwa mchungaji anayekufuata, nami sikuwa na tamaa yoyote kwa ajili ya ile siku mbaya. Wewe mwenyewe umelijua neno la midomo yangu; mbele za uso wako limetokea. 17 Usiwe kwangu kitu chenye kuogopesha.+ Wewe ni kimbilio langu katika siku ya msiba.+ 18 Wale wanaonitesa na wapatwe na aibu,+ lakini mimi binafsi nisipate aibu.+ Waache wao waingiwe na hofu, lakini mimi binafsi nisiingiwe na hofu. Leta juu yao ile siku ya msiba,+ na kuwavunja kwa mvunjiko mara mbili.+
19 Yehova ameniambia hivi: “Nenda, nawe usimame katika lango la wana wa watu ambalo wafalme wa Yuda huingilia na ambalo hutokea, na katika malango yote ya Yerusalemu.+ 20 Nawe uwaambie, ‘Sikieni neno la Yehova, ninyi wafalme wa Yuda na Yuda yote na ninyi wakaaji wote wa Yerusalemu, mnaoingilia malango haya.+ 21 Yehova amesema hivi: “Angalieni nafsi zenu,+ nanyi msibebe mzigo wowote katika siku ya sabato ili kuuingiza kupitia malango ya Yerusalemu.+ 22 Nanyi msitoe mzigo wowote katika nyumba zenu siku ya sabato; wala msifanye kazi yoyote.+ Nanyi mwitakase siku ya sabato, kama nilivyowaamuru mababu zenu;+ 23 lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao,+ nao wakafanya shingo+ yao kuwa ngumu ili wasisikie na ili wasipokee nidhamu.”’+
24 “‘“Na itatukia kwamba, mkinitii kabisa,”+ asema Yehova, “msiingize mzigo wowote kupitia malango ya jiji hili siku ya sabato na kuitakasa siku ya sabato+ kwa kutofanya kazi yoyote siku hiyo,+ 25 basi pia wafalme pamoja na wakuu+ hakika wataingia kupitia malango ya jiji hili, wakikaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi,+ wakipanda gari na farasi, wao pamoja na wakuu wao, watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu; na hakika jiji hili litakaliwa mpaka wakati usio na kipimo. 26 Na hakika watu watakuja kutoka katika majiji ya Yuda na kutoka pande zote kuzunguka Yerusalemu na kutoka katika nchi ya Benyamini+ na kutoka katika nchi tambarare ya chini+ na kutoka katika eneo lenye milima+ na kutoka katika Negebu,+ wakileta toleo zima la kuteketezwa+ na dhabihu+ na toleo la nafaka+ na ubani+ na kuleta dhabihu ya shukrani ndani ya nyumba ya Yehova.+
27 “‘“Lakini ikiwa hamtanitii kwa kuitakasa siku ya sabato na kutobeba mzigo,+ lakini mwingie nao kupitia malango ya Yerusalemu katika siku ya sabato, mimi pia nitawasha moto wa kuteketeza katika malango yake,+ nao hakika utaiteketeza minara ya makao ya Yerusalemu+ nao hautazimwa.”’”+
18 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema: 2 “Simama, ushuke mpaka nyumba ya mfinyanzi,+ na hapo nitakufanya usikie maneno yangu.”
3 Nami nikashuka mpaka nyumba ya mfinyanzi, na, tazama, alikuwa akifanya kazi juu ya magurudumu ya mfinyanzi. 4 Na chombo alichokuwa akitengeneza kwa udongo wa mfinyanzi kikaharibika mkononi mwa mfinyanzi, naye akageuka na kukifanya kuwa chombo kingine, kama ilivyokuwa sawa machoni pa mfinyanzi.+
5 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 6 “‘Je, mimi siwezi kuwatendea kama mfinyanzi huyu alivyotenda, enyi nyumba ya Israeli?’ asema Yehova. ‘Tazama! Kama udongo mkononi mwa mfinyanzi, ndivyo ninyi mlivyo mkononi mwangu, enyi nyumba ya Israeli.+ 7 Wakati wowote nikisema juu ya taifa na juu ya ufalme ili kuung’oa na kuubomoa na kuuharibu,+ 8 na kwa kweli taifa lile ligeuke kutoka katika ubaya wake ambao nilisema juu yake,+ mimi pia nitajuta juu ya ule msiba niliokuwa nimefikiria kuutimiza juu yake.+ 9 Lakini wakati wowote ambao huenda nikasema kuhusu taifa na kuhusu ufalme, kuujenga na kuupanda,+ 10 nao kwa kweli ufanye mabaya machoni pangu kwa kutoitii sauti yangu,+ mimi pia nitajuta kwa yale mema ambayo nilisema moyoni mwangu kuwa nitafanya kwa faida yake.’
11 “Na sasa, tafadhali, waambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama, ninafanya msiba juu yenu na kutafakari wazo fulani juu yenu.+ Geukeni, tafadhali, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya, na mfanye njia zenu na matendo yenu kuwa mema.”’”+
12 Nao wakasema: “Hakuna tumaini!+ Kwa maana sisi tutafuata mawazo yetu wenyewe, nasi tutafanya kila mmoja ukaidi wa moyo wake mbaya.”+
13 Kwa hiyo Yehova amesema hivi: “Ulizeni wenyewe, tafadhali, kati ya mataifa. Ni nani amesikia mambo kama haya? Kuna jambo lenye kuchukiza sana ambalo bikira wa Israeli amefanya kupita kiasi.+ 14 Je, theluji ya Lebanoni itatoka katika mwamba wa porini? Au, je, maji mageni, baridi, yanayotiririka, yatakaushwa? 15 Kwa maana watu wangu wamenisahau+ kwa kuwa wanakifukizia moshi wa dhabihu kitu cha ubatili,+ na kwa kuwa wanawakwaza watu katika njia zao,+ mapito ya zamani za kale,+ kutembea katika barabara, njia ambayo haijatengenezwa ikiwa na mafungu, 16 ili kuifanya nchi yao kuwa kitu cha kushangaza,+ kuwa ya kupigiwa mluzi mpaka wakati usio na kipimo.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao na kutikisa kichwa chake.+ 17 Nitawatawanya wao mbele ya adui kama kwa upepo wa mashariki.+ Nitawaonyesha wao mgongo, wala si uso,+ katika siku ya msiba wao.”
18 Nao wakasema: “Njooni, tutafakari juu ya Yeremia wazo fulani,+ kwa maana sheria haitaangamia kutoka kwa kuhani+ au shauri kutoka kwa mwenye hekima au neno kutoka kwa nabii.+ Njooni tumpige kwa ulimi,+ nasi tusisikilize lolote la maneno yake.”
19 Unitegee sikio, Ee Yehova, na kuisikiliza sauti ya wapinzani wangu.+ 20 Je, ubaya unapaswa kulipwa badala ya wema?+ Kwa maana wameichimbia nafsi yangu shimo.+ Ukumbuke kusimama kwangu mbele zako ili kusema mema kuwahusu wao, ili kuigeuza ghadhabu yako iondoke kwao.+ 21 Kwa hiyo uwatoe wana wao waone njaa,+ na kuwatoa wapatwe na nguvu za upanga;+ wake zao na wawe wanawake waliofiwa na watoto, na wajane.+ Wanaume wao na wauawe kwa tauni yenye kufisha, vijana wao na wapigwe na kuuawa kwa upanga vitani.+ 22 Kilio na kisikiwe kutoka katika nyumba zao, utakapoleta juu yao kwa ghafula kikundi cha waporaji.+ Kwa maana wamechimba shimo ili kunikamata, nao wameficha mitego kwa ajili ya miguu yangu.+
23 Lakini wewe, Ee Yehova, unajua vema shauri lao lote juu yangu ili kuniua.+ Usilifunike kosa lao, wala usiifute ile dhambi yao kutoka mbele zako; bali wawe watu waliokwazwa mbele zako.+ Katika wakati wa hasira yako uwachukulie hatua.+
19 Yehova amesema hivi: “Nenda, uchukue chupa ya udongo ya mfinyanzi+ na baadhi ya wanaume wazee wa watu na baadhi ya wanaume wazee wa makuhani. 2 Nawe uende katika bonde la mwana wa Hinomu,+ lililo kwenye mwingilio wa Lango la Vigae. Na hapo utangaze maneno ambayo nitakuambia.+ 3 Nawe useme, ‘Sikieni neno la Yehova, enyi wafalme wa Yuda nanyi wakaaji wa Yerusalemu.+ Yehova wa majeshi,+ Mungu wa Israeli, amesema hivi:
“‘“Tazama, ninaleta msiba juu ya mahali hapa, ambao yeyote akisikia habari zake, masikio yake yatawasha;+ 4 kwa sababu wameniacha+ mimi nao wamepafanya mahali hapa pasitambuliwe+ na kufukiza moshi wa dhabihu ndani yake kwa miungu mingine ambayo hawakuijua,+ wao pamoja na mababu zao na wafalme wa Yuda; nao wamepajaza mahali hapa damu ya wasio na hatia.+ 5 Nao walijenga mahali pa juu pa Baali ili kuwateketeza wana wao motoni kama matoleo mazima ya kuteketezwa kwa Baali,+ jambo ambalo sikuliamuru wala kusema juu yake,+ na ambalo halikuingia moyoni mwangu.”’+
6 “‘“Kwa hiyo, tazama! kuna siku zinakuja,” asema Yehova, “wakati mahali hapa hapataitwa tena Tofethi+ na bonde la mwana wa Hinomu,+ bali bonde la uuaji. 7 Nami nitalivunja shauri la Yuda na la Yerusalemu mahali hapa,+ nami nitawaangusha kwa upanga mbele ya adui zao na kwa mkono wa wale wanaoitafuta nafsi yao.+ Na maiti zao nitazitoa ziwe chakula kwa viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kwa wanyama wa dunia.+ 8 Nami nitalifanya jiji hili kuwa kitu cha kushangaza na kitu cha kupigiwa mluzi.+ Kila aliye wa mwisho atakayepita kando yake atatazama kwa mshangao na kupiga mluzi kwa sababu ya mapigo yake yote.+ 9 Nami nitawafanya wale nyama ya wana wao na nyama ya binti zao; nao watakula kila mmoja nyama ya mwenzake, kwa sababu ya kusongwa na kwa sababu ya mkazo ambao adui zao na wale wanaoitafuta nafsi yao watawabania.”’+
10 “Na uivunje ile chupa mbele ya macho ya wanaume wanaoenda pamoja nawe. 11 Nawe uwaambie, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Ndivyo nitakavyowavunja watu hawa na jiji hili kama mtu anavyokivunja chombo cha mfinyanzi hivi kwamba hakiwezi kurekebishwa tena;+ nao watazika katika Tofethi+ mpaka pasiwe na mahali zaidi pa kuzikia.”’+
12 “‘Hivyo ndivyo nitakavyopatendea mahali hapa,’ asema Yehova, ‘na wakaaji wake, kulifanya jiji hili kama Tofethi.+ 13 Na nyumba za Yerusalemu na nyumba za wafalme wa Yuda zitakuwa kama mahali pa Tofethi,+ zitakuwa najisi, yaani, zile nyumba zote ambazo juu ya paa zake walilifukizia moshi wa dhabihu jeshi lote la mbinguni+ na kuimiminia miungu mingine toleo la kinywaji.’”+
14 Kisha Yeremia akatoka Tofethi,+ ambapo Yehova alikuwa amemtuma ili kutoa unabii, akasimama katika ua wa nyumba ya Yehova na kuwaambia watu wote:+ 15 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta juu ya jiji hili na juu ya majiji yake yote msiba wote ambao nimesema juu yake, kwa sababu wamefanya shingo yao kuwa ngumu ili wasiyatii maneno yangu.’”+
20 Sasa Pashuri mwana wa Imeri,+ kuhani, ambaye pia alikuwa msimamizi mkuu katika nyumba ya Yehova,+ akaendelea kumsikiliza Yeremia alipokuwa akitoa unabii wa maneno hayo. 2 Ndipo Pashuri akampiga Yeremia nabii+ na kumweka katika mikatale+ iliyokuwa katika Lango la Juu la Benyamini, lililokuwa katika nyumba ya Yehova. 3 Lakini ikawa kesho yake kwamba Pashuri akamtoa Yeremia katika ile mikatale,+ na sasa Yeremia akamwambia:
“Yehova amekuita jina lako,+ si Pashuri, bali Hofu pande zote.+ 4 Kwa maana Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninakufanya wewe kuwa hofu kwako mwenyewe na kwa wapenzi wako wote, nao hakika wataanguka kwa upanga wa adui+ zao huku macho yako yakitazama;+ na Yuda wote nitawatia mkononi mwa mfalme wa Babiloni, naye kwa kweli atawapeleka uhamishoni huko Babiloni na kuwaua kwa upanga.+ 5 Nami nitavitoa vitu vyote vya jiji hili vilivyowekwa akiba na mazao yake yote na vitu vyake vyote vyenye thamani; na hazina zote za wafalme wa Yuda nitazitia mkononi mwa adui zao.+ Na hakika wao watavipora na kuvichukua na kuvipeleka Babiloni.+ 6 Na wewe, Ee Pashuri, na wakaaji wote wa nyumba yako, mtaenda utekwani;+ nawe utafika Babiloni na huko utakufa na huko wewe utazikwa pamoja na wapenzi wako wote,+ kwa sababu umewatolea unabii wa uwongo.’”+
7 Umenipumbaza, Ee Yehova, hivi kwamba nikapumbazika. Ulizitumia nguvu zako kunipinga mimi, hivi kwamba ukashinda.+ Nikawa chombo cha kuchekwa mchana kutwa; kila mtu ananidharau.+ 8 Kwa maana kila mara ninaposema, mimi hulia. Jeuri na uporaji ndizo ninazotangaza.+ Kwa maana neno la Yehova lilikuwa kwangu kisababishi cha shutuma na cha dhihaka mchana kutwa.+ 9 Nami nilisema: “Sitamtaja tena, wala sitasema tena katika jina lake.”+ Na moyoni mwangu hali hiyo ikawa kama moto unaowaka ambao umefungiwa ndani ya mifupa yangu; nami nikachoka kujizuia, nami sikuweza kuivumilia.+ 10 Kwa maana nilisikia habari mbaya za wengi.+ Kulikuwa na hofu pande zote. “Tangazeni, ili tumtangaze.”+ Kila mwanadamu anayeweza kufa anayeniambia “Amani!”—wanaangalia kuchechemea kwangu:+ “Labda atapumbazika,+ ili tumshinde na tujilipizie kisasi juu yake.” 11 Lakini Yehova alikuwa pamoja nami+ kama mwenye nguvu anayetisha.+ Ndiyo sababu wale wanaonitesa watajikwaa nao hawatashinda.+ Hakika watapatwa na aibu kabisa, kwa sababu hawatakuwa wamefanikiwa. Fedheha yao inayodumu mpaka wakati usio na kipimo haitasahauliwa.+
12 Lakini wewe, Ee Yehova wa majeshi, unamchunguza mwadilifu;+ unaziona figo na moyo.+ Na nione kisasi chako juu yao,+ kwa maana nimekufunulia wewe kesi yangu.+
13 Mwimbieni Yehova! Msifuni Yehova! Kwa maana ameikomboa nafsi ya maskini kutoka mkononi mwa watenda-maovu.+
14 Na ilaaniwe ile siku nilipozaliwa! Isibarikiwe ile siku ambayo mama yangu alinizaa!+ 15 Alaaniwe yule mtu aliyemletea baba yangu habari njema, akisema: “Amezaliwa kwako mwana, mwanamume!” Hakika yeye alimfanya ashangilie.+ 16 Na mtu huyo atakuwa kama majiji ambayo Yehova ameharibu hali Yeye hakuona majuto yoyote.+ Naye atasikia kilio wakati wa asubuhi na king’ora katikati ya mchana.+
17 Kwa nini kwa hakika hakuniua ndani ya tumbo la uzazi, ili mama yangu awe kaburi langu na tumbo lake la uzazi liwe na mimba mpaka wakati usio na kipimo?+ 18 Kwa nini nimetoka ndani ya tumbo la uzazi+ ili kuona kazi ngumu na huzuni+ na ili siku zangu zifikie mwisho wake katika aibu tupu?+
21 Neno+ lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, wakati Mfalme Sedekia+ alipotuma kwake Pashuri+ mwana wa Malkiya na Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, na kusema: 2 “Tafadhali muulize Yehova+ kwa ajili yetu, kwa sababu Nebukadreza mfalme wa Babiloni anapiga vita juu yetu.+ Labda Yehova atatutendea kulingana na kazi zake zote za ajabu, hivi kwamba yeye aondoke kwetu.”+
3 Na Yeremia akawaambia: “Mwambieni Sedekia hivi, 4 ‘Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi: “Tazama, ninazigeuza nyuma silaha za vita zilizo mkononi mwenu, mnazotumia kupigana na mfalme wa Babiloni,+ na Wakaldayo+ wanaowazingira ninyi nje ya ukuta, nami nitazikusanya katikati ya jiji hili.+ 5 Nami nitapigana nanyi+ kwa mkono ulionyooshwa na kwa mkono wenye nguvu na kwa hasira na kwa ghadhabu na kwa ukali mkubwa.+ 6 Nami nitawapiga wakaaji wa jiji hili, mwanadamu na mnyama pia. Watakufa kwa tauni kubwa.”’+
7 “‘“Na baada ya hayo,” asema Yehova, “Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na watumishi wake na watu na wale wanaobaki katika jiji hili baada ya tauni ile, na upanga na njaa, katika mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babiloni, katika mkono wa adui zao na katika mkono wa wale wanaoitafuta nafsi yao, na hakika yeye atawapiga kwa ukali wa upanga na kuwaua.+ Hatawasikitikia, wala kuwahurumia wala kuwa na rehema yoyote.”’+
8 “Nawe utawaambia hivi watu hawa, ‘Yehova amesema: “Tazama, ninaweka mbele yenu njia ya uzima na njia ya kifo.+ 9 Yeye anayeketi tuli katika jiji hili atakufa kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni;+ lakini yeye anayetoka nje na ambaye kwa kweli anajitia mkononi mwa Wakaldayo wanaowazingira ninyi ataendelea kuishi, na nafsi yake hakika itakuwa kama nyara kwake.”’+
10 “‘“Kwa maana nimekaza uso wangu juu ya jiji hili kwa ajili ya msiba wala si kwa ajili ya mema,”+ asema Yehova. “Litatiwa mkononi mwa mfalme wa Babiloni,+ na hakika ataliteketeza kwa moto.”+
11 “‘Na kwa habari ya nyumba ya mfalme wa Yuda, lisikieni neno la Yehova.+ 12 Enyi nyumba ya Daudi,+ Yehova amesema hivi: “Kila asubuhi+ toeni hukumu kwa haki,+ na kumkomboa kutoka mkononi mwa mpunjaji yeye anayenyang’anywa,+ ili ghadhabu yangu isitoke kama moto+ na kuteketeza na kusiwe na yeyote wa kuuzima kwa sababu ya ubaya wa matendo yenu.”’+
13 “‘Tazama, mimi niko dhidi yako, Ee mwanamke mkaaji wa nchi tambarare ya chini,+ Ee mwamba wa nchi tambarare,’ asema Yehova. ‘Na kuhusu ninyi ambao mnasema: “Ni nani atakayeshuka kupigana nasi? Na ni nani atakayekuja ndani ya makao yetu?”+ 14 Mimi pia nitawatoza ninyi+ hesabu kulingana na matunda ya matendo yenu,’+ asema Yehova. ‘Nami nitawasha moto katika msitu wake,+ na hakika huo utateketeza vitu vyote vinavyomzunguka.’”+
22 Yehova amesema hivi: “Shuka nyumbani kwa mfalme wa Yuda, nawe useme hapo neno hili. 2 Nawe useme, ‘Lisikie neno la Yehova, Ee mfalme wa Yuda unayeketi juu ya kiti cha ufalme cha Daudi,+ wewe pamoja na watumishi wako na watu wako, wale wanaoingia kupitia malango haya.+ 3 Yehova amesema hivi: “Toeni haki na uadilifu, nanyi mumkomboe yeye anayenyang’anywa kutoka mkononi mwa mpunjaji; wala msimtendee vibaya mkaaji mgeni yeyote, mvulana asiye na baba au mjane.+ Msiwatendee jeuri yoyote.+ Wala msimwage damu yoyote isiyo na hatia mahali hapa.+ 4 Kwa maana mkilifanya neno hili kwelikweli, hakika pia wataingia kupitia malango ya nyumba hii wafalme wanaoketi kwa ajili ya Daudi juu ya kiti chake cha ufalme,+ wakipanda magari na farasi, yeye pamoja na watumishi wake na watu wake.”’+
5 “‘Lakini ikiwa hamtayatii maneno haya, mimi ninaapa kwa nafsi yangu mwenyewe,’+ asema Yehova, ‘kwamba nyumba hii itakuwa ukiwa kabisa.’+
6 “Kwa maana Yehova amesema hivi kuhusu nyumba ya mfalme wa Yuda, ‘Wewe ni kama Gileadi kwangu, kichwa cha Lebanoni.+ Hakika nitakufanya uwe nyika;+ nayo majiji, hakuna hata moja litakalokaliwa.+ 7 Nami nitatakasa juu yako wale wanaoleta uharibifu,+ kila mmoja na silaha zake;+ nao wataikata mierezi+ yako iliyo bora zaidi na kuiangusha ndani ya moto.+ 8 Na kwa kweli mataifa mengi watapita kando ya jiji hili na kila mmoja atamwambia mwenzake: “Kwa nini Yehova alilitendea hivi jiji hili kuu?”+ 9 Nao watasema: “Kwa sababu wameliacha agano la Yehova Mungu+ wao na kuinamia miungu mingine na kuitumikia.”’+
10 “Msimlilie aliyekufa,+ wala msimsikitikie. Mlilieni sana yule anayeenda zake, kwa maana hatarudi tena wala kwa kweli hataiona nchi ya jamaa zake. 11 Kwa maana Yehova amesema hivi kumhusu Shalumu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda anayetawala badala ya Yosia baba yake,+ ambaye ameondoka mahali hapa, ‘Hatarudi hapo tena. 12 Kwa maana katika mahali ambapo wamempeleka uhamishoni ndipo atakapokufa, naye hataiona tena nchi hii.’+
13 “Ole wake anayejenga nyumba yake,+ lakini si kwa uadilifu, na vyumba vyake vya juu, lakini si kwa haki, kwa kutumia mwanadamu mwenzake anayetumikia bure, na ambaye hampi malipo yake;+ 14 yeye anayesema, ‘Nitajijengea nyumba yenye nafasi tele na vyumba vya juu vyenye nafasi kubwa;+ na madirisha yangu yatapanuliwa kwa ajili yake, nayo itafunikwa kwa mierezi+ na kupakwa rangi nyekundu.’+ 15 Je, utaendelea kutawala kwa sababu unashindana kwa kutumia mierezi? Naye baba yako, je, hakula na kunywa na kutekeleza haki na uadilifu?+ Kwa hiyo alifanikiwa.+ 16 Alitetea dai halali la mwenye kuteseka na maskini.+ Kwa hiyo akafanikiwa. ‘Je, hiyo haikuwa hivyo kwa sababu ya kunijua mimi?’ asema Yehova. 17 ‘Hakika macho yako na moyo wako haviko juu ya chochote ila pato lisilo la haki,+ na juu ya damu ya asiye na hatia ili kuimwaga,+ na juu ya kupunja na juu ya unyang’anyi ili kuyaendeleza mambo hayo.’
18 “Kwa hiyo Yehova amesema hivi kumhusu Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, ‘Hawataomboleza kwa ajili yake: “Aa! ndugu yangu! Na Aa! dada yangu!” Hawataomboleza kwa ajili yake: “Aa! Ee bwana! Na Aa! heshima yake!”+ 19 Atazikwa kwa maziko ya punda-dume,+ kwa kukokotwa na kutupwa, nje ya malango ya Yerusalemu.’+
20 “Panda mpaka Lebanoni+ na upaaze kilio, na juu ya Bashani+ upaaze sauti yako. Na ulie kutoka Abarimu,+ kwa sababu wale wote wanaokupenda sana wamevunjwa-vunjwa.+ 21 Nilisema nawe wakati ulipokuwa huna wasiwasi.+ Ulisema, ‘Sitatii.’+ Hii imekuwa njia yako tangu ujana wako, kwa maana hukuitii sauti yangu.+ 22 Upepo utawachunga wachungaji wako wote;+ na wale wanaokupenda sana wataingia utekwani.+ Kwa maana wakati huo utaona aibu na hakika ufedheheke kwa sababu ya msiba wako wote.+ 23 Ewe unayekaa katika Lebanoni,+ unayekaa katika kiota juu ya mierezi,+ lo! jinsi utakavyougua uchungu wa kuzaa utakapokujia,+ uchungu kama wa mwanamke anayezaa!”+
24 “‘Kama ninavyoishi,’ asema Yehova, ‘hata kama Konia+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, angekuwa pete ya muhuri+ kwenye mkono wangu wa kuume, ningekung’oa wewe kutoka hapo!+ 25 Nami nitakutia wewe katika mkono wa wale wanaoitafuta nafsi yako+ na katika mkono wa wale unaoogopa na katika mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babiloni na katika mkono wa Wakaldayo.+ 26 Nami nitakutupa wewe pamoja na mama yako+ aliyekuzaa mwende katika nchi nyingine ambayo hamkuzaliwa huko, nanyi mtakufa huko.+ 27 Na katika nchi ambayo watakuwa wakiiinua nafsi yao ili warudi, hawatarudi huko.+ 28 Je, mtu huyu Konia+ ni umbo tu lililodharauliwa, lililovunjwa vipande-vipande,+ au ni chombo ambacho hakipendezi?+ Kwa nini yeye na uzao wake ni lazima waangushwe chini na kutupwa katika nchi ambayo hawakuijua?’+
29 “Ee dunia, dunia, dunia, lisikie neno la Yehova.+ 30 Yehova amesema hivi, ‘Andikeni kwamba mtu huyu hana mtoto,+ kama mwanamume ambaye hatafanikiwa kwa vyovyote katika siku zake; kwa maana hakuna hata mmoja atakayefanikiwa kwa vyovyote kutoka kwa uzao wake,+ mwenye kuketi juu ya kiti cha ufalme cha Daudi+ na kutawala tena katika Yuda.’”
23 “Ole wao wachungaji wanaowaangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu!”+ asema Yehova.
2 Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi juu ya wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Ninyi mmewatawanya kondoo zangu; nanyi mliendelea kuwatawanya, nanyi hamkuwakazia fikira zenu.”+
“Tazama, ninakaza fikira zangu juu yenu kwa sababu ya ubaya wa matendo yenu,”+ asema Yehova.
3 “Nami nitakusanya mabaki ya kondoo zangu kutoka katika nchi zote ambako nilikuwa nimewatawanya,+ nami nitawarudisha kwenye uwanja wao wa malisho,+ na hakika wao watazaa na kuwa wengi.+ 4 Nami nitasimamisha juu yao wachungaji ambao kweli watawachunga;+ nao hawataogopa tena, wala hawataingiwa na hofu yoyote,+ na hakuna hata mmoja atakayekosekana,” asema Yehova.
5 “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitamsimamishia Daudi chipukizi adilifu.+ Na hakika mfalme atatawala+ na kutenda kwa busara na kutenda haki na uadilifu katika nchi.+ 6 Katika siku zake Yuda ataokolewa,+ na Israeli atakaa katika usalama.+ Na hili ndilo jina lake atakaloitwa, Yehova Ni Uadilifu Wetu.”+
7 “Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nao hawatasema tena, ‘Yehova yuko hai aliyewaleta wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri,’+ 8 bali, ‘Yehova yuko hai aliyepandisha na aliyeingiza uzao wa nyumba ya Israeli kutoka katika nchi ya kaskazini na kutoka katika nchi zote ambako nimewatawanya,’ na hakika wao watakaa katika nchi yao wenyewe.”+
9 Nao manabii, moyo wangu umevunjika ndani yangu. Mifupa yangu yote imeanza kutetemeka. Nimekuwa kama mtu ambaye amelewa,+ na kama mwanamume ambaye divai imemlemea, kwa sababu ya Yehova na kwa sababu ya maneno yake matakatifu. 10 Kwa maana nchi imejaa+ wazinzi.+ Kwa maana nchi inaomboleza+ kwa sababu ya laana, viwanja vya malisho vya nyika vimekauka;+ na mwenendo wao ni mbaya, na nguvu zao si kwa njia ya haki.
11 “Kwa maana nabii pamoja na kuhani wametiwa unajisi.+ Pia katika nyumba yangu mwenyewe nimeupata ubaya wao,”+ asema Yehova. 12 “Kwa hiyo njia yao itakuwa kwao kama mahali penye utelezi+ gizani, ambapo watasukumwa ndani yake na hakika waanguke.”+
“Kwa maana nitaleta msiba juu yao, mwaka wa kuwakazia fikira,”+ asema Yehova. 13 “Na katika manabii wa Samaria+ mimi nimeona jambo lisilofaa. Wametenda kama manabii waliochochewa na Baali,+ nao wanaendelea kuwafanya watu wangu, Israeli, waende huku na huku.+ 14 Na katika manabii wa Yerusalemu nimeona mambo yenye kuchukiza sana,+ kufanya uzinzi+ na kutembea katika uwongo;+ nao wameitia nguvu mikono ya watenda-maovu ili wasirudi,+ kila mmoja kutoka katika ubaya wake. Kwangu wote wamekuwa kama Sodoma,+ na wakaaji wake kama Gomora.”+
15 Kwa hiyo Yehova wa majeshi amesema hivi juu ya manabii: “Tazama, ninawalisha pakanga, nami nitawapa maji yaliyotiwa sumu wanywe.+ Kwa maana kutoka kwa manabii wa Yerusalemu uasi-imani+ umeenea katika nchi yote.”
16 Yehova wa majeshi amesema hivi: “Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowatolea ninyi unabii.+ Wanawafanya muwe ubatili.+ Wanasema maono ya moyo wao wenyewe+—si kutoka katika kinywa cha Yehova.+ 17 Wanawaambia tena na tena wale ambao hawaniheshimu, ‘Yehova amesema: “Ninyi mtakuwa na amani.”’+ Nao wamemwambia kila mtu anayetembea katika ukaidi wa moyo wake,+ ‘Hamtapatwa na msiba wowote.’+ 18 Kwa maana ni nani amesimama katika kikundi cha rafiki+ za Yehova ili aone na kulisikia neno lake?+ Ni nani amelikazia fikira neno lake ili alisikie?+ 19 Tazama! Dhoruba ya Yehova, ghadhabu, hakika itatoka, tufani inayozunguka.+ Itajizungusha juu ya kichwa cha waovu.+ 20 Hasira ya Yehova haitarudi nyuma mpaka atakapokuwa ametenda+ na mpaka atakapokuwa ametimiza mawazo ya moyo wake.+ Katika siku za mwisho ninyi mtalifikiria jambo hilo kwa uelewaji.+
21 “Sikuwatuma manabii, ingawa wao wenyewe walikimbia. Sikusema nao, ingawa wao wenyewe walitoa unabii.+ 22 Lakini ikiwa wangekuwa wamesimama katika kikundi changu cha rafiki,+ ndipo wangewafanya watu wangu wayasikie maneno yangu, nao wangewarudisha kutoka katika njia yao mbaya na kutoka katika ubaya wa matendo yao.”+
23 “Je, mimi ni Mungu aliye karibu,” asema Yehova, “na si Mungu aliye mbali?”+
24 “Au, je, mtu yeyote anaweza kujificha katika maficho nami nisimwone?”+ asema Yehova.
“Je, mimi kwa kweli sizijazi mbingu na dunia?”+ asema Yehova. 25 “Nimesikia yale ambayo manabii wanaotoa unabii wa uwongo katika jina langu+ wamesema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’+ 26 Itadumu mpaka wakati gani katika moyo wa manabii wanaotoa unabii wa uwongo na ambao ni manabii wa udanganyifu wa moyo wao wenyewe?+ 27 Wanafikiria kuwafanya watu wangu walisahau jina langu kwa njia ya ndoto zao ambazo wanaendelea kusimuliana,+ kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa sababu ya Baali.+ 28 Nabii ambaye ana ndoto, na asimulie ndoto hiyo; lakini yule ambaye ana neno langu, na aliseme neno langu kwa ukweli.”+
“Nyasi ina uhusiano gani na nafaka?”+ asema Yehova.
29 “Je, neno langu halilingani na moto,”+ asema Yehova, “na kama nyundo ya chuma ambayo huvunja mwamba?”+
30 “Kwa hiyo tazama, mimi niko dhidi ya manabii,”+ asema Yehova, “wale wanaoyaiba maneno yangu, kila mmoja kutoka kwa mwenzake.”+
31 “Tazama, mimi niko dhidi ya manabii,” asema Yehova, “wale wanaotumia ulimi wao ili kusema, ‘Neno!’”+
32 “Tazama, mimi niko dhidi ya manabii wa ndoto za uwongo,” asema Yehova, “wale wanaozisimulia na kuwafanya watu wangu kwenda huku na huku kwa sababu ya uwongo+ wao na kwa sababu ya kujisifu+ kwao.”
“Lakini mimi mwenyewe sikuwatuma wala kuwaamuru. Kwa hiyo hawatawafaidi watu hawa kwa vyovyote,”+ asema Yehova.
33 “Na watu hawa au nabii au kuhani wanapokuuliza, wakisema, ‘Mzigo wa Yehova ni nini?’+ wewe pia utawaambia, ‘ “Ninyi—Lo! jinsi mlivyo mzigo!+ Nami nitawaacha ninyi,”+ asema Yehova.’ 34 Naye nabii au kuhani au watu wanaosema, ‘Mzigo wa Yehova!’ Mimi pia nitakaza fikira zangu juu ya mtu huyo na juu ya nyumba yake.+ 35 Hivi ndivyo mnavyoendelea kuambiana mtu na mwenzake na mtu na ndugu yake, ‘Yehova ametoa jibu gani? Na Yehova amesema nini?’+ 36 Lakini msiutaje tena+ mzigo+ wa Yehova, kwa maana kwa kila mmoja mzigo unakuwa ni neno lake mwenyewe,+ nanyi mmeyabadili maneno ya Mungu aliye hai,+ Yehova wa majeshi, Mungu wetu.
37 “Utamwambia huyo nabii hivi, ‘Yehova amekupa jibu gani? Na Yehova amesema nini?+ 38 Na ikiwa mnaendelea kusema, “Mzigo wa Yehova!” basi Yehova amesema hivi: “Kwa sababu mnasema, ‘Hili neno ndilo mzigo wa Yehova,’ nilipoendelea kumtuma mtu kwenu, na kusema, ‘Msiseme: “Mzigo wa Yehova!”’ 39 kwa hiyo mimi hapa! Nami nitawapuuza ninyi, kabisa,+ nami nitawatupa pamoja na lile jiji nililowapa ninyi na mababu zenu—kutoka mbele zangu.+ 40 Nami nitatia juu yenu shutuma mpaka wakati usio na kipimo na fedheha mpaka wakati usio na kipimo, ambayo haitasahauliwa.”’”+
24 Na Yehova akanionyesha, na, tazama! vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya hekalu la Yehova, baada ya Nebukadreza mfalme wa Babiloni kumpeleka uhamishoni Yekonia+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, na wakuu wa Yuda na mafundi+ na wajenzi wa maboma, kutoka Yerusalemu ili awalete Babiloni.+ 2 Nacho kikapu kimoja, tini zilikuwa nzuri sana, kama tini za mapema;+ nacho kile kikapu cha pili, tini zilikuwa mbaya sana, hivi kwamba hazingeweza kuliwa kwa sababu ya ubaya.
3 Kisha Yehova akaniambia: “Unaona nini, Yeremia?” Basi nikasema: “Tini, zile tini nzuri zikiwa nzuri sana, na zile mbaya zikiwa mbaya sana, hivi kwamba haziwezi kuliwa kwa sababu ya ubaya.”+
4 Ndipo neno la Yehova likanijia, na kusema: 5 “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Kama hizi tini nzuri, ndivyo nitakavyowaona kwa njia nzuri+ wale wahamishwa wa Yuda, ambao nitawapeleka kutoka mahali hapa mpaka katika nchi ya Wakaldayo.+ 6 Nami nitaweka jicho langu juu yao kwa njia nzuri,+ na hakika mimi nitawarudisha katika nchi hii.+ Nami nitawajenga, wala sitawabomoa; nami nitawapanda, wala sitawang’oa.+ 7 Nami nitawapa moyo wa kunijua,+ kwamba mimi ni Yehova; nao watakuwa watu wangu,+ nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watarudi kwangu kwa moyo wao wote.+
8 “‘Na kama zile tini mbaya ambazo haziwezi kuliwa kwa sababu ya ubaya,+ kwa kweli Yehova amesema hivi: “Ndivyo nitakavyomtoa Sedekia+ mfalme wa Yuda na wakuu wake na mabaki wa Yerusalemu wanaobaki katika nchi hii+ na wale wanaokaa katika nchi ya Misri+— 9 mimi pia nitawatoa kwa ajili ya kutetemesha, kwa ajili ya msiba, katika falme zote za dunia,+ kwa ajili ya shutuma na kwa ajili ya neno la kimethali, kwa ajili ya suto+ na kwa ajili ya laana,+ katika mahali pote nitakapowatawanya.+ 10 Nami nitatuma juu yao upanga,+ njaa+ na tauni,+ mpaka waufikie mwisho wao kutoka katika nchi niliyowapa wao na mababu zao.”’”+
25 Neno lililomjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, yaani, mwaka wa kwanza wa Nebukadreza mfalme wa Babiloni; 2 ambalo Yeremia nabii alisema kuhusu watu wote wa Yuda na kuhusu wakaaji wote wa Yerusalemu, akisema:
3 “Tangu mwaka wa 13 wa Yosia+ mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, mpaka leo hii, miaka hii 23, neno la Yehova limenijia, nikaendelea kusema nanyi, nikiamka mapema na kusema, lakini hamkusikiliza.+ 4 Na Yehova alituma kwenu watumishi wake wote manabii, akiamka mapema na kuwatuma, lakini hamkusikiliza,+ wala hamkutega sikio lenu ili kusikiliza,+ 5 wao wakisema, ‘Tafadhali, geukeni kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya na kutoka katika ubaya wa matendo yake,+ nanyi mwendelee kukaa juu ya nchi ambayo Yehova aliwapa ninyi na mababu zenu tangu zamani za kale na mpaka wakati mrefu ujao.+ 6 Nanyi msifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiinamia, ili msinitie uchungu mimi kwa kazi ya mikono yenu, na ili nisiwaletee ninyi msiba.’+
7 “‘Lakini hamkunisikiliza mimi,’ asema Yehova, ‘kusudi mnitie uchungu kwa kazi ya mikono yenu, ili kujiletea wenyewe msiba.’+
8 “Kwa hiyo Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘ “Kwa sababu hamkuyatii maneno yangu, 9 tazama, ninatuma, nami nitazichukua familia zote za kaskazini,”+ asema Yehova, “nitatuma ujumbe kwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitawaleta wao juu ya nchi hii+ na juu ya wakaaji wake na juu ya haya mataifa yote kuzunguka pande zote;+ nami nitawaangamiza na kuwafanya kuwa kitu cha kushangaza na kitu cha kupigiwa mluzi+ na ukiwa mpaka wakati usio na kipimo.+ 10 Nami nitaangamiza kutoka ndani yao sauti ya furaha na sauti ya shangwe,+ sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi,+ sauti ya jiwe la kusagia la mkononi+ na nuru ya taa.+ 11 Na nchi hii yote itakuwa mahali palipoharibiwa, kitu cha kushangaza, na mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babiloni miaka 70.”’+
12 “‘Na itatukia kwamba miaka 70 itakapotimia+ nitatoza hesabu juu ya mfalme wa Babiloni na juu ya taifa lake,’+ asema Yehova, ‘kwa sababu ya kosa lao, juu ya nchi ya Wakaldayo,+ nami nitaifanya kuwa mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo.+ 13 Nami nitaleta juu ya nchi ile maneno yangu yote ambayo nimesema juu yake, yote ambayo yameandikwa katika kitabu hiki ambacho Yeremia ametoa unabii juu ya mataifa yote.+ 14 Kwa maana hata wao wenyewe, mataifa mengi na wafalme wakubwa,+ wamewatumia vibaya kama watumishi;+ nami nitawalipa kulingana na matendo yao na kulingana na kazi ya mikono yao.’”+
15 Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli ameniambia hivi: “Chukua kikombe hiki cha divai ya ghadhabu kutoka mkononi mwangu, nawe ukinyweshe+ mataifa yote ambayo ninakutuma kwao. 16 Nao lazima wanywe na kuyumba-yumba na kutenda kama wenda-wazimu kwa sababu ya upanga ninaotuma katikati yao.”+
17 Ndipo nikakichukua kile kikombe kutoka mkononi mwa Yehova na kukinywesha mataifa yote ambayo Yehova alikuwa amenituma kwao:+ 18 yaani, Yerusalemu na majiji ya Yuda na wafalme wake, wakuu wake, ili kuyafanya kuwa ukiwa, kitu cha kushangaza,+ kitu cha kupigiwa mluzi na laana, kama ilivyo leo hii;+ 19 Farao mfalme wa Misri na watumishi wake na wakuu wake na watu wake wote;+ 20 na jamii yote iliyochangamana, na wafalme wote wa nchi ya Usi,+ na wafalme wote wa nchi ya Wafilisti+ na Ashkeloni+ na Gaza+ na Ekroni+ na mabaki ya Ashdodi;+ 21 Edomu+ na Moabu+ na wana wa Amoni;+ 22 na wafalme wote wa Tiro+ na wafalme wote wa Sidoni+ na wafalme wa kisiwa kilicho katika eneo la bahari; 23 na Dedani+ na Tema+ na Buzi na wale wote wenye nywele zilizokatwa kwenye vipaji vya nyuso;+ 24 na wafalme wote wa Waarabu+ na wafalme wote wa jamii iliyochangamana wanaokaa nyikani; 25 na wafalme wote wa Zimri na wafalme wote wa Elamu+ na wafalme wote wa Wamedi;+ 26 na wafalme wote wa kaskazini walio karibu na walio mbali, mmoja baada ya mwingine, na falme nyingine zote za dunia zilizo juu ya uso wa nchi; naye mfalme wa Sheshaki+ atakunywa baada yao.
27 “Nawe utawaambia, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Kunyweni, mlewe, mtapike na kuanguka hivi kwamba msiweze kusimama+ kwa sababu ya upanga ninaotuma katikati yenu.”’+ 28 Na iwe kwamba wakikataa kukichukua kikombe kutoka mkononi mwako ili wanywe, wewe pia utawaambia, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Bila shaka mtakinywa.+ 29 Kwa maana, tazama! ninaanza kuleta msiba+ juu ya jiji ambalo linaitwa kwa jina langu, nanyi, je, mnapaswa kwa vyovyote kuachwa bila kuadhibiwa?”’+
“‘Hamtaachwa bila kuadhibiwa, kwa maana kuna upanga ambao ninaita juu ya wakaaji wote wa dunia,’ asema Yehova wa majeshi.
30 “Nawe utawatolea unabii kwa maneno haya yote, nawe utawaambia, ‘Yehova atanguruma kutoka juu,+ naye atatoa sauti yake kutoka katika makao yake matakatifu.+ Bila shaka atanguruma juu ya makao yake. Atapaaza sauti kama ile ya wale wanaokanyaga shinikizo la divai juu ya wakaaji wote wa dunia.’+
31 “‘Hakika kelele zitafika mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia, kwa maana Yehova ana ubishi na mataifa.+ Yeye binafsi atajiweka hukumuni na watu wote wenye mwili.+ Nao waovu atawatoa wauawe kwa upanga,’+ asema Yehova.
32 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Tazama! Msiba utaenda toka taifa mpaka taifa,+ na tufani kuu itaamshwa kutoka katika sehemu za mbali zaidi za dunia.+ 33 Na wale waliouawa na Yehova siku hiyo hakika watakuwa kutoka mwisho mmoja wa dunia mpaka mwisho wa pili wa dunia.+ Hawataombolezewa, wala kukusanywa wala kuzikwa.+ Watakuwa kama mbolea juu ya uso wa nchi.’+
34 “Pigeni mayowe, ninyi wachungaji, na mpaaze kilio!+ Na mgaegae,+ ninyi watu mashuhuri wa kundi,+ kwa sababu siku za kuchinjwa kwenu na za kutawanywa kwenu zimetimia,+ nanyi mtaanguka kama chombo kinachotamanika!+ 35 Na makimbilio yameangamia kwa wachungaji, na njia ya kuponyoka kwa watu mashuhuri wa kundi.+ 36 Sikilizeni! Kilio cha wachungaji, na kupiga mayowe kwa watu mashuhuri wa kundi, kwa maana Yehova anapora malisho yao. 37 Na makao yenye amani yamefanywa kukosa uhai kwa sababu ya hasira ya Yehova inayowaka.+ 38 Ametoka katika maficho yake kama mwana-simba mwenye manyoya shingoni,+ kwa maana nchi yao imekuwa kitu cha kushangaza kwa sababu ya upanga unaoonea na kwa sababu ya hasira yake inayowaka.”+
26 Katika mwanzo wa utawala wa kifalme wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, neno hili lilikuja kutoka kwa Yehova, na kusema: 2 “Yehova amesema hivi, ‘Simama katika ua wa nyumba ya Yehova,+ nawe useme kuhusu majiji yote ya Yuda yanayokuja kuinama katika nyumba ya Yehova, useme maneno yote nitakayokuamuru uwaambie.+ Usiondoe hata neno moja.+ 3 Labda watasikiliza na kurudi, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya,+ nami nitajuta msiba ninaofikiria kuleta juu yao kwa sababu ya ubaya wa matendo yao.+ 4 Nawe uwaambie: “Yehova amesema hivi, ‘Ikiwa hamtanisikiliza kwa kutembea katika sheria yangu+ ambayo nimeweka mbele yenu,+ 5 kwa kuyasikiliza maneno ya watumishi wangu manabii, ambao ninawatuma kwenu, nikiamka mapema na kuwatuma, ambao hamkuwasikiliza,+ 6 mimi, kwa upande wangu, nitaifanya nyumba hii kama ile iliyo katika Shilo,+ na jiji hili nitalifanya kuwa laana kwa mataifa yote ya dunia.’”’”+
7 Na makuhani na manabii na watu wote wakaanza kumsikia Yeremia akisema maneno hayo ndani ya nyumba ya Yehova.+ 8 Basi ikawa kwamba Yeremia alipokuwa amemaliza kusema yote ambayo Yehova alimwamuru kuwaambia watu wote, ndipo makuhani na manabii na watu wote wakamkamata, wakisema: “Hakika utakufa.+ 9 Kwa nini umetoa unabii katika jina la Yehova, ukisema, ‘Nyumba hii itakuwa kama ile iliyo katika Shilo,+ nalo jiji hili litafanywa ukiwa hivi kwamba halitakuwa na mkaaji’?” Na watu wote wakaendelea kujikutanisha kumzunguka Yeremia ndani ya nyumba ya Yehova.
10 Baada ya muda wakuu wa Yuda wakasikia maneno hayo, nao wakatoka katika nyumba ya mfalme wakapanda kwenda katika nyumba ya Yehova+ na kuketi katika mwingilio wa lango jipya la Yehova.+ 11 Na makuhani na manabii wakaanza kuwaambia wakuu na watu wote: “Mtu huyu anastahili hukumu ya kifo,+ kwa sababu ametoa unabii kulihusu jiji hili kama mlivyosikia kwa masikio yenu wenyewe.”+
12 Ndipo Yeremia akawaambia wakuu wote na watu wote: “Yehova ndiye aliyenituma kutoa unabii kuihusu nyumba hii na kulihusu jiji hili maneno yote ambayo mmeyasikia.+ 13 Na sasa fanyeni njia zenu na matendo yenu yawe mema,+ na mwitii sauti ya Yehova Mungu wenu, na Yehova ataujuta msiba ambao amesema juu yenu.+ 14 Na kwa habari yangu, tazama, mimi nipo hapa mkononi mwenu.+ Nitendeeni kulingana na yaliyo mema na kulingana na yaliyo sawa machoni penu.+ 15 Ila tu mnapaswa kujua kabisa kwamba, ikiwa mnaniua, ni damu isiyo na hatia ambayo mnajiletea juu yenu wenyewe na juu ya jiji hili na juu ya wakaaji wake,+ kwa maana kwa kweli Yehova alinituma kwenu niseme masikioni mwenu maneno haya yote.”+
16 Ndipo wakuu+ na watu wote wakawaambia makuhani na manabii: “Hakuna hukumu ya kifo anayostahili mtu huyu,+ kwa maana alisema nasi katika jina la Yehova Mungu wetu.”+
17 Na zaidi ya hayo, watu fulani kati ya wanaume wazee wa nchi wakasimama na kuanza kuliambia kutaniko lote la watu:+ 18 “Mika+ wa Moreshethi+ alikuwa akitoa unabii katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda+ naye akawaambia watu wote wa Yuda, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Sayuni utalimwa kama shamba,+ na Yerusalemu litakuwa marundo ya mabomoko,+ na mlima wa ile Nyumba utakuwa kama mahali pa juu pa msitu.”’+ 19 Je, Hezekia mfalme wa Yuda na wale wote wa Yuda walimuua? Je, hakumwogopa Yehova na kuanza kuutuliza uso wa Yehova,+ hivi kwamba Yehova akajuta ule msiba ambao alikuwa ametangaza juu yao?+ Basi sisi tunajifanyia msiba mkubwa juu ya nafsi zetu.+
20 “Na pia palikuwa na mtu aliyekuwa akitoa unabii katika jina la Yehova, Uriya mwana wa Shemaya kutoka Kiriath-yearimu.+ Naye aliendelea kutoa unabii juu ya jiji hili na juu ya nchi hii sawasawa na maneno yote ya Yeremia. 21 Na Mfalme Yehoyakimu+ na wanaume wake wote wenye nguvu na wakuu wote wakayasikia maneno yake, na mfalme akaanza kutafuta kumuua.+ Uriya aliposikia habari hizo, akaogopa+ mara moja, akakimbia, akaingia Misri. 22 Lakini Mfalme Yehoyakimu akatuma watu Misri, Elnathani mwana wa Akbori+ na watu wengine pamoja naye mpaka Misri. 23 Nao wakamleta Uriya kutoka Misri na kumleta kwa Mfalme Yehoyakimu, kisha akampiga na kumuua kwa upanga+ na kuitupa maiti yake katika makaburi ya wana wa watu.”
24 Zaidi ya hayo, mkono wa Ahikamu+ mwana wa Shafani+ ndio uliokuwa pamoja na Yeremia, asitiwe mkononi mwa watu ili auawe.+
27 Katika mwanzo wa ufalme wa Yehoyakimu mwana wa Yosia,+ mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema: 2 “Yehova ameniambia hivi, ‘Jitengenezee pingu na nira,+ nawe uziweke juu ya shingo yako.+ 3 Nawe uzipeleke kwa mfalme wa Edomu+ na kwa mfalme wa Moabu+ na kwa mfalme wa wana wa Amoni+ na kwa mfalme wa Tiro+ na kwa mfalme wa Sidoni+ kwa mkono wa wajumbe wanaokuja Yerusalemu kwa Sedekia mfalme wa Yuda. 4 Nawe uwape amri kwa ajili ya mabwana wao, na kusema:
“‘“Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli,+ amesema hivi; waambieni hivi mabwana wenu, 5 ‘Mimi mwenyewe nimeifanya dunia,+ wanadamu+ na wanyama+ walio juu ya uso wa dunia kwa nguvu zangu kuu+ na kwa mkono wangu ulionyooshwa;+ nami nimempa hiyo yeye ambaye nimemwona kuwa sawa machoni pangu.+ 6 Na sasa mimi mwenyewe nimezitia nchi hizi zote mkononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babiloni,+ mtumishi wangu;+ na nimempa hata wanyama wa mwituni ili wamtumikie.+ 7 Na mataifa yote lazima wamtumikie yeye+ na mwana wake na mjukuu wake mpaka uje wakati wa nchi yake mwenyewe,+ na mataifa mengi na wafalme wakuu watamtumikisha kama mtumishi.’+
8 “‘“‘Na itatukia kwamba lile taifa na ule ufalme ambao hautamtumikia Nebukadneza mfalme wa Babiloni; na lile ambalo halitatia shingo yake chini ya nira ya mfalme wa Babiloni, nitakaza fikira zangu juu ya taifa hilo kwa upanga+ na kwa njaa+ na kwa tauni,’+ asema Yehova, ‘mpaka nitakapokuwa nimewamaliza kabisa kwa mkono wake.’+
9 “‘“‘Nanyi msiwasikilize manabii+ wenu na waaguzi wenu na waota-ndoto+ wenu na watu wenu wenye kufanya uchawi na walozi+ wenu, ambao wanawaambia: “Ninyi hamtamtumikia mfalme wa Babiloni.”+ 10 Kwa maana wao wanawatolea unabii wa uwongo, kusudi mpelekwe mbali kutoka katika nchi yenu; nami niwatawanye, nanyi mwangamie.+
11 “‘“‘Nalo taifa litakalotia shingo yake chini ya nira ya mfalme wa Babiloni na kwa kweli limtumikie, mimi pia nitaliacha lipumzike juu ya nchi yake,’ asema Yehova, ‘nalo hakika litailima na kukaa ndani yake.’”’”+
12 Hata Sedekia+ mfalme wa Yuda nilimwambia kulingana na maneno haya yote,+ nikisema: “Tieni shingo zenu chini ya nira ya mfalme wa Babiloni, mkamtumikie yeye na watu wake, mwendelee kuishi.+ 13 Kwa nini wewe mwenyewe na watu wako mfe kwa upanga,+ kwa njaa+ na kwa tauni+ kulingana na yale ambayo Yehova amesema kuhusu lile taifa ambalo halitamtumikia mfalme wa Babiloni? 14 Nanyi msiyasikilize maneno ya manabii wanayowaambia, ‘Hamtamtumikia mfalme wa Babiloni,’+ kwa sababu wanawatolea unabii wa uwongo.+
15 “‘Kwa maana mimi sikuwatuma,’ asema Yehova, ‘lakini wanatoa unabii katika jina langu kwa uwongo, kusudi niwatawanye,+ nanyi mwangamie,+ ninyi pamoja na wale manabii wanaowatolea unabii.’”+
16 Nami nikawaambia makuhani na watu hawa wote, nikisema: “Yehova amesema hivi, ‘Msiyasikilize maneno ya manabii wenu wanaowatolea unabii, wakisema: “Tazama! Vyombo vya nyumba ya Yehova vitarudishwa kutoka Babiloni hivi karibuni!”+ Kwa maana wanawatolea ninyi unabii wa uwongo.+ 17 Msiwasikilize. Mtumikieni mfalme wa Babiloni, mwendelee kuishi.+ Kwa nini jiji hili liwe ukiwa?+ 18 Lakini ikiwa wao ni manabii na ikiwa wana neno la Yehova, tafadhali, acheni wamwombe Yehova wa majeshi,+ ili vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Yehova na katika nyumba ya mfalme wa Yuda na katika Yerusalemu visiende Babiloni.’
19 “Kwa maana Yehova wa majeshi amesema hivi kuhusu zile nguzo+ na kuhusu ile bahari+ na kuhusu yale mabehewa+ na kuhusu yale mabaki ya vyombo ambavyo vimebaki katika jiji hili,+ 20 ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babiloni hakuchukua alipompeleka uhamishoni Yekonia+ mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, kutoka Yerusalemu kwenda Babiloni, pamoja na watu wote wenye vyeo wa Yuda na Yerusalemu;+ 21 kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi kuhusu vile vyombo ambavyo vimebaki katika nyumba ya Yehova na nyumba ya mfalme wa Yuda na Yerusalemu,+ 22 ‘ “Vitapelekwa Babiloni+ navyo vitaendelea kuwa huko mpaka siku ile nitakapovikazia fikira,”+ asema Yehova. “Nami nitavileta na kuvirudisha mahali hapa.”’”+
28 Kisha ikawa kwamba mwaka huo, katika mwanzo wa ufalme wa Sedekia+ mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne, mwezi wa tano, Hanania+ mwana wa Azuri, yule nabii kutoka Gibeoni,+ akaniambia hivi ndani ya nyumba ya Yehova mbele ya macho ya makuhani na ya watu wote: 2 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babiloni.+ 3 Katika muda wa miaka miwili kamili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Yehova ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babiloni+ alivichukua kutoka mahali hapa ili kuvipeleka Babiloni.’” 4 “‘Na Yekonia+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, pamoja na wahamishwa wote wa Yuda ambao wameenda Babiloni+ nitawarudisha tena mahali hapa,’ asema Yehova, ‘kwa maana nitaivunja nira+ ya mfalme wa Babiloni.’”
5 Na Yeremia nabii akamwambia Hanania nabii mbele ya macho ya makuhani na mbele ya macho ya watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Yehova;+ 6 ndiyo, Yeremia nabii akasema: “Amina!+ Yehova na afanye hivyo! Yehova na ayatimize maneno yako ambayo umetoa unabii kwa kuvirudisha tena mahali hapa kutoka Babiloni vyombo vya nyumba ya Yehova na watu wote waliohamishwa!+ 7 Hata hivyo, tafadhali sikia neno hili ninalosema masikioni mwako na masikioni mwa watu wote.+ 8 Kwa habari ya manabii walionitangulia mimi na waliokutangulia wewe kutoka zamani za kale,+ wao pia walikuwa wakitoa unabii kuhusu nchi nyingi na kuhusu falme kubwa, juu ya vita na juu ya msiba na juu ya tauni.+ 9 Kwa habari ya nabii anayetoa unabii wa amani,+ wakati neno la nabii huyo litakapotimia yule nabii ambaye Yehova amemtuma kikweli atajulikana.”+
10 Ndipo Hanania nabii akaichukua ile nira kutoka shingoni mwa Yeremia nabii na kuivunja.+ 11 Na Hanania+ akasema mbele ya macho ya watu wote: “Yehova amesema hivi,+ ‘Hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babiloni katika muda wa miaka miwili kamili ili itoke shingoni mwa mataifa yote.’”+ Na Yeremia nabii akaenda zake.+
12 Ndipo neno la Yehova likamjia Yeremia,+ baada ya Hanania nabii kuivunja ile nira kutoka shingoni mwa Yeremia nabii, na kusema: 13 “Nenda, umwambie Hanania, ‘Yehova amesema hivi: “Umevunja nira+ za miti, na badala ya hizo utatengeneza nira za chuma.”+ 14 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Nitatia nira ya chuma juu ya shingo ya mataifa haya yote, ili yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babiloni;+ nao lazima watamtumikia.+ Nami nitampa hata wanyama wa mwituni.”’”+
15 Na Yeremia nabii akaendelea kumwambia Hanania+ nabii: “Tafadhali, sikiliza, Ee Hanania! Yehova hakukutuma wewe, bali wewe mwenyewe umewafanya watu hawa wautegemee uwongo.+ 16 Kwa hiyo Yehova amesema hivi, ‘Tazama! Ninakuondolea mbali kutoka katika uso wa nchi. Mwaka huu utakufa hakika,+ kwa maana umesema maasi ya waziwazi juu ya Yehova.’”+
17 Basi Hanania nabii akafa mwaka huo, katika mwezi wa saba.+
29 Na haya ndiyo maneno ya barua ambayo Yeremia nabii alituma kutoka Yerusalemu kwa mabaki ya wanaume wazee wa watu waliohamishwa na kwa makuhani na kwa manabii na kwa watu wote, ambao Nebukadneza alikuwa amewapeleka uhamishoni kutoka Yerusalemu kwenda Babiloni+ 2 baada ya Yekonia+ mfalme na malkia+ na maofisa wa makao ya mfalme, wakuu wa Yuda na Yerusalemu,+ na mafundi na wajenzi wa maboma+ kwenda kutoka katika Yerusalemu. 3 Ilikuwa kwa mkono wa Elasa mwana wa Shafani+ na Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia+ mfalme wa Yuda aliwatuma kwenda Babiloni kwa Nebukadneza mfalme wa Babiloni, na kusema:
4 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amewaambia hivi watu wote waliohamishwa, ambao nimewapeleka uhamishoni+ kutoka Yerusalemu kwenda Babiloni, 5 ‘Jengeni nyumba na kukaa ndani yake, mpande bustani na kula matunda yake.+ 6 Chukueni wake na kuzaa wana na binti;+ na kuwachukulia wana wenu wake na kuwaoza binti zenu kwa waume, ili wazae wana na binti; na muwe wengi huko, wala msiwe wachache. 7 Pia, tafuteni amani kwa ajili ya jiji ambamo nimewapeleka ninyi uhamishoni, nanyi msali kwa ajili yake kwa Yehova, kwa maana katika amani ya jiji hilo kutakuwa na amani kwa ajili yenu wenyewe.+ 8 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Msiache manabii wenu walio katikati yenu na waaguzi wenu wawadanganye,+ nanyi msisikilize ndoto zao ambazo wanaota.+ 9 Kwa maana ‘wanawatolea ninyi unabii wa uwongo katika jina langu. Mimi sikuwatuma,’+ asema Yehova.”’”
10 “Kwa maana Yehova amesema hivi, ‘Kupatana na kutimia kwa miaka 70 katika Babiloni nitawakazia ninyi fikira,+ nami nitawatimizia neno langu jema kwa kuwarudisha tena mahali hapa.’+
11 “‘Kwa maana mimi najua vema mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi,’+ asema Yehova, ‘mawazo ya amani, wala si ya msiba,+ ili kuwapa ninyi wakati ujao na tumaini.+ 12 Na hakika mtaniita na kuja na kusali kwangu, nami nitawasikiliza.’+
13 “‘Nanyi kwa kweli mtanitafuta na kunipata,+ kwa maana mtanitafuta kwa moyo wenu wote.+ 14 Nami nitajiacha mnipate,’+ asema Yehova. ‘Nami nitakusanya kundi lenu la mateka na kuwakusanya ninyi pamoja kutoka katika mataifa yote na kutoka katika mahali pote ambapo nimewatawanya ninyi,’+ asema Yehova. ‘Nami nitawarudisha katika mahali ambapo kutoka hapo niliwapeleka uhamishoni.’+
15 “Lakini mmesema, ‘Yehova ametuinulia manabii katika Babiloni.’
16 “Kwa maana Yehova amesema hivi kwa mfalme anayeketi juu ya kiti cha ufalme cha Daudi+ na kwa watu wote wanaokaa katika jiji hili, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni,+ 17 ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Tazama, ninatuma juu yao upanga,+ njaa+ na tauni,+ nami nitawafanya kuwa kama tini zilizopasuka ambazo haziwezi kuliwa kwa sababu ya ubaya.”’+
18 “‘Nami nitawafuatilia kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawatoa wawe kitu cha kutetemesha falme zote za dunia,+ kuwa laana na kuwa kitu cha kushangaza na kuwa kitu cha kupigiwa mluzi na kuwa kitu cha kushutumiwa katikati ya mataifa yote ambako hakika nitawatawanya,+ 19 kwa sababu hawakuyasikiliza maneno yangu,’ asema Yehova, ‘ambayo nimetuma kwao kupitia watumishi wangu manabii, nikiamka mapema na kuwatuma.’+
“‘Lakini hamkusikiliza,’+ asema Yehova.
20 “Nanyi sikieni neno la Yehova, ninyi nyote mliohamishwa,+ ambao nimewafukuza kutoka Yerusalemu kwenda Babiloni.+ 21 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi kumhusu Ahabu mwana wa Kolaya na kumhusu Sedekia mwana wa Maaseya, ambao wanawatolea ninyi unabii wa uwongo katika jina langu mwenyewe,+ ‘Tazama, nitawatia mkononi mwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni, naye atawapiga na kuwaua mbele ya macho yenu.+ 22 Na kutoka kwao hakika laana itachukuliwa na kundi zima la wahamishwa walio katika Babiloni, na kusema: “Yehova na akufanye kama Sedekia na kama Ahabu,+ ambao mfalme wa Babiloni aliwachoma motoni!”+ 23 kwa sababu wametenda upumbavu katika Israeli,+ nao wanaendelea kufanya uzinzi pamoja na wake za wenzao+ na kuendelea kusema uwongo kwa jina langu mwenyewe neno ambalo mimi sikuwaamuru.+
“‘“Mimi ndiye ninayejua nami ni shahidi,”+ asema Yehova.’”
24 “Nawe utamwambia hivi Shemaya+ wa Nehelamu, 25 ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Kwa sababu wewe umetuma barua+ katika jina lako kwa watu wote walioko Yerusalemu, na kwa Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, na kwa makuhani wote, ukisema, 26 ‘Yehova amekufanya wewe kuwa kuhani badala ya Yehoyada kuhani, ili uwe mwangalizi mkuu wa nyumba ya Yehova+ kuelekea mtu yeyote aliyetiwa wazimu+ na mwenye kujiendesha kama nabii, nawe utamtia katika mikatale na katika kongwa;+ 27 sasa, basi, kwa nini hukumkemea Yeremia wa Anathothi,+ ambaye anajiendesha kama nabii kwenu?+ 28 Kwa maana ndiyo sababu ametuma ujumbe kwetu Babiloni, akisema: “Ni wa muda mrefu! Jengeni nyumba na kukaa ndani yake, na kupanda bustani na kula matunda yake,+ — ”’”’”
29 Na Sefania+ kuhani akaisoma barua hii masikioni mwa Yeremia nabii.
30 Ndipo neno la Yehova likamjia Yeremia, na kusema: 31 “Tuma ujumbe kwa watu wote waliohamishwa,+ ukisema, ‘Yehova amesema hivi kumhusu Shemaya wa Nehelamu: “Kwa sababu Shemaya amewatolea ninyi unabii, lakini mimi mwenyewe sikumtuma, naye alijaribu kuwafanya mtegemee uwongo,+ 32 basi Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninakaza fikira zangu juu ya Shemaya+ wa Nehelamu na juu ya uzao wake.’+
“‘“‘Hatakuwa na mtu anayekaa katikati ya kikundi hiki cha watu;+ wala hatautazama wema ambao nitawafanyia watu wangu,’+ asema Yehova, ‘kwa maana amesema maasi ya waziwazi juu ya Yehova.’”’”+
30 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema: 2 “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Andika katika kitabu maneno yote nitakayokuambia.+ 3 Kwa maana, “tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitawakusanya mateka wa watu wangu, Israeli na Yuda,”+ Yehova amesema, “nami nitawarudisha katika nchi niliyowapa mababu zao, nao hakika wataimiliki tena.”’”+
4 Na haya ndiyo maneno ambayo Yehova amewaambia Israeli na Yuda. 5 Kwa maana Yehova amesema hivi: “Sauti ya kutetemeka tumeisikia, hofu,+ na hakuna amani. 6 Ulizeni, tafadhali, na mwone ikiwa mwanamume anajifungua mtoto. Kwa nini nimemwona kila mwanamume akiweka mikono juu ya viuno vyake kama mwanamke anayejifungua mtoto,+ na nyuso zote zimegeuka rangi?+ 7 Ole wangu! Kwa maana siku ile ni kuu,+ hivi kwamba hakuna nyingine kama hiyo,+ na ni wakati wa taabu kwa Yakobo.+ Lakini yeye ataokolewa kutoka katika hiyo.”
8 “Na itakuwa katika siku hiyo,” asema Yehova wa majeshi, “kwamba nitaivunja nira ya mtu kutoka shingoni mwako, na pingu zako nitazikata vipande viwili,+ na wageni hawatamtumia vibaya tena kama mtumishi. 9 Nao hakika watamtumikia Yehova Mungu wao na Daudi mfalme wao,+ ambaye nitawasimamishia.”+
10 “Nawe usiogope, Ee mtumishi wangu Yakobo,” asema Yehova, “wala usiingiwe na hofu, Ee Israeli.+ Kwa maana, tazama, ninakuokoa wewe kutoka mbali na uzao wako kutoka katika nchi yao ya utekwani.+ Na hakika Yakobo atarudi na kuwa huru kutokana na usumbufu naye atastarehe, wala hakutakuwa na mtu yeyote anayemtetemesha.”+
11 “Kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Yehova, “ili nikuokoe;+ lakini nitafanya maangamizi kati ya mataifa yote ambako nimekutawanya.+ Hata hivyo, kwako sitafanya maangamizi.+ Nami nitakurekebisha kwa kiwango kinachofaa, kwa kuwa sitakuacha kamwe bila kukuadhibu.”+
12 Kwa maana Yehova amesema hivi: “Hakuna matibabu kwa ajili ya kuvunjika kwako.+ Pigo lako ni la kudumu.+ 13 Hakuna yeyote anayetetea mambo yako, kidonda chako.+ Hakuna njia ya kuponya, hakuna matibabu, kwa ajili yako.+ 14 Wale wote wanaokupenda sana ndio wale ambao wamekusahau.+ Si wewe ambaye wanaendelea kukutafuta. Kwa maana nimekupiga kwa pigo la adui,+ kwa adhabu ya mtu mkatili,+ kwa sababu ya wingi wa makosa yako;+ dhambi zako zimekuwa nyingi.+ 15 Kwa nini unapaaza kilio kwa sababu ya kuvunjika kwako?+ Maumivu yako hayawezi kupona kwa sababu ya wingi wa makosa yako;+ dhambi zako zimekuwa nyingi. Nimekutendea mambo hayo. 16 Kwa hiyo wale wote wanaokumeza nao wenyewe watamezwa;+ nao adui zako wote, wote wataenda utekwani.+ Na wale wanaokupora hakika wataporwa, na wale wote wanaokunyakua nitawatoa wanyakuliwe.”+
17 “Kwa maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya mapigo yako,”+ asema Yehova. “Kwa maana walikuita mwanamke aliyefukuzwa:+ ‘Huyo ni Sayuni, ambaye hakuna yeyote anayemtafuta.’”+
18 Yehova amesema hivi: “Tazama, ninawakusanya mateka wa mahema ya Yakobo,+ nami nitazihurumia maskani zake. Na kwa kweli jiji litajengwa upya juu ya kilima chake;+ na mnara wa makao utaketi juu ya mahali pake panapoufaa.+ 19 Na kutoka kwao hakika shukrani zitatolewa, na sauti ya wale wanaocheka.+ Nami nitawazidisha, nao hawatakuwa wachache;+ nami nitawafanya kuwa wengi katika hesabu, nao hawatakuwa wanyonge.+ 20 Na wanawe watakuwa kama katika nyakati za zamani, na kusanyiko lake litafanywa imara mbele zangu.+ Nami nitakaza fikira zangu juu ya wakandamizaji wake wote.+ 21 Na mtu wake aliye mashuhuri atakuwa kutoka kwake,+ na mtawala wake atatoka katikati yake;+ nami nitamleta karibu, naye atanikaribia.”+
“Kwa maana, sasa, ni nani huyu ambaye ametoa moyo wake rehani ili kunikaribia?”+ asema Yehova. 22 “Nanyi hakika mtakuwa watu wangu,+ na mimi nitakuwa Mungu wenu.”+
23 Tazama! Dhoruba ya Yehova, ghadhabu, imetoka, tufani inayofagia ikisonga mbele.+ Itazunguka juu ya kichwa cha waovu.+ 24 Hasira ya Yehova inayowaka haitarudi nyuma mpaka atakapokuwa amefanya na mpaka atakapokuwa ametimiza mawazo ya moyo wake.+ Mtalifikiria jambo hilo katika siku za mwisho.+
31 “Wakati huo,” asema Yehova, “Nitakuwa Mungu kwa familia zote za Israeli; nao watakuwa watu wangu.”+
2 Yehova amesema hivi: “Watu waliookoka upanga walipata kibali nyikani,+ wakati Israeli alipokuwa akitembea ili kupata starehe yake.”+ 3 Kutoka mbali Yehova alinitokea, akisema: “Nimekupenda wewe kwa upendo mpaka wakati usio na kipimo.+ Ndiyo sababu nimekuvuta kwa fadhili zenye upendo.+ 4 Bado nitakujenga upya nawe kwa kweli utajengwa upya,+ Ee bikira wa Israeli. Bado utajipamba kwa matari yako na kwa kweli utaenda katika dansi ya wale wanaocheka.+ 5 Bado utapanda mashamba ya mizabibu katika milima ya Samaria.+ Hakika wapandaji watapanda na kuanza kula matunda.+ 6 Kwa maana kuna siku ambayo walinzi walio katika eneo lenye milima la Efraimu wataita, ‘Simameni, twende Sayuni, kwa Yehova Mungu wetu.’”+
7 Kwa maana Yehova amesema hivi: “Mlilieni Yakobo kwa sauti kubwa kwa kushangilia, na kupaaza kelele mbele ya mataifa.+ Tangazeni jambo hilo.+ Sifuni na kusema, ‘Waokoe, Ee Yehova, watu wako, mabaki ya Israeli.’+ 8 Tazama, ninawaleta kutoka katika nchi ya kaskazini,+ nami nitawakusanya kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+ Kati yao patakuwa na vipofu na vilema, mwanamke mwenye mimba na yule anayezaa, wote pamoja.+ Watarudi hapa wakiwa kutaniko kubwa.+ 9 Watakuja wakilia,+ nami nitawaleta wakiwa na maombi yao ya kusihi wakitaka kibali. Nitawatembeza kwenye mabonde ya mito ya maji,+ katika njia iliyo sawa ambayo ndani yake hawatakwazwa. Kwa maana mimi nimekuwa Baba kwa Israeli;+ naye Efraimu, yeye ni mzaliwa wangu wa kwanza.”+
10 Sikieni neno la Yehova, enyi mataifa, na kulitangaza kati ya visiwa vilivyo mbali,+ na kusema: “Yeye anayemtawanya Israeli atamkusanya pamoja,+ na hakika yeye atamweka kama mchungaji anavyoliweka kundi lake.+ 11 Kwa maana kwa kweli Yehova atamkomboa Yakobo+ na kumponya kutoka mkononi mwa yule aliye na nguvu kuliko yeye.+ 12 Nao hakika watakuja na kupiga vigelegele vya shangwe juu ya kilele cha Sayuni+ na kung’aa kwa sababu ya wema wa Yehova,+ kwa sababu ya nafaka na kwa sababu ya divai+ mpya na kwa sababu ya mafuta na kwa sababu ya watoto wa kundi na ng’ombe.+ Na nafsi yao itakuwa tu kama bustani iliyonyweshwa maji vizuri,+ nao hawatakuwa dhaifu tena.”+
13 “Wakati huo bikira atashangilia kwa dansi, pia vijana na wanaume wazee, wote pamoja.+ Nami nitayageuza maombolezo yao yawe furaha, nami nitawafariji na kuwafanya washangilie kutoka katika huzuni yao.+ 14 Nami nitaishibisha nafsi ya makuhani kwa mafuta,+ na watu wangu watashiba wema,”+ asema Yehova.
15 “Yehova amesema hivi, ‘Katika Rama+ sauti inasikiwa, maombolezo na kilio cha uchungu;+ Raheli+ akiwalilia wanawe.+ Amekataa kufarijiwa juu ya wanawe,+ kwa sababu hawako tena.’”+
16 Yehova amesema hivi: “‘Zuia sauti yako, usilie, na macho yako yasitoe machozi,+ kwa maana kuna thawabu kwa ajili ya utendaji wako,’ asema Yehova, ‘nao hakika watarudi kutoka katika nchi ya adui.’+
17 “‘Na kuna tumaini+ kwa ajili ya wakati wako ujao,’ asema Yehova, ‘na wana watarudi hakika katika eneo lao wenyewe.’”+
18 “Hakika nimemsikia Efraimu akijiombolezea,+ ‘Umenirekebisha,+ ili nipate kurekebishwa, kama ndama ambaye hajazoezwa.+ Unigeuze mimi, nami nitageuka bila kusita,+ kwa maana wewe ni Yehova Mungu wangu.+ 19 Kwa maana baada ya kugeuka kwangu nilihisi kujuta;+ na baada ya kujulishwa nililipiga paja kofi.+ Niliona aibu, na pia nikafedheheka,+ kwa maana nilikuwa nimechukua shutuma ya ujana wangu.’”+
20 “Je, Efraimu ni mwana mwenye thamani kwangu, au mtoto anayetendewa kwa upendo?+ Kwa maana kwa kiasi ninachosema vibaya juu yake bila shaka nitamkumbuka zaidi.+ Ndiyo sababu matumbo yangu yamekuwa na msukosuko kwa ajili yake.+ Kwa kuwa nitamhurumia kabisa,”+ asema Yehova.
21 “Jisimamishie alama za barabara. Jiwekee vibao vya ishara.+ Kaza moyo wako juu ya njia kuu, njia ambayo utaiendea.+ Rudi, Ee bikira wa Israeli. Rudi kwenye haya majiji yako.+ 22 Utaendelea kugeuka huku na huku mpaka wakati gani,+ Ee binti usiye mwaminifu?+ Kwa maana Yehova ameumba jambo jipya duniani: Mwanamke atajibana kwa mwanamume.”
23 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Bado watasema neno hili katika nchi ya Yuda na katika majiji yake, nitakapowakusanya mateka wao, ‘Yehova na akubariki,+ Ee makao ya uadilifu,+ Ee mlima mtakatifu.’+ 24 Na Yuda na majiji yake yote hakika watakaa ndani yake pamoja, wakulima na wale ambao wameondoka wakiwa na kundi.+ 25 Kwa maana nitaishibisha nafsi iliyochoka, nami nitaijaza kila nafsi ambayo ni dhaifu.”+
26 Ndipo nikaamka na kuanza kuona; nao usingizi wangu ulikuwa umekuwa mtamu kwangu.
27 “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitaipanda nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda uzao wa mwanadamu na uzao wa mnyama wa kufugwa.”+
28 “Na itakuwa kwamba kama nilivyokuwa macho kuwaelekea wao+ ili kung’oa na kubomoa na kuangusha na kuharibu na kudhuru,+ ndivyo nitakavyokuwa macho kuwaelekea ili kujenga na kupanda,”+ asema Yehova. 29 “Katika siku hizo hawatasema tena, ‘Akina baba ndio waliokula zabibu mbichi, lakini meno ya wana ndiyo yaliyotiwa ukakasi.’+ 30 Lakini kila mmoja atakufa kwa sababu ya kosa lake mwenyewe.+ Mtu yeyote atakayekula zabibu mbichi, meno yake ndiyo yatakayotiwa ukakasi.”
31 “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitafanya agano jipya+ pamoja na nyumba ya Israeli+ na nyumba ya Yuda;+ 32 si kama lile agano ambalo nilifanya pamoja na mababu zao katika ile siku nilipowashika mkono na kuwatoa katika nchi ya Misri,+ ‘agano langu ambalo wao walilivunja,+ ingawa mimi mwenyewe nilikuwa mume kwao,’+ asema Yehova.”
33 “Kwa maana hili ndilo agano+ nitakalofanya pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,”+ asema Yehova. “Nitaitia sheria yangu ndani yao,+ nami nitaiandika katika moyo wao.+ Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”+
34 “Nao hawatafundishana tena kila mtu na mwenzake wala kila mtu na ndugu yake,+ wakisema, ‘Mjueni Yehova!’+ kwa maana wote watanijua mimi, kuanzia yule aliye mdogo zaidi kati yao mpaka yule aliye mkubwa zaidi kati yao,”+ asema Yehova. “Kwa maana nitalisamehe kosa lao, na dhambi yao sitaikumbuka tena.”+
35 Yehova, Mpaji wa jua kwa ajili ya nuru wakati wa mchana,+ sheria+ za mwezi+ na nyota kwa ajili ya nuru wakati wa usiku,+ Yeye anayeichafua bahari ili mawimbi yake yawe na mchafuko,+ Yeye ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi,+ amesema hivi: 36 “‘Kama masharti haya yangeweza kuondolewa mbele zangu,’+ asema Yehova, ‘vivyo hivyo wale ambao ni uzao wa Israeli wangeweza kukoma wasiwe taifa mbele zangu sikuzote.’”+
37 Yehova amesema hivi: “‘Mbingu zilizo juu zikiweza kupimwa na misingi ya dunia iliyo chini ikiweza kuchunguzwa,+ vivyo hivyo mimi mwenyewe ningeweza kuukataa uzao wote wa Israeli kwa sababu ya yote ambayo wamefanya,’+ asema Yehova.”
38 “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “na hakika jiji litajengwa+ kwa ajili ya Yehova kutoka Mnara wa Hananeli+ mpaka Lango la Pembeni.+ 39 Na bado kamba ya kupimia+ itaenda mbele moja kwa moja kwenye kilima cha Garebu, nayo hakika itazunguka mpaka Goa. 40 Na nchi tambarare yote ya chini ya mizoga+ na ya majivu yenye mafuta,+ na matuta yote mpaka bonde la mto la Kidroni,+ mpaka kwenye pembe ya Lango la Farasi+ kuelekea mashariki, itakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova.+ Haitang’olewa, wala haitabomolewa tena mpaka wakati usio na kipimo.”+
32 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova katika mwaka wa kumi wa Sedekia mfalme wa Yuda,+ yaani, mwaka wa kumi na nane wa Nebukadreza.+ 2 Na wakati huo majeshi ya mfalme wa Babiloni yalikuwa yanazingira Yerusalemu;+ naye Yeremia nabii alikuwa chini ya kizuizi katika Ua wa Walinzi+ ulio katika nyumba ya mfalme wa Yuda; 3 kwa sababu Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemzuilia,+ akisema:
“Kwa nini unatoa unabii,+ ukisema, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama, ninalitia jiji hili mkononi mwa mfalme wa Babiloni, na hakika yeye ataliteka;+ 4 na Sedekia mwenyewe, mfalme wa Yuda, hataponyoka kutoka mkononi mwa Wakaldayo, kwa maana bila shaka atatiwa mkononi mwa mfalme wa Babiloni, na kinywa chake kitasema na kinywa cha yule, na macho yake yatayaona macho ya yule”’;+ 5 ‘naye atampeleka Sedekia mpaka Babiloni, naye ataendelea kuwa huko mpaka nitakapomkazia fikira,’+ asema Yehova; ‘ingawa ninyi mnaendelea kupigana na Wakaldayo, hamtafanikiwa’?”+
6 Na Yeremia akasema: “Neno la Yehova limenijia, na kusema, 7 ‘Tazama, Hanameli mwana wa Shalumu ndugu ya baba yako anakuja kwako, kusema: “Jinunulie shamba langu lililoko Anathothi,+ kwa sababu haki ya kukomboa ni yako, ulinunue.”’”+
8 Baada ya muda Hanameli mwana wa ndugu ya baba yangu akaingia kwangu, kulingana na lile neno la Yehova, ndani ya Ua wa Walinzi,+ naye akaniambia: “Tafadhali, nunua shamba langu lililoko Anathothi,+ lililo katika nchi ya Benyamini,+ kwa maana haki ya fungu la urithi ni yako, na mamlaka ya kukomboa ni yako. Linunue liwe lako.” Ndipo nikajua kwamba hilo lilikuwa neno la Yehova.+
9 Kwa hiyo nikanunua lile shamba lililoko Anathothi+ kutoka kwa Hanameli+ mwana wa ndugu ya baba yangu. Nami nikaanza kumpimia pesa,+ shekeli saba na vipande kumi vya fedha. 10 Kisha nikaandika katika hati+ na kutia muhuri+ na kuchukua mashahidi+ nilipokuwa nikipima+ pesa katika mizani. 11 Baada ya hayo nikachukua ile hati ya ununuzi, ile iliyotiwa muhuri kulingana na amri na masharti,+ na ile iliyoachwa wazi; 12 kisha nikampa hati ya ununuzi Baruku+ mwana wa Neria+ mwana wa Mahseya mbele ya macho ya Hanameli mwana wa ndugu ya baba yangu na mbele ya macho ya mashahidi, wale wenye kuandika katika ile hati ya ununuzi,+ mbele ya macho ya Wayahudi wote waliokuwa wameketi katika Ua wa Walinzi.+
13 Sasa nikamwamuru Baruku mbele ya macho yao, nikisema: 14 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Chukua hizi hati, hii hati ya ununuzi, iliyotiwa muhuri, na ile hati nyingine iliyoachwa wazi,+ nawe uziweke katika chombo cha udongo, ili zidumu kwa siku nyingi.’ 15 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Bado nyumba na mashamba na mizabibu zitanunuliwa katika nchi hii.’”+
16 Nami nikaanza kusali+ kwa Yehova baada ya kumpa Baruku+ mwana wa Neria+ ile hati ya ununuzi, nikisema: 17 “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova!+ Tazama, wewe mwenyewe umeziumba mbingu na dunia kwa nguvu zako kuu+ na kwa mkono wako ulionyooshwa.+ Jambo hilo lote si la ajabu mno kwako,+ 18 Wewe unayeonyesha fadhili zenye upendo kuelekea maelfu,+ na kulipa kosa la akina baba katika vifua vya wana wao baada yao,+ Mungu wa kweli, aliye Mkuu,+ Mwenye nguvu,+ Yehova wa majeshi+ ndilo jina lake,+ 19 mkuu katika shauri+ na mwingi katika matendo,+ wewe ambaye macho yako yamefunguliwa juu ya njia zote za wanadamu,+ ili kumpa kila mmoja kulingana na njia zake na kulingana na matunda ya matendo yake;+ 20 wewe uliyeweka ishara na miujiza katika nchi ya Misri mpaka leo hii na katika Israeli na kati ya wanadamu,+ ili ujifanyie jina, kama ilivyo leo hii.+ 21 Nawe ukawatoa watu wako Israeli katika nchi ya Misri,+ kwa ishara na kwa miujiza+ na kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa na kwa hali kuu ya kuogopesha.+
22 “Baada ya muda ukawapa nchi hii ambayo uliwaapia mababu zao kuwapa,+ nchi inayotiririka maziwa na asali.+ 23 Nao wakaingia na kuimiliki,+ lakini hawakuitii sauti yako, nao hawakutembea katika sheria yako.+ Mambo yote uliyowaamuru kufanya hawakuyafanya,+ hivi kwamba ukafanya msiba huu wote uwaangukie.+ 24 Tazama! Watu wamekuja na maboma ya kuzingira+ kwenye jiji ili kuliteka,+ na jiji hili hakika litatiwa mkononi mwa Wakaldayo wanaopiga vita juu yake,+ kwa sababu ya upanga+ na njaa+ na tauni;+ na lile ulilosema limetendeka, na, tazama, wewe unaliona.+ 25 Ingawa wewe mwenyewe umeniambia, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘Jinunulie lile shamba kwa pesa+ na kuchukua mashahidi,’+ ingawa lazima jiji lenyewe litatiwa mkononi mwa Wakaldayo.”+
26 Ndipo neno la Yehova likamjia Yeremia, na kusema: 27 “Mimi hapa, Yehova, Mungu wa wote wenye mwili.+ Je, kwangu mimi kuna jambo lolote ambalo ni la ajabu mno?+ 28 Kwa hiyo Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninalitia jiji hili katika mkono wa Wakaldayo na katika mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babiloni, naye lazima ataliteka.+ 29 Na Wakaldayo wanaopiga vita juu ya jiji hili wataingia ndani na kuliwasha jiji hili na kuliteketeza kwa moto+ na nyumba ambazo juu ya paa zake wamemfukizia Baali moshi wa dhabihu na kuimiminia miungu mingine matoleo ya kinywaji kwa kusudi la kunitia uchungu.’+
30 “‘Kwa maana wana wa Israeli na wana wa Yuda wamekuwa tu watendaji wa mambo mabaya machoni pangu, tangu ujana wao na kuendelea;+ kwa maana wana wa Israeli pia wananitia uchungu kwa kazi za mikono yao,’+ asema Yehova. 31 ‘Kwa maana jiji hili, tangu siku walipolijenga, mpaka leo hii, limekuwa tu kisababishi cha hasira ndani yangu+ na kisababishi cha ghadhabu ndani yangu, ili kuliondoa mbele za uso wangu,+ 32 kwa sababu ya ubaya wote wa wana wa Israeli+ na wa wana wa Yuda+ ambao wametenda ili kunitia uchungu,+ wao, wafalme+ wao, wakuu+ wao, makuhani+ wao na manabii+ wao, na watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu. 33 Nao wakaendelea kunipa mimi mgongo wala si uso;+ ingawa walikuwa wakifundishwa, kuamka mapema na kuwafundisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyesikiliza ili kupokea nidhamu.+ 34 Nao wakawa wakiweka machukizo yao katika nyumba ambayo jina langu limeitwa juu yake, ili kuitia unajisi.+ 35 Na zaidi ya hayo, walijenga mahali pa juu pa Baali+ palipo katika bonde la mwana wa Hinomu,+ ili kuwapitisha wana wao na binti zao motoni+ kwa Moleki,+ jambo ambalo sikuwaamuru,+ wala halikuingia moyoni mwangu kufanya chukizo hili,+ kwa kusudi la kufanya Yuda watende dhambi.’+
36 “Na sasa, basi, Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi kuhusu jiji hili ambalo ninyi mnasema hakika litatiwa mkononi mwa mfalme wa Babiloni kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni,+ 37 ‘Tazama, ninawakusanya pamoja kutoka katika nchi zote ambako nitakuwa nimewatawanya katika hasira yangu na katika ghadhabu yangu na katika hasira kuu;+ nami nitawarudisha mahali hapa na kuwakalisha katika usalama.+ 38 Na hakika wao watakuwa watu wangu,+ nami mwenyewe nitakuwa Mungu wao.+ 39 Nami nitawapa moyo mmoja+ na njia moja ili waniogope sikuzote, iwe kwa mema yao na kwa mema ya wana wao baada yao.+ 40 Nami nitafanya pamoja nao agano linalodumu mpaka wakati usio na kipimo,+ kwamba mimi sitageuka kutoka nyuma yao, ili niwatendee mema;+ nami nitatia ndani ya moyo wao hali ya kuniogopa mimi ili wasigeuke kando kutoka kwangu.+ 41 Nami nitafurahi juu yao ili niwatendee mema,+ nami nitawapanda katika nchi hii+ katika ukweli kwa moyo wangu wote na kwa nafsi yangu yote.’”
42 “Kwa maana Yehova amesema hivi, ‘Kama nilivyoleta huu msiba wote mkubwa juu ya watu hawa, ndivyo nitakavyoleta juu yao wema wote ambao ninasema kuwahusu.+ 43 Na hakika mashamba yatanunuliwa katika nchi hii+ ambayo ninyi mtakuwa mkisema: “Hiyo ni mahame yenye ukiwa+ yasiyo na mwanadamu wala mnyama wa kufugwa. Imetiwa mkononi mwa Wakaldayo.”’+
44 “‘Watu watanunua mashamba kwa pesa, na maandishi yatatiwa katika hati+ na muhuri kutiwa na mashahidi+ kuchukuliwa, katika nchi ya Benyamini,+ na katika maeneo yanayozunguka Yerusalemu,+ na katika majiji ya Yuda,+ na katika majiji ya eneo lenye milima, na katika majiji ya nchi tambarare ya chini,+ na katika majiji ya kusini,+ kwa sababu nitawarudisha mateka wao,’+ asema Yehova.”
33 Na neno la Yehova likamjia Yeremia mara ya pili, alipokuwa bado amefungiwa katika Ua wa Walinzi,+ likisema: 2 “Yehova, Mtengenezaji+ wa dunia, amesema hivi, Yehova Mfanyizaji+ wake ili kuifanya imara,+ Yehova ndilo jina lake,+ 3 ‘Niite, nami nitakujibu na kukuambia kwa utayari+ mambo makubwa na yasiyoweza kueleweka, usiyoyajua.’”+
4 “Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi kuhusu nyumba za jiji hili na kuhusu nyumba za wafalme wa Yuda ambazo zimebomolewa kwa sababu ya maboma ya kuzingira na kwa sababu ya upanga;+ 5 kuhusu wale wanaokuja kupiga vita juu ya Wakaldayo na kujaza mahali pengi kwa mizoga ya watu ambao nimewapiga na kuwaua katika hasira yangu na katika ghadhabu yangu,+ na kwa sababu ya wote ambao kutokana na ubaya wao nimeficha uso wangu kutoka kwenye jiji hili,+ 6 ‘Tazama, ninamletea yeye nguvu na afya;+ nami nitawaponya na kuwafunulia wingi wa amani na kweli.+ 7 Nami nitawarudisha mateka wa Yuda na mateka wa Israeli,+ nami nitawajenga kama pale mwanzoni.+ 8 Nami nitawatakasa kutoka katika kosa lao lote ambalo kupitia hilo wamenitendea dhambi,+ nami nitayasamehe makosa yao yote ambayo kupitia hayo wamenitendea dhambi na ambayo kupitia hayo wamenikosea.+ 9 Na hakika yeye atakuwa kwangu jina la furaha,+ sifa na uzuri kuelekea mataifa yote ya dunia ambayo yatasikia ule wema wote ambao ninawapa.+ Na hakika wao watakuwa na hofu+ na kufadhaika+ kwa sababu ya ule wema wote na kwa sababu ya ile amani yote ambayo ninampa.’”+
10 “Yehova amesema hivi, ‘Katika mahali hapa ambapo ninyi mtakuwa mkisema ni ukiwa usio na mwanadamu wala mnyama wa kufugwa, katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu ambazo ziko ukiwa+ pasipo na mwanadamu wala mkaaji wala mnyama wa kufugwa, bado itasikiwa+ 11 sauti ya furaha na sauti ya shangwe,+ sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi, sauti ya wale wanaosema: “Msifuni Yehova wa majeshi, kwa maana Yehova ni mwema;+ kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo!”’+
“‘Watakuwa wakileta toleo la shukrani katika nyumba ya Yehova,+ kwa maana nitawarudisha mateka wa nchi kama pale mwanzoni,’+ Yehova amesema.”
12 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Katika mahali hapa palipo ukiwa bila mwanadamu na hata mnyama wa kufugwa+ na katika majiji yake yote bado patakuwa na uwanja wa malisho wa wachungaji wanaolilaza kundi.’+
13 “‘Katika majiji ya eneo lenye milima, katika majiji ya nchi ya chini,+ na katika majiji ya kusini,+ na katika nchi ya Benyamini,+ na katika mazingira ya Yerusalemu,+ na katika majiji ya Yuda,+ bado makundi yatapita chini ya mikono ya mtu anayehesabu,’+ Yehova amesema.”
14 “‘Tazama! Siku zinakuja,’+ asema Yehova, ‘na hakika mimi nitalitimiza neno jema ambalo nimesema,+ kuihusu nyumba ya Israeli+ na kuihusu nyumba ya Yuda. 15 Katika siku hizo na katika wakati huo nitamchipushia Daudi chipukizi la uadilifu,+ na hakika yeye atatenda haki na uadilifu katika nchi.+ 16 Katika siku hizo Yuda ataokolewa+ na Yerusalemu litakaa katika usalama.+ Naye ataitwa hivi, Yehova Ni Uadilifu Wetu.’”+
17 “Kwa maana Yehova amesema hivi, ‘Hatakatiliwa mbali, kuhusu Daudi, mwanamume wa kuketi juu ya kiti cha ufalme cha nyumba ya Israeli.+ 18 Nao makuhani Walawi, hatakatiliwa mbali mwanamume kutoka mbele zangu wa kutoa toleo zima la kuteketezwa na kufukiza moshi pamoja na toleo la nafaka na kutoa dhabihu sikuzote.’”+
19 Na neno la Yehova likaendelea kumjia Yeremia, na kusema: 20 “Yehova amesema hivi, ‘Ikiwa ninyi mnaweza kulivunja agano langu la mchana na agano langu la usiku, ili mchana na usiku usije kwa wakati wake,+ 21 vivyo hivyo agano langu linaweza kuvunjwa pamoja na Daudi mtumishi wangu+ ili asiwe na mwana anayetawala akiwa mfalme juu ya kiti chake cha ufalme;+ pia pamoja na makuhani, Walawi, wahudumu wangu.+ 22 Kama jeshi la mbinguni lisivyoweza kuhesabiwa, wala mchanga wa bahari kupimwa,+ ndivyo nitakavyouzidisha uzao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaonihudumia.’”+
23 Na neno la Yehova likaendelea kumjia Yeremia, na kusema: 24 “Je, hujaona yale ambayo watu wa kikundi hiki wamesema, ‘Zile familia mbili ambazo Yehova amechagua,+ yeye pia atazikataa’? Nao wanaendelea kuwavunjia watu wangu heshima,+ hivi kwamba lisiendelee tena kuwa taifa mbele yao.
25 “Yehova amesema hivi, ‘Kama haingekuwa kweli kwamba nilikuwa nimeliweka agano langu la mchana na usiku,+ sheria za mbingu na dunia,+ 26 vivyo hivyo pia ningeukataa uzao wa Yakobo na wa Daudi mtumishi wangu,+ ili nisichukue kutoka kwa uzao wake watawala kuwa juu ya uzao wa Abrahamu, Isaka na Yakobo. Kwa maana nitawakusanya mateka+ wao nami nitawahurumia.’”+
34 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, wakati Nebukadreza mfalme wa Babiloni+ na jeshi lake lote+ na falme zote za dunia, mamlaka iliyo chini ya mkono wake,+ na vikundi vyote vya watu vilipokuwa vikipiga vita juu ya Yerusalemu na juu ya majiji yake yote,+ kusema:
2 “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Nenda, umwambie Sedekia mfalme wa Yuda,+ ndiyo, umwambie hivi: “Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninalitia jiji hili mkononi mwa mfalme wa Babiloni,+ naye ataliteketeza kwa moto.+ 3 Nawe mwenyewe hutaponyoka kutoka mkononi mwake, kwa sababu bila shaka utakamatwa na kutiwa mkononi mwake.+ Na macho yako yatayaona macho ya mfalme wa Babiloni,+ na kinywa chake kitasema na kinywa chako, nawe utaenda Babiloni.’ 4 Hata hivyo, lisikie neno la Yehova, Ee Sedekia mfalme wa Yuda,+ ‘Yehova amesema hivi kukuhusu wewe: “Hutakufa kwa upanga. 5 Utakufa kwa amani;+ nao watakufanyia mfukizo,+ kama ule mfukizo ambao waliwafanyia baba zako, wale wafalme wa zamani waliokutangulia,+ na ‘Aa, Ee bwana!’+ ndivyo watakavyosema wakikuombolezea,+ kwa maana ‘mimi mwenyewe nimesema neno hili,’ asema Yehova.”’”’”
6 Na Yeremia nabii akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda maneno hayo yote+ katika Yerusalemu, 7 wakati majeshi ya mfalme wa Babiloni yalipokuwa yakipiga vita juu ya Yerusalemu na juu ya majiji yote ya Yuda ambayo yalikuwa yamebaki,+ juu ya Lakishi+ na juu ya Azeka;+ kwa maana hayo, majiji yenye ngome,+ ndiyo yaliyobaki kati ya majiji ya Yuda.+
8 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano pamoja na watu wote waliokuwa Yerusalemu ili kuwatangazia uhuru,+ 9 kila mtu kumwachilia huru mtumishi wake wa kiume na kila mtu mjakazi wake, mwanamume Mwebrania+ na mwanamke Mwebrania, ili wasiwatumie kama watumishi, yaani, Myahudi, ambaye ni ndugu yake.+ 10 Basi wakuu+ wote wakatii, na watu wote waliokuwa wameingia katika agano la kwamba kila mtu amwachilie huru mtumishi wake wa kiume na kila mtu mjakazi wake, ili wasiwatumie tena kama watumishi, nao wakatii na kuwaachilia waende zao.+ 11 Lakini wakageuka+ baada ya hayo na kuanza kuwarudisha wale watumishi wa kiume na wajakazi ambao walikuwa wamewaachilia huru, nao wakawatiisha kama watumishi wa kiume na kama wajakazi.+ 12 Kwa hiyo neno la Yehova likamjia Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema:
13 “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Mimi mwenyewe nilifanya agano pamoja na mababu+ zenu katika siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri,+ kutoka katika nyumba ya watumishi,+ nikisema: 14 “Mwishoni mwa miaka saba mnapaswa kumwachilia kila mtu ndugu yake,+ Mwebrania,+ ambaye uliuziwa+ na ambaye amekutumikia miaka sita; nawe lazima umwachilie aende huru asiwe pamoja nawe.” Lakini mababu zenu hawakunisikiliza, wala hawakutega sikio lao.+ 15 Nanyi leo mnageuka na kufanya yaliyo sawa machoni pangu kwa kumtangazia uhuru kila mtu mwenzake, nanyi mnafanya agano mbele zangu+ ndani ya nyumba ambayo jina langu limeitwa juu yake.+ 16 Kisha mnageuka+ nyuma na kulitia unajisi jina langu+ na kumrudisha kila mtu mtumishi wake wa kiume na kila mtu mjakazi wake, ambaye mlimwachilia huru kwa kukubaliana na nafsi yao, nanyi mnawatiisha wawe watumishi wenu wa kiume na wajakazi wenu.’+
17 “Kwa hiyo Yehova amesema hivi, ‘Ninyi hamkunitii mimi kwa kuendelea kumtangazia uhuru+ kila mtu ndugu yake na kila mtu mwenzake. Tazama, mimi ninawatangazia ninyi uhuru,’+ asema Yehova, ‘upanga,+ tauni+ na njaa,+ na hakika mimi nitawatoa ninyi kwa ajili ya kutetemesha falme zote za dunia.+ 18 Nami nitawatoa wale watu wanaolivunja agano langu,+ kwa sababu hawakutenda yale maneno ya agano ambalo walifanya mbele zangu kwa yule ndama ambaye walimkata vipande viwili+ ili wapite katikati ya vipande vyake;+ 19 yaani, wakuu wa Yuda na wakuu wa Yerusalemu,+ maofisa wa makao ya mfalme na makuhani na watu wote wa nchi waliopita katikati ya vile vipande vya ndama— 20 ndiyo, nitawatia mkononi mwa adui zao na mkononi mwa wale wanaoitafuta nafsi yao;+ na maiti zao zitakuwa chakula kwa viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kwa wanyama wa dunia.+ 21 Na Sedekia mfalme wa Yuda+ na wakuu wake nitawatia mkononi mwa adui zao na mkononi mwa wale wanaoitafuta nafsi yao na mkononi mwa majeshi ya mfalme wa Babiloni+ ambayo yanaondoka kuwaacha ninyi.’+
22 “‘Tazama, mimi ninaamuru,’ asema Yehova, ‘na hakika mimi nitawarudisha katika jiji hili,+ nao watapiga vita juu yake na kuliteka na kuliteketeza kwa moto;+ na majiji ya Yuda nitayafanya kuwa mahame yenye ukiwa bila mkaaji.’”+
35 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova katika siku za Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, na kusema: 2 “Nenda katika nyumba ya Warekabu,+ na useme nao na kuwaleta katika nyumba ya Yehova, katika kimoja cha vyumba vya kulia chakula; nawe uwape divai wanywe.”
3 Kwa hiyo nikamchukua Yaazania mwana wa Yeremia mwana wa Habasinia na ndugu zake, na wanawe wote, na nyumba yote ya Warekabu, 4 nami nikawaleta katika nyumba ya Yehova, kwenye chumba cha kulia+ chakula cha wana wa Hanani mwana wa Igdalia, mtu wa Mungu wa kweli, kilichokuwa kando ya chumba cha kulia chakula cha wakuu ambacho kilikuwa juu ya chumba cha kulia chakula cha Maaseya mwana wa Shalumu+ mtunza-mlango. 5 Kisha nikatia mbele ya wana wa nyumba ya Warekabu vikombe vilivyojaa divai na bilauri na kuwaambia: “Kunyweni divai.”
6 Lakini wakasema: “Sisi hatutakunywa divai, kwa sababu Yonadabu mwana wa Rekabu,+ babu yetu, ndiye aliyeweka amri juu yetu, akisema, ‘Msinywe divai, ninyi wala wana wenu, mpaka wakati usio na kipimo.+ 7 Nanyi msijenge nyumba, wala msipande mbegu; wala msipande shamba la mizabibu, wala lisije kuwa lenu. Lakini mkae katika mahema siku zenu zote, ili mwendelee kuishi siku nyingi juu ya uso wa nchi ambapo mnakaa mkiwa wageni.’+ 8 Kwa hiyo tunaendelea kuitii sauti ya Yehonadabu mwana wa Rekabu babu yetu katika kila jambo ambalo alituamuru+ kwa kutokunywa divai yoyote siku zetu zote, sisi, wake zetu, wana wetu na binti zetu,+ 9 na kwa kutojenga nyumba za sisi kukaa ndani, hivi kwamba tusije tukawa na mizabibu yoyote wala shamba wala mbegu. 10 Nasi tunaendelea kukaa katika mahema na kutii na kufanya kulingana na yote ambayo Yonadabu+ babu yetu alituamuru.+ 11 Lakini ikawa kwamba Nebukadreza mfalme wa Babiloni alipokuja juu ya nchi+ tukaanza kusema, ‘Njooni, tuingie ndani ya Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Wakaldayo na kwa sababu ya jeshi la Wasiria, nasi tukae Yerusalemu.’”+
12 Na neno la Yehova likamjia Yeremia, na kusema: 13 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Nenda, uwaambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu: “Je, ninyi sikuzote hamkupokea himizo la kuyatii maneno yangu?”+ asema Yehova. 14 “Maneno ya Yehonadabu mwana wa Rekabu+ yametimizwa, ambayo aliwaamuru wanawe, wasinywe divai yoyote, nao hawajanywa yoyote mpaka leo hii, kwa sababu wameitii amri ya babu yao.+ Na kwa habari yangu, nimesema nanyi, nikiamka mapema na kusema,+ lakini hamkunitii mimi.+ 15 Nami niliendelea kutuma kwenu watumishi wangu wote manabii,+ nikiamka mapema na kuwatuma, na kusema, ‘Tafadhali rudini, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya,+ nanyi fanyeni matendo yenu kuwa mema,+ wala msiifuate miungu mingine ili kuitumikia.+ Na mwendelee kukaa katika nchi ambayo nimewapa ninyi na mababu zenu.’+ Lakini hamkutega sikio lenu, wala hamkunisikiliza.+ 16 Lakini wana wa Yehonadabu mwana wa Rekabu+ wameitenda amri ya babu yao ambayo aliwaamuru;+ lakini watu hawa, hawakunisikiliza mimi.”’”+
17 “Kwa hiyo Yehova, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta juu ya Yuda na juu ya wakaaji wote wa Yerusalemu ule msiba wote ambao nimesema juu yao,+ kwa sababu nimesema nao lakini hawakusikiliza, nami niliendelea kuwaita lakini hawakujibu.’”+
18 Na Yeremia akawaambia nyumba ya Warekabu: “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Kwa sababu mmeitii amri ya Yehonadabu+ babu yenu nanyi mnaendelea kuzishika amri zake zote na kufanya kulingana na yote ambayo aliwaamuru,+ 19 basi Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Hatakatiliwa mbali kutoka kwa Yonadabu mtu wa kusimama+ mbele zangu sikuzote.”’”+
36 Ikawa kwamba katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, neno hili likamjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema: 2 “Chukua kitabu cha kukunjwa,+ uandike ndani yake maneno+ yote ambayo nimekuambia juu ya Israeli na juu ya Yuda+ na juu ya mataifa yote,+ tangu siku niliyosema nawe, tangu siku za Yosia, mpaka leo hii.+ 3 Labda wale wa nyumba ya Yuda watausikiliza msiba wote ninaofikiria kuwatendea,+ kusudi warudi, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya,+ na ili mimi kwa kweli nisamehe kosa lao na dhambi yao.”+
4 Na Yeremia akamwita Baruku+ mwana wa Neria ili Baruku aandike kwa kinywa cha Yeremia maneno yote ya Yehova ambayo Yeye alikuwa amemwambia, katika kile kitabu cha kukunjwa.+ 5 Kisha Yeremia akamwamuru Baruku, akisema: “Nimefungiwa. Siwezi kuingia katika nyumba ya Yehova.+ 6 Na wewe mwenyewe utaingia na kusoma kwa sauti katika kitabu cha kukunjwa ambacho umeandika kupitia kinywa changu maneno ya Yehova+ masikioni mwa watu katika nyumba ya Yehova katika siku ya kufunga;+ na pia masikioni mwa Yuda wote wanaoingia kutoka katika majiji yao unapaswa kuyasoma kwa sauti.+ 7 Labda ombi lao la kutaka kibali litaanguka mbele za Yehova+ nao watarudi, kila mtu kutoka katika njia yake mbaya,+ kwa maana hasira na ghadhabu ni kuu ambazo Yehova amesema juu ya watu hawa.”+
8 Na Baruku+ mwana wa Neria akafanya kulingana na yote ambayo Yeremia nabii alikuwa amemwamuru, kusoma kwa sauti katika kile kitabu+ maneno ya Yehova kwenye nyumba ya Yehova.+
9 Sasa ikawa kwamba katika mwaka wa tano wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa tisa,+ watu wote katika Yerusalemu na watu wote waliokuwa wakiingia Yerusalemu kutoka katika majiji ya Yuda walitangaza kufunga mbele za Yehova.+ 10 Na Baruku akaanza kusoma kwa sauti katika kile kitabu maneno ya Yeremia kwenye nyumba ya Yehova, ndani ya chumba cha kulia chakula+ cha Gemaria+ mwana wa Shafani+ mwandikaji,+ katika ua wa juu, kwenye mwingilio wa lango jipya la nyumba ya Yehova,+ masikioni mwa watu wote.
11 Na Mikaya mwana wa Gemaria mwana wa Shafani+ akayasikia maneno yote ya Yehova katika kile kitabu. 12 Ndipo akashuka kwenye nyumba ya mfalme, kwenda katika chumba cha kulia chakula cha mwandishi, na, tazama! hapo ndipo wakuu wote walikuwa wameketi, Elishama+ mwandishi na Delaya+ mwana wa Shemaya na Elnathani+ mwana wa Akbori+ na Gemaria+ mwana wa Shafani+ na Sedekia mwana wa Hanania na wakuu wengine wote. 13 Na Mikaya+ akawaambia maneno yote ambayo alikuwa amesikia wakati Baruku aliposoma kwa sauti katika kile kitabu masikioni mwa watu.+
14 Ndipo wakuu wote wakamtuma Yehudi+ mwana wa Nethania mwana wa Shelemia mwana wa Kushi kwa Baruku,+ na kusema: “Kile kitabu cha kukunjwa ambacho ulisoma kwa sauti masikioni mwa watu—kichukue mkononi mwako uje.” Basi Baruku mwana wa Neria akakichukua kile kitabu mkononi mwake, akaingia kwao.+ 15 Kisha wakamwambia: “Tafadhali keti, ukisome kwa sauti masikioni mwetu.” Kwa hiyo Baruku+ akasoma kwa sauti masikioni mwao.
16 Sasa ikawa kwamba mara tu walipoyasikia yale maneno yote, wakaangaliana kwa hofu; nao wakamwambia Baruku: “Bila shaka tutamwambia mfalme maneno haya yote.”+ 17 Nao wakamuuliza Baruku, wakisema: “Tafadhali tuambie, Uliandikaje maneno haya yote kutoka kinywani mwake?”+ 18 Ndipo Baruku akawaambia: “Aliendelea kunitangazia maneno haya yote kutoka kinywani mwake, nami nilikuwa nikiandika kwa wino katika kitabu.”+ 19 Mwishowe wakuu wakamwambia Baruku: “Nenda, jifiche, wewe pamoja na Yeremia, ili kwamba mtu yeyote asijue mahali mlipo.”+
20 Kisha wakaingia kwa mfalme, kwenye ua,+ nao wakakiweka kile kitabu cha kukunjwa katika chumba cha kulia chakula+ cha Elishama+ mwandishi; nao wakaanza kusema maneno yale yote masikioni mwa mfalme.
21 Kwa hiyo mfalme akamtuma Yehudi+ kukichukua kile kitabu cha kukunjwa. Basi akakichukua kutoka katika chumba cha kulia chakula cha Elishama+ mwandishi.+ Na Yehudi akaanza kukisoma kwa sauti masikioni mwa mfalme na masikioni mwa wakuu wote waliokuwa wamesimama kando ya mfalme. 22 Na mfalme alikuwa ameketi katika nyumba ya majira ya baridi kali,+ katika mwezi wa tisa,+ na jiko la makaa+ lilikuwa linawaka mbele yake. 23 Kisha ikawa kwamba mara tu Yehudi alipokuwa amesoma safu za kurasa tatu au nne, akakipasua kwa kisu cha mwandishi, na pia akakitupa katika moto uliokuwa katika lile jiko mpaka kitabu chote kilipoishia ndani ya ule moto uliokuwa katika jiko.+ 24 Nao hawakuingiwa na hofu yoyote;+ na mfalme wala watumishi wake wote, waliokuwa wakisikiliza maneno hayo yote, hawakurarua mavazi yao.+ 25 Na hata Elnathani+ na Delaya+ na Gemaria+ wakamsihi mfalme asiteketeze kile kitabu cha kukunjwa, lakini hakuwasikiliza.+ 26 Na zaidi ya hayo, mfalme akawaamuru Yerahmeeli mwana wa mfalme na Seraya mwana wa Azrieli na Shelemia mwana wa Abdeeli waende kumleta Baruku mwandishi na Yeremia nabii.+ Lakini Yehova akaendelea kuwaficha.+
27 Na neno la Yehova likamjia Yeremia tena baada ya mfalme kukiteketeza kile kitabu cha kukunjwa pamoja na yale maneno ambayo Baruku+ alikuwa ameandika kutoka katika kinywa cha Yeremia,+ na kusema: 28 “Chukua tena kitabu cha kukunjwa, kingine, nawe uandike juu yake yale maneno yote ya kwanza yaliyokuwa juu ya kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda aliteketeza.+ 29 Nawe unapaswa kusema hivi juu ya Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Yehova amesema hivi: “Wewe mwenyewe umekiteketeza hiki kitabu cha kukunjwa,+ ukisema, ‘Kwa nini umeandika juu yake,+ ukisema: “Mfalme wa Babiloni atakuja bila shaka na hakika ataiharibu nchi hii na kumkomesha mwanadamu na mnyama kutoka ndani yake”?’+ 30 Kwa hiyo Yehova amesema hivi juu ya Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hatakuwa na mtu yeyote anayeketi juu ya kiti cha ufalme cha Daudi,+ na maiti yake itakuwa kitu kilichotupwa nje+ kwenye joto wakati wa mchana na kwenye baridi kali wakati wa usiku. 31 Nami nitamtoza hesabu yeye+ na uzao wake na watumishi wake kosa lao,+ nami nitaleta juu yao na juu ya wakaaji wa Yerusalemu na juu ya watu wa Yuda ule msiba wote ambao nimesema juu yao,+ nao hawakusikiliza.’”’”+
32 Na Yeremia akachukua kitabu kingine cha kukunjwa, akampa Baruku mwana wa Neria, mwandishi,+ ambaye aliandika juu yake kutoka kinywani+ mwa Yeremia maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa ameteketeza motoni;+ na maneno mengine mengi kama hayo yakaongezwa kwenye hayo.
37 Na Mfalme Sedekia+ mwana wa Yosia+ akaanza kutawala mahali pa Konia+ mwana wa Yehoyakimu,+ ambaye Nebukadreza mfalme wa Babiloni alimfanya kuwa mfalme katika nchi ya Yuda.+ 2 Na yeye na watumishi wake na watu wa nchi hawakuyasikiliza maneno ya Yehova+ ambayo alisema kupitia Yeremia nabii.+
3 Mfalme Sedekia akamtuma Yehukali+ mwana wa Shelemia na Sefania+ mwana wa Maaseya+ kuhani kwa Yeremia nabii, na kusema: “Tafadhali, sali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wetu.”+ 4 Na Yeremia alikuwa akiingia ndani na kutoka nje katikati ya watu,+ kwa sababu hawakuwa wamemtia kizuizini. 5 Na kulikuwa na jeshi la Farao lililotoka Misri;+ na Wakaldayo waliokuwa wakizingira Yerusalemu wakasikia habari kuwahusu. Basi wakaondoka mbele ya Yerusalemu.+ 6 Kisha neno la Yehova likamjia Yeremia nabii, na kusema: 7 “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Mwambieni hivi mfalme wa Yuda, yeye aliyewatuma kwangu kuniuliza habari:+ “Tazama! Jeshi la Farao ambalo linawajia ninyi kwa kusudi la kuwapa msaada litarudi nchini kwao, Misri.+ 8 Na hakika Wakaldayo watarudi tena na kupiga vita juu ya jiji hili na kuliteka na kuliteketeza kwa moto.”+ 9 Yehova amesema hivi: “Msizidanganye nafsi zenu,+ mkisema, ‘Bila shaka Wakaldayo wataenda zao waondoke juu yetu,’ kwa sababu hawataenda zao. 10 Kwa maana ikiwa mngelipiga na kuliua jeshi lote la Wakaldayo wanaopigana nanyi+ na kati yao wabaki watu waliochomwa,+ kila mmoja wao angesimama katika hema lake na kuliteketeza jiji hili kwa moto.”’”
11 Na ikawa kwamba wakati jeshi la Wakaldayo lilipokuwa limejiondoa juu ya Yerusalemu+ kwa sababu ya jeshi la Farao,+ 12 Yeremia akaanza kuondoka Yerusalemu ili kwenda katika nchi ya Benyamini+ na kupata fungu lake kutoka huko katikati ya watu. 13 Basi ikawa kwamba alipokuwa katika Lango la Benyamini,+ yule ofisa aliyekuwa mwangalizi ambaye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, alikuwa hapo. Mara moja akamshika Yeremia nabii, akisema: “Unakimbia kwenda kwa Wakaldayo!” 14 Lakini Yeremia akasema: “Ni uwongo!+ Mimi sikimbii kwenda kwa Wakaldayo.” Lakini yeye hakumsikiliza. Basi Iriya akaendelea kumshika Yeremia na kumleta kwa wakuu. 15 Na wakuu+ wakaanza kumkasirikia Yeremia,+ nao wakampiga+ na kumtia katika nyumba ya pingu,+ katika nyumba ya Yehonathani+ mwandishi, kwa maana walikuwa wameifanya hiyo kuwa kizuizi.+ 16 Yeremia alipokuja ndani ya nyumba ya tangi la maji+ na ndani ya vyumba vyenye ngome, ndipo Yeremia akaendelea kukaa humo siku nyingi.
17 Na Mfalme Sedekia akatuma watu kumchukua, na mfalme akaanza kumuuliza maswali katika nyumba yake mahali pa maficho.+ Naye akaendelea kusema: “Je, liko neno lolote kutoka kwa Yehova?” Yeremia akasema: “Liko!” Naye akaendelea kusema: “Utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babiloni!”+
18 Kisha Yeremia akamwambia Mfalme Sedekia: “Ni kwa njia gani nimetenda dhambi juu yako na juu ya watumishi wako na juu ya kikundi hiki cha watu,+ hivi kwamba mmenitia kizuizini? 19 Wako wapi, sasa, manabii wenu waliowatolea unabii, wakisema, ‘Mfalme wa Babiloni hatakuja juu yenu na juu ya nchi hii’?+ 20 Na sasa, sikiliza, tafadhali, Ee bwana wangu mfalme. Tafadhali, ombi langu la kibali+ na lifike mbele yako, nawe usinirudishe katika nyumba ya Yehonathani+ mwandishi, nisije nikafa humo.”+ 21 Ndipo Mfalme Sedekia akatoa amri, kisha wakamtia Yeremia kifungoni katika Ua wa Walinzi;+ wakampa mkate wa mviringo kila siku kutoka kwenye barabara ya waokaji,+ mpaka mkate wote ulipokwisha jijini.+ Na Yeremia akaendelea kukaa katika Ua wa Walinzi.+
38 Na Shefatia mwana wa Matani na Gedalia mwana wa Pashuri na Yukali+ mwana wa Shelemia na Pashuri mwana wa Malkiya+ wakayasikia maneno ambayo Yeremia alikuwa akiwaambia watu wote,+ akisema: 2 “Yehova amesema hivi, ‘Yule anayeendelea kukaa ndani ya jiji hili ndiye atakayekufa kwa upanga,+ kwa njaa+ na kwa tauni.+ Lakini yule atakayetoka nje kuwaendea Wakaldayo ndiye atakayeendelea kuishi na ndiye ambaye hakika nafsi yake itakuwa kama nyara kwake na ikiwa hai.’+ 3 Yehova amesema hivi, ‘Bila shaka jiji hili litatiwa mkononi mwa jeshi la mfalme wa Babiloni, naye hakika ataliteka.’”+
4 Na wakuu wakaanza kumwambia mfalme: “Tafadhali, acha mtu huyu auawe,+ kwa maana hivyo ndivyo anavyoidhoofisha mikono ya watu wa vita ambao wamebaki ndani ya jiji hili na mikono ya watu wote, kwa kuwaambia maneno haya.+ Kwa maana mtu huyu hatafuti amani ya watu hawa bali msiba.” 5 Kwa hiyo Mfalme Sedekia akasema: “Tazama! Yuko mikononi mwenu. Kwa maana hakuna jambo lolote ambalo mfalme anaweza kuwazuia ninyi.”+
6 Nao wakamchukua Yeremia na kumtupa ndani ya tangi la maji la Malkiya+ mwana wa mfalme, lililokuwa katika Ua wa Walinzi.+ Hivyo wakamshusha Yeremia ndani kwa kamba. Basi hapakuwa na maji ndani ya lile tangi, bali matope; na Yeremia akaanza kuzama katika yale matope.+
7 Na Ebed-meleki Mwethiopia,+ mtu aliyekuwa towashi na aliyekuwa katika nyumba ya mfalme, akasikia kwamba walikuwa wamemtia Yeremia ndani ya tangi; na mfalme alikuwa ameketi katika Lango la Benyamini.+ 8 Basi Ebed-meleki akatoka katika nyumba ya mfalme na kumwambia mfalme, akisema: 9 “Ee bwana wangu mfalme, watu hawa wametenda mabaya kwa yote ambayo wamemtendea Yeremia nabii, ambaye wamemtupa ndani ya tangi la maji, hivi kwamba atakufa+ hapo alipo kwa sababu ya njaa.+ Kwa maana hakuna mkate tena jijini.”
10 Ndipo mfalme akamwamuru Ebed-meleki Mwethiopia, akisema: “Chukua watu 30 chini ya usimamizi wako kutoka mahali hapa, nawe umwondoe Yeremia nabii katika lile tangi kabla hajafa.”+ 11 Kwa hiyo Ebed-meleki akawachukua wale watu chini ya usimamizi wake, akaingia katika nyumba ya mfalme mpaka chini ya hazina+ na kuchukua kutoka hapo vitambaa vizee-vizee na vipande vizee-vizee vya nguo na kuvishusha kwa Yeremia ndani ya lile tangi+ kwa kamba. 12 Ndipo Ebed-meleki Mwethiopia akamwambia Yeremia: “Tafadhali, tia hivi vitambaa vizee-vizee na vipande vizee-vizee vya nguo katika makwapa yako chini ya kamba.” Basi Yeremia akafanya hivyo.+ 13 Mwishowe wakamvuta Yeremia nje kwa zile kamba na kumtoa ndani ya lile tangi. Na Yeremia akaendelea kukaa katika Ua wa Walinzi.+
14 Na Mfalme Sedekia akatuma watu na kumchukua Yeremia nabii+ kwenye mlango wa tatu,+ ulio katika nyumba ya Yehova,+ kisha mfalme akamwambia Yeremia: “Ninakuuliza jambo fulani. Usinifiche jambo lolote.”+ 15 Ndipo Yeremia akamwambia Sedekia: “Ikiwa nitakuambia, je, hutaniua bila shaka? Na ikiwa nitakushauri, wewe hutanisikiliza.”+ 16 Kwa hiyo Mfalme Sedekia akamwapia Yeremia mahali pa maficho, akisema: “Kama anavyoishi Yehova, ambaye ametufanyia sisi nafsi+ hii, mimi sitakuua, wala sitakutia mkononi mwa watu hawa wanaoitafuta nafsi yako.”+
17 Basi Yeremia akamwambia Sedekia: “Yehova, Mungu wa majeshi,+ Mungu wa Israeli,+ amesema hivi, ‘Bila shaka ukitoka nje kwenda kwa wakuu wa mfalme wa Babiloni,+ hakika nafsi yako itaendelea kuishi na jiji hili halitateketezwa kwa moto, na wewe mwenyewe na nyumba yako hakika mtaendelea kuishi.+ 18 Lakini ikiwa hutaenda nje kwa wakuu wa mfalme wa Babiloni, jiji hili pia lazima litatiwa mkononi mwa Wakaldayo, nao kwa kweli wataliteketeza kwa moto,+ nawe hutaponyoka mkononi mwao.’”+
19 Kisha Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia: “Ninawaogopa Wayahudi ambao wamekimbia kwenda kwa Wakaldayo,+ wasije wakanitia katika mikono yao nao wakanitendea vibaya.”+ 20 Lakini Yeremia akasema: “Hawatakutia mkononi mwao. Tafadhali, itii sauti ya Yehova kwa habari ya mambo ninayokuambia, na itakuwa vema kwako,+ na nafsi yako itaendelea kuishi. 21 Lakini ikiwa unakataa kwenda nje,+ hili ndilo jambo ambalo Yehova amenionyesha: 22 Na, tazama! wanawake wote ambao wameachwa katika nyumba ya mfalme wa Yuda+ wanatolewa nje kwa wakuu wa mfalme wa Babiloni,+ nao wanasema,
‘Watu wanaoishi kwa amani pamoja nawe wamekushawishi+ na kukushinda.+
Wamefanya mguu wako uzame chini katika matope; wamerudi nyuma kwenda upande ule mwingine.’+
23 Nao wanawatoa nje wake zako wote na wana wako wote na kuwapeleka kwa Wakaldayo, nawe mwenyewe hutaponyoka mkononi mwao,+ lakini utakamatwa kwa mkono wa mfalme wa Babiloni, na kwa sababu yako jiji hili litateketezwa kwa moto.”+
24 Na Sedekia akamwambia Yeremia: “Mtu yeyote asijue mambo haya, ili usife. 25 Na ikiwa wakuu+ watasikia kwamba nimesema nawe nao kwa kweli waje kwako na kukuambia, ‘Tafadhali, tuambie, Ulimwambia nini mfalme? Usitufiche jambo lolote, nasi hatutakuua. Na mfalme alikuambia habari gani?’ 26 wewe pia utawaambia, ‘Nilikuwa nikitoa mbele ya mfalme ombi langu la kutaka kibali, kwamba asinirudishe katika nyumba ya Yehonathani+ ili nisife humo.’”
27 Baadaye wakuu wote wakamjia Yeremia na kuanza kumuuliza maswali. Yeye naye akawaambia kulingana na maneno hayo yote ambayo mfalme alikuwa ameamuru.+ Kwa hiyo wakanyamaza mbele yake, kwa maana habari hiyo haikusikiwa. 28 Na Yeremia akaendelea kukaa katika Ua wa Walinzi+ mpaka siku ambayo Yerusalemu lilitekwa.+ Na hilo likatukia wakati tu ambapo Yerusalemu lilitekwa.+
39 Katika mwaka wa tisa wa Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi,+ Nebukadreza mfalme wa Babiloni na jeshi lake lote alikuja Yerusalemu na kuanza kulizingira.+
2 Katika mwaka wa kumi na moja wa Sedekia, katika mwezi wa nne, katika siku ya tisa ya mwezi huo, jiji likapenywa.+ 3 Na wakuu wote wa mfalme wa Babiloni wakaingia na kuketi katika Lango la Kati,+ yaani, Nergal-shareza, Samgar-nebo, Sarsekimu, Rabsarisi, Nergal-shareza yule Rabmagi na wakuu wengine wote wa mfalme wa Babiloni.
4 Sasa ikawa kwamba mara tu Sedekia mfalme wa Yuda na watu wote wa vita walipowaona, wakaanza kukimbia+ na kwenda nje ya jiji wakati wa usiku kupitia njia ya bustani ya mfalme,+ kupitia lile lango lililo katikati ya zile kuta mbili; nao wakaendelea kutoka nje kupitia njia ya Araba.+ 5 Na jeshi la Wakaldayo likawafuatilia,+ nao wakamfikia Sedekia katika nchi tambarare ya jangwa la Yeriko.+ Kisha wakamchukua na kumleta kwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi+ ili atangaze hukumu juu yake.+ 6 Na mfalme wa Babiloni akawaua+ wana wa Sedekia katika Ribla mbele ya macho yake,+ na mfalme wa Babiloni akawaua watu wote wenye vyeo wa Yuda.+ 7 Naye akayapofusha macho ya Sedekia,+ kisha akamfunga kwa pingu za shaba, ili ampeleke Babiloni.
8 Na Wakaldayo wakateketeza kwa moto nyumba ya mfalme na nyumba za watu,+ nao wakazibomoa kuta za Yerusalemu.+ 9 Na Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi+ akawapeleka uhamishoni kule Babiloni+ wale watu wengine walioachwa ndani ya jiji, na wale waliokimbia ili kujiunga naye, na watu wengine walioachwa.
10 Na baadhi ya watu, watu wa hali ya chini ambao hawakuwa na chochote hata kidogo, Nebuzaradani mkuu wa walinzi akawaacha wabaki katika nchi ya Yuda;+ naye akawapa mashamba ya mizabibu na utumishi wa lazima katika siku hiyo.+
11 Zaidi ya hayo, Nebukadreza mfalme wa Babiloni akatoa amri kumhusu Yeremia kupitia Nebuzaradani mkuu wa walinzi, akisema: 12 “Mchukue, nawe umwangalie sana, wala usimtendee jambo lolote baya.+ Lakini vile atakavyokuambia, wewe mtendee vivyo hivyo.”+
13 Kwa hiyo Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi na Nebushazbani yule Rabsarisi, na Nergal-shareza yule Rabmagi na wakuu wote wa mfalme wakawatuma watu; 14 naam, waliwatuma watu na kumchukua Yeremia kutoka katika Ua wa Walinzi+ na kumtia mkononi mwa Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ ili amlete katika nyumba yake, ili akae katikati ya watu.
15 Na neno la Yehova likamjia Yeremia alipokuwa amefungiwa katika Ua wa Walinzi,+ na kusema: 16 “Nenda, umwambie Ebed-meleki+ Mwethiopia, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Tazama, ninayatimiza maneno yangu juu ya jiji hili kuwe msiba wala si mema,+ nayo hakika yatatimia mbele yako katika siku ile.”’+
17 “‘Nami nitakukomboa wewe katika siku ile,’+ asema Yehova, ‘nawe hutatiwa mkononi mwa watu ambao unawaogopa.’+
18 “‘Kwa maana bila shaka nitakuokoa, nawe hutaanguka kwa upanga; na hakika nafsi yako itakuwa kama nyara kwako,+ kwa sababu umenitegemea mimi,’+ asema Yehova.”
40 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova baada ya Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi kumtoa katika Rama,+ alipomchukua huku akiwa amefungwa kwa pingu za mkononi katikati ya wahamishwa wote wa Yerusalemu na wa Yuda, ambao walikuwa wakipelekwa uhamishoni katika Babiloni.+ 2 Ndipo yule mkuu wa walinzi akamchukua Yeremia na kumwambia: “Yehova Mungu wako alitangaza msiba huu juu ya mahali hapa,+ 3 ili Yehova autimize na kufanya jinsi ambavyo amesema, kwa sababu ninyi mumemtendea Yehova dhambi wala hamkuitii sauti yake. Na jambo hili limewapata ninyi.+ 4 Na sasa, tazama! Leo nimekufungua pingu zilizokuwa mikononi mwako. Ikiwa ni vema machoni pako uje pamoja nami kule Babiloni, njoo, nami nitakuangalia sana.+ Lakini ikiwa ni vibaya machoni pako kwenda pamoja nami kule Babiloni, acha. Angalia! Nchi nzima iko mbele yako. Kokote ambako ni kwema na sawa machoni pako kwenda, nenda huko.”+
5 Na alipokuwa bado hajaamua kurudi, Nebuzaradani akasema: “Rudi kwa Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ ambaye mfalme wa Babiloni amemweka juu ya majiji ya Yuda, nawe ukae pamoja naye katikati ya watu; au popote ambapo ni sawa machoni pako kwenda, nenda.”+
Ndipo mkuu wa walinzi akampa posho ya chakula na zawadi na kumwacha aende zake.+ 6 Kwa hiyo Yeremia akaja kwa Gedalia+ mwana wa Ahikamu kule Mispa+ na kuanza kukaa pamoja naye katikati ya watu waliobaki katika nchi.
7 Baadaye wakuu wote wa majeshi waliokuwa uwanjani,+ wao pamoja na watu wao, wakasikia kwamba mfalme wa Babiloni amemweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu ya nchi na kwamba alikuwa amemweka juu ya wanawake na watoto wadogo na baadhi ya watu wa hali ya chini wa nchi, ambao hawakuwa wamepelekwa uhamishoni katika Babiloni.+ 8 Basi wakamwendea Gedalia kule Mispa, Ishmaeli+ mwana wa Nethania na Yohanani+ na Yonathani, wana wa Karea, na Seraya mwana wa Tanhumethi na wana wa Efai Mnetofa+ na Yezania+ mwana wa yule Mmaakathi,+ wao pamoja na watu wao.+ 9 Na Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani+ akawaapia+ wao pamoja na watu wao, akisema: “Msiogope kuwatumikia Wakaldayo. Endeleeni kukaa katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babiloni, na itakuwa vema kwenu.+ 10 Na kwa habari yangu, tazama, ninakaa katika Mispa,+ ili kusimama mbele ya Wakaldayo watakaokuja kwetu. Nanyi kusanyeni divai+ na matunda ya wakati wa kiangazi na mafuta na mviweke katika vyombo vyenu na mkae katika majiji yenu ambayo mmeyateka.”
11 Na Wayahudi wote waliokuwa katika Moabu na katikati ya wana wa Amoni na katika Edomu na wale waliokuwa katika nchi nyingine zote,+ wao pia wakasikia kwamba mfalme wa Babiloni amewapa Yuda mabaki na kwamba alikuwa ameweka juu yao Gedalia+ mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani. 12 Na Wayahudi wote wakaanza kurudi kutoka mahali pote ambapo walikuwa wametawanywa, nao wakaendelea kuja nchini Yuda kwa Gedalia kule Mispa.+ Nao wakakusanya divai na matunda ya wakati wa kiangazi kwa wingi sana.
13 Naye Yohanani+ mwana wa Karea+ na wakuu wote wa majeshi waliokuwa uwanjani,+ wakamjia Gedalia kule Mispa. 14 Nao wakamwambia: “Je, hujui kabisa kwamba Baalisi mfalme wa wana wa Amoni,+ amemtuma Ishmaeli+ mwana wa Nethania+ ili akupige nafsi yako akuue?” Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu hakuwaamini.+
15 Na Yohanani+ mwana wa Karea mwenyewe akamwambia Gedalia, mahali pa maficho katika Mispa: “Nataka kwenda, sasa, nimpige na kumuua Ishmaeli mwana wa Nethania, kwa kuwa hakuna mtu atakayejua.+ Kwa nini akupige nafsi akuue, na kwa nini watu wote wa Yuda wanaokusanyika kwako watawanywe na mabaki ya Yuda yaangamie?”+ 16 Lakini Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ akamwambia Yohanani mwana wa Karea: “Usifanye jambo hili, kwa maana unasema uwongo kumhusu Ishmaeli.”+
41 Kwa hiyo ikawa kwamba katika mwezi wa saba, Ishmaeli+ mwana wa Nethania mwana wa Elishama+ wa uzao wa kifalme+ na aliye wa wakuu wa mfalme na watu wengine kumi pamoja naye+ wakamjia Gedalia mwana wa Ahikamu kule Mispa.+ Nao hapo wakaanza kula mkate pamoja kule Mispa.+ 2 Ndipo Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye wakasimama, wakampiga kwa upanga Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani.+ Kwa hiyo akamuua mtu ambaye mfalme wa Babiloni alikuwa amemweka juu ya nchi.+ 3 Na Wayahudi wote waliokuwa pamoja naye, yaani, pamoja na Gedalia, kule Mispa, na Wakaldayo waliokuwa hapo, yaani, watu wa vita, Ishmaeli akawapiga na kuwaua.
4 Na ikawa kwamba katika siku ya pili baada ya kuuawa kwa Gedalia, wakati hakuna mtu yeyote aliyejua habari hiyo,+ 5 wakaja watu kutoka Shekemu,+ kutoka Shilo+ na kutoka Samaria,+ watu 80 huku ndevu zao zikiwa zimenyolewa+ na mavazi yao yakiwa yameraruliwa nao wakiwa wamejitia mikato,+ na mkononi mwao walikuwa na toleo la nafaka na ubani+ ili wavilete katika nyumba ya Yehova. 6 Basi Ishmaeli mwana wa Nethania akatoka Mispa ili kuwapokea, akilia huku akitembea.+ Na ikawa kwamba mara tu alipokutana nao, akawaambia: “Njooni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.” 7 Lakini ikatukia kwamba mara tu walipokuja katikati ya jiji, Ishmaeli mwana wa Nethania akawaua na kuwatupa ndani ya tangi la maji, yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye.+
8 Lakini palikuwa na watu kumi kati yao ambao walimwambia Ishmaeli mara moja: “Usituue, kwa maana sisi tuna hazina zilizofichwa shambani, ngano na shayiri na mafuta na asali.”+ Kwa hiyo akajiepusha, naye hakuwaua katikati ya ndugu zao. 9 Sasa lile tangi la maji ambamo Ishmaeli+ aliitupa mizoga yote ya wale watu ambao aliwaua lilikuwa tangi kubwa, ambalo Mfalme Asa alitengeneza kwa sababu ya Baasha mfalme wa Israeli.+ Hilo ndilo Ishmaeli mwana wa Nethania alilijaza wale waliouawa.
10 Kisha Ishmaeli akawachukua mateka mabaki yote ya watu waliokuwa kule Mispa,+ binti za mfalme+ na watu wote waliokuwa wamebaki Mispa,+ ambao Nebuzaradani mkuu wa walinzi alikuwa ameweka chini ya ulinzi wa Gedalia mwana wa Ahikamu.+ Kwa hiyo Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka akaenda ili avuke kwenda kwa wana wa Amoni.+
11 Baadaye Yohanani+ mwana wa Karea na wakuu wote wa majeshi+ waliokuwa pamoja naye wakasikia ubaya wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ametenda. 12 Basi wakawachukua watu wote na kwenda kupiga vita juu ya Ishmaeli mwana wa Nethania, wakampata kando ya yale maji mengi yaliyokuwa katika Gibeoni.+
13 Kisha ikawa kwamba mara tu watu wote waliokuwa pamoja na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa majeshi waliokuwa pamoja naye, wakaanza kushangilia. 14 Na watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka kutoka Mispa+ wakageuka, wakarudi na kumwendea Yohanani mwana wa Karea. 15 Naye Ishmaeli mwana wa Nethania akakimbia+ pamoja na watu wanane kutoka mbele ya Yohanani, ili aende kwa wana wa Amoni.
16 Sasa Yohanani+ mwana wa Karea na wale wakuu wote wa majeshi waliokuwa pamoja naye wakachukua yale mabaki yote ya watu ambao walikuwa wamewarudisha kutoka kwa Ishmaeli mwana wa Nethania, kutoka Mispa, baada ya yeye kumpiga na kumuua Gedalia+ mwana wa Ahikamu, watu hodari, wanaume wa vita, na wake na watoto wadogo na maofisa wa makao ya mfalme, ambao alirudisha kutoka Gibeoni. 17 Basi wakaenda na kuanza kufanya makao katika mahali pa kukaa pa Kimhamu palipokuwa kando ya Bethlehemu,+ ili wazidi kwenda na kuingia Misri,+ 18 kwa sababu ya Wakaldayo;+ kwa maana walikuwa wameogopa kwa sababu yao,+ kwa kuwa Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amempiga na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu,+ ambaye mfalme wa Babiloni alikuwa amemweka juu ya nchi.+
42 Kisha wakuu wote wa majeshi na Yohanani+ mwana wa Karea na Yezania+ mwana wa Hoshaya+ na watu wote, kuanzia aliye mdogo zaidi mpaka aliye mkubwa zaidi, wakakaribia 2 na kumwambia Yeremia nabii: “Tafadhali, ombi letu la kutaka kibali na lifike mbele yako, nawe usali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wako,+ kwa ajili ya mabaki hawa wote, kwa maana tumeachwa mabaki, wachache kati ya wengi,+ kama macho yako yanavyotuona. 3 Yehova Mungu wako na atuambie njia tunayopaswa kuitembea na jambo tunalopaswa kulifanya.”+
4 Ndipo Yeremia nabii akawaambia: “Nimesikia. Tazama, ninasali kwa Yehova Mungu wenu kulingana na maneno yenu;+ na hakika itakuwa kwamba kila neno ambalo Yehova atawajibu ninyi mimi nitawaambia.+ Sitazuilia neno lolote kutoka kwenu.”+
5 Nao wakamwambia Yeremia: “Yehova na awe shahidi wa kweli na mwaminifu juu yetu+ ikiwa hatutafanya sawasawa kulingana na kila neno ambalo Yehova Mungu wako atakutuma kwetu.+ 6 Kama ni jema au ni baya, sauti ya Yehova Mungu wetu ambaye tunakutuma kwake ndiyo tutakayoitii, ili iwe vema kwetu kwa sababu tunaitii sauti ya Yehova Mungu wetu.”+
7 Sasa ikawa kwamba mwishoni mwa siku kumi neno la Yehova likamjia Yeremia.+ 8 Kwa hiyo akamwita Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa majeshi waliokuwa pamoja naye na watu wote, kuanzia aliye mdogo zaidi mpaka aliye mkubwa zaidi;+ 9 naye akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli, ambaye mlinituma kwake ili kufanya ombi lenu la kutaka kibali lifike mbele zake,+ amesema hivi, 10 ‘Ikiwa bila shaka mtaendelea kukaa katika nchi hii,+ mimi pia nitawajenga ninyi wala sitawabomoa, nami nitawapanda ninyi wala sitawang’oa;+ kwa maana hakika nitaujuta ule msiba ambao nimewaletea ninyi.+ 11 Msiwe na hofu kwa sababu ya mfalme wa Babiloni, ambaye mnamwogopa.’+
“‘Msiwe na hofu kwa sababu yake,’+ asema Yehova, ‘kwa maana mimi niko pamoja nanyi, ili kuwaokoa na kuwakomboa kutoka mkononi mwake.+ 12 Nami nitawapa ninyi rehema, na hakika yeye atakuwa na rehema juu yenu na kuwarudisha kwenye nchi yenu.+
13 “‘Lakini ikiwa mtasema: “Hapana; hatutakaa katika nchi hii!” ili kutoitii sauti ya Yehova Mungu wenu,+ 14 mkisema: “Hapana, bali tutaenda katika nchi ya Misri,+ ambapo hatutaona vita wala hatutaisikia sauti ya baragumu wala kushinda njaa kwa kukosa mkate; na hapo ndipo tutakapokaa”;+ 15 kwa hiyo hata sasa sikieni neno la Yehova, enyi mabaki ya Yuda. Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Hakika ninyi mkikaza nyuso zenu kuingia Misri nanyi kwa kweli mwingie ili kukaa huko mkiwa wageni,+ 16 itatukia pia kwamba ule upanga ambao mnaogopa utawafikia huko katika nchi ya Misri,+ na ile njaa ambayo mnaiogopa itawafuatilia kwa ukaribu mpaka Misri;+ nanyi mtakufa huko.+ 17 Na itakuwa kwamba watu wote ambao wamekaza nyuso zao kuingia Misri ili kukaa huko wakiwa wageni ndio watakaokufa kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni;+ nao hawatakuwa na mwenye kuokoka wala mwenye kuponyoka, kwa sababu ya ule msiba ambao ninaleta juu yao.”’+
18 “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Kama hasira yangu na ghadhabu yangu zilivyomwagwa juu ya wakaaji wa Yerusalemu,+ ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu kwa sababu ya ninyi kuingia Misri, na hakika mtakuwa laana na kitu cha kushangaza na tukano na shutuma,+ nanyi hamtapaona mahali hapa tena.’+
19 “Yehova amesema dhidi yenu, enyi mabaki ya Yuda. Msiingie Misri.+ Mnapaswa kujua hakika kwamba nimetoa ushahidi juu yenu leo,+ 20 kwamba mmetenda kosa juu ya nafsi zenu;+ kwa maana ninyi wenyewe mmenituma kwa Yehova Mungu wenu, mkisema, ‘Sali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wetu; nawe utuambie kulingana na kila jambo ambalo Yehova Mungu wetu atasema, nasi hakika tutafanya.’+ 21 Nami ninawaambia ninyi leo, lakini hakika hamtaitii sauti ya Yehova Mungu wenu wala jambo lolote ambalo amenituma nalo kwenu.+ 22 Na sasa jueni hakika kwamba kwa upanga,+ kwa njaa na kwa tauni mtakufa katika mahali pale panapowapendeza ninyi kuingia ili kukaa mkiwa wageni.”+
43 Basi ikawa kwamba mara tu Yeremia alipomaliza kuwaambia watu wote maneno yote ya Yehova Mungu wao ambayo Yehova Mungu wao alikuwa amemtuma nayo kwao, maneno hayo yote,+ 2 Azaria mwana wa Hoshaya+ na Yohanani+ mwana wa Karea na watu wote wenye kimbelembele+ wakamwambia Yeremia: “Ni uwongo ambao wewe unasema.+ Yehova Mungu wetu hakukutuma, kusema, ‘Msiingie Misri kukaa humo mkiwa wageni.’+ 3 Bali Baruku+ mwana wa Neria anakuchochea juu yetu ili kututia mkononi mwa Wakaldayo, ili watuue au watupeleke uhamishoni Babiloni.”+
4 Na Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa majeshi na watu wote hawakuitii sauti ya Yehova,+ ili waendelee kukaa katika nchi ya Yuda.+ 5 Basi Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa majeshi wakachukua mabaki wote wa Yuda waliokuwa wamerudi kutoka katika mataifa yote ambako walikuwa wametawanywa, ili kukaa kwa muda katika nchi ya Yuda,+ 6 wanaume na wake na watoto wadogo na binti za mfalme+ na kila nafsi ambayo Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi alikuwa ameacha wakae pamoja na Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ na Yeremia nabii na Baruku+ mwana wa Neria. 7 Na mwishowe wakaingia katika nchi ya Misri,+ kwa maana hawakuitii sauti ya Yehova; nao mwishowe wakafika mpaka Tahpanhesi.+
8 Ndipo neno la Yehova likamjia Yeremia katika Tahpanhesi, na kusema: 9 “Chukua mkononi mwako mawe makubwa, uyafiche katika saruji kwenye ngazi ya matofali iliyo kwenye mlango wa nyumba ya Farao katika Tahpanhesi mbele ya macho ya wanaume Wayahudi.+ 10 Nawe uwaambie, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Tazama, ninatuma watu na kumchukua Nebukadreza mfalme wa Babiloni,+ mtumishi wangu,+ nami nitakiweka kiti chake cha ufalme juu ya mawe haya ambayo nimeyaficha, na hakika yeye atanyoosha hema lake la fahari juu yake. 11 Naye ataingia na kuipiga nchi ya Misri.+ Yeyote aliyekusudiwa mapigo yenye kufisha atapigwa kwa mapigo yenye kufisha, na yeyote aliyekusudiwa kwenda utekwani ataenda utekwani, na yeyote aliyekusudiwa upanga atapigwa kwa upanga.+ 12 Nami nitawasha moto katika nyumba za miungu ya Misri;+ naye hakika ataiteketeza na kuipeleka mateka na kujifunga yeye mwenyewe katika nchi ya Misri, kama mchungaji anavyojifunga katika vazi lake,+ na kwa kweli ataondoka huko kwa amani. 13 Naye hakika atavunja vipande-vipande nguzo za Beth-shemeshi, lililo katika nchi ya Misri; na nyumba za miungu ya Misri ataziteketeza kwa moto.”’”
44 Neno lililomjia Yeremia kwa ajili ya Wayahudi wote waliokuwa wakikaa katika nchi ya Misri,+ wale waliokuwa wakikaa kule Migdoli+ na Tahpanhesi+ na Nofu+ na katika nchi ya Pathrosi,+ likisema: 2 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Ninyi wenyewe mmeona msiba wote ambao nimeleta juu ya Yerusalemu+ na juu ya majiji yote ya Yuda, na, tazama, hayo leo ni mahali palipoharibiwa, na ndani yake hamna mkaaji.+ 3 Ni kwa sababu ya ubaya wao ambao walifanya ili kunitia uchungu kwa kwenda kufukiza moshi wa dhabihu+ na kutoa utumishi kwa miungu mingine ambayo wao hawakuijua, wala ninyi wala mababu zenu.+ 4 Nami niliendelea kuwatuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiamka mapema na kuwatuma,+ nikisema: “Tafadhali, msifanye chukizo la aina hii ambalo nimelichukia.”+ 5 Lakini hawakusikiliza,+ wala hawakutega sikio lao ili kurudi kutoka katika ubaya wao kwa kutoifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu.+ 6 Kwa hiyo ghadhabu yangu, na hasira yangu, ilimwagwa nayo ikateketeza katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu;+ nazo zikawa mahali palipoharibiwa, mahame yenye ukiwa, kama ilivyo leo hii.’+
7 “Na sasa Yehova, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Kwa nini mnaleta msiba mkubwa juu ya nafsi+ zenu, ili mumkatilie mbali kutoka kwenu mwanamume na mwanamke, mtoto mdogo na yule anayenyonya,+ kutoka katikati ya Yuda, hivi kwamba hamjiachii mabaki; 8 kwa kunitia uchungu mimi kwa kazi za mikono yenu kwa kuifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu+ katika nchi ya Misri, ambako mnaingia ili kukaa mkiwa wageni; kwa kusudi la kusababisha kukatiliwa mbali kwenu na kwa kusudi la ninyi kuwa laana na shutuma kati ya mataifa yote ya dunia?+ 9 Je, mmeyasahau matendo mabaya ya mababu+ zenu na matendo mabaya ya wafalme wa Yuda+ na matendo mabaya ya wake zao+ na matendo mabaya yenu wenyewe na matendo mabaya ya wake zenu,+ ambayo wametenda katika nchi ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu? 10 Na mpaka leo hii hawakuona kuwa wamepondwa,+ wala hawakuogopa,+ wala hawakutembea katika sheria+ yangu na katika kanuni zangu ambazo niliweka mbele yenu na mbele ya mababu zenu.’+
11 “Kwa hiyo Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Tazama, ninakaza uso wangu juu yenu kwa ajili ya msiba na kwa ajili ya kukatilia mbali Yuda yote.+ 12 Nami nitachukua mabaki wa Yuda ambao walikaza nyuso zao ili kuingia katika nchi ya Misri wakae humo wakiwa wageni,+ na hakika wote watamalizika katika nchi ya Misri.+ Wataanguka kwa upanga; nao watamalizika kwa njaa,+ kuanzia aliye mdogo zaidi mpaka aliye mkubwa zaidi; watakufa kwa upanga na kwa njaa. Nao watakuwa laana, kitu cha kushangaza na tukano na shutuma.+ 13 Nami nitatoza hesabu juu ya wale wanaokaa katika nchi ya Misri, kama nilivyotoza hesabu juu ya Yerusalemu, kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni.+ 14 Na hakutakuwa na yeyote mwenye kuponyoka wala mwenye kuokoka kwa mabaki wa Yuda wanaoingia ili kukaa humo wakiwa wageni, katika nchi ya Misri,+ wa kurudi katika nchi ya Yuda ambayo wanaitamani kwa nafsi yao ili warudi kukaa humo;+ kwa maana hawatarudi, ila tu watu fulani walioponyoka.’”
15 Na wanaume wote waliojua kwamba wake zao walikuwa wakiifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu,+ na wake wote waliokuwa wanasimama wakiwa kutaniko kubwa, na watu wote waliokuwa wakikaa katika nchi ya Misri,+ katika Pathrosi,+ wakamjibu Yeremia, wakisema: 16 “Kuhusu lile neno ambalo umetuambia katika jina la Yehova, sisi hatutakusikiliza;+ 17 lakini hakika tutafanya kila neno ambalo limetoka katika kinywa chetu,+ ili kumfukizia ‘malkia wa mbingu’+ moshi wa dhabihu na kummiminia matoleo ya kinywaji,+ kama sisi wenyewe+ na mababu+ zetu, wafalme+ wetu na wakuu wetu tulivyofanya katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu, wakati tuliposhiba mkate na kuwa na hali njema, nasi hatukuona msiba wowote kamwe.+ 18 Na tangu tulipoacha kumfukizia ‘malkia wa mbingu’+ moshi wa dhabihu na kummiminia matoleo ya kinywaji tumekosa kila kitu, nasi tumemalizika kwa upanga na kwa njaa.+
19 “Pia, wakati tulipokuwa tukimfukizia ‘malkia wa mbingu’+ moshi wa dhabihu nasi tukawa na mwelekeo wa kummiminia matoleo ya kinywaji,+ je, tulimtolea keki za dhabihu bila kuwauliza waume zetu, ili kutengeneza sanamu yake, na kummiminia matoleo ya kinywaji?”+
20 Naye Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wake na watu wote, waliokuwa wakimjibu neno, akisema: 21 “Kuhusu ule moshi wa dhabihu ambao mlifukiza katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu,+ ninyi+ na mababu+ zenu, wafalme+ wenu na wakuu+ wenu na watu wa nchi, je, Yehova hakukumbuka mambo hayo nayo yakaingia moyoni mwake?+ 22 Mwishowe Yehova hakuweza kuvumilia kwa sababu ya ubaya wa matendo yenu, kwa sababu ya machukizo ambayo mlikuwa mmefanya,+ na hivyo nchi yenu ikawa mahali palipoharibiwa na kitu cha kushangaza na laana, bila mkaaji, kama ilivyo leo hii.+ 23 Kwa sababu mlifukiza moshi wa dhabihu,+ mkamtendea dhambi Yehova,+ hamkuitii sauti ya Yehova+ nanyi hamkutembea katika sheria yake+ na katika kanuni zake na katika vikumbusho vyake, ndiyo sababu msiba huu umewapata ninyi kama ilivyo leo hii.”+
24 Na Yeremia akaendelea kuwaambia watu wote na wanawake wote: “Sikieni neno la Yehova, Yuda wote mlio katika nchi ya Misri.+ 25 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Kuhusu ninyi wanaume na wake zenu,+ ninyi wanawake pia mnasema kwa vinywa vyenu, (na kwa mikono yenu mmetimiza,) mkisema: “Bila shaka tutatimiza nadhiri zetu ambazo tumeweka,+ ili kumfukizia ‘malkia wa mbingu’+ moshi wa dhabihu na kummiminia matoleo ya kinywaji.”+ Ninyi wanawake bila shaka mtazitimiza nadhiri zenu, nanyi bila shaka mtazifanya nadhiri zenu.’
26 “Kwa hiyo sikieni neno la Yehova, Yuda wote mnaokaa katika nchi ya Misri,+ ‘ “Tazama, mimi mwenyewe nimeapa kwa jina langu kuu,”+ Yehova amesema, “kwamba jina langu halitakuwa tena kitu cha kuitwa kwa kinywa cha mtu yeyote wa Yuda,+ akisema, ‘Kama anavyoishi Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova!’+ katika nchi yote ya Misri. 27 Tazama, ninakaa macho kuwaelekea wao kwa ajili ya msiba wala si kwa ajili ya mema;+ na watu wote wa Yuda walio katika nchi ya Misri hakika watamalizika kwa upanga na kwa njaa, mpaka watakapokoma kuwapo.+ 28 Nao wale wanaookoka upanga, watarudi kutoka katika nchi ya Misri kwenda katika nchi ya Yuda, hesabu yao wakiwa ni wachache;+ na wale wote wa mabaki ya Yuda, wanaoingia katika nchi ya Misri kukaa humo wakiwa wageni, watajua hakika ni neno la nani linalotimia, lile linalotoka kwangu au lile linalotoka kwao.”’”+
29 “‘Na hii ndiyo ishara kwenu,’+ asema Yehova, ‘kwamba ninakaza fikira zangu juu yenu katika mahali hapa, ili mpate kujua kwamba maneno yangu bila shaka yatatimia juu yenu kwa ajili ya msiba:+ 30 Yehova amesema hivi: “Tazama, ninamtia Farao Hofra mfalme wa Misri,+ mkononi mwa adui zake na mkononi mwa wale wanaoitafuta nafsi yake,+ kama nilivyomtia Sedekia mfalme wa Yuda mkononi mwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni, adui yake na yeye anayeitafuta nafsi yake.”’”+
45 Neno ambalo Yeremia nabii alimwambia Baruku+ mwana wa Neria alipoandika katika kitabu maneno haya kutoka kinywani mwa Yeremia+ katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, akisema:
2 “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi kukuhusu wewe, Ee Baruku, 3 ‘Umesema: “Ole wangu,+ sasa, kwa maana Yehova ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu! Nimechoka kwa sababu ya kuugua kwangu, nami sikupata mahali pa kupumzika.”’+
4 “Wewe mwambie hivi, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama! Kile ambacho nimekijenga ninakibomoa, na kile ambacho nimekipanda ninaking’oa, ndiyo, nchi yote.+ 5 Na wewe unaendelea kujitafutia makuu.+ Usiendelee kuyatafuta.”’+
“‘Kwa maana, tazama, ninaleta msiba juu ya wote wenye mwili,’+ asema Yehova, ‘nami nitakupa wewe nafsi yako kuwa nyara katika mahali pote utakapoenda.’”+
46 Hili ndilo neno la Yehova lililomjia Yeremia nabii kuhusu mataifa:+ 2 Kwa ajili ya Misri,+ kuhusu jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri,+ aliyekuwa kando ya mto Efrati kule Karkemishi,+ ambaye Nebukadreza mfalme wa Babiloni alimshinda katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda: 3 “Pangeni ngao ndogo na ngao kubwa, na mkaribie ili kupigana.+ 4 Fungeni farasi lijamu, na mpande, enyi wapanda-farasi, na msimame na kofia. Sugueni mikuki. Vaeni mavazi ya chuma.+
5 “‘Kwa nini nimewaona wakiwa wameingiwa na hofu? Wanarudi nyuma, na wanaume wao wenye nguvu wamevunjwa vipande-vipande; nao hakika wamekimbia, wala hawakugeuka.+ Kuna hofu pande zote,’+ asema Yehova. 6 ‘Mtu mwepesi asijaribu kukimbia, na mwanamume mwenye nguvu asijaribu kuponyoka.+ Juu kaskazini+ kando ya ukingo wa mto Efrati wamejikwaa na kuanguka.’+
7 “Ni nani huyu anayepanda juu kama Mto Nile, kama mito ambayo maji yake yanajirusha?+ 8 Misri inakuja kama Mto Nile,+ na kama mito maji yanajirusha.+ Nayo inasema, ‘Nitapanda. Nitaifunika dunia. Nitaliangamiza kwa urahisi jiji na wale wanaokaa ndani yake.’+ 9 Pandeni, enyi farasi; na kwenda kiwazimu, enyi magari! Wanaume wenye nguvu na waende, Kushi+ na Putu,+ wanaochukua ngao, na Ludimu,+ wanaoshika na kukanyaga upinde.
10 “Na siku ile ni ya Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, siku yake ya kisasi ya kujilipizia kisasi juu ya adui zake.+ Na hakika upanga utakula na kushiba na kujijaza damu yao, kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi, ana dhabihu+ katika nchi ya kaskazini kando ya mto Efrati.+
11 “Panda mpaka Gileadi uchukue zeri,+ Ee bikira, binti ya Misri.+ Umezidisha njia za kuponya bure tu. Hakuna matibabu kwa ajili yako.+ 12 Mataifa yamesikia aibu+ yako na kilio chako kimeijaza nchi.+ Kwa maana wamejikwaa, mwanamume mwenye nguvu juu ya mwanamume mwenye nguvu.+ Wameanguka chini pamoja, wote wawili.”
13 Neno ambalo Yehova alimwambia Yeremia nabii kuhusu kuja kwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni ili kuipiga nchi ya Misri:+ 14 “Lihubiri jambo hilo katika Misri, na mlitangaze kule Migdoli,+ na mlitangaze kule Nofu+ na Tahpanhesi.+ Semeni, ‘Simama, pia ujifanyie matayarisho,+ kwa maana hakika upanga utakula kukuzunguka pande zote.+ 15 Kwa nini watu wako wenye nguvu wamefagiliwa mbali?+ Hawakusimama, kwa maana Yehova mwenyewe amewasukumia mbali.+ 16 Hesabu kubwa wanajikwaa. Kwa kweli pia wanaanguka. Nao wanaendelea kuambiana: “Simameni, na acheni sisi turudi kwa watu wetu na kwa nchi ya jamaa zetu kwa sababu ya upanga unaoonea.”’ 17 Huko wametangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni kelele tupu.+ Ameachilia wakati wa sherehe upite.’+
18 “‘Kama ninavyoishi,’ asema Mfalme, ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi,+ ‘kama Tabori+ kati ya milima na kama Karmeli+ kando ya bahari yeye ataingia. 19 Jifanyie mzigo kwa ajili ya uhamisho,+ Ee mwanamke mkaaji, binti+ ya Misri. Kwa maana Nofu+ litakuwa kitu cha kushangaza na kwa kweli litawashwa moto, hivi kwamba lisiwe na mkaaji.+ 20 Misri ni ndama-jike mrembo sana. Kutoka upande wa kaskazini hakika mbu atakuja juu yake.+ 21 Na zaidi, askari-jeshi wake waliokodiwa walio katikati yake ni kama ndama waliononeshwa.+ Lakini wao pia wamerudi nyuma;+ wamekimbia pamoja. Hawakusimama.+ Kwa maana ile siku ya msiba wao imekuja juu yao, wakati wa kuwakazia fikira.’+
22 “‘Sauti yake ni kama ile ya nyoka ambaye anaenda;+ kwa maana watu wataenda wakiwa na nguvu, nao wataingia kwake wakiwa na mashoka, kama wale wanaokusanya kuni. 23 Hakika wataukata msitu wake,’+ asema Yehova, ‘kwa maana haukuweza kupenywa. Kwa maana wamekuwa wengi sana kuliko nzige,+ nao hawana hesabu. 24 Hakika binti+ ya Misri ataona aibu. Kwa kweli atatiwa mkononi mwa watu wa kaskazini.’+
25 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema, ‘Tazama, ninakaza fikira zangu juu ya Amoni+ kutoka No+ na juu ya Farao na juu ya Misri na juu ya miungu+ yake na juu ya wafalme+ wake, juu ya Farao na juu ya wale wote wanaomtegemea.’+
26 “‘Nami nitawatia mkononi mwa wale wanaoitafuta nafsi yao na mkononi mwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni+ na mkononi mwa watumishi wake; na baadaye watu watakaa ndani yake kama katika siku za zamani za kale,’+ asema Yehova.
27 “‘Nawe usiogope, Ee mtumishi wangu Yakobo, wala usiingiwe na hofu, Ee Israeli.+ Kwa maana, tazama, ninakuokoa kutoka mbali na uzao wako kutoka katika nchi yako ya utekwani.+ Na hakika Yakobo atarudi, hatakuwa na usumbufu naye atastarehe na kusiwe na yeyote wa kumtetemesha.+ 28 Nawe usiogope, Ee mtumishi wangu Yakobo,’ asema Yehova, ‘kwa maana mimi niko pamoja nawe.+ Kwa maana nitafanya maangamizi kati ya mataifa yote ambako nimekutawanya huko,+ lakini wewe sitakuangamiza.+ Hata hivyo, nitakutia adabu kwa kiwango kinachofaa,+ nami sitakuacha kamwe bila kukuadhibu.’”+
47 Hili ndilo lililokuwa neno la Yehova kwa Yeremia nabii kuwahusu Wafilisti+ kabla ya Farao kupiga Gaza.+ 2 Yehova amesema hivi:
“Tazama! Maji yanakuja+ kutoka kaskazini+ nayo yamekuwa mto unaofurika. Nayo yataifurikisha nchi na vyote vilivyomo, jiji na wale wanaokaa humo.+ Na hakika watu watalia, na kila mtu anayekaa katika nchi atapiga mayowe.+ 3 Kutokana na sauti ya kukanyaga kwa kwato za farasi-dume+ zake, kutokana na kuvuma kwa magari yake ya vita,+ machafuko ya magurudumu yake,+ akina baba hawatawageukia wana, kwa sababu ya kulegea kwa mikono yao, 4 kwa sababu ya siku ambayo inakuja kuwapora Wafilisti+ wote, kumkatilia mbali kutoka Tiro+ na kutoka Sidoni+ kila mwenye kuokoka aliyekuwa akisaidia.+ Kwa maana Yehova anawapora Wafilisti,+ ambao ni mabaki kutoka kisiwa cha Kaftori.+ 5 Upara+ utakuja Gaza.+ Ashkeloni+ limenyamazishwa. Ee mabaki ya nchi yao tambarare ya chini, utaendelea kujitia mikato mpaka wakati gani?+
6 “Aha, upanga wa Yehova!+ Je, mpaka wakati gani hutanyamaza kimya? Ingizwa ndani ya ala+ yako. Tulia na kunyamaza kimya.
7 “Huo unaweza kukaaje kimya, wakati Yehova ameupa amri? Huo ni kwa Ashkeloni na kwa pwani ya bahari.+ Hapo ndipo amechagua uwepo.”
48 Kuhusu Moabu,+ Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi:+ “Ole wake Nebo,+ kwa maana ameporwa! Kiriathaimu+ ameona aibu, ametekwa. Kilele kilicho salama kimeona aibu na kutiwa hofu.+ 2 Moabu+ haina sifa yoyote tena. Katika Heshboni+ wamefikiria msiba juu yake: ‘Njooni, tumkatilie mbali asiwe taifa.’+
“Wewe pia, Ee Madmeni, unapaswa kunyamaza kimya. Upanga unatembea nyuma yako. 3 Kuna sauti ya kilio kutoka Horonaimu,+ uporaji na mvunjiko mkubwa. 4 Moabu amevunjwa.+ Watoto wake wamefanya kilio kisikiwe. 5 Kwa maana katika njia ya kwenda mpaka Luhithi+ mtu anapanda akilia—kuna kilio. Kwa maana katika njia ya kushuka kutoka Horonaimu kuna kilio chenye kutaabisha juu ya ule mvunjiko+ ambao watu wamesikia.
6 “Kimbieni; ponyeni nafsi zenu,+ nanyi mnapaswa kuwa kama mberoshi nyikani.+ 7 Kwa sababu tegemeo lako liko katika kazi zako na katika hazina zako, wewe pia utatekwa.+ Na hakika Kemoshi+ ataenda uhamishoni,+ makuhani wake na wakuu wake wakati uleule.+ 8 Na mporaji atakuja juu ya kila jiji,+ na hakutakuwa na jiji lolote linaloweza kuponyoka.+ Na nchi tambarare ya chini hakika itaangamia na nchi tambarare itaharibiwa, jambo ambalo Yehova amesema.
9 “Mpeni Moabu alama ya barabara, kwa maana ataenda wakati wa mabomoko;+ na majiji yake yatakuwa kitu tu cha kushangaza, bila kuwa na mtu anayekaa humo.+
10 “Alaaniwe yule mtu anayetimiza utume wa Yehova kwa uzembe;+ na alaaniwe yule mtu anayeuzuilia upanga wake usimwage damu!
11 “Wamoabu wamekuwa wakistarehe tangu ujana wao,+ nao wanaendelea bila usumbufu juu ya machicha+ yao. Nao hawajamiminwa kutoka chombo kimoja ndani ya chombo kingine, nao hawajaenda uhamishoni. Ndiyo sababu ladha yao imesimama tuli ndani yao, na harufu yao haijabadilika.
12 “‘Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nami nitatuma kwao watu wanaoinamisha chombo, nao hakika watawainamisha;+ nao watamwaga kilicho ndani ya vyombo vyao, na mitungi yao mikubwa wataivunja vipande-vipande. 13 Na Wamoabu wataona aibu kwa sababu ya Kemoshi,+ kama wale wa nyumba ya Israeli walivyoona aibu kwa sababu ya Betheli, uhakika wao.+ 14 Kwa nini mna ujasiri wa kusema: “Sisi ni wanaume wenye uwezo na wanaume wenye nguvu+ kwa ajili ya vita”?’
15 “‘Moabu ameporwa, na mtu amepanda juu ya majiji yake.+ Na vijana wao walio bora zaidi wameshuka kwenda kuuawa,’+ asema Mfalme, ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi.+
16 “Maafa juu ya Wamoabu yako karibu kuja, na msiba wao unaharakisha sana.+ 17 Wale wote wanaowazunguka pande zote watawasikitikia, wale wote wanaolijua jina lao.+ Ninyi semeni, ‘Jinsi fimbo ya nguvu imevunjwa, fimbo ya urembo!’+
18 “Shuka chini kutoka katika utukufu, na kuketi katika kiu, Ee mwanamke mkaaji, binti+ ya Diboni;+ kwa maana mporaji wa Moabu amekuja juu yako. Kwa kweli yeye atapaharibu mahali pako penye ngome.+
19 “Simama tuli na kuiangalia njia, Ee mwanamke mkaaji wa Aroeri.+ Muulize yeye anayekimbia na yeye anayeponyoka. Sema, ‘Kumetokea nini?’+ 20 Moabu ameona aibu, kwa maana ameingiwa na hofu.+ Piga mayowe na kupaaza kilio. Tangazeni katika Arnoni+ kwamba Moabu ameporwa. 21 Na hukumu imekuja katika nchi iliyo tambarare,+ katika Holoni na katika Yahazi+ na juu ya Mefaathi,+ 22 na juu ya Diboni+ na juu ya Nebo+ na juu ya Beth-diblathaimu, 23 na juu ya Kiriathaimu+ na juu ya Beth-gamuli na juu ya Beth-meoni+ 24 na juu ya Keriothi+ na juu ya Bosra+ na juu ya majiji yote ya nchi ya Moabu, yale yaliyo mbali na yale yaliyo karibu.
25 “‘Pembe ya Moabu imekatwa,+ na mkono wake umevunjwa,’+ asema Yehova. 26 ‘Mlewesheni,+ kwa maana ameonyesha majivuno sana juu ya Yehova mwenyewe;+ na Moabu amegaagaa katika matapiko+ yake, naye amekuwa kitu cha kudhihakiwa, yeye mwenyewe.
27 “‘Na je, kwako Israeli hakuwa tu kitu cha kudhihakiwa?+ Au, je, alipatikana kati ya wezi wa waziwazi?+ Kwa maana ulikuwa ukijitikisa kichwa kila mara uliposema juu yake.
28 “‘Yaacheni majiji, mkae juu ya mwamba,+ ninyi wakaaji wa Moabu, na muwe kama njiwa ambaye hujenga kiota chake katika maeneo ya kinywa cha shimo.’”+
29 “Tumesikia habari za kiburi cha Moabu+—ana majivuno sana—habari za ustahiki wake na za kiburi chake na za majivuno yake na za kuinuka kwa moyo wake.”+
30 “‘Mimi mwenyewe nimeijua ghadhabu yake,’ asema Yehova, ‘na hivyo sivyo itakavyokuwa; maneno yake matupu+—kwa kweli hawatafanya kwa njia hiyo.+ 31 Ndiyo sababu nitapiga mayowe juu ya Moabu, nami nitapaaza kilio+ kwa ajili ya Moabu yote. Mtu atawaombolezea watu wa Kir-heresi.+
32 “‘Nitakulilia kwa kilio kinachoshinda kile kilio kwa ajili ya Yazeri,+ Ee mzabibu wa Sibma.+ Machipukizi yako yenye matawi mengi yameivuka bahari. Mpaka baharini—mpaka Yazeri+—yamefika. Mporaji ameanguka+ juu ya matunda yako ya wakati wa kiangazi na juu ya ukusanyaji wako wa zabibu.+ 33 Na kushangilia na shangwe zimeondolewa katika shamba la matunda na katika nchi ya Moabu.+ Nami nimeikomesha divai kutoka katika mashinikizo ya divai.+ Hakuna yeyote atakayezikanyaga kwa kupaaza sauti. Huko kupaaza sauti hakutakuwa kupaaza sauti.’”+
34 “‘Kutoka kwenye kilio katika Heshboni+ mpaka Eleale,+ mpaka Yahazi+ wamepaaza sauti yao,+ kutoka Soari+ mpaka Horonaimu,+ mpaka Eglath-shelishiya;+ kwa maana hata maji ya Nimrimu+ yatakuwa ukiwa mtupu. 35 Nami nitamkomesha katika Moabu,’ asema Yehova, ‘mtu anayeleta toleo mahali pa juu na mtu anayemfukizia mungu wake moshi wa dhabihu.+ 36 Ndiyo sababu moyo wangu mwenyewe utapiga-piga kwa ajili ya Moabu, kama tu filimbi;+ na kwa ajili ya watu wa Kir-heresi+ moyo wangu utapiga-piga, kama filimbi. Ndiyo sababu wingi ambao ametokeza hakika utaangamia.+ 37 Kwa maana kuna upara+ juu ya vichwa vyote, na ndevu zote zimekatwa.+ Kuna mikato+ juu ya mikono yote, na juu ya viuno kuna nguo za magunia!’”+
38 “‘Juu ya paa zote za Moabu na katika viwanja vyake vya watu wote—vyote—kuna maombolezo;+ kwa maana nimemvunja Moabu kama tu chombo ambacho hakipendezi,’+ asema Yehova. 39 ‘Jinsi ameingiwa na hofu! Pigeni mayowe! Jinsi Moabu ameugeuza mgongo! Ameona aibu.+ Na Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa na kitu chenye kuogopesha kwa wale wote wanaomzunguka pande zote.’”
40 “Kwa maana Yehova amesema hivi, ‘Tazama! Kama tai anayerukia mawindo,+ ndivyo mtu atakavyonyoosha mabawa yake juu ya Moabu.+ 41 Kwa kweli miji itatekwa, na mahali pake palipo imara hakika patakamatwa. Na moyo wa wanaume wenye nguvu wa Moabu lazima siku hiyo utakuwa kama moyo wa mke ambaye ana taabu ya kuzaa mtoto.’”+
42 “‘Na hakika Moabu ataangamizwa asiwe kikundi cha watu,+ kwa maana ameonyesha majivuno+ sana juu ya Yehova. 43 Hofu na shimo na mtego ziko juu yako, Ee mkaaji wa Moabu,’+ asema Yehova. 44 ‘Yeyote anayekimbia kwa sababu ya hofu ataanguka ndani ya shimo; na yeyote anayetoka ndani ya shimo atakamatwa katika mtego.’+
“‘Kwa maana nitaleta juu yake, juu ya Moabu, mwaka wa kuwakazia fikira,’+ asema Yehova. 45 ‘Katika kivuli cha Heshboni wale wanaokimbia wamesimama tuli bila nguvu. Kwa maana hakika moto utatoka katika Heshboni,+ na mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni;+ nao utateketeza vipaji vya nyuso za Moabu na utosi wa kichwa cha wana wa ghasia.’+
46 “‘Ole wako, Ee Moabu!+ Watu wa Kemoshi+ wameangamia. Kwa maana wana wako wamechukuliwa mateka na binti zako wakawa mateka. 47 Nami nitawakusanya mateka wa Moabu siku za mwisho,’+ asema Yehova. ‘Hukumu juu ya Moabu imefikia hapa.’”+
49 Kuhusu wana wa Amoni,+ Yehova amesema hivi: “Je, Israeli hana wana, au, je, yeye hana mrithi? Kwa nini Malkamu+ amemiliki Gadi,+ na watu wake mwenyewe wamekaa katika majiji ya Israeli?”+
2 “‘Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nami nitafanya king’ora cha vita+ kisikiwe juu ya Raba+ la wana wa Amoni; na hakika yeye atakuwa kilima cha mahame yenye ukiwa,+ na miji yake ya kandokando+ itawashwa katika moto.’+
“‘Na Israeli atawamiliki wale wanaommiliki,’+ Yehova amesema.
3 “‘Piga mayowe,+ Ee Heshboni,+ kwa maana Ai ameporwa! Paazeni kilio, enyi miji ya kandokando ya Raba. Jifungeni nguo za magunia.+ Ombolezeni, na mwende huku na huku kati ya mazizi ya mawe, kwa maana Malkamu ataenda uhamishoni,+ makuhani wake na wakuu wake, wote pamoja.+ 4 Kwa nini unajigamba kuhusu nchi tambarare ya chini,+ nchi yako tambarare ya chini inayotiririka, Ee binti usiye mwaminifu, wewe unayezitegemea hazina zako,+ ukisema: “Ni nani atakayenijia?”’”+
5 “‘Tazama, ninaleta juu yako jambo lenye kutia hofu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi, ‘kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka pande zote. Na hakika ninyi mtatawanywa, kila mmoja upande wake mwenyewe,+ na hapatakuwa na yeyote anayewakusanya pamoja wale wanaokimbia.’”
6 “‘Lakini baadaye nitawakusanya mateka wa wana wa Amoni,’+ asema Yehova.”
7 Kuhusu Edomu, Yehova wa majeshi amesema hivi: “Je, hakuna tena hekima+ yoyote katika Temani?+ Je, shauri limeangamia kutoka kwa wale walio na uelewaji? Je, hekima yao imeoza?+ 8 Kimbieni!+ Geukeni mkimbie! Shukeni ndani sana ili mkae,+ enyi wakaaji wa Dedani!+ Kwa maana yale maafa ya Edomu nitayaleta juu yake, wakati ambao nitakaza fikira zangu juu yake.+ 9 Ikiwa wakusanya-zabibu wangeingia kwako, je, hawangeacha masalio fulani? Ikiwa wezi wangekuja wakati wa usiku, hakika wangefanya uharibifu kiasi kile tu ambacho wangetosheka nacho.+ 10 Lakini mimi, nitamvua Esau awe uchi.+ Nitafunua mahali pake pa maficho,+ na mtu hataweza kujificha.+ Hakika uzao wake na ndugu zake na jirani zake wataporwa,+ naye hatakuwapo.+ 11 Waache wavulana wako wasio na baba.+ Mimi mwenyewe nitawahifadhi hai, na wajane wako watanitegemea mimi.”+
12 Kwa maana Yehova amesema hivi: “Tazama! Ingawa si desturi yao kukinywa kikombe, bila shaka watakinywa.+ Na wewe mwenyewe, je, utaachwa kabisa bila kuadhibiwa? Hutaachwa bila kuadhibiwa, kwa maana utakunywa bila shaka.”+
13 “Kwa maana nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe,”+ asema Yehova, “kwamba Bosra+ litakuwa kitu cha kushangaza,+ shutuma, uharibifu na laana tupu; na majiji yake yote yatakuwa mahali palipoharibiwa mpaka wakati usio na kipimo.”+
14 Kuna habari ambayo nimesikia kutoka kwa Yehova, na kuna mjumbe ambaye ametumwa kati ya mataifa, kusema: “Jikusanyeni pamoja, mje juu yake, na msimame kupigana.”+
15 “Kwa maana, tazama! Nimekufanya mdogo kwelikweli kati ya mataifa, umedharauliwa kati ya wanadamu.+ 16 Mtetemeko ambao ulisababisha umekudanganya, kimbelembele cha moyo wako,+ ewe unayekaa katika makimbilio ya mwamba, ukishika kilele cha kilima. Ingawa unajenga kiota chako juu kama tai,+ nitakushusha chini kutoka hapo,”+ asema Yehova. 17 “Na Edomu atakuwa kitu cha kushangaza.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao na kupiga mluzi kwa sababu ya mapigo yake yote.+ 18 Kama ilivyotokea katika maangamizi ya Sodoma na Gomora na miji yake jirani,”+ Yehova amesema, “vivyo hivyo hakuna mtu atakayekaa hapo, na hakuna mwana wa binadamu atakayekaa ndani yake akiwa mgeni.+
19 “Tazama! Mtu atapanda tu kama simba+ kutoka katika vichaka vyenye fahari kando ya Yordani kwenda kwenye makao yanayodumu,+ lakini katika muda mfupi nitamfanya akimbie kutoka kwake.+ Nami nitaweka juu yake yule ambaye amechaguliwa. Kwa maana ni nani aliye kama mimi,+ na ni nani atakayenipinga,+ na ni nani, sasa, aliye mchungaji anayeweza kusimama mbele zangu?+ 20 Kwa hiyo sikieni shauri la Yehova ambalo ametunga juu ya Edomu,+ na mawazo yake ambayo amefikiri juu ya wakaaji wa Temani:+ Hakika wadogo wa kundi watakokotwa huku na huku. Hakika kwa sababu yao atayafanya makao yao kuwa ukiwa.+ 21 Dunia imeanza kutetemeka kutokana na sauti ya kuanguka kwao.+ Kuna kilio!+ Sauti yake imesikiwa hata kwenye Bahari Nyekundu.+ 22 Tazama! Mtu atapaa na kurukia mawindo kama tai,+ naye atanyoosha mabawa yake juu ya Bosra;+ na moyo wa wanaume wenye nguvu wa Edomu siku hiyo utakuwa kama moyo wa mke aliye na taabu ya kuzaa mtoto.”+
23 Kuhusu Damasko:+ “Hamathi+ na Arpadi+ wameona aibu, kwa maana wamesikia habari mbaya. Wamebomoka.+ Katika bahari kuna hangaiko; haiwezi kukaa bila machafuko.+ 24 Damasko amekufa moyo. Amegeuka ili kukimbia, na wasiwasi mtupu umemshika.+ Taabu na uchungu wa kuzaa zimemshika, kama mwanamke anayezaa.+ 25 Kwa nini jiji lenye sifa halikuachwa, mji wa furaha? +
26 “Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika viwanja vyake vya watu wote, na wanaume wote wa vita watanyamazishwa katika siku hiyo,”+ asema Yehova wa majeshi. 27 “Nami nitawasha moto juu ya ukuta wa Damasko, nao utaiteketeza minara ya makao ya Ben-hadadi.”+
28 Kuhusu Kedari+ na falme za Hasori,+ ambazo Nebukadreza mfalme wa Babiloni alipiga,+ Yehova amesema hivi: “Simameni, nendeni mpaka Kedari, na muwapore wana wa Mashariki.+ 29 Mahema+ yao na makundi+ yao yatachukuliwa, vitambaa vyao vya mahema+ na vyombo vyao vyote. Na ngamia+ zao watachukuliwa kutoka kwao. Na hakika wao watawalilia, ‘Kuna hofu pande zote!’”+
30 “Kimbieni, kimbilieni mbali; shukeni ndani sana ili mkae, enyi wakaaji wa Hasori,”+ asema Yehova. “Kwa maana Nebukadreza mfalme wa Babiloni+ ametunga shauri juu yenu naye amefikiri wazo fulani juu yenu.”
31 “Simameni, pandeni juu ya taifa ambalo linastarehe,+ linalokaa katika usalama!”+ asema Yehova.
“Halina milango wala mapingo. Wanakaa peke yao.+ 32 Na ngamia+ zao wataporwa, na makundi yao yaliyo mengi yatakuwa nyara. Nami nitawatawanya kwa kila upepo,+ wale ambao nywele zao zimekatwa kwenye vipaji vya nyuso;+ nami nitaleta maafa yao kutoka katika maeneo yote karibu nalo,” asema Yehova. 33 “Na Hasori+ atakuwa pango la mbwa-mwitu,+ mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo. Hakuna mtu atakayekaa humo, na hakuna mwana wa binadamu atakayekaa humo akiwa mgeni.”+
34 Hili ndilo neno la Yehova lililomjia Yeremia nabii kuhusu Elamu+ mwanzoni mwa ufalme wa Sedekia+ mfalme wa Yuda, kusema: 35 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Tazama, ninauvunja upinde wa Elamu,+ mwanzo wa nguvu zao. 36 Nami nitaleta juu ya Elamu zile pepo nne kutoka katika miisho minne ya mbingu.+ Nami nitawatawanya kwenye pepo hizi zote,+ na hakutakuwa na taifa lolote ambako watu wa Elamu waliotawanywa+ hawatakuja ndani yake.’”
37 “Nami nitawavunja-vunja Waelamu mbele ya adui zao na mbele ya wale wanaoitafuta nafsi yao; nami nitaleta juu yao msiba, hasira yangu inayowaka,”+ asema Yehova. “Nami nitatuma upanga nyuma yao mpaka nitakapokuwa nimewaangamiza.”+
38 “Nami nitaweka kiti changu cha ufalme katika Elamu,+ nitaangamiza kutoka humo mfalme na wakuu,” asema Yehova.
39 “Na hakika itakuwa kwamba katika siku za mwisho+ nitawakusanya mateka wa Elamu,”+ asema Yehova.
50 Neno ambalo Yehova alisema kuhusu Babiloni,+ kuhusu nchi ya Wakaldayo,+ kupitia Yeremia nabii: 2 “Lihubirini jambo hilo kati ya mataifa na mlitangaze.+ Na mwinue ishara;+ mlitangaze. Msifiche jambo lolote. Semeni, ‘Babiloni ametekwa.+ Beli ameona aibu.+ Merodaki ameingiwa na hofu. Sanamu zake zimeona aibu.+ Sanamu zake za mavi zimeingiwa na hofu.’ 3 Kwa maana taifa limekuja juu yake kutoka kaskazini.+ Hilo ndilo linaloifanya nchi yake kuwa kitu cha kushangaza, hivi kwamba hakuna yeyote anayekaa ndani yake.+ Mwanadamu na pia mnyama wa kufugwa wamekimbia.+ Wameenda zao.”+
4 “Katika siku hizo na katika wakati huo,”+ asema Yehova, “wana wa Israeli, wao na wana wa Yuda pamoja, watakuja.+ Watatembea, wakilia huku wakitembea,+ nao watamtafuta Yehova Mungu wao.+ 5 Wataendelea kuuliza njia ya kwenda Sayuni, nyuso zao zikiwa zimeelekezwa upande huo,+ wakisema, ‘Njooni, tujiunge pamoja na Yehova katika agano ambalo halitasahauliwa, linalodumu mpaka wakati usio na kipimo.’+ 6 Watu wangu wamekuwa kundi la viumbe vinavyoangamia.+ Wachungaji wao wamewafanya waende huku na huku.+ Wamewapeleka juu ya milima.+ Wameenda kutoka mlima mpaka kilima. Wamepasahau mahali pao pa kupumzika.+ 7 Wale wote wanaowapata wamewala,+ na adui zao wamesema,+ ‘Hatutakuwa na hatia,+ kwa sababu wamemtendea dhambi Yehova ambaye ni makao ya uadilifu,+ Yehova ambaye ni tumaini la mababu zao.’”+
8 “Kimbieni kutoka katikati ya Babiloni, na mwondoke katika nchi ya Wakaldayo,+ na muwe kama wanyama wanaoongoza mbele ya kundi.+ 9 Kwa maana tazama, ninaamsha na kuleta juu ya Babiloni kutaniko la mataifa makubwa kutoka katika nchi ya kaskazini,+ na hakika wao watajipanga juu yake.+ Kutoka hapo atatekwa.+ Mishale ya mtu ni kama ya mwanamume mwenye nguvu ambaye harudi bila matokeo, akisababisha kufiwa na watoto.+ 10 Na Ukaldayo itakuwa nyara.+ Wale wote wanaomteka nyara watajishibisha,”+ asema Yehova.
11 “Kwa maana ninyi mliendelea kushangilia,+ kwa maana mliendelea kufurahi mlipokuwa mkiupora urithi wangu.+ Kwa maana mliendelea kukanyaga kama ndama-jike katika majani mororo,+ nanyi mkaendelea kulia kama farasi-dume.+ 12 Mama yenu ameona aibu sana.+ Yeye aliyewazaa ninyi amekata tamaa.+ Tazama! Yeye ndiye asiye na maana kabisa kati ya mataifa, nyika isiyo na maji na nchi tambarare ya jangwani.+ 13 Kwa sababu ya ghadhabu ya Yehova yeye hatakaliwa,+ naye atakuwa mahame yenye ukiwa.+ Na yeyote anayepita kando ya Babiloni, atatazama kwa mshangao na kupiga mluzi kwa sababu ya mapigo yake yote.+
14 “Jipangeni juu ya Babiloni kila upande,+ ninyi nyote mnaokanyaga upinde.+ Mpigeni mishale.+ Msiuache mshale wowote, kwa maana yeye amemtendea dhambi Yehova.+ 15 Pigeni kelele za vita juu yake kila upande.+ Ametoa mkono wake.+ Nguzo zake zimeanguka. Kuta zake zimebomolewa.+ Kwa maana ni kisasi cha Yehova.+ Jilipizieni kisasi juu yake. Kama alivyotenda, mtendeeni vivyo hivyo.+ 16 Mkatilieni mbali mpandaji wa mbegu kutoka Babiloni,+ na yule anayechukua mundu wakati wa mavuno. Kwa sababu ya upanga unaoonea kila mmoja atawageukia watu wake mwenyewe, na kila mmoja ataikimbilia nchi yake mwenyewe.+
17 “Israeli ni kondoo wa kundi aliyetawanywa.+ Simba wenyewe ndio wamemtawanya.+ Mara ya kwanza mfalme wa Ashuru amemla,+ na mara hii ya mwisho Nebukadreza mfalme wa Babiloni ameitafuna mifupa yake.+ 18 Kwa hiyo Yehova wa majeshi, Mungu wa Israseli, amesema hivi, ‘Tazama, ninakaza fikira zangu juu ya mfalme wa Babiloni na juu ya nchi yake kama nilivyokaza fikira zangu juu ya mfalme wa Ashuru.+ 19 Nami nitamrudisha Israeli kwenye uwanja wake wa malisho,+ na hakika yeye atalisha juu ya Karmeli+ na juu ya Bashani;+ na katika eneo lenye milima la Efraimu+ na la Gileadi+ nafsi yake itashiba.’”
20 “Na katika siku hizo na katika wakati huo,”+ asema Yehova, “kosa la Israeli litatafutwa,+ lakini halitakuwapo; na dhambi za Yuda,+ nazo hazitapatikana, kwa maana nitawasamehe wale nitakaowaacha wabaki.”+
21 “Juu ya nchi ya Merathaimu—njoo juu yake+ na juu ya wakaaji wa Pekodi.+ Mauaji ya kikatili na maangamizi na yawafikie,” asema Yehova, “na ufanye kulingana na yote ambayo nimekuamuru wewe.+ 22 Kuna sauti ya vita katika nchi, na anguko kubwa.+ 23 Jinsi nyundo ya chuma+ ya dunia yote imekatwa na kuvunjwa!+ Jinsi Babiloni amekuwa kitu cha kushangaza tu kati ya mataifa!+ 24 Nimekuwekea mtego nawe umekamatwa, Ee Babiloni, nawe mwenyewe hukujua jambo hilo.+ Ulipatikana na pia ukashikwa, kwa maana ulishindana na Yehova.+
25 “Yehova amefungua ghala lake, naye anatoa silaha za shutuma yake.+ Kwa maana kuna kazi aliyo nayo Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi, katika nchi ya Wakaldayo.+ 26 Ingieni kwake kutoka sehemu ya mbali zaidi.+ Fungueni maghala yake.+ Mrundikeni, kama wale wanaorundika,+ mkamwangamize.+ Naye asije akawa na mabaki yoyote.+ 27 Waueni ng’ombe-dume zake wote wachanga.+ Na washuke kwenda machinjoni.+ Ole wao, kwa maana siku yao imefika, wakati wa kuwakazia fikira!+
28 “Kuna sauti ya wale wanaokimbia na wale wanaoponyoka kutoka katika nchi ya Babiloni+ ili kutangaza katika Sayuni kisasi cha Yehova Mungu wetu,+ kisasi kwa ajili ya hekalu lake.+
29 “Iteni wapiga-mishale juu ya Babiloni, wote wanaokanyaga upinde.+ Pigeni kambi juu yake pande zote. Wenye kuponyoka na wasiwepo.+ Mlipeni yeye kulingana na matendo yake.+ Kulingana na yote ambayo ametenda, mtendeeni vivyo hivyo.+ Kwa maana yeye ametenda kwa kimbelembele juu ya Yehova, juu ya Mtakatifu wa Israeli.+ 30 Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika viwanja vyake vya watu wote,+ na hata wanaume wake wote wa vita watanyamazishwa katika siku hiyo,”+ asema Yehova.
31 “Tazama! Mimi niko dhidi yako,+ Ee Kimbelembele,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi, “kwa maana siku yako lazima itakuja, wakati ambapo nitakukazia fikira. 32 Na hakika Kiburi kitajikwaa na kuanguka,+ nacho hakitakuwa na yeyote wa kukiinua.+ Nami nitawasha moto katika majiji yake, nao utayateketeza mazingira yake yote.”+
33 Yehova wa majeshi amesema hivi: “Wana wa Israeli na wana wa Yuda wanakandamizwa pamoja, na wale wote wanaowachukua mateka wamewashika.+ Wamekataa kuwaachilia waende zao.+ 34 Mkombozi wao ni mwenye nguvu,+ Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+ Bila shaka ataendesha kesi yao,+ ili aipe nchi utulivu+ na kuwafadhaisha wakaaji wa Babiloni.”+
35 “Kuna upanga juu ya Wakaldayo,”+ asema Yehova, “na juu ya wakaaji wa Babiloni+ na juu ya wakuu+ wake na juu ya wenye hekima wake.+ 36 Kuna upanga juu ya wale wanaoongea maneno matupu,+ na hakika wao watatenda kipumbavu.+ Kuna upanga juu ya wanaume wake wenye nguvu,+ na kwa kweli wao wataingiwa na woga.+ 37 Kuna upanga juu ya farasi+ wao na juu ya magari yao ya vita na juu ya jamii yote iliyochangamana iliyo katikati yake,+ na hakika wao watakuwa wanawake.+ Kuna upanga juu ya hazina zake,+ nazo kwa kweli zitaporwa. 38 Kuna uharibifu juu ya maji yake, nayo lazima yatakaushwa.+ Kwa maana hiyo ni nchi ya sanamu za kuchongwa,+ na kwa sababu ya maono yao yenye kutia hofu wanaendelea kutenda kiwazimu. 39 Kwa hiyo wakaaji wa maeneo yasiyo na maji watakaa pamoja na wanyama wenye kupiga mayowe, na mbuni watakaa ndani yake;+ na ndani yake yeye hatakaliwa tena kamwe, wala yeye hatakaa mahali popote kwa kizazi baada ya kizazi.”+
40 “Kama yalivyokuwa maangamizi ya Mungu juu ya Sodoma na Gomora+ na miji yake jirani,”+ asema Yehova, “vivyo hivyo hakuna mtu atakayekaa humo, wala mwana wa binadamu hatakaa humo akiwa mgeni.+
41 “Tazama! Kikundi cha watu kinaingia kutoka kaskazini; na taifa kubwa+ na wafalme wakuu+ wataamshwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+ 42 Wanashika upinde na mkuki.+ Ni wakali nao hawataonyesha rehema yoyote.+ Sauti yao ni kama bahari ambayo imechafuka,+ nao watapanda juu ya farasi;+ wamejipanga kama mtu mmoja kwa ajili ya kupigana vita nawe, Ee binti ya Babiloni.+
43 “Mfalme wa Babiloni amesikia habari juu yao,+ na mikono yake imelegea.+ Kuna taabu! Maumivu makali yamemshika, kama mwanamke anayezaa.+
44 “Tazama! Mtu atapanda kama simba kutoka katika vichaka vyenye fahari kando ya Yordani kwenda kwenye makao yenye kudumu,+ lakini kwa kitambo kidogo nitawakimbiza kutoka kwake.+ Na yule ambaye amechaguliwa nitamweka juu yake.+ Kwa maana ni nani aliye kama mimi,+ na ni nani atakayenipinga,+ na ni nani, sasa, aliye mchungaji anayeweza kusimama mbele zangu?+ 45 Kwa hiyo sikieni shauri+ la Yehova ambalo ametunga juu ya Babiloni+ na mawazo yake ambayo amefikiri juu ya nchi ya Wakaldayo.+ Hakika wale wadogo wa kundi watakokotwa huku na huku.+ Hakika kwa sababu yao atayafanya makao yao kuwa ukiwa.+ 46 Kutokana na sauti ya kukamatwa kwa Babiloni, hakika dunia itaanza kutikiswa,+ na kati ya mataifa kilio kitasikiwa.”+
51 Yehova amesema hivi: “Tazama, ninaamsha upepo wenye kuharibu juu ya Babiloni+ na juu ya wakaaji wa Leb-kamai;+ 2 nami nitatuma Babiloni wapepetaji ambao kwa hakika watampepeta na kuifanya nchi yake kuwa tupu;+ kwa maana kwa kweli watakuwa juu yake pande zote katika siku ya msiba.+
3 “Yeye anayekanyaga upinde wake na asikanyage.+ Na yeyote asisimame akiwa amevaa vazi lake la chuma.
“Nanyi msiwahurumie vijana wake.+ Liangamizeni jeshi lake lote.+ 4 Nao wataanguka wakiwa wameuawa katika nchi ya Wakaldayo+ na wakiwa wamechomwa katika barabara zake.+
5 “Kwa maana Israeli na Yuda+ hawajafanywa wajane kutoka kwa Mungu wao, kutoka kwa Yehova wa majeshi.+ Kwa maana nchi ya hao imejawa na hatia machoni pa Mtakatifu wa Israeli.+
6 “Kimbieni kutoka katikati ya Babiloni,+ na kila mmoja wenu aiponye nafsi yake mwenyewe.+ Msifanywe kuwa wasio na uhai kupitia kosa lake.+ Kwa maana ni wakati wa kisasi cha Yehova.+ Kuna tendo ambalo anamlipa.+ 7 Babiloni amekuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yehova,+ yeye anailewesha dunia yote.+ Mataifa yamekunywa kutokana na divai yake.+ Ndiyo sababu mataifa yanaendelea kutenda kiwazimu.+ 8 Kwa ghafula Babiloni ameanguka, hivi kwamba amevunjwa.+ Pigeni mayowe juu yake.+ Chukueni zeri kwa ajili ya maumivu yake.+ Huenda akapona.”
9 “Tungemponya Babiloni, lakini yeye hakuponyeka. Mwacheni,+ nasi twende kila mmoja kwenye nchi yake mwenyewe.+ Kwa maana hukumu yake imefika mpaka mbinguni, nayo imeinuliwa mpaka kwenye anga lenye mawingu.+ 10 Yehova ametuletea matendo ya uadilifu.+ Njooni na acheni sisi tusimulie katika Sayuni kazi ya Yehova Mungu wetu.”+
11 “Isugueni mishale.+ Jazeni ngao za mviringo. Yehova ameiamsha roho ya wafalme wa Wamedi,+ kwa sababu wazo lake liko juu ya Babiloni,+ ili kumharibu. Kwa maana hicho ni kisasi cha Yehova, kisasi kwa ajili ya hekalu lake.+ 12 Inueni ishara+ juu ya kuta za Babiloni. Yatieni malindo nguvu.+ Wekeni walinzi. Watayarisheni wale wanaovizia.+ Kwa maana Yehova ametunga wazo naye pia hakika atafanya lile alilosema juu ya wakaaji wa Babiloni.”+
13 “Ee mwanamke unayekaa juu ya maji mengi,+ mwenye hazina nyingi,+ mwisho wako umekuja, kipimo+ chako cha kupata faida.+ 14 Yehova wa majeshi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe,+ ‘Nitakujaza watu, kama nzige,+ nao hakika watapiga kelele kwa kukuimbia.’+ 15 Yeye ndiye Mtengenezaji wa dunia kwa nguvu zake,+ Yeye anayeifanya imara nchi yenye kuzaa+ kwa hekima yake,+ na Yeye ambaye kwa uelewaji+ wake alizitandaza mbingu.+ 16 Kupitia sauti yake yeye huleta machafuko ya maji mbinguni, naye hufanya mivuke ipae kutoka katika mwisho wa dunia.+ Amefanya hata milango kwa ajili ya mvua,+ naye huleta upepo kutoka katika maghala yake. 17 Kila mtu amejiendesha kwa kukosa sana kutumia akili asiweze kujua.+ Kila fundi wa chuma ataona aibu kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+ kwa maana sanamu yake ya kuyeyushwa ni uwongo,+ na hamna roho ndani ya hizo.+ 18 Hizo ni ubatili,+ kazi ya mzaha.+ Wakati wa kuzikazia fikira, zitaangamia.+
19 “Yeye aliye Fungu la Yakobo si kama vitu hivyo,+ kwa maana yeye ndiye Mfanyizaji wa kila kitu,+ fimbo ya urithi wake.+ Yehova wa majeshi ndilo jina lake.”+
20 “Wewe ni rungu kwangu, kama silaha za vita,+ na kupitia wewe hakika nitayavunja mataifa vipande-vipande, na kupitia wewe nitaziangamiza falme. 21 Na kupitia wewe nitamvunja farasi na mpandaji wake vipande-vipande, na kupitia wewe nitalivunja gari la vita na mpandaji wake vipande-vipande.+ 22 Na kupitia wewe nitamvunja mwanamume na mwanamke vipande-vipande, na kupitia wewe nitamvunja mzee na mvulana vipande-vipande, na kupitia wewe nitamvunja mwanamume kijana na bikira vipande-vipande. 23 Na kupitia wewe nitamvunja mchungaji na kundi lake vipande-vipande, na kupitia wewe nitamvunja mkulima na jozi yake ya wanyama vipande-vipande, na kupitia wewe nitawavunja magavana na watawala-wasaidizi vipande-vipande. 24 Nami nitamlipa Babiloni na wakaaji wote wa Ukaldayo ubaya wao wote ambao wametenda katika Sayuni mbele ya macho yenu,”+ asema Yehova.
25 “Tazama, mimi niko dhidi yako,+ Ee mlima wenye kuharibu,”+ asema Yehova, “wewe mwenye kuiharibu dunia yote;+ nami nitaunyoosha mkono wangu juu yako na kukuviringisha kutoka katika miamba na kukufanya kuwa mlima ulioteketezwa.”+
26 “Na watu hawatachukua kutoka kwako jiwe la pembeni wala jiwe kwa ajili ya misingi,+ kwa sababu wewe utakuwa mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo,”+ asema Yehova.
27 “Inueni ishara katika nchi.+ Pigeni baragumu kati ya mataifa. Takaseni+ mataifa juu yake. Iteni falme za Ararati,+ Mini na Ashkenazi+ zije juu yake. Wekeni juu yake ofisa mwandikishaji. Pandisheni+ farasi kama nzige waliojaa miiba. 28 Takaseni juu yake mataifa, wafalme wa Umedi,+ magavana wake na watawala-wasaidizi wake wote na nchi yote ya mamlaka ya kila mmoja. 29 Dunia itetemeke na kuwa katika maumivu makali,+ kwa maana fikira za Yehova zimeinuka juu ya Babiloni ili kuifanya nchi ya Babiloni kuwa kitu cha kushangaza, bila mkaaji.+
30 “Wanaume wenye nguvu wa Babiloni wameacha kupigana. Wameendelea kuketi katika mahali imara. Nguvu zao zimekauka.+ Wamekuwa wanawake.+ Makao yake yamewashwa moto. Mapingo yake yamevunjwa.+
31 “Mkimbiaji mmoja anakimbia ili kukutana na mkimbiaji mwingine, na mleta-habari mmoja ili kukutana na mleta-habari mwingine,+ kumletea habari mfalme wa Babiloni kwamba jiji lake limetekwa kwenye miisho yote,+ 32 na kwamba vivuko vimeshikwa,+ na mashua zilizotengenezwa kwa mafunjo wameziteketeza kwa moto, na watu wa vita wameingiwa na hofu.”+
33 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Binti ya Babiloni ni kama uwanja wa kupuria.+ Ni wakati wa kumkanyagia chini awe mgumu. Bado kitambo kidogo na wakati wa mavuno utakuja kwa ajili yake.”+
34 “Nebukadreza mfalme wa Babiloni amenila;+ amenivuruga. Ameniweka kuwa kama chombo kitupu. Amenimeza kama nyoka mkubwa;+ amelijaza tumbo lake kwa vitu vyangu vyenye kupendeza. Amenioshea mbali. 35 ‘Jeuri niliyotendewa mimi na kutendewa mwili wangu na iwe juu ya Babiloni!’ mwanamke mkaaji wa Sayuni atasema.+ ‘Na damu yangu na iwe juu ya wakaaji wa Ukaldayo!’ Yerusalemu atasema.”+
36 Kwa hiyo Yehova amesema hivi: “Tazama, ninaendesha kesi yako,+ nami hakika nitalipiza kisasi kwa ajili yako.+ Nami nitaikausha bahari yake, nitavikausha visima vyake.+ 37 Na Babiloni atakuwa marundo ya mawe,+ pango la mbwa-mwitu,+ kitu cha kushangaza na kitu cha kupigiwa mluzi, bila mkaaji.+ 38 Wote pamoja watanguruma kama wana-simba wenye manyoya shingoni. Hakika watanguruma kama watoto wa simba.”
39 “Wakati watakapokuwa wamesisimuka nitaweka karamu zao na kuwalewesha, ili wafurahi;+ nao watalala usingizi unaodumu mpaka wakati usio na kipimo, ambamo hawataamka,”+ asema Yehova. 40 “Nitawashusha kama kondoo-dume kwenda machinjoni, kama kondoo-dume pamoja na mbuzi-dume.”+
41 “Jinsi Sheshaki alivyotekwa,+ na jinsi Sifa ya dunia yote ilivyokatwa!+ Jinsi Babiloni amekuwa kitu cha kushangaza katikati ya mataifa!+ 42 Bahari imekuja juu ya Babiloni. Amefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.+ 43 Majiji yake yamekuwa kitu cha kushangaza, nchi isiyo na maji na nchi tambarare ya jangwani.+ Kama nchi, ndani yao hakuna mtu atakayekaa, na katikati yao hakuna mwana wa binadamu atakayepita.+ 44 Nami nitakaza fikira zangu juu ya Beli+ katika Babiloni, nami nitatoa katika kinywa chake kile ambacho amemeza.+ Na mataifa hayatamiminika kwake tena.+ Pia, lazima ukuta wenyewe wa Babiloni uanguke.+
45 “Tokeni katikati yake, enyi watu wangu,+ na kila mmoja aiponye nafsi yake+ kutoka kwenye hasira ya Yehova inayowaka.+ 46 Au kama sivyo moyo wenu utakuwa na woga,+ nanyi mtaogopa kwa sababu ya habari ambayo itasikiwa katika nchi. Na habari hiyo itakuja katika muda wa mwaka mmoja, na baada yake katika muda wa mwaka mwingine kutakuwa na habari na jeuri katika dunia na mtawala juu ya mtawala. 47 Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja, nami nitakaza fikira zangu juu ya sanamu za kuchongwa za Babiloni;+ na nchi yake yote itaona aibu, na watu wake wote waliouawa wataanguka katikati yake.+
48 “Na mbingu na dunia na vyote vilivyomo hakika vitapiga vigelegele vya shangwe juu ya Babiloni,+ kwa maana waporaji watakuja kwake kutoka kaskazini,”+ asema Yehova. 49 “Babiloni hakuwa tu kisababishi cha kuanguka kwa waliouawa wa Israeli+ lakini pia kule Babiloni waliouawa wa dunia yote wameanguka.+
50 “Ninyi mlioponyoka upanga, endeleeni kwenda. Msisimame tuli.+ Mkumbukeni Yehova kutoka mbali,+ Yerusalemu na aingie katika moyo wenu.”+
51 “Tumeona aibu,+ kwa maana tumesikia shutuma.+ Fedheha imefunika nyuso zetu,+ kwa maana wageni wamekuja juu ya mahali patakatifu pa nyumba ya Yehova.”+
52 “Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitakaza fikira zangu juu ya sanamu zake za kuchongwa,+ na katika nchi yake yote aliyechomwa ataugua.”+
53 “Hata Babiloni akipaa juu mbinguni+ na hata akifanya kilele cha nguvu zake kisiweze kufikiwa,+ kutoka kwangu waporaji watakuja kwake,”+ asema Yehova.
54 “Sikilizeni! Kuna kilio kutoka Babiloni,+ na mshindo mkubwa kutoka nchi ya Wakaldayo,+ 55 kwa maana Yehova anampora Babiloni, na hakika yeye ataangamiza kutoka ndani yake ile sauti kubwa,+ na mawimbi yao yatakuwa na machafuko kama maji mengi.+ Kelele za sauti yao hakika zitapigwa. 56 Kwa maana atakuja juu yake, juu ya Babiloni, mporaji,+ na wanaume wake wenye nguvu hakika watakamatwa.+ Pinde zao zitavunjwa-vunjwa,+ kwa maana Yehova ni Mungu wa malipo.+ Bila shaka atalipa.+ 57 Nami nitawalewesha wakuu wake na watu wake wenye hekima, magavana wake na watawala-wasaidizi wake na wanaume wake wenye nguvu,+ nao watalala usingizi unaodumu mpaka wakati usio na kipimo, ambamo hawataweza kuamka,”+ asema Mfalme,+ ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi.+
58 Yehova wa majeshi amesema hivi: “Ukuta wa Babiloni, ingawa ni mpana, bila shaka utabomolewa;+ na malango yake, ingawa ni marefu, yatawashwa moto.+ Na vikundi vya watu vitafanya kazi bure tu,+ na vikundi vya mataifa vitafanya kazi kwa ajili ya moto tu;+ nao watajichosha tu.”
59 Neno ambalo Yeremia nabii alimwamuru Seraya mwana wa Neria+ mwana wa Mahseya+ alipoenda pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda kule Babiloni katika mwaka wa nne wa kuwa kwake mfalme; na Seraya ndiye aliyekuwa msimamizi wa makao. 60 Na Yeremia akaandika katika kitabu+ kimoja msiba wote ambao ungekuja juu ya Babiloni, haya maneno yote yaliyoandikwa juu ya Babiloni. 61 Na zaidi ya hayo, Yeremia akamwambia Seraya: “Mara tu utakapofika Babiloni na kumwona, lazima wewe pia uyasome kwa sauti maneno haya yote.+ 62 Nawe useme, ‘Ee Yehova, wewe mwenyewe umesema juu ya mahali hapa, kupakatilia mbali ili kwamba mkaaji+ yeyote asiwe ndani yake, mwanadamu wala mnyama wa kufugwa, bali pawe mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo.’ 63 Na itatukia kwamba utakapokuwa umemaliza kukisoma kitabu hiki, utakifunga kwenye jiwe, nawe lazima ukitupe katikati ya Efrati.+ 64 Na useme, ‘Hivi ndivyo Babiloni atakavyozama asiinuke tena kamwe kwa sababu ya msiba ambao ninaleta juu yake;+ nao hakika watajichosha.’”+
Maneno ya Yeremia yamefikia hapa.
52 Sedekia+ alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutawala,+ naye akatawala miaka 11 katika Yerusalemu.+ Na jina la mama yake lilikuwa Hamutali+ binti ya Yeremia wa Libna.+ 2 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ kulingana na yote aliyokuwa amefanya Yehoyakimu.+ 3 Kwa maana hayo yalitukia katika Yerusalemu na Yuda kwa sababu ya hasira ya Yehova, mpaka alipokuwa amewatupa kutoka mbele za uso wake.+ Na Sedekia akaanza kumwasi mfalme wa Babiloni.+ 4 Mwishowe ikawa kwamba katika mwaka wa tisa wa kuwa kwake mfalme,+ katika mwezi wa kumi, katika siku ya kumi ya mwezi huo, Nebukadreza mfalme wa Babiloni akaja, yeye pamoja na jeshi lake lote, juu ya Yerusalemu,+ nao wakaanza kupiga kambi juu yake na kujenga juu yake ukuta wa kumzingira pande zote.+ 5 Kwa hiyo jiji likazingirwa mpaka mwaka wa kumi na moja wa Mfalme Sedekia.+
6 Katika mwezi wa nne, katika siku ya tisa ya mwezi huo,+ njaa pia ikawa kali ndani ya jiji na hapakuwa na mkate kwa ajili ya watu wa nchi.+ 7 Mwishowe jiji likapenywa;+ nao watu wote wa vita, wakaanza kukimbia+ na kutoka katika jiji wakati wa usiku kupitia njia ya lango lililo kati ya zile kuta mbili kando ya bustani ya mfalme,+ huku Wakaldayo wakiwa wamelizunguka jiji pande zote; nao wakaendelea kwenda kupitia njia ya Araba.+ 8 Na jeshi la Wakaldayo likamfuatilia mfalme,+ nao wakamfikia Sedekia+ katika nchi tambarare za jangwa la Yeriko; na jeshi lake lote likatawanyika kutoka upande wake.+ 9 Ndipo wakamkamata mfalme na kumleta kwa mfalme wa Babiloni+ kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi,+ ili atangaze maamuzi ya hukumu juu yake.+ 10 Na mfalme wa Babiloni akawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake,+ na pia wakuu wote wa Yuda akawaua kule Ribla.+ 11 Naye akayapofusha macho ya Sedekia,+ kisha mfalme wa Babiloni akamfunga kwa pingu za shaba, akampeleka Babiloni+ na kumtia katika nyumba ya kifungo mpaka siku ya kufa kwake.
12 Na katika mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi huo, yaani, katika mwaka wa kumi na tisa wa Mfalme Nebukadreza,+ mfalme wa Babiloni, Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi, aliyekuwa akisimama mbele ya mfalme wa Babiloni, aliingia ndani ya Yerusalemu. 13 Naye akaiteketeza nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme na nyumba zote za Yerusalemu;+ na kila nyumba kubwa akaiteketeza kwa moto.+ 14 Na majeshi yote ya Wakaldayo yaliyokuwa pamoja na yule mkuu wa walinzi yakazibomoa kuta zote za Yerusalemu, kuzunguka pande zote.+
15 Na baadhi ya watu wa hali ya chini kati ya watu na wale watu wengine walioachwa katika jiji+ na wale waliokimbia wakajiunga na mfalme wa Babiloni na wale wafanyakazi stadi wengine Nebuzaradani mkuu wa walinzi akawapeleka uhamishoni.+ 16 Na wengine kati ya watu wa hali ya chini wa nchi Nebuzaradani yule mkuu wa walinzi akawaacha wabaki kuwa watunza-mizabibu na kuwa wafanyakazi wa kulazimishwa.+
17 Na zile nguzo za shaba+ za nyumba ya Yehova na yale mabehewa+ na ile bahari ya shaba+ iliyokuwa katika nyumba ya Yehova, Wakaldayo wakazivunja vipande-vipande na kuichukua shaba yake yote kuipeleka Babiloni.+ 18 Nao wakachukua makopo na sepetu+ na mikasi ya taa+ na mabakuli+ na vikombe na vyombo vyote vya shaba walivyokuwa wakitumia kuhudumu.+ 19 Na beseni+ na vyetezo na mabakuli na makopo na vinara vya taa+ na vikombe na mabakuli+ yaliyokuwa ya dhahabu halisi,+ na vile vilivyokuwa vya fedha halisi,+ yule mkuu wa walinzi akavichukua.+ 20 Na zile nguzo+ mbili, ile bahari+ moja, na wale ng’ombe-dume kumi na wawili wa shaba+ waliokuwa chini ya bahari, yale mabehewa, ambayo Mfalme Sulemani alikuwa ametengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yehova.+ Uzito wa shaba yake haukupimwa—vyombo hivyo vyote.+
21 Na kuhusu zile nguzo, kila nguzo ilikuwa na kimo cha mikono kumi na minane,+ na kamba ya urefu wa mikono kumi na miwili ingeweza kuizunguka;+ na unene wake ulikuwa upana wa vidole vinne, nayo ilikuwa na tundu. 22 Na lile kombe juu yake lilikuwa la shaba,+ na urefu wa lile kombe moja ulikuwa mikono mitano;+ na zile kamba za nyavu na makomamanga yaliyo juu ya lile kombe, kuzunguka pande zote,+ hivyo vyote vilikuwa vya shaba; na nguzo ya pili ilikuwa vivyo hivyo, pia yale makomamanga.+ 23 Na makomamanga yakawa 96, kandokando, makomamanga yote yakiwa 100 juu ya zile kamba za nyavu kuzunguka pande zote.+
24 Zaidi ya hayo, yule mkuu wa walinzi akamchukua Seraya+ mkuu wa makuhani na Sefania+ kuhani wa pili na wale watunza-milango watatu,+ 25 naye akachukua kutoka jijini ofisa mmoja wa makao ya mfalme ambaye alikuwa mkuu juu ya watu wa vita, na watu 7 kati ya wale wenye kuingia kwa mfalme,+ waliopatikana katika jiji, na mwandishi wa mkuu wa jeshi, mwenye kuwakusanya watu wa nchi, na watu 60 kati ya watu wa nchi, waliopatikana katikati ya jiji.+ 26 Basi Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi akawachukua na kuwapeleka kwa mfalme wa Babiloni kule Ribla.+ 27 Na mfalme wa Babiloni akawapiga na kuwaua+ watu hao kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi.+ Hivyo Yuda wakaenda uhamishoni kutoka katika nchi yao.+
28 Hawa ndio watu ambao Nebukadreza alipeleka uhamishoni: katika mwaka wa 7, Wayahudi 3,023.+
29 Katika mwaka wa 18 wa Nebukadreza,+ kutoka katika Yerusalemu kulikuwa na nafsi 832.
30 Katika mwaka wa 23 wa Nebukadreza, Nebuzaradani mkuu wa walinzi aliwapeleka Wayahudi uhamishoni, nafsi 745.+
Nafsi zote zilikuwa 4,600.
31 Mwishowe ikawa kwamba katika mwaka wa 37 wa uhamisho wa Yehoyakini+ mfalme wa Yuda, katika mwezi wa 12, katika siku ya 25 ya mwezi huo, Evil-merodaki mfalme wa Babiloni, katika mwaka wa kuwa kwake mfalme, akakiinua kichwa+ cha Yehoyakini mfalme wa Yuda na kumtoa katika nyumba ya gereza. 32 Naye akaanza kusema naye mambo mema na kukiweka kiti chake cha ufalme juu zaidi ya vile viti vya wafalme wengine waliokuwa pamoja naye katika Babiloni.+ 33 Naye akamvua mavazi yake ya gerezani,+ naye akala mkate+ mbele yake daima siku zote za maisha yake.+ 34 Nayo posho yake, alipewa posho daima kutoka kwa mfalme wa Babiloni, kila siku kama inavyostahili, mpaka siku ya kufa kwake,+ siku zote za maisha yake.