Maombolezo
א [ʼAʹleph]
1 Lo! jinsi ameketi akiwa mpweke,+ jiji lililokuwa limejaa watu!+
Jinsi amekuwa kama mjane,+ yule aliyekuwa na hesabu kubwa ya watu kati ya mataifa!+
Jinsi yule aliyekuwa binti ya kifalme kati ya wilaya za utawala amekuja kufanya kazi ya kulazimishwa!+
ב [Behth]
2 Yeye hulia sana usiku,+ na machozi yake yako kwenye mashavu
yake.+
Hana yeyote wa kumfariji kati ya wapenzi wake wote.+
ג [Giʹmel]
3 Yuda ameenda uhamishoni kwa sababu ya mateso+ na kwa sababu ya utumishi mwingi.+
Imekuwa lazima akae katikati ya mataifa.+ Hakupata mahali pa kupumzikia.
Wote waliokuwa wakimtesa wamemfikia kati ya hali zenye kutaabisha.+
ד [Daʹleth]
4 Njia za Sayuni zinaomboleza, kwa sababu hakuna yeyote anayekuja kwenye sherehe.+
Malango yake yote yamefanywa ukiwa;+ makuhani wake wanaugua.+
Mabikira wake wamepata huzuni, naye mwenyewe ana uchungu.+
ה [Heʼ]
5 Wapinzani wake wamekuwa kichwa.+ Adui zake hawajali.+
Kwa maana Yehova mwenyewe amemletea huzuni kwa sababu ya wingi wa makosa yake,+
Watoto wake mwenyewe wametembea wakiwa mateka mbele ya
adui.+
ו [Waw]
6 Na fahari yote ya binti Sayuni inaondoka.+
Wakuu wake wamekuwa kama paa ambao hawakupata malisho;+
Nao wanaendelea kutembea bila nguvu mbele ya yule anayewafuatilia.+
ז [Zaʹyin]
7 Yerusalemu amekumbuka katika siku za mateso yake na za watu wake wasio na makao
Vitu vyake vyote vyenye kutamanika vilivyokuwapo tangu siku za zamani za kale.+
Wakati watu wake walipoanguka mkononi mwa adui wala hakuwa na msaidizi,+
Adui walimwona. Wakacheka kuanguka kwake.+
ח [Chehth]
8 Yerusalemu amefanya dhambi waziwazi.+ Ndiyo sababu amekuwa chukizo.+
Wote waliokuwa wakimheshimu wamemtendea kwa dharau,+ kwa maana wameuona uchi wake.+
Yeye pia anaugua+ na kugeuza mgongo wake.
ט [Tehth]
9 Uchafu wake umo ndani ya marinda yake.+ Hakukumbuka wakati wake ujao,+
Naye huteremka chini kwa njia ya ajabu. Hana mfariji.+
Ee Yehova, uone mateso yangu,+ kwa maana adui amejivuna sana.+
י [Yohdh]
10 Adui amenyoosha mkono wake juu ya vitu vyake vyote vyenye kutamanika.+
Kwa maana ameona mataifa ambayo yameingia katika patakatifu pake,+
Ambayo uliamuru kwamba wasiingie katika kutaniko lako.
כ [Kaph]
11 Watu wake wote wanaugua; wanatafuta mkate.+
Wametoa vitu vyao vyenye kutamanika wapate chakula, ili kuiburudisha nafsi.+
Uone, Ee Yehova, na utazame, kwa maana nimekuwa kama mwanamke asiye na thamani.+
ל [Laʹmedh]
12 Je, haimaanishi chochote kwenu nyote mnaopita njiani? Tazameni, mwone.+
Je, kuna uchungu wowote ulio kama uchungu wangu ambao nimetendewa vikali,+
Ambao Yehova ametumia kuleta huzuni katika siku ya hasira yake inayowaka?+
מ [Mem]
13 Kutoka juu ameleta moto katika mifupa yangu,+ naye anatiisha kila mmoja wao.
Ametandaza wavu kwa ajili ya miguu yangu.+ Amenigeuza nirudi nyuma.
Amenifanya kuwa mwanamke aliye katika hali ya ukiwa. Siku nzima mimi ni mgonjwa.+
נ [Nun]
14 Amekaa macho kuona makosa yangu.+ Yanasokotana mkononi mwake.
Yamepanda juu shingoni mwangu.+ Nguvu zangu zimejikwaa.
Yehova amenitia mkononi mwa watu ambao siwezi kusimama dhidi yao.+
ס [Saʹmekh]
15 Yehova ametupa kutoka katikati yangu watu wangu wote wenye nguvu.+
Ameitisha mkutano juu yangu, ili kuvunja vipande-vipande vijana wangu.+
Yehova amekanyaga shinikizo la divai+ la binti Yuda aliye bikira.+
ע [ʽAʹyin]
16 Nalia juu ya mambo hayo kama mwanamke.+ Jicho langu, jicho langu linatiririka maji.+
Kwa maana mfariji amekuwa mbali sana nami, mtu wa kuiburudisha nafsi yangu.
פ [Peʼ]
17 Sayuni amenyoosha mikono yake.+ Hana mfariji.+
Yehova ametoa amri kuhusu Yakobo kwa adui zake wote wanaomzunguka.+
Yerusalemu limekuwa chukizo kati yao.+
צ [Tsa·dhehʹ]
18 Yehova ni mwadilifu,+ kwa maana nimekiasi kinywa chake.+
Sikilizeni sasa, enyi nyote vikundi vya watu, na mwone maumivu yangu.
Mabikira wangu na vijana wangu wameenda utekwani.+
ק [Qohph]
19 Nimeita wale wanaonipenda sana.+ Wao wenyewe wamenifanyia ujanja.
Makuhani wangu na wanaume wangu wazee wamekufa katika jiji,+
Walipolazimika kujitafutia chakula ili waziburudishe nafsi zao.+
ר [Rehsh]
20 Tazama, Ee Yehova, kwa maana nina dhiki kali. Matumbo yangu yako katika msukosuko.+
Moyo wangu umepinduliwa ndani yangu,+ kwa maana nimeasi kabisa.+
Huko nje upanga uliwaua watoto.+ Ndani ya nyumba ni sawasawa na kifo.+
ש [Shin]
21 Watu wamesikia jinsi ninavyougua kama mwanamke.+ Sina mfariji.+
Adui zangu wote wamesikia juu ya msiba wangu.+ Wamefurahi, kwa sababu wewe mwenyewe umefanya hayo.+
Hakika utaileta siku ambayo umetangaza,+ ili wawe kama mimi.+
ת [Taw]
22 Ubaya wao wote na uje mbele zako, nawe uwatendee vikali,+
Kama vile ulivyonitendea vikali kwa sababu ya makosa yangu yote.+
א [ʼAʹleph]
2 Lo! jinsi Yehova katika hasira yake anavyomfunika kwa wingu binti Sayuni!+
Ameutupa chini uzuri wa Israeli+ kutoka mbinguni mpaka duniani.+
Naye hakumbuki kiti cha miguu+ yake katika siku ya hasira yake.
ב [Behth]
2 Yehova amemeza, hakuonyesha huruma juu ya makao+ yoyote ya Yakobo.
Katika hasira yake amebomoa ngome+ za binti Yuda.
ג [Giʹmel]
3 Katika joto kali la hasira amekata kila pembe ya Israeli.+
Amerudisha mkono wake wa kuume kutoka mbele ya adui;+
Naye huendelea kuwaka katika Yakobo kama moto unaowaka ambao umeteketeza kuzunguka pande zote.+
ד [Daʹleth]
4 Amekanyaga upinde wake kama adui.+ Mkono wake wa kuume+ umesimama mahali pake
Kama mpinzani,+ naye alizidi kuua wote wanaotamanika machoni.+
Kama moto, amemwaga ghadhabu+ yake katika hema+ la binti Sayuni.
ה [Heʼ]
5 Yehova amekuwa kama adui.+ Amemeza Israeli.+
Amemeza minara yake yote ya makao;+ ameziharibu ngome zake.+
Naye hujaza vilio na maombolezo katika binti Yuda.+
ו [Waw]
6 Naye hukitendea jeuri kibanda+ chake kama kile kilicho katika bustani.+ Ameiharibu sherehe yake.
Yehova amefanya sherehe+ na sabato kusahauliwa katika Sayuni,
Naye katika shutuma zake za hasira haheshimu mfalme wala kuhani.+
ז [Zaʹyin]
7 Yehova ameitupilia mbali madhabahu yake.+ Patakatifu pake amepakataa kwa dharau.+
Ametia katika mkono wa adui kuta za minara ya makao yake.+
Wamepaaza sauti zao ndani ya nyumba ya Yehova, kama katika siku ya sherehe.+
ח [Chehth]
8 Yehova amekusudia kuuharibu ukuta+ wa binti Sayuni.
Amenyoosha kamba ya kupimia.+ Hakurudisha mkono wake usimeze.+
Naye hufanya boma na ukuta kuomboleza.+ Zimedhoofika zote pamoja.
ט [Tehth]
9 Malango+ yake yamezama chini kabisa. Ameharibu na kuvunja mapingo yake vipande-vipande.
Mfalme wake na wakuu wake wako kati ya mataifa.+ Hakuna sheria.+
Manabii wake pia hawakupata maono kutoka kwa Yehova.+
י [Yohdh]
10 Wanaume wazee wa binti Sayuni wanaketi chini, ambapo wamenyamaza.+
Wametia mavumbi juu ya vichwa vyao.+ Wamejifunga nguo za magunia.+
Mabikira wa Yerusalemu wameinamisha vichwa vyao chini kabisa.+
כ [Kaph]
11 Macho yangu yamechoka kabisa kwa machozi matupu.+ Matumbo yangu yako katika msukosuko.+
Ini langu limemwagwa chini kabisa,+ kwa sababu ya anguko la binti ya watu wangu,+
Kwa sababu ya kuzimia kwa mtoto mchanga na yule anayenyonya katika viwanja vya watu wote vya jiji.+
ל [Laʹmedh]
12 Waliendelea kuwaambia mama zao: “Iko wapi nafaka na divai?”+
Kwa sababu ya kuzimia kwao kama mtu aliyeuawa katika viwanja vya watu wote vya jiji,
Kwa sababu ya nafsi yao kumwagwa kwenye vifua vya mama zao.
מ [Mem]
13 Nitakutumia kama shahidi juu ya nini? Nitakufananisha na nini, Ee binti Yerusalemu?+
Nitakulinganisha na nini, ili nikufariji, Ee binti Sayuni uliye bikira?+
Kwa maana mvunjiko+ wako ni mkubwa kama bahari. Ni nani anayeweza kukuponya?+
נ [Nun]
14 Manabii wako mwenyewe wameona kwa ajili yako maono ya ubatili na vitu visivyotosheleza,+
Nao hawakufunua kosa lako ili kuirudisha hali yako ya mateka,+
Bali waliendelea kuona kwa ajili yako maono ya matangazo yasiyo na faida na yanayopotosha.+
ס [Saʹmekh]
15 Wote wanaopita barabarani wamekupigia makofi.+
Wamepiga mluzi+ wa mshangao na kuendelea kutikisa vichwa+ vyao kwa sababu ya binti Yerusalemu, wakisema:
“Je, hili ndilo lile jiji ambalo walikuwa wakisema hivi kwa habari zake, ‘Hili ndilo ukamilifu wa uzuri, furaha ya dunia yote’?”+
פ [Peʼ]
16 Adui zako wote wamefungua vinywa vyao juu yako.+
Wamepiga mluzi wa mshangao na kuendelea kusaga meno.+ Wamesema: “Tutammeza.+
Kweli hii ndiyo siku ambayo tumeitumaini.+ Tumepata! Tumeona!”+
ע [ʽAʹyin]
17 Yehova amefanya alilokuwa nalo akilini mwake.+ Ametimiza neno lake,+
Aliloamuru tangu siku za kale.+ Amebomoa wala hakuonyesha huruma.+
Naye hufanya adui ashangilie juu yako.+ Ameinua juu pembe ya adui zako.+
צ [Tsa·dhehʹ]
18 Moyo wao umemlilia Yehova,+ Ee ukuta wa binti Sayuni.+
Yatiririshe machozi kama mto mchana na usiku.+
Usife ganzi. Mboni ya jicho lako isikae kimya.
ק [Qohph]
19 Simama! Lia wakati wa usiku mwanzoni mwa makesha ya kuamkia asubuhi.+
Mwaga moyo+ wako mbele za uso+ wa Yehova kama maji.
Mwinulie mikono+ yako kwa sababu ya nafsi ya watoto wako,
Wanaozimia kwa sababu ya njaa kwenye sehemu ya mbele ya barabara zote.+
ר [Rehsh]
20 Tazama, Ee Yehova, nawe umwone+ yule ambaye umemtendea vikali namna hii.
Je, wanawake waendelee kula uzao wao wenyewe, watoto waliozaliwa wakiwa wamekomaa,+
Au, je, kuhani na nabii wauawe ndani ya patakatifu pa Yehova?+
ש [Shin]
21 Mvulana na mwanamume mzee+ wamelala chini katika mavumbi ya barabara.+
Mabikira wangu na vijana wangu wenyewe wameanguka kwa upanga.+
Umeua katika siku ya hasira yako.+ Umechinja;+ hukuwa na huruma.+
ת [Taw]
22 Umeyaita makao yangu ya kigeni kuzunguka pande zote kama katika siku ya sherehe.+
Na katika siku ya ghadhabu ya Yehova hapakuwa na yeyote mwenye kuponyoka wala mwenye kuokoka;+
Wale ambao nilizaa wakiwa wamekomaa na kuwalea, adui yangu aliwaangamiza.+
א [ʼAʹleph]
3 Mimi ndiye mwanamume ambaye ameona mateso+ kwa sababu ya fimbo ya ghadhabu yake.
2 Mimi ndiye ameongoza, naye hunitembeza katika giza wala si katika nuru.+
3 Kwa kweli, yeye hugeuza tena na tena mkono wake juu yangu mchana kutwa.+
ב [Behth]
4 Amefanya nyama yangu na ngozi yangu ichakae.+ Amevunja mifupa yangu.+
5 Amejenga juu yangu, ili anizunguke+ kwa mmea wenye sumu+ pamoja na magumu.
6 Amenifanya niketi mahali penye giza+ kama watu waliokufa zamani.+
ג [Giʹmel]
7 Amenizuia kana kwamba kwa ukuta wa mawe, ili nisiweze kutoka.+ Amefanya pingu zangu za shaba+ ziwe nzito.
8 Pia, nikiomba na kulilia msaada, yeye kwa kweli huizuia sala yangu.+
9 Amezuia njia zangu kwa mawe yaliyochongwa.+ Amepotosha barabara zangu.+
ד [Daʹleth]
10 Kwangu, yeye ni kama dubu anayevizia,+ kama simba mafichoni.+
11 Amevuruga njia zangu, naye huniachilia niwe bure tu. Amenifanya niwe mtu aliyeachwa ukiwa.+
12 Amekanyaga upinde wake,+ naye huniweka niwe shabaha ya mshale.+
ה [Heʼ]
13 Ameingiza ndani ya figo zangu mishale, wana wa podo lake.+
14 Nimekuwa kitu cha kuchekwa+ na watu wote wanaonipinga, nimekuwa kichwa cha wimbo wao mchana kutwa.+
15 Amenishibisha vitu vichungu.+ Amenijaza pakanga.+
ו [Waw]
16 Naye huvunja meno yangu kwa changarawe.+ Amenifanya nijikunje katika majivu.+
17 Wewe pia hunitupilia mbali ili nafsi yangu isiwe na amani. Nimepoteza kumbukumbu ya mema.+
18 Nami huendelea kusema: “Utukufu wangu umeangamia, na tarajio langu kutoka kwa Yehova.”+
ז [Zaʹyin]
19 Ukumbuke mateso yangu na hali yangu ya kukosa makao,+ pakanga na mmea wenye sumu.+
20 Hakika nafsi yako itakumbuka na kuinama juu yangu.+
21 Hili ndilo nitakalokumbuka moyoni mwangu.+ Ndiyo sababu nitaonyesha mtazamo wa kungojea.+
ח [Chehth]
22 Ni kutokana na matendo ya fadhili zenye upendo+ za Yehova kwamba hatujaisha,+ kwa maana hakika rehema zake hazitakoma.+
23 Ni mapya kila asubuhi.+ Uaminifu wako ni mwingi.+
24 “Yehova ni fungu langu,”+ nafsi yangu imesema, “ndiyo sababu nitaonyesha mtazamo wa kumngojea.”+
ט [Tehth]
25 Yehova ni mwema kwa yule anayemtumaini,+ kwa nafsi inayoendelea kumtafuta.+
26 Ni jambo jema kwa mtu kuungojea,+ ndiyo, kimyakimya,+ wokovu wa Yehova.+
27 Ni jambo jema kwa mwanamume kuchukua nira wakati wa ujana wake.+
י [Yohdh]
28 Acha aketi katika upweke na kukaa kimya,+ kwa sababu ameweka kitu fulani juu yake.+
29 Acha atie kinywa chake mavumbini.+ Labda kuna tumaini fulani.+
30 Acha ampe shavu lake yule anayempiga.+ Acha apate shibe yake ya shutuma.+
כ [Kaph]
31 Kwa maana Yehova hataendelea kuwatupilia mbali watu mpaka wakati usio na kipimo.+
32 Kwa maana, ijapokuwa ameleta huzuni,+ hakika pia ataonyesha rehema kulingana na wingi wa fadhili zake zenye upendo.+
33 Kwa maana si kutoka moyoni mwake mwenyewe kwamba amewatesa au kuwahuzunisha wana wa binadamu.+
ל [Laʹmedh]
34 Kuponda wafungwa wote wa dunia+ chini ya miguu ya mtu,+
35 Kugeuza kando hukumu ya mwanamume mbele za uso wa Aliye Juu Zaidi,+
36 Kupotosha mtu katika kesi yake, Yehova mwenyewe hayakubali mambo hayo.+
מ [Mem]
37 Basi, ni nani amesema kwamba jambo litokee wakati Yehova mwenyewe hakuamuru?+
38 Mambo mabaya na yaliyo mema hayatoki katika kinywa cha Aliye Juu Zaidi.+
39 Mwanadamu aliye hai, mwanamume, anawezaje kuzoea kulalamika+ kwa sababu ya dhambi yake?+
נ [Nun]
40 Na tutafute njia zetu na kuzichunguza,+ nasi turudi kabisa kwa Yehova.+
41 Acheni tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu aliye mbinguni:+
42 “Sisi wenyewe tumekosa, nasi tumejiendesha kwa uasi.+ Wewe mwenyewe hukusamehe.+
ס [Saʹmekh]
43 Umeweka kizuizi kwa hasira usiweze kufikiwa,+ nawe unaendelea kutufuatilia.+ Umeua; hukuonyesha huruma yoyote.+
44 Umeweka kizuizi cha wingu kubwa usiweze kufikiwa,+ ili sala isiweze kupenya.+
45 Unatufanya tuwe takataka na uchafu katikati ya vikundi vya watu.”+
פ [Peʼ]
46 Adui zetu wote wamefungua vinywa vyao juu yetu.+
47 Hofu na shimo vimekuwa vyetu,+ ukiwa na kuvunjika.+
48 Jicho langu huendelea kutiririka vijito vya maji kwa sababu ya kuvunjika kwa binti ya watu wangu.+
ע [ʽAʹyin]
49 Jicho langu limemwagika nalo halitatulia, hivi kwamba hakuna mapumziko,+
50 Mpaka Yehova atakapotazama chini na kuona kutoka mbinguni.+
51 Jicho langu limeitendea nafsi yangu vikali,+ kwa sababu ya binti wote wa jiji langu.+
צ [Tsa·dhehʹ]
52 Hakika adui zangu wameniwinda kama ndege,+ bila sababu.+
53 Wamenyamazisha uhai wangu shimoni kwenyewe,+ nao wakaendelea kunitupia mawe.
54 Maji yametiririka juu ya kichwa changu.+ Nimesema: “Hakika nitakatiliwa mbali!”+
ק [Qohph]
55 Nimeita jina lako, Ee Yehova, kutoka katika shimo la chini kabisa.+
56 Uisikilize sauti yangu.+ Usifiche sikio lako kwa ombi langu la kitulizo, kwa kilio changu cha kuomba msaada.+
57 Umekaribia katika siku ile ambayo niliendelea kukuita.+ Ukasema: “Usiogope.”+
ר [Rehsh]
58 Umechukua mashindano ya nafsi yangu, Ee Yehova.+ Umekomboa uhai wangu.+
59 Umeona kosa nililotendewa, Ee Yehova.+ Tafadhali fanya hukumu kwa ajili yangu.+
60 Umeona kisasi chao chote, fikira zao zote juu yangu.+
ש [Sin] au [Shin]
61 Umesikia shutuma zao, fikira zao zote juu yangu, Ee Yehova,+
62 Midomo ya wale wanaosimama kunipinga+ na kunong’ona kwao juu yangu mchana kutwa.+
63 Tazama wanapoketi na wanaposimama.+ Mimi ndiye kiini cha wimbo wao.+
ת [Taw]
64 Utawalipa tendo fulani, kulingana na kazi ya mikono yao, Ee Yehova.+
65 Utawapa dharau la moyo,+ laana yako kwao.+
66 Utawafuatilia katika hasira na kuwaangamiza+ chini ya mbingu za Yehova.+
א [ʼAʹleph]
4 Lo! jinsi inavyofifia dhahabu yenye kung’aa, dhahabu iliyo nzuri!+
Lo! jinsi mawe matakatifu+ yanavyomwagwa mbele ya barabara zote!+
ב [Behth]
2 Kwa habari ya wana wa Sayuni wenye thamani,+ waliopimwa uzito kwa kulinganishwa na dhahabu safi,
Lo! jinsi wamehesabiwa kama mitungi mikubwa ya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!+
ג [Giʹmel]
3 Hata mbwa-mwitu wametoa maziwa. Wamenyonyesha watoto wao.
ד [Daʹleth]
ה [Heʼ]
5 Wale waliokuwa wakila vitu vyenye kupendeza wameshikwa na mshangao barabarani.+
Wale waliokuwa wakilelewa katika nguo nyekundu+ wamekumbatia marundo ya majivu.+
ו [Waw]
6 Adhabu kwa kosa la binti ya watu wangu pia inakuwa kubwa kuliko adhabu kwa kosa la dhambi ya Sodoma,+
Lililoangamizwa kama kwa dakika moja, na ambalo hakuna mikono iliyojitokeza kulisaidia.+
ז [Zaʹyin]
7 Wanadhiri+ wake walikuwa safi kuliko theluji;+ walikuwa weupe kuliko maziwa.
Kwa kweli walikuwa wekundu+ kuliko marijani; kung’arishwa kwao kulikuwa kama yakuti.+
ח [Chehth]
8 Sura yao imekuwa nyeusi kuliko weusi wenyewe. Hawakutambuliwa barabarani.+
Ngozi yao imekauka juu ya mifupa yao.+ Imekauka kama mti.
ט [Tehth]
9 Wale waliouawa kwa upanga+ wamekuwa bora kuliko wale waliouawa kwa njaa,+
Kwa sababu hao hudhoofika, wakichomwa kwa sababu ya ukosefu wa mazao ya shambani.
י [Yohdh]
10 Mikono ya wanawake wenye huruma imetokosa watoto wao wenyewe.+
Wamekuwa kama mkate wa kufariji mtu wakati wa kuvunjika kwa binti ya watu wangu.+
כ [Kaph]
11 Yehova ametimiza ghadhabu yake.+ Amemwaga hasira yake inayowaka.+
Naye anawasha moto katika Sayuni, unaoteketeza misingi yake.+
ל [Laʹmedh]
12 Wafalme wa dunia na wakaaji wote wa nchi yenye kuzaa hawakuwa wameamini+
Kwamba mpinzani na adui wataingia katika malango ya Yerusalemu.+
מ [Mem]
13 Kwa sababu ya dhambi za manabii wake, makosa ya makuhani wake,+
Mlikuwa katikati yake wale wanaomwaga damu ya waadilifu.+
נ [Nun]
14 Wametanga-tanga kama vipofu+ barabarani.+ Wamechafuliwa na damu,+
Hivi kwamba hakuna wanaoweza kugusa mavazi yao.+
ס [Saʹmekh]
15 “Ondokeni njiani! Najisi!”+ Wamewapaazia sauti. “Ondokeni njiani! Ondokeni njiani! Msiguse!”+
Kwa maana wamekosa makao.+ Pia wametanga-tanga.+ Watu wamesema kati ya mataifa: “Hawatakaa tena kama wageni.+
פ [Peʼ]
16 Uso wa Yehova umewatawanya.+ Hatawatazama tena.+
Watu hawataonyesha kujali hata kwa walio makuhani.+ Hakika hawatawakubali hata walio wanaume wazee.”+
ע [ʽAʹyin]
17 Tukiwa tungali bado tunaishi, macho yetu huendelea kudhoofika bure kwa kutazamia msaada wetu.+
Wakati wa kutazama kwetu tumetazamia taifa ambalo haliwezi kuleta wokovu.+
צ [Tsa·dhehʹ]
18 Wamewinda hatua zetu+ hivi kwamba hakuna kutembea katika viwanja vyetu vya watu wote.
Mwisho wetu umekaribia. Siku zetu zimetimia, kwa maana mwisho wetu umekuja.+
ק [Qohph]
ר [Rehsh]
20 Pumzi ya mianzi ya pua zetu,+ mtiwa-mafuta wa Yehova,+ amenaswa katika shimo lao kubwa,+
Yule ambaye tumesema habari zake: “Tutaishi chini ya kivuli+ chake kati ya mataifa.”+
ש [Sin]
21 Furahi na kushangilia,+ Ee binti Edomu,+ wewe unayekaa katika nchi ya Usi.+
Kwako wewe pia kikombe kitapita.+ Utalewa na kujionyesha ukiwa uchi.+
ת [Taw]
22 Kosa lako, Ee binti Sayuni, limefikia mwisho wake.+ Hatakupeleka tena uhamishoni.+
Amegeuza fikira zake kwa kosa lako, Ee binti Edomu. Amefunua dhambi zako.+
5 Ee Yehova, ukumbuke yale yaliyotupata.+ Utazame, uone shutuma zetu.+
2 Fungu la urithi wetu limeenda kwa wageni, nyumba zetu kwa watu wa kutoka ugenini.+
3 Tumekuwa mayatima wasio na baba.+ Mama zetu ni kama wajane.+
4 Tumetumia pesa ili tunywe maji yetu wenyewe.+ Kuni zetu wenyewe zinatujia kwa bei.
5 Tumefuatiwa kwa ukaribu kwenye shingo zetu.+ Tumechoka. Hatukuachiwa pumziko lolote.+
6 Tumewapa mkono+ Misri;+ Ashuru,+ ili tushibe mkate.
7 Mababu zetu ndio wamefanya dhambi.+ Hawako tena. Lakini sisi, imekuwa lazima tuchukue makosa yao.+
8 Watumishi wametawala juu yetu.+ Hakuna anayetunyakua kutoka mkononi mwao.+
9 Tunauleta mkate wetu kwa kuhatarisha nafsi zetu,+ kwa sababu ya upanga wa nyika.
10 Ngozi yetu imekuwa moto kama tanuru, kwa sababu ya maumivu ya njaa.+
11 Wake wamenyenyekezwa katika Sayuni,+ mabikira katika majiji ya Yuda.
12 Wakuu wametundikwa kwa mkono wao.+ Hata nyuso za wanaume wazee hazikuheshimiwa.+
13 Hata vijana wameinua jiwe la kusagia la mkononi,+ na wavulana wamejikwaa chini ya kuni.+
14 Wanaume wazee wameacha kutoka langoni,+ vijana wamekomesha muziki wao wa vyombo.+
15 Furaha ya moyo wetu imekoma. Mchezo wetu wa dansi umebadilishwa uwe maombolezo matupu.+
16 Taji la kichwa chetu limeanguka.+ Ole wetu, sasa, kwa sababu tumefanya dhambi!+
17 Kwa sababu hiyo moyo wetu umekuwa mgonjwa.+ Kwa sababu ya mambo haya macho yetu yameingia giza,+
18 Kwa sababu ya mlima wa Sayuni ambao umefanywa ukiwa;+ mbweha wametembea juu yake.+
19 Lakini wewe, Ee Yehova, utaketi mpaka wakati usio na kipimo.+ Kiti chako cha ufalme ni cha kizazi baada ya kizazi.+
20 Kwa nini unatusahau milele,+ hivi kwamba unatuacha kwa siku nyingi?+
21 Uturudishe kwako,+ Ee Yehova, nasi tutarudi bila kukawia. Utuletee siku zilizo mpya kama katika zamani za kale.+
22 Hata hivyo, hakika umetukataa.+ Umetukasirikia sana.+