Mhubiri
1 Maneno ya mkutanishaji,+ mwana wa Daudi, mfalme katika Yerusalemu.+ 2 “Ubatili mkubwa zaidi!”+ mkutanishaji amesema, “ubatili mkubwa zaidi! Kila kitu ni ubatili!”+ 3 Mwanadamu anapata faida gani katika kazi yake yote iliyo ngumu anayoifanya+ kwa bidii chini ya jua?+ 4 Kizazi kinaenda,+ kizazi kinakuja;+ lakini dunia inasimama mpaka wakati usio na kipimo.+ 5 Pia jua limechomoza, na kushuka,+ nalo linajitahidi kwa nguvu kwenda mahali pake ambapo litachomoza tena.+
6 Upepo unaenda kusini, nao unazunguka kuelekea kaskazini.+ Unaendelea kuzungukazunguka sikuzote,+ nao unairudia mizunguko+ yake.
7 Mito yote ya wakati wa majira ya baridi kali+ inaenda baharini,+ hata hivyo bahari haijai.+ Mahali inapoenda mito hiyo ya majira ya baridi kali, hapo ndipo inarudi ili iende tena.+ 8 Mambo yote yanachosha;+ hakuna mtu anayeweza kuzungumza juu yake. Jicho halitosheki kuona,+ wala sikio halijai kwa sababu ya kusikia.+ 9 Lile ambalo limetokea, ndilo litakalotokea;+ na lile ambalo limefanywa, ndilo litakalofanywa; na kwa hiyo, hakuna jambo jipya chini ya jua.+ 10 Je, kuna lolote ambalo mtu anaweza kusema juu yake: “Ona hili; ni jipya”? Tayari limekuwako tangu wakati usio na kipimo.+ Jambo ambalo limetokea lilikuwako kabla ya wakati wetu.+ 11 Watu wa nyakati zilizopita hawakumbukwi, wala wale watakaokuja baadaye hawatakumbukwa.+ Nao pia hawatakumbukwa kati ya wale watakaokuja baadaye.+
12 Mimi, mkutanishaji, nilikuwa mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.+ 13 Nami nikakusudia moyoni mwangu kutafuta na kuchunguza jinsi hekima+ inavyohusiana na kila jambo ambalo limefanywa chini ya mbingu—shughuli yenye msiba ambayo Mungu amewapa wana wa binadamu wajishughulishe nayo.+ 14 Niliona kazi zote zilizofanywa chini ya jua,+ na, tazama! mambo yote yalikuwa ubatili na kufuatilia upepo.+
15 Lililopotoshwa haliwezi kunyooshwa,+ nalo linalokosekana haliwezi kuhesabiwa. 16 Mimi, naam, mimi mwenyewe nilisema moyoni mwangu:+ “Tazama! Mimi mwenyewe nimepata hekima nyingi kuliko yeyote aliyenitangulia katika Yerusalemu,+ nao moyo wangu mwenyewe umeona kwa wingi sana hekima na ujuzi.”+ 17 Nami nikauruhusu moyo wangu ujue hekima na wazimu,+ nami nimejua upumbavu,+ kwamba hayo pia ni kufuatilia upepo.+ 18 Kwa maana katika wingi wa hekima mna mambo mengi yenye kuudhi,+ hivi kwamba anayeongeza ujuzi anaongeza maumivu.+
2 Nilisema, naam mimi, moyoni mwangu:+ “Njoo basi, nikujaribu kwa kushangilia.+ Pia, uone mema.”+ Na tazama! hilo pia lilikuwa ubatili. 2 Nikasema juu ya kicheko: “Ni wazimu!”+ na juu ya shangwe:+ “Hii inafanya nini?”
3 Nikachunguza kwa moyo wangu kwa kuuchangamsha mwili wangu kwa divai,+ huku nikiuongoza moyo wangu kwa hekima,+ hata nipate kushika upumbavu mpaka nione kuna faida gani kwa wana wa binadamu katika mambo waliyofanya chini ya mbingu siku za maisha yao.+ 4 Nikafanya kazi kubwa zaidi.+ Nikajijengea nyumba;+ nikajipandia mashamba ya mizabibu.+ 5 Nikajifanyia mashamba na bustani,+ nikapanda humo aina zote za miti ya matunda. 6 Nikajifanyia vidimbwi vya maji+ ili kumwagilia maji msitu wenye miti.+ 7 Nikapata watumishi wa kiume na wajakazi,+ nikawa na wana waliozaliwa nyumbani mwangu.+ Pia, nikawa na mifugo, ng’ombe na kondoo kwa wingi kuliko wote walionitangulia katika Yerusalemu.+ 8 Pia nikajikusanyia fedha na dhahabu,+ na mali iliyo ya pekee kwa wafalme na wilaya za utawala.+ Nikajifanyia waimbaji wa kiume na wa kike+ na wale walio furaha tele+ ya wana wa binadamu, bibi, naam mabibi.+ 9 Nikawa mkuu zaidi na kuongezeka kuliko mtu yeyote aliyenitangulia katika Yerusalemu.+ Tena, nikaendelea kukaa na hekima yangu.+
10 Wala sikuyanyima macho yangu chochote ambacho yaliomba.+ Sikuunyima moyo wangu shangwe ya aina yoyote, kwa maana moyo wangu ulifurahia kazi yangu yote iliyo ngumu,+ nalo hilo likawa fungu langu katika kazi yangu yote iliyo ngumu.+ 11 Na mimi, naam, mimi nikageuka kuelekea kazi zangu zote ambazo mikono yangu ilikuwa imefanya na kuelekea kazi ngumu niliyokuwa nimejitahidi kuitimiza,+ na, tazama! kila kitu kilikuwa ubatili na kufuatilia upepo,+ wala hapakuwa na lolote lenye faida chini ya jua.+
12 Nami, naam mimi, nikageuka nione hekima+ na wazimu na upumbavu;+ kwa maana mtu wa udongo anayekuja baada ya mfalme anaweza kufanya nini? Jambo ambalo watu tayari wamefanya. 13 Nami, naam mimi, nikaona kwamba hekima ina faida kuliko upumbavu,+ kama vile nuru ilivyo na faida kuliko giza.+
14 Mtu yeyote mwenye hekima, macho yake yamo katika kichwa chake;+ lakini mjinga anaendelea kutembea katika giza tupu.+ Nami nimepata kujua, mimi pia, kwamba kuna mwisho mmoja ambao huwapata hao wote.+ 15 Nami mwenyewe nikasema moyoni mwangu:+ “Mwisho uleule unaompata mjinga+ utanipata mimi, naam mimi.”+ Kwa nini mimi basi, nikawa na hekima, hekima yenye kuzidi sana+ hivyo wakati huo? Kisha nikasema moyoni mwangu: “Hilo pia ni ubatili.” 16 Kwa maana mtu mwenye hekima hakumbukwi zaidi ya yule mjinga mpaka wakati usio na kipimo.+ Siku ambazo tayari zinakuja, kila mtu husahauliwa; naye mwenye hekima atakufa jinsi gani? Pamoja na mjinga.+
17 Nami nikauchukia uzima,+ kwa sababu ninavyoona ni kwamba kazi ambayo imefanywa chini ya jua ni yenye msiba,+ kwa maana kila jambo lilikuwa ni ubatili na kufuatilia upepo.+ 18 Nami, naam mimi, nikachukia kazi yangu yote iliyo ngumu ambayo niliifanya kwa bidii chini ya jua,+ ambayo ningemwachia mtu ambaye angekuja baada yangu.+ 19 Na ni nani anayejua kama atakuwa mwenye hekima au mpumbavu?+ Hata hivyo, atachukua usimamizi wa kazi yangu yote iliyo ngumu niliyoifanya kwa bidii ambayo ndani yake nilitumia hekima chini ya jua.+ Hilo pia ni ubatili. 20 Na mimi mwenyewe nikageuka niufanye moyo wangu ukate tamaa+ kuelekea kazi ngumu yote niliyokuwa nimefanya kwa bidii chini ya jua. 21 Kwa maana kuna mwanadamu ambaye amefanya kazi yake ngumu kwa hekima na kwa ujuzi na kwa ustadi,+ lakini mwanadamu ambaye hakufanyia kazi ngumu kitu hicho atapewa fungu lake huyo.+ Hilo pia ni ubatili na msiba mkubwa.+
22 Kwa maana mwanadamu hupata nini kwa ajili ya kazi yake yote iliyo ngumu na kwa ajili ya jitihada za moyo wake katika kufanya kazi ngumu chini ya jua?+ 23 Kwa maana siku zake zote, shughuli zake huleta maumivu na masumbuko,+ pia usiku moyo wake haulali kamwe.+ Hilo pia ni ubatili mtupu.
24 Kwa mwanadamu hakuna jambo bora kuliko kwamba ale, naam, anywe na kuifanya nafsi yake ione mema kwa sababu ya kazi yake ngumu.+ Hilo pia mimi nimeliona, naam mimi, ya kwamba linatoka kwenye mkono wa Mungu wa kweli.+ 25 Kwa maana ni nani ambaye hula+ na ni nani ambaye hunywa vizuri kuliko mimi?+
26 Kwa maana amempa mwanadamu aliye mwema mbele zake+ hekima na ujuzi na furaha,+ bali amempa mtenda-dhambi shughuli ya kukusanya na kuleta pamoja ili tu ampe mtu aliye mwema mbele za yule Mungu wa kweli.+ Hilo pia ni ubatili na kufuatilia upepo.+
3 Kuna wakati uliowekwa wa kila kitu,+ hata kuna wakati wa kila jambo chini ya mbingu: 2 wakati wa kuzaliwa+ na wakati wa kufa;+ wakati wa kupanda na wakati wa kung’oa kilichopandwa;+ 3 wakati wa kuua+ na wakati wa kuponya;+ wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga;+ 4 wakati wa kulia+ na wakati wa kucheka;+ wakati wa kuomboleza+ na wakati wa kurukaruka;+ 5 wakati wa kutupa mawe+ na wakati wa kukusanya mawe;+ wakati wa kukumbatia+ na wakati wa kuepuka kukumbatia;+ 6 wakati wa kutafuta+ na wakati wa kuacha kutafuta kilichopotea; wakati wa kuweka na wakati wa kutupa;+ 7 wakati wa kupasua+ na wakati wa kushona,+ wakati wa kukaa kimya+ na wakati wa kusema;+ 8 wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia;+ wakati wa vita+ na wakati wa amani.+ 9 Mtendaji ana faida gani katika jambo analofanyia kazi ngumu?+
10 Nimeona shughuli ambayo Mungu amewapa wana wa binadamu wajishughulishe nayo.+ 11 Amefanya kila kitu kiwe chenye kupendeza kwa wakati wake.+ Tena wakati usio na kipimo ameuweka ndani ya moyo wao,+ ili mwanadamu asiweze kugundua kazi ambazo Mungu wa kweli amefanya tangu mwanzo mpaka mwisho.+ 12 Nimekuja kujua kwamba hakuna jambo lingine bora kwao kuliko mtu kufurahi na kufanya mema maishani mwake;+ 13 na pia kwamba kila mtu ale, naam, anywe na kuona mema kwa ajili ya kazi yake yote iliyo ngumu.+ Hiyo ndiyo zawadi ya Mungu.+
14 Nimekuja kujua kwamba kila jambo ambalo Mungu wa kweli hufanya, litadumu mpaka wakati usio na kipimo.+ Haliongezewi kitu wala kuondolewa kitu;+ lakini Mungu wa kweli amelifanya,+ ili watu waogope kwa sababu yake.+
15 Jambo ambalo limekuwako, limekwisha kuwako, na litakalokuja, limekwisha kuwako;+ na Mungu wa kweli+ anatafuta kile kinachofuatiliwa.+
16 Tena, nimeona chini ya jua mahali pa haki palipokuwa na uovu na mahali pa uadilifu ulipokuwa uovu.+ 17 Mimi mwenyewe nimesema moyoni mwangu:+ “Mungu wa kweli atahukumu mwadilifu na mwovu+ pia, kwa maana hapo kuna wakati wa kila jambo na kuhusu kila kazi.”+
18 Mimi, naam mimi, nimesema moyoni mwangu kuhusu wana wa binadamu kwamba Mungu wa kweli atawachagua, ili wapate kuona kwamba wao wenyewe ni wanyama.+ 19 Kwa maana kuna mwisho ambao huwafikia wana wa binadamu na mwisho ambao huwafikia wanyama, nao hufikiwa na mwisho uleule.+ Anavyokufa mmoja, ndivyo anavyokufa yule mwingine;+ nao wote wana roho moja,+ hivi kwamba mwanadamu si bora kuliko mnyama, kwa kuwa yote ni ubatili. 20 Wote wanaenda mahali pamoja.+ Wote wametoka katika mavumbi,+ nao wote wanarudi mavumbini.+ 21 Ni nani anayejua roho ya wana wa binadamu, ikiwa inapanda juu; na roho ya mnyama, ikiwa inashuka chini duniani?+ 22 Nami nimeona kwamba hakuna jambo bora kuliko kwamba mwanadamu afurahie kazi zake,+ kwa maana hilo ndilo fungu lake; kwa kuwa ni nani atakayemleta aone mambo yatakayokuwako baada yake?+
4 Nami nikarudi nipate kuona matendo yote ya uonevu+ yanayofanywa chini ya jua, na, tazama! machozi ya wale wanaokandamizwa,+ lakini hawakuwa na mtu wa kuwafariji;+ nao wakandamizaji walikuwa na nguvu, hivi kwamba hawakuwa na mtu wa kuwafariji. 2 Nami nikawapongeza wafu ambao tayari walikuwa wamekufa badala ya wale wanaoishi waliokuwa wangali hai.+ 3 Kwa hiyo aliye afadhali kuliko hao wawili ni yule ambaye hajakuwapo bado,+ ambaye bado hajaona kazi yenye msiba inayofanywa chini ya jua.+
4 Nami nimeona kazi yote ngumu na ustadi wote katika kazi,+ ya kwamba maana yake ni mashindano kati ya mtu na mwenzake;+ hilo pia ni ubatili na kufuatilia upepo.
5 Mjinga anakunja mikono+ yake na kula nyama yake mwenyewe.+
6 Konzi moja ya pumziko ni afadhali kuliko konzi mbili za kazi ngumu na kufuatilia upepo.+
7 Mimi mwenyewe nikarudi nipate kuona ubatili ulio chini ya jua: 8 Kuna mtu mmoja, wala hakuna wa pili;+ naye hana mwana wala ndugu,+ lakini kazi yake ngumu haina mwisho. Pia, macho yake mwenyewe hayatosheki na utajiri:+ “Nami ninamfanyia nani kazi yote hii ngumu na kuinyima nafsi yangu mambo mazuri?”+ Hilo pia ni ubatili, nalo ni shughuli yenye msiba.+
9 Wawili ni afadhali kuliko mmoja,+ kwa maana wana thawabu nzuri kwa ajili ya kazi yao ngumu.+ 10 Kwa maana mmoja wao akianguka, yule mwingine anaweza kumwinua mwenzake.+ Lakini itakuwaje kwa yule aliye peke yake akianguka wakati ambapo hakuna mwingine wa kumwinua?+
11 Tena, wawili wakilala pamoja, watapata joto; lakini aliye peke yake anawezaje kupata joto?+ 12 Na mtu akiweza kumshinda nguvu mmoja aliye peke yake, wawili wakiwa pamoja wataweza kusimama dhidi yake.+ Nayo kamba yenye nyuzi tatu haiwezi kukatika upesi.
13 Mtoto mwenye uhitaji lakini mwenye hekima+ ni afadhali kuliko mfalme mzee lakini mjinga,+ ambaye haoni tena haja ya kukubali onyo.+ 14 Kwa maana ametoka gerezani akawe mfalme,+ ingawa katika ufalme wa huyu alizaliwa akiwa maskini.+ 15 Nimeona wote walio hai wanaotembea chini ya jua, jinsi inavyokuwa kwa mtoto wa pili, anayesimama mahali pa yule mwingine.+ 16 Hakuna mwisho wa watu wote, wote ambao aliwatangulia;+ wala watu baadaye hawatamshangilia,+ kwa maana hilo pia ni ubatili na kufuatilia upepo.+
5 Linda miguu+ yako wakati wowote unapoenda kwenye nyumba ya Mungu wa kweli; na usogee karibu usikie,+ badala ya kutoa dhabihu kama wanavyofanya wajinga,+ kwa maana hawajui kwamba wanalofanya ni baya.+
2 Usifanye haraka kuhusiana na kinywa chako; nao moyo wako,+ usiwe na haraka kusema neno mbele za Mungu wa kweli.+ Kwa maana Mungu wa kweli yuko mbinguni+ lakini wewe uko duniani. Ndiyo sababu maneno yako yanapaswa kuwa machache.+ 3 Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi,+ nayo sauti ya mjinga kwa sababu ya wingi wa maneno.+ 4 Wakati wowote unapoweka nadhiri kwa Mungu, usisite kuitimiza,+ kwa maana hapendezwi na wajinga.+ Kile unachoweka nadhiri, timiza.+ 5 Ni afadhali usiweke nadhiri,+ kuliko kuiweka na kukosa kuitimiza.+ 6 Usiruhusu kinywa chako kiufanye mwili wako utende dhambi,+ wala usiseme mbele ya malaika+ kwamba lilikuwa kosa.+ Kwa nini Mungu wa kweli akasirike kwa sababu ya sauti yako na kuiharibu kazi ya mikono yako?+ 7 Maana kwa sababu ya wingi wa shughuli kuna ndoto,+ pia kuna ubatili na maneno kwa wingi. Lakini mwogope Mungu wa kweli mwenyewe.+
8 Ukimwona mtu yeyote maskini akionewa na hukumu+ na uadilifu zikitwaliwa kijeuri katika wilaya ya utawala, usishangazwe na jambo hilo,+ kwa maana aliye juu zaidi kuliko yule aliye juu+ anaangalia,+ na kuna wale walio juu yao.
9 Pia, faida ya dunia iko kati yao wote;+ kwa ajili ya shamba mfalme mwenyewe ametumikiwa.+
10 Anayependa fedha hatatosheka na fedha, wala anayependa mali hatatosheka na mapato.+ Hilo pia ni ubatili.+
11 Vitu vizuri vinapoongezeka, hakika wenye kula vitu hivyo huongezeka.+ Naye mwenye vitu hivyo anapata faida gani, ila kuviangalia tu kwa macho yake?+
12 Usingizi wa mtumishi ni mtamu,+ bila kujali kama anakula kidogo au kingi; lakini wingi alio nao tajiri haumruhusu kulala.
13 Kuna msiba mbaya sana ambao nimeona chini ya jua: utajiri unaowekwa kwa ajili ya aliye nao na kumletea msiba.+ 14 Nao utajiri huo umepotea+ kwa sababu ya shughuli zenye msiba, naye amemzaa mwana wakati ambao hana chochote mkononi mwake.+
15 Alivyotoka mtu katika tumbo la mama yake, ndivyo atakavyoenda tena akiwa uchi,+ kama alivyokuja; wala hakuna chochote ambacho mtu anaweza kwenda nacho+ kwa ajili ya kazi yake ngumu, anachoweza kukichukua mkononi mwake.
16 Nao huu pia ni msiba mbaya sana: kama alivyokuja mtu, vivyo hivyo ataenda zake; na kuna faida gani kwa mtu anayefanya kazi ngumu sikuzote kwa ajili ya upepo?+ 17 Pia, siku zake zote yeye hula katika giza, akiwa na masumbuko makubwa kwelikweli,+ akiwa na ugonjwa na sababu ya kukasirika.
18 Tazama! Jambo bora zaidi ambalo mimi mwenyewe nimeona, ambalo linapendeza, ni kwamba mtu ale na anywe na kuona mema kwa sababu ya kazi yake yote iliyo ngumu+ anayoifanya kwa bidii chini ya jua kwa hesabu ya siku zote za maisha yake ambazo Mungu wa kweli amempa, kwa maana hilo ndilo fungu lake. 19 Pia kila mwanadamu ambaye Mungu amempa utajiri na mali,+ amempa hata na uwezo wa kula katika hizo+ na kuchukua fungu lake na kushangilia katika kazi yake ngumu.+ Hiyo ndiyo zawadi ya Mungu.+ 20 Kwa maana si mara nyingi atakumbuka siku za maisha yake, kwa maana Mungu wa kweli anamshughulisha kwa shangwe ya moyo wake.+
6 Kuna msiba ambao nimeuona chini ya jua, nao hutokea mara nyingi kati ya wanadamu: 2 mtu ambaye Mungu wa kweli humpa utajiri na mali na utukufu,+ na ambaye, katika nafsi yake, hana uhitaji wa chochote anachotamani,+ hata hivyo Mungu wa kweli hamruhusu kula kutokana nacho,+ bali mtu aliye mgeni+ tu anaweza kula. Hilo ni ubatili na ni ugonjwa mbaya. 3 Mwanamume akizaa mara mia moja,+ na aishi miaka mingi, mpaka siku za maisha yake ziwe nyingi,+ lakini nafsi yake haijatosheka na mambo mazuri+ na hata kaburi halijawa lake,+ lazima niseme kwamba mtu aliyezaliwa akiwa mfu ni bora kuliko huyo.+ 4 Kwa maana huyu amekuja bure naye huenda gizani, nalo jina lake litafunikwa kwa giza.+ 5 Hata jua lenyewe hakuliona, wala hakulijua.+ Huyu ana pumziko kuliko yule wa kwanza.+ 6 Hata ikiwa ameishi miaka elfu moja mara mbili na bado hajaona yaliyo mema,+ je, kila mtu haendi mahali pamoja?+
7 Kazi yote iliyo ngumu ya wanadamu hufanywa kwa ajili ya kinywa chao,+ lakini hata nafsi yao haishibi. 8 Kwa maana mtu mwenye hekima anapata faida gani kuliko mjinga?+ Mtu anayeteseka anapata nini kwa sababu ya kujua jinsi ya kutembea machoni pa watu walio hai? 9 Ni afadhali kuona kwa macho kuliko kutembea huku na huku kwa nafsi.+ Hilo pia ni ubatili na kufuatilia upepo.+
10 Chochote ambacho kimekuja kuwako, jina lake tayari limetangazwa, na imejulikana mwanadamu ni nini;+ naye hawezi kujitetea mbele ya mtu aliye na nguvu kuliko yeye.+
11 Kwa sababu kuna mambo mengi yanayosababisha ubatili mwingi,+ mwanadamu ana faida gani? 12 Kwa maana ni nani anayejua mwanadamu anapata mema gani maishani+ kwa hesabu ya siku za maisha yake ya ubatili, anapozitumia kama kivuli?+ Kwa maana ni nani anayeweza kumwambia mwanadamu litakalotokea baada yake chini ya jua?+
7 Jina ni bora kuliko mafuta mazuri,+ na siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa kwa mtu.+ 2 Ni afadhali kwenda katika nyumba ya maombolezo kuliko kwenda katika nyumba ya karamu,+ kwa sababu huo ndio mwisho wa wanadamu wote; naye aliye hai anapaswa kuliweka jambo hilo moyoni mwake. 3 Afadhali sikitiko kuliko kicheko,+ maana kwa kukunjamana uso moyo huwa afadhali.+ 4 Moyo wa watu wenye hekima umo katika nyumba ya maombolezo,+ lakini moyo wa wajinga umo katika nyumba ya kushangilia.+
5 Ni afadhali kusikia kemeo la mtu mwenye hekima+ kuliko kuwa mtu anayesikia wimbo wa wajinga.+ 6 Kwa maana kicheko cha mjinga+ ni kama sauti ya miiba chini ya chungu; na hilo pia ni ubatili. 7 Kwa kuwa uonevu mtupu unaweza kumfanya mtu mwenye hekima atende kiwazimu,+ na zawadi+ inaweza kuharibu moyo.+
8 Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake.+ Mtu mwenye subira ni bora kuliko mwenye roho ya majivuno.+ 9 Usiwe na haraka kuudhika katika roho yako,+ kwa maana kuudhika hukaa katika kifua cha wajinga.+
10 Usiseme: “Kwa nini siku za zamani zilikuwa bora kuliko hizi?”+ kwa maana hukuuliza hilo kwa hekima.+
11 Hekima pamoja na urithi ni nzuri na ni yenye faida kwa wale wanaoliona jua.+ 12 Kwa maana hekima ni ulinzi,+ kama vile pesa ni ulinzi;+ lakini faida ya ujuzi ni kwamba hekima huwahifadhi hai waliyo nayo.+
13 Ona kazi+ ya Mungu wa kweli, kwa maana ni nani anayeweza kunyoosha kitu alichokipotosha?+ 14 Katika siku njema uwe mwema,+ na katika siku yenye msiba ona kwamba Mungu wa kweli ameifanya hata hii sawasawa na ile,+ ili wanadamu wasipate kuvumbua chochote baada yao.+
15 Nimeona kila jambo katika siku zangu za ubatili.+ Yuko mwadilifu anayeangamia katika uadilifu wake,+ na yuko mwovu anayeendelea kuishi kwa muda mrefu katika ubaya wake.+
16 Usiwe mwadilifu kupita kiasi,+ wala kujionyesha kuwa na hekima kupita kiasi.+ Kwa nini ujiletee ukiwa?+ 17 Usiwe mwovu kupita kiasi,+ wala kuwa mpumbavu.+ Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?+ 18 Ni afadhali ushikilie upande mmoja, lakini usiachilie ule mwingine;+ kwa maana yeye anayemwogopa Mungu atatoka akiwa na zote hizo.+
19 Hekima ina nguvu zaidi kwa mwenye hekima kuliko watu kumi wenye mamlaka waliokuwa katika jiji.+ 20 Kwa maana hakuna mwanadamu aliye mwadilifu duniani ambaye huendelea kufanya mema na asifanye dhambi.+
21 Pia, usiweke moyoni mwako maneno yote ambayo huenda watu wakasema,+ ili kwamba usipate kumsikia mtumishi wako akikulaani.+ 22 Kwa maana moyo wako mwenyewe unajua vema kwamba hata mara nyingi wewe, naam hata wewe, umewalaani wengine.+
23 Mambo yote haya nimeyajaribu kwa hekima. Nilisema: “Nitakuwa na hekima.” Lakini ilikuwa mbali nami.+ 24 Lile ambalo limekuja kuwako liko mbali sana na ni lenye kina kirefu sana. Ni nani anayeweza kulitambua?+ 25 Mimi mwenyewe niligeuka, hata moyo wangu ukageuka,+ nipate kujua na kuchunguza na kutafuta hekima+ na sababu ya mambo,+ na kujua juu ya uovu wa ujinga na upumbavu wa wazimu;+ 26 nami nilikuwa nikivumbua: Jambo lenye maumivu zaidi ya kifo,+ nikampata mwanamke ambaye yeye mwenyewe ni nyavu za kuwinda na moyo wake ni nyavu za kukokota na ambaye mikono yake ni pingu.+ Mtu ni mwema mbele za macho ya Mungu wa kweli ikiwa anaponyoka kutoka kwake, lakini mtu anafanya dhambi ikiwa ananaswa naye.+
27 “Tazama! nimevumbua hili,” akasema mkutanishaji,+ “kitu kimoja kikichukuliwa baada ya kingine ili kujua jumla yake,+ 28 ambayo nafsi yangu imetafuta kwa kuendelea, wala sijaiona. Nimemwona mwanamume mmoja kati ya elfu moja,+ lakini sijamwona mwanamke mmoja kati yao wote.+ 29 Tazama! Nimeona hili peke yake, ya kwamba Mungu wa kweli aliwafanya wanadamu wakiwa wanyoofu,+ lakini wao wenyewe wametafuta mipango mingi.”+
8 Ni nani aliye kama mwenye hekima?+ Na ni nani anayeweza kujua tafsiri ya jambo?+ Hekima ya mwanadamu huufanya uso wake ung’ae, na hata ukali wa uso wake ubadilike uwe afadhali.+
2 Nasema: “Shika agizo la mfalme,+ na ufanye hivyo kwa kujali kiapo cha Mungu.+ 3 Usifanye haraka kuondoka mbele yake.+ Usisimame katika jambo baya.+ Kwa maana yote anayopenda kufanya, atafanya.+ 4 Kwa sababu neno la mfalme ndilo nguvu za kudhibiti;+ na ni nani anayeweza kumwambia: ‘Unafanya nini?’”
5 Anayeishika amri hatajua jambo lolote lenye msiba,+ na moyo wenye hekima utajua wakati na hukumu.+ 6 Kwa maana kuna wakati na hukumu hata kwa kila jambo,+ kwa sababu misiba iliyo juu ya wanadamu ni mingi.+ 7 Kwa maana hakuna mtu anayejua yatakayokuja kuwako,+ kwa sababu ni nani anayeweza kumwambia jinsi yatakavyokuja kuwa?
8 Hakuna mwanadamu aliye na nguvu juu ya roho ili kuizuia roho;+ wala hakuna nguvu zozote za kuzuia katika siku ya kifo;+ wala hakuna kuachiliwa katika vita.+ Wala uovu hautawaokoa wanaouzoea.+
9 Yote haya nimeyaona, nikatia moyoni mwangu kila kazi ambayo imefanywa chini ya jua, wakati ambao mwanadamu amemtawala mwanadamu kwa kumuumiza.+ 10 Lakini, ingawa iko hivyo, nimewaona waovu wakizikwa,+ jinsi walivyokuja na jinsi walivyokuwa wakiondoka mahali patakatifu+ na kusahaulika katika jiji walikotenda hivyo.+ Hilo pia ni ubatili.
11 Kwa maana hukumu juu ya kazi mbaya haikutekelezwa upesi,+ ndiyo sababu moyo wa wana wa binadamu umeazimia kabisa ndani yao kutenda yaliyo mabaya.+ 12 Ijapokuwa huenda mtenda-dhambi akawa anatenda yaliyo mabaya+ mara mia moja na kuendelea kwa muda mrefu anavyopenda, ninajua pia kwamba mambo yatawaendea vyema wale wanaomwogopa Mungu+ wa kweli, kwa sababu walimwogopa.+ 13 Lakini mambo hayatakuwa mema kwa mwovu,+ wala hatarefusha siku zake zilizo kama kivuli,+ kwa sababu hamwogopi Mungu.+
14 Kuna ubatili unaofanyika duniani, kwamba kuna watu waadilifu wanaopatwa na mambo kana kwamba ni kazi ya waovu,+ na kuna waovu wanaopatwa na mambo kana kwamba ni kazi ya waadilifu.+ Nilisema hilo pia ni ubatili.
15 Nami nikapongeza kushangilia,+ kwa sababu wanadamu hawana jambo bora chini ya jua kuliko kula na kunywa na kushangilia, na kwamba hilo liambatane nao katika kazi yao ngumu muda wa siku za maisha yao,+ ambazo Mungu wa kweli amewapa chini ya jua.+ 16 Kupatana na hayo, niliutia moyo wangu+ kujua hekima na kuona shughuli inayofanywa duniani,+ kwa sababu kuna mtu ambaye macho yake hayapati usingizi, mchana wala usiku.+
17 Nami nikaona kazi yote ya Mungu wa kweli,+ jinsi ambavyo wanadamu hawawezi kuvumbua kazi ambayo imefanywa chini ya jua;+ lakini hata wanadamu waendelee namna gani kufanya kazi kwa bidii kutafuta, bado hawagundui.+ Na hata wakisema kwamba wana hekima ya kutosha kuweza kujua,+ hawawezi kuvumbua.+
9 Kwa maana nilitia yote haya moyoni mwangu, na kutafuta yote haya,+ kwamba waadilifu na wenye hekima na kazi zao, wako katika mkono wa Mungu wa kweli.+ Wanadamu hawajui upendo wala chuki ambazo zimekuwa kabla yao.+ 2 Wote ni sawa katika lile ambalo wote wanalo.+ Kuna mwisho mmoja+ kwa mwadilifu+ na kwa mwovu,+ mtu mwema na mtu safi na mtu asiye safi, na mtu anayetoa dhabihu na mtu ambaye hatoi dhabihu. Mtu mwema ni sawa na mtenda-dhambi;+ mtu anayekula kiapo ni sawa na yeyote yule ambaye ameogopa kiapo rasmi.+ 3 Hili ndilo jambo lenye msiba katika yote ambayo yamefanywa chini ya jua, ya kwamba, kwa sababu wote hufikiwa na mwisho uleule,+ moyo wa wana wa binadamu pia umejaa mabaya;+ na kuna wazimu+ mioyoni mwao wakati wa maisha yao, na baada ya hayo—ni kwenda kwa wafu!+
4 Kwa maana kwa yeyote yule ambaye ameunganishwa na wote walio hai kuna uhakika, kwa sababu mbwa aliye hai+ ni afadhali kuliko simba aliyekufa.+ 5 Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa;+ lakini wafu, hawajui lolote kamwe,+ wala hawana malipo tena, kwa maana kumbukumbu lao limesahauliwa.+ 6 Pia, upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea,+ na mpaka wakati usio na kipimo hawana fungu lolote tena katika chochote ambacho kitafanywa chini ya jua.+
7 Nenda, ukale chakula chako kwa kushangilia na kunywa divai yako kwa moyo mchangamfu,+ kwa sababu tayari Mungu wa kweli amependezwa na kazi zako.+ 8 Katika kila pindi, mavazi yako na yawe meupe,+ wala kichwa chako kisikose mafuta.+ 9 Furahia maisha pamoja na mke unayempenda+ siku zote za maisha yako yaliyo ya ubatili ambayo umepewa na Yeye chini ya jua, siku zote za hali yako iliyo ya ubatili, kwa maana hilo ndilo fungu lako maishani+ na katika kazi yako ngumu unayoifanya kwa bidii chini ya jua. 10 Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote,+ kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi+ wala hekima+ katika Kaburi,*+ mahali unapokwenda.+
11 Nilirudi, nikaona chini ya jua kwamba si wenye mbio wanaoshinda katika mbio,+ wala wenye nguvu wanaoshinda katika pigano,+ wala pia wenye hekima wanaopata chakula,+ wala pia wenye uelewaji wanaokuwa na utajiri,+ wala wenye ujuzi wanaopata kibali;+ kwa sababu wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote.+ 12 Kwa maana mwanadamu+ pia hajui wakati wake.+ Kama vile samaki wanaonaswa katika wavu mbovu,+ na kama ndege wanaonaswa katika mtego,+ ndivyo wana wa binadamu wenyewe wanavyonaswa wakati wenye msiba,+ unapowaangukia ghafula.+
13 Pia nikaona jambo hili kuhusu hekima chini ya jua—nalo lilikuwa kuu kwangu: 14 Kulikuwa na jiji dogo, na wanaume waliokuwamo walikuwa wachache; mfalme mkuu akaja juu yake, akalizunguka na kujenga ngome+ zilizo kubwa ili kulishambulia. 15 Ndani yake mkapatikana mtu mwenye uhitaji lakini mwenye hekima, naye akaliokoa jiji hilo kwa sababu ya hekima yake.+ Lakini hakuna mtu aliyemkumbuka yule mtu mhitaji.+ 16 Na mimi mwenyewe nikasema: “Hekima ni bora kuliko uwezo;+ hata hivyo hekima ya mtu mwenye uhitaji hudharauliwa, na maneno yake hayasikilizwi.”+
17 Maneno ya wenye hekima yanayosemwa kwa utulivu husikiwa+ zaidi kuliko kelele za mtu anayetawala kati ya wajinga.+
18 Hekima ni bora kuliko silaha za vita, na mtenda-dhambi mmoja tu anaweza kuharibu mambo mengi mema.+
10 Nzi waliokufa ndio hufanya mafuta ya mtengenezaji wa marashi+ yanuke, na kutoa povu. Ndivyo upumbavu kidogo unavyomfanya mtu mwenye thamani kwa sababu ya hekima na utukufu.+
2 Moyo wa mwenye hekima upo upande wa mkono wake wa kuume,+ lakini moyo wa mjinga upo upande wa mkono wake wa kushoto.+ 3 Pia, katika njia yoyote ambayo mtu mpumbavu anatembea,+ moyo wake mwenyewe una kasoro, naye hakika humwambia kila mtu kwamba yeye ni mpumbavu.+
4 Roho ya mtawala ikiinuka juu yako, usiondoke mahali pako,+ kwa maana utulivu wenyewe hutuliza dhambi kubwa.+
5 Kuna jambo lenye msiba ambalo nimeona chini ya jua, kama wakati ambapo kuna kosa+ linalotokea kwa sababu ya mtu aliye katika mamlaka:+ 6 Upumbavu umewekwa katika vyeo vingi vya juu,+ lakini matajiri huendelea kukaa tu katika hali ya chini.
7 Nimeona watumishi juu ya farasi lakini wakuu wakitembea kwa miguu juu ya nchi kama watumishi tu.+
8 Anayechimba shimo yeye mwenyewe ataanguka ndani yake;+ naye anayebomoa ukuta wa mawe ataumwa na nyoka.+
9 Anayechimba mawe atajiumiza mwenyewe kwayo. Naye anayepasua miti atalazimika kujihadhari nayo.+
10 Ikiwa kifaa cha chuma kimepoteza makali na mtu asikinoe,+ ndipo atatumia nguvu zake mwenyewe. Kwa hiyo kutumia hekima kwa mafanikio huleta faida.+
11 Nyoka akiuma kabla ya kuchezeshwa,+ basi mtu anayejua kuutumia ulimi hapati faida yoyote.
12 Maneno ya kinywa cha mwenye hekima huleta kibali,+ bali mjinga humezwa na midomo yake.+ 13 Mwanzo wa maneno ya kinywa chake ni upumbavu,+ na mwisho wa kinywa chake ni wazimu wenye msiba. 14 Na mpumbavu husema maneno mengi.+
Mwanadamu hajui jinsi mambo yatakavyokuwa; na yale yatakayotokea baada yake, ni nani anayeweza kumwambia?+
15 Kazi ngumu ya wajinga huwachosha,+ kwa sababu hakuna hata mmoja amekuja kujua jinsi ya kwenda jijini.+
16 Ewe nchi, itakuwaje kwako wakati mfalme wako ni mvulana+ na wakuu wako huendelea kula hata asubuhi? 17 Ewe nchi, una furaha wakati mfalme wako ni mwana wa watu wenye vyeo na wakuu wako hula wakati unaofaa ili kuwa na uwezo, wala si kwa ajili ya kunywa tu.+
18 Kwa sababu ya uvivu mkubwa paa ya jengo hubonyea, na kwa kushusha mikono, nyumba huvuja.+
19 Mkate ni kwa ajili ya kicheko cha wafanyakazi, na divai hufanya maisha yafurahishe;+ lakini pesa ndizo hutokeza jibu katika mambo yote.+
20 Hata katika chumba chako cha kulala usimlaani mfalme,+ na katika chumba cha ndani unapolala usimlaani yeyote aliye tajiri;+ kwa maana kiumbe kinachoruka cha mbinguni kitafikisha sauti hiyo na kiumbe chenye mabawa kitasema jambo hilo.+
11 Tupa mkate+ wako juu ya uso wa maji,+ kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.+ 2 Wape fungu watu saba, au hata wanane,+ kwa maana hujui ni msiba gani utakaotokea duniani.+
3 Mawingu yakijaa maji, humwaga mvua kubwa juu ya dunia;+ nao mti ukianguka kuelekea kusini au kaskazini, mahali hapo hapo ulipoanguka+ ndipo utakapokuwa.
4 Anayeuangalia upepo hatapanda mbegu; naye anayetazama mawingu hatavuna.+
5 Kama vile usivyoijua njia ya roho katika mifupa ndani ya tumbo lake mwenye mimba,+ vivyo hivyo hujui kazi ya Mungu wa kweli, anayefanya mambo yote.+
6 Asubuhi panda mbegu zako na mpaka jioni usiache mkono wako upumzike;+ kwa maana hujui ni wapi hii itafanikiwa,+ hapa au pale, au ikiwa zote mbili zitakuwa njema.
7 Nuru ni tamu pia, na ni vema macho yaone jua;+ 8 kwa maana mwanadamu akiishi miaka mingi, na aishangilie hiyo yote.+ Na azikumbuke siku za giza,+ ingawa huenda zikawa nyingi; kila siku ambayo imekuja ni ubatili.+
9 Ewe kijana, shangilia+ katika ujana wako, na moyo wako ukufanyie mema siku za ujana wako, nawe utembee katika njia za moyo wako na katika mambo ambayo macho yako yameona.+ Lakini ujue kwamba kwa ajili ya mambo yote hayo, Mungu wa kweli atakuleta hukumuni.+ 10 Kwa hiyo, ondoa masumbuko moyoni mwako, nawe uondolee mbali msiba kutoka katika mwili wako;+ kwa maana ujana na upeo wa maisha ni ubatili.+
12 Mkumbuke, sasa, Muumba wako Mkuu katika siku za ujana wako,+ kabla siku zenye msiba hazijaja,+ au miaka iwe imefika wakati utasema:+ “Sipendezwi nayo”;+ 2 kabla jua na nuru na mwezi na nyota havijawa na giza,+ na mawingu yamerudi, kisha mvua kubwa; 3 katika siku ambayo watunzaji wa nyumba+ wanatetemeka, nao wanaume wenye nguvu wameinama,+ na wanawake wanaosaga+ wameacha kufanya kazi kwa sababu wamekuwa wachache, na mabibi wanaochungulia madirishani+ wameona giza; 4 na milango inayoelekea barabarani imefungwa,+ wakati sauti ya jiwe la kusaga inaposhuka,+ naye mtu huamshwa na sauti ya ndege, na mabinti wote wa wimbo hutoa sauti ya chini.+ 5 Pia, wameogopa chochote kilicho juu, na kuna vitisho njiani. Nao mti unaozaa lozi hutoa maua,+ naye panzi hujikokota, na pilipili hupasuka, kwa sababu mwanadamu anakwenda kwenye nyumba yake ya muda mrefu,+ nao waombolezaji wamezunguka barabarani;+ 6 kabla ile kamba ya fedha haijaondolewa, na bakuli la dhahabu kuvunjwa,+ na mtungi ulio kwenye bubujiko la maji kuvunjwa, na gurudumu la maji kuvunjwa. 7 Kisha mavumbi huirudia nchi+ kama yalivyokuwa, nayo roho+ yenyewe humrudia Mungu+ wa kweli aliyeitoa.+
8 “Ubatili mkubwa zaidi!” akasema mkutanishaji,+ “Kila kitu ni ubatili.”+
9 Na ijapokuwa mkutanishaji alipata kuwa na hekima,+ pia aliendelea kuwafundisha watu ujuzi,+ naye alitafakari na kutafuta kwa bidii,+ apate kupanga methali nyingi kwa utaratibu.+ 10 Mkutanishaji alijitahidi kutafuta maneno yenye kupendeza+ na kuandika maneno sahihi ya kweli.+
11 Maneno ya wenye hekima ni kama michokoo ya kuongoza ng’ombe,+ na kama tu misumari iliyopigiliwa ndani,+ ndivyo walivyo wale wanaoshughulika mno kukusanya maneno; wametolewa kutoka kwa mchungaji mmoja.+ 12 Kuhusu jambo lingine lolote zaidi ya haya, mwanangu, jihadhari: Hakuna mwisho wa kutungwa kwa vitabu vingi, na kushughulika navyo sana huuchosha mwili.+
13 Huu ndio mwisho wa mambo, kila jambo limekwisha sikiwa: Mwogope Mungu wa kweli+ na kushika amri zake.+ Kwa maana huo ndio wajibu wote wa mwanadamu. 14 Kwa maana Mungu wa kweli ataleta kila kazi katika hukumu, kuhusiana na kila jambo lililofichwa, liwe jema au baya.+
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.