Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Methali 1:1-31:31
  • Methali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Methali
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Methali

Methali

1 Methali+ za Sulemani+ mwana wa Daudi,+ mfalme wa Israeli,+ 2 ili mtu ajue hekima+ na nidhamu,+ na kutambua maneno ya uelewaji,+ 3 apokee nidhamu+ ambayo humpa mtu ufahamu,+ uadilifu+ na haki+ na unyoofu,+ 4 kuwapa werevu wale wasio na uzoefu,+ kumpa kijana ujuzi+ na uwezo wa kufikiri.+

5 Mtu mwenye hekima atasikiliza na kupata mafundisho zaidi,+ naye mtu mwenye uelewaji ndiye anayepata mwongozo stadi,+ 6 ili kuelewa methali na mafumbo,+ maneno ya watu wenye hekima+ na vitendawili vyao.+

7 Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa ujuzi.+ Wapumbavu wamedharau hekima na nidhamu.+

8 Mwanangu, sikiliza nidhamu ya baba yako,+ wala usiiache sheria ya mama yako.+ 9 Kwa maana hizo ni shada lenye kuvutia kichwani pako+ na mkufu bora shingoni pako.+

10 Mwanangu, watenda-dhambi wakijaribu kukushawishi, usikubali.+ 11 Wakizidi kusema: “Haya, njoo pamoja nasi. Na tuvizie ili kumwaga damu.+ Na tujifiche ili kuwashambulia, bila sababu, watu wasio na hatia.+ 12 Na tuwameze wakiwa hai+ kama Kaburi,*+ naam, wakiwa wazima, kama wale wanaoshuka shimoni.+ 13 Na tupate namna zote za vitu vyenye thamani.+ Na tujaze nyara katika nyumba zetu.+ 14 Unapaswa kupiga kura yako katikati yetu. Nasi sote tuwe na mfuko mmoja tu”+— 15 mwanangu, usiende njiani pamoja nao.+ Zuia mguu wako usiende katika barabara yao.+ 16 Maana miguu yao hukimbilia ubaya mtupu,+ nao huharakisha kwenda kumwaga damu.+ 17 Kwa maana wavu hutandikwa pasipo kusudi mbele ya macho ya kiumbe chochote chenye mabawa.+ 18 Basi wao wenyewe huwavizia ili kumwaga damu yao;+ hujificha ili wazishambulie nafsi zao.+ 19 Hayo ndiyo mapito ya kila mtu anayepata faida isiyo ya haki.+ Huiondoa nafsi yao walio nayo.+

20 Hekima ya kweli+ huendelea kulia kwa sauti kubwa barabarani.+ Hutoa sauti yake katika viwanja vya watu wote.+ 21 Inaita penye mwisho wa upande wa juu wa barabara yenye kelele.+ Husema maneno yake katika mahali pa kuingilia malango ya jiji:+

22 “Ninyi msio na uzoefu mtaendelea mpaka wakati gani kupenda kutokuwa na ujuzi?+ Nanyi wenye dhihaka mtaendelea mpaka wakati gani kujitakia dhihaka tupu?+ Nanyi wajinga mtaendelea mpaka wakati gani kuchukia ujuzi?+ 23 Geukeni mpate karipio langu.+ Ndipo mimi nitafanya roho yangu ibubujike juu yenu;+ nitawajulisha maneno yangu.+ 24 Kwa sababu nimewaita lakini mnaendelea kukataa.+ Nimenyoosha mkono wangu lakini hakuna yeyote anayetazama.+ 25 Nanyi mnazidi kupuuza mashauri yangu yote,+ wala hamkukubali karipio langu.+ 26 Mimi pia, kwa upande wangu, nitacheka taabu yenu wenyewe,+ na jambo mnalohofu litakapokuja nitafanya mzaha,+ 27 jambo mnalohofu litakapokuja kama dhoruba, na taabu yenu wenyewe itakapofika kama upepo wa dhoruba,+ na shida na nyakati ngumu zitakapowapata.+ 28 Wakati huo wataendelea kuniita, lakini sitaitika;+ wataendelea kunitafuta, lakini hawatanipata,+ 29 kwa sababu walichukia ujuzi,+ nao hawakuchagua kumwogopa Yehova.+ 30 Hawakukubali shauri langu;+ walipuuza makaripio yangu yote.+ 31 Basi watakula matunda ya njia yao,+ nao watashiba mashauri yao wenyewe.+ 32 Kwa maana uasi+ wa wasio na uzoefu utawaua wao,+ na kutojali kwa wajinga kutawaangamiza wao.+ 33 Kwa habari yake mtu anayenisikiliza, yeye atakaa salama+ wala hatasumbuliwa na hofu ya msiba.”+

2 Mwanangu, ikiwa utapokea maneno yangu+ na kujiwekea amri zangu kama hazina,+ 2 ili kwa sikio lako usikilize hekima kwa makini,+ ili uelekeze moyo wako kwenye utambuzi,+ 3 ikiwa utaita uelewaji+ na kupaaza sauti yako uite utambuzi,+ 4 ikiwa utaendelea kuutafuta kama fedha,+ na kuendelea kuutafuta kama hazina zilizofichika,+ 5 ndipo utakapoelewa kumwogopa+ Yehova, nawe utapata kumjua Mungu.+ 6 Kwa maana Yehova mwenyewe anatoa hekima;+ kinywani mwake hutoka ujuzi na utambuzi.+ 7 Naye atawawekea wanyoofu hazina ya hekima inayotumika;+ yeye ni ngao kwa wale wanaotembea kwa utimilifu,+ 8 kwa kushika mapito ya hukumu,+ naye atailinda njia ya washikamanifu wake.+ 9 Ndipo utakapoelewa uadilifu na hukumu na unyoofu, njia yote ya yaliyo mema.+

10 Hekima inapoingia moyoni mwako+ na ujuzi kupendeza nafsi yako,+ 11 uwezo wa kufikiri utakutunza,+ utambuzi utakulinda,+ 12 ili kukukomboa kutoka katika njia mbaya,+ na kutoka kwa mtu anayesema mambo mapotovu,+ 13 kutoka kwa wale wanaoacha mapito ya unyoofu ili watembee katika njia za giza,+ 14 kutoka kwa wale wanaofurahia kufanya mabaya,+ wanaoshangilia mambo mapotovu ya ubaya;+ 15 wale ambao mapito yao yamepotoka na ambao kwa ujumla ni wenye hila maishani mwao;+ 16 ili huo ukukomboe kutoka kwa mwanamke, naam, kutoka kwa mwanamke mgeni+ ambaye amefanya maneno yake kuwa laini,+ 17 anayemwacha rafiki wa ujana wake+ na ambaye amelisahau agano la Mungu wake.+ 18 Kwa maana nyumba yake huzama ndani ya kifo na mapito yake huzama ndani kwa wale wasiojiweza katika kifo.+ 19 Hakuna yeyote kati ya wale wanaolala naye atakayerudi, wala hawatayafikia tena mapito ya walio hai.+

20 Kusudi ni kwamba upate kutembea katika njia ya watu wema+ na kwamba upate kushika mapito ya waadilifu.+ 21 Kwa maana wanyoofu ndio watakaokaa duniani,+ na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake.+ 22 Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani;+ nao wenye hila, watang’olewa kutoka ndani yake.+

3 Mwanangu, usiisahau sheria yangu,+ na moyo wako upate kushika amri zangu,+ 2 kwa sababu utaongezewa+ urefu wa siku na miaka ya uzima+ na amani. 3 Fadhili zenye upendo na ukweli zisikuache.+ Zifunge shingoni pako.+ Ziandike kwenye kibao cha moyo wako,+ 4 na hivyo upate kibali na ufahamu mzuri machoni pa Mungu na machoni pa mtu wa udongo.+ 5 Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote+ wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe.+ 6 Mtambue yeye katika njia zako zote,+ naye atanyoosha mapito yako.+

7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe.+ Mwogope Yehova na ujiepushe na ubaya.+ 8 Na hilo liwe maponyo+ kwenye kitovu chako na burudisho kwa mifupa yako.+

9 Mheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye thamani+ na kwa matunda ya kwanza ya mazao yako yote.+ 10 Ndipo maghala yako yatakapojazwa kwa wingi;+ nayo mitungi yako ya shinikizo itafurika divai mpya.+

11 Ewe mwanangu, usikatae nidhamu ya Yehova;+ wala usichukie karipio lake,+ 12 kwa sababu yeye ambaye Yehova anampenda,+ humkaripia, kama vile baba anavyomkaripia mwana anayemfurahia.+

13 Mwenye furaha ni mtu ambaye amepata hekima,+ na mtu anayepata utambuzi,+ 14 kwa maana kuwa nayo kama mapato ni bora kuliko kuwa na mapato ya fedha na kuwa nayo kama mazao ni bora kuliko dhahabu+ yenyewe. 15 Ina thamani kuliko marijani,+ na mapendezi yako mengine yote hayawezi kulinganishwa nayo. 16 Urefu wa siku uko katika mkono wake wa kuume;+ na katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na utukufu.+ 17 Njia zake ni njia za uzuri, na barabara zake zote ni amani.+ 18 Ni mti wa uzima+ kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana+ wataitwa wenye furaha.+

19 Kwa hekima Yehova mwenyewe aliuweka msingi wa dunia.+ Aliziweka mbingu imara kwa utambuzi.+ 20 Kwa ujuzi wake vilindi vya maji vilitenganishwa,+ nazo anga zenye mawingu hutoa matone ya mvua nyepesi.+ 21 Mwanangu, zisiondoke machoni pako.+ Linda hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri,+ 22 nazo zitakuwa uzima kwa nafsi yako+ na kitu chenye kuvutia shingoni pako.+ 23 Ndipo utakapotembea kwa usalama+ njiani mwako, na hata mguu wako hautagonga chochote.+ 24 Unapolala hutahofu;+ nawe hakika utalala, nao usingizi wako utakuwa mtamu.+ 25 Hutaogopa kitu chochote chenye kuogopesha ghafula,+ wala dhoruba inayowajia waovu, kwa sababu inakuja.+ 26 Kwa maana Yehova mwenyewe atakuwa uhakika wako,+ naye hakika ataepusha mguu wako usinaswe.+

27 Usiwanyime watu mema wanayostahili,+ mkono wako ukiwa na uwezo wa kuyafanya.+ 28 Usimwambie mwenzako: “Nenda, kisha urudi na kesho nitakupa,” na kumbe una kitu anachohitaji.+ 29 Usimtungie mwenzako jambo lolote baya,+ wakati anapokaa nawe na kujiona salama.+ 30 Usigombane na mtu bila sababu,+ ikiwa hajakufanyia ubaya wowote.+

31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri,+ wala kuchagua yoyote kati ya njia zake.+ 32 Kwa maana mtu mwenye hila+ ni chukizo kwa Yehova,+ lakini urafiki Wake uko pamoja na watu wanyoofu.+ 33 Laana ya Yehova iko juu ya nyumba ya mwovu,+ lakini huyabariki makao ya waadilifu.+ 34 Atawadhihaki+ wale wenye dhihaka;+ lakini atawapa wapole kibali.+ 35 Wenye hekima watapata heshima,+ lakini wajinga wanainua aibu.+

4 Enyi wana, sikilizeni nidhamu ya baba+ na kutega sikio, ili mpate kujua uelewaji.+ 2 Kwa maana hakika nitawapa ninyi mafundisho mema.+ Sheria yangu msiiache.+ 3 Kwa maana nilikuwa mwana halisi kwa baba yangu,+ mchanga na wa pekee kwa mama yangu.+ 4 Naye baba alikuwa akinifundisha+ na kuniambia: “Moyo+ wako upate kushika sana maneno yangu.+ Shika amri zangu, uendelee kuishi.+ 5 Jipatie hekima,+ jipatie uelewaji.+ Usisahau, wala usiache maneno ya kinywa changu.+ 6 Usiiache, nayo itakutunza. Ipende, nayo itakulinda. 7 Hekima ndilo jambo kuu. Jipatie hekima;+ na pamoja na vyote unavyojipatia, jipatie uelewaji.+ 8 Iheshimu sana, nayo itakuinua. Itakutukuza+ kwa sababu unaikumbatia.+ 9 Itakuvika shada lenye kuvutia kichwani pako;+ na kukuvika taji lenye kupendeza.”+

10 Mwanangu, sikia maneno yangu na kuyakubali.+ Ndipo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.+ 11 Nitakufundisha katika njia ya hekima;+ nitakufanya utembee katika mapito ya unyoofu.+ 12 Unapotembea, mwendo wako hautasongwa;+ na ukikimbia, hutajikwaa.+ 13 Shika nidhamu;+ usiiache.+ Ilinde, kwa maana hiyo ndiyo uzima wako.+

14 Usiingie katika pito la waovu,+ wala usitembee na kuingia moja kwa moja katika njia ya wabaya.+ 15 Iepuke,+ usiipite;+ geuka mbali nayo, nawe uende zako.+ 16 Kwa maana hawalali wasipotenda jambo baya,+ nao hawapati usingizi wasipomkwaza mtu.+ 17 Kwa maana wamekula mkate wa uovu,+ nao hunywa divai ya matendo ya jeuri.+ 18 Lakini njia ya waadilifu ni kama nuru inayong’aa, inayozidi kuongezeka mpaka mchana mkamilifu.+ 19 Njia ya waovu ni kama giza;+ hawajui ni nini kinachoendelea kuwakwaza.+

20 Mwanangu, sikiliza kwa makini maneno yangu.+ Tega sikio lako kwa maneno yangu.+ 21 Na yasiondoke machoni pako.+ Yaweke katikati ya moyo wako.+ 22 Kwa maana ni uzima kwa wale wanaoyapata+ na afya kwa mwili wao wote.+ 23 Linda moyo wako kuliko vitu vingine vyote vinavyopaswa kulindwa,+ kwa maana ndiko zinakotoka chemchemi za uzima.+ 24 Ujiepushe na maneno yaliyopotoka;+ na hila ya midomo uiweke mbali nawe.+ 25 Macho yako yatazame mbele moja kwa moja,+ naam, macho yako yenye kung’aa yanapaswa kutazama mbele yako moja kwa moja.+ 26 Lainisha mapito ya mguu wako,+ nazo njia zako zote na zifanywe imara.+ 27 Usielekee mkono wa kuume wala wa kushoto.+ Ondoa mguu wako kutoka katika jambo baya.+

5 Mwanangu, sikiliza hekima yangu.+ Tega sikio usikie utambuzi wangu,+ 2 ili ulinde uwezo wako wa kufikiri;+ na midomo yako mwenyewe ilinde ujuzi.+

3 Kwa maana midomo ya mwanamke mgeni hudondoka-dondoka kama sega la asali,+ nalo kaakaa lake ni laini kuliko mafuta.+ 4 Lakini matokeo yake ni machungu kama pakanga;+ ni makali kama upanga wenye makali kuwili.+ 5 Miguu yake inashuka kwenye kifo.+ Hatua zake hushika Kaburi.*+ 6 Yeye hatafakari njia za uzima.+ Mapito yake yamepotoka wala hajui yanakoelekea.+ 7 Basi sasa, enyi wana, nisikilizeni+ wala msiache maneno ya kinywa changu.+ 8 Itenge njia yako mbali naye, wala usiukaribie mlango wa nyumba yake,+ 9 ili usije ukawapa wengine heshima yako,+ wala kukipa kilicho kikatili miaka yako;+ 10 ili wageni wasijishibishe kwa nguvu zako,+ wala vitu vyako ulivyovipata kwa maumivu visiwe ndani ya nyumba ya mgeni,+ 11 wala usije kulalamikia wakati wako ujao,+ nyama yako na mwili wako vitakapofikia mwisho.+ 12 Nawe utalazimika kusema: “Nimechukia nidhamu+ kama nini nao moyo wangu umedharau karipio+ kama nini! 13 Nami sikusikiliza sauti ya wafundishaji wangu,+ wala sikuwategea sikio langu walimu wangu.+ 14 Nimeingia kwa urahisi katika kila namna ya ubaya+ katikati ya kutaniko na kusanyiko.”+

15 Unywe maji ya birika lako mwenyewe, na maji yanayotiririka kutoka katikati ya kisima chako mwenyewe.+ 16 Je, chemchemi zako mwenyewe zitawanyike nje,+ na vijito vyako vya maji katika viwanja vya watu wote? 17 Na yawe yako peke yako, wala si ya wageni pamoja nawe.+ 18 Chemchemi yako ya maji na ibarikiwe,+ na ushangilie pamoja na mke wa ujana wako,+ 19 paa mwenye kupendeka na mbuzi wa milimani mwenye kuvutia.+ Na maziwa yake yakuleweshe nyakati zote.+ Upendo wake na ukufurahishe sikuzote.+ 20 Basi mwanangu, kwa nini umfurahie mwanamke mgeni au kukumbatia kifua cha mwanamke wa kigeni?+ 21 Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele za macho ya Yehova,+ naye anayatafakari mapito yake yote.+ 22 Makosa yake mwenyewe yatamkamata mwovu,+ naye atashikwa katika kamba za dhambi yake mwenyewe.+ 23 Atakufa yeye mwenyewe kwa sababu hakuna nidhamu,+ na kwa sababu ya upumbavu wake mwingi yeye hupotea.+

6 Mwanangu, ikiwa umekuwa mdhamini wa mwenzako,+ ikiwa wewe na mgeni mmepeana mikono katika mapatano,+ 2 ikiwa umenaswa na maneno ya kinywa chako,+ ikiwa umekamatwa na maneno ya kinywa chako, 3 basi chukua hatua hii, mwanangu, ujikomboe mwenyewe, kwa maana umejitia mkononi mwa mwenzako:+ Nenda ujinyenyekeze na kumsihi sana mwenzako.+ 4 Usiache macho yako yapate usingizi wowote, wala macho yako yenye kung’aa yasisinzie.+ 5 Jikomboe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji na kama ndege kutoka mkono wa mwindaji wa ndege.+

6 Mwendee chungu,+ ewe mvivu;+ zitazame njia zake upate kuwa na hekima. 7 Ijapokuwa hana kiongozi, ofisa wala mtawala, 8 yeye hutayarisha chakula chake wakati wa kiangazi;+ amekusanya akiba ya chakula chake wakati wa mavuno. 9 Ewe mvivu, utaendelea kulala hata wakati gani?+ Utaamka wakati gani kutoka katika usingizi wako?+ 10 Bado kulala kidogo, bado kusinzia kidogo, bado kukunja mikono ili kulala,+ 11 na hakika umaskini wako utakuja kama mnyang’anyi,+ na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.+

12 Mtu asiyefaa kitu,+ mtu wa mambo yenye kuumiza, anatembea akiwa na maneno mapotovu,+ 13 akikonyeza kwa jicho lake,+ akifanya ishara kwa mguu wake, na kuonyesha alama kwa vidole vyake.+ 14 Upotovu umo moyoni mwake.+ Anatunga jambo baya wakati wote.+ Huendelea kutokeza ugomvi.+ 15 Hiyo ndiyo sababu msiba wake utakuja ghafula;+ atavunjwa ghafula, wala hatapona.+

16 Kuna vitu sita ambavyo Yehova huchukia;+ naam, vitu saba vinachukiza nafsi yake:+ 17 macho ya majivuno,+ ulimi wa uwongo,+ na mikono inayomwaga damu isiyo na hatia,+ 18 moyo unaotunga hila zenye kuumiza,+ miguu iliyo myepesi kukimbilia ubaya,+ 19 shahidi wa uwongo anayesema uwongo,+ na yeyote anayetokeza magomvi kati ya ndugu.+

20 Ee mwanangu, shika amri ya baba yako,+ wala usiiache sheria ya mama yako.+ 21 Zifunge juu ya moyo wako sikuzote,+ zifunge shingoni pako.+ 22 Unapotembea huku na huku, itakuongoza;+ unapolala, itakulinda;+ na unapokuwa umeamka, hiyo yenyewe itakuhangaikia. 23 Kwa maana amri hiyo ni taa,+ na sheria ni nuru,+ nayo makaripio ya nidhamu ndiyo njia ya uzima,+ 24 yakulinde na mwanamke mbaya,+ na ulimi laini wa mwanamke mgeni.+ 25 Usiutamani urembo wake moyoni mwako,+ wala asikuchukue kwa macho yake yenye kung’aa,+ 26 kwa sababu ya mwanamke kahaba mtu hubaki tu na kipande cha mkate;+ lakini mke wa mwanamume mwingine, yeye huwinda hata nafsi yenye thamani.+ 27 Je, mtu anaweza kukusanya moto kifuani pake na mavazi yake yasiungue?+ 28 Au je, mtu anaweza kutembea juu ya makaa ya moto na miguu yake mwenyewe isiungue? 29 Ndivyo ilivyo kwa yule anayelala na mke wa mwenzake,+ mtu anayemgusa hatakosa kuadhibiwa.+ 30 Watu hawamdharau mwizi kwa sababu tu anaiba ili kushibisha nafsi yake akiwa na njaa. 31 Lakini, akipatikana, atalipa mara saba ya kiasi hicho; atatoa vitu vyote vyenye thamani vya nyumba yake.+ 32 Yeyote anayefanya uzinzi na mwanamke amepungukiwa moyoni;+ yule anayefanya hivyo anaiangamiza nafsi yake mwenyewe.+ 33 Atapata pigo na kukosa heshima,+ na shutuma yake haitafutiliwa mbali.+ 34 Kwa maana ghadhabu ya mwanamume ni wivu,+ naye hataonyesha huruma siku ya kulipiza kisasi.+ 35 Hatajali namna yoyote ya fidia, wala hataikubali zawadi yako hata iwe kubwa namna gani.

7 Mwanangu, shika maneno yangu,+ na uzitunze amri zangu kama hazina.+ 2 Shika amri zangu uendelee kuishi,+ na sheria yangu kama mboni+ ya macho yako. 3 Zifunge juu ya vidole vyako,+ na kuziandika juu ya kibao cha moyo wako.+ 4 Iambie hekima:+ “Wewe ni dada yangu”; na uite uelewaji “Mwanamke wa ukoo wangu,” 5 ili kukulinda na mwanamke mgeni,+ na mwanamke wa kigeni ambaye amefanya maneno yake mwenyewe kuwa laini.+ 6 Kwa maana penye dirisha la nyumba yangu, kupitia pazia+ langu nilitazama chini, 7 ili kuwachungulia wasio na uzoefu.+ Nilipendezwa kutambua kati ya wana, kijana ambaye amepungukiwa moyoni,+ 8 akipita barabarani, karibu na pembeni kwa mwanamke huyo, naye kijana huyo akashika njia inayoenda nyumbani kwa mwanamke huyo,+ 9 wakati wa gizagiza, jioni ya siku hiyo,+ usiku ukikaribia kuingia na kukiwa na giza. 10 Na, tazama! mwanamke akaja kumpokea, mwenye vazi la kahaba+ na ujanja wa moyo. 11 Yeye ni mwanamke mwenye msukosuko na mkaidi.+ Miguu yake haikai nyumbani mwake.+ 12 Mara yuko nje, mara yuko katika viwanja vya watu wote,+ naye huvizia karibu na kila pembe.+ 13 Naye mwanamke huyo akamkamata yule kijana na kumbusu.+ Huyo mwanamke ana uso usio na haya, naye akaanza kumwambia yule kijana:

14 “Nilipaswa kutoa dhabihu za ushirika.+ Leo nimetimiza nadhiri zangu.+ 15 Ndiyo sababu nimekuja kukupokea, niutafute uso wako, nikupate. 16 Nimepamba kitanda changu kwa matandiko, kwa vitu vyenye rangi mbalimbali, kitani cha Misri.+ 17 Nimetia kitanda changu manemane, udi na mdalasini.+ 18 Haya njoo, na tunywe na kushiba upendo mpaka asubuhi; na tufurahiane kwa maonyesho ya upendo.+ 19 Kwa maana mume hayumo nyumbani mwake; ameenda safari ya mbali.+ 20 Amechukua mfuko wa pesa mkononi mwake. Atarudi nyumbani kwake siku ya mwezi mpevu.”

21 Akampotosha kwa ushawishi wake mwingi.+ Akamtongoza kwa ulaini wa midomo yake.+ 22 Ghafula kijana huyo akamfuata,+ kama ng’ombe-dume anayeenda machinjoni, na kama mtu mpumbavu aliyefungwa pingu atiwe nidhamu, 23 mpaka mshale upasue ini lake,+ kama vile ndege anavyofanya haraka kuingia mtegoni,+ naye hajajua kwamba nafsi yake mwenyewe inahusika.+

24 Sasa basi, enyi wana, nisikilizeni na kutega sikio msikie maneno ya kinywa changu.+ 25 Moyo wako usikengeuke kuingia katika njia za mwanamke huyo. Usipotee na kuingia katika barabara zake.+ 26 Kwa maana amewafanya wengi waanguke wakiwa wamechinjwa,+ na wote ambao anawaua ni wengi.+ 27 Nyumba yake ni njia za kwenda katika Kaburi;*+ zinashuka kwenye vyumba vya ndani vya kifo.+

8 Je, hekima haendelei kupaaza sauti,+ na utambuzi haendelei kutoa sauti yake?+ 2 Husimama juu ya vilele,+ kando ya njia, kwenye makutano ya barabara. 3 Kando ya malango, kinywani pa mji,+ kwenye kiingilio cha malango huendelea kulia kwa sauti kubwa:+

4 “Ninawaita ninyi, enyi watu, nayo sauti yangu inawaita wana wa binadamu.+ 5 Enyi msio na uzoefu, eleweni werevu;+ nanyi wajinga, eleweni utambuzi wa moyo.+ 6 Sikilizeni, kwa maana ninasema juu ya mambo ya kwanza kabisa,+ nami ninaifungua midomo yangu kuhusu unyoofu.+ 7 Kwa maana kaakaa langu husema ukweli wenyewe+ kwa sauti ya chini; na uovu ni chukizo kwa midomo yangu.+ 8 Maneno yote ya kinywa changu ni ya uadilifu.+ Kati ya hayo hamna jambo lililopotoka wala lililo kombo.+ 9 Yote hayo yamenyooka kwa mtu mwenye utambuzi, na ni ya unyoofu kwa wale wanaopata ujuzi.+ 10 Chukueni nidhamu yangu wala si fedha, na ujuzi badala ya dhahabu bora.+ 11 Kwa maana hekima ni bora kuliko marijani,+ na vitu vingine vyote vyenye kupendeza haviwezi kulinganishwa nayo.+

12 “Mimi, hekima, nimefanya makao pamoja na werevu+ nami napata hata ujuzi wa uwezo wa kufikiri.+ 13 Kumwogopa Yehova humaanisha kuchukia yaliyo mabaya.+ Nimechukia kujiinua na kiburi+ na njia mbaya na kinywa kipotovu.+ 14 Nina mashauri+ na hekima inayotumika.+ Mimi—uelewaji;+ nina uwezo.+ 15 Kwa msaada wangu wafalme wenyewe huendelea kutawala, na maofisa wakuu wenyewe huendelea kuagiza juu ya uadilifu.+ 16 Kwa msaada wangu wakuu wenyewe huendelea kutawala wakiwa wakuu,+ nao watu wote wenye vyeo wanahukumu katika uadilifu.+ 17 Wanaonipenda mimi ninawapenda,+ nao wanaonitafuta mimi ndio wanaonipata.+ 18 Nina utajiri na utukufu,+ vitu vya urithi vyenye thamani na uadilifu.+ 19 Matunda yangu ni bora kuliko dhahabu, hata kuliko dhahabu safi, nayo mazao yangu ni bora kuliko fedha bora.+ 20 Mimi hutembea katika njia ya uadilifu,+ katikati ya barabara za hukumu,+ 21 ili kuwafanya wanaonipenda wawe na vitu halisi;+ nami huendelea kujaza maghala yao.+

22 “Yehova mwenyewe alinitokeza nikiwa mwanzo wa njia yake,+ nikiwa wa mapema zaidi kati ya kazi zake za zamani za kale.+ 23 Niliwekwa tangu wakati usio na kipimo,+ tangu mwanzoni, tangu nyakati za mapema kabla ya dunia.+ 24 Wakati ambapo hakukuwa na vilindi vya maji nilitokezwa kana kwamba kwa uchungu wa kuzaa,+ wakati ambapo hakukuwa na chemchemi zilizojaa sana maji. 25 Kabla milima yenyewe haijawekwa,+ kabla ya vilima, nilitokezwa kana kwamba kwa uchungu wa kuzaa, 26 kabla hajaifanya dunia+ na nchi tambarare na sehemu ya kwanza ya mavumbi ya nchi yenye kuzaa.+ 27 Alipozitayarisha mbingu nilikuwako;+ alipoagiza mviringo juu ya uso wa kilindi cha maji,+ 28 alipoweka imara mawingu makubwa yaliyo juu,+ alipofanya chemchemi za kilindi cha maji ziwe na nguvu,+ 29 alipoiwekea bahari sheria yake kwamba maji yasipite agizo lake,+ alipoiweka misingi ya dunia,+ 30 ndipo nilipokuwa kando yake nikiwa stadi wa kazi,+ nami nikawa yule ambaye yeye alimpenda sana+ kwa njia ya pekee siku baada ya siku, nami nikawa nikifurahi mbele zake wakati wote,+ 31 nikifurahi kwa sababu ya dunia yake yenye kutoa mazao,+ na vitu nilivyopenda sana vilihusiana na wana wa binadamu.+

32 “Na sasa, enyi wana, nisikilizeni; naam, wenye furaha ni wale wanaoshika njia zangu.+ 33 Sikiliza nidhamu upate kuwa na hekima,+ wala usipuuze hata kidogo.+ 34 Mwenye furaha ni yule anayenisikiliza kwa kukaa macho milangoni pangu siku baada ya siku, kwa kulinda kwenye vizingiti vya mahali pangu pa kuingilia.+ 35 Kwa maana anayenipata hakika atapata uzima,+ naye hupata nia njema kutoka kwa Yehova.+ 36 Lakini anayekosa kunipata anaifanyia nafsi yake jeuri;+ wale wote wanaonichukia vikali ndio wanaopenda kifo.”+

9 Hekima ya kweli+ imejenga nyumba yake;+ imechonga nguzo zake saba. 2 Imepanga kuchinja nyama zake; imechanganya divai yake; zaidi ya hayo, imepanga meza yake.+ 3 Imetuma watumishi wake wa kike, ili ipate kupaaza sauti juu ya vilele vya mji: 4 “Yeyote ambaye hana uzoefu, na ageuke aje hapa.”+ Amemwambia yeyote ambaye amepungukiwa moyoni:+ 5 “Njooni, mle mkate wangu na mshiriki kunywa divai ambayo nimechanganya.+ 6 Waacheni wasio na uzoefu mpate kuendelea kuishi,+ na mtembee moja kwa moja katika njia ya uelewaji.”+

7 Anayemrekebisha mtu mwenye dhihaka anajipatia aibu yeye mwenyewe,+ naye anayemkaripia mwovu—mna kasoro ndani yake.+ 8 Usimkaripie mtu mwenye dhihaka, asije akakuchukia.+ Mpe karipio mtu mwenye hekima naye atakupenda.+ 9 Mpe mtu mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima.+ Mpe ujuzi mtu mwadilifu naye atazidi kujifunza.

10 Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima,+ na kumjua aliye Mtakatifu Zaidi ni uelewaji.+ 11 Kwa maana nitafanya siku zako ziwe nyingi,+ nawe utaongezewa miaka ya uzima.+ 12 Ikiwa umekuwa na hekima, umekuwa na hekima kwa ajili yako mwenyewe;+ na ikiwa umefanya dhihaka, utaichukua, wewe peke yako.+

13 Mwanamke mwenye ujinga ana msukosuko.+ Yeye ni mjinga kabisa wala hajapata kujua lolote.+ 14 Naye ameketi katika mwingilio wa nyumba yake, juu ya kiti, mahali palipoinuka pa mji,+ 15 apate kuwapaazia sauti wanaopita njiani, wanaoenda moja kwa moja katika mapito yao:+ 16 “Yeyote ambaye hana uzoefu, na ageuke aje hapa.”+ Naye amemwambia yeyote ambaye amepungukiwa moyoni:+ 17 “Maji ya kuibwa ni matamu,+ na mkate unaoliwa katika siri—huo ni wenye kupendeza.”+ 18 Lakini yeye hajapata kujua kwamba wale wasiojiweza katika kifo wamo humo, kwamba walioitwa naye wamo mahali pa chini pa Kaburi.*+

10 Methali za Sulemani.+

Mwana mwenye hekima ndiye anayemfanya baba ashangilie,+ naye mwana mjinga ni huzuni ya mama yake.+ 2 Hazina za mwovu hazitakuwa na faida,+ lakini uadilifu ndio utakaokomboa kutoka katika kifo.+ 3 Yehova hataiacha nafsi ya mwadilifu iteswe na njaa,+ lakini atasukumia mbali tamaa ya waovu.+

4 Anayefanya kazi kwa mkono mlegevu atakuwa maskini,+ lakini mkono wa mwenye bidii ndio utakaomtajirisha.+

5 Mwana anayetenda kwa ufahamu anakusanya wakati wa kiangazi; mwana anayetenda kwa aibu analala usingizi mzito wakati wa mavuno.+

6 Baraka humkalia mwadilifu kichwani,+ lakini kinywa cha waovu, hufunika jeuri.+ 7 Kumbukumbu la mwadilifu litabarikiwa,+ lakini jina la waovu litaoza.+

8 Mwenye hekima moyoni atazikubali amri,+ lakini mwenye midomo ya upumbavu atakanyagiwa chini.+

9 Anayetembea kwa utimilifu atatembea salama,+ lakini anayepotoa njia zake atajifanya mwenyewe ajulikane.+

10 Anayekonyeza jicho lake atatokeza maumivu,+ na mwenye midomo ya upumbavu atakanyagiwa chini.+ 11 Kinywa cha mwadilifu ni chemchemi ya uzima;+ lakini kinywa cha waovu, hufunika jeuri.+

12 Chuki huchochea ugomvi,+ lakini upendo hufunika hata makosa yote.+

13 Hekima hupatikana kwenye midomo ya mtu mwenye uelewaji,+ lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa mtu ambaye amepungukiwa moyoni.+

14 Wenye hekima ndio wanaoweka hazina ya ujuzi,+ lakini kinywa cha mpumbavu kinakaribia uharibifu wenyewe.+

15 Vitu vyenye thamani vya tajiri ni mji wake wenye nguvu.+ Uharibifu wa watu wa hali ya chini ni umaskini wao.+

16 Utendaji wa mwadilifu hutokeza uzima;+ mazao ya mwovu hutokeza dhambi.+

17 Anayeshika nidhamu ni njia ya uzima,+ lakini anayeacha karipio anasababisha kupotea.+

18 Mtu anayefunika chuki ana midomo ya uwongo,+ naye anayeleta habari mbaya ni mjinga.+

19 Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na kosa,+ lakini anayezuia midomo yake anatenda kwa busara.+

20 Ulimi wa mwadilifu ni fedha bora,+ moyo wa mwovu una thamani ndogo.+

21 Midomo ya mwadilifu huendelea kulisha wengi,+ lakini wapumbavu huendelea kufa kwa sababu ya kupungukiwa moyoni.+

22 Baraka ya Yehova—hiyo ndiyo hutajirisha,+ naye haongezi maumivu pamoja nayo.+

23 Kwa mtu mjinga kuendeleza mwenendo mpotovu ni kama mchezo,+ lakini mtu mwenye utambuzi ana hekima.+

24 Kitu chenye kumwogopesha mwovu—hicho ndicho kitakachompata;+ lakini tamaa ya mwadilifu itatimizwa.+ 25 Kama wakati upepo wa dhoruba unapopita, ndivyo na mwovu asivyokuwapo tena;+ lakini mwadilifu ni msingi mpaka wakati usio na kipimo.+

26 Kama siki kwenye meno na kama moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mtu mvivu kwa wale wanaomtuma.+

27 Kumwogopa Yehova kutaongeza siku,+ lakini miaka ya waovu itafupishwa.+

28 Tarajio la waadilifu ni kushangilia,+ lakini tumaini lenyewe la waovu litapotea.+

29 Njia ya Yehova ni ngome kwa mtu asiye na lawama,+ lakini wale wanaozoea kutenda mambo yenye kuumiza wataharibiwa.+

30 Naye mwadilifu, mpaka wakati usio na kipimo hatafanywa apepesuke,+ lakini waovu, hawataendelea kukaa duniani.+

31 Kinywa cha mwadilifu—hicho huzaa tunda la hekima,+ lakini ulimi wa upotovu utakatiliwa mbali.+

32 Midomo ya mwadilifu​​—​hiyo hujua nia njema,+ lakini kinywa cha waovu ni upotovu.+

11 Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa Yehova,+ lakini jiwe kamili la mizani ni furaha kwake.

2 Je, kimbelembele kimekuja? Basi aibu itakuja;+ lakini wenye kiasi wana hekima.+

3 Utimilifu wa wanyoofu ndio huwaongoza,+ lakini upotovu wa wale wanaotenda kwa hila utawaharibu.+

4 Vitu vyenye thamani havitakuwa na faida yoyote siku ya ghadhabu,+ lakini uadilifu utakomboa kutoka katika kifo.+

5 Uadilifu wa mtu asiye na lawama ndio utakaoinyoosha njia yake,+ lakini mwovu ataanguka katika uovu wake mwenyewe.+ 6 Uadilifu wa wanyoofu ndio utakaowakomboa,+ lakini wale wanaotenda kwa hila wao wenyewe watakamatwa kwa tamaa yao.+

7 Mwovu anapokufa, tumaini lake hupotea;+ na hata tarajio linalotegemea nguvu limepotea.+

8 Mwadilifu ndiye huokolewa kutoka katika taabu,+ na mwovu huingia badala yake.+

9 Mwasi-imani humletea mwenzake uharibifu kwa kinywa chake,+ lakini waadilifu huokolewa kwa ujuzi.+

10 Mji huchangamka kwa sababu ya wema wa waadilifu,+ lakini watu hulia kwa shangwe waovu wanapoangamia.+

11 Mji huinuliwa kwa sababu ya baraka ya wanyoofu,+ lakini hubomolewa kwa sababu ya kinywa cha waovu.+

12 Mtu ambaye amepungukiwa moyoni amemdharau mwenzake,+ lakini mtu mwenye utambuzi mwingi hukaa kimya.+

13 Mtu anayetembea huku na huku akiwa mchongezi+ anafunua mazungumzo ya siri,+ lakini mtu mwaminifu katika roho anafunika jambo.+

14 Wakati ambapo hakuna mwongozo stadi, watu huanguka;+ lakini kwa wingi wa washauri kuna wokovu.+

15 Mtu ambaye amemwekea dhamana mgeni+ hakika atapatwa na mabaya, lakini anayechukia kufanya mapatano kwa kupeana mkono hukaa bila wasiwasi.

16 Mwanamke mwenye kuvutia ndiye anayepata utukufu;+ lakini watu wenye kuonea, kwa upande wao, hupata utajiri.

17 Mwanamume mwenye fadhili zenye upendo anaitendea kwa kuipa thawabu nafsi yake mwenyewe,+ lakini mtu mkatili anajiletea taabu.+

18 Mtu mwovu anapata mshahara wa uwongo,+ lakini anayepanda uadilifu, hupata mapato ya kweli.+

19 Anayesimama imara kwa ajili ya uadilifu anaelekea kupata uzima,+ lakini anayefuatilia yaliyo mabaya anaelekea kwenye kifo chake mwenyewe.+

20 Waliopotoka moyoni ni chukizo kwa Yehova,+ lakini wasio na lawama katika njia yao ni furaha kwake.+

21 Mkono ujaposhikana na mkono, mtu mbaya hatakosa kupewa adhabu;+ lakini uzao wa waadilifu hakika utaponyoka.+

22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe, ndivyo alivyo mwanamke mwenye umbo la kupendeza lakini anayegeuka na kuacha kuwa na akili.+

23 Tamaa ya waadilifu hakika ni njema;+ tumaini la waovu ni ghadhabu.+

24 Kuna mtu anayetawanya na bado anaongezewa;+ pia kuna mtu anayewanyima wengine yaliyo sawa, lakini hilo huleta uhitaji tu.+

25 Nafsi yenye ukarimu hiyo yenyewe itanoneshwa,+ naye anayenywesha wengine kwa ukarimu yeye mwenyewe pia atanyweshwa kwa ukarimu.+

26 Anayewanyima watu nafaka—watu watamlaani, lakini kuna baraka kwa ajili ya kichwa cha mtu anayekubali inunuliwe.+

27 Anayetafuta mema ataendelea kutafuta nia njema;+ lakini anayetafuta ubaya, huo utamjia.+

28 Anayetegemea utajiri wake​​—​yeye mwenyewe ataanguka;+ lakini waadilifu watasitawi kama majani.+

29 Yeyote anayeiletea nyumba yake taabu,+ ataumiliki upepo;+ na mtu mpumbavu atakuwa mtumishi wa mtu mwenye hekima moyoni.

30 Matunda ya mwadilifu ni mti wa uzima,+ naye anayevuta nafsi za watu ni mwenye hekima.+

31 Tazama! Mtu mwadilifu—katika dunia atapewa thawabu.+ Basi mwovu na mtenda-dhambi watapewa thawabu hata zaidi!+

12 Anayependa nidhamu anapenda ujuzi,+ lakini anayechukia karipio hatumii akili.+

2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Yehova,+ lakini yeye humtangaza mtu mwenye mawazo maovu kuwa mwovu.+

3 Hakuna mtu atakayefanywa imara kwa uovu;+ lakini mizizi ya waadilifu haitatikiswa.+

4 Mke mwenye uwezo ni taji kwa mume wake,+ lakini yule anayetenda kwa aibu ni kama ubovu kwenye mifupa ya mume wake.+

5 Fikira za waadilifu ni adili;+ uongozi wa waovu ni udanganyifu.+

6 Maneno ya waovu ni uviziaji kwa ajili ya kumwaga damu,+ lakini kinywa cha wanyoofu ndicho kitakachowakomboa.+

7 Waovu wamepinduliwa nao hawako tena,+ lakini nyumba ya waadilifu itaendelea kusimama.+

8 Mtu atasifiwa kwa sababu ya kinywa chake cha busara,+ lakini aliyepotoka moyoni atadharauliwa.+

9 Afadhali mtu anayeheshimiwa kidogo lakini ana mtumishi kuliko mtu anayejitukuza lakini hana mkate.+

10 Mwadilifu anatunza nafsi ya mnyama wake wa kufugwa,+ lakini rehema za waovu ni ukatili.+

11 Anayelima shamba lake yeye mwenyewe atashiba mkate,+ lakini anayefuatilia vitu visivyo na thamani amepungukiwa moyoni.+

12 Mwovu ametamani windo la watu wabaya ambalo limeshikwa katika wavu;+ lakini mzizi wa waadilifu, huzaa.+

13 Mtu mbaya hunaswa kwa kosa la midomo,+ lakini mwadilifu hutoka katika taabu.+

14 Kutokana na matunda ya kinywa cha mtu, yeye hushiba mema,+ na kazi yenyewe ya mikono ya mtu itamrudia.+

15 Njia ya mpumbavu ni sawa machoni pake,+ lakini anayesikiliza shauri ni mwenye hekima.+

16 Mtu mpumbavu ndiye hujulisha kinachomuudhi siku hiyohiyo,+ lakini mwerevu hufunika aibu.+

17 Anayetokeza uaminifu atasema kilicho cha uadilifu,+ lakini shahidi wa uwongo, atasema udanganyifu.+

18 Kuna mtu anayesema bila kufikiri kama kwa upanga unaochoma,+ lakini ulimi wa mwenye hekima huponya.+

19 Mdomo wa ukweli+ ndio utakaofanywa imara milele,+ lakini ulimi wa uwongo ni wa muda mfupi tu.+

20 Udanganyifu umo moyoni mwa wale wanaotunga madhara,+ lakini wale wanaoshauri amani wanashangilia.+

21 Hakuna kitu chochote chenye kudhuru kitakachompata mwadilifu,+ lakini waovu ndio watakaojazwa misiba.+

22 Midomo ya uwongo ni chukizo kwa Yehova,+ lakini wanaotenda kwa uaminifu ni furaha kwake.+

23 Mtu mwerevu anafunika ujuzi,+ lakini moyo wa wajinga hutangaza upumbavu.+

24 Mkono wa wenye bidii ndio utakaotawala,+ lakini mkono mlegevu utakuja kufanya kazi ya kulazimishwa.+

25 Hangaiko katika moyo wa mtu huufanya uiname,+ lakini neno jema huufanya ushangilie.+

26 Mwadilifu huchunguza malisho yake mwenyewe, lakini njia ya waovu huwafanya watange-tange.+

27 Uvivu hautatimua mawindo ya mtu,+ lakini bidii ni mali yenye thamani ya mtu.

28 Katika mapito ya uadilifu kuna uzima,+ na kusafiri katika njia yake kunamaanisha hakuna kifo.+

13 Mwana ni mwenye hekima palipo na nidhamu ya baba,+ lakini mtu mwenye dhihaka ni yule ambaye hajasikia kemeo.+

2 Kutokana na matunda ya kinywa chake, mtu atakula mema,+ lakini nafsi ya wale wanaotenda kwa hila ni ujeuri.+

3 Anayelinda kinywa chake anaitunza nafsi yake.+ Anayefungua wazi midomo yake—yeye atapata uharibifu.+

4 Mvivu anajionyesha kutamani, lakini nafsi yake haina chochote.+ Hata hivyo, nafsi ya wenye bidii itanoneshwa.+

5 Mwadilifu huchukia neno la uwongo,+ lakini waovu hutenda kwa aibu na kujiletea fedheha.+

6 Uadilifu humlinda mtu asiye na lawama katika njia yake,+ lakini uovu humpindua mtenda-dhambi.+

7 Kuna mtu anayejifanya kuwa tajiri lakini hana chochote;+ kuna mtu anayejifanya kuwa maskini lakini ana vitu vingi vyenye thamani.

8 Fidia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake,+ lakini maskini hajasikia kemeo.+

9 Nuru ya waadilifu itashangilia;+ lakini taa ya waovu—hiyo itazimwa.+

10 Kwa sababu ya kimbelembele mtu husababisha tu pambano,+ lakini wale wanaoshauriana pamoja wana hekima.+

11 Vitu vyenye thamani vinavyopatikana kwa ubatili hupungua,+ lakini mtu anayekusanya kwa mkono ndiye anayepata ongezeko.+

12 Tarajio lililocheleweshwa linafanya moyo uwe mgonjwa,+ lakini kitu kinachotamaniwa kinapokuja ni mti wa uzima.+

13 Yule ambaye amelidharau neno,+ atadaiwa rehani ya mtu mwenye deni; lakini mtu anayeiogopa amri ndiye atakayepewa thawabu.+

14 Sheria ya mwenye hekima ni chemchemi ya uzima,+ ili kumwepusha mtu na mitego ya kifo.+

15 Ufahamu mzuri huleta kibali,+ lakini njia ya wale wanaotenda kwa hila ni ngumu.+

16 Kila mtu aliye mwerevu atatenda kwa ujuzi,+ lakini mjinga ataeneza upumbavu kila mahali.+

17 Mjumbe mwovu ataanguka katika jambo baya,+ lakini mjumbe mwaminifu huponya.+

18 Anayepuuza nidhamu hupatwa na umaskini na aibu,+ lakini anayeshika karipio ndiye anayetukuzwa.+

19 Tamaa inapotimizwa inafurahisha nafsi;+ lakini kuepuka yaliyo mabaya ni chukizo kwa wajinga.+

20 Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima,+ lakini anayeshirikiana na wajinga atapatwa na mabaya.+

21 Watenda-dhambi ndio hufuatwa na msiba,+ lakini waadilifu ndio ambao wema huwapa thawabu.+

22 Mtu mwema atawaachia urithi wana wa wanawe, na mali ya mtenda-dhambi huwekwa akiba kwa ajili ya mwadilifu.+

23 Udongo uliolimwa wa watu maskini hutoa chakula kingi,+ lakini kuna mtu anayefagiliwa mbali kwa sababu ya ukosefu wa hukumu.+

24 Anayezuia fimbo yake anamchukia mwana wake,+ lakini anayempenda ni yule anayemwangalia kwa nidhamu.+

25 Mwadilifu anakula mpaka nafsi yake inaposhiba,+ lakini tumbo la waovu litakuwa tupu.+

14 Mwanamke mwenye hekima kwelikweli amejenga nyumba yake,+ lakini aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.+

2 Anayetembea katika unyoofu wake anamwogopa Yehova,+ lakini mtu mpotovu anamdharau Yeye katika njia zake.+

3 Fimbo ya majivuno imo katika kinywa cha mpumbavu,+ lakini midomo ya wenye hekima itawalinda.+

4 Mahali pasipo na ng’ombe hori ni safi, lakini mazao ni mengi kwa sababu ya nguvu za ng’ombe-dume.

5 Shahidi mwaminifu ni yule ambaye hatasema uwongo,+ lakini shahidi wa uwongo husema uwongo mtupu.+

6 Mtu mwenye dhihaka ametafuta hekima, asiipate; lakini kwa mtu mwenye uelewaji, ujuzi ni jambo rahisi.+

7 Toka mbele ya mjinga,+ kwa maana hakika hutaweza kuona midomo ya ujuzi.+

8 Hekima ya mwerevu ni kuelewa njia yake,+ lakini upumbavu wa wajinga ni udanganyifu.+

9 Wale wanaodhihaki hatia ni wapumbavu,+ lakini kuna makubaliano kati ya wanyoofu.+

10 Moyo unajua uchungu wa nafsi+ ya mtu mwenyewe, wala hapana mgeni atakayejiingiza katika kushangilia kwake.

11 Nyumba ya watu waovu itaharibiwa,+ lakini hema la wanyoofu litasitawi.+

12 Kuna njia ambayo imenyooka mbele ya mwanadamu,+ lakini njia za kifo ndizo mwisho wake baadaye.+

13 Hata katika kicheko moyo unaweza kuwa na maumivu;+ na kushangilia huishia katika huzuni.+

14 Asiye na imani moyoni ataridhika na matokeo ya njia zake mwenyewe,+ lakini mtu mwema ataridhika na matokeo ya shughuli zake.+

15 Mtu asiye na uzoefu huamini kila neno,+ lakini mtu mwerevu huzifikiria hatua zake.+

16 Mwenye hekima huogopa na kuepuka ubaya,+ lakini mjinga anakuwa na ghadhabu na mwenye kujitumaini.+

17 Yule anayekasirika upesi atatenda upumbavu,+ lakini mtu mwenye uwezo wa kufikiri huchukiwa.+

18 Wasio na uzoefu hakika watarithi upumbavu,+ lakini werevu watavaa ujuzi kama vazi la kichwani.+

19 Watu wabaya watainama mbele ya wema,+ nao watu waovu watainama katika malango ya mwadilifu.

20 Maskini ni chukizo hata kwa mwenzake,+ lakini tajiri ana rafiki wengi.+

21 Anayemdharau mwenzake anatenda dhambi,+ lakini mwenye furaha ni yule anayewaonyesha kibali wenye kuteseka.+

22 Je, wale wanaotunga madhara hawatatanga-tanga?+ Lakini kuna fadhili zenye upendo na ukweli kwa wale wanaotunga mema.+

23 Kwa kila kazi ngumu hutokea faida,+ lakini neno la midomo tu huelekea kuleta uhitaji.

24 Taji la wenye hekima ni utajiri wao; upumbavu wa wajinga ni upumbavu.+

25 Shahidi wa kweli anazikomboa nafsi,+ lakini mdanganyifu anasema uwongo mtupu.+

26 Katika kumwogopa Yehova kuna uhakika wenye nguvu,+ na wanawe watakuwa na kimbilio.+

27 Kumwogopa Yehova ni kisima cha uzima,+ ili kuepuka mitego ya kifo.+

28 Wingi wa watu ni pambo la mfalme,+ lakini kukosekana kwa watu ni uharibifu wa ofisa mkuu.+

29 Yule ambaye si mwepesi wa hasira ana utambuzi mwingi,+ lakini anayekosa subira anainua upumbavu.+

30 Moyo mtulivu ni uzima wa mwili wenye nyama,+ lakini wivu hufanya mifupa iwe na ubovu.+

31 Yeye anayempunja mtu wa hali ya chini amemletea shutuma Mtengenezaji wake,+ lakini anayemwonyesha maskini kibali anamtukuza Yeye.+

32 Kwa sababu ya ubaya wake mwovu atasukumwa chini,+ lakini mwadilifu atakuwa akipata kimbilio katika utimilifu wake.+

33 Hekima hukaa moyoni mwa mtu mwenye uelewaji,+ nayo hujulikana kati ya wajinga.

34 Uadilifu huinua taifa,+ lakini dhambi ni aibu kwa vikundi vya mataifa.+

35 Furaha ya mfalme imo katika mtumishi anayetenda kwa ufahamu,+ lakini ghadhabu yake humjia mtu anayetenda kwa aibu.+

15 Jibu, linapokuwa la upole, hugeuza ghadhabu,+ lakini neno linaloumiza hufanya hasira ipande.+

2 Ulimi wa watu wenye hekima hutenda mema kwa ujuzi,+ lakini kinywa cha wajinga hububujika upumbavu.+

3 Macho ya Yehova yako kila mahali,+ yakiwaangalia wabaya na wema.+

4 Utulivu wa ulimi ni mti wa uzima,+ lakini upotovu wake humaanisha kuvunjika katika roho.+

5 Yeyote aliye mpumbavu hudharau nidhamu ya baba yake,+ lakini mtu yeyote anayejali karipio ni mwerevu.+

6 Katika nyumba ya mwadilifu mna akiba nyingi,+ lakini katika mazao ya mwovu mna taabu.+

7 Midomo ya watu wenye hekima hutawanya ujuzi sikuzote,+ lakini moyo wa wajinga hauko hivyo.+

8 Dhabihu ya waovu ni chukizo kwa Yehova,+ lakini sala ya wanyoofu ni furaha kwake.+

9 Njia ya mwovu ni chukizo kwa Yehova,+ lakini humpenda mtu anayefuatilia uadilifu.+

10 Nidhamu ni mbaya kwa mtu anayeiacha njia;+ mtu yeyote anayechukia karipio atakufa.+

11 Kaburi* na mahali pa maangamizi+ viko mbele za Yehova.+ Basi, mioyo ya wana wa binadamu+ ni zaidi!

12 Mwenye dhihaka hampendi mtu anayemkaripia.+ Yeye hataenda kwa watu wenye hekima.+

13 Moyo wenye shangwe huchangamsha sura,+ lakini kwa sababu ya maumivu ya moyo roho hupata pigo.+

14 Moyo wa uelewaji hutafuta ujuzi,+ lakini kinywa cha watu wajinga hutafuta upumbavu.+

15 Siku zote za mwenye kuteseka ni mbaya,+ lakini mtu aliye mchangamfu moyoni huwa na karamu sikuzote.+

16 Afadhali kuwa na vitu vichache pamoja na kumwogopa Yehova+ kuliko kuwa na vitu vingi pamoja na mvurugo.+

17 Afadhali chakula cha mboga za majani mahali penye upendo+ kuliko ng’ombe-dume aliyenoneshwa pamoja na chuki.+

18 Mtu mwenye ghadhabu huchochea ugomvi,+ lakini yule ambaye hakasiriki upesi hutuliza mabishano.+

19 Njia ya mvivu ni kama boma la miiba,+ lakini mapito ya wanyoofu ni njia iliyofanywa kuwa laini.+

20 Mwana mwenye hekima ndiye humfanya baba yake ashangilie,+ lakini mtu mjinga anamdharau mama yake.+

21 Mtu ambaye amepungukiwa moyoni huonea shangwe upumbavu,+ lakini mtu mwenye utambuzi huenda mbele moja kwa moja.+

22 Mipango huvunjika mahali ambapo hapana mazungumzo ya siri,+ lakini katika wingi wa washauri mambo hutimizwa.+

23 Mtu hushangilia jibu la kinywa chake,+ nalo neno linalosemwa wakati unaofaa ni jema kama nini!+

24 Kwa yule anayetenda kwa ufahamu njia ya uzima inaelekea juu,+ ili kuliepuka Kaburi* lililo chini.+

25 Yehova ataibomoa nyumba ya watu waliojiinua,+ lakini atauweka imara mpaka wa mjane.+

26 Hila za mtu mbaya ni chukizo kwa Yehova,+ lakini maneno yenye kupendeza ni safi.+

27 Mtu anayepata faida isiyo ya haki anailetea nyumba yake mwenyewe taabu,+ lakini anayechukia zawadi ndiye atakayeendelea kuishi.+

28 Moyo wa mwadilifu hutafakari ili kujibu,+ lakini kinywa cha waovu hububujika mambo mabaya.+

29 Yehova yuko mbali sana na waovu,+ lakini huisikia sala ya waadilifu.+

30 Kung’aa kwa macho+ hufanya moyo ushangilie;+ habari+ ambayo ni njema huifanya mifupa inone.+

31 Sikio linalosikiliza karipio+ la uzima hukaa kati ya watu wenye hekima.+

32 Yeyote anayeepuka nidhamu+ anaikataa nafsi yake mwenyewe, lakini anayesikiliza karipio anajipatia utambuzi wa moyo.+

33 Kumwogopa Yehova ni nidhamu ya hekima,+ na kabla ya utukufu hutangulia unyenyekevu.+

16 Mipango ya moyo ni ya mtu wa udongo,+ lakini jibu la ulimi hutoka kwa Yehova.+

2 Njia zote za mwanadamu ni safi machoni pake mwenyewe,+ lakini Yehova anazipima roho.+

3 Mkabidhi Yehova mwenyewe kazi zako+ nayo mipango yako itafanywa imara.+

4 Yehova amefanya kila kitu kwa kusudi lake,+ naam, hata mwovu kwa ajili ya siku ya uovu.+

5 Kila mtu mwenye kiburi moyoni ni chukizo kwa Yehova.+ Mkono unaweza kuungana na mkono, hata hivyo mtu hatakosa adhabu.+

6 Kosa hufanyiwa upatanisho kwa fadhili zenye upendo na ukweli,+ na mtu huepuka uovu kwa kumwogopa Yehova.+

7 Yehova anapofurahia njia za mtu,+ huwafanya hata adui zake wawe na amani naye.+

8 Afadhali kuwa na kidogo pamoja na uadilifu+ kuliko kuwa na wingi pasipo haki.+

9 Huenda moyo wa mtu wa udongo ukaifikiria njia yake,+ lakini Yehova ndiye huzielekeza hatua zake.+

10 Uamuzi ulioongozwa na roho unapaswa kuwa katika midomo ya mfalme;+ kinywa chake hakipasi kukosa uaminifu katika hukumu.+

11 Kitu cha kupimia cha haki na mizani ni vya Yehova;+ mawe yote ya mizani ya mfuko ni kazi yake.+

12 Kufanya uovu ni chukizo kwa wafalme,+ kwa maana kiti cha ufalme hufanywa imara kwa uadilifu.+

13 Midomo ya uadilifu ni furaha ya mfalme mkuu;+ naye humpenda mtu anayesema mambo ya unyoofu.+

14 Ghadhabu ya mfalme ni kama wajumbe wa kifo,+ lakini mwenye hekima huigeuza.+

15 Katika nuru ya uso wa mfalme kuna uzima,+ nayo nia yake njema ni kama wingu la majira ya mvua ya masika.+

16 Kupata hekima ni bora kama nini kuliko dhahabu!+ Na kupata uelewaji kunapasa kuchaguliwa kuliko fedha.+

17 Njia kuu ya wanyoofu ni kuepuka ubaya.+ Anayeilinda njia yake anaitunza nafsi yake.+

18 Kiburi hutangulia kuanguka,+ na roho ya majivuno hutangulia kujikwaa.+

19 Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu+ pamoja na wapole kuliko kugawanya nyara pamoja na watu wanaojiinua.+

20 Anayetumia ufahamu katika jambo atapata mema,+ naye anayemtegemea Yehova+ ni mwenye furaha.

21 Mtu mwenye hekima moyoni itasemwa kwamba ana uelewaji,+ naye mwenye midomo mitamu huongeza ushawishi.+

22 Ufahamu ni kisima cha uzima+ kwa hao walio nao; nayo nidhamu ya wapumbavu ni upumbavu.+

23 Moyo wa mtu mwenye hekima hukifanya kinywa chake kionyeshe ufahamu,+ na kwenye midomo yake huongeza ushawishi.+

24 Maneno yenye kupendeza ni sega la asali,+ ni matamu kwa nafsi na maponyo mifupani.+

25 Kuna njia ambayo imenyooka mbele ya mwanadamu,+ lakini njia za kifo ndizo mwisho wake baadaye.+

26 Nafsi ya mfanyakazi mwenye bidii imemfanyia kazi kwa bidii,+ kwa sababu kinywa chake kimemkaza sana.+

27 Mtu asiyefaa kitu anachimbua lililo baya,+ na katika midomo yake ni kana kwamba kuna moto unaounguza.+

28 Mtu mwenye hila huendelea kutokeza ugomvi nyakati zote,+ na mchongezi anawatenganisha wale wanaofahamiana.+

29 Mtu wa jeuri atamshawishi mwenzake,+ naye hakika humfanya aende katika njia isiyo njema.+ 30 Anakonyeza-konyeza macho yake ili kupanga hila.+ Akikaza midomo yake, hakika yeye hukamilisha madhara.

31 Kichwa chenye mvi ni taji la uzuri+ kinapopatikana katika njia ya uadilifu.+

32 Asiye mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwanamume mwenye nguvu,+ naye anayezuia roho yake ni bora kuliko mtu anayeteka jiji.+

33 Watu hutupa kura ndani ya mkunjo wa nguo,+ lakini kila uamuzi unaofanywa kupitia kura hiyo hutoka kwa Yehova. +

17 Afadhali kipande kikavu cha mkate pamoja na utulivu+ kuliko nyumba iliyojaa dhabihu za kugombana.+

2 Mtumishi anayeonyesha ufahamu atamtawala mwana anayetenda kwa aibu,+ na kati ya ndugu atapata sehemu ya urithi.+

3 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,+ lakini Yehova ndiye mchunguzaji wa mioyo.+

4 Mtenda-maovu anasikiliza kwa makini mdomo wenye madhara.+ Mwongo anatega sikio asikilize ulimi unaotokeza shida.+

5 Anayemdhihaki maskini anamletea shutuma Mtengenezaji+ wake. Anayeshangilia msiba wa mwingine hatakosa adhabu.+

6 Taji la wazee ni wajukuu,+ na uzuri wa wana ni baba zao.+

7 Mdomo wa unyoofu haumstahili mtu asiye na akili.+ Sembuse mdomo wa uwongo kwa mtu mwenye kuheshimika!+

8 Zawadi ni jiwe la thamani linaloleta kibali machoni pa yule aliye nayo.+ Kila mahali anapogeukia anafanikiwa.+

9 Anayefunika makosa anatafuta upendo,+ naye anayeendelea kuongea juu ya jambo anawatenganisha watu wanaofahamiana.+

10 Kemeo huingia ndani zaidi katika mtu mwenye uelewaji+ kuliko kumpiga mjinga mara mia moja.+

11 Mtu mbaya huendelea kutafuta uasi tu,+ na mjumbe anayetumwa kwake ni mkatili.+

12 Afadhali mtu akutane na dubu aliyepoteza watoto wake+ kuliko kukutana na mjinga katika upumbavu wake.+

13 Mtu anayelipa ubaya kwa wema,+ ubaya hautaondoka nyumbani mwake.+

14 Mwanzo wa ugomvi ni kama mtu anayefungulia maji;+ kwa hiyo kabla mabishano hayajalipuka, jiondokee.+

15 Yeyote anayemtangaza mwovu kuwa mwadilifu+ na yeyote anayemtangaza mwadilifu kuwa mwovu+—wote wawili ni chukizo kwa Yehova.+

16 Kwa nini mjinga ana uwezo mkononi mwake wa kujipatia hekima,+ hali yeye hana utambuzi wa moyo?+

17 Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote,+ naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.+

18 Mtu aliyepungukiwa moyoni hupeana mikono,+ akitoa dhamana kamili mbele ya mwenzake.+

19 Mtu anayependa makosa anapenda mashindano.+ Mtu anayeinua mahali pake pa kuingilia anatafuta kuanguka.+

20 Mtu mwenye moyo mpotovu hatapata mema,+ naye anayebadilika-badilika kwa ulimi ataanguka katika msiba.+

21 Yeyote anayezaa mtoto mjinga—ni huzuni kwake;+ na baba ya mtoto asiye na akili hana shangwe.+

22 Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri,+ lakini roho iliyopondeka huikausha mifupa.+

23 Mwovu atachukua hata rushwa kifuani+ ili kupotosha mapito ya hukumu.+

24 Hekima iko mbele ya uso wa mtu mwenye uelewaji,+ lakini macho ya mjinga yako kwenye mwisho wa dunia.+

25 Mwana mjinga ni huzuni kwa baba yake+ na ni uchungu kwa mama aliyemzaa.+

26 Zaidi ya hayo, si vema kumtoza mwadilifu.+ Kuwapiga watu wenye kuheshimika ni kinyume cha jambo lililonyooka.+

27 Yeyote anayezuia maneno yake ana ujuzi,+ na mtu mwenye utambuzi ana roho ya utulivu.+

28 Hata mtu mpumbavu, anapokaa kimya, ataonwa kuwa mwenye hekima;+ yeyote anayefunga midomo yake, ataonwa kuwa mwenye uelewaji.

18 Mtu anayejitenga na wengine atatafuta mapendezi yake mwenyewe;+ atashindana na hekima yote inayotumika.+

2 Yeyote aliye mjinga hapendezwi na utambuzi hata kidogo,+ isipokuwa tu moyo wake ujifunue wenyewe.+

3 Mwovu anapoingia, dharau huingia pia;+ na ukosefu wa heshima+ huwa pamoja na shutuma.

4 Maneno ya kinywa cha mwanadamu ni kilindi cha maji.+ Kisima cha hekima ni kijito cha maji yanayobubujika.+

5 Si vema kumwonyesha mwovu upendeleo,+ wala kumpotosha mwadilifu katika hukumu.+

6 Midomo ya mtu aliye mjinga huingia katika mabishano,+ na kinywa chake huitisha mapigo.+

7 Kinywa cha mjinga ni uharibifu wake,+ na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.+

8 Maneno ya mchongezi ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa,+ vinavyoingia katika sehemu za ndani kabisa za tumbo.+

9 Pia, mtu anayejionyesha kuwa mvivu katika kazi yake+​​—​yeye ni ndugu ya mtu anayeleta uharibifu.+

10 Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu.+ Mwadilifu hukimbilia humo na kupewa ulinzi.+

11 Vitu vyenye thamani vya tajiri ni mji wake wenye nguvu,+ navyo ni kama ukuta wa ulinzi katika mawazo yake.+

12 Kabla ya kuanguka moyo wa mwanadamu huwa na kiburi,+ na kabla ya utukufu kuna unyenyekevu.+

13 Yeyote anapojibu jambo kabla ya kulisikia,+ huo ni upumbavu na aibu kwake.+

14 Roho ya mwanadamu inaweza kuvumilia ugonjwa wake;+ lakini ni nani anayeweza kuvumilia roho iliyopondeka?+

15 Moyo wa mtu mwenye uelewaji hujipatia ujuzi,+ nalo sikio la wenye hekima hutafuta kupata ujuzi.+

16 Zawadi ya mwanadamu itamfungulia nafasi kubwa,+ nayo itamwongoza hata mbele ya watu wakuu.+

17 Mtu wa kwanza katika kesi yake ni mwadilifu;+ mwenzake huingia naye hakika humchunguza kwa undani.+

18 Kura hutuliza hata magomvi,+ nayo huwatenganisha hata watu wenye nguvu.+

19 Ndugu aliyekosewa ni mgumu kuliko mji wenye nguvu;+ na kuna magomvi yaliyo kama pingo la mnara wa makao.+

20 Kutokana na matunda ya kinywa cha mtu, tumbo lake litashiba;+ atashiba hata mazao ya midomo yake.+

21 Kifo na uzima viko katika nguvu za ulimi,+ naye anayeupenda atakula matunda yake.+

22 Je, mtu amepata mke mwema?+ Amepata kitu chema,+ na mtu hupata nia njema kutoka kwa Yehova.+

23 Maskini husema kwa kusihi,+ lakini tajiri hujibu kwa ukali.+

24 Kuna rafiki wanaoelekea kuvunjana vipande-vipande,+ lakini yuko rafiki anayeshikamana na mtu kwa ukaribu zaidi kuliko ndugu.+

19 Mtu yeyote aliye maskini ambaye anatembea katika utimilifu ni bora+ kuliko mtu mwenye midomo iliyopotoka, na ambaye ni mjinga.+

2 Pia, si vema kwamba nafsi ikose ujuzi,+ naye anayefanya haraka kwa miguu yake anatenda dhambi.+

3 Upumbavu wa mtu wa udongo ndio unaopotosha njia yake,+ na kwa hiyo moyo wake unakuwa na ghadhabu juu ya Yehova.+

4 Mali ndizo huongeza rafiki wengi,+ lakini mtu wa hali ya chini hutenganishwa na mwenzake.+

5 Shahidi wa uwongo hatakosa adhabu,+ naye anayesema uwongo hataponyoka.+

6 Watu wengi huutuliza uso wa mtu mwenye cheo,+ na kila mtu ni rafiki yake anayetoa zawadi.+

7 Ndugu za mtu maskini wamemchukia wote.+ Nao, rafiki zake binafsi wamejitenga naye hata zaidi!+ Anawafuata akiwa na mambo ya kusema; nao hawapo.+

8 Anayejipatia moyo+ mzuri anapenda nafsi yake mwenyewe. Anayelinda utambuzi atapata mema.+

9 Shahidi wa uwongo hatakosa adhabu,+ naye anayesema uwongo ataangamia.+

10 Maisha ya anasa hayamfai yeyote aliye mjinga.+ Sembuse mtumishi kuwatawala wakuu!+

11 Ufahamu wa mtu hakika hupunguza hasira yake,+ na ni jambo lenye kupendeza anapopita kosa.+

12 Ghadhabu ya mfalme ni mngurumo kama ule wa mwana-simba mwenye manyoya shingoni,+ lakini nia yake njema ni kama umande juu ya majani.+

13 Mwana mjinga humaanisha shida kwa baba yake,+ na ugomvi wa mke ni kama paa inayovuja ambayo humfukuzia mbali mtu.+

14 Urithi kutoka kwa akina baba ni nyumba na mali,+ lakini mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.+

15 Uvivu huleta usingizi mzito,+ nayo nafsi yenye uvivu huteswa na njaa.+

16 Yeye anayeishika amri anailinda nafsi yake;+ anayedharau njia zake atauawa.+

17 Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova,+ na Yeye atamlipa matendo yake.+

18 Mtie mwana wako adabu wakati bado kuna tumaini;+ wala usiweke tamaa ya nafsi yako juu ya kumuua.+

19 Mtu mwenye ghadhabu kubwa atachukua adhabu;+ kwa maana ukimkomboa, utaendelea kufanya hivyo tena na tena.+

20 Sikiliza shauri na kukubali nidhamu,+ ili upate kuwa na hekima katika wakati wako ujao.+

21 Mna mipango mingi katika moyo wa mwanadamu,+ lakini shauri la Yehova ndilo litakalosimama.+

22 Kinachotamanika katika mtu wa udongo ni fadhili zake zenye upendo;+ na maskini ni bora kuliko mtu anayesema uwongo.+

23 Kumwogopa Yehova huelekeza kwenye uzima,+ na mtu atalala usiku akiwa ameridhika;+ mtu hatapatwa na lililo baya.+

24 Mvivu ameutia mkono wake katika bakuli la karamu;+ hawezi kuurudisha hata kwenye kinywa chake mwenyewe.+

25 Inakupasa umpige mwenye dhihaka,+ ili mtu ambaye hana uzoefu apate kuwa mwerevu;+ naye mtu mwenye uelewaji anapaswa kukaripiwa, ili apate kutambua ujuzi.+

26 Yeye anayemtendea vibaya baba yake na ambaye humfukuza mama yake+ ni mwana anayetenda kwa aibu na bila heshima.+

27 Mwanangu, acha kusikiliza nidhamu nawe utakengeuka kutoka katika maneno ya ujuzi.+

28 Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki haki,+ na kinywa chenyewe cha watu waovu humeza kitu chenye kuumiza.+

29 Hukumu zimefanywa imara kwa ajili ya wenye dhihaka,+ na mapigo kwa ajili ya mgongo wa wajinga.+

20 Divai ni mdhihaki,+ kileo husababisha msukosuko,+ na kila mtu anayepotezwa nacho hana hekima.+

2 Kuogopesha kwa mfalme ni mngurumo kama ule wa mwana-simba mwenye manyoya shingoni.+ Mtu yeyote anayejiletea hasira yake anaitendea dhambi nafsi yake mwenyewe.+

3 Ni utukufu kwa mtu kuepuka kugombana,+ lakini kila aliye mpumbavu atatumbukia humo.+

4 Kwa sababu ya majira ya baridi kali mvivu hatalima;+ atakuwa akiombaomba wakati wa mavuno, lakini hapatakuwa na chochote.+

5 Shauri moyoni mwa mtu ni kama kilindi cha maji,+ lakini mtu mwenye utambuzi ataliteka.+

6 Wanadamu wengi hutangaza fadhili zao wenyewe zenye upendo,+ lakini ni nani anayeweza kumpata mtu mwaminifu?+

7 Mwadilifu anatembea kwa utimilifu wake.+ Wanawe watakuwa na furaha baada yake.+

8 Mfalme anaketi juu ya kiti cha hukumu,+ akitawanya ubaya wote kwa macho yake.+

9 Ni nani anayeweza kusema: “Nimeusafisha moyo wangu;+ mimi nimekuwa safi kutokana na dhambi yangu”?+

10 Aina mbili za mawe ya mizani na aina mbili za vipimo vya efa+—vyote viwili ni chukizo kwa Yehova.+

11 Kwa matendo yake, mvulana hujitambulisha kama utendaji wake ni safi na mnyoofu.+

12 Sikio lenye kusikia na jicho lenye kuona—Yehova ndiye aliyevifanya vyote viwili.+

13 Usipende usingizi, usije ukaingia katika umaskini.+ Fungua macho yako; ushibe mkate.+

14 “Ni kibaya, ni kibaya!” asema mnunuzi, naye aenda zake.+ Kisha anajisifu.+

15 Kuna dhahabu, pia kuna wingi wa marijani; lakini midomo ya ujuzi ni vyombo vyenye thamani.+

16 Ikiwa mtu amemwekea mgeni dhamana, lichukue vazi lake;+ na ikiwa amejihusisha na mwanamke mgeni, chukua rehani kutoka kwake.+

17 Mkate unaopatikana kwa udanganyifu humpendeza mtu,+ lakini baadaye kinywa chake kitajaa changarawe.+

18 Kwa shauri mipango yenyewe hufanywa imara,+ na kwa mwongozo stadi endeleza vita vyako.+

19 Anayezunguka-zunguka akiwa mchongezi anafunua mazungumzo ya siri;+ wala usishirikiane na mtu anayeshawishiwa na midomo yake.+

20 Mtu yeyote anayemlaani baba yake na mama yake,+ taa yake itazimwa giza linapokaribia.+

21 Urithi hupatikana kwa pupa mwanzoni,+ lakini wakati wake ujao hautabarikiwa.+

22 Usiseme: “Nitalipiza uovu!”+  Mtumaini Yehova,+ naye atakuokoa.+

23 Aina mbili za mawe ya mizani ni chukizo kwa Yehova,+ na mizani ya kudanganya si nzuri.+

24 Hatua za mwanamume hutoka kwa Yehova.+ Naye mtu wa udongo anaweza kutambuaje njia yake?+

25 Ni mtego wakati mtu wa udongo amepaaza sauti kwa haraka, “Ni kitakatifu!”+ na baada ya kuweka nadhiri+ ndipo anaelekea kufanya uchunguzi.+

26 Mfalme mwenye hekima anawatawanya watu waovu,+ naye huzungusha gurudumu juu yao.+

27 Pumzi+ ya mtu wa udongo ni taa ya Yehova, inayochunguza kwa uangalifu sehemu zote za ndani kabisa za tumbo.+

28 Fadhili zenye upendo na ukweli—hizo humlinda mfalme;+ na kwa fadhili zenye upendo amedumisha kiti chake cha ufalme.+

29 Uzuri wa vijana ni nguvu zao,+ na utukufu wa wazee ni kichwa chao chenye mvi.+

30 Vidonda vya mapigo ndivyo huondolea mbali ubaya;+ na mapigo, sehemu za ndani kabisa za tumbo.+

21 Moyo wa mfalme ni kama vijito vya maji mkononi mwa Yehova.+ Huugeuza kuelekea popote anapopenda.+

2 Kila njia ya mwanadamu imenyooka machoni pake mwenyewe,+ lakini Yehova anaipima mioyo.+

3 Kutenda uadilifu na hukumu kunampendeza Yehova kuliko dhabihu.+

4 Macho yenye majivuno na moyo wa kiburi,+ taa ya waovu, ni dhambi.+

5 Mipango ya mwenye bidii bila shaka huleta faida,+ lakini kila mtu anayetenda haraka-haraka bila shaka huuelekea uhitaji.+

6 Kupata hazina kwa ulimi wa uwongo ni pumzi inayopeperushwa,+ kwa wale wanaotafuta kifo.+

7 Uporaji wa waovu utawaondolea mbali,+ kwa maana wamekataa kufanya haki.+

8 Mwanadamu, naam, mgeni, ni mpotovu katika njia yake;+ lakini aliye safi ni mnyoofu katika utendaji wake.+

9 Ni afadhali kukaa pembeni mwa paa+ kuliko kukaa pamoja na mke mgomvi, ingawa ni katika nyumba moja.+

10 Nafsi ya mwovu imetamani yaliyo mabaya;+ mwenzake hataonyeshwa kibali machoni pake.+

11 Kwa kumtoza mwenye dhihaka, asiye na uzoefu huwa mwenye hekima;+ na kwa kumpa mtu mwenye hekima ufahamu, yeye hupata ujuzi.+

12 Aliye Mwadilifu anaifikiria nyumba ya mwovu,+ akiwapindua waovu wapate msiba wao.+

13 Yeyote anayeziba sikio lake asisikie kilio cha kulalamika cha mtu wa hali ya chini,+ yeye mwenyewe ataita wala hatajibiwa.+

14 Zawadi inayotolewa katika siri hutuliza hasira;+ na rushwa kifuani+ hutuliza ghadhabu kali.

15 Mwadilifu hushangilia kufanya haki,+ lakini kitu cha kutisha huwapata wale wanaozoea kutenda mambo yenye kuumiza.+

16 Mtu anayeiacha njia ya ufahamu,+ atapumzika katika kutaniko la wale wasiojiweza katika kifo.+

17 Anayependa kujifurahisha atakuwa na uhitaji;+ anayependa divai na mafuta hatapata utajiri.+

18 Mwovu ni fidia ya mwadilifu;+ naye anayetenda kwa hila huchukua mahali pa wanyoofu.+

19 Ni afadhali kukaa nyikani kuliko kukaa pamoja na mke mgomvi pamoja na uchokozi.+

20 Kuna hazina yenye kutamanika na mafuta katika makao ya mwenye hekima,+ lakini mtu aliye mjinga atazimeza.+

21 Anayefuatilia uadilifu+ na fadhili zenye upendo atapata uzima, uadilifu na utukufu.+

22 Mtu mwenye hekima amepanda hata jiji la wanaume wenye nguvu, ili apate kushusha nguvu za uhakika wa jiji hilo.+

23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wake anailinda nafsi yake isipate taabu.+

24 Mtu mwenye kujigamba aliye na kimbelembele na mwenye kujidai, ndilo jina la mtu mwenye ghadhabu ya kimbelembele.+

25 Tamaa yenyewe ya mvivu itamuua, kwa maana mikono yake imekataa kufanya kazi.+ 26 Ametamani kwa hamu siku nzima, lakini aliye mwadilifu anatoa wala hanyimi kamwe.+

27 Dhabihu ya waovu ni chukizo.+ Na mtu anapoileta akiwa na mwenendo mpotovu+ ni zaidi.

28 Shahidi anayesema uwongo ataangamia,+ lakini mtu anayesikiliza atasema hata milele.+

29 Mtu mwovu ameufanya uso wake kuwa mgumu,+ lakini mtu mnyoofu ndiye atakayefanya njia zake imara.+

30 Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri lolote, katika kumpinga Yehova.+

31 Farasi ni kitu kilichowekwa tayari kwa ajili ya siku ya pigano,+ lakini wokovu ni wa Yehova.+

22 Ni afadhali kuchagua jina badala ya utajiri mwingi;+ kibali ni bora kuliko hata fedha na dhahabu.+

2 Mtu tajiri na maskini wamekutana.+ Mtengenezaji wao wote ni Yehova.+

3 Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha,+ lakini wasio na uzoefu wameendelea mbele nao lazima waumie.+

4 Matokeo ya unyenyekevu na kumwogopa Yehova ni utajiri na utukufu na uzima.+

5 Miiba na mitego imo katika njia ya mpotovu;+ yeye anayeilinda nafsi yake hukaa mbali nayo.+

6 Mlee mvulana kulingana na njia inayomfaa;+ hata atakapozeeka hatageuka kando na kuiacha.+

7 Mtu tajiri ndiye huwatawala maskini,+ na mkopaji ni mtumishi wa mtu anayemkopesha.+

8 Yeye anayepanda ukosefu wa uadilifu atavuna madhara,+ lakini fimbo ya ghadhabu yake itafikia mwisho wake.+

9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, kwa maana amempa mtu wa hali ya chini chakula chake.+

10 Mfukuze mwenye dhihaka, ili ugomvi utoke na ili mashtaka ya kisheria na ukosefu wa heshima vikome.+

11 Anayependa usafi wa moyo+—mfalme atakuwa mwenzake kwa sababu ya uvutio wa midomo yake.+

12 Macho ya Yehova mwenyewe yamelinda ujuzi,+ lakini yeye hupindua maneno ya mwenye hila.+

13 Mvivu amesema:+ “Kuna simba nje!+ Nitauawa katikati ya viwanja vya watu wote!”

14 Kinywa cha wanawake wageni ni shimo refu.+ Anayeshutumiwa na Yehova ataanguka ndani yake.+

15 Ujinga umefungwa pamoja na moyo wa mvulana;+ fimbo ya nidhamu ndiyo itakayouondolea mbali.+

16 Anayempunja mtu wa hali ya chini ili ajipatie vitu vingi,+ pia yeye anayempa tajiri, hakika atakuwa na uhitaji.+

17 Tega sikio lako usikie maneno ya wenye hekima,+ ili kuutia moyo wako katika ujuzi wangu.+ 18 Kwa maana inapendeza kwamba uyaweke tumboni mwako,+ ili yapate kufanywa imara midomoni mwako.+

19 Ili uhakika wako uuweke kwa Yehova,+ nimekupa wewe, naam, wewe, ujuzi leo.

20 Je, kufikia sasa sikukuandikia mashauri na ujuzi,+ 21 nikuonyeshe ukweli wa maneno ya kweli, ili urudishe maneno yaliyo kweli—kwa yule anayekutuma?+

22 Usimnyang’anye mtu wa hali ya chini kwa sababu yeye ni wa hali ya chini,+ wala usimkandamize mwenye kuteseka langoni.+ 23 Kwa maana Yehova mwenyewe atatetea kesi yao,+ naye hakika atawanyang’anya nafsi wale wanaowanyang’anya.+

24 Usishirikiane na mtu yeyote mwenye mazoea ya kukasirika;+ wala usiende pamoja na mtu wa mifoko ya ghadhabu, 25 ili usizoee njia yake na hakika uiwekee nafsi yako mtego.+

26 Usiwe kati ya wale wanaopeana mikono+ kwa mapatano, kati ya wale wanaoweka dhamana kwa ajili ya mikopo.+ 27 Ikiwa huna kitu cha kulipa, kwa nini achukue kitanda chako kutoka chini yako?

28 Usiusogeze nyuma mpaka wa zamani za kale, uliowekwa na mababu zako.+

29 Je, umemwona mtu stadi katika kazi yake? Yeye atasimama mbele ya wafalme;+ hatasimama mbele ya watu wa kawaida.

23 Ukiketi kula pamoja na mfalme, fikiria sana kilicho mbele yako,+ 2 nawe ujitie kisu kooni ikiwa una nafsi yenye tamaa.+ 3 Usionyeshe kuwa unatamani vyakula vyake vitamu, kwa maana ni vyakula vya uwongo.+

4 Usijitaabishe kutafuta utajiri.+ Acha kutegemea uelewaji wako mwenyewe.+ 5 Je, umeukazia macho, nao si kitu?+ Kwa maana hakika huo hujifanyia mabawa kama yale ya tai na kuruka kuelekea mbinguni.+

6 Usile chakula cha mtu mwenye jicho lisilo na ukarimu,+ wala kujionyesha kuwa unatamani vyakula vyake vitamu.+ 7 Kwa maana yeye ni kama mtu ambaye amefikiria ndani ya nafsi yake.+ “Kula na kunywa,” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.+ 8 Utatapika tonge ulilokula, nawe utakuwa umepoteza maneno yako matamu.+

9 Usiseme masikioni mwa mtu mjinga,+ kwa maana atayadharau maneno yako yenye busara.+

10 Usiusogeze nyuma mpaka wa zamani za kale,+ wala usiingie katika shamba la wavulana wasio na baba.+ 11 Kwa maana Mkombozi wao ana nguvu; yeye mwenyewe atatetea kesi yao dhidi yako wewe.+

12 Elekeza moyo wako kwenye nidhamu na sikio lako kwenye maneno ya ujuzi.+

13 Usimnyime mvulana nidhamu.+ Ukimpiga kwa fimbo, hatakufa. 14 Inakupasa wewe mwenyewe umpige kwa fimbo, upate kuikomboa nafsi yake na Kaburi.*+

15 Mwanangu, ikiwa moyo wako umekuwa na hekima,+ moyo wangu utashangilia, naam, moyo wangu.+ 16 Na figo zangu zitashangilia midomo yako inaposema mambo manyoofu.+

17 Moyo wako usiwaonee wivu watenda-dhambi,+ lakini umwogope Yehova mchana kutwa.+ 18 Kwa maana ndipo kutakapokuwa na wakati ujao,+ na tumaini lako mwenyewe halitakatiliwa mbali.+

19 Ewe mwanangu, sikia uwe na hekima, na kuuongoza moyo wako katika njia hiyo.+

20 Usiwe kati ya watu wanaokunywa divai mno,+ kati ya watu wanaokula nyama kwa ulafi.+ 21 Kwa maana mlevi na mlafi watakuwa maskini,+ na kusinzia kutamvika mtu nguo zilizopasuka.+

22 Msikilize baba yako aliyekuzaa,+ wala usimdharau mama yako kwa sababu tu amezeeka.+ 23 Nunua kweli+ wala usiiuze​—​hekima na nidhamu na uelewaji.+ 24 Baba ya mtu mwadilifu hakika atakuwa na shangwe;+ na mtu anayekuwa baba ya mwenye hekima atamshangilia pia.+ 25 Baba yako na mama yako watashangilia, naye mama aliyekuzaa atakuwa na shangwe.+

26 Mwanangu, nipe moyo wako, nayo macho yako na yapendezwe na njia zangu mwenyewe.+ 27 Kwa maana kahaba ni shimo refu+ na mwanamke mgeni ni kisima chembamba. 28 Kwa kweli, yeye huvizia, kama mnyang’anyi;+ naye huwaongeza wenye hila katika wanadamu.+

29 Ni nani aliye na ole? Ni nani aliye na wasiwasi? Ni nani aliye na ugomvi?+ Ni nani aliye na mahangaiko? Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu? Ni nani aliye na macho mazito? 30 Ni wale wanaokaa muda mrefu kwenye divai,+ wale wanaoenda kutafuta divai iliyochanganyika.+ 31 Usiitazame divai inapotoa rangi nyekundu, inapochemka katika kikombe, inaposhuka taratibu. 32 Mwisho wake inauma kama nyoka,+ nayo hutoa sumu kama nyoka.+ 33 Macho yako mwenyewe yataona mambo mageni, nao moyo wako mwenyewe utasema mambo yaliyopotoka.+ 34 Nawe utakuwa kama mtu anayelala katikati ya bahari, kama mtu anayelala juu ya mlingoti.+ 35 “Wamenipiga, lakini sikuwa mgonjwa; wamenichapa, lakini sikujua; Nitaamka wakati gani?+ Bado nitaitafuta hata zaidi.”+

24 Usiwaonee wivu watu wabaya,+ wala usitamani kuingia pamoja nao.+ 2 Kwa maana moyo wao huendelea kutafakari juu ya uporaji, nayo midomo yao huendelea kuongea juu ya matata.+

3 Nyumba hujengwa kwa hekima,+ na kwa utambuzi itasimamishwa imara.+ 4 Na kwa ujuzi vyumba vya ndani vitajazwa vitu vyote vyenye thamani na vyenye kupendeza.+

5 Mtu mwenye hekima katika nguvu ni mwanamume,+ na mtu mwenye ujuzi anaimarisha nguvu.+ 6 Kwa maana kwa mwongozo stadi utaendeleza vita vyako,+ na kwa wingi wa washauri kuna wokovu.+

7 Kwa mpumbavu, hekima ya kweli iko juu mno;+ hatafungua kinywa chake langoni.

8 Yeyote anayepanga hila ya kufanya ubaya ataitwa fundi wa mawazo ya uovu.+

9 Mwenendo mpotovu wa upumbavu ni dhambi,+ na mwenye dhihaka ni chukizo kwa wanadamu.+

10 Je, umejionyesha kuwa umevunjika moyo siku ya taabu?+ Nguvu zako zitakuwa chache.

11 Wakomboe wale wanaopelekwa kwenye kifo; na uwazuie wale wanaopepesuka wakielekea kuchinjwa.+ 12 Ikiwa utasema: “Tazama! Hatukujua hili,”+ je, yule anayeipima mioyo hatatambua hilo,+ na yule anayeichunguza nafsi yako mwenyewe hatajua+ hilo naye hakika hatamlipa mtu wa udongo kulingana na utendaji wake?+

13 Mwanangu, kula asali, kwa maana ni njema; asali tamu ya sega na iwe katika kaakaa lako.+ 14 Vivyo hivyo, ijue hekima kwa ajili ya nafsi yako.+ Ikiwa umeipata, basi kuna wakati ujao, na tumaini lako mwenyewe halitakatiliwa mbali.+

15 Usijifiche ili kushambulia makao ya mwadilifu kama anavyofanya mwovu;+ usipore mahali pake pa kupumzikia.+ 16 Kwa maana huenda mwadilifu akaanguka hata mara saba, naye hakika atasimama;+ lakini waovu watakwazwa na msiba.+

17 Adui yako anapoanguka, usishangilie; naye anapokwazwa, moyo wako usiwe na shangwe,+ 18 ili Yehova asipate kuona jambo hilo nalo liwe baya machoni pake, naye aigeuzie hasira yake mbali naye.+

19 Usiwake kwa hasira juu ya watenda-maovu. Usiwaonee wivu watu waovu.+ 20 Kwa maana mtu yeyote mbaya hatakuwa na wakati ujao;+ taa ya watu waovu itazimwa.+

21 Mwanangu, mwogope Yehova na mfalme.+ Usishirikiane na watu wanaotaka badiliko.+ 22 Kwa maana msiba wao utakuja ghafula,+ hivi kwamba ni nani anayejua juu ya kuangamizwa kwa watu wanaotaka badiliko?+

23 Maneno haya pia ni kwa ajili ya watu wenye hekima:+ Kuonyesha upendeleo katika hukumu si jambo zuri.+

24 Anayemwambia mtu mwovu: “Wewe ni mwadilifu,”+ watu watamlaani, na vikundi vya mataifa vitamshutumu. 25 Lakini kwao wanaomkaripia mambo yatakuwa yenye kupendeza,+ nayo baraka ya mema itawajia.+ 26 Anayejibu kwa njia ya unyoofu atabusu midomo.+

27 Tayarisha kazi yako huko nje, uifanye tayari kwa ajili yako shambani.+ Kisha ujenge nyumba yako.

28 Usimshuhudie mwenzako pasipo msingi.+ Ndipo ungekuwa mpumbavu kwa midomo yako.+ 29 Usiseme: “Nitamtendea kama vile tu alivyonitendea.+ Nitamlipa kila mtu kulingana na tendo lake.”+

30 Nilipitia kando ya shamba la mtu mvivu+ na kando ya shamba la mizabibu la mtu aliyepungukiwa moyoni.+ 31 Na tazama! Lote lilizaa magugu.+ Uso wake ulifunikwa na miiba, nao ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomolewa.+

32 Basi nikaona, mimi mwenyewe; nikaanza kutia jambo hilo moyoni;+ nikaona, nikaikubali nidhamu:+ 33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kukunja mikono kidogo ili kulala,+ 34 nao umaskini wako utakuja kama mnyang’anyi wa njia kuu na uhitaji wako kama mwanamume mwenye silaha.+

25 Hizi pia ni methali za Sulemani+ ambazo watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda,+ walinakili:

2 Utukufu wa Mungu ni kuweka jambo kuwa siri,+ nao utukufu wa wafalme ni kuchunguza jambo kabisa.+

3 Mbingu kwa kimo na dunia kwa kina,+ na moyo wa wafalme,+ hayo hayachunguziki.+

4 Takataka na iondolewe kwenye fedha, na yote itatoka ikiwa safi.+

5 Mwovu na aondolewe mbele ya mfalme,+ na kiti chake cha ufalme kitafanywa imara kwa uadilifu wenyewe.+

6 Usijiheshimu mwenyewe mbele ya mfalme,+ wala usisimame mahali pa wakuu.+ 7 Kwa maana ni afadhali yeye akuambie: “Njoo hapa,”+ kuliko akushushe mbele ya mtu mwenye cheo ambaye macho yako yamemwona.+

8 Usiende kwa haraka kufanya kesi, ili sasa swali lisiwe utafanya nini mwishowe mwenzako anapokuaibisha.+ 9 Jitetee kwa mwenzako,+ wala usifunue mazungumzo ya siri ya mwingine;+ 10 ili anayesikiliza asikuaibishe na habari yako mbaya iwe haiwezi kufutwa.

11 Neno linalosemwa wakati unaofaa ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu kwenye chombo cha fedha kilichopambwa.+

12 Pete ya dhahabu na pambo la dhahabu ya pekee, ndivyo alivyo mkaripiaji mwenye hekima kwenye sikio linalosikia.+

13 Kama baridi ya theluji+ siku ya mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wanaomtuma, kwa maana yeye huiburudisha nafsi ya mabwana wake.+

14 Kama wingu la mvuke na upepo bila mvua ndivyo alivyo mtu anayejisifu kwa uwongo juu ya zawadi.+

15 Kwa subira kiongozi hushawishiwa, na ulimi wa upole unaweza kuvunja mfupa.+

16 Je, umepata asali?+ Kula kiasi cha kukutosha, ili usiile kupita kiasi kisha uitapike.+

17 Fanya mguu wako uwe haba nyumbani kwa mwenzako, asije akakuchoka na hakika akuchukie.

18 Kama rungu ya vita na upanga na mshale mkali ndivyo alivyo mtu anayemshuhudia mwenzake kwa uwongo.+

19 Uhakika katika mtu mwenye hila siku ya taabu, ni kama jino lililovunjika na mguu ulioteguka.+

20 Yeye anayevua nguo siku ya baridi ni kama siki kwenye magadi na kama mwimbaji anayemwimbia mtu aliye na moyo wenye huzuni.+

21 Ikiwa mtu anayekuchukia ana njaa, mpe mkate ale; na ikiwa ana kiu, mpe maji anywe.+ 22 Kwa maana unakusanya makaa ya moto juu ya kichwa chake,+ na Yehova mwenyewe atakupa thawabu.+

23 Upepo wa kaskazini hutokeza mvua+ kana kwamba kwa uchungu wa kuzaa; nao ulimi unaofunua siri hutokeza uso ulioshutumiwa.+

24 Ni afadhali kukaa pembeni mwa paa kuliko kukaa pamoja na mke mgomvi, ingawa ni katika nyumba moja.+

25 Kama maji baridi kwa nafsi iliyochoka+ ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.+

26 Mwadilifu anapopepesuka mbele ya mwovu ni kama bubujiko la maji yaliyochafuka na kisima kilichoharibika.+

27 Si vizuri kula asali nyingi mno;+ na watu kujitafutia utukufu wao wenyewe, je, huo ni utukufu?+

28 Mtu asiyezuia roho yake ni kama jiji lililobomolewa, lisilo na ukuta.+

26 Kama theluji wakati wa kiangazi na kama mvua wakati wa mavuno,+ kadhalika mtu mjinga hastahili utukufu.+

2 Kama ndege alivyo na sababu ya kukimbia na mbayuwayu alivyo na sababu ya kuruka, hivyo laana haiji bila sababu halisi.+

3 Mjeledi ni wa farasi,+ lijamu+ ni ya punda, nayo fimbo ni ya mgongo wa watu wajinga.+

4 Usimjibu mtu yeyote mjinga kulingana na upumbavu wake, ili wewe nawe usiwe sawa na yeye.+

5 Mjibu mjinga kulingana na upumbavu wake, ili asipate kuwa mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe.+

6 Kama mtu anayekata-kata miguu yake, kama mtu anayekunywa jeuri tupu, ndivyo alivyo mtu anayetia mambo mikononi mwa mjinga.+

7 Je, miguu ya kilema imeteka maji? Ikiwa ndivyo basi kinywani mwa watu wajinga mna methali.+

8 Kama mtu anayefungia jiwe kwenye rundo la mawe, ndivyo alivyo mtu anayempa mtu mjinga utukufu.+

9 Kama gugu lenye miiba lilivyoingia katika mkono wa mlevi, ndivyo na methali ndani ya kinywa cha watu wajinga.+

10 Kama mpiga-mishale anayechoma kila kitu ndivyo alivyo mtu anayeajiri mjinga+ au anayeajiri wapita-njia.

11 Kama mbwa anayerudia matapiko yake, ndivyo mtu mjinga anavyorudia upumbavu wake.+

12 Je, umemwona mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe?+ Kuna tumaini zaidi kwa mjinga+ kuliko kwake.

13 Mvivu amesema: “Kuna mwana-simba njiani, simba katikati ya viwanja vya watu wote.”+

14 Kama vile mlango unavyogeuka katika bawaba zake, ndivyo alivyo mvivu katika kitanda chake.+

15 Mvivu ameutia mkono wake katika bakuli la karamu; amechoka mno asiweze kuurudisha kwenye kinywa chake.+

16 Machoni pake mwenyewe mvivu ni mwenye hekima+ kuliko watu saba wanaojibu kwa kutumia akili.

17 Mpita-njia yeyote anayekasirishwa na ugomvi usio wake ni kama mtu anayemshika mbwa masikio.+

18 Kama mtu mwenye wazimu anayetupa silaha za moto,+ mishale na kifo, 19 ndivyo alivyo mtu ambaye amemdanganya mwenzake na kusema: “Je, sikuwa nikifanya mzaha tu?”+

20 Pasipo na kuni moto huzimika, na pasipo na mchongezi ugomvi hutulia.+

21 Kama kuongeza makaa kwenye makaa yanayowaka na kuni kwenye moto, ndivyo mtu mgomvi hufanya ugomvi+ uwake moto.

22 Maneno ya mchongezi ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa, vinavyoingia katika sehemu za ndani kabisa za tumbo.+

23 Kama fedha inayofunika kipande cha chombo cha udongo, ndivyo ilivyo midomo yenye bidii pamoja na moyo mbaya.+

24 Kwa midomo yake, mtu mwenye chuki hujificha asitambuliwe, lakini ndani yake huweka udanganyifu.+ 25 Ijapokuwa yeye huifanya sauti yake kuwa yenye kupendeza,+ usimwamini,+ kwa maana mna machukizo saba+ moyoni mwake. 26 Chuki hufunikwa kwa udanganyifu. Ubaya wake utafunuliwa katika kutaniko.+

27 Anayechimba shimo ataanguka ndani yake,+ naye anayeviringisha jiwe—litarudi kwake.+

28 Ulimi wa uwongo humchukia mtu aliyepondwa nao,+ na kinywa chenye kubembeleza husababisha mapinduzi.+

27 Usijisifu kwa sababu ya siku inayofuata,+ kwa maana hujui siku itazaa nini.+

2 Mwingine na akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mgeni na afanye hivyo, wala si midomo yako mwenyewe.+

3 Uzito wa jiwe na mzigo wa mchanga+—lakini usumbufu wa mpumbavu ni mzito kuliko vyote viwili.+

4 Kuna ukatili wa ghadhabu, pia furiko la hasira,+ lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?+

5 Karipio lililofunuliwa+ ni afadhali kuliko upendo uliofichwa.

6 Vidonda vinavyosababishwa na mpenzi ni vya uaminifu,+ lakini busu za mtu mwenye chuki zinapatikana kwa maombi ya kusihi.+

7 Nafsi ambayo imeshiba itakanyagia chini asali ya sega, lakini kwa nafsi yenye njaa kila kitu kichungu ni kitamu.+

8 Kama ndege anayekimbia kiota chake,+ ndivyo alivyo mtu anayekimbia mahali pake.+

9 Mafuta na uvumba+ ndivyo huufanya moyo ushangilie, ndivyo pia utamu wa rafiki ya mtu kwa sababu ya shauri la nafsi.+

10 Usimwache rafiki yako au rafiki ya baba yako, wala usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku ya msiba wako. Jirani aliye karibu ni afadhali kuliko ndugu aliye mbali.+

11 Uwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie,+ ili nipate kumjibu anayenidhihaki.+

12 Mtu mwerevu ambaye ameuona msiba amejificha;+ wasio na uzoefu ambao wamepita wamepatwa na mabaya.+

13 Ikiwa mtu amemwekea mgeni dhamana, lichukue vazi lake;+ na ikiwa amejihusisha na mwanamke mgeni, chukua rehani kutoka kwake.+

14 Anayembariki mwenzake kwa sauti kubwa asubuhi na mapema, itahesabiwa kwake kuwa ni laana.+

15 Paa inayovuja maji ambayo humfukuza mtu katika siku ya mvua inayonyesha mfululizo ni sawa na mke mgomvi.+ 16 Mtu yeyote anayemzuia, ameuzuia upepo, na mkono wake wa kuume hukutana na mafuta.

17 Chuma hunolewa kwa chuma. Ndivyo mtu anavyounoa uso wa mwingine.+

18 Anayeulinda mtini atakula matunda yake,+ naye anayemlinda bwana wake ataheshimiwa.+

19 Kama uso unavyolingana na uso kwenye maji, kadhalika moyo wa mwanadamu hulingana na moyo wa mwanadamu mwenzake.

20 Kaburi* na mahali pa uharibifu+ hazitosheki;+ wala macho ya mwanadamu hayatosheki.+

21 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha,+ na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu;+ na mtu hulingana na sifa yake.+

22 Hata ukimtwanga mpumbavu awe laini kwa mtwangio katika kinu, pamoja na nafaka iliyovunjika, upumbavu wake hautamtoka.+

23 Unapaswa kujua vizuri hali ya kundi lako. Elekeza moyo wako kwenye makundi yako;+ 24 kwa maana hazina haitadumu mpaka wakati usio na kipimo,+ wala taji kwa vizazi vyote.

25 Majani mabichi yameondoka, na majani mapya yametokea, na majani ya milimani yamekusanywa.+ 26 Wana-kondoo dume hufaa kwa mavazi yako,+ nao mbuzi-dume ni bei ya shamba. 27 Pia kuna maziwa ya kutosha ya mbuzi kuwa chakula chako, na cha watu wa nyumbani mwako, na riziki+ ya wasichana wako.

28 Mwovu hukimbia wakati hakuna anayemfuatilia,+ lakini waadilifu ni kama mwana-simba mwenye uhakika.+

2 Kwa sababu ya makosa ya nchi wakuu wake hufuatana kwa wingi,+ lakini kwa sababu ya mtu mwenye utambuzi aliye na ujuzi wa lililo sawa, mkuu atakaa muda mrefu.+

3 Mwanamume maskini na ambaye anawapunja+ watu wa hali ya chini ni kama mvua ambayo hufagilia mbali na kusababisha ukosefu wa chakula.

4 Wale wanaoiacha sheria humsifu mwovu,+ lakini wale wanaoishika sheria hushindana nao.+

5 Watu wenye mwelekeo wa ubaya hawawezi kuelewa hukumu, lakini wale wanaomtafuta Yehova wanaweza kuelewa kila jambo.+

6 Afadhali maskini anayetembea katika utimilifu wake kuliko mtu yeyote aliyepotoka katika njia zake, ingawa ni tajiri.+

7 Mwana mwenye uelewaji anashika sheria,+ lakini anayeshirikiana na walafi humletea baba yake aibu.+

8 Anayezidisha vitu vyake vyenye thamani kwa faida+ na riba humkusanyia tu mtu anayeonyesha kibali kwa watu wa hali ya chini.+

9 Anayegeuzia mbali sikio lake asiisikie sheria+—hata sala yake ni chukizo.+

10 Anayewapoteza wanyoofu+ waingie katika njia mbaya ataanguka katika shimo lake mwenyewe,+ lakini wasio na kosa watapata mema.+

11 Mtu tajiri ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe,+ lakini mtu wa hali ya chini mwenye utambuzi humchunguza kabisa.+

12 Waadilifu wanaposhangilia,+ kuna uzuri mwingi; lakini waovu wanaposimama, mtu hujifanya asitambulike.+

13 Anayefunika makosa yake hatafanikiwa,+ lakini yeye anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+

14 Mwenye furaha ni mtu anayehofu sikuzote,+ lakini yeye anayeufanya moyo wake kuwa mgumu ataanguka katika msiba.+

15 Kama simba anayenguruma na dubu anayekimbia ili kushambulia ndivyo alivyo mtu mwovu anayetawala watu wa hali ya chini.+

16 Kiongozi anayepungukiwa na utambuzi wa kweli pia ana mazoea mengi ya upunjaji,+ lakini mtu anayechukia faida isiyo ya haki+ atarefusha siku zake.

17 Mtu aliyelemewa na hatia ya damu ya nafsi atalikimbilia shimo.+ Watu wasimzuie.

18 Anayetembea pasipo kosa ataokolewa,+ lakini yule ambaye amepotoka katika njia zake ataanguka mara moja.+

19 Anayelima udongo wake mwenyewe atakuwa na mkate wa kutosha,+ naye anayefuatilia vitu visivyo na thamani atakuwa na umaskini wa kutosha.+

20 Mtu mwenye matendo ya uaminifu atapata baraka nyingi,+ lakini yeye anayefanya haraka kupata utajiri hatabaki pasipo hatia.+

21 Si vema kuonyesha upendeleo,+ wala si vema kwa mwanamume kufanya kosa kwa sababu ya kipande tu cha mkate.

22 Mtu mwenye jicho la wivu hukimbilia vitu vyenye thamani,+ lakini hajui kwamba atakuwa na uhitaji.

23 Anayemkaripia mtu+ atapata kibali zaidi baadaye kuliko yeye anayebembeleza kwa ulimi wake.

24 Anayemnyang’anya baba yake na mama yake+ na kusema: “Si kosa,”+ ni rafiki ya mtu anayesababisha uharibifu.

25 Mwenye kiburi katika nafsi huchochea ugomvi,+ lakini yeye anayemtegemea Yehova atafanywa anenepe.+

26 Anayetegemea moyo wake mwenyewe ni mjinga,+ lakini yeye anayetembea katika hekima ndiye atakayeponyoka.+

27 Anayempa kitu maskini hatakuwa na uhitaji,+ lakini yeye anayeficha macho yake atapata laana nyingi.+

28 Waovu wanaposimama, mtu hujificha;+ lakini wanapoangamia, waadilifu huongezeka.+

29 Mtu anayekaripiwa+ tena na tena lakini anayeifanya shingo yake kuwa ngumu+ atavunjika ghafula, na hivyo pasipo kuponywa.+

2 Waadilifu wanapokuwa wengi, watu hushangilia;+ lakini mtu yeyote mwovu anapotawala, watu huugua.+

3 Mtu anayependa hekima humfanya baba yake ashangilie,+ lakini yeye anayeshirikiana na makahaba huharibu vitu vyenye thamani.+

4 Mfalme hufanya nchi iendelee kusimama kupitia haki,+ lakini mtu anayekula rushwa huibomoa.+

5 Mwanamume anayembembeleza rafiki yake+ anatandika wavu kwa ajili ya hatua zake.+

6 Katika kosa la mtu mbaya kuna mtego,+ lakini mwadilifu hupaaza sauti kwa shangwe na kufurahi.+

7 Mwadilifu anajua malalamiko halali ya watu wa hali ya chini.+ Aliye mwovu haufikirii ujuzi huo.+

8 Watu wenye maneno ya kujisifu huwasha mji+ moto, lakini wenye hekima hugeuzia mbali hasira.+

9 Mtu mwenye hekima akiisha kuingia katika hukumu pamoja na mtu mpumbavu—amesisimuka na pia amecheka, na hapana pumziko.+

10 Watu wenye kiu ya damu humchukia yeyote asiye na lawama;+ nao wanyoofu, huendelea kuitafuta nafsi ya kila mmoja.+

11 Mtu mjinga huiachilia roho yake yote, lakini mwenye hekima huituliza mpaka mwisho.+

12 Mahali ambapo mtawala anasikiliza maneno ya uwongo, wote wanaomhudumia watakuwa waovu.+

13 Maskini na mtu mwenye kukandamiza wamekutana;+ lakini Yehova anayatia nuru macho yao wote wawili.+

14 Mfalme anapohukumu watu wa hali ya chini kwa ukweli,+ kiti chake cha ufalme kitafanywa imara kwa wakati wote.+

15 Fimbo na karipio ndivyo hutia hekima;+ lakini mvulana aliyeachiliwa atamletea mama yake aibu.+

16 Waovu wanapokuwa wengi, makosa huwa tele; lakini waadilifu watatazama anguko lao.+

17 Mtie adabu mwana wako naye atakupumzisha na kukupa raha nyingi nafsini mwako.+

18 Mahali pasipo na maono watu hujiachilia,+ lakini wenye furaha ni wale wanaoishika sheria.+

19 Mtumishi hatakubali kurekebishwa kwa maneno tu,+ kwa maana anaelewa lakini hajali.+

20 Je, umemwona mtu mwenye haraka kwa maneno yake?+ Kuna tumaini zaidi kwa mjinga kuliko kwake.+

21 Mtu akimbembeleza mtumishi wake tangu ujanani, katika maisha yake ya baadaye hata atakuwa mtu asiye na shukrani.

22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi,+ na mtu yeyote mwenye mwelekeo wa ghadhabu ana makosa mengi.+

23 Majivuno ya mtu wa udongo yatamshusha,+ lakini yeye aliye na roho ya unyenyekevu atapata utukufu.+

24 Anayeshirikiana na mwizi anachukia nafsi yake mwenyewe.+ Huenda akasikia kiapo chenye laana, lakini asitoe habari yoyote.+

25 Kutetemeshwa na wanadamu ndiko huleta mtego,+ lakini yeye anayemtegemea Yehova atalindwa.+

26 Ni wengi wanaoutafuta uso wa mtawala,+ lakini hukumu ya mtu hutoka kwa Yehova.+

27 Mtu asiyetenda kwa haki ni chukizo kwa waadilifu,+ na mtu mnyoofu katika njia yake ni chukizo kwa mwovu.+

30 Maneno ya Aguri mwana wa Yake, ujumbe mzito.+ Maneno ya huyo mwanamume aliyomwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.

2 Kwa maana mimi nawapita watu wote kwa kutotumia akili,+ nami sina ule uelewaji wa wanadamu;+ 3 na sijajifunza hekima;+ nao ujuzi wa Aliye Mtakatifu Zaidi siujui.+

4 Ni nani ambaye amepanda mbinguni ili apate kushuka?+ Ni nani ambaye amekusanya upepo+ katika makonzi yake mawili? Ni nani ambaye ameyafunga maji ndani ya nguo ya kujitanda?+ Ni nani ambaye amefanya miisho yote ya dunia iinuke?+ Jina lake ni nani+ nalo jina la mwana wake ni nani, ikiwa unajua?+

5 Kila neno la Mungu ni safi.+ Yeye ni ngao kwao wanaomkimbilia.+ 6 Usiongeze chochote katika maneno yake+ asije akakukaripia, wala usionekane kuwa mwongo.+

7 Nimeomba mambo mawili kutoka kwako.+ Usininyime mambo hayo kabla sijafa.+ 8 Maneno yasiyo ya kweli na ya uwongo uyaondolee mbali nami.+ Usinipe umaskini wala utajiri.+ Acha nile chakula nilichoamriwa,+ 9 nisije nikashiba nikakukana,+ nikasema: “Yehova ni nani?”+ wala nisiwe maskini, nikaiba na kulishambulia jina la Mungu wangu.+

10 Usimchongee mtumishi kwa bwana wake,+ asije akakulaani, nawe usihesabiwe kuwa na hatia.+

11 Kuna kizazi cha watu ambao humlaani hata baba yao wala hawambariki hata mama yao.+

12 Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao+ wenyewe lakini ambao bado hawajaoshwa mavi yao.+

13 Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yamekwezwa kama nini! na ambao macho yao yenye kung’aa yameinuliwa.+

14 Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga na ambao mifupa yao ya taya ni visu vya kuchinjia,+ ili kuwala wenye kuteseka waondolewe duniani na maskini watoke kati ya wanadamu.+

15 Wadudu-ruba wana binti wawili wanaolia: “Nipe! Nipe!” Kuna vitu vitatu visivyoshiba, naam, kuna vinne ambavyo havijasema: “Inatosha!” 16 Kaburi*+ na tumbo la uzazi lililozuiwa,+ nchi ambayo haijashiba maji,+ na moto+ usiosema: “Inatosha!”+

17 Jicho ambalo humdhihaki baba na kudharau utii kwa mama+—kunguru wa bondeni wataling’oa na wana wa tai watalila.

18 Kuna mambo matatu ambayo yameonekana kuwa ya ajabu mno kwangu, naam, kuna manne ambayo sijapata kuyajua: 19 njia ya tai mbinguni, njia ya nyoka juu ya mwamba, njia ya meli katika moyo wa bahari+ na njia ya mwanamume pamoja na mwanamwali.+

20 Tazama, hii ndiyo njia ya mwanamke mzinzi: amekula, akapangusa kinywa chake na kusema: “Sijafanya kosa lolote.”+

21 Chini ya mambo matatu dunia imehangaishwa, na chini ya manne haiwezi kuvumilia: 22 chini ya mtumwa anapotawala akiwa mfalme,+ na mtu asiye na akili anapokuwa na chakula cha kutosha;+ 23 chini ya mwanamke anayechukiwa wakati anapochukuliwa na kuwa mke,+ na mjakazi anapompindua bimkubwa wake.+

24 Kuna vitu vinne vilivyo vidogo zaidi duniani, lakini vina hekima ya kisilika:+ 25 chungu ni kikundi cha watu wasio na nguvu,+ hata hivyo wakati wa kiangazi wao hutayarisha chakula chao;+ 26 wibari+ ni kikundi cha watu wasio na nguvu, hata hivyo wao hujenga nyumba yao kwenye mwamba;+ 27 nzige+ hawana mfalme, hata hivyo wao huenda mbele wote wakiwa wamegawanywa vikundi-vikundi;+ 28 mjusi+ hushika kwa mikono yake mwenyewe naye yumo katika jumba kuu la mfalme.

29 Kuna watatu wenye mwendo mzuri, na kuna wanne wanaotembea vyema: 30 simba, ambaye ndiye mwenye nguvu zaidi kati ya wanyama na wala harudi nyuma mbele ya yeyote;+ 31 mbwa-mwindaji au mbuzi-dume, na mfalme wa kikosi cha askari-jeshi cha watu wake mwenyewe.+

32 Ikiwa umetenda bila kutumia akili kwa kujiinua mwenyewe,+ na ikiwa umekaza fikira zako juu ya jambo hilo, weka mkono wako kwenye kinywa chako.+ 33 Kwa maana kupiga-piga maziwa ndiko hutokeza siagi, na kufinya pua ndiko hutokeza damu, na kuchochea hasira ndiko hutokeza ugomvi.+

31 Maneno ya Lemueli mfalme, ujumbe mzito+ ambao mama yake alimwambia ili kumrekebisha:+

2 Niseme nini, ewe mwanangu, niseme nini, ewe mwana wa tumbo langu,+ niseme nini, ewe mwana wa nadhiri zangu?+

3 Usiwape wanawake nguvu zako za uhai,+ wala njia zako kwa kitu ambacho hufanya wafalme wafutiliwe mbali.+

4 Haifai wafalme, ewe Lemueli, haifai wafalme kunywa divai wala maofisa wakuu kuuliza: “Kileo kiko wapi?”+ 5 ili mtu asinywe na kusahau jambo lililoagizwa na kupotosha haki ya yeyote wa wana wa mateso.+ 6 Mpeni kileo mtu yeyote anayekaribia kuangamia+ na kuwapa divai watu wenye uchungu katika nafsi.+ 7 Acheni mtu anywe na kuusahau umaskini wake, na mtu asiikumbuke taabu yake tena.

8 Fungua kinywa chako kwa ajili ya mtu asiyeweza kusema,+ ili kutetea watu wote wanaopitilia mbali.+ 9 Fungua kinywa chako, hukumu kwa uadilifu na kutetea mtu mwenye kuteseka na maskini.+

א [ʼAʹleph]

10 Mke mwenye uwezo, ni nani anayeweza kumpata?+ Thamani yake inapita sana ile ya marijani.

ב [Behth]

11 Moyo wa mume wake umemtegemea, wala hakuna faida inayokosekana.+

ג [Giʹmel]

12 Amemthawabisha mume wake kwa mema, wala si kwa mabaya, siku zote za maisha yake.+

ד [Daʹleth]

13 Ametafuta sufu na kitani, naye hufanya kazi yoyote inayopendeza mikono yake.+

ה [Heʼ]

14 Amekuwa kama meli za mfanyabiashara.+ Huleta chakula chake kutoka mbali.

ו [Waw]

15 Tena huamka kabla usiku haujaisha,+ na kuwapa watu wa nyumbani mwake chakula na kuwapa vijana wake wa kike fungu lao lililoamriwa.+

ז [Zaʹyin]

16 Amefikiria shamba, akalinunua;+ amepanda shamba la mizabibu kutokana na matunda ya mikono yake.+

ח [Chehth]

17 Amejifunga nguvu viunoni, naye ameitia nguvu mikono yake.+

ט [Tehth]

18 Ametambua kwamba biashara yake ni nzuri; taa yake haizimiki usiku.+

י [Yohdh]

19 Amenyoosha mikono yake kushika kijiti cha kusokotea uzi, nayo mikono yake mwenyewe imeshika gurudumu la kusokota nyuzi.+

כ [Kaph]

20 Amewanyooshea mkono wenye kuteseka, na mikono yake amemkunjulia maskini.+

ל [Laʹmedh]

21 Hana wasiwasi juu ya watu wa nyumbani mwake kwa sababu ya theluji, kwa maana watu wote wa nyumbani mwake wamevaa mavazi mawili.+

מ [Mem]

22 Amejitengenezea matandiko yenye mapambo.+ Mavazi yake ni ya kitani na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau.+

נ [Nun]

23 Mume wake+ ni mtu anayejulikana malangoni,+ anapoketi pamoja na wanaume wazee wa nchi.

ס [Saʹmekh]

24 Hata ametengeneza mavazi ya ndani+ na kuyauza, nao wafanya-biashara amewapa mishipi.

ע [ʽAʹyin]

25 Nguvu na fahari ndiyo mavazi yake,+ naye anaucheka wakati ujao.+

פ [Peʼ]

26 Hufungua kinywa chake kwa hekima,+ na sheria ya fadhili zenye upendo ziko katika ulimi wake.+

צ [Tsa·dhehʹ]

27 Anaangalia shughuli za nyumba yake, wala hali mkate wa uvivu.+

ק [Qohph]

28 Wanawe wamesimama na kumtangaza kuwa mwenye furaha,+ mume wake husimama, naye humsifu.+

ר [Rehsh]

29 Kuna binti wengi+ ambao wameonyesha uwezo, lakini wewe—wewe umewapita hao wote.+

ש [Shin]

30 Uvutio unaweza kudanganya,+ nayo sura yenye kupendeza inaweza kuwa ubatili;+ lakini mwanamke anayemwogopa Yehova ndiye anayejiletea sifa.+

ת [Taw]

31 Mpeni baadhi ya matunda ya mikono yake,+ nazo kazi zake na zimsifu malangoni.+

[Maelezo ya Chini]

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki