Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Zaburi 1:1-150:6
  • Zaburi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Zaburi
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Zaburi

Zaburi

KITABU CHA KWANZA

(Zaburi 1 – 41)

1 Mwenye furaha+ ni mtu ambaye hakutembea katika shauri la waovu,+

Na katika njia ya watenda-dhambi hakusimama,+

Na katika kiti cha wenye dhihaka hakuketi.+

 2 Bali mapendezi yake ni katika sheria ya Yehova,+

Naye huisoma sheria yake kwa sauti ya chini mchana na usiku.+

 3 Naye hakika atakuwa kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji,+

Ambao hutoa matunda yake katika majira yake+

Na ambao majani yake hayanyauki,+

Na kila jambo analofanya litafanikiwa.+

 4 Waovu hawako hivyo,

Bali wako kama makapi ambayo upepo hupeperusha.+

 5 Ndiyo sababu waovu hawatasimama katika hukumu,+

Wala watenda-dhambi katika kusanyiko la waadilifu.+

 6 Kwa maana Yehova anaijua njia ya waadilifu,+

Bali njia ya waovu itaangamia.+

2 Kwa nini mataifa yamekuwa na fujo+

Na vikundi vya mataifa vimeendelea kusema jambo la upuuzi?+

 2 Wafalme wa dunia wanachukua msimamo wao+

Nao maofisa wakuu wamejikusanya pamoja kama mtu mmoja+

Dhidi ya Yehova+ na dhidi ya mtiwa-mafuta wake,+

 3 Wakisema: “Na tuzikate pingu zao+

Na kuzitupa kamba zao mbali nasi!”+

 4 Yule anayeketi mbinguni+ atacheka;

Yehova mwenyewe atawadharau.+

 5 Wakati huo atasema nao katika hasira yake+

Na katika ghadhabu yake atawafadhaisha,+

 6 Na kusema: “Mimi, naam, mimi nimemweka mfalme wangu+

Juu ya Sayuni,+ mlima wangu mtakatifu.”+

 7 Acheni nirejezee agizo la Yehova;

Yeye ameniambia: “Wewe ni mwanangu;+

Mimi, leo, nimekuwa baba yako.+

 8 Niombe,+ ili nikupe mataifa yawe urithi wako+

Na miisho ya dunia iwe miliki yako mwenyewe.+

 9 Utawavunja kwa fimbo ya chuma ya enzi,+

Utawavunja vipande-vipande, kama chombo cha mfinyanzi.”+

10 Na sasa, enyi wafalme, onyesheni ufahamu;

Kubalini kurekebishwa, enyi waamuzi wa dunia.+

11 Mtumikieni Yehova kwa woga+

Na mshangilie kwa kutetemeka.+

12 Mbusuni mwana,+ ili Yeye asikasirike

Nanyi msiangamizwe kutoka njiani,+

Kwa maana hasira yake huwaka kwa urahisi.+

Wenye furaha ni wale wote wanaomkimbilia.+

Muziki wa Daudi alipokuwa akikimbia kwa sababu ya Absalomu mwana wake.+

3 Ee Yehova, kwa nini adui zangu wamekuwa wengi?+

Kwa nini wengi wanainuka dhidi yangu?+

 2 Wengi wanasema juu ya nafsi yangu:

“Hakuna wokovu kwa ajili yake kutoka kwa Mungu.”+ Sela.

 3 Na bado wewe, Ee Yehova, ni ngao inayonizunguka,+

Utukufu+ wangu na Mwenye kuinua kichwa changu.+

 4 Kwa sauti yangu nitamwita Yehova,

Naye atanijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.+ Sela.

 5 Nami nitajilaza nipate kulala usingizi;

Hakika nitaamka, kwa maana Yehova anaendelea kunitegemeza.+

 6 Sitaogopa maelfu kumi ya watu

Ambao wamejipanga dhidi yangu kunizunguka pande zote.+

 7 Usimame,+ Ee Yehova! Uniokoe,+ Ee Mungu wangu!+

Kwa maana utawapiga adui zangu wote kwenye taya.+

Utayavunja meno ya waovu.+

 8 Wokovu ni wa Yehova.+

Baraka yako iko juu ya watu wako.+ Sela.

Kwa kiongozi wa vinanda.+ Muziki wa Daudi.

4 Ninapoita, unijibu, Ee Mungu wangu mwadilifu.+

Katika taabu unifanyie nafasi pana

Nionyeshe kibali+ na kuisikia sala yangu.

 2 Enyi wana wa watu, utukufu+ wangu utatukanwa mpaka wakati gani,

Huku mkiendelea kupenda mambo ya upuuzi,

Huku mkiendelea kutafuta uwongo? Sela.

 3 Basi jueni kwamba hakika Yehova atamtendea mshikamanifu wake kwa njia ya pekee;+

Yehova mwenyewe atasikia ninapomwita.+

 4 Fadhaikeni, lakini msitende dhambi.+

Semeni moyoni mwenu, kitandani mwenu,+ na kunyamaza. Sela.

 5 Toeni dhabihu za uadilifu,+

Na kumtumaini Yehova.+

 6 Kuna wengi wanaosema: “Ni nani atakayetuonyesha mema?”

Inua nuru ya uso wako juu yetu,+ Ee Yehova.

 7 Hakika wewe utaupa moyo wangu shangwe+

Iliyo kubwa kuliko wakati ambapo nafaka yao na divai yao mpya imejaa.+

 8 Katika amani nitajilaza na kulala usingizi,+

Kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, hunifanya nikae kwa usalama.+

Kwa kiongozi wa Nehilothi. Muziki wa Daudi.

5 Kwa maneno yangu utege sikio,+ Ee Yehova;

Uelewe kuugua kwangu.

 2 Sikiliza kwa makini sauti ya kilio changu kwa ajili ya msaada,+

Ee Mfalme+ wangu na Mungu wangu, kwa maana kwako wewe ninasali.+

 3 Ee Yehova, asubuhi utasikia sauti yangu;+

Asubuhi nitajieleza kwako na kukaa macho.+

 4 Kwa maana wewe si Mungu anayependezwa na uovu;+

Hakuna mtu yeyote mbaya atakayekaa na wewe kwa muda wowote.+

 5 Hakuna watu wowote wenye kujisifu watakaosimama mbele za macho yako.+

Wewe huwachukia wote wanaozoea kufanya mambo yenye kuumiza;+

 6 Utawaangamiza wale wanaosema uwongo.+

Mtu anayemwaga damu+ na mdanganyifu+ Yehova anamchukia.

 7 Na mimi, katika wingi wa fadhili zako zenye upendo+

Nitaingia katika nyumba yako,+

Nitainama kulielekea hekalu lako takatifu kwa kukuogopa.+

 8 Ee Yehova, uniongoze katika uadilifu+ wako kwa sababu ya adui zangu;+

Uifanye njia yako iwe laini mbele yangu.+

 9 Kwa maana katika kinywa chao hakuna lolote lenye kutegemeka;+

Sehemu yao ya ndani ni shida kwelikweli.+

Koo yao ni kaburi lililo wazi;+

Wanatumia ulimi laini.+

10 Hakika Mungu atawahesabia hatia;+

Wataanguka kwa sababu ya mashauri yao wenyewe.+

Na watawanywe katika wingi wa makosa yao,+

Kwa sababu wamekuasi wewe.+

11 Lakini wote wanaokukimbilia watashangilia;+

Watapiga vigelegele vya shangwe+ mpaka wakati usio na kipimo.

Nawe utaweka kizuizi wasifikiwe,

Nao wanaolipenda jina lako watakushangilia.+

12 Kwa maana wewe mwenyewe utambariki mtu yeyote aliye mwadilifu,+ Ee Yehova;

Kana kwamba kwa ngao+ kubwa, utawazunguka pande zote+ kwa kibali chako.

Kwa kiongozi wa vinanda katika sauti ya nane ya chini.+ Muziki wa Daudi.

6 Ee Yehova, katika hasira yako usinikaripie,+

Na katika ghadhabu yako usinirekebishe.+

 2 Nionyeshe kibali, Ee Yehova, kwa maana mimi ninafifia.+

Niponye,+ Ee Yehova, kwa maana mifupa yangu imesumbuka.

 3 Naam, nafsi yangu imesumbuka sana;+

Nawe, Ee Yehova—hata wakati gani?+

 4 Urudi,+ Ee Yehova, uokoe nafsi yangu;+

Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako zenye upendo.+

 5 Kwa maana katika kifo wewe hutajwi;+

Katika Kaburi* ni nani atakayekusifu?+

 6 Nimechoshwa na kuugua kwangu;+

Usiku kucha nafanya kitanda changu kilowane;+

Kwa machozi yangu nafanya kitanda changu kifurike.+

 7 Kutokana na masumbufu jicho langu limekuwa dhaifu,+

Limezeeka kwa sababu ya wale wote wanaonionyesha uadui.+

 8 Ondokeni kwangu, ninyi nyote mnaozoea kutenda mambo yenye kuumiza,+

Kwa maana hakika Yehova atasikia sauti ya kulia kwangu.+

 9 Yehova mwenyewe atasikia kwelikweli ombi langu la kutaka kibali;+

Yehova ataikubali sala yangu.+

10 Adui zangu wote wataona aibu+ sana na kuwa na wasiwasi;

Watageuka, wataona aibu ghafula.+

Wimbo wa huzuni wa Daudi ambao alimwimbia Yehova kuhusu maneno ya Kushi Mbenyamini.

7 Ee Yehova Mungu wangu,+ nimekukimbilia wewe.+

Uniokoe kutoka kwa wale wote wanaonitesa na unikomboe,+

 2 Ili mtu yeyote asiirarue nafsi yangu vipande-vipande kama simba anavyofanya,+

Kuninyakua wakati ambapo hakuna mkombozi.+

 3 Ee Yehova Mungu wangu, ikiwa nimefanya hili,+

Ikiwa kuna ukosefu wowote wa haki katika mikono yangu,+

 4 Ikiwa nimemlipa ubaya yule anayenipa thawabu,+

Au ikiwa nimempora yeyote anayenionyesha uadui bila kufanikiwa,+

 5 Adui na aifuatilie nafsi yangu+

Naye afikie na kukanyagia chini uhai wangu

Na kufanya utukufu wangu ukae mavumbini. Sela.

 6 Usimame, Ee Yehova, katika hasira yako;+

Uinuke katika milipuko ya ghadhabu ya wale wanaonionyesha uadui,+

Na uamke kwa ajili yangu,+ kwa maana umetoa amri kwa ajili ya hukumu.+

 7 Nalo kusanyiko la vikundi vya mataifa na likuzunguke,

Nawe urudi juu dhidi yake.

 8 Yehova mwenyewe atavihukumu vikundi vya watu.+

Nihukumu, Ee Yehova, kulingana na uadilifu wangu+

Na kulingana na utimilifu+ wangu ulio ndani yangu.

 9 Tafadhali, ubaya wa waovu na ufikie mwisho,+

Nawe umwimarishe mwadilifu;+

Na Mungu akiwa mwadilifu+ anapima moyo+ na figo.+

10 Ngao yangu iko juu ya Mungu,+ Mwokozi wa wale walio wanyoofu moyoni.+

11 Mungu ni Mwamuzi mwadilifu,+

Na Mungu anazitupa shutuma kila siku.

12 Ikiwa mtu yeyote hatarudi,+ Yeye ataunoa upanga wake,+

Hakika ataupinda upinde wake, naye atauweka tayari ili kufyatuliwa.+

13 Naye atajitayarishia silaha za kifo;+

Mishale yake ataifanya kuwa yenye kuwaka moto.+

14 Tazama! Kuna mtu aliye na mimba ya jambo lenye kuumiza,+

Naye amechukua mimba ya taabu na hatakosa kuzaa uwongo.+

15 Amechimbua shimo, naye akalichimba;+

Lakini ataanguka katika shimo alilolifanyiza.+

16 Taabu yake itarudi juu ya kichwa chake mwenyewe,+

Na jeuri yake mwenyewe itashuka juu ya utosi wa kichwa chake.+

17 Nitamsifu Yehova kulingana na uadilifu wake,+

Nami nitalipigia muziki jina+ la Yehova Aliye Juu Zaidi.+

Kwa kiongozi wa Gitithi.+ Muziki wa Daudi.

8 Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu kama nini katika dunia yote,+

Wewe ambaye utukufu wako unasimuliwa juu ya mbingu!+

 2 Kutoka katika kinywa cha watoto na wanaonyonya umeiweka misingi ya nguvu,+

Kwa sababu ya wale wanaokuonyesha uadui,+

Ili kumkomesha adui na yule anayejilipizia kisasi.+

 3 Ninapoziona mbingu zako, kazi za vidole vyako,+

Mwezi na nyota ambazo umetayarisha,+

 4 Mwanadamu anayeweza kufa+ ni nini hivi kwamba umweke akilini,+

Na mwana wa mtu wa udongo hivi kwamba umtunze?+

 5 Pia ulimfanya mdogo kidogo kuliko wale walio kama Mungu,+

Kisha ulimvika taji+ la utukufu+ na fahari.

 6 Unamfanya atawale juu ya kazi za mikono yako;+

Kila kitu umekiweka chini ya miguu yake:+

 7 Kondoo na mbuzi na ng’ombe, wote hao,+

Na pia wanyama wa porini,+

 8 Ndege wa mbinguni na samaki wa baharini,+

Kitu chochote kinachopita katika njia za baharini.+

 9 Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu kama nini katika dunia yote!+

Kwa kiongozi wa Muth-labeni. Muziki wa Daudi.

א [ʼAʹleph]

9 Nitakusifu wewe, Ee Yehova, kwa moyo wangu wote;+

Nitazitangaza kazi zako zote za ajabu.+

 2 Nitakushangilia na kukufurahia,+

Nitalipigia jina lako muziki, Ee Uliye Juu Zaidi.+

ב [Behth]

 3 Adui zangu wanapogeuka nyuma,+

Watajikwaa na kuangamia kutoka mbele zako.+

 4 Kwa maana umetekeleza hukumu yangu na kesi yangu;+

Umeketi juu ya kiti cha ufalme ukihukumu kwa uadilifu.+

ג [Giʹmel]

 5 Umeyakemea mataifa,+ umemwangamiza mwovu.+

Jina lao umelifutilia mbali mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

 6 Ewe adui, ukiwa wako umefikia mwisho wake wa kudumu,+

Na majiji ambayo umeyang’oa.+

Kumbukumbu lao hakika litaangamia.+

ה [Heʼ]

 7 Yeye Yehova ataketi mpaka wakati usio na kipimo,+

Akifanya imara kiti chake cha ufalme kwa ajili ya hukumu.+

 8 Naye mwenyewe ataihukumu kwa uadilifu nchi yenye kuzaa;+

Atavihukumu vikundi vya mataifa kwa unyoofu.+

ו [Waw]

 9 Naye Yehova atakuwa kilele salama kwa ajili ya mtu yeyote aliyekandamizwa,+

Kilele salama wakati wa taabu.+

10 Na wale wanaolijua jina lako watakutegemea,+

Kwa maana hakika hutawaacha wale wanaokutafuta, Ee Yehova.+

ז [Zaʹyin]

11 Mpigieni Yehova muziki, yeye anayekaa Sayuni;+

Tangazeni matendo yake katikati ya vikundi vya watu.+

12 Kwa maana, wakati wa kutafuta umwagikaji wa damu,+ hakika atawakumbuka hao;+

Hakika yeye hatakisahau kilio cha wenye kuteseka.+

ח [Chehth]

13 Unionyeshe kibali, Ee Yehova; uone mateso yangu kutoka kwa wale wanaonichukia,+

Ewe unayeniinua kutoka katika malango ya kifo,+

14 Ili niyatangaze matendo yako yote yanayostahili sifa+

Katika malango+ ya binti Sayuni,+

Ili niushangilie wokovu wako.+

ט [Tehth]

15 Mataifa yamezama katika shimo walilolifanya;+

Mguu wao wenyewe umekamatwa+ katika wavu+ waliouficha.

16 Yehova anajulikana kwa hukumu ambayo ametekeleza.+

Mwovu amenaswa na utendaji wa mikono yake mwenyewe.+

Higayoni. Sela.

י [Yohdh]

17 Watu waovu+ watarudi katika Kaburi,*+

Naam, mataifa yote yanayomsahau Mungu.+

18 Kwa maana maskini hawatasahauliwa sikuzote,+

Wala tumaini la wapole halitaangamia kamwe.+

כ [Kaph]

19 Usimame, Ee Yehova! Mwanadamu anayeweza kufa asiwe na nguvu zaidi.+

Mataifa na yahukumiwe mbele za uso wako.+

20 Utie woga ndani yao, Ee Yehova,+

Ili mataifa yapate kujua kwamba wao ni wanadamu tu wanaoweza kufa.+ Sela.

ל [Laʹmedh]

10 Ee Yehova, kwa nini unaendelea kusimama mbali?+

Kwa nini unaendelea kujificha nyakati za taabu?+

 2 Katika majivuno yake, mwovu humfuatilia vikali mwenye kuteseka;+

Wanakamatwa na mawazo ambayo wametunga.+

 3 Kwa maana mwovu amejisifu kwa sababu ya tamaa yenye ubinafsi ya nafsi yake,+

Naye anayepata faida asiyostahili+ amejibariki;

נ [Nun]

Amekosa kumheshimu Yehova.+

 4 Kwa sababu ya kujigamba kwake, mwovu hatafuti;+

Mawazo yake yote ni: “Hakuna Mungu.”+

 5 Njia zake zinaendelea kufanikiwa wakati wote.+

Maamuzi yako ya hukumu yako juu sana asiweze kuyafikia;+

Nao wale wote wanaomwonyesha uadui, anawafanyia dhihaka.+

 6 Amesema katika moyo wake: “Sitatikiswa;+

Kizazi baada ya kizazi sitakuwa katika msiba.”+

פ [Peʼ]

 7 Kinywa chake kimejaa viapo na udanganyifu na ukandamizaji.+

Chini ya ulimi wake kuna taabu na mambo yenye kuumiza.+

 8 Yeye huketi akivizia makao;

Kutoka mafichoni atamuua mtu asiye na hatia.+

ע [ʽAʹyin]

Macho yake yanamtafuta mtu mwenye taabu.+

 9 Yeye anaendelea kuvizia katika mahali palipofichika kama simba mafichoni mwake.+

Anaendelea kuvizia+ ili amchukue kwa nguvu mtu fulani mwenye kuteseka.

Humchukua kwa nguvu mtu mwenye kuteseka anapouvuta pamoja wavu wake.+

10 Yeye anapondwa, anainama,

Na jeshi la watu waliohuzunika linaangukia kucha zake zenye nguvu.+

11 Yeye amesema katika moyo wake:+ “Mungu amesahau.+

Ameuficha uso wake.+

Hakika hatauona kamwe.”+

ק [Qohph]

12 Usimame,+ Ee Yehova. Ee Mungu, uinue mkono wako.+

Usiwasahau wenye kuteseka.+

13 Kwa nini mwovu amekosa kumheshimu Mungu?+

Amesema katika moyo wake: “Wewe hutatoza hesabu.”+

ר [Rehsh]

14 Kwa maana wewe mwenyewe umeona taabu na masumbufu.

Unaendelea kutazama, uyatie katika mkono wako.+

Mtu mwenye taabu,+ mvulana asiye na baba, anajikabidhi kwako.

Wewe mwenyewe umekuwa msaidizi wake.+

ש [Shin]

15 Uvunje mkono wa mwovu na mbaya.+

Uutafute uovu wake mpaka usiupate tena.+

16 Yehova ni Mfalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

Mataifa yameangamia kutoka katika dunia yake.+

ת [Taw]

17 Tamaa ya wapole hakika utaisikia,+ Ee Yehova.

Utautayarisha moyo wao.+

Utasikiliza kwa makini kwa sikio lako.+

18 Ili kumhukumu mvulana asiye na baba na mtu aliyepondwa,+

Ili mwanadamu anayeweza kufa, aliye wa dunia, asisababishe tena kutetemeka.+

Kwa kiongozi. Ya Daudi.

11 Nimemkimbilia Yehova.+

Mnawezaje kuthubutu kuiambia nafsi yangu:

“Kimbieni kwenye mlima wenu kama ndege!+

 2 Kwa maana, tazama! waovu huupinda upinde,+

Huutayarisha mshale wao juu ya kamba ya upinde,

Ili katika giza wawafyatulie walio wanyoofu moyoni.+

 3 Misingi inapobomolewa,

Yeyote aliye mwadilifu afanye nini?”+

 4 Yehova yumo katika hekalu lake takatifu.+

Yehova—kiti chake cha ufalme kiko mbinguni.+

Macho yake yanaangalia, macho yake yanayong’aa yanawachunguza+ wana wa binadamu.

 5 Yehova humchunguza mwadilifu na pia mwovu,+

Na mtu yeyote anayependa jeuri nafsi Yake hakika inamchukia.+

 6 Yeye atawanyeshea waovu mitego, moto na kiberiti+

Na upepo wenye kuunguza, vikiwa fungu la kikombe chao.+

 7 Kwa maana Yehova ni mwadilifu;+ yeye huyapenda matendo ya uadilifu.+

Wanyoofu ndio watakaouona uso wake.+

Kwa kiongozi katika sauti ya nane ya chini.+ Muziki wa Daudi.

12 Uniokoe,+ Ee Yehova, kwa maana mshikamanifu amefikia mwisho;+

Kwa maana watu waaminifu wametoweka kutoka katikati ya wana wa binadamu.

 2 Wao huendelea kusemezana mambo yasiyo ya kweli;+

Kwa midomo laini+ wao huendelea kusema wakiwa na mioyo miwili.+

 3 Yehova ataikata midomo yote iliyo laini,

Ulimi unaosema maneno makuu,+

 4 Wale ambao wamesema: “Kwa ulimi wetu tutashinda.+

Midomo yetu iko pamoja nasi. Ni nani atakayekuwa bwana kwetu?”

 5 “Kwa sababu ya kuporwa kwao wenye kuteseka, kwa sababu ya kuugua kwao maskini,+

Nitasimama wakati huu,” asema Yehova.+

“Nitamweka katika usalama mbali na mtu yeyote anayemdhihaki.”+

 6 Maneno ya Yehova ni maneno safi,+

Kama fedha iliyosafishwa katika tanuru ya kuyeyushia kwenye udongo, iliyosafishwa mara saba.

 7 Wewe mwenyewe, Ee Yehova, utawalinda;+

Utamhifadhi kila mmoja kutokana na kizazi hiki mpaka wakati usio na kipimo.

 8 Waovu wanatembea kuzunguka pande zote,

Kwa sababu uovu unatukuzwa katikati ya wana wa binadamu.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

13 Utanisahau mpaka wakati gani, Ee Yehova?+ Milele?+

Utanificha uso wako mpaka wakati gani?+

 2 Nitaweka upinzani katika nafsi yangu mpaka wakati gani,

Huzuni katika moyo wangu wakati wa mchana?

Adui yangu atainuliwa juu yangu mpaka wakati gani?+

 3 Unitazame; unijibu, Ee Yehova Mungu wangu.

Uyafanye macho yangu yang’ae,+ ili nisilale usingizi katika kifo.+

 4 Ili adui yangu asiseme: “Nimemshinda!”

Ili wapinzani wangu wasishangilie kwa sababu nimefanywa niyumbe-yumbe.+

 5 Nami nimezitegemea fadhili zako zenye upendo;+

Moyo wangu na ushangilie katika wokovu wako.+

 6 Nitamwimbia Yehova, kwa maana amenitendea kwa njia ya kunipa thawabu.+

Kwa kiongozi. Ya Daudi.

14 Asiye na akili amesema katika moyo wake:

“Hakuna Yehova.”+

Wametenda kwa uharibifu,+ wametenda kwa njia yenye kuchukiza katika shughuli zao.

Hakuna yeyote anayefanya mema.+

 2 Kutoka mbinguni Yehova amewatazama wana wa binadamu walio chini,+

Ili aone kama kuna yeyote ambaye ana ufahamu, yeyote anayemtafuta Yehova.+

 3 Wote wamegeuka kando,+ wote ni wafisadi kwa njia ileile;+

Hakuna yeyote anayefanya mema,+

Hakuna hata mmoja.+

 4 Je, hakuna yeyote kati ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza ambaye ana ujuzi,+

Wakila watu wangu kama vile ambavyo wamekula mkate?+

Hata hawajamwitia Yehova.+

 5 Hapo wao walijawa na hofu kubwa,+

Kwa maana Yehova yuko kati ya kizazi cha mwadilifu.+

 6 Shauri la mwenye kuteseka ninyi huliaibisha,

Kwa sababu Yehova ni kimbilio lake.+

 7 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+

Wakati ambapo Yehova anawakusanya tena mateka wa watu wake,+

Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.+

Muziki wa Daudi.

15 Ee Yehova, ni nani atakayekuwa mgeni katika hema lako?+

Ni nani atakayekaa katika mlima wako mtakatifu?+

 2 Yeye anayetembea bila kosa+ na kuzoea kutenda uadilifu+

Na kusema kweli katika moyo wake.+

 3 Yeye hakuchongea kwa ulimi wake.+

Hakumfanyia mwenzake jambo lolote baya,+

Wala hakumshutumu rafiki yake.+

 4 Machoni pake mtu yeyote mwenye kudharaulika hakika amekataliwa,+

Lakini yeye anawaheshimu wale wanaomwogopa Yehova.+

Ameapa juu ya jambo lililo baya kwake, na bado yeye habadiliki.+

 5 Pesa zake hakutoa ili apate faida,+

Wala hakuchukua rushwa dhidi ya mtu asiye na hatia.+

Yeye anayefanya mambo hayo hatatikiswa.+

Miktamu ya Daudi.

16 Unihifadhi, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+

 2 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Yehova; wema wangu si kwa ajili yako,+

 3 Bali kwa watakatifu walio duniani.

Wao, naam, wale mashuhuri, ndio ninaopendezwa nao kabisa.”+

 4 Maumivu huwa mengi kwa wale ambao, wakati kuna mtu mwingine, humfuata haraka.+

Sitamimina matoleo yao ya kinywaji ya damu,+

Nami sitayachukua majina yao juu ya midomo yangu.+

 5 Yehova ndiye sehemu ya fungu langu+ nililogawiwa na ya kikombe changu.+

Wewe unaishika sana kura yangu.

 6 Kamba za kupimia zimeniangukia mahali panapopendeza.+

Kwa kweli, miliki yangu mwenyewe naikubali.

 7 Nitambariki Yehova, ambaye amenipa shauri.+

Kwa kweli, nyakati za usiku figo zangu zimenirekebisha.+

 8 Nimemweka Yehova mbele yangu daima.+

Kwa sababu yuko upande wa mkono wangu wa kuume, sitatikiswa.+

 9 Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nao utukufu wangu una mwelekeo wa kuwa na shangwe.+

Pia, mwili wangu mwenyewe utakaa katika usalama.+

10 Kwa maana hutaiacha nafsi yangu katika Kaburi.*+

Hutamruhusu mshikamanifu wako aone shimo.+

11 Utanijulisha njia ya uzima.+

Shangwe ya kutosha iko pamoja na uso wako;+

Kuna uzuri upande wa mkono wako wa kuume milele.+

Sala ya Daudi.

17 Usikie jambo la uadilifu, Ee Yehova; Usikilize kwa makini kilio changu cha kusihi;+

Tega sikio kwa sala yangu bila midomo ya udanganyifu.+

 2 Hukumu yangu na itoke mbele zako;+

Macho yako mwenyewe na yaone unyoofu.+

 3 Umeuchunguza moyo wangu, umefanya ukaguzi wakati wa usiku,+

Umenisafisha; utagundua kwamba sijapanga hila.+

Kinywa changu hakitafanya kosa.+

 4 Nao utendaji wa wanadamu,

Kwa maneno ya midomo yako mimi mwenyewe nimejilinda na njia za mnyang’anyi.+

 5 Hatua zangu na zishike njia zako,+

Ambamo hatua za miguu yangu hakika hazitatikiswa.+

 6 Mimi mwenyewe nakuitia wewe, kwa sababu utanijibu, Ee Mungu.+

Tega sikio lako kwangu. Usikilize neno langu.+

 7 Uyafanye matendo yako ya fadhili zenye upendo yawe ya ajabu,+ Ee Mwokozi wa wale wanaotafuta kimbilio

Kutoka kwa waasi walio dhidi ya mkono wako wa kuume.+

 8 Unitunze kama mboni ya jicho,+

Katika kivuli cha mabawa yako unifiche,+

 9 Kwa sababu ya waovu ambao wamenipora.

Adui za nafsi yangu wanazidi kunizingira.+

10 Wamejizungushia mafuta yao wenyewe;+

Kwa vinywa vyao wamesema kwa majivuno;+

11 Sasa wametuzingira hatua zetu;+

Wanakaza macho yao ili kuelekeza duniani.+

12 Mfano wake ni ule wa simba anayetamani kurarua vipande-vipande+

Na ule wa mwana-simba anayekaa mahali palipofichika.

13 Usimame, Ee Yehova; umkabili usoni;+

Mfanye ainame; kwa upanga wako uiokoe nafsi yangu kutoka kwa mwovu,+

14 Kwa mkono wako, Ee Yehova, kutoka kwa watu,+

Kutoka kwa watu wa mfumo huu wa mambo,+ ambao fungu lao liko katika maisha haya,+

Na ambao tumbo lao wewe hulijaza kwa hazina iliyofichwa,+

Ambao wametosheka na wana+

Na ambao huwarundikia watoto wao vitu wanavyoacha.+

15 Nami, katika uadilifu nitauona uso wako;+

Nitatosheka kuliona umbo lako ninapoamka.+

Kwa kiongozi. Wa mtumishi wa Yehova, wa Daudi, aliyemwambia Yehova maneno ya wimbo huu siku ambayo Yehova alikuwa amemkomboa kutoka mkononi mwa adui zake wote na kutoka mkononi mwa Sauli.+ Naye akasema:

18 Nitakupenda wewe, Ee Yehova nguvu zangu.+

 2 Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu na Mwokoaji wangu.+

Mungu wangu ni mwamba wangu. Nitamkimbilia,+

Ngao yangu na pembe yangu ya wokovu, kilele changu salama.+

 3 Nitamwita, Yehova, Yule anayestahili kusifiwa,+

Nami nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.+

 4 Kamba za kifo zilinizunguka;+

Mafuriko ya ghafula ya watu wasiofaa kitu pia yaliendelea kuniogopesha.+

 5 Kamba za Kaburi* zilinizunguka;+

Mitego ya kifo ilinikabili.+

 6 Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,

Nami niliendelea kumlilia Mungu wangu kwa ajili ya msaada.+

Kutoka katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+

Nacho kilio changu cha msaada mbele zake sasa kikafika masikioni mwake.+

 7 Na dunia ikaanza kutikisika na kutetemeka,+

Nayo misingi ya milima ikasukasuka,+

Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+

 8 Moshi ukapanda katika mianzi ya pua yake, nao moto kutoka kinywani mwake ukaendelea kuteketeza;+

Makaa yakawaka moto kutoka kwake.

 9 Naye akaziinamisha mbingu, akashuka.+

Na giza zito lilikuwa chini ya miguu yake.

10 Naye akaja akiwa amepanda juu ya kerubi, akaja akiwa anaruka,+

Naye akaja akiruka juu ya mabawa ya roho.+

11 Kisha akalifanya giza kuwa mahali pake pa kujificha,+

Kama kibanda cha kumzunguka pande zote,

Maji yenye giza, mawingu mazito.+

12 Kutoka katika mwangaza ulio mbele yake kulikuwa na mawingu yake yaliyopita,+

Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto.+

13 Na mbinguni Yehova akaanza kunguruma,+

Na Aliye Juu Zaidi akaanza kutoa sauti yake,+

Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto.

14 Naye akaendelea kuitupa mishale yake, ili awatawanye;+

Naye akatupa umeme, ili awavuruge.+

15 Na sakafu za vijito vya maji zikaonekana,+

Na misingi ya nchi yenye kuzaa ikafunuliwa,+

Kwa kemeo lako, Ee Yehova, kwa mlipuko wa pumzi ya pua yako.+

16 Alikuwa akituma mkono kutoka juu, alikuwa akinichukua,+

Alikuwa akinitoa ndani ya maji makuu.+

17 Alikuwa akinikomboa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+

Na kutoka kwa wale wanaonichukia; kwa sababu walikuwa na nguvu kuliko mimi.+

18 Waliendelea kunikabili katika siku ya msiba wangu,+

Lakini Yehova akawa kama tegemeo kwa ajili yangu.+

19 Naye akanitoa nje mpaka mahali penye nafasi tele;+

Alikuwa akiniokoa, kwa sababu alikuwa amependezwa nami.+

20 Yehova hunipa thawabu kulingana na uadilifu wangu;+

Hunilipa kulingana na usafi wa mikono yangu.+

21 Kwa maana nimezishika njia za Yehova,+

Wala kwa uovu sikuondoka kwa Mungu wangu.+

22 Kwa maana maamuzi yake yote ya hukumu yako mbele yangu,+

Nazo sheria zake sitaziondoa kutoka kwangu.+

23 Nami nitajiendesha bila kosa mbele zake,+

Nami nitajiepusha na kosa.+

24 Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+

Kulingana na usafi wa mikono yangu mbele za macho yake.+

25 Kwa mtu mshikamanifu utatenda kwa ushikamanifu;+

Kwa mwanamume asiye na kosa, wewe utatenda kwa njia isiyo na kosa;+

26 Kwa mtu anayebaki safi utakuwa safi;+

Na kwa mpotovu utakuwa mwenye hila;+

27 Kwa sababu watu wenye kuteseka wewe mwenyewe utawaokoa;+

Bali macho yenye majivuno utayashusha.+

28 Kwa maana wewe mwenyewe utaiwasha taa yangu, Ee Yehova;+

Mungu wangu atafanya giza langu liangaze.+

29 Kwa maana kwa msaada wako ninaweza kukimbiza kikundi cha waporaji;+

Na kwa msaada wa Mungu wangu ninaweza kuupanda ukuta.+

30 Mungu wa kweli, njia yake ni kamilifu;+

Neno la Yehova limetakaswa.+

Yeye ni ngao kwa wale wote wanaomkimbilia.+

31 Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova?+

Na ni nani aliye mwamba ila Mungu wetu?+

32 Mungu wa kweli Ndiye anayenifunga sana mshipi wa nguvu,+

Naye ataifanya njia yangu kuwa kamilifu,+

33 Kuifanya miguu yangu iwe kama ya paa,+

Na kwenye mahali palipo juu kwangu yeye huendelea kunisimamisha.+

34 Anaifundisha mikono yangu kupigana vita,+

Na mikono yangu imepinda upinde wa shaba.+

35 Nawe utanipa ngao yako ya wokovu,+

Na mkono wako mwenyewe wa kuume utanitegemeza,+

Na unyenyekevu wako mwenyewe utanifanya kuwa mkuu.+

36 Utafanyiza nafasi kubwa ya kutosha kwa ajili ya hatua zangu zilizo chini yangu,+

Navyo vifundo vya miguu yangu hakika havitatetemeka.+

37 Nitawafuatilia adui zangu na kuwafikia;

Nami sitarudi mpaka waangamizwe.+

38 Nitawavunja vipande-vipande hivi kwamba wasiweze kusimama;+

Wataanguka chini ya miguu yangu.+

39 Nawe utanifunga mshipi wa nguvu kwa ajili ya vita;

Utawaangusha chini yangu wale wanaoniinukia.+

40 Nao adui zangu, utanipa upande wa nyuma wa shingo zao;+

Nao wale wanaonichukia vikali, nitawanyamazisha.+

41 Wanalia wapate msaada, lakini hakuna mwokozi,+

Kwa Yehova, lakini yeye hawajibu.+

42 Nami nitawatwanga wawe laini kama mavumbi mbele ya upepo;+

Nitawamwaga kama matope ya barabarani.+

43 Utaniokoa kutokana na watu wenye kutafuta-tafuta makosa.+

Utanichagua kuwa kiongozi wa mataifa.+

Watu ambao sijawajua​​—⁠watanitumikia.+

44 Kwa kusikia fununu tu watanitii;+

Wageni watanijia wakitetemeka.+

45 Wageni watakuwa dhaifu,

Nao watakuja wakitetemeka kutoka katika maboma yao.+

46 Yehova anaishi,+ na abarikiwe Mwamba wangu,+

Na Mungu wa wokovu wangu atukuzwe.+

47 Mungu wa kweli ndiye Mpaji wa matendo ya kisasi kwangu;+

Naye hutiisha vikundi vya watu chini yangu.+

48 Ananiokoa kutoka kwa adui zangu wenye hasira;+

Utaniinua juu ya wale wanaosimama dhidi yangu,+

Utanikomboa kutoka kwa mtu mwenye jeuri.+

49 Ndiyo sababu nitakusifu wewe kati ya mataifa, Ee Yehova,+

Nami nitalipigia jina lako muziki.+

50 Yeye anafanya matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake+

Na kuonyesha fadhili zenye upendo kwa mtiwa-mafuta wake,+

Kwa Daudi na kwa uzao wake mpaka wakati usio na kipimo.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

19 Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu;+

Nalo anga linatangaza kazi ya mikono yake.+

 2 Siku moja baada ya siku nyingine hufanya maneno yabubujike,+

Na usiku mmoja baada ya usiku mwingine huonyesha ujuzi.+

 3 Hakuna usemi, wala hakuna maneno;

Sauti yao haisikiki.+

 4 Kamba yake ya kupimia imefika duniani pote,+

Na maneno yake yamefika kwenye miisho ya nchi yenye kuzaa.+

Katika hizo amewekea jua hema,+

 5 Nalo ni kama bwana-arusi anapotoka katika chumba chake cha ndoa;+

Linashangilia kama mwanamume mwenye nguvu anapokimbia njiani.+

 6 Linaenda kutoka mwisho mmoja wa mbingu,

Nao mzunguko wake humalizikia katika ile miisho yake mingine;+

Wala hakuna chochote kilichofichwa kisiweze kupatwa na joto lake.+

 7 Sheria+ ya Yehova ni kamilifu,+ huirudisha nafsi.+

Kikumbusho+ cha Yehova ni chenye kutegemeka,+ humfanya asiye na uzoefu awe na hekima.+

 8 Maagizo+ kutoka kwa Yehova ni manyoofu,+ huufanya moyo ushangilie;+

Amri+ ya Yehova ni safi,+ huyafanya macho yang’ae.+

 9 Kumwogopa+ Yehova ni jambo safi, husimama milele.

Maamuzi ya hukumu+ ya Yehova ni ya kweli;+ yote yameonekana kuwa yenye uadilifu.+

10 Ni ya kutamaniwa kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi sana;+

Na tamu kuliko asali+ na asali yenye kutiririka ya sega.+

11 Pia, mtumishi wako mwenyewe ameonywa kupitia hayo;+

Katika kuyashika kuna thawabu kubwa.+

12 Makosa—ni nani anayeweza kuyatambua?+

Unitangaze kuwa sina hatia ya dhambi zilizofichwa.+

13 Pia umzuie mtumishi wako kutokana na matendo ya kimbelembele;+

Usiyaache yanitawale.+

Hapo ndipo nitakapokuwa kamili,+

Nami nitakuwa sina hatia ya makosa mengi.

14 Maneno ya kinywa changu na kutafakari kwa moyo wangu+

Na yawe yenye kupendeza mbele zako, Ee Yehova Mwamba+ wangu na Mkombozi wangu.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

20 Yehova na akujibu siku ya taabu.+

Jina la Mungu wa Yakobo na likulinde.+

 2 Na atume msaada wako kutoka katika mahali patakatifu,+

Na kukutegemeza kutoka Sayuni.+

 3 Na akumbuke matoleo yako yote ya zawadi,+

Naye na ayakubali matoleo yako ya kuteketezwa kuwa ni mafuta.+ Sela.

 4 Na akupe kulingana na moyo wako,+

Naye na alitimize kusudi lako lote.+

 5 Tutapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya wokovu wako,+

Nasi tutainua bendera zetu katika jina la Mungu wetu.+

Yehova na atimize maombi yako yote.+

 6 Sasa najua kwamba hakika Yehova humwokoa mtiwa-mafuta wake.+

Humjibu kutoka katika mbingu zake takatifu+

Kwa matendo ya kuokoa yenye nguvu ya mkono wake wa kuume.+

 7 Wengine hutaja kuhusu magari na wengine kuhusu farasi,+

Lakini sisi, tutataja kuhusu jina la Yehova Mungu wetu.+

 8 Hao wamevunjika na kuanguka;+

Lakini sisi, tumesimama, ili tupate kurudishwa.+

 9 Ee Yehova, umwokoe mfalme!+

Yeye atatujibu siku ambayo tutaita.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

21 Ee Yehova, mfalme hushangilia katika nguvu zako;+

Na katika wokovu wako jinsi anavyotaka kuwa na shangwe sana!+

 2 Tamaa ya moyo wake umempa,+

Na matakwa ya midomo yake hukuyazuilia.+ Sela.

 3 Kwa maana ulikutana naye ukiwa na baraka za mema,+

Na kumvika taji la dhahabu safi kichwani.+

 4 Alikuomba uhai. Ukampa huo,+

Urefu wa siku mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

 5 Utukufu wake ni mkuu katika wokovu wako.+

Heshima na fahari unaweka juu yake.+

 6 Kwa maana umemfanya abarikiwe sana milele;+

Unamfanya afurahie kwa shangwe mbele za uso wako.+

 7 Kwa maana mfalme anategemea Yehova,+

Naam, fadhili zenye upendo za Aliye Juu Zaidi. Hatatikiswa.+

 8 Mkono wako utawapata adui zako wote;+

Mkono wako wa kuume utawapata wale wanaokuchukia.

 9 Utawafanya wawe kama tanuru yenye moto wakati wako uliowekwa wa kukaza uangalifu wako;+

Yehova atawameza katika hasira yake, na moto utawateketeza.+

10 Utaangamiza wazaliwa wao kutoka duniani,+

Na uzao wao kutoka kati ya wana wa binadamu.+

11 Kwa maana wamekuelekezea mabaya;+

Wametunga mawazo wasiyoweza kutimiza.+

12 Kwa maana utawafanya wageuze migongo yao kwa kukimbia+

Kwa nyuzi za upinde wako ambazo unatayarisha dhidi ya nyuso zao.+

13 Na utukuzwe katika nguvu zako, Ee Yehova.+

Tutaimba na kuzipigia muziki nguvu zako.+

Kwa kiongozi juu ya Paa wa Mapambazuko. Muziki wa Daudi.

22 Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?+

Kwa nini uko mbali usiniokoe,+

Mbali na maneno ya mngurumo wangu?+

 2 Ee Mungu wangu, mimi huendelea kuita wakati wa mchana, nawe huitiki;+

Na wakati wa usiku, wala sinyamazi.+

 3 Lakini wewe ni mtakatifu,+

Unayekaa juu ya sifa za Israeli.+

 4 Baba zetu walikutegemea wewe;+

Walikutegemea, nawe ukaendelea kuwaokoa.+

 5 Walikulilia,+ nao wakawa salama;+

Walikutegemea, nao hawakuona aibu.+

 6 Lakini mimi ni mdudu,+ wala si mtu,

Shutuma kwa wanadamu na mwenye kudharaulika kwa watu.+

 7 Wale wote wanaoniona mimi, hunidharau;+

Wanaendelea kufungua vinywa vyao wazi, wanaendelea kutikisa vichwa vyao:+

 8 “Yeye alijitia mikononi mwa Yehova.+ Acha Yeye amwokoe!+

Na amkomboe, kwa kuwa yeye amependezwa naye!”+

 9 Kwa maana Wewe ndiye uliyenitoa tumboni,+

Wewe ndiye unayenifanya niwe na tegemeo nilipokuwa kwenye maziwa ya mama yangu.+

10 Nimetupwa kwako kutoka tumbo la uzazi;+

Kutoka katika tumbo la mama yangu wewe umekuwa Mungu wangu.+

11 Usikae mbali nami, kwa sababu taabu iko karibu,+

Kwa sababu hakuna msaidizi mwingine.+

12 Ng’ombe-dume wengi wachanga wamenizingira;+

Wale wenye nguvu wa Bashani wamenizunguka.+

13 Wamefungua vinywa vyao dhidi yangu,+

Kama simba anayerarua vipande-vipande na kunguruma.+

14 Nimemwagwa kama maji,+

Na mifupa yangu yote imetenganishwa.+

Moyo wangu umekuwa kama nta;+

Umeyeyuka ndani katika sehemu zangu za ndani.+

15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae cha udongo,+

Na ulimi wangu umefanywa ushikamane na ufizi wangu;+

Nawe unaniweka katika mavumbi ya kifo.+

16 Kwa maana mbwa wamenizingira;+

Kusanyiko la watenda-maovu limenizunguka.+

Wako kwenye mikono yangu na miguu yangu kama simba.+

17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote.+

Wao hutazama, hunikazia macho.+

18 Wanagawana mavazi yangu,+

Nao wanalipigia kura vazi langu.+

19 Lakini wewe, Ee Yehova, usikae mbali.+

Ewe nguvu zangu,+ ufanye haraka kuja kunisaidia.+

20 Uikomboe nafsi yangu kutokana na upanga,+

Nafsi yangu ya pekee kutokana na wayo wa mbwa;+

21 Uniokoe kutokana na kinywa cha simba,+

Na unijibu na kuniokoa kutokana na pembe za ng’ombe-mwitu.+

22 Nitalitangaza jina lako+ kwa ndugu zangu;+

Katikati ya kutaniko nitakusifu wewe.+

23 Ninyi mnaomwogopa Yehova, msifuni!+

Enyi nyote mlio uzao wa Yakobo, mtukuzeni!+

Na mwogopeni yeye, enyi nyote mlio uzao wa Israeli.+

24 Kwa maana hakudharau+

Wala kuchoshwa na mateso ya mwenye kuteseka;+

Naye hakumficha uso wake,+

Naye alipomlilia amsaidie alisikia.+

25 Kutoka kwako sifa yangu itakuwa katika kutaniko kubwa;+

Nadhiri zangu nitazitimiza mbele ya wale wanaomwogopa.+

26 Wapole watakula na kushiba;+

Wale wanaomtafuta watamsifu Yehova.+

Mioyo yenu na iishi milele.+

27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kurudi kwa Yehova.+

Na familia zote za mataifa zitainama mbele zako.+

28 Kwa maana ufalme ni wa Yehova,+

Naye anayatawala mataifa.+

29 Wote walio wanono wa dunia watakula na kuinama;+

Wote wanaoenda chini mavumbini watainama mbele zake,+

Wala hakuna atakayeihifadhi hai nafsi yake.+

30 Uzao utamtumikia;+

Kizazi hicho kitatangaziwa juu ya Yehova.+

31 Watakuja na kusema juu ya uadilifu wake+

Kwa kikundi cha watu kitakachozaliwa, kwamba ni yeye amefanya hilo.+

Muziki wa Daudi.

23 Yehova ni Mchungaji wangu.+

Sitakosa chochote.+

 2 Ananilaza katika malisho yenye majani mengi;+

Ananiongoza kando ya mahali pa kupumzika palipo na maji ya kutosha.+

 3 Anaiburudisha nafsi yangu.+

Ananiongoza katika mapito ya uadilifu kwa ajili ya jina lake.+

 4 Hata ingawa ninatembea katika bonde lenye kivuli kizito,+

Siogopi chochote kibaya,+

Kwa maana wewe uko pamoja nami;+

Fimbo yako na gongo lako ndivyo vitu vinavyonifariji.+

 5 Mbele yangu wewe unatayarisha meza mbele ya wale wanaonionyesha uadui.+

Umepaka kichwa changu mafuta;+

Kikombe changu kimejazwa vizuri.+

 6 Kwa hakika wema na fadhili zenye upendo zitanifuata siku zote za maisha yangu;+

Nami nitakaa katika nyumba ya Yehova siku nyingi.+

Ya Daudi. Muziki.

24 Dunia na vyote vinavyoijaza ni vya Yehova,+

Nchi yenye kuzaa na wale wanaokaa ndani yake.+

 2 Kwa maana yeye ameiweka imara juu ya bahari,+

Naye huiweka imara juu ya mito.+

 3 Ni nani anayeweza kuupanda mlima wa Yehova,+

Na ni nani anayeweza kusimama katika mahali pake patakatifu?+

 4 Yeyote asiye na hatia katika mikono yake na aliye safi moyoni,+

Ambaye hajaitendea nafsi Yangu kwa ubatili mtupu,+

Wala kuapa kwa udanganyifu.+

 5 Atachukua baraka kutoka kwa Yehova+

Na uadilifu kutoka kwa Mungu wake wa wokovu.+

 6 Hiki ndicho kizazi cha wale wanaomtafuta,

Cha wale wanaoutafuta uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.+ Sela.

 7 “Inueni vichwa vyenu, enyi malango,+

Na mjiinue, enyi miingilio ya kudumu,+

Ili Mfalme mtukufu apate kuingia!”+

 8 “Basi, Mfalme huyo mtukufu ni nani?”+

“Yehova mwenye nguvu na mwenye uwezo,+

Yehova mwenye uwezo katika vita.”+

 9 “Inueni vichwa vyenu, enyi malango;+

Naam, viinueni juu, enyi miingilio ya kudumu,

Ili Mfalme mtukufu apate kuingia!”+

10 “Basi, yeye ni nani, huyo Mfalme mtukufu?”

“Yehova wa majeshi—yeye ndiye Mfalme mtukufu.”+ Sela.

Ya Daudi.

א [ʼAʹleph]

25 Kwako wewe, Ee Yehova, naiinua nafsi yangu.+

ב [Behth]

 2 Ee Mungu wangu, nimekutegemea wewe;+

Ee nisione aibu.

Adui zangu na wasishangilie juu yangu.+

ג [Giʹmel]

 3 Pia, hakuna yeyote kati ya wale wanaokutumainia atakayeona aibu.+

Wale wanaotenda kwa hila bila kupata mafanikio wataona aibu.+

ד [Daʹleth]

 4 Nijulishe njia zako, Ee Yehova;+

Nifundishe mapito yako mwenyewe.+

ה [Heʼ]

 5 Nitembeze katika kweli yako na kunifundisha,+

Kwa maana wewe ni Mungu wangu wa wokovu.+

ו [Waw]

Nimekutumainia mchana kutwa.+

ז [Zaʹyin]

 6 Ukumbuke rehema zako,+ Ee Yehova, na fadhili zako zenye upendo,+

Kwa maana ni za tangu wakati usio na kipimo.+

ח [Chehth]

 7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu na maasi yangu.+

Unikumbuke kulingana na fadhili zako zenye upendo,+

Kwa ajili ya wema wako, Ee Yehova.+

ט [Tehth]

 8 Yehova ni mwema na mnyoofu.+

Ndiyo sababu yeye huwafundisha watenda-dhambi katika ile njia.+

י [Yohdh]

 9 Atawafanya wapole watembee katika uamuzi wake wa hukumu,+

Naye atawafundisha wapole njia yake.+

כ [Kaph]

10 Mapito yote ya Yehova ni fadhili zenye upendo na ukweli

Kwa wale wanaoshika agano lake+ na vikumbusho vyake.+

ל [Laʹmedh]

11 Kwa ajili ya jina lako, Ee Yehova,+

Usamehe kosa langu, kwa maana ni kubwa.+

מ [Mem]

12 Sasa, ni nani anayemwogopa Yehova?+

Atamfundisha katika njia ambayo yeye ataichagua.+

נ [Nun]

13 Nafsi yake itakaa katika wema,+

Na uzao wake mwenyewe utaimiliki dunia.+

ס [Saʹmekh]

14 Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wanaomwogopa,+

Pia agano lake, ili kuwafanya walijue.+

ע [ʽAʹyin]

15 Macho yangu yanamwelekea Yehova daima,+

Kwa maana yeye ndiye huitoa miguu yangu katika wavu.+

פ [Peʼ]

16 Unielekezee uso wako, na unionyeshe kibali;+

Kwa maana mimi niko peke yangu nami ni mwenye kuteseka.+

צ [Tsa·dhehʹ]

17 Taabu za moyo wangu zimeongezeka;+

Uniondoe katika mikazo iliyo juu yangu.+

ר [Rehsh]

18 Uone mateso yangu na taabu yangu,+

Na unisamehe dhambi zangu zote.+

19 Uone jinsi adui zangu wamekuwa wengi,+

Nao wamenichukia kwa chuki yenye jeuri.+

ש [Shin]

20 Uilinde nafsi yangu na kunikomboa.+

Nisione aibu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+

ת [Taw]

21 Utimilifu na unyoofu na zinilinde,+

Kwa maana nimekutumainia wewe.+

22 Ee Mungu, mkomboe Israeli kutoka katika taabu zake zote.+

Ya Daudi.

26 Unihukumu,+ Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika utimilifu wangu,+

Nami nimemtumaini Yehova, nisipate kutikisika.+

 2 Unichunguze, Ee Yehova, na kunijaribu;+

Usafishe figo zangu na moyo wangu.+

 3 Kwa maana fadhili zako zenye upendo ziko mbele ya macho yangu,

Nami nimetembea katika kweli yako.+

 4 Sikuketi na watu wasiosema kweli;+

Wala siingii pamoja na wale wanaoficha jinsi walivyo.+

 5 Nimelichukia kutaniko la watenda-maovu,+

Wala siketi pamoja na waovu.+

 6 Nitaiosha mikono yangu katika kutokuwa na hatia,+

Nami nitatembea nikizunguka madhabahu yako, Ee Yehova,+

 7 Ili kufanya utoaji shukrani usikiwe kwa sauti kubwa,+

Na kutangaza kazi zako zote za ajabu.+

 8 Yehova, nimependa makao ya nyumba yako+

Na mahali ambapo utukufu wako hukaa.+

 9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda-dhambi,+

Wala uhai wangu pamoja na watu wenye hatia ya damu,+

10 Ambao mikononi mwao wana mwenendo mpotovu,+

Na ambao mkono wao wa kuume umejaa rushwa.+

11 Mimi nami nitatembea katika utimilifu wangu.+

Ee unikomboe+ na kunionyesha kibali.+

12 Mguu wangu utasimama mahali tambarare;+

Kati ya makundi yaliyokutanika nitambariki Yehova.+

Ya Daudi.

27 Yehova ni nuru yangu+ na wokovu wangu.+

Nitamwogopa nani?+

Yehova ni ngome ya uhai wangu.+

Nitamhofu nani?+

 2 Watenda-maovu walipokuja karibu juu

yangu ili wapate kuila nyama yangu,+

Wao wakiwa ni wapinzani wangu na adui zangu,+

Wao walijikwaa na kuanguka.+

 3 Hata kambi ijapopiga hema dhidi yangu,+

Moyo wangu hautaogopa.+

Vita vijapozuka dhidi yangu,+

Bado nitakuwa na tegemeo wakati huo.+

 4 Nimemwomba Yehova jambo moja+—

Ndilo nitakalolitafuta,+

Kwamba nipate kukaa katika nyumba ya Yehova siku zote za maisha yangu,+

Ili kuuona uzuri wa Yehova+

Na kulitazama kwa uthamini hekalu lake.+

 5 Kwa maana atanificha mafichoni mwake katika siku ya msiba;+

Atanificha katika mahali pa siri pa hema lake;+

Ataniweka juu kwenye mwamba.+

 6 Na sasa kichwa changu kitakuwa juu, juu ya adui zangu wanaonizunguka pande zote;+

Nami nitatoa kwenye hema lake dhabihu za vigelegele vya shangwe;+

Nitamwimbia Yehova na kumpigia muziki.+

 7 Usikie, Ee Yehova, ninapoita kwa sauti yangu,+

Na unionyeshe kibali na kunijibu.+

 8 Moyo wangu umesema hivi juu yako: “Utafuteni uso wangu.”+

Nitautafuta uso wako, Ee Yehova.+

 9 Usinifiche uso wako.+

Usimgeuzie mbali mtumishi wako kwa hasira.+

Uwe msaada wangu.+

Usinitupe wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.+

10 Hata ikiwa baba yangu na mama yangu wangeniacha,+

Yehova mwenyewe angenichukua.+

11 Unifundishe njia yako, Ee Yehova,+

Na uniongoze katika njia ya unyoofu kwa sababu ya adui zangu.

12 Usinitie mikononi mwa nafsi ya wapinzani wangu;+

Kwa maana dhidi yangu wamesimama mashahidi wa uwongo,+

Na yeye anayetokeza jeuri.+

13 Kama nisingalikuwa na imani katika kuuona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai+—!

14 Mtumaini Yehova;+ uwe hodari na moyo wako uwe na nguvu.+

Naam, mtumaini Yehova.+

Ya Daudi.

28 Mimi huendelea kukuita wewe, Ee Yehova.+

Ee Mwamba wangu, usiwe kwangu kama kiziwi,+

Ili usininyamazie+

Nami nisilazimike kuwa kama wale wanaoshuka chini shimoni.+

 2 Uisikie sauti ya kusihi kwangu ninapokulilia unisaidie,

Wakati ninapoinua mikono+ yangu katika chumba cha ndani kabisa cha mahali pako patakatifu.+

 3 Usinikokote pamoja na watu waovu na pamoja na wanaotenda mambo yenye kuumiza,+

Wale wanaosema amani na wenzao+ lakini ambao katika mioyo yao mna jambo lililo baya.+

 4 Uwape kulingana na matendo yao+

Na kulingana na ubaya wa mazoea yao.+

Uwape kulingana na kazi ya mikono yao.+

Uwalipe matendo yao wenyewe.+

 5 Kwa maana hawajali utendaji wa Yehova,+

Wala kazi ya mikono yake.+

Yeye atawabomoa wala hatawajenga.

 6 Yehova na abarikiwe, kwa maana ameisikia sauti ya kusihi kwangu.+

 7 Yehova ni nguvu+ zangu na ngao+ yangu.

Moyo wangu umemtegemea yeye,+

Nami nimesaidiwa, hivi kwamba moyo wangu unashangilia,+

Nami nitamsifu kwa wimbo wangu.+

 8 Yehova ni nguvu kwa watu wake,+

Naye ni ngome ya wokovu mkuu wa mtiwa-mafuta wake.+

 9 Uwaokoe watu wako, na kuubariki urithi wako;+

Na uwachunge na kuwabeba mpaka wakati usio na kipimo.+

Muziki wa Daudi.

29 Mhesabieni Yehova, enyi wana wa wenye nguvu,

Mhesabieni Yehova utukufu na nguvu.+

 2 Mhesabieni Yehova utukufu wa jina lake.+

Mwinamieni Yehova katika pambo takatifu.+

 3 Sauti ya Yehova iko juu ya maji;+

Mungu mtukufu+ mwenyewe amenguruma.+

Yehova yuko juu ya maji mengi.+

 4 Sauti ya Yehova ina nguvu;+

Sauti ya Yehova ni yenye fahari.+

 5 Sauti ya Yehova inaivunja mierezi;

Naam, Yehova anaivunja vipande-vipande mierezi ya Lebanoni,+

 6 Naye huifanya irukeruke kama ndama,+

Lebanoni na Sirioni+ kama wana wa ng’ombe-mwitu.

 7 Sauti ya Yehova inapasua kwa miali ya moto;+

 8 Sauti ya Yehova huifanya nyika itetemeke,+

Yehova huifanya nyika ya Kadeshi+ itetemeke.

 9 Sauti ya Yehova huwafanya paa watetemeke kwa maumivu ya kuzaa+

Na kuivua kabisa misitu.+

Na katika hekalu lake kila mmoja anasema: “Utukufu!”+

10 Yehova ameketi juu ya gharika;+

Na Yehova huketi akiwa mfalme mpaka wakati usio na kipimo.+

11 Yehova atawapa watu wake nguvu kwelikweli.+

Yehova atawabariki kwa amani watu wake.+

Muziki. Wimbo wa kuzindua nyumba.+ Wa Daudi.

30 Nitakutukuza wewe, Ee Yehova, kwa maana umeniinua+

Nawe hukuwaruhusu adui zangu washangilie juu yangu.+

 2 Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, nawe ukaniponya.+

 3 Ee Yehova, umeitoa nafsi yangu kutoka katika Kaburi;*+

Umeendelea kuniweka nikiwa hai, ili nisipate kushuka ndani ya shimo.+

 4 Mpigieni Yehova muziki, enyi washikamanifu wake,+

Utoleeni shukrani ukumbusho wake mtakatifu;+

 5 Kwa sababu kuwa chini ya hasira yake ni kwa muda kidogo tu,+

Kuwa chini ya nia yake njema ni kwa muda wote wa maisha.+

Huenda kilio kikakaa wakati wa jioni,+ lakini asubuhi kuna vigelegele vya shangwe.+

 6 Mimi nimesema katika starehe yangu:+

“Sitatikiswa kamwe.”+

 7 Ee Yehova, umeusimamisha mlima wangu katika nguvu kwa nia yako njema.+

Uliuficha uso wako; nikawa na wasiwasi.+

 8 Niliendelea kukuita, Ee Yehova;+

Nami niliendelea kumsihi Yehova anipe kibali.+

 9 Damu yangu ina faida gani ninaposhuka katika shimo?+

Je, mavumbi yatakusifu wewe?+ Je, yatasema juu ya ukweli wako?+

10 Usikie, Ee Yehova, na kunionyesha kibali.+

Ee Yehova, uwe msaidizi wangu.+

11 Umenibadilishia maombolezo yangu yakawa kucheza dansi;+

Umefungua nguo yangu ya gunia, nawe unaendelea kunifunga shangwe,+

12 Ili utukufu wangu upate kukupigia muziki wala usinyamaze.+

Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu mpaka wakati usio na kipimo.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

31 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.+

Ee nisiaibike kamwe.+

Niokoe katika uadilifu wako.+

 2 Unitegee sikio lako.+

Unikomboe haraka.+

Uwe ngome yangu yenye miamba,+

Nyumba yenye ngome ili kuniokoa.+

 3 Kwa maana wewe ni mwamba wangu na ngome yangu;+

Nawe utaniongoza na kunielekeza+ kwa ajili ya jina lako.+

 4 Utanitoa katika wavu ambao wameuficha kwa ajili yangu,+

Kwa maana wewe ni ngome yangu.+

 5 Naikabidhi roho yangu mkononi mwako.+

Umenikomboa,+ Ee Yehova Mungu wa ukweli.+

 6 Nawachukia wale wanaoonyesha kujali sanamu zisizo na faida, za ubatili;+

Lakini mimi, namtegemea Yehova.+

 7 Nitakuwa na shangwe na kushangilia katika fadhili zako zenye upendo,+

Kwa kuwa umeona mateso yangu;+

Umejua juu ya taabu za nafsi yangu.+

 8 Wala hujanitia mkononi mwa adui.+

Umeisimamisha miguu yangu mahali penye nafasi tele.+

 9 Unionyeshe kibali, Ee Yehova, kwa maana niko katika dhiki kali.+

Mambo yenye kukera yamefanya jicho langu liwe dhaifu,+ naam, nafsi yangu na tumbo langu.+

10 Kwa maana uhai wangu umefikia mwisho kwa huzuni,+

Na miaka yangu kwa kuugua.+

Kwa sababu ya kosa langu nguvu zangu zimejikwaa,+

Na mifupa yangu imekuwa dhaifu.+

11 Nimekuwa shutuma+ kwa wale wote wanaonionyesha uadui,+

Na nimekuwa hivyo hata zaidi kwa jirani zangu,+

Na kitu chenye kutia hofu kwa rafiki zangu.+

Wakati wanaponiona nje, wamenikimbia.+

12 Nimesahaulika kama mtu ambaye amekufa na ambaye hayumo moyoni;+

Nimekuwa kama chombo kilichoharibika;+

13 Kwa maana nimeisikia habari mbaya kutoka kwa wengi,+

Pande zote kukiwa na woga.+

Wanapoungana kama kitu kimoja dhidi yangu,+

Wanapanga hila ili kuiondoa nafsi yangu.+

14 Lakini mimi⁠—​nimekutegemea wewe, Ee Yehova.+

Nimesema: “Wewe ni Mungu wangu.”+

15 Nyakati zangu ziko katika mkono wako.+

Unikomboe kutoka katika mkono wa adui zangu na kutoka kwa wale wanaonifuatilia.+

16 Uufanye uso wako umwangazie mtumishi wako.+

Uniokoe katika fadhili zako zenye upendo.+

17 Ee Yehova, nisiaibike, kwa maana nimekuita wewe.+

Waovu na waaibike;+

Na wakae kimya katika Kaburi.*+

18 Midomo inayosema uwongo na ishindwe kusema,+

Inayosema mambo dhidi ya mwadilifu,+ bila kujizuia katika majivuno na dharau.+

19 Jinsi ulivyo mwingi wema wako,+ ambao umewawekea hazina wale wanaokuogopa!+

Ambao umewapa wale wanaokukimbilia wewe,

Mbele ya wana wa binadamu.+

20 Utawaficha katika mahali pa siri pa uso wako+

Mbali na ukusanyikaji pamoja wa watu.+

Utawaficha katika kibanda chako mbali na kugombana kwa ndimi.+

21 Yehova na abarikiwe,+

Kwa maana amenionyesha fadhili zenye upendo za ajabu+ katika jiji lililo katika mkazo.+

22 Mimi nilisema hivi niliposhikwa na wasiwasi:+

“Hakika nitaangamizwa kutoka mbele za macho yako.”+

Bila shaka umeisikia sauti ya kusihi kwangu nilipokulilia unisaidie.+

23 Enyi washikamanifu wake wote, mpendeni Yehova.+

Yehova anawalinda waaminifu,+

Lakini anampa malipo tele yeyote anayeonyesha majivuno.+

24 Iweni hodari, nayo mioyo yenu na iwe na nguvu,+

Ninyi nyote mnaomngojea Yehova.+

Ya Daudi. Maskili.

32 Mwenye furaha ni mtu ambaye amesamehewa maasi yake, ambaye dhambi yake imefunikwa.+

 2 Mwenye furaha ni mtu ambaye Yehova hamhesabii kosa,+

Na ambaye katika roho yake hamna udanganyifu.+

 3 Nilipokaa kimya mifupa yangu ilichakaa kwa sababu ya kuugua kwangu mchana kutwa.+

 4 Kwa maana mkono wako ulikuwa mzito juu yangu mchana na usiku.+

Umajimaji wa uhai wangu umenyauka kama wakati wa joto kavu la kiangazi.+ Sela.

 5 Mwishowe niliungama dhambi yangu kwako, wala sikufunika kosa langu.+

Nilisema: “Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.”+

Nawe mwenyewe ukanisamehe kosa la dhambi zangu.+ Sela.

 6 Kwa sababu hiyo kila aliye mshikamanifu atasali kwako+

Katika wakati ule tu ambao wewe unaweza kupatikana.+

Nayo mafuriko ya maji mengi hayatamgusa.+

 7 Wewe ni mahali pangu pa kujificha; utanilinda kutokana na taabu.+

Utanizingira kwa vigelegele vya shangwe kwa sababu ya kuniokoa.+ Sela.

 8 “Nitakufanya uwe na ufahamu na kukufundisha katika njia unayopaswa kuiendea.+

Nitakupa shauri jicho langu likiwa linakutazama.+

 9 Msijifanye kama farasi au nyumbu wasio na uelewaji,+

Ambao roho yao yenye nguvu huzuiwa na hatamu au lijamu+

Kabla wao hawajakukaribia wewe.”+

10 Mwovu ana maumivu mengi;+

Lakini mtu anayemtegemea Yehova, fadhili zenye upendo humzingira.+

11 Shangilieni katika Yehova na kuwa na shangwe, enyi waadilifu;+

Na mpige vigelegele vya shangwe, ninyi nyote mlio wanyoofu katika moyo.+

33 Pigeni vigelegele vya shangwe, enyi waadilifu, kwa sababu ya Yehova.+

Sifa ni jambo linalofaa kwa wanyoofu.+

 2 Mtoleeni Yehova shukrani kwa kinubi;+

Mpigieni muziki kwa kinanda+ chenye nyuzi kumi.

 3 Mwimbieni wimbo mpya;+

Fanyeni yote mnayoweza katika kumpigia vinanda pamoja na vigelegele vya shangwe.+

 4 Kwa maana neno la Yehova ni la unyoofu,+

Nayo kazi yake yote ni kwa uaminifu.+

 5 Anapenda uadilifu na haki.+

Dunia imejawa na fadhili zenye upendo za Yehova.+

 6 Mbingu zilifanywa kwa neno la Yehova,+

Nayo majeshi yake yote yalifanywa kwa roho ya kinywa chake.+

 7 Anayakusanya maji ya bahari kana kwamba ni kwa bwawa,+

Akiweka katika maghala maji yenye kututumuka.

 8 Wale wote walio wa dunia na wamwogope Yehova.+

Wote wanaokaa katika nchi yenye kuzaa na wamhofu.+

 9 Kwa maana yeye mwenyewe alisema, na ikawa hivyo;+

Yeye mwenyewe alitoa amri, nayo ikasimama hivyo.+

10 Yehova mwenyewe amevunja shauri la mataifa;+

Amezuia fikira za vikundi vya watu.+

11 Shauri la Yehova litasimama milele;+

Mawazo ya moyo wake ni kwa kizazi kimoja baada ya kizazi kingine.+

12 Lenye furaha ni taifa ambalo Mungu wake ni Yehova,+

Watu ambao amewachagua wawe urithi wake.+

13 Kutoka mbinguni Yehova ametazama,+

Amewaona wana wote wa binadamu.+

14 Kutoka katika mahali palipofanywa imara ambako yeye hukaa+

Amewakazia macho wale wote wanaokaa duniani.

15 Anaifanyiza mioyo yao wote pamoja;+

Anazifikiria kazi zao zote.+

16 Hakuna mfalme anayeokolewa kwa wingi wa majeshi yake;+

Mtu mwenye nguvu haokolewi kwa wingi wa nguvu.+

17 Farasi ni udanganyifu kwa ajili ya wokovu,+

Na kwa wingi wa nguvu zake haokoi.+

18 Tazama! Jicho la Yehova linawaelekea wale wanaomwogopa,+

Wale wanaozingojea fadhili zake zenye upendo,+

19 Ili kuikomboa nafsi yao na kifo,+

Na kuwahifadhi hai wakati wa njaa.+

20 Nafsi yetu imekuwa ikimtarajia Yehova.+

Yeye ni msaidizi wetu na ngao yetu.+

21 Kwa maana moyo wetu hushangilia katika yeye;+

Kwa maana tumelitegemea jina lake takatifu.+

22 Fadhili zako zenye upendo, Ee Yehova, na ziwe juu yetu,+

Kwa vile tumeendelea kukungojea.+

Ya Daudi, alipokuwa akijifanya mwenda-wazimu+ mbele ya Abimeleki, hivi kwamba akamfukuza, naye akaenda zake.

א [ʼAʹleph]

34 Nitambariki Yehova nyakati zote;+

Daima sifa yake itakuwa katika kinywa changu.+

ב [Behth]

 2 Nafsi yangu itajisifu katika Yehova;+

Wapole watasikia na kushangilia.+

ג [Giʹmel]

 3 Mtukuzeni Yehova pamoja nami,+

Na tulikweze jina lake pamoja.+

ד [Daʹleth]

 4 Nilimuuliza Yehova, naye akanijibu,+

Naye akanikomboa kutoka katika mambo yote yenye kuniogopesha.+

ה [Heʼ]

 5 Walimtazama, wakang’aa,+

Nazo nyuso zao hazingeweza kuona haya kamwe.+

ז [Zaʹyin]

 6 Huyu mwenye kuteseka aliita, na Yehova mwenyewe akasikia.+

Na Yeye akamwokoa kutoka katika taabu zake zote.+

ח [Chehth]

 7 Malaika wa Yehova anapiga kambi pande zote kuwazunguka wanaomwogopa,+

Na yeye huwaokoa.+

ט [Tehth]

 8 Onjeni mwone ya kuwa Yehova ni mwema;+

Mwenye furaha ni mwanamume ambaye humkimbilia.+

י [Yohdh]

 9 Mwogopeni Yehova, enyi watakatifu wake,+

Kwa maana wale wanaomwogopa hawakosi chochote.+

כ [Kaph]

10 Wana-simba wenye manyoya shingoni wamekuwa na vichache na kukaa njaa;+

Lakini kwa wale wanaomtafuta Yehova, hawatakosa chochote chema.+

ל [Laʹmedh]

11 Njooni, enyi wana, nisikilizeni;+

Nitawafundisha kumwogopa Yehova.+

מ [Mem]

12 Ni nani mtu yule anayependezwa na uhai,+

Ambaye anapenda siku za kutosha ili kuona mema?+

נ [Nun]

13 Linda ulimi wako na yaliyo mabaya,+

Na midomo yako isiseme udanganyifu.+

ס [Saʹmekh]

14 Geuka kutoka katika yaliyo mabaya, na kufanya yaliyo mema;+

Utafute amani, na kuifuatia.+

ע [ʽAʹyin]

15 Macho ya Yehova yanawaelekea waadilifu,+

Na masikio yake yanakielekea kilio chao cha kuomba msaada.+

פ [Peʼ]

16 Uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda yaliyo mabaya,+

Ili kumbukumbu lao liondolewe mbali duniani.+

צ [Tsa·dhehʹ]

17 Wao walilia kwa sauti, naye Yehova mwenyewe akasikia,+

Naye akawakomboa kutoka katika taabu zao zote.+

ק [Qohph]

18 Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo;+

Naye huwaokoa wale waliopondwa roho.+

ר [Rehsh]

19 Mwadilifu ana misiba mingi,+

Lakini Yehova humkomboa kutoka katika yote hiyo.+

ש [Shin]

20 Yeye anailinda mifupa yote ya mtu huyo;

Hakuna hata mmoja uliovunjwa.+

ת [Taw]

21 Msiba utamuua mwovu;+

Na wale wanaomchukia mwadilifu watahesabiwa kuwa na hatia.+

22 Yehova anaikomboa nafsi ya watumishi wake;+

Wala hakuna yeyote kati ya wale wanaomkimbilia atakayehesabiwa kuwa na hatia.+

Ya Daudi.

35 Endesha kesi yangu dhidi ya wapinzani wangu, Ee Yehova;+

Upigane na wale wanaopigana nami.+

 2 Ushike ngao ndogo na ngao kubwa,+

Na usimame ili unisaidie.+

 3 Na uchomoe mkuki na shoka lenye makali kuwili ili kukutana na wale wanaonifuatilia.+

Uiambie nafsi yangu: “Mimi ni wokovu wako.”+

 4 Wale wanaoiwinda nafsi yangu na waone aibu na kufedheheka.+

Wale wanaonipangia hila nipatwe na msiba na warudishwe nyuma na kufedheheka.+

 5 Na wawe kama makapi mbele ya upepo,+

Naye malaika wa Yehova na awe akiwasukuma.+

 6 Njia yao na iwe giza na mahali penye kuteleza,+

Naye malaika wa Yehova na awe akiwafuatilia.

 7 Kwa maana wamenifichia bila sababu shimo lao lenye wavu;+

Wamelichimba bila sababu kwa ajili ya nafsi yangu.+

 8 Uharibifu na umjie bila yeye kujua,+

Na wavu wake mwenyewe aliouficha na umkamate;+

Na aanguke ndani yake apatwe na uharibifu.+

 9 Lakini nafsi yangu mwenyewe na iwe na shangwe katika Yehova;+

Na ishangilie katika wokovu wake.+

10 Mifupa yangu yote na iseme:+

“Ee Yehova, ni nani aliye kama wewe,+

Anayemkomboa mwenye kuteseka kutoka kwa mwenye nguvu kuliko yeye,+

Na kumkomboa mwenye kuteseka na maskini kutoka kwa mwenye kumnyang’anya?”+

11 Mashahidi wenye jeuri husimama;+

Huniuliza mambo nisiyojua.+

12 Hunilipa mema yangu kwa mabaya,+

Hasara kwa nafsi yangu.+

13 Lakini mimi, walipokuwa wagonjwa, mavazi yangu yalikuwa ni magunia,+

Nikaitesa nafsi yangu kwa kufunga,+

Nayo sala yangu mwenyewe ikawa ikirudi kifuani pangu.+

14 Kana kwamba ni kwa ajili ya mwenzangu, kana kwamba ni kwa ajili ya ndugu yangu,+

Nilitembea huku na huku kama mtu anayemwombolezea mama yake.+

Nikainama nikiwa na huzuni.

15 Lakini walishangilia na kukusanyika pamoja kuhusu kuchechemea kwangu;+

Walikusanyika pamoja dhidi yangu,+

Wakinipiga na kuniangusha wakati sikujua;+

Walinirarua vipande-vipande wala hawakukaa kimya.+

16 Kati ya wenye dhihaka, walioasi imani, kwa ajili ya keki,+

Kulikuwako kusaga meno yao dhidi yangu.+

17 Ee Yehova, utaendelea kuona hayo mpaka wakati gani?+

Uirudishe nafsi yangu kutoka katika maangamizi yao,+

Naam, yangu iliyo ya pekee+ kutoka kwa wana-simba wenye manyoya shingoni.

18 Nitakusifu katika kutaniko kubwa;+

Nitakusifu kati ya kikundi cha watu wengi.+

19 Wale ambao ni adui zangu bila sababu yoyote wasishangilie juu yangu;+

Nao wale wanaonichukia bila sababu, wasikonyeze jicho.+

20 Kwa maana hawasemi mambo ya amani;+

Bali juu ya wanyamavu wa dunia

Wanaendelea kupanga mambo ya udanganyifu.+

21 Nao hufungua kinywa chao wazi dhidi yangu.+

Wamesema: “Aha! Aha! jicho letu limeyaona.”+

22 Ee Yehova, umeona.+ Usikae kimya.+

Ee Yehova, usikae mbali nami.+

23 Uamke na ukae macho kwa ajili ya hukumu yangu,+

Kwa ajili ya kesi yangu,+ Ee Mungu wangu, naam, Yehova.

24 Nihukumu kulingana na uadilifu wako, Ee Yehova Mungu wangu,+

Nao wasishangilie juu yangu.+

25 Na wasiseme moyoni mwao: “Aha, nafsi yetu!”+

Na wasiseme: “Tumemmeza.”+

26 Na waone aibu na kufedheheka wote pamoja+

Wanaoshangilia msiba wangu.+

Na wavikwe aibu+ na fedheha wale wanaojivuna sana dhidi yangu.+

27 Wale wanaopendezwa na uadilifu wangu na wapige vigelegele kwa shangwe na kushangilia.+

Nao waseme daima:+

“Yehova na atukuzwe, ambaye anapendezwa na amani ya mtumishi wake.”+

28 Nao ulimi wangu mwenyewe na utamke uadilifu wako kwa sauti ya chini,+

Sifa yako mchana kutwa.+

Kwa kiongozi. Ya mtumishi wa Yehova, Daudi.

36 Maneno ya ukosaji kwa mtu mwovu yako katikati ya moyo wake;+

Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.+

 2 Kwa maana ametenda kwa ulaini machoni pake mwenyewe+

Asiweze kuliona kosa lake ili alichukie.+

 3 Maneno ya kinywa chake ni kuumiza na udanganyifu;+

Ameacha kuwa na ufahamu wa kufanya mema.+

 4 Yeye anaendelea kupanga hila ya kuumiza kitandani mwake.+

Husimama katika njia isiyo nzuri.+

Hakatai lililo baya.+

 5 Ee Yehova, fadhili zako zenye upendo ziko mbinguni;+

Uaminifu wako umefika mawinguni.+

 6 Uadilifu wako ni kama milima ya Mungu;+

Uamuzi wako wa hukumu ni kilindi kikubwa cha maji.+

Wewe huokoa mwanadamu na mnyama, Ee Yehova.+

 7 Jinsi zilivyo na thamani fadhili zako zenye upendo, Ee Mungu!+

Nao wana wa binadamu hupata kimbilio katika kivuli cha mabawa yako.+

 8 Wao hunywa na kushiba vinono vya nyumba yako;+

Nawe huwanywesha kwenye mito ya raha zako.+

 9 Kwa maana kwako wewe iko chemchemi ya uzima;+

Kwa nuru inayotoka kwako sisi tunaweza kuona nuru.+

10 Endeleza fadhili zako zenye upendo kwa wale wanaokujua,+

Na uadilifu wako kwa wale walio wanyoofu moyoni.+

11 Mguu wa majivuno usinijie;+

Nao mkono wa watu waovu, usinifanye kuwa mtu wa kutanga-tanga.+

12 Huko wanaotenda mambo yenye kuumiza wameanguka;+

Wamesukumwa chini nao wameshindwa kusimama.+

Ya Daudi.

א [ʼAʹleph]

37 Usijionyeshe umewaka hasira kwa sababu ya watenda-maovu.+

Usiwaonee wivu wale wanaofanya mambo yasiyo ya uadilifu.+

 2 Kwa maana watakauka haraka kama majani,+

Nao watafifia kama majani mapya ya kijani kibichi.+

ב [Behth]

 3 Mtegemee Yehova na ufanye mema;+

Ukae duniani, na utende kwa uaminifu.+

 4 Pia upate furaha tele katika Yehova,+

Naye atakupa maombi ya moyo wako.+

ג [Giʹmel]

 5 Mkabidhi Yehova njia yako,+

Na kumtegemea,+ naye mwenyewe atatenda.+

 6 Naye atauleta uadilifu wako kama nuru,+

Na haki yako kama katikati ya mchana.+

ד [Daʹleth]

 7 Kaa kimya mbele za Yehova+

Na kumngojea kwa kutamani.+

Usijionyeshe umewaka hasira kwa sababu ya mtu yeyote anayeifanikisha njia yake,+

Kwa sababu ya mtu anayetimiza mawazo yake.+

ה [Heʼ]

 8 Acha hasira na uache ghadhabu;+

Usijionyeshe umewaka hasira ili tu kufanya uovu.+

 9 Kwa maana watenda-maovu watakatiliwa mbali,+

Bali wale wanaomtumaini Yehova ndio watakaoimiliki dunia.+

ו [Waw]

10 Na bado muda kidogo tu, na mtu mwovu hatakuwako tena;+

Nawe hakika utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo.+

11 Bali wapole wataimiliki dunia,+

Nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.+

ז [Zaʹyin]

12 Mwovu anampangia hila mwadilifu,+

Naye anamsagia meno yake.+

13 Yehova mwenyewe atamcheka,+

Kwa maana hakika yeye anaona kwamba siku yake itakuja.+

ח [Chehth]

14 Waovu wamechomoa upanga na kuupinda upinde wao,+

Ili kumwangusha mwenye kuteseka na maskini,+

Ili kuwachinja walio wanyoofu katika njia yao.+

15 Upanga wao wenyewe utaingia katika moyo wao,+

Nazo pinde zao zitavunjwa.+

ט [Tehth]

16 Afadhali kidogo alicho nacho mtu mwadilifu+

Kuliko wingi wa watu wengi waovu.+

17 Kwa maana mikono ya waovu itavunjwa,+

Bali Yehova atakuwa anawategemeza watu waadilifu.+

י [Yohdh]

18 Yehova anazijua siku za watu wasio na kosa,+

Nao urithi wao wenyewe utaendelea mpaka wakati usio na kipimo.+

19 Hawataona aibu wakati wa msiba,+

Na katika siku za njaa watashiba.+

כ [Kaph]

20 Kwa maana waovu wataangamia,+

Nao adui za Yehova watakuwa kama malisho bora;

Lazima wao waufikie mwisho wao.+ Katika moshi lazima waufikie mwisho wao.+

ל [Laʹmedh]

21 Mwovu anakopa lakini halipi,+

Lakini mwadilifu anaonyesha kibali na anatoa zawadi.+

22 Kwa maana wale wanaobarikiwa naye wataimiliki dunia,+

Lakini wale anaowalaani watakatiliwa mbali.+

מ [Mem]

23 Hatua za mwanamume zimetayarishwa na Yehova,+

Na Yeye hupendezwa na njia yake.+

24 Ijapokuwa huenda akaanguka, yeye hatatupwa chini,+

Kwa maana Yehova anautegemeza mkono wake.+

נ [Nun]

25 Nilikuwa kijana, pia nimezeeka,+

Na bado sijamwona mtu yeyote mwadilifu akiwa ameachwa kabisa,+

Wala uzao wake ukitafuta mkate.+

26 Anaonyesha kibali na kukopesha mchana kutwa,+

Na kwa hiyo wazao wake watapata baraka.+

ס [Saʹmekh]

27 Geuka mbali kutoka kwa mambo mabaya na ufanye yaliyo mema,+

Na hivyo ukae mpaka wakati usio na kipimo.+

28 Kwa maana Yehova ni mpenda-haki,+

Naye hatawaacha washikamanifu wake.+

ע [ʽAʹyin]

Hakika watalindwa mpaka wakati usio na kipimo;+

Lakini wazao wa waovu, hakika watakatiliwa mbali.+

29 Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia,+

Nao watakaa milele juu yake.+

פ [Peʼ]

30 Kinywa cha mwadilifu ndicho kinachotamka hekima kwa sauti ya chini,+

Na ulimi wake ndio unaosema kwa njia ya haki.+

31 Sheria ya Mungu wake imo katika moyo wake;+

Hatua zake hazitayumba-yumba.+

צ [Tsa·dhehʹ]

32 Mwovu anaendelea kumwangalia mwadilifu+

Naye anatafuta kumuua.+

33 Lakini Yehova hatamwacha mkononi mwa huyo,+

Naye hatamtangaza kuwa mwovu anapohukumiwa.+

ק [Qohph]

34 Mtumaini Yehova na kuishika njia yake,+

Naye atakuinua uimiliki dunia.+

Watu waovu watakapokatiliwa mbali, wewe utaona hilo.+

ר [Rehsh]

35 Nimemwona mwovu akiwa mwonevu+

Na akijitandaza kama mti wenye majani mengi katika udongo wa asili.+

36 Na bado yeye akapitilia mbali, naye hakuwepo;+

Nami nikaendelea kumtafuta, wala hakupatikana.+

ש [Shin]

37 Mwangalie mtu asiye na lawama na uendelee kumwangalia mnyoofu,+

Kwa maana wakati ujao wa mtu huyo utakuwa wenye amani.+

38 Lakini wakosaji hakika wataangamizwa pamoja;+

Wakati ujao wa watu waovu hakika utakatiliwa mbali.+

ת [Taw]

39 Nao wokovu wa watu waadilifu ni kutoka kwa Yehova;+

Yeye ni ngome yao wakati wa taabu.+

40 Na Yehova atawasaidia na kuwaokoa.+

Atawaponya kutoka kwa watu waovu na kuwaokoa,+

Kwa sababu wamemkimbilia yeye.+

Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.

38 Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,+

Wala usinirekebishe katika ghadhabu yako.+

 2 Kwa maana mishale yako imepenya sana ndani yangu,+

Nao mkono wako umeshuka juu yangu.+

 3 Hakuna mahali popote pazima katika mwili wangu kwa sababu ya shutuma yako.+

Hakuna amani katika mifupa yangu kwa sababu ya dhambi yangu.+

 4 Kwa maana makosa yangu yamepita juu ya kichwa changu;+

Kama mzigo mzito, ni mazito sana kwangu.+

 5 Vidonda vyangu vinanuka, vina usaha,

Kwa sababu ya upumbavu wangu.+

 6 Nimeingiwa na wasiwasi, nimeinama kupita kiasi;+

Nimetembea huku na huku kwa huzuni mchana kutwa.+

 7 Kwa maana viuno vyangu vimejaa moto,

Wala hakuna mahali popote pazima katika mwili wangu.+

 8 Nimekufa ganzi na kupondwa kupita kiasi;

Nimenguruma kwa sababu ya kuugua kwa moyo wangu.+

 9 Ee Yehova, tamaa yangu yote iko mbele zako,

Wala kuugua kwangu hakujafichwa mbele zako.+

10 Moyo wangu mwenyewe umepiga-piga kwa nguvu, nguvu zangu zimeniacha,

Na nuru ya macho yangu mwenyewe haiko pamoja nami.+

11 Nao wenye kunipenda na wenzangu wanaendelea kusimama mbali na pigo langu,+

Na rafiki zangu wamesimama mbali.+

12 Lakini wale wanaoitafuta nafsi yangu wanatega mitego,+

Na wale wanaotaka kuniletea msiba wamesema mabaya,+

Nao kwa sauti ya chini wanaendelea kusema udanganyifu mchana kutwa.+

13 Lakini mimi, kama kiziwi, nikawa siwasikilizi;+

Na kama mtu asiyeweza kusema, nikawa sifungui kinywa changu.+

14 Nami nikawa kama mtu ambaye hasikii,

Na kinywani mwangu hamkuwa na hoja zozote za kupinga.

15 Kwa maana nilikungojea wewe, Ee Yehova;+

Wewe mwenyewe ukanijibu, Ee Yehova Mungu wangu.+

16 Kwa maana nilisema: “Kama sivyo watashangilia kwa sababu yangu;+

Mguu wangu uliposonga kwa kuyumba-yumba,+ hakika walijivuna sana dhidi yangu.”+

17 Kwa maana nilikuwa tayari kuchechemea,+

Na maumivu yangu yalikuwa mbele yangu daima.+

18 Kwa maana nilisema juu ya kosa langu mwenyewe;+

Nikaanza kuhangaikia dhambi yangu.+

19 Na adui zangu walio hai wakawa wenye nguvu,+

Na wale wenye kunichukia bila sababu wakawa wengi.+

20 Nao walikuwa wakinilipa mema yangu kwa mabaya;+

Wakaendelea kushindana nami kwa sababu ya kufuatilia kwangu mambo yaliyo mema.+

21 Usiniache, Ee Yehova.

Ee Mungu wangu, usikae mbali nami.+

22 Ufanye haraka unisaidie,+

Ee Yehova wokovu wangu.+

Kwa kiongozi wa Yeduthuni.+ Muziki wa Daudi.

39 Nilisema: “Nitalinda njia zangu+

Ili nisiendelee kutenda dhambi kwa ulimi wangu.+

Nitaweka lijamu kama mlinzi wa kinywa changu mwenyewe,+

Maadamu mtu yeyote mwovu yuko mbele yangu.”+

 2 Nikawa asiyeweza kusema kwa kukaa kimya;+

Nikaendelea kulinyamazia lililo jema,+

Na kuumia kwangu kukatengwa.

 3 Moyo wangu ukawa na moto ndani yangu;+

Wakati wa kuugua kwangu moto ukaendelea kuwaka.

Nilisema kwa ulimi wangu:

 4 “Ee Yehova, nijulishe mwisho wangu,+

Na kipimo cha siku zangu—ni kipimo gani,+

Ili nipate kujua kadiri nilivyo wa muda mfupi.+

 5 Tazama! Umezifanya siku zangu kuwa chache tu;+

Na urefu wa maisha yangu si kitu mbele zako.+

Kwa kweli kila mtu wa udongo, ingawa anasimama imara, si kitu ila pumzi tu.+ Sela.

 6 Kwa kweli mtu hutembea huku na huku kama kivuli tu.+

Kwa kweli wana msukosuko ambao ni ubatili.+

Mmoja anarundika vitu wala hajui ni nani atakayevikusanya.+

 7 Na sasa, nimetumainia nini, Ee Yehova?

Matarajio yangu yanakuelekea wewe.+

 8 Unikomboe kutoka katika makosa yangu yote.+

Usiniweke kama shutuma ya mtu asiye na akili.+

 9 Niliendelea kuwa asiyeweza kusema;+ sikuweza kufungua kinywa changu,+

Kwa maana wewe mwenyewe ulichukua hatua.+

10 Uniondolee pigo lako.+

Nimefikia mwisho kwa sababu ya uadui wa mkono wako.+

11 Umemrekebisha mtu kwa makaripio dhidi ya kosa,+

Nawe unakula vitu vyake vyenye kutamanika kama nondo.+

Kwa kweli kila mtu wa udongo ni pumzi tu.+ Sela.

12 Uisikie sala yangu, Ee Yehova,

Na usikilize kilio changu cha kutaka msaada.+

Usikae kimya machozi yangu yanapotoka.+

Kwa maana, kwako, mimi ni mkaaji mgeni tu,+

Mhamiaji kama vile mababu zangu wote.+

13 Usinitazame, ili nipate kung’aa+

Kabla sijaenda, nisiwepo.”+

Kwa kiongozi. Ya Daudi, muziki.

40 Nilimtumainia Yehova kwa bidii,+

Kwa hiyo akanitegea sikio lake na kusikia kilio changu cha kuomba msaada.+

 2 Yeye pia akaniinua kutoka katika shimo lenye kunguruma,+

Kutoka katika matope ya nchi.+

Kisha yeye akainua miguu yangu juu ya mwamba;+

Akazifanya imara hatua zangu.+

 3 Tena, akatia wimbo mpya katika kinywa changu,

Sifa kwa Mungu wetu.+

Wengi wataona hilo na kuogopa,+

Nao watamtegemea Yehova.+

 4 Mwenye furaha ni mwanamume ambaye amemfanya Yehova kuwa tegemeo lake+

Na ambaye hakuelekeza uso wake kwa watu wakaidi,

Wala kwa wale wanaogeukia uwongo.+

 5 Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi,+

Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea;+

Hakuna wa kulinganishwa nawe.+

Ikiwa ningetaka kueleza na kusema juu yake,

Zimekuwa nyingi sana kuliko vile ninavyoweza kusimulia.+

 6 Hukupendezwa na dhabihu na toleo;+

Haya masikio yangu uliyafungua.+

Hukutaka toleo la kuteketezwa na toleo la dhambi.+

 7 Kwa hiyo, nilisema: “Tazama nimekuja,+

Katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa juu yangu.+

 8 Ee Mungu wangu, nimependezwa na kufanya mapenzi yako,+

Na sheria yako imo ndani yangu.+

 9 Nimetangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+

Tazama! Siizuii midomo yangu.+

Ee Yehova, wewe mwenyewe unajua hivyo vema.+

10 Uadilifu wako sikuufunika moyoni mwangu.+

Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.+

Sikuficha fadhili zako zenye upendo na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+

11 Wewe mwenyewe, Ee Yehova, usinizuilie huruma zako.+

Fadhili zako zenye upendo na ukweli wako zinilinde daima.+

12 Kwa maana misiba ilinizunguka mpaka ikawa haihesabiki.+

Makosa yangu mengi zaidi yalinifikia kuliko vile nilivyoweza kuona;+

Yakawa mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,+

Nao moyo wangu mwenyewe uliniacha.+

13 Ee Yehova, upendezwe na kunikomboa.+

Ee Yehova, ufanye haraka kuja kunisaidia.+

14 Na waone aibu na kufedheheka wote pamoja+

Wale wanaoitafuta nafsi yangu wapate kuifagilia mbali.+

Wale wanaopendezwa na msiba wangu na wageuke na kufedheheshwa.+

15 Na wakodoe macho kwa mshangao kwa sababu ya aibu yao+

Wale wanaoniambia: “Aha! Aha!”+

16 Na hao washangilie na kukufurahia wewe,+

Wale wote wanaokutafuta.+

Na waseme daima: “Yehova na atukuzwe,”+

Wale wanaopenda wokovu wako.+

17 Lakini mimi ninateseka nami ni maskini.+

Yehova mwenyewe ananijali.+

Wewe ni msaidizi wangu na Mwokoaji wangu.+

Ee Mungu wangu, usichelewe mno.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

41 Mwenye furaha ni mtu yeyote anayetenda kwa kumfikiria mtu wa hali ya chini;+

Katika siku ya msiba Yehova atamwokoa.+

 2 Yehova mwenyewe atamlinda na kumhifadhi hai.+

Atatangazwa kuwa mwenye furaha duniani;+

Nawe huwezi kamwe kumtia mkononi mwa nafsi ya adui zake.+

 3 Yehova mwenyewe atamtegemeza katika kitanda cha ugonjwa;+

Kitanda chake chote hakika utakibadilisha wakati wa ugonjwa wake.+

 4 Mimi nami, nilisema: “Ee Yehova, nionyeshe kibali.+

Uiponye nafsi yangu, kwa maana nimekutendea dhambi.”+

 5 Nao adui zangu, wanasema mabaya juu yangu:+

“Atakufa wakati gani na jina lake kwa kweli lipotee?”

 6 Na mtu akija kuniona, moyo wake utasema mambo yasiyo ya kweli;+

Atajikusanyia jambo lenye kuumiza;

Atatoka nje; huko nje atalisema.+

 7 Wote wanaonichukia wananong’onezana juu yangu kwa muungano;+

Wanaendelea kupanga hila ya jambo baya juu yangu:+

 8 “Jambo lisilofaa kitu linamiminwa juu yake;+

Sasa kwa kuwa amelala chini, hatasimama tena.”+

 9 Pia mtu mwenye kuwa na amani nami, ambaye nimemtegemea,+

Ambaye alikuwa akila mkate wangu,+ amekiinua kisigino chake dhidi yangu.+

10 Wewe, Ee Yehova, unionyeshe kibali na kuniinua,+

Ili nipate kuwalipa.+

11 Kwa jambo hili ninajua kwamba umependezwa nami,

Kwa sababu adui yangu hapigi kelele za ushindi juu yangu.+

12 Nami, umenitegemeza kwa sababu ya utimilifu wangu,+

Nawe utaniweka mbele za uso wako mpaka wakati usio na kipimo.+

13 Yehova Mungu wa Israeli na abarikiwe+

Tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo.+

Amina na Amina.+

KITABU CHA PILI

(Zaburi 42 – 72)

Kwa kiongozi. Maskili kwa ajili ya wana wa Kora.+

42 Kama vile paa ambaye hutamani vijito vya maji,

Ndivyo nafsi yangu inavyokutamani wewe, Ee Mungu.+

 2 Kwa kweli nafsi yangu ina kiu kwa ajili ya Mungu,+ kwa ajili ya Mungu aliye hai.+

Ni wakati gani nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?+

 3 Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku,+

Huku wakiniambia mchana kutwa: “Mungu wako yuko wapi?”+

 4 Nitakumbuka mambo haya, nami nitaimimina nafsi yangu iliyo ndani yangu.+

Kwa maana nilikuwa nikipita pamoja na watu wengi,

Nilikuwa nikitembea polepole mbele yao kwenda kwenye nyumba ya Mungu,+

Kwa sauti ya vigelegele vya shangwe na shukrani,+

Ya umati unaofanya sherehe.+

 5 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+

Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?+

Mngojee Mungu,+

Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu.+

 6 Ee Mungu wangu, nafsi yangu mwenyewe imekata tamaa ndani yangu.+

Ndiyo sababu ninakukumbuka,+

Kutoka katika nchi ya Yordani na vilele vya Hermoni,+

Kutoka katika ule mlima mdogo.+

 7 Kilindi cha maji kinaita kilindi cha maji

Kwa sauti ya mabubujiko yako ya maji.

Mashuu yako yote na mawimbi yako+—

Yamepita juu yangu.+

 8 Wakati wa mchana Yehova ataamuru fadhili zake zenye upendo,+

Na wakati wa usiku wimbo wake utakuwa nami;+

Kutakuwako sala kwa Mungu wa uhai wangu.+

 9 Nitamwambia Mungu mwamba wangu:+

“Kwa nini umenisahau?+

Kwa nini natembea kwa huzuni kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?”+

10 Wale wanaonionyesha uadui wamenishutumu kwa mauaji dhidi ya mifupa yangu,+

Huku wakiniambia mchana kutwa: “Mungu wako yuko wapi?”+

11 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+

Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?+

Mngojee Mungu,+

Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu na kuwa ndiye Mungu wangu.+

43 Unihukumu,+ Ee Mungu,

Na uendeshe kesi+ yangu dhidi ya taifa lisilo shikamanifu.

Uniokoe kutoka kwa mtu wa udanganyifu na mwenye kukosa uadilifu.+

 2 Kwa maana wewe ni Mungu wa ngome yangu.+

Kwa nini umenitupilia mbali?

Kwa nini natembea kwa huzuni kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?+

 3 Tuma nuru yako na kweli yako.+

Na hivyo vyenyewe viniongoze.+

Navyo vinilete kwenye mlima wako mtakatifu na kwenye maskani yako kuu.+

 4 Nami nitakuja kwenye madhabahu ya Mungu,+

Kwa Mungu, ambaye ni kushangilia kwangu kwa furaha.+

Nami nitakusifu kwa kinubi, Ee Mungu, Mungu wangu.+

 5 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+

Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?

Mngojee Mungu,+

Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu na kuwa ndiye Mungu wangu.+

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Maskili.

44 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu,

Mababu zetu wenyewe wametusimulia+

Utendaji ambao ulifanya katika siku zao,+

Siku za zamani za kale.+

 2 Wewe mwenyewe kwa mkono wako uliwafukuzia mbali mataifa,+

Nawe ukawapanda hao badala yao.+

Ukavunja vikundi vya mataifa na kuwafukuza.+

 3 Kwa maana hawakuimiliki nchi hiyo kwa upanga wao wenyewe,+

Wala wokovu haukuletwa kwa mkono wao wenyewe.+

Kwa maana ulikuwa ni mkono wako wa kuume,+ naam, mkono wako na nuru ya uso wako,

Kwa sababu ulipendezwa nao.+

 4 Wewe mwenyewe ni Mfalme wangu, Ee Mungu.+

Amuru wokovu mkuu kwa ajili ya Yakobo.+

 5 Kupitia wewe tutawasukuma wapinzani wetu;+

Katika jina lako tutawakanyagia chini wale wanaosimama dhidi yetu.+

 6 Kwa maana sikuendelea kuutegemea upinde wangu+

Wala si upanga wangu uliokuwa ukiniokoa.+

 7 Kwa maana ulituokoa kutoka kwa wapinzani wetu,+

Nawe ukawafanya waone aibu wale wanaotuchukia vikali.+

 8 Tutamtolea Mungu sifa mchana kutwa,+

Nasi tutalisifu jina lako mpaka wakati usio na kipimo.+ Sela.

 9 Lakini sasa umetutupilia mbali na unaendelea kutufedhehesha,+

Wala huendi pamoja na majeshi yetu.+

10 Wewe unaendelea kutufanya tugeuke kutoka kwa adui zetu,+

Na wale wanaotuchukia vikali wamejinyakulia vitu.+

11 Wewe unatutoa kama kondoo, kama chakula,+

Nawe umetutawanya kati ya mataifa.+

12 Unawauza watu wako kwa bei ndogo sana,+

Wala hujapata faida yoyote kwa bei yao.

13 Unatuweka kuwa shutuma kwa jirani zetu,+

Kuwa dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka pande zote.+

14 Umetufanya kuwa neno la kimethali kati ya mataifa,+

Kuwa kitu cha kutikisiwa kichwa kati ya vikundi vya mataifa.+

15 Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa,

Nayo aibu ya uso wangu mwenyewe imenifunika,+

16 Kwa sababu ya sauti ya mtu anayeshutumu na kusema vibaya,

Kwa sababu ya adui na mtu anayejilipizia kisasi.+

17 Yote hayo ndiyo yametujia, nasi hatujakusahau,+

Wala hatujatenda kwa njia ya uwongo katika agano lako.+

18 Moyo wetu haujageuka nyuma kwa kukosa imani,+

Wala hatua za miguu yetu hazitoki katika njia yako.+

19 Kwa maana umetuponda katika mahali pa mbwa-mwitu,+

Nawe unatufunika kwa kivuli kizito.+

20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu,

Au kumnyooshea mungu mgeni mikono yetu,+

21 Je, Mungu mwenyewe hatachunguza hilo?+

Kwa maana yeye anajua siri za moyo.+

22 Lakini kwa ajili yako tumeuawa mchana kutwa;

Tumehesabiwa kuwa kondoo wa kuchinjwa.+

23 Uamke. Kwa nini unaendelea kulala usingizi, Ee Yehova?+

Uamke. Usiendelee kututupilia mbali milele.+

24 Kwa nini unaendelea kuuficha uso wako?

Kwa nini unasahau mateso yetu na ukandamizaji wetu?+

25 Kwa maana nafsi yetu imeinama chini mavumbini;+

Tumbo letu limeshikamana na udongo.

26 Usimame, utusaidie+

Na kutukomboa kwa ajili ya fadhili zako zenye upendo.+

Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi. Ya wana wa Kora. Maskili. Wimbo wa wanawake wapendwa.

45 Moyo wangu umesisimuka kwa sababu ya jambo jema.+

Ninasema: “Kazi zangu zinamhusu mfalme.”+

Ulimi wangu na uwe kalamu+ ya mwandikaji stadi.+

 2 Kwa kweli wewe una sura nzuri kuliko wana wa binadamu.+

Uvutio umemiminwa juu ya midomo yako.+

Ndiyo sababu Mungu amekubariki mpaka wakati usio na kipimo.+

 3 Funga upanga+ wako kwenye paja lako, ewe mwenye nguvu,+

Pamoja na utukufu wako na fahari yako.+

 4 Na katika fahari yako endelea mpaka ufanikiwe;+

Panda kwa kutetea kweli na unyenyekevu na uadilifu,+

Na mkono wako wa kuume utakufundisha mambo yenye kuogopesha.+

 5 Mishale yako ni mikali​—⁠vikundi vya watu vinaendelea kuanguka chini yako+—

Katika moyo wa adui za mfalme.+

 6 Mungu ni kiti chako cha ufalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele;+

Fimbo ya enzi ya ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.+

 7 Umependa uadilifu+ nawe unachukia uovu.+

Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako,+ amekutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia+ kuliko wenzako.+

 8 Mavazi yako yote ni manemane na udi na kida;+

Kutoka katika jumba kuu la mfalme la pembe,+ vinanda vimekufanya ushangilie.

 9 Binti+ za wafalme wamo kati ya wanawake wako wenye thamani.

Malkia+ amesimama kwenye mkono wako wa kuume akiwa amevaa dhahabu ya Ofiri.+

10 Sikiliza, ewe binti, uone, na utege sikio lako;

Na uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.+

11 Naye mfalme atautamani urembo wako,+

Kwa maana yeye ni bwana wako,+

Kwa hiyo mwinamie.+

12 Binti Tiro na zawadi pia+—

Walio matajiri kati ya watu watautuliza uso wako mwenyewe.+

13 Binti ya mfalme ana utukufu wote ndani ya nyumba;+

Mavazi yake yamepambwa kwa dhahabu.

14 Atapelekwa kwa mfalme akiwa na mavazi yaliyofumwa.+

Mabikira katika msafara wake ambao ni rafiki zake wanaingizwa ndani kwako.+

15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe;

Wataingia katika jumba la mfalme.

16 Mahali pa mababu+ zako patachukuliwa na wana wako,+

Ambao utawaweka kuwa wakuu katika dunia yote.+

17 Nitalitaja jina lako katika vizazi vyote vitakavyokuja.+

Ndiyo sababu vikundi vya watu vitakusifu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora+ juu ya Wanawali. Wimbo.

46 Kwetu Mungu ni kimbilio na nguvu,+

Msaada unaopatikana kwa utayari wakati wa

taabu.+

 2 Ndiyo sababu hatutaogopa, hata dunia ikibadilika+

Na hata milima ikitikisika na kuingia katika moyo wa bahari kuu;+

 3 Hata maji yake yakiwa na msukosuko, na kutoa povu,+

Hata milima ikitikiswa na ghasia yake.+ Sela.

 4 Kuna mto ambao vijito vyake hulifanya jiji la Mungu lishangilie,+

Maskani kuu takatifu zaidi ya Aliye Juu Zaidi.+

 5 Mungu yuko katikati ya jiji;+ halitatikisika.+

Mungu atalisaidia wakati wa mapambazuko ya asubuhi.+

 6 Mataifa yakawa na msukosuko,+ falme zikatikisika;

Akavumisha sauti yake, dunia ikayeyuka.+

 7 Yehova wa majeshi yuko pamoja nasi;+

Mungu wa Yakobo ni kilele chetu salama.+ Sela

 8 Njooni, tazameni matendo ya Yehova,+

Jinsi ambavyo ameweka matukio ya kushangaza duniani.+

 9 Anakomesha vita mpaka kwenye mwisho wa dunia.+

Upinde anauvunja na kuukata mkuki vipande-vipande;+

Magari ya kukokotwa anayateketeza motoni.+

10 “Salimuni amri, na mjue ya kwamba mimi ni Mungu.+

Nitatukuzwa kati ya mataifa,+

Nitatukuzwa duniani.”+

11 Yehova wa majeshi yuko pamoja nasi;+

Mungu wa Yakobo ni kilele chetu salama.+ Sela.

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora. Muziki.

47 Enyi vikundi vyote vya watu, pigeni makofi.+

Mpigieni Mungu kelele za ushindi kwa vigelegele vya shangwe.+

 2 Kwa maana Yehova, Aliye Juu Zaidi, ni mwenye kuogopesha,+

Mfalme mkuu juu ya dunia yote.+

 3 Atatiisha vikundi vya watu chini yetu+

Na vikundi vya mataifa chini ya miguu yetu.+

 4 Atatuchagulia urithi wetu,+

Fahari ya Yakobo, ambaye amempenda.+ Sela.

 5 Mungu amepanda juu kwa vigelegele vya shangwe,+

Yehova kwa sauti ya baragumu.+

 6 Mpigieni Mungu muziki, pigeni muziki.+

Mpigieni Mfalme wetu muziki, pigeni muziki.

 7 Kwa maana Mungu ni Mfalme wa dunia yote;+

Pigeni muziki, mkitenda kwa busara.+

 8 Mungu amekuwa mfalme juu ya mataifa.+

Mungu mwenyewe ameketi juu ya kiti chake kitakatifu cha ufalme.+

 9 Wakuu wa watu wamekusanyika pamoja,+

Pamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu.+

Kwa maana ngao za dunia ni za Mungu.+

Yeye amepanda juu sana.+

Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+

48 Yehova ni mkuu na wa kusifiwa sana+

Katika jiji la Mungu wetu,+ katika mlima wake mtakatifu.+

 2 Wenye ukuu wa kupendeza, shangwe ya dunia yote,+

Ni Mlima Sayuni ulioko sehemu za mbali za kaskazini,+

Mji wa Mfalme Mkuu.+

 3 Katika minara ya makao yake Mungu amejulikana kuwa kilele salama.+

 4 Kwa maana, Tazama! wafalme wenyewe wamekutana kwa mapatano,+

Wamepita karibu wakiwa pamoja.+

 5 Wao wenyewe waliona; nao wakashangaa.

Wakasumbuka, wakakimbizwa wakiwa na wasiwasi mkubwa.+

 6 Wakashikwa na kutetemeka wakiwa huko,+

Uchungu wa kuzaa kama ule wa mwanamke anayezaa.+

 7 Kwa upepo wa mashariki wewe unavunja meli za Tarshishi.+

 8 Kama vile tulivyosikia, ndivyo tumeona+

Katika jiji la Yehova wa majeshi, katika jiji la Mungu wetu.+

Mungu mwenyewe atalifanya imara mpaka wakati usio na kipimo.+ Sela

 9 Tumefikiria kwa uzito, Ee Mungu, juu ya fadhili zako zenye upendo+

Katikati ya hekalu lako.+

10 Kama jina lako,+ Ee Mungu, ndivyo ilivyo sifa yako

Mpaka kwenye miisho ya dunia.

Mkono wako wa kuume umejaa uadilifu.+

11 Mlima Sayuni+ na ushangilie,

Miji ya kandokando ya Yuda na ishangilie,+ kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu.+

12 Pigeni mwendo mkizunguka Sayuni, na kuuzunguka-zunguka;+

Hesabuni minara yake.+

13 Wekeni mioyo yenu juu ya boma lake.+

Kagueni minara ya makao yake,

Ili mpate kukisimulia kizazi cha wakati ujao.+

14 Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

Yeye mwenyewe atatuongoza mpaka tufe.+

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki.

49 Sikieni hili, enyi vikundi vyote vya watu.

Tegeni sikio, enyi wakaaji wote wa mfumo wa mambo,+

 2 Enyi wana wa wanadamu, naam, ninyi wana wa binadamu.

Wewe tajiri pamoja nawe maskini.+

 3 Kinywa changu mwenyewe kitasema mambo ya hekima,+

Na moyo wangu utatafakari mambo ya uelewaji.+

 4 Nitatega sikio langu nisikie maneno ya kimethali;+

Nitafumbua kitendawili+ changu kwa kinubi.

 5 Kwa nini niogope katika siku za uovu,+

Wakati ambapo kosa la wanaonipindua linanizingira?+

 6 Wale wanaotegemea riziki zao,+

Na ambao wanaendelea kujisifu juu ya wingi wa utajiri wao,+

 7 Hakuna hata mmoja wao anayeweza kumkomboa hata ndugu,+

Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake;

 8 (Nayo bei ya ukombozi wa nafsi yao ni yenye thamani sana+

Hivi kwamba imekoma mpaka wakati usio na kipimo)

 9 Hivi kwamba yeye aendelee kuishi milele na asilione shimo.+

10 Kwa maana yeye huona kwamba hata wenye hekima wanakufa,+

Mjinga na asiyetumia akili huangamia wote pamoja,+

Nao hulazimika kuwaachia wengine mali yao.+

11 Tamaa yao ya ndani ni kwamba nyumba zao ziwepo mpaka wakati usio na kipimo,+

Maskani zao mpaka kizazi baada ya kizazi.+

Wameyaita mashamba yao kwa majina yao.+

12 Na bado mtu wa udongo, ingawa katika heshima, hawezi kuendelea kukaa;+

Kwa kweli analingana na wanyama ambao wameangamizwa.+

13 Hiyo ndiyo njia ya wale wenye ujinga,+

Na ya wale wanaowafuata ambao wanapendezwa na maneno yao wenyewe. Sela.

14 Kama kondoo, wao wamewekewa Kaburi;*+

Kifo chenyewe kitawachunga;+

Nao wanyoofu watawatawala asubuhi,+

Nayo maumbo yao hayatakosa kuchakaa;+

Kaburi* badala ya makao yaliyo juu ni kwa ajili ya kila mmoja.+

15 Hata hivyo, Mungu mwenyewe ataikomboa nafsi yangu kutoka katika mkono wa Kaburi,*+

Kwa maana atanipokea. Sela.

16 Usiogope kwa sababu mtu fulani anapata utajiri,+

Kwa sababu utukufu wa nyumba yake unaongezeka,+

17 Kwa maana anapokufa hawezi kuchukua kitu chochote;+

Utukufu wake hautashuka chini pamoja naye.+

18 Kwa maana muda wote wa maisha yake alikuwa akiibariki nafsi yake mwenyewe;+

(Na watu watakusifu kwa sababu unajiendeleza vizuri)+

19 Nafsi yake mwishowe inafikia tu kwenye kizazi cha mababu zake.+

Hawataona nuru tena kamwe.+

20 Mtu wa udongo, ingawa katika heshima, ambaye haelewi,+

Kwa kweli analingana na wanyama ambao wameangamizwa.+

Muziki wa Asafu.+

50 Mwenye Uwezo,+ Mungu, Yehova,+ amesema mwenyewe,+

Naye anaiita dunia,+

Kutoka mashariki mpaka magharibi.+

 2 Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu mwenyewe ameangaza.+

 3 Mungu wetu atakuja naye hawezi kukaa kimya.+

Mbele zake kuna moto unaoteketeza,+

Na kumzunguka pande zote hali ya hewa imekuwa yenye dhoruba kali sana.+

 4 Yeye anaziita mbingu juu na dunia+

Ili atekeleze hukumu juu ya watu wake:+

 5 “Wakusanye kwangu washikamanifu wangu,+

Wale wanaofanya agano langu juu ya dhabihu.”+

 6 Na mbingu zinasema juu ya uadilifu wake,+

Kwa maana Mungu mwenyewe ni Mwamuzi.+ Sela.

 7 “Sikilizeni, enyi watu wangu, nami nitasema,+

Ee Israeli, nami nitatoa ushahidi dhidi yako.+

Mimi ni Mungu, Mungu wako.+

 8 Mimi siwakaripii kuhusiana na dhabihu zenu,+

Wala kuhusiana na matoleo yako mazima ya kuteketezwa yaliyo mbele zangu daima.+

 9 Sitachukua ng’ombe-dume katika nyumba yako,+

Wala mbuzi-dume katika mazizi yako.

10 Kwa maana kila mnyama wa mwituni ni wangu,+

Wanyama walio juu ya milima elfu moja.+

11 Najua vizuri kila kiumbe chenye mabawa cha milimani,+

Na makundi ya wanyama wa porini yako pamoja nami.+

12 Ningalikuwa na njaa, singalikuambia;

Kwa maana nchi yenye kuzaa+ na vyote vinavyoijaza ni vyangu.+

13 Je, nile nyama ya ng’ombe-dume wenye nguvu,+

Na je, ninywe damu ya mbuzi-dume?+

14 Toa shukrani zikiwa dhabihu yako kwa Mungu,+

Na umtimizie Aliye Juu Zaidi nadhiri zako;+

15 Na uniite katika siku ya taabu.+

Nitakuokoa, nawe utanitukuza.”+

16 Lakini Mungu atamwambia mwovu:+

“Una haki gani ya kuyataja masharti yangu,+

Na kwamba ulichukue agano langu kinywani mwako?+

17 Tazama, wewe—wewe umechukia nidhamu,+

Nawe unaendelea kuyatupa maneno yangu nyuma yako.+

18 Wakati wowote ulipomwona mwizi, naam, ulipendezwa naye;+

Nawe ulishirikiana na wazinzi.+

19 Umefungua kinywa chako kutoa lililo baya,+

Na ulimi wako unaushikamanisha na udanganyifu.+

20 Unaketi na kusema vibaya juu ya ndugu yako mwenyewe,+

Juu ya mwana wa mama yako unafichua kosa.+

21 Umeyafanya mambo hayo, nami nikaendelea kukaa kimya.+

Ulidhani kwamba kwa hakika mimi ningekuwa kama wewe.+

Nitakukaripia,+ nami nitayarekebisha mambo mbele ya macho yako.+

22 Tafadhali, enyi mnaomsahau Mungu eleweni hili,+

Nisije nikawararua vipande-vipande bila ya kuwa na mkombozi.+

23 Yule anayetoa shukrani zikiwa dhabihu yake ndiye anayenitukuza;+

Naye anayedumisha njia iliyowekwa,

Nitamfanya aone wokovu wa Mungu.”+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Nathani nabii alipoingia kwake baada ya Daudi kulala na Bath-sheba.+

51 Ee Mungu, unionyeshe kibali kulingana na fadhili zako zenye upendo.+

Ufutilie mbali makosa yangu kulingana na wingi wa rehema zako.+

 2 Unioshe kabisa kutokana na kosa langu,+

Na kunitakasa kutokana na dhambi yangu.+

 3 Kwa maana mimi mwenyewe nayajua makosa yangu,+

Na dhambi yangu iko mbele yangu daima.+

 4 Dhidi yako wewe, wewe peke yako, nimetenda dhambi,+

Nami nimefanya lililo baya machoni pako,+

Ili uwe mwadilifu unapoongea,+

Ili usiwe na lawama unapohukumu.+

 5 Tazama! Nilizaliwa kwa maumivu nikiwa na kosa,+

Na mama yangu alinichukua mimba katika dhambi.+

 6 Tazama! Umependezwa na ukweli wenyewe katika sehemu za ndani;+

Na katika mtu wa sirini unijulishe hekima tupu.+

 7 Unitakase kwa hisopo kutokana na dhambi, ili nipate kuwa safi;+

Unioshe, ili nipate kuwa mweupe kuliko theluji.+

 8 Unifanye nisikie kufurahi na kushangilia,+

Ili mifupa uliyoiponda ipate kuwa na shangwe.+

 9 Ufiche uso wako kutoka kwa dhambi zangu,+

Na ufutilie mbali makosa yangu yote.+

10 Uumbe moyo safi ndani yangu, Ee Mungu,+

Na kuweka ndani yangu roho mpya, iliyo imara.+

11 Usinitupilie mbali na uso wako;+

Wala usiniondolee roho yako takatifu.+

12 Unirudishie shangwe ya wokovu wako,+

Nawe unitegemeze kwa roho ya kupenda.+

13 Nitawafundisha wakosaji njia zako,+

Ili watenda-dhambi wageuke na kurudi kwako kabisa.+

14 Unikomboe kutokana na hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+

Ili ulimi wangu upate kutangaza uadilifu wako kwa shangwe.+

15 Ee Yehova, na uifungue hii midomo yangu,+

Ili kinywa changu mwenyewe kipate kutangaza sifa yako.+

16 Kwa maana hupendezwi na dhabihu—kama sivyo ningeitoa;+

Hupendezwi na toleo zima la kuteketezwa.+

17 Dhabihu kwa Mungu ni roho iliyovunjika;+

Moyo uliovunjika na kupondwa, Ee Mungu, hutaudharau.+

18 Kwa nia yako njema utendee Sayuni vema;+

Na ujenge kuta za Yerusalemu.+

19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za uadilifu,+

Na dhabihu za kuteketezwa na toleo zima;+

Ndipo ng’ombe-dume watakapotolewa katika madhabahu yako mwenyewe.+

Kwa kiongozi. Maskili. Ya Daudi, wakati Doegi Mwedomu alipokuja na kumwambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+

52 Kwa nini unajisifia yaliyo mabaya, ewe mwenye nguvu?+

Fadhili zenye upendo za Mungu ni za mchana kutwa.+

 2 Ulimi wako hupanga hila za kuleta shida, ukiwa umenolewa kama wembe,+

Ukifanya kazi kwa udanganyifu.+

 3 Umependa yaliyo mabaya kuliko yaliyo mema,+

Kusema uwongo kuliko kusema yaliyo ya uadilifu.+ Sela.

 4 Umependa maneno yote yenye kumeza,+

Ewe ulimi wenye udanganyifu.+

 5 Mungu mwenyewe pia atakubomoa milele;+

Atakupiga na kukuangusha na kukurarua kutoka katika hema lako,+

Naye atakung’oa kutoka katika nchi ya walio hai.+ Sela.

 6 Nao waadilifu wataona hilo na kuogopa,+

Nao watamcheka.+

 7 Huyo ndiye mwanamume ambaye hamweki Mungu kuwa ngome yake,+

Lakini anategemea wingi wa utajiri wake,+

Ambaye hulindwa kutokana na shida anazoleta.+

 8 Lakini nitakuwa kama mzeituni+ wenye majani mengi katika nyumba ya Mungu;

Nazitegemea fadhili zenye upendo za Mungu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

 9 Nitakusifu mpaka wakati usio na kipimo, kwa maana wewe umechukua hatua;+

Nami nitalitumainia jina lako, kwa sababu ni jema, mbele ya washikamanifu wako.+

Kwa kiongozi juu ya Mahalathi.+ Maskili. Ya Daudi.

53 Asiye na akili amesema katika moyo wake:

“Hakuna Yehova.”+

Wametenda kwa uharibifu na kutenda kwa njia yenye kuchukiza katika ukosefu wa uadilifu;+

Hakuna yeyote anayefanya mema.+

 2 Kutoka mbinguni Mungu amewatazama wana wa binadamu walio chini,+

Aone kama kuna yeyote ambaye ana ufahamu, yeyote anayemtafuta Yehova.+

 3 Wote wamegeuka nyuma, wote ni wafisadi katika njia ileile;+

Hakuna yeyote anayefanya mema,+

Hakuna hata mmoja.

4 Je, hakuna yeyote kati ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza ambaye ana ujuzi,+

Wakila watu wangu kama vile ambavyo wamekula mkate?+

Hata hawajamwitia Yehova.+

 5 Hapo wamejawa na hofu kubwa,+

Mahali ambapo hapakuwa na kitu chenye kutia hofu;+

Kwa maana hakika Mungu ataitawanya mifupa ya mtu yeyote anayepiga kambi dhidi yako.+

Hakika utawafanya waone aibu, kwa maana Yehova mwenyewe amewakataa.+

 6 Laiti wokovu mkuu wa Israeli ungetoka Sayuni!+

Wakati ambapo Yehova anawakusanya tena mateka wa watu wake,+

Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.+

Kwa kiongozi wa vinanda. Maskili. Ya Daudi. Wakati Wazifu walipokuja na kumwambia Sauli: “Je, Daudi hajifichi pamoja nasi?”+

54 Ee Mungu, uniokoe kwa jina lako,+

Nawe unitetee katika kesi yangu kwa uwezo wako.+

 2 Ee Mungu, uisikie sala yangu;+

Utege sikio usikie maneno ya kinywa changu.+

 3 Kwa maana kuna wageni ambao wameinuka dhidi yangu,

Na waonevu wanaoitafuta nafsi yangu.+

Hawajamweka Mungu mbele yao.+ Sela.

 4 Tazama! Mungu ni msaidizi wangu;+

Yehova yuko kati ya wale wanaoitegemeza nafsi yangu.

 5 Atawalipa adui zangu ubaya;+

Katika ukweli wako uwanyamazishe.+

 6 Nitakutolea dhabihu kwa kupenda.+

Nitalisifu jina lako, Ee Yehova, kwa maana ni jema.+

 7 Kwa maana alinikomboa kutoka katika kila taabu,+

Nalo jicho langu limewatazama adui zangu.+

Kwa kiongozi wa vinanda. Maskili. Ya Daudi.

55 Utege sikio, Ee Mungu, kwa sala yangu;+

Wala usijifiche kutoka kwa ombi langu la kutaka kibali.+

 2 Unisikilize kwa makini na kunijibu.+

Mahangaiko yangu yananisukuma huku na huku bila kuwa na utulivu,+

Sina jambo lingine la kufanya ila kuonyesha wasiwasi.

 3 Kwa sababu ya sauti ya adui, kwa sababu ya mkazo wa yule mwovu.+

Kwa maana wanaendelea kuniangushia mambo yenye kuumiza,+

Na kwa hasira wanadumisha uadui juu yangu.+

 4 Moyo wangu una maumivu makali ndani yangu,+

Na woga wa kifo umeniangukia.+

 5 Woga, naam, kutetemeka kunaingia ndani yangu,+

Na mtetemeko unanifunika.

 6 Nami naendelea kusema: “Laiti ningekuwa na mabawa kama ya njiwa!+

Ningeruka mbali na kukaa.+

 7 Tazama! ningeruka mbali;+

Ningekaa nyikani.+—Sela—

 8 Ningefanya haraka kwenda mahali pangu pa kuponyokea

Kutokana na upepo wenye kuvuma, kutokana na tufani.”+

 9 Uwavuruge, Ee Yehova, ugawanye ulimi wao,+

Kwa maana nimeona jeuri na kuzozana jijini.+

10 Mchana na usiku wanalizunguka pande zote juu ya kuta zake;+

Na mambo yenye kuumiza na taabu ziko ndani yake.+

11 Shida ziko ndani yake;

Na katika viwanja vyake vya watu wote ukandamizaji na udanganyifu haujaondoka.+

12 Kwa maana sikushutumiwa na adui;+

Kama ndivyo ningaliweza kuvumilia hilo.

Si mtu anayenichukia vikali aliyejivuna sana dhidi yangu;+

Kama ndivyo ningaliweza kujificha kutoka kwake.+

13 Lakini ilikuwa ni wewe, mwanadamu anayeweza kufa tunayelingana,+

Mtu tunayejuana na ambaye ni rafiki yangu,+

14 Kwa sababu tulikuwa tukifurahia pamoja urafiki ulio mtamu;+

Tulikuwa tukitembea kuingia katika nyumba ya Mungu pamoja na watu wengi.+

15 Ukiwa na uwe juu yao!+

Na washuke katika Kaburi* wakiwa hai;+

Kwa maana wakati wao wa kukaa ugenini mambo mabaya yamekuwa ndani yao.+

16 Mimi nami nitamlilia Mungu;+

Na Yehova mwenyewe ataniokoa.+

17 Jioni na asubuhi na katikati ya mchana sikosi kuhangaika nami naomboleza,+

Naye huisikia sauti yangu.+

18 Hakika ataikomboa na kuiweka nafsi yangu katika amani mbali na vita vinavyofanywa juu yangu,+

Kwa maana wakiwa umati wamekuja kuwa dhidi yangu.+

19 Mungu atasikia na kuwajibu,+

Naam, Yeye anayeketi juu ya kiti cha ufalme kama zamani+—Sela—

Wale ambao hawafanyi mabadiliko+

Na ambao hawajamwogopa Mungu.+

20 Amenyoosha mikono yake dhidi ya wale walio na amani pamoja naye;+

Amelitia unajisi agano lake.+

21 Maneno ya kinywa chake ni laini kuliko siagi,+

Lakini moyo wake una mwelekeo wa kupigana.+

Maneno yake ni laini kuliko mafuta,+

Lakini ni panga zilizochomolewa.+

22 Mtupie Yehova mzigo wako,+

Naye mwenyewe atakutegemeza.+

Hatamwacha kamwe mwadilifu atikisike.+

23 Lakini wewe mwenyewe, Ee Mungu, utawashusha mpaka kwenye shimo lililo chini kabisa.+

Nao watu wenye hatia ya damu na wadanganyifu, hawataishi nusu ya siku zao.+

Lakini mimi, nitakutegemea wewe.+

Kwa kiongozi juu ya Njiwa Mnyamavu kati ya wale walio mbali. Ya Daudi. Miktamu. Wakati Wafilisti walipomshika huko Gathi.+

56 Unionyeshe kibali, Ee Mungu, kwa sababu mwanadamu anayeweza kufa amenikamata.+

Akiwa anafanya vita mchana kutwa, yeye anaendelea kunikandamiza.+

 2 Adui zangu wameendelea kutanua kinywa mchana kutwa,+

Kwa maana kuna wengi wanaofanya vita juu yangu kwa kujitakia makuu.+

 3 Siku yoyote ile nitakayoogopa, mimi nitakutegemea wewe.+

 4 Katika umoja na Mungu nitalisifu neno lake.+

Nimeliweka tegemeo langu kwa Mungu; Sitaogopa.+

Mwenye mwili wa nyama anaweza kunitenda nini?+

 5 Mchana kutwa wanaendelea kuharibu mambo yangu ya kibinafsi;

Mawazo yao yote yako juu yangu kwa ajili ya ubaya.+

 6 Wao wanashambulia, wanajificha,+

Wao wanaendelea kuziangalia hatua zangu,+

Huku wakiwa wameingojea nafsi yangu.+

 7 Uwatupe kwa sababu ya madhara yao.+

Uvibomoe vikundi vya watu kwa hasira, Ee Mungu.+

 8 Wewe mwenyewe umetoa habari juu ya kuwa kwangu mkimbizi.+

Uyaweke machozi yangu katika kiriba chako.+

Je, hayamo katika kitabu chako?+

 9 Wakati huo, adui zangu watageuka, siku ambayo nitaita;+

Najua hili vema, kwamba Mungu yuko kwa ajili yangu.+

10 Katika umoja na Mungu,+ nitalisifu neno lake;

Katika umoja na Yehova, nitalisifu neno lake.+

11 Nimeweka tegemeo langu katika Mungu. Sitaogopa.+

Mtu wa udongo anaweza kunitenda nini?+

12 Juu yangu, Ee Mungu, kuna nadhiri zako.+

Nitakutolea maneno ya shukrani.+

13 Kwa maana umeikomboa nafsi yangu na kifo+—

Je, hukuikomboa miguu yangu isijikwae?+—

Ili nipate kutembea mbele za Mungu katika nuru ya wale walio hai.+

Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu. Alipokimbia kwa sababu ya Sauli, akaingia pangoni.+

57 Unionyeshe kibali, Ee Mungu, unionyeshe kibali,+

Kwa maana nafsi yangu imekukimbilia wewe;+

Na katika kivuli cha mabawa yako nimekimbilia mpaka shida zipitilie mbali.+

 2 Ninamwita Mungu Aliye Juu Zaidi, Mungu wa kweli anayezikomesha kwa sababu yangu.+

 3 Atatuma kutoka mbinguni na kuniokoa.+

Hakika atamvuruga yule anayenitanulia kinywa.+ Sela.

Mungu atatuma fadhili zake zenye upendo na ukweli wake.+

 4 Nafsi yangu iko katikati ya simba;+

Sina jambo lingine la kufanya ila kulala katikati ya wamezaji, naam, wana wa binadamu,

Ambao meno yao ni mikuki na mishale,+

Na ambao ulimi wao ni upanga mkali.+

 5 Utukuzwe juu ya mbingu, Ee Mungu;+

Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+

 6 Wametayarisha wavu kwa ajili ya hatua zangu;+

Nafsi yangu imeinama chini.+

Wamechimba mtego wa shimo mbele yangu;

Wameanguka ndani yake.+ Sela.

 7 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu,+

Moyo wangu uko imara.

Nitaimba na kupiga muziki.+

 8 Amka, Ee utukufu wangu;+

Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.+

Nitayaamsha mapambazuko.

 9 Nitakusifu katikati ya vikundi vya watu, Ee Yehova;+

Nitakupigia muziki katikati ya vikundi vya mataifa.+

10 Kwa maana fadhili zako zenye upendo ni kuu kufika mbinguni,+

Na ukweli wako mpaka angani.+

11 Utukuzwe juu ya mbingu, Ee Mungu;+

Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.

Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.

58 Katika kimya chenu je, kweli mnaweza kusema juu ya uadilifu?+

Je, mnaweza kuhukumu kwa unyoofu, enyi wana wa binadamu?+

 2 Badala yake, kwa moyo mnafanya mambo ambayo ni ya kukosa uadilifu kabisa duniani,+

Na kutayarisha barabara kwa ajili ya jeuri ya mikono yenu!+

 3 Waovu wamekuwa wapotovu kutoka katika tumbo la uzazi;+

Wametanga-tanga tangu tumboni na kuendelea;

Wanasema uwongo.+

 4 Sumu yao ni kama sumu ya nyoka,+

Viziwi kama swila anayeziba sikio lake,+

 5 Ambaye hataisikiliza sauti ya watumbuizaji,+

Ingawa mtu mwenye hekima anapiga mafundo kwa uganga.+

 6 Ee Mungu, yang’oe meno yaliyo kinywani mwao.+

Uvunje mifupa ya taya za wana-simba wenye manyoya shingoni, Ee Yehova.

 7 Na wayeyuke kana kwamba ni ndani ya maji yanayoenda zake;+

Na aupinde upinde kwa ajili ya mishale yake huku wanapoanguka.+

 8 Anatembea kama konokono anayeyeyuka;

Kama mimba ya mwanamke iliyoharibika hakika hawataliona jua.+

 9 Kabla vyungu vyenu havijapatwa na mkwamba uliowashwa,+

Ulio mbichi na pia ule unaowaka, ataipeperusha kama upepo wa dhoruba.+

10 Mwadilifu atashangilia kwa sababu ameona kisasi.+

Ataosha miguu yake katika damu ya mwovu.+

11 Nao wanadamu watasema:+ “Kwa kweli kuna matunda kwa ajili ya mwadilifu.+

Kwa kweli kuna Mungu ambaye anahukumu duniani.”+

Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu. Sauli alipowatuma watu, nao wakaendelea kuilinda nyumba, ili wamuue.+

59 Unikomboe kutoka kwa adui zangu, Ee Mungu wangu;+

Unilinde kutoka kwa wale wanaoinuka dhidi yangu.+

 2 Unikomboe kutoka kwa wanaotenda mambo yenye kuumiza,+

Na uniokoe kutoka kwa watu wenye hatia ya damu.

 3 Kwa maana, tazama! wamejificha wakiingojea nafsi yangu;+

Wenye nguvu hunishambulia,+

Bila ya uasi wowote upande wangu, wala dhambi yoyote upande wangu, Ee Yehova.+

 4 Ingawa hakuna kosa, wao hukimbia na kujitayarisha.+

Usimame ninapokuita, uone.+

 5 Nawe, Ee Yehova Mungu wa majeshi, ndiye Mungu wa Israeli.+

Uamke uyaelekezee mataifa yote fikira zako.+

Usiwape kibali wasaliti wowote wenye kuumiza.+ Sela.

 6 Wao wanaendelea kurudi wakati wa jioni;+

Wanaendelea kubweka kama mbwa+ na kulizunguka jiji pande zote.+

 7 Tazama! Wanaropoka kwa kinywa chao;+

Panga ziko midomoni mwao,+

Kwa maana ni nani anayesikiliza?+

 8 Lakini wewe mwenyewe, Ee Yehova, utawacheka;+

Utayadharau mataifa yote.+

 9 Ee Nguvu zangu, nitaendelea kulinda nikikuelekea wewe;+

Kwa maana Mungu ni kilele changu salama.+

10 Mungu wa fadhili zenye upendo kwangu atanikabili yeye mwenyewe;+

Mungu mwenyewe atanifanya niwatazame adui zangu.+

11 Usiwaue, ili watu wangu wasisahau.+

Tumia nguvu zako uwafanye watange-tange huku na huku,+

Na kuwashusha, Ee ngao yetu Yehova,+

12 Kwa sababu ya dhambi ya kinywa chao, neno la midomo yao;+

Na wakamatwe katika kiburi chao,+

Naam, kwa sababu ya laana na udanganyifu ambao wanajizoeza.

13 Uwakomeshe kwa hasira;+

Uwakomeshe ili wasiwepo;

Na wajue kwamba Mungu anatawala katika Yakobo mpaka kwenye miisho ya dunia.+ Sela.

14 Na warudi wakati wa jioni;

Na wabweke kama mbwa na kulizunguka jiji pande zote.+

15 Hao na watange-tange huku na huku kwa ajili ya chakula;+

Nao wasishibe wala kukaa usiku.+

16 Lakini mimi, nitaimba juu ya nguvu zako,+

Na asubuhi nitatangaza fadhili zako zenye upendo kwa shangwe.+

Kwa maana umekuwa kilele changu salama.+

Na mahali pa kukimbilia siku ya taabu yangu.+

17 Ee Nguvu zangu, nitakupigia muziki,+

Kwa maana Mungu ni kilele changu salama, Mungu wa fadhili zenye upendo kwangu.+

Kwa kiongozi juu ya Yungiyungi la Kikumbusho. Miktamu. Ya Daudi. Kwa ajili ya kufundishia.+ Wakati alipopambana na Aram-naharaimu na Aram-Soba, naye Yoabu akarudi na kupiga Edomu katika Bonde la Chumvi, naam, watu kumi na mbili elfu.+

60 Ee Mungu, umetutupilia mbali, umetubomoa,+

Umekasirika. Uturudishe.+

 2 Umeifanya dunia itikisike, umeipasua.+

Uyaponye matundu yake, kwa maana imetikisika.+

 3 Umewafanya watu wako waone magumu.+

Umetufanya tunywe divai ikatufanya tuyumbe-yumbe.+

 4 Umewapa ishara+ wale wanaokuogopa

Wakimbie kombokombo kwa sababu ya upinde. Sela.

 5 Ili wapendwa wako waokolewe,+

Ee, uokoe kwa mkono wako wa kuume na kutujibu.+

 6 Mungu mwenyewe amesema katika utakatifu wake:+

“Nitashangilia, nitamgawanya Shekemu awe fungu;+

Na nchi tambarare ya chini ya Sukothi nitaipima.+

 7 Gileadi ni yangu na Manase ni yangu,+

Na Efraimu ni ngome ya aliye mkuu wangu;

Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+

 8 Moabu ni chungu changu cha kuoshea.+

Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+

Nitapiga kelele za ushindi juu ya Ufilisti.”+

 9 Ni nani atakayenipeleka kwenye jiji lililozingirwa?+

Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?+

10 Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetutupilia mbali+

Na ambaye huendi pamoja na majeshi yetu ukiwa Mungu?+

11 Utusaidie kutoka katika taabu,+

Kwa maana wokovu wa mtu wa udongo haufai kitu.+

12 Mungu atatuwezesha kupata nguvu,+

Na yeye mwenyewe atawakanyagia chini wapinzani wetu.+

Kwa kiongozi wa vinanda. Ya Daudi.

61 Ee Mungu, usikie kilio changu cha kusihi.+

Uisikilize sala yangu.+

 2 Kutoka mwisho wa dunia nitakulilia wewe, naam, wewe, moyo wangu unapokuwa mnyonge.+

Uniongoze kwenye mwamba ambao uko juu kuliko mimi.+

 3 Kwa maana umekuwa kimbilio langu,+

Mnara wenye nguvu mbele ya uso wa adui.+

 4 Nitakuwa mgeni katika hema lako mpaka nyakati zisizo na

kipimo;+

Nitakimbilia maficho ya mabawa yako.+ Sela.

 5 Kwa maana wewe mwenyewe, Ee Mungu, umesikiliza nadhiri zangu.+

Umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.+

 6 Utaongeza siku kwenye siku za mfalme;+

Miaka yake itakuwa kama kizazi baada ya kizazi.+

 7 Atakaa mpaka wakati usio na kipimo mbele za Mungu;+

Uagize fadhili zenye upendo na ukweli, ili zipate kumlinda.+

 8 Kwa hiyo jina lako nitalipigia muziki milele,+

Ili nipate kutimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.+

Kwa kiongozi wa Yeduthuni. Muziki wa Daudi.

62 Kwa kweli nafsi yangu inamngojea Mungu kwa kimya.+

Wokovu wangu unatoka kwake.+

 2 Kwa kweli yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kilele changu salama;+

Sitatikiswa sana.+

 3 Mtaendelea mpaka wakati gani kumshambulia mtu ambaye mngetaka kumuua?+

Ninyi nyote ni kama ukuta unaoinama, ukuta wa mawe ambao unasukumwa ndani.+

4 Kwa kweli wanatoa mashauri ili kumshawishi mtu avunje heshima yake;+

Wanafurahia uwongo.+

Wanabariki kwa kinywa chao, lakini ndani yao wanalaani.+ Sela.

 5 Kwa kweli mngojee Mungu kwa kimya, Ee nafsi yangu,+

Kwa maana tumaini langu ni kutoka kwake.+

 6 Kwa kweli yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kilele changu salama;+

Sitatikiswa.+

 7 Wokovu wangu na utukufu wangu uko juu ya Mungu.+

Mwamba wangu wenye nguvu, kimbilio langu liko katika Mungu.+

 8 Mtegemeeni nyakati zote.+

Mimineni moyo wenu mbele zake.+

Mungu ni kimbilio letu.+ Sela.

 9 Kwa kweli wana wa mtu wa udongo ni pumzi,+

Wana wa wanadamu ni uwongo.+

Wanapowekwa juu ya mizani wote pamoja ni wepesi kuliko pumzi.+

10 Msitegemee upunjaji,+

Wala kuwa ubatili kwa sababu ya unyang’anyi mtupu.+

Mali ikiongezeka, msiiweke moyoni.+

11 Mungu amesema mara moja, mara mbili nimelisikia hili,+

Kwamba nguvu ni za Mungu.+

12 Pia fadhili zenye upendo ni zako, Ee Yehova,+

Kwa maana wewe mwenyewe humlipa kila mmoja kulingana na kazi yake.+

Muziki wa Daudi, alipokuwa katika nyika ya Yuda.+

63 Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+

Nafsi yangu ina kiu kwa ajili yako.+

Mwili wangu umezimia kwa kukutamani wewe.

Katika nchi iliyokauka na kuchoka, ambapo hakuna maji.+

 2 Hivyo nimekuona katika mahali patakatifu,+

Kwa kuona nguvu zako na utukufu wako.+

 3 Kwa sababu fadhili zako zenye upendo ni bora kuliko uzima,+

Midomo yangu mwenyewe itakusifu.+

 4 Kwa hiyo nitakusifu muda wote wa maisha yangu;+

Katika jina lako nitaiinua mikono yangu.+

 5 Nafsi yangu imeshiba sehemu bora, naam, mafuta,+

Na kwa midomo yenye vigelegele vya shangwe kinywa changu hutoa sifa.+

 6 Wakati ninapokukumbuka kitandani mwangu,+

Wakati wa makesha ya usiku natafakari juu yako.+

 7 Kwa maana umenisaidia,+

Na katika kivuli cha mabawa yako napiga vigelegele kwa shangwe.+

 8 Nafsi yangu imekufuata karibu-karibu;+

Mkono wako wa kuume unanishika sana.+

 9 Nao wale wanaoendelea kuitafuta nafsi yangu ili waiharibu,+

Wataingia katika sehemu za chini kabisa za dunia.+

10 Watatiwa katika nguvu za upanga;+

Watakuwa fungu la mbweha.+

11 Naye mfalme mwenyewe atashangilia katika Mungu.+

Kila anayeapa kwa jina lake atajisifu,+

Kwa maana kinywa cha wale wanaosema uwongo kitazibwa.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

64 Ee Mungu, uisikie sauti yangu katika hangaiko langu.+

Uulinde uhai wangu kutokana na hofu ya adui.+

 2 Unifiche mbali na mazungumzo ya siri ya watenda-maovu,+

Mbali na fujo ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza,+

 3 Ambao wamenoa ulimi wao kama upanga,+

Ambao wameulenga mshale wao, maneno machungu.+

 4 Ili wampige mtu asiye na lawama wakiwa mahali palipofichika.+

Wanampiga ghafula wala hawaogopi.+

 5 Wanashikilia maneno mabaya;+

Wanasema juu ya kuficha mitego.+

Wamesema: “Ni nani anayewaona?”+

 6 Wanaendelea kutafuta mambo yasiyo ya uadilifu;+

Wameficha mbinu ya werevu iliyofikiriwa sana,+

Na upande wa ndani wa kila mmoja, naam, moyo wake, una kina kirefu.+

 7 Lakini Mungu atawapiga ghafula kwa mshale.+

Wamepata majeraha,+

 8 Nao wanasababisha mtu ajikwae.+

Lakini ulimi wao huwapinga wao wenyewe.+

Wote wanaowatazama watatikisa kichwa chao,+

 9 Nao watu wote wa udongo wataogopa;+

Nao watatangaza utendaji wa Mungu.+

Nao hakika watakuwa na ufahamu katika kazi yake.+

10 Na mwadilifu atashangilia katika Yehova na kwa kweli atamkimbilia;+

Nao wote walio wanyoofu moyoni watajisifu.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo.

65 Kwa ajili yako kuna sifa—kimya—, Ee Mungu, katika Sayuni;+

Na kwako wewe nadhiri itatimizwa.+

 2 Ee msikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja.+

 3 Mambo yenye makosa yamekuwa na nguvu kuliko mimi.+

Nayo makosa yetu, wewe mwenyewe utayafunika.+

 4 Mwenye furaha ni yule unayemchagua na kumfanya akaribie,+

Ili apate kukaa katika nyua zako.+

Hakika tutashiba mema ya nyumba yako,+

Mahali patakatifu pa hekalu lako.+

 5 Utatujibu kwa mambo yenye kuogopesha katika uadilifu,+

Ee Mungu wa wokovu wetu,+

Tegemeo la mipaka yote ya dunia na wale walio mbali baharini.+

 6 Anaifanya imara milima kwa nguvu zake;+

Kwa kweli yeye amefungwa mshipi wa nguvu.+

 7 Anatuliza kelele za bahari,+

Kelele za mawimbi yake na ghasia za vikundi vya mataifa.+

 8 Na wakaaji wa sehemu za mbali zaidi wataogopa ishara zako;+

Unafanya kutokea kwa asubuhi na jioni kupige vigelegele kwa shangwe.+

 9 Umeielekezea dunia fikira zako, ili uipatie wingi;+

Unaitajirisha sana.

Kijito kinachotoka kwa Mungu kimejaa maji.+

Wewe unatayarisha nafaka yao,+

Kwa maana hivyo ndivyo unavyoitayarisha dunia.+

10 Mitaro yake inajazwa maji, madonge yake yanasawazishwa;+

Unailainisha kwa manyunyu mengi; unaibariki mimea yake.+

11 Umeuvika taji mwaka kwa wema wako,+

Nayo mapito yako yanadondoka mafuta.+

12 Viwanja vya malisho ya nyikani vinaendelea kudondoka mafuta,+

Navyo vilima vinajifunga shangwe kama mshipi.+

13 Malisho yamevikwa makundi,+

Na nchi tambarare za chini zimefunikwa na nafaka.+

Vitu hivyo vinapiga kelele za ushindi, naam, vinaimba.+

Kwa kiongozi. Wimbo, muziki.

66 Mpigieni Mungu kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+

 2 Upigieni muziki utukufu wa jina lake.+

Tukuzeni sifa yake.+

 3 Mwambieni Mungu: “Jinsi kazi zako zilivyo zenye kuogopesha!+

Kwa sababu ya wingi wa nguvu zako, adui zako watakujia wakitetemeka.+

 4 Watu wote wa dunia watakuinamia,+

Nao watakupigia muziki, watalipigia jina lako muziki.”+ Sela.

 5 Njooni mwone matendo ya Mungu.+

Kushughulika kwake na wana wa binadamu kunaogopesha.+

 6 Ameibadili bahari ikawa nchi kavu;+

Waliuvuka mto kwa miguu.+

Huko tukaanza kumshangilia.+

 7 Anatawala kwa nguvu zake mpaka wakati usio na kipimo.+

Macho yake mwenyewe yanaendelea kuyatazama mataifa.+

Nao wale ambao ni wakaidi, wasijiinue wenyewe.+ Sela.

 8 Mbarikini Mungu wetu, enyi vikundi vya watu,+

Na kuifanya sauti ya sifa kwake isikiwe.+

 9 Anaiweka nafsi yetu katika uhai,+

Wala hakuuruhusu mguu wetu utikisike.+

10 Kwa maana umetuchunguza, Ee Mungu;+

Umetusafisha kama kusafisha fedha.+

11 Umetuingiza katika wavu wa kuwindia;+

Umeweka mkazo juu ya viuno vyetu.

12 Umemfanya mwanadamu anayeweza kufa apande juu ya kichwa chetu;+

Tumepita katikati ya moto na katikati ya maji,+

Nawe ukatuleta kwenye kitulizo.+

13 Nitaingia nyumbani kwako nikiwa na matoleo mazima ya kuteketezwa;+

Nitakutimizia nadhiri zangu.+

14 Ambazo midomo yangu imefunguka ili iseme+

Na ambazo kinywa changu kimesema nilipokuwa katika dhiki kali.+

15 Nitakutolea matoleo mazima ya kuteketezwa ya vinono,+

Pamoja na moshi wa dhabihu wa kondoo-dume.

Nitatoa ng’ombe-dume pamoja na mbuzi-dume.+ Sela.

16 Njooni, sikilizeni, enyi nyote mnaomwogopa Mungu, nami nitasimulia+

Mambo ambayo ameitendea nafsi yangu.+

17 Nilimwitia kwa kinywa changu,+

Na ulimi wangu ukamtukuza.+

18 Ikiwa nimefikiria jambo lolote lenye kuumiza moyoni mwangu,

Yehova hatanisikia.+

19 Kwa kweli Mungu amesikia;+

Ameisikiliza sauti ya sala yangu.+

20 Mungu na abarikiwe, ambaye hakuigeuzia mbali sala yangu,

Wala fadhili zake zenye upendo mbali nami.+

Kwa kiongozi wa vinanda. Muziki, wimbo.

67 Mungu mwenyewe atatuonyesha kibali na kutubariki;+

Ataufanya uso wake utuangazie+—Sela—

 2 Ili njia yako ipate kujulikana duniani,+

Wokovu wako kati ya mataifa yote.+

 3 Vikundi vya watu na vikusifu, Ee Mungu;+

Vikundi vya watu, naam, vyote, na vikusifu.+

 4 Vikundi vya mataifa na vishangilie na kupiga vigelegele kwa shangwe,+

Kwa maana utavihukumu vikundi vya watu kwa unyoofu;+

Navyo vikundi vya mataifa, utaviongoza duniani. Sela.

 5 Vikundi vya watu na vikusifu, Ee Mungu;+

Vikundi vya watu, naam, vyote, na vikusifu.+

 6 Hakika dunia itatoa mazao yake;+

Mungu, Mungu wetu, atatubariki.+

 7 Mungu atatubariki,+

Na miisho yote ya dunia itamwogopa yeye.+

Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki, wimbo.

68 Mungu na asimame,+ adui zake na watawanyike,+

Na wale wanaomchukia vikali na wakimbie kwa sababu yake.+

 2 Kama vile moshi unavyofukuziwa mbali, na uwafukuzie mbali vivyo hivyo;+

Kama vile nta inavyoyeyuka kwa sababu ya moto,+

Waovu na waangamie vivyo hivyo kutoka mbele za Mungu.+

 3 Lakini waadilifu, na washangilie,+

Na wasisimuke mbele za Mungu,+

Na wafurahie kwa shangwe.+

 4 Mwimbieni Mungu, lipigieni jina lake muziki;+

Mwimbieni wimbo Yeye anayepanda akipitia nchi tambarare za jangwani+

Akiwa Yah, ambalo ndilo jina lake;+ na kushangilia mbele zake;

 5 Baba ya wavulana wasio na baba na mwamuzi wa wajane+

Ni Mungu katika makao yake matakatifu.+

 6 Mungu anawafanya wapweke wakae katika nyumba;+

Anawafanikisha kabisa wafungwa.+

Hata hivyo, walio wakaidi, lazima wakae katika nchi iliyokauka.+

 7 Ee Mungu, ulipoenda mbele ya watu wako,+

Ulipopiga mwendo jangwani+—Sela—

 8 Dunia ilitikisika,+

Nayo mbingu pia ikadondoka maji kwa sababu ya Mungu;+

Mlima huu Sinai ukatikisika kwa sababu ya Mungu,+ Mungu wa Israeli.+

 9 Ulisababisha mvua kubwa ianze kunyesha, Ee Mungu;+

Urithi wako, hata wakati ulipokuwa umechoka​—wewe mwenyewe uliupatia nguvu tena.+

10 Kambi yako ya mahema+​—wamekaa ndani yake;+

Kwa wema wako uliitayarisha kwa ajili ya mwenye kuteseka, Ee Mungu.+

11 Yehova mwenyewe anasema neno hili;+

Wanawake wanaotangaza habari njema ni jeshi kubwa.+

12 Hata wafalme wa majeshi wanakimbia, naam, wanakimbia.+

Lakini mwanamke anayekaa nyumbani, hugawa nyara.+

13 Ijapokuwa ninyi mliendelea kulala katikati ya marundo ya majivu ya kambi,

Kutakuwako mabawa ya njiwa yaliyofunikwa kwa fedha

Na manyoya yake yakiwa yamefunikwa kwa dhahabu ya kijani-manjano.+

14 Wakati Mweza-Yote alipowatawanya kotekote wafalme walio ndani yake,+

Theluji ilianza kuanguka Salmoni.+

15 Eneo lenye milima la Bashani+ ni mlima wa Mungu;+

Eneo lenye milima la Bashani ni mlima wenye vilele.+

16 Kwa nini ninyi, enyi milima yenye vilele, mnaendelea kutazama kwa wivu

Mlima ambao Mungu ametamani kukaa ndani yake?+

Naam, Yehova atakaa humo milele.+

17 Magari ya Mungu ya vita ni makumi ya maelfu, maelfu zaidi na zaidi.+

Yehova mwenyewe amekuja kutoka Sinai na kuingia mahali patakatifu.+

18 Umepanda juu;+

Umechukua mateka;+

Umechukua zawadi katika namna ya wanadamu,+

Naam, hata walio wakaidi,+ ili kukaa kati yao,+ Ee Yah Mungu.

19 Na abarikiwe Yehova, ambaye hutubebea mzigo wetu kila siku,+

Mungu wa kweli wa wokovu wetu.+ Sela.

20 Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu wa matendo ya kuokoa;+

Nazo njia za kutoka katika kifo+ ni za Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu.+

21 Kwa kweli Mungu mwenyewe atavunja vipande-vipande kichwa cha adui zake,+

Utosi wenye nywele wa mtu yeyote anayetembea katika hatia yake.+

22 Yehova amesema: “Kutoka Bashani nitarudisha,+

Nitawarudisha kutoka katika vilindi vya bahari,+

23 Ili upate kuosha mguu wako katika damu,+

Ili ulimi wa mbwa zako upate fungu lake kutoka katika adui.”+

24 Wameona maandamano yako, Ee Mungu,+

Maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, kuingia mahali patakatifu.+

25 Waimbaji walitangulia mbele, wapiga-vinanda wakawafuata;+

Katikati yao palikuwa na wanawali wakipiga matari.+

26 Katika makundi yaliyokutanika mbarikini Mungu,+

Yehova, enyi mnaotoka katika Chemchemi ya Israeli.+

27 Tazama Benyamini mdogo akiwatiisha,+

Wakuu wa Yuda pamoja na umati wao unaopaaza sauti,

Wakuu wa Zabuloni, wakuu wa Naftali.+

28 Mungu wako ameweka amri juu ya nguvu zako.+

Uonyeshe nguvu, Ee Mungu, wewe ambaye umechukua hatua kwa ajili yetu.+

29 Kwa sababu ya hekalu lako katika Yerusalemu,+

Wafalme watakuletea zawadi wewe mwenyewe.+

30 Umkemee mnyama-mwitu wa matete,+ kusanyiko la ng’ombe-dume,+

Na ndama za vikundi vya watu, kila mmoja akikanyaga-kanyaga vipande vya fedha.+

Ametawanya vikundi vya watu vinavyopenda mapigano.+

31 Vyombo vya shaba nyeusi vitatoka Misri;+

Kushi itanyoosha upesi mikono yake ikiwa na zawadi kwa Mungu.+

32 Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,+

Mpigieni Yehova muziki​—Sela—

33 Kwa Yule anayepanda mbingu ya mbingu za kale.+

Lo! Anavumisha sauti yake, sauti yenye nguvu.+

34 Mhesabieni Mungu nguvu.+

Adhama yake iko juu ya Israeli na nguvu zake ziko mawinguni.+

35 Mungu ni mwenye kuogopesha kutoka katika patakatifu pako pakuu.+

Ndiye Mungu wa Israeli, anayewapa watu nguvu na uwezo.+

Mungu na abarikiwe.+

Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi.+ Ya Daudi.

69 Uniokoe, Ee Mungu, kwa maana maji yamefika mpaka kwenye nafsi.+

 2 Nimezama katika matope mengi, mahali ambapo hapana udongo wa kusimama.+

Nimeingia katika maji mengi,

Na kijito kinachotiririka kimenifagilia mbali.+

 3 Nimechoka kwa sababu ya kuita kwangu;+

Koo yangu imekauka.

Macho yangu yameshindwa huku nikimngojea Mungu wangu.+

 4 Wale wanaonichukia bila sababu wamekuwa wengi hata kuliko nywele za kichwa changu.+

Wale wanaoninyamazisha, wakiwa ni adui zangu bila sababu, wamekuwa wengi.+

Kisha nikarudisha kile ambacho sikuwa nimechukua kwa unyang’anyi.

 5 Ee Mungu, wewe mwenyewe umeujua upumbavu wangu,

Nayo hatia yangu haikufichwa mbele zako.+

 6 Wale wanaokutumainia na wasione aibu kwa sababu yangu,+

Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.+

Wale wanaokutafuta na wasifedheheshwe kwa sababu yangu,+

Ee Mungu wa Israeli.+

 7 Kwa maana nimevumilia shutuma kwa sababu yako,+

Fedheha imeufunika uso wangu.+

 8 Nimetengwa na ndugu zangu,+

Na kuwa mgeni kwa wana wa mama yangu.+

 9 Kwa maana bidii nyingi kwa ajili ya nyumba yako imenila,+

Na shutuma za wale wanaokushutumu zimeniangukia.+

10 Nami nikalia kwa kufunga kwa nafsi yangu,+

Lakini ikawa shutuma kwangu.+

11 Nilipofanya magunia kuwa mavazi yangu,

Ndipo nikawa neno la kimethali kwao.+

12 Wale wanaoketi kwenye lango wakaanza kujishughulisha nami,+

Nikawa kiini cha nyimbo za watu wanaokunywa kileo.+

13 Lakini mimi, nilikutolea sala, Ee Yehova,+

Wakati unaofaa, Ee Mungu.+

Katika wingi wa fadhili zako zenye upendo unijibu kwa kweli ya wokovu wako.+

14 Unikomboe kutoka katika matope, ili nisizame.+

Na nikombolewe kutoka kwa wale wanaonichukia+ na kutoka katika kilindi cha maji.+

15 Kijito cha maji yanayotiririka kisinifagilie mbali,+

Wala kilindi kisinimeze,

Wala kisima kisifunge kinywa chake juu yangu.+

16 Unijibu, Ee Yehova, kwa maana fadhili zako zenye upendo ni njema.+

Kulingana na wingi wa rehema zako ugeuke kunielekea,+

17 Wala usimfiche mtumishi wako uso wako.+

Kwa sababu niko katika dhiki kali, unijibu upesi.+

18 Njoo karibu na nafsi yangu, uiokoe;+

Kwa sababu ya adui zangu, unikomboe.+

19 Wewe mwenyewe umejua shutuma yangu na aibu yangu na fedheha yangu.+

Wote wanaonionyesha uadui wako mbele zako.+

20 Shutuma imeuvunja moyo wangu, nalo jeraha haliwezi kuponywa.+

Nami niliendelea kutumainia mtu fulani aonyeshe kusikitika, lakini hapakuwa na yeyote;+

Na watu wa kufariji, lakini sikupata yeyote.+

21 Lakini walinipa mmea wenye sumu kuwa chakula,+

Na kwa ajili ya kiu yangu wakajaribu kuninywesha siki.+

22 Meza yao iliyo mbele yao na iwe mtego,+

Na vitu vilivyo kwa ajili ya hali njema yao na viwe mnaso.+

23 Macho yao na yatiwe giza ili yasione;+

Na ufanye viuno vyao viyumbe-yumbe daima.+

24 Umwage juu yao shutuma yako,+

Na hasira yako inayowaka iwapate.+

25 Kambi yao iliyozungushiwa ukuta na iwe ukiwa;+

Na kusiwe na mkaaji katika mahema yao.+

26 Kwa maana yule ambaye wewe mwenyewe umempiga, wamemfuatilia,+

Nao wanaendelea kusimulia maumivu ya wale ambao wewe uliwachoma.

27 Wape kosa juu ya kosa lao,+

Wala wasiingie katika uadilifu wako.+

28 Na wafutwe kutoka katika kitabu cha walio hai,+

Wala wasiandikwe pamoja na waadilifu.+

29 Lakini mimi ninateseka na nina maumivu.+

Wokovu wako mwenyewe, Ee Mungu, na unilinde.+

30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo,+

Nami nitamtukuza kwa kutoa shukrani.+

31 Hilo pia litampendeza Yehova kuliko ng’ombe-dume,+

Kuliko ng’ombe-dume mchanga mwenye pembe, mwenye kwato zilizogawanyika.+

32 Hakika wapole wataliona hilo; watashangilia.+

Ninyi mnaomtafuta Mungu, moyo wenu na uendelee kuwa hai.+

33 Kwa maana Yehova anawasikiliza maskini,+

Wala kwa kweli hatawadharau wafungwa wake mwenyewe.+

34 Mbingu na dunia na zimsifu,+

Bahari na vyote vinavyotembea ndani yake.+

35 Kwa maana Mungu mwenyewe ataokoa Sayuni+

Naye atayajenga majiji ya Yuda;+

Nao hakika watakaa humo na kuimiliki.+

36 Na uzao wa watumishi wake wataurithi,+

Na wale wanaolipenda jina lake ndio watakaokaa humo.+

Kwa kiongozi. Ya Daudi, ili kukumbusha.+

70 Ee Mungu, katika kunikomboa,+

Ee Yehova, ufanye haraka kuja kunisaidia.+

 2 Wale wanaoitafuta nafsi yangu na waone aibu na kufedheheka.+

Wale wanaofurahia msiba wangu na wageuke na kufedheheshwa.+

 3 Na warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao wale wanaosema: “Aha, aha!”+

 4 Wote wanaokutafuta na wafurahi na kushangilia katika wewe,+

Nao waseme daima: “Mungu atukuzwe!”—wale wanaoupenda wokovu wako.+

 5 Lakini mimi ninateseka nami ni maskini.+

Ee Mungu, uchukue hatua haraka kwa ajili yangu.+

Wewe ndiye msaada wangu na Mwokoaji wangu.+

Ee Yehova, usichelewe mno.+

71 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.+

Nisiaibike kamwe.+

 2 Unikomboe kwa uadilifu wako na kuniokoa.+

Tega sikio lako kwangu na uniokoe.+

 3 Uwe kwangu ngome ya mwamba ya kuingia ndani daima.+

Utoe amri ili kuniokoa,+

Kwa maana wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.+

 4 Ee Mungu wangu, uniokoe na mkono wa mwovu,+

Na mkono wa mtu anayetenda kwa njia isiyo ya haki na kwa ukandamizaji.+

 5 Kwa maana wewe ni tumaini langu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova, tegemeo langu tangu ujana wangu.+

 6 Nimekutegemea tangu tumboni;+

Wewe ndiye Yule anayenitenganisha na sehemu za ndani za mama yangu.+

Sifa yangu kwako ni ya daima.+

 7 Nimekuwa kama muujiza kwa watu wengi;+

Lakini wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.+

 8 Kinywa changu kimejawa na sifa zako,+

Mchana kutwa na uzuri wako.+

 9 Usinitupe wakati wa uzee;+

Wakati tu nguvu zangu zinapungua, usiniache.+

10 Kwa maana adui zangu wamesema juu yangu,+

Na walewale wanaoitafuta nafsi yangu wameshauriana pamoja,+

11 Wakisema: “Mungu mwenyewe amemwacha.+

Mfuatilieni na kumkamata, kwa maana hakuna mkombozi.”+

12 Ee Mungu, usikae mbali nami.+

Ee Mungu wangu, ufanye haraka kunisaidia.+

13 Hao na waaibike, hao na wafikie mwisho wao, wanaoshindana na nafsi yangu.+

Hao na wajifunike kwa shutuma na fedheha wanaonitafutia msiba.+

14 Lakini mimi, nitangoja daima,+

Nami nitaongezea sifa zako zote.

15 Kinywa changu mwenyewe kitasimulia uadilifu wako,+

Wokovu wako mchana kutwa,+

Kwa maana sijapata kujua hesabu yake.+

16 Nitaingia na nguvu kuu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu+ Yehova;

Nitautangaza uadilifu wako, naam, wako peke yako.+

17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,+

Na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu.+

18 Na mpaka wakati wa uzee na wa kuwa na kichwa chenye mvi, Ee Mungu, usiniache,+

Mpaka nikitangazie kizazi habari za mkono wako,+

Habari za nguvu zako, kwa wale wote watakaokuja.+

19 Uadilifu wako, Ee Mungu, unafika kileleni;+

Na kuhusu mambo makuu ambayo umeyafanya,+

Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?+

20 Kwa sababu umenifanya nione taabu nyingi na misiba,+

Unifufue tena;+

Na unipandishe tena kutoka katika vilindi vya maji vya dunia.+

21 Na uuongeze ukuu wangu,+

Na unizingire na kunifariji.+

22 Mimi pia, nitakusifu kwa chombo cha kinanda,+

Kuhusu ukweli wako, Ee Mungu wangu.+

Nitakupigia muziki kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli.+

23 Midomo yangu itapiga vigelegele kwa shangwe wakati wowote ninapokupigia muziki,+

Naam, nafsi yangu, ambayo umeikomboa.+

24 Pia, ulimi wangu mwenyewe, mchana kutwa, utasema juu ya uadilifu wako kwa sauti ya chini,+

Kwa maana wameaibika, kwa maana wamefedheheka, wale wanaonitafutia msiba.+

Kuhusu Sulemani.

72 Ee Mungu, umpe mfalme maamuzi yako ya hukumu,+

Na uadilifu wako mwana wa mfalme.+

 2 Na atetee kesi ya watu wako kwa uadilifu+

Na ya watu wako wenye kuteseka kwa hukumu.+

 3 Milima na iwapelekee watu amani,+

Na vilima pia, kwa uadilifu.

 4 Na ahukumu wenye kuteseka katikati ya watu,+

Na awaokoe wana wa maskini,

Na amponde mpunjaji.

 5 Watakuogopa maadamu jua lipo,+

Na mbele ya mwezi kwa kizazi baada ya kizazi.+

 6 Atashuka kama mvua juu ya majani yaliyofyekwa,+

Kama manyunyu mengi yanayolowesha dunia.+

 7 Katika siku zake aliye mwadilifu atachipuka,+

Na wingi wa amani mpaka mwezi utakapokuwa haupo tena.+

 8 Naye atakuwa na raia kutoka bahari mpaka bahari+

Na kutoka ule Mto+ mpaka miisho ya dunia.+

 9 Wakaaji wa maeneo yasiyo na maji watainama mbele yake,+

Na adui zake watayaramba mavumbi.+

10 Wafalme wa Tarshishi na wa visiwa+—

Watalipa ushuru.+

Wafalme wa Sheba na wa Seba—

Watatoa zawadi.+

11 Na wafalme wote watamsujudia;+

Nayo mataifa yote yatamtumikia.+

12 Kwa maana atamkomboa maskini anayelilia msaada,+

Pia mwenye kuteseka na yeyote ambaye hana msaidizi.+

13 Atamsikitikia mtu wa hali ya chini na maskini,+

Naye ataziokoa nafsi za maskini.+

14 Ataikomboa nafsi yao kutoka katika ukandamizaji na katika jeuri,

Nayo damu yao itakuwa na thamani machoni pake.+

15 Yeye na aishi,+ na apewe sehemu ya dhahabu ya Sheba.+

Na kwa ajili yake sala na itolewe daima;

Na abarikiwe mchana kutwa.+

16 Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani;+

Juu ya milima kutakuwa na mafuriko.+

Uzao wake utakuwa kama katika Lebanoni,+

Na wale wa kutoka katika jiji watachanuka kama majani ya dunia.+

17 Jina lake na liweko mpaka wakati usio na kipimo;+

Jina lake na liongezeke mbele ya jua,

Na kupitia yeye na wajibariki;+

Mataifa yote na yamtangaze kuwa mwenye furaha.+

18 Na abarikiwe Yehova Mungu, Mungu wa Israeli,+

Ambaye peke yake anafanya kazi za ajabu.+

19 Na jina lake tukufu na libarikiwe mpaka wakati usio na kipimo,+

Nao utukufu wake na uijaze dunia yote.+

Amina na Amina.

20 Sala za Daudi, mwana wa Yese,+ zimefikia mwisho wake.

KITABU CHA TATU

(Zaburi 73 – 89)

Muziki wa Asafu.+

73 Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio safi moyoni.+

 2 Mimi nami karibu miguu yangu igeuke kando,+

Hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza.+

 3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujisifu,+

Nilipokuwa nikiiona amani ya watu waovu.+

 4 Kwa maana hawana maumivu ya kifo;+

Na kitambi chao ni kinono.+

 5 Wala hawamo katika taabu ya mwanadamu anayeweza kufa,+

Wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.+

 6 Kwa hiyo majivuno yamekuwa mkufu shingoni pao;+

Jeuri huwafunika kama vazi.+

 7 Jicho lao limevimba kwa sababu ya unono;+

Wamezidi mawazo ya moyo.+

 8 Wao hudhihaki na kuzungumza juu ya yaliyo mabaya;+

Wanazungumza juu ya upunjaji kwa majivuno.+

 9 Wameweka kinywa chao mbinguni,+

Nao ulimi wao hutembea huku na huku duniani.+

10 Kwa hiyo yeye huwarudisha watu wake hapa,

Na maji yaliyojaa yanakaushwa kwa ajili yao.

11 Nao wamesema: “Mungu amepataje kujua?+

Na je, Aliye Juu Zaidi ana ujuzi?”+

12 Tazama! Hao ndio waovu waliostarehe mpaka wakati usio na kipimo.+

Wameongeza mali yao.+

13 Hakika nimeusafisha moyo wangu bure+

Na kuiosha mikono yangu katika kutokuwa na hatia.+

14 Nami nikapata mapigo mchana kutwa,+

Na rekebisho langu ni la kila asubuhi.+

15 Kama ningelisema: “Nitasimulia hadithi kama hiyo,”

Tazama! juu ya kizazi cha wana wako

Ningelitenda kwa hila.+

16 Nami nikaendelea kufikiria ili nijue hilo;+

Lilikuwa ni taabu machoni pangu.

17 Mpaka nilipoingia katika patakatifu pakuu pa Mungu.+

Nilitaka kuutambua wakati wao ujao.+

18 Hakika unawaweka kwenye udongo unaoteleza.+

Umewafanya waanguke kwenye uharibifu.+

19 Lo! Jinsi wamekuwa kitu cha kushangaza ghafula!+

Jinsi wameufikia mwisho wao, wamemalizwa kwa matisho ya ghafula!

20 Kama ndoto baada ya kuamka, Ee Yehova,+

Ndivyo utakavyoidharau sura yao utakapoamka.+

21 Kwa maana moyo wangu ulikuwa umetiwa uchungu+

Nami nilikuwa na maumivu makali kwenye figo zangu.+

22 Nami sikutumia akili wala singeweza kujua;+

Nilikuwa kama wanyama tu kwa maoni yako.+

23 Lakini niko pamoja nawe daima;+

Umeushika mkono wangu wa kuume.+

24 Utaniongoza kwa shauri lako,+

Na baadaye utanipeleka kwenye utukufu.+

25 Ni nani niliye naye mbinguni?+

Na isipokuwa wewe sina mapendezi mengine duniani.+

26 Mwili wangu na moyo wangu vimeshindwa.+

Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu mpaka wakati usio na kipimo.+

27 Kwa maana, tazama! Walewale wanaokaa mbali nawe wataangamia.+

Hakika utamnyamazisha kila mtu ambaye kwa njia isiyo ya adili anakuacha.+

28 Lakini mimi, kumkaribia Mungu ni kwema kwangu.+

Nimeweka kimbilio langu katika Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova,+

Ili kutangaza kazi zako zote.+

Maskili. Ya Asafu.+

74 Kwa nini, Ee Mungu, umetutupilia mbali milele?+

Kwa nini hasira yako inatoa moshi daima juu ya kundi la malisho yako?+

 2 Ulikumbuke kusanyiko lako ulilojipatia zamani za kale,+

Kabila ulilolikomboa liwe urithi wako,+

Huu Mlima Sayuni ambapo umekaa.+

 3 Uziinue hatua zako kwenye ukiwa wenye kudumu muda mrefu.+

Kila kitu katika mahali patakatifu adui amekitendea vibaya.+

 4 Wale wanaokuonyesha uadui wamenguruma katikati ya mahali pa kukutania.+

Wameweka ishara zao wenyewe kuwa ndizo ishara.+

 5 Mtu ana sifa mbaya ya kuwa kama yule anayeinua mashoka juu ya kichaka cha miti.

 6 Na sasa vitu vyake vilivyochongwa, kila kimoja, wao wanakipiga hata kwa kishoka na kwa mipini yenye ncha za chuma.+

 7 Wamepatupa ndani ya moto patakatifu pako.+

Wametia unajisi maskani ya jina lako mpaka chini.+

 8 Wao, hata uzao wao, wamesema pamoja moyoni mwao:

“Mahali pote pa kukutania pa Mungu katika nchi lazima pateketezwe.”+

 9 Hatujaona ishara zetu; hakuna nabii tena,+

Wala hakuna yeyote kwetu anayejua ni kwa muda gani.

10 Ee Mungu, mpinzani ataendelea kushutumu mpaka wakati gani?+

Je, adui ataendelea kulidharau jina lako milele?+

11 Kwa nini unaendelea kuuondoa mkono wako, naam, mkono wako wa kuume+

Kutoka katikati ya kifua chako ili kutumaliza sisi?

12 Hata hivyo Mungu ni Mfalme wangu tangu zamani za kale,+

Yeye anayefanya wokovu mkuu katikati ya dunia.+

13 Wewe mwenyewe uliichochea bahari kwa nguvu zako mwenyewe;+

Ulivunja vichwa vya wanyama wakubwa wa baharini katika maji.+

14 Wewe mwenyewe uliponda vipande-vipande vichwa vya Lewiathani.*+

Ukawapa watu kuwa chakula, wale wanaokaa katika maeneo yasiyo na maji.+

15 Wewe ndiye Yule aliyepasua bubujiko na mto;+

Wewe mwenyewe uliikausha mito inayotiririka daima.+

16 Mchana ni wako; pia, usiku ni wako.+

Wewe mwenyewe uliutayarisha mwanga, naam, jua.+

17 Ni wewe uliyeweka mipaka yote ya dunia;+

Majira ya kiangazi na majira ya baridi kali—wewe mwenyewe uliyafanyiza.+

18 Ukumbuke hili: Adui ameshutumu, Ee Yehova,+

Na kikundi cha watu wasio na akili kimelidharau jina lako.+

19 Usimpe mnyama-mwitu nafsi ya njiwa-tetere wako.+

Usiusahau milele uhai wa watu wako wanaoteseka.+

20 Ulitazame agano,+

Kwa maana sehemu za dunia zenye giza zimejaa makao ya jeuri.+

21 Mtu aliyepondwa na asirudi akiwa amefedheheshwa.+

Mwenye kuteseka na maskini na walisifu jina lako.+

22 Usimame, Ee Mungu, uendeshe kesi yako.+

Uikumbuke shutuma yako mchana kutwa kutoka kwa mtu asiye na akili.+

23 Usiisahau sauti ya wale wanaokuonyesha

uadui.+

Kelele za wale wanaosimama dhidi yako zinapaa daima.+

Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Muziki. Wa Asafu.+ Wimbo.

75 Tunakutolea shukrani, Ee Mungu; tunakutolea shukrani,+

Nalo jina lako liko karibu.+

Lazima watu wazitangaze kazi zako za ajabu.+

 2 “Kwa maana niliuchukua wakati uliowekwa;+

Mimi nikaanza kuhukumu kwa unyoofu.+

 3 Dunia na wakaaji wake wote wakiyeyuka,+

Ni mimi niliyezirekebisha nguzo zake.”+ Sela.

 4 Niliwaambia wapumbavu: “Msiwe wapumbavu,”+

Na waovu: “Msiinue pembe.+

 5 Msiinue pembe yenu juu.

Msiseme mkiwa na shingo yenye kiburi.+

 6 Kwa maana wala kutoka mashariki wala kutoka magharibi,

Wala kutoka kusini hakutoki kuinuliwa.

 7 Kwa maana Mungu ndiye mwamuzi.+

Humshusha huyu, na kumwinua yule.+

 8 Kwa maana kuna kikombe mkononi mwa Yehova,+

Kimejaa mchanganyiko, nayo divai inatoa povu.

Na hakika kutoka hicho yeye atayamwaga machicha yake;

Waovu wote wa dunia watayakamua, na kunywa.”+

 9 Lakini mimi, nitaeleza juu ya hayo mpaka wakati usio na kipimo;

Nitampigia muziki Mungu wa Yakobo.+

10 “Na pembe zote za waovu nitazikata.”+

Pembe za mwadilifu zitainuliwa.+

Kwa kiongozi wa vinanda. Muziki. Wa Asafu.+ Wimbo.

76 Mungu anajulikana katika Yuda;+

Katika Israeli jina lake ni kuu.+

 2 Na maficho yake yako katika Salemu,+

Na makao yake katika Sayuni.+

 3 Huko alivunja mishale ya upinde inayowaka,+

Ngao na upanga na vita.+ Sela.

 4 Umefunikwa na nuru, una utukufu kuliko milima ya mawindo.+

 5 Wenye nguvu moyoni wameporwa,+

Wamesinzia na kulala usingizi,+

Wala hakuna hata mmoja wa wanaume mashujaa ambaye ameiona mikono yake.+

 6 Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo, mwendesha-gari na farasi pia wamelala usingizi mzito.+

 7 Wewe—ni mwenye kuogopesha,+

Na ni nani anayeweza kusimama mbele zako kwa sababu ya nguvu za hasira yako?+

 8 Kutoka mbinguni ulifanya kesi isikiwe;+

Dunia iliogopa na kukaa kimya+

 9 Mungu aliposimama kwenye hukumu,+

Ili kuokoa wapole wote wa dunia.+ Sela.

10 Kwa maana ghadhabu ya mwanadamu itakusifu;+

Utajifunga ghadhabu iliyobaki.

11 Wekeni nadhiri na kumtimizia Yehova Mungu wenu, ninyi nyote mnaomzunguka pande zote.+

Na walete zawadi kwa kuogopa.+

12 Atainyenyekeza roho ya viongozi;+

Yeye ni mwenye kuogopesha kwa wafalme wa dunia.+

Kwa kiongozi juu ya Yeduthuni. Ya Asafu.+ Muziki.

77 Kwa sauti yangu nitamlilia Mungu mwenyewe,+

Kwa sauti yangu kwa Mungu, naye hakika atanisikiliza.+

 2 Katika siku ya taabu yangu nimemtafuta Yehova mwenyewe.+

Usiku, mkono wangu umenyooshwa wala haufi ganzi;

Nafsi yangu imekataa kufarijiwa.+

 3 Nitamkumbuka Mungu na kuwa na msukosuko;+

Nitaonyesha hangaiko, ili roho yangu izimie.+ Sela.

 4 Umezishika kope za macho yangu;+

Nimefadhaika, nami siwezi kusema.+

 5 Nimezifikiria siku za zamani za kale,+

Miaka ya wakati uliopita usio na kipimo.

 6 Nitakumbuka muziki wangu wa kinanda wakati wa usiku;+

Nitaonyesha hangaiko moyoni,+

Na roho yangu itatafuta kwa uangalifu.

 7 Je, Yehova ataendelea kutupa mpaka nyakati zisizo na kipimo,+

Na je, hatapendezwa tena kamwe?+

 8 Je, fadhili zake zenye upendo zimekoma milele?+

Je, neno lake limekuwa bure+ kwa kizazi baada ya kizazi?

 9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye kuonyesha kibali,+

Au je, amezifungia rehema zake kwa hasira?+ Sela.

10 Na je, nitaendelea kusema: “Hili ndilo linalonichoma,+

Kubadilika kwa mkono wa kuume wa Aliye Juu Zaidi”?+

11 Nitavikumbuka vitendo vya Yah;+

Kwa maana nitayakumbuka matendo yako ya ajabu ya zamani za kale.+

12 Nami hakika nitautafakari utendaji wako wote,+

Nami nitajishughulisha mwenyewe na matendo yako.+

13 Ee Mungu, njia yako iko katika mahali patakatifu.+

Ni nani aliye Mungu mkuu kama Mungu?+

14 Wewe ndiye Mungu wa kweli, unayefanya kwa njia ya ajabu.+

Umezijulisha nguvu zako katikati ya vikundi vya watu.+

15 Umewakomboa watu wako kwa mkono wako,+

Wana wa Yakobo na wa Yosefu. Sela.

16 Maji yamekuona wewe, Ee Mungu,

Maji yamekuona wewe; yakaanza kuwa na maumivu makali.+

Pia, vilindi vya maji vikaanza kutetemeka.+

17 Mawingu yamemwaga maji kwa kunguruma;+

Anga lenye kutanda mawingu limetoa sauti.

Pia, mishale yako mwenyewe ilienda huku na huku.+

18 Sauti ya mngurumo wako ilikuwa kama magurudumu ya gari;+

Umeme umetia nuru nchi yenye kuzaa;+

Dunia ikatetemeka na kuanza kutikisika.+

19 Njia yako ilikuwa baharini,+

Nalo pito lako lilikuwa katika maji mengi;

Nazo nyayo zako hazikupata kujulikana.

20 Umewaongoza watu wako kama kundi,+

Kwa mkono wa Musa na Haruni.+

Maskili. Ya Asafu.+

78 Sikilizeni sheria yangu, enyi watu wangu;+

Tegeni sikio lenu kwa maneno ya kinywa changu.+

 2 Katika neno la kimethali nitakifungua kinywa changu;+

Nitafanya vitendawili vya zamani za kale vibubujike,+

 3 Ambavyo tumevisikia na tunavijua,+

Na ambavyo baba zetu wenyewe wametusimulia;+

 4 Ambavyo hatuwafichi wana wao,+

Tukivisimulia hata kwa kizazi kitakachokuja,+

Sifa za Yehova na nguvu zake+

Na mambo yake ya ajabu ambayo amefanya.+

 5 Naye akatokeza kikumbusho katika Yakobo,+

Na sheria akaiweka katika Israeli,+

Mambo ambayo aliwaamuru mababu zetu,+

Wawajulishe wana wao;+

 6 Ili kizazi kitakachokuja, wana ambao wangezaliwa, wapate kuyajua,+

Ili wasimame na kuwasimulia wana wao,+

 7 Na kwamba wao watie uhakika wao katika Mungu+

Nao wasisahau matendo ya Mungu+ bali washike amri zake.+

 8 Nao wasiwe kama mababu zao,+

Kizazi chenye ukaidi na chenye kuasi,+

Kizazi ambacho hakikuwa kimetayarisha moyo wake+

Na ambacho roho yake haikuwa yenye kutegemeka kwa Mungu.+

 9 Wana wa Efraimu, wajapokuwa ni wapiga-upinde wenye silaha,+

Walirudi nyuma siku ya pigano.+

10 Hawakulishika agano la Mungu,+

Nao wakakataa kutembea katika sheria yake.+

11 Pia wakaanza kusahau matendo yake+

Na kazi zake za ajabu alizowafanya waone.+

12 Mbele ya mababu zao yeye alikuwa ametenda kwa njia ya ajabu.+

Katika nchi ya Misri,+ kiwanja cha Soani.+

13 Aliipasua bahari, ili awaruhusu kuvuka,+

Naye akayafanya maji yasimame kama bwawa.+

14 Naye akaendelea kuwaongoza kwa wingu wakati wa mchana+

Na usiku kucha kwa nuru ya moto.+

15 Aliipasua miamba nyikani,+

Ili awanyweshe kwa wingi kama vilindi vya maji.+

16 Naye akatokeza vijito katika mwamba+

Na kufanya maji yateremke kama mito.+

17 Nao wakaendelea kumtendea dhambi hata zaidi+

Kwa kumwasi Aliye Juu Zaidi katika eneo lisilo na maji;+

18 Nao wakamjaribu Mungu moyoni mwao+

Kwa kuomba chakula kwa ajili ya nafsi yao.+

19 Basi wakaanza kusema vibaya juu ya Mungu.+

Walisema: “Je, Mungu anaweza kutayarisha meza nyikani?”+

20 Tazama! Alipiga mwamba+

Ili maji yatiririke na mito ifurike.+

“Je, anaweza pia kutoa mkate,+

Au je, anaweza kuwatayarishia watu wake chakula?”+

21 Ndiyo sababu Yehova alisikia, akaanza kuwa na ghadhabu;+

Na moto ukawashwa juu ya Yakobo,+

Na hasira pia ikapanda juu ya Israeli.+

22 Kwa maana hawakuwa na imani katika Mungu,+

Wala hawakutegemea wokovu wake.+

23 Naye akaamuru anga lenye mawingu lililo juu,

Naye akaifungua milango ya mbingu.+

24 Naye akaendelea kuwanyeshea mana ili wale,+

Naye akawapa nafaka ya mbinguni.+

25 Wanadamu walikula mkate wa wenye nguvu;+

Aliwapa vyakula mpaka wakashiba.+

26 Akaanza kufanya upepo wa mashariki uvume mbinguni+

Na kufanya upepo wa kusini uvume kwa nguvu zake.+

27 Naye akawanyeshea chakula kama mavumbi,+

Hata viumbe vinavyoruka vyenye mabawa kama chembe za mchanga wa bahari.+

28 Naye akaendelea kuviangusha katikati ya kambi yake,+

Pande zote za maskani zake.+

29 Nao wakala na kujishibisha sana,+

Naye akawaletea walichotamani.+

30 Hawakuwa wameacha tamaa yao,

Chakula chao kilipokuwa kingali kinywani mwao,+

31 Ndipo ghadhabu ya Mungu ilipopanda juu yao.+

Naye akafanya mauaji kati ya wenye nguvu wao;+

Na vijana wa Israeli akawaangusha.

32 Ijapokuwa hayo yote walifanya dhambi zaidi+

Wala hawakuwa na imani katika kazi zake za ajabu.+

33 Kwa hiyo akakomesha siku zao kana kwamba ni pumzi tu,+

Na miaka yao kwa usumbufu.

34 Kadiri alivyowaua ndivyo pia walivyouliza habari zake,+

Nao wakarudi na kumtafuta Mungu.+

35 Nao wakaanza kukumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao,+

Na kwamba Mungu Aliye Juu Zaidi alikuwa Mlipiza-Kisasi wao.+

36 Nao wakajaribu kumpumbaza kwa kinywa chao;+

Na kwa ulimi wao wakajaribu kumwambia uwongo.+

37 Na moyo wao haukuwa imara kwake;+

Nao hawakuwa waaminifu katika agano lake.+

38 Lakini alikuwa mwenye rehema;+ akawa akilifunika kosa+ wala hakuharibu.+

Na mara nyingi akageuzia mbali hasira yake,+

Naye akawa haiamshi ghadhabu yake yote.

39 Naye akaendelea kukumbuka kwamba wao ni wenye mwili wa nyama,+

Kwamba roho inaenda wala hairudi.+

40 Jinsi walivyomwasi mara nyingi nyikani,+

Wakamhuzunisha jangwani!+

41 Nao wakawa wakimjaribu Mungu tena na tena,+

Nao wakamtia uchungu Mtakatifu wa Israeli.+

42 Hawakuukumbuka mkono wake,+

Ile siku ambayo aliwakomboa kutoka kwa mpinzani,+

43 Jinsi alivyoweka ishara zake katika Misri+

Na miujiza yake katika uwanja wa Soani;+

44 Na jinsi alivyoanza kubadili mifereji ya Nile iwe damu,+

Hivi kwamba hawakuweza kunywa kutoka katika vijito vyao wenyewe.+

45 Naye akaanza kuwatumia mainzi, ili yapate kuwala;+

Na vyura, ili wapate kuwaharibu.+

46 Naye akaanza kuwapa mende mazao yao,

Na kazi yao ngumu akawapa nzige.+

47 Akauua mzabibu wao kwa mvua ya mawe+

Na mikuyu yao kwa mawe ya mvua.+

48 Naye akawaacha wanyama wao wa kubeba mizigo wapigwe kwa mvua ya mawe+

Na mifugo yao kwa homa kali.

49 Akapeleka juu yao hasira yake inayowaka,+

Ghadhabu na shutuma na taabu,+

Wajumbe wa malaika wanaoleta msiba.+

50 Akatayarisha njia kwa ajili ya hasira yake.+

Hakuzuia nafsi zao zisipatwe na kifo;

Nayo maisha yao akayatia kwenye tauni.+

51 Mwishowe akawapiga na kuwaua wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+

Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu.+

52 Baadaye akawafanya watu wake waondoke kama kondoo,+

Na kuwaongoza kama kundi nyikani.+

53 Naye akaendelea kuwaongoza kwa usalama, wala hawakuhofu kamwe;+

Nayo bahari ikawafunika adui zao.+

54 Naye akawaleta katika eneo lake takatifu,+

Eneo hili lenye milima ambalo mkono wake wa kuume ulijipatia.+

55 Naye akayafukuza mataifa kwa sababu yao,+

Na kuwagawia urithi kwa kamba ya kupimia,+

Hivi kwamba akayafanya makabila ya Israeli yakae nyumbani kwao wenyewe.+

56 Nao wakaanza kumjaribu na kumwasi Mungu Aliye Juu Zaidi.+

Wala hawakushika vikumbusho vyake.+

57 Pia wakaendelea kugeuka na kutenda kwa hila kama mababu zao;+

Waligeuka huku na huku kama upinde uliolegea.+

58 Nao wakaendelea kumtia uchungu kwa mahali pao pa juu,+

Nao wakaendelea kumchochea awe na wivu kwa sanamu zao za kuchongwa.+

59 Mungu akasikia,+ akawa na ghadhabu,+

Na kwa hiyo akachukia sana Israeli.+

60 Naye mwishowe akaiacha maskani ya Shilo,+

Lile hema ambalo alikaa ndani yake katikati ya watu wa udongo.+

61 Naye akatia nguvu zake utekwani+

Na uzuri wake mkononi mwa mpinzani.+

62 Naye akaendelea kuwatia watu wake kwenye upanga,+

Naye akawa na ghadhabu juu ya urithi wake.+

63 Moto ukawateketeza wanaume wake vijana,

Na mabikira wake hawakusifiwa.+

64 Nao makuhani wake, wakaangushwa kwa upanga,+

Na wajane wao hawakulia.+

65 Kisha Yehova akaanza kuamka kana kwamba kutoka katika usingizi,+

Kama mtu mwenye nguvu akitokwa na ulevi wa divai.+

66 Naye akaanza kuwapiga adui zake kutoka nyuma;+

Akawapa shutuma inayodumu mpaka wakati usio na kipimo.+

67 Naye akakataa hema la Yosefu;+

Na kabila la Efraimu hakulichagua.+

68 Bali alichagua kabila la Yuda,+

Mlima Sayuni, ambao aliupenda.+

69 Naye akaanza kujenga patakatifu pake kama vilele,+

Kama dunia ambayo ameiwekea msingi mpaka wakati usio na kipimo.+

70 Na kwa hiyo akamchagua Daudi mtumishi wake+

Naye akamtoa katika mazizi ya kundi.+

71 Aache kuwafuata wale wa kike wanaonyonyesha+

Akamleta awe mchungaji juu ya Yakobo watu wake+

Na juu ya Israeli, urithi wake.+

72 Naye akaanza kuwachunga kulingana na utimilifu wa moyo wake,+

Naye akaanza kuwaongoza kwa ustadi wa mikono yake.+

Muziki wa Asafu.

79 Ee Mungu, mataifa yameingia katika urithi wako;+

Wamelitia unajisi hekalu lako takatifu;+

Wamefanya Yerusalemu kuwa rundo la mabomoko.+

 2 Wamewapa ndege wa mbinguni maiti ya watumishi wako iwe chakula chao,+

Na nyama ya washikamanifu wako kwa wanyama-mwitu wa dunia.+

 3 Wamemwaga damu yao kama maji

Kuzunguka Yerusalemu pande zote, wala hakuna mtu wa kuzika.+

 4 Tumekuwa shutuma kwa jirani zetu,+

Dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka pande zote.+

 5 Ee Yehova, utapandwa na hasira mpaka wakati gani? Milele?+

Hasira yako itawaka kama moto mpaka wakati gani?+

 6 Mwaga ghadhabu yako juu ya mataifa ambayo hayakukujua,+

Na juu ya falme ambazo hazikuliitia jina lako.+

 7 Kwa maana wamemla Yakobo,+

Nao wamefanya makao yake yawe ukiwa.+

 8 Usikumbuke dhidi yetu makosa ya mababu zetu.+

Ufanye haraka! Rehema zako na zitufikie,+

Kwa maana tumekuwa maskini sana.+

 9 Utusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+

Kwa ajili ya utukufu wa jina lako;+

Na utukomboe na kufunika dhambi zetu kwa sababu ya jina lako.+

10 Kwa nini mataifa yaseme: “Mungu wao yuko wapi?”+

Na ijulikane katika mataifa mbele ya macho yetu+

Juu ya kulipiza kisasi damu ya watumishi wako ambayo imemwagwa.+

11 Kuugua kwa mfungwa na kuingie mbele zako.+

Kulingana na ukuu wa mkono wako, uwahifadhi wale waliochaguliwa kwa ajili ya kifo.+

12 Na kuwalipa jirani zetu mara saba kifuani mwao+

Shutuma yao ambayo wamekushutumu nayo, Ee Yehova.+

13 Na sisi watu wako na kundi la malisho yako,+

Tutakushukuru mpaka wakati usio na kipimo;

Kutoka kizazi mpaka kizazi tutatangaza sifa yako.+

Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi.+ Kikumbusho. Ya Asafu.+ Muziki.

80 Ee Mchungaji wa Israeli, tega sikio,+

Wewe unayemwongoza Yosefu kama kundi.+

Wewe unayeketi juu ya makerubi,+ uangaze.+

 2 Mbele ya Efraimu na Benyamini na Manase, uamshe nguvu zako,+

Na uje kutuokoa.+

 3 Ee Mungu, uturudishe;+

Na uutie uso wako nuru, ili tupate kuokolewa.+

 4 Ee Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea kuwaka hasira juu ya sala ya watu wako mpaka wakati gani?+

 5 Umewalisha mkate wa machozi,+

Nawe unaendelea kuwafanya wanywe machozi kwa machozi kwa kiasi kikubwa.+

 6 Ulituweka tugombane na jirani zetu,+

Nao adui zetu wanaendelea kudharau kama wanavyopenda.+

 7 Ee Mungu wa majeshi, uturudishe;+

Na uutie uso wako nuru, ili tupate kuokolewa.+

 8 Ulifanya mzabibu uondoke Misri.+

Ukaendelea kuyafukuza mataifa, ili uupande.+

 9 Ulitengeneza nafasi mbele yake,+ ili upate kutia mizizi na kuijaza nchi.+

10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,

Na mierezi ya Mungu kwa matawi yake.+

11 Hatua kwa hatua uliyaeneza matawi yake mpaka baharini,+

Na machipukizi yake mpaka kwenye ule Mto.+

12 Kwa nini umebomoa kuta zake za mawe,+

Na kwa nini wale wote wanaopita barabarani wameuchuma?+

13 Nguruwe-mwitu kutoka msituni anaendelea kuula,+

Na makundi ya wanyama wa porini wanaendelea kuula.+

14 Ee Mungu wa majeshi, urudi, tafadhali;+

Utazame chini kutoka mbinguni, uone na kuutunza mzabibu huu,+

15 Na shina ambalo mkono wako wa kuume umepanda,+

Na umtazame mwana ambaye umemfanya kuwa mwenye nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+

16 Huo umeteketezwa kwa moto, umekatwa.+

Wanaangamia kutokana na kemeo la uso wako.+

17 Mkono wako na uwe juu yake mtu wa mkono wako wa kuume,+

Juu ya mwana wa binadamu ambaye umemfanya kuwa mwenye nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+

18 Nasi hatutageuka kutoka kwako.+

Utuhifadhi hai, ili tupate kuliitia jina lako.+

19 Ee Yehova Mungu wa majeshi, uturudishe;+

Uutie uso wako nuru, ili tupate kuokolewa.+

Kwa kiongozi juu ya Gitithi.+ Ya Asafu.

81 Mpigieni Mungu, nguvu zetu, vigelegele vya shangwe;+

Mpigieni Mungu wa Yakobo kelele za ushindi.+

 2 Anzisheni muziki+ na kuchukua tari,+

Kinubi chenye kupendeza pamoja na kinanda.+

 3 Katika mwezi mpya, pigeni baragumu;+

Katika mwezi mpevu, kwa ajili ya siku ya sherehe yetu.+

 4 Kwa maana ni sharti kwa ajili ya Israeli,+

Uamuzi wa hukumu wa Mungu wa Yakobo.

 5 Alimwamuru Yosefu liwe kikumbusho,+

Alipokuwa akipita juu ya nchi ya Misri.+

Lugha ambayo sikuijua, niliendelea kuisikia.+

 6 “Nililigeuza bega lake liondoke kwenye mzigo;+

Mikono yake ikaondoka kwenye kikapu.+

 7 Katika taabu uliita, nami nikakuokoa;+

Nikaanza kukujibu katika mahali palipofichika pa mngurumo.+

Nikakuchunguza kando ya maji ya Meriba.+ Sela.

 8 Sikieni, enyi watu wangu, nami nitatoa ushahidi dhidi yenu,+

Ee Israeli, ikiwa utanisikiliza.+

 9 Katikati yako hakutakuwa na mungu yeyote mgeni;+

Wala hutamwinamia mungu wa kigeni.+

10 Mimi, Yehova, ni Mungu wako,+

Yule anayekutoa katika nchi ya Misri.+

Fungua wazi kinywa chako, nami nitakijaza.+

11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu;+

Na Israeli hakuonyesha utayari wowote kunielekea.+

12 Na kwa hiyo nikawaacha waende katika ukaidi wa moyo wao;+

Wakatembea katika mashauri yao wenyewe.+

13 Laiti watu wangu wangekuwa wakinisikiliza,+

Laiti Israeli angetembea katika njia zangu!+

14 Adui zao ningewatiisha kwa urahisi,+

Nami ningegeuza mkono wangu dhidi ya wapinzani wao.+

15 Na wale wanaomchukia Yehova vikali, watakuja kwake wakitetemeka,+

Na wakati wao utakuwa mpaka wakati usio na kipimo.

16 Naye ataendelea kumlisha mafuta ya ngano,+

Na kutokana na mwamba nitakushibisha asali.”+

Muziki wa Asafu.

82 Mungu amesimama katika kusanyiko+ la Mungu;+

Anahukumu katikati ya miungu:+

 2 “Mtaendelea kuhukumu bila haki mpaka wakati gani+

Na kuonyesha ubaguzi kwa waovu?+ Sela.

 3 Iweni waamuzi kwa ajili ya mtu wa hali ya chini na mvulana asiye na baba.+

Kwa mtu mwenye kuteseka na maskini, mtendeeni haki.+

 4 Okoeni mtu wa hali ya chini na maskini;+

Wakomboeni kutoka katika mkono wa waovu.”+

 5 Hawajajua, wala hawaelewi;+

Wanaendelea kutembea huku na huku katika giza;+

Misingi yote ya dunia inatikiswa.+

 6 “Mimi mwenyewe nimesema, ‘Ninyi ni miungu,+

Nanyi nyote ni wana wa Aliye Juu Zaidi.+

 7 Hakika mtakufa kama wanadamu;+

Nanyi mtaanguka kama yeyote kati ya wakuu!’”+

 8 Usimame, Ee Mungu, uihukumu dunia;+

Kwa maana wewe mwenyewe unapaswa kuyamiliki mataifa yote.+

Wimbo. Muziki wa Asafu.+

83 Ee Mungu, usinyamaze;+

Usikae bila kusema, wala kukaa kimya, Ee Mungu.+

 2 Kwa maana, tazama! adui zako wanafanya fujo;+

Na wale wanaokuchukia vikali wameinua kichwa chao.+

 3 Wanaendeleza kwa ujanja mazungumzo ya siri juu ya watu wako;+

Nao wanapanga hila juu ya watu wako waliofichwa.+

 4 Wamesema: “Njooni, tuwafutilie mbali wasiwe taifa,+

Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”+

 5 Kwa maana kwa moyo wameshauriana kwa umoja;+

Naam, wakafanya agano dhidi yako,+

 6 Mahema ya Edomu+ na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+

 7 Gebali na Amoni+ na Amaleki,

Ufilisti+ pamoja na wakaaji wa Tiro.+

 8 Pia, Ashuru imejiunga nao;+

Wamekuwa mkono kwa wana wa Loti.+ Sela.

 9 Uwatendee kama Midiani,+ kama Sisera,+

Kama Yabini+ kwenye bonde la mto la Kishoni.+

10 Waliangamizwa huko En-dori;+

Wakawa mbolea kwa ajili ya udongo.+

11 Na uwafanye watu wao wenye vyeo wawe kama Orebu na kama Zeebu,+

Na watawala wao wadogo wote kama Zeba na kama Zalmuna,+

12 Ambao wamesema: “Na tumiliki makao ya Mungu.”+

13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama kisulisuli cha mbaruti,+

Kama majani makavu mbele ya upepo.+

14 Kama moto unaoteketeza msitu+

Na kama mwali wa moto unaounguza milima,+

15 Uwafuatilie vivyo hivyo tu kwa tufani yako+

Nawe uwasumbue kwa upepo wako wenye dhoruba.+

16 Ujaze nyuso zao aibu,+

Ili watu wapate kulitafuta jina lako, Ee Yehova.+

17 Na waone aibu na kusumbuka nyakati zote,+

Nao wafedheheshwe na kuangamia;+

18 Ili watu wajue+ kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova,+

Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi,+ juu ya dunia yote.+

Kwa kiongozi juu ya Gitithi.+ Ya wana wa Kora. Muziki.

84 Jinsi ilivyo nzuri maskani yako kuu,+

Ee Yehova wa majeshi!+

 2 Nafsi yangu imetamani sana na pia imedhoofika kwa kutamani nyua za Yehova.+

Moyo wangu mwenyewe na mwili wangu wenyewe humpigia Mungu aliye hai vigelegele kwa shangwe.+

 3 Hata ndege amepata nyumba,

Na mbayuwayu amepata kiota chake,

Ambapo ameweka vifaranga vyake—

Madhabahu yako kuu, Ee Yehova wa majeshi, Mfalme wangu na Mungu wangu!

 4 Wenye furaha ni wale wanaokaa katika nyumba yako!+

Bado wanaendelea kukusifu.+ Sela.

 5 Wanadamu wenye furaha ni wale ambao nguvu zao ziko kwako,+

Ambao njia kuu zimo moyoni mwao.+

 6 Wakipita katika nchi tambarare ya chini ya mibaka,+

Wanaigeuza kuwa bubujiko;

Naam, mfundishaji+ anajivika baraka.

 7 Wataendelea kutembea kutoka nguvu hata nguvu;+

Kila mmoja huonekana mbele za Mungu katika Sayuni.+

 8 Ee Yehova Mungu wa majeshi, usikie sala yangu;+

Utege sikio, Ee Mungu wa Yakobo.+ Sela.

 9 Ee ngao yetu, ona, Ee Mungu,+

Na uutazame uso wa mtiwa-mafuta wako.+

10 Kwa maana siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu moja kwingineko.+

Nimechagua kusimama mlangoni pa nyumba ya Mungu wangu+

Badala ya kuzunguka katika mahema ya uovu.+

11 Kwa maana Yehova Mungu ni jua+ na ngao;+

Yeye hutoa kibali na utukufu.+

Yehova mwenyewe hatawanyima jambo lolote jema wale wanaotembea bila kosa.+

12 Ee Yehova wa majeshi, mtu mwenye furaha ni yule anayekutegemea.+

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora. Muziki.

85 Ee Yehova, umependezwa na nchi yako;+

Umewarudisha wale waliochukuliwa mateka wa Yakobo.+

 2 Umelisamehe kosa la watu wako;+

Umeifunika dhambi yao yote.+ Sela.

 3 Umeizuia ghadhabu yako yote;+

Umegeuka kutoka kwenye moto wa hasira yako.+

 4 Utukusanye tena, Ee Mungu wa wokovu wetu,+

Na uache kutukasirikia.+

 5 Je, utapandwa na hasira kwa sababu yetu mpaka wakati usio na kipimo?+

Je, utarefusha hasira yako kizazi baada ya kizazi?+

 6 Je, hutatufanya hai tena,+

Ili watu wako wapate kushangilia ndani yako?+

 7 Ee Yehova, utuonyeshe fadhili zako zenye upendo,+

Nawe utupe wokovu wako.+

 8 Nitasikia jambo ambalo Mungu wa kweli Yehova atasema,+

Kwa maana atasema amani kwa watu wake+ na kwa washikamanifu wake,

Lakini wasirudi kujitumaini.+

 9 Hakika wokovu wake uko karibu na wale wanaomwogopa,+

Ili utukufu ukae katika nchi yetu.+

10 Nazo fadhili zenye upendo na ukweli, zimekutana;+

Uadilifu na amani—zimepigana busu.+

11 Ukweli utachipuka kutoka duniani,+

Nao uadilifu utatazama chini kutoka mbinguni.+

12 Pia, Yehova atatoa yaliyo mema,+

Nayo nchi yetu wenyewe itatoa mazao yake.+

13 Mbele zake uadilifu wenyewe utatembea,+

Nao utafanya njia kwa hatua zake.+

Sala ya Daudi

86 Utege sikio lako, Ee Yehova. Unijibu,+

Kwa maana ninateseka nami ni maskini.+

 2 Uilinde nafsi yangu, kwa maana mimi ni mshikamanifu.+

Umwokoe mtumishi wako​—​wewe ni Mungu wangu​—​anayekutegemea.+

 3 Unionyeshe kibali, Ee Yehova,+

Kwa maana ninaendelea kukuitia wewe mchana kutwa.+

 4 Uifanye nafsi ya mtumishi wako ishangilie,+

Kwa maana, Ee Yehova, ninakuinulia wewe nafsi yangu.+

 5 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni mwema+ na uko tayari kusamehe;+

Na fadhili zenye upendo ni nyingi kwa wale wote wanaokuitia.+

 6 Utege sikio, Ee Yehova, kwa sala yangu;+

Na uisikilize sauti yangu ya kusihi.+

 7 Katika siku ya taabu yangu nitakuitia wewe,+

Kwa maana utanijibu.+

 8 Hakuna yeyote aliye kama wewe katikati ya miungu, Ee Yehova,+

Wala hakuna kazi zozote kama zako.+

 9 Mataifa yote ambayo umeyafanya, yatakuja yenyewe,+

Nayo yatainama mbele zako, Ee Yehova,+

Na kulipa utukufu jina lako.+

10 Kwa maana wewe ni mkuu na unafanya mambo ya ajabu;+

Wewe ni Mungu, wewe peke yako.+

11 Unifundishe, Ee Yehova, juu ya njia yako.+

Nitatembea katika kweli yako.+

Unganisha moyo wangu ili kuliogopa jina lako.+

12 Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote,+

Nami nitalitukuza jina lako mpaka wakati usio na kipimo,

13 Kwa maana fadhili zako zenye upendo ni kuu kunielekea mimi,+

Nawe umeikomboa nafsi yangu kutoka katika Kaburi,* mahali pake pa chini kabisa.+

14 Ee Mungu, wenye kimbelembele wamesimama juu yangu;+

Nalo kusanyiko la wenye kuonea wameitafuta nafsi yangu,+

Nao hawajakuweka mbele yao.+

15 Lakini wewe, Ee Yehova, ni Mungu mwenye rehema na mwenye neema,+

Si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi wa fadhili zenye upendo na ukweli.+

16 Nigeukie na kunionyesha kibali.+

Umpe mtumishi wako nguvu zako,+

Na umwokoe mwana wa kijakazi wako.+

17 Unitendee ishara inayomaanisha wema,

Ili wale wanaonichukia wapate kuiona na kuaibika.+

Kwa maana wewe mwenyewe, Ee Yehova, umenisaidia na kunifariji.+

Ya wana wa Kora. Muziki, wimbo.

87 Msingi wake uko katika milima mitakatifu.+

 2 Yehova anapenda zaidi malango ya Sayuni+

Kuliko maskani zote za Yakobo.+

 3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, Ee jiji la Mungu wa kweli.+ Sela.

 4 Nitataja Rahabu na Babiloni+ kuwa kati ya wale wanaonijua mimi;

Tazama, Ufilisti+ na Tiro, pamoja na Kushi:+

“Huyu alizaliwa humo.”+

 5 Na juu ya Sayuni itasemwa:

“Kila mmoja alizaliwa humo.”+

Na Aliye Juu Zaidi+ atamfanya imara.+

 6 Yehova mwenyewe atatangaza, anapoandikisha vikundi vya watu:+

“Huyu alizaliwa humo.”+ Sela.

 7 Pia kutakuwako waimbaji na vilevile wachezaji wa dansi za mzunguko:+

“Mabubujiko yangu yote yamo ndani yako.”+

Wimbo, muziki wa wana wa Kora. Kwa kiongozi juu ya Mahalathi kwa ajili ya maitikio. Maskili ya Hemani+ Mwezra.

88 Ee Yehova, Mungu wa wokovu wangu,+

Wakati wa mchana nimepaaza kilio,+

Usiku pia, mbele zako.+

 2 Sala yangu itakuja mbele zako.+

Utege sikio lako kwa kilio changu cha kusihi.+

 3 Kwa maana nafsi yangu imepata misiba ya kutosha,+

Na maisha yangu yamekaribiana na Kaburi.*+

 4 Nimehesabiwa katikati ya wale wanaoshuka kuingia shimoni;+

Nimekuwa kama mwanamume ambaye hana nguvu,+

 5 Aliyewekwa huru katikati ya wafu,+

Kama waliouawa ambao wanalala kaburini,+

Ambao huwakumbuki tena

Na ambao wametenganishwa na mkono wako wenye kusaidia.+

 6 Umeniweka katika shimo lililo katika vina vya chini kabisa,

Katika mahali penye giza, katika abiso kubwa.+

 7 Ghadhabu yako imejitupa juu yangu,+

Nawe umenitesa kwa mashuu yako yote.+ Sela.

 8 Umewaweka rafiki zangu mbali nami;+

Umeniweka kuwa kama kitu chenye kuchukiza sana kwao.+

Niko chini ya kizuizi wala siwezi kwenda.+

 9 Jicho langu mwenyewe limedhoofika kwa sababu ya mateso yangu.+

Nimekuitia wewe, Ee Yehova, mchana kutwa;+

Nimekunyooshea mikono yangu.+

10 Je, utawafanyia wale waliokufa jambo la ajabu?+

Au je, wale wasiojiweza katika kifo watasimama,+

Je, watakusifu wewe?+ Sela.

11 Je, fadhili zako zenye upendo zitatangazwa katika kaburi,

Na uaminifu wako katika mahali pa maangamizi?+

12 Je, jambo lako la ajabu litajulikana katika giza,+

Au uadilifu wako katika nchi ya usahaulifu?+

13 Na bado wewe, Ee Yehova, nimekulilia unisaidie,+

Na asubuhi sala yangu inaendelea kukuelekea.+

14 Kwa nini, Ee Yehova, unaitupilia mbali nafsi yangu?+

Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?+

15 Ninateseka nami niko karibu kukata pumzi tangu uvulana;+

Nimevumilia sana vitu vyenye kuogopesha kutoka kwako.+

16 Miwako ya hasira yako inayowaka imepita juu yangu;+

Vitisho kutoka kwako mwenyewe vimeninyamazisha.+

17 Vimenizunguka kama maji mchana kutwa;+

Vyote vimenizingira kwa wakati mmoja.

18 Rafiki na mwenzangu umewaweka mbali nami;+

Mahali penye giza ndipo rafiki zangu.+

Maskili. Ya Ethani Mwezra.+

89 Nitaimba juu ya maonyesho ya fadhili zenye upendo za Yehova mpaka wakati usio na kipimo.+

Kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako kwa kizazi baada ya kizazi.+

 2 Kwa maana nimesema: “Fadhili zenye upendo zitakaa zikiwa zimejengwa mpaka wakati usio na kipimo;+

Kwa habari ya mbingu, wewe unaendeleza uaminifu wako imara ndani yake.”+

 3 “Nimefanya agano kumwelekea mchaguliwa wangu;+

Nimemwapia Daudi mtumishi wangu,+

 4 ‘Nitaufanya imara uzao wako mpaka wakati usio na kipimo,+

Nami nitakijenga kiti chako cha ufalme+ kwa kizazi baada ya kizazi.’” Sela.

 5 Na mbingu zitasifu tendo lako la ajabu, Ee Yehova,+

Naam, uaminifu wako katika kutaniko la watakatifu.

 6 Kwa maana ni nani kule angani anayeweza kulinganishwa na Yehova?+

Ni nani anayeweza kufanana na Yehova kati ya wana wa Mungu?+

 7 Mungu anapaswa kupewa heshima katikati ya kikundi cha rafiki za karibu cha watakatifu;+

Yeye ni mkuu na mwenye kuogopesha juu ya wote wanaomzunguka pande zote.+

 8 Ee Yehova Mungu wa majeshi,+

Ni nani aliye na nguvu kama wewe, Ee Yah?+

Na uaminifu wako unakuzunguka kotekote.+

 9 Unatawala juu ya kufurika kwa bahari;+

Inapoinua mawimbi yake wewe mwenyewe huyatuliza.+

10 Wewe mwenyewe umemponda Rahabu,+ kama mtu aliyeuawa.+

Kwa mkono wa nguvu zako umewatawanya adui zako.+

11 Mbingu ni yako,+ dunia pia ni yako;+

Nchi yenye kuzaa na vinavyoijaza+​—wewe mwenyewe umeviwekea msingi.+

12 Kaskazini na kusini—wewe mwenyewe uliziumba;+

Tabori+ na Hermoni+​—hupiga vigelegele kwa shangwe katika jina lako.+

13 Mkono wenye nguvu ni wako,+

Mkono wako una nguvu,+

Mkono wako wa kuume umeinuliwa.+

14 Uadilifu na hukumu ndizo mahali palipofanywa imara pa kiti chako cha ufalme;+

Fadhili zenye upendo na ukweli zinaingia mbele za uso wako.+

15 Wenye furaha ni watu wanaojua vigelegele vya shangwe.+

Ee Yehova, katika nuru ya uso wako wanaendelea kutembea.+

16 Katika jina lako wana shangwe mchana kutwa+

Na katika uadilifu wako wanainuliwa.+

17 Kwa maana wewe ni uzuri wa nguvu zao;+

Na kwa nia yako njema pembe yetu inainuliwa.+

18 Kwa maana ngao yetu ni ya Yehova,+

Na mfalme wetu ni wa Mtakatifu wa Israeli.+

19 Wakati huo uliongea na washikamanifu wako katika maono,+

Nawe ukasema:

“Nimempa mwenye nguvu msaada;+

Nimemwinua aliyechaguliwa kutoka katikati ya watu.+

20 Nimemwona Daudi mtumishi wangu;+

Kwa mafuta yangu matakatifu nimemtia mafuta,+

21 Ambaye mkono wangu mwenyewe utakuwa imara kwake,+

Ambaye mkono wangu mwenyewe utamtia nguvu.+

22 Hakuna adui atakayemdai chochote,+

Wala hakuna mwana wa uovu atakayemtesa.+

23 Na adui zake niliwavunja vipande-vipande kutoka mbele yake,+

Na wale wanaomchukia vikali niliendelea kuwapa mapigo.+

24 Na uaminifu wangu na fadhili zangu zenye upendo ziko pamoja naye,+

Na katika jina langu pembe yake imeinuliwa.+

25 Nami nimeweka mkono wake juu ya bahari+

Na mkono wake wa kuume juu ya mito.+

26 Yeye mwenyewe huniita, ‘Wewe ni Baba+ yangu,

Mungu+ wangu na Mwamba wa wokovu wangu.’+

27 Pia, mimi mwenyewe nitamweka kama mzaliwa wa kwanza,+

Aliye juu zaidi kati ya wafalme wa dunia.+

28 Nitahifadhi fadhili zangu zenye upendo kwake mpaka wakati usio na kipimo,+

Nalo agano langu litakuwa lenye uaminifu kwake.+

29 Nami hakika nitaweka imara uzao wake milele+

Na kiti chake cha ufalme kama siku za mbingu.+

30 Wanawe wakiiacha sheria yangu+

Nao wasitembee katika maamuzi yangu ya hukumu,+

31 Wakizitia unajisi sheria zangu,

Nao wasishike amri zangu,

32 Mimi pia nitaelekeza fikira zangu kwenye ukosaji wao kwa fimbo+

Na kwenye kosa lao kwa mapigo.+

33 Lakini fadhili zangu zenye upendo sitamwondolea mbali,+

Wala sitaufanya uaminifu wangu kuwa wa

uwongo.+

34 Sitalitia unajisi agano langu,+

Na maneno kutoka midomoni mwangu sitayabadili.+

35 Nimeapa mara moja katika utakatifu wangu,+

Sitamwambia Daudi uwongo.+

36 Uzao wake mwenyewe utakuwako mpaka wakati usio na kipimo,+

Na kiti chake cha ufalme kama vile jua lilivyo mbele zangu.+

37 Kama mwezi, kitafanywa imara mpaka wakati usio na kipimo,

Na kama vile shahidi mwaminifu angani.” Sela.

38 Lakini wewe—wewe umetupilia mbali nawe unaendelea kuchukia;+

Umemkasirikia mtiwa-mafuta wako.+

39 Umelikataa kwa dharau agano la mtumishi wako;

Umelitia unajisi taji lake mpaka chini.+

40 Umevunja mazizi yake yote ya mawe;+

Umefanya ngome zake kuwa mabomoko.+

41 Wote wanaopita njiani wamempora;+

Amekuwa shutuma kwa jirani zake.+

42 Umeuinua mkono wa kuume wa wapinzani wake;+

Umewafanya adui zake wote washangilie.+

43 Isitoshe, wewe tena unautendea upanga wake kama adui,+

Nawe umemfanya asipate ushindi katika pigano.+

44 Umeikomesha fahari yake,+

Nacho kiti chake cha ufalme umekitupa mpaka chini.+

45 Umefupisha siku za ujana wake;

Umemvika aibu.+ Sela.

46 Ee Yehova, utaendelea kujificha mpaka wakati gani? Wakati wote?+

Je, ghadhabu yako itaendelea kuwaka kama moto?+

47 Ukumbuke mimi nina urefu gani wa maisha.+

Je, ni kwa ubatili kwamba umewaumba wana wote wa binadamu?+

48 Ni mwanamume gani aliye hai ambaye hataona kifo?+

Je, anaweza kuiokoa nafsi yake katika mkono wa Kaburi?*+ Sela.

49 Yako wapi matendo yako ya kwanza ya fadhili zenye upendo, Ee Yehova,

Ambayo ulimwapia Daudi katika uaminifu wako?+

50 Ukumbuke, Ee Yehova, shutuma juu ya watumishi wako,+

Kuchukua kifuani pangu shutuma ya vikundi vyote vingi vya watu,+

51 Jinsi adui zako wameshutumu, Ee Yehova,+

Jinsi wameshutumu nyayo za mtiwa-mafuta wako.+

52 Yehova na abarikiwe mpaka wakati usio na kipimo. Amina na Amina.+

KITABU CHA NNE

(Zaburi 90 – 106)

Sala ya Musa, mtu wa Mungu wa kweli.+

90 Ee Yehova, wewe mwenyewe umekuwa makao yetu halisi+

Kwa kizazi baada ya kizazi.+

 2 Kabla ya kuzaliwa kwa milima,+

Au kutokezwa kwa dunia+ na nchi yenye kuzaa kana kwamba kwa maumivu ya kuzaa,+

Tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo wewe ni Mungu.+

 3 Unamfanya mwanadamu anayeweza kufa arudi kuwa kitu kilichopondwa,+

Nawe unasema: “Rudini, enyi wana wa binadamu.”+

 4 Kwa maana miaka elfu machoni pako ni kama jana ikiisha kupita,+

Na kama kesha la usiku.+

 5 Umewafagilia mbali;+ wanakuwa usingizi tu;+

Asubuhi, wao ni kama majani mabichi ambayo hubadilika.+

 6 Asubuhi huchanua maua na lazima yabadilike;+

Jioni, hunyauka na hakika hukauka.+

 7 Kwa maana tumefikia mwisho kwa hasira yako,+

Na kwa ghadhabu yako tumetiwa wasiwasi.+

 8 Umeyaweka makosa yetu moja kwa moja mbele zako,+

Mambo yetu yaliyofichika mbele za uso wako unaong’aa.+

 9 Kwa maana siku zetu zote zimepungua katika ghadhabu yako;+

Tumeimaliza miaka yetu kama mnong’ono tu.+

10 Kwa maana siku za miaka yetu ni miaka 70;+

Na ikiwa kwa sababu ya nguvu za pekee ni miaka 80,+

Hata hivyo hizo husisitiza kuleta taabu na mambo yenye kuumiza;+

Kwa maana lazima zipite upesi, nasi huruka na kwenda zetu.+

11 Ni nani anayejua nguvu za hasira yako+

Na ghadhabu yako kulingana na kukuogopa wewe?+

12 Utuonyeshe jinsi ya kuzihesabu siku zetu hivi kwamba+

Tupate kuuingiza moyo wa hekima.+

13 Urudi, Ee Yehova!+ Mpaka wakati gani?+

Nawe ujute juu ya watumishi wako.+

14 Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako zenye upendo,+

Ili tupate kupiga vigelegele kwa shangwe na kufurahi siku zetu zote.+

15 Utufanye tushangilie kulingana na siku ambazo umetutesa,+

Miaka ambayo tumeona msiba.+

16 Utendaji wako na uonekane kwa watumishi wako+

Na fahari yako juu ya wana wao.+

17 Nao uzuri wa Yehova Mungu wetu na uwe juu yetu,+

Na kazi ya mikono yetu uifanye imara juu yetu.+

Naam, kazi ya mikono yetu, uifanye imara.+

91 Yeyote anayekaa mahali pa siri+ pa Aliye Juu Zaidi+

Atajipatia makao katika kivuli cha Mweza-Yote.+

 2 Nitamwambia Yehova: “Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu,+

Mungu wangu, ambaye nitamtegemea.”+

 3 Kwa maana yeye mwenyewe atakukomboa kutoka katika mtego wa mwindaji wa ndege,+

Kutoka kwa tauni inayosababisha shida.+

 4 Kwa manyoya yake ataweka kizuizi usiweze kufikiwa,+

Nawe utapata kimbilio chini ya mabawa yake.+

Ukweli+ wake utakuwa ngao+ kubwa na boma.

 5 Hutaogopa kitu chochote chenye kutia hofu wakati wa usiku,+

Wala mshale+ unaoruka mchana,

 6 Wala tauni inayotembea gizani,+

Wala maangamizi yanayopora katikati ya mchana.+

 7 Elfu wataanguka upande wako

Na elfu kumi kwenye mkono wako wa kuume;

Haitakukaribia wewe.+

 8 Utatazama kwa macho yako tu+

Na kuona malipo ya waovu.+

 9 Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”+

Umemfanya Aliye Juu Zaidi awe makao yako;+

10 Hakuna msiba utakaokuangukia,+

Na hata pigo halitakaribia hema lako.+

11 Kwa maana atawaamuru malaika zake kukuhusu wewe,+

Ili kukulinda katika njia zako zote.+

12 Watakuchukua mikononi mwao,+

Ili usiugonge mguu wako juu ya jiwe lolote.+

13 Utamkanyaga mwana-simba na swila;+

Utamkanyagia chini mwana-simba mwenye manyoya shingoni na nyoka mkubwa.+

14 Kwa sababu ameweka upendo wake juu yangu,+

Mimi nitamwokoa pia.+

Nitamlinda kwa sababu amelijua jina langu.+

15 Ataniitia, nami nitamjibu.+

Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+

Nitamwokoa na kumtukuza.+

16 Nitamshibisha kwa wingi wa siku,+

Nami nitamfanya aone wokovu wangu.+

Muziki, wimbo, kwa ajili ya siku ya sabato.

92 Ni vema kumtolea Yehova shukrani+

Na kulipigia jina lako muziki, ewe Uliye Juu Zaidi;+

 2 Kutangaza asubuhi fadhili zako zenye upendo+

Na nyakati za usiku uaminifu wako.+

 3 Kwa kinanda cha nyuzi kumi na kwa udi,+

Kwa muziki unaovuma wa kinubi.+

 4 Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya utendaji wako;

Kwa sababu ya kazi za mikono yako, ninapiga vigelegele kwa shangwe.+

 5 Jinsi zilivyo kuu kazi zako, Ee Yehova!+

Fikira zako ni zenye kina kikubwa sana.+

 6 Mtu yeyote asiyetumia akili hawezi kuzijua,+

Wala yeyote aliye mjinga hawezi kuelewa hili.+

 7 Wakati waovu wanapochipuka kama majani+

Na wote wanaotenda mambo yenye kuumiza wanapochanuka,

Ni ili wao wapate kuangamizwa milele.+

 8 Lakini wewe uko juu mpaka wakati usio na kipimo, Ee Yehova.+

 9 Kwa maana, tazama! adui zako, Ee Yehova,+

Kwa maana, tazama! adui zako mwenyewe wataangamia;+

Wote wanaofanya mambo yenye kuumiza watatenganishwa.+

10 Lakini wewe utaiinua pembe yangu kama ile ya ng’ombe-mwitu;+

Nitajipaka mafuta mapya.+

11 Na jicho langu litawatazama adui zangu;+

Masikio yangu yatasikia habari za wale wanaosimama juu yangu, watenda-maovu.

12 Mwadilifu atachanua kama mtende;+

Kama mwerezi katika Lebanoni, atakuwa mkubwa.+

13 Wale ambao wamepandwa katika nyumba ya Yehova,+

Katika nyua za Mungu wetu,+ watachanuka.

14 Bado wataendelea kusitawi wakati wa kuwa na kichwa chenye mvi,+

Wataendelea kuwa wanono na wabichi,+

15 Ili kutangaza kwamba Yehova ni mnyoofu.+

Yeye ni Mwamba wangu,+ ambaye ndani yake hamna ukosefu wowote wa uadilifu.+

93 Yehova mwenyewe amekuwa mfalme!+

Amevaa adhama;+

Yehova amevaa—​amejifunga mshipi wa nguvu.+

Nchi yenye kuzaa pia hufanywa imara ili isipate kutikiswa.+

 2 Kiti chako cha ufalme kimefanywa imara tangu zamani za kale;+

Wewe ni wa tangu wakati usio na kipimo.+

 3 Mito imepaaza, Ee Yehova,

Mito imepaaza sauti yake;+

Mito inaendelea kupaaza mivumo yake.+

 4 Juu ya sauti ya maji mengi, mashuu makubwa ya bahari,+

Yehova ni mwenye fahari+ katika kilele.

 5 Vikumbusho vyako vimekuwa vyenye kutegemeka sana.+

Utakatifu unaifaa nyumba yako mwenyewe,+ Ee Yehova, kwa wingi wa siku.+

94 Ee Mungu wa matendo ya kisasi, Yehova,+

Ee Mungu wa matendo ya kisasi, uangaze!+

 2 Usimame mwenyewe, Ee Mwamuzi wa dunia.+

Uwalipe wenye majivuno.+

 3 Waovu wataendelea kuwako hata wakati gani, Ee Yehova,+

Waovu wataendelea kushangilia hata wakati gani?+

 4 Wanaendelea kuropoka, wanaendelea kusema ovyoovyo;+

Wote wanaofanya mambo yenye kuumiza wanaendelea kujivuna wenyewe.+

 5 Wanaendelea kuwavunja watu wako, Ee Yehova,+

Na urithi wako wanaendelea kuutesa.+

 6 Wanamuua mjane na mkaaji mgeni,+

Nao wanawaua wavulana wasio na baba.+

 7 Nao wanaendelea kusema: “Yah haoni;+

Na Mungu wa Yakobo haelewi hilo.”+

 8 Eleweni, ninyi msiotumia akili mlio kati ya watu;+

Nanyi wajinga, mtapata ufahamu wowote wakati gani?+

 9 Yule anayelipanda sikio, je, hawezi kusikia?+

Au Yule anayelifanya jicho, je, hawezi kutazama?+

10 Yule anayeyarekebisha mataifa, je, hawezi kukaripia,+

Naam, Yule anayewafundisha wanadamu ujuzi?+

11 Yehova anazijua fikira za wanadamu, kwamba hizo ni kama pumzi.+

12 Mwenye furaha ni mwanamume ambaye unamrekebisha,+ Ee Yah,

Na ambaye unamfundisha katika sheria yako mwenyewe,+

13 Ili kumpa utulivu kutokana na siku za msiba,+

Mpaka shimo lichimbwe kwa ajili ya mwovu.+

14 Kwa maana Yehova hatawaacha watu wake,+

Wala hatauacha urithi wake mwenyewe.+

15 Kwa maana uamuzi wa hukumu utarudi hata kwa uadilifu,+

Na wote walio wanyoofu moyoni wataufuata.

16 Ni nani atakayesimama kwa ajili yangu juu ya waovu?+

Ni nani atakayesimama kwa ajili yangu juu ya wanaotenda mambo yenye kuumiza?+

17 Kama Yehova hangenipa msaada,+

Baada ya muda kidogo nafsi yangu ingekaa penye kimya.+

18 Niliposema: “Hakika mguu wangu utatembea ukitikisika,”+

Fadhili zako zenye upendo, Ee Yehova, ziliendelea kunitegemeza.+

19 Fikira zangu zinazofadhaisha zilipokuwa nyingi ndani yangu,+

Faraja zako mwenyewe zilianza kuikumbatia nafsi yangu.+

20 Je, kiti cha ufalme kinachosababisha shida, kitashirikiana nawe,+

Na huku kinatunga matatizo kwa njia ya amri?+

21 Wao hushambulia vikali nafsi ya mwadilifu+

Na kutangaza kwamba damu ya mtu asiye na hatia ni yenye uovu.+

22 Lakini Yehova atakuwa kilele changu salama,+

Na Mungu wangu, mwamba wa kimbilio langu.+

23 Naye atayageuza madhara yao yarudi juu yao+

Naye atawanyamazisha kwa msiba wao wenyewe.+

Yehova Mungu wetu atawanyamazisha.+

95 Njooni tumpigie Yehova vigelegele kwa shangwe!+

Na tumpigie Mwamba wetu wa wokovu vigelegele vya ushindi.+

 2 Twendeni mbele za uso wake tukiwa na shukrani;+

Na tumpigie kelele za ushindi kwa nyimbo tamu.+

 3 Kwa maana Yehova ni Mungu mkuu+

Na Mfalme mkuu juu ya miungu mingine yote,+

 4 Yeye ambaye mkononi mwake mna vina vya ndani sana vya dunia+

Na ambaye vilele vya milima ni vyake;+

 5 Ambaye bahari, aliyoiumba yeye mwenyewe, ni yake+

Na ambaye mikono yake mwenyewe iliifanyiza nchi kavu.+

 6 Ingieni, tuabudu na kuinama;+

Na tupige magoti+ mbele za Yehova Mtengenezaji wetu.+

 7 Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake na kondoo wa mkono wake.+

Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+

 8 Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu kama huko Meriba,+

Kama katika ile siku ya Masa, nyikani,+

 9 Wakati mababu zenu waliponijaribu;+

Walinichunguza, pia waliuona utendaji wangu.+

10 Kwa miaka 40 nilichukizwa na kizazi hicho,+

Nami nikasema:

“Wao ni kikundi cha watu waliopotoka moyoni,+

Nao wenyewe hawajapata kuzijua njia zangu”;+

11 Ambao niliapa juu yao kwa hasira yangu:+

“Hawataingia katika mahali pangu pa kupumzikia.”+

96 Mwimbieni Yehova wimbo mpya.+

Mwimbieni Yehova, enyi watu wote wa dunia.+

 2 Mwimbieni Yehova, libarikini jina lake.+

Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+

 3 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa,+

Kazi zake za ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.+

 4 Kwa maana Yehova ni mkuu+ na wa kusifiwa sana.

Ni mwenye kuogopesha kuliko miungu mingine yote.+

 5 Kwa maana miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu isiyo na thamani;+

Lakini Yehova, amezifanya mbingu.+

 6 Utukufu na fahari ziko mbele zake;+

Nguvu na uzuri zipo katika patakatifu pake.+

 7 Mhesabieni Yehova, enyi familia za vikundi vya watu,+

Mhesabieni Yehova utukufu na nguvu.+

 8 Mhesabieni Yehova utukufu wa jina lake;+

Chukueni zawadi na mwingie katika nyua zake.+

 9 Mwinamieni Yehova katika pambo takatifu;+

Iweni na maumivu makali kwa sababu yake, enyi nyote watu wa dunia.+

10 Semeni kati ya mataifa: “Yehova amekuwa mfalme.+

Nchi yenye kuzaa pia hufanywa imara ili isitikiswe.+

Yeye atatetea kwa unyoofu vikundi vya watu katika kesi yao.”+

11 Mbingu na zifurahi, na dunia ishangilie.+

Bahari na ingurume na vitu vinavyoijaza.+

12 Nchi na ifurahi na vyote vilivyomo.+

Na wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie+

13 Mbele za Yehova. Kwa maana amekuja;+

Kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+

Ataihukumu kwa uadilifu nchi yenye kuzaa+

Na vikundi vya watu kwa uaminifu.+

97 Yehova amekuwa mfalme!+ Dunia na ishangilie.+

Na vile visiwa vingi vishangilie.+

 2 Mawingu na giza zito vinamzunguka;+

Uadilifu na hukumu ni mahali palipofanywa imara pa kiti chake cha ufalme.+

 3 Moto hutoka mbele zake,+

Nao huteketeza adui zake wanaomzunguka pande zote.+

 4 Umeme wake ulitia nuru nchi yenye kuzaa;+

Dunia iliona, ikawa na maumivu makali.+

 5 Milima ilianza kuyeyuka kama nta kwa sababu ya Yehova,+

Kwa sababu ya Bwana wa dunia nzima.+

 6 Mbingu zimeutangaza uadilifu wake,+

Navyo vikundi vyote vya watu vimeuona utukufu wake.+

 7 Wote wanaotumikia sanamu yoyote ya kuchongwa na waone aibu,+

Wale wanaojisifia miungu isiyo na thamani.+

Mwinamieni, enyi miungu yote.+

 8 Sayuni ilisikia na kuanza kushangilia,+

Na miji ya kandokando ya Yuda ilianza kushangilia+

Kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu, Ee Yehova.+

 9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote;+

Wewe uko juu sana katika kupanda kwako, juu ya miungu mingine yote.+

10 Enyi mnaompenda Yehova,+ chukieni yaliyo mabaya.+

Yeye anazilinda nafsi za washikamanifu wake;+

Huwakomboa kutoka katika mkono wa waovu.+

11 Nuru imemwangazia mwadilifu,+

Na shangwe kwa ajili ya walio wanyoofu moyoni.+

12 Shangilieni katika Yehova, enyi waadilifu,+

Na kutoa shukrani kwa ukumbusho wake mtakatifu.+

Muziki.

98 Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+

Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.+

Mkono wake wa kuume, naam, mkono wake mtakatifu, umempatia wokovu.+

 2 Yehova amefanya wokovu wake ujulikane;+

Ameufunua uadilifu wake machoni pa mataifa.+

 3 Amezikumbuka fadhili zake zenye upendo na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.+

Miisho yote ya dunia imeuona wokovu wa Mungu wetu.+

 4 Mpigieni Yehova kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+

Changamkeni na kupiga vigelegele kwa shangwe na kupiga muziki.+

 5 Mpigieni Yehova muziki kwa kinubi,+

Kwa kinubi na sauti ya muziki.+

 6 Kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu+

Pigeni kelele za ushindi mbele za Mfalme, Yehova.

 7 Bahari na ingurume na vyote vinavyoijaza,+

Nchi yenye kuzaa na wanaokaa humo.+

 8 Mito na ipige makofi;

Milima yote pamoja na ipige vigelegele kwa shangwe+

 9 Mbele za Yehova, kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+

Ataihukumu nchi yenye kuzaa kwa uadilifu+

Na vikundi vya watu kwa unyoofu.+

99 Yehova amekuwa mfalme.+ Vikundi vya watu na vifadhaike.+

Anaketi juu ya makerubi.+ Dunia na itetemeke.+

 2 Yehova ni mkuu katika Sayuni,+

Naye yuko juu ya vikundi vyote vya watu.+

 3 Na walisifu jina lako.+

Ni kuu na lenye kuogopesha, ni takatifu.+

 4 Na kwa nguvu za mfalme ameipenda hukumu.+

Wewe mwenyewe umeufanya imara unyoofu.+

Umetekeleza hukumu na uadilifu katika Yakobo.+

 5 Mtukuzeni Yehova Mungu wetu+ na kuinama chini penye kiti cha miguu yake;+

Yeye ni mtakatifu.+

 6 Musa na Haruni walikuwa kati ya makuhani wake,+

Na Samweli alikuwa kati ya wale walioliitia jina lake.+

Walikuwa wakimwita Yehova, naye akaendelea kuwajibu.+

 7 Katika nguzo ya wingu aliendelea kusema nao.+

Walishika vikumbusho vyake na sharti alilowapa.+

 8 Ee Yehova Mungu wetu, wewe mwenyewe uliwajibu.+

Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe,+

Na mwenye kulipiza kisasi juu ya matendo yao yenye sifa mbaya.+

 9 Mtukuzeni Yehova Mungu wetu+

Na mwiname kwenye mlima wake mtakatifu.+

Kwa maana Yehova Mungu wetu ni mtakatifu.+

Muziki wa kutoa shukrani.+

100 Mpigieni Yehova kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+

 2 Mtumikieni Yehova kwa kushangilia.+

Njooni mbele zake kwa vigelegele vya shangwe.+

 3 Jueni kwamba Yehova ni Mungu.+

Yeye ndiye aliyetufanya, wala si sisi wenyewe.+

Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.+

 4 Ingieni katika malango yake mkiwa na shukrani,+

Katika nyua zake mkiwa na sifa.+

Mtoleeni shukrani, libarikini jina lake.+

 5 Kwa maana Yehova ni mwema;+

Fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo,+

Na uaminifu wake ni wa kizazi baada ya kizazi.+

Ya Daudi. Muziki.

101 Nitaimba juu ya fadhili zenye upendo na hukumu.+

Kwako wewe, Ee Yehova, nitakupigia muziki.+

 2 Nitatenda kwa busara katika njia isiyo na kosa.+

Utanijia wakati gani?+

Nitatembea katika utimilifu wa moyo wangu ndani ya nyumba yangu.+

 3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu chochote kisichofaa.+

Nimelichukia tendo la wale wanaoiacha njia;+

Halishikamani nami.+

 4 Moyo mpotovu huondoka kwangu;+

Sijui lolote baya.+

 5 Yeyote anayemchongea mwenzake kwa siri,+

Huyo ninamnyamazisha.+

Yeyote mwenye macho yenye kiburi na mwenye moyo wa majivuno,+

Huyo siwezi kumvumilia.+

 6 Macho yangu yako juu ya waaminifu wa

dunia,+

Ili wapate kukaa pamoja nami.+

Yule anayetembea katika njia isiyo na kosa,+

Yeye ndiye atakayenihudumia.+

 7 Katika nyumba yangu hatakaa mtu yeyote anayefanya ujanja.+

Na yeyote anayesema uwongo, hatafanywa imara+

Mbele za macho yangu.+

 8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote wa dunia,+

Kukatilia mbali kutoka katika jiji+ la Yehova wote wanaotenda mambo yenye kuumiza.+

Sala ya mwenye kuteseka ikiwa atakuwa mnyonge na kumwaga hangaiko lake mbele za Yehova.+

102 Ee Yehova, uisikie sala yangu;+

Na kilio changu mwenyewe cha kuomba msaada na kije kwako.+

 2 Usinifiche uso wako siku nitakayokuwa katika dhiki kali.+

Utege sikio lako kwangu;+

Siku nitakayoita, ufanye haraka, unijibu.+

 3 Kwa maana siku zangu zimefikia mwisho kama moshi,+

Na mifupa yangu imefanywa kuwa na moto mkali kama jiko.+

 4 Moyo wangu umepigwa kama majani nao umekauka,+

Kwa maana nimesahau kula chakula changu.+

 5 Kwa sababu ya sauti ya kuugua kwangu+

Mifupa yangu imeshikamana na nyama yangu.+

 6 Nafanana na mwari wa jangwani.+

Nimekuwa kama bundi mdogo wa mahali palipofanywa ukiwa.

 7 Nimekonda,

Nami nimekuwa kama ndege aliye peke yake juu ya dari.+

 8 Adui zangu wamenishutumu mchana kutwa.+

Wale wanaonifanya mpumbavu hata wameapa kwa jina langu.+

 9 Kwa maana nimekula majivu kama mkate;+

Navyo vitu ninavyokunywa nimevichanganya hata pamoja na kulia,+

10 Kwa sababu ya shutuma zako na kuudhika kwako;+

Kwa maana umeniinua, ili unitupilie mbali.+

11 Siku zangu ni kama kivuli ambacho kimepungua,+

nami mwenyewe nimekauka kama majani tu.+

12 Lakini wewe, Ee Yehova, utakaa mpaka wakati usio na kipimo,+

Na ukumbusho wako utakuwa kwa kizazi baada ya kizazi.+

13 Wewe mwenyewe utasimama, utakuwa na rehema juu ya Sayuni,+

Kwa maana ni majira ya kumwonyesha kibali,

Kwa maana wakati uliowekwa umefika.+

14 Kwa maana watumishi wako wamepata raha katika mawe yake+

Nao wanaelekeza kibali chao kwenye mavumbi yake.+

15 Nayo mataifa yataogopa jina la Yehova,+

Na wafalme wote wa dunia utukufu wako.+

16 Kwa maana hakika Yehova atajenga Sayuni;+

Lazima ataonekana katika utukufu wake.+

17 Hakika ataielekea sala ya wale waliovuliwa kila kitu,+

Naye hataidharau sala yao.+

18 Hili limeandikwa kwa ajili ya kizazi cha wakati ujao;+

Na watu watakaoumbwa watamsifu Yah.+

19 Kwa maana yeye ametazama chini kutoka katika kilele chake kitakatifu,+

Kutoka katika mbingu Yehova ametazama chini, naam, kwenye dunia,+

20 Ili kusikia kuugua kwa mfungwa,+

Ili kuwafungua wale waliowekwa kwa ajili ya kifo;+

21 Ili jina la Yehova litangazwe katika Sayuni+

Na sifa yake katika Yerusalemu,+

22 Vikundi vya watu vitakapokusanywa vyote pamoja,+

Na falme ili kumtumikia Yehova.+

23 Alizitesa nguvu zangu njiani,+

Alizifupisha siku zangu.+

24 Nikasema: “Ee Mungu wangu,

Usiniondoe katikati ya siku zangu;+

Miaka yako ni ya vizazi vyote.+

25 Wewe uliiweka misingi ya dunia zamani za kale,+

Nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.+

26 Hizo zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utaendelea kusimama;+

Nazo zote zitachakaa kama vazi.+

Utazibadili kama mavazi, nazo zitamaliza zamu yake.+

27 Lakini wewe ni yuleyule, nayo miaka yako mwenyewe haitamalizika.+

28 Wana wa watumishi wako wataendelea kukaa;+

Na mbele zako uzao wao utafanywa imara.”+

Ya Daudi.

103 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,+

Naam, kila kitu kilicho ndani yangu, na kilibariki jina lake takatifu.+

 2 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,

Wala usiyasahau matendo yake yote,+

 3 Yeye anayesamehe makosa yako yote,+

Anayeponya magonjwa yako yote,+

 4 Anayeuokoa uhai wako kutoka katika shimo,+

Anayekuvika taji la fadhili zenye upendo na rehema,+

 5 Anayeushibisha muda wote wa maisha yako kwa mambo mema;+

Ujana wako unajifanya upya kama ule wa tai.+

 6 Yehova anatekeleza matendo ya uadilifu+

Na hukumu kwa wale wote wanaopunjwa.+

 7 Alimjulisha Musa njia zake,+

Matendo yake kwa wana wa Israeli.+

 8 Yehova ni mwenye rehema na mwenye neema,+

Si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo.+

 9 Yeye hataendelea kutafuta makosa wakati wote,+

Wala hataendelea kuweka kinyongo mpaka wakati usio na kipimo.+

10 Hakututendea kulingana na dhambi zetu;+

Wala kuleta juu yetu kile tunachostahili kulingana na makosa yetu.+

11 Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,+

Ndivyo fadhili zake zenye upendo zilivyo kuu kuwaelekea wale wanaomwogopa.+

12 Kama vile mashariki ilivyo mbali sana na magharibi,+

Ndivyo ameweka makosa yetu mbali sana na sisi.+

13 Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema,+

Ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa.+

14 Kwa maana yeye mwenyewe analijua vema umbo letu,+

Akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.+

15 Naye mwanadamu anayeweza kufa, siku zake ni kama zile za majani mabichi;+

Yeye huchanuka kama ua la shambani.+

16 Kwa maana upepo unapita juu yake, nalo halipo tena;+

Napo mahali pake hapataendelea kulitambua tena.+

17 Lakini fadhili zenye upendo za Yehova ni za tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo+

Kuwaelekea wale wanaomwogopa,+

Na uadilifu wake kwa wana wa wana,+

18 Kuwaelekea wale wanaolishika agano lake+

Na kuwaelekea wale wanaoyakumbuka maagizo yake ili kuyafanya.+

19 Yehova amekifanya imara kiti chake cha ufalme mbinguni;+

Nao ufalme wake mwenyewe umetawala juu ya kila kitu.+

20 Mbarikini Yehova, enyi malaika zake,+ mlio na uwezo katika nguvu, mnaolitenda neno lake,+

Kwa kuisikiliza sauti ya neno lake.+

21 Mbarikini Yehova, enyi majeshi yake yote,+

Enyi wahudumu wake, mnaofanya mapenzi yake.+

22 Mbarikini Yehova, enyi kazi zake zote,+

Katika mahali pote pa utawala wake.+

Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu.+

104 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu.+

Ee Yehova Mungu wangu, umekuwa mkuu sana.+

Umevaa utukufu na fahari,+

 2 Unayejifunika nuru kama vazi,+

Unayezitandaza mbingu kama hema,+

 3 Yule anayejenga vyumba vyake vya juu kwa boriti katika maji,+

Anayefanya mawingu kuwa gari lake,+

Anayetembea juu ya mabawa ya upepo,+

 4 Anayewafanya malaika zake kuwa roho,+

Na wahudumu wake kuwa moto unaoteketeza.+

 5 Ameiwekea dunia msingi juu ya mahali pake palipofanywa imara;+

Haitatikiswa mpaka wakati usio na kipimo, au milele.+

 6 Uliifunika kwa kilindi cha maji kama kwa vazi.+

Maji yalikuwa yamesimama juu ya milima.+

 7 Yakaanza kukimbia ulipoyakemea;+

Yakakimbia kwa wasiwasi mkubwa yaliposikia sauti ya mngurumo wako—

 8 Milima ikapanda juu,+

Nchi tambarare za mabonde zikashuka chini—

Mpaka mahali ulipoyawekea msingi wake.

 9 Uliweka mpaka, yasiupite,+

Ili yasiifunike dunia tena.+

10 Anatuma mabubujiko ndani ya mabonde yenye vijito;+

Yanaendelea kusonga mbele katikati ya milima.

11 Daima yanawapa maji ya kunywa wanyama wote wa porini;+

Punda-milia+ hukata kiu yao kwa ukawaida.

12 Juu yake hukaa viumbe vinavyoruka vya mbinguni;+

Kutoka katikati ya majani mengi yanaendelea kuvuma.+

13 Anainywesha maji milima kutoka katika vyumba vyake vya juu.+

Dunia imeshiba matunda ya kazi zako.+

14 Anafanya majani mabichi yachipuke kwa ajili ya wanyama,+

Na mimea ili itumikie wanadamu,+

Ili chakula kitokezwe duniani,+

15 Na divai ambayo hufanya moyo wa mwanadamu anayeweza kufa ushangilie,+

Kuufanya uso ung’ae kwa mafuta,+

Na mkate unaotegemeza moyo wa mwanadamu anayeweza kufa.+

16 Miti ya Yehova imeshiba,

Mierezi ya Lebanoni ambayo aliipanda.+

17 Ambamo ndege hutengeneza viota.+

Naye korongo, miberoshi ndiyo nyumba yake.+

18 Milima mirefu+ ni ya mbuzi wa milimani;+

Miamba ni kimbilio la wibari.+

19 Ameufanya mwezi kwa ajili ya nyakati zilizowekwa;+

Jua linajua vema mahali linapotua.+

20 Unasababisha giza, ili kuwe usiku;+

Katika hilo wanyama wote wa porini hutembea.

21 Wana-simba wenye manyoya shingoni wananguruma kwa ajili ya mawindo+

Na kwa ajili ya kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu mwenyewe.+

22 Jua huanza kuangaza+​—⁠nao huondoka

Nao hujilaza katika mahali pao pa kujificha.

23 Mwanadamu huuendea utendaji wake+

Na utumishi wake mpaka jioni.+

24 Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova!+

Zote umezifanya kwa hekima.+

Dunia imejaa vitu ulivyotokeza.+

25 Na kwa habari ya bahari hii iliyo kubwa na pana,+

Humo mna vitu vyenye kutambaa visivyo na hesabu,+

Viumbe hai, vidogo kwa vikubwa.+

26 Humo meli husafiri;+

Naye Lewiathani,*+ yeye umemfanyiza ili achezecheze humo.+

27 Wote hao—wanaendelea kukungojea wewe+

Ili uwape chakula chao wakati wa majira yake.+

28 Wao huokota kile unachowapa.+

Unaufungua mkono wako—wanashiba vitu vyema.+

29 Ukiuficha uso wako, wanaingiwa na wasiwasi.+

Ukiiondoa roho yao, wanakata pumzi,+

Na kurudi katika mavumbi yao.+

30 Ukiituma roho yako, wanaumbwa;+

Nawe unaufanya upya uso wa nchi.

31 Utukufu wa Yehova utakuwa mpaka wakati usio na kipimo.+

Yehova atashangilia kwa kazi zake.+

32 Anaitazama dunia, nayo inatetemeka;+

Anaigusa milima, nayo inatoa moshi.+

33 Nitamwimbia Yehova katika maisha yangu yote;+

Nitampigia Mungu wangu muziki maadamu nipo.+

34 Kutafakari kwangu juu yake na kuwe kwenye kupendeza.+

Mimi nami nitashangilia katika Yehova.+

35 Watenda-dhambi watamalizwa kabisa kutoka duniani;+

Nao waovu, hawatakuwapo tena.+

Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu. Msifuni Yah!+

105 Mshukuruni Yehova, liitieni jina lake,+

Yajulisheni matendo yake katikati ya vikundi vya watu.+

 2 Mwimbieni, mpigieni muziki,+

Jishughulisheni na kazi zake zote za ajabu.+

 3 Jisifuni katika jina lake takatifu.+

Moyo wa wale wanaomtafuta Yehova na ushangilie.+

 4 Mtafuteni Yehova na nguvu zake.+

Utafuteni uso wake daima.+

 5 Kumbukeni kazi zake za ajabu ambazo amefanya,+

Miujiza yake na maamuzi ya hukumu ya kinywa chake,+

 6 Enyi uzao wa Abrahamu mtumishi wake,+

Enyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+

 7 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+

Maamuzi yake ya hukumu yako duniani pote.+

 8 Amelikumbuka agano lake mpaka wakati usio na kipimo,+

Neno ambalo aliamuru, mpaka vizazi elfu,+

 9 Agano ambalo alifanya na Abrahamu,+

Na ahadi yake yenye kiapo aliyomwapia Isaka,+

10 Kiapo ambacho alikiendeleza kikiwa sharti kwa Yakobo,

Kama agano lenye kudumu kwa Israeli mpaka wakati usio na kipimo,+

11 Akisema: “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani+

Kuwa fungu la urithi wenu.”+

12 Huo ni wakati walipokuwa wachache,+

Naam, wachache sana, na wakaaji wageni humo.+

13 Nao wakaendelea kutembea kutoka kwa taifa moja mpaka kwa taifa lingine,+

Kutoka katika ufalme mmoja mpaka kwa kikundi kingine cha watu.+

14 Hakumruhusu binadamu yeyote awapunje,+

Bali aliwakaripia wafalme kwa sababu yao,+

15 Akisema: “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,+

Wala msiwatendee manabii wangu lolote lililo baya.”+

16 Naye akaitisha njaa juu ya nchi;+

Alivunja kila fimbo ambayo mikate ya mviringo ilining’inizwa juu yake.+

17 Akamtuma mtu mbele yao,

Ambaye aliuzwa awe mtumwa, Yosefu.+

18 Wakaitesa miguu yake kwa pingu,+

Nafsi yake ikaingia katika vyuma;+

19 Mpaka wakati neno lake lilipotimia,+

Maneno ya Yehova mwenyewe yakamsafisha.+

20 Mfalme akatuma watu ili apate kumwachilia,+

Mtawala wa vikundi vya watu, ili apate kumfungua.

21 Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake+

Na kuwa mtawala juu ya mali yake yote,+

22 Ili awafunge wakuu wake kama inavyopenda nafsi yake+

Na ili apate kuwafundisha hekima hata wanaume wake wazee.+

23 Na Israeli akaingia Misri,+

Na Yakobo mwenyewe akakaa akiwa mgeni katika nchi ya Hamu.+

24 Naye akaendelea kuwafanya watu wake wazaane sana,+

Na hatua kwa hatua akawafanya kuwa wenye uwezo kuliko adui zao.+

25 Akaiacha mioyo yao ibadilike ili kuwachukia watu wake,+

Ili wajiendeshe kwa ujanja juu ya watumishi wake.+

26 Alimtuma Musa mtumishi wake,+

Haruni aliyekuwa amemchagua.+

27 Wakaweka kati yao mambo ya ishara zake,+

Na miujiza katika nchi ya Hamu.+

28 Alituma giza na kwa hiyo akafanya kuwe na giza;+

Nao hawakuyaasi maneno yake.+

29 Aliyabadili maji yao yakawa damu,+

Akawaua samaki wao.+

30 Nchi yao ikajaa vyura,+

Katika vyumba vya ndani vya wafalme.

31 Alisema mainzi waingie,+

Na chawa katika maeneo yao yote.+

32 Aliifanya mvua yao iwe mvua ya mawe,+

Moto wenye mwali juu ya nchi.+

33 Naye akapiga mizabibu yao na mitini yao

Na kuvunja miti ya eneo lao.+

34 Akasema nzige waingie,+

Na nzige wachanga, wasio na hesabu.+

35 Nao wakala mimea yote katika nchi yao;+

Pia wakala mazao ya udongo wao.

36 Naye akapiga na kuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao,+

Mwanzo wa nguvu zao zote za uzazi.+

37 Naye akaanza kuwatoa nje wakiwa na fedha na dhahabu;+

Na katikati ya makabila yake hapakuwa na yeyote mwenye kujikwaa.

38 Misri ilishangilia walipoondoka,

Kwa maana hofu yao ilikuwa imewaangukia.+

39 Alitandaza wingu lifunike,+

Na moto utoe nuru wakati wa usiku.+

40 Waliomba, naye akaleta kware,+

Na kwa mkate kutoka mbinguni akaendelea kuwashibisha.+

41 Alifungua mwamba, na maji yakaanza kutiririka;+

Nayo yakapita katika maeneo yasiyo na maji kama mto.+

42 Kwa maana alilikumbuka neno lake takatifu kwa Abrahamu mtumishi wake.+

43 Kwa hiyo akawatoa watu wake kwa kushangilia,+

Wachaguliwa wake kwa vigelegele vya shangwe.+

44 Na hatua kwa hatua akawapa nchi za mataifa,+

Nao wakaendelea kumiliki kazi ngumu ya vikundi vya mataifa,+

45 Ili wapate kushika masharti yake+

Na kushika sheria zake.+

Msifuni Yah!+

106 Msifuni Yah!+

Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+

 2 Ni nani anayeweza kuyasema matendo yenye nguvu ya Yehova,+

Au anayeweza kufanya sifa yake yote isikiwe?+

 3 Wenye furaha ni wale wanaoshika haki,+

Wakitenda uadilifu wakati wote.+

 4 Unikumbuke, Ee Yehova, kwa nia njema kuelekea watu wako.+

Unitunze kwa wokovu wako,+

 5 Ili nipate kuona wema kwa wachaguliwa wako,+

Ili nipate kushangilia kwa shangwe ya taifa lako,+

Ili nipate kujisifu pamoja na urithi wako.+

 6 Tumetenda dhambi kama mababu zetu;+

Tumefanya kosa; tumetenda kwa uovu.+

 7 Mababu zetu huko Misri,

Hawakuonyesha ufahamu wowote katika kazi zako za ajabu.+

Hawakukumbuka wingi wa fadhili zako kuu zenye upendo,+

Bali walijiendesha kwa uasi penye bahari, kando ya Bahari Nyekundu.+

 8 Naye akawaokoa kwa ajili ya jina lake,+

Ili kufanya nguvu zake zijulikane.+

 9 Kwa hiyo akaikemea Bahari Nyekundu, nayo ikakauka hatua kwa hatua;+

Naye akawatembeza kupita katika kilindi cha maji kana kwamba ni nyikani;+

10 Na kwa hiyo akawaokoa kutoka katika mkono wa mchukiaji+

Na kuwakomboa kutoka katika mkono wa adui.+

11 Na maji yakaja kuwafunika wapinzani wao;+

Hakuna hata mmoja wao aliyebaki.+

12 Kisha wakawa na imani katika neno lake;+

Wakaanza kuimba sifa yake.+

13 Upesi wakasahau kazi zake;+

Hawakungojea shauri lake.+

14 Lakini walionyesha tamaa yao ya ubinafsi nyikani+

Na kumjaribu Mungu jangwani.+

15 Naye akawapa ombi lao+

Na kuwatumia ugonjwa unaodhoofisha ndani ya nafsi yao.+

16 Nao wakaanza kumwonea Musa wivu katika kambi,+

Hata Haruni mtakatifu wa Yehova.+

17 Kisha dunia ikafunguka na kummeza Dathani,+

Na kulifunika kusanyiko la Abiramu.+

18 Na moto ukawaka katikati ya kusanyiko lao;+

Mwali wa moto ukawateketeza waovu.+

19 Na zaidi ya hayo, wakatengeneza ndama katika Horebu+

Na kuinamia sanamu ya kuyeyushwa,+

20 Hivi kwamba wakabadili utukufu wangu+

Kwa ajili ya mfano wa ng’ombe mwenye kula majani.+

21 Walimsahau Mungu Mwokozi wao,+

Mtendaji wa mambo makuu nchini Misri,+

22 Kazi za ajabu katika nchi ya Hamu,+

Mambo yenye kuogopesha kwenye Bahari Nyekundu.+

23 Naye alikuwa karibu kusema waangamizwe,+

Isingalikuwa ni kwa sababu ya Musa mchaguliwa wake,

Aliyesimama penye mwanya mbele zake,+

Ili kuigeuza ghadhabu yake asiwaharibu.+

24 Nao wakaichukia nchi yenye kutamanika;+

Hawakuwa na imani katika neno lake.+

25 Nao wakaendelea kunung’unika katika mahema yao;+

Hawakuisikiliza sauti ya Yehova.+

26 Kwa hiyo akainua mkono wake katika kiapo juu yao,+

Kwamba angewafanya waanguke nyikani,+

27 Na kwamba angefanya uzao wao uanguke kati ya mataifa,+

Na kwamba angewatawanya katika nchi mbalimbali.+

28 Nao wakaanza kujishikamanisha na Baali wa Peori+

Na kula dhabihu za wafu.+

29 Walipokuwa wakisababisha uchungu kwa matendo yao,+

Tauni ikazuka katikati yao.+

30 Finehasi aliposimama na kuingilia kati,+

Ndipo tauni ikazuiwa.

31 Na ikahesabiwa kwake kuwa ni uadilifu

Kwa kizazi baada ya kizazi mpaka wakati usio na kipimo.+

32 Tena, wakafanya uchokozi katika maji ya Meriba,+

Hivi kwamba mambo yakamwendea Musa vibaya kwa sababu yao.+

33 Kwa maana waliitia uchungu roho yake

Naye akaanza kusema kwa midomo yake bila kufikiri.+

34 Hawakuangamiza vikundi vya watu,+

Kama Yehova alivyokuwa amewaambia.+

35 Nao wakachangamana na hayo mataifa+

Na kuanza kujifunza matendo yao.+

36 Nao waliendelea kutumikia sanamu zao,+

Nazo zikawa mtego kwao.+

37 Nao wakawa wakiwatoa dhabihu wana wao+

Na binti zao kwa roho waovu.+

38 Kwa hiyo wakaendelea kumwaga damu isiyo na hatia,+

Damu ya wana wao na binti zao,

Ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani;+

Na nchi ikachafuliwa na umwagaji wa damu.+

39 Nao wakawa wasio safi kwa sababu ya kazi zao+

Na wakaendelea kufanya uasherati kwa matendo yao.+

40 Na hasira ya Yehova ikaanza kuwaka juu ya watu wake;+

Naye akaja kuuchukia urithi wake.+

41 Naye akawatia mkononi mwa mataifa tena na tena,+

Ili wale wanaowachukia wapate kutawala juu yao,+

42 Na ili adui zao wapate kuwakandamiza,

Na ili wapate kutiishwa chini ya mkono wao.+

43 Akawakomboa mara nyingi,+

Lakini wao wakawa wakijiendesha kwa uasi katika mwendo wao wa kutokutii,+

Nao wakashushwa kwa sababu ya kosa lao.+

44 Naye akaiona taabu yao+

Alipokisikia kilio chao cha kusihi.+

45 Naye akalikumbuka agano lake juu yao,+

Naye akajuta kulingana na wingi wa fadhili zake kuu zenye upendo.+

46 Naye akawa akiwafanya wahurumiwe

Mbele ya wale wote waliokuwa wamewashika mateka.+

47 Utuokoe, Ee Yehova Mungu wetu,+

Na utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa+

Ili tulishukuru jina lako takatifu,+

Ili tukusifu kwa shangwe.+

48 Na abarikiwe Yehova Mungu wa Israeli+

kutoka wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo;+

Na watu wote waseme Amina.+

Msifuni Yah!

KITABU CHA TANO

(Zaburi 107 – 150)

107 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+

 2 Wote waliookolewa wa Yehova na waseme hivyo,+

Ambao amewaokoa kutoka katika mkono wa adui,+

 3 Na ambao amewakusanya pamoja kutoka katika nchi mbalimbali,+

Kutoka mashariki na kutoka magharibi,+

Kutoka kaskazini na kutoka kusini.+

 4 Walitanga-tanga nyikani,+ jangwani;+

Hawakupata njia yoyote ya kwenda kwenye jiji la kukaa.+

 5 Walikuwa na njaa, na kiu pia;+

Nafsi yao ndani yao ikaanza kuzimia.+

 6 Nao wakaendelea kumlilia Yehova katika taabu yao;+

Akawakomboa kutoka katika mikazo iliyokuwa juu yao,+

 7 Na kuwatembeza katika njia iliyo sawa,+

Ili waingie katika jiji la kukaa.+

 8 Watu na wamtolee Yehova shukrani kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo+

Na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.+

 9 Kwa maana ameishibisha nafsi iliyokauka;+

Na nafsi yenye njaa ameijaza vitu vyema.+

10 Kuna wale waliokuwa wakikaa katika giza na kivuli kizito,+

Wafungwa katika mateso na vyuma.+

11 Kwa maana waliyaasi+ maneno ya Mungu;+

Na shauri la Aliye Juu Zaidi hawakuwa wameliheshimu.+

12 Kwa hiyo, akautiisha moyo wao kwa taabu;+

Walijikwaa, wala hapakuwa na mtu mwenye kusaidia.+

13 Nao wakaanza kumwomba Yehova msaada katika taabu yao;+

Na kutoka katika mikazo iliyokuwa juu yao yeye akawaokoa kama kawaida.+

14 Akawatoa katika giza na kivuli kizito,+

Na hata kuzikata pingu zao.+

15 Watu na wamshukuru Yehova kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo+

Na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.+

16 Kwa maana ameivunja milango ya shaba,+

Naye ameyakata hata mapingo ya chuma.+

17 Wale waliokuwa wapumbavu, kwa sababu ya njia ya ukosaji wao+

Na kwa sababu ya makosa yao, mwishowe walijiletea mateso wenyewe.+

18 Nafsi yao ikachukia kila namna ya chakula,+

Nao wakayafikia malango ya kifo.+

19 Nao wakaanza kumwomba Yehova msaada katika taabu yao;+

Na kutoka katika mikazo iliyokuwa juu yao akawaokoa kama kawaida.+

20 Akatuma neno lake na kuwaponya+

Na kuwaokoa kutoka katika mashimo yao.+

21 Watu na wamshukuru Yehova kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo+

Na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.+

22 Na watoe dhabihu za kutoa shukrani+

Na kutangaza kazi zake kwa vigelegele vya shangwe.+

23 Wale wanaoshuka baharini kwa meli,+

Wanaofanya biashara katika maji mengi,+

24 Hao ndio ambao wameziona kazi za Yehova+

Na kazi zake za ajabu vilindini;+

25 Jinsi anavyosema neno na kutokeza upepo wenye tufani,+

Hivi kwamba unainua mawimbi yake.+

26 Wao hupanda juu mbinguni,

Hushuka mpaka chini.

Kwa sababu ya msiba nafsi yao hujikuta inayeyuka.+

27 Wanayumba-yumba na kwenda huku na huku kama mlevi,+

Na hata hekima yao yote huvurugika.+

28 Nao huanza kumpaazia Yehova kilio katika taabu yao,+

Naye huwatoa katika mikazo iliyo juu yao.+

29 Huituliza dhoruba ya upepo ikawa kimya,+

Hivi kwamba mawimbi ya bahari hukaa kimya.+

30 Nao hushangilia kwa sababu yanatulia,

Naye huwapeleka kwenye bandari inayowapendeza.+

31 Watu na wamtolee Yehova shukrani kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo+

Na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.+

32 Na wamtukuze katika kutaniko la watu;+

Na katika kikao cha wazee na wampe sifa.+

33 Yeye huigeuza mito iwe nyika,+

Na chemchemi za maji ziwe nchi yenye ukame,+

34 Nchi yenye kuzaa iwe nchi ya chumvi,+

Kwa sababu ya ubaya wa wale wanaokaa humo.

35 Huigeuza nyika iwe dimbwi la maji lenye matete,+

Na nchi ya eneo lisilo na maji iwe chemchemi za maji.+

36 Na huko huwafanya wenye njaa wakae,+

Hivi kwamba wanasimamisha imara jiji la kukaa.+

37 Nao hupanda mbegu viwanjani na kupanda mashamba ya mizabibu,+

Ili yapate kutokeza mimea yenye kutoa mazao.+

38 Naye huwabariki hivi kwamba wanakuwa wengi sana;+

Wala haachi ng’ombe wao wawe wachache.+

39 Tena wanakuwa wachache na kuchutama+

Kwa sababu ya kizuizi, msiba na huzuni.+

40 Anamwaga dharau juu ya watu wenye vyeo,+

Hivi kwamba anawafanya watange-tange katika mahali penye ukiwa, pasipo na njia.+

41 Lakini humlinda maskini kutokana na mateso+

Na kumgeuza kuwa familia nyingi kama kundi.+

42 Wanyoofu huona na kushangilia;+

Lakini ukosefu wote wa uadilifu utafunga kinywa chake.+

43 Ni nani mwenye hekima? Atayashika mambo

hayo+

Na kukaza fikira zake kwa matendo ya Yehova ya fadhili zenye upendo.+

Wimbo. Muziki wa Daudi.

108 Ee Mungu, moyo wangu uko imara.+

Nitaimba na kupiga muziki,+

Naam, utukufu wangu.+

 2 Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.+

Nitayaamsha mapambazuko.+

 3 Nitakusifu katikati ya vikundi vya watu, Ee Yehova;+

Nami nitakupigia muziki katikati ya vikundi vya mataifa+

 4 Kwa maana fadhili zako zenye upendo ni kuu mpaka mbinguni,+

Na ukweli wako mpaka angani.+

 5 Utukuzwe juu ya mbingu, Ee Mungu;+

Na utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+

 6 Ili wapendwa wako waokolewe,+

Ee, uokoe kwa mkono wako wa kuume na kunijibu.+

 7 Mungu mwenyewe amesema katika utakatifu wake:+

“Nitashangilia, nitamgawanya Shekemu+ awe fungu;+

Na nchi tambarare ya chini ya Sukothi+ nitaipima.

 8 Gileadi+ ni yangu; Manase+ ni yangu;

Na Efraimu ni ngome ya aliye mkuu wangu;+

Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+

 9 Moabu+ ni chungu changu cha kuoshea.+

Nitatupa kiatu+ changu juu ya Edomu.+

Nitapiga kelele za ushindi+ juu ya Ufilisti.”+

10 Ni nani atakayenipeleka kwenye jiji lenye ngome?+

Ni nani ambaye kwa kweli ataniongoza mpaka Edomu?+

11 Je, si wewe, Ee Mungu ambaye umetutupilia mbali+

Na ambaye huendi pamoja na majeshi yetu ukiwa Mungu?+

12 Utusaidie kutokana na taabu,+

Kwa maana wokovu wa mtu wa udongo haufai kitu.+

13 Mungu atatuwezesha kupata nguvu,+

Na yeye mwenyewe atawakanyagia chini wapinzani wetu.+

Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.

109 Ee Mungu wa sifa yangu,+ usikae kimya.+

 2 Kwa maana kinywa cha mwovu na kinywa cha udanganyifu vimefunguka juu yangu.+

Wamesema juu yangu kwa ulimi wa uwongo;+

 3 Na kwa maneno ya chuki wamenizingira,+

Nao wanaendelea kupigana nami bila sababu.+

 4 Wanaendelea kunipinga kwa sababu ya upendo wangu;+

Lakini kwangu kuna sala.+

 5 Nao wananitendea mabaya kwa yaliyo mema+

Na chuki kwa upendo wangu.+

 6 Mweke mtu mwovu juu yake,

Na mpinzani+ aendelee kusimama kwenye mkono wake wa kuume.

 7 Anapohukumiwa, na aende zake kama mwovu;

Na sala yake na iwe dhambi.+

 8 Siku zake na ziwe chache;+

Cheo chake cha uangalizi mtu mwingine na akichukue.+

 9 Wanawe na wawe wavulana wasio na baba+

Na mke wake awe mjane.+

10 Na wanawe watange-tange;+

Nao waombe-ombe,

Nao watafute chakula kutoka katika mahali pao penye ukiwa.+

11 Mla-riba na aweke mitego kwa ajili ya vyote alivyo navyo,+

Na wageni+ wapore mazao yake ya kazi ya taabu.+

12 Na akose mtu wa kumwonyesha fadhili zenye upendo,+

Wala kusiwe na mtu anayewaonyesha kibali wavulana wake wasio na baba.

13 Wazao wake na wakatiliwe mbali.+

Katika kizazi kinachofuata jina lao na lifutiliwe mbali.+

14 Kosa la mababu zao na likumbukwe na Yehova,+

Na dhambi ya mama yake+—isifutiliwe mbali.+

15 Na wawe mbele za Yehova daima;+

Naye akatilie mbali kumbukumbu lao kutoka duniani;+

16 Kwa sababu hakukumbuka kuonyesha fadhili zenye upendo,+

Bali aliendelea kumfuatilia mtu mwenye kuteseka na aliye maskini+

Na mwenye huzuni moyoni, ili kumuua.+

17 Naye aliendelea kuipenda laana,+ hivi kwamba ikamjia;+

Wala hakupendezwa na baraka,+

Hivi kwamba ikawa mbali naye;+

18 Naye akavikwa laana kuwa vazi lake.+

Kwa hiyo ikaja kama maji katikati yake+

Na kama mafuta ndani ya mifupa yake.

19 Na iwe kwake kama vazi ambalo yeye huvaa+

Na kama mshipi ambao yeye huendelea kujifunga daima.+

20 Hayo ndiyo malipo yanayotoka kwa Yehova ya mtu anayenipinga+

Na ya wale wanaosema maovu juu ya nafsi yangu.+

21 Lakini wewe ni Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu.+

Nitendee kwa ajili ya jina lako.+

Kwa sababu fadhili zako zenye upendo ni njema, unikomboe.+

22 Kwa maana nateseka nami ni maskini,+

Na moyo wangu umechomwa ndani yangu.+

23 Kama wakati kivuli kinapopungua, mimi nalazimika kwenda zangu;+

Nimekung’utwa kama nzige.

24 Magoti yangu yametetemeka kwa sababu ya kufunga,+

Na mwili wangu umekonda, bila kuwa na mafuta yoyote.+

25 Na kwao mimi nimekuwa kitu cha kushutumiwa.+

Wananiona—wanaanza kutikisa kichwa chao.+

26 Unisaidie, Ee Yehova Mungu wangu;+

Uniokoe kulingana na fadhili zako zenye upendo.+

27 Na wapate kujua ya kwamba huu ni mkono wako;+

Kwamba ni wewe mwenyewe, Ee Yehova, ambaye umelitenda.+

28 Wao na watangaze laana,+

Lakini wewe utangaze baraka.+

Wamesimama, lakini acha waone aibu,+

Na mtumishi wako na ashangilie.+

29 Wale wanaonipinga na wavikwe fedheha,+

Na acha wavae wenyewe aibu yao kana kwamba ni koti lisilo na mikono.+

30 Nitamsifu sana Yehova kwa kinywa changu,+

Na katikati ya watu wengi nitamsifu.+

31 Kwa maana yeye atasimama kwenye mkono wa kuume wa maskini,+

Ili amwokoe kutoka kwa wale wanaoihukumu nafsi yake.

Ya Daudi. Muziki.

110 Neno la Yehova kwa Bwana wangu ni:+

“Keti kwenye mkono wangu wa kuume+

Mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako.”+

2 Yehova ataituma fimbo+ ya nguvu zako kutoka Sayuni,+ akisema:

“Nenda ukitiisha katikati ya adui zako.”+

 3 Watu wako+ watajitoa kwa hiari+ katika siku ya jeshi lako.+

Katika fahari za utakatifu,+ kutoka tumbo la uzazi la mapambazuko,

Una kundi lako la vijana kama matone ya

umande.+

 4 Yehova ameapa+ (naye hatajuta):+

“Wewe ni kuhani mpaka wakati usio na kipimo+

Kwa mfano wa Melkizedeki!”+

 5 Yehova mwenyewe akiwa upande wako wa mkono wa kuume+

Hakika atawavunja vipande-vipande wafalme katika siku ya hasira yake.+

 6 Atatekeleza hukumu katikati ya mataifa;+

Atafanya maiti zijae.+

Hakika atamvunja vipande-vipande aliye kichwa juu ya nchi yenye hesabu kubwa ya watu.+

 7 Kutoka katika bonde la mto njiani atakunywa.+

Ndiyo sababu atakiinua kichwa chake juu.+

111 Msifuni Yah!+

א [ʼAʹleph]

Nitamsifu Yehova kwa moyo wangu wote+

ב [Behth]

Katika kikundi cha rafiki za karibu+ walio wanyoofu na katika kusanyiko.+

ג [Giʹmel]

 2 Kazi za Yehova ni kuu,+

ד [Daʹleth]

Zinazotafutwa na wale wote wanaopendezwa nazo.+

ה [Heʼ]

 3 Utendaji+ wake ni utukufu na fahari,+

ו [Waw]

Na uadilifu wake unasimama milele.+

ז [Zaʹyin]

 4 Amefanya ukumbusho kwa ajili ya kazi zake za ajabu.+

ח [Chehth]

Yehova ni mwenye neema na mwenye rehema.+

ט [Tehth]

 5 Amewapa chakula wale wanaomwogopa.+

י [Yohdh]

Mpaka wakati usio na kipimo, atalikumbuka agano lake.+

כ [Kaph]

 6 Nguvu za kazi zake amewatangazia watu wake,+

ל [Laʹmedh]

Kwa kuwapa urithi wa mataifa.+

מ [Mem]

 7 Kazi za mikono yake ni kweli na hukumu;+

נ [Nun]

Maagizo yake yote anayotoa ni yenye kutegemeka,+

ס [Saʹmekh]

 8 Yanategemezwa vema milele, mpaka wakati usio na kipimo,+

ע [ʽAʹyin]

Yanafanywa katika kweli na unyoofu.+

פ [Peʼ]

 9 Ameutuma ukombozi kwa watu wake.+

צ [Tsa·dhehʹ]

Mpaka wakati usio na kipimo ameamuru agano lake.+

ק [Qohph]

Jina lake ni takatifu na lenye kuogopesha.+

ר [Rehsh]

10 Kumwogopa Yehova ni mwanzo wa hekima.+

ש [Sin]

Wale wote wanaoyatenda maagizo yake wana ufahamu mwema.+

ת [Taw]

Sifa yake inasimama milele.+

112 Msifuni Yah!+

א [ʼAʹleph]  

Mwenye furaha ni mtu anayemwogopa Yehova,+

ב [Behth]

Ambaye amependezwa+ sana na amri zake.+

ג [Giʹmel]

 2 Uzao wake utakuwa wenye nguvu duniani.+

ד [Daʹleth]

Nacho kizazi cha wanyoofu, kitabarikiwa.+

ה [Heʼ]

 3 Vitu vyenye thamani na utajiri vimo nyumbani mwake;+

ו [Waw]

Nao uadilifu wake unasimama milele.+

ז [Zaʹyin]

 4 Ameangaza katika giza kama nuru kwa walio wanyoofu.+

ח [Chehth]

Yeye ni mwenye neema na mwenye rehema na mwadilifu.+

ט [Tehth]

 5 Mtu mwenye neema+ na anayekopesha+ ni mwema.

י [Yohdh]

Yeye hutegemeza mambo yake kwa haki.+

כ [Kaph]

 6 Kwa kuwa hatatikiswa kamwe.+

ל [Laʹmedh]

Mwadilifu atakuwa kumbukumbu mpaka wakati usio na kipimo.+

מ [Mem]

 7 Hataogopa hata habari mbaya.+

נ [Nun]

Moyo wake ni imara,+ umefanywa umtegemee Yehova.+

ס [Saʹmekh]

 8 Moyo wake hauwezi kutikiswa;+ hataogopa,+

ע [ʽAʹyin]

Mpaka awatazame wapinzani wake.+

פ [Peʼ]

 9 Amegawa kwa wingi; amewapa maskini.+

צ [Tsa·dhehʹ]

Uadilifu wake unasimama milele.+

ק [Qohph]

Pembe yake mwenyewe itainuliwa kwa utukufu.+

ר [Rehsh]

10 Mwovu ataona na hakika atakasirika.+

ש [Shin]

Atasaga meno yake na kuyeyuka.+

ת [Taw]

Tamaa ya waovu itaangamia.+

113 Msifuni Yah!+

Toeni sifa, enyi watumishi wa Yehova,+

Lisifuni jina la Yehova.+

 2 Jina la Yehova na libarikiwe+

Kutoka sasa mpaka wakati usio na kipimo.+

 3 Kutoka mapambazuko ya jua mpaka kutua kwake+

Jina la Yehova ni la kusifiwa.+

 4 Yehova amekuwa juu ya mataifa yote;+

Utukufu wake uko juu ya mbingu.+

 5 Ni nani aliye kama Yehova Mungu wetu,+

Yeye anayefanya makao yake juu?+

 6 Yeye anajishusha kutazama mbingu na dunia,+

 7 Akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka kwenye mavumbi;+

Humwinua maskini kutoka kwenye shimo la majivu,+

 8 Ili kumketisha pamoja na wenye vyeo,+

Wenye vyeo kati ya watu wake.+

 9 Anampa mwanamke tasa makao katika nyumba+

Kama mama ya wana aliye na shangwe.+

Msifuni Yah!+

114 Israeli alipotoka Misri,+

Nyumba ya Yakobo kutoka kwenye kikundi cha watu wanaosema maneno yasiyoeleweka,+

 2 Yuda ikawa mahali pake patakatifu,+

Israeli miliki yake kuu.+

 3 Bahari iliona na kukimbia;+

Yordani nao ulianza kurudi nyuma.+

 4 Milima ilirukaruka kama kondoo-dume,+

Vilima kama wana-kondoo.

 5 Ulikuwa na nini, Ee bahari, hata ukakimbia,+

Ee Yordani, hata ukaanza kurudi nyuma?+

 6 Enyi milima, hata mkarukaruka kama kondoo-dume;+

Enyi vilima, kama wana-kondoo?+

 7 Kwa sababu ya Bwana uwe na maumivu makali, Ee dunia,+

Kwa sababu ya Mungu wa Yakobo.

 8 Ambaye anabadili mwamba kuwa dimbwi la maji lenye matete,+

Jiwe gumu kuwa bubujiko la maji.+

115 Sisi hatuna chochote, Ee Yehova, sisi hatuna chochote,+

Bali jina lako ulitukuze+

Kulingana na fadhili zako zenye upendo, kulingana na ukweli wako.+

 2 Kwa nini mataifa yaseme:+

“Yuko wapi, sasa, Mungu wao?”+

 3 Lakini Mungu wetu yuko mbinguni;+

Kila kitu ambacho alipendezwa kufanya, amekifanya.+

 4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu,+

Kazi ya mikono ya mtu wa udongo.+

 5 Zina kinywa, lakini haziwezi kusema;+

Zina macho, lakini haziwezi kuona;+

 6 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia.+

Zina pua, lakini haziwezi kunusa.+

 7 Zina mikono, lakini haziwezi kugusa.+

Zina miguu, lakini haziwezi kutembea;+

Hazitoi sauti yoyote kwa koo zao.+

 8 Wale wanaozifanya watakuwa kama hizo,+

Wale wote wanaozitegemea.+

 9 Ee Israeli, mtegemeeni Yehova;+

Yeye ndiye msaada wao na ngao yao.+

10 Ee nyumba ya Haruni, mtegemeeni Yehova;+

Yeye ndiye msaada wao na ngao yao.+

11 Ninyi mnaomwogopa Yehova, mtegemeeni Yehova;+

Yeye ndiye msaada wao na ngao yao.+

12 Yehova mwenyewe ametukumbuka; atatoa baraka,+

Ataibariki nyumba ya Israeli,+

Ataibariki nyumba ya Haruni.+

13 Atawabariki wale wanaomwogopa Yehova,+

Wadogo kwa wakubwa.+

14 Yehova atawapa ninyi ongezeko,+

Ninyi na wana wenu.+

15 Ninyi ndio mliobarikiwa na Yehova,+

Mtengenezaji wa mbingu na dunia.+

16 Mbingu ni mbingu za Yehova,+

Bali dunia amewapa wana wa binadamu.+

17 Wafu wenyewe hawamsifu Yah,+

Wala wowote wanaoingia mahali penye kimya.+

18 Lakini sisi wenyewe tutambariki Yah+

Kutoka sasa mpaka wakati usio na kipimo.+

Msifuni Yah!+

116 Ninajawa na upendo, kwa sababu Yehova husikia+

Sauti yangu, kusihi kwangu.+

 2 Kwa maana yeye amenitegea sikio lake,+

Nami nitaita siku zangu zote.+

 3 Kamba za kifo zilinizunguka+

Na hali zenye kutaabisha za Kaburi* zikanipata.+

Nikaendelea kupata taabu na huzuni.+

 4 Lakini nikaliitia jina la Yehova:+

“Ah, Yehova, uiokoe nafsi yangu!”+

 5 Yehova ni mwenye neema na ni mwadilifu;+

Naye Mungu wetu, Yeye ni mwenye kuonyesha rehema.+

 6 Yehova anawalinda wasio na uzoefu.+

Nilikuwa maskini, naye akaniokoa.+

 7 Rudi mahali pako pa kupumzika, Ee nafsi yangu,+

Kwa maana Yehova mwenyewe amekutendea inavyofaa.+

 8 Kwa maana umeiokoa nafsi yangu kutokana na kifo,+

Jicho langu kutokana na machozi, mguu wangu kutokana na kujikwaa.+

 9 Nitatembea+ mbele za Yehova katika nchi za walio hai.+

10 Nilikuwa na imani,+ kwa maana nilisema.+

Mimi mwenyewe nilikuwa nimeteseka sana.

11 Mimi mwenyewe nilisema, wakati nilipokuwa na wasiwasi mkubwa:+

“Kila mwanadamu ni mwongo.”+

12 Nitamlipa Yehova nini+

Kwa ajili ya faida zake zote kwangu?+

13 Nitakichukua kikombe cha wokovu mkuu,+

Nami nitaliitia jina la Yehova.+

14 Nadhiri zangu nitamtimizia Yehova,+

Naam, mbele ya watu wake wote.

15 Ni chenye thamani machoni pa Yehova

Kifo cha washikamanifu wake.+

16 Ah, sasa, Ee Yehova,+

Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+

Mimi ni mtumishi wako, mwana wa kijakazi wako.+

Umezifungua pingu zangu.+

17 Nitakutolea wewe dhabihu ya kutoa shukrani,+

Nami nitaliitia jina la Yehova.+

18 Nadhiri zangu nitamtimizia Yehova,+

Naam, mbele ya watu wake wote,+

19 Katika nyua za nyumba ya Yehova,+

Katikati yako, Ee Yerusalemu.+

Msifuni Yah!+

117 Msifuni Yehova, enyi mataifa yote;+

Mtukuzeni, enyi jamii zote.+

 2 Kwa maana fadhili zake zenye upendo zimekuwa zenye nguvu kwetu sisi;+

Na ukweli+ wa Yehova ni wa mpaka wakati usio na kipimo.

Msifuni Yah!+

118 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+

 2 Israeli na aseme sasa:

“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+

 3 Wale wa nyumba ya Haruni na waseme sasa:+

“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+

 4 Wale wanaomwogopa Yehova na waseme sasa:+

“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+

 5 Kutoka katika hali zenye kutaabisha nilimwitia Yah;+

Yah akanijibu na kuniweka katika mahali penye nafasi pana.+

 6 Yehova yuko upande wangu; sitaogopa.+

Mtu wa udongo anaweza kunitenda nini?+

 7 Yehova yuko upande wangu kati ya wale wanaonisaidia,+

Hivi kwamba mimi nitawatazama wale wanaonichukia.+

 8 Ni afadhali kupata kimbilio katika Yehova+

Kuliko kumtegemea mtu wa udongo.+

 9 Ni afadhali kupata kimbilio katika Yehova+

Kuliko kuwategemea watu wenye vyeo.+

10 Mataifa yote yalinizunguka.+

Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova.+

11 Walinizingira, naam, walikuwa wamenizingira.+

Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova.

12 Walinizunguka kama nyuki;+

Walizimwa kama moto wa vichaka vya miiba.+

Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova.+

13 Ulinisukuma kwa nguvu ili nianguke,+

Lakini Yehova mwenyewe alinisaidia.+

14 Yah ni kinga yangu na nguvu zangu,+

Naye huwa wokovu kwangu.+

15 Sauti ya vigelegele vya shangwe na wokovu+

Imo katika mahema+ ya waadilifu.+

Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu.+

16 Mkono wa kuume wa Yehova unajiinua;+

Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu.+

17 Sitakufa, bali nitaendelea kuishi,+

Ili nizitangaze kazi za Yah.+

18 Yah alinirekebisha vikali,+

Lakini hakunitia mikononi mwa kifo.+

19 Nifungulieni malango ya uadilifu.+

Mimi nitayaingia; nitamsifu Yah.+

20 Hili ndilo lango la Yehova.+

Waadilifu wataliingia.+

21 Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+

Nawe ukawa wokovu wangu.+

22 Jiwe ambalo wajenzi walilikataa+

Limekuwa jiwe kuu la pembeni.+

23 Hili limetokana na Yehova mwenyewe;+

Ni la ajabu machoni petu.+

24 Hii ndiyo siku ambayo Yehova ameifanya;+

Tutaishangilia na kuifurahia.+

25 Ah, sasa, Yehova, uokoe, tafadhali!+

Ah, sasa, Yehova, ufanikishe, tafadhali!+

26 Na abarikiwe Yeye anayekuja katika jina la Yehova;+

Tumewabariki ninyi watu kutoka katika nyumba ya Yehova.+

27 Yehova ndiye Mungu,+

Naye hutupa nuru.+

Fungeni maandamano ya sherehe+ kwa matawi,+

Mpaka kwenye pembe za madhabahu.+

28 Wewe ni Mungu wangu, nami nitakusifu;+

Mungu wangu⁠—​nitakutukuza.+

29 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+

א [ʼAʹleph]

119 Wenye furaha ni wale wasio na kosa katika njia yao,+

Wale wanaotembea katika sheria ya Yehova.+

 2 Wenye furaha ni wale wanaoshika vikumbusho vyake;+

Wanaendelea kumtafuta kwa moyo wote.+

 3 Kwa kweli hawakuzoea kufanya ukosefu wowote wa uadilifu.+

Wametembea katika njia zake.+

 4 Wewe mwenyewe umetoa maagizo yako kwa kuamuru+

Yashikwe kwa uangalifu.+

 5 Laiti njia zangu zingefanywa imara+

Ili kushika masharti yako!+

 6 Ndipo singeona aibu,+

Ninapozitazama amri zako zote.+

 7 Nitakusifu katika unyoofu wa moyo,+

Ninapojifunza maamuzi yako ya hukumu yaliyo ya uadilifu.+

 8 Ninaendelea kushika masharti yako.+

Ee, usiniache kabisa.+

ב [Behth]

 9 Kijana+ ataisafishaje njia yake?

Kwa kujilinda kulingana na neno lako.+

 10 Nimekutafuta kwa moyo wangu wote.+

Usinipotoshe niache amri zako.+

 11 Moyoni mwangu nimeweka hazina ya maneno yako,+

Ili nisikutendee dhambi.+

 12 Umebarikiwa, Ee Yehova.

Unifundishe masharti yako.+

 13 Kwa midomo yangu nimetangaza+

Maamuzi yote ya hukumu ya kinywa chako.+

 14 Nimeshangilia katika njia ya vikumbusho vyako,+

Kama vile katika mambo mengine yote yenye thamani.+

 15 Nitajishughulisha na maagizo yako,+

Nami nitayatazama mapito yako.+

 16 Nitazipenda sheria zako.+

Sitalisahau neno lako.+

ג [Giʹmel]

 17 Umtendee mtumishi wako inavyofaa, ili nipate kuishi+

Na ili nipate kulishika neno lako.+

 18 Ufunue macho yangu, ili nipate kutazama+

Mambo ya ajabu kutoka katika sheria yako.+

 19 Mimi ni mkaaji mgeni tu katika nchi.+

Usinifiche amri zako.+

 20 Nafsi yangu imepondeka kwa kutamani+

Maamuzi yako ya hukumu wakati wote.+

 21 Umewakemea wenye kimbelembele waliolaaniwa,+

Ambao wanaziacha amri zako.+

 22 Niondolee shutuma na dharau,+

Kwa maana nimeshika vikumbusho vyako.+

 23 Hata wakuu wameketi; Wamesemezana dhidi yangu.+

Naye mtumishi wako, anajishughulisha na masharti yako.+

 24 Pia, ninavipenda vikumbusho vyako,+

Ni kama wanaume wa shauri langu.+

ד [Daʹleth]

 25 Nafsi yangu imekuwa ikishikamana na mavumbi.+

Nihifadhi hai kulingana na neno lako.+

 26 Nimezitangaza njia zangu mwenyewe, ili unijibu.+

Unifundishe masharti yako.+

 27 Unifanye nielewe njia ya maagizo yako mwenyewe,+

Ili nipate kujishughulisha na kazi zako za ajabu.+

 28 Nafsi yangu imekosa usingizi kwa sababu ya huzuni.+

Uniinue kulingana na neno lako.+

 29 Uniondolee njia ya uwongo,+

Na kunipa kibali kwa sheria yako.+

 30 Nimeichagua njia ya uaminifu.+

Nimeyaona maamuzi yako ya hukumu kuwa yenye kufaa.+

 31 Nimeshikamana na vikumbusho vyako.+

Ee Yehova, usiniaibishe.+

 32 Nitakimbia kwenye njia ya amri zako,+

Kwa sababu wewe huufanya moyo wangu upate nafasi.+

ה [Heʼ]

 33 Unifundishe, Ee Yehova, njia ya masharti yako,+

Ili nipate kuishika hata ile ya mwisho.+

 34 Unifanye nielewe, ili nipate kuishika sheria yako+

Nami nipate kuishika kwa moyo wote.+

 35 Unitembeze katika njia ya amri zako,+

Kwa maana nimependezwa nayo.+

 36 Uelekeze moyo wangu kwa vikumbusho vyako,+

Wala si kwa faida.+

 37 Uyafanye macho yangu yapite ili yasione jambo lisilofaa;+

Unihifadhi hai katika njia yako mwenyewe.+

 38 Umtimizie mtumishi wako maneno yako+

Ambayo yanamwelekeza kukuogopa wewe.+

 39 Ufanye shutuma yangu ipitilie mbali, ambayo nimeiogopa,+

Kwa maana maamuzi yako ya hukumu ni mema.+

 40 Tazama! nimeyatamani maagizo yako.+

Unihifadhi hai katika uadilifu wako.+

ו [Waw]

 41 Na fadhili zako zenye upendo na zinijie, Ee Yehova,+

Wokovu wako kulingana na maneno yako,+

 42 Nipate kumjibu yeye anayenishutumu kwa neno,+

Kwa maana nimelitegemea neno lako.+

 43 Wala usiondoe kabisa neno la kweli kutoka kinywani mwangu,+

Kwa maana nimengojea uamuzi wako mwenyewe wa hukumu.+

 44 Nami nitaishika sheria yako daima,+

Mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

 45 Nami nitatembea huku na huku katika mahali penye nafasi tele,+

Kwa maana nimeyatafuta maagizo yako.+

 46 Pia nitasema juu ya vikumbusho vyako mbele ya wafalme,+

Wala sitaona aibu.+

 47 Nami nitapendezwa na amri zako+

Ambazo nimezipenda.+

 48 Nami nitainua mikono yangu kwenye amri zako ambazo nimezipenda,+

Nami nitajishughulisha mwenyewe na masharti yako.+

ז [Zaʹyin]

 49 Ulikumbuke neno lako kwa mtumishi wako,+

Ambalo umenifanya nilingojee.+

 50 Hii ndiyo faraja yangu katika mateso yangu,+

Kwa maana maneno yako mwenyewe yamenihifadhi hai.+

 51 Wenye kimbelembele wamenidharau kupindukia.+

Sijageuka kando kutoka kwenye sheria yako.+

 52 Nimeyakumbuka maamuzi yako ya hukumu tangu wakati usio na kipimo, Ee Yehova,+

Nami najipatia faraja.+

 53 Hasira inayowaka imenishika kwa sababu ya waovu,+

Wanaoiacha sheria yako.+

 54 Masharti yako yamekuwa muziki kwangu+

Katika nyumba ya makao yangu ya kigeni.+

 55 Nimekumbuka jina lako usiku, Ee Yehova,+

Ili nipate kuishika sheria yako.+

 56 Yote hayo yamekuwa yangu,

Kwa sababu nimeyashika maagizo yako.+

ח [Chehth]

 57 Yehova ni fungu langu;+

Nimeahidi kuyashika maneno yako.+

 58 Nimeutuliza uso wako kwa moyo wangu wote.+

Unionyeshe kibali kulingana na maneno yako.+

 59 Nimezifikiria njia zangu,+

Ili nipate kuirudisha miguu yangu kwenye vikumbusho vyako.+

 60 Nilifanya haraka, nami sikukawia+

Kuzishika amri zako.+

 61 Kamba za waovu zilinizingira.+

Sikuisahau sheria yako.+

 62 Katikati ya usiku mimi huamka ili kukushukuru+

Kwa ajili ya maamuzi yako ya hukumu ya uadilifu.+

 63 Mimi ni mwenzao watu wote wanaokuogopa wewe,+

Na wale wanaoyashika maagizo yako.+

 64 Fadhili zako zenye upendo, Ee Yehova, zimeijaza dunia.+

Unifundishe masharti yako mwenyewe.+

ט [Tehth]

 65 Umemtendea mtumishi wako vema,+

Ee Yehova, kulingana na neno lako.+

 66 Unifundishe wema,+ kuwa na akili+ na ujuzi,+

Kwa maana nimeonyesha imani katika amri zako.+

 67 Kabla ya kuteseka nilikuwa nikifanya dhambi bila kukusudia,+

Bali sasa nimelishika neno lako.+

 68 Wewe ni mwema nawe unatenda mema.+

Unifundishe masharti yako.+

 69 Wenye kimbelembele wamenipaka uwongo.+

Bali mimi, nitayashika maagizo yako kwa moyo wangu wote.+

 70 Moyo wao umekosa hisia kama mafuta.+

Mimi nami, nimependezwa na sheria yako.+

 71 Ni vema kwamba nimeteseka,+

Ili nipate kujifunza masharti yako.+

 72 Sheria+ ya kinywa chako ni njema kwangu,+

Kuliko maelfu ya vipande vya dhahabu na fedha.+

י [Yohdh]

 73 Mikono yako mwenyewe imenifanya, nayo ikaniweka imara.+

Unifanye nielewe, ili nipate kujifunza amri zako.+

 74 Wale wanaokuogopa ndio wanaoniona na kushangilia,+

Kwa maana nimelingojea neno lako mwenyewe.+

 75 Najua vema, Ee Yehova, kwamba maamuzi yako ya hukumu ni uadilifu+

Na kwamba umenitesa kwa uaminifu.+

 76 Tafadhali, fadhili zako zenye upendo na zinifariji,+

Kulingana na maneno yako kwa mtumishi wako.+

 77 Rehema zako na zinijie, ili nipate kuendelea kuishi;+

Kwa maana sheria yako ndiyo inayonipendeza.+

 78 Wenye kimbelembele na waone aibu, kwa maana wamenipotosha bila sababu.+

Bali mimi, najishughulisha na maagizo yako.+

 79 Wale wanaokuogopa na warudi kwangu,+

Wale pia wanaovijua vikumbusho vyako.+

 80 Moyo wangu uwe hauna kosa katika masharti yako,+

Ili nisione aibu.+

כ [Kaph]

 81 Nafsi yangu imedhoofika kwa kutamani wokovu wako;+

Neno lako nimelingojea.+

 82 Macho yangu yamedhoofika kwa kutamani maneno yako,+

Huku mimi nikisema: “Utanifariji wakati gani?”+

 83 Kwa maana nimekuwa kama kiriba+ katika moshi.

Masharti yako sijayasahau.+

 84 Siku za mtumishi wako ni ngapi?+

Utatekeleza hukumu wakati gani juu ya wale wanaonitesa?+

 85 Wenye kimbelembele wamechimba mashimo ya mtego ili wanipate,+

Wale ambao hawakubaliani na sheria yako.+

 86 Amri zako zote ni uaminifu.+

Wamenitesa bila sababu. Ee unisaidie.+

 87 Baada ya muda kidogo wangeniangamiza duniani;+

Bali mimi sikuyaacha maagizo yako.+

 88 Unihifadhi hai kulingana na fadhili zako zenye upendo,+

Ili nipate kushika kikumbusho cha kinywa chako.+

ל [Laʹmedh]

 89 Mpaka wakati usio na kipimo, Ee Yehova,+

Neno lako limesimama mbinguni.+

 90 Uaminifu wako ni wa kizazi baada ya kizazi.+

Umeiweka dunia imara, ili ipate kuendelea kusimama.+

 91 Kulingana na maamuzi yako ya hukumu, vimesimama mpaka leo,+

Kwa maana vyote hivyo ni watumishi wako.+

 92 Ikiwa singaliipenda sheria yako,+

Basi ningaliangamia katika mateso yangu.+

 93 Sitayasahau maagizo yako mpaka wakati usio na kipimo,+

Kwa sababu umenihifadhi hai kupitia hayo.+

 94 Mimi ni wako. Uniokoe,+

Kwa sababu nimeyatafuta maagizo yako.+

 95 Waovu wameningojea wapate kuniangamiza.+

Nami ninaendelea kuvikazia fikira vikumbusho vyako.+

 96 Nimeona mwisho wa ukamilifu wote.+

Amri yako ni pana sana.

מ [Mem]

 97 Jinsi ninavyoipenda sheria yako!+

Ndiyo ninayoihangaikia mchana kutwa.+

 98 Amri yako hunifanya kuwa na hekima kuliko adui zangu,+

Kwa sababu ni yangu mpaka wakati usio na kipimo.+

 99 Nimepata kuwa na ufahamu kuliko walimu wangu wote,+

Kwa sababu vikumbusho vyako ndivyo ninavyohangaikia.+

100 Najiendesha kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,+

Kwa sababu nimeyashika maagizo yako.+

101 Nimeizuilia mbali miguu yangu kutoka katika kila pito baya,+

Kusudi nipate kulishika neno lako.+

102 Sijageuka kando kutoka katika maamuzi yako ya hukumu,+

Kwa maana wewe mwenyewe umenifundisha.+

103 Jinsi maneno yako yamekuwa laini katika kaakaa langu,

Kuliko asali kinywani mwangu!+

104 Ninajiendesha kwa uelewaji kwa sababu ya maagizo yako.+

Ndiyo sababu nimeichukia kila njia ya uwongo.+

נ [Nun]

105 Neno lako ni taa ya mguu wangu,+

Na nuru kwa barabara yangu.+

106 Nimetoa ahadi yenye kiapo, nami nitaitimiza,+

Kuyashika maamuzi yako ya hukumu ya uadilifu.+

107 Nimeteseka kwa kiasi kikubwa.+

Ee Yehova, unihifadhi hai kulingana na neno lako.+

108 Tafadhali furahia matoleo ya hiari ya kinywa changu, Ee Yehova,+

Na unifundishe maamuzi yako ya hukumu.+

109 Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima;+

Lakini sheria yako sijaisahau.+

110 Waovu wamenitegea mtego,+

Lakini sijaondoka katika maagizo yako.+

111 Nimevichukua vikumbusho vyako kuwa ni urithi mpaka wakati usio na kipimo,+

Kwa maana hivyo ni furaha ya moyo wangu.+

112 Nimeuelekeza moyo wangu ili kuyatenda masharti yako+

Mpaka wakati usio na kipimo, mpaka lile la mwisho.+

ס [Saʹmekh]

113 Nimewachukia wenye moyo nusu nusu,+

Lakini sheria yako nimeipenda.+

114 Wewe ni mahali pangu pa kujificha na ngao yangu.+

Kwa maana nimelingojea neno lako.+

115 Ondokeni kwangu, enyi watenda-maovu,+

Ili nipate kuzishika amri za Mungu wangu.+

116 Unitegemeze kulingana na neno lako, ili niendelee kuishi,+

Wala usiniaibishe kwa ajili ya tumaini langu.+

117 Unitegemeze, ili nipate kuokolewa,+

Nami nitayaangalia masharti yako daima.+

118 Umewarusha mbali wale wote wanaoondoka katika masharti yako;+

Kwa maana ujanja wao ni uwongo.+

119 Umewakomesha waovu wote wa dunia kama takataka.+

Kwa hiyo nimevipenda vikumbusho vyako.+

120 Mwili wangu umetetemeka kwa sababu ya kukuhofu;+

Nami nimeogopa kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu.+

ע [ʽAʹyin]

121 Nimetekeleza hukumu na uadilifu.+

Usiniache mikononi mwa wale wanaonipunja!+

122 Uwe mdhamini wa mtumishi wako kwa ajili ya lililo jema.+

Wenye kimbelembele wasinipunje.+

123 Macho yangu yamedhoofika kwa ajili ya wokovu wako+

Na kwa ajili ya neno lako la uadilifu.+

124 Mtendee mtumishi wako kulingana na fadhili zako zenye upendo,+

Na unifundishe masharti yako mwenyewe.+

125 Mimi ni mtumishi wako.+ Nifanye nielewe,+

Ili nipate kuvijua vikumbusho vyako.+

126 Ni wakati wa Yehova kutenda.+

Wameivunja sheria yako.+

127 Ndiyo sababu nimezipenda amri zako+

Kuliko dhahabu, naam, dhahabu safi.+

128 Ndiyo sababu nimeyaona maagizo yote juu ya mambo yote kuwa ni sawa;+

Nimechukia kila njia ya uwongo.+

פ [Peʼ]

129 Vikumbusho vyako ni vizuri ajabu.+

Ndiyo sababu nafsi yangu imevishika.+

130 Kufunuliwa kwa maneno yako hutoa nuru,+

Kukiwafanya wasio na uzoefu waelewe.+

131 Nimekifungua kinywa changu wazi, ili nipate kupumua,+

Kwa sababu nimezitamani amri zako.+

132 Unigeukie na kunionyesha kibali,+

Kulingana na uamuzi wako wa hukumu kuwaelekea wale wanaolipenda jina lako.+

133 Uweke imara hatua zangu katika maneno yako,+

Wala namna yoyote ya jambo lenye kuumiza lisinitawale.+

134 Unikomboe na yeyote anayewapunja wanadamu,+

Nami nitayashika maagizo yako.+

135 Ufanye uso wako umwangazie mtumishi wako,+

Na unifundishe masharti yako.+

136 Vijito vya maji vimetiririka kutoka machoni pangu+

Kwa sababu hawakuishika sheria yako.+

צ [Tsa·dhehʹ]

137 Wewe ni mwadilifu, Ee Yehova,+

Nayo maamuzi yako ya hukumu ni manyoofu.+

138 Umeviamuru vikumbusho+ vyako kwa uadilifu

Na kwa uaminifu mwingi.+

139 Bidii yangu imenimaliza,+

Kwa sababu wapinzani wangu wameyasahau maneno yako.+

140 Neno lako ni safi sana,+

Na mtumishi wako analipenda.+

141 Mimi ni mnyonge na wa kudharaulika.+

Sijayasahau maagizo

yako.+

142 Uadilifu wako ni uadilifu wa mpaka wakati usio na kipimo,+

Na sheria yako ni kweli.+

143 Nilipata taabu na magumu.+

Nilipendezwa na amri zako.+

144 Uadilifu wa vikumbusho vyako ni wa mpaka wakati usio na kipimo.+

Nifanye nielewe, ili nipate kuendelea kuishi.+

ק [Qohph]

145 Nimeita kwa moyo wangu wote.+ Unijibu, Ee Yehova.+

Nitayashika masharti yako.+

146 Nimekuitia wewe. Uniokoe!+

Nami nitavishika vikumbusho vyako.+

147 Nimeamka mapema wakati wa mapambazuko ya asubuhi,+ ili nipate kulilia msaada.+

Kwa maana nimeyangojea maneno yako.+

148 Macho yangu yametangulia makesha ya usiku,+

Ili nijishughulishe na neno lako.+

149 Uisikie sauti yangu kulingana na fadhili zako zenye upendo.+

Ee Yehova, unihifadhi hai kulingana na uamuzi wako wa hukumu.+

150 Wale wanaofuatilia mwenendo mpotovu+ wamekaribia;

Wameenda mbali na sheria yako.+

151 Wewe uko karibu, Ee Yehova+

Na amri zako zote

ni kweli.+

152 Zamani za kale nimejua baadhi ya vikumbusho vyako,+

Kwa maana umeviwekea msingi tangu zamani za kale.+

ר [Rehsh]

153 Uone mateso yangu na kuniokoa;+

Kwa maana sijaisahau sheria yako mwenyewe.+

154 Uendeshe kesi yangu na kunikomboa;+

Unihifadhi hai kulingana na neno lako.+

155 Wokovu uko mbali sana na waovu,+

Kwa maana hawajayatafuta masharti yako.+

156 Rehema zako ni nyingi, Ee Yehova.+

Unihifadhi hai kulingana na maamuzi yako ya hukumu.+

157 Wanaonitesa na adui zangu ni wengi.+

Sijaondoka katika vikumbusho vyako.+

158 Nimewaona wale wanaotenda kwa hila,+

Nami nimechukizwa, kwa sababu hawakulishika neno lako.+

159 Uone kwamba nimeyapenda maagizo yako.+

Ee Yehova, unihifadhi hai kulingana na fadhili zako zenye upendo.+

160 Kiini cha neno lako ni kweli,+

Na kila uamuzi wako wa hukumu wa uadilifu ni wa mpaka wakati usio na kipimo.+

ש [Sin] au [Shin]

161 Wakuu wamenitesa bila sababu,+

Lakini moyo wangu umekuwa ukiyahofu maneno yako.+

162 Ninafurahi kwa sababu ya neno lako+

Kama vile mtu anavyofanya anapopata nyara nyingi.+

163 Nimeuchukia uwongo,+ nami naendelea kuuchukia.+

Sheria yako nimeipenda.+

164 Mara saba wakati wa mchana nimekusifu+

Kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu ya uadilifu.+

165 Wale wanaoipenda sheria yako wana amani nyingi,+

Na hakuna kitu cha kuwakwaza.+

166 Nimeutumainia wokovu wako, Ee Yehova,+

Nami nimezitenda amri zako.+

167 Nafsi yangu imeshika vikumbusho vyako,+

Nami navipenda sana.+

168 Nimeyashika maagizo yako na vikumbusho vyako,+

Kwa maana njia zangu zote ziko mbele zako.+

ת [Taw]

169 Kilio changu cha kusihi na kije karibu mbele zako,

Ee Yehova.+

Kulingana na neno lako, nifanye nielewe.+

170 Ombi langu la kutaka kibali na liingie mbele zako.+

Kulingana na neno lako, unikomboe.+

171 Midomo yangu na ibubujike sifa,+

Kwa maana unanifundisha masharti yako.+

172 Ulimi wangu na uimbe maneno yako,+

Kwa maana amri zako zote ni uadilifu.+

173 Mkono wako na unisaidie,+

Kwa sababu nimeyachagua maagizo yako.+

174 Nimeutamani wokovu wako, Ee Yehova,+

Nami naipenda sheria yako.+

175 Nafsi yangu na iendelee kuishi na kukusifu,+

Nayo maamuzi yako ya hukumu na yanisaidie.+

176 Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea.+ Umtafute mtumishi wako,+

Kwa maana sijazisahau amri zako.+

Wimbo wa Mipando.

120 Nilimwita Yehova katika taabu yangu,+

Naye akanijibu.+

 2 Ee Yehova, uikomboe nafsi yangu kutokana na midomo ya uwongo,+

Kutokana na ulimi wenye ujanja.+

 3 Mtu atakupa nini, na mtu atakuongezea nini,

Ewe ulimi wenye ujanja?+

 4 Mishale iliyonolewa ya mwanamume mwenye nguvu,+

Pamoja na makaa yanayowaka moto ya miretemu.+

 5 Ole wangu, kwa maana nimekaa nikiwa mgeni katika Mesheki!+

Nimekaa pamoja na mahema ya Kedari.+

 6 Kwa maana nafsi yangu imekaa kwa muda mrefu+

Pamoja na watu wanaochukia amani.+

 7 Nasimama kwa ajili ya amani;+ lakini ninaposema,

Wao wanataka vita.+

Wimbo wa Mipando.

121 Nitainua macho yangu milimani.+

Msaada wangu utatoka wapi?+

 2 Msaada wangu unatoka kwa Yehova,+

Mtengenezaji wa mbingu na dunia.+

 3 Hawezi kamwe kuruhusu mguu wako utikisike.+

Yeye anayekulinda hawezi kamwe kusinzia.+

 4 Tazama! Hatasinzia wala kulala usingizi,+

Yeye anayelinda Israeli.+

 5 Yehova anakulinda.+

Yehova ni kivuli chako+ kwenye mkono wako wa kuume.+

 6 Wakati wa mchana, jua halitakupiga,+

Wala mwezi wakati wa usiku.+

 7 Yehova mwenyewe atakulinda na misiba yote.+

Atailinda nafsi yako.+

 8 Yehova mwenyewe atalinda kuondoka kwako na kuingia kwako+

Tangu sasa na mpaka wakati usio na

kipimo.+

Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.

122 Nilishangilia walipokuwa wakiniambia:+

“Na twende+ katika nyumba ya Yehova.”+

 2 Miguu yetu ilisimama+

Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.+

 3 Yerusalemu limejengwa kama jiji+

Ambalo limeunganishwa pamoja kwa umoja,+

 4 Ambalo makabila wamepanda kuelekea humo,+

Makabila ya Yah,+

Kama kikumbusho kwa Israeli+

Ili kulishukuru jina la Yehova.+

 5 Kwa maana huko viti vya ufalme vya hukumu vimewekwa,+

Viti vya ufalme kwa ajili ya nyumba ya Daudi.+

 6 Ombeni kwa ajili ya amani ya Yerusalemu.+

Wanaokupenda, Ee jiji, hawatakuwa na wasiwasi.+

 7 Amani na iendelee kuwa ndani ya boma lako,+

Ukosefu wa wasiwasi ndani ya minara ya makao yako.+

 8 Kwa ajili ya ndugu zangu na wenzangu nitasema sasa:+

“Amani na iwe ndani yako.”+

 9 Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu+

Nitaendelea kutafuta mema kwa ajili yako.+

Wimbo wa Mipando.

123 Nimekuinulia wewe

macho yangu,+

Ewe unayekaa mbinguni.+

 2 Tazama! Kama vile macho ya watumishi yalivyo kuelekea mkono wa bwana wao,+

Kama vile macho ya mjakazi yalivyo kuelekea mkono wa bimkubwa wake,+

Ndivyo yalivyo macho yetu kumwelekea Yehova Mungu wetu.+

Mpaka atuonyeshe kibali.+

 3 Utuonyeshe kibali, Ee Yehova, utuonyeshe kibali;+

Kwa maana tumeshiba sana dharau.+

 4 Nafsi yetu imeshiba sana dhihaka ya wale wanaostarehe,+

Dharau la wale wenye kiburi.+

Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.

124 “Kama Yehova hangekuwa upande wetu,”+

Sasa Israeli na aseme,+

 2 “Kama Yehova hangekuwa upande wetu+

Watu waliposimama dhidi yetu,+

 3 Ndipo wangetumeza hata tukiwa hai,+

Hasira yao ilipokuwa inawaka juu yetu.+

 4 Ndipo maji yangetufagilia mbali,+

Mto wenyewe ungepita juu ya nafsi yetu.+

 5 Ndipo yangepita juu ya nafsi yetu

Maji ya kimbelembele.+

 6 Na abarikiwe Yehova, ambaye hakututoa+

Tuwe mawindo kwa meno yao.+

 7 Nafsi yetu ni kama ndege ambaye ameponyoka+

Kutoka katika mtego wa watega-chambo.+

Mtego umevunjwa,+

Na sisi tumeponyoka.+

 8 Msaada wetu uko katika jina la Yehova,+

Mtengenezaji wa mbingu na dunia.”+

Wimbo wa Mipando.

125 Wale wanaomtegemea Yehova+

Ni kama Mlima Sayuni,+ ambao hauwezi kutikiswa, bali hukaa mpaka wakati usio na kipimo.+

 2 Yerusalemu—kama vile milima inavyolizunguka pande zote,+

Ndivyo Yehova amewazunguka watu wake pande zote+

Tangu sasa na mpaka wakati usio na kipimo.+

 3 Kwa maana fimbo ya enzi ya uovu haitaendelea kuwa juu ya+ kura ya waadilifu,

Ili waadilifu wasiunyooshe mkono wao juu ya kosa lolote.+

 4 Ee Yehova, utende mema kwa walio wema,+

Naam, kwa walio wanyoofu mioyoni mwao.+

 5 Na wale wanaogeuka kando kwenye njia zao zilizopotoka,+

Yehova atawafanya waende zao pamoja na wale wanaotenda mambo yenye kuumiza.+

Kutakuwa na amani juu ya Israeli.+

Wimbo wa Mipando.

126 Yehova alipowakusanya tena mateka wa Sayuni,+

Tulikuwa kama wale waliokuwa wanaota ndoto.+

 2 Wakati huo kinywa chetu kilijaa kicheko,+

Na ulimi wetu vigelegele vya shangwe.+

Wakati huo walianza kusema kati ya mataifa:+

“Yehova amefanya jambo kuu katika yale ambayo amewafanyia.”+

 3 Yehova amefanya jambo kuu katika yale ambayo ametufanyia.+

Tumekuwa na shangwe.+

 4 Ee Yehova, uirudishe jamii yetu ya mateka,+

Kama sakafu za vijito katika Negebu.+

 5 Wale wanaopanda mbegu kwa machozi+

Watavuna kwa vigelegele vya shangwe.+

 6 Yule ambaye bila shaka anaenda, naam, akilia,+

Akiwa amechukua mfuko uliojaa mbegu,+

Bila shaka ataingia kwa vigelegele vya shangwe,+

Akiwa amechukua miganda yake.+

Wimbo wa Mipando. Wa Sulemani.

127 Yehova mwenyewe asipoijenga nyumba,+

Ni bure kwamba wajenzi wake wameifanyia kazi ngumu.+

Yehova mwenyewe asipolilinda jiji,+

Ni bure kwamba mlinzi ameendelea kukaa macho.+

 2 Ni kazi ya bure kwamba ninyi mnaamka mapema,+

Kwamba mnakaa mpaka kuchelewa,+

Kwamba mnakula chakula kwa maumivu.+

Hivi ndivyo anavyompa hata mpendwa wake usingizi.+

 3 Tazama! Wana ni urithi kutoka kwa Yehova;+

Uzao wa tumbo ni thawabu.+

 4 Kama mishale mkononi mwa mwanamume mwenye nguvu,+

Ndivyo walivyo wana wa ujanani.+

 5 Mwenye furaha ni mwanamume ambaye amelijaza+ podo lake na hao.

Hawataona aibu,+

Kwa maana wataongea na adui langoni.

Wimbo wa Mipando.

128 Mwenye furaha ni kila mtu anayemwogopa Yehova.+

Anayetembea katika njia zake.+

 2 Kwa maana utakula kazi ngumu ya mikono yako mwenyewe.+

Utakuwa mwenye furaha na mambo yatakwendea vema.+

 3 Mke wako atakuwa kama mzabibu unaozaa matunda+

Katika sehemu za ndani kabisa za nyumba yako.

Wana wako watakuwa kama miche ya mizeituni+ kuizunguka meza yako pande zote.

 4 Tazama! Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mwanamume+

Anayemwogopa Yehova.+

 5 Yehova atakubariki kutoka Sayuni.+

Uone pia uzuri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako.+

 6 Na uone wana wa wana wako.+

Na kuwe na amani juu ya Israeli.+

Wimbo wa Mipando.

129 “Kwa muda mrefu wa kutosha wamenionyesha uadui tangu ujana wangu,”+

Israeli na aseme sasa,+

 2 “Kwa muda mrefu wa kutosha wamenionyesha uadui tangu ujana wangu;+

Hata hivyo hawajanishinda.+

 3 Walimaji wamelima juu ya mgongo wangu;+

Wameirefusha mitaro yao.”

 4 Yehova ni mwadilifu.+

Amezikata vipande-vipande kamba za waovu.+

 5 Wataona aibu na kurudi nyuma wenyewe,+

Wale wote wanaochukia Sayuni.+

 6 Watakuwa kama majani mabichi ya paa,+

Ambayo yamekauka kabla hayajang’olewa,+

 7 Ambayo mvunaji hajajaza mkono wake kwa hayo,+

Wala kifua chake yeyote anayekusanya miganda.

 8 Wala wanaopita karibu hawajasema:

“Baraka ya Yehova na iwe juu yenu.+

Tumewabariki ninyi katika jina la Yehova.”+

Wimbo wa Mipando.

130 Kutoka vilindini nimekuitia wewe, Ee Yehova.+

 2 Ee Yehova, uisikie sauti yangu.+

Masikio yako na yasikilize sauti ya kusihi kwangu.+

 3 Kama ungekuwa unaangalia makosa,+ Ee Yah,

Ee Yehova, ni nani angesimama?+

 4 Kwa maana kwako wewe kuna msamaha wa kweli,+

Ili upate kuogopwa.+

 5 Nimetumainia, Ee Yehova, nafsi yangu imetumainia,+

Nalo neno lake nimelingojea.+

 6 Nafsi yangu imemngojea Yehova+

Kuliko walinzi wanavyoingojea asubuhi,+

Ambao wanaingojea asubuhi.+

 7 Israeli na aendelee kumngojea Yehova.+

Kwa maana kuna fadhili zenye upendo kwa Yehova,+

Na ndivyo kulivyo na ukombozi mwingi kwake.+

 8 Na yeye mwenyewe atamkomboa Israeli kutoka katika makosa yake yote.+

Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.

131 Ee Yehova, moyo wangu haukuwa na majivuno,+

Wala macho yangu hayakuinuka juu sana;+

Wala sikutembea katika mambo makuu mno,+

Wala katika mambo yaliyo ya ajabu mno kwangu.+

 2 Hakika nimeituliza na kuinyamazisha nafsi yangu+

Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya juu ya mama yake.+

Nafsi yangu iko juu yangu kama mtoto aliyeachishwa kunyonya.+

 3 Israeli na amngojee Yehova+

Tangu sasa na mpaka wakati usio na kipimo.+

Wimbo wa Mipando.

132 Ukumbuke, Ee Yehova, juu ya Daudi+

Fedheha zake zote;+

 2 Jinsi alivyomwapia Yehova,+

Jinsi alivyomwekea nadhiri Mwenye Nguvu+ wa Yakobo:+

 3 “Sitaenda katika hema la nyumba yangu.+

Sitapanda katika kitanda changu cha fahari,+

 4 Sitaacha macho yangu kulala usingizi,+

Wala macho yangu yenye kung’aa kusinzia,+

 5 Mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yehova,+

Maskani kuu kwa ajili ya Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+

 6 Tazama! Tumeyasikia hayo huko Efratha,+

Tumeyapata katika viwanja vya msitu.+

 7 Na tuingie katika maskani yake kuu;+

Na tuiname kwenye kiti chake cha miguu.+

 8 Usimame, Ee Yehova, uende katika mahali pako pa kupumzika,+

Wewe na Sanduku+ la nguvu zako.+

 9 Makuhani wako na wavikwe uadilifu,+

Nao washikamanifu wako na wapige vigelegele kwa shangwe.+

10 Kwa sababu ya Daudi mtumishi wako,+

Usiugeuze nyuma uso wa mtiwa-mafuta wako.+

11 Yehova amemwapia Daudi,+

Kwa kweli hataliacha:+

“Kati ya uzao wa tumbo lako+

Nitaweka juu ya kiti chako cha ufalme.+

12 Ikiwa wana wako watalishika agano langu+

Na vikumbusho vyangu ambavyo nitawafundisha,+

Wana wao pia milele+

Wataketi juu ya kiti chako cha ufalme.”+

13 Kwa maana Yehova amechagua Sayuni;+

Amepatamani pawe makao kwa ajili yake mwenyewe:+

14 “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumzika milele;+

Nitakaa hapa, kwa maana nimepatamani.+

15 Bila shaka nitavibariki vyakula vyake.+

Maskini wake nitawashibisha kwa mkate.+

16 Na makuhani wake nitawavika wokovu;+

Na bila shaka washikamanifu wake watapiga vigelegele kwa shangwe.

17 Hapo nitaifanya pembe ya Daudi ikue.+

Nimetayarisha taa kwa ajili ya mtiwa-mafuta wangu.+

18 Adui zake nitawavika aibu;+

Lakini taji+ lake litasitawi juu yake.”+

Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.

133 Tazama! Jinsi ilivyo vyema na jinsi inavyopendeza

Ndugu kukaa pamoja kwa umoja!+

 2 Ni kama mafuta mazuri juu ya kichwa,+

Yanayoshuka juu ya ndevu,

Ndevu za Haruni,+

Yanayoshuka kwenye ukosi wa mavazi yake.+

 3 Ni kama umande+ wa Hermoni+

Unaoshuka kwenye milima ya Sayuni.+

Kwa maana huko Yehova aliamuru baraka iwepo,+

Naam, uzima mpaka wakati usio na kipimo.+

Wimbo wa Mipando.

134 Mbarikini Yehova,+

Ninyi nyote watumishi wa Yehova,+

Ninyi mnaosimama katika nyumba ya Yehova nyakati za usiku.+

 2 Inueni mikono yenu katika utakatifu+

Na kumbariki Yehova.+

 3 Yehova na awabariki kutoka Sayuni,+

Yeye ambaye ni Mtengenezaji wa mbingu na dunia.+

135 Msifuni Yah!+

Lisifuni jina la Yehova,+

Toeni sifa, enyi watumishi wa Yehova,+

 2 Ninyi mnaosimama katika nyumba ya Yehova,+

Katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.+

 3 Msifuni Yah, kwa maana Yehova ni mwema.+

Lipigieni jina lake muziki, kwa maana linapendeza.+

 4 Kwa maana Yah amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe,+

Israeli awe mali yake ya pekee.+

 5 Kwa maana mimi mwenyewe najua vema kwamba Yehova ni mkuu,+

Na Bwana wetu ni zaidi ya miungu mingine yote.+

 6 Kila kitu ambacho Yehova alipendezwa kufanya, amefanya+

Mbinguni na duniani, baharini na katika vilindi vyote vya maji.+

 7 Anafanya mivuke ipande kutoka mwisho wa dunia;+

Amefanya hata malango kwa ajili ya mvua;+

Anauleta upepo kutoka katika maghala yake,+

 8 Yeye aliyewapiga na kuwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,+

Mwanadamu na pia mnyama.+

 9 Alituma ishara na miujiza katikati yako, Ee Misri,+

Juu ya Farao na juu ya watumishi wake wote;+

10 Yeye aliyepiga mataifa mengi+

Na kuua wafalme wenye nguvu,+

11 Naam, Sihoni mfame wa Waamori+

Na Ogu mfalme wa Bashani+

Na falme zote za Kanaani,+

12 Na ambaye aliitoa nchi yao iwe urithi,+

Urithi kwa Israeli watu wake.+

13 Ee Yehova, jina lako ni la mpaka wakati usio na kipimo.+

Ee Yehova, ukumbusho wako ni wa mpaka kizazi baada ya kizazi.+

14 Kwa maana Yehova atawatetea watu wake,+

Naye atajuta kwa sababu ya watumishi wake.+

15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu,+

Kazi ya mikono ya mtu wa udongo.+

16 Zina kinywa, lakini haziwezi kusema lolote;+

Zina macho, lakini haziwezi kuona chochote;+

17 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia lolote.+

Pia hazina roho yoyote katika vinywa vyao.+

18 Wale wanaozifanya watakuwa tu kama hizo,+

Kila mtu anayezitegemea.+

19 Ee nyumba ya Israeli, mbarikini Yehova.+

Ee nyumba ya Haruni, mbarikini Yehova.+

20 Ee nyumba ya Lawi, mbarikini Yehova.+

Ninyi mnaomwogopa Yehova, mbarikini Yehova+.

21 Na abarikiwe Yehova kutoka Sayuni,+

Anayekaa katika Yerusalemu.+

Msifuni Yah!+

136 Mshukuruni Yehova, kwa maana ni mwema:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

 2 Mshukuruni Mungu wa miungu:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

 3 Mshukuruni Bwana wa mabwana:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

 4 Yule peke yake aliye Mtendaji wa mambo ya ajabu, mambo makuu:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

 5 Yule anayezifanya mbingu kwa uelewaji:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

 6 Yule anayeitandaza dunia juu ya maji:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

 7 Yule anayeifanya ile mianga mikubwa:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

 8 Naam, jua ili litawale wakati wa mchana:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

 9 Mwezi na nyota ili zitawale pamoja wakati wa usiku:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

10 Yule anayepiga Misri katika wazaliwa wao wa kwanza:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

11 Na Yule anayetoa Israeli kutoka katikati yao:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

12 Kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;

13 Yule anayekata Bahari Nyekundu sehemu-sehemu:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

14 Na aliyefanya Israeli wapite katikati yake:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

15 Na aliyemkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

16 Yule anayetembeza watu wake kupita nyikani:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

17 Yule anayepiga wafalme wakubwa:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

18 Na ambaye aliua wafalme wenye fahari:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

19 Naam, Sihoni mfalme wa Waamori:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

20 Na Ogu mfalme wa Bashani:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

21 Na ambaye aliitoa nchi yao iwe urithi:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

22 Urithi kwa Israeli mtumishi wake:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

23 Ambaye alitukumbuka tulipokuwa katika hali ya chini:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

24 Na ambaye alitunyakua kutoka kwa adui zetu tena na tena:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

25 Yule anayewapa chakula wote wenye mwili:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+

26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni:+

Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+

137 Kando ya mito ya Babiloni+—​huko tuliketi.+

Pia tulilia tulipokumbuka Sayuni.+

 2 Juu ya mierebi+ iliyo katikati yake

Tulitundika vinubi vyetu.+

 3 Kwa maana huko, wale waliokuwa wametushika mateka, walituomba maneno ya wimbo,+

Nao wale wanaotufanyia mzaha—wimbo wa kushangilia:+

“Tuimbieni mmoja wa nyimbo za Sayuni.”+

 4 Tunawezaje kuimba wimbo wa Yehova+

Kwenye nchi ya kigeni?+

 5 Kama nikikusahau, Ee Yerusalemu,+

Mkono wangu wa kuume na uwe msahaulifu.

 6 Ulimi wangu na ushikamane na kaakaa langu,+

Kama nisingekukumbuka,+

Kama nisingeinua Yerusalemu

Kuwa juu ya sababu yangu kuu ya kushangilia.+

 7 Ukumbuke,+ Ee Yehova, juu ya wana wa Edomu+ siku ya Yerusalemu,+

Waliokuwa wakisema: “Lifanye ukiwa! Lifanye ukiwa mpaka kwenye msingi ulio ndani yake!”+

 8 Ee binti Babiloni, ambaye utaporwa,+

Atakuwa ni mwenye furaha yeye atakayekupa thawabu+

Ya matendo yako mwenyewe ambayo ulitutendea.+

 9 Atakuwa ni mwenye furaha yeye anayewakamata na kuwavunja vipande-vipande+

Watoto wako juu ya mwamba.

Ya Daudi.

138 Nitakusifu kwa moyo wangu wote.+

Mbele ya miungu mingine nitakupigia muziki.+

 2 Nitainama kuelekea hekalu lako takatifu,+

Nami nitalisifu jina lako,+

Kwa sababu ya fadhili zako zenye upendo+ na kwa sababu ya ukweli wako.+

Kwa maana umeyatukuza maneno yako+ hata juu ya jina lako lote.+

 3 Katika siku niliyoita, ulinijibu;+

Ukaanza kunifanya niwe jasiri katika nafsi yangu kwa nguvu.+

 4 Wafalme wote wa dunia watakusifu wewe, Ee Yehova,+

Kwa maana watakuwa wameyasikia maneno ya kinywa chako.

 5 Nao wataimba juu ya njia za Yehova,+

Kwa maana utukufu wa Yehova ni mkuu.+

 6 Kwa maana Yehova yuko juu, hata hivyo yeye humwona mnyenyekevu;+

Lakini yeye anamjua mwenye kiburi kutoka mbali tu.+

 7 Kama nikitembea katikati ya taabu, wewe utanihifadhi hai.+

Kwa sababu ya hasira ya adui zangu wewe utaunyoosha mkono,+

Na mkono wako wa kuume utaniokoa.+

 8 Yehova mwenyewe atayamalizia mambo yaliyoko kwa ajili yangu.+

Ee Yehova, fadhili zako zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+

Usiziache kazi za mikono yako mwenyewe.+

Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.

139 Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.+

 2 Wewe mwenyewe umepata kujua kuketi kwangu na kusimama kwangu.+

Umeichunguza fikira yangu tokea mbali.+

 3 Umepima kusafiri kwangu na kulala kwangu nikiwa nimejinyoosha,+

Nawe umezijua njia zangu zote.+

 4 Kwa maana hamna neno hata moja katika ulimi wangu,+

Lakini, tazama! Ee Yehova, tayari unajua yote.+

 5 Nyuma na mbele umenizingira;

Nawe unauweka mkono wako juu yangu.

 6 Ujuzi wa namna hiyo ni wa ajabu mno kwangu.+

Ni wa juu sana hivi kwamba siwezi kuufikia.+

 7 Ni wapi ninapoweza kwenda mbali na roho yako,+

Na ni wapi ninapoweza kukimbilia mbali na uso wako?+

 8 Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa huko;+

Na kama ningetandika kitanda changu katika Kaburi,* tazama! ungekuwa huko.+

 9 Kama ningechukua mabawa+ ya mapambazuko,

Ili nipate kuishi katika bahari ya mbali sana,+

10 Huko, pia, mkono wako ungeniongoza+

Nao mkono wako wa kuume ungenishika.+

11 Na kama ningesema: “Hakika giza litanifunika haraka!”+

Ndipo usiku ungekuwa nuru kunizunguka.+

12 Hata giza lenyewe halingekuwa jeusi mno kwako,+

Lakini usiku wenyewe ungeng’aa kama mchana;+

Giza lingekuwa sawa tu na nuru.+

13 Kwa maana wewe mwenyewe uliumba figo zangu;+

Wewe uliniweka nikiwa nimekingwa katika tumbo la mama yangu.+

14 Nitakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia ya ajabu yenye kuogopesha.+

Kazi zako ni za ajabu,+

Kama vile nafsi yangu inavyojua vema.+

15 Mifupa yangu haikufichwa kwako+

Nilipofanyizwa katika siri,+

Nilipoungwa katika sehemu za chini kabisa+ za dunia.

16 Macho yako yalikiona kiini-tete changu,+

Na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa,

Kuhusiana na siku ambazo zilifanyizwa+

Na hakukuwako hata moja kati ya hizo.

17 Kwa hiyo, jinsi mawazo yako yalivyo yenye thamani kwangu!+

Ee Mungu, jinsi jumla yake yote ilivyo kuu!+

18 Kama ningejaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko hata chembe za mchanga.+

Nimeamka, na bado niko pamoja nawe.+

19 Laiti wewe, Ee Mungu, ungemuua mwovu!+

Ndipo hata watu wenye hatia ya damu+ hakika wangeniondokea,

20 Wanaosema mambo juu yako kulingana na wazo lao;+

Wamelitumia jina lako vibaya+—wapinzani wako.+

21 Je, mimi siwachukii wale wanaokuchukia vikali, Ee Yehova,+

Na je, sichukizwi na wale wanaokuasi?+

22 Kwa chuki kamili, ninawachukia.+

Wamekuwa adui halisi kwangu.+

23 Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.+

Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofadhaisha,+

24 Na uone kama ndani yangu mna njia yoyote yenye kuumiza,+

Na uniongoze katika njia+ ya mpaka wakati usio na kipimo.

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

140 Uniokoe, Ee Yehova, kutoka kwa watu wabaya;+

Unilinde na mtu mwenye matendo ya jeuri,+

 2 Wale ambao wamepanga mambo mabaya moyoni mwao,+

Ambao mchana kutwa wanaendelea kushambulia kama katika vita.+

 3 Wameunoa ulimi wao kama ule wa nyoka;+

Sumu ya kipiri-pembe iko chini ya midomo yao.+ Sela.

 4 Unilinde, Ee Yehova, na mikono ya mwovu;+

Unilinde na mtu mwenye matendo ya jeuri,+

Wale ambao wamepanga hila ya kuzisukuma hatua zangu.+

 5 Waliojiinua wenyewe wameficha mtego kwa ajili yangu;+

Nao wamezitandika kamba kama wavu kando ya njia.+

Wametega minaso kwa ajili yangu.+ Sela.

 6 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu.+

Utege sikio, Ee Yehova, usikie sauti ya kusihi kwangu.”+

 7 Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ nguvu za wokovu wangu,+

Umekinga kichwa changu katika siku ya jeshi lenye silaha.+

 8 Ee Yehova, usimpe mwovu tamaa zake.+

Usiunge mkono hila yake, ili wasipate kuinuliwa.+ Sela.

 9 Navyo vichwa vya wale wanaonizunguka,+

Taabu ya midomo yao wenyewe na ivifunike.+

10 Makaa yanayowaka moto na yaangushwe juu yao.+

Na waangushwe motoni,+ ndani ya mashimo yenye maji, ili wasipate kusimama.+

11 Yule mwenye kuongea makuu—na asifanywe imara duniani.+

Mtu wa jeuri—uovu na umwinde kwa mapigo yenye kurudiwa.+

12 Najua vema kwamba Yehova atatimiza+

Dai halali la mwenye kuteseka, hukumu ya maskini.+

13 Hakika waadilifu watalishukuru jina lako;+

Wanyoofu watakaa mbele za uso wako.+

Muziki wa Daudi.

141 Ee Yehova, nimekuitia wewe.+

Ufanye haraka kuja kwangu.+

Utege sikio kwa sauti yangu ninapokuita.+

 2 Sala yangu na itayarishwe kama uvumba+ mbele zako,+

Kuinuliwa kwa mikono yangu kama toleo la jioni la nafaka.+

 3 Uweke mlinzi, Ee Yehova, kwa ajili ya kinywa changu;+

Uweke mwangalizi juu ya mlango wa midomo yangu.+

 4 Usiuelekeze moyo wangu kwenye ubaya wowote,+

Ili kuendeleza matendo yenye sifa mbaya katika uovu+

Pamoja na watu wanaofanya mambo yenye kuumiza,+

Ili nisipate kujilisha vyakula vyao vitamu.+

 5 Mwadilifu akinipiga, zingekuwa fadhili zenye upendo;+

Naye akinikaripia, hiyo ingekuwa mafuta juu ya kichwa,+

Ambayo kichwa changu hakingetaka kukataa.+

Kwa maana bado kungekuwako sala yangu wakati wa misiba yao.+

 6 Waamuzi wao wametupwa chini kandokando ya mwamba,+

Lakini wameyasikia maneno yangu, kwamba ni yenye kupendeza.+

 7 Kama mtu anavyoatua na kupasua kuni juu ya nchi,

Ndivyo mifupa yetu imetawanywa katika kinywa cha Kaburi.*+

 8 Hata hivyo, macho yangu yanakuelekea wewe,+ Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu.+

Nimekukimbilia.+

Usiimwage nafsi yangu.+

 9 Uniweke mbali na mikono ya mtego ambao wamenitegea+

Na mbali na minaso ya wale wanaofanya mambo yenye kuumiza.+

10 Waovu wataanguka ndani ya nyavu zao wenyewe wote pamoja,+

Huku mimi nikipita kando.

Maskili. Ya Daudi, alipokuwa pangoni.+ Sala.

142 Kwa sauti yangu, nilimwomba Yehova msaada;+

Kwa sauti yangu, nilianza kumlilia Yehova anionyeshe kibali.+

 2 Mbele zake niliendelea kumwaga hangaiko langu;+

Mbele zake niliendelea kutangaza juu ya taabu yangu mwenyewe,+

 3 Roho+ yangu ilipozimia ndani yangu.

Ndipo wewe mwenyewe ulipoijua barabara yangu.+

Katika njia ambayo mimi hutembea+

Wametega mtego kwa ajili yangu.+

 4 Tazama kwenye mkono wa kuume uone

Kwamba hakuna yeyote anayenitambua mimi.+

Mahali pangu pa kukimbilia pameangamia;+

Hakuna yeyote anayeuliza habari za nafsi yangu.+

 5 Nilikuitia wewe, Ee Yehova, kwa ajili ya msaada.+

Nikasema: “Wewe ni kimbilio langu,+

Fungu+ langu katika nchi ya walio hai.”+

 6 Usikilize kilio changu cha kusihi,+

Kwa maana nimekuwa maskini sana.+

Unikomboe kutoka kwa watesaji wangu,+

Kwa maana wana nguvu kuliko mimi.+

 7 Uitoe nafsi yangu kutoka katika gereza la shimoni+

Ili kulisifu jina lako.+

Waadilifu na wakusanyike kunizunguka,+

Kwa sababu unanitendea inavyofaa.+

Muziki wa Daudi.

143 Ee Yehova, uisikie sala yangu;+

Utege sikio usikie kusihi kwangu.+

Katika uaminifu wako unijibu kwa uadilifu wako.+

 2 Wala usiingie katika hukumu pamoja na mtumishi wako;+

Kwa maana mbele zako, hakuna yeyote aliye hai anayeweza kuwa mwadilifu.+

 3 Kwa maana adui ameifuatilia nafsi yangu;+

Ameuponda uhai wangu mpaka chini.+

Amenifanya nikae katika mahali penye giza kama wale waliokufa kwa wakati usio na kipimo.+

 4 Na roho+ yangu inazimia ndani yangu;

Moyo wangu wenyewe umekufa ganzi katikati yangu.+

 5 Nimezikumbuka siku za zamani za kale;+

Nimetafakari juu ya utendaji wako wote;+

Kwa kupenda niliendelea kuhangaikia kazi ya mikono yako mwenyewe.+

 6 Nimekunyooshea mikono yangu;+

Nafsi yangu kwako ni kama nchi iliyochoka kabisa.+ Sela.

 7 Ufanye haraka, unijibu, Ee Yehova.+

Roho yangu imefikia mwisho.+

Usiufiche uso wako mbali nami,+

Kama sivyo nitakuwa kama wale wanaoshuka kuingia shimoni.+

 8 Asubuhi unifanye nisikie fadhili zako zenye upendo,+

Kwa maana nimekutegemea wewe.+

Unijulishe njia ninayopaswa kuitembea,+

Kwa maana nimekuinulia nafsi yangu.+

 9 Unikomboe kutoka kwa adui zangu, Ee Yehova.+

Nimejificha kwako.+

10 Unifundishe kufanya mapenzi yako,+

Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+

Roho yako ni nzuri;+

Na iniongoze katika nchi ya unyoofu.+

11 Kwa ajili ya jina lako,+ Ee Yehova, unihifadhi hai.+

Katika uadilifu+ wako na uitoe nafsi yangu katika taabu.+

12 Na katika fadhili zako zenye upendo uwanyamazishe adui zangu;+

Nawe uwaangamize wote wanaoichukia nafsi yangu,+

Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+

Ya Daudi.

144 Na abarikiwe Yehova Mwamba wangu,+

Anayeifundisha mikono yangu kwa ajili ya kupigana,+

Vidole vyangu kwa ajili ya vita;

 2 Fadhili zangu zenye upendo na ngome yangu,+

Kilele changu salama na Mwokoaji wangu,+

Ngao+ yangu na Yeye ambaye nimemkimbilia,+

Yule anayevitiisha vikundi vya watu chini yangu.+

 3 Ee Yehova, mwanadamu ni nini hata umtambue,+

Mwana wa binadamu anayeweza kufa+ hata umwangalie?

 4 Mwanadamu anafanana na pumzi tu;+

Siku zake ni kama kivuli kinachopita.+

 5 Ee Yehova, uinamishe mbingu zako ili upate kushuka;+

Uiguse milima ipate kutoa moshi.+

 6 Angaza kwa umeme ili upate kuwatawanya;+

Itume mishale yako ili upate kuwavuruga.+

 7 Unyooshe mikono yako kutoka katika kilele;+

Uniweke huru na kunikomboa kutoka katika maji mengi,+

Kutoka kwa mkono wa wageni,+

 8 Ambao kinywa chao kimesema mambo yasiyo ya kweli+

Na ambao mkono wao wa kuume ni mkono wa kuume wa uwongo.+

 9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya.+

Kwenye kinanda cha nyuzi kumi nitakupigia wewe muziki,+

10 Wewe unayewapa wafalme wokovu,+

Wewe unayemweka Daudi mtumishi wako huru kutokana na upanga wenye kuumiza.+

11 Uniweke huru na kunikomboa kutoka kwa mkono wa wageni,+

Ambao kinywa chao kimesema mambo yasiyo ya kweli+

Na ambao mkono wao wa kuume ni mkono wa kuume wa uwongo,+

12 Wanaosema: “Wana wetu ni kama mimea michanga iliyokua wakati wa ujana wao,+

Binti zetu ni kama nguzo za pembeni zilizochongwa kwa mtindo wa jumba la mfalme,

13 Maghala yetu yamejaa, yakitoa mali za aina moja baada ya nyingine,+

Makundi yetu yanaongezeka kwa maelfu, elfu kumi kwa moja, kwenye barabara zetu,

14 Ng’ombe zetu ni wazito, bila mpasuko wala mimba kutoka,+

Na hakuna kilio katika viwanja vyetu vya watu wote.+

15 Wenye furaha ni watu ambao mambo yako hivyo kwao!”

Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!+

Sifa, ya Daudi.

א [ʼAʹleph]

145 Nitakutukuza, Ee Mungu wangu Mfalme,+

Nami nitalibariki jina lako mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

ב [Behth]

 2 Mchana kutwa nitakubariki,+

Nami nitalisifu jina lako mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

ג [Giʹmel]

 3 Yehova ni mkuu na wa kusifiwa sana,+

Na ukuu wake hauchunguziki.+

ד [Daʹleth]

 4 Kizazi baada ya kizazi kitazipongeza kazi zako,+

Nao watatangaza juu ya matendo yako ya nguvu.+

ה [Heʼ]

 5 Fahari tukufu ya utukufu wako+

Na mambo ya kazi zako za ajabu nitayafanya yawe hangaiko langu.+

ו [Waw]

 6 Nao wataongea juu ya nguvu za mambo yako yenye kuogopesha;+

Nami nitautangaza ukuu wako.+

ז [Zaʹyin]

 7 Watabubujikwa na maneno wakitaja wingi wa wema wako,+

Na kwa sababu ya uadilifu wako watapiga vigelegele vya shangwe.+

ח [Chehth]

 8 Yehova ni mwenye neema na mwenye rehema,+

Si mwepesi wa hasira naye ni mkuu katika fadhili zenye upendo.+

ט [Tehth]

 9 Yehova ni mwema kwa wote,+

Na rehema zake ziko juu ya kazi zake zote.+

י [Yohdh]

10 Kazi zako zote zitakusifu, Ee Yehova,+

Na washikamanifu wako watakusifu.+

כ [Kaph]

11 Wataongea juu ya utukufu wa ufalme wako,+

Nao watasema juu ya nguvu zako,+

ל [Laʹmedh]

12 Kuwajulisha wana wa binadamu matendo yake yenye nguvu+

Na utukufu wa fahari ya ufalme wake.+

מ [Mem]

13 Ufalme wako ni ufalme kwa nyakati zote zisizo na kipimo,+

Na mamlaka yako ni ya kuendelea mpaka vizazi vyote vinavyofuata.+

ס [Saʹmekh]

14 Yehova anawategemeza wote wanaoanguka,+

naye anawainua wote ambao wameinama chini.+

ע [ʽAʹyin]

15 Macho ya wote yanakutazama yakiwa na tumaini,+

Nawe unawapa chakula chao katika majira

yake.+

פ [Peʼ]

16 Unaufumbua mkono wako+

Na kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.+

צ [Tsa·dhehʹ]

17 Yehova ni mwadilifu katika njia zake zote+

Na mshikamanifu katika kazi zake zote.+

ק [Qohph]

18 Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia,+

Wote wanaomwitia yeye katika ukweli.+

ר [Rehsh]

19 Atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao,+

Naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada, naye atawaokoa.+

ש [Shin]

20 Yehova anawalinda wale wote wanaompenda,+

Lakini atawaangamiza waovu wote.+

ת [Taw]

21 Kinywa changu kitasema sifa za Yehova;+

Na wote wenye mwili na walibariki jina lake takatifu mpaka wakati usio na kipimo, hata milele.+

146 Msifuni Yah!+

Msifu Yehova, Ee nafsi yangu.+

 2 Nitamsifu Yehova muda wote wa maisha yangu.+

Nitampigia Mungu wangu muziki maadamu nipo.+

 3 Msiweke tegemeo lenu katika watu wenye vyeo,+

Wala katika mtu wa udongo, ambaye hana wokovu wowote.+

 4 Roho yake hutoka,+ naye hurudi kwenye udongo wake;+

Siku hiyo mawazo yake hupotea.+

 5 Mwenye furaha ni yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,+

Ambaye tumaini lake liko katika Yehova Mungu wake,+

 6 Mtengenezaji wa mbingu na dunia,+

Wa bahari, na vyote vilivyomo,+

Yeye anayedumisha ukweli mpaka wakati usio na kipimo,+

 7 Yeye anayetekeleza hukumu kwa ajili ya waliopunjwa,+

Yeye anayewapa wenye njaa mkate.+

Yehova anawafungua wale waliofungwa.+

 8 Yehova anafungua macho ya vipofu;+

Yehova anawainua wale walioinama chini;+

Yehova anawapenda waadilifu.+

 9 Yehova anawalinda wakaaji wageni;+

Humtuliza mvulana asiye na baba na mjane,+

Lakini njia+ ya waovu yeye huipotosha.+

10 Yehova atakuwa mfalme mpaka wakati usio na kipimo,+

Mungu wako, Ee Sayuni, kwa kizazi baada ya kizazi.+

Msifuni Yah!+

147 Msifuni Yah,+

Kwa maana ni vema kumpigia Mungu wetu muziki;+

Kwa maana inapendeza​—sifa inafaa.+

 2 Yehova anajenga Yerusalemu;+

Huwakusanya pamoja waliotawanywa wa Israeli.+

 3 Anawaponya+ wenye mioyo iliyovunjika,+

Naye anafunga sehemu zao zenye maumivu.+

 4 Anahesabu idadi ya nyota;+

Zote anaziita kwa majina yake.+

 5 Bwana wetu ni mkuu na mwenye nguvu nyingi;+

Uelewaji wake hauwezi kusimuliwa.+

 6 Yehova anawatuliza wapole;+

Anawashusha waovu mpaka chini.+

 7 Mwitikieni Yehova kwa kutoa shukrani;+

Mpigieni Yehova muziki kwenye kinubi,+

 8 Yeye anayezifunika mbingu kwa mawingu,+

Yeye anayetayarisha mvua kwa ajili ya dunia,+

Yeye anayefanya milima ichipushe majani mabichi.+

 9 Anawapa wanyama chakula chao,+

Kunguru wachanga wanaoendelea kuita.+

10 Hapendezwi na nguvu za farasi,+

Wala hafurahii miguu ya mtu.+

11 Yehova anawafurahia wale wanaomwogopa,+

Wale wanaozingojea fadhili zake zenye upendo.+

12 Mpongeze Yehova,+ Ee Yerusalemu.

Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.+

13 Kwa maana ameyatia nguvu mapingo ya lango lako;

Amewabariki wana wako katikati yako.+

14 Anaweka amani katika eneo lako;+

Anaendelea kukushibisha kwa unono wa ngano.+

15 Anayatuma maneno yake duniani;+

Neno lake hukimbia haraka.

16 Anatoa theluji kama sufu;+

Anatawanya sakitu kama majivu.+

17 Anatupa barafu yake kama matonge.+

Mbele ya baridi yake ni nani anayeweza kusimama?+

18 Anatuma neno lake+ na kuviyeyusha.

Huufanya upepo uvume;+

Maji hutiririka.

19 Anamtangazia Yakobo neno lake,+

Na Israeli masharti+ yake na maamuzi yake ya hukumu.+

20 Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote;+

Nao hawajajua maamuzi yake ya hukumu.+

Msifuni Yah!+

148 Msifuni Yah!+

Msifuni Yehova kutoka mbinguni,+

Msifuni katika vilele.+

 2 Msifuni, enyi malaika zake wote.+

Msifuni, enyi jeshi lake lote.+

 3 Msifuni, enyi jua na mwezi.+

Msifuni, enyi nyota zote za nuru.+

 4 Msifuni, enyi mbingu za mbingu,+

Nanyi maji yaliyo juu ya mbingu.+

 5 Na vilisifu jina la Yehova;+

Kwa maana yeye mwenyewe aliamuru, navyo vikaumbwa.+

 6 Naye huendelea kuvisimamisha milele, mpaka wakati usio na kipimo.+

Amelitoa sharti, nalo halitapitilia mbali.+

 7 Msifuni Yehova kutoka duniani,+

Enyi wanyama wakubwa wa baharini, nanyi vilindi vyote vya maji,+

 8 Enyi moto na mvua ya mawe, theluji na moshi mzito,+

Enyi pepo zenye tufani, zinazotimiza neno lake,+

 9 Enyi milima, nanyi vilima vyote,+

Enyi miti ya matunda, nanyi mierezi yote,+

10 Enyi wanyama wa mwitu, nanyi wanyama wote wa kufugwa,+

Enyi vitu vinavyotambaa na ndege wenye mabawa,+

11 Enyi wafalme wa dunia,+ nanyi vikundi vyote vya mataifa,

Enyi wakuu,+ nanyi waamuzi wa dunia,+

12 Enyi vijana,+ nanyi mabikira pia,+

Enyi wazee+ pamoja na wavulana.+

13 Na walisifu jina la Yehova,+

Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana lisiweze kufikiwa.+

Utukufu wake uko juu ya dunia na mbingu.+

14 Naye ataiinua pembe ya watu wake,+

Sifa ya washikamanifu wake wote,+

Ya wana wa Israeli, watu walio karibu naye.+

Msifuni Yah!+

149 Msifuni Yah!+

Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+

Sifa yake katika kutaniko la washikamanifu.+

 2 Israeli na ashangilie katika Mtengenezaji Mkuu wake,+

Wana wa Sayuni—na wamshangilie Mfalme wao.+

 3 Na walisifu jina lake kwa kucheza dansi.+

Na wampigie muziki kwa tari na kinubi.+

 4 Kwa maana Yehova anawafurahia watu wake.+

Anawarembesha wapole kwa wokovu.+

 5 Washikamanifu na washangilie katika utukufu;

Na wapige vigelegele kwa shangwe vitandani mwao.+

 6 Nyimbo zinazomsifu sana Mungu na ziwe kooni mwao,+

Na upanga wenye makali kuwili uwe mkononi mwao,+

 7 Ili kutekeleza kisasi juu ya mataifa,+

Kuvikemea vikundi vya mataifa,+

 8 Ili kuwafunga wafalme wao kwa minyororo+

Na watu wao waliotukuzwa kwa pingu za chuma,

 9 Ili kutekeleza juu yao uamuzi wa hukumu ulioandikwa.+

Fahari ya namna hiyo ni ya washikamanifu wake wote.+

Msifuni Yah!+

150 Msifuni Yah!+

Msifuni Mungu katika mahali pake patakatifu.+

Msifuni katika anga la nguvu zake.+

 2 Msifuni kwa kazi zake zenye nguvu.+

Msifuni kulingana na wingi wa ukuu wake.+

 3 Msifuni kwa kupiga baragumu.+

Msifuni kwa kinanda na kinubi.+

 4 Msifuni kwa matari+ na kwa dansi ya mzunguko.+

Msifuni kwa vinanda+ na zumari.+

 5 Msifuni kwa matoazi yenye sauti tamu.+

Msifuni kwa matoazi ya kugonganishwa.+

 6 Kila kitu kinachopumua—na kimsifu Yah.+

Msifuni Yah!+

[Maelezo ya Chini]

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Pengine mamba.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Pengine mamba.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki