Zaburi
KITABU CHA KWANZA
1 Mwenye furaha+ ni mtu ambaye hakutembea katika shauri la waovu,+
Na katika njia ya watenda-dhambi hakusimama,+
Na katika kiti cha wenye dhihaka hakuketi.+
2 Bali mapendezi yake ni katika sheria ya Yehova,+
Naye huisoma sheria yake kwa sauti ya chini mchana na usiku.+
3 Naye hakika atakuwa kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji,+
Ambao hutoa matunda yake katika majira yake+
Na ambao majani yake hayanyauki,+
Na kila jambo analofanya litafanikiwa.+
5 Ndiyo sababu waovu hawatasimama katika hukumu,+
Wala watenda-dhambi katika kusanyiko la waadilifu.+
7 Acheni nirejezee agizo la Yehova;
Yeye ameniambia: “Wewe ni mwanangu;+
Mimi, leo, nimekuwa baba yako.+
Muziki wa Daudi alipokuwa akikimbia kwa sababu ya Absalomu mwana wake.+
5 Nami nitajilaza nipate kulala usingizi;
Hakika nitaamka, kwa maana Yehova anaendelea kunitegemeza.+
7 Usimame,+ Ee Yehova! Uniokoe,+ Ee Mungu wangu!+
Kwa maana utawapiga adui zangu wote kwenye taya.+
Utayavunja meno ya waovu.+
Kwa kiongozi wa vinanda.+ Muziki wa Daudi.
4 Ninapoita, unijibu, Ee Mungu wangu mwadilifu.+
Katika taabu unifanyie nafasi pana
Nionyeshe kibali+ na kuisikia sala yangu.
2 Enyi wana wa watu, utukufu+ wangu utatukanwa mpaka wakati gani,
Huku mkiendelea kupenda mambo ya upuuzi,
Huku mkiendelea kutafuta uwongo? Sela.
3 Basi jueni kwamba hakika Yehova atamtendea mshikamanifu wake kwa njia ya pekee;+
Yehova mwenyewe atasikia ninapomwita.+
7 Hakika wewe utaupa moyo wangu shangwe+
Iliyo kubwa kuliko wakati ambapo nafaka yao na divai yao mpya imejaa.+
8 Katika amani nitajilaza na kulala usingizi,+
Kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, hunifanya nikae kwa usalama.+
Kwa kiongozi wa Nehilothi. Muziki wa Daudi.
2 Sikiliza kwa makini sauti ya kilio changu kwa ajili ya msaada,+
Ee Mfalme+ wangu na Mungu wangu, kwa maana kwako wewe ninasali.+
4 Kwa maana wewe si Mungu anayependezwa na uovu;+
Hakuna mtu yeyote mbaya atakayekaa na wewe kwa muda wowote.+
5 Hakuna watu wowote wenye kujisifu watakaosimama mbele za macho yako.+
Wewe huwachukia wote wanaozoea kufanya mambo yenye kuumiza;+
7 Na mimi, katika wingi wa fadhili zako zenye upendo+
Nitaingia katika nyumba yako,+
Nitainama kulielekea hekalu lako takatifu kwa kukuogopa.+
8 Ee Yehova, uniongoze katika uadilifu+ wako kwa sababu ya adui zangu;+
Uifanye njia yako iwe laini mbele yangu.+
9 Kwa maana katika kinywa chao hakuna lolote lenye kutegemeka;+
Sehemu yao ya ndani ni shida kwelikweli.+
Koo yao ni kaburi lililo wazi;+
Wanatumia ulimi laini.+
10 Hakika Mungu atawahesabia hatia;+
Wataanguka kwa sababu ya mashauri yao wenyewe.+
Na watawanywe katika wingi wa makosa yao,+
Kwa sababu wamekuasi wewe.+
11 Lakini wote wanaokukimbilia watashangilia;+
Watapiga vigelegele vya shangwe+ mpaka wakati usio na kipimo.
Nawe utaweka kizuizi wasifikiwe,
Nao wanaolipenda jina lako watakushangilia.+
12 Kwa maana wewe mwenyewe utambariki mtu yeyote aliye mwadilifu,+ Ee Yehova;
Kana kwamba kwa ngao+ kubwa, utawazunguka pande zote+ kwa kibali chako.
Kwa kiongozi wa vinanda katika sauti ya nane ya chini.+ Muziki wa Daudi.
2 Nionyeshe kibali, Ee Yehova, kwa maana mimi ninafifia.+
Niponye,+ Ee Yehova, kwa maana mifupa yangu imesumbuka.
6 Nimechoshwa na kuugua kwangu;+
Usiku kucha nafanya kitanda changu kilowane;+
Kwa machozi yangu nafanya kitanda changu kifurike.+
7 Kutokana na masumbufu jicho langu limekuwa dhaifu,+
Limezeeka kwa sababu ya wale wote wanaonionyesha uadui.+
8 Ondokeni kwangu, ninyi nyote mnaozoea kutenda mambo yenye kuumiza,+
Kwa maana hakika Yehova atasikia sauti ya kulia kwangu.+
Wimbo wa huzuni wa Daudi ambao alimwimbia Yehova kuhusu maneno ya Kushi Mbenyamini.
7 Ee Yehova Mungu wangu,+ nimekukimbilia wewe.+
Uniokoe kutoka kwa wale wote wanaonitesa na unikomboe,+
2 Ili mtu yeyote asiirarue nafsi yangu vipande-vipande kama simba anavyofanya,+
Kuninyakua wakati ambapo hakuna mkombozi.+
3 Ee Yehova Mungu wangu, ikiwa nimefanya hili,+
Ikiwa kuna ukosefu wowote wa haki katika mikono yangu,+
4 Ikiwa nimemlipa ubaya yule anayenipa thawabu,+
Au ikiwa nimempora yeyote anayenionyesha uadui bila kufanikiwa,+
5 Adui na aifuatilie nafsi yangu+
Naye afikie na kukanyagia chini uhai wangu
Na kufanya utukufu wangu ukae mavumbini. Sela.
6 Usimame, Ee Yehova, katika hasira yako;+
Uinuke katika milipuko ya ghadhabu ya wale wanaonionyesha uadui,+
Na uamke kwa ajili yangu,+ kwa maana umetoa amri kwa ajili ya hukumu.+
7 Nalo kusanyiko la vikundi vya mataifa na likuzunguke,
Nawe urudi juu dhidi yake.
8 Yehova mwenyewe atavihukumu vikundi vya watu.+
Nihukumu, Ee Yehova, kulingana na uadilifu wangu+
Na kulingana na utimilifu+ wangu ulio ndani yangu.
10 Ngao yangu iko juu ya Mungu,+ Mwokozi wa wale walio wanyoofu moyoni.+
12 Ikiwa mtu yeyote hatarudi,+ Yeye ataunoa upanga wake,+
Hakika ataupinda upinde wake, naye atauweka tayari ili kufyatuliwa.+
14 Tazama! Kuna mtu aliye na mimba ya jambo lenye kuumiza,+
Naye amechukua mimba ya taabu na hatakosa kuzaa uwongo.+
16 Taabu yake itarudi juu ya kichwa chake mwenyewe,+
Na jeuri yake mwenyewe itashuka juu ya utosi wa kichwa chake.+
Kwa kiongozi wa Gitithi.+ Muziki wa Daudi.
8 Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu kama nini katika dunia yote,+
Wewe ambaye utukufu wako unasimuliwa juu ya mbingu!+
2 Kutoka katika kinywa cha watoto na wanaonyonya umeiweka misingi ya nguvu,+
Kwa sababu ya wale wanaokuonyesha uadui,+
Ili kumkomesha adui na yule anayejilipizia kisasi.+
4 Mwanadamu anayeweza kufa+ ni nini hivi kwamba umweke akilini,+
Na mwana wa mtu wa udongo hivi kwamba umtunze?+
9 Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu kama nini katika dunia yote!+
Kwa kiongozi wa Muth-labeni. Muziki wa Daudi.
א [ʼAʹleph]
ב [Behth]
4 Kwa maana umetekeleza hukumu yangu na kesi yangu;+
Umeketi juu ya kiti cha ufalme ukihukumu kwa uadilifu.+
ג [Giʹmel]
5 Umeyakemea mataifa,+ umemwangamiza mwovu.+
Jina lao umelifutilia mbali mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
6 Ewe adui, ukiwa wako umefikia mwisho wake wa kudumu,+
Na majiji ambayo umeyang’oa.+
Kumbukumbu lao hakika litaangamia.+
ה [Heʼ]
7 Yeye Yehova ataketi mpaka wakati usio na kipimo,+
Akifanya imara kiti chake cha ufalme kwa ajili ya hukumu.+
8 Naye mwenyewe ataihukumu kwa uadilifu nchi yenye kuzaa;+
Atavihukumu vikundi vya mataifa kwa unyoofu.+
ו [Waw]
9 Naye Yehova atakuwa kilele salama kwa ajili ya mtu yeyote aliyekandamizwa,+
Kilele salama wakati wa taabu.+
10 Na wale wanaolijua jina lako watakutegemea,+
Kwa maana hakika hutawaacha wale wanaokutafuta, Ee Yehova.+
ז [Zaʹyin]
11 Mpigieni Yehova muziki, yeye anayekaa Sayuni;+
Tangazeni matendo yake katikati ya vikundi vya watu.+
12 Kwa maana, wakati wa kutafuta umwagikaji wa damu,+ hakika atawakumbuka hao;+
Hakika yeye hatakisahau kilio cha wenye kuteseka.+
ח [Chehth]
13 Unionyeshe kibali, Ee Yehova; uone mateso yangu kutoka kwa wale wanaonichukia,+
Ewe unayeniinua kutoka katika malango ya kifo,+
14 Ili niyatangaze matendo yako yote yanayostahili sifa+
Katika malango+ ya binti Sayuni,+
Ili niushangilie wokovu wako.+
ט [Tehth]
16 Yehova anajulikana kwa hukumu ambayo ametekeleza.+
Mwovu amenaswa na utendaji wa mikono yake mwenyewe.+
Higayoni. Sela.
י [Yohdh]
כ [Kaph]
19 Usimame, Ee Yehova! Mwanadamu anayeweza kufa asiwe na nguvu zaidi.+
Mataifa na yahukumiwe mbele za uso wako.+
20 Utie woga ndani yao, Ee Yehova,+
Ili mataifa yapate kujua kwamba wao ni wanadamu tu wanaoweza kufa.+ Sela.
ל [Laʹmedh]
2 Katika majivuno yake, mwovu humfuatilia vikali mwenye kuteseka;+
Wanakamatwa na mawazo ambayo wametunga.+
3 Kwa maana mwovu amejisifu kwa sababu ya tamaa yenye ubinafsi ya nafsi yake,+
Naye anayepata faida asiyostahili+ amejibariki;
נ [Nun]
Amekosa kumheshimu Yehova.+
5 Njia zake zinaendelea kufanikiwa wakati wote.+
Maamuzi yako ya hukumu yako juu sana asiweze kuyafikia;+
Nao wale wote wanaomwonyesha uadui, anawafanyia dhihaka.+
פ [Peʼ]
7 Kinywa chake kimejaa viapo na udanganyifu na ukandamizaji.+
Chini ya ulimi wake kuna taabu na mambo yenye kuumiza.+
ע [ʽAʹyin]
Macho yake yanamtafuta mtu mwenye taabu.+
9 Yeye anaendelea kuvizia katika mahali palipofichika kama simba mafichoni mwake.+
Anaendelea kuvizia+ ili amchukue kwa nguvu mtu fulani mwenye kuteseka.
Humchukua kwa nguvu mtu mwenye kuteseka anapouvuta pamoja wavu wake.+
ק [Qohph]
ר [Rehsh]
14 Kwa maana wewe mwenyewe umeona taabu na masumbufu.
Unaendelea kutazama, uyatie katika mkono wako.+
Mtu mwenye taabu,+ mvulana asiye na baba, anajikabidhi kwako.
Wewe mwenyewe umekuwa msaidizi wake.+
ש [Shin]
16 Yehova ni Mfalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
Mataifa yameangamia kutoka katika dunia yake.+
ת [Taw]
17 Tamaa ya wapole hakika utaisikia,+ Ee Yehova.
Utautayarisha moyo wao.+
Utasikiliza kwa makini kwa sikio lako.+
18 Ili kumhukumu mvulana asiye na baba na mtu aliyepondwa,+
Ili mwanadamu anayeweza kufa, aliye wa dunia, asisababishe tena kutetemeka.+
Kwa kiongozi. Ya Daudi.
Mnawezaje kuthubutu kuiambia nafsi yangu:
“Kimbieni kwenye mlima wenu kama ndege!+
2 Kwa maana, tazama! waovu huupinda upinde,+
Huutayarisha mshale wao juu ya kamba ya upinde,
Ili katika giza wawafyatulie walio wanyoofu moyoni.+
4 Yehova yumo katika hekalu lake takatifu.+
Yehova—kiti chake cha ufalme kiko mbinguni.+
Macho yake yanaangalia, macho yake yanayong’aa yanawachunguza+ wana wa binadamu.
5 Yehova humchunguza mwadilifu na pia mwovu,+
Na mtu yeyote anayependa jeuri nafsi Yake hakika inamchukia.+
6 Yeye atawanyeshea waovu mitego, moto na kiberiti+
Na upepo wenye kuunguza, vikiwa fungu la kikombe chao.+
7 Kwa maana Yehova ni mwadilifu;+ yeye huyapenda matendo ya uadilifu.+
Wanyoofu ndio watakaouona uso wake.+
Kwa kiongozi katika sauti ya nane ya chini.+ Muziki wa Daudi.
12 Uniokoe,+ Ee Yehova, kwa maana mshikamanifu amefikia mwisho;+
Kwa maana watu waaminifu wametoweka kutoka katikati ya wana wa binadamu.
2 Wao huendelea kusemezana mambo yasiyo ya kweli;+
Kwa midomo laini+ wao huendelea kusema wakiwa na mioyo miwili.+
4 Wale ambao wamesema: “Kwa ulimi wetu tutashinda.+
Midomo yetu iko pamoja nasi. Ni nani atakayekuwa bwana kwetu?”
5 “Kwa sababu ya kuporwa kwao wenye kuteseka, kwa sababu ya kuugua kwao maskini,+
Nitasimama wakati huu,” asema Yehova.+
“Nitamweka katika usalama mbali na mtu yeyote anayemdhihaki.”+
6 Maneno ya Yehova ni maneno safi,+
Kama fedha iliyosafishwa katika tanuru ya kuyeyushia kwenye udongo, iliyosafishwa mara saba.
7 Wewe mwenyewe, Ee Yehova, utawalinda;+
Utamhifadhi kila mmoja kutokana na kizazi hiki mpaka wakati usio na kipimo.
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
2 Nitaweka upinzani katika nafsi yangu mpaka wakati gani,
Huzuni katika moyo wangu wakati wa mchana?
Adui yangu atainuliwa juu yangu mpaka wakati gani?+
3 Unitazame; unijibu, Ee Yehova Mungu wangu.
Uyafanye macho yangu yang’ae,+ ili nisilale usingizi katika kifo.+
4 Ili adui yangu asiseme: “Nimemshinda!”
Ili wapinzani wangu wasishangilie kwa sababu nimefanywa niyumbe-yumbe.+
6 Nitamwimbia Yehova, kwa maana amenitendea kwa njia ya kunipa thawabu.+
Kwa kiongozi. Ya Daudi.
14 Asiye na akili amesema katika moyo wake:
“Hakuna Yehova.”+
Wametenda kwa uharibifu,+ wametenda kwa njia yenye kuchukiza katika shughuli zao.
Hakuna yeyote anayefanya mema.+
2 Kutoka mbinguni Yehova amewatazama wana wa binadamu walio chini,+
Ili aone kama kuna yeyote ambaye ana ufahamu, yeyote anayemtafuta Yehova.+
3 Wote wamegeuka kando,+ wote ni wafisadi kwa njia ileile;+
Hakuna yeyote anayefanya mema,+
Hakuna hata mmoja.+
4 Je, hakuna yeyote kati ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza ambaye ana ujuzi,+
Wakila watu wangu kama vile ambavyo wamekula mkate?+
Hata hawajamwitia Yehova.+
7 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+
Wakati ambapo Yehova anawakusanya tena mateka wa watu wake,+
Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.+
Muziki wa Daudi.
15 Ee Yehova, ni nani atakayekuwa mgeni katika hema lako?+
Ni nani atakayekaa katika mlima wako mtakatifu?+
3 Yeye hakuchongea kwa ulimi wake.+
Hakumfanyia mwenzake jambo lolote baya,+
Wala hakumshutumu rafiki yake.+
4 Machoni pake mtu yeyote mwenye kudharaulika hakika amekataliwa,+
Lakini yeye anawaheshimu wale wanaomwogopa Yehova.+
Ameapa juu ya jambo lililo baya kwake, na bado yeye habadiliki.+
5 Pesa zake hakutoa ili apate faida,+
Wala hakuchukua rushwa dhidi ya mtu asiye na hatia.+
Yeye anayefanya mambo hayo hatatikiswa.+
Miktamu ya Daudi.
16 Unihifadhi, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+
2 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Yehova; wema wangu si kwa ajili yako,+
3 Bali kwa watakatifu walio duniani.
Wao, naam, wale mashuhuri, ndio ninaopendezwa nao kabisa.”+
4 Maumivu huwa mengi kwa wale ambao, wakati kuna mtu mwingine, humfuata haraka.+
Sitamimina matoleo yao ya kinywaji ya damu,+
Nami sitayachukua majina yao juu ya midomo yangu.+
5 Yehova ndiye sehemu ya fungu langu+ nililogawiwa na ya kikombe changu.+
Wewe unaishika sana kura yangu.
7 Nitambariki Yehova, ambaye amenipa shauri.+
Kwa kweli, nyakati za usiku figo zangu zimenirekebisha.+
9 Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nao utukufu wangu una mwelekeo wa kuwa na shangwe.+
Pia, mwili wangu mwenyewe utakaa katika usalama.+
11 Utanijulisha njia ya uzima.+
Shangwe ya kutosha iko pamoja na uso wako;+
Kuna uzuri upande wa mkono wako wa kuume milele.+
Sala ya Daudi.
17 Usikie jambo la uadilifu, Ee Yehova; Usikilize kwa makini kilio changu cha kusihi;+
Tega sikio kwa sala yangu bila midomo ya udanganyifu.+
3 Umeuchunguza moyo wangu, umefanya ukaguzi wakati wa usiku,+
Umenisafisha; utagundua kwamba sijapanga hila.+
Kinywa changu hakitafanya kosa.+
4 Nao utendaji wa wanadamu,
Kwa maneno ya midomo yako mimi mwenyewe nimejilinda na njia za mnyang’anyi.+
6 Mimi mwenyewe nakuitia wewe, kwa sababu utanijibu, Ee Mungu.+
Tega sikio lako kwangu. Usikilize neno langu.+
7 Uyafanye matendo yako ya fadhili zenye upendo yawe ya ajabu,+ Ee Mwokozi wa wale wanaotafuta kimbilio
Kutoka kwa waasi walio dhidi ya mkono wako wa kuume.+
12 Mfano wake ni ule wa simba anayetamani kurarua vipande-vipande+
Na ule wa mwana-simba anayekaa mahali palipofichika.
13 Usimame, Ee Yehova; umkabili usoni;+
Mfanye ainame; kwa upanga wako uiokoe nafsi yangu kutoka kwa mwovu,+
14 Kwa mkono wako, Ee Yehova, kutoka kwa watu,+
Kutoka kwa watu wa mfumo huu wa mambo,+ ambao fungu lao liko katika maisha haya,+
Na ambao tumbo lao wewe hulijaza kwa hazina iliyofichwa,+
Ambao wametosheka na wana+
Na ambao huwarundikia watoto wao vitu wanavyoacha.+
Kwa kiongozi. Wa mtumishi wa Yehova, wa Daudi, aliyemwambia Yehova maneno ya wimbo huu siku ambayo Yehova alikuwa amemkomboa kutoka mkononi mwa adui zake wote na kutoka mkononi mwa Sauli.+ Naye akasema:
18 Nitakupenda wewe, Ee Yehova nguvu zangu.+
2 Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu na Mwokoaji wangu.+
Mungu wangu ni mwamba wangu. Nitamkimbilia,+
Ngao yangu na pembe yangu ya wokovu, kilele changu salama.+
4 Kamba za kifo zilinizunguka;+
Mafuriko ya ghafula ya watu wasiofaa kitu pia yaliendelea kuniogopesha.+
6 Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,
Nami niliendelea kumlilia Mungu wangu kwa ajili ya msaada.+
Kutoka katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+
Nacho kilio changu cha msaada mbele zake sasa kikafika masikioni mwake.+
7 Na dunia ikaanza kutikisika na kutetemeka,+
Nayo misingi ya milima ikasukasuka,+
Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
8 Moshi ukapanda katika mianzi ya pua yake, nao moto kutoka kinywani mwake ukaendelea kuteketeza;+
Makaa yakawaka moto kutoka kwake.
10 Naye akaja akiwa amepanda juu ya kerubi, akaja akiwa anaruka,+
Naye akaja akiruka juu ya mabawa ya roho.+
Maji yenye giza, mawingu mazito.+
12 Kutoka katika mwangaza ulio mbele yake kulikuwa na mawingu yake yaliyopita,+
Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto.+
13 Na mbinguni Yehova akaanza kunguruma,+
Na Aliye Juu Zaidi akaanza kutoa sauti yake,+
Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto.
15 Na sakafu za vijito vya maji zikaonekana,+
Na misingi ya nchi yenye kuzaa ikafunuliwa,+
Kwa kemeo lako, Ee Yehova, kwa mlipuko wa pumzi ya pua yako.+
17 Alikuwa akinikomboa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+
Na kutoka kwa wale wanaonichukia; kwa sababu walikuwa na nguvu kuliko mimi.+
18 Waliendelea kunikabili katika siku ya msiba wangu,+
Lakini Yehova akawa kama tegemeo kwa ajili yangu.+
19 Naye akanitoa nje mpaka mahali penye nafasi tele;+
Alikuwa akiniokoa, kwa sababu alikuwa amependezwa nami.+
22 Kwa maana maamuzi yake yote ya hukumu yako mbele yangu,+
Nazo sheria zake sitaziondoa kutoka kwangu.+
24 Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+
Kulingana na usafi wa mikono yangu mbele za macho yake.+
25 Kwa mtu mshikamanifu utatenda kwa ushikamanifu;+
Kwa mwanamume asiye na kosa, wewe utatenda kwa njia isiyo na kosa;+
28 Kwa maana wewe mwenyewe utaiwasha taa yangu, Ee Yehova;+
Mungu wangu atafanya giza langu liangaze.+
29 Kwa maana kwa msaada wako ninaweza kukimbiza kikundi cha waporaji;+
Na kwa msaada wa Mungu wangu ninaweza kuupanda ukuta.+
30 Mungu wa kweli, njia yake ni kamilifu;+
Neno la Yehova limetakaswa.+
Yeye ni ngao kwa wale wote wanaomkimbilia.+
32 Mungu wa kweli Ndiye anayenifunga sana mshipi wa nguvu,+
Naye ataifanya njia yangu kuwa kamilifu,+
33 Kuifanya miguu yangu iwe kama ya paa,+
Na kwenye mahali palipo juu kwangu yeye huendelea kunisimamisha.+
35 Nawe utanipa ngao yako ya wokovu,+
Na mkono wako mwenyewe wa kuume utanitegemeza,+
Na unyenyekevu wako mwenyewe utanifanya kuwa mkuu.+
36 Utafanyiza nafasi kubwa ya kutosha kwa ajili ya hatua zangu zilizo chini yangu,+
Navyo vifundo vya miguu yangu hakika havitatetemeka.+
40 Nao adui zangu, utanipa upande wa nyuma wa shingo zao;+
Nao wale wanaonichukia vikali, nitawanyamazisha.+
42 Nami nitawatwanga wawe laini kama mavumbi mbele ya upepo;+
Nitawamwaga kama matope ya barabarani.+
Watu ambao sijawajua—watanitumikia.+
47 Mungu wa kweli ndiye Mpaji wa matendo ya kisasi kwangu;+
Naye hutiisha vikundi vya watu chini yangu.+
48 Ananiokoa kutoka kwa adui zangu wenye hasira;+
Utaniinua juu ya wale wanaosimama dhidi yangu,+
Utanikomboa kutoka kwa mtu mwenye jeuri.+
50 Yeye anafanya matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake+
Na kuonyesha fadhili zenye upendo kwa mtiwa-mafuta wake,+
Kwa Daudi na kwa uzao wake mpaka wakati usio na kipimo.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
2 Siku moja baada ya siku nyingine hufanya maneno yabubujike,+
Na usiku mmoja baada ya usiku mwingine huonyesha ujuzi.+
4 Kamba yake ya kupimia imefika duniani pote,+
Na maneno yake yamefika kwenye miisho ya nchi yenye kuzaa.+
Katika hizo amewekea jua hema,+
5 Nalo ni kama bwana-arusi anapotoka katika chumba chake cha ndoa;+
Linashangilia kama mwanamume mwenye nguvu anapokimbia njiani.+
6 Linaenda kutoka mwisho mmoja wa mbingu,
Nao mzunguko wake humalizikia katika ile miisho yake mingine;+
Wala hakuna chochote kilichofichwa kisiweze kupatwa na joto lake.+
7 Sheria+ ya Yehova ni kamilifu,+ huirudisha nafsi.+
Kikumbusho+ cha Yehova ni chenye kutegemeka,+ humfanya asiye na uzoefu awe na hekima.+
9 Kumwogopa+ Yehova ni jambo safi, husimama milele.
Maamuzi ya hukumu+ ya Yehova ni ya kweli;+ yote yameonekana kuwa yenye uadilifu.+
13 Pia umzuie mtumishi wako kutokana na matendo ya kimbelembele;+
Usiyaache yanitawale.+
Hapo ndipo nitakapokuwa kamili,+
Nami nitakuwa sina hatia ya makosa mengi.
14 Maneno ya kinywa changu na kutafakari kwa moyo wangu+
Na yawe yenye kupendeza mbele zako, Ee Yehova Mwamba+ wangu na Mkombozi wangu.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
3 Na akumbuke matoleo yako yote ya zawadi,+
Naye na ayakubali matoleo yako ya kuteketezwa kuwa ni mafuta.+ Sela.
5 Tutapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya wokovu wako,+
Nasi tutainua bendera zetu katika jina la Mungu wetu.+
Yehova na atimize maombi yako yote.+
6 Sasa najua kwamba hakika Yehova humwokoa mtiwa-mafuta wake.+
Humjibu kutoka katika mbingu zake takatifu+
Kwa matendo ya kuokoa yenye nguvu ya mkono wake wa kuume.+
7 Wengine hutaja kuhusu magari na wengine kuhusu farasi,+
Lakini sisi, tutataja kuhusu jina la Yehova Mungu wetu.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
21 Ee Yehova, mfalme hushangilia katika nguvu zako;+
Na katika wokovu wako jinsi anavyotaka kuwa na shangwe sana!+
9 Utawafanya wawe kama tanuru yenye moto wakati wako uliowekwa wa kukaza uangalifu wako;+
Yehova atawameza katika hasira yake, na moto utawateketeza.+
12 Kwa maana utawafanya wageuze migongo yao kwa kukimbia+
Kwa nyuzi za upinde wako ambazo unatayarisha dhidi ya nyuso zao.+
Kwa kiongozi juu ya Paa wa Mapambazuko. Muziki wa Daudi.
22 Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?+
Kwa nini uko mbali usiniokoe,+
Mbali na maneno ya mngurumo wangu?+
2 Ee Mungu wangu, mimi huendelea kuita wakati wa mchana, nawe huitiki;+
Na wakati wa usiku, wala sinyamazi.+
7 Wale wote wanaoniona mimi, hunidharau;+
Wanaendelea kufungua vinywa vyao wazi, wanaendelea kutikisa vichwa vyao:+
8 “Yeye alijitia mikononi mwa Yehova.+ Acha Yeye amwokoe!+
Na amkomboe, kwa kuwa yeye amependezwa naye!”+
9 Kwa maana Wewe ndiye uliyenitoa tumboni,+
Wewe ndiye unayenifanya niwe na tegemeo nilipokuwa kwenye maziwa ya mama yangu.+
10 Nimetupwa kwako kutoka tumbo la uzazi;+
Kutoka katika tumbo la mama yangu wewe umekuwa Mungu wangu.+
Na mifupa yangu yote imetenganishwa.+
Moyo wangu umekuwa kama nta;+
Umeyeyuka ndani katika sehemu zangu za ndani.+
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae cha udongo,+
Na ulimi wangu umefanywa ushikamane na ufizi wangu;+
Nawe unaniweka katika mavumbi ya kifo.+
16 Kwa maana mbwa wamenizingira;+
Kusanyiko la watenda-maovu limenizunguka.+
Wako kwenye mikono yangu na miguu yangu kama simba.+
21 Uniokoe kutokana na kinywa cha simba,+
Na unijibu na kuniokoa kutokana na pembe za ng’ombe-mwitu.+
23 Ninyi mnaomwogopa Yehova, msifuni!+
Enyi nyote mlio uzao wa Yakobo, mtukuzeni!+
Na mwogopeni yeye, enyi nyote mlio uzao wa Israeli.+
Wala kuchoshwa na mateso ya mwenye kuteseka;+
Naye hakumficha uso wake,+
Naye alipomlilia amsaidie alisikia.+
25 Kutoka kwako sifa yangu itakuwa katika kutaniko kubwa;+
Nadhiri zangu nitazitimiza mbele ya wale wanaomwogopa.+
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kurudi kwa Yehova.+
Na familia zote za mataifa zitainama mbele zako.+
29 Wote walio wanono wa dunia watakula na kuinama;+
Wote wanaoenda chini mavumbini watainama mbele zake,+
Wala hakuna atakayeihifadhi hai nafsi yake.+
31 Watakuja na kusema juu ya uadilifu wake+
Kwa kikundi cha watu kitakachozaliwa, kwamba ni yeye amefanya hilo.+
Muziki wa Daudi.
2 Ananilaza katika malisho yenye majani mengi;+
Ananiongoza kando ya mahali pa kupumzika palipo na maji ya kutosha.+
4 Hata ingawa ninatembea katika bonde lenye kivuli kizito,+
Siogopi chochote kibaya,+
Kwa maana wewe uko pamoja nami;+
Fimbo yako na gongo lako ndivyo vitu vinavyonifariji.+
5 Mbele yangu wewe unatayarisha meza mbele ya wale wanaonionyesha uadui.+
Umepaka kichwa changu mafuta;+
Kikombe changu kimejazwa vizuri.+
6 Kwa hakika wema na fadhili zenye upendo zitanifuata siku zote za maisha yangu;+
Nami nitakaa katika nyumba ya Yehova siku nyingi.+
Ya Daudi. Muziki.
3 Ni nani anayeweza kuupanda mlima wa Yehova,+
Na ni nani anayeweza kusimama katika mahali pake patakatifu?+
4 Yeyote asiye na hatia katika mikono yake na aliye safi moyoni,+
Ambaye hajaitendea nafsi Yangu kwa ubatili mtupu,+
Wala kuapa kwa udanganyifu.+
6 Hiki ndicho kizazi cha wale wanaomtafuta,
Cha wale wanaoutafuta uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.+ Sela.
Ili Mfalme mtukufu apate kuingia!”+
8 “Basi, Mfalme huyo mtukufu ni nani?”+
“Yehova mwenye nguvu na mwenye uwezo,+
Yehova mwenye uwezo katika vita.”+
9 “Inueni vichwa vyenu, enyi malango;+
Naam, viinueni juu, enyi miingilio ya kudumu,
Ili Mfalme mtukufu apate kuingia!”+
Ya Daudi.
א [ʼAʹleph]
25 Kwako wewe, Ee Yehova, naiinua nafsi yangu.+
ב [Behth]
ג [Giʹmel]
3 Pia, hakuna yeyote kati ya wale wanaokutumainia atakayeona aibu.+
Wale wanaotenda kwa hila bila kupata mafanikio wataona aibu.+
ד [Daʹleth]
ה [Heʼ]
ו [Waw]
Nimekutumainia mchana kutwa.+
ז [Zaʹyin]
6 Ukumbuke rehema zako,+ Ee Yehova, na fadhili zako zenye upendo,+
Kwa maana ni za tangu wakati usio na kipimo.+
ח [Chehth]
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu na maasi yangu.+
Unikumbuke kulingana na fadhili zako zenye upendo,+
Kwa ajili ya wema wako, Ee Yehova.+
ט [Tehth]
י [Yohdh]
כ [Kaph]
10 Mapito yote ya Yehova ni fadhili zenye upendo na ukweli
ל [Laʹmedh]
מ [Mem]
נ [Nun]
ס [Saʹmekh]
14 Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wanaomwogopa,+
Pia agano lake, ili kuwafanya walijue.+
ע [ʽAʹyin]
פ [Peʼ]
16 Unielekezee uso wako, na unionyeshe kibali;+
Kwa maana mimi niko peke yangu nami ni mwenye kuteseka.+
צ [Tsa·dhehʹ]
ר [Rehsh]
ש [Shin]
ת [Taw]
22 Ee Mungu, mkomboe Israeli kutoka katika taabu zake zote.+
Ya Daudi.
26 Unihukumu,+ Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika utimilifu wangu,+
Nami nimemtumaini Yehova, nisipate kutikisika.+
6 Nitaiosha mikono yangu katika kutokuwa na hatia,+
Nami nitatembea nikizunguka madhabahu yako, Ee Yehova,+
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda-dhambi,+
Wala uhai wangu pamoja na watu wenye hatia ya damu,+
Ya Daudi.
27 Yehova ni nuru yangu+ na wokovu wangu.+
2 Watenda-maovu walipokuja karibu juu
yangu ili wapate kuila nyama yangu,+
Wao wakiwa ni wapinzani wangu na adui zangu,+
Wao walijikwaa na kuanguka.+
3 Hata kambi ijapopiga hema dhidi yangu,+
Moyo wangu hautaogopa.+
Vita vijapozuka dhidi yangu,+
Bado nitakuwa na tegemeo wakati huo.+
4 Nimemwomba Yehova jambo moja+—
Ndilo nitakalolitafuta,+
Kwamba nipate kukaa katika nyumba ya Yehova siku zote za maisha yangu,+
Ili kuuona uzuri wa Yehova+
Na kulitazama kwa uthamini hekalu lake.+
5 Kwa maana atanificha mafichoni mwake katika siku ya msiba;+
Atanificha katika mahali pa siri pa hema lake;+
Ataniweka juu kwenye mwamba.+
6 Na sasa kichwa changu kitakuwa juu, juu ya adui zangu wanaonizunguka pande zote;+
Nami nitatoa kwenye hema lake dhabihu za vigelegele vya shangwe;+
Nitamwimbia Yehova na kumpigia muziki.+
Usimgeuzie mbali mtumishi wako kwa hasira.+
Uwe msaada wangu.+
Usinitupe wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.+
12 Usinitie mikononi mwa nafsi ya wapinzani wangu;+
Kwa maana dhidi yangu wamesimama mashahidi wa uwongo,+
Na yeye anayetokeza jeuri.+
13 Kama nisingalikuwa na imani katika kuuona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai+—!
Ya Daudi.
28 Mimi huendelea kukuita wewe, Ee Yehova.+
Ee Mwamba wangu, usiwe kwangu kama kiziwi,+
Ili usininyamazie+
Nami nisilazimike kuwa kama wale wanaoshuka chini shimoni.+
2 Uisikie sauti ya kusihi kwangu ninapokulilia unisaidie,
Wakati ninapoinua mikono+ yangu katika chumba cha ndani kabisa cha mahali pako patakatifu.+
3 Usinikokote pamoja na watu waovu na pamoja na wanaotenda mambo yenye kuumiza,+
Wale wanaosema amani na wenzao+ lakini ambao katika mioyo yao mna jambo lililo baya.+
4 Uwape kulingana na matendo yao+
Na kulingana na ubaya wa mazoea yao.+
Uwape kulingana na kazi ya mikono yao.+
Uwalipe matendo yao wenyewe.+
5 Kwa maana hawajali utendaji wa Yehova,+
Wala kazi ya mikono yake.+
Yeye atawabomoa wala hatawajenga.
6 Yehova na abarikiwe, kwa maana ameisikia sauti ya kusihi kwangu.+
7 Yehova ni nguvu+ zangu na ngao+ yangu.
Moyo wangu umemtegemea yeye,+
Nami nimesaidiwa, hivi kwamba moyo wangu unashangilia,+
Nami nitamsifu kwa wimbo wangu.+
9 Uwaokoe watu wako, na kuubariki urithi wako;+
Na uwachunge na kuwabeba mpaka wakati usio na kipimo.+
Muziki wa Daudi.
3 Sauti ya Yehova iko juu ya maji;+
Mungu mtukufu+ mwenyewe amenguruma.+
Yehova yuko juu ya maji mengi.+
7 Sauti ya Yehova inapasua kwa miali ya moto;+
8 Sauti ya Yehova huifanya nyika itetemeke,+
Yehova huifanya nyika ya Kadeshi+ itetemeke.
9 Sauti ya Yehova huwafanya paa watetemeke kwa maumivu ya kuzaa+
Na kuivua kabisa misitu.+
Na katika hekalu lake kila mmoja anasema: “Utukufu!”+
Muziki. Wimbo wa kuzindua nyumba.+ Wa Daudi.
30 Nitakutukuza wewe, Ee Yehova, kwa maana umeniinua+
Nawe hukuwaruhusu adui zangu washangilie juu yangu.+
2 Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, nawe ukaniponya.+
3 Ee Yehova, umeitoa nafsi yangu kutoka katika Kaburi;*+
Umeendelea kuniweka nikiwa hai, ili nisipate kushuka ndani ya shimo.+
5 Kwa sababu kuwa chini ya hasira yake ni kwa muda kidogo tu,+
Kuwa chini ya nia yake njema ni kwa muda wote wa maisha.+
Huenda kilio kikakaa wakati wa jioni,+ lakini asubuhi kuna vigelegele vya shangwe.+
7 Ee Yehova, umeusimamisha mlima wangu katika nguvu kwa nia yako njema.+
Uliuficha uso wako; nikawa na wasiwasi.+
9 Damu yangu ina faida gani ninaposhuka katika shimo?+
Je, mavumbi yatakusifu wewe?+ Je, yatasema juu ya ukweli wako?+
11 Umenibadilishia maombolezo yangu yakawa kucheza dansi;+
Umefungua nguo yangu ya gunia, nawe unaendelea kunifunga shangwe,+
12 Ili utukufu wangu upate kukupigia muziki wala usinyamaze.+
Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu mpaka wakati usio na kipimo.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
6 Nawachukia wale wanaoonyesha kujali sanamu zisizo na faida, za ubatili;+
Lakini mimi, namtegemea Yehova.+
7 Nitakuwa na shangwe na kushangilia katika fadhili zako zenye upendo,+
Kwa kuwa umeona mateso yangu;+
Umejua juu ya taabu za nafsi yangu.+
9 Unionyeshe kibali, Ee Yehova, kwa maana niko katika dhiki kali.+
Mambo yenye kukera yamefanya jicho langu liwe dhaifu,+ naam, nafsi yangu na tumbo langu.+
10 Kwa maana uhai wangu umefikia mwisho kwa huzuni,+
Na miaka yangu kwa kuugua.+
Kwa sababu ya kosa langu nguvu zangu zimejikwaa,+
Na mifupa yangu imekuwa dhaifu.+
11 Nimekuwa shutuma+ kwa wale wote wanaonionyesha uadui,+
Na nimekuwa hivyo hata zaidi kwa jirani zangu,+
Na kitu chenye kutia hofu kwa rafiki zangu.+
Wakati wanaponiona nje, wamenikimbia.+
12 Nimesahaulika kama mtu ambaye amekufa na ambaye hayumo moyoni;+
Nimekuwa kama chombo kilichoharibika;+
13 Kwa maana nimeisikia habari mbaya kutoka kwa wengi,+
Pande zote kukiwa na woga.+
Wanapoungana kama kitu kimoja dhidi yangu,+
Wanapanga hila ili kuiondoa nafsi yangu.+
15 Nyakati zangu ziko katika mkono wako.+
Unikomboe kutoka katika mkono wa adui zangu na kutoka kwa wale wanaonifuatilia.+
18 Midomo inayosema uwongo na ishindwe kusema,+
Inayosema mambo dhidi ya mwadilifu,+ bila kujizuia katika majivuno na dharau.+
19 Jinsi ulivyo mwingi wema wako,+ ambao umewawekea hazina wale wanaokuogopa!+
Ambao umewapa wale wanaokukimbilia wewe,
Mbele ya wana wa binadamu.+
20 Utawaficha katika mahali pa siri pa uso wako+
Mbali na ukusanyikaji pamoja wa watu.+
Utawaficha katika kibanda chako mbali na kugombana kwa ndimi.+
22 Mimi nilisema hivi niliposhikwa na wasiwasi:+
“Hakika nitaangamizwa kutoka mbele za macho yako.”+
Bila shaka umeisikia sauti ya kusihi kwangu nilipokulilia unisaidie.+
23 Enyi washikamanifu wake wote, mpendeni Yehova.+
Yehova anawalinda waaminifu,+
Lakini anampa malipo tele yeyote anayeonyesha majivuno.+
Ya Daudi. Maskili.
32 Mwenye furaha ni mtu ambaye amesamehewa maasi yake, ambaye dhambi yake imefunikwa.+
2 Mwenye furaha ni mtu ambaye Yehova hamhesabii kosa,+
Na ambaye katika roho yake hamna udanganyifu.+
3 Nilipokaa kimya mifupa yangu ilichakaa kwa sababu ya kuugua kwangu mchana kutwa.+
4 Kwa maana mkono wako ulikuwa mzito juu yangu mchana na usiku.+
Umajimaji wa uhai wangu umenyauka kama wakati wa joto kavu la kiangazi.+ Sela.
5 Mwishowe niliungama dhambi yangu kwako, wala sikufunika kosa langu.+
Nilisema: “Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.”+
Nawe mwenyewe ukanisamehe kosa la dhambi zangu.+ Sela.
6 Kwa sababu hiyo kila aliye mshikamanifu atasali kwako+
Katika wakati ule tu ambao wewe unaweza kupatikana.+
Nayo mafuriko ya maji mengi hayatamgusa.+
7 Wewe ni mahali pangu pa kujificha; utanilinda kutokana na taabu.+
Utanizingira kwa vigelegele vya shangwe kwa sababu ya kuniokoa.+ Sela.
8 “Nitakufanya uwe na ufahamu na kukufundisha katika njia unayopaswa kuiendea.+
Nitakupa shauri jicho langu likiwa linakutazama.+
9 Msijifanye kama farasi au nyumbu wasio na uelewaji,+
Ambao roho yao yenye nguvu huzuiwa na hatamu au lijamu+
Kabla wao hawajakukaribia wewe.”+
11 Shangilieni katika Yehova na kuwa na shangwe, enyi waadilifu;+
Na mpige vigelegele vya shangwe, ninyi nyote mlio wanyoofu katika moyo.+
33 Pigeni vigelegele vya shangwe, enyi waadilifu, kwa sababu ya Yehova.+
Sifa ni jambo linalofaa kwa wanyoofu.+
Fanyeni yote mnayoweza katika kumpigia vinanda pamoja na vigelegele vya shangwe.+
6 Mbingu zilifanywa kwa neno la Yehova,+
Nayo majeshi yake yote yalifanywa kwa roho ya kinywa chake.+
7 Anayakusanya maji ya bahari kana kwamba ni kwa bwawa,+
Akiweka katika maghala maji yenye kututumuka.
9 Kwa maana yeye mwenyewe alisema, na ikawa hivyo;+
Yeye mwenyewe alitoa amri, nayo ikasimama hivyo.+
11 Shauri la Yehova litasimama milele;+
Mawazo ya moyo wake ni kwa kizazi kimoja baada ya kizazi kingine.+
14 Kutoka katika mahali palipofanywa imara ambako yeye hukaa+
Amewakazia macho wale wote wanaokaa duniani.
16 Hakuna mfalme anayeokolewa kwa wingi wa majeshi yake;+
Mtu mwenye nguvu haokolewi kwa wingi wa nguvu.+
18 Tazama! Jicho la Yehova linawaelekea wale wanaomwogopa,+
Wale wanaozingojea fadhili zake zenye upendo,+
Ya Daudi, alipokuwa akijifanya mwenda-wazimu+ mbele ya Abimeleki, hivi kwamba akamfukuza, naye akaenda zake.
א [ʼAʹleph]
ב [Behth]
ג [Giʹmel]
ד [Daʹleth]
4 Nilimuuliza Yehova, naye akanijibu,+
Naye akanikomboa kutoka katika mambo yote yenye kuniogopesha.+
ה [Heʼ]
ז [Zaʹyin]
6 Huyu mwenye kuteseka aliita, na Yehova mwenyewe akasikia.+
Na Yeye akamwokoa kutoka katika taabu zake zote.+
ח [Chehth]
ט [Tehth]
י [Yohdh]
כ [Kaph]
10 Wana-simba wenye manyoya shingoni wamekuwa na vichache na kukaa njaa;+
Lakini kwa wale wanaomtafuta Yehova, hawatakosa chochote chema.+
ל [Laʹmedh]
מ [Mem]
נ [Nun]
ס [Saʹmekh]
ע [ʽAʹyin]
15 Macho ya Yehova yanawaelekea waadilifu,+
Na masikio yake yanakielekea kilio chao cha kuomba msaada.+
פ [Peʼ]
16 Uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda yaliyo mabaya,+
Ili kumbukumbu lao liondolewe mbali duniani.+
צ [Tsa·dhehʹ]
17 Wao walilia kwa sauti, naye Yehova mwenyewe akasikia,+
Naye akawakomboa kutoka katika taabu zao zote.+
ק [Qohph]
ר [Rehsh]
ש [Shin]
ת [Taw]
22 Yehova anaikomboa nafsi ya watumishi wake;+
Wala hakuna yeyote kati ya wale wanaomkimbilia atakayehesabiwa kuwa na hatia.+
Ya Daudi.
3 Na uchomoe mkuki na shoka lenye makali kuwili ili kukutana na wale wanaonifuatilia.+
Uiambie nafsi yangu: “Mimi ni wokovu wako.”+
4 Wale wanaoiwinda nafsi yangu na waone aibu na kufedheheka.+
Wale wanaonipangia hila nipatwe na msiba na warudishwe nyuma na kufedheheka.+
7 Kwa maana wamenifichia bila sababu shimo lao lenye wavu;+
Wamelichimba bila sababu kwa ajili ya nafsi yangu.+
8 Uharibifu na umjie bila yeye kujua,+
Na wavu wake mwenyewe aliouficha na umkamate;+
Na aanguke ndani yake apatwe na uharibifu.+
10 Mifupa yangu yote na iseme:+
“Ee Yehova, ni nani aliye kama wewe,+
Anayemkomboa mwenye kuteseka kutoka kwa mwenye nguvu kuliko yeye,+
Na kumkomboa mwenye kuteseka na maskini kutoka kwa mwenye kumnyang’anya?”+
13 Lakini mimi, walipokuwa wagonjwa, mavazi yangu yalikuwa ni magunia,+
Nikaitesa nafsi yangu kwa kufunga,+
Nayo sala yangu mwenyewe ikawa ikirudi kifuani pangu.+
14 Kana kwamba ni kwa ajili ya mwenzangu, kana kwamba ni kwa ajili ya ndugu yangu,+
Nilitembea huku na huku kama mtu anayemwombolezea mama yake.+
Nikainama nikiwa na huzuni.
15 Lakini walishangilia na kukusanyika pamoja kuhusu kuchechemea kwangu;+
Walikusanyika pamoja dhidi yangu,+
Wakinipiga na kuniangusha wakati sikujua;+
Walinirarua vipande-vipande wala hawakukaa kimya.+
16 Kati ya wenye dhihaka, walioasi imani, kwa ajili ya keki,+
Kulikuwako kusaga meno yao dhidi yangu.+
17 Ee Yehova, utaendelea kuona hayo mpaka wakati gani?+
Uirudishe nafsi yangu kutoka katika maangamizi yao,+
Naam, yangu iliyo ya pekee+ kutoka kwa wana-simba wenye manyoya shingoni.
19 Wale ambao ni adui zangu bila sababu yoyote wasishangilie juu yangu;+
Nao wale wanaonichukia bila sababu, wasikonyeze jicho.+
20 Kwa maana hawasemi mambo ya amani;+
Bali juu ya wanyamavu wa dunia
Wanaendelea kupanga mambo ya udanganyifu.+
23 Uamke na ukae macho kwa ajili ya hukumu yangu,+
Kwa ajili ya kesi yangu,+ Ee Mungu wangu, naam, Yehova.
26 Na waone aibu na kufedheheka wote pamoja+
Wanaoshangilia msiba wangu.+
Na wavikwe aibu+ na fedheha wale wanaojivuna sana dhidi yangu.+
27 Wale wanaopendezwa na uadilifu wangu na wapige vigelegele kwa shangwe na kushangilia.+
Nao waseme daima:+
“Yehova na atukuzwe, ambaye anapendezwa na amani ya mtumishi wake.”+
Kwa kiongozi. Ya mtumishi wa Yehova, Daudi.
36 Maneno ya ukosaji kwa mtu mwovu yako katikati ya moyo wake;+
Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.+
4 Yeye anaendelea kupanga hila ya kuumiza kitandani mwake.+
Husimama katika njia isiyo nzuri.+
Hakatai lililo baya.+
6 Uadilifu wako ni kama milima ya Mungu;+
Uamuzi wako wa hukumu ni kilindi kikubwa cha maji.+
Wewe huokoa mwanadamu na mnyama, Ee Yehova.+
7 Jinsi zilivyo na thamani fadhili zako zenye upendo, Ee Mungu!+
Nao wana wa binadamu hupata kimbilio katika kivuli cha mabawa yako.+
10 Endeleza fadhili zako zenye upendo kwa wale wanaokujua,+
Na uadilifu wako kwa wale walio wanyoofu moyoni.+
Ya Daudi.
א [ʼAʹleph]
37 Usijionyeshe umewaka hasira kwa sababu ya watenda-maovu.+
Usiwaonee wivu wale wanaofanya mambo yasiyo ya uadilifu.+
ב [Behth]
ג [Giʹmel]
ד [Daʹleth]
Na kumngojea kwa kutamani.+
Usijionyeshe umewaka hasira kwa sababu ya mtu yeyote anayeifanikisha njia yake,+
Kwa sababu ya mtu anayetimiza mawazo yake.+
ה [Heʼ]
9 Kwa maana watenda-maovu watakatiliwa mbali,+
Bali wale wanaomtumaini Yehova ndio watakaoimiliki dunia.+
ו [Waw]
10 Na bado muda kidogo tu, na mtu mwovu hatakuwako tena;+
Nawe hakika utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo.+
ז [Zaʹyin]
ח [Chehth]
14 Waovu wamechomoa upanga na kuupinda upinde wao,+
Ili kumwangusha mwenye kuteseka na maskini,+
Ili kuwachinja walio wanyoofu katika njia yao.+
ט [Tehth]
י [Yohdh]
18 Yehova anazijua siku za watu wasio na kosa,+
Nao urithi wao wenyewe utaendelea mpaka wakati usio na kipimo.+
כ [Kaph]
20 Kwa maana waovu wataangamia,+
Nao adui za Yehova watakuwa kama malisho bora;
Lazima wao waufikie mwisho wao.+ Katika moshi lazima waufikie mwisho wao.+
ל [Laʹmedh]
22 Kwa maana wale wanaobarikiwa naye wataimiliki dunia,+
Lakini wale anaowalaani watakatiliwa mbali.+
מ [Mem]
נ [Nun]
25 Nilikuwa kijana, pia nimezeeka,+
Na bado sijamwona mtu yeyote mwadilifu akiwa ameachwa kabisa,+
Wala uzao wake ukitafuta mkate.+
ס [Saʹmekh]
27 Geuka mbali kutoka kwa mambo mabaya na ufanye yaliyo mema,+
Na hivyo ukae mpaka wakati usio na kipimo.+
ע [ʽAʹyin]
Hakika watalindwa mpaka wakati usio na kipimo;+
Lakini wazao wa waovu, hakika watakatiliwa mbali.+
פ [Peʼ]
30 Kinywa cha mwadilifu ndicho kinachotamka hekima kwa sauti ya chini,+
Na ulimi wake ndio unaosema kwa njia ya haki.+
צ [Tsa·dhehʹ]
ק [Qohph]
34 Mtumaini Yehova na kuishika njia yake,+
Naye atakuinua uimiliki dunia.+
Watu waovu watakapokatiliwa mbali, wewe utaona hilo.+
ר [Rehsh]
35 Nimemwona mwovu akiwa mwonevu+
Na akijitandaza kama mti wenye majani mengi katika udongo wa asili.+
ש [Shin]
37 Mwangalie mtu asiye na lawama na uendelee kumwangalia mnyoofu,+
Kwa maana wakati ujao wa mtu huyo utakuwa wenye amani.+
38 Lakini wakosaji hakika wataangamizwa pamoja;+
Wakati ujao wa watu waovu hakika utakatiliwa mbali.+
ת [Taw]
40 Na Yehova atawasaidia na kuwaokoa.+
Atawaponya kutoka kwa watu waovu na kuwaokoa,+
Kwa sababu wamemkimbilia yeye.+
Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.
3 Hakuna mahali popote pazima katika mwili wangu kwa sababu ya shutuma yako.+
Hakuna amani katika mifupa yangu kwa sababu ya dhambi yangu.+
10 Moyo wangu mwenyewe umepiga-piga kwa nguvu, nguvu zangu zimeniacha,
Na nuru ya macho yangu mwenyewe haiko pamoja nami.+
11 Nao wenye kunipenda na wenzangu wanaendelea kusimama mbali na pigo langu,+
Na rafiki zangu wamesimama mbali.+
12 Lakini wale wanaoitafuta nafsi yangu wanatega mitego,+
Na wale wanaotaka kuniletea msiba wamesema mabaya,+
Nao kwa sauti ya chini wanaendelea kusema udanganyifu mchana kutwa.+
13 Lakini mimi, kama kiziwi, nikawa siwasikilizi;+
Na kama mtu asiyeweza kusema, nikawa sifungui kinywa changu.+
14 Nami nikawa kama mtu ambaye hasikii,
Na kinywani mwangu hamkuwa na hoja zozote za kupinga.
16 Kwa maana nilisema: “Kama sivyo watashangilia kwa sababu yangu;+
Mguu wangu uliposonga kwa kuyumba-yumba,+ hakika walijivuna sana dhidi yangu.”+
20 Nao walikuwa wakinilipa mema yangu kwa mabaya;+
Wakaendelea kushindana nami kwa sababu ya kufuatilia kwangu mambo yaliyo mema.+
Kwa kiongozi wa Yeduthuni.+ Muziki wa Daudi.
39 Nilisema: “Nitalinda njia zangu+
Ili nisiendelee kutenda dhambi kwa ulimi wangu.+
Nitaweka lijamu kama mlinzi wa kinywa changu mwenyewe,+
Maadamu mtu yeyote mwovu yuko mbele yangu.”+
2 Nikawa asiyeweza kusema kwa kukaa kimya;+
Nikaendelea kulinyamazia lililo jema,+
Na kuumia kwangu kukatengwa.
3 Moyo wangu ukawa na moto ndani yangu;+
Wakati wa kuugua kwangu moto ukaendelea kuwaka.
Nilisema kwa ulimi wangu:
4 “Ee Yehova, nijulishe mwisho wangu,+
Na kipimo cha siku zangu—ni kipimo gani,+
Ili nipate kujua kadiri nilivyo wa muda mfupi.+
5 Tazama! Umezifanya siku zangu kuwa chache tu;+
Na urefu wa maisha yangu si kitu mbele zako.+
Kwa kweli kila mtu wa udongo, ingawa anasimama imara, si kitu ila pumzi tu.+ Sela.
6 Kwa kweli mtu hutembea huku na huku kama kivuli tu.+
Kwa kweli wana msukosuko ambao ni ubatili.+
Mmoja anarundika vitu wala hajui ni nani atakayevikusanya.+
7 Na sasa, nimetumainia nini, Ee Yehova?
Matarajio yangu yanakuelekea wewe.+
9 Niliendelea kuwa asiyeweza kusema;+ sikuweza kufungua kinywa changu,+
Kwa maana wewe mwenyewe ulichukua hatua.+
11 Umemrekebisha mtu kwa makaripio dhidi ya kosa,+
Nawe unakula vitu vyake vyenye kutamanika kama nondo.+
Kwa kweli kila mtu wa udongo ni pumzi tu.+ Sela.
12 Uisikie sala yangu, Ee Yehova,
Na usikilize kilio changu cha kutaka msaada.+
Usikae kimya machozi yangu yanapotoka.+
Kwa maana, kwako, mimi ni mkaaji mgeni tu,+
Mhamiaji kama vile mababu zangu wote.+
Kwa kiongozi. Ya Daudi, muziki.
40 Nilimtumainia Yehova kwa bidii,+
Kwa hiyo akanitegea sikio lake na kusikia kilio changu cha kuomba msaada.+
2 Yeye pia akaniinua kutoka katika shimo lenye kunguruma,+
Kutoka katika matope ya nchi.+
Kisha yeye akainua miguu yangu juu ya mwamba;+
Akazifanya imara hatua zangu.+
3 Tena, akatia wimbo mpya katika kinywa changu,
Sifa kwa Mungu wetu.+
Wengi wataona hilo na kuogopa,+
Nao watamtegemea Yehova.+
4 Mwenye furaha ni mwanamume ambaye amemfanya Yehova kuwa tegemeo lake+
Na ambaye hakuelekeza uso wake kwa watu wakaidi,
Wala kwa wale wanaogeukia uwongo.+
5 Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi,+
Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea;+
Hakuna wa kulinganishwa nawe.+
Ikiwa ningetaka kueleza na kusema juu yake,
Zimekuwa nyingi sana kuliko vile ninavyoweza kusimulia.+
6 Hukupendezwa na dhabihu na toleo;+
Haya masikio yangu uliyafungua.+
Hukutaka toleo la kuteketezwa na toleo la dhambi.+
9 Nimetangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+
Tazama! Siizuii midomo yangu.+
Ee Yehova, wewe mwenyewe unajua hivyo vema.+
10 Uadilifu wako sikuufunika moyoni mwangu.+
Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.+
Sikuficha fadhili zako zenye upendo na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+
11 Wewe mwenyewe, Ee Yehova, usinizuilie huruma zako.+
Fadhili zako zenye upendo na ukweli wako zinilinde daima.+
12 Kwa maana misiba ilinizunguka mpaka ikawa haihesabiki.+
Makosa yangu mengi zaidi yalinifikia kuliko vile nilivyoweza kuona;+
Yakawa mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,+
Nao moyo wangu mwenyewe uliniacha.+
14 Na waone aibu na kufedheheka wote pamoja+
Wale wanaoitafuta nafsi yangu wapate kuifagilia mbali.+
Wale wanaopendezwa na msiba wangu na wageuke na kufedheheshwa.+
16 Na hao washangilie na kukufurahia wewe,+
Wale wote wanaokutafuta.+
Na waseme daima: “Yehova na atukuzwe,”+
Wale wanaopenda wokovu wako.+
17 Lakini mimi ninateseka nami ni maskini.+
Yehova mwenyewe ananijali.+
Wewe ni msaidizi wangu na Mwokoaji wangu.+
Ee Mungu wangu, usichelewe mno.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
41 Mwenye furaha ni mtu yeyote anayetenda kwa kumfikiria mtu wa hali ya chini;+
Katika siku ya msiba Yehova atamwokoa.+
2 Yehova mwenyewe atamlinda na kumhifadhi hai.+
Atatangazwa kuwa mwenye furaha duniani;+
Nawe huwezi kamwe kumtia mkononi mwa nafsi ya adui zake.+
3 Yehova mwenyewe atamtegemeza katika kitanda cha ugonjwa;+
Kitanda chake chote hakika utakibadilisha wakati wa ugonjwa wake.+
4 Mimi nami, nilisema: “Ee Yehova, nionyeshe kibali.+
Uiponye nafsi yangu, kwa maana nimekutendea dhambi.”+
Atatoka nje; huko nje atalisema.+
7 Wote wanaonichukia wananong’onezana juu yangu kwa muungano;+
Wanaendelea kupanga hila ya jambo baya juu yangu:+
9 Pia mtu mwenye kuwa na amani nami, ambaye nimemtegemea,+
Ambaye alikuwa akila mkate wangu,+ amekiinua kisigino chake dhidi yangu.+
11 Kwa jambo hili ninajua kwamba umependezwa nami,
Kwa sababu adui yangu hapigi kelele za ushindi juu yangu.+
12 Nami, umenitegemeza kwa sababu ya utimilifu wangu,+
Nawe utaniweka mbele za uso wako mpaka wakati usio na kipimo.+
13 Yehova Mungu wa Israeli na abarikiwe+
Tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo.+
Amina na Amina.+
KITABU CHA PILI
Kwa kiongozi. Maskili kwa ajili ya wana wa Kora.+
2 Kwa kweli nafsi yangu ina kiu kwa ajili ya Mungu,+ kwa ajili ya Mungu aliye hai.+
Ni wakati gani nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?+
3 Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku,+
Huku wakiniambia mchana kutwa: “Mungu wako yuko wapi?”+
4 Nitakumbuka mambo haya, nami nitaimimina nafsi yangu iliyo ndani yangu.+
Kwa maana nilikuwa nikipita pamoja na watu wengi,
Nilikuwa nikitembea polepole mbele yao kwenda kwenye nyumba ya Mungu,+
Kwa sauti ya vigelegele vya shangwe na shukrani,+
Ya umati unaofanya sherehe.+
5 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+
Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?+
Mngojee Mungu,+
Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu.+
6 Ee Mungu wangu, nafsi yangu mwenyewe imekata tamaa ndani yangu.+
Ndiyo sababu ninakukumbuka,+
Kutoka katika nchi ya Yordani na vilele vya Hermoni,+
Kutoka katika ule mlima mdogo.+
7 Kilindi cha maji kinaita kilindi cha maji
Kwa sauti ya mabubujiko yako ya maji.
Mashuu yako yote na mawimbi yako+—
Yamepita juu yangu.+
8 Wakati wa mchana Yehova ataamuru fadhili zake zenye upendo,+
Na wakati wa usiku wimbo wake utakuwa nami;+
Kutakuwako sala kwa Mungu wa uhai wangu.+
9 Nitamwambia Mungu mwamba wangu:+
“Kwa nini umenisahau?+
Kwa nini natembea kwa huzuni kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?”+
10 Wale wanaonionyesha uadui wamenishutumu kwa mauaji dhidi ya mifupa yangu,+
Huku wakiniambia mchana kutwa: “Mungu wako yuko wapi?”+
11 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+
Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?+
Mngojee Mungu,+
Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu na kuwa ndiye Mungu wangu.+
Na uendeshe kesi+ yangu dhidi ya taifa lisilo shikamanifu.
Uniokoe kutoka kwa mtu wa udanganyifu na mwenye kukosa uadilifu.+
2 Kwa maana wewe ni Mungu wa ngome yangu.+
Kwa nini umenitupilia mbali?
Kwa nini natembea kwa huzuni kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?+
3 Tuma nuru yako na kweli yako.+
Na hivyo vyenyewe viniongoze.+
Navyo vinilete kwenye mlima wako mtakatifu na kwenye maskani yako kuu.+
4 Nami nitakuja kwenye madhabahu ya Mungu,+
Kwa Mungu, ambaye ni kushangilia kwangu kwa furaha.+
Nami nitakusifu kwa kinubi, Ee Mungu, Mungu wangu.+
5 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+
Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?
Mngojee Mungu,+
Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu na kuwa ndiye Mungu wangu.+
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Maskili.
44 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu,
Mababu zetu wenyewe wametusimulia+
Utendaji ambao ulifanya katika siku zao,+
Siku za zamani za kale.+
2 Wewe mwenyewe kwa mkono wako uliwafukuzia mbali mataifa,+
Nawe ukawapanda hao badala yao.+
Ukavunja vikundi vya mataifa na kuwafukuza.+
3 Kwa maana hawakuimiliki nchi hiyo kwa upanga wao wenyewe,+
Wala wokovu haukuletwa kwa mkono wao wenyewe.+
Kwa maana ulikuwa ni mkono wako wa kuume,+ naam, mkono wako na nuru ya uso wako,
Kwa sababu ulipendezwa nao.+
5 Kupitia wewe tutawasukuma wapinzani wetu;+
Katika jina lako tutawakanyagia chini wale wanaosimama dhidi yetu.+
7 Kwa maana ulituokoa kutoka kwa wapinzani wetu,+
Nawe ukawafanya waone aibu wale wanaotuchukia vikali.+
10 Wewe unaendelea kutufanya tugeuke kutoka kwa adui zetu,+
Na wale wanaotuchukia vikali wamejinyakulia vitu.+
13 Unatuweka kuwa shutuma kwa jirani zetu,+
Kuwa dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka pande zote.+
14 Umetufanya kuwa neno la kimethali kati ya mataifa,+
Kuwa kitu cha kutikisiwa kichwa kati ya vikundi vya mataifa.+
16 Kwa sababu ya sauti ya mtu anayeshutumu na kusema vibaya,
Kwa sababu ya adui na mtu anayejilipizia kisasi.+
17 Yote hayo ndiyo yametujia, nasi hatujakusahau,+
Wala hatujatenda kwa njia ya uwongo katika agano lako.+
18 Moyo wetu haujageuka nyuma kwa kukosa imani,+
Wala hatua za miguu yetu hazitoki katika njia yako.+
23 Uamke. Kwa nini unaendelea kulala usingizi, Ee Yehova?+
Uamke. Usiendelee kututupilia mbali milele.+
Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi. Ya wana wa Kora. Maskili. Wimbo wa wanawake wapendwa.
2 Kwa kweli wewe una sura nzuri kuliko wana wa binadamu.+
Uvutio umemiminwa juu ya midomo yako.+
Ndiyo sababu Mungu amekubariki mpaka wakati usio na kipimo.+
4 Na katika fahari yako endelea mpaka ufanikiwe;+
Panda kwa kutetea kweli na unyenyekevu na uadilifu,+
Na mkono wako wa kuume utakufundisha mambo yenye kuogopesha.+
5 Mishale yako ni mikali—vikundi vya watu vinaendelea kuanguka chini yako+—
Katika moyo wa adui za mfalme.+
6 Mungu ni kiti chako cha ufalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele;+
Fimbo ya enzi ya ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.+
7 Umependa uadilifu+ nawe unachukia uovu.+
Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako,+ amekutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia+ kuliko wenzako.+
8 Mavazi yako yote ni manemane na udi na kida;+
Kutoka katika jumba kuu la mfalme la pembe,+ vinanda vimekufanya ushangilie.
9 Binti+ za wafalme wamo kati ya wanawake wako wenye thamani.
Malkia+ amesimama kwenye mkono wako wa kuume akiwa amevaa dhahabu ya Ofiri.+
14 Atapelekwa kwa mfalme akiwa na mavazi yaliyofumwa.+
Mabikira katika msafara wake ambao ni rafiki zake wanaingizwa ndani kwako.+
15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe;
Wataingia katika jumba la mfalme.
16 Mahali pa mababu+ zako patachukuliwa na wana wako,+
Ambao utawaweka kuwa wakuu katika dunia yote.+
17 Nitalitaja jina lako katika vizazi vyote vitakavyokuja.+
Ndiyo sababu vikundi vya watu vitakusifu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora+ juu ya Wanawali. Wimbo.
2 Ndiyo sababu hatutaogopa, hata dunia ikibadilika+
Na hata milima ikitikisika na kuingia katika moyo wa bahari kuu;+
4 Kuna mto ambao vijito vyake hulifanya jiji la Mungu lishangilie,+
Maskani kuu takatifu zaidi ya Aliye Juu Zaidi.+
5 Mungu yuko katikati ya jiji;+ halitatikisika.+
Mungu atalisaidia wakati wa mapambazuko ya asubuhi.+
9 Anakomesha vita mpaka kwenye mwisho wa dunia.+
Upinde anauvunja na kuukata mkuki vipande-vipande;+
Magari ya kukokotwa anayateketeza motoni.+
10 “Salimuni amri, na mjue ya kwamba mimi ni Mungu.+
Nitatukuzwa kati ya mataifa,+
Nitatukuzwa duniani.”+
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora. Muziki.
47 Enyi vikundi vyote vya watu, pigeni makofi.+
Mpigieni Mungu kelele za ushindi kwa vigelegele vya shangwe.+
8 Mungu amekuwa mfalme juu ya mataifa.+
Mungu mwenyewe ameketi juu ya kiti chake kitakatifu cha ufalme.+
9 Wakuu wa watu wamekusanyika pamoja,+
Pamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu.+
Kwa maana ngao za dunia ni za Mungu.+
Yeye amepanda juu sana.+
Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+
2 Wenye ukuu wa kupendeza, shangwe ya dunia yote,+
Ni Mlima Sayuni ulioko sehemu za mbali za kaskazini,+
Mji wa Mfalme Mkuu.+
3 Katika minara ya makao yake Mungu amejulikana kuwa kilele salama.+
7 Kwa upepo wa mashariki wewe unavunja meli za Tarshishi.+
8 Kama vile tulivyosikia, ndivyo tumeona+
Katika jiji la Yehova wa majeshi, katika jiji la Mungu wetu.+
Mungu mwenyewe atalifanya imara mpaka wakati usio na kipimo.+ Sela
10 Kama jina lako,+ Ee Mungu, ndivyo ilivyo sifa yako
Mpaka kwenye miisho ya dunia.
Mkono wako wa kuume umejaa uadilifu.+
11 Mlima Sayuni+ na ushangilie,
Miji ya kandokando ya Yuda na ishangilie,+ kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu.+
13 Wekeni mioyo yenu juu ya boma lake.+
Kagueni minara ya makao yake,
Ili mpate kukisimulia kizazi cha wakati ujao.+
14 Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
Yeye mwenyewe atatuongoza mpaka tufe.+
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki.
8 (Nayo bei ya ukombozi wa nafsi yao ni yenye thamani sana+
Hivi kwamba imekoma mpaka wakati usio na kipimo)
9 Hivi kwamba yeye aendelee kuishi milele na asilione shimo.+
10 Kwa maana yeye huona kwamba hata wenye hekima wanakufa,+
Mjinga na asiyetumia akili huangamia wote pamoja,+
Nao hulazimika kuwaachia wengine mali yao.+
11 Tamaa yao ya ndani ni kwamba nyumba zao ziwepo mpaka wakati usio na kipimo,+
Maskani zao mpaka kizazi baada ya kizazi.+
Wameyaita mashamba yao kwa majina yao.+
12 Na bado mtu wa udongo, ingawa katika heshima, hawezi kuendelea kukaa;+
Kwa kweli analingana na wanyama ambao wameangamizwa.+
13 Hiyo ndiyo njia ya wale wenye ujinga,+
Na ya wale wanaowafuata ambao wanapendezwa na maneno yao wenyewe. Sela.
14 Kama kondoo, wao wamewekewa Kaburi;*+
Kifo chenyewe kitawachunga;+
Nao wanyoofu watawatawala asubuhi,+
Nayo maumbo yao hayatakosa kuchakaa;+
Kaburi* badala ya makao yaliyo juu ni kwa ajili ya kila mmoja.+
15 Hata hivyo, Mungu mwenyewe ataikomboa nafsi yangu kutoka katika mkono wa Kaburi,*+
Kwa maana atanipokea. Sela.
18 Kwa maana muda wote wa maisha yake alikuwa akiibariki nafsi yake mwenyewe;+
(Na watu watakusifu kwa sababu unajiendeleza vizuri)+
20 Mtu wa udongo, ingawa katika heshima, ambaye haelewi,+
Kwa kweli analingana na wanyama ambao wameangamizwa.+
Muziki wa Asafu.+
50 Mwenye Uwezo,+ Mungu, Yehova,+ amesema mwenyewe,+
Naye anaiita dunia,+
Kutoka mashariki mpaka magharibi.+
2 Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu mwenyewe ameangaza.+
3 Mungu wetu atakuja naye hawezi kukaa kimya.+
Mbele zake kuna moto unaoteketeza,+
Na kumzunguka pande zote hali ya hewa imekuwa yenye dhoruba kali sana.+
7 “Sikilizeni, enyi watu wangu, nami nitasema,+
Ee Israeli, nami nitatoa ushahidi dhidi yako.+
Mimi ni Mungu, Mungu wako.+
8 Mimi siwakaripii kuhusiana na dhabihu zenu,+
Wala kuhusiana na matoleo yako mazima ya kuteketezwa yaliyo mbele zangu daima.+
11 Najua vizuri kila kiumbe chenye mabawa cha milimani,+
Na makundi ya wanyama wa porini yako pamoja nami.+
12 Ningalikuwa na njaa, singalikuambia;
Kwa maana nchi yenye kuzaa+ na vyote vinavyoijaza ni vyangu.+
16 Lakini Mungu atamwambia mwovu:+
“Una haki gani ya kuyataja masharti yangu,+
Na kwamba ulichukue agano langu kinywani mwako?+
21 Umeyafanya mambo hayo, nami nikaendelea kukaa kimya.+
Ulidhani kwamba kwa hakika mimi ningekuwa kama wewe.+
Nitakukaripia,+ nami nitayarekebisha mambo mbele ya macho yako.+
22 Tafadhali, enyi mnaomsahau Mungu eleweni hili,+
Nisije nikawararua vipande-vipande bila ya kuwa na mkombozi.+
23 Yule anayetoa shukrani zikiwa dhabihu yake ndiye anayenitukuza;+
Naye anayedumisha njia iliyowekwa,
Nitamfanya aone wokovu wa Mungu.”+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Nathani nabii alipoingia kwake baada ya Daudi kulala na Bath-sheba.+
51 Ee Mungu, unionyeshe kibali kulingana na fadhili zako zenye upendo.+
Ufutilie mbali makosa yangu kulingana na wingi wa rehema zako.+
4 Dhidi yako wewe, wewe peke yako, nimetenda dhambi,+
Nami nimefanya lililo baya machoni pako,+
Ili uwe mwadilifu unapoongea,+
Ili usiwe na lawama unapohukumu.+
6 Tazama! Umependezwa na ukweli wenyewe katika sehemu za ndani;+
Na katika mtu wa sirini unijulishe hekima tupu.+
7 Unitakase kwa hisopo kutokana na dhambi, ili nipate kuwa safi;+
Unioshe, ili nipate kuwa mweupe kuliko theluji.+
14 Unikomboe kutokana na hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+
Ili ulimi wangu upate kutangaza uadilifu wako kwa shangwe.+
19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za uadilifu,+
Na dhabihu za kuteketezwa na toleo zima;+
Ndipo ng’ombe-dume watakapotolewa katika madhabahu yako mwenyewe.+
Kwa kiongozi. Maskili. Ya Daudi, wakati Doegi Mwedomu alipokuja na kumwambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+
52 Kwa nini unajisifia yaliyo mabaya, ewe mwenye nguvu?+
Fadhili zenye upendo za Mungu ni za mchana kutwa.+
2 Ulimi wako hupanga hila za kuleta shida, ukiwa umenolewa kama wembe,+
Ukifanya kazi kwa udanganyifu.+
5 Mungu mwenyewe pia atakubomoa milele;+
Atakupiga na kukuangusha na kukurarua kutoka katika hema lako,+
Naye atakung’oa kutoka katika nchi ya walio hai.+ Sela.
7 Huyo ndiye mwanamume ambaye hamweki Mungu kuwa ngome yake,+
Lakini anategemea wingi wa utajiri wake,+
Ambaye hulindwa kutokana na shida anazoleta.+
8 Lakini nitakuwa kama mzeituni+ wenye majani mengi katika nyumba ya Mungu;
Nazitegemea fadhili zenye upendo za Mungu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
9 Nitakusifu mpaka wakati usio na kipimo, kwa maana wewe umechukua hatua;+
Nami nitalitumainia jina lako, kwa sababu ni jema, mbele ya washikamanifu wako.+
Kwa kiongozi juu ya Mahalathi.+ Maskili. Ya Daudi.
53 Asiye na akili amesema katika moyo wake:
“Hakuna Yehova.”+
Wametenda kwa uharibifu na kutenda kwa njia yenye kuchukiza katika ukosefu wa uadilifu;+
Hakuna yeyote anayefanya mema.+
2 Kutoka mbinguni Mungu amewatazama wana wa binadamu walio chini,+
Aone kama kuna yeyote ambaye ana ufahamu, yeyote anayemtafuta Yehova.+
3 Wote wamegeuka nyuma, wote ni wafisadi katika njia ileile;+
Hakuna yeyote anayefanya mema,+
Hakuna hata mmoja.
4 Je, hakuna yeyote kati ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza ambaye ana ujuzi,+
Wakila watu wangu kama vile ambavyo wamekula mkate?+
Hata hawajamwitia Yehova.+
5 Hapo wamejawa na hofu kubwa,+
Mahali ambapo hapakuwa na kitu chenye kutia hofu;+
Kwa maana hakika Mungu ataitawanya mifupa ya mtu yeyote anayepiga kambi dhidi yako.+
Hakika utawafanya waone aibu, kwa maana Yehova mwenyewe amewakataa.+
6 Laiti wokovu mkuu wa Israeli ungetoka Sayuni!+
Wakati ambapo Yehova anawakusanya tena mateka wa watu wake,+
Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.+
Kwa kiongozi wa vinanda. Maskili. Ya Daudi. Wakati Wazifu walipokuja na kumwambia Sauli: “Je, Daudi hajifichi pamoja nasi?”+
3 Kwa maana kuna wageni ambao wameinuka dhidi yangu,
Na waonevu wanaoitafuta nafsi yangu.+
Hawajamweka Mungu mbele yao.+ Sela.
Kwa kiongozi wa vinanda. Maskili. Ya Daudi.
2 Unisikilize kwa makini na kunijibu.+
Mahangaiko yangu yananisukuma huku na huku bila kuwa na utulivu,+
Sina jambo lingine la kufanya ila kuonyesha wasiwasi.
3 Kwa sababu ya sauti ya adui, kwa sababu ya mkazo wa yule mwovu.+
Kwa maana wanaendelea kuniangushia mambo yenye kuumiza,+
Na kwa hasira wanadumisha uadui juu yangu.+
8 Ningefanya haraka kwenda mahali pangu pa kuponyokea
Kutokana na upepo wenye kuvuma, kutokana na tufani.”+
10 Mchana na usiku wanalizunguka pande zote juu ya kuta zake;+
Na mambo yenye kuumiza na taabu ziko ndani yake.+
11 Shida ziko ndani yake;
Na katika viwanja vyake vya watu wote ukandamizaji na udanganyifu haujaondoka.+
12 Kwa maana sikushutumiwa na adui;+
Kama ndivyo ningaliweza kuvumilia hilo.
Si mtu anayenichukia vikali aliyejivuna sana dhidi yangu;+
Kama ndivyo ningaliweza kujificha kutoka kwake.+
13 Lakini ilikuwa ni wewe, mwanadamu anayeweza kufa tunayelingana,+
Mtu tunayejuana na ambaye ni rafiki yangu,+
14 Kwa sababu tulikuwa tukifurahia pamoja urafiki ulio mtamu;+
Tulikuwa tukitembea kuingia katika nyumba ya Mungu pamoja na watu wengi.+
Na washuke katika Kaburi* wakiwa hai;+
Kwa maana wakati wao wa kukaa ugenini mambo mabaya yamekuwa ndani yao.+
17 Jioni na asubuhi na katikati ya mchana sikosi kuhangaika nami naomboleza,+
Naye huisikia sauti yangu.+
18 Hakika ataikomboa na kuiweka nafsi yangu katika amani mbali na vita vinavyofanywa juu yangu,+
Kwa maana wakiwa umati wamekuja kuwa dhidi yangu.+
19 Mungu atasikia na kuwajibu,+
Naam, Yeye anayeketi juu ya kiti cha ufalme kama zamani+—Sela—
Wale ambao hawafanyi mabadiliko+
Na ambao hawajamwogopa Mungu.+
21 Maneno ya kinywa chake ni laini kuliko siagi,+
Lakini moyo wake una mwelekeo wa kupigana.+
Maneno yake ni laini kuliko mafuta,+
Lakini ni panga zilizochomolewa.+
23 Lakini wewe mwenyewe, Ee Mungu, utawashusha mpaka kwenye shimo lililo chini kabisa.+
Nao watu wenye hatia ya damu na wadanganyifu, hawataishi nusu ya siku zao.+
Lakini mimi, nitakutegemea wewe.+
Kwa kiongozi juu ya Njiwa Mnyamavu kati ya wale walio mbali. Ya Daudi. Miktamu. Wakati Wafilisti walipomshika huko Gathi.+
56 Unionyeshe kibali, Ee Mungu, kwa sababu mwanadamu anayeweza kufa amenikamata.+
Akiwa anafanya vita mchana kutwa, yeye anaendelea kunikandamiza.+
2 Adui zangu wameendelea kutanua kinywa mchana kutwa,+
Kwa maana kuna wengi wanaofanya vita juu yangu kwa kujitakia makuu.+
3 Siku yoyote ile nitakayoogopa, mimi nitakutegemea wewe.+
4 Katika umoja na Mungu nitalisifu neno lake.+
Nimeliweka tegemeo langu kwa Mungu; Sitaogopa.+
Mwenye mwili wa nyama anaweza kunitenda nini?+
5 Mchana kutwa wanaendelea kuharibu mambo yangu ya kibinafsi;
Mawazo yao yote yako juu yangu kwa ajili ya ubaya.+
6 Wao wanashambulia, wanajificha,+
Wao wanaendelea kuziangalia hatua zangu,+
Huku wakiwa wameingojea nafsi yangu.+
8 Wewe mwenyewe umetoa habari juu ya kuwa kwangu mkimbizi.+
Uyaweke machozi yangu katika kiriba chako.+
Je, hayamo katika kitabu chako?+
9 Wakati huo, adui zangu watageuka, siku ambayo nitaita;+
Najua hili vema, kwamba Mungu yuko kwa ajili yangu.+
13 Kwa maana umeikomboa nafsi yangu na kifo+—
Je, hukuikomboa miguu yangu isijikwae?+—
Ili nipate kutembea mbele za Mungu katika nuru ya wale walio hai.+
Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu. Alipokimbia kwa sababu ya Sauli, akaingia pangoni.+
57 Unionyeshe kibali, Ee Mungu, unionyeshe kibali,+
Kwa maana nafsi yangu imekukimbilia wewe;+
Na katika kivuli cha mabawa yako nimekimbilia mpaka shida zipitilie mbali.+
2 Ninamwita Mungu Aliye Juu Zaidi, Mungu wa kweli anayezikomesha kwa sababu yangu.+
3 Atatuma kutoka mbinguni na kuniokoa.+
Hakika atamvuruga yule anayenitanulia kinywa.+ Sela.
Mungu atatuma fadhili zake zenye upendo na ukweli wake.+
4 Nafsi yangu iko katikati ya simba;+
Sina jambo lingine la kufanya ila kulala katikati ya wamezaji, naam, wana wa binadamu,
Ambao meno yao ni mikuki na mishale,+
Na ambao ulimi wao ni upanga mkali.+
6 Wametayarisha wavu kwa ajili ya hatua zangu;+
Nafsi yangu imeinama chini.+
Wamechimba mtego wa shimo mbele yangu;
Wameanguka ndani yake.+ Sela.
Nitayaamsha mapambazuko.
9 Nitakusifu katikati ya vikundi vya watu, Ee Yehova;+
Nitakupigia muziki katikati ya vikundi vya mataifa.+
Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.
58 Katika kimya chenu je, kweli mnaweza kusema juu ya uadilifu?+
Je, mnaweza kuhukumu kwa unyoofu, enyi wana wa binadamu?+
2 Badala yake, kwa moyo mnafanya mambo ambayo ni ya kukosa uadilifu kabisa duniani,+
Na kutayarisha barabara kwa ajili ya jeuri ya mikono yenu!+
3 Waovu wamekuwa wapotovu kutoka katika tumbo la uzazi;+
Wametanga-tanga tangu tumboni na kuendelea;
Wanasema uwongo.+
6 Ee Mungu, yang’oe meno yaliyo kinywani mwao.+
Uvunje mifupa ya taya za wana-simba wenye manyoya shingoni, Ee Yehova.
7 Na wayeyuke kana kwamba ni ndani ya maji yanayoenda zake;+
Na aupinde upinde kwa ajili ya mishale yake huku wanapoanguka.+
9 Kabla vyungu vyenu havijapatwa na mkwamba uliowashwa,+
Ulio mbichi na pia ule unaowaka, ataipeperusha kama upepo wa dhoruba.+
11 Nao wanadamu watasema:+ “Kwa kweli kuna matunda kwa ajili ya mwadilifu.+
Kwa kweli kuna Mungu ambaye anahukumu duniani.”+
Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu. Sauli alipowatuma watu, nao wakaendelea kuilinda nyumba, ili wamuue.+
59 Unikomboe kutoka kwa adui zangu, Ee Mungu wangu;+
Unilinde kutoka kwa wale wanaoinuka dhidi yangu.+
2 Unikomboe kutoka kwa wanaotenda mambo yenye kuumiza,+
Na uniokoe kutoka kwa watu wenye hatia ya damu.
3 Kwa maana, tazama! wamejificha wakiingojea nafsi yangu;+
Wenye nguvu hunishambulia,+
Bila ya uasi wowote upande wangu, wala dhambi yoyote upande wangu, Ee Yehova.+
5 Nawe, Ee Yehova Mungu wa majeshi, ndiye Mungu wa Israeli.+
Uamke uyaelekezee mataifa yote fikira zako.+
Usiwape kibali wasaliti wowote wenye kuumiza.+ Sela.
6 Wao wanaendelea kurudi wakati wa jioni;+
Wanaendelea kubweka kama mbwa+ na kulizunguka jiji pande zote.+
10 Mungu wa fadhili zenye upendo kwangu atanikabili yeye mwenyewe;+
Mungu mwenyewe atanifanya niwatazame adui zangu.+
11 Usiwaue, ili watu wangu wasisahau.+
Tumia nguvu zako uwafanye watange-tange huku na huku,+
Na kuwashusha, Ee ngao yetu Yehova,+
12 Kwa sababu ya dhambi ya kinywa chao, neno la midomo yao;+
Na wakamatwe katika kiburi chao,+
Naam, kwa sababu ya laana na udanganyifu ambao wanajizoeza.
Uwakomeshe ili wasiwepo;
Na wajue kwamba Mungu anatawala katika Yakobo mpaka kwenye miisho ya dunia.+ Sela.
16 Lakini mimi, nitaimba juu ya nguvu zako,+
Na asubuhi nitatangaza fadhili zako zenye upendo kwa shangwe.+
Kwa maana umekuwa kilele changu salama.+
Na mahali pa kukimbilia siku ya taabu yangu.+
17 Ee Nguvu zangu, nitakupigia muziki,+
Kwa maana Mungu ni kilele changu salama, Mungu wa fadhili zenye upendo kwangu.+
Kwa kiongozi juu ya Yungiyungi la Kikumbusho. Miktamu. Ya Daudi. Kwa ajili ya kufundishia.+ Wakati alipopambana na Aram-naharaimu na Aram-Soba, naye Yoabu akarudi na kupiga Edomu katika Bonde la Chumvi, naam, watu kumi na mbili elfu.+
6 Mungu mwenyewe amesema katika utakatifu wake:+
“Nitashangilia, nitamgawanya Shekemu awe fungu;+
Na nchi tambarare ya chini ya Sukothi nitaipima.+
7 Gileadi ni yangu na Manase ni yangu,+
Na Efraimu ni ngome ya aliye mkuu wangu;
Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+
8 Moabu ni chungu changu cha kuoshea.+
Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+
Nitapiga kelele za ushindi juu ya Ufilisti.”+
10 Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetutupilia mbali+
Na ambaye huendi pamoja na majeshi yetu ukiwa Mungu?+
Kwa kiongozi wa vinanda. Ya Daudi.
2 Kutoka mwisho wa dunia nitakulilia wewe, naam, wewe, moyo wangu unapokuwa mnyonge.+
Uniongoze kwenye mwamba ambao uko juu kuliko mimi.+
4 Nitakuwa mgeni katika hema lako mpaka nyakati zisizo na
kipimo;+
Nitakimbilia maficho ya mabawa yako.+ Sela.
5 Kwa maana wewe mwenyewe, Ee Mungu, umesikiliza nadhiri zangu.+
Umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.+
7 Atakaa mpaka wakati usio na kipimo mbele za Mungu;+
Uagize fadhili zenye upendo na ukweli, ili zipate kumlinda.+
8 Kwa hiyo jina lako nitalipigia muziki milele,+
Ili nipate kutimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.+
Kwa kiongozi wa Yeduthuni. Muziki wa Daudi.
3 Mtaendelea mpaka wakati gani kumshambulia mtu ambaye mngetaka kumuua?+
Ninyi nyote ni kama ukuta unaoinama, ukuta wa mawe ambao unasukumwa ndani.+
4 Kwa kweli wanatoa mashauri ili kumshawishi mtu avunje heshima yake;+
Wanafurahia uwongo.+
Wanabariki kwa kinywa chao, lakini ndani yao wanalaani.+ Sela.
7 Wokovu wangu na utukufu wangu uko juu ya Mungu.+
Mwamba wangu wenye nguvu, kimbilio langu liko katika Mungu.+
9 Kwa kweli wana wa mtu wa udongo ni pumzi,+
Wana wa wanadamu ni uwongo.+
Wanapowekwa juu ya mizani wote pamoja ni wepesi kuliko pumzi.+
12 Pia fadhili zenye upendo ni zako, Ee Yehova,+
Kwa maana wewe mwenyewe humlipa kila mmoja kulingana na kazi yake.+
Muziki wa Daudi, alipokuwa katika nyika ya Yuda.+
63 Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+
Nafsi yangu ina kiu kwa ajili yako.+
Mwili wangu umezimia kwa kukutamani wewe.
Katika nchi iliyokauka na kuchoka, ambapo hakuna maji.+
5 Nafsi yangu imeshiba sehemu bora, naam, mafuta,+
Na kwa midomo yenye vigelegele vya shangwe kinywa changu hutoa sifa.+
9 Nao wale wanaoendelea kuitafuta nafsi yangu ili waiharibu,+
Wataingia katika sehemu za chini kabisa za dunia.+
11 Naye mfalme mwenyewe atashangilia katika Mungu.+
Kila anayeapa kwa jina lake atajisifu,+
Kwa maana kinywa cha wale wanaosema uwongo kitazibwa.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
64 Ee Mungu, uisikie sauti yangu katika hangaiko langu.+
Uulinde uhai wangu kutokana na hofu ya adui.+
2 Unifiche mbali na mazungumzo ya siri ya watenda-maovu,+
Mbali na fujo ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza,+
6 Wanaendelea kutafuta mambo yasiyo ya uadilifu;+
Wameficha mbinu ya werevu iliyofikiriwa sana,+
Na upande wa ndani wa kila mmoja, naam, moyo wake, una kina kirefu.+
8 Nao wanasababisha mtu ajikwae.+
Lakini ulimi wao huwapinga wao wenyewe.+
Wote wanaowatazama watatikisa kichwa chao,+
9 Nao watu wote wa udongo wataogopa;+
Nao watatangaza utendaji wa Mungu.+
Nao hakika watakuwa na ufahamu katika kazi yake.+
10 Na mwadilifu atashangilia katika Yehova na kwa kweli atamkimbilia;+
Nao wote walio wanyoofu moyoni watajisifu.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo.
2 Ee msikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja.+
4 Mwenye furaha ni yule unayemchagua na kumfanya akaribie,+
Ili apate kukaa katika nyua zako.+
Hakika tutashiba mema ya nyumba yako,+
Mahali patakatifu pa hekalu lako.+
5 Utatujibu kwa mambo yenye kuogopesha katika uadilifu,+
Ee Mungu wa wokovu wetu,+
Tegemeo la mipaka yote ya dunia na wale walio mbali baharini.+
8 Na wakaaji wa sehemu za mbali zaidi wataogopa ishara zako;+
Unafanya kutokea kwa asubuhi na jioni kupige vigelegele kwa shangwe.+
9 Umeielekezea dunia fikira zako, ili uipatie wingi;+
Unaitajirisha sana.
Kijito kinachotoka kwa Mungu kimejaa maji.+
Wewe unatayarisha nafaka yao,+
Kwa maana hivyo ndivyo unavyoitayarisha dunia.+
10 Mitaro yake inajazwa maji, madonge yake yanasawazishwa;+
Unailainisha kwa manyunyu mengi; unaibariki mimea yake.+
12 Viwanja vya malisho ya nyikani vinaendelea kudondoka mafuta,+
Navyo vilima vinajifunga shangwe kama mshipi.+
13 Malisho yamevikwa makundi,+
Na nchi tambarare za chini zimefunikwa na nafaka.+
Vitu hivyo vinapiga kelele za ushindi, naam, vinaimba.+
Kwa kiongozi. Wimbo, muziki.
66 Mpigieni Mungu kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+
3 Mwambieni Mungu: “Jinsi kazi zako zilivyo zenye kuogopesha!+
Kwa sababu ya wingi wa nguvu zako, adui zako watakujia wakitetemeka.+
7 Anatawala kwa nguvu zake mpaka wakati usio na kipimo.+
Macho yake mwenyewe yanaendelea kuyatazama mataifa.+
Nao wale ambao ni wakaidi, wasijiinue wenyewe.+ Sela.
12 Umemfanya mwanadamu anayeweza kufa apande juu ya kichwa chetu;+
Tumepita katikati ya moto na katikati ya maji,+
Nawe ukatuleta kwenye kitulizo.+
14 Ambazo midomo yangu imefunguka ili iseme+
Na ambazo kinywa changu kimesema nilipokuwa katika dhiki kali.+
15 Nitakutolea matoleo mazima ya kuteketezwa ya vinono,+
Pamoja na moshi wa dhabihu wa kondoo-dume.
Nitatoa ng’ombe-dume pamoja na mbuzi-dume.+ Sela.
16 Njooni, sikilizeni, enyi nyote mnaomwogopa Mungu, nami nitasimulia+
Mambo ambayo ameitendea nafsi yangu.+
20 Mungu na abarikiwe, ambaye hakuigeuzia mbali sala yangu,
Wala fadhili zake zenye upendo mbali nami.+
Kwa kiongozi wa vinanda. Muziki, wimbo.
4 Vikundi vya mataifa na vishangilie na kupiga vigelegele kwa shangwe,+
Kwa maana utavihukumu vikundi vya watu kwa unyoofu;+
Navyo vikundi vya mataifa, utaviongoza duniani. Sela.
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki, wimbo.
68 Mungu na asimame,+ adui zake na watawanyike,+
Na wale wanaomchukia vikali na wakimbie kwa sababu yake.+
2 Kama vile moshi unavyofukuziwa mbali, na uwafukuzie mbali vivyo hivyo;+
Kama vile nta inavyoyeyuka kwa sababu ya moto,+
Waovu na waangamie vivyo hivyo kutoka mbele za Mungu.+
4 Mwimbieni Mungu, lipigieni jina lake muziki;+
Mwimbieni wimbo Yeye anayepanda akipitia nchi tambarare za jangwani+
Akiwa Yah, ambalo ndilo jina lake;+ na kushangilia mbele zake;
6 Mungu anawafanya wapweke wakae katika nyumba;+
Anawafanikisha kabisa wafungwa.+
Hata hivyo, walio wakaidi, lazima wakae katika nchi iliyokauka.+
7 Ee Mungu, ulipoenda mbele ya watu wako,+
Ulipopiga mwendo jangwani+—Sela—
Nayo mbingu pia ikadondoka maji kwa sababu ya Mungu;+
Mlima huu Sinai ukatikisika kwa sababu ya Mungu,+ Mungu wa Israeli.+
9 Ulisababisha mvua kubwa ianze kunyesha, Ee Mungu;+
Urithi wako, hata wakati ulipokuwa umechoka—wewe mwenyewe uliupatia nguvu tena.+
10 Kambi yako ya mahema+—wamekaa ndani yake;+
Kwa wema wako uliitayarisha kwa ajili ya mwenye kuteseka, Ee Mungu.+
12 Hata wafalme wa majeshi wanakimbia, naam, wanakimbia.+
Lakini mwanamke anayekaa nyumbani, hugawa nyara.+
13 Ijapokuwa ninyi mliendelea kulala katikati ya marundo ya majivu ya kambi,
Kutakuwako mabawa ya njiwa yaliyofunikwa kwa fedha
Na manyoya yake yakiwa yamefunikwa kwa dhahabu ya kijani-manjano.+
14 Wakati Mweza-Yote alipowatawanya kotekote wafalme walio ndani yake,+
Theluji ilianza kuanguka Salmoni.+
15 Eneo lenye milima la Bashani+ ni mlima wa Mungu;+
Eneo lenye milima la Bashani ni mlima wenye vilele.+
16 Kwa nini ninyi, enyi milima yenye vilele, mnaendelea kutazama kwa wivu
Mlima ambao Mungu ametamani kukaa ndani yake?+
Naam, Yehova atakaa humo milele.+
17 Magari ya Mungu ya vita ni makumi ya maelfu, maelfu zaidi na zaidi.+
Yehova mwenyewe amekuja kutoka Sinai na kuingia mahali patakatifu.+
Umechukua mateka;+
Umechukua zawadi katika namna ya wanadamu,+
Naam, hata walio wakaidi,+ ili kukaa kati yao,+ Ee Yah Mungu.
19 Na abarikiwe Yehova, ambaye hutubebea mzigo wetu kila siku,+
Mungu wa kweli wa wokovu wetu.+ Sela.
20 Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu wa matendo ya kuokoa;+
Nazo njia za kutoka katika kifo+ ni za Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu.+
21 Kwa kweli Mungu mwenyewe atavunja vipande-vipande kichwa cha adui zake,+
Utosi wenye nywele wa mtu yeyote anayetembea katika hatia yake.+
23 Ili upate kuosha mguu wako katika damu,+
Ili ulimi wa mbwa zako upate fungu lake kutoka katika adui.”+
24 Wameona maandamano yako, Ee Mungu,+
Maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, kuingia mahali patakatifu.+
25 Waimbaji walitangulia mbele, wapiga-vinanda wakawafuata;+
Katikati yao palikuwa na wanawali wakipiga matari.+
26 Katika makundi yaliyokutanika mbarikini Mungu,+
Yehova, enyi mnaotoka katika Chemchemi ya Israeli.+
27 Tazama Benyamini mdogo akiwatiisha,+
Wakuu wa Yuda pamoja na umati wao unaopaaza sauti,
Wakuu wa Zabuloni, wakuu wa Naftali.+
28 Mungu wako ameweka amri juu ya nguvu zako.+
Uonyeshe nguvu, Ee Mungu, wewe ambaye umechukua hatua kwa ajili yetu.+
30 Umkemee mnyama-mwitu wa matete,+ kusanyiko la ng’ombe-dume,+
Na ndama za vikundi vya watu, kila mmoja akikanyaga-kanyaga vipande vya fedha.+
Ametawanya vikundi vya watu vinavyopenda mapigano.+
31 Vyombo vya shaba nyeusi vitatoka Misri;+
Kushi itanyoosha upesi mikono yake ikiwa na zawadi kwa Mungu.+
35 Mungu ni mwenye kuogopesha kutoka katika patakatifu pako pakuu.+
Ndiye Mungu wa Israeli, anayewapa watu nguvu na uwezo.+
Mungu na abarikiwe.+
Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi.+ Ya Daudi.
69 Uniokoe, Ee Mungu, kwa maana maji yamefika mpaka kwenye nafsi.+
2 Nimezama katika matope mengi, mahali ambapo hapana udongo wa kusimama.+
Nimeingia katika maji mengi,
Na kijito kinachotiririka kimenifagilia mbali.+
3 Nimechoka kwa sababu ya kuita kwangu;+
Koo yangu imekauka.
Macho yangu yameshindwa huku nikimngojea Mungu wangu.+
4 Wale wanaonichukia bila sababu wamekuwa wengi hata kuliko nywele za kichwa changu.+
Wale wanaoninyamazisha, wakiwa ni adui zangu bila sababu, wamekuwa wengi.+
Kisha nikarudisha kile ambacho sikuwa nimechukua kwa unyang’anyi.
6 Wale wanaokutumainia na wasione aibu kwa sababu yangu,+
Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.+
Wale wanaokutafuta na wasifedheheshwe kwa sababu yangu,+
Ee Mungu wa Israeli.+
9 Kwa maana bidii nyingi kwa ajili ya nyumba yako imenila,+
Na shutuma za wale wanaokushutumu zimeniangukia.+
12 Wale wanaoketi kwenye lango wakaanza kujishughulisha nami,+
Nikawa kiini cha nyimbo za watu wanaokunywa kileo.+
13 Lakini mimi, nilikutolea sala, Ee Yehova,+
Wakati unaofaa, Ee Mungu.+
Katika wingi wa fadhili zako zenye upendo unijibu kwa kweli ya wokovu wako.+
14 Unikomboe kutoka katika matope, ili nisizame.+
Na nikombolewe kutoka kwa wale wanaonichukia+ na kutoka katika kilindi cha maji.+
15 Kijito cha maji yanayotiririka kisinifagilie mbali,+
Wala kilindi kisinimeze,
Wala kisima kisifunge kinywa chake juu yangu.+
16 Unijibu, Ee Yehova, kwa maana fadhili zako zenye upendo ni njema.+
Kulingana na wingi wa rehema zako ugeuke kunielekea,+
19 Wewe mwenyewe umejua shutuma yangu na aibu yangu na fedheha yangu.+
Wote wanaonionyesha uadui wako mbele zako.+
20 Shutuma imeuvunja moyo wangu, nalo jeraha haliwezi kuponywa.+
Nami niliendelea kutumainia mtu fulani aonyeshe kusikitika, lakini hapakuwa na yeyote;+
Na watu wa kufariji, lakini sikupata yeyote.+
21 Lakini walinipa mmea wenye sumu kuwa chakula,+
Na kwa ajili ya kiu yangu wakajaribu kuninywesha siki.+
22 Meza yao iliyo mbele yao na iwe mtego,+
Na vitu vilivyo kwa ajili ya hali njema yao na viwe mnaso.+
26 Kwa maana yule ambaye wewe mwenyewe umempiga, wamemfuatilia,+
Nao wanaendelea kusimulia maumivu ya wale ambao wewe uliwachoma.
31 Hilo pia litampendeza Yehova kuliko ng’ombe-dume,+
Kuliko ng’ombe-dume mchanga mwenye pembe, mwenye kwato zilizogawanyika.+
32 Hakika wapole wataliona hilo; watashangilia.+
Ninyi mnaomtafuta Mungu, moyo wenu na uendelee kuwa hai.+
35 Kwa maana Mungu mwenyewe ataokoa Sayuni+
Naye atayajenga majiji ya Yuda;+
Nao hakika watakaa humo na kuimiliki.+
Kwa kiongozi. Ya Daudi, ili kukumbusha.+
2 Wale wanaoitafuta nafsi yangu na waone aibu na kufedheheka.+
Wale wanaofurahia msiba wangu na wageuke na kufedheheshwa.+
3 Na warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao wale wanaosema: “Aha, aha!”+
4 Wote wanaokutafuta na wafurahi na kushangilia katika wewe,+
Nao waseme daima: “Mungu atukuzwe!”—wale wanaoupenda wokovu wako.+
5 Lakini mimi ninateseka nami ni maskini.+
Ee Mungu, uchukue hatua haraka kwa ajili yangu.+
Wewe ndiye msaada wangu na Mwokoaji wangu.+
Ee Yehova, usichelewe mno.+
3 Uwe kwangu ngome ya mwamba ya kuingia ndani daima.+
Utoe amri ili kuniokoa,+
Kwa maana wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.+
4 Ee Mungu wangu, uniokoe na mkono wa mwovu,+
Na mkono wa mtu anayetenda kwa njia isiyo ya haki na kwa ukandamizaji.+
5 Kwa maana wewe ni tumaini langu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova, tegemeo langu tangu ujana wangu.+
6 Nimekutegemea tangu tumboni;+
Wewe ndiye Yule anayenitenganisha na sehemu za ndani za mama yangu.+
Sifa yangu kwako ni ya daima.+
10 Kwa maana adui zangu wamesema juu yangu,+
Na walewale wanaoitafuta nafsi yangu wameshauriana pamoja,+
13 Hao na waaibike, hao na wafikie mwisho wao, wanaoshindana na nafsi yangu.+
Hao na wajifunike kwa shutuma na fedheha wanaonitafutia msiba.+
15 Kinywa changu mwenyewe kitasimulia uadilifu wako,+
Wokovu wako mchana kutwa,+
Kwa maana sijapata kujua hesabu yake.+
16 Nitaingia na nguvu kuu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu+ Yehova;
Nitautangaza uadilifu wako, naam, wako peke yako.+
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,+
Na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu.+
18 Na mpaka wakati wa uzee na wa kuwa na kichwa chenye mvi, Ee Mungu, usiniache,+
Mpaka nikitangazie kizazi habari za mkono wako,+
Habari za nguvu zako, kwa wale wote watakaokuja.+
19 Uadilifu wako, Ee Mungu, unafika kileleni;+
Na kuhusu mambo makuu ambayo umeyafanya,+
Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?+
20 Kwa sababu umenifanya nione taabu nyingi na misiba,+
Unifufue tena;+
Na unipandishe tena kutoka katika vilindi vya maji vya dunia.+
22 Mimi pia, nitakusifu kwa chombo cha kinanda,+
Kuhusu ukweli wako, Ee Mungu wangu.+
Nitakupigia muziki kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli.+
23 Midomo yangu itapiga vigelegele kwa shangwe wakati wowote ninapokupigia muziki,+
Naam, nafsi yangu, ambayo umeikomboa.+
24 Pia, ulimi wangu mwenyewe, mchana kutwa, utasema juu ya uadilifu wako kwa sauti ya chini,+
Kwa maana wameaibika, kwa maana wamefedheheka, wale wanaonitafutia msiba.+
Kuhusu Sulemani.
7 Katika siku zake aliye mwadilifu atachipuka,+
Na wingi wa amani mpaka mwezi utakapokuwa haupo tena.+
12 Kwa maana atamkomboa maskini anayelilia msaada,+
Pia mwenye kuteseka na yeyote ambaye hana msaidizi.+
14 Ataikomboa nafsi yao kutoka katika ukandamizaji na katika jeuri,
Nayo damu yao itakuwa na thamani machoni pake.+
15 Yeye na aishi,+ na apewe sehemu ya dhahabu ya Sheba.+
Na kwa ajili yake sala na itolewe daima;
Na abarikiwe mchana kutwa.+
16 Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani;+
Juu ya milima kutakuwa na mafuriko.+
Uzao wake utakuwa kama katika Lebanoni,+
Na wale wa kutoka katika jiji watachanuka kama majani ya dunia.+
17 Jina lake na liweko mpaka wakati usio na kipimo;+
Jina lake na liongezeke mbele ya jua,
Na kupitia yeye na wajibariki;+
Mataifa yote na yamtangaze kuwa mwenye furaha.+
19 Na jina lake tukufu na libarikiwe mpaka wakati usio na kipimo,+
Nao utukufu wake na uijaze dunia yote.+
Amina na Amina.
20 Sala za Daudi, mwana wa Yese,+ zimefikia mwisho wake.
KITABU CHA TATU
Muziki wa Asafu.+
73 Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio safi moyoni.+
5 Wala hawamo katika taabu ya mwanadamu anayeweza kufa,+
Wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.+
10 Kwa hiyo yeye huwarudisha watu wake hapa,
Na maji yaliyojaa yanakaushwa kwa ajili yao.
15 Kama ningelisema: “Nitasimulia hadithi kama hiyo,”
Tazama! juu ya kizazi cha wana wako
Ningelitenda kwa hila.+
19 Lo! Jinsi wamekuwa kitu cha kushangaza ghafula!+
Jinsi wameufikia mwisho wao, wamemalizwa kwa matisho ya ghafula!
26 Mwili wangu na moyo wangu vimeshindwa.+
Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu mpaka wakati usio na kipimo.+
27 Kwa maana, tazama! Walewale wanaokaa mbali nawe wataangamia.+
Hakika utamnyamazisha kila mtu ambaye kwa njia isiyo ya adili anakuacha.+
28 Lakini mimi, kumkaribia Mungu ni kwema kwangu.+
Nimeweka kimbilio langu katika Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova,+
Ili kutangaza kazi zako zote.+
Maskili. Ya Asafu.+
74 Kwa nini, Ee Mungu, umetutupilia mbali milele?+
Kwa nini hasira yako inatoa moshi daima juu ya kundi la malisho yako?+
2 Ulikumbuke kusanyiko lako ulilojipatia zamani za kale,+
Kabila ulilolikomboa liwe urithi wako,+
Huu Mlima Sayuni ambapo umekaa.+
3 Uziinue hatua zako kwenye ukiwa wenye kudumu muda mrefu.+
Kila kitu katika mahali patakatifu adui amekitendea vibaya.+
4 Wale wanaokuonyesha uadui wamenguruma katikati ya mahali pa kukutania.+
Wameweka ishara zao wenyewe kuwa ndizo ishara.+
5 Mtu ana sifa mbaya ya kuwa kama yule anayeinua mashoka juu ya kichaka cha miti.
6 Na sasa vitu vyake vilivyochongwa, kila kimoja, wao wanakipiga hata kwa kishoka na kwa mipini yenye ncha za chuma.+
8 Wao, hata uzao wao, wamesema pamoja moyoni mwao:
“Mahali pote pa kukutania pa Mungu katika nchi lazima pateketezwe.”+
10 Ee Mungu, mpinzani ataendelea kushutumu mpaka wakati gani?+
Je, adui ataendelea kulidharau jina lako milele?+
11 Kwa nini unaendelea kuuondoa mkono wako, naam, mkono wako wa kuume+
Kutoka katikati ya kifua chako ili kutumaliza sisi?
12 Hata hivyo Mungu ni Mfalme wangu tangu zamani za kale,+
Yeye anayefanya wokovu mkuu katikati ya dunia.+
13 Wewe mwenyewe uliichochea bahari kwa nguvu zako mwenyewe;+
Ulivunja vichwa vya wanyama wakubwa wa baharini katika maji.+
14 Wewe mwenyewe uliponda vipande-vipande vichwa vya Lewiathani.*+
Ukawapa watu kuwa chakula, wale wanaokaa katika maeneo yasiyo na maji.+
17 Ni wewe uliyeweka mipaka yote ya dunia;+
Majira ya kiangazi na majira ya baridi kali—wewe mwenyewe uliyafanyiza.+
18 Ukumbuke hili: Adui ameshutumu, Ee Yehova,+
Na kikundi cha watu wasio na akili kimelidharau jina lako.+
21 Mtu aliyepondwa na asirudi akiwa amefedheheshwa.+
Mwenye kuteseka na maskini na walisifu jina lako.+
22 Usimame, Ee Mungu, uendeshe kesi yako.+
Uikumbuke shutuma yako mchana kutwa kutoka kwa mtu asiye na akili.+
23 Usiisahau sauti ya wale wanaokuonyesha
uadui.+
Kelele za wale wanaosimama dhidi yako zinapaa daima.+
Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Muziki. Wa Asafu.+ Wimbo.
75 Tunakutolea shukrani, Ee Mungu; tunakutolea shukrani,+
Nalo jina lako liko karibu.+
Lazima watu wazitangaze kazi zako za ajabu.+
6 Kwa maana wala kutoka mashariki wala kutoka magharibi,
Wala kutoka kusini hakutoki kuinuliwa.
8 Kwa maana kuna kikombe mkononi mwa Yehova,+
Kimejaa mchanganyiko, nayo divai inatoa povu.
Na hakika kutoka hicho yeye atayamwaga machicha yake;
Waovu wote wa dunia watayakamua, na kunywa.”+
9 Lakini mimi, nitaeleza juu ya hayo mpaka wakati usio na kipimo;
Nitampigia muziki Mungu wa Yakobo.+
Kwa kiongozi wa vinanda. Muziki. Wa Asafu.+ Wimbo.
4 Umefunikwa na nuru, una utukufu kuliko milima ya mawindo.+
5 Wenye nguvu moyoni wameporwa,+
Wamesinzia na kulala usingizi,+
Wala hakuna hata mmoja wa wanaume mashujaa ambaye ameiona mikono yake.+
6 Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo, mwendesha-gari na farasi pia wamelala usingizi mzito.+
Na ni nani anayeweza kusimama mbele zako kwa sababu ya nguvu za hasira yako?+
11 Wekeni nadhiri na kumtimizia Yehova Mungu wenu, ninyi nyote mnaomzunguka pande zote.+
Na walete zawadi kwa kuogopa.+
Kwa kiongozi juu ya Yeduthuni. Ya Asafu.+ Muziki.
77 Kwa sauti yangu nitamlilia Mungu mwenyewe,+
Kwa sauti yangu kwa Mungu, naye hakika atanisikiliza.+
2 Katika siku ya taabu yangu nimemtafuta Yehova mwenyewe.+
Usiku, mkono wangu umenyooshwa wala haufi ganzi;
Nafsi yangu imekataa kufarijiwa.+
6 Nitakumbuka muziki wangu wa kinanda wakati wa usiku;+
Nitaonyesha hangaiko moyoni,+
Na roho yangu itatafuta kwa uangalifu.
8 Je, fadhili zake zenye upendo zimekoma milele?+
Je, neno lake limekuwa bure+ kwa kizazi baada ya kizazi?
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye kuonyesha kibali,+
Au je, amezifungia rehema zake kwa hasira?+ Sela.
10 Na je, nitaendelea kusema: “Hili ndilo linalonichoma,+
Kubadilika kwa mkono wa kuume wa Aliye Juu Zaidi”?+
14 Wewe ndiye Mungu wa kweli, unayefanya kwa njia ya ajabu.+
Umezijulisha nguvu zako katikati ya vikundi vya watu.+
16 Maji yamekuona wewe, Ee Mungu,
Maji yamekuona wewe; yakaanza kuwa na maumivu makali.+
Pia, vilindi vya maji vikaanza kutetemeka.+
17 Mawingu yamemwaga maji kwa kunguruma;+
Anga lenye kutanda mawingu limetoa sauti.
Pia, mishale yako mwenyewe ilienda huku na huku.+
Dunia ikatetemeka na kuanza kutikisika.+
19 Njia yako ilikuwa baharini,+
Nalo pito lako lilikuwa katika maji mengi;
Nazo nyayo zako hazikupata kujulikana.
Maskili. Ya Asafu.+
2 Katika neno la kimethali nitakifungua kinywa changu;+
Nitafanya vitendawili vya zamani za kale vibubujike,+
4 Ambavyo hatuwafichi wana wao,+
Tukivisimulia hata kwa kizazi kitakachokuja,+
Sifa za Yehova na nguvu zake+
Na mambo yake ya ajabu ambayo amefanya.+
5 Naye akatokeza kikumbusho katika Yakobo,+
Na sheria akaiweka katika Israeli,+
Mambo ambayo aliwaamuru mababu zetu,+
Wawajulishe wana wao;+
6 Ili kizazi kitakachokuja, wana ambao wangezaliwa, wapate kuyajua,+
Ili wasimame na kuwasimulia wana wao,+
8 Nao wasiwe kama mababu zao,+
Kizazi chenye ukaidi na chenye kuasi,+
Kizazi ambacho hakikuwa kimetayarisha moyo wake+
Na ambacho roho yake haikuwa yenye kutegemeka kwa Mungu.+
17 Nao wakaendelea kumtendea dhambi hata zaidi+
Kwa kumwasi Aliye Juu Zaidi katika eneo lisilo na maji;+
19 Basi wakaanza kusema vibaya juu ya Mungu.+
Walisema: “Je, Mungu anaweza kutayarisha meza nyikani?”+
Ili maji yatiririke na mito ifurike.+
“Je, anaweza pia kutoa mkate,+
Au je, anaweza kuwatayarishia watu wake chakula?”+
21 Ndiyo sababu Yehova alisikia, akaanza kuwa na ghadhabu;+
Na moto ukawashwa juu ya Yakobo,+
Na hasira pia ikapanda juu ya Israeli.+
26 Akaanza kufanya upepo wa mashariki uvume mbinguni+
Na kufanya upepo wa kusini uvume kwa nguvu zake.+
27 Naye akawanyeshea chakula kama mavumbi,+
Hata viumbe vinavyoruka vyenye mabawa kama chembe za mchanga wa bahari.+
31 Ndipo ghadhabu ya Mungu ilipopanda juu yao.+
Naye akafanya mauaji kati ya wenye nguvu wao;+
Na vijana wa Israeli akawaangusha.
35 Nao wakaanza kukumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao,+
Na kwamba Mungu Aliye Juu Zaidi alikuwa Mlipiza-Kisasi wao.+
38 Lakini alikuwa mwenye rehema;+ akawa akilifunika kosa+ wala hakuharibu.+
Na mara nyingi akageuzia mbali hasira yake,+
Naye akawa haiamshi ghadhabu yake yote.
44 Na jinsi alivyoanza kubadili mifereji ya Nile iwe damu,+
Hivi kwamba hawakuweza kunywa kutoka katika vijito vyao wenyewe.+
48 Naye akawaacha wanyama wao wa kubeba mizigo wapigwe kwa mvua ya mawe+
Na mifugo yao kwa homa kali.
49 Akapeleka juu yao hasira yake inayowaka,+
Ghadhabu na shutuma na taabu,+
Wajumbe wa malaika wanaoleta msiba.+
50 Akatayarisha njia kwa ajili ya hasira yake.+
Hakuzuia nafsi zao zisipatwe na kifo;
Nayo maisha yao akayatia kwenye tauni.+
51 Mwishowe akawapiga na kuwaua wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+
Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu.+
53 Naye akaendelea kuwaongoza kwa usalama, wala hawakuhofu kamwe;+
Nayo bahari ikawafunika adui zao.+
54 Naye akawaleta katika eneo lake takatifu,+
Eneo hili lenye milima ambalo mkono wake wa kuume ulijipatia.+
55 Naye akayafukuza mataifa kwa sababu yao,+
Na kuwagawia urithi kwa kamba ya kupimia,+
Hivi kwamba akayafanya makabila ya Israeli yakae nyumbani kwao wenyewe.+
57 Pia wakaendelea kugeuka na kutenda kwa hila kama mababu zao;+
Waligeuka huku na huku kama upinde uliolegea.+
58 Nao wakaendelea kumtia uchungu kwa mahali pao pa juu,+
Nao wakaendelea kumchochea awe na wivu kwa sanamu zao za kuchongwa.+
60 Naye mwishowe akaiacha maskani ya Shilo,+
Lile hema ambalo alikaa ndani yake katikati ya watu wa udongo.+
65 Kisha Yehova akaanza kuamka kana kwamba kutoka katika usingizi,+
Kama mtu mwenye nguvu akitokwa na ulevi wa divai.+
66 Naye akaanza kuwapiga adui zake kutoka nyuma;+
Akawapa shutuma inayodumu mpaka wakati usio na kipimo.+
69 Naye akaanza kujenga patakatifu pake kama vilele,+
Kama dunia ambayo ameiwekea msingi mpaka wakati usio na kipimo.+
71 Aache kuwafuata wale wa kike wanaonyonyesha+
Akamleta awe mchungaji juu ya Yakobo watu wake+
Na juu ya Israeli, urithi wake.+
72 Naye akaanza kuwachunga kulingana na utimilifu wa moyo wake,+
Naye akaanza kuwaongoza kwa ustadi wa mikono yake.+
Muziki wa Asafu.
79 Ee Mungu, mataifa yameingia katika urithi wako;+
Wamelitia unajisi hekalu lako takatifu;+
Wamefanya Yerusalemu kuwa rundo la mabomoko.+
2 Wamewapa ndege wa mbinguni maiti ya watumishi wako iwe chakula chao,+
Na nyama ya washikamanifu wako kwa wanyama-mwitu wa dunia.+
5 Ee Yehova, utapandwa na hasira mpaka wakati gani? Milele?+
Hasira yako itawaka kama moto mpaka wakati gani?+
6 Mwaga ghadhabu yako juu ya mataifa ambayo hayakukujua,+
Na juu ya falme ambazo hazikuliitia jina lako.+
8 Usikumbuke dhidi yetu makosa ya mababu zetu.+
Ufanye haraka! Rehema zako na zitufikie,+
Kwa maana tumekuwa maskini sana.+
9 Utusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+
Kwa ajili ya utukufu wa jina lako;+
Na utukomboe na kufunika dhambi zetu kwa sababu ya jina lako.+
10 Kwa nini mataifa yaseme: “Mungu wao yuko wapi?”+
Na ijulikane katika mataifa mbele ya macho yetu+
Juu ya kulipiza kisasi damu ya watumishi wako ambayo imemwagwa.+
11 Kuugua kwa mfungwa na kuingie mbele zako.+
Kulingana na ukuu wa mkono wako, uwahifadhi wale waliochaguliwa kwa ajili ya kifo.+
12 Na kuwalipa jirani zetu mara saba kifuani mwao+
Shutuma yao ambayo wamekushutumu nayo, Ee Yehova.+
13 Na sisi watu wako na kundi la malisho yako,+
Tutakushukuru mpaka wakati usio na kipimo;
Kutoka kizazi mpaka kizazi tutatangaza sifa yako.+
Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi.+ Kikumbusho. Ya Asafu.+ Muziki.
4 Ee Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea kuwaka hasira juu ya sala ya watu wako mpaka wakati gani?+
5 Umewalisha mkate wa machozi,+
Nawe unaendelea kuwafanya wanywe machozi kwa machozi kwa kiasi kikubwa.+
9 Ulitengeneza nafasi mbele yake,+ ili upate kutia mizizi na kuijaza nchi.+
11 Hatua kwa hatua uliyaeneza matawi yake mpaka baharini,+
Na machipukizi yake mpaka kwenye ule Mto.+
13 Nguruwe-mwitu kutoka msituni anaendelea kuula,+
Na makundi ya wanyama wa porini wanaendelea kuula.+
14 Ee Mungu wa majeshi, urudi, tafadhali;+
Utazame chini kutoka mbinguni, uone na kuutunza mzabibu huu,+
15 Na shina ambalo mkono wako wa kuume umepanda,+
Na umtazame mwana ambaye umemfanya kuwa mwenye nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
17 Mkono wako na uwe juu yake mtu wa mkono wako wa kuume,+
Juu ya mwana wa binadamu ambaye umemfanya kuwa mwenye nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
18 Nasi hatutageuka kutoka kwako.+
Utuhifadhi hai, ili tupate kuliitia jina lako.+
Kwa kiongozi juu ya Gitithi.+ Ya Asafu.
5 Alimwamuru Yosefu liwe kikumbusho,+
Alipokuwa akipita juu ya nchi ya Misri.+
Lugha ambayo sikuijua, niliendelea kuisikia.+
7 Katika taabu uliita, nami nikakuokoa;+
Nikaanza kukujibu katika mahali palipofichika pa mngurumo.+
Nikakuchunguza kando ya maji ya Meriba.+ Sela.
10 Mimi, Yehova, ni Mungu wako,+
Yule anayekutoa katika nchi ya Misri.+
Fungua wazi kinywa chako, nami nitakijaza.+
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu;+
Na Israeli hakuonyesha utayari wowote kunielekea.+
12 Na kwa hiyo nikawaacha waende katika ukaidi wa moyo wao;+
Wakatembea katika mashauri yao wenyewe.+
15 Na wale wanaomchukia Yehova vikali, watakuja kwake wakitetemeka,+
Na wakati wao utakuwa mpaka wakati usio na kipimo.
Muziki wa Asafu.
3 Iweni waamuzi kwa ajili ya mtu wa hali ya chini na mvulana asiye na baba.+
Kwa mtu mwenye kuteseka na maskini, mtendeeni haki.+
Wimbo. Muziki wa Asafu.+
3 Wanaendeleza kwa ujanja mazungumzo ya siri juu ya watu wako;+
Nao wanapanga hila juu ya watu wako waliofichwa.+
5 Kwa maana kwa moyo wameshauriana kwa umoja;+
Naam, wakafanya agano dhidi yako,+
6 Mahema ya Edomu+ na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+
11 Na uwafanye watu wao wenye vyeo wawe kama Orebu na kama Zeebu,+
Na watawala wao wadogo wote kama Zeba na kama Zalmuna,+
Kwa kiongozi juu ya Gitithi.+ Ya wana wa Kora. Muziki.
2 Nafsi yangu imetamani sana na pia imedhoofika kwa kutamani nyua za Yehova.+
Moyo wangu mwenyewe na mwili wangu wenyewe humpigia Mungu aliye hai vigelegele kwa shangwe.+
3 Hata ndege amepata nyumba,
Na mbayuwayu amepata kiota chake,
Ambapo ameweka vifaranga vyake—
Madhabahu yako kuu, Ee Yehova wa majeshi, Mfalme wangu na Mungu wangu!
6 Wakipita katika nchi tambarare ya chini ya mibaka,+
Wanaigeuza kuwa bubujiko;
Naam, mfundishaji+ anajivika baraka.
10 Kwa maana siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu moja kwingineko.+
Nimechagua kusimama mlangoni pa nyumba ya Mungu wangu+
Badala ya kuzunguka katika mahema ya uovu.+
11 Kwa maana Yehova Mungu ni jua+ na ngao;+
Yeye hutoa kibali na utukufu.+
Yehova mwenyewe hatawanyima jambo lolote jema wale wanaotembea bila kosa.+
12 Ee Yehova wa majeshi, mtu mwenye furaha ni yule anayekutegemea.+
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora. Muziki.
5 Je, utapandwa na hasira kwa sababu yetu mpaka wakati usio na kipimo?+
Je, utarefusha hasira yako kizazi baada ya kizazi?+
8 Nitasikia jambo ambalo Mungu wa kweli Yehova atasema,+
Kwa maana atasema amani kwa watu wake+ na kwa washikamanifu wake,
Lakini wasirudi kujitumaini.+
Sala ya Daudi
2 Uilinde nafsi yangu, kwa maana mimi ni mshikamanifu.+
Umwokoe mtumishi wako—wewe ni Mungu wangu—anayekutegemea.+
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni mwema+ na uko tayari kusamehe;+
Na fadhili zenye upendo ni nyingi kwa wale wote wanaokuitia.+
9 Mataifa yote ambayo umeyafanya, yatakuja yenyewe,+
Nayo yatainama mbele zako, Ee Yehova,+
Na kulipa utukufu jina lako.+
11 Unifundishe, Ee Yehova, juu ya njia yako.+
Nitatembea katika kweli yako.+
Unganisha moyo wangu ili kuliogopa jina lako.+
12 Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote,+
Nami nitalitukuza jina lako mpaka wakati usio na kipimo,
13 Kwa maana fadhili zako zenye upendo ni kuu kunielekea mimi,+
Nawe umeikomboa nafsi yangu kutoka katika Kaburi,* mahali pake pa chini kabisa.+
14 Ee Mungu, wenye kimbelembele wamesimama juu yangu;+
Nalo kusanyiko la wenye kuonea wameitafuta nafsi yangu,+
Nao hawajakuweka mbele yao.+
15 Lakini wewe, Ee Yehova, ni Mungu mwenye rehema na mwenye neema,+
Si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi wa fadhili zenye upendo na ukweli.+
16 Nigeukie na kunionyesha kibali.+
Umpe mtumishi wako nguvu zako,+
Na umwokoe mwana wa kijakazi wako.+
17 Unitendee ishara inayomaanisha wema,
Ili wale wanaonichukia wapate kuiona na kuaibika.+
Kwa maana wewe mwenyewe, Ee Yehova, umenisaidia na kunifariji.+
Ya wana wa Kora. Muziki, wimbo.
87 Msingi wake uko katika milima mitakatifu.+
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, Ee jiji la Mungu wa kweli.+ Sela.
4 Nitataja Rahabu na Babiloni+ kuwa kati ya wale wanaonijua mimi;
Tazama, Ufilisti+ na Tiro, pamoja na Kushi:+
“Huyu alizaliwa humo.”+
7 Pia kutakuwako waimbaji na vilevile wachezaji wa dansi za mzunguko:+
“Mabubujiko yangu yote yamo ndani yako.”+
Wimbo, muziki wa wana wa Kora. Kwa kiongozi juu ya Mahalathi kwa ajili ya maitikio. Maskili ya Hemani+ Mwezra.
4 Nimehesabiwa katikati ya wale wanaoshuka kuingia shimoni;+
Nimekuwa kama mwanamume ambaye hana nguvu,+
5 Aliyewekwa huru katikati ya wafu,+
Kama waliouawa ambao wanalala kaburini,+
Ambao huwakumbuki tena
Na ambao wametenganishwa na mkono wako wenye kusaidia.+
6 Umeniweka katika shimo lililo katika vina vya chini kabisa,
Katika mahali penye giza, katika abiso kubwa.+
8 Umewaweka rafiki zangu mbali nami;+
Umeniweka kuwa kama kitu chenye kuchukiza sana kwao.+
Niko chini ya kizuizi wala siwezi kwenda.+
9 Jicho langu mwenyewe limedhoofika kwa sababu ya mateso yangu.+
Nimekuitia wewe, Ee Yehova, mchana kutwa;+
Nimekunyooshea mikono yangu.+
10 Je, utawafanyia wale waliokufa jambo la ajabu?+
Au je, wale wasiojiweza katika kifo watasimama,+
Je, watakusifu wewe?+ Sela.
11 Je, fadhili zako zenye upendo zitatangazwa katika kaburi,
Na uaminifu wako katika mahali pa maangamizi?+
15 Ninateseka nami niko karibu kukata pumzi tangu uvulana;+
Nimevumilia sana vitu vyenye kuogopesha kutoka kwako.+
16 Miwako ya hasira yako inayowaka imepita juu yangu;+
Vitisho kutoka kwako mwenyewe vimeninyamazisha.+
Maskili. Ya Ethani Mwezra.+
89 Nitaimba juu ya maonyesho ya fadhili zenye upendo za Yehova mpaka wakati usio na kipimo.+
Kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako kwa kizazi baada ya kizazi.+
2 Kwa maana nimesema: “Fadhili zenye upendo zitakaa zikiwa zimejengwa mpaka wakati usio na kipimo;+
Kwa habari ya mbingu, wewe unaendeleza uaminifu wako imara ndani yake.”+
4 ‘Nitaufanya imara uzao wako mpaka wakati usio na kipimo,+
Nami nitakijenga kiti chako cha ufalme+ kwa kizazi baada ya kizazi.’” Sela.
5 Na mbingu zitasifu tendo lako la ajabu, Ee Yehova,+
Naam, uaminifu wako katika kutaniko la watakatifu.
6 Kwa maana ni nani kule angani anayeweza kulinganishwa na Yehova?+
Ni nani anayeweza kufanana na Yehova kati ya wana wa Mungu?+
7 Mungu anapaswa kupewa heshima katikati ya kikundi cha rafiki za karibu cha watakatifu;+
Yeye ni mkuu na mwenye kuogopesha juu ya wote wanaomzunguka pande zote.+
8 Ee Yehova Mungu wa majeshi,+
Ni nani aliye na nguvu kama wewe, Ee Yah?+
Na uaminifu wako unakuzunguka kotekote.+
10 Wewe mwenyewe umemponda Rahabu,+ kama mtu aliyeuawa.+
Kwa mkono wa nguvu zako umewatawanya adui zako.+
11 Mbingu ni yako,+ dunia pia ni yako;+
Nchi yenye kuzaa na vinavyoijaza+—wewe mwenyewe umeviwekea msingi.+
12 Kaskazini na kusini—wewe mwenyewe uliziumba;+
Tabori+ na Hermoni+—hupiga vigelegele kwa shangwe katika jina lako.+
14 Uadilifu na hukumu ndizo mahali palipofanywa imara pa kiti chako cha ufalme;+
Fadhili zenye upendo na ukweli zinaingia mbele za uso wako.+
15 Wenye furaha ni watu wanaojua vigelegele vya shangwe.+
Ee Yehova, katika nuru ya uso wako wanaendelea kutembea.+
19 Wakati huo uliongea na washikamanifu wako katika maono,+
Nawe ukasema:
“Nimempa mwenye nguvu msaada;+
Nimemwinua aliyechaguliwa kutoka katikati ya watu.+
23 Na adui zake niliwavunja vipande-vipande kutoka mbele yake,+
Na wale wanaomchukia vikali niliendelea kuwapa mapigo.+
24 Na uaminifu wangu na fadhili zangu zenye upendo ziko pamoja naye,+
Na katika jina langu pembe yake imeinuliwa.+
28 Nitahifadhi fadhili zangu zenye upendo kwake mpaka wakati usio na kipimo,+
Nalo agano langu litakuwa lenye uaminifu kwake.+
30 Wanawe wakiiacha sheria yangu+
Nao wasitembee katika maamuzi yangu ya hukumu,+
31 Wakizitia unajisi sheria zangu,
Nao wasishike amri zangu,
32 Mimi pia nitaelekeza fikira zangu kwenye ukosaji wao kwa fimbo+
Na kwenye kosa lao kwa mapigo.+
33 Lakini fadhili zangu zenye upendo sitamwondolea mbali,+
Wala sitaufanya uaminifu wangu kuwa wa
uwongo.+
36 Uzao wake mwenyewe utakuwako mpaka wakati usio na kipimo,+
Na kiti chake cha ufalme kama vile jua lilivyo mbele zangu.+
37 Kama mwezi, kitafanywa imara mpaka wakati usio na kipimo,
Na kama vile shahidi mwaminifu angani.” Sela.
43 Isitoshe, wewe tena unautendea upanga wake kama adui,+
Nawe umemfanya asipate ushindi katika pigano.+
46 Ee Yehova, utaendelea kujificha mpaka wakati gani? Wakati wote?+
Je, ghadhabu yako itaendelea kuwaka kama moto?+
47 Ukumbuke mimi nina urefu gani wa maisha.+
Je, ni kwa ubatili kwamba umewaumba wana wote wa binadamu?+
48 Ni mwanamume gani aliye hai ambaye hataona kifo?+
Je, anaweza kuiokoa nafsi yake katika mkono wa Kaburi?*+ Sela.
49 Yako wapi matendo yako ya kwanza ya fadhili zenye upendo, Ee Yehova,
Ambayo ulimwapia Daudi katika uaminifu wako?+
50 Ukumbuke, Ee Yehova, shutuma juu ya watumishi wako,+
Kuchukua kifuani pangu shutuma ya vikundi vyote vingi vya watu,+
51 Jinsi adui zako wameshutumu, Ee Yehova,+
Jinsi wameshutumu nyayo za mtiwa-mafuta wako.+
52 Yehova na abarikiwe mpaka wakati usio na kipimo. Amina na Amina.+
KITABU CHA NNE
Sala ya Musa, mtu wa Mungu wa kweli.+
2 Kabla ya kuzaliwa kwa milima,+
Au kutokezwa kwa dunia+ na nchi yenye kuzaa kana kwamba kwa maumivu ya kuzaa,+
Tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo wewe ni Mungu.+
3 Unamfanya mwanadamu anayeweza kufa arudi kuwa kitu kilichopondwa,+
Nawe unasema: “Rudini, enyi wana wa binadamu.”+
5 Umewafagilia mbali;+ wanakuwa usingizi tu;+
Asubuhi, wao ni kama majani mabichi ambayo hubadilika.+
8 Umeyaweka makosa yetu moja kwa moja mbele zako,+
Mambo yetu yaliyofichika mbele za uso wako unaong’aa.+
9 Kwa maana siku zetu zote zimepungua katika ghadhabu yako;+
Tumeimaliza miaka yetu kama mnong’ono tu.+
10 Kwa maana siku za miaka yetu ni miaka 70;+
Na ikiwa kwa sababu ya nguvu za pekee ni miaka 80,+
Hata hivyo hizo husisitiza kuleta taabu na mambo yenye kuumiza;+
Kwa maana lazima zipite upesi, nasi huruka na kwenda zetu.+
14 Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako zenye upendo,+
Ili tupate kupiga vigelegele kwa shangwe na kufurahi siku zetu zote.+
17 Nao uzuri wa Yehova Mungu wetu na uwe juu yetu,+
Na kazi ya mikono yetu uifanye imara juu yetu.+
Naam, kazi ya mikono yetu, uifanye imara.+
91 Yeyote anayekaa mahali pa siri+ pa Aliye Juu Zaidi+
Atajipatia makao katika kivuli cha Mweza-Yote.+
3 Kwa maana yeye mwenyewe atakukomboa kutoka katika mtego wa mwindaji wa ndege,+
Kutoka kwa tauni inayosababisha shida.+
5 Hutaogopa kitu chochote chenye kutia hofu wakati wa usiku,+
Wala mshale+ unaoruka mchana,
6 Wala tauni inayotembea gizani,+
Wala maangamizi yanayopora katikati ya mchana.+
9 Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”+
Umemfanya Aliye Juu Zaidi awe makao yako;+
10 Hakuna msiba utakaokuangukia,+
Na hata pigo halitakaribia hema lako.+
13 Utamkanyaga mwana-simba na swila;+
Utamkanyagia chini mwana-simba mwenye manyoya shingoni na nyoka mkubwa.+
14 Kwa sababu ameweka upendo wake juu yangu,+
Mimi nitamwokoa pia.+
Nitamlinda kwa sababu amelijua jina langu.+
Muziki, wimbo, kwa ajili ya siku ya sabato.
92 Ni vema kumtolea Yehova shukrani+
Na kulipigia jina lako muziki, ewe Uliye Juu Zaidi;+
2 Kutangaza asubuhi fadhili zako zenye upendo+
Na nyakati za usiku uaminifu wako.+
3 Kwa kinanda cha nyuzi kumi na kwa udi,+
Kwa muziki unaovuma wa kinubi.+
4 Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya utendaji wako;
Kwa sababu ya kazi za mikono yako, ninapiga vigelegele kwa shangwe.+
7 Wakati waovu wanapochipuka kama majani+
Na wote wanaotenda mambo yenye kuumiza wanapochanuka,
Ni ili wao wapate kuangamizwa milele.+
8 Lakini wewe uko juu mpaka wakati usio na kipimo, Ee Yehova.+
9 Kwa maana, tazama! adui zako, Ee Yehova,+
Kwa maana, tazama! adui zako mwenyewe wataangamia;+
Wote wanaofanya mambo yenye kuumiza watatenganishwa.+
11 Na jicho langu litawatazama adui zangu;+
Masikio yangu yatasikia habari za wale wanaosimama juu yangu, watenda-maovu.
14 Bado wataendelea kusitawi wakati wa kuwa na kichwa chenye mvi,+
Wataendelea kuwa wanono na wabichi,+
15 Ili kutangaza kwamba Yehova ni mnyoofu.+
Yeye ni Mwamba wangu,+ ambaye ndani yake hamna ukosefu wowote wa uadilifu.+
93 Yehova mwenyewe amekuwa mfalme!+
Amevaa adhama;+
Yehova amevaa—amejifunga mshipi wa nguvu.+
Nchi yenye kuzaa pia hufanywa imara ili isipate kutikiswa.+
2 Kiti chako cha ufalme kimefanywa imara tangu zamani za kale;+
Wewe ni wa tangu wakati usio na kipimo.+
5 Vikumbusho vyako vimekuwa vyenye kutegemeka sana.+
Utakatifu unaifaa nyumba yako mwenyewe,+ Ee Yehova, kwa wingi wa siku.+
3 Waovu wataendelea kuwako hata wakati gani, Ee Yehova,+
Waovu wataendelea kushangilia hata wakati gani?+
4 Wanaendelea kuropoka, wanaendelea kusema ovyoovyo;+
Wote wanaofanya mambo yenye kuumiza wanaendelea kujivuna wenyewe.+
8 Eleweni, ninyi msiotumia akili mlio kati ya watu;+
Nanyi wajinga, mtapata ufahamu wowote wakati gani?+
11 Yehova anazijua fikira za wanadamu, kwamba hizo ni kama pumzi.+
12 Mwenye furaha ni mwanamume ambaye unamrekebisha,+ Ee Yah,
Na ambaye unamfundisha katika sheria yako mwenyewe,+
13 Ili kumpa utulivu kutokana na siku za msiba,+
Mpaka shimo lichimbwe kwa ajili ya mwovu.+
16 Ni nani atakayesimama kwa ajili yangu juu ya waovu?+
Ni nani atakayesimama kwa ajili yangu juu ya wanaotenda mambo yenye kuumiza?+
18 Niliposema: “Hakika mguu wangu utatembea ukitikisika,”+
Fadhili zako zenye upendo, Ee Yehova, ziliendelea kunitegemeza.+
19 Fikira zangu zinazofadhaisha zilipokuwa nyingi ndani yangu,+
Faraja zako mwenyewe zilianza kuikumbatia nafsi yangu.+
20 Je, kiti cha ufalme kinachosababisha shida, kitashirikiana nawe,+
Na huku kinatunga matatizo kwa njia ya amri?+
21 Wao hushambulia vikali nafsi ya mwadilifu+
Na kutangaza kwamba damu ya mtu asiye na hatia ni yenye uovu.+
Yehova Mungu wetu atawanyamazisha.+
95 Njooni tumpigie Yehova vigelegele kwa shangwe!+
Na tumpigie Mwamba wetu wa wokovu vigelegele vya ushindi.+
3 Kwa maana Yehova ni Mungu mkuu+
Na Mfalme mkuu juu ya miungu mingine yote,+
4 Yeye ambaye mkononi mwake mna vina vya ndani sana vya dunia+
Na ambaye vilele vya milima ni vyake;+
5 Ambaye bahari, aliyoiumba yeye mwenyewe, ni yake+
Na ambaye mikono yake mwenyewe iliifanyiza nchi kavu.+
6 Ingieni, tuabudu na kuinama;+
Na tupige magoti+ mbele za Yehova Mtengenezaji wetu.+
7 Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake na kondoo wa mkono wake.+
Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+
8 Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu kama huko Meriba,+
Kama katika ile siku ya Masa, nyikani,+
9 Wakati mababu zenu waliponijaribu;+
Walinichunguza, pia waliuona utendaji wangu.+
10 Kwa miaka 40 nilichukizwa na kizazi hicho,+
Nami nikasema:
“Wao ni kikundi cha watu waliopotoka moyoni,+
Nao wenyewe hawajapata kuzijua njia zangu”;+
11 Ambao niliapa juu yao kwa hasira yangu:+
“Hawataingia katika mahali pangu pa kupumzikia.”+
2 Mwimbieni Yehova, libarikini jina lake.+
Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+
5 Kwa maana miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu isiyo na thamani;+
Lakini Yehova, amezifanya mbingu.+
9 Mwinamieni Yehova katika pambo takatifu;+
Iweni na maumivu makali kwa sababu yake, enyi nyote watu wa dunia.+
10 Semeni kati ya mataifa: “Yehova amekuwa mfalme.+
Nchi yenye kuzaa pia hufanywa imara ili isitikiswe.+
Yeye atatetea kwa unyoofu vikundi vya watu katika kesi yao.”+
12 Nchi na ifurahi na vyote vilivyomo.+
Na wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie+
13 Mbele za Yehova. Kwa maana amekuja;+
Kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+
Ataihukumu kwa uadilifu nchi yenye kuzaa+
Na vikundi vya watu kwa uaminifu.+
2 Mawingu na giza zito vinamzunguka;+
Uadilifu na hukumu ni mahali palipofanywa imara pa kiti chake cha ufalme.+
7 Wote wanaotumikia sanamu yoyote ya kuchongwa na waone aibu,+
Wale wanaojisifia miungu isiyo na thamani.+
Mwinamieni, enyi miungu yote.+
8 Sayuni ilisikia na kuanza kushangilia,+
Na miji ya kandokando ya Yuda ilianza kushangilia+
Kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu, Ee Yehova.+
9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote;+
Wewe uko juu sana katika kupanda kwako, juu ya miungu mingine yote.+
10 Enyi mnaompenda Yehova,+ chukieni yaliyo mabaya.+
Yeye anazilinda nafsi za washikamanifu wake;+
Huwakomboa kutoka katika mkono wa waovu.+
Muziki.
98 Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+
Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.+
Mkono wake wa kuume, naam, mkono wake mtakatifu, umempatia wokovu.+
3 Amezikumbuka fadhili zake zenye upendo na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.+
Miisho yote ya dunia imeuona wokovu wa Mungu wetu.+
4 Mpigieni Yehova kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+
Changamkeni na kupiga vigelegele kwa shangwe na kupiga muziki.+
8 Mito na ipige makofi;
Milima yote pamoja na ipige vigelegele kwa shangwe+
9 Mbele za Yehova, kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+
Ataihukumu nchi yenye kuzaa kwa uadilifu+
Na vikundi vya watu kwa unyoofu.+
4 Na kwa nguvu za mfalme ameipenda hukumu.+
Wewe mwenyewe umeufanya imara unyoofu.+
Umetekeleza hukumu na uadilifu katika Yakobo.+
6 Musa na Haruni walikuwa kati ya makuhani wake,+
Na Samweli alikuwa kati ya wale walioliitia jina lake.+
Walikuwa wakimwita Yehova, naye akaendelea kuwajibu.+
8 Ee Yehova Mungu wetu, wewe mwenyewe uliwajibu.+
Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe,+
Na mwenye kulipiza kisasi juu ya matendo yao yenye sifa mbaya.+
9 Mtukuzeni Yehova Mungu wetu+
Na mwiname kwenye mlima wake mtakatifu.+
Kwa maana Yehova Mungu wetu ni mtakatifu.+
Muziki wa kutoa shukrani.+
100 Mpigieni Yehova kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+
3 Jueni kwamba Yehova ni Mungu.+
Yeye ndiye aliyetufanya, wala si sisi wenyewe.+
Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.+
4 Ingieni katika malango yake mkiwa na shukrani,+
Katika nyua zake mkiwa na sifa.+
Mtoleeni shukrani, libarikini jina lake.+
Fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo,+
Na uaminifu wake ni wa kizazi baada ya kizazi.+
Ya Daudi. Muziki.
2 Nitatenda kwa busara katika njia isiyo na kosa.+
Utanijia wakati gani?+
Nitatembea katika utimilifu wa moyo wangu ndani ya nyumba yangu.+
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu chochote kisichofaa.+
Nimelichukia tendo la wale wanaoiacha njia;+
Halishikamani nami.+
5 Yeyote anayemchongea mwenzake kwa siri,+
Huyo ninamnyamazisha.+
Yeyote mwenye macho yenye kiburi na mwenye moyo wa majivuno,+
Huyo siwezi kumvumilia.+
6 Macho yangu yako juu ya waaminifu wa
dunia,+
Ili wapate kukaa pamoja nami.+
Yule anayetembea katika njia isiyo na kosa,+
Yeye ndiye atakayenihudumia.+
7 Katika nyumba yangu hatakaa mtu yeyote anayefanya ujanja.+
Na yeyote anayesema uwongo, hatafanywa imara+
Mbele za macho yangu.+
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote wa dunia,+
Kukatilia mbali kutoka katika jiji+ la Yehova wote wanaotenda mambo yenye kuumiza.+
Sala ya mwenye kuteseka ikiwa atakuwa mnyonge na kumwaga hangaiko lake mbele za Yehova.+
2 Usinifiche uso wako siku nitakayokuwa katika dhiki kali.+
Utege sikio lako kwangu;+
Siku nitakayoita, ufanye haraka, unijibu.+
3 Kwa maana siku zangu zimefikia mwisho kama moshi,+
Na mifupa yangu imefanywa kuwa na moto mkali kama jiko.+
9 Kwa maana nimekula majivu kama mkate;+
Navyo vitu ninavyokunywa nimevichanganya hata pamoja na kulia,+
10 Kwa sababu ya shutuma zako na kuudhika kwako;+
Kwa maana umeniinua, ili unitupilie mbali.+
12 Lakini wewe, Ee Yehova, utakaa mpaka wakati usio na kipimo,+
Na ukumbusho wako utakuwa kwa kizazi baada ya kizazi.+
13 Wewe mwenyewe utasimama, utakuwa na rehema juu ya Sayuni,+
Kwa maana ni majira ya kumwonyesha kibali,
Kwa maana wakati uliowekwa umefika.+
14 Kwa maana watumishi wako wamepata raha katika mawe yake+
Nao wanaelekeza kibali chao kwenye mavumbi yake.+
19 Kwa maana yeye ametazama chini kutoka katika kilele chake kitakatifu,+
Kutoka katika mbingu Yehova ametazama chini, naam, kwenye dunia,+
20 Ili kusikia kuugua kwa mfungwa,+
Ili kuwafungua wale waliowekwa kwa ajili ya kifo;+
21 Ili jina la Yehova litangazwe katika Sayuni+
Na sifa yake katika Yerusalemu,+
26 Hizo zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utaendelea kusimama;+
Nazo zote zitachakaa kama vazi.+
Utazibadili kama mavazi, nazo zitamaliza zamu yake.+
27 Lakini wewe ni yuleyule, nayo miaka yako mwenyewe haitamalizika.+
Ya Daudi.
103 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,+
Naam, kila kitu kilicho ndani yangu, na kilibariki jina lake takatifu.+
2 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,
Wala usiyasahau matendo yake yote,+
3 Yeye anayesamehe makosa yako yote,+
Anayeponya magonjwa yako yote,+
4 Anayeuokoa uhai wako kutoka katika shimo,+
Anayekuvika taji la fadhili zenye upendo na rehema,+
5 Anayeushibisha muda wote wa maisha yako kwa mambo mema;+
Ujana wako unajifanya upya kama ule wa tai.+
8 Yehova ni mwenye rehema na mwenye neema,+
Si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo.+
9 Yeye hataendelea kutafuta makosa wakati wote,+
Wala hataendelea kuweka kinyongo mpaka wakati usio na kipimo.+
10 Hakututendea kulingana na dhambi zetu;+
Wala kuleta juu yetu kile tunachostahili kulingana na makosa yetu.+
11 Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,+
Ndivyo fadhili zake zenye upendo zilivyo kuu kuwaelekea wale wanaomwogopa.+
12 Kama vile mashariki ilivyo mbali sana na magharibi,+
Ndivyo ameweka makosa yetu mbali sana na sisi.+
13 Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema,+
Ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa.+
15 Naye mwanadamu anayeweza kufa, siku zake ni kama zile za majani mabichi;+
Yeye huchanuka kama ua la shambani.+
16 Kwa maana upepo unapita juu yake, nalo halipo tena;+
Napo mahali pake hapataendelea kulitambua tena.+
17 Lakini fadhili zenye upendo za Yehova ni za tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo+
Kuwaelekea wale wanaomwogopa,+
Na uadilifu wake kwa wana wa wana,+
18 Kuwaelekea wale wanaolishika agano lake+
Na kuwaelekea wale wanaoyakumbuka maagizo yake ili kuyafanya.+
19 Yehova amekifanya imara kiti chake cha ufalme mbinguni;+
Nao ufalme wake mwenyewe umetawala juu ya kila kitu.+
20 Mbarikini Yehova, enyi malaika zake,+ mlio na uwezo katika nguvu, mnaolitenda neno lake,+
Kwa kuisikiliza sauti ya neno lake.+
22 Mbarikini Yehova, enyi kazi zake zote,+
Katika mahali pote pa utawala wake.+
Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu.+
104 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu.+
Ee Yehova Mungu wangu, umekuwa mkuu sana.+
Umevaa utukufu na fahari,+
2 Unayejifunika nuru kama vazi,+
Unayezitandaza mbingu kama hema,+
3 Yule anayejenga vyumba vyake vya juu kwa boriti katika maji,+
Anayefanya mawingu kuwa gari lake,+
Anayetembea juu ya mabawa ya upepo,+
4 Anayewafanya malaika zake kuwa roho,+
Na wahudumu wake kuwa moto unaoteketeza.+
5 Ameiwekea dunia msingi juu ya mahali pake palipofanywa imara;+
Haitatikiswa mpaka wakati usio na kipimo, au milele.+
7 Yakaanza kukimbia ulipoyakemea;+
Yakakimbia kwa wasiwasi mkubwa yaliposikia sauti ya mngurumo wako—
Nchi tambarare za mabonde zikashuka chini—
Mpaka mahali ulipoyawekea msingi wake.
12 Juu yake hukaa viumbe vinavyoruka vya mbinguni;+
Kutoka katikati ya majani mengi yanaendelea kuvuma.+
13 Anainywesha maji milima kutoka katika vyumba vyake vya juu.+
Dunia imeshiba matunda ya kazi zako.+
14 Anafanya majani mabichi yachipuke kwa ajili ya wanyama,+
Na mimea ili itumikie wanadamu,+
Ili chakula kitokezwe duniani,+
15 Na divai ambayo hufanya moyo wa mwanadamu anayeweza kufa ushangilie,+
Kuufanya uso ung’ae kwa mafuta,+
Na mkate unaotegemeza moyo wa mwanadamu anayeweza kufa.+
16 Miti ya Yehova imeshiba,
Mierezi ya Lebanoni ambayo aliipanda.+
17 Ambamo ndege hutengeneza viota.+
Naye korongo, miberoshi ndiyo nyumba yake.+
21 Wana-simba wenye manyoya shingoni wananguruma kwa ajili ya mawindo+
Na kwa ajili ya kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu mwenyewe.+
24 Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova!+
Zote umezifanya kwa hekima.+
Dunia imejaa vitu ulivyotokeza.+
25 Na kwa habari ya bahari hii iliyo kubwa na pana,+
Humo mna vitu vyenye kutambaa visivyo na hesabu,+
Viumbe hai, vidogo kwa vikubwa.+
29 Ukiuficha uso wako, wanaingiwa na wasiwasi.+
Ukiiondoa roho yao, wanakata pumzi,+
Na kurudi katika mavumbi yao.+
35 Watenda-dhambi watamalizwa kabisa kutoka duniani;+
Nao waovu, hawatakuwapo tena.+
Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu. Msifuni Yah!+
5 Kumbukeni kazi zake za ajabu ambazo amefanya,+
Miujiza yake na maamuzi ya hukumu ya kinywa chake,+
6 Enyi uzao wa Abrahamu mtumishi wake,+
Enyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+
8 Amelikumbuka agano lake mpaka wakati usio na kipimo,+
Neno ambalo aliamuru, mpaka vizazi elfu,+
9 Agano ambalo alifanya na Abrahamu,+
Na ahadi yake yenye kiapo aliyomwapia Isaka,+
10 Kiapo ambacho alikiendeleza kikiwa sharti kwa Yakobo,
Kama agano lenye kudumu kwa Israeli mpaka wakati usio na kipimo,+
11 Akisema: “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani+
Kuwa fungu la urithi wenu.”+
13 Nao wakaendelea kutembea kutoka kwa taifa moja mpaka kwa taifa lingine,+
Kutoka katika ufalme mmoja mpaka kwa kikundi kingine cha watu.+
14 Hakumruhusu binadamu yeyote awapunje,+
Bali aliwakaripia wafalme kwa sababu yao,+
15 Akisema: “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,+
Wala msiwatendee manabii wangu lolote lililo baya.”+
16 Naye akaitisha njaa juu ya nchi;+
Alivunja kila fimbo ambayo mikate ya mviringo ilining’inizwa juu yake.+
18 Wakaitesa miguu yake kwa pingu,+
Nafsi yake ikaingia katika vyuma;+
19 Mpaka wakati neno lake lilipotimia,+
Maneno ya Yehova mwenyewe yakamsafisha.+
21 Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake+
Na kuwa mtawala juu ya mali yake yote,+
22 Ili awafunge wakuu wake kama inavyopenda nafsi yake+
Na ili apate kuwafundisha hekima hata wanaume wake wazee.+
24 Naye akaendelea kuwafanya watu wake wazaane sana,+
Na hatua kwa hatua akawafanya kuwa wenye uwezo kuliko adui zao.+
25 Akaiacha mioyo yao ibadilike ili kuwachukia watu wake,+
Ili wajiendeshe kwa ujanja juu ya watumishi wake.+
37 Naye akaanza kuwatoa nje wakiwa na fedha na dhahabu;+
Na katikati ya makabila yake hapakuwa na yeyote mwenye kujikwaa.
41 Alifungua mwamba, na maji yakaanza kutiririka;+
Nayo yakapita katika maeneo yasiyo na maji kama mto.+
42 Kwa maana alilikumbuka neno lake takatifu kwa Abrahamu mtumishi wake.+
44 Na hatua kwa hatua akawapa nchi za mataifa,+
Nao wakaendelea kumiliki kazi ngumu ya vikundi vya mataifa,+
45 Ili wapate kushika masharti yake+
Na kushika sheria zake.+
Msifuni Yah!+
Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+
2 Ni nani anayeweza kuyasema matendo yenye nguvu ya Yehova,+
Au anayeweza kufanya sifa yake yote isikiwe?+
4 Unikumbuke, Ee Yehova, kwa nia njema kuelekea watu wako.+
Unitunze kwa wokovu wako,+
5 Ili nipate kuona wema kwa wachaguliwa wako,+
Ili nipate kushangilia kwa shangwe ya taifa lako,+
Ili nipate kujisifu pamoja na urithi wako.+
7 Mababu zetu huko Misri,
Hawakuonyesha ufahamu wowote katika kazi zako za ajabu.+
Hawakukumbuka wingi wa fadhili zako kuu zenye upendo,+
Bali walijiendesha kwa uasi penye bahari, kando ya Bahari Nyekundu.+
9 Kwa hiyo akaikemea Bahari Nyekundu, nayo ikakauka hatua kwa hatua;+
Naye akawatembeza kupita katika kilindi cha maji kana kwamba ni nyikani;+
10 Na kwa hiyo akawaokoa kutoka katika mkono wa mchukiaji+
Na kuwakomboa kutoka katika mkono wa adui.+
19 Na zaidi ya hayo, wakatengeneza ndama katika Horebu+
Na kuinamia sanamu ya kuyeyushwa,+
20 Hivi kwamba wakabadili utukufu wangu+
Kwa ajili ya mfano wa ng’ombe mwenye kula majani.+
21 Walimsahau Mungu Mwokozi wao,+
Mtendaji wa mambo makuu nchini Misri,+
22 Kazi za ajabu katika nchi ya Hamu,+
Mambo yenye kuogopesha kwenye Bahari Nyekundu.+
23 Naye alikuwa karibu kusema waangamizwe,+
Isingalikuwa ni kwa sababu ya Musa mchaguliwa wake,
Aliyesimama penye mwanya mbele zake,+
Ili kuigeuza ghadhabu yake asiwaharibu.+
26 Kwa hiyo akainua mkono wake katika kiapo juu yao,+
Kwamba angewafanya waanguke nyikani,+
27 Na kwamba angefanya uzao wao uanguke kati ya mataifa,+
Na kwamba angewatawanya katika nchi mbalimbali.+
32 Tena, wakafanya uchokozi katika maji ya Meriba,+
Hivi kwamba mambo yakamwendea Musa vibaya kwa sababu yao.+
38 Kwa hiyo wakaendelea kumwaga damu isiyo na hatia,+
Damu ya wana wao na binti zao,
Ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani;+
Na nchi ikachafuliwa na umwagaji wa damu.+
41 Naye akawatia mkononi mwa mataifa tena na tena,+
Ili wale wanaowachukia wapate kutawala juu yao,+
42 Na ili adui zao wapate kuwakandamiza,
Na ili wapate kutiishwa chini ya mkono wao.+
Lakini wao wakawa wakijiendesha kwa uasi katika mwendo wao wa kutokutii,+
Nao wakashushwa kwa sababu ya kosa lao.+
45 Naye akalikumbuka agano lake juu yao,+
Naye akajuta kulingana na wingi wa fadhili zake kuu zenye upendo.+
47 Utuokoe, Ee Yehova Mungu wetu,+
Na utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa+
Ili tulishukuru jina lako takatifu,+
Ili tukusifu kwa shangwe.+
48 Na abarikiwe Yehova Mungu wa Israeli+
kutoka wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo;+
Na watu wote waseme Amina.+
Msifuni Yah!
KITABU CHA TANO
107 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+
3 Na ambao amewakusanya pamoja kutoka katika nchi mbalimbali,+
Kutoka mashariki na kutoka magharibi,+
Kutoka kaskazini na kutoka kusini.+
6 Nao wakaendelea kumlilia Yehova katika taabu yao;+
Akawakomboa kutoka katika mikazo iliyokuwa juu yao,+
8 Watu na wamtolee Yehova shukrani kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo+
Na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.+
13 Nao wakaanza kumwomba Yehova msaada katika taabu yao;+
Na kutoka katika mikazo iliyokuwa juu yao yeye akawaokoa kama kawaida.+
15 Watu na wamshukuru Yehova kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo+
Na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.+
17 Wale waliokuwa wapumbavu, kwa sababu ya njia ya ukosaji wao+
Na kwa sababu ya makosa yao, mwishowe walijiletea mateso wenyewe.+
19 Nao wakaanza kumwomba Yehova msaada katika taabu yao;+
Na kutoka katika mikazo iliyokuwa juu yao akawaokoa kama kawaida.+
21 Watu na wamshukuru Yehova kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo+
Na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.+
31 Watu na wamtolee Yehova shukrani kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo+
Na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.+
35 Huigeuza nyika iwe dimbwi la maji lenye matete,+
Na nchi ya eneo lisilo na maji iwe chemchemi za maji.+
37 Nao hupanda mbegu viwanjani na kupanda mashamba ya mizabibu,+
Ili yapate kutokeza mimea yenye kutoa mazao.+
40 Anamwaga dharau juu ya watu wenye vyeo,+
Hivi kwamba anawafanya watange-tange katika mahali penye ukiwa, pasipo na njia.+
43 Ni nani mwenye hekima? Atayashika mambo
hayo+
Na kukaza fikira zake kwa matendo ya Yehova ya fadhili zenye upendo.+
Wimbo. Muziki wa Daudi.
3 Nitakusifu katikati ya vikundi vya watu, Ee Yehova;+
Nami nitakupigia muziki katikati ya vikundi vya mataifa+
7 Mungu mwenyewe amesema katika utakatifu wake:+
“Nitashangilia, nitamgawanya Shekemu+ awe fungu;+
Na nchi tambarare ya chini ya Sukothi+ nitaipima.
8 Gileadi+ ni yangu; Manase+ ni yangu;
Na Efraimu ni ngome ya aliye mkuu wangu;+
Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+
10 Ni nani atakayenipeleka kwenye jiji lenye ngome?+
Ni nani ambaye kwa kweli ataniongoza mpaka Edomu?+
11 Je, si wewe, Ee Mungu ambaye umetutupilia mbali+
Na ambaye huendi pamoja na majeshi yetu ukiwa Mungu?+
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
109 Ee Mungu wa sifa yangu,+ usikae kimya.+
2 Kwa maana kinywa cha mwovu na kinywa cha udanganyifu vimefunguka juu yangu.+
Wamesema juu yangu kwa ulimi wa uwongo;+
Nao waombe-ombe,
Nao watafute chakula kutoka katika mahali pao penye ukiwa.+
12 Na akose mtu wa kumwonyesha fadhili zenye upendo,+
Wala kusiwe na mtu anayewaonyesha kibali wavulana wake wasio na baba.
16 Kwa sababu hakukumbuka kuonyesha fadhili zenye upendo,+
Bali aliendelea kumfuatilia mtu mwenye kuteseka na aliye maskini+
Na mwenye huzuni moyoni, ili kumuua.+
Hivi kwamba ikawa mbali naye;+
18 Naye akavikwa laana kuwa vazi lake.+
Kwa hiyo ikaja kama maji katikati yake+
Na kama mafuta ndani ya mifupa yake.
20 Hayo ndiyo malipo yanayotoka kwa Yehova ya mtu anayenipinga+
Na ya wale wanaosema maovu juu ya nafsi yangu.+
21 Lakini wewe ni Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu.+
Nitendee kwa ajili ya jina lako.+
Kwa sababu fadhili zako zenye upendo ni njema, unikomboe.+
24 Magoti yangu yametetemeka kwa sababu ya kufunga,+
Na mwili wangu umekonda, bila kuwa na mafuta yoyote.+
27 Na wapate kujua ya kwamba huu ni mkono wako;+
Kwamba ni wewe mwenyewe, Ee Yehova, ambaye umelitenda.+
29 Wale wanaonipinga na wavikwe fedheha,+
Na acha wavae wenyewe aibu yao kana kwamba ni koti lisilo na mikono.+
31 Kwa maana yeye atasimama kwenye mkono wa kuume wa maskini,+
Ili amwokoe kutoka kwa wale wanaoihukumu nafsi yake.
Ya Daudi. Muziki.
110 Neno la Yehova kwa Bwana wangu ni:+
“Keti kwenye mkono wangu wa kuume+
Mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako.”+
2 Yehova ataituma fimbo+ ya nguvu zako kutoka Sayuni,+ akisema:
“Nenda ukitiisha katikati ya adui zako.”+
3 Watu wako+ watajitoa kwa hiari+ katika siku ya jeshi lako.+
Katika fahari za utakatifu,+ kutoka tumbo la uzazi la mapambazuko,
Una kundi lako la vijana kama matone ya
umande.+
4 Yehova ameapa+ (naye hatajuta):+
“Wewe ni kuhani mpaka wakati usio na kipimo+
Kwa mfano wa Melkizedeki!”+
5 Yehova mwenyewe akiwa upande wako wa mkono wa kuume+
Hakika atawavunja vipande-vipande wafalme katika siku ya hasira yake.+
6 Atatekeleza hukumu katikati ya mataifa;+
Atafanya maiti zijae.+
Hakika atamvunja vipande-vipande aliye kichwa juu ya nchi yenye hesabu kubwa ya watu.+
א [ʼAʹleph]
Nitamsifu Yehova kwa moyo wangu wote+
ב [Behth]
Katika kikundi cha rafiki za karibu+ walio wanyoofu na katika kusanyiko.+
ג [Giʹmel]
ד [Daʹleth]
Zinazotafutwa na wale wote wanaopendezwa nazo.+
ה [Heʼ]
3 Utendaji+ wake ni utukufu na fahari,+
ו [Waw]
Na uadilifu wake unasimama milele.+
ז [Zaʹyin]
4 Amefanya ukumbusho kwa ajili ya kazi zake za ajabu.+
ח [Chehth]
Yehova ni mwenye neema na mwenye rehema.+
ט [Tehth]
5 Amewapa chakula wale wanaomwogopa.+
י [Yohdh]
Mpaka wakati usio na kipimo, atalikumbuka agano lake.+
כ [Kaph]
מ [Mem]
7 Kazi za mikono yake ni kweli na hukumu;+
8 Yanategemezwa vema milele, mpaka wakati usio na kipimo,+
ע [ʽAʹyin]
Yanafanywa katika kweli na unyoofu.+
פ [Peʼ]
9 Ameutuma ukombozi kwa watu wake.+
צ [Tsa·dhehʹ]
Mpaka wakati usio na kipimo ameamuru agano lake.+
ק [Qohph]
Jina lake ni takatifu na lenye kuogopesha.+
ר [Rehsh]
10 Kumwogopa Yehova ni mwanzo wa hekima.+
ש [Sin]
Wale wote wanaoyatenda maagizo yake wana ufahamu mwema.+
ת [Taw]
Sifa yake inasimama milele.+
א [ʼAʹleph]
Mwenye furaha ni mtu anayemwogopa Yehova,+
ג [Giʹmel]
2 Uzao wake utakuwa wenye nguvu duniani.+
ד [Daʹleth]
Nacho kizazi cha wanyoofu, kitabarikiwa.+
ה [Heʼ]
3 Vitu vyenye thamani na utajiri vimo nyumbani mwake;+
ו [Waw]
Nao uadilifu wake unasimama milele.+
ז [Zaʹyin]
4 Ameangaza katika giza kama nuru kwa walio wanyoofu.+
ח [Chehth]
Yeye ni mwenye neema na mwenye rehema na mwadilifu.+
ט [Tehth]
5 Mtu mwenye neema+ na anayekopesha+ ni mwema.
י [Yohdh]
Yeye hutegemeza mambo yake kwa haki.+
כ [Kaph]
6 Kwa kuwa hatatikiswa kamwe.+
ל [Laʹmedh]
Mwadilifu atakuwa kumbukumbu mpaka wakati usio na kipimo.+
מ [Mem]
7 Hataogopa hata habari mbaya.+
ס [Saʹmekh]
פ [Peʼ]
9 Amegawa kwa wingi; amewapa maskini.+
צ [Tsa·dhehʹ]
Uadilifu wake unasimama milele.+
ק [Qohph]
Pembe yake mwenyewe itainuliwa kwa utukufu.+
ר [Rehsh]
10 Mwovu ataona na hakika atakasirika.+
ש [Shin]
Atasaga meno yake na kuyeyuka.+
ת [Taw]
Tamaa ya waovu itaangamia.+
6 Yeye anajishusha kutazama mbingu na dunia,+
7 Akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka kwenye mavumbi;+
Humwinua maskini kutoka kwenye shimo la majivu,+
8 Ili kumketisha pamoja na wenye vyeo,+
Wenye vyeo kati ya watu wake.+
Nyumba ya Yakobo kutoka kwenye kikundi cha watu wanaosema maneno yasiyoeleweka,+
2 Yuda ikawa mahali pake patakatifu,+
Israeli miliki yake kuu.+
115 Sisi hatuna chochote, Ee Yehova, sisi hatuna chochote,+
Bali jina lako ulitukuze+
Kulingana na fadhili zako zenye upendo, kulingana na ukweli wako.+
7 Zina mikono, lakini haziwezi kugusa.+
Zina miguu, lakini haziwezi kutembea;+
Hazitoi sauti yoyote kwa koo zao.+
12 Yehova mwenyewe ametukumbuka; atatoa baraka,+
Ataibariki nyumba ya Israeli,+
Ataibariki nyumba ya Haruni.+
3 Kamba za kifo zilinizunguka+
Na hali zenye kutaabisha za Kaburi* zikanipata.+
Nikaendelea kupata taabu na huzuni.+
8 Kwa maana umeiokoa nafsi yangu kutokana na kifo,+
Jicho langu kutokana na machozi, mguu wangu kutokana na kujikwaa.+
9 Nitatembea+ mbele za Yehova katika nchi za walio hai.+
Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+
Mimi ni mtumishi wako, mwana wa kijakazi wako.+
Umezifungua pingu zangu.+
2 Kwa maana fadhili zake zenye upendo zimekuwa zenye nguvu kwetu sisi;+
Na ukweli+ wa Yehova ni wa mpaka wakati usio na kipimo.
Msifuni Yah!+
118 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+
3 Wale wa nyumba ya Haruni na waseme sasa:+
“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+
4 Wale wanaomwogopa Yehova na waseme sasa:+
“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+
5 Kutoka katika hali zenye kutaabisha nilimwitia Yah;+
Yah akanijibu na kuniweka katika mahali penye nafasi pana.+
7 Yehova yuko upande wangu kati ya wale wanaonisaidia,+
Hivi kwamba mimi nitawatazama wale wanaonichukia.+
11 Walinizingira, naam, walikuwa wamenizingira.+
Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova.
15 Sauti ya vigelegele vya shangwe na wokovu+
Imo katika mahema+ ya waadilifu.+
Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu.+
26 Na abarikiwe Yeye anayekuja katika jina la Yehova;+
Tumewabariki ninyi watu kutoka katika nyumba ya Yehova.+
29 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+
א [ʼAʹleph]
ב [Behth]
14 Nimeshangilia katika njia ya vikumbusho vyako,+
Kama vile katika mambo mengine yote yenye thamani.+
ג [Giʹmel]
23 Hata wakuu wameketi; Wamesemezana dhidi yangu.+
Naye mtumishi wako, anajishughulisha na masharti yako.+
ד [Daʹleth]
27 Unifanye nielewe njia ya maagizo yako mwenyewe,+
Ili nipate kujishughulisha na kazi zako za ajabu.+
ה [Heʼ]
37 Uyafanye macho yangu yapite ili yasione jambo lisilofaa;+
Unihifadhi hai katika njia yako mwenyewe.+
39 Ufanye shutuma yangu ipitilie mbali, ambayo nimeiogopa,+
Kwa maana maamuzi yako ya hukumu ni mema.+
ו [Waw]
43 Wala usiondoe kabisa neno la kweli kutoka kinywani mwangu,+
Kwa maana nimengojea uamuzi wako mwenyewe wa hukumu.+
45 Nami nitatembea huku na huku katika mahali penye nafasi tele,+
Kwa maana nimeyatafuta maagizo yako.+
48 Nami nitainua mikono yangu kwenye amri zako ambazo nimezipenda,+
Nami nitajishughulisha mwenyewe na masharti yako.+
ז [Zaʹyin]
52 Nimeyakumbuka maamuzi yako ya hukumu tangu wakati usio na kipimo, Ee Yehova,+
Nami najipatia faraja.+
ח [Chehth]
ט [Tehth]
י [Yohdh]
73 Mikono yako mwenyewe imenifanya, nayo ikaniweka imara.+
Unifanye nielewe, ili nipate kujifunza amri zako.+
75 Najua vema, Ee Yehova, kwamba maamuzi yako ya hukumu ni uadilifu+
Na kwamba umenitesa kwa uaminifu.+
77 Rehema zako na zinijie, ili nipate kuendelea kuishi;+
Kwa maana sheria yako ndiyo inayonipendeza.+
78 Wenye kimbelembele na waone aibu, kwa maana wamenipotosha bila sababu.+
Bali mimi, najishughulisha na maagizo yako.+
כ [Kaph]
82 Macho yangu yamedhoofika kwa kutamani maneno yako,+
Huku mimi nikisema: “Utanifariji wakati gani?”+
85 Wenye kimbelembele wamechimba mashimo ya mtego ili wanipate,+
Wale ambao hawakubaliani na sheria yako.+
88 Unihifadhi hai kulingana na fadhili zako zenye upendo,+
Ili nipate kushika kikumbusho cha kinywa chako.+
ל [Laʹmedh]
91 Kulingana na maamuzi yako ya hukumu, vimesimama mpaka leo,+
Kwa maana vyote hivyo ni watumishi wako.+
מ [Mem]
98 Amri yako hunifanya kuwa na hekima kuliko adui zangu,+
Kwa sababu ni yangu mpaka wakati usio na kipimo.+
99 Nimepata kuwa na ufahamu kuliko walimu wangu wote,+
Kwa sababu vikumbusho vyako ndivyo ninavyohangaikia.+
104 Ninajiendesha kwa uelewaji kwa sababu ya maagizo yako.+
Ndiyo sababu nimeichukia kila njia ya uwongo.+
נ [Nun]
108 Tafadhali furahia matoleo ya hiari ya kinywa changu, Ee Yehova,+
Na unifundishe maamuzi yako ya hukumu.+
111 Nimevichukua vikumbusho vyako kuwa ni urithi mpaka wakati usio na kipimo,+
Kwa maana hivyo ni furaha ya moyo wangu.+
112 Nimeuelekeza moyo wangu ili kuyatenda masharti yako+
Mpaka wakati usio na kipimo, mpaka lile la mwisho.+
ס [Saʹmekh]
116 Unitegemeze kulingana na neno lako, ili niendelee kuishi,+
Wala usiniaibishe kwa ajili ya tumaini langu.+
120 Mwili wangu umetetemeka kwa sababu ya kukuhofu;+
Nami nimeogopa kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu.+
ע [ʽAʹyin]
124 Mtendee mtumishi wako kulingana na fadhili zako zenye upendo,+
Na unifundishe masharti yako mwenyewe.+
128 Ndiyo sababu nimeyaona maagizo yote juu ya mambo yote kuwa ni sawa;+
Nimechukia kila njia ya uwongo.+
פ [Peʼ]
132 Unigeukie na kunionyesha kibali,+
Kulingana na uamuzi wako wa hukumu kuwaelekea wale wanaolipenda jina lako.+
133 Uweke imara hatua zangu katika maneno yako,+
Wala namna yoyote ya jambo lenye kuumiza lisinitawale.+
צ [Tsa·dhehʹ]
144 Uadilifu wa vikumbusho vyako ni wa mpaka wakati usio na kipimo.+
Nifanye nielewe, ili nipate kuendelea kuishi.+
ק [Qohph]
147 Nimeamka mapema wakati wa mapambazuko ya asubuhi,+ ili nipate kulilia msaada.+
Kwa maana nimeyangojea maneno yako.+
149 Uisikie sauti yangu kulingana na fadhili zako zenye upendo.+
Ee Yehova, unihifadhi hai kulingana na uamuzi wako wa hukumu.+
152 Zamani za kale nimejua baadhi ya vikumbusho vyako,+
Kwa maana umeviwekea msingi tangu zamani za kale.+
ר [Rehsh]
159 Uone kwamba nimeyapenda maagizo yako.+
Ee Yehova, unihifadhi hai kulingana na fadhili zako zenye upendo.+
160 Kiini cha neno lako ni kweli,+
Na kila uamuzi wako wa hukumu wa uadilifu ni wa mpaka wakati usio na kipimo.+
ש [Sin] au [Shin]
ת [Taw]
169 Kilio changu cha kusihi na kije karibu mbele zako,
Ee Yehova.+
Kulingana na neno lako, nifanye nielewe.+
176 Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea.+ Umtafute mtumishi wako,+
Kwa maana sijazisahau amri zako.+
Wimbo wa Mipando.
Wimbo wa Mipando.
8 Yehova mwenyewe atalinda kuondoka kwako na kuingia kwako+
Tangu sasa na mpaka wakati usio na
kipimo.+
Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.
4 Ambalo makabila wamepanda kuelekea humo,+
Makabila ya Yah,+
Kama kikumbusho kwa Israeli+
Ili kulishukuru jina la Yehova.+
5 Kwa maana huko viti vya ufalme vya hukumu vimewekwa,+
Viti vya ufalme kwa ajili ya nyumba ya Daudi.+
Wimbo wa Mipando.
2 Tazama! Kama vile macho ya watumishi yalivyo kuelekea mkono wa bwana wao,+
Kama vile macho ya mjakazi yalivyo kuelekea mkono wa bimkubwa wake,+
Ndivyo yalivyo macho yetu kumwelekea Yehova Mungu wetu.+
Mpaka atuonyeshe kibali.+
Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.
7 Nafsi yetu ni kama ndege ambaye ameponyoka+
Kutoka katika mtego wa watega-chambo.+
Mtego umevunjwa,+
Na sisi tumeponyoka.+
Wimbo wa Mipando.
125 Wale wanaomtegemea Yehova+
Ni kama Mlima Sayuni,+ ambao hauwezi kutikiswa, bali hukaa mpaka wakati usio na kipimo.+
2 Yerusalemu—kama vile milima inavyolizunguka pande zote,+
Ndivyo Yehova amewazunguka watu wake pande zote+
Tangu sasa na mpaka wakati usio na kipimo.+
3 Kwa maana fimbo ya enzi ya uovu haitaendelea kuwa juu ya+ kura ya waadilifu,
Ili waadilifu wasiunyooshe mkono wao juu ya kosa lolote.+
5 Na wale wanaogeuka kando kwenye njia zao zilizopotoka,+
Yehova atawafanya waende zao pamoja na wale wanaotenda mambo yenye kuumiza.+
Kutakuwa na amani juu ya Israeli.+
Wimbo wa Mipando.
2 Wakati huo kinywa chetu kilijaa kicheko,+
Na ulimi wetu vigelegele vya shangwe.+
Wakati huo walianza kusema kati ya mataifa:+
“Yehova amefanya jambo kuu katika yale ambayo amewafanyia.”+
6 Yule ambaye bila shaka anaenda, naam, akilia,+
Akiwa amechukua mfuko uliojaa mbegu,+
Bila shaka ataingia kwa vigelegele vya shangwe,+
Akiwa amechukua miganda yake.+
Wimbo wa Mipando. Wa Sulemani.
127 Yehova mwenyewe asipoijenga nyumba,+
Ni bure kwamba wajenzi wake wameifanyia kazi ngumu.+
Yehova mwenyewe asipolilinda jiji,+
Ni bure kwamba mlinzi ameendelea kukaa macho.+
2 Ni kazi ya bure kwamba ninyi mnaamka mapema,+
Kwamba mnakaa mpaka kuchelewa,+
Kwamba mnakula chakula kwa maumivu.+
Hivi ndivyo anavyompa hata mpendwa wake usingizi.+
5 Mwenye furaha ni mwanamume ambaye amelijaza+ podo lake na hao.
Hawataona aibu,+
Kwa maana wataongea na adui langoni.
Wimbo wa Mipando.
2 Kwa maana utakula kazi ngumu ya mikono yako mwenyewe.+
Utakuwa mwenye furaha na mambo yatakwendea vema.+
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu unaozaa matunda+
Katika sehemu za ndani kabisa za nyumba yako.
Wana wako watakuwa kama miche ya mizeituni+ kuizunguka meza yako pande zote.
Wimbo wa Mipando.
8 Wala wanaopita karibu hawajasema:
“Baraka ya Yehova na iwe juu yenu.+
Tumewabariki ninyi katika jina la Yehova.”+
Wimbo wa Mipando.
130 Kutoka vilindini nimekuitia wewe, Ee Yehova.+
7 Israeli na aendelee kumngojea Yehova.+
Kwa maana kuna fadhili zenye upendo kwa Yehova,+
Na ndivyo kulivyo na ukombozi mwingi kwake.+
8 Na yeye mwenyewe atamkomboa Israeli kutoka katika makosa yake yote.+
Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.
131 Ee Yehova, moyo wangu haukuwa na majivuno,+
Wala macho yangu hayakuinuka juu sana;+
Wala sikutembea katika mambo makuu mno,+
Wala katika mambo yaliyo ya ajabu mno kwangu.+
2 Hakika nimeituliza na kuinyamazisha nafsi yangu+
Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya juu ya mama yake.+
Nafsi yangu iko juu yangu kama mtoto aliyeachishwa kunyonya.+
Wimbo wa Mipando.
12 Ikiwa wana wako watalishika agano langu+
Na vikumbusho vyangu ambavyo nitawafundisha,+
Wana wao pia milele+
Wataketi juu ya kiti chako cha ufalme.”+
16 Na makuhani wake nitawavika wokovu;+
Na bila shaka washikamanifu wake watapiga vigelegele kwa shangwe.
Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.
2 Ni kama mafuta mazuri juu ya kichwa,+
Yanayoshuka juu ya ndevu,
Ndevu za Haruni,+
Yanayoshuka kwenye ukosi wa mavazi yake.+
Unaoshuka kwenye milima ya Sayuni.+
Kwa maana huko Yehova aliamuru baraka iwepo,+
Naam, uzima mpaka wakati usio na kipimo.+
Wimbo wa Mipando.
5 Kwa maana mimi mwenyewe najua vema kwamba Yehova ni mkuu,+
Na Bwana wetu ni zaidi ya miungu mingine yote.+
6 Kila kitu ambacho Yehova alipendezwa kufanya, amefanya+
Mbinguni na duniani, baharini na katika vilindi vyote vya maji.+
7 Anafanya mivuke ipande kutoka mwisho wa dunia;+
Amefanya hata malango kwa ajili ya mvua;+
Anauleta upepo kutoka katika maghala yake,+
13 Ee Yehova, jina lako ni la mpaka wakati usio na kipimo.+
Ee Yehova, ukumbusho wako ni wa mpaka kizazi baada ya kizazi.+
136 Mshukuruni Yehova, kwa maana ni mwema:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
2 Mshukuruni Mungu wa miungu:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
3 Mshukuruni Bwana wa mabwana:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
4 Yule peke yake aliye Mtendaji wa mambo ya ajabu, mambo makuu:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
5 Yule anayezifanya mbingu kwa uelewaji:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
6 Yule anayeitandaza dunia juu ya maji:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
7 Yule anayeifanya ile mianga mikubwa:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
8 Naam, jua ili litawale wakati wa mchana:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
9 Mwezi na nyota ili zitawale pamoja wakati wa usiku:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
10 Yule anayepiga Misri katika wazaliwa wao wa kwanza:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
11 Na Yule anayetoa Israeli kutoka katikati yao:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
12 Kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;
13 Yule anayekata Bahari Nyekundu sehemu-sehemu:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
14 Na aliyefanya Israeli wapite katikati yake:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
15 Na aliyemkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
16 Yule anayetembeza watu wake kupita nyikani:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
17 Yule anayepiga wafalme wakubwa:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
18 Na ambaye aliua wafalme wenye fahari:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
19 Naam, Sihoni mfalme wa Waamori:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
21 Na ambaye aliitoa nchi yao iwe urithi:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
22 Urithi kwa Israeli mtumishi wake:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
23 Ambaye alitukumbuka tulipokuwa katika hali ya chini:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
24 Na ambaye alitunyakua kutoka kwa adui zetu tena na tena:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
25 Yule anayewapa chakula wote wenye mwili:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni:+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+
3 Kwa maana huko, wale waliokuwa wametushika mateka, walituomba maneno ya wimbo,+
Nao wale wanaotufanyia mzaha—wimbo wa kushangilia:+
“Tuimbieni mmoja wa nyimbo za Sayuni.”+
6 Ulimi wangu na ushikamane na kaakaa langu,+
Kama nisingekukumbuka,+
Kama nisingeinua Yerusalemu
Kuwa juu ya sababu yangu kuu ya kushangilia.+
7 Ukumbuke,+ Ee Yehova, juu ya wana wa Edomu+ siku ya Yerusalemu,+
Waliokuwa wakisema: “Lifanye ukiwa! Lifanye ukiwa mpaka kwenye msingi ulio ndani yake!”+
Ya matendo yako mwenyewe ambayo ulitutendea.+
9 Atakuwa ni mwenye furaha yeye anayewakamata na kuwavunja vipande-vipande+
Watoto wako juu ya mwamba.
Ya Daudi.
2 Nitainama kuelekea hekalu lako takatifu,+
Nami nitalisifu jina lako,+
Kwa sababu ya fadhili zako zenye upendo+ na kwa sababu ya ukweli wako.+
Kwa maana umeyatukuza maneno yako+ hata juu ya jina lako lote.+
4 Wafalme wote wa dunia watakusifu wewe, Ee Yehova,+
Kwa maana watakuwa wameyasikia maneno ya kinywa chako.
6 Kwa maana Yehova yuko juu, hata hivyo yeye humwona mnyenyekevu;+
Lakini yeye anamjua mwenye kiburi kutoka mbali tu.+
7 Kama nikitembea katikati ya taabu, wewe utanihifadhi hai.+
Kwa sababu ya hasira ya adui zangu wewe utaunyoosha mkono,+
Na mkono wako wa kuume utaniokoa.+
8 Yehova mwenyewe atayamalizia mambo yaliyoko kwa ajili yangu.+
Ee Yehova, fadhili zako zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+
Usiziache kazi za mikono yako mwenyewe.+
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
139 Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.+
2 Wewe mwenyewe umepata kujua kuketi kwangu na kusimama kwangu.+
Umeichunguza fikira yangu tokea mbali.+
4 Kwa maana hamna neno hata moja katika ulimi wangu,+
Lakini, tazama! Ee Yehova, tayari unajua yote.+
5 Nyuma na mbele umenizingira;
Nawe unauweka mkono wako juu yangu.
7 Ni wapi ninapoweza kwenda mbali na roho yako,+
Na ni wapi ninapoweza kukimbilia mbali na uso wako?+
8 Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa huko;+
Na kama ningetandika kitanda changu katika Kaburi,* tazama! ungekuwa huko.+
12 Hata giza lenyewe halingekuwa jeusi mno kwako,+
Lakini usiku wenyewe ungeng’aa kama mchana;+
Giza lingekuwa sawa tu na nuru.+
13 Kwa maana wewe mwenyewe uliumba figo zangu;+
Wewe uliniweka nikiwa nimekingwa katika tumbo la mama yangu.+
14 Nitakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia ya ajabu yenye kuogopesha.+
Kazi zako ni za ajabu,+
Kama vile nafsi yangu inavyojua vema.+
15 Mifupa yangu haikufichwa kwako+
Nilipofanyizwa katika siri,+
Nilipoungwa katika sehemu za chini kabisa+ za dunia.
16 Macho yako yalikiona kiini-tete changu,+
Na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa,
Kuhusiana na siku ambazo zilifanyizwa+
Na hakukuwako hata moja kati ya hizo.
17 Kwa hiyo, jinsi mawazo yako yalivyo yenye thamani kwangu!+
Ee Mungu, jinsi jumla yake yote ilivyo kuu!+
18 Kama ningejaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko hata chembe za mchanga.+
Nimeamka, na bado niko pamoja nawe.+
19 Laiti wewe, Ee Mungu, ungemuua mwovu!+
Ndipo hata watu wenye hatia ya damu+ hakika wangeniondokea,
23 Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.+
Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofadhaisha,+
24 Na uone kama ndani yangu mna njia yoyote yenye kuumiza,+
Na uniongoze katika njia+ ya mpaka wakati usio na kipimo.
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
2 Wale ambao wamepanga mambo mabaya moyoni mwao,+
Ambao mchana kutwa wanaendelea kushambulia kama katika vita.+
4 Unilinde, Ee Yehova, na mikono ya mwovu;+
Unilinde na mtu mwenye matendo ya jeuri,+
Wale ambao wamepanga hila ya kuzisukuma hatua zangu.+
5 Waliojiinua wenyewe wameficha mtego kwa ajili yangu;+
Nao wamezitandika kamba kama wavu kando ya njia.+
Wametega minaso kwa ajili yangu.+ Sela.
6 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu.+
Utege sikio, Ee Yehova, usikie sauti ya kusihi kwangu.”+
7 Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ nguvu za wokovu wangu,+
Umekinga kichwa changu katika siku ya jeshi lenye silaha.+
10 Makaa yanayowaka moto na yaangushwe juu yao.+
Na waangushwe motoni,+ ndani ya mashimo yenye maji, ili wasipate kusimama.+
11 Yule mwenye kuongea makuu—na asifanywe imara duniani.+
Mtu wa jeuri—uovu na umwinde kwa mapigo yenye kurudiwa.+
Muziki wa Daudi.
141 Ee Yehova, nimekuitia wewe.+
Ufanye haraka kuja kwangu.+
Utege sikio kwa sauti yangu ninapokuita.+
2 Sala yangu na itayarishwe kama uvumba+ mbele zako,+
Kuinuliwa kwa mikono yangu kama toleo la jioni la nafaka.+
3 Uweke mlinzi, Ee Yehova, kwa ajili ya kinywa changu;+
Uweke mwangalizi juu ya mlango wa midomo yangu.+
4 Usiuelekeze moyo wangu kwenye ubaya wowote,+
Ili kuendeleza matendo yenye sifa mbaya katika uovu+
Pamoja na watu wanaofanya mambo yenye kuumiza,+
Ili nisipate kujilisha vyakula vyao vitamu.+
5 Mwadilifu akinipiga, zingekuwa fadhili zenye upendo;+
Naye akinikaripia, hiyo ingekuwa mafuta juu ya kichwa,+
Ambayo kichwa changu hakingetaka kukataa.+
Kwa maana bado kungekuwako sala yangu wakati wa misiba yao.+
6 Waamuzi wao wametupwa chini kandokando ya mwamba,+
Lakini wameyasikia maneno yangu, kwamba ni yenye kupendeza.+
7 Kama mtu anavyoatua na kupasua kuni juu ya nchi,
8 Hata hivyo, macho yangu yanakuelekea wewe,+ Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu.+
Nimekukimbilia.+
Usiimwage nafsi yangu.+
9 Uniweke mbali na mikono ya mtego ambao wamenitegea+
Na mbali na minaso ya wale wanaofanya mambo yenye kuumiza.+
Maskili. Ya Daudi, alipokuwa pangoni.+ Sala.
142 Kwa sauti yangu, nilimwomba Yehova msaada;+
Kwa sauti yangu, nilianza kumlilia Yehova anionyeshe kibali.+
2 Mbele zake niliendelea kumwaga hangaiko langu;+
Mbele zake niliendelea kutangaza juu ya taabu yangu mwenyewe,+
3 Roho+ yangu ilipozimia ndani yangu.
Ndipo wewe mwenyewe ulipoijua barabara yangu.+
Katika njia ambayo mimi hutembea+
Wametega mtego kwa ajili yangu.+
4 Tazama kwenye mkono wa kuume uone
Kwamba hakuna yeyote anayenitambua mimi.+
Mahali pangu pa kukimbilia pameangamia;+
Hakuna yeyote anayeuliza habari za nafsi yangu.+
6 Usikilize kilio changu cha kusihi,+
Kwa maana nimekuwa maskini sana.+
Unikomboe kutoka kwa watesaji wangu,+
Kwa maana wana nguvu kuliko mimi.+
7 Uitoe nafsi yangu kutoka katika gereza la shimoni+
Ili kulisifu jina lako.+
Waadilifu na wakusanyike kunizunguka,+
Kwa sababu unanitendea inavyofaa.+
Muziki wa Daudi.
143 Ee Yehova, uisikie sala yangu;+
Utege sikio usikie kusihi kwangu.+
Katika uaminifu wako unijibu kwa uadilifu wako.+
2 Wala usiingie katika hukumu pamoja na mtumishi wako;+
Kwa maana mbele zako, hakuna yeyote aliye hai anayeweza kuwa mwadilifu.+
3 Kwa maana adui ameifuatilia nafsi yangu;+
Ameuponda uhai wangu mpaka chini.+
Amenifanya nikae katika mahali penye giza kama wale waliokufa kwa wakati usio na kipimo.+
5 Nimezikumbuka siku za zamani za kale;+
Nimetafakari juu ya utendaji wako wote;+
Kwa kupenda niliendelea kuhangaikia kazi ya mikono yako mwenyewe.+
7 Ufanye haraka, unijibu, Ee Yehova.+
Roho yangu imefikia mwisho.+
Usiufiche uso wako mbali nami,+
Kama sivyo nitakuwa kama wale wanaoshuka kuingia shimoni.+
8 Asubuhi unifanye nisikie fadhili zako zenye upendo,+
Kwa maana nimekutegemea wewe.+
Unijulishe njia ninayopaswa kuitembea,+
Kwa maana nimekuinulia nafsi yangu.+
10 Unifundishe kufanya mapenzi yako,+
Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+
Roho yako ni nzuri;+
Na iniongoze katika nchi ya unyoofu.+
12 Na katika fadhili zako zenye upendo uwanyamazishe adui zangu;+
Nawe uwaangamize wote wanaoichukia nafsi yangu,+
Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+
Ya Daudi.
144 Na abarikiwe Yehova Mwamba wangu,+
Anayeifundisha mikono yangu kwa ajili ya kupigana,+
Vidole vyangu kwa ajili ya vita;
2 Fadhili zangu zenye upendo na ngome yangu,+
Kilele changu salama na Mwokoaji wangu,+
Ngao+ yangu na Yeye ambaye nimemkimbilia,+
Yule anayevitiisha vikundi vya watu chini yangu.+
7 Unyooshe mikono yako kutoka katika kilele;+
Uniweke huru na kunikomboa kutoka katika maji mengi,+
Kutoka kwa mkono wa wageni,+
8 Ambao kinywa chao kimesema mambo yasiyo ya kweli+
Na ambao mkono wao wa kuume ni mkono wa kuume wa uwongo.+
10 Wewe unayewapa wafalme wokovu,+
Wewe unayemweka Daudi mtumishi wako huru kutokana na upanga wenye kuumiza.+
11 Uniweke huru na kunikomboa kutoka kwa mkono wa wageni,+
Ambao kinywa chao kimesema mambo yasiyo ya kweli+
Na ambao mkono wao wa kuume ni mkono wa kuume wa uwongo,+
12 Wanaosema: “Wana wetu ni kama mimea michanga iliyokua wakati wa ujana wao,+
Binti zetu ni kama nguzo za pembeni zilizochongwa kwa mtindo wa jumba la mfalme,
13 Maghala yetu yamejaa, yakitoa mali za aina moja baada ya nyingine,+
Makundi yetu yanaongezeka kwa maelfu, elfu kumi kwa moja, kwenye barabara zetu,
14 Ng’ombe zetu ni wazito, bila mpasuko wala mimba kutoka,+
Na hakuna kilio katika viwanja vyetu vya watu wote.+
15 Wenye furaha ni watu ambao mambo yako hivyo kwao!”
Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!+
Sifa, ya Daudi.
א [ʼAʹleph]
145 Nitakutukuza, Ee Mungu wangu Mfalme,+
Nami nitalibariki jina lako mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
ב [Behth]
ג [Giʹmel]
ד [Daʹleth]
ה [Heʼ]
ו [Waw]
ז [Zaʹyin]
7 Watabubujikwa na maneno wakitaja wingi wa wema wako,+
Na kwa sababu ya uadilifu wako watapiga vigelegele vya shangwe.+
ח [Chehth]
8 Yehova ni mwenye neema na mwenye rehema,+
Si mwepesi wa hasira naye ni mkuu katika fadhili zenye upendo.+
ט [Tehth]
י [Yohdh]
כ [Kaph]
ל [Laʹmedh]
מ [Mem]
13 Ufalme wako ni ufalme kwa nyakati zote zisizo na kipimo,+
Na mamlaka yako ni ya kuendelea mpaka vizazi vyote vinavyofuata.+
ס [Saʹmekh]
ע [ʽAʹyin]
פ [Peʼ]
צ [Tsa·dhehʹ]
ק [Qohph]
ר [Rehsh]
19 Atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao,+
Naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada, naye atawaokoa.+
ש [Shin]
ת [Taw]
21 Kinywa changu kitasema sifa za Yehova;+
Na wote wenye mwili na walibariki jina lake takatifu mpaka wakati usio na kipimo, hata milele.+
3 Msiweke tegemeo lenu katika watu wenye vyeo,+
Wala katika mtu wa udongo, ambaye hana wokovu wowote.+
5 Mwenye furaha ni yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,+
Ambaye tumaini lake liko katika Yehova Mungu wake,+
6 Mtengenezaji wa mbingu na dunia,+
Wa bahari, na vyote vilivyomo,+
Yeye anayedumisha ukweli mpaka wakati usio na kipimo,+
7 Yeye anayetekeleza hukumu kwa ajili ya waliopunjwa,+
Yeye anayewapa wenye njaa mkate.+
Yehova anawafungua wale waliofungwa.+
8 Yehova anafungua macho ya vipofu;+
Yehova anawainua wale walioinama chini;+
Yehova anawapenda waadilifu.+
10 Yehova atakuwa mfalme mpaka wakati usio na kipimo,+
Mungu wako, Ee Sayuni, kwa kizazi baada ya kizazi.+
Msifuni Yah!+
8 Yeye anayezifunika mbingu kwa mawingu,+
Yeye anayetayarisha mvua kwa ajili ya dunia,+
Yeye anayefanya milima ichipushe majani mabichi.+
6 Naye huendelea kuvisimamisha milele, mpaka wakati usio na kipimo.+
Amelitoa sharti, nalo halitapitilia mbali.+
8 Enyi moto na mvua ya mawe, theluji na moshi mzito,+
Enyi pepo zenye tufani, zinazotimiza neno lake,+
10 Enyi wanyama wa mwitu, nanyi wanyama wote wa kufugwa,+
Enyi vitu vinavyotambaa na ndege wenye mabawa,+
13 Na walisifu jina la Yehova,+
Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana lisiweze kufikiwa.+
Utukufu wake uko juu ya dunia na mbingu.+
14 Naye ataiinua pembe ya watu wake,+
Sifa ya washikamanifu wake wote,+
Ya wana wa Israeli, watu walio karibu naye.+
Msifuni Yah!+
6 Nyimbo zinazomsifu sana Mungu na ziwe kooni mwao,+
Na upanga wenye makali kuwili uwe mkononi mwao,+
8 Ili kuwafunga wafalme wao kwa minyororo+
Na watu wao waliotukuzwa kwa pingu za chuma,
9 Ili kutekeleza juu yao uamuzi wa hukumu ulioandikwa.+
Fahari ya namna hiyo ni ya washikamanifu wake wote.+
Msifuni Yah!+
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Pengine mamba.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Pengine mamba.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.