Ayubu
1 Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi+ ambaye jina lake lilikuwa Ayubu;+ na mtu huyo alikuwa asiye na lawama+ na mnyoofu,+ na mwenye kumwogopa Mungu+ na kujiepusha na ubaya.+ 2 Na wana saba na binti watatu walizaliwa kwake.+ 3 Na mifugo+ yake ilikuwa ni kondoo elfu saba na ngamia elfu tatu na jozi mia tano za ng’ombe na punda-jike mia tano, pamoja na kundi kubwa sana la watumishi; na mtu huyo akawa mkuu kuliko watu wote wa Mashariki.+
4 Na wanawe walienda na kufanya karamu+ katika nyumba ya kila mmoja kwenye siku yake mwenyewe; nao wakatuma na kuwakaribisha dada zao watatu ili wale chakula na kunywa pamoja nao. 5 Na ilikuwa kwamba wakati siku za karamu zimemaliza mzunguko, Ayubu alikuwa akituma na kuwatakasa;+ naye aliamka asubuhi na mapema na kutoa dhabihu za kuteketezwa+ kulingana na hesabu yao wote; kwa kuwa Ayubu alisema, “labda wanangu wametenda dhambi nao wamemlaani+ Mungu moyoni mwao.”+ Hivyo ndivyo Ayubu alivyofanya sikuzote.+
6 Na ikaja siku ambapo wana wa Mungu wa kweli+ waliingia na kusimama mbele za Yehova,+ na hata Shetani+ akaingia katikati yao.+
7 Ndipo Yehova akamwambia Shetani: “Wewe unatoka wapi?” Naye Shetani akamjibu Yehova, akasema: “Ninatoka kuzurura huku na huku duniani+ na kutembea huku na huku ndani yake.”+ 8 Naye Yehova akaendelea kumwambia Shetani: “Je, umeuweka moyo wako juu ya mtumishi wangu Ayubu, kwamba hakuna yeyote aliye kama yeye duniani,+ mtu asiye na lawama+ na mnyoofu,+ mwenye kumwogopa Mungu+ na kujiepusha na ubaya?”+ 9 Ndipo Shetani akamjibu Yehova, akasema: “Je, Ayubu amemwogopa Mungu bure?+ 10 Je, wewe hukuweka ukuta kumzunguka+ yeye na kuzunguka nyumba yake na kuzunguka kila kitu alicho nacho pande zote? Umeibariki+ kazi ya mikono yake, na mifugo yake imeenea kotekote duniani. 11 Lakini, ili kuwe na badiliko, tafadhali nyoosha mkono wako, uguse kila kitu alicho nacho, uone kama hatakulaani wewe mbele za uso wako.”+ 12 Basi Yehova akamwambia Shetani: “Tazama! Kila kitu alicho nacho kimo mkononi mwako. Ila tu usinyooshe mkono wako juu yake mwenyewe!” Kwa hiyo Shetani akaondoka mbele za uso wa Yehova.+
13 Sasa ikaja siku ambapo wanawe na binti zake walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao, mzaliwa wa kwanza.+ 14 Na mjumbe+ akamjia Ayubu na kusema: “Ng’ombe walikuwa wakilima+ na punda-jike walikuwa wakilisha kando yao 15 ndipo Wasabea+ wakavamia na kuwachukua, nao wakawapiga na kuwaua watumishi kwa makali ya upanga; nami nikaponyoka, mimi peke yangu, ili nikuambie.”+
16 Huyu alipokuwa bado anasema, yule naye akaja na kusema: “Moto wa Mungu ulianguka kutoka mbinguni+ na kuwaka katikati ya kondoo na watumishi, ukawateketeza; nami nikaponyoka, mimi peke yangu, ili nikuambie.”
17 Huyu alipokuwa bado anasema, mwingine akaja na kusema: “Wakaldayo+ walifanyiza vikosi vitatu, wakawakimbilia ngamia na kuwachukua, nao wakawapiga na kuwaua watumishi kwa makali ya upanga; nami nikaponyoka, mimi peke yangu, ili nikuambie.”
18 Huyu alipokuwa bado anasema, mwingine bado akaja na kusema: “Wana wako na binti zako walikuwa wakila na kunywa divai+ katika nyumba ya ndugu yao, mzaliwa wa kwanza. 19 Na tazama! ukaja upepo mkubwa+ kutoka eneo la nyikani, nao ukazipiga pembe nne za ile nyumba, hivi kwamba ikawaangukia wale vijana, nao wakafa. Nami nikaponyoka, mimi peke yangu, ili nikuambie.”
20 Naye Ayubu akasimama, akalirarua+ koti lake lisilo na mikono, akanyoa+ kichwa chake, akaanguka chini+ na kuinama,+ 21 akasema:
“Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nikiwa uchi,+
Nami nitarudi huko nikiwa uchi.+
Yehova ametoa,+ na Yehova amechukua.+
Jina la Yehova na liendelee kubarikiwa.”+
22 Katika hayo yote Ayubu hakutenda dhambi, wala kumhesabia Mungu jambo lolote lisilofaa.+
2 Baadaye ikaja siku ambapo wana wa Mungu wa kweli waliingia na kusimama mbele za Yehova, na Shetani pia akaingia katikati yao na kusimama mbele za Yehova.+
2 Ndipo Yehova akamwambia Shetani: “Wewe unatoka wapi hasa?” Naye Shetani akamjibu Yehova, akasema: “Ninatoka kuzurura huku na huku duniani na kutembea huku na huku ndani yake.”+ 3 Naye Yehova akaendelea kumwambia Shetani: “Je, umeuweka moyo wako juu ya mtumishi wangu Ayubu,+ kwamba hakuna yeyote aliye kama yeye duniani, mtu asiye na lawama na mnyoofu,+ mwenye kumwogopa Mungu+ na kujiepusha na ubaya?+ Hata sasa bado anashikilia sana utimilifu wake,+ ingawa wewe unanichochea+ juu yake nimmeze bila sababu.”+ 4 Lakini Shetani+ akamjibu Yehova, akasema: “Ngozi kwa ngozi, na kila kitu alicho nacho mtu atakitoa kwa ajili ya nafsi yake.+ 5 Ili kuwe na badiliko, tafadhali nyoosha mkono wako, uguse kufikia mfupa wake na nyama yake, uone kama hatakulaani wewe mbele za uso wako.”+
6 Basi Yehova akamwambia Shetani: “Tazama, yumo mkononi mwako! Ila tu ujihadhari na nafsi yake!” 7 Kwa hiyo Shetani akaondoka mbele za uso wa Yehova,+ akampiga Ayubu kwa majipu+ hatari kuanzia wayo wa mguu wake mpaka kwenye utosi wa kichwa chake. 8 Naye akajichukulia kigae cha udongo cha kujikunia; naye akawa akiketi katikati ya majivu.+
9 Mwishowe mke wake akamwambia: “Je, bado unashikilia sana utimilifu wako?+ Mlaani Mungu, ufe!” 10 Lakini yeye akamwambia: “Wewe unasema kama anavyosema mmoja wa hao wanawake wasio na akili.+ Je, tukubali yaliyo mema tu kutoka kwa Mungu wa kweli, wala tusikubali pia yaliyo mabaya?”+ Katika hayo yote Ayubu hakutenda dhambi kwa midomo yake.+
11 Na rafiki watatu wa Ayubu wakasikia habari za msiba huo wote uliompata, nao wakaja, kila mmoja kutoka mahali pake, Elifazi Mtemani+ na Bildadi Mshua+ na Sofari Mnaamathi.+ Kwa hiyo wakakutana kwa mapatano+ ili waje kumsikitikia na kumfariji.+ 12 Walipoinua macho yao kutoka mbali hawakumtambua. Ndipo wakapaaza sauti zao, wakalia, wakararua+ kila mmoja koti lake lisilo na mikono na kurusha mavumbi kuelekea mbinguni juu ya vichwa vyao.+ 13 Nao wakaendelea kuketi+ chini pamoja naye siku saba, mchana na usiku, wala hakuna yeyote aliyemwambia neno lolote, kwa maana waliona kwamba yale maumivu+ ni makali sana.
3 Ilikuwa baada ya hayo kwamba Ayubu akafungua kinywa chake, akaanza kuilaani siku yake.+ 2 Basi Ayubu akajibu, akasema:
3 “Na iangamie ile siku niliyozaliwa,+
Pia ule usiku ambao mtu alisema, ‘Mwanamume amechukuliwa mimba!’
5 Giza na kivuli kizito kiichukue.
Wingu la mvua na likae juu yake.
Vitu vinavyotia mchana giza na viitie hofu.+
6 Usiku huo—giza na liuchukue;+
Usiwe na furaha katikati ya siku za mwaka;
Usiingie katikati ya hesabu ya miezi.
9 Nyota za wakati wa gizagiza lake na ziingiwe na giza;
Na ungojee nuru wala kusiwe na yoyote;
Nao usiione miali ya mapambazuko.
10 Kwa maana haukufunga milango ya tumbo la uzazi la mama yangu,+
Na hivyo kuficha taabu kutoka machoni pangu.
13 Kwa maana kufikia sasa ningalikuwa nimelala ili nisisumbuliwe;+
Ningalilala wakati huo; ningalikuwa ninapumzika+
14 Pamoja na wafalme na washauri wa dunia,+
Wale wanaojijengea mahali penye ukiwa,+
15 Au pamoja na wakuu walio na dhahabu,
Wale wanaozijaza nyumba zao fedha;
16 Au, kama mimba yenye kuharibika+ iliyofichwa, singalikuwako,
Kama watoto ambao hawajaona nuru.+
21 Kwa nini kuna wale wanaongojea kifo, wala hakipo,+
Ijapokuwa wanaendelea kuchimba wakikitafuta kuliko kutafuta hazina zilizofichwa?
22 Wale wanaoshangilia kwa raha,
Wanafurahi kwa sababu wanapata kaburi.
23 Kwa nini anampa nuru mwanamume, ambaye njia yake imefichwa,+
Na ambaye Mungu anamzungushia ukuta?+
24 Kwa maana kuugua kwangu huja mbele ya chakula changu,+
Na vilio vyangu vya kunguruma+ humwagika kama maji;
25 Kwa sababu nimehofu kitu chenye kutia hofu, nacho kinakuja juu yangu;
Na kile ambacho nimekiogopa kinanijia.+
26 Mimi sijawa bila mahangaiko, wala sijawa bila usumbufu,
Wala sijawa na pumziko, na bado msukosuko unakuja.”
4 Naye Elifazi+ Mtemani akajibu, akasema:
2 “Mtu akijaribu kusema nawe, je, utachoka?
Lakini ni nani anayeweza kuzuia maneno?
5 Lakini wakati huu yanakupata wewe, nawe unachoka;
Yanakugusa wewe, nawe unaingiwa na wasiwasi.
6 Je, heshima yako kwa Mungu siyo msingi wa uhakika wako?
Je, tumaini lako silo utimilifu+ wa njia zako?
7 Tafadhali, kumbuka hili: Je, ni nani aliyepata kuangamia bila hatia?
Na wanyoofu+ walipata kufutiliwa mbali wapi?
8 Kulingana na yale ambayo nimeona, wale wanaotunga madhara
Na wale wanaopanda taabu wataivuna wenyewe.+
9 Wao huangamia kupitia pumzi ya Mungu,
Nao hufikia mwisho kupitia roho ya hasira yake.
10 Kuna mngurumo wa simba, na sauti ya mwana-simba,
Lakini meno ya wana-simba wenye manyoya shingoni huvunjika.
11 Simba anaangamia kwa kukosa mawindo,
Na watoto wa simba hutenganishwa.
12 Sasa mimi nililetewa neno kwa siri,
Na sikio langu likasikia mnong’ono wake,+
13 Katika fikira zinazofadhaisha kutokana na maono ya usiku,
Wakati usingizi mzito unapowashika wanadamu.
14 Hofu ilinishika, na kutetemeka,
Nayo ikaijaza hofu mifupa yangu iliyo mingi.
15 Na roho fulani ikapita juu ya uso wangu;
Nywele za mwili wangu zikaanza kusimama.
16 Ikaanza kusimama tuli,
Lakini sikuitambua sura yake;
Umbo fulani lilikuwa mbele ya macho yangu;
Kulikuwa na utulivu, na sasa nikasikia sauti:
17 ‘Mwanadamu anayeweza kufa—je, anaweza kuwa mwenye haki kuliko Mungu mwenyewe?
Au, je, mwanamume anaweza kuwa safi kuliko Mtengenezaji wake mwenyewe?’
18 Tazama! Yeye hana imani katika watumishi wake,
Naye huwashtaki wajumbe wake kuwa na makosa.
19 Sembuse wale wanaokaa katika nyumba za udongo,
Ambao msingi wao umo mavumbini!+
Mtu huwaponda upesi kuliko nondo.
20 Kuanzia asubuhi mpaka jioni wao hupondwa vipande-vipande;
Wao huangamia milele bila yeyote kutia hilo moyoni.
21 Je, kamba yao ya hema iliyo ndani yao haikung’olewa?
Wao hufa kwa kukosa hekima.
5 “Ita, tafadhali! Je, kuna yeyote anayekujibu?
Nawe utamwendea nani kati ya watakatifu?
2 Kwa maana usumbufu utamuua mpumbavu,
Na mtu anayeshawishiwa kwa urahisi wivu utamuua.
5 Kile anachovuna mwenye njaa hukila;
Na hata mtu hukichukua kutoka kwenye kulabu za mchinjaji,
Na kwa kweli mtego hukamata riziki yao.
6 Kwa maana madhara hayatoki katika mavumbi matupu,
Wala taabu haichipuki katika udongo mtupu.
7 Kwa maana mwanadamu huzaliwa kwa ajili ya taabu,
Kama vile cheche za moto zinavyoruka juu.
8 Hata hivyo, mimi mwenyewe ningetoa maombi kwa Mungu,
Nami ningempelekea Mungu takwa langu,+
9 Kwake Yeye anayetenda mambo makuu yasiyochunguzika,
Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;+
10 Kwake Yeye anayenyesha mvua juu ya uso wa dunia+
Na kupeleka maji juu ya mashamba;+
11 Kwake Yeye anayewaweka mahali pa juu wale walio chini,+
Hivi kwamba wale walio na huzuni wanakuwa juu katika wokovu;
12 Kwake Yeye anayevunja hila za werevu,
Hivi kwamba mikono yao haifanyi kazi ikawa na matokeo;+
13 Kwake Yeye anayewakamata wenye hekima katika ujanja wao wenyewe,+
Hivi kwamba shauri la watu werevu linafanywa haraka-haraka;+
14 Wanakutana na giza hata wakati wa mchana,
Nao wanapapasa-papasa katikati ya mchana kana kwamba ni usiku;+
15 Na kwake Yeye anayeokoa kutoka kwa upanga unaotoka kinywani mwao,
Na maskini kutoka kwa mkono wa mwenye nguvu,+
16 Hivi kwamba panakuwa na tumaini kwa ajili ya mtu wa hali ya chini,+
Lakini ukosefu wa uadilifu kwa kweli hufunga kinywa chake.+
18 Kwa maana yeye husababisha maumivu, lakini hulifunga jeraha;
Yeye huvunja vipande-vipande, lakini mikono yake huponya.
19 Yeye atakukomboa kutoka katika taabu sita,+
Na katika saba kitu chochote chenye kudhuru hakitakugusa.+
20 Yeye atakukomboa kutoka katika kifo wakati wa njaa,+
Na kutoka katika nguvu za upanga wakati wa vita.
22 Utacheka uporaji na njaa,
Wala hutahitaji kuogopa mnyama-mwitu wa dunia.
23 Kwa maana agano lako litakuwa pamoja na mawe ya shambani,
Na mnyama wa mwituni atafanywa aishi kwa amani pamoja na wewe.+
24 Nawe hakika utajua kwamba amani ndiyo hema lako,
Nawe bila shaka utaenda kuyaona malisho yako, wala hutakosa chochote.
27 Tazama! Hayo ndiyo tumeyachunguza. Na ndivyo yalivyo.
Uyasikie, nawe—uyajue kwa ajili yako mwenyewe.”
6 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Laiti usumbufu+ wangu ungepimwa,
Na wakati huohuo wangeweka shida yangu katika mizani!
3 Kwa maana sasa ni nzito hata kuliko mchanga wa bahari.
Ndiyo sababu maneno yangu mwenyewe yamekuwa mazungumzo ya ovyoovyo.+
4 Kwa maana mishale ya Mweza-Yote iko nami,+
Ambayo roho yangu inainywa sumu yake;+
Vitisho kutoka kwa Mungu vinajipanga juu yangu.+
6 Je, vitu visivyo na ladha vitaliwa bila chumvi,
Au, je, umajimaji wenye utelezi wa mholi una ladha yoyote?
7 Nafsi yangu imekataa kugusa kitu chochote.
Ni kama ugonjwa ndani ya chakula changu.
8 Laiti ombi langu lingekuja
Na kwamba Mungu angenipa tumaini langu!
10 Bado ingekuwa ni faraja yangu;
Nami ningeruka kwa shangwe+ kutokana na maumivu yangu,
Hata ingawa hangekuwa na huruma, kwa maana sikuficha maneno+ ya Mtakatifu.+
11 Nguvu zangu ni nini, ndipo niendelee kungojea?+
Na mwisho wangu ni nini, ndipo niendelee kurefusha nafsi yangu?
12 Je, nguvu zangu ni nguvu za mawe?
Au, je, mwili wangu ni wa shaba?
13 Je, ni kwamba mimi sina uwezo wa kujipa msaada,
Na kazi yenye matokeo imeondolewa mbali nami?
14 Kwa habari ya mtu yeyote anayezuia fadhili zenye upendo kutoka kwa mwenzake,+
Yeye pia ataachilia mbali kumwogopa Mweza-Yote.+
15 Ndugu zangu wametenda kwa hila,+ kama mto wa majira ya baridi kali,
Kama mfereji wa mito ya majira ya baridi kali inayoendelea kukauka.
16 Ni myeusi kwa sababu ya barafu,
Theluji hujificha juu yake.
17 Katika majira yake hiyo hukosa maji,+ imenyamazishwa;
Kunapokuwa na joto kali hiyo hukaushwa kutoka mahali pake.+
18 Mapito ya njia yake yanageuzwa kando;
Huenda juu katika mahali patupu na kuangamia.
20 Hakika wameona aibu kwa sababu walikuwa wametumaini;
Wamekuja mpaka mahali hapo nao wanakata tamaa.+
22 Je, ni kwa sababu nimesema, ‘Nipe kitu,
Au, toeni zawadi kwa ajili yangu kutoka katika uwezo wenu;
23 Na mniokoe kutoka mkononi mwa adui,+
Na mnikomboe kutoka mkononi mwa waonevu’?+
26 Je, ninyi mnapanga hila ya kukaripia maneno,
Wakati maneno ya mtu aliyekata tamaa+ ni kwa ajili ya upepo tu?+
27 Ni kwa kadiri gani mtaendelea kupiga kura juu ya mtu asiye na baba,+
Na kumtumia mwenzenu kufanya biashara!+
29 Mrudi, tafadhali—ukosefu wowote wa uadilifu usitokee—
Ndiyo, rudini—uadilifu wangu bado umo ndani yake.+
30 Je, kuna ukosefu wa uadilifu katika ulimi wangu,
Au, je, kaakaa langu halitambui shida?
7 “Je, duniani hakuna kazi ya lazima+ kwa mwanadamu anayeweza kufa,
Na je, siku zake si kama siku za mfanyakazi wa kukodiwa?+
2 Kama mtumwa, yeye hupumua kwa kutamani kivuli,+
Naye hungojea mshahara wake kama mfanyakazi wa kukodiwa.+
4 Wakati ninapolala chini nimesema, ‘Nitaamka wakati gani?’+
Na jioni inapoisha, pia nimejawa na ukosefu wa utulivu mpaka mapambazuko ya asubuhi.
5 Nyama yangu imefunikwa na funza+ na madonge ya mavumbi;+
Ngozi yangu imefanyiza vikoko na kuyeyuka.+
6 Siku zangu zimepita upesi+ kuliko chombo cha mfumaji,
Nazo hufikia mwisho katika hali ya ukosefu wa tumaini.+
9 Wingu kwa hakika hufikia mwisho wake na kwenda zake;
Ndivyo ambavyo yeye anayeshuka katika Kaburi* hatapanda juu.+
11 Mimi pia sitazuia kinywa changu.
Nitasema katika taabu ya roho yangu;
Nitahangaikia uchungu wa nafsi yangu!+
13 Niliposema, ‘Kitanda changu kitanifariji,
Kitanda changu kitanisaidia kuchukua hangaiko langu,’
14 Hata hivyo umeniogopesha kwa ndoto,
Nawe kupitia maono hunifanya nishtuke kwa woga,
15 Hivi kwamba nafsi yangu inachagua kusongwa pumzi,
Kifo+ badala ya mifupa yangu.
16 Nimekataa huo;+ sitaishi mpaka wakati usio na kipimo.
Niache mimi, kwa sababu siku zangu ni upepo wa pumzi.+
17 Mwanadamu anayeweza kufa+ ni kitu gani ili kwamba umlee,
Na ndipo uuweke moyo wako juu yake,
18 Na ndipo umkazie uangalifu kila asubuhi,
Ndipo umjaribu kila dakika?+
20 Ikiwa nimetenda dhambi, ni nini ninaloweza kutimiza kukupinga wewe, Ee Mtazamaji wa wanadamu?+
Kwa nini umeniweka kuwa shabaha yako, hivi kwamba niwe mzigo kwako?
21 Na kwa nini usisamehe ukosaji wangu+
Na kuliachilia kosa langu?
Kwa maana sasa nitalala chini mavumbini;+
Nawe hakika utanitafuta, nami sitakuwapo.”
8 Naye Bildadi Mshua+ akajibu, akasema:
2 “Utaendelea kusema mambo haya mpaka wakati gani,+
Wakati maneno ya kinywa chako ni upepo mtupu wenye nguvu?+
4 Ikiwa wana wako mwenyewe wamemtendea dhambi,
Hivi kwamba anawaacha waingie mkononi mwa maasi yao,
5 Ikiwa wewe mwenyewe utamtafuta Mungu,+
Na ikiwa utamwomba kwa bidii kibali Mweza-Yote,
6 Ikiwa wewe ni safi na mnyoofu,+
Kufikia sasa angeamka kwa ajili yako
Naye hakika angerudisha makao yako ya uadilifu.
7 Pia, huenda ikawa mwanzo wako ulikuwa jambo dogo,
Lakini mwisho wako baadaye ungekuwa mkubwa sana.+
8 Kwa kweli, tafadhali uliza wale wa kizazi cha zamani,+
Nawe uelekeze fikira zako kwenye mambo ambayo baba zao waliyachunguza.+
10 Je, wao wenyewe hawatakufundisha, wakuambie,
Na je, hawatatoa maneno kutoka moyoni mwao?
11 Je, mmea wa mafunjo+ utakua uwe mrefu mahali pasipo na majimaji?
Je, tete litakua liwe kubwa bila maji?
15 Ataegemea juu ya nyumba yake, lakini haitaendelea kusimama;
Ataishika, lakini haitadumu.
17 Mizizi yake husokotana ndani ya rundo la mawe,
Anatazama nyumba ya mawe.
20 Tazama! Mungu mwenyewe hatamkataa mtu yeyote asiye na lawama,
Wala hataushika mkono wa watenda-maovu,
21 Mpaka atakapojaza kinywa chako kicheko,
Na midomo yako sauti ya shangwe.
9 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Kwa kweli najua ya kuwa iko hivyo.
Lakini mwanadamu anayeweza kufa anawezaje kuwa upande wa haki akiwa katika kesi na Mungu?+
4 Yeye ni mwenye hekima moyoni na mwenye nguvu katika uwezo.+
Ni nani anayeweza kumwonyesha ukaidi naye atoke bila madhara?+
5 Yeye anaiondoa milima,+ hivi kwamba watu hata wasijue kuihusu,
Yeye ambaye ameipindua katika hasira yake.+
9 Anafanyiza kundi-nyota la Ashi, kundi-nyota la Kesili,
Na kundi-nyota la Kima+ na vyumba vya ndani vya Kusini;
10 Anafanya mambo makuu yasiyochunguzika,+
Na mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.+
15 Ambaye siwezi kumjibu, hata ingawa ningekuwa upande wa haki.+
Ningeomba kibali kwa bidii kutoka kwa mpinzani wangu katika kesi.+
16 Kama ningemwita, je, angenijibu?+
Siamini kwamba angetega sikio kuisikiliza sauti yangu;
17 Ambaye ananichubua kwa dhoruba
Na kwa hakika kuzidisha majeraha yangu bila sababu.+
19 Ikiwa mtu yeyote ni mwenye nguvu katika uwezo, pale yeye yupo;+
Na ikiwa yeyote ni mwenye nguvu katika haki, laiti ningeitwa!
20 Kama ningekuwa upande wa haki, kinywa changu mwenyewe kingenitangaza kuwa mwovu;
Kama ningekuwa bila lawama, basi yeye angenitangaza kuwa mpotovu.
21 Kama ningekuwa bila lawama, nisingeijua nafsi yangu;
Ningeukataa uhai wangu.
23 Furiko la ghafula likisababisha kifo kwa ghafula,
Yeye angefanyia mzaha kukata tamaa kwa watu wasio na hatia.
30 Ikiwa kwa kweli ningejiosha katika maji ya theluji,
Nami kwa kweli nisafishe mikono yangu katika sabuni,+
31 Ndipo wewe ungenichovya katika shimo,
Na mavazi yangu kwa hakika yangenichukia.
35 Acha niseme wala nisimwogope,
Kwa maana mimi mwenyewe sina mwelekeo huo.
10 “Nafsi yangu inahisi kuchukizwa na uhai wangu.+
Nitaonyesha hangaiko langu kujihusu mwenyewe.
Nitasema kwa uchungu wa nafsi yangu!
2 Nitamwambia Mungu, ‘Usinitangaze kuwa mwovu.
Nijulishe kwa nini unashindana nami.
3 Je, ni vema kwako kwamba wewe utende kosa,+
Kwamba ukatae tokeo la kazi yenye nguvu ya mikono yako,+
Na kwamba kwa kweli uangazie shauri la waovu?
5 Je, siku zako ni kama siku za mwanadamu anayeweza kufa,+
Au, miaka yako ni kama siku za mwanamume,
6 Kwamba ujaribu kutafuta kosa langu
Nawe uendelee kuitafuta dhambi yangu?+
8 Mikono yako mwenyewe imeniunda hivi kwamba ikanifanyiza mimi+
Mzima pande zote, na bado unataka kunimeza.
9 Tafadhali, kumbuka kwamba umenifanyiza kutoka katika udongo+
Nawe utanifanya nirudi katika mavumbi.+
13 Nawe umeficha mambo hayo moyoni mwako.
Ninajua vema kwamba una mambo hayo.
14 Ikiwa nimetenda dhambi na umeendelea kunitazama+
Nawe hunichukulii kuwa sina hatia katika kosa langu;+
15 Ikiwa kweli nimekosea, ole wangu!+
Na ikiwa kweli niko upande wa haki, nisipate kuinua kichwa changu,+
Nikiwa nimejawa sana na aibu na kujawa na mateso.+
16 Nacho kikitenda kwa majivuno,+ utaniwinda kama mwana-simba,+
Nawe utajionyesha tena kuwa wa ajabu kwangu.
17 Utaleta mashahidi wako wapya mbele yangu,
Nawe utafanya usumbufu wako kuwa mkubwa zaidi juu yangu;
Magumu baada ya magumu yako pamoja nami.
18 Basi kwa nini ulinitoa nje ya tumbo la uzazi?+
Kama ningekata pumzi, ili hata jicho lisinione,
19 Ningekuwa kana kwamba sijapata kuwako;
Ningeletwa kutoka tumboni mpaka kaburini.’
22 Kwenye nchi ya giza kama weusi, ya kivuli kizito
Na ya mchafuko, ambako hakuangazi zaidi ya weusi.”
11 Naye Sofari Mnaamathi+ akajibu, akasema:
2 “Je, maneno mengi yatakosa kujibiwa,
Au, je, mwenye kujisifu tu atakuwa upande wa haki?
3 Je, maongezi yako matupu yatawanyamazisha watu,
Na je, utaendelea kudharau bila kuwa na mtu wa kukukemea?+
6 Ndipo angekuambia siri za hekima,
Kwa kuwa mambo ya hekima inayotumika ni mengi.
Pia, ungejua kwamba Mungu anaruhusu sehemu ya makosa yako yasahaulike kwa ajili yako.+
7 Je, unaweza kuvumbua mambo yenye kina ya Mungu,+
Au, je, unaweza kuvumbua kikomo chenyewe cha Mweza-Yote?
8 Iko juu kuliko mbingu. Wewe unaweza kutimiza nini?
9 Ina kipimo kirefu kuliko dunia,
Na ni pana kuliko bahari.
10 Akisonga mbele na kumshika mtu
Na kuita mahakama, basi ni nani anayeweza kumpinga?
11 Kwa kuwa yeye mwenyewe anajua vema watu wasiosema kweli.+
Anapoona jambo lenye kudhuru, je, yeye pia hatalikazia uangalifu?
12 Hata mtu asiye na akili atapata kusudi jema
Mara tu punda-mwitu anapozaliwa kuwa mwanadamu.
14 Ikiwa jambo lenye kudhuru limo mkononi mwako, liondolee mbali kabisa,
Wala usiache ukosefu wa uadilifu ukae katika mahema yako.
16 Kwa maana wewe—utaisahau taabu;
Utaikumbuka kama maji ambayo yamepita.
17 Na urefu wa maisha yako+ utainuka kwa wangavu kuliko katikati ya mchana;
Giza litakuwa kama asubuhi.+
18 Nawe utakuwa na tegemeo kwa maana kuna tumaini;
Nawe utatazama huku na huku kwa uangalifu—utalala kwa usalama.+
19 Nawe hakika utalala na kujinyoosha, pasipo mtu yeyote wa kukutetemesha.
Na hakika watu wengi watakutuliza;+
20 Nayo macho ya waovu yataisha nguvu;+
Na hakika mahali pa kukimbilia pataangamia kutoka kwao,+
Na tumaini lao litakuwa ni kukata pumzi kwa nafsi.”+
4 Ninakuwa mtu wa kudhihakiwa na wenzake,+
Mtu anayemwita Mungu ili amjibu.+
Mtu mwadilifu, asiye na lawama, amekuwa wa kudhihakiwa.
5 Katika fikira zake, mtu asiye na mahangaiko hudharau maangamizi;+
Yametayarishwa kwa ajili ya wale wenye miguu inayoyumba-yumba.+
6 Mahema ya waporaji hayana wasiwasi,+
Na wale wanaomtia Mungu ghadhabu wana usalama
Ulio wa mtu ambaye ameleta mungu mkononi mwake.+
7 Hata hivyo, tafadhali uliza wanyama wa kufugwa, nao watakufundisha;+
Pia viumbe vya mbinguni vyenye mabawa, navyo vitakuambia.+
14 Tazama! Yeye hubomoa, ili pasiwe na ujenzi;+
Yeye huifunga kwa ajili ya mwanadamu, ili isifunguliwe.+
20 Yeye anaondoa usemi kutoka kwa waaminifu,
Naye huondolea mbali akili ya watu wazee;
21 Yeye anamwaga dharau juu ya watu wenye vyeo,+
Naye hulegeza mshipi wa wenye nguvu;
22 Yeye anafunua mambo mazito kutoka katika giza,+
Naye huleta kivuli kizito kwenye nuru;
23 Anafanya mataifa kuwa makubwa, ili ayaharibu;+
Anaeneza mataifa, ili ayaondoe;
24 Anaondoa moyo wa walio vichwa vya watu wa nchi,
Ili aweze kuwafanya watange-tange katika mahali patupu,+ pasipo na njia.
13 “Tazama! Jicho langu limeona hayo yote,
Sikio langu limesikia nalo linayafikiria.
3 Hata hivyo mimi, kwa upande wangu, ningesema na Mweza-Yote mwenyewe,+
Nami ningependezwa kuhojiana na Mungu.
7 Je, ninyi mtasema maneno ya ukosefu wa uadilifu kwa ajili ya Mungu mwenyewe,
Na je, mtasema udanganyifu kwa ajili yake?+
9 Je, ingekuwa vema kwamba awachunguze ninyi?+
Au, je, mtacheza na yeye kama mtu anavyocheza na mwanadamu anayeweza kufa?
12 Maneno yenu ya kukumbukwa ni methali za majivu;
Vinundu vya ngao zenu ni kama vinundu vya ngao vya udongo.+
13 Nyamazeni mbele yangu, ili mimi mwenyewe nipate kusema.
Kisha na lije juu yangu jambo lolote lile!
14 Kwa nini ninabeba nyama ya mwili wangu katika meno yangu
Na kutia nafsi yangu mwenyewe mkononi mwangu?+
22 Ama uite ili mimi mwenyewe nijibu;
Au mimi niseme, nawe unipe jibu.
23 Mimi nina makosa na dhambi kwa njia gani?
Nijulishe maasi yangu na dhambi yangu.
25 Je, utafanya jani linalopeperushwa litetemeke,
Au kuendelea kuyafukuza majani makavu tu?
26 Kwa maana unaendelea kuandika juu yangu mambo machungu+
Nawe unanifanya niyapate matokeo ya makosa ya ujana wangu.+
27 Pia unaendelea kuiweka miguu yangu katika mikatale,+
Nawe unaziangalia njia zangu zote;
Unatia alama ya mstari wako kwa ajili ya nyayo za miguu yangu.
5 Ikiwa siku zake zimeamuliwa,+
Hesabu ya miezi yake iko kwako;
Umeweka amri kwa ajili yake ili asiweze kuvuka.
6 Geuza macho yako kutoka kwake ili apumzike,+
Mpaka apate raha kama mfanyakazi wa kukodiwa anavyopata katika siku yake.
8 Mzizi wake ukizeeka katika udongo
Na kisiki chake kikifa katika mavumbi,
9 Utachipuka unaponusa harufu ya maji+
Nao utatokeza tawi kama mmea mpya.+
12 Mwanadamu pia hulala chini wala haamki.+
Hawataamka mpaka mbingu itakapokuwa haipo tena,+
Wala hawataamshwa katika usingizi wao.+
14 Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?+
Mimi nitangojea siku zote za kazi yangu ya kulazimishwa,+
Mpaka kitulizo changu kije.+
18 Hata hivyo, mlima, unaoanguka, utafifia,
Na hata mwamba utaondolewa mahali pake.
19 Maji kwa hakika yanakula hata mawe;
Kumwagika kwake kunayachukua mavumbi ya dunia.
Ndivyo ulivyoliharibu tumaini la mwanadamu anayeweza kufa.
20 Unamshinda milele hivi kwamba yeye anaenda zake;+
Unauharibu uso wake hivi kwamba unamwacha aende zake.
21 Wanawe hupewa heshima, lakini yeye hajui hilo;+
Nao wanakuwa wasio na maana, lakini yeye hawafikirii.
22 Ila tu nyama yake iliyo juu yake ndiyo itakayoendelea kuuma,
Na nafsi yake ikiwa ingali ndani yake ndiyo itakayoendelea kuomboleza.”
15 Naye Elifazi Mtemani akajibu, akasema:
2 “Je, mtu mwenye hekima atajibu kwa ujuzi wa upepo,+
Au, je, atalijaza tumbo lake upepo wa mashariki?+
3 Kukaripia tu kwa neno hakutakuwa na faida yoyote,
Na maneno matupu peke yake hayatakuwa na faida.
4 Hata hivyo, wewe mwenyewe unafanya woga mbele za Mungu usiwe na nguvu zozote,
Nawe unapunguza kuwa na hangaiko lolote mbele za Mungu.
5 Kwa maana kosa lako linakizoeza kinywa chako,
Nawe unachagua ulimi wa watu werevu.
6 Kinywa chako kinakutangaza wewe kuwa mwovu, wala si mimi;
Na midomo yako mwenyewe inajibu juu yako.+
7 Je, wewe ndiye mwanadamu wa kwanza kabisa kuzaliwa,+
Au, je, ulizaliwa kwa uchungu kabla ya vilima?+
10 Mwenye kichwa chenye mvi na mzee pia, wote wapo pamoja nasi,+
Yeye aliye na siku nyingi kuliko baba yako.
11 Je, faraja za Mungu hazikutoshi wewe,
Au neno uliloambiwa kwa upole?
12 Kwa nini yaliyo moyoni mwako yanakuchukua,
Na kwa nini macho yako yanawaka?
13 Kwa maana wewe unaigeuza roho yako kinyume cha Mungu mwenyewe,
Nawe umeyatokeza maneno katika kinywa chako mwenyewe.
14 Mwanadamu anayeweza kufa ni nani ndipo awe safi,+
Au ndipo yeyote aliyezaliwa na mwanamke awe upande wa haki?
17 Nitakutangazia. Wewe nisikilize!+
Nimeona hata jambo hili, basi acha nilisimulie,
18 Lile ambalo watu wenye hekima+ wenyewe hulisema
Na ambalo hawakuficha, hilo likiwa limetoka kwa baba zao.
19 Wao peke yao walipewa nchi hiyo,
Wala hakuna mgeni aliyepita katikati yao.
20 Mwovu anapata mateso siku zake zote,
Pia hesabu ya miaka ambayo imewekewa mwonevu.
23 Anapotea njia akitafuta mkate—uko wapi?+
Anajua vema kwamba siku ya giza+ iko tayari mkononi mwake.
24 Taabu na maumivu huendelea kumtia hofu;+
Humshinda nguvu kama mfalme aliyejitayarisha kwa ajili ya shambulio.
25 Kwa sababu yeye ananyoosha mkono wake juu ya Mungu mwenyewe,
Naye anajaribu kujionyesha kuwa mkuu juu ya Mweza-Yote;+
26 Kwa sababu anakimbia juu yake kwa ugumu wa shingo,
Na vinundu vizito vya ngao zake;
27 Kwa sababu yeye kwa kweli anafunika uso wake kwa wingi wa mafuta yake
Naye anaongeza mafuta juu ya viuno vyake,+
28 Anakaa tu katika majiji ambayo yatafutiliwa mbali;
Katika nyumba ambamo watu hawataendelea kukaa,
Ambazo kwa hakika zimekusudiwa kuwa marundo ya mawe.
30 Yeye hatageuka kutoka gizani;
Mwali wa moto utakausha tawi lake,
Naye atageuka kando kwa mlipuko wa kinywa chake Yeye.+
31 Na asiwe na imani katika ubatili, akiwa anapotoshwa,
Kwa maana badala yake atapata ubatili mtupu;
32 Itatimizwa kabla ya siku yake.
Na chipukizi lake halitakuwa na majani mengi.+
33 Atatupa zabibu zake mbichi kama mzabibu,
Na kutupilia mbali maua yake kama mzeituni.
35 Taabu inatungwa mimba na mambo yenye kudhuru yanazaliwa,+
Nalo tumbo lao hutayarisha udanganyifu.”
16 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Nimesikia mambo mengi kama hayo.
Ninyi nyote ni wafariji wasumbufu!+
4 Mimi mwenyewe pia naweza kusema kama ninyi mnavyosema.
Laiti nafsi zenu zingekuwa mahali ilipo nafsi yangu,
Je, ningeng’aa kwa maneno juu yenu,+
Na je, ningetikisa kichwa changu juu yenu?+
5 Ningewatia ninyi nguvu kwa maneno ya kinywa changu,+
Na faraja ya midomo yangu mwenyewe ingetuliza—.
6 Nikiongea, maumivu yangu mwenyewe hayatulizwi,+
Nami nikiacha kufanya hivyo, ni nini kinachoondoka kwangu?
8 Pia unanikamata. Ni ushahidi,+
Hivi kwamba kukonda kwangu kunasimama juu yangu. Kunashuhudia usoni pangu.
9 Hasira yake imenirarua vipande-vipande, naye anashikilia uadui+ juu yangu.
Anasaga meno yake juu yangu.+
Adui yangu mwenyewe anayanoa macho yake juu yangu.+
10 Wamefungua vinywa vyao wazi juu yangu,+
Wamenipiga mashavu yangu kwa shutuma,
Wanakusanyika juu yangu wakiwa hesabu kubwa.+
12 Nilikuwa nimestarehe, lakini akanitikisa;+
Akanikamata nyuma ya shingo, akanivunja-vunja,
Naye ananiweka kuwa shabaha kwa ajili yake mwenyewe.
13 Wapiga-mishale+ wake wananizunguka;
Anapasua wazi figo+ zangu wala haoni huruma;
Anaimwaga nyongo yangu chini.
14 Anaendelea kunitoboa kama ukuta kwa kunitia tundu baada ya tundu;
Anakimbia juu yangu kama mtu mwenye nguvu.+
19 Pia sasa, tazama! yeye anayenishuhudia yuko mbinguni,
Na shahidi wangu yuko katika sehemu za juu.+
21 Na uamuzi utafanywa kati ya mwanamume na Mungu,
Kama ilivyo kati ya mwana wa binadamu na mwenzake.+
6 Naye ameniweka kuwa neno la kimethali+ la vikundi vya watu,
Hivi kwamba ninakuwa mtu ambaye uso wake ni wa kutemewa mate.+
8 Watu wanyoofu wanaangalia kwa mshangao,
Na hata mtu asiye na hatia anachacha kwa sababu ya mwasi-imani.
10 Hata hivyo, ninyi nyote mnaweza kuanza tena. Haya, tafadhali,
Kwa kuwa sioni yeyote mwenye hekima kati yenu.+
13 Nikiendelea kungojea, Kaburi* ndilo nyumba yangu;+
Nitatandika kitanda changu gizani.+
14 Nitalipaazia shimo+ sauti, ‘Wewe ni baba yangu!’
Na kumwambia funza,+ ‘Wewe ni mama yangu na dada yangu!’
16 Watashuka chini kwenye mapingo ya Kaburi,*
Wakati ambapo sisi, sote pamoja, tutashuka mavumbini.”+
18 Naye Bildadi Mshua akajibu, akasema:
2 “Ninyi mtachukua muda gani ili kukomesha maneno?
Mnapaswa kuelewa, ili baadaye tuseme.
4 Yeye anararua vipande-vipande nafsi yake katika hasira yake.
Je, dunia iachwe kwa ajili yako,
Au jiwe liondoke mahali pake?
10 Kamba imefichwa katika udongo kwa ajili yake,
Na kwa ajili yake chombo cha kunasia katika njia yake.
13 Utakula vipande vya ngozi yake;
Mzaliwa wa kwanza wa kifo atakula viungo vyake.
18 Watamsukuma kutoka nuruni kuingia gizani,
Nao watamfukuza kutoka katika nchi yenye kuzaa.
19 Hatakuwa na wazao wala watoto katikati ya watu wake,+
Wala hapatakuwa na mwokokaji mahali pake pa makao ya kigeni.
20 Watu walio Magharibi wataiangalia siku yake kwa mshangao,
Na hata watu walio Mashariki watashikwa na mtetemeko.
21 Ila tu hizo ndizo maskani za mkosaji,
Na hapa ndipo mahali pa mtu ambaye hajamjua Mungu.”
19 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Ninyi mtaendelea kunikasirisha nafsi yangu mpaka wakati gani+
Na kuendelea kuniponda kwa maneno?+
6 Jueni, basi, kwamba Mungu mwenyewe amenipotosha,
Naye ameuzungusha wavu wake wa kuwindia juu yangu.+
7 Tazama! Ninaendelea kupaaza sauti, ‘Jeuri!’ lakini sipati jibu lolote;+
Naendelea kulia nipewe msaada, lakini hakuna haki.+
8 Amezuia pito langu kwa ukuta wa mawe,+ nami siwezi kupita;
Naye anaweka giza katika barabara zangu.+
10 Ananibomoa pande zote, nami naenda zangu;
Naye anang’oa tumaini langu kama mti.
12 Vikosi vyake vinakuja kwa muungano na kujenga njia yao juu yangu,+
Nao wanapiga kambi kuzunguka hema langu.
14 Watu ninaofahamiana nao wamekoma kuwapo,+
Na wale ninaowajua wamenisahau,
15 Wale wanaokaa wakiwa wageni nyumbani mwangu;+ na vijakazi wangu wananiona kuwa mgeni;
Nimekuwa mgeni kwelikweli machoni pao.
16 Nimemwita mtumishi wangu, lakini hajibu.
Ninaendelea kumwomba huruma kwa kinywa changu mwenyewe.
21 Mnionyeshe kibali kidogo, mnionyeshe kibali kidogo, enyi rafiki zangu,+
Kwa kuwa mkono wenyewe wa Mungu umenigusa.+
23 Laiti sasa maneno yangu yangekuwa yameandikwa!
Laiti yangekuwa yameandikwa katika kitabu!
25 Nami mwenyewe najua vema kwamba mkombozi wangu+ yuko hai,
Na kwamba, akija baada yangu, yeye atasimama+ juu ya mavumbi.
26 Na baada ya ngozi yangu, ambayo wameichuna,—hii!
Lakini ijapokuwa kupungua kwa mwili wangu nitamwona Mungu,
27 Ambaye mimi mwenyewe nitamwona,+
Na ambaye macho yangu hakika yatamwona, bali si mgeni.
Figo zangu zimeisha nguvu ndani yangu kabisa.
28 Kwa maana ninyi mnasema, ‘Kwa nini tunaendelea kumtesa?’+
Wakati mzizi wenyewe wa jambo hili unapatikana ndani yangu.
29 Ogopeni kwa ajili yenu kwa sababu ya upanga,+
Kwa kuwa upanga unamaanisha ghadhabu juu ya makosa,
Ili ninyi mjue kwamba kuna mwamuzi.”+
20 Naye Sofari Mnaamathi akajibu, akasema:
2 “Ni kwa sababu hiyo fikira zangu zinazonifadhaisha zinanijibu,
Kwa sababu ya wasiwasi wangu wa ndani.
3 Nasikia himizo ambalo linanitusi;
Na roho ambayo haina uelewaji nilio nao mimi inanijibu.
5 Kwamba kilio cha shangwe cha watu waovu ni kifupi+
Na kushangilia kwa mwasi-imani ni kwa kitambo kidogo?
6 Ijapokuwa utukufu wake unapaa mbinguni+
Na kichwa chake chenyewe kinafika mawinguni,
7 Yeye anaangamia milele kama mavi yake;+
Wale wanaomwona watasema, ‘Yeye yuko wapi?’+
10 Wanawe watatafuta kibali cha watu wa hali ya chini,
Na mikono yake mwenyewe itarudisha vitu vyake vyenye thamani.+
11 Mifupa yake imekuwa yenye kujaa nguvu yake ya ujana,
Lakini italala pamoja naye katika mavumbi matupu.+
12 Ikiwa kilicho kibaya kina ladha tamu kinywani mwake,
Ikiwa anakiyeyusha chini ya ulimi wake,
13 Ikiwa anakihurumia wala hakiachi,
Na ikiwa anaendelea kukizuia katikati ya kaakaa lake,
14 Chakula chake hakika kitabadilishwa katika matumbo yake;
Kitakuwa nyongo ya swila ndani yake.
15 Amemeza mali, lakini ataitapika;
Mungu ataiondosha tumboni mwake.
18 Atairudisha mali yake aliyojipatia wala hataimeza;
Kama mali kutokana na biashara yake, lakini ambayo hataifurahia.+
19 Kwa maana ameponda vipande-vipande, amewaacha watu wa hali ya chini;
Ameinyakua nyumba ambayo hakuijenga.+
20 Kwa maana hakika hatajua starehe katika tumbo lake;
Hataponyoka kupitia vitu vyake vyenye kutamanika.+
21 Hakuna chochote kilichobaki kwa ajili yake ili kumeza;
Ndiyo sababu hali njema yake haitadumu.
23 Na iwe kwamba, ili kujaza tumbo lake,
Ataipeleka hasira yake inayowaka juu yake+
Naye atainyesha juu yake, ndani ya matumbo yake.
25 Mshale utachomoka kupitia mgongo wake,
Na silaha inayong’aa kupitia nyongo yake;+
Vitu vyenye kuogopesha vitaenda juu yake.+
26 Giza lote litawekwa akiba kwa ajili ya hazina zake;
Moto ambao hakuna mtu aliyeupepea utamteketeza;+
Mambo yatamwendea vibaya mwenye kuokoka aliye katika hema lake.
28 Mvua kubwa itaifagilia mbali nyumba yake;
Kutakuwa na vitu vilivyomwagwa katika siku ya hasira yake.+
4 Kwa habari yangu, je, hangaiko langu linaelekezwa kwa mwanadamu?
Au ni kwa nini roho yangu haikosi subira?
6 Na ikiwa nimekumbuka, pia nimetiwa wasiwasi,
Na mtetemeko umeushika mwili wangu.
8 Uzao wao umefanywa imara nao machoni pao,
Na wazao wao mbele ya macho yao.
10 Ng’ombe-dume wake kwa kweli hutia mimba, wala hapotezi shahawa;
Ng’ombe wake huzaa+ wala hatokwi na mimba.
11 Wanaendelea kuwatuma wavulana wao wadogo kama kundi,
Na watoto wao wa kiume wanaruka huku na huku.
14 Nao wanamwambia Mungu wa kweli, ‘Tuondokee!+
Nasi hatujaona upendezi wowote katika kuzijua njia zako.+
15 Mweza-Yote ana thamani gani, ndipo tumtumikie,+
Nasi tunajifaidi jinsi gani kwa kuwa tumewasiliana naye?’+
Ni mara ngapi yeye anagawanya maangamizi katika hasira yake?+
19 Mungu mwenyewe ataweka akiba ya madhara ya mtu kwa ajili ya wana wa mtu huyo;+
Atampa thawabu ili ajue hayo.+
21 Je, kupendezwa kwake kutakuwa nini katika nyumba yake baada yake,
Wakati hesabu ya miezi yake itakapokatwa mara mbili?+
23 Yeye mwenyewe atakufa wakati amejitosheleza kwa ukamili,+
Anapokuwa bila mahangaiko kabisa na akiwa amestarehe;
24 Wakati mapaja yake mwenyewe yamejaa mafuta
Na urojorojo wa mifupa yake unawekwa ukiwa na umajimaji.
29 Je, hamjawauliza wale wanaosafiri barabarani?
Na je, hamkagui kwa uangalifu ishara zao,
30 Kwamba katika siku ya msiba mwovu huachwa,+
Katika siku ya ghadhabu yeye hukombolewa?
31 Ni nani atakayemwambia juu ya njia yake usoni pake?+
Na ni nani atakayempa thawabu kwa ajili ya yale ambayo yeye mwenyewe amefanya?+
33 Kwake yeye madonge ya udongo wa bonde la mto hakika yatakuwa matamu,+
Naye atavuta wanadamu wote nyuma yake,+
Na wale waliokuwa mbele yake hawakuwa na hesabu.
34 Kwa hiyo ni kwa ubatili jinsi mnavyojaribu kunifariji,+
Na majibu yenu yanabaki kuwa ukosefu wa uaminifu!”
22 Naye Elifazi Mtemani akajibu, akasema:
2 “Je, mwanamume anaweza kuwa na faida kwa Mungu mwenyewe,+
Kwamba mtu mwenye ufahamu awe na faida kwake?
3 Je, Mweza-Yote anapendezwa kwa vyovyote kwa kuwa wewe ni mwadilifu,+
Au, kupata faida yoyote kwa kuwa wewe unafanya njia yako isiwe na lawama?+
6 Kwa maana wewe unanyakua rehani kutoka kwa ndugu zako bila sababu,+
Nawe unavua hata mavazi ya watu walio uchi.
10 Ndiyo sababu mitego ya ndege imekuzunguka pande zote,+
Na hofu ya ghafula inakutia wasiwasi;
11 Au giza, hivi kwamba huwezi kuona,
Na mkusanyo wa maji yanayosukasuka unakufunika.
13 Na bado umesema: ‘Kweli Mungu anajua nini?
Je, anaweza kuhukumu kupitia giza zito?
14 Mawingu ni mahali pake pa kujificha hivi kwamba haoni,
Naye hutembea huku na huku juu ya ngome ya mbingu.’
15 Je, utaendelea kuifuata njia ya zamani za kale
Ambayo watu wenye kudhuru wametembea,
16 Watu ambao wamenyakuliwa kabla ya wakati wao,+
Ambao msingi+ wao unamwagwa kama mto,
17 Ambao wanamwambia Mungu wa kweli: ‘Tuondokee!+
Na Mweza-Yote anaweza kutimiza nini juu yetu?’
20 ‘Kwa kweli wapinzani wetu wamefutiliwa mbali;
Na mabaki yao hakika moto utayateketeza.’
21 Tafadhali, fahamiana naye, na udumishe amani;
Hivyo mambo mema yatakujia.
23 Ukirudi kwa Mweza-Yote,+ utajengwa;
Ukiweka ukosefu wa uadilifu mbali na hema lako,
24 Na mawe ya madini yenye thamani yakiwekwa katika mavumbi
Na dhahabu ya Ofiri+ katika mwamba wa mabonde ya mito,
25 Pia Mweza-Yote kwelikweli atakuwa madini yako yenye thamani,
Na fedha, iliyo bora kabisa, kwako.+
26 Kwa maana ndipo utakapopata furaha tele katika Mweza-Yote,+
Nawe utamwinulia Mungu mwenyewe uso wako.+
28 Nawe utafanya uamuzi kuhusu jambo fulani, nalo litasimama kwako;
Na hakika nuru itaziangaza njia zako.+
29 Kwa maana lazima itakuwepo fedheha unaposema kwa kiburi;+
Lakini yeye atamwokoa mtu mwenye macho ya unyenyekevu.+
23 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Hata leo hangaiko+ langu ni uasi;
Mkono wangu wenyewe ni mzito kwa sababu ya kuugua kwangu.
4 Ningeleta mbele zake kesi ya hukumu,
Nami ningekijaza kinywa changu na hoja za kujibu;
5 Ningeyajua maneno anayonijibu,
Nami ningefikiria yale anayoniambia.+
7 Hapo mtu mnyoofu mwenyewe atanyoosha mambo pamoja na yeye,
Nami ningeenda nikiwa salama milele kutoka kwa mwamuzi wangu.
9 Kuelekea upande wa kushoto ambako anafanya kazi, lakini siwezi kumwona;
Anageuka kando upande wa kuume, lakini simwoni.
10 Kwa maana yeye anajua vema ile njia ninayoenda.+
Baada ya yeye kunijaribu, nitatoka nikiwa kama dhahabu.+
12 Siondoki katika amri ya midomo yake.+
Nimeyachukua kuwa hazina maneno ya kinywa chake+ kuliko yale niliyoamriwa.
13 Naye ana akili moja, na ni nani anayeweza kumpinga?+
Na nafsi yake mwenyewe ina tamaa, naye ataifanya.+
17 Kwa maana sikunyamazishwa kimya kwa sababu ya giza,
Wala kwa sababu weusi umeufunika uso wangu.
5 Tazama! kama punda-milia+ nyikani
Wameenda katika utendaji wao, kutafuta chakula.
Nchi tambarare ya jangwani inampa kila mmoja mkate kwa ajili ya wavulana.
6 Wanavuna chakula chake shambani,
Nao wanapora haraka shamba la mizabibu la mwovu.
8 Wanalowana maji kutokana na dhoruba ya mvua ya milimani,
Na kwa sababu hakuna mahali pa kujikinga+ wanalazimika kuukumbatia mwamba.
9 Wanamnyakua mvulana asiye na baba hata kutoka kwenye maziwa,+
Nao wanachukua kuwa rehani kile alicho nacho mwenye kuteseka.+
10 Wanalazimika kutembea uchi wakiwa bila vazi,
Nao wanalazimika kubeba masuke yaliyovunwa wakiwa na njaa.+
11 Wanashinda katikati ya mchana wakiwa kati ya ukuta wa matuta;
Wanalazimika kukanyaga mashinikizo ya divai, na bado wanakuwa na kiu.+
12 Kutoka katika jiji wanaokufa wanaendelea kuugua,
Na nafsi ya waliotiwa majeraha ya kufisha inalia ipewe msaada;+
Naye Mungu huona hilo kuwa si jambo lisilofaa.+
13 Kwa habari yao, wakawa katikati ya wale wanaoiasi nuru;+
Hawakuzitambua njia zake,
Wala hawakukaa katika barabara zake.
14 Muuaji anasimama wakati wa mchana,
Anamuua mwenye kuteseka na maskini;+
Na wakati wa usiku yeye huwa mwizi wa kawaida.+
15 Kwa habari ya jicho la mzinzi,+ limengojea giza la jioni,+
Likisema, ‘Hakuna jicho litakaloniona!’+
Naye hufunika uso wake.
16 Ametoboa shimo kuingia katika nyumba wakati wa giza;
Wakati wa mchana wanajifungia.
Hawajui nuru ya mchana.+
17 Kwa maana kwao asubuhi ni kama kivuli+ kizito,
Kwa maana wanazitambua hofu za ghafula za kivuli kizito.
18 Yeye ni mwepesi juu ya uso wa maji.
Mashamba yao yatalaaniwa duniani.+
Hatageuka kuelekea njia ya mashamba ya mizabibu.
20 Tumbo la uzazi litamsahau, funza atamnyonya kwa utamu,+
Yeye hatakumbukwa tena.+
Na ukosefu wa uadilifu utavunjwa kama mti.+
21 Anashughulika pamoja na mwanamke tasa ambaye hazai,
Na pamoja na mjane,+ ambaye yeye hamtendei wema wowote.
22 Naye hakika atawavuta watu wenye nguvu kwa uwezo wake;
Yeye atasimama asiwe na uhakika juu ya maisha yake.
24 Wamekuwa huko juu kwa muda kidogo, kisha hawako tena,+
Nao wameshushwa chini;+ wanang’olewa kama kila mtu mwingine,
Na kama suke la nafaka wanakatwa.
25 Basi kwa kweli sasa, ni nani atakayetoa uhakikisho kuwa mimi ni mwongo
Au kulifanya neno langu kuwa si kitu?”
25 Naye Bildadi+ Mshua akajibu, akasema:
2 “Utawala na hofu ziko kwake;+
Anafanya amani katika vilele vyake.
3 Je, majeshi yake yana hesabu?
Na ni juu ya nani nuru yake haiangazi?
4 Basi mwanadamu anayeweza kufa anawezaje kuwa upande wa haki mbele za Mungu,+
Au, mtu aliyezaliwa na mwanamke anawezaje kuwa safi?+
5 Tazama! Kuna hata mwezi, nao si mwangavu;
Nazo nyota zenyewe si safi machoni pake.
26 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Lo! Jinsi umekuwa msaada kwa mtu asiye na uwezo!
Lo! Jinsi umeokoa mkono usio na nguvu!+
4 Umemwambia nani maneno,
Na ni pumzi ya nani imetoka kwako?
7 Anaitandaza kaskazini juu ya mahali pasipo na kitu,+
Akiitundika dunia pasipo na kitu;
8 Anafunga maji katika mawingu yake,+
Hivi kwamba wingu kubwa halipasuki chini yayo;
9 Anaufunika uso wa kiti cha ufalme,
Anatandaza juu yake wingu lake.+
11 Nguzo za mbingu hutikisika,
Nazo hushangaa kwa sababu ya kemeo lake.
12 Kwa uwezo wake ameichochea bahari,+
Naye kwa uelewaji wake amemvunja vipande-vipande+ yule mshambuliaji.+
14 Tazama! Hizo ndizo kingo za njia zake,+
Nao ni mnong’ono ulioje wa jambo lililosikiwa juu yake!
Lakini kuhusu mngurumo wake wenye nguvu ni nani anayeweza kuonyesha uelewaji?”+
27 Naye Ayubu akatokeza tena neno lake la kimethali,+ akaendelea kusema:
2 “Kama Mungu anavyoishi,+ ambaye ameiondoa hukumu yangu,+
Na kama Mweza-Yote anavyoishi, ambaye ameitia uchungu nafsi yangu,+
3 Pumzi yangu ikiwa bado ni nzima ndani yangu,
Na roho ya Mungu imo ndani ya mianzi ya pua yangu,+
4 Midomo yangu haitasema ukosefu wa uadilifu
Wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu!
5 Ni jambo lisilowaziwa kwangu kwamba niwatangaze ninyi kuwa waadilifu!+
Mpaka nitakapokata pumzi, sitajiondolea utimilifu+ wangu!
6 Nimeishikilia haki yangu, nami sitaiachilia;+
Moyo wangu hautanidhihaki kwa ajili ya yoyote ya siku zangu.+
8 Kwa maana ni nini tumaini la mwasi-imani iwapo anamkatilia mbali,+
Iwapo Mungu anachukua nafsi yake kutoka kwake?+
10 Au, je, atapata furaha tele katika Mweza-Yote?
Je, atamwita Mungu nyakati zote?
13 Hilo ndilo fungu la mtu mwovu kutoka kwa Mungu;+
Na urithi wa waonevu watapokea kutoka kwa Mweza-Yote mwenyewe.
14 Wanawe wakiwa wengi, ni kwa ajili ya upanga;+
Na wazao wake wenyewe hawatakuwa na chakula cha kutosha.
15 Waokokaji wake mwenyewe watazikwa wakati wa tauni yenye kufisha,
Na wajane wao wenyewe hawatalia.+
16 Akirundika fedha kama mavumbi,
Naye akitayarisha mavazi kana kwamba ni udongo,
17 Yeye atatayarisha, lakini mwadilifu ndiye atakayevaa,+
Na yeye asiye na hatia ndiye atakayekuwa na fungu katika ile fedha.
19 Atalala akiwa tajiri, lakini hakuna chochote kitakachokusanywa;
Ameyafungua macho yake, lakini hakutakuwa na chochote.+
21 Upepo wa mashariki utamchukulia mbali+ naye ataenda zake,
Nao utamvurumisha mbali kutoka mahali pake.+
4 Amechimba shimo mbali sana na mahali ambapo watu hukaa ugenini,+
Mahali paliposahauliwa, mbali na mguu;
Baadhi ya wanadamu wanaoweza kufa wameshuka chini, wamening’inia.
5 Kwa habari ya dunia, chakula hutoka humo;+
Lakini chini yake, imepinduliwa kana kwamba ni kwa moto.
8 Wanyama wa mwituni wenye fahari hawajaikanyaga ikawa ngumu;
Mwana-simba hakutembea juu yake.
9 Ametia mkono wake juu ya jiwe gumu;
Ameipindua milima kutoka katika mizizi yake;
10 Amechimba ndani ya miamba mifereji iliyojaa maji,+
Na jicho lake limeona vitu vyote vyenye thamani.
16 Haiwezi kulipiwa kwa dhahabu ya Ofiri,+
Wala kwa jiwe la shohamu lisilopatikana kwa urahisi wala yakuti.
17 Dhahabu na kioo haviwezi kulinganishwa nayo,
Wala chombo chochote cha dhahabu safi hakiwezi kubadilishwa nayo.
18 Marijani+ na fuwele ya mawe havitatajwa,
Bali mfuko uliojaa hekima ni wenye thamani kuliko ule uliojaa lulu.+
21 Imefichwa kutoka machoni pa kila mtu aliye hai,+
Nayo imefichwa kutoka kwa viumbe vinavyoruka vya mbinguni.
22 Maangamizi na kifo zimesema,
‘Tumesikia habari zake kwa masikio yetu.’
23 Mungu, Yeye ndiye ameelewa njia yake,+
Naye mwenyewe amejua mahali pake,
24 Kwa maana yeye anatazama mpaka miisho ya dunia;+
Anaona chini ya mbingu zote,
Naye ameyapima maji kwa kipimo;+
26 Alipofanyiza sharti kwa ajili ya mvua,+
Na njia kwa ajili ya wingu la dhoruba lenye kunguruma,
27 Ndipo alipoiona hekima kisha akasema habari zake;
Aliitayarisha na pia akaichunguza kabisa.
28 Naye akamwambia mwanadamu,
‘Tazama! Kumwogopa Yehova—hiyo ndiyo hekima,+
Na kuacha ubaya ni uelewaji.’”+
29 Naye Ayubu akatokeza tena neno lake la kimethali, akaendelea kusema:
2 “Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa katika miezi ya zamani,+
Kama katika siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda;+
4 Kama nilivyokuwa katika siku zilizo bora za ujana wangu,+
Wakati urafiki wa karibu pamoja na Mungu ulikuwa katika hema langu;+
5 Wakati Mweza-Yote alipokuwa bado pamoja nami,
Wakati watumishi wangu walipokuwa wamenizunguka pande zote!
7 Nilipoenda kwenye lango lililo karibu na mji,+
Nilikuwa nikitayarisha kiti changu katika kiwanja cha watu wote!+
11 Kwa maana sikio lilisikiliza, likanitangaza kuwa mwenye furaha,
Nalo jicho liliona, likanishuhudia.
12 Kwa maana nilikuwa nikimwokoa mwenye kuteseka anayelia apewe msaada,+
Na mvulana asiye na baba na mtu yeyote ambaye hakuwa na msaidizi.+
13 Baraka+ ya mtu aliye karibu kuangamia—ilikuwa ikija juu yangu,
Na moyo wa mjane nilikuwa nikiufurahisha.+
14 Nilivaa uadilifu, nao ulikuwa ukinivika.+
Haki yangu ilikuwa kama koti lisilo na mikono—na kilemba.
17 Nami nilikuwa nikiivunja mifupa ya taya ya mkosaji,+
Na kutoka katika meno yake nikawa nikinyakua mawindo.
18 Na nilikuwa nikisema, ‘Nitakata pumzi+ ndani ya kiota changu,
Nami nitazidisha siku zangu kama chembe za mchanga.+
20 Utukufu wangu ni mpya kwangu,
Na upinde wangu mkononi mwangu utapiga tena na tena.’
23 Nao waliningojea kama kungojea mvua,+
Nao wakakifungua wazi kinywa chao kwa ajili ya mvua ya masika.+
25 Nilikuwa nikiwachagulia njia, nami nilikuwa nikikaa kama kichwa;
Nami nilikaa kama mfalme katikati ya majeshi yake,+
Kama mtu anayewafariji waombolezaji.+
Wale wenye siku chache kuliko mimi,+
Ambao baba zao ningekataa
Kuwaweka pamoja na mbwa wa kundi langu.
3 Wao ni tasa kwa sababu ya upungufu na njaa,
Wanatafuna eneo lisilo na maji,+
Ambapo jana palikuwa na dhoruba na ukiwa.
4 Walikuwa waking’oa mmea wa chumvi kando ya vichaka,
Na mzizi wa miretemu ulikuwa chakula chao.
6 Wanalazimika kukaa kwenye mteremko wa mabonde ya mito,
Katika matundu ya mavumbi na katika miamba.
7 Walilia katikati ya vichaka;
Walisongamana pamoja chini ya upupu.
11 Kwa kuwa aliifungua kamba yangu ya upinde na kuninyenyekeza,
Nao waliifungua lijamu kwa sababu yangu.
12 Wanasimama upande wa mkono wangu wa kuume kama kundi la waovu;
Wameachilia miguu yangu,
Lakini wakajenga juu yangu vizuizi vyao vyenye kuleta msiba.+
14 Walikuja kana kwamba ni kupitia pengo pana;
Wamejiviringisha katika dhoruba.
15 Vitisho vya ghafula vimegeuzwa juu yangu;
Cheo changu cha heshima kinafukuzwa kama upepo,
Na wokovu wangu umepitilia mbali kama wingu.
17 Mifupa+ yangu imetobolewa usiku na kuanguka kutoka kwangu,
Na maumivu yanayonitafuna hayapumziki.+
18 Vazi langu linabadilika kutokana na wingi wa nguvu;
Linanifunga kama ukosi wa vazi langu refu.
19 Amenishusha chini katika udongo,
Hivi kwamba nimekuwa kama mavumbi na majivu.
22 Unaniinua kwenye upepo, unanifanya niupande;
Kisha unaniyeyusha kwa kishindo.
23 Kwa maana najua vema kwamba utanirudisha kwenye kifo,+
Na kwenye nyumba ya kukutania ya kila mtu aliye hai.
24 Ila tu hakuna yeyote anayeunyoosha mkono wake juu ya rundo la mabomoko matupu,+
Wala wakati wa kudhoofika kwa mtu hakuna kilio cha kuomba msaada kuhusu mambo hayo.
27 Matumbo yangu yalichemshwa wala hayakukaa kimya;
Siku za mateso zilinikabili.
28 Nilitembea huku na huku kwa huzuni+ wakati ambapo hakukuwa nuru ya jua;
Nilisimama katika kutaniko, nikaendelea kulia nipewe msaada.
30 Ngozi yangu ikawa nyeusi+ na kuanguka kutoka kwangu,
Na mifupa yangu ikawaka moto kutokana na ukavu.
31 Na kinubi changu kikawa cha maombolezo matupu,
Na zumari yangu kwa ajili ya sauti ya watu wanaolia.
7 Ikiwa hatua zangu zinageuka kutoka katika njia,+
Au moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu tu,+
Au kasoro yoyote imeshikamana na mikono yangu,+
9 Ikiwa moyo wangu umeshawishiwa kumwelekea mwanamke,+
Nami nikaendelea kuvizia+ katika mlango wa rafiki yangu,
10 Basi mke wangu na amsagie mwanamume mwingine,
Wanaume wengine na wainame juu yake.+
12 Kwa maana huo ni moto ambao ungeteketeza mpaka kwenye maangamizi,+
Na katikati ya mazao yangu yote ungetia mizizi.
13 Ikiwa nilikuwa nikikataa hukumu ya haki ya mtumwa wangu
Au ya kijakazi wangu katika kesi yao juu yangu,
14 Basi naweza kufanya nini wakati Mungu atakaposimama?
Na wakati atakapotoza hesabu, naweza kumjibu nini?+
15 Je, Yeye aliyenifanya mimi tumboni hakumfanya yeye,+
Na je, si yeye Mmoja tu aliyetufanya sisi katika tumbo la uzazi?
16 Ikiwa nilikuwa nikiwanyima watu wa hali ya chini mapendezi yao,+
Na kuyafanya macho ya mjane yaishiwe nguvu,+
18 (Kwa maana tangu ujana wangu alikua pamoja nami kana kwamba pamoja na baba,
Na kutoka tumboni mwa mama yangu niliendelea kumwongoza huyo mjane);
19 Ikiwa nilikuwa nikiona mtu yeyote akiangamia kwa kukosa vazi,+
Au kwamba maskini hakuwa na cha kujifunika;
20 Ikiwa viuno vyake havikunibariki,+
Wala hakujipasha moto kwa sufu+ iliyokatwa ya wana-kondoo wangu;
21 Ikiwa nilitikisa mkono wangu huku na huku juu ya mvulana asiye na baba,+
Wakati nilipokuwa nikiona msaada wangu unahitajiwa katika lango,+
22 Acha mfupa wa bega langu uanguke kutoka katika bega lake,
Na acha mkono wangu uvunjwe kutoka kwenye mfupa wake wa juu.
25 Ikiwa nilikuwa nikishangilia kwa sababu mali yangu ilikuwa nyingi,+
Na kwa sababu mkono wangu ulikuwa umepata vitu vingi sana;+
27 Na moyo wangu ukaanza kushawishiwa kisiri+
Na mkono wangu ukakibusu kinywa changu,
28 Hilo pia lingekuwa kosa la kufikiriwa na waamuzi,
Kwa maana ningekuwa nimemkana Mungu wa kweli aliye juu.
29 Ikiwa nilikuwa nikishangilia kuangamia kwa mtu anayenichukia vikali,+
Au kuchangamka kwa sababu uovu umempata—
31 Ikiwa watu wa hema langu hawakusema,
‘Ni nani anayeweza kutokeza mtu ambaye hakushibishwa na chakula chake?’+—
33 Ikiwa kama mtu wa udongo niliyafunika makosa yangu+
Kwa kuficha kosa langu katika mfuko wa shati langu—
34 Kwa kuwa nilikuwa nikishtuka kwa sababu ya umati mkubwa,
Au dharau la familia lilikuwa likinitia hofu
Nami nilikuwa nikikaa kimya, sikuwa nikiondoka nje ya mlango.
35 Laiti ningekuwa na mtu wa kunisikiliza,+
Kwamba Mweza-Yote angenijibu+ kulingana na sahihi yangu!
Au kwamba mtu aliye na kesi juu yangu angeandika hati!
36 Hakika ningeibeba juu ya bega langu;
Ningeifunga kunizunguka kama taji la fahari.
38 Ikiwa nchi yangu ingelia kwa sababu yangu ipate msaada,
Na mitaro yake ingelia pamoja;
39 Ikiwa nimekula matunda yake bila pesa,+
Na nafsi ya wamiliki wake nimeifanya ipumue,+
40 Basi magugu yenye miiba na yatokee badala ya ngano,+
Na magugu yenye kunuka badala ya shayiri.”
Maneno ya Ayubu yamefika mwisho.
32 Basi hao watu watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa sababu alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.+ 2 Lakini hasira ya Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi,+ wa familia ya Ramu, ikawaka. Hasira yake ikamwakia Ayubu kwa sababu aliitangaza nafsi yake mwenyewe kuwa adilifu badala ya Mungu.+ 3 Pia, hasira yake ikawaka juu ya wale rafiki zake watatu kwa sababu hawakupata jibu bali walimtangaza Mungu kuwa mwovu.+ 4 Naye Elihu alikuwa amemngojea Ayubu kwa maneno, kwa sababu walikuwa wazee kwa siku kuliko yeye.+ 5 Na mwishowe Elihu akaona kwamba hakuna jibu kinywani+ mwa wale watu watatu, na hasira yake ikazidi kuwaka. 6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi, akajibu, akasema:
“Mimi ni kijana katika siku
Nanyi ni wazee.+
Ndiyo sababu nilikaa mbali nikaogopa
Kuwatangazia ninyi ujuzi wangu.
8 Hakika ni roho iliyo ndani ya wanadamu wanaoweza kufa
Na pumzi ya Mweza-Yote ndiyo inayowapa wao uelewaji.+
9 Si wale walio na siku nyingi tu ndio huwa na hekima,+
Wala si wale walio wazee tu ndio huelewa hukumu.+
10 Kwa hiyo nikasema, ‘Nisikilize mimi.
Nami, naam, mimi nitautangaza ujuzi wangu.’
11 Tazama! Nimeyangojea maneno yenu,
Niliendelea kutega sikio kwa namna yenu ya kufikiri,+
Mpaka mweze kutafuta maneno ya kusema.
12 Nami nikaendelea kuwakazia ninyi fikira,
Na tazama, hakuna yeyote anayemkaripia Ayubu,
Hakuna yeyote kati yenu anayejibu maneno yake,
13 Kwa hiyo msiseme, ‘Tumepata hekima;+
Ni Mungu anayemfukuzia mbali, wala si mwanadamu.’
14 Kwa kuwa hajapanga maneno juu yangu,
Kwa hiyo sitamjibu yeye kwa maneno yenu.
15 Wametishika, hawakujibu tena;
Maneno yamewaondoka.
16 Nami nimengojea, kwa maana hawaendelei kusema;
Kwa maana walisimama tuli, hawakujibu tena.
17 Nami, naam, mimi nitajibu sehemu yangu;
Nami, naam, mimi nitautangaza ujuzi wangu;
18 Kwa maana nimejaa maneno;
Roho imeleta mkazo+ juu yangu ndani ya tumbo langu.
22 Kwa maana hakika sijui jinsi ninavyoweza kutoa jina la cheo;
Mtengenezaji+ wangu angenichukulia mbali kwa urahisi.
33 “Hata hivyo, sasa, Ee Ayubu, tafadhali sikia maneno yangu,
Nawe tega sikio kwa maneno yangu yote.
2 Tafadhali, tazama! Lazima nifungue kinywa changu;
Ulimi wangu pamoja na kaakaa+ langu lazima viseme.
5 Ukiweza, nijibu,
Yapange maneno mbele yangu; usimame mahali pako.
7 Tazama! Hofu yoyote kutoka kwangu haitakutisha,
Wala mkazo+ kutoka kwangu hautakuwa mzito juu yako.
8 Ila tu umesema masikioni mwangu,
Nami nikaendelea kusikia sauti ya maneno yako,
Mimi ni safi, wala sina kosa.+
12 Tazama! Katika hayo hukuwa upande wa haki,+ ninakujibu;
Kwa maana Mungu anamzidi mwanadamu anayeweza kufa.+
15 Katika ndoto,+ maono+ ya usiku,
Wakati usingizi mzito unapowashika wanadamu,
Wakati wa kusinzia kitandani.+
16 Ndipo anapofungua sikio la wanadamu,+
Naye hutia muhuri wake kwa kuwasihi wao,
17 Ili kumgeuza mwanadamu kutoka katika tendo lake,+
Na ili afunike kiburi+ kutoka kwa mwanamume.
19 Naye kwa kweli hukaripiwa kwa maumivu kitandani mwake,
Na kugombana kwa mifupa yake huendelea mfululizo.
21 Nyama yake hukonda ikaacha kuonekana,
Na mifupa yake ambayo haikuonekana hakika hutokeza.
23 Ikiwa kuna mjumbe kwa ajili yake,
Msemaji, mmoja kati ya elfu,
Ili kumwambia mwanadamu unyoofu wake,
24 Ndipo anapompa kibali na kusema,
‘Mwachilie ili asishuke chini kuingia shimoni!+
Nimepata fidia!+
26 Yeye atamsihi Mungu ili amfurahie,
Naye ataona uso wake kwa kupaaza sauti kwa shangwe,+
Na Yeye ataurudisha uadilifu Wake kwa mwanadamu anayeweza kufa.
27 Yeye atawaimbia wanadamu na kusema,
‘Nimetenda dhambi;+ na nimepotosha lililo nyoofu,
Nalo hakika halikuwa jambo linalofaa kwangu.
29 Tazama! Mungu hufanya mambo hayo yote,
Mara mbili, mara tatu, kuhusiana na mwanamume,
30 Ili kuigeuza nafsi yake isiingie shimoni,+
Ili atiwe nuru kwa nuru ya wale walio hai.+
31 Kaza uangalifu, Ee Ayubu! Nisikilize mimi!
Nyamaza kimya, nami nitaendelea kusema.
32 Ikiwa kuna maneno yoyote ya kusema, nijibu;
Sema, kwa maana nimependezwa na uadilifu wako.
33 Ikiwa hakuna yoyote, basi wewe mwenyewe nisikilize mimi;+
Nyamaza kimya, nami nitakufundisha hekima.”
34 Naye Elihu akaendelea kujibu, akasema:
2 “Sikilizeni maneno yangu, enyi wenye hekima;
Nanyi mnaojua, nitegeeni sikio.
4 Acheni tujichagulie hukumu;
Acheni tujue yaliyo mema katikati yetu.
6 Je, mimi nasema uwongo juu ya hukumu yangu mwenyewe?
Jeraha langu kali haliponi ingawa hakuna kosa.’+
10 Kwa hiyo nisikilizeni mimi, ninyi watu walio na moyo wenye kufahamu.+
Hasha, Mungu wa kweli asitende kwa uovu,+
Na Mweza-Yote kutenda isivyo haki!+
11 Kwa maana yeye atamlipa+ mtu wa udongo kulingana na matendo yake,
Na kulingana na pito la mwanadamu yeye ataifanya ije juu yake.
13 Ni nani aliyemgawia dunia,
Na ni nani aliyemwekea nchi yenye kuzaa, hiyo yote?
16 Basi ikiwa una uelewaji, sikiliza mambo haya;
Tega sikio kwa sauti ya maneno yangu.
17 Kwa kweli, je, mtu yeyote anayechukia haki ataongoza,+
Na ikiwa mwenye nguvu ni mwadilifu, je, utamtangaza yeye kuwa mwovu?+
19 Yupo Yeye ambaye hajaonyesha upendeleo kwa wakuu
Wala hakumwonyesha mwenye cheo ufikirio kuliko yule wa hali ya chini,+
Kwa maana wao wote ni kazi ya mikono yake.+
20 Wanakufa ghafula,+ katikati ya usiku;+
Watu huyumba-yumba na kupitilia mbali,
Na wenye nguvu huondolewa pasipo mkono wa mtu.+
23 Kwa maana haweki wakati wowote kwa ajili ya mwanadamu yeyote
Aende kwa Mungu hukumuni.
28 Ili kukifanya kilio cha mtu wa hali ya chini kimfikie;
Na hivyo yeye hukisikia kilio cha watu wanaoteseka.+
29 Yeye mwenyewe anaposababisha utulivu, ni nani, basi, anayeweza kulaumu?
Na anapoficha uso wake,+ ni nani anayeweza kumwona,
Iwe ni kuelekea taifa+ au ni kuelekea mwanadamu, yote yakiwa ni mamoja?
31 Kwa maana, je, yeyote atamwambia Mungu mwenyewe,
‘Mimi nimevumilia, ijapokuwa sitendi kwa ufisadi;+
32 Ijapokuwa sioni lolote, nifundishe wewe mwenyewe;
Ikiwa nimetenda ukosefu wowote wa uadilifu,
Sitautenda tena’?+
33 Je, yeye atalilipia kama unavyopenda kwa sababu unakataa hukumu,
Kwa sababu wewe mwenyewe unachagua, wala si mimi?
Unalolijua vema, liseme.
34 Watu wenye moyo wa kuelewa+ wataniambia—
Hata mwanamume mwenye hekima anayenisikiliza,
35 ‘Ayubu mwenyewe anasema bila ujuzi,+
Na katika maneno yake hana ufahamu.’
37 Kwa maana anaongeza maasi juu ya dhambi yake;+
Anapiga makofi katikati yetu na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu wa kweli!”+
35 Naye Elihu akaendelea kujibu, akasema:
6 Kwa kweli ukitenda dhambi, ni nini unachotimiza dhidi yake?+
Na maasi yako kwa kweli yakiongezeka, unamtendea nini?
9 Kwa sababu ya ukandamizaji mwingi wanaendelea kuomba msaada;+
Wanaendelea kulia wapewe msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.+
10 Na ingawa hivyo hakuna yeyote ambaye amesema, ‘Yuko wapi Mungu, Mtengenezaji Mkuu wangu,+
Yeye anayetoa muziki wakati wa usiku?’+
11 Ni Yeye anayetufundisha+ sisi kuliko wanyama wa dunia,+
Naye anatufanya tuwe na hekima kuliko hata viumbe vinavyoruka vya mbinguni.
14 Sembuse basi unaposema kwamba humwoni!+
Kesi iko mbele zake, na kwa hiyo unapaswa umngojee kwa hangaiko.+
15 Na sasa kwa sababu hasira yake haijatoza hesabu,+
Yeye pia hakufuatilia kule kuchukua hatua kwa haraka inayopita kiasi.+
36 Naye Elihu akaendelea kusema:
2 “Nisubiri kidogo, nami nitakutangazia
Kwamba bado kuna maneno ya kusema kwa ajili ya Mungu.
5 Tazama! Mungu ni mwenye nguvu+ wala hatakataa;
Yeye ana uwezo wa nguvu za moyo;
6 Hatamhifadhi hai mtu yeyote aliye mwovu,+
Lakini atatoa hukumu ya wenye kuteseka.+
Yeye pia atawaketisha milele, nao watainuliwa.
9 Ndipo atawaambia kuhusu jinsi wanavyotenda
Na makosa yao, kwa sababu wanajivuna sana.
13 Na wale walio waasi-imani moyoni wataweka hasira.+
Hawapaswi kulia wapewe msaada kwa sababu amewafunga.
15 Atamwokoa mwenye kuteseka katika mateso yake,
Naye atafungua sikio lao katika ukandamizaji huo.
16 Naye hakika pia atakushawishi kutoka katika kinywa cha taabu!+
Mahali penye nafasi,+ wala si penye kufinyana, patakuwa badala yake,
Na faraja ya meza yako itajaa unono.+
18 Ili uwe mwangalifu kwamba ghadhabu+ isikushawishi upige makofi ya chuki,
Wala usiache fidia+ kubwa ikupotoshe.
19 Je, kilio chako cha kuomba msaada kitakuwa na matokeo?+ Hapana, wala katika taabu
Hata jitihada zako zote zenye nguvu.+
20 Usipumue kwa kutamani usiku,
Wakati watu wanaporudi kutoka mahali walipo.
22 Tazama! kwa nguvu zake, Mungu mwenyewe hutenda kwa njia iliyoinuliwa;
Ni nani aliye mfundishaji kama yeye?
23 Ni nani amemtaka atoe hesabu juu ya njia yake,+
Na ni nani amesema, ‘Wewe umetenda ukosefu wa uadilifu’?+
27 Kwa maana yeye huyateka matone ya maji;+
Yanajichuja kama mvua yawe ukungu wake,
28 Hivi kwamba mawingu yanadondoka,+
Yanadondoka kwa wingi juu ya wanadamu.
4 Nyuma yake sauti huvuma;
Yeye ananguruma+ kwa sauti ya ukuu wake,+
Naye hazizuii wakati sauti yake inaposikiwa.+
6 Kwa maana yeye anaiambia theluji, ‘Anguka kuelekea duniani,’+
Na pia mvua kubwa, ndiyo, mvua zake kubwa zenye nguvu.+
7 Anaweka muhuri juu ya mkono wa kila mtu wa udongo
Ili kila mwanadamu anayeweza kufa ajue kazi yake.
11 Ndiyo, yeye hubebesha wingu mzigo wa umajimaji,
Nuru+ yake hutawanya wingu kubwa,
12 Nalo linageuzwa huku na huku kwa uongozi wake ili yatende
Popote anapoyaamuru+ juu ya uso wa nchi yenye kuzaa ya dunia.
13 Iwe ni kwa fimbo+ au ni kwa nchi yake+
Au ni kwa fadhili zenye upendo,+ hulifanya liwe na matokeo.
19 Tujulishe yale tunayopaswa kumwambia;
Hatuwezi kutokeza maneno kwa sababu ya giza.
20 Je, yeye ajulishwe kwamba nataka kusema?
Au, je, mtu yeyote amesema kwamba jambo hilo lijulishwe?+
24 Kwa hiyo wanadamu na wamwogope.+
Yeye hawaangalii wowote walio na hekima katika moyo wao wenyewe.”+
38 Naye Yehova akaanza kumjibu Ayubu kutoka katika dhoruba ya upepo,+ akasema:
2 “Ni nani huyu anayefunika shauri
Kwa maneno yasiyo na ujuzi?+
5 Ni nani aliyeweka vipimo vyake, ikiwa unajua,
Au ni nani aliyenyoosha juu yake kamba ya kupimia?
6 Vikalio+ vyake vimeingizwa ndani ya nini,
Au ni nani aliyeweka jiwe lake la pembeni,
7 Nyota za asubuhi+ zilipopiga vigelegele pamoja kwa shangwe,
Na wana wote wa Mungu+ wakaanza kupaaza sauti kwa kushangilia?
8 Na ni nani aliyeizuia bahari kwa milango,+
Iliyoanza kwenda kama katika wakati ilipotoka katika tumbo la uzazi;
9 Nilipoliweka wingu liwe vazi lake
Na giza zito liwe utepe wake wa kufungia,
10 Nami nikaweka sharti langu juu yake
Na kuweka pingo na milango,+
11 Nami nikasema, ‘Unaweza kufika hapa, na usipite;+
Na hapa mawimbi yako yenye fahari yamewekewa mpaka’?+
12 Je, uliiamuru asubuhi+ tangu siku zako na kuendelea?
Je, uliyajulisha mapambazuko mahali pake,
13 Yapate kushika miisho ya dunia,
Ili waovu wakung’utwe kutoka ndani yake?+
16 Je, umeingia katika chemchemi za bahari,
Au, je, umetembea huku na huku+ ukitafuta kilindi cha maji?+
19 Basi sasa, iko wapi njia inayoenda mahali ambapo nuru hukaa?+
Sasa nalo giza, mahali pake ni wapi,
20 Ili ulipeleke kwenye mpaka wake
Na ili uzielewe barabara zinazoenda katika nyumba yake?
21 Je, umepata kujua kwa sababu wakati huo ulikuwa ukizaliwa,+
Na kwa sababu hesabu ya siku zako ni nyingi?
24 Basi sasa, iko wapi njia ambayo katika hiyo nuru hujigawanya,
Na ambayo upepo wa mashariki+ hutawanyika huku na huku juu ya dunia?
25 Ni nani ameugawanya mfereji kwa ajili ya mafuriko
Na njia kwa ajili ya wingu la dhoruba lenye kunguruma,+
26 Ili kulifanya linyeshe juu ya nchi isiyokuwa na mwanadamu,+
Juu ya nyika isiyokuwa na mtu wa udongo,
27 Ili kushibisha maeneo yenye kupigwa na dhoruba na yenye ukiwa
Na kusababisha majani kuchipuka?+
31 Je, unaweza kufunga vifungo vya kundi-nyota la Kima,
Au, je, unaweza kufungua kamba za kundi-nyota la Kesili?+
32 Je, unaweza kuleta kundi-nyota la Mazarothi katika wakati wake uliowekwa?
Na kwa habari ya kundi-nyota la Ashi, je, unaweza kuliongoza pamoja na wanawe?
35 Je, unaweza kuutuma umeme ili uende
Na kukuambia, ‘Sisi tupo hapa!’?
36 Ni nani aliyetia hekima+ katika tabaka za mawingu,
Au ni nani aliyeyapa uelewaji+ maajabu ya angani?
37 Ni nani anayeweza kuhesabu kwa ukamili mawingu kwa hekima,
Au mitungi ya maji ya mbingu—ni nani anayeweza kuipindua,+
38 Wakati mavumbi yanapomwagika kana kwamba ni fungu lililoyeyushwa,
Na madonge ya udongo kushikamana?
41 Ni nani anayemtayarishia kunguru chakula chake+
Wakati watoto wake wanapomlilia Mungu wapate msaada,
Wanapoendelea kutanga-tanga kwa sababu hakuna chakula chochote?
39 “Je, umepata kujua wakati uliowekwa wa mbuzi wa milimani kuzaa?+
Je, unaangalia wakati ule paa wanapozaa+ kwa uchungu?
2 Je, wewe huhesabu miezi ambayo wao hutimiza,
Au, je, umepata kujua wakati uliowekwa ambapo wao huzaa?
3 Wao huinama wanapotoa watoto wao,
Wanapoondoa uchungu wao.
4 Wana wao huwa wenye nguvu, huwa wakubwa porini;
Kwa kweli wao huenda zao wala hawarudi kwao.
5 Ni nani aliyemwachilia punda-milia+ awe huru,
Na ni nani aliyevifungua vifungo vya punda-mwitu,
6 Ambao nimeweka nchi tambarare ya jangwa kuwa nyumba yao
Na ambao makao yao ni nchi ya chumvi?+
10 Je, utamfunga imara ng’ombe-mwitu kwa kamba zake katika mtaro,
Au, je, yeye atalima+ nchi tambarare za chini nyuma yako?
11 Je, utamtegemea kwa kuwa ana nguvu nyingi,
Na, je, utamwachia yeye kazi yako ngumu?
12 Je, utamtegemea kwamba atarudisha mbegu zako
Na kwamba atakusanya kwenye uwanja wako wa kupuria?
14 Kwa maana yeye huyaacha mayai yake katika nchi
Naye huyatia joto katika mavumbi,
15 Naye husahau kwamba mguu fulani unaweza kuyavunja
Au hata mnyama wa mwituni anaweza kuyakanyaga.
16 Yeye huwatendea wanawe kwa ukali, kana kwamba si wake+—
Kazi yake ngumu ni ya ubatili kwa sababu yeye hana hofu.
18 Wakati anapopiga-piga mabawa yake juu,
Yeye humcheka farasi na mpandaji wake.
21 Yeye huparapara+ katika nchi tambarare ya chini na kufurahia nguvu;
Husonga mbele kukutana na silaha.+
23 Podo hupiga kelele juu yake,
Kichwa cha mkuki na pia fumo.
24 Yeye huimeza nchi kwa mwendo wa kishindo na msisimuko,
Wala haamini kwamba ni sauti ya baragumu.
25 Mara tu baragumu inapopiga yeye husema Aha!
Naye hunusa harufu ya pigano kutoka mbali sana,
Mshindo wa wakuu na kelele za vita.+
26 Je, ni kwa sababu ya uelewaji wako kwamba kipanga hupaa juu,
Kwamba yeye hunyoosha mabawa yake kuuelekea upepo wa kusini?
27 Au, je, ni kwa agizo lako kwamba tai+ huruka kuelekea juu
Na kwamba hujenga kiota chake huko juu,+
28 Kwamba yeye hukaa kwenye mwamba na wakati wa usiku hukaa
Juu ya ncha ya mwamba na mahali pasipoweza kufikiwa?
40 Naye Yehova akaendelea kumjibu Ayubu, akasema:
2 “Je, inampasa mtu anayetafuta makosa kushindana na Mweza-Yote?+
Mwenye kumkaripia Mungu na ajibu hayo yeye mwenyewe.”+
3 Naye Ayubu akamjibu Yehova, akasema:
4 “Tazama! Nimekuwa kitu kisicho na maana.+
Nitakujibu nini?
Nimeuweka mkono wangu juu ya kinywa changu.+
5 Nimesema mara moja, nami sitajibu;
Na mara mbili, nami sitaongeza lolote.”
6 Na Yehova akaendelea kumjibu Ayubu kutoka katika ile dhoruba ya upepo,+ akasema:
7 “Tafadhali, jifunge viuno vyako, kama mwanamume;+
Nitakuuliza maswali, nawe unijulishe.+
8 Kwa kweli, je, utaifanya haki yangu kuwa bure?
Je, utanitangaza mimi kuwa mwovu ili wewe uwe upande wa haki?+
9 Au, je, una mkono kama ule wa Mungu wa kweli,+
Na, je, unaweza kutoa mngurumo kwa sauti kama yake?+
13 Wafiche pamoja katika mavumbi,+
Funga nyuso zao katika mahali palipofichika,
14 Nami, naam, mimi nitakupongeza,
Kwa sababu mkono wako wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Tazama, sasa, Behemothi* ambaye nimemfanya na wewe pia.
Yeye hula majani+ kama ng’ombe.
16 Tazama, basi, nguvu zake zimo katika viuno vyake,
Na nishati+ zake zimo katika kano za tumbo lake.
17 Yeye huinamisha mkia wake kama mwerezi;
Kano za mapaja yake zimeungamana pamoja.
18 Mifupa yake ni mianzi ya shaba;
Mifupa yake yenye nguvu ni kama fimbo za chuma iliyofuliwa.
21 Yeye hulala chini ya miyungiyungi yenye miiba,
Katika mahali palipofichika penye matete+ na mahali penye majimaji.+
22 Miyungiyungi yenye miiba humzuia kwa kivuli chake;
Mierebi ya bonde la mto humzunguka.
23 Mto ukitenda kwa jeuri, yeye hakimbii kwa wasiwasi.
Ana uhakika, hata Yordani+ ukifurika juu ya kinywa chake.
24 Je, yeyote anaweza kumshika akiwa anaona?
Je, yeyote anaweza kuitoboa pua yake kwa mitego?
3 Je, atakusihi wewe sana,
Au, je, atakuambia maneno ya upole?
4 Je, atafanya agano pamoja nawe,
Ili umfanye kuwa mtumwa mpaka wakati usio na kipimo?
5 Je, utamchezea kama ndege,
Au, je, utamfunga kwa ajili ya wasichana wako wadogo?
6 Je, rafiki watafanya biashara juu yake?
Je, watamgawanya yeye katikati ya wafanya-biashara?
8 Tia mkono wako juu yake.
Kumbuka pigano hilo. Usifanye hivyo tena.
9 Tazama! Matarajio ya mtu kumhusu hakika yatakatishwa tamaa.
Mtu pia ataangushwa chini kwa kule kumwona tu.
11 Ni nani ambaye amenipa kitu kwanza, ndipo nilazimike kumpa thawabu?+
Vitu vyote ni vyangu chini ya mbingu zote.+
12 Sitanyamaza kimya kuhusu sehemu zake
Au habari ya nguvu zake na uzuri wa vipimo vyake.
13 Ni nani ambaye ameufunua uso wa mavazi yake?
Ni nani anayeweza kuingia ndani ya taya zake mbili?
14 Ni nani amepata kuifungua milango ya uso wake?
Meno yake kuzunguka pande zote ni yenye kuogopesha.
15 Mitaro ya magamba ndiyo majivuno yake,
Yaliyofungwa kana kwamba kwa muhuri uliokazwa.
16 Hayo huingiana yenyewe karibu-karibu,
Na hata hewa haiwezi kuingia katikati yake.
17 Yamefungamana kila moja na lingine;
Yanashikamana wala hayawezi kutenganishwa.
18 Chafya zake huangaza nuru,
Na macho yake ni kama miali ya mapambazuko.
19 Miwako ya umeme hutoka katika kinywa chake,
Hata cheche za moto hutoka.
20 Moshi hutoka katika mianzi ya pua yake,
Kama tanuru iliyowashwa moto kwa matete.
21 Nafsi yake huwasha moto makaa,
Na mwali wa moto hutoka katika kinywa chake.
22 Nguvu zinakaa katika shingo yake,
Na ukataji tamaa hukimbia mbele yake.
23 Makunjo ya nyama yake hushikamana pamoja;
Hayo ni kama kitu kilichoundwa katika kalibu juu yake, kisichoondoleka.
24 Moyo wake umetengenezwa kama jiwe,
Ndiyo, umetengenezwa kama jiwe la chini la kusagia.
30 Sehemu zake za chini ni kama vigae vilivyochongoka;
Yeye hujinyoosha kama kifaa cha kupuria+ juu ya matope.
31 Yeye huvichemsha vilindi kama chungu;
Huifanya bahari iwe kama chungu cha marhamu.
32 Hufanya njia ing’ae nyuma yake;
Mtu atafikiri kilindi cha maji ni kichwa chenye mvi.
33 Hakuna aliye kama yeye juu ya mavumbi,
Yeye aliyefanywa asiweze kutishika.
34 Yeye huona kila kitu kilicho juu.
Yeye ni mfalme juu ya wanyama-mwitu wote wenye fahari.”
42 Naye Ayubu akamjibu Yehova, akasema:
2 “Nimepata kujua kwamba unaweza kufanya mambo yote,+
Wala hakuna wazo lolote ambalo huwezi kulifikia.+
3 ‘Ni nani huyu anayefunika shauri bila ujuzi?’+
Kwa hiyo nilisema, lakini sikuwa ninaelewa
Mambo yaliyo ya ajabu mno kwangu, ambayo siyajui.+
5 Nimesikia habari zako kwa fununu,
Lakini sasa jicho langu mwenyewe linakuona wewe.
7 Na ikawa baada ya Yehova kumwambia Ayubu maneno hayo, ndipo Yehova akamwambia Elifazi Mtemani:
“Hasira yangu imewaka juu yako na rafiki zako wawili,+ kwa maana ninyi hamkusema mambo ya kweli+ kunihusu mimi kama mtumishi wangu Ayubu. 8 Na sasa chukueni ng’ombe-dume saba+ na kondoo-dume saba+ kisha mwende kwa mtumishi wangu Ayubu, nanyi mtoe dhabihu ya kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe; na Ayubu mtumishi wangu atasali kwa ajili yenu.+ Nitakubali uso wake peke yake ili nisiwatendee ninyi upumbavu wenye kufedhehesha, kwa maana hamkusema mambo ya kweli kunihusu mimi, kama mtumishi wangu Ayubu.”+
9 Basi Elifazi Mtemani na Bildadi Mshua na Sofari Mnaamathi wakaenda, wakafanya kama Yehova alivyowaambia; na kwa hiyo Yehova akaukubali uso wa Ayubu.
10 Na Yehova akaigeuza hali ya mateka ya Ayubu+ aliposali kwa ajili ya wale rafiki zake,+ na Yehova akaanza kumpa na kumwongezea Ayubu vyote vilivyokuwa vyake, kiasi cha mara mbili.+ 11 Na ndugu zake wote na dada zake wote na wale wote waliokuwa wakimjua+ hapo mwanzoni wakaendelea kuja kwake, nao wakaanza kula mkate pamoja naye+ katika nyumba yake na kusikitika pamoja naye na kumfariji juu ya msiba wote ambao Yehova alikuwa ameuruhusu uje juu yake; nao wakaanza kila mmoja wao kumpa kipande cha pesa na kila mmoja pete ya dhahabu.
12 Naye Yehova akaubariki+ mwisho wa Ayubu baadaye kuliko mwanzo wake,+ hivi kwamba akawa na kondoo kumi na nne elfu na ngamia elfu sita na jozi elfu moja za ng’ombe na punda-jike elfu moja. 13 Pia akawa na wana saba na binti watatu.+ 14 Naye akamwita yule wa kwanza jina Yemima na yule wa pili Kezia na yule wa tatu Kereni-hapuku. 15 Na hapakuonekana wanawake wowote walio warembo kama wale binti za Ayubu katika nchi yote, na baba yao akawapa urithi katikati ya ndugu zao.+
16 Naye Ayubu akaendelea kuishi miaka 140+ baada ya mambo hayo, akaona wanawe na wajukuu wake+—vizazi vinne. 17 Na mwishowe Ayubu akafa, akiwa mzee na mwenye kushiba siku.+
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Au kiboko.
Au mamba.