MAOMBOLEZO
א [Aleph]*
1 Lo! Jiji lililokuwa limejaa watu+ sasa limebaki ukiwa!
Limekuwa kama mjane, jiji lililokuwa na watu wengi miongoni mwa mataifa!+
Jiji lililokuwa binti ya mfalme kati ya mikoa* limefanywa kuwa mtumwa!+
ב [Beth]
2 Binti huyo analia sana usiku,+ na machozi yake yamefunika mashavu yake.
Miongoni mwa wapenzi wake wote hakuna yeyote wa kumfariji.+
Marafiki zake wote wamemsaliti;+ wamekuwa maadui wake.
ג [Gimel]
3 Yuda amepelekwa uhamishoni+ kwa mateso na utumwa wa kikatili.+
Ni lazima akae miongoni mwa mataifa;+ hana mahali pa kupumzika.
Wote waliokuwa wakimtesa wamemkabili katika mateso yake.
ד [Daleth]
4 Barabara zinazoelekea Sayuni zinaomboleza, kwa sababu hakuna yeyote anayekuja kwenye sherehe.+
Malango yake yote yamebaki ukiwa;+ makuhani wake wanalia kwa uchungu.
Mabikira* wake wanaomboleza, naye analia kwa maumivu makali.
ה [He]
5 Wapinzani wake sasa ni mabwana wakubwa wake; maadui wake hawajali.+
Kwa maana Yehova amemletea huzuni kwa sababu ya dhambi zake nyingi.+
Adui amewapeleka watoto wake utekwani.+
ו [Waw]
6 Fahari yote ya binti ya Sayuni imetoweka.+
Wakuu wake ni kama paa dume waliokosa malisho,
Nao wanatembea kwa uchovu mbele ya yule anayewafuatia.
ז [Zayin]
7 Katika siku za mateso yake na za kukosa makao, Yerusalemu hukumbuka
Vitu vyote vyenye thamani vilivyokuwa vyake siku za zamani za kale.+
Watu wake walipotiwa mikononi mwa adui, naye hakuwa na msaidizi,+
ח [Heth]
8 Yerusalemu ametenda dhambi nzito sana.+
Ndiyo sababu amekuwa kitu kinachochukiza sana.
Wote waliokuwa wakimheshimu sasa wanamtendea kama kitu kinachodharauliwa, kwa maana wameuona uchi wake.+
Yeye mwenyewe analia kwa maumivu+ na kujificha kwa aibu.
ט [Teth]
9 Uchafu wake umo ndani ya mavazi yake.
Hakufikiria wakati wake ujao.+
Alianguka kwa njia ya kushangaza; hana yeyote wa kumfariji.
Ee Yehova, yaangalie mateso yangu, kwa sababu adui amejitukuza.+
י [Yod]
10 Adui amechukua hazina zake zote.+
Kwa maana ameona* mataifa yakiingia mahali pake patakatifu,+
Watu ulioamuru wasiingie katika kutaniko lako.
כ [Kaph]
11 Watu wake wote wanalia kwa uchungu; wanatafuta mkate.+
Wamewapa vitu vyao vyenye thamani ili wapate kitu cha kula, angalau waendelee kuishi.*
Tazama, Ee Yehova, uone kwamba nimekuwa kama mwanamke asiyefaa kitu.*
ל [Lamed]
12 Enyi nyote mnaopita njiani, mateso yangu kwenu si kitu?
Tazameni mwone!
Je, kuna maumivu kama maumivu niliyoletewa,
Ambayo Yehova aliniletea katika siku ya hasira yake kali?+
מ [Mem]
13 Kutoka juu sana ameushusha moto mifupani mwangu,+ naye anautiisha kila mfupa.
Ametandaza wavu wa kunasa miguu yangu; amenilazimisha nirudi nyuma.
Amenifanya kuwa mwanamke aliye ukiwa.
Mchana kutwa mimi ni mgonjwa.
נ [Nun]
14 Dhambi zangu zimefungwa kama nira, mkono wake umezifunga pamoja.
Zimewekwa shingoni mwangu, nami nimeishiwa na nguvu.
Yehova amenitia mikononi mwa watu ambao siwezi kuwapinga.+
ס [Samekh]
15 Yehova amewatupa pembeni watu wote wenye nguvu kati yangu.+
Ameukusanya umati wa watu dhidi yangu ili kuwaponda vijana wangu wa kiume.+
Yehova amemkanyaga binti bikira wa Yuda katika shinikizo la divai.+
ע [Ayin]
16 Ninalia kwa sababu ya mambo haya;+ macho yangu yanatiririka machozi.
Kwa maana yeyote ambaye angenifariji au kuniburudisha yuko mbali sana nami.
Wanangu wamebaki ukiwa, kwa maana adui ameshinda.
פ [Pe]
17 Sayuni amenyoosha mikono yake;+ hana wa kumfariji.
Yehova amewaagiza maadui wote wanaomzunguka Yakobo wamshambulie.+
Yerusalemu limekuwa kitu cha kuchukiza sana kwao.+
צ [Tsade]
18 Yehova ni mwadilifu,+ kwa kuwa nimeasi amri zake.*+
Sikilizeni, enyi mataifa yote, mwone maumivu yangu.
Mabikira* wangu na vijana wangu wa kiume wamepelekwa utekwani.+
ק [Qoph]
19 Nimewaita wapenzi wangu, lakini wamenisaliti.+
Makuhani wangu na wazee wangu wameangamia jijini,
ר [Resh]
20 Tazama, Ee Yehova, kwa maana ninateseka sana.
Matumbo yangu yanasukasuka.
Moyo wangu umepinduka ndani yangu, kwa maana nimekuwa mwasi kabisa.+
Nje, upanga unaangamiza;+ ndani ya nyumba, ni kama kifo.
ש [Shin]
21 Watu wamesikia kilio changu cha uchungu; hakuna yeyote wa kunifariji.
Maadui wangu wote wamesikia kuhusu msiba wangu.+
Wanashangilia, kwa sababu uliuleta.
Lakini utaleta siku uliyotangaza,+ wakati huo watakuwa kama mimi.+
ת [Taw]
22 Uovu wao wote na uje mbele zako, na uwatese vikali,+
Kama tu ulivyonitesa vikali kwa sababu ya dhambi zangu zote.
Kwa maana vilio vyangu vya uchungu ni vingi, na moyo wangu ni mgonjwa.
א [Aleph]
2 Jinsi Yehova alivyomfunika binti ya Sayuni katika wingu la hasira yake!
Ameutupa chini urembo wa Israeli kutoka mbinguni mpaka duniani.+
Hajakumbuka kiti cha miguu yake+ katika siku ya hasira yake.
ב [Beth]
2 Yehova ameyameza makao yote ya Yakobo bila huruma.
Katika hasira yake amebomoa ngome za binti ya Yuda.+
Ameushusha chini ardhini na kuuchafua ufalme+ na wakuu wake.+
ג [Gimel]
3 Kwa hasira kali amezikata nguvu zote za* Israeli.
Aliuondoa mkono wake wa kuume adui alipokaribia,+
Na katika Yakobo aliendelea kuwaka kama moto ulioteketeza kila kitu kilicho karibu.+
ד [Daleth]
4 Ameukunja* upinde wake kama adui; mkono wake wa kuume uko tayari kama adui;+
Aliendelea kuwaua wote wanaotamanika machoni.+
Naye aliimwaga ghadhabu yake kama moto+ katika hema la binti ya Sayuni.+
ה [He]
Ameimeza minara yake yote;
Ameziharibu ngome zake zote.
Na katika binti ya Yuda anafanya maombolezo na kilio kiwe kingi.
ו [Waw]
6 Anakitendea kwa ukatili kibanda chake,+ kama kibanda kilicho katika bustani.
Yehova amesababisha sherehe na sabato zisahauliwe Sayuni,
Na kwa ghadhabu yake kali hamheshimu mfalme na kuhani.+
ז [Zayin]
Amesalimisha kuta za minara yake yenye ngome mikononi mwa adui.+
Wameinua sauti yao ndani ya nyumba ya Yehova,+ kama inavyokuwa siku ya sherehe.
ח [Heth]
8 Yehova ameazimia kuuharibu ukuta wa binti ya Sayuni.+
Ameinyoosha kamba ya kupimia.+
Hajauzuia mkono wake usilete maangamizi.*
Naye husababisha maboma na kuta ziomboleze.
Zote pamoja zimedhoofishwa.
ט [Teth]
9 Malango yake yamezama chini ardhini.+
Ameyaharibu na kuyavunja makomeo yake.
Mfalme wake na wakuu wake wako miongoni mwa mataifa.+
Hakuna sheria;* hata manabii wake hawapati maono kutoka kwa Yehova.+
י [Yod]
10 Wazee wa binti ya Sayuni wanaketi ardhini wakiwa kimya.+
Wanarusha mavumbi vichwani mwao na kuvaa nguo za magunia.+
Mabikira wa Yerusalemu wameinamisha vichwa vyao mpaka ardhini.
כ [Kaph]
11 Macho yangu yamechoka kabisa kwa sababu ya kumwaga machozi.+
Matumbo yangu yanasukasuka.
Ini langu limemwagika ardhini, kwa sababu ya kuanguka kwa binti ya* watu wangu,+
Kwa sababu ya watoto wadogo na watoto wanaonyonya wanaozimia kwenye viwanja vya mji.+
ל [Lamed]
12 Wanaendelea kuwauliza mama zao, “Iko wapi nafaka na divai?”+
Wanapozimia kama mtu aliyejeruhiwa katika viwanja vya mji,
Huku uhai wao ukitoka polepole wakiwa mikononi mwa mama zao.
מ [Mem]
13 Ninaweza kutumia nini kama ushahidi,
Au ninaweza kukufananisha na nini, Ee binti ya Yerusalemu?
Ninaweza kukulinganisha na nini, ili nikufariji, Ee bikira binti ya Sayuni?
Kwa maana jeraha lako* ni kubwa kama bahari.+ Ni nani anayeweza kukuponya?+
נ [Nun]
14 Maono ambayo manabii wako waliona kwa ajili yako yalikuwa ya uwongo na yasiyofaa kitu,+
Nao hawakufunua kosa lako ili kuzuia usipelekwe utekwani,+
Bali waliendelea kukupa maono yenye ujumbe wa uwongo na unaopotosha.+
ס [Samekh]
15 Wote wanaopita barabarani wanakupigia makofi kwa dharau.+
Wanapiga mluzi kwa mshangao+ na kumtikisia vichwa vyao binti ya Yerusalemu, wakisema:
“Je, hili ndilo jiji walilosema hivi kulihusu: ‘Lina urembo mkamilifu, ni shangwe ya dunia yote’?”+
פ [Pe]
16 Maadui wako wote wamefungua kinywa chao dhidi yako.
Wanapiga mluzi na kusaga meno yao wakisema: “Tumemmeza.+
Hii ndiyo siku tuliyokuwa tukiingojea!+ Imefika, nasi tumeiona!”+
ע [Ayin]
Amebomoa bila huruma.+
Amemruhusu adui ashangilie msiba wako; amezikweza nguvu za* wapinzani wako.
צ [Tsade]
18 Moyo wao unamlilia Yehova kwa sauti, Ee ukuta wa binti ya Sayuni.
Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku.
Usipumzike, macho yako yasiache kulia.*
ק [Qoph]
19 Inuka! Lia kwa sauti wakati wa usiku, mwanzoni mwa makesha ya usiku.
Umwage moyo wako kama maji mbele za uso wa Yehova.
Mwinulie mikono yako kwa ajili ya uhai wa* watoto wako,
Wanaozimia kwenye kila pembe ya barabara kwa sababu ya njaa kali.+
ר [Resh]
20 Tazama, Ee Yehova, umwone yule uliyemtesa vikali.
Je, wanawake wanapaswa kuendelea kula uzao wao wenyewe, watoto wao wenyewe waliokomaa,+
Au, je, makuhani na manabii wanapaswa kuuawa mahali patakatifu pa Yehova?+
ש [Shin]
21 Mvulana na mwanamume mzee wamelala chini barabarani wakiwa wamekufa.+
Mabikira* wangu na vijana wangu wa kiume wameuawa kwa upanga.+
Umeua katika siku ya hasira yako; umechinja bila huruma.+
ת [Taw]
22 Unakusanya vitisho kutoka kila upande kana kwamba ni siku ya sherehe.+
Katika siku ya ghadhabu ya Yehova, hakuna yeyote aliyeponyoka wala kuokoka;+
Wale niliowazaa* na kuwalea, adui yangu aliwaangamiza kabisa.+
א [Aleph]
3 Mimi ndiye mwanamume aliyepata mateso kwa sababu ya fimbo ya ghadhabu yake.
2 Amenifukuza, naye hunifanya nitembee gizani, si nuruni.+
3 Kwa kweli, yeye huniadhibu tena na tena kwa mkono wake mchana kutwa.+
ב [Beth]
4 Ameudhoofisha mwili wangu na ngozi yangu;
Ameivunja mifupa yangu.
5 Amenizingira; amenizungushia sumu+ kali na taabu.
6 Amenilazimisha niketi katika sehemu zenye giza, kama watu waliokufa zamani za kale.
ג [Gimel]
8 Na ninapolilia sana msaada, yeye hukataa* sala yangu.+
ד [Daleth]
10 Anangojea kunivizia kama dubu, kama simba aliye mafichoni.+
12 Ameukunja* upinde wake, naye hunifanya niwe shabaha ya mshale wake.
ה [He]
13 Amezichoma figo zangu kwa mishale ya* podo lake.
14 Nimekuwa kichekesho kwa mataifa yote, kichwa cha wimbo wao mchana kutwa.
15 Amenijaza mambo machungu na kunikoleza kwa pakanga.+
ו [Waw]
17 Unaninyima amani; nimesahau lililo jema.
18 Kwa hiyo ninasema: “Fahari yangu imetoweka, na pia matarajio yangu kwa Yehova.”
ז [Zayin]
19 Kumbuka mateso yangu na hali yangu ya kukosa makao,+ pakanga na sumu kali.+
20 Kwa hakika utakumbuka na kuinama juu yangu.+
21 Ninakumbuka hili moyoni mwangu; ndiyo sababu nitaonyesha mtazamo wa kungojea.+
ח [Heth]
22 Hatujaangamia kwa sababu ya upendo mshikamanifu wa Yehova,+
Kwa maana rehema zake hazikomi kamwe.+
23 Ni mpya kila asubuhi;+ uaminifu wako ni mwingi sana.+
24 Nimesema,* “Yehova ni fungu langu+ ndiyo sababu nitaonyesha mtazamo wa kumngojea yeye.”+
ט [Teth]
25 Yehova ni mwema kwa yule anayemtumaini,+ kwa mtu anayeendelea kumtafuta.+
26 Ni jambo jema kuungojea kimyakimya*+ wokovu wa Yehova.+
27 Ni jambo jema kwa mwanamume kubeba nira wakati wa ujana.+
י [Yod]
28 Acha akae peke yake na kunyamaza Mungu anapoiweka juu yake.+
29 Acha atie kinywa chake mavumbini;+ huenda ikawa bado kuna tumaini.+
30 Acha ampe shavu lake yule anayempiga; acha atukanwe vya kutosha.
כ [Kaph]
31 Kwa maana Yehova hatatutupa mbali milele.+
32 Ingawa amesababisha huzuni, ataonyesha pia rehema kulingana na upendo wake mwingi sana mshikamanifu.+
33 Kwa maana moyo wake haupendi kuwatesa au kuwahuzunisha wanadamu.+
ל [Lamed]
34 Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote wa dunia,+
35 Kumnyima mtu haki yake mbele za Aliye Juu Zaidi,+
36 Kumlaghai mtu katika kesi yake
—Yehova havumilii mambo kama hayo.
מ [Mem]
37 Kwa hiyo basi, ni nani anayeweza kusema na jambo likatendeka Yehova asipoamuru?
38 Kutoka katika kinywa cha Aliye Juu Zaidi,
Mambo mabaya na mema hayatoki pamoja.
39 Kwa nini mtu aliye hai alalamike kuhusu matokeo ya dhambi yake?+
נ [Nun]
40 Acheni tuzikague na kuzichunguza kwa makini njia zetu,+ na acheni tumrudie Yehova.+
41 Acheni tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni:+
42 “Tumetenda dhambi na kuasi,+ nawe hujatusamehe.+
ס [Samekh]
44 Umeziba kwa wingu njia ya kukukaribia, ili sala yetu isipenye.+
45 Unatufanya kuwa takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.”
פ [Pe]
46 Maadui wetu wote wanafungua vinywa vyao dhidi yetu.+
47 Hofu na mitego vimekuwa fungu letu,+ ukiwa na maangamizi.+
48 Vijito vya maji vinatiririka kutoka katika macho yangu kwa sababu ya maangamizi ya binti ya watu wangu.+
ע [Ayin]
51 Macho yangu yameniletea huzuni kwa sababu ya mabinti wote wa jiji langu.+
צ [Tsade]
52 Maadui wangu wameniwinda sana kama ndege bila sababu.
53 Wameunyamazisha uhai wangu shimoni; waliendelea kunitupia mawe.
54 Maji yalitiririka juu ya kichwa changu, nami nikasema: “Nimekwisha!”
ק [Qoph]
55 Nililiita jina lako kwa sauti, Ee Yehova, kutoka chini shimoni.+
56 Isikie sauti yangu; usizibe sikio lako ninapolilia msaada, ninapoomba kitulizo.
57 Ulinikaribia siku niliyokuita. Ulisema: “Usiogope.”
ר [Resh]
58 Umenitetea,* Ee Yehova, umeukomboa uhai wangu.+
59 Umeona, Ee Yehova, uovu niliotendewa; tafadhali nitendee haki.+
60 Umeona kisasi chao chote, njama zao zote walizopanga dhidi yangu.
ש [Sin] au [Shin]
61 Umesikia dhihaka zao, Ee Yehova, njama zao zote walizopanga dhidi yangu,+
62 Midomo ya wapinzani wangu na mambo wanayonong’ona dhidi yangu mchana kutwa.
63 Watazame; wananidhihaki kwa nyimbo zao wakiwa wameketi au wamesimama!
ת [Taw]
64 Utawalipa, Ee Yehova, kulingana na matendo yao.
65 Utaifanya mioyo yao kuwa migumu, kama laana kwao.
66 Utawafuatia kwa hasira yako na kuwaangamiza chini ya mbingu zako, Ee Yehova.
א [Aleph]
4 Jinsi dhahabu inayong’aa ilivyopoteza mng’ao wake, dhahabu bora!+
Jinsi mawe matakatifu+ yalivyotapakaa kwenye kila pembe ya barabara!+
ב [Beth]
2 Na wana wa Sayuni wenye thamani, ambao walipimwa kwa uzito wa* dhahabu safi,
Sasa wanaonwa kuwa kama magudulia ya udongo,
Kazi ya mikono ya mfinyanzi!
ג [Gimel]
3 Hata mbwamwitu huwapa watoto wao matiti wanyonye,
Lakini binti ya watu wangu amekuwa mkatili,+ kama mbuni nyikani.+
ד [Daleth]
4 Ulimi wa mtoto anayenyonya hushikamana na kaakaa lake kwa sababu ya kiu.
Watoto wadogo wanaombaomba mikate,+ lakini hakuna anayewapa.+
ה [He]
5 Wale waliokuwa wakila vyakula vitamu wanalala barabarani kwa sababu ya njaa kali.+
Wale waliolelewa wakivaa mavazi mekundu+ wamekumbatia marundo ya majivu.
ו [Waw]
6 Adhabu* ya binti ya watu wangu ni kubwa kuliko adhabu iliyotolewa kwa sababu ya dhambi ya Sodoma,+
ז [Zayin]
7 Wanadhiri wake+ walikuwa safi kuliko theluji, weupe kuliko maziwa.
Walikuwa wekundu kuliko marijani; walikuwa kama vito vya yakuti vilivyong’arishwa.
ח [Heth]
Ngozi yao imenyauka juu ya mifupa yao;+ imekuwa kama ukuni uliokauka.
ט [Teth]
9 Waliouawa kwa upanga ni afadhali kuliko waliokufa kwa njaa kali,+
Wale wanaokonda, wanaochomwa kana kwamba kwa upanga kwa sababu ya kukosa chakula kutoka shambani.
י [Yod]
10 Mikono ya wanawake wenye huruma imewachemsha watoto wao wenyewe.+
Wamekuwa chakula chao cha maombolezo wakati wa kuangamia kwa binti ya watu wangu.+
כ [Kaph]
Anawasha moto Sayuni unaoteketeza misingi yake.+
ל [Lamed]
12 Wafalme wa dunia na wakaaji wote wa ardhi inayozaa hawakuamini
Kwamba mpinzani na adui wangeingia katika malango ya Yerusalemu.+
מ [Mem]
13 Hilo lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, makosa ya makuhani wake,+
Waliomwaga damu ya waadilifu waliokuwa katika jiji hilo.+
נ [Nun]
14 Wametangatanga kama vipofu+ barabarani.
Wamechafuliwa na damu,+
Hivi kwamba hakuna yeyote anayeweza kuyagusa mavazi yao.
ס [Samekh]
15 “Nendeni zenu! Wachafu!” watu wanawaambia kwa sauti. “Nendeni zenu! Nendeni zenu! Msituguse!”
Kwa maana hawana makao, nao wanatangatanga.
Miongoni mwa mataifa watu wamesema: “Hawawezi kukaa hapa pamoja nasi.*+
פ [Pe]
Watu hawatawaheshimu makuhani,+ hawatawatendea wazee kwa fadhili.”+
ע [Ayin]
17 Hata sasa macho yetu yamechoka kabisa tukitarajia kupata msaada bila mafanikio.+
Tulitarajia na kutarajia kupata msaada kutoka kwa taifa ambalo halingeweza kutuokoa.+
צ [Tsade]
18 Wametuwinda katika kila hatua+ hivi kwamba hatungeweza kutembea kwenye viwanja vya jiji letu.
Mwisho wetu umekaribia; siku zetu zimekwisha, kwa maana mwisho wetu umefika.
ק [Qoph]
19 Waliotufuatia walikwenda kasi kuliko tai wa angani.+
Walitukimbiza milimani; walituvamia nyikani.
ר [Resh]
20 Pumzi ya mianzi ya pua zetu, mtiwa-mafuta wa Yehova,+ amenaswa katika shimo lao kubwa,+
Yule tuliyesema hivi kumhusu: “Tutaishi chini ya kivuli chake miongoni mwa mataifa.”
ש [Sin]
21 Furahi na kushangilia, Ee binti ya Edomu,+ unayekaa katika nchi ya Usi.
Lakini wewe pia utapitishiwa kikombe,+ nawe utalewa na kufunua uchi wako.+
ת [Taw]
22 Adhabu ya dhambi yako, Ee binti ya Sayuni, imekwisha.
Hatakupeleka tena uhamishoni.+
Lakini ataukazia uangalifu uovu wako, Ee binti ya Edomu.
Atafunua dhambi zako.+
5 Kumbuka, Ee Yehova, yale ambayo yametupata.
Tazama na uone aibu yetu.+
2 Wageni wamepewa urithi wetu, wageni wamepewa nyumba zetu.+
3 Tumekuwa mayatima, hatuna baba; mama zetu ni kama wajane.+
4 Ni lazima tulipe ili tunywe maji yetu wenyewe,+ na kuni zetu wenyewe tunazinunua.
6 Tunainyooshea mkono Misri+ na Ashuru,+ ili tupate chakula cha kutosha.*
7 Mababu zetu waliotenda dhambi hawapo tena, lakini ni lazima tuubebe uovu wao.
8 Sasa watumishi wanatutawala; hakuna yeyote wa kutunasua kutoka mikononi mwao.
9 Tunapata chakula chetu* kwa kuhatarisha uhai wetu,*+ kwa sababu ya upanga wa nyikani.
10 Ngozi yetu imekuwa moto kama tanuru, kwa sababu ya makali ya njaa.+
11 Wamewafedhehesha* wake walio Sayuni, mabikira walio katika majiji ya Yuda.+
12 Wakuu walitundikwa kwa mikono yao,+ na wazee hawakuheshimiwa.+
13 Vijana wa kiume wanabeba jiwe la kusagia, na wavulana wanajikwaa kwa sababu ya kubeba mizigo ya kuni.
14 Wazee wametoweka kwenye lango la jiji;+ vijana wa kiume hawapigi muziki wao.+
15 Shangwe imetoweka mioyoni mwetu; dansi zetu zimegeuka kuwa maombolezo.+
16 Taji limeanguka kutoka kwenye kichwa chetu. Ole wetu, kwa sababu tumetenda dhambi!
17 Kwa sababu hiyo moyo wetu ni mgonjwa,+
Na kwa sababu ya mambo haya macho yetu yamefifia,+
18 Kwa sababu ya Mlima Sayuni, ambao umeachwa ukiwa;+ sasa mbweha wanatangatanga juu yake.
19 Lakini wewe, Ee Yehova, umeketi kwenye kiti chako cha ufalme milele.
Kiti chako kinadumu kizazi baada ya kizazi.+
20 Kwa nini unatusahau milele na kutuacha kwa muda mrefu sana hivyo?+
21 Turudishe kwako, Ee Yehova, nasi tutakurudia bila kusita.+
Zifanye siku zetu ziwe mpya kama siku za zamani.+
22 Hata hivyo, umetukataa kabisa.
Unaendelea kutukasirikia vikali sana.+
Sura ya 1-4 ni nyimbo za maombolezo zilizoandikwa kwa kufuata alfabeti ya Kiebrania au mpangilio wa kishairi.
Au “wilaya za utawala.”
Au “Wanawali.”
Au “kumdhihaki.”
Yaani, watu wa Yerusalemu.
Au “wahuishe nafsi.”
Jiji la Yerusalemu linafananishwa na mwanamke.
Tnn., “nimekiasi kinywa chake.”
Au “Wanawali.”
Au “waihuishe nafsi.”
Tnn., “ameikata kila pembe ya.”
Tnn., “Ameukanyaga.”
Au “Ameharibu.”
Tnn., “usimeze.”
Au “mafundisho.”
Mfano wa kishairi ambao huenda unaonyesha huruma au sikitiko.
Au “jeraha lako la kuvunjika.”
Tnn., “ameikweza pembe ya.”
Tnn., “binti ya jicho lako asipumzike.”
Au “nafsi za.”
Au “Wanawali.”
Au “niliowazaa wakiwa na afya.”
Au “huizuia; huifungia nje.”
Au labda, “ananiacha kama shamba ambalo halijapandwa mbegu.”
Tnn., “Ameukanyaga.”
Tnn., “wana wa.”
Au “Nafsi yangu inasema.”
Au “kuungojea kwa subira.”
Au “Umezitetea kesi za nafsi yangu.”
Au “waliokuwa na thamani kama.”
Tnn., “Dhambi.”
Tnn., “bila mkono wa kulisaidia.”
Tnn., “weusi.”
Au “kuishi hapa wakiwa wageni.”
Tnn., “mikate ya kutosha ya kula.”
Tnn., “mikate yetu.”
Au “nafsi zetu.”
Au “Wamewabaka.”