BARUA YA KWANZA KWA WAKORINTHO
1 Paulo, aliyeitwa kuwa mtume+ wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu, 2 kwa kutaniko la Mungu lililo huko Korintho,+ kwenu ninyi ambao mmetakaswa katika muungano na Kristo Yesu,+ mlioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo,+ Bwana wao na wetu:
3 Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
4 Sikuzote ninamshukuru Mungu wangu kwa ajili yenu kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu mlizopewa katika Kristo Yesu; 5 kwa kuwa katika yeye mmetajirishwa katika kila jambo, katika uwezo kamili wa kusema na katika ujuzi kamili,+ 6 kama vile ushahidi kumhusu Kristo+ ulivyofanywa kuwa imara miongoni mwenu, 7 ili msipungukiwe hata kidogo katika zawadi yoyote, huku mkisubiri kwa hamu ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.+ 8 Yeye pia atawafanya ninyi muwe imara mpaka mwisho, ili msiwe na shtaka lolote katika siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.+ 9 Mungu ni mwaminifu,+ aliyewaita muwe na ushirika pamoja na Mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu.
10 Sasa ninawahimiza ninyi, akina ndugu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mseme kwa upatano, na kwamba kusiwe na migawanyiko kati yenu,+ bali kwamba muunganishwe kabisa katika akili ileile na njia ileile ya kufikiri.+ 11 Kwa maana baadhi ya watu wa nyumba ya Kloe wamenijulisha kuwahusu ninyi ndugu zangu, kwamba kuna ugomvi kati yenu. 12 Ninalomaanisha ni hili, kwamba kila mmoja wenu anasema: “Mimi ni wa Paulo,” “Lakini mimi ni wa Apolo,”+ “Lakini mimi ni wa Kefa,”* “Lakini mimi ni wa Kristo.” 13 Je, Kristo amegawanyika? Paulo hakuuawa kwenye mti kwa ajili yenu, sivyo? Au je, mlibatizwa katika jina la Paulo? 14 Ninamshukuru Mungu kwa kuwa sikumbatiza hata mmoja wenu isipokuwa Krispo+ na Gayo,+ 15 ili yeyote asiseme kwamba mlibatizwa katika jina langu. 16 Ndiyo, niliibatiza pia nyumba ya Stefana.+ Kuhusu wale wengine, sijui kama nilimbatiza mwingine yeyote. 17 Kwa maana Kristo alinituma, si kubatiza, bali kutangaza habari njema;+ na si kwa maneno ya hekima,* ili mti wa mateso* wa Kristo usifanywe kuwa kitu kisicho na maana.
18 Kwa maana maneno kuhusu mti wa mateso* ni upumbavu kwa wale wanaoangamia,+ lakini kwetu sisi tunaookolewa, ni nguvu za Mungu.+ 19 Kwa maana imeandikwa: “Nitaiangamiza hekima ya watu wenye hekima, nami nitaikataa* akili ya watu wenye akili.”+ 20 Yuko wapi mtu mwenye hekima? Yuko wapi mwandishi?* Yuko wapi anayebishania maneno katika mfumo huu wa mambo?* Je, Mungu hakuifanya hekima ya ulimwengu iwe upumbavu? 21 Kwa kuwa, katika hekima ya Mungu, ulimwengu haukumjua Mungu+ kupitia hekima yake,+ Mungu alipenda kuwaokoa wale wanaoamini kupitia upumbavu+ wa ujumbe unaohubiriwa.
22 Kwa maana Wayahudi wanaomba ishara+ na Wagiriki wanatafuta hekima; 23 lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyeuawa kwenye mti, kwa Wayahudi ni sababu ya kujikwaa lakini kwa mataifa ni upumbavu.+ 24 Hata hivyo, kwa wale walioitwa, Wayahudi na Wagiriki, Kristo ni nguvu za Mungu na hekima ya Mungu.+ 25 Kwa sababu kitu kipumbavu cha Mungu ni chenye hekima kuliko wanadamu, na kitu dhaifu cha Mungu ni chenye nguvu kuliko wanadamu.+
26 Kwa maana akina ndugu, mnaona mwito wake kwenu, kwamba si wengi wenye hekima kwa njia ya kimwili,*+ si wengi wenye nguvu, si wengi wa kutoka familia mashuhuri,+ 27 bali Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe watu wenye hekima; na Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu, ili aviaibishe vitu vyenye nguvu;+ 28 na Mungu alivichagua vitu vinyonge vya ulimwengu na vitu vinavyodharauliwa, vitu ambavyo si kitu, ili kuvifanya vitu ambavyo ni kitu visiwe kitu,+ 29 ili mtu yeyote asijisifu* machoni pa Mungu. 30 Lakini ni kwa sababu yake kwamba ninyi mko katika muungano na Kristo Yesu, ambaye kwetu amekuwa hekima kutoka kwa Mungu, pia uadilifu+ na utakaso+ na kuachiliwa huru kupitia fidia,+ 31 ili iwe kama ilivyoandikwa: “Yule anayejisifu, na ajisifu katika Yehova.”*+
2 Kwa hiyo, nilipokuja kwenu, akina ndugu, sikuja na maneno mengi+ au hekima nikiwatangazia siri takatifu+ ya Mungu. 2 Kwa maana niliamua kutojua kitu chochote kati yenu isipokuwa Yesu Kristo, naye akiwa ameuawa kwenye mti.+ 3 Nami nilikuja kwenu nikiwa dhaifu, mwenye woga na nikitetemeka sana; 4 na katika maneno yangu na mambo niliyohubiri sikutumia maneno ya kushawishi yenye hekima bali wonyesho wa roho na nguvu,+ 5 ili imani yenu iwe, si katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu.
6 Basi tunazungumza kuhusu hekima kati ya wale ambao ni wakomavu,+ lakini si hekima ya mfumo huu wa mambo* wala ile ya watawala wa mfumo huu wa mambo, ambao watapitilia mbali.+ 7 Bali tunazungumza kuhusu hekima ya Mungu katika siri takatifu,+ hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiagiza awali kabla ya mifumo ya mambo kwa ajili ya utukufu wetu. 8 Hakuna mtawala hata mmoja wa mfumo huu wa mambo* aliyeijua hekima hii,+ kwa maana kama wangejua hawangemuua* Bwana mwenye utukufu. 9 Lakini kama ilivyoandikwa: “Jicho halijaona na sikio halijasikia, wala hayajawaziwa katika moyo wa mwanadamu mambo ambayo Mungu amewatayarishia wale wanaompenda.”+ 10 Kwa maana Mungu ameyafunua kwetu+ kupitia roho yake,+ kwa maana roho huchunguza ndani ya mambo yote, hata mambo mazito* ya Mungu.+
11 Kwa maana ni nani kati ya wanadamu anayejua mambo ya mwanadamu isipokuwa roho ya mwanadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo, hakuna ambaye ameyajua mambo ya Mungu, isipokuwa roho ya Mungu. 12 Basi, sisi hatukupokea roho ya ulimwengu, bali tulipokea roho inayotoka kwa Mungu,+ ili tuyajue mambo ambayo Mungu ametupatia kwa fadhili. 13 Mambo hayo tunayasema pia, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya binadamu,+ bali kwa yale yanayofundishwa kwa roho,+ tunapofafanua* mambo ya kiroho kwa maneno ya kiroho.
14 Lakini mtu wa kimwili hayakubali* mambo ya roho ya Mungu, kwa maana hayo ni upumbavu kwake; naye hawezi kuyajua, kwa sababu yanachunguzwa kiroho. 15 Hata hivyo, mtu wa kiroho huchunguza mambo yote,+ lakini yeye mwenyewe hachunguzwi na mwanadamu yeyote. 16 Kwa maana “ni nani ameijua akili ya Yehova,* ndipo amfundishe?”+ Lakini sisi tunayo akili ya Kristo.+
3 Basi akina ndugu, mimi sikuweza kuzungumza nanyi kama watu wa kiroho,+ bali kama watu wa kimwili, kama watoto+ katika Kristo. 2 Niliwalisha maziwa, si chakula kigumu, kwa maana mlikuwa bado hamna nguvu za kutosha. Kwa kweli, hata sasa hamna nguvu za kutosha,+ 3 kwa maana bado ninyi ni wa kimwili.+ Kwa kuwa kuna wivu na mizozo kati yenu, je, ninyi si wa kimwili+ na je, hamtembei kama wanadamu wanavyotembea? 4 Kwa maana mtu mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” naye mwingine anasema, “Mimi ni wa Apolo,”+ je, hamfanyi kama wanadamu tu?
5 Basi, Apolo ni nani? Ndiyo, Paulo ni nani? Wahudumu+ ambao kupitia wao mlikuja kuwa waamini, kama vile Bwana alivyomwezesha kila mmoja. 6 Mimi nilipanda,+ Apolo akatia maji,+ lakini Mungu akaendelea kuikuza, 7 hivi kwamba anayepanda si kitu wala anayetia maji, bali Mungu anayeikuza.+ 8 Basi anayepanda na anayetia maji ni kitu kimoja,* lakini kila mtu atapokea thawabu yake kulingana na kazi yake mwenyewe.+ 9 Kwa maana sisi ni wafanyakazi wenzi wa Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu linalolimwa, jengo la Mungu.+
10 Kulingana na fadhili zisizostahiliwa za Mungu nilizopewa, niliweka msingi,+ nikiwa mjenzi mkuu mwenye ustadi,* hata hivyo, mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja na aendelee kuangalia jinsi anavyojenga juu yake. 11 Kwa maana hakuna mtu yeyote anayeweza kuweka msingi mwingine wowote zaidi ya ule uliowekwa, ambao ni Yesu Kristo.+ 12 Basi yeyote akijenga juu ya msingi huo dhahabu, fedha, mawe ya thamani, mbao, nyasi kavu, au majani makavu, 13 kazi ya kila mmoja itaonekana jinsi ilivyo,* kwa maana ile siku itaifichua, kwa sababu itafunuliwa kupitia moto,+ na moto wenyewe utaonyesha jinsi kila mmoja alivyojenga. 14 Ikiwa kazi ya yeyote aliyejenga juu yake itabaki, atapokea thawabu; 15 ikiwa kazi ya yeyote itateketea, atapata hasara, lakini yeye mwenyewe ataokolewa; hata hivyo, itakuwa ni kama kupitia moto.
16 Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu,+ na kwamba roho ya Mungu inakaa ndani yenu?+ 17 Yeyote akiliangamiza hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, nanyi ni hekalu hilo.+
18 Mtu yeyote asijidanganye: Ikiwa yeyote miongoni mwenu anafikiri ana hekima katika mfumo huu wa mambo,* acheni awe mpumbavu ili awe na hekima. 19 Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upumbavu kwa Mungu, kwa kuwa imeandikwa: “Yeye huwanasa wenye hekima katika ujanja wao wenyewe.”+ 20 Na tena: “Yehova* anajua kwamba kufikiri kwa watu wenye hekima ni ubatili.”+ 21 Basi yeyote asijisifu katika watu; kwa maana vitu vyote ni vyenu, 22 iwe ni Paulo au Apolo au Kefa*+ au ulimwengu au uzima au kifo au mambo yaliyopo sasa au mambo yatakayokuja, vitu vyote ni vyenu; 23 nanyi ni wa Kristo;+ naye Kristo ni wa Mungu.
4 Mtu anapaswa kutuona kuwa wahudumu* wa Kristo na wasimamizi wa siri takatifu za Mungu.+ 2 Katika hali hii, kinachotarajiwa katika wasimamizi ni kupatwa wakiwa waaminifu. 3 Basi kwangu si muhimu sana kuchunguzwa na ninyi au na mahakama.* Hata mimi sijichunguzi mwenyewe. 4 Kwa maana sioni kosa lolote dhidi yangu mwenyewe. Lakini hilo halithibitishi kuwa mimi ni mwadilifu; anayenichunguza ni Yehova.*+ 5 Kwa hiyo, msihukumu+ chochote kabla ya wakati unaofaa, mpaka Bwana aje. Ataleta mambo ya siri yaliyo ya giza kwenye nuru na pia kujulisha nia za mioyo, na ndipo kila mtu atakapopokea sifa yake kutoka kwa Mungu.+
6 Basi, akina ndugu, mambo haya nimeyatumia* kujihusu mimi mwenyewe na Apolo+ kwa faida yenu, ili kupitia sisi mjifunze kanuni hii: “Msipite mambo yaliyoandikwa,” ili msiwe na kiburi,+ na kumpendelea mtu mmoja kuliko mwingine. 7 Kwa maana ni nani anayekufanya wewe kuwa tofauti na mwingine? Kwa kweli, una nini ambacho hukupokea?+ Basi, ikiwa kwa kweli ulikipokea, kwa nini unajisifu kana kwamba hukukipokea?
8 Je, tayari mmetosheka? Je, tayari ninyi ni matajiri? Je, mmeanza kutawala mkiwa wafalme+ bila sisi? Ninatamani sana kwamba muwe mmeanza kutawala mkiwa wafalme, ili sisi pia tutawale pamoja nanyi tukiwa wafalme.+ 9 Kwa maana ninaona kwamba Mungu ametuweka sisi mitume mwisho katika wonyesho wa hadharani kama watu waliohukumiwa kifo,+ kwa sababu tumekuwa tamasha kwa ulimwengu,+ na kwa malaika, na kwa wanadamu. 10 Sisi ni wapumbavu+ kwa sababu ya Kristo, lakini ninyi ni wenye busara katika Kristo; sisi ni dhaifu, lakini ninyi ni wenye nguvu; ninyi mnaheshimika, lakini sisi hatuheshimiki. 11 Mpaka saa hii tunaendelea kuwa na njaa+ na kiu+ na kukosa mavazi ya kutosha* na kupigwa*+ na kuwa bila makao 12 na kufanya kazi ya taabu, tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe.+ Tunapotukanwa, tunabariki;+ tunapoteswa, tunavumilia kwa subira;+ 13 tunapochongewa, tunajibu kwa upole;*+ tumekuwa kama takataka ya ulimwengu, uchafu wa vitu vyote, mpaka sasa.
14 Ninaandika mambo haya, si ili niwaaibishe, bali niwaonye kama watoto wangu wapendwa. 15 Kwa maana ingawa huenda mkawa na walezi* 10,000 katika Kristo, hakika hamna baba wengi; kwa maana katika Kristo Yesu mimi nimekuwa baba yenu kupitia habari njema.+ 16 Kwa hiyo, ninawasihi, iweni waigaji wangu.+ 17 Ndiyo sababu ninamtuma Timotheo kwenu, kwa kuwa yeye ni mtoto wangu mpendwa na mwaminifu katika Bwana. Atawakumbusha njia* zangu kuhusiana na Kristo Yesu,+ kama vile ninavyofundisha kila mahali katika kila kutaniko.
18 Wengine wamekuwa na kiburi wakidhani kwamba siji kwenu. 19 Lakini nitakuja kwenu hivi karibuni, Yehova* akipenda, nami nitajua, si maneno ya wale walio na kiburi, bali nguvu zao. 20 Kwa maana Ufalme wa Mungu si maneno tu bali ni nguvu. 21 Mngependa nini? Je, nije kwenu nikiwa na fimbo+ au kwa upendo na upole wa roho?
5 Kwa kweli kuna habari kwamba kuna uasherati*+ miongoni mwenu, tena uasherati* ambao haujatokea hata miongoni mwa mataifa—mwanamume kuishi* na mke wa baba yake.+ 2 Na je, ninyi mnajivunia jambo hilo? Je, hampaswi kuomboleza+ ili mtu aliyefanya kitendo hicho aondolewe miongoni mwenu?+ 3 Ingawa sipo katika mwili, nipo katika roho, tayari nimemhukumu mtu huyo ambaye amefanya tendo hilo, kana kwamba nipo pamoja nanyi. 4 Mnapokusanyika pamoja katika jina la Bwana wetu Yesu, na kujua kwamba nipo nanyi katika roho pamoja na nguvu za Bwana wetu Yesu, 5 lazima mumkabidhi mtu wa namna hiyo kwa Shetani+ kwa ajili ya kuangamizwa kwa mwili, ili roho iokolewe katika siku ya Bwana.+
6 Kujisifu kwenu hakufai. Je, hamjui kwamba chachu* kidogo huchachisha donge lote?+ 7 Ondoeni chachu ya zamani, ili muwe donge jipya, kwa kuwa ninyi hamna chachu. Kwa maana, kwa kweli, Kristo mwanakondoo wetu wa Pasaka+ ametolewa dhabihu.+ 8 Basi na tufanye sherehe,+ si kwa chachu ya zamani, wala kwa chachu ya ubaya na uovu, bali kwa mikate isiyo na chachu ya unyoofu na kweli.
9 Katika barua yangu niliwaandikia mwache kushirikiana* na waasherati,* 10 si kumaanisha waasherati* wa ulimwengu huu+ au watu wenye pupa na wanyang’anyi au waabudu-sanamu. Kama ingekuwa hivyo, kwa kweli ingewabidi mwondoke katika ulimwengu.+ 11 Lakini sasa ninawaandikia mwache kushirikiana*+ na mtu yeyote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati* au mtu mwenye pupa+ au anayeabudu sanamu au mtukanaji* au mlevi+ au mnyang’anyi,+ hata msile chakula pamoja na mtu wa namna hiyo. 12 Kwa maana inanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Je, ninyi hamwahukumu wale walio ndani, 13 huku Mungu akiwahukumu wale walio nje?+ “Mwondoeni mtu mwovu miongoni mwenu.”+
6 Je, kuna yeyote kati yenu aliye na ugomvi na mwenzake+ atakayethubutu kwenda mahakamani mbele ya watu wasio waadilifu, na si mbele ya watakatifu? 2 Au je, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu?+ Na ikiwa ninyi mtauhukumu ulimwengu, je, hamna uwezo wa kuamua mambo madogo sana? 3 Je, hamjui kwamba tutawahukumu malaika?+ Basi, kwa nini isiwe mambo ya maisha haya? 4 Basi, ikiwa mna mambo ya maisha haya yanayohitaji kuamuliwa,+ je, mnawaweka watu wanaodharauliwa na kutaniko kuwa waamuzi? 5 Ninasema ili kuwatia ninyi aibu. Je, hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima miongoni mwenu anayeweza kuhukumu kati ya ndugu zake? 6 Badala yake ndugu anaenda mahakamani kumshtaki ndugu, na tena mbele ya wasio waamini!
7 Kwa kweli, tayari mmeshindwa mnapokuwa na mashtaka ya kisheria wenyewe kwa wenyewe. Je, si afadhali mkubali kukosewa?+ Je, si afadhali mkubali kupunjwa? 8 Badala yake, mnawakosea na kuwapunja, tena ndugu zenu!
9 Au je, hamjui kwamba watu wasio waadilifu hawataurithi Ufalme wa Mungu?+ Msipotoshwe.* Waasherati,*+ waabudu-sanamu,+ wazinzi,+ wanaume wanaofanya ngono na wanaume,*+ 10 wezi, watu wenye pupa,+ walevi,+ watukanaji,* na wanyang’anyi hawataurithi Ufalme wa Mungu.+ 11 Na bado baadhi yenu mlikuwa hivyo. Lakini mmeoshwa mkawa safi;+ mmetakaswa;+ mmetangazwa kuwa waadilifu+ katika jina la Bwana Yesu Kristo na kwa roho ya Mungu wetu.
12 Mambo yote ni halali* kwangu, lakini si mambo yote yenye faida.+ Mambo yote ni halali kwangu, lakini sitaruhusu kitu chochote kinitawale.* 13 Chakula ni kwa ajili ya tumbo, na tumbo ni kwa ajili ya chakula, lakini Mungu atavifanya vyote viwe si kitu.+ Mwili si kwa ajili ya uasherati,* bali ni kwa ajili ya Bwana,+ na Bwana ni kwa ajili ya mwili. 14 Lakini Mungu alimfufua Bwana+ na pia atatufufua sisi kutoka kwenye kifo+ kupitia nguvu zake.+
15 Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya Kristo?+ Basi, je, nivichukue viungo vya Kristo na kuviunganisha na kahaba? La hasha! 16 Je, hamjui kwamba yeyote ambaye ameungana na kahaba ni mwili mmoja naye? Kwa maana yeye anasema, “hao wawili watakuwa mwili mmoja.”+ 17 Lakini yeyote anayeungana na Bwana ana umoja naye katika roho.+ 18 Ukimbieni uasherati!*+ Dhambi nyingine yoyote ambayo huenda mtu akafanya iko nje ya mwili wake, lakini yeyote aliye na mazoea ya kufanya uasherati anautendea dhambi mwili wake mwenyewe.+ 19 Je, hamjui kwamba mwili wenu ni hekalu+ la roho takatifu ndani yenu, mliyopokea kutoka kwa Mungu?+ Pia, ninyi si mali yenu wenyewe,+ 20 kwa maana mlinunuliwa kwa bei.+ Kwa vyovyote, mtukuzeni Mungu+ katika mwili wenu.+
7 Basi kuhusu mambo ambayo mliandika, ni bora mwanamume asimguse* mwanamke; 2 lakini kwa sababu ya kuenea kwa uasherati,* kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe+ na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.+ 3 Mume na ampe mke wake haki yake, na mke pia na amfanyie vivyo hivyo mume wake.+ 4 Mke hana mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, bali mume wake anayo; vivyo hivyo, mume hana mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, bali mke wake anayo. 5 Msiwe mkinyimana ila kwa makubaliano kwa wakati uliowekwa, ili mtenge wakati kwa ajili ya sala na mje pamoja tena, ili Shetani asiendelee kuwajaribu kwa sababu mnakosa kujizuia.* 6 Hata hivyo, ninasema hilo ili kuwapa ruhusa, bali si amri. 7 Lakini ningependa watu wote wawe kama mimi nilivyo. Hata hivyo, kila mmoja ana zawadi yake+ mwenyewe kutoka kwa Mungu, mmoja kwa njia hii, mwingine kwa njia ile.
8 Sasa ninawaambia waseja na wajane, ni bora wabaki kama mimi nilivyo.+ 9 Lakini ikiwa hawawezi kujizuia,* acheni wafunge ndoa, kwa maana ni bora kufunga ndoa kuliko kuwaka tamaa.+
10 Kwa watu waliofunga ndoa ninatoa maagizo, si mimi bali ni Bwana, kwamba mke hapaswi kutengana na mume wake.+ 11 Lakini wakitengana, abaki bila kuolewa la sivyo apatane tena na mume wake; na mume hapaswi kumwacha mke wake.+
12 Lakini kwa wale wengine ninawaambia, ndiyo, mimi, si Bwana:+ Ikiwa ndugu yeyote ana mke asiyeamini na mke huyo anakubali kuishi pamoja naye, basi asimwache; 13 na ikiwa mwanamke ana mume asiyeamini na mume huyo anakubali kuishi pamoja naye, basi asimwache mume wake. 14 Kwa maana mume asiyeamini hutakaswa kuhusiana na mke wake, na mke asiyeamini hutakaswa kuhusiana na huyo ndugu; la sivyo, watoto wenu hawangekuwa safi, lakini sasa wao ni watakatifu. 15 Lakini yule asiyeamini akiamua kuondoka,* acha aondoke; ndugu au dada hajafungwa chini ya hali kama hizo, lakini Mungu amewaita ninyi kwenye amani.+ 16 Wewe mke, unajuaje kama utamwokoa mume wako?+ Au wewe mume, unajuaje kama utamwokoa mke wako?
17 Hata hivyo, kama Yehova* alivyompa kila mmoja fungu, kila mmoja na ajiendeshe kama Mungu alivyomwita.+ Ninatoa agizo hilo katika makutaniko yote. 18 Je, mtu yeyote aliitwa akiwa tayari ametahiriwa?+ Basi asibadili kutahiriwa kwake. Je, mtu yeyote ameitwa akiwa hajatahiriwa? Basi asitahiriwe.+ 19 Kutahiriwa hakuna maana, wala kutotahiriwa hakuna maana;+ lakini kushika amri za Mungu kuna maana.+ 20 Basi katika hali yoyote ambayo kila mmoja aliitwa, acheni abaki hivyo.+ 21 Je, uliitwa ukiwa mtumwa? Usiache hilo likuhangaishe;+ lakini ikiwa unaweza kuwa huru, basi tumia nafasi hiyo. 22 Kwa maana yeyote aliyeitwa katika Bwana akiwa mtumwa ni mtu aliyewekwa huru wa Bwana;+ vivyo hivyo yeyote aliyeitwa akiwa mtu aliye huru ni mtumwa wa Kristo. 23 Mlinunuliwa kwa bei;+ acheni kuwa watumwa wa wanadamu. 24 Akina ndugu, katika hali yoyote ambayo kila mmoja aliitwa, acheni abaki hivyo mbele za Mungu.
25 Sasa kuhusu mabikira,* sina amri kutoka kwa Bwana, lakini ninatoa maoni yangu+ nikiwa mtu aliyeonyeshwa rehema na Bwana kuwa mwaminifu. 26 Kwa hiyo, ninaona ni bora kwa mtu kuendelea kama alivyo kwa sababu ya ugumu uliopo. 27 Je, umefungwa kwa mke? Acha kutafuta kufunguliwa.+ Je, umewekwa huru kutoka kwa mke? Acha kutafuta mke. 28 Lakini hata kama ukifunga ndoa, hutakuwa ukifanya dhambi. Na kama bikira akifunga ndoa, mtu huyo hatakuwa akifanya dhambi. Hata hivyo, wale wanaofanya hivyo watakuwa na dhiki katika mwili wao. Lakini ninajaribu kuwaepusha ninyi.
29 Isitoshe, ninasema hivi akina ndugu, wakati uliobaki umepungua.+ Tangu sasa wale walio na wake na wawe kana kwamba hawana, 30 na wale wanaolia wawe kama wale wasiolia, na wale wanaoshangilia wawe kama wale wasioshangilia, na wale wanaonunua wawe kama wale wasio na kitu, 31 na wale wanaoutumia ulimwengu wawe kama wale wasioutumia kwa ukamili; kwa maana tamasha ya ulimwengu huu inabadilika. 32 Kwa kweli, ninataka msihangaike. Mwanamume ambaye hajaoa huhangaikia mambo ya Bwana, jinsi anavyoweza kupata kibali cha* Bwana. 33 Lakini mwanamume aliyeoa huhangaikia mambo ya ulimwengu,+ jinsi anavyoweza kupata kibali cha* mke wake, 34 naye amegawanyika. Zaidi ya hayo, mwanamke ambaye hajaolewa, na vilevile bikira, huhangaikia mambo ya Bwana,+ ili awe mtakatifu katika mwili wake na pia katika roho yake. Hata hivyo, mwanamke aliyeolewa huhangaikia mambo ya ulimwengu, jinsi anavyoweza kupata kibali cha* mume wake. 35 Lakini ninasema hivyo kwa faida yenu wenyewe, si ili niwazuie,* bali niwachochee kufanya jambo linalofaa na kumtumikia Bwana daima bila kukengeushwa fikira.
36 Lakini kama yeyote akiona kwamba anajiendesha isivyofaa kwa kubaki mseja,* na ikiwa amepita upeo wa ujana, basi inapaswa kuwa hivi: Acheni afanye anavyotaka; hafanyi dhambi. Acheni afunge ndoa.+ 37 Hata hivyo ikiwa yeyote ametulia moyoni mwake, na hana uhitaji wowote, lakini ana mamlaka juu ya nia yake mwenyewe naye amefanya uamuzi moyoni mwake kubaki mseja,* atafanya vema.+ 38 Vivyo hivyo yeyote anayefunga ndoa* anafanya vema, lakini yeyote asiyefunga ndoa atafanya vema zaidi.+
39 Mke amefungwa kwa muda wote ambao mume wake yuko hai.+ Lakini mume wake akilala usingizi katika kifo, yuko huru kuolewa na yeyote anayemtaka, katika Bwana tu.+ 40 Lakini kwa maoni yangu, mwanamke huyo atakuwa na furaha zaidi akibaki kama alivyo; na ninafikiri mimi pia nina roho ya Mungu.
8 Basi kuhusu chakula kilichotolewa kwa sanamu:+ Tunajua sote tuna ujuzi.+ Ujuzi huleta majivuno, lakini upendo hujenga.+ 2 Yeyote akifikiri anajua jambo fulani, bado hajalijua kama anavyopaswa kulijua. 3 Lakini ikiwa yeyote anampenda Mungu, huyo anajulikana naye.
4 Sasa kuhusu kula chakula kilichotolewa kwa sanamu, tunajua kwamba sanamu si kitu+ ulimwenguni na kwamba hakuna Mungu isipokuwa mmoja.+ 5 Kwa maana hata ingawa kuna wale wanaoitwa miungu, iwe ni mbinguni au duniani,+ kama vile kulivyo na “miungu” mingi na “mabwana” wengi, 6 kwa kweli kwetu kuna Mungu mmoja+ aliye Baba,+ ambaye vitu vyote vimetoka kwake na sisi kwa ajili yake;+ na kuna Bwana mmoja, Yesu Kristo, ambaye vitu vyote vimepitia kwake+ na sisi kupitia kwake.
7 Hata hivyo, si watu wote walio na ujuzi huu.+ Lakini wengine, kwa sababu zamani waliabudu sanamu, wanakula chakula kama kitu kilichotolewa dhabihu kwa sanamu,+ na dhamiri yao, kwa kuwa ni dhaifu, inatiwa unajisi.+ 8 Lakini chakula hakitafanya tumkaribie zaidi Mungu;+ hatupotezi chochote tusipokula, wala hatuongezi chochote tunapokula.+ 9 Lakini endeleeni kujihadhari kwamba haki yenu ya kuchagua isije ikawa kwa njia fulani kikwazo kwa wale walio dhaifu.+ 10 Kwa maana yeyote akikuona wewe uliye na ujuzi ukila mlo katika hekalu la sanamu, je, dhamiri ya huyo aliye dhaifu haitapata ujasiri kufikia hatua ya kula chakula kilichotolewa kwa sanamu? 11 Basi, kwa ujuzi wako, mtu ambaye ni dhaifu anaharibiwa, ndugu yako ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.+ 12 Mnapowatendea dhambi ndugu zenu katika njia hii na kuiumiza dhamiri yao dhaifu,+ mnamtendea dhambi Kristo. 13 Kwa sababu hiyo, ikiwa chakula kinamkwaza ndugu yangu, mimi sitakula nyama tena kamwe, ili nisije nikamkwaza ndugu yangu.+
9 Je, mimi siko huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sijamwona Yesu Bwana wetu?+ Je, ninyi si kazi yangu katika Bwana? 2 Hata kama mimi si mtume kwa wengine, hakika mimi ni mtume kwenu! Kwa maana ninyi ndio muhuri unaothibitisha utume wangu katika Bwana.
3 Kwa wale wanaonichunguza, ninajitetea hivi: 4 Sisi tuna haki* ya kula na kunywa, sivyo? 5 Sisi tuna haki ya kuambatana na mke ambaye ni mwamini,*+ kama wale mitume wengine na ndugu za Bwana+ na Kefa,*+ sivyo? 6 Au je, ni Barnaba+ na mimi pekee ambao hatuna haki ya kupata riziki bila kufanya kazi? 7 Ni mwanajeshi gani ambaye hutumika kwa gharama yake mwenyewe? Ni nani anayepanda shamba la mizabibu naye asile matunda yake?+ Au ni nani anayechunga mifugo naye asinywe maziwa ya mifugo yake?
8 Je, ninasema mambo haya kwa maoni ya kibinadamu? Au je, Sheria haisemi mambo hayo pia? 9 Kwa maana imeandikwa katika Sheria ya Musa: “Hupaswi kumfunga kinywa ng’ombe dume anapopura nafaka.”+ Je, ng’ombe dume ndio Mungu anaohangaikia? 10 Au, je, kweli anasema hivyo kwa ajili yetu? Kwa hakika hilo liliandikwa kwa ajili yetu, kwa sababu mtu anayelima na mtu anayepura anapaswa kufanya hivyo akiwa na tumaini la kupata fungu.
11 Ikiwa tumepanda vitu vya kiroho miongoni mwenu, je, ni jambo kubwa tukivuna kutoka kwenu vitu vya kimwili?+ 12 Ikiwa watu wengine wana haki ya kuwadai ninyi jambo hilo, je, sisi hatuna haki hiyo hata zaidi? Hata hivyo, hatujatumia haki* hii,+ bali tunavumilia mambo yote, ili kwa vyovyote tusiizuie habari njema kumhusu Kristo.+ 13 Je, hamjui kwamba watu wanaofanya kazi takatifu hula vitu vya hekalu, na kwamba wale wanaohudumu kwa kawaida kwenye madhabahu hupata fungu lao kutoka kwenye madhabahu?+ 14 Vivyo hivyo, pia, Bwana aliamuru kwamba wale wanaotangaza habari njema waishi kupitia habari njema.+
15 Lakini kati ya mipango hiyo sijatumia hata mmoja.+ Kwa kweli, sijaandika mambo haya ili nifanyiwe jambo hilo, kwa maana ingekuwa bora kwangu kufa kuliko—hakuna mtu atakayeondoa sababu zangu za kujisifu!+ 16 Sasa ikiwa ninatangaza habari njema, hiyo si sababu ya kufanya nijisifu, kwa maana nimewekewa sharti. Kwa kweli, ole wangu nisipotangaza habari njema!+ 17 Nikifanya hivyo kwa kupenda, nina thawabu; lakini hata nikifanya hivyo bila kupenda, bado nimekabidhiwa usimamizi.+ 18 Basi, thawabu yangu ni nini? Kwamba ninapotangaza habari njema, niitoe habari njema bila gharama, ili nisitumie vibaya mamlaka* yangu katika habari njema.
19 Kwa maana, ingawa niko huru kutoka kwa watu wote, nimejifanya kuwa mtumwa kwa wote, ili niwapate watu wengi iwezekanavyo. 20 Kwa Wayahudi nilikuwa kama Myahudi, ili niwapate Wayahudi;+ kwa wale walio chini ya sheria nilikuwa kama aliye chini ya sheria, ingawa mimi mwenyewe siko chini ya sheria, ili niwapate wale walio chini ya sheria.+ 21 Kwa wale wasio na sheria nilikuwa kama asiye na sheria, ingawa mimi siko bila sheria kwa Mungu bali niko chini ya sheria kwa Kristo,+ ili niwapate wale wasio na sheria. 22 Kwa walio dhaifu nilikuwa dhaifu, ili niwapate walio dhaifu.+ Nimekuwa mambo yote kwa watu wa namna zote, ili kwa vyovyote niwaokoe wengine. 23 Lakini ninafanya mambo yote kwa ajili ya habari njema, ili niishiriki pamoja na wengine.+
24 Je, hamjui kwamba wakimbiaji wote katika mbio hukimbia, lakini ni mmoja tu anayepokea tuzo? Kimbieni kwa njia itakayowawezesha kushinda tuzo.+ 25 Sasa kila mtu anayeshiriki katika shindano* hujizuia* katika mambo yote. Bila shaka, wao hushindana ili wapate taji linaloweza kuharibika,+ lakini sisi taji lisiloharibika.+ 26 Kwa hiyo, jinsi ninavyokimbia si bila kusudi;+ jinsi ninavyoelekeza ngumi zangu ni ili nisiwe nikipiga hewa; 27 lakini ninaupigapiga* mwili wangu+ na kuuongoza kama mtumwa, ili baada ya kuwahubiria wengine, kwa njia fulani mimi mwenyewe nisikataliwe.*
10 Basi akina ndugu, ninataka mjue kwamba mababu zetu wote walikuwa chini ya wingu+ na wote walipita katika bahari+ 2 na wote walibatizwa katika Musa kupitia wingu na bahari, 3 na wote walikula chakula kilekile cha kiroho+ 4 na wote walikunywa maji yaleyale ya kiroho.+ Kwa maana walikuwa wakinywa kutokana na mwamba wa kiroho uliowafuata, na mwamba huo ulimaanisha* Kristo.+ 5 Hata hivyo, Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa maana waliangamizwa nyikani.+
6 Basi mambo hayo yalikuwa vielelezo kwetu, ili tusitamani mambo mabaya, kama wao walivyotamani.+ 7 Wala tusiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyofanya; kama ilivyoandikwa: “Watu wakaketi ili wale na kunywa. Kisha wakasimama ili wajitumbuize.”+ 8 Wala tusifanye uasherati,* kama baadhi yao walivyofanya uasherati,* na 23,000 kati yao wakaanguka kwa siku moja.+ 9 Wala tusimjaribu Yehova,*+ kama baadhi yao walivyomjaribu, wakaangamizwa na nyoka.+ 10 Wala tusiwe wanung’unikaji,+ kama baadhi yao walivyonung’unika, wakaangamizwa na mwangamizaji.+ 11 Basi mambo hayo yaliwapata ili kuwa vielelezo, nayo yaliandikwa ili kuwa onyo kwetu sisi+ ambao tumefikiwa na miisho ya mifumo ya mambo.
12 Basi yule anayefikiri amesimama na ajihadhari asije akaanguka.+ 13 Hakuna majaribu ambayo yamewapata ninyi ila yale yaliyo ya kawaida kwa watu.+ Lakini Mungu ni mwaminifu, naye hatawaacha mjaribiwe kupita mnavyoweza kuhimili,+ bali pamoja na majaribu hayo ataifanya pia njia ya kutokea ili mweze kuyavumilia.+
14 Kwa hiyo, wapendwa wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.+ 15 Ninasema kana kwamba ni kwa watu wenye utambuzi; hukumuni wenyewe lile ninalosema. 16 Kikombe cha baraka ambacho tunabariki, je, si kushiriki katika damu ya Kristo?+ Mkate ambao tunamega, je, si kushiriki katika mwili wa Kristo?+ 17 Kwa sababu kuna mkate mmoja, sisi, ingawa tuko wengi, ni mwili mmoja,+ kwa maana sote tunakula mkate huo mmoja.
18 Tazameni Israeli kwa njia ya kimwili: Je, wale wanaokula dhabihu si washiriki pamoja na madhabahu?+ 19 Basi, niseme nini? Je, kile kilichotolewa dhabihu kwa sanamu ni kitu, au je, sanamu ni kitu? 20 Hapana; bali ninasema kwamba vitu ambavyo mataifa huvitoa dhabihu, wao huvitoa dhabihu kwa roho waovu, si kwa Mungu;+ nami sitaki muwe washiriki pamoja na roho waovu.+ 21 Hamwezi kuwa mkinywa kikombe cha Yehova* na kikombe cha roho waovu; hamwezi kuwa mkishiriki “meza ya Yehova”*+ na meza ya roho waovu. 22 Au je, ‘tunamchochea Yehova* kuwa na wivu’?+ Je, sisi tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
23 Mambo yote ni halali,* lakini si mambo yote yaliyo na faida. Mambo yote ni halali, lakini si mambo yote yanayojenga.+ 24 Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali faida ya yule mtu mwingine.+
25 Kuleni chochote kinachouzwa katika soko la nyama, bila kuchunguza kwa sababu ya dhamiri yenu, 26 kwa maana “dunia na vyote vilivyomo ni vya Yehova.”*+ 27 Mtu asiyeamini akiwaalika nanyi mtake kwenda, kuleni chochote kinachowekwa mbele yenu, bila kuchunguza kwa sababu ya dhamiri yenu. 28 Lakini yeyote akiwaambia, “Hiki ni kitu kilichotolewa katika dhabihu,” msile kwa sababu ya yule aliyewaambia na kwa sababu ya dhamiri.+ 29 Simaanishi dhamiri yako mwenyewe, bali ya yule mtu mwingine. Kwa maana kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?+ 30 Ikiwa ninakula nikiwa na shukrani, kwa nini nitukanwe juu ya kile ninachotolea shukrani?+
31 Kwa hiyo, iwe mnakula au mnakunywa au mnafanya jambo lingine lolote, fanyeni mambo yote kwa utukufu wa Mungu.+ 32 Epukeni kuwa vikwazo kwa Wayahudi na vilevile kwa Wagiriki na kwa kutaniko la Mungu,+ 33 kama vile ninavyojaribu kuwapendeza watu wote katika mambo yote, bila kutafuta faida yangu mwenyewe,+ bali faida ya walio wengi, ili wapate kuokolewa.+
11 Iweni waigaji wangu, kama vile mimi nilivyo mwigaji wa Kristo.+
2 Ninawapongeza kwa sababu katika mambo yote mnanikumbuka na mnayashika mapokeo kama vile nilivyowapa. 3 Lakini ninataka mjue kwamba kichwa cha kila mwanamume ni Kristo;+ nacho kichwa cha mwanamke ni mwanamume;+ nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.+ 4 Kila mwanamume ambaye husali au kutoa unabii akiwa na kitu juu ya kichwa chake hukiaibisha kichwa chake; 5 lakini kila mwanamke anayesali au kutoa unabii+ bila kufunika kichwa chake anakiaibisha kichwa chake, kwa maana ni kana kwamba yeye ni mwanamke mwenye kichwa kilichonyolewa. 6 Kwa maana ikiwa mwanamke hajifuniki, anapaswa kukatwa nywele zake; lakini ikiwa ni aibu kwa mwanamke kukatwa nywele au kunyolewa, anapaswa ajifunike.
7 Kwa maana mwanamume hapaswi kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano na utukufu wa Mungu,+ lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume. 8 Kwa maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke alitoka katika mwanamume.+ 9 Isitoshe, mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume.+ 10 Ndiyo sababu mwanamke anapaswa kuwa na ishara ya mamlaka juu ya kichwa chake kwa sababu ya malaika.+
11 Tena, kuhusiana na Bwana, mwanamke hajatenganishwa na mwanamume wala mwanamume hajatenganishwa na mwanamke. 12 Kwa maana kama vile mwanamke alivyotoka katika mwanamume,+ vivyo hivyo pia mwanamume amepitia katika mwanamke; lakini vitu vyote vimetoka kwa Mungu.+ 13 Hukumuni wenyewe: Je, inafaa mwanamke kusali kwa Mungu bila kufunika kichwa chake? 14 Je, maumbile yenyewe hayawafundishi kwamba nywele ndefu ni aibu kwa mwanamume, 15 lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu, ni utukufu kwake? Kwa maana amepewa nywele zake ziwe kitu cha kujifunika. 16 Hata hivyo, mtu yeyote akitaka kubishania desturi nyingine, sisi hatuna nyingine, wala makutaniko ya Mungu.
17 Lakini ninapoyatoa maagizo haya, siwapongezi ninyi, kwa sababu mnakutana pamoja, si kwa ajili ya wema, bali kwa ajili ya ubaya. 18 Kwanza kabisa, nasikia kwamba mnapokutana katika kutaniko, kuna migawanyiko kati yenu; na kwa kadiri fulani ninaamini jambo hilo. 19 Kwa maana lazima kutakuwa na madhehebu miongoni mwenu,+ ili wale waliokubaliwa kati yenu waonekane.
20 Mnapokutana mahali pamoja, kwa kweli si kwa sababu ya kula Mlo wa Jioni wa Bwana.+ 21 Kwa maana mnapokula, kila mtu hutangulia kula mlo wake mwenyewe wa jioni, hivi kwamba mmoja ana njaa lakini mwingine amelewa. 22 Je, hamna nyumba ambamo mnaweza kula na kunywa? Au je, mnalidharau kutaniko la Mungu na kuwaaibisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini ninyi? Je, niwapongeze? Kuhusu hilo siwapongezi.
23 Kwa maana nilipokea kutoka kwa Bwana kile nilichowapa ninyi pia, kwamba Bwana Yesu katika usiku+ ambao alisalitiwa alichukua mkate, 24 na baada ya kutoa shukrani, akaumega na kusema: “Huu unamaanisha mwili wangu,+ ambao ni kwa ajili yenu. Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.”+ 25 Akafanya vivyo hivyo na kile kikombe+ pia, baada ya wao kula mlo wa jioni, akisema: “Kikombe hiki kinamaanisha agano+ jipya kwa msingi wa damu yangu.+ Endeleeni kufanya hivi, kila mara mnapokinywa, kwa kunikumbuka mimi.”+ 26 Kwa maana kila mara mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mnaendelea kukitangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja.
27 Kwa hiyo, yeyote anayekula mkate au kukinywa kikombe cha Bwana isivyofaa atakuwa na hatia kuhusiana na mwili na damu ya Bwana. 28 Kwanza, acheni mtu ajichunguze mwenyewe na kuona kama anafaa,+ ndipo ale mkate na anywe kikombe. 29 Kwa maana yule anayekula na kunywa bila kuutambua mwili, anakula na kunywa hukumu dhidi yake mwenyewe. 30 Ndiyo sababu wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengi wamelala usingizi katika kifo.*+ 31 Lakini kama tungetambua jinsi sisi wenyewe tulivyo, hatungehukumiwa. 32 Hata hivyo, tunapohukumiwa, Yehova*+ anatutia nidhamu, ili tusihukumiwe pamoja na ulimwengu.+ 33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana pamoja ili kula mlo huo, mngojeane. 34 Ikiwa yeyote ana njaa, acheni ale nyumbani, ili mnapokutana pamoja isiwe kwa ajili ya kuhukumiwa.+ Lakini kuhusu mambo yaliyobaki, nitayarekebisha nitakapofika.
12 Basi kuhusu zawadi za kiroho,+ akina ndugu, sitaki mkose kujua. 2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wa mataifa,* mlikuwa mkishawishiwa na kuziabudu sanamu zisizo na sauti,+ mkizifuata popote zilipowaongoza. 3 Sasa ningetaka mjue kwamba hakuna mtu yeyote ambaye anaposema kwa roho ya Mungu, husema: “Yesu amelaaniwa!” na hakuna mtu anayeweza kusema: “Yesu ni Bwana!” isipokuwa kwa roho takatifu.+
4 Basi kuna zawadi mbalimbali, lakini kuna roho ileile;+ 5 na kuna huduma mbalimbali,+ na bado kuna Bwana yuleyule; 6 na kuna utendaji* mbalimbali, na bado ni Mungu yuleyule anayefanya utendaji huo wote katika kila mtu.+ 7 Lakini roho hufunuliwa katika kila mmoja kwa kusudi lenye faida.+ 8 Kwa maana mtu mmoja hupewa maneno ya* hekima kupitia roho, mwingine maneno ya ujuzi kulingana na roho ileile, 9 mwingine imani+ kwa roho ileile, mwingine zawadi za uponyaji+ kwa roho hiyo moja, 10 naye mwingine hupewa utendaji wa matendo yenye nguvu,+ mwingine kutoa unabii, mwingine utambuzi wa maneno yaliyoongozwa na roho,+ mwingine lugha* mbalimbali,+ na mwingine fasiri ya lugha.+ 11 Lakini ni roho ileile inayofanya utendaji huu wote, ikimgawia kila mmoja kama vile inavyopenda.
12 Kwa maana kama vile mwili ni mmoja lakini una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili huo, ingawa ni vingi, ni mwili mmoja,+ ndivyo pia alivyo Kristo. 13 Kwa maana kwa roho moja sote tulibatizwa katika mwili mmoja, iwe ni Wayahudi au ni Wagiriki, iwe ni watumwa au ni walio huru, nasi sote tulinyweshwa roho moja.
14 Kwa maana kwa kweli, mwili una viungo vingi, si kiungo kimoja.+ 15 Ikiwa mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono, mimi si sehemu ya mwili,” hilo halifanyi usiwe sehemu ya mwili. 16 Na ikiwa sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si sehemu ya mwili,” hilo halilifanyi lisiwe sehemu ya mwili. 17 Ikiwa mwili wote ungekuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Ikiwa wote ungekuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi? 18 Lakini sasa Mungu amepanga kila kiungo cha mwili kama alivyopenda.
19 Ikiwa vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? 20 Lakini sasa viungo ni vingi, lakini mwili mmoja. 21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sikuhitaji wewe,” au tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Siwahitaji ninyi.” 22 Badala yake viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu zaidi ni muhimu sana, 23 na sehemu za mwili ambazo tunafikiri hazistahili kuheshimiwa sana, tunazipa heshima zaidi,+ basi sehemu zetu ambazo hazivutii tunazitendea kwa heshima* zaidi, 24 bali sehemu zetu zinazopendeza hazihitaji kitu chochote. Lakini hivyo ndivyo Mungu alivyouunganisha mwili, akiipa heshima zaidi sehemu iliyokuwa na upungufu, 25 ili kusiwe na mgawanyiko katika mwili, bali viungo vyake vitunzane.+ 26 Kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote huumia pamoja nacho;+ au kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vingine vyote hushangilia pamoja nacho.+
27 Basi ninyi ni mwili wa Kristo,+ na kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.+ 28 Naye Mungu amewaweka watu mbalimbali katika kutaniko: kwanza, mitume;+ pili, manabii;+ tatu, walimu;+ kisha matendo yenye nguvu;+ kisha zawadi za uponyaji;+ huduma za kusaidia; uwezo wa kuelekeza;+ na lugha mbalimbali.+ 29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote hufanya matendo yenye nguvu? 30 Je, wote wana zawadi za uponyaji? Je, wote husema kwa lugha?+ Je, wote ni wakalimani?*+ 31 Lakini endeleeni kutafuta kwa bidii* zawadi zilizo kubwa zaidi.+ Na bado nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.+
13 Nikisema kwa lugha za wanadamu na za malaika lakini sina upendo, nimekuwa chuma kinachovuma au toazi linalolia. 2 Na ikiwa nina zawadi ya kutoa unabii nami ninazielewa siri zote takatifu na ujuzi wote,+ na ikiwa nina imani yenye nguvu hata niweze kuhamisha* milima, lakini sina upendo, mimi si kitu.*+ 3 Nami nikitoa mali zangu zote ili kuwalisha wengine,+ na nikiutoa mwili wangu ili nijisifu, lakini sina upendo,+ sipati faida yoyote.
4 Upendo+ ni wenye subira*+ na fadhili.+ Upendo hauna wivu.+ Haujigambi, haujivuni,+ 5 haujiendeshi bila adabu,+ hautafuti faida zake wenyewe,+ hauchokozeki.+ Hauweki hesabu ya ubaya.*+ 6 Haushangilii ukosefu wa uadilifu,+ bali hushangilia pamoja na kweli. 7 Huhimili mambo yote,+ huamini mambo yote,+ hutumaini mambo yote,+ huvumilia mambo yote.+
8 Upendo haushindwi kamwe. Lakini kama kuna zawadi za unabii, zitaondolewa; kama kuna lugha,* zitakoma; kama kuna ujuzi, utaondolewa. 9 Kwa maana tuna ujuzi usio kamili+ nasi tunatoa unabii usio kamili; 10 lakini kile kilicho kamili kitakapokuja, kile kisicho kamili kitaondolewa. 11 Nilipokuwa mtoto, nilikuwa nikisema kama mtoto, nikifikiri kama mtoto, nikiwaza kama mtoto; lakini kwa kuwa sasa nimekuwa mtu mzima, nimeziacha tabia za mtoto. 12 Kwa maana sasa tunaona kwa njia isiyo ya waziwazi* kupitia kioo cha chuma, lakini wakati huo itakuwa uso kwa uso. Kwa sasa sijui kikamili, lakini wakati huo nitajua kwa usahihi,* kama vile ninavyojulikana kwa usahihi. 13 Hata hivyo, sasa yanabaki mambo haya matatu: imani, tumaini, upendo; lakini lililo kubwa zaidi kati ya hayo ni upendo.+
14 Fuatieni upendo, na bado endeleeni kutafuta kwa bidii* zawadi za kiroho, lakini ni afadhali zaidi kwamba mtoe unabii.+ 2 Kwa maana yule anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu, bali na Mungu, kwa maana hakuna anayesikiliza,+ bali yeye husema kwa roho siri zilizo takatifu.+ 3 Hata hivyo, yule anayetoa unabii huwajenga na kuwatia moyo na kuwafariji watu kwa maneno yake. 4 Yule anayesema kwa lugha hujijenga mwenyewe, lakini yule anayetoa unabii hulijenga kutaniko. 5 Basi ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha,+ lakini ninapendelea zaidi mtoe unabii.+ Kwa kweli, yule anayetoa unabii ni mkubwa kuliko yule anayezungumza kwa lugha, isipokuwa afasiri* kwa ajili ya kutaniko ili lijengwe. 6 Lakini wakati huu, akina ndugu, kama ningekuja kwenu nikisema kwa lugha, ningewapa faida gani kama singezungumza nanyi kwa ufunuo+ au kwa ujuzi+ au kwa unabii au kwa fundisho?
7 Ndivyo ilivyo pia kwa vitu visivyo na uhai ambavyo hutoa sauti, iwe ni filimbi au kinubi. Kusipokuwa na tofauti kati ya sauti, kinachopigwa kwenye filimbi au kwenye kinubi kitajulikanaje? 8 Kwa maana tarumbeta ikipiga mwito usiojulikana, ni nani atakayejitayarisha kwa ajili ya vita? 9 Vivyo hivyo, msiposema maneno yanayoeleweka kwa urahisi kupitia lugha hiyo, watu watajuaje kinachosemwa? Kwa kweli, mtakuwa mkizungumza hewani. 10 Huenda kuna aina nyingi za maneno ulimwenguni, hata hivyo hakuna aina isiyo na maana. 11 Ikiwa sielewi maana ya maneno, nitakuwa mgeni kwa yule anayezungumza, naye anayezungumza atakuwa mgeni kwangu. 12 Nanyi pia, kwa kuwa mnatamani sana zawadi za roho, jitahidini kujawa na zawadi ambazo zitalijenga kutaniko.+
13 Kwa hiyo, yule anayezungumza kwa lugha na asali ili afasiri.*+ 14 Kwa maana ikiwa ninasali kwa lugha, ni zawadi yangu ya roho inayosali, lakini akili yangu haizai matunda. 15 Basi, nini kifanywe? Nitasali kwa zawadi ya roho, lakini nitasali pia kwa akili yangu. Nitaimba sifa kwa zawadi ya roho, lakini pia nitaimba sifa kwa akili yangu. 16 Kama sivyo, ukitoa sifa kwa zawadi ya roho, mtu wa kawaida miongoni mwenu atasemaje “Amina” unapotoa shukrani, kwa kuwa hajui unachosema? 17 Kweli, unatoa shukrani kwa njia nzuri, lakini yule mtu mwingine hajengwi. 18 Ninamshukuru Mungu kwamba ninasema kwa lugha nyingi kuliko ninyi nyote. 19 Hata hivyo, katika kutaniko afadhali niseme maneno matano kwa akili yangu,* ili pia niwafundishe* wengine, kuliko maneno elfu kumi kwa lugha.+
20 Akina ndugu, msiwe watoto wadogo katika uelewaji wenu,+ lakini iweni watoto wadogo kuhusiana na ubaya;+ nanyi muwe watu wazima katika uelewaji wenu.+ 21 Katika Sheria imeandikwa: “‘Nitazungumza na watu hawa kwa lugha za watu wa kigeni na kwa midomo ya wageni, na hata wakati huo watakataa kunisikiliza,’ asema Yehova.”*+ 22 Kwa hiyo, lugha si ishara kwa ajili ya waamini bali kwa wasio waamini,+ lakini unabii si kwa ajili ya wasio waamini bali ni kwa ajili ya waamini. 23 Basi kutaniko lote likikusanyika mahali pamoja na wote waseme kwa lugha, nao watu wa kawaida au wasio waamini waingie, je, hawatasema kwamba ninyi mmerukwa na akili? 24 Lakini ikiwa nyote mnatoa unabii na mtu asiye mwamini au mtu wa kawaida aingie, atakaripiwa na kuchunguzwa na wote. 25 Siri za moyo wake zitakuwa wazi, hivi kwamba ataanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu, akitangaza: “Kwa kweli Mungu yupo kati yenu.”+
26 Basi, tuseme nini akina ndugu? Mnapokusanyika pamoja, mmoja ana zaburi, mwingine ana fundisho, mwingine ana ufunuo, mwingine ana lugha, na mwingine ana fasiri.+ Mambo yote na yatendeke kwa ajili ya kujenga. 27 Mtu akisema kwa lugha, na wawe wawili au wasizidi watatu, na wafanye hivyo kwa zamu, na lazima mtu fulani afasiri.*+ 28 Lakini ikiwa hakuna mkalimani,* anapaswa kukaa kimya kutanikoni na kuzungumza moyoni mwake na kwa Mungu. 29 Manabii+ wawili au watatu na wazungumze, na wale wengine watambue maana. 30 Lakini ikiwa mwingine anapokea ufunuo akiwa ameketi hapo, msemaji wa kwanza anapaswa kukaa kimya. 31 Kwa maana nyote mnaweza kutoa unabii kila mtu kwa wakati wake, ili wote wajifunze na wote watiwe moyo.+ 32 Na zawadi za roho ya manabii zinapaswa kuelekezwa na manabii. 33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni wa amani.+
Kama ilivyo katika makutaniko yote ya watakatifu, 34 wanawake na wakae kimya katika makutaniko, kwa maana hawaruhusiwi kuzungumza.+ Badala yake, na wajitiishe,+ kama vile Sheria inavyosema pia. 35 Ikiwa wanataka kujifunza jambo fulani, acheni wawaulize waume zao nyumbani, kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kutanikoni.
36 Je, neno la Mungu lilitoka kwenu, au liliwafikia ninyi peke yenu?
37 Ikiwa yeyote anafikiri yeye ni nabii au amepewa zawadi ya roho, anapaswa kutambua kwamba mambo ninayowaandikia ni amri ya Bwana. 38 Lakini yeyote akiyapuuza, yeye pia atapuuzwa.* 39 Basi ndugu zangu, endeleeni kujitahidi kutoa unabii,+ na bado msikataze kusema kwa lugha.+ 40 Lakini mambo yote na yatendeke kwa adabu na kwa mpango.*+
15 Basi akina ndugu, ninawakumbusha kuhusu habari njema niliyowatangazia,+ nanyi mkaipokea pia, na mmechukua msimamo kwa ajili yake. 2 Kupitia hiyo ninyi pia mnaokolewa ikiwa mtaishika sana habari njema niliyowatangazia, isipokuwa iwe mlikuwa waamini bila kusudi.
3 Kwa maana kati ya mambo ya kwanza niliyowapa ni yale niliyopokea pia, kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kulingana na Maandiko;+ 4 na kwamba alizikwa,+ ndiyo, kwamba alifufuliwa+ siku ya tatu+ kulingana na Maandiko;+ 5 na kwamba alimtokea Kefa,*+ kisha wale 12.+ 6 Baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya 500 kwa wakati mmoja,+ na wengi kati yao bado tuko nao, ingawa wengine wamelala usingizi katika kifo. 7 Baadaye alimtokea Yakobo,+ kisha mitume wote.+ 8 Lakini mwisho kabisa alinitokea mimi pia+ kana kwamba kwa yule aliyezaliwa kabla ya wakati wake.
9 Kwa maana mimi ni mdogo zaidi kati ya mitume, nami sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kutaniko la Mungu.+ 10 Lakini kwa fadhili zisizostahiliwa za Mungu mimi niko kama nilivyo. Na fadhili zake zisizostahiliwa kwangu hazikuwa za bure, bali nilifanya kazi zaidi yao wote; lakini si mimi bali ni fadhili zisizostahiliwa za Mungu zilizo pamoja nami. 11 Iwe ni mimi au ni wao, hivi ndivyo tunavyohubiri, na hivyo ndivyo mlivyoamini.
12 Basi ikiwa inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu,+ kwa nini wengine kati yenu wanasema hakuna ufufuo wa wafu? 13 Kwa kweli, ikiwa hakuna ufufuo wa wafu, basi Kristo hakufufuliwa. 14 Lakini ikiwa Kristo hakufufuliwa, hakika kuhubiri kwetu ni bure, na imani yenu pia ni bure. 15 Isitoshe, tunaonekana pia kuwa mashahidi wa uwongo wa Mungu,+ kwa sababu tumetoa ushahidi dhidi ya Mungu kwa kusema kwamba alimfufua Kristo,+ ambaye hakumfufua ikiwa kwa kweli wafu hawatafufuliwa. 16 Kwa maana ikiwa wafu hawatafufuliwa, basi Kristo hakufufuliwa. 17 Isitoshe, ikiwa Kristo hakufufuliwa, imani yenu ni bure; nanyi mnabaki katika dhambi zenu.+ 18 Basi pia, wale ambao wamelala usingizi katika kifo wakiwa katika muungano na Kristo wameangamia.+ 19 Ikiwa ni katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi ndio wa kusikitikiwa kuliko mtu yeyote.
20 Lakini sasa Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, akiwa matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.+ 21 Kwa kuwa kifo kilikuja kupitia mwanadamu,+ ufufuo wa wafu pia unakuja kupitia mwanadamu.+ 22 Kwa maana kama vile katika Adamu wote wanakufa,+ vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywa kuwa hai.+ 23 Lakini kila mmoja kwa mpangilio wake unaofaa: Kristo aliye matunda ya kwanza,+ baadaye wale walio wa Kristo wakati wa kuwapo kwake.+ 24 Kisha, mwisho, atakapoukabidhi Ufalme kwa Mungu wake aliye Baba yake, atakapokuwa ameangamiza serikali yote na mamlaka yote na nguvu zote.+ 25 Kwa maana lazima atawale akiwa mfalme mpaka Mungu atakapoweka maadui wote chini ya miguu yake.+ 26 Na adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.+ 27 Kwa maana Mungu “alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake.”+ Lakini anaposema ‘vitu vyote vimetiishwa,’+ ni wazi kwamba hilo halimhusu Yule aliyevitiisha vitu vyote chini yake.+ 28 Lakini vitu vyote vitakapotiishwa kwake, ndipo Mwana mwenyewe atakapojitiisha pia kwa Yule aliyevitiisha vitu vyote kwake,+ ili Mungu awe vitu vyote kwa kila mtu.+
29 Kama sivyo, watafanya nini wale wanaobatizwa kwa kusudi la kuwa wafu?+ Ikiwa wafu hawatafufuliwa kamwe, kwa nini basi wanabatizwa kwa kusudi la kuwa hivyo? 30 Kwa nini sisi pia tumo hatarini kila saa?*+ 31 Ninakabili kifo kila siku. Hili ni hakika kama ilivyo furaha yangu kwenu, akina ndugu, niliyo nayo katika Kristo Yesu Bwana wetu. 32 Ikiwa kama watu wengine,* nimepigana na wanyama wa mwituni huko Efeso,+ hilo lina faida gani kwangu? Ikiwa wafu hawatafufuliwa, “acheni tule na tunywe, kwa maana kesho tutakufa.”+ 33 Msipotoshwe. Kushirikiana na watu wabaya huharibu tabia nzuri.*+ 34 Amkeni kwa njia ya uadilifu na msiwe na mazoea ya kufanya dhambi, kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninasema ili kuwafanya mwone aibu.
35 Hata hivyo, mtu fulani atauliza: “Wafu watafufuliwaje? Ndiyo, watakuja wakiwa na mwili wa aina gani?”+ 36 Wewe mtu usiye na akili! Kile unachopanda hakiwi hai isipokuwa kwanza kife. 37 Na kuhusu kile unachopanda, unapanda, si mwili utakaochipuka, bali ni mbegu tu, iwe ya ngano au mbegu ya aina nyingine; 38 lakini Mungu huipa mwili kama anavyopenda na huipa kila mbegu mwili wake. 39 Nyama zote si za aina moja, bali kuna ya wanadamu, kuna nyama ya mifugo, kuna nyama ya ndege, na nyingine ya samaki. 40 Na kuna miili ya mbinguni+ na miili ya duniani;+ lakini utukufu wa miili ya mbinguni ni wa namna moja, na ule wa miili ya duniani ni wa namna nyingine. 41 Utukufu wa jua ni wa namna moja, na utukufu wa mwezi ni mwingine,+ na utukufu wa nyota ni mwingine; kwa kweli, nyota moja hutofautiana na nyota nyingine kwa utukufu.
42 Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutoweza kuharibika.+ 43 Hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika utukufu.+ Hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu.+ 44 Hupandwa ukiwa mwili wa nyama; hufufuliwa ukiwa mwili wa roho. Ikiwa kuna mwili wa nyama, basi kuna mwili wa roho pia. 45 Basi imeandikwa hivi: “Mwanadamu wa kwanza Adamu akawa mtu aliye hai.”*+ Adamu wa mwisho akawa roho inayowapa watu uhai.+ 46 Hata hivyo, ule wa roho si wa kwanza. Ule wa nyama ndio wa kwanza, na baadaye ule wa roho. 47 Mtu wa kwanza ni wa kutoka duniani na ameumbwa kwa mavumbi;+ mtu wa pili ni wa kutoka mbinguni.+ 48 Kama yule aliyeumbwa kwa mavumbi, ndivyo walivyo pia wale walioumbwa kwa mavumbi; na kama alivyo yule wa mbinguni, ndivyo walivyo pia wale wa mbinguni.+ 49 Na kama vile ambavyo tumeuchukua mfano wa yule aliyeumbwa kwa mavumbi,+ vivyo hivyo pia tutauchukua mfano wa yule wa mbinguni.+
50 Lakini ninawaambia hivi, akina ndugu, kwamba nyama na damu haviwezi kuurithi Ufalme wa Mungu, wala uharibifu haurithi kutoweza kuharibika. 51 Tazama! Ninawaambia siri takatifu: Hatutalala usingizi katika kifo sisi sote, bali sote tutabadilishwa,+ 52 kwa muda mfupi, kufumba na kufumbua* jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho. Kwa maana tarumbeta italia,+ na wafu watafufuliwa wakiwa wasioweza kuharibika, nasi tutabadilishwa. 53 Kwa maana huu ulio wa kuharibika lazima uvae kutoweza kuharibika,+ na huu unaoweza kufa lazima uvae kutoweza kufa.+ 54 Lakini huu unaoweza kuharibika utakapovaa kutoweza kuharibika na huu unaoweza kufa utakapovaa kutoweza kufa, ndipo neno hili lililoandikwa litakapotimia: “Kifo kimemezwa milele.”+ 55 “Kifo, uko wapi ushindi wako? Kifo, uko wapi mchomo wako?”+ 56 Mchomo unaotokeza kifo ni dhambi,+ nazo nguvu za dhambi ni Sheria.*+ 57 Lakini tunamshukuru Mungu, kwa maana yeye hutupatia ushindi kupitia Bwana wetu Yesu Kristo!+
58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapendwa, iweni imara,+ thabiti, sikuzote mkiwa na mengi ya kufanya+ katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi yenu si ya bure+ kuhusiana na Bwana.
16 Basi kuhusu mchango kwa ajili ya watakatifu,+ fuateni mwongozo niliotoa kwa makutaniko ya Galatia. 2 Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu anapaswa kuweka kando kitu fulani kulingana na uwezo wake, ili michango isikusanywe nitakapofika. 3 Lakini nitakapofika huko, nitawatuma watu mtakaopendekeza katika barua zenu,+ wapeleke zawadi yenu ya fadhili Yerusalemu. 4 Hata hivyo, ikiwa itafaa mimi niende huko pia, wataenda pamoja nami.
5 Lakini nitakuja kwenu baada ya kupitia Makedonia, kwa maana nitapitia huko Makedonia;+ 6 na labda nitakaa kwa muda au hata nitakaa nanyi kipindi chote cha majira ya baridi, ili mnisindikize umbali fulani kule nitakapoenda. 7 Kwa maana sitaki kuwaona ninyi sasa ninapopita, kwa kuwa natumaini kukaa pamoja nanyi muda fulani,+ Yehova* akiruhusu. 8 Lakini nitakaa Efeso+ mpaka Sherehe ya Pentekoste, 9 kwa sababu nimefunguliwa mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji,+ lakini kuna wapinzani wengi.
10 Sasa Timotheo+ akifika, hakikisheni kwamba haogopi chochote akiwa kati yenu, kwa maana anafanya kazi ya Yehova,*+ kama mimi. 11 Kwa hiyo, mtu yeyote asimdharau. Msindikizeni kwa amani ili aje kwangu, kwa maana ninamsubiri nikiwa pamoja na akina ndugu.
12 Basi kumhusu Apolo+ ndugu yetu, nilimhimiza sana aje kwenu pamoja na akina ndugu. Hakukusudia kuja sasa, lakini atakuja atakapopata nafasi.
13 Kaeni macho,+ simameni imara katika imani,+ endeleeni kuwa kama wanaume,*+ iweni na nguvu.+ 14 Mambo yote mnayofanya yafanyeni kwa upendo.+
15 Sasa ninawahimiza, akina ndugu: Mnajua kwamba nyumba ya Stefana ndiyo matunda ya kwanza ya Akaya na kwamba walijitoa kuwahudumia watakatifu. 16 Endeleeni kujitiisha kwa watu wa aina hiyo na kwa wale wote wanaoshirikiana na kufanya kazi kwa bidii.+ 17 Lakini ninashangilia kuwapo kwa Stefana+ na Fortunato na Akaiko, kwa sababu wamejazia kutokuwapo kwenu hapa. 18 Kwa maana wameiburudisha roho yangu na yenu. Kwa hiyo, watambueni watu wa namna hiyo.
19 Makutaniko ya Asia yanawatumia salamu zao. Akila na Priska pamoja na kutaniko lililo katika nyumba yao+ wanawasalimu kwa moyo mkunjufu katika Bwana. 20 Ndugu wote wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
21 Hii ni salamu yangu, Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe.
22 Ikiwa yeyote hampendi Bwana, mtu huyo na alaaniwe. Njoo, Ee Bwana wetu! 23 Na muwe na fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu. 24 Upendo wangu na uwe pamoja nanyi nyote katika muungano na Kristo Yesu.
Pia anaitwa Petro.
Au “ujanja.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “nitaiweka kando.”
Yaani, mtaalamu wa Sheria.
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Au “kwa viwango vya wanadamu.”
Tnn., “mwili wowote usijisifu.”
Angalia Nyongeza A5.
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Au “hawangemtundika kwenye mti.”
Au “yenye kina.”
Au “tunapounganisha.”
Au “hayapokei.”
Angalia Nyongeza A5.
Au “ wana kusudi moja.”
Au “msimamizi wa kazi mwenye hekima.”
Tnn., “itafunuliwa.”
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Angalia Nyongeza A5.
Pia anaitwa Petro.
Au “wasaidizi.”
Au “baraza la wanadamu.”
Angalia Nyongeza A5.
Au “nimeyahamisha.”
Tnn., “kuwa uchi.”
Au “kupigwa huku na huku.”
Tnn., “tunasihi.”
Au “watunzaji.”
Au “mbinu.”
Angalia Nyongeza A5.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Tnn., “kuwa.”
Au “hamira.”
Au “kuchangamana.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Au “kuchangamana.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Au “mtu anayetumia maneno machafu.”
Au “Msidanganywe.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Au “wanaume wanaotenda au kukubali kutendewa mambo hayo.” Tnn., “wanaume wanaolala na wanaume.”
Au “watu wanaotumia maneno machafu.”
Au “yanakubalika.’
Au “sitakubali kuwa chini ya mamlaka ya kitu chochote.”
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Yaani, asifanye ngono na.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “kujidhibiti; kujiweza.”
Au “kujidhibiti; kujiweza.”
Au “kutengana.”
Angalia Nyongeza A5.
Au “wale ambao hawajawahi kufunga ndoa.”
Au “kumpendeza.”
Au “kumpendeza.”
Au “kumpendeza.”
Tnn., “nisiwawekee mtego.”
Au “kuelekea ubikira wake.”
Au “kuendelea kuwa bikira.”
Au “anayetoa ubikira wake katika ndoa.”
Tnn., “mamlaka.”
Au “kuwa na dada akiwa mke.”
Pia anaitwa Petro.
Tnn., “mamlaka.”
Au “haki.”
Au “kila mwanariadha.”
Au “hujidhibiti.”
Au “ninauadhibu; ninautia nidhamu sana.”
Au “nikose kustahili.”
Au “ulikuwa.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Angalia Nyongeza A5.
Angalia Nyongeza A5.
Angalia Nyongeza A5.
Angalia Nyongeza A5.
Au “yanakubalika.”
Angalia Nyongeza A5.
Inaonekana inamaanisha kifo cha kiroho.
Angalia Nyongeza A5.
Yaani, watu wasio waamini.
Au “kazi.”
Au “ujumbe wa.”
Au “ndimi.”
Au “kiasi.”
Au “watafsiri.”
Au “kujitahidi kupata.”
Au “kusogeza.”
Au “sifai kitu.”
Au “ustahimilivu.”
Au “makosa.”
Yaani, kuzungumza lugha nyingine kimuujiza.
Au “iliyo hafifu.”
Au “kikamili.”
Au “kujitahidi kupata.”
Au “atafsiri.”
Au “atafsiri.”
Au “uelewaji.”
Au “niwafundishe kwa mdomo.”
Angalia Nyongeza A5.
Au “atafsiri.”
Au “mtafsiri.”
Au labda, “Ikiwa yeyote hajui, ataendelea kutojua.”
Au “kwa utaratibu.”
Pia anaitwa Petro.
Au “wakati wote.”
Au labda, “kwa maoni ya kibinadamu.”
Au “hupotosha maadili.”
Au “nafsi iliyo hai.”
Au “kupepesa.”
Au “nayo Sheria huipa dhambi nguvu zake.”
Angalia Nyongeza A5.
Angalia Nyongeza A5.
Au “kuwa jasiri.”