Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • nwt Ezra 1:1-10:44
  • Ezra

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ezra
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Ezra

EZRA

1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi+ wa Uajemi, ili neno la Yehova lililosemwa na Yeremia+ litimie, Yehova aliichochea roho ya Mfalme Koreshi wa Uajemi atoe tangazo katika ufalme wake wote, ambalo pia aliliandika,+ akisema:

2 “Mfalme Koreshi wa Uajemi anasema hivi: ‘Yehova Mungu wa mbinguni amenipa falme zote za dunia,+ naye ameniagiza nimjengee nyumba Yerusalemu, nchini Yuda.+ 3 Yeyote miongoni mwenu, ninyi watu wake wote, Mungu wake na awe pamoja naye, na apande kwenda Yerusalemu, kule Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli—yeye ndiye Mungu wa kweli—ambaye nyumba yake ilikuwa Yerusalemu.* 4 Na mkaaji mgeni yeyote,+ popote alipo, majirani zake* wamsaidie kwa kumpa fedha na dhahabu, mali na wanyama wa kufugwa, pamoja na toleo la hiari kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa kweli,+ iliyokuwa Yerusalemu.’”

5 Ndipo viongozi wa ukoo* wa Yuda na Benjamini na makuhani na Walawi—kila mmoja ambaye roho yake ilichochewa na Mungu wa kweli—wakajitayarisha kupanda kwenda kujenga upya nyumba ya Yehova, iliyokuwa Yerusalemu. 6 Wale wote waliowazunguka wakawasaidia kwa kuwapa* vyombo vya fedha na dhahabu, mali, wanyama wa kufugwa, na vitu vyenye thamani, mbali na matoleo yote ya hiari.

7 Pia, Mfalme Koreshi akaleta vyombo vya nyumba ya Yehova ambavyo Nebukadneza alikuwa amechukua huko Yerusalemu na kuviweka katika nyumba ya mungu wake.+ 8 Mfalme Koreshi wa Uajemi akavikabidhi kwa Mithredathi mweka-hazina ambaye alivihesabu na kumpa Sheshbazari*+ mkuu wa Yuda.

9 Hii ndiyo idadi yake: vyombo 30 vya dhahabu vyenye umbo la kikapu, vyombo 1,000 vya fedha vyenye umbo la kikapu, vyombo 29 vya akiba, 10 mabakuli madogo 30 ya dhahabu, mabakuli madogo 410 ya fedha, vyombo vingine 1,000. 11 Vyombo vyote vya dhahabu na vya fedha vilikuwa 5,400. Sheshbazari alivibeba vyote wakati yeye na watu waliohamishwa+ walipoondoka Babiloni kwenda Yerusalemu.

2 Hawa ndio watu wa mkoa,* baadhi ya mateka waliopanda kutoka uhamishoni,+ ambao Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alikuwa amewapeleka uhamishoni Babiloni+ na ambao baadaye walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye jiji lake,+ 2 wale waliokuja na Zerubabeli,+ Yeshua,+ Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigvai, Rehumu, na Baana.

Idadi ya wanaume Waisraeli ilitia ndani:+ 3 wana wa Paroshi, 2,172; 4 wana wa Shefatia, 372; 5 wana wa Ara,+ 775; 6 wana wa Pahath-moabu,+ wa wana wa Yeshua na Yoabu, 2,812; 7 wana wa Elamu,+ 1,254; 8 wana wa Zatu,+ 945; 9 wana wa Zakai, 760; 10 wana wa Bani, 642; 11 wana wa Bebai, 623; 12 wana wa Azgadi, 1,222; 13 wana wa Adonikamu, 666; 14 wana wa Bigvai, 2,056; 15 wana wa Adini, 454; 16 wana wa Ateri, wa Hezekia, 98; 17 wana wa Besai, 323; 18 wana wa Yora, 112; 19 wana wa Hashumu,+ 223; 20 wana wa Gibari, 95; 21 wana wa Bethlehemu, 123; 22 wanaume wa Netofa, 56; 23 wanaume wa Anathothi,+ 128; 24 wana wa Azmavethi, 42; 25 wana wa Kiriath-yearimu, Kefira na Beerothi, 743; 26 wana wa Rama+ na Geba,+ 621; 27 wanaume wa Mikmasi, 122; 28 wanaume wa Betheli na Ai,+ 223; 29 wana wa Nebo,+ 52; 30 wana wa Magbishi, 156; 31 wana wa Elamu mwingine, 1,254; 32 wana wa Harimu, 320; 33 wana wa Lodi, Hadidi na Ono, 725; 34 wana wa Yeriko, 345; 35 wana wa Senaa, 3,630.

36 Makuhani:+ wana wa Yedaya+ wa nyumba ya Yeshua,+ 973; 37 wana wa Imeri,+ 1,052; 38 wana wa Pashuri,+ 1,247; 39 wana wa Harimu,+ 1,017.

40 Walawi:+ wana wa Yeshua na Kadmieli,+ wa wana wa Hodavia, 74. 41 Waimbaji:+ wana wa Asafu,+ 128. 42 Wana wa walinzi wa malango:+ wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni,+ wana wa Akubu,+ wana wa Hatita, wana wa Shobai, wote pamoja walikuwa 139.

43 Watumishi wa hekaluni:*+ wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi, 44 wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni, 45 wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Akubu, 46 wana wa Hagabu, wana wa Salmai, wana wa Hanani, 47 wana wa Gideli, wana wa Gahari, wana wa Reaya, 48 wana wa Resini, wana wa Nekoda, wana wa Gazamu, 49 wana wa Uza, wana wa Pasea, wana wa Besai, 50 wana wa Asna, wana wa Meunimu, wana wa Nefusimu, 51 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri, 52 wana wa Basluthi, wana wa Mehida, wana wa Harsha, 53 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema, 54 wana wa Nezia, wana wa Hatifa.

55 Wana wa watumishi wa Sulemani: wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Peruda,+ 56 wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli, 57 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-hazebaimu, wana wa Ami.

58 Watumishi wote wa hekaluni* na wana wa watumishi wa Sulemani walikuwa 392.

59 Na hawa ndio waliopanda kutoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubi, Adoni, na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kama ukoo wao* na asili yao ilikuwa ya Waisraeli:+ 60 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, 652. 61 Na kutoka kwa wana wa makuhani: wana wa Habaya, wana wa Hakozi,+ wana wa Barzilai, aliyemwoa mmoja kati ya mabinti wa Barzilai+ Mgileadi na kuitwa kwa jina lao. 62 Hao walichunguza kumbukumbu zao ili wathibitishe ukoo wao, lakini hawakupata majina ya koo zao, kwa hiyo hawakustahili kuwa makuhani.*+ 63 Gavana* akawaambia kwamba hawangeweza kula vitu vitakatifu kabisa+ mpaka apatikane kuhani ambaye angechunguza Urimu na Thumimu.+

64 Kutaniko lote lilikuwa na jumla ya watu 42,360,+ 65 mbali na watumwa wao wa kiume na wa kike, ambao walikuwa 7,337; walikuwa pia na waimbaji 200 wa kiume na wa kike. 66 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245, 67 ngamia 435, na punda 6,720.

68 Walipofika kwenye nyumba ya Yehova kule Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa koo* wakatoa matoleo ya hiari+ kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa kweli, ili kuijenga upya* mahali ilipokuwa.+ 69 Kulingana na uwezo wao walitoa mchango kwa ajili ya hazina ya kazi, drakma 61,000 za dhahabu,* na mina 5,000 za fedha,*+ na kanzu 100 za makuhani. 70 Na makuhani, Walawi, baadhi ya watu, waimbaji, walinzi wa malango, na watumishi wa hekaluni,* wakaanza kuishi katika majiji yao. Na Waisraeli wengine wote* wakaanza kuishi katika majiji yao.+

3 Mwezi wa saba+ ulipofika Waisraeli* walikuwa katika majiji yao; wakakusanyika Yerusalemu wakiwa na kusudi moja. 2 Yeshua+ mwana wa Yehosadaki na makuhani wenzake na Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli+ na ndugu zake wakasimama na kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli, ili kutoa dhabihu za kuteketezwa juu yake, kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa,+ mtu wa Mungu wa kweli.

3 Basi wakajenga madhabahu mahali ilipokuwa zamani, ingawa waliwaogopa watu wa nchi jirani,+ nao wakaanza kumtolea Yehova dhabihu za kuteketezwa juu yake, asubuhi na jioni.+ 4 Kisha wakafanya Sherehe ya Vibanda* kulingana na ilivyoandikwa,+ na siku baada ya siku walitoa idadi iliyohitajika ya dhabihu za kuteketezwa.+ 5 Baadaye walitoa dhabihu za kuteketezwa zilizotolewa kwa ukawaida+ na matoleo kwa ajili ya miezi mipya+ na majira yote yaliyotakaswa+ ya sherehe za Yehova, na pia toleo la hiari la kila mtu aliyemtolea Yehova kwa kupenda.+ 6 Tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba,+ walianza kumtolea Yehova dhabihu za kuteketezwa, ingawa bado msingi wa hekalu la Yehova haukuwa umewekwa.

7 Wakawapa pesa wakataji wa mawe+ na mafundi,+ na kuwapa Wasidoni na Watiro vyakula na vinywaji na mafuta ili walete mbao za mierezi kupitia bahari kutoka Lebanoni mpaka Yopa,+ kwa ruhusa ya Mfalme Koreshi wa Uajemi.+

8 Katika mwaka wa pili tangu walipofika kwenye nyumba ya Mungu wa kweli huko Yerusalemu, katika mwezi wa pili, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yehosadaki na ndugu zao wote, makuhani na Walawi, na wale wote waliorudi Yerusalemu kutoka utekwani+ wakaanza kazi; wakawaweka rasmi Walawi kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi wawe wasimamizi wa kazi ya nyumba ya Yehova. 9 Basi Yeshua, wanawe na ndugu zake, na Kadmieli na wanawe, wana wa Yuda, wakaungana ili kuwasimamia wale waliokuwa wakifanya kazi katika nyumba ya Mungu wa kweli, pamoja na wana wa Henadadi,+ wana wao na ndugu zao Walawi.

10 Wajenzi walipoweka msingi wa hekalu la Yehova,+ makuhani waliovaa mavazi rasmi, wakiwa na tarumbeta,+ na Walawi, wana wa Asafu, wakiwa na matoazi, wakasimama ili kumsifu Yehova kulingana na maagizo ya Mfalme Daudi wa Israeli.+ 11 Nao wakaanza kuimba kwa kuitikia+ wakimsifu na kumshukuru Yehova “kwa maana yeye ni mwema; upendo wake mshikamanifu kwa Israeli unadumu milele.”+ Kisha watu wote wakapaza sauti wakimsifu Yehova kwa sababu msingi wa nyumba ya Yehova ulikuwa umewekwa. 12 Makuhani wengi, Walawi, na viongozi wa koo*—wazee ambao walikuwa wameona ile nyumba ya kwanza+—wakalia kwa sauti kubwa walipoona msingi wa nyumba hii ukiwekwa, na wengine wengi wakapaza sauti yao yote kwa shangwe.+ 13 Hivyo watu hawakuweza kutofautisha kati ya sauti ya kushangilia na ya kulia, kwa maana watu walikuwa wakipaza sauti kubwa hivi kwamba sauti hiyo ikasikika mbali sana.

4 Maadui wa Yuda na Benjamini+ waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka uhamishoni+ walikuwa wakimjengea hekalu Yehova Mungu wa Israeli, 2 mara moja wakamfikia Zerubabeli na viongozi wa koo* na kuwaambia: “Acheni tujenge pamoja nanyi; kwa maana, sisi pia tunamwabudu* Mungu wenu+ na tumekuwa tukimtolea dhabihu tangu siku za Mfalme Esar-hadoni+ wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”+ 3 Hata hivyo, Zerubabeli na Yeshua na viongozi wa koo* za Israeli wakawaambia: “Hamna haki ya kujenga pamoja nasi nyumba ya Mungu wetu,+ kwa maana sisi wenyewe tutamjengea Yehova Mungu wa Israeli, kama alivyotuamuru Mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi.”+

4 Ndipo watu wa mataifa jirani wakazidi kuwavunja moyo* watu wa Yuda na kuwakatisha tamaa ili wasijenge.+ 5 Waliwakodi washauri ili kuvuruga mipango yao ya kujenga,+ siku zote za Mfalme Koreshi wa Uajemi mpaka wakati wa utawala wa Mfalme Dario+ wa Uajemi. 6 Mwanzoni mwa utawala wa Ahasuero, waliandika mashtaka dhidi ya wakaaji wa Yuda na Yerusalemu. 7 Na katika siku za utawala wa Mfalme Artashasta wa Uajemi, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli, na wenzake walimwandikia Mfalme Artashasta; wakaitafsiri barua hiyo katika Kiaramu,+ na kuiandika kwa herufi za Kiaramu.*

8 * Rehumu ofisa mkuu wa serikali na mwandishi Shimshai, walimwandikia Mfalme Artashasta barua ifuatayo dhidi ya Yerusalemu: 9 (Ilitoka kwa Rehumu ofisa mkuu wa serikali na mwandishi Shimshai na wenzao, yaani, waamuzi na magavana wadogo, waandishi, watu wa Ereki,+ Wababiloni, wakaaji wa Susa,+ yaani, Waelamu,+ 10 na mataifa mengine yote ambayo Asenapari mkuu na mheshimiwa aliwahamisha na kuwapeleka katika majiji ya Samaria,+ na wengine walio Ng’ambo ya Mto,* basi sasa 11 hii ndiyo nakala ya barua waliyomtumia.)

“Kwa Mfalme Artashasta kutoka kwa watumishi wako, watu walio Ng’ambo ya Mto: Sasa 12 tungependa kumjulisha mfalme kwamba Wayahudi waliokuja huku kutoka kwako wamefika Yerusalemu. Wanajenga upya lile jiji lenye uasi na uovu, nao wanamalizia kujenga kuta+ na kurekebisha misingi yake. 13 Sasa tungependa mfalme ajue kwamba ikiwa jiji hili litajengwa upya na kuta zake kukamilishwa, hawatalipa kodi, ushuru,+ wala ada, na jambo hilo litasababisha hasara kwa hazina za wafalme. 14 Na kwa kuwa sisi hula chumvi ya jumba la mfalme* na si vema kwetu kuona masilahi ya mfalme yakiathiriwa, ndiyo sababu tumetuma barua ili kumjulisha mfalme jambo hilo, 15 ili uchunguzi ufanywe katika kitabu cha kumbukumbu za mababu zako.+ Ndipo utakapoona katika kitabu hicho cha kumbukumbu kwamba hili ni jiji lenye uasi, linalowaletea hasara wafalme na mikoa,* na tangu zamani lilikuwa na wachochezi wa uasi. Ndiyo sababu jiji hili liliangamizwa.+ 16 Tunakujulisha mfalme kwamba jiji hili likijengwa upya na kuta zake kukamilishwa, hutaweza kutawala tena* eneo lililo Ng’ambo ya Mto.”+

17 Mfalme akatuma ujumbe ufuatao kwa Rehumu ofisa mkuu wa serikali na mwandishi Shimshai na wenzao walioishi Samaria na katika eneo lote lililo Ng’ambo ya Mto:

“Salamu! Na sasa 18 barua rasmi mliyotutumia imesomwa waziwazi* mbele yangu. 19 Niliagiza uchunguzi ufanywe na ikajulikana kwamba tangu zamani jiji hilo limewapinga wafalme, na limekuwa na uchochezi na uasi.+ 20 Kulikuwa na wafalme wenye nguvu juu ya Yerusalemu waliotawala eneo lote la Ng’ambo ya Mto, nao walikuwa wakilipwa kodi, ushuru, na ada. 21 Sasa toeni amri ili kusimamisha kazi ya wanaume hao, ili jiji hilo lisijengwe upya mpaka nitakapotoa agizo. 22 Hakikisheni amri hii inatekelezwa bila uzembe, ili masilahi ya mfalme yasiendelee kuathiriwa.”+

23 Sasa baada ya nakala ya barua rasmi ya Mfalme Artashasta kusomwa mbele ya Rehumu na mwandishi Shimshai na wenzao, mara moja wakaenda Yerusalemu na kuwalazimisha Wayahudi waache kujenga. 24 Ndipo kazi ya kujenga nyumba ya Mungu, iliyokuwa Yerusalemu, iliposimamishwa; na haikuendelea mpaka mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi.+

5 Ndipo nabii Hagai+ na nabii Zekaria,+ mjukuu wa Ido+ wakawatabiria Wayahudi waliokuwa Yuda na Yerusalemu, katika jina la Mungu wa Israeli aliyekuwa akiwaongoza. 2 Kisha Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli na Yeshua+ mwana wa Yehosadaki wakaanza kujenga upya nyumba ya Mungu,+ iliyokuwa Yerusalemu; na manabii wa Mungu walikuwa pamoja nao na waliwatia moyo.+ 3 Wakati huo Tatenai gavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto* na Shethar-bozenai na wenzao wakaja na kuwauliza: “Ni nani aliyewaagiza mjenge nyumba hii na kukamilisha nguzo hizi?”* 4 Pia, wakawauliza: “Wanaume wanaojenga jengo hili ni akina nani?” 5 Lakini Mungu alikuwa pamoja na* wazee wa Wayahudi,+ nao hawangeweza kuwazuia kabla ya kumwandikia Dario na kupata barua rasmi kuhusu jambo hilo kutoka kwake.

6 Hii ndiyo nakala ya barua ambayo Tatenai gavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto na Shethar-bozenai na wenzake, magavana wadogo wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto, walimtumia Mfalme Dario; 7 walimtumia habari hiyo, na hivi ndivyo walivyoandika:

“Kwa Mfalme Dario:

“Na uwe na amani nyingi! 8 Tungependa kumjulisha mfalme kwamba tulienda katika mkoa* wa Yuda kwenye nyumba ya yule Mungu mkuu, nayo inajengwa kwa mawe makubwa yaliyobingirishwa na kuwekwa mahali pake, na mbao zinawekwa katika kuta. Watu hao wanafanya kazi hiyo kwa bidii na inasonga mbele kwa jitihada zao. 9 Ndipo tukawauliza wazee wao: ‘Ni nani aliyewaagiza mjenge nyumba hii na kukamilisha nguzo hizi?’*+ 10 Pia, tuliwauliza majina yao ili tuandike majina ya viongozi wao na kukujulisha.

11 “Walitujibu hivi: ‘Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na dunia, na tunajenga upya nyumba iliyojengwa miaka mingi iliyopita, ambayo mfalme fulani mkuu wa Israeli aliijenga na kuikamilisha.+ 12 Lakini kwa sababu baba zetu walimkasirisha Mungu wa mbinguni,+ aliwatia mikononi mwa Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni, Mkaldayo, ambaye aliibomoa nyumba hii+ na kuwapeleka watu uhamishoni huko Babiloni.+ 13 Hata hivyo, katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi wa Babiloni, Mfalme Koreshi alitoa agizo la kuijenga upya nyumba hii ya Mungu.+ 14 Pia, Mfalme Koreshi alitoa katika hekalu la Babiloni vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua hekaluni huko Yerusalemu, na kuvileta katika hekalu la Babiloni.+ Alivikabidhi kwa mtu aitwaye Sheshbazari,*+ ambaye Koreshi alimteua kuwa gavana.+ 15 Koreshi alimwambia: “Chukua vyombo hivi, uvirudishe katika hekalu lililo Yerusalemu, na nyumba ya Mungu ijengwe upya mahali ilipokuwa awali.”+ 16 Ndipo Sheshbazari akaja, akaweka misingi ya nyumba ya Mungu,+ iliyo Yerusalemu; na tangu wakati huo mpaka leo inaendelea kujengwa lakini haijamalizika.’+

17 “Basi mfalme ukipenda, acha uchunguzi ufanywe katika nyumba ya hazina ya mfalme iliyo Babiloni, ili ijulikane kama Mfalme Koreshi alitoa agizo la kuijenga upya nyumba ya Mungu huko Yerusalemu;+ kisha wewe mfalme ututumie uamuzi wako kuhusu jambo hili.”

6 Ndipo Mfalme Dario akatoa agizo, nao wakafanya uchunguzi katika jengo la hifadhi* ambamo hazina ziliwekwa huko Babiloni. 2 Kisha kitabu cha kukunjwa kikapatikana kwenye ngome huko Ekibatana, katika mkoa* wa Umedi, nacho kilikuwa na ujumbe ufuatao:

3 “Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi, Mfalme Koreshi alitoa agizo hili kuhusu nyumba ya Mungu huko Yerusalemu:+ ‘Nyumba hiyo na ijengwe upya iwe mahali watakapotolea dhabihu, na misingi yake inapaswa kuwekwa; kimo chake kiwe mikono 60,* upana wake mikono 60,+ 4 na iwe na safu tatu za mawe makubwa yaliyobingirishwa na kuwekwa mahali pake na safu moja ya mbao;+ na gharama zote zilipwe kutoka katika nyumba ya mfalme.+ 5 Pia, vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu ambavyo Nebukadneza alivichukua katika hekalu lililokuwa Yerusalemu na kuvileta Babiloni+ virudishwe, ili viwekwe mahali pake katika hekalu huko Yerusalemu na vihifadhiwe katika nyumba ya Mungu.’+

6 “Basi, Tatenai gavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto,* Shethar-bozenai, na wenzenu, magavana wadogo wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto+—msikaribie mahali hapo. 7 Msiingilie kazi ya nyumba hiyo ya Mungu. Gavana wa Wayahudi na wazee wa Wayahudi watajenga upya nyumba hiyo ya Mungu mahali ilipokuwa zamani. 8 Pia, ninatoa agizo kuhusu jambo mnalopaswa kuwafanyia wazee hao wa Wayahudi kwa ajili ya kujenga upya nyumba hiyo ya Mungu: Gharama zao zote zitalipwa bila kuchelewa kutoka katika hazina ya mfalme,+ kodi inayokusanywa katika eneo lililo Ng’ambo ya Mto, ili ujenzi uendelee bila kukatizwa.+ 9 Na chochote kinachohitajiwa—ng’ombe dume wachanga+ pamoja na kondoo dume+ na wanakondoo+ kwa ajili ya dhabihu za kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano,+ chumvi,+ divai,+ na mafuta,+ kama watakavyosema makuhani walio Yerusalemu—waendelee kupewa vitu hivyo siku baada ya siku bila kukosa, 10 ili waendelee kutoa matoleo yanayompendeza Mungu wa mbinguni na kumwombea mfalme na wanawe wawe na maisha marefu.+ 11 Pia nimetoa agizo kwamba yeyote atakayevunja amri hii, nguzo itang’olewa katika nyumba yake naye atatundikwa juu ya nguzo hiyo, na nyumba yake itafanywa kuwa choo cha umma* kwa sababu ya kosa hilo. 12 Na Mungu aliyefanya jina lake likae huko+ na ampindue mfalme yeyote na watu watakaonyoosha mkono ili kukiuka agizo hili na kuiharibu nyumba ya Mungu, iliyo Yerusalemu. Mimi, Dario, ninatoa agizo hili. Nalo litekelezwe bila kukawia.”

13 Ndipo Tatenai gavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto, Shethar-bozenai,+ na wenzao, wakatekeleza bila kukawia kila jambo ambalo Mfalme Dario alikuwa ameagiza. 14 Nao wazee wa Wayahudi wakaendelea kujenga na kufanya maendeleo,+ wakitiwa moyo na nabii Hagai+ na Zekaria+ mjukuu wa Ido; wakamaliza kujenga kulingana na agizo la Mungu wa Israeli+ na agizo la Koreshi,+ Dario,+ na Mfalme Artashasta+ wa Uajemi. 15 Wakamaliza kujenga nyumba hiyo katika siku ya tatu ya mwezi wa Adari,* katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.

16 Ndipo Waisraeli, makuhani, Walawi,+ na watu wengine waliotoka uhamishoni wakaizindua* nyumba ya Mungu kwa shangwe. 17 Nao wakaleta kwa ajili ya kuzindua nyumba ya Mungu ng’ombe dume 100, kondoo dume 200, wanakondoo 400, na mbuzi dume 12 kuwa dhabihu ya dhambi kwa ajili ya Waisraeli wote, kulingana na idadi ya makabila ya Israeli.+ 18 Nao wakawapanga makuhani katika makundi yao na Walawi katika vikundi vyao kwa ajili ya utumishi wa Mungu huko Yerusalemu,+ kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Musa.+

19 Na watu hao waliotoka uhamishoni wakasherehekea Pasaka siku ya 14 ya mwezi wa kwanza.+ 20 Makuhani na Walawi wote, walikuwa wamejitakasa,+ hivyo wote walikuwa safi; basi wakachinja mnyama wa Pasaka kwa ajili ya watu wote waliotoka uhamishoni, kwa ajili ya makuhani wenzao, na kwa ajili yao wenyewe. 21 Kisha Waisraeli waliorudi kutoka uhamishoni wakala pamoja na kila mtu aliyekuwa amejiunga nao na kujitenga na uchafu wa mataifa ya nchi hiyo ili kumwabudu* Yehova Mungu wa Israeli.+ 22 Pia, wakasherehekea kwa shangwe Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu+ kwa siku saba, kwa maana Yehova aliwafanya washangilie na alikuwa ameugeuza moyo wa mfalme wa Ashuru ili awatendee mema,+ hivi kwamba akawaunga mkono* katika kazi ya nyumba ya Mungu wa kweli, Mungu wa Israeli.

7 Baada ya mambo hayo, wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta+ wa Uajemi, Ezra*+ akarudi. Alikuwa mwana wa Seraya,+ mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,+ 2 mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu, 3 mwana wa Amaria, mwana wa Azaria,+ mwana wa Merayothi, 4 mwana wa Zeraya, mwana wa Uzi, mwana wa Buki, 5 mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi,+ mwana wa Eleazari,+ mwana wa kuhani mkuu Haruni.+ 6 Huyo Ezra alitoka Babiloni. Alikuwa mwandishi* na aliijua vizuri* Sheria ya Musa,+ iliyotolewa na Yehova Mungu wa Israeli. Mfalme alimpa kila kitu alichoomba, kwa maana mkono wa Yehova Mungu wake ulikuwa juu yake.

7 Baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi,+ waimbaji,+ walinzi wa malango,+ na watumishi wa hekaluni,*+ wakapanda kwenda Yerusalemu katika mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta. 8 Naye Ezra akaja Yerusalemu mwezi wa tano, katika mwaka wa saba wa utawala wa mfalme huyo. 9 Alianza safari ya kutoka Babiloni siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, akafika Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kwa sababu mkono mwema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.+ 10 Ezra alikuwa ameutayarisha moyo wake* kuichunguza Sheria ya Yehova na kuifuata,+ na kufundisha masharti ya sheria hiyo na maamuzi yake katika Israeli.+

11 Ifuatayo ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alimpa Ezra aliyekuwa kuhani na mwandishi,* mwenye ujuzi mwingi* kuhusu amri za Yehova na masharti aliyowapa Waisraeli:

12 * “Artashasta,+ mfalme wa wafalme, kwa kuhani Ezra, mwandishi* wa Sheria ya Mungu wa mbinguni: Na uwe na amani kamili. Na sasa 13 nimetoa agizo kwamba kila mtu katika milki yangu ambaye ni mmoja wa watu wa Israeli na pia makuhani wao na Walawi, ambaye angependa kwenda nawe Yerusalemu aende.+ 14 Kwa maana umetumwa na mfalme na washauri wake saba ili kuchunguza kama watu walio Yuda na Yerusalemu wanafuata Sheria ya Mungu wako uliyo nayo,* 15 na kuchukua fedha na dhahabu ambayo mfalme na washauri wake wamemtolea kwa hiari Mungu wa Israeli, ambaye makao yake yako Yerusalemu, 16 pamoja na fedha na dhahabu yote ambayo utapokea* katika mkoa wote* wa Babiloni, na pia zawadi ambazo watu na makuhani hutoa kwa hiari kwa ajili ya nyumba ya Mungu wao iliyo Yerusalemu.+ 17 Na bila kukawia utanunua kwa pesa hizo ng’ombe dume,+ kondoo dume,+ wanakondoo,+ na matoleo yao ya nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji,+ nawe utavitoa juu ya madhabahu ya nyumba ya Mungu wenu huko Yerusalemu.

18 “Na fedha na dhahabu itakayobaki, wewe na ndugu zako mnaweza kuitumia mtakavyopenda, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu. 19 Na vyombo vyote utakavyopewa kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wako, unapaswa kuvipeleka mbele za Mungu huko Yerusalemu.+ 20 Na kitu kingine chochote unachohitaji kutoa kwa ajili ya nyumba ya Mungu wako, utakitoa kutoka katika hazina ya mfalme.+

21 “Mimi, Mfalme Artashasta, nimewaagiza waweka-hazina wote katika eneo lililo Ng’ambo ya Mto* wampe bila kukawia kila kitu atakachoomba Ezra,+ kuhani na mwandishi wa* Sheria ya Mungu wa mbinguni, 22 hata akiomba talanta 100 za fedha,* kori 100 za ngano,* bathi 100 za divai,*+ bathi 100 za mafuta,+ na chumvi isiyo na kipimo.+ 23 Kila jambo ambalo Mungu wa mbinguni ameagiza linapaswa kufanywa kwa bidii kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa mbinguni,+ ili ghadhabu yake isije dhidi ya milki yangu na wanangu.+ 24 Pia ninawajulisha kwamba hairuhusiwi kuwatoza kodi, wala ushuru,+ wala ada yoyote makuhani na Walawi, wanamuziki,+ walinzi wa malango, watumishi wa hekaluni,*+ na wafanyakazi wa nyumba hii ya Mungu.

25 “Na wewe, Ezra, kulingana na hekima uliyopewa na Mungu wako,* teua mahakimu na waamuzi ili wawahukumu watu wote katika eneo lililo Ng’ambo ya Mto, wote wanaojua sheria za Mungu wako; nanyi mnapaswa kumfundisha yeyote asiyezijua.+ 26 Na kila mtu ambaye hatafuata Sheria ya Mungu wako na sheria ya mfalme anapaswa kuhukumiwa upesi, iwe ni kuuawa, kufukuzwa nchini, kutozwa faini, au kufungwa gerezani.”

27 Yehova Mungu wa mababu zetu na asifiwe, ambaye alitia ndani ya moyo wa mfalme wazo la kuipamba nyumba ya Yehova iliyo Yerusalemu!+ 28 Naye amenitendea kwa upendo mshikamanifu mbele ya mfalme,+ washauri wake,+ na wakuu wote wa mfalme wenye nguvu. Hivyo nikajipa ujasiri* kwa sababu mkono wa Yehova Mungu ulikuwa juu yangu, nami nikawakusanya wanaume waliokuwa viongozi* katika Israeli ili wapande pamoja nami.

8 Basi hawa ndio waliokuwa viongozi wa koo* na hii ndiyo orodha ya ukoo wa wale waliopanda pamoja nami kutoka Babiloni wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:+ 2 ukoo wa wana wa Finehasi,+ Gershomu; wa wana wa Ithamari,+ Danieli; wa wana wa Daudi, Hatushi; 3 wa wana wa Shekania, wa wana wa Paroshi, Zekaria, na pamoja naye kulikuwa na wanaume 150 walioandikishwa; 4 wa wana wa Pahath-moabu,+ Elieho-enai mwana wa Zeraya, na wanaume 200 pamoja naye; 5 wa wana wa Zatu,+ Shekania mwana wa Yahazieli, na wanaume 300 pamoja naye; 6 wa wana wa Adini,+ Ebedi mwana wa Yonathani, na wanaume 50 pamoja naye; 7 wa wana wa Elamu,+ Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye; 8 wa wana wa Shefatia,+ Zebadia mwana wa Mikaeli, na wanaume 80 pamoja naye; 9 wa wana wa Yoabu, Obadia mwana wa Yehieli, na wanaume 218 pamoja naye; 10 wa wana wa Bani, Shelomithi mwana wa Yosifia, na wanaume 160 pamoja naye; 11 wa wana wa Bebai,+ Zekaria mwana wa Bebai, na wanaume 28 pamoja naye; 12 wa wana wa Azgadi,+ Yohanani mwana wa Hakatani, na wanaume 110 pamoja naye; 13 wa wana wa Adonikamu,+ wale waliokuwa wa mwisho, haya ndiyo majina yao: Elifeleti, Yeieli, na Shemaya, na wanaume 60 pamoja nao; 14 na wa wana wa Bigvai,+ Uthai na Zabudu, na wanaume 70 pamoja nao.

15 Nikawakusanya kwenye mto unaoelekea Ahava;+ nasi tukapiga kambi hapo siku tatu. Lakini nilipowakagua watu na makuhani, sikupata Mlawi hata mmoja. 16 Kwa hiyo nikawatuma wajumbe wawaite Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria, na Meshulamu, waliokuwa viongozi, na Yoyaribu na Elnathani, waliokuwa walimu. 17 Kisha nikawapa amri kuhusu Ido kiongozi wa Kasifia. Nikawaagiza wamwambie Ido na ndugu zake, watumishi wa hekaluni* waliokuwa huko Kasifia, watuletee wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu. 18 Kwa kuwa mkono mwema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea mwanamume mwenye busara kutoka kwa wana wa Mali+ mjukuu wa Lawi mwana wa Israeli, aliyeitwa Sherebia,+ na wanawe na ndugu zake, wanaume 18; 19 na Hashabia, na pamoja naye Yeshaya kutoka kwa Wamerari,+ ndugu zake na wana wao, wanaume 20. 20 Na kulikuwa na watumishi wa hekaluni* 220, ambao Daudi na wakuu walikuwa wamewatoa kwa ajili ya utumishi wa Walawi, wote walikuwa wametajwa kwa majina.

21 Kisha nikatangaza kwamba watu wafunge hapo kwenye mto Ahava, ili tujinyenyekeze mbele za Mungu wetu, na kumwomba atuongoze katika safari yetu, sisi na watoto wetu na mali zetu zote. 22 Niliona aibu kumwomba mfalme wanajeshi na wapanda farasi watulinde dhidi ya maadui njiani, kwa sababu tulikuwa tumemwambia mfalme: “Mkono mwema wa Mungu wetu uko juu ya wale wote wanaomtafuta,+ lakini nguvu zake na hasira yake iko dhidi ya wote wanaomwacha.”+ 23 Basi tukafunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hilo, naye akasikiliza maombi yetu.+

24 Kisha nikachagua wakuu 12 wa makuhani, yaani, Sherebia na Hashabia,+ pamoja na kumi kati ya ndugu zao. 25 Nikawapimia fedha na dhahabu na vyombo, mchango ambao mfalme na washauri wake na wakuu wake na Waisraeli wote waliokuwa hapo walitoa kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.+ 26 Basi nikapima na kuwakabidhi talanta 650 za fedha,* vyombo 100 vya fedha vyenye thamani ya talanta mbili, na talanta 100 za dhahabu, 27 mabakuli madogo 20 ya dhahabu yenye thamani ya dariki 1,000,* na vyombo viwili vya shaba bora, nyekundu inayong’aa, inayotamanika kama dhahabu.

28 Kisha nikawaambia: “Ninyi ni watakatifu kwa Yehova,+ na vyombo hivi ni vitakatifu, na fedha na dhahabu hii ni matoleo ya hiari kwa Yehova Mungu wa mababu zenu. 29 Mvilinde kwa makini hadi mtakapovipima mbele ya wakuu wa makuhani na Walawi na wakuu wa koo za Waisraeli huko Yerusalemu,+ katika vyumba vya* nyumba ya Yehova.” 30 Makuhani na Walawi wakapokea fedha na dhahabu na vyombo walivyopimiwa, ili wavilete Yerusalemu kwenye nyumba ya Mungu wetu.

31 Mwishowe tukaondoka kwenye mto Ahava+ siku ya 12 ya mwezi wa kwanza+ na kuelekea Yerusalemu, na mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye akatuokoa kutoka mikononi mwa maadui na wavamizi njiani. 32 Basi tukafika Yerusalemu+ na kukaa huko siku tatu. 33 Kisha siku ya nne tukapima ile fedha na dhahabu na vyombo katika nyumba ya Mungu wetu,+ tukamkabidhi Meremothi+ mwana wa kuhani Uriya, aliyekuwa pamoja na Eleazari mwana wa Finehasi, pamoja na Walawi Yozabadi+ mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui.+ 34 Kila kitu kilihesabiwa na kupimwa, na uzito wote ukaandikwa. 35 Wale waliotoka uhamishoni, waliokuwa utekwani, wakamtolea Mungu wa Israeli dhabihu za kuteketezwa, ng’ombe dume 12+ kwa ajili ya Waisraeli wote, kondoo dume 96,+ wanakondoo dume 77, mbuzi dume 12+ kwa ajili ya dhabihu ya dhambi; hizo zote zilikuwa dhabihu za kuteketezwa zilizotolewa kwa Yehova.+

36 Kisha tukawapa maliwali* wa mfalme+ na magavana waliokuwa Ng’ambo ya Mto*+ maagizo ya mfalme, nao wakawategemeza watu na nyumba ya Mungu wa kweli.+

9 Baada ya mambo hayo kufanywa, wakuu wakaja na kuniambia: “Watu wa Israeli na makuhani na Walawi hawajajitenga na watu wa mataifa ya nchi mbalimbali na mazoea yao yanayochukiza,+ ya Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wayebusi, Waamoni, Wamoabu, Wamisri,+ na Waamori.+ 2 Wamejichukulia baadhi ya mabinti wa mataifa hayo kuwa wake zao na kuwachukulia wana wao pia.+ Sasa wao, uzao mtakatifu,*+ wamechanganyika na watu wa mataifa ya nchi mbalimbali.+ Wakuu na watawala wasaidizi ndio wanaoongoza katika ukosefu huu wa uaminifu.”

3 Mara tu niliposikia jambo hilo, nikalirarua vazi langu na joho langu lisilo na mikono na kung’oa baadhi ya nywele za kichwa changu na ndevu zangu, nami nikaketi chini kwa mshtuko. 4 Kisha kila mtu aliyehofu* maneno ya Mungu wa Israeli akakusanyika kunizunguka kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu wa watu waliotoka uhamishoni, nami nilikuwa nimeketi chini kwa mshtuko mpaka wakati wa toleo la nafaka la jioni.+

5 Wakati wa toleo la nafaka la jioni,+ niliinuka kutoka mahali nilipokuwa nimeketi kwa aibu, vazi langu na joho langu lisilo na mikono likiwa limeraruka, nikapiga magoti na kumnyooshea mikono Yehova Mungu wangu. 6 Nikasema: “Ee Mungu wangu, ninaona aibu na haya kuuinua uso wangu kwako, Ee Mungu wangu, kwa sababu makosa yetu yameongezeka juu ya vichwa vyetu na hatia yetu imerundamana mpaka mbinguni.+ 7 Tangu siku za mababu zetu mpaka leo hii tumekuwa na hatia kubwa;+ na kwa sababu ya makosa yetu, sisi, wafalme wetu, na makuhani wetu, tumetiwa mikononi mwa wafalme wa nchi nyingine, tumeuawa kwa upanga,+ tumepelekwa utekwani,+ tumeporwa,+ tumetiwa aibu, kama ilivyo leo.+ 8 Lakini sasa kwa muda mfupi, Yehova Mungu wetu ametuonyesha kibali kwa kuruhusu baadhi yetu tuponyoke na kutupatia sehemu salama* mahali pake patakatifu,+ ili kuyafanya macho yetu yang’ae, Ee Mungu wetu, na kutupumzisha kidogo kutoka katika utumwa wetu. 9 Ingawa sisi ni watumwa,+ Mungu wetu hajatuacha utumwani; bali ametutendea kwa upendo mshikamanifu mbele ya wafalme wa Uajemi,+ ili kutupumzisha tuweze kuisimamisha nyumba ya Mungu wetu+ na kuijenga upya nyumba hiyo ambayo ni magofu na kutupatia ukuta wa mawe* katika Yuda na Yerusalemu.

10 “Lakini tuseme nini sasa, Ee Mungu wetu, baada ya hayo? Kwa maana tumeziacha amri zako, 11 ulizotupatia kupitia watumishi wako manabii, ukisema: ‘Nchi ambayo mnaingia kuimiliki ni nchi chafu kwa kuwa watu waliomo ni wachafu, kwa sababu ya matendo yao yanayochukiza ambayo wameyajaza kutoka mwisho mmoja hadi mwingine kwa uchafu wao.+ 12 Kwa hiyo, msiwaruhusu mabinti zenu waolewe na wana wao, wala msikubali wana wenu wawaoe mabinti zao;+ msiwatakie kamwe amani wala mafanikio,+ ili mzidi kupata nguvu na kula mema ya nchi na kuimiliki ili wana wenu wairithi milele.’ 13 Baada ya yote yaliyotupata kwa sababu ya matendo yetu maovu na hatia yetu kubwa—kwa maana wewe, Ee Mungu wetu, hujatutendea kulingana na makosa yetu,+ nawe umeruhusu sisi tulio hapa tuponyoke+— 14 je, tuvunje tena amri zako na kufanya mapatano ya ndoa* na watu wanaotenda mambo haya yanayochukiza?+ Je, hutatukasirikia vikali na kutuangamiza kabisa, hata kusiwe na yeyote atakayebaki wala kuokoka? 15 Ee Yehova Mungu wa Israeli, wewe ni mwadilifu,+ kwa maana tumeokoka na kubaki mpaka leo. Sasa tumesimama mbele zako tukiwa na hatia, kwa maana hatuwezi kusimama mbele zako kwa sababu ya jambo hili.”+

10 Ezra alipokuwa akisali+ na kuungama, akilia na kulala kifudifudi mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli, umati mkubwa wa wanaume, wanawake, na watoto wa Israeli wakakusanyika kumzunguka, kwa maana watu walikuwa wakilia sana. 2 Ndipo Shekania mwana wa Yehieli+ wa wana wa Elamu+ akamwambia Ezra: “Tumetenda kwa ukosefu wa uaminifu dhidi ya Mungu wetu kwa kuoa* wanawake wa kigeni kutoka kwa mataifa ya nchi hii.+ Ingawa hivyo, bado kuna tumaini kwa Israeli. 3 Basi na tufanye agano na Mungu wetu+ la kuwafukuza wake hao wote na watoto wao kulingana na mwongozo wa Yehova na wa wale wanaohofu* amri ya Mungu wetu.+ Na tutende kulingana na Sheria. 4 Simama, kwa maana jambo hili ni jukumu lako, nasi tuko pamoja nawe. Uwe imara na uchukue hatua.”

5 Ndipo Ezra akasimama, akawaapisha wakuu wa makuhani, Walawi, na Waisraeli wote kwamba watafanya kama ilivyosemwa.+ Basi wakaapa. 6 Sasa Ezra akaondoka mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli na kwenda katika chumba cha* Yehohanani mwana wa Eliashibu. Ingawa alienda huko, hakula chakula wala kunywa maji, kwa maana alikuwa akiomboleza kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu wa watu waliotoka uhamishoni.+

7 Ndipo wakatangaza kotekote katika Yuda na Yerusalemu kwamba watu wote waliotoka uhamishoni wakusanyike Yerusalemu; 8 na wakuu na wanaume wazee wakaamua kwamba yeyote ambaye hangekuja katika muda wa siku tatu, mali zake zote zingechukuliwa,* naye angefukuzwa kutoka kwenye kutaniko la watu waliotoka uhamishoni.+ 9 Basi wanaume wote wa Yuda na Benjamini wakakusanyika Yerusalemu katika muda wa siku tatu, yaani, katika mwezi wa tisa siku ya 20 ya mwezi huo. Watu wote walikuwa wameketi kwenye uwanja wa nyumba ya Mungu wa kweli, wakitetemeka kwa sababu ya jambo hilo na kwa sababu ya mvua kubwa.

10 Kisha kuhani Ezra akasimama na kuwaambia: “Mmetenda kwa ukosefu wa uaminifu kwa kuoa wanawake wa kigeni+ na hivyo mmeongeza hatia ya Israeli. 11 Sasa ungameni kwa Yehova Mungu wa mababu zenu na mfanye mapenzi yake. Jitengeni na watu wa mataifa na hawa wake wa kigeni.”+ 12 Ndipo kutaniko lote likajibu hivi kwa sauti kubwa: “Ni wajibu wetu kufanya kikamili mambo unayotuambia. 13 Hata hivyo, watu ni wengi, na haya ni majira ya mvua. Haiwezekani kusimama nje, na jambo hili halitamalizika kwa siku moja au mbili, kwa maana tumeasi sana katika jambo hili. 14 Basi, tafadhali, acha wakuu wetu waliwakilishe kutaniko lote;+ na watu wote katika majiji yetu ambao wameoa wanawake wa kigeni waje wakati uliowekwa, pamoja na wazee na waamuzi wa kila jiji, mpaka tutakapoituliza hasira inayowaka ya Mungu wetu kuhusiana na jambo hili.”

15 Hata hivyo, Yonathani mwana wa Asaheli na Yahzeya mwana wa Tikva wakapinga jambo hilo, na Meshulamu na Shabethai, waliokuwa Walawi,+ wakawaunga mkono. 16 Lakini watu waliotoka uhamishoni wakafanya kama ilivyokubaliwa; na kuhani Ezra na viongozi wa koo,* watu wote ambao majina yao yalikuwa yameorodheshwa, wakakusanyika peke yao siku ya kwanza ya mwezi wa kumi ili kuchunguza jambo hilo; 17 na kufikia siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakamaliza kuwachunguza wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni. 18 Na ikagunduliwa kwamba baadhi ya wana wa makuhani walikuwa wameoa wanawake wa kigeni:+ kutoka kwa wana wa Yeshua+ mwana wa Yehosadaki na ndugu zake, Maaseya, Eliezeri, Yaribu, na Gedalia. 19 Lakini wakaahidi* kuwafukuza wake zao, na kwa kuwa walikuwa na hatia, wangetoa kondoo dume wa kundi kwa ajili ya hatia yao.+

20 Kutoka kwa wana wa Imeri,+ kulikuwa na Hanani na Zebadia; 21 na kutoka kwa wana wa Harimu,+ Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli, na Uzia; 22 na kutoka kwa wana wa Pashuri,+ Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi, na Eleasa. 23 Na kutoka kwa Walawi, kulikuwa na Yozabadi, Shimei, Kelaya (yaani, Kelita), Pethahia, Yuda, na Eliezeri; 24 na kutoka kwa waimbaji, Eliashibu; na kutoka kwa walinzi wa malango, Shalumu, Telemu, na Uri.

25 Na kutoka Israeli, kutoka kwa wana wa Paroshi,+ kulikuwa na Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya, na Benaya; 26 na kutoka kwa wana wa Elamu,+ Matania, Zekaria, Yehieli,+ Abdi, Yeremothi, na Eliya; 27 na kutoka kwa wana wa Zatu,+ Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi, na Aziza; 28 na kutoka kwa wana wa Bebai,+ Yehohanani, Hanania, Zabai, na Athlai; 29 na kutoka kwa wana wa Bani, Meshulamu, Maluku, Adaya, Yashubu, Sheali, na Yeremothi; 30 na kutoka kwa wana wa Pahath-moabu,+ Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui, na Manase; 31 na kutoka kwa wana wa Harimu,+ Eliezeri, Ishiya, Malkiya,+ Shemaya, Shimeoni, 32 Benjamini, Maluku, na Shemaria; 33 kutoka kwa wana wa Hashumu,+ Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase, na Shimei; 34 kutoka kwa wana wa Bani, Maadai, Amramu, na Ueli, 35 Benaya, Bedeya, Keluhi, 36 Vania, Meremothi, Eliashibu, 37 Matania, Matenai, na Yaasu; 38 na kutoka kwa wana wa Binui, Shimei, 39 Shelemia, Nathani, Adaya, 40 Maknadebai, Shashai, Sharai, 41 Azareli, Shelemia, Shemaria, 42 Shalumu, Amaria, na Yosefu; 43 na kutoka kwa wana wa Nebo, Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli, na Benaya. 44 Wote hao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni,+ basi wakawafukuza wake zao pamoja na wana wao.+

Au labda, “aliye Yerusalemu.”

Tnn., “watu wa mahali pake.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “wakaitia nguvu mikono yao kwa.”

Labda ni Zerubabeli anayetajwa kwenye Ezr 2:2; 3:8.

Au “wilaya ya utawala.”

Au “Wanethini.” Tnn., “Waliotolewa.”

Au “Wanethini.” Tnn., “Waliotolewa.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “hawakustahili utumishi wa kikuhani kwa sababu hawakuwa safi.”

Au “Tirshatha,” cheo cha Kiajemi cha gavana wa mkoa.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “kuisimamisha.”

Kwa kawaida drakma ilikuwa sawa na dariki ya dhahabu ya Uajemi yenye uzito wa gramu 8.4. Si drakma ya Maandiko ya Kigiriki. Angalia Nyongeza B14.

Mina inayotajwa katika Maandiko ya Kiebrania ilikuwa na uzito wa gramu 570. Angalia Nyongeza B14.

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Tnn., “Waisraeli wote.”

Tnn., “wana wa Israeli.”

Au “Vibanda vya Muda.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “tunamtafuta.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “kuilegeza mikono ya.”

Au labda, “iliandikwa katika Kiaramu kisha ikatafsiriwa.”

Mwanzoni, maandishi ya Ezr 4:8 hadi 6:18 yaliandikwa katika Kiaramu.

Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”

Au “tunapokea mshahara wetu kutoka kwenye makao ya mfalme.”

Au “wilaya za utawala.”

Tnn., “hutakuwa na fungu katika.”

Au labda, “imetafsiriwa na kusomwa.”

Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”

Au “mihimili hii.”

Tnn., “macho ya Mungu wao yalikuwa juu ya.”

Au “wilaya ya utawala.”

Au “mihimili hii.”

Labda ni Zerubabeli anayetajwa kwenye Ezr 2:2; 3:8.

Tnn., “nyumba ya kumbukumbu.”

Au “wilaya ya utawala.”

Karibu mita 26.7 (futi 87.6). Angalia Nyongeza B14.

Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”

Au labda, “eneo la takataka; rundo la mavi.”

Angalia Nyongeza B15.

Au “wakaiweka wakfu.”

Tnn., “kumtafuta.”

Tnn., “akaitia nguvu mikono yao.”

Maana yake “Msaada.”

Au “Alinakili maandishi.”

Au “Alikuwa mwandishi stadi wa.”

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Au “alikuwa ameazimia moyoni mwake.”

Au “mtu aliyenakili maandishi.”

Au “aliyenakili maneno.”

Mwanzoni, maandishi ya Ezr 7:12 hadi 7:26 yaliandikwa katika Kiaramu.

Au “aliyenakili maandishi.”

Tnn., “iliyo mkononi mwako.”

Tnn., “utapata.”

Au, “wilaya yote ya utawala.”

Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”

Au “aliyenakili maandishi ya.”

Talanta ilikuwa sawa na kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.

Kori moja ilikuwa sawa na lita 220 (kilogramu 170 hivi). Angalia Nyongeza B14.

Bathi ilikuwa sawa na lita 22. Angalia Nyongeza B14.

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Tnn., “kulingana na hekima ya Mungu wako iliyo mkononi mwako.”

Au “nikajipa nguvu.”

Tnn., “vichwa.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Talanta ilikuwa sawa na kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.

Dariki ilikuwa sarafu ya dhahabu ya Waajemi. Angalia Nyongeza B14.

Au “majumba ya kulia chakula ya.”

Cheo kinachomaanisha “walinzi wa milki,” hapa cheo hicho kinawahusu magavana wa mikoa ya Milki ya Uajemi.

Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”

Tnn., “mbegu takatifu.”

Tnn., “aliyetetemeka kwa sababu ya.”

Tnn., “kigingi.”

Au “ukuta wa ulinzi.”

Au “na kuoana.”

Au “kwa kuwaingiza ndani ya nyumba zetu.”

Tnn., “wanaotetemekea.”

Au “jumba la kulia chakula la.”

Au “zingezuiliwa.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “walipeana mikono yao ili.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki