Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Wagalatia 1:1-6:18
  • Kwa Wagalatia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Wagalatia
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Kwa Wagalatia

Kwa Wagalatia

1 Paulo,+ mtume,+ si kutokana na wanadamu wala kupitia mwanadamu fulani, bali kupitia Yesu Kristo+ na Mungu Baba,+ aliyemfufua yeye kutoka kwa wafu,+ 2 na ndugu wote walio pamoja nami,+ kwa makutaniko ya Galatia:+

3 Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani+ kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo. 4 Alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu+ ili atukomboe kutoka katika mfumo mwovu wa mambo+ wa sasa, kulingana na mapenzi+ ya Mungu na Baba yetu, 5 kwake kuwe na utukufu milele na milele.+ Amina.

6 Mimi ninashangaa kwamba mnaondolewa upesi hivyo kutoka kwake Yeye+ aliyewaita ninyi kwa fadhili zisizostahiliwa+ za Kristo nanyi mnapelekwa kwenye habari njema ya aina nyingine.+ 7 Lakini si nyingine; isipokuwa tu kuna watu fulani wanaowataabisha+ ninyi na kutaka kupotosha habari njema juu ya Kristo.+ 8 Lakini, hata ikiwa sisi au malaika kutoka mbinguni tungewatangazia ninyi kuwa habari njema jambo fulani kupita lile tulilowatangazia ninyi kuwa habari njema, mtu huyo na alaaniwe.+ 9 Kama vile tulivyosema hapo juu, sasa mimi pia nasema tena, Mtu yeyote anayewatangazia ninyi jambo fulani kupita lile mlilopokea+ kuwa hilo ni habari njema, na alaaniwe.

10 Kwa kweli, je, sasa ninajaribu kushawishi wanadamu au Mungu? Au je, ninatafuta kuwapendeza wanadamu?+ Kama ningekuwa bado ninawapendeza wanadamu,+ mimi singekuwa mtumwa+ wa Kristo. 11 Kwa maana nawajulisha ninyi, akina ndugu, kwamba habari njema ambayo niliitangaza kuwa habari njema si jambo la kibinadamu;+ 12 kwa maana sikuipokea kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa hiyo, isipokuwa kupitia ufunuo wa Yesu Kristo.+

13 Bila shaka, ninyi mlisikia juu ya mwenendo wangu hapo zamani katika dini ya Kiyahudi,+ kwamba kufikia hatua ya kuzidi mno niliendelea kulitesa+ kutaniko la Mungu na kuliangamiza,+ 14 nami nilikuwa nikifanya maendeleo makubwa zaidi katika dini ya Kiyahudi kuliko watu wengi wa umri wangu katika jamii yangu,+ kwa kuwa nilikuwa mwenye bidii zaidi+ kwa ajili ya mapokeo+ ya baba zangu. 15 Lakini wakati Mungu, aliyenitenga mimi tangu tumbo la uzazi la mama yangu na kuniita+ kupitia fadhili zake zisizostahiliwa,+ alipoona vema 16 kumfunua Mwana wake kuhusiana nami,+ ili nitangaze habari njema juu yake kwa mataifa,+ mimi sikuingia mara moja katika mashauriano pamoja na watu wenye mwili na damu.+ 17 Wala sikupanda kwenda Yerusalemu kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu,+ bali nilienda nikaingia Arabia, nami nikarudi tena Damasko.+

18 Kisha miaka mitatu baadaye nilipanda kwenda Yerusalemu+ kumtembelea Kefa,+ nami nikakaa pamoja naye siku kumi na tano. 19 Lakini sikuona mwingine yeyote wa wale mitume, isipokuwa Yakobo+ ndugu+ ya Bwana. 20 Sasa kuhusu mambo ninayowaandikia ninyi, tazameni! machoni pa Mungu, mimi sisemi uwongo.+

21 Baada ya hayo nilienda+ katika maeneo ya Siria na ya Kilikia. 22 Lakini mimi sikujulikana kwa uso kwa makutaniko ya Yudea yaliyokuwa katika muungano na Kristo;+ 23 yalikuwa tu yakisikia: “Yule mtu ambaye hapo zamani alitutesa+ sasa anaitangaza habari njema juu ya imani ambayo hapo zamani aliiangamiza.”+ 24 Kwa hiyo wakaanza kumtukuza+ Mungu kwa sababu yangu.

2 Kisha baada ya miaka kumi na minne nilipanda tena kwenda Yerusalemu+ pamoja na Barnaba,+ nikichukua pia Tito pamoja nami. 2 Lakini nilipanda kwenda kutokana na ufunuo.+ Nami nikaweka mbele yao+ habari njema ambayo ninahubiri kati ya mataifa, hata hivyo, kwa faragha, mbele ya wale waliokuwa watu wenye kutokeza, ili isije kuwa kwamba kwa njia fulani nilikuwa ninakimbia+ au nilikuwa nimekimbia bure.+ 3 Lakini, hata Tito,+ aliyekuwa pamoja nami, hakulazimishwa kutahiriwa,+ ijapokuwa alikuwa Mgiriki. 4 Lakini kwa sababu ya akina ndugu wa uwongo+ walioingizwa ndani kimya-kimya,+ walioingia kisirisiri ili kupeleleza uhuru+ wetu tulio nao katika muungano na Kristo Yesu, ili watufanye sisi kuwa watumwa+ kabisa— 5 kwa hao sisi hatukuwaachia nafasi kwa kujitiisha,+ hapana, hata kwa saa moja, ili kweli+ ya habari njema iendelee kuwa pamoja nanyi.

6 Lakini kwa upande wa wale walioonekana kuwa ni kitu+—hata kama walikuwa watu wa namna gani hapo zamani haileti tofauti yoyote kwangu+—Mungu hafuati sura ya nje+ ya mwanadamu—kwangu, kwa kweli, hao watu wenye kutokeza hawakunipa jambo lolote jipya. 7 Bali, kinyume chake, walipoona kwamba nilikuwa nimekabidhiwa+ habari njema kwa ajili ya wale wasiotahiriwa,+ kama vile Petro alivyokuwa nayo kwa ajili ya wale waliotahiriwa+— 8 kwa maana Yeye aliyempa Petro nguvu zinazohitajika kwa ajili ya utume kwa wale waliotahiriwa alinipa mimi pia nguvu+ kwa ajili ya wale walio wa mataifa; 9 ndiyo, walipokuja kujua fadhili zisizostahiliwa+ nilizopewa,+ Yakobo+ na Kefa na Yohana, wale walioonekana kuwa nguzo,+ walinipa mimi na Barnaba+ mkono wa kuume wa kushirikiana pamoja,+ ili sisi twende kwa mataifa, bali wao waende kwa wale waliotahiriwa. 10 Ila sisi tuwakumbuke walio maskini.+ Jambo hili mimi pia nimejitahidi sana kulifanya.+

11 Hata hivyo, Kefa+ alipokuja Antiokia,+ nilimpinga uso kwa uso, kwa sababu alistahili kuhukumiwa hatia.+ 12 Kwa maana kabla ya kufika kwa watu fulani kutoka kwa Yakobo,+ alikuwa akila+ chakula pamoja na watu wa mataifa; lakini walipofika, akaanza kujiondoa na kujitenga mwenyewe, kwa kuwaogopa+ hao wa jamii ya waliotahiriwa.+ 13 Wale Wayahudi wengine pia walijiunga naye katika kufanya unafiki+ huo, hivi kwamba hata Barnaba+ akaongozwa pamoja nao katika unafiki wao. 14 Lakini nilipoona kwamba hawakuwa wakitembea kwa unyoofu kulingana na kweli ya habari njema,+ nilimwambia Kefa mbele yao wote:+ “Ikiwa wewe, ingawa ni Myahudi, unaishi kama vile mataifa wanavyoishi, na si kama Wayahudi wanavyoishi, kwa nini wewe unawalazimisha watu wa mataifa kuishi kulingana na mazoea ya Kiyahudi?”+

15 Sisi tulio Wayahudi kwa asili,+ na si watenda-dhambi+ kutoka kwa mataifa, 16 tukijua kama vile tunavyojua kwamba mtu hutangazwa kuwa mwadilifu,+ si kwa sababu ya matendo ya sheria, bali tu kupitia imani+ kumwelekea Kristo Yesu, hata sisi tumeweka imani yetu katika Kristo Yesu, ili tutangazwe kuwa waadilifu kutokana na imani kumwelekea Kristo,+ na si kutokana na matendo ya sheria, kwa sababu hakuna mwili wowote utakaotangazwa kuwa mwadilifu kutokana na matendo ya sheria.+ 17 Basi ikiwa sisi, katika kutafuta kutangazwa kuwa waadilifu kwa njia ya Kristo,+ sisi wenyewe pia tumepatikana kuwa watenda-dhambi,+ je, Kristo kwa kweli ni mhudumu wa dhambi?+ Hilo lisitendeke kamwe! 18 Kwa maana ikiwa ninayajenga tena yale mambo ambayo wakati mmoja niliyabomoa,+ mimi najionyesha mwenyewe kuwa mkosaji.+ 19 Kwa habari yangu, kupitia sheria nilikufa kuielekea sheria,+ ili niwe hai kumwelekea Mungu.+ 20 Mimi nimetundikwa mtini pamoja na Kristo.+ Si mimi tena niliye hai,+ bali Kristo ndiye anayeishi katika muungano na mimi.+ Kwa kweli, uhai ninaoishi sasa+ katika mwili naishi kwa imani ambayo ni kumwelekea Mwana wa Mungu, aliyenipenda mimi na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.+ 21 Mimi sizitupi fadhili zisizostahiliwa za Mungu;+ kwa maana ikiwa uadilifu ni kupitia sheria,+ Kristo kwa kweli alikufa bure tu.+

3 Enyi Wagalatia wasio na akili, ni nani huyo aliyewaleta chini ya uvutano mwovu,+ ninyi ambao machoni penu Yesu Kristo alionyeshwa waziwazi akiwa ametundikwa mtini?+ 2 Nataka kujifunza hili peke yake kutoka kwenu: Je, mlipokea roho+ kutokana na matendo ya sheria+ au kutokana na kusikia+ kwa njia ya imani? 3 Je, ninyi hamna akili kabisa? Baada ya kuanza katika roho,+ je, sasa mnamalizia katika mwili?+ 4 Je, mlipatwa na mateso mengi sana bila kusudi?+ Ikiwa kwa kweli ilikuwa bila kusudi lolote. 5 Kwa hiyo, yeye anayewapa ninyi roho+ na kufanya matendo yenye nguvu+ katikati yenu, je, yeye hufanya hivyo kutokana na matendo ya sheria au kutokana na kusikia kwa njia ya imani? 6 Kama vile Abrahamu “alivyokuwa na imani katika Yehova, na ikahesabiwa kwake kuwa ni uadilifu.”+

7 Hapana shaka mnajua kwamba wale wanaoshikamana na imani+ ndio wale walio wana wa Abrahamu.+ 8 Sasa Andiko, likitangulia kuona kwamba Mungu atawatangaza watu wa mataifa kuwa waadilifu kutokana na imani, lilitangaza habari njema kimbele kwa Abrahamu, yaani: “Kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”+ 9 Kwa sababu hiyo wale wanaoshikamana na imani wanabarikiwa+ pamoja na Abrahamu mwaminifu.+

10 Kwa maana wote wanaotegemea matendo ya sheria wako chini ya laana; kwa maana imeandikwa: “Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha kukunjwa cha Sheria ili ayafanye.”+ 11 Tena, kwamba hakuna yeyote ambaye kwa njia ya sheria hutangazwa kuwa mwadilifu+ kwa Mungu ni wazi, kwa maana “mwadilifu ataishi kwa sababu ya imani.”+ 12 Sasa Sheria haishikamani na imani, bali “yeye anayezifanya ataishi kwa hizo.”+ 13 Kristo kwa kutununua+ alituachilia huru+ kutoka katika laana ya Sheria kwa yeye kuwa laana+ badala yetu, kwa sababu imeandikwa: “Amelaaniwa kila mtu aliyetundikwa juu ya mti.”+ 14 Kusudi lilikuwa kwamba baraka ya Abrahamu ije kupitia Yesu Kristo kwa ajili ya mataifa,+ ili tuipokee roho iliyoahidiwa+ kupitia imani yetu.+

15 Akina ndugu, nasema kwa njia ya mfano wa mwanadamu: Agano lililohalalishwa, ingawa ni la mwanadamu, hakuna yeyote anayelifuta au kuongeza jambo juu yake.+ 16 Sasa ahadi zilitolewa kwa Abrahamu+ na kwa uzao wake.+ Haisemi: “Na kwa wazao,” kana kwamba ni wengi wa namna hiyo, bali kana kwamba ni mmoja:+ “Na kwa uzao wako,”+ ambaye ni Kristo.+ 17 Zaidi, mimi nasema hivi: Kuhusu agano lililohalalishwa na Mungu+ hapo kwanza, Sheria ambayo imekuja kuwapo miaka 430+ baadaye hailitangui, ili kuifuta ahadi.+ 18 Kwa maana ikiwa urithi ni kutokana na sheria, hautokani tena na ahadi;+ lakini Mungu amempa huo Abrahamu kwa fadhili kupitia ahadi.+

19 Basi, kwa nini Sheria? Iliongezwa ili kufanya makosa yawe wazi,+ mpaka ufike uzao+ ambao ulikuwa umepewa ahadi; na ilipitishwa kupitia malaika+ kwa mkono wa mpatanishi.+ 20 Sasa hakuna mpatanishi mahali ambapo ni mtu mmoja tu anayehusika, lakini Mungu ni mmoja tu.+ 21 Kwa hiyo, je, Sheria inapinga ahadi za Mungu?+ Hilo na lisitendeke kamwe! Kwa maana kama ingalitolewa sheria inayoweza kutoa uhai,+ kwa kweli uadilifu ungalikuwa kwa njia ya sheria.+ 22 Lakini Andiko+ liliyafunga mambo yote pamoja katika kifungo cha dhambi,+ ili ahadi inayotokana na imani kumwelekea Yesu Kristo ipewe wale wanaoamini.+

23 Hata hivyo, kabla ya ile imani kufika,+ tulikuwa tukilindwa chini ya sheria,+ tukiwekwa pamoja kifungoni, tukiitazamia imani iliyokusudiwa kufunuliwa.+ 24 Kwa sababu hiyo Sheria imekuwa mtunzaji wetu kutuongoza kwa Kristo,+ ili tutangazwe kuwa waadilifu+ kutokana na imani. 25 Lakini sasa kwa kuwa imani imefika,+ sisi hatuko tena chini ya mtunzaji.+

26 Ninyi nyote, kwa kweli, ni wana+ wa Mungu kupitia imani yenu katika Kristo Yesu. 27 Kwa maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo+ mmemvaa Kristo.+ 28 Hakuna Myahudi wala Mgiriki,+ hakuna mtumwa wala mtu huru,+ hakuna mwanamume wala mwanamke;+ kwa maana ninyi nyote ni mtu mmoja katika muungano na Kristo Yesu.+ 29 Zaidi ya hayo, ikiwa ninyi ni wa Kristo, ninyi kwa kweli ni uzao wa Abrahamu,+ warithi kuhusiana na ahadi.+

4 Basi nasema kwamba wakati mrithi anapokuwa angali mtoto mchanga hatofautiani hata kidogo na mtumwa,+ ingawa yeye ni bwana wa vitu vyote, 2 bali yeye yuko chini ya watu wenye kusimamia+ na chini ya wasimamizi-nyumba mpaka siku ambayo baba yake aliiweka kimbele. 3 Vivyo hivyo sisi pia, tulipokuwa watoto wachanga, tuliendelea kutumikishwa na mambo ya msingi+ yaliyo ya ulimwengu. 4 Lakini wakati kamili ulipofika,+ Mungu alimtuma Mwana wake,+ aliyezaliwa na mwanamke+ na aliyekuja kuwa chini ya sheria,+ 5 ili awaachilie huru kwa kuwanunua+ wale walio chini ya sheria,+ ili sisi nasi tufanywe kuwa wana.+

6 Sasa kwa sababu ninyi ni wana, Mungu ametuma roho+ ya Mwana wake ndani ya mioyo yetu nayo hupaaza sauti: “Abba, Baba!”+ 7 Basi, wewe si mtumwa tena bali ni mwana; na ikiwa ni mwana, pia ni mrithi kupitia Mungu.+

8 Hata hivyo, wakati hamkumjua Mungu,+ ndipo mlipoitumikia ile ambayo kwa asili si miungu.+ 9 Lakini sasa kwa kuwa mmemjua Mungu, au afadhali zaidi kwamba sasa Mungu amewajua ninyi,+ kwa nini mnarudi tena kwenye mambo ya msingi+ yaliyo dhaifu+ na yasiyo na maana na kutaka kuyatumikia kwa mara nyingine tena?+ 10 Mnashika kwa uangalifu mwingi siku+ na miezi+ na majira na miaka. 11 Mimi naogopa kwa ajili yenu, isiwe kwamba kwa njia fulani nimejitaabisha kwa ajili yenu bila kusudi+ lolote.

12 Akina ndugu, ninawaomba ninyi, Iweni kama nilivyo,+ kwa sababu mimi nilikuwa pia kama mlivyo.+ Hamkunitendea kosa lolote.+ 13 Lakini mnajua kwamba ilikuwa kupitia ugonjwa wa mwili wangu kwamba niliwatangazia ninyi habari njema mara ya kwanza.+ 14 Na lililokuwa jaribu kwenu katika mwili wangu, hamkulitendea kwa dharau au kulitemea mate kwa chuki; bali mlinipokea kama malaika+ wa Mungu, kama Kristo Yesu.+ 15 Basi, iko wapi ile furaha mliyokuwa nayo?+ Kwa maana nawatolea ninyi ushahidi kwamba, kama ingaliwezekana, mngaling’oa macho yenu na kunipa hayo.+ 16 Hivyo basi, je, nimekuwa adui+ yenu kwa sababu nawaambia ninyi kweli?+ 17 Wao wanawatafuta ninyi kwa bidii,+ si kwa uzuri, bali wanataka kuwazuia ninyi kutoka kwangu, ili mwatafute wao kwa bidii.+ 18 Hata hivyo, ni vema kwenu mkitafutwa kwa bidii kwa kusudi zuri+ nyakati zote, na si wakati tu mimi ninapokuwa pamoja nanyi,+ 19 watoto wangu wadogo,+ ambao tena nina maumivu ya kuwazaa mpaka Kristo aumbike ndani yenu.+ 20 Lakini ningependa kuwa pamoja nanyi sasa hivi+ na kusema kwa njia tofauti, kwa sababu nahangaika+ juu yenu.

21 Mniambie, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria,+ Je, hamsikii Sheria?+ 22 Kwa mfano, imeandikwa kwamba Abrahamu alipata wana wawili, mmoja kwa njia ya kijakazi+ na mmoja kwa njia ya mwanamke huru;+ 23 lakini yule wa kijakazi kwa kweli alizaliwa katika namna ya mwili,+ yule mwingine wa mwanamke huru kupitia ahadi.+ 24 Mambo haya yanasimama yakiwa tukio la mfano;+ kwa maana wanawake hawa wanamaanisha maagano mawili,+ moja kutoka Mlima Sinai,+ ambalo huzaa watoto kwa ajili ya utumwa, na ambalo ni Hagari. 25 Basi Hagari huyu anamaanisha Sinai,+ mlima ulio Arabia, naye analingana na Yerusalemu la leo, kwa maana liko katika utumwa+ pamoja na watoto wake. 26 Lakini Yerusalemu+ la juu liko huru, nalo ni mama yetu.+

27 Kwa maana imeandikwa: “Furahi, wewe mwanamke tasa usiyezaa; paaza sauti na kupaaza kilio kikubwa, wewe mwanamke ambaye huna maumivu ya kuzaa mtoto; kwa maana watoto wa mwanamke aliye na ukiwa ni wengi kuliko wale wa yule aliye na mume.”+ 28 Basi, akina ndugu, sisi ni watoto wa ahadi kama Isaka alivyokuwa.+ 29 Lakini kama ilivyokuwa wakati huo, yule aliyezaliwa katika namna ya mwili alianza kumtesa+ yule aliyezaliwa katika namna ya roho, ndivyo ilivyo pia na sasa.+ 30 Hata hivyo, Andiko linasema nini? “Mfukuze kijakazi na mwana wake, kwa maana mwana wa kijakazi hatakuwa mrithi hata kidogo pamoja na mwana wa mwanamke huru.”+ 31 Kwa hiyo, akina ndugu, sisi ni watoto, si wa kijakazi,+ bali wa yule mwanamke huru.+

5 Kristo alituweka huru+ tuwe na uhuru wa namna hiyo. Kwa hiyo simameni imara,+ na msijiache wenyewe kufungwa tena katika nira ya utumwa.+

2 Oneni! Mimi, Paulo, ninawaambia ninyi kwamba mkitahiriwa,+ Kristo hatakuwa na faida kwenu. 3 Zaidi ya hayo, natoa ushahidi tena kwa kila mtu anayetahiriwa kwamba yuko chini ya wajibu kuitimiza Sheria yote.+ 4 Mmetenganishwa na Kristo, hata muwe ninyi ni nani ambao mnajaribu kutangazwa kuwa waadilifu kwa njia ya sheria;+ mmeanguka kutoka kwenye fadhili zake zisizostahiliwa.+ 5 Kwa upande wetu sisi kwa njia ya roho tunangojea kwa hamu uadilifu uliotumainiwa kutokana na imani.+ 6 Kwa maana kwa habari ya Kristo Yesu tohara haina faida yoyote wala kutotahiriwa,+ bali imani+ inayotenda kupitia upendo+ ina faida.

7 Mlikuwa mnakimbia vyema.+ Ni nani aliyewazuia msiendelee kuitii kweli?+ 8 Ushawishi wa namna hii hautoki kwa Yule anayewaita ninyi.+ 9 Chachu kidogo huchachusha donge zima.+ 10 Nina uhakika+ juu yenu ninyi ambao mko katika muungano+ na Bwana kwamba hamtakuja kufikiri tofauti; lakini yule anayewasababishia ninyi taabu+ atachukua hukumu yake,+ hata awe ni nani. 11 Kwa habari yangu, akina ndugu, ikiwa bado ninahubiri tohara, kwa nini bado ninateswa? Basi, kwa kweli, kikwazo+ cha mti wa mateso+ kimefutwa.+ 12 Ningependa watu wanaojaribu kuwaangusha+ ninyi wajihasi wenyewe.+

13 Bila shaka, ninyi mliitiwa uhuru,+ akina ndugu; ila msiutumie uhuru huu kuuchochea mwili,+ bali kupitia upendo mtumikiane.+ 14 Kwa maana Sheria nzima hupata utimizo+ katika neno moja, yaani: “Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.”+ 15 Lakini, ikiwa mnaendelea kuumana na kulana,+ jihadharini kwamba msije mkaangamizana.+

16 Lakini nasema, Endeleeni kutembea kwa roho+ nanyi hamtatenda tamaa ya kimwili hata kidogo.+ 17 Kwa maana mwili katika tamaa yake unapingana na roho,+ na roho inapingana na mwili; kwa maana vitu hivyo vinapingana, hivi kwamba mambo yale ambayo mnapenda kufanya hamyafanyi.+ 18 Zaidi ya hayo, ikiwa mnaongozwa na roho,+ ninyi hamko chini ya sheria.+

19 Sasa matendo ya mwili ni wazi,+ nayo ni uasherati,+ uchafu, mwenendo mpotovu,+ 20 ibada ya sanamu, mazoea ya kuwasiliana na pepo,+ uadui, mizozo, wivu, milipuko ya hasira, magomvi, migawanyiko, madhehebu, 21 husuda, vipindi vya kulewa,+ karamu za kupindukia, na mambo kama hayo. Kuhusu mambo hayo mimi ninawaonya ninyi kimbele, kama vile nilivyowaonya kimbele, kwamba wale walio na mazoea ya kufanya+ mambo ya namna hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.+

22 Kwa upande mwingine, matunda ya roho+ ni upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema,+ imani, 23 upole, kujizuia.+ Hakuna sheria juu ya mambo hayo.+ 24 Zaidi ya hayo, wale walio wa Kristo Yesu waliutundika mwili mtini pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.+

25 Ikiwa tunaishi kwa roho, na tuendelee kutembea kwa utaratibu pia kwa roho.+ 26 Na tusiwe wenye kujisifu, wenye kuchochea mashindano+ juu ya mtu na mwenzake, tukioneana wivu.+

6 Akina ndugu, hata mtu akijikwaa katika kosa+ fulani kabla ya yeye kulijua, ninyi mlio na sifa za kustahili kiroho+ jaribuni kumrekebisha upya mtu huyo katika roho ya upole,+ huku kila mmoja wenu akiendelea kujiangalia,+ ili wewe pia usije ukajaribiwa.+ 2 Endeleeni kubebeana mizigo mizito,+ na hivyo kuitimiza sheria ya Kristo.+ 3 Kwa maana yeyote akifikiri kuwa yeye ni kitu wakati yeye si kitu,+ anaidanganya akili yake mwenyewe. 4 Lakini kila mmoja na athibitishe kazi yake mwenyewe ni nini,+ kisha atakuwa na sababu ya kufurahi kwa habari yake mwenyewe peke yake, na si kwa kujilinganisha+ na mtu yule mwingine. 5 Kwa maana kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe.+

6 Zaidi ya hayo, mtu yeyote anayefundishwa neno kwa mdomo+ na ashiriki+ katika mambo yote mema pamoja na yule anayetoa fundisho hilo la mdomo.+

7 Msipotoshwe:+ Mungu si wa kudhihakiwa.+ Kwa maana lolote lile analopanda mtu, atavuna hilo pia;+ 8 kwa sababu yeye anayepanda kwa mwili wake atavuna uharibifu kutokana na mwili wake,+ lakini yeye anayepanda kwa roho+ atavuna uzima wa milele kutokana na roho.+ 9 Kwa hiyo na tusife moyo katika kufanya yaliyo mema,+ kwa maana katika majira yanayofaa tutavuna ikiwa hatuchoki kabisa.+ 10 Kwa kweli, basi, tukiwa na wakati unaofaa kwa ajili ya hilo,+ tuwatendee wote mema, na hasa wale ambao katika imani ni jamaa zetu.+

11 Oneni kwamba nimewaandikia ninyi kwa herufi kubwa kwa mkono wangu mwenyewe.+

12 Wale wote wanaotaka kuwa na sura ya kupendeza katika mwili ndio wanaojaribu kuwalazimisha ninyi mtahiriwe,+ ili tu wasiteswe kwa ajili ya mti wa mateso wa Kristo,+ Yesu. 13 Kwa maana hata wale wanaotahiriwa wenyewe hawaishiki Sheria,+ lakini wanataka ninyi mtahiriwe ili wawe na sababu ya kujisifu katika mwili wenu. 14 Mimi nisijisifu kamwe, isipokuwa katika mti wa mateso+ wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia yeye ulimwengu umetundikwa mtini+ kwangu na mimi kwa ulimwengu. 15 Kwa maana tohara si kitu wala kutotahiriwa,+ bali kiumbe kipya+ ndicho kitu. 16 Na wale wote watakaotembea kwa utaratibu kwa kanuni hii ya mwenendo, juu yao kuwe na amani na rehema, ndiyo, juu ya Israeli wa Mungu.+

17 Kwa hiyo mtu yeyote asiwe akinitaabisha, kwa maana ninachukua mwilini mwangu alama+ za mtumwa wa Yesu.+

18 Akina ndugu, fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu Yesu Kristo ziwe pamoja na roho+ ambayo mnaonyesha. Amina.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki