HESABU
1 Na Yehova akasema na Musa katika jangwa la Sinai,+ katika hema ya mukutano,+ siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili kisha wao kutoka katika inchi ya Misri.+ Akamuambia: 2 “Muhesabie+ mukusanyiko wote wa Waisraeli,* kila mumoja wao* kulingana na familia yake, kulingana na jamaa zao za upande wa baba, kulingana na hesabu ya majina ya wanaume wote. 3 Wewe na Haruni munapaswa kuandikisha watu wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi+ wenye wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli, kulingana na vikundi vyao vya maaskari.*
4 “Muchukue mwanaume mumoja katika kila kabila; kila mumoja wao anapaswa kuwa kichwa cha jamaa yake ya upande wa baba.+ 5 Haya ni majina ya wanaume wenye watasimama pamoja na ninyi: katika kabila la Rubeni, Elisuri+ mwana wa Shedeuri; 6 katika kabila la Simeoni, Shelumieli+ mwana wa Zurishadai; 7 katika kabila la Yuda, Nashoni+ mwana wa Aminadabu; 8 katika kabila la Isakari, Netaneli+ mwana wa Zuari; 9 katika kabila la Zabuloni, Eliabu+ mwana wa Heloni; 10 kutoka kati ya wana wa Yosefu: katika kabila la Efraimu,+ Elishama mwana wa Amihudi; katika kabila la Manase, Gamalieli mwana wa Pedazuri; 11 katika kabila la Benyamini, Abidani+ mwana wa Gideoni; 12 katika kabila la Dani, Ahiezeri+ mwana wa Amishadai; 13 katika kabila la Asheri, Pagieli+ mwana wa Okrani; 14 katika kabila la Gadi, Eliasafu+ mwana wa Deueli; 15 katika kabila la Naftali, Ahira+ mwana wa Enani. 16 Ni hawa walichaguliwa kati ya mukusanyiko. Hao ndio wakubwa+ wa makabila ya baba zao, vichwa vya maelfu ya Israeli.”+
17 Kwa hiyo Musa na Haruni wakachukua wanaume hao wenye walikuwa wametajwa kwa majina. 18 Wakakusanya mukusanyiko wote siku ya kwanza ya mwezi wa pili, ili kila mwanaume aandikishwe kulingana na jina lake, familia yake, na jamaa zao za upande wa baba, kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi,+ 19 kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa. Kwa hiyo akawaandikisha katika jangwa la Sinai.+
20 Wana wa Rubeni, wazao wa muzaliwa wa kwanza wa Israeli,+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 21 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Rubeni ilikuwa elfu makumi ine na sita na mia tano (46 500).
22 Wazao wa Simeoni+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 23 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Simeoni ilikuwa elfu makumi tano na kenda na mia tatu (59 300).
24 Wazao wa Gadi+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 25 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Gadi ilikuwa elfu makumi ine na tano na mia sita makumi tano (45 650).
26 Wazao wa Yuda+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 27 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Yuda ilikuwa elfu makumi saba na ine na mia sita (74 600).
28 Wazao wa Isakari+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 29 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Isakari ilikuwa elfu makumi tano na ine na mia ine (54 400).
30 Wazao wa Zabuloni+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 31 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Zabuloni ilikuwa elfu makumi tano na saba na mia ine (57 400).
32 Wazao wa Yosefu kupitia Efraimu+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 33 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Efraimu ilikuwa elfu makumi ine na mia tano (40 500).
34 Wazao wa Manase+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 35 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Manase ilikuwa elfu makumi tatu na mbili na mia mbili (32 200).
36 Wazao wa Benyamini+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 37 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Benyamini ilikuwa elfu makumi tatu na tano na mia ine (35 400).
38 Wazao wa Dani+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 39 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Dani ilikuwa elfu makumi sita na mbili na mia saba (62 700).
40 Wazao wa Asheri+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 41 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Asheri ilikuwa elfu makumi ine na moja na mia tano (41 500).
42 Wazao wa Naftali+ waliandikwa kulingana na majina yao, familia zao, na jamaa zao za upande wa baba. Wanaume wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi walihesabiwa, 43 na hesabu ya wale wenye waliandikishwa katika kabila la Naftali ilikuwa elfu makumi tano na tatu na mia ine (53 400).
44 Hao ndio waliandikishwa na Musa na Haruni na wale wakubwa kumi na mbili (12) wa Israeli, kila mumoja aliwakilisha jamaa yake ya upande wa baba. 45 Waisraeli wote kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye wangeweza kutumika katika jeshi la Israeli waliandikishwa kulingana na jamaa yao ya upande wa baba, 46 na hesabu ya wale wote wenye waliandikishwa ilikuwa elfu mia sita na tatu na mia tano makumi tano (603 550).+
47 Lakini Walawi+ hawakuandikishwa kati yao, kulingana na kabila la baba zao.+ 48 Kwa hiyo Yehova akamuambia Musa: 49 “Ni kabila la Lawi tu ndilo hautaandikisha, na haupaswe kuwahesabia pamoja na Waisraeli wengine.+ 50 Unapaswa kuwaweka Walawi wasimamie tabenakulo ya Ushuhuda+ na vyombo vyake vyote na kila kitu chenye kuwa ndani yake.+ Watabeba tabenakulo hiyo na vyombo vyake vyote,+ na watatumikia kwenye tabenakulo,+ na watapiga kambi kuizunguka.+ 51 Kila wakati tabenakulo inahamishwa, Walawi ndio wanapaswa kuibomoa;+ na wakati inasimamishwa, Walawi ndio wanapaswa kuisimamisha; na kama mutu yeyote mwenye haruhusiwe* anakaribia anapaswa kuuawa.+
52 “Kila Mwisraeli anapaswa kusimamisha hema yake katika kambi yenye alipewa, kila mutu kulingana na mugawanyo wake wa makabila tatu (3),*+ kulingana na kikundi chake cha maaskari.* 53 Na Walawi wanapaswa kupiga kambi kuzunguka tabenakulo ya Ushuhuda, ili kasirani yangu isiwakie mukusanyiko wa Waisraeli;+ na Walawi wanapaswa kutunza* tabenakulo ya Ushuhuda.”+
54 Watu wa Israeli wakafanya mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru Musa. Ni vile walifanya kabisa.
2 Sasa Yehova akasema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 2 “Waisraeli wanapaswa kupiga kambi mahali mugawanyo wao wa makabila tatu (3)+ umepewa, kila mutu karibu na alama ya jamaa yake ya upande wa baba. Wanapaswa kupiga kambi kuangaliana na hema ya mukutano, kuizunguka pande zote.
3 “Wale wenye watapiga kambi upande wa mashariki, kuelekea mahali jua linatokea, ni mugawanyo wa makabila tatu (3) wa kambi ya Yuda kulingana na vikundi vyao vya maaskari;* mukubwa wa wana wa Yuda ni Nashoni+ mwana wa Aminadabu. 4 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi saba na ine na mia sita (74 600).+ 5 Wale wenye watapiga kambi karibu naye ni kabila la Isakari; mukubwa wa wana wa Isakari ni Netaneli+ mwana wa Zuari. 6 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi tano na ine na mia ine (54 400).+ 7 Kisha ni kabila la Zabuloni; mukubwa wa wana wa Zabuloni ni Eliabu+ mwana wa Heloni. 8 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi tano na saba na mia ine (57 400).+
9 “Watu wote wenye waliandikishwa katika majeshi ya kambi ya Yuda ni elfu mia moja makumi munane na sita na mia ine (186 400). Watakuwa wa kwanza kuvunja kambi.+
10 “Mugawanyo wa makabila tatu (3) wa kambi ya Rubeni+ kulingana na vikundi vyao vya maaskari* utakuwa kuelekea upande wa kusini; mukubwa wa wana wa Rubeni ni Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 11 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi ine na sita na mia tano (46 500).+ 12 Wale wenye watapiga kambi karibu naye ni kabila la Simeoni; mukubwa wa wana wa Simeoni ni Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 13 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi tano na kenda na mia tatu (59 300).+ 14 Kisha ni kabila la Gadi; mukubwa wa wana wa Gadi ni Eliasafu+ mwana wa Reueli. 15 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi ine na tano na mia sita makumi tano (45 650).+
16 “Watu wote wenye waliandikishwa katika majeshi ya kambi ya Rubeni ni elfu mia moja makumi tano na moja na mia ine makumi tano (151 450), na watakuwa wa pili kuvunja kambi.+
17 “Wakati hema ya mukutano inahamishwa,+ kambi ya Walawi inapaswa kuwa katikati ya kambi zingine.
“Wanapaswa kusafiri kwa kufuata utaratibu uleule wenye wanafuata wakati wanapiga kambi,+ kila mutu mahali pake, kulingana na migawanyo yao ya makabila tatu (3).
18 “Mugawanyo wa makabila tatu (3) wa kambi ya Efraimu kulingana na vikundi vyao vya maaskari* utakuwa kuelekea upande wa mangaribi; mukubwa wa wana wa Efraimu ni Elishama+ mwana wa Amihudi. 19 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi ine na mia tano (40 500).+ 20 Kabila la Manase litakuwa karibu naye;+ mukubwa wa wana wa Manase ni Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 21 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi tatu na mbili na mia mbili (32 200).+ 22 Kisha ni kabila la Benyamini; mukubwa wa wana wa Benyamini ni Abidani+ mwana wa Gideoni. 23 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi tatu na tano na mia ine (35 400).+
24 “Watu wote wenye waliandikishwa katika majeshi ya kambi ya Efraimu ni elfu mia moja na munane na mia moja (108 100), na watakuwa wa tatu (3) kuvunja kambi.+
25 “Mugawanyo wa makabila tatu (3) wa kambi ya Dani kulingana na vikundi vyao vya maaskari* utakuwa kuelekea upande wa kaskazini; mukubwa wa wana wa Dani ni Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 26 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi sita na mbili na mia saba (62 700).+ 27 Wenye watapiga kambi karibu naye ni kabila la Asheri; mukubwa wa wana wa Asheri ni Pagieli+ mwana wa Okrani. 28 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi ine na moja na mia tano (41 500).+ 29 Kisha ni kabila la Naftali; mukubwa wa wana wa Naftali ni Ahira+ mwana wa Enani. 30 Wale wenye waliandikishwa katika jeshi lake ni watu elfu makumi tano na tatu na mia ine (53 400).+
31 “Watu wote wenye waliandikishwa katika majeshi ya kambi ya Dani ni elfu mia moja makumi tano na saba na mia sita (157 600). Watakuwa wa mwisho kuvunja kambi,+ kulingana na migawanyo yao ya makabila tatu (3).”
32 Hao ndio Waisraeli wenye waliandikishwa kulingana na jamaa zao za upande wa baba; watu wote wenye waliandikishwa katika kambi hizo ili kuwa wanajeshi walikuwa elfu mia sita na tatu na mia tano makumi tano (603 550).+ 33 Lakini Walawi hawakuandikishwa+ pamoja na Waisraeli wengine,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa. 34 Waisraeli wakafanya mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru Musa. Ni vile walikuwa wanapiga kambi kulingana na migawanyo yao ya makabila tatu (3),+ na ni vile walikuwa wanavunja kambi,+ kila mumoja kulingana na familia yake na jamaa zao za upande wa baba.
3 Sasa hawa ndio walikuwa wazao wa familia ya* Haruni na Musa siku yenye Yehova alisema na Musa kwenye Mulima Sinai.+ 2 Haya ndiyo yalikuwa majina ya wana wa Haruni: Nadabu muzaliwa wa kwanza, Abihu,+ Eleazari,+ na Itamari.+ 3 Hayo ndiyo yalikuwa majina ya wana wa Haruni, makuhani wenye kutiwa mafuta wenye walikuwa wamewekwa katika madaraka* ili wafanye kazi ya ukuhani.+ 4 Lakini, Nadabu na Abihu walikufa mbele ya Yehova wakati walitoa moto wenye hauruhusiwe mbele ya Yehova+ katika jangwa la Sinai, na hawakukuwa na wana. Lakini Eleazari+ na Itamari+ waliendelea kufanya kazi ya ukuhani pamoja na Haruni baba yao.
5 Kisha Yehova akamuambia Musa: 6 “Leta karibu watu wa kabila la Lawi,+ na uwasimamishe mbele ya Haruni kuhani, na watamutumikia.+ 7 Watatimiza madaraka yao ya kumutumikia na ya kutumikia mukusanyiko wote mbele ya hema ya mukutano kwa kufanya kazi za tabenakulo. 8 Watatunza vifaa vyote+ vya hema ya mukutano na kutimiza madaraka yao ya kutumikia Waisraeli kwa kufanya kazi za tabenakulo.+ 9 Walawi utawapatia Haruni na wana wake. Ni watu wenye wametolewa, wamepewa Haruni kutoka kati ya Waisraeli.+ 10 Unapaswa kumuweka Haruni na wana wake katika madaraka, na watatimiza madaraka yao ya ukuhani,+ na mutu yeyote mwenye haruhusiwe* mwenye atakaribia atauawa.”+
11 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 12 “Kwa ngambo yangu, angalia! Mimi ninachukua Walawi kati ya Waisraeli pa nafasi ya wazaliwa wote wa kwanza* wa Waisraeli,+ na Walawi watakuwa wangu. 13 Kwa maana kila muzaliwa wa kwanza ni wangu.+ Siku yenye nilipiga kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri,+ nilijitakasia kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli kuanzia muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu mupaka wa munyama.+ Watakuwa wangu. Mimi ni Yehova.”
14 Yehova akaendelea kusema na Musa katika jangwa la Sinai,+ na kumuambia: 15 “Uandikishe wana wa Lawi kulingana na jamaa zao za upande wa baba na kulingana na familia zao. Unapaswa kuandikisha kila mwanaume kuanzia mwezi mumoja na zaidi.”+ 16 Kwa hiyo Musa akawaandikisha kama vile Yehova alimuagiza, kama vile alikuwa ameamuriwa. 17 Haya ndiyo yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohati, na Merari.+
18 Haya ndiyo yalikuwa majina ya wana wa Gershoni kulingana na familia zao: Libni na Shimei.+
19 Wana wa Kohati kulingana na familia zao walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli.+
20 Wana wa Merari kulingana na familia zao walikuwa Mali+ na Mushi.+
Hizo ndizo zilikuwa familia za Walawi kulingana na jamaa zao za upande wa baba.
21 Familia ya Walibni+ na familia ya Washimei zilitokana na Gershoni. Hizo ndizo zilikuwa familia za Wagershoni. 22 Hesabu ya wanaume wao wote wenye waliandikishwa kuanzia mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu saba na mia tano (7 500).+ 23 Familia za Wagershoni zilipiga kambi nyuma ya tabenakulo+ kuelekea upande wa mangaribi. 24 Mukubwa wa jamaa ya upande wa baba ya Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli. 25 Daraka la wana wa Gershoni+ katika hema ya mukutano lilikuwa kutunza tabenakulo na hema,+ kifuniko chake,+ kitambaa cha kuficha+ cha* muingilio wa hema ya mukutano, 26 mapazia yenye kuninginia+ ya kiwanja, kitambaa cha kuficha+ cha* muingilio wa kiwanja chenye kinazunguka tabenakulo na mazabahu, kamba za hema, na utumishi wote wenye unahusiana na vitu hivyo.
27 Familia ya Waamramu, familia ya Waishari, familia ya Wahebroni, na familia ya Wauzieli zilitokana na Kohati. Hizo ndizo zilikuwa familia za Wakohati.+ 28 Hesabu ya wanaume wote kuanzia mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu munane na mia sita (8 600); walikuwa na daraka la kutunza mahali patakatifu.+ 29 Familia za wana wa Kohati zilipiga kambi upande wa kusini wa tabenakulo.+ 30 Mukubwa wa jamaa ya upande wa baba ya familia za Wakohati alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.+ 31 Daraka lao lilikuwa kutunza Sanduku,+ meza,+ kinara cha taa,+ mazabahu,+ vyombo+ vyenye vilitumiwa ili kufanya utumishi wa mahali patakatifu, kitambaa cha kuficha,*+ na utumishi wote wenye ulihusiana na vitu hivyo.+
32 Kichwa cha wakubwa wa Walawi alikuwa Eleazari+ mwana wa Haruni kuhani, mwenye alikuwa mwangalizi juu ya wale wenye walipaswa kufanya kazi za mahali patakatifu.
33 Familia ya Wamali na familia ya Wamushi zilitokana na Merari. Hizo ndizo zilikuwa familia za Merari.+ 34 Hesabu ya wanaume wote wenye waliandikishwa kuanzia mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu sita na mia mbili (6 200).+ 35 Mukubwa wa jamaa ya upande wa baba ya familia za Merari alikuwa Zurieli mwana wa Abihaili. Walipiga kambi upande wa kaskazini wa tabenakulo.+ 36 Wana wa Merari walikuwa na daraka la kusimamia kadre za mbao+ za tabenakulo, fito zake,+ nguzo zake,+ vikalio vyake, vyombo vyake vyote,+ na utumishi wote wenye ulihusiana na vitu hivyo,+ 37 na pia nguzo zenye zilizunguka kiwanja pande zote na vikalio vyake,+ misumari yake ya hema, na kamba za hema hiyo.
38 Wale wenye walipiga kambi mbele ya tabenakulo kuelekea upande wa mashariki, mbele ya hema ya mukutano kuelekea mahali jua linatokea, walikuwa Musa na Haruni na wana wake. Walikuwa na daraka la kutunza patakatifu, hilo lilikuwa jambo lenye waliombwa kufanya kwa ajili ya Waisraeli. Mutu yeyote mwenye haruhusiwe* mwenye angekaribia alipaswa kuuawa.+
39 Wanaume wote Walawi kuanzia mwezi mumoja na zaidi, wenye Musa na Haruni waliandikisha kulingana na familia zao kama vile Yehova aliagiza, walikuwa elfu makumi mbili na mbili (22 000).
40 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Uandikishe wazaliwa wote wa kwanza wanaume wa Waisraeli kuanzia mwezi mumoja na zaidi,+ uwahesabie, na uandike majina yao. 41 Unapaswa kukamata Walawi kwa ajili yangu—mimi ni Yehova—pa nafasi ya wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli,+ na ukamate wanyama wa kufugwa wa Walawi pa nafasi ya wazaliwa wote wa kwanza wa wanyama wa kufugwa wa Waisraeli.”+ 42 Basi Musa akaandikisha wazaliwa wote wa kwanza kati ya Waisraeli, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru. 43 Hesabu ya wazaliwa wote wa kwanza wanaume wenye waliandikishwa kwa majina kuanzia mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu makumi mbili na mbili na mia mbili makumi saba na tatu (22 273).
44 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 45 “Chukua Walawi pa nafasi ya wazaliwa wote wa kwanza kati ya Waisraeli, na uchukue wanyama wa kufugwa wa Walawi pa nafasi ya wanyama wao wa kufugwa, na Walawi wanapaswa kuwa wangu. Mimi ni Yehova. 46 Ili kulipa bei ya ukombozi+ ya wale wazaliwa wa kwanza mia mbili makumi saba na tatu (273) wa Waisraeli wenye wanazidi hesabu ya Walawi,+ 47 kamata shekeli* tano (5) kwa ajili ya kila mumoja wao,+ kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.* Shekeli moja ni gera* makumi mbili (20).+ 48 Utamupatia Haruni na wana wake feza hizo zenye ni bei ya ukombozi ya wale wenye wanazidi hesabu ya Walawi.” 49 Kwa hiyo Musa akakamata feza za bei ya ukombozi kutoka kwa wale wenye walizidi bei ya ukombozi ya Walawi. 50 Alikamata feza hizo kutoka kwa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, shekeli elfu moja na mia tatu makumi sita na tano (1 365), kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu. 51 Kisha Musa akamupatia Haruni na wana wake zile feza za bei ya ukombozi kulingana na neno la* Yehova, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
4 Sasa Yehova akasema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 2 “Wana wa Kohati wanapaswa kuhesabiwa+ kati ya wana wa Lawi, kulingana na familia zao na kulingana na jamaa zao za upande wa baba, 3 wote wenye miaka kuanzia makumi tatu (30)+ mupaka makumi tano (50)+ wenye wako katika kikundi chenye kilipewa kazi ya kutumika katika hema ya mukutano.+
4 “Huu ndio utumishi wa wana wa Kohati katika hema ya mukutano.+ Ni kitu kitakatifu sana: 5 Haruni na wana wake wataingia wakati kambi inaondoka na watashusha pazia lenye kuficha+ na kufunika sanduku+ la Ushuhuda kwa pazia hilo. 6 Watatia kifuniko cha ngozi ya sili* juu yake na kutandika juu yake kitambaa cha rangi ya bluu na kutia fito za kubebea sanduku+ kwenye nafasi yazo.
7 “Pia watatandika kitambaa cha rangi ya bluu juu ya meza ya mikate ya wonyesho,+ na juu yake watatia sahani, vikombe, mabakuli, na mitungi ya toleo la kinywaji;+ toleo la mikate lenye linatolewa kwa ukawaida+ linapaswa kubakia juu ya meza hiyo. 8 Watatandika kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa juu ya vitu hivyo na watafunika meza hiyo kwa kifuniko cha ngozi ya sili* na kutia fito za kuibebea+ kwenye nafasi yazo. 9 Kisha watakamata kitambaa cha rangi ya bluu na kufunika kinara cha taa+ kwa ajili ya mwangaza, pamoja na taa zake,+ vifaa vyake vya kushikia tambi,* vyetezo vyake,+ na vyombo vyake vyote vya kuwekea mafuta vyenye vinatumiwa kwa ajili ya kinara hicho. 10 Watatia kinara hicho pamoja na vyombo vyake vyote ndani ya kifuniko cha ngozi ya sili* na kukitia kwenye ufito wa kubebea. 11 Na watatandika kitambaa cha rangi ya bluu juu ya mazabahu ya zahabu,+ wataifunika kwa kifuniko cha ngozi ya sili,* na watatia fito za kuibebea+ kwenye nafasi yazo. 12 Kisha watakamata vyombo vyote+ vya utumishi vyenye wanatumia kwa ukawaida ili kutumikia katika mahali patakatifu na kuvitia ndani ya kitambaa cha rangi ya bluu na kuvifunika kwa kifuniko cha ngozi ya sili* na watavitia kwenye ufito wa kubebea.
13 “Wataondoa majivu* kwenye mazabahu+ na kutandika kitambaa cha manyoya ya kondoo cha rangi ya zambarau juu ya mazabahu hiyo. 14 Watatia juu yake vyombo vyake vyote vyenye vinatumiwa wakati wanatumikia kwenye mazabahu: vyetezo, kanya,* vipao,* na mabakuli, vyombo vyote vya mazabahu;+ na watatandika juu yake kifuniko cha ngozi ya sili* na kuingiza fito za kuibebea+ kwenye nafasi yazo.
15 “Haruni na wana wake wanapaswa kumaliza kufunika mahali patakatifu+ na vifaa vyote vya mahali patakatifu wakati kambi itaondoka. Kisha wana wa Kohati wataingia ili kuvibeba,+ lakini hawapaswe kugusa mahali patakatifu ili wasikufe.+ Vitu hivyo ni daraka la* wana wa Kohati kuhusiana na hema ya mukutano.
16 “Eleazari+ mwana wa Haruni kuhani iko* na daraka la kusimamia mafuta kwa ajili ya mwangaza,+ uvumba wenye marashi,+ toleo la nafaka lenye linatolewa kwa ukawaida, na mafuta ya kutia mafuta.+ Ni yeye mwangalizi wa tabenakulo yote na vitu vyote vyenye kuwa ndani, pamoja na mahali patakatifu na vyombo vyake.”
17 Yehova akasema tena na Musa na Haruni, na kuwaambia: 18 “Musiache kabila la familia za Wakohati+ liondolewe katikati ya Walawi. 19 Lakini mufanye jambo hili kusudi waendelee kuishi na kusudi wasikufe kwa sababu ya kukaribia vitu vitakatifu sana.+ Haruni na wana wake wataingia na kumupatia kila mumoja wao kazi yake na vitu vyenye anapaswa kubeba. 20 Hawapaswe kuingia na kuona vitu vitakatifu hata kwa wakati kidogo, ili wasikufe.”+
21 Kisha Yehova akasema na Musa, na kumuambia: 22 “Wana wa Gershoni wanapaswa kuhesabiwa+ kulingana na jamaa zao za upande wa baba na familia zao. 23 Utaandikisha wale wote wenye miaka kuanzia makumi tatu (30) mupaka makumi tano (50) wenye wako katika kikundi chenye kimepewa kazi ya kutumika katika hema ya mukutano. 24 Hivi ndivyo vitu vyenye familia za Wagershoni zimepewa ili wavitunze na kuvibeba:+ 25 Watabeba vitambaa vya tabenakulo,+ hema ya mukutano, kifuniko chake na kifuniko cha ngozi ya sili* chenye kuwa juu yake,+ kitambaa cha kuficha cha* muingilio wa hema ya mukutano,+ 26 mapazia yenye kuninginia ya kiwanja,+ kitambaa cha kuficha cha* muingilio wa kiwanja+ chenye kinazunguka tabenakulo na mazabahu, kamba zake na vyombo vyake vyote na kila kitu chenye kinatumiwa katika utumishi wa tabenakulo. Hiyo ndiyo kazi yenye wamepewa. 27 Haruni na wana wake watasimamia utumishi wote wa Wagershoni na mizigo yao;+ utawapatia mizigo hiyo yote kuwa daraka lao. 28 Huo ndio utumishi wenye familia za Wagershoni zitafanya katika hema ya mukutano,+ na Itamari mwana wa Haruni kuhani atasimamia kazi zao.+
29 “Kuhusu wana wa Merari,+ utawaandikisha kulingana na familia yao na jamaa yao ya upande wa baba. 30 Utawaandikisha kuanzia miaka makumi tatu (30) mupaka makumi tano (50), wote wenye kuwa katika kikundi chenye kimepewa kazi ya kutumika katika hema ya mukutano. 31 Hivi ndivyo vitu vyenye wako na daraka la kubeba+ kuhusiana na utumishi wao kwenye hema ya mukutano: kadre za mbao+ za tabenakulo, fito zake,+ nguzo zake,+ vikalio vyake;+ 32 nguzo+ za kiwanja chenye kuzunguka pande zote, vikalio vyake,+ misumari yake ya hema,+ na kamba za hema hiyo pamoja na vifaa vyake vyote na utumishi wote wenye unahusiana na vitu hivyo. Utawapatia kulingana na majina yao vifaa vyenye wanapaswa kubeba. 33 Ni vile familia za wana wa Merari+ zitatumika kwenye hema ya mukutano, zitasimamiwa na Itamari mwana wa Haruni kuhani.”+
34 Basi Musa na Haruni na wakubwa+ wa mukusanyiko wakaandikisha wana wa Kohati+ kulingana na familia zao na jamaa yao ya upande wa baba, 35 wote wenye miaka kuanzia makumi tatu (30) mupaka makumi tano (50) wenye walikuwa katika kikundi chenye kilipewa kazi ya kutumika katika hema ya mukutano.+ 36 Wote wenye waliandikishwa kulingana na familia zao walikuwa elfu mbili na mia saba makumi tano (2 750).+ 37 Hao ndio waliandikishwa katika familia za Wakohati, wale wote wenye walikuwa wanatumika kwenye hema ya mukutano. Musa na Haruni waliwaandikisha kama vile Yehova aliagiza kupitia Musa.+
38 Wana wa Gershoni+ waliandikishwa kulingana na familia zao na jamaa yao ya upande wa baba, 39 wale wote wenye miaka kuanzia makumi tatu (30) mupaka makumi tano (50) wenye walikuwa katika kikundi chenye kilipewa kazi ya kutumika kwenye hema ya mukutano. 40 Wote wenye waliandikishwa kulingana na familia zao na jamaa yao ya upande wa baba walikuwa elfu mbili na mia sita makumi tatu (2 630).+ 41 Hao ndio waliandikishwa katika familia za wana wa Gershoni, wale wote wenye walikuwa wanatumika kwenye hema ya mukutano. Musa na Haruni waliwaandikisha kama vile Yehova aliagiza.+
42 Wana wa Merari waliandikishwa kulingana na familia zao na jamaa yao ya upande wa baba, 43 wale wote wenye miaka kuanzia makumi tatu (30) mupaka makumi tano (50) wenye walikuwa katika kikundi chenye kilipewa kazi ya kutumika kwenye hema ya mukutano.+ 44 Wale wote wenye waliandikishwa kati yao kulingana na familia zao walikuwa elfu tatu na mia mbili (3 200).+ 45 Hao ndio waliandikishwa katika familia za wana wa Merari, wenye Musa na Haruni waliandikisha kama vile Yehova aliagiza kupitia Musa.+
46 Musa na Haruni na wakubwa wa Israeli waliandikisha Walawi hao wote kulingana na familia zao na jamaa zao za upande wa baba; 47 walikuwa na miaka kuanzia makumi tatu (30) mupaka makumi tano (50), na wote walipewa kazi ya kutumika na kubeba mizigo ya hema ya mukutano.+ 48 Wote wenye waliandikishwa walikuwa elfu munane na mia tano makumi munane (8 580).+ 49 Waliandikishwa kama vile Yehova aliagiza kupitia Musa, kila mumoja kulingana na kazi yenye alipewa na kulingana na muzigo wake; waliandikishwa kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
5 Yehova akasema tena na Musa, na kumuambia: 2 “Amuru Waisraeli watoshe katika kambi kila mutu mwenye ukoma+ na kila mutu mwenye kuwa na mutiririko+ na kila mutu mwenye amejichafua kupitia mutu mwenye amekufa.*+ 3 Ikuwe mwanaume ao mwanamuke, munapaswa kuwatosha. Munapaswa kuwatosha katika kambi, ili wasiambukize+ kambi za wale wenye ninakaa* katikati yao.”+ 4 Kwa hiyo, Waisraeli wakafanya vile na wakawatosha katika kambi. Waisraeli wakafanya kama vile Yehova alimuambia Musa.
5 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 6 “Ambia Waisraeli, ‘Kama mwanaume ao mwanamuke anafanya zambi yoyote yenye mwanadamu anaweza kufanya na anakosa uaminifu kwa Yehova, mutu huyo amekuwa* na kosa.+ 7 Anapaswa* kuungama+ zambi yenye amefanya* na kulipa malipo yote kwa ajili ya hatia yake na pia kuongeza sehemu moja ya tano (1/5) ya samani ya malipo hayo;+ ataipatia ule mwenye alikosea. 8 Lakini kama ule mutu mwenye alikosewa hana mutu wa karibu wa jamaa yake wa kupokea malipo hayo, yanapaswa kurudishwa kwa Yehova na yatakuwa ya kuhani, isipokuwa kondoo-dume wa kufunika zambi mwenye kuhani atatumia ili kufunika zambi kwa ajili ya ule mwenye alifanya zambi.+
9 “‘Kila muchango mutakatifu+ kutoka kwa Waisraeli wenye unaletwa kwa kuhani utakuwa wake.+ 10 Vitu vitakatifu vya kila mutu vitaendelea kuwa vyake mwenyewe. Kila kitu chenye mutu anapatia kuhani, kitu hicho kitakuwa cha kuhani.’”
11 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 12 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Ni hivi mutafanya kama bibi ya mutu anajiendesha mubaya na anakosa uaminifu kwa bwana yake 13 na mwanaume mwingine anafanya ngono naye,+ lakini bwana yake hajue jambo hilo na halijavumbuliwa, na hivyo amejichafua lakini hakuna mutu wa kushuhudia juu yake na hajakamatwa: 14 Ikuwe bwana yake anakuwa na wivu na anakuwa na mashaka juu ya uaminifu wa bibi yake wakati amejichafua, ao ikuwe iko* na wivu na anakuwa na mashaka juu ya uaminifu wa bibi yake ijapokuwa hakujichafua, 15 mwanaume huyo anapaswa kumupeleka bibi yake kwa kuhani, pamoja na toleo kwa ajili yake, sehemu moja ya kumi (1/10) ya efa* ya unga wa shayiri. Hapaswe kumwanga mafuta juu ya toleo hilo wala kutia ubani juu yake, kwa sababu ni toleo la nafaka la wivu, toleo la nafaka la kukumbusha hatia.
16 “‘Kuhani atamuleta mwanamuke huyo mbele na kumusimamisha mbele ya Yehova.+ 17 Kisha kuhani atakamata maji matakatifu katika chombo cha udongo, na kuhani atakamata sehemu fulani ya mavumbi katika tabenakulo na kuyatia katika maji hayo. 18 Na kuhani atamusimamisha mwanamuke huyo mbele ya Yehova na atafungua nywele za mwanamuke huyo na kutia katika mikono ya mwanamuke huyo lile toleo la nafaka la kukumbusha, ni kusema, toleo la nafaka la wivu,+ na kuhani atakuwa ameshika katika mukono wake yale maji machungu yenye kuleta laana.+
19 “‘Kisha kuhani atamuapisha mwanamuke huyo, na kumuambia: “Kama hakuna mwanaume mwingine mwenye amefanya ngono na wewe wakati ulikuwa chini ya mamlaka ya bwana yako+ na kama haukujiendesha mubaya na kujichafua, basi maji haya machungu yenye kuleta laana yasikuwe na matokeo yoyote juu yako. 20 Lakini kama umejiendesha mubaya wakati uko chini ya mamlaka ya bwana yako kwa kujichafua, na umefanya ngono na mwanaume mwingine+ zaidi ya bwana yako—” 21 Kisha kuhani atamuapisha mwanamuke huyo kiapo chenye laana, na kuhani atamuambia mwanamuke huyo: “Yehova akufanye ukuwe kitu kwa ajili ya laana na kwa ajili ya kiapo kati ya watu wako, wakati Yehova anafanya paja* lako lianguke* na tumbo lako livimbe. 22 Maji haya yenye kuleta laana yataingia katika matumbotumbo yako na kufanya tumbo lako livimbe na yatafanya paja* lako lianguke.”* Na mwanamuke huyo atasema: “Amina! Amina!”*
23 “‘Kisha kuhani ataandika laana hizo katika kitabu na kuzifuta katika maji machungu. 24 Kisha atamunywesha mwanamuke huyo maji hayo machungu yenye kuleta laana, na maji hayo yenye kuleta laana yataingia katika mwili wake na kuleta uchungu. 25 Na kuhani atakamata toleo la nafaka la wivu+ katika mukono wa mwanamuke huyo na kutikisa lile toleo la nafaka mbele na nyuma mbele ya Yehova, na atalileta karibu na mazabahu. 26 Kuhani atakamata mukono mumoja wa toleo la nafaka ili kuwa toleo la kumbukumbu na kulichoma ili litoe moshi juu ya mazabahu,+ na kisha atamunywesha mwanamuke huyo maji hayo. 27 Wakati kuhani atamunywesha mwanamuke huyo maji hayo, kama amejichafua na amefanya tendo la kukosa uaminifu kwa bwana yake, maji yenye kuleta laana yataingia katika mwili wake na kuwa kitu kichungu, na tumbo lake litavimba, na paja* lake litaanguka,* na mwanamuke huyo atakuwa kitu cha kulaaniwa kati ya watu wake. 28 Lakini, kama mwanamuke huyo hakujichafua na iko* safi, basi hatapata azabu hiyo, na ataweza kupata mimba na kuzaa watoto.
29 “‘Hiyo ndiyo sheria kuhusu wivu,+ wakati mwanamuke anajiendesha mubaya na anajichafua wakati iko* chini ya mamlaka ya bwana yake, 30 ao kama mwanaume anakuwa na wivu na anakuwa na mashaka juu ya uaminifu wa bibi yake; mwanaume huyo atasimamisha bibi yake mbele ya Yehova, na kuhani atamutendea mwanamuke huyo kulingana na sheria yote hii. 31 Mwanaume huyo hatakuwa na hatia, lakini bibi yake atajibu kwa sababu ya hatia yake.’”
6 Yehova akasema tena na Musa na kumuambia: 2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Kama mwanaume ao mwanamuke anafanya naziri ya pekee ya kuishi akiwa Munaziri*+ kwa ajili ya Yehova, 3 anapaswa kujiepusha na divai na vinywaji vingine vyenye kulewesha. Hapaswe kunywa siki* ya divai ao siki ya kitu chochote chenye kulewesha.+ Hapaswe kunywa maji yoyote yenye yalitengenezwa na zabibu, wala kula zabibu, ikuwe za mubichi ao za kukauka. 4 Siku zote za Unaziri wake hapaswe kula kitu chochote chenye kilitengenezwa na muti wa muzabibu, kuanzia zabibu zenye hazijakomaa mupaka maganda yake.
5 “‘Siku zote za naziri ya Unaziri wake wembe haupaswe kupita juu ya kichwa chake.+ Ataendelea kuwa mutakatifu kwa kuacha nywele za kichwa chake zikuwe za murefu mupaka siku zenye alijiweka pembeni kwa ajili ya Yehova zimalizike. 6 Siku zote zenye alijitenga kwa ajili ya Yehova hapaswe kumukaribia* mutu mwenye amekufa.* 7 Hata kama baba yake ao mama yake ao ndugu yake ao dada yake anakufa, hapaswe kujichafua,+ kwa sababu alama ya Unaziri wake kwa Mungu iko juu ya kichwa chake.
8 “‘Yeye ni mutakatifu kwa ajili ya Yehova siku zote za Unaziri wake. 9 Lakini kama mutu anakufa pembeni yake bila kutazamia+ na anachafua nywele zake zenye zinaonyesha kwamba amejitenga kwa ajili ya Mungu,* anapaswa kunyoa kichwa chake+ siku yenye anahakikisha utakaso wake. Anapaswa kukinyoa siku ya saba (7). 10 Na siku ya munane (8), anapaswa kumupelekea kuhani njiwa-tetere wawili ao njiwa wawili wadogo kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 11 Kuhani atatayarisha ndege mumoja kuwa toleo la zambi na mwingine kuwa toleo la kuteketezwa na atafunika zambi kwa ajili yake kwa sababu ya zambi yake+ yenye inahusiana na mutu mwenye amekufa.* Kisha anapaswa kutakasa kichwa chake siku hiyo. 12 Na anapaswa kujitenga tena kwa ajili ya Yehova kwa ajili ya siku za Unaziri wake, na ataleta mwana-kondoo dume katika mwaka wake wa kwanza kuwa toleo la hatia. Lakini, zile siku za kwanza hazitahesabiwa kwa sababu alichafua Unaziri wake.
13 “‘Hii ndiyo sheria kuhusu Munaziri: Wakati atamaliza siku za Unaziri wake,+ ataletwa kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 14 Pale atamutolea Yehova toleo lake: mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza mwenye hana kasoro kwa ajili ya toleo la kuteketezwa,+ mwana-kondoo dike mumoja katika mwaka wake wa kwanza mwenye hana kasoro kwa ajili ya toleo la zambi,+ kondoo-dume mumoja mwenye hana kasoro kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ 15 kitunga cha mikate ya muviringo yenye haina chachu yenye ilitengenezwa na unga muzuri wenye ulichanganywa na mafuta, mikate myembamba yenye haina chachu yenye ilipakwa mafuta, na toleo la nafaka+ na matoleo ya vinywaji ya zabihu hizo.+ 16 Kuhani atatoa vitu hivyo mbele ya Yehova na atatoa toleo la zambi na toleo la kuteketezwa la mutu huyo. 17 Atamutolea Yehova kondoo-dume kwa ajili ya zabihu ya ushirika pamoja na kitunga cha mikate yenye haina chachu, na kuhani atatoa toleo la nafaka+ na toleo la kinywaji la zabihu hiyo.
18 “‘Kisha Munaziri huyo atanyoa nywele za murefu za kichwa chake*+ kwenye muingilio wa hema ya mukutano, na atakamata nywele hizo za kichwa chake zenye zilikuwa za murefu wakati wa Unaziri wake na kuzitia katika moto wenye kuwa chini ya zabihu ya ushirika. 19 Na kuhani atakamata bega lenye kutokoteshwa+ la ule kondoo-dume, mukate mumoja wa muviringo wenye hauna chachu katika kile kitunga, na mukate mumoja mwembamba wenye hauna chachu, na kuvitia katika mikono ya Munaziri huyo kisha alama ya Unaziri wake kunyolewa. 20 Na kuhani atatikisa vitu hivyo mbele na nyuma vikiwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova.+ Ni kitu kitakatifu kwa ajili ya kuhani, pamoja na kifua cha toleo la kutikiswa na muguu wenye ulitolewa kuwa muchango.+ Kisha, Munaziri huyo anaweza kunywa divai.
21 “‘Hii ndiyo sheria kuhusu Munaziri+ mwenye anafanya naziri: Kama anafanya naziri na anaweza kumutolea Yehova toleo lenye haliombwe katika mambo yenye anaombwa ili kutimiza Unaziri wake, basi anapaswa kutimiza naziri yake kulingana na sheria ya Unaziri wake.’”
22 Kisha Yehova akamuambia Musa: 23 “Umuambie Haruni na wana wake, ‘Ni hivi mutabariki+ watu wa Israeli. Muwaambie:
24 “Yehova akubariki+ na kukulinda.
25 Yehova afanye uso wake ukuangazie,+ na akuonyeshe wema.
26 Yehova ainue uso wake kukuelekea na akupatie amani.”’+
27 Na wanapaswa kuweka jina langu juu ya watu wa Israeli,+ ili niwabariki.”+
7 Siku yenye Musa alimaliza kusimamisha tabenakulo,+ aliitia mafuta+ na kuitakasa, pamoja na vyombo vyake vyote, mazabahu, na vyombo vyake vyote.+ Wakati alikuwa ametia mafuta na kutakasa vitu hivyo,+ 2 wakubwa wa Israeli,+ vichwa vya jamaa zao za upande wa baba, wakatoa toleo. Wakubwa hao wa makabila wenye walisimamia kazi ya kuandikisha watu 3 wakaleta mbele ya Yehova toleo lao la magari sita (6) ya kukokotwa yenye kufunikwa na ngombe-dume kumi na mbili (12), wakubwa wawili gari moja la kukokotwa na kila mukubwa ngombe-dume mumoja; na walileta vitu hivyo mbele ya tabenakulo. 4 Yehova akamuambia Musa: 5 “Pokea vitu hivyo kutoka kwao, kwa maana vitatumiwa katika utumishi wa hema ya mukutano, na unapaswa kupatia Walawi vitu hivyo, kila mumoja kulingana na mahitaji ya kazi yake.”
6 Kwa hiyo Musa akapokea magari hayo ya kukokotwa na ngombe na kuwapatia Walawi. 7 Alipatia wana wa Gershoni magari mbili ya kukokotwa na ngombe-dume ine (4), kulingana na mahitaji ya kazi zao;+ 8 na akapatia wana wa Merari magari ine (4) ya kukokotwa na ngombe-dume munane (8), kulingana na mahitaji ya kazi zao, chini ya usimamizi wa Itamari mwana wa Haruni kuhani.+ 9 Lakini hakupatia wana wa Kohati kitu chochote kwa sababu kazi zao zilitia ndani utumishi wa mahali patakatifu,+ na walibeba vitu vitakatifu kwenye mabega yao.+
10 Sasa wakubwa hao wakaleta toleo lao wakati wa kuzinduliwa+ kwa mazabahu* katika siku yenye ilitiwa mafuta. Wakati wakubwa walileta toleo lao mbele ya mazabahu, 11 Yehova akamuambia Musa: “Kila siku, mukubwa mumoja atatoa toleo lake kwa ajili ya kuzinduliwa kwa mazabahu.”*
12 Mwenye alitoa toleo lake siku ya kwanza alikuwa Nashoni+ mwana wa Aminadabu wa kabila la Yuda. 13 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli* mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,*+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 14 kikombe kimoja cha zahabu chenye* uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 15 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 16 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 17 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Nashoni mwana wa Aminadabu.+
18 Siku ya pili, Netaneli+ mwana wa Zuari, mukubwa wa wana wa Isakari, alitoa toleo. 19 Alitoa toleo la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 20 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 21 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 22 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 23 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Netaneli mwana wa Zuari.
24 Siku ya tatu (3), mukubwa wa wana wa Zabuloni, Eliabu+ mwana wa Heloni, 25 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 26 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 27 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 28 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 29 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Eliabu+ mwana wa Heloni.
30 Siku ya ine (4), mukubwa wa wana wa Rubeni, Elisuri+ mwana wa Shedeuri, 31 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 32 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 33 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 34 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 35 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Elisuri+ mwana wa Shedeuri.
36 Siku ya tano (5), mukubwa wa wana wa Simeoni, Shelumieli+ mwana wa Zurishadai, 37 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 38 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 39 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 40 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 41 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Shelumieli+ mwana wa Zurishadai.
42 Siku ya sita (6), mukubwa wa wana wa Gadi, Eliasafu+ mwana wa Deueli, 43 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 44 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 45 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 46 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 47 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Eliasafu+ mwana wa Deueli.
48 Siku ya saba (7), mukubwa wa wana wa Efraimu, Elishama+ mwana wa Amihudi, 49 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 50 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 51 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 52 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 53 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Elishama+ mwana wa Amihudi.
54 Siku ya munane (8), mukubwa wa wana wa Manase, Gamalieli+ mwana wa Pedazuri, 55 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 56 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 57 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 58 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 59 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Gamalieli+ mwana wa Pedazuri.
60 Siku ya kenda (9), mukubwa+ wa wana wa Benyamini, Abidani+ mwana wa Gideoni, 61 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 62 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 63 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 64 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 65 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Abidani+ mwana wa Gideoni.
66 Siku ya kumi (10), mukubwa wa wana wa Dani, Ahiezeri+ mwana wa Amishadai, 67 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 68 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 69 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 70 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 71 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Ahiezeri+ mwana wa Amishadai.
72 Siku ya kumi na moja (11), mukubwa wa wana wa Asheri, Pagieli+ mwana wa Okrani, 73 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 74 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 75 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 76 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 77 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Pagieli+ mwana wa Okrani.
78 Siku ya kumi na mbili (12), mukubwa wa wana wa Naftali, Ahira+ mwana wa Enani, 79 alitoa toleo lake la sahani moja ya feza yenye uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130) na bakuli moja la feza lenye uzito wa shekeli makumi saba (70) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vilikuwa vinajaa unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 80 kikombe kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli kumi (10), chenye kujaa uvumba; 81 ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 82 mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi;+ 83 na kwa ajili ya zabihu ya ushirika,+ ngombe wawili, kondoo-dume tano (5), mbuzi-dume tano, na wana-kondoo dume tano kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo la Ahira+ mwana wa Enani.
84 Ni hilo lilikuwa toleo kwa ajili ya kuzindua+ mazabahu,* toleo lenye lilitoka kwa wakubwa wa Israeli siku yenye mazabahu ilitiwa mafuta: sahani kumi na mbili (12) za feza, mabakuli kumi na mbili ya feza, vikombe kumi na mbili vya zahabu;+ 85 kila sahani ya feza ilikuwa na uzito wa shekeli mia moja makumi tatu (130), na kila bakuli lilikuwa na uzito wa shekeli makumi saba (70), feza yote yenye ilitengeneza vyombo hivyo ilikuwa na uzito wa shekeli elfu mbili na mia ine (2 400) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu;+ 86 vile vikombe kumi na mbili (12) vya zahabu vyenye kujaa uvumba vilikuwa na uzito wa shekeli kumi (10) kila kikombe kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu, zahabu yote yenye ilitengeneza vikombe hivyo ilikuwa na uzito wa shekeli mia moja makumi mbili (120). 87 Ngombe-dume wote kwa ajili ya toleo la kuteketezwa walikuwa kumi na mbili (12), pia kondoo-dume kumi na mbili, wana-kondoo dume kumi na mbili kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja na matoleo yao ya nafaka, na wana-mbuzi kumi na mbili kwa ajili ya toleo la zambi; 88 na ngombe-dume wote kwa ajili ya zabihu ya ushirika walikuwa makumi mbili na ine (24), kondoo-dume makumi sita (60), mbuzi-dume makumi sita, na wana-kondoo dume makumi sita kila mumoja alikuwa na mwaka mumoja. Ni hilo lilikuwa toleo kwa ajili ya kuzindua+ mazabahu* kisha kuitia mafuta.+
89 Kila mara wakati Musa aliingia katika hema ya mukutano ili kuzungumuza na Mungu,*+ alikuwa anasikia sauti inazungumuza naye kutoka juu ya kifuniko+ cha sanduku la Ushuhuda, kutoka katikati ya wale makerubi wawili;+ na Mungu alikuwa anasema naye.
8 Yehova akasema na Musa, na kumuambia: 2 “Sema na Haruni na umuambie, ‘Wakati unawasha taa, taa hizo saba (7) zinapaswa kuangazia nafasi yenye kuwa mbele ya kinara cha taa.’”+ 3 Kwa hiyo Haruni akafanya hivi: Akawasha taa za kinara hicho kwa ajili ya nafasi yenye kuwa mbele ya kinara cha taa,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa. 4 Kinara hicho cha taa kilitengenezwa hivi: Kilitengenezwa na zahabu kwa kutumia nyundo;* kuanzia shina lake mupaka maua yake, kilitengenezwa kwa kutumia nyundo.+ Kinara hicho cha taa kilitengenezwa kulingana na maono+ yenye Yehova alikuwa amemuonyesha Musa.
5 Yehova akasema tena na Musa, na kumuambia: 6 “Uchukue Walawi kati ya Waisraeli, na uwatakase.+ 7 Utawatakasa hivi: Nyunyiza* maji ya kutakasa zambi juu yao, na wanapaswa kunyoa mwili wao wote kwa wembe, wafue nguo zao, na wajitakase.+ 8 Kisha watakamata ngombe-dume mudogo+ na toleo lake la nafaka+ la unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta, na utakamata ngombe-dume mwingine mudogo kwa ajili ya toleo la zambi.+ 9 Na utawaleta Walawi mbele ya hema ya mukutano na kukusanya mukusanyiko wote wa Waisraeli.+ 10 Wakati utaleta Walawi mbele ya Yehova, Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.+ 11 Na Haruni anapaswa kuwatoa* Walawi mbele ya Yehova kama toleo la kutikiswa+ kutoka kwa Waisraeli, na watafanya utumishi wa Yehova.+
12 “Kisha Walawi wataweka mikono yao juu ya vichwa vya wale ngombe-dume.+ Kisha pale, umutolee Yehova ngombe-dume mumoja kwa ajili ya toleo la zambi na mwingine kwa ajili ya toleo la kuteketezwa ili kufunika zambi+ kwa ajili ya Walawi. 13 Na utasimamisha Walawi mbele ya Haruni na wana wake na kuwatoa* kama toleo la kutikiswa kwa ajili ya Yehova. 14 Unapaswa kutenga Walawi kutoka kati ya Waisraeli, na Walawi watakuwa wangu.+ 15 Kisha, Walawi wataingia ili kutumika kwenye hema ya mukutano. Ni vile utawatakasa na kuwatoa* kama toleo la kutikiswa. 16 Kwa maana wao ni watu wenye walitolewa, walitolewa kwangu kutoka kati ya Waisraeli. Nitachukua Walawi kwa ajili yangu mwenyewe pa nafasi ya wazaliwa wote wa kwanza* wa Waisraeli.+ 17 Kwa maana kila muzaliwa wa kwanza kati ya Waisraeli ni wangu, mwanadamu na munyama.+ Niliwatakasa ili wakuwe wangu siku yenye nilimupiga na kumuua kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri.+ 18 Nitachukua Walawi pa nafasi ya wazaliwa wote wa kwanza kati ya Waisraeli. 19 Walawi nitawapatia Haruni na wana wake wakiwa watu wenye walitolewa kutoka kati ya Waisraeli, ili wafanye utumishi kwa ajili ya Waisraeli kwenye hema ya mukutano+ na ili wafunike zambi kwa ajili ya Waisraeli, kusudi pigo lolote lisitokee kati ya Waisraeli+ kwa sababu watu wa Israeli wanakaribia mahali patakatifu.”
20 Musa na Haruni na mukusanyiko wote wa Waisraeli wakawafanyia Walawi mambo hayo. Waisraeli waliwafanyia Walawi kulingana na mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru Musa juu ya Walawi. 21 Kwa hiyo Walawi wakajitakasa na kufua nguo zao,+ kisha Haruni akawatoa* kuwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova.+ Halafu Haruni akafunika zambi kwa ajili yao ili kuwatakasa.+ 22 Kisha mambo hayo, Walawi wakaingia ili kufanya utumishi wao kwenye hema ya mukutano mbele ya Haruni na wana wake. Kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa kuhusu Walawi, ni vile waliwafanyia.
23 Sasa Yehova akasema na Musa, na kumuambia: 24 “Jambo hili linahusu Walawi: Kuanzia miaka makumi mbili na tano (25) na zaidi, mwanaume atajiunga na kikundi cha wale wenye kufanya utumishi kwenye hema ya mukutano. 25 Lakini kisha miaka makumi tano (50), ataacha kufanya kazi katika kikundi cha wenye kufanya utumishi huo na hatatumika tena. 26 Anaweza kutumikia ndugu zake wenye kufanya kazi mbalimbali kwenye hema ya mukutano, lakini hapaswe kufanya utumishi pale. Ni vile utafanya kuhusu Walawi na kazi zao.”+
9 Yehova akasema na Musa katika jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza+ wa mwaka wa pili kisha wao kutoka katika inchi ya Misri, akamuambia: 2 “Waisraeli wanapaswa kutayarisha zabihu ya Pasaka+ kwa wakati wake wenye uliwekwa.+ 3 Siku ya kumi na ine (14) ya mwezi huo wakati giza linaanza,* munapaswa kuitayarisha kwa wakati wake wenye uliwekwa. Munapaswa kuitayarisha kulingana na sheria zake zote na utaratibu wake wote.”+
4 Kwa hiyo Musa akaambia Waisraeli watayarishe zabihu ya Pasaka. 5 Kisha wakatayarisha zabihu ya Pasaka katika jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na ine (14) ya mwezi huo wakati giza linaanza.* Waisraeli wakafanya kulingana na mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
6 Sasa kulikuwa watu wenye hawakukuwa safi kwa sababu waligusa maiti,*+ kwa hiyo hawakuweza kutayarisha zabihu ya Pasaka siku hiyo. Basi watu hao wakaenda mbele ya Musa na Haruni siku hiyo,+ 7 na wakamuambia: “Sisi hatuko safi kwa sababu tumegusa maiti.* Sababu gani tukatazwe kumutolea Yehova toleo kwa wakati wenye uliwekwa kati ya Waisraeli?”+ 8 Kwa hiyo Musa akawaambia: “Mungojee pale, na nisikie mambo yenye Yehova ataamuru juu yenu.”+
9 Kisha Yehova akamuambia Musa: 10 “Waambie Waisraeli, ‘Hata kama mutu yeyote kati yenu ao wa vizazi vyenu vya kesho anajichafua kwa kugusa maiti*+ ao kama amesafiri mbali, bado anapaswa kumutayarishia Yehova zabihu ya Pasaka. 11 Wataitayarisha katika mwezi wa pili,+ siku ya kumi na ine (14) wakati giza linaanza.* Wanapaswa kuikula pamoja na mikate yenye haina chachu na mboga chungu za majani.+ 12 Hawapaswe kuacha kitu chochote mupaka asubui,+ na hawapaswe kuvunja mufupa wowote wa zabihu hiyo.+ Wanapaswa kuitayarisha kulingana na sheria zote za Pasaka. 13 Lakini kama mutu alikuwa safi ao hakukuwa katika safari na amepuuza kutayarisha zabihu ya Pasaka, basi mutu huyo anapaswa* kuondolewa* katikati ya watu wake,+ kwa sababu hakumutolea Yehova toleo hilo kwa wakati wenye uliwekwa. Mutu huyo atajibu kwa sababu ya zambi yake.
14 “‘Na kama mukaaji mugeni anaishi pamoja na ninyi, anapaswa pia kumutayarishia Yehova zabihu ya Pasaka.+ Anapaswa kufanya vile kulingana na sheria na utaratibu wa Pasaka.+ Kutakuwa sheria moja kwa ajili yenu, kwa ajili ya mukaaji mugeni na kwa ajili ya mwenyeji wa inchi.’”+
15 Sasa siku yenye tabenakulo ilisimamishwa,+ wingu lilifunika tabenakulo, hema ya Ushuhuda, lakini mangaribi kitu chenye kilikuwa kama moto kilikaa juu ya tabenakulo mupaka asubui.+ 16 Iliendelea kuwa vile: Wingu lilifunika tabenakulo wakati wa muchana, na kitu chenye kilikuwa kama moto wakati wa usiku.+ 17 Kila mara wakati wingu hilo liliinuka kutoka juu ya hema, Waisraeli waliondoka bila kukawia,+ na mahali wingu hilo lilisimama, ni pale Waisraeli walipiga kambi.+ 18 Kwa agizo la Yehova Waisraeli walikuwa wanaondoka, na kwa agizo la Yehova walikuwa wanapiga kambi.+ Waliendelea kupiga kambi muda wote wenye wingu hilo lilikaa juu ya tabenakulo. 19 Wakati wingu hilo lilikuwa linabakia juu ya tabenakulo kwa siku nyingi, Waisraeli walikuwa wanamutii Yehova na hawakukuwa wanaondoka.+ 20 Wakati fulani wingu hilo lilikuwa linakaa siku kidogo juu ya tabenakulo. Kwa agizo la Yehova waliendelea kupiga kambi, na kwa agizo la Yehova walikuwa wanaondoka. 21 Wakati fulani wingu hilo lilisimama tu kuanzia mangaribi mupaka asubui, na wakati wingu hilo liliinuka asubui, walikuwa wanaondoka. Ikuwe muchana ao usiku, walikuwa wanaondoka.+ 22 Kama ilikuwa siku mbili, mwezi mumoja, ao wakati murefu zaidi, wakati wote wenye wingu hilo lilibakia juu ya tabenakulo, Waisraeli waliendelea kupiga kambi na hawakukuwa wanaondoka. Lakini wakati liliinuka, walikuwa wanaondoka. 23 Kwa agizo la Yehova walikuwa wanaondoka, na kwa agizo la Yehova walikuwa wanapiga kambi. Walitimiza mambo yenye Yehova aliwaomba kama vile Yehova aliwaagiza kupitia Musa.
10 Kisha Yehova akamuambia Musa: 2 “Jitengenezee tarumbeta mbili,+ uzitengeneze na feza kwa kutumia nyundo,* na uzitumie kuita mukusanyiko na kuvunja kambi. 3 Wakati tarumbeta zote mbili zinapigwa, mukusanyiko wote unapaswa kukusanyika mbele yako kwenye muingilio wa hema ya mukutano.+ 4 Kama tarumbeta moja tu inapigwa, wakubwa peke yao, vichwa vya maelfu ya Israeli, watakusanyika mbele yako.+
5 “Wakati mutapiga tarumbeta kwa mulio wenye kubadilika-badilika, wale wenye kupiga kambi upande wa mashariki+ wanapaswa kuondoka. 6 Wakati munapiga tarumbeta mara ya pili kwa mulio wenye kubadilika-badilika, wale wenye kupiga kambi upande wa kusini+ wanapaswa kuondoka. Tarumbeta itapigwa kwa njia hiyo kila mara wakati kambi moja inaondoka.
7 “Sasa wakati munaita kutaniko kusudi likusanyike pamoja, munapaswa kupiga tarumbeta,+ lakini hapana kwa mulio wenye kubadilika-badilika. 8 Wana wa Haruni, makuhani, wanapaswa kupiga tarumbeta;+ na kutumia tarumbeta itakuwa sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote.
9 “Kama munaenda kupigana vita na mukandamizaji mwenye kuwatesa katika inchi yenu, munapaswa kupiga mulio wa vita kwa tarumbeta hizo,+ na Yehova Mungu wenu atawakumbuka na kuwaokoa katika mikono ya maadui wenu.
10 “Pia, katika siku zenu za kushangilia+—wakati wa sikukuu zenu+ na kwenye mwanzo wa miezi yenu—mutapiga tarumbeta hizo juu ya matoleo yenu ya kuteketezwa+ na zabihu zenu za ushirika;+ tarumbeta hizo zitafanya Mungu wenu awakumbuke. Mimi ni Yehova Mungu wenu.”+
11 Sasa katika mwaka wa pili, mwezi wa pili, siku ya makumi mbili (20) ya mwezi huo,+ lile wingu liliinuka kutoka juu ya tabenakulo+ ya Ushuhuda. 12 Kwa hiyo Waisraeli wakaanza kuondoka katika jangwa la Sinai kulingana na utaratibu wenye uliwekwa wa kuanza safari,+ na wingu hilo likasimama katika jangwa la Parani.+ 13 Hiyo ilikuwa mara ya kwanza yenye waliondoka kulingana na agizo la Yehova kupitia Musa.+
14 Kwa hiyo mugawanyo wa makabila tatu (3) wa kambi ya wana wa Yuda uliondoka kwanza kulingana na vikundi vyao vya maaskari,* na Nashoni+ mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wa kikundi chao cha maaskari. 15 Kiongozi wa kikundi cha maaskari cha kabila la wana wa Isakari alikuwa Netaneli+ mwana wa Zuari. 16 Kiongozi wa kikundi cha maaskari cha kabila la wana wa Zabuloni alikuwa Eliabu+ mwana wa Heloni.
17 Wakati tabenakulo ilibomolewa,+ wana wa Gershoni+ na wana wa Merari,+ wenye walibeba tabenakulo hiyo, waliondoka.
18 Kisha mugawanyo wa makabila tatu (3) wa kambi ya Rubeni uliondoka kulingana na vikundi vyao vya maaskari,* na Elisuri+ mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wa kikundi chao cha maaskari. 19 Kiongozi wa kikundi cha maaskari cha kabila la wana wa Simeoni alikuwa Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 20 Kiongozi wa kikundi cha maaskari cha kabila la wana wa Gadi alikuwa Eliasafu+ mwana wa Deueli.
21 Kisha Wakohati, wenye walibeba vyombo vya patakatifu,+ wakaondoka. Tabenakulo ilipaswa kusimamishwa wakati wangefika.
22 Kisha mugawanyo wa makabila tatu (3) wa kambi ya wana wa Efraimu uliondoka kulingana na vikundi vyao vya maaskari,* na Elishama+ mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wa kikundi chao cha maaskari. 23 Kiongozi wa kikundi cha maaskari cha kabila la wana wa Manase alikuwa Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 24 Kiongozi wa kikundi cha maaskari cha kabila la wana wa Benyamini alikuwa Abidani+ mwana wa Gideoni.
25 Kisha mugawanyo wa makabila tatu (3) wa kambi ya wana wa Dani uliondoka kulingana na vikundi vyao vya maaskari,* walikuwa kikundi cha nyuma cha kulinda kambi zote, na Ahiezeri+ mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wa kikundi chao cha maaskari. 26 Kiongozi wa kikundi cha maaskari cha kabila la wana wa Asheri alikuwa Pagieli+ mwana wa Okrani. 27 Kiongozi wa kikundi cha maaskari cha kabila la wana wa Naftali alikuwa Ahira+ mwana wa Enani. 28 Huo ndio utaratibu wenye Waisraeli na vikundi vyao vya maaskari* walifuata wakati walikuwa wanaondoka.+
29 Kisha Musa akamuambia Hobabu mwana wa Reueli,*+ Mumidiani, baba mukwe wa Musa: “Tunaenda mahali kwenye Yehova alisema, ‘Nitawapatia ninyi mahali pale.’+ Kuja basi pamoja na sisi,+ na tutakutendea muzuri, kwa sababu Yehova ameahidi mambo ya muzuri kwa ajili ya Israeli.”+ 30 Lakini akamuambia: “Sitaenda. Nitarudia katika inchi yangu na kwa watu wa jamaa yangu.” 31 Kwa hiyo Musa akamuambia: “Tafazali usituache, kwa maana unajua mahali tunapaswa kupiga kambi katika jangwa, na unaweza kuwa kiongozi wetu.* 32 Na kama unakuja pamoja na sisi,+ kila jambo la muzuri lenye Yehova atatutendea, hakika tutakutendea wewe.”
33 Kwa hiyo wakaanza safari ya siku tatu (3) kutoka kwenye mulima wa Yehova,+ na sanduku+ la agano la Yehova lilisafiri mbele yao safari hiyo ya siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumuzikia.+ 34 Na wingu la Yehova+ lilikuwa juu yao wakati wa muchana wakati waliondoka mahali walikuwa wamepiga kambi.
35 Kila mara wakati Sanduku hilo lilisafirishwa, Musa alikuwa anasema: “Simama, Ee Yehova,+ na uache maadui wako wasambazwe, na uache wale wenye kukuchukia wakimbie kutoka mbele yako.” 36 Na wakati lilipumuzika, alikuwa anasema: “Ee Yehova, rudia kwa maelfu ya Israeli yenye hayana hesabu.”*+
11 Sasa watu wakaanza kulalamika kwa uchungu mbele ya Yehova. Wakati Yehova alisikia malalamiko yao, kasirani yake ikawaka, na moto kutoka kwa Yehova ukaanza kuwaka juu yao na kuteketeza wamoja kati yao kwenye sehemu za pembeni-pembeni ya kambi. 2 Wakati watu walianza kumulilia Musa, naye alimulilia* Yehova,+ na moto ukazimika. 3 Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Tabera,* kwa sababu moto kutoka kwa Yehova uliwaka juu yao.+
4 Kisha watu wengi+ wenye walichangamana nao* wakaonyesha tamaa ya uchoyo,+ na Waisraeli pia wakaanza tena kulia na kusema: “Ni nani atatupatia nyama tukule?+ 5 Tunakumbuka sana samaki wenye tulikuwa tunakula bila kulipa katika inchi ya Misri, na matango, matikiti-maji, vitunguu vya majani, vitunguu, na vitunguu saumu!+ 6 Lakini sasa tunakuwa* wazaifu. Hatuone kitu kingine chochote isipokuwa hii mana.”+
7 Lakini, mana+ ilikuwa kama mbegu za mumea wa mugiligilani,+ na ilionekana kama ulimbo* wa bedola. 8 Watu walikuwa wanaenda kila mahali kuiokota na waliisaga kwenye majiwe ya kusagia ya mukono ao waliitwanga katika kinu. Kisha waliitokotesha katika vyungu vya kupikia ao waliitumia kutengeneza mikate ya muviringo,+ na ilikuwa tamu kama keki tamu yenye ilitiwa mafuta. 9 Wakati umande ulianguka juu ya kambi usiku, mana pia ilianguka juu yake.+
10 Musa akasikia watu wanalia katika kila familia, kila mutu kwenye muingilio wa hema yake. Na Yehova akakasirika sana,+ na Musa pia akachukizwa sana na jambo hilo. 11 Kisha Musa akamuambia Yehova: “Sababu gani unamutesa mutumishi wako? Sababu gani sikubaliwe mbele ya macho yako, na hivyo umetia muzigo wa watu wote hawa juu yangu?+ 12 Je, ni mimi nilibeba mimba ya watu hawa wote? Je, ni mimi niliwazaa, ndiyo sababu unaniambia, ‘Uwabebe katika kifua chako, kama vile mutumishi* anabebaka mutoto mudogo,’ na kuwapeleka katika inchi yenye uliapa kwamba utapatia mababu zao?+ 13 Nitapata wapi nyama ya kupatia watu hawa wote? Kwa sababu wanaendelea kulia mbele yangu, na kusema, ‘Utupatie nyama tukule!’ 14 Siwezi kubeba watu hawa wote peke yangu; ni muzigo muzito sana kwangu.+ 15 Kama utaendelea kunitendea hivi, tafazali uniue sasa hivi.+ Kama nimekubaliwa mbele ya macho yako, usinifanye nione musiba mwingine tena.”
16 Yehova akamujibu Musa: “Unikusanyie wanaume makumi saba (70) kutoka kati ya wazee wa Israeli, wanaume wenye unajua kuwa ni wazee na maofisa wa watu,+ na uwapeleke kwenye hema ya mukutano, na kuwaagiza wasimame pale pamoja na wewe. 17 Nitashuka+ na kuzungumuza na wewe pale,+ na nitakamata sehemu fulani ya roho+ yenye kuwa juu yako na kuitia juu yao, na watakusaidia kubeba muzigo wa watu hawa ili usiubebe peke yako.+ 18 Utaambia watu, ‘Mujitakase kwa ajili ya kesho,+ kwa maana hakika mutakula nyama, kwa sababu mumelia katika masikio ya Yehova+ na mumesema: “Ni nani atatupatia nyama tukule? Hali yetu ilikuwa muzuri zaidi katika inchi ya Misri.”+ Hakika Yehova atawapatia nyama, na mutakula.+ 19 Hamutakula kwa siku moja tu ao siku mbili ao siku tano (5) ao siku kumi (10) ao siku makumi mbili (20), 20 lakini kwa mwezi muzima, mupaka wakati itatokea katika matundu ya pua zenu na kuwachukiza,+ kwa sababu mulimukataa Yehova, mwenye kuwa katikati yenu, na mulikuwa munalia mbele yake, na kusema: “Sababu gani tumetoka Misri?”’”+
21 Kisha Musa akasema: “Watu wenye niko kati yao ni wanaume elfu mia sita (600 000)+ wenye kutembea kwa miguu, na wewe mwenyewe umesema, ‘Nitawapatia nyama, na watakula nyama ya kutosha kwa mwezi muzima’! 22 Kama makundi yote na mifugo yote inachinjwa, je, itawaenea? Ao kama samaki wote wa bahari wanakamatwa, je, watawaenea?”
23 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Je, mukono wa Yehova ni mufupi sana?+ Sasa utaona kama jambo lenye ninasema litatimia kwako ao hapana.”
24 Kwa hiyo Musa akatoka na kuwaambia watu maneno ya Yehova. Na akakusanya wanaume makumi saba (70) kutoka kati ya wazee wa watu na kuwaagiza wasimame kuzunguka hema.+ 25 Kisha Yehova akashuka katika wingu+ na kuzungumuza naye,+ na akakamata sehemu fulani ya roho+ yenye ilikuwa juu yake na kuiweka juu ya kila mumoja wa wale wazee makumi saba (70). Na wakati tu roho hiyo ilishuka juu yao, wakaanza kutenda kama manabii,*+ lakini hawakufanya vile tena.
26 Watu wawili kati ya wanaume hao walikuwa wangali katika kambi. Majina yao yalikuwa Eldadi na Medadi. Na roho ikaanza kushuka juu yao, kwa maana walikuwa kati ya wale wenye majina yao yalikuwa yameandikwa, lakini hawakuenda kwenye hema. Kwa hiyo wakaanza kutenda kama manabii katika kambi. 27 Na kijana mumoja mwanaume akakimbia na kumuambia Musa: “Eldadi na Medadi wanatenda kama manabii katika kambi!” 28 Kisha Yoshua+ mwana wa Nuni, mutumishi wa Musa tangu ujana wake, akajibu na kusema: “Bwana wangu Musa, uwakataze!”+ 29 Lakini Musa akamuambia: “Je, unanisikilia wivu? Hapana, ningependa watu wote wa Yehova wakuwe manabii na hivyo Yehova angetia roho yake juu yao!” 30 Kisha wakati fulani Musa akarudia katika kambi pamoja na wazee wa Israeli.
31 Kisha upepo kutoka kwa Yehova ukavuma kwa kushitukia na kuanza kuleta ndege kware kutoka katika bahari na kuwaangusha kuzunguka kambi,+ mwendo wa siku moja hivi upande huu na mwendo wa siku moja hivi upande mwingine, kuzunguka kambi pande zote, na wakafikia urefu wa mikono* mbili hivi kutoka kwenye udongo. 32 Kwa hiyo siku hiyo yote na usiku wote, na siku yote yenye ilifuata, watu waliendelea kukusanya ndege kware. Hakuna mwenye alikusanya chini ya homeri* kumi (10), na waliendelea kujianikia ndege kware kuzunguka kambi pande zote. 33 Lakini wakati nyama ilikuwa ingali katikati ya meno yao, mbele waitafune, kasirani ya Yehova ikawaka juu ya watu, na Yehova akaanza kupiga watu kwa mauaji makubwa sana.+
34 Kwa hiyo wakaita mahali pale Kibrot-hataava,*+ kwa sababu ni pale walizika watu wenye walikuwa na tamaa ya uchoyo.+ 35 Kutoka Kibrot-hataava watu wakasafiri mupaka Haseroti, na wakaendelea kukaa Haseroti.+
12 Sasa Miriamu na Haruni wakaanza kusema mubaya juu ya Musa kwa sababu ya mwanamuke Mukushi mwenye alikuwa ameoa, kwa sababu alikuwa amechukua mwanamuke Mukushi.+ 2 Walikuwa wanasema: “Je, Yehova amezungumuza kupitia Musa tu? Je, hajazungumuza kupitia sisi pia?”+ Na Yehova alikuwa anasikiliza.+ 3 Sasa mwanaume huyu Musa alikuwa mupole sana kuliko watu wote*+ juu ya uso wa dunia.
4 Mara moja Yehova akamuambia Musa, Haruni, na Miriamu: “Ninyi watatu (3), muende kwenye hema ya mukutano.” Kwa hiyo wote watatu wakaenda. 5 Na Yehova akashuka katika nguzo ya wingu+ na kusimama kwenye muingilio wa hema ya mukutano na akaita Haruni na Miriamu. Wote wawili wakaenda mbele. 6 Kisha akawaambia: “Tafazali, musikie maneno yangu. Kama kungekuwa nabii wa Yehova kati yenu, ningejijulisha kwake katika maono,+ na ningesema naye katika ndoto.+ 7 Lakini haiko vile juu ya mutumishi wangu Musa! Amepewa nyumba yangu yote.*+ 8 Ninazungumuzaka naye uso kwa uso,*+ waziwazi, hapana kwa vitendawili; na anaonaka umbo ya Yehova. Sababu gani, basi, hamukuogopa kusema mubaya juu ya mutumishi wangu, juu ya Musa?”
9 Kwa hiyo kasirani ya Yehova ikawaka juu yao, naye akaenda na kuwaacha. 10 Lile wingu likaondoka juu ya hema, na angalia! Miriamu alikuwa amepigwa kwa ukoma mweupe kama teluji.*+ Kisha Haruni akageuka na kumuangalia Miriamu, na akaona kwamba alikuwa amepigwa ukoma.+ 11 Mara moja Haruni akamuambia Musa: “Ninakuomba, bwana wangu! Tafazali, usituhesabie zambi hii! Tumetenda kwa upumbavu katika jambo lenye tumefanya. 12 Tafazali, usimuache aendelee kuwa kama mutu mwenye amekufa, mwenye nusu ya mwili wake imeoza wakati wa kuzaliwa!” 13 Na Musa akaanza kumulilia Yehova, na kusema: “Ee Mungu, tafazali umuponyeshe! Tafazali!”+
14 Yehova akamujibu Musa: “Kama baba yake angemutemea mate moja kwa moja kwenye uso wake, je, hangepata haya kwa siku saba (7)? Acha awekwe mbali na watu inje ya kambi kwa siku saba,+ kisha anaweza kurudishwa ndani.” 15 Kwa hiyo Miriamu akawekwa mbali na watu inje ya kambi kwa siku saba (7),+ na watu hawakuvunja kambi mupaka wakati Miriamu alirudishwa ndani. 16 Kisha watu wakaondoka Haseroti+ na wakaanza kupiga kambi katika jangwa la Parani.+
13 Sasa Yehova akasema na Musa, na kumuambia: 2 “Tuma wanaume ili wapeleleze* inchi ya Kanaani, yenye ninapatia Waisraeli. Tuma mwanaume mumoja kutoka katika kila kabila la babu yake, kila mumoja wao anapaswa kuwa mukubwa+ kati yao.”+
3 Kwa hiyo Musa akawatuma kutoka katika jangwa la Parani+ kama vile Yehova aliagiza. Wanaume hao wote walikuwa vichwa vya Waisraeli. 4 Haya ndiyo majina yao: kutoka katika kabila la Rubeni, Shamua mwana wa Zakuri; 5 kutoka katika kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori; 6 kutoka katika kabila la Yuda, Kalebu+ mwana wa Yefune; 7 kutoka katika kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu; 8 kutoka katika kabila la Efraimu, Hoshea+ mwana wa Nuni; 9 kutoka katika kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu; 10 kutoka katika kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi; 11 kutoka katika kabila la Yosefu,+ kwa ajili ya kabila la Manase,+ Gadi mwana wa Susi; 12 kutoka katika kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali; 13 kutoka katika kabila la Asheri, Seturi mwana wa Mikaeli; 14 kutoka katika kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofsi; 15 kutoka katika kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki. 16 Hayo ndiyo majina ya wanaume wenye Musa alituma ili kupeleleza inchi. Na Musa alimupatia Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.*+
17 Wakati Musa alikuwa anawatuma ili kupeleleza inchi ya Kanaani, aliwaambia: “Mupande kule kuingia Negebu, na kisha mupande kwenye eneo lenye milima.+ 18 Munapaswa kuangalia namna inchi hiyo iko+ na kama watu wenye kuishi ndani yake ni wenye nguvu ao ni wazaifu, wako kidogo ao wako wengi, 19 na kama inchi hiyo ni ya muzuri ao ni ya mubaya na kama miji yenye wanaishi ndani ni kambi ao ni ngome. 20 Na muchunguze kama ni inchi tajiri* ao maskini*+ na kama iko na miti ao haina. Munapaswa kuwa hodari+ na kukamata matunda fulani ya inchi hiyo.” Sasa ilikuwa kipindi cha kukomaa kwa zabibu za kwanza.+
21 Kwa hiyo wakapanda na kupeleleza inchi kuanzia jangwa la Zini+ mupaka Rehobu,+ karibu na Lebo-hamati.*+ 22 Wakati walipanda na kuingia Negebu, walifika Hebroni,+ kwenye Ahimani, Sheshai, na Talmai,+ Waanaki,+ walikuwa wanaishi. Na muji wa Hebroni ulijengwa miaka saba (7) mbele ya muji wa Soani wa Misri. 23 Wakati walifika kwenye Bonde* la Eshkoli,+ walikata pale tawi lenye kishada kimoja cha zabibu, na lilibebwa na wanaume wawili kwenye muti, na pia matunda fulani ya makomamanga na tini.+ 24 Wakaita mahali pale Bonde* la Eshkoli*+ kwa sababu ya kishada chenye Waisraeli walikata pale.
25 Wakati siku makumi ine (40) zilimalizika,+ wakarudia kisha kupeleleza inchi hiyo. 26 Kwa hiyo wakarudia kwa Musa na Haruni na mukusanyiko wote wa Waisraeli katika jangwa la Parani, pale Kadeshi.+ Wakaletea habari mukusanyiko wote na kuwaonyesha matunda ya inchi hiyo. 27 Hii ndiyo habari yenye walimuambia Musa: “Tuliingia katika inchi kwenye ulitutuma, na kwa kweli inatiririka maziwa na asali,+ na haya ndiyo matunda yake.+ 28 Lakini, watu wenye kuishi katika inchi hiyo ni wenye nguvu, na miji yenye ngome ni mikubwa sana. Tuliona pia Waanaki kule.+ 29 Waamaleki+ wanaishi katika inchi ya Negebu,+ na Wahiti, Wayebusi,+ na Waamori+ wanaishi katika eneo lenye milima, na Wakanaani+ wanaishi karibu na bahari+ na pembeni-pembeni ya Yordani.”
30 Kisha Kalebu akajaribu kutuliza watu wenye walisimama mbele ya Musa kwa kusema: “Tupande mara moja, na kwa kweli tutairiti, kwa maana hakika tunaweza kumushinda.”+ 31 Lakini wanaume wenye walipanda pamoja naye wakasema: “Hatuwezi kupanda ili kupigana na watu hao, kwa sababu wako na nguvu kutupita.”+ 32 Na wakaendelea kupatia Waisraeli habari ya mubaya+ juu ya inchi yenye walipeleleza, kwa kusema: “Inchi yenye tulipita ndani yake ili kuipeleleza ni inchi yenye inamezaka wakaaji wake, na watu wote wenye tuliona kule ni watu wenye ukubwa wa ajabu.+ 33 Na tuliona kule Wanefili, wana wa Anaki,+ wenye wanatokana na Wanefili, na mbele yao tulionekana kama panzi, nao walituona vilevile.”
14 Kisha mukusanyiko wote ukapandisha sauti yao, na watu wakaendelea kulalamika na kulia usiku huo wote.+ 2 Waisraeli wote wakaanza kumunungunikia Musa na Haruni,+ na mukusanyiko wote ukawanungunikia, na kusema: “Ingekuwa muzuri kama tungekufia katika inchi ya Misri, ao ingekuwa muzuri kama tungekufia katika jangwa hili! 3 Sababu gani Yehova anatuleta kwenye inchi hii ili tuuawe kwa upanga?+ Bibi zetu na watoto wetu watakuwa vitu vyenye vinanyanganywa katika vita.+ Je, haiko muzuri zaidi turudie Misri?”+ 4 Hata walikuwa wanaambiana: “Tuchague kiongozi na turudie Misri!”+
5 Basi Musa na Haruni wakaanguka uso chini mbele ya kutaniko lote la Waisraeli lenye lilikuwa limekusanyika. 6 Yoshua+ mwana wa Nuni na Kalebu+ mwana wa Yefune, wenye walikuwa kati ya watu ambao walipeleleza inchi, wakapasua nguo zao, 7 na wakaambia mukusanyiko wote wa Waisraeli hivi: “Inchi yenye tulipita ndani yake ili kuipeleleza ni inchi ya muzuri sana, ya muzuri kabisa.+ 8 Kama Yehova anapendezwa na sisi, hakika atatuingiza katika inchi hii na kutupatia ikuwe yetu, inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+ 9 Lakini musimuasi Yehova, na musiogope watu wa inchi hiyo,+ kwa maana tutawameza.* Ulinzi wao umeondolewa juu yao, na Yehova iko* pamoja na sisi.+ Musiwaogope.”
10 Lakini, mukusanyiko wote ukasema wapigwe majiwe.+ Hata hivyo utukufu wa Yehova ukatokea juu ya hema ya mukutano mbele ya watu wote wa Israeli.+
11 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Watu hawa wataendelea kunikosea heshima mupaka wakati gani,+ na watakataa kuniamini mupaka wakati gani ijapokuwa alama zote zenye nilifanya kati yao?+ 12 Acha niwapige kwa ugonjwa wa kuambukiza na kuwafukuza, na acha nikufanye wewe kuwa taifa kubwa zaidi na lenye nguvu zaidi kuliko wao.”+
13 Lakini Musa akamuambia Yehova: “Kisha Wamisri, wenye katikati yao ulitosha watu hawa kwa nguvu zako, watasikia,+ 14 na wataambia wakaaji wa inchi hii juu ya jambo hilo. Wakaaji hao pia wamesikia kwamba wewe, Yehova, uko kati ya watu hawa+ na umewatokea uso kwa uso.+ Wewe ni Yehova, na wingu lako limesimama juu yao, na unawatangulia katika nguzo ya wingu wakati wa muchana na katika nguzo ya moto wakati wa usiku.+ 15 Kama unaua watu hawa wote mara moja,* mataifa yenye yamesikia sifa zako yatasema hivi: 16 ‘Yehova hakuweza kuingiza watu hawa katika inchi yenye aliapa kuwa angewapatia, ndiyo sababu aliwachinja katika jangwa.’+ 17 Sasa, tafazali, Ee Yehova, acha nguvu zako zikuwe kubwa, kama vile uliahidi wakati ulisema, 18 ‘Yehova, hakasirike haraka na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu,*+ mwenye kusamehe kosa na uovu, lakini hatakosa hata kidogo kupatia azabu wenye kosa, mwenye kuleta azabu juu ya wana kwa sababu ya kosa la baba zao, juu ya kizazi cha tatu (3) na juu ya kizazi cha ine (4).’+ 19 Tafazali, samehe kosa la watu hawa kulingana na upendo wako mwingi mushikamanifu, kama vile umesamehe watu hawa kuanzia Misri mupaka sasa.”+
20 Kisha Yehova akasema: “Ninawasamehe kama vile unasema.+ 21 Lakini kwa upande mwingine, kama vile hakika ninaishi, dunia yote itajaa utukufu wa Yehova.+ 22 Hata hivyo, hakuna mutu hata mumoja kati ya watu hao wenye wameona utukufu wangu na alama+ zenye nilifanya katika inchi ya Misri na katika jangwa na wenye bado wameendelea kunijaribu+ mara hizi kumi (10) na hawasikilize sauti yangu+ 23 mwenye ataona inchi yenye niliapa kwamba nitapatia baba zao. Hapana, hakuna mutu hata mumoja katikati ya wale wenye kunikosea heshima mwenye ataiona.+ 24 Lakini kwa sababu mutumishi wangu Kalebu+ alikuwa na roho tofauti na aliendelea kunifuata kwa moyo wote, hakika nitamuingiza katika inchi kwenye alienda, na wazao wake watairiti.+ 25 Kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani+ wanaishi katika bonde,* kesho mugeuke na kuelekea kwenye jangwa kupitia njia ya Bahari Nyekundu.”+
26 Kisha Yehova akamuambia Musa na Haruni: 27 “Mukusanyiko huu wa watu waovu utaendelea kuninungunikia mupaka wakati gani?+ Nimesikia mambo yenye Waisraeli wako wananungunika juu yangu.+ 28 Uwaambie, ‘“Kama vile hakika ninaishi,” ni vile Yehova anasema, “nitawatendea mambo yaleyale yenye nimesikia munasema!+ 29 Maiti zenu zitaanguka katika jangwa hili,+ ndiyo, watu wote katikati yenu kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi wenye waliandikishwa, ninyi wote wenye mumeninungunikia.+ 30 Hakuna mutu kati yenu mwenye ataingia katika inchi yenye niliapa* kwamba mutaishi ndani yake+ isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+
31 “‘“Na nitaingiza watoto wenu, wenye mulisema kwamba watakuwa vitu vyenye vinanyanganywa katika vita,+ na watafikia kujua inchi yenye mumekataa.+ 32 Lakini maiti zenu zitaanguka katika jangwa hili. 33 Sasa wana wenu watakuwa wachungaji katika jangwa kwa miaka makumi ine (40),+ na watajibu kwa sababu ya matendo yenu ya kukosa uaminifu* mupaka wakati maiti ya mutu wa mwisho kati yenu itaanguka katika jangwa.+ 34 Kulingana na hesabu ya siku zenye mulipeleleza inchi, siku makumi ine (40),+ siku moja kwa mwaka mumoja, siku moja kwa mwaka mumoja, mutajibu kwa sababu ya makosa yenu kwa miaka makumi ine,+ kwa sababu mutajua maana ya kunipinga mimi.*
35 “‘“Mimi, Yehova, nimesema. Ni vile nitatendea mukusanyiko huu wa watu waovu, wale wenye wamekusanyika pamoja ili kunipinga: Wataishia katika jangwa hili, na watakufia ndani.+ 36 Wanaume wenye Musa alituma ili kupeleleza inchi na wenye walifanya mukusanyiko wote umunungunikie wakati walileta habari ya mubaya juu ya inchi hiyo,+ 37 ndiyo, wanaume hao wenye walileta habari ya mubaya juu ya inchi hiyo watapigwa na kufa mbele ya Yehova.+ 38 Lakini Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune, wenye walikuwa kati ya wale wenye walienda ili kupeleleza inchi, hakika wataendelea kuishi.”’”+
39 Wakati Musa aliambia Waisraeli wote maneno hayo, watu wakaanza kuomboleza sana. 40 Tena, wakaamuka asubui sana na kujaribu kupanda mupaka kwenye kichwa cha mulima, na kusema: “Sasa tuko tayari kupanda mupaka mahali kwenye Yehova alituambia, kwa maana tumefanya zambi.”+ 41 Lakini Musa akasema: “Sababu gani munavunja agizo la Yehova? Jambo hilo halitakuwa na matokeo ya muzuri. 42 Musipande, kwa sababu Yehova haiko pamoja na ninyi; na mutashindwa na maadui wenu.+ 43 Kwa maana Waamaleki na Wakanaani watapigana na ninyi kule,+ na mutaanguka kwa upanga. Kwa sababu muliacha kumufuata Yehova, Yehova hatakuwa pamoja na ninyi.”+
44 Hata hivyo, kwa kimbelembele wakapanda kuelekea kwenye kichwa cha mulima,+ lakini sanduku la agano la Yehova halikutoka katikati ya kambi na Musa hakutoka katikati ya kambi.+ 45 Kisha Waamaleki na Wakanaani wenye walikuwa wanaishi katika mulima huo wakashuka na wakawashambulia, wakawasambaza mupaka Horma.+
15 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Wakati mutaingia mwishowe katika inchi yenye ninawapatia muishi ndani yake,+ 3 na kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto kutoka katika mifugo ao kutoka katika kundi—ikuwe toleo la kuteketezwa+ ao zabihu ya kutimiza naziri ya pekee ao toleo la kujipendea+ ao toleo lenye linatolewa wakati wa sikukuu zenu za vipindi,+ ili kumutolea Yehova harufu ya kumupendeza*+— 4 mutu mwenye anatoa toleo lake anapaswa pia kumutolea Yehova toleo la nafaka la unga muzuri,+ sehemu moja ya kumi (1/10) ya efa,* yenye kuchanganywa na sehemu moja ya ine (1/4) ya hini* ya mafuta. 5 Pia munapaswa kutoa divai ili kuwa toleo la kinywaji, sehemu moja ya ine (1/4) ya hini, pamoja na toleo la kuteketezwa+ ao kwa ajili ya zabihu ya kila mwana-kondoo dume. 6 Ao kwa ajili ya kondoo-dume, mutatoa toleo la nafaka la sehemu mbili za kumi (2/10) za kipimo cha efa ya unga muzuri wenye kuchanganywa na sehemu moja ya tatu (1/3) ya hini ya mafuta. 7 Na munapaswa kutoa divai ili kuwa toleo la kinywaji, sehemu moja ya tatu (1/3) ya hini, kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova.
8 “‘Lakini kama munamutolea Yehova munyama dume kutoka katika mifugo ili akuwe toleo la kuteketezwa+ ao zabihu ya kutimiza naziri ya pekee+ ao zabihu za ushirika,+ 9 munapaswa pia kutoa munyama dume huyo kutoka katika mifugo pamoja na toleo la nafaka+ la sehemu tatu za kumi (3/10) za kipimo cha efa ya unga muzuri wenye kuchanganywa na nusu ya hini ya mafuta. 10 Munapaswa pia kutoa divai ili kuwa toleo la kinywaji,+ nusu ya hini, kuwa toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto, kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova. 11 Ni vile inapaswa kufanywa kwa ajili ya kila ngombe-dume ao kwa ajili ya kila kondoo-dume ao kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume katikati ya wana-kondoo dume ao kila mbuzi katikati ya mbuzi. 12 Ikuwe munatoa wanyama wangapi, ni vile munapaswa kufanya kwa ajili ya kila munyama, kulingana na hesabu yao. 13 Ni vile kila Mwisraeli mwenyeji wa kizalikio anapaswa kutoa toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto, kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova.
14 “‘Kama mugeni mwenye anaishi pamoja na ninyi ao mutu fulani mwenye ameishi katikati yenu kwa muda wa vizazi vingi anatoa pia toleo kwa njia ya moto, kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova, anapaswa kufanya kama vile munafanya.+ 15 Ninyi watu wa kutaniko na mugeni mwenye anaishi na ninyi mutakuwa na sheria moja. Itakuwa sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote. Mukaaji mugeni atakuwa sawasawa na ninyi mbele ya Yehova.+ 16 Kutakuwa sheria moja na uamuzi mumoja wa hukumu kwa ajili yenu na kwa ajili ya mugeni mwenye anaishi pamoja na ninyi.’”
17 Yehova akaendelea kumuambia Musa: 18 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Wakati mutaingia katika inchi kwenye ninawapeleka 19 na mukule mukate wowote wa* inchi hiyo,+ mutamutolea Yehova muchango. 20 Mutatoa muchango wa matunda ya kwanza+ ya unga wenu wa chenga-chenga kuwa mikate ya muviringo. Mutautoa kama muchango wenye unatoka katika kiwanja cha kupigia-pigia nafaka. 21 Sehemu fulani ya matunda ya kwanza ya unga wenu wa chenga-chenga mutamutolea Yehova kuwa muchango katika vizazi vyenu vyote.
22 “‘Sasa kama munafanya kosa na munashindwa kufuata amri hizi zote zenye Yehova amemuambia Musa, 23 mambo yote yenye Yehova amewaamuru kupitia Musa kuanzia siku yenye Yehova aliamuru na kuendelea kwa ajili ya vizazi vyenu, 24 na kama kosa hilo lilifanywa bila kukusudia na bila mukusanyiko kujua, mukusanyiko wote unapaswa kutoa ngombe-dume mumoja mudogo kuwa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya harufu ya kumupendeza* Yehova, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji kulingana na utaratibu wa kawaida,+ na mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi.+ 25 Kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mukusanyiko wote wa Waisraeli, nao watasamehewa kosa hilo,+ kwa sababu lilikuwa kosa, na wamemuletea Yehova toleo lao lenye linatolewa kwa njia ya moto na toleo lao la zambi mbele ya Yehova kwa ajili ya kosa lao. 26 Mukusanyiko wote wa Waisraeli na mugeni mwenye kuishi kati yao watasamehewa kosa hilo, kwa sababu watu wote walifanya kosa hilo bila kukusudia.
27 “‘Kama mutu yeyote anafanya* zambi bila kukusudia, basi atatoa mbuzi-dike katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la zambi.+ 28 Na kuhani atafunika zambi kwa ajili ya mutu huyo mwenye alifanya* kosa kwa kutenda zambi bila kukusudia mbele ya Yehova, ili kufunika zambi kwa ajili ya zambi hiyo, na mutu huyo atasamehewa.+ 29 Kuhusu wenyeji wa kizalikio wenye kuwa kati ya Waisraeli na mugeni mwenye kuishi katikati yao, kutakuwa sheria moja kwa ajili yenu kuhusu kufanya jambo fulani bila kukusudia.+
30 “‘Lakini mutu mwenye anafanya* kosa kwa makusudi,+ akuwe mwenyeji wa kizalikio ao mukaaji mugeni, anamutukana Yehova na anapaswa kuondolewa* katikati ya watu wake. 31 Kwa kuwa amezarau neno la Yehova na amevunja amri yake, mutu huyo anapaswa kabisa kuondolewa asikuwe* tena.+ Kosa lake liko juu yake.’”+
32 Wakati Waisraeli walikuwa katika jangwa, walimukuta mutu fulani anaokota kuni siku ya Sabato.+ 33 Wale wenye walimukuta anaokota kuni wakamuleta mbele ya Musa na Haruni na mukusanyiko wote. 34 Wakatia mutu huyo katika kifungo+ kwa sababu jambo lenye alipaswa kufanyiwa halikukuwa limeonyeshwa waziwazi.
35 Na Yehova akamuambia Musa: “Mutu huyo anapaswa kabisa kuuawa,+ na mukusanyiko wote unapaswa kumupiga majiwe inje ya kambi.”+ 36 Kwa hiyo mukusanyiko wote ukamupeleka inje ya kambi na ukamupiga majiwe na kumuua, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
37 Yehova akaendelea kumuambia Musa hivi: 38 “Sema na Waisraeli na uwaambie kama wanapaswa kujitengenezea upindo wa nyuzi-nyuzi kwenye mwisho-mwisho wa nguo zao katika vizazi vyao vyote, na wanapaswa kutia uzi ya rangi ya bluu juu ya upindo huo wa nyuzi-nyuzi wa mwisho-mwisho wa nguo.+ 39 ‘Munapaswa kutengeneza upindo huo wa nyuzi-nyuzi ili muuone na kukumbuka amri zote za Yehova na kuzishika.+ Hamupaswe kufuata mioyo yenu na macho yenu, yenye kuwaongoza kwenye ukahaba wa kiroho.+ 40 Hilo litawasaidia kukumbuka, na mutashika amri zangu zote na kuwa watakatifu mbele ya Mungu wenu.+ 41 Mimi ni Yehova Mungu wenu, mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri ili nijionyeshe kuwa Mungu wenu.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+
16 Kisha Kora+ mwana wa Ishari,+ mwana wa Kohati,+ mwana wa Lawi,+ akaungana na Datani na Abiramu wana wa Eliabu,+ na Oni mwana wa Peleti, kutoka katikati ya wana wa Rubeni.+ 2 Wakasimama ili kumupinga Musa wao pamoja na wanaume Waisraeli mia mbili makumi tano (250), wakubwa wa mukusanyiko, wanaume wenye kuchaguliwa wa kutaniko, watu wa maana. 3 Kwa hiyo wakakusanyika ili kumupinga+ Musa na Haruni na kuwaambia: “Mumetuchokesha! Mukusanyiko wote ni mutakatifu,+ watu wote, na Yehova iko* katikati yao.+ Sababu gani, basi, munajiinua juu ya kutaniko la Yehova?”
4 Wakati Musa alisikia jambo hilo, mara moja akaanguka uso chini. 5 Kisha akamuambia Kora na watu wote wenye walimuunga mukono, “Asubui Yehova ataonyesha ni nani mwenye kuwa wake+ na ni nani mwenye kuwa mutakatifu na ni nani anapaswa kumukaribia,+ na mutu yeyote mwenye atachagua+ ni yeye atamukaribia. 6 Mufanye hivi: Mukamate vyetezo,+ Kora na wote wenye kukuunga mukono,+ 7 na kesho mutie moto ndani na kutia uvumba juu yake mbele ya Yehova, na mutu mwenye Yehova atachagua,+ ni yeye mutakatifu. Ninyi wana wa Lawi+ mumevuka mipaka!”
8 Kisha Musa akamuambia Kora: “Musikilize, tafazali, ninyi wana wa Lawi. 9 Je, munaona ni jambo la kidogo sana kwenu kwamba Mungu wa Israeli amewatenga na mukusanyiko wa Israeli+ na kuwaruhusu mumukaribie ili kufanya utumishi wa tabenakulo ya Yehova na kusimama mbele ya mukusanyiko ili kuwatumikia,+ 10 na kuwaleta karibu naye ninyi pamoja na ndugu zenu wote, wana wa Lawi? Je, ni lazima pia mujaribu kunyanganya ukuhani?+ 11 Kwa sababu hiyo, wewe na watu wote wenye kukuunga mukono wenye wanakusanyika pamoja munamupinga Yehova. Kuhusu Haruni, yeye ni nani ili mumunungunikie?”+
12 Kisha wakati fulani Musa akatuma ujumbe ili waite Datani na Abiramu+ wana wa Eliabu, lakini wakasema: “Hatutakuja! 13 Je, ni jambo la kidogo sana kwamba umetutosha katika inchi yenye kutiririka maziwa na asali ili utuue katika jangwa?+ Sasa, je, unataka pia kujifanya mutawala mwenye mamlaka yote juu yetu?* 14 Na tena, haujatuleta katika inchi yoyote yenye kutiririka maziwa na asali+ wala kutupatia uriti wa mashamba na mashamba ya mizabibu. Je, unataka kutoboa macho ya watu hawa? Sisi hatutakuja!”
15 Kwa hiyo Musa akakasirika sana na kumuambia Yehova: “Usikubali toleo lao la nafaka. Sijakamata hata punda wao mumoja, wala sijatendea mubaya hata mutu mumoja kati yao.”+
16 Kisha Musa akamuambia Kora: “Fika kesho mbele ya Yehova pamoja na watu wote wenye wanakuunga mukono, wewe na watu hao na Haruni. 17 Kila mumoja wenu anapaswa kukamata chetezo chake na kutia uvumba juu yake, na kila mumoja atapeleka chetezo chake mbele ya Yehova, vyetezo mia mbili makumi tano (250), pia wewe na Haruni, kila mumoja na chetezo chake.” 18 Kwa hiyo kila mumoja wao akakamata chetezo chake, na wakatia moto na uvumba juu ya vyetezo hivyo na kusimama kwenye muingilio wa hema ya mukutano pamoja na Musa na Haruni. 19 Wakati Kora alikuwa amekusanya watu wote wenye walimuunga mukono+ ili kumupinga Musa na Haruni kwenye muingilio wa hema ya mukutano, utukufu wa Yehova ukatokea mukusanyiko wote.+
20 Kisha Yehova akamuambia Musa na Haruni, 21 “Mujitenge na kikundi hiki, ili niwaharibu mara moja.”+ 22 Kwa hiyo, wakaanguka uso chini na kusema: “Ee Mungu, Mungu wa roho ya watu wote,*+ je, zambi ya mutu mumoja ikufanye ukasirikie mukusanyiko wote?”+
23 Kisha Yehova akamuambia Musa: 24 “Sema na mukusanyiko na uwaambie, ‘Mutoke kuzunguka pande zote za mahema ya Kora, Datani, na Abiramu!’”+
25 Kisha Musa akasimama na kuenda kwa Datani na Abiramu, na wazee+ wa Israeli wakaenda pamoja naye. 26 Akaambia mukusanyiko wote: “Tafazali, mutoke karibu na mahema ya watu hawa waovu na musiguse kitu chao chochote, ili musiharibiwe katika zambi yao yote.” 27 Mara moja wakatoka karibu na mahema ya Kora, Datani, na Abiramu, wakatoka kila upande, na Datani na Abiramu wakatoka inje, wakasimama kwenye muingilio wa mahema yao, pamoja na bibi zao, wana wao, na watoto wao wadogo.
28 Kisha Musa akasema: “Kupitia jambo hili mutajua kama Yehova amenituma nifanye mambo haya yote, kama hayatoke katika moyo wangu:* 29 Kama watu hawa wanakufa namna wanadamu wengine wote wanakufaka na kama azabu yao inakuwa sawa na ile ya wanadamu wengine wote, basi Yehova hakunituma.+ 30 Lakini kama Yehova anawatendea jambo fulani lenye haliko la kawaida na udongo ufunguke* na kuwameza na vitu vyao vyote na washuke katika Kaburi* wakiwa wazima, mutajua kwa kweli kama watu hawa wamemukosea Yehova heshima.”
31 Wakati alimaliza tu kusema maneno hayo yote, udongo wenye ulikuwa chini yao ukapasuka.+ 32 Na dunia ikafunguka* na kumeza watu hao, pamoja na watu wa nyumba zao na watu wote wa Kora+ na vitu vyao vyote. 33 Kwa hiyo watu hao pamoja na watu wao wote wakaingia katika Kaburi* wakiwa wazima, na dunia ikawafunika, basi hawakukuwa tena katikati ya kutaniko.+ 34 Waisraeli wote wenye walikuwa wamewazunguka wakakimbia wakati walisikia kilio chao, kwa maana walisema: “Tunaogopa dunia isitumeze!” 35 Kisha moto ukatoka kwa Yehova+ na kuteketeza wale wanaume mia mbili makumi tano (250) wenye walikuwa wanatoa uvumba.+
36 Sasa Yehova akamuambia Musa: 37 “Umuambie Eleazari mwana wa Haruni kuhani atoshe vyetezo+ katika moto, kwa sababu ni vitakatifu. Umuambie pia asambaze moto huo mbali kidogo. 38 Vyetezo vya wanaume wenye waliuawa kwa sababu ya zambi yao* vinapaswa kufanywa kuwa mabamba membamba ya metali ili kufunika mazabahu,+ kwa sababu walivipeleka mbele ya Yehova, na vikakuwa vitakatifu. Vinapaswa kuwa alama kwa Waisraeli.’”+ 39 Kwa hiyo Eleazari kuhani akakamata vyetezo vya shaba vyenye vililetwa na wale wenye walikuwa wameteketezwa kwa moto, na akavipiga-piga ili vifunike mazabahu, 40 kama vile Yehova alikuwa amemuambia kupitia Musa. Hilo lilikumbusha Waisraeli kwamba mutu yeyote mwenye haruhusiwe* mwenye haiko muzao wa Haruni hapaswe kukaribia ili kuchoma uvumba mbele ya Yehova+ na kwamba mutu yeyote hapaswe kuwa kama Kora na wale wenye walimuunga mukono.+
41 Siku yenye ilifuata, mukusanyiko wote wa Waisraeli ukaanza kunungunikia Musa na Haruni,+ na kusema: “Ninyi wawili mumeua watu wa Yehova.” 42 Wakati mukusanyiko ulikuwa umekusanyika ili kupinga Musa na Haruni, basi waligeuka kuelekea hema ya mukutano, na angalia! wingu lilifunika hema hiyo, na utukufu wa Yehova ukaanza kuonekana.+
43 Musa na Haruni wakaenda mbele ya hema ya mukutano,+ 44 na Yehova akamuambia Musa: 45 “Ninyi wanaume, mujitenge na mukusanyiko huu, kusudi niwaharibu mara moja.”+ Kwa hiyo wakaanguka uso chini.+ 46 Kisha Musa akamuambia Haruni, “Kamata chetezo na utie moto ndani yake kutoka katika mazabahu+ na utie uvumba juu yake na uende haraka kwenye mukusanyiko na ufunike zambi kwa ajili yao,+ kwa sababu kasirani imetoka kwa Yehova. Pigo limeanza!” 47 Mara moja Haruni akakamata chetezo, kama vile Musa alikuwa amemuambia, na akakimbia katikati ya kutaniko, na angalia! pigo lilikuwa limeanza kati ya watu. Kwa hiyo akatia uvumba juu ya chetezo na kuanza kufunika zambi kwa ajili ya watu. 48 Akaendelea kusimama katikati ya wafu na wazima, na mwishowe pigo hilo likaisha. 49 Watu wenye walikufa kutokana na pigo hilo walikuwa elfu kumi na ine na mia saba (14 700), zaidi ya wale wenye walikufa kwa sababu ya Kora. 50 Mwishowe wakati Haruni alirudia kwa Musa kwenye muingilio wa hema ya mukutano, pigo hilo lilikuwa limesimamishwa.
17 Sasa Yehova akamuambia Musa: 2 “Sema na Waisraeli na uchukue kutoka kwao fimbo moja kwa ajili ya kila jamaa ya upande wa baba, kutoka kwa wakubwa wa kila jamaa ya upande wa baba,+ fimbo kumi na mbili (12) kwa ujumla. Andika jina la kila mumoja wao kwenye fimbo yake. 3 Unapaswa kuandika jina la Haruni kwenye fimbo ya Lawi, kwa sababu kuko fimbo moja kwa ajili ya kichwa cha kila jamaa ya upande wa baba. 4 Weka fimbo hizo ndani ya hema ya mukutano mbele ya Ushuhuda,+ mahali ninakutokea kwa ukawaida.+ 5 Na fimbo ya mutu mwenye ninachagua+ itatokeza matumba,* na nitamaliza manunguniko ya Waisraeli juu yangu,+ yenye wananungunika pia juu yenu.”+
6 Kwa hiyo Musa akasema na Waisraeli, na wakubwa wao wote wakamupatia fimbo—fimbo moja kwa ajili ya kila mukubwa wa jamaa ya upande wa baba, fimbo kumi na mbili (12)—na fimbo ya Haruni ilikuwa kati ya fimbo zao. 7 Kisha Musa akaweka fimbo hizo mbele ya Yehova katika hema ya Ushuhuda.
8 Siku yenye ilifuata, wakati Musa aliingia katika hema ya Ushuhuda, angalia! fimbo ya Haruni kwa ajili ya nyumba ya Lawi ilikuwa imetokeza matumba* na ilikuwa inatoa maua na kuzaa matunda yenye kukomaa ya muti wa lozi. 9 Kisha Musa akaondoa fimbo zote hizo mbele ya Yehova na kuzileta mbele ya watu wote wa Israeli. Wakaziangalia, na kila mutu akachukua fimbo yake.
10 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Rudisha fimbo ya Haruni+ mbele ya Ushuhuda ili iwekwe kuwa alama+ kwa wana wa uasi,+ ili manunguniko yao juu yangu yaishe na ili wasikufe.” 11 Mara moja Musa akafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru. Ni vile alifanya kabisa.
12 Kisha Waisraeli wakamuambia Musa, “Sasa tutakufa, hakika tutaisha, sisi wote tutaisha! 13 Mutu yeyote mwenye hata anakaribia tabenakulo ya Yehova atakufa!+ Je, ni lazima sisi wote tufikie kufa kwa njia hiyo?”+
18 Kisha Yehova akamuambia Haruni: “Wewe na wana wako na jamaa yako ya upande wa baba mutajibu kwa sababu ya kila kosa lenye litafanywa kuhusu patakatifu,+ na wewe na wana wako mutajibu kwa sababu ya kila kosa lenye litafanywa kuhusu ukuhani wenu.+ 2 Pia uwalete karibu ndugu zako wa kabila la Lawi, kabila la mababu zako, ili wajiunge na wewe+ na kukutumikia wewe na wana wako mbele ya hema ya Ushuhuda.+ 3 Wanapaswa kutimiza madaraka yao kukuelekea na kuelekea hema yote.+ Lakini, hawapaswe kukaribia vyombo vya mahali patakatifu na mazabahu, kusudi ninyi pamoja nao musikufe.+ 4 Watajiunga na wewe na kutimiza madaraka yao kuhusiana na hema ya mukutano na utumishi wote wa hema hiyo, na mutu yeyote mwenye haruhusiwe* hapaswe kuwakaribia ninyi.+ 5 Munapaswa kutimiza daraka lenu kuelekea mahali patakatifu+ na mazabahu,+ kusudi kasirani isikuje tena+ juu ya watu wa Israeli. 6 Mimi mwenyewe nimechukua ndugu zenu, Walawi, kutoka kati ya Waisraeli kuwa zawadi kwa ajili yenu.+ Wametolewa kwa Yehova ili wafanye utumishi wa hema ya mukutano.+ 7 Wewe na wana wako muko na daraka la kufanya kazi za ukuhani zenye zinahusu mazabahu na vitu vyenye kuwa ndani ya pazia,+ na munapaswa kufanya utumishi huo.+ Nimewapatia utumishi wa ukuhani kama zawadi, na mutu yeyote mwenye haruhusiwe* mwenye atakaribia anapaswa kuuawa.”+
8 Yehova akaendelea kumuambia Haruni: “Mimi mwenyewe nilikuweka usimamie michango yenye inafanywa kwa ajili yangu.+ Nimekupatia wewe na wana wako sehemu fulani ya vitu vyote vitakatifu vyenye Waisraeli wanatoa kama muchango ili vikuwe posho lenu la kudumu.+ 9 Hivi vitakuwa vitu vyenu kutoka katikati ya matoleo yote matakatifu sana yenye yanatolewa kwa njia ya moto: kila toleo lenye wanatoa, kutia ndani matoleo yao ya nafaka+ na matoleo yao ya zambi+ na matoleo yao ya hatia+ yenye wananiletea. Ni vitu vitakatifu sana kwa ajili yako na kwa ajili ya wana wako. 10 Utakula vitu hivyo mahali patakatifu zaidi.+ Kila mwanaume anaweza kuvikula. Vitakuwa vitu vitakatifu kwa ajili yako.+ 11 Vitu hivi pia vitakuwa vyako: zawadi zenye wanatoa pamoja+ na matoleo yote ya kutikiswa+ ya Waisraeli. Nimekupatia wewe na watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke vitu hivyo ili vikuwe posho lenu la kudumu.+ Kila mutu mwenye kuwa safi katika nyumba yako anaweza kula vitu hivyo.+
12 “Mafuta yote ya muzuri sana na divai yote mupya ya muzuri sana na nafaka, matunda yao ya kwanza,+ yenye wanamupatia Yehova, ninakupatia wewe.+ 13 Matunda yote ya kwanza yenye kukomaa ya inchi yao, yenye watamuletea Yehova, yatakuwa yako.+ Kila mutu mwenye kuwa safi katika nyumba yako anaweza kula matunda hayo.
14 “Kila kitu chenye kimewekwa kwa ajili ya kusudi takatifu* katika Israeli kitakuwa chako.+
15 “Kila muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote vyenye uzima,*+ mwenye watamutolea Yehova, ikuwe mwanadamu ao munyama, atakuwa wako. Lakini, unapaswa kabisa kumukomboa muzaliwa wa kwanza wa wanadamu,+ na muzaliwa wa kwanza wa wanyama wenye hawako safi.+ 16 Utamukomboa muzaliwa wa kwanza kwa bei ya ukombozi wakati iko* na mwezi mumoja na zaidi, kwa samani yenye ilikadiriwa ya shekeli* tano (5) za feza,+ kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.* Ni gera* makumi mbili (20). 17 Lakini haupaswe kumukomboa ngombe-dume mwenye ni muzaliwa wa kwanza ao mwana-kondoo dume mwenye ni muzaliwa wa kwanza ao mbuzi mwenye ni muzaliwa wa kwanza.+ Hao ni watakatifu. Utanyunyiza* damu yao kwenye mazabahu,+ na mafuta yao utayachoma kusudi yatoe moshi yakiwa toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto ili kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova.+ 18 Na nyama yao itakuwa yako.+ Itakuwa yako sawa na kifua cha toleo la kutikiswa na muguu wa kuume. 19 Michango yote mitakatifu yenye Waisraeli watamutolea Yehova,+ nimekupatia wewe na watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke kuwa posho lenu la kudumu.+ Ni agano la chumvi lenye kudumu* mbele ya Yehova kwa ajili yako na uzao wako pamoja na wewe.”
20 Yehova akaendelea kumuambia Haruni: “Hautakuwa na uriti katika inchi yao, na hautakuwa na sehemu yoyote ya udongo kati yao.+ Mimi ni fungu lako na uriti wako kati ya Waisraeli.+
21 “Sasa ona kwamba nimepatia wana wa Lawi kila sehemu moja ya kumi (1/10)+ katika Israeli kuwa uriti wao kwa sababu ya utumishi wenye wanatimiza, utumishi wa hema ya mukutano. 22 Watu wa Israeli wasikaribie tena hema ya mukutano, ili wasikuwe na hatia ya zambi na kufa. 23 Walawi peke yao ndio watafanya utumishi wa hema ya mukutano, na wao ndio watajibu kwa ajili ya kosa lao.+ Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kwamba hawapaswe kukamata uriti kati ya Waisraeli.+ 24 Kwa maana nimepatia Walawi sehemu moja ya kumi (1/10) yenye watu wa Israeli wanamutolea Yehova kuwa muchango ili ikuwe uriti wao. Ndiyo sababu nimewaambia, ‘Hawapaswe kukamata uriti kati ya Waisraeli.’”+
25 Kisha Yehova akamuambia Musa: 26 “Unapaswa kuwaambia Walawi, ‘Mutapokea kutoka kwa Waisraeli sehemu moja ya kumi (1/10) yenye nimewapatia ninyi kutoka kwao ili ikuwe uriti wenu,+ na munapaswa kumutolea Yehova muchango wa sehemu moja ya kumi kutoka katika sehemu hiyo ya kumi (1/10).+ 27 Na sehemu hiyo itaonwa kuwa muchango wenu, kama nafaka kutoka kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka+ ao divai yote yenye inatoka katika kikamulio cha divai ao mafuta yote yenye yanatoka katika kikamulio cha mafuta. 28 Kwa njia hiyo mutamutolea pia Yehova muchango kutoka katika sehemu zote za kumi zenye munapokea kutoka kwa Waisraeli, na kutoka katika sehemu hizo munapaswa kumupatia Haruni kuhani muchango kwa ajili ya Yehova. 29 Mutamutolea Yehova kila namna ya muchango kutoka katika zawadi zote za muzuri sana zenye munapokea+ kuwa kitu kitakatifu.’
30 “Na unapaswa kuwaambia, ‘Wakati munatoa vitu vya muzuri sana kutoka katika zawadi hizo kuwa muchango, basi muchango huo wa Walawi utaonwa kama mbegu kutoka katika kiwanja cha kupigia-pigia nafaka na kama divai yenye inatoka katika kikamulio cha divai ao mafuta yenye yanatoka katika kikamulio cha mafuta. 31 Ninyi na watu wa nyumba zenu munaweza kula vitu hivyo mahali popote, kwa sababu ni malipo kwa ajili ya utumishi wenu kwenye hema ya mukutano.+ 32 Hamutakuwa na hatia ya zambi katika jambo hili wakati wote wenye mutanitolea muchango wa vitu vya muzuri sana kutoka katika zawadi hizo, na hamupaswe kuchafua vitu vitakatifu vya Waisraeli, ili musikufe.’”+
19 Yehova akasema tena na Musa na Haruni, na kuwaambia: 2 “Hii ni amri ya sheria yenye Yehova ameamuru, ‘Ambia Waisraeli wakukamatie ngombe-dike wa rangi nyekundu mwenye kuwa sawa, mwenye hana kasoro yoyote+ na mwenye nira haijafungwa juu yake. 3 Mutamupatia Eleazari kuhani ngombe-dike huyo, na atamupeleka inje ya kambi, na atachinjwa mbele yake. 4 Kisha Eleazari kuhani atakamata kwa kidole chake sehemu fulani ya damu ya ngombe-dike huyo na kuinyunyiza* mara saba (7) kuelekea upande wa mbele wa hema ya mukutano.+ 5 Kisha ngombe-dike huyo atateketezwa kwa moto mbele ya macho yake. Ngozi yake na nyama yake na damu yake pamoja na mavi yake vitateketezwa kwa moto.+ 6 Na kuhani atakamata muti wa mwerezi, hisopo,+ na kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa na kutupa vitu hivyo katika moto mahali ngombe-dike huyo anateketezwa kwa moto. 7 Kisha kuhani atafua nguo zake na kuoga ndani ya maji, halafu anaweza kurudia katika kambi; lakini kuhani huyo hatakuwa safi mupaka mangaribi.
8 “‘Mutu mwenye aliteketeza kwa moto ngombe-dike huyo atafua nguo zake na kuoga ndani ya maji, na hatakuwa safi mupaka mangaribi.
9 “‘Mutu mwenye kuwa safi atakusanya majivu ya ngombe-dike+ huyo na kuyapeleka mahali kwenye kuwa safi inje ya kambi, na mukusanyiko wa Waisraeli utayaweka ili kutayarisha maji ya kutakasa.+ Ni toleo la zambi. 10 Ule mwenye kukusanya majivu ya ngombe-dike huyo atafua nguo zake na hatakuwa safi mupaka mangaribi.
“‘Hiyo itakuwa sheria ya kudumu kwa Waisraeli na mugeni mwenye anaishi katikati yao.+ 11 Kila mutu mwenye anagusa mutu mwenye amekufa* hatakuwa safi kwa siku saba (7).+ 12 Mutu huyo atajitakasa kwa maji hayo siku ya tatu (3), na siku ya saba (7) atakuwa safi. Lakini kama hajitakase siku ya tatu, hatakuwa safi siku ya saba. 13 Kila mutu mwenye anagusa maiti ya mutu yeyote mwenye amekufa* na hajitakase amechafua tabenakulo ya Yehova,+ na mutu huyo anapaswa* kuondolewa* katikati ya Israeli.+ Kwa sababu maji ya kutakasa+ hayajanyunyizwa* juu yake, ataendelea kuwa muchafu. Uchafu wake ungali juu yake.
14 “‘Hii ndiyo sheria kuhusu mutu mwenye anakufia ndani ya hema: Kila mutu mwenye anaingia katika hema hiyo na kila mutu mwenye tayari alikuwa ndani ya hema hiyo hatakuwa safi kwa siku saba (7). 15 Kila chombo chenye kuwa wazi chenye kifuniko chake hakijafungwa juu yake hakiko safi.+ 16 Kila mutu mwenye kuwa katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba mwenye anagusa mutu mwenye aliuawa kwa upanga ao maiti ao mufupa wa mutu ao kaburi hatakuwa safi kwa siku saba (7).+ 17 Watakamata, kwa ajili ya mutu huyo mwenye haiko safi, sehemu fulani ya majivu ya toleo la zambi lenye liliteketezwa kwa moto na kumwanga maji yenye yalishotwa kwenye muto juu ya majivu hayo katika chombo. 18 Kisha mutu mwenye kuwa safi+ atakamata hisopo+ na kuichovya ndani ya maji hayo na kuyanyunyiza* juu ya hema na juu ya vyombo vyote na juu ya watu wenye walikuwa* pale na juu ya mutu mwenye aligusa mufupa ao mutu mwenye aliuawa ao maiti ao kaburi. 19 Mutu mwenye kuwa safi atanyunyiza* maji hayo juu ya mutu mwenye haiko safi siku ya tatu (3) na siku ya saba (7), na atamutakasa zambi yake siku ya saba;+ kisha atafua nguo zake na kuoga ndani ya maji, na atakuwa safi mangaribi.
20 “‘Lakini mutu mwenye haiko safi na mwenye hatajitakasa, mutu huyo anapaswa* kuondolewa* katikati ya kutaniko,+ kwa sababu amechafua patakatifu pa Yehova. Maji ya kutakasa hayakunyunyizwa* juu yake, kwa hiyo yeye haiko safi.
21 “‘Hii itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yao: Ule mwenye ananyunyiza* maji ya kutakasa+ anapaswa kufua nguo zake, na ule mwenye anagusa maji ya kutakasa hatakuwa safi mupaka mangaribi. 22 Kila kitu chenye mutu mwenye haiko safi anagusa hakitakuwa safi, na mutu mwenye anakigusa hatakuwa* safi mupaka mangaribi.’”+
20 Katika mwezi wa kwanza, mukusanyiko wote wa Waisraeli ulifika katika jangwa la Zini, na watu wakaanza kukaa Kadeshi.+ Ni pale Miriamu+ alikufia na kuzikwa.
2 Sasa hapakukuwa maji kwa ajili ya mukusanyiko,+ na wakakusanyika ili kupinga Musa na Haruni. 3 Watu wakabishana na Musa,+ na kusema: “Ingekuwa muzuri kama tungekufa wakati ndugu zetu walikufa mbele ya Yehova! 4 Sababu gani mumeleta kutaniko la Yehova katika jangwa hili kusudi sisi na mifugo yetu tukufie hapa?+ 5 Na sababu gani mulitutosha Misri ili kutuleta mahali hapa pabaya?+ Haiko mahali pa mbegu na tini na mizabibu na makomamanga, na hakuna maji ya kunywa.”+ 6 Kisha Musa na Haruni wakatoka mbele ya kutaniko na kuenda kwenye muingilio wa hema ya mukutano na wakaanguka uso chini, na utukufu wa Yehova ukaanza kuwatokea.+
7 Kisha Yehova akamuambia Musa: 8 “Kamata ile fimbo na ukusanye mukusanyiko pamoja, wewe na Haruni ndugu yako, na museme na mwamba mbele ya macho yao ili utoe maji, na utatosha maji katika mwamba huo kwa ajili yao na kupatia mukusanyiko na mifugo yao maji ya kunywa.”+
9 Kwa hiyo, Musa akakamata ile fimbo kutoka mbele ya Yehova,+ kama vile Yeye alikuwa amemuamuru. 10 Kisha Musa na Haruni wakakusanya kutaniko pamoja mbele ya mwamba huo, na akawaambia, “Musikie, sasa, ninyi waasi! Je, tunapaswa kuwatoshea maji katika mwamba huu?”+ 11 Basi Musa akainua mukono wake na kupiga mwamba huo mara mbili kwa fimbo yake, na maji yakaanza kutoka kwa wingi, na mukusanyiko na mifugo yao wakaanza kunywa.+
12 Kisha wakati fulani Yehova akamuambia Musa na Haruni: “Kwa sababu hamukuonyesha imani kwangu na hamukunitakasa mbele ya macho ya watu wa Israeli, hamutaingiza kutaniko hili katika inchi yenye nitawapatia.”+ 13 Hayo ndiyo maji ya Meriba,*+ mahali kwenye Waisraeli walibishana na Yehova, na hivyo akatakaswa kati yao.
14 Kisha Musa akatuma wajumbe kutoka Kadeshi ili waende kwa mufalme wa Edomu:+ “Ndugu yako Israeli+ anasema hivi, ‘Unajua muzuri magumu yote yenye tumepata. 15 Baba zetu walienda Misri,+ na tuliishi Misri miaka mingi,*+ na Wamisri walitutesa sisi na baba zetu.+ 16 Mwishowe tulimulilia Yehova,+ na akatusikia na akatuma malaika+ na akatutosha Misri, na sasa tuko hapa Kadeshi, muji wenye kuwa kwenye mupaka wa eneo lako. 17 Tafazali uturuhusu tupite katika inchi yako. Hatutapita katika shamba lolote ao shamba la mizabibu, na hatutakunywa maji ya kisima chochote. Tutatembea katika Barabara ya Mufalme bila kugeuka upande wa kuume ao wa kushoto mupaka wakati tutakuwa tumepita katika eneo lako.’”+
18 Lakini, Edomu akamuambia, “Usipite katika eneo letu. Ukipita, nitakuja na upanga ili kukutana na wewe.” 19 Basi Waisraeli wakamuambia, “Tutapanda katika barabara kubwa, na kama sisi na mifugo yetu tunakunywa maji yako, tutalipa.+ Hatutaki kitu kingine chochote isipokuwa kupita kwa miguu.”+ 20 Lakini akasema, “Hamutapita.”+ Kwa hiyo Edomu akatoka ili kukutana naye na alikuwa na watu wengi na jeshi lenye* nguvu. 21 Basi Edomu akakataa kuruhusu Israeli apite katika eneo lake; kwa hiyo Waisraeli wakageuka na kumuacha.+
22 Watu wa Israeli, mukusanyiko wote, wakatoka Kadeshi na kufika kwenye Mulima Hori.+ 23 Kisha Yehova akasema na Musa na Haruni katika Mulima Hori karibu na mupaka wa inchi ya Edomu: 24 “Haruni atakusanywa kwa watu wake.*+ Hataingia katika inchi yenye nitapatia Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili muliasi agizo langu kuhusu maji ya Meriba.+ 25 Chukua Haruni na Eleazari mwana wake na uwalete juu kwenye Mulima Hori. 26 Vua Haruni nguo zake+ na umuvalishe Eleazari+ mwana wake, na Haruni atakufia kule.”*
27 Kwa hiyo Musa akafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru, na wakapanda Mulima Hori mbele ya macho ya mukusanyiko wote. 28 Basi Musa akamuvua Haruni nguo zake na kuzivalisha Eleazari mwana wake. Kisha, Haruni akakufia kule kwenye kichwa cha mulima huo.+ Na Musa na Eleazari wakashuka kutoka kwenye mulima. 29 Wakati mukusanyiko wote uliona kwamba Haruni alikuwa amekufa, nyumba yote ya Israeli ikamulia Haruni kwa siku makumi tatu (30).+
21 Wakati mufalme Mukanaani wa Aradi,+ mwenye aliishi Negebu, alisikia kama Israeli alikuwa amekuja kupitia njia ya Atarimu, alishambulia Israeli na kukamata mateka wamoja kati yao. 2 Kwa hiyo Israeli akafanya naziri hii kwa Yehova: “Kama unatia watu hawa katika mukono wangu, hakika nitaharibu miji yao.” 3 Kwa hiyo Yehova akasikiliza sauti ya Israeli na akatia Wakanaani katika mikono yao, na wakawaharibu pamoja na miji yao. Basi wakaita mahali pale Horma.*+
4 Wakati waliendelea na safari yao kutoka Mulima Hori+ kupitia njia ya Bahari Nyekundu ili kuzunguka inchi ya Edomu,+ watu wakachoka* kwa sababu ya safari. 5 Na watu wakaendelea kusema mubaya juu ya Mungu na juu ya Musa,+ na kusema: “Sababu gani mumetupandisha kutoka Misri ili tukufie katika jangwa? Hakuna chakula na maji,+ na sisi tumechukia* mukate huu wenye kuzaraulika.”+ 6 Kwa hiyo Yehova akatuma nyoka wenye sumu* kati ya watu, na nyoka hao wakaendelea kuuma watu, na hivyo Waisraeli wengi wakakufa.+
7 Kwa hiyo watu wakakuja kwa Musa na kumuambia: “Tumefanya zambi kwa kusema mubaya juu ya Yehova na juu yako.+ Umulilie Yehova ili atuondolee nyoka hawa.” Na Musa akamulilia Mungu kwa ajili ya watu.+ 8 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Tengeneza nyoka mwenye sumu* wa mufano na umuweke juu ya nguzo. Basi wakati mutu yeyote ameumwa, ataangalia mufano huo ili aendelee kuishi.” 9 Mara moja Musa akatengeneza nyoka wa shaba+ na kumuweka juu ya nguzo,+ na kila mara wakati nyoka alikuwa ameuma mutu na mutu huyo aangalie nyoka huyo wa shaba, aliendelea kuishi.+
10 Kisha Waisraeli wakaondoka na kupiga kambi Oboti.+ 11 Halafu wakaondoka Oboti na kupiga kambi Iye-abarimu,+ katika jangwa lenye linaangaliana na Moabu, kuelekea upande wa mashariki. 12 Kutoka pale wakaondoka na kupiga kambi karibu na Bonde* la Zeredi.+ 13 Kutoka pale wakaondoka na kupiga kambi katika eneo la Arnoni,+ lenye kuwa katika jangwa na lenye linasambaa kuanzia mupaka wa Waamori, kwa maana Arnoni ni mupaka wa Moabu, katikati ya Moabu na Waamori. 14 Ndiyo sababu kitabu cha Vita za Yehova kinazungumuzia “Vahebu katika eneo la Sufa na mabonde ya Arnoni, 15 na muteremuko wa* mabonde, wenye unasambaa kuelekea makao ya Ari na kufika kwenye mupaka wa Moabu.”
16 Kisha wakasafiri mupaka Beeri. Ni kuhusu kisima hicho Yehova alimuambia Musa: “Wakusanye watu, ili niwapatie maji.”
17 Wakati huo, Israeli aliimba wimbo huu:
“Bubujika, Ee kisima!—Mukijibu!*
18 Kisima chenye wakubwa walichimba, chenye watu wenye vyeo kati ya watu walichimba,
Kwa fimbo ya kamanda na kwa fimbo zao wenyewe.”
Kisha wakatoka katika jangwa na kuenda Matana, 19 kutoka Matana mupaka Nahalieli, na kutoka Nahalieli mupaka Bamoti.+ 20 Wakatoka Bamoti na kuenda kwenye bonde lenye kuwa katika eneo* la Moabu,+ kwenye kichwa cha Pisga,+ yenye inaangaliana na Yeshimoni.*+
21 Sasa Israeli akatuma wajumbe kwa Sihoni, mufalme wa Waamori, ili wamuambie:+ 22 “Uturuhusu tupite katika inchi yako. Hatutageuka na kuingia katika shamba ao shamba la mizabibu. Hatutakunywa maji ya kisima chochote. Tutatembea katika Barabara ya Mufalme mupaka wakati tutakuwa tumepita katika eneo lako.”+ 23 Lakini Sihoni hakuruhusu Israeli apitie katika eneo lake. Tofauti na hiyo, Sihoni akakusanya watu wake wote na kuenda kushambulia Israeli katika jangwa na akafika Yahazi na kuanza kupigana na Israeli.+ 24 Lakini Israeli akamushinda kwa upanga+ na akakamata inchi yake+ kuanzia Arnoni+ mupaka Yaboki,+ karibu na Waamoni, kwa sababu muji wa Yazeri+ uko kwenye mupaka wa eneo la Waamoni.+
25 Kwa hiyo Israeli akakamata miji hiyo yote, na wakaanza kuishi katika miji yote ya Waamori,+ katika Heshboni na miji yake yote ya pembeni-pembeni.* 26 Kwa maana Heshboni ulikuwa muji wa Sihoni, mufalme wa Waamori, mwenye alikuwa amepigana na mufalme wa Moabu na kukamata inchi yake yote mupaka Arnoni. 27 Ndiyo maana watu walitunga usemi huu wa kimezali wa uchokozi:
“Mukuje Heshboni.
Muji wa Sihoni ujengwe na kufanywa imara kabisa.
28 Kwa maana moto ulitoka Heshboni, mwali wa moto ulitoka katika muji wa Sihoni.
Umeteketeza muji wa Ari wa Moabu, mabwana wa mahali pa juu pa Arnoni.
29 Ole wako, Moabu! Mutaharibiwa, Enyi watu wa Kemoshi!+
Anafanya watoto wake wanaume kuwa wakimbizi na watoto wake wanamuke kuwa watu wenye walikamatwa mateka wa Sihoni, mufalme wa Waamori.
30 Tuwatupie mishale;
Heshboni utaharibiwa mupaka Diboni;+
Tuuharibu mupaka Nofa;
Moto utasambaa mupaka Medeba.”+
31 Kwa hiyo Israeli akaanza kuishi katika inchi ya Waamori. 32 Kisha Musa akatuma watu fulani wapeleleze Yazeri.+ Wakakamata miji yake ya pembeni-pembeni* na wakafukuza Waamori wenye walikuwa kule. 33 Kisha wakageuka na kupanda kupitia Njia ya Bashani. Na Ogu+ mufalme wa Bashani akatoka pamoja na watu wake wote ili kupigana nao kule Edrei.+ 34 Yehova akamuambia Musa: “Usimuogope,+ kwa maana nitamutia yeye na watu wake wote na inchi yake katika mukono wako,+ na utamutendea kama vile ulimutendea Sihoni mufalme wa Waamori, mwenye aliishi Heshboni.”+ 35 Kwa hiyo wakaendelea kumupiga na kumuua, yeye pamoja na wana wake na watu wake wote, mupaka hapakukuwa hata mumoja wa watu wake mwenye aliokoka,+ na wakakamata inchi yake.+
22 Kisha Waisraeli wakaondoka na kupiga kambi kwenye maeneo tambarare ya jangwa la Moabu ngambo ya Yordani kutoka Yeriko.+ 2 Sasa Balaki+ mwana wa Sipori aliona mambo yote yenye Israeli alikuwa ametendea Waamori, 3 na Moabu akaogopa sana watu hao, kwa sababu walikuwa wengi sana; kwa kweli, Moabu akaogopa na kuchukizwa sana kwa sababu ya Waisraeli.+ 4 Kwa hiyo Moabu akaambia wazee wa Midiani:+ “Sasa kutaniko hili litameza maeneo yetu yote yenye kutuzunguka, kama vile ngombe-dume anamezaka majani katika pori.”
Balaki mwana wa Sipori alikuwa mufalme wa Moabu wakati huo. 5 Alituma wajumbe kwa Balaamu mwana wa Beori kule Petori,+ karibu na ule Muto* katika inchi yenye alizaliwa ndani. Alimuita, na kumuambia: “Angalia! Watu fulani wametoka Misri. Angalia! Wamefunika uso wa* dunia,*+ na wanakaa hapa tu mbele yangu. 6 Basi, tafazali, kuja na ulaani watu hawa kwa ajili yangu,+ kwa maana wako na nguvu kuliko mimi. Pengine ninaweza kuwashinda na kuwafukuza katika inchi, kwa maana ninajua muzuri kama ule mwenye unabariki amebarikiwa na ule mwenye unalaani amelaaniwa.”
7 Kwa hiyo wazee wa Moabu na wazee wa Midiani wakasafiri na malipo ya uaguzi katika mikono yao na kuenda kwa Balaamu+ na wakamuambia maneno ya Balaki. 8 Halafu akawaambia: “Mulale hapa, na nitawaletea neno lolote lenye Yehova ataniambia.” Kwa hiyo wakubwa wa Moabu wakabakia kwa Balaamu.
9 Kisha Mungu akamutokea Balaamu na kusema:+ “Wanaume hawa wenye wako pamoja na wewe ni nani?” 10 Balaamu akamuambia Mungu wa kweli: “Balaki mwana wa Sipori, mufalme wa Moabu, amenitumia ujumbe, na kusema, 11 ‘Angalia! Watu wenye wanatoka Misri wanafunika uso wa* dunia.* Sasa kuja na uwalaani kwa ajili yangu.+ Pengine ninaweza kupigana nao na kuwafukuza.’” 12 Lakini Mungu akamuambia Balaamu: “Usiende pamoja nao. Usilaani watu hao, kwa maana wamebarikiwa.”+
13 Balaamu akaamuka asubui na kuambia wakubwa wa Balaki: “Muende katika inchi yenu, kwa maana Yehova amekataa kuniruhusu niende pamoja na ninyi.” 14 Kwa hiyo wakubwa wa Moabu wakaondoka na wakarudia kwa Balaki na kumuambia: “Balaamu amekataa kuja pamoja na sisi.”
15 Lakini, Balaki akatuma tena wakubwa, wengi zaidi na wenye kuheshimika zaidi kuliko wale wa kikundi cha kwanza. 16 Wakafika kwa Balaamu na kumuambia: “Balaki mwana wa Sipori amesema, ‘Tafazali, usiruhusu kitu chochote kikuzuie kuja kwangu, 17 kwa maana nitakuonyesha heshima kubwa na nitafanya kila kitu chenye utaniambia nifanye. Kwa hiyo, kuja, tafazali, na ulaani watu hawa kwa ajili yangu.’” 18 Lakini Balaamu akajibu watumishi wa Balaki: “Hata kama Balaki ananipatia nyumba yake mwenyewe yenye kujaa feza na zahabu, siwezi kufanya jambo lolote lenye linavunja agizo la Yehova Mungu wangu, ikuwe jambo la kidogo ao la mukubwa.+ 19 Lakini tafazali, mubakie hapa usiku wa leo pia, ili nijue Yehova ataniambia jambo gani lingine.”+
20 Kisha Mungu akamutokea Balaamu usiku na kumuambia: “Kama wanaume hao wamekuja kukuita, uende pamoja nao. Lakini utasema tu maneno yenye nitakuambia useme.”+ 21 Basi Balaamu akaamuka asubui na akamutandika punda* wake na kuenda pamoja na wakubwa wa Moabu.+
22 Lakini kasirani ya Mungu ikawaka sana kwa sababu Balaamu alikuwa anaenda, na malaika wa Yehova akasimama katika njia ili kumupinga. Sasa Balaamu alikuwa amepanda juu ya punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye. 23 Na wakati punda huyo aliona malaika wa Yehova amesimama katika njia akiwa na upanga wenye kuchomolewa katika mukono wake, alijaribu kutoka katika njia ili aingie katika eneo la mashamba. Lakini Balaamu akaanza kumupiga punda huyo ili arudie katika njia. 24 Kisha malaika wa Yehova akasimama katika njia nyembamba katikati ya mashamba mbili ya mizabibu, na kulikuwa ukuta wa majiwe kwenye pande zote mbili. 25 Wakati punda aliona malaika wa Yehova, akaanza kujisukuma kwenye ukuta na kufinya muguu wa Balaamu kwenye ukuta, na Balaamu akaanza kumupiga tena.
26 Sasa malaika wa Yehova akapita tena na kusimama mahali pembamba kwenye hakukuwa nafasi ya kugeukia upande wa kuume ao kushoto. 27 Wakati punda aliona malaika wa Yehova, akalala chini, chini ya Balaamu, kwa hiyo Balaamu akakasirika sana na kuendelea kumupiga punda kwa fimbo yake. 28 Mwishowe Yehova akamufanya punda huyo aseme,*+ na akamuambia Balaamu: “Nimekutendea nini yenye inafanya unipige mara hizi tatu (3)?”+ 29 Balaamu akamujibu punda huyo: “Ni kwa sababu umenifanya nionekane kuwa mupumbavu. Kama tu ningekuwa na upanga katika mukono wangu, ningekuua!” 30 Kisha punda akamuambia Balaamu: “Je, mimi siko punda wako mwenye umepanda maisha yako yote mupaka leo? Je, kuko siku nimekutendea hivi zamani?” Akajibu: “Hapana!” 31 Kisha Yehova akafungua macho ya Balaamu,+ naye akaona malaika wa Yehova amesimama katika njia akiwa na upanga wenye kuchomolewa katika mukono wake. Mara moja Balaamu akainama na kushusha uso chini.
32 Kisha malaika wa Yehova akamuambia: “Sababu gani umemupiga punda wako mara hizi tatu (3)? Angalia! Mimi mwenyewe nimekuja ili kukupinga, kwa sababu njia yako haipatane na mapenzi yangu.+ 33 Punda aliniona na akajaribu kunikwepa mara hizi tatu (3).+ Kama hangenikwepa! Kufikia sasa ningekuwa nimekuua na kumuacha punda akiwa muzima.” 34 Balaamu akamuambia malaika wa Yehova: “Nimetenda zambi, kwa sababu sikujua kama ni wewe ulisimama katika njia ili kukutana na mimi. Na sasa kama jambo hilo ni la mubaya mbele ya macho yako, mimi nitarudia.” 35 Lakini malaika wa Yehova akamuambia Balaamu: “Uende pamoja na wanaume hao, lakini utasema tu maneno yenye nitakuambia.” Kwa hiyo Balaamu akaendelea kuenda pamoja na wakubwa wa Balaki.
36 Wakati Balaki alisikia kama Balaamu amefika, akaenda inje mara moja ili kumupokea katika muji wa Moabu, wenye kuwa pembeni ya Arnoni kwenye mupaka wa Moabu. 37 Balaki akamuambia Balaamu: “Je, sikutuma wakuite? Sababu gani haukukuja kwangu? Je, uliwaza siwezi kukuonyesha heshima kubwa?”+ 38 Balaamu akamujibu Balaki: “Sasa nimekuja kwako. Lakini, je, nitaruhusiwa kusema jambo fulani? Ninaweza kusema tu maneno yenye Mungu anatia katika kinywa changu.”+
39 Kwa hiyo Balaamu akaenda pamoja na Balaki, na wakafika Kiriat-husoti. 40 Balaki akatoa zabihu za ngombe na kondoo na akatuma sehemu kwa Balaamu na kwa wakubwa wenye walikuwa pamoja naye. 41 Asubui Balaki akamuchukua Balaamu na kumupandisha mupaka Bamot-baali; na kule aliweza kuona watu hao wote.+
23 Kisha Balaamu akamuambia Balaki: “Jenga hapa mazabahu saba (7),+ na unitayarishie ngombe-dume saba na kondoo-dume saba.” 2 Mara moja Balaki akafanya kama vile Balaamu alikuwa amesema. Na Balaki na Balaamu wakatoa ngombe-dume mumoja na kondoo-dume mumoja juu ya kila mazabahu.+ 3 Halafu Balaamu akamuambia Balaki: “Bakia hapa karibu na toleo lako la kuteketezwa, na mimi nitaenda. Pengine Yehova atazungumuza na mimi. Kila jambo lenye atanifunulia, nitakuambia.” Kwa hiyo akaenda juu ya kilima chenye kuwa wazi.
4 Kisha Mungu akazungumuza na Balaamu,+ Balaamu akamuambia: “Nilisimamisha mazabahu saba (7) katika mistari, na nilitoa ngombe-dume mumoja na kondoo-dume mumoja juu ya kila mazabahu.” 5 Yehova akatia neno hili katika kinywa cha Balaamu:+ “Rudia kwa Balaki, na haya ndiyo mambo yenye utasema.” 6 Kwa hiyo akarudia na akaona kwamba Balaki na wakubwa wote wa Moabu walikuwa wanasimama karibu na toleo lake la kuteketezwa. 7 Kisha akasema usemi huu wa kimezali:+
“Balaki mufalme wa Moabu amenileta kutoka Aramu,+
Kutoka katika milima ya mashariki:
‘Kuja umulaani Yakobo kwa ajili yangu.
Ndiyo, kuja ulaumu Israeli.’+
8 Namna gani ninaweza kulaani watu wenye Mungu hajalaani?
Na namna gani ninaweza kulaumu watu wenye Yehova hajalaumu?+
9 Kutoka kwenye sehemu ya juu ya miamba ninawaona,
Na kutoka kwenye vilima ninawaona.
10 Ni nani anaweza kuhesabia chembe za mavumbi ya Yakobo+
Ao hata kuhesabia sehemu moja ya ine (1/4) ya Israeli?
Acha nikufe* kifo cha watu wanyoofu,
Na mwisho wangu ukuwe kama mwisho wao.”
11 Kisha Balaki akamuambia Balaamu: “Ni jambo gani hili umenitendea? Nilikuleta ili ulaani maadui wangu, na sasa kuliko kuwalaani umewabariki tu.”+ 12 Balaamu akajibu: “Je, sipaswe kusema neno lolote lenye Yehova anatia katika kinywa changu?”+
13 Balaki akamuambia: “Tafazali, tuende mahali pengine kwenye unaweza kuwaona. Utaona wamoja katikati yao; hautawaona wote. Ukiwa pale uwalaani kwa ajili yangu.”+ 14 Kwa hiyo akamupeleka kwenye shamba la Sofimu, kwenye kichwa cha Pisga,+ na akajenga mazabahu saba (7) na kutoa ngombe-dume mumoja na kondoo-dume mumoja juu ya kila mazabahu.+ 15 Kwa hiyo Balaamu akamuambia Balaki: “Bakia hapa karibu na toleo lako la kuteketezwa wakati ninaenda pale kuzungumuza Naye.” 16 Na Yehova akazungumuza na Balaamu na kutia neno hili katika kinywa chake:+ “Rudia kwa Balaki, na hili ndilo jambo lenye utasema.” 17 Kwa hiyo akarudia kwa Balaki na akaona kwamba Balaki alikuwa anangojea akiwa karibu na toleo lake la kuteketezwa, na wakubwa wa Moabu walikuwa pamoja naye. Balaki akamuuliza: “Yehova amesema nini?” 18 Kisha Balaamu akasema usemi huu wa kimezali:+
“Simama, Balaki, na usikilize.
Unisikie, Ee mwana wa Sipori.
19 Mungu haiko mwanadamu bure mwenye anasemaka uongo,+
Wala haiko mwana wa binadamu mwenye anabadilishaka nia yake.*+
Wakati anasema jambo fulani, je, hatalifanya?
Wakati anasema, je, hatalitimiza?+
21 Havumilie nguvu zozote za uchawi juu ya Yakobo,
Na haruhusu taabu yoyote imufikie Israeli.
22 Mungu anawatosha Misri.+
Yeye ni kama pembe za ngombe-dume wa pori kwa ajili yao.+
23 Kwa maana hakuna alama za mambo ya mubaya juu ya Yakobo,+
Wala hakuna uaguzi wowote juu ya Israeli.+
Wakati huu inaweza kusemwa kuhusu Yakobo na Israeli:
‘Muangalie mambo yenye Mungu ametenda!’
24 Kikundi hiki cha watu kitasimama kama simba,
Na kama simba, kitajiinua.+
Hakitalala chini mupaka kikule mawindo
Na kunywa damu ya watu wenye kuuawa.”
25 Kisha Balaki akamuambia Balaamu: “Ikiwa kwa upande mumoja hauwezi kuwalaani hata kidogo, basi kwa upande mwingine haupaswe kuwabariki pia.” 26 Balaamu akamujibu Balaki: “Je, sikukuambia, ‘Nitafanya mambo yote yenye Yehova anasema’?”+
27 Balaki akamuambia Balaamu: “Tafazali kuja na uache nikupeleke mahali pengine. Pengine itakuwa sawa mbele ya macho ya Mungu wa kweli uwalaani kwa ajili yangu ukiwa mahali pale.”+ 28 Kwa hiyo Balaki akamupeleka Balaamu kwenye kichwa cha Mulima Peori, wenye unaangaliana na Yeshimoni.*+ 29 Kisha Balaamu akamuambia Balaki: “Jenga mazabahu saba (7) hapa, na unitayarishie ngombe-dume saba na kondoo-dume saba.”+ 30 Kwa hiyo Balaki akafanya kama vile Balaamu alikuwa amesema, na akatoa ngombe-dume mumoja na kondoo-dume mumoja juu ya kila mazabahu.
24 Wakati Balaamu aliona kwamba ilimupendeza* Yehova kubariki Israeli, hakuenda tena kutafuta alama za mambo ya mubaya,+ lakini aligeuza uso wake kuelekea jangwa. 2 Wakati Balaamu aliinua macho yake na kuona Israeli amepiga kambi kulingana na makabila yake,+ roho ya Mungu ikakuja juu ya Balaamu.+ 3 Kisha akasema usemi huu wa kimezali:+
“Maneno ya Balaamu mwana wa Beori,
Na maneno ya mwanaume mwenye macho yake yamefunguliwa,
4 Maneno ya mutu mwenye anasikia neno la Mungu,
Mwenye aliona maono ya Mweza-Yote,
Mwenye aliinama chini macho yake yakiwa wazi:+
5 Mahema yako yanapendeza sana, Ee Yakobo,
Tabenakulo zako, Ee Israeli!+
6 Yameenea mbali kama mabonde,
Kama bustani pembeni ya muto,+
Kama mimea ya aloe yenye Yehova amepanda,
Kama miti ya mierezi pembeni ya maji.
7 Maji yanaendelea kutiririka kutoka katika mbeketi zake mbili za ngozi,
8 Mungu anamutosha Misri;
Yeye ni kama pembe za ngombe-dume wa pori kwa ajili yao.
Atateketeza mataifa kwa moto, wakandamizaji wake,+
Na mifupa yao ataitafuna-tafuna, na atawapasua-pasua kwa mishale yake.
9 Ameshutama, amelala chini kama simba,
Na kama simba, ni nani anapima kumuamusha?
Wale wenye wanakubariki wamebarikiwa,
Na wale wenye wanakulaani wamelaaniwa.”+
10 Kisha Balaki akamukasirikia sana Balaamu. Balaki akapiga mikono kwa zarau na kumuambia Balaamu: “Nilikuita kusudi ulaani maadui wangu,+ lakini sasa kuliko kuwalaani umewabariki mara hizi tatu (3). 11 Sasa uende kwako mara moja. Nilitaka kukuonyesha heshima kubwa,+ lakini angalia! Yehova amekufanya usipate heshima.”
12 Balaamu akamujibu Balaki: “Je, sikuambia wajumbe wenye ulituma, 13 ‘Hata kama Balaki ananipatia nyumba yake yenye kujaa feza na zahabu, siwezi kwa mapenzi yangu* mwenyewe kufanya jambo lolote lenye linavunja agizo la Yehova, ikuwe jambo la muzuri ao la mubaya. Nitasema tu jambo lenye Yehova ataniambia’?+ 14 Na sasa ninaenda kwa watu wangu. Kuja na uache nikuambie mambo yenye watu hawa watatendea watu wako wakati wenye kuja.”* 15 Kwa hiyo akasema usemi huu wa kimezali:+
“Maneno ya Balaamu mwana wa Beori,
Na maneno ya mwanaume mwenye macho yake yamefunguliwa,+
16 Maneno ya mutu mwenye anasikia neno la Mungu,
Na ule mwenye kuwa na ujuzi wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi,
Aliona maono ya Mweza-Yote
Wakati alikuwa anainama chini macho yake yakiwa wazi:
17 Nitamuona, lakini hapana sasa;
Nitamuangalia, lakini hapana sasa hivi.
Na hakika atapasua paji la uso la Moabu+
Na mufupa wa kichwa wa wana wote wa fujo.
18 Na Edomu itakuwa uriti,+
Ndiyo, Seiri+ uriti wa maadui wake,+
Wakati Israeli atakuwa anaonyesha uhodari wake.
19 Na katika Yakobo atatoka mutu mwenye ataendelea kunyenyekeza,+
Na atamuharibu mutu yeyote mwenye ataokoka katika muji.”
20 Wakati alimuona Amaleki, akaendelea kusema usemi huu wa kimezali:
21 Wakati aliona Wakeni,+ akaendelea kusema usemi huu wa kimezali:
“Makao yenu yako salama, na makao yenu yamejengwa juu ya mwamba.
22 Lakini mutu fulani atateketeza Kayini kwa moto.
Kunabakia wakati gani mbele Ashuru akubebe ukiwa umetekwa?”
23 Na akaendelea kusema usemi wake wa kimezali:
“Ole! Ni nani ataokoka wakati Mungu atafanya vile?
24 Mashua* zitatoka katika maeneo ya Kitimu ya pembeni ya bahari,+
Na zitamutesa Ashuru,+
Na kumutesa Eberi.
Lakini yeye pia hatakuwa tena.”
25 Kisha Balaamu+ akasimama na akaenda na kurudia kwake. Balaki pia akaenda zake.
25 Wakati Israeli alikuwa anakaa Shitimu,+ watu walianza kufanya uasherati na mabinti wa Moabu.+ 2 Wanamuke hao walialika watu kwenye zabihu za miungu yao,+ na watu wakaanza kula na kuinamia miungu yao.+ 3 Kwa hiyo Israeli akajiunga na ibada ya* Baali wa Peori,+ na Yehova akakasirikia Israeli. 4 Yehova akamuambia Musa: “Chukua viongozi wote wa* watu hawa na uwatundike wakati wa muchana* mbele ya Yehova, kusudi kasirani yenye kuwaka ya Yehova isiendelee kuwaka juu ya Israeli.” 5 Kisha Musa akaambia waamuzi wa Israeli:+ “Kila mumoja wenu aue watu wake wenye walijiunga na ibada ya* Baali wa Peori.”+
6 Lakini wakati huo, mumoja kati ya Waisraeli akamuleta mwanamuke Mumidiani karibu na ndugu zake+ mbele ya macho ya Musa na ya mukusanyiko wote wa Waisraeli, wakati walikuwa wanalia kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 7 Wakati Finehasi+ mwana wa Eleazari mwana wa Haruni kuhani aliona jambo hilo, akasimama mara moja kutoka katikati ya mukusanyiko na kukamata mukuki katika mukono wake. 8 Kisha akamufuata mwanaume huyo wa Israeli mupaka katika hema na akawatoboa wote wawili, mwanaume wa Israeli na mwanamuke huyo kupitia viungo vya uzazi vya mwanamuke huyo. Kwa hiyo pigo lenye lilikuja juu ya Waisraeli likasimamishwa.+ 9 Watu wenye walikufa katika pigo hilo walikuwa elfu makumi mbili na ine (24 000).+
10 Kisha Yehova akamuambia Musa: 11 “Finehasi+ mwana wa Eleazari mwana wa Haruni kuhani amegeuzia mbali kasirani yangu kali juu ya watu wa Israeli kwa sababu hakuvumilia ushindani wowote kunielekea kati yao.+ Kwa hiyo sikuharibu Waisraeli hata kama ninatia mukazo juu ya kushikamana na mimi tu.+ 12 Kwa hiyo, useme, ‘Ninamupatia agano langu la amani. 13 Na litakuwa agano la ukuhani wa kudumu kwa ajili yake na uzao wake kisha yeye,+ kwa maana hakuvumilia ushindani wowote kumuelekea Mungu wake+ na alifunika zambi kwa ajili ya watu wa Israeli.’”
14 Kumbe, jina la mwanaume huyo wa Israeli mwenye aliuawa pamoja na mwanamuke Mumidiani lilikuwa Zimri mwana wa Salu, mukubwa wa jamaa ya upande wa baba ya Wasimeoni. 15 Jina la mwanamuke Mumidiani mwenye aliuawa lilikuwa Kozbi binti ya Suri;+ Suri alikuwa kiongozi wa ukoo mbalimbali wa jamaa ya upande wa baba kule Midiani.+
16 Kisha wakati Yehova akamuambia Musa: 17 “Mushambulie Wamidiani na muwapige na kuwaua,+ 18 kwa sababu wamekuwa wakiwasumbua kupitia njia zao za udanganyifu katika jambo la Peori+ na pia kuhusu Kozbi binti ya mukubwa wa Midiani, dada yao mwenye aliuawa+ ile siku ya pigo katika jambo la Peori.”+
26 Kisha pigo hilo,+ Yehova akamuambia Musa na Eleazari mwana wa Haruni kuhani: 2 “Muhesabie mukusanyiko wote wa Waisraeli kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi, kulingana na jamaa zao za upande wa baba, muhesabie wale wote wenye wanaweza kutumika katika jeshi katika Israeli.”+ 3 Kwa hiyo Musa na Eleazari+ kuhani wakasema na watu katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu+ karibu na Yordani kule Yeriko,+ na kuwaambia: 4 “Muwahesabie kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi, kama vile Yehova alimuamuru Musa.”+
Sasa wana wa Israeli wenye walitoka katika inchi ya Misri walikuwa: 5 Rubeni,+ muzaliwa wa kwanza wa Israeli; wana wa Rubeni+ walikuwa: kutoka kwa Hanoki, familia ya Wahanoki; kutoka kwa Palu, familia ya Wapalu; 6 kutoka kwa Hezroni, familia ya Wahezroni; kutoka kwa Karmi, familia ya Wakarmi. 7 Ni hizo zilikuwa familia za Warubeni, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi ine na tatu na mia saba makumi tatu (43 730).+
8 Mwana wa Palu alikuwa Eliabu. 9 Na wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Datani, na Abiramu. Huyu Datani na Abiramu walikuwa wenye kuchaguliwa wa mukusanyiko wenye walimupinga Musa+ na Haruni pamoja na kikundi cha Kora+ wakati walimupinga Yehova.+
10 Kisha dunia ikafunguka* na kuwameza. Kuhusu Kora, alikufa pamoja na watu wenye walimuunga mukono wakati moto uliteketeza watu mia mbili makumi tano (250).+ Na wakakuwa mufano wa kuonya.+ 11 Lakini, wana wa Kora hawakukufa.+
12 Wana wa Simeoni+ kulingana na familia zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, familia ya Wanemueli; kutoka kwa Yamini, familia ya Wayamini; kutoka kwa Yakini, familia ya Wayakini; 13 kutoka kwa Zera, familia ya Wazera; kutoka kwa Shauli, familia ya Washauli. 14 Ni hizo zilikuwa familia za Wasimeoni: elfu makumi mbili na mbili na mia mbili (22 200).+
15 Wana wa Gadi+ kulingana na familia zao walikuwa: kutoka kwa Sefoni, familia ya Wasefoni; kutoka kwa Hagi, familia ya Wahagi; kutoka kwa Shuni, familia ya Washuni; 16 kutoka kwa Ozni, familia ya Waozni; kutoka kwa Eri, familia ya Waeri; 17 kutoka kwa Arodi, familia ya Waarodi; kutoka kwa Areli, familia ya Waareli. 18 Ni hizo zilikuwa familia za wana wa Gadi, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi ine na mia tano (40 500).+
19 Wana wa Yuda+ walikuwa Eri na Onani.+ Lakini, Eri na Onani walikufa katika inchi ya Kanaani.+ 20 Na wana wa Yuda kulingana na familia zao walikuwa: kutoka kwa Shela,+ familia ya Washela; kutoka kwa Perezi,+ familia ya Waperezi; kutoka kwa Zera,+ familia ya Wazera. 21 Na wana wa Perezi walikuwa: kutoka kwa Hezroni,+ familia ya Wahezroni; kutoka kwa Hamuli,+ familia ya Wahamuli. 22 Ni hizo zilikuwa familia za Yuda, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi saba na sita na mia tano (76 500).+
23 Wana wa Isakari+ kulingana na familia zao walikuwa: kutoka kwa Tola,+ familia ya Watola; kutoka kwa Puva, familia ya Wapuni; 24 kutoka kwa Yashubu, familia ya Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, familia ya Washimroni. 25 Ni hizo zilikuwa familia za Isakari, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi sita na ine na mia tatu (64 300).+
26 Wana wa Zabuloni+ kulingana na familia zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, familia ya Waseredi; kutoka kwa Eloni, familia ya Waeloni; kutoka kwa Yahleeli, familia ya Wayahleeli. 27 Ni hizo zilikuwa familia za Wazabuloni, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi sita na mia tano (60 500).+
28 Wana wa Yosefu+ kulingana na familia zao walikuwa: Manase na Efraimu.+ 29 Wana wa Manase+ walikuwa: kutoka kwa Makiri,+ familia ya Wamakiri; na Makiri alikuwa baba ya Gileadi;+ kutoka kwa Gileadi, familia ya Wagileadi. 30 Hawa ndio walikuwa wana wa Gileadi: kutoka kwa Yezeri, familia ya Wayezeri; kutoka kwa Heleki, familia ya Waheleki; 31 kutoka kwa Asrieli, familia ya Waasrieli; kutoka kwa Shekemu, familia ya Washekemu; 32 kutoka kwa Shemida, familia ya Washemida; kutoka kwa Heferi, familia ya Waheferi. 33 Sasa Selofehadi mwana wa Heferi hakukuwa na watoto wanaume, alikuwa na watoto wanamuke tu,+ na majina ya watoto wanamuke wa Selofehadi+ yalikuwa Mala, Noa, Hogla, Milka, na Tirsa. 34 Ni hizo zilikuwa familia za Manase, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi tano na mbili na mia saba (52 700).+
35 Hawa ndio walikuwa wana wa Efraimu+ kulingana na familia zao: kutoka kwa Shutela,+ familia ya Washutela; kutoka kwa Bekeri, familia ya Wabekeri; kutoka kwa Tahani, familia ya Watahani. 36 Na hawa ndio walikuwa wana wa Shutela: kutoka kwa Erani, familia ya Waerani. 37 Ni hizo zilikuwa familia za wana wa Efraimu, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi tatu na mbili na mia tano (32 500).+ Hao ndio walikuwa wana wa Yosefu kulingana na familia zao.
38 Wana wa Benyamini+ kulingana na familia zao walikuwa: kutoka kwa Bela,+ familia ya Wabela; kutoka kwa Ashbeli, familia ya Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, familia ya Waahiramu; 39 kutoka kwa Shefufamu, familia ya Washufamu; kutoka kwa Hufamu, familia ya Wahufamu. 40 Wana wa Bela walikuwa Ardi na Naamani:+ kutoka kwa Ardi, familia ya Waardi; kutoka kwa Naamani, familia ya Wanaamani. 41 Hao ndio walikuwa wana wa Benyamini kulingana na familia zao, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi ine na tano na mia sita (45 600).+
42 Hawa ndio walikuwa wana wa Dani+ kulingana na familia zao: kutoka kwa Shuhamu, familia ya Washuhamu. Ni hizo zilikuwa familia za Dani kulingana na familia zao. 43 Familia zote za Washuhamu, za watu wenye waliandikishwa katika familia hizo, zilikuwa elfu makumi sita na ine na mia ine (64 400).+
44 Wana wa Asheri+ kulingana na familia zao walikuwa: kutoka kwa Imna, familia ya Waimna; kutoka kwa Ishvi, familia ya Waishvi; kutoka kwa Beria, familia ya Waberia; 45 kutoka kwa wana wa Beria: kutoka kwa Heberi, familia ya Waheberi; kutoka kwa Malkieli, familia ya Wamalkieli. 46 Jina la binti ya Asheri lilikuwa Sera. 47 Ni hizo zilikuwa familia za wana wa Asheri, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi tano na tatu na mia ine (53 400).+
48 Wana wa Naftali+ kulingana na familia zao walikuwa: kutoka kwa Yahzeeli, familia ya Wayahzeeli; kutoka kwa Guni, familia ya Waguni; 49 kutoka kwa Yezeri, familia ya Wayezeri; kutoka kwa Shilemu, familia ya Washilemu. 50 Ni hizo zilikuwa familia za Naftali kulingana na familia zao, na watu wenye waliandikishwa katika familia hizo walikuwa elfu makumi ine na tano na mia ine (45 400).+
51 Hii ndiyo hesabu ya wale wote wenye waliandikishwa kati ya Waisraeli: elfu mia sita na moja na mia saba makumi tatu (601 730).+
52 Kisha Yehova akamuambia Musa: 53 “Inchi itagawanywa kuwa uriti kati ya watu hao kulingana na oroza ya majina.*+ 54 Kwa ajili ya vikundi vikubwa, utaongeza uriti, na kwa ajili ya vikundi vidogo, utapunguza uriti.+ Kila kikundi kitapewa uriti kulingana na hesabu ya watu wenye waliandikishwa. 55 Lakini, inchi itagawanywa kwa kura.+ Watu watapokea uriti wao kulingana na majina ya makabila ya baba zao. 56 Kila uriti utaamuliwa kwa kura na kugawanywa kati ya vikundi vikubwa na vikundi vidogo.”
57 Sasa hawa ndio wenye waliandikishwa kati ya Walawi+ kulingana na familia zao: kutoka kwa Gershoni, familia ya Wagershoni; kutoka kwa Kohati,+ familia ya Wakohati; kutoka kwa Merari, familia ya Wamerari. 58 Ni hizi zilikuwa familia za Walawi: familia ya Walibni,+ familia ya Wahebroni,+ familia ya Wamali,+ familia ya Wamushi,+ familia ya Wakora.+
Kohati alikuwa baba ya Amramu.+ 59 Na jina la bibi ya Amramu lilikuwa Yokebedi,+ binti ya Lawi; mwenye bibi ya Lawi alimuzalia katika inchi ya Misri. Na alimuzalia Amramu: Haruni na Musa na Miriamu dada yao.+ 60 Kisha Haruni akamuzaa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Itamari.+ 61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa kwa sababu ya kutoa moto wenye hauruhusiwe mbele ya Yehova.+
62 Wale wote wenye waliandikishwa walikuwa elfu makumi mbili na tatu (23 000), wanaume wote kuanzia mwezi mumoja na zaidi.+ Kwa maana hawakuandikishwa kati ya Waisraeli,+ kwa sababu hawakupaswa kupewa uriti kati ya Waisraeli.+
63 Hao ndio waliandikishwa na Musa na Eleazari kuhani wakati waliandikisha Waisraeli katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu karibu na Yordani kule Yeriko. 64 Lakini hakuna hata mumoja kati yao mwenye alikuwa ameandikishwa na Musa na Haruni kuhani wakati walihesabia Waisraeli katika jangwa la Sinai.+ 65 Kwa maana Yehova alikuwa amesema kuwahusu: “Hakika watakufa katika jangwa.”+ Kwa hiyo hakuna mutu hata mumoja kati yao mwenye alibakia isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+
27 Kisha mabinti wa Selofehadi,+ mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, wa familia za Manase mwana wa Yosefu, wakakaribia. Majina ya mabinti hao yalikuwa Mala, Noa, Hogla, Milka, na Tirsa. 2 Wakasimama mbele ya Musa, mbele ya Eleazari kuhani, mbele ya wakubwa,+ na mbele ya mukusanyiko wote kwenye muingilio wa hema ya mukutano na wakasema: 3 “Baba yetu alikufa katika jangwa, lakini hakukuwa katika kikundi chenye kilijiunga pamoja ili kumupinga Yehova, watu wenye walimuunga Kora mukono,+ lakini alikufa kwa sababu ya zambi yake mwenyewe na hakukuwa na mutoto yeyote mwanaume. 4 Sababu gani jina la baba yetu lipotee katika familia yake kwa sababu hakukuwa na mutoto mwanaume? Utupatie uriti kati ya ndugu za baba yetu.” 5 Kwa hiyo Musa akapeleka jambo lao mbele ya Yehova.+
6 Kisha Yehova akamuambia Musa hivi: 7 “Mabinti wa Selofehadi wanasema kweli. Unapaswa kabisa kuwapatia uriti kati ya ndugu za baba yao na kupitisha uriti wa baba yao kwao.+ 8 Na uambie Waisraeli, ‘Kama mutu anakufa bila kuwa na mutoto mwanaume, basi mutapitisha uriti wake kwa mutoto wake mwanamuke. 9 Na kama hana mutoto mwanamuke, mutapatia ndugu zake uriti wake. 10 Na kama hana ndugu, mutapatia ndugu za baba yake uriti wake. 11 Na kama baba yake hana ndugu, mutapatia uriti wake mutu wa karibu mwenye iko* na uhusiano wa damu pamoja naye katika familia yake, naye ataukamata kuwa mali yake. Hii itakuwa sheria ya uamuzi wa hukumu kwa ajili ya Waisraeli, kama vile Yehova amemuamuru Musa.’”
12 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Panda katika mulima huu wa Abarimu,+ na uone inchi yenye nitapatia Waisraeli.+ 13 Kisha kuiona, utakusanywa pia kwa watu wako,*+ kama vile Haruni ndugu yako alikusanywa,+ 14 kwa sababu wakati mukusanyiko ulikuwa unagombana na mimi katika jangwa la Zini, muliasi agizo langu la kunitakasa mbele yao kupitia maji.+ Hayo ndiyo maji ya Meriba+ kule Kadeshi+ katika jangwa la Zini.”+
15 Kisha Musa akamuambia Yehova: 16 “Yehova, Mungu wa roho ya watu wote,* aweke juu ya mukusanyiko mwanaume 17 mwenye atatoka inje na kuingia ndani mbele yao na kuwatosha inje na kuwaingiza ndani, ili mukusanyiko wa Yehova usikuwe kama kondoo wenye hawana muchungaji.” 18 Kwa hiyo Yehova akamuambia Musa: “Chukua Yoshua mwana wa Nuni, mwanaume mwenye roho iko ndani yake, na utie mukono wako juu yake.+ 19 Kisha umusimamishe mbele ya kuhani Eleazari na mbele ya mukusanyiko wote, na umuweke katika madaraka mbele ya macho yao.+ 20 Utamupatia sehemu fulani ya mamlaka* yako,+ ili mukusanyiko wote wa Waisraeli umusikilize.+ 21 Atasimama mbele ya Eleazari kuhani, mwenye atauliza kwa ajili yake kulingana na hukumu ya Urimu+ mbele ya Yehova. Kwa agizo lake watu watatoka inje na kwa agizo lake wataingia ndani, yeye na Waisraeli wote wenye kuwa pamoja naye na mukusanyiko wote.”
22 Kwa hiyo Musa akafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru. Akamuchukua Yoshua na kumusimamisha mbele ya Eleazari kuhani na mbele ya mukusanyiko wote, 23 na akaweka mikono yake juu yake na kumuweka katika madaraka,+ kama vile Yehova alikuwa amesema kupitia Musa.+
28 Tena Yehova akamuambia Musa: 2 “Amuru Waisraeli na uwaambie, ‘Muhakikishe kwamba munanitolea toleo langu, mukate wangu. Matoleo yangu yenye yanatolewa kwangu kwa njia ya moto kuwa harufu ya kunipendeza* yanapaswa kutolewa kwa wakati wake wenye uliwekwa.’+
3 “Na uwaambie, ‘Hili ndilo toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto lenye mutamutolea Yehova: wana-kondoo dume wawili wa mwaka mumoja wenye hawana kasoro kuwa toleo la kawaida la kuteketezwa.+ 4 Utatoa mwana-kondoo dume mumoja asubui, na mwana-kondoo dume mwingine utamutoa mangaribi wakati giza linaanza,*+ 5 pamoja na sehemu moja ya kumi (1/10) ya efa* ya unga muzuri wenye kuchanganywa na sehemu moja ya ine (1/4) ya hini* ya mafuta ya zeituni zenye kupondwa-pondwa kuwa toleo la nafaka.+ 6 Ni toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida,+ lenye lilianzishwa kwenye Mulima Sinai kuwa harufu ya muzuri,* toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, 7 pamoja na toleo lake la kinywaji, sehemu moja ya ine (1/4) ya hini kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume.+ Umwange pombe katika mahali patakatifu kuwa toleo la kinywaji kwa ajili ya Yehova. 8 Na utatoa mwana-kondoo dume mwingine mangaribi wakati giza linaanza.* Pamoja na toleo la nafaka kama lile lenye lilitolewa asubui pamoja na toleo lilelile la kinywaji, utalitoa kuwa toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova.+
9 “‘Lakini, siku ya Sabato,+ toleo litakuwa la wana-kondoo dume wawili wa mwaka mumoja wenye hawana kasoro na sehemu mbili za kumi (2/10) za kipimo cha efa ya unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kuwa toleo la nafaka, pamoja na toleo lake la kinywaji. 10 Hilo ndilo toleo la kuteketezwa kwa ajili ya Sabato, pamoja na toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la kinywaji.+
11 “‘Kwenye mwanzo wa kila mwezi* mutamutolea Yehova toleo la kuteketezwa la ngombe-dume wawili wadogo, kondoo-dume mumoja, na wana-kondoo dume saba (7) wenye hawana kasoro kila mumoja wa mwaka mumoja,+ 12 na sehemu tatu za kumi (3/10) za unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kuwa toleo la nafaka+ kwa ajili ya kila ngombe-dume na sehemu mbili za kumi (2/10) za unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kuwa toleo la nafaka kwa ajili ya kondoo-dume mumoja,+ 13 na sehemu moja ya kumi (1/10) ya unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta kuwa toleo la nafaka kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume, kuwa toleo la kuteketezwa, harufu ya muzuri,*+ toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto. 14 Na matoleo ya kinywaji ya matoleo hayo yanapaswa kuwa nusu ya hini ya divai kwa ajili ya ngombe-dume+ na sehemu moja ya tatu (1/3) ya hini kwa ajili ya kondoo-dume+ na sehemu moja ya ine (1/4) ya hini kwa ajili ya mwana-kondoo dume.+ Hilo ndilo toleo la kuteketezwa lenye linapaswa kutolewa kila mwezi kwa mwaka muzima. 15 Pia, mwana-mbuzi mumoja atatolewa kwa Yehova kuwa toleo la zambi zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida pamoja na toleo lake la kinywaji.
16 “Katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na ine (14) ya mwezi huo, itakuwa Pasaka ya Yehova.+ 17 Na siku ya kumi na tano (15) ya mwezi huo, kutakuwa sikukuu. Mikate yenye haina chachu itakuliwa kwa siku saba (7).+ 18 Katika siku ya kwanza kutakuwa mukusanyiko mutakatifu. Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu. 19 Na mutamutolea Yehova toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa njia ya moto la ngombe-dume wawili wadogo, kondoo-dume mumoja, na wana-kondoo dume saba (7) kila mumoja wa mwaka mumoja. Munapaswa kutoa wanyama wenye hawana kasoro.+ 20 Munapaswa kuwatoa pamoja na matoleo yao ya nafaka ya unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta;+ sehemu tatu za kumi (3/10) kwa ajili ya ngombe-dume na sehemu mbili za kumi (2/10) kwa ajili ya kondoo-dume mumoja. 21 Mutatoa sehemu moja ya kumi (1/10) kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo dume saba (7), 22 na pia mbuzi mumoja kuwa toleo la zambi ili kufunika zambi kwa ajili yenu. 23 Zaidi ya toleo la kuteketezwa la asubui, lenye kuwa kwa ajili ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida, mutatoa vitu hivyo. 24 Mutatoa vitu hivyo kama chakula* kwa njia ileile kila siku kwa siku saba (7), toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova. Linapaswa kutolewa pamoja na toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la kinywaji. 25 Siku ya saba (7) mutakuwa na mukusanyiko mutakatifu.+ Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu.+
26 “‘Siku ya matunda ya kwanza yenye kukomaa,+ wakati munamutolea Yehova toleo la nafaka mupya,+ mutafanya mukusanyiko mutakatifu katika sikukuu yenu ya majuma.+ Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu.+ 27 Mutatoa kuwa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya harufu ya kumupendeza* Yehova: ngombe-dume wawili wadogo, kondoo-dume mumoja, na wana-kondoo dume saba (7) kila mumoja wa mwaka mumoja,+ 28 na toleo lao la nafaka la unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi (3/10) kwa ajili ya kila ngombe-dume, na sehemu mbili za kumi (2/10) kwa ajili ya ule kondoo-dume mumoja, 29 sehemu moja ya kumi (1/10) kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo dume saba (7), 30 na pia mwana-mbuzi mumoja ili kufunika zambi kwa ajili yenu.+ 31 Mutatoa vitu hivyo zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la nafaka. Watakuwa wanyama wenye hawana kasoro,+ pamoja na matoleo yao ya kinywaji.
29 “‘Na katika mwezi wa saba (7), siku ya kwanza ya mwezi huo, mutakuwa na mukusanyiko mutakatifu. Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu.+ Mutapiga tarumbeta siku hiyo.+ 2 Mutatoa kuwa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya harufu ya kumupendeza* Yehova: ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na wana-kondoo dume saba (7) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro, 3 na toleo lao la nafaka la unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta; sehemu tatu za kumi (3/10) kwa ajili ya ngombe-dume, sehemu mbili za kumi (2/10) kwa ajili ya kondoo-dume, 4 na sehemu moja ya kumi (1/10) kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo dume saba (7), 5 na mwana-mbuzi dume mumoja kuwa toleo la zambi ili kufunika zambi kwa ajili yenu. 6 Vitu hivyo vinaongezwa kwenye toleo la kuteketezwa la kila mwezi na toleo lake la nafaka+ na toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la nafaka,+ pamoja na matoleo yake ya kinywaji,+ kulingana na utaratibu wa kawaida wa matoleo hayo, ili kuwa harufu ya muzuri,* toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.
7 “‘Na siku ya kumi (10) ya mwezi huo wa saba (7), mutakuwa na mukusanyiko mutakatifu,+ na munapaswa kujitesa.* Hamupaswe kufanya kazi yoyote. + 8 Na mutatoa kuwa toleo la kuteketezwa kwa Yehova, kuwa harufu ya muzuri:* ngombe-dume mumoja mudogo, kondoo-dume mumoja, na wana-kondoo dume saba (7) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro.+ 9 Na kwa ajili ya toleo lao la nafaka la unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta: sehemu tatu za kumi (3/10) kwa ajili ya ngombe-dume, sehemu mbili za kumi (2/10) kwa ajili ya kondoo-dume mumoja, 10 sehemu moja ya kumi (1/10) kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo dume saba (7), 11 na pia mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, zaidi ya toleo la zambi la kufunika zambi+ na toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la nafaka, pamoja na matoleo ya kinywaji ya matoleo hayo.
12 “‘Na siku ya kumi na tano (15) ya mwezi wa saba (7), mutakuwa na mukusanyiko mutakatifu. Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu, na munapaswa kumufanyia Yehova sikukuu kwa siku saba.+ 13 Na mutatoa toleo la kuteketezwa,+ toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova: ngombe-dume wadogo kumi na tatu (13), kondoo-dume wawili, na wana-kondoo dume kumi na ine (14) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro.+ 14 Na kwa ajili ya toleo lao la nafaka la unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta: sehemu tatu za kumi (3/10) kwa ajili ya kila ngombe-dume kati ya wale ngombe-dume kumi na tatu (13), sehemu mbili za kumi (2/10) kwa ajili ya kila kondoo-dume kati ya wale kondoo-dume wawili, 15 na sehemu moja ya kumi (1/10) kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo dume kumi na ine (14), 16 na pia mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida, toleo lake la nafaka, na toleo lake la kinywaji.+
17 “‘Na siku ya pili, ngombe-dume wadogo kumi na mbili (12), kondoo-dume wawili, na wana-kondoo dume kumi na ine (14) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro,+ 18 na toleo lao la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya ngombe-dume, kondoo-dume, na wana-kondoo dume kufuatana na hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida, 19 na pia mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la nafaka pamoja na matoleo ya kinywaji ya matoleo hayo.+
20 “‘Na siku ya tatu (3), ngombe-dume kumi na moja (11), kondoo-dume wawili, na wana-kondoo dume kumi na ine (14) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro,+ 21 na toleo lao la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya ngombe-dume, kondoo-dume, na wana-kondoo dume kufuatana na hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida, 22 na pia mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
23 “‘Na siku ya ine (4), ngombe-dume kumi (10), kondoo-dume wawili, na wana-kondoo dume kumi na ine (14) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro,+ 24 na toleo lao la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya ngombe-dume hao, kondoo-dume, na wana-kondoo dume kufuatana na hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida, 25 na pia mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida, toleo lake la nafaka, na toleo lake la kinywaji.+
26 “‘Na siku ya tano (5), ngombe-dume kenda (9), kondoo-dume wawili, na wana-kondoo dume kumi na ine (14) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro,+ 27 na toleo lao la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya ngombe-dume, kondoo-dume, na wana-kondoo dume kufuatana na hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida, 28 na pia mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
29 “‘Na siku ya sita (6), ngombe-dume munane (8), kondoo-dume wawili, na wana-kondoo dume kumi na ine (14) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro,+ 30 na toleo lao la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya ngombe-dume hao, kondoo-dume, na wana-kondoo dume kufuatana na hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida, 31 na pia mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida, na toleo lake la nafaka, na matoleo yake ya kinywaji.+
32 “‘Na siku ya saba (7), ngombe-dume saba, kondoo-dume wawili, na wana-kondoo dume kumi na ine (14) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro,+ 33 na toleo lao la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya ngombe-dume hao, kondoo-dume, na wana-kondoo dume kufuatana na hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida, 34 na pia mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida, toleo lake la nafaka, na toleo lake la kinywaji.+
35 “‘Siku ya munane (8), mutakuwa na mukusanyiko mukubwa. Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu.+ 36 Mutatoa kuwa toleo la kuteketezwa, toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova: ngombe-dume mumoja, kondoo-dume mumoja, na wana-kondoo dume saba (7) kila mumoja wa mwaka mumoja, wanyama wote hao hawapaswe kuwa na kasoro,+ 37 na toleo lao la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya ngombe-dume, kondoo-dume, na wana-kondoo dume kufuatana na hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida, 38 na pia mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi, zaidi ya toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
39 “‘Mutamutolea Yehova matoleo hayo wakati wa sikukuu zenu za vipindi,+ zaidi ya matoleo yenu ya naziri+ na matoleo yenu ya kujipendea+ ili kuwa matoleo yenu ya kuteketezwa+ na matoleo yenu ya nafaka+ na matoleo yenu ya kinywaji+ na zabihu zenu za ushirika.’”+ 40 Musa akaambia Waisraeli mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru.
30 Kisha Musa akasema na vichwa+ vya makabila ya Israeli, na kuwaambia: “Hili ndilo neno lenye Yehova ameamuru: 2 Kama mwanaume anafanya naziri+ kwa Yehova ao anaapa kiapo+ cha kujifunga naziri ya kujiepusha na kitu fulani,* hapaswe kuvunja neno lake.+ Anapaswa kufanya kila jambo lenye aliapa kufanya.+
3 “Na kama mwanamuke anafanya naziri kwa Yehova ao anajifunga naziri ya kujiepusha na kitu fulani wakati angali kijana na anaishi katika nyumba ya baba yake 4 na baba yake akisikia naziri yake ao naziri ya kujiepusha na kitu fulani yenye amejifunga* na baba yake hapinge jambo hilo, naziri zake zote zitaendelea, na kila naziri ya kujiepusha na kitu fulani yenye amejifunga itaendelea. 5 Lakini kama baba yake anamukataza wakati anasikia kwamba amejifunga naziri ao naziri za kujiepusha na kitu fulani, naziri hiyo haitaendelea. Yehova atamusamehe kwa sababu baba yake alimukataza.+
6 “Lakini, kama anaolewa na bwana wakati iko* chini ya naziri yake ao ahadi yenye amejifunga bila kufikiri 7 na bwana yake akisikia juu ya naziri hiyo na hapinge jambo hilo siku yenye anasikia juu ya naziri hiyo, naziri zake ao naziri za kujiepusha na kitu fulani zenye amejifunga zitaendelea. 8 Lakini kama bwana yake anamukataza siku yenye anasikia juu ya naziri hiyo, bwana huyo anaweza kuvunja naziri hiyo ao ahadi yenye mwanamuke huyo alijifunga bila kufikiri,+ na Yehova atamusamehe mwanamuke huyo.
9 “Lakini kama mujane ao mwanamuke mwenye ndoa yake ilivunjika anafanya naziri, kila jambo lenye amejifunga litabakia lenye kufungwa juu yake.
10 “Lakini, kama mwanamuke alijifunga naziri ao naziri ya kujiepusha na kitu fulani wakati alikuwa katika nyumba ya bwana yake 11 na bwana yake alisikia naziri yake na hakupinga jambo hilo ao kulikataa, naziri zake zote ao naziri yoyote ya kujiepusha na kitu fulani yenye alijifunga itaendelea. 12 Lakini kama bwana yake alivunja kabisa naziri zozote ao naziri yoyote ya kujiepusha na kitu fulani yenye mwanamuke huyo aliapa katika siku yenye alizisikia, naziri hizo hazitaendelea.+ Bwana yake alizivunja, na Yehova atamusamehe mwanamuke huyo. 13 Kuhusu naziri yoyote ao kiapo chochote chenye kutia ndani naziri ya kujiima kitu fulani,* bwana yake anapaswa kuikubali ao bwana yake anapaswa kuivunja. 14 Lakini kama bwana yake hamupinge siku kwa siku, basi amekubali naziri zote ao naziri zote za kujiepusha na kitu fulani zenye kuwa juu ya mwanamuke huyo. Anazikubali kwa sababu hakupinga siku yenye alimusikia anafanya naziri hizo. 15 Lakini kama bwana yake anazivunja kisha pale, wakati fulani kisha siku yenye alizisikia, atapata matokeo ya hatia ya mwanamuke huyo.+
16 “Hayo ndiyo masharti yenye Yehova alimuamuru Musa kuhusu bwana na bibi yake, na kuhusu baba na binti yake mudogo mwenye kuishi katika nyumba ya baba yake.”
31 Kisha Yehova akamuambia Musa: 2 “Lipiza kisasi+ juu ya Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli.+ Kisha utakusanywa kwa watu wako.”*+
3 Kwa hiyo Musa akasema na watu, na kuwaambia: “Mutayarishe wanaume wenye kuwa kati yenu ili wapigane na Midiani na kulipiza kisasi cha Yehova juu ya Midiani. 4 Mutatuma katika jeshi wanaume elfu moja (1 000) kutoka katika kila kabila kati ya makabila yote ya Israeli.” 5 Kwa hiyo kutoka kati ya maelfu ya Israeli,+ wanaume elfu moja (1 000) walichaguliwa katika kila kabila, wanaume elfu kumi na mbili (12 000) walitayarishwa kwa ajili ya vita.*
6 Kisha Musa akawatuma kwenye jeshi, wanaume elfu moja (1 000) wa kila kabila, pamoja na Finehasi+ mwana wa Eleazari kuhani kwa ajili ya jeshi, mwenye alikuwa na vyombo vitakatifu na tarumbeta za kutoa tangazo+ katika mukono wake. 7 Wakapigana na Midiani, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa, na wakaua wanaume wote. 8 Kati ya watu wenye waliuawa, kulikuwa wafalme tano (5) wa Midiani, ni kusema, Evi, Rekemu, Suri, Huru, na Reba. Pia walimuua Balaamu+ mwana wa Beori kwa upanga. 9 Lakini Waisraeli walibeba wanamuke na watoto wa Midiani wakiwa wametekwa. Pia walinyanganya mifugo yao yote, wanyama wao wote, na vitu vyao vyote. 10 Na waliteketeza kwa moto miji yote yenye Wamidiani waliishi ndani na kambi zao zote.* 11 Na walikamata vitu vyote vyenye vinachukuliwa katika vita na vitu vyote vyenye vinanyanganywa katika vita, watu na wanyama. 12 Kisha wakaleta watu wenye walikamatwa mateka, vitu vyenye vinanyanganywa katika vita, na vitu vyenye vinachukuliwa katika vita mbele ya Musa na Eleazari kuhani na mukusanyiko wote wa Waisraeli, kwenye kambi katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu+ karibu na Yordani kule Yeriko.
13 Kisha Musa na Eleazari kuhani na wakubwa wote wa mukusanyiko wakatoka ili kukutana nao inje ya kambi. 14 Lakini Musa akakasirika sana kwa sababu ya wanaume wenye waliwekwa ili kusimamia jeshi, wakubwa wa maelfu na wakubwa wa mamia wenye walikuwa wanarudia kutoka kwenye vita. 15 Musa akawaambia: “Hamukuua wanamuke wote? 16 Muangalie! Wao ndio kupitia neno la Balaamu walishawishi Waisraeli wakose uaminifu+ kwa Yehova katika jambo la Peori,+ na hivyo pigo likakuja juu ya mukusanyiko wa Yehova.+ 17 Sasa muue kila mutoto mwanaume kati ya watoto na kila mwanamuke mwenye amekwisha kufanya ngono na mwanaume. 18 Lakini musiue vijana wanamuke wote wenye hawajafanya ngono na mwanaume.+ 19 Na munapaswa kupiga kambi inje ya kambi kwa siku saba (7). Kila mumoja kati yenu mwenye ameua mutu* na kila mumoja kati yenu mwenye amegusa mutu mwenye aliuawa+ anapaswa kujitakasa+ siku ya tatu (3) na siku ya saba, ninyi na watu wenu wenye walikamatwa mateka. 20 Na munapaswa kutakasa kutokana na zambi kila nguo, kila kitu cha ngozi, kila kitu chenye kilitengenezwa na manyoya ya mbuzi, na kila kitu cha mbao.”
21 Kisha Eleazari kuhani akaambia wanaume wa jeshi wenye walikuwa wameenda katika vita: “Hii ndiyo amri ya sheria yenye Yehova amemuamuru Musa, 22 ‘Ni zahabu, feza, shaba, chuma, bati, na risasi tu, 23 kila kitu chenye hakiwezi kuungua katika moto, mutakipitisha katika moto, na kitakuwa safi. Lakini, kinapaswa pia kusafishwa kwa maji ya kutakasa.+ Kila kitu chenye kinaweza kuungua katika moto, mutakipitisha ndani ya maji. 24 Na munapaswa kufua nguo zenu siku ya saba (7) na kuwa safi, na kisha munaweza kuingia katika kambi.’”+
25 Kisha Yehova akamuambia Musa hivi: 26 “Hesabia vitu vyenye vinanyanganywa katika vita, hesabia watu na wanyama wenye walikamatwa mateka; ufanye vile pamoja na Eleazari kuhani na vichwa vya jamaa za upande wa baba za mukusanyiko. 27 Ugawe vitu vyenye vinanyanganywa katika sehemu mbili ili maaskari wenye walienda katika vita wapate sehemu moja na watu wengine wote wa mukusanyiko sehemu ingine.+ 28 Na kwa ajili ya kodi ya Yehova, mutachukua kati ya maaskari wenye walienda katika vita nafsi* moja kati ya kila nafsi mia tano (500), za wanadamu, za mifugo, za punda, na za kundi. 29 Mutachukua nafsi hiyo katika nusu yao na kuipatia Eleazari kuhani kuwa muchango wa Yehova.+ 30 Katika nusu yenye Waisraeli walipewa, utachukua nafsi moja kati ya nafsi makumi tano (50), za wanadamu, za mifugo, za punda, za kundi, na kila namna ya munyama wa kufugwa, na kuwapatia Walawi,+ wenye wanafanya kazi zenye zinahusiana na tabenakulo ya Yehova.”+
31 Kwa hiyo Musa na Eleazari kuhani wakafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa. 32 Vitu vyenye vinachukuliwa katika vita, vitu vyenye vilibakia vyenye watu wenye walienda katika vita walikuwa wamenyanganya, vilikuwa wanyama elfu mia sita makumi saba na tano (675 000) wa kundi, 33 wanyama elfu makumi saba na mbili (72 000) wa mifugo, 34 na punda elfu makumi sita na moja (61 000). 35 Wanamuke wenye walikuwa hawajafanya ngono na mwanaume+ walikuwa wanamuke* elfu makumi tatu na mbili (32 000). 36 Na nusu yenye ilikuwa fungu la wale wenye walienda katika vita ilikuwa wanyama elfu mia tatu makumi tatu na saba na mia tano (337 500) wa kundi. 37 Kodi kwa ajili ya Yehova yenye ilitoka katika kundi ilikuwa mia sita makumi saba na tano (675). 38 Na kulikuwa wanyama elfu makumi tatu na sita (36 000) wa mifugo, na kodi juu yao kwa ajili ya Yehova ilikuwa makumi saba na mbili (72). 39 Na kulikuwa punda elfu makumi tatu na mia tano (30 500), na kodi juu yao kwa ajili ya Yehova ilikuwa makumi sita na moja (61). 40 Na kulikuwa wanadamu* elfu kumi na sita (16 000), na kodi juu yao kwa ajili ya Yehova ilikuwa watu* makumi tatu na mbili (32). 41 Kisha Musa akamupatia Eleazari kuhani kodi hiyo kuwa muchango wa Yehova,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
42 Katika ile nusu ya Waisraeli, yenye Musa alikuwa ametenga na sehemu ya wanaume wenye walipigana vita, 43 ile nusu ya wanyama wa kundi ilikuwa elfu mia tatu makumi tatu na saba na mia tano (337 500), 44 na ya mifugo, wanyama elfu makumi tatu na sita (36 000), 45 na ya punda, elfu makumi tatu na mia tano (30 500), 46 na ya watu,* elfu kumi na sita (16 000). 47 Kisha Musa akachukua katika nusu hiyo ya Waisraeli nafsi moja kati ya nafsi makumi tano (50), za wanadamu na za wanyama, na akazipatia Walawi,+ wenye walifanya kazi ya tabenakulo ya Yehova,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
48 Kisha wanaume wenye waliwekwa ili kusimamia maelfu ya jeshi,+ wakubwa wa maelfu na wakubwa wa mamia, wakamuendea Musa, 49 na wakamuambia Musa: “Watumishi wako wamehesabia wanaume wa vita wenye kuwa chini ya usimamizi wetu, na hakuna hata mumoja kati yetu mwenye amekosekana.+ 50 Kwa hiyo ruhusu kila mumoja wetu atoe vitu vyenye alipata ili vikuwe toleo la Yehova, vitu vya zahabu, minyororo myembamba ya kifundo cha muguu, vikomo, pete za kutia muhuri, mahereni ya masikio, na vitu vingine vya kujipamba, ili kufunika zambi kwa ajili yetu* mbele ya Yehova.”
51 Kwa hiyo Musa na Eleazari kuhani wakapokea zahabu hiyo kutoka kwao, vitu vyote vya kujipamba. 52 Zahabu yote ya muchango wenye walimutolea Yehova ilikuwa shekeli* elfu kumi na sita na mia saba makumi tano (16 750), kutoka kwa wakubwa wa maelfu na wakubwa wa mamia. 53 Maaskari walikuwa wamejikamatia kila mumoja vitu vyenye vinanyanganywa katika vita. 54 Musa na Eleazari kuhani walipokea zahabu hiyo kutoka kwa wakubwa wa maelfu na wakubwa wa mamia na waliileta katika hema ya mukutano ili ikuwe kikumbusho* mbele ya Yehova kwa ajili ya watu wa Israeli.
32 Sasa wana wa Rubeni+ na wana wa Gadi+ walikuwa na mifugo mingi sana, na wakaona kwamba inchi ya Yazeri+ na inchi ya Gileadi ilikuwa eneo la muzuri kwa ajili ya mifugo. 2 Kwa hiyo wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakamuendea Musa, Eleazari kuhani, na wakubwa wa mukusanyiko na kusema: 3 “Ataroti, Diboni, Yazeri, Nimra, Heshboni,+ Eleale, Sebamu, Nebo,+ na Beoni,+ 4 inchi yenye Yehova alishinda mbele ya mukusanyiko wa Israeli,+ ni inchi ya muzuri kwa ajili ya mifugo, na watumishi wako wana mifugo mingi.”+ 5 Wakaendelea kusema, “Kama tumekubaliwa mbele ya macho yako, acha inchi hiyo ipewe watumishi wako kuwa uriti. Usituvukishe ngambo ya Yordani.”
6 Kisha Musa akaambia wana wa Gadi na wana wa Rubeni: “Je, itaomba ndugu zenu waende katika vita wakati ninyi munaendelea kukaa hapa? 7 Sababu gani munavunja moyo watu wa Israeli ili wasivuke kuingia katika inchi yenye hakika Yehova atawapatia? 8 Ni vile baba zenu walifanya wakati niliwatuma kutoka Kadesh-barnea ili waone inchi hiyo.+ 9 Wakati walipanda mupaka kwenye Bonde* la Eshkoli+ na kuona inchi hiyo, walivunja moyo watu wa Israeli ili wasiingie katika inchi yenye Yehova angewapatia.+ 10 Kasirani ya Yehova iliwaka siku hiyo na hivyo akaapa:+ 11 ‘Wanaume wenye walitoka Misri kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi hawataona inchi+ yenye nilimuapia Abrahamu, Isaka, na Yakobo,+ kwa sababu hawakunifuata kwa moyo wote— 12 isipokuwa Kalebu+ mwana wa Yefune, Mukenizi, na Yoshua+ mwana wa Nuni, kwa sababu wamemufuata Yehova kwa moyo wote.’+ 13 Kwa hiyo kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Israeli na akawafanya watange-tange katika jangwa kwa miaka makumi ine (40),+ mupaka wakati kizazi chote chenye kilikuwa kinafanya uovu mbele ya macho ya Yehova kilifikia mwisho wake.+ 14 Na sasa ninyi mumesimama mahali pa baba zenu mukiwa kundi la watenda-zambi wenye wanaongeza kasirani yenye kuwaka ya Yehova juu ya Israeli. 15 Kama munageuka na kuacha kumufuata, hakika atawaacha tena katika jangwa, na mutaleta uharibifu juu ya watu hawa wote.”
16 Kisha wakati fulani wakamuendea tena na kusema: “Uturuhusu tujenge hapa mazizi* ya majiwe kwa ajili ya mifugo yetu na miji kwa ajili ya watoto wetu. 17 Lakini sisi tutaendelea kuwa tayari kwa ajili ya vita+ na tutaenda mbele ya Waisraeli mupaka wakati tutakuwa tumewafikisha mahali pao, wakati huo watoto wetu watakaa katika miji yenye ngome, wakiwa salama kutokana na wakaaji wa inchi. 18 Hatutarudia katika nyumba zetu mupaka wakati kila Mwisraeli atakuwa amepokea eneo lake kuwa uriti.+ 19 Kwa maana hatutapokea uriti pamoja nao ngambo ingine ya Yordani na kuendelea, kwa sababu tumepokea uriti wetu upande wa mashariki wa Yordani.”+
20 Musa akawajibu: “Kama mutafanya hivi: Kama mutakamata silaha mbele ya Yehova kwa ajili ya vita;+ 21 na kama kila mumoja wenu atakamata silaha na kuvuka Yordani mbele ya Yehova wakati anafukuza maadui wake kutoka mbele yake+ 22 mupaka wakati inchi itatiishwa mbele ya Yehova,+ kisha munaweza kurudia+ na hamutakuwa na hatia mbele ya Yehova na Israeli. Basi inchi hiyo itakuwa uriti wenu mbele ya Yehova.+ 23 Lakini kama hamufanye vile, mutakuwa mumemutendea Yehova zambi. Katika hali hiyo, mujue kwamba zambi yenu itawapata. 24 Kwa hiyo munaweza kujenga miji kwa ajili ya watoto wenu na mazizi* kwa ajili ya makundi yenu,+ lakini munapaswa kufanya mambo yenye mumeahidi.”
25 Wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakamuambia Musa hivi: “Watumishi wako watafanya kama vile bwana wangu anaamuru. 26 Watoto wetu, bibi zetu, mifugo yetu, wanyama wetu wote wa kufugwa watabakia pale katika miji ya Gileadi,+ 27 lakini watumishi wako watavuka, kila mwanaume mwenye kubeba silaha ili kupigana vita mbele ya Yehova,+ kama vile bwana wangu anasema.”
28 Kwa hiyo Musa akatoa amri juu yao kwa Eleazari kuhani, Yoshua mwana wa Nuni, na vichwa vya jamaa za upande wa baba za makabila ya Israeli. 29 Musa akawaambia: “Kama wana wa Gadi na wana wa Rubeni wanavuka Yordani pamoja na ninyi, kila mwanaume mwenye kubeba silaha ili kupigana vita mbele ya Yehova, na kama inchi inatiishwa mbele yenu, basi mutawapatia inchi ya Gileadi kuwa uriti.+ 30 Lakini kama hawakamate silaha na kuvuka pamoja na ninyi, basi wataishi kati yenu katika inchi ya Kanaani.”
31 Basi wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakajibu: “Watumishi wako watafanya mambo yenye Yehova amewaambia. 32 Tutakamata silaha na kuvuka kuingia inchi ya Kanaani mbele ya Yehova,+ lakini uriti wetu utakuwa ngambo hii ya Yordani.” 33 Kwa hiyo Musa akawapatia—wana wa Gadi, wana wa Rubeni,+ na nusu ya kabila la Manase+ mwana wa Yosefu—ufalme wa Sihoni+ mufalme wa Waamori na ufalme wa Ogu+ mufalme wa Bashani, inchi ya miji yake katika maeneo hayo, na miji ya inchi yenye kuizunguka.
34 Na wana wa Gadi wakajenga* Diboni,+ Ataroti,+ Aroeri,+ 35 Atrot-shofani, Yazeri,+ Yogbeha,+ 36 Bet-nimra,+ Bet-harani,+ miji yenye ngome, na wakajenga mazizi* ya majiwe kwa ajili ya makundi. 37 Na wana wa Rubeni wakajenga Heshboni,+ Eleale,+ Kiriataimu,+ 38 Nebo,+ na Baal-meoni+—majina ya miji hiyo yalibadilishwa—na Sibma; na wakaanza kupatia miji yenye walijenga upya majina ya mupya.
39 Wana wa Makiri+ mwana wa Manase walishambulia inchi ya Gileadi na wakaikamata na kufukuza Waamori wenye walikuwa katika inchi hiyo. 40 Kwa hiyo Musa akamupatia Makiri mwana wa Manase inchi ya Gileadi, na akaanza kukaa katika inchi hiyo.+ 41 Na Yairi mwana wa Manase akawashambulia na akakamata vijiji vyao vya mahema, na akaanza kuviita Hawot-yairi.*+ 42 Na Noba akashambulia na kukamata muji wa Kenati na miji yake ya pembeni-pembeni,* na akaanza kuuita Noba, jina lake mwenyewe.
33 Ni hizi zilikuwa hatua za safari ya watu wa Israeli wakati walitoka katika inchi ya Misri+ kulingana na vikundi vyao vya maaskari*+ wakiongozwa na Musa na Haruni.+ 2 Musa aliendelea kuandika mahali walikuwa wanaondoka kulingana na hatua za safari yao kama vile Yehova aliagiza, na ni hizi zilikuwa hatua za safari yao kuanzia mahali waliondoka mupaka mahali pengine:+ 3 Waliondoka Ramesesi+ katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano (15) ya mwezi huo.+ Siku hiyohiyo kisha Pasaka,+ Waisraeli waliondoka kwa uhodari* mbele ya macho ya Wamisri wote. 4 Wakati huo, Wamisri walikuwa wanazika wazaliwa wao wote wa kwanza wenye Yehova alikuwa amepiga na kuua kati yao,+ kwa kuwa Yehova alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.+
5 Kwa hiyo Waisraeli wakaondoka Ramesesi na kupiga kambi Sukoti.+ 6 Kisha wakaondoka Sukoti na kupiga kambi Etamu,+ yenye kuwa kwenye mwisho-mwisho wa jangwa. 7 Halafu wakaondoka Etamu na wakageuka na kurudia nyuma kuelekea Pihahiroti, yenye kuangaliana na Baal-sefoni,+ na wakapiga kambi mbele ya Migdoli.+ 8 Kisha wakaondoka Pihahiroti na kupita katikati ya bahari+ mupaka jangwa+ na wakaendelea kusafiri kwa siku tatu (3) katika jangwa la Etamu+ na kupiga kambi kule Mara.+
9 Kisha wakaondoka Mara na kufika Elimu. Sasa kule Elimu kulikuwa chemchemi kumi na mbili (12) za maji na miti ya mitende makumi saba (70), kwa hiyo wakapiga kambi pale.+ 10 Halafu wakaondoka Elimu na kupiga kambi karibu na Bahari Nyekundu. 11 Kisha wakaondoka kwenye Bahari Nyekundu na kupiga kambi katika jangwa la Sini.+ 12 Halafu wakaondoka katika jangwa la Sini na kupiga kambi Dofka. 13 Kisha wakati fulani wakaondoka Dofka na kupiga kambi Alushi. 14 Kisha wakaondoka Alushi na kupiga kambi Refidimu,+ kwenye hakukuwa maji ya kunywa kwa ajili ya watu. 15 Halafu wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika jangwa la Sinai.+
16 Wakaondoka katika jangwa la Sinai na kupiga kambi Kibrot-hataava.+ 17 Kisha wakaondoka Kibrot-hataava na kupiga kambi Haseroti.+ 18 Kisha pale wakaondoka Haseroti na kupiga kambi Ritma. 19 Kisha wakaondoka Ritma na kupiga kambi Rimon-peresi. 20 Halafu wakaondoka Rimon-peresi na kupiga kambi Libna. 21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi Risa. 22 Kisha wakaondoka Risa na kupiga kambi Kehelata. 23 Halafu wakaondoka Kehelata na kupiga kambi kwenye Mulima Sheferi.
24 Kisha wakaondoka kwenye Mulima Sheferi na kupiga kambi Harada. 25 Halafu wakaondoka Harada na kupiga kambi Makeloti. 26 Kisha wakaondoka+ Makeloti na kupiga kambi Tahati. 27 Halafu wakaondoka Tahati na kupiga kambi Tera. 28 Kisha wakaondoka Tera na kupiga kambi Mitka. 29 Kisha wakati fulani wakaondoka Mitka na kupiga kambi Hashmona. 30 Kisha wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moseroti. 31 Halafu wakaondoka Moseroti na kupiga kambi Bene-yaakani.+ 32 Na wakaondoka Bene-yaakani na kupiga kambi Hor-hagidgadi. 33 Halafu wakaondoka Hor-hagidgadi na kupiga kambi Yotbata.+ 34 Kisha wakati fulani wakaondoka Yotbata na kupiga kambi Abrona. 35 Halafu wakaondoka Abrona na kupiga kambi Esion-geberi.+ 36 Kisha wakaondoka Esion-geberi na kupiga kambi katika jangwa la Zini,+ ni kusema, Kadeshi.
37 Kisha wakati fulani wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mulima Hori,+ kwenye mupaka wa inchi ya Edomu. 38 Na Haruni kuhani akapanda juu ya Mulima Hori kwa agizo la Yehova na akakufia kule katika mwaka wa makumi ine (40) kisha Waisraeli kutoka katika inchi ya Misri, katika mwezi wa tano (5), siku ya kwanza ya mwezi huo.+ 39 Haruni alikuwa na miaka mia moja makumi mbili na tatu (123) wakati alikufa juu ya Mulima Hori.
40 Sasa mufalme wa Aradi,+ Mukanaani mwenye alikuwa anaishi Negebu katika inchi ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Kisha wakati fulani wakaondoka kwenye Mulima Hori+ na kupiga kambi Salmona. 42 Halafu wakaondoka Salmona na kupiga kambi Punoni. 43 Kisha wakaondoka Punoni na kupiga kambi Oboti.+ 44 Halafu wakaondoka Oboti na kupiga kambi Iye-abarimu, kwenye mupaka wa Moabu.+ 45 Kisha wakati fulani wakaondoka Iyimu na kupiga kambi Dibon-gadi.+ 46 Halafu wakaondoka Dibon-gadi na kupiga kambi Almon-diblataimu. 47 Kisha wakaondoka Almon-diblataimu na kupiga kambi kwenye milima ya Abarimu+ mbele ya Nebo.+ 48 Mwishowe wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu karibu na Yordani kule Yeriko.+ 49 Wakaendelea kupiga kambi pembeni ya Muto Yordani, kuanzia Bet-yeshimoti mupaka Abel-shitimu,+ katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu.
50 Yehova akasema na Musa katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu karibu na Yordani kule Yeriko, na akamuambia: 51 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Muko munavuka Muto Yordani ili kuingia katika inchi ya Kanaani.+ 52 Munapaswa kufukuza wakaaji wote wa inchi hiyo kutoka mbele yenu na kuharibu majiwe yao ya kuchongwa+ na sanamu zao zote za metali,*+ na munapaswa kubomoa kila mahali pao patakatifu pa juu.+ 53 Na mutariti inchi hiyo na kuishi ndani yake, kwa maana hakika nitawapatia inchi hiyo ili muiriti.+ 54 Munapaswa kugawanya inchi hiyo kwa kura+ ili kuwa uriti kati ya familia zenu. Kwa kikundi kikubwa mutaongeza uriti wake, na kwa kikundi kidogo mutapunguza uriti wake.+ Uriti wa kila mutu utakuwa mahali kwenye kura yake itaangukia. Mutapokea uriti wenu wa inchi kulingana na makabila ya baba zenu.+
55 “‘Lakini, kama hamufukuze wakaaji wa inchi hiyo kutoka mbele yenu,+ wale wenye mutaacha watakuwa kama vitu vya kuumiza katika macho yenu na kama miiba kwenye mbavu zenu, na watawasumbua katika inchi kwenye mutaishi.+ 56 Na nitawatendea ninyi mambo yenye nilikusudia kuwatendea wao.’”+
34 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Patia Waisraeli maagizo haya: ‘Wakati mutaingia katika inchi ya Kanaani,+ hiyo ndiyo inchi yenye itawaangukia kuwa uriti, inchi ya Kanaani kulingana na mipaka yake.+
3 “‘Mupaka wenu wa kusini utaanzia kwenye jangwa la Zini pembeni ya Edomu, na mupaka wenu wa kusini kwenye upande wa mashariki utakuwa kuanzia mwisho wa Bahari ya Chumvi.*+ 4 Mupaka wenu utakunja na kuenda upande wa kusini wa mupando wa Akrabimu+ na utaendelea mupaka Zini, na kuishia upande wa kusini wa Kadesh-barnea.+ Kisha utaenda Hasar-adari+ na kuendelea mupaka Asimoni. 5 Mupaka huo utakunja kule Asimoni na kuelekea kwenye Bonde la Muto* la Misri, na kuishia kwenye Bahari.*+
6 “‘Mupaka wenu wa mangaribi utakuwa Bahari Kubwa* na eneo la pembeni ya bahari. Huo utakuwa mupaka wenu wa mangaribi.+
7 “‘Sasa huu ndio utakuwa mupaka wenu wa kaskazini: Mutatia alama ya mupaka wenu kuanzia Bahari Kubwa mupaka Mulima Hori. 8 Kuanzia Mulima Hori mutatia alama ya mupaka kufikia Lebo-hamati,*+ na mupaka huo utaishia Sedadi.+ 9 Na utaendelea kufikia Zifroni, na kuishia Hasar-enani.+ Huo utakuwa mupaka wenu wa kaskazini.
10 “‘Kisha mutatia alama ya mupaka wenu wa mashariki kuanzia Hasar-enani mupaka Shefamu. 11 Mupaka huo utaanzia Shefamu kufikia Ribla upande wa mashariki wa Aini, na utashuka na kuvuka muteremuko wa mashariki wa Bahari ya Kinereti.*+ 12 Mupaka huo utaendelea kufikia Yordani na kuishia kwenye Bahari ya Chumvi.+ Hiyo ndiyo itakuwa inchi yenu+ na mipaka yenye kuizunguka.’”
13 Kwa hiyo Musa akawapatia Waisraeli maagizo, na kuwaambia: “Hiyo ndiyo inchi yenye mutagawanya kwa kura ili kuwa uriti wenu,+ kama vile Yehova ameamuru kuipatia makabila kenda (9) na nusu. 14 Kwa maana kabila la Rubeni kulingana na jamaa yao ya upande wa baba, kabila la Gadi kulingana na jamaa yao ya upande wa baba, na nusu ya kabila la Manase tayari yamekamata uriti wao.+ 15 Makabila hayo mbili na nusu tayari yamekamata uriti wao upande wa mashariki wa eneo la Yordani karibu na Yeriko, kuelekea mahali jua linatokea.”+
16 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 17 “Haya ndiyo majina ya wanaume wenye watawagawia inchi ili muiriti: Eleazari+ kuhani na Yoshua+ mwana wa Nuni. 18 Na mutakamata mukubwa mumoja katika kila kabila ili kugawanya inchi kuwa uriti wenu.+ 19 Haya ndiyo majina ya wanaume hao: katika kabila la Yuda,+ Kalebu+ mwana wa Yefune; 20 katika kabila la wana wa Simeoni,+ Shemueli mwana wa Amihudi; 21 katika kabila la Benyamini,+ Elidadi mwana wa Kisloni; 22 katika kabila la wana wa Dani,+ mukubwa mumoja, Buki mwana wa Yogli; 23 kati ya wana wa Yosefu+ katika kabila la wana wa Manase,+ mukubwa mumoja, Hanieli mwana wa Efodi; 24 katika kabila la wana wa Efraimu,+ mukubwa mumoja, Kemueli mwana wa Shiftani; 25 katika kabila la wana wa Zabuloni,+ mukubwa mumoja, Elisafani mwana wa Parnaki; 26 katika kabila la wana wa Isakari,+ mukubwa mumoja, Paltieli mwana wa Azani; 27 katika kabila la wana wa Asheri,+ mukubwa mumoja, Ahihudi mwana wa Shelomi, 28 katika kabila la wana wa Naftali,+ mukubwa mumoja, Pedaheli mwana wa Amihudi.” 29 Hao ndio wanaume wenye Yehova aliamuru wagawie Waisraeli inchi katika inchi ya Kanaani.+
35 Yehova akaendelea kusema na Musa katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu karibu na Yordani+ kule Yeriko, na kumuambia: 2 “Waagize Waisraeli wapatie Walawi miji ya kuishi ndani katika uriti wenye watariti,+ na wanapaswa kupatia Walawi malisho kuzunguka miji hiyo.+ 3 Wataishi katika miji hiyo, na malisho yatakuwa kwa ajili ya mifugo yao, mali zao, na wanyama wao wengine wote. 4 Malisho ya miji yenye mutapatia Walawi yatakuwa na ukubwa wa mikono* elfu moja (1 000) kutoka kwenye ukuta kuzunguka muji pande zote. 5 Mutapima inje ya muji mikono elfu mbili (2 000) upande wa mashariki, mikono elfu mbili upande wa kusini, mikono elfu mbili upande wa mangaribi, na mikono elfu mbili upande wa kaskazini; muji utakuwa katikati. Ni hayo yatakuwa malisho ya miji yao.
6 “Miji yenye mutapatia Walawi itakuwa miji sita (6) ya makimbilio,+ yenye mutatoa ili muuaji akimbilie ndani,+ pia mutawapatia miji ingine makumi ine na mbili (42). 7 Miji yote yenye mutapatia Walawi itakuwa makumi ine na munane (48), pamoja na malisho yake.+ 8 Miji yenye mutawapatia yatatoka katika uriti wa Waisraeli.+ Mutakamata miji mingi katika kikundi kikubwa, na miji kidogo katika kikundi kidogo.+ Kila kikundi kitapatia Walawi miji fulani katikati ya miji yake kulingana na uriti wenye kitapokea.”
9 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 10 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Muko munavuka Yordani ili kuingia katika inchi ya Kanaani.+ 11 Munapaswa kuchagua miji yenye kuwafaa ninyi ili ikuwe miji ya makimbilio, mahali kwenye muuaji mwenye anaua mutu* bila kukusudia anapaswa kukimbilia.+ 12 Miji hiyo itakuwa makimbilio yenu ili kumuepuka mulipiza-kisasi cha damu,+ ili muuaji asiuawe kabla ya kuhukumiwa mbele ya mukusanyiko.+ 13 Miji sita (6) ya makimbilio yenye mutatoa itatumiwa kwa kusudi hilo. 14 Mutatoa miji tatu (3) ngambo hii ya Yordani+ na miji tatu katika inchi ya Kanaani+ ili ikuwe miji ya makimbilio. 15 Miji hiyo sita (6) itakuwa makimbilio kwa ajili ya Waisraeli, kwa ajili ya mukaaji mugeni,+ na kwa ajili ya muhamiaji kati yenu, ili mutu yeyote mwenye anaua mutu* bila kukusudia akimbilie kule.+
16 “‘Lakini kama mutu alimupiga kwa kifaa cha chuma na anakufa, yeye ni muuaji wa kukusudia. Muuaji huyo anapaswa kabisa kuuawa.+ 17 Na kama alimupiga kwa jiwe lenye linaweza kuua na mutu huyo anakufa, yeye ni muuaji wa kukusudia. Muuaji huyo anapaswa kabisa kuuawa. 18 Na kama alimupiga kwa kifaa cha muti chenye kinaweza kuua na mutu huyo anakufa, yeye ni muuaji wa kukusudia. Muuaji huyo anapaswa kabisa kuuawa.
19 “‘Mulipiza-kisasi cha damu ndiye ataua muuaji wa kukusudia. Wakati atakutana naye, atamuua yeye mwenyewe. 20 Kama kifo kilitokea kwa kuwa alimusukuma kwa sababu ya chuki ao alimutupia kitu fulani kwa nia mubaya,*+ 21 ao kwa sababu ya chuki alimupiga kwa mukono, na akakufa, mutu huyo mwenye alimupiga anapaswa kabisa kuuawa. Yeye ni muuaji wa kukusudia. Mulipiza-kisasi cha damu ataua muuaji huyo wa kukusudia wakati atakutana naye.
22 “‘Lakini kama ilikuwa kwa kushitukia na alimusukuma hapana kwa sababu ya chuki ao alimutupia kitu chochote bila kuwa na nia mubaya,*+ 23 ao kama hakumuona na akamwangushia jiwe na hakukuwa adui yake ao hakukuwa anatafuta kumuumiza, na mutu huyo akakufa, 24 basi mukusanyiko unapaswa kuhukumu kati ya mutu mwenye alimupiga na mulipiza-kisasi cha damu, kulingana na hukumu hizo.+ 25 Kisha mukusanyiko utamuokoa muuaji huyo katika mukono wa mulipiza-kisasi cha damu na kumurudisha katika muji wake wa makimbilio kwenye alikuwa amekimbilia, na atakaa kule mupaka wakati kuhani mukubwa mwenye alitiwa mafuta matakatifu atakufa.+
26 “‘Lakini kama muuaji anatoka inje ya mupaka wa muji wa makimbilio kwenye alikimbilia, 27 na kama mulipiza-kisasi cha damu anamupata inje ya mupaka wa muji wake wa makimbilio na anaua muuaji huyo, yeye hana hatia ya damu. 28 Kwa maana anapaswa kukaa katika muji wake wa makimbilio mupaka wakati kuhani mukubwa atakufa. Lakini kisha kuhani mukubwa kufa, muuaji anaweza kurudia katika inchi yenye ni mali yake.+ 29 Mambo hayo yatakuwa sheria za hukumu katika vizazi vyenu vyote kila mahali kwenye mutaishi.
30 “‘Kila mutu mwenye anaua mutu* anapaswa kuuawa kama muuaji wa kukusudia+ kwa ushuhuda wa* mashahidi;+ lakini hakuna mutu mwenye atauawa* kwa ushuhuda wa shahidi mumoja tu. 31 Hamupaswe kukamata bei ya ukombozi kwa ajili ya uzima wa* muuaji wa kukusudia mwenye anastahili kufa, kwa maana anapaswa kabisa kuuawa.+ 32 Na hamupaswe kukamata bei ya ukombozi kwa ajili ya mutu mwenye amekimbilia katika muji wake wa makimbilio, na hivyo kumuruhusu arudie kuishi katika inchi yake mbele ya kuhani mukubwa kufa.
33 “‘Hamupaswe kuchafua inchi yenye munaishi ndani yake, kwa sababu damu inachafua inchi,+ na hakuwezi kuwa kufunika zambi kwa ajili ya damu yenye imemwangwa juu ya inchi isipokuwa kwa kumwanga damu ya ule mwenye aliimwanga.+ 34 Haupaswe kuchafua inchi yenye munaishi ndani yake, yenye ninakaa ndani yake; kwa maana mimi, Yehova, ninakaa katikati ya watu wa Israeli.’”+
36 Vichwa vya familia za wazao wa Gileadi mwana wa Makiri+ mwana wa Manase wa familia za wana wa Yosefu wakakaribia na kusema mbele ya Musa na wakubwa, vichwa vya familia za Waisraeli. 2 Wakasema: “Yehova alimuamuru bwana wangu agawie Waisraeli inchi kwa kura+ kuwa uriti; na bwana wangu aliamuriwa na Yehova kwamba uriti wa Selofehadi ndugu yetu aupatie mabinti wake.+ 3 Lakini kama wanaolewa na wanaume wa kabila lingine la Waisraeli, uriti wa wanamuke hao utaondolewa pia katika uriti wa baba zetu na kuongezwa kwenye uriti wa kabila lenye wataingia ndani wakati huo, kwa hiyo uriti huo utaondolewa katika uriti wetu wenye tulipokea kwa kura. 4 Sasa wakati Yubile+ inafika kwa ajili ya watu wa Israeli, uriti wa wanamuke hao utaongezwa pia kwenye uriti wa kabila lenye wataingia ndani wakati huo, na hivyo uriti wao utaondolewa katika uriti wa kabila la baba zetu.”
5 Basi Musa akaamuru Waisraeli kama vile Yehova aliagiza: “Kabila la wana wa Yosefu linasema kweli. 6 Yehova ameamuru neno hili kwa ajili ya mabinti wa Selofehadi: ‘Wanaweza kuolewa na mutu yeyote mwenye wanapenda. Lakini, wanapaswa kuolewa na mutu mwenye anatoka katika familia ya kabila la baba yao. 7 Hakuna uriti wa Waisraeli wenye unapaswa kutoka katika kabila moja kuenda katika kabila lingine, kwa sababu Waisraeli wanapaswa kushikamana na uriti wa kabila la mababu zao. 8 Na kila binti mwenye kuwa na uriti kati ya makabila ya Israeli anapaswa kuwa bibi ya muzao wa kabila la baba yake,+ ili Waisraeli waendelee kuchunga uriti wa mababu zao. 9 Hakuna uriti wenye unapaswa kutoka katika kabila moja kuenda katika kabila lingine, kwa sababu makabila ya Israeli yanapaswa kushikamana na uriti wao wenyewe.’”
10 Mabinti wa Selofehadi walifanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.+ 11 Kwa hiyo Mala, Tirsa, Hogla, Milka, na Noa, mabinti wa Selofehadi,+ waliolewa na wana wa ndugu za baba yao. 12 Wakakuwa bibi za wanaume wa familia za Manase mwana wa Yosefu ili uriti wao ubakie katika kabila la familia ya baba yao.
13 Hizo ndizo amri na maamuzi ya hukumu yenye Yehova alipatia Waisraeli kupitia Musa kwenye maeneo tambarare ya jangwa la Moabu karibu na Yordani kule Yeriko.+
Tnn., “wana wa Israeli.”
Ao “kila kichwa.”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Tnn., ”mugeni yeyote,” ni kusema, mutu mwenye haiko Mulawi.
Ao “alama (bendera) yake.”
Tnn., “majeshi yao.”
Ao “kulinda; kutumikia kwenye.”
Tnn., “majeshi yao.”
Tnn., “majeshi yao.”
Tnn., “majeshi yao.”
Tnn., “majeshi yao.”
Tnn., “hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya.”
Tnn., “wenye mikono yao ilikuwa imejazwa.”
Tnn., “mugeni yeyote,” ni kusema, mutu mwenye haiko wa familia ya Haruni.
Tnn., “ya kila muzaliwa wa kwanza mwenye anafungua tumbo la uzazi.”
Ao “pazia la.”
Ao “pazia la.”
Ao “pazia.”
Tnn., “Mugeni yeyote,” ni kusema, mutu mwenye haiko Mulawi.
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “kulingana na shekeli takatifu.”
Gera moja ilikuwa sawa na grame 0.57 (aunsi troi 0.01835). Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “kinywa cha.”
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “koleo zake.”
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “majivu yenye mafuta,” ni kusema, majivu yenye kujaa mafuta ya zabihu.
Ao “nyuma.”
Ao “sepetu; bêches.”
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “muzigo wa.”
Ao “eko.”
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “pazia la.”
Ao “pazia la.”
Ao “kupitia nafsi.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “ninapiga hema.”
Ao “nafsi hiyo imekuwa.”
Tnn., “Wanapaswa.”
Tnn., “wamefanya.”
Ao “eko.”
Sehemu ya kumi ya efa ilikuwa sawa na litre 2.2 (vibaba 2). Angalia Nyongeza B14.
Inaonekana neno hili linamaanisha viungo vya uzazi.
Ao “liharibike.” Hii inaweza kumaanisha kupoteza uwezo wa kuzaa.
Inaonekana neno hili linamaanisha viungo vya uzazi.
Ao “liharibike.” Hii inaweza kumaanisha kupoteza uwezo wa kuzaa.
Ao “Ikuwe vile! Ikuwe vile!”
Inaonekana neno hili linamaanisha viungo vya uzazi.
Ao “litaharibika.” Hii inaweza kumaanisha kupoteza uwezo wa kuzaa.
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Katika Kiebrania ni na·zirʹ, maana yake ni “Mwenye Alitengwa; Mwenye Alitolewa kwa Mungu; Mwenye Aliwekwa Pembeni.”
Ao “vinaigre.”
Ao “kuja karibu na.”
Ao “kukaribia nafsi yenye imekufa.” Angalia Maana ya Maneno, “nafsi.”
Ao “anachafua kichwa cha Unaziri wake.”
Ao “nafsi yenye imekufa.”
Ao “kichwa cha Unaziri wake.”
Ao “kumutolea Mungu mazabahu.”
Ao “kumutolea Mungu mazabahu.”
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “kulingana na shekeli takatifu.”
Ao “bakuli moja la kidogo la zahabu lenye.”
Ao “kumutolea Mungu mazabahu.”
Ao “kumutolea Mungu mazabahu.”
Tnn., “naye.”
Ao “hama, marteau.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Tnn., “kuwatikisa,” ni kusema, kuwafanya waende mbele na nyuma.
Tnn., “kuwatikisa,” ni kusema, kuwafanya waende mbele na nyuma.
Tnn., “kuwatikisa,” ni kusema, kuwafanya waende mbele na nyuma.
Ao “wazaliwa wote wa kwanza wenye kufungua matumbo ya uzazi.”
Tnn., “akawatikisa,” ni kusema, akawafanya waende mbele na nyuma.
Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”
Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”
Ao “kwa sababu ya nafsi ya mutu.”
Ao “kwa sababu ya nafsi ya mutu.”
Ao “kwa sababu ya nafsi.”
Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”
Ao “nafsi hiyo inapaswa.”
Ao “kuuawa kutoka.”
Ao “hama, marteau.”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Ni kusema, Yetro.
Ao “macho yetu.”
Ao “makumi ya maelfu ya Israeli.”
Ao “akaomba dua kwa.”
Maana yake “Kuteketea kwa Moto,” ni kusema, moto mukubwa.
Inaonekana ni watu wenye hawakuwa Waisraeli.
Ao “nafsi zetu zinakuwa.”
Ulimbo ni umajimaji wa muti wenye kukamatana ao kunata-nata.
Ao “mulezi mwanaume.”
Ao “wakaanza kutoa unabii.”
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Homeri moja ilikuwa sawa na litre 220 (vibaba 200). Angalia Nyongeza B14.
Maana yake “Makaburi ya Watu Wenye Tamaa Kubwa.”
Ao “munyenyekevu sana, kuliko mutu mwingine yeyote.”
Tnn., “Anajionyesha kuwa muaminifu katika nyumba yangu yote.”
Tnn., “kinywa kwa kinywa.”
Ao “neige.”
Ao “wachunguze.”
Ao “Yehoshua,” maana yake “Yehova Ni Wokovu.”
Tnn., “yenye kunona.”
Tnn., “yenye kukonda.”
Ao “njia ya kuingia Hamati.”
Ao “Bonde la Muto.”
Ao “Bonde la Muto.”
Maana yake “Kishada cha Zabibu.”
Tnn., “wao ni mukate kwetu.”
Ao “eko.”
Tnn., “kama mutu mumoja.”
Ao “fazili nyingi zenye upendo.”
Ao “eneo tambarare la chini.”
Tnn., “niliinua mukono wangu.”
Tnn., “ya ukahaba.”
Ao “ya kuwa maadui wangu.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Sehemu moja ya kumi ya efa ilikuwa sawa na litre 2.2 (vibaba 2). Angalia Nyongeza B14.
Hini moja ilikuwa sawa na litre 3.67 (painti 7.75). Angalia Nyongeza B14.
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “chakula chochote cha.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “nafsi yoyote inafanya.”
Ao “nafsi hiyo yenye ilifanya.”
Ao “nafsi yenye inafanya.”
Ao “kuuawa kutoka.”
Ao “nafsi hiyo inapaswa kuondolewa isikuwe.”
Ao “eko.”
Ao “kupiga ubwana juu yetu.”
Tnn., “Mungu wa roho za miili yote.”
Ao “haiko mapenzi yangu mwenyewe.”
Tnn., “ufungue kinywa chake.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “ikafungua kinywa chake.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “walitendea zambi nafsi zao wenyewe.”
Tnn., “mugeni yeyote.”
Tumba ni jicho la mumea lenye linageuka kuwa ua, jani, ao tawi.
Tumba ni jicho la mumea lenye linageuka kuwa ua, jani, ao tawi.
Tnn., “mugeni,” ni kusema, mutu mwenye haiko wa familia ya Haruni.
Tnn., “mugeni,” ni kusema, mutu mwenye haiko wa familia ya Haruni.
Ni kusema, kila kitu chenye kilifanywa kuwa kitakatifu kwa ajili ya Mungu kwa kuwa hakiwezi kukombolewa ao kukamatwa tena.
Tnn., “wa miili yote.”
Ao “eko.”
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “shekeli takatifu.”
Gera moja ilikuwa sawa na grame 0.57 (aunsi troi 0.01835). Angalia Nyongeza B14.
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ni kusema, agano lenye kudumu na lenye halibadilike.
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “maiti ya nafsi yoyote ya mwanadamu.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “maiti, nafsi ya mutu yeyote mwenye amekufa.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nafsi hiyo inapaswa.”
Ao “kuuawa kutoka.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “nafsi zenye zilikuwa.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “nafsi hiyo inapaswa.”
Ao “atauawa kutoka.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “nafsi yenye inakigusa haitakuwa.”
Maana yake “Kugombana.”
Tnn., “siku nyingi.”
Tnn., “mukono wenye.”
Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.
Tnn., “atakusanywa na kukufia kule.”
Maana yake “Uharibifu.”
Ao “nafsi ya watu ikachoka.”
Ao “nafsi zetu zimechukia.”
Ao “wenye moto.”
Ao “mukali.”
Ao “Bonde la Muto.”
Tnn., “kinywa cha.”
Ao “Mukimbie.”
Tnn., “eneo la mashamba.”
Ao pengine, “jangwa, nyika.”
Ao “yenye kuizunguka.”
Ao “yenye kuizunguka.”
Inaonekana ni Efrati.
Tnn., “jicho la.”
Ao “inchi.”
Tnn., “jicho la.”
Ao “inchi.”
Tnn., “punda-dike.”
Tnn., “akafungua kinywa cha punda-dike huyo.”
Ao “nafsi yangu ikufe.”
Ao “mwenye anasikitikaka.”
Ao “eko.”
Ao pengine, “jangwa; nyika.”
Tnn., “ilikuwa muzuri katika macho ya.”
Ao “uzao wake umepandwa.”
Tnn., “kutoka katika moyo wangu.”
Ao “katika siku za mwisho.”
Ao “mashua za maji; bateaux.”
Ao “akashikamana na.”
Tnn., “vichwa vyote vya.”
Ao “mbele ya jua.”
Ao “wenye walishikamana na.”
Tnn., “ikafungua kinywa chake.”
Ao “kulingana na hesabu ya majina yenye yaliandikishwa.”
Ao “eko.”
Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.
Tnn., “Mungu wa roho za miili yote.”
Ao “heshima.”
Ao “ya kunituliza.” Tnn., “ya kunipumuzisha.”
Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”
Sehemu moja ya kumi ya efa ilikuwa sawa na litre 2.2 (vibaba 2). Angalia Nyongeza B14.
Hini moja ilikuwa sawa na litre 3.67 (painti 7.75). Angalia Nyongeza B14.
Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”
Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Tnn., “wa miezi yenu.”
Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”
Tnn., “mukate.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”
Ao “kutesa nafsi zenu.” Kwa ujumla inaeleweka kuwa “kujitesa” kunamaanisha njia mbalimbali za kujinyima, kutia ndani kufunga.
Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”
Ao “kufunga sharti juu ya nafsi yake.”
Ao “amefunga juu ya nafsi yake.”
Ao “eko.”
Ao “naziri ya kutesa nafsi.”
Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.
Ao ”kwa ajili ya jeshi.”
Ao “kambi zao zote zenye kuzungukwa na kuta.”
Ao “nafsi.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nafsi.”
Ao “nafsi za wanadamu.”
Ao “nafsi.”
Ao “nafsi za wanadamu.”
Ao “kwa ajili ya nafsi zetu.”
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “ukumbusho.”
Ao “Bonde la Muto.”
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
Ao “wakajenga upya.”
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
Maana yake “Vijiji vya Mahema vya Yairi.”
Ao “yenye kuizunguka.”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Tnn., “mukono wenye kuinuliwa.”
Tnn., “sanamu za kuyeyushwa.”
Ni kusema, Bahari Yenye Kufa.
Angalia Maana ya Maneno.
Ni kusema, ile Bahari Kubwa, Mediterania.
Ni kusema, Mediterania.
Ao “muingilio wa Hamati.”
Ni kusema, ziwa la Genesareti, ao Bahari ya Galilaya.
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Ao “anapiga nafsi.”
Ao “anapiga nafsi.”
Tnn., “wakati alikuwa anamuvizia.”
Tnn., “bila kumuvizia.”
Ao “nafsi.”
Tnn., “kinywa cha.”
Ao “nafsi yenye itauawa.”
Ao “nafsi ya.”