ZABURI
KITABU CHA KWANZA
(Zaburi 1-41)
1 Mwenye furaha ni mtu ambaye hatembei katika mashauri ya waovu
Na hasimami katika njia ya watenda dhambi+
Naye haketi katika kiti cha wenye dhihaka.+
2 Lakini anapendezwa na sheria ya Yehova,+
Naye huisoma sheria Yake kwa sauti ya chini* mchana na usiku.+
3 Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji,
Mti unaozaa matunda katika majira yake,
Na majani yake hayanyauki.
Na kila jambo analofanya litafanikiwa.+
4 Waovu hawako hivyo;
Wao ni kama makapi yanayopeperushwa mbali na upepo.
5 Ndiyo sababu waovu hawataendelea kusimama katika hukumu;+
Wala watenda dhambi hawataendelea kusimama katika kusanyiko la waadilifu.+
3 Wanasema: “Na tuzikate pingu zao
Na kuzitupa kamba zao!”
4 Yule anayeketi kwenye kiti cha ufalme mbinguni atacheka;
Yehova atawadhihaki.
5 Wakati huo ataongea nao kwa hasira yake
Na kuwatisha kwa hasira yake inayowaka,
6 Akisema: “Mimi mwenyewe nimemweka mfalme wangu+
Juu ya Sayuni,+ mlima wangu mtakatifu.”
8 Niombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako
Na miisho ya dunia kuwa miliki yako.+
10 Basi sasa, enyi wafalme, onyesheni ufahamu;
Kubalini kurekebishwa,* enyi waamuzi wa dunia.
11 Mtumikieni Yehova kwa woga,
Na mshangilie mkitetemeka.
12 Mheshimuni* mwana,+ la sivyo Mungu atawaka hasira
Nanyi mtaangamia kutoka njiani,+
Kwa maana hasira Yake huwaka upesi.
Wenye furaha ni wale wote wanaomkimbilia Yeye.
Muziki wa Daudi alipokuwa akimkimbia Absalomu mwanawe.+
3 Ee Yehova, kwa nini maadui wangu wamekuwa wengi sana?+
Kwa nini watu wengi sana wanainuka dhidi yangu?+
2 Wengi wanasema hivi kunihusu:*
4 Nitamlilia Yehova kwa sauti kubwa,
Naye atanijibu kutoka kwenye mlima wake mtakatifu.+ (Sela)
5 Nitajilaza chini na kulala usingizi;
Nami nitaamka nikiwa salama,
Kwa maana Yehova anaendelea kunitegemeza.+
6 Siogopi makumi ya maelfu
Waliojipanga dhidi yangu kila upande.+
7 Inuka, Ee Yehova! Niokoe,+ Ee Mungu wangu!
Kwa maana utawapiga maadui wangu wote kwenye utaya;
Utayavunja meno ya waovu.+
8 Wokovu ni wa Yehova.+
Baraka yako iko juu ya watu wako. (Sela)
Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Muziki wa Daudi.
4 Ninapokuita, unijibu, Ee Mungu wangu mwadilifu.+
Nitengenezee njia ya kutoroka* taabu yangu.
Nionyeshe kibali na usikie sala yangu.
2 Enyi wanadamu, mtaendelea mpaka lini kuibadili heshima yangu kuwa aibu?
Mtaendelea mpaka lini kupenda mambo yasiyo na faida na kutafuta mambo ya uwongo? (Sela)
3 Jueni kwamba Yehova atamtendea mshikamanifu wake kwa njia ya pekee;*
Yehova atasikia ninapomlilia.
4 Kasirika, lakini usitende dhambi.+
Zungumza moyoni mwako, kitandani mwako, na unyamaze kimya. (Sela)
5 Toa dhabihu za uadilifu,
Na umtumaini Yehova.+
6 Kuna wengi wanaosema: “Ni nani atakayetuonyesha jambo lolote jema?”
Acha nuru ya uso wako ituangazie, Ee Yehova.+
7 Umeujaza moyo wangu shangwe nyingi sana
Kuliko wale walio na mavuno mengi sana ya nafaka na divai mpya.
8 Nitajilaza chini na kulala usingizi kwa amani,+
Kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, hunifanya niishi kwa usalama.+
Kwa kiongozi wa Nehilothi.* Muziki wa Daudi.
5 Sikiliza maneno yangu, Ee Yehova;+
Sikiliza kwa makini kilio changu cha uchungu.
2 Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada,
Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa sababu ninasali kwako.
3 Ee Yehova, utasikia sauti yangu asubuhi;+
Asubuhi nitakueleza mahangaiko yangu+ na kusubiri kwa hamu.
5 Hakuna mtu yeyote mwenye kiburi anayeweza kusimama mbele zako.*
Yehova anawachukia kabisa watu wakatili na wadanganyifu.*+
7 Lakini nitaingia katika nyumba yako+ kwa sababu ya upendo wako mwingi mshikamanifu;+
Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu* nikiwa na heshima na woga kukuelekea.+
8 Niongoze, Ee Yehova, katika uadilifu wako kwa sababu ya maadui wangu;
Ifanye njia yako iwe wazi kwangu.+
9 Kwa maana hakuna lolote wanalosema linaloweza kutumainiwa;
Ndani yao hamna lolote isipokuwa nia ya kudhuru.
10 Lakini Mungu atawatangaza kuwa na hatia;
Njama zao wenyewe zitasababisha waanguke.+
Na wafukuzwe kwa sababu ya dhambi zao nyingi,
Kwa maana wamekuasi wewe.
11 Lakini wale wote wanaokukimbilia watashangilia;+
Watapaza sauti kwa shangwe daima.
Nawe utawakinga wasifikiwe,
Na wale wanaolipenda jina lako watashangilia kwa sababu yako.
12 Kwa maana utambariki yeyote aliye mwadilifu, Ee Yehova;
Utawazunguka kwa kibali kana kwamba kwa ngao kubwa.+
Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda vilivyopatanishwa na sauti ya Sheminithi.* Muziki wa Daudi.
6 Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,
Na usinirekebishe katika ghadhabu yako.+
2 Nionyeshe kibali,* Ee Yehova, kwa maana ninadhoofika.
Niponye, Ee Yehova,+ kwa maana mifupa yangu inatetemeka.
6 Nimechoka kwa sababu ya kulia kwa uchungu;+
Usiku kucha ninakilowesha kitanda changu kwa machozi;*
Kochi langu nalifanya lifurike kwa machozi.+
7 Jicho langu limedhoofika kwa sababu ya huzuni yangu;+
Limeingia giza* kwa sababu ya wote wanaoninyanyasa.
8 Niondokeeni, ninyi nyote mnaotenda maovu,
Kwa maana Yehova atasikia sauti ya kilio changu.+
9 Yehova atasikia ombi langu la kutaka kibali;+
Yehova ataikubali sala yangu.
10 Maadui wangu wote wataaibishwa na kutamaushwa;
Watarudi nyuma ghafla kwa aibu.+
Wimbo wa huzuni* wa Daudi ambao alimwimbia Yehova kwa sababu ya maneno ya Kushi Mbenjamini.
7 Ee Yehova Mungu wangu, nimekukimbilia wewe.+
Niokoe kutoka kwa wale wote wanaonitesa na unifanye nisalimike.+
2 La sivyo watanirarua* vipandevipande kama simba anavyofanya,+
Watanibeba na kwenda nami pasipo na yeyote wa kuniokoa.
3 Ee Yehova Mungu wangu, ikiwa nimekosea katika jambo hili,
Ikiwa nimetenda isivyo haki,
4 Ikiwa nimemkosea anayenitendea wema,+
Au ikiwa nimempora adui yangu bila sababu,*
5 Basi acha adui anikimbize na kunipita;*
Acha aukanyagie uhai wangu ardhini
Na kuufanya utukufu wangu utokomee mavumbini. (Sela)
6 Inuka katika hasira yako, Ee Yehova;
Simama ukabiliane na hasira kali ya maadui wangu;+
Amka kwa ajili yangu, na uamuru kwamba haki itendeke.+
7 Acha mataifa yakuzingire;
Nawe utachukua hatua dhidi yao kutoka juu.
8 Yehova atayahukumu mataifa.+
Nihukumu, Ee Yehova, kulingana na uadilifu wangu
Na kulingana na utimilifu wangu.+
9 Tafadhali, yakomeshe matendo maovu ya waovu.
Lakini umwimarishe mwadilifu,+
Kwa kuwa wewe ni Mungu mwadilifu+ anayechunguza mioyo+ na hisia zilizo ndani kabisa.*+
10 Mungu ni ngao yangu,+ Mwokozi wa wale walio wanyoofu moyoni.+
13 Hutayarisha silaha zake zinazoua;
Huweka tayari mishale yake inayowaka moto.+
14 Mtazame yule aliye na mimba ya uovu;
Hutunga mimba ya matatizo na kuzaa uwongo.+
15 Huchimba shimo na kuzidisha kina chake,
Lakini huanguka katika shimo hilohilo alilolichimba.+
16 Matatizo anayosababisha yatarudi juu ya kichwa chake mwenyewe;+
Ukatili wake utaanguka juu ya utosi wa kichwa chake.
Kwa kiongozi; juu ya Gitithi.* Muziki wa Daudi.
8 Ee Yehova Bwana wetu, jinsi jina lako lilivyo kuu katika dunia yote;
2 Kutoka katika vinywa vya watoto wadogo na wanaonyonya+ umeimarisha nguvu
Kwa sababu ya maadui wako,
Ili kumnyamazisha adui na yule anayelipiza kisasi.
3 Ninapoziona mbingu zako, kazi za vidole vyako,
Mwezi na nyota ambazo umetayarisha,+
4 Mwanadamu anayeweza kufa ni nini hivi kwamba unamweka akilini,
Na mwana wa mtu hivi kwamba unamtunza?+
5 Ulimfanya awe mdogo kidogo kuliko wale walio kama Mungu,*
Nawe ukamvika taji la utukufu na fahari.
6 Ulimpa mamlaka juu ya kazi za mikono yako;+
Umeweka kila kitu chini ya miguu yake:
7 Kondoo wote na ng’ombe wote,
Na pia wanyama wa mwituni,+
8 Ndege wa angani na samaki wa baharini,
Kitu chochote kinachopita katika njia za baharini.
9 Ee Yehova Bwana wetu, jinsi jina lako lilivyo kuu katika dunia yote!
Kwa kiongozi; juu ya Muth-labeni.* Muziki wa Daudi.
א [Aleph]
9 Nitakusifu, Ee Yehova, kwa moyo wangu wote;
Nitasimulia kuhusu kazi zako zote zinazostaajabisha.+
ב [Beth]
3 Maadui wangu wanapokimbia,+
Watajikwaa na kuangamia kutoka mbele zako.
4 Kwa maana unatetea njia yangu ya haki;
Unaketi kwenye kiti chako cha ufalme ukihukumu kwa uadilifu.+
ג [Gimel]
5 Umeyakemea mataifa+ na kuwaangamiza waovu,
Na hivyo kulifuta jina lao milele na milele.
ה [He]
7 Lakini Yehova ameketi kwenye kiti cha ufalme milele;+
Amekiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme kwa ajili ya haki.+
ו [Waw]
ז [Zayin]
11 Mwimbieni sifa Yehova, anayekaa Sayuni;
Tangazeni matendo yake miongoni mwa mataifa.+
12 Kwa maana Yule anayelipiza kisasi kwa ajili ya damu yao anawakumbuka;+
Hatasahau kilio cha wanaoteseka.+
ח [Heth]
13 Nionyeshe kibali, Ee Yehova; angalia ninavyoteswa na wale wanaonichukia,
Wewe unayeniinua kutoka katika malango ya kifo,+
14 Ili nitangaze katika malango ya binti ya Sayuni matendo yako yanayostahili sifa,+
Na kushangilia kwa sababu ya matendo yako ya wokovu.+
ט [Teth]
15 Mataifa yamezama chini katika shimo walilochimba;
Mguu wao wenyewe umenaswa katika wavu waliouficha.+
16 Yehova anajulikana kwa hukumu anazotekeleza.+
Mwovu amenaswa katika kazi za mikono yake mwenyewe.+
Higayoni.* (Sela)
י [Yod]
17 Waovu watageuka na kuelekea Kaburini,*
Mataifa yote yanayomsahau Mungu.
כ [Kaph]
19 Inuka, Ee Yehova! Usiache mwanadamu anayeweza kufa ashinde.
Mataifa na yahukumiwe mbele zako.*+
20 Wapige kwa woga, Ee Yehova,+
Acha mataifa yajue kwamba wao ni wanadamu tu wanaoweza kufa. (Sela)
ל [Lamed]
10 Ee Yehova, kwa nini unasimama mbali?
Kwa nini unajificha nyakati za taabu?+
Humkosea heshima Yehova.
4 Kwa sababu ya kiburi chake, mwovu hafanyi uchunguzi wowote;
Mawazo yake yote ni: “Hakuna Mungu.”+
5 Njia zake huendelea kufanikiwa,+
Lakini hukumu zako zimepita uelewaji wake;+
Huwadhihaki* maadui wake wote.
פ [Pe]
8 Huvizia karibu na makao;
Kutoka mahali anapojificha humuua mtu asiye na hatia.+
ע [Ayin]
Macho yake yanamtafuta mtu asiye na kosa.+
9 Hungojea mahali alipojificha kama simba katika pango* lake.+
Hungojea ili amkamate asiye na uwezo.
Humkamata asiye na uwezo anapouvuta wavu wake na kuufunga.+
10 Mtu huyo hupondwa na kuangushwa chini;
Watu wasio na kosa huanguka mikononi mwake.*
11 Yeye husema moyoni mwake: “Mungu amesahau.+
Ameugeuzia mbali uso wake.
Haoni kamwe.”+
ק [Qoph]
12 Inuka, Ee Yehova.+ Ee Mungu, inua mkono wako.+
Usiwasahau wasio na uwezo.+
13 Kwa nini mwovu amemkosea Mungu heshima?
Husema moyoni mwake: “Hutanifanya niwajibike.”
ר [Resh]
14 Lakini unaona mateso na taabu.
Wewe huendelea kutazama na kuchukua hatua.+
ש [Shin]
16 Yehova ni Mfalme milele na milele.+
Mataifa yameangamia kutoka duniani.+
ת [Taw]
17 Lakini utasikia ombi la wapole, Ee Yehova.+
Utaiimarisha mioyo yao+ na kuwasikiliza kwa makini.+
18 Utawatendea haki mayatima na wale wanaopondwa,+
Ili mwanadamu anayeweza kufa ambaye ni mavumbi asiwaogopeshe tena.+
Kwa kiongozi. Wa Daudi.
11 Nimemkimbilia Yehova.+
Basi mnawezaje kuniambia:*
“Kimbilia kwenye mlima wako kama ndege!
2 Tazama jinsi waovu wanavyoukunja upinde;
Huutia mshale wao kwenye kamba ya upinde,
Ili wawapige kutoka gizani wale walio wanyoofu moyoni.
3 Misingi* inapobomolewa,
Mtu mwadilifu anaweza kufanya nini?”
4 Yehova yumo katika hekalu lake takatifu.+
Kiti cha ufalme cha Yehova kiko mbinguni.+
Macho yake mwenyewe yanatazama, macho yake yaliyo makini* yanawachunguza wanadamu.+
7 Kwa maana Yehova ni mwadilifu;+ yeye hupenda matendo ya uadilifu.+
Kwa kiongozi; umepatanishwa na sauti ya Sheminithi.* Muziki wa Daudi.
12 Niokoe, Ee Yehova, kwa maana mtu mshikamanifu hayupo tena;
Watu waaminifu wametoweka kutoka miongoni mwa wanadamu.
3 Yehova ataikata kabisa midomo yote inayosifusifu
Na ulimi unaojigamba kupindukia,+
4 Wale wanaosema: “Tutashinda kwa ndimi zetu.
Tunatumia midomo yetu tupendavyo;
Ni nani atakayekuwa bwana mkubwa wetu?”+
5 “Kwa sababu wale wanaoteswa wanakandamizwa,
Kwa sababu ya kilio cha uchungu cha maskini,+
Nitainuka na kutenda,” asema Yehova.
“Nitawaokoa kutoka kwa wale wanaowatendea kwa dharau.”*
6 Maneno ya Yehova ni safi;+
Ni kama fedha iliyosafishwa katika tanuru la udongo,* iliyosafishwa mara saba.
7 Utawalinda, Ee Yehova;+
Utamlinda kila mmoja wao milele kutokana na kizazi hiki.
8 Waovu wanatembea huku na huku kwa uhuru
Kwa sababu wanadamu wanaendeleza upotovu.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
13 Ee Yehova, utanisahau mpaka lini? Milele?
Utanificha uso wako mpaka lini?+
2 Nitahangaika kwa wasiwasi mpaka lini,
Nikiwa na huzuni moyoni mwangu kila siku?
Adui yangu atanishinda mpaka lini?+
3 Nitazame na unijibu, Ee Yehova Mungu wangu.
Yatie nuru macho yangu, ili nisilale usingizi katika kifo,
4 Ili adui yangu asiseme: “Nimemshinda!”
Usiruhusu wapinzani wangu washangilie kuanguka kwangu.+
5 Lakini mimi, ninautumaini upendo wako mshikamanifu;+
Moyo wangu utashangilia kwa sababu ya matendo yako ya wokovu.+
6 Nitamwimbia Yehova, kwa maana amenithawabisha kwelikweli.*+
Kwa kiongozi. Wa Daudi.
14 Mpumbavu* husema moyoni mwake:
“Hakuna Yehova.”+
Matendo yao yamepotoka, na shughuli zao zinachukiza;
Hakuna yeyote anayetenda mema.+
2 Lakini Yehova anawatazama wanadamu kutoka mbinguni
Ili aone ikiwa kuna yeyote aliye na ufahamu, ikiwa kuna yeyote anayemtafuta Yehova.+
3 Wote wamegeuka kando;+
Wote wamepotoka.
Hakuna yeyote anayetenda mema,
Hakuna hata mmoja.
4 Je, hakuna mtenda maovu yeyote anayeelewa?
Wanawala watu wangu kana kwamba wanakula mkate.
Hawamwiti Yehova.
5 Lakini watajawa na hofu kubwa,+
Kwa maana Yehova yuko pamoja na kizazi cha waadilifu.
6 Ninyi waovu hujaribu kuharibu mipango ya mtu wa hali ya chini,
Lakini Yehova ni kimbilio lake.+
7 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+
Yehova anapowakusanya tena watu wake waliotekwa,
Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.
Muziki wa Daudi.
15 Ee Yehova, ni nani anayeweza kuwa mgeni katika hema lako?
Ni nani anayeweza kukaa katika mlima wako mtakatifu?+
4 Humkataa mtu yeyote anayedharauliwa,+
Lakini huwaheshimu wale wanaomwogopa Yehova.
Havunji ahadi yake, hata ikimletea hasara.*+
Yeyote anayefanya mambo hayo hatatikiswa kamwe.*+
Miktamu* ya Daudi.
16 Nilinde, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+
2 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Yehova, Chanzo changu cha wema.
3 Na watakatifu walio duniani,
Watukufu, ndio ninaopendezwa nao sana.”+
4 Wale wanaoifuatia miungu mingine huzidisha huzuni yao.+
Sitamimina kamwe matoleo yao ya vinywaji ya damu,
Wala midomo yangu haitataja majina yao.+
5 Yehova ni fungu langu, sehemu niliyogawiwa,+ na kikombe changu.+
Unaulinda urithi wangu.
6 Nimepimiwa sehemu zinazopendeza.
Naam, nimeridhika na urithi wangu.+
7 Nitamsifu Yehova, ambaye amenipa ushauri.+
Hata wakati wa usiku, mawazo yangu ya ndani kabisa* hunirekebisha.+
8 Ninamweka Yehova mbele yangu daima.+
Kwa sababu yuko mkono wangu wa kulia, sitatikiswa kamwe.*+
9 Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nafsi yangu yote ina* shangwe.
Nami ninaishi* kwa usalama.
10 Kwa maana hutaniacha* Kaburini.*+
Hutamruhusu mshikamanifu wako aone shimo.*+
11 Unanijulisha njia ya uzima.+
Sala ya Daudi.
17 Sikia sihi yangu ya kuomba haki, Ee Yehova;
Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada;
Sikiliza sala yangu ninayosema bila udanganyifu.+
2 Nawe ufanye uamuzi wa haki kwa niaba yangu;+
Macho yako na yaone yaliyo sawa.
3 Umeuchunguza moyo wangu, umenikagua wakati wa usiku;+
Umenisafisha;+
Utagundua kwamba sijapanga njama ya kutenda uovu wowote,
Na kinywa changu hakijatenda dhambi.
4 Kuhusiana na shughuli za wanadamu,
Kulingana na neno la midomo yako, ninaepuka njia za mnyang’anyi.+
5 Acha hatua zangu zibaki kwenye njia zako
Ili miguu yangu isijikwae.+
6 Ninakuita wewe, kwa sababu utanijibu,+ Ee Mungu.
Nitegee sikio lako.* Sikia maneno yangu.+
7 Onyesha upendo wako mshikamanifu kwa njia yenye kustaajabisha,+
Ee Mwokozi wa wale wanaokimbilia mkono wako wa kuume
Kutoka kwa wale wanaokuasi.
9 Nilinde kutokana na waovu wanaonishambulia,
Kutokana na maadui wangu* wanaoweza kufa ambao wananizingira.+
10 Wamekufa ganzi;*
Kwa kinywa chao wanaongea kwa kiburi;
11 Sasa wanatuzingira;+
Wanatafuta nafasi ya kutuangusha.*
12 Yeye ni kama simba anayetamani kurarua windo lake vipandevipande,
Kama mwanasimba anayenyemelea mafichoni.
13 Inuka, Ee Yehova, ukabiliane naye+ na kumwangusha chini;
Niokoe* kutoka kwa mwovu kwa kutumia upanga wako;
14 Niokoe kwa mkono wako, Ee Yehova,
Kutoka kwa watu wa ulimwengu huu,* ambao fungu lao liko katika maisha haya,+
Wale ambao unawajaza kwa vitu vizuri unavyoandaa+
Na ambao huwaachia urithi wana wao wengi.
Kwa kiongozi. Wa Daudi mtumishi wa Yehova, aliyemwambia Yehova maneno ya wimbo huu siku ambayo Yehova alimwokoa kutoka mikononi mwa maadui wake wote na kutoka mikononi mwa Sauli. Alisema:+
18 Ninakupenda, Ee Yehova, nguvu zangu.+
2 Yehova ni jabali langu na ngome yangu na Mwokozi wangu.+
Mungu wangu ni mwamba wangu,+ ninayemkimbilia,
Ngao yangu na pembe* yangu ya wokovu,* kimbilio langu salama.*+
3 Ninamlilia Yehova, anayestahili kusifiwa,
Nami nitaokolewa kutoka kwa maadui wangu.+
6 Katika taabu yangu nilimwita Yehova,
Niliendelea kumlilia Mungu wangu anisaidie.
Akiwa katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+
Na kilio changu cha kumwomba msaada kilifika masikioni mwake.+
7 Kisha dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika;+
Misingi ya milima ikasukasuka
Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
8 Moshi ulipanda kutoka katika mianzi ya pua yake,
Na moto unaoteketeza kabisa ukatoka kinywani mwake;+
Makaa ya mawe yanayowaka moto mkali yakatoka kwake.
10 Alipanda juu ya kerubi, akaja akiruka.+
Akashuka chini kwa ghafla juu ya mabawa ya kiumbe wa roho.*+
12 Kutoka katika mwangaza ulio mbele zake
Mvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto yakapasua mawingu.
13 Kisha Yehova akaanza kunguruma mbinguni;+
Aliye Juu Zaidi aliifanya sauti yake isikike+
Kwa mvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto.
15 Sakafu za vijito zikaonekana;*+
Misingi ya nchi ikafunuliwa kwa kemeo lako, Ee Yehova,
Kwa mlipuko wa pumzi kutoka katika mianzi ya pua yako.+
16 Aliunyoosha mkono wake kutoka juu;
Alinishika na kunivuta kutoka katika maji yenye kina.+
17 Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+
Kutoka kwa wale wanaonichukia, waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.+
18 Walinikabili katika siku ya msiba wangu,+
Lakini Yehova alikuwa tegemeo langu.
20 Yehova hunithawabisha kulingana na uadilifu wangu;+
21 Kwa maana nimezishika njia za Yehova,
Nami sijamwacha kwa uovu Mungu wangu.
22 Hukumu zake zote ziko mbele yangu;
Sitazipuuza sheria zake.
25 Kwa mtu mshikamanifu unatenda kwa ushikamanifu;+
Kwa mtu asiye na lawama unatenda bila lawama;+
26 Kwa walio safi unajidhihirisha mwenyewe kuwa safi,+
Lakini kwa waliopotoka unajidhihirisha mwenyewe kuwa mwenye busara.+
28 Kwa maana ni wewe unayeiwasha taa yangu, Ee Yehova,
Mungu wangu ambaye hulifanya giza langu liangaze.+
29 Kwa msaada wako ninaweza kukabiliana na kundi la wavamizi;+
Kwa nguvu za Mungu ninaweza kuupanda ukuta.+
Yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia.+
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova?+
Na ni nani aliye mwamba isipokuwa Mungu wetu?+
33 Huifanya miguu yangu iwe kama ya paa;
Hunifanya nisimame mahali palipo juu.+
34 Huizoeza mikono yangu kupigana vita;
Mikono yangu inaweza kuukunja upinde wa shaba.
35 Wewe hunipa ngao yako ya wokovu,+
Mkono wako wa kuume hunitegemeza,*
Na unyenyekevu wako hunifanya niwe mkuu.+
37 Nitawafuatia maadui wangu na kuwapita;
Sitarudi mpaka watakapoangamizwa kabisa.
38 Nitawaponda wasiweze kuinuka;+
Wataanguka chini ya miguu yangu.
39 Utanipa nguvu kwa ajili ya vita;
Utawafanya maadui wangu waanguke chini yangu.+
41 Wanalilia msaada, lakini hakuna mtu wa kuwaokoa;
Hata wanamlilia Yehova, lakini yeye hawajibu.
42 Nitawaponda wawe laini kama mavumbi katika upepo;
Nitawatupa nje kama matope barabarani.
43 Utaniokoa kutoka kwa watu wanaotafuta makosa.+
Utaniweka kuwa kiongozi wa mataifa.+
Watu ambao siwajui watanitumikia.+
44 Watanitii watakaposikia fununu tu;
Wageni watakuja wakijikunyata mbele zangu.+
45 Wageni watakosa ujasiri;*
Watakuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
46 Yehova yuko hai! Mwamba wangu na asifiwe!+
Mungu wa wokovu wangu na akwezwe.+
47 Mungu wa kweli hunilipizia kisasi;+
Huyatiisha mataifa chini yangu.
48 Yeye huniokoa kutoka kwa maadui wangu wenye hasira;
Unaniinua juu ya wale wanaonishambulia;+
Unaniokoa kutoka kwa mtu mkatili.
49 Ndiyo sababu nitakutukuza wewe miongoni mwa mataifa, Ee Yehova,+
50 Yeye hutenda matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake;*+
Humtendea mtiwa-mafuta wake kwa upendo mshikamanifu,+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
2 Siku baada ya siku zinabubujisha maneno yake,
Na usiku baada ya usiku zinafunua ujuzi.
3 Hakuna usemi, wala hakuna maneno;
Sauti zake hazisikiki.
4 Lakini sauti zake zimefika* katika dunia yote,
Na ujumbe wake umefika mpaka kwenye miisho ya dunia inayokaliwa.+
Amepiga hema mbinguni kwa ajili ya jua;
5 Ni kama bwana harusi anayetoka katika chumba chake;
Linashangilia kama mwanamume hodari anayekimbia kwenye njia yake.
6 Linachomoza kutoka mwisho mmoja wa mbingu,
Nalo huzunguka mpaka mwisho mwingine;+
Na hakuna chochote kinachojificha joto lake.
7 Sheria ya Yehova ni kamilifu,+ hurudisha nguvu.*+
Kikumbusho cha Yehova kinategemeka,+ humfanya asiye na uzoefu awe na hekima.+
8 Maagizo kutoka kwa Yehova ni ya uadilifu, huufanya moyo ushangilie;+
Amri ya Yehova ni safi, huyafanya macho yang’ae.+
9 Kumwogopa Yehova ni jambo safi,+ hudumu milele.
Hukumu za Yehova ni za kweli; zote ni za uadilifu.+
10 Zinatamanika kuliko dhahabu,
Na tamu zaidi kuliko asali,+ asali inayodondoka kutoka katika sega.
12 Ni nani anayeweza kutambua makosa?+
Nitangaze kuwa sina hatia ya dhambi nisizojua.
14 Maneno ya kinywa changu na kutafakari kwa moyo wangu
Na yakupendeze wewe,+ Ee Yehova, Mwamba wangu+ na Mkombozi wangu.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
20 Yehova na akujibu katika siku ya taabu.
Jina la Mungu wa Yakobo na likulinde.+
3 Na akumbuke matoleo yako yote ya zawadi;
Na aikubali kwa upendeleo* dhabihu yako ya kuteketezwa. (Sela)
5 Tutapaza sauti kwa shangwe kwa sababu ya matendo yako ya wokovu;+
Tutainua bendera zetu katika jina la Mungu wetu.+
Yehova na atimize maombi yako yote.
6 Sasa ninajua kwamba Yehova humwokoa mtiwa-mafuta wake.+
7 Wengine hutegemea magari ya vita na wengine farasi,+
Lakini sisi tunaliitia jina la Yehova Mungu wetu.+
8 Wamedondoka na kuanguka,
Lakini sisi tumeinuka na kurudishwa.+
9 Ee Yehova, mwokoe mfalme!+
Atatujibu siku ambayo tutaomba msaada.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
21 Ee Yehova, mfalme hushangilia kwa sababu ya nguvu zako;+
Jinsi anavyoshangilia sana kwa sababu ya matendo yako ya wokovu!+
2 Umetosheleza tamaa ya moyo wake,+
Nawe hujamnyima ombi la midomo yake. (Sela)
5 Matendo yako ya wokovu humletea utukufu mkubwa.+
Unamtunukia adhama na fahari.
7 Kwa maana mfalme anamtumaini Yehova;+
Kwa sababu ya upendo mshikamanifu wa Aliye Juu Zaidi, hatatikiswa kamwe.*+
8 Mkono wako utawapata maadui wako wote;
Mkono wako wa kuume utawapata wale wanaokuchukia.
9 Utawafanya wawe kama tanuru lenye moto mkali utakapofika wakati ulioweka wa kuwakazia uangalifu.
Yehova atawameza kwa hasira yake, na moto utawateketeza kabisa.+
10 Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani,
Na uzao wao kutoka kati ya wanadamu.
13 Inuka, Ee Yehova, katika nguvu zako.
Tutauimbia sifa* uwezo wako.
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Paa Jike wa Mapambazuko.”* Muziki wa Daudi.
22 Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?+
Kwa nini uko mbali usiweze kuniokoa,
Mbali na vilio vyangu vya maumivu makali?+
2 Mungu wangu, ninaendelea kukuita wakati wa mchana, nawe hunijibu;+
Na wakati wa usiku sinyamazi.
8 “Alijikabidhi mwenyewe kwa Yehova. Acha Yeye amwokoe!
Acha Yeye amwokoe, kwa sababu Yeye anampenda sana!”+
9 Wewe ndiye uliyenitoa tumboni,+
Ni Wewe uliyenifanya nihisi nikiwa salama kwenye matiti ya mama yangu.
10 Nimewekwa chini ya utunzaji wako* tangu nilipozaliwa;
Tangu nilipokuwa katika tumbo la mama yangu, umekuwa Mungu wangu.
13 Wanafungua vinywa vyao wazi dhidi yangu,+
Kama simba anayenguruma ambaye anararua windo lake vipandevipande.+
14 Nimemwagwa kama maji;
Mifupa yangu yote imeteguka.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae;+
Ulimi wangu unashikamana na fizi zangu;+
Unanishusha chini kwenye mavumbi ya kifo.+
16 Kwa maana mbwa wananizunguka;+
Wananizingira kama kundi la watenda maovu,+
Kama simba, wanaishambulia mikono yangu na miguu yangu.+
17 Ninaweza kuhesabu mifupa yangu yote.+
Wananitazama na kunikodolea macho.
18 Wanagawana mavazi yangu,
Nao wanalipigia kura vazi langu.+
19 Lakini wewe, Ee Yehova, usiendelee kukaa mbali.+
Wewe ni nguvu zangu; njoo haraka unisaidie.+
20 Niokoe* kutoka kwa upanga,
Uhai wangu wenye thamani* kutoka katika makucha ya* mbwa;+
21 Niokoe kutoka katika kinywa cha simba+ na pembe za ng’ombe dume wa mwituni;
Nijibu na uniokoe.
23 Ninyi mnaomwogopa Yehova, msifuni!
Enyi nyote uzao wa* Yakobo, mtukuzeni!+
Mwogopeni yeye, enyi nyote uzao wa* Israeli.
24 Kwa maana hajadharau wala kuchukizwa na mateso ya yule anayekandamizwa;+
Hajauficha uso wake kutoka kwake.+
Alipomlilia amsaidie, alisikia.+
25 Nitakusifu katika kutaniko kubwa;+
Nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanaomwogopa.
Na ufurahie maisha* milele.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Yehova.
Familia zote za mataifa zitainama chini mbele zako.+
28 Kwa maana ufalme ni wa Yehova;+
Anayatawala mataifa.
29 Watu wote wenye ufanisi* duniani watakula na kumwinamia;
Wote wanaoshuka mavumbini watapiga magoti mbele zake;
Hakuna yeyote kati yao anayeweza kuokoa uhai wao.*
30 Wazao wao watamtumikia;*
Kizazi kitakachokuja kitaambiwa kumhusu Yehova.
31 Watakuja na kusimulia uadilifu wake.
Watawaambia watu ambao bado hawajazaliwa mambo aliyofanya.
Muziki wa Daudi.
23 Yehova ni Mchungaji wangu.+
Sitakosa chochote.+
2 Hunilaza katika malisho yenye majani mengi;
Huniongoza katika njia za* uadilifu kwa ajili ya jina lake.+
4 Hata nikitembea katika bonde lenye kivuli kizito,+
Siogopi madhara yoyote,+
Kwa maana wewe uko pamoja nami;+
Fimbo yako na gongo lako hunipa uhakika.*
5 Wewe huniandalia meza mbele ya maadui wangu.+
6 Kwa hakika wema na upendo mshikamanifu utanifuatia sikuzote za maisha yangu,+
Nami nitakaa katika nyumba ya Yehova siku zangu zote.+
Muziki wa Daudi.
24 Dunia na vyote vilivyomo ni vya Yehova,+
Nchi inayozaa na wale wanaokaa ndani yake.
2 Kwa maana ameiweka imara kabisa juu ya bahari+
Na kuiweka imara kabisa juu ya mito.
3 Ni nani anayeweza kuupanda mlima wa Yehova,+
Na ni nani anayeweza kusimama mahali pake patakatifu?
4 Yeyote mwenye mikono isiyo na hatia na mwenye moyo safi,+
Ambaye hajaapa kwa uwongo kwa uhai Wangu,*
Wala kuapa kwa udanganyifu.+
6 Hiki ndicho kizazi cha wale wanaomtafuta,
Cha wale wanaoutafuta uso wako, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)
8 Mfalme huyu mtukufu ni nani?
10 Mfalme huyu mtukufu ni nani?
Yehova wa majeshi—yeye ndiye Mfalme mtukufu.+ (Sela)
Wa Daudi.
א [Aleph]
25 Nakugeukia wewe,* Ee Yehova.
ב [Beth]
Usiruhusu maadui wangu wanicheke.+
ג [Gimel]
3 Kwa hakika hakuna yeyote anayekutumaini atakayeaibishwa,+
Lakini aibu inawangoja wale wanaotenda kwa hila bila sababu.+
ד [Daleth]
ה [He]
5 Nitembeze katika kweli yako na kunifundisha,+
Kwa maana wewe ni Mungu wa wokovu wangu.
ו [Waw]
Ninakutumaini mchana kutwa.
ז [Zayin]
ח [Heth]
7 Usikumbuke dhambi na makosa niliyotenda nilipokuwa kijana.
ט [Teth]
8 Yehova ni mwema na mnyoofu.+
Ndiyo sababu yeye huwafundisha watenda dhambi njia wanayopaswa kuishi.+
י [Yod]
כ [Kaph]
10 Njia zote za Yehova ni upendo mshikamanifu na uaminifu
ל [Lamed]
11 Kwa ajili ya jina lako, Ee Yehova,+
Nisamehe kosa langu, ingawa ni kubwa.
מ [Mem]
12 Ni nani anayemwogopa Yehova?+
Atamfundisha kuhusu njia anayopaswa kuchagua.+
נ [Nun]
ס [Samekh]
ע [Ayin]
פ [Pe]
16 Nielekezee uso wako na kunionyesha kibali,
Kwa maana niko peke yangu na sina uwezo.
צ [Tsade]
17 Taabu za moyo wangu zimeongezeka;+
Niondolee maumivu yangu makali.
ר [Resh]
19 Tazama jinsi maadui wangu walivyo wengi
Na jinsi wanavyonichukia vikali.
ש [Shin]
20 Ulinde uhai wangu* na uniokoe.+
Usiruhusu niaibishwe, kwa maana nimekukimbilia wewe.
ת [Taw]
22 Ee Mungu, mwokoe* Israeli kutoka katika taabu zake zote.
Wa Daudi.
26 Unihukumu, Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika utimilifu wangu;+
Nimemtumaini Yehova bila kuyumbayumba.+
3 Kwa maana upendo wako mshikamanifu uko mbele yangu daima,
Nami ninatembea katika kweli yako.+
6 Nitanawa mikono yangu katika ukosefu wa hatia,
Nami nitapiga mwendo kuzunguka madhabahu yako, Ee Yehova,
7 Ili niifanye sauti ya utoaji shukrani isikike+
Na kutangaza kazi zako zote zinazostaajabisha.
9 Usinifagilie mbali* pamoja na watenda dhambi+
Wala kuniua pamoja na watu wakatili,*
10 Ambao mikono yao hutenda matendo ya* aibu,
Na ambao mkono wao wa kulia umejaa rushwa.
11 Lakini mimi, nitatembea katika utimilifu wangu.
Niokoe* na kunionyesha kibali.
Wa Daudi.
27 Yehova ni nuru yangu+ na wokovu wangu.
Nimwogope nani?+
Yehova ni ngome ya uhai wangu.+
Nimhofu nani?
2 Waovu waliponishambulia ili waunyafue mwili wangu,+
Wapinzani wangu na maadui wangu ndio waliojikwaa na kuanguka.
3 Hata jeshi likipiga kambi ili kunishambulia,
Moyo wangu hautaogopa.+
Hata vita vikizuka dhidi yangu,
Bado nitaendelea kuwa jasiri.
4 Nimemwomba Yehova jambo moja
—Ndilo nitakalolitafuta—
Kwamba nikae katika nyumba ya Yehova sikuzote za maisha yangu,+
Ili kuutazama uzuri wa Yehova
5 Kwa maana atanificha katika banda lake siku ya msiba;+
Atanificha mahali pa siri katika hema lake;+
Ataniweka juu kwenye mwamba.+
6 Sasa kichwa changu kiko juu sana ya maadui wangu wanaonizingira;
Nitatoa dhabihu katika hema lake kwa kelele za shangwe;
Nitamwimbia sifa* Yehova.
8 Moyo wangu umesema hivi kwa niaba yako:
“Utafute uso wangu.”
Nitautafuta uso wako, Ee Yehova.+
9 Usinifiche uso wako.+
Usimfukuze kwa hasira mtumishi wako.
Wewe ni msaidizi wangu;+
Usinitupe wala usiniache, Mungu wa wokovu wangu.
11 Nifundishe njia yako, Ee Yehova,+
Niongoze katika kijia cha unyoofu kwa sababu ya maadui wangu.
12 Usinitie mikononi mwa maadui wangu,+
Kwa maana mashahidi wa uwongo wameinuka dhidi yangu,+
Nao wanatoa vitisho vya kunitendea kwa ukatili.
13 Ningekuwa wapi ikiwa singekuwa na imani
Naam, mtumaini Yehova.
Wa Daudi.
28 Ninaendelea kukulilia wewe, Ee Yehova Mwamba wangu;+
Usiwe kama kiziwi kwangu.
2 Sikia sihi zangu ninapokulilia unisaidie
Ninapoinua mikono yangu kuelekea chumba cha ndani zaidi cha mahali pako patakatifu.+
3 Usinikokote pamoja na waovu, pamoja na wale wanaotenda mambo yanayodhuru,+
Wale wanaoongea na jirani yao maneno ya amani lakini uovu uko mioyoni mwao.+
4 Walipe kulingana na matendo yao,+
Kulingana na mazoea yao maovu.
Walipe kulingana na kazi ya mikono yao,
Kulingana na mambo waliyotenda.+
Atawabomoa kabisa naye hatawajenga.
6 Yehova na asifiwe,
Kwa maana amesikia sihi zangu za kuomba msaada.
Amenisaidia, na moyo wangu unashangilia,
Kwa hiyo nitamsifu kwa wimbo wangu.
8 Yehova ni nguvu kwa watu wake;
Yeye ni ngome, anamletea mtiwa-mafuta wake wokovu mkubwa.+
9 Waokoe watu wako, na uubariki urithi wako.+
Wachunge na kuwabeba mikononi mwako milele.+
Muziki wa Daudi.
29 Mpeni Yehova anachostahili, enyi wana wa watu hodari,
Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
2 Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili.
Mwinamieni* Yehova katika mapambo matakatifu.*
3 Sauti ya Yehova husikika juu ya maji;
Mungu mtukufu hunguruma.+
Yehova yuko juu ya maji mengi.+
4 Sauti ya Yehova ina nguvu;+
Sauti ya Yehova ina fahari.
5 Sauti ya Yehova inavunja mierezi;
Naam, Yehova anaipasua-pasua mierezi ya Lebanoni.+
7 Sauti ya Yehova hupiga kwa miali ya moto;+
8 Sauti ya Yehova huifanya nyika itetemeke;+
Yehova huifanya nyika ya Kadeshi+ itetemeke.
9 Sauti ya Yehova humfanya paa atetemeke na kuzaa
Nayo huivua kabisa misitu.+
Na wote walio katika hekalu lake husema: “Utukufu!”
10 Yehova huketi kwenye kiti cha ufalme juu ya mafuriko ya maji;*+
Yehova huketi kwenye kiti cha ufalme akiwa Mfalme milele.+
11 Yehova atawapa nguvu watu wake.+
Yehova atawabariki watu wake kwa amani.+
Muziki. Wimbo wa kuizindua nyumba. Wa Daudi.
2 Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, nawe ukaniponya.+
3 Ee Yehova, umeniinua* kutoka Kaburini.*+
Ulifanya niendelee kuwa hai; uliniokoa nisizame shimoni.*+
4 Mwimbieni sifa* Yehova, enyi washikamanifu wake,+
Lishukuruni jina lake takatifu;*+
5 Kwa sababu hasira yake ni ya muda mfupi tu,+
Huenda kukawa na kilio jioni, lakini asubuhi, kuna kilio cha shangwe.+
6 Nilipokuwa na amani, nilisema:
“Sitatikiswa kamwe.”*
7 Ee Yehova, nilipokuwa na kibali chako,* ulinifanya niwe imara kama mlima.+
Lakini ulipouficha uso wako, niliogopa.+
8 Niliendelea kukulilia wewe, Ee Yehova;+
Nami niliendelea kukusihi wewe, Ee Yehova, unionyeshe kibali.
9 Kuna faida gani nikifa,* nikishuka shimoni?*+
Je, mavumbi yatakusifu?+ Je, yatasimulia kuhusu uaminifu wako?+
10 Sikia, Ee Yehova, na unionyeshe kibali.+
Ee Yehova, uwe msaidizi wangu.+
11 Umebadili maombolezo yangu kuwa dansi;
Umenivua nguo zangu za magunia, nawe unanivisha shangwe,
12 Ili niimbe* sifa yako, nisinyamaze.
Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu milele.
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
31 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.+
Acha nisiaibishwe kamwe.+
Niokoe kwa sababu ya uadilifu wako.+
2 Nitegee sikio lako.*
Njoo haraka uniokoe.+
Uwe kwangu mlima ambao ni ngome,
Ngome ya kuniokoa.+
3 Kwa maana wewe ni jabali langu na ngome yangu;+
5 Naiweka roho yangu mikononi mwako.+
Umenikomboa, Ee Yehova, Mungu wa ukweli.*+
6 Ninawachukia wale wanaoabudu sanamu zisizo na faida, za ubatili,
Lakini mimi, ninamtumaini Yehova.
7 Nitashangilia sana kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu,
Kwa maana umeona dhiki yangu;+
Unajua mateso makali yaliyo ndani yangu.*
8 Hujanitia mikononi mwa adui,
Lakini unanifanya nisimame mahali salama.*
9 Nionyeshe kibali, Ee Yehova, kwa maana niko katika dhiki.
Maumivu makali yamefanya macho yangu yadhoofike,+ na pia mwili wangu wote.*+
Nguvu zangu zinapungua kwa sababu ya dhambi yangu;
Mifupa yangu inadhoofika.+
11 Ninadhihakiwa na maadui wangu wote,+
Hasa majirani wangu.
Na rafiki zangu wananiogopa;
Wanaponiona hadharani, wananikimbia.+
12 Wameniondoa moyoni* mwao na kunisahau, kana kwamba nimekufa;
Mimi ni kama gudulia lililovunjika.
13 Nimesikia uvumi mwingi wa uovu;
Nimezungukwa na hofu.+
14 Lakini ninakutumaini wewe, Ee Yehova.+
Ninatangaza: “Wewe ni Mungu wangu.”+
15 Siku* zangu zimo mkononi mwako.
Niokoe kutoka mikononi mwa maadui wangu na kutoka kwa wale wanaonitesa.+
16 Ifanye nuru ya uso wako imwangazie mtumishi wako.+
Niokoe kwa upendo wako mshikamanifu.
17 Ee Yehova, naomba nisiaibishwe ninapokulilia wewe.+
18 Midomo inayosema uwongo na iwe bubu,+
Midomo inayoongea kwa kiburi dhidi ya mwadilifu, kwa majivuno na dharau.
19 Jinsi wema wako ulivyo mwingi sana!+
Umewahifadhia wale wanaokuogopa,+
Nawe umeuonyesha mbele ya wanadamu wote, kwa niaba ya wale wanaokukimbilia wewe.+
21 Yehova na asifiwe,
Kwa maana kwa njia yenye kustaajabisha, amenionyesha upendo wake mshikamanifu+ katika jiji lililozingirwa.+
22 Lakini mimi nilishikwa na wasiwasi nikasema:
“Nitaangamia kutoka mbele zako.”+
Lakini ulisikia sihi zangu za kuomba msaada nilipokulilia kwa sauti.+
23 Mpendeni Yehova, enyi nyote mlio washikamanifu kwake!+
Wa Daudi. Maskili.*
32 Mwenye furaha ni mtu ambaye amesamehewa kosa lake, ambaye dhambi yake imefunikwa.*+
2 Mwenye furaha ni mtu ambaye Yehova hamwoni kuwa mwenye hatia,+
Asiye na udanganyifu katika roho yake.
3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilidhoofika kwa sababu ya kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.+
4 Kwa maana usiku na mchana mkono wako ulinilemea.*+
Nguvu zangu zilitoweka* kama mvuke katika joto kavu la kiangazi. (Sela)
5 Mwishowe nikaungama dhambi yangu kwako;
Sikufunika kosa langu.+
Nilisema: “Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.”+
Nawe ukanisamehe kosa la dhambi zangu.+ (Sela)
Ndipo hata mafuriko hayatamfikia.
7 Wewe ni mahali pangu pa kujificha;
Utanilinda nisipatwe na taabu.+
Utanizunguka kwa kelele za shangwe za ukombozi.+ (Sela)
8 “Nitakupa ufahamu na kukufundisha njia unayopaswa kufuata.+
Nitakupa ushauri jicho langu likikutazama.+
9 Usiwe kama farasi au nyumbu, asiye na uelewaji,+
Ambaye ni lazima msisimko wake udhibitiwe kwa hatamu au lijamu
Kabla hajakukaribia.”
10 Mwovu ana maumivu mengi;
Lakini mtu anayemtumaini Yehova amezungukwa na upendo Wake mshikamanifu.+
11 Furahini kwa sababu ya Yehova na kushangilia, enyi waadilifu;
Pazeni sauti kwa shangwe, ninyi nyote mlio wanyoofu moyoni.
33 Pazeni sauti kwa shangwe, enyi waadilifu, kwa sababu ya Yehova.+
Ni jambo linalofaa kwa wanyoofu kumsifu yeye.
2 Mshukuruni Yehova kwa kinubi;
Mwimbieni sifa* kwa kinanda chenye nyuzi kumi.
3 Mwimbieni wimbo mpya;+
Pigeni nyuzi kwa ustadi, na kupaza sauti kwa shangwe.
4 Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+
Na kila jambo analofanya linategemeka.
5 Anapenda uadilifu na haki.+
Dunia imejaa upendo mshikamanifu wa Yehova.+
7 Huyakusanya maji ya bahari kana kwamba ni bwawa;+
Huyaweka mawimbi makubwa ya maji katika maghala.
8 Dunia yote na imwogope Yehova.+
Wakaaji wa nchi* na wamhofu.
12 Lenye furaha ni taifa ambalo Mungu wake ni Yehova,+
Watu ambao amewachagua kuwa miliki yake mwenyewe.+
13 Yehova anatazama chini kutoka mbinguni;
Anawaona wanadamu wote.+
14 Kutoka katika makao yake,
Anawakazia macho wakaaji wa dunia.
15 Yeye ndiye anayeumba mioyo ya wote;
Huchunguza kazi zao zote.+
18 Tazama! Jicho la Yehova linawalinda wale wanaomwogopa,+
Wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu,
19 Ili awaokoe* kutoka katika kifo
Na kuwahifadhi hai wakati wa njaa kali.+
20 Tunamtarajia Yehova.
Yeye ni msaidizi wetu na ngao yetu.+
21 Mioyo yetu hushangilia kwa sababu yake,
Kwa maana tunalitumaini jina lake takatifu.+
Wa Daudi, alipojifanya mwenda wazimu+ mbele ya Abimeleki, hivi kwamba akamfukuza, naye akaenda zake.
א [Aleph]
34 Nitamsifu Yehova nyakati zote;
Sifa yake itakuwa midomoni mwangu daima.
ב [Beth]
ג [Gimel]
3 Mtukuzeni Yehova pamoja nami;+
Na tulikweze jina lake pamoja.
ד [Daleth]
4 Nilimwomba Yehova ushauri, naye akanijibu.+
Aliniokoa kutoka katika mambo yote yanayoniogopesha.+
ה [He]
5 Wale waliomtazama waling’aa;
Nyuso zao hazingeweza kuona aibu.
ז [Zayin]
6 Mtu huyo wa hali ya chini aliita, na Yehova akasikia.
Alimwokoa kutoka katika taabu zake zote.+
ח [Heth]
ט [Teth]
8 Onjeni mwone kwamba Yehova ni mwema;+
Mwenye furaha ni mtu anayemkimbilia.
י [Yod]
9 Mwogopeni Yehova, ninyi nyote watakatifu wake,
Kwa maana wale wanaomwogopa hawakosi chochote.+
כ [Kaph]
10 Hata wanasimba* wenye nguvu wamelemewa na njaa,
Lakini wale wanaomtafuta Yehova hawatakosa chochote chema.+
ל [Lamed]
11 Njooni, wanangu, nisikilizeni;
Nitawafundisha kumwogopa Yehova.+
מ [Mem]
12 Ni nani miongoni mwenu anayependa uzima
Na angependa kuishi siku nyingi njema?+
נ [Nun]
ס [Samekh]
ע [Ayin]
15 Macho ya Yehova yanawatazama waadilifu,+
Na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba msaada.+
פ [Pe]
16 Lakini uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda maovu,
Ili afutilie mbali kumbukumbu lao lote kutoka duniani.+
צ [Tsade]
ק [Qoph]
ר [Resh]
ש [Shin]
20 Anailinda mifupa yake yote;
Haujavunjwa hata mmoja.+
ת [Taw]
21 Msiba utamuua mwovu;
Wale wanaomchukia mwadilifu watahesabiwa kuwa na hatia.
22 Yehova anaukomboa uhai wa* watumishi wake;
Hakuna yeyote anayemkimbilia atakayepatikana na hatia.+
Wa Daudi.
3 Inua mkuki wako na shoka lako la vita* dhidi ya wale wanaonifuatia.+
Niambie:* “Mimi ni wokovu wako.”+
4 Wale wanaowinda uhai wangu* na waaibishwe na kufedheheshwa.+
Acha wale wanaopanga njama ya kuniangamiza wakimbie kwa aibu.
5 Na wawe kama makapi katika upepo;
Malaika wa Yehova na awafukuze.+
6 Njia yao na iwe na giza na utelezi
Malaika wa Yehova anapowafuatia.
7 Kwa maana bila sababu wameficha wavu wa kunitega;
Na bila sababu wamenichimbia shimo.
9 Lakini mimi nitashangilia kwa sababu ya Yehova;
Nitakuwa na shangwe kwa sababu ya matendo yake ya wokovu.
10 Mifupa yangu yote itasema:
“Ee Yehova, ni nani aliye kama wewe?
Unawaokoa wasio na uwezo kutoka kwa wale wanaowazidi nguvu,+
Wasio na uwezo na maskini kutoka kwa wale wanaowanyang’anya.”+
11 Mashahidi wenye nia mbaya hunikabili,+
Na kuniuliza mambo nisiyoyajua.
12 Wananilipa uovu kwa mema niliyotenda,+
Na kunifanya nihisi kama mtu aliyefiwa.
13 Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo za magunia;
Nilijitesa kwa kufunga,
Na sala yangu ilipokosa kujibiwa,*
14 Nilitembea huku na huku nikiomboleza kana kwamba ninamwombolezea rafiki au ndugu yangu;
Niliinama chini kwa huzuni, kama mtu anayemwombolezea mama yake.
15 Lakini nilipojikwaa, walishangilia na kukusanyika pamoja;
Walikusanyika pamoja ili wanivizie na kuniua;
Walinirarua vipandevipande nao hawakunyamaza.
17 Ee Yehova, utatazama tu mpaka lini?+
18 Kisha nitakushukuru katika kutaniko kubwa;+
Nitakusifu katikati ya umati wa watu.
19 Usiruhusu wale ambao ni maadui wangu bila sababu wanicheke;
Usiruhusu wale wanaonichukia bila sababu+ wakonyeze macho yao kwa hila.+
20 Kwa maana hawasemi maneno ya amani,
Lakini wanapanga njama kwa hila dhidi ya watu wenye amani nchini.+
21 Wanafungua kinywa chao wazi ili wanishtaki,
Wakisema: “Aha! Aha! Macho yetu yameliona.”
22 Ee Yehova, umeona jambo hilo. Usinyamaze.+
Ee Yehova, usikae mbali nami.+
23 Amka, inuka unitetee,
Mungu wangu, Yehova, nitetee katika kesi yangu.
24 Nihukumu kulingana na uadilifu wako,+ Ee Yehova Mungu wangu;
Usiruhusu wanicheke.
25 Wasiseme kamwe moyoni mwao: “Aha! Tulipata tulichotaka!”*
Wasiseme kamwe: “Tumemmeza.”+
26 Acha wote waaibishwe na kufedheheshwa,
Wale wanaonicheka kwa sababu ya msiba wangu.
Acha wale wanaojikweza juu yangu wavishwe aibu na fedheha.
27 Lakini acha wale wanaofurahia uadilifu wangu wapaze sauti kwa shangwe;
Na waseme daima:
“Yehova na atukuzwe, anayefurahia amani ya mtumishi wake.”+
Kwa kiongozi. Wa Daudi, mtumishi wa Yehova.
36 Dhambi huzungumza na mwovu ndani kabisa ya moyo wake;
Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.+
2 Kwa maana hujisifusifu sana machoni pake mwenyewe
Hivi kwamba hawezi kutambua kosa lake na kulichukia.+
3 Maneno ya kinywa chake yanadhuru na ni ya udanganyifu;
Haonyeshi ufahamu wowote wa kutenda mema.
4 Hupanga njama zinazodhuru hata kitandani mwake.
Hufuatia njia isiyo njema;
Hakatai lililo baya.
5 Ee Yehova, upendo wako mshikamanifu unafika mpaka mbinguni,+
Uaminifu wako mpaka mawinguni.
Unawahifadhi* wanadamu na wanyama, Ee Yehova.+
7 Jinsi upendo wako mshikamanifu ulivyo na thamani sana, Ee Mungu!+
Katika kivuli cha mabawa yako,
Wanadamu hukimbilia.+
8 Wanakunywa na kushiba vitu vinono vya* nyumba yako,+
Nawe huwanywesha kwenye kijito cha vitu vyako vinavyofurahisha.+
10 Endelea kuwatendea kwa upendo wako mshikamanifu wale wanaokujua,+
Na kuwaonyesha uadilifu wako walio wanyoofu moyoni.+
11 Usiruhusu mguu wa mwenye kiburi unikanyage
Wala mkono wa mwovu unifukuze.
12 Watenda maovu wameanguka huko;
Wamepigwa na kuangushwa chini na hawawezi kusimama.+
Wa Daudi.
א [Aleph]
2 Watanyauka haraka kama majani+
Na kusinyaa kama majani yaliyochipuka ya kijani kibichi.
ב [Beth]
4 Pata furaha tele* katika Yehova,
Naye atatosheleza tamaa za moyo wako.
ג [Gimel]
6 Ataufanya uadilifu wako ung’ae kama mapambazuko,
Na haki yako kama jua la adhuhuri.
ד [Daleth]
Usikasirishwe na mtu
Anayefanikiwa kutekeleza njama zake.+
ה [He]
ו [Waw]
10 Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawatakuwepo tena;+
Utapaangalia mahali walipokuwa,
Nao hawatakuwepo.+
ז [Zayin]
12 Mtu mwovu hupanga njama dhidi ya mwadilifu;+
Humsagia meno yake.
13 Lakini Yehova atamcheka,
Kwa maana Anajua kwamba siku yake itakuja.+
ח [Heth]
14 Waovu huchomoa panga zao na kuzikunja* pinde zao
Ili kumwangusha chini aliyekandamizwa na pia maskini,
Ili kuwachinja wale ambao njia yao imenyooka.
15 Lakini upanga wao utauchoma moyo wao wenyewe;+
Pinde zao zitavunjwa.
ט [Teth]
16 Kidogo alicho nacho mwadilifu ni bora
Kuliko wingi wa vitu walivyo navyo watu wengi waovu.+
17 Kwa maana mikono ya waovu itavunjwa,
Lakini Yehova atawategemeza waadilifu.
י [Yod]
19 Hawataaibishwa wakati wa msiba;
Wakati wa njaa kali watakuwa na chakula tele.
כ [Kaph]
20 Lakini waovu wataangamia;+
Maadui wa Yehova watatoweka kama malisho bora kabisa;
Watatoweka kama moshi.
ל [Lamed]
22 Wale Anaowabariki wataimiliki dunia,
Lakini wale Anaowalaani wataangamizwa.+
מ [Mem]
24 Hata akianguka, hataangushwa chini kabisa,+
נ [Nun]
25 Nilikuwa kijana lakini sasa nimezeeka,
Lakini sijamwona mtu yeyote mwadilifu akiwa ameachwa,+
26 Sikuzote anakopesha bila faida,+
Na watoto wake watapata baraka.
ס [Samekh]
27 Acha uovu, utende mema,+
Nawe utaishi milele.
28 Kwa maana Yehova anapenda haki,
Naye hatawaacha washikamanifu wake.+
ע [Ayin]
פ [Pe]
צ [Tsade]
32 Mwovu humtazama mwadilifu,
Akitafuta kumuua.
ק [Qoph]
34 Mtumaini Yehova na ufuate njia yake,
Naye atakukweza uimiliki dunia.
Waovu watakapoangamizwa,+ utaona jambo hilo.+
ר [Resh]
35 Nimemwona mtu mkatili, mwovu
Akisambaa kama mti wenye majani mengi katika udongo wake wa asili.+
ש [Shin]
37 Mwangalie mtu asiye na lawama,*
Na uendelee kumwangalia mnyoofu,+
Kwa maana wakati ujao wa mtu huyo utakuwa na amani.+
38 Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa;
Wakati ujao wa watu waovu utakomeshwa.+
ת [Taw]
40 Yehova atawasaidia na kuwaokoa.+
Atawanusuru kutoka kwa waovu na kuwaokoa,
Kwa sababu wanamkimbilia yeye.+
Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.
38 Ee Yehova, usinikaripie kwa hasira yako,
Wala usinirekebishe kwa ghadhabu yako.+
2 Kwa maana mishale yako imenichoma ndani kabisa,
Na mkono wako unanikandamiza chini.+
3 Mwili wangu wote ni mgonjwa kwa sababu ya hasira yako kali.
Hakuna amani katika mifupa yangu kwa sababu ya dhambi yangu.+
4 Kwa maana dhambi zangu zimetanda juu ya kichwa changu;+
Kama mzigo mzito, ni nzito sana siwezi kuzibeba.
5 Vidonda vyangu vinanuka na vina usaha
Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6 Nimesononeka na kushuka moyo kupita kiasi;
Ninatembea huku na huku mchana kutwa kwa huzuni.
8 Nimekufa ganzi na kupondeka kabisa;
Moyo wangu wenye maumivu makali unanifanya nilie kwa sauti kubwa.*
9 Ee Yehova, unajua mambo yote ninayotamani,
Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa machoni pako.
10 Moyo wangu unadundadunda, nguvu zangu zimetoweka,
Na nuru ya macho yangu imetoweka.+
11 Rafiki zangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,
Na rafiki zangu wa karibu wanasimama mbali.
12 Wale wanaotafuta uhai wangu* wanatega mitego;
Wale wanaojaribu kunidhuru wanazungumza kuhusu kuniangamiza;+
Wananong’onezana uwongo mchana kutwa.
14 Nimekuwa kama mtu asiyeweza kusikia,
Ambaye kinywa chake hakina lolote la kujitetea.
16 Kwa maana nilisema: “Acha wasinicheke
Wala kujikweza juu yangu mguu wangu ukiteleza.”
17 Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,
Na maumivu yangu yalikuwa pamoja nami daima.+
20 Walinilipa uovu kwa mema niliyotenda;
Walinipinga kwa sababu ya kufuatia mambo mema.
21 Usiniache, Ee Yehova.
Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami.+
22 Njoo haraka unisaidie,
Ee Yehova, wokovu wangu.+
Kwa kiongozi; wa Yeduthuni.*+ Muziki wa Daudi.
39 Nilisema: “Nitailinda hatua yangu
Ili niepuke kutenda dhambi kwa ulimi wangu.+
Nitakilinda kinywa changu kwa lijamu+
Maadamu mtu yeyote mwovu yuko mbele yangu.”
2 Nilinyamaza na kukaa kimya;+
Niliendelea kunyamaza hata kuhusu jambo jema,
Lakini maumivu yangu yalikuwa makali.*
3 Moyo wangu uliteketea polepole* ndani yangu.
Nilipokuwa nikiwaza sana,* moto huo uliendelea kuwaka.
Kisha ulimi wangu ukasema:
5 Kwa kweli, umefanya siku zangu ziwe chache tu;*+
Na urefu wa maisha yangu kuwa si kitu mbele zako.+
Kwa hakika kila mwanadamu, ingawa anaonekana yuko salama, si kitu ila pumzi tu.+ (Sela)
6 Kwa hakika kila mwanadamu hutembea huku na huku kama kivuli.
Hukimbia huku na huku* bila sababu.
Hurundika mali, bila kujua ni nani atakayeifurahia.+
7 Sasa basi, ninaweza kutumaini nini, Ee Yehova?
Wewe ndiye tumaini langu pekee.
8 Niokoe kutoka katika makosa yangu yote.+
Usimruhusu mpumbavu anifanye kuwa kitu cha kudharauliwa.
10 Niondolee pigo lako.
Nimedhoofika kabisa kwa sababu mkono wako unanipiga.
11 Unamrekebisha mwanadamu kwa kumwadhibu kwa sababu ya kosa lake;+
Unaharibu kabisa vitu anavyothamini sana kama nondo* anavyoharibu.
Kwa kweli kila mwanadamu ni pumzi tu.+ (Sela)
12 Sikia sala yangu, Ee Yehova,
Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada.+
Usipuuze machozi yangu.
13 Usinitazame kwa ukali ili nichangamke
Kabla sijafa* na kutoweka.”
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
40 Nilimtumaini Yehova kwa bidii,*
Naye akanitegea sikio lake na kusikia* kilio changu cha kuomba msaada.+
2 Akanipandisha kutoka katika shimo linalonguruma,
Kutoka katika matope yenye utelezi.
Akaiweka miguu yangu juu ya jabali;
Akanifanya nisimame mahali palipo imara.
3 Kisha akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,+
Asifiwe Mungu wetu.
Wengi watatazama kwa hofu
Na kumtumaini Yehova.
4 Mwenye furaha ni mtu anayemtumaini Yehova
Na ambaye hawatumaini wakaidi au watu wadanganyifu.*
5 Jinsi ulivyotenda mambo mengi sana,
Ee Yehova Mungu wangu,
Kazi zako zinazostaajabisha na mawazo yako kutuelekea.+
Hakuna yeyote anayeweza kulinganishwa nawe;+
Ikiwa ningejaribu kusimulia na kuongea kuzihusu,
Zingekuwa nyingi sana kwangu kusimulia!+
Hukuomba dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za dhambi.+
7 Kisha nikasema: “Tazama, nimekuja.
Katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa kunihusu.+
9 Ninatangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+
Tazama! Siizuii midomo yangu,+
Ee Yehova, kama unavyojua vema.
10 Siufuniki uadilifu wako moyoni mwangu.
Ninatangaza uaminifu wako na wokovu wako.
Siufichi upendo wako mshikamanifu na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+
11 Ee Yehova, usininyime rehema yako.
Upendo wako mshikamanifu na ukweli wako na unilinde daima.+
12 Misiba inayonizunguka ni mingi sana haihesabiki.+
Makosa yangu mengi yananilemea hivi kwamba siwezi kuona njia yangu;+
Ni mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,
Nami nimevunjika moyo.
13 Tafadhali, Ee Yehova, uwe tayari kuniokoa.+
Ee Yehova, njoo haraka unisaidie.+
14 Wote wanaotaka kuniua*
Na waaibishwe na kufedheheshwa.
Wale wanaofurahia msiba wangu
Na wakimbie kwa aibu.
15 Wale wanaoniambia: “Aha! Aha!”
Na washtuke kwa sababu ya aibu yao.
Wale wanaopenda matendo yako ya wokovu na waseme daima:
“Yehova na atukuzwe.”+
17 Lakini sina uwezo, nami ni maskini;
Yehova na anitunze.
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
41 Mwenye furaha ni mtu yeyote anayemjali mtu wa hali ya chini;+
Yehova atamwokoa siku ya msiba.
2 Yehova atamlinda na kumhifadhi hai.
Atatangazwa kuwa mwenye furaha duniani;+
Hutamtia kamwe mikononi mwa maadui wake ili wamtendee wapendavyo.*+
3 Yehova atamtegemeza kwenye kitanda chake cha ugonjwa;+
Wakati huo wa ugonjwa utakibadili kabisa kitanda chake.
4 Kwa maana nilisema: “Ee Yehova, nionyeshe kibali.+
Niponye,*+ kwa maana nimekutendea dhambi.”+
5 Lakini maadui wangu wanasema mambo maovu kunihusu:
“Atakufa lini jina lake litoweke?”
6 Mmoja wao akija kuniona, moyo wake husema uwongo.
Hukusanya mambo yenye kudhuru ya kusema;
Kisha hutoka nje na kuyaeneza kotekote.
7 Wote wanaonichukia wananong’onezana;
Wanapanga njama ya uovu dhidi yangu:
8 “Amepatwa na jambo linaloogopesha;
Sasa kwa kuwa yuko chini, hatainuka tena.”+
9 Hata mtu niliyekuwa na amani naye, ambaye nilimwamini,+
Aliyekuwa akila mkate wangu, amekiinua kisigino chake dhidi yangu.*+
10 Lakini wewe, Ee Yehova, nionyeshe kibali na kuniinua,
Ili niwalipize.
11 Kwa njia hii nitajua kwamba unapendezwa nami:
Adui yangu asipoweza kupaza sauti kwa ushindi dhidi yangu.+
Amina na Amina.
KITABU CHA PILI
(Zaburi 42-72)
Kwa kiongozi. Maskili* ya wana wa Kora.+
42 Kama paa anayetamani vijito vya maji,
Ndivyo ninavyokutamani, Ee Mungu.
2 Nina kiu kwa ajili ya Mungu, kwa ajili ya Mungu aliye hai.+
Nije lini na kuonekana mbele za Mungu?+
3 Machozi yangu ni chakula changu usiku na mchana;
Mchana kutwa watu wananidhihaki wakisema: “Mungu wako yuko wapi?”+
4 Ninayakumbuka mambo haya, nami naimwaga nafsi* yangu,
Kwa maana wakati fulani nilitembea pamoja na umati;
Nilikuwa nikitembea kimyakimya* mbele zao kwenda katika nyumba ya Mungu,
Kwa sauti za shangwe na shukrani,
Za umati unaofanya sherehe.+
5 Kwa nini nimesononeka?+
Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu?
6 Mungu wangu, nimesononeka.+
Ndiyo sababu ninakukumbuka,+
Kutoka katika nchi ya Yordani na vilele vya Hermoni,
Kutoka Mlima Mizari.*
7 Vilindi vya maji vinaita vilindi vya maji
Kwa sauti ya maporomoko yako ya maji.
Mawimbi yako makubwa yamenilemea.+
8 Wakati wa mchana Yehova atanipa upendo wake mshikamanifu,
Na usiku wimbo wake utakuwa pamoja nami—sala kwa Mungu wa uhai wangu.+
9 Nitamwambia Mungu, jabali langu:
“Kwa nini umenisahau?+
Kwa nini nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?”+
10 Maadui wangu wananidhihaki kwa chuki kali sana;**
Mchana kutwa wananidhihaki wakisema: “Mungu wako yuko wapi?”+
11 Kwa nini nimesononeka?
Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu?
Niokoe kutoka kwa mtu mdanganyifu na asiye mwadilifu.
2 Kwa maana wewe ni Mungu wangu, ngome yangu.+
Kwa nini umenitupa?
Kwa nini nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?+
3 Itume nuru yako na kweli yako.+
4 Kisha nitakuja kwenye madhabahu ya Mungu,+
Kwa Mungu, shangwe yangu inayofurika.
Nami nitakusifu kwa kinubi,+ Ee Mungu, Mungu wangu.
5 Kwa nini nimesononeka?
Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu?
Kwa kiongozi. Wa wana wa Kora.+ Maskili.*
44 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu wenyewe,
Mababu zetu wametusimulia,+
Mambo uliyotimiza katika siku zao,
Siku za zamani za kale.
Uliyapondaponda mataifa na kuyafukuza.+
Badala yake, waliimiliki kwa mkono wako wa kuume na uwezo wako+ na nuru ya uso wako,
Kwa maana ulipendezwa nao.+
5 Kwa nguvu zako tutawafukuza maadui wetu;+
Katika jina lako tutawakanyagia chini wale wanaoinuka dhidi yetu.+
6 Kwa maana siutumaini upinde wangu,
Na upanga wangu hauwezi kuniokoa.+
7 Ni wewe uliyetuokoa kutoka kwa maadui wetu,+
Wewe uliyewaaibisha wale wanaotuchukia.
8 Tutamsifu Mungu mchana kutwa,
Nasi tutalishukuru jina lako milele. (Sela)
9 Lakini sasa umetutupa na kutuaibisha,
Nawe huendi pamoja na majeshi yetu.
10 Unaendelea kutufanya tumkimbie adui yetu;+
Wale wanaotuchukia wanachukua chochote wanachotaka.
11 Unatutia mikononi mwao ili tunyafuliwe kama kondoo;
Umetutawanya miongoni mwa mataifa.+
13 Unatufanya kuwa shutuma kwa majirani wetu,
Kitu cha kudhihakiwa na kufanyiwa mzaha na wale wote wanaotuzunguka.
14 Unatufanya kuwa kitu cha kudharauliwa* miongoni mwa mataifa,+
Kitu cha kutikisiwa kichwa na mataifa.
15 Ninaaibika mchana kutwa,
Nami nimelemewa na aibu yangu,
16 Kwa sababu ya sauti za wale wanaonidhihaki na kunitukana,
Kwa sababu ya adui yetu anayelipiza kisasi.
17 Tumepatwa na mambo haya yote, lakini hatujakusahau,
Wala hatujavunja agano lako.+
18 Moyo wetu haujakengeuka;
Hatua zetu hazitoki katika njia yako.
19 Lakini umetuponda mahali ambapo mbwamwitu wanakaa;
Umetufunika kwa kivuli kizito.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu
Au ikiwa tutamnyooshea mungu wa kigeni mikono yetu tunaposali,
21 Je, Mungu hatagundua hilo?
Anajua siri za moyo.+
22 Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa;
Tumehesabiwa kuwa kondoo wa kuchinjwa.+
23 Amka. Kwa nini unaendelea kulala usingizi, Ee Yehova?+
Amka! Usiendelee kututupa milele.+
24 Kwa nini unauficha uso wako?
Kwa nini unasahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 Kwa maana tumeshushwa chini mavumbini;
Miili yetu imegandamizwa ardhini.+
26 Amka utusaidie!+
Tuokoe* kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Wa wana wa Kora.+ Maskili.* Wimbo wa upendo.
45 Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema.
Ninasema: “Wimbo wangu unamhusu* mfalme.”+
Ulimi wangu na uwe kalamu+ ya mnakili* stadi.+
2 Una sura nzuri kuliko wanadamu wote.
Maneno yenye fadhili hutiririka kutoka katika midomo yako.+
Ndiyo sababu Mungu amekubariki milele.+
4 Na katika fahari yako endelea mpaka ushinde;*+
Panda utetee kweli na unyenyekevu na uadilifu,+
Na mkono wako wa kulia utatimiza* mambo yanayoogopesha.
7 Ulipenda uadilifu+ na kuchukia uovu.+
Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia+ kuliko wenzako.
8 Mavazi yako yote yametiwa manukato ya manemane na udi na kida;
Kutoka katika jumba tukufu la mfalme lililotengenezwa kwa pembe za tembo, vinanda vinakufanya ushangilie.
9 Mabinti wa wafalme ni miongoni mwa wanawake wako wanaoheshimiwa.
Malkia amesimama mkono wako wa kulia, akiwa amepambwa kwa dhahabu ya Ofiri.+
10 Sikiliza, Ee binti, sikiliza kwa makini na utege sikio lako;
Wasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 Naye mfalme atautamani urembo wako,
Kwa maana yeye ni bwana wako,
Kwa hiyo mwinamie.
12 Binti ya Tiro ataleta zawadi;
Watu matajiri zaidi watatafuta kibali chako.*
13 Katika jumba la mfalme,* binti ya mfalme ana utukufu mwingi ajabu;
Mavazi yake yamepambwa kwa* dhahabu.
14 Atapelekwa kwa mfalme akiwa na mavazi yaliyofumwa kwa ustadi mkubwa.*
Mabikira wenzake wanaomfuata wanaletwa ndani mbele ya mfalme.
15 Wataletwa kwa furaha na shangwe;
Wataingia katika jumba la mfalme.
16 Wana wako watachukua mahali pa mababu zako.
Utawaweka kuwa wakuu katika dunia yote.+
17 Nitalitangaza jina lako katika vizazi vyote vijavyo.+
Ndiyo sababu mataifa yatakusifu milele na milele.
Kwa kiongozi. Wa wana wa Kora.+ Kulingana na mtindo wa Alamothi.* Wimbo.
2 Ndiyo sababu hatutaogopa, hata dunia ikibadilika,
Hata milima ikianguka katika vilindi vya bahari,+
3 Hata maji yake yakinguruma na povu lake kufurika,+
Hata milima ikitikiswa na msukosuko wake. (Sela)
4 Kuna mto ambao vijito vyake hufanya jiji la Mungu lishangilie,+
Hema la ibada la Aliye Juu Zaidi lililo takatifu na tukufu.
5 Mungu yuko katika jiji hilo;+ haliwezi kupinduliwa.
Mungu atalisaidia wakati wa mapambazuko.+
6 Mataifa yalikuwa katika msukosuko, falme zilipinduliwa;
Alipaza sauti yake, dunia ikayeyuka.+
8 Njooni mtazame matendo ya Yehova,
Jinsi alivyotenda mambo yanayostaajabisha duniani.
9 Anakomesha vita katika dunia yote.+
Anauvunja upinde na kuuvunja mkuki vipandevipande;
Anayateketeza magari ya vita motoni.*
10 “Salimuni amri na mjue kwamba mimi ni Mungu.
Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+
47 Enyi mataifa yote, pigeni makofi.
Mpigieni Mungu kelele za ushindi kwa vigelegele vya shangwe.
2 Kwa maana Yehova, Aliye Juu Zaidi, ni mwenye kuogopesha;+
Yeye ndiye Mfalme mkuu juu ya dunia yote.+
3 Huyatiisha mataifa chini yetu;
Huyaweka mataifa chini ya miguu yetu.+
5 Mungu amepanda juu kwa kelele za shangwe;
Yehova, kwa sauti ya pembe.*
6 Mwimbieni Mungu sifa,* mwimbieni sifa.
Mwimbieni sifa Mfalme wetu, mwimbieni sifa.
7 Kwa maana Mungu ni Mfalme wa dunia yote;+
Mwimbieni sifa, na mwonyeshe ufahamu.
8 Mungu amekuwa Mfalme juu ya mataifa.+
Mungu huketi kwenye kiti chake kitakatifu cha ufalme.
9 Viongozi wa mataifa wamekusanyika pamoja
Pamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu.
Kwa maana watawala wa dunia ni wa* Mungu.
Amekwezwa sana.+
Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+
48 Yehova ni mkuu na anastahili kabisa kusifiwa
Katika jiji la Mungu wetu, katika mlima wake mtakatifu.
2 Urefu wake unavutia, shangwe ya dunia yote,+
Ni Mlima Sayuni ulio mbali sana kaskazini,
Jiji la Mfalme Mkuu.+
4 Kwa maana tazama! wafalme wamekusanyika;*
Wamesonga mbele pamoja.
5 Walipoliona, walishangaa.
Wakashikwa na wasiwasi na kukimbia kwa hofu.
6 Wakaanza kutetemeka wakiwa huko,
Wakashikwa na uchungu kama wa mwanamke anayezaa.
7 Kwa upepo wa mashariki unavunjavunja meli za Tarshishi.
8 Mambo tuliyosikia, tumejionea wenyewe
Katika jiji la Yehova wa majeshi, katika jiji la Mungu wetu.
Mungu ataliimarisha kabisa milele.+ (Sela)
9 Tunautafakari upendo wako mshikamanifu, Ee Mungu,+
Katika hekalu lako.
10 Kama jina lako, Ee Mungu, sifa yako
Hufika mpaka kwenye miisho ya dunia.+
Mkono wako wa kuume umejaa uadilifu.+
12 Pigeni mwendo kuzunguka Sayuni; lizungukeni pande zote;
Hesabuni minara yake.+
13 Wekeni mioyo yenu juu ya maboma yake.*+
Kagueni minara yake yenye ngome,
Ili msimulie vizazi vijavyo kulihusu.
14 Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu+ milele na milele.
Yeye mwenyewe atatuongoza kwa umilele wote.*+
Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+
49 Sikieni hili, enyi mataifa yote.
3 Kinywa changu mwenyewe kitasema maneno ya hekima,
Na kutafakari kwa moyo wangu+ kutaonyesha kwamba nina uelewaji.
4 Nitasikiliza methali;
Nitategua kitendawili changu kwa kinubi.
6 Wale wanaotumaini mali zao+
Na kujigamba kuhusu utajiri wao mwingi,+
7 Hakuna yeyote kati yao anayeweza kamwe kumkomboa ndugu yake
Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake,+
8 (Bei ya fidia* kwa ajili ya uhai wao* ni yenye thamani sana
Hivi kwamba hawawezi kamwe kulipa);
10 Anaona kwamba hata watu wenye hekima hufa;
Wapumbavu na wasiotumia akili huangamia pamoja,+
Nao hulazimika kuwaachia wengine mali zao.+
11 Ndani yao wanatamani nyumba zao zidumu milele,
Mahema yao kizazi baada ya kizazi.
Wameyaita mashamba yao kwa majina yao.
12 Lakini mwanadamu, ingawa anaheshimiwa, hataendelea kuishi;+
Yeye si bora kuliko wanyama wanaoangamia.+
13 Hiyo ndiyo njia ya wapumbavu+
Na ya wale wanaowafuata, wanaofurahia maneno yao yasiyo na maana. (Sela)
14 Kama kondoo, wamepangiwa kwenda Kaburini.*
Kifo kitawachunga;
Wanyoofu watawatawala+ asubuhi.
16 Usiogope mtu anapotajirika,
Fahari ya nyumba yake ikiongezeka,
17 Kwa maana akifa hawezi kwenda na kitu chochote;+
Fahari yake haitashuka shimoni pamoja naye.+
18 Kwa maana wakati wa maisha yake anajipongeza mwenyewe.+
(Watu hukusifu unapopata ufanisi.)+
19 Lakini mwishowe hujiunga na kizazi cha mababu zake.
Hawataona nuru tena kamwe.
20 Mtu ambaye haelewi jambo hili, ingawa anaheshimiwa,+
Yeye si bora kuliko wanyama wanaoangamia.
Muziki wa Asafu.+
2 Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu huangaza.
3 Mungu wetu atakuja na hawezi kunyamaza.+
5 “Nikusanyieni washikamanifu wangu,
Wale wanaofanya agano pamoja nami kwa dhabihu.”+
6 Mbingu zinatangaza uadilifu wake,
Kwa maana Mungu mwenyewe ni Mwamuzi.+ (Sela)
7 “Sikilizeni, enyi watu wangu, nami nitaongea;
Israeli, nitatoa ushahidi dhidi yako.+
Mimi ni Mungu, Mungu wako.+
8 Siwakaripii kwa sababu ya dhabihu zenu,
Wala kwa sababu ya dhabihu zenu nzima za kuteketezwa ambazo daima ziko mbele zangu.+
10 Kwa maana kila mnyama wa mwituni ni wangu,+
Hata wanyama walio juu ya milima elfu moja.
11 Ninamjua kila ndege wa milimani;+
Wanyama wasio na idadi wa mbugani ni wangu.
12 Ningekuwa na njaa, nisingekwambia,
Kwa maana nchi inayozaa na kila kitu kilichomo ni changu.+
13 Je, nitakula nyama ya ng’ombe dume
Na kunywa damu ya mbuzi?+
14 Toa shukrani zikiwa dhabihu yako kwa Mungu,+
Na utimize nadhiri zako kwa Aliye Juu Zaidi;+
15 Nililie wakati wa taabu.+
Nitakuokoa, nawe utanitukuza.”+
16 Lakini Mungu atamwambia mwovu:
19 Unatumia kinywa chako kueneza mabaya,
Na udanganyifu umeshikamana na ulimi wako.+
21 Ulipofanya mambo hayo, niliendelea kunyamaza,
Kwa hiyo ukafikiri kwamba nitakuwa kama wewe.
Lakini sasa nitakukaripia,
Nami nitatangaza kesi yangu dhidi yako.+
22 Tafadhali, zingatieni jambo hili, ninyi mnaomsahau Mungu,+
Nisije nikawararua vipandevipande asiwepo yeyote wa kuwaokoa.
23 Yule anayetoa shukrani kuwa dhabihu yake ananitukuza,+
Na yule anayefuata njia iliyowekwa,
Nitamfanya aone wokovu wa Mungu.”+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi, nabii Nathani alipokuja kwake baada ya Daudi kulala na Bath-sheba.+
51 Ee Mungu, nionyeshe kibali kulingana na upendo wako mshikamanifu.+
Yafute kabisa makosa yangu kulingana na rehema zako nyingi.+
Kwa hiyo, wewe ni mwadilifu unapoongea,
Wewe ni mwenye haki katika hukumu yako.+
6 Tazama! Unapendezwa na ukweli katika utu wa ndani;+
Ufundishe utu wangu wa ndani kabisa* hekima ya kweli.
7 Nisafishe kutoka katika dhambi yangu kwa hisopo, ili niwe safi;+
Nioshe, ili niwe mweupe kuliko theluji.+
8 Acha nisikie sauti za shangwe na furaha,
Ili mifupa uliyoiponda ishangilie.+
11 Usinitupe kutoka mbele zako;*
Wala usiniondolee roho yako takatifu.
13 Nitawafundisha wakosaji njia zako,+
Ili watenda dhambi wakurudie.
14 Niokoe kutoka katika hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+
Ili ulimi wangu utangaze uadilifu wako kwa shangwe.+
15 Ee Yehova, ifungue midomo yangu,
Ili kinywa changu kitangaze sifa yako.+
17 Dhabihu zinazompendeza Mungu ni roho iliyovunjika;
18 Kwa nia yako njema litendee jiji la Sayuni jambo jema;
Zijenge kuta za Yerusalemu.
19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za uadilifu,
Dhabihu za kuteketezwa na matoleo mazima;
Kisha ng’ombe dume watatolewa kwenye madhabahu yako.+
Kwa kiongozi. Maskili.* Wa Daudi, Doegi Mwedomu alipokuja na kumwambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+
52 Kwa nini unajigamba kuhusu matendo yako maovu, ewe mwenye nguvu?+
Upendo mshikamanifu wa Mungu unadumu mchana kutwa.+
3 Unapenda uovu kuliko mema,
Kusema uwongo kuliko kusema ukweli. (Sela)
4 Unapenda kila neno linalodhuru,
Ewe ulimi mdanganyifu!
5 Ndiyo sababu Mungu atakubomoa milele na milele;+
Atakunyakua na kukurarua kutoka katika hema lako;+
Atakung’oa kutoka katika nchi ya walio hai.+ (Sela)
7 “Huyu ndiye mwanamume ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake,*+
Lakini aliutumaini utajiri wake mwingi+
8 Lakini mimi nitakuwa kama mzeituni wenye majani mengi katika nyumba ya Mungu;
Ninautumaini upendo mshikamanifu wa Mungu,+ milele na milele.
9 Nitakusifu milele kwa sababu umechukua hatua;+
Mbele ya washikamanifu wako,
Nitalitumaini jina lako,+ kwa maana ni jema.
Kwa kiongozi; katika mtindo wa Mahalathi.* Maskili.* Wa Daudi.
53 Mpumbavu* husema moyoni mwake:
“Hakuna Yehova.”+
Matendo yao maovu yamepotoka na yanachukiza;
Hakuna yeyote anayetenda mema.+
2 Lakini Mungu anawatazama wanadamu kutoka mbinguni+
Ili aone ikiwa kuna yeyote aliye na ufahamu, ikiwa kuna yeyote anayemtafuta Yehova.+
3 Wote wamekengeuka;
Wote wamepotoka.
Hakuna yeyote anayetenda mema,
Hakuna hata mmoja.+
4 Je, hakuna mtenda maovu yeyote anayeelewa?
Wanawala watu wangu kwa pupa kana kwamba wanakula mkate.
Hawamwiti Yehova.+
5 Lakini watajawa na hofu kubwa,
Hofu ambayo hawajawahi kamwe kuwa nayo,*
Kwa maana Mungu ataitawanya mifupa ya wale wanaowashambulia ninyi.*
Mtawaaibisha, kwa maana Yehova amewakataa wao.
6 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+
Yehova anapowakusanya tena watu wake waliotekwa,
Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.
Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Maskili.* Wa Daudi, Wazifu walipokuja na kumwambia Sauli: “Daudi anajificha miongoni mwetu.”+
2 Ee Mungu, isikie sala yangu;+
Sikiliza maneno ya kinywa changu.
4 Tazama! Mungu ni msaidizi wangu;+
Yehova yuko pamoja na wale wanaonitegemeza.
6 Nitakutolea dhabihu+ kwa hiari.
Nitalisifu jina lako, Ee Yehova, kwa maana ni jema.+
Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Maskili.* Wa Daudi.
2 Nisikilize na unijibu.+
Hangaiko langu linanisumbua,+
Nami nimefadhaika
3 Kwa sababu ya mambo ambayo adui anasema
Na mkazo kutoka kwa mwovu.
Kwa maana wananirundikia taabu,
Na kwa hasira wana chuki kali kunielekea.+
5 Hofu na kutetemeka hunijia,
Na woga hunishika.
6 Daima ninasema: “Laiti ningekuwa na mabawa kama ya njiwa!
Ningeruka mbali na kukaa kwa usalama.
7 Tazama! Ningekimbia na kwenda mbali sana.+
Ningekaa nyikani.+ (Sela)
8 Ningeenda haraka mahali pa kujificha
Mbali na upepo mkali, mbali na dhoruba.”
10 Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake;
Ndani yake kuna fitina na taabu.+
11 Uharibifu uko ndani yake;
Ukandamizaji na udanganyifu hauondoki kamwe katika uwanja wake.+
12 Kwa maana si adui anayenidhihaki;+
La sivyo ningevumilia.
Si adui aliyeinuka dhidi yangu;
La sivyo ningeweza kujificha.
14 Tulikuwa tukifurahia pamoja urafiki wa karibu sana;
Katika nyumba ya Mungu tulikuwa tukitembea pamoja na umati.
15 Na wapatwe na maangamizi!+
Na washuke Kaburini* wakiwa hai;
Kwa maana uovu hukaa miongoni mwao na ndani yao.
16 Lakini mimi, nitamlilia Mungu,
Na Yehova ataniokoa.+
Watakataa kubadilika,
Wale ambao hawajamwogopa Mungu.+
21 Maneno yake ni laini kuliko siagi,+
Lakini mzozo umo moyoni mwake.
Maneno yake ni laini kuliko mafuta,
Lakini ni panga zilizochomolewa.+
Hataruhusu kamwe mwadilifu aanguke.*+
23 Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha chini kwenye shimo lenye kina kabisa.+
Watu hao wenye hatia ya damu ambao ni wadanganyifu hawataishi nusu ya siku zao.+
Lakini mimi, nitakutumaini wewe.
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Njiwa Mnyamavu Aliye Mbali.” Wa Daudi. Miktamu.* Wafilisti walipomkamata kule Gathi.+
56 Nionyeshe kibali, Ee Mungu, kwa sababu mwanadamu anayeweza kufa ananishambulia.*
Mchana kutwa wanaendelea kunipiga vita na kunikandamiza.
2 Maadui wangu wanajaribu mchana kutwa kuning’ata;
Wengi wanapigana nami kwa kiburi.
3 Ninapoogopa,+ ninakutumaini wewe.+
4 Katika Mungu—ninayelisifu neno lake—
Katika Mungu ninaweka tumaini langu; siogopi.
Mwanadamu ambaye ni duni tu atanifanya* nini?+
5 Mchana kutwa wanavuruga mambo yangu;
Jambo pekee wanalowazia ni kunidhuru.+
7 Wakatae kwa sababu ya uovu wao.
Yaangushe mataifa kwa hasira yako, Ee Mungu.+
8 Unafuatia kutangatanga kwangu.+
Yakusanye machozi yangu katika kiriba chako cha ngozi.+
Je, hayajaandikwa katika kitabu chako?+
9 Maadui wangu watakimbia siku nitakayoomba msaada.+
Nina hakika kuhusu jambo hili: Mungu yuko upande wangu.+
10 Katika Mungu—ninayelisifu neno lake—
Katika Yehova—ninayelisifu neno lake—
11 Katika Mungu ninaweka tumaini langu; siogopi.+
Mwanadamu ambaye ni duni tu atanifanya nini?+
13 Kwa maana umeniokoa kutoka katika kifo+
Na kuizuia miguu yangu isijikwae,+
Ili nitembee mbele za Mungu katika nuru ya walio hai.+
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.* Alipomkimbia Sauli na kuingia pangoni.+
57 Nionyeshe kibali, Ee Mungu, nionyeshe kibali,
Kwa maana ninakukimbilia,+
Ninakimbilia kivuli cha mabawa yako mpaka matatizo haya yapite.+
2 Ninamlilia Mungu Aliye Juu Zaidi,
Mungu wa kweli, anayeyakomesha kwa ajili yangu.
3 Atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa.+
Atamtamausha yule anayejaribu kuning’ata. (Sela)
Mungu atatuma upendo wake mshikamanifu na uaminifu wake.+
4 Nimezungukwa na simba;+
Nimelazimika kulala miongoni mwa watu wanaotaka kuninyafua,
Ambao meno yao ni mikuki na mishale
Na ambao ulimi wao ni upanga mkali.+
5 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+
Wamechimba shimo mbele yangu,
Lakini wao wenyewe wameanguka ndani yake.+ (Sela)
7 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu,+
Moyo wangu uko imara.
Nitaimba na kupiga muziki.
8 Amka, utukufu wangu.
Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.
Nitayaamsha mapambazuko.+
10 Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkubwa, uko juu kama mbingu,+
Na uaminifu wako, unafika mpaka angani.
11 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.*
58 Je, mnaweza kuzungumza kuhusu uadilifu wakati mmenyamaza?+
Je, mnaweza kuhukumu kwa unyoofu, enyi wanadamu?+
3 Waovu wanakengeuka* tangu kuzaliwa;
Ni wakaidi, waongo tangu wanapozaliwa.
4 Sumu yao ni kama sumu ya nyoka;+
Wao ni viziwi kama swila anayeziba sikio lake.
5 Hataisikiliza sauti ya wanaomchezesha,
Hata wafanye uchawi kwa ustadi kadiri gani.
6 Ee Mungu, yavunje meno yao vinywani mwao!
Yavunje mataya ya hawa simba,* Ee Yehova!
7 Na watoweke kama maji yanayotiririka na kwenda zake.
Mungu na aukunje upinde wake na kuwaangusha kwa mishale yake.
8 Na wawe kama konokono anayeyeyuka anapotembea;
Kama mtoto anayefia tumboni mwa mwanamke, mtoto asiyeona jua kamwe.
9 Kabla vyungu vyenu vya kupikia havijapata moto wa kuni za mkwamba,
Atazifagilia mbali kuni zenye unyevu na zinazowaka moto, kama kwa kimbunga.+
11 Kisha watu watasema: “Kwa hakika kuna thawabu kwa ajili ya mwadilifu.+
Kwa hakika kuna Mungu anayehukumu duniani.”+
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.* Sauli alipowatuma watu waichunguze nyumba ya Daudi* ili wamuue.+
2 Niokoe kutoka kwa wale wanaotenda uovu,
Na uniokoe kutoka kwa watu wakatili.*
3 Tazama! Wananivizia;+
Wanaume wenye nguvu wananishambulia
Lakini si kwa sababu nimeasi au kutenda dhambi,+ Ee Yehova.
4 Ingawa sikutenda kosa lolote, wanakimbia na kujitayarisha kunishambulia.
Inuka ninapokuita, uone.
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova Mungu wa majeshi, ni Mungu wa Israeli.+
Amka uyakazie uangalifu mataifa yote.
Usiwaonyeshe rehema wasaliti wowote wenye nia ya kudhuru.+ (Sela)
7 Tazama kinachomwagika* kutoka katika kinywa chao;
Midomo yao ni kama panga,+
Kwa maana wanauliza: “Ni nani anayesikiliza?”+
10 Mungu anayenitendea kwa upendo mshikamanifu atanisaidia;+
Mungu ataniwezesha niwatazame maadui wangu wakishindwa.+
11 Usiwaue, ili watu wangu wasisahau.
Kwa nguvu zako wafanye watangetange;
Waangushe, Ee Yehova, ngao yetu.+
12 Kwa sababu ya dhambi ya kinywa chao, neno la midomo yao,
Kiburi chao na kiwanase,+
Kwa sababu ya matusi na udanganyifu wanaosema.
13 Waangamize kwa hasira yako kali;+
Waangamize kabisa, ili wasiwepo tena;
Wafanye wajue kwamba Mungu anatawala katika Yakobo na mpaka kwenye miisho ya dunia.+ (Sela)
15 Acha watangetange wakitafuta chakula;+
Usiwaruhusu washibe au kupata makao.
16 Lakini mimi, nitaimba kuhusu nguvu zako;+
Asubuhi nitatangaza kwa shangwe kuhusu upendo wako mshikamanifu.
17 Ee Nguvu zangu, nitakuimbia sifa,*+
Kwa maana wewe Mungu ni kimbilio langu salama, Mungu unayenitendea kwa upendo mshikamanifu.+
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Yungiyungi la Kikumbusho.” Miktamu.* Wa Daudi. Wa kufundisha. Alipopigana na Aram-naharaimu na Aram-Soba, kisha Yoabu akarudi na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi.+
60 Ee Mungu, ulitukataa; ulipenya katika vikosi vyetu vya ulinzi.+
Ulitukasirikia; lakini sasa tupokee tena!
2 Uliifanya dunia itetemeke; uliipasua ikafunguka.
Ziba nyufa zake, kwa maana inaporomoka.
3 Uliwafanya watu wako wateseke.
Ulitufanya tunywe divai inayosababisha tuyumbeyumbe.+
4 Wape* ishara wale wanaokuogopa
Wakimbie na kuukwepa upinde. (Sela)
5 Ili wapendwa wako waokolewe,
Tuokoe kwa mkono wako wa kuume na utujibu.+
6 Mungu ameongea katika utakatifu wake:*
7 Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu,+
Na Efraimu ni kofia ya kukinga* kichwa changu;
Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+
8 Moabu ni beseni langu la kuogea.+
Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+
Nitapaza sauti kwa ushindi juu ya Ufilisti.”+
9 Ni nani atakayenipeleka kwenye jiji lililozingirwa?*
Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?+
10 Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetukataa,
Mungu wetu, ambaye haendi tena na majeshi yetu?+
11 Tusaidie katika taabu yetu,
Kwa maana wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote.+
Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Wa Daudi.
61 Ee Mungu, sikia kilio changu cha kuomba msaada.
Sikiliza sala yangu.+
Niongoze kwenye mwamba ulio juu kuliko mimi.+
3 Kwa maana wewe ni kimbilio langu,
Mnara ulio imara unaonilinda dhidi ya adui.+
5 Kwa maana wewe, Ee Mungu, umesikia nadhiri zangu.
Umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.+
6 Utamwongezea mfalme siku za maisha yake,+
Na miaka yake itatoka kizazi hadi kizazi.
7 Ataketi kwenye kiti cha ufalme* milele mbele za Mungu;+
Mpe upendo wako mshikamanifu na uaminifu, ili vimlinde.+
Kwa kiongozi; wa Yeduthuni.* Muziki wa Daudi.
62 Kwa kweli, ninamngojea Mungu kimyakimya.
Wokovu wangu unatoka kwake.+
2 Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;*+
Kamwe, sitatikiswa sana.+
3 Mtaendelea mpaka lini kumshambulia mtu ili kumuua?+
Ninyi nyote ni hatari kama ukuta ulioinama, ukuta wa mawe unaokaribia kuanguka.*
4 Kwa maana wanashauriana ili kumwangusha kutoka katika cheo chake cha juu;*
Wanafurahia kusema uwongo.
Kwa kinywa chao wanabariki, lakini ndani yao wanalaani.+ (Sela)
6 Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;
Sitatikiswa kamwe.+
7 Wokovu wangu na utukufu wangu unamtegemea Mungu.
Mwamba wangu imara, kimbilio langu, ni Mungu.+
8 Mtumainini nyakati zote, enyi watu.
Mwageni mioyo yenu mbele zake.+
Mungu ni kimbilio letu.+ (Sela)
9 Wanadamu ni pumzi tu,
Wana wa binadamu ni njozi ya uwongo.+
Wanapowekwa pamoja kwenye mizani, ni wepesi kuliko pumzi.+
10 Msitegemee upunjaji
Wala kuwa na matumaini ya uwongo katika unyang’anyi.
Mali zako zikiongezeka, usizikazie moyoni mwako.+
11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimelisikia jambo hili:
Kwamba nguvu ni za Mungu.+
12 Pia upendo mshikamanifu ni wako, Ee Yehova,+
Kwa maana unamlipa kila mtu kulingana na matendo yake.+
Muziki wa Daudi, alipokuwa katika nyika ya Yuda.+
63 Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+
Nina kiu kwa ajili yako.+
2 Kwa hiyo nimekutazama mahali patakatifu;
Nimeziona nguvu zako na utukufu wako.+
4 Basi nitakusifu maisha yangu yote;
Katika jina lako nitaiinua mikono yangu.
5 Nimeridhika na fungu bora ambalo ni zuri kabisa,*
Kwa hiyo kinywa changu kitakusifu kwa midomo yenye shangwe.+
6 Ninakukumbuka wewe nikiwa kitandani mwangu;
Ninatafakari kukuhusu katika makesha ya usiku.+
8 Ninashikamana nawe;
Mkono wako wa kuume hunishika kwa nguvu.+
9 Lakini wale wanaotaka kuniua*
Watashuka katika sehemu zenye kina zaidi za dunia.
10 Watatiwa katika nguvu za upanga;
Watakuwa chakula cha mbwamwitu.*
11 Lakini mfalme atashangilia kwa sababu ya Mungu.
Kila mtu anayeapa katika jina la Mungu atashangilia,*
Kwa maana kinywa cha wale wanaosema uwongo kitanyamazishwa.
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
64 Ee Mungu, sikia sauti yangu ninapokusihi.+
Ulinde uhai wangu kutokana na hofu ya adui.
2 Nikinge kutokana na njama za siri za waovu,+
Kutoka kwa umati wa watenda maovu.
3 Wanaunoa ulimi wao kama upanga;
Wanayalenga maneno yao ya ukatili kama mishale,
4 Ili wampige mtu asiye na hatia wakiwa mafichoni;
Wanampiga ghafla, bila kuogopa.
5 Wanashikamana sana na kusudi lao ovu;*
Wanazungumzia jinsi ya kuficha mitego yao.
Wanasema: “Ni nani atakayeiona?”+
6 Wanatafuta njia mpya za kutenda uovu;
Wanatunga kwa siri mbinu zao za ujanja;+
Fikira zilizo ndani ya moyo wa kila mmoja wao hazieleweki kamwe.
7 Lakini Mungu atawapiga mishale;+
Watajeruhiwa kwa ghafla na mshale.
8 Ulimi wao wenyewe utasababisha waanguke;+
Wote wanaowatazama watatikisa kichwa.
9 Ndipo watu wote wataogopa,
Nao watatangaza mambo ambayo Mungu ametenda,
Nao watayafahamu matendo yake.+
10 Mwadilifu atashangilia kwa sababu ya Yehova na kumkimbilia;+
Wote walio wanyoofu moyoni watashangilia.*
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo.
2 Ee Msikiaji wa sala, watu wa kila aina* watakujia.+
4 Mwenye furaha ni yule unayemchagua na kumleta karibu
Ili akae katika nyua zako.+
5 Utatujibu kwa matendo ya uadilifu yanayoogopesha,+
Ee Mungu wa wokovu wetu;
Wewe ndiye Tegemeo la miisho yote ya dunia+
Na wa wale walio mbali ng’ambo ya bahari.
6 Uliimarisha kabisa milima kwa nguvu zako;
Umevaa uwezo.+
8 Wale wanaokaa sehemu za mbali wataogopeshwa na ishara zako;+
Utawafanya wale wanaoishi upande wa mashariki mpaka upande wa magharibi wapaze sauti kwa shangwe.
Kijito kinachotoka kwa Mungu kimejaa maji;
Unawapa nafaka,+
Kwa maana hivyo ndivyo ulivyoitayarisha dunia.
10 Unajaza maji katika mitaro yake na kusawazisha udongo wake uliolimwa;*
Unailainisha kwa manyunyu ya mvua; unabariki mimea yake.+
Yanapaza sauti kwa ushindi, naam, yanaimba.+
Kwa kiongozi. Wimbo. Muziki.
66 Mpazieni Mungu sauti ya ushindi, dunia yote.+
2 Liimbieni sifa* jina lake tukufu.
Tukuzeni sifa yake.+
3 Mwambieni Mungu: “Kazi zako zinaogopesha kwelikweli!+
Kwa sababu ya nguvu zako nyingi,
Maadui wako watajikunyata mbele zako.+
5 Njooni mwone kazi za Mungu.
Mambo aliyowatendea wanadamu yanaogopesha.+
Huko tulishangilia kwa sababu yake.+
7 Anatawala milele+ kwa nguvu zake.
Macho yake yanachunguza mataifa.+
Wale ambao ni wakaidi hawapaswi kujikweza.+ (Sela)
8 Msifuni Mungu wetu, enyi mataifa,+
Sauti ya sifa yake na isikiwe.
10 Kwa maana umetuchunguza, Ee Mungu;+
Umetusafisha kama fedha inavyosafishwa.
11 Ulituingiza katika wavu wa kuwindia;
Ulitutwika mzigo mzito.*
12 Ulimruhusu mwanadamu anayeweza kufa apande juu yetu;*
Tulipita motoni na katika maji;
Kisha ukatuleta mahali penye kitulizo.
13 Nitaingia katika nyumba yako nikiwa na dhabihu nzima za kuteketezwa;+
Nitatimiza nadhiri zangu kwako+
14 Ambazo midomo yangu iliahidi+
Na kinywa changu kilisema nilipokuwa katika taabu.
15 Nitakutolea dhabihu za kuteketezwa za wanyama waliononeshwa
Pamoja na moshi wa dhabihu za kondoo dume.
Nitatoa ng’ombe dume pamoja na mbuzi dume. (Sela)
16 Njooni msikilize, ninyi nyote mnaomwogopa Mungu,
Nami nitawaambia mambo aliyonitendea.+
17 Nilimwita kwa kinywa changu
Na kumtukuza kwa ulimi wangu.
18 Ikiwa nilihifadhi moyoni mwangu jambo lolote linalodhuru,
Yehova hangenisikia.+
20 Asifiwe Mungu, ambaye hakukataa sala yangu
Wala kuninyima upendo wake mshikamanifu.
Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Muziki. Wimbo.
67 Mungu atatuonyesha kibali na kutubariki;
Atatuangazia nuru ya uso wake+ (Sela)
3 Mataifa na yakusifu wewe, Ee Mungu;
Mataifa yote na yakusifu.
Utayaongoza mataifa ya dunia. (Sela)
5 Mataifa na yakusifu, Ee Mungu;
Mataifa yote na yakusifu wewe.
Kwa kiongozi. Wa Daudi. Muziki. Wimbo.
68 Mungu na ainuke, maadui wake na watawanyike,
Wale wanaomchukia na wakimbie kutoka mbele zake.+
2 Wapeperushe mbali kama moshi unavyopeperushwa;
Kama nta inavyoyeyuka karibu na moto,
Waovu na waangamie vivyo hivyo kutoka mbele za Mungu.+
3 Lakini waadilifu na washangilie;+
Na wafurikwe na shangwe mbele za Mungu;
Na wafurahi na kushangilia.
4 Mwimbieni Mungu; liimbieni sifa* jina lake.+
Mwimbieni Yule anayepanda kupitia jangwa tambarare.*
Jina lake ni Yah!*+ Shangilieni mbele zake!
Lakini ni lazima watu wakaidi* waishi katika nchi iliyokauka.+
8 Dunia ilitetemeka;+
Mbingu zilinyesha* mvua kwa sababu ya Mungu;
Huu Mlima Sinai ulitetemeka kwa sababu ya Mungu, Mungu wa Israeli.+
9 Ulisababisha mvua kubwa inyeshe, Ee Mungu;
Uliwatia nguvu tena watu wako waliochoka.*
10 Walikaa katika kambi yako yenye mahema;+
Kwa wema wako, uliwaandalia maskini, Ee Mungu.
11 Yehova anatoa amri;
Wanawake wanaotangaza habari njema ni jeshi kubwa.+
12 Wafalme na majeshi yao wanakimbia,+ wanakimbia!
Mwanamke anayebaki nyumbani anagawiwa nyara.+
13 Ingawa ninyi wanaume mlikuwa mkilala katikati ya mioto kambini,*
Kutakuwa na mabawa ya njiwa yaliyofunikwa kwa fedha,
Yenye manyoya ya dhahabu bora.*
16 Enyi milima yenye vilele, kwa nini mnautazama kwa wivu,
Kwa kweli, Yehova atakaa huko milele.+
17 Magari ya Mungu ya vita ni makumi ya maelfu, maelfu kwa maelfu.+
Yehova ametoka Sinai na kuingia mahali patakatifu.+
18 Ulipanda juu;+
Ulichukua mateka;
Ulichukua wanaume kuwa zawadi,+
Naam, hata walio wakaidi,+ ili ukae miongoni mwao, Ee Yah Mungu.
19 Na asifiwe Yehova, anayetubebea mzigo wetu kila siku,+
Mungu wa kweli wa wokovu wetu. (Sela)
20 Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu anayeokoa;+
Na Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu huokoa kutoka katika kifo.+
21 Naam, Mungu atapondaponda vichwa vya maadui wake,
Utosi wenye nywele wa mtu yeyote anayeendelea kuwa na* hatia.+
22 Yehova amesema: “Nitawarudisha kutoka Bashani;+
Nitawarudisha kutoka katika vilindi vya bahari,
23 Ili mguu wako ufunikwe na damu+
Na ulimi wa mbwa wako upate fungu lake kutoka kwa maadui.”
24 Wanaona misafara yako, Ee Mungu,
Misafara ya Mungu wangu, Mfalme wangu, inayoingia mahali patakatifu.+
25 Waimbaji wanatangulia mbele, wanamuziki wanaopiga vinanda wanawafuata;+
Katikati yao kuna wanawake vijana wakipiga matari.+
26 Katika umati uliokutanika,* msifuni Mungu;
Msifuni Yehova, enyi mnaotoka katika Chemchemi ya Israeli.+
27 Huko Benjamini,+ aliye mdogo zaidi, anawatiisha,
Pia wakuu wa Yuda pamoja na umati wao wenye kelele,
Wakuu wa Zabuloni, wakuu wa Naftali.
28 Mungu wako ameamuru kwamba utakuwa na nguvu.
Onyesha nguvu zako, Ee Mungu, wewe ambaye umetenda kwa niaba yetu.+
30 Wakemee wanyama wa mwituni walio kwenye matete,
Kusanyiko la ng’ombe dume+ na ndama wao,
Mpaka mataifa yatakapoinama chini yakileta* vipande vya fedha.
Lakini anayatawanya mataifa yanayopenda vita.
33 Yule anayepanda mbingu ya kale kati ya mbingu.+
Tazama! Hunguruma kwa sauti yake, sauti yake yenye nguvu.
34 Tambueni nguvu za Mungu.+
Fahari yake iko juu ya Israeli,
Na nguvu zake ziko angani.*
35 Mungu anaogopesha kutoka katika mahali pake patakatifu penye utukufu.+
Yeye ni Mungu wa Israeli,
Anayewapa watu uwezo na nguvu.+
Asifiwe Mungu.
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Wa Daudi.
69 Niokoe, Ee Mungu, kwa maana maji yanahatarisha uhai wangu.*+
2 Nimezama chini katika matope yenye kina, mahali pasipo na udongo mgumu.+
Nimefika katika maji yenye kina,
Na kijito kinachotiririka haraka kimenifagilia mbali.+
3 Nimechoka kupaza sauti;+
Koo langu limekauka.
Macho yangu yamechoka nikimngojea Mungu wangu.+
4 Wale wanaonichukia bila sababu+
Ni wengi sana kuliko nywele za kichwa changu.
Wale wanaotaka kuniangamiza,
Maadui wangu wenye hila,* wamekuwa wengi.
Nililazimishwa kurudisha kitu ambacho sikuiba.
5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu,
Na hatia yangu haijafichika mbele zako.
6 Acha wale wanaokutumaini wasiaibishwe kwa sababu yangu,
Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.
Wale wanaokutafuta na wasifedheheshwe kwa sababu yangu,
Ee Mungu wa Israeli.
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,
Mgeni kwa wana wa mama yangu.+
11 Nilipoyafanya magunia kuwa mavazi yangu,
Nikawa kitu cha kudharauliwa nao.*
12 Wale wanaoketi kwenye lango la jiji huzungumza kunihusu,
Na walevi huimba juu yangu katika nyimbo zao.
13 Lakini sala yangu na ikufikie,
Ee Yehova, kwa wakati unaofaa.+
Katika upendo wako mwingi mshikamanifu, Ee Mungu,
Nijibu kwa matendo yako hakika ya wokovu.+
14 Niokoe kutoka katika matope;
Usiache nizame.
Niokoe kutoka kwa wale wanaonichukia
Na kutoka katika maji yenye kina.+
15 Usiache mafuriko yenye kasi yanifagilie mbali,+
Wala kilindi kinimeze,
16 Nijibu, Ee Yehova, kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mwema.+
Nijibu haraka, kwa maana ninataabika.+
18 Nikaribie uniokoe;*
Nikomboe kwa sababu ya maadui wangu.
19 Unajua shutuma yangu na aibu yangu na fedheha yangu.+
Unawaona maadui wangu wote.
20 Shutuma imeuvunja moyo wangu, na jeraha haliwezi kuponywa.*
Nilitarajia kuhurumiwa, lakini sikuhurumiwa hata kidogo,+
Nilitarajia kupata watu wa kunifariji, lakini sikupata yeyote.+
22 Meza yao na iwe mtego kwao,
Na ufanisi wao uwe kitu cha kuwanasa.+
23 Acha macho yao yatiwe giza wasiweze kuona,
Na ufanye viuno vyao vitetemeke daima.
26 Kwa maana wanamfuatia yule uliyempiga,
Nao huendelea kusimulia kuhusu maumivu ya wale uliowajeruhi.
27 Ongeza hatia zaidi juu ya hatia yao,
Nao wasiwe na fungu lolote katika uadilifu wako.
29 Lakini ninateseka, nami nina maumivu.+
Ee Mungu, nguvu zako za kuokoa na zinilinde.
30 Nitaliimbia sifa jina la Mungu,
Nami nitamtukuza kwa kutoa shukrani.
31 Jambo hilo litampendeza Yehova kuliko ng’ombe dume,
Kuliko ng’ombe dume mchanga mwenye pembe na kwato.+
32 Wapole wataona jambo hilo na kushangilia.
Mioyo yenu na ihuishwe, ninyi mnaomtafuta Mungu.
34 Mbingu na dunia na zimsifu,+
Bahari na kila kitu kinachoogelea ndani yake.
35 Kwa maana Mungu ataliokoa Sayuni+
Naye atayajenga upya majiji ya Yuda,
Nao watakaa humo na kuimiliki.*
Kwa kiongozi. Wa Daudi, wa kukumbusha.
70 Ee Mungu, niokoe;
Ee Yehova, njoo haraka unisaidie.+
2 Wale wanaotaka kuniua*
Na waaibishwe na kufedheheshwa.
Wale wanaofurahia msiba wangu
Na wakimbie kwa aibu.
3 Wale wanaosema: “Aha! Aha!”
Na wakimbizwe kwa aibu.
4 Lakini acha wale wanaokutafuta
Wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.+
Wale wanaopenda matendo yako ya wokovu na waseme daima:
“Mungu na atukuzwe!”
Wewe ni msaidizi wangu na mwokozi wangu.+
Ee Yehova, usikawie.+
71 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.
Usiache niaibishwe kamwe.+
2 Niokoe na kuninusuru kwa uadilifu wako.
Nitegee sikio lako* na uniokoe.+
3 Uwe ngome ya mwamba kwangu
Ambamo ninaweza kuingia sikuzote.
Toa amri ya kuniokoa,
Kwa maana wewe ni jabali langu na ngome yangu.+
4 Ee Mungu wangu, niokoe kutoka mikononi mwa mwovu,+
Kutoka katika makucha ya mkandamizaji asiyetenda haki.
5 Kwa maana wewe ni tumaini langu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova;
6 Nimekutegemea tangu nilipozaliwa;
Wewe ndiye uliyenitoa tumboni mwa mama yangu.+
Ninakusifu daima.
7 Nimekuwa kama muujiza kwa watu wengi,
Lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 Kinywa changu kimejaa sifa zako;+
Mchana kutwa ninasimulia kuhusu fahari yako.
10 Maadui wangu wanasema mambo mabaya kunihusu,
Na wale wanaotaka kuniua* wanapanga njama pamoja,+
11 Wakisema: “Mungu amemwacha.
Mkimbizeni na kumkamata, kwa maana hakuna yeyote wa kumwokoa.”+
12 Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami.
Ee Mungu wangu, njoo haraka unisaidie.+
13 Wale wanaonipinga
Na waaibishwe na kuangamia.+
Wale wanaonitakia msiba
Na wafunikwe na aibu na fedheha.+
14 Lakini mimi, nitaendelea kungoja;
Nitakusifu hata zaidi.
15 Kinywa changu kitasimulia uadilifu wako,+
Mchana kutwa kitasimulia matendo yako ya wokovu,
16 Nitakuja na kutangaza matendo yako yenye nguvu,
Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova;
Nitatangaza uadilifu wako, wako peke yako.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu nilipokuwa kijana,+
Na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako zinazostaajabisha.+
18 Ee Mungu, hata nikizeeka na kuwa na mvi, usiniache.+
19 Uadilifu wako, Ee Mungu, unafika vileleni;+
Umetenda mambo makuu;
Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?+
20 Ingawa umenifanya nipate taabu nyingi na misiba mingi,+
Nihuishe tena;
21 Ongeza ukuu wangu
Nizunguke na kunifariji.
22 Kisha nitakusifu kwa zeze
Kwa sababu ya uaminifu wako, Ee Mungu wangu.+
Nitaimba sifa zako* kwa kinubi,
Ee Mtakatifu wa Israeli.
24 Ulimi wangu utaongea* kuhusu uadilifu wako mchana kutwa,+
Kwa maana wale wanaotaka kuniangamiza wataaibishwa na kufedheheshwa.+
Zaburi Inayomhusu Sulemani.
72 Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako,
Na umzawadie mwana wa mfalme uadilifu wako.+
2 Na atetee kesi ya watu wako kwa uadilifu,
Na ya watu wako wa hali ya chini kwa haki.+
3 Milima na iwaletee watu amani,
Na vilima vilete uadilifu.
4 Na awalinde* watu wa hali ya chini miongoni mwa mataifa,
Na awaokoe watoto* wa mtu maskini,
Na amponde mpunjaji.+
6 Atakuwa kama mvua inayonyeshea majani yaliyofyekwa,
Kama manyunyu ya mvua yanayoinywesha dunia.+
7 Katika siku zake mwadilifu atasitawi,*+
Na amani itakuwa nyingi+ mpaka mwezi utakapokuwa haupo tena.
9 Wakaaji wa jangwani watainama chini mbele yake,
Na maadui wake wataramba mavumbi.+
10 Wafalme wa Tarshishi na wa visiwa watalipa ushuru.+
Wafalme wa Sheba na wa Seba watatoa zawadi.+
11 Wafalme wote watainama chini mbele yake,
Na mataifa yote yatamtumikia.
12 Kwa maana atamwokoa maskini anayelilia msaada,
Pia mtu wa hali ya chini na yeyote ambaye hana msaidizi.
13 Atamhurumia mtu wa hali ya chini na maskini,
Naye ataokoa uhai wa* maskini.
14 Atawaokoa* kutoka katika ukandamizaji na ukatili,
Na damu yao itakuwa na thamani machoni pake.
15 Na aishi na kupewa dhahabu ya Sheba.+
Sala na zitolewe daima kwa ajili yake,
Na abarikiwe mchana kutwa.
16 Kutakuwa na nafaka nyingi duniani;+
Itafurika juu ya milima.
17 Jina lake na lidumu milele,+
Na lisitawi maadamu jua lipo.
Watu na wajipatie baraka kupitia yeye;+
Mataifa yote na yamtangaze kuwa mwenye furaha.
Amina na Amina.
20 Huo ndio mwisho wa sala za Daudi, mwana wa Yese.+
KITABU CHA TATU
(Zaburi 73-89)
Muziki wa Asafu.+
73 Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio safi moyoni.+
2 Lakini mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kukengeuka;
Hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza.+
6 Kwa hiyo, kiburi ni mkufu wao;+
Ukatili huwafunika kama vazi.
7 Ufanisi wao* hufanya macho yao yanenepe;
Wamezidi mawazo ya moyo.
8 Wanadhihaki na kusema mambo maovu.+
Kwa kiburi, wanatoa vitisho vya kuwakandamiza wengine.+
9 Wanaongea kana kwamba wako juu kama mbingu,
Na ndimi zao hutamba duniani.
10 Kwa hiyo watu wake huwageukia,
Nao hunywa maji yao mengi.
11 Wanasema: “Mungu anajuaje?+
Je, Aliye Juu Zaidi ana ujuzi kweli?”
12 Naam, hivyo ndivyo walivyo waovu, ambao sikuzote wanastarehe.+
Wanaendelea kuongeza mali zao.+
13 Kwa hakika nimeusafisha moyo wangu bure
Na kunawa mikono yangu katika ukosefu wa hatia.+
15 Lakini kama ningesema mambo hayo,
Ningewasaliti watu wako.*
16 Nilipojaribu kulielewa jambo hilo,
Lilinitaabisha
17 Mpaka nilipoingia mahali patakatifu pa Mungu penye utukufu,
Nami nikatambua wakati wao ujao.
18 Kwa hakika unawaweka kwenye ardhi yenye utelezi.+
Unawafanya waanguke katika uharibifu wao.+
19 Jinsi wanavyoangamizwa kwa ghafla!+
Jinsi wanavyofikia kwa ghafla mwisho wao unaotisha!
20 Kama ndoto wakati wa kuamka, Ee Yehova,
Utakapoinuka, utaitupilia mbali* sanamu yao.
22 Nilikuwa mpumbavu wala sikuwa na uelewaji;
Nilikuwa kama mnyama asiye na akili mbele zako.
23 Lakini sasa niko pamoja nawe sikuzote;
Umeushika mkono wangu wa kulia.+
25 Ni nani niliye naye mbinguni?
Isipokuwa wewe tu, sitamani chochote duniani.+
26 Mwili wangu na moyo wangu unaweza kudhoofika,
Lakini Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu milele.+
27 Kwa kweli, wale wanaojitenga mbali nawe wataangamia.
Utamwangamiza* kila mtu anayekuacha kwa upotovu.*+
28 Lakini kwa upande wangu, kumkaribia Mungu ni jambo jema kwangu.+
Nimemfanya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova kuwa kimbilio langu,
Ili nizitangaze kazi zako zote.+
74 Ee Mungu, kwa nini umetukataa milele?+
Kwa nini hasira yako inawaka* dhidi ya kundi la malisho yako?+
Ukumbuke Mlima Sayuni, mahali unapokaa.+
3 Zielekeze hatua zako kwenye magofu ya kudumu.+
Adui ameharibu kila kitu mahali patakatifu.+
4 Maadui wako walinguruma ndani ya mahali pako pa mkutano.*+
Wameweka bendera zao wenyewe ziwe ishara humo.
5 Walikuwa kama watu wanaotumia mashoka kufyeka msitu wenye miti mingi.
6 Walivunjavunja michongo yake yote+ kwa mashoka na fito za chuma.
7 Walichoma moto mahali pako patakatifu.+
Walichafua hema la ibada lenye jina lako, wakaliangusha chini.
8 Wao pamoja na uzao wao wamesema mioyoni mwao:
“Sehemu zote za Mungu za mikutano* zilizo nchini ni lazima ziteketezwe.”
9 Hatuoni ishara yoyote;
Hakuna tena nabii yeyote,
Na hakuna yeyote miongoni mwetu anayejua hali hii itaendelea hadi lini.
10 Ee Mungu, mpinzani ataendelea kudhihaki mpaka lini?+
Je, adui ataendelea kulidharau jina lako milele?+
11 Kwa nini unauzuia mkono wako, mkono wako wa kuume?+
Uchomoe kifuani mwako* na kuwaangamiza?
12 Lakini Mungu ni Mfalme wangu tangu zamani za kale,
Yeye anayefanya matendo ya wokovu duniani.+
13 Uliitibua bahari kwa nguvu zako;+
Uliviponda vichwa vya wanyama wakubwa sana wa baharini.
14 Uliviponda vichwa vya Lewiathani;*
Ukawapa watu wamle kama chakula chao, wale wanaokaa jangwani.
16 Mchana ni wako, na usiku pia.
18 Kumbuka dhihaka za adui, Ee Yehova,
Jinsi taifa pumbavu linavyodharau jina lako.+
19 Usiwape wanyama wa mwituni uhai wa* njiwa tetere wako.
Usiusahau milele uhai wa watu wako wanaoteseka.
20 Likumbuke lile agano,
Kwa maana sehemu za dunia zenye giza zimejaa makao ya ukatili.
21 Mtu aliyepondwa na asigeuke na kwenda zake akiwa amekata tamaa;+
Watu wa hali ya chini na maskini na walisifu jina lako.+
22 Inuka, Ee Mungu, na utetee kesi yako.
Kumbuka jinsi wapumbavu wanavyokudhihaki mchana kutwa.+
23 Usisahau mambo ambayo maadui wako wanasema.
Kelele za wale wanaokuasi zinapanda juu daima.
Kwa kiongozi. Umepatanishwa na muziki wa “Usiharibu.” Wimbo wa Asafu.+
75 Tunakushukuru, Ee Mungu, tunakushukuru;
Jina lako liko karibu,+
Na watu wanatangaza kazi zako zinazostaajabisha.
2 Unasema: “Ninapoweka wakati hususa,
Ninahukumu kwa haki.
3 Dunia na wakaaji wake wote walipoyeyushwa,
Mimi ndiye niliyeziimarisha nguzo zake.” (Sela)
4 Ninawaambia wenye kujigamba, “Msijigambe,”
Na waovu, “Msikweze nguvu zenu.*
5 Msikweze nguvu zenu* juu sana
Au kuongea kwa kiburi.
6 Kwa maana kukwezwa
Hakutoki mashariki wala magharibi wala kusini.
7 Kwa maana Mungu ni Mwamuzi.+
Humshusha huyu na kumkweza yule.+
8 Kwa maana kuna kikombe mkononi mwa Yehova;+
Divai inatoa povu nayo imechanganywa kikamili.
Hakika ataimwaga,
Na waovu wote duniani watainywa, mpaka machicha yake.”+
9 Lakini mimi, nitalitangaza hilo milele;
Nitamwimbia sifa* Mungu wa Yakobo.
10 Kwa maana anasema: “Nitazikata nguvu* zote za waovu.”
Lakini nguvu* za waadilifu zitakwezwa.
Kwa kiongozi; uimbwe kwa ala za nyuzi. Muziki wa Asafu.+ Wimbo.
3 Huko aliivunja mishale inayowaka ya upinde,
Ngao na upanga na silaha za vita.+ (Sela)
4 Unang’aa kwa uangavu;*
Una fahari kuliko milima ya mawindo.
5 Wenye moyo jasiri wameporwa.+
Wamelala usingizi;
Mashujaa wote hawakuwa na uwezo.+
6 Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo,
Mwendeshaji wa gari na farasi wote wamelala usingizi mzito.+
7 Ni wewe peke yako unayeogopesha.+
Na ni nani anayeweza kustahimili hasira yako kali?+
8 Kutoka mbinguni ulitangaza hukumu;+
Dunia iliogopa na kunyamaza+
9 Mungu alipoinuka ili kutekeleza hukumu,
Ili kuwaokoa wapole wote walio duniani.+ (Sela)
10 Kwa maana ghadhabu ya mwanadamu itakuletea sifa;+
Nawe utajipamba kwa mabaki ya ghadhabu yao.
11 Wekeni nadhiri zenu kwa Yehova Mungu wenu na kuzitimiza,+
Wote wanaomzunguka na walete zawadi yao kwa woga.+
12 Atakinyenyekeza kiburi cha* viongozi;
Yeye huwaogopesha wafalme wa dunia.
Kwa kiongozi; mtindo wa Yeduthuni.* Muziki wa Asafu.+
77 Kwa sauti yangu nitamlilia Mungu;
Nitamlilia Mungu kwa sauti kubwa, naye atanisikia.+
2 Katika siku ya taabu yangu ninamtafuta Yehova.+
Usiku ninamnyooshea mikono yangu bila kuacha.*
Siwezi* kufarijiwa.
4 Unazishika kope zangu ili nisifumbe macho;
Nimefadhaika, nami siwezi kuongea.
5 Mawazo yangu yanarudi katika siku za zamani za kale,+
Miaka mingi iliyopita.
7 Je, Yehova atatutupa mbali milele?+
Je, hatatuonyesha tena kamwe kibali chake?+
8 Je, upendo wake mshikamanifu utakoma milele?
Je, ahadi yake itakosa kutimia katika vizazi vyote?
9 Je, Mungu amesahau kuonyesha kibali chake,+
Au je, hasira yake imekomesha rehema yake? (Sela)
10 Je, ni lazima niendelee kusema: “Hili ndilo linalonitaabisha:*+
Aliye Juu Zaidi amebadili msimamo wake kutuelekea”?*
11 Nitazikumbuka kazi za Yah;
Nitayakumbuka matendo yako yanayostaajabisha ya zamani za kale.
12 Nitautafakari utendaji wako wote
Na kutafakari shughuli zako.+
13 Ee Mungu, njia zako ni takatifu.
Ee Mungu, ni mungu gani aliye mkuu kama wewe?+
14 Wewe ndiye Mungu wa kweli, unayetenda mambo yanayostaajabisha.+
Umeyafunulia mataifa nguvu zako.+
16 Maji yalikuona, Ee Mungu,
Maji yalikuona yakavurugika.+
Na vilindi vya maji vikatibuka.
17 Mawingu yakamwaga maji.
Anga lenye mawingu likanguruma,
Na mishale yako ikaruka huku na kule.+
18 Sauti ya mngurumo+ wako ilikuwa kama magurudumu ya gari la vita;
Mimweko ya radi iliangaza dunia inayokaliwa;*+
Dunia ilitikisika na kutetemeka.+
19 Njia yako ilipita baharini,+
Kijia chako kilipita katika maji mengi;
Lakini nyayo zako hazingeweza kuonekana.
78 Sikilizeni sheria* yangu, enyi watu wangu;
Tegeni sikio lenu kwa maneno ya kinywa changu.
2 Nitakifungua kinywa changu kwa methali.
Nitafumbua mafumbo ya zamani za kale.+
3 Mambo ambayo tumesikia na tunayojua,
Ambayo baba zetu wametusimulia,+
4 Hatutawaficha wana wao;
Tutakisimulia kizazi kijacho mambo hayo+
Matendo ya Yehova yanayostahili sifa na nguvu zake,+
Mambo yanayostaajabisha aliyotenda.+
5 Alianzisha kikumbusho katika Yakobo
Na kuweka sheria katika Israeli;
Aliwaamuru mababu zetu
Wawajulishe watoto wao mambo hayo,+
6 Ili kizazi kijacho,
Watoto ambao hawajazaliwa, wayajue.+
Kisha wao watawasimulia watoto wao.+
7 Halafu watoto hao watamtumaini Mungu.
8 Kisha hawatakuwa kama mababu zao,
Kizazi chenye ukaidi na uasi,+
Kizazi kilichokuwa na moyo unaoyumbayumba*+
Na ambacho hakikuwa na roho ya uaminifu kwa Mungu.
9 Waefraimu walijihami kwa upinde,
Lakini walikimbia siku ya vita.
14 Aliwaongoza kwa wingu wakati wa mchana
Na usiku kucha kwa mwangaza wa moto.+
15 Aliipasua miamba nyikani,
Akawanywesha maji ya kutosha kana kwamba yanatoka vilindini.+
16 Alivitoa vijito kutoka kwenye jabali
Na kufanya maji yatiririke chini kama mito.+
17 Lakini waliendelea kumtendea dhambi
Kwa kumwasi jangwani yule Aliye Juu Zaidi;+
18 Walimjaribu* Mungu moyoni mwao+
Walidai wapewe chakula walichotamani.*
19 Kwa hiyo wakalalamika kumhusu Mungu,
Wakisema: “Je, Mungu anaweza kuandaa meza nyikani?”+
20 Tazama! Aliupiga mwamba
Hivi kwamba maji yakatiririka na vijito vikafurika.+
“Je, anaweza pia kutupatia mkate,
Au je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”+
21 Yehova alipowasikia, alikasirika sana;+
Moto+ ukawaka dhidi ya Yakobo,
Na hasira yake ikawaka dhidi ya Israeli+
22 Kwa sababu hawakudhihirisha imani katika Mungu;+
Hawakuutumaini uwezo wake wa kuwaokoa.
23 Basi akaliamuru anga lililo juu lenye mawingu,
Naye akaifungua milango ya mbingu.
24 Akaendelea kuwanyeshea mana ili wale;
Akawapa nafaka ya mbinguni.+
26 Aliuvumisha upepo wa mashariki mbinguni
Na kwa nguvu zake akaufanya upepo wa kusini uvume.+
27 Naye akawanyeshea nyama kama mavumbi,
Ndege kama mchanga kwenye ufuo wa bahari.
28 Aliwaangusha katikati ya kambi yake,
Pande zote kuzunguka mahema yake.
29 Nao wakala na kujilazimisha kula zaidi;
Aliwapa walichotamani.+
30 Lakini kabla hawajatosheleza kikamili tamaa yao,
Chakula kilipokuwa kingali kinywani mwao,
31 Ghadhabu ya Mungu ikawaka dhidi yao.+
Akawaua wanaume wenye nguvu zaidi;+
Aliwaangamiza wanaume vijana wa Israeli.
32 Licha ya hayo walizidi kutenda dhambi+
Nao hawakudhihirisha imani katika kazi zake zinazostaajabisha.+
33 Basi akazikatisha siku zao kana kwamba ni pumzi tu,+
Na miaka yao kwa matukio ya ghafla yenye kutisha.
34 Lakini kila mara alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta;+
Walirudi na kumtafuta Mungu,
35 Wakikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao+
36 Lakini walijaribu kumdanganya kwa kinywa chao
Na kumwambia uwongo kwa ulimi wao.
Mara nyingi aliizuia hasira yake+
Badala ya kuichochea ghadhabu yake yote.
42 Hawakuzikumbuka nguvu zake,*
Siku ambayo aliwaokoa* kutoka kwa adui,+
43 Jinsi alivyoonyesha ishara zake kule Misri+
Na miujiza yake katika eneo la Soani,
44 Na jinsi alivyobadili mifereji ya Nile kuwa damu+
Hivi kwamba hawangeweza kunywa maji kutoka katika vijito vyake.
46 Mazao yao aliwapa parare wanaokula sana,
Matunda ya kazi yao ngumu akayapa makundi ya nzige.+
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe+
Na mikuyu yao kwa mawe ya mvua.
49 Aliwamwagia hasira yake inayowaka,
Hasira kali na ghadhabu na taabu,
Makundi ya malaika yanayoleta msiba.
50 Alitayarisha njia kwa ajili ya hasira yake.
Hakuwalinda wasife;*
Naye aliwaua kwa ugonjwa hatari.
51 Mwishowe aliwaangamiza wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+
Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu.
52 Kisha akawatoa nje watu wake kama kundi la kondoo+
Na kuwaongoza nyikani kama kundi la mifugo.
54 Naye akawaleta katika eneo lake takatifu,+
Eneo hili lenye milima ambalo mkono wake wa kuume ulilitwaa.+
55 Aliyafukuza mataifa kutoka mbele yao;+
Akawagawia urithi kwa kamba ya kupimia;+
Aliyafanya makabila ya Israeli yakae katika makao yao.+
56 Lakini waliendelea kumjaribu* Mungu Aliye Juu Zaidi, na kumwasi;+
Hawakusikiliza vikumbusho vyake.+
57 Pia walipotoka na kutenda kwa hila kama mababu zao.+
Hawakutegemeka kama upinde uliolegea usivyotegemeka.+
58 Waliendelea kumkasirisha kwa mahali pao pa juu,+
Nao wakachochea hasira yake kali* kwa sanamu zao za kuchongwa.+
59 Mungu alisikia na kuwaka hasira,+
Kwa hiyo akaikataa kabisa Israeli.
61 Aliacha ishara ya nguvu zake ipelekwe utekwani;
Fahari yake itiwe mikononi mwa adui.+
62 Aliwatoa watu wake wauawe kwa upanga+
Naye akaukasirikia vikali urithi wake.
63 Moto uliwateketeza kabisa vijana wake wa kiume,
Na mabikira wake hawakuimbiwa nyimbo za harusi.*
65 Kisha Yehova akaamka kana kwamba anatoka usingizini,+
Kama mwanamume hodari+ aamkavyo baada ya divai kumtoka.
66 Naye akawakimbiza maadui wake;+
Akawatia aibu ya kudumu.
67 Alilikataa hema la Yosefu;
Hakulichagua kabila la Efraimu.
69 Alipafanya mahali pake patakatifu pawe mahali pa kudumu kama mbingu,*+
Kama dunia ambayo ameiimarisha milele.+
70 Alimchagua Daudi+ mtumishi wake
Na kumtoa katika mazizi ya kondoo,+
71 Alimwondoa katika kazi ya kuchunga kondoo wanaonyonyesha;
Akamfanya kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake,+
Na wa Israeli, urithi wake.+
Muziki wa Asafu.+
79 Ee Mungu, mataifa yamevamia urithi wako;+
Yamelichafua hekalu lako takatifu;+
Yamebadili Yerusalemu kuwa rundo la magofu.+
2 Wamewapa ndege wa angani maiti za watumishi wako kuwa chakula chao
Na miili ya washikamanifu wako wamewapa wanyama wa mwituni wa dunia.+
3 Wamemwaga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,
Na hakuna aliyebaki wa kuwazika.+
4 Tumekuwa kitu cha kushutumiwa na majirani wetu;+
Wale wanaotuzunguka wanatudhihaki na kutufanyia mzaha.
5 Ee Yehova, utaendelea kuwaka hasira mpaka lini? Milele?+
Ghadhabu yako itaendelea kuwaka kama moto mpaka lini?+
6 Yamwagie ghadhabu yako mataifa ambayo hayakujui
Na falme ambazo haziliitii jina lako.+
7 Kwa maana wamemnyafua Yakobo
Nao wameifanya nchi yake ukiwa.+
8 Usitufanye tuwajibike kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+
Tuonyeshe haraka rehema yako,+
Kwa maana tumeshushwa chini sana.
9 Tusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+
Kwa ajili ya jina lako tukufu;
10 Kwa nini mataifa yaseme: “Mungu wao yuko wapi?”+
Na ijulikane miongoni mwa mataifa mbele ya macho yetu
Kwamba damu iliyomwagwa ya watumishi wako imelipiziwa kisasi.+
11 Na usikie kilio cha maumivu cha mfungwa.+
Tumia nguvu zako kuu* kuwahifadhi* wale waliohukumiwa kifo.*+
13 Kisha sisi, watu wako na kondoo wa malisho yako,+
Tutakushukuru milele;
Nasi tutatangaza sifa yako kizazi mpaka kizazi.+
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Kikumbusho. Muziki wa Asafu.+
80 Ee Mchungaji wa Israeli, sikiliza,
Wewe unayemwongoza Yosefu kama kundi la kondoo.+
4 Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea mpaka lini kuwa na hasira kali kuelekea* sala ya watu wako?+
5 Unawalisha machozi kama mkate,
Nawe unawanywesha machozi kupita kiasi.
6 Unawaruhusu majirani wetu wagombane kwa sababu yetu;
Maadui wetu wanaendelea kutudhihaki wapendavyo.+
7 Ee Mungu wa majeshi, turudishe;
Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+
8 Uliufanya mzabibu+ uondoke Misri.
Uliyafukuza mataifa na kuupanda.+
9 Ulitayarisha nafasi kwa ajili yake,
Nao ukatia mizizi na kujaa nchini.+
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,
Na mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
11 Matawi yake yalienea mpaka baharini,
Na machipukizi yake mpaka kwenye Mto Efrati.+
12 Kwa nini umebomoa kuta za mawe za shamba la mzabibu huo,+
Hivi kwamba wote wanaopita karibu nao wanachuma matunda yake?+
13 Nguruwe wa mwituni wanauharibu,
Na wanyama wa porini wanaula.+
14 Ee Mungu wa majeshi, rudi tafadhali.
Tazama chini kutoka mbinguni uone!
Utunze mzabibu huu,+
15 Shina* ambalo mkono wako wa kuume umepanda,+
Na umtazame mwana ambaye umemtia nguvu* kwa ajili yako mwenyewe.+
16 Umechomwa moto,+ umekatwa.
Wanaangamia kwa kemeo lako.*
17 Mkono wako na umtegemeze mwanamume aliye kwenye mkono wako wa kuume,
Mwana wa binadamu uliyemtia nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
18 Kisha hatutageuka kutoka kwako.
Tuhifadhi hai, ili tuliitie jina lako.
19 Ee Yehova Mungu wa majeshi, turudishe;
Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+
Kwa kiongozi; juu ya Gitithi.* Wa Asafu.+
81 Mshangilieni Mungu kwa sauti, nguvu zetu.+
Mpazieni sauti kwa ushindi Mungu wa Yakobo.
2 Anzisheni muziki na kuchukua tari,
Kinubi chenye sauti tamu pamoja na kinanda.
4 Kwa maana ni agizo kwa Israeli,
Sheria ya Mungu wa Yakobo.+
Nilisikia sauti* ambayo sikuitambua:
6 “Niliuinua mzigo kutoka begani mwake;+
Mikono yake iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
Nilikujaribu katika maji ya Meriba.*+ (Sela)
8 Sikieni, watu wangu, nami nitatoa ushahidi dhidi yenu.
Ee Israeli, laiti ungenisikiliza.+
9 Hakutakuwa na mungu yeyote wa kigeni miongoni mwenu;
Nanyi hamtamwinamia mungu wa kigeni.+
10 Mimi, Yehova, ni Mungu wako,
Niliyekutoa nchini Misri.+
Fungua wazi kinywa chako, nami nitakijaza.+
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu;
Israeli hakujitiisha kwangu.+
14 Ningewatiisha haraka maadui wao;
Ningeugeuza mkono wangu dhidi ya wapinzani wao.+
15 Wale wanaomchukia Yehova watajikunyata mbele zake,
Na mwisho* wao utakuwa wa milele.
Muziki wa Asafu.+
3 Mteteeni* mtu wa hali ya chini na yatima.+
Mtendeeni kwa haki mtu asiye na uwezo na maskini.+
4 Mwokoeni mtu wa hali ya chini na maskini;
Waokoeni kutoka mkononi mwa mwovu.”
7 Lakini mtakufa kama wanadamu wanavyokufa;+
Nanyi mtaanguka kama mkuu mwingine yeyote anavyoanguka!’”+
8 Inuka, Ee Mungu, uihukumu dunia,+
Kwa maana mataifa yote ni yako.
Wimbo. Muziki wa Asafu.+
83 Ee Mungu, usinyamaze;+
Usikae kimya wala kutulia, Ee Mungu.
3 Kwa hila wanapanga njama kwa siri dhidi ya watu wako;
Wanapanga njama dhidi ya watu wako unaowathamini.*
4 Wanasema: “Njooni, acheni tuwaangamize wakiwa taifa,+
Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena kamwe.”
5 Kwa umoja wanatunga mbinu;*
6 Mahema ya Edomu na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+
7 Gebali na Amoni+ na Amaleki,
9 Watendee kama ulivyoitendea Midiani,+
Kama ulivyomtendea Sisera na Yabini kwenye kijito cha* Kishoni.+
10 Waliangamizwa kule En-dori;+
Wakawa mbolea juu ya ardhi.
11 Wafanye viongozi wao wawe kama Orebu na Zeebu+
Na wakuu* wao kama Zeba na Zalmuna,+
12 Kwa maana walisema: “Na tuimiliki nchi ambamo Mungu anakaa.”
13 Ee Mungu wangu, wafanye wawe kama mchongoma unaopeperushwa,*+
Kama majani makavu yanayopeperushwa na upepo.
14 Kama moto unaoteketeza kabisa msitu,
Kama mwali wa moto unaounguza milima,+
15 Wafuatie vivyo hivyo kwa tufani yako+
Na kuwaogopesha kwa dhoruba yako ya upepo.+
16 Funika nyuso zao kwa aibu,*
Ili walitafute jina lako, Ee Yehova.
17 Na waaibishwe na kuogopeshwa milele;
Na wafedheheshwe na kuangamia;
18 Na watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova,+
Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.+
Kwa kiongozi; juu ya Gitithi.* Muziki wa wana wa Kora.+
Moyo wangu na mwili wangu humshangilia kwa sauti Mungu aliye hai.
3 Hata ndege hupata makao huko
Na mbayuwayu hujipatia kiota,
Ambamo huyatunza makinda wake
Karibu na madhabahu yako tukufu, Ee Yehova wa majeshi,
Mfalme wangu na Mungu wangu!
4 Wenye furaha ni wale wanaokaa katika nyumba yako!+
Wanaendelea kukusifu.+ (Sela)
6 Wanapopita katika Bonde la Mibaka,*
Wanalifanya kuwa mahali penye chemchemi;
Na mvua ya mapema hulivisha* baraka.
7 Wataendelea kutembea kutoka nguvu hadi nguvu zaidi;+
Kila mmoja wao hufika mbele za Mungu kule Sayuni.
8 Ee Yehova Mungu wa majeshi, isikie sala yangu;
Sikiliza, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)
10 Kwa maana siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu moja kwingineko!+
Ninachagua kusimama kwenye kizingiti cha nyumba ya Mungu wangu
Badala ya kukaa katika mahema ya uovu.
Yehova hatawanyima jambo lolote jema
Wale wanaotembea kwa utimilifu.+
12 Ee Yehova wa majeshi,
Mwenye furaha ni mtu anayekutumaini.+
Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+
3 Uliizuia ghadhabu yako yote;
Uliiacha hasira yako kali.+
5 Je, utatughadhibikia milele?+
Je, utaendelea kukasirika kizazi baada ya kizazi?
6 Je, hutatuhuisha tena
Ili watu wako washangilie kwa sababu yako?+
7 Ee Yehova, tutendee kwa upendo mshikamanifu,+
Nawe utupe wokovu wako.
8 Nitasikiliza jambo ambalo Mungu wa kweli Yehova anasema,
Kwa maana atawaambia watu wake kuhusu amani,+ washikamanifu wake,
Lakini wasianze tena kujiamini kupita kiasi.+
9 Kwa hakika wokovu wake uko karibu na wale wanaomwogopa,+
Ili utukufu wake ukae katika nchi yetu.
10 Upendo mshikamanifu utakutana na uaminifu;
Uadilifu utabusiana na amani.+
11 Uaminifu utachipuka duniani,
Na uadilifu utatazama chini kutoka mbinguni.+
13 Uadilifu utatembea mbele zake+
Na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.
Sala ya Daudi.
2 Ulinde uhai wangu,* kwa maana mimi ni mshikamanifu.+
Mwokoe mtumishi wako anayekutumaini,
Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+
4 Mfanye mtumishi wako ashangilie,
Kwa maana ninakugeukia wewe,* Ee Yehova.
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni mwema+ na uko tayari kusamehe;+
Una upendo mwingi mshikamanifu kwa wote wanaokuitia.+
6 Ee Yehova, sikiliza sala yangu;
Na usikilize sihi zangu za kuomba msaada.+
11 Nifundishe, Ee Yehova, kuhusu njia yako.+
Nitatembea katika kweli yako.+
Unganisha moyo wangu* ili niliogope jina lako.+
12 Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote,+
Nami nitalitukuza jina lako milele,
13 Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkuu kwangu,
14 Ee Mungu, watu wenye kimbelembele wanainuka dhidi yangu;+
Kundi la wanaume wakatili wanataka kuniua,*
15 Lakini wewe, Ee Yehova, ni Mungu mwenye rehema na huruma,*
Si mwepesi wa hasira, nawe una upendo mwingi mshikamanifu na uaminifu.*+
16 Nigeukie na kunionyesha kibali.+
Mpe mtumishi wako nguvu zako,+
Na umwokoe mwana wa kijakazi wako.
17 Nionyeshe ishara ya* wema wako,
Ili wale wanaonichukia waione na kuaibika.
Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni msaidizi wangu na mfariji wangu.
Muziki wa wana wa Kora.+ Wimbo.
87 Msingi wa jiji lake uko katika milima mitakatifu.+
2 Yehova anapenda malango ya Sayuni+
Kuliko mahema yote ya Yakobo.
3 Mambo matukufu yanasemwa kukuhusu, Ee jiji la Mungu wa kweli.+ (Sela)
4 Nitamhesabu Rahabu+ na Babiloni kuwa kati ya wale wanaonijua* mimi;
Tazama, Ufilisti na Tiro, pamoja na Kushi.
Itasemwa hivi: “Huyu alizaliwa humo.”
5 Na kuhusu Sayuni itasemwa:
“Kila mtu alizaliwa humo.”
Na Aliye Juu Zaidi atamwimarisha kabisa.
6 Yehova atatangaza hivi atakapoyaandikisha mataifa:
“Huyu alizaliwa humo.” (Sela)
7 Waimbaji+ na wale wanaocheza dansi za mzunguko+ watasema:
“Chemchemi zangu zote zimo ndani yako.”*+
Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+ Kwa kiongozi; kwa mtindo wa Mahalathi,* uimbwe kwa zamu. Maskili* ya Hemani+ Mwezra.
88 Ee Yehova, Mungu wa wokovu wangu,+
Wakati wa mchana ninalia kwa sauti,
Na usiku ninakuja mbele zako.+
4 Tayari nimehesabiwa miongoni mwa wale wanaoshuka shimoni;*+
Nimekuwa mtu asiye na uwezo wowote,*+
5 Aliyeachwa kati ya watu waliokufa
Kama waliouawa wanaolala kaburini,
Ambao huwakumbuki tena
Na ambao wametengwa mbali na utunzaji* wako.
6 Umeniweka katika shimo lenye kina kirefu sana,
Sehemu zenye giza, shimo kubwa.*
7 Ghadhabu yako inanilemea sana,+
Nawe unanilemea kwa mawimbi yako yenye nguvu. (Sela)
8 Umewafukuza rafiki zangu mbali sana nami;+
Umenifanya niwe kitu kinachowachukiza.
Nimenaswa na siwezi kutoroka.
9 Jicho langu limedhoofika kwa sababu ya mateso yangu.+
Ee Yehova, ninakulilia mchana kutwa;+
Ninakunyooshea mikono yangu.
10 Je, utawatendea maajabu waliokufa?
Je, wale waliokufa ambao hawana uwezo wanaweza kuinuka na kukusifu?+ (Sela)
11 Je, upendo wako mshikamanifu utatangazwa kaburini,
Na uaminifu wako mahali pa maangamizi?*
12 Je, maajabu yako yatajulikana gizani
Au uadilifu wako katika nchi ya waliosahauliwa?+
14 Kwa nini, Ee Yehova, unanikataa?*+
Kwa nini unanificha uso wako?+
15 Tangu nilipokuwa kijana,
Nimeteseka nami niko karibu kuangamia;+
Nimekufa ganzi kwa sababu ya mambo yanayotisha unayoruhusu yanipate.
16 Hasira yako inayowaka inanilemea;+
Vitisho vyako vinaniangamiza.
17 Vinanizunguka mchana kutwa kama maji;
Vinanizingira ili kunibana pande zote.*
18 Umewafukuza rafiki zangu na wenzangu mbali sana nami;+
Giza limekuwa mwenzangu.
89 Nitaimba kuhusu jinsi Yehova anavyoonyesha upendo mshikamanifu milele.
Kwa kinywa changu ninavitangazia vizazi vyote uaminifu wako.
2 Kwa maana nimesema: “Upendo mshikamanifu utajengwa* milele,+
Nawe umeuimarisha kabisa uaminifu wako mbinguni.”
4 ‘Nitauimarisha kabisa uzao wako*+ milele,
Nami nitakijenga kiti chako cha ufalme kwa vizazi vyote.’”+ (Sela)
5 Mbingu zinasifu maajabu yako, Ee Yehova,
Naam, uaminifu wako katika kutaniko la watakatifu.
6 Kwa maana ni nani mbinguni anayeweza kulinganishwa na Yehova?+
Ni nani miongoni mwa wana wa Mungu+ aliye kama Yehova?
7 Mungu anaogopwa katika baraza* la watakatifu;+
Yeye ni mtukufu na mwenye kuogopesha kwa wote wanaomzunguka.+
8 Ee Yehova Mungu wa majeshi,
Ni nani aliye na nguvu kama wewe, Ee Yah?+
Uaminifu wako unakuzunguka.+
10 Umemponda Rahabu+ kama mtu aliyeuawa.+
Kwa mkono wako wenye nguvu umewatawanya maadui wako.+
14 Uadilifu na haki ndio msingi wa kiti chako cha ufalme;+
Upendo mshikamanifu na uaminifu husimama mbele zako.+
15 Wenye furaha ni watu wanaojua kelele za shangwe.+
Ee Yehova, wanatembea katika nuru ya uso wako.
16 Wanashangilia mchana kutwa kwa sababu ya jina lako,
Na kwa sababu ya uadilifu wako wanakwezwa.
18 Kwa maana ngao yetu ni ya Yehova,
Mfalme wetu ni wa Mtakatifu wa Israeli.+
19 Wakati huo uliwaambia hivi washikamanifu wako katika maono:
21 Mkono wangu utamtegemeza,+
Na mkono wangu utamwimarisha.
22 Hakuna adui atakayemtoza ushuru,
Na hakuna mwovu atakayemkandamiza.+
24 Uaminifu wangu na upendo wangu mshikamanifu uko pamoja naye,+
Na katika jina langu nguvu zake zitakwezwa.*
26 Atasema kwa sauti: ‘Wewe ni Baba yangu,
Mungu wangu na Mwamba wa wokovu wangu.’+
28 Nitadumisha upendo wangu mshikamanifu kumwelekea milele,+
Na agano langu nililofanya pamoja naye halitavunjika kamwe.+
30 Wanawe wakiiacha sheria yangu
Na wasipotembea kulingana na maagizo yangu,*
31 Wakizivunja sheria zangu
Na wasiposhika amri zangu,
32 Basi nitaadhibu uasi wao* kwa fimbo+
Na kosa lao kwa viboko.
33 Lakini sitaacha kamwe kumtendea kwa upendo wangu mshikamanifu+
Wala sitakosa kutimiza ahadi yangu.*
35 Nimeapa katika utakatifu wangu, mara moja kwa wakati wote;
Sitamwambia Daudi uwongo.+
37 Kama mwezi, kitaimarishwa kabisa milele
Kama shahidi mwaminifu angani.” (Sela)
38 Lakini wewe mwenyewe umemtupa mbali na kumkataa;+
Umemkasirikia sana mtiwa-mafuta wako.
39 Umelikataa kwa dharau agano ulilofanya na mtumishi wako;
Umelichafua* taji lake kwa kulitupa ardhini.
40 Umezivunja kuta zake zote za mawe;*
Umezifanya ngome zake kuwa magofu.
41 Wote wanaopita karibu naye wamempora;
Yeye ni shutuma kwa jirani zake.+
43 Pia umeusukuma nyuma upanga wake,
Na kumfanya ashindwe vitani.
44 Umekomesha fahari yake
Na kukitupa ardhini kiti chake cha ufalme.
45 Umefupisha siku zake za ujana;
Umemvisha aibu. (Sela)
46 Ee Yehova, utaendelea kujificha mpaka lini? Utajificha milele?+
Je, ghadhabu yako itaendelea kuwaka kama moto?
47 Kumbuka jinsi maisha yangu yalivyo mafupi!+
Je, uliwaumba wanadamu wote bila kusudi?
48 Ni mwanadamu gani anayeweza kuishi na asione kifo kamwe?+
Je, anaweza kujiokoa mwenyewe* kutoka katika nguvu za Kaburi?* (Sela)
49 Yako wapi matendo yako ya zamani ya upendo mshikamanifu, Ee Yehova,
Ambayo ulimwapia Daudi katika uaminifu wako?+
50 Kumbuka, Ee Yehova, dhihaka ambazo watumishi wako wanavurumishiwa;
Jinsi ninavyolazimika kuvumilia* dhihaka za mataifa yote;
51 Jinsi ambavyo maadui wako wamevurumisha matusi, Ee Yehova;
Jinsi ambavyo wameitukana kila hatua ya mtiwa-mafuta wako.
52 Yehova na asifiwe milele. Amina na Amina.+
KITABU CHA NNE
(Zaburi 90-106)
Sala ya Musa, mtu wa Mungu wa kweli.+
90 Ee Yehova, umekuwa makao yetu*+ katika vizazi vyote.
2 Kabla milima haijazaliwa
Au kabla hujaiumba* dunia na nchi inayozaa,+
Tangu milele hadi milele, wewe ni Mungu.+
3 Unamfanya mwanadamu anayeweza kufa arudi mavumbini;
Unasema: “Rudini, enyi wanadamu.”+
4 Kwa maana miaka elfu moja machoni pako ni kama siku ya jana ambayo tayari imepita,+
Kama kesha moja tu la usiku.
6 Asubuhi yanachanua maua na kusitawi,
Lakini ifikapo jioni yamenyauka na kukauka.+
7 Kwa maana tumemezwa na hasira yako+
Na kutishwa na ghadhabu yako.
Lakini imejaa taabu na huzuni;
Nayo hupita haraka, nasi hutokomea.+
11 Ni nani anayeweza kuelewa nguvu za hasira yako?
Ghadhabu yako ni kubwa kama hofu unayostahili kuonyeshwa.+
12 Tufundishe jinsi ya kuhesabu siku zetu+
Ili tupate moyo wa hekima.
13 Rudi, Ee Yehova!+ Hali hiyo itadumu mpaka lini?+
Wahurumie watumishi wako.+
14 Tushibishe asubuhi kwa upendo wako mshikamanifu,+
Ili tupaze sauti kwa shangwe na kushangilia+ siku zetu zote.
15 Tufanye tushangilie kulingana na siku ambazo umetutesa,+
Kwa kadiri ya miaka mingi tuliyopata msiba.+
16 Watumishi wako na waone utendaji wako,
Na wana wao waone fahari yako.+
17 Kibali chako, Ee Yehova Mungu wetu, na kiwe juu yetu;
Na uifanikishe* kazi ya mikono yetu.
Naam, ifanikishe* kazi ya mikono yetu.+
3 Kwa maana atakuokoa usinaswe na mtego wa mwindaji wa ndege,
Kutoka kwa ugonjwa wa kuambukiza unaoangamiza.
4 Kwa manyoya yake atakufunika,
Nawe utapata kimbilio chini ya mabawa yake.+
Uaminifu wake+ utakuwa ngao kubwa+ na ukuta wa ulinzi.*
5 Hutaogopa vitisho vya usiku,+
Wala mshale unaoruka mchana,+
6 Wala ugonjwa wa kuambukiza unaonyemelea gizani,
Wala maangamizi yanayoharibu wakati wa adhuhuri.
8 Utayaona tu kwa macho yako
Unaposhuhudia adhabu* ya waovu.
9 Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”
Umemfanya Aliye Juu Zaidi kuwa makao* yako;+
10 Hutapatwa na msiba,+
Na hakuna pigo litakalokaribia hema lako.
13 Utamkanyaga mwanasimba na swila;
Utamkanyagia chini simba mwenye manyoya marefu shingoni na nyoka mkubwa.+
14 Mungu alisema: “Kwa sababu ananipenda,* nitamwokoa.+
Nitamlinda kwa sababu analijua* jina langu.+
15 Ataniita, nami nitamjibu.+
Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+
Nitamwokoa na kumtukuza.
Muziki. Wimbo wa siku ya Sabato.
92 Ni vema kukushukuru, Ee Yehova+
Na kuliimbia sifa* jina lako, Ee Uliye Juu Zaidi,
2 Kutangaza upendo wako mshikamanifu+ asubuhi
Na uaminifu wako nyakati za usiku,
3 Kwa kinanda cha nyuzi kumi na kwa udi,
Kwa sauti tamu ya kinubi.+
4 Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya matendo yako;
Kwa sababu ya kazi za mikono yako ninapaza sauti kwa shangwe.
5 Jinsi kazi zako zilivyo kuu, Ee Yehova!+
Jinsi mawazo yako yalivyo na kina sana!+
6 Mtu yeyote asiyetumia akili hawezi kuyajua;
Na hakuna mtu yeyote mjinga anayeweza kuelewa hili:+
8 Lakini wewe umekwezwa milele, Ee Yehova.
9 Kwa kweli, watazame maadui wako wakishindwa, Ee Yehova,
Tazama jinsi maadui wako watakavyoangamia;
Watenda maovu wote watatawanywa.+
11 Macho yangu yatawaangalia maadui wangu wakishindwa;+
Masikio yangu yatasikia kuhusu kuangamia kwa watu waovu wanaonishambulia.
12 Lakini waadilifu watasitawi kama mtende
Na kuwa wakubwa kama mwerezi kule Lebanoni.+
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yehova;
Wanasitawi katika nyua za Mungu wetu.+
14 Hata wakati wa uzeeni* wataendelea kunawiri;+
Wataendelea kuwa na nguvu* na kuwa wabichi,+
15 Wakitangaza kwamba Yehova ni mnyoofu.
Yeye ni Mwamba wangu,+ ambaye hana ukosefu wowote wa uadilifu.
93 Yehova amekuwa Mfalme!+
Amevaa adhama;
Yehova amevaa nguvu;
Huzivaa kama mshipi.
Dunia imeimarishwa kabisa;
Haiwezi kusogezwa.*
3 Mito imefurika, Ee Yehova,
Mito imefurika na kunguruma;
Mito inaendelea kufurika na kugonga kwa kishindo.
4 Ana nguvu kuliko sauti ya maji mengi,
Ana nguvu kuliko mawimbi makubwa ya bahari,+
Yehova ni mwenye fahari mbinguni.+
5 Vikumbusho vyako vinategemeka sana.+
Utakatifu unaipamba* nyumba yako nyakati zote,+ Ee Yehova.
94 Ee Mungu wa kisasi, Yehova,+
Ee Mungu wa kisasi, angaza!
2 Inuka, Ee Mwamuzi wa dunia.+
Walipe wanachostahili watu wenye kiburi.+
3 Waovu wataendelea mpaka lini, Ee Yehova,
Waovu wataendelea mpaka lini kushangilia?+
4 Wanaropoka na kuongea kwa kiburi;
Watenda dhambi wote wanajigamba kujihusu.
5 Wanawaponda watu wako, Ee Yehova,+
Na kuukandamiza urithi wako.
6 Wanamuua mjane na mkaaji mgeni,
Na kuwaua mayatima.
8 Eleweni jambo hili, ninyi msiotumia akili;
Ninyi wajinga, ni lini mtakapoonyesha ufahamu?+
9 Yule aliyetengeneza* sikio, je, hawezi kusikia?
Yule aliyeumba jicho, je, hawezi kuona?+
10 Yule anayeyarekebisha mataifa, je, hawezi kukaripia?+
Yeye Ndiye anayewafundisha watu ujuzi!+
11 Yehova anajua mawazo ya wanadamu,
Ya kwamba ni pumzi tu.+
12 Mwenye furaha ni mtu unayemrekebisha, Ee Yah,+
Unayemfundisha kwa sheria yako,+
13 Ili kumpa utulivu katika siku za msiba,
Mpaka shimo litakapochimbwa kwa ajili ya mwovu.+
15 Kwa maana kwa mara nyingine tena hukumu itakuwa ya uadilifu,
Na wote walio wanyoofu moyoni wataifuata.
16 Ni nani atakayeinuka dhidi ya waovu kwa ajili yangu?
Ni nani atakayenitetea dhidi ya watenda maovu?
18 Niliposema: “Mguu wangu unateleza,”
Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova, uliendelea kunitegemeza.+
20 Je, kiti cha ufalme* chenye ufisadi kinaweza kuungana nawe
23 Atafanya matendo yao maovu yawarudie.+
Atawaangamiza* kwa uovu wao wenyewe.
Yehova Mungu wetu atawaangamiza.*+
95 Njooni, na tumshangilie Yehova kwa sauti!
Na tumpazie sauti kwa ushindi Mwamba wetu wa wokovu.+
3 Kwa maana Yehova ni Mungu mkuu,
Mfalme mkuu juu ya miungu mingine yote.+
4 Sehemu zenye kina za dunia zimo mkononi mwake;
Vilele vya milima ni vyake.+
6 Njooni, tuabudu na kuinama;
Na tupige magoti mbele za Yehova Muumba wetu.+
Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+
8 Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu kama mlivyofanya kule Meriba,*+
Kama katika siku ya Masa* kule nyikani,+
9 Mababu zenu waliponijaribu;+
Walinipima, ingawa walikuwa wameona matendo yangu.+
10 Kwa miaka 40 nilichukizwa na kizazi hicho, nikasema:
“Wao ni watu wanaopotoka sikuzote katika mioyo yao;
Hawajazijua njia zangu.”
11 Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu:
“Hawataingia katika pumziko langu.”+
96 Mwimbieni Yehova wimbo mpya.+
Mwimbieni Yehova, dunia yote!+
2 Mwimbieni Yehova; lisifuni jina lake.
Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+
3 Tangazeni utukufu wake miongoni mwa mataifa,
Kazi zake zinazostaajabisha miongoni mwa mataifa yote.+
4 Yehova ni mkuu na anastahili kusifiwa kuliko wote.
Anaogopesha kuliko miungu mingine yote.
7 Mpeni Yehova anachostahili, enyi familia za mataifa,
Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
8 Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili;+
Leteni zawadi na mwingie katika nyua zake.
10 Tangazeni miongoni mwa mataifa: “Yehova amekuwa Mfalme!+
Dunia imeimarishwa kabisa, haiwezi kusogezwa.*
Atayahukumu* mataifa kwa haki.”+
11 Mbingu na zishangilie, dunia na iwe na shangwe;
Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza;+
12 Mashamba na vitu vyote vilivyomo na vishangilie.+
Wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie kwa sauti+
13 Mbele za Yehova, kwa maana anakuja,*
Anakuja kuihukumu dunia.
97 Yehova amekuwa Mfalme!+
Dunia na iwe na shangwe.+
Na visiwa vyake vingi vishangilie.+
4 Umeme wake wa radi huiangazia nchi;
Dunia huona na kutetemeka.+
5 Milima huyeyuka kama nta mbele za Yehova,+
Mbele za Bwana wa dunia yote.
6 Mbingu hutangaza uadilifu wake,
Na mataifa yote huona utukufu wake.+
7 Wote wanaoabudu sanamu yoyote ya kuchongwa na waaibishwe,+
Wale wanaojigamba kuhusu miungu yao ya ubatili.+
Mwinamieni,* enyi miungu yote.+
9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote;
Umekwezwa juu zaidi ya miungu mingine yote.+
10 Enyi mnaompenda Yehova, chukieni maovu.+
11 Nuru imemwangazia mwadilifu+
Na shangwe walio wanyoofu moyoni.
12 Shangilieni kwa sababu ya Yehova, enyi waadilifu,
Na mlishukuru jina lake takatifu.*
Muziki.
Mkono wake wa kuume, mkono wake mtakatifu, umeleta wokovu.*+
3 Amekumbuka upendo wake mshikamanifu na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.+
Miisho yote ya dunia imeona wokovu kutoka kwa* Mungu wetu.+
4 Mpazieni Yehova sauti ya ushindi, dunia yote.
Changamkeni na kupaza sauti kwa shangwe na kuimba sifa.*+
5 Mwimbieni sifa* Yehova kwa kinubi,
Kwa kinubi na wimbo mtamu.
6 Kwa tarumbeta na mlio wa pembe,+
Pazeni sauti kwa ushindi mbele za Mfalme, Yehova.
7 Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza,
Dunia na wote wanaokaa humo.
8 Mito na ipige makofi;
Milima na ipaze sauti pamoja kwa shangwe+
9 Mbele za Yehova, kwa maana anakuja* kuihukumu dunia.
99 Yehova amekuwa Mfalme.+ Mataifa na yatetemeke.
Anaketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi.+ Dunia na itikisike.
2 Yehova ni mkuu Sayuni,
Naye yuko juu ya mataifa yote.+
3 Na walisifu jina lako kuu,+
Kwa maana linaogopesha, nalo ni takatifu.
4 Yeye ni mfalme hodari anayependa haki.+
Umeimarisha kabisa mambo manyoofu.
Umetekeleza haki na uadilifu+ katika Yakobo.
6 Musa na Haruni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,+
Na Samweli alikuwa miongoni mwa wale walioliita jina lake.+
Walikuwa wakimwita Yehova,
Naye alikuwa akiwajibu.+
7 Alikuwa akiongea nao kutoka katika nguzo ya wingu.+
Walishika vikumbusho vyake na amri aliyowapa.+
8 Ee Yehova Mungu wetu, uliwajibu.+
9 Mkwezeni Yehova Mungu wetu+
Na mwiname chini* mbele ya mlima wake mtakatifu,+
Kwa maana Yehova Mungu wetu ni mtakatifu.+
Muziki wa shukrani.
100 Mpazieni Yehova sauti ya ushindi, dunia yote.+
2 Mtumikieni Yehova kwa kushangilia.+
Njooni mbele zake kwa kelele za shangwe.
3 Jueni* kwamba Yehova ni Mungu.+
Yeye ndiye aliyetuumba, na sisi ni mali yake.*+
Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.+
Mshukuruni yeye; lisifuni jina lake.+
5 Kwa maana Yehova ni mwema;+
Upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
Na uaminifu wake katika vizazi vyote.+
Muziki wa Daudi.
101 Nitaimba kuhusu upendo mshikamanifu na haki.
Nitakuimbia sifa,* Ee Yehova.
2 Nitatenda kwa busara na bila lawama.*
Utanijia lini?
Nitatembea kwa utimilifu wa moyo+ ndani ya nyumba yangu.
3 Sitaweka kitu chochote kisichofaa* mbele ya macho yangu.
4 Moyo uliopotoka uko mbali nami;
Sitakubali* jambo lililo ovu.
Yeyote aliye na macho ya kiburi na moyo wenye majivuno,
Sitamvumilia.
6 Nitawatazama waaminifu wa dunia,
Ili wakae nami.
Yule anayetembea bila lawama* atanihudumia.
7 Hakuna mtu yeyote mdanganyifu atakayekaa katika nyumba yangu,
Na hakuna mwongo atakayesimama mbele yangu.*
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha* waovu wote wa dunia,
Nitawaangamiza waovu wote kutoka katika jiji la Yehova.+
Sala ya mtu aliyekandamizwa, anapokuwa amekata tamaa* na kummwagia Yehova mahangaiko yake.+
2 Usinifiche uso wako ninapokuwa katika taabu.+
3 Kwa maana siku zangu zinatoweka kama moshi,
Na mifupa yangu imeungua na kuwa myeusi kama tanuru.+
4 Moyo wangu umepigwa kama majani na umenyauka,+
Kwa maana ninasahau kula chakula changu.
6 Mimi ni kama mwari wa nyikani;
Mimi ni kama bundi mdogo katikati ya magofu.
8 Mchana kutwa maadui wangu wananidhihaki.+
Wale wanaonidhihaki* wanatumia jina langu kama laana.
9 Kwa maana ninakula majivu kama mkate,+
Na kinywaji changu kimechanganyika na machozi,+
10 Kwa sababu ya hasira yako na ghadhabu yako,
Kwa maana uliniinua juu ili unitupe tu pembeni.
13 Kwa hakika utainuka na kulionyesha rehema Sayuni,+
Kwa maana ni wakati wa kulionyesha kibali chako;+
Wakati uliowekwa umefika.+
15 Mataifa yataliogopa jina la Yehova,
Na wafalme wote wa dunia utukufu wako.+
18 Hili limeandikwa kwa ajili ya kizazi cha wakati ujao,+
Ili watu watakaozaliwa* baadaye wamsifu Yah.
19 Kwa maana yeye hutazama chini kutoka katika makao yake matakatifu yaliyo juu,+
Kutoka mbinguni Yehova huitazama dunia,
20 Ili asikie kilio cha maumivu cha mfungwa,+
Ili awaweke huru wale waliohukumiwa kifo,+
21 Ili jina la Yehova litangazwe Sayuni+
Na sifa yake Yerusalemu,
22 Mataifa na falme
Zinapokusanyika pamoja ili kumtumikia Yehova.+
23 Alininyang’anya nguvu zangu kabla ya wakati;
Alifupisha siku zangu.
24 Nikasema: “Ee Mungu wangu,
Usiniangamize nikiwa katikati ya maisha yangu,
Wewe ambaye miaka yako inadumu katika vizazi vyote.+
25 Zamani za kale uliiweka misingi ya dunia,
Na mbingu ni kazi ya mikono yako.+
26 Zitaangamia, lakini wewe utadumu;
Zote zitachakaa kama vazi.
Na kama nguo utazibadili, nazo zitatokomea.
27 Lakini wewe ni yuleyule, na miaka yako haitaisha kamwe.+
28 Watoto wa watumishi wako watakaa kwa usalama,
Na uzao wao utaimarishwa kabisa mbele zako.”+
Wa Daudi.
103 Nafsi yangu na imsifu Yehova;
Kila kitu kilicho ndani yangu na kilisifu jina lake takatifu.
2 Nafsi yangu na imsifu Yehova;
Nami nisisahau kamwe mambo yote aliyotenda.+
3 Husamehe makosa yako yote+
Na kuyaponya magonjwa yako yote;+
4 Huukomboa uhai wako kutoka shimoni*+
Na kukuvika taji la upendo wake mshikamanifu na rehema.+
5 Hukushibisha kwa vitu vyema+ maisha yako yote,
Hivi kwamba ujana wako unarudishwa upya kama ule wa tai.+
10 Hajatutendea kulingana na dhambi zetu,+
Wala hajatupa adhabu tuliyostahili kulingana na makosa yetu.+
11 Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,
Ndivyo upendo wake mshikamanifu ulivyo mkubwa kuelekea wale wanaomwogopa.+
12 Kama mashariki ilivyo mbali sana na magharibi,
Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali sana na sisi.+
13 Kama baba anavyowaonyesha wanawe rehema,
Ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa.+
16 Lakini upepo unapovuma, linatoweka,
Kana kwamba halikuwahi kuwepo.*
17 Lakini upendo mshikamanifu wa Yehova ni wa milele na milele*
Kuelekea wale wanaomwogopa,+
Na uadilifu wake kuelekea watoto wa watoto wao,+
18 Kuelekea wale wanaolishika agano lake+
Na wale walio waangalifu ili kuyashika maagizo yake.
19 Yehova amekiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme mbinguni;+
Nao ufalme wake unatawala kila kitu.+
20 Msifuni Yehova, enyi malaika wake wote,+ mlio na nguvu nyingi,
22 Msifuni Yehova, kazi zake zote,
Kila mahali anapotawala.*
Nafsi yangu yote na imsifu Yehova.
104 Nafsi yangu na imsifu Yehova.+
Ee Yehova Mungu wangu, wewe ni mkuu sana.+
3 Hujenga boriti za vyumba vyake vya juu katika maji yaliyo juu,*+
Akiyafanya mawingu kuwa gari lake,+
Akienda juu ya mabawa ya upepo.+
4 Huwafanya malaika wake kuwa roho,
Wahudumu wake kuwa moto unaoteketeza kabisa.+
6 Uliifunika kwa vilindi vya maji kama kwa vazi.+
Maji yalisimama juu ya milima.
7 Kwa kemeo lako yalikimbia;+
Kwa sauti ya mngurumo wako yalikimbia kwa wasiwasi
8 —Milima ilipanda+ na mabonde yakashuka—
Mahali ulipokusudia yawepo.
9 Uliweka mpaka ambao hayapaswi kuvuka,+
Ili yasiifunike dunia tena kamwe.
10 Wewe hupeleka chemchemi katika mabonde;*
Kati ya milima zinatiririka.
11 Zinawapa maji wanyama wote wa mwituni;
Punda mwitu hukata kiu yake.
12 Juu yake ndege wa angani hukaa;
Wanaimba katikati ya majani mengi.
13 Anainywesha milima maji kutoka katika vyumba vyake vya juu.+
Dunia hushibishwa kwa matunda ya kazi zako.+
14 Anaotesha majani kwa ajili ya ng’ombe
Na mimea kwa ajili ya matumizi ya wanadamu,+
Ili chakula kikue ardhini
15 Na divai inayofanya moyo wa mwanadamu ushangilie,+
Mafuta yanayofanya uso ung’ae,
Na mkate unaotegemeza moyo wa mwanadamu anayeweza kufa.+
16 Miti ya Yehova imetosheka,
Mierezi ya Lebanoni aliyopanda,
17 Ambamo ndege hutengeneza viota.
Makao ya korongo+ ni miberoshi.
19 Ameuumba mwezi ili upime nyakati zilizowekwa;
Jua linajua vizuri wakati wa kutua.+
20 Wewe unaleta giza, usiku unaingia,+
Wakati ambapo wanyama wote wa mwituni wanazunguka-zunguka.
22 Jua linapochomoza,
Wanarudi na kulala katika mapango yao.
23 Mwanadamu huenda kwenye kazi yake,
Naye hufanya kazi kwa jasho mpaka jioni.
24 Jinsi kazi zako zilivyo nyingi sana, Ee Yehova!+
Umezifanya zote kwa hekima.+
Dunia imejaa vitu ulivyoumba.
25 Kisha kuna bahari, ni kubwa sana na pana,
Imejaa viumbe walio hai wasio na idadi, wadogo kwa wakubwa.+
27 Wote wanakungojea wewe
Uwape chakula chao kwa wakati wake.+
28 Wanakusanya unachowapa.+
Unapofumbua mkono wako, wanashiba vitu vyema.+
29 Ukiuficha uso wako, wanahangaika.
Ukiiondoa roho yao, wanakufa na kurudi mavumbini.+
30 Ukiituma roho yako, wanaumbwa,+
Nawe unaifanya ardhi iwe na sura mpya.
31 Utukufu wa Yehova utadumu milele.
Yehova atashangilia kwa sababu ya kazi zake.+
32 Huitazama dunia, inatetemeka;
Huigusa milima, inafuka moshi.+
34 Mawazo yangu na yampendeze.*
Nitashangilia kwa sababu ya Yehova.
35 Watenda dhambi watatoweka duniani,
Na waovu hawatakuwapo tena.+
Nafsi yangu na imsifu Yehova. Msifuni Yah!*
3 Jivunieni jina lake takatifu.+
Mioyo ya wale wanaomtafuta Yehova na ishangilie.+
4 Mtafuteni Yehova+ na nguvu zake.
Utafuteni uso* wake daima.
5 Kumbukeni kazi zinazostaajabisha alizofanya,
Miujiza yake na hukumu alizotangaza,+
6 Enyi uzao wa* Abrahamu mtumishi wake,+
Enyi wana wa Yakobo, watu wake aliowachagua.+
7 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+
Hukumu zake ziko duniani kote.+
8 Anakumbuka agano lake milele,+
Ahadi aliyotoa,* hata kufikia vizazi elfu,+
9 Agano alilofanya na Abrahamu,+
Na kiapo alichomwapia Isaka,+
10 Alichotoa kama amri kwa Yakobo
Na kama agano la kudumu kwa Israeli,
11 Akisema, “Nitakupa nchi ya Kanaani+
Kuwa urithi wako uliogawiwa.”+
13 Walitembeatembea kutoka taifa moja hadi taifa lingine,
Kutoka ufalme mmoja hadi ufalme mwingine.+
14 Hakumruhusu mtu yeyote awakandamize,+
Lakini kwa sababu yao aliwakaripia wafalme,+
15 Akisema, “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,
Wala msiwatendee manabii wangu jambo lolote baya.”+
17 Alimtuma mtu awatangulie
Ambaye aliuzwa kuwa mtumwa, Yosefu.+
18 Waliifunga* miguu yake kwa pingu,+
Shingo yake ilitiwa katika vyuma;*
19 Mpaka wakati ambapo neno lake lilitimia,+
Neno la Yehova ndilo lililomsafisha.
20 Mfalme aliamuru afunguliwe,+
Mtawala wa mataifa akamweka huru.
21 Akamweka kuwa bwana mkubwa wa nyumba yake,
Mtawala wa mali zake zote,+
22 Ili awe na mamlaka juu ya* wakuu wake kama alivyopenda*
Na kuwafundisha wazee wake hekima.+
23 Kisha Israeli akaja Misri,+
Na Yakobo akakaa akiwa mgeni katika nchi ya Hamu.
24 Mungu aliwafanya watu wake waongezeke sana;+
Aliwafanya wawe na nguvu kuliko maadui wao,+
25 Akaruhusu mioyo yao ibadilike ili wawachukie watu wake,
Ili wapange njama dhidi ya watumishi wake.+
27 Walifanya ishara zake kati yao,
Miujiza yake katika nchi ya Hamu.+
28 Alilituma giza na nchi ikawa giza;+
Hawakuasi maneno yake.
29 Alibadili maji yao yakawa damu
Na kuwaua samaki wao.+
30 Nchi yao ikajaa vyura,+
Hata katika vyumba vya mfalme.
33 Aliipiga mizabibu yao na mitini yao
Na kuivunjavunja miti ya eneo lao.
34 Aliagiza nzige wavamie,
Nzige wachanga wasio na idadi.+
35 Walikula kabisa mimea yote nchini,
Nao wakala kabisa mazao ya ardhi.
36 Kisha akamuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao,+
Mwanzo wa nguvu zao za uzazi.
37 Aliwatoa nje watu wake wakiwa na fedha na dhahabu;+
Na hakuna yeyote katika makabila yake aliyejikwaa.
42 Kwa maana aliikumbuka ahadi takatifu aliyompa Abrahamu mtumishi wake.+
43 Kwa hiyo akawatoa watu wake wakishangilia,+
Watu wake aliowachagua aliwatoa kwa kilio cha shangwe.
44 Aliwapa nchi za mataifa;+
Walirithi vitu ambavyo mataifa mengine yalikuwa yametaabika kuvipata,+
45 Ili waweze kutii maagizo yake+
Na kushika sheria zake.
Msifuni Yah!*
106 Msifuni Yah!*
2 Ni nani anayeweza kutangaza kikamili matendo ya Yehova yenye nguvu
Au kutangaza matendo yake yote yanayostahili sifa?+
3 Wenye furaha ni wale wanaotenda haki,
Ambao sikuzote wanatenda yaliyo sawa.+
4 Nikumbuke, Ee Yehova, unapowaonyesha kibali* watu wako.+
Nitunze kwa matendo yako ya wokovu,
5 Ili nifurahie wema unaowaonyesha watu wako uliowachagua,+
Ili nishangilie pamoja na taifa lako,
Ili nikusifu kwa fahari* pamoja na urithi wako.
7 Mababu zetu kule Misri hawakuthamini* kazi zako zinazostaajabisha.
Hawakukumbuka upendo wako mwingi mshikamanifu,
Bali waliasi baharini, kando ya Bahari Nyekundu.+
9 Aliikemea Bahari Nyekundu, ikakauka;
Aliwaongoza katika vilindi vyake kana kwamba wanapitia jangwani;*+
10 Aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui yao+
Na kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.+
13 Lakini walisahau haraka mambo aliyotenda;+
Hawakungojea ushauri wake.
15 Aliwapa walichoomba,
Lakini akawapiga kwa ugonjwa uliowadhoofisha.+
17 Kisha dunia ikafunguka na kummeza Dathani
Na kuwafunika wale waliokusanyika pamoja na Abiramu.+
18 Moto uliwaka katika kundi lao;
Mwali wa moto ukawateketeza kabisa waovu.+
19 Walitengeneza ndama kule Horebu
Na kuiinamia sanamu ya chuma;*+
20 Waliubadili utukufu wangu
Kwa mfano wa ng’ombe dume anayekula nyasi.+
21 Walimsahau Mungu+ Mwokozi wao,
Aliyetenda mambo makuu nchini Misri,+
22 Kazi zinazostaajabisha katika nchi ya Hamu,+
Mambo yanayoogopesha kwenye Bahari Nyekundu.+
23 Alikuwa karibu kuamuru waangamizwe,
Lakini Musa, mchaguliwa wake, akaingilia kati*
Ili kuzuia hasira yake inayoangamiza.+
26 Kwa hiyo akainua mkono wake na kuapa kuwahusu
Kwamba angewaangusha nyikani;+
27 Angewaangusha wazao wao miongoni mwa mataifa,
Naye angewatawanya katika nchi mbalimbali.+
30 Lakini Finehasi alipoinuka na kuingilia kati,
Pigo hilo lilikomeshwa.+
31 Na jambo hilo likahesabiwa kwake kuwa uadilifu
Katika vizazi vyote milele.+
33 Waliitia uchungu roho yake,
Naye akaongea bila kufikiri kwa midomo yake.+
37 Waliwatoa dhabihu wana wao
Na mabinti wao kwa roho waovu.+
38 Waliendelea kumwaga damu isiyo na hatia,+
Damu ya wana wao na mabinti wao wenyewe
Ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani;+
Na nchi ikachafuliwa kwa umwagaji wa damu.
39 Wakawa wachafu kwa sababu ya kazi zao;
Walifanya ukahaba wa kiroho kwa matendo yao.+
40 Kwa hiyo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya watu wake,
Naye akauchukia sana urithi wake.
42 Maadui wao waliwakandamiza,
Nao wakatiishwa chini ya nguvu zao.*
43 Aliwaokoa mara nyingi,+
Lakini walikuwa wakiasi na kukosa kutii,+
Nao walikuwa wakifedheheshwa kwa sababu ya makosa yao.+
45 Na kwa ajili yao alikuwa akikumbuka agano lake,
Naye alikuwa akiwahurumia,* akichochewa na upendo wake mwingi* mshikamanifu.+
46 Alikuwa akisababisha wahurumiwe
Na wote waliowachukua mateka.+
47 Tuokoe, Ee Yehova Mungu wetu,+
Na kutukusanya kutoka katika mataifa+
Ili tulishukuru jina lako takatifu
Na watu wote waseme, “Amina!”*
Msifuni Yah!*
KITABU CHA TANO
(Zaburi 107-150)
2 Wale waliokombolewa* na Yehova na waseme jambo hilo,
Wale aliowakomboa kutoka mikononi mwa* adui,+
3 Wale aliowakusanya pamoja kutoka katika nchi mbalimbali,+
Kutoka mashariki na kutoka magharibi,*
Kutoka kaskazini na kutoka kusini.+
4 Walitangatanga nyikani, jangwani;
Hawakupata njia ya kwenda katika jiji ambamo wangeweza kuishi.
5 Walikuwa na njaa na kiu;
Walidhoofika kwa sababu ya uchovu.
8 Watu na wamshukuru Yehova+ kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu
Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.+
10 Baadhi yao walikuwa wakiishi katika giza zito sana,
Wafungwa walioteseka na kufungwa kwa vyuma.
11 Kwa maana walikuwa wameliasi neno la Mungu;
Waliudharau ushauri wa Aliye Juu Zaidi.+
12 Kwa hiyo aliinyenyekeza mioyo yao kupitia taabu;+
Walijikwaa, na hakukuwa na yeyote wa kuwasaidia.
13 Walimlilia Yehova awasaidie walipokuwa wakitaabika;
Akawaokoa kutoka katika dhiki yao.
14 Aliwatoa katika giza zito sana,
Na kuzikata pingu zao.+
15 Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu+
Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.
16 Kwa maana ameivunja milango ya shaba
Na kuyakata makomeo ya chuma.+
18 Walipoteza hamu ya kula kila aina ya chakula;*
Waliyakaribia malango ya kifo.
19 Walikuwa wakimlilia Yehova awasaidie walipokuwa wakitaabika;
Naye alikuwa akiwaokoa kutoka katika dhiki yao.
20 Alikuwa akituma neno lake na kuwaponya+
Na kuwaokoa kutoka katika mashimo ambamo walikuwa wamenaswa.
21 Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu
Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.
22 Na watoe dhabihu za shukrani+
Na kutangaza kazi zake kwa kilio cha shangwe.
23 Wale wanaosafiri kwa meli baharini,
Wanaofanya biashara yao kwenye maji mengi,+
24 Wameziona kazi za Yehova
Na kazi zake zinazostaajabisha zilizo vilindini;+
25 Jinsi dhoruba ya upepo inavyoinuka kwa neno lake,+
Na kuyainua mawimbi ya bahari.
26 Hayo huinuka juu angani;
Hushuka chini kwa nguvu vilindini.
Ujasiri wao* huyeyuka kwa sababu ya msiba unaokaribia.
27 Wao hugaagaa na kupepesuka kama mlevi,
Na ustadi wao wote unakosa manufaa kabisa.+
28 Kisha wanamlilia Yehova kwa sauti wanapotaabika,+
Naye huwaokoa kutoka katika dhiki yao.
29 Yeye huituliza dhoruba ya upepo;
Mawimbi ya bahari hunyamaza.+
30 Wanashangilia yanapotulia,
Naye huwaongoza kwenda kwenye bandari wanayotamani.
31 Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu
Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.+
33 Yeye hubadili mito kuwa jangwa,
Na chemchemi za maji kuwa ardhi iliyokauka,+
34 Nchi inayozaa kuwa nchi iliyoharibika yenye chumvi,+
Kwa sababu ya uovu wa wale wanaokaa humo.
35 Yeye hulibadili jangwa kuwa madimbwi ya maji yenye matete,
Na nchi kavu kuwa chemchemi za maji.+
38 Huwabariki, nao huongezeka sana;
Haachi ng’ombe wao wapungue.+
39 Kisha wanakuwa wachache tena na kuaibishwa
Kwa sababu ya ukandamizaji, msiba, na huzuni.
40 Huwamwagia wakuu dharau
Na kuwafanya watangetange jangwani kusiko na njia.+
41 Lakini huwalinda* maskini ili wasikandamizwe+
Na kufanya familia zao ziwe nyingi kama kundi la kondoo.
43 Yeyote aliye na hekima atayachunguza mambo hayo+
Naye atatafakari kwa makini matendo ya Yehova ya upendo mshikamanifu.+
Wimbo. Muziki wa Daudi.
108 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu.
Nitaimba na kupiga muziki kwa nafsi yangu yote.*+
2 Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.+
Nitayaamsha mapambazuko.
3 Nitakusifu miongoni mwa mataifa, Ee Yehova,
Nami nitakuimbia sifa* miongoni mwa mataifa.
4 Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkubwa, uko juu kama mbingu,+
Na uaminifu wako, unafika mpaka angani.
5 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+
6 Ili wapendwa wako waokolewe,
Tuokoe kwa mkono wako wa kuume na unijibu.+
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake:*
8 Gileadi+ ni yangu, na Manase ni yangu,
Na Efraimu ni kofia ya kukinga* kichwa changu;+
Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+
9 Moabu ni beseni langu la kuogea.+
Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+
Nitapaza sauti kwa ushindi juu ya Ufilisti.”+
10 Ni nani atakayenipeleka kwenye lile jiji lenye ngome?
Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?+
11 Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetukataa,
Mungu wetu, ambaye haendi tena na majeshi yetu?+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
109 Ee Mungu ninayekusifu,+ usinyamaze.
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu hufumbua vinywa vyao dhidi yangu.
Wanaongea kunihusu kwa ndimi za uwongo;+
3 Wananizingira kwa maneno ya chuki,
Na kunishambulia bila sababu.+
4 Wananipinga licha ya kwamba ninawapenda;+
Lakini ninaendelea kusali.
6 Mweke mtu mwovu amhukumu;
Mpinzani* na asimame mkono wake wa kulia.
9 Watoto wake* na wawe mayatima,
Na mke wake awe mjane.
10 Watoto wake* na watangetange wakiombaomba,
Wakitafuta chakula katika nyumba zao zilizoharibiwa.
11 Anayemdai na achukue kwa nguvu* vitu vyote alivyo navyo,
Wageni na wapore mali zake.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea kwa fadhili,*
Na asiwepo mtu yeyote wa kuwahurumia watoto wake mayatima.
14 Kosa la mababu zake na likumbukwe na Yehova,+
Na dhambi ya mama yake isifutwe.
15 Yehova na akumbuke daima waliyotenda;
Na afutilie mbali kumbukumbu lao kutoka duniani.+
16 Kwa maana hakukumbuka kutenda kwa fadhili,*+
Bali aliendelea kumfuatia mtu aliyekandamizwa,+ maskini, na aliyevunjika moyo
Ili amuue.+
17 Alipenda kulaani, kwa hiyo laana hiyo ikampata;
Hakupenda kubariki, kwa hiyo hakupata baraka yoyote.
18 Alivishwa laana kama vazi lake.
Nazo zikamwagwa mwilini mwake kama maji,
Mifupani mwake kama mafuta.
19 Laana zake na ziwe kama vazi analojifunika+
Na kama mshipi anaovaa daima.
20 Hayo ndiyo malipo yanayotoka kwa Yehova ya mtu anayenipinga+
Na ya wale wanaosema mambo maovu dhidi yangu.
21 Lakini wewe, Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu,
Tenda kwa niaba yangu kwa ajili ya jina lako.+
Niokoe, kwa sababu upendo wako mshikamanifu ni mwema.+
23 Ninapitilia mbali kama kivuli kinachofifia;
Nimekung’utwa kama nzige.
24 Magoti yangu yanalegea kwa sababu ya kufunga;
Mwili wangu umekonda, unazidi kupungua.*
25 Nimekuwa kitu cha kudhihakiwa nao.+
Wanaponiona, wanatikisa vichwa vyao.+
26 Nisaidie, Ee Yehova Mungu wangu;
Niokoe kwa upendo wako mshikamanifu.
27 Na wajue kwamba mkono wako ndio uliotenda hili;
Kwamba wewe, Ee Yehova, umetenda hili.
28 Waache watangaze laana, lakini wewe toa baraka.
Na waaibishwe wanapoinuka dhidi yangu,
Lakini acha mtumishi wako ashangilie.
30 Kinywa changu kitamsifu Yehova kwa bidii;
Nitamsifu yeye mbele ya watu wengi.+
31 Kwa maana atasimama mkono wa kulia wa maskini
Ili amwokoe kutoka kwa wale wanaomhukumu.
Muziki wa Daudi.
110 Yehova alimtangazia hivi Bwana wangu:
2 Yehova atainyoosha fimbo ya ufalme ya nguvu zako kutoka Sayuni, akisema:
“Nenda ukitiisha kati ya maadui wako.”+
3 Watu wako watajitoa kwa hiari katika siku ya jeshi lako.*
Katika utakatifu wenye fahari, kutoka katika tumbo la uzazi la mapambazuko,
Una kundi lako la vijana kama matone ya umande.
4 Yehova ameapa naye hatabadili nia yake:*
Atamponda kiongozi wa* nchi kubwa sana.*
7 Atakunywa* maji ya kijito kilicho kando ya barabara.
Kwa hiyo, atakiinua juu kichwa chake.
א [Aleph]
Nitamsifu Yehova kwa moyo wangu wote+
ב [Beth]
Katika kikundi kilichokusanyika cha watu wanyoofu na katika kutaniko.
ג [Gimel]
2 Kazi za Yehova ni kuu;+
ד [Daleth]
Wale wote wanaopendezwa nazo hujifunza kuzihusu.+
ה [He]
3 Utendaji wake ni wenye utukufu na fahari,
ו [Waw]
Na uadilifu wake unadumu milele.+
ז [Zayin]
4 Hufanya kazi zake zinazostaajabisha zikumbukwe.+
ח [Heth]
Yehova ni mwenye huruma* na mwenye rehema.+
ט [Teth]
5 Huwapa chakula wale wanaomwogopa.+
י [Yod]
Hukumbuka agano lake milele.+
כ [Kaph]
6 Amewafunulia watu wake kazi zake zenye nguvu
ל [Lamed]
Kwa kuwapa urithi wa mataifa.+
מ [Mem]
7 Kazi za mikono yake ni kweli na haki;+
נ [Nun]
Maagizo yake yote yanategemeka.+
ס [Samekh]
8 Yanategemeka* sikuzote, sasa na milele;
ע [Ayin]
Msingi wake ni kweli na uadilifu.+
פ [Pe]
9 Amewakomboa watu wake.+
צ [Tsade]
Aliamuru kwamba agano lake linapaswa kudumu milele.
ק [Qoph]
Jina lake ni takatifu na linaogopesha.+
ר [Resh]
10 Kumwogopa Yehova ni mwanzo wa hekima.+
ש [Sin]
Wale wote wanaotii maagizo yake wana ufahamu mzuri.+
ת [Taw]
Sifa yake hudumu milele.
א [Aleph]
Mwenye furaha ni mtu anayemwogopa Yehova,+
ב [Beth]
Anayependezwa sana na amri zake.+
ג [Gimel]
2 Wazao wake watakuwa wenye nguvu duniani,
ד [Daleth]
Na kizazi cha mtu mnyoofu kitabarikiwa.+
ה [He]
3 Nyumbani mwake mna mali na utajiri,
ו [Waw]
Na uadilifu wake unadumu milele.
ז [Zayin]
4 Yeye humwangazia mnyoofu kama nuru gizani.+
ח [Heth]
Ni mwenye huruma* na mwenye rehema+ na ni mwadilifu.
ט [Teth]
5 Mambo humwendea vema mtu anayekopesha kwa ukarimu.*+
י [Yod]
Hufanya mambo yake kwa haki.
כ [Kaph]
6 Hatatikiswa kamwe.+
ל [Lamed]
Mwadilifu atakumbukwa milele.+
מ [Mem]
7 Hataogopa habari mbaya.+
נ [Nun]
Moyo wake ni imara, unamtumaini Yehova.+
ס [Samekh]
Hatimaye atawatazama maadui wake wakishindwa.+
פ [Pe]
9 Amegawa kwa wingi;* amewapa maskini.+
צ [Tsade]
Uadilifu wake unadumu milele.+
ק [Qoph]
Nguvu zake mwenyewe zitakwezwa* kwa utukufu.
ר [Resh]
10 Mwovu ataona na kukasirika.
ש [Shin]
Atasaga meno yake na kuyeyuka.
ת [Taw]
Tamaa za mwovu zitaangamia.+
113 Msifuni Yah!*
Msifuni, enyi watumishi wa Yehova,
Lisifuni jina la Yehova.
2 Jina la Yehova na lisifiwe
Kuanzia sasa mpaka milele.+
3 Kuanzia jua linapochomoza mpaka linapotua,
Jina la Yehova na lisifiwe.+
6 Huinama chini ili atazame mbingu na dunia,+
7 Akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka mavumbini.
Humwinua juu maskini kutoka kwenye rundo la majivu*+
8 Ili amketishe pamoja na viongozi,
Pamoja na viongozi wa watu wake.
Msifuni Yah!*
114 Israeli alipotoka Misri,+
Nyumba ya Yakobo ilipotoka kati ya watu waliozungumza lugha ya kigeni,
2 Yuda ikawa mahali pake patakatifu,
Israeli, miliki yake.+
4 Milima ilirukaruka kama kondoo dume,+
Vilima, kama wanakondoo.
5 Ee bahari, ni nini kilichofanya ukimbie?+
Ee Yordani, kwa nini ulirudi nyuma?+
6 Enyi milima, kwa nini mlirukaruka kama kondoo dume,
Kama wanakondoo, enyi vilima?
7 Tetemeka, Ee dunia, kwa sababu ya Bwana,
Kwa sababu ya Mungu wa Yakobo,+
8 Anayeubadili mwamba kuwa dimbwi la maji lenye matete,
Mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.+
115 Usitutukuze sisi, Ee Yehova, usitutukuze sisi,*
Bali litukuze jina lako+
Kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu na uaminifu wako.+
2 Kwa nini mataifa yaseme:
“Yuko wapi Mungu wao?”+
3 Mungu wetu yuko mbinguni;
Hufanya lolote apendalo.
4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu,
Kazi ya mikono ya mwanadamu.+
5 Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea;+
Zina macho, lakini haziwezi kuona;
6 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia;
Zina pua, lakini haziwezi kunusa;
7 Zina mikono, lakini haziwezi kugusa;
Zina miguu, lakini haziwezi kutembea;+
Hazitoi sauti yoyote kwa koo zake.+
10 Ee nyumba ya Haruni,+ mtumainini Yehova;
—Yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.
13 Atawabariki wale wanaomwogopa Yehova,
Wadogo kwa wakubwa.
18 Lakini sisi tutamsifu Yah
Kuanzia sasa mpaka milele.
Msifuni Yah!*
Nililemewa na taabu na huzuni.+
4 Lakini nikaliita jina la Yehova:+
“Ee, Yehova, niokoe!”*
6 Yehova anawalinda wasio na uzoefu.+
Nilishushwa chini, akaniokoa.
7 Acha nafsi* yangu ipumzike tena,
Kwa maana Yehova amenitendea kwa fadhili.
9 Nitatembea mbele za Yehova katika nchi ya walio hai.
10 Nilikuwa na imani, ndio maana niliongea;+
Niliteseka sana.
11 Basi nikashikwa na hofu na kusema:
“Kila mwanadamu ni mwongo.”+
12 Nitamlipa Yehova nini
Kwa mema yote aliyonitendea?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu,*
Nami nitaliitia jina la Yehova.
14 Nitamtimizia Yehova nadhiri zangu
Mbele ya watu wake wote.+
16 Ninakusihi, Ee Yehova,
Kwa maana mimi ni mtumishi wako.
Mimi ni mtumishi wako, mwana wa kijakazi wako.
Umezifungua pingu zangu.+
17 Nitakutolea dhabihu ya shukrani;+
Nitaliitia jina la Yehova.
18 Nitamtimizia Yehova nadhiri zangu+
Mbele ya watu wake wote,+
19 Katika nyua za nyumba ya Yehova,+
Kati yako, Ee Yerusalemu.
118 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+
Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
2 Watu wa Israeli na waseme sasa:
“Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”
3 Watu wa nyumba ya Haruni na waseme sasa:
“Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”
4 Wale wanaomwogopa Yehova na waseme sasa:
“Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”
6 Yehova yuko upande wangu; sitaogopa.+
Mwanadamu atanifanya nini?+
8 Ni bora kumkimbilia Yehova
Kuliko kuwatumaini wanadamu.+
9 Ni bora kumkimbilia Yehova
Kuliko kuwatumaini wakuu.+
11 Yalinizingira, naam, yalinizingira kabisa,
Lakini katika jina la Yehova,
Niliyafukuza.
12 Yalinizingira kama nyuki,
Lakini yalizimwa haraka kama moto unaoteketeza miiba.
Katika jina la Yehova,
Niliyafukuza.+
13 Nilisukumwa kwa nguvu* ili nianguke,
Lakini Yehova alinisaidia.
14 Yah ni mahali pangu pa kujificha na nguvu zangu,
Naye amekuwa wokovu wangu.+
15 Sauti ya shangwe na wokovu*
Imo katika mahema ya waadilifu.
Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
16 Mkono wa kuume wa Yehova unajikweza;
Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
17 Sitakufa, hapana, nitaishi,
Ili nizitangaze kazi za Yah.+
19 Nifungulieni malango ya uadilifu;+
Nitaingia humo na kumsifu Yah.
20 Hili ndilo lango la Yehova.
Waadilifu wataingia humo.+
21 Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+
Nawe ukawa wokovu wangu.
24 Hii ndiyo siku ambayo Yehova ameifanya;
Tutaishangilia na kuifurahia.
25 Yehova, tuokoe, tafadhali, tunakusihi!
Yehova, tupe ushindi, tafadhali!
26 Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova;+
Tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yehova.
27 Yehova ni Mungu;
Hutupatia nuru.+
28 Wewe ni Mungu wangu, nami nitakusifu;
Mungu wangu, nitakukweza.+
א [Aleph]
3 Hawatendi uovu wowote;
Wanatembea katika njia zake.+
4 Umeamuru
Kwamba maagizo yako yafuatwe kwa uangalifu.+
6 Ndipo sitaaibishwa+
Ninapokazia uangalifu amri zako zote.
7 Nitakusifu kwa moyo mnyoofu
Ninapojifunza hukumu zako za uadilifu.
8 Nitayashika masharti yako.
Kamwe usiniache kabisa.
ב [Beth]
9 Kijana anaweza kuisafishaje njia yake?
Kwa kujilinda kulingana na neno lako.+
10 Ninakutafuta kwa moyo wangu wote.
Usiache nikengeuke kutoka katika amri zako.+
12 Na usifiwe, Ee Yehova;
Nifundishe masharti yako.
13 Kwa midomo yangu ninatangaza
Hukumu zote ulizonena.
16 Ninazipenda sana sheria zako.
Sitalisahau neno lako.+
ג [Gimel]
17 Nitendee kwa fadhili mimi mtumishi wako,
Ili niishi na kulishika neno lako.+
18 Yafumbue macho yangu ili nione wazi
Mambo yanayostaajabisha katika sheria yako.
19 Mimi ni mgeni tu nchini.+
Usinifiche amri zako.
20 Ninapondeka* kwa kutamani sana
Hukumu zako nyakati zote.
21 Unawakemea wenye kimbelembele,
Watu waliolaaniwa wanaokengeuka kutoka katika amri zako.+
22 Niondolee* dhihaka na dharau,
Kwa maana nimeshika vikumbusho vyako.
23 Hata wakuu wanapoketi pamoja na kusema mambo mabaya kunihusu,
Mimi mtumishi wako ninatafakari* masharti yako.
ד [Daleth]
25 Ninalala kifudifudi mavumbini.+
Nihifadhi hai kulingana na neno lako.+
26 Nilikwambia kuhusu njia zangu, nawe ukanijibu;
Nifundishe masharti yako.+
28 Nimekosa usingizi kwa sababu ya huzuni.
Nitie nguvu kulingana na neno lako.
29 Niondolee njia ya udanganyifu,+
Na unionyeshe kibali kwa kunipa sheria yako.
30 Nimechagua njia ya uaminifu.+
Ninatambua kwamba hukumu zako zinafaa.
31 Ninashikamana na vikumbusho vyako.+
Ee Yehova, usiache nikatishwe tamaa.*+
32 Nitaifuata kwa bidii* njia ya amri zako
Kwa sababu wewe huufanya moyo wangu uwe na nafasi kwa ajili yake.*
ה [He]
34 Nipe uelewaji,
Ili niweze kushika sheria yako
Na kuitii kwa moyo wangu wote.
37 Yageuzie mbali macho yangu yasitazame mambo yasiyofaa;+
Nihifadhi hai katika njia yako.
39 Niondolee aibu ninayoogopa sana,
Kwa maana hukumu zako ni njema.+
40 Tazama jinsi ninavyoyatamani sana maagizo yako!
Nihifadhi hai katika uadilifu wako.
ו [Waw]
41 Acha nijionee upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova,+
Wokovu wako kulingana na ahadi yako;*+
42 Kisha nitamjibu yule anayenidhihaki,
Kwa maana ninalitumaini neno lako.
43 Usiondoe kabisa neno la kweli kutoka kinywani mwangu,
Kwa maana nimetumaini* hukumu yako.
44 Nitaishika sheria yako daima,
Milele na milele.+
46 Nitaongea kuhusu vikumbusho vyako mbele ya wafalme,
Nami sitaaibika.+
47 Ninazipenda sana amri zako,
Naam, ninazipenda.+
48 Nitainua mikono yangu kuelekea amri zako, ambazo ninazipenda,+
ז [Zayin]
50 Hilo ndilo faraja yangu katika mateso yangu,+
Kwa maana neno lako limenihifadhi hai.
51 Wenye kimbelembele wananidhihaki sana,
Lakini sikengeuki kutoka kwenye sheria yako.+
53 Nimeshikwa na hasira kali kwa sababu ya waovu,
Wanaoiacha sheria yako.+
54 Masharti yako ni nyimbo kwangu
Popote ninapoishi.*
55 Wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, Ee Yehova,+
Ili niweze kuishika sheria yako.
56 Nimezoea kufanya hivyo
Kwa sababu nimeyatii maagizo yako.
ח [Heth]
59 Nimezichunguza njia zangu,
Ili niirudishe miguu yangu kwenye vikumbusho vyako.+
60 Ninafanya haraka wala sikawii
Kuzishika amri zako.+
61 Kamba za waovu zinanizunguka,
Lakini siisahau sheria yako.+
62 Katikati ya usiku ninaamka ili kukushukuru+
Kwa sababu ya hukumu zako za uadilifu.
63 Mimi ni rafiki ya wote wanaokuogopa wewe
Na ya wale wanaoyatii maagizo yako.+
64 Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova, umeijaza dunia;+
Nifundishe masharti yako.
ט [Teth]
65 Umenitendea mema mimi mtumishi wako,
Ee Yehova, kulingana na neno lako.
66 Nifundishe busara na ujuzi,+
Kwa maana nimezitumaini amri zako.
68 Wewe ni mwema+ na kazi zako ni njema.
Nifundishe masharti yako.+
69 Wenye kimbelembele hunipaka uwongo,
Lakini ninayatii maagizo yako kwa moyo wangu wote.
71 Ni vema kwamba nimeteswa,+
Ili nijifunze masharti yako.
י [Yod]
73 Mikono yako iliniumba na kunifinyanga.
Nipe uelewaji,
Ili nijifunze amri zako.+
76 Tafadhali, upendo wako mshikamanifu+ na unifariji,
Kulingana na ahadi yako uliyonipa* mimi mtumishi wako.
78 Wenye kimbelembele na waaibishwe,
Kwa maana wananikosea bila sababu.*
Lakini nitayatafakari* maagizo yako.+
79 Acha wale wanaokuogopa warudi kwangu,
Wale wanaojua vikumbusho vyako.
כ [Kaph]
83 Kwa maana mimi ni kama kiriba cha ngozi kilichokaushwa na moshi,
Lakini siyasahau masharti yako.+
84 Mimi mtumishi wako nisubiri kwa siku ngapi?
Ni lini utakapowahukumu wale wanaonitesa?+
85 Wenye kimbelembele wananichimbia mashimo,
Wale wanaoasi sheria yako.
86 Amri zako zote zinategemeka.
Watu wananitesa bila sababu; nisaidie!+
87 Karibu waniangamize kutoka duniani,
Lakini sikuyaacha maagizo yako.
88 Nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu,
Ili nishike vikumbusho ulivyosema.
ל [Lamed]
89 Milele, Ee Yehova,
Neno lako litadumu mbinguni.+
90 Uaminifu wako umekuwepo kwa vizazi vyote.+
Umeiimarisha kabisa dunia, ili idumu.+
91 Kwa sababu ya hukumu zako zinadumu* mpaka leo,
Kwa maana zote ni watumishi wako.
92 Kama singeipenda sana sheria yako,
Ningekuwa nimeangamia katika mateso yangu.+
93 Sitayasahau kamwe maagizo yako,
Kwa sababu kupitia hayo umenihifadhi hai.+
95 Waovu wanasubiri kuniangamiza,
Lakini ninavikazia sana fikira vikumbusho vyako.
96 Nimeona mwisho wa ukamilifu wote,
Lakini amri yako haina mpaka.*
מ [Mem]
97 Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako!+
98 Amri yako hunifanya niwe na hekima kuliko maadui wangu,+
Kwa sababu ninayo milele.
100 Ninatenda kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,
Kwa sababu ninayatii maagizo yako.
101 Ninakataa kutembea kwenye njia yoyote ya uovu,+
Ili nishike neno lako.
102 Sigeuki kando kutoka katika hukumu zako,
Kwa maana umenifundisha.
103 Jinsi maneno yako yalivyo matamu kwenye kaakaa langu,
Kuliko asali kinywani mwangu!+
104 Kwa sababu ya maagizo yako ninatenda kwa uelewaji.+
Ndiyo sababu ninaichukia kila njia ya uwongo.+
נ [Nun]
105 Neno lako ni taa ya mguu wangu,
Na nuru ya njia yangu.+
106 Nimeweka kiapo, nami nitakitimiza,
Kwamba nitazishika hukumu zako za uadilifu.
107 Nimeteseka sana.+
Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na neno lako.+
108 Tafadhali yafurahie matoleo yangu ya hiari ya kukusifu,*+ Ee Yehova,
Na unifundishe hukumu zako.+
110 Waovu wamenitegea mtego,
Lakini sijakengeuka kutoka katika maagizo yako.+
111 Ninavichukua vikumbusho vyako kuwa mali yangu ya kudumu,*
Kwa maana hivyo ni shangwe ya moyo wangu.+
112 Nimeazimia* kuyatii masharti yako
Nyakati zote, mpaka mwisho.
ס [Samekh]
115 Kaeni mbali nami, enyi waovu,+
Ili nizishike amri za Mungu wangu.
118 Unawakataa wote wanaokengeuka kutoka katika masharti yako,+
Kwa maana ni waongo na wadanganyifu.
119 Unawatupilia mbali waovu wote walio duniani kana kwamba ni takataka.*+
Ndiyo sababu ninavipenda vikumbusho vyako.
120 Mwili wangu unatetemeka kwa sababu ya kukuhofu;
Ninaogopa hukumu zako.
ע [Ayin]
121 Nimetenda yaliyo ya haki na uadilifu.
Usiniache mikononi mwa wale wanaonikandamiza!
122 Nihakikishie hali njema mimi mtumishi wako;
Wenye kimbelembele wasinikandamize.
125 Mimi ni mtumishi wako; nipe uelewaji,+
Ili nijue vikumbusho vyako.
126 Wakati umefika wa Yehova kutenda,+
Kwa maana wameivunja sheria yako.
128 Kwa hiyo, ninayaona mafundisho* yote yanayotoka kwako kuwa yanafaa;+
Ninaichukia kila njia ya uwongo.+
פ [Pe]
129 Vikumbusho vyako ni vizuri sana.
Ndiyo sababu ninavishika.
134 Niokoe* kutoka kwa wanadamu wanaokandamiza,
Nami nitayatii maagizo yako.
136 Macho yangu yanatiririkwa na machozi
Kwa sababu watu hawatii sheria yako.+
צ [Tsade]
138 Vikumbusho unavyotoa ni vya uadilifu
Navyo vinategemeka kabisa.
139 Bidii yangu inanila,+
Kwa sababu maadui wangu wameyasahau maneno yako.
141 Mimi ni duni na mwenye kudharauliwa;+
Hata hivyo, sijayasahau maagizo yako.
143 Hata nikipatwa na taabu na shida,
Nitaendelea kuzipenda sana amri zako.
144 Uadilifu wa vikumbusho vyako ni wa milele.
Nipe uelewaji,+ ili niendelee kuishi.
ק [Qoph]
145 Ninakuita kwa moyo wangu wote. Nijibu, Ee Yehova.
Nitayashika masharti yako.
146 Ninakulilia wewe; niokoe!
Nitashika vikumbusho vyako.
149 Isikie sauti yangu kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+
Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na haki yako.
150 Watu wenye mwenendo wa aibu* hunikaribia;
Wako mbali sana na sheria yako.
152 Zamani za kale nilijifunza kuhusu vikumbusho vyako,
Ambavyo umeviweka vidumu milele.+
ר [Resh]
153 Yatazame mateso yangu na uniokoe,+
Kwa maana sijaisahau sheria yako.
155 Wokovu uko mbali sana na waovu,
Kwa maana hawajayatafuta masharti yako.+
156 Rehema zako ni nyingi, Ee Yehova.+
Nihifadhi hai kulingana na haki yako.
157 Wanaonitesa na pia maadui wangu ni wengi;+
Lakini sijakengeuka kutoka katika vikumbusho vyako.
158 Ninawatazama wenye hila kwa chuki kali,
Kwa sababu hawalishiki neno lako.+
159 Tazama jinsi ninavyoyapenda sana maagizo yako!
Ee Yehova, nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+
160 Kiini hasa cha neno lako ni kweli,+
Na hukumu zako zote za uadilifu zinadumu milele.
ש [Sin] au [Shin]
162 Ninashangilia kwa sababu ya neno lako+
Kama mtu anayepata nyara nyingi.
164 Mara saba kwa siku ninakusifu wewe
Kwa sababu ya hukumu zako za uadilifu.
166 Ninayatazamia matendo yako ya wokovu, Ee Yehova,
Nami ninazishika amri zako.
167 Ninavishika vikumbusho vyako,
Nami navipenda sana.+
168 Ninayatii maagizo yako na vikumbusho vyako,
Kwa maana unajua mambo yote ninayotenda.+
ת [Taw]
169 Kilio changu cha kuomba msaada na kikufikie wewe, Ee Yehova.+
Nifanye nielewe, kulingana na neno lako.+
170 Ombi langu la kutaka kibali na lifike mbele zako.
Niokoe, kama ulivyoahidi.*
171 Midomo yangu na ifurikwe na sifa,+
Kwa maana wewe hunifundisha masharti yako.
172 Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako,+
Kwa maana amri zako zote ni za uadilifu.
174 Ninautamani sana wokovu wako, Ee Yehova,
Nami ninaipenda sana sheria yako.+
175 Acha niishi ili nikusifu;+
Hukumu zako na ziwe msaada wangu.
176 Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea.+ Nitafute mimi mtumishi wako,
Kwa maana sijazisahau amri zako.+
Wimbo wa Safari za Kupanda.*
2 Ee Yehova, niokoe kutoka kwa midomo inayosema uwongo
Na kutoka kwa ulimi mdanganyifu.
5 Ole wangu, kwa maana nimeishi kama mgeni Mesheki!+
Nimekuwa nikiishi kati ya mahema ya Kedari.+
6 Nimekuwa nikiishi mbali kwa muda mrefu
Pamoja na watu wanaochukia amani.+
7 Mimi ni mtu wa amani, lakini ninapoongea,
Wao wanataka vita.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
121 Ninayainua macho yangu nitazame milimani.+
Msaada wangu utatoka wapi?
2 Msaada wangu hutoka kwa Yehova,+
Muumba wa mbingu na dunia.
3 Hataruhusu kamwe mguu wako uteleze.*+
Yeye anayekulinda hatasinzia kamwe.
4 Tazama! Hatasinzia kamwe wala kulala usingizi,
Yeye anayelinda Israeli.+
5 Yehova anakulinda.
Yehova ni kivuli+ kwenye mkono wako wa kulia.+
7 Yehova atakulinda dhidi ya madhara yote.+
8 Yehova atakulinda katika mambo yote unayofanya*
Kuanzia sasa mpaka milele.
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
122 Nilishangilia waliponiambia:
“Na twende katika nyumba ya Yehova.”+
2 Na sasa miguu yetu imesimama
Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.+
3 Yerusalemu limejengwa kama jiji
Ambalo limeunganishwa pamoja kama kitu kimoja.+
4 Makabila yamepanda kwenda humo,
Makabila ya Yah,*
Kulingana na kikumbusho walichopewa Waisraeli,
Ili walishukuru jina la Yehova.+
6 Ombeni ili Yerusalemu liwe na amani.+
Wale wanaokupenda, Ee jiji, watakuwa salama.
7 Amani na idumu ndani ya maboma yako,*
Usalama ndani ya minara yako yenye ngome.
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu nitasema:
“Amani na iwe ndani yako.”
9 Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu,+
Nitakutakia mema.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
123 Nayainua macho yangu kukuelekea wewe,+
Wewe unayeketi kwenye kiti cha ufalme mbinguni.
2 Kama macho ya watumishi yanavyoutazama mkono wa bwana wao,
Na macho ya kijakazi yanavyoutazama mkono wa bimkubwa wake,
Ndivyo macho yetu yanavyokutazama wewe, Ee Yehova Mungu wetu+
Mpaka utakapotuonyesha kibali.+
3 Tuonyeshe kibali, Ee Yehova, tuonyeshe kibali,
Kwa maana tumedharauliwa vya kutosha.+
4 Tumedhihakiwa vya kutosha na* watu wanaojitumaini
Na kudharauliwa na wenye kiburi.
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
124 “Kama Yehova hangekuwa pamoja nasi”+
—Watu wa Israeli na waseme sasa—
2 “Kama Yehova hangekuwa pamoja nasi+
Watu walipokuja kutushambulia,+
3 Basi wangetumeza tukiwa hai+
Hasira yao ilipokuwa ikiwaka dhidi yetu.+
4 Kisha maji yangetufagilia mbali,
Mafuriko yangetufunika.+
5 Maji yenye nguvu yangetulemea.
6 Yehova na asifiwe,
Kwa maana hakututia katika meno yao kama mawindo.
7 Sisi* ni kama ndege aliyeponyoka
Kutoka katika mtego wa mwindaji;+
Mtego ulivunjika,
Nasi tukaponyoka.+
8 Msaada wetu uko katika jina la Yehova,+
Muumba wa mbingu na dunia.”
Wimbo wa Safari za Kupanda.
2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,+
Ndivyo Yehova anavyowazunguka watu wake+
Kuanzia sasa mpaka milele.
3 Fimbo ya ufalme ya uovu haitadumu katika nchi waliyogawiwa waadilifu,+
5 Lakini wale wanaogeuka na kufuata njia zao zilizopotoka,
Yehova atawaondoa pamoja na watenda maovu.+
Amani na iwe juu ya Israeli.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
126 Yehova alipowakusanya na kuwarudisha mateka wa Sayuni,+
Tulifikiri tunaota ndoto.
2 Wakati huo kinywa chetu kilijaa kicheko
Na ulimi wetu kelele za shangwe.+
Wakati huo ilisemwa miongoni mwa mataifa:
“Yehova amewatendea mambo makuu.”+
3 Yehova ametutendea mambo makuu,+
Nasi tuna shangwe nyingi sana.
4 Wakusanye na kuwarudisha watu wetu waliotekwa, Ee Yehova,
Kama vijito vya Negebu.*
5 Wale wanaopanda mbegu kwa machozi
Watavuna kwa kelele za shangwe.
6 Yule anayetoka kwenda nje, ingawa analia,
Akiwa amebeba mfuko wake uliojaa mbegu,
Kwa hakika atarudi kwa kelele za shangwe,+
Akiwa amebeba masuke yake.+
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Sulemani.
127 Yehova asipoijenga nyumba,
Wale wanaoijenga wanafanya kazi ngumu ya bure.+
Yehova asipolilinda jiji,+
Mlinzi anakesha bure.
2 Mnajisumbua bure kuamka mapema,
Na kuchelewa kulala,
Mkitaabika kupata chakula,
Kwa maana yeye huwaandalia anaowapenda na kuwapa usingizi.+
4 Kama mishale mkononi mwa mwanamume hodari,
Ndivyo walivyo watoto ambao mtu anawazaa akiwa kijana.+
5 Mwenye furaha ni mwanamume anayelijaza podo lake watoto.+
Hawataaibishwa,
Kwa maana watazungumza na maadui katika lango la jiji.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
2 Utakula mazao ambayo mkono wako ulifanya kazi ngumu kuyapata.
Utakuwa na furaha na kufurahia ufanisi.+
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu unaozaa matunda mengi nyumbani mwako;+
Watoto wako watakuwa kama machipukizi ya mzeituni kuzunguka meza yako.
4 Tazama! Hivyo ndivyo mwanamume anayemwogopa Yehova
Atakavyobarikiwa.+
5 Yehova atakubariki kutoka Sayuni.
Na uone Yerusalemu likipata ufanisi sikuzote za maisha yako+
6 Na uone watoto wa watoto wako.
Na amani iwe juu ya Israeli.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
129 “Wamenishambulia daima tangu nilipokuwa kijana”+
—Watu wa Israeli na waseme sasa—
2 “Wamenishambulia daima tangu nilipokuwa kijana;+
Lakini hawajanishinda.+
3 Wale wanaolima kwa jembe la plau wamelima mgongoni mwangu;+
Wameirefusha mitaro yao.”
5 Wataaibishwa na kukimbia kwa fedheha,
Wale wote wanaolichukia Sayuni.+
6 Watakuwa kama majani juu ya paa
Yanayonyauka kabla hayajang’olewa,
7 Ambayo hayawezi kujaa mkononi mwa mvunaji
Wala mikononi mwa yule anayekusanya masuke.
8 Wale wanaopita karibu nao hawatasema:
“Baraka ya Yehova na iwe juu yenu;
Tunawabariki katika jina la Yehova.”
Wimbo wa Safari za Kupanda.
130 Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Yehova.+
2 Ee Yehova, isikie sauti yangu.
Masikio yako na yasikilize sihi zangu za kuomba msaada.
5 Ninamtumaini Yehova, nafsi yangu yote inamtumaini;
Ninangoja neno lake.
6 Ninamngojea Yehova kwa hamu,+
Kuliko walinzi wanavyoingojea asubuhi,+
Naam, kuliko walinzi wanavyoingojea asubuhi.
7 Watu wa Israeli na waendelee kumngojea Yehova,
Kwa maana Yehova ni mshikamanifu katika upendo wake,+
Naye ana nguvu nyingi za kukomboa.
8 Atawakomboa watu wa Israeli kutoka katika makosa yao yote.
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
131 Ee Yehova, moyo wangu hauna kiburi,
Wala macho yangu hayana majivuno;+
Wala sijitafutii mambo makubwa sana,+
Wala mambo yanayopita uwezo wangu.
2 Hasha, badala yake nimeituliza na kuinyamazisha nafsi yangu*+
Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya aliye na mama yake;
Nimeridhika kama mtoto aliyeachishwa kunyonya.
3 Watu wa Israeli na wamngojee Yehova+
Kuanzia sasa mpaka milele.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
132 Ee Yehova, mkumbuke Daudi
Na mateso yake yote;+
2 Jinsi alivyomwapia Yehova,
Jinsi alivyomwekea nadhiri hii Mwenye Nguvu wa Yakobo:+
3 “Sitaingia katika hema langu, nyumbani mwangu.+
Sitalala kwenye kochi langu, kitandani mwangu;
4 Sitayaruhusu macho yangu yalale usingizi,
Wala kope zangu kusinzia
5 Mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yehova,
9 Makuhani wako na wavae uadilifu,
Washikamanifu wako na wapaze sauti kwa shangwe.
11 Yehova amemwapia Daudi;
Kwa hakika hatakosa kutimiza neno lake:
12 Wana wako wakilishika agano langu
Na vikumbusho vyangu ninavyowafundisha,+
Wana wao pia
Wataketi kwenye kiti chako cha ufalme milele.”+
14 “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumzikia milele;
Nitakaa hapa,+ kwa maana nimepatamani.
15 Nitapabariki sana kwa vyakula;
Nitawashibisha maskini wake kwa mikate.+
17 Huko nitazifanya nguvu za Daudi zikue.*
Nimemtayarishia taa mtiwa-mafuta wangu.+
18 Nitawavisha aibu maadui wake,
Lakini taji lililo kwenye kichwa chake litasitawi.”+
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
133 Tazama! Jinsi ilivyo vema na jinsi inavyopendeza
Ndugu kukaa pamoja kwa umoja!+
2 Ni kama mafuta bora yanayomiminwa kichwani+
Yanayotiririka kwenye ndevu,
Ndevu za Haruni,+
Na kutiririka mpaka kwenye ukosi wa mavazi yake.
Huko ndiko Yehova alikoamuru baraka yake
—Uzima wa milele.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
134 Msifuni Yehova,
Enyi nyote watumishi wa Yehova,+
Ninyi mnaosimama katika nyumba ya Yehova nyakati za usiku.+
3 Yehova, Muumba wa mbingu na dunia,
Na awabariki kutoka Sayuni.
135 Msifuni Yah!*
Lisifuni jina la Yehova;
Msifuni, enyi watumishi wa Yehova,+
2 Ninyi mnaosimama katika nyumba ya Yehova,
Katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.+
3 Msifuni Yah, kwa maana Yehova ni mwema.+
Liimbieni sifa* jina lake, kwa maana linapendeza.
5 Kwa maana ninajua vizuri kwamba Yehova ni mkuu;
Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu mingine yote.+
6 Yehova hufanya kila jambo apendalo+
Mbinguni na duniani, baharini na katika vilindi vyote.
7 Huyafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia;
Hutengeneza radi* kwa ajili ya mvua;
Huutoa upepo katika maghala yake.+
8 Aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,
Wanadamu na wanyama pia.+
10 Aliyaangamiza mataifa mengi+
Na kuwaua wafalme hodari+
11 —Sihoni mfalme wa Waamori,+
Ogu mfalme wa Bashani,+
Na falme zote za Kanaani.
12 Aliitoa nchi yao kuwa urithi,
Urithi kwa watu wake Waisraeli.+
13 Ee Yehova, jina lako linadumu milele.
Ee Yehova, umaarufu wako unadumu* katika vizazi vyote.+
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu,
Kazi ya mikono ya mwanadamu.+
16 Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea;+
Zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia.
Hazina pumzi vinywani mwake.+
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Yehova.
Ee nyumba ya Haruni, msifuni Yehova.
20 Ee nyumba ya Lawi, msifuni Yehova.+
Enyi mnaomwogopa Yehova, msifuni Yehova.
Msifuni Yah!+
2 Mshukuruni Mungu wa miungu,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
3 Mshukuruni Bwana wa mabwana,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
4 Yeye peke yake ndiye anayetenda mambo makuu yanayostaajabisha,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+
6 Aliitandaza dunia juu ya maji,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
7 Aliiumba ile mianga mikubwa,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
8 Jua litawale mchana,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
9 Mwezi na nyota zitawale usiku,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
10 Aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
11 Aliwatoa Waisraeli kutoka kati yao,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
12 Kwa mkono wenye nguvu+ na mkono ulionyooshwa,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
14 Aliwavusha Waisraeli katikati yake,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
15 Alimkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
16 Aliwaongoza watu wake kupitia nyikani,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
17 Aliwaua wafalme wakuu,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
18 Aliwaua wafalme hodari,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
19 Sihoni+ mfalme wa Waamori,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
20 Na Ogu+ mfalme wa Bashani,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
21 Aliitoa nchi yao kuwa urithi,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
22 Urithi kwa Israeli mtumishi wake,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
24 Alituokoa tena na tena kutoka kwa maadui wetu,+
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni,
Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
137 Kando ya mito ya Babiloni,+ hapo ndipo tulipoketi.
Tulilia tulipokumbuka Sayuni.+
3 Kwa maana huko, waliotuteka walitaka tuwaimbie,+
Waliotudhihaki walitaka tuwatumbuize:
“Tuimbieni mojawapo ya nyimbo za Sayuni.”
4 Tunawezaje kuimba wimbo wa Yehova
Katika nchi ya kigeni?
6 Ulimi wangu na ushikamane na kaakaa langu
Nisipokukumbuka,
Nisipoliweka Yerusalemu juu ya
Sababu zangu kuu zaidi za kushangilia.+
7 Kumbuka, Ee Yehova,
Mambo ambayo Waedomu walisema siku ambayo Yerusalemu lilianguka:
“Libomoeni! Libomoeni mpaka kwenye misingi yake!”+
8 Ee binti ya Babiloni, uliye karibu kuangamizwa,+
Mwenye furaha ni yule atakayekupa thawabu yako
Kwa maovu uliyotutendea.+
9 Mwenye furaha ni yule atakayewakamata kwa nguvu watoto wako
Na kuwaponda juu ya miamba.+
Wa Daudi.
138 Nitakusifu kwa moyo wangu wote.+
Mbele ya miungu mingine,
Nitaimba sifa.*
2 Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu,*+
Nami nitalisifu jina lako+
Kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu na uaminifu wako.
Kwa maana umelitukuza neno lako na jina lako juu ya vitu vingine vyote.*
4 Wafalme wote wa dunia watakusifu wewe, Ee Yehova,+
Kwa maana watakuwa wamesikia ahadi ulizotoa.
5 Wataimba kuhusu njia za Yehova,
Kwa maana utukufu wa Yehova ni mkuu.+
7 Hata nikitembea katikati ya hatari, utanihifadhi hai.+
Unaunyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya maadui wangu;
Mkono wako wa kuume utaniokoa.
8 Yehova atayatimiza mambo yote kwa niaba yangu.
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
139 Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.+
2 Unajua wakati ninapoketi na wakati ninaposimama.+
Unatambua mawazo yangu kutoka mbali.+
4 Kabla sijatamka neno lolote kwa ulimi wangu,
Tazama! Ee Yehova, tayari unalijua vizuri.+
5 Unanizingira nyuma na mbele;
Nawe unauweka mkono wako juu yangu.
6 Ujuzi huo unazidi ufahamu wangu.*
Uko juu sana nisiweze kuufikia.*+
7 Ninaweza kujificha wapi mbali na roho yako,
Na ni wapi ninapoweza kukimbia mbali na uso wako?+
8 Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa huko,
Na kama ningetandika kitanda changu Kaburini,* tazama! ungekuwa huko.+
9 Kama ningeruka kwa mabawa ya mapambazuko
Ili niishi kando ya bahari iliyo mbali zaidi,
10 Hata huko mkono wako ungeniongoza
Na mkono wako wa kuume ungenishika.+
11 Nikisema: “Hakika giza litanificha!”
Basi usiku unaonizunguka utakuwa nuru.
12 Hata giza halitakuwa zito mno kwako,
Lakini usiku utakuwa mwangavu kama mchana;+
Kwako giza ni sawa na nuru.+
14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia inayoogopesha na kustaajabisha.+
16 Macho yako hata yaliniona nikiwa kiinitete;
Sehemu zake zote ziliandikwa katika kitabu chako
Kuhusiana na siku ambazo zingeumbwa,
Kabla sehemu yoyote haijakuwepo.
17 Kwa hiyo kwangu mimi, mawazo yako ni yenye thamani sana!+
Ee Mungu, jinsi jumla yake ilivyo kubwa sana!+
18 Nikijaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko chembe za mchanga.+
Nikiamka, bado nipo pamoja nawe.*+
19 Ee Mungu, laiti ungewaua waovu!+
Ndipo watu wakatili* wangeniondokea,
20 Wale wanaosema mambo mabaya kukuhusu kwa nia ovu;*
Wao ni maadui wako wanaolitumia jina lako kwa njia isiyofaa.+
22 Ninawachukia kwelikweli;+
Hakika wamekuwa maadui wangu.
23 Nichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.+
Nipime, uyajue mawazo yangu yanayonihangaisha.*+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
140 Niokoe, Ee Yehova, kutoka kwa watu waovu;
Nilinde kutoka kwa watu wakatili,+
2 Wale wanaopanga njama za uovu mioyoni mwao+
Na kuchochea vita mchana kutwa.
4 Nilinde, Ee Yehova, kutoka mikononi mwa waovu;+
Nilinde kutoka kwa watu wakatili,
Wale wanaopanga njama ya kunitega miguu.
5 Wenye kiburi huuficha mtego ili uninase;
Kwa kamba wanautandaza wavu kando ya njia.+
Wanatega mitego ya kuninasa.+ (Sela)
6 Ninamwambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu.
Sikiliza, Ee Yehova, sihi zangu za kuomba msaada.”+
7 Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu, Mwokozi wangu mwenye nguvu,
Wewe hukinga kichwa changu katika siku ya vita.+
8 Ee Yehova, usitosheleze tamaa za waovu.
Usiruhusu njama zao zifanikiwe, ili wasijikweze. (Sela)+
9 Vichwa vya wale wanaonizingira
Na vifunikwe na uovu unaosemwa na midomo yao.+
10 Makaa ya mawe yanayowaka na yawanyeshee kama mvua.+
11 Mchongezi na asipate makao duniani.*+
Uovu na uwafuatie watu wakatili na kuwaangamiza.
12 Ninajua kwamba Yehova atawatetea watu wa hali ya chini
Na kuwatendea haki maskini.+
Muziki wa Daudi.
141 Ee Yehova, ninakulilia wewe.+
Njoo haraka unisaidie.+
Sikiliza ninapokulilia.+
2 Sala yangu na itayarishwe kama uvumba+ mbele zako,+
Mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama toleo la jioni la nafaka.+
3 Weka mlinzi wa kinywa changu, Ee Yehova,
Weka ulinzi kwenye mlango wa midomo yangu.+
4 Usiache moyo wangu uelekee kwenye jambo lolote ovu,+
Nisishirikiane na watu waovu kutenda mambo mapotovu;
Nisile kamwe vyakula vyao vitamu.
5 Mwadilifu akinipiga, hilo litakuwa tendo la upendo mshikamanifu;+
Akinikaripia, hilo litakuwa kama mafuta kwenye kichwa changu,+
Ambayo kichwa changu hakiwezi kamwe kukataa.+
Nitaendelea kusali hata wanapopatwa na misiba.
6 Ingawa waamuzi wao wanatupwa chini kutoka kwenye jabali,
Watu watayasikiliza maneno yangu, kwa maana yanapendeza.
7 Kama mtu anavyolima na kuuvunja-vunja udongo,
Ndivyo mifupa yetu ilivyotawanywa kwenye mlango wa Kaburi.*
8 Lakini macho yangu yanakutazama wewe, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+
Nimekukimbilia wewe.
Usiniue.*
9 Nilinde dhidi ya mataya ya mtego walionitegea,
Dhidi ya mitego ya watenda maovu.
10 Waovu wote wataanguka pamoja ndani ya nyavu zao wenyewe+
Huku nikipitia karibu nazo kwa usalama.
Maskili.* Wa Daudi, alipokuwa pangoni.+ Sala.
142 Kwa sauti yangu ninamlilia Yehova anisaidie;+
Kwa sauti yangu ninamsihi Yehova anionyeshe kibali.
2 Ninamwaga mahangaiko yangu mbele zake;
Mbele zake ninaeleza taabu yangu+
3 Roho yangu inapozimia ndani yangu.*
Ndipo unapoitazama barabara yangu.+
Katika njia ninayotembea,
Wanaficha mtego wa kuninasa.
Sina mahali popote pa kukimbilia;+
Hakuna yeyote anayenihangaikia.
5 Ninakulilia unisaidie, Ee Yehova.
6 Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada,
Kwa maana nimeshushwa chini sana.
Niokoe kutoka kwa wale wanaonitesa,+
Kwa maana wana nguvu kuliko mimi.
7 Nitoe katika gereza lililo chini ya ardhi
Ili nilisifu jina lako.
Waadilifu na wakusanyike kunizunguka
Kwa sababu unanitendea kwa fadhili.
Muziki wa Daudi.
143 Ee Yehova, isikie sala yangu;+
Sikiliza sihi yangu ya kuomba msaada.
Nijibu katika uaminifu wako na katika uadilifu wako.
2 Usinihukumu mimi mtumishi wako,
Kwa maana hakuna yeyote aliye hai anayeweza kuwa mwadilifu mbele zako.+
3 Kwa maana adui ananifuatia;
Ameuponda uhai wangu ardhini.
Amenifanya nikae gizani kama wale waliokufa zamani za kale.
5 Ninazikumbuka siku za kale;
Ninatafakari utendaji wako wote;+
Ninatafakari* kwa bidii kazi ya mikono yako.
6 Ninakunyooshea mikono yangu;
Mimi ni kama nchi iliyokauka yenye kiu kwa ajili yako.+ (Sela)
8 Acha nisikie upendo wako mshikamanifu asubuhi,
Kwa maana ninakutumaini wewe.
9 Niokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Yehova.
Ninatafuta ulinzi wako.+
10 Nifundishe kufanya mapenzi yako,+
Kwa maana wewe ni Mungu wangu.
Roho yako ni nzuri;
Na iniongoze kwenye nchi tambarare.*
11 Ee Yehova, nihifadhi hai kwa ajili ya jina lako.
Katika uadilifu wako, niokoe kutoka katika taabu.+
12 Katika upendo wako mshikamanifu, waangamize* maadui wangu;+
Waangamize wote wanaoninyanyasa,+
Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+
Wa Daudi.
144 Yehova, Mwamba wangu,+ na asifiwe,
Anayeizoeza mikono yangu kwa ajili ya vita,
Vidole vyangu kwa ajili ya kupigana.+
2 Yeye ni upendo wangu mshikamanifu na ngome yangu,
Kimbilio langu salama* na mwokozi wangu,
Ngao yangu na Yule ambaye nimejificha ndani yake,+
Yule anayeyatiisha mataifa chini yangu.+
3 Ee Yehova, mwanadamu ni nini hata umtambue,
Mwana wa mtu anayeweza kufa ni nini hata umkazie uangalifu?+
7 Inyooshe mikono yako kutoka juu;
Niokoe na kuninusuru kutoka katika maji mengi,
Kutoka katika mkono* wa wageni,+
8 Ambao kinywa chao kinasema uwongo
Na ambao wanainua juu mkono wao wa kulia ili kuapa kwa uwongo.*
9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya.+
Nitakuimbia sifa* kwa kinanda cha nyuzi kumi,
10 Wewe unayewapa wafalme ushindi,*+
Wewe unayemwokoa mtumishi wako Daudi kutokana na upanga hatari.+
11 Niokoe na kuninusuru kutoka katika mkono wa wageni,
Ambao vinywa vyao husema uwongo
Na ambao wanainua mkono wao wa kulia ili kuapa kwa uwongo.
12 Ndipo wana wetu watakuwa kama mimea michanga inayokua haraka,
Mabinti wetu kama nguzo za pembeni zilizochongwa kwa ajili ya jumba la mfalme.
13 Maghala yetu yatafurika mazao ya kila aina;
Makundi yetu ya kondoo yataongezeka kwa maelfu, kwa makumi ya maelfu.
14 Ng’ombe wetu, wakiwa na mimba, hawatapatwa na jambo baya* wala mimba kuharibika,
Hakutakuwa na kilio cha kuteseka katika viwanja vyetu vya mji.
15 Wenye furaha ni watu wenye hali hizo!
Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!+
Sifa ya Daudi.
א [Aleph]
ב [Beth]
ג [Gimel]
ד [Daleth]
4 Kizazi baada ya kizazi kitasifu kazi zako;
Watasimulia matendo yako yenye nguvu.+
ה [He]
5 Watasema kuhusu fahari tukufu ya ukuu wako+
Nami nitatafakari kazi zako zinazostaajabisha.
ו [Waw]
6 Watasema kuhusu matendo yako yanayoogopesha,*
Nami nitautangaza ukuu wako.
ז [Zayin]
7 Watabubujikwa na maneno wanapokumbuka wema wako mwingi,+
Nao watapaza sauti kwa shangwe kwa sababu ya uadilifu wako.+
ח [Heth]
ט [Teth]
9 Yehova ni mwema kwa wote,+
Na rehema zake zinaonekana katika kazi zake zote.
י [Yod]
כ [Kaph]
מ [Mem]
13 Ufalme wako ni ufalme wa milele,
Na mamlaka yako hudumu katika vizazi vyote.+
ס [Samekh]
ע [Ayin]
15 Macho yote yanakutazama yakiwa na tumaini;
Unawapa chakula chao katika majira yake.+
פ [Pe]
16 Unaufumbua mkono wako
Na kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.+
צ [Tsade]
ק [Qoph]
ר [Resh]
ש [Shin]
ת [Taw]
21 Kinywa changu kitatangaza sifa za Yehova;+
Kila kitu kilicho hai na kilisifu* jina lake takatifu milele na milele.+
Nafsi yangu yote na imsifu Yehova.+
2 Nitamsifu Yehova maisha yangu yote.
Nitamwimbia sifa* Mungu wangu maadamu ninaishi.
5 Mwenye furaha ni yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaidizi wake,+
Ambaye anamtumaini Yehova Mungu wake,+
6 Muumba wa mbingu na dunia,
Wa bahari, na vyote vilivyomo,+
Yeye ambaye ni mwaminifu daima,+
7 Yeye anayetekeleza haki kwa ajili ya waliopunjwa,
Yehova anawaachilia huru wafungwa.*+
8 Yehova anafungua macho ya vipofu;+
Yehova anawainua juu wale walioinama chini;+
Yehova anawapenda waadilifu.
9 Yehova anawalinda wakaaji wageni;
Humtegemeza yatima na mjane,+
10 Yehova atakuwa Mfalme milele,+
Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi baada ya kizazi.
Msifuni Yah!*
147 Msifuni Yah!*
3 Huwaponya waliovunjika moyo;
Huyafunga majeraha yao.
4 Huhesabu idadi ya nyota;
Zote anaziita kwa majina.+
6 Yehova huwainua wapole,+
Lakini huwatupa chini waovu.
7 Mwimbieni Yehova kwa shukrani;
Mwimbieni sifa Mungu wetu kwa kinubi,
8 Yeye anayezifunika mbingu kwa mawingu,
Yeye anayeiletea dunia mvua,+
Yeye anayechipusha majani+ milimani.
12 Mtukuze Yehova, Ee Yerusalemu.
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
13 Huyafanya makomeo ya malango ya jiji lako yawe imara;
Huwabariki wana wako walio ndani yako.
15 Huituma amri yake duniani;
Neno lake hukimbia upesi sana.
17 Huyatupa chini mawe yake ya mvua* kama chembe za mkate.+
Ni nani anayeweza kustahimili baridi yake?+
18 Hulituma neno lake, nayo inayeyuka.
Huufanya upepo wake uvume,+ maji yanatiririka.
19 Anamtangazia Yakobo neno lake,
Na Israeli masharti yake na hukumu zake.+
20 Hajalifanyia hivyo taifa lingine lolote;+
Hawajui lolote kuhusu hukumu zake.
148 Msifuni Yah!*
Msifuni Yehova kutoka mbinguni,+
Msifuni katika vilele.
2 Msifuni, enyi malaika wake wote.+
Msifuni, enyi jeshi lake lote.+
3 Msifuni, enyi jua na mwezi.
Msifuni, enyi nyota zote zinazong’aa.+
4 Msifuni, enyi mbingu zilizo juu kabisa*
Na maji yaliyo juu ya mbingu.
5 Na vilisifu jina la Yehova,
Kwa maana aliamuru, navyo vikaumbwa.+
7 Msifuni Yehova kutoka duniani,
Enyi viumbe wakubwa wa baharini na pia vilindi vyote vya maji,
8 Enyi radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu mazito,
Ewe kimbunga, unayetekeleza neno lake,+
9 Enyi milima na vilima vyote,+
Enyi miti ya matunda na mierezi yote,+
10 Enyi wanyama wa mwituni+ na wanyama wote wa kufugwa,
Enyi viumbe mnaotambaa na ndege wenye mabawa,
11 Enyi wafalme wa dunia, nanyi mataifa yote,
Enyi wakuu na waamuzi wote wa dunia,+
12 Enyi vijana wa kiume na wa kike,*
Wazee pamoja na watoto.*
13 Na walisifu jina la Yehova,
Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana lisiweze kufikiwa.+
Ukuu wake uko juu ya dunia na mbingu.+
14 Ataikweza nguvu* ya watu wake,
Kwa sifa ya washikamanifu wake wote,
Ya wana wa Israeli, watu walio karibu naye.
Msifuni Yah!*
149 Msifuni Yah!*
2 Watu wa Israeli na washangilie kwa sababu ya Muumba wao Mkuu;+
Wana wa Sayuni na washangilie kwa sababu ya Mfalme wao.
4 Kwa maana Yehova anawafurahia watu wake.+
Anawapamba wapole kwa wokovu.+
5 Washikamanifu na washangilie kwa utukufu;
Na wapaze sauti kwa shangwe vitandani mwao.+
6 Nyimbo zinazomsifu Mungu na ziwe kooni mwao,
Na upanga wenye makali pande mbili uwe mkononi mwao,
7 Ili kuyalipiza kisasi mataifa
Na kuyaadhibu mataifa,
8 Ili kuwafunga wafalme wao kwa pingu
Na viongozi wao kwa pingu za chuma,
9 Ili kutekeleza hukumu iliyoandikwa kuwahusu.+
Heshima hii ni ya washikamanifu wake wote.
Msifuni Yah!*
Msifuni Mungu katika mahali pake patakatifu.+
Msifuni katika anga la* nguvu zake.+
2 Msifuni kwa kazi zake zenye nguvu.+
Msifuni kwa ukuu wake usio na kifani.+
3 Msifuni kwa kupiga pembe.+
Msifuni kwa kinanda na kinubi.+
4 Msifuni kwa tari+ na kwa dansi ya mzunguko.
Msifuni kwa nyuzi+ na filimbi.*+
5 Msifuni kwa matoazi yanayolia.
Msifuni kwa matoazi yanayogonganishwa.+
6 Kila kitu kinachopumua—na kimsifu Yah.
Au “huitafakari sheria Yake.”
Au “wanatafakari kuhusu.”
Au “wanashauriana.”
Au “Kristo.”
Au “onyo.”
Tnn., “Mbusuni.”
Au “kuihusu nafsi yangu.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “Nitengenezee nafasi pana katika.”
Au “atamfanya mshikamanifu wake aonekane kuwa tofauti; atamtenga kando mshikamanifu wake kwa ajili yake mwenyewe.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “katika uwepo wako.”
Au “anamchukia mtu anayemwaga damu na ambaye ni mdanganyifu.”
Au “mahali pako patakatifu.”
Au “Wanatumia ulimi laini.”
Angalia Kamusi.
Au “rehema.”
Au “nafsi yangu inasumbuka.”
Au “uiokoe nafsi yangu.”
Au “hawakukumbuki.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “ninakifanya kitanda changu kiogelee.”
Au “Limezeeka.”
Au “Wimbo wa maombolezo.
Au “watairarua nafsi yangu.”
Au labda, “Nilipomwacha hai yule anayenipinga bila sababu.”
Au “na kuipita nafsi yangu.”
Au “anayejaribu mioyo na figo.”
Au “huvurumisha shutuma zake.”
Au “Nitalipigia muziki.”
Angalia Kamusi.
Au labda, “Wewe ambaye fahari yako inasimuliwa juu ya mbingu!”
Au “kuliko malaika.”
Angalia Kamusi.
Au “Nitalipigia muziki.”
Au “kilele salama.”
Angalia Kamusi.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “mbele za uwepo wako.”
Au “tamaa ya nafsi yake.”
Au labda, “Mwenye pupa hujibariki mwenyewe.”
Au “Hujitutumua kwa.”
Au “Sitapepesuka (Sitayumbayumba) kamwe.”
Au “pori.”
Au “katika makucha yake.”
Au “kuiambia nafsi yangu.”
Au “Misingi ya haki.”
Au “yanayong’aa.”
Au “Nafsi yake inamchukia; Yeye binafsi anamchukia.”
Au labda, “makaa ya mawe yanayowaka.”
Au “watajionea kibali chake.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “Wanaongea kwa mdomo laini.”
Tnn., “kwa moyo na moyo.”
Au “wanaojitutumua mbele yao.”
Au labda, “tanuru la kuyeyusha lililowekwa ardhini.”
Au “ameshughulika nami kwa njia inayothawabisha.”
Au “Asiyetumia akili.”
Au “kwa utimilifu.”
Au “hawaaibishi.”
Tnn., “Havunji kiapo chake, hata kinapomletea hasara.”
Au “hatapepesuka (hatayumbayumba) kamwe.”
Angalia Kamusi.
Au “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”
Au “sitapepesuka (sitayumbayumba) kamwe.”
Tnn., “utukufu wangu una.”
Au “Mwili wangu huishi.”
Au “hutaiacha nafsi yangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au labda, “aone uharibifu.”
Tnn., “pamoja na uso wako.”
Au “uzuri.”
Au “Inama chini na unisikilize.”
Au “maadui wangu walio dhidi ya nafsi.”
Au “Wamefunikwa na mafuta yao wenyewe.”
Au “kututupa chini.”
Au “Iokoe nafsi yangu.”
Au “mfumo huu wa mambo.”
Au “kuona sura yako.”
Angalia Kamusi.
Au “mwokozi wangu mwenye nguvu.”
Au “kilele changu salama.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “upepo.”
Au “Mifereji ya maji ikaonekana.”
Au “mahali penye nafasi kubwa.”
Au “ukosefu wa hatia.”
Au “ukosefu wa hatia.”
Au “wanaoteseka.”
Tnn., “unayashusha macho ya kiburi.”
Au “hunidumisha.”
Au “Vifundo vya miguu yangu havitateleza.”
Au “Utanionyesha migongo ya maadui wangu.”
Au “nitawanyamazisha.”
Au “watafifia.”
Au “nitalipigia muziki.”
Au “humpa ushindi mkubwa mfalme wake.”
Tnn., “mbegu yake.”
Au labda, “kamba yake ya kupimia imefika.”
Au “huirudisha nafsi.”
Au “iliyosafishwa.”
Au “dhambi nyingi.”
Tnn., “aione kuwa mafuta.”
Au “ushauri wako wote.”
Au “ushindi.”
Au “iliyosafishwa.”
Tnn., “Urefu wa siku.”
Tnn., “mbele za uso wako.”
Au “hatapepesuka (hatayumbayumba) kamwe.”
Tnn., “kulenga nyuso zao.”
Tnn., “kamba zako za upinde.”
Tnn., “Tutauimbia na kuupigia muziki.”
Labda ni sauti au mtindo wa muziki.
Au “Umeketi kwenye kiti cha ufalme kati ya (juu ya).”
Au “hawakuaibishwa.”
Au “Mimi ni fedheha kwa wanadamu na ninadharauliwa na watu.”
Tnn., “Nimetupwa kwako.”
Au “Iokoe nafsi yangu.”
Tnn., “Uhai pekee nilio nao,” yaani, nafsi yake.
Tnn., “mkono wa.”
Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “Moyo wako na uishi.”
Tnn., “wanene.”
Au “nafsi zao.”
Tnn., “Mbegu itamtumikia.”
Au labda, “maji matulivu.”
Au “Huiburudisha nafsi yangu.”
Tnn., “mapito ya; vijia vya.”
Au “hunifariji.”
Au “Unakipaka.”
Au “nafsi Yangu,” ikirejelea mtu kuapa kwa uhai wa Yehova.
Au “haki.”
Au “Inukeni.”
Au “Nainua nafsi yangu kwako.”
Au “Ambazo ni za tangu nyakati za kale.”
Tnn., “katika hukumu.”
Au “Nafsi yake itajionea.”
Tnn., “mbegu yake itamiliki.”
Au “Ilinde nafsi yangu.”
Tnn., “mkomboe.”
Au “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”
Tnn., “Siketi.”
Au “sichangamani na wanafiki.”
Tnn., “kuketi.”
Tnn., “Usiifagilie mbali nafsi yangu.”
Au “watu wanaomwaga damu.”
Au “mwenendo wa.”
Tnn., “Nikomboe.”
Tnn., “makusanyiko.”
Au “kutazama kwa kutafakari.”
Au “mahali pake patakatifu.”
Au “Nitampigia muziki.”
Au labda, “Kwa hakika nina imani kwamba nitauona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai.”
Au “kaburini.”
Au “Mwabuduni.”
Au labda, “kwa sababu ya fahari ya utakatifu wake.”
Inaonekana ni safu ya milima ya Lebanoni.
Au “bahari ya mbinguni.”
Au “umenivuta.”
Au “umeiinua nafsi yangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “kaburini.”
Au “Mpigieni muziki.”
Tnn., “Ushukuruni ukumbusho wake.”
Au “nia yake njema.”
Au “Sitapepesuka (sitayumbayumba) kamwe.”
Au “nia yako njema.”
Tnn., “Damu yangu ina faida gani.”
Au “kaburini.”
Au “Ili utukufu wangu uimbe.”
Au “Inama chini na unisikilize.”
Au “Mungu mwaminifu.”
Au “mateso ya nafsi yangu.”
Au “penye nafasi kubwa.”
Au “nafsi yangu na tumbo langu.”
Au “akilini.”
Au “kuiondoa nafsi yangu.”
Tnn., “Nyakati.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “katika uwepo wako.”
Tnn., “Kutoka kwa ugomvi wa ndimi.”
Angalia Kamusi.
Au “imesamehewa.”
Au “hasira yako ilinilemea.”
Au “Unyevunyevu wa uhai wangu ulibadilika.”
Au “Mpigieni muziki.”
Au “pumzi ya.”
Au “jeshi lote la mbinguni liliumbwa.”
Au “ardhi inayozaa.”
Au “mashauri ya.”
Au “mawazo.”
Au “mashauri.”
Au “la ushindi.”
Au “aokoe nafsi zao.”
Au “Nafsi yangu itajigamba.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni ambao ni.”
Au “waliovunjika moyo.”
Au “misiba mingi.”
Au “anaikomboa nafsi ya.”
Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.
Au “shoka lenye makali pande zote mbili.”
Au “Iambie nafsi yangu.”
Au “wanaowinda nafsi yangu.”
Au “iliporudi kwenye kifua changu.”
Au labda, “Wasiomwogopa Mungu wanadhihaki ili wapate keki.”
Tnn., “Uhai pekee nilio nao,” yaani, nafsi yake.
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au “Aha! Nafsi yetu.”
Au “utatafakari.”
Tnn., “kama milima ya Mungu.”
Au “Unawaokoa.”
Tnn., “mafuta ya.”
Au “Usiwake hasira.”
Au “nchini.”
Au “Pata shangwe nyingi sana.”
Tnn., “Mvingirishie.”
Au “subira.”
Au labda, “Usikasirike, kwa maana hasira itakuongoza tu kwenye madhara.”
Au “kuzitia nyuzi.”
Tnn., “siku za wasio na lawama.”
Au “hufadhili.”
Au “huimarisha.”
Au “anamtegemeza kwa mkono Wake.”
Au “chakula.”
Au “huzungumza hekima kwa sauti ya chini.”
Au “mtu anayeshika utimilifu.”
Tnn., “Viuno vyangu vimejaa moto.”
Au “ningurume.”
Au “nafsi yangu.”
Tnn., “wako hai.”
Au labda, “Lakini wale ambao ni maadui wangu bila sababu ni wengi.”
Angalia Kamusi.
Au “yalichochewa.”
Tnn., “uliwaka moto.”
Au “nikipiga kite.”
Au “nijue jinsi ninavyopita upesi.”
Tnn., “ziwe vipimo vya mkono.”
Tnn., “Hupiga kelele.”
Aina fulani ya wadudu waharibifu.
Au “Mlowezi.”
Tnn., “sijapita.”
Au “Nilimngojea Yehova kwa subira.”
Au “akainama chini ili kunisikiliza, akasikia.”
Au “waongo.”
Au “Hukupendezwa na.”
Au “ninatamani.”
Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”
Au “Hutamtia kamwe katika tamaa ya maadui wake; au katika nafsi ya maadui wake.” Angalia Kamusi.
Au “Iponye nafsi yangu.”
Au “amenigeuka.”
Tnn., “mbele za uwepo wako.”
Au “Milele na milele.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “polepole.”
Au “ule mlima mdogo.”
Yaani, inayoweza kusababisha mauaji.
Au labda, “kana kwamba wanaiponda mifupa yangu.”
Angalia Kamusi.
Au “Toa.”
Au “wokovu mkuu.”
Au “kutokana na bei yao.”
Tnn., “methali.”
Tnn., “Tukomboe.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “Kazi zangu zinamhusu.”
Au “mwandishi.”
Au “ufanikiwe.”
Tnn., “utakufundisha.”
Au “haki.”
Au “watautuliza uso wako.”
Tnn., “Ndani.”
Tnn., “yametiwa mapambo ya.”
Au labda, “kwa majoho yaliyotariziwa.”
Angalia Kamusi.
Au “kilele chetu salama.”
Au labda, “Anaziteketeza ngao motoni.”
Au “pembe ya kondoo dume; tarumbeta.”
Au “Mpigieni Mungu muziki.”
Tnn., “ngao za dunia ni za.”
Au “kilele salama.”
Au “wamekutana kama walivyokubaliana.”
Tnn., “Mabinti wa Yuda na washangilie.”
Au “kuta zake zenye ngome.”
Au labda, “mpaka tufe.”
Au “wa mfumo wa mambo.”
Tnn., “Wana wa wanadamu na pia wana wa mtu.”
Tnn., “kosa la.”
Au “ukombozi.”
Au “nafsi yao.”
Au “kaburi.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “ataikomboa nafsi yangu.”
Tnn., “mkono wa.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Yule Mungu, Yehova.”
Au “Kutoka mashariki mpaka magharibi.”
Tnn., “mbuzi dume.”
Au “mafundisho.”
Tnn., “kuyatupa maneno yangu nyuma yako.”
Au labda, “unaungana naye.”
Au “Unamharibia sifa.”
Au “akilini mwangu.”
Tnn., “wewe peke yako.”
Au “Na nilikuwa na dhambi tangu mama yangu aliponichukua mimba.”
Au “utu wangu wa sirini.”
Au “Ufiche uso wako.”
Au “uyafute kabisa.”
Tnn., “mbele za uwepo wako.”
Tnn., “Nitegemeze kwa kunipa roho ya utayari.”
Au “hutaudharau.”
Angalia Kamusi.
Au “ngome yake.”
Au “kujificha katika.”
Tnn., “taabu anazosababisha.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “Asiye na akili.”
Au labda, “Hofu mahali pasipo na chochote cha kuhofu.”
Tnn., “wanaopiga kambi dhidi yenu.”
Angalia Kamusi.
Au “uamue kesi yangu.”
Au “nafsi yangu.”
Au “Hawamweki Mungu mbele yao.”
Tnn., “wanyamazishe.”
Angalia Kamusi.
Au “Na usijifiche ninaposali kukuomba msaada.”
Tnn., “ugawanye ndimi zao.”
Au “mwanadamu, mtu tunayelingana.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “nimevurugika.”
Tnn., “Atanikomboa.”
Yaani, rafiki yake wa zamani anayetajwa katika mstari wa 13 na 14.
Au “ayumbeyumbe; apepesuke.”
Angalia Kamusi.
Au “anataka kuning’ata.”
Tnn., “Mwili wa nyama utanifanya.”
Angalia Kamusi.
Au “Nitakupigia muziki.”
Angalia Kamusi.
Au “wamepotoka.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “waichunguze ile nyumba.”
Au “wenye kiu ya damu.”
Au “Wananguruma.”
Au “kinachobubujika.”
Au “kilele changu salama.”
Au “wangurume.”
Au “nitakupigia muziki.”
Angalia Kamusi.
Au labda, “Umewapa.”
Au labda, “mahali pake patakatifu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Tnn., “ngome ya.”
Au labda, “lenye ngome.”
Au “Moyo wangu unapodhoofika.”
Au “Atakaa.”
Au “nitalipigia muziki.”
Angalia Kamusi.
Au “kilele changu salama.”
Au labda, “Ninyi nyote, kana kwamba alikuwa ukuta ulioinama, ukuta wa mawe unaokaribia kuanguka.”
Au “heshima yake.”
Au “Kwa kweli, Ee nafsi yangu, mngojee.”
Tnn., “Mwili wangu unazimia.”
Tnn., “Nimeridhika kana kwamba nina mafuta na nimejaa mafuta.”
Au “kuiangamiza nafsi yangu.”
Au “mbweha.”
Au “atajigamba.”
Au “Wanatiana moyo kutenda uovu.”
Au “watajigamba.”
Tnn., “watu wote wenye mwili.”
Au “Mahali pako patakatifu.”
Tnn., “ifurike.”
Au “matuta yake.”
Tnn., “vinadondosha mafuta.”
Tnn., “kudondosha.”
Au “nchi tambarare za chini zimefunikwa.”
Au “Lipigieni muziki.”
Au “Hufanya nafsi zetu kuwa hai.”
Au “iyumbeyumbe; itetemeke.”
Tnn., “Uliweka mzigo mzito kwenye viuno vyetu.”
Tnn., “juu ya vichwa vyetu.”
Au “itamheshimu.”
Au “lipigieni muziki.”
Au labda, “juu ya mawingu.”
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Tnn., “mwamuzi.”
Au “waasi.”
Tnn., “ulipotangulia mbele ya.”
Tnn., “zilidondosha.”
Tnn., “Uliutia nguvu tena urithi wako.”
Au labda, “katikati ya mazizi ya kondoo.”
Au “yenye mchanganyiko wa rangi ya manjano na kijani kibichi.”
Au “Ni kana kwamba theluji ilianguka Salmoni.”
Au “ni mlima mrefu.”
Au “anatamani uwe.”
Au “anayetembeatembea katika.”
Tnn., “Katika makusanyiko.”
Au labda, “yakikanyagia chini.”
Au labda, “Mabalozi watatoka.”
Au “Mpigieni muziki.”
Tnn., “mawinguni.”
Au “nafsi yangu.”
Au “Wale ambao ni maadui wangu bila sababu.”
Au “Nilipoinyenyekeza nafsi yangu.”
Au labda, “Nilipolia na kufunga.”
Tnn., “Nilikuwa methali kwao.”
Au “shimo lifumbe.”
Au “Ikaribie nafsi yangu uikomboe.”
Au “nami nimefikia hatua ya kukata tamaa.”
Au “mmea wenye sumu.”
Au “hasira yako kali.”
Au “Kambi yao iliyozingirwa na ukuta.”
Au “kitabu cha uzima.”
Yaani, ile nchi.
Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”
Au “Inama chini na unisikilize.”
Au “Wewe ni tegemeo langu.”
Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”
Au “kuyahesabu.”
Tnn., “mkono wako.”
Au “vilindi vya.”
Au “Nitakupigia muziki.”
Au “umeikomboa nafsi yangu.”
Au “utatafakari.”
Tnn., “awahukumu.”
Au “wana.”
Tnn., “atachipuka.”
Au “Atatawala.”
Au “nafsi za.”
Au “Atazikomboa nafsi zao.”
Au “wanaojigamba.”
Au “Kitambi chao kimenenepa.”
Tnn., “Mafuta yao.”
Tnn., “Ningekisaliti kizazi cha wana wako.”
Tnn., “utaidharau.”
Tnn., “katika figo zangu.”
Tnn., “Utamnyamazisha.”
Au “kukosa uaminifu.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “inafuka moshi.”
Tnn., “Likumbuke kusanyiko lako ulilojipatia.”
Au “kusanyiko.”
Au “Sehemu zote ambazo Mungu anaabudiwa.”
Au “Uchomoe kutoka katika makunjo ya vazi lako.”
Angalia Kamusi.
Au “mwanga.”
Au “nafsi ya.”
Tnn., “pembe yenu.”
Tnn., “pembe yenu.”
Au “Nitampigia muziki.”
Tnn., “pembe.”
Tnn., “pembe.”
Au “Umefunikwa na nuru.”
Tnn., “Atainyenyekeza roho ya.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “bila kufa ganzi.”
Au “Nafsi yangu haiwezi.”
Tnn., “roho yangu inazimia.”
Au “muziki wangu wa nyuzi.”
Tnn., “Roho yangu inatafuta.”
Au “linalonichoma.”
Tnn., “amebadili mkono wake wa kuume dhidi yetu.”
Tnn., “mkono wako.”
Tnn., “umewakomboa.”
Au “ardhi inayozaa.”
Tnn., “Kwa mkono.”
Angalia Kamusi.
Au “mafundisho.”
Tnn., “ambao haujatayarishwa.”
Au “ukuta.”
Tnn., “Walimtahini.”
Au “chakula kwa ajili ya nafsi yao.”
Au “wa malaika.”
Au “Mlipiza-Kisasi.”
Tnn., “akifunika.”
Au labda, “Kwamba roho inaenda nayo hairudi.”
Au “wakamtia uchungu.”
Tnn., “Hawakuukumbuka mkono wake.”
Tnn., “aliwakomboa.”
Au labda, “homa kali.”
Au “Hakulinda nafsi zao zisife.”
Tnn., “kumtahini.”
Au “wivu wake.”
Tnn., “hawakusifiwa.”
Tnn., “Alipajenga mahali pake patakatifu kama vilele.”
Tnn., “ufunike.”
Tnn., “mkono wako.”
Au labda, “kuwaweka huru.”
Tnn., “wana wa kifo.”
Au labda, “katikati ya.”
Au “Funua uangavu wako.”
Tnn., “kuwaka hasira dhidi ya.”
Au “Shina kuu la mzabibu.”
Au “ulitazame tawi ambalo umelitia nguvu.”
Tnn., “kwa kemeo la uso wako.”
Angalia Kamusi.
Yaani, Mungu.
Au “lugha.”
Tnn., “katika mahali palipofichika pa ngurumo.”
Maana yake “Kugombana.”
Tnn., “Walitembea katika mashauri yao.”
Tnn., “wakati.”
Tnn., “atamlisha,” yaani, watu wa Mungu.
Tnn., “mafuta ya ngano.”
Au “walio kama miungu.”
Au “Hukumuni kwa ajili ya.”
Au “ni kama miungu.”
Au “wanainua vichwa vyao.”
Tnn., “waliofichwa.”
Tnn., “Wanashauriana kwa moyo mmoja.”
Au “Wamefanya agano.”
Tnn., “Wamekuwa mkono kwa.”
Au “korongo la.”
Au “viongozi.”
Au “kama mbaruti.”
Tnn., “Jaza nyuso zao aibu.”
Angalia Kamusi.
Au “linavyopendwa sana.”
Tnn., “inakazia.”
Au “bonde lenye vichaka vya mibaka.”
Au labda, “Na mfundishaji hujifunika mwenyewe.”
Au labda, “Itazame ngao yetu, Ee Mungu.”
Tnn., “Uliifunika.”
Au “Tukusanye tena.”
Au “ufanisi.”
Au “Inama chini na unisikilize.”
Au “Ilinde nafsi yangu.”
Au “ninakuinulia wewe nafsi yangu.”
Au “Nipe moyo ambao haujagawanyika.”
Au “umeiokoa nafsi yangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “wanaitafuta nafsi yangu.”
Au “hawajakuweka mbele yao.”
Au “neema.”
Au “kweli.”
Au “uthibitisho wa.”
Au “wanaonitambua.”
Au “Kwangu mimi, wewe ni chanzo cha vitu vyote.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “Inama chini na unisikilize.”
Angalia Kamusi.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “kaburini.”
Au “mtu asiye na nguvu.”
Tnn., “mkono.”
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au “katika Abadoni.”
Au “unaikataa nafsi yangu.”
Au labda, “Vinanizingira vyote kwa pamoja.”
Angalia Kamusi.
Au “utadumu.”
Tnn., “Nitaiimarisha kabisa mbegu yako.”
Au “kusanyiko.”
Tnn., “pembe yetu inakwezwa.”
Tnn., “pembe yake itakwezwa.”
Au “Nitaweka mamlaka yake.”
Tnn., “Nitaiimarisha mbegu yake.”
Au “hukumu zangu.”
Au “kutotii kwao.”
Tnn., “Wala kuwa mwongo kuhusu uaminifu wangu.”
Tnn., “Mbegu yake itadumu.”
Au “Umelitia unajisi.”
Au “Umeyavunja mabanda yake yote ya mawe.”
Tnn., “Umeuinua juu mkono wa kulia wa maadui wake.”
Au “kuiokoa nafsi yake.”
Tnn., “mkono wa Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “kubeba kifuani mwangu.”
Au labda, “kimbilio letu.”
Au “hujatokeza kama kwa uchungu wa kuzaa.”
Au “Unajua makosa yetu.”
Au “Maisha yetu yanadidimia.”
Au “kupiga kite.”
Au “kwa sababu ya uwezo wa pekee.”
Au “uimarishe kabisa.”
Au “iimarishe kabisa.”
Au “boma.”
Tnn., “malipo.”
Au labda, “ngome; kimbilio.”
Tnn., “amejiunga nami.”
Au “analitambua.”
Au “aone wokovu kutoka kwangu.”
Au “kulipigia muziki.”
Au “majani.”
Tnn., “utaikweza pembe yangu kama ya.”
Au “wakiwa na mvi.”
Tnn., “kuwa wanene.”
Au “kutikiswa.”
Au “unaifaa.”
Tnn., “aliyelipanda.”
Tnn., “nimekaa katika ukimya.”
Au “Mawazo yenye kufadhaisha.”
Au “yalipokuwa mengi ndani yangu.”
Au “Faraja zako ziliibembeleza nafsi yangu.”
Au “watawala; mahakimu.”
Au “kwa kutoa amri.”
Tnn., “Na damu ya asiye na hatia wanaitangaza kuwa na hatia (ovu).”
Au “kilele changu salama.”
Tnn., “Atawanyamazisha.”
Tnn., “atawanyamazisha.”
Tnn., “mbele za uso wake.”
Tnn., “wa mkono wake.”
Maana yake “Kugombana.”
Maana yake “Kujaribu; Jaribu.”
Au “adhama.”
Au “Mwabuduni.”
Au labda, “kwa sababu ya fahari ya utakatifu wake.”
Au “kutikiswa.”
Au “Ataamua kesi ya.”
Au “amekuja.”
Au “Mwabuduni.”
Tnn., “Mabinti wa Yuda wana.”
Au “nafsi za.”
Tnn., “nguvu za.”
Tnn., “muushukuru ukumbusho wake.”
Au “umemletea ushindi.”
Au “ushindi wa.”
Au “kupiga muziki.”
Au “Mpigieni muziki.”
Au “amekuja.”
Au labda, “katikati ya.”
Au “kuabudu.”
Tnn., “ulilipiza kisasi.”
Au “mwabudu.”
Au “Tambueni.”
Au labda, “hatukujiumba wenyewe.”
Au “Nitakupigia muziki.”
Au “utimilifu.”
Au “cha ubatili.”
Au “Matendo yao hayashikamani nami.”
Tnn., “Sitajua.”
Au “Nitamwangamiza.”
Au “kwa utimilifu.”
Tnn., “mbele ya macho yangu.”
Au “nitawaangamiza.”
Au “anapokuwa dhaifu.”
Au “Inama chini na unisikilize.”
Au labda, “Nimekonda sana.”
Au “wanaonifanya nionekane mpumbavu.”
Au “ni kama kivuli kinachorefuka.”
Au “jina lako litadumu.” Tnn., “ukumbusho wako utadumu.”
Tnn., “watakaoumbwa.”
Au “kaburini.”
Au “neema.”
Au “fadhili nyingi zenye upendo.”
Tnn., “Na mahali pake hapalijui tena.”
Au “tangu milele hadi milele.”
Tnn., “mkiisikia sauti ya neno lake.”
Au “Kila mahali pa enzi yake kuu.”
Au “adhama.”
Tnn., “katika maji.”
Au “Haitatikiswa.”
Au “makorongo.”
Au “Wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Angalia Kamusi.
Au “Nitampigia muziki.”
Au labda, “Kutafakari kwangu kumhusu na kupendeze.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “mpigieni muziki.”
Au labda, “Zungumzieni.”
Au “uwepo.”
Au “wazao wa.” Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “Neno aliloamuru.”
Tnn., “Aliuvunja kila ufito wa mikate.” Labda ni fito zilizotumiwa kuhifadhia mikate.
Tnn., “Waliitesa.”
Au “Nafsi yake iliingia katika chuma.”
Tnn., “Ili awafunge.”
Au “kama nafsi ilivyotaka.”
Aina ya mbu anayeitwa hak·kin·namʹ katika Kiebrania.
Au “miali ya moto.”
Tnn., “hofu yao.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “nia njema.”
Au “nijigambe kukuhusu.”
Au “hawakuelewa maana ya.”
Au “nyikani.”
Au “aliyebaki.”
Au “sanamu ya kuyeyushwa.”
Tnn., “akasimama kwenye pengo hilo mbele zake.”
Au “wakashikamana.”
Yaani, dhabihu zilizotolewa kwa watu waliokufa au kwa miungu ambayo haina uhai.
Maana yake “Kugombana.”
Au “kujifunza.”
Tnn., “mkono wao.”
Au “akighairi.”
Au “mkubwa; mkuu.”
Au “tupate shangwe kwa kukusifu.”
Au “Milele na milele.”
Au “Na iwe hivyo!”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “walionunuliwa.”
Au “katika nguvu za.”
Au “Kutoka mapambazuko ya jua na kutoka machweo ya jua.”
Au “amezitosheleza nafsi zilizokauka.”
Au “kuzishibisha nafsi zenye njaa.”
Au “Walichukia kabisa vyakula vyote.”
Au “Nafsi yao.”
Tnn., “kwenye kiti cha.”
Au “huwainua juu,” yaani, ili wasifikiwe.
Tnn., “hata kwa utukufu wangu.”
Au “nitakupigia muziki.”
Au labda, “mahali pake patakatifu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Tnn., “ngome ya.”
Au “Mshtaki.”
Au “mwovu.”
Tnn., “Wanawe.”
Au “Wanawe.”
Au “Wala riba na waviwekee mitego.”
Au “upendo mshikamanifu.”
Au “Kizazi chake kijacho na kiangamizwe.”
Au “upendo mshikamanifu.”
Tnn., “Mwili wangu umekuwa mwembamba, hauna mafuta.”
Au “joho lisilo na mikono.”
Au “siku ambayo jeshi lako litakusanyika.”
Au “hataghairi.”
Au “miongoni mwa.”
Tnn., “Ataponda kichwa cha.”
Au “dunia nzima.”
Anayerejelewa ni “Bwana wangu” anayetajwa katika mstari wa 1.
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “neema.”
Au “Yana msingi mzuri.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “neema.”
Au “fadhili.”
Au “ni thabiti; ni imara.”
Au “kwa ukarimu.”
Tnn., “Pembe yake mwenyewe itakwezwa.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Anayeketi juu kwenye kiti cha ufalme?”
Au labda, “jaa la takataka.”
Tnn., “wana.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Hatustahili chochote, Ee Yehova, hatustahili chochote.”
Tnn., “wana.”
Tnn., “kwenye kimya.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au labda, “Ninapenda kwa sababu Yehova huisikia.”
Au “huinama chini ili kunisikiliza.”
Tnn., “katika siku zangu.”
Tnn., “Nilipatwa na taabu za Sheoli.”
Au “iokoe nafsi yangu.”
Au “neema.”
Angalia Kamusi.
Au “Umeiokoa nafsi yangu.”
Au “wokovu mkuu.”
Au “Ni cha bei kubwa sana.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “koo zote.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “mahali penye nafasi kubwa.”
Au labda, “pamoja na wale wanaonisaidia.”
Au labda, “Ulinisukuma kwa nguvu.”
Au “ushindi.”
Tnn., “kichwa cha pembeni.”
Au “wanaoshika utimilifu.”
Tnn., “Laiti njia zangu zingekuwa zimeimarishwa kabisa.”
Au “Nitajifunza.”
Au “Nafsi yangu inapondeka.”
Tnn., “Vingirisha mbali nami.”
Au “ninajifunza.”
Tnn., “njia.”
Au “kujifunza.”
Au “niaibishwe.”
Tnn., “Nitakimbia katika.”
Au labda, “huufanya moyo wangu uwe na ujasiri.”
Au “Nitembeze.”
Au “kwa faida za.”
Au “neno lako.”
Au labda, “Ambayo hutolewa kwa wale wanaokuogopa.”
Au “neno lako.”
Au “ninangojea.”
Au “mahali penye nafasi kubwa.”
Au “nitajifunza.”
Au “Kumbuka ahadi yako uliyompa.”
Au “Ambalo ulinifanya nisubiri.”
Au “Katika nyumba ninamoishi kama mgeni.”
Au “Ninautuliza (ninatafuta tabasamu ya) uso wako.”
Au “neno lako.”
Au “nilikuwa nikitenda dhambi bila kukusudia.”
Tnn., “hauna hisia, ni kama mafuta.”
Au “ninalingojea neno lako.”
Au “neno lako ulilonipa.”
Au labda, “kwa kusema uwongo.”
Au “nitajifunza.”
Au “ninalingojea neno lako.”
Yaani, kazi zake zote za uumbaji.
Tnn., “ni pana sana.”
Au “Ninajifunza kuihusu.”
Au “ninajifunza.”
Tnn., “matoleo ya hiari ya kinywa changu.”
Au “Nafsi yangu imo mikononi mwangu daima.”
Au “urithi wangu wa milele.”
Tnn., “Nimeuelekeza moyo wangu.”
Au “moyo uliogawanyika.”
Au “Ninalingojea neno lako.”
Au “kulingana na neno lako.”
Au “liaibishwe.”
Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “takataka” katika mstari huu linarejelea uchafu unaotoka katika fedha au dhahabu inapoyeyushwa.
Au “neno lako la.”
Au “iliyosafishwa.”
Au “maagizo.”
Tnn., “kuhemahema.”
Tnn., “Kulingana na uamuzi wako kuwaelekea.”
Au “Zifanye hatua zangu ziwe imara.”
Tnn., “Nikomboe.”
Au “utabasamu kunielekea.”
Au “alfajiri.”
Au “Ninayangojea maneno yako.”
Au “nijifunze.”
Au “mwenendo mpotovu.”
Au “Iendeshe kesi yangu.”
Au “neno lako.”
Au “Hakuna cha kuwakwaza.”
Au “kulingana na neno lako.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “Naye atakuongezea nini?”
Au “uyumbe.”
Au “Atailinda nafsi yako.”
Tnn., “unapotoka nje na unapoingia ndani.”
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “kuta zako zenye ngome.”
Au “Nafsi yetu imechoshwa na dhihaka nyingi za.”
Au “Nafsi yetu.”
Au “wasiielekeze mikono yao kutenda.”
Au “makorongo ya kusini.”
Au “Wana.”
Au “unafuatilia.”
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Tnn., “Ili uogopwe.”
Au “nimejituliza na kujinyamazisha mwenyewe.” Angalia Kamusi.
Au “Hema tukufu la ibada.”
Au “hema lake tukufu la ibada.”
Tnn., “Usiugeuze nyuma uso wa.”
Tnn., “Mmoja kutoka katika uzao wa tumbo lako.”
Tnn., “nitaifanya pembe ya Daudi ikue.”
Au labda, “mahali patakatifu.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Lipigieni muziki.”
Au “mali yake anayothamini sana.”
Au “Huufanya mvuke upande.”
Au labda, “malango.”
Au “jina lako linadumu.” Tnn., “ukumbusho wako unadumu.”
Au “ataamua kesi ya.”
Au “ataghairi kuwahusu.”
Au “kwa uelewaji.”
Tnn., “sehemu sehemu.”
Tnn., “Huipa chakula miili yote.”
Yaani, Babiloni.
Au labda, “unyauke.”
Au labda, “Nitaipinga miungu mingine kwa kukupigia muziki.”
Au “mahali pake patakatifu.”
Au labda, “umelitukuza neno lako juu ya jina lako lote.”
Au “niwe na ujasiri katika nafsi yangu.”
Tnn., “Unanipima.”
Au “ni wa ajabu sana kwangu.”
Au “Umezidi kabisa uelewaji wangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au labda, “Ulinifuma pamoja.”
Au “Nafsi yangu inajua.”
Au labda, “nitakuwa bado ninayahesabu.”
Au “wenye hatia ya damu.”
Au “kulingana na mawazo yao.”
Au “yanayonifadhaisha.”
Au “Mashimo yenye umajimaji.”
Au “nchini.”
Au “katika uwepo wako.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Usiimwage chini nafsi yangu.”
Angalia Kamusi.
Au “Ninapoishiwa na nguvu.”
Tnn., “anayenitambua.”
Tnn., “Fungu langu.”
Au “Ninaishiwa na nguvu.”
Au “Ninajifunza.”
Tnn., “Roho yangu imefikia.”
Au “kaburini.”
Au “Kwa maana ninakuinulia nafsi yangu.”
Au “katika nchi ya unyoofu.”
Tnn., “wanyamazishe.”
Au “Kilele changu salama.”
Au “kunja.”
Au “udhibiti.”
Tnn., “Na mkono wao wa kulia ni mkono wa kulia wa uwongo.”
Au “Nitakupigia muziki.”
Au “wokovu.”
Au “hawatapasukiwa na mimba.”
Au “hauwezi kueleweka.”
Au “nguvu zako.”
Au “neema.”
Au “kwa unyoofu.”
Tnn., “Miili yote na isifu.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Nitampigia muziki.”
Au “viongozi.”
Au “Pumzi.”
Tnn., “mkate.”
Tnn., “waliofungwa.”
Au “huipotosha njia ya waovu.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “kumpigia muziki.”
Tnn., “mafuta ya ngano.”
Au “Huitupa chini barafu yake.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Tnn., “mbingu za mbingu.”
Tnn., “mabikira.”
Au “Wakubwa kwa wadogo.”
Tnn., “pembe.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “wampigie muziki.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “anga linalotoa ushahidi kuhusu.”
Au “zumari.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.