Amosi
1 Maneno ya Amosi, aliyekuwa kati ya wafugaji wa kondoo kutoka Tekoa,+ ambayo aliona katika maono kuhusu Israeli+ katika siku za Uzia+ mfalme wa Yuda na katika siku za Yeroboamu+ mwana wa Yoashi,+ mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya lile tetemeko la nchi.+ 2 Naye akasema:
“Yehova—atanguruma kutoka Sayuni,+ naye atatoa sauti yake kutoka Yerusalemu;+ navyo viwanja vya malisho vya wachungaji vitaomboleza, na kilele cha Karmeli kitakauka.”+
3 “Yehova amesema hivi, ‘ “Kwa sababu ya maasi matatu ya Damasko,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu wamepura Gileadi+ kwa vifaa vya kupuria vya chuma. 4 Nami nitapeleka moto+ juu ya nyumba ya Hazaeli,+ nao utaiteketeza minara ya makao ya Ben-hadadi.+ 5 Nami nitavunja pingo la Damasko+ na kumkatilia mbali mkaaji kutoka Bikath-aveni, na anayeshika fimbo ya enzi kutoka Beth-edeni; na watu wa Siria wataenda Kiri+ wakiwa wahamishwa,” Yehova amesema.’
6 “Yehova amesema hivi, ‘ “Kwa sababu ya maasi matatu ya Gaza,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu walilipeleka uhamishoni kundi zima la wahamishwa+ ili kuwatia mkononi mwa Edomu.+ 7 Nami nitapeleka moto kwenye ukuta wa Gaza,+ nao utaiteketeza minara ya makao yake. 8 Nami nitakatilia mbali mkaaji kutoka Ashdodi,+ na anayeshika fimbo ya enzi kutoka Ashkeloni;+ nami nitageuza mkono wangu+ juu ya Ekroni,+ na mabaki ya Wafilisti yataangamia,”+ Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema.’
9 “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Tiro,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu ya kulitia mkononi mwa Edomu kundi zima la wahamishwa, na kwa sababu hawakukumbuka agano la ndugu.+ 10 Nami nitapeleka moto kwenye ukuta wa Tiro, nao utaiteketeza minara ya makao yake.’+
11 “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Edomu,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake mwenyewe kwa upanga,+ na kwa sababu aliharibu sifa zake mwenyewe za rehema,+ na hasira yake huendelea kurarua milele, na ghadhabu yake—ameishika daima.+ 12 Nami nitapeleka moto katika Temani,+ nao utaiteketeza minara ya makao ya Bosra.’+
13 “Yehova amesema hivi, ‘ “Kwa sababu ya maasi matatu ya wana wa Amoni,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia,+ kwa sababu waliwapasua wanawake wenye mimba wa Gileadi, kwa kusudi la kupanua eneo lao wenyewe.+ 14 Nami nitawasha moto kwenye ukuta wa Raba,+ nao utaiteketeza minara ya makao yake, pamoja na sauti ya king’ora siku ya pigano, pamoja na tufani siku ya upepo wa dhoruba.+ 15 Na mfalme wao ataenda uhamishoni, yeye pamoja na wakuu wake,”+ Yehova amesema.’
2 “Yehova amesema hivi, ‘ “Kwa sababu ya maasi matatu ya Moabu,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa kuwa aliteketeza mifupa ya mfalme wa Edomu ili kupata chokaa.+ 2 Nami nitapeleka moto ndani ya Moabu, nao utaiteketeza minara ya makao ya Keriothi,+ na Moabu atakufa kati ya kelele, na sauti ya king’ora, na sauti ya baragumu.+ 3 Nami nitamkatilia mbali mwamuzi kutoka katikati yake, na wakuu wake wote nitawaua pamoja naye,”+ Yehova amesema.’
4 “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Yuda,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu wamekataa sheria ya Yehova,+ na kwa sababu hawakushika masharti yake mwenyewe; bali uwongo wao,+ ambao mababu zao walikuwa wametembea ndani yake, uliendelea kuwapoteza.+ 5 Nami nitapeleka moto ndani ya Yuda, nao utaiteketeza minara ya makao ya Yerusalemu.’+
6 “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Israeli,+ na kwa sababu ya manne, sitaizuia, kwa sababu waliuza mtu mwadilifu kwa sababu tu ya fedha, na maskini kwa bei ya pea moja ya viatu.+ 7 Wanatamani sana mavumbi ya dunia yaliyo kwenye vichwa vya watu wa hali ya chini;+ nao huipotosha njia ya watu wapole;+ na mwanamume na baba yake wamemwendea msichana yuleyule,+ kwa kusudi la kulitia unajisi jina langu takatifu.+ 8 Nao hujinyoosha+ kando ya kila madhabahu+ juu ya mavazi yaliyotwaliwa kama rehani; na divai ya wale ambao wametozwa wao huinywa katika nyumba ya miungu yao.’+
9 “ ‘Lakini mimi, nilikuwa nimemwangamiza Mwamori+ kwa sababu yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, na ambaye alikuwa na nguvu kama miti mikubwa;+ nami nikaangamiza matunda yake juu na mizizi yake chini.+ 10 Nami mwenyewe niliwatoa ninyi kutoka nchi ya Misri,+ nami nikaendelea kuwatembeza kupitia nyikani miaka 40,+ ili mwimiliki nchi ya Mwamori.+ 11 Nami nikaendelea kuwasimamisha baadhi ya wana wenu kuwa manabii+ na baadhi ya wanaume wenu vijana kuwa Wanadhiri.+ Je, kwa kweli haipaswi kuwa hivyo, enyi wana wa Israeli?’ asema Yehova.
12 “ ‘Lakini mliendelea kuwapa Wanadhiri divai wanywe,+ nanyi mkaweka amri juu ya manabii, mkisema: “Msitoe unabii.”+ 13 Tazama, mimi nakifanya kile kilicho chini yenu kiyumbe-yumbe, kama vile linavyoyumba-yumba gari la kukokotwa ambalo limejazwa kabisa mafungu ya nafaka iliyokatwa hivi karibuni. 14 Na mahali pa kukimbilia pataangamia kutoka kwa yule aliye mwepesi,+ wala hakuna yeyote mwenye nguvu atakayeimarisha nguvu zake, wala hakuna mwanamume yeyote mwenye nguvu ambaye ataiponya nafsi yake.+ 15 Wala yeyote anayetumia upinde hatasimama, wala yeyote aliye mwepesi kwa miguu yake hataponyoka, wala mpandaji yeyote wa farasi hataiponya nafsi yake.+ 16 Na yule aliye na moyo wenye nguvu kati ya wanaume wenye nguvu, atakimbia akiwa uchi katika siku ile,’+ asema Yehova.”
3 “Lisikieni neno hili ambalo Yehova amesema kuwahusu ninyi,+ enyi wana wa Israeli, kuhusu familia nzima niliyoitoa katika nchi ya Misri,+ nikisema, 2 ‘Mimi nimewajua ninyi peke yenu+ kati ya familia zote za nchi.+ Hiyo ndiyo sababu nitawatoza ninyi hesabu kwa sababu ya makosa yenu yote.+
3 “‘Je, watu wawili watatembea pamoja isipokuwa wawe wamekutana kwa mapatano?+ 4 Je, simba atanguruma mwituni wakati hana mawindo yoyote?+ Je, mwana-simba mwenye manyoya shingoni atatoa sauti mafichoni mwake ikiwa hakukamata chochote? 5 Je, ndege ataanguka ndani ya mtego chini ikiwa hakuna mnaso kwa ajili yake?+ Je, mtego huteguka udongoni ikiwa haujakamata chochote kamwe? 6 Je, baragumu ikipigwa katika jiji, watu wenyewe pia hawatetemeki?+ Je, msiba ukitokea katika jiji, Yehova siye pia aliyetenda? 7 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hatafanya lolote isipokuwa awe amewafunulia watumishi wake manabii jambo lake la siri.+ 8 Kuna simba ambaye amenguruma!+ Ni nani hataogopa? Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova mwenyewe amesema! Ni nani ambaye hatatoa unabii?’+
9 “ ‘Litangazeni kwenye minara ya makao katika Ashdodi na juu ya minara ya makao ya nchi ya Misri,+ na kusema: “Kusanyikeni pamoja juu ya milima ya Samaria,+ mwone machafuko mengi yaliyo katikati yake na visa vya upunjaji vilivyo ndani yake.+ 10 Nao hawajajua jinsi ya kufanya yaliyo manyoofu,”+ asema Yehova, “wale wanaoweka jeuri+ akiba na uporaji katika minara ya makao yao.” ’
11 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kuna adui kuzunguka nchi,+ naye atazishusha nguvu zako zikutoke, na minara ya makao yako itaporwa.’+
12 “Yehova amesema hivi, ‘Kama vile mchungaji anavyonyakua miguu miwili au kipande cha sikio kutoka katika kinywa cha simba,+ ndivyo wana wa Israeli watakavyonyakuliwa, wale wanaokaa katika Samaria kwenye kitanda cha utukufu+ na kwenye kitanda cha Damasko.’+
13 “ ‘Sikieni na kutoa ushahidi+ katika nyumba ya Yakobo,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Mungu wa majeshi. 14 ‘Maana, siku yangu ya kutoza hesabu+ kwa sababu ya maasi ya Israeli juu yake, mimi nitazitoza hesabu pia madhabahu za Betheli;+ na pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.+ 15 Nami nitaiangusha nyumba ya wakati wa majira ya baridi+ kali pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi.’+
“ ‘Na nyumba za pembe za tembo zitaangamia,+ na nyumba nyingi zitakwisha,’+ asema Yehova.”
4 “Lisikieni neno hili, ninyi ng’ombe za Bashani,+ mlio juu ya mlima wa Samaria,+ mnaopunja watu wa hali ya chini,+ mnaoponda walio maskini, mnaowaambia mabwana zenu, ‘Leteni, tunywe!’ 2 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameapa kwa utakatifu wake,+ ‘ “Tazama! Kuna siku zinazokuja juu yenu, naye atawainua ninyi kwa kulabu za mchinjaji na sehemu yenu ya mwisho kwa ndoano.+ 3 Nanyi mtakwenda kupitia matundu,+ kila mmoja akienda mbele moja kwa moja; nanyi mtatupwa nje kwenye Harmoni,” asema Yehova.’
4 “ ‘Enyi watu, njooni Betheli, mfanye makosa.+ Fanyeni makosa mara nyingi katika Gilgali,+ na mlete dhabihu zenu asubuhi; na sehemu zenu za kumi katika siku ya tatu.+ 5 Fukizeni dhabihu ya shukrani kutoka kwa kile kilichotiwa chachu,+ na mtangaze matoleo ya hiari;+ litangazeni, kwa maana hivyo ndivyo mmependa, enyi wana wa Israeli,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
6 “ ‘Mimi pia, niliwapa ninyi usafi wa meno+ katika majiji yenu yote na upungufu wa mkate katika mahali penu pote;+ lakini hamkurudi kwangu,’+ asema Yehova.
7 “ ‘Mimi pia, nilizuia mvua isiwanyeshee ninyi kukiwa kungali miezi mitatu kabla ya mavuno;+ nami nikainyesha katika jiji moja, lakini jiji lingine sikuinyesha. Kuna sehemu moja ya shamba ambayo ilinyeshewa, lakini sehemu ya shamba ambayo sikuinyeshea ilikauka.+ 8 Na majiji mawili au matatu yakayumba-yumba kwenda kwenye jiji moja ili kunywa maji,+ nao hawakutosheka;+ lakini hamkurudi kwangu,’ asema Yehova.
9 “ ‘Niliwapiga ninyi kwa kuunguza na kwa ukungu.+ Bustani zenu na mashamba yenu ya matunda mliongeza, lakini mitini yenu na mizeituni yenu ililiwa na kiwavi;+ hata hivyo hamkurudi kwangu,’+ asema Yehova.
10 “ ‘Nilituma kati yenu ninyi tauni kama ile ya Misri.+ Niliwaua vijana wenu kwa upanga,+ pamoja na kuchukua mateka farasi zenu.+ Nami nikaendelea kufanya harufu ya kunuka ya kambi zenu ipande hata kuingia puani mwenu;+ lakini hamkurudi kwangu,’+ asema Yehova.
11 “ ‘Nilisababisha maangamizi kati yenu, kama maangamizi ya Mungu juu ya Sodoma na Gomora.+ Nanyi mkawa kama kipande cha mti kilichonyakuliwa kutoka motoni;+ lakini hamkurudi kwangu,’+ asema Yehova.
12 “Kwa hiyo hayo ndiyo nitakayokutendea, Ee Israeli. Kwa sababu nitakutendea mambo hayo, jitayarishe kukutana na Mungu wako,+ Ee Israeli. 13 Kwa maana, tazama! Mfanyizaji wa milima+ na Muumba wa upepo,+ Yeye anayemwambia mtu wa udongo shughuli zake za akilini,+ Yeye anayefanya mapambazuko kuwa giza,+ na Yeye anayetembea mahali pa juu pa dunia,+ Yehova Mungu wa majeshi ndilo jina lake.”+
5 “Lisikieni neno hili ninalosema juu yenu kama wimbo wa huzuni,+ Ee nyumba ya Israeli:
2 “Israeli, bikira,+ ameanguka;+
Hawezi kusimama tena.+
Ameachwa juu ya nchi yake mwenyewe;
Hakuna anayemsimamisha.+
3 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Jiji lililokuwa likitoka nje likiwa na elfu moja litaachwa na mia; na lile lililokuwa likitoka nje likiwa na mia moja litaachwa na kumi, kwa nyumba ya Israeli.’+
4 “Kwa maana Yehova ameiambia hivi nyumba ya Israeli, ‘Nitafuteni mimi,+ mwendelee kuishi.+ 5 Wala msitafute Betheli,+ wala msiende Gilgali,+ wala msivuke Beer-sheba;+ kwa sababu Gilgali litakwenda uhamishoni;+ Betheli nalo litakuwa kitu cha uchawi.+ 6 Mtafuteni Yehova, Ee nyumba ya Yosefu,+ mwendelee kuishi,+ ili asitende kama vile moto,+ nao usije ukateketeza, na Betheli lisikose mtu wa kuuzima,+ 7 enyi mnaoigeuza haki kuwa pakanga tupu,+ ninyi ambao mmeutupa chini uadilifu.+ 8 Mtengenezaji wa kundi-nyota la Kima+ na kundi-nyota+ la Kesili,+ na Yeye ambaye anageuza kivuli kizito+ kiwe asubuhi, na Yeye ambaye amefanya mchana uwe na giza kama usiku,+ Yeye ambaye anaita maji ya bahari, ili ayamwage kwenye uso wa dunia+—Yehova ndilo jina lake;+ 9 yeye ambaye anasababisha uporaji uje ghafula juu ya mtu mwenye nguvu, ili uporaji uje hata juu ya mahali penye ngome.
10 “ ‘Katika lango wao wamemchukia mwenye kukaripia,+ nao humchukia msemaji wa mambo makamilifu.+ 11 Basi, kwa sababu mnamtoza mtu wa hali ya chini kodi ya shamba,+ nanyi mnaendelea kuchukua kutoka kwake ushuru wa nafaka; mmejenga nyumba za mawe yaliyochongwa,+ lakini hamtaendelea kukaa ndani yake; nanyi mmepanda mashamba ya mizabibu yenye kupendeza, lakini hamtaendelea kunywa divai yake.+ 12 Kwa maana nimejua hesabu za maasi+ yenu na jinsi dhambi zenu zilivyo kubwa,+ enyi mnaomwonyesha mtu mwadilifu uadui,+ ninyi mnaochukua pesa za hongo,+ na ambao mmewafukuza watu maskini+ langoni.+ 13 Basi yeye aliye na ufahamu atakaa kimya wakati huo, kwa maana utakuwa wakati wenye taabu.+
14 “ ‘Tafuteni yaliyo mema, wala si yaliyo mabaya,+ kusudi mwendelee kuishi;+ ndipo Yehova Mungu wa majeshi apate kuwa pamoja nanyi, kama vile ambavyo mmesema.+ 15 Chukieni yaliyo mabaya, pendeni yaliyo mema,+ na mwipatie haki nafasi langoni.+ Huenda ikawa Yehova Mungu wa majeshi atawapa kibali+ mabaki ya Yosefu.’+
16 “Basi Yehova aliye Yehova Mungu wa majeshi amesema hivi, ‘Kutakuwako maombolezo katika viwanja vyote vya watu wote,+ na katika barabara zote watu watakuwa wakisema: “Ah! Ah!” Nao watamwita mkulima aje kuomboleza,+ na kuwaita wale wenye uzoefu wa maombolezo waje kulia.’+ 17 ‘Na kutakuwako maombolezo katika mashamba yote ya mizabibu;+ kwa maana nitapita katikati yako,’+ Yehova amesema.
18 “ ‘Ole wao wanaoitamani siku ya Yehova!+ Basi, siku ya Yehova itamaanisha nini kwenu?+ Itakuwa giza, wala si nuru,+ 19 kama vile tu mtu anavyomkimbia simba, kisha dubu anakutana naye; na kama vile alivyoingia ndani ya nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, naye nyoka akamuuma.+ 20 Je, siku ya Yehova haitakuwa giza, wala si nuru; na je, haitakuwa na weusi, wala si mwangaza?+ 21 Nimechukia, nimezikataa sherehe zenu,+ wala sitafurahia harufu ya makusanyiko yenu makuu.+ 22 Lakini ninyi mkinitolea matoleo mazima ya kuteketezwa,+ hata katika matoleo yenu ya zawadi sitapata furaha,+ wala sitatazama dhabihu zenu za ushirika za vinono.+ 23 Ondoeni kutoka kwangu mchafuko wa nyimbo zenu; wala sauti tamu ya vinanda vyenu sitaki kusikia.+ 24 Na haki itiririke kama maji,+ na uadilifu kama mto unaotiririka daima.+ 25 Je, mlinisogezea karibu dhabihu na matoleo ya zawadi nyikani miaka 40, Ee nyumba ya Israeli?+ 26 Nanyi mtamchukua Sakuthi mfalme wenu+ na Kaiwani, sanamu zenu, nyota ya mungu wenu, ambaye mlijifanyia ninyi wenyewe.+ 27 Nami nitawafanya mwende uhamishoni ng’ambo ya Damasko,’+ yeye ambaye jina lake ni Yehova Mungu wa majeshi, amesema.”+
6 “Ole wao wanaostarehe+ katika Sayuni na wale wanaotegemea mlima wa Samaria! Hao ndio wale walio mashuhuri wa sehemu kuu ya mataifa, na nyumba ya Israeli imewajia. 2 Shikeni njia mpaka Kalne, mkaone; na kutoka hapo endeni mpaka Hamathi+ jiji lililo na hesabu kubwa ya watu, na mshuke mpaka Gathi+ la Wafilisti. Je, hayo ni bora kuliko falme hizi, au je, eneo lao ni kubwa kuliko eneo lenu?+ 3 Je, mnaiondoa akilini mwenu ile siku yenye msiba,+ na je, mnaleta karibu makao ya jeuri?+ 4 Ninyi watu mnaojilaza katika vitanda vya pembe za tembo+ na kujitandaza katika vitanda vyao, na mnaokula kondoo-dume kati ya kundi na ng’ombe-dume wachanga kutoka kati ya ndama waliononeshwa;+ 5 ambao mnatunga kulingana na sauti ya kinanda,+ ambao, kama Daudi, mmejitengenezea vyombo vya nyimbo;+ 6 ambao mnakunywa kwa mabakuli ya divai,+ na ambao mnatia mafuta kwa kutumia mafuta yenu yaliyo bora kabisa,+ na ambao hamkuwa wagonjwa kutokana na msiba wa Yosefu.+
7 “Basi sasa wataenda uhamishoni wakiwa mbele ya wale wanaoenda uhamishoni,+ na karamu za kupindukia za wale wanaojitandaza zitaondoka.
8 “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameapa kwa nafsi yake mwenyewe,’+ asema Yehova Mungu wa majeshi, ‘ “Mimi ninachukia kiburi cha Yakobo,+ na minara ya makao yake nimeichukia,+ nami nitalitoa hilo jiji na vitu vyote vinavyolijaza.+ 9 Na itakuwa kwamba wanaume kumi wakibaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.+ 10 Na ndugu ya baba yake atawachukua mmoja mmoja, naye atawachoma moto mmoja mmoja, ili kuiondoa mifupa ndani ya nyumba.+ Naye atamwambia yeyote yule aliye katika sehemu za ndani kabisa za nyumba, ‘Je, bado una wengine zaidi?’ Naye atalazimika kusema, ‘Hamna mtu!’ Naye atalazimika kusema, ‘Nyamaza kimya! Kwa maana huu si wakati wa kutaja kwa vyovyote jina la Yehova.’ ”+
11 “ ‘Kwa maana ni Yehova anayeamuru,+ naye ataipiga ile nyumba kubwa kwa kuifanya kuwa mabomoko na ile nyumba ndogo kwa kuifanya kuwa magofu.+
12 “ ‘Je, farasi watakimbia juu ya mwamba, au je, mtu atalima hapo kwa kutumia ng’ombe? Kwa maana ninyi mmeigeuza haki iwe mmea wenye sumu,+ na kuyageuza matunda ya uadilifu yawe pakanga, 13 ninyi mnaoshangilia jambo ambalo halipo;+ ambao mnasema: “Je, hatukujitwalia pembe kwa nguvu zetu wenyewe?”+ 14 Tazama! Mimi ninasimamisha taifa juu yenu,+ Ee nyumba ya Israeli,’ asema Yehova Mungu wa majeshi, ‘nao watawakandamiza ninyi kutoka maingilio ya Hamathi+ mpaka kwenye bonde la mto la Araba.’ ”
7 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova alinifanya nione, na, tazama! alikuwa akifanyiza kundi la nzige mwanzoni mwa kuota kwa mimea iliyopandwa baadaye.+ Na, tazama! ilikuwa mimea iliyopandwa baadaye baada ya majani yaliyofyekwa ya mfalme. 2 Na ikawa kwamba lilipomaliza kula kabisa majani ya nchi, nikasema: “Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, tafadhali samehe.+ Ni nani atakayesimama katika Yakobo? Maana yeye ni mdogo!”+
3 Yehova akajuta juu ya jambo hilo.+ “Hilo halitatokea,” Yehova akasema.
4 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova alinifanya nione, na, tazama! Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova alikuwa anaita mashindano kupitia kwa moto;+ nao ukateketeza kabisa kilindi kikubwa cha maji na kuteketeza kabisa ile sehemu ya shamba. 5 Nami nikasema: “Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, tafadhali zuilia.+ Ni nani atakayesimama katika Yakobo? Maana yeye ni mdogo!”+
6 Yehova akajuta juu ya jambo hilo.+ “Hilo pia halitatokea,” Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova akasema.
7 Hili ndilo alilonifanya nione, na, tazama! Yehova alikuwa juu ya ukuta uliotengenezwa kwa timazi,+ na timazi ilikuwa mkononi mwake. 8 Ndipo Yehova akaniambia: “Unaona nini, Amosi?” Basi nikasema: “Timazi.” Yehova akaendelea kusema: “Tazama, naweka timazi katikati ya watu wangu Israeli.+ Nami sitawasamehe zaidi tena.+ 9 Na mahali pa juu pa Isaka+ patafanywa kuwa ukiwa, na patakatifu+ pa Israeli pataharibiwa;+ nami nitasimama kuipiga nyumba ya Yeroboamu kwa upanga.”+
10 Naye Amazia kuhani wa Betheli+ akapeleka habari kwa Yeroboamu+ mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi amepanga hila juu yako ndani ya nyumba ya Israeli.+ Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.+ 11 Kwa maana Amosi amesema hivi, ‘Kwa upanga Yeroboamu atakufa; naye Israeli bila shaka ataenda uhamishoni kutoka katika nchi yake mwenyewe.’ ”+
12 Kisha Amazia akamwambia Amosi: “Ewe mwonaji,+ nenda, kimbia uende zako kwenye nchi ya Yuda, ukale mkate huko, na huko unaweza kutoa unabii. 13 Lakini usiendelee tena kutoa unabii katika Betheli,+ kwa maana ni mahali patakatifu pa mfalme+ napo ni nyumba ya ufalme.”
14 Ndipo Amosi akajibu na kumwambia Amazia: “Mimi sikuwa nabii, wala sikuwa mwana wa nabii,+ bali nilikuwa mchungaji+ na mminyaji wa tini za mikuyu. 15 Naye Yehova akanichukua nisifuatane na kundi tena, na Yehova akaendelea kuniambia, ‘Nenda, watolee unabii watu wangu Israeli.’+ 16 Basi sasa lisikie neno la Yehova, ‘Je, unasema: “Usitoe unabii juu ya Israeli,+ wala usiache neno lolote lianguke+ juu ya nyumba ya Isaka”? 17 Basi Yehova amesema hivi: “Kwa habari ya mke wako, atakuwa kahaba jijini.+ Nao wana na binti zako wataanguka kwa upanga. Nayo nchi yako itagawanywa kwa kamba ya kupimia. Na wewe mwenyewe utakufa katika nchi isiyo safi;+ naye Israeli, bila shaka ataenda uhamishoni kutoka katika nchi yake mwenyewe.” ’ ”+
8 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova alinifanya nione, na, tazama! kulikuwako kikapu cha matunda ya wakati wa kiangazi.+ 2 Kisha akasema: “Unaona nini,+ Amosi?” Basi nikasema: “Kikapu cha matunda ya wakati wa kiangazi.”+ Na Yehova akaendelea kuniambia: “Mwisho umewafikia watu wangu Israeli.+ Nami sitawasamehe zaidi tena.+ 3 ‘Na nyimbo za hekalu zitakuwa mayowe siku hiyo,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Kutakuwako mizoga mingi.+ Kila mahali mtu fulani ataitupa—kimya!’
4 “Sikieni hili, ninyi mnaouma maskini,+ ili kuwakomesha wapole wa dunia,+ 5 mkisema, ‘Mwezi mpya utapita wakati gani,+ tukauze nafaka?+ Pia sabato,+ tukauze nafaka; ili kuifanya efa kuwa ndogo+ na kuifanya shekeli kuwa kubwa na kuipotosha mizani ya udanganyifu;+ 6 ili tununue watu wa hali ya chini kwa fedha tu na maskini kwa bei ya pea moja ya viatu, na ili tuuze takataka tupu ya nafaka?’+
7 “Yehova ameapa kwa Ukuu wa Yakobo,+ ‘Kamwe sitazisahau kazi zao zote.+ 8 Je, haitakuwa kwa sababu hii kwamba nchi itafadhaika,+ na kila mkaaji ndani yake ataomboleza;+ nayo yote, itainuka kama tu Nile na kurushwarushwa na kuzama kama mto Nile wa Misri?’+
9 “ ‘Na itakuwa katika siku hiyo,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘kwamba nitalifanya jua lishuke katikati ya mchana,+ nami nitailetea nchi giza siku ya mwangaza. 10 Nami nitazigeuza sherehe zenu ziwe maombolezo+ na nyimbo zenu zote ziwe nyimbo za huzuni. Nitatia nguo za magunia juu ya viuno vyote na juu ya kila kichwa nitatia upara.+ Nami nitafanya hali iwe kama kuombolezea mwana wa pekee,+ na matokeo yake ya mwisho kama siku yenye uchungu.’
11 “ ‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nami nitaleta njaa katika nchi, wala si njaa ya mkate, nami nitaleta kiu, wala si kiu ya maji, bali ya kuyasikia maneno ya Yehova.+ 12 Nao wataenda wakiyumba-yumba kutoka bahari mpaka bahari, kutoka kaskazini hata mashariki. Watazidi kwenda huku na huku wakitafuta neno la Yehova, lakini hawatalipata.+ 13 Katika siku hiyo mabikira wenye kupendeza watazimia, pia vijana, kwa sababu ya kiu;+ 14 wale wanaoapa kwa hatia ya Samaria,+ na ambao husema: “Kama anavyoishi mungu wako, Ee Dani!”+ na, “Kama inavyoishi njia ya Beer-sheba!”+ Nao wataanguka, wala hawatasimama tena.’ ”+
9 Nilimwona Yehova akiwa juu ya madhabahu,+ naye akasema: “Kipige kichwa cha nguzo, ili vizingiti vitikisike. Na uvikate vyote kichwani.+ Na sehemu yao ya mwisho nitaua kwa upanga. Hakuna yeyote kati yao anayekimbia atakayefanikiwa kukimbia, na hakuna yeyote kati yao anayeponyoka ambaye atafanikiwa kutoroka.+ 2 Wakichimba chini kuingia katika Kaburi,* toka humo mkono wangu mwenyewe utawachukua;+ nao wakienda juu mbinguni, toka huko nitawashusha chini.+ 3 Nao wakijificha katika kilele cha Karmeli, nitawatafuta kwa uangalifu na kuwachukua kutoka huko.+ Na wakijificha kwenye sakafu ya bahari kutoka mbele za macho yangu,+ huko chini nitamwamuru nyoka, naye atawauma. 4 Nao wakienda utekwani mbele ya adui zao, kutoka huko nitaamuru upanga, nao utawaua;+ nami nitaweka macho yangu juu yao kwa mabaya, wala si kwa mema.+ 5 Naye Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, Yeye ndiye anayeigusa nchi, ikayeyuka;+ na wakaaji wote ndani yake wataomboleza.+ Nayo yote itainuka kama Nile, na kuzama kama mto Nile wa Misri.+
6 “ ‘Yeye anayejenga ngazi zake huko mbinguni,+ na jengo lake juu ya dunia ambayo ameiwekea msingi;+ yeye anayeyaita maji ya bahari,+ ili ayamwage juu ya uso wa dunia+—Yehova ndilo jina lake.’+
7 “ ‘Je, ninyi si kama wana wa Wakushi kwangu, enyi wana wa Israeli?’ asema Yehova. ‘Je, sikuleta Israeli kutoka nchi ya Misri,+ na Wafilisti+ kutoka Krete, na Siria kutoka Kiri?’+
8 “ ‘Tazama! Macho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova yako juu ya ufalme wenye dhambi,+ naye atauangamiza kutoka juu ya uso wa nchi.+ Hata hivyo, sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,’+ asema Yehova. 9 ‘Kwa maana, tazama! Ninaamuru, nami nitaipepeta nyumba ya Israeli katika mataifa yote,+ kama vile mtu anavyopepeta kichujio, lisianguke chini jiwe la mviringo hata moja. 10 Kwa upanga watakufa—watenda-dhambi wote katika watu wangu,+ wale wanaosema: “Taabu hiyo haitakuja karibu wala kutufikia sisi.” ’+
11 “ ‘Katika siku hiyo nitakisimamisha+ kibanda+ cha Daudi ambacho kimeanguka,+ nami nitayarekebisha matundu yao. Na mabomoko yake nitayasimamisha, nami nitakijenga kama katika siku za kale,+ 12 ili kwamba wamiliki mabaki ya Edomu,+ na mataifa yote ambayo juu yao jina langu limeitwa,’+ asema Yehova, anayefanya hayo.
13 “ ‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘na anayelima atampita anayevuna,+ na anayekanyaga zabibu atampita anayechukua mbegu;+ na milima itatiririka divai tamu,+ na vilima vyote vitayeyuka.+ 14 Nami nitakusanya na kurudisha mateka wa watu wangu Israeli,+ nao watajenga majiji yaliyofanywa ukiwa na kukaa ndani yake,+ watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake, watafanyiza bustani na kula matunda yake.’+
15 “ ‘Nami nitawapanda juu ya nchi yao, wala hawatang’olewa tena kutoka katika nchi yao ambayo nimewapa,’+ Yehova Mungu wako amesema.”
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.