ZABURI
KITABU CHA KWANZA
(Zaburi 1-41)
1 Mwenye furaha ni mutu mwenye hatembee kulingana na shauri la waovu
Na hasimame katika njia ya watenda-zambi+
Naye hakae katika kiti cha wenye kuzihaki.+
2 Lakini anapendezwa na sheria ya Yehova,+
Na anasoma sheria Yake kwa sauti ya chini* muchana na usiku.+
3 Atakuwa kama muti wenye kupandwa pembeni ya mito midogo ya maji,
Muti wenye unazaa matunda katika wakati wake,
Na majani yake hayakauke.
Na kila jambo lenye anafanya litafanikiwa.+
4 Waovu hawako vile;
Wako kama maganda ya mbegu yenye kupeperushwa mbali na upepo.
5 Ndiyo sababu waovu hawataendelea kusimama katika hukumu;+
Wala watenda-zambi hawataendelea kusimama katika mukusanyiko wa wenye haki.+
2 Sababu gani mataifa yako na musukosuko
Na vikundi vya watu vinasema kwa sauti ya chini-chini* jambo lenye halina maana?+
3 Wanasema: “Tukate pingu zao
Na kutupa kamba zao!”
4 Ule mwenye kukaa akiwa mufalme kule mbinguni atacheka;
Yehova atawachekelea.
5 Wakati huo atasema nao katika kasirani yake
Na kuwaogopesha sana katika kasirani yake yenye kuwaka,
6 Kwa kusema: “Mimi mwenyewe nimemuweka mufalme wangu+
Juu ya Sayuni,+ mulima wangu mutakatifu.”
11 Mumutumikie Yehova kwa woga,
Na mushangilie mukitetemeka.
12 Mumuheshimie* mwana,+ kama hamufanye vile Mungu* atakasirika sana
Na ninyi mutaangamia kutoka katika njia,+
Kwa maana kasirani Yake inawaka haraka.
Wenye furaha ni wale wote wenye wanamukimbilia Yeye.
Muziki wa Daudi wakati alikuwa anamukimbia Absalomu mwana wake.+
3 Ee Yehova, sababu gani wapinzani wangu wamekuwa wengi sana?+
Sababu gani watu wengi sana wanainuka ili kunipinga?+
7 Simama, Ee Yehova! Uniokoe,+ Ee Mungu wangu!
Baraka yako iko juu ya watu wako. (Sela)
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Muziki wa Daudi.
4 Wakati ninakuita, unijibu, Ee Mungu wangu mwenye haki.+
Unitengenezee njia ya kuponyoka* taabu yangu.
Unionyeshe wema na usikie sala yangu.
2 Ninyi wana wa binadamu, mutaendelea mupaka wakati gani kugeuza heshima yangu kuwa haya?
Mutaendelea mupaka wakati gani kupenda mambo yenye hayana mafaa yoyote na kutafuta mambo ya uongo? (Sela)
3 Mujue kwamba Yehova atamutendea mushikamanifu wake kwa njia ya pekee;*
Yehova atasikia wakati nitamuita.
4 Mukasirike, lakini musitende zambi.+
Museme katika moyo wenu, kwenye kitanda chenu, na munyamaze kimya. (Sela)
6 Kuko watu wengi wenye kusema: “Ni nani atatuonyesha jambo lolote la muzuri?”
Mwangaza wa uso wako utuangazie, Ee Yehova.+
7 Umejaza moyo wangu shangwe nyingi sana
Kuliko wale wenye kuwa na mavuno mengi sana ya nafaka na divai mupya.
8 Nitajilaza chini na kulala usingizi kwa amani,+
Kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, unanifanya niishi katika usalama.+
Kwa kiongozi wa Nehiloti.*
Muziki wa Daudi.
5 Sikiliza maneno yangu, Ee Yehova;+
Sikiliza kwa uangalifu kilio changu cha maumivu.
2 Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada,
Ee Mufalme wangu na Mungu wangu, kwa sababu ninasali kwako.
3 Ee Yehova, utasikia sauti yangu asubui;+
Asubui nitakuelezea mahangaiko yangu+ na kungojea kwa hamu.
4 Kwa maana wewe hauko Mungu mwenye anafurahia uovu;+
Hakuna mutu yeyote mubaya mwenye anaweza kukaa pamoja na wewe.+
5 Hakuna mutu yeyote mwenye kiburi mwenye anaweza kusimama mbele yako.
Yehova anachukia watu wenye jeuri na wadanganyifu.*+
7 Lakini nitaingia katika nyumba yako+ kwa sababu ya upendo wako mwingi mushikamanifu;+
Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu* nikiwa na woga wenye heshima kukuelekea.+
8 Uniongoze, Ee Yehova, katika haki yako kwa sababu ya maadui wangu;
Fanya njia yako ikuwe wazi kwangu.+
9 Kwa maana hakuna kitu chochote chenye wanasema chenye kinaweza kutumainiwa;
Ndani yao hamuna kitu chochote isipokuwa tu nia mubaya.
10 Lakini Mungu atawatangaza kuwa na hatia;
Mipango yao mibaya itafanya waanguke.+
Wafukuzwe kwa sababu ya makosa yao mengi,
Kwa maana wamekuasi wewe.
11 Lakini wale wote wenye kukukimbilia watashangilia;+
Watapiga vigelegele vya shangwe sikuzote.
Na utaweka kizuizi ili wasifikiwe,
Na wale wenye kupenda jina lako watashangilia katika wewe.
12 Kwa maana utamubariki mutu yeyote mwenye haki, Ee Yehova;
Utawazunguka kwa kuwakubali kama vile kwa ngao kubwa.+
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba vyenye vimepatanishwa na sauti ya Sheminiti.* Muziki wa Daudi.
6 Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,
Na usinirekebishe katika kasirani yako kali.+
2 Unionyeshe wema,* Ee Yehova, kwa maana ninakuwa muzaifu.
Uniponyeshe, Ee Yehova,+ kwa maana mifupa yangu inatetemeka.
6 Nimechoka kwa sababu ya kilio changu cha maumivu;+
Usiku wote ninalowanisha kitanda changu kwa machozi;*
Kiti changu ninakifanya kijae kilio.+
7 Jicho langu limekuwa zaifu kwa sababu ya huzuni yangu,+
Limefifia* kwa sababu ya wale wote wenye kunisumbua.
8 Mutoke mbele yangu, ninyi wote wenye kutenda uovu,
Kwa maana Yehova atasikia sauti ya kilio changu.+
9 Yehova atasikia ombi langu la kuomba rehema;+
Yehova atakubali sala yangu.
10 Maadui wangu wote watapatishwa haya na kufazaishwa;
Watarudia nyuma katika haya ya kushitukia.+
Wimbo wa huzuni* wa Daudi wenye alimuimbia Yehova kuhusu maneno ya Kushi Mubenyamini.
7 Ee Yehova Mungu wangu, nimekukimbilia wewe.+
Uniokoe kutoka kwa wale wote wenye kunitesa na unikomboe.+
2 Kama haufanye vile watanipasua* vipande-vipande kama vile simba anafanya,+
Watanibeba kinguvu pasipo mutu yeyote wa kuniokoa.
3 Ee Yehova Mungu wangu, kama nimekosea katika jambo hili,
Kama nimetenda kwa njia yenye haiko ya haki,
4 Kama nimemukosea mwenye ananitendea wema,+
Ao kama nimenyanganya vitu vya adui yangu bila sababu,*
5 Basi adui anifuatilie na kunifikia;*
Akanyangie uzima wangu chini kwenye udongo
Na kufanya utukufu wangu upotelee katika mavumbi. (Sela)
6 Simama katika hasira yako, Ee Yehova;
Simama upambane na kasirani kali ya maadui wangu,+
Amuka kwa ajili yangu, na uombe kwamba haki itendeke.+
7 Acha mataifa yakuzunguke;
Na utawakamatia hatua kutoka juu.
8 Yehova atahukumu vikundi vya watu.+
Unihukumu, Ee Yehova, kulingana na haki yangu
Na kulingana na uaminifu-mushikamanifu wangu.+
9 Tafazali, maliza matendo maovu ya waovu.
Lakini umufanye imara mwenye haki,+
Kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye haki+ mwenye anachunguza mioyo+ na hisia za ndani kabisa.*+
10 Mungu ni ngao yangu,+ Mwokozi wa wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.+
12 Kama mutu yeyote hatubu,+ Yeye ananoa upanga wake;+
Anakunja upinde wake na kuufanya ukuwe tayari.+
13 Anatayarisha silaha zake zenye kuua;
Anafanya mishale yake yenye kuwaka moto ikuwe tayari.+
14 Angalia ule mwenye kuwa na mimba ya uovu;
Anachukua mimba ya taabu na kuzaa uongo.+
15 Anachimba shimo na kuongeza urefu wake,
Lakini anaanguka katika shimo lilelile lenye alichimba.+
16 Taabu yenye anatokeza itarudia juu ya kichwa chake mwenyewe;+
Jeuri yake itaanguka juu ya sehemu ya juu ya katikati ya kichwa chake.
17 Nitamusifu Yehova kwa sababu ya haki yake;+
Kwa kiongozi; juu ya Gititi.*
Muziki wa Daudi.
8 Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu sana katika dunia yote;
2 Kutoka katika kinywa cha watoto na watoto wenye kunyonya+ umeimarisha nguvu
Kwa sababu ya maadui wako,
Ili kumunyamazisha adui na mulipiza-kisasi.
3 Wakati ninaona mbingu zako, kazi za vidole vyako,
Mwezi na nyota zenye umetayarisha,+
4 Mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umuweke katika akili,
Na mwana wa binadamu ili umuhangaikie?+
5 Ulimufanya kuwa mudogo kidogo kuliko wale wenye kuwa kama Mungu,*
Na ulimuvalisha taji la utukufu na uzuri.
6 Ulimupatia mamlaka juu ya kazi za mikono yako;+
Umeweka kila kitu chini ya miguu yake:
7 Makundi yote na ngombe wote,
Na pia wanyama wa pori,+
8 Ndege wa mbinguni na samaki wa bahari,
Kitu chochote chenye kinapita katika njia za bahari.
9 Ee Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu sana katika dunia yote!
Kwa kiongozi; juu ya Mut-labeni.* Muziki wa Daudi.
א [Aleph]
ב [Beth]
3 Wakati maadui wangu wanakimbia,+
Watajikwaa na kuangamia wasikuwe tena mbele yako.
4 Kwa maana unatetea njia yangu ya haki;
Unakaa kwenye kiti chako cha ufalme ukihukumu kwa haki.+
ג [Gimel]
5 Umekemea mataifa+ na kuharibu waovu,
Na hivyo unafuta jina lao milele na milele.
ה [He]
7 Lakini Yehova amekaa akiwa mufalme milele;+
Amefanya imara kabisa kiti chake cha ufalme kwa ajili ya haki.+
8 Atahukumu kwa haki dunia yenye kuikaliwa na watu;*+
Atafanya maamuzi ya hukumu yenye haki kwa ajili ya mataifa.+
ו [Waw]
9 Yehova atakuwa kimbilio salama* kwa ajili ya wale wenye kukandamizwa,+
Kimbilio salama katika nyakati za taabu.+
10 Wale wenye kujua jina lako watakutegemea wewe;+
Hautaacha hata kidogo wale wenye kukutafuta, Ee Yehova.+
ז [Zayin]
11 Mumuimbie Yehova sifa, mwenye kukaa Sayuni;
Mujulishe matendo yake kati ya vikundi vya watu.+
12 Kwa maana Ule mwenye analipiza kisasi kwa ajili ya damu yao anawakumbuka;+
Hatasahau kilio cha wenye kuteseka.+
ח [Heth]
13 Unionyeshe wema, Ee Yehova; angalia namna wale wenye kunichukia wananitesa,
Wewe mwenye kuniinua kutoka katika milango mikubwa ya kifo,+
14 Ili nitangaze katika milango mikubwa ya binti ya Sayuni+ matendo yako yenye kustahili sifa,
Na kushangilia katika matendo yako ya wokovu.+
ט [Teth]
15 Mataifa yamezama chini katika shimo lenye walichimba;
16 Yehova anajulikana kupitia hukumu zenye anafanya.+
Muovu amenaswa katika kazi za mikono yake mwenyewe.+
Higayoni.* (Sela)
י [Yod]
17 Waovu watarudia nyuma kuelekea Kaburi,*
Mataifa yote yenye kumusahau Mungu.
כ [Kaph]
19 Simama, Ee Yehova! Usiache mwanadamu mwenye anaweza kufa ashinde.
Acha mataifa yahukumiwe mbele yako.+
20 Uwapige kwa woga, Ee Yehova,+
Mataifa yajue kwamba wao ni wanadamu tu wenye wanaweza kufa. (Sela)
ל [Lamed]
10 Ee Yehova, sababu gani unasimama mbali?
Sababu gani unajificha nyakati za taabu?+
2 Muovu anamufuatilia kwa kiburi mutu mwenye hana uwezo,+
Lakini atanaswa katika mipango mibaya yenye anafanya.+
3 Kwa maana muovu anajisifu kuhusu tamaa zake za uchoyo*+
Na anamubariki mwenye pupa;*
נ [Nun]
Anamukosea Yehova heshima.
4 Katika kiburi chake, muovu hafanye uchunguzi wowote;
Mawazo yake yote ni: “Hakuna Mungu.”+
5 Njia zake zinaendelea kufanikiwa,+
Lakini hukumu zako zimepita uelewaji wake;+
Anachekelea* maadui wake wote.
6 Anasema katika moyo wake: “Sitatikiswa* hata kidogo;
Kwa maana kizazi kwa kizazi
Sitaona musiba hata kidogo.”+
פ [Pe]
7 Kinywa chake kimejaa laana, uongo, na mambo ya kuogopesha;+
Chini ya ulimi wake kuko taabu na mambo yenye kuumiza.+
8 Anavizia karibu na makao;
Kutoka mahali kwenye anajificha anaua mutu mwenye hana kosa.+
ע [Ayin]
Macho yake yanatafuta mutu mwenye taabu.+
9 Anangojea mahali kwenye alijificha kama simba katika pango lake.*+
Anangojea ili amukamate mwenye hana uwezo.
Anamukamata mwenye hana uwezo wakati anakokota wavu wake na kuufunga.*+
10 Mutu huyo anapondwa na kuangushwa chini;
Watu wenye taabu wanaanguka katika mikono yake.*
11 Anasema katika moyo wake: “Mungu amesahau.+
Amegeuzia mbali uso wake.
Haone hata kidogo.”+
ק [Qoph]
12 Simama, Ee Yehova.+ Ee Mungu, inua mukono wako.+
Usisahau wenye hawana uwezo.+
13 Sababu gani muovu amemukosea Mungu heshima?
Anasema katika moyo wake: “Hautaniomba nitoe hesabu.”
ר [Resh]
14 Lakini wewe unaona mateso na taabu.
Unaendelea kuangalia na kushugulikia mambo.+
ש [Shin]
16 Yehova ni Mufalme milele na milele.+
Mataifa yameangamia yasikuwe tena katika dunia.+
ת [Taw]
17 Lakini utasikia ombi la wapole, Ee Yehova.+
Utafanya mioyo yao kuwa imara+ na utawakazia sana uangalifu.+
18 Utawatendea haki wenye hawana baba na wale wenye kupondwa,+
Ili mwanadamu wa udongo mwenye anaweza kufa asiwaogopeshe tena.+
Kwa kiongozi. Ya Daudi.
11 Nimemukimbilia Yehova.+
Basi namna gani munaweza kuniambia:*
“Kimbilia kwenye mulima wako kama ndege!
2 Angalia namna waovu wanakunja upinde;
Wanatia mushale wao kwenye kamba ya upinde,
Ili wapige kutoka katika giza wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.
4 Yehova iko* katika hekalu lake takatifu.+
Kiti cha ufalme cha Yehova kiko mbinguni.+
Macho yake mwenyewe yanaangalia, macho yake yenye kuwa na uangalifu* yanachunguza wana wa binadamu.+
6 Atanyeshea waovu mitego;*
Moto na kiberiti+ na upepo wenye kuunguza vitakuwa fungu la kikombe chao.
7 Kwa maana Yehova ni mwenye haki;+ anapenda matendo yenye haki.+
Watu wanyoofu wataona uso wake.*+
Kwa kiongozi; imepatanishwa na sauti ya Sheminiti.* Muziki wa Daudi.
12 Uniokoe, Ee Yehova, kwa maana mutu mushikamanifu haiko tena;
Watu waaminifu hawako tena kati ya wana wa binadamu.
3 Yehova atakata midomo yote yenye kusifu-sifu
Na ulimi wenye kujisifu sana,+
4 Wale wenye kusema: “Tutashinda kupitia ndimi zetu.
Tunatumia midomo yetu namna tunapenda;
Ni nani atakuwa bwana wetu?”+
5 “Kwa sababu wale wenye kuteswa wanakandamizwa,
Kwa sababu ya kilio cha maumivu cha maskini,+
Nitasimama ili kutenda,” ni vile Yehova anasema.
“Nitawaokoa kutoka kwa wale wenye kuwatendea kwa zarau.”*
6 Maneno ya Yehova yako safi;+
Yako kama feza yenye ilisafishwa katika tanuru ya udongo,* yenye ilisafishwa mara saba (7).
7 Utawalinda, Ee Yehova;+
Utamulinda kila mumoja wao milele kutokana na kizazi hiki.
8 Waovu wanatembea huku na huku bila kujizuia
Kwa sababu wana wa binadamu wanaendeleza upotovu.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
13 Ee Yehova, utanisahau mupaka wakati gani? Milele?
Utanificha uso wako mupaka wakati gani?+
2 Nitahangaika* kwa wasiwasi mupaka wakati gani,
Nikiwa na huzuni katika moyo wangu kila siku?
Adui yangu atanishinda mupaka wakati gani?+
3 Uniangalie na unijibu, Ee Yehova Mungu wangu.
Upatie macho yangu mwangaza, ili nisilale usingizi katika kifo,
4 Ili adui yangu asiseme: “Nimemushinda!”
Usiruhusu wapinzani wangu washangilie kuanguka kwangu.+
5 Lakini mimi, ninategemea upendo wako mushikamanifu;+
Moyo wangu utashangilia katika matendo yako ya wokovu.+
6 Nitamuimbia Yehova, kwa maana amenipatia zawabu nyingi.*+
Kwa kiongozi. Ya Daudi.
14 Mupumbavu* anasema katika moyo wake:
“Hakuna Yehova.”+
Matendo yao yamepotoka, na shuguli zao zinachukiza;
Hakuna mwenye kutenda mema.+
2 Lakini Yehova anaangalia wana wa binadamu akiwa mbinguni
Ili aone kama kuko mutu yeyote mwenye kuwa na ufahamu, kama kuko mutu yeyote mwenye kumutafuta Yehova.+
3 Wote wameenda pembeni;+
Wote wamepotoka katika njia ileile.
Hakuna mwenye kutenda mema,
Hakuna hata mumoja.
4 Je, hakuna hata mumoja kati ya wakosaji mwenye anaelewa?
Wanameza watu wangu kama vile wanakula mukate.
Hawamuitie Yehova.
6 Ninyi wakosaji munajaribu kuvuruga mipango ya mutu wa hali ya chini,
Lakini Yehova ni kimbilio lake.+
7 Aa! kama tu wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+
Wakati Yehova atakusanya tena watu wake wenye walikamatwa mateka,
Yakobo ashangilie, Israeli afurahi.
Muziki wa Daudi.
15 Ee Yehova, ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema yako?
Ni nani anaweza kukaa katika mulima wako mutakatifu?+
2 Ule mwenye anatembea bila kosa,*+
Mwenye anazoea kufanya mambo yenye kuwa sawa+
Na kusema kweli katika moyo wake.+
Havunje ahadi yake,* hata wakati inamuletea matatizo.+
Mutu yeyote mwenye kufanya mambo hayo hatatikiswa* hata kidogo.+
Miktamu* ya Daudi.
16 Unilinde, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+
2 Nimemuambia Yehova: “Wewe ni Yehova, Chanzo changu cha wema.
3 Na watakatifu wenye kuwa katika dunia,
Watukufu, ndio wananipendeza sana.”+
4 Wale wenye kufuatilia miungu mingine wanaongeza huzuni zao.+
Sitamwanga hata kidogo matoleo yao ya vinywaji ya damu,
Wala midomo yangu haitataja majina yao.+
5 Yehova ni fungu langu, fungu lenye niligawiwa,+ na kikombe changu.+
Unalinda uriti wangu.
6 Nafasi zenye kupendeza zimepimwa kwa ajili yangu.
Ndiyo, nimetosheka na uriti wangu.+
7 Nitamusifu Yehova, mwenye amenipa shauri.+
Hata wakati wa usiku, mawazo yangu ya ndani kabisa yananirekebisha.*+
8 Ninamuweka Yehova mbele yangu kila wakati.+
Kwa sababu iko* kwenye mukono wangu wa kuume, sitatikiswa* hata kidogo.+
9 Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nafsi yangu yote iko na* shangwe.
Na ninakaa* kwa usalama.
10 Kwa maana hautaniacha* katika Kaburi.*+
Hautaruhusu mushikamanifu wako aone shimo.*+
11 Unanijulisha njia ya uzima.+
Sala ya Daudi.
17 Sikia kilio changu cha kuomba haki, Ee Yehova;
Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada;
Sikiliza sala yangu yenye inasemwa bila udanganyifu.+
2 Na wewe ufanye uamuzi wa haki kwa ajili yangu;+
Macho yako yaone mambo yenye kuwa sawa.
3 Umechunguza moyo wangu, umenichunguza wakati wa usiku;+
Umenisafisha;+
Utavumbua kwamba sijapanga kufanya jambo lolote la mubaya,
Na kinywa changu hakijakosea.
4 Kuhusu shuguli za wanadamu,
Kulingana na neno la midomo yako, ninaepuka njia za munyanganyi.+
5 Hatua zangu zibakie kwenye njia zako
Ili miguu yangu isijikwae.+
6 Ninakuitia wewe, kwa sababu utanijibu,+ Ee Mungu.
Unitegee sikio lako.* Sikia maneno yangu.+
7 Onyesha upendo wako mushikamanifu kwa njia ya ajabu,+
Ee Mwokozi wa wale wenye kutafuta kimbilio kwenye mukono wako wa kuume
Kutoka kwa wale wenye kukuasi.
9 Unilinde kutokana na waovu wenye kunishambulia,
Kutokana na maadui wangu* wenye wanaweza kufa wenye wananizunguka.+
10 Wamekuwa watu wenye hawahisi chochote;*
Kwa kinywa chao wanasema kwa kiburi;
11 Sasa wanatuzunguka;+
Wanatafuta nafasi ya kutuangusha.*
12 Yeye ni kama simba mwenye kuwa tayari kupasua mawindo vipande-vipande,
Kama mwana-simba mwenye kushutama akivizia.
13 Simama, Ee Yehova, upigane naye+ na kumuangusha chini;
Uniokoe* kutoka kwa muovu kwa kutumia upanga wako;
14 Uniokoe kupitia mukono wako, Ee Yehova,
Kutoka kwa watu wa ulimwengu huu,* wenye fungu lao liko katika maisha haya,+
Wale wenye unajaza kwa vitu vya muzuri vyenye unatoa+
Na wenye wanaachia uriti wana wao wengi.
Kwa kiongozi. Wa Daudi mutumishi wa Yehova, mwenye alimuambia Yehova maneno ya wimbo huu siku yenye Yehova alimuokoa katika mukono wa maadui wake wote na katika mukono wa Sauli. Alisema:+
18 Ninakupenda, Ee Yehova, nguvu zangu.+
2 Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu na Ule mwenye ananiokoa.+
Mungu wangu ni mwamba wangu,+ mwenye ninakimbilia,
Ngao yangu na pembe* yangu ya wokovu,* kimbilio langu salama.*+
3 Ninamuitia Yehova, mwenye anastahili kusifiwa,
Na nitaokolewa kutoka kwa maadui wangu.+
4 Kamba za kifo zilinizunguka;+
Mafuriko ya kushitukia ya watu wenye hawana mafaa yoyote yaliniogopesha sana.+
6 Katika taabu yangu nilimuitia Yehova,
Niliendelea kumulilia Mungu wangu anisaidie.
Akiwa katika hekalu lake akasikia sauti yangu,+
Na kilio changu cha kumuomba musaada kikafika katika masikio yake.+
7 Kisha dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika;+
Misingi ya milima ikatetemeka
Na ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
8 Moshi ulipanda kutoka katika matundu ya pua yake,
Na moto wenye kuteketeza ukatoka katika kinywa chake;+
Makaa yenye kuwaka yakatoka kwake.
10 Alipanda juu ya kerubi na akakuja akiruka.+
Akashuka chini haraka juu ya mabawa ya roho.*+
12 Kutoka katika mwangaza wenye kuwa mbele yake
Mvua ya majiwe na makaa yenye moto yakapasua mawingu.
13 Kisha Yehova akaanza kunguruma mbinguni;+
Mwenye Kuwa Juu Zaidi akafanya sauti yake isikike+
Kupitia mvua ya majiwe na makaa yenye moto.
15 Sehemu za chini za mito midogo zikaonekana;*+
Misingi ya inchi ikafunuliwa kwa kemeo lako, Ee Yehova,
Kwa mulipuko wa pumuzi kutoka katika matundu ya pua yako.+
16 Akiwa juu, alininyooshea mukono;
Akanishika na kunikokota kutoka katika maji yenye kuenda chini sana.+
17 Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+
Kutoka kwa wale wenye kunichukia, wenye walikuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.+
18 Walinishambulia katika siku ya musiba wangu,+
Lakini Yehova alikuwa tegemeo langu.
20 Yehova ananipatia zawabu kulingana na haki yangu;+
Ananilipa kulingana na kukosa kuwa na hatia kwa* mikono yangu.+
21 Kwa maana nimeshika njia za Yehova,
Na sijamuacha kwa uovu Mungu wangu.
22 Hukumu zake zote ziko mbele yangu;
Sitazarau sheria zake.
24 Yehova anilipe kulingana na haki yangu,+
Kulingana na kukosa kuwa na hatia kwa mikono yangu mbele yake.+
25 Kwa mutu mushikamanifu unatenda kwa ushikamanifu;+
Kwa mutu mwenye hana lawama unatenda bila lawama;+
26 Kwa mwenye kuwa safi unajionyesha kuwa safi,+
Lakini kwa mwenye kupotoka unajionyesha kuwa mwenye busara.+
28 Kwa maana wewe ndiye unawasha taa yangu, Ee Yehova,
Mungu wangu mwenye anafanya giza langu liangaze.+
29 Kwa musaada wako ninaweza kushambulia kikundi cha wanyanganyi;+
Kwa nguvu za Mungu ninaweza kupanda ukuta.+
Yeye ni ngao kwa wote wenye kumukimbilia.+
31 Kwa maana ni nani iko* Mungu isipokuwa Yehova?+
Na ni nani iko* mwamba isipokuwa Mungu wetu?+
33 Anafanya miguu yangu ikuwe kama ya paa;
Ananifanya nisimame mahali pa juu.+
34 Anazoeza mikono yangu kwa ajili ya vita;
Mikono yangu inaweza kukunja upinde wa shaba.
35 Unanipatia ngao yako ya wokovu,+
Mukono wako wa kuume unanitegemeza,
Na unyenyekevu wako unanifanya nikuwe mukubwa.+
37 Nitafuatilia maadui wangu na kuwafikia;
Sitarudia mupaka wakati watakuwa wamefutwa.
38 Nitawaponda ili wasiweze kusimama;+
Wataanguka chini ya miguu yangu.
39 Utanipatia nguvu kwa ajili ya vita;
Utafanya maadui wangu waanguke chini yangu.+
41 Wanalilia musaada, lakini hakuna mutu wa kuwaokoa;
Hata wanamulilia Yehova, lakini yeye hawajibu.
42 Nitawatwanga ili wakuwe laini kama mavumbi katika upepo;
Nitawatupa inje kama matope katika barabara.
43 Utaniokoa kutokana na tabia ya watu ya kutafuta-tafuta makosa.+
Utaniweka kuwa kichwa cha mataifa.+
Watu wenye sikujua watanitumikia.+
44 Watanitii wakati watasikia habari kidogo tu;
Wageni watakuja wakijikunja kwa woga mbele yangu.+
45 Wageni watakosa uhodari;*
Watakuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
46 Yehova ni mwenye kuishi! Mwamba wangu asifiwe!+
Mungu wa wokovu wangu atukuzwe.+
47 Mungu wa kweli ananilipizia kisasi;+
Anatiisha vikundi vya watu chini yangu.
48 Ananiokoa kutoka kwa maadui wangu wenye kasirani;
Unaniinua juu ya wale wenye kunishambulia;+
Unaniokoa kutokana na mutu mwenye jeuri.
50 Anatenda matendo makubwa ya wokovu kwa ajili ya mufalme wake;*+
Anaonyesha upendo mushikamanifu kwa mutiwa-mafuta wake,+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
2 Siku kwa siku maneno yavyo yanabubujika,
Na usiku kwa usiku vinafunua ujuzi.
3 Hakuna usemi, na hakuna maneno;
Sauti yao haisikike.
4 Lakini sauti yao* imefika katika dunia yote,
Na ujumbe wao mupaka kwenye miisho ya dunia yenye kuikaliwa na watu.*+
Amesimamisha hema mbinguni kwa ajili ya jua;
5 Ni kama bwana-arusi mwenye anatoka katika chumba chake cha arusi;
Linashangilia kama mwanaume mwenye nguvu mwenye anakimbia kwenye njia yake.
6 Linatokea kwenye mwisho mumoja wa mbingu,
Na linazunguka mupaka mwisho mwingine wa mbingu;+
Na hakuna kitu chochote chenye kinafichwa kisipatwe na joto lake.
7 Sheria ya Yehova ni kamilifu,+ inarudisha nguvu.*+
Kikumbusho cha Yehova kinategemeka,+ kinamufanya mwenye hana uzoefu akuwe na hekima.+
8 Maagizo kutoka kwa Yehova ni yenye haki, yanafanya moyo ushangilie;+
Amri ya Yehova ni safi, inafanya macho yangae.+
9 Kumuogopa Yehova+ ni jambo safi, kunadumu milele.
Hukumu za Yehova ni za kweli; zote ni zenye haki.+
10 Ni zenye kutamanika zaidi kuliko zahabu,
Na ziko tamu zaidi kuliko asali,+ asali yenye kuanguka matone-matone kutoka katika sega.
12 Ni nani anaweza kutambua makosa?+
Unitangaze kuwa sina hatia ya zambi zenye sijue.
14 Maneno ya kinywa changu na kufikiri sana* kwa moyo wangu
Vikupendeze wewe,+ Ee Yehova, Mwamba wangu+ na Mukombozi wangu.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
20 Yehova akujibu katika siku ya taabu.
Jina la Mungu wa Yakobo likulinde.+
3 Akumbuke matoleo yako yote ya zawadi;
Akubali kwa wema* toleo lako la kuteketezwa. (Sela)
5 Tutapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya matendo yako ya wokovu;+
Tutainua bendera zetu katika jina la Mungu wetu.+
Yehova atimize maombi yako yote.
6 Sasa ninajua kwamba Yehova anamuokoa mutiwa-mafuta wake.+
7 Watu fulani wanategemea magari na wengine farasi,+
Lakini sisi tunaitia jina la Yehova Mungu wetu.+
8 Wameporomoka na kuanguka,
Lakini sisi tumesimama na kurudishwa wima.+
9 Ee Yehova, okoa mufalme!+
Atatujibu siku yenye tutaomba musaada.+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
21 Ee Yehova, mufalme anashangilia katika nguvu zako;+
Anashangilia sana kabisa katika matendo yako ya wokovu!+
2 Umetimiza tamaa ya moyo wake,+
Na haujamuima ombi la midomo yake. (Sela)
5 Matendo yako ya wokovu yanamuletea utukufu mukubwa.+
Unamupatia heshima na uzuri.
7 Kwa maana mufalme anamutegemea Yehova;+
Kwa sababu ya upendo mushikamanifu wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi, hatatikiswa* hata kidogo.+
8 Mukono wako utapata maadui wako wote;
Mukono wako wa kuume utapata wale wenye kukuchukia.
9 Utawafanya wakuwe kama tanuru yenye moto kwa wakati wenye uliwekwa wa kuwakazia uangalifu.
Yehova atawameza kwa kasirani yake, na moto utawateketeza.+
10 Utaharibu wazao wao* kutoka katika dunia,
Na uzao wao kutoka kati ya wana wa binadamu.
11 Kwa maana walikusudia kukutendea mambo ya mubaya;+
Wamefanya mipango mibaya yenye haitakuwa na matokeo ya muzuri.+
13 Simama, Ee Yehova, katika nguvu zako.
Tutaimbia uwezo wako sifa.*
Kwa kiongozi; imepatanishwa na
“Paa Dike wa Mapambazuko.”*
Muziki wa Daudi.
22 Mungu wangu, Mungu wangu, sababu gani umeniacha?+
Sababu gani uko mbali usiweze kuniokoa,
Mbali na vilio vyangu vya uchungu?+
2 Mungu wangu, ninaendelea kuita wakati wa muchana, na wewe haunijibu;+
Na wakati wa usiku sinyamaze.
8 “Alijitia katika mikono ya Yehova. Acha Yeye amukomboe!
Acha Yeye amuokoe, kwa sababu Yeye anamupenda sana!”+
9 Wewe ndiye ulinitosha katika tumbo la uzazi,+
Ni Wewe ulinifanya nijisikie salama kwenye maziwa ya mama yangu.
10 Nimewekwa chini ya utunzaji wako* tangu kuzaliwa kwangu;
Tangu wakati nilikuwa katika tumbo la uzazi la mama yangu, umekuwa Mungu wangu.
12 Ngombe-dume wengi wadogo wananizunguka;+
Ngombe-dume wenye nguvu wa Bashani wananizunguka kwa ajili ya vita.+
13 Wanafungua vinywa vyao wazi juu yangu,+
Kama simba mwenye kunguruma mwenye anapasua mawindo yake vipande-vipande.+
14 Nimemwangwa kama maji;
Mifupa yangu yote imeteguka.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kipande cha chombo cha udongo;+
Ulimi wangu unashikamana na fizi* zangu;+
Unanishusha chini kwenye mavumbi ya kifo.+
16 Kwa maana imbwa wananizunguka;+
Wananizunguka kwa ajili ya vita kama kikundi cha watenda maovu,+
Kama vile simba, wako kwenye mikono yangu na miguu yangu.+
17 Ninaweza kuhesabu mifupa yangu yote.+
Wananiangalia na kunikazia macho.
19 Lakini wewe, Ee Yehova, usiendelee kukaa mbali.+
Wewe ni nguvu zangu; kuja haraka unisaidie.+
20 Uniokoe* kutokana na upanga,
Uzima wangu wenye samani* kutokana na muguu wa* imbwa;+
21 Uniokoe kutoka katika kinywa cha simba+ na pembe za ngombe-dume wa pori;
Unijibu na uniokoe.
23 Ninyi wenye kumuogopa Yehova, mumusifu!
Ninyi wote uzao wa* Yakobo, mumutukuze!+
Mumuogope sana, ninyi wote uzao wa* Israeli.
Wakati alimulilia amusaidie, alisikia.+
25 Nitakusifu katika kutaniko kubwa;+
Nitatimiza naziri zangu mbele ya wale wenye kumuogopa.
Mufurahie maisha* milele.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumuendea Yehova.
Familia zote za mataifa zitainama mbele yako.+
28 Kwa maana ufalme ni wa Yehova;+
Anatawala juu ya mataifa.
29 Watu wote wenye kufanikiwa* katika dunia watakula na kumuinamia;
Wale wote wenye kushuka katika mavumbi watapiga magoti mbele yake;
Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye anaweza kulinda uzima wao.*
30 Wazao wao watamutumikia;*
Kizazi chenye kitakuja kitaambiwa kuhusu Yehova.
31 Watakuja na kusimulia kuhusu haki yake.
Wataambia watu wenye bado hawajazaliwa mambo yenye amefanya.
Muziki wa Daudi.
23 Yehova ni Muchungaji wangu.+
Sitakosa kitu.+
2 Ananilalisha katika malisho yenye majani mengi;
Ananiongoza kwenye nafasi za kupumuzikia zenye maji mengi.*+
Ananiongoza katika njia za* haki kwa ajili ya jina lake.+
4 Hata kama ninatembea katika bonde lenye kivuli kizito,+
Siogope jambo lolote lenye kuumiza,+
Kwa maana wewe uko pamoja na mimi;+
5 Unanitayarishia meza mbele ya maadui wangu.+
6 Hakika wema na upendo mushikamanifu vitanifuata sikuzote za maisha yangu,+
Na nitakaa katika nyumba ya Yehova siku zangu zote.+
Ya Daudi. Muziki.
24 Dunia na vyote vyenye kuwa ndani yake ni vya Yehova,+
Inchi yenye kuzaa na wale wenye kukaa juu yake.
2 Kwa maana ameiweka imara kabisa juu ya bahari+
Na kuiweka imara kabisa juu ya mito.
3 Ni nani anaweza kupanda mulima wa Yehova,+
Na ni nani anaweza kusimama mahali pake patakatifu?
4 Mutu yeyote mwenye mikono yenye haina kosa na mwenye moyo safi,+
Mwenye hajaapa kiapo cha uongo kwa uzima Wangu,*
Wala kuapa kwa udanganyifu.+
6 Hiki ni kizazi cha wale wenye kumutafuta,
Cha wale wenye kutafuta uso wako, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)
7 Muinue vichwa vyenu, ninyi milango mikubwa;+
Mufunguke,* ninyi miingilio ya zamani,
Ili Mufalme mwenye utukufu aingie!+
8 Mufalme huyu mwenye utukufu ni nani?
9 Muinue vichwa vyenu, ninyi milango mikubwa;+
Mufunguke, ninyi miingilio ya zamani,
Ili Mufalme mwenye utukufu aingie!
10 Yeye ni nani, huyo Mufalme mwenye utukufu?
Yehova wa majeshi—yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.+ (Sela)
Ya Daudi.
א [Aleph]
25 Ninageukia kwako,* Ee Yehova.
ב [Beth]
Usiruhusu maadui wangu washangilie juu ya magumu yangu.+
ג [Gimel]
3 Hakika hakuna mutu yeyote mwenye kukutumainia mwenye atapatishwa haya,+
Lakini haya inangojea wale wenye kutenda kwa udanganyifu bila sababu.+
ד [Daleth]
ה [He]
5 Unitembeze katika kweli yako na unifundishe,+
Kwa maana wewe ni Mungu wangu wa wokovu.
ו [Waw]
Ninakutumainia muchana wote.
ז [Zayin]
ח [Heth]
7 Usikumbuke zambi zenye nilifanya wakati nilikuwa kijana na makosa yangu.
ט [Teth]
8 Yehova ni mwema na munyoofu.+
Ndiyo sababu anafundisha watenda-zambi namna ya kuishi.+
י [Yod]
כ [Kaph]
10 Njia za Yehova ni upendo mushikamanifu na uaminifu
Kwa ajili ya wale wenye kushika agano lake+ na vikumbusho vyake.+
ל [Lamed]
11 Kwa ajili ya jina lako, Ee Yehova,+
Unisamehe kosa langu, hata kama ni kubwa.
מ [Mem]
12 Ni nani mwenye kumuogopa Yehova?+
Atamufundisha kuhusu njia yenye anapaswa kuchagua.+
נ [Nun]
ס [Samekh]
ע [Ayin]
פ [Pe]
16 Unielekezee uso wako na unionyeshe wema,
Kwa maana niko peke yangu na sina uwezo.
צ [Tsade]
17 Taabu za moyo wangu zimeongezeka;+
Unitoshe katika uchungu wangu.
ר [Resh]
19 Angalia namna maadui wangu ni wengi
Na namna wananichukia sana.
ש [Shin]
20 Linda uzima wangu* na uniokoe.+
Usiruhusu nipatishwe haya, kwa maana nimekukimbilia wewe.
ת [Taw]
22 Ee Mungu, okoa* Israeli katika taabu zake zote.
Ya Daudi.
26 Unihukumu, Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika uaminifu-mushikamanifu wangu;+
Nimemutegemea Yehova bila kuyumba-yumba.+
6 Nitanawa mikono yangu katika kukosa kuwa na hatia,
Na nitatembea kuzunguka mazabahu yako, Ee Yehova,
7 Ili nifanye sauti ya kutoa shukrani isikike+
Na ili nitangaze kazi zako zote za ajabu.
9 Usinifagilie mbali* pamoja na watenda-zambi+
Wala kuondoa uzima wangu pamoja na watu wenye jeuri,*
10 Wenye mikono yao inajiingiza katika mwenendo wa haya,
Na wenye mukono wao wa kuume umejaa rushwa.*
11 Lakini mimi, nitatembea katika uaminifu-mushikamanifu wangu.
Uniokoe* na unionyeshe wema.
Ya Daudi.
27 Yehova ni mwangaza wangu+ na wokovu wangu.
Nimuogope nani?+
Yehova ni ngome ya uzima wangu.+
Nimuhofu nani?
2 Wakati waovu walinishambulia ili wameze mwili wangu,+
Wapinzani wangu na maadui wangu ndio walijikwaa na kuanguka.
Hata kama vita inaanza juu yangu,
Bado nitaendelea kuwa hodari.
4 Nimemuomba Yehova jambo moja
—Ni hilo nitatafuta—
Kwamba nikae katika nyumba ya Yehova sikuzote za maisha yangu,+
Ili kuangalia uzuri wa Yehova
5 Kwa maana atanificha katika kibanda chake siku ya musiba;+
Atanificha mahali pa siri katika hema yake;+
Atanitia juu kwenye mwamba.+
6 Sasa kichwa changu kiko juu sana ya maadui wangu wenye kunizunguka;
Nitatoa zabihu katika hema yake kwa makelele ya shangwe;
Nitamuimbia Yehova sifa.*
8 Ukizungumuza kwa ajili yako, moyo wangu umesema:
“Tafuta uso wangu.”
Nitatafuta uso wako, Ee Yehova.+
9 Usinifiche uso wako.+
Usimufukuze mutumishi wako katika kasirani yako.
Wewe ni musaidizi wangu;+
Usinitupe wala usiniache, Mungu wangu wa wokovu.
12 Usinitie katika mukono wa maadui wangu,+
Kwa maana mashahidi wa uongo wameinuka juu yangu,+
Na wananiogopesha kupitia jeuri.
Ndiyo, umutumainie Yehova.
Ya Daudi.
28 Ninaendelea kukuita, Ee Yehova Mwamba wangu;+
Usikuwe kama kiziwi kwangu.
2 Sikia vilio vyangu wakati ninakulilia unisaidie
Wakati ninainua mikono yangu kuelekea chumba cha ndani zaidi cha patakatifu pako.+
3 Usinikokote pamoja na waovu, pamoja na wale wenye kuzoea kutenda mambo yenye kuumiza,+
Wale wenye kuongea na mwanadamu mwenzao maneno ya amani wakati uovu uko katika mioyo yao.+
4 Uwalipe kulingana na matendo yao,+
Kulingana na mazoea yao maovu.
Uwalipe kulingana na kazi ya mikono yao,
Kulingana na mambo yenye wametenda.+
Atawabomoa na hatawajenga.
6 Yehova asifiwe,
Kwa maana amesikia vilio vyangu vya kuomba musaada.
Nimepokea musaada wake, na moyo wangu unashangilia,
Kwa hiyo nitamusifu kwa wimbo wangu.
8 Yehova ni nguvu kwa watu wake;
Yeye ni ngome, anamuletea mutiwa-mafuta wake wokovu mukubwa.+
9 Uokoe watu wako, na ubariki uriti wako.+
Uwachunge na uwabebe katika mikono yako milele.+
Muziki wa Daudi.
29 Mumupatie Yehova kile chenye anastahili, ninyi wana wa watu wenye nguvu,
Mumupatie Yehova kile chenye anastahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
2 Mumupatie Yehova utukufu wenye jina lake linastahili.
Mumuinamie* Yehova katika mapambo matakatifu.*
3 Sauti ya Yehova inasikika juu ya maji;
Mungu mwenye utukufu ananguruma.+
Yehova iko* juu ya maji mengi.+
4 Sauti ya Yehova iko na nguvu;+
Sauti ya Yehova ni yenye kupendeza sana.
5 Sauti ya Yehova inavunja mierezi;
Ndiyo, Yehova anapasua-pasua mierezi ya Lebanoni.+
6 Anafanya Lebanoni* iruke-ruke kama kitoto-dume cha ngombe,
Na Sirioni+ kama ngombe-dume mudogo wa pori.
7 Sauti ya Yehova inapiga kwa miali ya moto;+
8 Sauti ya Yehova inafanya jangwa litetemeke;+
Yehova anafanya jangwa la Kadeshi+ litetemeke.
9 Sauti ya Yehova inafanya paa atetemeke na kuzaa
Na inafanya mapori yakuwe wazi kabisa.+
Na wote wenye kuwa katika hekalu lake wanasema: “Utukufu!”
11 Yehova atapatia watu wake nguvu.+
Yehova atabariki watu wake kwa amani.+
Muziki. Wimbo wa kuzindua nyumba. Wa Daudi.
30 Nitakutukuza, Ee Yehova, kwa maana umeniinua* juu;
Haukuruhusu maadui wangu washangilie juu yangu.+
2 Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, na wewe ukaniponyesha.+
3 Ee Yehova, umeniinua* kutoka katika Kaburi.*+
Ulilinda uzima wangu; uliniokoa nisizame katika shimo.*+
4 Mumuimbie Yehova sifa,* ninyi washikamanifu wake,+
Mushukuru jina lake takatifu;*+
5 Kwa sababu kuwa chini ya kasirani yake ni kwa wakati mufupi tu,+
Kilio kinaweza kutokea mangaribi, lakini asubui, vigelegele vya shangwe.+
6 Wakati nilikuwa na amani, nilisema:
“Sitatikiswa* hata kidogo.”
7 Ee Yehova, wakati nilikuwa katika wema wako,* ulinifanya imara kama mulima.+
Lakini wakati ulificha uso wako, niliogopa sana.+
8 Niliendelea kukuita, Ee Yehova;+
Na niliendelea kumulilia Yehova ili anionyeshe wema.
9 Kuko faida gani kama ninakufa,* kama ninashuka katika shimo?*+
Je, mavumbi yatakusifu?+ Je, yataongea kuhusu uaminifu wako?+
10 Sikia, Ee Yehova, na unionyeshe wema.+
Ee Yehova, ukuwe musaidizi wangu.+
11 Umegeuza maombolezo yangu kuwa dansi;
Umenitosha nguo yangu ya gunia, na unanivalisha shangwe,
12 Ili niimbe* sifa yako na nisinyamaze.
Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu milele.
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
31 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.+
Nisipatishwe haya hata kidogo.+
Uniokoe kwa sababu ya haki yako.+
2 Unitegee sikio lako.*
Kuja haraka uniokoe.+
Ukuwe kwangu mulima wenye ni ngome,
Mahali kwenye ngome ili kuniokoa.+
3 Kwa maana wewe ni mwamba wangu na ngome yangu;+
5 Ninaweka roho yangu katika mukono wako.+
Umenikomboa, Ee Yehova, Mungu wa ukweli.*+
6 Ninachukia wale wenye kushikamana na sanamu zenye hazina mafaa yoyote, za bure-bure,
Lakini mimi, ninamutegemea Yehova.
7 Nitashangilia sana katika upendo wako mushikamanifu,
Kwa maana umeona mateso yangu;+
Unajua taabu yangu nyingi.*
8 Haukunitia katika mukono wa adui,
Lakini unanifanya nisimame mahali salama.*
9 Unionyeshe wema, Ee Yehova, kwa maana niko katika taabu.
Uchungu umefanya macho yangu yakuwe zaifu,+ na pia mwili wangu wote.*+
Nguvu zangu zinapunguka kwa sababu ya zambi yangu;
Mifupa yangu inakuwa zaifu.+
11 Ninazarauliwa na maadui wangu wote,+
Zaidi sana majirani wangu.
Na wenye kunijua wananiogopa;
Wakati wananiona mahali kwenye watu, wananikimbia.+
12 Nimeondolewa katika moyo wao* na nimesahauliwa, kama vile nimekufa;
Niko kama mutungi wenye kuvunjika.
13 Nimesikia habari nyingi za uovu zenye haziko hakika;
Woga mukubwa unanizunguka.+
Wakati wanakusanyika pamoja kama mutu mumoja ili kunishambulia,
14 Lakini ninakutegemea wewe, Ee Yehova.+
Ninatangaza: “Wewe ni Mungu wangu.”+
15 Siku* zangu ziko katika mukono wako.
Uniokoe katika mukono wa maadui wangu na kutoka kwa wale wenye kunitesa.+
16 Fanya uso wako umuangazie mutumishi wako.+
Uniokoe kupitia upendo wako mushikamanifu.
17 Ee Yehova, nisipatishwe haya wakati ninakuitia.+
18 Acha midomo yenye kusema uongo ikuwe bubu,+
Midomo yenye kuongea kwa kiburi juu ya mwenye haki, kwa majivuno na zarau.
Umeuweka kwa ajili ya wale wenye kukuogopa,+
Na umeuonyesha mbele ya wanadamu wote, kwa ajili ya wale wenye kukukimbilia wewe.+
20 Utawaficha mahali pa siri mbele yako+
Mbali na mipango mibaya ya wanadamu;
Utawaficha katika kibanda chako
21 Yehova asifiwe,
Kwa maana kwa njia ya ajabu, amenionyesha upendo wake mushikamanifu+ katika muji wenye kuzungukwa kwa ajili ya vita.+
22 Lakini mimi niliogopa sana na nikasema:
“Nitaangamia nisikuwe mbele yako.”+
Lakini ulisikia vilio vyangu vya kuomba musaada wakati nilikulilia kwa sauti kubwa.+
23 Mumupende Yehova, ninyi wote wenye kuwa washikamanifu kwake!+
Ya Daudi. Maskili.*
32 Mwenye furaha ni mutu mwenye amesamehewa kosa lake, mwenye zambi yake imefunikwa.*+
2 Mwenye furaha ni mutu mwenye Yehova hamuhesabie kuwa na hatia,+
Mwenye katika roho yake hamuna udanganyifu.
3 Wakati nilinyamaza, mifupa yangu ilikuwa zaifu kwa sababu ya kulia kwa maumivu muchana wote.+
4 Kwa maana usiku na muchana mukono wako ulikuwa* muzito juu yangu.+
Nguvu zangu zilikauka* kama maji katika joto yenye kukauka ya kipindi cha joto. (Sela)
Nilisema: “Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.”+
Na ulisamehe kosa la zambi zangu.+ (Sela)
Halafu hata maji ya garika hayatamufikia.
7 Wewe ni mahali pangu pa kujificha;
Utanilinda nisipatwe na taabu.+
Utanizunguka kwa vigelegele vya shangwe ya ukombozi.+ (Sela)
8 “Nitakupatia ufahamu na kukufundisha katika njia yenye unapaswa kufuata.+
Nitakupatia shauri jicho langu likikuangalia.+
9 Usikuwe kama farasi ao nyumbu, mwenye hana uelewaji,+
Mwenye musisimuko wake unapaswa kuzuiwa kupitia lijamu* ao kupitia hatamu*
Mbele akukaribie.”
10 Maumivu ya muovu ni mengi;
Lakini mwenye kumutegemea Yehova amezungukwa na upendo Wake mushikamanifu.+
11 Mushangilie katika Yehova na kufurahi, ninyi wenye haki;
Mupige vigelegele vya shangwe, ninyi wote wenye kuwa wanyoofu katika moyo.
33 Mupige vigelegele vya shangwe, kwa sababu ya Yehova, ninyi wenye haki.+
Ni jambo lenye kufaa kwa wanyoofu kumusifu yeye.
2 Mumushukuru Yehova kwa kinubi;
Mumuimbie sifa* kwa chombo cha kamba kumi (10).
3 Mumuimbie wimbo mupya;+
Mupige kamba kwa ufundi, pamoja na vigelegele vya shangwe.
4 Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+
Na kila jambo lenye anafanya linategemeka.
5 Anapenda uadilifu* na haki.+
Dunia imejaa upendo mushikamanifu wa Yehova.+
6 Kwa neno la Yehova mbingu zilifanywa,+
Na kwa roho* ya kinywa chake kila kitu chenye kuwa katika mbingu kilifanywa.*
7 Anakusanya maji ya bahari kama vile ukuta wa maji;+
Anatia maji yenye mawimbi makubwa katika madepo.
8 Dunia yote imuogope Yehova.+
Wakaaji wa inchi yenye kuzaa wamuogope sana.
13 Yehova anaangalia chini akiwa mbinguni;
Anaona wana wote wa binadamu.+
14 Akiwa katika makao yake,
Anakazia macho wakaaji wa dunia.
15 Yeye ndiye anaumba mioyo ya wote;
Anachunguza kazi zao zote.+
16 Hakuna mufalme mwenye anaokolewa kupitia jeshi kubwa;+
Mutu mwenye nguvu haokolewe kupitia nguvu zake nyingi.+
18 Angalia! Jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa,+
Wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu,
Na kulinda uzima wao wakati wa njaa.+
20 Tunamungojea* Yehova.
Yeye ni musaidizi wetu na ngao yetu.+
21 Mioyo yetu inashangilia katika yeye,
Kwa maana tunategemea jina lake takatifu.+
א [Aleph]
34 Nitamusifu Yehova nyakati zote;
Sifa yake itakuwa kwenye midomo yangu kila wakati.
ב [Beth]
ג [Gimel]
ד [Daleth]
4 Nilimuuliza Yehova, na akanijibu.+
Aliniokoa katika mambo yote yenye kuniogopesha.+
ה [He]
5 Wale wenye walimuangalia walingaa;
Nyuso zao hazingeweza kupatishwa haya.
ז [Zayin]
6 Mutu huyu wa hali ya chini aliita, na Yehova akasikia.
Alimuokoa katika taabu zake zote.+
ח [Heth]
ט [Teth]
י [Yod]
כ [Kaph]
10 Hata wana-simba wenye nguvu* wamelemewa na njaa,
Lakini wale wenye kumutafuta Yehova hawatakosa kitu kizuri.+
ל [Lamed]
מ [Mem]
נ [Nun]
ס [Samekh]
ע [Ayin]
15 Macho ya Yehova yako juu ya wenye haki,+
Na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba musaada.+
פ [Pe]
16 Lakini uso wa Yehova unapinga wale wenye kutenda mambo ya mubaya,
Ili afute kumbukumbu lao lote katika dunia.+
צ [Tsade]
ק [Qoph]
ר [Resh]
ש [Shin]
ת [Taw]
21 Musiba utamuua muovu;
Wale wenye kumuchukia mwenye haki watapatikana na hatia.
22 Yehova anakomboa uzima wa* watumishi wake;
Hakuna mutu yeyote kati ya wenye kumukimbilia mwenye atapatikana na hatia.+
Ya Daudi.
35 Ee Yehova, utetee kesi yangu ya hukumu mbele ya wapinzani wangu;+
Pigana na wale wenye kupigana na mimi.+
3 Inua mukuki wako na shoka lako la vita* juu ya wale wenye kunifuatilia.+
Uniambie:* “Mimi ni wokovu wako.”+
4 Acha wale wenye kuwinda uzima wangu* wapatishwe haya na kufezeheshwa.+
Acha wale wenye kufanya mupango wa kuniharibu wakimbie kwa sababu ya haya.
5 Acha wakuwe kama maganda ya mbegu katika upepo;
Acha malaika wa Yehova awafukuze.+
6 Acha njia yao ikuwe giza na uterezi
Wakati malaika wa Yehova anawafuatilia.
8 Acha musiba umufikie bila kutazamia;
Acha wavu wenye alificha umunase;*
Acha aanguke ndani yake na kuharibiwa.+
9 Lakini mimi nitashangilia* katika Yehova;
Nitakuwa na shangwe kwa sababu ya matendo yake ya wokovu.
10 Mifupa yangu yote itasema:
“Ee Yehova, ni nani mwenye kuwa kama wewe?
Unaokoa wenye hawana uwezo kutoka kwa wale wenye nguvu zaidi,+
Wenye hawana uwezo na maskini kutoka kwa wale wenye kuwanyanganya.”+
13 Lakini wakati walikuwa wagonjwa, nilivaa nguo za magunia;
Nilijitesa* kwa kufunga,
Na wakati sala yangu ilikuwa inarudia bila kujibiwa,*
14 Nilitembea huku na huku nikiomboleza kama vile ninamuombolezea rafiki ao ndugu yangu;
Niliinama kwa sababu ya huzuni, kama mutu mwenye kumuombolezea mama yake.
15 Lakini wakati nilijikwaa, walishangilia na kukusanyika pamoja;
Walikusanyika pamoja ili wanivizie na wanipige na kuniua;
Walinipasua vipande-vipande na hawakunyamaza.
17 Ee Yehova, utaangalia tu mupaka wakati gani?+
18 Kisha nitakushukuru katika kutaniko kubwa;+
Nitakusifu katika vikundi vya watu.
19 Usiruhusu wale wenye kuwa maadui wangu bila sababu washangilie juu ya magumu yangu;
Usiruhusu wale wenye kunichukia bila sababu+ wafinye macho yao kwa nia mubaya.+
20 Kwa maana hawaseme maneno ya amani,
Lakini wanafanya mupango kwa udanganyifu juu ya watu wenye amani wa inchi.+
21 Wanafungua kinywa chao wazi ili kunishitaki,
Wakisema: “Aha! Aha! Macho yetu yameona hilo.”
22 Ee Yehova, umeona jambo hilo. Usinyamaze.+
Ee Yehova, usikae mbali na mimi.+
23 Amuka, simama ili unitetee,
Mungu wangu, Yehova, unitetee katika kesi yangu ya hukumu.
24 Unihukumu kulingana na haki yako,+ Ee Yehova Mungu wangu;
Usiruhusu washangilie juu ya magumu yangu.
25 Wasiseme hata kidogo katika moyo wao: “Aha! Tulipata kile tulitaka!”*
Wasiseme hata kidogo: “Tumemumeza.”+
26 Acha wote wapatishwe haya na kufezeheshwa,
Wale wenye kushangilia juu ya musiba wangu.
Acha wale wenye kujiinua juu yangu wavalishwe haya na aibu.
27 Lakini acha wale wenye kufurahia haki yangu wapige vigelegele vya shangwe;
Acha waseme kila wakati:
“Yehova atukuzwe, mwenye anafurahia amani ya mutumishi wake.”+
Kwa kiongozi. Ya Daudi,
mutumishi wa Yehova.
36 Kosa linazungumuza na muovu ndani kabisa ya moyo wake;
Hakuna kumuogopa Mungu mbele ya macho yake.+
2 Kwa maana anajisifu-sifu sana mbele ya macho yake mwenyewe
Ili asiweze kutambua kosa lake na kulichukia.+
3 Maneno ya kinywa chake yanaumiza na ni ya udanganyifu;
Haonyeshe ufahamu wowote wa kutenda mambo ya muzuri.
4 Anafanya mipango yenye kuumiza hata katika kitanda chake.
Anafuata njia yenye haiko ya muzuri;
Hakatae mambo ya mubaya.
5 Ee Yehova, upendo wako mushikamanifu unafika mupaka mbinguni,+
Uaminifu wako mupaka kwenye mawingu.
Unalinda* mwanadamu na munyama, Ee Yehova.+
7 Upendo wako mushikamanifu ni wenye samani sana, Ee Mungu!+
Katika kivuli cha mabawa yako,
wana wa binadamu wanakimbilia.+
8 Wanakunywa na kushiba vitu vyenye kunona vya* nyumba yako,+
Na unawanywesha kwenye muto wa vitu vyako vyenye kufurahisha.+
10 Endelea kuonyesha upendo wako mushikamanifu kwa wale wenye kukujua,+
Na haki yako, kwa wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.+
11 Usiruhusu muguu wa mwenye majivuno unikanyange
Wala mukono wa muovu unifukuze.
12 Wakosaji wameanguka kule;
Wamepigwa na kuangushwa chini na hawawezi kusimama.+
Ya Daudi.
א [Aleph]
ב [Beth]
ג [Gimel]
6 Atafanya haki yako ingae kama mwangaza wa asubui sana,
Na haki yako kama jua la katikati ya muchana.
ד [Daleth]
Usikasirishwe na mutu
Mwenye anafanikiwa katika kutimiza mipango yake ya mubaya.+
ה [He]
ו [Waw]
10 Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena;+
Utaangalia mahali walikuwa,
Nao hawatakuwa pale.+
ז [Zayin]
12 Mutu muovu anapanga mupango mubaya juu ya mwenye haki;+
Anamusagia meno yake.
13 Lakini Yehova atamucheka,
Kwa maana Anajua kwamba siku yake itakuja.+
ח [Heth]
14 Waovu wanachomoa panga zao na kukunja* pinde zao
Ili kumuangusha chini mwenye kukandamizwa na maskini,
Ili kuchinja wale wenye njia yao imenyooka.
15 Lakini upanga wao utatoboa moyo wao wenyewe;+
Pinde zao zitavunjwa.
ט [Teth]
17 Kwa maana mikono ya waovu itavunjwa,
Lakini Yehova atategemeza wenye haki.
י [Yod]
18 Yehova anajua mambo yenye watu wenye hawana lawama wanapambana nayo,*
Na uriti wao utadumu milele.+
19 Hawatapatishwa haya wakati wa musiba;
Wakati wa njaa watakuwa na chakula kingi.
כ [Kaph]
20 Lakini waovu wataangamia;+
Maadui wa Yehova wataisha kama vile malisho yenye utukufu;
Wataisha kama moshi.
ל [Lamed]
22 Wale wenye kubarikiwa Naye watariti dunia,
Lakini wale wenye kulaaniwa Naye wataharibiwa.+
מ [Mem]
נ [Nun]
26 Sikuzote anakopesha bila kuomba faida,+
Na watoto wake watapata baraka.
ס [Samekh]
27 Geuka na uache mambo ya mubaya na utende mambo ya muzuri,+
Na utaishi milele.
ע [Ayin]
פ [Pe]
צ [Tsade]
32 Muovu anamuangalia mwenye haki,
Akitafuta kumuua.
33 Lakini Yehova hatamuacha katika mukono wa mutu huyo+
Wala hatamupata na hatia wakati atahukumiwa.+
ק [Qoph]
34 Tumainia Yehova na ufuate njia yake,
Naye atakuinua ili uriti dunia.
Wakati waovu wataharibiwa,+ utaona jambo hilo.+
ר [Resh]
35 Nimemuona mutu mwenye hana huruma, muovu
Akienea kama muti wenye majani mengi katika udongo wake wa asili.+
36 Lakini alikufa kwa kushitukia na hakukuwa tena;+
Niliendelea kumutafuta, na hangeweza kupatikana.+
ש [Shin]
37 Angalia mutu mwenye hana lawama,*
Na uendelee kumuangalia munyoofu,+
Kwa maana wakati wenye kuja wa mutu huyo utakuwa wenye amani.+
38 Lakini wakosaji wote wataharibiwa;
Wakati wenye kuja wa watu waovu utakomeshwa.+
ת [Taw]
40 Yehova atawasaidia na kuwaokoa.+
Atawaokoa kutoka kwa waovu na kuwakomboa,
Kwa sababu wanamukimbilia yeye.+
Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.
38 Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,
Wala usinirekebishe katika kasirani yako kali.+
2 Kwa maana mishale yako imenitoboa ndani kabisa,
Na mukono wako unanifinyia chini.+
3 Mwili wangu wote ni mugonjwa* kwa sababu ya kasirani yako kali.
Hakuna amani ndani ya mifupa yangu kwa sababu ya zambi yangu.+
4 Kwa maana makosa yangu yamekuwa mengi sana juu ya kichwa changu;+
Kama muzigo muzito, ni mengi sana siwezi kuyabeba.
5 Vidonda vyangu vinanuka na viko na usaha
Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6 Nimesumbuka na kushuka moyo sana;
Ninatembea huku na huku muchana wote nikiwa na huzuni.
8 Sihisi tena chochote na nimepondwa kabisa;
Moyo wangu wenye uchungu mwingi unanifanya nilie kwa maumivu kwa sauti kubwa.*
9 Ee Yehova, tamaa zangu zote ziko mbele yako,
Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa mbele yako.
10 Moyo wangu unapiga-piga, nguvu zangu zimeisha,
Na mwangaza wa macho yangu umeisha.+
11 Marafiki wangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,
Na marafiki wangu wa karibu wanasimama mbali.
12 Wale wenye kutafuta uzima wangu* wanatega mitego;
Wale wenye kujaribu kunifanya mubaya wanazungumuza kuhusu kuniharibu;+
Wanasema udanganyifu kwa sauti ya chini muchana wote.
14 Nimekuwa kama mutu mwenye hawezi kusikia,
Mwenye kinywa chake hakina jambo lolote la kusema ili kujitetea.
16 Kwa maana nilisema: “Acha wasishangilie juu ya magumu yangu
Wala kujiinua juu yangu kama muguu wangu unatereza.”
17 Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,
Na maumivu yangu yalikuwa pamoja na mimi sikuzote.+
19 Lakini maadui wangu wako na nguvu* na wako na uwezo,*
Wale wenye kunichukia bila sababu wamekuwa wengi sana.
20 Walinilipa ubaya kwa wema;
Walikuwa wananipinga kwa sababu ya kufuatilia mambo mema.
21 Usiniache, Ee Yehova.
Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali na mimi.+
22 Fanya haraka ili unisaidie,
Ee Yehova, wokovu wangu.+
Kwa kiongozi; wa Yedutuni.*+ Muziki wa Daudi.
Nitalinda kinywa changu kwa kitu cha kufunga kinywa+
Wakati wote wenye mutu yeyote muovu iko* mbele yangu.”
2 Nilikuwa bubu na nilikuwa kimya;+
Niliendelea kunyamaza hata kuhusu mambo ya muzuri,
Lakini maumivu yangu yalikuwa makali.*
3 Moyo wangu uliteketea polepole* ndani yangu.
Wakati nilikuwa ninafikiri sana,* moto huo uliendelea kuwaka.
Kisha ulimi wangu ukasema:
4 “Ee Yehova, unisaidie kujua namna mwisho wangu utakuwa,
Na kipimo cha siku zangu,+
Ili nijue ufupi wa maisha yangu.*
5 Kwa kweli, umefanya siku zangu zikuwe kidogo tu;*+
Na urefu wa maisha yangu hauko kitu mbele yako.+
Hakika kila mwanadamu, hata kama anaonekana kuwa salama, haiko kitu lakini pumuzi tu.+ (Sela)
6 Hakika kila mwanadamu anatembea huku na huku kama kivuli.
Anakimbia huku na huku* bila sababu.
Anarundika mali, bila kujua ni nani ataifurahia.+
7 Basi, ninaweza kutumainia nini, Ee Yehova?
Wewe ndiye tumaini langu pekee.
8 Uniokoe katika makosa yangu yote.+
Usiruhusu mupumbavu anifanye kuwa kitu cha kuzarauliwa.
10 Uniondolee pigo lako.
Nimekuwa muzaifu kabisa kwa sababu mukono wako unanipiga.
11 Unamurekebisha mwanadamu kwa kumupatia azabu kwa sababu ya kosa lake;+
Unaharibu kabisa vitu vyenye anapenda sana kama vile nondo* anaharibu.
Hakika kila mwanadamu ni pumuzi tu.+ (Sela)
12 Sikia sala yangu, Ee Yehova,
Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada.+
Usijifanye kuwa hauone machozi yangu.
Kwa maana mimi niko mukaaji mugeni tu mbele yako,+
13 Ondoa macho yako ya ukali juu yangu ili nichangamuke
Mbele nikufe na kupotea.”
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
40 Nilimutumainia Yehova kwa bidii,*
Naye akanitegea sikio lake* na kusikia kilio changu cha kuomba musaada.+
2 Akanipandisha kutoka katika shimo lenye kunguruma,
Kutoka katika matope yenye uterezi.
Akatia miguu yangu juu ya mwamba;
Akanifanya nisimame mahali kwenye kuko salama.
3 Kisha akatia wimbo mupya katika kinywa changu,+
Mungu wetu asifiwe.
Wengi wataangalia na kuogopa sana
Na kuweka tegemeo lao katika Yehova.
4 Mwenye furaha ni mutu mwenye anamutegemea Yehova
Na mwenye hatumainie watu wenye wako kichwa-nguvu ao watu wadanganyifu.*
5 Mambo yenye umefanya ni mengi sana,
Ee Yehova Mungu wangu,
Kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea.+
Hakuna mwenye anaweza kulinganishwa na wewe;+
Kama ningejaribu kueleza na kuongea kuzihusu,
Zingekuwa nyingi sana kwangu kusimulia!+
Haukuomba matoleo ya kuteketezwa na matoleo ya zambi.+
7 Kisha nikasema: “Angalia, nimekuja.
Katika kitabu cha kukunjwa* imeandikwa juu yangu.+
9 Ninatangaza habari njema ya haki katika kutaniko kubwa.+
Angalia! Sizuie midomo yangu,+
Ee Yehova, kama vile unajua muzuri.
10 Sifunike haki yako katika moyo wangu.
Ninatangaza uaminifu wako na wokovu wako.
Sifiche upendo wako mushikamanifu na kweli yako katika kutaniko kubwa.”+
11 Ee Yehova, usiniime rehema yako.
Upendo wako mushikamanifu na kweli yako vinilinde kila wakati.+
12 Misiba yenye kunizunguka ni mingi sana haiwezi kuhesabika.+
Makosa yangu mengi yananilemea kiasi ya kwamba siwezi kuona njia yangu;+
Ni mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,
Na nimevunjika moyo.
13 Tafazali, Ee Yehova, ukuwe tayari kuniokoa.+
Ee Yehova, fanya haraka ili unisaidie.+
14 Acha wale wote wenye kutafuta kuondoa uzima wangu*
Wapatishwe haya na kufezeheshwa.
Acha wale wenye kufurahia musiba wangu
Wakimbie kwa sababu ya aibu.
15 Acha wale wenye kuniambia: “Aha! Aha!”
Washituke kwa sababu ya haya yao wenyewe.
Acha wale wenye kupenda matendo yako ya wokovu waseme sikuzote:
“Yehova atukuzwe.”+
17 Lakini mimi sina uwezo, na niko maskini;
Yehova anikazie uangalifu.
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
41 Mwenye furaha ni mutu yeyote mwenye anamuhangaikia mutu wa hali ya chini;+
Yehova atamuokoa katika siku ya musiba.
2 Yehova atamuchunga na kulinda uzima wake.
Atatangazwa kuwa mwenye furaha katika dunia;+
Hautamutia hata kidogo katika mukono wa maadui wake ili wamutendee vile wanapenda.*+
3 Yehova atamutegemeza kwenye kitanda chake cha ugonjwa;+
Wakati wa ugonjwa wake utabadilisha kabisa kitanda chake.
4 Kwa maana nilisema: “Ee Yehova, unionyeshe wema.+
Uniponyeshe,*+ kwa maana nimekutendea zambi.”+
5 Lakini maadui wangu wanasema mambo maovu kunihusu:
“Atakufa wakati gani na jina lake lipotee?”
6 Kama mumoja wao anakuja kuniona, moyo wake unasema uongo.
Anakusanya jambo lenye kuumiza la kusema;
Kisha anatoka inje na kulieneza kila mahali.
7 Wale wote wenye kunichukia wanaambiana kwa sauti ya chini-chini;
Wanapanga kunifanyia jambo fulani la mubaya:
9 Hata mutu mwenye nilikuwa ninaishi naye kwa amani, mwenye nilitumainia,+
Mwenye alikuwa anakula mukate wangu, ameinua kisigino chake ili kuniumiza.*+
10 Lakini wewe, Ee Yehova, unionyeshe wema na uniinue,
Ili niwalipe.
11 Kwa njia hii nitajua kwamba unapendezwa na mimi:
Wakati adui yangu hataweza kupiga vigelegele vya ushindi juu yangu.+
12 Lakini mimi, unanitegemeza kwa sababu ya uaminifu-mushikamanifu wangu;+
Utaniweka mbele yako milele.+
Amina na Amina.
KITABU CHA PILI
(Zaburi 42-72)
2 Niko na kiu kwa ajili ya Mungu, kwa ajili ya Mungu mwenye kuishi.+
Nikuje wakati gani na kuonekana mbele ya Mungu?+
3 Machozi yangu ni chakula changu muchana na usiku;
4 Ninakumbuka mambo haya, na ninamwanga nafsi* yangu,
Kwa maana wakati fulani nilitembea pamoja na kikundi cha watu;
Nilizoea kutembea kwa huzuni* mbele yao mupaka kwenye nyumba ya Mungu,
Kwa sauti za shangwe na shukrani,
Za watu wengi wenye kufanya sikukuu.+
5 Sababu gani nimepoteza tumaini?*+
Sababu gani musukosuko huu uko ndani yangu?
6 Mungu wangu, nimepoteza* tumaini.+
Ndiyo sababu ninakukumbuka,+
Kutoka katika inchi ya Yordani na vichwa vya Hermoni,
Kutoka kwenye Mulima Mizari.*
7 Maji yenye kuenda chini sana yanaita maji yenye kuenda chini sana
Kwa sauti ya maporomoko yako ya maji.
Mawimbi yako yote makubwa yamenilemea.+
8 Wakati wa muchana Yehova atanipatia upendo wake mushikamanifu,
Na usiku wimbo wake utakuwa pamoja na mimi—sala kwa Mungu wa uzima wangu.+
9 Nitamuambia Mungu, mwamba wangu:
“Sababu gani umenisahau?+
Sababu gani nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?”+
10 Maadui wangu wananichokoza kwa chuki kali sana;*
11 Sababu gani nimepoteza* tumaini?
Sababu gani musukosuko huu uko ndani yangu?
Uniokoe kutoka kwa mutu wa udanganyifu na ukosefu wa haki.
2 Kwa maana wewe ni Mungu wangu, ngome yangu.+
Sababu gani umenitupa?
Sababu gani nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?+
3 Tuma mwangaza wako na kweli yako.+
4 Kisha nitakuja kwenye mazabahu ya Mungu,+
Kwa Mungu, shangwe yangu nyingi sana.
Na nitakusifu kwa kinubi,+ Ee Mungu, Mungu wangu.
5 Sababu gani nimepoteza* tumaini?
Sababu gani musukosuko huu uko ndani yangu?
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Maskili.*
44 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu wenyewe,
Mababu zetu wametuelezea,+
Mambo yenye ulitimiza katika siku zao,
Siku za zamani sana.
Uliponda-ponda mataifa na kuyafukuza.+
Lakini, ilikuwa kwa mukono wako wa kuume na mukono wako+ na mwangaza wa uso wako,
Kwa maana ulipendezwa nao.+
5 Kwa nguvu zako tutafukuza maadui wetu;+
Katika jina lako tutawakanyangia chini wale wenye kusimama juu yetu.+
6 Kwa maana sitegemee upinde wangu,
Na upanga wangu hauwezi kuniokoa.+
7 Wewe ndiye ulituokoa kutoka kwa maadui wetu,+
Wewe ndiye ulipatisha haya wale wenye kutuchukia.
8 Tutamusifu Mungu muchana wote,
Na tutashukuru jina lako milele. (Sela)
9 Lakini sasa umetutupa na kutupatisha haya,
Na hauende pamoja na majeshi yetu.
10 Unaendelea kutufanya tumukimbie adui yetu;+
Wale wenye kutuchukia wanakamata kitu chochote chenye wanataka.
11 Unatutoa ili tumezwe kama kondoo;
Umetusambaza kati ya mataifa.+
13 Unatufanya kuwa kitu cha haya kwa majirani wetu,
Kitu cha kuzihakiwa na kuchekelewa na wale wote wenye kutuzunguka pande zote.
14 Unatufanya kuwa kitu cha kuzarauliwa* kati ya mataifa,+
Kitu chenye vikundi vya watu vinatikisia kichwa.
15 Ninajisikia mwenye kufezeheshwa muchana wote,
Na ninalemewa na haya yangu,
16 Kwa sababu ya sauti za zihaka zao na matukano yao,
Kwa sababu ya adui yetu mwenye kulipiza kisasi.
17 Mambo hayo yote yamekuja juu yetu, lakini hatujakusahau,
Na hatujavunja agano lako.+
18 Moyo wetu haujakengeuka;
Hatua zetu hazitoke katika njia yako.
19 Lakini umetuponda mahali mbweha wanakaa;
Umetufunika kwa kivuli kizito.
20 Kama tumesahau jina la Mungu wetu
Ao kama tunamunyooshea mungu wa kigeni mikono yetu wakati tunasali,
21 Je, Mungu hatavumbua hilo?
Anajua siri za moyo.+
22 Kwa ajili yako tunauawa muchana wote;
Tumehesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.+
23 Amuka. Sababu gani unaendelea kulala usingizi, Ee Yehova?+
Amuka! Usiendelee kututupa milele.+
24 Sababu gani unaficha uso wako?
Sababu gani unasahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 Kwa maana tumeshushwa chini mupaka katika mavumbi;
Miili yetu imefinywa kwenye udongo.+
26 Simama ili utusaidie!+
Utuokoe* kwa sababu ya upendo wako mushikamanifu.+
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Maua ya Mayungiyungi.” Ya wana wa Kora.+ Maskili.* Wimbo wa upendo.
45 Moyo wangu umechangamushwa na jambo moja la muzuri.
Ninasema: “Wimbo wangu unahusu* mufalme.”+
Acha ulimi wangu ukuwe kalamu ya mwandikaji*+ mwenye ufundi.+
2 Uko na sura ya muzuri sana kuliko wana wote wa binadamu.
Maneno yenye kupendeza yanatiririka kutoka katika midomo yako.+
Ndiyo sababu Mungu amekubariki milele.+
4 Na katika utukufu wako endelea mupaka upate ushindi;*+
Panda utetee kweli na unyenyekevu na haki,+
Na mukono wako wa kuume utatimiza* mambo yenye kuogopesha sana.
5 Mishale yako ni mikali, inaangusha vikundi vya watu mbele yako;+
Inatoboa mioyo ya maadui wa mufalme.+
7 Ulipenda haki+ na kuchukia uovu.+
Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta+ kwa mafuta ya furaha+ kuliko wenzako.
8 Nguo zako zote zimetiwa marashi ya manemane na udi na kida;
Kutoka katika nyumba kubwa ya kifalme yenye kujengwa kwa pembe za tembo, vyombo vya kamba vinakufanya ushangilie.
9 Mabinti wa wafalme wanapatikana kati ya wanamuke wako wa heshima.
Malkia amesimama kwenye mukono wako wa kuume, akiwa amepambwa kwa zahabu ya Ofiri.+
10 Sikiliza, Ee binti, sikiliza kwa uangalifu na utege sikio lako;
Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
13 Binti ya mufalme ni mwenye kupendeza sana katika nyumba ya mufalme;
Nguo zake zimepambwa kwa* zahabu.
14 Atapelekwa kwa mufalme akiwa amevaa nguo zenye kusukwa kwa ufundi mukubwa.*
Mabikira wenzake wenye kumufuata wanaingizwa ndani mbele ya mufalme.
15 Wataletwa kwa furaha na shangwe;
Wataingia katika nyumba ya kifalme.
16 Wana wako watakamata mahali pa mababu zako.
Utawaweka kuwa wakubwa katika dunia yote.+
17 Nitatangaza jina lako katika vizazi vyote vyenye kuja.+
Ndiyo sababu vikundi vya watu vitakusifu milele na milele.
2 Ndiyo sababu hatutaogopa, hata kama dunia inabadilika,
Hata kama milima inaanguka katika sehemu za chini kabisa za bahari,+
3 Hata kama maji yake yananguruma na kutosha pofu nyingi,+
Hata kama milima inatikiswa kwa sababu ya musukosuko wake. (Sela)
4 Kuko muto wenye mito yake midogo inafanya muji wa Mungu ushangilie,+
Tabenakulo takatifu na kubwa ya Mwenye Kuwa Juu Zaidi.
5 Mungu iko* katika muji huo;+ hauwezi kupinduliwa.
Mungu atausaidia wakati kunapambazuka.*+
6 Mataifa yalikuwa katika musukosuko, falme zilipinduliwa;
Alipandisha sauti yake, na dunia ikayeyuka.+
8 Mukuje na mujionee matendo ya Yehova,
Namna amefanya mambo yenye kushangaza katika dunia.
9 Anamaliza vita katika dunia yote.+
Anavunja upinde na kuvunja mukuki vipande-vipande;
Anateketeza kwa moto magari ya kukokotwa ya vita.*
10 “Muache na mujue kwamba mimi ni Mungu.
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki.
47 Ninyi vikundi vyote vya watu, mupige mikono.
Mumupigie Mungu vigelegele vya ushindi pamoja na vigelegele vya shangwe.
2 Kwa maana Yehova Mwenye Kuwa Juu Zaidi ni mwenye kuogopesha sana;+
Yeye ndiye Mufalme mukubwa juu ya dunia yote.+
3 Anatiisha vikundi vya watu chini yetu;
Anatia mataifa chini ya miguu yetu.+
5 Mungu amepanda juu katika vigelegele vya shangwe;
Yehova, katika sauti ya baragumu.*
6 Mumuimbie Mungu sifa,* muimbe sifa.
Mumuimbie sifa Mufalme wetu, muimbe sifa.
7 Kwa maana Mungu ni Mufalme wa dunia yote;+
Muimbe sifa, na muonyeshe ufahamu.
8 Mungu amekuwa Mufalme juu ya mataifa.+
Mungu anakaa kwenye kiti chake kitakatifu cha ufalme.
9 Viongozi wa vikundi vya watu wamekusanyika pamoja
Pamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu.
Kwa maana watawala wa dunia ni wa* Mungu.
Ameinuliwa sana.+
Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+
48 Yehova ni mukubwa na anastahili kabisa kusifiwa
Katika muji wa Mungu wetu, katika mulima wake mutakatifu.
2 Urefu wake unavutia, shangwe ya dunia yote,+
Ni Mulima Sayuni wenye kuwa mbali sana kaskazini,
Muji wa Mufalme Mukubwa.+
4 Kwa maana angalia! wafalme wamekusanyika;*
Wamesonga mbele pamoja.
5 Wakati waliona hilo, walishangaa.
Walishikwa na wasiwasi na kukimbia kwa woga mukubwa.
6 Kutetemeka kuliwashika wakiwa kule,
Uchungu kama wa mwanamuke mwenye kuzaa.
7 Kwa upepo wa mashariki unavunja-vunja mashua* za Tarshishi.
8 Mambo yenye tulisikia, tumejionea sasa sisi wenyewe
Katika muji wa Yehova wa majeshi, katika muji wa Mungu wetu.
Mungu ataufanya kuwa imara kabisa milele.+ (Sela)
10 Kama jina lako, Ee Mungu, sifa yako
Inafika mupaka kwenye miisho ya dunia.+
Mukono wako wa kuume umejaa haki.+
13 Muweke mioyo yenu juu ya maboma yake.*+
Muchunguze minara yake yenye ngome,
Ili muelezee vizazi vyenye kuja kuhusu muji huo.
14 Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu+ milele na milele.
Atatuongoza kwa umilele wote.*+
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki.
49 Musikie hili, ninyi vikundi vyote vya watu.
4 Nitasikiliza mezali;
Nitaleta maana ya kitendawili changu kwa kinubi.
5 Sababu gani niogope katika nyakati za taabu,+
Wakati ninazungukwa na uovu wa* wale wenye kujaribu kunipindua?
6 Wale wenye kutegemea mali zao+
Na kujisifu kuhusu utajiri wao mwingi,+
7 Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye anaweza hata kidogo kumukomboa ndugu yake
Wala kumupatia Mungu bei ya ukombozi kwa ajili yake,+
8 (Bei ya ukombozi kwa ajili ya uzima wao* ni yenye samani sana
Kiasi ya kwamba hawawezi hata kidogo kuipata);
10 Anaona kwamba hata watu wenye hekima wanakufaka;
Wajinga na wenye hawana akili wanapotea pamoja,+
Na wanalazimika kuachia wengine mali zao.+
11 Tamaa yenye kuwa dani yao ni kwamba nyumba zao zidumu milele,
Mahema yao kizazi kwa kizazi.
Wameita mashamba yao kwa majina yao.
12 Lakini mwanadamu, hata kama anaheshimiwa, hataendelea kuishi;+
Haiko muzuri kuliko wanyama wenye wanakufaka.+
13 Hiyo ndiyo njia ya wajinga+
Na ya wale wenye kuwafuata, wenye wanafurahia maneno yao yenye hayana maana. (Sela)
14 Kama kondoo, wamepangiwa kuenda katika Kaburi.*
Kifo kitakuwa muchungaji wao;
Wanyoofu watawatawala+ asubui.
16 Usiogope kwa sababu mutu fulani anakuwa tajiri,
Kwa sababu utukufu wa nyumba yake unaongezeka,
17 Kwa maana wakati anakufa hawezi kuenda na kitu;+
Utukufu wake hautashuka katika shimo pamoja naye.+
18 Kwa maana wakati wa maisha yake anajipongeza mwenyewe.*+
(Watu wanakusifu wakati unafanikiwa.)+
19 Lakini mwishowe anajiunga na kizazi cha mababu zake.
Hawataona tena mwangaza hata siku moja.
20 Mutu mwenye haelewe jambo hili, hata kama anaheshimiwa,+
Haiko muzuri kuliko wanyama wenye wanakufaka.
Muziki wa Asafu.+
50 Mungu wa miungu, Yehova,+ amesema;
Anaita dunia
Kutoka mahali jua linatokea mupaka mahali linashukia.*
2 Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu anaangaza.
3 Mungu wetu atakuja na hawezi kubakia kimya.+
5 “Munikusanyie washikamanifu wangu,
Wale wenye kufanya agano pamoja na mimi kupitia zabihu.”+
6 Mbingu zinatangaza haki yake,
Kwa maana Mungu mwenyewe ni Muamuzi.+ (Sela)
7 “Munisikilize, Enyi watu wangu, na mimi nitasema;
Israeli, nitatoa ushahidi juu yako.+
Mimi ni Mungu, Mungu wako.+
8 Sikukaripie kwa sababu ya zabihu zako,
Wala kwa sababu ya matoleo yako mazima ya kuteketezwa yenye kuwa mbele yangu kila wakati.+
10 Kwa maana kila munyama wa pori ni wangu,+
Hata wanyama wenye kuwa juu ya milima elfu moja (1 000).
11 Ninajua kila ndege wa milima;+
Wanyama wa pori wenye hawana hesabu ni wangu.
12 Kama ningekuwa na njaa, singekuambia,
Kwa maana inchi yenye kuzaa na kila kitu chenye kuwa ndani ni changu.+
13 Je, nitakula nyama ya ngombe-dume
Na kunywa damu ya mbuzi?+
14 Toa shukrani zikiwa zabihu yako kwa Mungu,+
Na utimize naziri zako kwa Mwenye Kuwa Juu Zaidi;+
15 Uniitie wakati wa taabu.+
Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.”+
16 Lakini Mungu atamuambia muovu:
19 Unatumia kinywa chako kueneza mambo ya mubaya,
Na udanganyifu umeshikamana na ulimi wako.+
21 Wakati ulifanya mambo hayo, nilibakia kimya,
Kwa hiyo ukafikiri kwamba nitakuwa tu kama wewe.
Lakini sasa nitakukaripia,
Na nitakushitaki.+
22 Tafazali, mufikirie jambo hili, ninyi wenye kumusahau Mungu,+
Ili nisiwapasue vipande-vipande bila mutu wa kuwaokoa.
23 Ule mwenye anatoa shukrani kuwa zabihu yake ananitukuza,+
Na kuhusu ule mwenye anafuata njia yenye iliwekwa,
Nitamufanya aone wokovu wa Mungu.”+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi, wakati nabii Natani alikuja kwa Daudi kisha yeye kulala na Bat-sheba.+
51 Unionyeshe wema, Ee Mungu, kulingana na upendo wako mushikamanifu.+
Futa makosa yangu kulingana na rehema yako kubwa.+
4 Kukuelekea wewe—wewe zaidi ya wote*—nimetenda zambi;+
Nimetenda mambo ya mubaya mbele ya macho yako.+
Kwa hiyo, uko mwenye haki wakati unasema,
Uko mwenye haki katika hukumu yako.+
6 Angalia! Unapendezwa na kweli katika mutu wa ndani;+
Fundisha mutu wangu wa ndani kabisa* hekima ya kweli.
7 Unisafishe kutokana na zambi yangu kwa hisopo, ili nikuwe safi;+
8 Acha nisikie sauti za shangwe na furaha,
Ili mifupa yenye uliponda ishangilie.+
11 Usinitupe kutoka mbele yako;
Wala usiondoe roho yako takatifu juu yangu.
13 Nitafundisha wakosaji njia zako,+
Ili watenda-zambi warudie kwako.
14 Uniokoe kutokana na hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+
Ili ulimi wangu utangaze kwa shangwe haki yako.+
15 Ee Yehova, fungua midomo yangu,
Ili kinywa changu kitangaze sifa yako.+
17 Zabihu zenye zinamupendeza Mungu ni roho yenye kuvunjika;
18 Kwa nia yako njema tendea Sayuni mambo mema;
Jenga kuta za Yerusalemu.
19 Halafu utafurahia zabihu za haki,
Zabihu za kuteketezwa na matoleo mazima;
Kisha ngombe-dume watatolewa kwenye mazabahu yako.+
Kwa kiongozi. Maskili.* Ya Daudi, wakati Doegi Mwedomu alikuja na kumuambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+
52 Sababu gani unajisifu kuhusu matendo yako maovu, wewe mwenye nguvu?+
Upendo mushikamanifu wa Mungu unadumu muchana wote.+
3 Unapenda uovu kuliko mema,
Kusema uongo kuliko kusema mambo yenye kuwa sawa. (Sela)
4 Unapenda kila neno lenye kuumiza,
Ee ulimi mudanganyifu!
5 Ndiyo sababu Mungu atakubomoa milele na milele;+
Atakukamata haraka na kukupasua kutoka katika hema yako;+
Atakungoa kutoka katika inchi ya wazima.+ (Sela)
7 “Huyu ndiye mwanaume mwenye hakumufanya Mungu kuwa kimbilio lake,*+
Lakini alitumainia utajiri wake mwingi+
8 Lakini mimi nitakuwa kama muzeituni wenye majani mengi katika nyumba ya Mungu;
Ninategemea upendo mushikamanifu wa Mungu,+ milele na milele.
9 Nitakusifu milele kwa sababu umekamata hatua;+
Mbele ya washikamanifu wako,
Nitatumainia jina lako,+ kwa maana ni muzuri.
Kwa kiongozi; katika mutindo wa Mahalati.* Maskili.* Ya Daudi.
53 Mupumbavu* anasema katika moyo wake:
“Hakuna Yehova.”+
Matendo yao yenye hayako ya haki yamepotoka na yanachukiza;
Hakuna mwenye kutenda mema.+
2 Lakini Mungu anaangalia wana wa binadamu akiwa mbinguni+
Ili aone kama kuko mutu yeyote mwenye kuwa na ufahamu, kama kuko mutu yeyote mwenye kumutafuta Yehova.+
3 Wote wamekengeuka;
Wote pamoja wamepotoka.
Hakuna mwenye kutenda mema,
Hakuna hata mumoja.+
4 Je, hakuna hata mumoja kati ya wakosaji mwenye anaelewa?
Wanameza watu wangu kama vile wanakula mukate.
Hawamuitie Yehova.+
5 Lakini watajaa woga mukubwa,
Woga wenye hawajapata kuwa nao hata siku moja,*
Kwa maana Mungu atasambaza mifupa ya wale wenye kuwashambulia ninyi.*
Mutawapatisha haya, kwa maana Yehova amewakataa wao.
6 Aa! kama tu wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+
Wakati Yehova atakusanya tena watu wake wenye walikamatwa mateka,
Yakobo ashangilie, Israeli afurahi.
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Maskili.* Ya Daudi, wakati Wazifu waliingia na kumuambia Sauli: “Daudi anajificha kati yetu.”+
2 Ee Mungu, sikia sala yangu;+
Sikiliza maneno ya kinywa changu.
3 Kwa maana wageni wanasimama ili kunishambulia,
Hawamuheshimie Mungu.*+ (Sela)
6 Nitakutolea zabihu+ kwa kujipendea.
Nitasifu jina lako, Ee Yehova, kwa maana ni muzuri.+
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Maskili.* Ya Daudi.
2 Unisikilize na unijibu.+
Hangaiko langu linanifanya nikose utulivu,+
Na nimevurugika
3 Kwa sababu ya mambo yenye adui anasema
Na mukazo kutoka kwa muovu.
Kwa maana wanarundika taabu juu yangu,
Na kwa kasirani wananiwekea chuki.+
5 Woga na kutetemeka vinakuja juu yangu,
Na kutetemeka kunanishika.
6 Ninaendelea kusema: “Kama tu ningekuwa na mabawa kama njiwa!
Ningeruka mbali na kukaa kwa usalama.
7 Angalia! Ningekimbia na kuenda mbali sana.+
Ningekaa katika jangwa.+ (Sela)
8 Ningeenda haraka mahali pa kujificha
Mbali na upepo mukali, mbali na zoruba.”
10 Usiku na muchana wanazunguka juu ya kuta zake;
Ndani yake kuko nia mubaya na taabu.+
11 Uharibifu uko ndani yake;
Ukandamizaji na udanganyifu haviondoke hata kidogo katika kiwanja chake cha watu wote.+
12 Kwa maana haiko adui ndiye ananichokoza;+
Ingekuwa vile ningevumilia.
Haiko adui ndiye amesimama ili kunishambulia;
Ingekuwa vile ningejificha asinipate.
14 Tulikuwa tunafurahia pamoja urafiki wa karibu sana;
Katika nyumba ya Mungu tulikuwa tunatembea pamoja na kikundi cha watu.
15 Uharibifu uwapate!+
Washuke katika Kaburi* wakiwa wazima;
Kwa maana uovu unakaa kati yao na ndani yao.
16 Lakini mimi, nitamuita Mungu,
Na Yehova ataniokoa.+
17 Mangaribi na asubui na katikati ya muchana, ninahangaika na kulia kwa maumivu,*+
Na anasikia sauti yangu.+
18 Ataniokoa* na kunipatia* amani mbali na wale wenye kupigana na mimi,
Kwa maana vikundi vya watu vinakuja kunishambulia.+
Watakataa kubadilika,
Wale wenye hawajamuogopa Mungu.+
21 Maneno yake ni laini kuliko siagi,+
Lakini muzozo uko katika moyo wake.
Maneno yake ni laini kuliko mafuta,
Lakini ni panga zenye kuchomolewa.+
Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.*+
23 Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha chini kwenye shimo la murefu kabisa.+
Watu hao wenye hatia ya damu wenye ni wadanganyifu hawataishi nusu ya siku zao.+
Lakini mimi, nitakutegemea wewe.
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Njiwa Munyamavu Mwenye Kuwa Mbali.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati Wafilisti walimukamata kule Gati.+
56 Unionyeshe wema, Ee Mungu, kwa sababu mwanadamu mwenye anaweza kufa ananishambulia.*
Muchana wote wanaendelea kunipiga vita na kunikandamiza.
2 Maadui wangu wanatafuta kuniuma muchana wote;
Wengi wanapigana na mimi kwa kiburi.
3 Wakati ninaogopa,+ ninakutegemea wewe.+
4 Katika Mungu—mwenye ninasifu neno lake—
Katika Mungu ninaweka tegemeo langu; siogope.
Mwanadamu bure anaweza kunifanya* nini?+
5 Muchana wote wanaharibu mambo yangu;
Jambo pekee lenye wanafikiria ni kunifanya mubaya.+
7 Uwakatae kwa sababu ya uovu wao.
Angusha mataifa kwa kasirani yako, Ee Mungu.+
8 Unafuatilia kutanga-tanga kwangu.+
Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi.+
Je, hayaandikwe katika kitabu chako?+
9 Maadui wangu watakimbia siku yenye nitaomba musaada.+
Niko hakika na jambo hili: Mungu iko* upande wangu.+
10 Katika Mungu—mwenye ninasifu neno lake—
Katika Yehova—mwenye ninasifu neno lake—
11 Katika Mungu ninaweka tegemeo langu; siogope.+
Mwanadamu bure anaweza kunifanya nini?+
13 Kwa maana umeniokoa* katika kifo+
Na umezuia miguu yangu isijikwae,+
Ili nitembee mbele ya Mungu katika mwangaza wa wazima.+
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati alimukimbia Sauli na kuingia katika pango.+
57 Unionyeshe wema, Ee Mungu, unionyeshe wema,
Na ninakimbilia kivuli cha mabawa yako mupaka magumu yangu yapite.+
2 Ninamuita Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi,
Mungu wa kweli, mwenye anamaliza magumu hayo kwa ajili yangu.
3 Atatuma musaada kutoka mbinguni na kuniokoa.+
Atamuvuruga ule mwenye anataka kuniuma. (Sela)
Mungu atatuma upendo wake mushikamanifu na uaminifu wake.+
Nimelazimika kulala kati ya watu wenye wanataka kunimeza,
Wenye meno yao ni mikuki na mishale
Na wenye ulimi wao ni upanga mukali.+
5 Uinuliwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako ukuwe juu ya dunia yote.+
Wamechimba shimo mbele yangu,
Lakini wao wenyewe wameanguka ndani.+ (Sela)
7 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu,+
Moyo wangu uko imara.
Nitaimba na kupiga muziki.
8 Amuka, utukufu wangu.
Amuka, Ee chombo cha kamba; na wewe pia, Ee kinubi.
10 Kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwingi, uko juu kama mbingu,+
Na uaminifu wako, unafika mupaka kwenye anga.
11 Uinuliwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako ukuwe juu ya dunia yote.+
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.*
58 Je, munaweza kuzungumuza kuhusu haki wakati mumenyamaza?+
Je, munaweza kuhukumu kwa unyoofu, ninyi wana wa binadamu?+
2 Kuliko kufanya vile, munapanga ukosefu wa haki katika moyo wenu,+
Na mikono yenu inaeneza jeuri katika inchi.+
5 Hatasikiliza sauti ya watu wenye kuchezesha nyoka,
Hata wafanye uchawi kwa ufundi namna gani.
6 Ee Mungu, vunja meno yao katika vinywa vyao!
Vunja mataya* ya simba hawa,* Ee Yehova!
7 Acha waishe kama maji yenye kukauka.
Acha Yeye akunje upinde wake na kuwaangusha kwa mishale yake.
8 Acha wakuwe kama konokono mwenye anayeyuka wakati anatembea;
Kama mutoto mwenye alikufia katika tumbo la mwanamuke na mwenye haone jua hata kidogo.
9 Mbele vyungu vyenu vya kupikia havijapata moto wa kuni za muti wa mukwamba,
Ataharibu umajimaji na tawi lenye kuwaka, kama kwa upepo wa zoruba.+
11 Kisha watu watasema: “Hakika kuko zawabu kwa ajili ya mwenye haki.+
Kwa kweli kuko Mungu mwenye anahukumu katika dunia.”+
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati Sauli alituma watu wachunguze nyumba ya Daudi* ili wamuue.+
59 Uniokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Mungu wangu;+
Unilinde kutoka kwa wale wenye kusimama ili kunishambulia.+
2 Uniokoe kutoka kwa wale wenye kutenda uovu,
Na uniokoe kutoka kwa watu wenye jeuri.*
Wanaume wenye nguvu wananishambulia
Lakini haiko kwa sababu nimeasi ao kutenda zambi,+ Ee Yehova.
4 Hata kama sikutenda kosa lolote, wanakimbia na kujitayarisha ili kushambulia.
Simama wakati ninakuita na uone.
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova Mungu wa majeshi, ni Mungu wa Israeli.+
Amuka ili ukazie uangalifu wako mataifa yote.
Usionyeshe rehema wasaliti wowote wenye nia mubaya.+ (Sela)
7 Angalia kile kinamwangika* kutoka katika kinywa chao;
Midomo yao ni kama panga,+
Kwa maana wanasema: “Ni nani anasikiliza?”+
10 Mungu mwenye ananitendea kwa upendo mushikamanifu atanisaidia;+
Mungu ataniwezesha niangalie kwa furaha kushindwa kwa maadui wangu.+
11 Usiwaue, ili watu wangu wasisahau.
Kwa nguvu zako uwafanye watange-tange;
Uwaangushe, Ee Yehova, ngao yetu.+
12 Kwa sababu ya zambi ya kinywa chao, neno la midomo yao,
Acha kiburi chao kiwanase,+
Kwa sababu ya laana na udanganyifu wenye wanasema.
13 Uwamalize kwa kasirani yako kali;+
Uwamalize, ili wasikuwe tena;
Uwafanye wajue kwamba Mungu anatawala katika Yakobo na mupaka kwenye miisho ya dunia.+ (Sela)
15 Acha watange-tange wakitafuta chakula;+
Usiwaruhusu washibe wala kupata makao.
16 Lakini mimi, nitaimba kuhusu nguvu zako;+
Asubui nitatangaza kwa shangwe kuhusu upendo wako mushikamanifu.
17 Ee Nguvu zangu, nitakuimbia sifa,*+
Kwa maana Mungu ni kimbilio langu salama, Mungu mwenye kunionyesha upendo mushikamanifu.+
Kwa kiongozi; imepatanishwa na
“Ua la Yungiyungi la Kikumbusho.” Miktamu.* Ya Daudi. Ya kufundisha. Wakati alipigana na Aram-naharaimu na Aram-Soba, na Yoabu akarudia
na akapiga na kuua Waedomu elfu
kumi na mbili (12 000) katika
Bonde la Chumvi.+
60 Ee Mungu, ulitukataa; ulipasua njia katika vikundi vyetu vya ulinzi.+
Ulitukasirikia; lakini sasa utukubali tena!
2 Ulifanya dunia itetemeke; uliipasua ikafunguka.
Funga mipasuko yake, kwa maana inaanguka.
3 Ulifanya watu wako wateseke.
Ulitufanya tukunywe divai yenye inatufanya tuyumbe-yumbe.+
4 Patia* alama wale wenye kukuogopa
Ili wakimbie na kukwepa upinde. (Sela)
5 Ili wapendwa wako waokolewe,
Utuokoe kupitia mukono wako wa kuume na utujibu.+
6 Mungu amesema katika utakatifu wake:*
7 Gileadi ni yangu, na Manase+ ni yangu,
Na Efraimu ni kofia ya chuma* ya kichwa changu;
Yuda ni fimbo yangu ya kamanda.+
8 Moabu ni beseni yangu ya kunawia.+
Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+
Nitapiga vigelegele vya ushindi juu ya Ufilisti.”+
9 Ni nani atanipeleka katika muji wenye kuzungukwa kwa ajili ya vita?*
Ni nani ataniongoza mupaka Edomu?+
10 Je, haiko wewe, Ee Mungu, mwenye umetukataa,
Mungu wetu, mwenye haende tena na majeshi yetu?+
11 Utusaidie katika taabu yetu,
Kwa maana wokovu kutoka kwa wanadamu hauna mafaa yoyote.+
Kwa kiongozi; iimbwe kwa
vyombo vya kamba. Ya Daudi.
61 Ee Mungu, sikia kilio changu cha kuomba musaada.
Sikiliza sala yangu.+
Uniongoze kwenye mwamba wenye kuwa juu kuliko mimi.+
3 Kwa maana wewe ni kimbilio langu,
Munara wenye nguvu wenye unanilinda na adui.+
5 Kwa maana wewe, Ee Mungu, umesikia naziri zangu.
Umenipatia uriti wa wale wenye kuogopa jina lako.+
7 Atakaa akiwa mufalme* milele mbele ya Mungu;+
Umupatie* upendo wako mushikamanifu na uaminifu, ili vimulinde.+
Kwa kiongozi; Ya Yedutuni.* Muziki wa Daudi.
62 Kwa kweli, ninamungojea* Mungu kimya-kimya.
Wokovu wangu unatoka kwake.+
2 Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;*+
Sitatikiswa sana hata kidogo.+
3 Mutaendelea mupaka wakati gani kumushambulia mutu ili kumuua?+
Ninyi wote muko hatari kama ukuta wenye kuinama, ukuta wa majiwe wenye unakaribia kuanguka.*
4 Kwa maana wanafanya shauri pamoja ili kumuangusha kutoka kwenye cheo chake cha juu;*
Wanafurahia kusema uongo.
Kwa kinywa chao wanabariki, lakini ndani yao wanalaani.+ (Sela)
6 Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;
Sitatikiswa hata kidogo.+
7 Wokovu wangu na utukufu wangu unamutegemea Mungu.
Mwamba wangu wenye nguvu, kimbilio langu, ni Mungu.+
8 Mumutegemee nyakati zote, Enyi watu.
Mumwange mioyo yenu mbele yake.+
Mungu ni kimbilio letu.+ (Sela)
9 Wana wa binadamu ni pumuzi tu,
Wana wa wanadamu ni udanganyifu.+
Wakati wanatiwa pamoja kwenye mizani,* ni wepesi kuliko pumuzi tu.+
10 Musitegemee upunjaji
Wala kuwa na matumaini ya uongo katika unyanganyi.
Kama mali zenu zinaongezeka, musiweke moyo wenu juu ya mali hizo.+
11 Mungu amezungumuza mara moja, mara mbili nimesikia jambo hili:
Kwamba nguvu ni za Mungu.+
12 Pia upendo mushikamanifu ni wako, Ee Yehova,+
Kwa maana unamulipa kila mutu kulingana na matendo yake.+
Muziki wa Daudi, wakati alikuwa katika jangwa la Yuda.+
63 Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+
2 Kwa hiyo nimekuangalia katika mahali patakatifu;
Nimeona nguvu zako na utukufu wako.+
4 Basi nitakusifu maisha yangu yote;
Katika jina lako nitainua mikono yangu.
5 Nimetosheka* na fungu bora lenye kuwa la muzuri kabisa,*
Kwa hiyo kinywa changu kitakusifu kwa midomo yenye shangwe.+
6 Ninakukumbuka wewe nikiwa kwenye kitanda changu;
7 Kwa maana wewe ni musaidizi wangu,+
Nami ninapiga vigelegele vya shangwe katika kivuli cha mabawa yako.+
9 Lakini wale wenye kutafuta kuharibu uzima wangu*
Watashuka katika sehemu za chini kabisa za dunia.
10 Watatiwa katika nguvu za upanga;
Watakuwa chakula cha mbweha.
11 Lakini mufalme atashangilia katika Mungu.
Kila mutu mwenye anaapa katika jina Lake atashangilia,*
Kwa maana kinywa cha wenye kusema uongo kitanyamazishwa.
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
64 Sikia sauti yangu, Ee Mungu, wakati ninakulilia.+
Linda uzima wangu kutokana na woga wa adui.
2 Unilinde kutokana na mipango mibaya yenye waovu wanafanya kwa uficho,+
Kutokana na kikundi cha wakosaji.
3 Wananoa ulimi wao kama vile upanga;
Wanalenga maneno yao makali kama mishale,
4 Ili wamupige mutu mwenye hana kosa wakiwa mahali pao pa kujificha;
Wanamupiga bila kutazamia, bila kuogopa.
5 Wanashikamana sana na kusudi lao la uovu;*
Wanazungumuzia namna ya kuficha mitego yao.
Wanasema: “Ni nani ataiona?”+
6 Wanatafuta njia za mupya za kutenda makosa;
Wanapanga kwa siri mipango yao ya ujanja;+
Mawazo yenye kuwa ndani ya moyo wa kila mumoja wao hayaeleweke kabisa.
7 Lakini Mungu atawapiga mishale;+
Bila kutazamia, wataumizwa na mushale.
8 Ulimi wao wenyewe utawafanya waanguke;+
Wale wote wenye kuangalia watatikisa kichwa.
10 Mwenye haki atashangilia katika Yehova na kumukimbilia;+
Wote wenye kuwa wanyoofu katika moyo watashangilia.*
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo.
2 Ee Musikiaji wa sala, watu wa namna zote watakuendea.*+
4 Mwenye furaha ni ule mwenye unachagua na kumuleta karibu+
Ili akae katika viwanja vyako.
5 Utatujibu kwa matendo ya haki yenye kuogopesha sana,+
Ee Mungu wa wokovu wetu;
Wewe ndiye Tegemeo la miisho yote ya dunia+
Na la wale wenye kuwa mbali ngambo ya bahari.
8 Wakaaji wa sehemu za mbali wataogopeshwa na alama zako;+
Utafanya wale wenye kuishi mahali jua linatokea mupaka mahali jua linashukia wapige vigelegele vya shangwe.
10 Unajaza maji katika mifereji yake na kusawazisha udongo wake wenye umelimwa;*
Unaifanya kuwa laini kwa matone ya mvua; unabariki mimea yake.+
Yanapiga vigelegele vya ushindi, ndiyo, yanaimba.+
Kwa kiongozi. Wimbo. Muziki.
66 Mumupigie Mungu vigelegele vya ushindi, dunia yote.+
2 Muimbie jina lake lenye utukufu sifa.*
Mutukuze sifa yake.+
3 Muambie Mungu: “Kazi zako ni zenye kuogopesha sana!+
Kwa sababu ya nguvu zako nyingi,
Maadui wako watajikunja kwa woga mbele yako.+
5 Mukuje na muone kazi za Mungu.
Mambo yenye alitendea wana wa binadamu ni yenye kuogopesha sana.+
Kule tulishangilia katika yeye.+
7 Anatawala milele+ kwa nguvu zake.
Macho yake yanachunguza mataifa.+
Wale wenye wako kichwa-nguvu hawapaswe kujiinua.+ (Sela)
8 Mumusifu Mungu wetu, ninyi vikundi vya watu,+
Na sauti ya sifa yake isikike.
10 Kwa maana umetuchunguza, Ee Mungu;+
Umetusafisha kama vile feza inasafishwa.
12 Uliruhusu mwanadamu mwenye anaweza kufa apande juu yetu;*
Tulipita katika moto na katika maji;
Kisha ulituleta mahali kwenye kitulizo.
13 Nitaingia katika nyumba yako nikiwa na matoleo mazima ya kuteketezwa;+
Nitatimiza naziri zenye niliweka kwako+
14 Zenye midomo yangu iliahidi+
Na kinywa changu kilisema wakati nilikuwa katika taabu.
15 Nitakutolea matoleo ya kuteketezwa ya wanyama wenye kunenepa
Pamoja na moshi wa kondoo-dume wa zabihu.
Nitatoa ngombe-dume pamoja na mbuzi-dume. (Sela)
16 Mukuje na musikilize, ninyi wote wenye kumuogopa Mungu,
Na nitawaambia mambo yenye amenitendea.+
17 Nilimuita kwa kinywa changu
Na kumutukuza kwa ulimi wangu.
18 Kama ningeweka katika moyo wangu jambo fulani lenye kuumiza,
Yehova hangenisikia.+
20 Mungu asifiwe, mwenye hakukataa sala yangu
Wala kuniima upendo wake mushikamanifu.
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo
vya kamba. Muziki. Wimbo.
67 Mungu atatuonyesha wema na kutubariki;
Atafanya uso wake utuangazie+ (Sela)
3 Vikundi vya watu vitakusifu, Ee Mungu;
Vikundi vyote vya watu vikusifu.
4 Mataifa yashangilie na kupiga vigelegele vya shangwe,+
Kwa maana utahukumu vikundi vya watu kwa haki.+
Utaongoza mataifa ya dunia. (Sela)
5 Vikundi vya watu vikusifu, Ee Mungu;
Vikundi vyote vya watu vikusifu.
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki. Wimbo.
68 Mungu asimame, maadui wake wasambazwe,
Na wale wenye kumuchukia wakimbie kutoka mbele yake.+
2 Uwapeperushe mbali kama vile moshi unapeperushwa mbali;
Kama vile nta* inayeyuka mbele ya moto,
Waovu waangamie kwa njia hiyo kutoka mbele ya Mungu.+
4 Mumuimbie Mungu; muimbie jina lake sifa.*+
Mumuimbie Ule mwenye kupanda kupitia maeneo tambarare ya jangwa.*
Jina lake ni Yah!*+ Mushangilie mbele yake!
Lakini watu wenye wako kichwa-nguvu* lazima waishi katika inchi yenye kukauka.+
8 Dunia ilitetemeka;+
Mbingu ilimwanga* mvua kwa sababu ya Mungu;
Huu Mulima Sinai ulitetemeka kwa sababu ya Mungu, Mungu wa Israeli.+
9 Ulifanya mvua inyeshe kwa wingi, Ee Mungu;
Ulitia nguvu tena watu* wako wenye kuchoka.
10 Walikaa katika kambi yako yenye mahema;+
Kwa wema wako, uliandalia maskini, Ee Mungu.
12 Wafalme wa majeshi wanakimbia,+ wanakimbia!
Mwanamuke mwenye anabakia kwenye nyumba anapewa sehemu yake ya vitu vyenye vilichukuliwa katika vita.+
13 Hata kama ninyi wanaume mulikuwa munalala kati ya mioto ya kambi,*
Kutakuwa mabawa ya njiwa yenye kufunikwa kwa feza,
Yenye manyoya ya zahabu safi.*
16 Sababu gani munaangalia kwa wivu, ninyi milima yenye vichwa,
Kwa kweli, Yehova atakaa kule milele.+
17 Magari ya Mungu ya vita ni makumi ya maelfu, maelfu kwa maelfu.+
Yehova ametoka Sinai na kuingia mahali patakatifu.+
Ulichukua watu wenye walikamatwa mateka;
Ulikamata zawadi katika umbo ya wanadamu,+
Ndiyo, hata wenye wako kichwa-nguvu,+ ili ukae kati yao, Ee Yah Mungu.
19 Yehova asifiwe, yeye mwenye anatubebea muzigo wetu kila siku,+
Mungu wa kweli wa wokovu wetu. (Sela)
20 Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu mwenye kuokoa;+
Na Yehova Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi anaokoa katika kifo.+
21 Ndiyo, Mungu ataponda-ponda vichwa vya maadui wake,
Ataponda-ponda sehemu ya juu ya katikati ya kichwa yenye nywele ya mutu yeyote mwenye anaendelea* katika hatia yake.+
22 Yehova amesema: “Nitawarudisha kutoka Bashani;+
Nitawarudisha kutoka sehemu za chini kabisa za bahari,
23 Ili muguu wako ufunikwe na damu+
Na ulimi wa imbwa zako upate fungu lake kutoka kwa maadui.”
24 Wanaona misururu yako, Ee Mungu,
Misururu ya Mungu wangu, Mufalme wangu, ikiingia mahali patakatifu.+
25 Waimbaji wanatangulia mbele, wapiga-muziki wenye kupiga vyombo vya kamba wanawafuata;+
Katikati yao kuko vijana wanamuke wenye kupiga ngoma za kidogo.*+
26 Katika vikundi vya watu wenye kukutanika,* mumusifu Mungu;
Mumusifu Yehova, ninyi wenye kutoka katika Chemchemi ya Israeli.+
27 Kule Benyamini,+ ule mudogo zaidi, anawatiisha,
Pia wakubwa wa Yuda pamoja na kikundi chao cha watu wenye fujo,
Wakubwa wa Zabuloni, wakubwa wa Naftali.
28 Mungu wako ameamuru kwamba utakuwa na nguvu.
Onyesha nguvu zako, Ee Mungu, wewe mwenye umetenda kwa ajili yetu.+
30 Kemea wanyama wa pori wenye kuwa katika matete,
Mukusanyiko wa ngombe-dume+ na vitoto-dume vyao,
Mupaka wakati vikundi vya watu vitainama vikileta* vipande vya feza.
Lakini anasambaza vikundi vya watu wenye kupenda vita.
31 Vitu vya shaba nyekundu vitaletwa kutoka* Misri;+
Kushi itafanya haraka ili kumupatia Mungu zawadi.
33 Ule mwenye anapanda mbingu ya zamani ya zile mbingu.+
Angalia! Ananguruma kwa sauti yake, sauti yake yenye nguvu.
34 Mutambue nguvu za Mungu.+
Ukubwa wake uko juu ya Israeli,
Na nguvu zake ziko katika anga.*
35 Mungu ni mwenye kuogopesha sana kutoka katika patakatifu pake* pakubwa.+
Yeye ni Mungu wa Israeli,
Mwenye kupatia watu uwezo na nguvu.+
Mungu asifiwe.
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Maua ya Mayungiyungi.” Ya Daudi.
69 Uniokoe, Ee Mungu, kwa maana maji yanatia uzima wangu katika hatari.*+
2 Nimezama katika matope yenye kuenda chini sana, mahali kwenye hakuna udongo mugumu.+
Nimeingia katika maji yenye kuenda chini sana,
Na muto mudogo wenye kuteremuka haraka umenifagilia mbali.+
3 Nimechoka kwa sababu ya kuita;+
Koo langu limekauka.
Macho yangu yamechoka wakati ninamungojea Mungu wangu.+
Wale wenye kutaka kuniua,
Maadui wangu wadanganyifu,* wamekuwa wengi.
Nililazimishwa kurudisha kitu chenye sikuiba.
5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu,
Na hatia yangu haifichwe mbele yako.
6 Wale wenye kukutumainia wasipatishwe haya kwa sababu yangu,
Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi.
Wale wenye kukutafuta wasifezeheshwe kwa sababu yangu,
Ee Mungu wa Israeli.
8 Nimekuwa mugeni kwa ndugu zangu,
Mugeni kwa wana wa mama yangu.+
11 Wakati nilifanya magunia kuwa nguo zangu,
Nikakuwa kitu cha kuzarauliwa mbele yao.*
12 Nimekuwa mutu wa kusemwa-semwa na wale wenye kukaa katika mulango mukubwa wa muji,
Na walevi wanaimba juu yangu katika nyimbo zao.
13 Lakini sala yangu ikufikie,
Ee Yehova, kwa wakati wenye kufaa.+
Katika upendo wako mwingi mushikamanifu, Ee Mungu,
Unijibu kwa matendo yako hakika ya wokovu.+
14 Uniokoe katika matope;
Usiache nizame.
Uniokoe kutoka kwa wale wenye kunichukia
Na katika maji yenye kuenda chini sana.+
15 Usiache maji ya garika yenye kuteremuka haraka yanifagilie mbali,+
Wala maji yenye kuenda chini sana yanimeze,
16 Unijibu, Ee Yehova, kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwema.+
Unijibu haraka, kwa maana niko katika taabu.+
18 Unikaribie na uniokoe;*
Unikomboe kwa sababu ya maadui wangu.
19 Unajua lawama yangu na haya yangu na aibu yangu.+
Unaona maadui wangu wote.
20 Lawama imevunja moyo wangu, na kidonda hakiwezi kupona.*
Nilitumaini kwamba nitahurumiwa, lakini sikuhurumiwa hata kidogo,+
Na nilitumaini kupata watu wa kunifariji, lakini sikupata hata mumoja.+
22 Meza yao ikuwe mutego kwao,
Na mafanikio yao yakuwe kitu cha kuwanasa.+
23 Macho yao yatiwe giza ili wasione,
Na ufanye viuno vyao vitetemeke kila wakati.
24 Uwamwangie kasirani yako kali,
Na kasirani yako yenye kuwaka iwapate.+
26 Kwa maana wanamufuatilia ule mwenye ulipiga,
Na wanaendelea kusimulia kuhusu maumivu ya wale wenye uliumiza.
27 Ongeza hatia zaidi juu ya hatia yao,
Na wasikuwe na fungu lolote katika haki yako.
29 Lakini ninateseka, na niko katika maumivu.+
Ee Mungu, nguvu zako za kuokoa zinilinde.
30 Nitaimbia jina la Mungu sifa,
Na nitamutukuza kwa kutoa shukrani.
31 Jambo hilo litamufurahisha Yehova zaidi kuliko ngombe-dume,
32 Wapole wataona jambo hilo na kushangilia.
Mioyo yenu ikuwe tena na uzima, ninyi wenye kumutafuta Mungu.
34 Mbingu na dunia zimusifu,+
Bahari na kila kitu chenye kutembea ndani.
Kwa kiongozi. Ya Daudi,
ya kukumbusha.
70 Ee Mungu, uniokoe;
Ee Yehova, fanya haraka ili unisaidie.+
2 Acha wale wenye kutafuta kuondoa uzima wangu*
Wapatishwe haya na kufezeheshwa.
Acha wale wenye kufurahia musiba wangu
Wakimbie kwa sababu ya aibu.
3 Acha wale wenye kusema: “Aha! Aha!”
Wakimbizwe kwa sababu ya haya.
4 Lakini acha wale wenye kukutafuta
Wafurahi na kushangilia katika wewe.+
Acha wale wenye kupenda matendo yako ya wokovu waseme sikuzote:
“Mungu atukuzwe!”
Wewe ni musaidizi wangu na mwokozi wangu.+
Ee Yehova, usikawie.+
71 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.
Usiache nipatishwe haya hata kidogo.+
2 Katika haki yako uniokoe na kunikomboa.
Unitegee sikio lako* na kuniokoa.+
3 Ukuwe ngome ya mwamba kwa ajili yangu
Kwenye ninaweza kuingia sikuzote.
Toa amri ya kuniokoa,
Kwa maana wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.+
4 Ee Mungu wangu, uniokoe kutoka katika mukono wa muovu,+
Kutoka katika kushikwa na mukandamizaji mwenye hana haki.
5 Kwa maana wewe ni tumaini langu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova;
6 Nimekutegemea tangu kuzaliwa kwangu;
Wewe ndiye ulinitosha katika tumbo la uzazi la mama yangu.+
Ninakusifu kila wakati.
7 Nimekuwa kama muujiza kwa watu wengi,
Lakini wewe ni kimbilio lenye nguvu.
8 Kinywa changu kimejaa sifa zako;+
Muchana wote ninasimulia kuhusu utukufu wako.
10 Maadui wangu wanasema mubaya juu yangu,
Na wale wenye kutafuta kuondoa uzima wangu* wanafanya pamoja mupango mubaya,+
11 Kwa kusema: “Mungu amemuacha.
Mumufuatilie na kumukamata, kwa maana hakuna mutu wa kumuokoa.”+
12 Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali na mimi.
Ee Mungu wangu, fanya haraka ili unisaidie.+
Acha wale wenye kutafuta musiba wangu
Wafunikwe haya na aibu.+
14 Lakini mimi, nitaendelea kungojea;
Nitakusifu hata zaidi.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako,+
Muchana wote kitasimulia matendo yako ya wokovu,
16 Nitakuja na kutangaza matendo yako yenye nguvu,
Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova;
Nitatangaza haki yako, yako tu.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,+
Na mupaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu.+
18 Ee Mungu, hata wakati nitazeeka na kuwa na imvi, usiniache.+
Acha niambie kizazi chenye kitafuata kuhusu nguvu zako*
Na kuambia wale wote wenye watakuja kuhusu uwezo wako.+
19 Haki yako, Ee Mungu, inafika kwenye nafasi za juu;+
Umetenda mambo makubwa;
Ee Mungu, ni nani mwenye kuwa kama wewe?+
20 Hata kama umenifanya nipate taabu nyingi na misiba mingi,+
Unipatie tena uzima;
21 Ongeza ukubwa wangu
Na unizunguke na kunifariji.
22 Kisha nitakusifu kwa chombo cha kamba
Kwa sababu ya uaminifu wako, Ee Mungu wangu.+
Nitaimba sifa zako* kwa kinubi,
Ee Mutakatifu wa Israeli.
23 Midomo yangu itapiga vigelegele vya shangwe wakati ninakuimbia sifa,+
24 Ulimi wangu utaongea* muchana wote kuhusu haki yako,+
Kwa maana wale wenye kutafuta kuniharibu watapatishwa haya na kufezeheshwa.+
Kuhusu Sulemani.
72 Ee Mungu, umupatie mufalme hukumu zako,
Na umupatie mwana wa mufalme haki yako.+
3 Milima iletee watu amani,
Na vilima vilete haki.
4 Acha atetee* watu wa hali ya chini katika taifa,
Acha aokoe wana wa maskini,
Na acha amuponde mupunjaji.+
6 Atakuwa kama mvua yenye kuanguka juu ya majani yenye yalikatwa,
Kama matone ya mvua yenye kumwangilia dunia maji.+
7 Katika siku zake mwenye haki atasitawi,*+
Na amani itakuwa nyingi+ mupaka wakati mwezi utakuwa hauko tena.
10 Wafalme wa Tarshishi na wa visiwa watalipa ushuru.+
Wafalme wa Sheba na wa Seba watatoa zawadi.+
11 Wafalme wote watainama mbele yake,
Na mataifa yote yatamutumikia.
12 Kwa maana ataokoa maskini mwenye kulilia musaada,
Pia mutu wa hali ya chini na mutu yeyote mwenye hana musaidizi.
14 Atawaokoa* katika ukandamizaji na katika jeuri,
Na damu yao itakuwa na samani mbele ya macho yake.
15 Aishi na kupewa zahabu ya Sheba.+
Sala ziendelee kutolewa kwa ajili yake,
Na abarikiwe muchana wote.
Watu wajipatie baraka kupitia yeye;+
Mataifa yote yamutangaze kuwa mwenye furaha.
Amina na Amina.
20 Huu ndio mwisho wa sala za Daudi, mwana wa Yese.+
KITABU CHA TATU
(Zaburi 73-89)
Muziki wa Asafu.+
73 Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale wenye kuwa safi katika moyo.+
2 Lakini mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kutoka katika njia;
Hatua zangu zilikuwa karibu kutereza.+
6 Kwa hiyo, kiburi ni mukufu wao wa shingo;+
Jeuri inawafunika kama nguo.
7 Mafanikio* yao yanafanya macho yao yavimbe;
Wamezidi mawazo ya moyo.
8 Wanachekelea na kusema mambo maovu.+
Kwa kiburi, wanaogopesha ili kukandamiza.+
9 Wanaongea kama vile wako juu kama mbingu,
Na ndimi zao zinatembea huku na huku zikijisifu katika dunia.
10 Kwa hiyo watu wake wanawaendea,
Na wanakunywa kutokana na maji yao mengi.
11 Wanasema: “Mungu anajua namna gani?+
Je, Mwenye Kuwa Juu Zaidi iko* kabisa na ujuzi?”
12 Ndiyo, hiyo ndiyo hali ya waovu, wenye sikuzote wanafurahia maisha.+
Wanaendelea kuongeza mali zao.+
13 Hakika nimesafisha moyo wangu bure
Na kunawa mikono yangu katika kukosa kuwa na hatia.+
16 Wakati nilijaribu kuelewa jambo hilo,
Lilinisumbua
17 Mupaka wakati niliingia katika patakatifu pakubwa pa Mungu,
Na nikatambua wakati wao wenye kuja.
18 Hakika unawatia kwenye udongo wenye kutereza.+
Unawafanya waanguke katika uharibifu wao.+
19 Wanaharibiwa bila kutazamia kabisa!+
Wanamalizika kwa kushitukia kabisa wakati wanafikia mwisho wao mubaya sana!
20 Kama ndoto wakati wa kuamuka, Ee Yehova,
Wakati utasimama, utatupilia mbali* sanamu yao.
22 Sikukuwa na akili na nilikosa uelewaji;
Nilikuwa kama munyama mwenye hana akili mbele yako.
25 Ni nani mwenye niko naye kule mbinguni?
Na sitamani kitu chochote katika dunia isipokuwa wewe tu.+
26 Mwili wangu na moyo wangu unaweza kuchoka,
Lakini Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu milele.+
27 Kwa kweli, wale wenye kujitenga mbali na wewe wataangamia.
Utaharibu* kila mutu mwenye anakuacha kwa sababu ya upotovu.*+
28 Lakini mimi, kumukaribia Mungu ni jambo la muzuri kwangu.+
Nimemufanya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova kuwa kimbilio langu,
Ili nitangaze kazi zako zote.+
74 Ee Mungu, sababu gani umetukataa milele?+
Sababu gani kasirani yako inawaka* juu ya kundi la malisho yako?+
Kumbuka Mulima Sayuni, kwenye umekaa.+
3 Elekeza hatua zako kwenye mabomoko ya kudumu.+
Adui ameharibu kila kitu katika mahali patakatifu.+
4 Maadui wako walinguruma ndani ya mahali pako pa mukutano.*+
Wamesimamisha bendera zao wenyewe ili zikuwe alama kule.
5 Walikuwa kama watu wenye kutumia mashoka ili kukata pori lenye miti yenye kusongamana.
6 Walivunja-vunja michongo yake yote+ kwa mashoka na fito za chuma.
7 Waliunguza patakatifu pako.+
Walichafua tabenakulo yenye kubeba jina lako, wakaiangusha chini.
8 Wao pamoja na uzao wao wamesema katika mioyo yao:
“Kila mahali pa mukutano pa Mungu* katika inchi lazima pateketezwe kwa moto.”
9 Hatuone alama yoyote;
Hakuna tena nabii yeyote,
Na hakuna hata mutu mumoja kati yetu mwenye anajua kama hali hii itaendelea mupaka wakati gani.
10 Ee Mungu, mupinzani ataendelea kuchokoza mupaka wakati gani?+
Je, adui ataendelea kukosea heshima jina lako milele?+
11 Sababu gani unazuia mukono wako, mukono wako wa kuume?+
Uuchomoe katika kifua chako* na kuwaharibu.
12 Lakini Mungu ni Mufalme wangu tangu zamani sana,
Yeye mwenye kufanya matendo ya wokovu katika dunia.+
14 Uliponda vichwa vya Leviatani;*
Ukapatia watu Leviatani kuwa chakula, wale wenye kukaa katika jangwa.
15 Ulipasua njia kwa ajili ya chemchemi na mito midogo;+
Ulikausha mito yenye inaendelea kutiririka.+
16 Muchana ni wako, na usiku pia.
Uliumba kitu cha kutoa mwangaza na jua.+
18 Kumbuka zihaka za adui, Ee Yehova,
Namna taifa pumbavu linakosea heshima jina lako.+
19 Usipatie wanyama wa pori uzima wa* njiwa-tetere wako.
Usisahau milele uzima wa watu wako wenye kuteseka.
20 Kumbuka lile agano,
Kwa maana sehemu za dunia zenye giza zimejaa makao ya jeuri.
21 Mutu mwenye amepondwa asigeuke na kuenda zake akiwa amepoteza tumaini;+
Watu wa hali ya chini na maskini wasifu jina lako.+
22 Simama, Ee Mungu, na utetee kesi yako ya hukumu.
Kumbuka namna wapumbavu wanakuchokoza muchana wote.+
23 Usisahau mambo yenye maadui wako wanasema.
Makelele ya wale wenye kukupinga yanapanda juu kila wakati.
Kwa kiongozi. Imepatanishwa
na muziki wa “Usiharibu.” Ya Asafu.+ Wimbo.
75 Tunakushukuru, Ee Mungu, tunakushukuru;
Jina lako liko karibu,+
Na watu wanatangaza kazi zako za ajabu.
2 Unasema: “Wakati ninaweka muda,
Ninahukumu kwa haki.
3 Wakati dunia na wakaaji wake wote waliyeyushwa,
Mimi ndiye nilifanya nguzo zake zikuwe imara.” (Sela)
4 Ninaambia wenye kujisifu, “Musijisifu,”
Na waovu, “Musiinue nguvu zenu.*
6 Kwa maana kuinuliwa hakutoke
Mashariki wala mangaribi wala kusini.
7 Kwa maana Mungu ni Muamuzi.+
Anashusha mutu mumoja na kuinua mwingine.+
8 Kwa maana kuko kikombe katika mukono wa Yehova;+
Divai inatoa pofu na imechanganywa kwa ukamili.
9 Lakini mimi, nitatangaza hilo milele;
Nitamuimbia Mungu wa Yakobo sifa.*
10 Kwa maana anasema: “Nitakata nguvu* zote za waovu.”
Lakini nguvu* za wenye haki zitainuliwa.
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Muziki wa Asafu.+ Wimbo.
3 Kule alivunja mishale ya upinde yenye kuwaka,
Ngao na upanga na silaha za vita.+ (Sela)
4 Unangaa sana;*
Uko na utukufu kuliko milima ya mawindo.
5 Vitu vya watu wenye moyo hodari vimenyanganywa.+
Wamelala usingizi;
Wapiganaji-vita wote hawakukuwa na uwezo.+
6 Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo,
Muendesha-gari na farasi pia wamelala usingizi muzito.+
7 Wewe peke yako ndiye mwenye kuogopesha sana.+
Na ni nani anaweza kuvumilia kasirani yako kali?+
8 Kutoka mbinguni ulitangaza hukumu;+
Dunia iliogopa na kunyamaza+
9 Wakati Mungu alisimama ili kuleta hukumu,
Ili kuokoa wapole wote wa dunia.+ (Sela)
10 Kwa maana kasirani kali ya mwanadamu itakuletea sifa;+
Na utajipamba kwa mabaki ya kasirani yao kali.
11 Muweke naziri zenu kwa Yehova Mungu wenu na kuzitimiza,+
Acha wote wenye kumuzunguka walete zawadi yao kwa woga.+
12 Atanyenyekeza kiburi* cha viongozi;
Yeye anaogopesha wafalme wa dunia.
Kwa kiongozi; juu ya Yedutuni.*
Ya Asafu.+ Muziki.
77 Kwa sauti yangu nitamulilia Mungu;
Nitamulilia Mungu, naye atanisikia.+
2 Katika siku ya taabu yangu ninamutafuta Yehova.+
Usiku ninamunyooshea mikono yangu bila kuacha.*
Siwezi* kufarijiwa.
4 Unashika kope zangu ili nisifunge macho;
Nimefazaika na siwezi kusema.
5 Mawazo yangu yanarudia katika siku za zamani sana,+
Miaka mingi ya zamani sana.
6 Wakati wa usiku ninakumbuka wimbo wangu;*+
Ninafikiri sana* katika moyo wangu;+
Ninatafuta* kwa bidii.
7 Je, Yehova atatutupa milele?+
Je, hakuna siku atatuonyesha tena wema wake?+
8 Je, upendo wake mushikamanifu utakoma milele?
Je, ahadi yake itakosa kutimia katika vizazi vyote?
9 Je, Mungu amesahau kuonyesha wema wake,+
Ao je, kasirani yake imekomesha rehema yake? (Sela)
10 Je, ni lazima niendelee kusema: “Hili ndilo jambo lenye kunisumbua:*+
Mwenye Kuwa Juu Zaidi amebadilisha musimamo wake kutuelekea”?*
11 Nitakumbuka kazi za Yah;
Nitakumbuka matendo yako ya ajabu ya zamani sana.
13 Ee Mungu, njia zako ni takatifu.
Ee Mungu, ni mungu gani mwenye kuwa mukubwa kama wewe?+
14 Wewe ndiye Mungu wa kweli, mwenye kutenda mambo ya ajabu.+
Umefunulia vikundi vya watu nguvu zako.+
16 Maji yalikuona, Ee Mungu,
Maji yalikuona na yakavurugika.+
Na maji yenye kuenda chini sana yakachafuka.
17 Mawingu yakamwanga maji.
Anga lenye mawingu likanguruma,
Na mishale yako ikaruka huku na kule.+
18 Sauti ya mungurumo wako+ ilikuwa kama magurudumu* ya gari;
Miangaza ya umeme wa radi iliangazia dunia yenye kuikaliwa na watu;*+
Dunia ilitikisika na kutetemeka.+
19 Njia yako ilipita katika bahari,+
Pito lako katika maji mengi;
Lakini alama za miguu yako hazingeweza kuonekana.
78 Musikilize sheria yangu,* watu wangu;
Mutege sikio lenu kwenye maneno ya kinywa changu.
2 Nitafungua kinywa changu kwa mezali.
Nitaleta maana ya vitendawili vya zamani sana.+
3 Mambo yenye tumesikia na kujua,
Yenye baba zetu wametuelezea,+
4 Hatutawaficha wana wao;
Tutaelezea kizazi chenye kuja+
Matendo ya Yehova yenye kustahili sifa na nguvu zake,+
Mambo ya ajabu yenye amefanya.+
5 Alitia kikumbusho katika Yakobo
Na kuweka sheria katika Israeli;
Aliamuru mababu zetu
Wajulishe watoto wao mambo hayo,+
6 Ili kizazi chenye kitafuata,
Watoto wenye hawajazaliwa, wayajue.+
Wao pia wataelezea watoto wao.+
7 Halafu watoto hao watatia tumaini lao katika Mungu.
8 Kisha hawatakuwa kama mababu zao,
Kizazi chenye kiko kichwa-nguvu na chenye kuasi,+
Kizazi chenye kilikuwa na moyo wenye kuyumba-yumba*+
Na chenye hakikukuwa na roho ya uaminifu kwa Mungu.
9 Waefraimu walikuwa wenye kubeba upinde,
Lakini walikimbia siku ya vita.
14 Aliwaongoza kupitia wingu wakati wa muchana
Na usiku wote kupitia mwangaza wa moto.+
15 Alipasua miamba katika jangwa,
Akawanywesha maji ya kutosha kama vile yanatoka katika maji yenye kuenda chini sana.+
16 Alifanya mito midogo itoke katika mwamba
Na kufanya maji yatiririke chini kama mito.+
17 Lakini waliendelea kumutendea zambi
Kwa kumuasi katika jangwa ule Mwenye Kuwa Juu Zaidi;+
18 Walishindana na* Mungu katika moyo wao+
Kwa kuomba kwa mukazo chakula chenye walitamani.*
19 Kwa hiyo wakasema mubaya juu ya Mungu,
Wakisema: “Je, Mungu anaweza kuandaa meza katika jangwa?”+
20 Angalia! Alipiga mwamba
Na hivyo maji yakatiririka na mito midogo ikajaa sana.+
“Je, anaweza pia kutupatia mukate,
Ao je, anaweza kupatia watu wake nyama?”+
21 Wakati Yehova aliwasikia, akakasirika sana;+
Moto+ ukawaka juu ya Yakobo,
Na kasirani yake ikawaka juu ya Israeli+
22 Kwa sababu hawakukuwa na imani katika Mungu;+
Hawakutegemea uwezo wake wa kuwaokoa.
23 Kwa hiyo akaamuru anga la juu lenye mawingu,
Na akafungua milango ya mbingu.
26 Alivumisha upepo wa mashariki katika mbingu
Na kwa nguvu zake akafanya upepo wa kusini uvume.+
27 Na akawanyeshea nyama kama mavumbi,
Ndege kama muchanga pembeni ya bahari.
28 Aliwaangusha katikati ya kambi yake,
Kuzunguka mahema yake pande zote.
29 Na walikula na kula kwa ulafi;
Aliwapatia kile walitamani.+
30 Lakini mbele watosheleze kikamili tamaa yao,
Wakati chakula kilikuwa kingali katika kinywa chao,
31 Kasirani kali ya Mungu ikawaka juu yao.+
Akaua wanaume wao wenye nguvu zaidi;+
Aliharibu wanaume vijana wa Israeli.
33 Kwa hiyo akakomesha siku zao kama vile ni pumuzi tu,+
Na miaka yao kwa mambo ya kushitukia yenye kuogopesha sana.
34 Lakini kila mara wakati alikuwa anawaua, walikuwa wanamutafuta;+
Walirudia na kumutafuta Mungu,
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao+
Na kwamba Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi alikuwa Mukombozi* wao.+
36 Lakini walijaribu kumudanganya kwa kinywa chao
Na kumuambia uongo kwa ulimi wao.
Mara nyingi alizuia hasira yake+
Kuliko kuchochea kasirani yake kali yote.
42 Hawakukumbuka nguvu zake,*
Siku yenye aliwaokoa* kutoka kwa mupinzani,+
43 Namna alionyesha alama zake kule Misri+
Na miujiza yake katika eneo la Soani,
44 Na namna alibadilisha mifereji ya Muto Nile kuwa damu+
Na hivyo hawangeweza kunywa maji ya mito yake midogo.
46 Mazao yao aliyapatia nzige wenye kula sana,
Matunda ya kazi yao ya nguvu akayapatia nzige wenye kupatikana kwa wingi.+
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya majiwe+
Na miti yao ya mikuyu kwa majiwe ya mvua.
49 Alimwanga juu yao kasirani yake yenye kuwaka,
Kasirani kali na hasira na taabu,
Vikundi vya malaika wenye kuleta musiba.
50 Alitayarisha njia kwa ajili ya kasirani yake.
Hakuwalinda wasikufe;*
Na aliwaua kwa ugonjwa wa kuambukiza.
51 Mwishowe alipiga na kuua wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+
Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu.
52 Kisha akapeleka watu wake inje kama kundi+
Na kuwaongoza katika jangwa kama kundi la wanyama.
54 Na aliwaleta katika eneo lake takatifu,+
Eneo hili lenye milima lenye mukono wake wa kuume ulijipatia.+
55 Alifukuza mataifa kutoka mbele yao;+
Akawagawia uriti kwa kamba ya kupimia;+
Alifanya makabila ya Israeli yakae katika makao yao.+
56 Lakini waliendelea kushindana na* Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi, na kumuasi;+
Hawakusikiliza vikumbusho vyake.+
57 Pia walipotoka na walikuwa wadanganyifu kama mababu zao.+
Hawakutegemeka kama vile upinde wenye kuregea.+
58 Waliendelea kumukasirisha kupitia mahali pao pa juu,+
Na walichochea kasirani yake kali* kupitia sanamu zao za kuchongwa.+
59 Mungu alisikia na kukasirika sana,+
Kwa hiyo akakataa kabisa Israeli.
61 Aliacha alama ya nguvu zake ipelekwe katika utekwa;
Utukufu wake utiwe katika mukono wa adui.+
62 Alitoa watu wake ili wauawe kwa upanga+
Naye akakasirikia sana uriti wake.
63 Moto uliteketeza kabisa wanaume wake vijana,
Na mabikira wake hawakuimbiwa nyimbo za arusi.*
65 Kisha Yehova akaamuka kama vile kutoka katika usingizi,+
Kama mwanaume mwenye nguvu+ mwenye anaamuka kisha divai kumutoka.
66 Naye akakimbiza maadui wake;+
Akawapatisha haya ya kudumu.
67 Alikataa hema ya Yosefu;
Hakuchagua kabila la Efraimu.
69 Alifanya patakatifu pake kuwa mahali pa kudumu kama mbingu,*+
Kama dunia yenye amefanya kuwa imara milele.+
70 Alimuchagua Daudi+ mutumishi wake
Na kumutosha katika mazizi* ya kondoo,+
71 Alimutosha katika kazi ya kuchunga kondoo-dike wenye kunyonyesha;
Akamufanya kuwa muchungaji juu ya Yakobo, watu wake,+
Na juu ya Israeli, uriti wake.+
Muziki wa Asafu.+
79 Ee Mungu, mataifa yamevamia uriti wako;+
Yamechafua hekalu lako takatifu;+
Yamegeuza Yerusalemu kuwa rundo la mabomoko.+
2 Yamepatia ndege wa mbinguni maiti za watumishi wako kuwa chakula
Na miili ya washikamanifu wako yameipatia wanyama wa pori wa dunia.+
3 Yamemwanga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,
Na hakuna mwenye alibakia ili kuwazika.+
4 Tumekuwa kitu cha kulaumiwa na majirani wetu;+
Wale wenye kutuzunguka wanatuzihaki na kutuchekelea.
5 Ee Yehova, utaendelea kukasirika sana mupaka wakati gani? Milele?+
Kasirani yako kali itaendelea kuwaka kama vile moto mupaka wakati gani?+
6 Mwanga kasirani yako kali juu ya mataifa yenye hayakujue
Na juu ya falme zenye haziitie jina lako.+
7 Kwa maana wamemumeza Yakobo
Na wamefanya inchi yake ikuwe ukiwa.+
8 Usituombe tutoe hesabu kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+
Utuonyeshe haraka rehema yako,+
Kwa maana tumeshushwa chini sana.
10 Sababu gani mataifa yaseme: “Mungu wao iko* wapi?”+
Acha ijulikane kati ya mataifa mbele ya macho yetu
Kwamba damu yenye ilimwangwa ya watumishi wako imelipiziwa kisasi.+
11 Sikia kilio cha maumivu cha mufungwa.+
Tumia nguvu zako kubwa* ili kulinda* wale wenye walihukumiwa kifo.*+
13 Kisha sisi, watu wako na kundi la malisho yako,+
Tutakushukuru milele;
Na tutatangaza sifa yako kizazi kwa kizazi.+
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Maua ya Mayungiyungi.” Kikumbusho. Ya Asafu.+ Muziki.
80 Ee Muchungaji wa Israeli, sikiliza,
Wewe mwenye kumuongoza Yosefu kama vile kundi.+
4 Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea mupaka wakati gani kuchukia* sala ya watu wako?+
5 Unawalisha machozi kama mukate,
Na unawanywesha machozi kupita kipimo.
6 Unaruhusu majirani wetu wagombane kwa sababu yetu;
Maadui wetu wanaendelea kutuchekelea namna wanapenda.+
7 Ee Mungu wa majeshi, uturudishe;
Uso wako utuangazie, ili tuokolewe.+
8 Ulifanya muzabibu+ uondoke Misri.
Ulifukuza mataifa na kupanda muzabibu huo.+
9 Ulitayarisha nafasi kwa ajili yake,
Nao ukatia mizizi na kujaa katika inchi.+
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,
Na mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
12 Sababu gani umebomoa kuta za majiwe za shamba la muzabibu huo,+
Na hivyo wale wote wenye wanapita karibu nao wanachuma matunda yake?+
13 Nguruwe wa pori wanauharibu,
Na wanyama wa pori wanaukula.+
14 Ee Mungu wa majeshi, rudia tafazali.
Angalia chini ukiwa mbinguni na uone!
Tunza muzabibu huu,+
15 Shina* lenye mukono wako wa kuume umepanda,+
Na uangalie mwana mwenye* umemutia nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
16 Umeteketezwa kwa moto,+ umekatwa.
Wanaangamia kwa kemeo lako.*
17 Mukono wako umutegemeze mwanaume mwenye kuwa kwenye mukono wako wa kuume,
Mwana wa binadamu mwenye umemutia nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
18 Kisha hatutageuka na kukuacha.
Linda uzima wetu, ili tuitie jina lako.
19 Ee Yehova Mungu wa majeshi, uturudishe;
Uso wako utuangazie, ili tuokolewe.+
Kwa kiongozi; juu ya Gititi.* Ya Asafu.+
81 Mumupigie Mungu, nguvu zetu, vigelegele vya shangwe.+
Mumupigie Mungu wa Yakobo vigelegele vya ushindi.
2 Muanzishe muziki na kukamata ngoma ya kidogo,*
Kinubi chenye mulio mutamu pamoja na chombo cha kamba.
3 Mupige baragumu wakati wa mwezi mupya,+
Wakati wa mwezi wenye kuenea, kwa ajili ya siku ya sikukuu yetu.+
4 Kwa maana ni agizo kwa ajili ya Israeli,
Sheria ya Mungu wa Yakobo.+
Nilisikia sauti* yenye sikutambua:
6 “Niliinua muzigo kutoka kwenye bega lake;+
Mikono yake iliwekwa huru kutoka kwenye kitunga.
Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba.*+ (Sela)
8 Musikie, watu wangu, na nitatoa ushahidi juu yenu.
Ee Israeli, kama tu utanisikiliza.+
9 Kati yenu, hakutakuwa mungu yeyote wa kigeni;
Na hamutamuinamia mungu wa kigeni.+
10 Mimi, Yehova, ni Mungu wako,
Mwenye alikutosha katika inchi ya Misri.+
Fungua wazi kinywa chako, na nitakijaza.+
11 Lakini watu wangu hawakusikiliza sauti yangu;
Israeli hakujitiisha kwangu.+
14 Ningetiisha haraka maadui wao;
Ningegeuza mukono wangu ili kushambulia wapinzani wao.+
15 Wale wenye kumuchukia Yehova watajikunja mbele yake,
Na mwisho* wao utakuwa wa milele.
Muziki wa Asafu.+
3 Mutetee* mutu wa hali ya chini na mwenye hana baba.+
Mutendee kwa haki mutu mwenye hana uwezo na maskini.+
4 Mumuokoe mutu wa hali ya chini na maskini;
Muwaokoe katika mukono wa muovu.”
8 Simama, Ee Mungu, na uhukumu dunia,+
Kwa maana mataifa yote ni yako.
Wimbo. Muziki wa Asafu.+
3 Kwa udanganyifu wanafanya mupango kwa uficho ili kushambulia watu wako;
Wanafanya mupango ili kushambulia watu wako wenye unapenda sana.*
5 Wanafanya mupango mubaya kwa umoja;*
Wamefanya mapatano* ili kukushambulia+—
6 Mahema ya Edomu na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+
9 Uwatendee kama vile ulitendea Midiani,+
Kama vile ulitendea Sisera na Yabini kwenye muto mudogo wa* Kishoni.+
10 Waliharibiwa kule En-dori;+
Wakakuwa mbolea juu ya udongo.
11 Fanya watu wao wenye vyeo wakuwe kama Orebu na Zeebu+
Na wakubwa* wao kama Zeba na Zalmuna,+
12 Kwa maana walisema: “Turiti inchi kwenye Mungu anakaa.”
13 Ee Mungu wangu, uwafanye wakuwe kama muchongoma wenye kupeperushwa,*+
Kama majani yenye kukauka yenye yanapeperushwa huku na huku na upepo.
14 Kama moto wenye unateketeza pori,
Kama mwali wa moto wenye unaunguza milima,+
15 Uwafuatilie basi kwa zoruba yako yenye upepo mukali+
Na kuwaogopesha sana kupitia upepo wako wa zoruba.+
17 Wapatishwe haya na kuogopeshwa sana milele;
Wafezeheshwe na kuangamia;
18 Wajue kwamba wewe, mwenye jina lako ni Yehova,+
Wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.+
Kwa kiongozi; juu ya Gititi.* Ya wana wa Kora.+ Muziki.
Moyo wangu na mwili wangu vinamupigia Mungu mwenye kuishi vigelegele vya shangwe.
3 Hata ndege anapata makao kule
Na mbaruwayu anajipatia chicha,*
Kwenye anatunza vitoto vyake
Karibu na mazabahu yako kubwa, Ee Yehova wa majeshi,
Mufalme wangu na Mungu wangu!
4 Wenye furaha ni wale wenye wanakaa katika nyumba yako!+
Wanaendelea kukusifu.+ (Sela)
5 Wenye furaha ni watu wenye wanapata nguvu kutoka kwako,+
Wenye mioyo yao imekazwa juu ya barabara kubwa.
6 Wakati wanapita katika Bonde la Mibaka,*
Wanalifanya kuwa mahali kwenye chemchemi;
Na mvua ya kwanza inalivalisha* baraka.
7 Wataendelea kutembea kutoka nguvu mupaka nguvu zaidi;+
Kila mumoja wao anaonekana mbele ya Mungu kule Sayuni.
8 Ee Yehova Mungu wa majeshi, sikia sala yangu;
Sikiliza, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)
10 Kwa maana siku moja katika viwanja vyako inapita siku elfu moja (1 000) mahali pengine popote!+
Ninachagua kusimama kwenye muingilio wa* nyumba ya Mungu wangu
Kuliko kukaa katika mahema ya uovu.
Yehova hatawaima jambo lolote la muzuri
Wale wenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu.+
12 Ee Yehova wa majeshi,
Mwenye furaha ni mutu mwenye anakutegemea.+
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki.
3 Ulizuia gazabu yako yote;
Uliacha kasirani yako kali.+
5 Je, utatukasirikia sana milele?+
Je, utaendelea kukasirika kizazi kwa kizazi?
6 Je, hautatupatia tena uzima
Ili watu wako washangilie katika wewe?+
7 Utuonyeshe upendo wako mushikamanifu, Ee Yehova,+
Na utupatie wokovu wako.
8 Nitasikiliza jambo lenye Mungu wa kweli Yehova anasema,
Kwa maana ataambia watu wake,+ washikamanifu wake, kuhusu amani,
Lakini wasianze tena kujiaminia kupita kiasi.+
9 Hakika wokovu wake uko karibu na wale wenye kumuogopa,+
Ili utukufu wake ukae katika inchi yetu.
10 Upendo mushikamanifu utakutana na uaminifu;
Haki pamoja na amani vitapatiana busu.+
11 Uaminifu utachipuka katika dunia,
Na haki itaangalia chini ikiwa mbinguni.+
13 Haki itatembea mbele yake+
Na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.
Sala ya Daudi.
2 Linda uzima wangu,* kwa maana niko mushikamanifu.+
Okoa mutumishi wako mwenye anakutegemea,
Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova, uko mwema+ na uko tayari kusamehe;+
Uko na upendo mwingi mushikamanifu kwa ajili ya wale wote wenye wanakuitia.+
6 Ee Yehova, sikiliza sala yangu;
Na usikilize vilio vyangu vya kuomba musaada.+
8 Hakuna mutu yeyote mwenye kuwa kama wewe kati ya miungu, Ee Yehova,+
Hakuna kazi zenye kuwa kama kazi zako.+
11 Unifundishe, Ee Yehova, kuhusu njia yako.+
Nitatembea katika kweli yako.+
Unganisha moyo wangu* ili niogope jina lako.+
12 Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote,+
Na nitatukuza jina lako milele,
13 Kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwingi kunielekea,
Na umeokoa uzima wangu* katika sehemu za chini kabisa za Kaburi.*+
14 Ee Mungu, watu wenye kimbelembele wanasimama ili kunishambulia;+
Kikundi cha wanaume wenye hawana huruma kinatafuta kuondoa uzima wangu,*
15 Lakini wewe, Ee Yehova, uko Mungu mwenye rehema na huruma,*
Haukasirike haraka na uko mwenye upendo mwingi mushikamanifu na uaminifu.*+
16 Geuka kunielekea na unionyeshe wema.+
Patia mutumishi wako nguvu zako,+
Na umuokoe mwana wa mutumwa wako mwanamuke.
17 Unionyeshe alama ya* wema wako,
Ili wale wenye kunichukia waione na kupatishwa haya.
Kwa maana wewe, Ee Yehova, uko musaidizi wangu na mufariji wangu.
Ya wana wa Kora.+ Muziki. Wimbo.
87 Musingi wa muji wake uko katika milima mitakatifu.+
2 Yehova anapenda milango mikubwa ya Sayuni+
Kuliko mahema yote ya Yakobo.
3 Mambo yenye utukufu yanasemwa kukuhusu, Ee muji wa Mungu wa kweli.+ (Sela)
4 Nitamuhesabia Rahabu+ na Babiloni kuwa kati ya wale wenye kunijua;*
Angalia, Ufilisti na Tiro, pamoja na Kushi.
Itasemwa: “Huyu alizaliwa kule.”
5 Na kuhusu Sayuni itasemwa:
“Kila mumoja wao alizaliwa kule.”
Na Mwenye Kuwa Juu Zaidi atamufanya kuwa imara kabisa.
6 Yehova atatangaza, wakati ataandikisha vikundi vya watu:
“Huyu alizaliwa kule.” (Sela)
7 Waimbaji+ na wale wenye kucheza dansi za muzunguko+ watasema:
“Chemchemi zangu zote ziko ndani yako.”*+
Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+ Kwa kiongozi; kwa mutindo wa Mahalati,* uimbwe kwa kubadilishana. Maskili* ya Hemani+ Mwezra.
88 Ee Yehova, Mungu wa wokovu wangu,+
Wakati wa muchana ninalia kwa sauti,
Na usiku ninakuja mbele yako.+
4 Tayari nimehesabiwa kati ya wale wenye kushuka katika shimo;*+
Nimekuwa mutu mwenye hana uwezo,*+
5 Mwenye ameachwa kati ya wafu
Kama watu wenye waliuawa ambao wanalala katika kaburi,
Wenye haukumbuke tena
Na wenye wametengwa mbali na utunzaji* wako.
6 Umenitia katika shimo lenye kuwa chini sana,
Sehemu zenye giza, katika abiso kubwa.
7 Kasirani yako kali inanilemea sana,+
Na unanilemea kupitia mawimbi yako yenye nguvu. (Sela)
8 Umefukuza wenye kunijua mbali sana na mimi;+
Umenifanya kuwa kitu chenye kuwachukiza.
Nimenaswa na siwezi kuponyoka.
9 Jicho langu limechoka kwa sababu ya mateso yangu.+
Ee Yehova, ninakuitia muchana wote;+
Ninakunyooshea mikono yangu.
10 Je, utatenda mambo ya ajabu kwa ajili ya wafu?
Je, wale wenye hawana uwezo katika kifo wanaweza kusimama ili kukusifu?+ (Sela)
11 Je, upendo wako mushikamanifu utatangazwa katika kaburi,
Uaminifu wako mahali pa uharibifu?*
12 Je, mambo yako ya ajabu yatajulikana katika giza
Ao haki yako katika inchi ya usahaulifu?+
14 Sababu gani, Ee Yehova, unanikataa?*+
Sababu gani unanificha uso wako?+
15 Tangu ujana wangu,
Nimeteseka na niko karibu kuangamia;+
Sihisi chochote kwa sababu ya mambo yenye kuogopesha yenye unaruhusu yanipate.
16 Kasirani yako yenye kuwaka inanilemea;+
Mambo yako yenye kuogopesha sana yananiharibu.
17 Yananizunguka kama maji muchana wote;
Yananizunguka kutoka pande zote.*
18 Umefukuza marafiki wangu na wenzangu mbali sana na mimi;+
Giza limekuwa mwenzangu.
89 Nitaimba kuhusu maonyesho ya Yehova ya upendo mushikamanifu milele.
Kwa kinywa changu nitajulisha vizazi vyote uaminifu wako.
2 Kwa maana nimesema: “Upendo mushikamanifu utajengwa* milele,+
Na umefanya uaminifu wako ukuwe imara kabisa kule mbinguni.”
4 ‘Nitafanya uzao wako ukuwe* imara kabisa+ milele,
Na nitajenga kiti chako cha ufalme kwa vizazi vyote.’”+ (Sela)
5 Mbingu zinasifu mambo yako ya ajabu, Ee Yehova,
Ndiyo, uaminifu wako katika kutaniko la watakatifu.
6 Kwa maana ni nani mbinguni mwenye anaweza kulinganishwa na Yehova?+
Ni nani kati ya wana wa Mungu+ mwenye kuwa kama Yehova?
7 Mungu ni mwenye kuogopwa sana katika baraza la* watakatifu;+
Yeye ni mukubwa na mwenye kuogopesha sana kwa wote wenye kumuzunguka.+
8 Ee Yehova Mungu wa majeshi,
Ni nani mwenye kuwa na nguvu kama wewe, Ee Yah?+
Uaminifu wako unakuzunguka.+
10 Umemuponda Rahabu+ kama mutu mwenye aliuawa.+
Kwa mukono wako wenye nguvu umesambaza maadui wako.+
14 Uadilifu* na haki ndio musingi wa kiti chako cha ufalme;+
Upendo mushikamanifu na uaminifu vinasimama mbele yako.+
15 Wenye furaha ni watu wenye wanajua vigelegele vya shangwe.+
Ee Yehova, wanatembea katika mwangaza wa uso wako.
16 Wanashangilia katika jina lako muchana wote,
Na katika haki yako wanainuliwa.
18 Kwa maana ngao yetu ni ya Yehova,
Mufalme wetu ni wa Mutakatifu wa Israeli.+
19 Wakati huo uliambia washikamanifu wako katika maono na kusema:
21 Mukono wangu utamutegemeza,+
Na mukono wangu utamutia nguvu.
22 Hakuna adui mwenye atamulipisha ushuru,
Na hakuna mwenye haiko mwenye haki mwenye atamukandamiza.+
23 Nitavunja maadui wake vipande-vipande ili wasikuwe tena mbele yake+
Na nitapiga na kuua wale wenye kumuchukia.+
24 Uaminifu wangu na upendo wangu mushikamanifu viko pamoja naye,+
Na katika jina langu nguvu zake zitainuliwa.*
26 Ataniambia kwa sauti: ‘Wewe ni Baba yangu,
Mungu wangu na Mwamba wa wokovu wangu.’+
28 Nitadumisha upendo wangu mushikamanifu kwa ajili yake milele,+
Na agano langu lenye nilifanya pamoja naye halitavunjika hata siku moja.+
30 Kama wana wake wanaacha sheria yangu
Na hawatembee kulingana na maagizo yangu,*
31 Kama wanavunja sheria zangu
Na hawashike amri zangu,
32 Basi nitapatia azabu kukosa kutii kwao* kwa kutumia fimbo+
Na kosa lao kwa kutumia viboko.
33 Lakini sitaacha hata kidogo kumutendea kwa upendo wangu mushikamanifu+
Wala sitakosa kutimiza ahadi yangu.*
35 Nimeapa katika utakatifu wangu, mara moja kwa wakati wote;
Sitamuambia Daudi uongo.+
37 Kama mwezi, kitafanywa kuwa imara kabisa milele
Kama shahidi muaminifu katika anga.” (Sela)
38 Lakini wewe mwenyewe umemutupa mbali na kumukataa;+
Umemukasirikia sana mutiwa-mafuta wako.
39 Umekataa kwa zarau agano lenye ulifanya na mutumishi wako;
Umechafua taji lake kwa kulitupa chini.
40 Umebomoa kuta zake zote za majiwe;*
Umefanya ngome yake kuwa mabomoko.
41 Wote wenye kupita karibu naye wamenyanganya vitu vyake;
Yeye ni kitu cha haya kwa majirani wake.+
43 Pia umesukumia upanga wake nyuma,
Na umemufanya asishinde katika vita.
44 Umekomesha utukufu wake
Na umetupa chini kiti chake cha ufalme.
45 Umefupisha siku za ujana wake;
Umemuvalisha haya. (Sela)
46 Ee Yehova, utaendelea kujificha mupaka wakati gani? Utajificha milele?+
Je, kasirani yako kali itaendelea kuwaka kama moto?
47 Kumbuka namna maisha yangu ni mafupi sana!+
Je, uliumba wanadamu wote bila kusudi?
48 Ni mwanadamu gani anaweza kuishi na asikufe hata siku moja?+
Je, anaweza kujiokoa* katika nguvu za Kaburi?* (Sela)
49 Yako wapi matendo yako ya zamani ya upendo mushikamanifu, Ee Yehova,
Yenye ulimuapia Daudi katika uaminifu wako?+
50 Kumbuka, Ee Yehova, zihaka zenye zilitupwa juu ya watumishi wako;
Namna ninalazimika kuvumilia* zihaka za vikundi vyote vya watu;
51 Namna maadui wako wametupa matusi, Ee Yehova;
Namna wametukana kila hatua ya mutiwa-mafuta wako.
52 Yehova asifiwe milele. Amina na Amina.+
KITABU CHA INE
(Zaburi 90-106)
Sala ya Musa, mutu wa
Mungu wa kweli.+
90 Ee Yehova, umekuwa makao yetu*+ katika vizazi vyote.
2 Mbele milima haijazaliwa
Ao mbele haujatokeza* dunia na inchi yenye kuzaa,+
Tangu milele mupaka milele, wewe ni Mungu.+
3 Unamufanya mwanadamu mwenye anaweza kufa arudie katika mavumbi;
Unasema: “Murudie, ninyi wana wa binadamu.”+
4 Kwa maana miaka elfu moja (1 000) mbele ya macho yako ni kama vile siku ya jana ikiisha kupita,+
Kama vile kesha moja la usiku.
9 Siku zetu zinafifia* kwa sababu ya kasirani yako kali;
Na miaka yetu inafikia mwisho kama sauti ya chini-chini.
10 Urefu wa maisha yetu ni miaka makumi saba (70),
Lakini imejaa taabu na huzuni;
Na inapita haraka, na tunaenda zetu.+
11 Ni nani anaweza kuelewa nguvu za hasira yako?
Kasirani yako kali ni kubwa kama woga wenye unastahili kuonyeshwa.+
13 Rudia, Ee Yehova!+ Hilo litaendelea mupaka wakati gani?+
Sikilia huruma watumishi wako.+
14 Utushibishe asubui kwa upendo wako mushikamanifu,+
Ili tupige vigelegele vya shangwe na kushangilia+ siku zetu zote.
15 Utufanye tushangilie kulingana na siku zenye umetutesa,+
Kwa kadiri ya miaka mingi yenye tumepata musiba.+
Ndiyo, fanya kazi ya mikono yetu ifanikiwe.*+
91 Mutu yeyote mwenye kukaa mahali pa siri pa Mwenye Kuwa Juu Zaidi+
Ataishi katika kivuli cha Mweza-Yote.+
3 Kwa maana atakuokoa katika mutego wa muwindaji wa ndege,
Katika ugonjwa wa kuambukiza wenye kuharibu.
Uaminifu wake+ utakuwa ngao kubwa+ na ukuta wa ulinzi.*
5 Hautaogopa mambo yenye kuogopesha sana ya usiku,+
Wala mushale wenye kuruka muchana,+
6 Wala ugonjwa wa kuambukiza wenye kuwinda kimya-kimya katika giza,
Wala uharibifu wenye kuharibu katikati ya muchana.
7 Elfu moja (1 000) wataanguka pembeni yako
Na elfu kumi (10 000) kwenye mukono wako wa kuume,
Lakini haitakukaribia wewe.+
9 Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”
Umemufanya Mwenye Kuwa Juu Zaidi kuwa makao yako;*+
10 Hakuna musiba wenye utakufikia,+
Na hakuna pigo lenye litakaribia hema yako.
13 Utakanyanga mwana-simba na nyoka-kobra;
Utamukanyangia chini simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo na nyoka mukubwa.+
14 Mungu alisema: “Kwa sababu ananipenda,* nitamuokoa.+
Nitamulinda kwa sababu anajua* jina langu.+
Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+
Nitamuokoa na kumutukuza.
Muziki. Wimbo wa siku ya Sabato.
92 Ni muzuri kumushukuru Yehova+
Na kuimbia jina lako sifa,* Ee Mwenye Kuwa Juu Zaidi,
2 Kutangaza upendo wako mushikamanifu+ asubui
Na uaminifu wako nyakati za usiku,
3 Kwa chombo cha kamba kumi (10) na kwa udi,
Kwa mulio mutamu wa kinubi.+
4 Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya matendo yako;
Kwa sababu ya kazi za mikono yako ninapiga vigelegele vya shangwe.
5 Kazi zako ni kubwa sana, Ee Yehova!+
Mawazo yako ni mazito sana!+
6 Mutu yeyote mwenye hana akili hawezi kuyajua;
Na hakuna mupumbavu mwenye anaweza kuelewa hili:+
7 Wakati waovu wanachipuka kama magugu*
Na wakati wakosaji wote wanasitawi,
Ni ili waharibiwe milele.+
8 Lakini wewe umeinuliwa milele, Ee Yehova.
9 Kwa kweli, angalia kwa furaha kushindwa kwa maadui wako, Ee Yehova,
Angalia namna maadui wako wataangamia;
Wakosaji wote watasambazwa.+
11 Macho yangu yataangalia kwa furaha kushindwa kwa maadui wangu;+
Masikio yangu yatasikia kuhusu kuanguka kwa watu waovu wenye kunishambulia.
12 Lakini wenye haki watasitawi kama muti wa mutende
Na watakuwa wakubwa kama mwerezi katika Lebanoni.+
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yehova;
Wanasitawi katika viwanja vya Mungu wetu.+
14 Hata wakati wa uzee* wataendelea kusitawi;+
Wataendelea kuwa na nguvu* na kuwa wabichi,+
15 Wakitangaza kwamba Yehova ni munyoofu.
Yeye ni Mwamba wangu,+ mwenye ndani yake hakuna ukosefu wa haki.
93 Yehova amekuwa Mufalme!+
3 Mito imekuwa na mawimbi makubwa, Ee Yehova,
Mito imekuwa na mawimbi makubwa na imenguruma;
Mito inaendelea kuwa na mawimbi makubwa na kutoa kishindo.
4 Iko* na nguvu kuliko sauti ya maji mengi,
Iko* na nguvu kuliko mawimbi makubwa ya bahari,+
Yehova ni mukubwa katika nafasi za juu.+
5 Vikumbusho vyako vinategemeka sana.+
Utakatifu unapamba* nyumba yako+ nyakati zote, Ee Yehova.
94 Ee Mungu wa kisasi, Yehova,+
Ee Mungu wa kisasi, angaza!
2 Simama, Ee Muamuzi wa dunia.+
Lipa wenye majivuno kile wanastahili.+
3 Waovu wataendelea mupaka wakati gani, Ee Yehova,
Waovu wataendelea kushangilia mupaka wakati gani?+
4 Wanasema maneno mengi yenye hayana maana na kuongea kwa kiburi;
Wakosaji wote wanajisifu.
5 Wanaponda watu wako, Ee Yehova,+
Na kukandamiza uriti wako.
6 Wanaua mujane na mukaaji mugeni,
Na kuua watoto wenye hawana baba.
8 Muelewe jambo hili, ninyi wenye hamuna akili;
Ninyi wapumbavu, ni wakati gani mutaonyesha ufahamu?+
9 Ule mwenye alifanya* sikio, je, hawezi kusikia?
Ule mwenye aliumba jicho, je, hawezi kuona?+
10 Ule mwenye kurekebisha mataifa, je, hawezi kukaripia?+
Yeye Ndiye anafundisha watu ujuzi!+
11 Yehova anajua mawazo ya wanadamu,
Kwamba ni pumuzi tu.+
12 Mwenye furaha ni mutu mwenye unarekebisha, Ee Yah,+
Mwenye unafundisha mambo yenye kuwa katika sheria yako,+
13 Ili kumupatia utulivu katika siku za musiba,
Mupaka wakati shimo litachimbwa kwa ajili ya waovu.+
15 Kwa maana hukumu itakuwa tena yenye haki,
Na wote wenye kuwa wanyoofu katika moyo wataifuata.
16 Ni nani atasimama ili kushambulia waovu kwa ajili yangu?
Ni nani atanitetea juu ya wakosaji?
18 Wakati nilisema: “Muguu wangu unatereza,”
Upendo wako mushikamanifu, Ee Yehova, uliendelea kunitegemeza.+
20 Je, kiti cha ufalme chenye upotovu kinaweza* kuungana na wewe
23 Atafanya matendo yao maovu yawarudilie.+
Atawaharibu* kupitia uovu wao wenyewe.
Yehova Mungu wetu atawaharibu.*+
95 Mukuje, tumupigie Yehova vigelegele vya shangwe!
Tumupigie vigelegele vya ushindi Mwamba wetu wa wokovu.+
3 Kwa maana Yehova ni Mungu mukubwa,
Mufalme mukubwa juu ya miungu mingine yote.+
4 Sehemu za chini kabisa za dunia ziko katika mukono wake;
Vichwa vya milima ni vyake.+
6 Mukuje, tuabudu na kuinama;
Tupige magoti mbele ya Yehova Mutengenezaji wetu.+
Leo kama munasikiliza sauti yake,+
8 Musifanye moyo wenu kuwa mugumu kama vile mulifanya kule Meriba,*+
Kama katika siku ya Masa* katika jangwa,+
9 Wakati mababu zenu walinijaribu;+
Wakanipima, hata kama walikuwa wameona kazi zangu.+
10 Kwa miaka makumi ine (40) nilichukizwa na kizazi hicho, na nikasema:
“Wao ni watu wenye kupotoka sikuzote katika mioyo yao;
Hawajafikia kujua njia zangu.”
11 Kwa hiyo niliapa katika kasirani yangu:
“Hawataingia katika pumuziko langu.”+
96 Mumuimbie Yehova wimbo mupya.+
Mumuimbie Yehova, dunia yote!+
2 Mumuimbie Yehova; musifu jina lake.
Mutangaze habari njema za wokovu wake siku kwa siku.+
4 Yehova ni mukubwa na anastahili kusifiwa sana.
Ni mwenye kuogopesha sana kuliko miungu mingine yote.
5 Miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu yenye haina mafaa yoyote,+
Lakini Yehova ndiye alifanya mbingu.+
7 Mumupatie Yehova kile chenye anastahili, ninyi familia za vikundi vya watu,
Mumupatie Yehova kile chenye anastahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
8 Mumupatie Yehova utukufu wenye jina lake linastahili;+
Mulete zawadi na muingie katika viwanja vyake.
10 Mutangaze kati ya mataifa: “Yehova amekuwa Mufalme!+
Dunia* imewekwa imara kabisa, haiwezi kuhamishwa.*
Atahukumu vikundi vya watu kwa haki.”*+
11 Mbingu zishangilie, na dunia ifurahi;
Bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza;+
12 Maeneo ya mashamba na vyote vyenye kuwa ndani yake vishangilie.+
Wakati uleule miti yote ya pori ipige vigelegele vya shangwe+
13 Mbele ya Yehova, kwa maana anakuja,*
Anakuja kuhukumu dunia.
97 Yehova amekuwa Mufalme!+
Dunia ifurahi.+
Visiwa vingi vishangilie.+
2 Mawingu na giza nzito vinamuzunguka pande zote;+
4 Umeme wake wa radi unaangazia inchi;
Dunia inauona na kutetemeka.+
6 Mbingu zinatangaza haki yake,
Na vikundi vyote vya watu vinaona utukufu wake.+
7 Acha wale wote wenye kutumikia sanamu yoyote ya kuchongwa wapatishwe haya,+
Wale wenye kujisifu kuhusu miungu yao yenye haina mafaa yoyote.+
Mumuinamie,* ninyi miungu yote.+
9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote;
Umeinuliwa juu zaidi kuliko miungu mingine yote.+
10 Enyi wenye kumupenda Yehova, muchukie mambo ya mubaya.+
11 Mwangaza umeangazia wenye haki+
Na shangwe imeangazia wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.
12 Mushangilie katika Yehova, ninyi wenye haki,
Na mushukuru jina lake takatifu.*
Muziki.
Mukono wake wa kuume, mukono wake mutakatifu, umeleta wokovu.*+
3 Amekumbuka upendo wake mushikamanifu na uaminifu wake kuelekea nyumba ya Israeli.+
Miisho yote ya dunia imeona wokovu* wa Mungu wetu.+
4 Mumupigie Yehova vigelegele vya ushindi, dunia yote.
Muchangamuke na mupige vigelegele vya shangwe na kuimba sifa.*+
5 Mumuimbie Yehova sifa* kwa kinubi,
Kwa kinubi na wimbo mutamu.
6 Kwa tarumbeta na sauti ya baragumu,+
Mupige vigelegele vya ushindi mbele ya Mufalme, Yehova.
7 Acha bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza,
Dunia* na wale wenye kukaa ndani yake.
8 Mito ipige mikono;
Milima ipige pamoja vigelegele vya shangwe+
9 Mbele ya Yehova, kwa maana anakuja* kuhukumu dunia.
99 Yehova amekuwa Mufalme.+ Acha vikundi vya watu vitetemeke.
Anakaa akiwa mufalme juu ya* makerubi.+ Acha dunia itikisike.
3 Acha wasifu jina lako kubwa,+
Kwa maana ni lenye kuogopesha sana na liko takatifu.
4 Yeye ni mufalme mwenye nguvu ambaye anapenda haki.+
Umefanya mambo manyoofu yakuwe imara kabisa.
Umeleta haki na uadilifu*+ katika Yakobo.
6 Musa na Haruni walikuwa kati ya makuhani wake,+
Na Samweli alikuwa kati ya wale wenye walikuwa wanaitia jina lake.+
Walikuwa wanamuita Yehova,
Na alikuwa anawajibu.+
7 Alikuwa anasema nao kutoka katika nguzo ya wingu.+
Walishika vikumbusho vyake na agizo lenye aliwapatia.+
8 Ee Yehova Mungu wetu, uliwajibu.+
9 Mumutukuze Yehova Mungu wetu+
Na muiname* mbele ya mulima wake mutakatifu,+
Kwa maana Yehova Mungu wetu ni mutakatifu.+
Muziki wa shukrani.
100 Mumupigie Yehova vigelegele vya ushindi, dunia yote.+
2 Mumutumikie Yehova kwa furaha.+
Muingie mbele yake kwa vigelegele vya shangwe.
3 Mujue* kwamba Yehova ni Mungu.+
Yeye ndiye alituumba, na sisi tuko mali yake.*+
Tuko watu wake na kondoo wa malisho yake.+
Mumushukuru yeye; musifu jina lake.+
5 Kwa maana Yehova ni mwema;+
Upendo wake mushikamanifu unadumu milele,
Na uaminifu wake katika vizazi vyote.+
Ya Daudi. Muziki.
101 Nitaimba kuhusu upendo mushikamanifu na haki.
Nitakuimbia sifa,* Ee Yehova.
2 Nitatenda kwa busara na bila lawama.*
Utakuja kwangu wakati gani?
Nitatembea kwa uaminifu-mushikamanifu wa moyo+ ndani ya nyumba yangu.
3 Sitatia mbele ya macho yangu kitu chenye hakina mafaa yoyote.
Ninachukia matendo ya wale wenye kukengeuka na kuacha mambo yenye kuwa sawa;+
Sitashirikiana nao hata kidogo.*
4 Moyo wenye kupotoka uko mbali na mimi;
Sitakubali* mambo ya mubaya.
Mutu yeyote mwenye kuwa na macho yenye kiburi na moyo wenye majivuno,
Sitamuvumilia.
6 Nitaangalia waaminifu wa dunia,
Ili wakae pamoja na mimi.
Ule mwenye kutembea bila lawama* atanitumikia.
7 Hakuna mutu yeyote mudanganyifu mwenye atakaa katika nyumba yangu,
Na hakuna muongo yeyote mwenye atasimama mbele yangu.*
Sala ya mutu mwenye kukandamizwa wakati amepoteza tumaini*
na anamwanga hangaiko lake
mbele ya Yehova.+
2 Usinifiche uso wako wakati niko katika taabu.+
3 Kwa maana siku zangu zinaisha kama moshi,
Na mifupa yangu imeungua na kuwa myeusi kama jiko.+
4 Moyo wangu umepigwa kama majani na umekauka,+
Kwa maana ninasahau kula chakula changu.
6 Ninafanana na mwari wa jangwa;
Niko kama bundi mudogo kati ya mabomoko.
7 Ninalala bila kupata usingizi;*
Niko kama ndege mwenye kuwa peke yake kwenye sehemu ya juu ya nyumba.+
8 Maadui wangu wananichokoza muchana wote.+
Wale wenye kunichekelea* wanatumia jina langu kama laana.
9 Kwa maana ninakula majivu kama mukate,+
Na kinywaji changu kimechanganywa na machozi,+
10 Kwa sababu ya hasira yako na kasirani yako kali,
Kwa maana uliniinua juu ili tu unitupe pembeni.
13 Hakika utasimama na kuonyesha Sayuni rehema,+
Kwa maana ni wakati wa kuonyesha muji huo wema wako;+
Wakati wenye uliwekwa umefika.+
15 Mataifa yataogopa jina la Yehova,
Na wafalme wote wa dunia wataogopa utukufu wako.+
18 Hili limeandikwa kwa ajili ya kizazi cha siku zenye kuja,+
Ili watu wenye bado hawajazaliwa* wamusifu Yah.
19 Kwa maana anaangalia chini akiwa katika nafasi yake takatifu ya juu,+
Akiwa mbinguni Yehova anaona dunia,
20 Ili asikie kilio cha maumivu cha mufungwa,+
Ili aweke huru wale wenye walihukumiwa kifo,+
21 Ili jina la Yehova litangazwe katika Sayuni+
Na sifa yake katika Yerusalemu,
22 Wakati vikundi vya watu na falme
Wanakusanyika pamoja ili kumutumikia Yehova.+
23 Alininyanganya nguvu zangu mbele ya wakati;
Alifupisha siku zangu.
24 Nilisema: “Ee Mungu wangu,
Usiniharibu nikiwa katikati ya maisha yangu,
Wewe mwenye miaka yako inadumu katika vizazi vyote.+
26 Hizo zitaangamia, lakini wewe utaendelea kuwa;
Zote zitazeeka kama vile nguo.
Utazibadilisha kama vile nguo, na zitapita.
27 Lakini wewe ni uleule, na miaka yako haitafikia mwisho hata siku moja.+
28 Watoto wa watumishi wako watakaa kwa usalama,
Na uzao wao utafanywa kuwa imara kabisa mbele yako.”+
Ya Daudi.
103 Acha nimusifu* Yehova;
Acha kila kitu chenye kuwa ndani yangu kisifu jina lake takatifu.
3 Anasamehe makosa yako yote+
Na anaponyesha magonjwa yako yote;+
4 Anaokoa uzima wako kutoka katika shimo*+
Na anakuvalisha taji la upendo wake mushikamanifu na rehema.+
5 Anakushibisha kwa vitu vya muzuri+ maisha yako yote,
Na hivyo ujana wako unafanywa upya kama ule wa tai.+
11 Kwa maana kama vile mbingu ziko juu kuliko dunia,
Ni vile upendo wake mushikamanifu uko mwingi kuelekea wale wenye kumuogopa.+
12 Kama vile mahali jua linatokea kuko mbali sana na mahali jua linashukia,
Ni vile ametia zambi zetu mbali sana na sisi.+
13 Kama vile baba anaonyesha wana wake rehema,
Ni vile Yehova ameonyesha rehema wale wenye kumuogopa.+
15 Kuhusu mwanadamu mwenye anaweza kufa, siku zake ziko kama za majani;+
Anachanuka kama ua la shamba.+
16 Lakini wakati upepo unavuma, haliko tena,
Kama vile halijapata kuwa pale.*
17 Lakini upendo mushikamanifu wa Yehova ni wa umilele wote*
Kuelekea wale wenye kumuogopa,+
Na haki yake kuelekea watoto wa watoto wao,+
18 Kuelekea wale wenye kushika agano lake+
Na wale wenye kuwa waangalifu ili kushika maagizo yake.
19 Yehova amefanya kiti chake cha ufalme kikuwe imara kabisa mbinguni;+
Na ufalme wake unatawala juu ya kila kitu.+
22 Mumusifu Yehova, kazi zake zote,
Mahali pote penye anatawala.*
Nafsi yangu yote imusifu Yehova.
Ee Yehova Mungu wangu, uko mukubwa sana.+
3 Anajenga nguzo za vyumba vyake vya juu katika maji yenye kuwa juu,*+
Anafanya mawingu kuwa gari lake,+
Akienda juu ya mabawa ya upepo.+
4 Anafanya malaika wake kuwa roho,
Watumishi wake kuwa moto wenye kuteketeza.+
6 Uliifunika kwa maji yenye kuenda chini sana kama kwa nguo.+
Maji yalisimama juu ya milima.
7 Kwa kemeo lako yalikimbia;+
Kwa sauti ya mungurumo wako yalikimbia kwa woga mukubwa
8 —Milima ilipanda+ na mabonde yakashuka—
Mahali kwenye ulifanya kwa ajili yake.
9 Uliweka mupaka wenye hayapaswe kuvuka,+
Ili yasifunike dunia tena hata siku moja.
10 Anatuma chemchemi katika mabonde;
Kati ya milima zinatiririka.
11 Zinapatia maji wanyama wote wa pori;
Punda wa pori wanakata kiu yao.
12 Juu yake ndege wa anga wanakaa;
Wanaimba katikati ya majani mengi.
13 Anamwangilia milima maji ya vyumba vyake vya juu.+
Dunia inashiba matunda ya kazi zako.+
14 Anaotesha majani kwa ajili ya ngombe
Na mimea ili wanadamu waitumie,+
Ili kukomalisha chakula juu ya udongo
15 Na divai yenye inafanya moyo wa mwanadamu ufurahi,+
Mafuta yenye inafanya uso ungae,
Na mukate wenye unategemeza moyo wa mwanadamu mwenye anaweza kufa.+
16 Miti ya Yehova imeshiba,
Mierezi ya Lebanoni yenye alipanda,
17 Kwenye ndege wanatengeneza chicha.*
Makao ya korongo+ ni miti ya miberoshi.
19 Amefanya mwezi ili uonyeshe nyakati zenye ziliwekwa;
Jua linajua muzuri wakati wa kushuka.+
20 Unaleta giza, na usiku unaingia,+
Wakati wanyama wote wa pori wanazunguka-zunguka.
22 Wakati jua linatokea,
Wanarudia na kulala katika mapango yao.
23 Mwanadamu anaenda kwenye kazi yake,
Na anafanya kazi kwa jasho mupaka mangaribi.
24 Kazi zako ni nyingi sana, Ee Yehova!+
Umezifanya zote kwa hekima.+
Dunia imejaa vitu vyenye umefanya.
25 Kuko bahari, kubwa sana na pana,
Inajaa viumbe vyenye uzima vyenye havina hesabu, vidogo na vikubwa.+
27 Wote wanakungojea wewe
Ili uwapatie chakula chao kwa wakati wake.+
28 Wanakusanya kile unawapatia.+
Wakati unafungua mukono wako, wanashiba vitu vya muzuri.+
29 Wakati unaficha uso wako, wanavurugika.
Kama unaondoa roho yao, wanakufa na kurudia katika mavumbi.+
31 Utukufu wa Yehova utadumu milele.
Yehova atashangilia katika kazi zake.+
32 Anaangalia dunia, na inatetemeka;
Anagusa milima, na inatoa moshi.+
33 Nitamuimbia Yehova+ maisha yangu yote;
Nitamuimbia Mungu wangu sifa* wakati wote wenye nitakuwa muzima.+
34 Mawazo yangu yamupendeze.*
Nitashangilia katika Yehova.
Acha nimusifu* Yehova. Mumusifu Yah!*
3 Mujisifu juu ya jina lake takatifu.+
Mioyo ya wale wenye kumutafuta Yehova ishangilie.+
4 Mumutafute Yehova+ na nguvu zake.
Mutafute uso* wake bila kuacha.
5 Mukumbuke kazi za ajabu zenye amefanya,
Miujiza yake na hukumu zenye ametangaza,+
6 Ninyi uzao wa* Abrahamu mutumishi wake,+
Ninyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+
7 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+
Hukumu zake ziko katika dunia yote.+
8 Anakumbuka agano lake milele,+
Ahadi yenye alitoa,* mupaka vizazi elfu,+
9 Agano lenye alifanya pamoja na Abrahamu,+
Na kiapo chenye alimuapia Isaka,+
10 Chenye aliweka kuwa amri kwa Yakobo
Na kuwa agano la kudumu kwa Israeli,
11 Akisema, “Nitakupatia inchi ya Kanaani+
Kuwa uriti wenu wenye muligawiwa.”+
12 Ilikuwa vile wakati walikuwa hesabu kidogo,+
Ndiyo, kidogo sana, na walikuwa wageni katika inchi.+
13 Walitembea-tembea kutoka taifa moja mupaka taifa lingine,
Kutoka ufalme mumoja mupaka kikundi kingine cha watu.+
14 Hakumuruhusu mutu yeyote awakandamize,+
Lakini kwa sababu yao alikaripia wafalme,+
15 Kwa kusema, “Musiguse watiwa-mafuta wangu,
Na musitendee manabii wangu jambo lolote la mubaya.”+
17 Alituma mutu mumoja awatangulie
Mwenye aliuzishwa ili kuwa mutumwa, Yosefu.+
18 Walifunga* miguu yake kwa pingu,+
Shingo yake ilitiwa katika vyuma;*
19 Mupaka wakati neno lake lilitimia,+
Neno la Yehova ndilo lilimusafisha.
20 Mufalme alituma watu wamufungue,+
Mutawala wa vikundi vya watu alimuweka huru.
21 Akamufanya kuwa bwana wa nyumba yake,
Mutawala juu ya mali zake zote,+
22 Ili akuwe na mamlaka juu ya* wakubwa wake namna alipenda*
Na ili afundishe wazee wake hekima.+
23 Kisha Israeli akaingia Misri,+
Na Yakobo akakaa akiwa mugeni katika inchi ya Hamu.
24 Mungu alifanya watu wake waongezeke sana;+
Aliwafanya wakuwe na nguvu kuliko wapinzani wao,+
25 Aliruhusu mioyo yao ibadilike ili wachukie watu wake,
Ili wafanye mupango mubaya juu ya watumishi wake.+
27 Walifanya alama zake kati yao,
Miujiza yake katika inchi ya Hamu.+
28 Alituma giza na inchi ikakuwa giza;+
Hawakuasi maneno yake.
29 Alibadilisha maji yao kuwa damu
Na kuua samaki wao.+
30 Inchi yao ikajaa vyura,+
Hata katika vyumba vya kifalme.
31 Aliagiza mainzi wavamie
Na imbu katika maeneo yao yote.+
33 Alipiga mizabibu yao na miti yao ya tini
Na kuvunja-vunja miti ya eneo lao.
34 Alisema nzige wavamie,
Nzige wadogo wenye hawakukuwa na hesabu.+
35 Walikula mimea yote katika inchi,
Na walimeza mazao ya udongo.
36 Kisha akapiga na kuua kila muzaliwa wa kwanza katika inchi yao,+
Mwanzo wa nguvu zao za uzazi.
37 Alipeleka watu wake inje wakiwa na feza na zahabu;+
Na hakuna mutu yeyote kati ya makabila yake mwenye alijikwaa.
39 Alitandika wingu ili liwafunike+
Na moto ili utoe mwangaza wakati wa usiku.+
42 Kwa maana alikumbuka ahadi takatifu yenye alimupatia Abrahamu mutumishi wake.+
43 Kwa hiyo akatosha watu wake wakishangilia,+
Alitosha wachaguliwa wake kwa vigelegele vya shangwe.
44 Aliwapatia inchi za mataifa;+
Waliriti vitu vyenye vikundi vingine vya watu vilikuwa vimetumika sana ili kuvitengeneza,+
45 Ili watii maagizo yake+
Na kushika sheria zake.
Mumusifu Yah!*
2 Ni nani anaweza kutangaza kikamili matendo ya Yehova yenye nguvu
Ao kutangaza matendo yake yote yenye kustahili sifa?+
3 Wenye furaha ni wale wenye wanatenda haki,
Wenye sikuzote wanatenda mambo yenye kuwa sawa.+
4 Unikumbuke, Ee Yehova, wakati unaonyesha watu wako wema.*+
Unitunze kupitia matendo yako ya wokovu,
5 Ili nifurahie wema wenye unaonyesha wachaguliwa wako,+
Ili nishangilie pamoja na taifa lako,
Ili nikusifu kwa majivuno* pamoja na uriti wako.
7 Mababu zetu kule Misri hawakuona kazi zako za ajabu kuwa za maana.*
Hawakukumbuka upendo wako mwingi mushikamanifu,
Lakini waliasi kwenye bahari, pembeni ya Bahari Nyekundu.+
9 Alikemea Bahari Nyekundu, na ikakauka;
Aliwaongoza katika sehemu za chini kabisa kama vile katika jangwa;+
10 Aliwaokoa kutoka katika mukono wa adui yao+
Na aliwakomboa kutoka katika mukono wa adui.+
13 Lakini walisahau haraka mambo yenye alifanya;+
Hawakungojea shauri lake.
17 Kisha dunia ikafunguka na kumumeza Datani
Na kufunika wale wenye walikusanyika pamoja na Abiramu.+
18 Moto uliwaka kati ya kikundi chao;
Mwali wa moto uliteketeza waovu.+
19 Walitengeneza kitoto-dume cha ngombe kule Horebu
Na kuinamia sanamu ya metali;*+
20 Pa nafasi ya utukufu wangu
Walitia mufano wa ngombe-dume mwenye kula majani.+
21 Walimusahau Mungu+ Mwokozi wao,
Mwenye alifanya mambo makubwa katika Misri,+
22 Kazi za ajabu katika inchi ya Hamu,+
Matendo yenye kuogopesha sana kwenye Bahari Nyekundu.+
23 Alikuwa karibu kuagiza waharibiwe,
Lakini Musa, muchaguliwa wake, akamulilia*
Ili kuzuia kasirani yake yenye kuharibu.+
26 Kwa hiyo akainua mukono wake na kuapa kuwahusu
Kwamba angefanya waanguke katika jangwa;+
27 Angefanya wazao wao waanguke kati ya mataifa,
Na angewasambaza katika inchi mbalimbali.+
30 Lakini wakati Finehasi alisimama na kuingilia kati,
Pigo hilo likasimamishwa.+
31 Na jambo hilo likahesabiwa kwake kuwa haki
Katika vizazi vyote milele.+
33 Walitia uchungu roho yake,
Naye akaongea bila kufikiri kupitia midomo yake.+
37 Walikuwa wanatoa watoto wao wanaume kuwa zabihu
Na watoto wao wanamuke kwa pepo wachafu.+
38 Waliendelea kumwanga damu yenye haina kosa,+
Damu ya watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke
Wenye walitoa kuwa zabihu kwa sanamu za Kanaani;+
Na inchi ikachafuliwa kupitia umwangaji wa damu.
39 Wakakuwa wachafu kwa sababu ya kazi zao;
Walifanya ukahaba wa kiroho kupitia matendo yao.+
40 Kwa hiyo kasirani ya Yehova ikawaka juu ya watu wake,
Na akachukia sana uriti wake.
42 Maadui wao waliwakandamiza,
Na wakatiishwa chini ya nguvu zao.*
43 Aliwaokoa mara nyingi,+
Lakini walikuwa wanaasi na kukosa kutii,+
Na walikuwa wanashushwa chini kwa sababu ya kosa lao.+
45 Kwa ajili yao alikuwa anakumbuka agano lake,
Na alikuwa anasikia huruma,* akichochewa na upendo wake mwingi mushikamanifu.+
46 Alikuwa anawafanya wasikiliwe huruma
Na wale wote wenye waliwakamata mateka.+
47 Utuokoe, Ee Yehova Mungu wetu,+
Na kutukusanya kutoka katika mataifa+
Ili tushukuru jina lako takatifu
Na acha watu wote waseme, “Amina!”*
Mumusifu Yah!*
KITABU CHA TANO
(Zaburi 107-150)
2 Acha wale wenye walikombolewa* na Yehova waseme jambo hilo,
Wale wenye alikomboa katika mukono wa* mupinzani,+
3 Wale wenye alikusanya pamoja kutoka katika inchi mbalimbali,+
Kutoka mashariki na kutoka mangaribi,*
Kutoka kaskazini na kutoka kusini.+
4 Walitanga-tanga katika nyika, katika jangwa;
Hawakupata njia ya kuenda katika muji kwenye wangeweza kuishi.
5 Walikuwa na njaa na kiu;
Walizimia* kwa sababu ya kuchoka sana.
8 Watu wamushukuru Yehova+ kwa sababu ya upendo wake mushikamanifu
Na kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.+
10 Wamoja kati yao walikuwa wanaishi katika giza nzito sana,
Wafungwa katika mateso na vyuma.
11 Kwa maana walikuwa wameasi neno la Mungu;
Hawakuheshimia shauri la Mwenye Kuwa Juu Zaidi.+
12 Kwa hiyo alinyenyekeza mioyo yao kupitia taabu;+
Walijikwaa, na hapakukuwa mutu yeyote wa kuwasaidia.
13 Walimuomba Yehova awasaidie katika taabu yao;
Akawaokoa katika shida yao.
14 Aliwatosha katika giza nzito sana,
Na kukata pingu zao.+
15 Watu wamushukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mushikamanifu+
Na kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.
18 Walipoteza hamu ya kula* vyakula vyote;
Walikaribia milango mikubwa ya kifo.
19 Walikuwa wanamuomba Yehova awasaidie katika taabu yao;
Na alikuwa anawaokoa katika shida yao.
20 Alikuwa anatuma neno lake na kuwaponyesha+
Na kuwaokoa katika mashimo yenye walikuwa wamenaswa ndani.
21 Watu wamushukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mushikamanifu
Na kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.
22 Acha watoe zabihu za shukrani+
Na kutangaza kazi zake kwa vigelegele vya shangwe.
23 Wale wenye kusafiri kwa mashua* juu ya bahari,
Wenye kufanya biashara yao juu ya maji mengi,+
24 Wameona kazi za Yehova
Na kazi zake za ajabu katika mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana;+
25 Namna zoruba yenye upepo mukali inainuka kwa neno lake,+
Na kuinua mawimbi ya bahari.
26 Wanapanda juu mupaka kwenye anga;
Wanashuka mupaka katika sehemu za chini kabisa.
Uhodari wao unayeyuka* kwa sababu ya musiba wenye kukaribia.
27 Wanayumba-yumba na kuenda huku na huku kama mulevi,
Na ufundi wao wote unakuwa hauna mafaa yoyote.+
28 Kisha wanamulilia Yehova kwa sauti kubwa katika taabu yao,+
Na anawaokoa katika shida yao.
29 Anatuliza zoruba yenye upepo mukali;
Mawimbi ya bahari yananyamaza.+
30 Wanashangilia wakati yanatulia,
Na anawaongoza mupaka kwenye bandari* yenye wanatamani.
31 Watu wamushukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mushikamanifu
Na kwa sababu ya kazi zake za ajabu zenye anatendea wana wa binadamu.+
33 Anageuza mito kuwa jangwa,
Na chemchemi za maji kuwa udongo wenye kukauka,+
34 Eneo lenye kuzaa kuwa eneo lenye chumvi ambalo limeachwa,+
Kwa sababu ya uovu wa wale wenye kukaa ndani yake.
35 Anageuza jangwa kuwa viziwa vya maji vyenye matete,
Na inchi kavu kuwa chemchemi za maji.+
38 Anawabariki na wanaongezeka sana;
Haache ngombe wao wapunguke.+
39 Lakini tena wanakuwa kidogo na kunyenyekezwa
Kwa sababu ya ukandamizaji, musiba, na huzuni.
40 Anamwanga zarau juu ya watu wenye vyeo
Na kuwafanya watange-tange kwenye hakuna njia katika maeneo yenye yameachwa.+
41 Lakini analinda* maskini ili wasikandamizwe+
Na kufanya familia zao zikuwe nyingi sana kama kundi.
42 Watu wanyoofu wanaona jambo hilo na kushangilia;+
Lakini watu wote wenye hawako wenye haki wanafunga vinywa vyao.+
43 Mutu yeyote mwenye kuwa na hekima atachunguza mambo hayo+
Na atafikiria kwa uangalifu matendo ya Yehova ya upendo mushikamanifu.+
Wimbo. Muziki wa Daudi.
108 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu.
Nitaimba na kupiga muziki kwa nafsi yangu yote.*+
2 Amuka, Ee chombo cha kamba; na wewe pia, Ee kinubi.+
Nitaamusha mapambazuko.*
3 Nitakusifu kati ya vikundi vya watu, Ee Yehova,
Na nitakuimbia sifa* kati ya mataifa.
4 Kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwingi, uko juu kama mbingu,+
Na uaminifu wako, unafika mupaka kwenye anga.
5 Uinuliwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako ukuwe juu ya dunia yote.+
6 Ili wapendwa wako waokolewe,
Utuokoe kupitia mukono wako wa kuume na unijibu.+
7 Mungu amesema katika utakatifu wake:*
8 Gileadi+ ni yangu, na Manase ni yangu,
Na Efraimu ni kofia ya chuma* ya kichwa changu;+
Yuda ni fimbo yangu ya kamanda.+
9 Moabu ni beseni yangu ya kunawia.+
Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+
Nitapiga vigelegele vya ushindi juu ya Ufilisti.”+
10 Ni nani atanipeleka katika muji wenye ngome?
Ni nani ataniongoza mupaka Edomu?+
11 Je, haiko wewe, Ee Mungu, mwenye umetukataa,
Mungu wetu, mwenye haende tena na majeshi yetu?+
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
109 Ee Mungu mwenye ninasifu,+ usibakie kimya.
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananifungulia vinywa vyao.
Wanasema kunihusu kwa ndimi za uongo;+
3 Wananizunguka na maneno ya chuki,
Na wananishambulia bila sababu.+
4 Wananipinga hata kama mimi ninawapenda;+
Lakini ninaendelea kusali.
5 Wananilipa ubaya kwa wema.+
Na chuki kwa upendo wangu.+
6 Weka mutu muovu juu yake;
Acha mupinzani* asimame kwenye mukono wake wa kuume.
9 Acha watoto* wake wakuwe bila baba,
Na bibi yake akuwe mujane.
10 Acha watoto* wake wakuwe watu wenye kutanga-tanga wakiomba-omba,
Wakitafuta chakula mbali na nyumba zao zenye kuharibiwa.
12 Mutu yeyote asimutendee kwa fazili,*
Na mutu yeyote asionyeshe wema watoto wake wenye hawana baba.
14 Yehova akumbuke kosa la mababu zake,+
Na zambi ya mama yake isifutwe.
15 Yehova aendelee kukumbuka mambo yenye wamefanya;
Na aondoe kumbukumbu lao lisikuwe tena katika dunia.+
16 Kwa maana hakukumbuka kuonyesha fazili,*+
Lakini aliendelea kumufuatilia mutu mwenye kukandamizwa,+ maskini, na mutu mwenye kuvunjika moyo
Ili amuue.+
17 Alipenda kulaani, kwa hiyo laana hiyo ikamupata;
Hakutaka kubariki, kwa hiyo hakupata baraka yoyote.
18 Alivalishwa laana kama nguo yake.
Na laana hizo zikamwangwa katika mwili wake kama maji,
Katika mifupa yake kama mafuta.
20 Hayo ndiyo malipo kutoka kwa Yehova ya mutu mwenye kunipinga+
Na ya wale wenye kusema mambo maovu juu yangu.*
21 Lakini wewe, Yehova Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi,
Tenda kwa faida yangu kwa ajili ya jina lako.+
Uniokoe, kwa sababu upendo wako mushikamanifu ni mwema.+
23 Ninapitilia mbali kama kivuli chenye kufifia;
Nimekungutwa kama nzige.
24 Magoti yangu yanaregea kwa sababu ya kufunga;
Mwili wangu umekonda, na ninaendelea kuwa muzaifu.*
25 Nimekuwa kitu chao cha kuchokoza.+
Wakati wananiona, wanatikisa vichwa vyao.+
26 Unisaidie, Ee Yehova Mungu wangu;
Uniokoe kupitia upendo wako mushikamanifu.
27 Wajue kwamba mukono wako ndio ulitenda hili;
Kwamba wewe, Ee Yehova, umetenda hili.
28 Watangaze laana, lakini wewe utoe baraka.
Wapatishwe haya wakati wanasimama ili kunishambulia,
Lakini mutumishi wako ashangilie.
30 Kinywa changu kitamusifu Yehova kwa bidii;
Nitamusifu mbele ya watu wengi.+
31 Kwa maana atasimama kwenye mukono wa kuume wa maskini
Ili amuokoe kutoka kwa wale wenye kumuhukumu.*
Ya Daudi. Muziki.
110 Yehova alimuambia Bwana wangu:
2 Yehova atanyoosha fimbo ya ufalme ya nguvu zako kutoka Sayuni, na kusema:
“Uende utawale katikati ya maadui wako.”+
3 Watu wako watajitoa kwa kujipendea katika siku ya jeshi lako.*
Katika utakatifu wenye kupendeza sana, kutoka katika tumbo la uzazi la mapambazuko,*
Uko na kikundi chako cha vijana kama vile matone ya umande.
4 Yehova ameapa kiapo na hatabadilisha mawazo yake:*
Ataponda kiongozi wa* inchi kubwa sana.*
7 Yeye* atakunywa maji ya muto mudogo wenye kuwa pembeni ya barabara.
Kwa hiyo, atainua juu kichwa chake.
א [Aleph]
Nitamusifu Yehova kwa moyo wangu wote+
ב [Beth]
Katika kikundi chenye kimekusanyika cha watu wanyoofu na katika kutaniko.
ג [Gimel]
ה [He]
ז [Zayin]
4 Anafanya kazi zake za ajabu zikumbukwe.+
ח [Heth]
Yehova ni mwenye huruma* na mwenye rehema.+
ט [Teth]
5 Anapatia chakula wale wenye kumuogopa.+
י [Yod]
Anakumbuka agano lake milele.+
כ [Kaph]
מ [Mem]
ס [Samekh]
פ [Pe]
9 Amepatia watu wake ukombozi.+
צ [Tsade]
Aliamuru kwamba agano lake linapaswa kudumu milele.
ק [Qoph]
Jina lake ni takatifu na ni lenye kuogopesha sana.+
ר [Resh]
10 Kumuogopa Yehova ni mwanzo wa hekima.+
ש [Sin]
Wale wote wenye kushika maagizo yake wanaonyesha ufahamu muzuri.+
ת [Taw]
Sifa yake inadumu milele.
א [Aleph]
ג [Gimel]
ה [He]
ז [Zayin]
4 Anaangazia watu wanyoofu kama mwangaza katika giza.+
ח [Heth]
Ni mwenye huruma,* mwenye rehema+ na mwenye haki.
ט [Teth]
5 Mambo yanamuendea muzuri mutu mwenye kukopesha kwa ukarimu.*+
י [Yod]
Anafanya mambo yake kwa haki.
כ [Kaph]
ל [Lamed]
Mwenye haki atakumbukwa milele.+
מ [Mem]
7 Hataogopa habari ya mubaya.+
נ [Nun]
Moyo wake uko imara, unamutegemea Yehova.+
ס [Samekh]
8 Moyo wake hauwezi kutikiswa;* haogope;+
ע [Ayin]
Mwishowe ataangalia kwa furaha kushindwa kwa maadui wake.+
פ [Pe]
9 Amegawa kwa wingi;* amepatia maskini.+
צ [Tsade]
Haki yake inadumu milele.+
ק [Qoph]
Nguvu zake mwenyewe zitainuliwa* kwa utukufu.
ר [Resh]
10 Muovu ataona na kukasirika.
ש [Shin]
Atasaga meno yake na kuyeyuka.
ת [Taw]
Tamaa za waovu zitaangamia.+
113 Mumusifu Yah!*
Mumusifu, ninyi watumishi wa Yehova,
Musifu jina la Yehova.
2 Jina la Yehova lisifiwe
Kuanzia sasa na milele.+
Anainua maskini kutoka kwenye rundo la majivu*+
8 Ili kumufanya akae pamoja na watu wenye vyeo,
Pamoja na watu wenye vyeo kati ya watu wake.
Mumusifu Yah!*
114 Wakati Israeli alitoka Misri,+
Wakati nyumba ya Yakobo ilitoka kati ya watu wenye kuzungumuza luga ya kigeni,
2 Yuda ikakuwa patakatifu* pake,
Israeli, eneo la utawala wake.+
4 Milima iliruka-ruka kama kondoo-dume,+
Vilima, kama wana-kondoo.
5 Ni nini ilikufanya ukimbie, Ee bahari?+
Sababu gani ulirudia nyuma, Ee Yordani?+
6 Sababu gani muliruka-ruka kama kondoo-dume, Enyi milima,
Kama wana-kondoo, enyi vilima?
7 Tetemeka, Ee dunia, kwa sababu ya Bwana,
Kwa sababu ya Mungu wa Yakobo,+
8 Mwenye anageuza mwamba kuwa kiziwa cha maji chenye matete,
Jiwe ngumu kuwa chemchemi za maji.+
115 Usitupatie sisi, Ee Yehova, usitupatie sisi,*
Lakini wewe upatie jina lako utukufu+
Kwa sababu ya upendo wako mushikamanifu na uaminifu wako.+
2 Sababu gani mataifa yaseme:
3 Mungu wetu iko* mbinguni;
Anafanya kila kitu chenye anapenda.
4 Sanamu zao ni feza na zahabu,
Kazi ya mikono ya mwanadamu.+
5 Ziko na kinywa, lakini haziwezi kusema;+
Ziko na macho, lakini haziwezi kuona;
6 Ziko na masikio, lakini haziwezi kusikia;
Ziko na pua, lakini haziwezi kunusa;
7 Ziko na mikono, lakini haziwezi kugusa;
Ziko na miguu, lakini haziwezi kutembea;+
Hazitoe sauti yoyote kwa koo yao.+
10 Ee nyumba ya Haruni,+ mumutegemee Yehova;
—Yeye ndiye musaada wao na ngao yao.
13 Atabariki wale wenye kumuogopa Yehova,
Wadogo na wakubwa.
18 Lakini sisi tutamusifu Yah
Kuanzia sasa na milele.
Mumusifu Yah!*
Nililemewa na taabu na huzuni.+
4 Lakini niliitia jina la Yehova:+
“Ee, Yehova, niokoe!”*
6 Yehova analinda wenye hawana uzoefu.+
Nilishushwa chini, na aliniokoa.
7 Acha nafsi* yangu ipumuzike tena,
Kwa maana Yehova amenitendea kwa fazili.
9 Nitatembea mbele ya Yehova katika inchi ya wazima.
10 Nilikuwa na imani, ndio maana nilisema;+
Niliteseka sana.
11 Sasa mimi, niliogopa na kusema:
“Kila mwanadamu ni muongo.”+
12 Nitamulipa Yehova nini
Kwa mema yote yenye amenitendea?
13 Nitainua kikombe cha wokovu,*
Na nitaitia jina la Yehova.
16 Ninakulilia, Ee Yehova,
Kwa maana mimi ni mutumishi wako.
Mimi ni mutumishi wako, mwana wa mutumwa wako mwanamuke.
Umenifungua katika vifungo vyangu.+
17 Nitakutolea zabihu ya shukrani;+
Nitaitia jina la Yehova.
18 Nitamutimizia Yehova naziri zangu+
Mbele ya watu wake wote,+
19 Katika viwanja vya nyumba ya Yehova,+
Katikati yako, Ee Yerusalemu.
118 Mumushukuru Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+
Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
2 Israeli aseme sasa:
“Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”
3 Watu wa nyumba ya Haruni waseme sasa:
“Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”
4 Wale wenye kumuogopa Yehova waseme sasa:
“Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”
6 Yehova iko* upande wangu; sitaogopa.+
Mwanadamu anaweza kunifanya nini?+
7 Yehova iko* upande wangu akiwa musaidizi wangu;*+
Nitaangalia kwa furaha kushindwa kwa wale wenye kunichukia.+
8 Ni muzuri kumukimbilia Yehova
Kuliko kutegemea wanadamu.+
9 Ni muzuri kumukimbilia Yehova
Kuliko kutegemea wakubwa.+
11 Yalinizunguka, ndiyo, yalinizunguka kabisa,
Lakini katika jina la Yehova,
Niliyafukuza.
12 Yalinizunguka kama nyuki,
Lakini yalizimwa haraka kama moto kati ya miiba.
Katika jina la Yehova,
Niliyafukuza.+
13 Nilisukumwa kwa nguvu* ili nianguke,
Lakini Yehova alinisaidia.
14 Yah ni mahali pangu pa kujificha na nguvu zangu,
Na amekuwa wokovu wangu.+
15 Sauti ya shangwe na wokovu*
Iko katika mahema ya wenye haki.
Mukono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
16 Mukono wa kuume wa Yehova unajiinua;
Mukono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
17 Sitakufa, hapana, nitaishi,
Ili nitangaze kazi za Yah.+
19 Munifungulie milango mikubwa ya haki;+
Nitaingia ndani na kumusifu Yah.
20 Huu ni mulango mukubwa wa Yehova.
Wenye haki wataingia kupitia mulango huo.+
21 Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+
Na ukakuwa wokovu wangu.
24 Hii ndiyo siku yenye Yehova amefanya;
Tutaifurahia na kuishangilia.
25 Yehova, utuokoe, tafazali, tunakulilia!
Yehova, utupatie ushindi, tafazali!
26 Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova;+
Tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yehova.
27 Yehova ni Mungu;
Anatupatia mwangaza.+
28 Wewe ni Mungu wangu, na nitakusifu;
Mungu wangu, nitakutukuza.+
א [Aleph]
119 Wenye furaha ni wale wenye hawana lawama* katika njia yao,
Wenye wanatembea katika sheria ya Yehova.+
3 Hawatende ukosefu wowote wa haki;
Wanatembea katika njia zake.+
4 Umeamuru
Kwamba maagizo yako yafuatwe kwa uangalifu.+
6 Halafu singepatishwa haya+
Wakati ninafikiria amri zako zote.
7 Nitakusifu kwa moyo munyoofu
Wakati ninajifunza hukumu zako za haki.
8 Nitashika masharti yako.
Usiniache kabisa hata siku moja.
ב [Beth]
9 Namna gani kijana anaweza kufanya njia yake iendelee kuwa safi?
Kwa kujilinda kulingana na neno lako.+
10 Ninakutafuta kwa moyo wangu wote.
Usiache nikengeuke na kuacha amri zako.+
12 Usifiwe, Ee Yehova;
Unifundishe masharti yako.
13 Kwa midomo yangu ninatangaza
Hukumu zote zenye umesema.
16 Ninapenda sana sheria zako.
Sitasahau neno lako.+
ג [Gimel]
17 Tendea mutumishi wako kwa fazili,
Ili niishi na kushika neno lako.+
18 Fungua macho yangu ili nione waziwazi
Mambo ya ajabu katika sheria yako.
19 Niko mugeni tu katika inchi.+
Usinifiche amri zako.
20 Ninaungua kwa kutamani sana*
Hukumu zako nyakati zote.
21 Unakemea wenye kimbelembele,
Watu wenye kulaaniwa wenye wanakengeuka na kuacha amri zako.+
22 Uniondolee* zarau na zihaka,
Kwa maana nimeshika vikumbusho vyako.
23 Hata wakati wakubwa wanakaa pamoja na kusema mambo ya mubaya juu yangu,
Mutumishi wako anafikiri sana juu ya* masharti yako.
ד [Daleth]
25 Ninalala* uso chini katika mavumbi.+
Linda uzima wangu kulingana na neno lako.+
26 Nilikuambia kuhusu njia zangu, na ukanijibu;
Unifundishe masharti yako.+
28 Nimekosa* usingizi kwa sababu ya huzuni.
Unitie nguvu kulingana na neno lako.
29 Uniondolee njia ya udanganyifu,+
Na unionyeshe wema kupitia sheria yako.
30 Nimechagua njia ya uaminifu.+
Ninatambua kwamba hukumu zako ziko sawa.
31 Ninashikamana na vikumbusho vyako.+
Ee Yehova, usiniache nikatishwe tumaini.*+
ה [He]
34 Unipatie uelewaji,
Ili niweze kushika sheria yako
Na kuifuata kwa moyo wangu wote.
36 Elekeza moyo wangu kwenye vikumbusho vyako,
Hapana kwenye faida ya uchoyo.+
37 Geuzia mbali macho yangu ili yasiangalie mambo yenye hayana mafaa yoyote;+
Linda uzima wangu katika njia yako.
39 Uniondolee haya yenye ninaogopa sana,
Kwa maana hukumu zako ziko muzuri.+
40 Angalia namna ninatamani sana maagizo yako!
Linda uzima wangu katika haki.
ו [Waw]
41 Acha nijionee upendo wako mushikamanifu, Ee Yehova,+
Wokovu wako kulingana na ahadi yako;*+
42 Kisha nitamujibu ule mwenye kunichokoza,
Kwa maana ninaweka tegemeo langu katika neno lako.
43 Usiondoe kabisa neno la kweli katika kinywa changu,
Kwa maana nimetumainia* hukumu yako.
44 Nitashika sheria yako kila wakati,
Milele na milele.+
47 Ninapenda sana amri zako,
Ndiyo, ninazipenda.+
ז [Zayin]
50 Hiyo ndiyo faraja yangu katika mateso yangu,+
Kwa maana neno lako limelinda uzima wangu.
53 Nimeshikwa na kasirani yenye kuwaka kwa sababu ya waovu,
Wenye kuacha sheria yako.+
54 Masharti yako ni nyimbo kwangu
Mahali popote kwenye ninaishi.*
55 Wakati wa usiku ninakumbuka jina lako, Ee Yehova,+
Ili niweze kushika sheria yako.
56 Nimezoea kufanya vile
Kwa sababu nimeshika maagizo yako.
ח [Heth]
59 Nimechunguza njia zangu,
Ili nirudishe miguu yangu kwenye vikumbusho vyako.+
60 Ninafanya haraka na sikawie
Kushika amri zako.+
62 Katikati ya usiku ninaamuka ili kukushukuru+
Kwa sababu ya hukumu zako za haki.
63 Niko rafiki ya wote wenye kukuogopa
Na ya wale wenye kushika maagizo yako.+
64 Upendo wako mushikamanifu, Ee Yehova, umejaza dunia;+
Unifundishe masharti yako.
ט [Teth]
65 Umemutendea muzuri mutumishi wako,
Ee Yehova, kulingana na neno lako.
66 Unifundishe akili ya muzuri na ujuzi,+
Kwa maana nimeweka tegemeo langu katika amri zako.
68 Wewe ni mwema+ na kazi zako ni za muzuri.
Unifundishe masharti yako.+
69 Wenye kimbelembele wananipakaa uongo,
Lakini ninashika maagizo yako kwa moyo wangu wote.
י [Yod]
73 Mikono yako ilinifanya na kuniumba.
Unipatie uelewaji,
Ili nijifunze amri zako.+
76 Tafazali acha upendo wako mushikamanifu+ unifariji,
Kulingana na ahadi yenye* ulimupatia mutumishi wako.
Lakini nitafikiri sana juu ya* maagizo yako.+
79 Wale wenye kukuogopa warudie kwangu,
Wale wenye kujua vikumbusho vyako.
כ [Kaph]
84 Mutumishi wako atangojea kwa siku ngapi?
Ni wakati gani utaleta hukumu juu ya wale wenye kunitesa?+
85 Wenye kimbelembele wananichimbia mashimo,
Wale wenye kuasi sheria yako.
86 Amri zako zote ni zenye kutegemeka.
Watu wananitesa bila sababu; unisaidie!+
87 Karibu waniharibu kutoka katika dunia,
Lakini sikuacha maagizo yako.
88 Linda uzima wangu kwa sababu ya upendo wako mushikamanifu,
Ili nishike vikumbusho vyenye umesema.
ל [Lamed]
90 Uaminifu wako ni katika vizazi vyote.+
Umeweka dunia imara kabisa, ili iendelee kusimama.+
91 Kwa hukumu zako vinadumu* mupaka leo,
Kwa maana vyote hivyo ni watumishi wako.
93 Sitasahau hata kidogo maagizo yako,
Kwa sababu kupitia hayo umelinda uzima wangu.+
95 Waovu wanangojea kuniharibu,
Lakini ninakazia uangalifu vikumbusho vyako.
מ [Mem]
97 Ninapenda sana sheria yako!+
Ninafikiri sana* juu yake muchana wote.+
98 Amri yako inanifanya kuwa na hekima kuliko maadui wangu,+
Kwa sababu niko nayo milele.
99 Niko na ufahamu mwingi kuliko walimu wangu wote,+
Kwa sababu ninafikiri sana juu ya* vikumbusho vyako.
100 Ninatenda kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,
Kwa sababu ninashika maagizo yako.
101 Ninakataa kutembea kwenye njia yoyote ya uovu,+
Ili nishike neno lako.
102 Sigeuke pembeni na kuacha hukumu zako,
Kwa maana umenifundisha.
104 Kwa sababu ya maagizo yako ninatenda kwa uelewaji.+
Ndiyo sababu ninachukia kila njia ya uongo.+
נ [Nun]
106 Nimeapa kiapo, na nitakitimiza,
Kwamba nitashika hukumu zako za haki.
107 Nimeteswa sana.+
Ee Yehova, linda uzima wangu kulingana na neno lako.+
111 Ninakamata vikumbusho vyako kuwa mali yangu ya kudumu,*
Kwa maana hivyo ni shangwe ya moyo wangu.+
112 Nimeazimia* kutii masharti yako
Nyakati zote, mupaka mwisho.
ס [Samekh]
115 Mukae mbali na mimi, ninyi waovu,+
Ili nishike amri za Mungu wangu.
118 Unakataa wale wote wenye kukengeuka na kuacha masharti yako,+
Kwa maana ni waongo na wadanganyifu.
119 Unatupilia mbali waovu wote wa dunia kama vile ni takataka yenye haina mafaa yoyote.+
Ndiyo sababu ninapenda vikumbusho vyako.
ע [Ayin]
121 Nimetenda mambo ya haki na ya uadilifu.*
Usiniache katika mukono wa wakandamizaji wangu!
122 Uhakikishe kama mutumishi wako iko* katika hali ya muzuri;
Wenye kimbelembele wasinikandamize.
125 Mimi ni mutumishi wako; unipatie uelewaji,+
Ili nijue vikumbusho vyako.
126 Wakati umefika wa Yehova kutenda,+
Kwa maana wamevunja sheria yako.
פ [Pe]
129 Vikumbusho vyako ni vya muzuri sana.
Ndiyo sababu ninavishika.*
132 Geuka kunielekea na unionyeshe wema,+
Kulingana na hukumu yako kuelekea wale wenye kupenda jina lako.+
134 Uniokoe* kutoka kwa wanadamu wenye kukandamiza,
Na nitashika maagizo yako.
136 Machozi yanatiririka kutoka katika macho yangu
Kwa sababu watu hawashike sheria yako.+
צ [Tsade]
138 Vikumbusho vyenye unatoa ni vya haki
Na vinategemeka kabisa.
139 Bidii yangu inanikula,+
Kwa sababu wapinzani wangu wamesahau maneno yako.
143 Hata kama ninapatwa na taabu na magumu,
Nitaendelea kupenda sana amri zako.
144 Haki ya vikumbusho vyako ni ya milele.
Unipatie uelewaji,+ ili niendelee kuishi.
ק [Qoph]
145 Ninakuita kwa moyo wangu wote. Unijibu, Ee Yehova.
Nitashika masharti yako.
146 Ninakuitia; uniokoe!
Nitashika vikumbusho vyako.
149 Sikiliza sauti yangu kwa sababu ya upendo wako mushikamanifu.+
Ee Yehova, linda uzima wangu kulingana na haki yako.
150 Watu wenye kujiingiza katika mwenendo wa haya* wananikaribia;
Wako mbali sana na sheria yako.
152 Zamani sana nilijifunza kuhusu vikumbusho vyako,
Kwamba umeviweka ili vidumu milele.+
ר [Resh]
153 Angalia mateso yangu na uniokoe,+
Kwa maana sijasahau sheria yako.
155 Wokovu uko mbali sana na waovu,
Kwa maana hawajatafuta masharti yako.+
156 Rehema yako ni kubwa, Ee Yehova.+
Linda uzima wangu kulingana na haki yako.
157 Wenye kunitesa na pia wapinzani wangu ni wengi;+
Lakini sijakengeuka na kuacha vikumbusho vyako.
158 Ninaangalia watu wadanganyifu kwa chuki kali,
Kwa sababu hawashike neno lako.+
159 Ona namna ninapenda sana maagizo yako!
Ee Yehova, linda uzima wangu kwa sababu ya upendo wako mushikamanifu.+
160 Chanzo kabisa cha neno lako ni kweli,+
Na hukumu zako zote za haki zinadumu milele.
ש [Sin] ao [Shin]
162 Ninashangilia kwa sababu ya neno lako+
Kama mutu mwenye anapata vitu vingi katika vita.
164 Mara saba (7) kwa siku ninakusifu wewe
Kwa sababu ya hukumu zako za haki.
165 Wale wenye kupenda sheria yako wako na amani nyingi;+
Hakuna kitu chochote chenye kinaweza kuwafanya wajikwae.*
166 Ninatumainia matendo yako ya wokovu, Ee Yehova,
Na ninashika amri zako.
168 Ninashika maagizo yako na vikumbusho vyako,
Kwa maana unajua mambo yote yenye ninafanya.+
ת [Taw]
169 Kilio changu cha kuomba musaada kikufikie, Ee Yehova.+
Unifanye nielewe, kulingana na neno lako.+
170 Ombi langu la kuomba rehema lifike mbele yako.
Uniokoe, kama vile umeahidi.*
171 Midomo yangu itoe sifa nyingi,+
Kwa maana wewe unanifundisha masharti yako.
172 Ulimi wangu uimbe kuhusu neno lako,+
Kwa maana amri zako zote ni za haki.
174 Ninatamani sana wokovu wako, Ee Yehova,
Na ninapenda sana sheria yako.+
176 Nimetanga-tanga kama kondoo mwenye amepotea.+ Tafuta mutumishi wako,
Kwa maana sijasahau amri zako.+
Wimbo wa Safari za Kupanda.*
2 Ee Yehova, niokoe* kutokana na midomo yenye kusema uongo
Na kutokana na ulimi mudanganyifu.
5 Ole wangu, kwa maana nimeishi kama mugeni katika Mesheki!+
Nimekuwa nikiishi kati ya mahema ya Kedari.+
7 Mimi ni mutu wa amani, lakini wakati ninasema,
Wao wanataka vita.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
121 Ninainua macho yangu kuelekea milima.+
Musaada wangu utatoka wapi?
3 Hataruhusu hata kidogo muguu wako utereze.*+
Yeye mwenye kukulinda hatasinzia hata kidogo.
5 Yehova anakulinda.
Yehova ni kivuli+ kwenye mukono wako wa kuume.+
7 Yehova atakulinda na mambo yote yenye kuumiza.+
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
122 Nilishangilia wakati waliniambia:
“Tuende kwenye nyumba ya Yehova.”+
2 Na sasa miguu yetu inasimama
Ndani ya milango yako mikubwa, Ee Yerusalemu.+
4 Makabila yamepanda kuenda kwenye muji huo,
Makabila ya Yah,*
Kulingana na kikumbusho chenye Israeli walipewa,
Ili kushukuru jina la Yehova.+
6 Muombe Yerusalemu ikuwe na amani.+
Wale wenye kukupenda, Ee muji, watakuwa salama.
7 Amani iendelee ndani ya boma zako,*
Usalama ndani ya minara yako yenye ngome.
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na wenzangu nitasema:
“Amani ikuwe ndani yako.”
9 Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu,+
Nitatafuta mema kwa ajili yako.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
123 Ninainua macho yangu kukuelekea wewe,+
Wewe mwenye kukaa ukiwa mufalme mbinguni.
2 Kama vile macho ya watumishi yanaangalia mukono wa bwana wao,
Na macho ya mutumishi mwanamuke yanaangalia mukono wa bimukubwa wake,
Ni vile macho yetu yanamuangalia Yehova Mungu wetu+
Mupaka wakati atatuonyesha wema.+
3 Utuonyeshe wema, Ee Yehova, utuonyeshe wema,
Kwa maana tumezarauliwa kwa ukamili.+
4 Tumechekelewa kwa ukamili na* watu wenye kujitumainia
Na tumezarauliwa na watu wenye kiburi.
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
124 “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi”+
—Israeli aseme sasa—
2 “Kama Yehova hangekuwa pamoja na sisi+
Wakati watu walisimama ili kutushambulia,+
3 Basi wangetumeza tukiwa wazima+
Wakati kasirani yao ilikuwa inawaka juu yetu.+
5 Maji yenye nguvu yangetulemea.*
6 Yehova asifiwe,
Kwa maana hakututia katika meno yao kama mawindo.
7 Tuko* kama ndege mwenye aliponyoka
Katika mutego wa muwindaji;+
Mutego ulivunjika,
Na sisi tukaponyoka.+
8 Musaada wetu uko katika jina la Yehova,+
Mutengenezaji wa mbingu na dunia.”
Wimbo wa Safari za Kupanda.
125 Wale wenye kumutegemea Yehova+
Wako kama Mulima Sayuni, wenye hauwezi kutikiswa
Lakini unadumu milele.+
2 Kama vile milima inazunguka Yerusalemu,+
Ni vile Yehova anazunguka watu wake+
Kuanzia sasa na milele.
3 Fimbo ya ufalme ya uovu haitadumu katika inchi yenye iligawiwa wenye haki,+
5 Lakini wale wenye kugeuka pembeni na kufuata njia zao zenye kupotoka,
Yehova atawaondoa pamoja na wakosaji.+
Amani ikuwe juu ya Israeli.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
126 Wakati Yehova alikusanya na kurudisha watu wenye walikamatwa mateka wa Sayuni,+
Tuliwaza tulikuwa tunaota ndoto.
2 Wakati huo kinywa chetu kilijaa kicheko
Na ulimi wetu vigelegele vya shangwe.+
Wakati huo walisema kati ya mataifa:
“Yehova amewatendea mambo makubwa.”+
3 Yehova ametutendea mambo makubwa,+
Na tuko na furaha kubwa sana.
4 Kusanya na urudishe watu wetu wenye walikamatwa mateka, Ee Yehova,
Kama mito midogo ya Negebu.*
5 Wale wenye kupanda mbegu kwa machozi
Watavuna kwa vigelegele vya shangwe.
6 Ule mwenye anaenda inje, hata kama iko* analia,
Akiwa amebeba mufuko wake wa mbegu,
Hakika atarudia kwa vigelegele vya shangwe,+
Akiwa amebeba mafungu yake ya mbegu.+
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Sulemani.
127 Kama Yehova hajenge nyumba,
Wale wenye kuijenga wanafanya kazi ya nguvu ya bure.+
Kama Yehova halinde muji,+
Mulinzi anakesha bure.
2 Ni bure kwamba munaamuka asubui sana,
Kwamba munachelewa kulala,
Kwamba munafanya kazi ya jasho ili kupata chakula,
Kwa maana yeye anaandalia wale wenye anapenda na anawapatia usingizi.+
5 Mwenye furaha ni mwanaume mwenye anawajaza katika mufuko wake wa mishale.+
Hawatapatishwa haya,
Kwa maana watazungumuza na maadui katika mulango mukubwa wa muji.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
2 Utakula vitu vyenye mukono wako ulifanya kazi ya nguvu ili kuvipata.
Utakuwa na furaha na kufurahia mafanikio.+
3 Bibi yako atakuwa kama muzabibu wenye kuzaa matunda mengi ndani ya nyumba yako;+
Wana wako watakuwa kama machipukizi ya muzeituni kuzunguka meza yako.
4 Angalia! Ni vile mwanaume mwenye kumuogopa Yehova
Atabarikiwa.+
5 Yehova atakubariki kutoka Sayuni.
Na uone Yerusalemu ikisitawi sikuzote za maisha yako+
6 Na uone wana wa wana wako.
Amani ikuwe juu ya Israeli.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
129 “Wamenishambulia kila wakati tangu ujana wangu”+
—Israeli aseme sasa—
2 “Wamenishambulia kila wakati tangu ujana wangu;+
Lakini hawajanishinda.+
3 Walimaji wamelima kwenye mugongo wangu;+
Wamerefusha mifereji yao.”
5 Watapatishwa haya na kukimbia kwa sababu ya aibu,
Wale wote wenye kuchukia Sayuni.+
6 Watakuwa kama majani kwenye sehemu za juu za nyumba
Yenye yanakauka mbele yangolewe,
7 Yenye hayawezi kujaa katika mukono wa muvunaji
Wala katika mikono ya ule mwenye kukusanya mafungu ya mbegu.
8 Wale wenye kupita karibu hawatasema:
“Baraka ya Yehova ikuwe juu yenu;
Tunawabariki katika jina la Yehova.”
Wimbo wa Safari za Kupanda.
130 Ninakuita nikiwa katika sehemu za chini kabisa, Ee Yehova.+
2 Ee Yehova, sikia sauti yangu.
Masikio yako yasikilize vilio vyangu vya kuomba musaada.
5 Ninamutumainia Yehova, nafsi yangu yote inamutumainia;
Ninangojea neno lake.
6 Ninamungojea* Yehova kwa hamu,+
Kuliko namna walinzi wanangojea asubui,+
Ndiyo, kuliko namna walinzi wanangojea asubui.
7 Israeli aendelee kumungojea Yehova,
Kwa maana Yehova ni mushikamanifu katika upendo wake,+
Na iko* na nguvu nyingi za kukomboa.
8 Atakomboa Israeli katika makosa yao yote.
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
131 Ee Yehova, moyo wangu hauna majivuno,
Wala macho yangu hayana kiburi;+
Wala sijitafutie mambo makubwa sana,+
Wala mambo yenye kupita uwezo wangu.
2 Hapana, lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu*+
Kama mutoto mwenye ameachishwa kunyonya akiwa katika mikono ya mama yake;
Nimetosheka* kama mutoto mwenye ameachishwa kunyonya.
3 Israeli amungojee Yehova+
Kuanzia sasa na milele.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
132 Ee Yehova, umukumbuke Daudi
Na mateso yake yote;+
2 Namna alimuapia Yehova,
Namna alimuwekea naziri Mwenye Nguvu wa Yakobo:+
3 “Sitaingia katika hema yangu, katika nyumba yangu.+
Sitalala kwenye kiti changu, kwenye kitanda changu;
4 Sitaruhusu macho yangu yalale usingizi,
Wala kope zangu zisinzie
5 Mupaka wakati nitapata mahali kwa ajili ya Yehova,
9 Makuhani wako wavae haki,
Na washikamanifu wako wapige vigelegele vya shangwe.
11 Yehova amemuapia Daudi;
Hakika hatakosa kutimiza neno lake:
12 Kama wana wako wanashika agano langu
Na vikumbusho vyangu vyenye ninawafundisha,+
Wana wao pia
Watakaa kwenye kiti chako cha ufalme milele.”+
14 “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumuzikia milele;
Nitakaa hapa,+ kwa maana hiyo ndiyo tamaa yangu.
15 Nitapabariki sana kwa vyakula;
Nitashibisha maskini wake kwa mikate.+
17 Kule nitafanya nguvu za Daudi zikomae.*
Nimetayarisha taa kwa ajili ya mutiwa-mafuta wangu.+
18 Nitavalisha maadui wake haya,
Lakini taji lenye kuwa kwenye kichwa chake litasitawi.”+
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
2 Ni kama mafuta ya muzuri yenye kumwangwa juu ya kichwa+
Yenye kuteremuka kwenye ndevu,
Ndevu za Haruni,+
Na kuteremuka mupaka kwenye shingo ya nguo zake.
Ni kule Yehova aliamuru baraka yake
—Uzima wa milele.
Wimbo wa Safari za Kupanda.
134 Mumusifu Yehova,
Ninyi watumishi wote wa Yehova,+
Ninyi wenye kusimama katika nyumba ya Yehova nyakati za usiku.+
3 Yehova, Mutengenezaji wa mbingu na dunia,
Awabariki kutoka Sayuni.
135 Mumusifu Yah!*
Musifu jina la Yehova;
Mutoe sifa, ninyi watumishi wa Yehova,+
2 Ninyi wenye kusimama katika nyumba ya Yehova,
Katika viwanja vya nyumba ya Mungu wetu.+
3 Mumusifu Yah, kwa maana Yehova ni mwema.+
Muimbie jina lake sifa,* kwa maana ni lenye kupendeza.
5 Kwa maana ninajua muzuri kwamba Yehova ni mukubwa;
Bwana wetu ni mukubwa kuliko miungu mingine yote.+
6 Yehova anafanya kila kitu chenye anapenda kufanya+
Katika mbingu na juu ya dunia, katika bahari na katika sehemu za chini kabisa.
7 Anafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia;
Anatokeza umeme wa radi kwa ajili ya* mvua;
Analeta upepo kutoka katika madepo yake.+
8 Alipiga na kuua muzaliwa wa kwanza wa Misri,
Mwanadamu na munyama pia.+
10 Alipiga na kuua mataifa mengi+
Na kuua wafalme wenye nguvu+
11 —Sihoni mufalme wa Waamori,+
Ogu mufalme wa Bashani,+
Na falme zote za Kanaani.
12 Alitoa inchi yao kuwa uriti,
Uriti kwa watu wake Israeli.+
13 Ee Yehova, jina lako linadumu milele.
Ee Yehova, sifa yako inadumu* katika vizazi vyote.+
15 Sanamu za mataifa ni feza na zahabu,
Kazi ya mikono ya mwanadamu.+
16 Ziko na kinywa, lakini haziwezi kusema;+
Ziko na macho, lakini haziwezi kuona;
17 Ziko na masikio, lakini haziwezi kusikia.
Hakuna pumuzi katika kinywa chao.+
19 Ee nyumba ya Israeli, mumusifu Yehova.
Ee nyumba ya Haruni, mumusifu Yehova.
20 Ee nyumba ya Lawi, mumusifu Yehova.+
Ninyi wenye kumuogopa Yehova, mumusifu Yehova.
Mumusifu Yah!+
2 Mumushukuru Mungu wa miungu,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
3 Mumushukuru Bwana wa mabwana,
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
4 Yeye peke yake ndiye anafanya mambo makubwa ya ajabu,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+
6 Alitandika dunia juu ya maji,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
7 Alifanya vitu vikubwa vya kutoa mwangaza,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,
8 Jua ili litawale muchana,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,
9 Mwezi na nyota ili vitawale usiku,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
10 Alipiga na kuua muzaliwa wa kwanza wa Misri,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
11 Alitosha Israeli katikati yao,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,
12 Kwa mukono wenye nguvu+ na mukono wenye kunyooshwa,
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
13 Aligawa Bahari Nyekundu katika sehemu mbili,*+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
14 Alifanya Israeli apite katikati ya ile bahari,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
15 Alimukunguta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
16 Alipitisha watu wake katika jangwa,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
17 Alipiga na kuua wafalme wakubwa,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
18 Aliua wafalme wenye nguvu,
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
19 Sihoni+ mufalme wa Waamori,
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele,
20 Na Ogu+ mufalme wa Bashani,
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
21 Alitoa inchi yao kuwa uriti,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
22 Uriti kwa Israeli mutumishi wake,
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
23 Alitukumbuka wakati tulikuwa katika hali ya chini,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+
24 Aliendelea kutuokoa kutoka kwa wapinzani wetu,+
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
26 Mumushukuru Mungu wa mbinguni,
Kwa maana upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
137 Pembeni ya mito ya Babiloni,+ ni pale tulikaa.
Tulilia wakati tulikumbuka Sayuni.+
3 Kwa maana kule, wenye walitukamata walituomba tuwaimbie wimbo,+
Wale wenye kutuchekelea walitaka tuwafurahishe:
“Mutuimbie moja ya nyimbo za Sayuni.”
4 Namna gani tunaweza kuimba wimbo wa Yehova
Kwenye udongo wa kigeni?
6 Ulimi wangu ushikamane na kaakaa* langu
Kama sikukumbuke,
Kama sitie Yerusalemu juu ya
Sababu zangu kubwa zaidi za kushangilia.+
7 Kumbuka, Ee Yehova,
Mambo yenye Waedomu walisema siku yenye Yerusalemu ilianguka:
“Muibomoe! Muibomoe mupaka kwenye misingi yake!”+
8 Ee binti ya Babiloni, mwenye kuwa karibu kuharibiwa,+
Mwenye furaha ni ule mwenye atakupatia zawabu
Mambo yenye ulitutendea.+
9 Mwenye furaha ni ule mwenye atakamata watoto wako
Na kuwapiga-piga juu ya miamba.+
Ya Daudi.
138 Nitakusifu kwa moyo wangu wote.+
Mbele ya miungu mingine,
Nitaimba sifa.*
2 Nitainama kuelekea hekalu lako takatifu,*+
Na nitasifu jina lako+
Kwa sababu ya upendo wako mushikamanifu na uaminifu wako.
Kwa maana umetukuza neno lako na jina lako juu ya vitu vingine vyote.*
4 Wafalme wote wa dunia watakusifu, Ee Yehova,+
Kwa maana watakuwa wamesikia ahadi zenye ulitoa.
5 Wataimba kuhusu njia za Yehova,
Kwa maana utukufu wa Yehova ni mukubwa.+
6 Ijapokuwa Yehova iko* juu, yeye anaona wanyenyekevu,+
Lakini wenye majivuno anawajua tu kwa mbali.+
7 Hata kama ninatembea katikati ya hatari, utalinda uzima wangu.+
Unanyoosha mukono wako juu ya kasirani ya maadui wangu;
Mukono wako wa kuume utaniokoa.
8 Yehova atatimiza mambo yote kwa ajili yangu.
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
139 Ee Yehova, umenichunguza kabisa, na unanijua.+
2 Unajua wakati ninakaa na wakati ninasimama.+
Unatambua mawazo yangu kwa mbali.+
5 Unanizunguka nyuma na mbele;
Na unatia mukono wako juu yangu.
6 Ujuzi wa namna hiyo unapita uelewaji wangu.*
Uko juu sana, siwezi kuufikia.*+
8 Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa kule,
Na kama ningetandika kitanda changu katika Kaburi,* angalia! ungekuwa kule.+
9 Kama ningeruka kwa mabawa ya mapambazuko*
Ili niishi pembeni ya bahari ya mbali sana,
10 Hata kule mukono wako ungeniongoza
Na mukono wako wa kuume ungenishika.+
11 Kama ninasema: “Hakika giza litanificha!”
Basi usiku wenye kunizunguka ungekuwa mwangaza.
12 Hata giza halingekuwa nzito sana kwako,
Lakini usiku ungekuwa wenye kungaa kama muchana;+
Kwako giza ni sawa na mwangaza.+
14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia yenye kuogopesha sana na ya ajabu.+
15 Mifupa yangu haikufichwa mbele ya macho yako
Wakati nilifanywa katika siri,
Wakati nilisukwa katika sehemu za chini kabisa za dunia.+
16 Macho yako hata yaliniona wakati nilikuwa kiini-tete;
Sehemu zake zote ziliandikwa katika kitabu chako
Kuhusiana na siku zenye sehemu hizo ziliumbwa,
Mbele sehemu yoyote kati ya hizo ikuwe.
17 Kwa hiyo kwangu mimi, mawazo yako ni yenye samani sana!+
Ee Mungu, hesabu yote ya mawazo hayo ni kubwa sana!+
18 Kama ninajaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko chembe za muchanga.+
Wakati ninaamuka, ningali pamoja na wewe.*+
19 Ee Mungu, ingekuwa muzuri kama ungeua waovu!+
Halafu watu wenye jeuri* wangeniondokea,
20 Wale wenye kusema mambo ya mubaya juu yako kwa nia yenye uovu;*
Wao ni wapinzani wako wenye kutumia jina lako kwa njia yenye haifae.+
22 Ninawachukia kwelikweli;+
Wamekuwa maadui wangu kabisa.
23 Unichunguze kabisa, Ee Mungu, na ujue moyo wangu.+
Unichunguze, na ujue mawazo yangu yenye kuhangaisha.*+
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
140 Uniokoe, Ee Yehova, kutoka kwa watu waovu;
Unilinde kutoka kwa watu wenye jeuri,+
2 Wale wenye kufanya mipango ya uovu katika mioyo yao+
Na kuchochea ugomvi muchana wote.
4 Unilinde, Ee Yehova, kutokana na mikono ya waovu;+
Unilinde kutokana na watu wenye jeuri,
Wale wenye kufanya mupango wa kunifanya nijikwae.
Wanatega mitego ya kuninasa.+ (Sela)
6 Ninamuambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu.
Sikiliza, Ee Yehova, vilio vyangu vya kuomba musaada.”+
7 Ee Yehova Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Mwokozi wangu mwenye nguvu,
Wewe unalinda kichwa changu katika siku ya vita.+
8 Ee Yehova, usitimize tamaa za waovu.
Usiruhusu mipango yao mibaya ifanikiwe, ili wasijiinue.+ (Sela)
9 Vichwa vya wale wenye kunizunguka
Vifunikwe na uovu wenye kusemwa na midomo yao.+
10 Makaa yenye kuwaka yawanyeshee.+
11 Muchongezi asipate makao juu ya dunia.*+
Uovu ufuatilie watu wenye jeuri na uwapige na kuwaua.
12 Ninajua kwamba Yehova atatetea watu wa hali ya chini
Na kupatia maskini haki.+
Muziki wa Daudi.
141 Ee Yehova, ninakuitia.+
Kuja haraka unisaidie.+
Sikiliza wakati ninakuita.+
2 Sala yangu ikuwe kama uvumba+ wenye kutayarishwa mbele yako,+
Mikono yangu yenye kuinuliwa ikuwe kama toleo la nafaka la mangaribi.+
3 Weka mulinzi kwa ajili ya kinywa changu, Ee Yehova,
Weka ulinzi kwenye mulango wa midomo yangu.+
4 Usiache moyo wangu uelekee kwenye jambo lolote la mubaya,+
Ili nisishiriki katika matendo maovu pamoja na watu waovu;
Nisikule hata kidogo vyakula vyao vitamu.
5 Kama mwenye haki ananipiga, hilo litakuwa tendo la upendo mushikamanifu;+
Kama ananikaripia, hilo litakuwa kama mafuta kwenye kichwa changu,+
Yenye kichwa changu hakitakataa hata kidogo.+
Sala yangu itaendelea hata wakati wa misiba yao.
6 Hata kama waamuzi wao wanatupwa chini kutoka kwenye muteremuko mukali,
Watu watasikiliza maneno yangu, kwa maana ni yenye kupendeza.
7 Kama vile wakati mutu analima na kuvunja-vunja udongo,
Ni vile mifupa yetu imesambazwa kwenye kinywa cha Kaburi.*
8 Lakini macho yangu yanakuangalia, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova.+
Nimekukimbilia.
Usiondoe uzima wangu.*
9 Unilinde kutokana na mataya* ya mutego wenye wamenitegea,
Kutokana na mitego ya watenda-maovu.
10 Waovu wataanguka wote pamoja ndani ya nyavu zao* wenyewe+
Lakini mimi nitapita karibu nayo kwa usalama.
Maskili.* Ya Daudi, wakati alikuwa katika pango.+ Sala.
142 Kwa sauti yangu ninamuita Yehova anisaidie;+
Kwa sauti yangu ninamulilia Yehova anionyeshe wema.
2 Mbele yake ninamwanga mahangaiko yangu;
Mbele yake ninaeleza taabu yangu+
3 Wakati roho yangu inazimia ndani yangu.*
Kisha unaangalia barabara yangu.+
Katika njia kwenye ninatembea,
Wanaficha mutego wa kuninasa.
5 Ninakuita unisaidie, Ee Yehova.
6 Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada,
Kwa maana nimeshushwa chini sana.
Uniokoe kutoka kwa wale wenye kunitesa,+
Kwa maana ni wenye nguvu kuliko mimi.
7 Unitoshe* katika gereza la chini ya udongo
Ili nisifu jina lako.
Wenye haki wakusanyike kunizunguka
Kwa sababu unanitendea kwa fazili.
Muziki wa Daudi.
143 Ee Yehova, sikia sala yangu;+
Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada.
Unijibu katika uaminifu wako na katika haki yako.
2 Usiingie katika hukumu pamoja na mutumishi wako,
Kwa maana hakuna mutu yeyote mwenye uzima ambaye anaweza kuwa mwenye haki mbele yako.+
3 Kwa maana adui ananifuatilia;*
Ameponda uzima wangu katika udongo.
Amenifanya nikae katika giza kama wale wenye walikufa zamani sana.
5 Ninakumbuka siku za zamani;
Ninafikiri sana* juu ya utendaji wako wote;+
Ninafikiri kwa bidii juu ya* kazi ya mikono yako.
6 Ninakunyooshea mikono yangu;
Niko* kama inchi yenye kukauka yenye kuwa na kiu kwa ajili yako.+ (Sela)
8 Acha nisikie upendo wako mushikamanifu asubui,
Kwa maana ninakutegemea wewe.
9 Uniokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Yehova.
Ninatafuta ulinzi wako.+
10 Unifundishe kufanya mapenzi yako,+
Kwa maana wewe ni Mungu wangu.
Roho yako ni ya muzuri;
Iniongoze kwenye inchi tambarare.*
11 Ee Yehova, linda uzima wangu kwa ajili ya jina lako.
Katika haki yako, uniokoe mimi* katika taabu.+
12 Katika upendo wako mushikamanifu, maliza* maadui wangu;+
Haribu wote wenye kunitesa,+
Kwa maana mimi ni mutumishi wako.+
Ya Daudi.
144 Yehova, Mwamba wangu,+ asifiwe,
Yeye mwenye kuzoeza mikono yangu kwa ajili ya pigano,
Vidole vyangu kwa ajili ya vita.+
2 Yeye ni upendo wangu mushikamanifu na ngome yangu,
Kimbilio langu salama* na mwokozi wangu,
Ngao yangu na Ule mwenye nimejificha ndani yake,+
Ule mwenye kutiisha vikundi vya watu chini yangu.+
3 Ee Yehova, mwanadamu ni nini ili umutambue,
Mwana wa mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umukazie uangalifu?+
7 Nyoosha mikono yako ukiwa juu;
Uniokoe na kunikomboa katika maji mengi,
8 Wenye vinywa vyao vinasema uongo
Na wenye wanainua mukono wao wa kuume ili kuapa kwa uongo.*
9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mupya.+
Nitakuimbia sifa,* kwa chombo cha kamba kumi (10),
10 Wewe mwenye kupatia wafalme ushindi,*+
Wewe mwenye kumuokoa mutumishi wako Daudi kutokana na upanga hatari.+
11 Uniokoe na kunikomboa katika mukono wa wageni,
Wenye vinywa vyao vinasema uongo
Na wenye wanainua mukono wao wa kuume ili kuapa kwa uongo.
12 Halafu watoto wetu wanaume watakuwa kama mimea michanga yenye kukomaa haraka,
Watoto wetu wanamuke kama nguzo za pembe zenye kuchongwa kwa ajili ya nyumba ya mufalme.
13 Madepo yetu yatajaa sana mazao ya kila namna;
Makundi yetu katika maeneo yetu ya mashamba yataongezeka kwa maelfu, kwa makumi ya maelfu.
14 Ngombe wetu, wakiwa na mimba, hawatapatwa na jambo la mubaya* wala mimba kuharibika,
Hakutakuwa kilio cha kuteseka katika viwanja vyetu vya watu wote.
15 Wenye furaha ni watu wenye kuwa katika hali hiyo!
Wenye furaha ni watu wenye Mungu wao ni Yehova!+
Sifa ya Daudi.
א [Aleph]
ב [Beth]
ג [Gimel]
ד [Daleth]
ה [He]
5 Watasema kuhusu utukufu mukubwa wa ukubwa wako+
Na mimi nitafikiri sana* juu ya kazi zako za ajabu.
ו [Waw]
ז [Zayin]
7 Watachangamuka wakati watakumbuka wema wako mwingi,+
Na watapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya haki yako.+
ח [Heth]
ט [Teth]
י [Yod]
כ [Kaph]
11 Watatangaza utukufu wa ufalme wako+
Na kusema kuhusu nguvu zako,+
ל [Lamed]
12 Ili kujulisha wanadamu matendo yako yenye nguvu+
Na utukufu mukubwa wa ufalme wako.+
מ [Mem]
13 Ufalme wako ni ufalme wa milele,
Na mamlaka yako yanadumu katika vizazi vyote.+
ס [Samekh]
ע [Ayin]
פ [Pe]
צ [Tsade]
ק [Qoph]
ר [Resh]
ש [Shin]
ת [Taw]
21 Kinywa changu kitatangaza sifa ya Yehova;+
Acha kila kiumbe chenye uzima kisifu* jina lake takatifu milele na milele.+
Nafsi yangu yote imusifu Yehova.+
2 Nitamusifu Yehova maisha yangu yote.
Nitamuimbia Mungu wangu sifa* wakati wote wenye nitakuwa muzima.
5 Mwenye furaha ni ule mwenye Mungu wa Yakobo ni musaidizi wake,+
Mwenye anamutumainia Yehova Mungu wake,+
6 Mutengenezaji wa mbingu na dunia,
Wa bahari, na vyote vyenye kuwa ndani,+
Yeye mwenye kuwa muaminifu sikuzote,+
7 Yeye mwenye kutenda haki kwa ajili ya wale wenye walipunjwa,
Yeye mwenye kupatia wenye njaa mukate.+
Yehova anaachilia huru wafungwa.+
8 Yehova anafungua macho ya vipofu;+
Yehova anasimamisha wale wenye kuinama chini;+
Yehova anapenda wenye haki.
9 Yehova analinda wakaaji wageni;
Anamutegemeza mutoto mwenye hana baba na mujane,+
10 Yehova atakuwa Mufalme milele,+
Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi kwa kizazi.
Mumusifu Yah!*
3 Anaponyesha wenye kuvunjika moyo;
Anafunga vidonda vyao.
7 Mumuimbie Yehova kwa shukrani;
Mumuimbie Mungu wetu sifa kwa kinubi,
8 Yeye mwenye kufunika mbingu kwa mawingu,
Yeye mwenye kupatia dunia mvua,+
Yeye mwenye kuchipusha majani+ juu ya milima.
12 Umutukuze Yehova, Ee Yerusalemu.
Umusifu Mungu wako, Ee Sayuni.
13 Anafanya mapingo* ya milango mikubwa ya muji wako yakuwe yenye nguvu;
Anabariki wana wako wenye kuwa ndani yako.
15 Anatuma amri yake katika dunia;
Neno lake linakimbia haraka sana.
17 Anatupa chini majiwe yake ya mvua* kama vipande vya mukate.+
Ni nani anaweza kuvumilia baridi yake?+
18 Anatuma neno lake, na inayeyuka.
Anafanya upepo wake uvume,+ na maji yanatiririka.
148 Mumusifu Yah!*
Mumusifu Yehova kutoka mbinguni,+
Mumusifu katika nafasi za juu.
2 Mumusifu, ninyi malaika wake wote.+
Mumusifu, ninyi jeshi lake lote.+
3 Mumusifu, jua na mwezi.
Mumusifu, nyota zote zenye kungaa.+
4 Mumusifu, Enyi mbingu zenye kuwa juu sana*
Na maji yenye kuwa juu ya mbingu.
5 Visifu jina la Yehova,
Kwa maana aliamuru, na vikaumbwa.+
7 Mumusifu Yehova kutoka katika dunia,
Ninyi viumbe vikubwa vya bahari na maji yote yenye kuenda chini sana,
8 Ninyi umeme wa radi na mvua ya majiwe, teluji* na mawingu mazito,
Wewe upepo wa zoruba, ninyi wenye kutenda neno lake,+
9 Ninyi milima na vilima vyote,+
Ninyi miti ya matunda na mierezi yote,+
10 Ninyi wanyama wa pori+ na wanyama wote wa kufugwa,
Ninyi viumbe vyenye kutambaa na ndege wenye mabawa,
11 Ninyi wafalme wa dunia, na ninyi mataifa yote,
Ninyi wakubwa na waamuzi wote wa dunia,+
12 Ninyi vijana wanaume na vijana wanamuke,*
Wazee pamoja na vijana.
13 Wasifu jina la Yehova,
Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana haliwezi kufikiwa.+
Ukubwa wake uko juu ya dunia na mbingu.+
14 Atainua nguvu* ya watu wake,
Kwa ajili ya sifa ya washikamanifu wake wote,
Ya wana wa Israeli, watu wenye kuwa karibu naye.
Mumusifu Yah!*
149 Mumusifu Yah!*
2 Israeli ashangilie katika Mutengenezaji wake Mukubwa;+
Wana wa Sayuni wafurahi katika Mufalme wao.
4 Kwa maana Yehova anafurahia watu wake.+
Anapamba wapole kwa wokovu.+
5 Washikamanifu washangilie kwa utukufu;
Wapige vigelegele vya shangwe kwenye vitanda vyao.+
6 Nyimbo za kumusifu Mungu zikuwe katika koo yao,
Na upanga wenye makali pande mbili ukuwe katika mukono wao,
7 Ili kulipiza kisasi juu ya mataifa
Na kupatia vikundi vya watu azabu,
8 Ili kufunga wafalme wao kwa minyororo
Na watu wao wenye vyeo kwa pingu za chuma,
9 Ili kuleta hukumu yenye iliandikwa kwa ajili yao.+
Heshima hii ni ya washikamanifu wake wote.
Mumusifu Yah!*
Mumusifu Mungu katika mahali pake patakatifu.+
Mumusifu katika anga la* nguvu zake.+
2 Mumusifu kwa sababu ya kazi zake zenye nguvu.+
Mumusifu kwa sababu ya ukubwa wake mwingi sana.+
3 Mumusifu kwa kupiga baragumu.+
Mumusifu kwa chombo cha kamba na kinubi.+
4 Mumusifu kwa ngoma ya kidogo*+ na kwa dansi ya muzunguko.
Mumusifu kwa kamba+ na filimbi.*+
5 Mumusifu kwa matoazi yenye kulia.
Mumusifu kwa matoazi yenye kugonganishwa.+
6 Kila kitu chenye kupumua—kimusifu Yah.
Ao “anatafakari juu ya sheria Yake; anafikiri sana juu ya sheria Yake.”
Ao “vinatafakari juu ya; vinafikiri sana juu ya.”
Ao “wanafanya shauri pamoja.”
Ao “Kristo wake.”
Ao “Muonywe.”
Tnn., “Mumubusu.”
Tnn., “yeye.”
Ao “kuhusu nafsi yangu.”
Angalia Maana ya Maneno.
Utaya ni mufupa wa kinywa wenye kubeba meno.
Tnn., “Unitengenezee nafasi kubwa katika.”
Ao “atamufanya mushikamanifu wake aonekane kuwa tofauti; atamutia pembeni mushikamanifu wake kwa ajili yake mwenyewe.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mutu mwenye kumwanga damu na ambaye ni mudanganyifu.”
Ao “patakatifu pako.”
Ao “Wanatumia ulimi laini.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “rehema.”
Ao “nafsi yangu inavurugika.”
Ao “uokoe nafsi yangu.”
Ao “kukukumbuka.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “ninafanya kitanda changu kiogelee.”
Ao “Limezeeka.”
Ao “Wimbo wa maombolezo.
Ao “watapasua nafsi yangu.”
Ao pengine, “Wakati sikumuharibu ule mwenye ananipinga bila sababu.”
Ao “na kufikia nafsi yangu.”
Ao “mwenye anajaribu mioyo na figo.”
Ao “anavurumisha lawama zake.”
Ao “Nitapigia jina la Yehova muziki.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao pengine, “Wewe mwenye utukufu wako unasimuliwa juu ya mbingu!”
Ao “kuliko malaika.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Nitapigia jina lako muziki.”
Ao “inchi yenye kuzaa.”
Ao “mahali salama pa juu.”
Ao “makila yenye.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “tamaa ya nafsi yake.”
Ao pengine, “Mwenye pupa anajibariki.”
Ao “Anajitutumua mbele ya.”
Ao “Sitayumba-yumba.”
Ao “kichaka chake.”
Ao “makila yake na kuifunga.”
Ao “katika makucha yake yenye nguvu.”
Ao “yatima.”
Ao “kuambia nafsi yangu.”
Ao “misingi ya haki.”
Ao “eko.”
Ao “yenye kungaa.”
Ao “Nafsi yake inachukia; Yeye mwenyewe anachukia.”
Ao pengine, “makaa yenye kuwaka.”
Ao “watajionea wema wake.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “Wanaongea kwa mudomo laini.”
Tnn., “kwa moyo na moyo.”
Ao “wenye wanajitutumua mbele yao.”
Ao pengine, “tanuru ya kuyeyusha yenye kuwekwa katika udongo.”
Ao “Nafsi yangu itahangaika.”
Ao “amenitendea kwa ukarimu.”
Ao “Mwenye hana akili.”
Ao “eko.”
Ao “kwa uaminifu-mushikamanifu.”
Ao “hawapatishe haya marafiki wake.”
Tnn., “kiapo chake.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “hatayumba-yumba.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “hisia zangu za ndani kabisa zinanirekebisha.” Tnn., “figo zangu zinanirekebisha.”
Ao “eko.”
Ao “sitayumba-yumba.”
Tnn., “utukufu wangu uko na.”
Ao “Mwili wangu unaishi.”
Ao “hautaiacha nafsi yangu.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao pengine, “aone uharibifu.”
Tnn., “pamoja na uso wako.”
Ao “Uzuri uko.”
Ao “Inama chini na unisikilize.”
Ao “maadui wangu wenye kushambulia nafsi.”
Ao “Wamefunikwa na mafuta yao wenyewe.”
Ao “kututupa chini.”
Ao “Uokoe nafsi yangu.”
Ao “mupangilio huu wa mambo (mufumo huu wa mambo).”
Ao “kuona umbo yako.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mwokozi wangu mwenye nguvu.”
Ao “mahali pangu salama pa juu.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “upepo.”
Ao “Mifereji ya maji ikaonekana.”
Ao “mahali penye nafasi kubwa.”
Tnn., “usafi wa.”
Ao “wenye kuteseka.”
Tnn., “macho yenye majivuno.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “Vifundo vya miguu yangu havitatereza.”
Ao “Utanipatia migongo ya maadui wangu.”
Tnn., “nitanyamazisha.”
Ao “watafifia.”
Ao “nitapigia jina lako muziki.”
Ao “Anamupatia ushindi mukubwa mufalme wake.”
Tnn., “mbegu yake.”
Ao pengine, “kamba yao ya kupimia.”
Ao “inchi yenye kuzaa.”
Ao “inarudisha nafsi.”
Ao “yenye ilisafishwa.”
Ao “makosa mengi.”
Ao “kutafakari.”
Tnn., “Aone kuwa mafuta.”
Ao “shauri lako lote liendeke muzuri.”
Ao “ushindi.”
Ao “yenye ilisafishwa.”
Tnn., “Urefu wa siku.”
Tnn., “mbele ya uso wako.”
Ao “hatayumba-yumba.”
Tnn., “matunda yao.”
Tnn., “kulenga nyuso zao.”
Tnn., “kamba zako za upinde.”
Tnn., “Tutaimbia na kupigia muziki uwezo wako.”
Pengine ni sauti ao mutindo wa muziki.
Ao “Umekaa ukiwa mufalme kati ya (juu ya).”
Ao “hawakupatishwa haya.”
Ao “Ninalaumiwa.”
Tnn., “Nimetupwa kwako.”
Inaonekana ni kitu chenye kutengenezwa na nyuki ili kuweka asali na chenye kinayeyuka haraka.
Fizi ni nyama zenye kushikilia meno katika kinywa.
Ao “Uokoe nafsi yangu.”
Tnn., “Kitu changu cha pekee,” ni kusema, nafsi yake, ao uzima wake.
Tnn., “mukono wa.”
Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “Moyo wenu uishi.”
Tnn., “wanene.”
Ao “nafsi zao.”
Tnn., “Mbegu yao itamutumikia.”
Ao pengine, “maji matulivu.”
Ao “Anaburudisha nafsi yangu.”
Tnn., “mapito yenye.”
Gongo ni fimbo yenye kuvimba kwenye mwisho wake mumoja.
Ao “vinanifariji.”
Ao “Unapakaa.”
Ao “nafsi Yangu,” inamaanisha uzima wa Yehova wenye mutu anaapa kwa huo.
Ao “Musimame.”
Ao “Ninainua nafsi yangu kwako.”
Ao “Vyenye ni vya tangu nyakati za zamani.”
Tnn., “katika hukumu.”
Ao “Nafsi yake itajionea.”
Tnn., “mbegu yake itariti.”
Ao “makila.”
Ao “nafsi yangu.”
Tnn., “komboa.”
Ao “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”
Tnn., “Sikae.”
Ao “sichangamane na wanafiki.”
Tnn., “kukaa.”
Ao “Usifagilie mbali nafsi yangu.”
Ao “watu wenye kumwanga damu.”
Ao “kata-midomo.”
Tnn., “Unikomboe.”
Tnn., “Katika mikusanyiko.”
Ao “kuangalia kwa kufikiri sana.”
Ao “patakatifu pake.”
Ao “Nitamupigia Yehova muziki.”
Ao pengine, “Hakika niko na imani kwamba nitaona wema wa Yehova katika inchi ya wazima.”
Ao “kaburi.”
Ao “Mumuabudu.”
Ao pengine, “kwa sababu ya utukufu wa utakatifu wake.”
Ao “eko.”
Inaonekana ni mustari wa milima ya Lebanoni.
Ao “bahari ya mbinguni.”
Ao “umenivuta.”
Ao “umeinua nafsi yangu.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “kaburi.”
Ao “Mumupigie Yehova muziki.”
Tnn., “ukumbusho wake.”
Ao “kuwa chini ya nia yake njema.”
Ao “Sitayumba-yumba.”
Ao “nilikuwa katika nia yako njema.”
Tnn., “Damu yangu iko na faida gani.”
Ao “kaburi.”
Ao “Ili utukufu wangu uimbe.”
Ao “Uiname chini na unisikilize.”
Ao “makila yenye.”
Ao “Mungu muaminifu.”
Ao “taabu ya nafsi yangu.”
Ao “mahali penye nafasi kubwa.”
Ao “nafsi yangu na tumbo langu.”
Ao “akili yao.”
Ao “nafsi yangu.”
Tnn., “Nyakati.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “Mbali na ugomvi wa ndimi.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “imesamehewa.”
Ao “kukosa kupendezwa kwako kulikuwa.”
Ao “Umajimaji wa uzima wangu ulibadilika.”
Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.
Hatamu ni kamba ya kumuongozea farasi ao punda.
Ao “Mumupigie muziki.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “pumuzi.”
Ao “jeshi lote la mbinguni lilifanywa.”
Ao “shauri la.”
Ao “mawazo.”
Ao “shauri la Yehova litasimama.”
Ao “la ushindi.”
Ao “aokoe nafsi yao.”
Ao “Nafsi yetu inamungojea.”
Ao “Nafsi yangu itajisifu.”
Ao “wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao “eko.”
Ao “wenye kuvunjika moyo.”
Ao “Misiba ya mwenye haki ni mingi.”
Ao “nafsi ya.”
Mara nyingi ilibebwa na wapiga-mishale.
Ao “shoka lenye makali pande zote mbili.”
Ao “Uambie nafsi yangu.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao “makila.”
Ao “wamechimbia nafsi yangu.”
Ao “makila yenye alificha imunase.”
Ao “nafsi yangu itashangilia.”
Ao “kufanya nafsi yangu ijisikie.”
Ao “Nilitesa nafsi yangu.”
Ao “ilikuwa inarudia kwenye kifua changu.”
Ao pengine, “Wenye hawamuogope Mungu wananichekelea ili wapate keki.”
Ao “Uokoe nafsi yangu.”
Tnn., “Kitu changu cha pekee,” ni kusema, nafsi yake, ao uzima wake.
Ao “wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao “Aha! Nafsi yetu.”
Ao “utatafakari; utafikiri sana.”
Tnn., “kama milima ya Mungu.”
Ao “Unaokoa.”
Tnn., “unono wa.”
Ao “Usiwake kasirani.”
Ao “inchi.”
Ao “Pata shangwe kubwa sana.”
Tnn., “Viringisha njia yako juu ya.”
Ao “kwa uvumilivu.”
Ao pengine, “Usikasirike, kwa maana kasirani itakuongoza tu kwenye mambo yenye kuumiza.”
Ao “kutia kamba kwenye.”
Ao “eko.”
Tnn., “siku za watu wenye hawana lawama.”
Ao “ni mwenye kuonyesha wema.”
Ao “anafanya imara.”
Ao “kwa mukono Wake.”
Ao “chakula.”
Ao “kinazungumuza hekima kwa sauti ya chini.”
Ao “mutu mwenye kushika uaminifu-mushikamanifu.”
Tnn., “Hakuna mahali popote pazima katika mwili wangu.”
Tnn., “Viuno vyangu vimejaa moto.”
Ao “ningurume.”
Ao “nafsi yangu.”
Tnn., “wako wazima.”
Ao pengine, “Lakini wale wenye ni maadui wangu bila sababu ni wengi.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Ao “yalichochewa.”
Tnn., “uliwaka moto.”
Ao “ninalia kwa maumivu.”
Ao “nijue namna ninapita haraka.”
Tnn., “zikuwe viganja vya mukono.”
Tnn., “Anafanya fujo.”
Nondo ni kidudu fulani cha kuruka chenye kinakula nguo.
Ao “Muhamiaji.”
Ao “Nilimungojea Yehova kwa uvumilivu.”
Ao “akainama chini ili kunisikiliza.”
Ao “waongo.”
Ao “Haukupendezwa na.”
Tnn., “mukunjo wa kitabu.”
Ao “ninatamani.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao “katika tamaa ya maadui wake; ao katika nafsi ya maadui wake.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Uponyeshe nafsi yangu.”
Ao “eko.”
Ao “amenigeukia.”
Ao “Tangu milele mupaka milele.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nafsi yangu inakutamani.”
Ao “eko.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “polepole.”
Ao “nafsi yangu imepoteza tumaini.”
Ao “nafsi yangu imepoteza.”
Ao “ule mulima mudogo.”
Ao pengine, “kama vile wanaponda mifupa yangu.”
Ao “eko.”
Ao “nafsi yangu imepoteza.”
Ao “nafsi yangu imepoteza.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Toa.”
Ao “wokovu mukubwa.”
Ao “kutokana na bei yao.”
Tnn., “mezali.”
Tnn., “Utukomboe.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “Kazi zangu zinahusu.”
Ao “mwandishi.”
Ao “mafanikio.”
Tnn., “utakufundisha.”
Ao “haki.”
Ao “watatuliza uso wako.”
Tnn., “kwa vikalio vya.”
Ao pengine, “akiwa amevaa kanzu zenye michoro ya uzi imeshonewa juu yake.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Ni kusema, wakati mwangaza wa asubui utaanza kutokea.
Ao “eko.”
Ao “mahali petu salama pa juu.”
Ao pengine, “ngao.”
Ao “eko.”
Ao “pembe ya kondoo-dume; tarumbeta.”
Ao “Mumupigie Mungu muziki.”
Tnn., “ngao za dunia ni za.”
Ao “mahali salama pa juu.”
Ao “wamekutana kwa mapatano.”
Ao “mashua za maji; bateaux.”
Ao “Tunatafakari.”
Tnn., “Mabinti wa Yuda washangilie.”
Ao “kuta zake zenye ngome.”
Ao pengine, “mupaka wakati tutakufa.”
Ao “mupangilio wa mambo (mufumo wa mambo).”
Tnn., “Wana wa wanadamu na pia wana wa binadamu.”
Ao “kutafakari.”
Tnn., “kosa la.”
Ao “nafsi yao.”
Ao “kaburi.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “atakomboa nafsi yangu.”
Tnn., “mukono wa.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “anapongeza nafsi yake.”
Ao “Kuanzia mashariki mupaka mangaribi.”
Tnn., “mbuzi-dume.”
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
Ao “agizo.”
Tnn., “kutupa maneno yangu nyuma yako.”
Ao pengine, “unajiunga naye.”
Ao “Unamuharibishia sifa.”
Ao “katika akili yangu.”
Tnn., “wewe tu.”
Ao “Na nilikuwa na zambi tangu wakati mama yangu alichukua mimba yangu.”
Ao “mutu wangu mwenye kuwa katika siri.”
Ao “neige.”
Ao “Ficha uso wako mbali.”
Ao “ufute.”
Tnn., “Unitegemeze kwa kunipatia roho yenye kuwa tayari.”
Ao “hautauzarau.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “ngome yake.”
Ao “kujificha katika.”
Tnn., “taabu zenye analeta.”
Angalia Maana ya Maneno.
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Mwenye hana akili.”
Ao pengine, “Woga mahali kwenye hakuna kitu cha kuogopa.”
Tnn., “wenye kupiga kambi ili kuwashambulia ninyi.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “utetee shitaka langu.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao “Hawamuweke Mungu mbele yao.”
Ao “eko.”
Ao “wenye kutegemeza nafsi yangu.”
Tnn., “uwanyamazishe.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Na usijifiche wakati ninasali ili kukuomba musaada.”
Tnn., “ugawanye ulimi wao.”
Ao “mwanadamu, mutu mwenye kuwa sawa na mimi.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nimevurugika.”
Tnn., “Atanikomboa.”
Ao “kupatia nafsi yangu.”
Ni kusema, ule rafiki wa zamani mwenye kutajwa katika mustari wa 13 na 14.
Ao “ayumbe-yumbe.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “anataka kuniuma.”
Tnn., “Nyama inaweza kunifanya.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao “eko.”
Ao “umeokoa nafsi yangu.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nafsi yangu inakukimbilia.”
Ao “Nafsi yangu imezungukwa.”
Ao “makila.”
Ao “Nafsi yangu imeinama.”
Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Ao “Nitakupigia muziki.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “wamepotoka.”
Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
Ao “wana-simba hawa wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “ile nyumba.”
Ao “wenye kiu cha damu.”
Ao “Wanavizia nafsi yangu.”
Ao “Wanabweka.”
Ao “kinabubujika.”
Ao “mahali pangu salama pa juu.”
Ao “wabweke.”
Ao “nitakupigia muziki.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao pengine, “Umepatia.”
Ao pengine, “mahali pake patakatifu.”
Ao “Eneo Tambarare la Chini.”
Tnn., “ngome.”
Ao pengine, “wenye ngome.”
Ao “unakuwa zaifu.”
Tnn., “siku za.”
Ao “atakaa.”
Ao “Umugawie.”
Ao “nitapigia jina lako muziki.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nafsi yangu inamungojea.”
Ao “mahali pangu salama pa juu.”
Ao pengine, “Ninyi wote, kama vile alikuwa ukuta wenye kuinama, ukuta wa majiwe wenye unakaribia kuanguka.”
Ao “heshima yake.”
Ao “Kwa kweli, Ee nafsi yangu, umungojee.”
Ao “kilo.”
Ao “Nafsi yangu iko na kiu.”
Tnn., “Mwili wangu unazimia.”
Ao “Nafsi yangu imetosheka.”
Tnn., “kama vile kwa mafuta na unono.”
Ao “Ninatafakari.”
Ao “Nafsi yangu inashikamana.”
Ao “kuharibu nafsi yangu; kuniua.”
Ao “atajisifu.”
Ao “Wanatiana moyo kutenda uovu.”
Ao “watajisifu.”
Tnn., “watu wote wenye mwili.”
Ao “Patakatifu pako.”
Tnn., “Alifanya.”
Tnn., “Amevaa.”
Tnn., “Anatuliza.”
Tnn., “ijae sana.”
Ao “matuta yake.”
Tnn., “yanaangusha matone-matone ya mafuta.”
Tnn., “kuangusha matone-matone.”
Ao “maeneo tambarare ya chini.”
Ao “Mupigie muziki jina lake lenye utukufu.”
Ao “Anafanya nafsi yetu iishi.”
Ao “iyumbe-yumbe.”
Ao “makila ya kuwinda nayo.”
Tnn., “kwenye viuno vyetu.”
Tnn., “juu ya kichwa chetu.”
Ao “itamuheshimia.”
Inaonekana ni kitu chenye kutengenezwa na nyuki ili kuweka asali na chenye kinayeyuka haraka.
Ao “mupigie jina lake muziki.”
Ao pengine, “juu ya mawingu.”
“Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Tnn., “muamuzi.”
Ao “waasi.”
Tnn., “ulienda inje mbele ya.”
Tnn., “iliangusha matone-matone ya.”
Tnn., “uriti.”
Ao pengine, “katikati ya mazizi ya kondoo.”
Ao “yenye rangi ya manjano-kijani.”
Ao “Neige.”
Ao “Ilikuwa kama vile teluji ilianguka Salmoni.”
Ao “ni mulima mukubwa sana.”
Ao “anatamani ukuwe.”
Ao “anatembea-tembea.”
Ao “matari.”
Tnn., “Katika mikusanyiko.”
Ao pengine, “vikikanyangia chini.”
Ao pengine, “Mabalozi (Ambassadeurs) watatoka.”
Ao “Mumupigie Yehova muziki.”
Tnn., “mawingu.”
Tnn., “pako.”
Ao “yamekuja kwenye nafsi yangu.”
Ao “Wale wenye kuwa maadui wangu bila sababu.”
Ao “nilinyenyekeza nafsi yangu.”
Ao pengine, “Wakati nililia na kufunga.”
Tnn., “Nikakuwa mezali kwao.”
Ao “shimo lifunge.”
Ao “Karibia nafsi yangu na uikomboe.”
Ao “na nimefikia hatua ya kupoteza tumaini.”
Ao “mumea wenye sumu.”
Ao “vinaigre.”
Ao “Kambi yao yenye kuta.”
Ao “kitabu cha uzima.”
Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.
Ni kusema, kuriti ile inchi.
Ao “nafsi yangu.”
Ao “Uiname chini na unisikilize.”
Ao “Wewe ni tegemeo langu.”
Ao “kutafuta nafsi yangu.”
Ao “kupinga nafsi yangu.”
Ao “kuhesabia.”
Tnn., “mukono wako.”
Ao “maji yenye kuenda chini sana ya.”
Ao “Nitakupigia muziki.”
Ao “umekomboa nafsi yangu.”
Ao “utatafakari; utafikiri sana.”
Tnn., “ahukumu.”
Tnn., “atachipuka.”
Ao “Atatawala.”
Ni kusema, Efrati.
Ao “nafsi za.”
Ao “Atakomboa nafsi zao.”
Ao “wenye kujisifu.”
Ao “Tumbo lao limenenepa.”
Tnn., “Unono.”
Ao “eko.”
Tnn., “kizazi cha wana wako.”
Tnn., “utazarau.”
Tnn., “katika figo zangu.”
Tnn., “Utanyamazisha.”
Ao “kukosa uaminifu.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “inatoa moshi.”
Tnn., “mukusanyiko wako.”
Ao “mukusanyiko.”
Ao “Kila mahali kwenye Mungu anaabudiwa.”
Ao “kutoka katika mikunjo ya nguo yako.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nafsi ya.”
Tnn., “pembe yenu.”
Tnn., “pembe yenu.”
Machicha ni masalio ya pombe yenye kubakia chini ya chombo.
Ao “Nitamupigia Mungu wa Yakobo muziki.”
Tnn., “pembe.”
Tnn., “pembe.”
Ao “Umefunikwa mwangaza.”
Tnn., “roho.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “bila kufa ganzi.”
Ao “Nafsi yangu haiwezi.”
Tnn., “roho yangu inazimia.”
Ao “muziki wangu wa kamba.”
Ao “Ninatafakari.”
Tnn., “Roho yangu inatafuta.”
Ao “kunitoboa.”
Tnn., “mukono wake wa kuume usituelekee.”
Ao “nitatafakari.”
Tnn., “mukono wako.”
Tnn., “umekomboa.”
Ao “mipeto; pneus.”
Ao “inchi yenye kuzaa.”
Tnn., “Kupitia mukono.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “agizo langu.”
Tnn., “wenye ulikuwa haujatayarishwa.”
Ao “ukuta.”
Tnn., “Walimujaribu.”
Ao “chakula kwa ajili ya nafsi yao.”
Ao “wa malaika.”
Ao “Mulipiza-Kisasi.”
Tnn., “anafunika.”
Ao pengine, “Kwamba roho inaenda na hairudie.”
Ao “wakamutia uchungu.”
Tnn., “mukono wake.”
Tnn., “aliwakomboa.”
Ao pengine, “homa kali.”
Ao “Hakulinda nafsi yao isikufe.”
Tnn., “kumujaribu.”
Ao “wivu wake.”
Tnn., “Na mabikira wake hawakusifiwa.”
Tnn., “Alijenga patakatifu pake kama nafasi za juu.”
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
Tnn., “ufunike.”
Ao “eko.”
Tnn., “mukono wako.”
Ao pengine, “kuweka huru.”
Tnn., “wana wa kifo.”
Ao pengine, “katikati ya.”
Ao “Funua uangavu wako.”
Tnn., “kuwaka kasirani juu ya.”
Ni kusema, Efrati.
Ao “Shina kubwa la muzabibu.”
Ao “tawi lenye.”
Tnn., “kwa kemeo la uso wako.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “tari.”
Ao “luga.”
Tnn., “katika mahali penye kufichwa pa mungurumo.”
Maana yake “Ugomvi.”
Tnn., “Walitembea katika mashauri yao.”
Tnn., “wakati.”
Tnn., “atamukulisha yeye,” ni kusema, atakulisha watu wa Mungu.
Tnn., “mafuta ya ngano.”
Ao “katika mukusanyiko wa Mungu.”
Ao “wenye kuwa kama Mungu.”
Ao “Muhukumu kwa ajili ya.”
Ao “muko kama Mungu.”
Ao “Usikuwe bubu.”
Ao “wanainua vichwa vyao.”
Tnn., “wenye kufichwa.”
Tnn., “Wanafanya shauri kwa moyo mumoja.”
Ao “agano.”
Tnn., “Wamekuwa mukono kwa.”
Ao “bonde la muto la.”
Ao “viongozi.”
Ao “kama aina fulani ya muchicha.”
Tnn., “Jaza.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “yenye kupendwa sana.”
Ao “nyumba ya ndege; kiota.”
Ao “bonde la miti midogo-midogo ya mibaka.”
Ao pengine, “Na mufundishaji anajifunika mwenyewe.”
Ao pengine, “Angalia ngao yetu, Ee Mungu.”
Ao “kizingiti cha.”
Tnn., “Ulifunika.”
Ao “Utukusanye tena.”
Ao “mafanikio.”
Ao “Inama chini na unisikilize.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao “nafsi ya mutumishi wako ishangilie.”
Ao “ninakuinulia nafsi yangu.”
Ao “Nipatie moyo wenye haugawanyike.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “kinatafuta nafsi yangu.”
Ao “hawakukuweka mbele yao.”
Ao “neema.”
Ao “kweli.”
Ao “uhakikisho wa.”
Ao “kunitambua.”
Ao “Kwangu mimi, wewe uko chanzo cha vitu vyote.”
Angalia Maana ya Maneno.
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Inama chini na usikilize.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “kaburi.”
Ao “kama mutu mwenye hana nguvu.”
Tnn., “mukono.”
Ao “katika Abadoni.”
Ao “unakataa nafsi yangu.”
Ao pengine, “yote kwa wakati mumoja.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “utadumu.”
Tnn., “mbegu yako ikuwe.”
Ao “mukusanyiko wa.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “pembe yetu inainuliwa.”
Tnn., “pembe yake itainuliwa.”
Ao “mamlaka yake.”
Tnn., “mbegu yake ikuwe.”
Ao “hukumu zangu.”
Ao “uasi wao.”
Tnn., “Wala kuwa muongo kuhusu uaminifu wangu.”
Tnn., “Mbegu yake itadumu.”
Ao “vibanda vyake vya majiwe.”
Tnn., “Umeinua juu mukono wa kuume wa wapinzani wake.”
Ao “kuokoa nafsi yake.”
Tnn., “mukono wa Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “kubeba katika kifua changu.”
Ao pengine, “kimbilio letu.”
Ao “haujatokeza kama kwa maumivu ya kuzaa.”
Ao “Unajua makosa yetu.”
Ao “Maisha yetu yanafifia.”
Ao “eko.”
Ao “kwa sababu ya uwezo wa pekee.”
Ao “Fanya kazi ya mikono yetu ikuwe imara kabisa.”
Ao “fanya kazi ya mikono yetu ikuwe imara kabisa.”
Ao “Kupitia manyoya yake ataweka kizuizi ili usifikiwe.”
Ao “boma.”
Tnn., “malipo.”
Ao pengine, “ngome yako; kimbilio lako.”
Tnn., “amejiunga na mimi.”
Ao “anatambua.”
Ao “aone wokovu kutoka kwangu.”
Ao “kupigia jina lako muziki.”
Ao “majani.”
Tnn., “pembe yangu kama ya.”
Ao “wakati wa kuwa na kichwa chenye imvi.”
Tnn., “kuwa wanene.”
Ao “mushipi.”
Ao “Inchi yenye kuzaa.”
Ao “kutikisika.”
Ao “Eko.”
Ao “Eko.”
Ao “unafaa.”
Tnn., “alipanda.”
Tnn., “nafsi yangu ingekuwa imekaa katika ukimya.”
Ao “mawazo yenye kusumbua.”
Ao “yalikuwa mengi ndani yangu.”
Ao “Faraja zako zilituliza nafsi yangu.”
Ao “watawala wenye upotovu wanaweza; waamuzi wenye upotovu wanaweza.”
Ao “kwa njia ya amri.”
Ao “nafsi ya mwenye haki.”
Tnn., “Na damu ya mwenye hana kosa wanaitangaza kuwa na hatia (yenye uovu).”
Ao “mahali pangu salama pa juu.”
Tnn., “Atawanyamazisha.”
Tnn., “atawanyamazisha.”
Tnn., “mbele ya uso wake.”
Tnn., “wa mukono wake.”
Maana yake “Ugomvi.”
Maana yake “Kujaribu; Jaribu.”
Ao “heshima.”
Ao “Mumuabudu.”
Ao pengine, “kwa sababu ya utukufu wa utakatifu wake.”
Ao “Inchi yenye kuzaa.”
Ao “kutikisika.”
Ao “Atatetea kwa haki mashitaka ya vikundi vya watu.”
Ao “amekuja.”
Ao “inchi yenye kuzaa.”
Angalia Maana ya Maneno.
Inaonekana ni kitu chenye kutengenezwa na nyuki ili kuweka asali na chenye kinayeyuka haraka.
Ao “Mumuabudu.”
Tnn., “Mabinti wa Yuda wamefurahi.”
Ao “nafsi za.”
Tnn., “nguvu za.”
Tnn., “ukumbusho wake.”
Ao “umemuletea ushindi.”
Ao “ushindi.”
Ao “kupiga muziki.”
Ao “Mumupigie Yehova muziki.”
Ao “Inchi yenye kuzaa.”
Ao “amekuja.”
Ao “inchi yenye kuzaa.”
Ao pengine, “katikati ya.”
Ao “eko.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “kuabudu.”
Tnn., “ulilipiza kisasi juu yao.”
Ao “muabudu.”
Ao “Mutambue.”
Ao pengine, “haiko sisi wenyewe.”
Ao “Nitakupigia muziki.”
Ao “kwa uaminifu-mushikamanifu.”
Ao “Matendo yao hayashikamane na mimi.”
Tnn., “Sitajua.”
Ao “Nitamuharibu.”
Ao “kwa uaminifu-mushikamanifu.”
Tnn., “mbele ya macho yangu.”
Ao “nitaharibu.”
Ao “anakuwa zaifu.”
Ao “Inama chini na unisikilize.”
Ao pengine, “Nimekonda sana na nimekuwa zaifu.”
Ao “wenye kunifanya nionekane kuwa mupumbavu.”
Ao “kivuli chenye kurefuka.”
Ao “jina lako litadumu.” Tnn., “ukumbusho wako utadumu.”
Tnn., “hawajaumbwa.”
Ao “nafsi yangu imusifu.”
Ao “nafsi yangu imusifu.”
Ao “kaburi.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mwenye neema.”
Ao “fazili nyingi zenye upendo.”
Tnn., “Na mahali pake hapalijue tena.”
Ao “tangu milele mupaka milele.”
Ao “wenye uwezo katika nguvu.”
Tnn., “kwa kusikia sauti ya (mulio wa) neno lake.”
Ao “Mahali pote pa mamlaka yake makubwa zaidi.”
Ao “nafsi yangu imusifu.”
Ao “heshima.”
Tnn., “katika maji.”
Ao “Haitatikisika.”
Ao “nyumba; viota.”
Ao “Wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao “mashua za maji; bateaux.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Nitamupigia Mungu wangu muziki.”
Ao pengine, “Acha kufikiri sana kwangu juu yake kupendeze.”
Ao “nafsi yangu imusifu.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “mumupigie muziki.”
Ao pengine, “Museme.”
Ao “kuwapo.”
Ao “wazao wa.” Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “Neno lenye aliamuru.”
Tnn., “Alivunja kila fimbo ya mukate.” Inawezekana ni fimbo zenye zilikuwa zinatumiwa ili kuwekea mikate.
Tnn., “Walitesa.”
Ao “Nafsi yake iliingia katika chuma.”
Tnn., “Ili afunge.”
Ao “kwa njia yenye kupendeza nafsi yake.”
Ao “miali ya moto.”
Tnn., “wao.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “nia njema.”
Ao “nijisifie wewe.”
Ao “hawakuelewa maana ya kazi zako za ajabu.”
Ao “alibakia.”
Ao “ulifanya nafsi yao kuwa zaifu.”
Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”
Tnn., “akasimama kwenye mupasuko huo mbele yake.”
Ao “wakashikamana.”
Ni kusema, zabihu zenye zilitolewa kwa watu wenye walikuwa wamekufa ao kwa miungu yenye haina uzima.
Maana yake “Ugomvi.”
Ao “kujifunza.”
Tnn., “mukono wao.”
Ao “anasikitika.”
Ao “tushangilie katika sifa yako.”
Ao “Tangu milele mupaka milele.”
Ao “Ikuwe vile!”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “walinunuliwa.”
Ao “nguvu za.”
Ao “Kutoka mahali jua linatokea na kutoka mahali jua linashukia.”
Ao “Nafsi yao ilizimia.”
Ao “nafsi yenye kukauka.”
Ao “nafsi yenye njaa.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Ao “Nafsi yao ilichukia kabisa.”
Ao “mashua za maji; bateaux.”
Ao “Nafsi yao inayeyuka.”
Bandari ni mahali mashua zinaegesha.
Tnn., “kiti cha.”
Ao “anainua juu,” ni kusema, ili wasifikiwe.
Tnn., “hata utukufu wangu.”
Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Ao “nitakupigia muziki.”
Ao pengine, “katika mahali pake patakatifu.”
Ao “Eneo Tambarare la Chini.”
Tnn., “ngome.”
Ao “mushitaki.”
Ao “aonekane kuwa muovu.”
Tnn., “wana.”
Tnn., “wana.”
Ao “Wenye kuomba faida ya juu sana wawekee mitego.”
Ao “eko.”
Ao “upendo mushikamanifu.”
Ao “Kizazi chake chenye kuja kiharibiwe.”
Ao “upendo mushikamanifu.”
Ao “mushipi.”
Ao “nafsi yangu.”
Tnn., “Mwili wangu umekuwa mwembamba, hauna mafuta.”
Ao “koti yenye haina mikono.”
Ao “kuhukumu nafsi yake.”
Ao “siku yenye jeshi lako litajitayarisha kwa ajili ya vita.”
Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Ao “hatasikitika.”
Ao “kati ya.”
Tnn., “kichwa cha.”
Ao “dunia yote.”
Mwenye kuzungumuziwa ni “Bwana wangu” ambaye anatajwa katika mustari wa 1.
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “neema.”
Ao “Yako na musingi muzuri.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “neema.”
Ao “neema.”
Ao “umeazimia; uko imara.”
Ao “kwa ukarimu.”
Tnn., “Pembe yake mwenyewe itainuliwa.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “eko.”
Ao “Mwenye anakaa akiwa mufalme?”
Ao pengine, “yalala.”
Tnn., “wana.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “mahali patakatifu.”
Ao “Hatuna kitu, Ee Yehova, hatuna kitu.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Tnn., “wana.”
Tnn., “katika ukimya.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao pengine, “Ninapenda kwa sababu Yehova anasikia.”
Ao “anainama chini ili kunisikiliza.”
Tnn., “katika siku zangu.”
Tnn., “Taabu za Sheoli zilinipata.”
Ao “okoa nafsi yangu.”
Ao “neema.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Umeokoa nafsi yangu.”
Ao “wokovu mukubwa.”
Tnn., “chenye samani.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “ukoo wote mbalimbali.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “mahali penye nafasi kubwa.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao pengine, “pamoja na wale wenye kunisaidia.”
Ao pengine, “Ulinisukuma kwa nguvu.”
Ao “ushindi.”
Tnn., “kichwa cha pembe.”
Ao “wenye wanashika uaminifu-mushikamanifu.”
Tnn., “Ingekuwa muzuri kama njia zangu zingekuwa zimefanywa imara kabisa.”
Ao “Nitajifunza.”
Ao “Nafsi yangu inaungua kwa kutamani sana.”
Tnn., “Uviringishie mbali na mimi.”
Ao “anajifunza.”
Ao “Nafsi yangu inalala.”
Tnn., “njia.”
Ao “kujifunza.”
Ao “Nafsi yangu imekosa.”
Ao “nipatishwe haya.”
Tnn., “Nitakimbia katika.”
Ao pengine, “unafanya moyo wangu ukuwe na uhakika.”
Ao “Unitembeze.”
Ao “neno lako.”
Ao pengine, “Yenye imetolewa kwa wale wenye kukuogopa.”
Ao “neno lako.”
Ao “ninangojea.”
Ao “mahali penye nafasi kubwa.”
Ao “nitajifunza.”
Ao “ahadi yako yenye ulimupatia.”
Ao “Lenye ulinifanya ningojee.”
Ao “Katika nyumba kwenye ninaishi nikiwa mugeni.”
Ao “Ninatuliza (ninatafuta kicheko cha) uso wako.”
Ao “neno lako.”
Ao “nilikuwa ninatenda zambi bila kujua.”
Tnn., “hauna hisia, kama mafuta.”
Ao “ninangojea neno lako.”
Ao “neno lenye.”
Ao pengine, “kwa kusema uongo.”
Ao “nitajifunza.”
Ao “Nafsi yangu inatamani sana.”
Ao “ninangojea neno lako.”
Ni kusema, kazi zake zote za uumbaji.
Tnn., “ni pana sana.”
Ao “Ninajifunza.”
Ao “ninajifunza.”
Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.
Tnn., “matoleo ya kujipendea ya kinywa changu.”
Ao “Nafsi yangu iko katika mukono wangu kila wakati.”
Ao “uriti wangu wa milele.”
Tnn., “Nimeelekeza moyo wangu.”
Ao “moyo wenye kugawanyika.”
Ao “Ninangojea neno lako.”
Ao “kulingana na neno lako.”
Ao “lipatishwe haya.”
Tnn., “Nyama yangu inatetemeka.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Ao “neno lako la.”
Ao “yenye kusafishwa.”
Ao “agizo.”
Ao “nafsi yangu inavishika.”
Tnn., “kuhemahema.”
Ao “Fanya hatua zangu zikuwe imara.”
Tnn., “Unikomboe.”
Ao “Uonyeshe mutumishi wako kicheko.”
Ao “wakati wa gizagiza la asubui.”
Ao “ninangojea maneno yako.”
Ao “nijifunze.”
Ao “mwenendo muchafu.”
Ao “Uendeshe kesi yangu ya hukumu.”
Ao “neno lako.”
Ao “Kwao hakuna kikwazo chochote.”
Ao “Nafsi yangu inashika.”
Ao “kulingana na neno lako.”
Ao “nafsi yangu iishi.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “okoa nafsi yangu.”
Tnn., “Naye atakuongezea nini?”
Ao “Nafsi yangu imekuwa ikiishi.”
Ao “utikisike.”
Ao “nafsi yako.”
Tnn., “wakati unatoka inje na wakati unaingia ndani.”
“Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “kuta zako zenye ngome.”
Ao “Nafsi yetu imechokeshwa sababu ya kuchekelewa sana na.”
Ao “yangefunika nafsi yetu.”
Ao “yangelemea nafsi yetu.”
Ao “Nafsi yetu iko.”
Ao “wasielekeze mikono yao kwenye.”
Ao “mabonde ya kusini.”
Ao “eko.”
Ao “Watoto.”
Ao “unafuatilia.”
“Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Tnn., “Ili wakuogope.”
Ao “Nafsi yangu inamungojea.”
Ao “eko.”
Ao “nimejituliza na kujinyamazisha mwenyewe.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Nafsi yangu imetosheka.”
Ao “Tabenakulo kubwa.”
Ao “tabenakulo yake kubwa.”
Tnn., “Usigeuzie nyuma uso wa.”
Tnn., “wa uzao wa tumbo lako la uzazi.”
Tnn., “pembe ya Daudi ikomae.”
Ao pengine, “katika patakatifu.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “Mupigie jina lake muziki.”
Ao “mali yake yenye anapendezwa nayo sana.”
Ao “mivuke ipande.”
Ao pengine, “Anatengeneza milango kwa ajili ya.”
Ao “jina lako linadumu.” Tnn., “ukumbusho wako unadumu.”
Ao “atatetea mashitaka ya.”
Ao “atasikitikia.”
Ao “kwa uelewaji.”
Tnn., “vipande-vipande.”
Tnn., “miili yote.”
Ni kusema, katikati ya Babiloni.
Ao pengine, “ukauke.”
Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.
Ao pengine, “Nitapinga miungu mingine kwa kukupigia muziki.”
Ao “patakatifu pako.”
Ao pengine, “umetukuza neno lako juu ya jina lako lote.”
Ao “nisikuwe na woga katika nafsi yangu.”
Ao “eko.”
Tnn., “Unanipima.”
Ao “ni wa kushangaza sana kwangu.”
Ao “Uko mwingi sana, siwezi kuuelewa.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Ao pengine, “Ulinisuka pamoja.”
Ao “Nafsi yangu inajua.”
Ao pengine, “nitakuwa ningali ninayahesabu.”
Ao “wenye hatia ya damu.”
Ao “kulingana na wazo lao.”
Ao “yenye kusumbua.”
Ao “makila.”
Ao “Ndani ya mashimo yenye maji.”
Ao “katika inchi.”
Ao “katika kuwapo kwako.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Usimwange nafsi yangu.”
Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
Ao “makila yao.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Wakati nguvu zinaniisha.”
Tnn., “ananitambua.”
Ao “anahangaikia nafsi yangu.”
Tnn., “Fungu langu.”
Ao “Tosha nafsi yangu.”
Ao “anafuatilia nafsi yangu.”
Ao “Nguvu zangu zinaisha.”
Ao “Ninatafakari.”
Ao “Ninajifunza.”
Ao “Nafsi yangu iko.”
Tnn., “Roho yangu imefikia.”
Ao “kaburi.”
Ao “Kwa maana ninakuinulia nafsi yangu.”
Ao “katika inchi ya unyoofu.”
Ao “uokoe nafsi yangu.”
Tnn., “nyamazisha.”
Ao “Mahali pangu salama pa juu.”
Ao “kunja.”
Ao “kushikwa na.”
Tnn., “Na mukono wao wa kuume ni mukono wa kuume wa uongo.”
Ao “Nitakupigia muziki.”
Ao “wokovu.”
Ao “hawatapasukiwa na mimba.”
Ao “hauwezi kueleweka.”
Ao “nitatafakari.”
Ao “nguvu zako.”
Ao “neema.”
Ao “kwa unyoofu.”
Tnn., “Miili yote isifu.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “Nitamupigia Mungu wangu muziki.”
Ao “watu wenye vyeo.”
Ao “Pumuzi.”
Ao “anapotosha njia ya waovu.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “kumupigia Mungu wetu muziki.”
Ao “mwenye uwezo katika nguvu.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Tnn., “mafuta ya ngano.”
Ao “neige.”
Ao “barafu yake.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Tnn., “mbingu za mbingu.”
Ao “neige.”
Tnn., “mabikira.”
Tnn., “pembe.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “wamupigie muziki.”
Ao “tari.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “anga lenye kutoa ushahidi juu ya.”
Ao “tari.”
Ao “zumari.”
Ao “Haleluya!” “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.