Barua ya Kwanza kwa Wakorintho
1 Paulo, aliyeitwa kuwa mtume+ wa Yesu Kristo kupitia mapenzi ya Mungu,+ na Sosthene+ ndugu yetu 2 kwa kutaniko la Mungu lililo katika Korintho,+ kwenu ninyi ambao mmetakaswa+ katika muungano na Kristo Yesu, mlioitwa kuwa watakatifu,+ pamoja na wote ambao kila mahali wanaliitia jina+ la Bwana wetu, Yesu Kristo, Bwana wao na wetu:+
3 Na muwe na fadhili zisizostahiliwa+ na amani+ kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.+
4 Sikuzote ninamshukuru Mungu kwa ajili yenu kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu mlizopewa katika Kristo Yesu;+ 5 kwamba katika kila jambo mmetajirishwa+ katika yeye, katika uwezo kamili wa kusema na katika ujuzi kamili,+ 6 kama vile ushahidi juu ya Kristo+ ulivyofanywa kuwa imara katikati yenu, 7 ili kwamba msipungukiwe katika zawadi+ yoyote hata kidogo, huku mkiungojea kwa hamu ufunuo+ wa Bwana wetu Yesu Kristo. 8 Yeye pia atawafanya ninyi imara+ mpaka mwisho, ili msiwe na shtaka+ lolote katika siku+ ya Bwana wetu Yesu Kristo.+ 9 Mungu ni mwaminifu,+ aliyewaita kuingia katika ushirika+ pamoja na Mwana wake Yesu Kristo Bwana wetu.
10 Sasa nawahimiza+ ninyi, akina ndugu, kupitia jina+ la Bwana wetu Yesu Kristo kwamba nyote mseme kwa upatano,+ na kwamba kusiwe na migawanyiko+ katikati yenu, bali kwamba muunganishwe vema katika akili ileile na katika njia ileile ya kufikiri.+ 11 Kwa maana, ndugu zangu, wale wa nyumba ya Kloe walinifunulia+ juu yenu kwamba kuna magombano kati yenu. 12 Ninalomaanisha ni hili, kwamba kila mmoja wenu anasema: “Mimi ni wa Paulo,” “Lakini mimi ni wa Apolo,”+ “Lakini mimi ni wa Kefa,” “Lakini mimi ni wa Kristo.” 13 Kristo amegawanyika.+ Je, Paulo alitundikwa mtini kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa+ katika jina la Paulo? 14 Mimi nashukuru kwa kuwa sikubatiza hata mmoja wenu isipokuwa Krispo+ na Gayo,+ 15 ili yeyote asiseme kwamba mlibatizwa katika jina langu. 16 Ndiyo, niliibatiza pia nyumba ya Stefana.+ Kuhusu wale wengine, sijui kama nilimbatiza mwingine yeyote. 17 Kwa maana Kristo alinituma,+ si kwenda kubatiza, bali kwenda kutangaza habari njema, si kwa maneno ya hekima,+ ili mti wa mateso wa Kristo usifanywe kutofaa kitu.
18 Kwa maana neno juu ya mti wa mateso ni upumbavu+ kwa wale wanaoangamia,+ lakini kwetu sisi tunaookolewa+ ni nguvu za Mungu.+ 19 Kwa maana imeandikwa: “Nitaiangamiza hekima ya watu wenye hekima,+ na akili ya watu wenye akili+ nitaitupa kando.”+ 20 Yuko wapi mtu mwenye hekima? Yuko wapi mwandishi?+ Yuko wapi mwenye kubishania+ maneno wa mfumo huu wa mambo?+ Je, Mungu hakuifanya hekima ya ulimwengu iwe upumbavu?+ 21 Maana, kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kupitia hekima yake+ haukuja kumjua Mungu,+ Mungu aliona vema kupitia upumbavu+ wa linalohubiriwa awaokoe wale wanaoamini.
22 Kwa maana Wayahudi wanaomba ishara+ na Wagiriki wanatafuta hekima;+ 23 lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyetundikwa mtini,+ kwa Wayahudi ni sababu ya kujikwaa+ lakini kwa mataifa ni upumbavu;+ 24 hata hivyo, kwa wale walioitwa, Wayahudi na Wagiriki, Kristo ni nguvu+ za Mungu na hekima+ ya Mungu. 25 Kwa sababu kitu kipumbavu cha Mungu ni chenye hekima zaidi kuliko wanadamu, na kitu dhaifu cha Mungu ni chenye nguvu zaidi kuliko wanadamu.+
26 Kwa maana mnaona mwito wake kwenu, akina ndugu, kwamba si wengi wenye hekima+ katika njia ya kimwili walioitwa,+ si wengi wenye nguvu,+ si wengi wa uzawa wa cheo; 27 bali Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu,+ ili awaaibishe watu wenye hekima; na Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu, ili aviaibishe vitu vyenye nguvu;+ 28 na Mungu alivichagua vitu vinyonge vya ulimwengu na vitu vinavyodharauliwa, vitu ambavyo si kitu,+ ili kuvifanya viwe si kitu+ vitu ambavyo ni kitu 29 ili mwili wowote usijisifu+ machoni pa Mungu. 30 Lakini ni kwa sababu yake kwamba ninyi mko katika muungano na Kristo Yesu, ambaye kwetu amekuwa hekima+ kutoka kwa Mungu, pia uadilifu+ na utakaso+ na kuachiliwa huru kupitia fidia;+ 31 ili iwe kama ilivyoandikwa: “Yeye anayejisifu, na ajisifu katika Yehova.”+
2 Na kwa hiyo mimi, nilipokuja kwenu, akina ndugu, sikuja na wingi wa maneno+ au wa hekima nikiwatangazia siri takatifu+ ya Mungu. 2 Kwa maana niliamua kutojua kitu chochote katikati yenu isipokuwa Yesu Kristo,+ naye akiwa ametundikwa mtini. 3 Nami nilikuja kwenu katika udhaifu na katika woga na kwa kutetemeka kwingi;+ 4 na maneno yangu na mambo niliyohubiri hayakuwa kwa maneno yenye kushawishi ya hekima bali kwa wonyesho wa roho na nguvu,+ 5 ili imani yenu iwe, si katika hekima+ ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu.+
6 Basi tunasema hekima katikati ya wale ambao ni wakomavu,+ lakini si hekima+ ya mfumo huu wa mambo wala ile ya watawala wa mfumo huu wa mambo,+ ambao watakuja kuwa si kitu.+ 7 Bali tunasema hekima ya Mungu katika siri takatifu,+ hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliagiza kimbele kabla ya mifumo+ ya mambo kwa ajili ya utukufu wetu. 8 Hekima hii hakuna hata mmoja wa watawala+ wa mfumo huu wa mambo aliyeijua,+ kwa maana kama wao wangaliijua hawangalimtundika mtini+ Bwana mwenye utukufu. 9 Lakini kama ilivyoandikwa: “Jicho halijaona na sikio halijasikia, wala hayajawaziwa katika moyo wa mwanadamu mambo ambayo Mungu amewatayarishia wale wanaompenda.”+ 10 Kwa maana ni kwetu sisi Mungu ameyafunua+ kupitia roho+ yake, kwa maana roho+ huchunguza ndani ya mambo yote, hata mambo mazito+ ya Mungu.
11 Kwa maana ni nani kati ya wanadamu anayejua mambo ya mwanadamu isipokuwa roho+ ya mwanadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo, pia, hakuna ambaye amekuja kuyajua mambo ya Mungu, isipokuwa roho+ ya Mungu. 12 Basi sisi tulipokea, si roho+ ya ulimwengu, bali roho+ inayotoka kwa Mungu, ili tuyajue mambo ambayo Mungu ametupa sisi kwa fadhili.+ 13 Mambo hayo tunayasema pia, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya binadamu,+ bali kwa yale yanayofundishwa kwa roho,+ tunapounganisha mambo ya kiroho pamoja na maneno ya kiroho.+
14 Lakini mtu wa kimwili hayapokei mambo ya roho ya Mungu, kwa maana hayo ni upumbavu kwake; naye hawezi kuyajua,+ kwa sababu hayo huchunguzwa kiroho. 15 Hata hivyo, mtu wa kiroho+ huchunguza mambo yote, lakini yeye mwenyewe hachunguzwi+ na mwanadamu yeyote. 16 Kwa maana “ni nani ameijua akili ya Yehova,+ ndipo amfundishe?”+ Lakini sisi tunayo akili+ ya Kristo.
3 Na kwa hiyo, akina ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu wa kiroho,+ bali kama watu wa kimwili, kama watoto+ katika Kristo. 2 Niliwalisha ninyi maziwa, si chakula,+ kwa maana mlikuwa bado hamna nguvu za kutosha. Kwa kweli, hata sasa hamna nguvu za kutosha,+ 3 kwa maana bado ninyi ni wa kimwili.+ Kwa kuwa kuna wivu na mizozo kati yenu,+ je, ninyi si wa kimwili na je, hamtembei kama wanadamu wanavyotembea?+ 4 Kwa maana mtu anaposema: “Mimi ni wa Paulo,” lakini mwingine anasema: “Mimi ni wa Apolo,”+ je, ninyi si wanadamu tu?
5 Basi, Apolo+ ni nani? Ndiyo, Paulo ni nani? Wahudumu+ ambao kupitia wao mlikuja kuwa waamini, kama vile Bwana alivyompa kila mmoja. 6 Mimi nilipanda,+ Apolo akatia maji,+ lakini Mungu akaendelea kuikuza;+ 7 hivi kwamba yeye anayepanda si kitu+ wala yeye anayetia maji, bali Mungu anayeikuza.+ 8 Basi yeye anayepanda na yeye anayetia maji ni kitu kimoja,+ lakini kila mtu atapokea thawabu yake mwenyewe kulingana na kazi yake mwenyewe.+ 9 Kwa maana sisi ni wafanyakazi wenzi wa Mungu.+ Ninyi ni shamba la Mungu linalolimwa,+ jengo la Mungu.+
10 Kulingana na fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu nilizopewa, mimi kama msimamizi wa ujenzi mwenye hekima niliweka msingi,+ lakini mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja na aendelee kuangalia jinsi anavyojenga juu yake.+ 11 Kwa maana hakuna mtu anayeweza kuweka msingi+ mwingine wowote kuliko ule uliowekwa, ambao ni Yesu Kristo.+ 12 Basi yeyote akijenga juu ya msingi huo dhahabu, fedha, mawe ya thamani, vifaa vya mbao, nyasi kavu, majani makavu, 13 kazi ya kila mmoja itafunuliwa, kwa maana ile siku itaifichua, kwa sababu itafunuliwa kwa njia ya moto;+ na moto wenyewe utaonyesha kazi ya kila mmoja ni ya aina gani. 14 Kazi ya yeyote ambayo ameijenga juu yake ikibaki,+ atapokea thawabu;+ 15 kazi ya yeyote ikiteketea, atapata hasara, lakini yeye mwenyewe ataokolewa;+ lakini, ikiwa hivyo, itakuwa ni kama kupitia katika moto.+
16 Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu,+ na kwamba roho ya Mungu inakaa ndani yenu?+ 17 Yeyote akiliangamiza hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza yeye;+ kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu,+ nanyi ni+ hekalu+ hilo.
18 Yeyote asiwe akijishawishi mwenyewe: Yeyote kati yenu akifikiri yeye ni mwenye hekima+ katika mfumo huu wa mambo, acheni awe mpumbavu, ili awe mwenye hekima.+ 19 Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upumbavu kwa Mungu;+ kwa maana imeandikwa: “Yeye huwakamata wenye hekima katika ujanja+ wao wenyewe.” 20 Na tena: “Yehova anajua kwamba kufikiri kwa watu wenye hekima ni kwa ubatili.”+ 21 Kwa hiyo yeyote asiwe akijisifu katika watu; kwa maana vitu vyote ni vyenu,+ 22 kama ni Paulo au Apolo+ au Kefa au ulimwengu au uzima au kifo au mambo yaliyo hapa sasa au mambo yatakayokuja,+ vitu vyote ni vyenu; 23 nanyi ni wa Kristo;+ naye Kristo ni wa Mungu.+
4 Acheni mtu atukadirie sisi hivyo kuwa tuko chini ya+ Kristo nasi ni wasimamizi-nyumba+ wa siri takatifu+ za Mungu. 2 Mbali na hilo, katika hali hii, kinachoangaliwa katika wasimamizi-nyumba+ ni mtu kupatwa akiwa mwaminifu.+ 3 Basi kwangu ni jambo dogo sana kwamba ninyi au baraza la kibinadamu mnichunguze.+ Hata mimi sijichunguzi mwenyewe. 4 Kwa maana sifahamu+ kitu chochote dhidi yangu mwenyewe. Lakini kwa hilo sionyeshwi kuwa mwadilifu, bali yeye anayenichunguza ni Yehova.+ 5 Kwa hiyo msihukumu+ kitu chochote kabla ya wakati unaofaa, mpaka Bwana aje,+ atakayeyaleta kwenye nuru mambo ya siri yaliyo ya giza+ na pia kuyafunua mashauri ya mioyo,+ na ndipo kila mtu atakapopata sifa yake kutoka kwa Mungu.+
6 Basi, akina ndugu, mambo haya nimeyahamisha ili kuyatumia juu yangu mwenyewe na Apolo+ kwa faida yenu, ili katika hali yetu mjifunze kanuni: “Msipite mambo yaliyoandikwa,”+ ili msijivune+ mtu mmoja-mmoja kwa kumpendelea mtu mmoja juu ya mwingine.+ 7 Kwa maana ni nani anayekufanya wewe kuwa tofauti+ na mwingine? Kwa kweli, una nini ambacho hukupokea?+ Basi, ikiwa kwa kweli ulikipokea,+ kwa nini unajisifu+ kana kwamba hukukipokea?
8 Ninyi tayari mmepata shibe yenu, sivyo? Ninyi tayari ni matajiri, sivyo?+ Mmeanza kutawala mkiwa wafalme+ bila sisi, sivyo? Nami ningalipenda kwamba muwe mmeanza kutawala mkiwa wafalme, ili sisi pia tutawale pamoja nanyi tukiwa wafalme.+ 9 Kwa maana inaonekana kwangu kwamba Mungu ametuweka sisi mitume mwisho katika wonyesho wa hadharani+ kama watu waliowekewa kifo,+ kwa sababu tumekuwa tamasha+ kwa ulimwengu, na kwa malaika,+ na kwa wanadamu.+ 10 Sisi ni wapumbavu+ kwa sababu ya Kristo, lakini ninyi ni wenye busara+ katika Kristo; sisi ni dhaifu,+ lakini ninyi ni wenye nguvu;+ ninyi mna sifa njema,+ lakini sisi tumo katika aibu.+ 11 Mpaka saa hii sisi tunaendelea kupata njaa+ na pia kupata kiu+ na kuvaa mavazi machache+ na kupigwa+ huku na huku na kuwa bila makao+ 12 na kufanya kazi ya kutaabika,+ tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe.+ Tunapotukanwa, tunabariki;+ tunapoteswa, tunavumilia;+ 13 tunapoharibiwa sifa, tunasihi;+ tumekuwa kama takataka ya ulimwengu, uchafu wa vitu vyote, mpaka sasa.+
14 Ninaandika mambo haya, si ili kuwaaibisha ninyi, bali kuwaonya kama watoto wangu wapendwa.+ 15 Kwa maana ingawa huenda mkawa na watunzaji+ elfu kumi katika Kristo, hakika hamna baba wengi;+ kwa maana katika Kristo Yesu mimi nimekuwa baba yenu kupitia habari njema.+ 16 Kwa hiyo, nawasihi ninyi, iweni waigaji wangu.+ 17 Ndiyo sababu ninamtuma Timotheo kwenu,+ kwa kuwa yeye ni mtoto wangu mpendwa+ na mwaminifu katika Bwana; naye atawakumbusha ninyi njia zangu kuhusiana na Kristo Yesu,+ kama vile ninavyofundisha kila mahali katika kila kutaniko.
18 Wengine wamejivuna+ kana kwamba siji kwenu. 19 Lakini nitakuja kwenu hivi karibuni, Yehova akipenda,+ nami nitajua, si maneno ya wale ambao wanajivuna, bali nguvu zao. 20 Kwa maana ufalme wa Mungu hauko katika maneno, bali katika nguvu.+ 21 Mnataka nini? Je, nije kwenu nikiwa na fimbo,+ au kwa upendo na upole wa roho?+
5 Kwa kweli kuna habari kwamba kuna uasherati+ katikati yenu, tena uasherati wa namna ambayo hata haimo kati ya mataifa, kwamba mwanamume fulani ana mke wa baba yake.+ 2 Na je, ninyi mnajivuna,+ na badala yake hamwombolezi,+ ili mtu aliyefanya kitendo hicho aondolewe mbali kutoka kati yenu?+ 3 Mimi kwa kweli, ijapokuwa sipo katika mwili bali nipo katika roho, tayari nimemhukumu,+ kana kwamba nipo, mtu huyo ambaye amefanya tendo la namna hiyo, 4 kwamba katika jina la Bwana wetu Yesu, wakati mnapokuwa mmekusanyika pamoja, pia roho yangu pamoja na nguvu za Bwana wetu Yesu,+ 5 mkamkabidhi mtu wa namna hiyo kwa Shetani+ kwa ajili ya kuangamizwa kwa mwili, ili roho+ iokolewe katika siku ya Bwana.+
6 Sababu ya kujisifu+ kwenu si nzuri. Je, hamjui kwamba chachu kidogo huchachisha+ donge lote?+ 7 Ondoleeni mbali chachu ya zamani, ili muwe donge jipya,+ kulingana na mlivyo bila chachu. Kwa maana, kwa kweli, Kristo+ pasaka+ yetu ametolewa dhabihu.+ 8 Kwa hiyo na tufanye sherehe,+ si kwa chachu+ ya zamani, wala si kwa chachu+ ya ubaya na uovu,+ bali kwa keki zisizo na chachu za unyoofu na kweli.+
9 Katika barua yangu niliwaandikia ninyi mwache kuchangamana katika ushirika na waasherati, 10 si kumaanisha kabisa na waasherati+ wa ulimwengu+ huu au watu wenye pupa na wanyang’anyi au waabudu-sanamu. Ikiwa hivyo, kwa kweli ingewabidi mwondoke katika ulimwengu.+ 11 Lakini sasa ninawaandikia ninyi mwache kuchangamana katika ushirika+ pamoja na mtu yeyote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa+ au mwabudu-sanamu au mtukanaji au mlevi+ au mnyang’anyi, hata msile chakula pamoja na mtu wa namna hiyo. 12 Kwa maana inanihusu nini kuwahukumu wale walio nje?+ Je, ninyi hamwahukumu wale walio ndani,+ 13 huku Mungu akiwahukumu wale walio nje?+ “Ondoeni yule mtu mwovu kati yenu.”+
6 Je, yeyote kati yenu aliye na kesi+ juu ya mwingine anathubutu kwenda mahakamani mbele ya watu wasio waadilifu,+ na si mbele ya watakatifu?+ 2 Au je, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu+ ulimwengu?+ Na ikiwa ninyi mtauhukumu ulimwengu, je, hamstahili kuamua mambo yaliyo madogo sana?+ 3 Je, hamjui kwamba tutawahukumu malaika?+ Kwa nini, basi, isiwe mambo ya maisha haya? 4 Basi, ikiwa ninyi mna mambo ya maisha haya ya kuamuliwa,+ je, mnawaweka kuwa waamuzi wale watu wanaodharauliwa na kutaniko?+ 5 Ninasema ili kuwatia ninyi aibu.+ Je, ni kweli kwamba hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima+ kati yenu atakayeweza kuhukumu kati ya ndugu zake, 6 bali ndugu anaenda mahakamani pamoja na ndugu, na tena mbele ya wasio waamini?+
7 Basi, kwa kweli, inamaanisha kushindwa kwenu kabisa kwamba mnakuwa na mashtaka ya kisheria+ mtu na mwenzake. Kwa nini msiache mkosewe+ badala ya hivyo? Kwa nini msiache mpunjwe+ badala ya hivyo? 8 Kinyume cha hilo, mnawakosea na kuwapunja, tena ndugu zenu.+
9 Kwani! Je, hamjui kwamba watu wasio waadilifu hawataurithi ufalme wa Mungu?+ Msipotoshwe. Wala waasherati,+ wala waabudu-sanamu,+ wala wazinzi,+ wala wanaume wanaowekwa kwa ajili ya makusudi yasiyo ya asili,+ wala wanaume wanaolala na wanaume,+ 10 wala wezi, wala watu wenye pupa,+ wala walevi,+ wala watukanaji, wala wanyang’anyi hawataurithi ufalme wa Mungu.+ 11 Na bado wengine wenu mlikuwa hivyo.+ Lakini mmeoshwa mkawa safi,+ lakini mmetakaswa,+ lakini mmetangazwa kuwa waadilifu+ katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo+ na kwa roho ya Mungu wetu.+
12 Mambo yote ni halali kwangu; lakini si mambo yote yenye faida.+ Mambo yote ni halali+ kwangu; lakini mimi sitaruhusu kitu chochote kinitawale.+ 13 Vyakula kwa ajili ya tumbo, na tumbo kwa ajili ya vyakula;+ lakini Mungu atafanya hilo na pia hivyo viwe si kitu.+ Basi mwili si kwa ajili ya uasherati, bali kwa ajili ya Bwana;+ na Bwana ni kwa ajili ya mwili.+ 14 Lakini Mungu alimfufua Bwana+ na pia atatufufua sisi kutoka kwenye kifo+ kupitia nguvu zake.+
15 Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo+ vya Kristo?+ Basi, je, nitavichukua viungo vya Kristo na kuvifanya kuwa viungo vya kahaba?+ Hilo lisitendeke kamwe! 16 Kwani! Je, hamjui kwamba yeye ambaye ameungana na kahaba ni mwili mmoja naye? Kwa maana, “Hao wawili,” yeye asema, “watakuwa mwili mmoja.”+ 17 Lakini yeye ambaye ameungana na Bwana ni roho+ moja+ naye. 18 Ukimbieni uasherati.+ Kila dhambi nyingine ambayo mtu huenda akafanya iko nje ya mwili wake, lakini yeye aliye na mazoea ya kufanya uasherati anautendea dhambi mwili+ wake mwenyewe. 19 Kwani! Je, hamjui kwamba mwili wenu ni hekalu+ la roho takatifu ndani yenu,+ mliyo nayo kutoka kwa Mungu? Pia, ninyi si mali yenu wenyewe,+ 20 kwa maana mlinunuliwa kwa bei.+ Kwa vyovyote, mtukuzeni+ Mungu katika mwili+ wenu.
7 Basi kuhusu mambo ambayo mliandika habari zake, ni vema mwanamume asimguse+ mwanamke; 2 lakini, kwa sababu ya kuenea kwa uasherati,+ kila mwanamume na awe na mke+ wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe. 3 Mume na ampe mke wake haki+ yake; lakini mke pia na amfanyie vivyo hivyo mume wake.+ 4 Mke hana mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, bali mume wake anayo;+ vivyo hivyo, pia, mume hana mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, bali mke wake anayo.+ 5 Msiwe mkinyimana haki hiyo,+ ila kwa makubaliano kwa wakati uliowekwa,+ ili mtenge wakati kwa ajili ya sala na mje pamoja tena, ili Shetani asiendelee kuwajaribu+ kwa sababu ya ninyi kukosa kujizuia.+ 6 Hata hivyo, nasema hilo kwa njia ya kutoa ruhusa,+ si kwa njia ya amri.+ 7 Lakini ningalipenda watu wote wawe kama mimi mwenyewe nilivyo.+ Hata hivyo, kila mmoja ana zawadi+ yake mwenyewe kutoka kwa Mungu, mmoja kwa njia hii, mwingine kwa njia ile.
8 Sasa nawaambia waseja+ na wajane, ni vema kwao wabaki kama mimi nilivyo.+ 9 Lakini ikiwa hawawezi kujizuia,+ acheni wafunge ndoa,+ kwa maana ni bora kufunga ndoa kuliko kuwaka tamaa.+
10 Kwa watu waliofunga ndoa natoa maagizo, lakini si mimi bali ni Bwana,+ kwamba mke hapaswi kuondoka kwa mume wake;+ 11 lakini kwa kweli akiondoka, na akae mseja kama sivyo apatane tena na mume wake; na mume hapaswi kumwacha mke wake.
12 Lakini kwa wale wengine nawaaambia, ndiyo, mimi, si Bwana:+ Ikiwa ndugu yeyote ana mke asiyeamini, na bado mke huyo anakubali kukaa pamoja naye, basi asimwache; 13 na mwanamke aliye na mume asiyeamini, na bado mume huyo anakubali kukaa pamoja naye, basi asimwache mume wake. 14 Kwa maana mume asiyeamini hutakaswa kuhusiana na mke wake, na mke asiyeamini hutakaswa kuhusiana na huyo ndugu; kama sivyo, watoto wenu kwa kweli hawangekuwa safi,+ lakini sasa wao ni watakatifu.+ 15 Lakini yule asiyeamini akiondoka, acha aondoke;+ ndugu au dada hayumo katika utumwa chini ya hali za namna hiyo, lakini Mungu amewaita ninyi kwenye amani.+ 16 Kwa maana, wewe mke, unajuaje kama utamwokoa mume wako?+ Au, wewe mume, unajuaje kama utamwokoa mke wako?+
17 Isipokuwa, kama Yehova alivyompa kila mmoja fungu,+ kila mmoja na ajiendeshe kama Mungu alivyomwita.+ Na ndivyo ninavyoagiza+ katika makutaniko yote. 18 Je, mtu yeyote aliitwa akiwa ametahiriwa?+ Acheni asiwe asiyetahiriwa. Je, mtu yeyote ameitwa akiwa katika kutotahiriwa?+ Acheni asitahiriwe.+ 19 Kutahiriwa+ hakumaanishi kitu, na kutotahiriwa+ hakumaanishi kitu, lakini kushika amri za Mungu kuna maana.+ 20 Katika hali yoyote ile ambayo kila mmoja aliitwa,+ acheni abaki katika hiyo.+ 21 Je, uliitwa ukiwa mtumwa? Usiache hilo likutie wasiwasi;+ lakini ikiwa unaweza pia kuwa huru, afadhali utwae nafasi hiyo. 22 Kwa maana yeyote katika Bwana aliyeitwa akiwa mtumwa ni mtu aliyewekwa huru wa Bwana;+ vivyo hivyo yeye aliyeitwa akiwa mtu aliye huru+ ni mtumwa+ wa Kristo. 23 Mlinunuliwa kwa bei;+ acheni kuwa watumwa+ wa wanadamu. 24 Katika hali+ yoyote ile ambayo kila mmoja aliitwa, akina ndugu, acheni abaki katika hali hiyo akishirikiana na Mungu.
25 Sasa kuhusu mabikira sina amri kutoka kwa Bwana, lakini natoa maoni+ yangu nikiwa mtu aliyeonyeshwa rehema na Bwana+ kuwa mwaminifu.+ 26 Kwa hiyo naona hili kuwa ni jema kwa sababu ya uhitaji uliopo pamoja nasi, kwamba ni vema kwa mtu kuendelea kama alivyo.+ 27 Je, umefungwa kwa mke?+ Uache kutafuta kufunguliwa.+ Je, umefunguliwa kutoka kwa mke? Uache kutafuta mke. 28 Lakini hata kama ukifunga ndoa, hutakuwa ukifanya dhambi.+ Na kama bikira akifunga ndoa, mtu huyo hatakuwa akifanya dhambi. Hata hivyo, wale wanaofanya hivyo watakuwa na dhiki katika mwili wao.+ Lakini mimi ninawaepusha ninyi.
29 Zaidi ya hayo, nasema hili, akina ndugu, wakati uliobaki umepungua.+ Tangu sasa wale walio na wake na wawe kana kwamba hawana,+ 30 na pia wale wanaolia wawe kama wale wasiolia, na wale wanaoshangilia wawe kama wale wasioshangilia, na wale wanaonunua wawe kama wale wasio na kitu, 31 na wale wanaoutumia ulimwengu+ wawe kama wale wasioutumia kwa ukamili; kwa maana tamasha ya ulimwengu huu inabadilika.+ 32 Kwa kweli, nataka ninyi msiwe na mahangaiko.+ Mwanamume ambaye hajaoa huhangaikia mambo ya Bwana, jinsi anavyoweza kupata kibali cha Bwana. 33 Lakini mwanamume aliyeoa huhangaikia+ mambo ya ulimwengu, jinsi anavyoweza kupata kibali cha mke wake,+ 34 naye amegawanyika. Zaidi ya hayo, mwanamke mseja, na bikira, huhangaikia mambo ya Bwana,+ ili awe mtakatifu katika mwili wake na pia katika roho yake. Hata hivyo, mwanamke aliyeolewa huhangaikia mambo ya ulimwengu, jinsi anavyoweza kupata kibali cha mume wake.+ 35 Lakini nasema jambo hili kwa faida yenu ya kibinafsi, si ili niwategee mtego, bali ili niwasukume ninyi kwenye lile linalofaa+ na lile linalomaanisha kumhudumia Bwana daima bila kukengeushwa fikira.+
36 Lakini kama yeyote akiona kwamba anajiendesha isivyofaa kuelekea ubikira+ wake, ikiwa huo umepita upeo wa ujana, na hivyo ndivyo inavyopaswa kutendeka, acheni afanye lile analotaka; hafanyi dhambi. Acheni afunge ndoa.+ 37 Lakini ikiwa yeyote ametulia katika moyo wake, akiwa hana uhitaji wowote, lakini ana mamlaka juu ya nia yake mwenyewe naye amefanya uamuzi huu katika moyo wake mwenyewe, kutunza ubikira wake mwenyewe, yeye atafanya vema.+ 38 Kwa hiyo yeye pia anayeufungisha ndoa ubikira wake anafanya vema,+ lakini yeye asiyeufungisha ndoa atafanya vema zaidi.+
39 Mke amefungwa wakati wote ambao mume wake yuko hai.+ Lakini mume wake akilala usingizi katika kifo, yeye yuko huru kuolewa na yeyote anayemtaka, katika Bwana tu.+ 40 Lakini mwanamke huyo ni mwenye furaha zaidi akibaki kama alivyo,+ kwa maoni yangu. Hakika nafikiri mimi pia nina roho ya Mungu.+
8 Basi kuhusu vyakula vinavyotolewa kwa sanamu:+ tunajua sisi sote tuna ujuzi.+ Ujuzi huleta majivuno, lakini upendo hujenga.+ 2 Yeyote akifikiri amejipatia ujuzi juu ya kitu fulani,+ bado hajakijua kama vile anavyopaswa kukijua.+ 3 Lakini ikiwa yeyote anampenda Mungu,+ huyo anajulikana naye.+
4 Sasa kuhusu kula+ vyakula vinavyotolewa kwa sanamu, tunajua kwamba sanamu si kitu+ katika ulimwengu, na kwamba hakuna Mungu isipokuwa mmoja.+ 5 Kwa maana hata ingawa kuna wale wanaoitwa “miungu,”+ iwe wako mbinguni+ au duniani,+ kama vile kulivyo na “miungu” mingi na “mabwana” wengi,+ 6 kwa kweli kwetu sisi kuna Mungu mmoja+ aliye Baba,+ ambaye vitu vyote vimetoka kwake, na sisi kwa ajili yake;+ na kuna Bwana+ mmoja, Yesu Kristo,+ ambaye vitu vyote vimepitia kwake,+ na sisi kupitia yeye.
7 Hata hivyo, si watu wote walio na ujuzi huu;+ bali wengine, wakiwa wameizoea sanamu mpaka sasa, hula chakula kama kitu kilichotolewa dhabihu kwa sanamu,+ na dhamiri yao, kwa kuwa ni dhaifu, inatiwa unajisi.+ 8 Lakini chakula hakitatupendekeza kwa Mungu;+ tukikosa kula, hatupungukiwi, na, tukila, hatupati sifa kwetu wenyewe.+ 9 Lakini endeleeni kuangalia kwamba hii mamlaka yenu isije kuwa kwa njia fulani kikwazo kwa wale walio dhaifu.+ 10 Kwa maana yeyote akikuona wewe, uliye na ujuzi, ukiwa umeketi kwenye mlo katika hekalu la sanamu, je, dhamiri ya huyo aliye dhaifu haitajengwa kufikia hatua ya kula vyakula vilivyotolewa kwa sanamu?+ 11 Kwa kweli, kwa ujuzi wako, mtu ambaye ni dhaifu anaharibiwa, ndugu yako ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.+ 12 Lakini ninyi mnapotenda dhambi hivyo juu ya ndugu zenu na kuiumiza dhamiri+ yao iliyo dhaifu, mnamtendea dhambi Kristo. 13 Kwa hiyo, ikiwa chakula kinamkwaza ndugu yangu,+ mimi sitakula nyama tena kamwe, ili nisije nikamkwaza+ ndugu yangu.
9 Je, mimi si huru?+ Je, mimi si mtume?+ Je, mimi sijamwona Yesu Bwana wetu?+ Je, ninyi si kazi yangu katika Bwana? 2 Ikiwa mimi si mtume kwa wengine, hakika mimi ni mtume kwenu, kwa maana ninyi ndio muhuri unaothibitisha+ utume wangu kuhusiana na Bwana.
3 Kwa wale wanaonichunguza, najitetea hivi:+ 4 Sisi tuna mamlaka ya kula+ na kunywa, sivyo? 5 Sisi tuna mamlaka ya kumchukua pamoja nasi dada akiwa mke,+ hata kama vile mitume wale wengine na ndugu za Bwana+ na Kefa,+ sivyo? 6 Au je, ni Barnaba+ na mimi peke yetu tusio na mamlaka ya kujiepusha kufanya kazi ya kimwili?+ 7 Ni nani ambaye hutumika akiwa askari kwa gharama yake mwenyewe? Ni nani ambaye hupanda shamba la mizabibu na asile matunda yake?+ Au ni nani ambaye huchunga kundi na asinywe sehemu ya maziwa ya kundi?+
8 Je, ninasema mambo haya kwa viwango vya kibinadamu?+ Au je, Sheria+ haisemi mambo hayo pia? 9 Kwa maana katika sheria ya Musa imeandikwa: “Hupaswi kumfunga kinywa ng’ombe-dume anapopura nafaka.”+ Je, ni ng’ombe ambao Mungu anajali? 10 Au, je, yeye hasemi hilo kwa ajili yetu tu? Kwa kweli hilo liliandikwa kwa ajili yetu,+ kwa sababu mtu anayelima anapaswa kulima akiwa na tumaini na mtu anayepura anapaswa kupura akiwa na tumaini la kula.+
11 Ikiwa tumepanda vitu vya kiroho+ kwenu, je, ni jambo kubwa tukivuna kutoka kwenu vitu vilivyo kwa ajili ya mwili?+ 12 Ikiwa watu wengine hushiriki mamlaka hii juu yenu,+ je, si hivyo hata zaidi kwetu? Hata hivyo, sisi hatujatumia mamlaka hii,+ bali tunavumilia mambo yote, ili tusiweke kizuizi chochote kwa habari njema+ juu ya Kristo. 13 Je, hamjui kwamba watu wanaofanya kazi takatifu hula+ vitu vya hekalu, na wale wanaohudumu+ daima kwenye madhabahu hupata fungu lao wenyewe pamoja na madhabahu? 14 Vivyo hivyo, pia, Bwana aliagiza+ kuwa wale wanaotangaza habari njema waishi kwa njia ya habari njema.+
15 Lakini mimi sijatumia hata mmoja wa mipango hiyo.+ Kwa kweli, sijaandika mambo haya ili iwe hivyo kuhusiana na mimi, kwa maana ingekuwa vizuri zaidi kwangu nife kuliko—hakuna mtu atakayefanya sababu yangu ya kujisifu+ iwe bure! 16 Ikiwa, sasa, ninatangaza habari njema,+ hiyo si sababu ya mimi kujisifu, kwa maana nimewekewa sharti.+ Kwa kweli, ole+ wangu mimi ikiwa sitangazi habari njema! 17 Kama nikifanya hilo kwa kupenda,+ nina thawabu;+ lakini kama nikifanya hilo kinyume cha kupenda kwangu, vyovyote vile nina usimamizi-nyumba+ niliokabidhiwa. 18 Basi, thawabu yangu ni nini? Kwamba ninapotangaza habari njema niitoe habari njema bila gharama,+ kusudi nisitumie vibaya mamlaka yangu katika habari njema.
19 Kwa maana, ingawa niko huru kutoka kwa watu wote, nimejifanya kuwa mtumwa+ kwa wote, ili niwapate+ watu walio wengi zaidi. 20 Na kwa hiyo kwa Wayahudi+ nilikuwa kama Myahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria nilikuwa kama aliye chini ya sheria,+ ingawa mimi mwenyewe siko chini ya sheria,+ ili niwapate wale walio chini ya sheria. 21 Kwa wale wasio na sheria+ nilikuwa kama asiye na sheria,+ ijapokuwa mimi siko bila sheria kwa Mungu bali niko chini ya sheria+ kwa Kristo,+ ili niwapate wale wasio na sheria. 22 Kwa walio dhaifu nilikuwa dhaifu, ili niwapate walio dhaifu.+ Nimekuwa mambo yote kwa watu wa namna zote,+ ili kwa vyovyote niwaokoe wengine. 23 Lakini ninafanya mambo yote kwa ajili ya habari njema, ili niishiriki+ hiyo pamoja na wengine.
24 Je, hamjui kwamba wakimbiaji+ katika mbio wote hukimbia, lakini ni mmoja tu anayepokea tuzo?+ Kimbieni+ kwa namna ya kwamba mweze kupata tuzo.+ 25 Zaidi ya hayo, kila mtu anayeshiriki katika shindano hujizuia+ katika mambo yote. Basi wao, bila shaka, hushindana ili wapate taji+ linaloharibika, lakini sisi ili tupate taji lisiloharibika.+ 26 Kwa hiyo, jinsi ninavyokimbia+ si bila uhakika; jinsi ninavyoelekeza ngumi zangu ni ili nisiwe nikipiga hewa;+ 27 lakini naupigapiga mwili+ wangu na kuuongoza kama mtumwa, ili, baada ya mimi kuwahubiria wengine, mimi mwenyewe nisikataliwe+ kwa njia fulani.
10 Basi sitaki mkose kujua, akina ndugu, kwamba mababu zetu walikuwa wote chini ya wingu+ na wote walipita katika bahari + 2 na wote walibatizwa katika Musa+ kupitia wingu na bahari; 3 na wote walikula chakula kilekile cha kiroho+ 4 na wote walikunywa maji+ yaleyale ya kiroho. Kwa maana walikuwa wakinywa kutokana na mwamba+ wa kiroho uliowafuata, na mwamba+ huo ulimaanisha Kristo.+ 5 Hata hivyo, Mungu hakuonyesha kibali+ chake juu ya walio wengi kati yao, kwa maana waliangamizwa+ nyikani.
6 Basi mambo hayo yalikuwa vielelezo kwetu sisi, ili tusiwe watu wanaotamani mambo mabaya,+ kama wao walivyoyatamani. 7 Wala tusiwe waabudu-sanamu, kama baadhi yao walivyofanya;+ kama ilivyoandikwa: “Watu wakaketi ili wale na kunywa, nao wakasimama wapate kujifurahisha.”+ 8 Wala tusifanye uasherati, kama baadhi yao walivyofanya uasherati,+ na kuanguka, 23,000 kati yao katika siku moja.+ 9 Wala tusimjaribu Yehova,+ kama baadhi yao walivyomjaribu,+ na kuangamizwa na nyoka.+ 10 Wala tusiwe wanung’unikaji, kama baadhi yao walivyonung’unika,+ na kuangamizwa na mwangamizaji.+ 11 Basi mambo hayo yaliendelea kuwapata kuwa vielelezo, nayo yaliandikwa ili kuwa onyo+ kwetu sisi ambao tumefikiwa na miisho ya mifumo ya mambo.+
12 Kwa hiyo yeye anayefikiri kuwa amesimama na ajihadhari kwamba asianguke.+ 13 Hakuna jaribu ambalo limewapata ninyi ila lile lililo kawaida kwa watu.+ Lakini Mungu ni mwaminifu,+ naye hatawaacha ninyi mjaribiwe kupita mnavyoweza kuhimili,+ bali pamoja na hilo jaribu ataifanya pia njia ya kutokea+ kusudi mweze kulivumilia.
14 Kwa hiyo, wapendwa wangu, ikimbieni+ ibada ya sanamu.+ 15 Nasema kana kwamba ni kwa watu wenye utambuzi;+ hukumuni ninyi wenyewe lile ninalosema. 16 Kikombe+ cha baraka ambacho tunabariki, je, hicho si kushiriki katika damu ya Kristo? Ule mkate ambao tunamega,+ je, huo si kushiriki katika mwili wa Kristo?+ 17 Kwa sababu kuna mkate mmoja, sisi, ingawa tuko wengi,+ ni mwili mmoja,+ kwa maana sisi sote tunakula huo mkate mmoja.+
18 Tazameni kile ambacho ni Israeli kwa njia ya kimwili:+ Je, wale wanaokula dhabihu si washiriki pamoja na madhabahu?+ 19 Basi, niseme nini? Kwamba kile ambacho kimetolewa dhabihu kwa sanamu ni kitu, au kwamba sanamu ni kitu?+ 20 Hapana; bali nasema kwamba vitu ambavyo mataifa huvitoa dhabihu wao huvitoa dhabihu kwa roho waovu,+ na si kwa Mungu; nami sitaki ninyi muwe washiriki pamoja na roho waovu.+ 21 Hamwezi kuwa mkinywa kikombe cha Yehova+ na kikombe cha roho waovu; hamwezi kuwa mkishiriki “meza ya Yehova”+ na meza ya roho waovu. 22 Au je, “tunamchochea Yehova kuwa na wivu”?+ Je, sisi tuna nguvu+ zaidi kuliko yeye?
23 Mambo yote ni halali; lakini si mambo yote yaliyo na faida.+ Mambo yote ni halali;+ lakini si mambo yote yanayojenga.+ 24 Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe,+ bali ile ya yule mtu mwingine.+
25 Endeleeni kula kila kitu kinachouzwa katika soko la nyama,+ bila kuchunguza kwa sababu ya dhamiri yenu;+ 26 kwa maana “dunia na vyote vinavyoijaza+ ni vya Yehova.”+ 27 Yeyote kati ya wasio waamini akiwaalika nanyi mtake kwenda, kuleni kila kitu kinachowekwa mbele yenu,+ bila kuchunguza kwa sababu ya dhamiri yenu.+ 28 Lakini yeyote akiwaambia ninyi: “Hiki ni kitu kilichotolewa katika dhabihu,” msile kwa sababu ya yule aliyefunua hilo na kwa sababu ya dhamiri.+ 29 “Dhamiri,” nasema, si yako mwenyewe, bali ile ya yule mtu mwingine. Kwa maana kwa nini iwe kwamba uhuru wangu unahukumiwa na dhamiri ya mtu mwingine?+ 30 Ikiwa nakula nikiwa na shukrani, kwa nini nitukanwe juu ya kile ninachotolea shukrani?+
31 Kwa hiyo, kama mnakula au mnakunywa au mnafanya jambo lingine lolote, fanyeni mambo yote kwa utukufu wa Mungu.+ 32 Epukeni kuwa vikwazo+ kwa Wayahudi na vilevile kwa Wagiriki na kwa kutaniko la Mungu, 33 kama vile mimi ninavyowapendeza watu wote katika mambo yote,+ bila kutafuta faida yangu mwenyewe+ bali ile ya walio wengi, ili wapate kuokolewa.+
11 Iweni waigaji wangu, kama vile mimi nilivyo mwigaji wa Kristo.+
2 Sasa nawasifu ninyi kwa sababu katika mambo yote mnanikumbuka na mnayashika sana mapokeo+ kama vile nilivyowapa ninyi. 3 Lakini nataka mjue kwamba kichwa cha kila mwanamume ni Kristo;+ nacho kichwa cha mwanamke ni mwanamume;+ nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.+ 4 Kila mwanamume ambaye husali au kutoa unabii akiwa na kitu juu ya kichwa chake hukiaibisha kichwa chake;+ 5 lakini kila mwanamke ambaye husali au kutoa unabii+ kichwa chake kikiwa hakijafunikwa hukiaibisha kichwa chake,+ kwa maana ni kana kwamba yeye ni mwanamke mwenye kichwa kilichonyolewa.+ 6 Kwa maana ikiwa mwanamke hajifuniki, na akatwe nywele pia; lakini ikiwa inafedhehesha kwa mwanamke kukatwa nywele au kunyolewa,+ basi na afunikwe.+
7 Kwa maana mwanamume hapaswi kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano+ na utukufu wa Mungu;+ lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.+ 8 Kwa maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke alitoka katika mwanamume;+ 9 na, zaidi ya hayo, mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume.+ 10 Ndiyo sababu mwanamke anapaswa kuwa na ishara ya mamlaka juu ya kichwa chake+ kwa sababu ya malaika.+
11 Tena, kuhusiana na Bwana mwanamke si bila mwanamume wala mwanamume si bila mwanamke.+ 12 Kwa maana kama vile mwanamke ametoka katika mwanamume,+ vivyo hivyo pia mwanamume amepitia katika mwanamke;+ lakini vitu vyote vimetoka kwa Mungu.+ 13 Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa mwanamke kusali kwa Mungu pasipo kichwa chake kufunikwa? 14 Je, maumbile yenyewe hayawafundishi ninyi kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu, ni aibu kwake; 15 lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu, ni utukufu+ kwake? Kwa sababu yeye amepewa nywele zake ziwe badala ya vazi la kichwani.+ 16 Hata hivyo, mtu yeyote akiwa na mwelekeo wa kubishania+ desturi fulani nyingine,+ sisi hatuna nyingine, wala makutaniko ya Mungu.
17 Lakini, ninapoyatoa maagizo haya, siwasifu ninyi kwa sababu mnakutana pamoja, si kwa ajili ya wema, bali kwa ajili ya ubaya kabisa.+ 18 Kwa maana kwanza kabisa, mnapokuja pamoja katika kutaniko, nasikia kwamba kuna migawanyiko katikati yenu;+ nami naamini jambo hilo kwa kiasi fulani. 19 Kwa maana lazima pia yaweko madhehebu+ katikati yenu, ili watu waliokubaliwa wapate pia kufunuliwa katikati yenu.+
20 Kwa hiyo, mnapokuja pamoja mahali pamoja, haiwezekani kula mlo wa jioni wa Bwana.+ 21 Kwa maana, mnapoula, kila mtu hutangulia kula mlo wake mwenyewe wa jioni, hivi kwamba mmoja ana njaa lakini mwingine amelewa. 22 Je, hamna nyumba za kulia mlo na kunywea?+ Au je, mnalidharau kutaniko la Mungu na kuwaaibisha wale wasio na kitu?+ Nitawaambia ninyi nini? Je, nitawasifu ninyi? Katika hilo siwasifu ninyi.
23 Kwa maana nilipokea kutoka kwa Bwana kile nilichowapa ninyi pia, kwamba Bwana Yesu katika ule usiku+ aliokuwa akienda kutolewa alichukua mkate 24 na, baada ya kutoa shukrani, akaumega+ na kusema: “Huu unamaanisha mwili+ wangu ambao ni kwa ajili yenu. Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka+ mimi.” 25 Akafanya vivyo hivyo kuhusu kile kikombe+ pia, baada ya yeye kula mlo wa jioni, akisema: “Kikombe hiki kinamaanisha agano jipya+ kwa msingi wa damu+ yangu. Endeleeni kufanya hivi, kila mara mnapokinywa, kwa kunikumbuka+ mimi.” 26 Kwa maana kila mara+ mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mnaendelea kukitangaza kifo+ cha Bwana, mpaka atakapofika.+
27 Kwa hiyo yeyote anayeula mkate au kukinywa kikombe cha Bwana isivyofaa atakuwa na hatia+ kuhusiana na mwili na damu+ ya Bwana. 28 Kwanza acheni mtu ajichunguze mwenyewe na kuona kama anafaa,+ na basi ale mkate na anywe kikombe. 29 Kwa maana yeye anayekula na kunywa anakula na kunywa hukumu+ juu yake mwenyewe ikiwa hautambui mwili. 30 Ndiyo sababu wengi katikati yenu ni dhaifu na wagonjwa-wagonjwa, na wengi wamelala+ katika kifo. 31 Lakini kama tungalitambua sisi wenyewe ni nani, hatungalihukumiwa.+ 32 Hata hivyo, tunapohukumiwa,+ Yehova+ anatutia nidhamu, ili tusihukumiwe+ pamoja na ulimwengu.+ 33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokuja pamoja kula mlo huo,+ mngojeane. 34 Ikiwa yeyote ana njaa, acheni ale nyumbani,+ ili msije pamoja kwa ajili ya kuhukumiwa.+ Lakini mambo yaliyobaki nitayarekebisha nitakapofika.
12 Basi kuhusu zawadi za kiroho,+ akina ndugu, sitaki mkose kujua. 2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wa mataifa,+ mlikuwa mkiongozwa kwenye zile sanamu+ zisizo na sauti+ kama vile mlivyoongozwa. 3 Kwa hiyo ningetaka mjue kwamba hakuna mtu yeyote ambaye anaposema kwa roho ya Mungu, husema: “Yesu amelaaniwa!”+ na hakuna mtu anayeweza kusema: “Yesu ni Bwana!” isipokuwa kwa roho takatifu.+
4 Basi kuna zawadi za namna mbalimbali,+ lakini kuna roho ileile;+ 5 na kuna huduma+ za namna mbalimbali, na bado kuna Bwana+ yuleyule; 6 na kuna utendaji wa namna mbalimbali,+ na bado ni Mungu yuleyule+ anayefanya utendaji wote katika watu wote.+ 7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa roho kwa kusudi lenye faida.+ 8 Kwa mfano, mtu mmoja hupewa maneno ya hekima+ kupitia roho, mwingine maneno ya ujuzi+ kulingana na roho ileile, 9 mwingine imani+ kwa roho ileile, mwingine zawadi za maponyo+ kwa roho moja hiyo, 10 mwingine bado hupewa utendaji wa matendo yenye nguvu,+ mwingine kutoa unabii,+ mwingine utambuzi+ wa maneno yaliyoongozwa na roho,+ mwingine lugha+ tofauti, na mwingine fasiri+ ya lugha. 11 Lakini ni roho ileile moja inayofanya utendaji huu wote,+ ikimgawia+ kila mtu mmoja mmoja kama vile inavyopenda.+
12 Kwa maana kama vile mwili ni mmoja lakini una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili huo, ijapokuwa ni vingi, ni mwili+ mmoja, ndivyo pia alivyo Kristo.+ 13 Kwa kweli kwa roho moja sote tulibatizwa+ katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au ni Wagiriki, kama ni watumwa au ni walio huru, nasi sote tulinyweshwa+ roho moja.
14 Kwa maana mwili, kwa kweli, si kiungo kimoja, bali vingi.+ 15 Kama mguu ungesema: “Kwa sababu mimi si mkono, mimi si sehemu ya mwili,” sababu hiyo haiufanyi usiwe sehemu ya mwili.+ 16 Na kama sikio lingesema: “Kwa sababu mimi si jicho, mimi si sehemu ya mwili,” sababu hiyo hailifanyi lisiwe sehemu ya mwili.+ 17 Kama mwili wote ungekuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Kama huo wote ungekuwa kusikia, kunusa kungekuwa wapi? 18 Lakini sasa Mungu ameviweka viungo katika mwili, kila kimoja, kama vile alivyopenda.+
19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja,+ mwili ungekuwa wapi? 20 Lakini sasa hivyo ni viungo vingi,+ lakini mwili mmoja. 21 Jicho haliwezi kuuambia mkono: “Sikuhitaji wewe”; au, tena, kichwa hakiwezi kuiambia miguu: “Siwahitaji ninyi.” 22 Lakini badala yake ni kwamba vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu+ zaidi ni vya lazima, 23 na zile sehemu za mwili ambazo tunafikiri kuwa zina heshima kidogo, hizo tunazizungushia heshima nyingi zaidi,+ na kwa hiyo sehemu zetu ambazo huonekana kuwa hazivutii zinapendeza zaidi, 24 lakini sehemu zetu zenye kupendeza hazihitaji kitu chochote. Hata hivyo, Mungu aliuungamanisha mwili, akiipa heshima iliyo nyingi zaidi sehemu iliyokuwa na upungufu, 25 ili kusiwe na mgawanyiko katika mwili, bali ili viungo vyake vitunzane+ kwa njia ileile. 26 Na kiungo kimoja kikiumia, vile viungo vingine vyote huumia+ pamoja nacho; au kiungo kimoja kikitukuzwa,+ vile viungo vingine vyote hushangilia pamoja nacho.+
27 Basi ninyi ni mwili wa Kristo, nanyi ni viungo mkiwa mmoja-mmoja.+ 28 Naye Mungu amewaweka watu mbalimbali katika kutaniko,+ kwanza, mitume;+ pili, manabii;+ tatu, walimu,+ kisha matendo yenye nguvu;+ kisha zawadi za maponyo;+ utumishi wenye msaada,+ uwezo wa kuelekeza,+ lugha tofauti.+ 29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote hufanya matendo yenye nguvu? 30 Je, wote wana zawadi za maponyo? Je, wote husema kwa lugha?+ Je, wote ni watafsiri?+ 31 Lakini endeleeni kutafuta kwa bidii zawadi+ zilizo kubwa zaidi. Na bado nawaonyesha ninyi njia iliyo bora zaidi.+
13 Nikisema kwa lugha+ za wanadamu na za malaika lakini sina upendo, nimekuwa chombo cha shaba nyeupe kinachovuma au toazi+ linalolia. 2 Na ikiwa nina zawadi ya kutoa unabii+ nami nazijua siri takatifu+ zote na ujuzi+ wote, na ikiwa nina imani yote kuweza kuhamisha milima,+ lakini sina upendo, mimi si kitu.+ 3 Nami nikitoa mali zangu zote ili kuwalisha wengine,+ nami nikiutoa mwili wangu,+ ili nijisifu, lakini sina upendo,+ sipati faida hata kidogo.
4 Upendo+ ni wenye ustahimilivu+ na wenye fadhili.+ Upendo hauna wivu,+ haujigambi,+ haujivuni,+ 5 haujiendeshi bila adabu,+ hautafuti faida zake wenyewe,+ hauchokozeki.+ Hauweki hesabu ya ubaya.+ 6 Haushangilii juu ya ukosefu wa uadilifu,+ bali hushangilia pamoja na kweli.+ 7 Huhimili mambo yote,+ huamini mambo yote,+ hutumaini mambo yote,+ huvumilia mambo yote.+
8 Upendo haushindwi kamwe.+ Lakini kama kuna zawadi za kutoa unabii, zitaondolewa mbali; kama kuna lugha, zitakoma; kama kuna ujuzi, utaondolewa mbali.+ 9 Kwa maana tuna ujuzi wa sehemu+ tu nasi tunatoa unabii kwa sehemu+ tu; 10 lakini wakati kile kilicho kamili kitakapofika,+ kile kilicho kwa sehemu tu kitaondolewa mbali. 11 Nilipokuwa mtoto, nilikuwa nikisema kama mtoto, nikifikiri kama mtoto, nikiwaza kama mtoto; lakini kwa kuwa sasa nimekuwa mtu mzima,+ nimeziondolea mbali tabia za mtoto. 12 Kwa maana wakati wa sasa tunaona kwa njia isiyo ya waziwazi kupitia kioo cha chuma,+ lakini wakati huo itakuwa uso kwa uso.+ Wakati wa sasa najua kwa sehemu tu, lakini wakati huo nitajua kwa usahihi kama vile ninavyojulikana kwa usahihi.+ 13 Sasa, hata hivyo, inabaki imani, tumaini, upendo, hayo matatu; lakini lililo kubwa zaidi kati ya hayo ni upendo.+
14 Fuatieni upendo, na bado endeleeni kutafuta kwa bidii zawadi za kiroho,+ lakini ni afadhali zaidi kwamba mtoe unabii.+ 2 Kwa maana yeye anayesema kwa lugha husema, si na wanadamu, bali na Mungu, kwa maana hakuna anayesikia,+ bali yeye husema kwa roho siri zilizo takatifu.+ 3 Hata hivyo, yeye anayetoa unabii huwajenga+ na kuwatia moyo na kuwafariji watu kwa maneno yake. 4 Yeye anayesema kwa lugha hujijenga mwenyewe, lakini yeye anayetoa unabii hulijenga kutaniko. 5 Basi ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha,+ lakini napendelea zaidi kwamba mtoe unabii.+ Kwa kweli, yeye anayetoa unabii ni mkubwa kuliko yeye anayesema kwa lugha,+ isipokuwa, kwa kweli, yeye atafsiri, ili kutaniko lijengwe. 6 Lakini wakati huu, akina ndugu, kama ningekuja kwenu nikisema kwa lugha, ningewapa faida gani isipokuwa kama ningesema nanyi ama kwa ufunuo+ au kwa ujuzi+ au kwa unabii au kwa fundisho?
7 Kama ilivyo, vitu visivyo na uhai hutoa sauti,+ kama ni filimbi au kinubi; kisipofanya tofauti kati ya sauti, itajulikanaje ni nini kinachopigwa kwenye filimbi au kwenye kinubi? 8 Kwa maana kwa kweli, tarumbeta ikipiga mwito usiojulikana, ni nani atakayejitayarisha kwa ajili ya vita?+ 9 Vivyo hivyo pia, ninyi msiposema maneno yenye kueleweka kwa urahisi+ kupitia hiyo lugha, watu watajuaje linalosemwa? Kwa kweli, mtakuwa mkisema hewani.+ 10 Huenda kuna aina nyingi sana za sauti za maneno katika ulimwengu, na bado hakuna aina isiyo na maana. 11 Basi, ikiwa sielewi nguvu za sauti ya maneno, nitakuwa mgeni+ kwa yeye anayesema, na yeye anayesema atakuwa mgeni kwangu. 12 Ndivyo pia ninyi wenyewe, kwa kuwa mnatamani kwa bidii zawadi za roho,+ tafuteni kujawa nazo kwa ajili ya kulijenga kutaniko.+
13 Kwa hiyo yeye anayesema kwa lugha na asali ili aitafsiri.+ 14 Kwa maana ikiwa ninasali kwa lugha, ni zawadi yangu ya roho inayosali,+ lakini akili yangu haizai matunda. 15 Basi, nini lifanywe? Nitasali kwa zawadi ya roho, lakini nitasali pia kwa akili yangu. Nitaimba sifa+ kwa zawadi ya roho, lakini pia nitaimba sifa kwa akili yangu.+ 16 Kama sivyo, ukitoa sifa kwa zawadi ya roho, yule mtu aliyeketi kwenye kiti cha mtu wa kawaida atasemaje “Amina”+ kwa utoaji wako wa shukrani, kwa kuwa hajui lile unalosema? 17 Kweli, unatoa shukrani kwa njia nzuri, lakini yule mtu mwingine hajengwi.+ 18 Ninamshukuru Mungu, ninasema kwa lugha nyingi zaidi kuliko ninyi nyote.+ 19 Hata hivyo, katika kutaniko ingekuwa afadhali niseme maneno matano kwa akili yangu, ili pia niwafundishe wengine kwa mdomo, kuliko maneno elfu kumi kwa lugha.+
20 Akina ndugu, msiwe watoto wachanga katika nguvu za uelewaji,+ lakini iweni watoto kuhusiana na ubaya;+ hata hivyo iweni watu wazima katika nguvu za uelewaji.+ 21 Katika Sheria imeandikwa: “ ‘Nitasema na watu hawa kwa lugha za watu wa ugenini na kwa midomo ya wageni,+ na bado hata wakati huo hawatanisikiliza,’ asema Yehova.”+ 22 Kwa sababu hiyo lugha ni kwa ajili ya ishara,+ si kwa waamini, bali kwa wasio waamini,+ lakini kutoa unabii, si kwa ajili ya wasio waamini, bali ni kwa ajili ya waamini.+ 23 Kwa hiyo, kutaniko lote likija pamoja mahali pamoja nao wote waseme kwa lugha,+ lakini watu wa kawaida au wasio waamini waingie, je, hawatasema kwamba ninyi ni wenda-wazimu? 24 Lakini ikiwa ninyi nyote mnatoa unabii na mtu yeyote asiye mwamini au mtu wa kawaida aingie, yeye hukaripiwa nao wote,+ huchunguzwa sana na wote; 25 siri za moyo wake hufunuliwa,+ hivi kwamba ataanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu, akitangaza: “Kwa kweli Mungu yupo katikati yenu.”+
26 Basi, nini lifanywe akina ndugu? Mnapokuja pamoja, mmoja ana zaburi, mwingine ana fundisho, mwingine ana ufunuo, mwingine ana lugha, mwingine ana fasiri.+ Mambo yote na yatendeke kwa ajili ya kujenga.+ 27 Na mtu akisema kwa lugha, na wawe wawili au, ikiwa ni zaidi, watatu, wasipite hapo, na kwa zamu; na mtu fulani atafsiri.+ 28 Lakini ikiwa hakuna mtafsiri, na akae kimya katika kutaniko na aseme moyoni mwake mwenyewe+ na kwa Mungu. 29 Zaidi ya hayo, manabii+ wawili au watatu na waseme, na wale wengine waitambue maana.+ 30 Lakini ikiwa kuna ufunuo kwa mwingine+ wakati ameketi hapo, yule wa kwanza na akae kimya. 31 Kwa maana nyote mnaweza kutoa unabii+ mtu mmoja-mmoja, ili wote wajifunze na wote watiwe moyo.+ 32 Na zawadi za roho ya manabii zinapaswa kuelekezwa na manabii. 33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko,+ bali ni wa amani.+
Kama ilivyo katika makutaniko yote ya watakatifu, 34 wanawake na wakae kimya+ katika makutaniko, kwa maana hairuhusiwi kwao kusema, bali na wajitiishe,+ kama Sheria+ inavyosema. 35 Basi, ikiwa wanataka kujifunza jambo fulani, acheni wawaulize waume zao wenyewe nyumbani, kwa maana inafedhehesha+ kwa mwanamke kusema katika kutaniko.
36 Kwani! Je, neno la Mungu lilitoka kwenu,+ au je, liliwafikia ninyi tu?
37 Kama yeyote anafikiri kuwa yeye ni nabii au amepewa zawadi ya roho, acheni ayatambue mambo ninayowaandikia ninyi, kwa sababu hayo ni amri ya Bwana.+ 38 Lakini ikiwa yeyote hajui, yeye anaendelea bila kujua. 39 Kwa hiyo, ndugu zangu, endeleeni kutafuta kwa bidii kutoa unabii,+ na bado msikataze kusema kwa lugha.+ 40 Lakini mambo yote na yatendeke kwa adabu na kwa mpango.+
15 Basi nawajulisha ninyi, akina ndugu, habari njema+ niliyowatangazia,+ mliyoipokea pia, ambayo katika hiyo mnasimama+ pia, 2 ambayo kupitia hiyo ninyi pia mnaokolewa,+ kupitia maneno ambayo niliwatangazia ninyi habari njema, ikiwa mnaishika sana, isipokuwa, kwa kweli, iwe mlikuwa waamini bila kusudi.+
3 Kwa maana niliwapa ninyi, kati ya mambo ya kwanza, yale niliyopokea+ pia, kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kulingana na Maandiko;+ 4 na kwamba alizikwa,+ ndiyo, kwamba alifufuliwa+ siku ya tatu+ kulingana na Maandiko;+ 5 na kwamba alimtokea Kefa,+ kisha wale kumi na wawili.+ 6 Baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa wakati mmoja, ambao walio wengi kati yao wapo mpaka sasa,+ lakini wengine wamelala usingizi katika kifo. 7 Baadaye alimtokea Yakobo,+ kisha mitume wote;+ 8 lakini mwisho kabisa alinitokea mimi+ pia kana kwamba kwa mmoja aliyezaliwa kabla ya wakati wake.
9 Kwa maana mimi ni mdogo+ zaidi kati ya mitume, nami sifai kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa+ kutaniko la Mungu. 10 Lakini kwa fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu mimi niko kama nilivyo. Na fadhili zake zisizostahiliwa zilizonielekea mimi hazikuwa za bure,+ bali nilifanya kazi kuwapita wao wote,+ lakini si mimi bali ni fadhili zisizostahiliwa za Mungu zilizo pamoja nami.+ 11 Hata hivyo, hata kama ni mimi au ni wao, ndivyo sisi tunahubiri na ndivyo ninyi mmeamini.+
12 Basi ikiwa Kristo anahubiriwa kwamba amefufuliwa kutoka kwa wafu,+ kwa nini wengine kati yenu wanasema hakuna ufufuo wa wafu?+ 13 Ikiwa, kwa kweli, hakuna ufufuo wa wafu, basi Kristo hakufufuliwa.+ 14 Lakini ikiwa Kristo hakufufuliwa, hakika kuhubiri kwetu ni bure, na imani yetu ni bure.+ 15 Zaidi ya hayo, tunaonekana pia kuwa mashahidi wa uwongo wa Mungu,+ kwa sababu tumetoa ushahidi+ juu ya Mungu kwamba yeye alimfufua Kristo,+ lakini ambaye hakumfufua ikiwa kwa kweli wafu hawatafufuliwa.+ 16 Kwa maana ikiwa wafu hawatafufuliwa, basi Kristo hakufufuliwa. 17 Na tena, ikiwa Kristo hakufufuliwa, imani yenu ni bure; ninyi bado mko katika dhambi zenu.+ 18 Kwa kweli, pia, wale waliolala usingizi katika kifo katika muungano+ na Kristo waliangamia.+ 19 Ikiwa ni katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo,+ sisi ndio wa kusikitikiwa zaidi kati ya watu wote.
20 Hata hivyo, sasa Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu,+ matunda ya kwanza+ ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.+ 21 Kwa kuwa kifo+ ni kupitia mwanadamu, ufufuo+ wa wafu pia ni kupitia mwanadamu. 22 Kwa maana kama vile katika Adamu wote wanakufa,+ vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywa kuwa hai.+ 23 Lakini kila mmoja katika daraja lake mwenyewe: Kristo aliye matunda ya kwanza,+ baadaye wale walio wa Kristo wakati wa kuwapo kwake.+ 24 Halafu, ule mwisho, wakati atakapomkabidhi ufalme Mungu wake ambaye pia ni Baba yake, wakati atakapokuwa ameangamiza serikali yote na mamlaka yote na nguvu zote.+ 25 Kwa maana ni lazima atawale akiwa mfalme mpaka Mungu awe ameweka adui zote chini ya miguu yake.+ 26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.+ 27 Kwa maana Mungu “alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake.”+ Lakini anaposema kwamba ‘vitu vyote vimetiishwa,’+ ni wazi kwamba iko hivyo isipokuwa kwa yule aliyevitiisha vitu vyote kwake.+ 28 Lakini vitu vyote vitakapokuwa vimetiishwa kwake,+ ndipo Mwana mwenyewe atakapojitiisha pia kwa Yeye+ aliyevitiisha vitu vyote kwake, ili Mungu awe vitu vyote kwa kila mtu.+
29 Kama sivyo, watafanya nini wale wanaobatizwa kwa kusudi la kuwa wafu?+ Ikiwa wafu hawatafufuliwa kamwe,+ kwa nini pia wanabatizwa+ kwa kusudi la kuwa hivyo? 30 Kwa nini sisi pia tumo hatarini kila saa?+ 31 Nakabili kifo kila siku.+ Hili nathibitisha kwa furaha+ niliyo nayo juu yenu, akina ndugu, ambayo ninayo katika Kristo Yesu Bwana wetu. 32 Ikiwa, kama wanadamu, nimepigana na wanyama-mwitu katika Efeso,+ hiyo ina faida gani kwangu? Ikiwa wafu hawatafufuliwa, “na tule na tunywe, kwa maana kesho tutakufa.”+ 33 Msipotoshwe. Mashirika mabaya huharibu tabia nzuri.+ 34 Amkeni muwe na utimamu wa akili+ katika njia ya uadilifu na msiwe na mazoea ya kufanya dhambi, kwa maana wengine hawamjui Mungu.+ Ninasema ili kuwafanya ninyi mwone aibu.+
35 Hata hivyo, mtu fulani atasema: “Wafu watafufuliwaje? Ndiyo, watakuja wakiwa na mwili wa namna gani?”+ 36 Wewe mtu usiye na akili! Kile unachopanda hakiwi hai isipokuwa kwanza kife;+ 37 na kwa habari ya kile unachopanda, unapanda, si mwili utakaochipuka, bali mbegu tupu,+ huenda ikawa, ni ya ngano au yoyote kati ya zile nyingine; 38 lakini Mungu huipa mwili+ kama inavyompendeza,+ na kwa kila moja ya hizo mbegu mwili wake yenyewe. 39 Nyama yote si nyama ya aina moja, bali kuna moja ya wanadamu, na kuna nyama nyingine ya mifugo, na nyama nyingine ya ndege, na nyingine ya samaki.+ 40 Na kuna miili ya mbinguni,+ na miili ya duniani;+ lakini utukufu+ wa miili ya mbinguni ni wa namna moja, na ule wa miili ya duniani ni wa namna nyingine. 41 Utukufu wa jua+ ni wa namna moja, na utukufu wa mwezi+ ni mwingine, na utukufu wa nyota+ ni mwingine; kwa kweli, nyota hutofautiana na nyota kwa utukufu.
42 Ndivyo ulivyo pia ufufuo wa wafu.+ Hupandwa katika uharibifu, hufufuliwa katika kutoweza kuharibika.+ 43 Hupandwa katika aibu,+ hufufuliwa katika utukufu.+ Hupandwa katika udhaifu,+ hufufuliwa katika nguvu.+ 44 Hupandwa ukiwa mwili wa nyama,+ hufufuliwa ukiwa mwili wa roho.+ Ikiwa kuna mwili wa nyama, kuna wa roho pia. 45 Hata imeandikwa hivi: “Mtu wa kwanza Adamu akawa nafsi hai.”+ Adamu wa mwisho akawa roho+ inayotoa uhai.+ 46 Hata hivyo, wa kwanza si ule ulio wa roho, bali ni ule ulio wa nyama, baadaye ule ulio wa roho.+ 47 Mtu wa kwanza ni wa kutoka duniani na amefanywa kwa mavumbi;+ mtu wa pili ni wa kutoka mbinguni.+ 48 Kama alivyo yule aliyefanywa kwa mavumbi,+ ndivyo walivyo pia wale waliofanywa kwa mavumbi; na kama alivyo yule wa mbinguni,+ ndivyo walivyo pia wale wa mbinguni.+ 49 Na kama vile ambavyo tumeuchukua mfano+ wa yeye aliyefanywa kwa mavumbi, vivyo hivyo pia tutauchukua mfano+ wa yule wa mbinguni.
50 Hata hivyo, hili nasema, akina ndugu, kwamba nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu,+ wala uharibifu haurithi kutoweza kuharibika.+ 51 Tazama! Nawaambia ninyi siri takatifu: Hatutalala usingizi katika kifo sisi sote, bali sisi sote tutabadilishwa,+ 52 kwa muda mfupi, kufumba na kufumbua jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho. Kwa maana tarumbeta+ italia, na wafu watafufuliwa wakiwa wasioweza kuharibika, nasi tutabadilishwa. 53 Kwa maana huu ulio wa kuharibika lazima uvae kutoweza kuharibika,+ na huu unaoweza kufa+ lazima uvae kutoweza kufa. 54 Lakini huu ulio wenye kuharibika utakapovaa kutoweza kuharibika na huu unaoweza kufa utakapovaa kutoweza kufa, ndipo litakapotimia hili neno lililoandikwa: “Kifo+ kimemezwa milele.”+ 55 “Kifo, uko wapi ushindi wako? Kifo, uko wapi mchomo wako?”+ 56 Mchomo+ unaotokeza kifo ni dhambi, lakini nguvu za dhambi ni Sheria.+ 57 Lakini shukrani kwake Mungu, kwa maana yeye hutupa sisi ushindi kupitia Bwana wetu Yesu Kristo!+
58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapendwa, iweni imara,+ thabiti, sikuzote mkiwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana,+ mkijua kwamba kazi yenu si ya bure+ kuhusiana na Bwana.
16 Basi kuhusu mchango+ ulio kwa ajili ya watakatifu,+ kama vile nilivyoyapa maagizo makutaniko ya Galatia,+ ninyi wenyewe pia fanyeni vivyo hivyo. 2 Kila siku ya kwanza ya juma acheni kila mmoja wenu kwenye nyumba yake mwenyewe aweke kando kitu fulani katika akiba kulingana na anavyofanikiwa, ili nitakapofika michango isifanywe wakati huo. 3 Lakini nitakapofika hapo, watu wowote mtakaokubali kwa barua,+ nitawatuma hao kuipeleka zawadi yenu ya fadhili mpaka Yerusalemu. 4 Hata hivyo, ikiwa inafaa mimi kwenda huko pia, wao wataenda huko pamoja nami.
5 Lakini nitakuja kwenu wakati nitakapokuwa nimekwenda kupitia Makedonia, kwa maana ninaenda kupitia Makedonia;+ 6 na labda nitakaa au hata nitapisha majira ya baridi kali nikiwa pamoja nanyi, ili mnisindikize+ hatua fulani mahali ambapo huenda nitakuwa nikienda. 7 Kwa maana sitaki kuwaona ninyi sasa wakati ninapopita, kwa maana natumaini kukaa pamoja nanyi kwa wakati fulani,+ Yehova+ akiruhusu.+ 8 Lakini ninakaa katika Efeso+ mpaka sherehe ya Pentekoste; 9 kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji,+ lakini kuna wapinzani wengi.
10 Hata hivyo, Timotheo+ akifika, hakikisheni kwamba haogopi akiwa kati yenu, kwa maana anafanya kazi ya Yehova,+ kama mimi. 11 Kwa hiyo, mtu yeyote asimdharau.+ Msindikizeni hatua fulani kwa amani, ili anifikie hapa, kwa maana ninamngojea nikiwa pamoja na akina ndugu.
12 Basi kumhusu Apolo+ ndugu yetu, nilimsihi sana aje kwenu akiwa na akina ndugu, na bado hayakuwa mapenzi yake hata kidogo aje sasa; lakini atakuja atakapopata nafasi.
13 Kaeni macho,+ simameni imara katika imani,+ endeleeni kuwa kama wanaume,+ iweni na nguvu.+ 14 Mambo yenu yote na yatendeke kwa upendo.+
15 Sasa nawahimiza ninyi, akina ndugu: Mnajua kwamba nyumba ya Stefana ndiyo matunda ya kwanza+ ya Akaya na kwamba walijitoa kuwahudumia watakatifu.+ 16 Ninyi pia endeleeni kujitiisha kwa watu wa aina hiyo na kwa kila mtu anayeshirikiana na kufanya kazi ya jasho.+ 17 Lakini nashangilia kuwapo kwa Stefana+ na Fortunato na Akaiko, kwa sababu wao wamejazia kutokuwapo kwenu hapa. 18 Kwa maana wameiburudisha roho+ yangu na yenu. Kwa hiyo watambueni watu wa namna hiyo.+
19 Makutaniko ya Asia yanawatumia ninyi salamu+ zao. Akila na Priska pamoja na kutaniko lililo katika nyumba yao+ wanawasalimu ninyi kwa ukunjufu wa moyo katika Bwana. 20 Ndugu wote wanawasalimu ninyi. Salimianeni kwa busu takatifu.+
21 Hii ni salamu yangu, ya Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe.+
22 Ikiwa yeyote hana upendo kwa Bwana, mtu huyo na alaaniwe.+ Uje, Ee Bwana wetu!+ 23 Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu na ziwe pamoja nanyi. 24 Upendo wangu na uwe pamoja nanyi nyote katika muungano na Kristo Yesu.