Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Waroma 1:1-16:27
  • Kwa Waroma

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Waroma
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Kwa Waroma

Kwa Waroma

1 Paulo, mtumwa+ wa Yesu Kristo aliyeitwa+ kuwa mtume,+ aliyetengwa kwa ajili ya habari njema ya Mungu,+ 2 aliyoahidi kimbele kupitia manabii+ wake katika Maandiko matakatifu, 3 kuhusu Mwana wake, aliyetokana na uzao wa Daudi+ kulingana na mwili,+ 4 lakini ambaye kwa nguvu+ alitangazwa kuwa Mwana wa Mungu+ kulingana na roho+ ya utakatifu kwa njia ya ufufuo kutoka kwa wafu+—ndiyo, Yesu Kristo Bwana wetu, 5 ambaye kupitia yeye tulipokea fadhili zisizostahiliwa+ na utume+ ili kuwe na utii wa imani kati ya mataifa+ yote kuhusu jina lake, 6 mataifa ambayo kati yake ninyi pia ni wale walioitwa kuwa wa Yesu Kristo— 7 kwa wale wote walio katika Roma wakiwa wapendwa wa Mungu, walioitwa+ wawe watakatifu:+

Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani+ kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.+

8 Kwanza kabisa, namshukuru+ Mungu wangu kupitia Yesu Kristo kuhusu ninyi nyote, kwa sababu imani yenu inazungumzwa+ kotekote ulimwenguni. 9 Kwa maana Mungu, ambaye ninamtolea utumishi mtakatifu kwa roho yangu kuhusiana na ile habari njema juu ya Mwana wake, ni shahidi+ wangu wa jinsi ninavyowataja sikuzote katika sala zangu bila kuacha,+ 10 nikiomba kwamba ikiwa kwa vyovyote inawezekana sasa mwishowe nipate kufanikiwa katika mapenzi+ ya Mungu ili nije kwenu. 11 Kwa maana ninatamani kuwaona ninyi,+ ili niwape sehemu ya zawadi ya kiroho+ kusudi mfanywe imara; 12 au, badala ya hivyo, kwamba kuwe na ubadilishanaji wa kitia-moyo kati yenu,+ kila mmoja kupitia imani ya mwingine,+ yenu na yangu pia.

13 Lakini, akina ndugu,+ sitaki mkose kujua kwamba mara nyingi nilikusudia kuja kwenu+ ili niweze kujipatia matunda fulani+ kati yenu pia kama vile ilivyo kati ya mataifa mengine, lakini nimezuiwa mpaka sasa. 14 Mimi nina deni kwa Wagiriki na kwa Wabaribari pia, kwa wenye hekima+ na kwa wasio na akili pia: 15 kwa hiyo nina hamu ya kuitangaza habari njema+ kwenu pia mlio huko Roma.+ 16 Kwa maana siionei aibu+ habari njema; kwa kweli, hiyo ni nguvu za Mungu+ kwa ajili ya wokovu kwa kila mtu aliye na imani,+ kwa Myahudi kwanza+ na pia kwa Mgiriki;+ 17 kwa maana katika hiyo uadilifu+ wa Mungu unafunuliwa kwa sababu ya imani+ na kuelekea imani, kama vile ilivyoandikwa: “Lakini mwadilifu—ataishi kwa njia ya imani.”+

18 Kwa maana ghadhabu+ ya Mungu inafunuliwa kutoka mbinguni juu ya watu wote wasiomwogopa Mungu na wasio waadilifu+ ambao wanaikandamiza kweli+ katika njia isiyo ya uadilifu,+ 19 kwa sababu yale yanayoweza kujulikana juu ya Mungu yamefunuliwa katikati yao,+ kwa maana Mungu aliyafunua kwao.+ 20 Kwa maana sifa zake ambazo hazionekani,+ zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea,+ kwa sababu zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa,+ yaani, nguvu zake za milele+ na Uungu,+ hivi kwamba hawana sababu ya kujitetea.+ 21 Kwa sababu, ijapokuwa walimjua Mungu, hawakumtukuza yeye kuwa Mungu wala hawakumshukuru,+ bali wakawa wajinga+ katika kufikiri kwao na moyo wao usio na ufahamu ukaingiwa na giza.+ 22 Ijapokuwa walisisitiza kuwa ni wenye hekima, wakawa wapumbavu+ 23 na kuugeuza utukufu+ wa Mungu asiye na uharibifu kuwa kitu kama sanamu+ ya mwanadamu aliye na uharibifu na ya ndege na viumbe vyenye miguu minne na vitu vinavyotambaa.+

24 Kwa hiyo, kwa kupatana na tamaa za mioyo yao, Mungu aliwaacha katika uchafu,+ ili miili+ yao ivunjiwe heshima kati yao,+ 25 yaani, wale walioibadili kweli+ ya Mungu kwa ajili ya uwongo+ nao wakauheshimu mno uumbaji na kuutolea utumishi mtakatifu badala ya kumtolea Yeye aliyeumba, anayebarikiwa milele. Amina. 26 Ndiyo sababu Mungu aliwaacha katika hamu za ngono yenye kufedhehesha,+ kwa maana wanawake wao walibadili matumizi yao wenyewe ya asili kuwa yale yaliyo kinyume cha asili;+ 27 na vivyo hivyo pia hata wanaume waliacha matumizi ya asili ya mwanamke+ na kuwakiana tamaa kali katika uchu wao kuelekeana wao wenyewe, wanaume kwa wanaume,+ wakitenda mambo machafu+ na kupokea ndani yao wenyewe malipo kamili,+ yaliyostahili kosa lao.+

28 Na kama vile ambavyo hawakukubali kumjua Mungu katika ujuzi sahihi,+ Mungu aliwaacha katika hali ya akili iliyokataliwa,+ ili wafanye mambo yasiyofaa,+ 29 wakiwa wamejawa na ukosefu wote wa uadilifu,+ uovu,+ tamaa,+ ubaya,+ wakiwa wamejaa wivu,+ uuaji,+ mizozo,+ udanganyifu,+ mwelekeo wenye madhara,+ wakiwa wanong’onezaji,+ 30 wasengenyaji,+ wenye kumchukia Mungu, wenye dharau,+ wenye majivuno,+ wenye kujidai,+ wenye kutunga mambo mabaya,+ wasiotii wazazi,+ 31 wasio na uelewaji,+ waongo kwa mapatano,+ wasio na upendo wa asili,+ wasio na rehema.+ 32 Ijapokuwa hawa wanajua vema kabisa amri ya uadilifu ya Mungu,+ kwamba wale wanaozoea kufanya mambo ya namna hiyo wanastahili kifo,+ wao wanaendelea kuyafanya na vilevile hukubaliana+ na wale wanaozoea kuyafanya.

2 Kwa hiyo wewe huna sababu ya kujitetea, Ee mwanadamu,+ hata uwe nani, ukihukumu;+ kwa maana katika jambo lile ambalo unamhukumu mwingine, unajihukumu mwenyewe kuwa una hatia, kwa sababu wewe unayehukumu+ una mazoea ya kufanya mambo hayo hayo.+ 2 Sasa tunajua kwamba, kupatana na kweli,+ hukumu ya Mungu iko juu ya wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo.

3 Lakini je, wewe unafikiri, Ee mwanadamu,+ kwamba utaponyoka hukumu ya Mungu wakati unapohukumu wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo na bado wewe unayafanya?+ 4 Au je, wewe unadharau utajiri wa fadhili+ zake na uvumilivu wenye subira+ na ustahimilivu,+ kwa sababu hujui kwamba sifa ya fadhili za Mungu inajaribu kukuongoza wewe kwenye toba?+ 5 Lakini kulingana na ugumu+ wako na moyo wako usiotubu+ unajiwekea mwenyewe akiba ya ghadhabu+ katika siku ya ghadhabu+ na ya kufunuliwa+ kwa hukumu ya uadilifu ya Mungu.+ 6 Naye atamlipa kila mmoja kulingana na matendo yake:+ 7 uzima wa milele kwa wale wanaotafuta utukufu na heshima na kutoharibika,+ kwa uvumilivu katika kazi iliyo njema; 8 hata hivyo, kwa wale wenye ugomvi+ na wale wasioitii kweli+ bali hutii ukosefu wa uadilifu kutakuwa na ghadhabu na hasira,+ 9 dhiki na taabu, juu ya nafsi ya kila mtu anayefanya mabaya, ya Myahudi+ kwanza na pia ya Mgiriki;+ 10 bali utukufu na heshima na amani kwa kila mtu anayefanya mema,+ kwa Myahudi kwanza+ na pia kwa Mgiriki.+ 11 Kwa maana hakuna ubaguzi kwa Mungu.+

12 Kwa mfano, wale wote waliofanya dhambi bila sheria wataangamia pia bila sheria;+ bali wale wote waliofanya dhambi chini ya sheria+ watahukumiwa kwa sheria.+ 13 Kwa maana wasikiaji wa sheria sio walio waadilifu mbele za Mungu, bali watendaji+ wa sheria watatangazwa kuwa waadilifu.+ 14 Kwa maana wakati watu wa mataifa+ wasio na sheria+ wanapofanya kwa asili mambo ya sheria,+ watu hawa, ijapokuwa hawana sheria, wao ni sheria kwao wenyewe. 15 Wao ndio wanaoonyesha kuwa yaliyomo katika sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao,+ huku dhamiri+ yao ikiwatolea ushahidi na, katikati ya fikira zao wenyewe, wanashtakiwa+ au hata kutetewa. 16 Hili litakuwa katika siku Mungu anapohukumu kupitia Kristo Yesu+ mambo ya siri+ ya wanadamu,+ kulingana na habari njema ninayoitangaza.+

17 Sasa, ikiwa wewe ni Myahudi kwa jina+ na unategemea sheria+ na kujivunia Mungu,+ 18 nawe unajua mapenzi yake+ na kuyakubali mambo yaliyo bora kabisa kwa sababu unafundishwa kwa mdomo kutokana na Sheria;+ 19 nawe umesadikishwa kwamba wewe ni kiongozi wa walio vipofu,+ nuru kwa wale walio katika giza,+ 20 mrekebishaji wa wale wasio na akili,+ mwalimu wa watoto wachanga,+ na ukiwa na picha+ ya ujuzi na ya ile kweli+ katika Sheria— 21 hata hivyo, je, wewe unayemfundisha mtu mwingine, hujifundishi mwenyewe?+ Wewe, unayehubiri “Usiibe,”+ je, wewe huiba?+ 22 Wewe, unayesema “Usifanye uzinzi,” je, wewe hufanya uzinzi?+ Wewe, unayechukizwa na sanamu, je, wewe huiba+ katika mahekalu? 23 Wewe, unayejivunia sheria, je, kwa kuivunja Sheria+ unamvunjia Mungu heshima? 24 Kwa maana “jina la Mungu linafanyiwa makufuru katikati ya mataifa kwa sababu yenu”;+ kama ilivyoandikwa.

25 Kwa kweli, kutahiriwa+ kuna faida ikiwa tu unazoea kuifuata sheria;+ lakini ikiwa wewe ni mvunjaji wa sheria,+ kutahiriwa kwako kumekuwa kutotahiriwa.+ 26 Kwa hiyo, ikiwa mtu asiyetahiriwa+ huyashika matakwa+ ya uadilifu ya Sheria, kutotahiriwa kwake kutahesabiwa kuwa kutahiriwa, sivyo?+ 27 Na mtu asiyetahiriwa aliye hivyo kwa asili, kwa kuishika Sheria, atakuhukumu+ wewe ambaye ukiwa na sheria zilizoandikwa na ukiwa na hali ya kutahiriwa unaivunja sheria. 28 Kwa maana yeye si Myahudi aliye hivyo kwa nje,+ wala kutahiriwa si kule ambako ni kwa nje juu ya mwili.+ 29 Bali yeye ni Myahudi aliye hivyo kwa ndani,+ na kutahiriwa kwake ni kule kwa moyo+ kupitia roho, wala si kupitia sheria zilizoandikwa.+ Sifa+ ya mtu huyo hutoka, si kwa wanadamu, bali kwa Mungu.+

3 Basi, Myahudi+ ana ubora gani, au ni nini faida ya kutahiriwa?+ 2 Ni nyingi katika kila njia. Kwanza kabisa, kwa sababu wao walikabidhiwa maneno matakatifu ya Mungu.+ 3 Basi, hali ikoje? Ikiwa wengine hawakuonyesha imani,+ je, ukosefu wao wa imani labda utafanya uaminifu+ wa Mungu usiwe na matokeo?+ 4 Hilo lisitendeke kamwe! Bali Mungu na aonekane kuwa wa kweli,+ ingawa kila mwanadamu aonekane kuwa mwongo,+ kama ilivyoandikwa: “Ili uonekane kuwa mwadilifu katika maneno yako na ushinde wakati unapohukumiwa.”+ 5 Hata hivyo, ikiwa ukosefu wetu wa uadilifu unatokeza wazi uadilifu+ wa Mungu, tutasema nini? Je, Mungu hukosa haki+ anapofungulia ghadhabu yake? (Ninasema kama mwanadamu+ anavyosema.) 6 Hilo lisitendeke kamwe! Ikiwa hivyo, Mungu atauhukumu ulimwengu jinsi gani?+

7 Lakini ikiwa kwa sababu ya uwongo wangu kweli ya Mungu+ imefanywa ionekane wazi zaidi kwa utukufu wake, kwa nini bado mimi pia ninahukumiwa kuwa mtenda-dhambi?+ 8 Na kwa nini isisemwe, kama tunavyoshtakiwa kwa uwongo+ na kama watu fulani wanavyosema kuwa sisi husema: “Na tufanye mambo mabaya ili mambo mema yaje”?+ Hukumu+ juu ya watu hao inapatana na haki.+

9 Tuseme nini basi? Je, sisi tuna hali bora?+ Sivyo hata kidogo! Kwa maana hapo juu tumefanya shtaka kwamba Wayahudi na vilevile Wagiriki wote wako chini ya dhambi;+ 10 kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwanadamu mwadilifu, hakuna hata mmoja;+ 11 hakuna yeyote aliye na ufahamu wowote, hakuna yeyote anayemtafuta Mungu.+ 12 Watu wote wamepotoka, wote pamoja wamekuwa wasiofaa kitu; hakuna yeyote anayetenda fadhili, hakuna hata mmoja.”+ 13 “Koo yao ni kaburi lililo wazi, wamedanganya kwa ndimi zao.”+ “Sumu ya nyoka iko nyuma ya midomo yao.”+ 14 “Na kinywa chao kimejaa kulaani na maneno machungu.”+ 15 “Miguu yao inaharakisha kwenda kumwaga damu.”+ 16 “Uharibifu na taabu zimo katika njia zao,+ 17 nao hawajaijua njia ya amani.”+ 18 “Hakuna kumwogopa Mungu mbele ya macho yao.”+

19 Sasa tunajua kwamba mambo yote ambayo Sheria+ inasema, inawaambia wale walio chini ya Sheria, ili kila kinywa kizibwe+ na ulimwengu wote ustahili+ adhabu kutoka kwa Mungu.+ 20 Kwa hiyo hakuna mwili wowote utakaotangazwa kuwa mwadilifu+ kutokana na matendo ya sheria+ mbele zake, kwa maana ujuzi sahihi juu ya dhambi ni kwa njia ya sheria.+

21 Lakini sasa uadilifu+ wa Mungu umefunuliwa bila sheria, kama unavyotolewa ushahidi+ na Sheria+ na Manabii;+ 22 ndiyo, uadilifu wa Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo,+ kwa ajili ya wote walio na imani.+ Kwa maana hakuna tofauti.+ 23 Kwa maana wote wamefanya dhambi+ na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,+ 24 nayo ni zawadi ya bure+ kwamba wanatangazwa kuwa waadilifu kwa fadhili zake zisizostahiliwa+ kupitia kuachiliwa huru kwa njia ya fidia+ ambayo Kristo Yesu alilipa. 25 Mungu alimweka kuwa toleo la kupatanisha+ kupitia imani katika damu+ yake. Ilikuwa hivyo ili kuonyesha wazi uadilifu wake mwenyewe, kwa sababu alikuwa akizisamehe dhambi+ zilizotokea wakati uliopita wakati Mungu alipokuwa akivumilia kwa subira;+ 26 ili kuonyesha wazi uadilifu+ wake mwenyewe katika majira haya yaliyopo, ili awe mwadilifu hata anapomtangaza kuwa mwadilifu+ mtu aliye na imani katika Yesu.

27 Basi, kujisifu+ kuko wapi? Kumefungiwa nje. Kupitia sheria+ gani? Ile ya matendo?+ Hapana, bali kupitia sheria ya imani.+ 28 Kwa maana tunaamua kwamba mtu hutangazwa kuwa mwadilifu kwa imani bila matendo ya sheria.+ 29 Au je, yeye ni Mungu wa Wayahudi peke yao?+ Je, yeye si wa watu wa mataifa pia?+ Ndiyo, wa watu wa mataifa pia,+ 30 ikiwa kwa kweli Mungu ni mmoja,+ atakayewatangaza watu waliotahiriwa+ kuwa waadilifu kutokana na imani na watu wasiotahiriwa+ kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao. 31 Basi, je, tunaifuta sheria kupitia imani yetu?+ Hilo lisitendeke kamwe! Kinyume cha hilo, sisi tunaiimarisha sheria.+

4 Kwa kuwa iko hivyo, tutasema nini juu ya Abrahamu babu+ yetu kulingana na mwili? 2 Kwa mfano, kama Abrahamu angetangazwa kuwa mwadilifu kwa sababu ya matendo,+ angekuwa na sababu ya kujisifu; lakini si mbele za Mungu. 3 Kwa maana andiko linasema nini? “Abrahamu alionyesha imani katika Yehova, na hilo likahesabiwa kwake kuwa ni uadilifu.”+ 4 Basi kwa mtu anayefanya kazi,+ malipo yanahesabiwa kuwa ni deni,+ wala si kuwa ni fadhili zisizostahiliwa.+ 5 Kwa upande mwingine, kwa mtu asiyefanya kazi bali anayeweka imani+ katika yeye anayemtangaza kuwa mwadilifu yule asiyemwogopa Mungu, imani yake inahesabiwa kuwa ni uadilifu.+ 6 Kama vile Daudi pia anavyosema juu ya furaha ya mtu ambaye Mungu humhesabia kuwa ni uadilifu bila matendo: 7 “Wenye furaha ni wale ambao matendo yao ya kuasi sheria yamesamehewa+ na ambao dhambi zao zimefunikwa;+ 8 mwenye furaha ni mtu ambaye Yehova hatahesabu dhambi yake kamwe.”+

9 Basi, je, furaha hiyo huja juu ya watu waliotahiriwa au pia juu ya watu wasiotahiriwa?+ Kwa maana tunasema: “Imani yake ilihesabiwa kwa Abrahamu kuwa ni uadilifu.”+ 10 Basi, ilihesabiwa chini ya hali gani? Alipokuwa katika kutahiriwa au katika kutotahiriwa?+ Si katika kutahiriwa, bali katika kutotahiriwa. 11 Naye alipokea ishara,+ yaani, kutahiriwa, kuwa muhuri wa uadilifu kwa imani aliyokuwa nayo alipokuwa katika hali yake ya kutotahiriwa, ili yeye awe baba+ ya wale wote walio na imani+ wakiwa katika kutotahiriwa, kusudi wahesabiwe uadilifu; 12 na baba ya uzao uliotahiriwa, si kwa wale tu wanaoshikamana na kutahiriwa, bali pia kwa wale wanaotembea kwa utaratibu katika hatua za imani hiyo wakiwa katika hali ya kutotahiriwa ambayo baba+ yetu Abrahamu alikuwa nayo.

13 Kwa maana ahadi+ ile kwamba awe mrithi wa ulimwengu hakuipata Abrahamu au uzao wake kupitia sheria, bali ilikuwa kupitia uadilifu kwa njia ya imani.+ 14 Kwa maana ikiwa wale ambao hushikamana sana na sheria ni warithi, imani imefanywa kuwa isiyofaa kitu na ahadi imefutwa.+ 15 Kwa kweli Sheria hutokeza ghadhabu,+ lakini mahali ambapo hapana sheria, hapana pia kosa lolote.+

16 Kwa hiyo ilitokana na imani, ili iwe kulingana na fadhili zisizostahiliwa,+ kusudi ahadi+ iwe hakika kwa uzao+ wake wote, si kwa ule tu unaoshikamana na Sheria, bali pia kwa ule unaoshikamana na imani ya Abrahamu. (Yeye ndiye baba+ yetu sote, 17 kama ilivyoandikwa: “Nimekuweka wewe kuwa baba ya mataifa mengi.”)+ Hili lilikuwa machoni pa Yule ambaye katika yeye alikuwa na imani, ndiyo, machoni pa Mungu, anayewafanya wafu kuwa hai+ na kuyaita mambo yasiyokuwako kana kwamba yamekuwako.+ 18 Ijapokuwa alikuwa amepita hali ya kuwa na tumaini,+ bado kwa kutegemea tumaini alikuwa na imani, ili awe baba ya mataifa+ mengi kwa kupatana na yale yaliyokuwa yamesemwa: “Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”+ 19 Na, ijapokuwa hakudhoofika katika imani, alifikiria juu ya mwili wake mwenyewe, ukiwa sasa tayari umekufa,+ kwa kuwa alikuwa mwenye umri wa karibu miaka mia moja,+ pia hali ya kufa ya tumbo la uzazi la Sara.+ 20 Lakini kwa sababu ya ahadi+ ya Mungu yeye hakusitasita kwa ukosefu wa imani,+ bali akawa mwenye nguvu kwa imani+ yake, akimpa Mungu utukufu 21 na akiwa amesadikishwa kikamili kwamba lile alilokuwa ameahidi alikuwa na uwezo pia wa kulifanya.+ 22 Kwa sababu hiyo “ikahesabiwa kwake kuwa ni uadilifu.”+

23 Hata hivyo, haikuandikwa kwa ajili yake tu+ kwamba “ilihesabiwa+ kwake,” 24 bali pia kwa ajili yetu ambao itahesabiwa, kwa sababu tunamwamini yeye aliyemfufua Yesu Bwana wetu kutoka kwa wafu.+ 25 Yeye alitolewa kwa ajili ya makosa+ yetu na kufufuliwa kwa ajili ya kututangaza sisi kuwa waadilifu.+

5 Basi, kwa kuwa sasa tumetangazwa kuwa waadilifu kutokana na imani,+ na tufurahie amani+ pamoja na Mungu kupitia Bwana wetu Yesu Kristo, 2 ambaye kupitia yeye pia tumekaribia+ kwa njia ya imani kuingia katika fadhili hizi zisizostahiliwa ambamo sasa tunasimama; na acheni tufurahi, kwa kutegemea tumaini+ la utukufu wa Mungu. 3 Na si hilo tu, bali na tufurahi tukiwa katika dhiki,+ kwa kuwa tunajua kwamba dhiki hutokeza uvumilivu;+ 4 nao uvumilivu, hali yenye kukubaliwa;+ nayo hali yenye kukubaliwa, tumaini,+ 5 nalo tumaini halikatishi tamaa;+ kwa sababu upendo wa Mungu+ umemiminwa ndani ya mioyo+ yetu kupitia roho takatifu,+ ambayo tulipewa.

6 Kwa maana, kwa kweli, tulipokuwa tungali bado dhaifu,+ Kristo alikufa wakati uliowekwa kwa ajili ya watu wasiomwogopa Mungu.+ 7 Kwa maana ni vigumu kwa yeyote kufa kwa ajili ya mtu mwadilifu;+ kwa kweli, labda, mtu anaweza kuthubutu kufa+ kwa ajili ya mtu mwema.+ 8 Lakini Mungu hupendekeza upendo+ wake mwenyewe kwetu kwa kuwa, tulipokuwa tungali watenda-dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.+ 9 Kwa hiyo, kwa kuwa tumetangazwa kuwa waadilifu sasa kwa damu yake,+ tutaokolewa kutokana na ghadhabu+ kupitia yeye hata zaidi. 10 Kwa maana, ikiwa tulipokuwa adui+ tulipatanishwa na Mungu kupitia kifo cha Mwana wake,+ tutaokolewa kwa uhai wake+ hata zaidi, kwa kuwa sasa tumepatanishwa. 11 Na si hilo tu, bali pia tunafurahi katika Mungu kupitia Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia yeye sasa tumepokea huo upatanisho.+

12 Hiyo ndiyo sababu, kama vile kupitia mtu mmoja+ dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo+ kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi+​—​. 13 Kwa maana kabla ya Sheria kuwako dhambi ilikuwa katika ulimwengu, lakini mtu yeyote hahesabiwi dhambi wakati hakuna sheria.+ 14 Hata hivyo, kifo kilitawala kama mfalme tangu Adamu mpaka Musa,+ hata juu ya wale ambao hawakuwa wamefanya dhambi inayofanana na kosa la Adamu,+ aliye mfano wake yeye aliyepaswa kuja.+

15 Lakini sivyo ilivyo kwa ile zawadi kama ilivyokuwa kwa lile kosa. Kwa maana ikiwa kwa kosa la mtu mmoja wengi walikufa, fadhili zisizostahiliwa za Mungu na zawadi yake ya bure ikiwa pamoja na fadhili zisizostahiliwa kupitia mtu mmoja+ Yesu Kristo zilizidi sana kwa wengi.+ 16 Pia, sivyo ilivyo kwa ile zawadi ya bure+ kama ilivyokuwa kwa njia ambayo mambo yalitendeka kupitia mtu mmoja aliyefanya dhambi.+ Kwa maana hukumu+ ilitokana na kosa moja katika hatia,+ lakini zawadi ilitokana na makosa mengi katika tangazo la uadilifu.+ 17 Kwa maana ikiwa kwa kosa la mtu mmoja+ kifo kilitawala kama mfalme+ kupitia mtu huyo, wale wanaopokea wingi wa fadhili zisizostahiliwa+ na zawadi ya bure+ ya uadilifu watatawala hata zaidi wakiwa wafalme+ katika uzima kupitia mtu mmoja, Yesu Kristo.+

18 Kwa hiyo, basi, kama vile kupitia kosa moja matokeo kwa watu wa namna zote yalikuwa kuhukumiwa hatia,+ vivyo hivyo pia kupitia tendo moja la kutetewa kuwa haki+ matokeo kwa watu wa namna zote+ ni wao kutangazwa kuwa waadilifu kwa ajili ya uzima.+ 19 Kwa maana kama vile kupitia kutotii kwa mtu mmoja wengi+ walifanywa watenda-dhambi, vivyo hivyo pia kupitia kutii+ kwa mtu mmoja wengi+ watafanywa kuwa waadilifu.+ 20 Basi Sheria+ iliingia kando ya hali hiyo ili makosa yazidi.+ Lakini mahali ambapo dhambi ilizidi,+ fadhili zisizostahiliwa+ zilizidi hata zaidi. 21 Kwa kusudi gani? Kwamba, kama vile dhambi ilivyotawala kama mfalme pamoja na kifo,+ vivyo hivyo pia fadhili zisizostahiliwa+ zitawale kama mfalme kupitia uadilifu kwa tazamio la uzima wa milele+ kupitia Yesu Kristo Bwana wetu.

6 Kwa hiyo, tuseme nini? Je, tuendelee kuwa katika dhambi, ili fadhili zisizostahiliwa ziwe nyingi?+ 2 Hilo lisitendeke kamwe! Kwa kuwa tulikufa kuhusiana na dhambi,+ tutaendeleaje kuishi tena katika hiyo?+ 3 Au je, hamjui kwamba sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu+ tulibatizwa katika kifo chake?+ 4 Kwa hiyo tulizikwa+ pamoja naye kupitia ubatizo wetu katika kifo chake, ili, kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka kwa wafu kupitia utukufu wa Baba,+ vivyo hivyo sisi pia tunapaswa tutembee katika hali mpya ya uzima.+ 5 Kwa maana ikiwa tumeungana pamoja naye katika mfano wa kifo chake,+ hakika sisi pia tutaunganishwa pamoja naye katika mfano wa ufufuo+ wake; 6 kwa sababu tunajua kwamba utu wetu wa zamani ulitundikwa mtini pamoja naye,+ ili mwili wetu wenye dhambi ufanywe kuwa usiotenda,+ ili tusiendelee tena kuwa watumwa wa dhambi.+ 7 Kwa maana yeye ambaye amekufa ameondolewa hatia ya dhambi yake.+

8 Zaidi ya hayo, ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pia pamoja naye.+ 9 Kwa maana tunajua kwamba Kristo hafi tena,+ kwa kuwa sasa amekwisha kufufuliwa kutoka kwa wafu;+ kifo si bwana juu yake tena. 10 Kwa maana kifo alichokufa, alikufa kuhusiana na dhambi mara moja kwa wakati wote;+ lakini uzima anaoishi, anaishi kwa kuhusiana na Mungu.+ 11 Vivyo hivyo ninyi pia: jihesabuni wenyewe kuwa wafu+ kwelikweli kuhusiana na dhambi lakini walio hai+ kuhusiana na Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.

12 Kwa hiyo msiache dhambi iendelee kutawala kama mfalme+ katika miili yenu inayoweza kufa hivi kwamba mzitii tamaa+ zake. 13 Wala msiendelee kuvitoa viungo vyenu kwa dhambi+ kuwa silaha za ukosefu wa uadilifu,+ bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama walio hai+ kutoka kwa wafu, pia viungo vyenu kwa Mungu kuwa silaha+ za uadilifu. 14 Kwa maana dhambi haipaswi kuwa bwana juu yenu, kwa kuwa ninyi hamko chini ya sheria+ bali chini ya fadhili zisizostahiliwa.+

15 Tuseme nini basi? Je, tufanye dhambi kwa sababu hatuko chini ya sheria+ bali chini ya fadhili zisizostahiliwa?+ Hilo lisitendeke kamwe! 16 Je, hamjui kwamba ikiwa mnaendelea kujitoa wenyewe kwa yeyote kuwa watumwa ili kumtii yeye, ninyi ni watumwa wake kwa sababu mnamtii yeye,+ ama watumwa wa dhambi+ kwa kutazamia kifo+ ama wa utii+ kwa kutazamia uadilifu?+ 17 Lakini ni shukrani kwa Mungu kwamba mlikuwa watumwa wa dhambi lakini kutoka moyoni mkawa wenye kutii namna ile ya fundisho ambayo mliwekwa chini yake.+ 18 Ndiyo, kwa kuwa mliwekwa huru+ kutoka katika dhambi, mlikuja kuwa watumwa+ wa uadilifu.+ 19 Ninasema kwa maneno ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wa mwili+ wenu: kwa maana kama mlivyovitoa viungo+ vyenu kuwa watumwa wa ukosefu wa usafi+ na uasi-sheria kwa kutazamia uasi-sheria, basi sasa vitoeni viungo vyenu viwe watumwa wa uadilifu kwa kutazamia utakatifu.+ 20 Kwa maana mlipokuwa watumwa wa dhambi,+ mlikuwa huru kwa habari ya uadilifu.

21 Basi, ni tunda+ gani ambalo kwa kawaida mlikuwa nalo wakati huo? Mambo+ ambayo sasa mnayaonea aibu. Kwa maana mwisho wa mambo hayo ni kifo.+ 22 Hata hivyo, sasa, kwa sababu mliwekwa huru kutoka katika dhambi lakini mkawa watumwa kwa Mungu,+ mnapata tunda+ lenu katika utakatifu, na mwisho ni uzima wa milele.+ 23 Kwa maana mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo,+ lakini zawadi+ ambayo Mungu hutoa ni uzima wa milele+ kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.+

7 Akina ndugu, je, inawezekana kwamba hamjui (kwa maana ninasema na wale wanaoijua sheria,) kuwa Sheria ni bwana juu ya mtu wakati tu anapokuwa hai?+ 2 Kwa mfano, mwanamke aliyeolewa amefungwa na sheria kwa mume wake akiwa hai; lakini mume wake akifa, yeye amefunguliwa kutoka katika sheria ya mume wake.+ 3 Hivyo, basi, mume wake anapokuwa hai, mwanamke huyo ataitwa mzinzi ikiwa atakuwa wa mwanamume mwingine.+ Lakini mume wake akifa, yeye yuko huru kutoka katika sheria ya mume, hivi kwamba mwanamke huyo si mzinzi akiwa wa mwanamume mwingine.+

4 Hivyo, ndugu zangu, ninyi pia mlifanywa wafu kuhusiana na Sheria+ kupitia mwili wa Kristo, ili muwe wa mwingine,+ muwe wa yule aliyefufuliwa kutoka kwa wafu,+ ili tumzalie Mungu matunda.+ 5 Kwa maana tulipokuwa tunapatana na mwili,+ tamaa zenye dhambi zilizotokezwa kupitia Sheria zilikuwa zikifanya kazi katika viungo vyetu ili tuzalie kifo matunda.+ 6 Lakini sasa tumefunguliwa kutoka katika Sheria,+ kwa sababu tumekufa+ kwa kile ambacho kilikuwa kimetufunga, ili tuwe watumwa+ katika maana mpya kwa roho,+ wala si katika maana ya zamani kwa njia ya sheria zilizoandikwa.+

7 Basi, tuseme nini? Je, Sheria ni dhambi?+ Isiwe hivyo kamwe! Kwa kweli singejua dhambi+ kama isingekuwa kwa sababu ya Sheria; na, kwa mfano, mimi singejua tamaa+ kama Sheria haingesema: “Usitamani.”+ 8 Lakini dhambi, kwa kuchochewa na amri hiyo,+ ilifanyiza ndani yangu tamaa ya kila namna, kwa maana bila sheria dhambi ilikuwa imekufa.+ 9 Kwa kweli, wakati mmoja nilikuwa hai bila sheria;+ lakini amri ilipofika,+ dhambi ikawa hai tena, lakini mimi nikafa.+ 10 Na amri iliyokuwa ya kuongoza kwenye uzima,+ niliiona hii kuwa ya kuongoza kwenye kifo.+ 11 Kwa maana dhambi, kwa kuchochewa na amri, ilinishawishi+ na kuniua kupitia hiyo. 12 Kwa sababu hiyo, kwa upande wake, Sheria ni takatifu,+ na amri ni takatifu na ya uadilifu+ na njema.+

13 Basi, je, lililo jema lilikuja kuwa kifo kwangu? Isiwe hivyo kamwe! Lakini dhambi ilikuwa hivyo, ili ionyeshwe kuwa dhambi ndiyo inayoniletea kifo kupitia lile lililo jema;+ ili dhambi iwe dhambi zaidi kupitia amri.+ 14 Kwa maana tunajua kwamba Sheria ni ya kiroho;+ lakini mimi ni wa kimwili, nimeuzwa chini ya dhambi.+ 15 Kwa maana lile ninalofanya silijui. Kwa maana lile ninalolitaka, hilo sizoei kulifanya; bali lile ninalochukia ndilo ninalofanya. 16 Hata hivyo, ikiwa lile ambalo sitaki ndilo ninalofanya,+ nakubali kwamba Sheria ni nzuri.+ 17 Lakini sasa anayefanya hilo si mimi tena, bali ni dhambi inayokaa ndani yangu.+ 18 Kwa maana najua kwamba ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai jambo lolote jema;+ kwa maana nina uwezo wa kutaka,+ bali uwezo wa kufanya+ yaliyo mazuri haupo. 19 Kwa maana lile jema ninalotaka silifanyi,+ bali lile baya nisilotaka ndilo ninalozoea kulifanya. 20 Basi, ikiwa lile nisilotaka ndilo ninalofanya, anayelifanya hilo si mimi tena, bali ni ile dhambi inayokaa ndani yangu.+

21 Basi, mimi naona sheria hii katika hali yangu: kwamba ninapotaka kufanya yaliyo sawa,+ yaliyo mabaya yapo pamoja nami.+ 22 Kwa kweli naipenda+ sheria ya Mungu kulingana na mtu+ niliye kwa ndani, 23 lakini mimi naona ndani ya viungo+ vyangu sheria nyingine ikipigana+ na sheria ya akili+ yangu na kunichukua mateka kwa sheria ya dhambi+ iliyo ndani ya viungo vyangu. 24 Maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa kutoka katika mwili unaopatwa na kifo hiki?+ 25 Shukrani kwa Mungu kupitia Yesu Kristo Bwana wetu!+ Basi, kwa akili yangu mimi mwenyewe ni mtumwa wa sheria+ ya Mungu, lakini kwa mwili wangu mimi ni mtumwa wa sheria ya dhambi.+

8 Kwa hiyo wale walio katika muungano na Kristo Yesu hawana hukumu ya hatia.+ 2 Kwa maana sheria+ ya ile roho+ ambayo hutokeza uzima+ katika muungano na Kristo Yesu imewaweka ninyi huru+ kutoka katika sheria ya dhambi na kifo.+ 3 Kwa maana, Sheria+ ikiwa haina uwezo, huku ilipokuwa dhaifu+ kupitia mwili, Mungu, kwa kumtuma Mwana+ wake mwenyewe akiwa katika mfano wa mwili+ wenye dhambi+ na kuhusu dhambi, aliihukumu dhambi katika mwili, 4 ili takwa la uadilifu la Sheria litimizwe+ ndani yetu sisi tunaotembea, si kupatana na mwili, bali kupatana na roho.+ 5 Kwa maana wale wanaopatana na mwili hukaza akili zao juu ya mambo ya mwili,+ lakini wale wanaopatana na roho juu ya mambo ya roho.+ 6 Kwa maana kukaza akili juu ya mwili humaanisha kifo,+ bali kukaza akili juu ya roho+ humaanisha uzima na amani; 7 kwa sababu kukaza akili juu ya mwili humaanisha uadui+ na Mungu, kwa maana mwili haujitiishi+ chini ya sheria ya Mungu, nao kwa kweli hauwezi kujitiisha. 8 Kwa hiyo wale wanaopatana na mwili+ hawawezi kumpendeza Mungu.

9 Hata hivyo, ninyi hampatani na mwili, bali mnapatana na roho,+ ikiwa kweli roho ya Mungu inakaa ndani yenu.+ Lakini ikiwa mtu yeyote hana roho+ ya Kristo, mtu huyo si wake. 10 Lakini ikiwa Kristo yuko katika muungano pamoja na ninyi,+ mwili kwa kweli umekufa kwa sababu ya dhambi, bali roho ni uzima+ kwa sababu ya uadilifu. 11 Basi, ikiwa roho ya yule aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu inakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu+ ataifanya pia miili yenu inayoweza kufa iwe hai+ kupitia roho yake inayokaa ndani yenu.

12 Basi, akina ndugu, sisi tuna wajibu, si kwa mwili ili tuishi kupatana na mwili;+ 13 kwa maana ikiwa mnaishi kupatana na mwili hakika ninyi mtakufa;+ bali mkiyaua mazoea ya mwili+ kwa roho, mtaishi. 14 Kwa maana wote wanaoongozwa na roho ya Mungu, hao ndio wana wa Mungu.+ 15 Kwa maana hamkupokea roho ya utumwa inayosababisha woga+ tena, bali mlipokea roho+ ya kufanywa kuwa wana,+ roho ambayo kupitia hiyo tunapaaza sauti: “Abba,+ Baba!” 16 Roho+ yenyewe hutoa ushahidi+ pamoja na roho+ yetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu.+ 17 Basi, ikiwa sisi ni watoto, sisi pia ni warithi: warithi wa Mungu kwelikweli, lakini warithi+ pamoja na Kristo, mradi tu tunateseka+ pamoja ili pia tutukuzwe pamoja.+

18 Kwa sababu hiyo nahesabu kwamba mateso+ ya majira haya si kitu kwa kulinganisha na utukufu+ utakaofunuliwa ndani yetu. 19 Kwa maana uumbaji+ unangojea na kutazamia kwa hamu+ kufunuliwa kwa wana wa Mungu.+ 20 Kwa maana uumbaji ulitiishwa chini ya ubatili,+ si kwa mapenzi yake wenyewe bali kupitia yeye aliyeutiisha hivyo, juu ya msingi wa tumaini+ 21 kwamba uumbaji+ wenyewe pia utawekwa huru+ kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu. 22 Kwa maana tunajua kwamba uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja mpaka sasa. 23 Si hilo tu, bali sisi wenyewe pia tulio na matunda ya kwanza,+ yaani, ile roho, ndiyo, sisi wenyewe tunaugua+ ndani yetu wenyewe, huku tukingojea kwa bidii kufanywa kuwa wana,+ kuachiliwa huru kutoka katika miili yetu kwa njia ya fidia. 24 Kwa maana tuliokolewa katika tumaini hili;+ lakini tumaini linaloonekana si tumaini, kwa maana mtu anapoona kitu, je, yeye hukitumainia? 25 Lakini tukitumainia+ kile ambacho hatuoni,+ sisi huendelea kukingojea kwa uvumilivu.+

26 Vivyo hivyo roho+ pia hujiunga kutoa msaada kwa ajili ya udhaifu wetu;+ kwa maana lile tatizo kuhusu tunalohitaji kusali hatujui,+ lakini roho+ yenyewe hutuombea pamoja na kuugua kusikotamkwa. 27 Lakini yeye ambaye huichunguza mioyo+ anajua ni nini maana ya roho,+ kwa sababu inaomba kupatana na Mungu kwa ajili ya watakatifu.+

28 Basi tunajua kwamba Mungu hufanya kazi+ zake zote zishirikiane pamoja kwa ajili ya mema ya wale wanaompenda Mungu, wale ambao wameitwa kulingana na kusudi lake;+ 29 kwa sababu wale aliowapa utambuzi+ wake wa kwanza pia aliwaagiza kimbele+ wafananishwe+ na mfano+ wa Mwana wake, ili awe mzaliwa wa kwanza+ kati ya ndugu+ wengi. 30 Zaidi ya hayo, wale aliowaagiza kimbele+ hao ndio aliowaita+ pia; na wale aliowaita hao ndio aliowatangaza kuwa waadilifu+ pia. Mwishowe wale aliowatangaza kuwa waadilifu hao ndio aliowatukuza pia.+

31 Basi, tuseme nini kuhusu mambo haya? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, ni nani atakayekuwa dhidi yetu?+ 32 Yeye ambaye hakujizuia hata Mwana+ wake mwenyewe bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote,+ kwa nini yeye pia pamoja naye hatatupa sisi kwa fadhili vitu vingine vyote?+ 33 Ni nani atakayefanya shtaka juu ya waliochaguliwa wa Mungu?+ Mungu Ndiye anayewatangaza kuwa waadilifu.+ 34 Ni nani ambaye atahukumu kuwa na hatia? Kristo Yesu ndiye aliyekufa, ndiyo, afadhali zaidi kusema yeye ndiye aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, aliye kwenye mkono wa kuume+ wa Mungu, ambaye pia hutuombea.+

35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo?+ Je, ni dhiki au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga?+ 36 Kama ilivyoandikwa: “Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, tumehesabiwa kuwa kondoo wa kuchinjwa.”+ 37 Kinyume chake, katika mambo haya yote tunatokea tukiwa tumeshinda+ kabisa kupitia yeye aliyetupenda. 38 Kwa maana nimesadiki kwamba wala kifo wala uzima+ wala malaika+ wala serikali+ wala mambo yaliyopo sasa wala mambo yatakayokuja wala nguvu+ 39 wala kimo wala kina wala uumbaji mwingine wowote havitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.+

9 Ninasema kweli+ katika Kristo; sisemi uwongo,+ kwa kuwa dhamiri yangu inanitolea ushahidi katika roho takatifu, 2 kwamba nina huzuni kubwa na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.+ 3 Kwa maana ningetaka mimi mwenyewe nitenganishwe na Kristo, niwe aliyelaaniwa kwa ajili ya ndugu zangu,+ jamaa zangu kulingana na mwili,+ 4 ambao ni Waisraeli,+ ambao kule kufanywa wana+ ni kwao na utukufu+ na maagano+ na kupewa Sheria+ na utumishi mtakatifu+ na ahadi;+ 5 ambao mababu+ ni wao na ambao Kristo alitoka kwao kulingana na mwili:+ Mungu,+ aliye juu ya wote, abarikiwe milele. Amina.

6 Hata hivyo, si kwamba neno la Mungu lilikuwa limeshindwa.+ Kwa maana si wote wanaotokana na Israeli ni “Israeli” kikweli.+ 7 Wala si wote walio watoto kwa sababu wao ni uzao wa Abrahamu,+ bali: “Ule utakaoitwa ‘uzao wako’ utakuwa kupitia Isaka.”+ 8 Yaani, watoto kwa njia ya mwili+ si watoto wa Mungu kikweli,+ bali watoto kwa njia ya ahadi+ huhesabiwa kuwa ndio uzao. 9 Kwa maana neno la ahadi lilikuwa hivi: “Wakati huu nitakuja na Sara atapata mwana.”+ 10 Lakini si tukio hilo peke yake, bali pia Rebeka alipochukua mimba ya mapacha+ kwa yule mwanamume mmoja, Isaka babu yetu: 11 kwa maana walipokuwa bado hawajazaliwa wala kufanya jambo lolote jema au baya,+ ili kusudi la Mungu kuhusu kuchagua liendelee kutegemea, si matendo, bali Yeye ambaye huita,+ 12 Rebeka aliambiwa: “Mkubwa atakuwa mtumwa wa mdogo.”+ 13 Kama ilivyoandikwa: “Nilimpenda Yakobo, lakini nilimchukia Esau.”+

14 Basi, tuseme nini? Je, Mungu ana ukosefu wa haki?+ Isiwe hivyo kamwe! 15 Kwa maana yeye anamwambia Musa: “Nitamwonyesha rehema yeyote ninayetaka kumwonyesha rehema, nami nitamwonyesha huruma yeyote ninayetaka kumwonyesha huruma.”+ 16 Hivyo basi, haitegemei yule anayetaka wala yule anayekimbia, bali hutegemea Mungu,+ aliye na rehema.+ 17 Kwa maana Andiko linamwambia Farao: “Kwa sababu hii nimekuacha ubaki, ili kuhusiana na wewe nionyeshe nguvu zangu, na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”+ 18 Hivyo basi, yeye humwonyesha rehema yule ambaye yeye anataka,+ lakini yeye ambaye anataka kumwacha humwacha awe mkaidi.+

19 Kwa hiyo utaniambia: “Kwa nini bado analaumu? Kwa maana ni nani ambaye amepinga mapenzi yake yaliyo wazi?”+ 20 Basi, Ee mwanadamu,+ kwa kweli wewe ni nani ndipo uthubutu kumjibu Mungu?+ Je, kitu kilichofinyangwa kitamwambia yeye aliyekifinyanga, “Kwa nini ulinifanya mimi hivi?”+ 21 Kwani? Je, mfinyanzi+ hana mamlaka juu ya udongo wa mfinyanzi kufanya kutokana na donge lilelile chombo kimoja kwa matumizi yenye kuheshimika, kingine kwa matumizi yasiyo na heshima?+ 22 Basi, ikiwa Mungu, ingawa alikuwa na nia ya kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha nguvu zake, alivumilia kwa ustahimilivu mwingi vyombo vya ghadhabu vilivyofanywa kuwa vyenye kufaa kwa ajili ya uharibifu,+ 23 ili ajulishe utajiri+ wa utukufu wake juu ya vyombo+ vya rehema, alivyotayarisha kimbele kwa ajili ya utukufu,+ 24 yaani, sisi, ambao alituita si kutoka kati ya Wayahudi peke yao bali pia kutoka kati ya mataifa,+ kuna ubaya gani? 25 Ni kama anavyosema pia katika Hosea: “Wale ambao si watu wangu+ nitawaita ‘watu wangu,’ na mwanamke ambaye hakuwa mpendwa nitamwita ‘mpendwa’;+ 26 na mahali ambapo waliambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ hapo wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’ ”+

27 Zaidi ya hayo, Isaya anapaaza sauti kuhusu Israeli: “Ijapokuwa hesabu ya wana wa Israeli huenda ikawa kama mchanga wa bahari,+ ni mabaki watakaookolewa.+ 28 Kwa maana Yehova atatoza hesabu duniani, na kuimaliza na kuifupisha.”+ 29 Pia, kama Isaya alivyokuwa amesema wakati uliotangulia: “Kama Yehova wa majeshi+ hangalituachia sisi uzao, tungalikuwa kama Sodoma, nasi tungalifanywa kama Gomora.”+

30 Basi, tuseme nini? Kwamba watu wa mataifa, ijapokuwa hawakuwa wakiufuatilia uadilifu,+ waliufikia uadilifu, uadilifu unaotokana na imani;+ 31 lakini Israeli, ijapokuwa alikuwa akiifuatilia sheria ya uadilifu, hakuifikia sheria.+ 32 Kwa sababu gani? Kwa sababu aliifuatilia, si kwa imani, bali kama kwa matendo.+ Walijikwaa juu ya “jiwe la kukwaza”;+ 33 kama ilivyoandikwa: “Tazama! Ninaweka katika Sayuni jiwe+ la kukwaza na mwamba wa kuangusha,+ lakini yeye anayemwamini hatakata tamaa.”+

10 Akina ndugu, nia njema ya moyo wangu na dua yangu kwa Mungu kwa ajili yao, kwa kweli, ni kwa ajili ya wokovu wao.+ 2 Kwa maana nawatolea ushahidi kwamba wana bidii+ kwa ajili ya Mungu; lakini si kulingana na ujuzi sahihi;+ 3 kwa maana, kwa sababu ya kukosa kujua uadilifu wa Mungu+ bali wakitafuta kujiwekea uadilifu wao wenyewe,+ hawakujitiisha kwa uadilifu wa Mungu.+ 4 Kwa maana Kristo ndiye mwisho wa Sheria,+ ili kila mtu anayeonyesha imani awe na uadilifu.+

5 Kwa maana Musa anaandika kwamba mtu ambaye amefanya uadilifu wa Sheria ataishi kwa huo.+ 6 Lakini uadilifu unaotokana na imani husema kwa namna hii: “Usiseme moyoni mwako,+ ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’+ yaani, kumleta Kristo+ chini; 7 au, ‘Ni nani atakayeshuka katika abiso?’+ yaani, kumleta Kristo juu kutoka kwa wafu.”+ 8 Lakini linasema nini? “Lile neno liko karibu nawe, katika kinywa chako mwenyewe na katika moyo wako mwenyewe”;+ yaani, “neno”+ la imani, ambalo sisi tunahubiri.+ 9 Kwa maana ukitangaza waziwazi lile ‘neno lililo katika kinywa chako mwenyewe,’+ kwamba Yesu ni Bwana,+ na kuonyesha imani moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu,+ utaokolewa.+ 10 Kwa maana kwa moyo+ mtu huonyesha imani kwa ajili ya uadilifu, lakini kwa kinywa mtu hufanya tangazo la hadharani+ kwa ajili ya wokovu.

11 Kwa maana Andiko linasema: “Yeyote anayemwamini+ hatakata tamaa.”+ 12 Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Mgiriki,+ kwa maana kuna Bwana yuleyule juu ya wote, aliye tajiri+ kwa wale wote wanaomwitia. 13 Kwa maana “kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.”+ 14 Hata hivyo, watawezaje kumwitia yeye ambaye hawajamwamini?+ Nao watamwaminije yeye ambaye hawajamsikia? Nao watasikiaje bila mtu wa kuhubiri?+ 15 Nao watahubirije isipokuwa wawe wametumwa?+ Kama ilivyoandikwa: “Jinsi ilivyo yenye kupendeza miguu ya wale wanaotangaza habari njema ya mambo mema!”+

16 Hata hivyo, si wote waliotii habari njema.+ Kwa maana Isaya anasema: “Yehova, ni nani aliyeliamini jambo ambalo limesikiwa kutoka kwetu?”+ 17 Kwa hiyo imani hufuata jambo lililosikiwa.+ Nalo jambo lililosikiwa ni kupitia neno kumhusu Kristo.+ 18 Hata hivyo nauliza, Je, walikosa kusikia? Kwani, kwa kweli, “sauti yao ilifika+ katika dunia yote, na maneno yao mpaka miisho ya dunia inayokaliwa.”+ 19 Hata hivyo, nauliza, je, Israeli walikosa kujua?+ Kwanza Musa anasema: “Nitawachochea ninyi kuwa na wivu kupitia lile ambalo si taifa; nitawachochea ninyi kuwa na hasira kali kupitia taifa jinga.”+ 20 Lakini Isaya anakuwa mjasiri sana na kusema: “Wale ambao hawakuwa wakinitafuta walinipata;+ nikajifunua kwa wale ambao hawakuwa wakiuliza juu yangu.”+ 21 Lakini kwa habari ya Israeli yeye anasema: “Mchana kutwa nimewanyooshea mikono yangu watu wasiotii+ na wanaojibu kwa ujeuri.”+

11 Basi, nauliza, Je, Mungu aliwakataa watu wake?+ Hilo lisitendeke kamwe! Kwa maana mimi pia ni Mwisraeli,+ wa uzao wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.+ 2 Mungu hakuwakataa watu wake, aliowatambua kwanza.+ Je, hamjui linavyosema Andiko kumhusu Eliya, anapomwomba Mungu dhidi ya Israeli?+ 3 “Yehova, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami peke yangu nimebaki, nao wanaitafuta nafsi yangu.”+ 4 Lakini, neno la Mungu+ linamwambia nini? “Nimebakiza watu elfu saba kwa ajili yangu mwenyewe, watu ambao hawakumpigia Baali goti.”+ 5 Basi, kwa njia hiyo katika majira ya sasa kumetokea pia mabaki+ kulingana na kuchaguliwa+ ambako kunatokana na fadhili zisizostahiliwa. 6 Basi ikiwa ni kwa fadhili zisizostahiliwa,+ si kwa sababu ya matendo+ tena; kama sivyo, fadhili zisizostahiliwa haziwi tena fadhili zisizostahiliwa.+

7 Tuseme nini, basi? Jambo lilelile ambalo Israeli anatafuta kwa bidii yeye hakulipata,+ lakini wale waliochaguliwa+ walilipata. Wale wengine hisia zao zilifanywa kuwa nzito;+ 8 kama ilivyoandikwa: “Mungu amewapa roho ya usingizi mzito,+ macho ili wasione na masikio ili wasisikie, mpaka leo hii.”+ 9 Pia, Daudi anasema: “Meza yao na iwe kwao mnaso na mtego na kikwazo na malipo;+ 10 macho yao na yatiwe giza ili yasione, na sikuzote wauinamishe mgongo wao.”+

11 Kwa hiyo nauliza, Je, walijikwaa hivi kwamba wakaanguka+ kabisa? Hilo lisitendeke kamwe! Lakini kwa kujikwaa+ kwao kuna wokovu kwa watu wa mataifa,+ kuwachochea wao kuwa na wivu.+ 12 Sasa ikiwa kujikwaa kwao humaanisha utajiri kwa ulimwengu, na kupungua kwao humaanisha utajiri kwa watu wa mataifa,+ hesabu+ yao kamili itamaanisha hivyo hata zaidi!

13 Sasa nasema nanyi mlio watu wa mataifa. Kwa maana kama nilivyo, kwa kweli, mtume+ kwa mataifa,+ naitukuza+ huduma+ yangu, 14 ili labda kwa njia yoyote ile niwachochee kuwa na wivu wale ambao ni mwili wangu mwenyewe na kuokoa+ baadhi yao kutoka katikati yao.+ 15 Kwa maana ikiwa kutupwa kwao+ humaanisha upatanisho+ kwa ulimwengu, kupokewa kwao kutamaanisha nini isipokuwa uzima kutoka kwa wafu? 16 Zaidi, ikiwa sehemu inayochukuliwa kuwa matunda ya kwanza+ ni takatifu, donge liko hivyo pia; na ikiwa mzizi ni mtakatifu,+ matawi yako hivyo pia.

17 Hata hivyo, ikiwa matawi mengine yalikatwa lakini wewe, ujapokuwa mzeituni wa mwitu, ulipandikizwa katikati yake+ na kuwa mshiriki wa mzizi wa unono+ wa mzeituni,+ 18 usiwe ukifurahi juu ya hayo matawi. Ingawa hivyo, ikiwa unafurahi juu yake,+ si wewe unayeuchukua mzizi,+ bali ni mzizi unaokuchukua wewe.+ 19 Basi, wewe utasema: “Matawi yalikatwa+ ili mimi nipandikizwe.”+ 20 Vema! Kwa sababu ya ukosefu wao wa imani+ yalikatwa, lakini wewe umesimama kwa imani.+ Uache kuwa na mawazo ya kujivuna,+ bali uogope.+ 21 Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachilia matawi ya asili, vivyo hivyo hatakuacha wewe.+ 22 Kwa hiyo, ona fadhili+ na ukali+ wa Mungu. Kuna ukali kuwaelekea wale walioanguka,+ lakini kuna fadhili za Mungu kukuelekea wewe, ila tu ukae+ katika fadhili zake; kama sivyo, wewe pia utakatwa.+ 23 Wao pia, ikiwa hawatadumu katika ukosefu wao wa imani, watapandikizwa;+ kwa maana Mungu anaweza kuwapandikiza tena. 24 Kwa maana ikiwa wewe ulikatwa kutoka kwenye mzeituni ulio wa asili ya mwituni na kupandikizwa+ kinyume cha asili katika mzeituni wa bustanini, si afadhali zaidi kwamba hawa walio wa asili wapandikizwe katika mzeituni wao wenyewe!+

25 Kwa maana sitaki ninyi, akina ndugu, mkose kuijua siri hii takatifu,+ kusudi msiwe wenye busara machoni penu wenyewe: kwamba, kwa sehemu, kumekuwa na kutiwa uzito kwa hisi+ za Israeli mpaka hesabu+ kamili ya watu wa mataifa iwe imeingia,+ 26 na kwa namna hii Israeli+ wote wataokolewa. Kama ilivyoandikwa: “Mkombozi atatoka katika Sayuni+ na kuondolea mbali mazoea ya kutomwogopa Mungu kutoka katika Yakobo.+ 27 Na hili ndilo agano kwa upande wangu pamoja nao,+ nitakapoondolea mbali dhambi zao.”+ 28 Ni kweli, kuhusiana na habari njema wao ni adui kwa ajili yenu,+ lakini kuhusiana na kuchagua kwa Mungu wao ni wapendwa kwa ajili ya mababu zao.+ 29 Kwa maana zawadi na mwito wa Mungu si mambo ambayo yeye atajutia.+ 30 Kwa maana kama vile ninyi wakati mmoja mlivyokuwa hamtii+ Mungu lakini sasa mmeonyeshwa rehema+ kwa sababu ya kutotii kwao,+ 31 ndivyo pia hawa sasa wamekuwa wasiotii ikitokeza rehema kwenu,+ ili wao wenyewe pia waonyeshwe rehema sasa. 32 Kwa maana Mungu amewafunga wote pamoja katika kutotii,+ ili awaonyeshe wao wote rehema.+

33 Lo! Jinsi kilivyo kina cha utajiri+ wa Mungu na hekima+ na ujuzi!+ Jinsi hukumu+ zake zisivyochunguzika na njia zake zisivyotafutika! 34 Kwa maana “ni nani amekuja kuijua akili+ ya Yehova, au ni nani amekuwa mshauri wake?”+ 35 Au, “Ni nani amempa yeye kwanza, hivi kwamba iwe lazima arudishiwe?”+ 36 Kwa sababu vitu vyote ni kutoka kwake na kwa yeye na kwa ajili yake.+ Kwake yeye na kuwe na utukufu milele.+ Amina.

12 Kwa sababu hiyo nawasihi ninyi kwa huruma za Mungu, akina ndugu, mtoe miili+ yenu iwe dhabihu+ iliyo hai,+ takatifu,+ yenye kukubalika kwa Mungu,+ utumishi mtakatifu+ pamoja na nguvu zenu za kufikiri.+ 2 Na acheni kufanyizwa+ kulingana na mfumo huu wa mambo, bali mgeuzwe kwa kufanya upya akili yenu,+ ili mjihakikishie wenyewe+ mapenzi+ ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.

3 Kwa maana kupitia fadhili zisizostahiliwa nilizopewa namwambia kila mtu hapo kati yenu asijifikirie mwenyewe zaidi kuliko ilivyo lazima kufikiri;+ bali kufikiri ili awe na akili timamu,+ kila mmoja kama Mungu alivyomgawia kipimo+ cha imani.+ 4 Kwa maana kama vile tulivyo na viungo vingi katika mwili mmoja,+ lakini viungo hivyo havifanyi kazi ileile, 5 ndivyo sisi, ingawa tuko wengi, ni mwili mmoja+ katika muungano na Kristo, lakini viungo ambavyo kila kimoja ni cha kile kingine.+ 6 Basi, kwa kuwa tuna zawadi zinazotofautiana+ kulingana na fadhili zisizostahiliwa+ tulizopewa, kama ni unabii, na tutoe unabii kulingana na imani tuliyogawiwa; 7 au ni huduma, na tuwe katika huduma+ hii; au yeye anayefundisha,+ na awe katika kufundisha+ kwake; 8 au yeye anayehimiza, na awe katika kuhimiza+ kwake; yeye anayegawa, na afanye hivyo kwa ukarimu;+ yeye anayesimamia,+ na afanye hivyo kwa bidii ya kweli; yeye anayeonyesha rehema,+ na afanye hivyo kwa uchangamfu.

9 Upendo+ wenu na uwe bila unafiki.+ Chukieni maovu,+ shikamaneni na mema.+ 10 Katika upendo wa kindugu+ iweni na upendo mwororo kwa mtu na mwenzake. Katika kuonyeshana heshima+ iweni wa kwanza. 11 Msiwe wavivu katika kazi zenu.+ Wakeni roho.+ Mtumikieni Yehova.+ 12 Shangilieni katika tumaini.+ Vumilieni chini ya dhiki.+ Dumuni katika sala.+ 13 Shirikini pamoja na watakatifu kulingana na mahitaji yao.+ Fuateni mwendo wa ukaribishaji-wageni.+ 14 Endeleeni kuwabariki wale wanaowatesa;+ muwe mkibariki+ wala msiwe mkilaani.+ 15 Shangilieni pamoja na watu wanaoshangilia;+ lieni pamoja na watu wanaolia. 16 Mwafikirie wengine kama vile mnavyojifikiria wenyewe;+ msiwe mkikaza akili juu ya mambo makuu,+ bali mwongozwe na mambo ya hali ya chini.+ Msiwe wenye busara machoni penu wenyewe.+

17 Msimlipe yeyote uovu kwa uovu.+ Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote. 18 Ikiwezekana, kwa kadiri inavyowategemea ninyi, iweni wenye kufanya amani+ na watu wote. 19 Wapendwa, msijilipizie kisasi+ wenyewe bali iachieni nafasi ghadhabu;+ kwa maana imeandikwa: “Kisasi ni changu; mimi nitalipa, asema Yehova.”+ 20 Lakini, “ikiwa adui yako ana njaa, mlishe; ikiwa ana kiu, mpe kitu anywe;+ kwa maana kwa kufanya hivyo utakusanya makaa yenye moto juu ya kichwa chake.”+ 21 Usiache ushindwe na uovu, bali endelea kuushinda uovu kwa wema.+

13 Kila nafsi na ijitiishe+ kwa mamlaka zilizo kubwa,+ kwa maana hakuna mamlaka+ isipokuwa kwa njia ya Mungu;+ mamlaka zilizopo zimesimamishwa na Mungu+ katika vyeo vyao vya kadiri.+ 2 Kwa hiyo yeye anayepinga mamlaka amechukua msimamo kupingana na mpango wa Mungu; wale ambao wamechukua msimamo kupingana nao watapokea hukumu juu yao wenyewe.+ 3 Kwa maana wale wanaotawala ni kitu cha kuogopesha, si kwa kitendo chema, bali kwa kibaya.+ Basi, je, unataka usiogope hiyo mamlaka? Endelea kufanya mema,+ nayo itakusifu wewe; 4 kwa maana hiyo ni mhudumu wa Mungu kwako kwa faida yako.+ Lakini ikiwa unafanya mabaya,+ ogopa: kwa maana haichukui upanga bila kusudi; kwa maana hiyo ni mhudumu wa Mungu, mlipiza-kisasi+ ili kuonyesha ghadhabu juu ya yeye anayefanya mabaya.

5 Kwa hiyo kuna sababu ya lazima kwenu muwe mkijitiisha, si kwa sababu ya ghadhabu hiyo tu, bali pia kwa sababu ya dhamiri+ yenu. 6 Kwa maana hiyo ndiyo sababu mnalipa kodi pia; kwa maana wao ni watumishi+ wa Mungu kwa watu wote wakitumikia daima kwa kusudi hili. 7 Wapeni wote haki zao, yeye anayetaka kodi, kodi;+ yeye anayetaka ushuru, ushuru; yeye anayetaka woga, woga+ huo; yeye anayetaka heshima, heshima+ hiyo.

8 Msiwe na deni la hata jambo moja la mtu yeyote,+ isipokuwa kupendana;+ kwa maana yeye anayempenda mwanadamu mwenzake ameitimiza sheria.+ 9 Kwa maana sheria zinazosema, “Usifanye uzinzi,+ Usiue,+ Usiibe,+ Usitamani,”+ na amri nyingine yoyote iliyoko, zimejumlishwa katika neno hili, yaani, “Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.”+ 10 Upendo+ haumfanyii uovu jirani ya mtu;+ kwa hiyo upendo ndio utimizo wa sheria.+

11 Fanyeni hivi, pia, kwa sababu mnayajua majira, kwamba tayari ni saa ya ninyi kuamka+ kutoka katika usingizi, kwa maana sasa wokovu wetu uko karibu zaidi kuliko wakati tulipokuwa waamini.+ 12 Usiku umesonga sana; mchana+ umekaribia. Kwa hiyo na tuyaondoe matendo ya giza+ na tuvae silaha+ za nuru. 13 Kama katika wakati wa mchana na tujiendeshe kwa adabu,+ si katika karamu za kupindukia na vipindi vya kulewa,+ si katika ngono isiyo halali na mwenendo mpotovu,+ si katika mizozo+ na wivu. 14 Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo,+ na msiwe mkipanga kimbele kwa ajili ya tamaa za mwili.+

14 Mkaribisheni mtu aliye na udhaifu+ katika imani yake, lakini msifanye maamuzi juu ya maswali ya ndani.+ 2 Mtu mmoja ana imani ya kula kila kitu,+ lakini mtu aliye dhaifu hula mboga za majani. 3 Yeye anayekula asimdharau yeye asiyekula,+ na yeye asiyekula asimhukumu yeye anayekula, kwa maana Mungu amemkaribisha huyo. 4 Wewe ni nani ili umhukumu mtumishi wa nyumbani wa mwingine?+ Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au kuanguka.+ Kwa kweli, atasimamishwa, kwa maana Yehova anaweza kumsimamisha. +

5 Mtu mmoja anahukumu siku moja kuwa juu ya nyingine;+ mtu mwingine anahukumu siku moja kuwa kama nyingine zote;+ kila mtu na asadikishwe kikamili katika akili yake mwenyewe. 6 Yeye anayeishika siku huishika kwa ajili ya Yehova. Pia, yeye anayekula, anakula kwa ajili ya Yehova,+ kwa maana yeye humshukuru Mungu;+ na yeye asiyekula hali chakula kwa ajili ya Yehova,+ na bado yeye humshukuru Mungu.+ 7 Kwa kweli, hakuna hata mmoja wetu anayeishi kwa ajili yake mwenyewe tu,+ na hakuna yeyote anayekufa kwa ajili yake mwenyewe tu; 8 kwa maana tukiishi, tunaishi kwa ajili ya Yehova,+ na tukifa, tunakufa kwa ajili ya Yehova.+ Kwa hiyo tukiishi na tukifa, sisi ni wa Yehova.+ 9 Kwa maana kwa kusudi hili Kristo alikufa na kuwa hai tena,+ ili awe Bwana juu ya waliokufa+ na walio hai+ pia.

10 Lakini kwa nini wewe unamhukumu ndugu yako?+ Au kwa nini wewe pia unamdharau ndugu yako? Kwa maana sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu+ cha Mungu; 11 kwa maana imeandikwa: “ ‘Kama ninavyoishi,’ asema Yehova,+ ‘kila goti litapigwa mbele zangu, na kila ulimi utakiri waziwazi kwa Mungu.’ ”+ 12 Hivyo, basi, kila mmoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.+

13 Kwa hiyo sisi na tusiwe tukihukumiana+ tena, bali badala yake fanyeni hili kuwa uamuzi+ wenu, kutokuweka mbele ya ndugu+ kikwazo+ au sababu ya kujikwaa. 14 Najua nami nasadikishwa katika Bwana Yesu kwamba hakuna kitu ambacho ndani yake chenyewe ni najisi;+ ni pale tu ambapo mtu anakiona kitu kuwa najisi, kwake yeye hicho huwa najisi.+ 15 Kwa maana ikiwa ndugu yako anahuzunishwa kwa sababu ya chakula, wewe hutembei tena kupatana na upendo.+ Kwa chakula chako usimwangamize yule ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.+ 16 Kwa hiyo, msiache msemwe vibaya kwa mema mnayofanya. 17 Kwa maana ufalme wa Mungu+ haumaanishi kula na kunywa,+ bali unamaanisha uadilifu+ na amani+ na shangwe+ pamoja na roho takatifu. 18 Kwa maana yeye ambaye kwa habari hii anamtumikia Kristo anakubalika kwa Mungu naye ana kibali cha wanadamu.+

19 Hivyo, basi, na tufuatilie mambo yanayofanya kuwe na amani+ na mambo ambayo ni ya kujengana.+ 20 Acheni kuibomoa kazi ya Mungu kwa ajili ya chakula+ tu. Ni kweli, vitu vyote ni safi, lakini ni jambo baya kwa mtu ambaye hula kukiwa na hali ya kukwaza.+ 21 Ni vema kutokula nyama au kunywa divai au kufanya jambo lolote ambalo ndugu yako anakwazika juu yake.+ 22 Imani uliyo nayo, uwe nayo kupatana na wewe mwenyewe machoni pa Mungu.+ Mwenye furaha ni mtu asiyejitia mwenyewe hukumuni kwa yale anayokubali. 23 Lakini ikiwa ana shaka, yeye akila tayari atakuwa amehukumiwa kuwa mwenye hatia,+ kwa sababu hali kwa imani. Kwa kweli, kila kitu ambacho hakitokani na imani ni dhambi.+

15 Ingawa hivyo, sisi tulio na nguvu tunapaswa kuchukua udhaifu wa wale wasio na nguvu,+ na tusiwe tukijipendeza wenyewe.+ 2 Kila mmoja wetu na ampendeze jirani yake katika yaliyo mema kwa ajili ya kujengwa kwake.+ 3 Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe;+ bali kama ilivyoandikwa: “Shutuma za wale waliokuwa wanakushutumu zimeniangukia.”+ 4 Kwa maana mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa+ ili kutufundisha+ sisi, ili kupitia uvumilivu+ wetu na kupitia faraja+ kutokana na Maandiko tuwe na tumaini.+ 5 Sasa Mungu anayetoa uvumilivu na faraja na awawezeshe ninyi kati yenu wenyewe kuwa na mtazamo uleule wa akili+ ambao Kristo Yesu alikuwa nao, 6 ili kwa umoja+ na kwa kinywa kimoja mpate kumtukuza Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo.

7 Kwa hiyo mkaribishane,+ kama vile Kristo pia alivyotukaribisha sisi,+ kwa kusudi la kumpa Mungu utukufu. 8 Kwa maana nasema kwamba kwa kweli Kristo alikuwa mhudumu+ wa wale waliotahiriwa+ kwa ajili ya ukweli+ wa Mungu, ili kuthibitisha ahadi+ ambazo Yeye aliwapa mababu zao, 9 na kwamba mataifa+ yamtukuze Mungu kwa ajili ya rehema+ yake. Kama ilivyoandikwa: “Ndiyo sababu nitakukiri wewe waziwazi kati ya mataifa nami nitalipigia jina lako muziki.”+ 10 Naye anasema tena: “Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake.”+ 11 Na tena: “Msifuni Yehova, enyi mataifa yote, na vikundi vyote vya watu vimsifu yeye.”+ 12 Na tena Isaya anasema: “Patakuwa na mzizi wa Yese,+ na patakuwa na mmoja ambaye atasimama ili kutawala mataifa;+ na mataifa yatamtumainia yeye.”+ 13 Mungu anayetoa tumaini na awajaze ninyi shangwe yote na amani kwa kuamini kwenu, ili mzidi katika tumaini kwa nguvu za roho takatifu.+

14 Sasa mimi mwenyewe pia ninasadikishwa juu yenu, ndugu zangu, kwamba ninyi wenyewe mmejaa wema pia, kwa kuwa mmejawa na ujuzi+ wote, na kwamba mnaweza pia kuonyana.+ 15 Hata hivyo, ninawaandikia ninyi kwa kusema waziwazi zaidi juu ya mambo fulani, kana kwamba ninawakumbusha+ ninyi tena, kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa nilizopewa kutoka kwa Mungu+ 16 ili niwe mtumishi wa watu wote wa Kristo Yesu kwa mataifa,+ nikifanya kazi takatifu ya habari njema+ ya Mungu, ili toleo,+ yaani, mataifa haya, likubalike,+ likiwa limetakaswa kwa roho takatifu.+

17 Kwa hiyo nina sababu ya kufurahi katika Kristo Yesu+ kwa habari ya mambo yanayohusiana na Mungu.+ 18 Kwa maana sitathubutu kusema jambo moja ikiwa hilo si kati ya mambo yale ambayo Kristo alifanya kupitia mimi+ ili mataifa yawe yenye utiifu,+ kwa njia ya neno+ na tendo langu, 19 kwa nguvu za ishara na mambo ya ajabu,+ kwa nguvu za roho takatifu; hivi kwamba kutoka Yerusalemu na kuzunguka+ mpaka Ilirikamu nimehubiri kikamili habari njema juu ya Kristo.+ 20 Kwa kweli, katika njia hii, nilikusudia kwamba nisitangaze habari njema mahali ambapo Kristo tayari alikuwa amekwisha kutajwa jina, ili nisiwe nikijenga juu ya msingi wa mtu mwingine;+ 21 bali, kama ilivyoandikwa: “Wale ambao hawajatangaziwa juu yake wataona, na wale ambao hawajasikia wataelewa.”+

22 Kwa hiyo pia nilizuiwa mara nyingi nisiwafikie ninyi.+ 23 Lakini sasa kwa kuwa sina tena eneo lisiloguswa katika maeneo haya, na kwa miaka kadhaa nikiwa nimetamani kuwafikia ninyi+ 24 wakati nitakapokuwa nimeenda Uhispania,+ natumaini, zaidi ya yote, nitakapokuwa safarini kwenda huko, niwaangalie ninyi kidogo nanyi mnisindikize+ kidogo kwenda huko baada ya mimi kutosheka kwa kiasi fulani na ushirika wenu. 25 Lakini sasa nakaribia kusafiri kwenda Yerusalemu ili kuwahudumia watakatifu.+ 26 Kwa maana wale walio katika Makedonia na Akaya+ wamependezwa kushiriki vitu vyao kwa kuwatolea mchango+ fulani walio maskini kati ya watakatifu katika Yerusalemu. 27 Kweli, wamependezwa kufanya hivyo, na bado walikuwa wadeni kwao; kwa maana ikiwa mataifa wameshiriki mambo yao ya kiroho,+ wao pia wana deni la kuwahudumia hadharani kwa vitu ambavyo ni kwa ajili ya mwili.+ 28 Kwa sababu hiyo nikiisha kumaliza hili na kuwafikishia salama tunda+ hili, nitaondoka nikipitia kwenu kwenda Uhispania.+ 29 Zaidi ya hayo, najua kwamba nitakapokuja kwenu nitakuja nikiwa na kipimo kamili cha baraka kutoka kwa Kristo.+

30 Sasa nawahimiza ninyi, akina ndugu, kupitia Bwana wetu Yesu Kristo na kupitia upendo wa roho,+ kwamba mjikaze pamoja nami katika sala kwa Mungu kwa ajili yangu,+ 31 ili nikombolewe+ kutoka kwa wale wasioamini katika Yudea na kwamba huduma yangu ambayo ni kwa ajili ya Yerusalemu+ ikubalike kwa watakatifu,+ 32 ili nitakapofika kwenu nikiwa na shangwe kwa mapenzi ya Mungu niburudishwe+ pamoja nanyi. 33 Mungu anayetoa amani na awe pamoja nanyi nyote.+ Amina.

16 Nampendekeza kwenu Fibi dada yetu, ambaye ni mhudumu+ wa kutaniko lililo katika Kenkrea,+ 2 ili kwamba mkamkaribishe+ katika Bwana kwa njia inayowastahili watakatifu, na kwamba mkamsaidie katika jambo lolote ambalo huenda akawahitaji ninyi,+ kwa maana yeye mwenyewe pia alikuwa mtetezi wa wengi, ndiyo, wangu mimi mwenyewe.

3 Wapeni salamu zangu Priska na Akila+ wafanyakazi wenzangu+ katika Kristo Yesu, 4 ambao wamehatarisha shingo+ zao wenyewe kwa ajili ya nafsi yangu, ambao si mimi tu bali pia makutaniko yote ya mataifa yanawashukuru;+ 5 na salimuni kutaniko lililo katika nyumba yao.+ Salimuni Epaineto mpendwa wangu, aliye matunda ya kwanza+ ya Asia kwa ajili ya Kristo. 6 Salimuni Maria, ambaye amefanya kazi nyingi kwa ajili yenu. 7 Salimuni Androniko na Yunia jamaa+ zangu na mateka wenzangu,+ ambao ni watu maarufu kati ya mitume na ambao wamekuwa katika muungano+ na Kristo muda mrefu zaidi ya mimi.

8 Mpeni salamu+ zangu Ampliato mpendwa wangu katika Bwana. 9 Salimuni Urbano mfanyakazi mwenzetu katika Kristo, na Stako mpendwa wangu. 10 Salimuni+ Apele, aliyekubaliwa katika Kristo. Salimuni wale wa nyumbani mwa Aristobulo. 11 Salimuni Herodioni aliye wa jamaa+ yangu. Salimuni wale wa nyumbani mwa Narkiso walio katika Bwana.+ 12 Salimuni Trifaina na Trifosa, wanawake wanaofanya kazi kwa bidii katika Bwana. Salimuni Persisi mpendwa wetu, kwa maana mwanamke huyo alifanya kazi nyingi katika Bwana. 13 Salimuni Rufo aliye mchaguliwa katika Bwana, na mama yake na yangu. 14 Salimuni Asinkrito, Flegoni, Hermesi, Patroba, Hermasi, na akina ndugu walio pamoja nao. 15 Salimuni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa, na watakatifu wote walio pamoja nao.+ 16 Salimianeni kwa busu takatifu.+ Makutaniko yote ya Kristo yanawasalimu ninyi.

17 Sasa nawahimiza ninyi, akina ndugu, waangalieni wale wanaosababisha migawanyiko+ na kusababisha kukwazika kinyume cha fundisho+ ambalo mmejifunza, nanyi mjiepushe nao.+ 18 Kwa maana watu wa namna hiyo ni watumwa, si wa Bwana wetu Kristo, bali wa matumbo+ yao wenyewe; na kwa maneno laini+ na maneno ya kusifusifu+ wao huishawishi mioyo ya wasio na lawama. 19 Kwa maana utii wenu umekuja kujulikana na wote.+ Kwa hiyo nashangilia juu yenu. Lakini nataka ninyi muwe wenye hekima+ kuhusu yaliyo mema, bali wasio na hatia+ kuhusu yaliyo maovu.+ 20 Kwa upande wake, Mungu anayetoa amani+ atamponda Shetani+ chini ya miguu yenu upesi. Fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu Yesu na ziwe pamoja nanyi.+

21 Timotheo mfanyakazi mwenzangu anawasalimu ninyi, na pia Lukio na Yasoni na Sosipata jamaa+ zangu.

22 Mimi, Tertio, ambaye nimeiandika barua hii, nawasalimu ninyi katika Bwana.

23 Gayo,+ mkaribishaji wangu na wa kutaniko lote, anawasalimu ninyi. Erasto msimamizi wa jiji+ anawasalimu ninyi, na pia Kwarto ndugu yake. 24 ——

25 Sasa kwa yeye+ anayeweza kuwafanya ninyi kuwa imara kulingana na habari njema ninayotangaza na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kwa kupatana na ufunuo wa siri takatifu+ ambayo imewekwa katika siri tangu nyakati za zamani za kale 26 lakini sasa imefunuliwa+ na kujulishwa kupitia maandiko ya kinabii kati ya mataifa yote kwa kupatana na amri ya Mungu anayedumu milele ili kuendeleza utii kwa njia ya imani;+ 27 kwa Mungu, mwenye hekima peke yake,+ kuwe na utukufu+ kupitia Yesu Kristo+ milele. Amina.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki