Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • nwt 1 Nyakati 1:1-29:30
  • 1 Mambo ya Nyakati

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 1 Mambo ya Nyakati
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
1 Mambo ya Nyakati

KITABU CHA KWANZA CHA MAMBO YA NYAKATI

1 Adamu,

Sethi,+

Enoshi,

2 Kenani,

Mahalaleli,+

Yaredi,+

3 Enoko,+

Methusela,

Lameki,+

4 Noa,+

Shemu,+ Hamu, na Yafethi.+

5 Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali,+ Mesheki,+ na Tirasi.+

6 Wana wa Gomeri walikuwa Ashkenazi, Rifathi, na Togarma.+

7 Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Rodanimu.

8 Wana wa Hamu walikuwa Kushi,+ Misraimu, Putu, na Kanaani.+

9 Wana wa Kushi walikuwa Seba,+ Havila, Sabta, Raama,+ na Sabteka.

Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.+

10 Kushi akamzaa Nimrodi.+ Nimrodi alikuwa shujaa wa kwanza duniani.

11 Misraimu akamzaa Ludimu,+ Anamimu, Lehabimu, Naftuhimu,+ 12 Pathrusimu,+ Kasluhimu (hao ndio waliowazaa Wafilisti),+ na Kaftorimu.+

13 Kanaani akamzaa Sidoni,+ mzaliwa wake wa kwanza, na Hethi,+ 14 na pia Wayebusi,+ Waamori,+ Wagirgashi,+ 15 Wahivi,+ Waarkia, Wasini, 16 Waarvadi,+ Wasemari, na Wahamathi.

17 Wana wa Shemu walikuwa Elamu,+ Asihuru,+ Arpakshadi, Ludi, na Aramu,

na* Usi, Huli, Getheri, na Mashi.+

18 Arpakshadi akamzaa Shela,+ naye Shela akamzaa Eberi.

19 Eberi alizaa wana wawili. Mmoja aliitwa Pelegi,*+ kwa sababu katika siku zake dunia ilikuwa imegawanyika.* Ndugu yake aliitwa Yoktani.

20 Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hazarmavethi, Yera,+ 21 Hadoramu, Uzali, Dikla, 22 Obali, Abimaeli, Sheba, 23 Ofiri,+ Havila,+ na Yobabu; wote hao walikuwa wana wa Yoktani.

24 Wazao wa Shemu walikuwa

Arpakshadi,

Shela,

25 Eberi,

Pelegi,+

Reu,+

26 Serugi,+

Nahori,+

Tera,+

27 Abramu, yaani, Abrahamu.+

28 Wana wa Abrahamu walikuwa Isaka+ na Ishmaeli.+

29 Hizi ndizo asili za koo zao: mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli alikuwa Nebayothi,+ kisha Kedari,+ Adbeeli, Mibsamu,+ 30 Mishma, Duma, Masa, Hadadi, Tema, 31 Yeturi, Nafishi, na Kedema. Hao ndio waliokuwa wana wa Ishmaeli.

32 Wana waliozaliwa na Ketura,+ suria wa Abrahamu, walikuwa Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani,+ Ishbaki, na Shua.+

Wana wa Yokshani walikuwa Sheba na Dedani.+

33 Wana wa Midiani walikuwa Efa,+ Eferi, Hanoki, Abida, na Eldaa.

Hao wote walikuwa wana wa Ketura.

34 Abrahamu akamzaa Isaka.+ Wana wa Isaka walikuwa Esau+ na Israeli.+

35 Wana wa Esau walikuwa Elifazi, Reueli, Yeushi, Yalamu, na Kora.+

36 Wana wa Elifazi walikuwa Temani,+ Omari, Sefo, Gatamu, Kenasi, Timna, na Amaleki.+

37 Wana wa Reueli walikuwa Nahathi, Zera, Shamma, na Miza.+

38 Wana wa Seiri+ walikuwa Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, Dishoni, Ezeri, na Dishani.+

39 Wana wa Lotani walikuwa Hori na Homamu. Dada ya Lotani alikuwa Timna.+

40 Wana wa Shobali walikuwa Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.

Wana wa Sibeoni walikuwa Aya na Ana.+

41 Mwana* wa Ana alikuwa Dishoni.

Wana wa Dishoni walikuwa Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.+

42 Wana wa Ezeri+ walikuwa Bilhani, Zaavani, na Akani.

Wana wa Dishani walikuwa Usi na Arani.+

43 Hawa ndio wafalme waliotawala katika nchi ya Edomu+ kabla mfalme yeyote hajawatawala Waisraeli:*+ Bela mwana wa Beori; jiji lake liliitwa Dinhaba. 44 Bela alipokufa, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra+ alianza kutawala baada yake. 45 Yobabu alipokufa, Hushamu kutoka katika nchi ya Watemani alianza kutawala baada yake. 46 Hushamu alipokufa, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyewashinda Wamidiani katika eneo* la Moabu, alianza kutawala baada yake. Jiji lake liliitwa Avithi. 47 Hadadi alipokufa, Samla kutoka Masreka alianza kutawala baada yake. 48 Samla alipokufa, Shauli kutoka Rehobothi karibu na ule Mto alianza kutawala baada yake. 49 Shauli alipokufa, Baal-hanani mwana wa Akbori alianza kutawala baada yake. 50 Baal-hanani alipokufa, Hadadi alianza kutawala baada yake. Jiji lake liliitwa Pau, na mke wake aliitwa Mehetabeli binti ya Matredi, binti ya Mezahabu. 51 Kisha Hadadi akafa.

Mashehe* wa Edomu walikuwa Shehe Timna, Shehe Alva, Shehe Yethethi,+ 52 Shehe Oholibama, Shehe Ela, Shehe Pinoni, 53 Shehe Kenasi, Shehe Temani, Shehe Mibsari, 54 Shehe Magdieli, na Shehe Iramu. Hao ndio waliokuwa mashehe wa Edomu.

2 Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli:+ Rubeni,+ Simeoni,+ Lawi,+ Yuda,+ Isakari,+ Zabuloni,+ 2 Dani,+ Yosefu,+ Benjamini,+ Naftali,+ Gadi,+ na Asheri.+

3 Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela. Binti ya Shua, mwanamke Mkanaani, alimzalia wana hao watatu.+ Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, hakumpendeza Yehova, kwa hiyo Akamuua.+ 4 Tamari,+ binti mkwe wa Yuda, alimzalia Yuda wana walioitwa Perezi+ na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.

5 Wana wa Perezi walikuwa Hezroni na Hamuli.+

6 Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli, na Dara. Wote walikuwa watano.

7 Mwana* wa Karmi alikuwa Akari,* aliyewaletea Waisraeli msiba,*+ ambaye alikosa uaminifu kuhusiana na kitu kilichopaswa kuharibiwa.+

8 Mwana* wa Ethani alikuwa Azaria.

9 Wana waliozaliwa na Hezroni walikuwa Yerahmeeli,+ Ramu,+ na Kelubai.*

10 Ramu alimzaa Aminadabu.+ Aminadabu akamzaa Nashoni+ mkuu wa wazao wa Yuda. 11 Nashoni akamzaa Salma.+ Salma akamzaa Boazi.+ 12 Boazi akamzaa Obedi. Obedi akamzaa Yese.+ 13 Yese akamzaa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu,+ wa tatu Shimea,+ 14 wa nne Nethaneli, wa tano Radai, 15 wa sita Ozemu, na wa saba Daudi.+ 16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili.+ Wana wa Seruya walikuwa Abishai,+ Yoabu,+ na Asaheli,+ wana watatu. 17 Abigaili alimzaa Amasa,+ na baba ya Amasa alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.

18 Kalebu* mwana wa Hezroni aliwazaa wana kupitia Azuba mke wake na kupitia Yeriothi; na hawa ndio waliokuwa wana wa Azuba: Yesheri, Shobabu, na Ardoni. 19 Azuba alipokufa, Kalebu alimwoa Efrathi,+ aliyemzalia Kalebu mwana aliyeitwa Huru.+ 20 Huru akamzaa Uri. Uri akamzaa Bezaleli.+

21 Baadaye Hezroni akalala na binti ya Makiri+ baba ya Gileadi.+ Hezroni alikuwa na umri wa miaka 60 alipomwoa, naye akamzalia Segubu. 22 Segubu akamzaa Yairi,+ aliyekuwa na majiji 23 katika nchi ya Gileadi.+ 23 Baadaye Geshuri+ na Siria+ wakachukua Hawoth-yairi+ kutoka kwao, pamoja na Kenathi+ na miji yake, majiji 60. Wote hao walikuwa wazao wa Makiri baba ya Gileadi.

24 Baada ya Hezroni+ kufa huko Kalebu-efratha, Abiya mke wake alimzalia Hezroni mwana aliyeitwa Ashuri,+ baba ya Tekoa.+

25 Wana wa Yerahmeeli mzaliwa wa kwanza wa Hezroni walikuwa Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya. 26 Yerahmeeli alikuwa na mke mwingine aliyeitwa Atara. Alikuwa mama ya Onamu. 27 Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerahmeeli walikuwa Maazi, Yamini, na Ekeri. 28 Wana wa Onamu walikuwa Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa Nadabu na Abishuri. 29 Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, alimzalia Abishuri wana walioitwa Abani na Molidi. 30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu. Lakini Seledi alikufa bila watoto.* 31 Mwana* wa Apaimu alikuwa Ishi. Na mwana* wa Ishi alikuwa Sheshani, na mwana* wa Sheshani alikuwa Alai. 32 Wana wa Yada ndugu ya Shamai walikuwa Yetheri na Yonathani. Lakini Yetheri alikufa bila watoto.* 33 Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hao ndio waliokuwa wazao wa Yerahmeeli.

34 Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, alikuwa na mabinti tu. Sheshani alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha. 35 Sheshani akamchukua binti yake na kumpa Yarha mtumishi wake awe mke wake, na binti huyo akamzalia mwana aliyeitwa Atai. 36 Atai akamzaa Nathani. Nathani akamzaa Zabadi. 37 Zabadi akamzaa Eflali. Eflali akamzaa Obedi. 38 Obedi akamzaa Yehu. Yehu akamzaa Azaria. 39 Azaria akamzaa Helezi. Helezi akamzaa Eleasa. 40 Eleasa akamzaa Sismai. Sismai akamzaa Shalumu. 41 Shalumu akamzaa Yekamia. Yekamia akamzaa Elishama.

42 Wana wa Kalebu*+ ndugu ya Yerahmeeli walikuwa Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa baba ya Zifu, na wana wa Maresha baba ya Hebroni. 43 Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema. 44 Shema akamzaa Rahamu baba ya Yorkeamu. Rekemu akamzaa Shamai. 45 Mwana wa Shamai alikuwa Maoni. Maoni alikuwa baba ya Beth-suri.+ 46 Efa suria wa Kalebu alimzaa Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akamzaa Gazezi. 47 Wana wa Yahdai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafu. 48 Maaka suria wa Kalebu alimzaa Sheberi na Tirhana. 49 Baada ya muda akamzaa Shaafu baba ya Madmana+ na Sheva baba ya Makbena na Gibea.+ Binti ya Kalebu+ alikuwa Aksa.+ 50 Hao ndio waliokuwa wazao wa Kalebu.

Wana wa Huru+ mzaliwa wa kwanza wa Efratha+ walikuwa Shobali baba ya Kiriath-yearimu,+ 51 Salma baba ya Bethlehemu,+ na Harefu baba ya Beth-gaderi. 52 Shobali baba ya Kiriath-yearimu alikuwa na wana hawa: Haroe na nusu ya watu wa Menuhothi. 53 Koo za Kiriath-yearimu zilikuwa Waithri,+ Waputhu, Washumathi, na Wamishra. Wasorathi+ na Waeshtaoli+ walitokana na koo hizo. 54 Wana wa Salma walikuwa Bethlehemu,+ Wanetofa, Atroth-beth-yoabu, na nusu ya Wamanahathi, na Wazori. 55 Koo za waandishi walioishi Yabesi zilikuwa Watirathi, Washimea, na Wasukathi. Hao walikuwa Wakeni+ wazao wa Hamathi baba wa nyumba ya Rekabu.+

3 Hawa ndio wana wa Daudi waliozaliwa Hebroni:+ mzaliwa wa kwanza aliitwa Amnoni,+ mama yake aliitwa Ahinoamu+ kutoka Yezreeli; wa pili, Danieli, mama yake aliitwa Abigaili+ Mkarmeli; 2 wa tatu, Absalomu,+ mwana wa Maaka binti ya Talmai mfalme wa Geshuri; wa nne, Adoniya+ mwana wa Hagithi; 3 wa tano, Shefatia, ambaye mama yake aliitwa Abitali; na wa sita, Ithreamu, ambaye mama yake aliitwa Egla, mke wa Daudi. 4 Aliwazaa wana hao sita kule Hebroni; alitawala huko kwa miaka 7 na miezi 6, naye alitawala kule Yerusalemu kwa miaka 33.+

5 Aliwazaa wana wafuatao huko Yerusalemu:+ Shimea, Shobabu, Nathani,+ na Sulemani;+ mama ya wana hao wanne alikuwa Bath-sheba+ binti ya Amieli. 6 Alikuwa na wana wengine tisa ambao ni Ibhari, Elishama, Elifeleti, 7 Noga, Nefegi, Yafia, 8 Elishama, Eliada, na Elifeleti. 9 Hao wote walikuwa wana wa Daudi, bila kuhesabu wana wa masuria, na dada yao alikuwa Tamari.+

10 Mwana wa Sulemani alikuwa Rehoboamu;+ mwana wa Rehoboamu alikuwa Abiya,+ mwana wa Abiya alikuwa Asa,+ mwana wa Asa alikuwa Yehoshafati,+ 11 mwana wa Yehoshafati alikuwa Yehoramu,+ mwana wa Yehoramu alikuwa Ahazia,+ mwana wa Ahazia alikuwa Yehoashi,+ 12 mwana wa Yehoashi alikuwa Amazia,+ mwana wa Amazia alikuwa Azaria,+ mwana wa Azaria alikuwa Yothamu,+ 13 mwana wa Yothamu alikuwa Ahazi,+ mwana wa Ahazi alikuwa Hezekia,+ mwana wa Hezekia alikuwa Manase,+ 14 mwana wa Manase alikuwa Amoni,+ mwana wa Amoni alikuwa Yosia.+ 15 Wana wa Yosia walikuwa Yohanani mzaliwa wa kwanza, wa pili, Yehoyakimu,+ wa tatu, Sedekia,+ wa nne, Shalumu. 16 Wana wa Yehoyakimu walikuwa Yekonia+ mwanawe na Sedekia mwana wa Yekonia. 17 Wana wa Yekonia aliyekuwa mfungwa walikuwa Shealtieli, 18 Malkiramu, Pedaya, Shenazari, Yekamia, Hoshama, na Nedabia. 19 Wana wa Pedaya walikuwa Zerubabeli+ na Shimei; na wana wa Zerubabeli walikuwa Meshulamu na Hanania (na dada yao alikuwa Shelomithi); 20 naye alikuwa na wana wengine watano ambao ni Hashuba, Oheli, Berekia, Hasadia, na Yushab-hesedi. 21 Wana wa Hanania walikuwa Pelatia na Yeshaya; mwana* wa Yeshaya alikuwa Refaya; mwana* wa Refaya alikuwa Arnani; mwana* wa Arnani alikuwa Obadia; mwana* wa Obadia alikuwa Shekania; 22 na wana wa Shekania walikuwa Shemaya na wana wa Shemaya walikuwa Hatushi, Igali, Baria, Nearia, na Shafati—jumla ya wana sita. 23 Na wana wa Nearia walikuwa Elioenai, Hizkia, na Azrikamu, wana watatu. 24 Na wana wa Elioenai walikuwa Hodavia, Eliashibu, Pelaya, Akubu, Yohanani, Delaya, na Anani, wana saba.

4 Wana wa Yuda walikuwa Perezi,+ Hezroni,+ Karmi, Huru,+ na Shobali.+ 2 Reaya mwana wa Shobali alimzaa Yahathi; Yahathi akamzaa Ahumai na Lahadi. Hizo ndizo zilizokuwa koo za Wasorathi.+ 3 Hawa ndio waliokuwa wana wa baba ya Etamu:+ Yezreeli, Ishma, na Idbashi (na dada yao aliitwa Haselelponi), 4 Penueli alimzaa Gedori, na Ezeri akamzaa Husha. Hao ndio waliokuwa wana wa Huru,+ mzaliwa wa kwanza wa Efratha na baba ya Bethlehemu.+ 5 Ashuri+ baba ya Tekoa+ alikuwa na wake wawili, Hela na Naara. 6 Naara akamzalia Ashuri wana hawa: Ahuzamu, Heferi, Temeni, na Haahashtari. Hao ndio waliokuwa wana wa Naara. 7 Na wana wa Hela walikuwa Serethi, Ishari, na Ethnani. 8 Kosi alimzaa Anubu, Zobeba, na familia za Aharheli mwana wa Harumi.

9 Yabesi aliheshimiwa sana kuliko ndugu zake; na mama yake alimwita jina Yabesi, akisema: “Nilimzaa kwa uchungu.”* 10 Yabesi akamlilia Mungu wa Israeli, akisema: “Laiti ungenibariki na kupanua eneo langu na kuuruhusu mkono wako uwe pamoja nami na kuniokoa kutoka katika msiba, ili msiba huo usinidhuru!” Basi Mungu akatimiza ombi lake.

11 Kelubu ndugu ya Shuha akamzaa Mehiri, aliyekuwa baba ya Eshtoni. 12 Eshtoni akamzaa Beth-rafa, Pasea, na Tehina, baba ya Ir-nahashi. Hao ndio waliokuwa wanaume wa Reka. 13 Na wana wa Kenasi walikuwa Othnieli+ na Seraya, na mwana* wa Othnieli alikuwa Hathathi. 14 Meonothai akamzaa Ofra. Seraya akamzaa Yoabu baba ya Ge-harashimu,* walipewa jina hilo kwa sababu walikuwa mafundi.

15 Wana wa Kalebu+ mwana wa Yefune walikuwa Iru, Ela, na Naamu; na mwana* wa Ela alikuwa Kenasi. 16 Wana wa Yehaleleli walikuwa Zifu, Zifa, Tiria, na Asareli. 17 Wana wa Ezra walikuwa Yetheri, Meredi, Eferi, na Yaloni; alishika* mimba na kumzaa Miriamu, Shamai, na Ishba baba ya Eshtemoa. 18 (Na mke wake Myahudi alimzaa Yeredi baba ya Gedori, Heberi baba ya Soko, na Yekuthieli baba ya Zanoa.) Hao ndio waliokuwa wana wa Bithia, binti ya Farao, aliyeolewa na Meredi.

19 Wana wa mke wa Hodia, dada ya Nahamu, walikuwa baba za Keila Mgarmi na Eshtemoa Mmaakathi. 20 Na wana wa Shimoni walikuwa Amnoni, Rina, Ben-hanani, na Tiloni. Na wana wa Ishi walikuwa Zohethi na Ben-zohethi.

21 Wana wa Shela+ mwana wa Yuda walikuwa Eri baba ya Leka, Laada baba ya Maresha, na familia za wafumaji wa vitambaa bora wa nyumba ya Ashbea, 22 na Yokimu, wanaume wa Kozeba, Yoashi, na Sarafi, waliowaoa wanawake Wamoabu, na Yashubi-lehemu. Habari hizi ni za zamani za kale.* 23 Hao ndio wafinyanzi walioishi Netaimu na Gedera. Waliishi huko na kumtumikia mfalme.

24 Wana wa Simeoni+ walikuwa Nemueli, Yamini, Yaribu, Zera, na Shauli.+ 25 Mwana wa Shauli alikuwa Shalumu, mwana wa Shalumu alikuwa Mibsamu, na mwana wa Mibsamu alikuwa Mishma. 26 Na wana wa Mishma walikuwa Hamueli, Zakuri mwana wa Hamueli, na Shimei mwana wa Zakuri. 27 Na Shimei alikuwa na wana 16 na mabinti 6; lakini ndugu zake hawakuwa na wana wengi, na hakuna familia yao yoyote iliyokuwa na wana wengi kama wanaume wa Yuda.+ 28 Waliishi Beer-sheba,+ Molada,+ Hasar-shuali,+ 29 Bilha, Esemu,+ Toladi, 30 Bethueli,+ Horma,+ Siklagi,+ 31 Beth-markabothi, Hasar-susimu,+ Beth-biri, na Shaaraimu. Hayo yalikuwa majiji yao mpaka wakati wa utawala wa Daudi.

32 Waliishi Etamu, Aini, Rimoni, Tokeni, na Ashani,+ majiji matano, 33 pamoja na vijiji vyao vilivyozunguka majiji hayo mpaka Baali. Hizo ndizo orodha za koo zao zilizoandikishwa na mahali walipoishi. 34 Na Meshobabu, Yamleki, Yosha mwana wa Amazia, 35 Yoeli, Yehu mwana wa Yoshibia mwana wa Seraya mwana wa Asieli, 36 na Elioenai, Yaakoba, Yeshohaya, Asaya, Adieli, Yesimieli, Benaya, 37 na Ziza mwana wa Shifi mwana wa Aloni mwana wa Yedaya mwana wa Shimri mwana wa Shemaya; 38 watu hao waliotajwa kwa majina walikuwa wakuu katika koo zao, na idadi ya watu katika nyumba ya mababu zao iliongezeka. 39 Nao walienda kwenye njia ya kuingia Gedori, upande wa mashariki wa bonde, ili kutafuta malisho ya wanyama wao. 40 Hatimaye walipata malisho mazuri yenye majani mengi, na nchi ilikuwa kubwa, yenye utulivu, na amani. Wahamu ndio walioishi katika nchi hiyo awali.+ 41 Watu hao ambao majina yao yameorodheshwa walikuja katika siku za utawala wa Mfalme Hezekia+ wa Yuda, wakayabomoa mahema ya Wahamu na Wameunimu waliokuwa huko. Waliwaangamiza tangu siku hiyo; wakachukua eneo lao kwa sababu lilikuwa na malisho kwa ajili ya wanyama wao.

42 Baadhi ya watu wa kabila la Simeoni, wanaume 500, walienda kwenye Mlima Seiri+ wakiwa na Pelatia, Nearia, Refaya, na Uzieli, wana wa Ishi ambao waliwaongoza. 43 Kisha wakawaangamiza Waamaleki+ waliobaki ambao walikuwa wametoroka, nao wamekuwa wakiishi huko mpaka leo.

5 Hawa ndio wana wa Rubeni,+ mzaliwa wa kwanza wa Israeli. Yeye ndiye aliyekuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa sababu alikichafua* kitanda cha baba yake,+ haki yake ya mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu+ mwana wa Israeli, kwa hiyo hakuandikishwa katika orodha ya ukoo kwamba ana haki ya mzaliwa wa kwanza. 2 Ingawa Yuda+ alikuwa mkuu kuliko ndugu zake na kiongozi alitoka kwake,+ haki ya mzaliwa wa kwanza ilikuwa ya Yosefu. 3 Wana wa Rubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi.+ 4 Wana wa Yoeli walikuwa Shemaya mwanawe, Gogu mwana wa Shemaya, Shimei mwana wa Gogu, 5 Mika mwana wa Shimei, Reaya mwana wa Mika, Baali mwana wa Reaya, 6 na Beera mwana wa Baali, ambaye Mfalme Tilgath-pilneseri+ wa Ashuru alimpeleka uhamishoni; alikuwa mkuu wa Warubeni. 7 Ndugu zake walioandikishwa katika orodha ya koo kulingana na koo zao na kulingana na wazao wao walikuwa, Yeieli, aliyekuwa kiongozi wao, Zekaria, 8 na Bela mwana wa Azazi mwana wa Shema mwana wa Yoeli, aliyeishi Aroeri+ mpaka Nebo na Baal-meoni.+ 9 Naye aliishi upande wa mashariki mpaka mahali ambapo nyika inaanzia kwenye Mto Efrati,+ kwa maana mifugo yao ilikuwa imeongezeka sana katika nchi ya Gileadi.+ 10 Katika siku za utawala wa Sauli, walipigana vita na Wahagri, nao wakawashinda, wakakaa katika mahema yao kwenye eneo lote lililo upande wa mashariki wa Gileadi.

11 Wazao wa Gadi waliishi karibu nao katika nchi ya Bashani mpaka kule Saleka.+ 12 Yoeli ndiye aliyekuwa kiongozi wao, Shafamu alikuwa wa pili, na Yanai na Shafati walikuwa viongozi kule Bashani. 13 Na ndugu zao wa koo* zao walikuwa Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia, na Eberi, jumla ya watu saba. 14 Hao ndio waliokuwa wana wa Abihaili mwana wa Huri mwana wa Yaroa mwana wa Gileadi mwana wa Mikaeli mwana wa Yeshishai mwana wa Yahdo mwana wa Buzi. 15 Ahi mwana wa Abdieli mwana wa Guni alikuwa kiongozi wa ukoo wao.* 16 Waliishi Gileadi,+ kule Bashani+ na katika miji yake, na katika malisho yote ya Sharoni kufikia mipakani mwake. 17 Wote waliandikishwa kulingana na koo zao katika siku za utawala wa Mfalme Yothamu+ wa Yuda na katika siku za utawala wa Mfalme Yeroboamu*+ wa Israeli.

18 Watu wa kabila la Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase walikuwa na mashujaa hodari 44,760 katika jeshi lao waliobeba ngao na mapanga na kujihami kwa pinde,* nao walikuwa wamezoezwa kwa ajili ya vita. 19 Walipigana vita na Wahagri,+ Wayeturi, Wanafishi,+ na Wanodabu. 20 Mungu aliwasaidia kupigana nao, akawatia mikononi mwao Wahagri na wote waliokuwa pamoja nao, kwa maana walimwomba Mungu awasaidie vitani, akasikiliza maombi yao kwa sababu walimtumaini.+ 21 Waliteka nyara mifugo yao—ngamia 50,000, kondoo 250,000, na punda 2,000—na pia watu 100,000. 22 Wengi waliuawa, kwa sababu Mungu wa kweli ndiye aliyepigana vita hivyo.+ Nao waliendelea kuishi katika nchi yao mpaka walipopelekwa uhamishoni.+

23 Wazao wa nusu ya kabila la Manase+ waliishi katika nchi hiyo kuanzia Bashani mpaka Baal-hermoni na Seniri na Mlima Hermoni.+ Walikuwa wengi sana. 24 Hawa ndio waliokuwa viongozi wa koo* zao: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia, na Yahdieli; walikuwa mashujaa hodari, wanaume maarufu, na viongozi wa koo* zao. 25 Lakini hawakutenda kwa uaminifu kumwelekea Mungu wa mababu zao, wakafanya ukahaba na miungu ya mataifa yaliyokuwa nchini,+ mataifa ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza kutoka mbele yao. 26 Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaichochea roho ya Mfalme Pulu wa Ashuru+ (yaani, Mfalme Tilgath-pilneseri+ wa Ashuru) hivi kwamba akawapeleka uhamishoni watu wa kabila la Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, akawapeleka Hala, Habori, Hara, na mto Gozani,+ nao wako huko hadi leo.

6 Wana wa Lawi+ walikuwa Gershoni, Kohathi,+ na Merari.+ 2 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari,+ Hebroni, na Uzieli.+ 3 Watoto* wa Amramu+ walikuwa Haruni,+ Musa,+ na pia Miriamu.+ Na wana wa Haruni walikuwa Nadabu, Abihu,+ Eleazari,+ na Ithamari.+ 4 Eleazari alimzaa Finehasi;+ Finehasi akamzaa Abishua. 5 Abishua akamzaa Buki; Buki akamzaa Uzi. 6 Uzi akamzaa Zeraya; Zeraya akamzaa Merayothi. 7 Merayothi akamzaa Amaria; Amaria akamzaa Ahitubu.+ 8 Ahitubu akamzaa Sadoki;+ Sadoki akamzaa Ahimaazi.+ 9 Ahimaazi akamzaa Azaria; Azaria akamzaa Yohanani. 10 Yohanani akamzaa Azaria. Alitumikia akiwa kuhani katika nyumba ambayo Sulemani alijenga Yerusalemu.

11 Azaria akamzaa Amaria; Amaria akamzaa Ahitubu. 12 Ahitubu akamzaa Sadoki;+ Sadoki akamzaa Shalumu. 13 Shalumu akamzaa Hilkia;+ Hilkia akamzaa Azaria. 14 Azaria akamzaa Seraya;+ Seraya akamzaa Yehosadaki.+ 15 Na Yehosadaki alipelekwa uhamishoni wakati Yehova alipowapeleka watu wa Yuda na Yerusalemu uhamishoni kwa mkono wa Nebukadneza.

16 Wana wa Lawi walikuwa Gershomu,* Kohathi, na Merari. 17 Haya ndiyo majina ya wana wa Gershomu: Libni na Shimei.+ 18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli.+ 19 Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi.

Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi kulingana na mababu zao:+ 20 kutoka katika ukoo wa Gershomu,+ Libni mwana wa Gershomu, Yahathi mwana wa Libni, Zima mwana wa Yahathi, 21 Yoa mwana wa Zima, Ido mwana wa Yoa, Zera mwana wa Ido, Yeatherai mwana wa Zera. 22 Wana* wa Kohathi walikuwa Aminadabu mwanawe, Kora+ mwana wa Aminadabu, Asiri mwana wa Kora, 23 Elkana mwana wa Asiri, Ebiasafu+ mwana wa Elkana, Asiri mwana wa Ebiasafu, 24 Tahathi mwana wa Asiri, Urieli mwana wa Tahathi, Uzia mwana wa Urieli, na Shauli mwana wa Uzia. 25 Wana wa Elkana walikuwa Amasai na Ahimothi. 26 Kwa habari ya Elkana, wana wa Elkana walikuwa Zofai mwanawe, Nahathi mwana wa Zofai, 27 Eliabu mwana wa Nahathi, Yerohamu mwana wa Eliabu, Elkana+ mwana wa Yerohamu. 28 Wana wa Samweli+ walikuwa Yoeli mzaliwa wa kwanza na wa pili Abiya.+ 29 Wana* wa Merari walikuwa Mali,+ Libni mwana wa Mali, Shimei mwana wa Libni, Uza mwana wa Shimei, 30 Shimei mwana wa Uza, Hagia mwana wa Shimei, na Asaya mwana wa Hagia.

31 Hao ndio watu ambao Daudi aliwaweka ili waongoze uimbaji katika nyumba ya Yehova baada ya Sanduku kuletwa likae* humo.+ 32 Ndio waliokuwa na jukumu la kusimamia uimbaji katika hema la ibada, yaani, hema la mkutano mpaka Sulemani alipoijenga nyumba ya Yehova huko Yerusalemu,+ nao walitekeleza utumishi wao kulingana na maagizo waliyopewa.+ 33 Hawa ndio wanaume waliotumikia pamoja na wana wao: kutoka katika ukoo wa Wakohathi, Hemani+ mwimbaji, mwana wa Yoeli+ mwana wa Samweli 34 mwana wa Elkana+ mwana wa Yerohamu mwana wa Elieli mwana wa Toa 35 mwana wa Sufu mwana wa Elkana mwana wa Mahathi mwana wa Amasai 36 mwana wa Elkana mwana wa Yoeli mwana wa Azaria mwana wa Sefania 37 mwana wa Tahathi mwana wa Asiri mwana wa Ebiasafu mwana wa Kora 38 mwana wa Ishari mwana wa Kohathi mwana wa Lawi mwana wa Israeli.

39 Asafu+ ndugu yake alisimama kwenye mkono wake wa kulia; Asafu alikuwa mwana wa Berekia mwana wa Shimea 40 mwana wa Mikaeli mwana wa Baaseya mwana wa Malkiya 41 mwana wa Ethni mwana wa Zera mwana wa Adaya 42 mwana wa Ethani mwana wa Zima mwana wa Shimei 43 mwana wa Yahathi mwana wa Gershomu mwana wa Lawi.

44 Wazao wa Merari+ ndugu zao walikuwa kwenye mkono wake wa kushoto; kulikuwa na Ethani+ mwana wa Kishi mwana wa Abdi mwana wa Maluku 45 mwana wa Hashabia mwana wa Amazia mwana wa Hilkia 46 mwana wa Amzi mwana wa Bani mwana wa Shemeri 47 mwana wa Mali mwana wa Mushi mwana wa Merari mwana wa Lawi.

48 Ndugu zao Walawi waliwekwa* ili watekeleze utumishi wote wa hema la ibada, nyumba ya Mungu wa kweli.+ 49 Haruni na wanawe+ walifukiza moshi wa dhabihu kwenye madhabahu ya dhabihu ya kuteketezwa+ na kwenye madhabahu ya uvumba,+ wakitekeleza majukumu yaliyohusiana na vitu vitakatifu kabisa, ili kufunika dhambi za Waisraeli,+ kulingana na yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu wa kweli alikuwa ameamuru. 50 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Haruni:+ Eleazari mwanawe, Finehasi mwana wa Eleazari,+ Abishua mwana wa Finehasi, 51 Buki mwana wa Abishua, Uzi mwana wa Buki, Zeraya mwana wa Uzi, 52 Merayothi mwana wa Zeraya, Amaria mwana wa Merayothi, Ahitubu+ mwana wa Amaria, 53 Sadoki+ mwana wa Ahitubu, na Ahimaazi mwana wa Sadoki.

54 Haya ndiyo yaliyokuwa makao yao kulingana na kambi zao* katika eneo lao: wazao wa Haruni waliokuwa wa ukoo wa Wakohathi, waliangukiwa na kura ya kwanza, 55 waliwapa Hebroni+ katika nchi ya Yuda, pamoja na malisho yake. 56 Lakini mashamba ya jiji na vijiji vyake walimpa Kalebu+ mwana wa Yefune. 57 Na wazao wa Haruni walipewa majiji haya ya* makimbilio:+ Hebroni,+ na pia Libna+ na malisho yake, Yatiri,+ Eshtemoa na malisho yake,+ 58 Hileni na malisho yake, Debiri+ na malisho yake, 59 Ashani+ na malisho yake, na Beth-shemeshi+ na malisho yake; 60 na kutoka katika kabila la Benjamini, Geba+ na malisho yake, Alemethi na malisho yake, na Anathothi+ na malisho yake. Majiji yao yote kwa ajili ya koo zao yalikuwa majiji 13.+

61 Wakohathi waliobaki walipewa* majiji kumi, kutoka katika ukoo wa kabila, kutoka katika nusu ya kabila, nusu ya kabila la Manase.+

62 Wagershomu kulingana na koo zao walipewa majiji 13 kutoka katika kabila la Isakari, kabila la Asheri, kabila la Naftali, na kabila la Manase kule Bashani.+

63 Wamerari kulingana na koo zao walipewa majiji 12 kutoka katika kabila la Rubeni, kabila la Gadi, na kabila la Zabuloni.+

64 Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi majiji hayo na malisho yake.+ 65 Isitoshe, waliwapa kwa kura majiji hayo kutoka katika kabila la Yuda, kabila la Simeoni, na kabila la Benjamini, ambayo yametajwa majina yao.

66 Baadhi ya koo za Wakohathi zilipewa majiji kutoka katika kabila la Efraimu, yakawa maeneo yao.+ 67 Waliwapa majiji ya* makimbilio, Shekemu+ na malisho yake katika eneo lenye milima la Efraimu, Gezeri+ na malisho yake, 68 Yokmeamu na malisho yake, Beth-horoni+ na malisho yake, 69 Aiyaloni+ na malisho yake, na Gath-rimoni+ na malisho yake; 70 na koo zilizobaki za Wakohathi zilipewa kutoka katika nusu ya kabila la Manase, Aneri na malisho yake na Bileamu na malisho yake.

71 Wagershomu walipewa kutoka katika ukoo wa nusu ya kabila la Manase, Golani+ kule Bashani na malisho yake na Ashtarothi na malisho yake;+ 72 na kutoka katika kabila la Isakari, Kedeshi na malisho yake, Daberathi+ na malisho yake,+ 73 Ramothi na malisho yake, na Anemu na malisho yake; 74 na kutoka katika kabila la Asheri, Mashali na malisho yake, Abdoni na malisho yake,+ 75 Hukoki na malisho yake, na Rehobu+ na malisho yake; 76 na kutoka katika kabila la Naftali, Kedeshi+ kule Galilaya+ na malisho yake, Hamoni na malisho yake, na Kiriathaimu na malisho yake.

77 Wamerari waliobaki walipewa kutoka katika kabila la Zabuloni,+ Rimono na malisho yake, Tabori na malisho yake; 78 na katika eneo la Yordani kule Yeriko, upande wa mashariki wa Yordani, kutoka katika kabila la Rubeni, walipewa Beseri kule nyikani na malisho yake, Yahazi+ na malisho yake, 79 Kedemothi+ na malisho yake, na Mefaathi na malisho yake; 80 na kutoka katika kabila la Gadi, Ramothi kule Gileadi na malisho yake, Mahanaimu+ na malisho yake, 81 Heshboni+ na malisho yake, na Yazeri+ na malisho yake.

7 Sasa wana wa Isakari walikuwa Tola, Pua, Yashubu, na Shimroni+—wana wanne. 2 Na wana wa Tola walikuwa Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu, na Shemueli, viongozi wa koo* zao. Wazao wa Tola walikuwa mashujaa hodari, na idadi yao katika siku za Daudi ilikuwa 22,600. 3 Na wazao* wa Uzi walikuwa Izrahia na wana wa Izrahia: Mikaeli, Obadia, Yoeli, na Ishia—wote watano walikuwa wakuu.* 4 Na pamoja nao, kulingana na wazao wao, kulingana na koo* zao, kulikuwa na wanajeshi 36,000 katika jeshi lao waliokuwa tayari kwa ajili ya vita, kwa maana walikuwa na wake wengi na wana wengi. 5 Na ndugu zao wa koo zote za Isakari walikuwa mashujaa hodari 87,000 walioandikishwa katika orodha ya koo.+

6 Wana wa Benjamini+ walikuwa Bela,+ Bekeri,+ na Yediaeli+—wana watatu. 7 Na wana wa Bela walikuwa Esboni, Uzi, Uzieli, Yerimothi, na Iri—wana watano—viongozi wa koo zao, mashujaa hodari, na 22,034 walikuwa wameandikishwa katika orodha ya ukoo* wao.+ 8 Na wana wa Bekeri walikuwa Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi, Alemethi—hao wote walikuwa wana wa Bekeri. 9 Na wale walioandikishwa katika orodha ya ukoo wao kulingana na wazao wao kuhusiana na viongozi wa koo* zao walikuwa mashujaa hodari 20,200. 10 Na wana wa Yediaeli+ walikuwa Bilhani na wana wa Bilhani walikuwa Yeushi, Benjamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi, na Ahishahari. 11 Hao wote walikuwa wana wa Yediaeli, kulingana na viongozi wa koo za mababu zao, mashujaa hodari 17,200 waliokuwa tayari kujiunga na jeshi kwa ajili ya vita.

12 Washupimu na Wahupimu walikuwa wana wa Ire;+ Wahushimu walikuwa wana wa Aheri.

13 Wana wa Naftali+ walikuwa Yahzieli, Guni, Yezeri, na Shalumu—wazao* wa Bilha.+

14 Wana wa Manase:+ Asrieli, aliyezaliwa na suria wake Msiria. (Suria huyo alimzaa Makiri+ baba ya Gileadi. 15 Makiri alimtafutia mke Hupimu na Shupimu, na dada yake aliitwa Maaka.) Mwana wa pili aliitwa Selofehadi, lakini Selofehadi+ alizaa mabinti.+ 16 Maaka, mke wa Makiri, alizaa mwana na kumwita jina Pereshi; na ndugu yake aliitwa Shereshi; na wanawe walikuwa Ulamu na Rekemu. 17 Na mwana* wa Ulamu alikuwa Bedani. Hao ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase. 18 Na dada yake alikuwa Hamolekethi. Alimzaa Ishodi, Abiezeri, na Mala. 19 Na wana wa Shemida walikuwa Ahiani, Shekemu, Likhi, na Aniamu.

20 Wana wa Efraimu+ walikuwa Shuthela,+ Beredi mwana wa Shuthela, Tahathi mwana wa Beredi, Eleada mwana wa Tahathi, na Tahathi mwana wa Eleada, 21 Zabadi mwana wa Eleada, Shuthela mwana wa Zabadi, Ezeri, na Eleadi. Wanaume wa Gathi+ waliozaliwa nchini waliwaua kwa sababu waliteremka huko kuchukua mifugo yao. 22 Efraimu baba yao aliendelea kuomboleza kwa siku nyingi, na ndugu zake walikuwa wakija kumfariji. 23 Baadaye akalala na mke wake, naye akapata mimba na kuzaa mwana. Lakini akamwita mwana huyo Beria* kwa sababu mama yake alikuwa katika nyumba ya Efraimu wakati wa msiba. 24 Na binti yake alikuwa Sheera, aliyejenga Beth-horoni ya Chini+ na ya Juu+ na Uzen-sheera. 25 Na kulikuwa na Refa mwanawe, Reshefu, Tela mwana wa Reshefu, Tahani mwana wa Tela, 26 Ladani mwana wa Tahani, Amihudi mwana wa Ladani, Elishama mwana wa Amihudi, 27 Nuni mwana wa Elishama, na Yoshua*+ mwana wa Nuni.

28 Walimiliki na kuishi Betheli+ na katika miji yake, na upande wa mashariki, Naarani, na upande wa magharibi, Gezeri na miji yake, na Shekemu* na miji yake, mpaka Aya na miji yake; 29 na kando ya wazao wa Manase, walimiliki Beth-sheani+ na miji yake, Taanaki+ na miji yake, Megido+ na miji yake, na Dori+ na miji yake. Wazao wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi humo.

30 Wana wa Asheri walikuwa Imna, Ishva, Ishvi, na Beria,+ na dada yao aliitwa Sera.+ 31 Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba ya Birzaithi. 32 Heberi akamzaa Yafleti, Shomeri, na Hothamu, na Shua dada yao. 33 Wana wa Yafleti walikuwa Pasaki, Bimhali, na Ashvathi. Hao ndio waliokuwa wana wa Yafleti. 34 Wana wa Shemeri* walikuwa Ahi, Roga, Yehuba, na Aramu. 35 Wana wa Helemu* ndugu yake walikuwa Sofa, Imna, Sheleshi, na Amali. 36 Wana wa Sofa walikuwa Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra, 37 Beseri, Hodi, Shama, Shilsha, Ithrani, na Beera. 38 Wana wa Yetheri walikuwa Yefune, Pispa, na Ara. 39 Wana wa Ula walikuwa Ara, Hanieli, na Risia. 40 Hao wote walikuwa wana wa Asheri, viongozi wa koo* zao, watu wa pekee, mashujaa hodari, viongozi wa wakuu; na wanaume wao walioandikishwa jeshini kwa ajili ya vita katika orodha ya koo+ walikuwa 26,000.+

8 Benjamini+ alimzaa Bela+ mzaliwa wake wa kwanza, wa pili Ashbeli,+ wa tatu Ahara, 2 wa nne Noha, na wa tano Rafa. 3 Wana wa Bela walikuwa Adari, Gera,+ Abihudi, 4 Abishua, Naamani, Ahoa, 5 Gera, Shefufani, na Huramu. 6 Hawa walikuwa wana wa Ehudi, viongozi wa koo* za wakaaji wa Geba,+ waliopelekwa uhamishoni kule Manahathi: 7 Naamani, Ahiya, na Gera—ndiye aliyewapeleka uhamishoni, naye alimzaa Uza na Ahihudi. 8 Shaharaimu aliwazaa watoto katika eneo* la Moabu baada ya kuwafukuza Wamoabu. Wake zake walikuwa Hushimu na Baara.* 9 Na kupitia Hodeshi mke wake, alimzaa Yobabu, Sibia, Mesha, Malkamu, 10 Yeuzi, Sakia, na Mirma. Hao walikuwa wanawe, viongozi wa koo.*

11 Na kupitia Hushimu alimzaa Abitubu na Elpaali. 12 Na wana wa Elpaali walikuwa Eberi, Mishamu, Shemedi (aliyejenga Ono+ na Lodi+ pamoja na miji yake), 13 Beria, na Shema. Hao walikuwa viongozi wa koo* za wakaaji wa Aiyaloni.+ Hao ndio waliowafukuza wakaaji wa Gathi. 14 Na kulikuwa na Ahio, Shashaki, Yeremothi, 15 Zebadia, Aradi, Ederi, 16 Mikaeli, Ishpa, Yoha, wana wa Beria; 17 na Zebadia, Meshulamu, Hizki, Heberi, 18 Ishmerai, Izlia, Yobabu, wana wa Elpaali; 19 na Yakimu, Zikri, Zabdi, 20 Elienai, Zilethai, Elieli, 21 Adaya, Beraya, Shimrathi, wana wa Shimei; 22 na Ishpani, Eberi, Elieli, 23 Abdoni, Zikri, Hanani, 24 Hanania, Elamu, Anthothiya, 25 Ifdeya, Penueli, wana wa Shashaki; 26 na Shamsherai, Sheharia, Athalia, 27 Yaareshia, Eliya, Zikri, wana wa Yerohamu. 28 Hao walikuwa viongozi wa koo* zao kulingana na wazao wao. Viongozi hao waliishi Yerusalemu.

29 Yeieli, baba ya Gibeoni, aliishi Gibeoni.+ Mke wake aliitwa Maaka.+ 30 Na mwana wake mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, kisha Suri, Kishi, Baali, Nadabu, 31 Gedori, Ahio, na Zekeri. 32 Miklothi alimzaa Shimea. Na wote waliishi karibu na ndugu zao kule Yerusalemu, pamoja na ndugu zao wengine.

33 Neri+ alimzaa Kishi; Kishi akamzaa Sauli;+ Sauli akamzaa Yonathani,+ Malki-shua,+ Abinadabu,+ na Eshbaali.*+ 34 Na mwana wa Yonathani aliitwa Merib-baali.*+ Merib-baali akamzaa Mika.+ 35 Na wana wa Mika walikuwa Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi. 36 Ahazi akamzaa Yehoada; Yehoada akamzaa Alemethi, Azmavethi, na Zimri. Zimri akamzaa Mosa. 37 Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Rafa, Rafa akamzaa Eleasa, Eleasa akamzaa Aseli. 38 Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia, na Hanani. Hao wote ndio waliokuwa wana wa Aseli. 39 Na wana wa Esheki ndugu yake walikuwa Ulamu mzaliwa wake wa kwanza, wa pili Yeushi, na wa tatu Elifeleti. 40 Na wana wa Ulamu walikuwa mashujaa hodari walioweza kushika* upinde, nao walikuwa na wana wengi na wajukuu wengi, jumla yao 150. Hao wote walikuwa wazao wa Benjamini.

9 Waisraeli wote waliandikishwa kulingana na ukoo wao, na koo hizo zimeandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli. Na watu wa Yuda walipelekwa uhamishoni kule Babiloni kwa sababu hawakuwa waaminifu.+ 2 Baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, na watumishi wa hekaluni*+ walikuwa wakaaji wa kwanza kurudi katika miliki yao kwenye majiji yao. 3 Na baadhi ya wazao wa Yuda,+ wa Benjamini,+ wa Efraimu, na wa Manase walioishi Yerusalemu walikuwa: 4 Uthai mwana wa Amihudi mwana wa Omri mwana wa Imri mwana wa Bani, kutoka kwa wazao wa Perezi+ mwana wa Yuda. 5 Na kutoka kwa wazao wa Washilo, Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe. 6 Na wana wa Zera,+ Yeueli na ndugu zao 690.

7 Na kutoka kwa wazao wa Benjamini, Salu mwana wa Meshulamu mwana wa Hodavia mwana wa Hasenua, 8 Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi mwana wa Mikri, na Meshulamu mwana wa Shefatia mwana wa Reueli mwana wa Ibniya. 9 Na ndugu zao kulingana na ukoo wao walikuwa 956. Wanaume hao wote walikuwa viongozi wa koo zao.*

10 Na kutoka kwa makuhani, kulikuwa na Yedaya, Yehoyaribu, Yakini,+ 11 Azaria mwana wa Hilkia mwana wa Meshulamu mwana wa Sadoki mwana wa Merayothi mwana wa Ahitubu, kiongozi wa nyumba ya* Mungu wa kweli, 12 Adaya mwana wa Yerohamu mwana wa Pashuri mwana wa Malkiya, Maasai mwana wa Adieli mwana wa Yahzera mwana wa Meshulamu mwana wa Meshilemithi mwana wa Imeri, 13 na ndugu zao, viongozi wa koo* zao, mashujaa 1,760, wanaume wenye uwezo waliokuwa tayari kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli.

14 Na kutoka kwa Walawi, kulikuwa na Shemaya+ mwana wa Hashubu mwana wa Azrikamu mwana wa Hashabia kutoka kwa wazao wa Merari; 15 na Bakbakari, Hereshi, Galali, Matania mwana wa Mika mwana wa Zikri mwana wa Asafu, 16 Obadia mwana wa Shemaya mwana wa Galali mwana wa Yeduthuni, na Berekia mwana wa Asa mwana wa Elkana, aliyekuwa akiishi katika vijiji vya Wanetofa.+

17 Walinzi wa malango+ walikuwa Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani, na ndugu yao Shalumu alikuwa kiongozi, 18 na kufikia wakati huo alikuwa katika lango la mfalme upande wa mashariki.+ Hao walikuwa walinzi wa malango wa kambi za Walawi. 19 Na Shalumu mwana wa Kore mwana wa Ebiasafu mwana wa Kora, na ndugu zake wa ukoo wake,* Wakora, walisimamia majukumu ya utumishi wa walinzi wa milango ya hema, na baba zao walikuwa wakisimamia kambi ya Yehova wakiwa walinzi wa njia ya kuingilia. 20 Finehasi+ mwana wa Eleazari+ ndiye aliyekuwa kiongozi wao zamani; Yehova alikuwa pamoja naye. 21 Zekaria+ mwana wa Meshelemia alikuwa mlinzi wa lango la kuingia katika hema la mkutano.

22 Wote waliochaguliwa kuwa walinzi kwenye vizingiti walikuwa 212. Waliishi katika vijiji vyao kulingana na orodha ya ukoo wao.+ Daudi na Samweli yule mwonaji+ waliwaweka katika wadhifa wa kuaminiwa. 23 Watu hao pamoja na wana wao walisimamia utumishi wa ulinzi wa malango ya nyumba ya Yehova,+ nyumba ya hema. 24 Walinzi wa malango walikuwa pande zote nne—mashariki, magharibi, kaskazini, na kusini.+ 25 Mara kwa mara, ndugu zao walipaswa kuja kwa siku saba kutoka katika vijiji vyao ili kutumikia pamoja nao. 26 Kulikuwa na walinzi wakuu* wanne waliowekwa katika wadhifa huo wa kuaminiwa. Walikuwa Walawi, nao walisimamia vyumba* na hazina za nyumba ya Mungu wa kweli.+ 27 Walikuwa wakikesha usiku kucha katika vituo vyao kuzunguka nyumba yote ya Mungu wa kweli, kwa maana walishughulikia utumishi wa ulinzi na kutunza ufunguo, nao walikuwa wakifungua nyumba hiyo asubuhi baada ya asubuhi.

28 Baadhi yao walisimamia vyombo+ vya utumishi; walikuwa wakivihesabu vilipokuwa vikiingizwa ndani na kuvihesabu vilipotolewa nje. 29 Baadhi yao waliwekwa kusimamia vyombo, kusimamia vyombo vyote vitakatifu,+ na kusimamia unga laini,+ divai,+ mafuta,+ ubani,+ na mafuta ya zeri.+ 30 Baadhi ya wana wa makuhani walichanganya manukato ya mafuta ya zeri. 31 Na Matithia mmoja wa Walawi, aliyekuwa mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, Mkora, alipewa wadhifa wa kuaminiwa wa kusimamia vitu vilivyookwa kwenye vikaangio.+ 32 Baadhi ya ndugu zao Wakohathi walisimamia mikate ya tabaka,*+ waliitayarisha kila sabato.+

33 Hao walikuwa waimbaji, viongozi wa koo* za Walawi katika vyumba* vya nyumba hiyo, wale ambao hawakupewa kazi nyingine; kwa maana usiku na mchana walikuwa na wajibu wa kushika zamu zao. 34 Hao walikuwa viongozi wa koo* za Walawi kulingana na ukoo wao, viongozi. Waliishi Yerusalemu.

35 Yeieli, baba ya Gibeoni, aliishi Gibeoni.+ Mke wake aliitwa Maaka. 36 Na mwana wake mzaliwa wa kwanza aliitwa Abdoni, kisha Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu, 37 Gedori, Ahio, Zekaria, na Miklothi. 38 Miklothi alimzaa Shimeamu. Na wote waliishi karibu na ndugu zao kule Yerusalemu, pamoja na ndugu zao wengine. 39 Neri+ akamzaa Kishi; Kishi akamzaa Sauli;+ Sauli akamzaa Yonathani,+ Malki-shua,+ Abinadabu,+ na Eshbaali. 40 Na mwana wa Yonathani aliitwa Merib-baali.+ Merib-baali akamzaa Mika.+ 41 Na wana wa Mika walikuwa Pithoni, Meleki, Tahrea, na Ahazi. 42 Ahazi akamzaa Yara; Yara akamzaa Alemethi, Azmavethi, na Zimri. Zimri akamzaa Mosa. 43 Mosa akamzaa Binea na Refaya mwanawe, Refaya akamzaa Eleasa, Eleasa akamzaa Aseli. 44 Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia, na Hanani. Hao ndio waliokuwa wana wa Aseli.

10 Sasa Wafilisti walikuwa wakipigana na Waisraeli. Na wanaume wa Israeli wakawakimbia Wafilisti, na wengi wakauawa kwenye Mlima Gilboa.+ 2 Wafilisti wakamkaribia sana Sauli na wanawe, nao wakamuua Yonathani, Abinadabu, na Malki-shua,+ wana wa Sauli. 3 Vita vikawa vikali sana dhidi ya Sauli, na wapiga mishale wakampata na kumjeruhi.+ 4 Ndipo Sauli akamwambia mtu aliyembebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nao, ili watu hawa wasiotahiriwa wasije kunitendea kikatili.”*+ Lakini mtu aliyembebea silaha hakutaka kufanya hivyo, kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akachukua upanga na kuuangukia.+ 5 Mtu aliyembebea silaha alipoona kwamba Sauli amekufa, yeye pia akauangukia upanga wake mwenyewe na kufa. 6 Basi Sauli na wanawe watatu wakafa, na watu wote wa nyumba yake wakafa pamoja.+ 7 Watu wote wa Israeli waliokuwa bondeni* walipoona kwamba kila mtu amekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaanza kuyaacha majiji yao na kukimbia; kisha Wafilisti wakaja na kukaa humo.

8 Siku iliyofuata, Wafilisti walipokuja kuwavua waliouawa vitu walivyokuwa navyo, walimkuta Sauli na wanawe wakiwa wameanguka kwenye Mlima Gilboa.+ 9 Basi wakamvua mavazi yake, wakamkata kichwa na kuchukua silaha zake, nao wakatuma ujumbe kotekote katika nchi ya Wafilisti ili habari hizo zienezwe kwa sanamu+ zao na watu. 10 Kisha wakaweka silaha zake katika nyumba ya* mungu wao na kulitundika fuvu lake kwenye nyumba ya Dagoni.+

11 Wakaaji wote wa Yabeshi+ kule Gileadi waliposikia mambo yote ambayo Wafilisti walikuwa wamemtendea Sauli,+ 12 mashujaa wote wakaondoka na kubeba maiti ya Sauli na maiti za wanawe. Wakawaleta Yabeshi na kuzika mifupa yao chini ya mti mkubwa kule Yabeshi,+ nao wakafunga kwa siku saba.

13 Kwa hiyo Sauli alikufa kwa sababu hakuwa mwaminifu kwa Yehova kwa maana hakutii neno la Yehova,+ na pia kwa sababu alitafuta ushauri kutoka kwa mtu aliyewasiliana na roho+ 14 badala ya kutafuta ushauri kutoka kwa Yehova. Kwa hiyo Akamuua na kumpa Daudi mwana wa Yese ufalme.+

11 Baada ya muda Waisraeli wote wakakusanyika kwa Daudi kule Hebroni+ na kusema: “Tazama! Sisi ni mfupa wako na nyama yako.*+ 2 Zamani, Sauli alipokuwa mfalme, ni wewe uliyewaongoza Waisraeli vitani.*+ Na Yehova Mungu wako alikuambia hivi: ‘Utawachunga watu wangu Waisraeli, nawe utakuwa kiongozi wa watu wangu Waisraeli.’”+ 3 Basi wazee wote wa Israeli wakaja kwa mfalme huko Hebroni, na Daudi akafanya agano nao huko Hebroni mbele za Yehova. Kisha wakamtia mafuta Daudi awe mfalme wa Israeli,+ kulingana na neno la Yehova kupitia Samweli.+

4 Baadaye Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu, yaani, Yebusi,+ ambako Wayebusi+ walikuwa wakiishi. 5 Wakaaji wa Yebusi walimdhihaki Daudi wakisema: “Hutaingia humu kamwe!”+ Hata hivyo, Daudi aliiteka ngome ya Sayuni,+ ambayo sasa ni Jiji la Daudi.+ 6 Kwa hiyo Daudi akasema: “Yeyote atakayekuwa wa kwanza kuwashambulia Wayebusi atakuwa kiongozi* na mkuu.” Basi Yoabu+ mwana wa Seruya akawa wa kwanza kupanda huko kuwashambulia, akawa kiongozi. 7 Kisha Daudi akaanza kukaa katika ngome hiyo. Ndiyo sababu waliiita Jiji la Daudi. 8 Akaanza kujenga jiji hilo pande zote, kuanzia kwenye Kilima* mpaka kwenye maeneo yanayozunguka, na Yoabu akajenga upya sehemu zilizobaki za jiji hilo. 9 Kwa hiyo Daudi akawa mkuu zaidi na zaidi,+ na Yehova wa majeshi alikuwa pamoja naye.

10 Sasa hawa ndio viongozi wa mashujaa hodari wa Daudi, waliomuunga mkono kwa dhati katika utawala wake, pamoja na Waisraeli wote, ili wamweke kuwa mfalme kulingana na neno alilosema Yehova kuhusu Israeli.+ 11 Hii ndiyo orodha ya mashujaa hodari wa Daudi: Yashobeamu+ mwana wa Mhakmoni, kiongozi wa wale watatu.+ Wakati mmoja, alitumia mkuki wake kuwaua watu 300.+ 12 Aliyemfuata ni Eleazari+ mwana wa Dodo mwana wa Ahohi.+ Alikuwa miongoni mwa mashujaa hao watatu hodari. 13 Alikuwa na Daudi kule Pas-damimu,+ ambako Wafilisti walikuwa wamekusanyika kwa ajili ya vita. Basi palikuwa na shamba lililojaa shayiri, na watu walikuwa wamekimbia kwa sababu ya Wafilisti. 14 Lakini alisimama katikati ya shamba hilo na kuwazuia Wafilisti wasiingie humo, naye aliendelea kuwaua Wafilisti, hivi kwamba Yehova akawapa ushindi* mkubwa.+

15 Viongozi watatu kati ya wale viongozi 30 walishuka mwambani kwa Daudi, katika pango la Adulamu,+ wakati jeshi la Wafilisti lilipokuwa limepiga kambi katika Bonde la* Refaimu.+ 16 Wakati huo Daudi alikuwa ndani ya ngome, na kikosi cha wanajeshi Wafilisti kilikuwa Bethlehemu. 17 Kisha Daudi akasema alichotamani: “Laiti ningekunywa maji kutoka katika tangi lililo karibu na lango la Bethlehemu!”+ 18 Ndipo wale mashujaa watatu wakaingia kwa nguvu katika kambi ya Wafilisti, wakateka maji kutoka katika tangi hilo lililo karibu na lango la Bethlehemu na kumletea Daudi; lakini Daudi akakataa kuyanywa, akayamwaga mbele za Yehova. 19 Akasema: “Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia, kulingana na maoni ya Mungu wangu, kufanya hivyo! Je, ninywe damu ya wanaume hawa waliohatarisha uhai wao?”*+ Kwa maana walihatarisha uhai wao kwenda kuyaleta. Basi akakataa kuyanywa. Hayo ndiyo mambo waliyotenda mashujaa wake watatu hodari.

20 Abishai+ ndugu ya Yoabu+ akawa kiongozi wa wengine watatu; alitumia mkuki wake kuwaua watu 300, naye alikuwa maarufu kama wale watatu.+ 21 Ingawa alikuwa mashuhuri zaidi kuliko wale wengine watatu, na alikuwa kiongozi wao, hakuwa shujaa kama wale watatu wa kwanza.

22 Benaya+ mwana wa Yehoyada alikuwa mwanamume jasiri* aliyefanya mambo mengi ya kishujaa kule Kabzeeli.+ Aliwaua wana wawili wa Arieli wa Moabu, naye aliingia ndani ya shimo la maji siku ya theluji na kumuua simba.+ 23 Alimuua pia mwanamume Mmisri aliyekuwa mkubwa isivyo kawaida—mwenye urefu wa mikono mitano.*+ Ingawa Mmisri huyo alikuwa na mkuki mkononi kama mti wa wafumaji wa nguo,+ Benaya alikabiliana naye akiwa na fimbo, akamnyang’anya Mmisri huyo mkuki kutoka mkononi mwake na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.+ 24 Benaya mwana wa Yehoyada alifanya mambo hayo, naye alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu hodari. 25 Ingawa alikuwa mashuhuri hata kuliko wale 30, hakuwa shujaa kama wale watatu.+ Lakini Daudi alimweka kuwa kiongozi wa walinzi wake binafsi.

26 Mashujaa hodari jeshini walikuwa Asaheli+ ndugu ya Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo wa Bethlehemu,+ 27 Shamothi Mharori, Helezi Mpeloni, 28 Ira+ mwana wa Ikeshi Mtekoa, Abiezeri+ Mwanathothi, 29 Sibekai+ Mhusha, Ilai Mwahohi, 30 Maharai+ Mnetofa, Heledi+ mwana wa Baana Mnetofa, 31 Ithai mwana wa Ribai wa jiji la Gibea la Wabenjamini,+ Benaya Mpirathoni, 32 Hurai kutoka katika makorongo* ya Gaashi,+ Abieli Mwarbathi, 33 Azmavethi Mbaharumu, Eliaba Mshaalboni, 34 wana wa Hashemu Mgizoni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari, 35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifali mwana wa Uru, 36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni, 37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai, 38 Yoeli ndugu ya Nathani, Mibhari mwana wa Hagri, 39 Seleki Mwamoni, Naharai Mberothi, aliyembebea silaha Yoabu mwana wa Seruya; 40 Ira Mwithri, Garebu Mwithri, 41 Uria+ Mhiti, Zabadi mwana wa Alai, 42 Adina mwana wa Shiza Mrubeni, kiongozi wa Warubeni, aliyekuwa na watu 30; 43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithini, 44 Uziya Mwashtarothi, Shama na Yeieli, wana wa Hothamu Mwaroeri; 45 Yediaeli mwana wa Shimri, na Yoha ndugu yake, Mtisi; 46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, na Ithma Mmoabu; 47 Elieli, Obedi, na Yaasieli Mmesoba.

12 Hao ndio wanaume walioenda kumwona Daudi kule Siklagi+ wakati ambapo hakuwa na uhuru wa kutembea popote kwa sababu ya Sauli+ mwana wa Kishi, nao walikuwa miongoni mwa mashujaa hodari waliomuunga mkono vitani.+ 2 Walijihami kwa upinde, nao waliweza kutumia mkono wa kulia na mkono wa kushoto+ kurusha mawe kwa kombeo+ au kupiga mishale kwa upinde. Walikuwa wazao wa ndugu za Sauli, kutoka Benjamini.+ 3 Kiongozi wao alikuwa Ahiezeri, pamoja na Yoashi, wote wawili walikuwa wana wa Shemaa Mgibea;+ Yezieli na Peleti wana wa Azmavethi,+ Baraka, Yehu Mwanathothi, 4 Ishmaya Mgibeoni,+ shujaa hodari miongoni mwa wale 30+ na kiongozi wa wale 30; pia Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi Mgedera, 5 Eluzai, Yerimothi, Bealia, Shemaria, Shefatia Mharifu, 6 Elkana, Ishia, Azareli, Yoezeri, na Yashobeamu, Wakora;+ 7 na Yoela na Zebadia wana wa Yerohamu wa Gedori.

8 Baadhi ya Wagadi walienda kujiunga na Daudi katika ngome kule nyikani;+ walikuwa mashujaa hodari, wanajeshi waliozoezwa kwa ajili ya vita, waliosimama tayari wakiwa na ngao kubwa na mkuki, nao walikuwa na nyuso kama za simba na walikimbia mbio sana* kama swala milimani. 9 Ezeri ndiye aliyekuwa kiongozi wao, wa pili Obadia, wa tatu Eliabu, 10 wa nne Mishmana, wa tano Yeremia, 11 wa sita Atai, wa saba Elieli, 12 wa nane Yohanani, wa tisa Elzabadi, 13 wa kumi Yeremia, wa kumi na moja Makbanai. 14 Hao walikuwa wazao wa Gadi,+ viongozi wa jeshi. Mwenye uwezo mdogo zaidi angeweza kuwashinda watu 100, na mwenye uwezo mkubwa zaidi angeweza kuwashinda watu 1,000.+ 15 Hao ndio wanaume waliovuka Yordani katika mwezi wa kwanza wakati kingo za mto huo zilipokuwa zimefurika, nao waliwafukuza watu wote waliokuwa wakiishi mabondeni, upande wa mashariki na wa magharibi.

16 Baadhi ya wanaume wa Benjamini na Yuda walikuja pia kwa Daudi katika ngome yake.+ 17 Kisha Daudi akatoka na kuwaambia: “Ikiwa mmekuja kwangu kwa amani ili kunisaidia, moyo wangu utaungana nanyi. Lakini ikiwa mmekuja kunisaliti kwa maadui wangu wakati mikono yangu haijatenda kosa lolote, Mungu wa mababu zetu na aone hilo na kuhukumu.”+ 18 Kisha roho ikamjia* Amasai,+ kiongozi wa wale 30, akasema:

“Sisi ni wako, Ee Daudi, nasi tuko pamoja nawe, Ee mwana wa Yese.+

Amani, amani iwe yako, na amani iwe na yule anayekusaidia,

Kwa maana Mungu wako anakusaidia.”+

Basi Daudi akawakaribisha na kuwaweka wawe miongoni mwa viongozi wa wanajeshi.

19 Baadhi ya watu wa kabila la Manase walitoroka pia na kujiunga na Daudi alipokuja pamoja na Wafilisti kupigana na Sauli; lakini hakuwasaidia Wafilisti, kwa sababu baada ya watawala wa Wafilisti+ kushauriana, walimfukuza wakisema: “Atatoroka na kwenda kwa Sauli bwana wake, na jambo hilo litahatarisha vichwa vyetu.”+ 20 Alipoenda Siklagi,+ watu hawa wa kabila la Manase walitoroka na kujiunga naye: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu, na Zilethai, viongozi wa maelfu katika kabila la Manase.+ 21 Walimsaidia Daudi kupigana na kundi la wavamizi, kwa sababu wote walikuwa wanaume hodari walio jasiri,+ nao wakawa wakuu katika jeshi lake. 22 Siku baada ya siku watu waliendelea kuja kumsaidia Daudi+ mpaka kambi yake ikawa kubwa kama kambi ya Mungu.+

23 Hii ndiyo idadi ya viongozi wa wale waliojihami kwa ajili ya vita ambao walijiunga na Daudi kule Hebroni+ ili kumpa utawala wa Sauli kulingana na agizo la Yehova.+ 24 Wanaume wa Yuda waliobeba ngao kubwa na mkuki walikuwa 6,800, waliojihami kwa ajili ya vita. 25 Kutoka kwa Wasimeoni, kulikuwa na wanajeshi 7,100, wanaume jasiri na hodari.

26 Kutoka kwa Walawi, 4,600. 27 Yehoyada+ alikuwa kiongozi wa wana wa Haruni,+ naye alikuwa pamoja na watu 3,700, 28 na pia Sadoki,+ kijana aliyekuwa hodari na jasiri, pamoja na wakuu 22 kutoka katika ukoo wake.*

29 Kutoka kwa Wabenjamini, ndugu za Sauli,+ kulikuwa na wanaume 3,000, ambao wengi wao, hapo awali, walikuwa wakilinda masilahi ya nyumba ya Sauli. 30 Kutoka kwa Waefraimu, kulikuwa na wanaume hodari 20,800, waliokuwa jasiri na maarufu katika koo zao.*

31 Na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase, kulikuwa na wanaume 18,000 waliotajwa kwa majina ili waje kumweka Daudi kuwa mfalme. 32 Kutoka kwa kabila la Isakari, kulikuwa na viongozi 200 ambao walielewa nyakati na kujua yale ambayo Waisraeli walipaswa kufanya, na ndugu zao wote walikuwa chini ya uongozi wao. 33 Kutoka kwa Zabuloni, kulikuwa na wanaume 50,000 walioweza kutumikia jeshini, waliojipanga kivita wakiwa na silaha zote za vita, wote walijiunga na Daudi kwa ushikamanifu usiogawanyika.* 34 Kutoka kwa Naftali, kulikuwa na wakuu 1,000, nao walikuwa pamoja na wanaume 37,000 wenye ngao kubwa na mkuki. 35 Kutoka kwa Wadani, wale waliojipanga kivita walikuwa 28,600. 36 Na kutoka kwa Asheri, wale walioweza kutumikia jeshini na kujipanga kivita walikuwa 40,000.

37 Kutoka ng’ambo ya Yordani,+ kutoka kwa Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase, kulikuwa na wanajeshi 120,000 waliokuwa na aina zote za silaha za vita. 38 Hao wote walikuwa wanaume wa vita, walioungana pamoja vitani; walikuja Hebroni kwa moyo kamili ili kumweka Daudi kuwa mfalme wa Israeli yote, na pia Waisraeli wengine wote walikuwa na nia moja ya* kumweka Daudi kuwa mfalme.+ 39 Nao walikaa huko pamoja na Daudi kwa siku tatu, wakila na kunywa, kwa kuwa ndugu zao walikuwa wamefanya matayarisho kwa ajili yao. 40 Pia majirani wao, na hata wale waliokuwa mbali kufikia Isakari, Zabuloni, na Naftali, walikuwa wakileta vyakula kwa punda, ngamia, nyumbu, na ng’ombe—walileta unga, keki za tini zilizoshinikizwa na keki za zabibu kavu, divai, mafuta, na ng’ombe na kondoo wengi sana, kwa maana watu walishangilia nchini Israeli.

13 Daudi alishauriana na wakuu wa maelfu na wa mamia na kila kiongozi.+ 2 Kisha Daudi akaliambia kutaniko lote la Waisraeli: “Mkiona ni vema na ikiwa ni jambo linalokubalika kwa Yehova Mungu wetu, acheni tutume ujumbe kwa ndugu zetu waliobaki katika maeneo yote ya Israeli na pia kwa makuhani na Walawi katika majiji yao+ yenye malisho waje kuungana nasi. 3 Na acheni tulirudishe Sanduku+ la Mungu wetu.” Kwa maana hawakuwa wamelitunza katika siku za Sauli.+ 4 Kutaniko lote likakubali kufanya hivyo, kwa maana watu wote waliliona kuwa jambo jema. 5 Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia mto wa Misri* mpaka Lebo-Hamathi,*+ ili walete Sanduku la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu.+

6 Daudi na Waisraeli wote wakapanda kwenda Baala,+ mpaka Kiriath-yearimu, jiji la Yuda, ili kuleta kutoka huko Sanduku la Mungu wa kweli, Yehova, anayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi,+ mahali ambapo watu husali katika jina lake. 7 Hata hivyo, walilitoa Sanduku la Mungu wa kweli katika nyumba ya Abinadabu na kuliweka juu ya gari jipya la kukokotwa,+ na Uza na Ahio walikuwa wakiliongoza gari hilo.+ 8 Daudi na Waisraeli wote walikuwa wakisherehekea mbele za Mungu wa kweli kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, vinanda vinginevyo, matari,+ matoazi,+ na tarumbeta.+ 9 Lakini walipofika kwenye uwanja wa kupuria wa Kidoni, Uza aliunyoosha mkono wake haraka na kulikamata Sanduku hilo, kwa sababu ng’ombe walikuwa karibu kuliangusha. 10 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Uza, Naye akamuua kwa sababu aliunyoosha mkono wake na kulikamata Sanduku+ hilo, naye akafa hapo mbele za Mungu.+ 11 Lakini Daudi akakasirika kwa sababu hasira kali ya Yehova iliwaka dhidi ya Uza; na tangu siku hiyo mahali hapo panaitwa Peres-uza.*

12 Basi Daudi akamwogopa Mungu wa kweli siku hiyo na kusema: “Ninawezaje kulileta kwangu Sanduku la Mungu wa kweli?”+ 13 Daudi hakulileta Sanduku hilo mahali alipokuwa katika Jiji la Daudi, lakini aliagiza lipelekwe katika nyumba ya Obed-edomu, Mgathi. 14 Sanduku la Mungu wa kweli lilikaa pamoja na watu wa nyumba ya Obed-edomu, likabaki katika nyumba yake kwa miezi mitatu, na Yehova akaendelea kuwabariki watu wa nyumba ya Obed-edomu na vitu vyote alivyokuwa navyo.+

14 Mfalme Hiramu+ wa Tiro aliwatuma wajumbe kwa Daudi, pamoja na mbao za mierezi, waashi,* na maseremala ili wamjengee Daudi nyumba.*+ 2 Na Daudi alijua kwamba Yehova alikuwa amemwimarisha kabisa kuwa mfalme wa Israeli,+ kwa maana ufalme wake ulikuwa umekwezwa sana kwa ajili ya watu Wake Waisraeli.+

3 Daudi alichukua wake+ zaidi huko Yerusalemu, na Daudi akazaa wana na mabinti zaidi.+ 4 Haya ndiyo majina ya watoto wake waliozaliwa Yerusalemu:+ Shamua, Shobabu, Nathani,+ Sulemani,+ 5 Ibhari, Elishua, Elpeleti, 6 Noga, Nefegi, Yafia, 7 Elishama, Beeliada, na Elifeleti.

8 Wafilisti waliposikia kwamba Daudi alikuwa ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Waisraeli wote,+ Wafilisti wote wakapanda kuja kumtafuta Daudi.+ Daudi aliposikia jambo hilo, akaenda kukabiliana nao. 9 Kisha Wafilisti wakaja na kuvamia tena na tena katika Bonde la* Refaimu.+ 10 Daudi akamuuliza Mungu: “Je, nipande kwenda kuwashambulia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Ndipo Yehova akamwambia: “Panda uende, nami hakika nitawatia mikononi mwako.”+ 11 Basi Daudi akapanda kwenda Baal-perasimu,+ naye akawaua huko. Ndipo Daudi akasema: “Mungu wa kweli amewapasua na kuwapita maadui wangu kwa mkono wangu, kama ufa uliopasuliwa na maji.” Ndiyo sababu walipaita mahali hapo Baal-perasimu.* 12 Wafilisti wakaacha miungu yao hapo, na Daudi alipotoa amri, miungu hiyo iliteketezwa motoni.+

13 Baadaye Wafilisti wakaja tena na kuvamia bondeni.*+ 14 Daudi akamwomba Mungu ushauri tena, lakini Mungu wa kweli akamwambia: “Usipande moja kwa moja na kuwafuatia. Badala yake, zunguka nyuma yao, uwashambulie mbele ya vichaka vya mibaka.+ 15 Na utakaposikia sauti ya watu wakipiga mwendo juu ya vichaka vya mibaka, washambulie, kwa sababu mimi Mungu wa kweli nitakuwa nimetangulia mbele yako ili kuliua jeshi la Wafilisti.”+ 16 Basi Daudi akafanya kama Mungu wa kweli alivyomwamuru,+ wakaliua jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni mpaka Gezeri.+ 17 Umaarufu wa Daudi ukaenea katika nchi zote, na Yehova akayafanya mataifa yote yamwogope Daudi.+

15 Naye akaendelea kujijengea nyumba katika Jiji la Daudi, akatayarisha mahali kwa ajili ya Sanduku la Mungu wa kweli na kupiga hema kwa ajili yake.+ 2 Huo ndio wakati ambao Daudi alisema: “Hakuna mtu yeyote anayepaswa kubeba Sanduku la Mungu wa kweli isipokuwa Walawi, kwa maana Yehova amewachagua ili walibebe Sanduku la Yehova na kumhudumia sikuzote.”+ 3 Kisha Daudi akawakusanya Waisraeli wote Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Yehova na kulileta mahali alipotayarisha kwa ajili yake.+

4 Daudi akawakusanya wazao wa Haruni+ na Walawi:+ 5 kutoka kwa Wakohathi, mkuu Urieli na ndugu zake 120; 6 kutoka kwa Wamerari, mkuu Asaya+ na ndugu zake 220; 7 kutoka kwa Wagershomu, mkuu Yoeli+ na ndugu zake 130; 8 kutoka kwa wazao wa Elisafani,+ mkuu Shemaya na ndugu zake 200; 9 kutoka kwa wazao wa Hebroni, mkuu Elieli na ndugu zake 80; 10 kutoka kwa wazao wa Uzieli,+ mkuu Aminadabu na ndugu zake 112. 11 Tena, Daudi akawaita makuhani Sadoki+ na Abiathari+ na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli, na Aminadabu, 12 akawaambia: “Ninyi ndio viongozi wa koo* za Walawi. Jitakaseni, ninyi na ndugu zenu, nanyi mlipandishe Sanduku la Yehova, Mungu wa Israeli mpaka mahali ambapo nimetayarisha kwa ajili yake. 13 Kwa kuwa mara ya kwanza hamkulibeba,+ hasira ya Yehova Mungu wetu iliwaka dhidi yetu,+ kwa sababu hatukutafuta utaratibu unaofaa.”+ 14 Basi makuhani na Walawi wakajitakasa ili walipandishe Sanduku la Yehova Mungu wa Israeli.

15 Kisha Walawi wakalibeba Sanduku la Mungu wa kweli mabegani mwao kwa kutumia fito zake,+ kama Musa alivyoamuru kwa neno la Yehova. 16 Ndipo Daudi akawaambia wakuu wa Walawi wawaweke ndugu zao waimbaji ili waimbe kwa shangwe na sauti kubwa, kwa ala za muziki: vinanda, vinubi,+ na matoazi.+

17 Basi Walawi wakamweka Hemani+ mwana wa Yoeli na, kutoka kati ya ndugu zake, Asafu+ mwana wa Berekia na, kutoka kati ya ndugu zao Wamerari, Ethani+ mwana wa Kushaya. 18 Walikuwa pamoja na ndugu zao wa kikundi cha pili,+ Zekaria, Beni, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, na Mikneya na Obed-edomu na Yeieli walinzi wa malango. 19 Waimbaji Hemani,+ Asafu,+ na Ethani waliwekwa kupiga matoazi ya shaba;+ 20 na Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya, na Benaya walipiga vinanda vilivyopatanishwa na sauti ya Alamothi;*+ 21 na Matithia,+ Elifelehu, Mikneya, Obed-edomu, Yeieli, na Azazia walipiga vinubi vilivyopatanishwa na sauti ya Sheminithi,*+ ili waongoze uimbaji. 22 Kenania+ mkuu wa Walawi alisimamia usafirishaji, kwa maana alikuwa stadi, 23 na Berekia na Elkana walikuwa walinzi wa malango kwa ajili ya Sanduku. 24 Makuhani Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya, na Eliezeri walipiga tarumbeta kwa sauti kubwa mbele ya Sanduku la Mungu wa kweli,+ na Obed-edomu na Yehia walitumikia pia wakiwa walinzi wa malango kwa ajili ya Sanduku.

25 Kisha Daudi na wazee wa Israeli na wakuu wa maelfu walikuwa wakitembea kandokando ili kulipandisha sanduku la agano la Yehova kutoka katika nyumba ya Obed-edomu+ wakishangilia.+ 26 Mungu wa kweli alipowasaidia Walawi waliokuwa wakilibeba sanduku la agano la Yehova, waliwatoa dhabihu ng’ombe dume saba wachanga na kondoo dume saba.+ 27 Daudi alikuwa amevaa joho lisilo na mikono la kitambaa bora, kama walivyovaa Walawi wote waliobeba Sanduku hilo, waimbaji, na Kenania mkuu wa usafirishaji na wa waimbaji; Daudi pia alikuwa amevaa efodi ya kitani.+ 28 Waisraeli wote walikuwa wakilipandisha sanduku la agano la Yehova kwa kelele za shangwe,+ wakipiga pembe, tarumbeta,+ matoazi, na kupiga kwa sauti kubwa vinanda na vinubi.+

29 Lakini sanduku la agano la Yehova lilipofika kwenye Jiji la Daudi,+ Mikali, binti ya Sauli,+ akaangalia chini kupitia dirishani, akamwona Mfalme Daudi akirukaruka na kusherehekea; akaanza kumdharau moyoni mwake.+

16 Basi wakaliingiza Sanduku la Mungu wa kweli na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amepiga ili aliweke humo;+ nao wakatoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika mbele za Mungu wa kweli.+ 2 Daudi alipomaliza kutoa dhabihu za kuteketezwa+ na dhabihu za ushirika,+ akawabariki watu katika jina la Yehova. 3 Isitoshe, aliwagawia Waisraeli wote, kila mwanamume na mwanamke, mkate mmoja wa mviringo, keki ya tende, na keki ya zabibu kavu. 4 Kisha akawaweka baadhi ya Walawi wahudumu mbele ya Sanduku la Yehova,+ wamheshimu,* wamshukuru, na kumsifu Yehova Mungu wa Israeli. 5 Asafu+ alikuwa kiongozi, na wa pili Zekaria; naye Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-edomu, na Yeieli+ walipiga vinanda na vinubi;+ na Asafu alipiga matoazi,+ 6 na makuhani Benaya na Yahazieli walipiga tarumbeta daima mbele ya sanduku la agano la Mungu wa kweli.

7 Hiyo ndiyo siku ambayo Daudi kwa mara ya kwanza alitunga* wimbo huu wa kumshukuru Yehova na kumwagiza Asafu+ na ndugu zake wauimbe:

8 “Mshukuruni Yehova,+ liitieni jina lake,

Yajulisheni mataifa matendo yake!+

9 Mwimbieni, mwimbieni sifa,*+

Tafakarini* kazi zake zote zinazostaajabisha.+

10 Jivunieni jina lake takatifu.+

Mioyo ya wale wanaomtafuta Yehova na ishangilie.+

11 Mtafuteni Yehova+ na nguvu zake,

Utafuteni uso* wake daima.+

12 Kumbukeni kazi zinazostaajabisha alizofanya,+

Miujiza yake na hukumu alizotangaza,

13 Enyi uzao wa* Israeli mtumishi wake,+

Enyi wana wa Yakobo, watu wake aliowachagua.+

14 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+

Hukumu zake ziko duniani kote.+

15 Kumbukeni agano lake milele,

Ahadi aliyotoa,* hata kufikia vizazi elfu,+

16 Agano alilofanya na Abrahamu,+

Na kiapo alichomwapia Isaka,+

17 Alichotoa kama amri kwa Yakobo+

Na kama agano la kudumu kwa Israeli,

18 Akisema, ‘Nitakupa nchi ya Kanaani+

Kuwa urithi wako uliogawiwa.’+

19 Mlipokuwa wachache,

Naam, wachache sana, nanyi mlikuwa wageni nchini.+

20 Walitembeatembea kutoka taifa moja hadi taifa lingine,

Kutoka ufalme mmoja hadi ufalme mwingine.+

21 Hakumruhusu mtu yeyote awakandamize,+

Lakini kwa sababu yao aliwakaripia wafalme,+

22 Akisema, ‘Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,

Wala msiwatendee manabii wangu jambo lolote baya.’+

23 Mwimbieni Yehova, dunia yote!

Tangazeni wokovu wake siku baada ya siku!+

24 Tangazeni utukufu wake miongoni mwa mataifa,

Kazi zake zinazostaajabisha miongoni mwa mataifa yote.

25 Kwa maana Yehova ni mkuu na anastahili kusifiwa kuliko wote.

Anaogopesha kuliko miungu mingine yote.+

26 Miungu yote ya mataifa ni miungu ya ubatili,+

Lakini Yehova ndiye aliyeziumba mbingu.+

27 Mbele zake kuna utukufu* na fahari;+

Katika makao yake kuna nguvu na shangwe.+

28 Mpeni Yehova anachostahili, enyi familia za mataifa,

Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+

29 Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili;+

Leteni zawadi na mje mbele zake.+

Mwinamieni* Yehova katika mapambo matakatifu.*+

30 Tetemekeni mbele zake, dunia yote!

Dunia imeimarishwa kabisa; haiwezi kusogezwa.*+

31 Mbingu na zishangilie, dunia na iwe na shangwe;+

Tangazeni miongoni mwa mataifa: ‘Yehova amekuwa Mfalme!’+

32 Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza;

Mashamba na vitu vyote vilivyomo na vishangilie.

33 Wakati uleule miti ya msituni na ishangilie kwa sauti mbele za Yehova,

Kwa maana anakuja* kuihukumu dunia.

34 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+

35 Nanyi semeni, ‘Tuokoe, Ee Mungu wa wokovu wetu,+

Tukusanye na kutuokoa kutoka katika mataifa,

Ili tulishukuru jina lako takatifu+

Na tushangilie kukusifu wewe.+

36 Yehova, Mungu wa Israeli, na asifiwe

Kwa umilele wote.’”*

Na watu wote wakasema, “Amina!”* nao wakamsifu Yehova.

37 Kisha Daudi akamwacha Asafu+ na ndugu zake hapo mbele ya sanduku la agano la Yehova ili wahudumu daima mbele ya Sanduku+ hilo, kulingana na utaratibu wa kila siku.+ 38 Obed-edomu na ndugu zake, watu 68, na Obed-edomu mwana wa Yeduthuni, na Hosa walikuwa walinzi wa malango; 39 na kuhani Sadoki+ na makuhani wenzake walikuwa mbele ya hema la ibada la Yehova mahali pa juu kule Gibeoni+ 40 ili wamtolee Yehova kwa ukawaida dhabihu za kuteketezwa kwenye madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa, asubuhi na jioni, na kufanya mambo yote yaliyoandikwa katika Sheria ya Yehova aliyowaamuru Waisraeli wafuate.+ 41 Walikuwa pamoja na Hemani na Yeduthuni+ na wanaume wengine waliochaguliwa na kutajwa majina ili wamshukuru Yehova,+ kwa sababu “upendo wake mshikamanifu unadumu milele”;+ 42 nao walikuwa pamoja na Hemani+ na Yeduthuni ili wapige tarumbeta, matoazi, na ala zilizotumiwa kumsifu* Mungu wa kweli; na wana wa Yeduthuni+ walikuwa langoni. 43 Kisha watu wote wakaenda nyumbani kwao, na Daudi akaenda kuwabariki watu wa nyumba yake mwenyewe.

17 Mara tu Daudi alipoanza kuishi katika nyumba yake mwenyewe,* alimwambia hivi nabii Nathani:+ “Mimi hapa ninaishi katika nyumba ya mierezi+ huku sanduku la agano la Yehova likiwa ndani ya vitambaa vya mahema.”+ 2 Nathani akamwambia Daudi: “Fanya jambo lolote lililo moyoni mwako, kwa sababu Mungu wa kweli yuko pamoja nawe.”

3 Usiku huohuo, neno hili la Mungu likamjia Nathani: 4 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Si wewe utakayenijengea nyumba nitakayokaa ndani yake.+ 5 Kwa maana sijakaa ndani ya nyumba tangu siku nilipowatoa nje Waisraeli mpaka leo, bali nimekuwa nikihama hema moja hadi hema lingine na kutoka hema moja la ibada hadi hema lingine la ibada.*+ 6 Wakati wote nilipotembea na Waisraeli wote, je, niliwahi wakati wowote kumuuliza mwamuzi yeyote wa Israeli niliyemweka awachunge watu wangu, ‘Kwa nini hukunijengea nyumba ya mierezi?’”’

7 “Sasa mwambie hivi mtumishi wangu Daudi: ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Nilikutoa malishoni, ili usiendelee kuchunga kondoo, uwe kiongozi wa watu wangu Waisraeli.+ 8 Nami nitakuwa pamoja nawe popote utakapoenda,+ nami nitawaangamiza maadui wako wote kutoka mbele yako;+ nami nitakujengea jina kama jina la watu maarufu duniani.+ 9 Nitachagua mahali kwa ajili ya watu wangu Waisraeli na kuwaweka humo, nao wataishi humo na hawatasumbuliwa tena; na watu waovu hawatawakandamiza* tena kama walivyofanya zamani,+ 10 tangu siku nilipowaweka waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli.+ Nami nitawashinda maadui wako wote.+ Pia, ninakuambia, ‘Yehova atakujengea nyumba.’*

11 “‘“Siku zako zitakapokwisha nawe uzikwe pamoja na mababu zako, nitamwinua mzao wako* baada yako, mmoja wa wana wako,+ nami nitauimarisha kabisa ufalme wake.+ 12 Yeye ndiye atakayenijengea nyumba,+ nami nitakiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme milele.+ 13 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu.+ Sitauondoa upendo wangu mshikamanifu kutoka kwake+ kama nilivyouondoa kutoka kwa yule aliyekutangulia.+ 14 Nitamfanya asimame katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele,+ na kiti chake cha ufalme kitadumu milele.”’”+

15 Nathani alimwambia Daudi maneno hayo yote na maono hayo yote.

16 Ndipo Mfalme Daudi akaingia na kuketi mbele za Yehova na kusema: “Mimi ni nani, Ee Yehova Mungu? Na nyumba yangu ni nini hivi kwamba umenileta mpaka hapa nilipofika?+ 17 Na kana kwamba hilo halitoshi, Ee Mungu, unasema pia kwamba nyumba yangu mimi mtumishi wako itadumu kwa muda mrefu,+ nawe umeniona kuwa mtu anayepaswa kukwezwa zaidi,* Ee Yehova Mungu. 18 Mimi mtumishi wako Daudi nitakwambia nini zaidi kuhusu heshima uliyonipa na wewe unanijua vizuri sana mimi mtumishi wako?+ 19 Ee Yehova, kwa ajili yangu mimi mtumishi wako na kupatana na moyo wako* umetenda mambo haya yote makuu kwa kufunua ukuu wako.+ 20 Ee Yehova, hakuna aliye kama wewe,+ na hakuna Mungu ila wewe;+ mambo yote tuliyosikia kwa masikio yetu yanathibitisha jambo hilo. 21 Na kuna taifa gani lingine duniani lililo kama watu wako Waisraeli?+ Wewe Mungu wa kweli ulienda na kuwakomboa wakiwa watu wako.+ Ulijijengea jina kwa matendo yako makuu na yenye kuogopesha,+ ukayafukuza mataifa kutoka mbele ya watu wako+ uliowakomboa kutoka Misri. 22 Uliwafanya watu wako Waisraeli wawe watu wako milele;+ na wewe, Ee Yehova, ukawa Mungu wao.+ 23 Sasa, Ee Yehova, ahadi uliyotoa kunihusu mimi mtumishi wako na nyumba yangu na ithibitike kuwa ya uaminifu milele, na ufanye kama ulivyoahidi.+ 24 Jina lako na lidumu na kukwezwa+ milele, ili watu waseme, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, ni Mungu kwa Israeli,’ na nyumba yangu mimi mtumishi wako Daudi na iimarishwe kabisa mbele zako.+ 25 Kwa maana wewe, Mungu wangu, umenifunulia mimi mtumishi wako kusudi lako la kunijengea nyumba.* Ndiyo sababu mimi mtumishi wako nina ujasiri wa kutoa sala hii kwako. 26 Na sasa, Ee Yehova, wewe ndiye Mungu wa kweli, nawe umeahidi mambo hayo mema kunihusu mimi mtumishi wako. 27 Basi na ufurahie kuibariki nyumba yangu mimi mtumishi wako, na idumu milele mbele zako, kwa sababu wewe, Ee Yehova, umeibariki, nayo imebarikiwa milele.”

18 Wakati fulani baadaye, Daudi aliwashinda Wafilisti na kuwatiisha, akachukua jiji la Gathi+ na miji yake kutoka mikononi mwa Wafilisti.+ 2 Kisha akawashinda Wamoabu,+ na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na kumletea ushuru.+

3 Daudi alimshinda Mfalme Hadadezeri+ wa Soba+ karibu na Hamathi+ alipokuwa akienda kuimarisha mamlaka yake katika eneo la Mto Efrati.+ 4 Daudi akateka magari 1,000 ya vita, wapanda farasi 7,000, na wanajeshi 20,000 wanaotembea kwa miguu.+ Kisha Daudi akawakata farasi wote mishipa ya miguu isipokuwa farasi 100 waliokokota magari.+ 5 Wasiria wa Damasko walipokuja kumsaidia Mfalme Hadadezeri wa Soba, Daudi aliwaua Wasiria 22,000.+ 6 Halafu Daudi akaweka kambi za kijeshi kule Siria ya Damasko, na Wasiria wakawa watumishi wa Daudi na kumletea ushuru. Yehova alimpa Daudi ushindi* popote alipoenda.+ 7 Isitoshe, Daudi alichukua ngao za mviringo za dhahabu kutoka kwa watumishi wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu. 8 Daudi alichukua shaba nyingi sana kutoka Tibhathi na Kuni, majiji ya Hadadezeri. Sulemani aliitumia kutengenezea Bahari ya Shaba,+ nguzo, na vyombo vya shaba.+

9 Mfalme Tou wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi alikuwa amelishinda jeshi lote la Mfalme Hadadezeri+ wa Soba,+ 10 mara moja alimtuma Hadoramu mwana wake kwa Mfalme Daudi ili amjulie hali na kumpongeza kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumshinda (kwa maana mara nyingi Hadadezeri alimshambulia Tou), na Hadoramu alimletea Daudi kila aina ya vitu vya dhahabu, fedha, na shaba. 11 Mfalme Daudi akavitakasa vitu hivyo ili viwe vya Yehova,+ pamoja na fedha na dhahabu aliyokuwa amechukua kutoka kwa mataifa yote: kutoka kwa Waedomu na Wamoabu, kutoka kwa Waamoni,+ Wafilisti,+ na Waamaleki.+

12 Abishai+ mwana wa Seruya+ aliwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.+ 13 Aliweka kambi za kijeshi huko Edomu, na Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi.+ Yehova alimpa Daudi ushindi* popote alipoenda.+ 14 Daudi akaendelea kutawala Israeli yote,+ naye aliwatawala watu wake wote kwa haki na uadilifu.+ 15 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa mkuu wa jeshi,+ Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi alifanya kazi ya kuweka kumbukumbu, 16 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shavsha alikuwa mwandishi. 17 Benaya mwana wa Yehoyada aliwasimamia Wakerethi+ na Wapelethi.+ Na wana wa Daudi walikuwa na cheo cha kwanza baada ya mfalme.

19 Baadaye Nahashi mfalme wa Waamoni akafa, na mwanawe akawa mfalme baada yake.+ 2 Ndipo Daudi akasema: “Nitamtendea kwa upendo mshikamanifu+ Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinitendea kwa upendo mshikamanifu.” Basi Daudi akawatuma wajumbe ili wamfariji baada ya kufiwa na baba yake. Lakini watumishi wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni+ kumfariji Hanuni, 3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni: “Je, unafikiri kwamba Daudi anawatuma wafariji kwako ili kumheshimu baba yako? Je, watumishi wake hawajaja kwako ili kufanya uchunguzi kamili na kukupindua wewe na kuipeleleza nchi?” 4 Kwa hiyo Hanuni akawachukua watumishi wa Daudi, akawanyoa,+ akakata nguo zao katikati kwenye matako na kuwafukuza. 5 Daudi alipoambiwa kuhusu wanaume hao, mara moja akawatuma wanaume wengine waende kukutana nao, kwa sababu wanaume hao walikuwa wameaibishwa sana; mfalme akawaambia: “Kaeni Yeriko+ mpaka ndevu zenu zitakapoota, kisha mrudi.”

6 Baada ya muda Waamoni wakaona kuwa wananuka mbele ya Daudi, kwa hiyo Hanuni na Waamoni wakatuma talanta 1,000 za fedha* ili kukodi magari ya vita na wapanda farasi kutoka Mesopotamia,* Aram-maaka, na Soba.+ 7 Basi wakakodi magari 32,000 ya vita, pamoja na mfalme wa Maaka na watu wake. Kisha wakaja na kupiga kambi mbele ya Medeba.+ Waamoni wakakusanyika pamoja kutoka katika majiji yao, wakaja ili kupigana vita.

8 Daudi aliposikia habari hizo, alimtuma Yoabu+ na jeshi lote, kutia ndani mashujaa wake hodari zaidi.+ 9 Nao Waamoni wakatoka na kujipanga kivita kwenye lango la jiji huku wafalme waliokuja wakiwa peke yao uwanjani.

10 Yoabu alipoona kwamba anashambuliwa upande wa mbele na wa nyuma, alichagua baadhi ya wanajeshi bora Israeli na kuwapanga kivita ili wapigane na Wasiria.+ 11 Wanaume waliobaki aliwaweka chini ya usimamizi wa* Abishai ndugu yake,+ ili awapange kivita kupigana na Waamoni. 12 Kisha akasema: “Ikiwa Wasiria+ watanizidi nguvu, basi mtaniokoa; lakini Waamoni wakiwazidi ninyi nguvu, nitawaokoa. 13 Ni lazima tuwe imara na jasiri+ kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya majiji ya Mungu wetu, naye Yehova atafanya yaliyo mema machoni pake.”

14 Kisha Yoabu na wanaume wake wakasonga mbele kwenda kupigana vita na Wasiria, nao wakamkimbia.+ 15 Waamoni walipoona kwamba Wasiria wamekimbia, wakamkimbia pia Abishai ndugu yake na kuingia jijini. Baada ya hayo, Yoabu akarudi Yerusalemu.

16 Wasiria walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, waliwatuma wajumbe wawaite Wasiria waliokuwa katika eneo la Mto Efrati,+ wakiongozwa na Shofaki mkuu wa jeshi la Hadadezeri.+

17 Daudi alipoambiwa habari hiyo, akawakusanya Waisraeli wote mara moja, wakavuka Yordani na kuwafikia, wakajipanga kivita ili kupigana nao. Daudi alijipanga kivita ili kupigana na Wasiria, nao wakapigana naye.+ 18 Lakini Wasiria waliwakimbia Waisraeli; Daudi akawaua Wasiria 7,000 walioendesha magari ya vita na wanajeshi 40,000 waliotembea kwa miguu, akamuua Shofaki mkuu wa jeshi. 19 Watumishi wa Hadadezeri walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli,+ mara moja wakafanya amani na Daudi, wakawa watumishi wake;+ na Wasiria hawakutaka kuwasaidia tena Waamoni.

20 Mwanzoni mwa mwaka,* wakati ambapo wafalme huenda vitani, Yoabu+ aliwaongoza wanajeshi vitani, wakaiharibu nchi ya Waamoni; Yoabu akaenda na kuzingira Raba,+ lakini Daudi akabaki Yerusalemu.+ Yoabu alishambulia jiji la Raba na kulibomoa kabisa.+ 2 Kisha Daudi akachukua taji lililokuwa kwenye kichwa cha Malkamu, akapata kwamba uzito wa taji hilo ulikuwa talanta moja* ya dhahabu, nalo lilikuwa na mawe yenye thamani; Daudi akavishwa taji hilo kichwani. Alichukua pia nyara nyingi sana kutoka katika jiji hilo.+ 3 Akawatoa nje watu waliokuwa ndani yake, akawapa kazi+ ya kukata mawe kwa misumeno na kufanya kazi kwa vifaa vya chuma vyenye ncha kali na kwa mashoka. Hivyo ndivyo Daudi alivyofanya katika majiji yote ya Waamoni. Hatimaye Daudi na wanajeshi wote wakarudi Yerusalemu.

4 Baada ya hayo, wakapigana tena na Wafilisti kule Gezeri. Wakati huo Sibekai+ Mhusha alimuua Sipai, aliyekuwa mzao wa Warefaimu,+ nao wakatiishwa.

5 Wakapigana tena na Wafilisti, na Elhanani mwana wa Yairi akamuua Lahmi ndugu ya Goliathi+ Mgathi, aliyekuwa na mkuki wenye mpini kama mti wa wafumaji wa nguo.+

6 Vita vikatokea tena huko Gathi,+ ambako kulikuwa na mwanamume mkubwa isivyo kawaida,+ mwenye vidole 6 katika kila mkono na vidole 6 katika kila mguu, jumla ya vidole 24; naye pia alikuwa mzao wa Warefaimu.+ 7 Aliendelea kuwadhihaki+ Waisraeli. Basi Yonathani mwana wa Shimea,+ ndugu ya Daudi, akamuua.

8 Watu hao walikuwa wazao wa Warefaimu+ huko Gathi,+ na Daudi na watumishi wake ndio waliowaua.

21 Kisha Shetani* akasimama dhidi ya Waisraeli na kumchochea Daudi awahesabu Waisraeli.+ 2 Basi Daudi akamwambia Yoabu+ na wakuu wa watu: “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-sheba mpaka Dani;+ kisha mniletee habari ili nijue idadi yao.” 3 Lakini Yoabu akasema: “Yehova na azidishe idadi ya watu wake mara 100! Bwana wangu mfalme, hao wote tayari ni watumishi wako bwana wangu, sivyo? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivyo? Kwa nini uwafanye Waisraeli wawe na hatia?”

4 Lakini neno la mfalme likawa na nguvu kuliko neno la Yoabu. Basi Yoabu akaondoka na kusafiri kotekote Israeli, kisha akarudi Yerusalemu.+ 5 Basi Yoabu akampa Daudi idadi ya watu walioandikishwa. Wanaume wote wa Israeli waliojihami kwa mapanga walikuwa 1,100,000, na wanaume wa Yuda waliojihami kwa mapanga walikuwa 470,000.+ 6 Lakini hakuwaandikisha watu wa kabila la Lawi na Benjamini miongoni mwao,+ kwa sababu neno la mfalme lilimchukiza Yoabu.+

7 Basi jambo hilo halikumpendeza hata kidogo Mungu wa kweli, kwa hiyo akawaletea Waisraeli ugonjwa hatari. 8 Basi Daudi akamwambia Mungu wa kweli: “Nimetenda dhambi+ kubwa kwa kufanya jambo hili. Na sasa, tafadhali, nisamehe kosa langu mimi mtumishi wako,+ kwa maana nimetenda kwa upumbavu sana.”+ 9 Kisha Yehova akamwambia hivi Gadi,+ mwonaji wa Daudi: 10 “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Ninakupa mambo matatu ya kuchagua. Chagua jambo nitakalokutendea.”’” 11 Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Yehova anasema hivi: ‘Chagua 12 ikiwa unataka miaka mitatu ya njaa kali,+ au ikiwa unataka maadui wako wakufagilie mbali kwa miezi mitatu huku upanga wao ukikuandama,+ au siku tatu za upanga kutoka kwa Yehova—nchi ikumbwe na ugonjwa hatari+—huku malaika wa Yehova akileta maangamizi+ katika eneo lote la Israeli.’ Sasa fikiria jibu ninalopaswa kumpa Yule aliyenituma.” 13 Kwa hiyo Daudi akamwambia Gadi: “Jambo hilo linanihuzunisha sana. Tafadhali, acha nianguke mkononi mwa Yehova, kwa maana rehema zake ni nyingi sana;+ lakini usiniache nianguke mkononi mwa mwanadamu.”+

14 Ndipo Yehova akaleta ugonjwa hatari+ Israeli hivi kwamba watu 70,000 miongoni mwa Waisraeli wakafa.+ 15 Zaidi ya hilo, Mungu wa kweli alimtuma malaika katika jiji la Yerusalemu ili kuliangamiza; lakini alipokuwa karibu kuliangamiza, Yehova akaona jambo hilo na kughairi* kwa sababu ya msiba huo,+ akamwambia malaika aliyekuwa akiwaangamiza watu: “Imetosha!+ Sasa shusha mkono wako.” Malaika wa Yehova alikuwa amesimama karibu na uwanja wa kupuria nafaka wa Ornani+ Myebusi.+

16 Daudi alipoinua macho yake, alimwona malaika wa Yehova akiwa amesimama kati ya dunia na mbingu akiwa ameshika mkononi mwake upanga uliochomolewa+ na kuelekezwa Yerusalemu. Mara moja, Daudi na wazee, wakiwa wamevaa nguo za magunia,+ wakajiangusha chini kifudifudi.+ 17 Daudi akamwambia Mungu wa kweli: “Je, si mimi niliyesema watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi, na mimi ndiye niliyekosea;+ lakini kondoo hawa—wamefanya nini? Ee Yehova Mungu wangu, tafadhali, acha mkono wako uniadhibu mimi na nyumba ya baba yangu; lakini usiwapige watu wako.”+

18 Ndipo malaika wa Yehova akamwambia Gadi+ amwambie Daudi apande na kumjengea Yehova madhabahu kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Ornani Myebusi.+ 19 Basi Daudi akapanda kulingana na neno la Gadi, alilosema katika jina la Yehova. 20 Wakati huo, Ornani akageuka na kumwona huyo malaika, na wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha. Wakati huo Ornani alikuwa akipura ngano. 21 Daudi alipopanda na kufika kwake, Ornani alitazama na kumwona Daudi, mara moja akatoka kwenye uwanja wa kupuria na kumwinamia Daudi kifudifudi. 22 Daudi akamwambia Ornani: “Niuzie* uwanja wa kupuria ili nimjengee Yehova madhabahu kwenye uwanja huo. Niuzie kwa bei kamili, ili ugonjwa hatari ambao umewakumba watu ukomeshwe.”+ 23 Lakini Ornani akamwambia Daudi: “Uchukue uwe wako, bwana wangu mfalme fanya lolote unaloona ni jema.* Tazama, ninatoa ng’ombe kwa ajili ya dhabihu za kuteketezwa na kifaa cha kupuria+ utakachotumia kama kuni na ngano ya toleo la nafaka. Ninatoa vitu hivi vyote.”

24 Hata hivyo, Mfalme Daudi akamwambia Ornani: “Hapana, ni lazima niununue kwa bei kamili, kwa sababu sitachukua kitu chako na kumpa Yehova au kutoa dhabihu za kuteketezwa ambazo hazinigharimu chochote.”+ 25 Basi Daudi akampimia Ornani shekeli 600 za dhahabu* kwa ajili ya uwanja huo. 26 Kisha Daudi akamjengea Yehova madhabahu+ mahali hapo na kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika, akasali kwa Yehova, ambaye sasa alimjibu kwa kushusha moto+ kutoka mbinguni kwenye madhabahu hiyo ya dhabihu za kuteketezwa. 27 Kisha Yehova akamwagiza yule malaika+ aurudishe upanga wake kwenye ala. 28 Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Yehova amemjibu kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani Myebusi, akaendelea kutoa dhabihu hapo. 29 Hata hivyo, lile hema la ibada la Yehova ambalo Musa alikuwa ametengeneza nyikani na ile madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa vilikuwa mahali pa juu kule Gibeoni wakati huo.+ 30 Lakini Daudi hakuweza kwenda mbele yake ili kutafuta ushauri wa Mungu, kwa maana aliogopa upanga wa malaika wa Yehova.

22 Ndipo Daudi akasema: “Hii ndiyo nyumba ya Yehova Mungu wa kweli, na hii ndiyo madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa kwa ajili ya Waisraeli.”+

2 Kisha Daudi akaagiza wakaaji wageni+ waliokuwa katika nchi ya Israeli wakusanywe, naye akawapa kazi ya kukata mawe na kuyachonga ili yatumiwe kujenga nyumba ya Mungu wa kweli.+ 3 Daudi pia alitayarisha kiasi kikubwa sana cha chuma ili kitumiwe kutengenezea misumari ya milango ya malango na pia vibanio, na shaba nyingi sana hivi kwamba haingeweza kupimwa,+ 4 na pia mbao za mierezi+ zisizohesabika, kwa maana Wasidoni+ na Watiro+ walimletea Daudi mbao nyingi sana za mierezi. 5 Daudi akasema: “Mwanangu Sulemani ni mchanga na hana uzoefu,*+ na nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Yehova itakuwa na utukufu usio na kifani,+ hivi kwamba umaarufu na umaridadi+ wake utajulikana katika nchi zote.+ Kwa hiyo, nitafanya matayarisho kwa ajili yake.” Basi Daudi akatayarisha vifaa vingi sana kabla ya kifo chake.

6 Isitoshe, alimwita Sulemani mwanawe na kumwagiza amjengee nyumba Yehova Mungu wa Israeli. 7 Daudi alimwambia hivi Sulemani mwanawe: “Moyo wangu ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu.+ 8 Lakini neno la Yehova lilinijia likisema, ‘Umemwaga damu nyingi sana, nawe umepigana vita vikubwa. Hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ kwa maana umemwaga damu nyingi sana duniani mbele zangu. 9 Tazama! Utazaa mwana+ atakayekuwa mtu wa amani,* nami nitampumzisha kutokana na maadui wake wote wanaomzunguka,+ kwa maana jina lake litakuwa Sulemani,*+ nami nitawapa Waisraeli amani na utulivu katika siku zake.+ 10 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu.+ Atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake.+ Nitakiimarisha kabisa kiti cha ufalme wake juu ya Israeli milele.’+

11 “Sasa, mwanangu, Yehova na awe pamoja nawe, nawe ufanikiwe na kujenga nyumba ya Yehova Mungu wako, kama alivyosema kukuhusu wewe.+ 12 Ila tu Yehova akupe busara na uelewaji+ atakapokupa mamlaka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Yehova Mungu wako.+ 13 Utafanikiwa ikiwa utashika kwa uangalifu masharti+ na sheria* ambazo Yehova alimwamuru Musa awape Waisraeli.+ Uwe jasiri na imara. Usiogope wala usihofu.+ 14 Tazama, nimejitahidi kabisa kufanya matayarisho kwa ajili ya nyumba ya Yehova, nimeweka talanta 100,000* za dhahabu na talanta 1,000,000 za fedha na shaba nyingi sana+ na chuma hivi kwamba haviwezi kupimwa, nami nimetayarisha mbao na mawe,+ lakini utaongeza vitu hivyo. 15 Una wafanyakazi wengi sana—wakataji wa mawe, waashi,+ maseremala, na wafanyakazi wenye ustadi wa kila aina.+ 16 Dhahabu, fedha, shaba, na chuma haviwezi kupimwa.+ Haya, anza kazi, Yehova na awe pamoja nawe.”+

17 Kisha Daudi akawaagiza wakuu wote wa Israeli wamsaidie Sulemani mwanawe, akawaambia: 18 “Je, Yehova, Mungu wenu hayuko pamoja nanyi, na je, hajawapumzisha pande zote? Kwa maana aliwatia mikononi mwangu wakaaji wa nchi, na nchi imetiishwa mbele za Yehova na mbele ya watu wake. 19 Basi azimieni kwa moyo wenu wote na nafsi* yenu yote kumtafuta Yehova Mungu wenu,+ anzeni kujenga mahali patakatifu pa Yehova Mungu wa kweli,+ ili mlilete sanduku la agano la Yehova na vyombo vitakatifu vya Mungu wa kweli+ katika nyumba iliyojengwa kwa ajili ya jina la Yehova.”+

23 Daudi alipokuwa amezeeka na kukaribia mwisho wa maisha yake,* alimweka Sulemani mwanawe kuwa mfalme wa Israeli.+ 2 Akawakusanya wakuu wote wa Israeli, makuhani,+ na Walawi.+ 3 Walawi waliokuwa na umri wa miaka 30 na zaidi walihesabiwa;+ idadi yao, mwanamume kwa mwanamume,* ilikuwa 38,000. 4 Walawi 24,000 kati yao walikuwa wasimamizi wa kazi ya nyumba ya Yehova, na kulikuwa na maofisa na waamuzi 6,000,+ 5 na walinzi 4,000 wa malango,+ na watu 4,000 walimsifu+ Yehova kwa ala ambazo Daudi alisema hivi kuzihusu: “Nilizitengeneza ili zitumiwe kumsifu Mungu.”

6 Kisha Daudi akawapanga* katika vikundi+ kulingana na wana hawa wa Lawi: Gershoni, Kohathi, na Merari.+ 7 Kutoka kwa Wagershoni: Ladani na Shimei. 8 Wana wa Ladani walikuwa Yehieli kiongozi wao, Zethamu, na Yoeli,+ wana watatu. 9 Wana wa Shimei walikuwa Shelomothi, Hazieli, na Harani, wana watatu. Hao walikuwa viongozi wa koo* za Ladani. 10 Na wana wa Shimei walikuwa Yahathi, Zina, Yeushi, na Beria. Hao wanne walikuwa wana wa Shimei. 11 Yahathi alikuwa kiongozi na wa pili alikuwa Ziza. Lakini kwa kuwa Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi, walihesabiwa kama ukoo* mmoja nao walipewa majukumu yaleyale.

12 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari,+ Hebroni, na Uzieli,+ wana wanne. 13 Wana wa Amramu walikuwa Haruni+ na Musa.+ Lakini Haruni alitengwa kando daima+ ili atakase Patakatifu Zaidi, yeye na wanawe, ili watoe dhabihu mbele za Yehova, wamhudumie, na kutangaza baraka katika jina lake sikuzote.+ 14 Majina ya wana wa Musa, mtu wa Mungu wa kweli, yaliorodheshwa miongoni mwa kabila la Walawi. 15 Wana wa Musa walikuwa Gershomu+ na Eliezeri.+ 16 Shebueli+ alikuwa kiongozi wa wana wa Gershomu. 17 Rehabia+ alikuwa kiongozi wa wazao* wa Eliezeri; Eliezeri hakuwa na wana wengine, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana. 18 Shelomithi+ alikuwa kiongozi wa wana wa Ishari.+ 19 Wana wa Hebroni walikuwa Yeria kiongozi wao, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.+ 20 Wana wa Uzieli+ walikuwa Mika kiongozi wao na wa pili Ishia.

21 Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi.+ Wana wa Mali walikuwa Eleazari na Kishi. 22 Eleazari alikufa, lakini hakuwa na wana ila mabinti tu. Basi wana wa Kishi, watu wao wa ukoo,* waliwaoa. 23 Wana wa Mushi walikuwa Mali, Ederi, na Yeremothi, wana watatu.

24 Hao ndio waliokuwa wana wa Lawi kulingana na koo zao,* viongozi wa koo zao,* wale walioandikishwa na kuhesabiwa na kuorodheshwa kulingana na majina yao na ambao walitekeleza kazi ya utumishi wa nyumba ya Yehova, kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi. 25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema hivi: “Yehova Mungu wa Israeli amewapumzisha watu wake,+ naye atakaa Yerusalemu milele.+ 26 Pia Walawi hawatalazimika kubeba hema la ibada wala chombo chake chochote kinachotumiwa katika utumishi wa hema hilo.”+ 27 Kwa maana kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi wenye umri wa miaka 20 na zaidi walihesabiwa. 28 Jukumu lao lilikuwa kuwasaidia wana wa Haruni+ katika utumishi wa nyumba ya Yehova, kusimamia nyua,+ vyumba vya kulia chakula, kukitakasa kila kitu kitakatifu, na kazi yoyote iliyohitaji kufanywa katika utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli. 29 Waliwasaidia katika kazi ya mikate ya tabaka,*+ unga laini wa toleo la nafaka, mikate myembamba isiyo na chachu,+ keki zilizookwa, unga wa kukandwa uliochanganywa,+ na vipimo vyote vya wingi na ukubwa. 30 Walipaswa kusimama asubuhi baada ya asubuhi+ ili kumshukuru na kumsifu Yehova, na walipaswa kufanya hivyo jioni pia.+ 31 Walisaidia wakati wowote ambapo dhabihu za kuteketezwa zilitolewa kwa Yehova nyakati za Sabato,+ miezi mipya,+ na wakati wa sherehe za majira,+ kulingana na idadi iliyoamriwa katika sheria kuzihusu, nao walifanya hivyo kwa ukawaida mbele za Yehova. 32 Walitimiza pia majukumu yao kuhusiana na hema la mkutano, mahali patakatifu, na kuhusiana na ndugu zao wana wa Haruni katika utumishi wa nyumba ya Yehova.

24 Basi hivi ndivyo vilivyokuwa vikundi vya wazao wa Haruni: Wana wa Haruni walikuwa Nadabu, Abihu,+ Eleazari, na Ithamari.+ 2 Hata hivyo, Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao,+ nao hawakuwa na wana wowote; lakini Eleazari+ na Ithamari waliendelea kutumikia wakiwa makuhani. 3 Daudi, pamoja na Sadoki+ kutoka kwa wana wa Eleazari na Ahimeleki kutoka kwa wana wa Ithamari, waliwagawa katika vikundi kulingana na mpangilio wao wa utumishi. 4 Kwa kuwa wana wa Eleazari walikuwa na viongozi wengi kuliko wana wa Ithamari, waliwagawa ifaavyo: Wana wa Eleazari walikuwa na viongozi 16 wa koo zao,* na wana wa Ithamari walikuwa na viongozi 8 wa koo zao.*

5 Pia, waliwagawa kwa kura,+ kikundi kimoja pamoja na kingine, kwa maana kulikuwa na wakuu wa mahali patakatifu na wakuu wa Mungu wa kweli kutoka kwa wana wa Eleazari na pia wana wa Ithamari. 6 Kisha Shemaya mwana wa Nethaneli mwandishi wa Walawi akaandika majina yao mbele ya mfalme, wakuu, kuhani Sadoki,+ Ahimeleki+ mwana wa Abiathari,+ na viongozi wa koo* za makuhani na za Walawi, ukoo* mmoja ulichaguliwa kutoka kwa Eleazari na ukoo mmoja ulichaguliwa kutoka kwa Ithamari.

7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu; ya pili Yedaya, 8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu, 9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini, 10 ya saba Hakozi, ya nane Abiya,+ 11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania, 12 ya 11 Eliashibu, ya 12 Yakimu, 13 ya 13 Hupa, ya 14 Yeshebeabu, 14 ya 15 Bilga, ya 16 Imeri, 15 ya 17 Heziri, ya 18 Hapisesi, 16 ya 19 Pethahia, ya 20 Yehezkeli, 17 ya 21 Yakini, ya 22 Gamuli, 18 ya 23 Delaya, ya 24 Maazia.

19 Huo ndio uliokuwa mpangilio wao wa utumishi+ walipokuwa wakiingia katika nyumba ya Yehova kulingana na utaratibu uliowekwa na Haruni babu yao, kama Yehova Mungu wa Israeli alivyokuwa amemwamuru.

20 Hawa ndio Walawi waliobaki: kutoka kwa wana wa Amramu+ kulikuwa na Shubaeli;+ kutoka kwa wana wa Shubaeli, Yehdeya; 21 wana wa Rehabia:+ kutoka kwa wana wa Rehabia, Ishia kiongozi wao; 22 kutoka kwa Waishari, Shelomothi;+ kutoka kwa wana wa Shelomothi, Yahathi; 23 na kutoka kwa wana wa Hebroni, Yeria+ kiongozi wao, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, wa nne Yekameamu; 24 kutoka kwa wana wa Uzieli, Mika; kutoka kwa wana wa Mika, Shamiri. 25 Ndugu ya Mika alikuwa Ishia; kutoka kwa wana wa Ishia, Zekaria.

26 Wana wa Merari+ walikuwa Mali na Mushi; kutoka kwa wana wa Yaazia, Beno. 27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibri; 28 kutoka kwa Mali, Eleazari, ambaye hakuwa na wana wowote;+ 29 Kishi: kutoka kwa wana wa Kishi, Yerahmeeli; 30 na wana wa Mushi walikuwa Mali, Ederi, na Yerimothi.

Hao ndio waliokuwa wana wa Lawi kulingana na koo zao.* 31 Na pia walipiga kura+ kama walivyofanya ndugu zao wana wa Haruni mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki, na viongozi wa koo* za makuhani na za Walawi. Kuhusiana na koo,* kiongozi alikuwa sawa kabisa na ndugu yake mdogo.

25 Isitoshe, Daudi na wakuu wa vikundi vya utumishi waliwatenga baadhi ya wana wa Asafu, Hemani, na Yeduthuni+ ili watoe unabii kwa kutumia vinubi, vinanda,+ na matoazi.+ Hii ndiyo orodha ya wanaume waliowekwa rasmi kwa ajili ya utumishi huo: 2 kutoka kwa wana wa Asafu: Zakuri, Yosefu, Nethania, na Asharela, wana wa Asafu waliokuwa chini ya usimamizi wa Asafu, aliyetoa unabii chini ya usimamizi wa mfalme. 3 Kutoka kwa Yeduthuni,+ wana wa Yeduthuni walikuwa: Gedalia, Zeri, Yeshaya, Shimei, Hashabia, na Matithia,+ wana sita, waliokuwa chini ya usimamizi wa Yeduthuni baba yao, aliyetoa unabii kwa kutumia kinubi, akimshukuru na kumsifu Yehova.+ 4 Kutoka kwa Hemani,+ wana wa Hemani walikuwa: Bukia, Matania, Uzieli, Shebueli, Yerimothi, Hanania, Hanani, Eliatha, Gidalti, Romamti-ezeri, Yoshbekasha, Malothi, Hothiri, na Mahaziothi. 5 Hao wote walikuwa wana wa Hemani, mwonaji wa mfalme kuhusiana na mambo ya Mungu wa kweli ili kumtukuza;* basi Mungu wa kweli alimpa Hemani wana 14 na mabinti 3. 6 Hao wote walikuwa chini ya usimamizi wa baba yao wakiwa waimbaji katika nyumba ya Yehova, wakitumia matoazi, vinanda, na vinubi+ kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli.

Asafu, Yeduthuni, na Hemani walikuwa chini ya usimamizi wa mfalme.

7 Idadi yao pamoja na ndugu zao waliozoezwa kumwimbia Yehova, wote wakiwa stadi, ilikuwa 288. 8 Basi walipiga kura+ ili kupanga zamu zao, mdogo sawa na mkubwa, mwenye ustadi pamoja na mwanafunzi.

9 Kura ya kwanza ilimwangukia Asafu kwa ajili ya Yosefu,+ ya pili Gedalia+ (yeye na ndugu zake na wanawe walikuwa 12); 10 ya tatu Zakuri,+ wanawe na ndugu zake, 12; 11 ya nne Izri, wanawe na ndugu zake, 12; 12 ya tano Nethania,+ wanawe na ndugu zake, 12; 13 ya sita Bukia, wanawe na ndugu zake, 12; 14 ya saba Yesharela, wanawe na ndugu zake, 12; 15 ya nane Yeshaya, wanawe na ndugu zake, 12; 16 ya tisa Matania, wanawe na ndugu zake, 12; 17 ya kumi Shimei, wanawe na ndugu zake, 12; 18 ya 11 Azareli, wanawe na ndugu zake, 12; 19 ya 12 Hashabia, wanawe na ndugu zake, 12; 20 ya 13 Shubaeli,+ wanawe na ndugu zake, 12; 21 ya 14 Matithia, wanawe na ndugu zake, 12; 22 ya 15 Yeremothi, wanawe na ndugu zake, 12; 23 ya 16 Hanania, wanawe na ndugu zake, 12; 24 ya 17 Yoshbekasha, wanawe na ndugu zake, 12; 25 ya 18 Hanani, wanawe na ndugu zake, 12; 26 ya 19 Malothi, wanawe na ndugu zake, 12; 27 ya 20 Eliatha, wanawe na ndugu zake, 12; 28 ya 21 Hothiri, wanawe na ndugu zake, 12; 29 ya 22 Gidalti,+ wanawe na ndugu zake, 12; 30 ya 23 Mahaziothi,+ wanawe na ndugu zake, 12; 31 ya 24 Romamti-ezeri,+ wanawe na ndugu zake, 12.

26 Hivi ndivyo vilivyokuwa vikundi vya walinzi:+ kutoka kwa Wakora, Meshelemia+ mwana wa Kore wa wana wa Asafu. 2 Na Meshelemia alikuwa na wana: Zekaria mzaliwa wa kwanza, wa pili Yediaeli, wa tatu Zebadia, wa nne Yathnieli, 3 wa tano Elamu, wa sita Yehohanani, wa saba Elieho-enai. 4 Na Obed-edomu alikuwa na wana: Shemaya mzaliwa wa kwanza, wa pili Yehozabadi, wa tatu Yoa, wa nne Sakari, wa tano Nethaneli, 5 wa sita Amieli, wa saba Isakari, na wa nane Peulethai; kwa maana Mungu alikuwa amembariki.

6 Na Shemaya mwana wake alizaa wana waliokuwa viongozi wa koo zao,* kwa maana walikuwa wanaume hodari wenye uwezo. 7 Wana wa Shemaya walikuwa: Othni, Refaeli, Obedi, na Elzabadi; na Elihu na Semakia ndugu zake, walikuwa wanaume wenye uwezo pia. 8 Hao wote walikuwa wazao wa wana wa Obed-edomu; wao pamoja na wana wao na ndugu zao walikuwa wanaume wenye uwezo waliostahili kwa ajili ya utumishi huo, watu 62 wa Obed-edomu. 9 Na Meshelemia+ alikuwa na wana na ndugu, wanaume 18 wenye uwezo. 10 Na Hosa wa wana wa Merari alikuwa na wana. Shimri ndiye aliyekuwa kiongozi, kwa maana ingawa hakuwa mzaliwa wa kwanza, baba yake alimweka kuwa kiongozi, 11 wa pili Hilkia, wa tatu Tebalia, wa nne Zekaria. Wana wote wa Hosa na ndugu zake walikuwa 13.

12 Katika vikundi hivyo vya walinzi wa malango, viongozi walikuwa na kazi kama za ndugu zao, kuhudumu katika nyumba ya Yehova. 13 Kwa hiyo walipiga kura,+ mdogo sawa na mkubwa kulingana na koo zao,* kwa ajili ya malango mbalimbali. 14 Kura ya upande wa mashariki ilimwangukia Shelemia. Wakapiga kura kwa ajili ya Zekaria mwanawe, mshauri mwenye busara, aliangukiwa na kura ya upande wa kaskazini. 15 Obed-edomu alipata kura ya upande wa kusini, na wanawe+ walipewa kazi ya maghala. 16 Shupimu na Hosa+ walipata kura ya upande wa magharibi, karibu na Lango la Shalekethi kando ya barabara kuu inayoelekea juu, kikundi cha ulinzi karibu na kikundi kingine cha ulinzi; 17 kulikuwa na Walawi sita upande wa mashariki; wanne kila siku upande wa kaskazini, na wanne kila siku upande wa kusini; na kwenye maghala,+ wawili wawili; 18 kwa ajili ya baraza upande wa magharibi, kulikuwa na wanne kwenye barabara kuu+ na wawili barazani. 19 Hivyo ndivyo vilivyokuwa vikundi vya walinzi wa malango vya wana wa Wakora na wa Wamerari.

20 Kuhusu Walawi, Ahiya alisimamia hazina za nyumba ya Mungu wa kweli na hazina za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu.*+ 21 Wana wa Ladani: wana wa Mgershoni mwana wa Ladani, viongozi wa koo* za Ladani Mgershoni, kulikuwa na Yehieli+ 22 na wana wa Yehieli, Zethamu na Yoeli ndugu yake. Walisimamia hazina za nyumba ya Yehova.+ 23 Kutoka kwa Waamramu, Waishari, Wahebroni, na Wauzieli,+ 24 Shebueli mwana wa Gershomu mwana wa Musa alikuwa kiongozi aliyesimamia maghala. 25 Na kuhusu ndugu zake, kutoka kwa Eliezeri+ kulikuwa na Rehabia+ mwana wa Eliezeri, Yeshaya mwana wa Rehabia, Yoramu mwana wa Yeshaya, Zikri mwana wa Yoramu, na Shelomothi mwana wa Zikri. 26 Huyu Shelomothi na ndugu zake walisimamia hazina zote za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu,+ ambavyo Mfalme Daudi,+ viongozi wa koo,*+ wakuu wa maelfu na wa mamia, na wakuu wa jeshi walikuwa wamevifanya kuwa vitakatifu. 27 Baadhi ya vitu walivyopata vitani+ na baadhi ya nyara+ walizifanya kuwa takatifu ili kuidumisha nyumba ya Yehova; 28 pia, vitu vyote ambavyo Samweli mwonaji,+ Sauli mwana wa Kishi, Abneri+ mwana wa Neri, na Yoabu+ mwana wa Seruya+ walikuwa wamevifanya kuwa vitakatifu. Kitu chochote ambacho mtu yeyote alikifanya kuwa kitakatifu kiliwekwa chini ya usimamizi wa Shelomithi na ndugu zake.

29 Kutoka kwa Waishari,+ Kenania na wanawe walipewa kazi za nje za usimamizi wakiwa maofisa na waamuzi+ wa Israeli.

30 Kutoka kwa Wahebroni,+ Hashabia na ndugu zake, wanaume 1,700 wenye uwezo, waliwasimamia wakuu wa Israeli katika eneo lililokuwa upande wa magharibi wa Yordani kuhusiana na kazi zote za Yehova na utumishi wa mfalme. 31 Kutoka kwa Wahebroni, Yeriya+ alikuwa kiongozi wa Wahebroni kulingana na nasaba ya ukoo wao.* Katika mwaka wa 40 wa utawala wa Daudi,+ walitafutwa, na wanaume hodari wenye uwezo wakapatikana miongoni mwao kule Yazeri,+ Gileadi. 32 Na ndugu zake walikuwa 2,700, wanaume wenye uwezo, viongozi wa koo.* Basi Mfalme Daudi akawaweka wawasimamie watu wa kabila la Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, katika kila jambo la Mungu wa kweli na la mfalme.

27 Hii ndiyo idadi ya Waisraeli, viongozi wa koo,* wakuu wa maelfu na wa mamia,+ na maofisa wao waliomhudumia mfalme+ katika kila jambo lililohusu vikundi ambavyo viliingia ndani na kutoka nje mwezi baada ya mwezi, miezi yote ya mwaka; kila kikundi kilikuwa na watu 24,000.

2 Msimamizi wa kikundi cha kwanza kwa ajili ya mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu+ mwana wa Zabdieli, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 3 Kati ya wana wa Perezi,+ yeye ndiye aliyekuwa kiongozi wa wakuu wote wa vikundi vilivyopewa zamu ya kutumikia katika mwezi wa kwanza. 4 Msimamizi wa kikundi cha mwezi wa pili alikuwa Dodai+ Mwahohi,+ na Miklothi ndiye aliyekuwa kiongozi, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 5 Msimamizi wa kikundi cha tatu kilichopewa zamu ya kutumikia katika mwezi wa tatu alikuwa Benaya+ mwana wa Yehoyada+ mkuu wa makuhani, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 6 Huyo Benaya alikuwa shujaa hodari miongoni mwa wale 30 na ndiye aliyekuwa msimamizi wao, na kiongozi wa kikundi chake alikuwa Amizabadi mwanawe. 7 Msimamizi wa nne kwa ajili ya mwezi wa nne alikuwa Asaheli,+ ndugu ya Yoabu,+ na baada yake Zebadia mwanawe, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 8 Msimamizi wa tano kwa ajili ya mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahia, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 9 Msimamizi wa sita kwa ajili ya mwezi wa sita alikuwa Ira+ mwana wa Ikeshi Mtekoa,+ na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 10 Msimamizi wa saba kwa ajili ya mwezi wa saba alikuwa Helezi+ Mpeloni kutoka kwa Waefraimu, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 11 Msimamizi wa nane kwa ajili ya mwezi wa nane alikuwa Sibekai+ Mhusha kutoka kwa Wazera,+ na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 12 Msimamizi wa tisa kwa ajili ya mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri+ Mwanathothi+ kutoka kwa Wabenjamini, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 13 Msimamizi wa kumi kwa ajili ya mwezi wa kumi alikuwa Maharai+ Mnetofa kutoka kwa Wazera,+ na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 14 Msimamizi wa 11 kwa ajili ya mwezi wa 11 alikuwa Benaya+ Mpirathoni kutoka kwa wana wa Efraimu, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 15 Msimamizi wa 12 kwa ajili ya mwezi wa 12 alikuwa Heldai Mnetofa, wa Othnieli, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000.

16 Hawa ndio waliokuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Wa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri; wa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maaka; 17 wa kabila la Lawi, Hashabia mwana wa Kemueli; wa wazao wa Haruni, Sadoki; 18 wa kabila la Yuda, Elihu,+ mmoja wa ndugu za Daudi; wa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli; 19 wa kabila la Zabuloni, Ishmaya mwana wa Obadia; wa kabila la Naftali, Yerimothi mwana wa Azrieli; 20 wa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia; wa nusu ya kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaya; 21 wa nusu ya kabila la Manase kule Gileadi, Ido mwana wa Zekaria; wa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri;+ 22 wa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa wakuu wa makabila ya Israeli.

23 Daudi hakuwahesabu wale waliokuwa na umri wa miaka 20 kurudi chini, kwa sababu Yehova alikuwa ameahidi kwamba angewafanya Waisraeli wawe wengi kama nyota za mbinguni.+ 24 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa ameanza kuwahesabu, lakini hakumaliza; hasira ya Mungu iliwaka dhidi ya Waisraeli kwa sababu ya jambo hilo,+ na idadi hiyo haikuandikwa katika masimulizi ya historia ya nyakati za Mfalme Daudi.

25 Azmavethi mwana wa Adieli ndiye aliyesimamia hazina za mfalme.+ Yonathani mwana wa Uzia alisimamia maghala yaliyokuwa* mashambani, katika majiji, vijijini, na katika minara. 26 Ezri mwana wa Kelubu aliwasimamia wafanyakazi waliolima mashamba. 27 Shimei Mrama alisimamia mashamba ya mizabibu; Zabdi Mshifi alisimamia maghala ya divai iliyotengenezwa kwa zabibu zilizozalishwa katika mashamba ya mizabibu. 28 Baal-hanani Mgederi alisimamia mashamba ya mizeituni na mikuyu+ katika Shefela;+ Yoashi alisimamia maghala ya mafuta. 29 Shitrai Msharoni alisimamia makundi ya ng’ombe yaliyolisha kule Sharoni,+ na Shafati mwana wa Adlai alisimamia makundi ya ng’ombe katika mabonde tambarare.* 30 Obili Mwishmaeli alisimamia ngamia; Yehdeya Mmeronothi alisimamia punda. 31 Yazizi Mhagri alisimamia makundi ya kondoo na mbuzi. Hao wote ndio waliokuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi.

32 Yonathani,+ mpwa wa Daudi, alikuwa mshauri, mwanamume mwenye uelewaji na pia mwandishi, na Yehieli mwana wa Hakmoni aliwatunza wana wa mfalme.+ 33 Ahithofeli+ alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai+ Mwarki alikuwa rafiki ya* mfalme. 34 Baada ya Ahithofeli kulikuwa na Yehoyada mwana wa Benaya+ na Abiathari;+ na Yoabu+ alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.

28 Kisha Daudi akawakusanya Yerusalemu wakuu wote wa Israeli: wakuu wa makabila, viongozi wa vikundi+ vilivyomhudumia mfalme, wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia,+ wasimamizi wa mali zote za mfalme na mifugo yake+ na wa wanawe,+ pamoja na maofisa wa makao ya mfalme na kila mwanamume hodari mwenye uwezo.+ 2 Halafu Mfalme Daudi akasimama na kusema:

“Nisikilizeni, ndugu zangu na watu wangu. Moyo wangu ulitamani kujenga nyumba ambamo sanduku la agano la Yehova lingekaa* na ambayo ingekuwa kiti cha miguu cha Mungu wetu,+ nami nilifanya matayarisho ya kuijenga.+ 3 Lakini Mungu wa kweli akaniambia, ‘Hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ kwa maana wewe ni mtu wa vita, nawe umemwaga damu.’+ 4 Hata hivyo, Yehova Mungu wa Israeli alinichagua kutoka katika nyumba yote ya baba yangu niwe mfalme wa Israeli milele,+ kwa maana alimchagua Yuda kuwa kiongozi+ na kutoka katika nyumba ya Yuda aliichagua nyumba ya baba yangu,+ na kati ya wana wa baba yangu alinikubali mimi niwe mfalme wa Israeli yote.+ 5 Na kutoka kati ya wanangu wote—kwa maana Yehova amenipa wana wengi+—alimchagua Sulemani mwanangu+ aketi kwenye kiti cha ufalme wa Yehova juu ya Israeli.+

6 “Akaniambia, ‘Sulemani mwana wako ndiye atakayeijenga nyumba yangu na nyua zangu, kwa maana nimemchagua yeye kuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake.+ 7 Nitauimarisha kabisa ufalme wake milele+ ikiwa atazishika kwa dhati amri zangu na sheria zangu,*+ kama anavyofanya sasa.’ 8 Basi, nasema machoni pa Waisraeli wote, kutaniko la Yehova, na masikioni mwa Mungu wetu: Shikeni kwa uangalifu na mtafute amri zote za Yehova Mungu wenu, ili mwimiliki nchi nzuri+ na kuwaachia wana wenu kuwa urithi wa kudumu baada yenu.

9 “Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako na kumtumikia kwa moyo kamili*+ na kwa nafsi* yenye shangwe;* kwa maana Yehova huichunguza kabisa mioyo yote,+ naye hutambua kila mwelekeo wa fikira.+ Ukimtafuta, atakuruhusu umpate,+ lakini ukimwacha, atakukataa milele.+ 10 Ona kwamba Yehova amekuchagua wewe ujenge nyumba ili iwe mahali patakatifu. Uwe jasiri, anza kazi.”

11 Kisha Daudi akampa Sulemani mwana wake ramani ya ujenzi+ wa ukumbi+ na ya nyumba zake, maghala yake, vyumba vyake vya darini, vyumba vyake vya ndani, na nyumba ya kifuniko cha upatanisho.*+ 12 Alimpa ramani ya kila kitu alichoambiwa kupitia mwongozo wa roho kuhusu ujenzi wa nyua+ za nyumba ya Yehova, vyumba vyote vya kulia chakula vilivyoizunguka, hazina za nyumba ya Mungu wa kweli, na hazina za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu;*+ 13 pia kuhusu vikundi vya makuhani+ na Walawi, kuhusu kazi zote za utumishi wa nyumba ya Yehova, na kuhusu vyombo vyote vya utumishi wa nyumba ya Yehova; 14 pia kuhusu uzito wa dhahabu, dhahabu ya vyombo vyote vya utumishi mbalimbali, uzito wa vyombo vyote vya fedha, na vyombo vyote vya utumishi mbalimbali; 15 pia uzito wa vinara vya taa vya dhahabu+ na taa zake za dhahabu, uzito wa vinara mbalimbali vya taa na taa zake, na uzito wa vinara vya taa vya fedha, uzito wa kila kinara cha taa na taa zake kulingana na matumizi yake; 16 pia kuhusu uzito wa dhahabu za meza za mikate ya tabaka,*+ uzito wa kila meza, na pia fedha kwa ajili ya meza za fedha, 17 kuhusu nyuma,* mabakuli, magudulia ya dhahabu safi, na uzito wa mabakuli madogo ya dhahabu,+ uzito wa kila bakuli dogo, na uzito wa mabakuli madogo ya fedha, uzito wa kila bakuli dogo. 18 Pia alimpa uzito wa dhahabu safi kwa ajili ya madhabahu ya uvumba+ na kwa ajili ya mfano wa lile gari,+ yaani, wale makerubi+ wa dhahabu walionyoosha mabawa yao na kulifunika sanduku la agano la Yehova. 19 Daudi akasema: “Mkono wa Yehova ulikuwa juu yangu, naye alinipa ufahamu wa kuandika+ mambo yote kuhusu ramani hii ya ujenzi.”+

20 Kisha Daudi akamwambia Sulemani mwanawe: “Uwe jasiri na imara na uanze kazi. Usiogope wala usihofu, kwa maana Yehova Mungu, Mungu wangu, yuko pamoja nawe.+ Hatakuacha wala kukutupa,+ lakini atakuwa pamoja nawe mpaka kazi yote ya utumishi wa nyumba ya Yehova itakapokamilika. 21 Na hivi ndivyo vikundi vya makuhani+ na vya Walawi+ kwa ajili ya utumishi wote wa nyumba ya Mungu wa kweli. Una wafanyakazi walio tayari, na wenye ustadi wa kufanya utumishi wa kila aina,+ na pia wakuu+ na watu wote watakaotekeleza maagizo yako yote.”

29 Sasa Mfalme Daudi akaliambia kutaniko lote: “Mwanangu Sulemani, ambaye Mungu amemchagua+ ni mchanga na hana uzoefu,*+ na kazi hii ni kubwa, kwa maana si hekalu* kwa ajili ya mwanadamu, bali ni kwa ajili ya Yehova Mungu.+ 2 Nami nimejitahidi kabisa kufanya matayarisho kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu, nimetoa dhahabu ya kutengenezea vitu vya dhahabu, fedha ya kutengenezea vitu vya fedha, shaba ya kutengenezea vitu vya shaba, chuma kwa ajili ya vitu vya chuma,+ mbao+ za kutengenezea vitu vya mbao, mawe ya shohamu, na vito vinavyounganishwa kwa saruji, na vijiwe maridadi vya mviringo, kila aina ya mawe yenye thamani, na mawe mengi sana ya alabasta. 3 Isitoshe, kwa sababu ninaipenda nyumba ya Mungu wangu,+ ninatoa pia hazina yangu binafsi+ ya dhahabu na fedha kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu, pamoja na vitu vyote nilivyotayarisha kwa ajili ya nyumba hiyo takatifu, 4 na pia talanta 3,000* za dhahabu ya Ofiri+ na talanta 7,000 za fedha iliyosafishwa, ili zitumiwe kufunika kuta za nyumba, 5 dhahabu ya kutengenezea vitu vya dhahabu na fedha ya kutengenezea vitu vya fedha, na kwa ajili ya kazi yote itakayofanywa na mafundi. Basi ni nani anayejitolea kuja leo akiwa na zawadi mkononi kwa ajili ya Yehova?”+

6 Basi wakuu wa koo,* wakuu wa makabila ya Israeli, wakuu wa maelfu na wa mamia,+ na wakuu wa kazi za mfalme+ wakajitolea kwa hiari. 7 Nao wakatoa kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli: talanta 5,000 za dhahabu, dariki 10,000,* talanta 10,000 za fedha, talanta 18,000 za shaba, na talanta 100,000 za chuma. 8 Mtu yeyote aliyekuwa na mawe yenye thamani aliyatoa kwa ajili ya hazina ya nyumba ya Yehova, chini ya usimamizi wa Yehieli+ Mgershoni.+ 9 Watu walishangilia kwa sababu walitoa matoleo hayo ya hiari, kwa maana walimtolea Yehova matoleo hayo ya hiari kwa moyo kamili,+ na Mfalme Daudi pia alishangilia sana.

10 Kisha Daudi akamsifu Yehova mbele ya kutaniko lote. Daudi akasema: “Na usifiwe, Ee Yehova Mungu wa Israeli baba yetu, kwa umilele wote.* 11 Ee Yehova, ukuu ni wako+ na nguvu+ na uzuri na fahari na utukufu,*+ kwa maana kila kitu mbinguni na duniani ni chako.+ Ufalme ni wako, Ee Yehova.+ Wewe Ndiye unayejikweza mwenyewe ukiwa mkuu* juu ya vyote. 12 Utajiri na utukufu hutoka kwako,+ nawe hutawala kila kitu,+ na mkononi mwako mna nguvu+ na uwezo,+ na mkono wako unaweza kumfanya mtu awe mkuu+ na unaweza kuwapa wote nguvu.+ 13 Na sasa, Ee Mungu wetu, tunakushukuru na kulisifu jina lako linalovutia.

14 “Lakini, mimi ni nani na watu wangu ni nani hivi kwamba tukutolee matoleo haya ya hiari? Kwa maana kila kitu kinatoka kwako, nasi tumekupa vitu vinavyotoka mkononi mwako mwenyewe. 15 Kwa maana sisi ni wakaaji wageni mbele zako na wahamiaji, kama walivyokuwa mababu zetu wote.+ Kwa kuwa siku zetu duniani ni kama kivuli+—hatuna tumaini. 16 Ee Yehova Mungu wetu, utajiri huu wote ambao tumetayarisha ili kukujengea nyumba kwa ajili ya jina lako takatifu unatoka mkononi mwako mwenyewe, wote ni mali yako. 17 Ee Mungu wangu, najua vizuri kwamba wewe huuchunguza moyo,+ na kwamba unapendezwa na utimilifu.*+ Kwa unyoofu wa moyo wangu, nimetoa kwa hiari vitu hivi vyote, nami nimefurikwa na shangwe kuwaona watu wako walio hapa wakikutolea matoleo ya hiari. 18 Ee Yehova, Mungu wa Abrahamu, Isaka, na Israeli, mababu zetu, idumishe mielekeo hii na fikira hizi katika mioyo ya watu wako milele, na uielekeze mioyo yao kwako.+ 19 Mpe mwanangu Sulemani moyo kamili,*+ ili ashike amri zako, vikumbusho vyako,+ na masharti yako na kufanya mambo haya yote na kujenga hekalu* ambalo nimelifanyia matayarisho.”+

20 Kisha Daudi akaliambia kutaniko lote: “Sasa msifuni Yehova Mungu wenu.” Na kutaniko lote likamsifu Yehova Mungu wa mababu zao, wakainama chini na kumsujudia Yehova na mfalme. 21 Nao wakaendelea kumtolea Yehova dhabihu na kumtolea Yehova dhabihu za kuteketezwa+ siku iliyofuata, ng’ombe dume wachanga 1,000, kondoo dume 1,000, wanakondoo dume 1,000, na matoleo yake ya vinywaji;+ walitoa dhabihu nyingi sana kwa ajili ya Waisraeli wote.+ 22 Wakaendelea kula na kunywa mbele za Yehova siku hiyo kwa shangwe nyingi,+ nao wakamweka Sulemani mwana wa Daudi kuwa mfalme kwa mara ya pili na kumtia mafuta mbele za Yehova ili awe kiongozi,+ na pia Sadoki kuwa kuhani.+ 23 Na Sulemani akaketi kwenye kiti cha ufalme cha Yehova+ akiwa mfalme baada ya Daudi baba yake, akafanikiwa, na Waisraeli wote walimtii. 24 Wakuu wote,+ mashujaa wote hodari,+ na pia wana wote wa Mfalme Daudi+ wakajitiisha wenyewe chini ya Mfalme Sulemani. 25 Na Yehova akamfanya Sulemani kuwa mkuu sana machoni pa Waisraeli wote na kumpa fahari ya kifalme ambayo hakuna mfalme yeyote wa Israeli aliyewahi kuwa nayo kabla yake.+

26 Kwa hiyo Daudi mwana wa Yese alitawala Israeli yote, 27 alitawala Israeli kwa miaka 40. Alitawala huko Hebroni kwa miaka 7,+ na Yerusalemu kwa miaka 33.+ 28 Naye akafa akiwa amezeeka kabisa;+ aliishi maisha marefu yenye kuridhisha, akiwa na utajiri, na utukufu; na Sulemani mwanawe akawa mfalme baada yake.+ 29 Historia ya Mfalme Daudi, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, imeandikwa katika maandishi ya mwonaji Samweli, nabii Nathani,+ na mwonaji Gadi,+ 30 pamoja na utawala wake wote, ukuu wake, na matukio yanayohusu nyakati zake na nyakati za Israeli na falme zote zilizomzunguka.

Wafuatao ni wana wa Aramu. Angalia Mwa 10:23.

Maana yake “Mgawanyiko.”

Au “wakaaji wa dunia walikuwa wamegawanyika.”

Tnn., “Wana.”

Tnn., “wana wa Israeli.”

Tnn., “shamba.”

Shehe alikuwa mkuu wa kabila.

Tnn., “Wana.”

Maana yake “Mleta Msiba; Anayesababisha Watu Watengwe.” Katika Yos 7:1, anaitwa pia Akani.

Au “taabu; aliyesababisha watengwe.”

Tnn., “Wana.”

Pia anaitwa Kalebu katika mstari wa 18, 19, na 42.

Pia anaitwa Kelubai katika mstari wa 9.

Tnn., “wana.”

Tnn., “Wana.”

Tnn., “wana.”

Tnn., “wana.”

Tnn., “wana.”

Pia anaitwa Kelubai katika mstari wa 9.

Tnn., “wana.”

Tnn., “wana.”

Tnn., “wana.”

Tnn., “wana.”

Huenda jina Yabesi linahusiana na neno la Kiebrania linalomaanisha “uchungu.”

Tnn., “wana.”

Maana yake “Bonde la Mafundi.”

Tnn., “wana.”

Inawezekana ni Bithia anayetajwa katika mstari wa 18.

Au “Maneno haya ni ya utamaduni wa kale.”

Au “alikitia unajisi.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, Yeroboamu wa Pili.

Tnn., “na kukanyaga upinde.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “Wana.”

Pia anaitwa Gershoni katika mstari wa 1.

Au “Wazao.”

Au “Wazao.”

Tnn., “lipumzike.”

Tnn., “walitolewa.”

Au “kambi zao zilizozingirwa na kuta.”

Au labda, “jiji hili la,” kulingana na Yos 21:13.

Au “walipewa kwa kura.”

Au labda, “jiji la,” kulingana na Yos 21:21.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “wana.”

Tnn., “viongozi.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “wana.”

Tnn., “wana.”

Maana yake “Wakati wa Msiba.”

Au “Yehoshua,” linalomaanisha “Yehova Ni Wokovu.”

Au labda, “Gaza,” ingawa si jiji la Gaza kule Ufilisti.

Pia anaitwa Shomeri katika mstari wa 32.

Inaelekea ni sawa na “Hothamu” katika mstari wa 32.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “shamba.”

Au labda, “baada ya kuwafukuza wake zake Hushimu na Baara.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Pia aliitwa Ish-boshethi.

Pia aliitwa Mefiboshethi.

Tnn., “kukanyaga.”

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Tnn., “vichwa vya akina baba kwa ajili ya nyumba za baba zao.”

Au “hekalu la.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “wenye uwezo.”

Au “vyumba vya kulia chakula.”

Yaani, mikate ya wonyesho.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “vyumba vya kulia chakula.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “wasije kunitesa.”

Au “katika nchi tambarare ya chini.”

Au “hekalu la.”

Tnn., “Tuna uhusiano wa damu nawe.”

Tnn., “uliyekuwa ukiwatoa nje na kuwaingiza ndani Waisraeli.”

Tnn., “kichwa.”

Au “Milo.” Neno la Kiebrania linalomaanisha “jaza.”

Au “wokovu.”

Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”

Au “nafsi zao.”

Tnn., “mwana wa mwanamume jasiri.”

Urefu wake ulikuwa karibu mita 2.23 (futi 7.3). Angalia Nyongeza B14.

Angalia Kamusi.

Au “walikuwa wepesi.”

Tnn., “ikamvaa.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “wote waliojiunga na Daudi hawakuwa na mioyo miwili.”

Tnn., “walikuwa na moyo mmoja katika.”

Au “kuanzia Shihori huko Misri.”

Au “njia ya kuingia Hamathi.”

Au labda, “katikati ya.”

Maana yake “Ghadhabu Dhidi ya Uza.”

Au “wajenzi wa kuta.”

Au “jumba la mfalme.”

Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”

Maana yake “Bwana Anayepasua na Kupita.”

Au “kwenye nchi tambarare ya chini.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Angalia Kamusi.

Angalia Kamusi.

Tnn., “wamkumbuke.”

Au “alichangia.”

Au “mpigieni muziki.”

Au labda, “Zungumzeni kuhusu.”

Au “uwepo.”

Au “wazao wa.” Tnn., “mbegu ya.”

Tnn., “Neno aliloamuru.”

Au “adhama.”

Au “Mwabuduni.”

Au labda, “kwa sababu ya fahari ya utakatifu wake.”

Au “kutikiswa; kufanywa ipepesuke.”

Au “amekuja.”

Au “milele na milele.”

Au “Na iwe hivyo!”

Au “na ala za wimbo wa.”

Au “jumba lake mwenyewe la mfalme.”

Labda inamaanisha “kutoka kambi moja ya mahema hadi nyingine na kutoka eneo moja la kuishi hadi lingine.”

Tnn., “hawatawachosha.”

Au “ukoo wa kifalme.”

Tnn., “nitainua mbegu yako.”

Au “mtu mwenye cheo kikubwa.”

Au “kulingana na mapenzi yako.”

Au “ukoo wa kifalme.”

Au “wokovu.”

Au “wokovu.”

Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.

Tnn., “Aram-naharaimu.”

Tnn., “mikononi mwa.”

Yaani, majira ya kuchipua.

Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.

Au labda, “mpinzani.”

Au “kuhuzunika.”

Tnn., “Nipe.”

Tnn., “kilicho chema machoni pako.”

Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.

Au “hana uwezo.”

Tnn., “mtulivu.”

Linatokana na neno la Kiebrania linalomaanisha “Amani.”

Tnn., “hukumu.”

Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.

Angalia Kamusi.

Tnn., “akiwa amezeeka na akiwa amejaa siku.”

Tnn., “kichwa kwa kichwa.”

Au “akawagawa.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “wana.”

Tnn., “ndugu zao.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, mikate ya wonyesho.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “kuinua pembe yake.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “vitu vilivyowekwa wakfu.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Tnn., “hazina zilizokuwa.”

Tnn., “nchi tambarare za chini.”

Au “msiri wa.”

Tnn., “lingepumzikia.”

Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”

Au “wenye ujitoaji kamili.”

Angalia Kamusi.

Au “kwa hiari.”

Au “nyumba ya kufunika dhambi.”

Au “vilivyowekwa wakfu.”

Yaani, mikate ya wonyesho.

Wingi wa kifaa kinachoitwa uma.

Au “hana uwezo.”

Au “ngome; jumba la mfalme.”

Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Dariki ilikuwa sarafu ya dhahabu ya Waajemi. Angalia Nyongeza B14.

Au “milele na milele.”

Au “adhama.”

Tnn., “kichwa.”

Au “hali ya kutokuwa na lawama; unyoofu.”

Au “wenye ujitoaji kamili.”

Au “ngome au jumba la mfalme.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki