Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • nwt Nehemia 1:1-13:31
  • Nehemia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nehemia
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Nehemia

NEHEMIA

1 Maneno ya Nehemia*+ mwana wa Hakalia: Sasa katika mwezi wa Kislevu,* mwaka wa 20, mimi nilikuwa katika ngome ya* Shushani.*+ 2 Wakati huo Hanani,+ mmoja wa ndugu zangu, akaja pamoja na watu wengine kutoka Yuda, nami nikawauliza kuhusu Wayahudi waliobaki walioponyoka kutoka utekwani,+ na pia kuhusu Yerusalemu. 3 Wakanijibu: “Wale waliobaki na kuponyoka utekwani ambao wamebaki katika mkoa* ule wako katika hali mbaya sana na yenye kuaibisha.+ Kuta za Yerusalemu zimebomolewa,+ na malango yake yameteketezwa kwa moto.”+

4 Mara tu niliposikia maneno hayo, nikaketi chini na kuanza kulia na kuomboleza kwa siku nyingi, nami nikaendelea kufunga+ na kusali mbele za Mungu wa mbinguni. 5 Nikasema: “Ee Yehova, Mungu wa mbinguni, Mungu mkuu na mwenye kuogopesha, unayeshika agano lako na kuwatendea kwa upendo mshikamanifu wale wanaokupenda na kushika amri zako,+ 6 tafadhali, tega sikio lako na ufungue macho yako ili usikilize sala ambayo mimi mtumishi wako ninakutolea leo, mchana na usiku,+ kuhusu watumishi wako Waisraeli, nikiungama dhambi ambazo watu wa Israeli wamekutendea. Tumetenda dhambi, mimi pamoja na nyumba ya baba yangu.+ 7 Kwa hakika tumetenda mambo mapotovu dhidi yako+ kwa kuwa hatukushika amri, masharti, na sheria ulizompa* mtumishi wako Musa.+

8 “Tafadhali, kumbuka neno ulilomwamuru* Musa mtumishi wako, ukisema: ‘Msipotenda kwa uaminifu, nitawatawanya miongoni mwa mataifa.+ 9 Lakini mkinirudia na kuzishika amri zangu na kuzitii, hata ingawa mtakuwa mmetawanyika mpaka kwenye mwisho wa mbingu, nitawakusanya+ na kuwaleta mahali ambapo nimepachagua ili jina langu likae hapo.’+⁠ 10 Wao ni watumishi wako na watu wako, uliowakomboa kwa uwezo wako mkubwa na kwa mkono wako wenye nguvu.+ 11 Ee Yehova, tafadhali, tega sikio lako usikilize sala yangu mimi mtumishi wako na sala ya watumishi wako wanaofurahia kulihofu jina lako, na tafadhali, nipe mimi mtumishi wako mafanikio leo, ili mtu huyu anihurumie.”+

Basi mimi nilikuwa msimamizi wa vinywaji vya mfalme.+

2 Katika mwezi wa Nisani,* mwaka wa 20+ wa utawala wa Mfalme Artashasta,+ divai ililetwa mbele yake, nami kama kawaida, nikaichukua divai hiyo na kumpa mfalme.+ Lakini sikuwahi kuonekana nikiwa mwenye huzuni mbele yake. 2 Ndipo mfalme akaniambia: “Kwa nini unaonekana umehuzunika sana na wewe si mgonjwa? Lazima una huzuni moyoni.” Ndipo nikaogopa sana.

3 Kisha nikamwambia mfalme: “Mfalme na aishi muda mrefu! Kwa nini nisiwe na huzuni wakati lile jiji, mahali ambapo mababu zangu wamezikwa ni magofu, na malango yake yameteketezwa kwa moto?”+ 4 Ndipo mfalme akaniuliza: “Basi unataka nini?” Mara moja nikasali kwa Mungu wa mbinguni.+ 5 Kisha nikamjibu mfalme: “Ukipenda, Ee mfalme, na ikiwa mimi mtumishi wako nimepata kibali chako, niruhusu niende Yuda, kwenye jiji ambalo mababu zangu wamezikwa ili nilijenge upya.”+ 6 Ndipo mfalme akaniuliza hivi huku malkia wake akiwa ameketi kando yake: “Safari yako itachukua muda gani, nawe utarudi lini?” Basi jambo hilo likampendeza mfalme, akaniruhusu niende,+ nami nikamwambia muda hususa.+

7 Kisha nikamwambia mfalme: “Ukipenda, Ee mfalme, naomba nipewe barua niwapelekee magavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto,*+ ili waniruhusu kupita hadi nifike Yuda salama salimini, 8 pia barua nimpelekee Asafu mtunzaji wa Bustani ya Mfalme,* ili anipe mbao za kujengea mihimili ya malango ya Ngome+ ya ile Nyumba* na kuta za jiji+ na nyumba nitakayoishi.” Basi mfalme akanipa barua hizo,+ kwa sababu mkono mwema wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu.+

9 Mwishowe nikafika kwa magavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto na kuwapa barua za mfalme. Pia, mfalme alinipa wakuu wa jeshi na wapanda farasi. 10 Sanbalati+ Mhoroni na Tobia+ ofisa* Mwamoni+ waliposikia jambo hilo, walikasirika sana kwa sababu mtu fulani alikuwa amekuja kuwatendea watu wa Israeli jambo jema.

11 Hatimaye nikafika Yerusalemu, nami nikakaa huko kwa siku tatu. 12 Nikaondoka usiku, mimi pamoja na wanaume wachache, nami sikumwambia mtu yeyote mambo ambayo Mungu wangu alikuwa ameweka moyoni mwangu ili nilifanyie jiji la Yerusalemu, wala sikuwa na mnyama mwingine ila mnyama aliyenibeba. 13 Nikatoka nje usiku kupitia Lango la Bondeni,+ nikapita mbele ya Chemchemi ya Nyoka Mkubwa, nikaelekea kwenye Lango la Marundo ya Majivu,+ nami nikachunguza kuta za Yerusalemu zilizokuwa zimebomolewa na malango yake yaliyokuwa yameteketezwa kwa moto.+ 14 Kisha nikapita kuelekea kwenye Lango la Chemchemi+ na kuelekea kwenye Kidimbwi cha Mfalme, lakini mnyama aliyenibeba hangeweza kupita kwa sababu hapakuwa na nafasi ya kutosha. 15 Hata hivyo, nikaendelea kupanda juu bondeni*+ usiku, nami nikaendelea kuukagua ukuta, nami nikaingia kupitia Lango la Bondeni, kisha nikarudi.

16 Watawala wasaidizi+ hawakujua nilikokwenda au jambo nililokuwa nikifanya, kwa sababu sikuwa nimewaambia Wayahudi jambo lolote, wala makuhani, wala wakuu, wala watawala wasaidizi, wala wafanyakazi wengineo. 17 Hatimaye nikawaambia: “Mnaona hali mbaya sana tunayokabili, jinsi Yerusalemu lilivyobaki magofu na malango yake yameteketezwa kwa moto. Njooni, tujenge upya kuta za Yerusalemu, ili aibu hii isiendelee.” 18 Kisha nikawaambia jinsi mkono mwema wa Mungu wangu ulivyokuwa juu yangu+ na pia maneno ambayo mfalme alikuwa ameniambia.+ Ndipo wakasema: “Twendeni tukajenge.” Basi wakaimarishana* ili kufanya kazi hiyo njema.+

19 Sasa Sanbalati Mhoroni, Tobia+ ofisa* Mwamoni,+ na Geshemu Mwarabu+ waliposikia jambo hilo, wakaanza kutudhihaki+ na kutudharau wakisema: “Mnafanya nini? Je, mnamwasi mfalme?”+ 20 Lakini nikawajibu: “Mungu wa mbinguni, Ndiye atakayetufanikisha,+ nasi watumishi wake tutasimama na kujenga; lakini ninyi hamna fungu wala haki ya kudai chochote wala kumbukumbu* katika Yerusalemu.”+

3 Kuhani mkuu Eliashibu+ na ndugu zake makuhani wakaanza kujenga Lango la Kondoo.+ Wakalitakasa*+ na kuweka milango yake; wakalitakasa mpaka kwenye Mnara wa Mea,+ na mpaka kwenye Mnara wa Hananeli.+ 2 Sehemu iliyofuata ilikuwa ikijengwa na watu wa Yeriko;+ na sehemu iliyofuata ikajengwa na Zakuri mwana wa Imri.

3 Wana wa Hasenaa walijenga Lango la Samaki;+ walilitengeneza kwa mbao,+ wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake. 4 Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Meremothi+ mwana wa Uriya mwana wa Hakozi, naye Meshulamu+ mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli akarekebisha sehemu iliyofuata, naye Sadoki mwana wa Baana akarekebisha sehemu iliyofuata. 5 Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Watekoa,+ lakini watu wao mashuhuri hawakutaka kujishusha ili kushiriki kufanya* utumishi wa mabwana wao.

6 Yoyada mwana wa Pasea na Meshulamu mwana wa Besodeya wakarekebisha Lango la Jiji la Kale;+ walilitengeneza kwa mbao, wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake. 7 Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Melatia Mgibeoni+ na Yadoni Mmeronothi, watu wa Gibeoni na Mispa,+ waliokuwa chini ya mamlaka ya* gavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto.*+ 8 Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa mafundi wa dhahabu, na sehemu iliyofuata ikarekebishwa na Hanania, mmoja wa watengenezaji wa marashi;* nao wakatandaza mawe* Yerusalemu mpaka kwenye Ukuta Mpana.+ 9 Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Refaya mwana wa Huru, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu. 10 Kisha Yedaya mwana wa Harumafu akarekebisha sehemu iliyofuata, yaani, mbele ya nyumba yake mwenyewe, na sehemu iliyofuata ikarekebishwa na Hatushi mwana wa Hashabneya.

11 Malkiya mwana wa Harimu+ na Hashubu mwana wa Pahath-moabu+ wakarekebisha sehemu nyingine,* na pia Mnara wa Majiko ya Kuokea.+ 12 Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Shalumu mwana wa Haloheshi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, pamoja na mabinti zake.

13 Hanuni na wakaaji wa Zanoa+ walirekebisha Lango la Bondeni;+ wakalijenga na kuweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake, pia walirekebisha sehemu ya ukuta yenye urefu wa mikono 1,000* mpaka kwenye Lango la Marundo ya Majivu.+ 14 Malkiya mwana wa Rekabu, mkuu wa wilaya ya Beth-hakeremu+ alirekebisha Lango la Marundo ya Majivu; akalijenga na kuweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake.

15 Shaluni mwana wa Kolhoze, mkuu wa wilaya ya Mispa,+ alirekebisha Lango la Chemchemi;+ akalijenga na kuweka paa lake, milango yake, makomeo yake, na mapingo yake, na pia alirekebisha ukuta wa Kidimbwi+ cha Mfereji unaoelekea kwenye Bustani ya Mfalme+ mpaka kwenye Ngazi+ inayoshuka kutoka Jiji la Daudi.+

16 Baada yake Nehemia mwana wa Azbuki, mkuu wa nusu ya wilaya ya Beth-suri,+ alirekebisha kuanzia mbele ya Makaburi ya Daudi+ mpaka kwenye kidimbwi+ kilichokuwa kimetengenezwa hadi kwenye Nyumba ya Wenye Nguvu.

17 Walawi walirekebisha sehemu iliyofuata: Rehumu mwana wa Bani; na baada yake Hashabia, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila,+ akarekebisha kwa ajili ya wilaya yake. 18 Ndugu zao wakarekebisha sehemu iliyofuata: Bavai mwana wa Henadadi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila.

19 Sehemu iliyofuata, mbele ya njia inayopanda kuelekea Ghala la Silaha karibu na Nguzo ya Kutegemeza Ukuta,+ ilirekebishwa na Ezeri mwana wa Yeshua,+ mkuu wa Mispa.

20 Baada yake Baruku mwana wa Zabai+ akafanya kazi kwa bidii na kurekebisha sehemu nyingine, kuanzia Nguzo ya Kutegemeza Ukuta mpaka lango la nyumba ya kuhani mkuu Eliashibu.+

21 Meremothi+ mwana wa Uriya mwana wa Hakozi alirekebisha sehemu nyingine, kuanzia lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu.

22 Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na makuhani, wanaume wa wilaya ya Yordani.*+ 23 Kisha Benjamini na Hashubu wakarekebisha mbele ya nyumba yao wenyewe. Na baada yao Azaria mwana wa Maaseya mwana wa Ananiya akarekebisha karibu na nyumba yake. 24 Baada yake Binui mwana wa Henadadi akarekebisha sehemu nyingine, kuanzia nyumba ya Azaria mpaka kwenye Nguzo ya Kutegemeza Ukuta+ na mpaka pembeni.

25 Baada yake Palali mwana wa Uzai akarekebisha mbele ya Nguzo ya Kutegemeza Ukuta na mnara unaotoka katika Nyumba ya Mfalme,*+ upande wa juu wa Ua wa Walinzi.+ Baada yake kulikuwa na Pedaya mwana wa Paroshi.+

26 Na watumishi wa hekaluni*+ walioishi Ofeli+ wakafanya marekebisho hadi mbele ya Lango la Maji+ upande wa mashariki na mnara uliochomoza.

27 Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Watekoa,+ kutoka mbele ya ule mnara mkuu uliochomoza mpaka kwenye ukuta wa Ofeli.

28 Makuhani walirekebisha sehemu iliyo juu ya Lango la Farasi,+ kila mmoja mbele ya nyumba yake mwenyewe.

29 Kisha Sadoki+ mwana wa Imeri akarekebisha sehemu iliyokuwa mbele ya nyumba yake.

Na sehemu iliyofuata ikarekebishwa na Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki.+

30 Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Hanania mwana wa Shelemia na Hanuni mwana wa sita wa Zalafu.

Naye Meshulamu+ mwana wa Berekia akarekebisha sehemu iliyokuwa mbele ya jumba lake.

31 Malkiya, mshiriki wa chama cha mafundi wa dhahabu, alirekebisha sehemu iliyofuata mpaka kwenye nyumba ya watumishi wa hekaluni*+ na wafanyabiashara, mbele ya Lango la Ukaguzi mpaka kwenye chumba cha dari cha pembeni.

32 Mafundi wa dhahabu na wafanyabiashara walirekebisha sehemu iliyokuwa kati ya chumba cha dari cha pembeni na Lango la Kondoo.+

4 Mara tu Sanbalati+ aliposikia kwamba tunajenga upya ukuta, alishikwa na ghadhabu na kukasirika sana,* naye akazidi kuwadhihaki Wayahudi. 2 Akasema hivi mbele ya ndugu zake na jeshi la Samaria: “Wayahudi hawa wanyonge wanafanya nini? Je, watafanya kazi hii peke yao? Je, watatoa dhabihu? Je, watamaliza kwa siku moja? Je, watayatoa mawe yaliyoungua kutoka katika marundo ya vifusi ili yafae kwa ujenzi?”+

3 Basi Tobia+ Mwamoni,+ aliyekuwa amesimama kando yake, akasema: “Hata mbweha akipanda juu ya kile wanachojenga, atauangusha ukuta wao wa mawe.”

4 Sikiliza, Ee Mungu wetu, kwa maana tunadharauliwa;+ na urudishe dharau yao juu ya vichwa vyao wenyewe,+ nawe uwafanye wawe nyara na mateka katika nchi nyingine. 5 Usiifunike hatia yao wala usiifute dhambi yao kutoka mbele zako,+ kwa maana wamewatukana wajenzi.

6 Basi tukaendelea kujenga, na ukuta wote ukaungana kufikia nusu ya kimo chake, nao watu wakaendelea kufanya kazi kwa moyo wote.

7 Sasa mara tu Sanbalati, Tobia,+ Waarabu,+ Waamoni, na Waashdodi+ waliposikia kwamba kazi ya kurekebisha kuta za Yerusalemu inasonga mbele na kwamba mianya ilikuwa ikizibwa, wakakasirika sana. 8 Wakapanga njama pamoja ili kupigana na Yerusalemu na kuleta vurugu humo. 9 Lakini tulisali kwa Mungu wetu na kuweka walinzi dhidi yao mchana na usiku.

10 Hata hivyo, watu wa Yuda walikuwa wakisema: “Wafanyakazi* wameishiwa na nguvu, na kuna vifusi vingi sana; hatutafaulu kamwe kuujenga ukuta.”

11 Maadui wetu wakaendelea kusema: “Kabla hawajajua au kutuona, tutaingia kati yao, tuwaue, na kuikomesha kazi.”

12 Kila mara Wayahudi walioishi karibu nao walipokuja, walikuwa wakituambia tena na tena:* “Watatushambulia kutoka kila upande.”

13 Basi nikaweka wanaume kwenye sehemu za chini zaidi zilizo wazi nyuma ya ukuta, nikawapanga kulingana na familia zao, wakiwa na mapanga yao, mikuki yao, na pinde zao. 14 Nilipoona jinsi walivyoogopa, mara moja nikasimama na kuwaambia wakuu+ na watawala wasaidizi na watu wengine wote: “Msiwaogope.+ Mkumbukeni Yehova, ambaye ni mkuu na mwenye kuogopesha;+ nanyi mpigane kwa ajili ya ndugu zenu, wana wenu na mabinti zenu, wake zenu na nyumba zenu.”

15 Sasa baada ya maadui wetu kusikia kwamba tunajua walichokuwa wakifanya na kwamba Mungu wa kweli alikuwa amevuruga mpango wao, sote tukarudi kuujenga ukuta. 16 Tangu siku hiyo na kuendelea, nusu ya wanaume wangu walikuwa wakifanya kazi+ na nusu nyingine walikuwa wakishika mikuki, ngao, pinde, na kuvaa makoti ya vita. Na wakuu+ walisimama nyuma ya watu wote wa nyumba ya Yuda 17 waliokuwa wakijenga ukuta. Watu waliokuwa wakibeba mizigo walifanya kazi kwa mkono mmoja, huku wakiwa wameshika silaha kwa mkono mwingine. 18 Na kila mjenzi alikuwa amejifunga upanga kiunoni huku akijenga, na mtu wa kupiga pembe+ alikuwa amesimama kando yangu.

19 Ndipo nikawaambia wakuu na watawala wasaidizi na watu wengine wote: “Kazi hii ni kubwa na nzito, nasi tumetawanyika kwenye ukuta kila mmoja mbali na mwenzake. 20 Mtakaposikia mlio wa pembe, kusanyikeni mahali tulipo. Mungu wetu atatupigania.”+

21 Basi tukaendelea kufanya kazi huku nusu ya wanaume wakiwa wameshika mikuki, kuanzia mapambazuko mpaka nyota zilipoonekana. 22 Wakati huo nikawaambia watu: “Kila mwanaume na mtumishi wake na wakae ndani ya Yerusalemu usiku, nao watakuwa walinzi usiku na watafanya kazi mchana.” 23 Basi mimi, ndugu zangu, watumishi wangu,+ na walinzi waliofuatana nami hatukuvua mavazi yetu kamwe, na kila mmoja wetu aliendelea kushika silaha yake kwa mkono wa kulia.

5 Hata hivyo, watu na wake zao wakaanza kulalamika sana kuhusu ndugu zao Wayahudi.+ 2 Baadhi yao walikuwa wakisema: “Sisi na wana wetu na mabinti zetu ni wengi. Tunahitaji nafaka ili tule tuendelee kuishi.” 3 Na wengine walikuwa wakisema: “Tunatoa mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu yetu na nyumba zetu kuwa rehani ili tupate nafaka wakati wa njaa.” 4 Na wengine walikuwa wakisema: “Tumekopa pesa kwa kuweka rehani mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu ili kulipa ushuru wa mfalme.+ 5 Sasa sisi na ndugu zetu ni watu wa mwili mmoja na damu moja,* na watoto wetu ni sawa na watoto wao; lakini tumelazimika kuwafanya wana na mabinti zetu kuwa watumwa, na baadhi ya mabinti zetu tayari wako utumwani.+ Na hatuna uwezo wa kuzuia jambo hili, kwa sababu mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu yamechukuliwa na wengine.”

6 Nilikasirika sana niliposikia kilio chao na maneno hayo. 7 Kwa hiyo nikatafakari mambo hayo moyoni mwangu, kisha nikawashutumu wakuu na watawala wasaidizi na kuwaambia: “Kila mmoja wenu anamtoza riba* ndugu yake mwenyewe.”+

Pia, nikapanga kusanyiko kubwa kwa sababu yao. 8 Nikawaambia: “Kwa kadiri tulivyoweza, tumewanunua ndugu zetu wenyewe, Wayahudi, waliouzwa kwa mataifa; lakini je, sasa mtawauza ndugu zenu wenyewe,+ nasi tulazimike kuwanunua tena?” Ndipo wakanyamaza kimya, hawakuwa na lolote la kusema. 9 Kisha nikawaambia: “Jambo mnalofanya si jema. Je, hampaswi kutembea kwa kumwogopa Mungu+ wetu ili mataifa, maadui wetu, wasitushutumu? 10 Zaidi ya hayo, mimi, ndugu zangu, na watumishi wangu tunawakopesha pesa na nafaka. Tafadhali, tuache kukopesha kwa riba.+ 11 Tafadhali, warudishieni leo hii mashamba yao,+ mashamba yao ya mizabibu, na mizeituni yao, na nyumba zao, na pia sehemu moja ya mia* ya pesa zao, nafaka, divai mpya, na mafuta mnayowadai kama riba.”

12 Ndipo wakasema: “Tutawarudishia vitu hivyo bila kuwadai chochote. Tutafanya sawasawa na ulivyotuagiza.” Basi nikawaita makuhani na kuwaapisha wanaume hao ili watimize ahadi hiyo. 13 Pia, nikakung’uta vazi langu* na kusema: “Mungu wa kweli na amkung’ute hivi kutoka nyumbani mwake na kutoka katika mali zake kila mwanamume ambaye hatatimiza ahadi hii, na akung’utwe hivi na kubaki bila chochote.” Ndipo kutaniko lote likajibu: “Amina!”* Wakamsifu Yehova, na watu wakafanya kama walivyoahidi.

14 Isitoshe, tangu siku mfalme aliponiteua kuwa gavana+ katika nchi ya Yuda, kuanzia mwaka wa 20+ mpaka mwaka wa 32+ wa utawala wa Mfalme Artashasta,+ miaka 12, mimi na ndugu zangu hatukula chakula kilichokuwa haki ya gavana.+ 15 Lakini magavana walionitangulia waliwalemea watu, kila siku walichukua kutoka kwao shekeli 40 za fedha* kwa ajili ya mkate na divai. Pia, watumishi wao waliwakandamiza watu. Lakini mimi sikufanya hivyo+ kwa sababu nilimwogopa Mungu.+

16 Isitoshe, mimi pia nilishiriki kujenga ukuta huu, nasi hatukuchukua hata shamba moja;+ watumishi wangu wote walikusanyika hapo ili kufanya kazi. 17 Kulikuwa na Wayahudi na watawala wasaidizi 150 waliokula kwenye meza yangu, na pia watu waliokuja kwetu kutoka mataifa jirani. 18 Kila siku nilitayarishiwa* ng’ombe dume mmoja, kondoo sita walio bora, na ndege wengi, na kila baada ya siku kumi tuliandaliwa kwa wingi divai ya kila aina. Licha ya hayo sikudai chakula kilichokuwa haki ya gavana, kwa kuwa tayari watu walikuwa wamelemewa na kazi. 19 Ee Mungu wangu, nikumbuke na kunitendea wema,* kwa ajili ya yote niliyowatendea watu hawa.+

6 Sasa mara tu Sanbalati, Tobia,+ Geshemu Mwarabu,+ na maadui wetu wengine wote walipoambiwa kwamba nimejenga upya+ ukuta na hakuna mwanya wowote ukutani (ingawa kufikia wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango),+ 2 mara moja Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe wakisema: “Njoo, tupange wakati ili tukutane kwenye vijiji vya Bonde Tambarare la Ono.”+ Lakini walikuwa wakipanga njama ya kunidhuru. 3 Basi nikawatuma wajumbe kwao nikisema: “Ninafanya kazi kubwa sana, siwezi kushuka chini. Kwa nini kazi isimame ili nije kwenu?” 4 Wakanitumia ujumbe uleule mara nne, nami nikawapa jibu lilelile kila mara.

5 Kisha Sanbalati akamtuma mtumishi wake kwangu akiwa na ujumbe uleule mara ya tano, akaja na barua iliyokuwa wazi mkononi mwake. 6 Ilikuwa imeandikwa hivi: “Kuna habari zinazoenezwa katika mataifa, na Geshemu+ anasema pia kwamba wewe na Wayahudi mnapanga kuasi.+ Hii ndiyo sababu unajenga ukuta; na kulingana na habari hizo unataka kuwa mfalme wao. 7 Pia, umeweka manabii ili watangaze kukuhusu kotekote Yerusalemu, ‘Kuna mfalme katika Yuda!’ Na sasa mfalme atajulishwa mambo haya. Basi njoo, tuzungumzie jambo hili pamoja.”

8 Hata hivyo, nikamtumia jibu hili: “Hakuna jambo lolote unalosema ambalo limetendeka; umeyabuni wewe mwenyewe.”* 9 Kwa maana wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakisema: “Mikono yao italegea kazini, na kazi hiyo haitafanywa.”+ Sasa, ninasali, itie nguvu mikono yangu.+

10 Kisha nikaenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya mwana wa Mehetabeli, alipokuwa amejifungia ndani. Akasema: “Tupange wakati ili tukutane katika nyumba ya Mungu wa kweli, ndani ya hekalu, nasi tufunge milango ya hekalu, kwa maana wanakuja kukuua. Wanakuja kukuua usiku.” 11 Lakini nikasema: “Je, mtu kama mimi anapaswa kukimbia? Je, mtu kama mimi anaweza kuingia hekaluni na aendelee kuishi?+ Sitaingia!” 12 Ndipo nikatambua kwamba Mungu hakuwa amemtuma, bali Tobia na Sanbalati+ walikuwa wamemkodi ili atabiri maneno hayo kunihusu. 13 Alikuwa amekodiwa ili aniogopeshe na kunifanya nitende dhambi, kisha wawe na sababu ya kuniharibia sifa ili wanishutumu.

14 Ee Mungu wangu, mkumbuke Tobia+ na Sanbalati na matendo haya yote, na pia Noadia yule nabii wa kike na manabii wengine ambao daima walijaribu kuniogopesha.

15 Mwishowe ukuta ulikamilishwa katika siku ya 25 ya mwezi wa Eluli,* kwa muda wa siku 52.

16 Mara tu maadui wetu wote waliposikia habari hiyo na mataifa yote jirani yalipoona jambo hilo, wakaaibika sana,+ nao wakatambua kwamba kazi hii ilikuwa imefanywa kwa msaada wa Mungu wetu. 17 Siku hizo wakuu+ wa Yuda walikuwa wakimtumia Tobia barua nyingi, naye alikuwa akiwajibu. 18 Watu wengi huko Yuda walikuwa wameapa kumuunga mkono, kwa sababu alikuwa amemwoa binti ya Shekania mwana wa Ara,+ na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti ya Meshulamu+ mwana wa Berekia. 19 Pia, kila mara walikuwa wakiniambia mambo mema kumhusu na kumjulisha mambo niliyosema. Naye Tobia alikuwa akinitumia barua za kuniogopesha.+

7 Mara tu ukuta ulipojengwa upya+ nikaweka milango;+ kisha walinzi wa malango,+ waimbaji,+ na Walawi+ wakawekwa rasmi. 2 Kisha nikamweka ndugu yangu Hanani+ asimamie Yerusalemu, pamoja na Hanania mkuu wa Ngome,+ kwa maana alikuwa mwanamume mwaminifu zaidi na alimwogopa Mungu wa kweli+ kuliko watu wengine wengi. 3 Basi nikawaambia: “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka mchana kabisa, na wanapolinda wanapaswa kufunga milango na kuweka makomeo. Kisha wapange wakaaji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja katika kituo chake cha ulinzi alichogawiwa na kila mmoja mbele ya nyumba yake.” 4 Sasa jiji lilikuwa kubwa na pana, na watu walikuwa wachache,+ na nyumba hazikuwa zimejengwa upya.

5 Lakini Mungu wangu akaweka wazo moyoni mwangu niwakusanye wakuu, watawala wasaidizi, na watu ili waandikishwe kulingana na ukoo wao.+ Kisha nikapata kitabu cha orodha za koo za wale waliokuja mwanzoni, na kilikuwa na habari zifuatazo:

6 Hawa ndio watu wa mkoa* waliopanda kutoka utekwani huko uhamishoni, ambao Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni alikuwa amewapeleka uhamishoni+ na ambao baadaye walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye jiji lake,+ 7 wale waliokuja na Zerubabeli,+ Yeshua,+ Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Misperethi, Bigvai, Nehumu, na Baana.

Idadi ya wanaume Waisraeli ilitia ndani:+ 8 wana wa Paroshi, 2,172; 9 wana wa Shefatia, 372; 10 wana wa Ara,+ 652; 11 wana wa Pahath-moabu,+ wa wana wa Yeshua na Yoabu,+ 2,818; 12 wana wa Elamu,+ 1,254; 13 wana wa Zatu, 845; 14 wana wa Zakai, 760; 15 wana wa Binui, 648; 16 wana wa Bebai, 628; 17 wana wa Azgadi, 2,322; 18 wana wa Adonikamu, 667; 19 wana wa Bigvai, 2,067; 20 wana wa Adini, 655; 21 wana wa Ateri, wa Hezekia, 98; 22 wana wa Hashumu, 328; 23 wana wa Besai, 324; 24 wana wa Harifu, 112; 25 wana wa Gibeoni,+ 95; 26 wanaume wa Bethlehemu na Netofa, 188; 27 wanaume wa Anathothi,+ 128; 28 wanaume wa Beth-azmavethi, 42; 29 wanaume wa Kiriath-yearimu,+ Kefira, na Beerothi,+ 743; 30 wanaume wa Rama na Geba,+ 621; 31 wanaume wa Mikmasi,+ 122; 32 wanaume wa Betheli+ na Ai,+ 123; 33 wanaume wa ile Nebo nyingine, 52; 34 wana wa Elamu mwingine, 1,254; 35 wana wa Harimu, 320; 36 wana wa Yeriko, 345; 37 wana wa Lodi, Hadidi, na Ono,+ 721; 38 wana wa Senaa, 3,930.

39 Makuhani:+ wana wa Yedaya wa nyumba ya Yeshua, 973; 40 wana wa Imeri, 1,052; 41 wana wa Pashuri,+ 1,247; 42 wana wa Harimu,+ 1,017.

43 Walawi:+ Wana wa Yeshua, wa nyumba ya Kadmieli,+ wa wana wa Hodeva, 74; 44 Waimbaji:+ wana wa Asafu,+ 148. 45 Walinzi wa malango:+ wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni, wana wa Akubu,+ wana wa Hatita, wana wa Shobai, 138.

46 Watumishi wa hekaluni:*+ Wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi, 47 wana wa Kerosi, wana wa Sia, wana wa Padoni, 48 wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Salmai, 49 wana wa Hanani, wana wa Gideli, wana wa Gahari, 50 wana wa Reaya, wana wa Resini, wana wa Nekoda, 51 wana wa Gazamu, wana wa Uza, wana wa Pasea, 52 wana wa Besai, wana wa Meunimu, wana wa Nefushesimu, 53 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri, 54 wana wa Baslithi, wana wa Mehida, wana wa Harsha, 55 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema, 56 wana wa Nezia, wana wa Hatifa.

57 Wana wa watumishi wa Sulemani:+ wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Perida, 58 wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli, 59 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-hazebaimu, wana wa Amoni. 60 Watumishi wote wa hekaluni*+ na wana wa watumishi wa Sulemani walikuwa 392.

61 Na hawa ndio waliopanda kutoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubi, Adoni, na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kama ukoo wao* na asili yao ilikuwa ya Waisraeli:+ 62 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, 642. 63 Na kutoka kwa makuhani: wana wa Habaya, wana wa Hakozi,+ wana wa Barzilai,+ aliyemwoa mmoja kati ya mabinti wa Barzilai Mgileadi na kuitwa kwa jina lao. 64 Hao walichunguza kumbukumbu zao ili wathibitishe ukoo wao, lakini hawakupata majina ya koo zao, kwa hiyo hawakustahili kuwa makuhani.*+ 65 Gavana*+ akawaambia kwamba hawapaswi kula vitu vitakatifu kabisa+ mpaka apatikane kuhani ambaye angechunguza Urimu na Thumimu.+

66 Kutaniko lote lilikuwa na jumla ya watu 42,360,+ 67 mbali na watumwa wao wa kiume na wa kike,+ ambao walikuwa 7,337; walikuwa pia na waimbaji 245 wa kiume na wa kike.+ 68 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245, 69 ngamia 435, na punda 6,720.

70 Baadhi ya viongozi wa koo* walitoa mchango kwa ajili ya kazi.+ Gavana* alitoa kwa ajili ya hazina drakma 1,000 za dhahabu,* mabakuli 50, na kanzu 530 za makuhani.+ 71 Na baadhi ya viongozi wa koo* walitoa kwa ajili ya hazina ya kazi drakma 20,000 za dhahabu na mina 2,200 za fedha.* 72 Na wale watu wengine walitoa drakma 20,000 za dhahabu, mina 2,000 za fedha, na kanzu 67 za makuhani.

73 Na makuhani, Walawi, walinzi wa malango, waimbaji,+ baadhi ya watu, watumishi wa hekaluni,* na Waisraeli wengine wote wakaanza kuishi katika majiji yao.+ Kufikia mwezi wa saba,+ Waisraeli wote* walikuwa wakiishi katika majiji yao.+

8 Kisha watu wote wakakusanyika wakiwa na kusudi moja katika uwanja wa jiji uliokuwa mbele ya Lango la Maji,+ wakamwambia Ezra+ mwandishi* alete kitabu cha Sheria ya Musa,+ ambayo Yehova alikuwa ameamuru Waisraeli waifuate.+ 2 Basi kuhani Ezra akaleta Sheria mbele ya kutaniko+ la wanaume, wanawake, na wote walioweza kusikiliza na kuelewa, katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba.+ 3 Naye akaisoma kwa sauti kubwa+ katika uwanja wa jiji mbele ya Lango la Maji, kuanzia asubuhi hadi adhuhuri, akawasomea wanaume, wanawake, na wote ambao wangeweza kuelewa; nao watu wakasikiliza kwa makini+ kitabu cha Sheria. 4 Na Ezra mwandishi* alikuwa amesimama juu ya jukwaa la mbao, lililotengenezwa kwa kusudi hilo; na Matithia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia, na Maaseya walisimama upande wake wa kulia; na upande wake wa kushoto Pedaya, Mishaeli, Malkiya,+ Hashumu, Hash-badana, Zekaria, na Meshulamu.

5 Ezra akakifungua kitabu mbele ya watu wote, kwa maana alikuwa juu kuliko watu wote. Alipokuwa akikifungua, watu wote wakasimama. 6 Kisha Ezra akamsifu Yehova Mungu wa kweli, Aliye mkuu, kisha watu wote wakajibu, “Amina!* Amina!”+ nao wakainua mikono yao juu. Kisha wakamsujudia Yehova huku nyuso zao zikigusa ardhi. 7 Nao Yeshua, Bani, Sherebia,+ Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi,+ Hanani, na Pelaya, waliokuwa Walawi, walikuwa wakiwafafanulia watu Sheria,+ huku watu wakiwa wamesimama. 8 Wakaendelea kukisoma kitabu hicho kwa sauti kubwa, wakaisoma Sheria ya Mungu wa kweli, huku wakiifafanua waziwazi na kueleza maana yake; hivyo wakawasaidia watu kuelewa mambo yaliyokuwa yakisomwa.*+

9 Na Nehemia ambaye alikuwa gavana,* Ezra+ aliyekuwa kuhani na mwandishi,* na Walawi waliokuwa wakiwafundisha watu wakawaambia hivi watu wote: “Hii ni siku takatifu kwa Yehova Mungu wenu.+ Msiomboleze wala kulia.” Kwa maana watu wote walikuwa wakilia walipokuwa wakisikiliza maneno ya Sheria. 10 Akawaambia: “Nendeni mkale vitu bora* na kunywa vitu vitamu, na muwapelekee mafungu ya vyakula+ wale ambao hawana chochote; kwa maana hii ni siku takatifu kwa Bwana wetu, nanyi msihuzunike, kwa maana shangwe ya Yehova ndiyo ngome* yenu.” 11 Nao Walawi walikuwa wakiwatuliza watu wote, wakisema: “Nyamazeni! kwa maana hii ni siku takatifu, nanyi msihuzunike.” 12 Basi watu wote wakaenda zao kula na kunywa na kupeana mafungu ya chakula na kushangilia sana,+ kwa maana walielewa maneno waliyokuwa wameambiwa.+

13 Siku iliyofuata viongozi wa koo* za watu wote, makuhani, na Walawi wakakusanyika karibu na Ezra mwandishi* ili wapate ufahamu zaidi wa maneno ya Sheria. 14 Kisha wakaona imeandikwa katika Sheria kwamba Yehova alikuwa ameamuru kupitia Musa kwamba Waisraeli wanapaswa kukaa katika vibanda* wakati wa sherehe, mwezi wa saba,+ 15 na kwamba wanapaswa kutangaza+ katika majiji yao yote na kotekote Yerusalemu wakisema: “Nendeni katika eneo lenye milima mlete matawi ya mizeituni, ya misonobari, ya mihadasi na ya mitende, na matawi ya miti mingine yenye majani mengi ili mjenge vibanda, kama ilivyoandikwa.”

16 Basi watu wakaenda kuleta matawi hayo ili kujijengea vibanda, kila mtu juu ya paa lake, na pia katika nyua zao, na katika nyua za nyumba ya Mungu wa kweli,+ na katika uwanja wa jiji wa Lango la Maji,+ na katika uwanja wa jiji wa Lango la Efraimu.+ 17 Basi watu wote wa kutaniko waliokuwa wamerudi kutoka utekwani wakajenga vibanda nao wakakaa katika vibanda hivyo, kwa maana Waisraeli hawakuwa wamefanya hivyo tangu siku za Yoshua+ mwana wa Nuni mpaka siku hiyo, basi wakashangilia sana.+ 18 Na siku baada ya siku kitabu cha Sheria ya Mungu wa kweli kilikuwa kikisomwa,+ tangu siku ya kwanza hadi siku ya mwisho. Nao wakafanya sherehe hiyo kwa siku saba, na siku ya nane walifanya kusanyiko takatifu, kama ilivyoagizwa.+

9 Siku ya 24 ya mwezi huo, Waisraeli wakakusanyika; walikuwa wamefunga wakiwa wamevaa nguo za magunia na kujirushia mavumbi.+ 2 Kisha wazao wa Waisraeli wakajitenga na wageni wote,+ wakasimama na kuungama dhambi zao wenyewe na makosa ya baba zao.+ 3 Kisha wakasimama mahali walipokuwa na kusoma kwa sauti kitabu cha Sheria+ ya Yehova Mungu wao kwa robo siku;* na kwa robo nyingine ya siku walikuwa wakiungama na kumwinamia Yehova Mungu wao.

4 Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia,+ Bani, na Kenani wakasimama kwenye jukwaa+ la Walawi na kumlilia Yehova Mungu wao kwa sauti kubwa. 5 Nao Walawi, yaani, Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabneya, Sherebia, Hodia, Shebania, na Pethahia wakasema: “Simameni, msifuni Yehova Mungu wenu kwa umilele wote.*+ Na walisifu jina lako tukufu, ambalo limekwezwa juu kuliko baraka zote na sifa zote.

6 “Wewe peke yako ndiye Yehova;+ uliumba mbingu, naam, mbingu za mbingu na jeshi lake lote, dunia na vyote vilivyo juu yake, bahari na vyote vilivyomo. Nawe unavihifadhi vyote hai, na jeshi la mbinguni linakuinamia wewe. 7 Wewe ndiye Yehova Mungu wa kweli, uliyemchagua Abramu,+ ukamtoa katika jiji la Uru+ la Wakaldayo na ukampa jina Abrahamu.+ 8 Nawe ukaona moyo wake ukiwa mwaminifu mbele zako;+ basi ukafanya agano naye ili umpe nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi, na Wagirgashi, ili kuupa uzao wake* nchi hiyo;+ nawe ukatimiza ahadi zako, kwa maana wewe ni mwadilifu.

9 “Basi ukaona mateso ya mababu zetu huko Misri,+ nawe ukasikia kilio chao kwenye Bahari Nyekundu. 10 Kisha ukafanya ishara na miujiza dhidi ya Farao na watumishi wake wote na watu wote wa nchi yake,+ kwa maana ulijua waliwatendea kwa kimbelembele.+ Ukajijengea jina ambalo limedumu hadi leo hii.+ 11 Nawe ukaitenganisha bahari mbele yao, wakavuka bahari juu ya nchi kavu,+ na wale waliowafuatia ukawatupa ndani ya maji mengi kama vile jiwe linavyotupwa ndani ya bahari iliyochafuka.+ 12 Uliwaongoza mchana kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto, ili kuwaangazia njia waliyopaswa kupitia.+ 13 Nawe ukashuka kwenye Mlima Sinai+ ukazungumza nao kutoka mbinguni+ na kuwapa hukumu za uadilifu, sheria za kweli,* masharti bora na amri bora.+ 14 Ukawajulisha Sabato yako takatifu+ na kuwapa amri, masharti, na sheria kupitia Musa mtumishi wako. 15 Walipokuwa na njaa uliwapa mkate kutoka mbinguni,+ walipokuwa na kiu ukawapa maji kutoka kwenye mwamba,+ na ukawaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa* kwamba utawapatia.

16 “Lakini mababu zetu, wakatenda kwa kimbelembele+ na kuwa wakaidi,*+ nao hawakusikiliza amri zako. 17 Walikataa kusikiliza+ wala hawakukumbuka matendo yako ya ajabu uliyofanya miongoni mwao, lakini wakawa wakaidi,* nao wakachagua kiongozi ili warudi Misri ambako walikuwa watumwa.+ Lakini wewe ni Mungu uliye tayari kusamehe,* mwenye huruma* na rehema, usiye mwepesi wa hasira, una upendo mwingi mshikamanifu,*+ nawe hukuwaacha.+ 18 Hata walipojitengenezea sanamu ya ndama wa chuma* na kusema, ‘Huyu ndiye Mungu wenu aliyewaongoza kutoka Misri,’+ nao wakatenda matendo makubwa ya ukosefu wa heshima, 19 hata wakati huo, kwa rehema zako nyingi, hukuwaacha nyikani.+ Nguzo ya wingu iliyowaongoza njiani mchana haikuondoka juu yao, wala nguzo ya moto iliyowaangazia njia usiku.+ 20 Nawe ukawapa roho yako njema ili iwape ufahamu,+ hukuwanyima mana vinywani mwao,+ na walipohisi kiu ukawapa maji.+ 21 Kwa miaka 40 uliwapa chakula nyikani.+ Hawakukosa chochote. Mavazi yao hayakuchakaa,+ wala miguu yao haikuvimba.

22 “Uliwapa falme na mataifa, ukawagawia kipande kwa kipande,+ nao wakamiliki nchi ya Sihoni,+ yaani, nchi ya mfalme wa Heshboni,+ na pia nchi ya Ogu+ mfalme wa Bashani. 23 Nawe ukawafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za mbinguni.+ Kisha ukawaleta katika nchi ambayo ulikuwa umewaahidi mababu zao kwamba wanapaswa kuingia na kuimiliki.+ 24 Basi wana wao wakaingia na kuimiliki nchi hiyo,+ nawe ukawatiisha Wakanaani walioishi katika nchi hiyo,+ ukawatia mikononi mwao, wao pamoja na wafalme wao na wakaaji wa nchi, ili wawatendee wapendavyo. 25 Wakateka majiji yenye ngome+ na ardhi yenye rutuba,*+ wakamiliki nyumba zilizojaa vitu vyema vya kila aina, visima ambavyo tayari vilikuwa vimechimbwa, mashamba ya mizabibu, mizeituni,+ na miti ya matunda kwa wingi. Hivyo wakala na kushiba na kunenepa, nao wakaufurahia wema wako mwingi.

26 “Hata hivyo, hawakutii, bali walikuasi+ na kuigeuzia mgongo Sheria yako.* Wakawaua manabii wako waliowaonya wakurudie, nao wakatenda matendo makubwa ya ukosefu wa heshima.+ 27 Kwa sababu hiyo uliwatia mikononi mwa maadui wao,+ walioendelea kuwatesa.+ Lakini walipokuwa wakiteseka walikulilia, nawe uliwasikia ukiwa mbinguni; na kwa sababu ya rehema zako nyingi, uliwapa waokozi waliowaokoa kutoka mikononi mwa maadui wao.+

28 “Lakini mara tu walipopata utulivu, walitenda tena yaliyo maovu mbele zako,+ nawe ulikuwa ukiwaacha mikononi mwa maadui wao, ambao waliwakandamiza.*+ Kisha walirudi na kukuomba msaada,+ nawe uliwasikiliza ukiwa mbinguni na kuwaokoa tena na tena kwa sababu ya rehema zako nyingi.+ 29 Ingawa uliwaonya ili wairudie Sheria yako, walitenda kwa kimbelembele na kukataa kusikiliza amri zako;+ nao wakatenda dhambi kwa kutofuata masharti yako, ambayo mtu akiyafuata ataishi.+ Lakini walikugeuzia mgongo na kufanya shingo zao ziwe ngumu, nao wakakataa kukusikiliza. 30 Uliwaonyesha subira+ kwa miaka mingi na ukaendelea kuwaonya kwa roho yako kupitia manabii wako, lakini walikataa kusikiliza. Mwishowe ukawatia mikononi mwa mataifa ya nchi hizo.+ 31 Na kwa sababu ya rehema zako nyingi, hukuwaangamiza+ wala kuwaacha, kwa maana wewe ni Mungu mwenye huruma* na rehema.+

32 “Na sasa, Ee Mungu wetu, Mungu mkuu, mwenye nguvu, mwenye kuogopesha, unayeshika agano lako na kutenda kwa upendo mshikamanifu,+ usiyaone kuwa madogo mateso yote yaliyotupata sisi, wafalme wetu, wakuu wetu,+ makuhani wetu,+ manabii wetu,+ mababu zetu, na watu wako wote tangu siku za wafalme wa Ashuru+ mpaka leo hii. 33 Umekuwa mwadilifu katika mambo yote yaliyotupata, kwa maana umetenda kwa uaminifu; lakini ni sisi tuliotenda uovu.+ 34 Wafalme wetu, wakuu wetu, makuhani wetu, na mababu zetu hawajashika Sheria yako wala kusikiliza amri zako wala vikumbusho ulivyowapa* ili kuwaonya. 35 Hata walipokuwa kwenye ufalme wao wakifurahia wema mwingi uliowapa na katika nchi kubwa na yenye rutuba* uliyowapa, hawakukutumikia+ wala kuacha mazoea yao maovu. 36 Basi leo hii sisi ni watumwa+—naam, watumwa katika nchi ambayo uliwapa mababu zetu ili wale matunda yake na vitu vyake vyema. 37 Mazao yake mengi ni ya wafalme uliowafanya watutawale kwa sababu ya dhambi zetu.+ Wanatutawala wapendavyo na kuitendea mifugo yetu wapendavyo, tunateseka sana.

38 “Basi kwa sababu ya hayo yote, tunafanya mapatano thabiti+ kwa maandishi, nayo yamethibitishwa kwa muhuri wa wakuu wetu, Walawi wetu, na makuhani wetu.”+

10 Wale walioyathibitisha kwa kutia muhuri+ walikuwa:

Gavana* Nehemia, mwana wa Hakalia,

Na Sedekia, 2 Seraya, Azaria, Yeremia, 3 Pashuri, Amaria, Malkiya, 4 Hatushi, Shebania, Maluku, 5 Harimu,+ Meremothi, Obadia, 6 Danieli,+ Ginethoni, Baruku, 7 Meshulamu, Abiya, Miyamini, 8 Maazia, Bilgai, na Shemaya; hao ndio makuhani.

9 Pia Walawi: Yeshua mwana wa Azania, Binui wa wana wa Henadadi, Kadmieli,+ 10 na ndugu zao Shebania, Hodia, Kelita, Pelaya, Hanani, 11 Mika, Rehobu, Hashabia, 12 Zakuri, Sherebia,+ Shebania, 13 Hodia, Bani, na Beninu.

14 Viongozi wa watu: Paroshi, Pahath-moabu,+ Elamu, Zatu, Bani, 15 Buni, Azgadi, Bebai, 16 Adoniya, Bigvai, Adini, 17 Ateri, Hezekia, Azuri, 18 Hodia, Hashumu, Besai, 19 Harifu, Anathothi, Nebai, 20 Magpiashi, Meshulamu, Heziri, 21 Meshezabeli, Sadoki, Yadua, 22 Pelatia, Hanani, Anaya, 23 Hoshea, Hanania, Hashubu, 24 Haloheshi, Pilha, Shobeki, 25 Rehumu, Hashabna, Maaseya, 26 Ahiya, Hanani, Anani, 27 Maluku, Harimu, na Baana.

28 Watu wengine wote—makuhani, Walawi, walinzi wa malango, waimbaji, watumishi wa hekaluni,* kila mtu aliyejitenga na mataifa yaliyokuwa nchini ili afuate Sheria ya Mungu wa kweli,+ pamoja na wake zao, wana wao, na mabinti wao, kila mtu mwenye ujuzi na uelewaji*— 29 wakajiunga na ndugu zao, wakuu wao, wakajifunga kwa kiapo na laana, kwamba watatembea katika Sheria ya Mungu wa kweli, iliyotolewa kupitia Musa mtumishi wa Mungu wa kweli, na kufuata kwa makini amri zote za Yehova Bwana wetu, hukumu zake, na masharti yake. 30 Hatutakubali mabinti wetu waolewe na watu wa mataifa yaliyo nchini, wala hatutakubali wana wetu wawaoe mabinti wao.+

31 Ikiwa watu wa mataifa hayo wataleta bidhaa zao na kila aina ya nafaka ili watuuzie katika siku ya Sabato, hatutanunua chochote kutoka kwao siku ya Sabato+ au siku nyingine takatifu.+ Pia, mwaka wa saba+ hatutalima mashamba na tutayafuta madeni yote.+

32 Pia, tukajiwekea wajibu kwamba kila mmoja wetu atoe sehemu ya tatu ya shekeli* kila mwaka kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya* Mungu wetu,+ 33 kwa ajili ya mkate wa tabaka,*+ toleo la nafaka la kila siku,+ dhabihu za kawaida za kuteketezwa za Sabato+ na miezi mipya,+ na kwa ajili ya sherehe rasmi,+ kwa ajili ya vitu vitakatifu, kwa ajili ya dhabihu za dhambi+ ili kufunika dhambi za Waisraeli, na kwa ajili ya kazi zote za nyumba ya Mungu wetu.

34 Pia, tukapiga kura ili kupanga wakati ambao kila ukoo* wa makuhani, Walawi, na watu wangeleta kuni kwenye nyumba ya Mungu wetu wakati uliowekwa, mwaka baada ya mwaka, ili kuwasha moto kwenye madhabahu ya Yehova Mungu wetu, kama ilivyoandikwa katika Sheria.+ 35 Pia tutaleta kwenye nyumba ya Yehova mazao ya kwanza yaliyokomaa ya nchi yetu na matunda ya kwanza yaliyoiva ya kila mti wa matunda, mwaka baada ya mwaka,+ 36 vilevile tutatoa wazaliwa wetu wa kwanza wa kiume na pia wa mifugo yetu—kama ilivyoandikwa katika Sheria+—wazaliwa wetu wa kwanza wa ng’ombe na wa kondoo. Tutawaleta kwenye nyumba ya Mungu wetu, kwa makuhani wanaohudumu kwenye nyumba ya Mungu wetu.+ 37 Pia, unga wetu wa kwanza ambao haujakobolewa,+ michango yetu, matunda ya mti wa kila aina,+ divai mpya, na mafuta,+ tutawapelekea makuhani kwenye maghala* ya nyumba ya Mungu wetu,+ pia tutawapa Walawi sehemu ya kumi ya mazao ya mashamba yetu,+ kwa maana Walawi ndio wanaokusanya sehemu za kumi za mazao katika miji yetu yote ya kilimo.

38 Na kuhani, mwana wa Haruni, anapaswa kuwa pamoja na Walawi wanapokusanya sehemu ya kumi; Walawi nao wanapaswa kuleta sehemu ya kumi ya ile sehemu ya kumi katika nyumba ya Mungu wetu,+ kwenye vyumba vya* ghala. 39 Kwa maana Waisraeli na Walawi wanapaswa kuleta mchango+ wa nafaka, divai mpya, na mafuta+ kwenye maghala,* ambamo mna vyombo vya mahali patakatifu, na pia walinzi wa malango, waimbaji, na makuhani wanaohudumu. Hatutaipuuza nyumba ya Mungu wetu.+

11 Sasa wakuu wa watu walikuwa wakiishi Yerusalemu;+ lakini watu wengine wote walipiga kura+ ili mtu mmoja kati ya watu kumi aishi Yerusalemu, lile jiji takatifu, na wale wengine tisa waliishi katika majiji mengine. 2 Isitoshe, watu waliwabariki wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.

3 Na hawa ndio viongozi wa mkoa* walioishi Yerusalemu. (Waisraeli wengine wote, makuhani, Walawi, watumishi wa hekaluni,*+ na wana wa watumishi wa Sulemani,+ waliishi katika majiji mengine ya Yuda, kila mmoja katika sehemu aliyomiliki jijini.+

4 Pia, baadhi ya watu wa Yuda na Benjamini waliishi Yerusalemu.) Kati ya watu wa Yuda kulikuwa na Athaya mwana wa Uzia mwana wa Zekaria mwana wa Amaria mwana wa Shefatia mwana wa Mahalaleli wa wana wa Perezi,+ 5 na Maaseya mwana wa Baruku mwana wa Kolhoze mwana wa Hazaya mwana wa Adaya mwana wa Yoyaribu mwana wa Zekaria mwana wa Mshela. 6 Wana wote wa Perezi walioishi Yerusalemu walikuwa wanaume mashujaa 468.

7 Hawa ndio waliokuwa watu wa Benjamini: Salu+ mwana wa Meshulamu mwana wa Yoedi mwana wa Pedaya mwana wa Kolaya mwana wa Maaseya mwana wa Ithieli mwana wa Yeshaya, 8 na baada yake Gabai na Salai, watu 928; 9 na Yoeli mwana wa Zikri alikuwa msimamizi wao, na Yuda mwana wa Hasenua alikuwa wa pili katika usimamizi wa jiji.

10 Kutoka kwa makuhani: Yedaya mwana wa Yoyaribu, Yakini,+ 11 Seraya mwana wa Hilkia mwana wa Meshulamu mwana wa Sadoki mwana wa Merayothi mwana wa Ahitubu,+ kiongozi wa nyumba ya* Mungu wa kweli; 12 na ndugu zao waliofanya kazi ya ile nyumba, watu 822; na Adaya mwana wa Yerohamu mwana wa Pelalia mwana wa Amzi mwana wa Zekaria mwana wa Pashuri+ mwana wa Malkiya, 13 na ndugu zake, viongozi wa koo,* watu 242, na Amashisai mwana wa Azareli mwana wa Azai mwana wa Meshilemothi mwana wa Imeri, 14 na ndugu zao 128 waliokuwa wanaume hodari na jasiri; na msimamizi wao alikuwa Zabdieli, aliyetoka katika familia mashuhuri.

15 Na kutoka kwa Walawi: Shemaya+ mwana wa Hashubu mwana wa Azrikamu mwana wa Hashabia mwana wa Buni, 16 na Shabethai+ na Yozabadi,+ wa viongozi wa Walawi, waliosimamia kazi za nje ya nyumba ya Mungu wa kweli; 17 na Matania,+ mwana wa Mika mwana wa Zabdi mwana wa Asafu,+ kiongozi wa waimbaji, aliyeongoza sifa wakati wa sala,+ na Bakbukia, wa pili kati ya ndugu zake, na Abda mwana wa Shamua mwana wa Galali mwana wa Yeduthuni.+ 18 Walawi wote katika jiji takatifu walikuwa 284.

19 Na walinzi wa malango walikuwa Akubu, Talmoni,+ na ndugu zao waliolinda malango walikuwa 172.

20 Waisraeli wengine wote, makuhani, na Walawi walikuwa katika majiji mengine yote ya Yuda, kila mmoja katika eneo alilorithi.* 21 Watumishi wa hekaluni*+ walikuwa wakiishi Ofeli,+ nao Siha na Gishpa waliwasimamia watumishi wa hekaluni.*

22 Msimamizi wa Walawi walioishi Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani mwana wa Hashabia mwana wa Matania+ mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, waimbaji; alisimamia kazi ya nyumba ya Mungu wa kweli. 23 Kwa maana mfalme alikuwa ametoa amri kwa ajili ya waimbaji,+ na kulikuwa na mpango hususa kuhusu mahitaji yao ya kila siku. 24 Na Pethahia mwana wa Meshezabeli wa wana wa Zera mwana wa Yuda alikuwa mshauri wa mfalme* katika kila jambo lililowahusu watu.

25 Kuhusu maeneo na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-arba+ na miji yake, Diboni na miji yake, Yekabzeeli+ na vijiji vyake, 26 huko Yeshua, Molada,+ Beth-peleti,+ 27 Hasar-shuali,+ Beer-sheba na miji yake, 28 Siklagi,+ Mekona na miji yake, 29 En-rimoni,+ Sora,+ na Yarmuthi, 30 Zanoa,+ Adulamu na vijiji vyake, Lakishi+ na mashamba yake, na huko Azeka+ na miji yake. Waliishi* kuanzia Beer-sheba mpaka Bonde la Hinomu.+

31 Na watu wa Benjamini waliishi Geba,+ Mikmashi, Aiya, Betheli+ na miji yake, 32 Anathothi,+ Nobu,+ Ananiya, 33 Hasori, Rama,+ Gitaimu, 34 Hadidi, Seboimu, Nebalati, 35 Lodi, na Ono,+ bonde la mafundi. 36 Na baadhi ya vikundi vya Walawi kutoka Yuda waliishi katika eneo la Benjamini.

12 Hawa ndio makuhani na Walawi waliopanda kwenda na Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli,+ na Yeshua:+ Seraya, Yeremia, Ezra, 2 Amaria, Maluku, Hatushi, 3 Shekania, Rehumu, Meremothi, 4 Ido, Ginethoi, Abiya, 5 Miyamini, Maadia, Bilga, 6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya, 7 Salu, Amoki, Hilkia, na Yedaya. Hao ndio waliokuwa viongozi wa makuhani na ndugu zao katika siku za Yeshua.

8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli,+ Sherebia, Yuda, na Matania+ aliyeongoza uimbaji wa nyimbo za shukrani akiwa pamoja na ndugu zake. 9 Walisimama wakitazamana na ndugu zao Bakbukia na Uni wakati wa zamu za kulinda.* 10 Yeshua alimzaa Yoyakimu, Yoyakimu alimzaa Eliashibu,+ naye Eliashibu alimzaa Yoyada.+ 11 Naye Yoyada alimzaa Yonathani, naye Yonathani akamzaa Yadua.

12 Katika siku za Yoyakimu, hawa ndio waliokuwa makuhani, viongozi wa koo:* wa Seraya,+ Meraya; wa Yeremia, Hanania; 13 wa Ezra,+ Meshulamu; wa Amaria, Yehohanani; 14 wa Maluki, Yonathani; wa Shebania, Yosefu; 15 wa Harimu,+ Adna; wa Merayothi, Helkai; 16 wa Ido, Zekaria; wa Ginethoni, Meshulamu; 17 wa Abiya,+ Zikri; wa Miniamini, . . . ;* wa Moadia, Piltai; 18 wa Bilga,+ Shamua; wa Shemaya, Yehonathani; 19 wa Yoyaribu, Matenai; wa Yedaya,+ Uzi; 20 wa Salai, Kalai; wa Amoki, Eberi; 21 wa Hilkia, Hashabia; wa Yedaya, Nethaneli.

22 Viongozi wa koo* za Walawi na za makuhani katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani, na Yadua+ waliandikishwa, vilevile makuhani, mpaka wakati wa ufalme wa Dario Mwajemi.

23 Walawi waliokuwa viongozi wa koo* waliandikishwa katika kitabu cha historia ya nyakati, mpaka siku za Yohanani mwana wa Eliashibu. 24 Viongozi wa Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia, na Yeshua+ mwana wa Kadmieli,+ na ndugu zao walisimama wakitazamana walipokuwa wakiimba sifa na kumshukuru Mungu kulingana na maagizo ya Daudi+ mtu wa Mungu wa kweli, kikundi cha ulinzi kwa kikundi cha ulinzi. 25 Matania,+ Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni, na Akubu+ walikuwa walinzi wa malango,+ walilinda maghala yaliyokuwa karibu na malango. 26 Hao walitumikia katika siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua+ mwana wa Yozadaki na katika siku za gavana Nehemia na Ezra+ aliyekuwa kuhani na mwandishi.*

27 Wakati wa kuzindua kuta za Yerusalemu, Walawi walitafutwa kila mahali walipokuwa ili waje Yerusalemu kusherehekea uzinduzi kwa kushangilia, kwa nyimbo za shukrani,+ na kwa matoazi, vinanda, na vinubi. 28 Na wana wa waimbaji* wakakusanyika pamoja kutoka katika wilaya,* kutoka maeneo yaliyokuwa karibu na Yerusalemu, na kutoka vijiji vya Wanetofa,+ 29 kutoka Beth-gilgali,+ na kutoka mashamba ya Geba+ na Azmavethi,+ kwa maana waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu. 30 Na makuhani na Walawi wakajitakasa na kuwatakasa watu,+ malango,+ na ukuta.+

31 Kisha nikawaleta wakuu wa Yuda juu ya ukuta. Nikapanga makundi mawili makubwa yaliyoimba nyimbo za shukrani na vikundi vya kuwafuata, kikundi kimoja kilienda upande wa kulia wa ukuta kuelekea Lango la Marundo ya Majivu.+ 32 Hoshaya na nusu ya wakuu wa Yuda walitembea nyuma yao, 33 pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu, 34 Yuda, Benjamini, Shemaya, na Yeremia. 35 Walikuwa pamoja na baadhi ya wana wa makuhani waliokuwa na tarumbeta:+ Zekaria mwana wa Yonathani mwana wa Shemaya mwana wa Matania mwana wa Mikaya mwana wa Zakuri mwana wa Asafu,+ 36 na ndugu zake Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda, na Hanani, wakiwa na vyombo vya muziki vya Daudi+ mtu wa Mungu wa kweli; na Ezra+ mwandishi* akawatangulia. 37 Kwenye Lango la Chemchemi+ walipanda moja kwa moja Ngazi+ ya Jiji la Daudi+ kupitia njia inayopanda kwenye ukuta juu ya Nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji+ upande wa mashariki.

38 Kundi la pili lililoimba nyimbo za shukrani lilitembea kuelekea kushoto,* nami nikalifuata pamoja na nusu ya watu, juu ya ukuta kwenye Mnara wa Majiko ya Kuokea+ mpaka kwenye Ukuta Mpana+ 39 na kupita juu ya Lango la Efraimu+ na juu ya Lango la Jiji la Kale+ mpaka kwenye Lango la Samaki,+ Mnara wa Hananeli,+ Mnara wa Mea, na mpaka kwenye Lango la Kondoo;+ kisha wakasimama kwenye Lango la Mlinzi.

40 Mwishowe yale makundi mawili yaliyoimba nyimbo za shukrani yakasimama mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli; mimi pia nikasimama pamoja na nusu ya watawala wasaidizi waliokuwa pamoja nami, 41 na makuhani Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, na Hanania, wakiwa na tarumbeta, 42 na Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu, na Ezeri. Na waimbaji hao wakaimba kwa sauti kubwa wakiongozwa na Izrahia.

43 Siku hiyo walitoa dhabihu nyingi na kushangilia,+ kwa maana Mungu wa kweli aliwafanya washangilie kwa shangwe kubwa. Wanawake na watoto wakashangilia pia,+ hivi kwamba sauti za kushangilia jijini Yerusalemu zikasikika mbali sana.+

44 Siku hiyo wanaume waliwekwa ili kusimamia maghala+ ya michango,+ mazao ya kwanza,+ na sehemu za kumi.+ Kutoka katika mashamba ya majiji walipaswa kukusanya kwenye maghala hayo mafungu yaliyoamriwa na Sheria+ kwa ajili ya makuhani na Walawi,+ kwa maana kulikuwa na shangwe huko Yuda kwa sababu ya makuhani na Walawi waliokuwa wakihudumu. 45 Nao wakaanza kushughulikia majukumu waliyopewa na Mungu wao na kutimiza wajibu wa kutakasa, kama walivyofanya waimbaji na walinzi wa malango, kulingana na maagizo ya Daudi na ya Sulemani mwanawe. 46 Kwa maana zamani za kale katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa na viongozi wa* waimbaji wa nyimbo za kumsifu na kumshukuru Mungu.+ 47 Na katika siku za Zerubabeli+ na siku za Nehemia, Waisraeli wote walitoa mafungu kwa ajili ya waimbaji+ na walinzi wa malango,+ kulingana na uhitaji wa kila siku. Pia, waliweka kando fungu kwa ajili ya Walawi,+ na Walawi waliweka kando fungu kwa ajili ya wazao wa Haruni.

13 Siku hiyo kitabu cha Musa kilisomwa watu wote wakisikia,+ na wakaona imeandikwa kwamba Mwamoni au Mmoabu+ hapaswi kamwe kuingia katika kutaniko la Mungu wa kweli,+ 2 kwa maana hawakuwapokea Waisraeli kwa mkate na maji, badala yake walimkodi Balaamu ili awalaani.+ Hata hivyo, Mungu wetu aliigeuza laana hiyo kuwa baraka.+ 3 Mara tu waliposikia Sheria, wakaanza kuwatenga watu wote wenye asili ya kigeni* ili wasichangamane na Waisraeli.+

4 Sasa kabla ya wakati huo, kuhani aliyesimamia maghala* ya nyumba ya* Mungu wetu+ alikuwa Eliashibu,+ mtu wa ukoo wa Tobia.+ 5 Alikuwa amempa ghala kubwa,* mahali ambapo zamani walipatumia kuweka toleo la nafaka, ubani, na vyombo na sehemu ya kumi ya nafaka, divai mpya, na mafuta,+ vitu ambavyo Walawi,+ waimbaji, na walinzi wa malango walipaswa kupewa, pamoja na michango kwa ajili ya makuhani.+

6 Wakati huo wote mimi sikuwa Yerusalemu, kwa maana nilirudi kwa mfalme katika mwaka wa 32+ wa utawala wa Mfalme Artashasta+ wa Babiloni; na baada ya muda fulani nikamwomba mfalme ruhusa ya kuondoka. 7 Kisha nikafika Yerusalemu, nami nikaona jambo baya sana ambalo Eliashibu+ alikuwa amefanya kwa kumpa Tobia+ ghala katika ua wa nyumba ya Mungu wa kweli. 8 Jambo hilo lilinikasirisha sana, basi nikavitupa nje ya ghala* vitu vyote vya nyumba ya Tobia. 9 Kisha nikatoa amri, nao wakayatakasa maghala;* nami nikavirudisha humo vyombo vya nyumba ya Mungu wa kweli,+ pamoja na toleo la nafaka na ubani.+

10 Pia, nikagundua kwamba Walawi+ hawakuwa wakipewa mafungu yao,+ hivyo Walawi na waimbaji waliofanya kazi walikuwa wameondoka, kila mmoja akaenda kwenye shamba lake.+ 11 Basi nikawakemea watawala wasaidizi+ na kuwauliza: “Kwa nini nyumba ya Mungu wa kweli imepuuzwa?”+ Kwa hiyo nikawakusanya na kuwarudisha kwenye kazi zao. 12 Na watu wote wa Yuda wakaleta kwenye maghala sehemu ya kumi+ ya nafaka, divai mpya, na mafuta.+ 13 Kisha nikawaweka kuhani Shelemia, Sadoki mwandishi,* na Pedaya aliyekuwa Mlawi wasimamie maghala, na msaidizi wao alikuwa Hanani mwana wa Zakuri mwana wa Matania, kwa maana walionwa kuwa wanaume wenye kutegemeka. Walikuwa na jukumu la kuwagawia ndugu zao.

14 Unikumbuke mimi,+ Ee Mungu wangu, kuhusu jambo hili, nawe usiyafutilie mbali matendo yangu ya upendo mshikamanifu ambayo nimetenda kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na utumishi wake.*+

15 Siku hizo niliwaona watu huko Yuda wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya Sabato,+ wakileta marundo ya nafaka na kuyapakia juu ya punda, wakileta divai, zabibu, tini, na kuingiza kila aina ya mzigo Yerusalemu siku ya Sabato.+ Basi nikawaonya wasiuze bidhaa siku hiyo.* 16 Na Watiro walioishi jijini walikuwa wakileta samaki na bidhaa za kila aina na kuwauzia watu wa Yuda na Yerusalemu siku ya Sabato.+ 17 Basi nikawakemea wakuu wa Yuda na kuwaambia: “Ni uovu gani huu mnaofanya, hata mnaitia unajisi siku ya Sabato? 18 Je, mababu zenu hawakufanya hivyo, hivi kwamba Mungu wetu akatuletea sisi na pia jiji letu msiba huu wote? Sasa mnazidisha hasira yake inayowaka dhidi ya Israeli kwa kuitia unajisi Sabato.”+

19 Hivyo, mara tu vivuli vilipoanza kuangukia malango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe. Pia niliwaambia kwamba hawapaswi kuifungua mpaka Sabato iishe, nami nikawaweka baadhi ya watumishi wangu mwenyewe malangoni ili mizigo yoyote isiingizwe siku ya Sabato. 20 Basi wafanyabiashara na wauzaji wa bidhaa za kila aina wakalala nje ya Yerusalemu mara moja au mbili. 21 Ndipo nikawaonya na kuwaambia: “Kwa nini mnalala mbele ya ukuta usiku? Mkifanya hivyo tena, nitawaondoa kwa nguvu.” Tangu wakati huo hawakuja tena siku ya Sabato.

22 Nikawaambia Walawi kwamba wanapaswa kujitakasa kwa ukawaida na kuja kulinda malango ili siku ya Sabato iendelee kuwa takatifu.+ Ee Mungu wangu, unikumbuke pia kwa jambo hili, na unihurumie kwa sababu ya upendo wako mwingi mshikamanifu.+

23 Siku hizo niliwaona pia Wayahudi waliokuwa wameoa* wanawake Waashdodi,+ Waamoni,+ na Wamoabu.+ 24 Nusu ya wana wao walizungumza Kiashdodi na lugha za mataifa mbalimbali, lakini hakuna yeyote kati yao aliyejua kuzungumza lugha ya Wayahudi. 25 Ndipo nikawakemea na kuwalaani, nikawapiga baadhi ya wanaume hao,+ nikazing’oa nywele zao na kuwaapisha hivi kwa Mungu: “Msikubali mabinti wenu waolewe na wana wao, na msikubali mabinti wao waolewe na wana wenu au ninyi wenyewe.+ 26 Je, Mfalme Sulemani wa Israeli hakutenda dhambi kwa sababu yao? Hakukuwa na mfalme kama yeye miongoni mwa mataifa mengi;+ naye alipendwa na Mungu wake,+ hivi kwamba Mungu akamweka kuwa mfalme wa nchi yote ya Israeli. Lakini wake wa kigeni walimfanya hata yeye atende dhambi.+ 27 Je, si jambo linaloshangaza kwenu kutenda uovu huu mkubwa kwa kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”+

28 Mmoja wa wana wa Yoyada+ mwana wa kuhani mkuu Eliashibu+ alikuwa amemwoa binti ya Sanbalati+ Mhoroni. Kwa hiyo nikamfukuza kutoka mbele yangu.

29 Wakumbuke, Ee Mungu wangu, kwa sababu wamechafua ukuhani na agano la ukuhani+ na pia Walawi.+

30 Nami nikawatakasa kutokana na uchafu wote wa kigeni, nami nikawapa makuhani na Walawi majukumu yao, kila mmoja katika utumishi wake,+ 31 nami nikapanga ili kuni+ ziletwe wakati unaofaa na pia mazao ya kwanza yaliyokomaa.

Unikumbuke na kunitendea wema,* Ee Mungu wangu.+

Maana yake “Yah Hufariji.”

Angalia Nyongeza B15.

Au “jumba la mfalme la.”

Au “Susa.”

Au “wilaya ya utawala.”

Tnn., “maamuzi ya hukumu uliyomwagiza.”

Au “onyo ulilompa.”

Angalia Nyongeza B15.

Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”

Au “msitu wa mfalme.”

Au “Hekalu.”

Tnn., “mtumishi.”

Au “korongoni.”

Tnn. “wakaitia nguvu mikono yao.”

Tnn., “mtumishi.”

Au “haki ya kumiliki.”

Au “Wakaliweka wakfu.”

Tnn., “hawakutia shingo zao kwenye.”

Tnn., “walio wa kiti cha ufalme cha.”

Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”

Au “wachanganyaji wa manukato.”

Au “wakatandaza mabamba ya mawe.”

Au “sehemu iliyopimwa.”

Mita 445 hivi (futi 1, 460). Angalia Nyongeza B14.

Au labda, “wilaya jirani.”

Au “Jumba la Mfalme.”

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Au “aliudhika.”

Au “Wabeba mizigo.”

Tnn., “mara kumi.”

Tnn., “nyama ya mwili wa ndugu zetu ni sawa na nyama ya mwili wetu.”

Au “faida.”

Au “asilimia moja,” yaani, kila mwezi.

Tnn., “nikatikisa kifua changu.”

Au “Na iwe hivyo!”

Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.

Au “Kila siku nilitayarishiwa kwa gharama yangu.”

Au “na kunipa kibali.”

Tnn., “yanatoka moyoni mwako.”

Angalia Nyongeza B15.

Au “wilaya ya utawala.”

Au “Wanethini.” Tnn., “Waliotolewa.”

Au “Wanethini wote.” Tnn., “Wote Waliotolewa.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “hawakustahili utumishi wa kikuhani kwa sababu hawakuwa safi.”

Au “Tirshatha,” cheo cha Kiajemi cha gavana wa mkoa.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “Tirshatha,” cheo cha Kiajemi cha gavana wa mkoa.

Kwa kawaida ilikuwa sawa na dariki ya dhahabu ya Uajemi yenye uzito wa gramu 8.4. Si drakma inayotajwa katika Maandiko ya Kigiriki. Angalia Nyongeza B14.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Mina inayotajwa katika Maandiko ya Kiebrania ilikuwa na uzito wa gramu 570. Angalia Nyongeza B14.

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Tnn., “Israeli yote.”

Au “aliyenakili maandishi.”

Au “aliyenakili maandishi.”

Au “Na iwe hivyo!”

Au “wakaeleza maana ya usomaji huo.”

Au “Tirshatha,” cheo cha Kiajemi cha gavana wa mkoa.

Au “aliyenakili maandishi.”

Tnn., “vitu vinono.”

Au “nguvu.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “aliyenakili maandishi.”

Au “vibanda vya muda.”

Au “kwa saa tatu.”

Au “milele hata milele.”

Tnn., “mbegu yake.”

Au “sheria zinazotegemeka.”

Tnn., “uliinua mkono wako.”

Tnn., “na kufanya shingo yao kuwa ngumu.”

Tnn., “wakafanya shingo yao kuwa ngumu.”

Au “Mungu mwenye matendo ya kusamehe.”

Au “neema.”

Au “fadhili nyingi zenye upendo.”

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Au “iliyonona.”

Tnn., “kuitupa Sheria yako nyuma yao.”

Au “waliwaponda.”

Au “neema.”

Au “maonyo uliyowapa.”

Au “iliyonona.”

Au “Tirshatha,” cheo cha Kiajemi cha gavana wa mkoa.

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Au labda, “wote wenye umri wa kutosha kuelewa.”

Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.

Au “hekalu la.”

Yaani, mkate wa wonyesho.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “majumba ya kulia chakula.”

Au “majumba ya kulia chakula ya.”

Au “majumba ya kulia chakula.”

Au “wilaya ya utawala.”

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Au “hekalu la.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “urithi wake mwenyewe.”

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”

Tnn., “alikuwa kwenye mkono wa mfalme.”

Au “Walipiga kambi.”

Au labda, “wakati wa utumishi.”

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Inaonekana jina fulani limeondolewa hapa katika maandishi ya Kiebrania.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Au “aliyenakili maandishi.”

Au “Na waimbaji waliozoezwa.”

Yaani, wilaya iliyozunguka Yordani.

Au “aliyenakili maandishi.”

Au “lilitembea mbele.”

Tnn., “vichwa vya.”

Au “wenye asili mbalimbali.”

Au “majumba ya kulia chakula.”

Au “hekalu la.”

Au “jumba la kulia chakula.”

Au “jumba la kulia chakula.”

Au “majumba ya kulia chakula.”

Au “aliyenakili maandishi.”

Au “utunzaji wake.”

Au labda, “nikawaonya siku hiyo wasiuze bidhaa.”

Au “wamewaingiza ndani ya nyumba zao.”

Au “na kunipa kibali.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki