UFUNUO KWA YOHANA
1 Ufunuo* kupitia Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa+ ili kuwaonyesha watumwa wake+ mambo yanayopaswa kutukia hivi karibuni. Naye alimtuma malaika wake na kupitia yeye akautoa kwa ishara kwa mtumwa wake Yohana,+ 2 aliyetoa ushahidi kuhusu neno ambalo Mungu alisema na kuhusu ushahidi ambao Yesu Kristo alitoa, ndiyo, kuhusu mambo yote aliyoyaona. 3 Mwenye furaha ni yule anayesoma kwa sauti na wale wanaosikia maneno ya unabii huu, na wanaoshika mambo yaliyoandikwa humo,+ kwa kuwa wakati uliowekwa uko karibu.
4 Yohana, kwa makutaniko saba+ yaliyo katika mkoa wa Asia:
Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa “Yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja,”+ na kutoka kwa zile roho saba+ zilizo mbele ya kiti chake cha ufalme, 5 na kutoka kwa Yesu Kristo, “Shahidi Mwaminifu,”+ “mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,”+ na “Mtawala wa wafalme wa dunia.”+
Yeye anayetupenda+ na aliyetuweka huru kutoka katika dhambi zetu kupitia damu yake mwenyewe+— 6 naye alitufanya tuwe ufalme,+ makuhani+ kwa Mungu na Baba yake—ndiyo, na awe na utukufu na nguvu milele. Amina.
7 Tazama! Anakuja na mawingu,+ na kila jicho litamwona, na wale waliomchoma;* na makabila yote ya dunia yatajipigapiga kwa huzuni kwa sababu yake.+ Ndiyo, Amina.
8 “Mimi ndiye Alfa na Omega,”*+ asema Yehova* Mungu, “Yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja, Mweza-Yote.”+
9 Mimi Yohana, ndugu yenu na mshiriki pamoja nanyi katika dhiki+ na ufalme+ na uvumilivu+ katika ushirika na Yesu,+ nilikuwa katika kisiwa kinachoitwa Patmo kwa sababu ya kuzungumza kumhusu Mungu na kutoa ushahidi kumhusu Yesu. 10 Kwa mwongozo wa roho nilikuja kuwa katika siku ya Bwana, nami nikasikia nyuma yangu sauti yenye nguvu kama ya tarumbeta, 11 ikisema: “Yale unayoona, yaandike katika kitabu cha kukunjwa kisha uyatume kwa yale makutaniko saba: katika Efeso,+ katika Smirna,+ katika Pergamamu,+ katika Thiatira,+ katika Sardi,+ katika Filadelfia,+ na katika Laodikia.”+
12 Nikageuka ili nimwone yule aliyekuwa akizungumza nami, nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu,+ 13 na katikati ya vinara hivyo vya taa palikuwa na mtu kama mwana wa binadamu,+ aliyevaa vazi lililofika chini miguuni na kifuani alikuwa amevaa mshipi wa dhahabu. 14 Zaidi ya hayo, kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji, na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto,+ 15 na miguu yake ilikuwa kama shaba safi+ inapowaka katika tanuru, na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi. 16 Na kwenye mkono wake wa kuume kulikuwa na nyota saba,+ na kutoka katika kinywa chake upanga mkali, mrefu, wenye makali pande mbili+ ulikuwa umechomoza, na sura yake ilikuwa* kama jua linapong’aa kabisa.+ 17 Nilipomwona, nikaanguka miguuni pake kana kwamba nimekufa.
Naye akaweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope. Mimi ndiye wa Kwanza+ na wa Mwisho,+ 18 na aliye hai,+ nami nilikufa,+ lakini tazama! ninaishi milele na milele,+ nami nina funguo za kifo na za Kaburi.*+ 19 Kwa hiyo andika mambo uliyoona, na mambo yaliyopo, na mambo yatakayotukia baada ya haya. 20 Kuhusu siri takatifu ya zile nyota saba ulizoona kwenye mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu: Zile nyota saba zinamaanisha wale malaika wa yale makutaniko saba, na vile vinara saba vya taa vinamaanisha yale makutaniko saba.+
2 “Kwa malaika+ wa kutaniko lililo huko Efeso+ andika: Haya ndiyo mambo anayosema yule anayeshika zile nyota saba kwenye mkono wake wa kuume, na kutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu:+ 2 ‘Ninayajua matendo yako, na kazi yako ya jasho na uvumilivu, na kwamba huwavumilii watu wabaya, nawe unawajaribu wale wanaosema kwamba wao ni mitume,+ lakini wao sio, nawe uliwagundua kuwa waongo. 3 Wewe pia unaonyesha uvumilivu, na umestahimili kwa ajili ya jina langu+ nawe hujachoka.+ 4 Hata hivyo, nina jambo hili dhidi yako, kwamba umeacha upendo uliokuwa nao mwanzoni.
5 “‘Kwa hiyo kumbuka pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, nawe utubu+ na kufanya matendo uliyofanya mwanzoni. Usipofanya hivyo, nitakuja kwako, nami nitakiondoa kinara chako cha taa+ kutoka mahali pake, usipotubu.+ 6 Hata hivyo, ninakusifu kwa jambo hili: kwamba unachukia matendo ya madhehebu ya Nikolao,+ ambayo mimi pia ninayachukia. 7 Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko:+ Yule atakayeshinda+ nitampa ruhusa ya kula matunda ya ule mti wa uzima,+ ulio katika paradiso ya Mungu.’
8 “Na kwa malaika wa kutaniko lililo huko Smirna andika: Haya ndiyo mambo anayosema, ‘wa Kwanza na wa Mwisho,’+ aliyekufa na akawa hai tena:+ 9 ‘Ninajua dhiki na umaskini wako—lakini wewe ni tajiri+—na kufuru la wale wanaojiita Wayahudi na kwa kweli sio, bali wao ni sinagogi la Shetani.+ 10 Usiogope mateso yatakayokupata hivi karibuni.+ Tazama! Ibilisi ataendelea kuwatupa gerezani baadhi yenu ili mjaribiwe kwa ukamili, nanyi mtapata dhiki kwa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufikia kifo, nami nitakupa taji la uzima.+ 11 Yule aliye na sikio na asikie+ yale ambayo roho inayaambia makutaniko: Yule atakayeshinda,+ kifo cha pili hakitamdhuru hata kidogo.’+
12 “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Pergamamu andika: Haya ndiyo mambo anayosema yule aliye na ule upanga mkali, mrefu na wenye makali pande mbili:+ 13 ‘Ninajua mahali unapokaa, yaani, mahali kilipo kiti cha ufalme cha Shetani; lakini bado unaendelea kulishika imara jina langu,+ nawe hukukana imani yako kwangu+ hata katika siku za Antipa, shahidi wangu mwaminifu+ aliyeuawa+ kando yenu, mahali anapokaa Shetani.
14 “‘Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako, kwamba unao hapo wale wanaofuata fundisho la Balaamu,+ aliyemfundisha Balaki+ kuweka kikwazo mbele ya wana wa Israeli, ili wale vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na kufanya uasherati.*+ 15 Vivyo hivyo, pia una wale wanaofuata fundisho la madhehebu ya Nikolao.+ 16 Basi tubu. Usipofanya hivyo, ninakuja kwako upesi, nami nitapigana nao kwa ule upanga mrefu wa kinywa changu.+
17 “‘Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko:+ Yule atakayeshinda+ nitampa baadhi ya mana iliyofichwa,+ nami nitampa jiwe dogo jeupe, na kwenye jiwe hilo, jina jipya limeandikwa ambalo hakuna yeyote anayelijua ila yule anayelipokea.’
18 “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Thiatira+ andika: Haya ndiyo mambo anayosema Mwana wa Mungu, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto+ na ambaye miguu yake ni kama shaba safi:+ 19 ‘Ninayajua matendo yako, na upendo wako na imani na huduma na uvumilivu wako, na kwamba matendo yako ya hivi karibuni yanazidi yale uliyofanya mwanzoni.
20 “‘Hata hivyo, nina jambo hili dhidi yako, kwamba unamvumilia yule mwanamke Yezebeli,+ anayejiita nabii, naye anafundisha na kuwapotosha watumwa wangu wafanye uasherati*+ na kula vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu. 21 Nami nilimpa muda wa kutubu, lakini hataki kutubu uasherati* wake. 22 Tazama! niko karibu kumtupa katika kitanda cha ugonjwa, na kuwatupa katika dhiki kuu wale wanaofanya uzinzi pamoja naye, ikiwa hawatatubu matendo yake. 23 Nami nitawaua watoto wake kwa ugonjwa hatari, hivi kwamba makutaniko yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mawazo ya ndani kabisa* na mioyo, nami nitampa kila mmoja wenu kulingana na matendo yake.+
24 “‘Hata hivyo, ninawaambia wale wengine kati yenu walio huko Thiatira, wote wasiofuata fundisho hili, wale ambao hawakujua yale yanayoitwa “mambo mazito ya Shetani”:+ Mimi siwaongezei mzigo mwingine wowote. 25 Hata hivyo, shikeni imara lile mlilo nalo mpaka nitakapokuja.+ 26 Na yule atakayeshinda na kushika matendo yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,+ 27 kama vile nilivyopokea kutoka kwa Baba yangu, naye atawachunga watu kwa fimbo ya chuma+ hivi kwamba watavunjwa vipandevipande kama vyombo vya udongo. 28 Nami nitampa nyota ya asubuhi.+ 29 Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko.’
3 “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Sardi andika: Haya ndiyo mambo anayosema yule aliye na zile roho saba za Mungu+ na zile nyota saba:+ ‘Ninayajua matendo yako, kwamba una jina* kuwa uko hai, lakini umekufa.+ 2 Uwe macho,+ na uyatie nguvu mambo yanayobaki yaliyokuwa tayari kufa, kwa maana mimi sikuona kazi zako zikiwa zimefanywa kikamili* mbele za Mungu wangu. 3 Kwa hiyo, endelea kuzingatia* jinsi ulivyopokea na jinsi ulivyosikia, na uendelee kulishika, na utubu.+ Hakika usipoamka, nitakuja kama mwizi,+ nawe hutajua kamwe saa nitakayokuja juu yako.+
4 “‘Hata hivyo, una watu wachache* katika Sardi ambao hawakuyatia unajisi mavazi yao,+ nao watatembea pamoja nami wakiwa na mavazi meupe,+ kwa sababu wanastahili. 5 Kwa hiyo, yule atakayeshinda+ atavikwa mavazi meupe,+ na kwa vyovyote sitalifuta* jina lake kutoka katika kitabu cha uzima,+ bali nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu na mbele ya malaika zake.+ 6 Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko.’
7 “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Filadelfia andika: Haya ndiyo mambo anayosema yule aliye mtakatifu,+ aliye wa kweli,+ aliye na ufunguo wa Daudi,+ anayefungua hivi kwamba hakuna yeyote atakayefunga na anayefunga hivi kwamba hakuna yeyote anayefungua: 8 ‘Ninayajua matendo yako—tazama! nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa,+ usioweza kufungwa na yeyote. Nami ninajua kwamba una nguvu kidogo, nawe ulilishika neno langu na hukulikana jina langu. 9 Tazama! Nitawafanya wale wa sinagogi la Shetani wanaosema ni Wayahudi ingawa sio,+ lakini wanasema uwongo—tazama! nitawafanya waje wainame* mbele ya miguu yako na kuwafanya wajue kwamba nimekupenda wewe. 10 Kwa sababu ulilishika neno kuhusu uvumilivu wangu,*+ mimi pia nitakulinda kutokana na ile saa ya jaribu+ itakayokuja juu ya dunia nzima inayokaliwa, ili kuwajaribu wale wanaokaa duniani. 11 Ninakuja upesi.+ Endelea kushika imara kile ulicho nacho, ili yeyote asilichukue taji lako.+
12 “‘Yule atakayeshinda—nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, naye hataondoka humo kamwe, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu+ na jina la jiji la Mungu wangu, Yerusalemu Jipya+ linaloshuka kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu jipya.+ 13 Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko.’
14 “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Laodikia+ andika: Haya ndiyo mambo anayosema Amina,+ shahidi+ mwaminifu na wa kweli,+ mwanzo wa uumbaji wa Mungu:+ 15 ‘Ninayajua matendo yako, kwamba wewe si baridi wala si moto. Laiti ungekuwa baridi au moto. 16 Basi kwa sababu wewe ni vuguvugu na si moto+ wala si baridi,+ nitakutapika kutoka kinywani mwangu. 17 Kwa sababu unasema, “Mimi ni tajiri,+ nimejipatia utajiri na sihitaji kitu chochote,” lakini hujui kwamba wewe ni mwenye taabu na wa kusikitikiwa na maskini na kipofu na uko uchi, 18 ninakushauri ununue kutoka kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili uwe tajiri, na mavazi meupe ili uvae na kwamba aibu ya uchi wako isifunuliwe,+ na dawa ya macho ya kupaka katika macho yako+ ili uweze kuona.+
19 “‘Wale wote ninaowapenda, mimi huwakaripia na kuwatia nidhamu.+ Basi uwe mwenye bidii na utubu.+ 20 Tazama! Nimesimama mlangoni na ninapiga hodi. Mtu yeyote akiisikia sauti yangu na kuufungua mlango, nitaingia ndani ya nyumba yake na kula mlo wa jioni pamoja naye, naye pamoja nami. 21 Yule atakayeshinda+ nitampa ruhusa ya kuketi pamoja nami kwenye kiti changu cha ufalme,+ kama vile nilivyoshinda na kuketi+ pamoja na Baba yangu kwenye kiti chake cha ufalme. 22 Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko.’”
4 Baada ya hayo nikaona, na tazama! mlango uliofunguliwa mbinguni, na sauti ya kwanza niliyoisikia ikizungumza nami ilikuwa kama ya tarumbeta, ikisema: “Panda uje huku, nami nitakuonyesha mambo ambayo lazima yatendeke.” 2 Baada ya hayo mara moja nikawa katika nguvu za roho, na tazama! kiti cha ufalme kilikuwa mahali pake mbinguni, na kulikuwa na mtu aliyeketi kwenye kile kiti.+ 3 Na Yule aliyeketi alionekana kama jiwe la yaspi+ na jiwe jekundu lenye thamani, na kuzunguka kile kiti cha ufalme kulikuwa na upinde wa mvua ulioonekana kama zumaridi.+
4 Kuzunguka kile kiti cha ufalme kulikuwa na viti vya ufalme 24, na kwenye viti hivyo vya ufalme niliona wameketi wazee 24+ waliovaa mavazi meupe, na juu ya vichwa vyao mataji ya dhahabu. 5 Kwenye kile kiti cha ufalme kulitokea radi+ na sauti na ngurumo;+ na kulikuwa na taa saba za moto zikiwaka mbele ya kile kiti cha ufalme, ambazo zinamaanisha zile roho saba za Mungu.+ 6 Mbele ya kile kiti cha ufalme kulikuwa na kitu kinachofanana na bahari ya kioo,+ kama fuwele.
Katikati ya kile kiti cha ufalme* na kuzunguka kile kiti kulikuwa na viumbe hai wanne+ waliojaa macho mbele na nyuma. 7 Kiumbe hai wa kwanza alikuwa kama simba,+ na kiumbe hai wa pili alikuwa kama ng’ombe dume mchanga,+ na kiumbe hai wa tatu+ alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na kiumbe hai wa nne+ alikuwa kama tai anayeruka.+ 8 Kuhusu wale viumbe hai wanne, kila mmoja wao alikuwa na mabawa sita; walikuwa na macho kila mahali pande zote na chini yao.+ Na mchana na usiku wanaendelea kusema: “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova*+ Mungu, Mweza-Yote, aliyekuwako na aliyeko na anayekuja.”+
9 Kila mara wale viumbe hai wanapompa utukufu na heshima na shukrani Yule anayeketi kwenye kile kiti cha ufalme, Yule anayeishi milele na milele,+ 10 wale wazee 24+ huanguka chini mbele za Yule anayeketi kwenye kile kiti cha ufalme na kumwabudu Yule anayeishi milele na milele, nao hutupa mataji yao mbele ya kile kiti wakisema: 11 “Unastahili, Ee Yehova* Mungu wetu, kupokea utukufu+ na heshima+ na nguvu,+ kwa sababu uliumba vitu vyote,+ na kwa sababu ya mapenzi yako vilitokea navyo vikaumbwa.”
5 Nami nikaona katika mkono wa kuume wa Yule aliyeketi kwenye kile kiti cha ufalme,+ kitabu cha kukunjwa kilichoandikwa pande zote mbili,* kilichofungwa kabisa kwa mihuri saba. 2 Nami nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kubwa: “Ni nani anayestahili kukifungua kile kitabu cha kukunjwa na kuvunja mihuri yake?” 3 Lakini hakuna yeyote mbinguni au duniani au chini ya dunia aliyeweza kukifungua kitabu hicho cha kukunjwa au kutazama ndani yake. 4 Nikalia sana kwa sababu hakupatikana yeyote aliyestahili kukifungua kitabu hicho cha kukunjwa au kutazama ndani yake. 5 Lakini mmoja wa wale wazee akaniambia: “Acha kulia. Tazama! Simba wa kabila la Yuda,+ mzizi+ wa Daudi,+ ameshinda+ ili akifungue kitabu hicho cha kukunjwa na mihuri yake saba.”
6 Nami nikamwona mwanakondoo+ aliyeonekana kana kwamba amechinjwa,+ akiwa amesimama katikati ya kile kiti cha ufalme na katikati ya wale viumbe hai wanne na katikati ya wale wazee,+ akiwa na pembe saba na macho saba, na macho hayo yanamaanisha roho saba za Mungu+ ambazo zimetumwa katika dunia nzima. 7 Mara moja akaja na kukichukua kutoka katika mkono wa kuume wa Yule aliyeketi kwenye kile kiti cha ufalme.+ 8 Alipokichukua kile kitabu cha kukunjwa, wale viumbe hai wanne na wale wazee 24+ wakaanguka chini mbele ya Mwanakondoo, na kila mmoja alikuwa na kinubi na mabakuli ya dhahabu yaliyojaa uvumba. (Uvumba huo unamaanisha sala za watakatifu.)+ 9 Nao wanaimba wimbo mpya,+ wakisema: “Wewe unastahili kukichukua kile kitabu cha kukunjwa na kufungua mihuri yake, kwa sababu ulichinjwa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu+ kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa,+ 10 na ukawafanya kuwa ufalme+ na makuhani kwa Mungu wetu,+ nao watatawala wakiwa wafalme+ juu ya dunia.”
11 Nami nikaona, na kusikia sauti ya malaika wengi kuzunguka kile kiti cha ufalme na wale viumbe hai na wale wazee, na idadi yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu na maelfu ya maelfu,+ 12 nao walikuwa wakisema kwa sauti kubwa: “Mwanakondoo aliyechinjwa+ anastahili kupokea uwezo na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.”+
13 Nami nikasikia kila kiumbe kilicho mbinguni na duniani na chini ya dunia+ na baharini, na vitu vyote vilivyo ndani yake, vikisema: “Yule anayeketi kwenye kile kiti cha ufalme+ na Mwanakondoo+ na wawe na baraka na heshima+ na utukufu na nguvu milele na milele.”+ 14 Wale viumbe hai wanne walikuwa wakisema: “Amina!” na wale wazee wakaanguka chini na kuabudu.
6 Naye Mwanakondoo+ alipofungua mmoja wa ile mihuri saba,+ nikaona, na kumsikia mmoja wa wale viumbe hai wanne+ akisema kwa sauti kama ya ngurumo: “Njoo!” 2 Nami nikaona, na tazama! farasi mweupe,+ na yule aliyeketi juu yake alikuwa na upinde; naye akapewa taji,+ naye akaenda akishinda na kukamilisha ushindi wake.+
3 Alipofungua muhuri wa pili, nikamsikia kiumbe hai wa pili+ akisema: “Njoo!” 4 Mwingine akatokea, farasi mwenye rangi ya moto, na yule aliyeketi juu yake akapewa ruhusa ya kuondoa amani duniani ili wauane, naye akapewa upanga mkubwa.+
5 Alipofungua muhuri wa tatu,+ nikamsikia kiumbe hai wa tatu+ akisema: “Njoo!” Nami nikaona, na tazama! farasi mweusi, na yule aliyeketi juu yake alikuwa na mizani mkononi mwake. 6 Nami nikasikia kitu kama sauti katikati ya wale viumbe hai wanne ikisema: “Kibaba* cha ngano kwa dinari*+ moja na vibaba vitatu vya shayiri kwa dinari moja; na usidhuru divai na mafuta ya zeituni.”+
7 Alipofungua muhuri wa nne, nikasikia sauti ya kiumbe hai wa nne+ akisema: “Njoo!” 8 Nami nikaona, na tazama! farasi wa rangi ya kijivu, na yule aliyeketi juu yake alikuwa na jina Kifo. Na Kaburi* lilikuwa likimfuata kwa ukaribu. Nao wakapewa mamlaka juu ya sehemu ya nne ya dunia, ili kuua kwa upanga mrefu na kwa upungufu wa chakula+ na kwa ugonjwa hatari na kwa wanyama wa mwituni wa dunia.+
9 Alipofungua muhuri wa tano, nikaona chini ya madhabahu+ nafsi*+ za wale waliouawa kwa sababu ya neno la Mungu na kwa sababu ya ushahidi waliokuwa wametoa.+ 10 Wakasema kwa sauti kubwa: “Bwana Mwenye Enzi Kuu, mtakatifu na wa kweli,+ utajizuia mpaka lini kuhukumu na kulipiza kisasi cha damu yetu juu ya wale wanaokaa duniani?”+ 11 Na kila mmoja wao akapewa kanzu nyeupe,+ nao wakaambiwa waendelee kupumzika kwa muda mfupi, mpaka idadi itimie ya watumwa wenzao na ndugu zao waliokuwa karibu kuuawa kama vile wao walivyouawa.+
12 Nami nikaona alipofungua muhuri wa sita, na tetemeko kubwa la ardhi likatokea; na jua likawa jeusi kama gunia la manyoya,* na mwezi mzima ukawa kama damu,+ 13 na nyota za mbinguni zikaanguka duniani kama mtini unaotikiswa na upepo mkali unavyoangusha tini zake mbichi. 14 Na mbingu ikaondoka kama kitabu cha kukunjwa kinachokunjwa,+ na kila mlima na kila kisiwa vikaondolewa mahali pake.+ 15 Na wafalme wa dunia, maofisa wa cheo cha juu, viongozi wa kijeshi, matajiri, wenye nguvu, kila mtumwa, na kila mtu aliye huru wakajificha katika mapango na katika miamba ya milima.+ 16 Nao wanaendelea kuiambia milima na miamba: “Tuangukieni,+ mtufiche kutoka kwenye uso wa Yule anayeketi kwenye kile kiti cha ufalme+ na kutoka kwenye ghadhabu ya Mwanakondoo,+ 17 kwa sababu siku kuu ya ghadhabu yao imekuja,+ na ni nani anayeweza kusimama?”+
7 Baada ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama juu ya pembe nne za dunia, wakizishika kwa nguvu zile pepo nne za dunia ili upepo wowote usivume juu ya dunia au juu ya bahari au juu ya mti wowote. 2 Nami nikamwona malaika mwingine akipanda kutoka mashariki,* akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai; naye akawaambia kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliopewa ruhusa ya kuidhuru dunia na bahari, 3 akisema: “Msiidhuru dunia au bahari au miti, hadi tutakapowatia muhuri+ watumwa wa Mungu wetu katika mapaji ya nyuso zao.”+
4 Nami nikaisikia idadi ya wale waliotiwa muhuri, 144,000,+ waliotiwa muhuri kutoka kila kabila la wana wa Israeli:+
5 Kutoka kabila la Yuda 12,000 waliotiwa muhuri;
kutoka kabila la Rubeni 12,000;
kutoka kabila la Gadi 12,000;
6 kutoka kabila la Asheri 12,000;
kutoka kabila la Naftali 12,000;
kutoka kabila la Manase+ 12,000;
7 kutoka kabila la Simeoni 12,000;
kutoka kabila la Lawi 12,000;
kutoka kabila la Isakari 12,000;
8 kutoka kabila la Zabuloni 12,000;
kutoka kabila la Yosefu 12,000;
kutoka kabila la Benjamini 12,000 waliotiwa muhuri.
9 Baada ya hapo nikaona, na tazama! umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka mataifa yote na makabila na jamii na lugha,+ wakiwa wamesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwanakondoo, wakiwa wamevaa kanzu nyeupe;+ na walikuwa na matawi ya mitende mikononi mwao.+ 10 Nao wanaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Wokovu unatoka kwa Mungu wetu, anayeketi kwenye kiti cha ufalme,+ na kwa Mwanakondoo.”+
11 Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha ufalme na wale wazee+ na wale viumbe hai wanne, nao wakaanguka kifudifudi mbele ya kile kiti cha ufalme na kumwabudu Mungu, 12 wakisema: “Amina! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uwezo na nguvu ziwe kwa Mungu wetu milele na milele.+ Amina.”
13 Ndipo mmoja wa wale wazee akaniuliza: “Hawa waliovaa kanzu nyeupe,+ ni nani nao walitoka wapi?” 14 Basi nikamwambia mara moja: “Bwana wangu, wewe ndiye unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wale wanaotoka katika ile dhiki kuu,+ nao wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwanakondoo.+ 15 Ndiyo sababu wako mbele ya kile kiti cha ufalme cha Mungu, nao wanamtolea utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake; na Yule anayeketi kwenye kiti cha ufalme+ atatandaza hema lake juu yao.+ 16 Hawatakuwa na njaa wala kiu tena, wala jua halitawachoma wala joto lolote lenye kuunguza,+ 17 kwa sababu Mwanakondoo,+ aliye katikati ya kile kiti cha ufalme, atawachunga+ na kuwaongoza kwenye chemchemi za maji* ya uzima.+ Na Mungu atafuta kila chozi katika macho yao.”+
8 Alipofungua+ muhuri wa saba,+ kukawa na kimya mbinguni kwa karibu nusu saa. 2 Nami nikawaona wale malaika saba+ wanaosimama mbele za Mungu, nao wakapewa tarumbeta saba.
3 Malaika mwingine, akiwa ameshika chombo cha uvumba* cha dhahabu,+ akafika na kusimama kwenye madhabahu, naye akapewa kiasi kikubwa cha uvumba+ ili autoe pamoja na sala za watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu+ ambayo ilikuwa mbele ya kile kiti cha ufalme. 4 Moshi wa uvumba kutoka kwenye mkono wa huyo malaika ukapanda pamoja na sala+ za watakatifu mbele za Mungu. 5 Lakini mara moja malaika huyo akachukua kile chombo cha uvumba, akakijaza moto kutoka kwenye madhabahu na kukitupa duniani. Kukatokea ngurumo na sauti na radi+ na tetemeko la ardhi. 6 Na wale malaika saba wenye tarumbeta saba+ wakajitayarisha kuzipiga.
7 Malaika wa kwanza akaipiga tarumbeta yake. Kukawa na mvua ya mawe na moto uliochanganyika na damu, nao ukatupwa duniani;+ na theluthi moja ya dunia ikateketezwa, na theluthi moja ya miti ikateketezwa, na mimea yote mibichi ikateketezwa.+
8 Malaika wa pili akaipiga tarumbeta yake. Na kitu fulani kama mlima mkubwa unaowaka moto kikatupwa ndani ya bahari.+ Na theluthi moja ya bahari ikawa damu;+ 9 na theluthi moja ya viumbe hai* wa baharini wakafa,+ na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.
10 Malaika wa tatu akaipiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa inayowaka kama taa ikaanguka kutoka mbinguni, ikaanguka juu ya theluthi moja ya mito na juu ya chemchemi za maji.*+ 11 Jina la nyota hiyo ni Pakanga. Na theluthi moja ya maji ikageuka kuwa pakanga, na wanadamu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.+
12 Malaika wa nne akaipiga tarumbeta yake. Na theluthi moja ya jua ikapigwa,+ pia theluthi moja ya mwezi, na theluthi moja ya nyota, ili theluthi moja ya hizo itiwe giza+ na mchana usiwe na nuru kwa theluthi moja, na usiku vivyo hivyo.
13 Nami nikaona na kusikia tai akiruka katikati ya mbingu akisema kwa sauti kubwa: “Ole, ole, ole+ wao wanaokaa duniani kwa sababu ya milio mingine ya tarumbeta za wale malaika watatu walio karibu kuzipiga tarumbeta zao!”+
9 Malaika wa tano akaipiga tarumbeta yake.+ Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka kutoka mbinguni mpaka duniani, naye akapewa ufunguo wa shimo refu lisilo na mwisho.*+ 2 Akalifungua shimo refu lisilo na mwisho,* na moshi ukapanda kutoka katika lile shimo kama moshi wa tanuru kubwa, na jua likatiwa giza,+ pia hewa, kwa moshi wa lile shimo. 3 Na nzige wakatoka katika moshi huo wakaja duniani,+ nao wakapewa mamlaka, mamlaka kama ile ya nge wa dunia. 4 Wakaambiwa wasidhuru majani ya dunia au mmea wowote au mti wowote, isipokuwa watu wasio na muhuri wa Mungu kwenye mapaji ya nyuso zao.+
5 Na nzige hao walipewa ruhusa, si ya kuwaua, bali ya kuwatesa kwa miezi mitano, na mateso yao yalikuwa kama mateso ya mtu anapoumwa na nge.+ 6 Katika siku hizo watu watatafuta kifo lakini hawatakipata kamwe, nao watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.
7 Wale nzige walionekana kama farasi waliotayarishwa kwa ajili ya vita;+ na juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu kilichoonekana kama mataji ya dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu, 8 lakini walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama ya simba,+ 9 nao walikuwa na mabamba ya kifuani kama mabamba ya kifuani ya chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari ya farasi yakikimbia kwenda vitani.+ 10 Pia, wana mikia yenye miiba kama nge, na katika mikia yao wana mamlaka ya kuumiza watu kwa miezi mitano.+ 11 Wana mfalme juu yao, yule malaika wa shimo refu lisilo na mwisho.*+ Katika Kiebrania jina lake ni Abadoni,* lakini katika Kigiriki jina lake ni Apolioni.*
12 Ole mmoja umepita. Tazama! Ole mbili zaidi+ zinakuja baada ya mambo haya.
13 Malaika wa sita+ akaipiga tarumbeta yake.+ Nami nikasikia sauti moja kutoka katika zile pembe za madhabahu ya dhahabu+ iliyo mbele za Mungu 14 ikimwambia malaika wa sita aliyekuwa na tarumbeta: “Wafungue malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Efrati.”+ 15 Na wale malaika wanne, ambao wametayarishwa kwa ajili ya ile saa na siku na mwezi na mwaka wakafunguliwa ili waue theluthi moja ya watu.
16 Idadi ya majeshi ya wapanda farasi ilikuwa makumi mawili ya maelfu ya makumi ya maelfu;* niliisikia idadi yao. 17 Na hivi ndivyo nilivyowaona wale farasi katika maono na wale walioketi juu yao: Walikuwa na mabamba ya kifuani ya rangi nyekundu ya moto na ya bluu ya hayasinthi na ya manjano ya kiberiti, na vichwa vya wale farasi vilikuwa kama vichwa vya simba,+ na moto na moshi na kiberiti vilitoka katika vinywa vyao. 18 Theluthi moja ya watu iliuawa kwa hayo mapigo matatu, kwa ule moto na moshi na kiberiti vilivyotoka katika vinywa vyao. 19 Kwa maana mamlaka ya wale farasi imo katika vinywa vyao na katika mikia yao, kwa maana mikia yao ni kama nyoka na ina vichwa, nao wanaitumia kudhuru.
20 Lakini watu waliobaki ambao hawakuuawa kwa yale mapigo hawakutubu matendo ya mikono yao; hawakuacha kuabudu roho waovu na sanamu za dhahabu na fedha na shaba na mawe na miti, ambazo haziwezi kuona wala kusikia wala kutembea.+ 21 Nao hawakutubu mauaji yao wala mazoea yao ya kuwasiliana na roho wala uasherati* wao wala wizi wao.
10 Nami nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni, akiwa amepambwa* wingu, na upinde wa mvua ulikuwa juu ya kichwa chake, na uso wake ulikuwa kama jua,+ na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto, 2 na mkononi mwake alikuwa na kitabu kidogo cha kukunjwa kilichofunguliwa. Naye akaweka mguu wake wa kuume juu ya bahari, na mguu wa kushoto juu ya dunia, 3 naye akapaza sauti kubwa kama simba anaponguruma.+ Na alipopaza sauti, sauti za zile ngurumo saba+ zikazungumza.
4 Basi zile ngurumo saba zilipozungumza, nilikuwa karibu kuandika; lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema: “Yatie muhuri mambo ambayo zile ngurumo saba zilisema, nawe usiyaandike.” 5 Malaika niliyemwona amesimama juu ya bahari na juu ya dunia akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni, 6 naye akaapa kwa Yule anayeishi milele na milele,+ aliyeiumba mbingu na vitu vilivyo ndani yake na dunia na vitu vilivyo ndani yake na bahari na vitu vilivyo ndani yake:+ “Hakuna kukawia tena. 7 Lakini katika siku ambazo yule malaika wa saba+ atakuwa karibu kuipiga tarumbeta yake,+ ile siri takatifu+ ambayo Mungu aliwatangazia ikiwa habari njema watumwa wake manabii+ itamalizika.”
8 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema nami tena na kuniambia: “Nenda, ukichukue kile kitabu cha kukunjwa kilichofunguliwa, kilicho mkononi mwa malaika ambaye amesimama juu ya bahari na juu ya dunia.”+ 9 Nikaenda kwa yule malaika na kumwambia anipe kile kitabu kidogo cha kukunjwa. Akaniambia: “Kichukue ukile,+ nacho kitafanya tumbo lako liwe na uchungu, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.” 10 Nikakichukua kile kitabu kidogo cha kukunjwa kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila,+ na kinywani mwangu kilikuwa kitamu kama asali,+ lakini baada ya kukila, tumbo langu likawa na uchungu. 11 Nao wakaniambia: “Lazima utoe unabii tena kuhusu jamii na mataifa na lugha na wafalme wengi.”
11 Nami nikapewa utete unaofanana na fimbo,*+ nikaambiwa: “Simama upime patakatifu pa hekalu la Mungu na madhabahu na wale wanaoabudu ndani yake. 2 Lakini kuhusu ua ulio nje ya patakatifu pa hekalu, uache wala usiupime, kwa sababu umepewa mataifa, nao watalikanyaga lile jiji takatifu+ chini ya miguu yao kwa miezi 42.+ 3 Nitawafanya mashahidi wangu wawili watoe unabii kwa siku 1,260 wakiwa wamevaa nguo za magunia.” 4 Hao wanafananishwa na ile mizeituni+ miwili na vile vinara viwili vya taa,+ na wamesimama mbele za Bwana wa dunia.+
5 Yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwateketeza adui zao. Hivyo ndivyo anavyopaswa kuuawa mtu yeyote anayetaka kuwadhuru. 6 Hawa wana mamlaka ya kufunga anga*+ ili mvua isinyeshe+ katika siku zao za kutoa unabii, nao wana mamlaka juu ya maji ili kuyageuza kuwa damu+ na kuipiga dunia kwa kila aina ya mapigo mara nyingi wapendavyo.
7 Watakapomaliza kutoa ushahidi, yule mnyama wa mwituni anayepanda kutoka katika shimo refu lisilo na mwisho* atapigana nao na kuwashinda na kuwaua.+ 8 Na maiti zao zitakuwa kwenye barabara kuu ya lile jiji kubwa ambalo katika maana ya kiroho linaitwa Sodoma na Misri, ambako pia Bwana wao aliuawa kwenye mti. 9 Na watu wa jamii na makabila na lugha na mataifa watazitazama maiti zao kwa siku tatu na nusu,+ wala hawataruhusu maiti zao zilazwe kaburini. 10 Na wale wanaokaa duniani wanashangilia juu yao na kusherehekea, nao watatumiana zawadi, kwa sababu hao manabii wawili waliwatesa watu wanaokaa duniani.
11 Baada ya zile siku tatu na nusu, roho ya uhai kutoka kwa Mungu ikaingia ndani yao,+ wakasimama kwa miguu yao, na woga mkubwa ukawaingia wale waliowaona. 12 Nao wakasikia sauti kubwa kutoka mbinguni ikiwaambia: “Pandeni mje huku.” Nao wakapanda kuingia mbinguni katika wingu, na adui zao wakawaona.* 13 Tetemeko kubwa la ardhi likatokea saa hiyo, na sehemu ya kumi ya jiji ikaanguka; na watu 7,000 wakauawa na tetemeko hilo la ardhi, na wale wengine wakawa na hofu na kumpa utukufu Mungu wa mbinguni.
14 Ole wa pili+ umepita. Tazama! Ole wa tatu unakuja upesi.
15 Malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake.+ Na sauti kubwa zikasikika mbinguni, zikisema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa Ufalme wa Bwana wetu+ na wa Kristo wake,+ naye atatawala akiwa mfalme milele na milele.”+
16 Na wale wazee 24+ waliokuwa wameketi kwenye viti vyao vya ufalme mbele za Mungu wakaanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu, 17 wakisema: “Tunakushukuru wewe, Yehova* Mungu, Mweza-Yote, yule aliyeko+ na aliyekuwako, kwa sababu umechukua nguvu zako kuu na kuanza kutawala ukiwa mfalme.+ 18 Lakini mataifa wakawa na ghadhabu, nayo ghadhabu yako mwenyewe ikaja, na wakati uliowekwa ukafika kwa ajili ya kuhukumiwa kwa wafu na kuwapa thawabu+ watumwa wako manabii+ na watakatifu na wale wanaoliogopa jina lako, wadogo kwa wakubwa, na kuwaharibu wale wanaoiharibu dunia.”*+
19 Na patakatifu pa hekalu la Mungu palipo mbinguni pakafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana katika patakatifu pa hekalu lake.+ Na kukatokea radi na sauti na ngurumo na tetemeko la ardhi na mvua kubwa ya mawe.
12 Kisha ishara kubwa ikaonekana mbinguni: Mwanamke+ aliyepambwa* jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake palikuwa na taji la nyota 12, 2 naye alikuwa na mimba. Na alikuwa akilia akiwa katika maumivu na uchungu wa kuzaa.
3 Ishara nyingine ikaonekana mbinguni. Tazama! Joka mkubwa wa rangi ya moto,+ mwenye vichwa saba na pembe kumi na mataji saba* juu ya vichwa vyake; 4 na mkia wake unakokota theluthi moja ya nyota+ za mbinguni, naye akazitupa chini duniani.+ Na huyo joka akaendelea kusimama mbele ya yule mwanamke+ aliyekuwa karibu kuzaa, ili atakapozaa, ammeze mtoto wake.
5 Na yule mwanamke akazaa mwana,+ wa kiume, atakayechunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.+ Na mtoto wake akanyakuliwa* mpaka kwa Mungu na kwenye kiti chake cha ufalme. 6 Na yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotayarishwa na Mungu, na hapo watamlisha kwa siku 1,260.+
7 Na vita vikatokea ghafla mbinguni: Mikaeli*+ na malaika zake wakapigana na yule joka, naye joka na malaika zake wakapigana nao 8 lakini hawakushinda,* wala mahali hapakupatikana tena mbinguni kwa ajili yao. 9 Basi yule joka mkubwa+ akatupwa chini, yule nyoka wa zamani,+ anayeitwa Ibilisi+ na Shetani,+ anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa;+ akatupwa chini duniani,+ na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye. 10 Nikasikia sauti kubwa mbinguni ikisema:
“Sasa kumekuwa na wokovu+ na nguvu na Ufalme wa Mungu wetu+ na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu mshtaki wa ndugu zetu ametupwa chini, anayewashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu!+ 11 Nao wakamshinda+ kwa sababu ya damu ya Mwanakondoo+ na kwa sababu ya neno lao la kutoa ushahidi,+ nao hawakupenda nafsi zao*+ hata walipokabili kifo. 12 Kwa sababu hiyo furahini, enyi mbingu nanyi mnaokaa ndani yake! Ole wa dunia na wa bahari,+ kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.”+
13 Sasa yule joka alipoona kwamba ametupwa chini duniani,+ alimtesa yule mwanamke+ aliyezaa mtoto wa kiume. 14 Lakini yule mwanamke akapewa mabawa mawili ya tai mkubwa,+ ili aruke kwenda nyikani mahali pake, ambapo atalishwa kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati*+ mbali na uso wa yule nyoka.+
15 Naye nyoka akatapika maji kama mto kutoka katika kinywa chake nyuma ya yule mwanamke, ili kumzamisha katika mto huo. 16 Lakini dunia ikaja kumsaidia mwanamke, nayo dunia ikafungua kinywa chake na kuumeza mto ambao yule joka aliutapika kutoka katika kinywa chake. 17 Basi yule joka akawa na ghadhabu kumwelekea yule mwanamke, naye akaenda zake kupigana na wale waliobaki wa uzao wake,*+ wanaoshika amri za Mungu na walio na kazi ya kutoa ushahidi kumhusu Yesu.+
13 Naye* akasimama tuli juu ya mchanga wa bahari.
Nami nikamwona mnyama wa mwituni+ akipanda kutoka baharini,+ naye alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, na mataji kumi* juu ya pembe zake, lakini juu ya vichwa vyake majina yenye makufuru. 2 Basi yule mnyama wa mwituni niliyemwona alikuwa kama chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu, na kinywa chake kilikuwa kama kinywa cha simba. Na yule joka+ akampa huyo mnyama nguvu zake na kile kiti chake cha ufalme na mamlaka kubwa.+
3 Nikaona kimoja kati ya vichwa vyake kikiwa kimejeruhiwa vibaya lakini jeraha hilo la kifo lilipona,+ na dunia yote ikamfuata kwa mshangao yule mnyama wa mwituni. 4 Nao wakamwabudu yule joka kwa sababu alimpa mamlaka yule mnyama wa mwituni, nao wakamwabudu mnyama wa mwituni kwa maneno haya: “Ni nani aliye kama huyu mnyama wa mwituni, na ni nani anayeweza kupigana naye?” 5 Akapewa kinywa kinachosema mambo makuu na makufuru, akapewa pia mamlaka ya kutenda kwa miezi 42.+ 6 Naye akafungua kinywa chake kwa kumkufuru+ Mungu ili kulikufuru jina lake na makao yake, na hata wale wanaokaa mbinguni.+ 7 Akapewa ruhusa ya kupigana vita na watakatifu na kuwashinda,+ na akapewa mamlaka juu ya kila kabila na watu na lugha na taifa. 8 Na wale wote wanaokaa duniani watamwabudu. Tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu, hakuna jina la hata mmoja wao lililoandikwa katika kitabu cha kukunjwa cha uzima+ cha Mwanakondoo aliyechinjwa.+
9 Ikiwa yeyote ana sikio, na asikie.+ 10 Ikiwa yeyote amekusudiwa kwenda utekwani, ataenda utekwani. Ikiwa yeyote ataua* kwa upanga, naye lazima auawe kwa upanga.+ Hapa ndipo watakatifu+ wanahitaji uvumilivu+ na imani.+
11 Kisha nikamwona mnyama mwingine wa mwituni akipanda kutoka katika dunia, naye alikuwa na pembe mbili kama mwanakondoo, lakini akaanza kuzungumza kama joka.+ 12 Anatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza wa mwituni+ aliye machoni pake. Naye huifanya dunia na wale wanaokaa duniani wamwabudu yule mnyama wa kwanza wa mwituni, ambaye jeraha lake la kifo lilipona.+ 13 Naye hufanya ishara kubwa, hata hufanya moto ushuke kutoka mbinguni mpaka duniani machoni pa wanadamu.
14 Naye huwapotosha wale wanaokaa duniani, kwa sababu ya ishara alizoruhusiwa kufanya machoni pa yule mnyama wa mwituni, huku akiwaambia wale wanaokaa duniani watengeneze sanamu+ ya yule mnyama wa mwituni aliyekuwa na pigo la upanga lakini bado akabaki hai.+ 15 Naye akaruhusiwa kuipa pumzi* ile sanamu ya mnyama wa mwituni, ili ile sanamu ya mnyama wa mwituni iweze kusema na pia kufanya wale wote wanaokataa kuiabudu ile sanamu ya mnyama wa mwituni wauawe.
16 Anawalazimisha watu wote—wadogo kwa wakubwa, matajiri kwa maskini, walio huru kwa watumwa—ili wote watiwe alama kwenye mkono wao wa kulia au kwenye paji la uso wao,+ 17 na ili yeyote asiweze kununua au kuuza isipokuwa mtu aliye na ile alama, jina+ la yule mnyama wa mwituni au namba ya jina lake.+ 18 Hapa ndipo hekima inapohitajiwa: Yule aliye na ufahamu na afanye hesabu ya namba ya yule mnyama wa mwituni, kwa maana ni namba ya mwanadamu, na namba yake ni 666.+
14 Kisha nikaona, na tazama! Mwanakondoo+ amesimama juu ya Mlima Sayuni,+ na pamoja naye 144,000+ walioandikwa jina lake na jina la Baba yake+ kwenye mapaji ya nyuso zao. 2 Nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa; na sauti niliyosikia ilikuwa kama ya waimbaji wanaofuatanisha sauti zao wakipiga vinubi vyao. 3 Nao wanaimba kana kwamba ni wimbo mpya+ mbele ya kile kiti cha ufalme na mbele ya wale viumbe hai wanne+ na wale wazee,+ na hakuna yeyote aliyeweza kujifunza kikamili wimbo ule ila wale 144,000,+ ambao wamenunuliwa kutoka duniani. 4 Hao ndio wale ambao hawakujitia unajisi na wanawake; kwa kweli, wao ni mabikira.+ Hao ndio wanaoendelea kumfuata Mwanakondoo popote anapoenda.+ Hao walinunuliwa+ kutoka kati ya wanadamu wakiwa matunda ya kwanza+ kwa Mungu na kwa Mwanakondoo, 5 na hamna udanganyifu uliopatikana katika vinywa vyao; wao hawana dosari.+
6 Nami nikamwona malaika mwingine akiruka katikati ya mbingu,* naye alikuwa na habari njema ya milele ili aitangaze kwa wale wanaokaa duniani, kwa kila taifa na kabila na lugha na watu.+ 7 Alikuwa akisema kwa sauti kubwa: “Mwogopeni Mungu na kumpa utukufu, kwa sababu saa ya hukumu yake imefika,+ kwa hiyo mwabuduni Yule aliyeziumba mbingu na dunia na bahari+ na chemchemi za maji.”*
8 Na mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema: “Ameanguka! Babiloni Mkubwa+ ameanguka,+ yule aliyeyafanya mataifa yote yanywe divai ya hamu* ya uasherati* wake!”+
9 Malaika mwingine, wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kubwa: “Yeyote akimwabudu yule mnyama wa mwituni+ na sanamu yake na kupokea alama kwenye paji la uso wake au kwenye mkono wake,+ 10 yeye pia atakunywa divai ya hasira ya Mungu inayomwagwa ndani ya kikombe cha ghadhabu Yake bila kuchanganywa na kitu,+ naye atateswa kwa moto na kiberiti+ machoni pa malaika watakatifu na machoni pa Mwanakondoo. 11 Na moshi wa kuteswa kwao unapanda milele na milele,+ nao hawana pumziko mchana na usiku, wale wanaomwabudu yule mnyama wa mwituni na sanamu yake na yeyote anayepokea alama ya jina lake.+ 12 Hapa ndipo watakatifu wanapohitaji uvumilivu,+ wale wanaoshika amri za Mungu na kushika imara imani+ kwa Yesu.”
13 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wenye furaha ni wafu wanaokufa katika muungano na Bwana+ tangu wakati huu na kuendelea. Ndiyo, roho inasema, acheni wapumzike kutokana na kazi yao ngumu, kwa maana mambo waliyotenda yanaambatana nao moja kwa moja.”*
14 Kisha nikaona, na tazama! wingu jeupe, na mtu fulani kama mwana wa binadamu alikuwa ameketi juu ya wingu hilo,+ akiwa na taji la dhahabu juu ya kichwa chake na mundu mkali mkononi mwake.
15 Malaika mwingine akatokea katika patakatifu pa hekalu, akimwambia kwa sauti kubwa yule aliyeketi juu ya lile wingu: “Tia ndani mundu wako uvune, kwa sababu saa ya kuvuna imefika, kwa maana mavuno ya dunia yameiva kabisa.”+ 16 Na yule aliyeketi juu ya wingu akautia mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.
17 Na bado malaika mwingine akatokea katika patakatifu pa hekalu palipo mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali.
18 Na bado malaika mwingine akatokea katika madhabahu naye alikuwa na mamlaka juu ya moto. Naye akamwambia kwa sauti kubwa yule aliyekuwa na mundu mkali: “Tia ndani mundu wako mkali ukusanye vishada vya mzabibu wa dunia, kwa sababu zabibu zake zimeiva.”+ 19 Yule malaika akatia mundu wake katika dunia na kuukusanya mzabibu wa dunia, naye akautupa ndani ya shinikizo kubwa la divai la hasira ya Mungu.+ 20 Lile shinikizo la divai likakanyagiwa nje ya jiji, na damu ikatoka katika lile shinikizo la divai hata kufikia juu kwenye lijamu za farasi umbali wa stadia 1,600.*
15 Nami nikaona huko mbinguni ishara nyingine kubwa na ya ajabu sana, malaika saba+ wenye mapigo saba. Hayo ndiyo ya mwisho, kwa sababu kupitia hayo hasira ya Mungu inamalizika.+
2 Nami nikaona kitu kama bahari ya kioo+ iliyochanganyika na moto, na wale wanaomshinda+ yule mnyama wa mwituni na sanamu yake+ na ile namba ya jina lake+ walikuwa wamesimama kando ya ile bahari ya kioo, wakiwa wameshika vinubi vya Mungu. 3 Walikuwa wanaimba wimbo wa Musa+ mtumwa wa Mungu na wimbo wa Mwanakondoo,+ wakisema:
“Matendo yako ni makuu na ya ajabu,+ Yehova* Mungu, Mweza-Yote.+ Njia zako ni za uadilifu na za kweli,+ Mfalme wa umilele.+ 4 Ni nani ambaye kwa kweli hatakuogopa wewe, Yehova,* na kulitukuza jina lako, kwa kuwa wewe peke yako ni mshikamanifu?+ Kwa maana mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako,+ kwa sababu amri zako za uadilifu zimefunuliwa.”
5 Baada ya hayo nikaona, patakatifu pa hema la ushahidi+ pakifunguliwa mbinguni,+ 6 na wale malaika saba wenye mapigo saba+ wakatokea katika patakatifu, wakiwa wamevaa kitani safi, kinachong’aa na wakiwa wamefunga mishipi ya dhahabu kifuani. 7 Mmoja wa wale viumbe hai wanne akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa hasira ya Mungu,+ anayeishi milele na milele. 8 Na patakatifu pakajaa moshi kwa sababu ya utukufu wa Mungu+ na kwa sababu ya nguvu zake, na hakuna yeyote aliyeweza kuingia patakatifu mpaka yale mapigo saba+ ya wale malaika saba yalipomalizika.
16 Nami nikasikia sauti kubwa kutoka katika patakatifu+ ikiwaambia wale malaika saba: “Nendeni mkamwage yale mabakuli saba ya hasira ya Mungu juu ya dunia.”+
2 Malaika wa kwanza akaenda na kumwaga bakuli lake juu ya dunia.+ Na kidonda chenye maumivu na kilicho hatari+ kikawapata watu waliokuwa na alama ya yule mnyama wa mwituni+ na waliokuwa wakiiabudu sanamu yake.+
3 Malaika wa pili akamwaga bakuli lake ndani ya bahari.+ Nayo ikawa damu+ kama ya mwanadamu aliyekufa, na kila kiumbe aliye hai akafa,* ndiyo, vitu vilivyo ndani ya bahari.+
4 Malaika wa tatu akamwaga bakuli lake ndani ya mito na chemchemi za maji.*+ Nazo zikawa damu.+ 5 Nikamsikia malaika aliye juu ya maji akisema: “Wewe, Ambaye uko na uliyekuwako,+ Mshikamanifu,+ wewe ni mwadilifu, kwa kuwa umetoa hukumu hizi,+ 6 kwa sababu waliimwaga damu ya watakatifu na ya manabii,+ nawe umewapa damu wanywe;+ wanastahili hivyo.”+ 7 Nikasikia madhabahu ikisema: “Ndiyo, Yehova* Mungu, Mweza-Yote,+ hukumu zako* ni za kweli na za uadilifu.”+
8 Malaika wa nne akamwaga bakuli lake juu ya jua,+ nalo jua likapewa ruhusa ya kuwaunguza watu kwa moto. 9 Na wale watu wakaunguzwa na joto hilo kali, lakini wakalikufuru jina la Mungu, aliye na mamlaka juu ya mapigo haya, nao hawakutubu wala kumpa utukufu.
10 Malaika wa tano akamwaga bakuli lake juu ya kiti cha ufalme cha yule mnyama wa mwituni. Na ufalme wake ukatiwa giza,+ nao wakaanza kuzitafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu yao, 11 lakini wakamkufuru Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu yao na vidonda vyao, nao hawakutubu matendo yao.
12 Malaika wa sita akamwaga bakuli lake juu ya mto mkubwa Efrati,+ na maji yake yakakauka+ ili kutayarisha njia kwa ajili ya wafalme+ wanaotoka mashariki.*
13 Nami nikaona maneno matatu machafu yaliyoongozwa na roho* ambayo yalionekana kama vyura yakitoka katika kinywa cha yule joka+ na katika kinywa cha yule mnyama wa mwituni na katika kinywa cha yule nabii wa uwongo. 14 Kwa kweli, hayo ni maneno yanayoongozwa na roho waovu nayo yanafanya ishara,+ nayo yanakwenda kwa wafalme wa dunia nzima inayokaliwa, ili kuwakusanya pamoja kwa vita+ vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.+
15 “Tazama! Ninakuja kama mwizi.+ Mwenye furaha ni yule anayekaa macho+ na kutunza mavazi yake ya nje, ili asije akatembea uchi na watu waitazame aibu yake.”+
16 Nayo yakawakusanya pamoja mahali panapoitwa katika Kiebrania Har-Magedoni.*+
17 Malaika wa saba akamwaga bakuli lake juu ya hewa. Ndipo sauti kubwa ikatokea katika patakatifu+ kwenye kile kiti cha ufalme, ikisema: “Imetimia!” 18 Kukawa na radi na sauti na ngurumo, na kukatokea tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijawahi kutokea tangu wanadamu walipoumbwa duniani,+ tetemeko hilo la ardhi lilikuwa kubwa sana na lilienea sana. 19 Lile jiji kubwa+ likapasuka na kuwa sehemu tatu, na majiji ya mataifa yakaanguka; na Babiloni Mkubwa+ akakumbukwa mbele za Mungu, ili kumpa kikombe cha divai cha hasira ya ghadhabu yake.+ 20 Pia, kila kisiwa kikatoweka, na milima haikupatikana tena.+ 21 Ndipo mvua kubwa ya mawe, kila jiwe likiwa na uzito wa karibu talanta moja,* ikanyesha kutoka mbinguni juu ya watu,+ nao watu wakamkufuru Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe,+ kwa kuwa pigo hilo lilikuwa kubwa mno.
17 Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na mabakuli saba+ akaja na kuniambia: “Njoo, nitakuonyesha hukumu dhidi ya yule kahaba mkubwa anayekaa juu ya maji mengi,+ 2 ambaye wafalme wa dunia walifanya uasherati* naye,+ na watu wanaokaa duniani walileweshwa kwa divai ya uasherati* wake.”+
3 Naye akanichukua katika nguvu za roho akanipeleka nyikani. Nami nikamwona mwanamke ameketi juu ya mnyama wa mwituni mwenye rangi nyekundu aliyejaa majina ya makufuru na aliyekuwa na vichwa saba na pembe kumi. 4 Yule mwanamke alikuwa amevaa nguo za rangi ya zambarau+ na nyekundu, naye alikuwa amepambwa kwa dhahabu na mawe ya thamani na lulu,+ na mkononi mwake alikuwa na kikombe cha dhahabu kilichojaa machukizo na mambo machafu ya uasherati* wake. 5 Alikuwa ameandikwa kwenye paji la uso wake jina la fumbo: “Babiloni Mkubwa, mama wa makahaba+ na wa machukizo ya dunia.”+ 6 Nami nikaona kwamba yule mwanamke amelewa damu ya watakatifu na damu ya mashahidi wa Yesu.+
Basi, nilipomwona nilishangaa sana. 7 Ndipo yule malaika akaniambia: “Kwa nini ulishangaa? Nitakuambia fumbo la yule mwanamke+ na la yule mnyama wa mwituni anayembeba na aliye na vichwa saba na pembe kumi:+ 8 Mnyama wa mwituni uliyemwona alikuwako, lakini hayuko, na bado yuko karibu kupanda kutoka katika shimo refu lisilo na mwisho,*+ naye ataenda kwenye uharibifu. Na watu wanaokaa duniani ambao majina yao hayajaandikwa katika kitabu cha kukunjwa cha uzima+ tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu watashangaa watakapoona jinsi yule mnyama wa mwituni alivyokuwako, lakini hayuko, na bado atakuwapo.
9 “Hilo linahitaji akili yenye hekima: Vile vichwa saba+ vinamaanisha milima saba, ambapo yule mwanamke huketi juu yake. 10 Na kuna wafalme saba: Watano wameanguka, mmoja yuko, na yule mwingine bado hajafika; lakini atakapofika, lazima akae kwa muda mfupi. 11 Na yule mnyama wa mwituni aliyekuwako lakini hayuko,+ yeye pia ni mfalme wa nane, lakini anatokana na wale saba, naye anaenda zake kwenye uharibifu.
12 “Pembe kumi ulizoona zinamaanisha wafalme kumi ambao bado hawajapokea ufalme, lakini wanapokea mamlaka wakiwa wafalme kwa saa moja pamoja na yule mnyama wa mwituni. 13 Hao wana wazo moja, kwa hiyo wanampa yule mnyama wa mwituni nguvu na mamlaka yao. 14 Nao watapigana na Mwanakondoo,+ lakini kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme,+ Mwanakondoo atawashinda.+ Pia, wale walio pamoja naye walioitwa na waliochaguliwa na walio waaminifu watawashinda.”+
15 Akaniambia: “Yale maji uliyoyaona, ambapo yule kahaba ameketi, yanamaanisha jamii za watu na umati na mataifa na lugha.+ 16 Na zile pembe kumi+ ulizoona, na yule mnyama wa mwituni,+ hao watamchukia yule kahaba+ na kumfanya kuwa ukiwa na uchi, nao watakula nyama yake na kumteketeza kabisa kwa moto.+ 17 Kwa maana Mungu alitia hilo ndani ya mioyo yao ili kutekeleza wazo lake,+ ndiyo, kutekeleza lile wazo lao moja kwa kumpa yule mnyama wa mwituni+ ufalme wao, mpaka maneno ya Mungu yatakapokwisha kutimizwa. 18 Na yule mwanamke+ uliyemwona anamaanisha lile jiji kubwa lililo na ufalme juu ya wafalme wa dunia.”
18 Baada ya hayo nikamwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kubwa, na dunia ikatiwa nuru kwa utukufu wake. 2 Naye akasema kwa sauti yenye nguvu: “Ameanguka! Babiloni Mkubwa ameanguka,+ naye amekuwa makao ya roho waovu na mahali pa kuvizia pa kila roho mchafu* na kila ndege mchafu anayechukiwa!+ 3 Kwa sababu ya divai ya hamu* ya uasherati* wake, mataifa yote yamenaswa,+ na wafalme wa dunia walifanya uasherati naye,+ na wafanyabiashara* wa dunia walikuwa matajiri kutokana na nguvu za anasa yake isiyo na aibu.”
4 Nami nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: “Tokeni kwake, watu wangu,+ ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake, na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya mapigo yake.+ 5 Kwa maana dhambi zake zimekusanyika pamoja mpaka mbinguni,+ naye Mungu amekumbuka matendo yake yasiyo ya haki.*+ 6 Mlipeni kama alivyowatendea wengine,+ ndiyo, mlipeni mara mbili kwa yale aliyotenda;+ katika kikombe+ alichochanganya, mtilieni mchanganyiko mara mbili.+ 7 Kwa kadiri alivyojitukuza na kuishi katika anasa isiyo na aibu, kwa kadiri hiyo mpeni mateso na maombolezo. Kwa maana anaendelea kusema moyoni mwake: ‘Ninaketi nikiwa malkia, mimi si mjane, nami sitaona maombolezo kamwe.’+ 8 Hiyo ndiyo sababu mapigo yake yatakuja katika siku moja, kifo na kuomboleza na njaa kali, naye atateketezwa kabisa kwa moto,+ kwa sababu Yehova* Mungu, aliyemhukumu, ni mwenye nguvu.+
9 “Na wafalme wa dunia waliofanya uasherati* naye na kuishi naye katika anasa isiyo na aibu watalia na kujipiga-piga kwa huzuni kwa sababu yake watakapoona moshi unaotokana na kuteketea kwake. 10 Watasimama mbali kwa sababu ya kuogopa kuteseka kwake na kusema: ‘Ole, ole, wewe jiji kubwa,+ Babiloni wewe jiji lenye nguvu, kwa sababu hukumu yako imefika katika saa moja!’
11 “Pia, wafanyabiashara wa dunia wanalia na kuomboleza kwa sababu yake, kwa kuwa hakuna yeyote wa kununua tena bidhaa zao zilizojaa, 12 mizigo iliyojaa ya dhahabu, fedha, mawe ya thamani, lulu, kitani bora, vitambaa vya zambarau, hariri, na vitambaa vyekundu; na kila kitu kilichotengenezwa kwa mbao zenye manukato; na kila aina ya kitu kilichotengenezwa kwa pembe za tembo, na kwa mbao za thamani, shaba, chuma, na marumaru; 13 pia mdalasini, viungo vya Kihindi, uvumba, mafuta yenye marashi, ubani, divai, mafuta ya zeituni, unga laini, ngano, ng’ombe, kondoo, farasi, magari, watumwa, na uhai wa binadamu.* 14 Ndiyo, tunda zuri ulilotamani* limekuacha, na vitu vyote vitamu na vitu vyenye fahari vimetoweka kutoka kwako, navyo havitapatikana tena kamwe.
15 “Wafanyabiashara waliouza vitu hivyo, waliopata utajiri kutokana naye, watasimama mbali kwa sababu ya kuogopa kuteseka kwake nao watalia na kuomboleza, 16 wakisema: ‘Ole, ole, lile jiji kubwa lililovaa kitani bora, zambarau, na kitambaa chekundu, na lililopambwa sana kwa mapambo ya dhahabu, mawe ya thamani, na lulu,+ 17 kwa sababu katika saa moja mali nyingi hivyo zimeharibiwa!’
“Na kila kapteni wa meli na kila mtu anayesafiri baharini na mabaharia na wale wote ambao hupata riziki baharini walisimama mbali 18 na kusema kwa sauti kubwa huku wakitazama moshi uliotokana na kuteketezwa kwake: ‘Ni jiji gani lililo kama lile jiji kubwa?’ 19 Wakatupa mavumbi juu ya vichwa vyao na kupaza kilio, wakilia na kuomboleza, wakisema: ‘Ole, ole, lile jiji kubwa, ambalo wale wote waliokuwa na meli baharini walikuwa matajiri kutokana na utajiri wake, kwa sababu katika saa moja ameharibiwa!’+
20 “Furahini kwa sababu yake, enyi mbingu,+ pia ninyi watakatifu+ na mitume na manabii, kwa sababu Mungu ametangaza hukumu juu yake kwa ajili yenu!”+
21 Na malaika mwenye nguvu akainua jiwe lililo kama jiwe kubwa la kusagia na kulitupa baharini, akisema: “Hivi ndivyo Babiloni lile jiji kubwa litakavyotupwa chini kwa kasi sana, naye hatapatikana tena.+ 22 Na sauti ya waimbaji ambao hufuatanisha sauti zao kwa kinubi, ya wanamuziki, ya wapiga-filimbi, na ya wapiga-tarumbeta haitasikiwa tena ndani yako. Na hakuna fundi anayefanya kazi yoyote atakayepatikana tena ndani yako, na hakuna sauti ya jiwe la kusagia itakayosikiwa tena ndani yako. 23 Hakuna nuru ya taa itakayoangaza tena ndani yako, na hakuna sauti ya bwana harusi na bibi harusi itakayosikiwa tena ndani yako; kwa kuwa wafanyabiashara wako walikuwa watu wenye vyeo vya juu duniani, kwa maana mataifa yote yalipotoshwa kwa mazoea yako ya kuwasiliana na roho.+ 24 Ndiyo, ndani yake ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu+ na ya wale wote ambao wameuawa duniani.”+
19 Baada ya hayo nikasikia kitu kama sauti kubwa ya umati mkubwa mbinguni. Wakasema: “Msifuni Yah!*+ Wokovu na utukufu na nguvu ni za Mungu wetu, 2 kwa sababu hukumu zake ni za kweli na za uadilifu.+ Kwa maana ametekeleza hukumu juu ya yule kahaba mkubwa aliyeipotosha dunia kwa uasherati* wake, naye amelipiza kisasi damu ya watumwa wake iliyo mkononi mwake.”*+ 3 Na papo hapo, wakasema kwa mara ya pili: “Msifuni Yah!*+ Na moshi kutoka kwake* unaendelea kupanda milele na milele.”+
4 Na wale wazee 24+ na wale viumbe hai wanne+ wakaanguka chini na kumwabudu Mungu anayeketi kwenye kiti cha ufalme na kusema: “Amina! Msifuni Yah!”*+
5 Pia, sauti ikatoka katika kile kiti cha ufalme na kusema: “Endeleeni kumsifu Mungu wetu, enyi nyote watumwa wake+ mnaomwogopa, wadogo kwa wakubwa.”+
6 Nami nikasikia kitu kama sauti ya umati mkubwa na kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo nzito. Wakasema: “Msifuni Yah,*+ kwa sababu Yehova* Mungu wetu, Mweza-Yote,+ ameanza kutawala akiwa mfalme!+ 7 Acheni tufurahi na tuwe na shangwe nyingi na tumpe utukufu, kwa sababu ndoa ya Mwanakondoo imefika na mke wake amejitayarisha. 8 Ndiyo, ameruhusiwa kuvaa kitani bora, changavu, safi—kwa maana hicho kitani bora kinamaanisha matendo ya uadilifu ya watakatifu.”+
9 Naye ananiambia, “Andika: Wenye furaha ni wale walioalikwa kwenye mlo wa jioni wa ndoa ya Mwanakondoo.”+ Pia, ananiambia: “Hayo ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.” 10 Ndipo nikaanguka chini mbele ya miguu yake ili kumwabudu. Lakini ananiambia: “Uwe mwangalifu! Usifanye hivyo!+ Mimi ni mtumwa mwenzako tu na wa ndugu zako walio na kazi ya kutoa ushahidi kumhusu Yesu.+ Mwabudu Mungu!+ Kwa maana kutoa ushahidi kumhusu Yesu ndilo kusudi la unabii.”+
11 Nami nikaona mbingu imefunguliwa, na tazama! farasi mweupe.+ Na yule aliyeketi juu yake anaitwa Mwaminifu+ na wa Kweli,+ naye anahukumu na kupigana vita kwa uadilifu.+ 12 Macho yake ni mwali wa moto,+ na juu ya kichwa chake kuna mataji mengi.* Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe, 13 naye amevaa vazi la nje lililo na damu,* na jina analoitwa ni Neno+ la Mungu. 14 Pia, majeshi ya mbinguni yalikuwa yakimfuata juu ya farasi weupe, nayo yalikuwa yamevaa kitani bora cheupe, safi. 15 Na kinywani mwake upanga mrefu mkali unachomoza,+ upanga ambao atatumia kuyapiga mataifa, naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.+ Isitoshe, anakanyaga shinikizo la divai ya hasira ya ghadhabu ya Mungu Mweza-Yote.+ 16 Na kwenye vazi lake la nje, ndiyo, kwenye paja lake, ana jina lililoandikwa, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.+
17 Nikaona pia malaika amesimama katika jua, naye akaita kwa sauti kubwa na kuwaambia ndege wote wanaoruka katikati ya mbingu:* “Njooni hapa, mkusanyike pamoja kwenye mlo mkubwa wa jioni wa Mungu,+ 18 ili mle nyama za wafalme na nyama za viongozi wa kijeshi na nyama za watu wenye nguvu+ na nyama za farasi na za wale wanaoketi juu yao,+ na nyama za wote, za watu huru na vilevile za watumwa na za wadogo kwa wakubwa.”
19 Nami nikamwona yule mnyama wa mwituni na wafalme wa dunia na majeshi yao wamekusanyika pamoja ili kupigana vita na yule anayeketi juu ya farasi na jeshi lake.+ 20 Na yule mnyama wa mwituni akakamatwa, na yule nabii+ wa uwongo pamoja naye, aliyefanya mbele yake ishara alizotumia kuwapotosha wale waliopokea alama ya yule mnyama wa mwituni+ na wale wanaoiabudu sanamu yake.+ Wakiwa bado hai, wote wawili walitupwa ndani ya ziwa la moto linalowaka kwa kiberiti.+ 21 Lakini wale wengine wakauawa kwa ule upanga mrefu unaochomoza kinywani mwa yule anayeketi juu ya farasi.+ Na ndege wote wakashiba kutokana na nyama zao.+
20 Nami nikamwona malaika akishuka kutoka mbinguni akiwa na ufunguo wa shimo refu lisilo na mwisho*+ na mnyororo mkubwa mkononi mwake. 2 Akamkamata yule joka,+ yule nyoka wa zamani,+ ambaye ni Ibilisi+ na Shetani,+ na kumfunga kwa miaka 1,000. 3 Naye akamtupa katika shimo refu lisilo na mwisho*+ akalifunga na kulitia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena mpaka ile miaka 1,000 itakapokwisha. Baada ya hapo atafunguliwa kwa muda mfupi.+
4 Nami nikaona viti vya ufalme, na wale walioketi kwenye viti hivyo wakapewa mamlaka ya kuhukumu. Ndiyo, niliona nafsi* za wale waliouawa* kwa sababu ya ushahidi waliotoa kumhusu Yesu na kwa sababu ya kusema kumhusu Mungu, na wale ambao hawakumwabudu yule mnyama wa mwituni au sanamu yake na ambao hawakupokea ile alama kwenye paji la uso wao na kwenye mkono wao.+ Nao wakawa hai na kutawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo+ kwa miaka 1,000. 5 (Wale wafu+ wengine hawakuwa hai mpaka ile miaka 1,000 ilipokwisha.) Huo ndio ufufuo wa kwanza.+ 6 Mwenye furaha na mtakatifu ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza;+ kifo cha pili+ hakina mamlaka juu ya hao,+ bali watakuwa makuhani+ wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka 1,000.+
7 Sasa mara tu ile miaka 1,000 itakapokwisha, Shetani atafunguliwa kutoka katika gereza lake, 8 naye ataenda kuyapotosha yale mataifa yaliyo katika pembe nne za dunia, Gogu na Magogu, ili kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita. Idadi yao ni kama mchanga wa bahari. 9 Nao wakaenda katika dunia yote na kuizunguka kambi ya watakatifu na lile jiji linalopendwa. Lakini moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza.+ 10 Na Ibilisi aliyekuwa akiwapotosha alitupwa ndani ya lile ziwa la moto na kiberiti, ambamo wote wawili, yule mnyama wa mwituni+ na yule nabii wa uwongo, tayari walikuwa;+ nao watateswa* mchana na usiku milele na milele.
11 Nami nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na Yule aliyeketi juu yake.+ Dunia na mbingu zikatoweka kutoka mbele zake,+ na hazikupatikana tena. 12 Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wakiwa wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima.+ Wafu wakahukumiwa kutokana na yale mambo yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao.+ 13 Na bahari ikawatoa wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi* vikawatoa wafu waliokuwa ndani yake, nao wakahukumiwa kila mmoja kulingana na matendo yake.+ 14 Na kifo na Kaburi* vikatupwa ndani ya lile ziwa la moto.+ Hilo linamaanisha kifo cha pili,+ lile ziwa la moto.+ 15 Zaidi ya hayo, yeyote ambaye hakupatikana ameandikwa katika kile kitabu cha uzima+ alitupwa ndani ya lile ziwa la moto.+
21 Nami nikaona mbingu mpya na dunia mpya;+ kwa maana mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza zilikuwa zimepitilia mbali,+ na bahari+ haipo tena. 2 Pia, nikaona lile jiji takatifu, Yerusalemu Jipya, likishuka kutoka mbinguni kwa Mungu+ likiwa limetayarishwa kama bibi harusi aliyepambwa kwa ajili ya mume wake.+ 3 Ndipo nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha ufalme ikisema: “Tazama! Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.+ 4 Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao,+ na kifo hakitakuwapo tena,+ wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.+ Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”
5 Na Yule aliyeketi kwenye kiti cha ufalme+ akasema: “Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.”+ Pia anasema: “Andika, kwa maana maneno haya ni ya uaminifu* na ya kweli.” 6 Naye akaniambia: “Yametimia! Mimi ndiye Alfa na Omega,* mwanzo na mwisho.+ Yeyote aliye na kiu nitampa maji bure* kutoka kwenye chemchemi* ya maji ya uzima.+ 7 Yeyote anayeshinda atarithi vitu hivi, nami nitakuwa Mungu wake naye atakuwa mwanangu. 8 Lakini kuhusu waoga na wale wasio na imani+ na wale wenye kuchukiza katika uchafu wao na wauaji+ na waasherati*+ na wale wanaozoea kuwasiliana na roho na wanaoabudu sanamu na waongo wote,+ fungu lao litakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na kiberiti.+ Hili linamaanisha kifo cha pili.”+
9 Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na mabakuli saba yaliyojaa mapigo saba ya mwisho+ akaja na kuniambia: “Njoo, nami nitakuonyesha bibi harusi, mke wa Mwanakondoo.”+ 10 Basi akanichukua katika nguvu za roho akanipeleka kwenye mlima mkubwa na mrefu sana, naye akanionyesha lile jiji takatifu Yerusalemu likishuka kutoka mbinguni kwa Mungu+ 11 na likiwa na utukufu wa Mungu.+ Mwangaza wake ulikuwa kama jiwe la thamani zaidi, kama jiwe la yaspi lenye kung’aa kwa uangavu kama fuwele.+ 12 Lilikuwa na ukuta mkubwa na mrefu sana nalo lilikuwa na malango 12, na malaika 12 kwenye malango hayo, na majina ya makabila 12 ya wana wa Israeli yalikuwa yameandikwa kwenye malango hayo. 13 Upande wa mashariki kulikuwa na malango matatu, upande wa kaskazini malango matatu, upande wa kusini malango matatu, na upande wa magharibi malango matatu.+ 14 Ukuta wa lile jiji pia ulikuwa na mawe ya msingi 12, na juu ya mawe hayo kulikuwa na majina 12 ya mitume 12+ wa Mwanakondoo.
15 Basi yule aliyekuwa akizungumza nami alikuwa ameshika utete wa kupimia wa dhahabu ili alipime lile jiji na malango yake na ukuta wake.+ 16 Na lile jiji lilikuwa mraba, na urefu wake ni mkubwa kama upana wake. Naye akalipima jiji kwa utete, stadia 12,000;* urefu wake na upana wake na kimo chake ni sawa. 17 Pia, akapima ukuta wake, mikono 144,* kulingana na kipimo cha mwanadamu, na wakati huohuo kipimo cha malaika. 18 Basi ule ukuta ulitengenezwa kwa yaspi,+ na jiji lilikuwa dhahabu safi kama kioo safi. 19 Misingi ya ukuta wa jiji ilikuwa imepambwa kwa kila namna ya jiwe la thamani: msingi wa kwanza ulikuwa yaspi, wa pili yakuti, wa tatu kalkedoni, wa nne zumaridi, 20 wa tano sardoniksi, wa sita sardio, wa saba krisolito, wa nane beroli, wa tisa topazi, wa kumi krisopraso, wa kumi na moja hayasinthi, wa kumi na mbili amethisto. 21 Pia, yale malango 12 yalikuwa lulu 12; kila lango lilitengenezwa kwa lulu moja. Na barabara kuu ya jiji ilikuwa dhahabu safi, kama kioo kiangavu.
22 Sikuona hekalu ndani yake, kwa maana Yehova* Mungu Mweza-Yote+ ndiye hekalu lake, na pia Mwanakondoo. 23 Na lile jiji halihitaji jua wala mwezi kuliangazia, kwa maana utukufu wa Mungu uliliangazia,+ na taa yake ilikuwa yule Mwanakondoo.+ 24 Na mataifa yatatembea kwa nuru yake,+ na wafalme wa dunia wataleta utukufu wao ndani yake. 25 Malango yake hayatafungwa kamwe mchana, kwa maana hakutakuwa na usiku humo.+ 26 Nao wataleta utukufu na heshima ya mataifa ndani yake.+ 27 Lakini chochote kilicho najisi na yeyote anayetenda mambo yanayochukiza na ya udanganyifu hataingia kamwe humo;+ watakaoingia ni wale tu walioandikwa katika kile kitabu cha kukunjwa cha uzima cha Mwanakondoo.+
22 Naye akanionyesha mto wa maji ya uzima,+ mwangavu kama fuwele, ukitiririka kutoka katika kiti cha ufalme cha Mungu na cha Mwanakondoo+ 2 ukiteremka katikati ya barabara yake kuu. Pande zote mbili za ule mto zilikuwa na miti ya uzima iliyozaa mazao 12 ya matunda, ikizaa matunda yake kila mwezi. Na majani ya ile miti yalikuwa ya kuponya mataifa.+
3 Na hakutakuwa tena na laana yoyote. Bali kiti cha ufalme cha Mungu na cha Mwanakondoo+ kitakuwa katika jiji hilo, na watumwa wake watamtolea utumishi mtakatifu; 4 nao watauona uso wake,+ na jina lake litakuwa kwenye mapaji ya nyuso zao.+ 5 Pia, hakutakuwa na usiku tena,+ na hawahitaji nuru ya taa au ya jua, kwa maana Yehova* Mungu ataangaza nuru yake juu yao,+ nao watatawala wakiwa wafalme milele na milele.+
6 Akaniambia: “Maneno haya ni ya uaminifu* na ya kweli;+ ndiyo, Yehova,* Mungu aliyewaongoza manabii,+ alimtuma malaika wake ili kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo lazima yatendeke upesi. 7 Tazama! Ninakuja upesi.+ Mwenye furaha ni yeyote anayeshika maneno ya unabii wa kitabu hiki cha kukunjwa.”+
8 Basi mimi, Yohana, ndiye niliyekuwa nikisikia na kuona mambo haya. Niliposikia na kuyaona, nikaanguka chini kuabudu miguuni pa yule malaika aliyekuwa akinionyesha mambo haya. 9 Lakini yeye akaniambia: “Uwe mwangalifu! Usifanye hivyo! Mimi ni mtumwa mwenzako tu na wa ndugu zako manabii na wa wale wanaoshika maneno ya kitabu hiki cha kukunjwa. Mwabudu Mungu.”+
10 Pia akaniambia: “Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki cha kukunjwa, kwa maana wakati uliowekwa uko karibu. 11 Yule anayetenda ukosefu wa uadilifu na aendelee kutenda ukosefu wa uadilifu, na mwenye uchafu aendelee katika uchafu wake; lakini mwadilifu na aendelee kufanya uadilifu, na mtakatifu aendelee katika utakatifu.
12 “‘Tazama! Ninakuja upesi, nikiwa na thawabu ninayotoa, ili kumlipa kila mmoja kulingana na matendo yake.+ 13 Mimi ndiye Alfa na Omega,*+ wa kwanza na wa mwisho, mwanzo na mwisho. 14 Wenye furaha ni wale wanaofua kanzu zao,+ ili wawe na mamlaka ya kwenda kwenye miti ya uzima+ na waweze kuingia katika jiji kupitia malango yake.+ 15 Nje kuna mbwa* na wale walio na mazoea ya kuwasiliana na roho, waasherati,* wauaji, waabudu-sanamu, na kila mtu anayependa uwongo na aliye na mazoea ya kusema uwongo.’+
16 “‘Mimi, Yesu, nilimtuma malaika wangu kuwatolea ninyi ushahidi kuhusu mambo haya kwa ajili ya makutaniko. Mimi ndiye mzizi na uzao wa Daudi+ na nyota nyangavu ya asubuhi.’”+
17 Na roho na bibi harusi+ huendelea kusema, “Njoo!” na yeyote anayesikia na aseme, “Njoo!” na yeyote aliye na kiu aje;+ yeyote anayetaka achukue maji ya uzima bure.+
18 “Ninamtolea ushahidi kila mtu anayesikia maneno ya unabii wa kitabu hiki cha kukunjwa: Yeyote akiongeza kwenye mambo haya,+ Mungu atamwongezea mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki;+ 19 na yeyote akiondoa lolote kutoka katika maneno ya kitabu cha unabii huu, Mungu ataondoa fungu lake kutoka katika ile miti ya uzima+ na kutoka katika lile jiji takatifu,+ mambo yaliyoandikwa katika kitabu hiki cha kukunjwa.
20 “Yule anayetoa ushahidi kuhusu mambo haya anasema, ‘Ndiyo, mimi ninakuja upesi.’”+
“Amina! Njoo, Bwana Yesu.”
21 Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu na ziwe pamoja na watakatifu.
Au “Kufichua siri.”
Au “waliomdunga.”
Au “herufi A na Z.” Alfa ni herufi ya kwanza na Omega ni herufi ya mwisho katika alfabeti ya Kigiriki.
Angalia Nyongeza A5.
Au “uso wake ulikuwa.”
Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Au “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”
Au “unajulikana.”
Au “zimekamilika.”
Au “kukumbuka.”
Tnn., “majina machache.”
Au “sitaliondoa.”
Au “wasujudu.”
Au labda, “ulifuata mfano wangu wa uvumilivu.”
Au “Katikati pamoja na kile kiti cha ufalme.”
Angalia Nyongeza A5.
Angalia Nyongeza A5.
Tnn., “upande wa ndani na wa nyuma.”
Angalia Nyongeza B14.
Sarafu ya fedha ya Kiroma iliyolingana na mshahara wa siku moja. Angalia Nyongeza B14.
Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.
Inaonekana ni uhai unaowakilishwa na damu yao iliyomwagwa kwenye madhabahu. Angalia Kamusi.
Huenda lililotengenezwa kwa manyoya ya mbuzi.
Au “mawio ya jua.”
Au “mabubujiko ya maji.”
Au “chetezo.”
Au “viumbe wenye nafsi.”
Au “mabubujiko ya maji.”
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Maana yake “Uharibifu.”
Maana yake “Mwangamizaji.”
Au “20,000 mara 10,000,” yaani, 200,000,000.
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Au “amefunikwa.”
Au “fimbo ya kupimia.”
Au “mbingu.”
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au “walikuwa wakiwatazama.”
Angalia Nyongeza A5.
Au “kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”
Au “aliyevikwa.”
Au “tepe saba za kichwani za kifalme.”
Au “akachukuliwa.”
Maana yake “Ni Nani Aliye Kama Mungu?”
Au labda, “lakini alishindwa [yaani, joka].”
Au “uhai wao.” Angalia Kamusi.
Yaani, nyakati tatu na nusu.
Tnn., “mbegu yake.”
Yaani, yule joka.
Au “tepe kumi za kichwani za kifalme.”
Au labda, “Ikiwa yeyote atalazimika kuuawa.”
Au “roho.”
Au “katikati ya anga; juu.”
Au “mabubujiko ya maji.”
Au “hasira.”
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Au “pamoja nao.”
Karibu kilomita 296 (maili 184). Stadiamu moja ilikuwa sawa na mita 185 (futi 606.95). Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza A5.
Angalia Nyongeza A5.
Au “kila nafsi ikafa.”
Au “mabubujiko ya maji.”
Angalia Nyongeza A5.
Au “maamuzi yako ya hukumu.”
Au “mawio ya jua.”
Tnn., “roho waovu.”
Neno la Kigiriki, Har Ma·ge·donʹ, kutokana na neno la Kiebrania linalomaanisha “Mlima wa Megido.”
Talanta ya Kigiriki ilikuwa sawa na kilogramu 20.4. Angalia Nyongeza B14.
Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au labda, “pumzi chafu; maneno yaliyoongozwa na roho.”
Au “hasira.”
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “wafanyabiashara wanaosafiri.”
Au “uhalifu wake.”
Angalia Nyongeza A5.
Angalia Kamusi.
Au “nafsi za binadamu.”
Au “ambalo nafsi yako ililitamani.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Tnn., “kutoka mkononi mwake.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Yaani, “kutoka kwa Babiloni.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Angalia Nyongeza A5.
Au “tepe nyingi za kichwani za kifalme.”
Au labda, “lililonyunyiziwa damu.”
Au “katikati ya anga; juu.”
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Tnn.,” waliouawa kwa shoka.”
Au “watazuiliwa; watafungwa gerezani.”
Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.
Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.
Au “kutegemeka.”
Au “herufi A na Z.” Alfa ni herufi ya kwanza na Omega ni herufi ya mwisho katika alfabeti ya Kigiriki.
Au “bila gharama.”
Au “mabubujiko.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Karibu kilomita 2,220 (maili 1,379). Stadiamu moja ilikuwa sawa na mita 185 (futi 606.95). Angalia Nyongeza B14.
Karibu mita 64 (futi 210). Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza A5.
Angalia Nyongeza A5.
Au “kutegemeka.”
Angalia Nyongeza A5.
Au “herufi A na Z.” Alfa ni herufi ya kwanza na Omega ni herufi ya mwisho katika alfabeti ya Kigiriki.
Yaani, wale ambao matendo yao yanamchukiza Mungu.
Angalia Kamusi, “Uasherati.”