Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • nwt Waamuzi 1:1-21:25
  • Waamuzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waamuzi
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Waamuzi

WAAMUZI

1 Baada ya kifo cha Yoshua,+ Waisraeli* walimuuliza Yehova,+ “Ni nani kati yetu atakayeenda kwanza kupigana na Wakanaani?” 2 Yehova akawajibu, “Kabila la Yuda litaenda kwanza kupigana nao.+ Tazama! Ninaitia nchi hiyo mikononi mwao.”* 3 Ndipo watu wa kabila la Yuda wakawaambia ndugu zao wa kabila la Simeoni, “Twendeni pamoja katika eneo tulilopewa*+ tukapigane na Wakanaani. Nasi tutaenda nanyi katika eneo mlilopewa.” Basi watu wa kabila la Simeoni wakaenda pamoja nao.

4 Watu wa kabila la Yuda walipoenda, Yehova akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao,+ wakawashinda watu 10,000 huko Bezeki. 5 Wakamkuta Adoni-bezeki huko Bezeki, wakapigana naye na kuwashinda Wakanaani+ na Waperizi.+ 6 Adoni-bezeki akakimbia, wakamkimbiza na kumshika, wakamkata vidole gumba vya mikono na vya miguu. 7 Kisha Adoni-bezeki akasema, “Kuna wafalme 70 waliokatwa vidole gumba vya mikono na vya miguu wanaookota chakula chini ya meza yangu. Mungu amenilipa kulingana na matendo yangu.” Baadaye wakampeleka Yerusalemu,+ akafia huko.

8 Kisha watu wa Yuda wakashambulia jiji la Yerusalemu+ na kuliteka; wakawaua wakaaji wake kwa upanga na kuliteketeza jiji. 9 Baadaye watu wa Yuda wakaenda kupigana na Wakanaani waliokaa katika eneo lenye milima na waliokaa Negebu na Shefela.+ 10 Basi watu wa kabila la Yuda wakawashambulia Wakanaani waliokaa Hebroni (zamani Hebroni liliitwa Kiriath-arba), nao wakamuua Sheshai, Ahimani, na Talmai.+

11 Kisha wakawashambulia wakaaji wa Debiri.+ (Hapo awali Debiri liliitwa Kiriath-seferi.)+ 12 Ndipo Kalebu+ akasema, “Yeyote atakayeshambulia na kuteka jiji la Kiriath-seferi, nitampa binti yangu Aksa awe mke wake.”+ 13 Othnieli+ mwana wa Kenasi,+ ndugu mdogo wa Kalebu, akaliteka. Kwa hiyo akampa Aksa binti yake awe mke wake. 14 Mwanamke huyo alipokuwa akienda nyumbani kwake, akamsihi mume wake amwombe baba* yake shamba. Kisha mwanamke huyo akashuka kutoka juu ya punda wake.* Kalebu akamuuliza: “Unataka nini?” 15 Akamwambia, “Tafadhali nibariki, kwa maana umenipa shamba upande wa kusini;* nipe pia Guloth-maimu.”* Basi Kalebu akampa Gulothi ya Juu na Gulothi ya Chini.

16 Na wazao wa Mkeni,+ baba mkwe wa Musa,+ walitoka katika lile jiji la mitende+ pamoja na watu wa Yuda na kwenda katika nyika ya Yuda, upande wa kusini wa Aradi.+ Wakakaa huko pamoja na wenyeji.+ 17 Lakini watu wa kabila la Yuda wakasonga mbele pamoja na ndugu zao wa kabila la Simeoni, wakawashambulia Wakanaani waliokaa Sefathi na kuliangamiza jiji hilo.+ Kwa hiyo wakaliita Horma.*+ 18 Kisha watu wa kabila la Yuda wakateka Gaza+ na eneo lake, Ashkeloni+ na eneo lake, na Ekroni+ na eneo lake. 19 Yehova alikuwa pamoja na watu wa kabila la Yuda, nao wakamiliki eneo lenye milima, lakini hawakuweza kuwafukuza wakaaji wa bondeni,* kwa sababu walikuwa na magari ya vita yenye miundu ya chuma.*+ 20 Wakampa Kalebu jiji la Hebroni, kama Musa alivyoahidi,+ naye akawafukuza kutoka humo wale wana watatu wa Anaki.+

21 Lakini Wabenjamini hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa Yerusalemu, kwa hiyo Wayebusi wanakaa na Wabenjamini jijini Yerusalemu mpaka leo.+

22 Wakati huo, watu wa nyumba ya Yosefu+ wakashambulia Betheli, na Yehova alikuwa pamoja nao.+ 23 Na nyumba ya Yosefu ikatuma watu wakapeleleze jiji la Betheli (zamani liliitwa Luzi),+ 24 na wapelelezi hao wakamwona mtu akitoka jijini. Wakamwambia, “Tafadhali tuonyeshe njia ya kuingia jijini, nasi tutakutendea kwa fadhili.”* 25 Basi akawaonyesha njia ya kuingia jijini, kisha wakawaua watu wote kwa upanga, lakini wakamwacha huru mtu huyo na familia yake.+ 26 Naye akaenda katika nchi ya Wahiti, akajenga jiji na kuliita Luzi. Hilo ndilo jina la jiji hilo mpaka leo.

27 Watu wa kabila la Manase hawakumiliki Beth-sheani na miji yake,* Taanaki+ na miji yake, Dori na miji yake, Ibleamu na miji yake, na Megido na miji yake.+ Wakanaani hawakukubali kutoka katika nchi hiyo. 28 Waisraeli walipopata nguvu, waliwatumikisha Wakanaani,+ lakini hawakuwafukuza wote.+

29 Wala Waefraimu hawakuwafukuza Wakanaani waliokaa Gezeri. Wakanaani waliendelea kukaa kati yao huko Gezeri.+

30 Watu wa kabila la Zabuloni hawakuwafukuza wakaaji wa Kitroni na wakaaji wa Nahaloli.+ Wakanaani waliendelea kukaa kati yao na kufanya kazi za kulazimishwa.+

31 Waasheri hawakuwafukuza wakaaji wa Ako, Sidoni,+ Alabu, Akzibu,+ Helba, Afiki,+ na Rehobu.+ 32 Basi Waasheri wakaendelea kukaa kati ya Wakanaani waliokaa katika nchi hiyo, kwa sababu hawakuwafukuza.

33 Watu wa kabila la Naftali hawakuwafukuza wakaaji wa Beth-shemeshi na Beth-anathi,+ lakini waliendelea kukaa kati ya Wakanaani.+ Wakawatumikisha wakaaji wa Beth-shemeshi na wa Beth-anathi.

34 Waamori waliwazuia watu wa kabila la Dani wasishuke bondeni,* hivyo wakabaki milimani.+ 35 Kwa hiyo Waamori hawakukubali kutoka kwenye Mlima Heresi, na Aiyaloni,+ na Shaalbimu.+ Lakini watu wa nyumba ya Yosefu walipopata nguvu zaidi, waliwatumikisha. 36 Eneo la Waamori lilianzia kwenye mwinuko wa Akrabimu,+ kuanzia Sela kwenda milimani.

2 Kisha malaika wa Yehova+ akatoka Gilgali+ na kwenda Bokimu na kusema: “Niliwatoa Misri na kuwaleta katika nchi ambayo niliapa kwamba ningewapa mababu zenu.+ Pia nikasema, ‘Sitavunja kamwe agano langu pamoja nanyi.+ 2 Nanyi msifanye agano na wakaaji wa nchi hii,+ bomoeni madhabahu zao.’+ Lakini hamkutii sauti yangu.+ Kwa nini hamkutii? 3 Ndiyo maana nilisema, ‘Sitawafukuza kutoka mbele yenu,+ nao watakuwa mtego kwenu,+ nanyi mtashawishiwa kuifuata miungu yao.’”+

4 Malaika wa Yehova alipowaambia Waisraeli wote maneno hayo, watu wakaanza kulia kwa sauti kubwa. 5 Kwa hiyo wakapaita mahali hapo Bokimu,* nao wakamtolea Yehova dhabihu hapo.

6 Yoshua alipowaruhusu watu waende zao, kila Mwisraeli alienda kwenye eneo lake la urithi ili kuimiliki nchi.+ 7 Na watu wakaendelea kumtumikia Yehova sikuzote za Yoshua na sikuzote za wazee walioendelea kuishi baada ya Yoshua kufa ambao walikuwa wameona mambo yote makuu ambayo Yehova aliwatendea Waisraeli.+ 8 Kisha Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Yehova, akafa akiwa na umri wa miaka 110.+ 9 Basi wakamzika kwenye eneo lake la urithi kule Timnath-heresi+ katika eneo lenye milima la Efraimu, upande wa kaskazini wa Mlima Gaashi.+ 10 Na watu wote wa kizazi hicho wakafa na kuzikwa kama walivyozikwa mababu zao,* na kizazi kingine kikatokea ambacho hakikumjua Yehova wala mambo aliyowafanyia Waisraeli.

11 Na Waisraeli wakatenda maovu machoni pa Yehova, wakaabudu* Mabaali.+ 12 Basi wakamwacha Yehova, Mungu wa baba zao, aliyewatoa katika nchi ya Misri.+ Nao wakafuata miungu mingine, miungu ya watu waliowazunguka,+ wakaiinamia, na hivyo wakamkasirisha Yehova.+ 13 Wakamwacha Yehova na kuabudu Baali na sanamu za Ashtorethi.+ 14 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli, akawatia mikononi mwa waporaji, nao wakapora mali zao.+ Akawatia* mikononi mwa maadui waliowazunguka+ wala hawakuweza tena kuwashinda maadui wao.+ 15 Popote walipoenda, mkono wa Yehova uliwapinga na kuwaletea msiba,+ kama Yehova alivyokuwa amesema na kama Yehova alivyokuwa amewaapia,+ nao wakateseka sana.+ 16 Basi Yehova alikuwa akiwapa waamuzi ambao waliwaokoa kutoka mikononi mwa waporaji.+

17 Lakini walikataa kuwasikiliza hata waamuzi hao, nao walifanya ukahaba na miungu mingine na kuiinamia. Waliacha haraka njia ambayo mababu zao walifuata, ambao walitii amri za Yehova.+ Walikataa kutii. 18 Wakati wowote Yehova alipowapa waamuzi,+ Yehova alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa kutoka mikononi mwa maadui wao sikuzote za mwamuzi huyo; kwa maana Yehova aliwahurumia*+ kwa sababu ya kilio chao cha uchungu kilichosababishwa na wale waliowakandamiza+ na wale waliowatesa.

19 Hata hivyo mwamuzi huyo alipokufa, walitenda tena mambo maovu zaidi kuliko baba zao kwa kuifuata miungu mingine, kuiabudu na kuiinamia.+ Hawakuacha mazoea yao na tabia yao ya ukaidi. 20 Mwishowe hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli,+ akasema, “Kwa sababu taifa hili limevunja agano langu+ nililofanya na mababu zao, na halijanitii,+ 21 basi mimi sitafukuza kutoka mbele yao taifa hata moja ambalo Yoshua aliacha alipokufa.+ 22 Nitafanya hivyo ili kuwajaribu Waisraeli nione kama wataishika njia yangu mimi, Yehova,+ na kutembea katika njia hiyo kama baba zao walivyofanya.” 23 Kwa hiyo Yehova akaruhusu mataifa hayo yabaki. Hakuyafukuza haraka, wala hakuyatia mikononi mwa Yoshua.

3 Haya ndiyo mataifa ambayo Yehova aliyaruhusu yabaki ili yawajaribu Waisraeli wote ambao hawakuwa wamepigana vita vyovyote katika nchi ya Kanaani+ 2 (kusudi vizazi vilivyofuata vya Waisraeli, yaani, wale ambao hawakuwa wameona vita wafunzwe vita): 3 watawala watano wa Wafilisti,+ Wakanaani wote, Wasidoni,+ na Wahivi+ waliokaa katika Mlima Lebanoni+ kutoka Mlima Baal-hermoni mpaka Lebo-hamathi.*+ 4 Nao walitumiwa kuwajaribu Waisraeli ili kuona kama watatii amri ambazo Yehova aliwapa baba zao kupitia Musa.+ 5 Kwa hiyo, Waisraeli waliishi miongoni mwa Wakanaani,+ Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi. 6 Waisraeli walioa mabinti kutoka mataifa hayo, na kuruhusu mabinti wao waolewe na wana wao, nao wakaanza kuabudu miungu yao.+

7 Basi Waisraeli wakatenda maovu machoni pa Yehova, wakamsahau Yehova Mungu wao, na kuabudu Mabaali+ na miti mitakatifu.*+ 8 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli, naye akawatia* mikononi mwa Kushan-rishathaimu mfalme wa Mesopotamia.* Na Waisraeli wakamtumikia Kushan-rishathaimu kwa miaka minane. 9 Waisraeli walipomlilia Yehova awasaidie,+ Yehova aliwapa mwokozi ili awaokoe,+ Othnieli+ mwana wa Kenasi, ndugu mdogo wa Kalebu. 10 Roho ya Yehova ikamjia,+ akawa mwamuzi wa Israeli. Alipoenda vitani, Yehova alimtia Kushan-rishathaimu mfalme wa Mesopotamia* mikononi mwake, naye akamshinda Kushan-rishathaimu. 11 Baada ya hapo nchi ikawa na amani* kwa miaka 40. Kisha Othnieli mwana wa Kenasi akafa.

12 Waisraeli wakaanza tena kutenda maovu machoni pa Yehova.+ Basi Yehova akamruhusu Egloni mfalme wa Moabu+ awashinde Waisraeli, kwa sababu walitenda maovu machoni pa Yehova. 13 Isitoshe Egloni akawakusanya Waamoni+ na Waamaleki.+ Nao wakawashambulia Waisraeli na kuliteka jiji la mitende.+ 14 Na Waisraeli wakamtumikia Egloni mfalme wa Moabu kwa miaka 18.+ 15 Ndipo Waisraeli wakamlilia Yehova awasaidie.+ Basi Yehova akawapa mwokozi,+ Ehudi+ mwana wa Gera, Mbenjamini+ aliyetumia mkono wa kushoto.+ Baada ya muda Waisraeli wakamtuma Ehudi apeleke ushuru kwa Egloni mfalme wa Moabu. 16 Ehudi akatengeneza upanga wenye makali pande mbili uliokuwa na urefu wa mkono mmoja,* akaufunga kiunoni ndani ya vazi lake upande wa kulia. 17 Kisha akampelekea Egloni mfalme wa Moabu ushuru huo. Egloni alikuwa mnene sana.

18 Baada ya Ehudi kutoa ule ushuru, akaondoka pamoja na watu waliokuwa wameubeba. 19 Lakini walipofika kwenye sanamu za mawe* huko Gilgali,+ akarudi kwa mfalme na kumwambia: “Nina ujumbe wako wa siri, Ee mfalme.” Basi mfalme akasema, “Ondokeni!” Ndipo watumishi wake wote wakaondoka. 20 Naye Ehudi akamkaribia alipokuwa ameketi peke yake darini katika chumba chake chenye baridi. Kisha Ehudi akasema, “Nina ujumbe wako kutoka kwa Mungu.” Kwa hiyo akasimama kutoka katika kiti chake cha ufalme. 21 Ndipo Ehudi akauchomoa upanga kwa mkono wake wa kushoto kutoka upande wa kulia wa kiuno chake na kumchoma mfalme tumboni. 22 Upanga ukazama tumboni mwake pamoja na mpini wake, na mafuta yakaufunika upanga huo kwa sababu hakuuchomoa, na kinyesi kikatoka. 23 Naye Ehudi akatoka nje kupitia barazani,* akafunga kwa ufunguo milango ya chumba cha darini. 24 Baada ya Ehudi kuondoka, watumishi wa mfalme walirudi na kuona milango ya chumba cha darini ikiwa imefungwa kwa ufunguo. Kwa hiyo wakasema, “Labda ameenda msalani katika chumba chake cha ndani.” 25 Waliendelea kungoja kwa muda mrefu mpaka wakaaibika, lakini walipoona kwamba hafungui milango ya chumba cha darini, wakachukua ufunguo na kuifungua, wakamwona bwana wao ameanguka sakafuni akiwa amekufa!

26 Ehudi akatoroka walipokuwa wanangoja, naye akapita karibu na sanamu za mawe,*+ akafika salama salimini kule Seira. 27 Alipofika huko, akapiga pembe*+ katika eneo lenye milima la Efraimu;+ na Waisraeli wakashuka pamoja naye kutoka milimani, yeye akiwa mbele yao. 28 Ndipo akawaambia, “Nifuateni, kwa sababu Yehova amewatia maadui wenu, Wamoabu, mikononi mwenu.” Nao wakamfuata, wakateka vivuko vya Yordani ili kuwazuia Wamoabu wasikimbie, na hawakumruhusu mtu yeyote avuke. 29 Wakati huo waliwaua Wamoabu wapatao 10,000,+ na wote walikuwa wanaume wenye nguvu na mashujaa; hakuna hata mmoja wao aliyeponyoka.+ 30 Basi siku hiyo Waisraeli wakawashinda Wamoabu; na nchi ikawa na amani* kwa miaka 80.+

31 Baada ya Ehudi, akaja Shamgari+ mwana wa Anathi, aliyewaua wanaume 600 Wafilisti+ kwa mchokoo wa ng’ombe;+ yeye pia aliwaokoa Waisraeli.

4 Baada ya Ehudi kufa, Waisraeli wakaanza tena kutenda maovu machoni pa Yehova.+ 2 Kwa hiyo Yehova akawatia mikononi mwa* Yabini mfalme wa Kanaani,+ aliyetawala Hasori. Mkuu wa jeshi lake aliitwa Sisera, naye aliishi Haroshethi+ ya mataifa.* 3 Waisraeli wakamlilia Yehova+ kwa sababu Yabini alikuwa na magari 900 ya vita yenye miundu ya chuma,*+ na kwa miaka 20 aliwakandamiza sana Waisraeli.+

4 Basi Debora, nabii wa kike,+ mke wa Lapidothi, ndiye aliyekuwa mwamuzi wa Israeli wakati huo. 5 Naye alizoea kuketi chini ya mtende wa Debora uliokuwa kati ya Rama+ na Betheli+ katika eneo lenye milima la Efraimu; Waisraeli walikuwa wakienda kwake ili kupata maamuzi. 6 Akatuma mjumbe amwite Baraka+ mwana wa Abinoamu kutoka Kedesh-naftali,+ akamwambia, “Yehova Mungu wa Israeli anakuamuru hivi: ‘Nenda* katika Mlima Tabori ukiwa na wanaume 10,000 kutoka kabila la Naftali na la Zabuloni. 7 Nitakuletea Sisera, mkuu wa jeshi la Yabini na magari yake ya vita na majeshi yake kwenye kijito cha* Kishoni,+ nami nitamtia mikononi mwako.’”+

8 Ndipo Baraka akamwambia, “Ukienda pamoja nami, nitaenda, lakini usipoenda pamoja nami, sitaenda.” 9 Basi Debora akamwambia, “Hakika nitaenda pamoja nawe. Hata hivyo, hutapata sifa katika vita hivyo, kwa kuwa Yehova atamtia Sisera mikononi mwa mwanamke.”+ Ndipo Debora akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi.+ 10 Baraka akawaita watu wa kabila la Zabuloni na Naftali+ waje Kedeshi, na wanaume 10,000 wakamfuata. Debora pia akamfuata.

11 Lakini Heberi Mkeni alikuwa amejitenga na Wakeni,+ waliokuwa wazao wa Hobabu, baba mkwe wa Musa,+ naye alipiga hema lake karibu na mti mkubwa uliokuwa Saananimu, kule Kedeshi.

12 Wakamwambia Sisera kwamba Baraka mwana wa Abinoamu amepanda kwenda kwenye Mlima Tabori.+ 13 Mara moja Sisera akakusanya magari yake yote ya vita—magari 900 yenye miundu ya chuma*—na wanajeshi wote walioandamana naye kutoka Haroshethi ya mataifa na kwenda kwenye kijito cha* Kishoni.+ 14 Ndipo Debora akamwambia Baraka: “Inuka! Kwa maana hii ndiyo siku ambayo Yehova atamtia Sisera mikononi mwako. Yehova anakutangulia.” Na Baraka akashuka Mlima Tabori akifuatwa na wanaume 10,000. 15 Kisha Yehova akamvuruga+ Sisera na magari yake yote ya vita na jeshi lake lote na kuwaangamiza kwa upanga wa Baraka. Ndipo Sisera akatoka katika gari lake na kukimbia kwa miguu. 16 Baraka akayafuatia yale magari ya vita na lile jeshi mpaka Haroshethi ya mataifa. Jeshi lote la Sisera likaangamizwa kwa upanga; hakubaki hata mtu mmoja.+

17 Lakini Sisera akakimbia kwa miguu mpaka kwenye hema la Yaeli+ mke wa Heberi Mkeni,+ kwa maana kulikuwa na amani kati ya Yabini+ mfalme wa Hasori na nyumba ya Heberi Mkeni. 18 Kisha Yaeli akatoka nje kumpokea Sisera, akamwambia, “Karibu bwana wangu, karibu ndani. Usiogope.” Basi akaingia ndani ya hema lake, naye Yaeli akamfunika kwa blanketi. 19 Sisera akamwambia, “Tafadhali, nipe maji kidogo ya kunywa, kwa maana nina kiu.” Basi Yaeli akafungua kiriba cha ngozi chenye maziwa na kumpa anywe,+ kisha akamfunika tena. 20 Sisera akamwambia, “Simama kwenye mlango wa hema, na mtu yeyote akija kukuuliza kama kuna yeyote hemani, mwambie, ‘Hakuna!’”

21 Lakini Yaeli mke wa Heberi akachukua kigingi cha hema na nyundo. Kisha Sisera alipokuwa amelala usingizi mzito kwa sababu ya uchovu, Yaeli akaenda kimyakimya na kukipigilia kile kigingi kichwani mwake,* nacho kikapenya mpaka udongoni, akafa.+

22 Baraka alipokuwa anamtafuta Sisera, Yaeli akatoka nje kumpokea, akamwambia, “Njoo nikuonyeshe mtu unayemtafuta.” Baraka akamfuata hemani, akamwona Sisera akiwa amekufa, kigingi kikiwa kichwani mwake.

23 Basi siku hiyo, Mungu akamshinda Yabini mfalme wa Kanaani mbele ya Waisraeli.+ 24 Na Waisraeli wakaendelea kuwa na nguvu* na kumshinda Yabini mfalme wa Kanaani,+ mpaka walipomwangamiza Yabini mfalme wa Kanaani.+

5 Siku hiyo Debora+ pamoja na Baraka+ mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:+

 2 “Kwa sababu ya nywele ndefu* katika Israeli,

Kwa sababu ya watu kujitolea,+

Msifuni Yehova!

 3 Sikilizeni, enyi wafalme! Tegeni sikio, enyi watawala!

Nitamwimbia Yehova.

Nitamwimbia sifa* Yehova,+ Mungu wa Israeli.+

 4 Yehova, ulipotoka Seiri,+

Ulipopiga mwendo kutoka eneo la Edomu,

Dunia ilitikisika, na mbingu zikamwaga maji,

Naam, mawingu yakamwaga maji.

 5 Milima iliyeyuka* mbele za uso wa Yehova,+

Hata Sinai kutoka mbele za uso wa Yehova,+ Mungu wa Israeli.+

 6 Katika siku za Shamgari+ mwana wa Anathi,

Katika siku za Yaeli,+ barabara hazikuwa na watu;

Wasafiri walipita vichochoroni.

 7 Wanavijiji katika Israeli walitoweka;

Walitoweka, mpaka mimi Debora+ nilipotokea,

Mpaka nilipotokea kama mama katika Israeli.+

 8 Walichagua miungu mipya;+

Kisha kukawa na vita malangoni.+

Hakukuwa na ngao, wala mkuki,

Kati ya wanaume 40,000 katika Israeli.

 9 Moyo wangu uko pamoja na makamanda wa Israeli,+

Waliojitolea na kwenda pamoja na watu.+

Msifuni Yehova!

10 Ninyi mnaopanda juu ya punda wa hudhurungi,

Ninyi mnaoketi kwenye mazulia bora,

Nanyi mnaotembea barabarani,

Fikirieni mambo haya!

11 Sauti za wanaoteka maji zilisikika mahali pa kuteka maji;

Walisimulia matendo ya uadilifu ya Yehova,

Matendo ya uadilifu ya wanavijiji katika Israeli.

Kisha watu wa Yehova wakashuka malangoni.

12 Amka, amka, Ee Debora!+

Amka, amka, imba wimbo!+

Inuka, Baraka!+ Wachukue mateka wako, Ee mwana wa Abinoamu!

13 Ndipo waliobaki wakashuka kwenda kwa watu mashuhuri;

Watu wa Yehova wakashuka kuja kwangu ili kupigana na wanaume wenye nguvu.

14 Walitoka Efraimu, wale walio bondeni;*

Wanakufuata, Ee Benjamini, kati ya watu wako.

Kutoka Makiri+ makamanda walishuka,

Na kutoka Zabuloni wale wanaobeba fimbo za wanaowaandikisha watu jeshini.*

15 Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora,

Walikuwa pamoja naye kama Baraka+ alivyokuwa pamoja naye.

Alipelekwa kwa miguu bondeni.*+

Kati ya vikundi vya Rubeni watu waliuchunguza sana moyo wao.

16 Kwa nini uliketi chini kama mnyama aliyelemewa na mizigo,*

Ukiwasikiliza wakiwapigia kondoo zumari?+

Kwa kuwa watu walisitasita sana kati ya vikundi vya Rubeni.

17 Watu wa Gileadi walibaki ng’ambo ya Yordani;+

Kabila la Dani, kwa nini mliendelea kukaa kwenye meli?+

Watu wa kabila la Asheri waliketi kizembe kando ya bahari,

Na kuendelea kukaa bandarini.+

18 Watu wa Zabuloni walihatarisha uhai wao* karibu wafe;

Naftali pia,+ kwenye vilima vilivyo wazi.+

19 Wafalme walikuja, wakapigana vita;

Wafalme wa Kanaani wakapigana+

Huko Taanaki, kando ya maji ya Megido.+

Hawakuchukua fedha kama nyara.+

20 Kutoka mbinguni nyota zilipigana;

Kutoka kwenye njia zake zilipigana na Sisera.

21 Mafuriko ya Kishoni yaliwafagilia* mbali,+

Mafuriko ya* kale, mafuriko ya* Kishoni.

Uliwakanyaga wenye nguvu, Ee nafsi* yangu.

22 Ndipo kwato za farasi zilipokanyaga kwa kishindo

Farasi dume walipokimbia kwa kasi.+

23 ‘Mlaani Merozi,’ akasema malaika wa Yehova,

‘Naam, walaani wakaaji wake,

Kwa sababu hawakuja kumsaidia Yehova,

Kumsaidia Yehova pamoja na mashujaa.’

24 Amebarikiwa sana Yaeli kati ya wanawake wote+

Mke wa Heberi+ Mkeni;

Naam, amebarikiwa kuliko wanawake wote wanaokaa katika mahema.

25 Aliomba maji; Yaeli akampa maziwa.

Alimpa maziwa ya mgando* katika bakuli kubwa.+

26 Alinyoosha mkono wake akachukua kigingi cha hema,

Na kwa mkono wake wa kulia akachukua nyundo ya fundi.

Akampiga Sisera kwa nyundo, akamponda kichwa,

Akampasua na kumtoboa kichwa.+

27 Alianguka katikati ya miguu yake; alianguka na kulala kimya;

Alianguka katikati ya miguu yake akafa;

Alipoangukia, hapo ndipo alipolala akiwa ameshindwa.

28 Kupitia dirishani mwanamke aliangalia nje,

Mama ya Sisera alitazama

kupitia viunzi vya dirisha,

‘Mbona gari lake la vita limechelewa kuja?

Mbona vishindo vya kwato za farasi wake vimechelewa sana?’+

29 Wanawake wenye hekima zaidi nyumbani mwake walimjibu;

Naam, yeye pia alisema tena na tena moyoni mwake,

30 ‘Bila shaka wanagawana nyara walizopata,

Msichana mmoja, wasichana wawili, kwa kila shujaa,

Nguo iliyotiwa rangi kwa ajili ya Sisera, nyara ya nguo iliyotiwa rangi,

Vazi lililopambwa,* nguo iliyotiwa rangi, mavazi mawili yaliyopambwa

Kwa ajili ya shingo za waliochukua nyara.’

31 Maadui wako wote na waangamie,+ Ee Yehova,

Lakini wanaokupenda na wawe kama jua linalochomoza katika utukufu wake.”

Na nchi ikawa na amani* kwa miaka 40.+

6 Lakini Waisraeli wakatenda tena mambo maovu machoni pa Yehova,+ basi Yehova akawatia mikononi mwa Wamidiani kwa miaka saba.+ 2 Na Wamidiani wakawakandamiza Waisraeli.+ Kwa sababu ya Wamidiani, Waisraeli wakachimba mashimo ya kujificha* katika milima, mapango, na mahali pagumu kufikiwa.+ 3 Waisraeli walipopanda mbegu, Wamidiani, Waamaleki,+ na watu wa Mashariki+ waliwashambulia. 4 Nao walikuwa wakipiga kambi ili kuwashambulia na kuharibu mazao yote nchini hadi Gaza, na hawakuwaachia Waisraeli chakula chochote, wala kondoo, ng’ombe dume, au punda.+ 5 Walikuja na mifugo yao na mahema mengi sana kama nzige,+ na wao pamoja na ngamia wao hawangeweza kuhesabiwa,+ walikuja ili kuiharibu nchi. 6 Basi Wamidiani wakawafanya Waisraeli kuwa maskini sana; na Waisraeli wakamlilia Yehova awasaidie.+

7 Waisraeli walipomlilia Yehova awasaidie kwa sababu ya Wamidiani,+ 8 Yehova aliwaletea Waisraeli nabii aliyewaambia hivi: “Yehova Mungu wa Israeli anasema, ‘Niliwatoa Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa.+ 9 Nikawaokoa kutoka mikononi mwa Wamisri na mikononi mwa wote waliowakandamiza, nikawafukuza mbele yenu na kuwapa ninyi nchi yao.+ 10 Kisha nikawaambia, “Mimi ni Yehova Mungu wenu.+ Msiogope miungu ya Waamori ambao mnakaa katika nchi yao.”+ Lakini hamkunitii.’”*+

11 Baadaye malaika wa Yehova akaja+ na kuketi chini ya mti mkubwa wa Yoashi Mwabiezeri uliokuwa Ofra.+ Gideoni mwanawe+ alikuwa akipura ngano katika shinikizo la divai ili Wamidiani wasiione. 12 Ndipo malaika wa Yehova akamtokea, akamwambia hivi: “Yehova yuko pamoja nawe,+ ewe shujaa hodari.” 13 Gideoni akamwambia, “Niwie radhi, bwana wangu, lakini ikiwa Yehova yuko pamoja nasi, kwa nini mambo haya yote yametupata?+ Yako wapi matendo yake ya ajabu ambayo baba zetu walitusimulia,+ wakisema, ‘Yehova ndiye aliyetutoa Misri?’+ Sasa Yehova ametuacha,+ naye ametutia mikononi mwa Wamidiani.” 14 Ndipo Yehova akamgeukia na kumwambia, “Nenda kwa nguvu ulizo nazo, nawe utawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wamidiani.+ Je, si mimi ninayekutuma?” 15 Gideoni akamjibu, “Niwie radhi, Yehova. Ninawezaje kuwaokoa Waisraeli? Ukoo wangu ndio mdogo* zaidi katika kabila la Manase, nami ni mdogo kabisa katika nyumba ya baba yangu.” 16 Lakini Yehova akamwambia, “Kwa sababu nitakuwa pamoja nawe,+ utawashinda Wamidiani kana kwamba ni mtu mmoja.”

17 Ndipo Gideoni akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, nionyeshe ishara kwamba ni wewe unayeongea nami. 18 Tafadhali usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea zawadi yangu na kuiweka mbele yako.”+ Basi akasema, “Sitaondoka mpaka utakaporudi.” 19 Kwa hiyo Gideoni akaingia nyumbani na kutayarisha mwanambuzi na kuoka mikate isiyo na chachu kwa kutumia efa* ya unga.+ Akaweka nyama katika kikapu na kutia mchuzi katika chungu cha kupikia; kisha akampelekea chini ya ule mti mkubwa.

20 Sasa yule malaika wa Mungu wa kweli akamwambia, “Chukua nyama na mikate hiyo isiyo na chachu, uviweke juu ya lile jiwe kubwa, na umimine mchuzi juu yake.” Akafanya hivyo. 21 Ndipo malaika wa Yehova akanyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kwa ncha yake akaigusa ile nyama na ile mikate isiyo na chachu, na moto ukatoka kwenye lile jiwe na kuiteketeza ile nyama na ile mikate isiyo na chachu.+ Kisha malaika wa Yehova akatoweka. 22 Ndipo Gideoni akatambua kwamba huyo alikuwa malaika wa Yehova.+

Mara moja Gideoni akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, kwa sababu nimemwona malaika wa Yehova uso kwa uso!”+ 23 Lakini Yehova akamwambia, “Uwe na amani. Usiogope;+ hutakufa.” 24 Basi Gideoni akamjengea Yehova madhabahu hapo, ambayo mpaka leo hii inaitwa Yehova-shalomu.*+ Bado iko huko Ofra ya Waabiezeri.

25 Usiku huo Yehova akamwambia, “Mchukue ng’ombe dume mchanga wa baba yako, ng’ombe dume mchanga wa pili mwenye miaka saba, nawe ubomoe madhabahu ya Baali ambayo ni ya baba yako, na ukate mti mtakatifu* ulio kando yake.+ 26 Baada ya kumjengea Yehova Mungu wako madhabahu juu ya ngome hii kwa mawe yaliyopangwa vizuri, mchukue yule ng’ombe dume mchanga wa pili unitolee dhabihu ya kuteketezwa juu ya kuni za ule mti mtakatifu* ambao ulikata.” 27 Basi Gideoni akawachukua wanaume kumi kati ya watumishi wake na kufanya kama Yehova alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa sana watu wa nyumba ya baba yake na wakaaji wa jiji, hakufanya mambo hayo mchana, aliyafanya usiku.

28 Wakaaji wa jiji walipoamka asubuhi na mapema, waliona kwamba madhabahu ya Baali ilikuwa imebomolewa na ule mti mtakatifu* uliokuwa kando yake ulikuwa umekatwa, na yule ng’ombe dume mchanga wa pili alikuwa ameteketezwa juu ya madhabahu iliyokuwa imejengwa. 29 Wakaulizana, “Ni nani aliyefanya jambo hili?” Baada ya kufanya uchunguzi, wakasema, “Gideoni mwana wa Yoashi ndiye aliyefanya jambo hili.” 30 Kwa hiyo wakaaji wa jiji wakamwambia hivi Yoashi: “Mtoe nje mwana wako, anapaswa kufa kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukata mti mtakatifu* uliokuwa kando yake.” 31 Ndipo Yoashi+ akawaambia watu wote waliomkabili, “Je, ni lazima mumtetee Baali? Je, ni lazima mumwokoe? Yeyote anayemtetea anapaswa kuuawa asubuhi hii.+ Ikiwa yeye ni mungu, acheni ajitetee mwenyewe,+ kwa sababu mtu fulani amebomoa madhabahu yake.” 32 Siku hiyo akamwita Gideoni jina Yerubaali,* akisema, “Acheni Baali ajitetee mwenyewe, kwa sababu mtu fulani amebomoa madhabahu yake.”

33 Wamidiani wote+ na Waamaleki+ na watu wa Mashariki wakaungana;+ wakavuka* na kupiga kambi katika Bonde la* Yezreeli. 34 Kisha roho ya Yehova ikamjia* Gideoni+ naye akapiga pembe,*+ na Waabiezeri+ wakakusanyika na kumfuata. 35 Akatuma wajumbe katika nchi yote ya kabila la Manase, wakakusanyika pia na kumfuata. Akatuma pia wajumbe kotekote katika nchi ya Asheri, Zabuloni, na Naftali, nao wakaja kukutana naye.

36 Kisha Gideoni akamwambia hivi Mungu wa kweli: “Ikiwa utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi,+ 37 ninaweka manyoya ya kondoo kwenye uwanja wa kupuria. Ikiwa kutakuwa na umande juu ya manyoya hayo peke yake lakini ardhi yote inayozunguka manyoya hayo iwe kavu, ndipo nitakapojua kwamba utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi.” 38 Na ikawa hivyo. Alipoamka mapema siku iliyofuata na kukamua manyoya hayo, maji ya umande yalijaa kwenye bakuli kubwa. 39 Hata hivyo, Gideoni akamwambia hivi Mungu wa kweli: “Tafadhali usinikasirikie, nakuomba jambo moja zaidi. Tafadhali niruhusu nifanye jaribio lingine moja tu kwa manyoya haya. Tafadhali, acha manyoya peke yake yawe makavu, na ardhi yote iwe na umande.” 40 Basi Mungu akafanya hivyo usiku huo; manyoya peke yake yakawa makavu, na ardhi yote ikawa na umande.

7 Ndipo Yerubaali, yaani, Gideoni,+ na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaamka mapema na kupiga kambi karibu na Chemchemi ya Harodi, nayo kambi ya Wamidiani ilikuwa bondeni* upande wa kaskazini wa kambi yao karibu na kilima cha More. 2 Yehova akamwambia Gideoni, “Watu ulio nao ni wengi sana kwangu mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao.+ Waisraeli wasije wakajigamba mbele zangu wakisema, ‘Mkono wangu mwenyewe uliniokoa.’+ 3 Sasa tafadhali, watangazie hivi watu wote: ‘Mtu yeyote anayeogopa na kutetemeka, arudi nyumbani.’”+ Basi Gideoni akawajaribu kwa maneno hayo. Ndipo watu 22,000 wakarudi nyumbani, wakabaki watu 10,000.

4 Lakini Yehova akamwambia hivi Gideoni: “Watu hawa bado ni wengi sana. Wapeleke kwenye maji ili niwajaribu kwa ajili yako. Mtu yeyote nitakayekuambia, ‘Huyu ataenda pamoja nawe,’ ataenda pamoja nawe, lakini yeyote nitakayekwambia, ‘Huyu hataenda pamoja nawe,’ basi hataenda.” 5 Basi Gideoni akawapeleka watu kwenye maji.

Kisha Yehova akamwambia Gideoni, “Watenganishe watu wote wanaoramba maji kama mbwa anavyoramba na watu wanaopiga magoti kunywa maji.” 6 Wale waliochota maji kwa mikono yao na kuyaramba walikuwa wanaume 300. Lakini wengine wote walipiga magoti walipokunywa maji.

7 Sasa Yehova akamwambia hivi Gideoni: “Nitawatumia wanaume hawa 300 walioramba maji kuwaokoa ninyi, nami nitawatia Wamidiani mikononi mwako.+ Lakini waambie wengine wote warudi nyumbani.” 8 Kwa hiyo wakachukua vyakula na pembe* za wanaume hao Waisraeli, kisha Gideoni akawaambia wote warudi nyumbani, akabaki na wale 300 peke yao. Kambi ya Wamidiani ilikuwa upande wa chini bondeni.+

9 Usiku huo, Yehova akamwambia hivi: “Nenda uishambulie kambi, kwa maana nimeitia mikononi mwako.+ 10 Lakini ikiwa unaogopa kuishambulia, nenda kwanza kambini na Pura mtumishi wako. 11 Sikiliza wanayosema, nawe utapata ujasiri wa* kuwashambulia.” Ndipo yeye na Pura mtumishi wake wakashuka mpaka ukingoni mwa kambi hiyo ya kijeshi.

12 Wamidiani na Waamaleki na watu wote wa Mashariki+ walikuwa wamejaa bondeni nao walikuwa wengi kama nzige, na ngamia wao hawangeweza kuhesabiwa,+ walikuwa wengi kama chembe za mchanga kwenye ufuo wa bahari. 13 Gideoni alipofika, mtu fulani alikuwa akimsimulia mwenzake ndoto, akisema, “Katika ndoto niliona mkate wa shayiri wa mviringo ukivingirika hadi kwenye kambi ya Wamidiani. Ukalipiga hema kwa nguvu na kuliangusha.+ Naam, ukalipindua hema hilo, likaanguka chini.” 14 Basi mwenzake akasema, “Bila shaka huo ni upanga wa Gideoni+ mwana wa Yoashi, mwanamume Mwisraeli. Mungu amewatia Wamidiani na kambi yote mikononi mwake.”+

15 Mara tu Gideoni alipomsikia akisimulia ndoto hiyo na kueleza maana yake,+ akainama chini na kuabudu. Kisha akarudi katika kambi ya Waisraeli na kusema, “Twendeni, kwa kuwa Yehova ameitia kambi ya Wamidiani mikononi mwenu.” 16 Basi akawagawa wale wanaume 300 katika vikosi vitatu na kuwapa wote pembe*+ na mitungi mikubwa mitupu yenye mienge. 17 Akawaambia, “Nitazameni na kufanya kama tu nitakavyofanya. Nitakapofika kwenye ukingo wa kambi, fanyeni kama nitakavyofanya. 18 Nitakapopiga pembe,* mimi na wote walio pamoja nami, ninyi pia zipigeni pembe* kuizunguka kambi yote na kupaza sauti, ‘Upanga wa Yehova na wa Gideoni!’”

19 Gideoni na wale wanaume 100 waliokuwa pamoja naye wakaja kwenye ukingo wa kambi mwanzoni mwa kesha la katikati ya usiku,* baada tu ya askari walinzi kuanza zamu. Wakazipiga zile pembe*+ na kuivunjavunja ile mitungi mikubwa waliyokuwa wamebeba mikononi mwao.+ 20 Ndipo vile vikosi vitatu vikapiga pembe* na kuivunjavunja ile mitungi mikubwa. Wakashika mienge kwa mikono ya kushoto na zile pembe kwa mikono ya kulia na kuzipiga, wakipaza sauti, “Upanga wa Yehova na wa Gideoni!” 21 Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka ile kambi, na jeshi lote likakimbia huku likipiga kelele.+ 22 Wanaume hao 300 wakaendelea kupiga pembe,* na Yehova akawafanya waanze kuuana wao kwa wao katika kambi yote;+ na jeshi likakimbia hadi Beth-shita, likafika Serera, hadi mpakani mwa Abel-mehola+ karibu na Tabathi.

23 Wanaume Waisraeli wakakusanywa kutoka katika kabila la Naftali, Asheri, na kabila lote la Manase,+ nao wakawafuatia Wamidiani. 24 Gideoni akatuma wajumbe katika eneo lote lenye milima la Efraimu, akisema, “Shukeni mkawashambulie Wamidiani, wazuieni wasivuke vijito vyote vya maji kufikia Beth-bara na pia Yordani.” Basi watu wote wa Efraimu wakakusanyika pamoja, nao wakawazuia kuvuka vijito vyote vya maji kufikia Beth-bara na Yordani. 25 Pia wakawakamata wale wakuu wawili wa Midiani, yaani, Orebu na Zeebu; wakamuua Orebu juu ya mwamba wa Orebu+ na kumuua Zeebu kwenye shinikizo la divai la Zeebu. Wakaendelea kuwafuatia Wamidiani,+ nao wakamletea Gideoni kichwa cha Orebu na cha Zeebu katika eneo la Yordani.

8 Ndipo watu wa Efraimu wakamuuliza Gideoni, “Kwa nini umetutendea hivi? Kwa nini hukutuita ulipoenda kupigana na Wamidiani?”+ Nao wakamshutumu vikali.+ 2 Lakini akawaambia, “Mimi nimefanya nini nikilinganishwa nanyi? Je, masalio ya Efraimu+ si bora kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?+ 3 Mungu aliwatia mikononi mwenu Orebu na Zeebu,+ wakuu wa Midiani, lakini mimi nimefanya nini nikilinganishwa nanyi?” Gideoni aliposema hivyo* hasira yao ikapoa.*

4 Gideoni na wale wanaume 300 waliokuwa pamoja naye wakafika Yordani na kuvuka. Ingawa walikuwa wamechoka, waliendelea kuwafuatia maadui wao. 5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali wapeni mikate watu walio pamoja nami, kwa kuwa wamechoka nami ninawafuatia Zeba na Zalmuna, wafalme wa Midiani.” 6 Lakini wakuu wa Sukothi wakamwambia, “Je, tayari umewakamata Zeba na Zalmuna ili tuwape wanajeshi wako mikate?” 7 Ndipo Gideoni akawaambia, “Ni sawa, lakini Yehova atakapowatia Zeba na Zalmuna mikononi mwangu, nitawacharaza ninyi kwa miiba na michongoma ya nyikani.”+ 8 Naye akatoka huko na kwenda Penueli, akawaomba pia mikate, lakini watu wa Penueli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyomjibu. 9 Basi akawaambia pia watu wa Penueli, “Nitakaporudi baada ya kushinda, nitaubomoa mnara huu.”+

10 Basi Zeba na Zalmuna walikuwa Karkori pamoja na wanajeshi wao wapatao 15,000. Hao tu ndio waliobaki wa jeshi lote la watu wa Mashariki,+ kwa kuwa wenzao 120,000 waliotumia upanga waliuawa. 11 Gideoni akaendelea kupanda kupitia eneo la watu waliokaa mahemani upande wa mashariki wa Noba na Yogbeha+ na kushambulia kambi ya maadui ambao hawakuwa wamejitayarisha kupigana. 12 Zeba na Zalmuna walipokimbia, Gideoni aliwafuatia na kuwakamata hao wafalme wawili wa Midiani, Zeba na Zalmuna, na jeshi lao lote likaogopa.

13 Kisha Gideoni mwana wa Yoashi akarudi kutoka vitani kupitia njia inayopanda kwenda Heresi. 14 Alipokuwa njiani, alimkamata kijana mmoja wa Sukothi na kumuuliza maswali. Basi kijana huyo akamwandikia majina 77 ya wakuu na wazee wa Sukothi. 15 Ndipo akarudi kwa watu wa Sukothi na kuwaambia, “Ndio hawa Zeba na Zalmuna ambao mlinidhihaki kuwahusu mkisema, ‘Je, tayari umewakamata Zeba na Zalmuna ndipo tuwape mikate wanaume wako waliochoka?’”+ 16 Ndipo akawachukua wazee wa jiji hilo na kuwacharaza kwa miiba na michongoma ya nyikani, akawafunza somo wanaume wa Sukothi.+ 17 Kisha akabomoa mnara wa Penueli+ na kuwaua watu wa jiji hilo.

18 Akawauliza Zeba na Zalmuna, “Watu mliowaua kule Tabori walikuwaje?” Wakasema, “Walikuwa kama wewe, walikuwa kama wana wa mfalme.” 19 Ndipo akasema, “Ni ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, ikiwa hamngewaua, mimi pia singewaua ninyi.” 20 Kisha akamwambia Yetheri mzaliwa wake wa kwanza, “Haya, waue.” Lakini kijana huyo hakuchomoa upanga wake; aliogopa kwa sababu alikuwa kijana tu. 21 Basi Zeba na Zalmuna wakamwambia, “Tuue wewe mwenyewe, kwa maana mwanamume hujulikana kwa nguvu zake.”* Basi Gideoni akawaua Zeba na Zalmuna+ na kuchukua mapambo yenye umbo la mwezi mwandamo yaliyokuwa shingoni mwa ngamia wao.

22 Baadaye Waisraeli wakamwambia Gideoni, “Tutawale, wewe na mwana wako na mjukuu wako pia, kwa maana umetuokoa kutoka mikononi mwa Wamidiani.”+ 23 Lakini Gideoni akawaambia, “Mimi sitawatawala, wala mwanangu. Yehova ndiye atakayewatawala.”+ 24 Pia akawaambia, “Ningependa kuomba jambo moja: Kila mmoja wenu anipe pete ya puani aliyochukua nyara.” (Walikuwa na pete za puani za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)+ 25 Wakasema, “Tutakupa.” Basi wakatandaza nguo na kila mmoja wao akaweka pete ya puani aliyochukua nyara. 26 Na zile pete za puani za dhahabu ambazo aliwaomba zilikuwa na uzito wa shekeli 1,700 za dhahabu,* mbali na yale mapambo yenye umbo la mwezi mwandamo, hereni, mavazi ya sufu ya rangi ya zambarau yaliyovaliwa na wafalme Wamidiani, na mikufu iliyokuwa shingoni mwa ngamia.+

27 Basi Gideoni akatumia dhahabu hiyo kutengeneza efodi*+ na kuiweka hadharani katika jiji lake la Ofra;+ na huko Waisraeli wote wakafanya nayo ukahaba wa kiroho,+ ikawa mtego kwa Gideoni na kwa nyumba yake.+

28 Hivyo Wamidiani+ wakashindwa na Waisraeli, na hawakupigana nao* tena; na nchi ikawa na amani* kwa miaka 40 katika siku za Gideoni.+

29 Basi Yerubaali+ mwana wa Yoashi akarudi nyumbani kwake na kukaa huko.

30 Gideoni akawa na wana 70,* kwa sababu alikuwa na wake wengi. 31 Na suria* wake aliyekuwa Shekemu akamzalia mwana, na Gideoni akamwita Abimeleki.+ 32 Gideoni mwana wa Yoashi akafa baada ya kuishi maisha marefu, akazikwa katika kaburi la Yoashi baba yake katika jiji la Ofra la Waabiezeri.+

33 Mara tu baada ya Gideoni kufa, Waisraeli wakaanza tena kufanya ukahaba wa kiroho na Mabaali,+ nao wakamfanya Baal-berithi kuwa mungu wao.+ 34 Na Waisraeli hawakumkumbuka Yehova Mungu wao+ aliyewaokoa kutoka mikononi mwa maadui wao waliowazunguka;+ 35 wala hawakuwa na upendo mshikamanifu kwa nyumba ya Yerubaali, yaani, Gideoni, aliyewatendea Waisraeli mambo mengi mema.+

9 Baada ya muda Abimeleki+ mwana wa Yerubaali akaenda Shekemu kwa ndugu za mama yake na kwa familia yote ya babu yake,* akawaambia hivi: 2 “Tafadhali waulizeni viongozi wote* wa Shekemu, ‘Je, ni afadhali zaidi kwenu kutawaliwa na wana wote 70 wa Yerubaali+ au na mtu mmoja tu? Kumbukeni kwamba mimi ni mfupa wenu na nyama yenu.’”*

3 Basi ndugu za mama yake wakawaambia viongozi wote wa Shekemu maneno hayo kwa niaba yake, nao wakaamua kumfuata* Abimeleki kwa maana walisema: “Yeye ni ndugu yetu.” 4 Wakampa Abimeleki vipande 70 vya fedha kutoka katika nyumba ya* Baal-berithi,+ naye akavitumia kuwakodi watu wazembe na wahuni ili wamfuate. 5 Kisha akaenda nyumbani kwa baba yake huko Ofra+ na kuwaua ndugu zake,+ wana 70 wa Yerubaali, juu ya jiwe moja. Yothamu mwana mdogo zaidi wa Yerubaali ndiye aliyeokoka peke yake, kwa sababu alijificha.

6 Kisha viongozi wote wa Shekemu na wakaaji wote wa Beth-milo wakakusanyika pamoja na kumweka Abimeleki kuwa mfalme,+ karibu na ule mti mkubwa, penye nguzo iliyokuwa Shekemu.

7 Walipomwambia Yothamu habari hizo, akaenda mara moja na kusimama juu ya kilele cha Mlima Gerizimu,+ akawaambia hivi kwa sauti kubwa: “Nisikilizeni, enyi viongozi wa Shekemu, naye Mungu atawasikiliza.

8 “Siku moja miti ilitaka kumtia mafuta mmoja wao awe mfalme. Basi ikauambia mzeituni, ‘Tutawale.’+ 9 Lakini mzeituni ukaiambia, ‘Je, niache kuzalisha mafuta yangu yanayotumiwa kumtukuza Mungu na wanadamu, niende kuitawala miti mingine?’ 10 Kisha miti ikauambia mtini, ‘Njoo ututawale.’ 11 Lakini mtini ukaiambia, ‘Je, niache kuzalisha matunda yangu matamu niende kuitawala miti mingine?’ 12 Kisha miti ikauambia mzabibu, ‘Njoo ututawale.’ 13 Mzabibu ukasema, ‘Je, niache kutoa divai yangu nzuri inayomfurahisha Mungu na wanadamu niende kuitawala miti?’ 14 Mwishowe miti mingine yote ikauambia mkwamba,* ‘Njoo ututawale.’+ 15 Ndipo mkwamba ukaiambia miti hiyo, ‘Ikiwa kweli mnanitia mafuta niwe mfalme wenu, njooni mkae chini ya kivuli changu. Kama sivyo, moto na utoke ndani yangu na kuiteketeza mierezi ya Lebanoni.’

16 “Je, mmetenda kwa unyoofu na heshima kwa kumweka Abimeleki kuwa mfalme,+ na je, mmemtendea wema Yerubaali na nyumba yake, je, mmemtendea anavyostahili? 17 Baba yangu alipowapigania,+ alihatarisha uhai wake* ili kuwaokoa kutoka mikononi mwa Wamidiani.+ 18 Lakini leo mmeasi nyumba ya baba yangu na kuwaua wanawe 70 juu ya jiwe moja.+ Kisha mkamweka Abimeleki, mwana wa kijakazi wake,+ awe mfalme juu ya viongozi wa Shekemu kwa sababu tu yeye ni ndugu yenu. 19 Basi ikiwa leo mmemtendea Yerubaali na nyumba yake kwa unyoofu na heshima, shangilieni pamoja na Abimeleki naye pia ashangilie pamoja nanyi. 20 Kama sivyo, moto na utoke kwa Abimeleki na kuwateketeza viongozi wa Shekemu na Beth-milo,+ pia moto utoke kwa viongozi wa Shekemu na Beth-milo na kumteketeza Abimeleki.”+

21 Ndipo Yothamu+ akakimbilia Beeri, akaishi huko kwa sababu alimwogopa Abimeleki ndugu yake.

22 Abimeleki alitawala* Israeli kwa miaka mitatu. 23 Ndipo Mungu akaacha uadui utokee* kati ya Abimeleki na viongozi wa Shekemu, nao wakamtendea Abimeleki kwa hila. 24 Hayo yalitokea ili kulipiza ukatili waliotendewa wale wana 70 wa Yerubaali, na ili hatia ya damu iwe juu ya Abimeleki ndugu yao kwa sababu aliwaua,+ na juu ya viongozi wa Shekemu kwa sababu walimsaidia kuua ndugu zake. 25 Basi viongozi wa Shekemu wakaweka watu wamvizie Abimeleki milimani, wakamwibia kila mtu aliyepita karibu nao. Abimeleki akaambiwa mambo hayo.

26 Basi Gaali mwana wa Ebedi na ndugu zake wakavuka kuingia Shekemu,+ nao viongozi wa Shekemu wakamtumaini. 27 Wakaenda kuvuna zabibu katika mashamba yao ya mizabibu na kuzikanyaga katika shinikizo la divai, wakafanya sherehe, kisha wakaingia katika nyumba ya mungu wao,+ wakala, wakanywa, na kumlaani Abimeleki. 28 Ndipo Gaali mwana wa Ebedi akasema, “Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani ili tumtumikie? Je, yeye si mwana wa Yerubaali,+ na je, Zebuli si mjumbe wake? Watumikieni wana wa Hamori, baba ya Shekemu! Kwa nini tumtumikie Abimeleki? 29 Laiti watu hawa wangekuwa chini ya amri yangu, ningemwondoa Abimeleki.” Kisha akamwambia hivi Abimeleki: “Ongeza jeshi lako, uje tupigane.”

30 Zebuli mkuu wa jiji aliposikia maneno ya Gaali mwana wa Ebedi, akakasirika sana. 31 Kwa hiyo akawatuma kwa siri* wajumbe kwa Abimeleki, akisema, “Gaali mwana wa Ebedi na ndugu zake wako Shekemu, wanalichochea jiji likupinge. 32 Basi njoo usiku pamoja na watu wako mwavizie shambani. 33 Mara tu jua linapochomoza asubuhi, amkeni mapema mlishambulie jiji; atakapokuja na watu wake kuwashambulia, jitahidini kabisa kumshinda.”*

34 Basi Abimeleki na watu wake wote wakaja usiku, wakalivizia jiji la Shekemu wakiwa vikosi vinne. 35 Gaali mwana wa Ebedi alipotoka nje na kusimama kwenye lango la jiji, Abimeleki na watu wake wakatoka mafichoni. 36 Gaali alipowaona, akamwambia Zebuli, “Tazama! Kuna watu wanaoshuka kutoka milimani.” Lakini Zebuli akamwambia, “Unaona vivuli vya milima ukifikiri ni watu.”

37 Baadaye Gaali akasema, “Tazama! Watu wanashuka kutoka katikati ya nchi, na kikosi kimoja kinakuja kupitia njia ya mti mkubwa wa Meonenimu.” 38 Ndipo Zebuli akamwambia, “Umesahau ulivyojigamba ukisema, ‘Abimeleki ni nani ili tumtumikie?’+ Je, hawa si wale watu uliowadharau? Sasa nenda upigane nao.”

39 Basi Gaali akawaongoza viongozi wa Shekemu kupigana na Abimeleki. 40 Gaali akashindwa na kukimbia, naye Abimeleki akamkimbiza, na watu wengi wakauawa mpaka kwenye lango la jiji.

41 Abimeleki akaendelea kukaa Aruma, naye Zebuli+ akawafukuza Gaali na ndugu zake kutoka Shekemu. 42 Kesho yake watu wakatoka na kwenda shambani, na Abimeleki akaambiwa jambo hilo. 43 Basi akachukua watu wake na kuwagawa katika vikosi vitatu na kuvizia shambani. Alipoona watu wakitoka jijini, akawashambulia na kuwaua. 44 Abimeleki na kikosi chake wakaenda mbio na kusimama kwenye lango la jiji, na vikosi viwili vikawashambulia na kuwaua watu wote waliokuwa shambani. 45 Abimeleki akapigana na jiji hilo siku nzima na kuliteka. Akawaua wakaaji wake, kisha akalibomoa jiji hilo+ na kulitia chumvi.

46 Viongozi wote wa mnara wa Shekemu waliposikia habari hizo, wakaenda haraka katika ngome ya nyumba ya* El-berithi.+ 47 Abimeleki alipoambiwa kwamba viongozi wote wa Shekemu wamekusanyika pamoja, 48 akapanda Mlima Salmoni pamoja na watu wake. Akachukua shoka, akakata tawi la mti na kulibeba begani, akawaambia hivi watu wake: “Mlivyoona nikifanya, fanyeni vivyo hivyo haraka!” 49 Basi watu wote wakakata pia matawi na kumfuata Abimeleki. Kisha wakayaweka kuzunguka ile ngome na kuiteketeza. Na watu wote waliokuwa ndani ya mnara wa Shekemu wakafa pia, watu karibu 1,000, wanaume na wanawake.

50 Kisha Abimeleki akaenda Thebesi; akalishambulia jiji la Thebesi na kuliteka. 51 Kulikuwa na mnara imara katikati ya jiji hilo, wanaume na wanawake wote, na viongozi wote wa jiji hilo wakakimbilia humo. Wakajifungia ndani yake na kupanda juu ya paa lake. 52 Abimeleki akaenda kwenye mnara huo na kuushambulia. Akaenda kwenye mlango wa mnara ili auchome moto. 53 Ndipo mwanamke fulani akaangusha jiwe la kusagia juu ya kichwa cha Abimeleki na kumpasua kichwa.+ 54 Abimeleki akamwita haraka mtumishi aliyembebea silaha na kumwambia, “Chomoa upanga wako uniue, watu wasije wakasema, ‘Mwanamke ndiye aliyemuua.’” Basi mtumishi wake akamchoma upanga, naye akafa.

55 Wanaume Waisraeli walipoona kwamba Abimeleki amekufa, wote wakarudi nyumbani. 56 Hivyo Mungu akalipiza kisasi kwa sababu ya uovu ambao Abimeleki alimtendea baba yake kwa kuwaua ndugu zake 70.+ 57 Pia Mungu akafanya watu wa Shekemu waadhibiwe kwa sababu ya uovu wao wote. Basi laana ya Yothamu+ mwana wa Yerubaali+ ikawapata.

10 Baada ya Abimeleki, alitokea Tola mwana wa Pua, mwana wa Dodo, wa kabila la Isakari, ili awaokoe Waisraeli.+ Aliishi Shamiri katika eneo lenye milima la Efraimu. 2 Alikuwa mwamuzi wa Waisraeli kwa miaka 23. Kisha akafa na kuzikwa huko Shamiri.

3 Baada yake akatokea Yairi Mgileadi, naye akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa miaka 22. 4 Alikuwa na wana 30 waliopanda juu ya punda 30, nao walikuwa na majiji 30 katika nchi ya Gileadi, ambayo mpaka leo yanaitwa Hawoth-yairi.+ 5 Kisha Yairi akafa na kuzikwa huko Kamoni.

6 Waisraeli wakaanza tena kutenda maovu machoni pa Yehova,+ nao wakaanza kuabudu Mabaali,+ sanamu za Ashtorethi, miungu ya Aramu,* miungu ya Sidoni, miungu ya Moabu,+ miungu ya Waamoni,+ na miungu ya Wafilisti.+ Wakamwacha Yehova wala hawakuendelea kumtumikia. 7 Basi hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli, naye akawatia mikononi mwa Wafilisti na Waamoni.+ 8 Kwa hiyo wakawatesa na kuwakandamiza sana Waisraeli mwaka huo—kwa miaka 18 waliwakandamiza Waisraeli wote waliokuwa ng’ambo ya Yordani katika nchi iliyokuwa ya Waamori kule Gileadi. 9 Waamoni pia walikuwa wakivuka Yordani ili kupigana na watu wa kabila la Yuda, Benjamini, na Efraimu; Waisraeli wakataabika sana. 10 Ndipo Waisraeli wakamlilia Yehova awasaidie,+ wakisema, “Tumekutendea dhambi Mungu wetu kwa sababu tumekuacha na kuabudu Mabaali.”+

11 Lakini Yehova akawaambia Waisraeli, “Je, sikuwaokoa kutoka Misri+ na kutoka mikononi mwa Waamori,+ Waamoni, Wafilisti,+ 12 Wasidoni, Waamaleki, na Wamidiani walipokuwa wakiwakandamiza? Mliponililia, niliwaokoa kutoka mikononi mwao. 13 Lakini mliniacha na kuabudu miungu mingine.+ Ndiyo sababu sitawaokoa tena.+ 14 Nendeni mkaililie miungu mliyochagua iwasaidie.+ Na iwaokoe kutoka katika taabu yenu.”+ 15 Lakini Waisraeli wakamwambia Yehova, “Tumetenda dhambi. Tutendee upendavyo. Lakini tunakusihi utuokoe leo hii.” 16 Wakaondoa miungu ya kigeni waliyokuwa nayo na kumtumikia Yehova,+ naye hakuweza tena kuvumilia* kuwaona Waisraeli wakiteseka.+

17 Baadaye Waamoni+ wakakusanyika na kupiga kambi huko Gileadi. Nao Waisraeli wakakusanyika na kupiga kambi huko Mispa. 18 Ndipo wakaaji wa Gileadi na wakuu wao wakaulizana, “Ni nani atakayetuongoza kupigana na Waamoni?+ Atakayefanya hivyo atakuwa kiongozi wa wakaaji wote wa Gileadi.”

11 Yeftha+ Mgileadi alikuwa shujaa hodari; mama yake alikuwa kahaba na baba yake aliitwa Gileadi. 2 Lakini mke wa Gileadi pia akazaa wana. Wana hao walipokua, walimfukuza Yeftha na kumwambia, “Hutarithi chochote katika nyumba ya baba yetu kwa sababu wewe ni mwana wa mwanamke mwingine.” 3 Basi Yeftha akawakimbia ndugu zake akaenda kuishi katika nchi ya Tobu. Na watu wazembe wakajiunga naye na kumfuata.

4 Baada ya muda, Waamoni wakapigana na Waisraeli.+ 5 Waamoni walipokuwa wakipigana na Waisraeli, wazee wa Gileadi wakaenda mara moja kumchukua Yeftha kutoka katika nchi ya Tobu. 6 Wakamwambia hivi Yeftha: “Njoo uwe kamanda wetu ili tupigane na Waamoni.” 7 Lakini Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi, “Je, si ninyi mlionichukia sana na kunifukuza kutoka nyumbani mwa baba yangu?+ Kwa nini mnanijia sasa mkiwa na matatizo?” 8 Ndipo wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, “Ni kweli, lakini sasa tumerudi kwako. Ukienda pamoja nasi kupigana na Waamoni, utakuwa kiongozi wetu na wa wakaaji wote wa Gileadi.”+ 9 Ndipo Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi, “Mkinirudisha ili nipigane na Waamoni na Yehova anisaidie kuwashinda, bila shaka nitakuwa kiongozi wenu!” 10 Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, “Yehova na awe shahidi* kati yetu na kutuhukumu tusipofanya unayosema.” 11 Basi Yeftha akaenda pamoja na wazee wa Gileadi, na watu wakamweka kuwa kiongozi na kamanda wao. Na Yeftha akasema tena masharti yake yote mbele za Yehova huko Mispa.+

12 Kisha Yeftha akatuma wajumbe kwa mfalme wa Waamoni,+ akisema, “Nimekukosea nini hivi kwamba umekuja kuishambulia nchi yangu?” 13 Mfalme wa Waamoni akawaambia wajumbe wa Yeftha, “Nimekuja kupigana nanyi kwa sababu Waisraeli walipotoka Misri+ walichukua nchi yangu, kuanzia Arnoni+ mpaka Yaboki hadi Yordani.+ Basi sasa irudishe kwa amani.” 14 Lakini Yeftha akawatuma tena wajumbe kwa mfalme wa Waamoni 15 ili wamwambie:

“Yeftha anasema hivi: ‘Waisraeli hawakuchukua nchi ya Wamoabu+ wala nchi ya Waamoni,+ 16 kwa sababu Waisraeli walipotoka Misri, walipitia nyikani hadi Bahari Nyekundu+ na mpaka Kadeshi.+ 17 Kisha Waisraeli wakatuma wajumbe kwa mfalme wa Edomu,+ wakisema, “Tafadhali turuhusu tupitie katika nchi yako,” lakini mfalme wa Edomu akakataa. Kisha wakatuma wajumbe kwa mfalme wa Moabu,+ naye pia akakataa. Basi Waisraeli wakaendelea kukaa Kadeshi.+ 18 Walipopitia nyikani, waliizunguka nchi ya Edomu+ na nchi ya Moabu. Wakapitia upande wa mashariki wa nchi ya Moabu+ na kupiga kambi katika eneo la Arnoni; hawakufika kwenye mpaka wa Moabu kwa sababu Mto Arnoni ulikuwa mpaka wa Moabu.+

19 “‘Kisha Waisraeli wakatuma wajumbe kwa Sihoni mfalme wa Waamori, mfalme wa Heshboni, wakamwambia hivi: “Tafadhali, turuhusu tupitie katika nchi yako twende katika nchi yetu.”+ 20 Lakini Sihoni hakuwaruhusu Waisraeli wapitie katika eneo lake kwa sababu hakuwaamini, basi Sihoni akawakusanya watu wake na kupiga kambi huko Yahazi na kupigana na Waisraeli.+ 21 Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli akamtia Sihoni na watu wake wote mikononi mwao, Waisraeli wakawashinda na kumiliki nchi yote ya Waamori, wakaaji wa nchi hiyo.+ 22 Basi wakamiliki eneo lote la Waamori kutoka Arnoni mpaka Yaboki na kuanzia nyikani mpaka Yordani.+

23 “‘Yehova Mungu wa Israeli ndiye aliyewafukuza Waamori kutoka mbele ya watu wake Israeli,+ na sasa je, unataka kuwafukuza Waisraeli? 24 Je, humiliki nchi yoyote unayopewa na mungu wako Kemoshi?+ Basi kila mtu ambaye Yehova Mungu wetu amemfukuza kutoka mbele yetu, ndiye tutakayemfukuza.+ 25 Je, una nguvu kuliko Balaki+ mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu? Yeye hakushindana na Waisraeli wala kupigana nao. 26 Waisraeli walipokuwa wakikaa katika jiji la Heshboni na miji yake,*+ Aroeri na miji yake, na katika majiji yote yaliyo ukingoni mwa Mto Arnoni kwa miaka 300, kwa nini hamkuyakomboa wakati huo?+ 27 Sijakukosea, lakini umenikosea kwa kunishambulia. Yehova ambaye ni Mwamuzi+ na aamue leo kati ya Waisraeli na Waamoni.’”

28 Lakini mfalme wa Waamoni hakusikiliza ujumbe wa Yeftha.

29 Roho ya Yehova ikamjia Yeftha,+ naye akapitia Gileadi na Manase na kufika Mispe kule Gileadi,+ na kutoka Mispe akaenda kupigana na Waamoni.

30 Ndipo Yeftha akaweka nadhiri+ kwa Yehova akisema, “Ukiwatia Waamoni mikononi mwangu, 31 yeyote atakayetoka nje ya mlango wa nyumba yangu ili kunipokea nitakaporudi baada ya kuwashinda Waamoni atakuwa wa Yehova,+ nami nitamtoa kama dhabihu ya kuteketezwa.”+

32 Basi Yeftha akaenda kupigana na Waamoni, na Yehova akawatia mikononi mwake. 33 Akawaua watu wengi kutoka Aroeri mpaka Minithi, majiji 20, mpaka Abel-keramimu. Kwa hiyo Waamoni wakashindwa na Waisraeli.

34 Mwishowe Yeftha akafika nyumbani kwake Mispa,+ na tazama! binti yake akatoka ili kumpokea, huku akipiga tari na kucheza dansi! Naye alikuwa ndiye mtoto pekee. Yeftha hakuwa na mwana wala binti mwingine ila yeye. 35 Yeftha alipomwona, akararua mavazi yake na kusema, “Ole wangu, binti yangu! Umenivunja moyo,* kwa kuwa nimesababisha uende mbali. Nimetoa ahadi kwa Yehova, na siwezi kuivunja.”+

36 Lakini akamwambia, “Baba yangu, ikiwa umetoa ahadi kwa Yehova, nitendee kama ulivyoahidi,+ kwa kuwa Yehova amelipiza kisasi dhidi ya maadui wako, Waamoni.” 37 Kisha akamwambia baba yake, “Naomba jambo hili: Niruhusu niwe peke yangu kwa miezi miwili, acha niende milimani nikaulilie ubikira wangu pamoja na wasichana wenzangu.”*

38 Ndipo akamwambia, “Nenda!” Basi akamruhusu aende kwa miezi miwili, akaenda milimani pamoja na wasichana wenzake kuulilia ubikira wake. 39 Baada ya miezi miwili, akarudi kwa baba yake, kisha baba yake akatimiza nadhiri aliyoweka kumhusu.+ Hakufanya ngono na mwanamume yeyote. Basi kukawa na desturi* hii katika Israeli: 40 Kila mwaka, wasichana Waisraeli walienda kumpongeza binti ya Yeftha Mgileadi siku nne kwa mwaka.

12 Watu wa kabila la Efraimu wakaitwa, nao wakavuka na kufika Zafoni,* wakamuuliza Yeftha, “Kwa nini hukutuita ulipovuka kwenda kupigana na Waamoni?+ Tutakuteketeza pamoja na nyumba yako.” 2 Lakini Yeftha akawaambia, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa pamoja na Waamoni. Nikawaomba ninyi mnisaidie, lakini hamkuniokoa kutoka mikononi mwao. 3 Nilipoona kwamba hamji kuniokoa, nikaamua kuhatarisha uhai wangu* na kwenda kupigana na Waamoni,+ na Yehova akawatia mikononi mwangu. Basi kwa nini mmekuja kupigana nami leo?”

4 Ndipo Yeftha akawakusanya watu wote wa Gileadi,+ wakapigana na watu wa Efraimu; na watu wa Gileadi wakawashinda Waefraimu kwa kuwa walisema, “Ninyi watu wa Gileadi ni wakimbizi tu kutoka Efraimu na kutoka Manase.” 5 Watu wa Gileadi wakateka vivuko vya Yordani+ ili kuwazuia Waefraimu wasivuke; na Waefraimu waliokuwa wakikimbia waliposema: “Naomba nivuke”; watu wa Gileadi walimuuliza kila mmoja wao, “Wewe ni Mwefraimu?” Aliposema: “Hapana!” 6 walimwambia, “Tafadhali sema Shibolethi.” Lakini alisema, “Sibolethi,” kwa kuwa hangeweza kutamka neno hilo kwa usahihi. Kwa hiyo walimkamata na kumuua kwenye vivuko vya Yordani. Basi Waefraimu 42,000 wakauawa wakati huo.

7 Yeftha alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka sita, kisha Yeftha Mgileadi akafa na kuzikwa katika jiji lake kule Gileadi.

8 Baada yake, Ibzani kutoka Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.+ 9 Alikuwa na watoto wa kiume 30 na wa kike 30. Akawaoza binti zake 30 nje ya ukoo wake, na akaleta wanawake 30 kutoka nje ya ukoo wake ili waolewe na watoto wake wa kiume. Alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka saba. 10 Kisha Ibzani akafa na kuzikwa Bethlehemu.

11 Na baada yake, Eloni Mzabuloni akawa mwamuzi wa Israeli kwa miaka kumi. 12 Kisha Eloni Mzabuloni akafa na kuzikwa Aiyaloni katika nchi ya Zabuloni.

13 Na baada yake, Abdoni mwana wa Hileli Mpirathoni akawa mwamuzi wa Israeli. 14 Alikuwa na wana 40 na wajukuu 30 waliopanda juu ya punda 70. Alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka minane. 15 Kisha Abdoni mwana wa Hileli Mpirathoni akafa na kuzikwa Pirathoni katika nchi ya Efraimu katika mlima wa Mwamaleki.+

13 Waisraeli wakaanza tena kutenda maovu machoni pa Yehova,+ na Yehova akawatia mikononi mwa Wafilisti+ kwa miaka 40.

2 Basi, kulikuwa na mtu mmoja huko Sora+ wa kabila la Dani+ aliyeitwa Manoa.+ Mke wake alikuwa tasa.+ 3 Siku moja malaika wa Yehova akamtokea mwanamke huyo na kumwambia, “Wewe ni tasa na huna mtoto. Lakini utapata mimba na kuzaa mwana.+ 4 Kwa hiyo, uwe mwangalifu usinywe divai wala chochote chenye kileo,+ na usile kitu chochote kisicho safi.+ 5 Tazama! Utapata mimba na kuzaa mwana; na hakuna wembe utakaogusa kichwa chake+ kwa sababu mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu kuzaliwa,* naye atawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wafilisti.”+

6 Ndipo mwanamke huyo akaenda na kumwambia hivi mume wake: “Mtu fulani wa Mungu wa kweli alinijia, na alikuwa kama malaika wa Mungu wa kweli, naye alikuwa mwenye kuogopesha sana. Sikumuuliza alikotoka, wala hakuniambia jina lake.+ 7 Lakini aliniambia, ‘Tazama! Utapata mimba na kuzaa mwana. Basi usinywe divai wala chochote chenye kileo, wala usile kitu chochote kisicho safi, kwa sababu mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu kuzaliwa* mpaka kufa kwake.’”

8 Manoa akamsihi Yehova akisema, “Nakuomba Yehova. Tafadhali, tunaomba yule mtu wa Mungu wa kweli uliyekuwa umemtuma hivi punde arudi ili atufundishe jinsi ya kumlea mtoto atakayezaliwa.” 9 Basi Mungu wa kweli akamsikiliza Manoa, na yule malaika wa Mungu wa kweli akamjia tena huyo mwanamke alipokuwa ameketi shambani; lakini Manoa mume wake hakuwepo. 10 Mwanamke huyo akakimbia haraka na kumwambia mume wake, “Yule mtu aliyenijia siku ile amenitokea tena.”+

11 Kwa hiyo Manoa akaondoka na kufuatana na mke wake. Akaja kwa mtu huyo na kumuuliza, “Ni wewe uliyezungumza na mke wangu?” naye akajibu: “Ni mimi.” 12 Ndipo Manoa akasema, “Maneno yako na yatimie! Mtoto huyo ataishi maisha ya aina gani, naye atafanya kazi gani?”+ 13 Basi malaika wa Yehova akamwambia hivi Manoa: “Mke wako na ajiepushe na kila kitu nilichomtajia.+ 14 Asile kitu chochote kinachotokana na mzabibu, asinywe divai wala chochote chenye kileo,+ na asile kitu chochote kisicho safi.+ Anapaswa kuzingatia mambo yote niliyomwagiza.”

15 Sasa Manoa akamwambia malaika wa Yehova, “Tafadhali kaa kidogo, tukuandalie mwanambuzi.”+ 16 Lakini malaika wa Yehova akamwambia Manoa, “Hata nikikaa, sitakula chakula chenu; lakini ukipenda unaweza kukitoa kwa Yehova kuwa dhabihu ya kuteketezwa.” Manoa hakujua kwamba mtu huyo alikuwa malaika wa Yehova. 17 Kisha Manoa akamuuliza malaika wa Yehova, “Unaitwa nani,+ ili neno lako litakapotimia tukuheshimu?” 18 Hata hivyo, malaika wa Yehova akamwambia: “Kwa nini unataka kujua jina langu, wakati jina lenyewe ni la ajabu?”

19 Basi Manoa akachukua mwanambuzi na toleo la nafaka, akamtolea Yehova juu ya mwamba. Naye akafanya jambo la kushangaza huku Manoa na mke wake wakitazama. 20 Mwali wa moto ulipokuwa ukipaa kuelekea mbinguni, malaika wa Yehova akapaa katika huo mwali uliotoka katika madhabahu huku Manoa na mke wake wakitazama. Basi wakaanguka chini kifudifudi. 21 Malaika wa Yehova hakumtokea tena Manoa na mke wake. Ndipo Manoa akatambua kwamba huyo alikuwa malaika wa Yehova.+ 22 Kisha Manoa akamwambia hivi mke wake: “Hakika tutakufa, kwa sababu tumemwona Mungu.”+ 23 Lakini mke wake akamwambia, “Kama Yehova angetaka kutuua, hangekubali dhabihu ya kuteketezwa+ na toleo la nafaka kutoka mikononi mwetu, naye hangetuonyesha mambo haya yote, wala hangetuambia mambo haya yote.”

24 Baadaye mwanamke huyo akazaa mwana na kumpa jina Samsoni;+ na mvulana huyo akazidi kukua, na Yehova akaendelea kumbariki. 25 Baada ya muda roho ya Yehova ikaanza kumchochea+ huko Mahane-dani+ kati ya Sora na Eshtaoli.+

14 Ndipo Samsoni akaenda Timna, na akiwa huko akamwona mwanamke Mfilisti.* 2 Basi akarudi na kuwaambia hivi wazazi wake: “Nimevutiwa na mwanamke fulani Mfilisti huko Timna, ninaomba mniletee awe mke wangu.” 3 Lakini baba yake na mama yake wakamwambia, “Je, huwezi kupata mke kati ya watu wetu wa ukoo na kati ya ndugu zetu wote?+ Je, ni lazima uoe mke kutoka kati ya Wafilisti wasiotahiriwa?” Lakini Samsoni akamwambia baba yake, “Niletee mwanamke huyo, kwa sababu ndiye anayenifaa.”* 4 Lakini wazazi wake hawakujua kwamba Yehova aliongoza jambo hilo, kwa sababu Alikuwa akitafuta nafasi ya kuwapiga Wafilisti, kwa kuwa Wafilisti walikuwa wakiwatawala Waisraeli wakati huo.+

5 Basi Samsoni akaenda na baba yake na mama yake hadi Timna. Alipofika katika mashamba ya mizabibu ya Timna, simba* akamjia akinguruma. 6 Ndipo roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ naye akampasua simba huyo vipande viwili, kama mtu anavyompasua mwanambuzi kwa mikono yake. Lakini hakumwambia baba yake au mama yake jambo alilofanya. 7 Kisha akaenda kuzungumza na yule mwanamke, na bado Samsoni aliona kwamba anamfaa.+

8 Baadaye alipokuwa akirudi kumchukua mwanamke huyo aende naye nyumbani,+ alienda kuangalia ule mzoga wa simba, nao ulikuwa na nyuki wengi na asali. 9 Basi akakwangua asali hiyo na kuitia mikononi mwake, akaila huku akitembea. Alipomfikia baba yake na mama yake, akawagawia ili wale. Lakini hakuwaambia kwamba aliikwangua kutoka katika mzoga wa simba.

10 Na baba yake akaenda kumwona yule mwanamke, naye Samsoni akafanya karamu huko, kwa maana hivyo ndivyo vijana wa kiume walivyokuwa wakifanya. 11 Na watu walipomwona, wakamletea vijana 30 wa kuandamana naye. 12 Kisha Samsoni akawaambia, “Nina kitendawili. Mkikitegua katika siku saba za karamu, nitawapa mavazi 30 ya kitani na mavazi mengine 30. 13 Lakini mkishindwa kukitegua, mtanipa mavazi 30 ya kitani na mavazi mengine 30.” Wakamwambia, “Tega kitendawili chako, tusikie.” 14 Basi akawaambia,

“Mlo ulitoka katika mlaji,

Na kitu kitamu kilitoka kwa mwenye nguvu.”+

Nao hawakuweza kutegua kitendawili hicho kwa siku tatu. 15 Siku ya nne wakamwambia hivi mke wa Samsoni: “Mshawishi mume+ wako ili atutegulie kitendawili hicho. Kama sivyo, tutakuteketeza kwa moto pamoja na watu wa nyumba ya baba yako. Je, mlitualika hapa ili mchukue mali zetu?” 16 Basi mke wa Samsoni akamlilia na kusema, “Hakika unanichukia; hunipendi.+ Uliwategea watu wangu kitendawili, lakini hujaniambia maana yake.” Samsoni akamwambia, “Hata sijamwambia baba yangu wala mama yangu! Nikwambie wewe?” 17 Lakini akaendelea kumlilia siku zilizobaki za karamu hiyo ya siku saba. Hatimaye Samsoni akamtegulia kitendawili hicho katika siku ya saba, kwa sababu alimsumbua sana. Ndipo mwanamke huyo akawaambia watu wake maana ya kitendawili hicho.+ 18 Basi siku ya saba kabla ya jua kutua,* wanaume wa jiji hilo wakamwambia hivi Samsoni:

“Ni nini kitamu kuliko asali,

Na ni nani mwenye nguvu kuliko simba?”+

Akawaambia:

“Kama hamngelima na ng’ombe wangu mchanga,+

Hamngekitegua kitendawili changu.”

19 Kisha roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ akaenda Ashkeloni,+ akawaua watu 30, akachukua mavazi yao na kuwapa watu waliotegua kitendawili.+ Akarudi nyumbani kwa baba yake akiwa amekasirika sana.

20 Kisha wakamchukua mke wa Samsoni+ na kumpa mmoja wa wale vijana walioandamana naye.+

15 Baada ya muda, wakati wa mavuno ya ngano, Samsoni alimchukua mwanambuzi na kwenda kumtembelea mke wake. Akasema: “Ningependa kuingia nikamwone mke wangu katika chumba cha kulala.”* Lakini baba ya mwanamke huyo hakumruhusu kuingia. 2 Baba ya mwanamke huyo akasema, “Nilidhani, ‘Hakika unamchukia.’+ Kwa hiyo nikampa kijana mwenzako.+ Dada yake mdogo ni mrembo kuliko yeye. Tafadhali, mchukue huyo badala yake.” 3 Hata hivyo, Samsoni akawaambia, “Wakati huu Wafilisti hawatanilaumu nikiwadhuru.”

4 Basi Samsoni akaenda na kuwakamata mbweha 300. Kisha akachukua mienge, akawafunga mikia wawili-wawili na kuweka mwenge mmoja kati ya kila mikia miwili. 5 Halafu akaiwasha moto ile mienge na kuwaachilia mbweha hao waingie katika mashamba ya nafaka ya Wafilisti. Basi akateketeza kila kitu kuanzia masuke mpaka nafaka iliyo shambani, na pia mashamba ya mizabibu na ya mizeituni.

6 Wafilisti wakauliza: “Ni nani aliyefanya hivi?” Wakaambiwa: “Ni Samsoni, mkwe wa yule Mtimna, kwa sababu alimchukua mke wa Samsoni na kumpa kijana mwenzake.”+ Kwa hiyo Wafilisti wakaenda na kumteketeza mwanamke huyo na baba yake.+ 7 Kisha Samsoni akawaambia, “Kama haya ndiyo mambo mnayofanya, sitawaacha mpaka nitakapolipiza kisasi.”+ 8 Basi akawapiga na kuwaua watu wengi, mmoja baada ya mwingine, kisha akashuka na kwenda kukaa pangoni katika mwamba wa Etamu.

9 Baadaye Wafilisti wakapanda na kupiga kambi kule Yuda, nao walikuwa wakizunguka-zunguka katika mji wa Lehi.+ 10 Ndipo watu wa Yuda wakawauliza, “Kwa nini mmekuja kutushambulia?” Wakajibu: “Tumekuja kumkamata* Samsoni, na kumtendea kama alivyotutendea.” 11 Basi wanaume 3,000 wa Yuda wakashuka kwenye pango lililo katika mwamba wa Etamu, wakamuuliza Samsoni, “Je, hujui kwamba Wafilisti wanatutawala?+ Kwa nini umetutendea hivi?” Akawajibu: “Nimewatendea kama walivyonitendea.” 12 Lakini wakamwambia, “Tumekuja kukukamata* ili tukutie mikononi mwa Wafilisti.” Samsoni akawaambia, “Niapieni kwamba ninyi hamtanidhuru.” 13 Wakamwambia, “Usiogope, tutakufunga tu na kukupeleka kwao, lakini hatutakuua.”

Basi wakamfunga kwa kamba mbili mpya na kumtoa mwambani. 14 Alipofika Lehi, Wafilisti walishangilia sana kumwona. Kisha roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ na kamba alizofungwa mikononi zikawa kama nyuzi za kitani zilizochomwa moto, nazo zikalegea* na kuanguka kutoka mikononi mwake.+ 15 Akaona utaya mbichi wa punda dume; akauchukua na kuutumia kuua wanaume 1,000.+ 16 Kisha Samsoni akasema:

“Kwa utaya wa punda—rundo moja, marundo mawili!

Kwa utaya wa punda nimeua wanaume 1,000.”+

17 Baada ya kusema hayo, aliutupa utaya huo na kupaita mahali hapo Ramath-lehi.*+ 18 Kisha akahisi kiu sana, akamlilia Yehova akisema, “Ni wewe uliyemtumia mtumishi wako kuleta ukombozi huu mkubwa. Je, sasa nife kwa kiu na kuchukuliwa na watu wasiotahiriwa?” 19 Basi Mungu akapasua mahali penye shimo huko Lehi, na maji yakatiririka kutoka humo.+ Alipoyanywa, roho yake ikamrudia* akapata nguvu tena. Ndiyo sababu aliiita sehemu hiyo En-hakore,* nayo iko Lehi mpaka leo.

20 Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka 20 katika siku za Wafilisti.+

16 Siku moja Samsoni alienda Gaza, akamwona kahaba fulani na kuingia nyumbani mwake. 2 Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni ameingia humu.” Basi wakamzingira na kumvizia usiku kucha kwenye lango la jiji. Wakakaa kimya usiku kucha, wakisema miongoni mwao, “Kesho asubuhi tutamuua.”

3 Lakini Samsoni akaendelea kulala mpaka usiku wa manane. Kisha akaamka na kung’oa malango ya jiji pamoja na miimo yake miwili na komeo. Akajitwika mabegani na kuipeleka kwenye kilele cha mlima ulio karibu na Hebroni.

4 Baada ya hayo akampenda mwanamke fulani katika Bonde* la Soreki, aliyeitwa Delila.+ 5 Basi watawala wa Wafilisti wakaenda kwa mwanamke huyo na kumwambia, “Mdanganye*+ ili ujue chanzo cha nguvu zake nyingi na jinsi tunavyoweza kumshinda, kumfunga, na kumdhibiti. Na kila mmoja wetu atakupa vipande 1,100 vya fedha.”

6 Baadaye Delila akamwambia Samsoni, “Naomba uniambie chanzo cha nguvu zako nyingi na kitu kinachoweza kutumiwa kukufunga na kukudhibiti.” 7 Samsoni akamwambia, “Wakinifunga kwa kamba saba mbichi za upinde, nitakuwa dhaifu kama mwanadamu mwingine yeyote.” 8 Basi watawala wa Wafilisti wakamletea mwanamke huyo kamba saba mbichi za upinde, akamfunga nazo. 9 Nao wakawaficha watu fulani katika chumba cha ndani ili wamvizie, basi Delila akamwambia, “Wafilisti wamekuja kukushambulia, Samsoni!” Ndipo akazikata hizo kamba kwa urahisi kama uzi wa kitani unavyokatika unapoguswa na moto.+ Nao hawakujua siri ya nguvu zake.

10 Basi Delila akamwambia Samsoni: “Umenihadaa* na kunidanganya. Sasa tafadhali, niambie unaweza kufungwa kwa kitu gani?” 11 Kwa hiyo akamwambia, “Wakinifunga kwa kamba mpya ambazo hazijatumiwa, nitakuwa dhaifu kama mwanadamu mwingine yeyote.” 12 Basi Delila akachukua kamba mpya akamfunga nazo, kisha akamwambia hivi Samsoni kwa sauti kubwa: “Wafilisti wamekuja kukushambulia, Samsoni!” (Wakati huo watu waliokuwa wakimvizia walikuwa wamejificha katika chumba cha ndani.) Ndipo akazikata kamba hizo kutoka mikononi mwake kama nyuzi.+

13 Kisha Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa umenihadaa na kunidanganya.+ Niambie unaweza kufungwa kwa kitu gani?” Akamjibu, “Kwa kufuma vishungi saba vya nywele zangu kwa uzi wa mtande.” 14 Basi akavifunga kwa kigingi na kumwambia hivi kwa sauti kubwa: “Wafilisti wamekuja kukushambulia, Samsoni!” Basi akaamka kutoka usingizini na kung’oa kigingi hicho cha wafumaji na uzi wa mtande.

15 Sasa Delila akamwambia, “Unawezaje kusema ‘Nakupenda’+ wakati moyo wako haupo pamoja nami? Umenihadaa mara tatu na hujaniambia chanzo cha nguvu zako nyingi.”+ 16 Delila alimsumbua Samsoni siku baada ya siku na kumshinikiza, akamchosha* hivi kwamba akatamani kufa.+ 17 Mwishowe akamfunulia moyo wake na kumwambia, “Kichwa changu hakijawahi kamwe kuguswa na wembe, kwa kuwa mimi ni Mnadhiri wa Mungu tangu kuzaliwa.*+ Nikinyolewa, nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu kama wanadamu wengine wote.”

18 Delila alipoona kwamba Samsoni amemfunulia moyo wake, akawaita mara moja watawala wa Wafilisti+ na kuwaambia, “Njooni, kwa maana sasa amenifunulia moyo wake.” Basi watawala wa Wafilisti wakaja kwa Delila wakiwa na zile pesa. 19 Delila akamlaza Samsoni mapajani; akamwita mtu ili amnyoe vile vishungi saba vya nywele zake. Ndipo Delila akaanza kumdhibiti, kwa maana alikuwa akiishiwa na nguvu. 20 Kisha Delila akamwambia hivi kwa sauti kubwa: “Wafilisti wamekuja kukushambulia, Samsoni!” Ndipo akaamka kutoka usingizini na kusema, “Nitatoka nje kama awali+ na kujinasua.” Lakini hakujua kwamba Yehova alikuwa amemwacha. 21 Basi Wafilisti wakamkamata na kumng’oa macho. Wakampeleka Gaza na kumfunga kwa pingu mbili za shaba, akawa akisaga nafaka gerezani. 22 Lakini nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa.+

23 Watawala wa Wafilisti wakakusanyika ili kusherehekea na kumtolea dhabihu nyingi mungu wao Dagoni,+ kwa kuwa walisema, “Mungu wetu amemtia mikononi mwetu adui yetu Samsoni!” 24 Watu walipomwona, wakamsifu mungu wao wakisema, “Mungu wetu amemtia mikononi mwetu adui yetu aliyeharibu nchi yetu+ na kuua watu wengi kati yetu.”+

25 Mioyo yao ilipojaa furaha wakasema, “Mwiteni Samsoni atutumbuize.” Basi wakamwita Samsoni kutoka gerezani ili awatumbuize; wakamsimamisha katikati ya nguzo. 26 Samsoni akamwambia hivi mvulana aliyekuwa amemshika mkono: “Niache niguse nguzo zinazotegemeza nyumba hii, ili niziegemee.” 27 (Basi nyumba hiyo ilikuwa imejaa wanaume na wanawake. Na watawala wote wa Wafilisti walikuwemo, na darini kulikuwa na watu wapatao 3,000, wanaume na wanawake, waliokuwa wakimtazama Samsoni akiwatumbuiza.)

28 Ndipo Samsoni+ akamlilia Yehova akisema, “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, nikumbuke, tafadhali, na kunitia nguvu,+ tafadhali, mara hii moja tu, Ee Mungu, acha niwalipize kisasi Wafilisti kwa ajili ya jicho moja tu, kati ya macho yangu mawili.”+

29 Kisha Samsoni akazishika nguzo mbili za katikati zilizotegemeza nyumba hiyo, nguzo moja kwa mkono wa kulia na ile nyingine kwa mkono wa kushoto. 30 Kisha Samsoni akasema hivi kwa sauti kubwa: “Acha nife* pamoja na Wafilisti!” Ndipo akasukuma nguzo hizo kwa nguvu zake zote, na nyumba hiyo ikawaangukia watawala na watu wote waliokuwemo.+ Kwa hiyo watu aliowaua wakati wa kifo chake walikuwa wengi kuliko aliowaua maishani mwake.+

31 Baadaye ndugu zake na watu wote wa familia ya baba yake wakaja kumchukua. Wakamzika kati ya Sora+ na Eshtaoli katika kaburi la Manoa+ baba yake. Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka 20.+

17 Kulikuwa na mtu mmoja katika eneo lenye milima la Efraimu+ aliyeitwa Mika. 2 Siku moja alimwambia hivi mama yake: “Vile vipande 1,100 vya fedha ulivyoibiwa na ukamlaani aliyekuibia, nikiwa nasikia—mimi ndiye niliyevichukua.” Mama yake akamwambia, “Yehova na akubariki mwanangu.” 3 Basi akamrudishia mama yake vile vipande 1,100 vya fedha, lakini mama yake akasema, “Nitazitakasa fedha hizi kwa ajili ya Yehova zitoke mikononi mwangu ili mwanangu azitumie kutengeneza sanamu ya kuchongwa na sanamu ya chuma.*+ Sasa nakurudishia fedha hizi.”

4 Baada ya kumrudishia mama yake fedha hizo, mama yake akachukua vipande 200 vya fedha na kumpa mfua fedha. Naye akatengeneza sanamu ya kuchongwa na sanamu ya chuma;* na sanamu hizo zikawekwa katika nyumba ya Mika. 5 Na Mika alikuwa na nyumba ya miungu, naye akatengeneza efodi*+ na sanamu za terafimu*+ na kumweka mmoja wa wanawe awe kuhani wake.+ 6 Siku hizo hakukuwa na mfalme katika Israeli.+ Kila mtu alifanya jambo aliloona ni jema machoni pake.*+

7 Basi kulikuwa na kijana fulani kutoka Bethlehemu+ kule Yuda aliyetoka katika ukoo wa Yuda. Alikuwa Mlawi+ na alikuwa ameishi huko kwa muda. 8 Kijana huyo akaondoka katika jiji la Bethlehemu katika nchi ya Yuda ili atafute mahali pengine pa kuishi. Alipokuwa akisafiri, alifika katika eneo lenye milima la Efraimu, katika nyumba ya Mika.+ 9 Mika akamuuliza, “Unatoka wapi?” Akamjibu, “Mimi ni Mlawi kutoka Bethlehemu kule Yuda, natafuta mahali pa kuishi.” 10 Basi Mika akamwambia, “Kaa pamoja nami, uwe kama baba* na kuhani wangu. Nitakupa vipande kumi vya fedha kwa mwaka, mavazi, na chakula.” Kwa hiyo Mlawi huyo akaingia nyumbani mwake. 11 Mlawi huyo akakubali kukaa na Mika, naye akawa kama mmoja wa wanawe. 12 Isitoshe, Mika akamweka Mlawi huyo kuwa kuhani wake,+ akaishi nyumbani mwa Mika. 13 Basi Mika akasema, “Sasa najua kwamba Yehova atanitendea mema, kwa maana Mlawi amekuwa kuhani wangu.”

18 Siku hizo hakukuwa na mfalme katika Israeli.+ Na siku hizo watu wa kabila la Dani+ walikuwa wakitafuta mahali pa kukaa, kwa sababu kufikia wakati huo hawakuwa wamepata urithi miongoni mwa makabila ya Israeli.+

2 Watu wa kabila la Dani wakawatuma wanaume watano mashujaa kutoka miongoni mwao, waliotoka Sora na Eshtaoli,+ ili waipeleleze nchi na kuichunguza. Wakawaambia, “Nendeni mkaichunguze nchi.” Walipofika kwenye eneo lenye milima la Efraimu, nyumbani kwa Mika,+ wakalala huko usiku huo. 3 Walipokaribia nyumba ya Mika, walimsikia* yule kijana na kutambua kwamba alikuwa Mlawi, basi wakaenda kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta huku? Unafanya nini hapa? Ni kazi gani iliyokuleta hapa?” 4 Akawaeleza mambo ambayo Mika alimtendea na kuwaambia, “Ameniajiri ili niwe kuhani wake.”+ 5 Ndipo wakamwambia, “Tafadhali, muulize Mungu ikiwa safari yetu itafanikiwa.” 6 Kuhani huyo akawaambia, “Nendeni kwa amani. Yehova yuko pamoja nanyi katika safari yenu.”

7 Basi wanaume hao watano wakaendelea na safari na kufika Laishi.+ Wakaona jinsi wakaaji wa huko walivyoishi kama Wasidoni bila kumtegemea yeyote. Walikuwa watu watulivu wasio na wasiwasi,+ na hakukuwa na mtawala yeyote aliyewakandamiza wala kuwasumbua. Waliishi mbali sana na Wasidoni, na hawakushughulika na watu wengine.

8 Wanaume hao waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli,+ ndugu zao wakawauliza, “Mambo yaliendaje?” 9 Wakajibu, “Twendeni tukapigane nao, kwa kuwa tumeona nchi yao ni nzuri sana. Kwa nini mnasitasita? Msikawie kwenda kumiliki nchi hiyo. 10 Mtakapofika, mtakuta watu wasio na wasiwasi,+ na nchi yao ni kubwa. Mungu amewapa ninyi nchi hiyo ambayo haipungukiwi na kitu chochote duniani.”+

11 Basi wanaume 600 wa kabila la Dani wenye silaha wakatoka Sora na Eshtaoli.+ 12 Nao wakaenda na kupiga kambi karibu na Kiriath-yearimu+ kule Yuda. Ndiyo sababu eneo hilo lililo upande wa magharibi wa Kiriath-yearimu, linaitwa Mahane-dani*+ mpaka leo. 13 Wakatoka huko na kwenda kwenye eneo lenye milima la Efraimu, wakafika nyumbani kwa Mika.+

14 Kisha wale wanaume watano waliokuwa wameenda kuipeleleza nchi ya Laishi+ wakawaambia hivi ndugu zao: “Je, mnajua kwamba nyumba hizi zina efodi,* terafimu,* sanamu ya kuchongwa, na sanamu ya chuma?*+ Fikirieni mtakalofanya.” 15 Basi wakaenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi,+ nyumbani kwa Mika, ili kumjulia hali. 16 Wakati huo, wale wanaume 600 wa kabila la Dani+ wenye silaha, walikuwa wamesimama langoni. 17 Wale wanaume watano walioenda kuipeleleza nchi+ wakaingia ndani ili kuchukua ile sanamu ya kuchongwa, ile efodi,*+ zile terafimu,*+ na ile sanamu ya chuma.*+ (Yule kuhani+ alikuwa amesimama langoni pamoja na wale wanaume 600 wenye silaha.) 18 Nao wakaingia katika nyumba ya Mika wakachukua ile sanamu ya kuchongwa, ile efodi,* zile terafimu,* na ile sanamu ya chuma.* Kuhani huyo akawauliza, “Mnafanya nini?” 19 Lakini wakamwambia, “Nyamaza. Funika kinywa chako kwa mkono wako, tufuate ili uwe baba* na kuhani wetu. Je, ni bora kwako kuwa kuhani wa nyumba ya mtu mmoja+ au kuhani wa kabila na ukoo katika Israeli?”+ 20 Ndipo kuhani huyo akaridhika, akachukua ile efodi,* zile terafimu,* na ile sanamu ya kuchongwa,+ akaenda nao.

21 Basi wakaanza safari yao, huku wakitanguliwa na watoto, mifugo, na vitu vyao vyenye thamani. 22 Walipokuwa umbali fulani kutoka nyumbani kwa Mika, wanaume walioishi karibu na Mika walikusanyika pamoja, wakawafuatia na kuwafikia wale watu wa kabila la Dani. 23 Walipowapigia kelele watu wa kabila la Dani, waligeuka na kumuuliza Mika, “Una shida gani? Kwa nini umekuja na umati huu?” 24 Basi akasema, “Mmechukua miungu niliyojitengenezea na kuondoka na kuhani wangu pia. Mkaniacha bila chochote. Mnawezaje kuniuliza, ‘Una shida gani?’” 25 Ndipo wale wanaume wa kabila la Dani wakamwambia, “Usitufokee; la sivyo, wanaume hawa wenye hasira watakushambulia na kukuua wewe na watu wa nyumbani mwako.” 26 Basi watu wa kabila la Dani wakaendelea na safari, na Mika alipoona kwamba wamemzidi nguvu, akageuka na kurudi nyumbani kwake.

27 Baada ya kuchukua miungu ya Mika, pamoja na kuhani wake, wakaenda kuwashambulia watu watulivu na wasio na wasiwasi+ wa Laishi.+ Wakawaua kwa upanga na kuteketeza jiji lao. 28 Hawakuwa na mtu wa kuwaokoa, kwa sababu waliishi mbali sana na Wasidoni katika bonde* la Beth-rehobu,+ nao hawakushughulika na watu wengine. Watu wa kabila la Dani wakalijenga upya jiji hilo na kuishi humo. 29 Wakaliita jiji hilo Dani+ sawa na jina la baba yao, Dani, mtoto wa Israeli.+ Lakini mwanzoni jiji hilo liliitwa Laishi.+ 30 Kisha watu wa kabila la Dani wakaanza kuabudu ile sanamu ya kuchongwa,+ naye Yonathani+ mwana wa Gershomu,+ mwana wa Musa, na wanawe wakawa makuhani wa kabila la Dani mpaka wakaaji walipopelekwa uhamishoni. 31 Nao wakaisimamisha ile sanamu ya kuchongwa iliyotengenezwa na Mika, na sanamu hiyo ikaendelea kuwa huko sikuzote ambazo nyumba ya Mungu wa kweli ilikuwa Shilo.+

19 Katika siku hizo, wakati ambapo hakukuwa na mfalme katika Israeli,+ Mlawi fulani aliyekuwa akiishi mbali katika eneo lenye milima la Efraimu+ alimwoa suria kutoka Bethlehemu+ kule Yuda. 2 Lakini suria huyo hakuwa mwaminifu kwake, akamwacha mume wake na kurudi Bethlehemu nyumbani kwa baba yake kule Yuda. Naye akakaa huko kwa miezi minne. 3 Basi mume wake akaenda kumsihi arudi; alienda na mtumishi wake wa kiume na punda wawili. Mwanamke huyo akamkaribisha katika nyumba ya baba yake. Baba yake alifurahi kumwona. 4 Basi baba mkwe wake, yaani, baba ya yule msichana, akamshawishi akae hapo kwa siku tatu; wakala na kunywa; naye akalala huko.

5 Siku ya nne, walipoamka asubuhi na mapema ili waanze safari, baba ya yule msichana akamwambia hivi mkwe wake: “Kula chakula kidogo ili upate nguvu,* kisha uende.” 6 Basi wakaketi, na wote wawili wakala na kunywa; kisha baba ya yule msichana akamwambia huyo mwanamume, “Tafadhali, lala hapa usiku huu, ustarehe.”* 7 Mwanamume huyo alipotaka kuondoka, baba mkwe wake akamsihi sana abaki, naye akalala tena usiku huo.

8 Alipoamka asubuhi na mapema siku ya tano ili aende, baba ya msichana huyo akasema, “Tafadhali, kula chakula kidogo ili upate nguvu.”* Nao wakakaa mpaka jioni sana, na wote wawili wakaendelea kula. 9 Yule mwanamume alipotaka kuondoka pamoja na suria* wake na mtumishi wake, baba mkwe wake, yaani, baba ya yule msichana, akamwambia, “Tazama! Mchana umekwisha, jioni inakaribia. Tafadhali, lala hapa usiku huu, ustarehe. Amkeni mapema kesho na kuanza safari yenu ya kwenda nyumbani kwenu.”* 10 Hata hivyo, mwanamume huyo hakutaka kulala huko tena, basi akaondoka na kusafiri mpaka Yebusi, yaani, Yerusalemu.+ Alikuwa na punda wake wawili wenye matandiko, suria wake, na mtumishi wake.

11 Walipokaribia Yebusi, ilikuwa jioni sana. Basi yule mtumishi akamuuliza bwana wake, “Tunaweza kulala katika jiji hili la Wayebusi usiku huu?” 12 Lakini bwana wake akamjibu hivi: “Hatutalala katika jiji la watu ambao si Waisraeli. Tutaendelea na safari mpaka Gibea.”+ 13 Kisha akamwambia hivi mtumishi wake: “Twende, tujitahidi kufika Gibea au Rama; tulale katika mojawapo ya majiji hayo.”+ 14 Basi wakaendelea na safari, na jua likaanza kutua walipokaribia Gibea, jiji la Wabenjamini.

15 Wakaingia Gibea ili walale humo usiku. Wakaketi katika uwanja wa jiji, lakini hakuna yeyote aliyewakaribisha ili walale nyumbani mwake usiku.+ 16 Baadaye jioni hiyo, mzee fulani aliingia jijini kutoka shambani mwake. Alizaliwa katika eneo lenye milima la Efraimu,+ na kwa muda fulani alikuwa akiishi Gibea; lakini wenyeji wa jiji hilo walikuwa Wabenjamini.+ 17 Alipotazama na kumwona yule msafiri katika uwanja wa jiji, mzee huyo akamuuliza, “Unaenda wapi, na umetoka wapi?” 18 Akajibu, “Tunatoka Bethlehemu kule Yuda nasi tunaenda mbali katika eneo lenye milima la Efraimu, nyumbani kwetu. Nilienda Bethlehemu katika nchi ya Yuda,+ nami ninaenda kwenye nyumba ya Yehova,* lakini sijakaribishwa na yeyote. 19 Tuna nyasi na chakula cha kutosha kwa ajili ya punda wetu,+ na pia nina mkate+ na divai kwa ajili yangu, suria* wangu, na mtumishi wangu. Hatujapungukiwa na kitu chochote.” 20 Hata hivyo, mzee huyo akasema, “Uwe na amani! Nitawapa chochote mnachohitaji. Lakini msilale hapa kwenye uwanja wa jiji.” 21 Ndipo akamkaribisha nyumbani mwake na kuwalisha* punda wake. Kisha wakanawa miguu, wakala, na kunywa.

22 Walipokuwa wakila na kunywa, wanaume fulani wahuni katika jiji hilo wakaizingira nyumba na kuugonga mlango kwa fujo, huku wakimwambia hivi mzee huyo mwenye nyumba, “Mtoe nje yule mwanamume aliyeingia nyumbani mwako, ili tufanye ngono naye.”+ 23 Ndipo mwenye nyumba akatoka nje na kuwaambia, “Sivyo, ndugu zangu, msifanye uovu. Tafadhali, mtu huyu ni mgeni wangu. Msifanye jambo hili la aibu. 24 Hapa nina binti bikira na pia suria wa mwanamume huyu. Acheni niwatoe nje, ili mwatendee mambo ya aibu, ikiwa mnataka kufanya hivyo.*+ Lakini msimtendee mwanamume huyu jambo hili la aibu.”

25 Lakini wanaume hao hawakumsikiliza, basi yule mtu akamtoa nje kwa nguvu suria* wake.+ Wakambaka na kumtendea vibaya usiku kucha mpaka asubuhi. Kisha kulipopambazuka wakamwacha aende zake. 26 Asubuhi na mapema, mwanamke huyo akaja kwenye nyumba ya yule mtu alimokuwa bwana wake, akaanguka chini mlangoni, akalala hapo mpaka kulipopambazuka. 27 Bwana wake alipoamka asubuhi na kufungua milango ya nyumba ili atoke na kuendelea na safari, akamwona yule mwanamke, suria wake, akiwa amelala mlangoni, mikono yake ikiwa kwenye kizingiti. 28 Akamwambia, “Amka twende.” Lakini hakusema lolote. Kwa hiyo mwanamume huyo akamwinua na kumweka juu ya punda, wakaondoka na kuelekea nyumbani.

29 Alipofika nyumbani kwake, akachukua kisu na kuikatakata ile maiti ya suria wake vipande 12, akapeleka kipande katika kila eneo* la Israeli. 30 Wote walioona jambo hilo wakasema, “Jambo kama hili halijawahi kutokea kamwe wala kuonekana tangu Waisraeli walipotoka Misri mpaka leo. Fikirieni jambo hili,* mshauriane,+ kisha mtuambie tutakalofanya.”

20 Ndipo Waisraeli wote kutoka Dani+ hadi Beer-sheba na kutoka nchi ya Gileadi+ wakakusanyika kwa umoja* mbele za Yehova kule Mispa.+ 2 Basi wakuu wa watu na wa makabila yote ya Israeli wakachukua nafasi zao katika kutaniko la watu wa Mungu—wanajeshi 400,000 wenye mapanga waliotembea kwa miguu.+

3 Wabenjamini wakasikia kwamba wanaume Waisraeli walikuwa wameenda Mispa.

Ndipo wanaume Waisraeli wakauliza, “Tuambieni, jambo hili linalochukiza lilitendekaje?”+ 4 Kwa hiyo yule Mlawi,+ mume wa mwanamke aliyeuawa, akajibu: “Mimi na suria wangu tulifika Gibea+ katika nchi ya Wabenjamini ili tulale usiku. 5 Kisha wakaaji* wa Gibea wakaja kunishambulia na kuizingira nyumba usiku. Walitaka kuniua, lakini wakambaka suria wangu, naye akafa.+ 6 Basi nikachukua maiti ya suria wangu na kuikatakata vipandevipande, kisha nikavipeleka vipande hivyo katika maeneo* yote ya urithi ya Waisraeli,+ kwa sababu walitenda jambo la aibu na lenye kufedhehesha katika Israeli. 7 Sasa enyi Waisraeli wote, toeni ushauri na mapendekezo yenu+ kuhusu jambo hili.”

8 Basi watu wote wakasimama pamoja* na kusema, “Hakuna yeyote kati yetu atakayerudi katika hema lake au nyumbani kwake. 9 Hivi ndivyo tutakavyowatendea watu wa Gibea: Tuchague watu kwa kura ili waende kupigana nao.+ 10 Tutachukua wanaume 10 kati ya 100 kutoka katika makabila yote ya Israeli, na 100 kati ya 1,000 na 1,000 kati ya 10,000 wawatafutie chakula wanajeshi, ili wawaadhibu wakaaji wa Gibea katika nchi ya Benjamini, kwa sababu ya jambo hili la aibu walilotenda katika Israeli.” 11 Kwa hiyo wanaume wote Waisraeli wakakusanyika na kuungana pamoja* ili kulishambulia jiji hilo.

12 Kisha makabila ya Israeli yakatuma wanaume kwa watu wa kabila la Benjamini, wakawauliza, “Kwa nini mmetenda jambo hili linalochukiza? 13 Sasa waleteni wahuni hao wa Gibea,+ ili tuwaue na kuondoa kabisa uovu katika Israeli.”+ Lakini Wabenjamini walikataa kuwasikiliza ndugu zao Waisraeli.

14 Ndipo Wabenjamini wakakusanyika kutoka katika majiji yao kwenda Gibea ili kupigana na wanaume Waisraeli. 15 Siku hiyo Wabenjamini walikusanya wanaume 26,000 wenye mapanga kutoka katika majiji yao, na pia wanaume 700 mashujaa kutoka Gibea. 16 Jeshi hilo lilikuwa na wanaume 700 mashujaa waliotumia mkono wa kushoto. Kila mmoja wao aliweza kurusha jiwe kwa kombeo na kulenga unywele* bila kukosea.

17 Waisraeli kwa upande wao walikusanya wanaume 400,000 wenye mapanga,+ na kila mmoja wao alikuwa mpiganaji mwenye uzoefu. 18 Wakapanda kwenda Betheli kumwomba Mungu ushauri.+ Basi Waisraeli wakamuuliza hivi: “Ni nani kati yetu anayepaswa kutuongoza kupigana na Wabenjamini?” Yehova akajibu, “Kabila la Yuda litaongoza.”

19 Baada ya hayo, Waisraeli wakaamka asubuhi na kupiga kambi ili kushambulia Gibea.

20 Basi wanaume Waisraeli wakaenda kupigana na Wabenjamini; wakajipanga kivita ili kushambulia Gibea. 21 Kisha Wabenjamini wakatoka Gibea na kuwaua wanaume 22,000 Waisraeli siku hiyo. 22 Hata hivyo, wanajeshi Waisraeli wakaonyesha ujasiri na kujipanga tena kwa ajili ya vita mahali walipojipanga siku ya kwanza. 23 Ndipo Waisraeli wakapanda kwenda kumlilia Yehova mpaka jioni na kumuuliza hivi Yehova: “Je, twende tena kupigana na ndugu zetu, Wabenjamini?”+ Yehova akawaambia, “Pandeni mkapigane nao.”

24 Basi Waisraeli wakawakaribia Wabenjamini siku ya pili. 25 Nao Wabenjamini wakatoka Gibea ili kupigana nao siku ya pili, wakawaua Waisraeli wengine 18,000,+ wote wakiwa na mapanga. 26 Ndipo wanaume wote wa Israeli wakapanda kwenda Betheli. Wakalia na kukaa huko mbele za Yehova,+ nao wakafunga+ siku hiyo mpaka jioni na kumtolea Yehova dhabihu za kuteketezwa+ na dhabihu za ushirika.+ 27 Baada ya hayo, wanaume Waisraeli wakaomba ushauri wa Yehova,+ kwa kuwa sanduku la agano la Mungu wa kweli lilikuwa huko siku hizo. 28 Basi Finehasi+ mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni, alikuwa akihudumu* mbele ya sanduku hilo siku hizo. Wakamuuliza, “Je, twende tena kupigana na ndugu zetu Wabenjamini, au tusiende?”+ Yehova akawajibu hivi: “Nendeni, kwa sababu kesho nitawatia mikononi mwenu.” 29 Ndipo Waisraeli wakaweka wanaume kuzunguka Gibea ili walivizie.+

30 Waisraeli wakapanda kwenda kupigana na Wabenjamini siku ya tatu, wakajipanga kivita ili kushambulia Gibea kama walivyofanya awali.+ 31 Wabenjamini walipoenda kupigana na jeshi hilo, walivutwa mbali na jiji.+ Kisha, kama awali, wakaanza kuwashambulia na kuwaua watu kwenye barabara kuu; barabara moja inaenda Betheli na nyingine Gibea, wakawaua wanaume Waisraeli wapatao 30 mashambani.+ 32 Wabenjamini wakasema, “Tunawashinda kama awali.”+ Lakini Waisraeli wakasema, “Tukimbieni na kuwavuta mbali na jiji lao waje kwenye barabara kuu.” 33 Basi wanaume wote wa Israeli wakatoka walipokuwa na kwenda kujipanga kivita kule Baal-tamari, na Waisraeli waliokuwa wakivizia wakatoka mahali walipokuwa wamejificha karibu na Gibea. 34 Kisha wanaume 10,000 mashujaa kutoka kotekote Israeli wakaja mbele ya Gibea, na mapigano yakawa makali. Lakini Wabenjamini hawakujua kwamba walikuwa karibu kuangamizwa.

35 Yehova akawashinda Wabenjamini+ mbele ya Waisraeli; siku hiyo Waisraeli waliwaua wanaume 25,100 Wabenjamini waliokuwa na mapanga.+

36 Hata hivyo, wanaume Waisraeli walipokimbia kutoka Benjamini,+ Wabenjamini walifikiri kwamba wangewashinda, lakini walikimbia kwa sababu waliwategemea Waisraeli wenzao waliokuwa wakivizia jiji la Gibea.+ 37 Na wale waliokuwa wakivizia wakatoka haraka na kukimbia kuelekea Gibea. Wakasambaa na kuwaua kwa upanga watu wote waliokuwa jijini.

38 Basi wanaume wa Israeli walikuwa wamepanga kwamba wanaume waliovizia jiji watoe ishara kwa kufanya moshi upande juu kutoka jijini.

39 Waisraeli walipogeuka na kukimbia, wanaume Wabenjamini wakaanza kuwashambulia, wakawaua wanaume Waisraeli wapatao 30,+ huku wakisema, “Ni wazi kwamba tunawashinda tena, kama tulivyowashinda awali.”+ 40 Lakini ile ishara ya wingu la moshi ikaanza kupanda kutoka jijini. Wabenjamini walipogeuka, waliona moto ukiteketeza jiji lote na moshi ukipanda angani. 41 Kisha wanaume Waisraeli wakageuka kwa ghafla na kuwakimbiza, Wabenjamini wakashtuka, kwa kuwa waliona kwamba wataangamizwa. 42 Basi wakawakimbia wanaume Waisraeli na kuelekea nyikani, lakini Waisraeli wakawakimbiza na kuwashambulia; wanaume Waisraeli waliotoka majijini wakawashambulia pia na kuwaua. 43 Wakawazingira Wabenjamini na kuwafuata himahima. Wakawakanyaga-kanyaga mbele ya Gibea, upande wa mashariki. 44 Hatimaye wanaume 18,000 Wabenjamini wakaangamizwa, wote walikuwa mashujaa hodari.+

45 Basi wanaume Wabenjamini wakageuka na kukimbilia nyikani kwenye mwamba wa Rimoni,+ na Waisraeli wakawaua Wabenjamini 5,000 kwenye barabara kuu, nao wakaendelea kuwafuatia mpaka Gidomu; wakawaua wanaume wengine 2,000. 46 Siku hiyo, Wabenjamini 25,000 wenye mapanga waliuawa,+ wote walikuwa mashujaa hodari. 47 Lakini wanaume 600 walikimbilia nyikani kwenye mwamba wa Rimoni, na kukaa kwenye mwamba huo kwa miezi minne.

48 Na wanaume Waisraeli wakarudi kuwashambulia Wabenjamini na kuwaua kwa upanga watu wote waliokuwa jijini pamoja na mifugo, kila kitu kilichobaki. Pia, waliteketeza kwa moto majiji yote katika maeneo waliyopitia.

21 Sasa wanaume Waisraeli walikuwa wameapa hivi kule Mispa:+ “Hakuna yeyote kati yetu atakayekubali binti yake aolewe na mwanamume Mbenjamini.”+ 2 Kwa hiyo, watu wakaja Betheli+ na kukaa huko mbele za Mungu wa kweli mpaka jioni, wakipaza sauti na kulia kwa uchungu. 3 Nao walikuwa wakisema hivi: “Ee Yehova Mungu wa Israeli, kwa nini jambo hili limetokea katika Israeli? Kwa nini tukose kabila moja la Israeli leo?” 4 Siku iliyofuata, watu wakaamka mapema na kujenga madhabahu hapo ili watoe dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika.+

5 Kisha Waisraeli wakaulizana, “Ni kabila gani kati ya makabila yote ya Israeli ambalo halikukusanyika mbele za Yehova?” kwa kuwa walifanya kiapo kikubwa kwamba yeyote ambaye hakufika Mispa mbele za Yehova lazima auawe. 6 Basi Waisraeli wakahuzunika kwa sababu ya mambo yaliyowapata ndugu zao Wabenjamini. Wakasema, “Leo kabila moja limekatwa kutoka Israeli. 7 Kwa kuwa tumeapa mbele za Yehova+ kwamba hatutakubali kamwe binti zetu waolewe nao, tutapata wapi wake kwa ajili ya wanaume waliobaki?”+

8 Wakaulizana, “Ni kabila gani la Israeli ambalo halikufika Mispa mbele za Yehova?”+ Wakagundua kwamba hakuna yeyote kutoka Yabesh-gileadi aliyekuja kambini kukusanyika na Waisraeli wengine. 9 Watu walipohesabiwa, wakagundua kwamba hakuna mkaaji hata mmoja wa Yabesh-gileadi aliyekuwepo. 10 Basi wakawatuma wanaume 12,000 waliokuwa mashujaa zaidi. Wakawaamuru hivi: “Nendeni, mkawaue kwa upanga wakaaji wa Yabesh-gileadi, msiache wanawake wala watoto.+ 11 Hivi ndivyo mnavyopaswa kufanya: mnapaswa kumwangamiza kila mwanamume, na pia kila mwanamke ambaye amefanya ngono na mwanamume.” 12 Miongoni mwa wakaaji wa Yabesh-gileadi walipata mabikira 400 ambao hawajawahi kufanya ngono na mwanamume. Basi wakawaleta kambini huko Shilo,+ katika nchi ya Kanaani.

13 Kisha Waisraeli waliokusanyika wakawatumia ujumbe wa amani Wabenjamini waliokuwa kwenye mwamba wa Rimoni.+ 14 Basi Wabenjamini wakarudi wakati huo. Waisraeli wakawapa Wabenjamini wanawake waliowachukua kule Yabesh-gileadi,+ lakini walikuwa wachache kuliko wanaume. 15 Na watu wakahuzunika kwa sababu ya mambo yaliyowapata Wabenjamini+ kwa kuwa Yehova alileta mgawanyiko katika makabila ya Israeli. 16 Wazee wa Waisraeli wakauliza, “Kwa kuwa wanawake wote Wabenjamini waliuawa, tufanye nini ili tupate wake kwa ajili ya wanaume waliobaki?” 17 Wakajibu, “Wabenjamini waliobaki wanapaswa kupewa urithi ili kabila lolote lisiangamizwe kutoka Israeli. 18 Lakini haturuhusiwi kuwapa binti zetu wawe wake zao, kwa sababu Waisraeli wameapa hivi: ‘Alaaniwe yeyote anayempa Mbenjamini mke.’”+

19 Ndipo wakasema, “Jamani! Kuna sherehe ya Yehova inayofanywa kila mwaka kule Shilo,+ jiji lililo upande wa kaskazini wa Betheli na upande wa mashariki wa barabara kuu inayopanda kutoka Betheli kwenda Shekemu na upande wa kusini wa Lebona.” 20 Kisha wakawaamuru hivi wanaume Wabenjamini: “Nendeni mkavizie katika mashamba ya mizabibu. 21 Mtakapoona wasichana wa* Shilo wakitoka ili kucheza dansi za mzunguko, tokeni katika mashamba ya mizabibu na kila mmoja wenu ajichukulie mke miongoni mwa wasichana hao wa Shilo, kisha mrudi katika nchi ya Benjamini. 22 Na baba zao au ndugu zao wakija kutulalamikia, tutawaambia, ‘Tutendeeni kwa fadhili kwa niaba yao, kwa sababu tulipoenda vitani hatukuweza kupata mke kwa ajili ya kila mmoja wao,+ nanyi hamngeweza kuwapa wake na kuepuka hatia.’”+

23 Basi hivyo ndivyo wanaume Wabenjamini walivyofanya; walijichukulia wake miongoni mwa wanawake waliokuwa wakicheza dansi. Kisha wakarudi katika urithi wao, wakajenga tena majiji yao,+ na kuishi humo.

24 Wakati huo Waisraeli wakatawanyika kutoka huko, na kila mmoja akarudi kwa kabila lake na kwa ukoo wake, kila mmoja akarudi katika urithi wake.

25 Siku hizo hakukuwa na mfalme katika Israeli.+ Kila mtu alifanya jambo aliloona ni jema machoni pake.*

Tnn., “wana wa Israeli.”

Au “Nimewapa nchi hiyo.”

Tnn., “kura yangu.”

Yaani, baba ya Aksa.

Au labda, “akapiga makofi akiwa juu ya punda ili kumwita baba yake.”

Au “eneo la Negebu.”

Yaani, “Chemchemi za (Mabakuli ya) Maji.”

Maana yake “Maangamizi.”

Au “nchi tambarare ya chini.”

Tnn., “magari ya chuma.”

Tnn., “tutakuonyesha upendo mshikamanifu.”

Au “miji jirani.”

Au “nchi tambarare ya chini.”

Maana yake “Wanaolia.”

Tnn., “wakakusanywa kwa mababu zao.” Huu ni msemo wa kishairi unaorejelea kifo.

Au “wakatumikia.”

Tnn., “Akawauza.”

Au “alighairi.”

Au “njia ya kuingia Hamathi.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “akawauza.”

Tnn., “Aram-naharaimu.”

Tnn., “Aramu.”

Tnn., “ikapumzika.”

Huenda ni mkono mfupi wenye urefu wa sentimita 38 hivi (inchi 15). Angalia Nyongeza B14.

Au labda, “machimbo ya mawe.”

Au labda, “sehemu ya kuingizia hewa.”

Au labda, “kwenye machimbo.”

Au “tarumbeta.”

Tnn., “ikapumzika.”

Tnn., “akawauza kwa.”

Au “Harosheth-ha-goimu.”

Tnn., “magari 900 ya chuma.”

Au “Wapange wanaume wako kwa ajili ya vita.”

Au “korongo kavu la.”

Tnn., “magari 900 ya chuma.”

Au “korongo kavu la.”

Yaani, pembeni mwa paji la uso kati ya jicho na sikio.

Tnn., “mkono wa Waisraeli ukazidi kuwa na nguvu.”

Au “mashujaa waliokuwa na nywele ndefu.”

Au “Nitampigia muziki.”

Au labda, “ilitetemeka.”

Au “nchi tambarare ya chini.”

Au labda, “walio na vifaa vya mwandishi.”

Au “nchi tambarare ya chini.”

Au “Kwa nini uliketi kati ya mizigo miwili.”

Au “walidharau nafsi zao.“

Au “Kijito cha Kishoni kiliwafagilia.”

Au “Kijito cha.”

Au “kijito cha.”

Angalia Kamusi.

Au “alimpa mtindi.”

Yaani, “vazi lililotariziwa.”

Tnn., “ikapumzika.”

Au labda, “maghala yaliyo chini ya ardhi.”

Tnn., “hamkuisikiliza sauti yangu.”

Tnn., “Elfu yangu ndiyo ndogo.”

Efa ya unga ilikuwa karibu kilogramu 13. Angalia Nyongeza B14.

Maana yake “Yehova Ni Amani.”

Angalia Kamusi.

Angalia Kamusi.

Angalia Kamusi.

Angalia Kamusi.

Maana yake “Acheni Baali Ajitetee Kisheria (Apambane).”

Au “wakavuka mto.”

Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”

Au “ikamfunika.”

Au “tarumbeta.”

Au “nchi tambarare ya chini.”

Au “tarumbeta.”

Tnn., “na mikono yako itakuwa na nguvu za.”

Au “tarumbeta.”

Au “tarumbeta.”

Au “tarumbeta.”

Kuanzia saa 4 hivi usiku hadi saa 8 usiku.

Au “tarumbeta.”

Au “tarumbeta.”

Au “tarumbeta.”

Tnn., “neno hilo.”

Tnn., “roho yao ikatulia.”

Tnn., “kwa maana jinsi mwanamume alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake.”

Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.

Au “kizibao cha kuhani.”

Tnn., “hawakuinua kichwa chao.”

Tnn., “ikapumzika.”

Tnn., “alikuwa na wana 70 waliotoka katika viuno vyake.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “familia ya nyumba ya baba ya mama yake.”

Au labda, “wamiliki wote wa mashamba.”

Tnn., “nina uhusiano wa damu nanyi.”

Tnn., “mioyo yao ilielekea kumfuata.”

Au “hekalu la.”

Mkwamba ni mti wenye miiba.

Au “nafsi yake.”

Au “alijitwalia mamlaka juu ya.”

Tnn., “akatuma roho mbaya.”

Au “hila.”

Au “mtendeeni kadiri ya uwezo wenu.”

Au “hekalu la.”

Au “Siria.”

Au “na nafsi yake ikakosa subira kwa sababu ya.”

Tnn., “msikilizaji.”

Au “miji jirani.”

Tnn., “Umenishusha chini sana.”

Au “nikalie pamoja na rafiki zangu kwa sababu sitaolewa kamwe.”

Au “sheria.”

Au labda, “wakavuka kuelekea kaskazini.”

Au “Niliiweka nafsi yangu mikononi mwangu.”

Tnn., “kutoka tumboni.”

Tnn., “kutoka tumboni.”

Tnn., “mwanamke wa binti za Wafilisti.”

Tnn., “anafaa machoni pangu.”

Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”

Au labda, “kabla hajaingia katika chumba cha ndani.”

Au “chumba cha ndani.”

Au “kumfunga.”

Au “kukufunga.”

Tnn., “zikayeyuka.”

Maana yake “Kilima cha Utaya.”

Au “nguvu zake zikamrudia.”

Maana yake “Chemchemi ya Anayeita.”

Au “Korongo.”

Au “Mshawishi.”

Au “Umenichezea.”

Au “nafsi yake ikachoka.”

Tnn., “kutoka tumboni mwa mama yangu.”

Au “nafsi yangu ife.”

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Au “kizibao cha kuhani.”

Au “miungu ya familia; sanamu.”

Au “alilofikiri linafaa.”

Au “mshauri.”

Au “walitambua lafudhi ya.”

Maana yake “Kambi ya Dani.”

Au “kizibao cha kuhani.”

Au “miungu ya familia; sanamu.”

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Au “kizibao cha kuhani.”

Au “miungu ya familia; sanamu.”

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Au “kizibao cha kuhani.”

Au “miungu ya familia; sanamu.”

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Au “mshauri.”

Au “kizibao cha kuhani.”

Au “miungu ya familia; sanamu.”

Au “nchi tambarare ya chini.”

Au “ili moyo wako uendelee kuishi.”

Au “uchangamshe moyo wako.”

Au “ili moyo wako uendelee kuishi.”

Au “mke.”

Tnn., “katika hema lenu.”

Au labda, “ninatumikia katika nyumba ya Yehova.”

Au “mke.”

Au “na kuwapa chakula cha mifugo.”

Au “muwatendee vibaya kama mnavyotaka.”

Au “mke.”

Au “kabila.”

Tnn., “Wekeni moyo wenu juu ya jambo hili.”

Tnn., “kama mtu mmoja.”

Au labda, “wamiliki wa mashamba.”

Au “makabila.”

Tnn., “kama mtu mmoja.”

Tnn., “kama mtu mmoja.”

Au “shabaha.”

Tnn., “akisimama.”

Tnn., “mabinti wa.”

Au “alilofikiri linafaa.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki