Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Hosea 1:1-14:9
  • Hosea

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hosea
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Hosea

Hosea

1 Neno la Yehova+ lililomjia Hosea+ mwana wa Beeri katika siku+ za Uzia,+ Yothamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda, na katika siku za Yeroboamu+ mwana wa Yoashi,+ mfalme wa Israeli. 2 Mwanzo wa neno la Yehova kupitia Hosea, Yehova alimwambia Hosea: “Nenda,+ jichukulie mke wa uasherati na watoto wa uasherati, kwa maana kwa sababu ya uasherati hakika nchi imegeuka isimfuate Yehova.”+

3 Naye akaenda na kumchukua Gomeri binti ya Diblaimu, naye akapata mimba, baadaye akamzalia mwana.+

4 Na Yehova akaendelea kumwambia: “Mwite jina lake Yezreeli,+ kwa maana bado kitambo kidogo tu nami nitatoza hesabu kwa sababu ya vitendo vya kumwaga damu vya Yezreeli juu ya nyumba ya Yehu,+ nami nitakomesha utawala wa kifalme wa nyumba ya Israeli.+ 5 Na itakuwa katika siku hiyo kwamba nitauvunja upinde+ wa Israeli katika nchi tambarare ya chini ya Yezreeli.”

6 Naye akapata mimba tena, akazaa binti. Na Yeye akamwambia: “Mwite jina lake Lo-ruhama,+ maana sitaionyesha rehema+ tena nyumba ya Israeli, kwa sababu hakika nitawaondolea mbali.+ 7 Lakini nitaionyesha rehema nyumba ya Yuda,+ nami nitawaokoa kupitia kwa Yehova Mungu wao;+ wala sitawaokoa kwa upinde wala kwa upanga wala kwa vita, wala kwa farasi wala kwa wapanda-farasi.”+

8 Na mwishowe akamwachisha Lo-ruhama kunyonya, kisha akapata mimba na kuzaa mwana. 9 Basi Mungu akasema: “Mwite jina lake Lo-ami, kwa sababu ninyi si watu wangu nami sitakuwa wenu.

10 “Na hesabu ya wana wa Israeli itakuwa kama chembe za mchanga wa bahari ambao hauwezi kupimwa wala kuhesabiwa.+ Na itakuwa kwamba mahali ambapo walikuwa wakiambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’+ wataambiwa, ‘Wana wa Mungu aliye hai.’+ 11 Na wana wa Yuda na wana wa Israeli hakika watakusanywa pamoja katika umoja+ nao kwa kweli watajiwekea kichwa kimoja nao watatoka katika ile nchi,+ kwa maana siku ya Yezreeli+ itakuwa kuu.

2 “Waambieni ndugu zenu, ‘Watu wangu!’+ na dada zenu, ‘Ee mwanamke uliyeonyeshwa rehema!’+ 2 Fanyeni kesi na mama yenu;+ fanyeni kesi, kwa maana yeye si mke wangu+ nami si mume wake.+ Naye anapaswa kuondolea mbali uasherati wake kutoka mbele yake na matendo yake ya uzinzi kutoka katikati ya maziwa yake,+ 3 ili nisimvue nguo awe uchi+ na kumtendea kama katika siku ya kuzaliwa kwake,+ na kwa kweli kumfanya kama nyika+ na kumfanya kama nchi isiyo na maji+ na kumuua kwa kiu.+ 4 Nami sitawaonyesha wanawe rehema,+ kwa maana wao ni wana wa uasherati.+ 5 Kwa maana mama yao amefanya uasherati.+ Yeye mwenye kuwachukua mimba ametenda kwa njia ya aibu,+ kwa maana amesema, ‘Nataka kuwafuata wale wanaonipenda kwa tamaa nyingi,+ wale wanaonipa mkate na maji, sufu na kitani, mafuta na kinywaji.’+

6 “Kwa sababu hiyo ninazungushia njia yako ukuta wa miiba; nami nitasimamisha ukuta wa mawe juu yake,+ ili asipate kuona barabara zake.+ 7 Naye kwa kweli atawafuata wale wanaompenda kwa tamaa nyingi, lakini hatawafikia;+ naye hakika atawatafuta, lakini hatawapata. Naye atasema, ‘Nataka kwenda, nirudi kwa mume wangu,+ yule wa kwanza,+ kwa maana hali ilikuwa nzuri zaidi kwangu wakati huo kuliko ilivyo sasa.’+ 8 Lakini yeye mwenyewe hakutambua+ kwamba mimi ndiye niliyempa nafaka+ na divai tamu na mafuta, na kwamba nilimfanya awe na fedha nyingi, na dhahabu, ambayo waliitumia kwa Baali.+

9 “ ‘Kwa sababu hiyo nitarudi na kuondolea mbali nafaka yangu wakati wake na divai yangu tamu katika majira yake,+ nami nitanyakua sufu yangu na kitani changu vinavyofunika uchi wake.+ 10 Na sasa nitazifunua sehemu zake za siri zionekane na macho ya wale wanaompenda kwa tamaa nyingi,+ na hakuna mwanamume atakayemnyakua mkononi mwangu.+ 11 Nami hakika nitakomesha furaha+ yake yote, sherehe+ yake, mwezi wake mpya+ na sabato yake na majira yake yote ya sherehe. 12 Nami nitaufanya kuwa ukiwa mzabibu+ wake na mtini+ wake, ambao amesema hivi kuuhusu: “Hizo ni zawadi zangu nilizopewa, ambazo wale wanaonipenda kwa tamaa nyingi wamenipa”; nami nitazifanya kuwa msitu,+ na mnyama wa mwituni atazila. 13 Nami nitamtoza hesabu+ kwa ajili ya siku za sanamu za Baali+ alizokuwa akifukizia moshi,+ wakati alipokuwa akijipamba kwa pete yake na pambo+ lake na kuwafuata wale wanaompenda kwa tamaa nyingi,+ naye alinisahau+ mimi,’ asema Yehova.

14 “ ‘Kwa sababu hiyo ninamshawishi mwanamke huyu, nami nitamfanya aende nyikani,+ na nitasema kwa kufikia moyo wake.+ 15 Nami nitampa mashamba yake ya mizabibu kuanzia wakati huo+ na kuendelea, na nchi tambarare ya chini ya Akori+ kama lango la tumaini; naye hakika atajibu hapo kama katika siku za ujana wake+ na kama katika siku ya kutoka kwake katika nchi ya Misri.+ 16 Na itakuwa katika siku hiyo,’ asema Yehova, ‘kwamba utaniita mimi Mume wangu, nawe hutaniita tena Mmiliki wangu.’+

17 “ ‘Nami nitaondoa majina ya sanamu za Baali kutoka katika kinywa chake,+ nazo hazitakumbukwa tena kwa majina yake.+ 18 Na kwa ajili yao hakika nitafanya agano siku hiyo na mnyama wa mwituni+ na kiumbe kinachoruka cha mbinguni na kitu kinachotambaa cha nchi, nami nitavunja kutoka katika nchi upinde na upanga na vita,+ nami nitawafanya walale salama salimini.+ 19 Nami nitakuchumbia mpaka wakati usio na kipimo,+ nitakuchumbia uwe wangu katika uadilifu na katika haki na katika fadhili zenye upendo na katika rehema.+ 20 Nami nitakuchumbia uwe wangu katika uaminifu; nawe hakika utamjua Yehova.’+

21 “ ‘Na itakuwa katika siku hiyo kwamba mimi nitajibu,’ asema Yehova, ‘nitazijibu mbingu, mbingu nazo zitaijibu dunia;+ 22 dunia nayo itaijibu nafaka+ na divai tamu na mafuta; vitu hivyo navyo vitajibu Yezreeli [‘Mungu atapanda mbegu’].+ 23 Nami hakika nitampanda yeye duniani kama mbegu kwa ajili yangu,+ nami nitamwonyesha rehema yeye ambaye hakuonyeshwa rehema,+ nami nitawaambia wale ambao si watu wangu: “Ninyi ni watu wangu”;+ wao nao watasema: “Wewe ni Mungu wangu.” ’ ”+

3 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Nenda tena, mpende mwanamke anayependwa na rafiki+ yako na ambaye anafanya uzinzi, kama vile Yehova alivyowapenda wana wa Israeli+ ingawa wanageukia miungu mingine+ na kupenda keki za zabibu kavu.”+

2 Nami nikajinunulia huyo mwanamke kwa vipande kumi na tano vya fedha+ na kipimo kimoja cha homeri ya shayiri na nusu homeri ya shayiri. 3 Ndipo nikamwambia: “Utakaa ukiwa wangu muda wa siku nyingi.+ Usifanye uasherati,+ nawe usiwe wa mwanamume mwingine;+ nami pia nitakuwa vivyo hivyo kwako.”

4 Hiyo ni kwa sababu wana wa Israeli watakaa muda wa siku nyingi bila mfalme+ wala mkuu wala dhabihu+ wala nguzo wala efodi+ wala terafimu.+ 5 Baadaye wana wa Israeli watarudi na hakika watamtafuta Yehova Mungu wao,+ na Daudi mfalme wao;+ nao watakuja kwa Yehova+ na kwa wema wake wakitetemeka katika siku za mwisho.+

4 Sikieni neno la Yehova, enyi wana wa Israeli, kwa maana Yehova ana kesi na wakaaji wa nchi,+ kwa maana hakuna kweli+ wala fadhili zenye upendo wala kumjua Mungu katika nchi.+ 2 Kuna mambo ambayo yameenea, kutangaza laana+ na kuzoea kufanya udanganyifu+ na uuaji+ na wizi+ na uzinzi,+ na vitendo vya kumwaga damu vimegusana na vitendo vingine vya kumwaga damu.+ 3 Ndiyo sababu nchi itaomboleza+ na kila mkaaji ndani yake atadhoofika pamoja na mnyama wa mwituni na kiumbe kinachoruka cha mbinguni, na hata samaki wa baharini watakusanywa katika kifo.+

4 “Hata hivyo, mtu yeyote asishindane,+ wala mtu yeyote asikaripie, kwa maana watu wako ni kama wale wanaoshindana na kuhani.+ 5 Nawe hakika utajikwaa wakati wa mchana,+ na hata nabii atajikwaa pamoja nawe, kama wakati wa usiku.+ Nami nitamnyamazisha mama yako.+ 6 Hakika watu wangu watanyamazishwa, kwa sababu hakuna ujuzi.+ Kwa kuwa wewe mwenyewe umeukataa ujuzi,+ mimi pia nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu;+ na kwa sababu unaendelea kuisahau sheria ya Mungu wako,+ hata mimi nitawasahau wana wako.+ 7 Kulingana na wingi wao, ndivyo wamenitendea dhambi.+ Wamebadili utukufu wangu kuwa aibu tupu.+ 8 Wanazidi kula dhambi ya watu wangu, nao huendelea kuinua nafsi zao kwenye kosa lao.+

9 “Na itakuwa kwa watu kama vile itakavyokuwa kwa kuhani;+ nami hakika nitawatoza hesabu kwa sababu ya njia zao;+ nami nitarudisha matendo yao juu yao.+ 10 Nao watakula, lakini hawatashiba.+ Watawatendea wanawake kama makahaba; lakini hawataongezeka,+ kwa sababu wameacha kumjali Yehova.+ 11 Uasherati na divai na divai tamu ndivyo vinavyoondoa kusudi jema.+ 12 Watu wangu mwenyewe wanaendelea kuuliza habari+ kutoka kwa sanamu yao ya mti,+ na fimbo yao ya mkononi huwaambia; kwa maana roho ya uasherati imewafanya watange-tange,+ nao kwa uasherati hutoka chini ya Mungu wao.+ 13 Wao hutoa dhabihu juu ya vilele vya milima,+ nao hufukiza moshi wa dhabihu juu ya vilima,+ chini ya mti mnene na mlubna na mti mkubwa, kwa sababu kivuli chake ni kizuri.+ Ndiyo sababu binti zenu hufanya uasherati na binti-wakwe zenu hufanya uzinzi.

14 “Sitatoza hesabu juu ya binti zenu kwa sababu wanafanya uasherati, wala juu ya binti-wakwe zenu kwa sababu wanafanya uzinzi. Kwa maana, kwa habari ya wanaume, hujiendea zao wenyewe pamoja na makahaba,+ nao hutoa dhabihu pamoja na wanawake makahaba wa hekaluni;+ na watu ambao hawaelewi+ watakanyagiwa chini. 15 Ijapokuwa unafanya uasherati, Ee Israeli,+ Yuda asiwe na hatia,+ nanyi msije Gilgali,+ wala msiende Beth-aveni+ wala kuapa ‘Kama anavyoishi Yehova!’+ 16 Kwa maana, kama vile ng’ombe mkaidi, ndivyo Israeli amekuwa mkaidi.+ Je, ni wakati huu kwamba Yehova atawachunga kama vile mwana-kondoo dume katika mahali penye nafasi pana? 17 Efraimu ameshikamana na sanamu.+ Mwache!+ 18 Pombe yao ya ngano ikishamalizika,+ hakika wamemtendea mwanamke kama kahaba.+ Hakika wanaomkinga+ wamependa aibu.+ 19 Upepo umemfunika mabawa yake.+ Nao watapatwa na aibu kutokana na dhabihu zao.”+

5 “Sikieni hili, enyi makuhani,+ na mkaze uangalifu, enyi nyumba ya Israeli, na ninyi, enyi nyumba ya mfalme,+ tegeni sikio, kwa maana hukumu hii inawahusu ninyi; kwa maana mmekuwa mtego+ katika Mispa na kama wavu uliotandazwa juu ya Tabori.+ 2 Na wale wanaoasi wamehusika sana+ katika kazi ya kuua, nami nilikuwa himizo kwao wote.+ 3 Mimi binafsi nimejua Efraimu,+ Israeli nayo haikufichwa kutoka kwangu.+ Kwa sasa, Ee Efraimu, umewatendea wanawake kama makahaba;+ Israeli imejitia unajisi.+ 4 Matendo yao hayawaruhusu kurudi kwa Mungu wao,+ kwa sababu kuna roho ya uasherati+ katikati yao; nao hawakumtambua Yehova.+ 5 Na kiburi cha Israeli kimeshuhudia mbele ya uso wake;+ na Israeli na Efraimu wamekwazwa katika kosa lao.+ Yuda pia amejikwaa pamoja nao.+ 6 Walienda kumtafuta Yehova wakiwa na makundi yao na mifugo yao, lakini hawakuweza kumpata.+ Alikuwa amejiondoa kwao. 7 Wamemtendea hila+ Yehova mwenyewe, kwa maana wamezaa wana wa kigeni.+ Sasa, mwezi mmoja utawameza pamoja na mafungu yao ya mashamba.+

8 “Pigeni baragumu+ katika Gibea,+ tarumbeta katika Rama! Pigeni kelele za vita katika Beth-aveni+—nyuma yako, Ee Benyamini!+ 9 Ee Efraimu, utakuwa kitu cha kushangaza katika siku ya kukemewa.+ Nimejulisha maneno yenye kutegemeka+ kati ya makabila ya Israeli. 10 Wakuu wa Yuda wamekuwa kama watu wanaosogeza nyuma mpaka.+ Nitamwaga ghadhabu yangu kama maji juu yao. 11 Efraimu ameonewa, amepondwa kwa haki,+ kwa maana alikuwa amejiamulia mwenyewe kumfuata adui yake.+ 12 Nami nilikuwa kama nondo+ kwa Efraimu na kama kuoza kwa nyumba ya Yuda.

13 “Na Efraimu akaona ugonjwa wake, na Yuda kidonda chake.+ Ndipo Efraimu akaenda Ashuru+ na kupeleka ujumbe kwa mfalme mkuu.+ Lakini huyo hakuweza kuwaponya ninyi,+ wala kuwaondolea kidonda kwa dawa yoyote.+ 14 Kwa maana mimi nitakuwa kama mwana-simba kwa Efraimu+ na kama mwana-simba mwenye manyoya shingoni kwa nyumba ya Yuda. Mimi, mimi mwenyewe nitararua vipande-vipande nami nitaenda na kuchukulia mbali, na hapatakuwa na mkombozi.+ 15 Nitaenda, nitarudi mahali pangu mpaka watakapoibeba hatia yao;+ nao hakika watautafuta uso wangu.+ Watanitafuta,+ wanapokuwa katika dhiki kali.”+

6 “Njooni, turudi kwa Yehova,+ kwa maana yeye mwenyewe amerarua vipande-vipande,+ lakini atatuponya.+ Alizidi kupiga, lakini atatufunga kitambaa.+ 2 Atatufanya hai baada ya siku mbili.+ Katika siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.+ 3 Nasi tutajua, tutafanya bidii kumjua Yehova.+ Kutokea kwake kumefanywa imara+ kama mapambazuko.+ Naye atakuja kwetu kama mvua inayonyesha;+ kama mvua ya masika ambayo huilowesha dunia.”+

4 “Nitakufanyia nini, Ee Efraimu? Nitakufanyia nini, Ee Yuda,+ wakati fadhili zenu zenye upendo ni kama mawingu ya asubuhi na kama umande ambao hutoweka mapema? 5 Ndiyo sababu nitawakatakata kwa kutumia manabii;+ nitawaua kwa maneno ya kinywa changu.+ Na hukumu juu yako zitakuwa kama nuru inayotokea.+ 6 Kwa maana mimi ninapendezwa na fadhili zenye upendo,+ na si dhabihu;+ ninapendezwa na kumjua Mungu kuliko matoleo mazima ya kuteketezwa.+ 7 Lakini wao wenyewe, kama mtu wa udongo, wamevunja lile agano.+ Hapo ndipo wamenitendea kwa hila.+ 8 Gileadi+ ni mji wa watu wanaotenda madhara; alama za nyayo zao ni damu.+ 9 Na kama ilivyo katika kumvizia mtu,+ ushirika wa makuhani ni vikundi vyenye kupora.+ Wao hufanya mauaji katika Shekemu+ kando ya njia, kwa sababu wameendeleza mwenendo mpotovu.+ 10 Nimeona jambo lenye kuchukiza+ sana katika nyumba ya Israeli. Humo Efraimu+ anafanya uasherati. Israeli amejitia unajisi.+ 11 Zaidi ya hilo, Ee Yuda, mavuno yamewekwa kwa ajili yako, wakati nitakapowarudisha tena watu wangu waliotekwa.”+

7 “Wakati ninapotaka kuponya Israeli,+ ndipo kosa la Efraimu pia hufunuliwa,+ na mambo mabaya ya Samaria;+ kwa maana wamezoea kusema uwongo,+ na mwizi huingia ndani; kikundi cha waporaji hushambulia ghafula upande wa nje.+ 2 Na hawauambii moyo+ wao kwamba mimi nitakumbuka ubaya wao wote.+ Sasa matendo yao yamewazunguka.+ Yamekuja mbele za uso wangu.+ 3 Wao humfanya mfalme ashangilie kwa ubaya wao, na wakuu kwa udanganyifu wao.+ 4 Wote ni wazinzi,+ kama tanuru ambalo mwokaji amewasha, ambaye huacha kuchochea baada ya kukanda unga mpaka unapotiwa chachu. 5 Wakuu wamekuwa wagonjwa+ katika siku ya mfalme wetu—kuna ghadhabu kwa sababu ya divai.+ Amenyoosha mkono wake pamoja na wenye kudharau. 6 Kwa maana wameleta moyo wao karibu kama kwenye tanuru;+ unawaka ndani yao.+ Mwokaji wao analala usiku wote; kufika asubuhi tanuru lao linawaka kama kwa moto unaotoa miali.+ 7 Wao wote hupata moto, kama tanuru, nao huwateketeza waamuzi wao. Wafalme wao wote wameanguka;+ hakuna yeyote kati yao anayeniita.+

8 “Lakini Efraimu naye huchangamana binafsi na vikundi vya watu.+ Efraimu amekuwa keki ya mviringo ambayo haikugeuzwa upande mwingine.+ 9 Wageni wamekula nguvu zake,+ na yeye mwenyewe hakupata kujua hilo.+ Pia, mvi zimekuwa nyeupe juu yake, lakini yeye mwenyewe hakupata kujua hilo. 10 Na kiburi cha Israeli kimeshuhudia mbele ya uso wake,+ nao hawakurudi kwa Yehova Mungu wao,+ wala hawakumtafuta kwa sababu ya hayo yote.+ 11 Na Efraimu ni kama njiwa+ mjinga, asiye na ufahamu.+ Wameita Misri;+ wameenda Ashuru.+

12 “Njia yoyote ile wanayoiendea, nitatandaza juu yao wavu wangu.+ Nitawashusha chini kama viumbe vinavyoruka vya mbinguni.+ Nitawatia nidhamu kulingana na habari iliyopelekwa kwenye kusanyiko lao.+ 13 Ole wao,+ kwa maana wamenikimbia!+ Na waporwe, kwa maana wamenikosea! Nami mwenyewe nikachukua hatua ya kuwakomboa,+ bali wao wenyewe wamesema uwongo juu yangu.+ 14 Nao hawakuniita mimi kwa moyo+ wao niwape msaada, ingawa waliendelea kupiga mayowe vitandani mwao. Wakaendelea kuwa na uzembe+ kwa sababu ya nafaka na divai yao tamu; wakazidi kunigeuka mimi.+ 15 Na mimi nilitia nidhamu;+ niliitia mikono yao nguvu,+ lakini waliendelea kunipangia mambo mabaya.+ 16 Nao wakaanza kurudi, lakini hawakurudi kwenye ibada ya kweli;+ walikuwa wamekuwa kama upinde uliolegea.+ Wakuu wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya shutuma za ulimi wao.+ Hiyo itakuwa ni dhihaka yao katika nchi ya Misri.”+

8 “Tia baragumu+ katika kinywa chako! Mtu fulani anakuja kama tai+ juu ya nyumba ya Yehova, kwa sababu wamelivunja agano langu,+ nao wameikosea sheria yangu.+ 2 Wao wanazidi kunililia, ‘Ee Mungu wangu, sisi, Israeli, tumekujua.’+

3 “Israeli ametupilia mbali wema.+ Adui na amfuatilie.+ 4 Wao wenyewe wameweka wafalme,+ lakini si kwa sababu yangu. Wameweka wakuu, lakini mimi sikuwa na habari. Wamejifanyia sanamu+ kwa fedha yao na dhahabu yao, kusudi wakatiliwe mbali.+ 5 Ndama wako ametupiliwa mbali,+ Ee Samaria. Hasira yangu imewaka juu yao.+ Wataendelea mpaka wakati gani kutoweza kuwa na hali isiyo na hatia?+ 6 Kwa maana katika Israeli kimetokea hata kitu hiki.+ Fundi tu ndiye aliyekifanya,+ wala si Mungu; kwa maana ndama wa Samaria atavunjika vipande-vipande.+

7 “Kwa maana wao huendelea kupanda upepo, nao watavuna+ upepo wa dhoruba. Hakuna chochote chenye nafaka inayosimama.+ Hakuna chipukizi lolote linalotoa unga.+ Chipukizi lolote likiutokeza, wageni wataumeza.+

8 “Israeli watamezwa.+ Sasa watakuja kuwa kati ya mataifa,+ kama chombo ambacho hakipendezi.+ 9 Kwa maana wao wenyewe wamepanda kwenda Ashuru,+ kama punda-milia aliyejitenga.+ Kwa habari ya Efraimu, wamekodi wapenzi.+ 10 Pia, ingawa wanaendelea kuwakodi kati ya mataifa,+ sasa mimi nitawakusanya pamoja; nao watakuwa katika maumivu makali+ kwa kitambo kidogo kwa sababu ya mzigo wa mfalme na wakuu.

11 “Kwa maana Efraimu amezidisha madhabahu ili kutenda dhambi.+ Amekuwa na madhabahu ili atende dhambi.+ 12 Ndipo nikamwandikia mambo mengi ya sheria yangu;+ nayo yamehesabiwa kuwa kama kitu kigeni.+ 13 Walizidi kunitolea dhabihu ya nyama kuwa dhabihu za zawadi,+ nao wakaendelea kula vitu ambavyo Yehova hakufurahia.+ Sasa atakumbuka kosa lao na kutoza hesabu kwa sababu ya dhambi zao.+ Ndipo wao waliporudi Misri.+ 14 Naye Israeli akaanza kumsahau Mtengenezaji wake+ na kujenga mahekalu;+ naye Yuda akazidisha majiji yenye ngome.+ Nami nitapeleka moto katika majiji yake nao utateketeza minara ya makao ya kila mmoja.”+

9 “Usishangilie, Ee Israeli.+ Usitende kwa shangwe kama vikundi vya watu.+ Kwa maana kwa kufanya uasherati umeondoka kando ya Mungu wako.+ Umependa zawadi za kukodiwa juu ya viwanja vyote vya kupuria nafaka.+ 2 Uwanja wa kupuria na shinikizo la divai haviwalishi wao,+ nayo divai tamu inamkatisha tamaa.+ 3 Hawataendelea kukaa katika nchi ya Yehova,+ naye Efraimu atarudi Misri,+ nao watakula vitu vilivyo najisi katika Ashuru.+ 4 Hawataendelea kummiminia Yehova divai.+ Na dhabihu zao hazitampendeza;+ hizo ni kama mkate wa nyakati za maombolezo+ kwao; wote wanaoula watajitia unajisi. Kwa maana mkate wao ni kwa ajili ya nafsi zao wenyewe; hautaingia katika nyumba ya Yehova.+ 5 Ninyi mtafanya nini katika siku ya mkutano na katika siku ya sherehe ya Yehova?+ 6 Kwa maana, tazama! lazima watakwenda kwa sababu ya uporaji.+ Misri itawakusanya pamoja;+ Memfisi+ nayo itawazika. Upupu nao utachukua vitu vyao vyenye kutamanika vya fedha;+ miti yenye miiba itakuwa katika mahema yao.+

7 “Siku za kukaziwa fikira zitakuja;+ siku za malipo yanayostahili zitakuja.+ Watu wa Israeli watajua habari hiyo.+ Nabii atakuwa mpumbavu,+ mtu wa neno lililoongozwa na roho atatiwa wazimu kwa sababu ya wingi wa makosa yako,+ hata uadui kuwa mwingi.”

8 Mlinzi+ wa Efraimu alikuwa pamoja na Mungu wangu.+ Kuhusu nabii,+ kuna mtego wa mwindaji wa ndege katika njia zake zote;+ kuna uadui katika nyumba ya Mungu wake. 9 Wamejiingiza sana katika kuleta uharibifu,+ kama katika siku za Gibea.+ Atakumbuka kosa lao;+ atakazia fikira dhambi zao.

10 “Nilimkuta Israeli kama zabibu nyikani.+ Niliwaona mababu zenu kama tini ya mapema katika mtini ulio katika majira yake ya kwanza.+ Wao wenyewe waliingia kwa Baali wa Peori,+ nao wakajiweka wakfu kwa kitu kile cha aibu, wakawa wenye kuchukiza+ kama kile kitu walichokipenda.+ 11 Na kwa habari ya Efraimu, utukufu wao hurukia mbali kama kiumbe kinachoruka,+ hata kusiwe na kuzaa, wala tumbo lenye mimba wala kuchukua mimba.+ 12 Kwa maana ingawa wanalea wana wao, mimi pia nitawaondolea watoto wao hata kusiwe na mtu;+ kwa sababu—ole wao pia nitakapogeuka kutoka kwao!+ 13 Efraimu, ambaye nimemwona kama Tiro akiwa amepandwa katika uwanja wa malisho,+ ndiyo, Efraimu anakusudiwa kumtolea muuaji watoto wake.”+

14 Wape, Ee Yehova, kile inachokupasa kuwapa.+ Wape tumbo lenye kuharibu mimba+ na maziwa yanayokauka.

15 “Ubaya wao wote ulikuwa katika Gilgali,+ kwa maana hapo nililazimika kuwachukia.+ Nitawafukuzia mbali kutoka katika nyumba yangu mwenyewe kwa sababu ya uovu wa matendo yao.+ Sitaendelea kuwapenda.+ Wakuu wao wote wanatenda kwa ukaidi.+ 16 Efraimu atapigwa aanguke.+ Mzizi wao utakauka.+ Hawatazaa matunda yoyote.+ Pia, hata wakizaa, nitaviua vitu vyenye kutamanika vya tumbo lao.”+

17 Mungu wangu+ atawakataa, kwa maana hawakumsikiliza,+ nao watakuwa wakimbizi katikati ya mataifa.+

10 “Israeli ni mzabibu unaoharibika.+ Yeye huendelea kutokeza matunda kwa ajili yake mwenyewe.+ Naye amezidisha madhabahu zake kulingana na wingi wa matunda yake.+ Wao huweka nguzo nzuri+ kulingana na wema wa nchi yake. 2 Moyo wao umekuwa na unafiki;+ sasa watapatikana na hatia.

“Kuna yule atakayevunja madhabahu zao; atapora nguzo zao.+ 3 Kwa maana sasa watasema, ‘Hatuna mfalme yeyote,+ kwa kuwa hatukumwogopa Yehova. Naye mfalme atatufanyia nini?’

4 “Wao husema maneno, wakila viapo vya uwongo,+ wakifanya agano;+ na hukumu imechipuka kama mmea wenye sumu katika mitaro ya shamba.+ 5 Wakaaji wa Samaria wataogopa kwa sababu ya sanamu ya ndama ya Beth-aveni;+ kwa maana watu wake wataiombolezea, na vilevile makuhani wake wa miungu ya kigeni waliokuwa wakishangilia juu yake, kwa sababu ya utukufu wake, kwa maana itakuwa imeenda uhamishoni mbali nayo.+ 6 Nayo itachukuliwa Ashuru na mtu fulani iwe zawadi kwa mfalme mkuu.+ Efraimu naye atapata aibu,+ na Israeli atalionea aibu shauri lake.+ 7 Samaria na mfalme wake hakika watanyamazishwa,+ kama tawi lililokatwa juu ya uso wa maji. 8 Na mahali pa juu pa Beth-aveni,+ dhambi ya Israeli,+ pataangamizwa. Miiba na mibaruti+ itakuja juu ya madhabahu zao.+ Na hakika watu wataiambia milima, ‘Tufunikeni!’ na vilima, ‘Tuangukieni!’+

9 “Umetenda dhambi+ kuanzia siku za Gibea,+ Ee Israeli. Huko walisimama tuli. Vita juu ya wana wenye kukosa uadilifu katika Gibea havikupata kuwafikia.+ 10 Wakati nitakapopenda nitawatia nidhamu pia.+ Na vikundi vya watu vitakusanyika juu yao watakapofungwa pamoja na makosa yao mawili.+

11 “Na Efraimu alikuwa ndama-jike aliyezoezwa, anayependa kupura;+ nami mwenyewe nikapita juu ya shingo yake yenye kupendeza. Nafanya mtu fulani ampande Efraimu.+ Yuda hulima;+ Yakobo humlimia.+ 12 Mjipandie mbegu kwa uadilifu;+ mvune kulingana na fadhili zenye upendo.+ Mjilimie udongo unaofaa kwa kilimo,+ kukiwa kungali na wakati wa kumtafuta Yehova mpaka atakapokuja+ na kuwatolea ninyi mafundisho kwa uadilifu.+

13 “Ninyi mmelima uovu.+ Nanyi mmevuna ukosefu wa uadilifu.+ Mmekula matunda ya udanganyifu,+ kwa maana mmetegemea njia yenu,+ katika wingi wa watu wenu wenye nguvu.+ 14 Na fujo imetokea kati ya watu wako,+ na majiji yako yenye ngome yataporwa yote,+ kama vile Shalmani alivyopora nyumba ya Arbeli, katika siku ya pigano ambapo mama mmoja alivunjwa vipande-vipande kando ya wanawe.+ 15 Mtu fulani atawafanyia vivyo hivyo, Ee Betheli, kwa sababu ya ubaya wenu mwingi.+ Hakika mfalme wa Israeli atanyamazishwa+ wakati wa mapambazuko.”

11 “Israeli alipokuwa mvulana, ndipo nikampenda,+ na kutoka Misri nilimwita mwanangu.+

2 “Waliwaita.+ Kwa kadiri hiyohiyo walienda mbali kutoka mbele yao.+ Wakaanza kutoa dhabihu kwa sanamu za Baali,+ nao wakaanza kufukiza moshi wa dhabihu kwa sanamu za kuchongwa.+ 3 Lakini mimi, nilimfundisha Efraimu kutembea,+ nikawachukua mikononi mwangu;+ wala hawakutambua kwamba nilikuwa nimewaponya.+ 4 Nilizidi kuwavuta kwa kamba za mtu wa udongo, kwa kamba za upendo,+ hata nikawa kwao kama wale wanaoondoa nira kwenye mfupa wa mataya yao,+ nami kwa upole nikamletea kila mmoja wao chakula.+ 5 Hatarudi katika nchi ya Misri, bali Ashuru atakuwa mfalme wake,+ kwa sababu walikataa kurudi.+ 6 Na upanga utazunguka-zunguka katika majiji yake+ na kukomesha mapingo yake na kula+ kwa sababu ya mashauri yao.+ 7 Na watu wangu wanaelekea kunikosea uaminifu.+ Nao huwaita kuelekea juu; wala hakuna yeyote anayesimama.

8 “Nawezaje kukuacha, Ee Efraimu?+ Nawezaje kukutoa, Ee Israeli?+ Nawezaje kukufanya uwe kama Adma?+ Nawezaje kukuweka uwe kama Seboiimu?+ Moyo wangu umebadilika ndani yangu;+ na wakati huohuo huruma zangu zimewaka. 9 Sitaonyesha hasira yangu inayowaka.+ Sitaharibu tena Efraimu,+ kwa maana mimi ni Mungu,+ mimi si mwanadamu, mimi ndiye Mtakatifu katikati yako;+ wala sitakuja nikiwa na hasira. 10 Watatembea kwa kumfuata Yehova.+ Atanguruma kama simba;+ kwa maana yeye mwenyewe atanguruma,+ na wana watakuja wakitetemeka kutoka upande wa magharibi.+ 11 Watakuja kutoka Misri+ wakitetemeka kama ndege, na kama njiwa kutoka nchi ya Ashuru;+ nami nitawafanya wakae katika nyumba zao,” asema Yehova.+

12 “Efraimu amenizunguka kwa maneno ya uwongo,+ na nyumba ya Israeli kwa udanganyifu. Lakini Yuda bado anatembea pamoja na Mungu,+ naye ni mwaminifu kwa aliye Mtakatifu Zaidi.”

12 “Efraimu anajilisha upepo+ na kufukuza upepo wa mashariki siku nzima.+ Anazidisha uwongo na uporaji.+ Nao hufanya agano na Ashuru,+ na mafuta hupelekwa Misri.

2 “Naye Yehova ana kesi na Yuda,+ kumtoza Yakobo hesabu kulingana na njia zake;+ atamlipa kulingana na matendo yake.+ 3 Alimkamata ndugu yake kwenye kisigino ndani ya tumbo,+ na kwa nguvu zake zenye msukumo alishindana na Mungu.+ 4 Akaendelea kushindana na malaika, naye mwishowe akashinda.+ Alilia, ili apate kujiombea kibali kwa bidii.”+

Alimkuta Betheli,+ na huko Yeye akaanza kusema nasi.+ 5 Na Yehova Mungu wa majeshi,+ Yehova ni ukumbusho wake.+

6 “Na wewe inakupasa kurudi kwa Mungu wako,+ ushike fadhili zenye upendo+ na haki;+ nawe umtumaini Mungu wako sikuzote.+ 7 Mfanya-biashara ana mizani ya udanganyifu mkononi mwake;+ amependa kupunja.+ 8 Na Efraimu anaendelea kusema, ‘Kwa kweli nimekuwa tajiri;+ nimejipatia vitu vyenye thamani.+ Na kuhusu kazi yangu yote ya kutaabika, hawatanipata nikiwa na kosa lililo dhambi.’+

9 “Lakini mimi ni Yehova Mungu wako kuanzia nchi ya Misri.+ Na bado nitakufanya ukae katika mahema kama katika siku za wakati uliowekwa. 10 Nami nilisema na manabii,+ nikazidisha maono, nikaendelea kutoa mifano kupitia mkono wa manabii.+

11 “Mambo ya uchawi,+ pia yasiyo ya kweli,+ yametokea Gileadi. Wametoa dhabihu za ng’ombe katika Gilgali.+ Zaidi ya hayo, madhabahu zao ni kama mafungu ya mawe katika matuta ya shamba.+ 12 Na Yakobo akakimbia kwenda katika nchi ya Siria,+ na Israeli+ akaendelea kutumikia apate mke,+ naye akalinda kondoo apate mke.+ 13 Na Yehova kupitia nabii akaleta Israeli kutoka Misri,+ naye akalindwa kupitia nabii.+ 14 Efraimu alichukiza akatia uchungu,+ na matendo yake ya kumwaga damu anayaacha juu yake mwenyewe,+ na Bwana-Mkuu wake atamlipa yeye shutuma zake.”+

13 “Efraimu aliposema, alitetemesha; yeye alichukuliwa kwa uzito katika Israeli.+ Lakini akawa na hatia kuhusiana na Baali,+ akafa.+ 2 Na sasa wanafanya dhambi zaidi na kujifanyia sanamu ya kuyeyushwa kutoka kwenye fedha+ yao, sanamu kulingana na uelewaji wao wenyewe,+ yote hiyo ni kazi ya mafundi.+ Nao wanaziambia, ‘Acheni wanadamu wanaotoa dhabihu wabusu ndama.’+ 3 Kwa hiyo watakuwa kama mawingu ya asubuhi+ na kama umande unaotoweka mapema; kama makapi yanayopeperushwa mbali kutoka kwenye uwanja wa kupuria+ na kama moshi kutoka katika tundu la paa.

4 “Lakini mimi ni Yehova Mungu wako kuanzia nchi ya Misri,+ wala hukuwa unamjua Mungu mwingine yeyote ila mimi; wala hapakuwa na mwokozi mwingine yeyote ila mimi.+ 5 Mimi mwenyewe nilikujua wewe nyikani,+ katika nchi yenye homa nyingi.+ 6 Pia wakashiba kulingana na malisho yao.+ Walishiba, kisha moyo wao ukaanza kujiinua.+ Ndiyo sababu walinisahau mimi.+ 7 Nami nitakuwa kwao kama mwana-simba.+ Nitaendelea kutazama kama chui kando ya njia.+ 8 Nitakutana nao kama dubu ambaye amepoteza watoto wake,+ nitaurarua ukuta wa moyo wao. Nami nitawala hapo kama simba;+ mnyama wa mwituni atawararua vipande-vipande.+ 9 Hakika atakuharibu wewe,+ Ee Israeli, kwa sababu ilikuwa juu yangu, juu ya msaidizi wako.+

10 “Basi, yuko wapi mfalme wako, apate kukuokoa katika majiji yako yote,+ na waamuzi wako, ambao ulisema hivi kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?+ 11 Ndipo nilikupa mfalme katika hasira yangu,+ nami nitamwondolea mbali katika ghadhabu yangu.+

12 “Kosa la Efraimu limefungwa, dhambi yake imewekwa akiba kama hazina.+ 13 Uchungu wa mwanamke anayezaa utamshika yeye.+ Yeye ni mwana asiye na hekima,+ kwa maana katika majira yake, hatasimama wakati wana watakapotoka katika tumbo la uzazi.+

14 “Nitawakomboa wao kutoka katika mkono wa Kaburi;*+ nitawaokoa wao+ kutoka kwenye kifo. Ee Kifo, iko wapi michomo yako?+ Ee Kaburi,* yako wapi maangamizi yako?+ Huruma itafichwa kutoka machoni pangu.+

15 “Hata yeye akizaa sana+ kama mimea ya matete, upepo wa mashariki, upepo wa Yehova, utakuja.+ Unakuja kutoka nyikani, nao utakausha kisima chake na kukausha bubujiko lake.+ Huyo atapora hazina ya vyombo vyote vyenye kutamanika.+

16 “Samaria atahesabiwa kuwa na hatia,+ kwa maana kwa kweli yeye amemwasi Mungu wake.+ Wataanguka kwa upanga.+ Watoto wao wenyewe watavunjwa vipande-vipande,+ na wanawake wao wenye mimba watapasuliwa.”+

14 “Ee Israeli, rudi kwa Yehova Mungu wako,+ kwa maana umejikwaa katika kosa lako.+ 2 Chukueni maneno pamoja nanyi mrudi kwa Yehova.+ Mwambieni hivi, enyi nyote, ‘Samehe kosa letu;+ na ukubali lililo jema, nasi tutatoa ng’ombe-dume wachanga wa midomo yetu.+ 3 Ashuru yenyewe haitatuokoa.+ Hatutapanda farasi.+ Na hatutaiambia tena kazi ya mikono yetu: “Ee Mungu wetu!” kwa sababu ni kupitia wewe kwamba mvulana asiye na baba huonyeshwa rehema.’+

4 “Nitaponya ukosefu wao wa uaminifu.+ Nitawapenda kwa kupenda kwangu mwenyewe,+ kwa maana hasira yangu imegeuka kutoka kwake.+ 5 Nitakuwa kama umande kwa Israeli.+ Atachanua kama yungiyungi, na kueneza mizizi yake kama mti wa Lebanoni. 6 Matawi yake yatasambaa, na utukufu wake utakuwa kama ule wa mzeituni,+ na harufu yake nzuri itakuwa kama ile ya mti wa Lebanoni. 7 Watakaa tena katika kivuli chake.+ Watakuza nafaka, nao watachipuka kama mzabibu.+ Ukumbusho wake utakuwa kama divai ya Lebanoni.

8 “Efraimu atasema, ‘Nina nini tena na sanamu?’+

“Hakika mimi mwenyewe nitatoa jibu, nami nitaendelea kumtazama.+ Mimi ni kama mberoshi wenye majani mengi.+ Matunda kwa ajili yako yatapatikana kwangu.”

9 Ni nani aliye na hekima, apate kuelewa mambo haya?+ Mwenye busara, apate kuyajua?+ Kwa maana njia za Yehova zimenyooka,+ na waadilifu ndio watakaotembea katika hizo;+ bali wakosaji ndio watakaojikwaa katika hizo.+

[Maelezo ya Chini]

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki