Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Danieli 1:1-12:13
  • Danieli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Danieli
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Danieli

Danieli

1 Katika mwaka wa tatu wa ufalme wa Yehoyakimu+ mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babiloni alikuja Yerusalemu na kulizingira.+ 2 Baada ya muda Yehova akamtia Yehoyakimu mfalme wa Yuda+ mkononi mwake, pamoja na sehemu ya vyombo+ vya nyumba ya Mungu wa kweli, naye akavileta katika nchi ya Shinari+ nyumbani kwa mungu wake; akaleta vyombo hivyo kwenye nyumba ya hazina ya mungu wake.+

3 Ndipo mfalme akamwambia Ashpenazi ofisa mkuu wa makao yake ya kifalme+ awalete baadhi ya wana wa Israeli na wa uzao wa kifalme na wa watu wenye vyeo,+ 4 watoto ambao hawakuwa na kasoro yoyote,+ bali wenye sura nzuri, wenye ufahamu katika hekima yote, wenye ujuzi,+ wenye utambuzi kuhusu mambo yanayojulikana,+ ambao pia walikuwa na uwezo wa kusimama katika jumba la mfalme;+ na kuwafundisha maandishi na lugha ya Wakaldayo. 5 Tena mfalme akawawekea posho ya kila siku katika vyakula vitamu+ vya mfalme na katika divai yake ya kunywa, ili kuwalisha miaka mitatu, ndipo mwishowe wasimame mbele ya mfalme.

6 Basi kati yao walikuwa baadhi ya wana wa Yuda, Danieli,+ Hanania, Mishaeli na Azaria.+ 7 Naye ofisa mkuu wa makao ya mfalme akawapa majina.+ Basi akamwita Danieli jina Belteshaza;+ Hanania akamwita Shadraki; Mishaeli akamwita Meshaki; naye Azaria akamwita Abednego.+

8 Lakini Danieli aliazimia moyoni mwake kwamba hatajitia unajisi+ kwa vyakula vitamu vya mfalme wala kwa divai yake ya kunywa. Naye akazidi kumwomba ofisa mkuu wa makao ya mfalme ili asijitie unajisi.+ 9 Basi Mungu wa kweli akampa Danieli fadhili zenye upendo na rehema mbele ya yule ofisa mkuu wa makao ya mfalme.+ 10 Ndipo huyo ofisa mkuu wa makao ya mfalme akamwambia Danieli: “Mimi namwogopa bwana wangu mfalme, ambaye ameagiza chakula chenu na kinywaji chenu.+ Kwa nini, basi, aone nyuso zenu zina sura ya huzuni zikilinganishwa na watoto ambao wana umri kama wenu, na kwa nini mkifanye kichwa changu kiwe na hatia mbele ya mfalme?” 11 Lakini Danieli akamwambia mlinzi ambaye ofisa mkuu wa makao ya mfalme+ alikuwa amemweka juu ya Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria: 12 “Tafadhali, uwajaribu watumishi wako kwa siku kumi, na watupe mboga za majani+ tule na maji tunywe; 13 kisha sura zetu na sura za wale watoto wanaokula vyakula vitamu vya mfalme zionekane mbele yako, nawe uwatendee watumishi wako kulingana na unavyoona.”

14 Mwishowe akawasikiliza kwa jambo hilo, akawajaribu kwa siku kumi. 15 Na mwishoni mwa zile siku kumi, sura zao zikaonekana kuwa bora na zilizonenepa kuliko za wale watoto wote waliokuwa wakila vyakula vitamu vya mfalme.+ 16 Kwa hiyo yule mlinzi akaendelea kuondoa vyakula vyao vitamu na divai yao ya kunywa, akawapa mboga za majani.+ 17 Basi Mungu wa kweli akawapa watoto hao wanne ujuzi na ufahamu katika maandishi na hekima yote;+ naye Danieli alikuwa akielewa maono na ndoto za aina zote.+

18 Basi mwishoni mwa siku ambazo mfalme alikuwa amesema waletwe ndani,+ ofisa mkuu wa makao ya mfalme pia akawaleta ndani, mbele ya Nebukadneza. 19 Naye mfalme akaanza kusema nao, na kati yao wote hakupatikana yeyote aliye kama Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria;+ nao wakaendelea kusimama mbele ya mfalme.+ 20 Na katika kila jambo la hekima na la uelewaji+ alilowauliza mfalme, akawaona kuwa bora mara kumi kuliko makuhani+ wote wenye kufanya uchawi na wafanya-mazingaombwe+ waliokuwa katika ufalme wake wote. 21 Naye Danieli akaendelea kudumu kufikia mwaka wa kwanza wa Koreshi mfalme.+

2 Na katika mwaka wa pili wa ufalme wa Nebukadneza, Nebukadneza aliota ndoto;+ na roho yake ikaanza kuhangaika,+ usingizi wake ukatoweka. 2 Basi mfalme akaagiza waitwe makuhani wote wenye kufanya uchawi+ na wafanya-mazingaombwe na walozi na Wakaldayo ili wamwambie mfalme ndoto zake.+ Nao wakaingia na kusimama mbele ya mfalme. 3 Ndipo mfalme akawaambia: “Kuna ndoto ambayo nimeota, na roho yangu imehangaika kwa kutaka kuijua ndoto hiyo.” 4 Basi Wakaldayo wakasema na mfalme katika lugha ya Kiaramu:+ “Ee mfalme, uishi mpaka wakati usio na kipimo.+ Waambie watumishi wako ndoto hiyo, nasi tutaonyesha tafsiri yake.”+

5 Mfalme akajibu na kuwaambia Wakaldayo: “Mimi natangaza neno hili: Msiponijulisha ndoto hiyo, na tafsiri yake, mtakatwa vipande-vipande,+ na nyumba zenu zitageuzwa kuwa vyoo vya watu wote.+ 6 Bali mkionyesha ndoto hiyo na tafsiri yake, mtapokea zawadi na tuzo na heshima kubwa kutoka kwangu.+ Basi nionyesheni ndoto hiyo na tafsiri yake.”

7 Kisha wakajibu mara ya pili na kusema: “Mfalme na awaambie watumishi wake ndoto hiyo, nasi tutaonyesha tafsiri yake.”

8 Mfalme akajibu na kusema: “Hakika mimi najua kwamba mnajaribu kupata wakati, kwa vile mmejua kuwa ninatangaza neno hili. 9 Kwa kuwa msiponijulisha ndoto hiyo, kuna hukumu moja+ tu juu yenu. Lakini mmekubaliana kusema mbele yangu uwongo na neno lenye kosa,+ mpaka wakati ubadilishwe. Basi niambieni ndoto hiyo, nami nitajua kwamba mnaweza kuonyesha tafsiri yake.”

10 Wakaldayo wakajibu mbele ya mfalme, na kusema: “Hakuna binadamu yeyote juu ya nchi kavu anayeweza kuonyesha jambo hili la mfalme, kwa vile hakuna mfalme mkuu wala gavana ambaye amepata kuuliza jambo kama hili kutoka kwa kuhani yeyote mwenye kufanya uchawi, wala mfanya-mazingaombwe wala Mkaldayo. 11 Lakini jambo hili ambalo mfalme anauliza ni gumu, wala hakuna mtu mwingine yeyote anayeweza kulionyesha mbele ya mfalme isipokuwa miungu,+ ambao makao yao hayako kamwe pamoja na wenye mwili wa nyama.”+

12 Kwa sababu hiyo mfalme akakasirika na kuwa na ghadhabu sana,+ naye akaagiza watu wote wenye hekima wa Babiloni waangamizwe.+ 13 Nalo agizo likatolewa, na watu wenye hekima wakawa karibu kuuawa; nao wakamtafuta Danieli na wenzake, ili wauawe.

14 Ndipo wakati huo, kwa shauri na akili,+ Danieli akamzungumzia Arioko mkuu wa walinzi wa mfalme, aliyekuwa ameenda kuwaua watu wenye hekima wa Babiloni. 15 Akamuuliza Arioko ofisa wa mfalme: “Kwa nini mfalme ametoa agizo kali namna hii?” Ndipo Arioko akamjulisha Danieli jambo hilo.+ 16 Basi Danieli mwenyewe akaingia na kuomba mfalme ampe wakati maalumu ili amwonyeshe mfalme tafsiri ile.+

17 Kisha Danieli akaenda nyumbani kwake; naye akawajulisha wenzake jambo hilo, Hanania, Mishaeli na Azaria, 18 ili waombe rehema+ kutoka kwa Mungu wa mbinguni+ kuhusu siri hiyo,+ kwamba Danieli na wenzake pamoja na wale watu wengine wenye hekima wa Babiloni wasiangamizwe.+

19 Ndipo Danieli akafunuliwa siri hiyo katika maono ya usiku.+ Basi Danieli akambariki+ Mungu wa mbinguni. 20 Danieli akajibu na kusema: “Jina la Mungu na libarikiwe+ kutoka wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo, maana hekima na nguvu ni zake.+ 21 Naye anabadili nyakati na majira,+ akiondoa wafalme na kuwasimamisha wafalme,+ akiwapa hekima wenye hekima na kuwapa ujuzi wale wanaojua utambuzi.+ 22 Yeye anafunua mambo mazito na yale yaliyofichwa,+ akijua yaliyo katika giza;+ nayo nuru+ hukaa kwake. 23 Nami nakusifu wewe na kukuhimidi,+ Ee Mungu wa mababu zangu, kwa maana umenipa mimi hekima+ na nguvu. Na sasa umenijulisha tulilokuomba, kwa kuwa umetujulisha jambo lile la mfalme.”+

24 Kwa sababu hiyo Danieli akaingia kwa Arioko,+ ambaye mfalme alikuwa amemweka awaangamize watu wenye hekima wa Babiloni.+ Akaenda, akamwambia hivi: “Usiangamize yeyote kati ya watu wenye hekima wa Babiloni. Nipeleke mbele ya mfalme,+ nimwonyeshe mfalme ile tafsiri.”

25 Ndipo Arioko akampeleka Danieli haraka-haraka mbele ya mfalme, akamwambia hivi: “Nimepata mwanamume mmoja kutoka kwa wahamishwa+ wa Yuda anayeweza kumjulisha mfalme ile tafsiri.” 26 Basi mfalme akajibu na kumwambia Danieli, ambaye jina lake aliitwa Belteshaza:+ “Je, una uwezo wa kutosha kuniambia ndoto niliyoona, na tafsiri yake?”+ 27 Danieli akajibu mbele ya mfalme na kusema: “Siri ambayo mfalme anauliza, watu wenye hekima, wala wafanya-mazingaombwe, wala makuhani wenye kufanya uchawi wala wanajimu hawawezi kumwonyesha mfalme.+ 28 Hata hivyo, kuna Mungu mbinguni ambaye ni Mfunuaji wa siri,+ naye amemjulisha Mfalme Nebukadneza mambo yatakayotokea katika siku za mwisho.+ Ndoto yako na maono ya kichwa chako kitandani mwako ndiyo haya:

29 “Wewe, Ee mfalme, ukiwa kitandani+ mwako mawazo yako yalikuja kuhusu mambo yatakayotokea baada ya haya, na Aliye Mfunuaji wa siri amekujulisha mambo yatakayotokea.+ 30 Lakini mimi sikufunuliwa siri hii kwa sababu nina hekima ndani yangu kuliko watu wengine walio hai,+ bali kusudi mfalme mwenyewe aambiwe tafsiri, upate kujua mawazo ya moyo wako.+

31 “Wewe, Ee mfalme, ulikuwa ukiangalia, na tazama! sanamu fulani kubwa sana. Sanamu hiyo, iliyokuwa kubwa na ambayo mwangaza wake ulikuwa usio wa kawaida, ilikuwa imesimama mbele yako, na sura yake ilitia hofu. 32 Na sanamu hiyo ilikuwa na kichwa cha dhahabu safi,+ kifua na mikono ya fedha,+ tumbo na mapaja ya shaba,+ 33 miguu ya chuma,+ nyayo zake zilikuwa sehemu moja chuma na sehemu nyingine udongo uliofinyangwa.+ 34 Uliendelea kutazama mpaka jiwe likakatwa bila kutumia mikono,+ nalo likaipiga sanamu hiyo juu ya nyayo zake za chuma na za udongo uliofinyangwa, likaziponda.+ 35 Wakati huo kile chuma, ule udongo uliofinyangwa, ile shaba, ile fedha na ile dhahabu, zote pamoja, zilipondwa na kuwa kama makapi yanayotoka kwenye uwanja wa kupuria wa wakati wa kiangazi,+ kisha upepo ukazipeleka mbali hivi kwamba alama zake hazikuonekana hata kidogo.+ Na lile jiwe lililoipiga sanamu ile likawa mlima mkubwa, na kuijaza dunia yote.+

36 “Hii ndiyo ndoto ile, nasi tutaisema tafsiri yake mbele ya mfalme.+ 37 Wewe, Ee mfalme, uliye mfalme wa wafalme, wewe ambaye Mungu wa mbinguni amekupa ufalme,+ uwezo, na nguvu na heshima, 38 na amekupa mkononi mwako,+ popote pale ambapo wana wa binadamu hukaa, wanyama wa mwituni na viumbe vya mbinguni vyenye mabawa, na amekufanya kuwa mtawala juu ya vyote hivyo. Wewe ndiye kile kichwa cha dhahabu.+

39 “Na baada yako utasimama ufalme+ mwingine ulio mdogo kwako;+ na ufalme mwingine, wa tatu, wa shaba, ambao utaitawala dunia yote.+

40 “Ufalme wa nne+ nao utakuwa wenye nguvu kama chuma.+ Kwa vile chuma huponda na kusaga vitu vingine vyote, basi, kama chuma ambacho huvunja-vunja, huo utaziponda na kuzivunja-vunja hizi nyingine zote.+

41 “Na kama vile ulivyoona kuwa nyayo na vidole vya miguu vilikuwa sehemu moja ni udongo uliofinyangwa na nyingine ni chuma,+ ufalme huo utakuwa umegawanyika,+ lakini ugumu fulani wa chuma utakuwa ndani yake, kama vile ulivyoona chuma kimechanganyikana na udongo mbichi.+ 42 Na kuhusu vidole vya miguu ambavyo vilikuwa sehemu moja ni chuma na nyingine ni udongo uliofinyangwa, sehemu moja ya ufalme huo itakuwa yenye nguvu na nyingine itakuwa dhaifu. 43 Na kama ulivyoona chuma kimechanganyikana na udongo mbichi, watachanganyikana na uzao wa wanadamu; lakini hawatashikamana pamoja, huyu na yule, kama vile chuma kisivyochanganyikana na udongo uliofinyangwa.

44 “Na katika siku za wafalme hao,+ Mungu wa mbinguni+ atausimamisha ufalme+ ambao hautaharibiwa kamwe.+ Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote.+ Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote,+ nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo;+ 45 kama vile ulivyoona kwamba kutoka katika mlima jiwe lilikatwa bila kutumia mikono,+ na kwamba liliponda kile chuma, ile shaba, ule udongo uliofinyangwa, ile fedha na ile dhahabu.+ Mungu Mkuu+ mwenyewe amemjulisha mfalme mambo yatakayotokea baada ya haya.+ Na ndoto hiyo ni yenye kutegemeka, na tafsiri yake ni yenye kuaminika.”+

46 Wakati huo Mfalme Nebukadneza akaanguka kifudifudi, akampa Danieli heshima kubwa, na kusema apewe tuzo na kutolewa uvumba.+ 47 Mfalme akamwambia Danieli: “Kwa kweli Mungu wenu ni Mungu wa miungu+ na Bwana wa wafalme+ na Mfunuaji wa siri, kwa sababu uliweza kufunua siri hii.”+ 48 Basi mfalme akamfanya Danieli kuwa mtu mkuu,+ akampa zawadi nyingi kubwa, naye akamfanya kuwa mtawala juu ya wilaya yote ya utawala ya Babiloni na mkuu wa manaibu wa maliwali juu ya watu wote wenye hekima wa Babiloni.+ 49 Naye Danieli akatoa ombi kwa mfalme, naye akaweka Shadraki, Meshaki na Abednego+ juu ya usimamizi wa wilaya ya utawala ya Babiloni, lakini Danieli akawa katika makao ya mfalme.+

3 Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu+ ya dhahabu, ambayo urefu wake ulikuwa mikono 60 na upana wake mikono 6. Akaisimamisha katika nchi tambarare ya Dura katika wilaya ya utawala ya Babiloni.+ 2 Naye Mfalme Nebukadneza akatuma watu wawakusanye maliwali, manaibu wa maliwali+ na magavana, washauri, waweka-hazina, waamuzi, mahakimu watekeleza-sheria+ na wasimamizi wote wa wilaya za utawala waje kwenye mzinduo+ wa sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.

3 Ndipo maliwali,+ manaibu wa maliwali na magavana, washauri, waweka-hazina, waamuzi, mahakimu watekeleza-sheria na wasimamizi wa wilaya zote za utawala wakaanza kujikusanya kwa ajili ya kuzinduliwa kwa sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha, wakawa wanasimama mbele ya sanamu ambayo Nebukadneza alikuwa ameisimamisha. 4 Na mtangazaji+ akapaaza sauti: “Enyi vikundi vya watu, vya mataifa na lugha mnaamriwa+ 5 kwamba, wakati mtakaposikia sauti ya baragumu, zumari, zeze, kinubi chenye pembe tatu, kinanda, zumari-tete na aina zote za vyombo vya muziki,+ mwanguke chini na kuiabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza ameisimamisha. 6 Na yeyote ambaye hataanguka chini na kuabudu+ atatupwa wakati huohuo+ ndani ya tanuru inayowaka moto.”+ 7 Kwa hiyo, wakati ambapo vikundi vyote vya watu vilisikia sauti ya baragumu, zumari, zeze, kinubi chenye pembe tatu, kinanda na aina zote za vyombo vya muziki, vikundi vyote vya watu,+ vya mataifa na lugha vikaanguka chini na kuiabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.

8 Kwa hiyo, wakati huohuo Wakaldayo fulani wakakaribia na kuwashtaki Wayahudi.+ 9 Wakajibu na kumwambia Mfalme Nebukadneza: “Ee mfalme, uishi mpaka nyakati zisizo na kipimo.+ 10 Wewe mwenyewe, Ee mfalme, ulitoa amri kwamba kila mtu anayesikia sauti ya baragumu, zumari, zeze, kinubi chenye pembe tatu, kinanda, na zumari-tete na aina zote za vyombo vya muziki,+ aanguke chini na kuabudu ile sanamu ya dhahabu; 11 na kwamba yeyote ambaye haanguki chini na kuabudu atupwe ndani ya tanuru inayowaka moto.+ 12 Kuna Wayahudi fulani ambao uliweka juu ya usimamizi wa wilaya ya utawala ya Babiloni,+ Shadraki, Meshaki na Abednego; wanaume hao hawakukujali wewe, Ee mfalme, hawaitumikii miungu yako mwenyewe, wala sanamu ya dhahabu ambayo umeisimamisha hawaiabudu.”+

13 Ndipo Nebukadneza, akiwa na ghadhabu na hasira,+ akasema Shadraki, Meshaki na Abednego waletwe ndani.+ Basi wanaume hao wakaletwa mbele ya mfalme. 14 Nebukadneza akawauliza: “Je, ni kweli, enyi Shadraki, Meshaki na Abednego, kwamba ninyi hamwitumikii miungu yangu,+ wala sanamu ya dhahabu ambayo nimeisimamisha hamwiabudu?+ 15 Basi sasa ikiwa mko tayari ili mnaposikia sauti ya baragumu, zumari, zeze, kinubi chenye pembe tatu, kinanda, zumari-tete na aina zote za vyombo vya muziki,+ mwanguke chini na kuiabudu sanamu ambayo nimeitengeneza, ni vema. Lakini msipoabudu, mtatupwa wakati huohuo ndani ya tanuru inayowaka moto. Na ni mungu gani huyo anayeweza kuwaokoa ninyi kutoka mikononi mwangu?”+

16 Shadraki, Meshaki na Abednego wakajibu, nao wakamwambia mfalme: “Ee Nebukadneza, si lazima tukujibu neno lolote kuhusu jambo hili.+ 17 Kama ni hivyo, Mungu ambaye tunamtumikia anaweza kutuokoa. Yeye atatuokoa+ kutoka katika tanuru inayowaka moto na kutoka mkononi mwako, Ee mfalme. 18 Lakini kama sivyo, ujue hivi, Ee mfalme, kwamba sisi hatuitumikii miungu yako, na sanamu ambayo umeisimamisha hatutaiabudu.”+

19 Ndipo Nebukadneza akajaa ghadhabu, na sura ya uso wake ikabadilika juu ya Shadraki, Meshaki na Abednego. Akasema kwamba tanuru itiwe moto mara saba kuliko ilivyokuwa kawaida kuitia moto. 20 Naye akawaambia wanaume fulani wenye nguvu+ waliokuwa katika jeshi lake wawafunge Shadraki, Meshaki na Abednego, ili wawatupe ndani ya ile tanuru inayowaka moto.+

21 Ndipo wanaume hao wakafungwa wakiwa na nguo zao za kujitanda, mavazi yao na kofia zao na nguo zao nyingine, wakatupwa ndani ya ile tanuru inayowaka moto. 22 Na kwa kuwa neno la mfalme lilikuwa kali na tanuru ilitiwa moto kupita kiasi, hao wanaume ambao waliwachukua Shadraki, Meshaki na Abednego ndio waliouawa na mwali wa moto. 23 Lakini hao wanaume wengine watatu, Shadraki, Meshaki na Abednego, wakaanguka wakiwa wamefungwa katikati ya ile tanuru inayowaka moto.+

24 Ndipo Mfalme Nebukadneza akaogopa, akasimama haraka. Akawauliza maofisa wake wakuu wa kifalme: “Je, hatukutupa wanaume watatu ndani ya moto wakiwa wamefungwa?”+ Wakajibu na kumwambia mfalme: “Ndiyo, Ee mfalme.” 25 Akajibu na kusema: “Tazama! Mimi naona wanaume wanne wakitembea wakiwa huru katikati ya moto, nao hawana dhara lolote, na sura ya yule wa nne inafanana na mwana wa miungu.”+

26 Ndipo Nebukadneza akakaribia mlango wa tanuru inayowaka moto.+ Akajibu na kusema: “Shadraki, Meshaki na Abednego, enyi watumishi wa Mungu Aliye Juu Zaidi,+ tokeni nje, mje hapa!” Ndipo Shadraki, Meshaki na Abednego wakaanza kutoka katikati ya moto ule. 27 Na maliwali, manaibu wa maliwali, magavana na maofisa wakuu+ wa mfalme waliokuwa wamekusanyika wakawaona hao wanaume, kwamba ule moto haukuwa na nguvu juu ya miili yao,+ wala unywele wowote wa vichwa vyao haukuwa umeungua,+ wala hata nguo zao za kujitanda hazikuwa zimebadilishwa, wala harufu ya moto haikuwapata.

28 Nebukadneza akajibu na kusema: “Abarikiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego,+ aliyemtuma malaika wake+ na kuwaokoa watumishi wake waliomtegemea,+ na ambao walibadili neno la mfalme na kutoa miili yao, kwa maana hawakutumikia kamwe+ wala kuabudu+ mungu yeyote mwingine ila Mungu wao wenyewe.+ 29 Nami natoa agizo,+ kwamba kikundi chochote cha watu, cha taifa au lugha ambacho kinasema jambo lolote baya juu ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, kikatwe vipande-vipande,+ na nyumba zao zigeuzwe kuwa choo cha watu wote;+ kwa maana hakuna mungu mwingine yeyote anayeweza kuokoa kama huyu.”+

30 Ndipo mfalme akawafanya Shadraki, Meshaki na Abednego wafanikiwe katika wilaya ya utawala ya Babiloni.+

4 “Mfalme Nebukadneza, kwa vikundi vyote vya watu, vya mataifa na lugha ambavyo vinakaa katika dunia yote:+ Amani yenu na iwe nyingi.+ 2 Nimeona vema nitangaze ishara na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Zaidi amenifanyia.+ 3 Jinsi zilivyo kuu ishara zake, na jinsi maajabu yake yalivyo yenye nguvu!+ Ufalme wake ni ufalme wa mpaka wakati usio na kipimo,+ na utawala wake ni wa kizazi baada ya kizazi.+

4 “Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nikistarehe+ nyumbani mwangu, na kufanikiwa katika jumba langu la kifalme.+ 5 Kuna ndoto ambayo niliona, nayo ikaanza kuniogopesha.+ Na kulikuwa na picha za mawazo kitandani mwangu na maono ya kichwa changu yaliyoanza kuniogopesha.+ 6 Nami nikatoa agizo kwamba watu wote wenye hekima wa Babiloni waletwe mbele yangu, ili wanijulishe tafsiri ya ndoto hiyo.+

7 “Ndipo makuhani wenye kufanya uchawi, wafanya-mazingaombwe, Wakaldayo+ na wanajimu+ walikuwa wanaingia; nami nikasema mbele yao ndoto ile ilikuwa nini, bali tafsiri yake hawakuniambia.+ 8 Mwishowe Danieli akaingia mbele yangu, ambaye jina lake ni Belteshaza+ kulingana na jina la mungu wangu+ na ambaye ndani yake mna roho ya miungu mitakatifu;+ nami nikasema mbele yake ndoto ile:

9 “ ‘Ee Belteshaza mkuu wa makuhani wenye kufanya uchawi,+ kwa kuwa mimi mwenyewe najua vema kwamba roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako+ na kwamba hakuna siri yoyote ambayo inakusumbua,+ niambie maono ya ndoto yangu ambayo nimeona na tafsiri yake.+

10 “ ‘Basi katika maono ya kichwa changu kitandani mwangu nikawa ninaona,+ na, tazama! mti+ fulani katikati ya dunia, ambao ulikuwa mrefu sana.+ 11 Mti huo ulikua, ukawa na nguvu, mwishowe urefu wake ukafika mbinguni, nao ulikuwa unaonekana mpaka sehemu za mwisho za dunia nzima.+ 12 Majani yake yalikuwa mazuri, na matunda yake yalikuwa mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Chini yake wanyama+ wa mwituni walitafuta kivuli,+ na juu ya matawi yake ndege wa mbinguni walikuwa wakikaa,+ na kila kitu chenye mwili kilikuwa kikila chakula kutokana na mti huo.

13 “ ‘Niliendelea kutazama katika maono ya kichwa changu kitandani mwangu, na, tazama! mlinzi,+ aliye mtakatifu,+ akishuka kutoka mbinguni. 14 Alikuwa akiita kwa sauti kubwa, naye alikuwa akisema hivi: “Ukateni mti uanguke,+ na kuyakata matawi yake. Angusheni majani yake, na kutawanya matunda yake. Mnyama na akimbie kutoka chini yake, na ndege kutoka katika matawi yake.+ 15 Hata hivyo, kiacheni kisiki chake katika udongo, kikiwa na pingu ya chuma na ya shaba, katikati ya majani ya mwituni; na acheni kilowane maji ya umande wa mbinguni, fungu lake na liwe pamoja na mnyama katikati ya majani ya nchi.+ 16 Moyo wake na ubadilishwe usiwe wa mwanadamu, nao upewe moyo wa mnyama,+ na nyakati saba+ zipite juu yake. 17 Jambo hilo ni kulingana na agizo la walinzi,+ na ombi hilo ni kulingana na neno la watakatifu, kusudi watu wanaoishi wajue kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu+ na kwamba humpa yeyote yule amtakaye ufalme huo,+ na humweka juu yake mwanadamu aliye wa hali ya chini zaidi.”+

18 “ ‘Hiyo ndiyo ndoto ambayo mimi, Mfalme Nebukadneza, niliona; nawe, Ee Belteshaza, sema tafsiri yake, kwa maana watu wengine wote wenye hekima wa ufalme wangu wameshindwa kunijulisha tafsiri yake.+ Bali wewe una uwezo, kwa kuwa roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.’+

19 “Ndipo Danieli, ambaye jina lake ni Belteshaza,+ alishangaa kwa muda fulani, na mawazo yake yakaanza kumwogopesha.+

“Mfalme akasema, ‘Ee Belteshaza, usiache ndoto ile na tafsiri yake ikuogopeshe.’+

“Belteshaza akajibu na kusema, ‘Ee bwana wangu, ndoto hiyo na iwahusu wale wanaokuchukia, na tafsiri yake iwahusu adui zako.+

20 “ ‘Mti ulioona, ambao ulikua, ukawa mkubwa na kupata nguvu, na ambao urefu wake mwishowe ulifika mbinguni na ambao ulionekana duniani kote,+ 21 na majani yake yalikuwa mazuri, na ambao matunda yake yalikuwa mengi, na ambao juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote; ambao chini yake wanyama wa mwituni walikaa, na ambao juu ya matawi yake ndege wa mbinguni walikuwa wakikaa,+ 22 ni wewe, Ee mfalme,+ kwa sababu wewe umekuwa mkubwa ukapata nguvu, na ukuu wako umekuwa mkubwa na kufika mbinguni,+ na utawala wako umefika mpaka sehemu za mwisho za dunia.+

23 “ ‘Na kwa sababu mfalme aliona mlinzi, aliye mtakatifu,+ akishuka kutoka mbinguni, ambaye pia alikuwa akisema: “Ukateni mti uanguke, na kuuharibu. Hata hivyo, kiacheni kisiki chake katika udongo, lakini kikiwa na pingu ya chuma na ya shaba, katikati ya majani ya mwituni, na kilowane maji kwa umande wa mbinguni, fungu lake na liwe pamoja na wanyama wa mwituni mpaka nyakati saba zipite juu yake,”+ 24 hii ndiyo tafsiri, Ee mfalme, na amri+ ya Aliye Juu Zaidi+ ndiyo itakayompata bwana wangu mfalme.+ 25 Nawe watakufukuzia mbali kutoka kati ya wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa mwituni,+ nao watakupa majani ule kama ng’ombe,+ nawe utalowana maji kwa umande wa mbinguni, na nyakati saba+ zitapita juu yako, mpaka ujue ya kuwa Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu,+ na kwamba humpa yeyote yule amtakaye ufalme huo.+

26 “ ‘Na kwa kuwa walisema kisiki cha mti huo kiachwe,+ ufalme wako utakuwa hakika kwako baada ya wewe kujua kwamba mbingu zinatawala.+ 27 Kwa hiyo, Ee mfalme, shauri langu na likubalike kwako,+ nawe uziondoe dhambi zako kwa uadilifu,+ na uovu wako kwa kuwaonyesha maskini rehema.+ Labda mafanikio yako yatarefushwa.’ ”+

28 Hayo yote yalimpata Mfalme Nebukadneza.+

29 Mwishoni mwa miezi kumi na miwili, alikuwa akitembea juu ya jumba la mfalme la Babiloni. 30 Mfalme alikuwa anasema:+ “Je, hili si Babiloni Mkubwa, ambalo mimi mwenyewe nimelijenga kwa ajili ya nyumba ya kifalme kwa nguvu za uwezo wangu+ na kwa ajili ya heshima ya utukufu wa enzi yangu?”+

31 Neno lile lilipokuwa bado kinywani mwa mfalme, sauti ikashuka kutoka mbinguni: “Wewe unaambiwa, Ee Mfalme Nebukadneza, ‘Ufalme umeondoka kwako.+ 32 Nao wanakufukuzia mbali kutoka kati ya wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa mwituni.+ Watakupa majani ule kama ng’ombe, na nyakati saba zitapita juu yako, mpaka ujue kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu, na kwamba humpa yeyote yule amtakaye ufalme huo.’ ”+

33 Wakati huohuo+ neno lile likatimia juu ya Nebukadneza, naye akafukuziwa mbali kutoka kati ya wanadamu, akaanza kula majani kama ng’ombe. Mwili wake ukalowana maji kwa umande wa mbinguni, mpaka nywele zake zikawa ndefu kama manyoya ya tai na kucha zake kama kucha za ndege.+

34 “Na mwishoni mwa siku zile,+ mimi, Nebukadneza, niliinua macho yangu juu kuelekea mbinguni,+ ndipo uelewaji wangu ukaanza kurudi kwangu; nami nikambariki Aliye Juu Zaidi,+ nami nikamsifu na kumtukuza Yeye anayeishi mpaka wakati usio na kipimo,+ kwa maana utawala wake ni utawala wa mpaka wakati usio na kipimo na ufalme wake ni wa kizazi baada ya kizazi.+ 35 Na wakaaji wote wa dunia wanaonwa kuwa si kitu,+ naye anafanya kulingana na mapenzi yake kati ya majeshi ya mbinguni na wakaaji wa dunia.+ Wala hakuna yeyote anayeweza kuzuia mkono wake+ au anayeweza kumuuliza, ‘Umekuwa ukifanya nini?’+

36 “Ndipo wakati huohuo uelewaji wangu ukaanza kurudi kwangu, nayo heshima ya ufalme wangu, utukufu wangu wa enzi na fahari zikaanza kurudi kwangu;+ nao maofisa wangu wakuu wa kifalme na wakuu wangu wakaanza kunitafuta kwa hamu, nami nikarudishwa tena juu ya ufalme wangu mwenyewe, nikaongezewa ukuu usio wa kawaida.+

37 “Basi mimi, Nebukadneza, namsifu na kumkweza na kumtukuza Mfalme wa mbinguni,+ kwa sababu kazi zake zote ni kweli na njia zake ni haki,+ na kwa sababu wale wanaotembea kwa kiburi yeye anaweza kuwafedhehesha.”+

5 Mfalme Belshaza+ naye alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake elfu, naye akanywa divai mbele ya hao elfu.+ 2 Akiwa amechochewa na divai,+ Belshaza akasema viletwe vyombo vya dhahabu na fedha+ ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka hekalu lililokuwa Yerusalemu, ili mfalme na wakuu wake, masuria wake na wake zake wadogo wavinywee.+ 3 Basi wakavileta ndani vile vyombo vya dhahabu ambavyo walikuwa wamevitoa katika hekalu la Mungu lililokuwa Yerusalemu, naye mfalme na wakuu wake, masuria wake na wake zake wadogo wakavinywea. 4 Wakanywa divai, wakaisifu miungu ya dhahabu na fedha, shaba, chuma, miti na mawe.+

5 Ndipo wakati huohuo vidole vya mkono wa mtu vikatokea na kuandika mbele ya kinara cha taa juu ya lipu ya ukuta wa jumba la mfalme,+ naye mfalme akawa anaona sehemu ya nyuma ya mkono uliokuwa ukiandika. 6 Na wakati huo, kwa habari ya mfalme, sura yake ikabadilika, mawazo yake yakaanza kumwogopesha,+ viungo vya viuno vyake vikalegea,+ magoti yake yakawa yanagongana.+

7 Mfalme akaita kwa sauti kubwa akasema waletwe ndani wafanya-mazingaombwe, Wakaldayo na wanajimu.+ Mfalme akawaambia watu wenye hekima wa Babiloni: “Mtu yeyote atakayesoma maandishi haya na kunionyesha tafsiri yake kamili, atavikwa mavazi ya zambarau,+ pamoja na mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atakuwa mtawala wa tatu katika ufalme.”+

8 Basi wakaingia watu wote wenye hekima wa mfalme, lakini hawakuwa na uwezo wa kutosha kuweza kusoma maandishi hayo wala kumwambia mfalme tafsiri yake.+ 9 Kwa hiyo Mfalme Belshaza akaogopa sana na rangi ya uso wake ikaanza kubadilika ndani yake; na wakuu wake wakahangaika.+

10 Malkia naye, kwa sababu ya maneno ya mfalme na wakuu wake, akaingia ndani ya jumba la karamu. Malkia akasema: “Ee mfalme, uishi mpaka wakati usio na kipimo.+ Usiache mawazo yako yakuogopeshe, wala rangi ya uso wako ibadilike. 11 Kuna mtu mwenye uwezo katika ufalme wako ambaye ndani yake mna roho ya miungu mitakatifu;+ na katika siku za baba yako nuru na ufahamu na hekima kama hekima ya miungu zilipatikana ndani yake, na baba yako mwenyewe, Mfalme Nebukadneza, akamweka awe mkuu+ wa makuhani wenye kufanya uchawi, na wafanya-mazingaombwe, na Wakaldayo na wanajimu, Ee mfalme; 12 kwa kuwa roho isiyo ya kawaida na ujuzi na ufahamu wa kutafsiri ndoto+ na kueleza vitendawili na kufungua mafundo ilikuwa imepatikana ndani yake,+ ndani ya Danieli, ambaye mfalme alimpa jina Belteshaza.+ Basi Danieli na aitwe, apate kuonyesha tafsiri kamili.”

13 Basi Danieli akaletwa mbele ya mfalme. Mfalme akasema na kumuuliza Danieli: “Je, wewe ndiye Danieli ambaye ni mmoja wa wahamishwa wa Yuda,+ ambao baba yangu mfalme aliwatoa Yuda?+ 14 Nimesikia pia kuhusu wewe kwamba roho ya miungu imo ndani yako,+ na nuru na ufahamu na hekima+ isiyo ya kawaida zimepatikana ndani yako. 15 Basi watu wenye hekima na wafanya-mazingaombwe wameletwa mbele yangu, ili wasome maandishi haya, waniambie tafsiri yake; lakini hawana uwezo wa kutosha kunionyesha tafsiri kamili ya neno hilo.+ 16 Nami mwenyewe nimesikia habari zako, kwamba unaweza kutoa tafsiri+ na kufungua mafundo. Basi, ukiweza kusoma maandishi haya na kunijulisha tafsiri yake kamili, utavikwa mavazi ya zambarau, pamoja na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utakuwa mtawala wa tatu katika ufalme.”+

17 Ndipo Danieli akajibu na kusema mbele ya mfalme: “Zawadi zako na ziwe zako mwenyewe, na tuzo zako uwape wengine.+ Hata hivyo, mimi nitamsomea mfalme maandishi haya, nami nitamjulisha tafsiri yake.+ 18 Basi wewe, Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Zaidi+ alimpa baba yako Nebukadneza+ ufalme na ukuu na heshima na utukufu wa enzi.+ 19 Na kwa sababu ya ukuu ambao Yeye alimpa, vikundi vyote vya watu, vya mataifa na lugha vilitetemeka na kuogopa mbele yake.+ Mtu yeyote aliyetaka kumuua, alimuua; mtu yeyote aliyetaka kumpiga, alimpiga; na mtu yeyote aliyetaka kumwinua, alimwinua; na mtu yeyote aliyetaka kumfedhehesha, alimfedhehesha.+ 20 Lakini moyo wake ulipojivuna na roho yake ikawa ngumu, akatenda kwa kimbelembele,+ alishushwa kutoka katika kiti cha ufalme wake, akaondolewa heshima yake.+ 21 Naye akafukuziwa mbali kutoka kati ya wanadamu, na moyo wake ukafanywa kama ule wa mnyama, naye akakaa pamoja na punda-mwitu.+ Wakawa wanampa majani ale kama ng’ombe, mwili wake ukalowa maji kwa umande wa mbingu,+ mpaka alipojua kwamba Mungu Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu, na kwamba humweka juu yake yeyote yule anayemtaka.+

22 “Na wewe, Belshaza mwana wake,+ hukunyenyekeza moyo wako,+ ijapokuwa ulijua hayo yote.+ 23 Bali ulijiinua juu ya Bwana wa mbingu,+ nao wakaleta mbele yako vyombo vya nyumba yake;+ na wewe pamoja na wakuu wako, masuria wako na wake zako wadogo mmekuwa mkivinywea divai. Nawe umeisifu miungu minyonge ya fedha na ya dhahabu, shaba, chuma, miti na mawe,+ ambayo haioni chochote, wala kusikia chochote, wala kujua chochote;+ lakini hukumtukuza+ Mungu ambaye pumzi yako imo mkononi mwake+ na ambaye njia zako zote ni zake.+ 24 Basi sehemu ya nyuma ya mkono ilitumwa kutoka mbele zake, na maandishi haya yakaandikwa.+ 25 Na haya ndiyo maandishi ambayo yaliandikwa: MENE, MENE, TEKELI na PARSINI.

26 “Hii ndiyo tafsiri ya neno: MENE, Mungu amehesabu siku za ufalme wako naye ameukomesha.+

27 “TEKELI, wewe umepimwa katika mizani, ukaonekana kuwa umepungukiwa.+

28 “PERESI, ufalme wako umegawanywa na kupewa Wamedi na Waajemi.”+

29 Ndipo Belshaza akatoa amri, nao wakamvika Danieli mavazi ya zambarau, pamoja na mkufu wa dhahabu shingoni mwake; nao wakatangaza kumhusu yeye kwamba atakuwa mtawala wa tatu katika ufalme.+

30 Usiku huohuo Belshaza mfalme Mkaldayo akauawa,+ 31 naye Dario+ Mmedi akaupokea ufalme, akiwa na umri wa kama miaka 62.

6 Ilionekana vema kwa Dario, naye akaweka maliwali 120 juu ya ufalme, ili wawe juu ya ufalme wote;+ 2 na juu yao maofisa wakuu watatu, ambao Danieli alikuwa mmoja wao,+ ili maliwali+ hao wawe wakiwapa habari sikuzote ili mfalme asipate hasara.+ 3 Basi ikawa kwamba Danieli huyo akajipatia sifa+ juu ya wale maofisa wakuu na maliwali, kwa maana roho isiyo ya kawaida ilikuwa ndani yake;+ naye mfalme alikuwa anakusudia kumwinua juu ya ufalme wote.

4 Ndipo maofisa wakuu na maliwali walikuwa wanatafuta daima kisingizio fulani juu ya Danieli kuhusiana na ufalme huo;+ lakini hawakuweza kupata kisingizio chochote wala jambo lolote lenye ufisadi, kwa vile alikuwa mwenye kutegemeka wala haukupatikana ndani yake uzembe wowote wala jambo lolote lenye ufisadi.+ 5 Basi wanaume hao wakasema: “Hatutapata kisingizio chochote juu ya Danieli huyu, isipokuwa tukitafute juu yake katika sheria ya Mungu wake.”+

6 Basi hao maofisa wakuu na maliwali wakaingia kwa mfalme pamoja,+ nao wakamwambia jambo hili: “Ee Mfalme Dario, uishi mpaka wakati usio na kipimo.+ 7 Maofisa wote wakuu wa ufalme, manaibu wa maliwali na maliwali, maofisa wakuu wa kifalme na magavana, wamefanya shauri pamoja ili kuweka sheria ya kifalme+ na kupiga marufuku, kwamba mtu yeyote atakayetoa ombi kwa mungu yeyote au mwanadamu kwa siku 30 isipokuwa kwako, Ee mfalme, atupwe ndani ya shimo la simba.+ 8 Na sasa, Ee mfalme, isimamishe imara sheria hiyo na kutia sahihi maandishi hayo,+ ili yasibadilishwe, kulingana na sheria ya Wamedi na Waajemi,+ ambayo haifutwi.”+

9 Kulingana na hayo, Mfalme Dario akatia sahihi maandishi hayo na ile amri ya marufuku.+

10 Lakini mara Danieli alipojua kwamba maandishi hayo yametiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, kisha, huku madirisha yaliyo katika chumba chake cha dari yakiwa yamefunguliwa kwa ajili yake kuelekea Yerusalemu,+ alikuwa akipiga magoti na kusali+ mara tatu kwa siku+ na kutoa sifa mbele za Mungu wake,+ kama vile alivyokuwa akifanya kwa ukawaida kabla ya hayo.+ 11 Ndipo hao wanaume wakajazana ndani na kumkuta Danieli akiomba kibali mbele za Mungu wake.+

12 Kisha wakakaribia na kusema mbele ya mfalme kuhusu ile amri ya marufuku ya mfalme: “Je, hakuna amri ya marufuku ambayo wewe umetia sahihi inayosema kwamba mtu yeyote anayetoa ombi kwa mungu yeyote au mwanadamu kwa siku 30 isipokuwa kwako, Ee mfalme, atupwe ndani ya shimo la simba?”+ Mfalme akajibu na kusema: “Jambo hilo limesimamishwa imara kulingana na sheria ya Wamedi na Waajemi, ambayo haifutwi.”+ 13 Papo hapo wakajibu, nao wakasema mbele ya mfalme: “Danieli,+ ambaye ni mmoja wa wahamishwa wa Yuda,+ hakukujali wewe, Ee mfalme, wala hakujali ile amri ya marufuku uliyotia sahihi, bali yeye anatoa maombi yake mara tatu kwa siku.”+ 14 Basi mara tu mfalme aliposikia lile neno, likamchukiza sana,+ naye akaelekeza akili zake kwa Danieli ili amwokoe;+ naye akazidi kujitahidi kumkomboa mpaka jua lilipotua. 15 Mwishowe wanaume hao wakaingia pamoja kwa mfalme, nao wakamwambia mfalme: “Ujue, Ee mfalme, ya kuwa sheria ya Wamedi na Waajemi ni kwamba amri ya marufuku+ au sheria yoyote ambayo mfalme mwenyewe huisimamisha imara haipasi kubadilishwa.”+

16 Ndipo mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli na kumtupa ndani ya shimo la simba.+ Mfalme akamwambia Danieli: “Mungu wako, ambaye unamtumikia daima, yeye mwenyewe atakuokoa.”+ 17 Na jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye kinywa cha shimo lile, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake ya muhuri na kwa pete ya muhuri ya wakuu wake, ili kwamba jambo lolote lisibadilishwe kumhusu Danieli.+

18 Ndipo mfalme akaenda katika jumba lake, akafunga usiku kucha,+ wala hakuna vyombo vyovyote vya muziki vilivyoletwa mbele yake, na usingizi wake ukamtoka.+ 19 Mwishowe mfalme akaondoka wakati wa mapambazuko, katika nuru ya asubuhi, akafanya haraka kwenda moja kwa moja kwenye lile shimo la simba. 20 Alipolikaribia lile shimo, akampaazia Danieli sauti kwa huzuni. Mfalme akasema kwa sauti na kumwambia Danieli: “Ee Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai, je, Mungu wako unayemtumikia daima+ amekuokoa kutoka kwa hao simba?”+ 21 Mara moja Danieli akasema na mfalme: “Ee mfalme, uishi mpaka wakati usio na kipimo. 22 Mungu wangu mwenyewe+ alimtuma malaika+ wake na kufunga vinywa vya simba,+ nao hawakuniangamiza, kwa kuwa nimeonekana kuwa mtu asiye na hatia mbele zake;+ na pia mbele yako, Ee mfalme, mimi sijafanya tendo lolote lenye kudhuru.”+

23 Ndipo mfalme akafurahi sana,+ akaamuru Danieli atolewe ndani ya lile shimo. Na Danieli akatolewa ndani ya lile shimo, wala hakupatwa na dhara lolote, kwa sababu alikuwa amemtegemea Mungu wake.+

24 Na mfalme akatoa amri, nao wakawaleta hao wanaume waliomshtaki Danieli,+ wakawatupa ndani ya lile shimo la simba,+ wana wao na wake zao;+ nao simba wakawashinda nguvu watu hao hata kabla ya kufika chini ya shimo hilo, nao wakaivunja mifupa yao yote.+

25 Ndipo Mfalme Dario mwenyewe akaandikia vikundi vyote vya watu, vya mataifa na lugha vinavyokaa katika dunia yote:+ “Amani yenu na iwe nyingi sana!+ 26 Agizo+ limetoka kwangu kwamba, katika kila mamlaka ya ufalme wangu, watu wawe wakitetemeka na kuogopa mbele za Mungu wa Danieli.+ Kwa maana yeye ni Mungu aliye hai na Yeye anaishi mpaka wakati usio na kipimo,+ na ufalme wake+ ni ufalme ambao hautaharibiwa kamwe,+ na mamlaka yake ni ya milele.+ 27 Anaokoa na kukomboa+ na kufanya ishara na maajabu mbinguni+ na duniani,+ kwa maana amemwokoa Danieli kutoka katika makucha ya simba.”

28 Basi Danieli huyo akafanikiwa katika ufalme wa Dario+ na katika ufalme wa Koreshi Mwajemi.+

7 Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza+ mfalme wa Babiloni, Danieli aliona ndoto na maono ya kichwa chake kitandani mwake.+ Ndipo akaandika ndoto hiyo.+ Akasimulia masimulizi kamili ya mambo hayo. 2 Danieli akasema:

“Niliona katika maono yangu usiku, na, tazama! pepo nne+ za mbingu zilikuwa zikiichafua bahari kubwa.+ 3 Na wanyama wakubwa mno wanne+ walikuwa wakitoka baharini,+ kila mmoja akiwa tofauti+ na wale wengine.

4 “Wa kwanza alikuwa kama simba,+ naye alikuwa na mabawa ya tai.+ Nami nikaendelea kutazama mpaka mabawa yake yakang’olewa, naye akainuliwa juu ya dunia+ na kusimamishwa kwa miguu miwili kama mwanadamu, naye akapewa moyo wa mwanadamu.+

5 “Na, tazama! mnyama mwingine, wa pili, aliye kama dubu.+ Naye alikuwa ameinuliwa upande mmoja,+ na kulikuwa na mifupa mitatu ya mbavu kinywani mwake kati ya meno yake; nao walikuwa wakimwambia hivi, ‘Simama, ule nyama nyingi.’+

6 “Kisha nikaendelea kuona, na, tazama! mnyama mwingine, aliye kama chui,+ lakini mgongoni mwake alikuwa na mabawa manne ya kiumbe kinachoruka. Na mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne,+ naye akapewa utawala kwelikweli.

7 “Baada ya hayo nikaendelea kuona katika maono ya usiku, na, tazama! mnyama wa nne, mwenye kuogopesha na mwenye kutisha na mwenye nguvu isivyo kawaida.+ Naye alikuwa na meno ya chuma, yaliyo makubwa. Alikuwa akirarua na kuvunja, na mabaki aliyakanyaga kwa miguu yake. Naye alikuwa tofauti na wale wanyama wengine wote waliokuwa kabla yake, naye alikuwa na pembe kumi.+ 8 Nikaendelea kuziangalia sana zile pembe, na, tazama! pembe nyingine, iliyo ndogo,+ ikatokea katikati ya hizo, na pembe tatu kati ya zile za kwanza zikang’olewa mbele yake. Na, tazama! kulikuwa na macho kama macho ya mwanadamu katika pembe hiyo, na kulikuwa na kinywa kinachosema mambo makuu.+

9 “Nikaendelea kutazama mpaka viti vya ufalme vikawekwa+ na Mzee wa Siku+ akaketi. Mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji,+ na nywele za kichwa chake zilikuwa kama sufu safi.+ Kiti chake cha ufalme kilikuwa ni miali ya moto;+ magurudumu yake yalikuwa ni moto unaowaka.+ 10 Kulikuwa na mto wa moto unaotiririka kutoka mbele zake.+ Kulikuwa na maelfu elfu walioendelea kumtumikia,+ na elfu kumi mara elfu kumi walioendelea kusimama mbele zake.+ Ile Mahakama+ ikaketi, na vitabu vikafunguliwa.

11 “Nikaendelea kutazama wakati huo kwa sababu ya sauti ya maneno makuu ambayo ile pembe ilikuwa ikisema;+ nikaendelea kutazama mpaka mnyama huyo akauawa na mwili wake ukaharibiwa naye akatupwa katika moto unaowaka.+ 12 Lakini wale wanyama wengine,+ walinyang’anywa utawala wao, na maisha yao yakarefushwa kwa wakati mmoja na majira.+

13 “Nikaendelea kuona katika maono ya usiku, na, tazama! mtu fulani kama mwana wa binadamu+ alikuwa anakuja na mawingu+ ya mbingu; naye akaja kwa Mzee wa Siku,+ nao wakamleta karibu mbele zake Yule.+ 14 Naye akapewa utawala+ na heshima+ na ufalme,+ ili vikundi vyote vya watu, vya mataifa na lugha vimtumikie yeye.+ Utawala wake ni utawala unaodumu mpaka wakati usio na kipimo ambao hautapitilia mbali, na ufalme wake ni ufalme ambao hautaharibiwa.+

15 “Basi, mimi Danieli, roho yangu ilihuzunika ndani yangu kwa sababu ya hayo, na yale maono ya kichwa changu yakaanza kuniogopesha.+ 16 Nikasonga karibu na mmoja wa wale waliokuwa wamesimama, ili nimwombe habari yenye kuaminika kuhusu mambo hayo yote.+ Naye akaniambia hivi, huku akiendelea kunijulisha tafsiri ya mambo hayo,

17 “ ‘Kuhusu hawa wanyama wakubwa mno, kwa kuwa ni wanne,+ kuna wafalme wanne ambao watasimama kutoka katika dunia.+ 18 Lakini watakatifu+ wa Aliye Mkuu Zaidi+ wataupokea ufalme, nao watamiliki ufalme+ huo mpaka wakati usio na kipimo, milele na milele.’

19 “Ndipo nikatamani kuhakikisha kuhusu yule mnyama wa nne, ambaye alikuwa tofauti na wale wengine wote, mwenye kuogopesha isivyo kawaida, mwenye meno ya chuma na makucha ya shaba, aliyekuwa akirarua na kuvunja, na ambaye alikuwa akikanyaga mabaki kwa miguu yake;+ 20 na kuhusu zile pembe kumi zilizokuwa kichwani mwake,+ na ile pembe nyingine+ iliyotokea na ambayo mbele yake tatu zilianguka,+ naam, ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa kinachosema mambo makuu+ na ambayo umbo lake lilikuwa kubwa kuliko zile pembe nyingine.

21 “Nikaendelea kutazama wakati pembe hiyo ilipofanya vita juu ya watakatifu, nayo ikawa inawashinda,+ 22 mpaka Mzee wa Siku+ alipokuja na hukumu ikatolewa kwa faida ya watakatifu wa Aliye Mkuu Zaidi,+ na wakati hususa ukafika ambapo watakatifu waliumiliki ufalme.+

23 “Haya ndiyo aliyosema, ‘Kuhusu yule mnyama wa nne, kuna ufalme wa nne ambao utakuja kuwa duniani, ambao utakuwa tofauti na zile falme nyingine zote; nao utararua dunia yote na kuikanyagia chini na kuivunja.+ 24 Na kuhusu zile pembe kumi, kuna wafalme kumi watakaosimama kutoka katika ufalme huo;+ na bado mwingine atasimama baada yao, naye atakuwa tofauti na wale wa kwanza,+ naye atawafedhehesha wafalme watatu.+ 25 Naye atasema maneno mabaya kumhusu yule Aliye Juu Zaidi,+ naye atawasumbua bila kikomo watakatifu wa Aliye Mkuu Zaidi.+ Na yeye atakusudia kubadili nyakati+ na sheria,+ na wao watatiwa mkononi mwake kwa wakati mmoja, na nyakati na nusu ya wakati.+ 26 Nayo ile Mahakama ikaketi,+ na mwishowe wakauondolea mbali utawala wake, ili wamwangamize na kumharibu kabisa.+

27 “ ‘Na ufalme na utawala na ukuu wa falme zote chini ya mbingu zote wakapewa watu ambao ni watakatifu wa Aliye Mkuu Zaidi.+ Ufalme wao ni ufalme unaodumu mpaka wakati usio na kipimo,+ na tawala zote zitawatumikia na kuwatii wao.’+

28 “Huu ndio mwisho wa jambo hilo. Nami, Danieli, mawazo yangu yalizidi kuniogopesha sana, hata rangi ya uso wangu ikabadilika; hata hivyo jambo hilo nikaliweka moyoni mwangu.”+

8 Katika mwaka wa tatu wa ufalme wa Mfalme Belshaza,+ kuna ndoto niliyoona, mimi, Danieli, baada ya ile iliyonitokea pale mwanzoni.+ 2 Nami nikaanza kuona katika maono hayo; ikawa kwamba, nilipokuwa nikiona, nilikuwa katika ngome ya Shushani,+ iliyo katika wilaya ya utawala ya Elamu;+ nami nikaona katika maono hayo, nami nilikuwa kando ya mfereji wa Ulai.+ 3 Nilipoinua macho yangu, ndipo nikaona, na, tazama! kondoo-dume+ amesimama mbele ya huo mfereji, naye alikuwa na pembe mbili. Na hizo pembe mbili zilikuwa ndefu, lakini moja ilikuwa ndefu kuliko ile nyingine, na ile ndefu ndiyo iliyotokea baadaye.+ 4 Nikamwona huyo kondoo-dume akisukuma kuelekea upande wa magharibi na wa kaskazini na wa kusini, wala hakuna wanyama-mwitu wowote walioendelea kusimama mbele yake, wala hakuna yeyote aliyekomboa kutoka mkononi mwake.+ Naye akafanya kulingana na mapenzi yake, akajivuna sana.

5 Mimi nami nikaendelea kumwangalia sana, na, tazama! kulikuwa na mbuzi-dume+ akija kutoka upande wa magharibi akiwa juu ya uso wa dunia yote, naye hakuwa akigusa nchi. Huyo mbuzi-dume alikuwa na pembe yenye kuonekana wazi kati ya macho yake.+ 6 Akaja mpaka akamfikia yule kondoo-dume mwenye zile pembe mbili, ambaye nilikuwa nimemwona amesimama mbele ya ule mfereji; akaja akikimbia kumwelekea akiwa na ghadhabu yake yenye nguvu.

7 Nami nikamwona akimkaribia yule kondoo-dume, naye akaanza kuonyesha uchungu kumwelekea, akampiga na kumwangusha yule kondoo-dume, akazivunja zile pembe zake mbili, na huyo kondoo-dume hakuwa na nguvu za kusimama mbele yake. Basi akamwangusha katika nchi na kumkanyagia chini, na huyo kondoo-dume hakuwa na wa kumkomboa kutoka mkononi mwake.+

8 Ndipo yule mbuzi-dume akajivuna mno;+ lakini mara alipokuwa na nguvu, ile pembe kubwa ikavunjwa, na badala yake kukatokea pembe nne zenye kuonekana wazi, kuelekea zile pepo nne za mbingu.+

9 Na katika moja ya hizo ikatoka pembe nyingine ndogo,+ nayo ikaendelea kuwa kubwa zaidi kuelekea upande wa kusini na kuelekea mashariki na kuelekea lile Pambo.+ 10 Nayo ikaendelea kuwa kubwa ikalifikia jeshi la mbinguni,+ hivi kwamba ikaangusha mpaka duniani sehemu ya jeshi hilo na sehemu ya nyota,+ nayo ikazikanyaga.+ 11 Nayo ikajivuna sana hata kwa Mkuu+ wa jeshi, na dhabihu ya daima+ ikaondolewa mbali kutoka kwake, na mahali palipofanywa imara pa patakatifu pake pakatupwa chini.+ 12 Na jeshi likatolewa mwishowe,+ pamoja na ile dhabihu ya daima,+ kwa sababu ya makosa;+ nayo ikaendelea kutupa kweli+ chini,+ ikatenda na kupata mafanikio.+

13 Nami nikamsikia mtakatifu+ fulani akisema, na mtakatifu mwingine akamwambia yule mtakatifu aliyekuwa akisema: “Je, maono ya dhabihu ya daima+ na ya makosa yanayosababisha ukiwa+ yatakuwa kwa muda mrefu kadiri gani, ili kufanya mahali patakatifu na pia jeshi viwe vitu vya kukanyagwa-kanyagwa?”+ 14 Kwa hiyo akaniambia: “Hata jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; na mahali patakatifu pataletwa katika hali yake inayofaa.”+

15 Ndipo ikawa kwamba, mimi Danieli, nilipokuwa nikiona maono hayo na kutafuta uelewaji,+ tazama! mbele yangu alikuwa amesimama mtu fulani mwenye sura kama ya mwanamume.+ 16 Nikaanza kusikia sauti ya mtu wa udongo katikati ya mfereji wa Ulai,+ naye akaita na kusema: “Gabrieli,+ mweleweshe yule pale jambo hilo lililoonwa.”+ 17 Kwa hiyo akaja kando ya mahali nilipokuwa nimesimama, lakini alipokuja niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Naye akaniambia: “Elewa,+ Ee mwana wa binadamu,+ kwamba maono hayo ni ya wakati wa mwisho.”+ 18 Naye alipokuwa akisema nami, nikawa nimelala usingizi mzito kifudifudi.+ Basi akanigusa na kunisimamisha mahali nilipokuwa nimesimama.+ 19 Naye akasema: “Tazama, nakujulisha mambo yatakayotokea wakati wa mwisho wa shutuma, kwa sababu ni kwa wakati uliowekwa wa mwisho.+

20 “Yule kondoo-dume uliyemwona mwenye pembe mbili anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi.+ 21 Na yule mbuzi-dume mwenye manyoya anawakilisha mfalme wa Ugiriki;+ na ile pembe kubwa iliyokuwa kati ya macho yake, inawakilisha mfalme wa kwanza.+ 22 Na baada ya hiyo kuvunjwa, hivi kwamba kukawa na nne zilizosimama badala yake,+ kuna falme nne zitakazosimama kutoka katika taifa lake, lakini si kwa nguvu zake.

23 “Na wakati wa mwisho wa ufalme wao, wakosaji watendapo kufikia kikomo, atasimama mfalme mwenye sura kali ambaye anaelewa maneno magumu.+ 24 Na nguvu zake zitakuwa nyingi sana, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe.+ Naye atasababisha uharibifu kwa njia ya ajabu,+ naye atafanikiwa na kutenda kwa njia yenye matokeo. Naye atawaharibu wenye nguvu, pamoja na watu watakatifu.+ 25 Na kulingana na ufahamu wake atafanya udanganyifu ufanikiwe mkononi mwake.+ Na atajivuna sana moyoni mwake,+ naye atawaharibu wengi wakati ambapo hakuna mahangaiko.+ Na atasimama kumpinga Mkuu wa wakuu,+ lakini atavunjwa pasipo kutumia mkono.+

26 “Na lile jambo lililoonwa kuhusu jioni na asubuhi, ambalo limesemwa, ni kweli.+ Lakini wewe yaweke siri maono hayo, kwa maana bado ni ya siku nyingi.”+

27 Na mimi, Danieli, nikachoka kabisa, nikawa mgonjwa kwa muda wa siku fulani.+ Kisha nikaamka na kufanya kazi ya mfalme;+ lakini nikaendelea kuonekana nimekufa ganzi kwa sababu ya lile jambo lililoonwa, wala hakuna mtu aliyelielewa.+

9 Katika mwaka wa kwanza wa Dario mwana wa Ahasuero+ wa uzao wa Wamedi,+ aliyekuwa amefanywa kuwa mfalme juu ya ufalme wa Wakaldayo;+ 2 katika mwaka wa kwanza wa utawala wake mimi, Danieli, nilitambua kwa vitabu hesabu ya miaka ambayo kuhusu hiyo neno la Yehova lilimjia nabii Yeremia,+ ya kutimiza ukiwa wa Yerusalemu,+ yaani, miaka 70.+ 3 Nami nikaelekeza uso wangu+ kwa Yehova Mungu wa kweli, ili kumtafuta kwa sala+ na maombi, pamoja na kufunga na nguo za magunia na majivu.+ 4 Nikaanza kusali kwa Yehova Mungu wangu, na kuungama na kusema:+

“Ah, Yehova Mungu wa kweli, aliye Mkuu+ na Mwenye kuogopesha, anayeshika agano+ na fadhili zenye upendo+ kwa wale wanaompenda na kwa wale wanaoshika amri zake,+ 5 tumetenda dhambi,+ tumekosa, tumetenda kwa uovu na kuasi;+ nasi tumegeuka kando kutoka katika amri zako na kutoka katika maamuzi yako ya hukumu.+ 6 Nasi hatukuwasikiliza watumishi wako manabii,+ ambao kwa jina lako wamesema na wafalme wetu, wakuu wetu na mababu zetu na watu wote wa nchi.+ 7 Kwako wewe, Ee Yehova, kuna uadilifu, lakini kwetu sisi kuna aibu ya uso kama ilivyo leo hii,+ kwa watu wa Yuda na kwa wakaaji wa Yerusalemu na kwa watu wote wa Israeli, wale walio karibu na wale walio mbali katika nchi zote ambako uliwatawanya kwa sababu ya ukosefu wao wa uaminifu waliokutendea.+

8 “Ee Yehova, kwetu sisi kuna aibu ya uso, kwa wafalme wetu, kwa wakuu wetu na kwa mababu zetu, kwa maana tumekutendea dhambi.+ 9 Kwake Yehova Mungu wetu, kuna rehema+ na msamaha,+ kwa maana tumemwasi.+ 10 Nasi hatukutii sauti ya Yehova Mungu wetu, kwa kutembea katika sheria zake ambazo aliweka mbele yetu kwa mkono wa watumishi wake manabii.+ 11 Na watu wote wa Israeli wamevunja sheria yako, wamegeuka kando kwa kutotii sauti yako,+ hata ukatumwagia laana na kiapo rasmi+ ambacho kimeandikwa katika sheria ya Musa mtumishi wa Mungu wa kweli, kwa maana tumemtendea Yeye dhambi. 12 Naye akayatimiza maneno yake ambayo alikuwa amesema juu yetu+ na juu ya waamuzi wetu waliotuhukumu,+ kwa kuleta juu yetu msiba mkubwa, kwa maana yaliyofanywa Yerusalemu hayajapata kufanywa chini ya mbingu zote.+ 13 Kama vile ilivyoandikwa katika sheria ya Musa,+ msiba huu wote—umekuja juu yetu,+ nasi hatukuutuliza uso wa Yehova Mungu wetu kwa kuacha makosa yetu+ na kwa kuonyesha ufahamu katika ukweli wako.+

14 “Naye Yehova akakaa macho kuelekea msiba huo na mwishowe akauleta juu yetu,+ kwa maana Yehova Mungu wetu ni mwadilifu katika kazi zake zote ambazo amefanya; nasi hatukutii sauti yake.+

15 “Na sasa, Ee Yehova Mungu wetu, wewe uliyewatoa watu wako katika nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu,+ ukajifanyia jina kama ilivyo leo hii,+ sisi tumetenda dhambi,+ tumetenda kwa uovu. 16 Ee Yehova, kulingana na matendo yako yote ya uadilifu,+ tafadhali, hasira yako na ghadhabu yako na zigeuke kutoka kwenye jiji lako Yerusalemu, mlima wako mtakatifu;+ kwa maana Yerusalemu na watu wako ni vitu vya kushutumiwa na watu wote wanaotuzunguka+ kwa sababu ya dhambi zetu na kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+ 17 Basi sasa, Ee Mungu wetu, sikiliza sala ya mtumishi wako na maombi yake, ufanye uso wako uangaze+ juu ya patakatifu pako ambapo pamefanywa ukiwa,+ kwa ajili ya Yehova. 18 Tega sikio lako, Ee Mungu wangu, usikie.+ Fungua macho yako uone hali zetu za ukiwa na jiji ambalo limeitwa kwa jina lako;+ kwa maana si kulingana na matendo yetu ya uadilifu kwamba tunaleta maombi yetu mbele zako,+ bali ni kulingana na rehema zako nyingi.+ 19 Ee Yehova, usikie.+ Ee Yehova, usamehe.+ Ee Yehova, sikiliza utende.+ Usikawie,+ kwa ajili yako mwenyewe, Ee Mungu wangu, kwa maana jina lako mwenyewe limeitwa juu ya jiji lako na juu ya watu wako.”+

20 Nilipokuwa ningali nasema na kusali na kuungama dhambi yangu+ na dhambi ya watu wangu Israeli+ na kupeleka ombi langu la kupata kibali liingie mbele za Yehova Mungu wangu, kuhusu mlima mtakatifu+ wa Mungu wangu, 21 nami nilipokuwa ningali nasema katika sala, tazama, yule mwanamume Gabrieli,+ ambaye nilikuwa nimemwona katika maono mwanzoni,+ baada ya kuchoshwa na uchovu, akawa anafika kando yangu wakati wa toleo la zawadi la jioni.+ 22 Naye akanifanya nielewe na kusema nami hivi:

“Ee Danieli, sasa nimekuja kukufanya upate ufahamu kwa kuelewa.+ 23 Mwanzoni mwa maombi yako neno lilitolewa, nami nimekuja kutoa habari, kwa maana wewe ni mtu mwenye kutamanika sana.+ Basi lifikirie jambo hilo,+ na upate kuelewa jambo lililoonwa.

24 “Kuna majuma 70 ambayo yameamuliwa juu ya watu wako+ na juu ya jiji lako takatifu,+ ili kukomesha makosa,+ na kumaliza kabisa dhambi,+ na kufanya upatanisho kwa ajili ya kosa,+ na kuleta uadilifu mpaka wakati usio na kipimo,+ na kupiga muhuri+ juu ya maono na nabii, na kupatia mafuta Patakatifu pa Patakatifu.+ 25 Nawe ujue na ufahamu kwamba tangu kutolewa kwa lile neno+ la kurudisha na kujenga upya Yerusalemu+ mpaka Masihi+ aliye Kiongozi,+ kutakuwa na majuma 7, pia majuma 62.+ Atarudi na kujengwa hakika, pamoja na kiwanja cha watu wote na handaki, lakini katika dhiki ya nyakati.

26 “Na baada ya yale majuma 62 Masihi atakatiliwa mbali,+ bila kuwa na chochote kwa ajili yake.+

“Na watu wa kiongozi anayekuja wataharibu+ jiji na mahali patakatifu.+ Na mwisho wake utakuwa kwa mafuriko. Na mpaka ule mwisho kutakuwa na vita; kilichoamuliwa ni ukiwa.+

27 “Naye ataendelea kulitendesha agano+ kwa ajili ya wengi kwa juma moja;+ na katika nusu ya juma hilo atakomesha dhabihu na toleo la zawadi.+

“Na juu ya bawa la machukizo kutakuwa na yule anayesababisha ukiwa;+ na mpaka maangamizi, kitu kile kilichoamuliwa kitamwagika pia juu ya yule anayekaa ukiwa.”+

10 Katika mwaka wa tatu wa Koreshi+ mfalme wa Uajemi kuna jambo alilofunuliwa Danieli, ambaye jina lake aliitwa Belteshaza;+ na jambo hilo lilikuwa kweli, na kulikuwa na utumishi mkubwa wa kijeshi.+ Naye akaelewa jambo lile, naye akaelewa jambo lililoonwa.+

2 Siku hizo mimi, Danieli, nilikuwa nikiomboleza+ kwa majuma matatu kamili. 3 Sikula mkate mtamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, nami sikujipaka mafuta kwa vyovyote mpaka kumalizika kwa yale majuma matatu kamili.+ 4 Na katika siku ya 24 ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa kwenye ukingo wa ule mto mkubwa, yaani, Hidekeli,+ 5 mimi pia niliinua macho yangu nikaona, na, tazama, palikuwa na mwanamume fulani amevaa kitani,+ viuno vyake+ vimefungwa dhahabu ya Ufazi.+ 6 Na mwili wake ulikuwa kama krisolito,+ na uso wake kama umeme,+ na macho yake kama mienge yenye kuwaka moto,+ na mikono yake na miguu yake ilionekana kama shaba iliyong’arishwa,+ na sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati. 7 Nami Danieli nikaona yale maono peke yangu; lakini watu waliokuwa pamoja nami hawakuona maono hayo.+ Hata hivyo, walishikwa na mtetemeko mkubwa, wakakimbia na kujificha.

8 Mimi nami—niliachwa peke yangu, nikaona hayo maono makubwa. Na ndani yangu hazikubaki nguvu zozote, na sura yangu ikabadilika na kuharibika, wala sikubaki na nguvu zozote.+ 9 Nami nikaanza kusikia sauti ya maneno yake; nami nilipokuwa nikiisikia sauti ya maneno yake, nilikuwa nimelala usingizi mzito kifudifudi,+ uso wangu ukiwa chini.+ 10 Na, tazama! mkono fulani ukanigusa,+ nao ukanitikisa polepole niinuke kwa magoti yangu na viganja vya mikono yangu. 11 Naye akaniambia:

“Ee Danieli, wewe mtu mwenye kutamanika sana,+ elewa maneno ninayokuambia,+ na usimame wima mahali ulipokuwa umesimama, maana sasa nimetumwa kwako.”

Naye aliposema nami neno hilo, nikasimama wima, nikitetemeka.

12 Akaendelea kuniambia: “Usiogope,+ Ee Danieli, kwa maana tangu siku ya kwanza ulipoelekeza moyo wako ili kupata uelewaji+ na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako,+ maneno yako yamesikiwa, nami mwenyewe nimekuja kwa sababu ya maneno yako.+ 13 Lakini mkuu+ wa ufalme wa Uajemi+ alikuwa amesimama katika upinzani+ juu yangu kwa siku 21, na, tazama! Mikaeli,+ aliye mmoja wa hao wakuu wa mbele,+ akaja kunisaidia; nami nikabaki hapo kando ya wafalme wa Uajemi.+ 14 Nami nimekuja kukufanya utambue mambo yatakayowapata watu wako+ katika siku za mwisho,+ kwa kuwa hayo bado ni maono+ ya siku ambazo zitakuja.”+

15 Basi aliposema nami maneno hayo, nilikuwa nimeelekeza uso wangu chini+ nami nikawa siwezi kusema. 16 Na, tazama! mtu fulani anayefanana na wana wa binadamu akaigusa midomo yangu,+ nami nikaanza kufungua kinywa changu na kusema+ na kumwambia yule aliyekuwa amesimama mbele yangu: “Ee bwana wangu,+ kwa sababu ya maono yale nilikuwa na misukosuko, wala sikubaki na nguvu zozote.+ 17 Basi ni jinsi gani mtumishi wa huyu bwana wangu aliweza kusema na huyu bwana wangu?+ Lakini mimi, mpaka sasa nguvu zozote hazikubaki ndani yangu, wala hakuna pumzi yoyote iliyobaki ndani yangu.”+

18 Ndipo yule mwenye sura ya mtu wa udongo akanigusa tena na kunitia nguvu.+ 19 Kisha akasema: “Usiogope,+ Ee mtu mwenye kutamanika sana.+ Na uwe na amani.+ Uwe na nguvu, ndiyo, uwe na nguvu.”+ Mara tu aliposema nami, nikapata nguvu halafu nikasema: “Bwana wangu na aseme,+ kwa maana umenitia nguvu.”+ 20 Basi akaendelea kusema:

“Je, kweli unajua kwa nini nimekuja kwako? Na sasa nitarudi kupigana na mkuu wa Uajemi.+ Ninapoenda, tazama! pia mkuu wa Ugiriki anakuja.+ 21 Hata hivyo, nitakuambia mambo yaliyoandikwa katika maandishi ya kweli,+ wala hakuna yeyote anayenitegemeza kwa nguvu katika mambo haya isipokuwa Mikaeli,+ yule mkuu wenu.+

11 “Lakini mimi, katika mwaka wa kwanza wa Dario Mmedi+ nilisimama kama mwenye kumtia nguvu na kama ngome kwake. 2 Na sasa nitakuambia yaliyo kweli:+

“Tazama! Bado kutakuwa na wafalme watatu wenye kusimama kwa ajili ya Uajemi,+ na yule wa nne+ atakusanya utajiri mwingi kuliko wengine wote.+ Na mara tu atakapopata nguvu katika utajiri wake, ataamsha kila kitu kupigana na ufalme wa Ugiriki.+

3 “Na mfalme mwenye nguvu atasimama na kutawala kwa mamlaka kubwa sana+ na kufanya kulingana na mapenzi yake.+ 4 Naye atakapokuwa amesimama,+ ufalme wake utavunjwa na kugawanywa kuelekea pepo nne+ za mbinguni,+ lakini si kwa wazao+ wakewala si kulingana na mamlaka yake ambayo aliitumia kutawala; kwa sababu ufalme wake utang’olewa, hata kwa ajili ya wengine zaidi ya hao.

5 “Na mfalme wa kusini atakuwa na nguvu, pia mmoja wa wakuu wake; naye atamshinda na kutawala kwa mamlaka kubwa sana kuliko uwezo wa kutawala wa yule mwingine.

6 “Na mwishoni mwa miaka fulani watashirikiana, na binti ya mfalme wa kusini atakuja kwa mfalme wa kaskazini ili kufanya mpango wa usawa. Lakini binti huyo hatabaki na nguvu za mkono wake;+ wala mfalme huyo hatasimama, wala mkono wake; na binti huyo atatolewa, yeye mwenyewe, na wale wanaomleta, na yeye aliyemzaa, na yeye anayemtia nguvu nyakati hizo. 7 Na mmoja anayetoka katika chipukizi+ la mizizi ya binti huyo atasimama mahali pa mfalme, naye atalijia jeshi na kuja kupigana na ngome ya mfalme wa kaskazini naye atatenda juu yao na kushinda. 8 Na pia pamoja na miungu yao,+ na sanamu zao za kuyeyushwa, na vyombo vyao vyenye kutamanika vya fedha na vya dhahabu, naye ataingia Misri pamoja na mateka. Na yeye mwenyewe atasimama mbali na mfalme wa kaskazini kwa miaka fulani.

9 “Naye ataingia katika ufalme wa mfalme wa kusini na kurudi katika nchi yake mwenyewe.

10 “Basi kuhusu wanawe, watajichochea na kukusanya umati wa majeshi makubwa. Naye atakuja na kufurika na kupita katikati. Lakini atarudi, naye atajichochea mpaka kwenye ngome yake.

11 “Na mfalme wa kusini atajitia uchungu naye ataenda kupigana naye, yaani, na mfalme wa kaskazini; naye atasimamisha umati wa watu, na umati huo utatiwa mkononi mwake.+ 12 Na umati huo utachukuliwa mbali. Moyo wake utainuliwa,+ naye ataangusha makumi ya maelfu; lakini hatatumia nafasi yake yenye nguvu.

13 “Na mfalme wa kaskazini atarudi na kusimamisha umati wa watu ulio mkubwa kuliko ule wa kwanza; naye atakuja mwishoni mwa nyakati zile, miaka fulani, atafanya hivyo na jeshi kubwa+ na mali nyingi sana.+ 14 Na nyakati hizo kuna wengi watakaosimama kumpinga mfalme wa kusini.

“Nao wana wa wanyang’anyi wa watu wako watachukuliwa ili kujaribu kutimiza maono;+ nao watajikwaa.+

15 “Na mfalme wa kaskazini atakuja na kujenga boma la kuzingira na kuteka jiji lenye ngome.+ Nayo mikono ya kusini, haitasimama, wala watu wake waliochaguliwa; wala hakutakuwa na nguvu za kuendelea kusimama. 16 Na yule anayekuja kupigana naye atafanya kulingana na mapenzi yake, wala hakuna atakayesimama mbele yake. Naye atasimama katika nchi ya lile Pambo,+ na maangamizi yatakuwa mkononi mwake.+ 17 Naye atakaza uso wake+ kuja na nguvu za ufalme wake wote, naye atakuwa na masharti+ ya usawa pamoja naye; naye atatenda kwa njia yenye matokeo.+ Naye atapewa uwezo kumharibu yule binti wa wanawake. Na binti huyo hatasimama, naye hataendelea kuwa wake.+ 18 Naye atageuza uso wake kuelekea nchi za pwani+ na kuteka wengi. Na kiongozi mmoja ataikomesha shutuma kwa ajili yake mwenyewe kutoka kwa huyo hivi kwamba shutuma yake haitakuwapo. Atafanya irudi kwake yule. 19 Naye atageuza uso wake kuelekea ngome za nchi yake mwenyewe, naye atajikwaa na kuanguka, wala hatapatikana.+

20 “Na katika cheo chake+ atasimama mtu anayepitisha mtozaji+ kati ya ufalme wenye utukufu, na katika siku chache atavunjwa, lakini si kwa hasira wala kwa vita.

21 “Na katika cheo chake atasimama mtu wa kudharauliwa,+ nao hawatampa heshima ya ufalme; naye ataingia wakati ambapo hakuna mahangaiko+ na kuushika ufalme kwa ulaini.+ 22 Na kuhusu mikono ya mafuriko,+ itapatwa na mafuriko kwa sababu yake, nayo itavunjwa;+ kama itakavyokuwa pia+ kwa Kiongozi+ wa agano.+ 23 Na kwa sababu ya wao kushirikiana naye, ataendeleza udanganyifu na kupanda na kuwa na nguvu kupitia taifa dogo.+ 24 Wakati ambapo hakuna mahangaiko,+ yeye ataingia katika unono wa wilaya ya utawala na kufanya yale ambayo hawakufanya baba wala baba za baba zake. Atatawanya kati yao vitu vya kuporwa na nyara na mali; naye atapanga hila zake juu ya mahali penye ngome,+ lakini ni kwa muda tu.

25 “Naye ataamsha nguvu zake na moyo wake juu ya mfalme wa kusini kwa jeshi kubwa; naye mfalme wa kusini atajichochea kwa ajili ya vita kwa kutumia jeshi kubwa mno na lenye nguvu. Naye hatasimama, kwa sababu watapanga hila juu yake. 26 Na wale wanaokula vyakula vyake vitamu watasababisha kuvunjika kwake.

“Na jeshi lake litafagiliwa mbali kwa mafuriko, na wengi wataanguka wakiwa wameuawa.

27 “Na moyo wa hao wafalme wawili utakuwa na mwelekeo wa kufanya yaliyo mabaya, nao wataendelea kusema+ uwongo kwenye meza moja.+ Lakini hakuna litakalofanikiwa,+ kwa maana mwisho bado ni kwa wakati uliowekwa.+

28 “Naye atarudi katika nchi yake akiwa na kiasi kikubwa cha mali, na moyo wake utakuwa kinyume cha agano takatifu.+ Naye atatenda kwa njia yenye matokeo+ na kurudi katika nchi yake.

29 “Atarudi kwa wakati uliowekwa,+ naye atakuja kupigana na kusini;+ lakini hapo mwisho mambo hayatakuwa kama wakati wa kwanza. 30 Na meli za Kitimu zitakuja juu yake,+ naye atahuzunika.

“Naye atarudi na kumwaga shutuma+ juu ya agano+ takatifu na kutenda kwa njia yenye matokeo; naye atarudi na kuwafikiria wale wanaoliacha agano takatifu. 31 Na kutakuwa na mikono itakayosimama, kutoka kwake; nayo itapatia unajisi patakatifu,+ ile ngome, na kuondoa dhabihu ya daima.+

“Nao watalisimamisha lile chukizo+ linalosababisha ukiwa.+

32 “Naye, kwa kutumia maneno laini,+ atawaongoza kwenye uasi-imani+ wale wanaotenda kwa uovu juu ya lile agano.+ Lakini watu wale wanaomjua Mungu wao,+ watashinda+ na kutenda kwa njia yenye matokeo. 33 Na wale walio na ufahamu+ kati ya watu, watawawezesha wengi kuwa na uelewaji.+ Nao watakwazwa kwa upanga na kwa mwali wa moto, kwa kutekwa na kwa kuporwa,+ kwa siku fulani. 34 Lakini watakapokwazwa watasaidiwa kwa msaada kidogo;+ na wengi watajiunga nao kwa ulaini.+ 35 Na baadhi ya wale wenye ufahamu watakwazwa,+ ili kufanya kazi ya kusafisha kwa sababu yao na kutakasa na kufanya weupe,+ mpaka wakati wa mwisho;+ kwa maana bado ni kwa wakati uliowekwa.+

36 “Na mfalme huyo atafanya kulingana na mapenzi yake, naye atajiinua na kujitukuza juu ya kila mungu;+ naye atasema mambo ya ajabu kinyume cha Mungu wa miungu.+ Naye atapata mafanikio mpaka shutuma ile itakapokuwa imetimizwa;+ kwa sababu jambo lililoamuliwa lazima lifanywe. 37 Na kwa Mungu wa baba zake hataonyesha kujali; na kwa tamaa ya wanawake na kwa mungu mwingine yeyote hataonyesha kujali, bali atajitukuza juu ya kila mtu.+ 38 Lakini kwa mungu wa ngome, katika cheo chake atampa utukufu; na kwa mungu ambaye baba zake hawakujua atampa utukufu kwa dhahabu na fedha na mawe ya thamani na vitu vyenye kutamanika. 39 Naye atatenda kwa njia yenye matokeo juu ya ngome zilizoimarishwa, pamoja na mungu wa kigeni. Yeyote anayemtambua atamfanya awe na utukufu mwingi, naye atawafanya watawale kati ya wengi; naye ataigawa nchi kwa bei.

40 “Na wakati wa mwisho mfalme wa kusini+ atasukumana naye, na mfalme wa kaskazini atafanya mashambulizi makali juu yake kwa magari na kwa wapanda-farasi na kwa meli nyingi; naye ataingia katika nchi hizo na kufurika na kupita katikati. 41 Pia ataingia+ katika nchi ya lile Pambo,+ na kutakuwako nchi nyingi zitakazokwazwa.+ Lakini hizi ndizo zitakazoponyoka mkononi mwake, Edomu na Moabu+ na ile sehemu kuu ya wana wa Amoni. 42 Naye ataendelea kunyoosha mkono wake juu ya nchi hizo; nayo nchi ya Misri+ haitaponyoka. 43 Naye atatawala juu ya hazina zilizofichwa za dhahabu na fedha na juu ya vitu vyote vyenye kutamanika vya Misri. Na Walibya na Waethiopia watafuata nyayo zake.

44 “Lakini kutakuwako habari ambazo zitamsumbua,+ kutoka upande wa mashariki+ na kutoka kaskazini, naye ataenda kwa ghadhabu kubwa ili kuangamiza na kuharibu wengi.+ 45 Naye atasimamisha mahema yake makubwa kati ya ile bahari kuu na mlima mtakatifu wa lile Pambo;+ naye ataenda mpaka mwisho wake,+ wala hatakuwa na wa kumsaidia.+

12 “Na Mikaeli+ atasimama wakati huo, yule mkuu+ anayesimama+ kwa ajili ya wana wa watu wako.+ Na kutakuwa na wakati wa taabu ambayo haijapata kutokea tangu kuwapo kwa taifa lolote mpaka wakati huo.+ Na wakati huo watu wako wataponyoka,+ kila mmoja anayepatikana ameandikwa katika kile kitabu.+ 2 Na kutakuwa na wengi kati ya wale waliolala katika mavumbi ya nchi ambao wataamka,+ hawa kwa ajili ya uzima unaodumu mpaka wakati usio na kipimo+ na wale kwa ajili ya shutuma na chuki zinazodumu mpaka wakati usio na kipimo.+

3 “Na wale walio na ufahamu watang’aa kama mwangaza wa anga;+ na wale wanaoleta wengi kwenye uadilifu,+ watang’aa mpaka wakati usio na kipimo, milele kama nyota.

4 “Na wewe, Ee Danieli, yafanye siri maneno hayo na kukifunga kitabu kwa muhuri,+ mpaka wakati wa mwisho.+ Wengi watakwenda huku na huku, na ujuzi wa kweli utakuwa mwingi.”+

5 Nami Danieli nikaona, na tazama! watu wengine wawili walikuwa wamesimama,+ mmoja kwenye ukingo huu wa mto na yule mwingine kwenye ukingo ule mwingine wa mto.+ 6 Ndipo mmoja akamwambia yule mtu aliyevaa kitani,+ aliyekuwa juu ya maji ya ule mto: “Itakuwa muda gani kufikia mwisho wa mambo hayo ya ajabu?”+ 7 Nami nikaanza kumsikia yule mtu aliyevaa kitani, ambaye alikuwa juu ya maji ya ule mto, alipoinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbingu na kuapa+ kwa Yule aliye hai kwa wakati usio na kipimo:+ “Itakuwa ni kwa wakati uliowekwa, nyakati zilizowekwa na nusu ya wakati.+ Na mara tu baada ya kuvunjwa vipande-vipande kwa nguvu za watu watakatifu kutakapokwisha,+ mambo hayo yote yatakwisha.”

8 Mimi nami nikasikia, lakini sikuweza kuelewa;+ basi nikauliza: “Ee bwana wangu, mwisho wa mambo hayo utakuwa nini?”+

9 Naye akaniambia tena: “Nenda, Danieli, kwa sababu maneno hayo yamewekwa siri na kufungwa kwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.+ 10 Wengi watajitakasa+ na kujifanya weupe+ na kusafishwa.+ Na waovu watatenda kwa uovu,+ wala hakuna waovu wowote watakaoelewa;+ bali wale walio na ufahamu wataelewa.+

11 “Na kutoka wakati wa kuondolewa+ kwa ile dhabihu ya daima+ na kusimamishwa kwa lile chukizo+ linalosababisha ukiwa, kutakuwa na siku 1,290.

12 “Mwenye furaha+ ni yule anayeendelea kutarajia na anayefika kwenye zile siku 1,335!

13 “Wewe nawe, nenda zako kuelekea ule mwisho;+ nawe utapumzika,+ lakini utasimama kwa ajili ya fungu lako mwishoni mwa zile siku.”+

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki