Ezra
1 Na katika mwaka wa kwanza wa Koreshi+ mfalme wa Uajemi, ili neno la Yehova kwa kinywa cha Yeremia+ litimizwe, Yehova aliiamsha+ roho ya Koreshi mfalme wa Uajemi, hivi kwamba akatangaza mwito+ katika utawala wake wote, na pia kwa maandishi,+ akisema:
2 “Koreshi mfalme wa Uajemi amesema hivi,+ ‘Yehova Mungu wa mbinguni+ amenipa falme zote za dunia,+ naye mwenyewe amenipa utume nimjengee nyumba katika Yerusalemu,+ huko Yuda. 3 Yeyote aliye katikati yenu ninyi watu wake wote, Mungu wake na awe pamoja naye.+ Basi na apande na kwenda Yerusalemu, huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli—yeye ndiye Mungu wa kweli+—iliyokuwa Yerusalemu.+ 4 Na yeyote aliyebaki mahali popote anapokaa akiwa mgeni,+ watu wa mahali pake na wamsaidie kwa fedha na kwa dhahabu na kwa mali na kwa wanyama wa kufugwa pamoja na toleo la hiari+ kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa kweli, iliyokuwa Yerusalemu.’”
5 Ndipo vichwa+ vya upande wa baba vya Yuda na vya Benyamini na makuhani na Walawi wakasimama, ndiyo, kila mmoja ambaye Mungu wa kweli aliiamsha roho+ yake, ili kwenda kujenga upya nyumba ya Yehova,+ iliyokuwa Yerusalemu. 6 Na wale wote waliowazunguka wakaitia nguvu+ mikono yao kwa vyombo vya fedha, kwa dhahabu, kwa mali na kwa wanyama wa kufugwa na kwa vitu bora, mbali na vyote vilivyotolewa kwa hiari.+
7 Pia, Mfalme Koreshi mwenyewe akaleta vyombo vya nyumba ya Yehova,+ ambavyo Nebukadneza alikuwa ameleta kutoka Yerusalemu+ na kuviweka katika nyumba ya mungu wake.+ 8 Basi Koreshi mfalme wa Uajemi akavitoa na kuviweka chini ya Mithredathi mweka-hazina na kuvihesabu na kumpa Sheshbazari+ mkuu wa Yuda.+
9 Basi hii ndiyo hesabu yake: vyombo 30 vya dhahabu vyenye umbo la kikapu, vyombo 1,000 vya fedha vyenye umbo la kikapu, vyombo 29 vya akiba, 10 mabakuli+ madogo 30 ya dhahabu, mabakuli madogo ya namna ya pili, 410 ya fedha, vyombo vingine 1,000. 11 Vyombo vyote vya dhahabu na vya fedha vilikuwa 5,400. Sheshbazari+ alileta kila kitu pamoja na wale waliohamishwa+ ambao walitoka Babiloni kwenda Yerusalemu.
2 Na hawa ndio wana wa wilaya ya utawala+ waliotoka utekwani mwa wale waliohamishwa,+ ambao Nebukadneza mfalme wa Babiloni alikuwa amewapeleka uhamishoni+ katika Babiloni na ambao baadaye walirudi+ Yerusalemu na Yuda,+ kila mmoja kwenye jiji lake mwenyewe; 2 wale waliokuja pamoja na Zerubabeli,+ Yeshua,+ Nehemia, Seraya,+ Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigvai, Rehumu, Baana.
Hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli: 3 Wana wa Paroshi,+ 2,172; 4 wana wa Shefatia,+ 372; 5 wana wa Ara,+ 775; 6 wana wa Pahath-moabu,+ wa wana wa Yeshua na Yoabu,+ 2,812; 7 wana wa Elamu,+ 1,254; 8 wana wa Zatu,+ 945; 9 wana wa Zakai,+ 760; 10 wana wa Bani,+ 642; 11 wana wa Bebai,+ 623; 12 wana wa Azgadi,+ 1,222; 13 wana wa Adonikamu,+ 666; 14 wana wa Bigvai,+ 2,056; 15 wana wa Adini,+ 454; 16 wana wa Ateri,+ wa Hezekia, 98; 17 wana wa Besai,+ 323; 18 wana wa Yora, 112; 19 wana wa Hashumu,+ 223; 20 wana wa Gibari,+ 95; 21 wana wa Bethlehemu,+ 123; 22 wanaume wa Netofa,+ 56; 23 wanaume wa Anathothi,+ 128; 24 wana wa Azmavethi,+ 42; 25 wana wa Kiriath-yearimu,+ Kefira na Beerothi, 743; 26 wana wa Rama+ na Geba,+ 621; 27 wanaume wa Mikmasi,+ 122; 28 wanaume wa Betheli+ na Ai,+ 223; 29 wana wa Nebo,+ 52; 30 wana wa Magbishi, 156; 31 wana wa ile Elamu+ nyingine, 1,254; 32 wana wa Harimu,+ 320; 33 wana wa Lodi,+ Hadidi+ na Ono,+ 725; 34 wana wa Yeriko,+ 345; 35 wana wa Senaa,+ 3,630.
36 Makuhani:+ Wana wa Yedaya+ wa nyumba ya Yeshua,+ 973; 37 wana wa Imeri,+ 1,052; 38 wana wa Pashuri,+ 1,247; 39 wana wa Harimu,+ 1,017.
40 Walawi:+ Wana wa Yeshua+ na Kadmieli,+ wa wana wa Hodavia,+ 74. 41 Waimbaji, wana wa Asafu,+ 128. 42 Wana wa watunza-malango, wana wa Shalumu,+ wana wa Ateri,+ wana wa Talmoni,+ wana wa Akubu,+ wana wa Hatita,+ wana wa Shobai, wote pamoja, 139.
43 Wanethini:+ Wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi,+ 44 wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni,+ 45 wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Akubu, 46 wana wa Hagabu, wana wa Salmai,+ wana wa Hanani, 47 wana wa Gideli, wana wa Gahari,+ wana wa Reaya, 48 wana wa Resini,+ wana wa Nekoda, wana wa Gazamu, 49 wana wa Uza, wana wa Pasea,+ wana wa Besai, 50 wana wa Asna, wana wa Meunimu, wana wa Nefusimu;+ 51 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri,+ 52 wana wa Basluthi, wana wa Mehida, wana wa Harsha,+ 53 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema,+ 54 wana wa Nezia, wana wa Hatifa.+
55 Wana wa watumishi wa Sulemani:+ Wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Peruda,+ 56 wana wa Yaalaya, wana wa Darkoni, wana wa Gideli,+ 57 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-hazebaimu, wana wa Ami.+
58 Wanethini+ wote na wana wa watumishi wa Sulemani walikuwa 392.+
59 Na hawa ndio waliotoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubi, Adoni na Imeri, nao hawakuweza kujua nyumba ya baba zao wala uzao wao,+ kama walikuwa wa Israeli: 60 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda,+ 652. 61 Nao wana wa makuhani:+ wana wa Habaya, wana wa Hakozi,+ wana wa Barzilai,+ aliyechukua mke kutoka kati ya binti za Barzilai+ Mgileadi naye akaja kuitwa kwa jina lao. 62 Hao ndio wale waliotafuta kitabu chao cha kuandikisha ili kuthibitisha ukoo wao waziwazi, wakakuta hawamo, basi wakazuiwa wasiwe katika ukuhani kwa kuwa ni najisi.+ 63 Basi huyo Tirshatha+ akawaambia kwamba hawangeweza kula+ katika vile vitu vitakatifu zaidi mpaka kuhani mwenye Urimu+ na Thumimu asimame.
64 Kutaniko zima likiwa kundi moja+ lilikuwa watu 42,360,+ 65 zaidi ya hao watumwa wao na vijakazi wao, ambao walikuwa 7,337; nao walikuwa na waimbaji+ 200, wa kiume na wa kike. 66 Farasi zao walikuwa 736, nyumbu zao 245,+ 67 ngamia zao 435, punda zao 6,720.+
68 Na watu fulani walio vichwa+ vya nyumba za ukoo wa upande wa baba,+ walipokuja katika nyumba ya Yehova,+ iliyokuwa Yerusalemu,+ walitoa matoleo ya hiari+ kwa nyumba ya Mungu wa kweli, ili kuisimamisha mahali pake.+ 69 Kulingana na nguvu zao walitoa dhahabu+ kwa ajili ya hazina ya kazi, drakma 61,000, na fedha,+ mina 5,000, na kanzu+ 100 za makuhani. 70 Na makuhani na Walawi na wengine kati ya watu,+ na waimbaji na watunza-malango na Wanethini wakaanza kukaa katika majiji yao, na Israeli wote katika majiji yao.+
3 Mwezi wa saba+ ulipofika, wana wa Israeli walikuwa katika majiji yao. Na watu wakaanza kukusanyika Yerusalemu+ kama mtu mmoja.+ 2 Naye Yeshua+ mwana wa Yehosadaki na ndugu zake makuhani na Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli+ na ndugu zake wakasimama na kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli, ili kutoa dhabihu za kuteketezwa juu yake, kulingana na yaliyoandikwa+ katika sheria ya Musa mtu wa Mungu wa kweli.
3 Basi wakaisimamisha madhabahu imara mahali pake,+ kwa maana woga uliwashika kwa sababu ya vikundi vya watu wa nchi,+ nao wakaanza kutoa juu yake dhabihu za kuteketezwa kwa Yehova, dhabihu za kuteketezwa za asubuhi na za jioni.+ 4 Kisha wakafanya sherehe ya vibanda+ kulingana na yaliyoandikwa,+ na dhabihu za kuteketezwa siku kwa siku kwa hesabu kulingana na kanuni ya kile kilichotakiwa kila siku.+ 5 Na baadaye kulikuwa na toleo la kuteketezwa la daima+ na lile la miezi mipya+ na kwa ajili ya majira yote yaliyotakaswa ya sherehe+ za Yehova na kwa ajili ya kila mtu aliyetoa kwa kupenda toleo la hiari+ kwa Yehova. 6 Tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba+ walianza kutoa dhabihu za kuteketezwa kwa Yehova, wakati msingi wa hekalu la Yehova ulikuwa haujawekwa bado.
7 Nao wakawapa pesa+ wachongaji+ wa mawe na mafundi,+ na kuwapa Wasidoni+ na Watiro+ vyakula+ na vinywaji na mafuta,+ ili walete miti ya mierezi kutoka Lebanoni+ mpaka kwenye bahari iliyoko Yopa,+ kulingana na ruhusa waliyopewa na Koreshi+ mfalme wa Uajemi.
8 Na katika mwaka wa pili wa kuja kwao kwenye nyumba ya Mungu wa kweli huko Yerusalemu,+ katika mwezi wa pili, Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli+ na Yeshua+ mwana wa Yehosadaki na wengineo wa ndugu zao, makuhani na Walawi, na wale wote waliokuwa wametoka utekwani+ kwenda Yerusalemu wakaanza kazi; basi wakawaweka katika vyeo Walawi+ kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi wawe wasimamizi wa kazi ya nyumba ya Yehova.+ 9 Kwa hiyo Yeshua,+ wanawe na ndugu zake, na Kadmieli na wanawe, wana wa Yuda, wakasimama kama kikundi kimoja ili wawe wasimamizi wa wafanyakazi katika nyumba ya Mungu wa kweli, pia wana wa Henadadi,+ wana wao na ndugu zao, Walawi.
10 Wajenzi walipoweka msingi+ wa hekalu la Yehova, ndipo makuhani katika mavazi rasmi,+ wakiwa na tarumbeta,+ na Walawi wana wa Asafu,+ wakiwa na matoazi,+ wakasimama ili kumsifu Yehova kulingana na mwelekezo+ wa Daudi mfalme wa Israeli. 11 Nao wakaanza kuitikia kwa kumsifu+ na kumtolea Yehova shukrani, “kwa kuwa yeye ni mwema,+ kwa maana fadhili zake zenye upendo kwa Israeli ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+ Nao watu wote wakapaaza sauti+ kubwa kwa kumsifu Yehova juu ya kuwekwa kwa msingi wa nyumba ya Yehova. 12 Na wengi kati ya makuhani+ na Walawi na vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba,+ wazee ambao walikuwa wameona ile nyumba ya kwanza,+ walikuwa wakilia+ kwa sauti kubwa wakati wa kuwekwa msingi+ wa nyumba hii mbele ya macho yao, huku wengine wengi wakipaaza sauti kwa shangwe.+ 13 Kwa hiyo watu hawakuweza kutofautisha kati ya sauti ya watu ya kushangilia+ na ile ya kulia, kwa maana watu walikuwa wakipaaza sauti kubwa, na sauti hiyo ikasikiwa hata mbali sana.
4 Adui+ za Yuda na Benyamini waliposikia kwamba wana wa Uhamisho+ wanamjengea Yehova Mungu wa Israeli hekalu, 2 wakamfikia Zerubabeli+ mara moja akiwa pamoja na vichwa+ vya nyumba za ukoo wa upande wa baba na kuwaambia: “Acheni tujenge pamoja nanyi;+ kwa maana, kama ninyi, sisi pia tunamtafuta Mungu wenu+ nasi tunamtolea dhabihu tangu siku za Esar-hadoni+ mfalme wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”+ 3 Hata hivyo, Zerubabeli na Yeshua+ na wengineo wa vichwa+ vya nyumba za ukoo wa upande wa baba za Israeli wakawaambia: “Haiwahusu ninyi kujenga pamoja nasi nyumba kwa ajili ya Mungu wetu,+ kwa maana sisi wenyewe tutamjengea Yehova Mungu wa Israeli, kama alivyotuamuru Mfalme Koreshi,+ mfalme wa Uajemi.”
4 Ndipo watu wa nchi wakazidi kuilegeza+ mikono ya watu wa Yuda na kuwavunja moyo wasijenge+ 5 na kuwalipa+ washauri ili kulivunja shauri lao siku zote za Koreshi mfalme wa Uajemi mpaka wakati wa utawala wa Dario+ mfalme wa Uajemi. 6 Na wakati wa utawala wa Ahasuero, mwanzoni mwa utawala wake, waliandika shtaka+ juu ya wakaaji wa Yuda na Yerusalemu. 7 Pia, katika siku za Artashasta, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli na wale wenzake walimwandikia Artashasta mfalme wa Uajemi, na maandishi ya barua hiyo yaliandikwa kwa herufi za Kiaramu na kutafsiriwa katika lugha ya Kiaramu.+
8 Rehumu ofisa mkuu wa serikali na Shimshai, mwandishi, wakamwandikia Mfalme Artashasta barua dhidi ya Yerusalemu, kama inavyofuata: 9 Ndipo Rehumu+ ofisa mkuu wa serikali na Shimshai, mwandishi, na wenzao wengine, waamuzi na magavana wadogo ng’ambo ya Mto,+ waandishi,+ watu wa Ereki,+ Wababiloni,+ wakaaji wa Susa,+ yaani, Waelamu,+ 10 na mataifa+ mengine ambao Asenapari+ mkuu na mheshimiwa aliwapeleka uhamishoni na kuwakalisha katika majiji ya Samaria,+ na wale wengine ng’ambo ya Mto, —; basi sasa 11 hii ndiyo nakala ya barua waliyotuma kuhusu jambo hilo:
“Kwa Artashasta+ mfalme wa watumishi wako, watu walio ng’ambo ya Mto: Basi 12 na ijulikane kwa mfalme kwamba Wayahudi waliokuja hapa kwetu kutoka kwako wamefika Yerusalemu. Wanajenga lile jiji baya na lenye kuasi, nao wanakamilisha kuta+ na kurekebisha misingi. 13 Sasa mfalme na ajue kwamba, jiji hili likijengwa na kuta zake kukamilishwa, hawatatoa kodi+ wala ushuru+ wala ada, na jambo hilo litaleta hasara kwa hazina+ za wafalme. 14 Basi kwa vile sisi hula chumvi ya jumba la mfalme, na haifai sisi kuona mfalme akinyimwa, ndiyo sababu tumetuma na kumjulisha mfalme jambo hilo, 15 ili ufanywe uchunguzi wa kitabu cha kumbukumbu+ za mababu zako wa kale. Ndipo utakapopata kujua katika kitabu hicho cha kumbukumbu kwamba jiji hilo ni jiji lenye kuasi linalosababisha hasara kwa wafalme na wilaya za utawala, na ndani yake mlikuwa na wachochezi wa uasi tangu siku za zamani. Ndiyo sababu jiji hilo limefanywa ukiwa.+ 16 Tunamjulisha mfalme kwamba, jiji hilo likijengwa na kuta zake kukamilishwa, wewe pia hakika hutakuwa na fungu lolote ng’ambo ya Mto.”+
17 Mfalme akapeleka neno kwa Rehumu+ ofisa mkuu wa serikali na Shimshai mwandishi na wenzao+ waliokaa katika Samaria na wale wengine ng’ambo ya Mto:
“Salamu!+ Basi 18 ile barua rasmi ambayo mmetutumia imesomwa waziwazi mbele yangu. 19 Kwa hiyo mimi nimetoa agizo, nao wamechunguza+ na kupata kwamba jiji hilo limekuwa likisimama kuwapinga wafalme tangu siku za kale na uasi na maasi yameendelezwa humo.+ 20 Na kulikuwa na wafalme wenye nguvu+ juu ya Yerusalemu waliotawala watu wote ng’ambo ya Mto,+ nao walikuwa wakipewa kodi, ushuru na ada.+ 21 Sasa waagizeni wanaume hao wakome, ili jiji hilo lisijengwe upya mpaka nitakapotoa agizo. 22 Kwa hiyo iweni waangalifu kusiwe na uzembe kuhusu kutenda jambo hili, ili madhara hayo yasiongezeke yawe kwa hasara ya wafalme.”+
23 Ikawa kwamba baada ya kusomwa kwa nakala ya barua rasmi ya Mfalme Artashasta mbele ya Rehumu+ na Shimshai+ mwandishi na wenzao,+ walifanya haraka kwenda Yerusalemu kwa Wayahudi na kuwakomesha kwa kutumia nguvu za silaha.+ 24 Wakati huo ndipo kazi ikakoma kwenye nyumba ya Mungu, iliyokuwa Yerusalemu; nayo ikakoma mpaka mwaka wa pili wa kutawala kwa Dario+ mfalme wa Uajemi.
5 Naye Hagai+ nabii na Zekaria+ mjukuu wa Ido,+ nabii, wakawatolea unabii Wayahudi waliokuwa katika Yuda na Yerusalemu, kwa jina+ la Mungu wa Israeli aliyekuwa juu yao.+ 2 Ndipo Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli+ na Yeshua+ mwana wa Yehosadaki wakasimama na kuanza kujenga upya nyumba ya Mungu, iliyokuwa Yerusalemu; na manabii+ wa Mungu walikuwa pamoja nao kuwapa msaada. 3 Wakati huo Tatenai+ gavana wa ng’ambo ya Mto+ na Shethar-bozenai na wenzao wakaja kwao, na kuwaambia hivi: “Ni nani aliyewapa agizo la kujenga nyumba hii na kukamilisha muundo huu wa nguzo?”+ 4 Kisha wakawaambia hivi: “Majina ya wanaume wanaojenga jengo hili ni nani?” 5 Nalo jicho+ la Mungu lilikuwa juu ya+ wanaume wazee wa Wayahudi, nao hawakuwakomesha mpaka habari imwendee Dario halafu barua rasmi kuhusu jambo hilo irudishwe.
6 Hii ndiyo nakala+ ya barua ambayo Tatenai+ gavana wa ng’ambo ya Mto+ na Shethar-bozenai+ na wenzake,+ magavana wadogo waliokuwa ng’ambo ya Mto, walipeleka kwa Mfalme Dario; 7 walipeleka neno kwake, na maandishi ndani yake yalikuwa hivi:
“Kwa Mfalme Dario:
“Amani nyingi!+ 8 Mfalme na ajue kwamba tulienda katika wilaya ya utawala+ ya Yuda kwenye nyumba ya yule Mungu mkuu,+ nayo inajengwa kwa mawe yaliyowekwa kwa kuviringishwa, na mbao zinawekwa katika kuta; na kazi hiyo inafanywa kwa bidii na inafanya maendeleo mikononi mwao. 9 Ndipo tukawauliza hao wanaume wazee. Tuliwaambia hivi: ‘Ni nani aliyewapa agizo la kujenga nyumba hii na kukamilisha muundo huu wa nguzo?’+ 10 Pia tuliwauliza majina yao, ili tukujulishe, tupate kuyaandika majina ya wanaume wanaowaongoza.+
11 “Nao walitujibu neno hili, wakisema: ‘Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na dunia,+ nasi tunajenga upya nyumba ambayo ilikuwa imejengwa miaka mingi kabla ya hii, ambayo mfalme mkuu wa Israeli alijenga na kukamilisha.+ 12 Hata hivyo, kwa sababu baba zetu walimkasirisha+ Mungu wa mbinguni, aliwatia+ mkononi mwa Nebukadneza+ mfalme wa Babiloni, Mkaldayo,+ naye akaibomoa nyumba hii+ na kuwapeleka watu uhamishoni huko Babiloni.+ 13 Ingawa hivyo, katika mwaka wa kwanza wa Koreshi+ mfalme wa Babiloni, Mfalme Koreshi alitoa agizo la kuijenga upya nyumba hii ya Mungu.+ 14 Na pia vyombo vya dhahabu na fedha+ vya nyumba ya Mungu ambavyo Nebukadneza alivichukua kutoka katika hekalu, lililokuwa Yerusalemu, na kuvileta katika hekalu la Babiloni,+ Mfalme+ Koreshi alivitoa katika hekalu la Babiloni, vikapewa mtu anayeitwa Sheshbazari,+ aliyemfanya kuwa gavana.+ 15 Naye akamwambia: “Chukua vyombo hivi.+ Nenda, uviweke katika hekalu lililoko Yerusalemu, nayo nyumba ya Mungu ijengwe upya mahali pake.”+ 16 Wakati huyo Sheshbazari alipokuja, aliweka misingi ya nyumba ya Mungu,+ iliyoko Yerusalemu; na tangu wakati huo mpaka sasa inajengwa lakini haijamalizika.’+
17 “Na sasa ikiwa inaonekana vema kwa mfalme, acha ufanywe uchunguzi+ katika nyumba ya hazina za mfalme iliyopo hapo Babiloni, ili ionekane kama kweli Mfalme Koreshi alitoa agizo+ la kuijenga upya nyumba hiyo ya Mungu katika Yerusalemu; naye mfalme atutumie uamuzi wake kuhusu jambo hili.”
6 Ndipo Mfalme Dario akatoa agizo, nao wakafanya uchunguzi katika nyumba ya kumbukumbu+ za hazina zilizowekwa katika Babiloni. 2 Kisha kitabu fulani cha kukunjwa kikapatikana huko Ekibatana, katika mahali penye ngome palipokuwa katika wilaya ya utawala ya Umedi,+ nayo kumbukumbu hii ilikuwa imeandikwa ndani yake hivi:
3 “Katika mwaka wa kwanza wa Mfalme Koreshi,+ Mfalme Koreshi alitoa agizo kuhusu nyumba ya Mungu katika Yerusalemu: Nyumba hiyo na ijengwe upya iwe mahali pao pa kutolea dhabihu,+ na misingi yake iwekwe, urefu wake uwe mikono 60, upana wake mikono 60,+ 4 kwa mistari mitatu ya mawe yaliyowekwa kwa kuviringishwa+ na mstari mmoja wa mbao;+ na gharama itolewe kutoka katika nyumba ya mfalme.+ 5 Na virudishwe pia vyombo vya dhahabu na fedha+ vya nyumba ya Mungu ambavyo Nebukadneza+ alichukua kutoka katika hekalu lililokuwa Yerusalemu na kuvileta Babiloni, ili vifike kwenye hekalu lililoko Yerusalemu katika mahali pake na kuwekwa katika nyumba ya Mungu.+
6 “Basi Tatenai+ gavana wa ng’ambo ya Mto,+ Shethar-bozenai+ na wenzao, magavana+ wadogo walio ng’ambo ya Mto, msikaribie mahali hapo.+ 7 Jitengeni na kazi ya hiyo nyumba ya Mungu.+ Gavana wa Wayahudi na wanaume wazee wa Wayahudi watajenga upya hiyo nyumba ya Mungu mahali pake. 8 Nami nimetoa agizo+ kuhusu jambo mtakalowafanyia hao wanaume wazee wa Wayahudi, kwa ajili ya kujengwa upya kwa nyumba ya Mungu; wanaume hao watapewa gharama mara moja+ kutoka katika hazina ya kifalme+ ya kodi, ng’ambo ya Mto bila kuacha.+ 9 Na kile kinachohitajiwa, ng’ombe-dume wachanga+ pamoja na kondoo-dume+ na wana-kondoo+ kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano,+ chumvi,+ divai+ na mafuta,+ kama vile wanavyosema makuhani walioko Yerusalemu, wapewe vitu hivyo kwa kuendelea siku kwa siku bila kukosa; 10 ili waendelee+ kuleta matoleo ya kutuliza+ kwa Mungu wa mbinguni na kusali kwa ajili ya uhai wa mfalme na wanawe.+ 11 Nami nimetoa agizo kwamba yeyote atakayevunja+ amri hii, mti+ utang’olewa kutoka katika nyumba yake naye atatundikwa juu yake,+ na nyumba yake itageuzwa kuwa choo cha watu wote kwa sababu hiyo.+ 12 Na Mungu aliyefanya jina lake+ likae hapo na apindue mfalme na mtu yeyote atakayenyoosha mkono wake ili kuivunja na kuiharibu+ nyumba hiyo ya Mungu, iliyoko Yerusalemu. Mimi, Dario, natoa agizo. Nalo litendwe mara moja.”
13 Ndipo Tatenai gavana wa ng’ambo ya Mto,+ Shethar-bozenai,+ na wenzao, wakafanya mara moja kulingana na neno ambalo Mfalme Dario alikuwa ametoa. 14 Nao wanaume wazee+ wa Wayahudi wakajenga+ na kufanya maendeleo wakichochewa na unabii wa Hagai+ nabii na Zekaria+ mjukuu wa Ido,+ wakajenga na kuimaliza kutokana na agizo la Mungu wa Israeli+ na kutokana na agizo la Koreshi+ na Dario+ na Artashasta+ mfalme wa Uajemi. 15 Nao wakaimaliza nyumba hii siku ya tatu ya mwezi wa Adari,+ yaani, katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.
16 Nao wana wa Israeli, makuhani na Walawi+ na wengineo wa waliokuwa wahamishwa wa hapo zamani+ wakaizindua+ nyumba hii ya Mungu kwa shangwe. 17 Nao wakaleta kwa ajili ya kuzindua nyumba hii ya Mungu ng’ombe-dume mia moja, kondoo-dume mia mbili, wana-kondoo mia nne, wakatoa mbuzi-dume kumi na wawili kwa ajili ya toleo la dhambi kwa Israeli wote, kulingana na hesabu ya makabila ya Israeli.+ 18 Nao wakaweka makuhani kwa vikundi vyao na Walawi kwa migawanyo yao,+ kwa ajili ya utumishi wa Mungu ulio katika Yerusalemu, kulingana na agizo la kitabu cha Musa.+
19 Na watu hao waliokuwa wahamishwa hapo zamani wakafanya pasaka+ siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.+ 20 Na kwa vile makuhani na Walawi walikuwa wamejitakasa+ wakiwa kikundi kimoja, wote walikuwa safi, basi wakachinja mnyama wa pasaka+ kwa ajili ya waliokuwa wahamishwa hapo zamani na kwa ajili ya ndugu zao makuhani na kwa ajili yao wenyewe. 21 Kisha wana wa Israeli waliokuwa wametoka Uhamishoni wakala,+ na kila mtu aliyekuwa amejitenga na kuja kwao na kuuacha uchafu+ wa mataifa ya hiyo nchi, ili kumtafuta Yehova Mungu wa Israeli.+ 22 Nao wakafanya sherehe za keki zisizo na chachu+ kwa siku saba nao wakashangilia; kwa maana Yehova aliwafanya washangilie, naye alikuwa ameugeuza+ moyo wa mfalme wa Ashuru kuwaelekea ili kuitia nguvu mikono yao katika kazi ya nyumba ya Mungu wa kweli, Mungu wa Israeli.
7 Na baada ya mambo hayo katika utawala wa Artashasta+ mfalme wa Uajemi, Ezra+ mwana wa Seraya+ mwana wa Azaria mwana wa Hilkia+ 2 mwana wa Shalumu+ mwana wa Sadoki mwana wa Ahitubu+ 3 mwana wa Amaria+ mwana wa Azaria+ mwana wa Merayothi+ 4 mwana wa Zeraya+ mwana wa Uzi+ mwana wa Buki+ 5 mwana wa Abishua+ mwana wa Finehasi+ mwana wa Eleazari+ mwana wa Haruni+ mkuu wa makuhani+— 6 huyo Ezra alitoka Babiloni; naye alikuwa mwandikaji stadi+ katika sheria ya Musa,+ ambayo Yehova Mungu wa Israeli alikuwa ametoa, hata mfalme akampa maombi yake yote, kulingana na mkono wa Yehova Mungu wake juu yake.+
7 Kwa hiyo baadhi ya wana wa Israeli na wa makuhani+ na Walawi+ na waimbaji+ na watunza-malango+ na Wanethini+ wakaenda Yerusalemu katika mwaka wa saba wa Mfalme Artashasta.+ 8 Mwishowe akaja Yerusalemu mwezi wa tano, yaani, katika mwaka wa saba wa huyo mfalme. 9 Kwa maana katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza yeye mwenyewe alipanga safari ya kutoka Babiloni, na katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano akaja Yerusalemu, kulingana na mkono mwema wa Mungu wake juu yake.+ 10 Kwa maana Ezra mwenyewe alikuwa ameutayarisha+ moyo wake kutafuta shauri katika sheria ya Yehova+ na kuifanya+ na kufundisha+ sharti+ na haki+ katika Israeli.
11 Na hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alimpa Ezra kuhani, mwandikaji,+ mwandikaji wa maneno ya sheria za Yehova na masharti yake kwa Israeli:
12 “Artashasta,+ mfalme wa wafalme,+ kwa Ezra kuhani, mwandikaji wa sheria ya Mungu wa mbinguni:+ Amani na ikamilishwe.+ Basi 13 mimi nimetoa agizo+ kwamba kila mtu katika utawala wangu+ ambaye ni mmoja wa watu wa Israeli na makuhani wao na Walawi, ambaye yuko tayari kwenda Yerusalemu pamoja nawe, aende.+ 14 Kwa kuwa agizo lilitolewa kutoka mbele ya mfalme na washauri wake saba+ ili kuchunguza+ kuhusu Yuda na Yerusalemu katika sheria+ ya Mungu wako+ iliyo mkononi mwako, 15 na kuleta fedha na dhahabu ambayo mfalme na washauri wake wamejitolea kutoa+ kwa Mungu wa Israeli, ambaye makao yake yako Yerusalemu,+ 16 na fedha na dhahabu yote ambayo utapata katika wilaya yote ya utawala ya Babiloni pamoja na zawadi ya watu+ na makuhani ambao wanatoa kwa hiari kwa nyumba ya Mungu wao,+ iliyoko Yerusalemu; 17 kwa hiyo utanunua kwa pesa hizo mara moja ng’ombe-dume,+ kondoo-dume,+ wana-kondoo+ na matoleo yao ya nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ nawe utavileta kwenye madhabahu ya nyumba ya Mungu wenu,+ iliyoko Yerusalemu.+
18 “Na lolote linaloonekana kuwa jema kwako na kwa ndugu zako kuifanyia ile fedha na dhahabu iliyobaki,+ kulingana na mapenzi+ ya Mungu wenu, fanyeni.+ 19 Na vyombo+ unavyopewa kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wako, uvipeleke vyote mbele za Mungu katika Yerusalemu.+ 20 Na mahitaji mengineyo ya nyumba ya Mungu wako ambayo una wajibu wa kutoa, utayatoa kutoka katika nyumba ya hazina za mfalme.+
21 “Nami mwenyewe, Mfalme Artashasta, nimetoa agizo+ kwa waweka-hazina+ wote walioko ng’ambo ya Mto,+ kwamba kila kitu anachowaomba Ezra+ kuhani, mwandikaji wa sheria ya Mungu wa mbinguni, kitafanywa mara moja, 22 hata kufikia talanta mia moja+ za fedha na vipimo vya kori+ mia moja vya ngano na vipimo vya bathi+ mia moja vya divai+ na vipimo vya bathi mia moja vya mafuta,+ na chumvi+ bila kikomo. 23 Mambo yote yaliyoagizwa+ na Mungu wa mbinguni na yafanywe kwa bidii+ kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa mbinguni,+ ili ghadhabu isije juu ya utawala wa mfalme na wanawe.+ 24 Nanyi mnajulishwa kwamba hairuhusiwi kutoza kodi,+ wala ushuru+ wala ada yoyote juu ya yeyote wa makuhani+ na Walawi,+ wanamuziki,+ watunza-milango,+ Wanethini,+ na wafanyakazi wa hii nyumba ya Mungu.
25 “Na wewe, Ezra, kulingana na hekima+ ya Mungu wako iliyo katika mkono wako, weka mahakimu na waamuzi ili sikuzote wawahukumu+ watu wote walio ng’ambo ya Mto, yaani, wale wote wanaojua sheria za Mungu wako; na kila mtu ambaye hajazijua, ninyi mtamfundisha.+ 26 Na kila mtu ambaye hatatenda sheria ya Mungu wako+ na sheria ya mfalme, na ahukumiwe mara moja, iwe ni kifo+ au ni kufukuzwa,+ au kutozwa pesa+ au kifungo.”
27 Na abarikiwe Yehova Mungu wa mababu zetu,+ ambaye ameweka jambo hili katika moyo+ wa mfalme, kuirembesha+ nyumba ya Yehova, iliyoko Yerusalemu! 28 Naye amenipa fadhili zenye upendo+ mbele ya mfalme na washauri+ wake na kuhusu wakuu wote wa mfalme wenye nguvu. Mimi nami nikajitia nguvu kulingana na mkono+ wa Yehova Mungu wangu juu yangu, nami nikawakusanya wakuu kutoka katika Israeli ili waende pamoja nami.
8 Basi hawa ndio waliokuwa vichwa vya nyumba zao za ukoo wa upande wa baba+ na maandikisho ya kiukoo+ ya wale walioenda nami kutoka Babiloni wakati wa utawala wa Artashasta,+ mfalme: 2 Wa wana wa Finehasi,+ Gershomu; wa wana wa Ithamari,+ Danieli;+ wa wana wa Daudi,+ Hatushi; 3 wa wana wa Shekania, wa wana wa Paroshi,+ Zekaria, na wanaume 150 waliandikishwa pamoja naye; 4 wa wana wa Pahath-moabu,+ Elieho-enai mwana wa Zeraya, na wanaume 200 pamoja naye; 5 wa wana wa Zatu,+ Shekania mwana wa Yahazieli, na wanaume 300 pamoja naye; 6 na wa wana wa Adini,+ Ebedi mwana wa Yonathani, na wanaume 50 pamoja naye; 7 na wa wana wa Elamu,+ Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye; 8 na wa wana wa Shefatia,+ Zebadia mwana wa Mikaeli, na wanaume 80 pamoja naye; 9 wa wana wa Yoabu, Obadia mwana wa Yehieli, na wanaume 218 pamoja naye; 10 na wa wana wa Bani,+ Shelomithi mwana wa Yosifia, na wanaume 160 pamoja naye; 11 na wa wana wa Bebai, Zekaria mwana wa Bebai,+ na wanaume 28 pamoja naye; 12 na wa wana wa Azgadi,+ Yohanani mwana wa Hakatani, na wanaume 110 pamoja naye; 13 na wa wana wa Adonikamu,+ wale waliokuwa wa mwisho, na haya ndiyo yaliyokuwa majina yao: Elifeleti, Yeieli na Shemaya, na wanaume 60 pamoja nao; 14 na wa wana wa Bigvai,+ Uthai na Zabudu, na wanaume 70 pamoja nao.
15 Nami nikawakusanya kwenye mto+ unaokuja Ahava;+ nasi tukaendelea kupiga kambi hapo siku tatu, ili niwakague watu+ na makuhani+ kwa uangalifu, wala sikupata hata mmoja wa wana wa Lawi+ hapo. 16 Kwa hiyo nikatuma waletwe Eliezeri, Arieli, Shemaya na Elnathani na Yaribu na Elnathani na Nathani na Zekaria na Meshulamu, walio vichwa, na Yoyaribu na Elnathani, wafundishaji.+ 17 Kisha nikawapa amri kuhusu Ido aliye kichwa huko Kasifia, nami nikatia maneno katika vinywa+ vyao waseme na Ido na ndugu zake Wanethini+ huko Kasifia, watuletee wahudumu+ kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu. 18 Basi, kulingana na mkono mwema+ wa Mungu wetu juu yetu, wakatuletea mwanamume mwenye busara+ kutoka kwa wana wa Mali+ mjukuu wa Lawi+ mwana wa Israeli, yaani, Sherebia+ na wanawe na ndugu zake, 18; 19 na Hashabia na pamoja naye Yeshaya kutoka kwa wana wa Merari,+ ndugu zake, na wana wao, 20. 20 Na kutoka kwa Wanethini, ambao Daudi na wakuu waliwatoa kwa ajili ya utumishi wa Walawi, Wanethini 220, wote walikuwa wametajwa kwa majina yao.
21 Ndipo nikatangaza kwamba watu wafunge hapo penye mto Ahava, ili tujinyenyekeze+ mbele za Mungu wetu, tutafute kutoka kwake njia iliyo sawa+ kwa ajili yetu na kwa ajili ya watoto wetu+ na kwa ajili ya mali zetu zote. 22 Kwa maana niliona haya kumwomba mfalme jeshi+ na wapanda-farasi+ ili kutusaidia juu ya adui zetu njiani, kwa sababu tulikuwa tumemwambia mfalme: “Mkono+ wa Mungu wetu uko juu ya wote wanaomtafuta kwa wema,+ bali nguvu zake na hasira zake+ ziko juu ya wote wanaomwacha.”+ 23 Basi tukafunga+ na kumwomba+ Mungu wetu kuhusu jambo hilo, naye akakubali maombi+ yetu.
24 Kisha nikatenga kutoka kwa wakuu wa makuhani watu 12, yaani, Sherebia,+ Hashabia,+ na ndugu zao 10 pamoja nao. 25 Nami nikawapimia fedha na dhahabu na vyombo,+ ule mchango ambao mfalme+ na washauri wake+ na wakuu wake na Waisraeli+ wote waliopatikana walikuwa wamechanga kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu. 26 Basi nikapima mikononi mwao talanta 650 za fedha+ na vyombo 100 vya fedha vyenye thamani ya talanta mbili, na talanta 100 za dhahabu, 27 na mabakuli madogo 20 ya dhahabu yenye thamani ya dariki 1,000 na vyombo viwili vya shaba nzuri, nyekundu inayong’aa, bora kama dhahabu.
28 Kisha nikawaambia: “Ninyi ni kitu kitakatifu+ kwa Yehova, na vyombo+ hivi ni kitu kitakatifu, na hii fedha na dhahabu ni toleo la hiari kwa Yehova Mungu wa mababu zenu. 29 Kaeni macho na mlinde mpaka mtakapovipima+ mbele ya wakuu wa makuhani na Walawi na wakuu wa baba za Israeli katika Yerusalemu, katika majumba ya kulia chakula+ ya nyumba ya Yehova.” 30 Nao makuhani na Walawi wakapokea uzito wa fedha na dhahabu na vyombo, ili wavilete Yerusalemu kwenye nyumba ya Mungu wetu.+
31 Mwishowe tukasafiri kutoka mto Ahava+ siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza+ ili kwenda Yerusalemu, na mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye akatukomboa+ kutoka mkononi mwa adui na watu wenye kuvizia njiani. 32 Basi tukafika Yerusalemu+ na kukaa humo siku tatu. 33 Kisha siku ya nne tukapima hiyo fedha na dhahabu+ na vyombo+ katika nyumba ya Mungu wetu na kuviweka mkononi mwa Meremothi+ mwana wa Uriya kuhani na pamoja naye Eleazari mwana wa Finehasi na pamoja naye Yozabadi+ mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui,+ Walawi, 34 kulingana na hesabu na kulingana na kipimo cha kila kitu, halafu uzito wote ukaandikwa wakati huo. 35 Wale waliotoka utekwani, waliokuwa wahamishwa hapo kwanza,+ wenyewe wakamtolea Mungu wa Israeli dhabihu za kuteketezwa,+ ng’ombe-dume+ 12 kwa ajili ya Israeli wote, kondoo-dume+ 96, wana-kondoo dume+ 77, mbuzi-dume 12 kama toleo la dhambi, kila kitu kama toleo la kuteketezwa kwa Yehova.
36 Kisha sheria+ za mfalme tukawapa maliwali+ na magavana+ wa mfalme walio ng’ambo ya Mto,+ nao wakawasaidia watu+ na nyumba ya Mungu wa kweli.
9 Na mara mambo hayo yalipokwisha, wakuu+ wakanikaribia, wakisema: “Watu wa Israeli na makuhani na Walawi hawajajitenga+ na watu wa nchi kuhusiana na machukizo yao,+ yaani, Wakanaani,+ Wahiti,+ Waperizi,+ Wayebusi,+ Waamoni,+ Wamoabu,+ Wamisri+ na Waamori.+ 2 Kwa maana wamekubali baadhi ya binti zao kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya wana wao;+ nao, ule uzao mtakatifu,+ wamechanganyika+ na vikundi vya watu wa nchi, na mkono wa wakuu na watawala-wasaidizi umekuwa wa kwanza+ kabisa katika ukosefu huu wa uaminifu.”
3 Ikawa kwamba mara tu niliposikia jambo hili nilipasua vazi+ na koti langu lisilo na mikono, nami nikaanza kung’oa sehemu ya nywele za kichwa changu+ na za ndevu zangu, nikaendelea kukaa nikiwa nimepigwa na bumbuazi.+ 4 Pia wakaja kujikusanya kwangu, kila mtu akitetemeka+ kwa sababu ya maneno ya Mungu wa Israeli juu ya kukosa uaminifu kwa watu waliohamishwa, nami nikiwa nimeketi huku nimepigwa na bumbuazi mpaka wakati wa toleo la nafaka la jioni.+
5 Na wakati wa toleo la nafaka+ la jioni nikasimama kutoka kwenye fedheha yangu, vazi langu na koti langu likiwa limepasuliwa, kisha nikainama nikapiga magoti+ na kumnyooshea mikono Yehova Mungu wangu.+ 6 Nami nikasema:+ “Ee Mungu wangu, naona aibu+ na haya+ kukuinulia uso wangu, Ee Mungu wangu, kwa maana makosa+ yetu yameongezeka juu ya vichwa vyetu na hatia yetu imeongezeka sana hata kufika mbinguni.+ 7 Tangu siku za mababu zetu+ tumekuwa katika hatia kubwa mpaka leo hii;+ na kwa sababu ya makosa yetu, sisi wenyewe, wafalme wetu,+ makuhani wetu,+ tumetiwa mikononi mwa wafalme wa nchi hizi kwa upanga,+ kwa kutekwa+ na kuporwa+ na kwa aibu ya uso,+ kama ilivyo leo hii. 8 Na sasa kwa muda kidogo kibali+ kutoka kwa Yehova Mungu wetu kimekuja kwa kutuachia wale walioponyoka+ na kwa kutupa sisi kigingi katika mahali pake patakatifu, kufanya macho yetu yang’ae,+ Ee Mungu wetu, na kutuamsha kidogo kutoka katika utumwa wetu.+ 9 Kwa maana sisi ni watumishi;+ na katika utumishi wetu Mungu hakutuacha,+ bali hutupa sisi fadhili zenye upendo mbele ya wafalme wa Uajemi,+ kutuamsha ili tuisimamishe nyumba ya Mungu+ wetu na kurudisha mahali pake palipofanywa ukiwa+ na kutupa sisi ukuta wa mawe+ katika Yuda na katika Yerusalemu.
10 “Na sasa tuseme nini, Ee Mungu wetu, baada ya hayo? Kwa maana tumeziacha amri zako,+ 11 ulizoamuru kupitia watumishi wako manabii, ukisema, ‘Nchi ambayo ninyi mnaingia kuimiliki ni nchi chafu kwa sababu ya uchafu wa watu wa nchi zile,+ kwa sababu ya machukizo yao+ ambayo wamejaza ndani yake kutoka mwisho mpaka mwisho+ kwa uchafu wao.+ 12 Na sasa ninyi msiwape wana wao binti zenu,+ wala binti zao msiwakubali kwa ajili ya wana wenu; nanyi msiwatakie amani wala mafanikio+ mpaka wakati usio na kipimo, ili mpate nguvu+ na mle mema ya nchi na kuimiliki kwa ajili ya wana wenu mpaka wakati usio na kipimo.’+ 13 Na baada ya yote ambayo yamekuja juu yetu kwa sababu ya matendo yetu mabaya+ na hatia yetu kubwa—kwa maana wewe mwenyewe, Ee Mungu wetu, umepunguza uzito wa makosa yetu,+ nawe umetupa sisi wale walioponyoka kama hawa+— 14 je, tena tuanze kuvunja sheria zako kwa kufanya mapatano ya ndoa+ na watu wa machukizo haya?+ Je, hutatukasirikia mpaka mwisho,+ hata kusiwe na yeyote anayebaki+ wala yeyote anayeponyoka? 15 Ee Yehova Mungu wa Israeli, wewe ni mwadilifu,+ kwa maana tumebaki tukiwa watu walioponyoka, kama ilivyo leo hii. Tupo hapa mbele zako katika hatia yetu,+ kwa maana haiwezekani kusimama mbele zako kwa sababu ya jambo hili.”+
10 Ikawa kwamba mara tu Ezra alipokuwa amesali+ na kuungama akilia na kulala kifudifudi+ mbele ya nyumba+ ya Mungu wa kweli, watu wa Israeli wakakusanyika pamoja kwake, kutaniko kubwa sana, wanaume na wanawake na watoto, kwa maana watu hao walikuwa wamelia sana.+ 2 Ndipo Shekania mwana wa Yehieli+ wa wana wa Elamu+ akamwambia Ezra: “Sisi—sisi tumemtendea Mungu wetu kwa njia isiyo ya uaminifu, kwa kuwapa makao wake wa kigeni kutoka kwa vikundi vya watu wa nchi hii.+ Na bado sasa kuna tumaini+ kwa Israeli kuhusu jambo hili. 3 Basi na tufanye agano+ na Mungu wetu tuwaondolee mbali+ wake wote na wale waliozaliwa nao kulingana na shauri la Yehova na la wale wanaotetemeka+ kwa ajili ya sheria+ ya Mungu wetu, ili ifanywe kulingana na sheria.+ 4 Simama, kwa maana jambo hili ni wajibu wako, nasi tuko pamoja nawe. Uwe na nguvu na utende.”
5 Ndipo Ezra akasimama, akawafanya wakuu wa makuhani, Walawi na Israeli wote waape+ kufanya kulingana na neno hilo. Basi wakaapa. 6 Kisha Ezra akasimama kutoka mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli, akaenda katika jumba la kulia chakula+ la Yehohanani mwana wa Eliashibu. Ingawa alienda huko, hakula mkate+ wala kunywa maji, kwa kuwa alikuwa anaomboleza+ juu ya ukosefu wa uaminifu wa watu waliohamishwa.
7 Ndipo wakatangaza mwito kotekote katika Yuda na Yerusalemu ili watu wote waliokuwa wahamishwa hapo zamani+ wakusanyike pamoja huko Yerusalemu; 8 na yeyote ambaye hangekuja+ katika muda wa siku tatu kulingana na shauri la wakuu+ na wanaume wazee—mali zake zote zingepigwa marufuku+ na yeye mwenyewe angetengwa+ kutoka kwenye kutaniko la waliohamishwa. 9 Basi wanaume wote wa Yuda na Benyamini wakakusanyika Yerusalemu katika muda wa siku tatu, yaani, katika mwezi wa 9+ siku ya 20 ya mwezi huo, na watu wote wakaendelea kuketi mahali palipo wazi pa nyumba ya Mungu wa kweli, wakitetemeka kwa sababu ya jambo hilo na kwa sababu ya manyunyu ya mvua.+
10 Mwishowe Ezra kuhani akasimama, akawaambia: “Ninyi wenyewe mmetenda kwa kukosa uaminifu kwa vile mmewapa makao wanawake wa kigeni+ ili kuongezea hatia ya Israeli.+ 11 Na sasa ungameni+ kwa Yehova Mungu wa mababu zenu na kufanya mapenzi yake+ na kujitenga na vikundi vya watu wa nchi hii na wake wa kigeni.”+ 12 Kwa hiyo kutaniko lote likajibu na kusema kwa sauti kubwa: “Tuna wajibu wa kufanya sawasawa na ulivyosema.+ 13 Hata hivyo, watu ni wengi, na haya ni majira ya manyunyu ya mvua, wala haiwezekani kusimama nje; na kazi hii haitachukua siku moja au mbili, kwa maana tumeasi kwa kadiri kubwa katika jambo hili. 14 Basi, tafadhali, wakuu+ wetu na waliwakilishe kutaniko zima; na wale wote walio katika majiji yetu ambao wamewapa makao wake wa kigeni, na waje kwa nyakati zilizowekwa, pamoja na wanaume wazee wa kila jiji moja moja na waamuzi wake, mpaka tuwe tumegeuza kutoka kwetu hasira inayowaka ya Mungu wetu, kwa sababu ya jambo hili.”
15 (Hata hivyo, Yonathani mwana wa Asaheli na Yahzeya mwana wa Tikva wakasimama kupinga+ jambo hilo, na Meshulamu na Shabethai+ Walawi ndio waliowasaidia.) 16 Na hao waliokuwa wahamishwa hapo zamani+ wakafanya hivyo; kisha Ezra kuhani na wanaume waliokuwa vichwa vya upande wa baba kwa ajili ya nyumba zao za ukoo,+ wote kwa majina yao, wakajitenga na kuanza kuketi katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi+ ili kuuliza jambo hilo.+ 17 Hatua kwa hatua wakamaliza mambo ya wale wanaume waliokuwa wamewapa makao wake wa kigeni+ kufikia siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza. 18 Na ikapatikana kwamba baadhi ya wana wa makuhani+ walikuwa wamewapa makao wake wa kigeni; wa wana wa Yeshua+ mwana wa Yehosadaki+ na ndugu zake, Maaseya na Eliezeri na Yaribu na Gedalia. 19 Lakini wakaahidi kwa kupeana mikono kwamba watawafukuza wake zao, na kwamba, kwa kuwa walikuwa na hatia,+ kondoo-dume+ wa kundi atolewe kwa ajili ya hatia yao.
20 Na wa wana wa Imeri+ kulikuwa na Hanani na Zebadia; 21 na wa wana wa Harimu,+ Maaseya na Eliya na Shemaya na Yehieli na Uzia; 22 na wa wana wa Pashuri,+ Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Eleasa. 23 Na wa Walawi, Yozabadi na Shimei na Kelaya (yaani, Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri; 24 na wa waimbaji, Eliashibu; na wa watunza-malango, Shalumu na Telemu na Uri.
25 Na wa Israeli, wa wana wa Paroshi+ kulikuwa na Ramia na Izia na Malkiya na Miyamini na Eleazari na Malkiya na Benaya; 26 na wa wana wa Elamu,+ Matania, Zekaria na Yehieli+ na Abdi na Yeremothi na Eliya; 27 na wa wana wa Zatu,+ Elioenai, Eliashibu, Matania na Yeremothi na Zabadi na Aziza; 28 na wa wana wa Bebai,+ Yehohanani, Hanania, Zabai, Athlai; 29 na wa wana wa Bani, Meshulamu, Maluku na Adaya, Yashubu na Sheali na Yeremothi; 30 na wa wana wa Pahath-moabu,+ Adna na Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli na Binui na Manase; 31 na wa wana wa Harimu,+ Eliezeri, Ishiya, Malkiya,+ Shemaya, Shimeoni, 32 Benyamini, Maluku na Shemaria; 33 na wa wana wa Hashumu,+ Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei; 34 na wa wana wa Bani, Maadai, Amramu na Ueli, 35 Benaya, Bedeya, Keluhi, 36 Vania, Meremothi, Eliashibu, 37 Matania, Matenai na Yaasu; 38 na wa wana wa Binui, Shimei 39 na Shelemia na Nathani na Adaya, 40 Maknadebai, Shashai, Sharai, 41 Azareli na Shelemia, Shemaria, 42 Shalumu, Amaria, Yosefu; 43 wa wana wa Nebo, Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai na Yoeli na Benaya. 44 Hao wote walikuwa wamewachukua wake wa kigeni,+ nao wakawafukuza wake pamoja na wana.