Nehemia
1 Maneno ya Nehemia+ mwana wa Hakalia: Ikawa kwamba katika mwezi wa Kislevu,+ katika mwaka wa 20,+ mimi nilikuwa katika ngome ya Shushani.+ 2 Ndipo Hanani,+ mmoja wa ndugu zangu, akaingia, yeye pamoja na watu wengine kutoka Yuda, nami nikawauliza+ habari za Wayahudi,+ wale walioponyoka,+ mabaki ya wale mateka,+ na pia habari za Yerusalemu. 3 Basi wakaniambia: “Wale waliobaki, ambao wamebaki kutoka utekwani, kule katika wilaya ya utawala,+ wako katika hali mbaya sana+ na katika aibu;+ na ukuta+ wa Yerusalemu umebomoka, na malango+ yake yameteketezwa kwa moto.”
4 Na ikawa kwamba, mara tu niliposikia maneno hayo, nikaketi chini na kuanza kulia na kuomboleza kwa siku kadhaa, nikazidi kufunga+ na kusali mbele za Mungu wa mbinguni.+ 5 Nami nikasema: “Ah, Yehova Mungu wa mbinguni, Mungu mkuu na mwenye kuogopesha,+ anayeshika agano+ na fadhili zenye upendo kuwaelekea wale wanaompenda+ na kushika amri zake,+ 6 tafadhali, tega sikio+ lako na ufungue macho yako, upate kusikiliza sala ya mtumishi wako,+ ambayo ninatoa mbele zako leo, mchana na usiku,+ kuhusu wana wa Israeli watumishi wako, huku nikiungama+ dhambi+ za wana wa Israeli ambazo tumekutendea. Tumetenda dhambi, mimi pamoja na nyumba ya baba yangu.+ 7 Bila shaka tumekutendea kwa upotovu+ wala hatukushika amri+ na masharti+ na maamuzi ya hukumu+ uliyomwamuru Musa mtumishi wako.+
8 “Tafadhali, likumbuke+ lile neno ulilomwamuru Musa mtumishi wako, ukisema, ‘Ikiwa ninyi hamtakuwa waaminifu, mimi nami nitawatawanya kati ya vikundi vya watu.+ 9 Mtakaporudi kwangu+ na kuzishika amri zangu+ na kuzifanya,+ hata watu wenu waliotawanywa wawe katika mwisho wa mbingu, kutoka huko nitawakusanya+ na kuwaleta+ mahali ambapo nimepachagua ili jina langu likae hapo.’+ 10 Nao ni watumishi wako+ na watu wako,+ uliowakomboa kwa uwezo wako mkubwa+ na kwa mkono wako wenye nguvu.+ 11 Ah, tafadhali, Yehova, tega sikio lako kwa sala ya mtumishi wako na kwa sala+ ya watumishi wako wanaofurahia kuliogopa jina lako;+ na, tafadhali, mpe mafanikio mtumishi wako leo+ na kumfanya ahurumiwe mbele ya mtu huyu.”+
Basi mimi nilikuwa mnyweshaji+ wa mfalme.
2 Na ikawa kwamba katika mwezi wa Nisani,+ katika mwaka wa 20+ wa Mfalme Artashasta,+ divai ilikuwa mbele yake, na mimi, kama kawaida, nikaichukua divai hiyo na kumpa mfalme.+ Lakini sikuwa nimepata kuwa na huzuni mbele yake kamwe.+ 2 Kwa hiyo mfalme akaniambia: “Kwa nini uso wako una huzuni+ na wewe si mgonjwa? Hii ni huzuni ya moyo tu.”+ Basi nikaogopa sana.
3 Ndipo nikamwambia mfalme: “Mfalme na aishi mpaka wakati usio na kipimo!+ Kwa nini uso wangu usiwe na huzuni wakati lile jiji,+ nyumba ya makaburi ya mababu zangu,+ limefanywa ukiwa, na malango yake yameteketezwa kwa moto?”+ 4 Naye mfalme akaniambia: “Ni jambo gani hili unalotaka?”+ Mara moja nikasali+ kwa Mungu wa mbinguni.+ 5 Kisha nikamwambia mfalme: “Ikiwa inaonekana vema kwa mfalme,+ na ikiwa mtumishi wako anaonekana mwema mbele yako,+ unitume Yuda, kwenye jiji la makaburi ya mababu zangu, nipate kulijenga upya.”+ 6 Ndipo mfalme akaniambia, huku malkia wake akiwa ameketi kando yake: “Safari yako itachukua muda gani, nawe utarudi wakati gani?” Basi ikaonekana vema+ kwa mfalme kunituma, nilipompa wakati uliowekwa.+
7 Nami nikaendelea kumwambia mfalme: “Ikiwa inaonekana vema kwa mfalme, na nipewe barua+ kwa magavana+ walio ng’ambo ya Mto,+ ili waniruhusu nipite mpaka nifike Yuda; 8 pia barua kwa Asafu mtunzaji wa bustani ya mfalme, ili anipe miti ya kujenga kwa mbao malango ya Ngome+ ya nyumba,+ na kwa ajili ya ukuta+ wa jiji na kwa ajili ya nyumba ambayo nitaingia.” Basi mfalme akanipa barua hizo, kulingana na mkono mwema wa Mungu wangu uliokuwa juu yangu.+
9 Mwishowe nikaja kwa magavana+ walio ng’ambo ya Mto na kuwapa barua za mfalme. Tena mfalme akanituma pamoja na wakuu wa jeshi na wapanda-farasi. 10 Wakati Sanbalati+ Mhoroni+ na Tobia+ yule mtumishi, Mwamoni,+ waliposikia jambo hilo, ndipo likaonekana kuwa baya sana+ kwao kwamba mtu fulani amekuja kuwatafutia mema wana wa Israeli.
11 Mwishowe nikaja Yerusalemu, nikaendelea kukaa huko siku tatu. 12 Kisha nikaondoka usiku, mimi pamoja na wanaume wachache, nami sikumwambia mtu yeyote+ mambo ambayo Mungu wangu alikuwa akiweka katika moyo wangu kuyafanya kwa ajili ya Yerusalemu,+ wala sikuwa na mnyama yeyote wa kufugwa ila yule mnyama wa kufugwa niliyempanda. 13 Nami nikatoka nje usiku kupitia Lango la Bonde+ na mbele ya Chemchemi ya Nyoka Mkubwa na kwenye Lango la Marundo ya Majivu,+ nami nikazidi kuzichunguza kuta+ za Yerusalemu, jinsi zilivyokuwa zimebomolewa na malango+ yake kuteketezwa kwa moto. 14 Nami nikapita kuelekea Lango la Chemchemi+ na kwenye Kidimbwi cha Mfalme, na yule mnyama wa kufugwa aliyekuwa chini yangu hakuwa na mahali pa kupitia. 15 Lakini nikaendelea kupanda katika bonde la mto+ usiku, nami nikaendelea kuuchunguza ukuta; kisha nikarudi na kuingia kupitia Lango la Bonde,+ na kwa hiyo nikarudi.
16 Na wale watawala-wasaidizi+ hawakujua nilikokwenda wala jambo nililokuwa nikifanya; nami bado sikuwa nimewaambia lolote Wayahudi wala makuhani wala watu wenye vyeo wala watawala-wasaidizi wala wale wengine waliofanya kazi hiyo. 17 Mwishowe nikawaambia: “Ninyi mnaona hali mbaya tuliyo nayo, jinsi ambavyo Yerusalemu limeharibiwa na malango yake kuteketezwa kwa moto. Njooni tujenge upya ukuta wa Yerusalemu, ili tusiendelee kuwa kitu cha aibu tena.”+ 18 Nami nikaendelea kuwaambia kuhusu mkono+ wa Mungu wangu, jinsi ulivyokuwa mwema juu yangu,+ na pia kuhusu maneno ya mfalme,+yale aliyoniambia. Ndipo wakasema: “Na twende, tukajenge.” Basi wakaitia mikono yao nguvu kwa ajili ya kazi hiyo njema.+
19 Basi, wakati Sanbalati+ Mhoroni na Tobia+ yule mtumishi,+ Mwamoni,+ na Geshemu+ Mwarabu+ waliposikia jambo hilo, wakaanza kutudhihaki+ na kutudharau wakisema: “Ni nini hili mnalofanya? Je, mnamwasi mfalme?”+ 20 Hata hivyo, nikawajibu, nikawaambia: “Mungu wa mbinguni,+ Yeye ndiye atakayetupatia mafanikio,+ na sisi watumishi wake, tutasimama, nasi tutajenga; lakini ninyi hamna fungu+ lolote, wala dai la haki, wala ukumbusho+ wowote katika Yerusalemu.”
3 Naye Eliashibu+ kuhani mkuu na ndugu zake, makuhani, wakaondoka na kujenga Lango la Kondoo.+ Wao wenyewe walilitakasa+ na kuisimamisha milango yake; wakalitakasa mpaka kwenye Mnara wa Mea,+ mpaka Mnara wa Hananeli.+ 2 Na watu wa Yeriko+ wakajenga kando yao. Naye Zakuri mwana wa Imri akajenga kando yao.
3 Nao wana wa Hasenaa wakajenga Lango la Samaki;+ wao wenyewe wakalijenga kwa mbao+ na kuisimamisha milango+ yake, makomeo yake na mapingo+ yake. 4 Naye Meremothi+ mwana wa Uriya+ mwana wa Hakozi akafanya kazi ya kurekebisha kando yao, naye Meshulamu+ mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli akafanya kazi ya kurekebisha kando yao; naye Sadoki mwana wa Baana akafanya kazi ya kurekebisha kando yao. 5 Nao Watekoa+ wakafanya kazi ya kurekebisha kando yao; lakini watu wao walio mashuhuri+ hawakutia shingo zao katika utumishi wa mabwana zao.
6 Naye Yoyada mwana wa Pasea na Meshulamu mwana wa Besodeya wakarekebisha Lango la Jiji la Kale;+ wao walilijenga kwa mbao na kuisimamisha milango yake na komeo zake na mapingo+ yake. 7 Nao Melatia Mgibeoni+ na Yadoni Mmeronothi,+ wakafanya kazi ya kurekebisha kando yao, watu wa Gibeoni+ na Mispa,+ walio wa kiti cha gavana+ ng’ambo ya Mto.+ 8 Naye Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa mafundi wa dhahabu,+ akafanya kazi ya kurekebisha kando yake; naye Hanania mshiriki wa wachanganyaji wa marhamu+ akafanya kazi ya kurekebisha kando yake; nao wakatandaza mawe katika Yerusalemu mpaka kwenye ule Ukuta Mpana.+ 9 Naye Refaya mwana wa Huru, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akafanya kazi ya kurekebisha kando yao. 10 Naye Yedaya mwana wa Harumafu akafanya kazi ya kurekebisha kando yao mbele ya nyumba yake mwenyewe;+ naye Hatushi mwana wa Hashabneya akafanya kazi ya kurekebisha kando yake.
11 Nao Malkiya mwana wa Harimu+ na Hashubu mwana wa Pahath-moabu+ wakarekebisha sehemu nyingine iliyopimwa, na pia Mnara wa Jiko la Kuokea.+ 12 Naye Shalumu mwana wa Haloheshi, mkuu+ wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akafanya kazi ya kurekebisha kando yake, yeye na binti zake.
13 Hanuni na wakaaji wa Zanoa+ wakarekebisha Lango la Bonde;+ wao wenyewe walilijenga na kuisimamisha milango+ yake, makomeo+ yake na mapingo+ yake, na pia urefu wa mikono elfu moja katika ukuta mpaka kwenye Lango la Marundo ya Majivu.+ 14 Naye Malkiya mwana wa Rekabu mkuu wa wilaya ya Beth-hakeremu+ akarekebisha Lango la Marundo ya Majivu; yeye mwenyewe alilijenga na kuisimamisha milango yake, makomeo yake na mapingo yake.
15 Naye Shaluni mwana wa Kolhoze mkuu wa wilaya ya Mispa,+ akarekebisha Lango la Chemchemi;+ yeye mwenyewe akalijenga na kuliweka paa na kuisimamisha milango+ yake, makomeo yake na mapingo yake, na pia ukuta wa Kidimbwi+ cha Mfereji unaoelekea kwenye Bustani ya Mfalme+ mpaka kwenye Ngazi+ inayoshuka kutoka Jiji la Daudi.+
16 Baada yake Nehemia mwana wa Azbuki, mkuu wa nusu ya wilaya ya Beth-suri,+ akafanya kazi ya kurekebisha mpaka mbele ya Makaburi+ ya Daudi na mpaka kwenye kidimbwi+ ambacho kilikuwa kimetengenezwa na mpaka kwenye Nyumba ya Wenye Nguvu.+
17 Baada yake Walawi+ wakafanya kazi ya kurekebisha, Rehumu mwana wa Bani;+ na kando yake Hashabia, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila,+ akafanya kazi ya kurekebisha kwa ajili ya wilaya yake. 18 Baada yake ndugu zao wakafanya kazi ya kurekebisha, Bavai mwana wa Henadadi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila.
19 Naye Ezeri mwana wa Yeshua,+ mkuu wa Mispa,+ akarekebisha kando yake sehemu nyingine iliyopimwa mbele ya mahali pa kupandia kwenda katika Ghala la Silaha karibu na Nguzo.+
20 Baada yake Baruku mwana wa Zabai+ akafanya kazi kwa bidii+ na kurekebisha sehemu nyingine iliyopimwa, kutoka kwenye Nguzo mpaka lango la nyumba ya Eliashibu,+ kuhani mkuu.
21 Baada yake Meremothi mwana wa Uriya+ mwana wa Hakozi akarekebisha sehemu nyingine iliyopimwa, kutoka lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu.
22 Na baada yake makuhani, watu wa Wilaya ya Yordani,+ wakafanya kazi ya kurekebisha. 23 Baada yao Benyamini na Hashubu wakafanya kazi ya kurekebisha mbele ya nyumba yao wenyewe. Baada yao Azaria mwana wa Maaseya mwana wa Ananiya akafanya kazi ya kurekebisha karibu na nyumba yake mwenyewe. 24 Baada yake Binui mwana wa Henadadi akarekebisha sehemu nyingine iliyopimwa, kutoka nyumba ya Azaria mpaka kwenye Nguzo+ na mpaka pembeni.
25 Baada yake Palali mwana wa Uzai akafanya kazi ya kurekebisha mbele ya Nguzo na mnara unaotoka katika Nyumba ya Mfalme,+ ule wa juu ambao ni wa Ua wa Walinzi.+ Baada yake kulikuwa na Pedaya mwana wa Paroshi.+
26 Nao Wanethini+ walikuwa wakaaji wa Ofeli;+ walifanya kazi ya kurekebisha mpaka mbele ya Lango la Maji+ upande wa mashariki na mnara wenye kutokeza.
27 Baada yao Watekoa+ wakarekebisha sehemu nyingine iliyopimwa, kutoka mbele ya ule mnara mkubwa wenye kutokeza mpaka kwenye ukuta wa Ofeli.
28 Makuhani wakafanya kazi ya kurekebisha juu ya Lango la Farasi,+ kila mmoja mbele ya nyumba yake mwenyewe.
29 Baada yao Sadoki+ mwana wa Imeri akafanya kazi ya kurekebisha mbele ya nyumba yake mwenyewe.
Na baada yake Shemaya mwana wa Shekania, mtunzaji wa Lango la Mashariki,+ akafanya kazi ya kurekebisha.
30 Baada yake Hanania mwana wa Shelemia na Hanuni mwana wa sita wa Zalafu wakarekebisha sehemu nyingine iliyopimwa.
Baada yake Meshulamu+ mwana wa Berekia akafanya kazi ya kurekebisha mbele ya jumba+ lake mwenyewe.
31 Baada yake Malkiya, mshiriki wa chama cha mafundi wa dhahabu,+ akafanya kazi ya kurekebisha mpaka kwenye nyumba ya Wanethini+ na wafanya-biashara,+ mbele ya Lango la Ukaguzi na mpaka kwenye chumba cha dari cha pembeni.
32 Na kati ya chumba cha dari cha pembeni na Lango la Kondoo,+ mafundi wa dhahabu na wafanya-biashara wakafanya kazi ya kurekebisha.
4 Basi ikawa kwamba, mara tu Sanbalati+ aliposikia tunajenga upya ukuta, alikasirika+ na kuudhika sana, naye akazidi kuwadhihaki+ Wayahudi. 2 Akaanza kusema mbele ya ndugu zake+ na jeshi la Samaria, ndiyo, akasema: “Hawa Wayahudi wanyonge wanafanya nini? Je, watajitegemea wenyewe? Je, watatoa dhabihu?+ Je, watamaliza katika siku moja? Je, watafufua mawe kutoka kwenye marundo ya takataka+ chafu ingawa yameungua?”
3 Basi Tobia+ Mwamoni+ alikuwa kando yake, naye akasema: “Hata wanachokijenga, mbweha+ akipanda juu yake, ataubomoa ukuta wao wa mawe.”
4 Sikiliza,+ Ee Mungu wetu, kwa maana tumedharauliwa;+ na uzirudishe shutuma+ zao juu ya vichwa vyao wenyewe, nawe uwatoe waporwe katika nchi ya utekwani. 5 Wala usifunike kosa+ lao na dhambi yao kutoka mbele zako. Lisifutiliwe mbali, kwa maana wamewakosea wajenzi.
6 Basi tukaendelea kujenga ukuta, kisha ukuta mzima ukaungana kufikia nusu ya kimo chake, watu nao wakaendelea kuwa na moyo wa kufanya kazi.+
7 Basi ikawa kwamba, mara tu Sanbalati+ na Tobia+ na Waarabu+ na Waamoni+ na Waashdodi+ waliposikia kwamba kazi ya kurekebisha kuta za Yerusalemu imesonga mbele, kwa maana mashimo yalikuwa yameanza kuzibwa, wakakasirika sana. 8 Ndipo wote wakaanza kupanga hila+ pamoja ili kuja kupiga vita juu ya Yerusalemu na kunisumbua. 9 Lakini sisi tulisali+ kwa Mungu wetu na kuweka ulinzi mchana na usiku kwa sababu yao.
10 Na Yuda wakaanza kusema: “Nguvu za mbeba-mizigo+ zimefifia, na kuna takataka+ nyingi sana; nasi hatuna uwezo wa kuendelea kujenga ukuta.”
11 Tena adui zetu wakazidi kusema: “Hawatajua+ wala hawataona mpaka tuwe tumeingia katikati yao, nasi tutawaua na kuikomesha kazi.”
12 Na ikawa kwamba, kila mara Wayahudi wanaokaa karibu nao walipoingia, wakatuambia mara kumi: “Wao watakuja kutoka mahali pote ambapo ninyi mtarudi kwetu sisi.”
13 Basi nikaweka wanaume mahali pa chini zaidi nyuma ya ukuta katika mahali palipo wazi, nami nikaweka watu kulingana na familia zao wakiwa na panga+ zao, mikuki+ yao na pinde zao. 14 Nilipoona woga wao, mara moja nikasimama na kuwaambia watu wenye vyeo+ na watawala-wasaidizi+ na wale watu wengine: “Msiogope+ kwa sababu yao. Mkumbukeni Yehova, Yeye ambaye ni mkuu+ na Mwenye kuogopesha;+ na mpigane kwa ajili ya ndugu zenu,+ wana wenu na binti zenu, wake zenu na nyumba zenu.”
15 Basi ikawa kwamba, mara tu adui zetu waliposikia tumekwisha kujua, na ya kuwa Mungu wa kweli amevunja shauri+ lao, nasi sote tumerudi kwenye ukuta, kila mtu kwenye kazi yake, 16 ndiyo, ikawa kwamba tangu siku hiyo na kuendelea nusu ya wanaume wangu vijana+ walikuwa wakifanya kazi na nusu yao walikuwa wanashika mikuki, ngao, pinde na mavazi ya chuma;+ na wakuu+ walikuwa nyuma ya nyumba nzima ya Yuda. 17 Na kuhusu wajenzi walio juu ya ukuta na wale waliochukua mizigo ya wachukuzi, kila mmoja alikuwa akifanya kazi kwa mkono wake mmoja, na mkono wa pili+ ukiwa umeshika silaha.+ 18 Na wajenzi walikuwa wamejifunga, kila mmoja upanga wake kiunoni+ mwake, wakijenga;+ na yule wa kupiga baragumu+ alikuwa kando yangu.
19 Nami nikawaambia watu wenye vyeo na watawala-wasaidizi+ na wale watu wengine: “Kazi hii ni kubwa na nzito, nasi tumetawanyika kwenye ukuta kila mtu akiwa mbali na mwingine. 20 Mahali mtakaposikia sauti ya baragumu, mtajikusanya hapo tulipo sisi. Mungu wetu mwenyewe atatupigania.”+
21 Tulipokuwa tukifanya kazi, nusu ya wale wengine walikuwa wameshika mikuki, tangu mapambazuko mpaka kutokea kwa nyota. 22 Zaidi ya hayo, nikawaambia watu wakati huo: “Wanaume na wakae usiku katikati ya Yerusalemu,+ kila mmoja na mtumishi wake, nao wawe walinzi wetu wakati wa usiku na wafanyakazi wakati wa mchana.” 23 Lakini kunihusu mimi+ na ndugu zangu+ na watumishi+ wangu na walinzi+ waliokuwa nyuma yangu, hatukuwa tukivua mavazi yetu, kila mmoja alikuwa na silaha+ yake katika mkono wake wa kuume.
5 Hata hivyo, kulitokea kilio+ kikubwa cha watu na wake zao juu ya ndugu zao Wayahudi.+ 2 Na wengine wao walikuwa wakisema: “Tunatoa wana wetu na binti zetu kuwa rehani ili tupate nafaka, tule na tuishi.”+ 3 Wengine nao walikuwa wakisema: “Tunatoa mashamba yetu na mizabibu yetu na nyumba zetu kuwa rehani+ ili tupate nafaka wakati wa upungufu wa chakula.” 4 Wengine nao walikuwa wakisema: “Tumekopa pesa kwa ajili ya ushuru+ wa mfalme juu ya mashamba yetu na mizabibu yetu.+ 5 Na sasa jamaa zetu ni sawa na jamaa za ndugu zetu;+ wana wetu ni sawa na wana wao, lakini tazama, tunawashusha wana wetu na binti zetu kuwa watumwa,+ na tayari wengine kati ya binti zetu wamefanywa watumwa; wala hakuna nguvu mikononi mwetu kwa kuwa mashamba yetu na mizabibu yetu imekuwa ya wengine.”
6 Basi nikakasirika sana mara tu niliposikia kilio chao na maneno hayo. 7 Kwa hiyo moyo wangu ukatafakari ndani yangu, nami nikaanza kuwalaumu+ watu wenye vyeo na watawala-wasaidizi, na kuwaambia: “Mnatoza riba,+ kila mmoja kutoka kwa ndugu yake mwenyewe.”
Pia nikapanga kusanyiko kubwa kwa sababu yao.+ 8 Nami nikawaambia: “Sisi wenyewe tumewanunua+ ndugu zetu Wayahudi waliouzwa kwa mataifa, kwa kadiri ya uwezo wetu; je, wakati uleule ninyi mtawauza ndugu zenu,+ na je, wauzwe kwetu?” Ndipo wakanyamaza kimya, wala hawakupata neno lolote la kusema.+ 9 Nami nikaendelea kusema: “Jambo hili mnalofanya si zuri.+ Je, hampaswi kutembea kwa kumwogopa+ Mungu+ kwa sababu ya shutuma+ za mataifa, adui zetu?+ 10 Na pia mimi, ndugu zangu na watumishi wangu tunatoa pesa na nafaka kwa mkopo kati yao. Tafadhali, tuache kukopesha kwa faida.+ 11 Tafadhali, warudishieni leo mashamba yao,+ mizabibu yao, mizeituni na nyumba zao, na kiasi cha sehemu moja kwa mia cha pesa na nafaka, divai mpya na mafuta mnachowatoza kama faida.”
12 Ndipo wakasema: “Tutarudisha,+ wala hatutataka chochote kutoka kwao.+ Tutafanya sawasawa na unavyosema.”+ Basi nikawaita makuhani na kuwaapisha watende kulingana na neno hilo.+ 13 Pia, nikakung’uta vazi kifuani pangu, nikasema: “Mungu wa kweli na amkung’ute hivi kutoka nyumbani mwake na kutoka katika mali yake kila mtu ambaye hatendi jambo hilo; mtu huyo na akung’utwe hivi na kuwa tupu.” Ndipo kutaniko lote wakasema: “Amina!”+ Nao wakaanza kumsifu Yehova.+ Na watu wakafanya kulingana na neno hilo.+
14 Jambo lingine ni kwamba: Tangu siku aliponiweka kuwa gavana+ wao katika nchi ya Yuda, kutoka mwaka wa 20+ mpaka mwaka wa 32+ wa Mfalme Artashasta,+ miaka 12, mimi na ndugu zangu hatukula mkate ambao ni haki ya gavana.+ 15 Na kuhusu wale magavana waliokuwa kabla yangu, walikuwa wamewalemea watu, nao walikuwa wakichukua kutoka kwao kila siku shekeli 40 za fedha kwa ajili ya mkate na divai. Pia, watumishi wao waliwaonea watu.+ Bali mimi sikufanya hivyo+ kwa sababu ya kumwogopa Mungu.+
16 Na zaidi ya hayo, mimi nilishiriki katika kazi ya kujenga ukuta huu,+ nasi hatukuchukua hata shamba moja;+ na watumishi wangu wote walikusanyika hapo kwa ajili ya kazi hiyo. 17 Na Wayahudi na watawala-wasaidizi, watu 150, na wale waliokuwa wanatujia kutoka kwa mataifa yaliyotuzunguka walikuwa mezani pangu.+ 18 Na kile kilichoandaliwa kila siku, ng’ombe-dume mmoja, kondoo bora sita na ndege waliandaliwa kwa ajili yangu, halafu kila namna ya divai+ ikaandaliwa kwa wingi mara moja kila baada ya siku kumi. Na pamoja na hayo sikutaka mkate ulio haki ya gavana, kwa maana kazi ya utumishi juu ya watu hawa ilikuwa yenye kulemea. 19 Ukumbuke kwa ajili yangu,+ Ee Mungu wangu, kwa wema,+ yote ambayo nimefanya kwa ajili ya watu hawa.+
6 Basi ikawa kwamba, mara tu Sanbalati+ na Tobia+ na Geshemu+ Mwarabu+ na wale adui zetu wengine walipoambiwa kuwa nimejenga upya ukuta+ na kwamba hakuna shimo lolote limebaki ndani yake (ingawa kufikia wakati huo sikuwa nimeisimamisha milango+ katika malango),+ 2 Sanbalati na Geshemu wakanitumia neno mara moja, wakisema: “Njoo, tukutane+ pamoja kwa mapatano katika vijiji vya nchi tambarare ya bondeni ya Ono.”+ Lakini walikuwa wanapanga kuniumiza.+ 3 Kwa hiyo nikawatumia wajumbe,+ nikisema: “Kazi ninayofanya ni kubwa,+ nami siwezi kushuka. Kwa nini kazi isimame kwa kuiacha ili nije kwenu?”+ 4 Hata hivyo, wakanitumia neno lilelile mara nne, nami nikazidi kuwajibu neno lilelile.
5 Mwishowe Sanbalati+ akatuma mtumishi wake akiwa na neno lilelile mara ya tano, pamoja na barua iliyokuwa wazi mkononi mwake. 6 Humo ilikuwa imeandikwa hivi: “Imesemwa katika mataifa, na Geshemu+ anasema, kwamba wewe pamoja na Wayahudi mnapanga kuasi.+ Ndiyo sababu unajenga ukuta; nawe unataka kuwa mfalme kwao,+ kulingana na maneno hayo. 7 Hata kuna manabii ambao umeweka ili wakutangaze wewe kotekote Yerusalemu, wakisema, ‘Kuna mfalme katika Yuda!’ Na sasa mfalme ataambiwa mambo hayo. Basi njoo, tushauriane pamoja.”+
8 Hata hivyo, nikamtumia neno, nikisema: “Mambo kama hayo unayosema hayajatokea,+ bali unayatunga moyoni mwako mwenyewe.”+ 9 Kwa kuwa wote walikuwa wakijaribu kututia woga, wakisema: “Mikono+ yao italegea waache kazi, hivi kwamba haitafanywa.” Lakini sasa itie mikono yangu nguvu.+
10 Nami nikaingia nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya mwana wa Mehetabeli, naye alikuwa amejifungia+ kabisa. Akasema: “Tukutane kwa mapatano+ katika nyumba ya Mungu wa kweli, ndani ya hekalu,+ halafu tufunge milango ya hekalu; kwa maana wanakuja kukuua, ndiyo, watakuja kukuua usiku.”+ 11 Lakini nikasema: “Je, mwanamume kama mimi anapaswa kukimbia?+ Na ni nani kama mimi anayeweza kuingia hekaluni kisha akaishi?+ Sitaingia!” 12 Kwa hiyo nikachunguza, na tazama, si Mungu+ aliyemtuma, bali alitoa+ unabii huo juu yangu kwa vile Tobia na Sanbalati+ walikuwa wamemlipa.+ 13 Kwa sababu hii alikuwa amelipwa+ ili niogope+ na kufanya hivyo, nami nitende dhambi,+ ili wawe na nafasi ya kueneza sifa mbaya juu yangu,+ wapate kunishutumu.+
14 Wakumbuke+ Tobia+ na Sanbalati, Ee Mungu wangu, kulingana na matendo hayo ya kila mmoja wao, na pia Noadia nabii wa kike+ na wale manabii wengine walioendelea kujaribu kunitia woga.
15 Mwishowe ukuta+ ukakamilika siku ya 25 ya mwezi wa Eluli, katika muda wa siku 52.
16 Na ikawa kwamba, mara tu adui zetu+ waliposikia jambo hilo na mataifa yote yaliyotuzunguka kuona jambo hilo, mara moja wakaona aibu sana machoni pao wenyewe, nao wakatambua kwamba kazi hii ilifanywa kutokana na msaada wa Mungu wetu.+ 17 Katika siku hizo pia watu wenye vyeo+ wa Yuda walikuwa wakimtumia Tobia+ barua nyingi, na zile za Tobia zilikuwa pia zikiwafikia. 18 Kwa maana wengi katika Yuda walikuwa wamejiapisha kwake, kwa vile alikuwa mwana-mkwe wa Shekania mwana wa Ara;+ naye Yehohanani mwana wake alikuwa amemchukua binti ya Meshulamu+ mwana wa Berekia. 19 Pia, walizidi kusema mambo mema kumhusu yeye mbele yangu.+ Nao wakazidi kumpelekea maneno yangu. Kulikuwa na barua ambazo Tobia alituma ili kunitia woga.+
7 Na ikawa kwamba, mara tu ukuta ulipojengwa upya,+ nikaisimamisha milango+ yake mara moja. Kisha watunza-malango+ na waimbaji+ na Walawi+ wakawekwa rasmi. 2 Nami nikaweka usimamizi wa Yerusalemu chini ya Hanani ndugu yangu na Hanania+ mkuu wa Ngome,+ kwa maana alikuwa mwanamume mwenye kutegemeka+ sana naye alimwogopa+ Mungu wa kweli kuliko wengine wengi. 3 Basi nikawaambia: “Malango+ ya Yerusalemu hayapaswi kufunguliwa mpaka jua liwake kabisa; nao waifunge milango na kuiweka komeo+ wao wakiwa wamesimama kando. Nanyi wekeni walinzi wa wakaaji wa Yerusalemu, kila mmoja katika kituo chake mwenyewe cha ulinzi na kila mmoja mbele ya nyumba yake mwenyewe.”+ 4 Basi jiji lilikuwa pana na kubwa, na kulikuwa na watu wachache ndani yake,+ wala hakukuwa na nyumba zozote zilizojengwa.
5 Lakini Mungu wangu akaweka wazo moyoni+ mwangu kwamba nikusanye watu wenye vyeo na watawala-wasaidizi na watu ili wajiandikishe kiukoo.+ Ndipo nikakipata kitabu cha uandikishaji wa kiukoo+ cha wale waliokuja pale mwanzoni, na ndani nikakuta imeandikwa:
6 Hawa ndio wana wa wilaya ya utawala+ waliokuja kutoka utekwani+ mwa wale waliohamishwa ambao Nebukadneza+ mfalme wa Babiloni alikuwa amewapeleka uhamishoni,+ na ambao baadaye walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye jiji lake mwenyewe;+ 7 wale waliokuja pamoja na Zerubabeli,+ Yeshua,+ Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai,+ Bilshani, Misperethi, Bigvai, Nehumu, Baana.
Hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli: 8 Wana wa Paroshi,+ 2,172; 9 wana wa Shefatia,+ 372; 10 wana wa Ara,+ 652; 11 wana wa Pahath-moabu,+ wa wana wa Yeshua na Yoabu,+ 2,818; 12 wana wa Elamu,+ 1,254; 13 wana wa Zatu,+ 845; 14 wana wa Zakai,+ 760; 15 wana wa Binui,+ 648; 16 wana wa Bebai,+ 628; 17 wana wa Azgadi,+ 2,322; 18 wana wa Adonikamu,+ 667; 19 wana wa Bigvai,+ 2,067; 20 wana wa Adini,+ 655; 21 wana wa Ateri,+ wa Hezekia, 98; 22 wana wa Hashumu,+ 328; 23 wana wa Besai,+ 324; 24 wana wa Harifu,+ 112; 25 wana wa Gibeoni,+ 95; 26 wanaume wa Bethlehemu+ na Netofa,+ 188; 27 wanaume wa Anathothi,+ 128; 28 wanaume wa Beth-azmavethi,+ 42; 29 wanaume wa Kiriath-yearimu,+ Kefira+ na Beerothi,+ 743; 30 wanaume wa Rama+ na Geba,+ 621; 31 wanaume wa Mikmasi,+ 122; 32 wanaume wa Betheli+ na Ai,+ 123; 33 wanaume wa ile Nebo+ nyingine, 52; 34 wana wa ile Elamu+ nyingine, 1,254; 35 wana wa Harimu,+ 320; 36 wana wa Yeriko,+ 345; 37 wana wa Lodi,+ Hadidi+ na Ono,+ 721; 38 wana wa Senaa,+ 3,930.
39 Makuhani: Wana wa Yedaya+ wa nyumba ya Yeshua, 973; 40 wana wa Imeri,+ 1,052; 41 wana wa Pashuri,+ 1,247; 42 wana wa Harimu,+ 1,017.
43 Walawi: Wana wa Yeshua, wa Kadmieli,+ wa wana wa Hodeva,+ 74; 44 Waimbaji,+ wana wa Asafu,+ 148. 45 Watunza-malango,+ wana wa Shalumu,+ wana wa Ateri, wana wa Talmoni,+ wana wa Akubu,+ wana wa Hatita, wana wa Shobai,+ 138.
46 Wanethini:+ Wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi,+ 47 wana wa Kerosi, wana wa Sia, wana wa Padoni,+ 48 wana wa Lebana, wana wa Hagaba,+ wana wa Salmai, 49 wana wa Hanani,+ wana wa Gideli, wana wa Gahari, 50 wana wa Reaya,+ wana wa Resini,+ wana wa Nekoda, 51 wana wa Gazamu, wana wa Uza, wana wa Pasea, 52 wana wa Besai,+ wana wa Meunimu, wana wa Nefushesimu,+ 53 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri,+ 54 wana wa Baslithi, wana wa Mehida, wana wa Harsha,+ 55 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema,+ 56 wana wa Nezia, wana wa Hatifa.+
57 Wana wa watumishi wa Sulemani:+ Wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Perida,+ 58 wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli,+ 59 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-hazebaimu, wana wa Amoni.+ 60 Wanethini+ wote na wana wa watumishi wa Sulemani walikuwa 392.
61 Na hawa ndio waliotoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubi, Adoni na Imeri,+ nao hawakuweza kujua nyumba ya baba zao wala uzao wao, kama walikuwa wa Israeli: 62 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda,+ 642. 63 Na wa makuhani:+ wana wa Habaya, wana wa Hakozi,+ wana wa Barzilai,+ aliyechukua mke kutoka kati ya binti za Barzilai+ Mgileadi naye akaitwa kwa jina lao. 64 Hao ndio wale waliotafuta kitabu chao cha kuandikisha, ili kuthibitisha ukoo wao waziwazi, nacho hakikupatikana,+ basi wakazuiwa wasiwe katika ukuhani kwa kuwa walikuwa najisi.+ 65 Basi huyo Tirshatha+ akawaambia kwamba hawapaswi kula+ vitu vitakatifu zaidi mpaka kuhani mwenye Urimu+ na Thumimu+ asimame.
66 Kutaniko zima likiwa kundi moja lilikuwa watu 42,360,+ 67 zaidi ya hao watumwa+ wao na vijakazi wao, ambao walikuwa 7,337;+ nao walikuwa na waimbaji 245, wa kiume+ na wa kike.+ 68 Farasi zao walikuwa 736, nyumbu zao 245.+ 69 Ngamia walikuwa 435. Punda+ walikuwa 6,720.+
70 Na kulikuwa na sehemu fulani ya vichwa+ vya nyumba za ukoo wa upande wa baba+ waliotoa vitu kwa ajili ya kazi.+ Huyo Tirshatha+ mwenyewe alitoa kwa ajili ya hazina drakma 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, kanzu 530 za makuhani.+ 71 Na palikuwa na sehemu fulani ya vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba waliotoa kwa ajili ya hazina ya kazi drakma 20,000 za dhahabu na mina 2,200 za fedha.+ 72 Na watu wale wengine walitoa drakma 20,000 za dhahabu na mina 2,000 za fedha na kanzu 67 za makuhani.
73 Na makuhani+ na Walawi na watunza-malango na waimbaji+ na wengine kati ya watu na Wanethini+ na Israeli wote wakaanza kukaa katika majiji yao.+ Mwezi wa saba ulipofika,+ tayari wana wa Israeli walikuwa katika majiji yao.+
8 Na watu wote wakajikusanya kama mtu mmoja+ katika kiwanja cha watu wote+ kilichokuwa mbele ya Lango la Maji.+ Ndipo wakamwambia Ezra+ mwandikaji akilete kitabu+ cha sheria ya Musa,+ ambayo Yehova alikuwa ameamuru Israeli.+ 2 Basi Ezra kuhani+ akaleta sheria mbele ya kutaniko+ la wanaume na la wanawake na vilevile la wote wenye akili ya kutosha kuweza kusikiliza,+ katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba.+ 3 Naye akaendelea kusoma+ ndani ya kile kitabu kwa sauti mbele ya kiwanja cha watu wote kilichoko mbele ya Lango la Maji, kuanzia mapambazuko+ mpaka katikati ya mchana, mbele ya wanaume na wanawake na mbele ya wale wengine wenye akili; na watu wote wakasikiliza+ kwa makini+ kitabu cha sheria. 4 Na Ezra mwandikaji akaendelea kusimama juu ya jukwaa+ la mbao, ambalo walikuwa wametengeneza kwa ajili ya pindi hiyo; na kando yake kwenye mkono wake wa kuume walisimama Matithia na Shema na Anaya na Uria na Hilkia na Maaseya, na upande wake wa kushoto Pedaya na Mishaeli na Malkiya+ na Hashumu+ na Hash-badana, Zekaria na Meshulamu.
5 Naye Ezra akakifungua+ kitabu mbele ya macho ya watu wote, kwa maana alikuwa juu ya watu wote; naye alipokifungua, watu wote wakasimama.+ 6 Ndipo Ezra akambariki Yehova+ Mungu wa kweli, Yeye aliye mkuu, halafu watu wote wakajibu, “Amina! Amina!”+ kwa kuinua juu mikono+ yao. Kisha wakainama+ na kumsujudia Yehova kifudifudi.+ 7 Naye Yeshua na Bani na Sherebia,+ Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi,+ Hanani, Pelaya,+ hata Walawi, walikuwa wakiwafafanulia watu sheria,+ hao watu wakiwa wamesimama.+ 8 Wakaendelea kusoma+ kwa sauti katika kitabu hicho, katika sheria ya Mungu wa kweli, nayo ikafafanuliwa, na kuelezwa maana yake; nao wakaendelea kufafanua usomaji huo.+
9 Na Nehemia,+ yaani, huyo Tirshatha,+ na Ezra+ kuhani, mwandikaji, na Walawi waliokuwa wakiwafundisha watu wakawaambia watu wote: “Leo ni siku takatifu kwa Yehova Mungu wenu.+ Msiomboleze wala kulia.”+ Kwa maana watu wote walikuwa wakilia walipokuwa wakisikiliza maneno ya sheria.+ 10 Naye akaendelea kuwaambia: “Nendeni, mle vitu vinono na kunywa vitu vitamu, nanyi mkampelekee mafungu+ ya vitu yule ambaye hakutayarishiwa kitu; kwa maana leo ni siku takatifu kwa Bwana wetu, wala msiwe na uchungu, kwa maana shangwe ya Yehova ndiyo ngome yenu.” 11 Na Walawi walikuwa wanawaamuru watu wote wanyamaze, wakisema: “Nyamazeni! kwa maana leo ni siku takatifu; wala msiwe na uchungu.” 12 Basi watu wote wakaenda zao kula na kunywa na kupeleka mafungu+ ya vitu na kushangilia sana,+ kwa maana walikuwa wameelewa maneno ambayo walijulishwa.+
13 Na katika siku ya pili vichwa vya upande wa baba vya watu wote, makuhani na Walawi, wakajikusanya kwa Ezra mwandikaji, ili kupata ufahamu katika yale maneno ya sheria.+ 14 Ndipo wakapata imeandikwa katika sheria kwamba Yehova alikuwa ameamuru kupitia Musa+ kwamba wana wa Israeli wakae katika vibanda+ wakati wa sherehe katika mwezi wa saba,+ 15 na kwamba watangaze+ na kutoa mwito katika majiji yao yote na kotekote katika Yerusalemu,+ wakisema: “Nendeni katika eneo lenye milima,+ mlete majani ya mizeituni+ na majani ya miti ya mafuta na majani ya mihadasi na majani ya mitende na majani ya miti yenye matawi ili kujenga vibanda, kulingana na yale ambayo yameandikwa.”
16 Basi watu wakaenda na kuleta majani hayo na kujijengea vibanda, kila mmoja juu ya paa+ yake mwenyewe na katika nyua zao na katika nyua+ za nyumba ya Mungu wa kweli na katika kiwanja cha watu wote+ cha Lango la Maji+ na katika kiwanja cha watu wote cha Lango la Efraimu.+ 17 Basi kutaniko lote la wale waliorudi kutoka utekwani wakajenga vibanda na kuanza kukaa katika vibanda hivyo; kwa maana wana wa Israeli hawakuwa wamefanya hivyo tangu siku za Yoshua mwana wa Nuni+ mpaka siku hiyo, hivi kwamba kukawa na shangwe kubwa sana.+ 18 Na kitabu cha sheria ya Mungu wa kweli kikasomwa kwa sauti kubwa siku baada ya siku,+ tangu siku ya kwanza mpaka siku ya mwisho; nao wakaendelea kufanya sherehe hiyo siku saba; na katika siku ya nane kukawa na kusanyiko kuu, kulingana na ile kanuni.+
9 Na katika siku ya 24 ya mwezi huu+ wana wa Israeli wakakusanyika, wakifunga+ na kuvaa nguo za magunia+ na mavumbi+ juu yao. 2 Nao uzao wa Israeli wakajitenga+ na wageni+ wote, wakasimama na kuungama+ dhambi zao wenyewe+ na makosa ya baba zao.+ 3 Kisha wakasimama mahali pao+ na kusoma kwa sauti katika kitabu cha sheria+ ya Yehova Mungu wao kwa muda wa saa tatu wakati wa mchana;+ na kwa muda wa saa tatu nyingine walikuwa wakiungama+ na kumwinamia Yehova Mungu wao.+
4 Nao Yeshua na Bani, Kadmieli, Shebania,+ Buni, Sherebia, Bani na Kenani wakapanda kwenye jukwaa+ la Walawi na kupaaza sauti kubwa+ kwa Yehova Mungu wao. 5 Nao Walawi, Yeshua na Kadmieli, Bani, Hashabneya, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni, mbarikini+ Yehova Mungu wenu milele na milele.+ Na walibariki jina lako tukufu,+ ambalo limeinuliwa juu ya baraka na sifa zote.
6 “Wewe peke yako ndiye Yehova;+ wewe mwenyewe umezifanya mbingu,+ hata mbingu za mbingu, na jeshi lao lote,+ dunia+ na vyote vilivyo juu yake,+ bahari+ na vyote vilivyomo;+ nawe unavihifadhi vyote hai; na jeshi+ la mbinguni linakuinamia wewe. 7 Wewe ndiye Yehova Mungu wa kweli, uliyemchagua Abramu+ na kumleta kutoka Uru la Wakaldayo+ na kulifanya jina lake kuwa Abrahamu.+ 8 Nawe ukaona moyo wake kuwa ni mwaminifu mbele zako;+ basi ukafanya lile agano+ pamoja na yeye ili umpe nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori na Waperizi na Wayebusi na Wagirgashi, kuupa uzao wake;+ nawe ukatimiza maneno yako, kwa maana wewe ni mwadilifu.+
9 “Kwa hiyo ukaona+ mateso ya mababu zetu huko Misri, nawe ukasikia+ kilio chao kwenye Bahari Nyekundu. 10 Ndipo ukatoa ishara na miujiza juu ya Farao na watumishi wake wote na watu wote wa nchi yake,+ kwa maana ulijua kwamba walitenda kwa kimbelembele+ juu yao; nawe ukajifanyia jina+ kama ilivyo leo hii. 11 Nawe ukapasua+ bahari mbele yao, nao wakavuka katikati ya bahari juu ya nchi kavu;+ na wale waliokuwa wakiwafuatilia ukawatupa ndani ya vilindi vya bahari+ kama jiwe+ katika maji yenye nguvu.+ 12 Nawe ukawaongoza kwa nguzo ya wingu wakati wa mchana,+ na kwa nguzo ya moto wakati wa usiku,+ ili kuwaangazia+ njia wanayopaswa kuipitia. 13 Nawe ukashuka chini kwenye Mlima Sinai+ na kusema nao kutoka mbinguni+ na kuwapa maamuzi ya hukumu+ yaliyo manyoofu na sheria za kweli,+ masharti+ na amri+ nzuri. 14 Nawe ukawajulisha sabato+ yako takatifu, na amri na masharti na sheria ukawaamuru kupitia Musa mtumishi wako.+ 15 Nawe ukawapa mkate kutoka mbinguni kwa ajili ya njaa yao,+ na kutoka katika mwamba ukawaletea maji kwa ajili ya kiu yao,+ nawe ukawaambia waingie+ na kuimiliki nchi ambayo kwa kiapo ulikuwa umeuinua mkono wako ili kuwapa.+
16 “Nao wenyewe, mababu zetu, wakatenda kwa kimbelembele+ na kufanya shingo zao kuwa ngumu,+ wala hawakusikiliza amri zako. 17 Kwa hiyo wakakataa kusikiliza,+ wala hawakuyakumbuka+ matendo yako ya ajabu ambayo ulikuwa umewafanyia, bali wakafanya shingo zao kuwa ngumu+ na kujichagulia mkuu+ ili kurudi kwenye hali yao ya utumwa katika Misri. Lakini wewe ni Mungu wa matendo ya kusamehe,+ mwenye neema+ na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi+ wa fadhili zenye upendo, nawe hukuwaacha.+ 18 Ndiyo, walipokuwa wamejitengenezea sanamu ya ndama+ ya kuyeyushwa na kuanza kusema, ‘Huyu ndiye Mungu wako aliyekuongoza kutoka Misri,’+ nao wakatenda matendo makubwa ya kukosa heshima, 19 wewe mwenyewe, katika rehema zako nyingi hukuwaacha+ nyikani. Nguzo ya wingu haikuondoka juu yao wakati wa mchana ili kuwaongoza njiani,+ wala nguzo ya moto haikuondoka juu yao usiku ili kuwaangazia njia wanayopaswa kuipitia.+ 20 Nawe ukawapa roho+ yako njema ili kuwapa hekima, nawe hukuwanyima mana vinywani mwao,+ na maji ukawapa kwa ajili ya kiu yao.+ 21 Na kwa miaka 40+ ukawapa chakula nyikani. Hawakukosa chochote.+ Mavazi yao hayakuchakaa,+ wala miguu yao haikuvimba.+
22 “Nawe ukawapa falme+ na vikundi vya watu, ukawagawia fungu kwa fungu;+ hivi kwamba wakamiliki nchi ya Sihoni,+ nchi ya mfalme wa Heshboni,+ na nchi ya Ogu+ mfalme wa Bashani.+ 23 Na wana wao ukawafanya kuwa wengi kama nyota za mbinguni.+ Kisha ukawaleta katika nchi+ ambayo ulikuwa umewaahidi mababu zao+ kwamba wanapaswa waingie na kuimiliki. 24 Basi wana wao+ wakaingia, wakaichukua nchi hiyo na kuimiliki,+ nawe ukatiisha+ mbele yao wakaaji wa nchi hiyo, Wakanaani,+ na kuwatia mikononi mwao, pamoja na wafalme+ wao na vikundi vya watu wa nchi,+ ili wawatendee kulingana na mapenzi yao.+ 25 Nao wakaanza kuteka majiji yenye ngome+ na udongo mnono+ na kumiliki nyumba zilizojaa vitu vyote vyema,+ matangi yaliyochimbwa chini,+ mashamba ya mizabibu na ya mizeituni+ na miti ya vyakula kwa wingi, nao wakaanza kula na kushiba+ na kunenepa+ na kufanikiwa katika wema wako mkubwa.+
26 “Hata hivyo, wakakosa kutii,+ wakakuasi+ na kuzidi kutupa sheria yako nyuma ya migongo yao,+ wakawaua manabii wako mwenyewe,+ waliotoa ushahidi juu yao ili kuwarudisha kwako;+ nao wakaendelea kutenda matendo ya ukosefu mkubwa wa heshima.+ 27 Kwa sababu hiyo ukawatia mkononi mwa adui zao,+ walioendelea kuwataabisha;+ lakini wakati wa taabu yao walikuwa wakikulilia,+ nawe mwenyewe ulikuwa ukisikia kutoka mbinguni kwenyewe;+ nawe kulingana na rehema+ zako nyingi ukawapa waokozi+ waliowaokoa kutoka mkononi mwa adui zao.+
28 “Lakini mara tu walipopata kupumzika, wakatenda tena mabaya mbele zako,+ nawe ukawaacha mkononi mwa adui zao, ambao waliwakanyagia chini.+ Kisha wakawa wanarudi na kukulilia wapate msaada,+ nawe ukasikia kutoka mbinguni kwenyewe+ na kuwakomboa kulingana na rehema zako nyingi, tena na tena.+ 29 Ingawa ulikuwa ukitoa ushahidi+ juu yao ili kuwarudisha kwenye sheria yako,+ wao walitenda kwa kimbelembele+ wala hawakusikiliza amri zako; nao wakayatendea dhambi+ maamuzi yako ya hukumu,+ ambayo, mtu akiyafanya, ataishi pia kwa hayo.+ Nao wakazidi kutokeza bega+ la ukaidi, wakaifanya shingo yao kuwa ngumu,+ wala hawakusikiliza.+ 30 Lakini uliwavumilia kwa miaka mingi+ nawe ukaendelea kutoa ushahidi+ juu yao kwa roho yako kupitia manabii wako, wala hawakutega sikio.+ Mwishowe ukawatia mikononi mwa watu wa nchi hizo.+ 31 Na katika rehema zako nyingi hukuwaangamiza+ wala kuwaacha;+ kwa maana wewe ni Mungu mwenye neema+ na rehema.+
32 “Na sasa, Ee Mungu wetu, Mungu mkuu,+ mwenye nguvu+ na mwenye kuogopesha,+ anayeshika agano+ na fadhili zenye upendo,+ usiache magumu yote ambayo yametupata sisi,+ wafalme+ wetu, wakuu+ wetu na makuhani+ wetu na manabii+ wetu na mababu+ zetu na watu wako wote tangu siku za wafalme wa Ashuru mpaka leo hii,+ yaonekane kuwa madogo mbele zako.+ 33 Nawe ni mwadilifu+ kuhusu mambo yote ambayo yametupata, kwa maana umetenda kwa uaminifu,+ lakini sisi ndio tumetenda kwa uovu.+ 34 Nao wafalme wetu, wakuu wetu, makuhani wetu na mababu zetu,+ hawakutenda sheria yako,+ wala kusikiliza amri zako+ wala shuhuda zako ambazo ulitumia kutoa ushahidi+ juu yao. 35 Na wao wenyewe—wakati wa ufalme wao+ na katikati ya vitu vyako vingi vilivyo vyema+ ambavyo uliwapa na katika nchi pana na nono+ uliyowapa, hawakukutumikia+ wala kurudi kutoka katika mazoea yao mabaya.+ 36 Tazama! Sisi leo ni watumwa;+ na tazama! sisi ni watumwa+ juu ya nchi ambayo uliwapa mababu zetu, ili wale matunda yake na vitu vyake vyema, 37 na mazao yake yamejaa+ kwa ajili ya wafalme+ ambao umeweka juu yetu kwa sababu ya dhambi zetu,+ nao wanatawala juu ya miili yetu na juu ya wanyama wetu wa kufugwa, kulingana na mapenzi yao, nasi tumo katika taabu kubwa.+
38 “Basi kwa sababu ya hayo yote tunaweka mapatano yenye kutegemeka,+ katika maandishi na kushuhudiwa vilevile kwa kutiwa muhuri+ wa wakuu wetu, Walawi wetu na makuhani wetu.”+
10 Basi wale walioushuhudia kwa kutia muhuri+ walikuwa:
Nehemia+ yule Tirshatha,+ mwana wa Hakalia,+
Na Sedekia, 2 Seraya,+ Azaria, Yeremia, 3 Pashuri, Amaria, Malkiya, 4 Hatushi, Shebania, Maluku, 5 Harimu,+ Meremothi, Obadia, 6 Danieli,+ Ginethoni, Baruku, 7 Meshulamu, Abiya, Miyamini, 8 Maazia, Bilgai na Shemaya, hao wakiwa ni makuhani.
9 Pia Walawi: Yeshua+ mwana wa Azania, Binui wa wana wa Henadadi,+ Kadmieli 10 na ndugu zao Shebania,+ Hodia, Kelita, Pelaya, Hanani, 11 Mika, Rehobu, Hashabia, 12 Zakuri, Sherebia,+ Shebania, 13 Hodia, Bani na Beninu.
14 Vichwa vya watu: Paroshi, Pahath-moabu,+ Elamu, Zatu, Bani, 15 Buni, Azgadi, Bebai, 16 Adoniya, Bigvai, Adini, 17 Ateri, Hezekia, Azuri, 18 Hodia, Hashumu, Besai, 19 Harifu, Anathothi, Nebai, 20 Magpiashi, Meshulamu, Heziri, 21 Meshezabeli, Sadoki, Yadua, 22 Pelatia, Hanani, Anaya, 23 Hoshea, Hanania, Hashubu, 24 Haloheshi, Pilha, Shobeki, 25 Rehumu, Hashabna, Maaseya, 26 na Ahiya, Hanani, Anani, 27 Maluku, Harimu, Baana.
28 Na kuhusu watu wengine, makuhani,+ Walawi,+ watunza-malango,+ waimbaji,+ Wanethini+ na kila mtu aliyejitenga na watu wa zile nchi+ na kufuata sheria+ ya Mungu wa kweli, wake zao, wana wao na binti zao, kila mtu mwenye ujuzi na uelewaji,+ 29 walikuwa wakishikamana na ndugu zao,+ watu wao mashuhuri,+ na kuingia katika laana+ na kiapo,+ kwamba watatembea katika sheria ya Mungu wa kweli, ambayo ilitolewa kupitia mkono wa Musa mtumishi wa Mungu wa kweli,+ na kushika+ na kufanya amri zote za Yehova Bwana wetu+ na maamuzi yake ya hukumu na masharti yake;+ 30 na kwamba tusiwape watu wa nchi binti zetu, wala tusiwachukulie wana wetu binti zao.+
31 Na kuhusu wale watu wa nchi+ waliokuwa wakileta mali na kila namna ya nafaka siku ya sabato ili kuuza, tusichukue chochote kutoka kwao siku ya sabato+ wala katika siku takatifu,+ na kwamba tuuache mwaka wa saba+ na deni la kila mkono.+
32 Pia, tukajiwekea amri za kutoa, kila mmoja wetu, sehemu ya tatu ya shekeli kila mwaka kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wetu,+ 33 kwa ajili ya mkate wa tabaka+ na toleo la nafaka la daima+ na toleo la kuteketezwa la daima la sabato,+ miezi mipya,+ kwa ajili ya sherehe rasmi+ na kwa ajili ya vitu vitakatifu+ na kwa ajili ya matoleo ya dhambi+ ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli na kazi yote ya nyumba ya Mungu wetu.+
34 Pia, tukapiga kura+ kuhusu matoleo ya kuni+ ambayo makuhani, Walawi na watu walipaswa kuleta kwenye nyumba ya Mungu wetu, kulingana na nyumba ya mababu zetu, kwa wakati uliowekwa, mwaka baada ya mwaka, ili kuwasha moto juu ya madhabahu ya Yehova Mungu wetu,+ kulingana na yaliyoandikwa katika sheria;+ 35 na kuleta kwenye nyumba ya Yehova matunda ya kwanza yaliyoiva ya udongo wetu+ na matunda ya kwanza yaliyoiva ya mazao yote ya kila namna ya mti,+ mwaka baada ya mwaka; 36 na mzaliwa wa kwanza+ wa wana wetu na wa wanyama wetu wa kufugwa,+ kulingana na mambo yaliyoandikwa katika sheria,+ na mzaliwa wa kwanza wa mifugo yetu na wa makundi yetu,+ kuwaleta katika nyumba ya Mungu wetu, kwa makuhani waliokuwa wakihudumu katika nyumba ya Mungu wetu.+ 37 Pia, mazao ya kwanza ya unga wetu wenye chenga-chenga+ na michango+ yetu na matunda ya kila namna ya mti,+ divai mpya+ na mafuta+ inatupasa tulete kwa makuhani katika majumba ya kulia chakula+ ya nyumba ya Mungu wetu, pia sehemu ya kumi kutoka katika udongo wetu tuwaletee Walawi,+ kwa maana wao, Walawi, ndio hupokea sehemu ya kumi katika majiji yetu yote ya kilimo.
38 Na kuhani, mwana wa Haruni, atakuwa pamoja na Walawi wakati Walawi wanapopokea sehemu ya kumi; Walawi nao inawapasa watoe sehemu ya kumi ya ile sehemu ya kumi kwa nyumba ya Mungu wetu+ katika majumba ya kulia chakula+ ya nyumba ya kuweka akiba ya vitu. 39 Kwa maana wana wa Israeli na wana wa Walawi wanapaswa kuleta mchango+ wa nafaka, divai mpya+ na mafuta katika majumba ya kulia chakula, na humo ndimo mna vyombo vya patakatifu na makuhani waliokuwa wakihudumu,+ na watunza-malango+ na waimbaji;+ nasi hatupaswi kuipuuza nyumba ya Mungu wetu.+
11 Basi wakuu+ wa watu walikuwa na makao yao katika Yerusalemu;+ lakini wale watu wengine walipiga kura+ kuleta ndani mtu mmoja kati ya watu kumi ili waishi Yerusalemu lile jiji takatifu,+ na wale watu wengine, sehemu tisa, waishi katika yale majiji mengine. 2 Na zaidi ya hayo, watu wakawabariki+ watu wote waliojitolea+ kukaa Yerusalemu.
3 Na hawa ndio vichwa vya wilaya ya utawala+ ambao walikaa Yerusalemu;+ lakini katika majiji ya Yuda walikaa Israeli,+ makuhani+ na Walawi,+ na Wanethini+ na wana wa watumishi wa Sulemani,+ kila mmoja katika urithi wake, katika majiji yao.+
4 Pia, sehemu ya wana wa Yuda na sehemu ya wana wa Benyamini walikaa Yerusalemu.+ Kati ya wana wa Yuda kulikuwa na Athaya mwana wa Uzia mwana wa Zekaria mwana wa Amaria mwana wa Shefatia mwana wa Mahalaleli wa wana wa Perezi;+ 5 na Maaseya mwana wa Baruku mwana wa Kolhoze mwana wa Hazaya mwana wa Adaya mwana wa Yoyaribu mwana wa Zekaria mwana wa Mshela. 6 Wana wote wa Perezi waliokuwa wakikaa Yerusalemu walikuwa 468, wanaume wenye uwezo.
7 Na hawa ndio waliokuwa wana wa Benyamini:+ Salu mwana wa Meshulamu+ mwana wa Yoedi mwana wa Pedaya mwana wa Kolaya mwana wa Maaseya mwana wa Ithieli mwana wa Yeshaya; 8 na baada yake Gabai na Salai, wanaume 928; 9 na Yoeli mwana wa Zikri, mwangalizi juu yao, na Yuda mwana wa Hasenua juu ya jiji akiwa mwangalizi wa pili.
10 Wa makuhani: Yedaya mwana wa Yoyaribu,+ Yakini,+ 11 Seraya mwana wa Hilkia mwana wa Meshulamu+ mwana wa Sadoki+ mwana wa Merayothi mwana wa Ahitubu,+ kiongozi wa nyumba ya Mungu wa kweli; 12 na ndugu zao waliokuwa wakifanya kazi ya ile nyumba,+ watu 822; na Adaya mwana wa Yerohamu+ mwana wa Pelalia mwana wa Amzi mwana wa Zekaria mwana wa Pashuri+ mwana wa Malkiya,+ 13 na ndugu zake, vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba,+ watu 242, na Amashisai mwana wa Azareli mwana wa Azai mwana wa Meshilemothi mwana wa Imeri, 14 na ndugu zao, mashujaa,+ wanaume wenye nguvu 128, na kulikuwa na mwangalizi+ juu yao, Zabdieli mwana wa wakuu.
15 Na wa Walawi:+ Shemaya mwana wa Hashubu mwana wa Azrikamu mwana wa Hashabia+ mwana wa Buni, 16 na Shabethai+ na Yozabadi,+ wa vichwa vya Walawi, juu ya kazi za nje za nyumba ya Mungu wa kweli; 17 na Matania+ mwenyewe, mwana wa Mika mwana wa Zabdi mwana wa Asafu,+ kiongozi wa nyimbo za sifa,+ ndiye aliyesifu katika sala,+ na Bakbukia alikuwa wa pili wa ndugu zake, na Abda mwana wa Shamua mwana wa Galali+ mwana wa Yeduthuni.+ 18 Walawi wote katika jiji takatifu+ walikuwa 284.
19 Na watunza-malango+ walikuwa Akubu, Talmoni+ na ndugu zao waliokuwa wakilinda malangoni,+ 172.
20 Na wale wengine wa Israeli, wa makuhani na wa Walawi, walikuwa katika majiji mengine yote ya Yuda, kila mmoja katika fungu lake mwenyewe la urithi.+ 21 Na Wanethini+ walikuwa wakikaa katika Ofeli;+ na Siha na Gishpa walikuwa juu ya Wanethini.
22 Na mwangalizi+ wa Walawi katika Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani mwana wa Hashabia mwana wa Matania+ mwana wa Mika+ wa wana wa Asafu,+ waimbaji,+ kuhusiana na kazi ya nyumba ya Mungu wa kweli. 23 Kwa maana mfalme alikuwa ametoa amri kwa ajili yao,+ na kulikuwa na mpango kamili kwa ajili ya waimbaji kulingana na mahitaji ya kila siku.+ 24 Na Pethahia mwana wa Meshezabeli wa wana wa Zera mwana wa Yuda alikuwa kando ya mfalme kuhusiana na kila jambo la watu.
25 Na kuhusu makao+ katika mashamba yao, kulikuwa na sehemu ya wana wa Yuda waliokaa katika Kiriath-arba+ na miji yake ya kandokando na katika Diboni na miji yake ya kandokando na katika Yekabzeeli+ na makao yake, 26 na katika Yeshua na katika Molada+ na katika Beth-peleti+ 27 na katika Hasar-shuali+ na katika Beer-sheba+ na miji yake ya kandokando 28 na katika Siklagi+ na katika Mekona na miji yake ya kandokando 29 na katika En-rimoni+ na katika Sora+ na katika Yarmuthi,+ 30 Zanoa,+ Adulamu+ na makao yake, Lakishi+ na mashamba yake, Azeka+ na miji yake ya kandokando. Nao wakapiga kambi kutoka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.+
31 Na wana wa Benyamini walikuwa kutoka Geba,+ Mikmashi+ na Aiya+ na Betheli+ na miji yake ya kandokando, 32 Anathothi,+ Nobu,+ Ananiya, 33 Hasori, Rama,+ Gitaimu,+ 34 Hadidi, Seboimu, Nebalati, 35 Lodi+ na Ono,+ bonde la mafundi. 36 Na kati ya Walawi kulikuwa na migawanyo ya Yuda iliyokaa Benyamini.
12 Na hawa ndio makuhani na Walawi waliokwenda pamoja na Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli+ na Yeshua:+ Seraya, Yeremia, Ezra, 2 Amaria,+ Maluku, Hatushi, 3 Shekania, Rehumu, Meremothi, 4 Ido, Ginethoi, Abiya, 5 Miyamini, Maadia, Bilga, 6 Shemaya,+ na Yoyaribu, Yedaya,+ 7 Salu, Amoki,+ Hilkia, Yedaya.+ Hao ndio waliokuwa vichwa vya makuhani na ndugu zao katika siku za Yeshua.+
8 Na Walawi walikuwa Yeshua,+ Binui,+ Kadmieli,+ Sherebia, Yuda, Matania,+ waliosimamia utoaji wa shukrani, yeye na ndugu zake. 9 Na Bakbukia na Uni na ndugu zao walielekeana nao kwa zamu za ulinzi. 10 Yeshua akamzaa Yoyakimu, na Yoyakimu+ akamzaa Eliashibu,+ na Eliashibu akamzaa Yoyada.+ 11 Na Yoyada akamzaa Yonathani, na Yonathani akamzaa Yadua.+
12 Na katika siku za Yoyakimu kulikuwa na makuhani, vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba:+ kwa ajili ya Seraya,+ Meraya; kwa ajili ya Yeremia, Hanania; 13 kwa ajili ya Ezra,+ Meshulamu; kwa ajili ya Amaria, Yehohanani; 14 kwa ajili ya Maluki, Yonathani; kwa ajili ya Shebania,+ Yosefu; 15 kwa ajili ya Harimu,+ Adna; kwa ajili ya Merayothi, Helkai; 16 kwa ajili ya Ido, Zekaria; kwa ajili ya Ginethoni, Meshulamu; 17 kwa ajili ya Abiya,+ Zikri; kwa ajili ya Miniamini, —; kwa ajili ya Moadia, Piltai; 18 kwa ajili ya Bilga,+ Shamua; kwa ajili ya Shemaya, Yehonathani; 19 na kwa ajili ya Yoyaribu, Matenai; kwa ajili ya Yedaya,+ Uzi; 20 kwa ajili ya Salai, Kalai; kwa ajili ya Amoki, Eberi; 21 kwa ajili ya Hilkia, Hashabia; kwa ajili ya Yedaya,+ Nethaneli.
22 Walawi katika siku za Eliashibu,+ Yoyada+ na Yohanani na Yadua+ waliandikwa kama vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba, pia makuhani, mpaka wakati wa ufalme wa Dario Mwajemi.
23 Wana wa Lawi wakiwa vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba+ waliandikwa katika kitabu cha mambo ya nyakati hizo, mpaka siku za Yohanani mwana wa Eliashibu. 24 Na vichwa vya Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia+ na Yeshua mwana wa Kadmieli+ na ndugu zao kuwaelekea ili kutoa sifa na shukrani kulingana na amri+ ya Daudi yule mtu wa Mungu wa kweli, kikundi cha ulinzi kwa kikundi cha ulinzi. 25 Matania+ na Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni, Akubu+ walikuwa wakilinda wakiwa watunza-malango,+ kikundi cha ulinzi kando ya maghala ya malango. 26 Hao walikuwa katika siku za Yoyakimu+ mwana wa Yeshua+ mwana wa Yozadaki+ na katika siku za Nehemia+ gavana na Ezra+ kuhani, mwandikaji.+
27 Nao wakawatafuta Walawi wakati wa kuzindua+ ukuta wa Yerusalemu, ili kuwaleta kutoka mahali pao pote kuja Yerusalemu kuzindua na kushangilia kwa kutoa shukrani+ na kwa kuimba,+ kwa matoazi na vinanda+ na kwa vinubi.+ 28 Na wana wa waimbaji wakakusanyika kutoka katika Wilaya,+ kutoka katika sehemu zote zenye kuzunguka Yerusalemu na kutoka katika makao ya Wanetofa,+ 29 na kutoka katika Beth-gilgali+ na kutoka katika mashamba ya Geba+ na Azmavethi,+ kwa maana kulikuwa na makao+ ambayo waimbaji walikuwa wamejijengea kuzunguka Yerusalemu pande zote. 30 Na makuhani na Walawi wakajitakasa+ wenyewe na kuwatakasa watu+ na malango+ na ukuta.+
31 Ndipo nikawaleta wakuu+ wa Yuda juu ya ukuta. Tena nikaweka makundi mawili makubwa ya waimbaji ya kutoa shukrani+ na maandamano, na moja lilitembea kuelekea upande wa kuume juu ya ukuta kwenda kwenye Lango la Marundo ya Majivu.+ 32 Na Hoshaya na nusu ya wakuu wa Yuda wakaanza kutembea nyuma yao, 33 pia Azaria, Ezra na Meshulamu, 34 Yuda na Benyamini na Shemaya na Yeremia; 35 pia wana wa makuhani wakiwa na tarumbeta,+ Zekaria mwana wa Yonathani mwana wa Shemaya mwana wa Matania mwana wa Mikaya mwana wa Zakuri+ mwana wa Asafu,+ 36 na ndugu zake Shemaya na Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli na Yuda, Hanani, pamoja na vyombo vya nyimbo+ vya Daudi yule mtu wa Mungu wa kweli; na Ezra+ mwandikaji akiwa mbele yao. 37 Na kwenye Lango la Chemchemi+ wakaenda moja kwa moja mbele yao juu ya Ngazi+ ya Jiji la Daudi+ kupitia mpando wa ukuta juu ya Nyumba ya Daudi mpaka Lango la Maji+ upande wa mashariki.
38 Na lile kundi la pili la waimbaji la kutoa shukrani+ lilitembea upande wa mbele, nami nikalifuata, pia nusu ya watu, kwenye ukuta juu ya Mnara wa Majiko ya Kuokea+ na kwenda mpaka kwenye Ukuta Mpana,+ 39 na juu ya Lango la Efraimu+ na kwenda mpaka kwenye Lango la Jiji la Kale+ mpaka kwenye Lango la Samaki+ na Mnara wa Hananeli+ na Mnara wa Mea+ na kwenda mpaka kwenye Lango la Kondoo;+ nao wakaja kusimama kwenye Lango la Mlinzi.
40 Baadaye hayo makundi mawili ya waimbaji+ yakaja kusimama katika nyumba+ ya Mungu wa kweli, pia mimi vilevile na watawala-wasaidizi pamoja nami,+ 41 na makuhani, Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, Hanania wakiwa na tarumbeta,+ 42 na Maaseya na Shemaya, na Eleazari na Uzi na Yehohanani na Malkiya na Elamu na Ezeri. Na waimbaji pamoja na Izrahia yule mwangalizi wakaendelea kusikika.+
43 Nao wakatoa dhabihu kubwa+ siku hiyo na kushangilia,+ kwa maana Mungu wa kweli alikuwa amewafanya washangilie kwa shangwe+ kubwa. Na pia wanawake+ na watoto+ wakashangilia, hata kushangilia kwa Yerusalemu kukasikika mbali sana.+
44 Tena wanaume wakawekwa siku hiyo juu ya majumba+ ya maghala,+ ya michango,+ ya mazao ya kwanza+ na ya sehemu za kumi,+ ili kukusanya ndani yake mafungu yaliyohitajiwa na sheria+ kutoka katika mashamba ya majiji kwa ajili ya makuhani na Walawi;+ kwa maana shangwe ya Yuda ilitokana na makuhani na Walawi+ waliokuwa wakihudumu. 45 Nao wakaanza kushughulikia wajibu wa Mungu wao na wajibu+ wa utakaso,+ pia waimbaji+ na watunza-malango,+ kulingana na amri ya Daudi na Sulemani mwana wake. 46 Kwa maana katika siku za Daudi na Asafu, katika wakati uliopita, kulikuwa na viongozi wa waimbaji+ na wimbo wa sifa na kutoa shukrani kwa Mungu.+ 47 Na Israeli wote katika siku za Zerubabeli+ na katika siku za Nehemia+ walikuwa wakitoa mafungu kwa ajili ya waimbaji+ na watunza-malango+ kulingana na uhitaji wa kila siku. Nao walikuwa wakiyatakasa kwa Walawi;+ nao Walawi walikuwa wakiyatakasa kwa wana wa Haruni.
13 Siku hiyo kitabu+ cha Musa kilisomwa+ masikioni mwa watu; na ndani yake ikapatikana imeandikwa kwamba Mwamoni+ wala Mmoabu+ asiingie katika kutaniko la Mungu wa kweli mpaka wakati usio na kipimo,+ 2 kwa maana hawakuwapokea wana wa Israeli kwa mkate+ na kwa maji,+ bali walimlipa Balaamu+ ili awalaani.+ Hata hivyo, Mungu wetu aliigeuza laana hiyo kuwa baraka.+ 3 Basi ikawa kwamba, mara waliposikia sheria hiyo,+ wakaanza kutenga+ kutoka katika Israeli ile jamii yote iliyochangamana.
4 Basi kabla ya hayo, Eliashibu+ kuhani aliyesimamia jumba la kulia chakula+ la nyumba ya Mungu wetu alikuwa mtu wa jamaa ya Tobia;+ 5 naye alimtengenezea jumba kubwa la kulia chakula,+ mahali ambapo hapo kwanza walikuwa wakiweka kwa ukawaida toleo la nafaka,+ ubani na vyombo na sehemu ya kumi ya nafaka, divai mpya+ na mafuta,+ ambavyo ni haki ya Walawi+ na waimbaji na watunza-malango, na michango kwa ajili ya makuhani.
6 Na wakati huo wote mimi sikuwa katika Yerusalemu, kwa maana nilirudi kwa mfalme katika mwaka wa 32+ wa Artashasta+ mfalme wa Babiloni, na wakati fulani baadaye nikaomba mfalme ruhusa ya kutokuwapo.+ 7 Kisha nikaja Yerusalemu nami nikauona ubaya ambao Eliashibu+ alikuwa amefanya kwa ajili ya Tobia+ kwa kumtengenezea jumba katika ua wa nyumba+ ya Mungu wa kweli. 8 Nalo jambo hilo likawa baya sana kwangu.+ Kwa hiyo nikavitupa+ nje ya jumba hilo la kulia chakula vyombo vyote vya nyumba ya Tobia. 9 Baada ya hayo nikaamuru nao wakatakasa+ majumba ya kulia chakula;+ nami nikavirudisha humo vyombo+ vya nyumba ya Mungu wa kweli, pamoja na toleo la nafaka na ubani.+
10 Nami nikagundua kwamba Walawi hawakuwa wamepewa mafungu yao,+ hivi kwamba Walawi na waimbaji waliofanya kazi walikimbia, kila mmoja akaenda katika shamba lake mwenyewe.+ 11 Nami nikaanza kuwalaumu+ watawala-wasaidizi+ na kusema: “Kwa nini nyumba ya Mungu wa kweli imepuuzwa?”+ Kwa hiyo nikawakusanya pamoja na kuwasimamisha mahali pao pa kusimama. 12 Na Yuda wote wakaleta ndani ya maghala+ sehemu ya kumi+ ya nafaka+ na ya divai mpya+ na ya mafuta.+ 13 Kisha nikamweka Shelemia kuhani na Sadoki mwandikaji na Pedaya wa Walawi kusimamia maghala; na chini ya usimamizi wao kulikuwa na Hanani mwana wa Zakuri mwana wa Matania,+ kwa maana walionwa kuwa watu waaminifu;+ nao walikuwa na daraka la kuwagawia+ ndugu zao.
14 Unikumbuke+ mimi kuhusu jambo hili, Ee Mungu wangu, nawe usifutilie mbali+ matendo yangu ya fadhili zenye upendo ambayo nimetenda kuhusiana na nyumba+ ya Mungu wangu na kuilinda.
15 Katika siku hizo niliona katika Yuda watu wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya sabato+ na kuingiza marundo ya nafaka na kuyapakia+ juu ya punda,+ na pia divai, zabibu na tini+ na kila namna ya mzigo, na kuviingiza Yerusalemu siku ya sabato;+ nami nikatoa ushahidi juu yao siku waliyokuwa wakiuza vyakula. 16 Na Watiro+ walikaa katika jiji, wakiingiza samaki na kila namna ya mali+ na kuwauzia wana wa Yuda katika siku ya sabato Yerusalemu. 17 Kwa hiyo nikaanza kuwalaumu watu wenye vyeo+ wa Yuda na kuwaambia: “Ni jambo gani baya hili mnalofanya ninyi, hata kuitia unajisi siku ya sabato? 18 Je, mababu zenu hawakufanya hivyo,+ hivi kwamba Mungu akaleta juu yetu msiba huu wote,+ na pia juu ya jiji hili? Na bado mnaiongeza hasira inayowaka juu ya Israeli kwa kuitia sabato unajisi.”+
19 Na ikawa kwamba, mara malango ya Yerusalemu yalipoingia giza kabla ya sabato, nikaamuru mara moja na malango yakaanza kufungwa.+ Tena nikasema kwamba wasiyafungue mpaka baada ya sabato; nami nikaweka malangoni baadhi ya watumishi wangu ili mzigo wowote usiingie ndani siku ya sabato.+ 20 Kwa hiyo wafanya-biashara na wauzaji wa kila namna ya mali wakakaa nje ya Yerusalemu usiku huo mara ya kwanza na mara ya pili. 21 Ndipo nikatoa ushahidi+ juu yao na kuwaambia: “Kwa nini mnakaa usiku mbele ya ukuta? Mkifanya hivyo tena, nitawadhuru.”+ Tangu wakati huo na kuendelea hawakuja siku ya sabato.
22 Nao Walawi+ nikawaambia kwamba wawe wakijitakasa+ kwa ukawaida na kuingia ndani, wakiyalinda malango+ ili kutakasa+ siku ya sabato. Ee Mungu wangu, likumbuke+ jambo hili pia kwa ajili yangu, nawe unihurumie kulingana na wingi wa fadhili zako zenye upendo.+
23 Pia, katika siku hizo niliwaona Wayahudi ambao walikuwa wamewapa makao+ wake Waashdodi,+ Waamoni na Wamoabu.+ 24 Na kuhusu wana wao, nusu walisema lugha ya Kiashdodi, wala hakuna mmoja wao aliyejua kusema lugha ya Kiyahudi,+ ila lugha ya vikundi vya watu mbalimbali. 25 Ndipo nikaanza kuwalaumu na kuwalaani+ na kuwapiga watu fulani+ kati yao na kuzing’oa nywele zao na kuwaapisha kwa Mungu:+ “Hampaswi kuwapa wana wao binti zenu, wala hampaswi kuwakubali binti zao wowote kwa ajili ya wana wenu wala kwa ajili yenu.+ 26 Je, haikuwa kwa sababu yao kwamba Sulemani mfalme wa Israeli alitenda dhambi?+ Na hapakuwa na mfalme kama yeye katika hayo mataifa mengi;+ naye alipendwa na Mungu wake,+ hivi kwamba Mungu akamfanya kuwa mfalme juu ya Israeli wote. Lakini wake wa kigeni walimfanya hata yeye atende dhambi.+ 27 Na je, si jambo ambalo halijasikiwa kwenu kutenda ubaya huu wote mkubwa kwa kukosa uaminifu kwa Mungu wetu, kwa kuwapa makao wake wa kigeni?”+
28 Na mmoja wa wana wa Yoyada+ mwana wa Eliashibu+ kuhani mkuu alikuwa mwana-mkwe wa Sanbalati+ Mhoroni.+ Kwa hiyo nikamfukuza atoke kwangu.+
29 Ee Mungu wangu, uwakumbuke kwa sababu waliutia unajisi+ ukuhani na agano+ la ukuhani na la Walawi.+
30 Nami nikawatakasa+ kutokana na kila kitu cha kigeni na kuwagawia makuhani na Walawi zamu zao, kila mmoja kwa kazi yake mwenyewe,+ 31 yaani, ya kuleta kuni+ kwa nyakati zilizowekwa na ya matunda ya kwanza yaliyoiva.
Unikumbuke+ kwa ajili ya wema,+ Ee Mungu wangu.