Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati
1 Naye Sulemani mwana wa Daudi akaendelea kupata nguvu katika ufalme wake,+ na Yehova Mungu wake alikuwa pamoja naye,+ akaendelea kumfanya kuwa mkuu zaidi.+
2 Na Sulemani akasema na Israeli wote, kwa wakuu wa maelfu+ na wa mamia+ na kwa waamuzi+ na wakuu wote wa Israeli,+ vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba.+ 3 Kisha Sulemani na kutaniko lote pamoja naye wakaenda mahali pa juu palipokuwa katika Gibeoni;+ kwa maana hapo ndipo lilipokuwa lile hema la mkutano+ la Mungu wa kweli, ambalo Musa mtumishi+ wa Yehova alitengeneza nyikani. 4 Hata hivyo, Daudi alikuwa amelileta sanduku+ la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu+ mpaka mahali ambapo Daudi alikuwa amelitayarishia,+ kwa maana alikuwa amelisimamishia hema katika Yerusalemu.+ 5 Na ile madhabahu ya shaba+ ambayo Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru+ alikuwa ametengeneza ilikuwa imewekwa mbele ya maskani ya Yehova; na Sulemani na kutaniko wakatoa maombi yao mbele yake kama kawaida. 6 Kisha Sulemani akafanya matoleo hapo mbele za Yehova juu ya ile madhabahu ya shaba ya hema la mkutano, naye akatoa juu yake matoleo elfu moja ya kuteketezwa.+
7 Usiku huo Mungu akamtokea Sulemani na kumwambia: “Omba! Nikupe nini?”+ 8 Ndipo Sulemani akamwambia Mungu: “Wewe Ndiye uliyemwonyesha Daudi baba yangu+ fadhili kubwa zenye upendo na kunifanya niwe mfalme mahali pake.+ 9 Sasa, Ee Yehova Mungu, acha ahadi yako kwa Daudi baba yangu itimie,+ kwa maana wewe mwenyewe umenifanya kuwa mfalme+ juu ya watu wengi sana kama chembe za mavumbi ya dunia.+ 10 Sasa unipe hekima na ujuzi+ ili nitoke mbele ya watu hawa na ili niingie ndani,+ kwa maana ni nani anayeweza kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?”+
11 Ndipo Mungu akamwambia Sulemani: “Kwa sababu jambo hili liko moyoni+ mwako nawe hukuomba mali, utajiri wala heshima wala nafsi ya wale wanaokuchukia, wala hata hukuomba wingi wa siku,+ bali unaomba hekima na ujuzi kwa ajili yako ili uwahukumu watu wangu ambao nimekufanya kuwa mfalme juu yao,+ 12 unapewa hekima na ujuzi;+ pia nitakupa mali na utajiri na heshima ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekutangulia amepata kuwa navyo,+ wala baada yako hakuna yeyote atakayekuwa navyo.”+
13 Basi Sulemani akatoka pale mahali pa juu palipokuwa katika Gibeoni,+ kutoka mbele ya hema la mkutano,+ akaja Yerusalemu, akaendelea kutawala juu ya Israeli.+ 14 Na Sulemani akaendelea kukusanya magari na farasi wa vita hivi kwamba akawa na magari elfu moja na mia nne na farasi wa vita kumi na mbili elfu,+ akawaweka katika majiji ya magari+ na karibu na mfalme katika Yerusalemu. 15 Na mfalme akafanya fedha na dhahabu iliyomo Yerusalemu kuwa kama mawe;+ naye akafanya mierezi iwe kama mikuyu+ iliyoko Shefela+ kwa wingi. 16 Na farasi wa Sulemani walisafirishwa kutoka Misri,+ na wanabiashara wa mfalme wakawa wakichukua kundi la farasi kwa bei fulani.+ 17 Nao wakawa wakipandisha na kusafirisha kwa ukawaida gari kutoka Misri kwa vipande 600 vya fedha na farasi kwa vipande 150; na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa wafalme wote wa Wahiti na wafalme wa Siria.+ Walikuwa wakisafirisha vitu kupitia hao.
2 Basi Sulemani akatoa amri kwamba nyumba+ ijengwe kwa ajili ya jina la Yehova+ na nyumba kwa ajili ya ufalme wake.+ 2 Na Sulemani akahesabu watu 70,000 wawe wabeba-mizigo na 80,000 wawe wachongaji wa mawe mlimani,+ na 3,600 wawe waangalizi juu yao.+ 3 Tena Sulemani akatuma watu kwa Hiramu+ mfalme wa Tiro, akisema: “Kama ulivyomtendea Daudi+ baba yangu, ulivyokuwa ukimletea mierezi ili ajijengee nyumba ya kukaa,— 4 tazama, ninajenga+ nyumba kwa ajili ya jina+ la Yehova Mungu wangu, ili niitakase+ kwake, ili kufukiza mbele zake uvumba uliotiwa manukato,+ pamoja na mkate+ wa tabaka wa daima na matoleo ya kuteketezwa wakati wa asubuhi na jioni,+ wakati wa sabato+ na wakati wa miezi mipya+ na kwenye majira ya sherehe+ ya Yehova Mungu wetu. Hayo yatakuwa juu ya Israeli mpaka wakati usio na kipimo.+ 5 Na nyumba nitakayoijenga itakuwa kuu,+ kwa maana Mungu wetu ni mkuu kuliko miungu mingine yote.+ 6 Na ni nani angeweza kuwa na nguvu za kumjengea nyumba?+ Kwa maana mbingu na mbingu za mbingu hazimtoshi,+ na mimi ni nani+ kwamba nimjengee nyumba isipokuwa tu iwe ya kufukizia moshi wa uvumba mbele zake?+ 7 Na sasa niletee mwanamume mwenye ujuzi ili afanye kazi kwa kutumia dhahabu na fedha na shaba+ na chuma na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na uzi mwekundu na wa bluu, na anayejua jinsi ya kuchonga michoro, pamoja na wale walio na ustadi ambao wako pamoja nami katika Yuda na Yerusalemu, ambao Daudi baba yangu amewatayarisha.+ 8 Nawe uniletee mierezi,+ miberoshi+ na misandali+ kutoka Lebanoni,+ kwa maana mimi najua vema kwamba watumishi wako wana uzoefu wa kukata miti ya Lebanoni,+ (na, tazama, watumishi wangu wako pamoja na watumishi wako,) 9 ili kunitayarishia miti kwa hesabu kubwa, kwa maana ile nyumba nitakayoijenga itakuwa kuu, ndiyo, kuu ajabu. 10 Na, tazama! kwa wakusanyaji wa mbao, wakataji wa miti, ninatoa chakula kwa watumishi wako, kori 20,000 za ngano,+ na kori 20,000 za shayiri, na bathi 20,000 za divai,+ na bathi 20,000 za mafuta.”
11 Ndipo Hiramu mfalme wa Tiro+ akatoa neno katika maandishi, akalituma kwa Sulemani: “Kwa sababu Yehova aliwapenda+ watu wake, amekufanya wewe kuwa mfalme juu yao.”+ 12 Na Hiramu akaendelea kusema: “Abarikiwe Yehova Mungu wa Israeli,+ aliyezifanya mbingu na dunia,+ kwa sababu amempa Mfalme Daudi mwana mwenye hekima, mwenye uzoefu katika busara na uelewaji,+ atakayejenga nyumba kwa ajili ya Yehova na nyumba kwa ajili ya ufalme wake.+ 13 Na sasa namtuma mtu mwenye ustadi, mwenye uzoefu katika uelewaji, Hiram-abi,+ 14 mwana wa mwanamke wa wana wa Dani lakini ambaye baba yake alikuwa mtu wa Tiro, mwenye uzoefu, afanye mapambo ya dhahabu na fedha, shaba,+ chuma, mawe+ na miti, sufu iliyotiwa rangi ya zambarau,+ uzi wa bluu+ na kitambaa laini+ na uzi mwekundu+ na kuchonga kila namna ya michoro+ na kubuni kila namna ya kitu+ atakachoweza kupewa pamoja na watu wako wenye ustadi na watu wenye ustadi wa bwana wangu Daudi baba yako. 15 Na sasa ile ngano na shayiri, mafuta na divai ambavyo bwana wangu ameahidi, na avilete kwa watumishi wake.+ 16 Nasi tutakata miti+ kutoka Lebanoni kulingana na mahitaji yako yote,+ nasi tutakuletea kama vyelezo kupitia baharini+ mpaka Yopa,+ nawe utaichukua na kuipeleka Yerusalemu.”
17 Ndipo Sulemani akawahesabu watu wote waliokuwa wakaaji wageni, waliokuwa katika nchi ya Israeli,+ baada ya ile hesabu ya watu ambayo Daudi alikuwa amechukua;+ kukapatikana watu 153,600. 18 Kwa hiyo akawafanya 70,000 kati yao wawe wabeba-mizigo+ na 80,000 wawe wachongaji+ wa mawe mlimani na waangalizi 3,600 wa kuwafanya watu watumikie.+
3 Mwishowe Sulemani akaanza kujenga nyumba ya Yehova+ katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria,+ ambapo Yehova alikuwa amemtokea Daudi baba yake,+ mahali ambapo Daudi alikuwa ametayarisha kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani+ Myebusi. 2 Basi akaanza kujenga katika mwezi wa pili, siku ya pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake.+ 3 Na vitu hivi Sulemani akaviweka kuwa msingi kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu wa kweli, urefu wa kipimo cha mikono kulingana na kipimo cha zamani ukiwa mikono 60, na upana mikono 20.+ 4 Na ukumbi+ uliokuwa mbele ya huo urefu ulikuwa mikono 20 mbele ya upana wa nyumba, na kimo chake kilikuwa 120; naye akafunika upande wa ndani kwa dhahabu safi. 5 Na ile nyumba kuu+ akaifunika kwa miberoshi, kisha akaifunika kwa dhahabu nzuri,+ halafu akaweka juu yake maumbo ya mtende+ na minyororo.+ 6 Tena, akaitandaza nyumba kwa mawe ya thamani kwa ajili ya uzuri;+ na dhahabu+ ilikuwa dhahabu ya kutoka katika nchi ya dhahabu. 7 Naye akafunika kwa dhahabu ile nyumba, maboriti, vizingiti na kuta zake na milango yake;+ akachonga makerubi juu ya kuta.+
8 Naye akajenga nyumba ya Patakatifu Zaidi,+ urefu wake kuhusiana na upana wa nyumba ulikuwa mikono 20, na upana wake ulikuwa mikono 20;+ kisha akaifunika kwa dhahabu nzuri kiasi chake talanta 600. 9 Na uzito wa misumari+ ulikuwa shekeli 50 za dhahabu; naye akavifunika vyumba vya dari kwa dhahabu.
10 Kisha akatengeneza makerubi+ wawili katika nyumba ya Patakatifu Zaidi kwa kutumia ufundi wa kufanya mifano, akawafunika kwa dhahabu.+ 11 Na urefu wa mabawa ya wale makerubi+ ulikuwa mikono 20, bawa moja la urefu wa mikono 5 lilifika kwenye ukuta wa nyumba ile, na lile bawa lingine la urefu wa mikono 5 likiwa linafika kwenye bawa la yule kerubi mwingine.+ 12 Na bawa la yule kerubi mmoja la urefu wa mikono 5 lilikuwa linafika kwenye ukuta wa nyumba ile, na lile bawa lingine la mikono 5 lilishikana na bawa la yule kerubi mwingine.+ 13 Mabawa ya hao makerubi yalikuwa yamenyooshwa urefu wa mikono 20; nao walikuwa wamesimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea upande wa ndani.
14 Tena akatengeneza pazia+ la uzi wa bluu+ na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na uzi mwekundu na kitambaa laini, na kulipamba kwa makerubi juu yake.+
15 Kisha akatengeneza nguzo mbili+ mbele ya nyumba ile, urefu wa mikono 35, na kombe+ lililokuwa juu ya kila moja lilikuwa na urefu wa mikono 5. 16 Tena, akatengeneza minyororo+ yenye mtindo wa mkufu na kuiweka juu ya vilele vya zile nguzo, akatengeneza makomamanga+ mia moja na kuyaweka kwenye ile minyororo. 17 Naye akasimamisha zile nguzo mbele ya hekalu, moja upande wa kuume na nyingine upande wa kushoto, kisha ile ya upande wa kuume akaiita jina Yakini na jina la ile ya upande wa kushoto Boazi.+
4 Kisha akatengeneza ile madhabahu ya shaba,+ urefu wake ukiwa ni mikono 20, na upana wake mikono 20, na kimo chake mikono 10.+
2 Naye akatengeneza bahari ya kuyeyushwa+ urefu wa mikono 10 kutoka ukingo wake mmoja mpaka ukingo wake mwingine, ikiwa ni mviringo kuzunguka pande zote, na kimo chake kilikuwa mikono 5, na kamba ya mikono 30 ingeweza kuizunguka pande zote.+ 3 Na kulikuwa na mapambo yenye umbo la kibuyu+ chini yake kwenye mviringo wote, yakiizunguka, 10 katika kila urefu wa mkono mmoja, yakiizunguka ile bahari pande zote.+ Yale mapambo yenye umbo la kibuyu yalikuwa katika mistari miwili, yakiwa yamefanyizwa katika myeyusho wake. 4 Ilikuwa imesimama juu ya ng’ombe-dume kumi na wawili,+ watatu wakitazama kaskazini na watatu wakitazama magharibi na watatu wakitazama kusini na watatu wakitazama mashariki; na bahari ilikuwa juu yao, na sehemu zao za nyuma zote zilielekea upande wa ndani.+ 5 Na unene wake ulikuwa upana wa kiganja kimoja; na ukingo wake ulikuwa kama muundo wa ukingo wa kikombe, ua la yungiyungi.+ Nayo ikiwa kitu cha kuhifadhia, ingeweza kuchukua vipimo elfu tatu vya bathi.+
6 Tena akatengeneza beseni kumi, akaweka tano upande wa kuume na tano upande wa kushoto,+ ili kuoshea humo.+ Wakawa wakioshea humo vitu vinavyohusiana na toleo la kuteketezwa.+ Lakini ile bahari ilikuwa kwa ajili ya makuhani kuogea humo.+
7 Kisha akatengeneza vinara vya taa+ vya dhahabu, kumi vya muundo mmoja,+ akaviweka katika hekalu, vitano upande wa kuume na vitano upande wa kushoto.+
8 Tena akatengeneza meza kumi, akaziweka katika hekalu, tano upande wa kuume na tano upande wa kushoto,+ halafu akatengeneza mabakuli mia moja ya dhahabu.
9 Kisha akatengeneza ua+ wa makuhani+ na ule ua mkuu na milango ya ule ua,+ akaifunika milango yake kwa shaba. 10 Naye akaweka ile bahari upande wa kuume, upande wa mashariki, kuelekea kusini.+
11 Mwishowe Hiramu akatengeneza makopo+ na sepetu+ na mabakuli.+
Basi Hiramu akamaliza kuifanya kazi aliyomfanyia Mfalme Sulemani kwenye nyumba ya Mungu wa kweli. 12 Zile nguzo+ mbili na yale makombe ya mviringo+ juu ya zile nguzo mbili na zile kamba mbili za nyavu+ za kufunika yale makombe mawili ya mviringo yaliyokuwa juu ya zile nguzo 13 na yale makomamanga+ mia nne kwa ajili ya zile kamba mbili za nyavu, mistari miwili ya makomamanga kwa kila kamba ya nyavu ili kufunika yale makombe mawili ya mviringo yaliyokuwa juu ya zile nguzo,+ 14 na yale mabehewa+ kumi na zile beseni+ kumi juu ya yale mabehewa; 15 ile bahari+ moja na wale ng’ombe-dume kumi na wawili walio chini yake,+ 16 na makopo na sepetu+ na nyuma+ na vyombo+ vyake vyote ambavyo Hiram-abivu+ alimtengenezea Mfalme Sulemani kwa ajili ya nyumba ya Yehova, vya shaba iliyong’arishwa. 17 Mfalme aliviyeyushia katika Wilaya ya Yordani katika ule udongo mzito kati ya Sukothi+ na Sereda.+ 18 Basi Sulemani akatengeneza vyombo hivyo vyote kwa wingi sana, kwa maana uzito wa ile shaba haukujulikana.+
19 Na Sulemani akatengeneza vyombo+ vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Mungu wa kweli na ile madhabahu ya dhahabu+ na zile meza+ zenye ule mkate wa wonyesho juu yake, 20 na vinara vya taa+ na taa+ zake za dhahabu safi, ili kuziwasha mbele ya chumba cha ndani kabisa+ kulingana na kanuni; 21 na maua na taa na mikasi ya tambi,+ ya dhahabu, (ilikuwa ndiyo dhahabu safi zaidi,) 22 na mikasi ya taa na mabakuli na vikombe na vyetezo, vya dhahabu safi,+ na mwingilio wa nyumba,+ milango yake ya ndani ya Patakatifu Zaidi na milango+ ya nyumba ya hekalu, ya dhahabu.
5 Mwishowe kazi yote ambayo Sulemani alipaswa kufanya kwa ajili ya nyumba ya Yehova ikamalizika,+ na Sulemani akaanza kuingiza vitu ambavyo Daudi baba yake alivifanya kuwa vitakatifu;+ naye akaweka fedha na dhahabu na vyombo vyote katika hazina za nyumba ya Mungu wa kweli.+ 2 Ndipo Sulemani akaanza kuwakusanya katika Yerusalemu wanaume wazee wa Israeli+ na vichwa vyote vya makabila,+ wakuu wa nyumba za ukoo wa upande wa baba+ za wana wa Israeli, ili kulileta sanduku+ la agano la Yehova kutoka+ katika Jiji la Daudi,+ yaani, Sayuni.+ 3 Basi watu wote wa Israeli wakakusanyika kwa mfalme kwenye sherehe, ile ya mwezi wa saba.+
4 Basi wanaume wote wazee wa Israeli wakaja,+ na Walawi wakaanza kulichukua Sanduku.+ 5 Nao wakalipandisha Sanduku+ na hema la mkutano+ na vyombo vyote vitakatifu+ vilivyokuwa katika hema. Makuhani Walawi wakavipandisha.+ 6 Na Mfalme Sulemani na kusanyiko lote la Waisraeli, waliokutana naye kwa wakati uliowekwa mbele ya lile Sanduku walikuwa wakitoa dhabihu+ za kondoo na ng’ombe ambao hawangeweza kuhesabiwa kwa sababu ya wingi. 7 Ndipo makuhani wakaliingiza sanduku la agano la Yehova mahali pake, ndani ya chumba cha ndani kabisa+ cha nyumba, ndani ya Patakatifu Zaidi,+ chini ya mabawa ya wale makerubi.+ 8 Basi makerubi waliendelea kunyoosha mabawa yao juu ya mahali pa lile Sanduku, hivi kwamba makerubi walilifunika Sanduku na miti yake+ kutoka juu.+ 9 Lakini ile miti ilikuwa mirefu, hivi kwamba ncha za miti hiyo zilionekana katika Patakatifu mbele ya chumba cha ndani kabisa, lakini hazikuonekana nje, nayo iko hapo mpaka leo hii.+ 10 Hamkuwa na chochote ndani ya lile Sanduku ila yale mabamba+ mawili ambayo Musa aliwapa katika Horebu,+ wakati Yehova alipofanya agano+ na wana wa Israeli walipokuwa wakitoka Misri.+
11 Na ikawa kwamba makuhani walipoondoka mahali patakatifu (kwa maana makuhani wote waliopatikana walikuwa wamejitakasa+—hapakuwa na uhitaji wa kufuata ile migawanyo);+ 12 na Walawi+ waliokuwa waimbaji wa wote hawa, yaani, wa Asafu,+ wa Hemani,+ wa Yeduthuni+ na wa wana wao na wa ndugu zao, waliovaa mavazi ya kitambaa laini pamoja na matoazi+ na vinanda+ na vinubi,+ walikuwa wamesimama upande wa mashariki wa ile madhabahu na pamoja nao makuhani wenye kufikia hesabu ya 120 wakipiga tarumbeta;+ 13 na ikawa kwamba mara tu wapiga-tarumbeta na waimbaji walipokuwa kama mtu mmoja+ kwa kutokeza sauti moja isikike katika kumsifu na kumshukuru Yehova, na mara tu walipopaaza sauti kwa tarumbeta na kwa matoazi na kwa vyombo vya nyimbo+ na kwa kumsifu+ Yehova, “kwa maana yeye ni mwema,+ kwa maana fadhili zake zenye upendo+ ni za mpaka wakati usio na kipimo,” nyumba ile ikajaa wingu,+ nyumba ya Yehova,+ 14 na makuhani hawakuweza kusimama ili kuhudumu kwa sababu ya lile wingu;+ kwa maana utukufu+ wa Yehova uliijaza nyumba ya Mungu wa kweli.
6 Ndipo Sulemani aliposema:+ “Yehova mwenyewe alisema kwamba atakaa katika giza zito;+ 2 nami nimejenga nyumba ya makao yaliyoinuliwa+ kwa ajili yako na mahali palipofanywa imara kwa ajili yako ili ukae humo mpaka wakati usio na kipimo.”+
3 Kisha mfalme akageuza uso wake, akaanza kulibariki+ kutaniko lote la Israeli, huku kutaniko lote la Israeli likiwa limesimama.+ 4 Naye akaendelea kusema: “Na abarikiwe Yehova Mungu wa Israeli,+ aliyesema kwa kinywa chake mwenyewe na Daudi baba yangu+ na kwa mikono yake mwenyewe ametimiza,+ akisema, 5 ‘Kuanzia ile siku nilipowatoa watu wangu katika nchi ya Misri, sikuchagua jiji kutoka katika makabila yote ya Israeli ili kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ ili liwe hapo, wala sikumchagua mwanadamu awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli.+ 6 Bali nitachagua Yerusalemu+ ili jina langu liwe hapo, nami nitamchagua Daudi awe juu ya watu wangu Israeli.’+ 7 Na likawa jambo lililo moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli.+ 8 Lakini Yehova akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu lilikuwa jambo lililo moyoni mwako kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu, ulifanya vema, kwa sababu lilikuwa jambo lililo moyoni mwako.+ 9 Ila tu wewe mwenyewe hutaijenga nyumba hiyo,+ bali mwana wako atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayeijenga nyumba kwa ajili ya jina langu.’+ 10 Na Yehova akatimiza neno lake+ alilokuwa amesema, ili nisimame mahali pa Daudi baba yangu+ na kuketi juu ya kiti cha ufalme+ cha Israeli, kama Yehova alivyosema,+ na ili nijenge nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli,+ 11 na ili niweke hapo lile Sanduku+ ambamo mna agano la Yehova alilofanya na wana wa Israeli.”+
12 Naye akaanza kusimama mbele ya madhabahu ya Yehova mbele ya kutaniko lote la Israeli,+ naye sasa akainyoosha mikono yake.+ 13 (Kwa maana Sulemani alikuwa amejenga jukwaa+ la shaba na kuliweka katikati ya ua.+ Urefu wake ulikuwa mikono mitano, na upana wake ulikuwa mikono mitano, na kimo chake kilikuwa mikono mitatu; naye akaendelea kusimama juu yake.) Naye akapiga magoti+ mbele ya kutaniko lote la Israeli, akainyoosha mikono yake kuelekea mbinguni.+ 14 Akaendelea kusema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli,+ hakuna Mungu kama wewe+ mbinguni wala duniani, anayeshika agano+ na fadhili zenye upendo kwa watumishi wako wanaotembea mbele zako kwa moyo wao wote;+ 15 wewe ambaye umemtimizia mtumishi wako Daudi baba yangu yale uliyomwahidi,+ hivi kwamba ukatoa hiyo ahadi kwa kinywa chako mwenyewe, na kwa mkono wako mwenyewe umetimiza kama ilivyo leo hii.+ 16 Na sasa, Ee Yehova Mungu wa Israeli, umtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu yale uliyomwahidi, ukisema, ‘Mwanamume wa kwako hatakatiliwa mbali mbele zangu asiketi juu ya kiti cha ufalme cha Israeli,+ ikiwa tu wana wako+ wataangalia njia yao kwa kutembea katika sheria yangu+ kama vile ambavyo wewe umetembea mbele zangu.’+ 17 Na sasa, Ee Yehova Mungu wa Israeli,+ acha ahadi+ uliyomwahidi mtumishi wako Daudi itimie.+
18 “Lakini, je, kweli Mungu atakaa pamoja na wanadamu duniani?+ Tazama! Mbingu, ndiyo, mbingu za mbingu, haziwezi kukutosha;+ sembuse basi, nyumba hii ambayo nimeijenga!+ 19 Nawe ugeuke kuielekea sala ya mtumishi wako+ na ombi lake la kutaka kibali,+ Ee Yehova Mungu wangu, kwa kusikiliza kilio cha kusihi+ na sala ambayo mtumishi wako anatoa mbele zako,+ 20 ili macho yako yafunguliwe+ kuielekea nyumba hii mchana na usiku, kuelekea mahali ambapo ulisema utaweka jina lako,+ kwa kuisikiliza sala ambayo mtumishi wako anatoa kuelekea mahali hapa.+ 21 Nawe usikilize kusihi kwa mtumishi+ wako na kwa watu wako Israeli wanaposali kuelekea mahali hapa,+ ili wewe usikie ukiwa katika makao yako, ukiwa mbinguni;+ nawe usikie na kusamehe.+
22 “Mwanadamu akimtendea dhambi mwanadamu mwenzake+ naye amlaani ili kumtia+ chini ya wajibu wa laana hiyo, naye kwa kweli aingie katika laana hiyo mbele ya madhabahu yako katika nyumba hii,+ 23 basi na usikie ukiwa mbinguni,+ nawe utende+ na kuwahukumu watumishi wako ili kumlipa yule mwovu kwa kuweka njia yake juu ya kichwa chake mwenyewe+ na kwa kumtangaza mwadilifu+ kuwa ni mwadilifu kwa kumpa kulingana na uadilifu wake mwenyewe.+
24 “Na watu wako Israeli wakishindwa mbele ya adui+ kwa sababu waliendelea kukutendea dhambi,+ nao kwa kweli warudi+ na kulisifu jina lako+ na kusali+ na kutoa ombi la kutaka kibali mbele zako katika nyumba hii,+ 25 basi na usikie ukiwa mbinguni,+ nawe usamehe+ dhambi ya watu wako Israeli, nawe uwarudishe+ katika nchi uliyowapa wao na mababu zao.+
26 “Mbingu zikifungwa hivi kwamba hakuna mvua inayonyesha,+ kwa sababu waliendelea kukutendea dhambi,+ nao kwa kweli wasali kuelekea mahali hapa+ na kulisifu jina lako, nao wageuke kutoka katika dhambi yao kwa sababu uliendelea kuwatesa,+ 27 basi na usikie ukiwa mbinguni, nawe usamehe dhambi ya watumishi wako, naam, ya watu wako Israeli, kwa sababu unawafundisha+ kuhusu njia nzuri+ wanayopaswa kutembea ndani yake; nawe unyeshe mvua+ juu ya nchi yako ambayo umewapa watu wako kuwa fungu la urithi.+
28 “Njaa ikitokea+ katika nchi, tauni+ ikitokea, kukitokea joto lenye kuunguza,+ ukungu,+ nzige+ na mende;+ adui+ zao wakiwazingira katika nchi ya malango yao+—pigo la namna yoyote na ugonjwa wa namna yoyote+ — 29 sala yoyote,+ ombi lolote la kutaka kibali+ ambalo huenda likatolewa na mwanadamu au na watu wako wote Israeli,+ kwa sababu wanajua kila mmoja wao pigo+ lake na maumivu yake mwenyewe; wakati anaponyoosha mikono yake kuelekea nyumba hii,+ 30 basi na usikie ukiwa mbinguni, makao yako,+ nawe usamehe+ na kumpa kila mmoja kulingana na njia zake zote,+ kwa sababu unaujua moyo wake+ (kwa maana ni wewe peke yako unayejua vema moyo wa wanadamu);+ 31 kusudi wakuogope+ kwa kutembea katika njia zako siku zote ambazo wako hai juu ya uso wa nchi ambayo uliwapa mababu zetu.+
32 “Na pia kwa mgeni ambaye si sehemu ya watu wako Israeli+ na ambaye anatoka katika nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako kuu+ na mkono wako wenye nguvu+ na mkono wako ulionyooshwa,+ nao kwa kweli waje na kusali kuelekea nyumba hii,+ 33 basi na usikilize ukiwa mbinguni, katika makao yako yaliyofanywa imara,+ nawe ufanye kulingana na yote ambayo mgeni huyo anakuomba;+ kusudi watu wote wa dunia wapate kulijua jina lako+ nao wakuogope+ kama vile watu wako Israeli wanavyokuogopa, na ili wajue kwamba jina lako limeitwa juu ya nyumba hii ambayo nimeijenga.+
34 “Watu wako wakitoka kwenda vitani+ kupigana na adui zao katika njia ambayo unawatuma,+ nao kwa kweli wasali+ kwako wakielekea upande wa jiji hili ambalo umelichagua na nyumba ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako,+ 35 basi usikie ukiwa mbinguni sala yao na ombi lao la kutaka kibali,+ nawe ufanye hukumu kwa ajili yao.+
36 “Nao wakikutendea dhambi+ (kwa sababu hakuna mwanadamu asiyetenda dhambi),+ nawe uwakasirikie na kuwatia mkononi mwa adui, na wenye kuwateka wawachukue mateka na kuwapeleka katika nchi ya adui iliyo mbali au iliyo karibu;+ 37 nao warudiwe na fahamu katika nchi ile ambayo wamechukuliwa mateka, nao hakika warudi na kutoa kwako ombi la kutaka kibali katika nchi ambayo wao ni mateka,+ wakisema, ‘Tumetenda dhambi,+ tumekosa+ nasi tumetenda uovu’;+ 38 nao kwa kweli warudi kwako kwa moyo wao wote+ na kwa nafsi yao yote katika nchi ambayo wao ni mateka+ wa wale waliowachukua mateka, nao kwa kweli wasali kuelekea upande wa nchi yao uliyowapa mababu zao na jiji ambalo umelichagua+ na nyumba ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako;+ 39 basi usikie ukiwa mbinguni, katika makao yako yaliyofanywa imara,+ sala yao na maombi yao ya kutaka kibali,+ nawe ufanye hukumu+ kwa ajili yao na kuwasamehe+ watu wako ambao wamekutendea dhambi.
40 “Basi, tafadhali, Ee Mungu wangu, macho+ yako yafunguliwe na masikio+ yako yaisikilize sala inayohusu mahali hapa. 41 Na sasa usimame,+ Ee Yehova Mungu, uingie katika pumziko lako,+ wewe pamoja na Sanduku la nguvu zako.+ Makuhani wako, Ee Yehova Mungu, na wavikwe wokovu, nao washikamanifu wako washangilie katika wema.+ 42 Ee Yehova Mungu, usiugeuze nyuma uso wa mtiwa-mafuta wako.+ Ee uzikumbuke fadhili zenye upendo kwa Daudi mtumishi wako.”+
7 Basi mara tu Sulemani alipomaliza kusali,+ moto ukashuka kutoka mbinguni,+ ukateketeza lile toleo la kuteketezwa+ na zile dhabihu, na utukufu+ wa Yehova ukaijaza nyumba ile. 2 Na makuhani hawakuweza kuingia ndani ya nyumba ya Yehova+ kwa sababu utukufu wa Yehova ulikuwa umeijaza nyumba ya Yehova. 3 Na wana wote wa Israeli walikuwa wakitazama wakati moto uliposhuka na utukufu wa Yehova ulipokuwa juu ya nyumba ile, kisha wakainama+ kifudifudi mara moja, juu ya sakafu ya mawe, wakasujudu+ na kumshukuru Yehova, “kwa maana yeye ni mwema,+ kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+
4 Na mfalme na watu wote walikuwa wakitoa dhabihu mbele za Yehova.+ 5 Na Mfalme Sulemani akatoa dhabihu ya ng’ombe 22,000 na kondoo 120,000.+ Hivyo ndivyo mfalme na watu wote walivyoizindua+ nyumba ya Mungu wa kweli. 6 Na makuhani+ walikuwa wamesimama katika vituo vyao vya kazi, na Walawi+ wakiwa na vyombo vya nyimbo+ kwa Yehova ambavyo Daudi+ mfalme alikuwa amevitengeneza ili kumshukuru Yehova, “kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo,” wakati Daudi alipokuwa akitoa sifa kwa mkono wao; na makuhani walikuwa wakipiga kwa sauti kubwa zile tarumbeta+ mbele zao, huku Israeli wote wakiwa wamesimama.
7 Kisha Sulemani akatakasa+ sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya nyumba ya Yehova, kwa sababu alitolea hapo yale matoleo ya kuteketezwa+ na vile vipande vya mafuta vya dhabihu za ushirika, kwa maana madhabahu ya shaba+ ambayo Sulemani alikuwa ametengeneza haikuweza kutoshea toleo la kuteketezwa na toleo la nafaka+ na vipande vya mafuta.+ 8 Na Sulemani akaifanya sherehe+ hiyo wakati huo kwa siku saba, na Israeli wote pamoja naye,+ kutaniko kubwa sana+ kuanzia maingilio ya Hamathi+ kushuka mpaka kwenye bonde la mto la Misri.+ 9 Lakini katika siku ya nane wakafanya kusanyiko kuu,+ kwa sababu kule kuzinduliwa kwa madhabahu walikuwa wamekufanya kwa siku saba na ile sherehe kwa siku saba. 10 Na katika siku ya 23 ya mwezi wa 7 akawaruhusu watu waende zao nyumbani kwao, wakiwa na shangwe+ na kuchangamka moyoni kutokana na wema+ ambao Yehova alikuwa amemtendea Daudi na Sulemani na Israeli watu wake.+
11 Hivyo Sulemani akaimaliza nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme;+ na kila jambo ambalo lilikuwa limeingia moyoni mwa Sulemani kufanya kuhusiana na nyumba ya Yehova na nyumba yake mwenyewe yeye alifanikiwa. 12 Sasa Yehova akamtokea+ Sulemani wakati wa usiku na kumwambia: “Nimeisikia sala yako,+ nami nimechagua+ mahali hapa kwa ajili yangu mwenyewe ili pawe nyumba ya dhabihu.+ 13 Ninapofunga mbingu ili mvua isinyeshe+ nami ninapoamuru panzi waile nchi+ nami nikileta tauni katikati ya watu wangu,+ 14 na watu wangu+ ambao jina langu limeitwa+ juu yao wajinyenyekeze+ na kusali+ na kuutafuta uso wangu+ na wageuke kutoka katika njia zao mbaya,+ basi mimi nitasikia nikiwa mbinguni+ na kusamehe dhambi yao,+ nami nitaiponya nchi yao.+ 15 Sasa macho+ yangu yatakuwa wazi na masikio+ yangu yatasikiliza sala katika mahali hapa. 16 Na sasa naichagua+ na kuitakasa nyumba hii ili jina langu+ liwe hapo mpaka wakati usio na kipimo,+ na macho yangu na moyo wangu vitakuwa hapo sikuzote.+
17 “Na wewe ukitembea mbele zangu, kama Daudi+ baba yako alivyotembea, kwa kutenda kulingana na yote ambayo nimekuamuru,+ nawe uyashike masharti+ yangu na maamuzi yangu ya hukumu+ 18 mimi pia nitakifanya imara kiti cha ufalme wako,+ kama nilivyofanya agano pamoja na Daudi baba yako,+ nikisema, ‘Hakuna mwanamume wa kwako atakayekatiliwa mbali asitawale juu ya Israeli.’+ 19 Lakini mkigeuka+ nyuma na kwa kweli mziache kanuni zangu+ na amri zangu+ ambazo nimeweka mbele yenu, nanyi kwa kweli mwende kuitumikia miungu mingine+ na kuiinamia,+ 20 mimi pia nitawang’oa kutoka katika nchi yangu ambayo nimewapa;+ na nyumba hii ambayo nimeitakasa+ kwa ajili ya jina langu, nitaitupilia mbali kutoka mbele za uso wangu,+ nami nitaifanya kuwa neno la kimethali+ na shutuma kati ya vikundi vyote vya watu.+ 21 Na nyumba hii iliyokuwa marundo ya mabomoko,+ kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao+ na kwa hakika aseme, ‘Kwa sababu gani Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+ 22 Nao watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova+ Mungu wa mababu zao, aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri,+ nao wakashikamana na miungu mingine+ na kuiinamia na kuitumikia.+ Ndiyo sababu alileta juu yao msiba huu wote.’”+
8 Na ikawa kwamba mwishoni mwa miaka 20,+ muda ambao Sulemani alitumia kujenga ile nyumba ya Yehova+ na nyumba yake mwenyewe,+ 2 yale majiji ambayo Hiramu+ alikuwa amempa Sulemani—Sulemani aliyajenga upya na kuwakalisha humo wana wa Israeli. 3 Na zaidi ya hayo, Sulemani akaenda Hamath-soba na kulishinda. 4 Ndipo akajenga upya Tadmori katika nyika na majiji yote yenye maghala+ aliyokuwa amejenga katika Hamathi.+ 5 Naye akajenga Beth-horoni ya Juu+ na Beth-horoni ya Chini,+ majiji yenye ngome yaliyo na kuta,+ milango na mapingo,+ 6 na Baalathi+ na majiji yote yenye maghala yaliyokuwa yamekuwa ya Sulemani na majiji yote ya magari+ na majiji ya wapanda-farasi+ na kila kitu chenye kutamanika cha Sulemani+ ambacho alikuwa ametamani kukijenga katika Yerusalemu na katika Lebanoni+ na katika nchi yote ya mamlaka yake.
7 Na watu wote waliokuwa wameachwa wa Wahiti+ na Waamori+ na Waperizi+ na Wahivi+ na Wayebusi,+ ambao hawakuwa sehemu ya Israeli,+ 8 kutoka kwa wana wao waliokuwa wameachwa baada yao katika nchi, ambao wana wa Israeli hawakuwaangamiza,+ Sulemani akaendelea kuwaandikisha+ kwa ajili ya kazi ya kulazimishwa mpaka leo hii.+ 9 Lakini Sulemani hakumfanya yeyote kati ya wana wa Israeli kuwa mtumwa kwa ajili ya kazi yake;+ kwa maana hao walikuwa mashujaa wa vita+ na wakuu wa maamiri wake wasaidizi na wakuu wa waendesha-magari+ wake na wakuu wa wapanda-farasi+ wake. 10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa wasaidizi+ wa Mfalme Sulemani, watu 250, wasimamizi wa kazi juu ya watu.+
11 Na Sulemani akamtoa binti ya Farao+ katika Jiji la Daudi,+ akampeleka katika nyumba aliyokuwa amemjengea,+ kwa maana alisema: “Ingawa yeye ni mke wangu, asikae katika nyumba ya Daudi mfalme wa Israeli, kwa maana mahali ambapo sanduku la Yehova limeletwa ni patakatifu.”+
12 Ndipo wakati huo Sulemani akamtolea Yehova dhabihu+ za kuteketezwa juu ya ile madhabahu+ ya Yehova ambayo alikuwa amejenga mbele ya ukumbi,+ 13 kama desturi ya kila siku+ ili kutoa matoleo kulingana na amri ya Musa kwa ajili ya sabato+ na kwa ajili ya miezi mipya+ na kwa ajili ya sherehe rasmi+ mara tatu kwa mwaka,+ kwenye sherehe ya keki zisizo na chachu+ na kwenye sherehe ya majuma+ na kwenye sherehe ya vibanda.+ 14 Tena akaweka ile migawanyo+ ya makuhani juu ya utumishi wao kulingana na kanuni ya Daudi baba yake,+ na Walawi+ katika vituo vyao vya kazi, ili kusifu+ na kuhudumu+ mbele ya makuhani kama desturi ya kila siku,+ na watunza-malango katika migawanyo yao kwa ajili ya malango mbalimbali,+ kwa maana hivyo ndivyo ilivyokuwa amri ya Daudi mtu wa Mungu wa kweli. 15 Nao hawakuiacha amri ya mfalme kwa makuhani na Walawi kuhusu jambo lolote na kuhusu akiba ya mali.+ 16 Basi kazi yote ya Sulemani ilikuwa katika hali iliyotayarishwa+ kuanzia siku ya kuweka msingi wa nyumba ya Yehova mpaka ilipomalizika.+ Basi nyumba ya Yehova ikamalizika.+
17 Wakati huo ndipo Sulemani alipoenda Esion-geberi+ na Elothi+ kando ya bahari katika nchi ya Edomu.+ 18 Naye Hiramu+ kupitia watumishi wake akampelekea kwa ukawaida meli na watumishi wenye ujuzi wa bahari,+ nao wakawa wakienda Ofiri+ pamoja na watumishi wa Sulemani na kuchukua kutoka huko talanta 450+ za dhahabu,+ wakamletea Mfalme Sulemani.+
9 Na malkia wa Sheba+ akasikia habari za Sulemani, naye akaja Yerusalemu ili kumjaribu Sulemani kwa maswali yenye kutatanisha,+ pamoja na msafara wenye kuvutia sana na ngamia+ wenye kuchukua mafuta ya zeri,+ na dhahabu+ nyingi sana, na mawe ya thamani.+ Mwishowe akaingia kwa Sulemani na kumwambia kila jambo lililokuwa moyoni mwake.+ 2 Naye Sulemani akamwambia mambo yake yote,+ hakuna jambo lolote lililofichwa kwa Sulemani ambalo hakumwambia yule malkia.+
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima+ ya Sulemani na ile nyumba aliyokuwa amejenga,+ 4 na chakula cha meza+ yake na kuketi kwa watumishi wake na utumishi wa mezani wa wale wenye kumhudumia na mavazi+ yao na wanyweshaji+ wake na mavazi yao, na dhabihu zake za kuteketezwa+ alizotoa kwa ukawaida katika nyumba ya Yehova,+ basi haikubaki roho yoyote ndani yake. 5 Kwa hiyo akamwambia mfalme: “Ni la kweli neno lile nililosikia katika nchi yangu kuhusu mambo yako na kuhusu hekima yako.+ 6 Nami sikuyaamini+ maneno yao mpaka nilipokuja ili nijionee kwa macho yangu mwenyewe;+ na, tazama! sikuambiwa hata nusu ya wingi wa hekima yako.+ Umezidi ile habari niliyosikia.+ 7 Watu wako ni wenye furaha,+ na ni wenye furaha hawa watumishi wako wanaosimama mbele yako daima na kuisikiliza hekima yako.+ 8 Na abarikiwe Yehova Mungu wako,+ ambaye amependezwa+ nawe kwa kukuweka juu ya kiti chake cha ufalme+ uwe mfalme kwa ajili ya Yehova Mungu wako;+ kwa sababu Mungu wako alipenda+ Israeli, ili kuisimamisha mpaka wakati usio na kipimo, hivi kwamba akakuweka juu yao uwe mfalme+ ili utende uamuzi wa hukumu+ na uadilifu.”+
9 Ndipo akampa mfalme talanta 120 za dhahabu,+ na mafuta ya zeri+ kwa wingi sana, na mawe ya thamani;+ na kulikuwa hakujapata kuwa na mafuta ya zeri kama yale ambayo malkia wa Sheba alimpa Mfalme Sulemani.+
10 Na zaidi ya hayo, watumishi wa Hiramu+ na watumishi wa Sulemani walioleta dhahabu+ kutoka Ofiri walileta mbao za misandali+ na mawe ya thamani.+ 11 Na mfalme akatengeneza kwa zile mbao za misandali ngazi+ kwa ajili ya nyumba ya Yehova na kwa ajili ya nyumba ya mfalme+ na pia vinubi+ na vinanda+ vya waimbaji,+ na vitu kama hivyo havikuwa vimepata kuonekana kabla ya hapo katika nchi ya Yuda.
12 Na Mfalme Sulemani akampa malkia+ wa Sheba vyote vilivyompendeza, ambavyo aliomba, zaidi ya thamani ya vitu alivyomletea mfalme. Basi akageuka, akaenda katika nchi yake, yeye pamoja na watumishi wake.+
13 Na uzito wa dhahabu iliyoletwa kwa Sulemani katika mwaka mmoja ulijumlika kuwa talanta 666 za dhahabu,+ 14 zaidi ya zile zilizoletwa na wasafiri na wanabiashara+ waliokuwa wakileta na wafalme wote wa Waarabu+ na magavana wa nchi waliokuwa wakimletea Sulemani dhahabu na fedha.
15 Na Mfalme Sulemani akatengeneza ngao kubwa mia mbili za dhahabu iliyochanganywa+ (akaweka shekeli mia sita za dhahabu iliyochanganywa kwenye kila ngao kubwa),+ 16 na ngao ndogo mia tatu za dhahabu iliyochanganywa (akaweka mina tatu za dhahabu kwenye kila ngao ndogo).+ Kisha mfalme akaziweka katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni.+
17 Tena mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha ufalme cha pembe za tembo na kukifunika kwa dhahabu safi.+ 18 Na kulikuwa na vipandio sita vilivyoelekea kwenye kile kiti cha ufalme, na kulikuwa na kiti cha miguu cha dhahabu kwenye kile kiti cha ufalme, (vilikuwa vimeunganishwa), na kulikuwa na mikono ya kiti upande huu na upande ule kando ya mahali pa kuketi, na simba+ wawili walisimama kando ya ile mikono ya kiti.+ 19 Na kulikuwa na simba+ kumi na wawili waliosimama hapo juu ya vile vipandio sita, upande huu na upande ule. Hakuna ufalme mwingine wowote uliokuwa na kiti kilichotengenezwa hivyo.+ 20 Na vyombo+ vyote vya kunywea vya Mfalme Sulemani vilikuwa vya dhahabu,+ na vyombo vyote vya Nyumba ya Msitu wa Lebanoni+ vilikuwa vya dhahabu safi. Hapakuwa na kitu chochote cha fedha; haikuhesabiwa kuwa kitu+ katika siku za Sulemani. 21 Kwa maana meli za mfalme zilikuwa zikienda Tarshishi+ pamoja na watumishi wa Hiramu.+ Mara moja kila miaka mitatu meli za Tarshishi zilikuja, zikiwa zimebeba dhahabu na fedha,+ pembe za tembo,+ na sokwe na tausi.+
22 Basi Mfalme Sulemani alikuwa mkuu katika utajiri+ na hekima+ kuliko wafalme wengine wote wa dunia. 23 Na wafalme wote wa dunia walikuwa wakiutafuta+ uso wa Sulemani ili wasikie hekima+ yake, ambayo Mungu wa kweli alikuwa ametia moyoni mwake.+ 24 Nao walikuwa wakileta kila mmoja zawadi yake,+ vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu+ na mavazi,+ silaha na mafuta ya zeri, farasi na nyumbu kama kawaida ya kila mwaka.+ 25 Na Sulemani akawa na vibanda elfu nne vya farasi+ na magari na farasi+ wa vita kumi na mbili elfu, naye akaviweka vitu hivyo katika majiji ya magari+ na karibu na mfalme katika Yerusalemu. 26 Naye akawa mtawala juu ya wafalme wote kuanzia ule Mto hadi kwenye nchi ya Wafilisti na hadi kwenye mpaka wa Misri.+ 27 Tena mfalme akaifanya fedha iliyomo Yerusalemu kuwa kama mawe; naye akaifanya mierezi iwe kama mikuyu+ iliyoko Shefela+ kwa wingi.+ 28 Na kulikuwa na wale waliomletea Sulemani farasi+ kutoka Misri+ na kutoka katika nchi nyingine zote.
29 Na mambo mengine ya Sulemani,+ ya kwanza na ya mwisho, je, hayakuandikwa kati ya maneno ya Nathani+ nabii na katika unabii wa Ahiya+ Mshilo,+ na katika kumbukumbu ya maono ya Ido+ mwonaji kumhusu Yeroboamu+ mwana wa Nebati?+ 30 Na Sulemani akaendelea kutawala katika Yerusalemu juu ya Israeli yote kwa miaka 40. 31 Mwishowe Sulemani akalala pamoja na mababu zake. Basi wakamzika katika Jiji la Daudi baba yake;+ na Rehoboamu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.+
10 Na Rehoboamu+ akaenda Shekemu,+ kwa maana Waisraeli wote walikuja Shekemu ili kumfanya kuwa mfalme. 2 Na ikawa kwamba mara tu Yeroboamu+ mwana wa Nebati aliposikia habari hizo alipokuwa angali Misri,+ (kwa maana alikuwa amekimbia kwa sababu ya Sulemani mfalme,) Yeroboamu akarudi mara moja kutoka Misri.+ 3 Basi wakatuma watu wamwite, na Yeroboamu na Israeli wote wakaja, wakamwambia Rehoboamu, wakisema:+ 4 “Baba yako aliifanya nira yetu kuwa ngumu;+ na sasa wewe ufanye ule utumishi mgumu wa baba yako na ile nira nzito+ aliyoweka juu yetu kuwa rahisi, nasi tutakutumikia.”+
5 Ndipo akawaambia: “Na kupite siku tatu. Kisha mrudi kwangu.” Basi watu wakaenda zao. 6 Na Mfalme Rehoboamu akaanza kushauriana+ na wanaume wazee waliokuwa wakimhudumia Sulemani baba yake sikuzote alipokuwa angali hai, akisema: “Mnatoa shauri gani la kuwajibu watu hawa?”+ 7 Basi wakasema naye, wakimwambia: “Ukiwa mwema kwa watu hawa na kuwapendeza na kusema nao maneno mema,+ wao pia watakuwa watumishi wako sikuzote.”+
8 Hata hivyo, akaliacha shauri+ la wanaume wazee walilomshauri, naye akaanza kushauriana na vijana waliokua pamoja naye,+ waliokuwa wakimhudumia.+ 9 Naye akawaambia: “Mnatoa shauri gani+ ili tuwajibu watu hawa ambao wamesema nami, wakiniambia, ‘Ifanye nira ambayo baba yako aliweka juu yetu iwe rahisi’?”+ 10 Ndipo wale vijana waliokua pamoja naye wakamwambia, wakisema: “Waambie hivi watu ambao wamesema nawe, ‘Baba yako aliifanya nira yetu kuwa nzito, lakini wewe ifanye iwe rahisi juu yetu’; wewe waambie hivi,+ ‘Kidole changu kidogo kwa hakika kitakuwa kinene kuliko kiuno cha baba yangu.+ 11 Na sasa baba yangu aliweka juu yenu nira nzito, lakini mimi nitaizidisha nira yenu.+ Baba yangu aliwatia ninyi adabu kwa fimbo, lakini mimi nitawatia adabu kwa mijeledi.’”+
12 Na Yeroboamu na watu wote wakamjia Rehoboamu siku ya tatu, kama mfalme alivyosema: “Rudini kwangu siku ya tatu.”+ 13 Na mfalme akaanza kuwajibu kwa ukali.+ Basi Mfalme Rehoboamu akaliacha shauri+ la wanaume wazee,+ 14 naye akasema nao kulingana na lile shauri la vijana,+ akisema: “Nitaifanya nira yenu iwe nzito zaidi, nami nitaizidisha. Baba yangu aliwatia ninyi adabu kwa fimbo, lakini mimi nitawatia adabu kwa mijeledi.”+ 15 Na mfalme hakuwasikiliza watu; kwa maana Mungu wa kweli+ ndiye aliyeongoza mambo ili Yehova atimize neno+ lake alilomwambia Yeroboamu mwana wa Nebati+ kupitia Ahiya+ Mshilo.+
16 Nao Israeli wote, kwa sababu mfalme hakuwasikiliza, hao watu sasa wakamjibu mfalme, wakisema: “Tuna fungu gani katika Daudi?+ Wala hakuna urithi katika mwana wa Yese.+ Kila mmoja aende kwa miungu yake,+ Ee Israeli! Sasa angalia nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi.”+ Kwa hiyo Israeli wote wakaanza kwenda katika mahema yao.
17 Naye Rehoboamu akaendelea kutawala juu ya wana wa Israeli waliokuwa wakikaa katika majiji ya Yuda.+
18 Basi Mfalme Rehoboamu akamtuma Hadoramu,+ aliyekuwa juu ya wale walioandikishwa kufanya kazi ya kulazimishwa, lakini wana wa Israeli wakampiga kwa mawe,+ naye akafa. Naye Mfalme Rehoboamu akafaulu kupanda katika gari lake, akakimbia kwenda Yerusalemu.+ 19 Na Waisraeli wakaendeleza maasi+ yao juu ya nyumba ya Daudi mpaka leo hii.
11 Rehoboamu alipofika Yerusalemu,+ mara moja akaikutanisha nyumba ya Yuda na Benyamini,+ wanaume bora, watu hodari wa vita,+ watu 180,000, wapigane na Israeli ili kuurudisha ufalme kwa Rehoboamu. 2 Ndipo neno la Yehova likamjia Shemaya+ mtu wa Mungu wa kweli, na kusema: 3 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani mfalme wa Yuda+ na Israeli wote katika Yuda na Benyamini, ukisema, 4 ‘Yehova amesema hivi: “Msipande kwenda kupigana na ndugu zenu.+ Mrudi kila mmoja nyumbani kwake, kwa maana jambo hili limetokea kwa mwongozo wangu.”’”+ Basi wakalitii neno la Yehova, wakarudi, ili wasiende kupigana na Yeroboamu.+
5 Na Rehoboamu akaendelea kukaa Yerusalemu, akajenga majiji yenye ngome katika Yuda. 6 Basi akajenga upya Bethlehemu+ na Etamu+ na Tekoa,+ 7 na Beth-suri+ na Soko+ na Adulamu,+ 8 na Gathi+ na Maresha+ na Zifu,+ 9 na Adoraimu na Lakishi+ na Azeka,+ 10 na Sora+ na Aiyaloni+ na Hebroni,+ majiji yenye ngome, yaliyokuwa katika Yuda na Benyamini. 11 Zaidi ya hayo, akaimarisha mahali penye ngome+ na kuweka viongozi+ ndani yake na akiba za chakula na mafuta na divai, 12 na katika majiji yote mbalimbali akaweka ngao+ kubwa na mikuki;+ naye akaendelea kuyaimarisha kwa kiwango kikubwa sana. Na watu wa Yuda na Benyamini wakaendelea kuwa wake.
13 Na makuhani na Walawi waliokuwa katika Israeli yote wakasimama upande wake kutoka katika maeneo yao yote. 14 Kwa maana Walawi waliviacha viwanja vyao vya malisho+ na miliki+ yao kisha wakaja Yuda na Yerusalemu,+ kwa sababu Yeroboamu+ na wanawe walikuwa wamewaondoa+ wasiwe makuhani kwa Yehova. 15 Naye akajiwekea mwenyewe katika cheo makuhani wa mahali pa juu+ na wa roho waovu wenye umbo la mbuzi+ na wa wale ndama aliokuwa ametengeneza.+ 16 Na wale waliowafuata kutoka katika makabila yote ya Israeli, ambao walikuwa wakitoa moyo wao kumtafuta Yehova Mungu wa Israeli, wakaja Yerusalemu+ kumtolea dhabihu+ Yehova Mungu wa mababu zao. 17 Nao wakaendelea kuutia nguvu ufalme wa Yuda+ na kumthibitisha Rehoboamu mwana wa Sulemani kwa miaka mitatu, kwa maana walitembea katika njia ya Daudi na Sulemani kwa miaka mitatu.+
18 Ndipo Rehoboamu akamchukua Mahalathi binti ya Yerimothi mwana wa Daudi awe mke wake, na ya Abihaili binti ya Eliabu+ mwana wa Yese. 19 Baada ya muda akamzalia wana, Yeushi na Shemaria na Zahamu. 20 Na baada yake akamchukua Maaka+ mjukuu wa Absalomu.+ Baada ya muda akamzalia Abiya+ na Atai na Ziza na Shelomithi. 21 Na Rehoboamu alimpenda zaidi Maaka mjukuu wa Absalomu kuliko wale wake+ zake wengine wote na masuria wake; kwa maana alikuwa amechukua wake 18, pia masuria 60, hivi kwamba akawa na wana 28 na binti 60. 22 Kwa hiyo Rehoboamu akamweka Abiya mwana wa Maaka katika cheo awe kichwa, awe kiongozi kati ya ndugu zake, kwa maana alifikiria kumfanya kuwa mfalme. 23 Hata hivyo, akatenda kwa uelewaji+ na kuwagawanya baadhi ya wanawe wote kwenye nchi zote za Yuda na Benyamini,+ kwenye majiji yote yenye ngome,+ akawapa chakula kwa wingi+ na kuwachukulia wake wengi.+
12 Na ikawa kwamba mara tu ufalme wa Rehoboamu ulipofanywa imara+ na mara tu alipokuwa na nguvu, akaiacha sheria ya Yehova,+ na pia Israeli+ wote pamoja naye. 2 Na ikawa kwamba katika mwaka wa tano wa Mfalme Rehoboamu,+ Shishaki+ mfalme wa Misri akaja kushambulia Yerusalemu, (kwa maana walikuwa wamejiendesha kwa ukosefu wa uaminifu kwa Yehova,)+ 3 akiwa na magari+ 1,200 na wapanda-farasi 60,000; na hawakuwa na hesabu+ wale watu waliotoka Misri pamoja naye —Walibya,+ Wasukii na Waethiopia.+ 4 Naye akayateka majiji yenye ngome yaliyokuwa ya Yuda,+ na mwishowe akaja mpaka Yerusalemu.+
5 Sasa Shemaya+ nabii akamjia Rehoboamu na wakuu wa Yuda waliokuwa wamekusanyika Yerusalemu kwa sababu ya Shishaki, naye akawaambia: “Yehova amesema hivi, ‘Ninyi mmeniacha mimi,+ nami pia nimewaacha ninyi+ mkononi mwa Shishaki.’” 6 Ndipo wakuu wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza+ na kusema: “Yehova ni mwadilifu.”+ 7 Na Yehova alipoona+ kwamba wamejinyenyekeza, neno la Yehova likamjia Shemaya,+ na kusema: “Wamejinyenyekeza.+ Sitawaharibu, na baada ya kitambo kidogo nitawafanya waponyoke, na ghadhabu yangu haitamwagika juu ya Yerusalemu kwa mkono wa Shishaki.+ 8 Lakini wao watakuwa watumishi wake,+ ili wajue tofauti kati ya utumishi+ wangu na utumishi kwa falme za nchi.”+
9 Basi Shishaki+ mfalme wa Misri akapanda kushambulia Yerusalemu, akachukua hazina za nyumba ya Yehova+ na hazina za nyumba ya mfalme.+ Akachukua kila kitu; kwa hiyo akazichukua zile ngao za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.+ 10 Basi Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba mahali pake, akaziweka chini ya wakuu wa wakimbiaji,+ walinzi+ wa mlango wa nyumba ya mfalme.+ 11 Na ikawa ikitukia kwamba kila mara mfalme akija katika nyumba ya Yehova, wakimbiaji waliingia na kuzichukua na kuzirudisha katika chumba cha walinzi cha wakimbiaji.+ 12 Na kwa sababu alijinyenyekeza, hasira ya Yehova ikageuka,+ ikaondoka juu yake, naye hakufikiria kuwaharibu kabisa.+ Na zaidi ya hayo, kulikuwa na mambo mema katika Yuda.+
13 Na Mfalme Rehoboamu akaendelea kuimarisha cheo chake katika Yerusalemu na kuendelea kutawala; kwa maana Rehoboamu+ alikuwa na umri wa miaka 41 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 17 katika Yerusalemu, jiji+ ambalo Yehova alichagua kutoka katika makabila yote ya Israeli ili kuweka jina lake humo.+ Na jina la mama yake lilikuwa Naama+ Mwamoni.+ 14 Lakini yeye alifanya yaliyokuwa mabaya,+ kwa maana hakuwa ameufanya imara moyo wake ili kumtafuta Yehova.+
15 Na mambo ya Rehoboamu, ya kwanza na ya mwisho,+ je, hayakuandikwa kati ya maneno ya Shemaya+ nabii na Ido+ mwonaji kulingana na maandikisho ya kiukoo? Na kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu+ na Yeroboamu+ wakati wote. 16 Mwishowe Rehoboamu akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa katika Jiji la Daudi;+ na Abiya+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
13 Abiya alianza kutawala Yuda+ katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yeroboamu. 2 Akatawala miaka mitatu katika Yerusalemu, na jina la mama yake lilikuwa Mikaya+ binti ya Urieli wa Gibea.+ Na vita vikatokea kati ya Abiya na Yeroboamu.+
3 Basi Abiya akaingia vitani na jeshi la wanaume wenye nguvu wa vita,+ mia nne elfu, wanaume waliochaguliwa. Naye Yeroboamu akajipanga kivita kupigana naye akiwa na wanaume waliochaguliwa mia nane elfu, mashujaa, wanaume wenye nguvu.+ 4 Sasa Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, ulio katika eneo lenye milima la Efraimu,+ na kusema: “Mnisikilize, Ee Yeroboamu na Israeli wote. 5 Je, si juu yenu kujua kwamba Yehova Mungu wa Israeli mwenyewe alimpa Daudi+ ufalme juu ya Israeli mpaka wakati usio na kipimo,+ kwake na kwa wanawe,+ kwa agano la chumvi?+ 6 Na Yeroboamu+ mwana wa Nebati, mtumishi+ wa Sulemani mwana wa Daudi, akasimama na kumwasi+ bwana wake.+ 7 Na watu wazembe,+ watu wasiofaa kitu,+ wakaendelea kujikusanya kando yake. Mwishowe wakawa na nguvu kuliko Rehoboamu mwana wa Sulemani, wakati Rehoboamu+ alipokuwa mchanga na mwenye moyo mwoga,+ naye hakuweza kusimama kupigana nao.
8 “Na sasa ninyi mnafikiri juu ya kusimama imara kupigana na ufalme wa Yehova mkononi mwa wana wa Daudi,+ huku mkiwa umati mkubwa+ nanyi mna ndama wa dhahabu ambao Yeroboamu aliwatengenezea ninyi kuwa miungu.+ 9 Je, hamkuwafukuza makuhani+ wa Yehova, wana wa Haruni, na Walawi, na je, hamwendelei kujifanyia makuhani kama vikundi vya watu wa nchi?+ Na yeyote aliyekuja na kujaza mkono wake nguvu kupitia ng’ombe-dume mchanga na kondoo-dume saba, akawa kuhani wa vitu ambavyo si miungu.+ 10 Lakini sisi, Yehova ndiye Mungu wetu,+ nasi hatujamwacha; lakini makuhani wanamtumikia Yehova, wana wa Haruni, na pia Walawi katika kazi.+ 11 Nao wanamfukizia Yehova toleo la kuteketezwa asubuhi baada ya asubuhi na jioni baada ya jioni+ na pia uvumba uliotiwa manukato;+ na tabaka za mkate ziko juu ya meza ya dhahabu safi,+ na kuna kinara cha taa+ cha dhahabu na taa zake ili kuwaka jioni baada ya jioni;+ kwa sababu tunashika wajibu+ kwa Yehova Mungu wetu, lakini ninyi mmemwacha.+ 12 Na tazama! pamoja nasi yuko mbele yetu Mungu wa kweli+ pamoja na makuhani+ wake na tarumbeta+ za ishara kwa ajili ya kupiga king’ora cha vita juu yenu. Enyi wana wa Israeli, msipigane na Yehova Mungu wa mababu zenu,+ kwa maana hamtafanikiwa.”+
13 Naye Yeroboamu akapeleka kikundi cha kuvizia kizunguke kwenda nyuma yao, hivi kwamba wakawa mbele ya Yuda na kile kikundi cha kuvizia kikawa nyuma yao.+ 14 Wakati wale wa Yuda walipogeuka, tazama, hapo walikuwa na pigano mbele na nyuma.+ Nao wakaanza kumlilia Yehova,+ huku makuhani wakipiga tarumbeta kwa sauti kubwa. 15 Na watu wa Yuda wakaanza kupiga kelele za vita.+ Na ikawa kwamba, watu wa Yuda walipopiga kelele za vita, ndipo Mungu wa kweli akamshinda+ Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Abiya+ na Yuda. 16 Na wana wa Israeli wakaanza kukimbia kutoka mbele ya Yuda, ndipo Mungu akawatia mkononi mwao.+ 17 Na Abiya na watu wake wakawapiga kwa mauaji makubwa; na waliouawa wa Israeli wakaendelea kuanguka chini, wanaume waliochaguliwa, mia tano elfu. 18 Basi wana wa Israeli wakatiishwa wakati huo, lakini wana wa Yuda walishinda kwa sababu walimtegemea+ Yehova Mungu wa mababu zao. 19 Na Abiya akaendelea kumfuatilia Yeroboamu, akateka majiji kutoka kwake, Betheli+ na miji yake ya kandokando, na Yeshana na miji yake ya kandokando, na Efraini na miji yake ya kandokando.+ 20 Na Yeroboamu hakuwa na nguvu+ tena katika siku za Abiya; lakini Yehova akampiga,+ hivi kwamba akafa.
21 Na Abiya akaendelea kujitia nguvu.+ Baada ya muda akajichukulia wake 14,+ akazaa wana 22+ na binti 16. 22 Na yale mambo mengine ya Abiya, njia zake na maneno yake, yameandikwa katika ufafanuzi wa nabii Ido.+
14 Mwishowe Abiya akalala pamoja na mababu zake,+ nao wakamzika katika Jiji la Daudi;+ na Asa+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake. Katika siku zake nchi haikuwa na usumbufu+ kwa miaka kumi.
2 Na Asa akafanya yaliyokuwa mema na sawa machoni pa Yehova Mungu wake. 3 Basi akaondoa madhabahu za kigeni+ na mahali pa juu,+ akazivunja nguzo takatifu+ na kuikata miti mitakatifu.+ 4 Tena akawaambia Yuda wamtafute+ Yehova Mungu wa mababu zao na kutenda sheria+ na amri.+ 5 Kwa hiyo akaondoa katika majiji yote ya Yuda mahali pa juu na vinara vya uvumba;+ na ufalme ukaendelea bila usumbufu+ mbele yake. 6 Naye akajenga majiji yenye ngome katika Yuda,+ kwa maana nchi haikuwa na usumbufu; na hapakuwa na vita juu yake wakati wa miaka hiyo, kwa maana Yehova alimpa pumziko.+ 7 Basi akawaambia Yuda: “Acheni tujenge majiji haya na tujenge kuta+ za kuzunguka na minara,+ milango yenye pande mbili na mapingo.+ Nchi bado inapatikana kwa ajili yetu, kwa sababu tumemtafuta Yehova Mungu wetu.+ Tumemtafuta, naye anatupa pumziko kuzunguka pande zote.”+ Nao wakajenga na kufanikiwa.+
8 Na Asa akawa na jeshi lenye kuchukua ngao kubwa+ na mkuki,+ watu 300,000 kutoka Yuda.+ Na kutoka Benyamini wale wanaochukua ngao ndogo na kupinda upinde+ walikuwa 280,000.+ Hao wote walikuwa mashujaa, wanaume wenye nguvu.
9 Baadaye Zera Mwethiopia+ akaenda kupigana nao akiwa na jeshi la watu milioni moja+ na magari mia tatu, akaja mpaka Maresha.+ 10 Ndipo Asa akatoka kwenda juu yake, nao wakajipanga kivita katika bonde la Sefatha kule Maresha. 11 Naye Asa akaanza kumwita Yehova Mungu+ wake, na kusema: “Ee Yehova, kwa habari ya kusaidia, si kitu kwako kama kuna wengi au wale wasio na nguvu.+ Utusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana sisi tunakuegemea wewe,+ nasi kwa jina lako+ tumekuja kupigana na umati huu. Ee Yehova, wewe ni Mungu wetu.+ Usiache mwanadamu anayeweza kufa apate nguvu juu yako.”+
12 Ndipo Yehova akawashinda+ Waethiopia mbele ya Asa na mbele ya Yuda, na Waethiopia wakakimbia. 13 Na Asa na watu waliokuwa pamoja naye wakaendelea kuwafuatilia mpaka Gerari,+ na walio wa Waethiopia wakaendelea kuanguka mpaka wakati ambapo hapakuwa na yeyote aliye hai kati yao; kwa maana walivunjwa vipande-vipande mbele za Yehova+ na mbele ya jeshi lake.+ Baadaye wakachukua kiasi kikubwa sana cha nyara.+ 14 Tena wakayapiga majiji yote pande zote kuzunguka Gerari, kwa maana hofu+ ya Yehova ilikuwa imekuja juu yao; nao wakayapora majiji yote, kwa maana kulikuwa na vitu vingi vya kupora katika majiji hayo.+ 15 Na hata wakayapiga mahema+ yenye mifugo hivi kwamba wakateka+ kwa wingi sana mifugo na ngamia,+ kisha wakarudi Yerusalemu.
15 Sasa roho+ ya Mungu ikaja juu ya Azaria mwana wa Odedi.+ 2 Kwa hiyo akaenda mbele ya Asa na kumwambia: “Mnisikilize mimi, Ee Asa na Yuda wote na Benyamini! Yehova yuko pamoja nanyi ikiwa ninyi mko pamoja naye;+ nanyi mkimtafuta,+ atawaruhusu mumpate, lakini mkimwacha yeye atawaacha ninyi.+ 3 Na kwa siku nyingi Israeli+ hawakuwa na Mungu wa kweli wala kuhani mwenye kufundisha+ wala Sheria. 4 Lakini waliporudi kwa Yehova Mungu wa Israeli,+ wakiwa katika taabu yao,+ na kumtafuta, basi aliwaruhusu wampate.+ 5 Na nyakati hizo hapakuwa na amani kwa yule anayetoka wala kwa yule anayeingia,+ kwa sababu kulikuwa na machafuko mengi kati ya wakaaji wote wa nchi mbalimbali.+ 6 Nao walivunjwa vipande-vipande, taifa kupigana na taifa+ na jiji kupigana na jiji, kwa sababu Mungu aliendelea kuwatia katika machafuko kwa kila namna ya taabu.+ 7 Nanyi iweni hodari+ na msiache mikono yenu ilegee,+ kwa sababu kuna thawabu kwa ajili ya kazi yenu.”+
8 Na mara tu Asa alipoyasikia maneno hayo na unabii wa Odedi+ nabii, akajipa moyo, akaondoa kabisa machukizo+ katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na katika majiji aliyokuwa ameteka kutoka katika eneo lenye milima la Efraimu,+ na kuifanya upya madhabahu ya Yehova iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Yehova.+ 9 Naye akaanza kukusanya pamoja Yuda wote na Benyamini+ na wakaaji wageni+ waliokuwa pamoja nao kutoka katika Efraimu na Manase na Simeoni, kwa maana walikuwa wamekimbia wakamwendea kutoka katika Israeli wakiwa hesabu kubwa walipoona kwamba Yehova Mungu wake alikuwa pamoja naye.+ 10 Basi wakakusanywa pamoja katika Yerusalemu mwezi wa tatu wa mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa. 11 Ndipo wakamtolea Yehova dhabihu siku hiyo kutokana na zile nyara walizoleta, ng’ombe mia saba na kondoo elfu saba. 12 Zaidi ya hayo, wakaingia katika agano+ ili kumtafuta Yehova Mungu wa mababu zao kwa moyo wao wote na kwa nafsi yao yote;+ 13 kwamba yeyote ambaye hangemtafuta Yehova Mungu wa Israeli, auawe,+ iwe ni mdogo au ni mkubwa,+ iwe ni mwanamume au ni mwanamke.+ 14 Basi wakamwapia+ Yehova kwa sauti kubwa na kwa sauti za shangwe na kwa tarumbeta na kwa baragumu. 15 Na Yuda wote wakaanza kushangilia+ juu ya lile jambo waliloapa; kwa maana walikuwa wameapa kwa moyo wao wote nao walikuwa wamemtafuta kwa furaha kamili hivi kwamba yeye aliwaruhusu wampate;+ na Yehova akaendelea kuwapa pumziko kuzunguka pande zote.+
16 Naye Asa mfalme+ akamwondoa hata Maaka+ nyanya yake asiwe malkia,+ kwa sababu alikuwa ametengeneza sanamu yenye kutisha kwa ajili ya mti mtakatifu;+ kisha Asa akaikata sanamu yake yenye kutisha+ na kuiponda na kuiteketeza kwa moto+ katika bonde la mto la Kidroni.+ 17 Na mahali pa juu+ hapakuondolewa katika Israeli.+ Ila moyo wa Asa ulikuwa mkamilifu siku zake zote.+ 18 Naye akaanza kuviingiza ndani ya nyumba ya Mungu wa kweli vitu ambavyo baba yake alivifanya kuwa vitakatifu na vitu+ ambavyo yeye mwenyewe alivifanya kuwa vitakatifu, fedha na dhahabu na vyombo.+ 19 Wala vita havikutokea mpaka katika mwaka wa 35 wa utawala wa Asa.+
16 Katika mwaka wa 36 wa utawala wa Asa, Baasha+ mfalme wa Israeli alikuja kupigana na Yuda na kuanza kujenga Rama,+ ili asimruhusu mtu yeyote kutoka nje wala kuingia ndani kwa Asa mfalme wa Yuda.+ 2 Sasa Asa akatoa fedha na dhahabu katika hazina za nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme,+ akazipeleka kwa Ben-hadadi+ mfalme wa Siria,+ aliyekuwa akikaa Damasko,+ akisema: 3 “Kuna agano kati yangu na wewe na kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, ninakuletea fedha na dhahabu. Nenda, vunja agano lako na Baasha+ mfalme wa Israeli, ili aondoke kwangu.”+
4 Basi Ben-hadadi akamsikiliza Mfalme Asa, akatuma wakuu wake wa majeshi kushambulia majiji ya Israeli, hivi kwamba wakapiga Iyoni+ na Dani+ na Abel-maimu+ na mahali pote penye maghala+ pa majiji ya Naftali.+ 5 Na ikawa kwamba mara tu Baasha aliposikia habari hizo, mara moja akaacha kujenga Rama na kuikomesha kazi yake.+ 6 Naye Asa mfalme akawachukua Yuda wote,+ nao wakachukua mawe ya Rama+ na miti yake ambayo Baasha alitumia kujenga,+ naye kwa vitu hivyo akaanza kujenga Geba+ na Mispa.+
7 Na wakati huo Hanani+ mwonaji akamjia Asa mfalme wa Yuda, kisha akamwambia: “Kwa sababu ulimwegemea mfalme wa Siria+ wala hukumwegemea Yehova Mungu wako,+ kwa sababu hiyo jeshi la mfalme wa Siria limeponyoka kutoka mkononi mwako. 8 Je, Waethiopia+ na Walibya+ hawakuwa jeshi kubwa sana kwa wingi, kwa magari na kwa wapanda-farasi;+ na kwa sababu ulimwegemea Yehova, je, hakuwatia mkononi mwako?+ 9 Kwa maana, kwa habari ya Yehova, macho+ yake yanaenda huku na huku duniani+ kote ili aonyeshe nguvu zake kwa ajili ya wale ambao moyo+ wao ni mkamilifu kumwelekea yeye. Umetenda kwa upumbavu+ kwa habari hii, kwa maana tangu sasa na kuendelea kutakuwa na vita juu yako.”+
10 Hata hivyo, Asa akaudhika kwa sababu ya yule mwonaji, akamtia katika nyumba ya mikatale,+ kwa sababu alimwonea ghadhabu juu ya jambo hilo.+ Na Asa akaanza kuwakandamiza+ baadhi ya watu wakati huohuo. 11 Na, tazama! mambo ya Asa, ya kwanza na ya mwisho, yameandikwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Yuda na wa Israeli.
12 Na Asa, katika mwaka wa 39 wa utawala wake, akapata ugonjwa katika miguu yake mpaka akawa mgonjwa sana;+ na hata katika ugonjwa wake hakumtafuta Yehova+ bali waponyaji.+ 13 Mwishowe Asa akalala pamoja na mababu zake,+ akafa katika mwaka wa 41 wa utawala wake. 14 Kwa hiyo wakamzika katika kaburi lake lenye fahari+ alilokuwa amejichimbia katika Jiji la Daudi;+ nao wakamlaza katika kitanda kilichojazwa mafuta ya zeri+ na aina mbalimbali za marhamu+ iliyochanganywa katika marhamu ya aina ya pekee.+ Tena wakamfanyia mfukizo wa mazishi+ ulio mkubwa isivyo kawaida.
17 Na Yehoshafati+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake na kuimarisha cheo chake juu ya Israeli. 2 Naye akaweka majeshi katika majiji yote yenye ngome ya Yuda na kuweka kambi za kijeshi katika nchi ya Yuda na katika majiji ya Efraimu ambayo Asa baba yake alikuwa ameyateka.+ 3 Na Yehova akaendelea kuwa pamoja na Yehoshafati,+ kwa sababu alitembea katika njia za zamani za Daudi babu yake+ wala hakutafuta Mabaali.+ 4 Kwa kuwa alimtafuta Mungu wa baba yake,+ naye akatembea katika amri yake,+ wala si kulingana na matendo ya Israeli.+ 5 Na Yehova akaendelea kuufanya imara ufalme mkononi mwake;+ na Yuda wote wakaendelea kumpa Yehoshafati zawadi,+ naye akawa na utajiri na utukufu mwingi.+ 6 Na moyo wake ukawa jasiri katika njia+ za Yehova, naye akaondoa hata mahali pa juu+ na miti mitakatifu+ katika Yuda.
7 Na katika mwaka wa tatu wa utawala wake akawaita wakuu wake, yaani, Ben-haili na Obadia na Zekaria na Nethaneli na Mikaya, ili wafundishe katika majiji ya Yuda, 8 na pamoja nao Walawi, Shemaya na Nethania na Zebadia na Asaheli na Shemiramothi na Yehonathani na Adoniya na Tobaya na Tob-adoniya Walawi, na pamoja nao Elishama na Yehoramu makuhani.+ 9 Nao wakaanza kufundisha+ katika Yuda, nao walikuwa na kitabu cha sheria ya Yehova;+ nao wakaendelea kuzunguka katika majiji yote ya Yuda na kufundisha kati ya watu.
10 Na hofu+ ya Yehova ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda pande zote, nao hawakupigana vita na Yehoshafati.+ 11 Na kutoka kwa Wafilisti walikuwa wakimletea Yehoshafati zawadi+ na pesa zikiwa ushuru.+ Pia Waarabu+ walikuwa wakimletea makundi, kondoo-dume elfu saba na mia saba na mbuzi-dume elfu saba na mia saba.+
12 Na Yehoshafati akaendelea kusonga na kuwa mkuu zaidi;+ naye akaendelea kujenga ngome+ na majiji ya maghala+ katika Yuda. 13 Naye akawa na shughuli nyingi katika majiji ya Yuda; na mashujaa wa vita,+ wanaume wenye nguvu,+ walikuwa katika Yerusalemu. 14 Na hivi vilikuwa vyeo vyao kulingana na nyumba za mababu zao: Wa Yuda wakuu wa maelfu, Adna mkuu, na mashujaa, wanaume wenye nguvu, 300,000 walikuwa pamoja naye.+ 15 Na Yehohanani mkuu alikuwa chini yake, na watu 280,000 walikuwa pamoja naye. 16 Na Amasia mwana wa Zikri mwenye kujitolea+ kwa Yehova alikuwa chini yake, na mashujaa, wanaume wenye nguvu, 200,000 walikuwa pamoja naye. 17 Na kutoka katika Benyamini+ palikuwa na yule shujaa, mwanamume mwenye nguvu Eliada, na wanaume 200,000 wenye upinde na ngao walikuwa pamoja naye.+ 18 Na Yehozabadi alikuwa chini ya amri yake, na wanaume 180,000 waliotayarishwa kwa ajili ya jeshi walikuwa pamoja naye. 19 Hao ndio waliokuwa wakimhudumia mfalme zaidi ya wale ambao mfalme aliweka katika majiji yenye ngome+ kotekote katika Yuda.
18 Na Yehoshafati akawa na utajiri na utukufu kwa wingi;+ lakini akafanya mapatano ya ndoa+ pamoja na Ahabu.+ 2 Basi miaka fulani baadaye akashuka kwa Ahabu huko Samaria;+ na Ahabu akamchinjia yeye na watu waliokuwa pamoja naye kondoo+ na ng’ombe kwa wingi. Naye akaanza kumshawishi+ wapande kupigana na Ramothi-gileadi.+ 3 Na Ahabu mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Je, utaenda pamoja nami kule Ramothi-gileadi?”+ Ndipo akamwambia: “Mimi ni sawa na wewe, na watu wangu ni kama watu wako na tu pamoja nawe katika vita.”+
4 Hata hivyo, Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli: “Tafadhali, kwanza kabisa uliza+ upate neno la Yehova.” 5 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawakusanya manabii+ pamoja, watu mia nne, akawaambia: “Je, twende kupiga vita juu ya Ramothi-gileadi, au nijiepushe?”+ Nao wakaanza kusema: “Panda uende, na Mungu wa kweli atalitia jiji hilo mkononi mwa mfalme.”
6 Lakini Yehoshafati akasema: “Je, hayupo hapa tena nabii wa Yehova?+ Basi na tuulize kupitia yeye.”+ 7 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati:+ “Bado kuna mtu mmoja+ ambaye tunaweza kumuuliza Yehova kupitia yeye, lakini hakika mimi ninamchukia,+ kwa maana katika siku zake zote yeye hatoi unabii wa mema kunihusu mimi, ila wa ubaya.+ Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.”+ Hata hivyo, Yehoshafati akasema: “Mfalme asiseme jambo kama hilo.”+
8 Basi mfalme wa Israeli akamwita ofisa wa makao ya mfalme+ na kusema: “Mlete haraka Mikaya mwana wa Imla.”+ 9 Sasa mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi kila mmoja juu ya kiti chake cha ufalme, wakiwa wamevaa mavazi ya kifalme,+ nao walikuwa wameketi katika uwanja wa kupuria kwenye mwingilio wa lango la Samaria; na manabii wote walikuwa wakitenda kama manabii mbele yao.+ 10 Ndipo Sedekia mwana wa Kenaana akajitengenezea pembe+ za chuma na kusema: “Yehova amesema hivi,+ ‘Kwa kutumia hizi utawasukuma Wasiria mpaka uwaangamize.’”+ 11 Na wale manabii wengine wote walikuwa wakitoa unabii kama huo, wakisema: “Panda uende Ramothi-gileadi, upate mafanikio,+ na Yehova hakika atalitia jiji lile mkononi mwa mfalme.”+
12 Na yule mjumbe aliyeenda kumwita Mikaya akamwambia, akisema: “Tazama! Maneno ya manabii kwa kauli moja ni mema kwa mfalme; tafadhali, neno lako na liwe kama la mmoja wao,+ nawe useme mema.”+ 13 Lakini Mikaya akasema: “Kama Yehova anavyoishi,+ lile ambalo Mungu wangu atasema, hilo ndilo nitakalosema.”+ 14 Ndipo akaingia kwa mfalme, naye mfalme akamwambia: “Mikaya, je, twende kupiga vita juu ya Ramothi-gileadi, au nijiepushe?” Mara moja akasema: “Panda uende na kufanikiwa; nao watatiwa mkononi mwenu.”+ 15 Kwa hiyo mfalme akamwambia: “Ninakuapisha mara ngapi+ kwamba usiniambie jambo lolote ila kweli katika jina la Yehova?”+ 16 Basi akasema: “Hakika ninawaona Israeli wote wametawanyika juu ya milima, kama kondoo wasio na mchungaji.+ Na Yehova akasema: ‘Hawa hawana mabwana.+ Kila mmoja na arudi kwa amani nyumbani kwake.’”+
17 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Je, sikukuambia, ‘Hatatoa unabii wa mambo mema kunihusu, ila tu mabaya’?”+
18 Naye akaendelea kusema: “Basi sikieni neno la Yehova:+ Hakika ninamwona Yehova ameketi juu ya kiti chake cha ufalme+ na jeshi+ lote la mbinguni limesimama upande wake wa kuume na wa kushoto.+ 19 Na Yehova akasema, ‘Ni nani atakayemdanganya Ahabu mfalme wa Israeli ili apande kwenda na kuanguka huko Ramothi-gileadi?’ Na kukawa na mazungumzo, huyu akisema hivi, na yule akisema vile.+ 20 Mwishowe roho+ fulani akaja na kusimama mbele za Yehova, akasema, ‘Mimi nitamdanganya.’ Ndipo Yehova akamwambia, ‘Kwa njia gani?’+ 21 Naye akasema, ‘Nitaenda nami nitakuwa roho ya udanganyifu katika kinywa cha manabii wake wote.’+ Kwa hiyo akasema, ‘Utamdanganya, na tena utashinda.+ Nenda, ukafanye hivyo.’+ 22 Na sasa, tazama, Yehova ametia roho ya udanganyifu katika kinywa cha hawa manabii wako wote;+ lakini Yehova mwenyewe ametangaza msiba juu yako.”+
23 Sasa Sedekia+ mwana wa Kenaana+ akakaribia, akampiga Mikaya+ kwenye shavu+ na kusema: “Ni katika njia gani hasa roho ya Yehova ilinipita mimi ikaenda kusema na wewe?”+ 24 Kwa hiyo Mikaya akasema: “Tazama! Utaona ni njia gani siku ile+ utakapoingia katika chumba cha ndani kabisa ili ujifiche.”+ 25 Ndipo mfalme wa Israeli akasema: “Mchukueni Mikaya, mmrudishe kwa Amoni mkuu wa jiji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.+ 26 Nanyi mseme, ‘Mfalme amesema hivi: “Mtieni mtu huyu katika kizuizi,+ mkamlishe kwa posho iliyopunguzwa ya mkate+ na maji yaliyopunguzwa mpaka nitakaporudi kwa amani.”’”+ 27 Basi Mikaya akasema: “Ukirudi kwa amani kwa vyovyote, Yehova hakusema nami.” Naye akaongezea:+ “Sikieni, enyi watu wote.”+
28 Na mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakapanda kwenda mpaka Ramothi-gileadi.+ 29 Sasa mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Mimi nitajibadili sura+ na kuingia vitani, lakini wewe vaa mavazi yako.”+ Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadili sura, kisha wakaingia vitani.+ 30 Naye mfalme wa Siria alikuwa amewaamuru wale wakuu wa magari yake, akisema: “Msipigane na mdogo wala na mkuu, ila na mfalme wa Israeli peke yake.”+ 31 Na ikawa kwamba mara tu wale wakuu wa magari walipomwona Yehoshafati, wakaambiana: “Ndiye mfalme wa Israeli.”+ Basi wakageuka juu yake kupigana; na Yehoshafati akaanza kulia apewe msaada,+ na Yehova akamsaidia,+ na Mungu akawashawishi mara moja waondoke kwake.+ 32 Na ikawa kwamba mara tu wale wakuu wa magari walipoona kwamba yeye hakuwa mfalme wa Israeli, mara moja wakaacha kumfuata.+
33 Na palikuwa na mtu aliyepinda upinde bila kujua, lakini akampiga+ mfalme wa Israeli katikati ya viungio na vazi la chuma, naye akamwambia mwendesha-gari:+ “Geuza mkono wako, uniondoe katika kambi, kwa sababu nimeumizwa vibaya.”+ 34 Na pigano likazidi kuwa kali siku hiyo, na ikawa lazima kumweka mfalme wa Israeli akiwa amesimama katika gari akiwaelekea Wasiria mpaka jioni; na mwishowe akafa wakati wa kutua kwa jua.+
19 Kisha Yehoshafati mfalme wa Yuda akarudi kwa amani+ nyumbani kwake Yerusalemu. 2 Sasa Yehu+ mwana wa Hanani+ mwonaji+ akaenda mbele yake na kumwambia Mfalme Yehoshafati: “Je, waovu wanapaswa kupewa msaada,+ na je, unapaswa kuwapenda+ wale wanaomchukia+ Yehova? Kwa sababu hiyo kuna ghadhabu+ juu yako inayotoka mbele za uso wa Yehova. 3 Hata hivyo, kuna mambo mema+ ambayo yameonekana kwako, kwa sababu umeiondoa miti mitakatifu katika nchi+ nawe umetayarisha moyo wako kumtafuta Mungu wa kweli.”+
4 Na Yehoshafati akaendelea kukaa Yerusalemu; naye akaanza kutoka tena na kwenda katikati ya watu kutoka Beer-sheba+ mpaka eneo lenye milima la Efraimu,+ ili kuwarudisha kwa Yehova Mungu wa mababu zao.+ 5 Naye akaweka waamuzi katika nchi yote katika majiji yote yenye ngome ya Yuda, jiji baada ya jiji.+ 6 Naye akawaambia wale waamuzi: “Oneni mnalofanya,+ kwa sababu hamhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Yehova;+ naye yupo pamoja nanyi katika jambo la hukumu.+ 7 Na sasa hofu+ ya Yehova na iwe juu yenu.+ Iweni waangalifu na mtende,+ kwa maana hakuna ukosefu wowote wa uadilifu+ wala ubaguzi+ wala kuchukua rushwa kwa upande wa Yehova Mungu wetu.”+
8 Na katika Yerusalemu pia Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi+ na makuhani+ na baadhi ya vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba+ za Israeli kwa ajili ya uamuzi+ wa Yehova na kwa ajili ya kesi+ za wakaaji wa Yerusalemu. 9 Tena akaweka amri juu yao, akisema: “Hivi ndivyo mnavyopaswa kufanya katika kumwogopa+ Yehova kwa uaminifu na kwa moyo kamili. 10 Na kuhusu kila kesi itakayokuja kwenu ya ndugu zenu wanaokaa katika majiji yao, inayohusu kumwaga damu,+ inayohusu sheria+ na amri+ na masharti+ na maamuzi ya hukumu,+ lazima mwaonye kwamba wasimkosee Yehova ili ghadhabu+ isije juu yenu na juu ya ndugu zenu. Hivyo ndivyo mnavyopaswa kufanya ili msipate hatia. 11 Na, tazama, yupo Amaria mkuu wa makuhani aliye juu yenu kwa ajili ya kila jambo la Yehova;+ na Zebadia mwana wa Ishmaeli kiongozi wa nyumba ya Yuda kwa ajili ya kila jambo la mfalme; nanyi mna Walawi wakiwa maofisa kwa ajili yenu. Iweni na nguvu,+ mtende, na Yehova+ awe pamoja na mambo yaliyo mema.”+
20 Na ikawa kwamba baadaye wana wa Moabu+ na wana wa Amoni+ na pamoja nao baadhi ya Waamonimu+ wakaja kupigana vita na Yehoshafati.+ 2 Basi watu wakaja na kumwambia Yehoshafati, wakisema: “Umati mkubwa umekuja kukushambulia kutoka katika eneo la bahari, kutoka Edomu;+ na, tazama, wako huko Hasason-tamari, yaani, En-gedi.”+ 3 Ndipo Yehoshafati akaogopa,+ akauelekeza uso wake kumtafuta Yehova.+ Kwa hiyo akatangaza mfungo+ kwa ajili ya Yuda yote. 4 Mwishowe watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kuuliza habari kutoka kwa Yehova.+ Wakaja kutoka katika majiji yote ya Yuda ili kutafuta shauri kwa Yehova.+
5 Ndipo Yehoshafati akasimama katika kutaniko la Yuda na la Yerusalemu ndani ya nyumba ya Yehova+ mbele ya ule ua mpya,+ 6 naye akasema:+
“Ee Yehova Mungu wa mababu zetu,+ je, wewe si Mungu mbinguni,+ na je, wewe hutawali juu ya falme zote za mataifa,+ na je, mkononi mwako hamna nguvu na uwezo, wala hakuna anayeweza kusimama imara kupingana nawe?+ 7 Je, wewe mwenyewe, Ee Mungu wetu,+ hukuwafukuza wakaaji wa nchi hii kutoka mbele ya watu wako Israeli,+ kisha ukaikabidhi+ kwa uzao wa Abrahamu, mpendwa wako,+ mpaka wakati usio na kipimo? 8 Nao wakaanza kukaa ndani yake, nao wakakujengea patakatifu ndani yake kwa ajili ya jina lako,+ wakisema, 9 ‘Tukipatwa na msiba,+ upanga, hukumu mbaya, au tauni+ au njaa,+ acheni tusimame mbele ya nyumba hii+ na mbele zako (kwa maana jina lako+ limo katika nyumba hii), ili tukuombe msaada ili kutuondoa katika taabu yetu, nawe usikie na kuokoa.’+ 10 Na sasa, tazama, wana wa Amoni,+ na Moabu+ na eneo lenye milima la Seiri,+ ambao hukuruhusu Israeli wawavamie walipokuwa wakitoka katika nchi ya Misri, bali waligeukia mbali kutoka kwao wala hawakuwaangamiza,+ 11 ndiyo, tazama, wanatupa sisi thawabu+ ya kuja kutufukuza tuondoke katika miliki yako ambayo ulitufanya tuimiliki.+ 12 Ee Mungu wetu, je, hutafanya hukumu juu yao?+ Kwa maana hakuna nguvu ndani yetu mbele ya umati huu mkubwa unaokuja juu yetu;+ nasi wenyewe hatujui tunalopaswa kufanya,+ lakini macho yetu yanakuelekea wewe.”+
13 Na wakati huo wote watu wote wa Yuda walikuwa wamesimama mbele za Yehova,+ hata watoto wao,+ wake zao na wana wao.
14 Sasa kwa habari ya Yahazieli mwana wa Zekaria mwana wa Benaya mwana wa Yeieli mwana wa Matania, Mlawi, wa wana wa Asafu,+ roho+ ya Yehova ikaja juu yake katikati ya kutaniko. 15 Basi akasema: “Sikilizeni kwa makini, Yuda wote nanyi wakaaji wa Yerusalemu na Mfalme Yehoshafati! Tazama, Yehova amewaambia ninyi hivi, ‘Msiogope+ wala msiwe na hofu kwa sababu ya umati huu mkubwa; kwa maana vita si vyenu bali ni vya Mungu.+ 16 Washukieni kesho. Tazama, wanapanda kuja kwa njia nyembamba ya Sisi; nanyi hakika mtawakuta mwishoni mwa bonde la mto mbele ya nyika ya Yerueli. 17 Hamtahitaji kupigana+ katika kisa hiki. Simameni mahali penu, simameni tuli,+ mkauone wokovu+ wa Yehova kwa ajili yenu. Ee Yuda na Yerusalemu, msiogope wala msiwe na hofu.+ Kesho waendeeni, na Yehova atakuwa pamoja nanyi.’”+
18 Ndipo mara moja Yehoshafati akainama kifudifudi,+ na Yuda wote na wakaaji wa Yerusalemu wakaanguka mbele za Yehova ili kumsujudia Yehova.+ 19 Kisha Walawi+ wa wana wa Wakohathi+ na wa wana wa Wakora+ wakasimama ili kumsifu Yehova Mungu wa Israeli, kwa sauti kubwa isivyo kawaida.+
20 Nao wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda katika nyika+ ya Tekoa.+ Na walipokuwa wakienda, Yehoshafati akasimama na kusema: “Nisikieni, enyi Yuda nanyi wakaaji wa Yerusalemu!+ Iweni na imani+ katika Yehova Mungu wenu, ili mdumu muda mrefu. Iweni na imani katika manabii wake,+ hivyo mfanikiwe.”
21 Tena akafanya shauri+ na watu na kuweka waimbaji+ kwa ajili ya Yehova na wale wanaotoa sifa+ katika pambo takatifu+ wakienda mbele ya wale watu wenye silaha,+ na kusema: “Mpeni Yehova sifa,+ kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+
22 Na wakati walipoanza kupaaza vigelegele vya shangwe na sifa, Yehova akaweka watu wa kuvizia+ juu ya wana wa Amoni, Moabu na eneo lenye milima la Seiri waliokuwa wakija Yuda, nao wakaanza kupigana wenyewe.+ 23 Na wana wa Amoni na Moabu wakasimama kushambulia wakaaji wa eneo lenye milima la Seiri+ ili kuwaangamiza na kuwaharibu; na mara tu walipowamaliza wakaaji wa Seiri, wakasaidiana kuangamizana wao kwa wao.+
24 Lakini Yuda wakaja kwenye mnara wa mlinzi wa nyika.+ Walipogeuza nyuso zao kuelekea ule umati, tazama, pale, mizoga yao ikiwa imeanguka chini+ bila yeyote kuponyoka. 25 Basi Yehoshafati na watu wake wakaja kupora nyara+ walizokuwa nazo, na katika nyara hizo wakakuta kwa wingi mali na mavazi na vyombo vyenye kutamanika; nao wakaendelea kuwavua mpaka waliposhindwa kuchukua zaidi.+ Nao wakapora nyara kwa siku tatu, kwa maana zilikuwa nyingi. 26 Na katika siku ya nne wakakutana pamoja kwenye nchi tambarare ya chini ya Baraka, kwa maana walimbariki Yehova hapo.+ Ndiyo sababu walipaita mahali hapo jina+ Nchi Tambarare ya Chini ya Baraka—mpaka leo hii.
27 Ndipo watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakarudi, Yehoshafati akiwa mbele yao, ili warudi Yerusalemu kwa kushangilia, kwa kuwa Yehova alikuwa amewafanya washangilie juu ya adui zao.+ 28 Basi wakaja Yerusalemu wakiwa na vinanda+ na vinubi+ na tarumbeta,+ kwenye nyumba ya Yehova.+ 29 Na hofu+ ya Mungu ikawa juu ya falme zote za nchi waliposikia kwamba Yehova amepiga vita juu ya adui za Israeli.+ 30 Kwa hiyo ufalme wa Yehoshafati haukuwa na usumbufu wowote, na Mungu wake akaendelea kumpa pumziko kuzunguka pande zote.+
31 Na Yehoshafati+ akaendelea kutawala juu ya Yuda. Alipoanza kutawala alikuwa na umri wa miaka 35, naye akatawala miaka 25 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Azuba+ binti ya Shilhi. 32 Naye akaendelea kutembea katika njia ya Asa+ baba yake, naye hakugeuka kando kutoka katika njia hiyo, kwa kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova.+ 33 Ila tu mahali pa juu+ hapakuondolewa; na watu walikuwa bado hawajatayarisha moyo wao kwa ajili ya Mungu wa mababu zao.+
34 Na mambo mengine ya Yehoshafati, ya kwanza na ya mwisho, tazama, yameandikwa kati ya maneno ya Yehu+ mwana wa Hanani,+ yaliyoingizwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Israeli. 35 Na baada ya hayo Yehoshafati mfalme wa Yuda akawa na ushirika na Ahazia+ mfalme wa Israeli, aliyetenda kwa uovu.+ 36 Kwa hiyo akamfanya kuwa mshirika pamoja naye katika ujenzi wa meli za kwenda Tarshishi+ nao wakajenga meli kule Esion-geberi.+ 37 Hata hivyo, Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii juu ya Yehoshafati, akisema: “Kwa sababu umefanya ushirika na Ahazia,+ hakika Yehova atazivunja kazi zako.”+ Basi zile meli zikavunjwa,+ nazo hazikuwa na nguvu za kwenda Tarshishi.+
21 Mwishowe Yehoshafati akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa pamoja na mababu zake+ katika Jiji la Daudi; na Yehoramu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake. 2 Naye alikuwa na ndugu, wana wa Yehoshafati, Azaria na Yehieli na Zekaria na Azaria na Mikaeli na Shefatia, hao wote walikuwa wana wa Yehoshafati mfalme wa Israeli. 3 Basi baba yao akawapa zawadi+ nyingi za fedha na dhahabu na vitu bora pamoja na majiji yenye ngome katika Yuda;+ lakini ufalme akampa Yehoramu,+ kwa maana yeye ndiye aliyekuwa mzaliwa wa kwanza.+
4 Wakati Yehoramu aliposimama kuwa juu ya ufalme wa baba yake, alikiimarisha cheo chake, kwa hiyo akawaua ndugu zake+ wote kwa upanga na pia baadhi ya wakuu wa Israeli. 5 Yehoramu alikuwa na umri wa miaka 32 alipoanza kutawala, naye akatawala+ miaka 8 katika Yerusalemu. 6 Naye akaendelea kutembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ kama walivyofanya wale wa nyumba ya Ahabu; kwa maana binti ya Ahabu alikuwa amekuwa mke wake,+ naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+ 7 Na Yehova hakutaka kuiharibu nyumba ya Daudi,+ kwa sababu ya lile agano+ alilokuwa amefanya pamoja na Daudi, na kama alivyokuwa amesema kwamba atampa+ yeye na wanawe taa sikuzote.+
8 Katika siku zake Edomu+ waliasi kutoka chini ya mkono wa Yuda,+ nao wakaweka mfalme atawale juu yao.+ 9 Basi Yehoramu pamoja na wakuu wake wakavuka na pia magari yote pamoja naye. Na ikawa kwamba aliondoka wakati wa usiku, akawapiga na kuwaua Waedomu waliokuwa wamemzunguka na pia wale wakuu wa magari. 10 Lakini Edomu wakaendelea kuasi kutoka chini ya mkono wa Yuda mpaka leo hii. Wakati huo ndipo Libna+ wakaanza kuasi kutoka chini ya mkono wake, kwa sababu yeye alikuwa amemwacha Yehova Mungu wa mababu zake.+ 11 Yeye pia alikuwa ametengeneza mahali pa juu+ katika milima ya Yuda, ili awasababishe wakaaji wa Yerusalemu kufanya uasherati,+ na ili afukuzie Yuda mbali.+
12 Mwishowe maandishi+ yakaja kwake kutoka kwa Eliya+ nabii, na kusema: “Yehova Mungu wa Daudi babu yako, amesema hivi, ‘Kwa sababu hukutembea katika njia za Yehoshafati+ baba yako wala katika njia za Asa+ mfalme wa Yuda, 13 bali unatembea katika njia ya wafalme wa Israeli+ na kuwafanya Yuda na wakaaji wa Yerusalemu wafanye uasherati+ kama vile nyumba ya Ahabu ilivyofanya watu wafanye uasherati,+ na hata umewaua ndugu zako, nyumba ya baba yako, waliokuwa bora kuliko wewe;+ 14 tazama! Yehova analeta pigo kubwa+ kwa watu wako+ na kwa wana wako+ na kwa wake zako na kwa mali zako zote. 15 Nawe utakuwa na magonjwa mengi,+ na ugonjwa wa matumbo yako, mpaka matumbo yako yatakapotoka nje kwa sababu ya ugonjwa huo siku baada ya siku.’”+
16 Kwa hiyo Yehova akaamsha juu ya Yehoramu roho+ ya Wafilisti+ na Waarabu+ waliokuwa kando ya Waethiopia.+ 17 Basi wakapanda na kuingia Yuda na kuifungua kwa nguvu na kuteka mali zote zilizokuwa katika nyumba ya mfalme+ na pia wanawe na wake zake,+ wala hakuachiwa mwana yeyote ila Yehoahazi,+ mwana wake aliye mdogo zaidi. 18 Na baada ya hayo yote Yehova akampiga katika matumbo yake kwa ugonjwa ambao haukuweza kuponywa.+ 19 Na ikawa kwamba katika siku zilizofuata, kipindi cha miaka miwili kamili kilipokwisha, matumbo+ yake yakatoka nje wakati wa ugonjwa wake, na mwishowe akafa katika magonjwa yake mabaya; na watu wake hawakumfanyia mfukizo kama ule mfukizo+ waliowafanyia mababu zake. 20 Alianza kutawala akiwa na umri wa miaka 32, naye akatawala miaka 8 katika Yerusalemu. Mwishowe akaenda zake bila kutamaniwa.+ Basi wakamzika katika Jiji la Daudi,+ lakini si katika makaburi ya wafalme.+
22 Kisha wakaaji wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia+ mwana wake mdogo zaidi kuwa mfalme mahali pake, (kwa kuwa kikundi cha waporaji kilichokuja na Waarabu+ kambini kilikuwa kimewaua wale wakubwa wote,)+ na Ahazia mwana wa Yehoramu akaanza kutawala akiwa mfalme wa Yuda. 2 Ahazia alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala,+ naye akatawala mwaka mmoja katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Athalia+ mjukuu wa Omri.+
3 Yeye pia alitembea katika njia za nyumba ya Ahabu,+ kwa maana mama yake+ alikuwa mshauri wake katika kutenda maovu. 4 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, kama nyumba ya Ahabu, kwa maana wao walikuwa washauri+ wake baada ya kifo cha baba yake, kwa uharibifu wake. 5 Yeye pia alitembea katika shauri lao,+ hivi kwamba akaenda pamoja na Yehoramu+ mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana vita na Hazaeli+ mfalme wa Siria kule Ramothi-gileadi,+ ambako wapiga-mishale walimpiga Yehoramu.+ 6 Kwa hiyo akarudi Yezreeli+ ili apone yale majeraha waliyokuwa wamemtia kule Rama+ alipopigana na Hazaeli mfalme wa Siria.
Naye Azaria+ mwana wa Yehoramu+ mfalme wa Yuda akashuka ili amwone Yehoramu+ mwana wa Ahabu kule Yezreeli, kwa maana alikuwa mgonjwa.+ 7 Lakini kuanguka+ kwa Ahazia kulitokana na Mungu,+ alipomjia Yehoramu; naye alipokuja, alienda+ pamoja na Yehoramu kwa Yehu+ mjukuu wa Nimshi,+ ambaye Yehova alikuwa amemtia mafuta+ ili aikatilie mbali nyumba ya Ahabu.+ 8 Na ikawa kwamba mara Yehu alipoanza kubishana na nyumba ya Ahabu,+ akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa ndugu za Ahabu, wahudumu wa Ahazia,+ naye akawaua.+ 9 Kisha akaenda kumtafuta Ahazia, na mwishowe wakamkamata,+ akiwa amejificha Samaria,+ nao wakamleta kwa Yehu. Kisha wakamuua na kumzika,+ kwa kuwa walisema: “Yeye ni mjukuu wa Yehoshafati,+ aliyemtafuta Yehova kwa moyo wake wote.”+ Na hapakuwa na yeyote wa nyumba ya Ahazia wa kushika mamlaka ya ufalme huo.
10 Kwa habari ya Athalia+ mama ya Ahazia, yeye aliona kwamba mwana wake amekufa. Kwa hiyo akasimama, akauangamiza uzao wote wa kifalme wa nyumba ya Yuda.+ 11 Hata hivyo, Yehoshabeathi+ binti ya mfalme akamchukua Yehoashi+ mwana wa Ahazia, akamwiba kutoka kati ya wana wa mfalme waliopaswa kuuawa, akamweka yeye na mlezi wake wa kike katika chumba cha ndani cha vitanda. Na Yehoshabeathi binti ya Mfalme Yehoramu,+ mke wa Yehoyada+ kuhani, (kwa maana alikuwa dada ya Ahazia,) akaendelea kumficha kwa sababu ya Athalia, naye hakumuua.+ 12 Naye akaendelea kuwa pamoja nao katika nyumba ya Mungu wa kweli akiwa amefichwa kwa miaka sita,+ Athalia alipokuwa akitawala kama malkia+ juu ya nchi.+
23 Na katika mwaka wa saba Yehoyada+ akajionyesha kuwa hodari, akawachukua wakuu wa mamia,+ yaani, Azaria mwana wa Yerohamu, na Ishmaeli mwana wa Yehohanani na Azaria mwana wa Obedi na Maaseya mwana wa Adaya na Elishafati mwana wa Zikri, pamoja naye katika agano. 2 Kisha wakazunguka Yuda yote na kuwakusanya Walawi+ kutoka katika majiji yote ya Yuda na vichwa+ vya nyumba za ukoo wa upande wa baba+ za Israeli. Basi wakaja Yerusalemu. 3 Ndipo kutaniko lote wakafanya agano+ pamoja na mfalme katika nyumba+ ya Mungu wa kweli, kisha akawaambia:
“Tazama! Mwana+ wa mfalme atatawala,+ kama Yehova alivyoahidi kuhusiana na wana wa Daudi.+ 4 Hivi ndivyo mtakavyofanya: sehemu ya tatu kati yenu mnaoingia siku ya sabato,+ ya makuhani+ na ya Walawi,+ watakuwa watunza-milango;+ 5 na sehemu ya tatu watakuwa katika nyumba ya mfalme;+ na sehemu ya tatu watakuwa kwenye Lango la Msingi;+ na watu wote watakuwa katika nyua+ za nyumba ya Yehova. 6 Na msimruhusu mtu yeyote aingie katika nyumba ya Yehova+ ila makuhani na wale Walawi wanaohudumu.+ Hao ndio watakaoingia, kwa sababu wao ni kikundi kitakatifu,+ na watu wote watashika huo wajibu kwa Yehova. 7 Na Walawi wanapaswa kumzunguka mfalme pande zote,+ kila mmoja akiwa na silaha zake mkononi mwake; na mtu yeyote atakayeingia ndani ya nyumba, anapaswa kuuawa. Nanyi mwendelee kuwa na mfalme anapoingia ndani na anapotoka nje.”
8 Na wale Walawi na Yuda wote wakafanya kulingana na yote ambayo Yehoyada+ kuhani alikuwa ameamuru.+ Basi kila mmoja wao akachukua watu wake waliokuwa wakiingia wakati wa sabato pamoja na wale waliokuwa wakitoka nje wakati wa sabato,+ kwa kuwa Yehoyada kuhani hakuwa ameviachisha kazi vile vikundi vya migawanyo.+ 9 Tena Yehoyada kuhani akawapa wale wakuu wa mamia+ mikuki na ngao na ngao za mviringo+ zilizokuwa za Mfalme Daudi,+ ambazo zilikuwa katika nyumba ya Mungu wa kweli.+ 10 Naye akawasimamisha watu wote,+ kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, kuanzia upande wa kuume wa nyumba mpaka upande wa kushoto wa nyumba, kando ya madhabahu na kando ya nyumba, pande zote karibu na mfalme. 11 Kisha wakamtoa nje mwana wa mfalme,+ wakamvika taji+ na ule Ushuhuda,+ wakamfanya kuwa mfalme, hivyo Yehoyada na wanawe wakamtia mafuta+ na kusema: “Mfalme na aishi!”+
12 Athalia aliposikia sauti ya watu wakikimbia na kumsifu mfalme,+ mara moja akaingia kwa watu katika nyumba ya Yehova. 13 Kisha akaona, na tazama, mfalme alikuwa amesimama kando ya nguzo+ yake katika mwingilio, na wakuu+ na tarumbeta+ kando ya mfalme, na watu wote wa nchi walikuwa wakishangilia+ na kupiga+ tarumbeta, na waimbaji+ walikuwa na vyombo vya nyimbo na wale wanaotoa ishara za kutoa sifa. Athalia akayararua mavazi yake mara moja na kusema: “Ni hila! Ni hila!”+ 14 Lakini Yehoyada kuhani akawatoa nje wale wakuu wa mamia, watu waliochaguliwa wa jeshi, na kuwaambia: “Mwondoeni katikati ya vikosi;+ na yeyote atakayemfuata, auawe kwa upanga!” Kwa maana kuhani yule alikuwa amesema: “Msimuue ndani ya nyumba ya Yehova.” 15 Basi wakamkamata. Alipofika katika mwingilio wa lango la farasi la nyumba ya mfalme, wakamuua hapo mara moja.+
16 Ndipo Yehoyada akafanya agano kati yake na watu wote na mfalme kwamba wao wataendelea kuwa watu+ wa Yehova. 17 Kisha watu wote wakaenda kwenye nyumba ya Baali, wakaibomoa;+ nao wakazivunja madhabahu+ zake na sanamu+ zake, nao, mbele ya zile madhabahu, wakamuua+ Matani+ kuhani wa Baali. 18 Tena Yehoyada akavitia vyeo vya nyumba ya Yehova mkononi mwa makuhani na Walawi, ambao Daudi+ alikuwa amewaweka katika migawanyo juu ya nyumba ya Yehova ili watoe dhabihu za kuteketezwa za Yehova kulingana na yale ambayo yameandikwa katika sheria ya Musa,+ kwa kushangilia pamoja na nyimbo kwa mikono ya Daudi. 19 Kwa hiyo akawaweka watunza-malango+ kando ya malango+ ya nyumba ya Yehova ili yeyote aliye najisi katika jambo lolote asiingie. 20 Sasa akawachukua wakuu wa mamia+ na mabwana na watawala juu ya watu na watu wote wa nchi na kumshusha mfalme kutoka katika nyumba ya Yehova.+ Kisha wakaja moja kwa moja kupitia lango la juu mpaka kwenye nyumba ya mfalme, wakamketisha mfalme juu ya kiti cha ufalme.+ 21 Na watu wote wa nchi wakaendelea kushangilia;+ nalo jiji halikuwa na usumbufu, nao walikuwa wamemuua Athalia kwa upanga.+
24 Yehoashi+ alikuwa na umri wa miaka 7 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 40 katika Yerusalemu.+ Na jina la mama yake lilikuwa Sibia kutoka Beer-sheba.+ 2 Na Yehoashi+ akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni+ pa Yehova siku zote za Yehoyada kuhani.+ 3 Na Yehoyada akampa wake wawili, naye akazaa wana na mabinti.+
4 Ikawa baadaye kwamba kurekebisha nyumba ya Yehova kukawa moyoni mwa Yehoashi.+ 5 Kwa hiyo akawakusanya makuhani+ na Walawi na kuwaambia: “Nendeni katika majiji ya Yuda, mkusanye pesa kutoka kwa Israeli wote ili kuirekebisha+ nyumba ya Mungu wenu mwaka baada ya mwaka;+ nanyi mtende jambo hili haraka.” Na Walawi hawakutenda haraka.+ 6 Basi mfalme akamwita Yehoyada aliye kichwa na kumwambia:+ “Kwa nini hujawadai Walawi walete kutoka Yuda na Yerusalemu kodi takatifu iliyoagizwa na Musa+ mtumishi wa Yehova, ile ya kutaniko la Israeli, kwa ajili ya hema la Ushuhuda?+ 7 Kwa maana wana wa Athalia yule mwanamke mwovu+ walikuwa wamevunja na kuingia ndani ya nyumba ya Mungu wa kweli,+ na hata vitu vyote vitakatifu+ vya nyumba ya Yehova walikuwa wamevitolea Mabaali.”+ 8 Ndipo mfalme akatoa amri, nao wakatengeneza sanduku+ na kuliweka nje kwenye lango la nyumba ya Yehova. 9 Kisha wakatoa mwito katika Yuda na Yerusalemu yote ili kumletea Yehova ile kodi takatifu+ iliyoagizwa na Musa+ mtumishi wa Mungu wa kweli juu ya Israeli nyikani. 10 Na wakuu+ wote na watu wote wakaanza kushangilia,+ nao wakaendelea kuleta na kuitia ndani ya lile sanduku+ mpaka wote walipokuwa wametoa.
11 Na ikawa kwamba kwa wakati unaofaa akawa akiliweka lile sanduku chini ya uangalizi wa mfalme kwa mkono wa Walawi,+ na mara tu walipoona kuna pesa nyingi,+ mwandishi+ wa mfalme na mjumbe wa mkuu wa makuhani wakaja na kuzitoa katika sanduku, kisha wakaliinua na kulirudisha mahali pake. Hivyo ndivyo walivyofanya siku baada ya siku, hivi kwamba wakakusanya pesa kwa wingi. 12 Kisha mfalme na Yehoyada wakawa wakiwapa waliokuwa wakifanya+ kazi katika utumishi wa nyumba ya Yehova,+ nao wakaandika wachongaji wa mawe+ na mafundi+ ili kuirekebisha nyumba ya Yehova,+ na pia wafanyakazi wa chuma na shaba ili kuirekebisha nyumba ya Yehova.+ 13 Na wafanyakazi wakaanza kutenda,+ na kazi ya kurekebisha ikaendelea kusonga mbele mkononi mwao, na mwishowe wakaisimamisha nyumba ya Mungu wa kweli kama inavyopaswa kuwa kimuundo na kuitia nguvu. 14 Na mara tu walipomaliza, wakaleta pesa zilizobaki mbele ya mfalme na Yehoyada, nao wakatengeneza vyombo vya nyumba ya Yehova, vyombo vya huduma+ na vya kutoa matoleo na vikombe+ na vyombo vya dhahabu+ na vya fedha; nao wakawa watoaji wa dhabihu za kuteketezwa+ katika nyumba ya Yehova kwa ukawaida siku zote za Yehoyada.
15 Na Yehoyada akawa mzee na mwenye kushiba miaka+ naye akafa mwishowe, akiwa na umri wa miaka 130 wakati wa kifo chake. 16 Basi wakamzika katika Jiji la Daudi pamoja na wafalme,+ kwa sababu alikuwa ametenda mema katika Israeli+ na kwa Mungu wa kweli na kwa nyumba Yake.
17 Na baada ya kifo cha Yehoyada, wakuu+ wa Yuda wakaja na kumwinamia mfalme. Na wakati huo mfalme akawasikiliza.+ 18 Na mwishowe wakaiacha nyumba ya Yehova Mungu wa mababu zao, wakaanza kuitumikia miti mitakatifu+ na sanamu,+ hivi kwamba kukawa na ghadhabu juu ya Yuda na Yerusalemu kwa sababu ya hiyo hatia yao.+ 19 Naye akaendelea kutuma manabii+ katikati yao ili kuwarudisha kwa Yehova; nao wakaendelea kutoa ushuhuda juu yao, lakini hawakusikiliza.+
20 Na roho+ ya Mungu ikamfunika+ Zekaria+ mwana wa Yehoyada+ kuhani, hivi kwamba akasimama juu ya watu na kuwaambia: “Mungu wa kweli amesema hivi, ‘Kwa nini mnazivunja amri za Yehova, hivi kwamba hamwezi kufanikiwa?+ Kwa sababu mmemwacha Yehova, yeye naye atawaacha ninyi.’”+ 21 Mwishowe wakapanga hila juu yake,+ wakampiga kwa mawe+ kwa amri ya mfalme katika ua wa nyumba ya Yehova. 22 Na Yehoashi mfalme hakukumbuka fadhili zenye upendo ambazo Yehoyada baba yake alikuwa amemwonyesha,+ hivi kwamba akamuua mwana wake, ambaye, alipokuwa akifa, alisema: “Yehova na aone jambo hili na kulidai.”+
23 Na ikawa kwamba mwanzoni mwa mwaka,+ jeshi la Siria+ likaja kupigana naye,+ nao wakaanza kuvamia Yuda na Yerusalemu. Ndipo wakawaangamiza wakuu+ wote wa watu kutoka katikati ya watu, nao wakapeleka nyara yao yote kwa mfalme wa Damasko.+ 24 Kwa maana jeshi la Wasiria lilivamia kwa hesabu ndogo ya watu,+ na Yehova mwenyewe akatia mkononi mwao jeshi lililo na hesabu kubwa sana,+ kwa sababu walikuwa wamemwacha Yehova Mungu wa mababu zao; nao wakafanya hukumu juu ya Yehoashi.+ 25 Nao walipoondoka kwake (kwa kuwa walimwacha akiwa na magonjwa mengi),+ watumishi wake mwenyewe wakapanga hila+ juu yake kwa sababu ya damu+ ya wana wa Yehoyada+ kuhani; wakamuua kitandani mwake, hata akafa.+ Kisha wakamzika katika Jiji la Daudi,+ lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.+
26 Na hawa ndio waliopanga hila juu yake: Zabadi+ mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni na Yehozabadi mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabu. 27 Na kwa habari ya wanawe na wingi wa matangazo juu yake+ na kuwekwa msingi+ wa nyumba ya Mungu wa kweli, tazama, yameandikwa katika ufafanuzi wa Kitabu+ cha Wafalme. Na Amazia+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
25 Amazia+ alikuwa mfalme akiwa na umri wa miaka 25, naye akatawala miaka 29 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Yehoadani+ wa Yerusalemu. 2 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova,+ ila tu si kwa moyo kamili.+ 3 Na ikawa kwamba mara tu ufalme ulipokuwa umeimarishwa kwake, akawaua+ mara moja wale watumishi+ wake waliompiga na kumuua mfalme, baba yake.+ 4 Naye hakuwaua wana wao, bali alifanya kulingana na yale ambayo yameandikwa katika sheria, katika kitabu cha Musa,+ ambayo Yehova aliamuru, akisema: “Akina baba wasife kwa sababu ya wana,+ wala wana wasife kwa sababu ya akina baba;+ bali kila mmoja afe kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe.”+
5 Na Amazia akawakusanya Yuda na kuwasimamisha kulingana na nyumba ya mababu,+ kulingana na wakuu wa maelfu+ na kulingana na wakuu wa mamia+ kwa ajili ya Yuda wote na Benyamini; naye akawaandikisha kuanzia umri wa miaka 20+ na zaidi, na mwishowe akakuta kwamba walikuwa wanaume bora 300,000 wanaoingia jeshini, wanaotumia mkuki+ na ngao kubwa.+ 6 Tena akaandika kutoka katika Israeli mashujaa, wanaume wenye nguvu mia moja elfu kwa talanta mia moja za fedha. 7 Na mtu fulani wa Mungu wa kweli+ akamjia, akisema: “Ee mfalme, usiache jeshi la Israeli liende pamoja nawe, kwa maana Yehova hayuko pamoja na Israeli,+ yaani, wana wote wa Efraimu. 8 Lakini wewe mwenyewe nenda, utende, uwe hodari kwa ajili ya vita.+ Mungu wa kweli anaweza kukufanya ujikwae mbele ya adui; kwa maana Mungu ana nguvu za kusaidia+ na za kusababisha kujikwaa.”+ 9 Ndipo Amazia+ akamwambia yule mtu wa Mungu wa kweli: “Lakini zifanyweje zile talanta mia moja ambazo nimewapa majeshi ya Israeli?”+ Mtu wa Mungu wa kweli akajibu, akasema: “Yehova ana uwezo wa kukupa nyingi zaidi kuliko hizo.”+ 10 Basi Amazia akawatenga, yaani, yale majeshi yaliyomjia kutoka Efraimu, ili waende kwao. Hata hivyo, hasira yao ikawaka sana juu ya Yuda, nao wakarudi kwao wakiwaka hasira.+
11 Naye Amazia akajipa moyo, akawaongoza watu wake, akaenda katika Bonde la Chumvi;+ naye akawapiga wana wa Seiri,+ elfu kumi kati yao.+ 12 Na wana wa Yuda wakakamata watu elfu kumi wakiwa hai. Basi wakawaleta kwenye kilele cha mwamba, wakawatupa kutoka kilele cha mwamba ule; nao wote wakapasuka.+ 13 Na wale askari-jeshi ambao Amazia alirudisha wasiende pamoja naye vitani,+ wakaanza kuvamia majiji ya Yuda, kuanzia Samaria+ mpaka Beth-horoni,+ wakawapiga elfu tatu kati yao na kuchukua nyara nyingi.
14 Lakini ikawa kwamba baada ya Amazia kurudi kutoka kuwapiga Waedomu, akaleta miungu+ ya wana wa Seiri na kujisimamishia iwe miungu,+ naye akaanza kuinama mbele yake,+ naye akaanza kuifukizia moshi wa dhabihu.+ 15 Kwa hiyo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Amazia, na hivyo akamtumia nabii na kumwambia: “Kwa nini umeitafuta+ miungu ya watu+ ambayo haikuwakomboa watu wake kutoka mkononi mwako?”+ 16 Na ikawa kwamba aliposema naye, mara moja mfalme akamwambia: “Je, tulikuweka wewe kuwa mshauri wa mfalme?+ Acha kwa faida yako mwenyewe.+ Kwa nini wakupige na kukuua?” Kwa hiyo yule nabii akaacha, lakini akasema: “Hakika ninajua kwamba Mungu ameazimia kukuangamiza wewe,+ kwa sababu umetenda hivi+ wala hukulisikiliza shauri langu.”+
17 Na Amazia mfalme wa Yuda akatafuta shauri na kutuma ujumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli,+ na kusema: “Njoo! Tutazamane uso kwa uso.”+ 18 Ndipo Yehoashi mfalme wa Israeli akatuma ujumbe kwa Amazia mfalme wa Yuda, na kusema:+ “Gugu lenye miiba lililokuwa katika Lebanoni lilituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa katika Lebanoni,+ na kusema, ‘Mpe mwanangu binti yako awe mke wake.’+ Hata hivyo, mnyama wa mwituni+ aliyekuwa katika Lebanoni akapita karibu, akalikanyaga lile gugu lenye miiba. 19 Umesema moyoni mwako, Tazama, umepiga Edomu.+ Na moyo+ wako umekuinua ili utukuzwe.+ Sasa endelea kukaa nyumbani kwako mwenyewe.+ Kwa nini ujiingize katika mzozo katika hali zisizofaa+ hata uanguke, wewe na Yuda pamoja nawe?”+
20 Lakini Amazia hakusikiliza; kwa maana jambo hilo lilitoka kwa Mungu wa kweli+ kwa kusudi la kuwatia mkononi mwake, kwa sababu walikuwa wameitafuta miungu ya Edomu.+ 21 Basi Yehoashi mfalme wa Israeli akapanda,+ nao wakatazamana uso kwa uso,+ yeye na Amazia mfalme wa Yuda, kule Beth-shemeshi,+ ya Yuda. 22 Na Yuda wakashindwa mbele ya Israeli,+ hata wakaanza kukimbia, kila mmoja kwenda katika hema lake.+ 23 Naye Yehoashi mfalme wa Israeli akamkamata+ Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, kule Beth-shemeshi, kisha akamleta Yerusalemu,+ naye akabomoa shimo katika ukuta wa Yerusalemu, kuanzia Lango la Efraimu+ mpaka kwenye Lango la Pembeni,+ urefu wa mikono mia nne. 24 Naye akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika nyumba ya Mungu wa kweli na Obed-edomu+ na hazina za nyumba ya mfalme+ na mateka, kisha akarudi Samaria.+
25 Na Amazia+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda akaendelea kuishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.+ 26 Na mambo mengine ya Amazia, ya kwanza na ya mwisho,+ tazama! je, hayakuandikwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Yuda na Israeli?+ 27 Na kutoka wakati Amazia alipogeuka akaacha kumfuata Yehova, wakapanga hila+ juu yake katika Yerusalemu. Mwishowe akakimbilia Lakishi;+ lakini wakatuma watu kumfuatilia huko Lakishi, wakamuua huko.+ 28 Kwa hiyo wakambeba juu ya farasi,+ wakamzika pamoja na mababu zake katika jiji la Yuda.+
26 Ndipo watu+ wote wa Yuda wakamchukua Uzia,+ akiwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya+ kuwa mfalme mahali pa Amazia+ baba yake. 2 Yeye ndiye aliyejenga upya Elothi+ kisha akalirudisha kwa Yuda baada ya mfalme kulala pamoja na mababu zake.+ 3 Uzia+ alianza kutawala akiwa na umri wa miaka 16, naye akatawala miaka 52 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Yekolia+ wa Yerusalemu. 4 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova,+ kulingana na yote ambayo Amazia baba yake alikuwa amefanya.+ 5 Naye akaendelea kuwa na mwelekeo wa kumtafuta+ Mungu katika siku za Zekaria, aliyekuwa akiwafundisha watu kumwogopa Mungu wa kweli;+ na katika zile siku alizokuwa akimtafuta Yehova, Mungu wa kweli alimfanikisha.+
6 Naye akatoka kwenda kupigana na Wafilisti,+ akapenya ukuta wa Gathi+ na ukuta wa Yabne+ na ukuta wa Ashdodi,+ kisha akajenga majiji katika eneo la Ashdodi+ na katikati ya Wafilisti. 7 Na Mungu wa kweli akaendelea kumsaidia+ juu ya Wafilisti na juu ya Waarabu+ waliokuwa wakikaa katika Gurbaali na Meunimu.+ 8 Na Waamoni+ wakaanza kumpa Uzia ushuru.+ Mwishowe sifa+ yake ikaenea mpaka Misri, kwa kuwa alionyesha nguvu kwa kiwango kisicho cha kawaida. 9 Zaidi ya hayo, Uzia akajenga minara+ katika Yerusalemu kando ya Lango la Pembeni+ na kando ya Lango la Bonde+ na kando ya Nguzo, naye akaitia nguvu. 10 Tena akajenga minara+ nyikani, na kuchimba matangi mengi ya maji (kwa maana alikuwa na mifugo mingi sana), na pia katika Shefela+ na katika nchi tambarare ya juu. Palikuwa na wakulima na watunza-mizabibu katika milima na katika Karmeli, kwa maana alipenda kilimo.
11 Tena Uzia akawa na jeshi la kupigana vita, wale wanaoingia katika utumishi wa kijeshi vikosi vikosi,+ kulingana na hesabu ya uandikisho+ wao kwa mkono wa Yeieli mwandishi+ na Maaseya ofisa aliye chini ya+ Hanania mmoja wa wakuu wa mfalme.+ 12 Hesabu kamili ya vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba,+ ya mashujaa,+ wanaume wenye nguvu,+ ilikuwa elfu mbili na mia sita. 13 Na chini ya amri yao majeshi yalikuwa ni watu mia tatu na saba elfu na mia tano wa kupigana vita wakiwa na nguvu za kijeshi ili kumsaidia mfalme kupigana na adui.+ 14 Na Uzia akaendelea kuwafanyia matayarisho, jeshi lote, ngao+ na mikuki+ na kofia+ na mavazi ya chuma+ na pinde+ na mawe ya kombeo.+ 15 Tena akatengeneza mitambo ya vita katika Yerusalemu, ubuni wa mafundi, ili iwekwe juu ya minara+ na juu ya sehemu za pembeni, ili irushe mishale na mawe makubwa. Basi sifa+ yake ikaenea mbali sana, kwa kuwa alisaidiwa kwa njia ya ajabu mpaka akawa na nguvu.
16 Hata hivyo, mara tu alipopata nguvu, moyo wake ukawa na majivuno+ hata kufikia hatua ya kusababisha uharibifu,+ hivi kwamba akatenda kwa ukosefu wa uaminifu kwa Yehova Mungu wake, akaingia katika hekalu la Yehova ili kufukiza uvumba juu ya madhabahu ya uvumba.+ 17 Mara moja Azaria kuhani na makuhani wa Yehova pamoja naye, wanaume mashujaa 80, wakaingia nyuma yake. 18 Kisha wakasimama kumpinga Uzia mfalme+ na kumwambia: “Si kazi yako,+ Ee Uzia, kumfukizia Yehova uvumba, bali ni kazi ya makuhani, wana wa Haruni,+ waliotakaswa, kufukiza uvumba. Ondoka ndani ya patakatifu; kwa maana umetenda kwa ukosefu wa uaminifu, wala jambo hilo si utukufu+ wowote kwako mbele za Yehova Mungu.”
19 Lakini Uzia akawa na ghadhabu,+ huku mkononi mwake akiwa na chetezo,+ cha kufukiza uvumba, na, alipokuwa na ghadhabu juu ya makuhani, ukoma+ ukatokea+ katika paji la uso wake mbele ya wale makuhani katika nyumba ya Yehova kando ya madhabahu ya uvumba. 20 Wakati Azaria yule mkuu wa makuhani na makuhani wote walipogeuka kumwelekea, tazama, alikuwa amepigwa na ukoma katika paji la uso wake!+ Kwa hiyo wakaanza kumtoa hapo upesi, naye mwenyewe pia akafanya haraka kutoka nje, kwa sababu Yehova alikuwa amempiga.+
21 Na Uzia+ mfalme akaendelea kuwa mwenye ukoma mpaka siku ya kufa kwake, naye akaendelea kukaa katika nyumba fulani akiwa ameondolewa wajibu wake, akiwa mwenye ukoma;+ kwa sababu alikuwa ametengwa na nyumba ya Yehova, huku Yothamu mwana wake akiwa juu ya nyumba ya mfalme, akiwahukumu watu wa nchi.
22 Na yale mambo mengine ya Uzia,+ ya kwanza na ya mwisho, Isaya+ mwana wa Amozi+ nabii ameyaandika. 23 Mwishowe Uzia akalala pamoja na mababu zake; na kwa hiyo wakamzika pamoja na mababu zake, lakini katika uwanja wa kuzikia wa wafalme,+ kwa maana walisema: “Yeye ni mwenye ukoma.” Na Yothamu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
27 Yothamu+ alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 16 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Yerusha+ binti ya Sadoki. 2 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova,+ kulingana na yote ambayo Uzia baba yake alikuwa amefanya.+ Ila tu hakulivamia hekalu la Yehova.+ Hata hivyo, watu bado walikuwa wakitenda kwa uharibifu.+ 3 Yeye alijenga lango la juu+ la nyumba ya Yehova, naye akafanya ujenzi mkubwa katika ukuta wa Ofeli.+ 4 Naye akajenga majiji+ katika eneo lenye milima la Yuda,+ akajenga ngome+ na minara+ msituni.+ 5 Naye akapigana vita na mfalme wa wana wa Amoni,+ na mwishowe akawa na nguvu kuliko wao, hivi kwamba wana wa Amoni wakampa mwaka huo talanta mia moja za fedha na vipimo+ elfu kumi vya ngano+ na elfu kumi vya shayiri.+ Wana wa Amoni walimlipa vitu hivyo, pia katika mwaka wa pili na wa tatu.+ 6 Basi Yothamu akaendelea kujitia nguvu, kwa maana alitayarisha njia zake mbele za Yehova Mungu wake.+
7 Na yale mambo mengine ya Yothamu+ na vita vyake vyote na njia zake, tazama, yameandikwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Israeli na wa Yuda. 8 Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 16 katika Yerusalemu.+ 9 Mwishowe Yothamu akalala pamoja na mababu zake,+ nao wakamzika katika Jiji la Daudi.+ Na Ahazi+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
28 Ahazi+ alikuwa na umri wa miaka 20 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 16 katika Yerusalemu,+ naye hakufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova kama Daudi babu yake.+ 2 Bali alitembea katika njia za wafalme wa Israeli,+ na hata akatengeneza sanamu za kuyeyushwa+ za Mabaali.+ 3 Naye akafukiza moshi wa dhabihu+ katika bonde la mwana wa Hinomu,+ akateketeza wanawe+ katika moto, kulingana na machukizo+ ya mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya wana wa Israeli.+ 4 Naye alitoa dhabihu kwa ukawaida+ na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu na juu+ ya vilima+ na chini ya kila namna ya mti wenye majani mengi.+
5 Kwa hiyo Yehova Mungu wake akamtia mkononi+ mwa mfalme wa Siria,+ nao wakampiga na kuchukua kutoka kwake hesabu kubwa ya mateka na kuwaleta Damasko.+ Naye pia akatiwa mkononi mwa mfalme wa Israeli,+ naye akampiga kwa mauaji makubwa. 6 Basi Peka+ mwana wa Remalia+ akaua katika Yuda watu 120,000 katika siku moja, wote wakiwa ni wanaume mashujaa, kwa sababu walimwacha Yehova+ Mungu wa mababu zao. 7 Tena, Zikri, mwanamume mwenye nguvu wa Efraimu,+ akamuua Maaseya mwana wa mfalme na Azrikamu kiongozi wa nyumba na Elkana yule aliyekuwa wa pili kwa mfalme. 8 Na tena wana wa Israeli wakawachukua mateka ndugu zao mia mbili elfu, wanawake, wana na mabinti; na pia wakapora nyara nyingi kutoka kwao, kisha wakaleta nyara hizo Samaria.+
9 Na palikuwa na nabii wa Yehova hapo ambaye jina lake lilikuwa Odedi. Basi akaenda mbele ya jeshi lililokuwa likija Samaria na kuwaambia: “Tazama! Yehova Mungu wa mababu zenu aliwatia hao mkononi mwenu kwa sababu ya ghadhabu+ yake juu ya Yuda, hivi kwamba mkafanya mauaji kati yao kwa ghadhabu+ ambayo imefika mpaka mbinguni.+ 10 Na sasa mnafikiria kuwafanya wana wa Yuda na wana wa Yerusalemu kuwa watumishi+ na wajakazi wenu. Hata hivyo, je, ninyi wenyewe hamna visa vya hatia juu ya Yehova Mungu wenu? 11 Na sasa nisikilizeni, na mwarudishe mateka ambao mmewateka kutoka kwa ndugu zenu,+ kwa maana hasira ya Yehova inayowaka iko juu yenu.”+
12 Ndipo watu fulani wa vichwa+ vya wana wa Efraimu,+ Azaria mwana wa Yehohanani, Berekia mwana wa Meshilemothi na Yehizkia mwana wa Shalumu na Amasa mwana wa Hadlai, wakasimama kuwapinga wale waliokuwa wakiingia kutoka katika shughuli hiyo ya kijeshi, 13 nao wakawaambia: “Msiingize mateka humu, kwa sababu tutakuwa na hatia juu ya Yehova. Mnafikiria kuziongeza dhambi zetu na hatia yetu, kwa maana sisi tuna hatia kubwa,+ na kuna hasira inayowaka+ juu ya Israeli.” 14 Basi wale watu wenye silaha+ wakawaacha wale mateka+ na ile nyara mbele ya wakuu+ na kutaniko lote. 15 Kisha watu waliochaguliwa kwa majina+ yao wakasimama na kuwachukua wale mateka, na wote waliokuwa uchi wakawavika nguo kutokana na zile nyara. Basi wakawavika+ na kuwapa viatu, wakawalisha+ na kuwapa vinywaji+ na kuwapaka mafuta. Tena, kuhusu wowote wenye kutetemeka, wakawasafirisha+ juu ya punda na kuwaleta Yeriko,+ jiji la mitende,+ kando ya ndugu zao. Kisha wakarudi Samaria.+
16 Wakati huo Mfalme Ahazi+ akatuma ujumbe kwa wafalme wa Ashuru+ ili wamsaidie. 17 Na kwa mara nyingine tena Waedomu+ wakaingia na kuwapiga Yuda na kuchukua mateka. 18 Nao Wafilisti+ wakavamia majiji ya Shefela+ na Negebu+ katika Yuda na kuteka Beth-shemeshi+ na Aiyaloni+ na Gederothi+ na Soko+ na miji yake ya kandokando na Timna+ na miji yake ya kandokando na Gimzo na miji yake ya kandokando; nao wakaanza kukaa humo. 19 Kwa kuwa Yehova alinyenyekeza+ Yuda kwa sababu ya Ahazi mfalme wa Israeli, kwa sababu aliachilia mambo katika Yuda,+ nao wakatenda kwa ukosefu mkubwa sana wa uaminifu kumwelekea Yehova.
20 Mwishowe Tilgath-pilneseri+ mfalme wa Ashuru akaja kupigana naye na kumtaabisha,+ naye hakumtia nguvu. 21 Kwa kuwa Ahazi alichukua mali yote katika nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme+ na ya wakuu+ na kumpa zawadi mfalme wa Ashuru;+ lakini jambo hilo halikumsaidia kamwe. 22 Hata hivyo, wakati alipokuwa akimtaabisha, yeye, yaani, Mfalme Ahazi, alizidi kutenda kwa ukosefu wa uaminifu kumwelekea Yehova.+ 23 Naye akaanza kuitolea dhabihu miungu+ ya Damasko+ iliyokuwa ikimpiga, naye akasema: “Kwa sababu miungu ya wafalme wa Siria inawasaidia wao,+ mimi nitaitolea dhabihu, ili inisaidie.”+ Nayo ikawa kisababishi cha kumfanya yeye na Israeli wote wajikwae.+ 24 Zaidi ya hayo, Ahazi akavikusanya vyombo+ vya nyumba ya Mungu wa kweli na kuvikata vipande-vipande vyombo vya nyumba ya Mungu wa kweli,+ akaifunga milango+ ya nyumba ya Yehova, akajitengenezea madhabahu katika kila pembe katika Yerusalemu.+ 25 Na katika majiji yote, majiji ya Yuda, akajenga mahali pa juu+ kwa ajili ya kuifukizia miungu mingine moshi wa uvumba,+ hivi kwamba akamtia uchungu+ Yehova Mungu wa mababu zake.
26 Na yale mambo yake mengine+ na njia zake, ya kwanza na ya mwisho, tazama, yameandikwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Yuda na wa Israeli. 27 Mwishowe Ahazi akalala pamoja na mababu zake, nao wakamzika katika jiji, Yerusalemu, kwa maana hawakumpeleka kwenye makaburi ya wafalme wa Israeli.+ Na Hezekia mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
29 Hezekia+ alikuwa mfalme akiwa na umri wa miaka 25, naye akatawala miaka 29 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Abiya binti ya Zekaria.+ 2 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova,+ kulingana na yote ambayo Daudi babu yake alikuwa amefanya.+ 3 Yeye mwenyewe, katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake, katika mwezi wa kwanza, aliifungua milango ya nyumba ya Yehova na kuanza kuirekebisha.+ 4 Kisha akawaleta makuhani na Walawi na kuwakusanya mahali palipo wazi+ upande wa mashariki. 5 Naye akawaambia: “Nisikilizeni, enyi Walawi. Sasa jitakaseni+ na mwitakase nyumba ya Yehova Mungu wa mababu zenu, na mwondoe kitu kichafu kutoka mahali patakatifu.+ 6 Kwa maana baba zetu wametenda kwa ukosefu wa uaminifu+ nao wametenda mabaya machoni pa Yehova Mungu wetu,+ hivi kwamba walimwacha+ na kugeuza nyuso zao kutoka kwenye maskani ya Yehova+ na kumpa visogo vyao. 7 Pia walifunga milango+ ya ukumbi na kuzima taa,+ nao hawakufukiza uvumba,+ wala hawakumtolea Mungu wa Israeli dhabihu ya kuteketezwa katika mahali patakatifu.+ 8 Na ghadhabu+ ya Yehova ikaja juu ya Yuda na Yerusalemu, hivi kwamba akawafanya kuwa kitu cha kutetemesha watu,+ kitu cha kushangaza+ na kisababishi cha kupiga mluzi,+ kama vile mnavyoona kwa macho yenu wenyewe. 9 Na tazama, mababu zetu walianguka kwa upanga,+ na wana wetu na binti zetu na wake zetu walikuwa utekwani kwa sababu ya hayo.+ 10 Sasa ninataka moyoni mwangu kufanya agano+ pamoja na Yehova Mungu wa Israeli, ili hasira yake inayowaka igeuke kutoka kwetu. 11 Sasa, wanangu, msijipumzishe,+ kwa maana Yehova amewachagua ninyi msimame mbele zake ili kumhudumia+ na kuwa wahudumu+ wake na kuwa wenye kufukiza moshi wa dhabihu.”+
12 Ndipo Walawi+ wakasimama, Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria wa wana wa Wakohathi;+ na kutoka kwa wana wa Merari,+ Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yehaleleli; na kutoka kwa Wagershoni,+ Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa; 13 na kutoka kwa wana wa Elisafani,+ Shimri na Yeueli; na kutoka kwa wana wa Asafu,+ Zekaria na Matania; 14 na kutoka kwa wana wa Hemani,+ Yehieli na Shimei; na kutoka kwa wana wa Yeduthuni,+ Shemaya na Uzieli. 15 Ndipo wakawakusanya ndugu zao na kujitakasa+ na kuja kulingana na amri ya mfalme kwa maneno+ ya Yehova, ili kuitakasa+ nyumba ya Yehova. 16 Sasa makuhani wakaingia ndani ya nyumba ya Yehova ili kufanya utakaso, nao wakauondoa uchafu wote walioupata katika hekalu la Yehova mpaka kwenye ua+ wa nyumba ya Yehova. Nao Walawi wakauchukua ili waupeleke nje katika bonde la mto la Kidroni+ upande wa nje. 17 Basi wakaanza kutakasa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, na katika siku ya nane ya mwezi huo wakaja katika ukumbi+ wa Yehova; nao wakaitakasa nyumba ya Yehova katika siku nane, na katika siku ya kumi na sita ya mwezi wa kwanza+ wakamaliza.
18 Kisha wakaingia kwa Hezekia mfalme na kusema: “Tumeitakasa nyumba yote ya Yehova, madhabahu+ ya toleo la kuteketezwa na vyombo+ vyake vyote, na meza+ ya mkate wa tabaka na vyombo vyake vyote.+ 19 Nasi tumetayarisha vyombo+ vyote ambavyo Mfalme Ahazi+ aliondoa katika utumishi wakati wa utawala wake katika ukosefu wake wa uaminifu,+ nasi tumevitakasa;+ na tazama, viko mbele ya madhabahu ya Yehova.”
20 Naye Hezekia+ mfalme akaondoka mapema,+ akawakusanya wakuu+ wa jiji, na kupanda kwenda katika nyumba ya Yehova. 21 Nao wakaleta ng’ombe-dume saba+ na kondoo-dume saba na wana-kondoo dume saba na mbuzi-dume saba wawe toleo la dhambi+ kwa ajili ya ufalme na kwa ajili ya patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Basi akawaambia wana wa Haruni, makuhani,+ wawatoe wawe toleo juu ya madhabahu ya Yehova. 22 Kwa hiyo wakawachinja+ wale ng’ombe na makuhani wakapokea damu+ na kuinyunyiza+ juu ya madhabahu; kisha wakawachinja wale kondoo-dume+ na kuinyunyiza damu+ juu ya madhabahu, nao wakawachinja wana-kondoo na kuinyunyiza damu juu ya madhabahu. 23 Kisha wakawaleta karibu wale mbuzi-dume+ wa toleo la dhambi mbele ya mfalme na kutaniko na kuweka mikono yao juu yao.+ 24 Sasa makuhani wakawachinja na kutoa toleo la dhambi kwa damu yao juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli wote;+ kwa sababu mfalme alisema toleo la kuteketezwa na toleo la dhambi liwe+ kwa ajili ya Israeli+ wote.
25 Wakati huohuo akawaweka Walawi+ katika nyumba ya Yehova, wakiwa na matoazi,+ na vinanda+ na vinubi,+ kulingana na amri ya Daudi+ na ya Gadi+ mwonaji wa mfalme na ya nabii Nathani,+ kwa maana amri hiyo ilikuwa kulingana na mkono wa Yehova kupitia manabii wake.+ 26 Basi Walawi wakaendelea kusimama wakiwa na vyombo+ vya Daudi, na pia makuhani wakiwa na tarumbeta.+
27 Ndipo Hezekia akasema dhabihu ya kuteketezwa itolewe juu ya madhabahu; na wakati lile toleo la kuteketezwa lilipoanza, wimbo+ wa Yehova ukaanza na pia tarumbeta, chini ya mwelekezo wa vyombo vya Daudi mfalme wa Israeli. 28 Na kutaniko lote wakainama+ huku wimbo ukivuma+ na tarumbeta zikipigwa—hayo yote yakaendelea mpaka lile toleo la kuteketezwa lilipomalizika. 29 Na mara tu walipomaliza kulitoa, mfalme na wote waliokuwa pamoja naye wakainama na kusujudu.+ 30 Sasa Hezekia mfalme na wakuu+ wakawaambia Walawi wamsifu Yehova kwa maneno ya Daudi+ na ya Asafu+ yule mwonaji. Kwa hiyo wakaanza kutoa sifa kwa kushangilia,+ wakaendelea kuinama na kusujudu.+
31 Mwishowe Hezekia akajibu na kusema: “Sasa mmeujaza+ mkono wenu nguvu kwa ajili ya Yehova. Karibieni, mlete dhabihu+ na dhabihu za shukrani+ katika nyumba ya Yehova.” Nalo kutaniko likaanza kuleta dhabihu na dhabihu za shukrani, na pia kila mtu aliyekuwa na moyo wa kupenda, akaleta matoleo ya kuteketezwa.+ 32 Na hesabu ya matoleo ya kuteketezwa ambayo kutaniko hilo lilileta ikawa ng’ombe 70, kondoo-dume 100, wana-kondoo dume 200—hao wote wakiwa ni toleo la kuteketezwa kwa Yehova;+ 33 na pia matoleo matakatifu, ng’ombe 600 na wanyama 3,000 kati ya kundi. 34 Ila tu makuhani+ walikuwa wachache mno, nao hawakuweza kuchuna ngozi yale matoleo yote ya kuteketezwa.+ Kwa hiyo ndugu+ zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ilipoisha+ na mpaka makuhani walipokuwa wamejitakasa,+ kwa kuwa Walawi walikuwa wanyoofu+ zaidi wa moyo katika kujitakasa kuliko makuhani. 35 Na, pia, matoleo ya kuteketezwa+ yalikuwa mengi sana pamoja na vipande vya mafuta+ vya dhabihu za ushirika+ pamoja na matoleo ya kinywaji+ kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa. Hivyo utumishi wa nyumba ya Yehova ukatayarishwa.+ 36 Kwa hiyo Hezekia na watu wote wakashangilia kwa sababu Mungu wa kweli alikuwa amefanya matayarisho kwa ajili ya watu,+ kwa sababu jambo hilo lilikuwa limetokea kwa ghafula.+
30 Na Hezekia akatuma ujumbe kwa Israeli+ wote na Yuda, na hata akaandika barua kwa Efraimu+ na Manase,+ waje Yerusalemu katika nyumba ya Yehova+ ili kumfanyia pasaka+ Yehova Mungu wa Israeli. 2 Hata hivyo, mfalme na wakuu+ wake na kutaniko+ lote katika Yerusalemu wakaazimia kufanya pasaka katika mwezi wa pili;+ 3 kwa maana hawakuweza kuifanya wakati huo,+ kwa sababu makuhani+ wa kutosha hawakuwa wamejitakasa na watu hawakuwa wamekusanyika Yerusalemu. 4 Na jambo hilo lilikuwa sawa machoni pa mfalme na machoni pa kutaniko lote.+ 5 Basi wakaamua kueneza mwito+ huo katika Israeli yote, kuanzia Beer-sheba+ mpaka Dani,+ ili waje na kufanya pasaka kwa Yehova Mungu wa Israeli katika Yerusalemu; kwa maana hawakuwa wamefanya hivyo+ wakiwa umati kulingana na yale ambayo yameandikwa.+
6 Kwa hiyo wakimbiaji+ walio na zile barua kutoka katika mkono wa mfalme na wa wakuu+ wake wakaenda katika Israeli yote na Yuda, kulingana na amri ya mfalme, na kusema: “Ninyi wana wa Israeli, rudini+ kwa Yehova Mungu+ wa Abrahamu, Isaka na Israeli, ili yeye arudi kwa wale walioponyoka+ ambao wamebaki kati yenu kutoka katika mkono wa wafalme wa Ashuru.+ 7 Na msiwe kama mababu zenu+ na kama ndugu zenu waliotenda kwa ukosefu wa uaminifu kumwelekea Yehova Mungu wa mababu zao, hivi kwamba akawafanya kuwa kitu cha kushangaza,+ kama vile mnavyoona. 8 Sasa msifanye shingo+ zenu kuwa ngumu kama walivyofanya mababu zenu. Mpeni Yehova nafasi+ na mje katika patakatifu pake+ ambapo amepatakasa+ mpaka wakati usio na kipimo na kumtumikia+ Yehova Mungu wenu, ili hasira yake inayowaka+ iondoke kwenu. 9 Kwa maana wakati mtakaporudi+ kwa Yehova, ndugu zenu na wana wenu wataonyeshwa rehema+ mbele ya wale wanaowashika mateka, na kuruhusiwa kurudi katika nchi hii;+ kwa kuwa Yehova Mungu wenu, ni mwenye neema+ na rehema,+ wala hatageuza uso kutoka kwenu mkirudi kwake.”+
10 Kwa hiyo wale wakimbiaji+ wakaendelea, wakapita jiji baada ya jiji katika nchi yote ya Efraimu+ na Manase, mpaka Zabuloni; lakini wakaendelea kuwafanyia mzaha na kuwadharau.+ 11 Ni watu mmoja mmoja+ tu kutoka Asheri na Manase na kutoka Zabuloni waliojinyenyekeza,+ hivi kwamba wakaja Yerusalemu. 12 Mkono wa Mungu wa kweli ukawa katika Yuda pia ili kuwapa moyo mmoja+ ili watende amri+ ya mfalme na wakuu kuhusu lile jambo la Yehova.+
13 Nao wakakusanyika Yerusalemu,+ watu wengi sana, ili kufanya sherehe+ ya keki zisizo na chachu katika mwezi wa pili,+ kutaniko lenye watu wengi sana. 14 Kisha wakasimama na kuziondoa madhabahu+ zilizokuwa Yerusalemu, wakaziondoa madhabahu+ zote za uvumba, nao wakazitupa katika bonde la mto la Kidroni.+ 15 Kisha wakachinja mnyama wa pasaka+ katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili; na makuhani na Walawi walikuwa wametiwa aibu, hivi kwamba wakajitakasa+ na kuleta matoleo ya kuteketezwa kwenye nyumba ya Yehova. 16 Nao wakaendelea kusimama+ mahali pao kulingana na kanuni yao, kulingana na sheria ya Musa yule mtu wa Mungu wa kweli, makuhani+ wakinyunyiza damu iliyopokewa kutoka mkononi mwa Walawi. 17 Kwa maana palikuwa na wengi katika kutaniko ambao hawakuwa wamejitakasa; na Walawi+ walikuwa wakisimamia kuchinjwa kwa wanyama wa pasaka+ kwa ajili ya wote ambao hawakuwa safi, ili kuwatakasa kwa Yehova. 18 Kwa maana palikuwa na hesabu kubwa ya watu, wengi kutoka Efraimu+ na Manase,+ Isakari na Zabuloni,+ ambao hawakuwa wamejitakasa,+ kwa maana hawakula pasaka kulingana na yale ambayo yameandikwa;+ lakini Hezekia akasali kwa ajili yao,+ na kusema: “Yehova aliye mwema+ na amkubali 19 kila mtu ambaye ameutayarisha moyo+ wake ili kumtafuta Mungu wa kweli, Yehova Mungu wa mababu zake, ingawa hajatakaswa kwa ajili ya kilicho kitakatifu.”+ 20 Basi Yehova akamsikiliza Hezekia na kuwaponya watu.+
21 Hivyo wana wa Israeli waliokuwa Yerusalemu wakafanya sherehe+ ya keki zisizo na chachu kwa siku saba kwa shangwe kubwa;+ na Walawi+ na makuhani+ walikuwa wakimtolea Yehova sifa siku baada ya siku kwa vyombo vyenye sauti kubwa, naam, kwa Yehova.+ 22 Tena Hezekia akasema kwa moyo+ wa Walawi wote waliokuwa wakitenda kwa busara njema kumwelekea Yehova.+ Nao wakala sherehe rasmi kwa siku saba,+ wakitoa dhabihu za ushirika+ na kuungama+ kwa Yehova Mungu wa mababu zao.
23 Kisha kutaniko lote likaamua+ kuifanya kwa siku saba zaidi,+ basi wakaifanya kwa siku saba kwa kushangilia. 24 Kwa maana Hezekia mfalme wa Yuda alichanga+ kwa ajili ya kutaniko ng’ombe elfu moja na kondoo elfu saba, na wakuu+ wakachanga kwa ajili ya kutaniko ng’ombe elfu moja na kondoo elfu kumi; na hesabu kubwa ya makuhani+ wakaendelea kujitakasa. 25 Na kutaniko lote la Yuda+ na makuhani na Walawi+ na kutaniko lote lililokuja kutoka katika Israeli+ na wakaaji wageni+ waliokuja kutoka katika nchi ya Israeli+ na wale wanaokaa Yuda wakaendelea kushangilia.+ 26 Na kukawa na shangwe kubwa Yerusalemu, kwa maana tangu siku za Sulemani+ mwana wa Daudi mfalme wa Israeli hakukuwa na shangwe kama hiyo katika Yerusalemu.+ 27 Mwishowe makuhani, Walawi, wakasimama na kuwabariki+ watu; na sauti yao ikasikilizwa, hivi kwamba sala yao ikaingia katika makao yake matakatifu, mbinguni.+
31 Na mara tu walipomaliza hayo yote, Waisraeli+ wote waliokuwa hapo wakaenda katika majiji ya Yuda,+ nao wakazivunja nguzo takatifu+ na kuikata miti mitakatifu+ na kupabomoa mahali pa juu+ na madhabahu+ kutoka katika Yuda+ yote na Benyamini na katika Efraimu+ na Manase+ mpaka walipomaliza; kisha wana wote wa Israeli wakarudi katika majiji yao, kila mmoja kwenye miliki yake.
2 Kisha Hezekia akaweka migawanyo+ ya makuhani na ya Walawi+ katika migawanyo yao, kila mmoja kulingana na utumishi wake kwa ajili ya makuhani+ na kwa ajili ya Walawi+ kuhusiana na toleo la kuteketezwa+ na dhabihu za ushirika+ ili kuhudumu+ na kutoa shukrani+ na sifa+ katika malango ya kambi za Yehova. 3 Na kulikuwa na fungu la mfalme kutoka katika mali zake mwenyewe+ kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa,+ kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa ya asubuhi+ na jioni, na pia matoleo ya kuteketezwa kwa ajili ya sabato+ na kwa ajili ya miezi mipya+ na kwa ajili ya majira ya sherehe,+ kulingana na yaliyoandikwa katika sheria ya Yehova.+
4 Tena akawaambia watu, wakaaji wa Yerusalemu, kwamba watoe fungu la makuhani+ na la Walawi,+ ili waishike+ kabisa sheria ya Yehova.+ 5 Na mara tu lile neno lilipoenea, wana wa Israeli+ wakazidisha mazao ya kwanza ya nafaka,+ divai mpya,+ na mafuta+ na asali+ na mazao yote ya shamba,+ nao wakaleta kwa wingi sehemu ya kumi ya kila kitu.+ 6 Na wana wa Israeli na wa Yuda waliokuwa wakikaa katika majiji ya Yuda,+ wao wenyewe wakaleta sehemu ya kumi ya ng’ombe na kondoo na sehemu ya kumi ya vitu vitakatifu,+ vitu vilivyotakaswa kwa Yehova Mungu wao. Wakaleta, nao wakatoa mafungu juu ya mafungu. 7 Katika mwezi wa tatu+ walianzisha mafungu kwa kuweka tabaka ya chini zaidi, na katika mwezi wa saba+ wakamaliza. 8 Wakati Hezekia na wakuu+ walipokuja na kuona yale mafungu, wakambariki+ Yehova na watu wake Israeli.+
9 Baada ya muda Hezekia akawauliza makuhani na Walawi habari za yale mafungu.+ 10 Ndipo Azaria+ mkuu wa makuhani wa nyumba ya Sadoki+ akamwambia, ndiyo, akasema: “Tangu walipoanza kuleta mchango+ ndani ya nyumba ya Yehova kumekuwako kula na kushiba+ na kuwa na ziada kwa wingi;+ kwa kuwa Yehova mwenyewe amewabariki watu wake,+ na kilichobaki ni hiki kiasi kingi.”
11 Kwa hiyo Hezekia akasema vyumba vya kulia chakula+ vitayarishwe katika nyumba ya Yehova. Basi wakavitayarisha. 12 Nao wakaendelea kuleta ule mchango+ na ile sehemu ya kumi+ na vile vitu vitakatifu kwa uaminifu;+ na Konania Mlawi alikuwa akiwasimamia akiwa kiongozi, na Shimei ndugu yake alikuwa wa pili. 13 Na Yehieli na Azazia na Nahathi na Asaheli na Yerimothi na Yozabadi na Elieli na Ismakia na Mahathi na Benaya walikuwa wajumbe kando ya Konania na Shimei ndugu yake, kwa agizo la Hezekia mfalme, na Azaria+ alikuwa ndiye kiongozi wa nyumba ya Mungu wa kweli. 14 Na Kore mwana wa Imna Mlawi alikuwa mtunza-lango+ upande wa mashariki,+ mwenye kusimamia matoleo ya hiari+ ya Mungu wa kweli, ili kutoa mchango+ wa Yehova na vitu vitakatifu zaidi.+ 15 Na chini yake palikuwa na Edeni na Miniamini na Yeshua na Shemaya, Amaria na Shekania, katika majiji ya makuhani,+ katika vyeo vyenye kutegemeka,+ ili kuwapa ndugu zao katika migawanyo,+ wakubwa na wadogo kwa kiwango sawasawa;+ 16 mbali na maandikisho ya kiukoo+ ya wanaume wenye umri wa kuanzia miaka mitatu na zaidi,+ kati ya wale wote wanaoingia katika nyumba ya Yehova kama desturi ya kila siku, kwa ajili ya utumishi wao kulingana na wajibu wao kufuatana na migawanyo yao.
17 Huu ndio uandikisho wa kiukoo wa makuhani kulingana na nyumba za baba+ zao na pia za Walawi,+ kuanzia umri wa miaka 20+ na zaidi, kulingana na wajibu wao katika migawanyo+ yao; 18 kwa ajili ya uandikisho wa kiukoo kati ya watoto wao wote, wake zao na wana wao na binti zao, kwa ajili ya kutaniko lote, kwa sababu walijitakasa+ katika vyeo vyao vyenye kutegemeka+ kwa ajili ya kilicho kitakatifu; 19 na kwa ajili ya wana wa Haruni,+ makuhani, katika mashamba ya viwanja+ vya malisho vya majiji yao. Katika majiji yote mbalimbali kulikuwa na watu waliowekwa kulingana na majina yao, ili kumpa mafungu kila mwanamume kati ya makuhani na kwa uandikisho wote wa kiukoo kati ya Walawi.
20 Na Hezekia akafanya hivyo katika Yuda yote, naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mema+ na sawa+ na yenye uaminifu+ mbele za Yehova Mungu wake. 21 Na katika kila kazi aliyoanza katika utumishi+ wa nyumba ya Mungu wa kweli na katika sheria+ na katika amri ili kumtafuta+ Mungu wake, alitenda kwa moyo wake wote,+ naye akafanikiwa.+
32 Baada ya mambo hayo na mwendo huu wa uaminifu+ Senakeribu+ mfalme wa Ashuru+ akaja na kuvamia Yuda na kupiga kambi juu ya majiji yenye ngome,+ naye akaendelea kufikiria kuyafanya yawe yake kwa kuyavunja.
2 Hezekia alipoona kwamba Senakeribu amekuja na uso+ wake uko tayari kupiga vita juu ya Yerusalemu, 3 ndipo akaamua yeye pamoja na wakuu+ wake na wanaume wake wenye nguvu kuyaziba maji ya mabubujiko yaliyokuwa nje ya jiji;+ nao wakamsaidia. 4 Basi watu wengi wakakusanywa, nao wakaziba chemchemi zote na mto+ unaofurika kupitia katikati ya nchi, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kupata maji mengi?”
5 Tena akajipa moyo na kujenga ukuta wote uliovunjika+ na kusimamisha minara+ juu yake, na upande wa nje ukuta mwingine,+ akarekebisha Kilima+ cha Jiji la Daudi, na kutengeneza silaha+ kwa wingi na ngao.+ 6 Naye akaweka wakuu wa majeshi+ juu ya watu na kuwakusanya kwake katika kiwanja cha watu wote+ cha lango la jiji na kusema na moyo+ wao, akiwaambia: 7 “Iweni hodari na wenye nguvu.+ Msiogope+ wala msiwe na hofu+ kwa sababu ya mfalme wa Ashuru+ na kwa sababu ya umati wote ulio pamoja naye;+ kwa maana kuna wengi walio pamoja nasi kuliko wale walio pamoja naye. 8 Yeye, mkono wa nyama uko pamoja naye,+ lakini sisi, Yehova Mungu wetu yuko pamoja nasi+ ili kutusaidia na kupigana vita vyetu.”+ Na watu wakaanza kujitegemeza juu ya maneno ya Hezekia mfalme wa Yuda.+
9 Baada ya hayo Senakeribu+ mfalme wa Ashuru akawatuma watumishi wake mpaka Yerusalemu, wakati alipokuwa katika Lakishi+ pamoja na uwezo wake wote wa kifalme,+ kwenda kwa Hezekia mfalme wa Yuda na kwa Wayudea wote waliokuwa Yerusalemu, akisema:
10 “Senakeribu mfalme wa Ashuru amesema hivi,+ ‘Ni kitu gani mnachokitegemea huku mkiketi kimya katika Yerusalemu mkiwa mmezingirwa?+ 11 Je, Hezekia+ siye anayewashawishi+ ninyi ili kuwatoa mfe kwa njaa na kwa kiu, akisema: “Yehova Mungu wetu atatukomboa kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru”?+ 12 Je, Hezekia siye aliyeondoa mahali pa juu+ na madhabahu+ zake kisha akawaambia Yuda na Yerusalemu: “Mnapaswa kuinama+ mbele ya madhabahu moja+ nanyi mfukize juu yake moshi wa dhabihu”?+ 13 Je, ninyi hamjui yale ambayo mimi mwenyewe na mababu zangu tulivitendea vikundi vyote vya watu wa nchi?+ Je, miungu+ ya mataifa ya zile nchi iliweza kukomboa hata kidogo nchi yao kutoka mkononi mwangu? 14 Kati ya miungu yote ya mataifa hayo ambayo mababu zangu waliangamiza ni nani aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka mkononi mwangu, hivi kwamba Mungu wenu aweze kuwakomboa ninyi kutoka mkononi mwangu?+ 15 Na sasa msiache Hezekia awadanganye+ wala kuwashawishi+ ninyi hivyo wala msimwamini, kwa maana hakuna mungu yeyote wa taifa lolote au ufalme aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka mkononi mwangu na kutoka mkononi mwa mababu zangu. Basi, Mungu wenu atawezaje kuwakomboa ninyi kutoka mkononi mwangu!’”+
16 Na bado watumishi wake wakasema mabaya zaidi juu ya Yehova Mungu wa kweli,+ na juu ya Hezekia mtumishi wake. 17 Na hata akaandika barua+ za kumshutumu Yehova Mungu wa Israeli+ na kuongea vibaya juu yake, akisema: “Kama miungu+ ya mataifa ya nchi, ambayo haikuwakomboa watu wake kutoka mkononi mwangu,+ vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hatawakomboa watu wake kutoka mkononi mwangu.” 18 Nao+ wakaendelea kuwaita watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta kwa sauti kubwa+ katika lugha ya Wayahudi+ ili kuwaogopesha+ na kuwatia wasiwasi, ili kwamba wapate kuliteka jiji. 19 Nao wakaendelea kusema vibaya+ juu ya Mungu wa Yerusalemu+ kama vile walivyofanya juu ya miungu ya vikundi vya watu wa dunia, iliyo kazi ya mikono ya mwanadamu.+ 20 Lakini Hezekia+ mfalme na Isaya+ mwana wa Amozi,+ nabii,+ wakaendelea kusali kuhusu jambo hilo+ na kuendelea kuzililia mbingu ili kupata msaada.+
21 Na Yehova akamtuma malaika+ na kumfutilia mbali kila shujaa, mwanamume mwenye nguvu,+ na kiongozi na mkuu katika kambi ya mfalme wa Ashuru,+ hivi kwamba akarudi katika nchi yake akiwa na haya usoni. Baadaye akaingia katika nyumba ya mungu wake na humo watu fulani waliotoka katika viuno vyake mwenyewe wakamwangusha kwa upanga.+ 22 Kwa hiyo Yehova akamwokoa Hezekia na wakaaji wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru+ na kutoka mkononi mwa wengine wote na kuwapa pumziko kuzunguka pande zote.+ 23 Na kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakileta zawadi+ kwa Yehova katika Yerusalemu na vitu bora kwa Hezekia mfalme wa Yuda,+ naye akaja kuinuliwa+ machoni pa mataifa yote baada ya hayo.
24 Katika siku hizo Hezekia akawa mgonjwa kufikia hatua ya kufa,+ naye akaanza kusali+ kwa Yehova. Basi Yeye akasema naye,+ na Yeye akampa ishara.+ 25 Lakini Hezekia hakurudisha kulingana na mema aliyotendewa,+ kwa kuwa moyo wake ulikuwa wenye majivuno+ na kukawa na ghadhabu+ juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu. 26 Hata hivyo, Hezekia akajinyenyekeza+ kwa sababu ya majivuno ya moyo wake, yeye pamoja na wakaaji wa Yerusalemu, na ghadhabu ya Yehova haikuja juu yao katika siku za Hezekia.+
27 Na Hezekia akawa na utajiri na utukufu kwa wingi sana;+ akajijengea maghala kwa ajili ya fedha na kwa ajili ya dhahabu+ na kwa ajili ya mawe ya thamani+ na kwa ajili ya mafuta ya zeri+ na kwa ajili ya ngao+ na kwa ajili ya vyombo vyote vyenye kutamanika;+ 28 na pia maghala+ kwa ajili ya mazao ya nafaka na divai mpya+ na mafuta, na pia vibanda+ kwa ajili ya wanyama wote wa aina mbalimbali na vibanda kwa ajili ya makundi ya wanyama. 29 Naye akajipatia majiji, na pia wanyama wa kundi+ na wa mifugo+ kwa wingi; kwa maana Mungu alimpa mali nyingi sana.+ 30 Na Hezekia ndiye aliyeziba+ chemchemi ya juu ya maji+ ya Gihoni+ na kuyaelekeza moja kwa moja chini upande wa magharibi mpaka Jiji la Daudi,+ na Hezekia akaendelea kufanikiwa katika kila moja ya kazi zake.+ 31 Na hivyo ikawa kupitia wasemaji wa wakuu wa Babiloni+ waliotumwa kwake+ ili kuuliza habari za ile ishara+ iliyotendeka katika nchi, Mungu wa kweli akamwacha+ ili kumjaribu,+ apate kujua kila jambo lililokuwa moyoni mwake.+
32 Na yale mambo mengine+ ya Hezekia na matendo yake ya fadhili zenye upendo,+ tazama, yameandikwa katika maono ya Isaya nabii, mwana wa Amozi,+ katika Kitabu+ cha Wafalme wa Yuda na Israeli. 33 Mwishowe Hezekia akalala pamoja na mababu zake,+ nao wakamzika katika mpando wa kwenda kwenye makaburi ya wana wa Daudi;+ na Yuda wote na wakaaji wa Yerusalemu wakampa heshima wakati wa kifo chake.+ Na Manase+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
33 Manase+ alikuwa na umri wa miaka 12 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 55 katika Yerusalemu.+
2 Naye akafanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ kulingana na machukizo+ ya mataifa ambayo Yehova alikuwa amefukuza kutoka mbele ya wana wa Israeli.+ 3 Kwa hiyo akajenga tena mahali pa juu+ ambapo Hezekia baba yake alikuwa amebomoa,+ akasimamisha madhabahu+ kwa Mabaali+ na kutengeneza miti mitakatifu,+ naye akaanza kuliinamia+ jeshi lote la mbinguni+ na kulitumikia.+ 4 Naye akajenga madhabahu+ katika nyumba ya Yehova, ambayo Yehova alikuwa amesema hivi kuihusu: “Jina langu litakuwa katika Yerusalemu mpaka wakati usio na kipimo.”+ 5 Naye akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni+ katika nyua mbili+ za nyumba ya Yehova.+ 6 Naye mwenyewe akawapitisha wanawe mwenyewe motoni+ katika bonde la mwana wa Hinomu,+ akafanya uchawi+ na kutumia uaguzi+ na kufanya ulozi+ na kufanyiza wenye kuwasiliana na pepo+ na wajuzi wa kubashiri+ matukio. Alifanya kwa kiasi kikubwa yale yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, na kumtia uchungu.+
7 Zaidi ya hayo, akaweka sanamu ya kuchongwa+ aliyokuwa ametengeneza katika nyumba ya Mungu wa kweli,+ ambayo Mungu alikuwa amemwambia Daudi na Sulemani mwana wake hivi kuihusu: “Katika nyumba hii na katika Yerusalemu, ambalo nimelichagua+ kutoka katika makabila yote ya Israeli, nitaliweka jina langu+ mpaka wakati usio na kipimo.+ 8 Nami sitauondoa mguu wa Israeli tena utoke katika nchi niliyowagawia+ mababu zao,+ mradi tu wawe waangalifu kufanya yote ambayo nimewaamuru+ kuhusiana na sheria+ yote na masharti+ na maamuzi ya hukumu+ kupitia mkono wa Musa.”+ 9 Na Manase+ akaendelea kuwashawishi Yuda+ na wakaaji wa Yerusalemu wafanye mabaya zaidi+ kuliko yale mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyaangamiza kutoka mbele ya wana wa Israeli.+
10 Na Yehova akaendelea kusema na Manase na watu wake, lakini hawakusikiliza.+ 11 Mwishowe Yehova akaleta juu yao+ wakuu wa jeshi la mfalme wa Ashuru,+ nao wakamteka Manase katika mashimo+ na kumfunga+ kwa pingu mbili za shaba, wakampeleka Babiloni. 12 Na mara tu jambo hilo lilipomtaabisha,+ akautuliza uso wa Yehova Mungu wake,+ akaendelea kujinyenyekeza+ sana kwa sababu ya Mungu wa mababu zake. 13 Naye akaendelea kusali kwake Yeye, hivi kwamba Yeye akakubali kusihiwa+ naye kisha Yeye akasikia ombi lake la kutaka kibali, akamrudisha Yerusalemu kwenye ufalme wake;+ na Manase akapata kujua kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli.+
14 Na baada ya hayo akajenga ukuta wa nje+ kwa ajili ya Jiji la Daudi+ upande wa magharibi wa Gihoni+ katika bonde la mto na mpaka Lango la Samaki,+ akauzungusha mpaka Ofeli+ na kuufanya kuwa mrefu sana. Tena akaweka wakuu wa jeshi katika majiji yote yenye ngome katika Yuda.+ 15 Naye akaiondoa miungu ya kigeni+ na ule mfano wa sanamu+ kutoka katika nyumba ya Yehova na madhabahu+ zote alizokuwa amejenga katika mlima wa nyumba ya Yehova na katika Yerusalemu, kisha akavitupa nje ya jiji. 16 Tena akatayarisha madhabahu ya Yehova+ na kuanza kutoa juu yake dhabihu za ushirika+ na dhabihu za shukrani,+ akaendelea kuwaambia Yuda wamtumikie Yehova Mungu wa Israeli.+ 17 Hata hivyo, watu walikuwa bado wanatoa dhabihu katika mahali pa juu;+ ila tu ilikuwa ni kwa Yehova Mungu wao.
18 Na yale mambo mengine ya Manase na sala+ yake kwa Mungu wake na maneno ya waonaji+ walioendelea kusema naye katika jina la Yehova Mungu wa Israeli, tazama, yamo kati ya mambo ya wafalme wa Israeli.+ 19 Na kuhusu sala+ yake na jinsi ombi+ lake lilivyojibiwa na dhambi+ yake yote na ukosefu wake wa uaminifu+ na vile vituo, mahali ambapo alijenga mahali pa juu+ na kusimamisha miti mitakatifu+ na sanamu za kuchongwa+ kabla ya kujinyenyekeza,+ tazama, yameandikwa kati ya maneno ya waonaji wake. 20 Mwishowe Manase akalala pamoja na mababu zake,+ nao wakamzika+ katika nyumba yake; na Amoni+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
21 Amoni+ alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka miwili katika Yerusalemu.+ 22 Naye akafanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ kama alivyofanya Manase baba yake;+ na Amoni akatoa dhabihu+ kwa sanamu zote za kuchongwa+ ambazo Manase+ baba yake alikuwa ametengeneza, naye akaendelea kuzitumikia.+ 23 Naye hakujinyenyekeza+ kwa sababu ya Yehova kama Manase baba yake alivyojinyenyekeza,+ kwa maana Amoni ndiye aliyezidisha hatia.+ 24 Mwishowe watumishi wake wakampangia hila+ na kumuua ndani ya nyumba yake mwenyewe.+ 25 Lakini watu wa nchi wakawapiga na kuwaua+ wale wote waliompangia hila+ Mfalme Amoni,+ kisha watu+ wa nchi wakamfanya Yosia+ mwana wake kuwa mfalme mahali pake.
34 Yosia+ alikuwa na umri wa miaka 8+ alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 31 katika Yerusalemu.+ 2 Naye akafanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova+ na kutembea katika njia za Daudi babu yake;+ naye hakugeuka kando upande wa kuume wala wa kushoto.+
3 Na katika mwaka wa nane wa kutawala kwake, alipokuwa angali mvulana,+ akaanza kumtafuta+ Mungu wa Daudi babu yake; na katika mwaka wa kumi na mbili akaanza kutakasa+ Yuda na Yerusalemu kutokana na mahali pa juu+ na miti mitakatifu+ na sanamu za kuchongwa+ na sanamu za kuyeyushwa. 4 Tena wakabomoa mbele yake zile madhabahu+ za Mabaali;+ na vile vinara vya uvumba+ vilivyokuwa juu akavikata kutoka juu yazo; na ile miti mitakatifu+ na sanamu za kuchongwa+ na sanamu za kuyeyushwa akazivunja vipande-vipande na kuzifanya kuwa mavumbi,+ kisha akayanyunyiza juu ya uso wa makaburi ya wale waliokuwa wakizitolea dhabihu.+ 5 Na mifupa+ ya makuhani akaiteketeza juu ya madhabahu zao.+ Kwa hiyo akatakasa Yuda na Yerusalemu.
6 Pia, katika majiji ya Manase+ na Efraimu+ na Simeoni na mpaka Naftali, katika mahali pao palipoharibiwa kuzunguka pande zote, 7 hata alibomoa madhabahu+ na miti mitakatifu,+ na sanamu za kuchongwa+ akaziponda na kuzifanya kuwa mavumbi;+ na vinara vyote vya uvumba+ akavikata katika nchi yote ya Israeli, kisha akarudi Yerusalemu.
8 Na katika mwaka wa kumi na nane+ wa kutawala kwake, alipokuwa ameitakasa nchi na nyumba, akawatuma Shafani+ mwana wa Azalia na Maaseya mkuu wa jiji na Yoa mwana wa Yoahazi karani wakarekebisha+ nyumba ya Yehova Mungu wake. 9 Nao wakamjia Hilkia+ kuhani mkuu na kumpa pesa zilizokuwa zikiletwa katika nyumba ya Mungu, ambazo Walawi watunza-milango+ walikuwa wamekusanya kutoka mkononi mwa Manase+ na Efraimu+ na kutoka kwa wale wengine wa Israeli+ na kutoka kwa Yuda wote na Benyamini na wakaaji wa Yerusalemu. 10 Kisha wakazitia mkononi mwa wafanyakazi waliowekwa juu ya nyumba ya Yehova.+ Nao wafanyakazi waliokuwa wakitenda kazi katika nyumba ya Yehova wakazitumia kutengeneza na kuirekebisha nyumba. 11 Basi wakawapa mafundi na wajenzi+ ili wanunue mawe yaliyochongwa+ na mbao kwa ajili ya vibanio na kujenga kwa boriti zile nyumba ambazo wafalme+ wa Yuda walibomoa.
12 Na watu hao walikuwa wakifanya kazi ile kwa uaminifu;+ na juu yao wakawekwa Yahathi na Obadia, Walawi, kutoka kwa wana wa Merari,+ na Zekaria na Meshulamu, kutoka kwa wana wa Wakohathi,+ wawe waangalizi. Na Walawi, ambao kila mmoja wao alikuwa mjuzi wa vyombo vya nyimbo,+ 13 walikuwa juu ya wabeba-mizigo,+ na waangalizi+ wa wafanyakazi wote kwa ajili ya utumishi mbalimbali; na kutoka kwa Walawi+ kulikuwa na waandishi+ na maofisa na watunza-malango.+
14 Sasa walipokuwa wakitoa pesa+ zilizokuwa zinaletwa katika nyumba ya Yehova, Hilkia+ kuhani akakipata kile kitabu+ cha sheria ya Yehova+ kupitia mkono wa Musa.+ 15 Kwa hiyo Hilkia akamjibu na kumwambia Shafani+ mwandishi: “Nimepata kile kitabu chenyewe cha sheria katika nyumba ya Yehova.” Basi Hilkia akampa Shafani kile kitabu. 16 Kisha Shafani akampelekea mfalme kile kitabu, akaendelea kumjibu mfalme, akisema: “Yote ambayo yametiwa mkononi mwa watumishi wako wanayafanya. 17 Nao wanamimina pesa ambazo zimo ndani ya nyumba ya Yehova na kuzitia katika mkono wa watu waliowekwa na katika mkono wa wale wanaofanya kazi.”+ 18 Na Shafani mwandishi akaendelea kumletea mfalme habari, akisema: “Hilkia kuhani amenipa+ kitabu+ fulani.” Na Shafani akaanza kukisoma mbele ya mfalme.+
19 Na ikawa kwamba mara tu mfalme alipoyasikia maneno ya ile sheria, akayararua mavazi yake mara moja.+ 20 Kisha mfalme akawaamuru Hilkia+ na Ahikamu+ mwana wa Shafani na Abdoni mwana wa Mika na Shafani+ mwandishi+ na Asaya+ mtumishi wa mfalme, akisema: 21 “Nendeni, muulizeni+ Yehova kwa ajili yangu+ na kwa ajili ya mabaki katika Israeli na katika Yuda kuhusu maneno ya kile kitabu+ ambacho kimepatikana, kwa maana ghadhabu ya Yehova ambayo itamwagwa juu yetu ni kubwa+ kwa sababu mababu zetu hawakulishika neno la Yehova kwa kutenda kulingana na yote ambayo yameandikwa katika kitabu hiki.”+
22 Basi Hilkia pamoja na wale ambao mfalme alikuwa amesema wakaenda kwa Hulda+ nabii,+ mke wa Shalumu mwana wa Tikva mwana wa Harhasi mtunzaji wa mavazi,+ kwa kuwa alikuwa akikaa Yerusalemu katika eneo la pili; nao wakaanza kusema naye hivyo. 23 Naye akawaambia:
“Yehova Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Mwambieni hivi mtu ambaye amewatuma ninyi kwangu: 24 “Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta msiba+ juu ya mahali hapa na wakaaji wake,+ laana+ zote ambazo zimeandikwa katika kile kitabu walichosoma mbele ya mfalme wa Yuda,+ 25 kwa sababu wameniacha+ na kwenda kuifukizia moshi wa dhabihu miungu mingine,+ ili kunitia uchungu+ kwa matendo yote ya mikono yao,+ na ili ghadhabu+ yangu imwagike juu ya mahali hapa wala isizimwe.’”+ 26 Na mfalme wa Yuda, anayewatuma mkamuulize Yehova, mwambieni hivi: “Yehova Mungu wa Israeli, amesema hivi,+ ‘Kuhusu yale maneno+ ambayo umeyasikia, 27 kwa sababu moyo+ wako ulikuwa mwororo hivi kwamba ukajinyenyekeza+ kwa sababu ya Mungu uliposikia maneno yake kuhusu mahali hapa na wakaaji wake, nawe ukajinyenyekeza mbele zangu,+ ukayararua+ mavazi yako na kulia mbele zangu, mimi, naam, mimi nimesikia,+ asema Yehova. 28 Tazama, nitakukusanya wewe kwa mababu zako, nawe hakika utakusanywa kwenye uwanja wa kaburi lako kwa amani,+ na macho yako hayatauona msiba+ wote ninaouleta juu ya mahali hapa na wakaaji wake.’”’”+
Ndipo wakamletea mfalme jibu. 29 Na mfalme akatuma na kukusanya wanaume wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu.+ 30 Sasa mfalme akapanda kwenda katika nyumba ya Yehova+ akiwa na wanaume wote wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu na makuhani+ na Walawi na watu wote, wakubwa kwa wadogo; naye akaanza kusoma+ masikioni mwao maneno yote ya kile kitabu cha agano, kilichokuwa kimepatikana katika nyumba ya Yehova.+ 31 Na mfalme akaendelea kusimama mahali pake+ naye akafanya agano+ mbele za Yehova ili kumfuata Yehova na kushika amri+ zake na shuhuda+ zake na masharti+ yake kwa moyo wake wote+ na kwa nafsi yake yote,+ ili kutenda+ yale maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki.+ 32 Na zaidi ya hayo, akawafanya wale wote waliopatikana katika Yerusalemu na Benyamini wachukue msimamo wao katika hilo. Na wakaaji wa Yerusalemu wakafanya kulingana na agano la Mungu, Mungu wa mababu zao.+ 33 Kisha Yosia akaondoa machukizo+ yote kutoka katika nchi zote za wana wa Israeli,+ naye akawafanya wote waliopatikana katika Israeli wachukue utumishi, wamtumikie Yehova Mungu wao. Siku zake zote hawakugeuka kando wasimfuate Yehova Mungu wa mababu zao.+
35 Ndipo Yosia+ akamfanyia Yehova pasaka+ katika Yerusalemu nao wakachinja mnyama wa pasaka+ katika siku ya kumi na nne+ ya mwezi wa kwanza.+ 2 Kwa hiyo akawaweka makuhani juu ya vitu vilivyo chini ya utunzaji+ wao na kuwatia moyo+ waendelee na utumishi wa nyumba ya Yehova.+ 3 Naye akawaambia Walawi, wafundishaji+ wa Israeli yote, wale walio watakatifu kwa Yehova: “Wekeni Sanduku takatifu+ ndani ya nyumba+ aliyojenga Sulemani mwana wa Daudi mfalme wa Israeli; lisiendelee kuwa mzigo juu ya mabega yenu.+ Sasa mtumikieni+ Yehova Mungu wenu, na Israeli watu wake. 4 Na mfanye matayarisho kulingana na nyumba ya mababu+ zenu kufuatana na migawanyo+ yenu, kulingana na maandishi+ ya Daudi mfalme wa Israeli na kulingana na maandishi+ ya Sulemani mwana wake. 5 Na msimame+ mahali patakatifu kulingana na vikundi vya nyumba ya mababu kwa ajili ya ndugu zenu, wana wa watu, na fungu la nyumba ya ukoo wa upande wa baba+ ya Walawi.+ 6 Na mchinje mnyama wa pasaka+ na mjitakase+ na kufanya matayarisho kwa ajili ya ndugu zenu ili kufanya kulingana na neno la Yehova kupitia Musa.”+
7 Sasa Yosia akawachangia wana wa watu makundi, wana-kondoo dume na wana-mbuzi dume, hao wote kuwa wanyama wa pasaka kwa ajili ya wote waliokuwapo, hesabu yao 30,000, na ng’ombe, 3,000.+ Hao walitoka katika mali za mfalme.+ 8 Na wakuu+ wake wakatoa mchango uwe toleo la hiari kwa ajili ya watu,+ kwa ajili ya makuhani na kwa ajili ya Walawi. Hilkia+ na Zekaria na Yehieli wakiwa viongozi wa nyumba ya Mungu wa kweli wakawapa makuhani kwa ajili ya wanyama wa pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi elfu mbili na mia sita, na ng’ombe mia tatu. 9 Na Konania na Shemaya na Nethaneli ndugu zake na Hashabia na Yeieli na Yozabadi, wakuu wa Walawi, wakachangia Walawi kwa ajili ya wanyama wa pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi elfu tano, na ng’ombe mia tano.
10 Na utumishi ukatayarishwa+ na makuhani wakaendelea kusimama+ mahali pao,+ na Walawi kwa migawanyo yao,+ kulingana na amri ya mfalme.+ 11 Nao wakachinja mnyama wa pasaka+ na makuhani+ wakanyunyiza+ damu kutoka mkononi mwao, huku Walawi wakiwachuna ngozi.+ 12 Tena wakatayarisha matoleo ya kuteketezwa ili kuvipa vikundi+ kulingana na nyumba ya ukoo wa upande wa baba,+ kwa wana wa watu, ili kumtolea Yehova toleo+ kulingana na yaliyoandikwa katika kitabu cha Musa;+ na pia wale ng’ombe wakawafanya hivyo. 13 Nao wakapika+ toleo la pasaka+ juu ya moto kulingana na desturi; na vile vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu wakavipika+ katika vyungu vya kupikia na katika vyungu vyenye makalio ya mviringo na katika mabakuli ya karamu, kisha wakalileta haraka kwa wana wote wa watu.+ 14 Na baadaye wakafanya matayarisho kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani,+ kwa sababu makuhani wana wa Haruni walikuwa wakitoa dhabihu za kuteketezwa+ na vipande vyenye mafuta+ mpaka usiku, Walawi nao wakafanya matayarisho+ kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, wana wa Haruni.
15 Na waimbaji+ wana wa Asafu+ walikuwa katika cheo chao kulingana na amri ya Daudi+ na ya Asafu+ na ya Hemani+ na ya Yeduthuni,+ mwonaji+ wa mfalme; na watunza-malango+ walikuwa katika malango mbalimbali.+ Hawakuhitaji kuacha utumishi wao, kwa sababu ndugu zao Walawi walikuwa wamewafanyia matayarisho.+ 16 Na utumishi wote wa Yehova ulitayarishwa siku hiyo ili kuifanya pasaka+ na kutoa matoleo ya kuteketezwa juu ya madhabahu ya Yehova, kulingana na amri ya Mfalme Yosia.+
17 Na wana wa Israeli waliopatikana wakaifanya pasaka+ wakati huo na pia sherehe ya keki zisizo na chachu kwa siku saba.+ 18 Na pasaka kama hiyo haikuwa imefanywa kamwe katika Israeli tangu siku za nabii Samweli,+ wala wafalme+ wengine wa Israeli hawakuwa wamefanya pasaka kama ile ambayo ilifanywa na Yosia na makuhani na Walawi na Yuda wote na Israeli waliopatikana na wakaaji wa Yerusalemu. 19 Pasaka hii ilifanywa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yosia.+
20 Baada ya hayo yote Yosia alipokuwa ameitayarisha nyumba, Neko+ mfalme wa Misri+ akapanda kuja kupigana kule Karkemishi+ kando ya Efrati. Ndipo Yosia+ akatoka kwenda kupambana naye.+ 21 Kwa hiyo akamtumia wajumbe, na kusema: “Nina nini na wewe, Ee mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekuja kupigana nawe leo, lakini vita vyangu ni juu ya nyumba nyingine ambayo Mungu mwenyewe ameniambia niivuruge. Jiepushe kwa faida yako mwenyewe kwa sababu ya Mungu, ambaye yuko pamoja nami, wala usiache yeye akuangamize.”+ 22 Na Yosia hakugeuza uso wake kutoka kwake,+ lakini akajibadili sura+ ili kupigana naye wala hakuyasikiliza maneno ya Neko+ kutoka kinywani mwa Mungu. Basi akaja kupigana katika nchi tambarare ya bondeni ya Megido.+
23 Na wapiga-mishale+ wakampiga Mfalme Yosia, hivi kwamba mfalme akawaambia watumishi wake: “Nishusheni, kwa sababu nimeumizwa vibaya sana.”+ 24 Kwa hiyo watumishi wake wakamshusha kutoka katika gari lile, wakampandisha katika gari lake la pili la vita na kumpeleka Yerusalemu.+ Hivyo akafa+ na kuzikwa katika uwanja wa makaburi ya mababu zake;+ na Yuda wote na Yerusalemu walikuwa wakimwombolezea+ Yosia. 25 Na Yeremia+ akaanza kumwimbia Yosia wimbo wa maombolezo;+ na waimbaji wote wanaume na waimbaji wanawake+ huendelea kusema juu ya Yosia katika nyimbo zao za huzuni mpaka leo hii; nao wameziweka kuwa sharti juu ya Israeli, nazo tazama, zimeandikwa kati ya nyimbo za maombolezo.+
26 Na yale mambo mengine+ ya Yosia na matendo yake ya fadhili zenye upendo,+ kulingana na yale ambayo yameandikwa katika sheria+ ya Yehova, 27 na mambo yake, ya kwanza na ya mwisho,+ tazama, yameandikwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Israeli na Yuda.
36 Kisha watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi+ mwana wa Yosia na kumfanya kuwa mfalme mahali pa baba yake katika Yerusalemu.+ 2 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka 23 alipoanza kutawala, naye akatawala miezi mitatu katika Yerusalemu.+ 3 Hata hivyo, mfalme wa Misri akamwondoa Yerusalemu+ na kuitoza nchi talanta mia moja za fedha+ na talanta moja ya dhahabu. 4 Zaidi ya hayo, mfalme+ wa Misri akamfanya Eliakimu+ ndugu yake kuwa mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu na kulibadili jina lake kuwa Yehoyakimu; lakini Neko+ akamchukua Yehoahazi ndugu yake na kumpeleka Misri.+
5 Yehoyakimu+ alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 11 katika Yerusalemu;+ naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova Mungu wake.+ 6 Nebukadneza+ mfalme wa Babiloni akapanda+ kuja kumshambulia ili amfunge kwa pingu mbili za shaba apate kumchukua mpaka Babiloni.+ 7 Na sehemu ya vyombo+ vya nyumba ya Yehova, Nebukadneza+ akavipeleka Babiloni kisha akaviweka katika jumba lake la kifalme kule Babiloni.+ 8 Na yale mambo mengine+ ya Yehoyakimu na machukizo+ yake aliyoyatenda na mambo yaliyopatikana juu yake, tazama, yameandikwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Israeli na Yuda; na Yehoyakini+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
9 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala miezi mitatu+ na siku kumi katika Yerusalemu; naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+ 10 Na mwanzoni+ mwa mwaka Mfalme Nebukadneza akatuma watu,+ akamleta Babiloni+ pamoja na vyombo vyenye kutamanika vya nyumba ya Yehova.+ Tena akamfanya Sedekia+ ndugu ya baba yake kuwa mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu.+
11 Sedekia+ alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 11 katika Yerusalemu.+ 12 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya+ machoni pa Yehova Mungu wake. Hakujinyenyekeza+ kwa ajili ya nabii+ Yeremia+ kwa agizo la Yehova. 13 Naye akamwasi hata Mfalme Nebukadneza,+ aliyekuwa amemwapisha kwa Mungu;+ naye akaendelea kuifanya shingo yake kuwa ngumu+ na kuufanya moyo wake kuwa mgumu+ ili asirudi kwa Yehova Mungu wa Israeli. 14 Hata wakuu wote wa makuhani+ na watu wenyewe wakatenda kwa ukosefu wa uaminifu kwa kiasi kikubwa, kulingana na machukizo+ yote ya mataifa, hivi kwamba wakaitia unajisi nyumba ya Yehova aliyokuwa ameitakasa katika Yerusalemu.+
15 Na Yehova Mungu wa mababu zao akaendelea kutuma juu yao kupitia kwa wajumbe wake,+ akatuma tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake+ na makao yake.+ 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki+ wale wajumbe wa Mungu wa kweli na kuyadharau maneno+ yake na kuwafanyia mzaha+ manabii wake, mpaka ghadhabu+ ya Yehova ikapanda juu ya watu wake, mpaka kukawa hakuna kuponywa.+
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo,+ ambaye aliwaua vijana wao kwa upanga+ katika nyumba ya patakatifu pao,+ wala hakumhurumia kijana wala bikira, mzee wala mkongwe.+ Kila kitu Yeye alikitia mkononi mwake. 18 Na vyombo+ vyote, vikubwa+ kwa vidogo, vya nyumba ya Mungu wa kweli na hazina za nyumba ya Yehova na hazina+ za mfalme+ na za wakuu wake, kila kitu akakipeleka Babiloni. 19 Naye akaiteketeza nyumba ya Mungu wa kweli+ na kuubomoa ukuta+ wa Yerusalemu; na minara yake yote ya makao wakaiteketeza kwa moto na pia vyombo vyake vyote vyenye kutamanika,+ ili kufanya uharibifu.+ 20 Tena akawachukua mateka mpaka Babiloni wale waliobaki kutokana na upanga,+ nao wakawa watumishi wake+ na wa wanawe mpaka mamlaka ya kifalme ya Uajemi+ ilipoanza kutawala; 21 ili kulitimiza neno la Yehova kupitia kinywa cha Yeremia,+ mpaka nchi ilipokuwa imelipa sabato zake.+ Siku zote za kukaa ukiwa ilishika sabato, ili kutimiza miaka 70.+
22 Na katika mwaka wa kwanza wa Koreshi+ mfalme wa Uajemi,+ ili neno la Yehova+ kupitia kinywa cha Yeremia+ litimizwe, Yehova aliiamsha roho+ ya Koreshi mfalme wa Uajemi, hivi kwamba akatangaza mwito katika ufalme wake wote, na pia kwa maandishi,+ akisema: 23 “Koreshi mfalme wa Uajemi+ amesema hivi, ‘Yehova Mungu wa mbinguni amenipa falme zote za dunia,+ naye mwenyewe amenipa utume nimjengee nyumba katika Yerusalemu, huko Yuda.+ Yeyote aliye katikati yenu ninyi watu wake wote,+ Yehova Mungu wake na awe pamoja naye.+ Basi apande na kwenda.’”+