Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
5 Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri na Magogu+ na Madai+ na Yavani+ na Tubali na Mesheki+ na Tirasi.+
6 Na wana wa Gomeri walikuwa Ashkenazi+ na Rifathi+ na Togarma.+
7 Na wana wa Yavani walikuwa Elisha+ na Tarshishi,+ Kitimu+ na Rodanimu.+
8 Wana wa Hamu walikuwa Kushi+ na Misraimu,+ Putu+ na Kanaani.+
9 Na wana wa Kushi walikuwa Seba+ na Havila na Sabta+ na Raama+ na Sabteka.+
Na wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.+
10 Na Kushi akamzaa Nimrodi.+ Ni yeye wa kwanza kuwa mwanamume mwenye nguvu duniani.+
11 Misraimu naye akamzaa Ludimu+ na Anamimu na Lehabimu na Naftuhimu+ 12 na Pathrusimu+ na Kasluhimu+ (ambao Wafilisti+ walitokana nao) na Kaftorimu.+
13 Kanaani naye akamzaa Sidoni+ mzaliwa wake wa kwanza na Hethi+ 14 na Myebusi+ na Mwamori+ na Mgirgashi+ 15 na Mhivi+ na Mwarkia na Msini+ 16 na Mwarvadi+ na Msemari+ na Mhamathi.+
17 Wana wa Shemu+ walikuwa Elamu+ na Asihuru+ na Arpakshadi+ na Ludi+ na Aramu,
Na Usi na Huli na Getheri na Mashi.+
18 Arpakshadi naye akamzaa Shela,+ na Shela akamzaa Eberi.+
19 Na Eberi alizaa wana wawili. Jina la mmoja lilikuwa ni Pelegi,+ kwa sababu katika siku zake dunia ilikuwa imegawanyika; na jina la ndugu yake lilikuwa ni Yoktani.
20 Yoktani naye akazaa Almodadi na Shelefu na Hazarmavethi na Yera+ 21 na Hadoramu na Uzali na Dikla+ 22 na Obali na Abimaeli na Sheba+ 23 na Ofiri+ na Havila+ na Yobabu;+ hao wote ndio waliokuwa wana wa Yoktani.
28 Wana wa Abrahamu walikuwa Isaka+ na Ishmaeli.+
29 Hizi ndizo asili za familia zao: Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli alikuwa Nebayothi+ na Kedari+ na Adbeeli na Mibsamu,+ 30 Mishma na Duma,+ Masa, Hadadi+ na Tema, 31 Yeturi, Nafishi na Kedema.+ Hao ndio waliokuwa wana wa Ishmaeli.
32 Nao wana wa Ketura,+ suria wa Abrahamu,+ aliwazaa Zimrani na Yokshani na Medani+ na Midiani+ na Ishbaki+ na Shua.+
Na wana wa Yokshani walikuwa Sheba na Dedani.+
33 Na wana wa Midiani walikuwa Efa+ na Eferi na Hanoki na Abida na Eldaa.+
Wote hao walikuwa wana wa Ketura.
34 Naye Abrahamu akamzaa Isaka.+ Wana wa Isaka walikuwa Esau+ na Israeli.+
35 Wana wa Esau walikuwa Elifazi, Reueli+ na Yeushi na Yalamu na Kora.+
36 Wana wa Elifazi walikuwa Temani+ na Omari, Sefo na Gatamu, Kenasi+ na Timna+ na Amaleki.+
37 Wana wa Reueli walikuwa Nahathi, Zera, Shamma na Miza.+
38 Na wana wa Seiri+ walikuwa Lotani na Shobali na Sibeoni na Ana+ na Dishoni na Ezeri na Dishani.+
39 Na wana wa Lotani walikuwa Hori na Homamu. Na dada ya Lotani alikuwa Timna.+
40 Wana wa Shobali walikuwa Alvani na Manahathi na Ebali, Shefo na Onamu.+
Na wana wa Sibeoni walikuwa Aya na Ana.+
41 Wana wa Ana walikuwa Dishoni.+
Na wana wa Dishoni walikuwa Hemdani na Eshbani na Ithrani na Kerani.+
42 Wana wa Ezeri+ walikuwa Bilhani na Zaavani na Akani.+
Wana wa Dishani walikuwa Usi na Arani.+
43 Na hawa ndio wafalme waliotawala katika nchi ya Edomu+ kabla ya mfalme+ yeyote kuwatawala wana wa Israeli: Bela mwana wa Beori, ambaye jina la jiji lake lilikuwa Dinhaba.+ 44 Mwishowe Bela akafa, na Yobabu mwana wa Zera+ kutoka Bosra+ akaanza kutawala mahali pake. 45 Mwishowe Yobabu akafa, na Hushamu+ kutoka katika nchi ya Watemani+ akaanza kutawala mahali pake. 46 Mwishowe Hushamu akafa, na Hadadi+ mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani+ katika uwanda wa Moabu, akaanza kutawala mahali pake. Na jina la jiji lake lilikuwa Avithi.+ 47 Mwishowe Hadadi akafa, na Samla kutoka Masreka+ akaanza kutawala mahali pake. 48 Mwishowe Samla akafa, na Shauli kutoka Rehobothi+ kando ya ule Mto akaanza kutawala mahali pake. 49 Mwishowe Shauli akafa, na Baal-hanani mwana wa Akbori+ akaanza kutawala mahali pake. 50 Mwishowe Baal-hanani akafa, na Hadadi akaanza kutawala mahali pake; na jina la jiji lake lilikuwa Pau, nalo jina la mke wake lilikuwa Mehetabeli, binti ya Matredi, binti ya Mezahabu.+ 51 Mwishowe Hadadi akafa.
Nao mashehe wa Edomu wakawa ni shehe Timna, shehe Alva, shehe Yethethi,+ 52 shehe Oholibama, shehe Ela, shehe Pinoni,+ 53 shehe Kenasi, shehe Temani, shehe Mibsari,+ 54 shehe Magdieli, shehe Iramu.+ Hao ndio waliokuwa mashehe+ wa Edomu.
2 Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli:+ Rubeni,+ Simeoni,+ Lawi+ na Yuda,+ Isakari+ na Zabuloni,+ 2 Dani,+ Yosefu+ na Benyamini,+ Naftali,+ Gadi+ na Asheri.+
3 Wana wa Yuda walikuwa Eri+ na Onani+ na Shela.+ Binti ya Shua, mwanamke Mkanaani, alimzalia wana hao watatu. Na Eri mzaliwa wa kwanza wa Yuda akawa mbaya machoni pa Yehova, hivi kwamba yeye akamuua.+ 4 Na Tamari+ binti-mkwe wake ndiye aliyemzalia Perezi+ na Zera. Wana wote wa Yuda walikuwa watano.
5 Wana wa Perezi walikuwa Hezroni na Hamuli.+
6 Na wana wa Zera+ walikuwa Zimri na Ethani na Hemani na Kalkoli na Dara.+ Jumla yao walikuwa watano.
7 Na wana wa Karmi+ walikuwa Akari aliyeleta taabu juu ya Israeli,+ ambaye alitenda tendo la kukosa uaminifu kwa habari ya kile kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuangamizwa.+
8 Na wana wa Ethani+ walikuwa Azaria.
9 Na wana wa Hezroni+ aliozaa walikuwa Yerahmeeli+ na Ramu+ na Kelubai.
10 Ramu naye akamzaa Aminadabu.+ Naye Aminadabu akamzaa Nashoni+ mkuu wa wana wa Yuda. 11 Naye Nashoni akamzaa Salma.+ Naye Salma akamzaa Boazi.+ 12 Naye Boazi akamzaa Obedi.+ Naye Obedi akamzaa Yese.+ 13 Naye Yese akamzaa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu,+ na Abinadabu+ wa pili, na Shimea+ wa tatu, 14 Nethaneli wa nne, Radai wa tano, 15 Ozemu wa sita, Daudi+ wa saba. 16 Na dada zao walikuwa Seruya na Abigaili;+ na wana wa Seruya walikuwa Abishai+ na Yoabu+ na Asaheli,+ watatu. 17 Abigaili naye alimzaa Amasa;+ na baba ya Amasa alikuwa Yetheri,+ Mwishmaeli.
18 Naye Kalebu mwana wa Hezroni,+ akazaa wana kupitia kwa Azuba mke wake na kupitia kwa Yeriothi; na hawa ndio waliokuwa wana wa mke wake: Yesheri na Shobabu na Ardoni. 19 Mwishowe Azuba akafa. Kwa hiyo Kalebu akamchukua Efrathi,+ ambaye baada ya muda alimzalia Huru.+ 20 Naye Huru akamzaa Uri.+ Naye Uri akamzaa Bezaleli.+
21 Na baadaye Hezroni akalala na binti ya Makiri+ baba ya Gileadi.+ Naye alikuwa na umri wa miaka 60 alipomchukua binti huyo, lakini akamzalia Segubu. 22 Naye Segubu akamzaa Yairi,+ aliyekuja kuwa na majiji 23+ katika nchi ya Gileadi. 23 Baadaye Geshuri+ na Siria+ wakachukua Hawoth-yairi+ kutoka kwao, na Kenathi+ na miji yake ya kandokando, majiji 60. Hao wote ndio waliokuwa wana wa Makiri baba ya Gileadi.
24 Na baada ya kifo cha Hezroni+ katika Kalebu-efratha, Abiya akiwa mke wa Hezroni, ndipo alipomzalia Ashuri baba ya Tekoa.+
25 Na wana wa Yerahmeeli+ mzaliwa wa kwanza wa Hezroni walikuwa Ramu+ mzaliwa wa kwanza na Buna na Oreni na Ozemu, Ahiya. 26 Na Yerahmeeli akaja kuwa na mke mwingine, ambaye jina lake lilikuwa Atara. Yeye ndiye alikuwa mama ya Onamu. 27 Na wana wa Ramu+ mzaliwa wa kwanza wa Yerahmeeli walikuwa Maazi na Yamini na Ekeri. 28 Na wana wa Onamu+ walikuja kuwa Shamai na Yada. Na wana wa Shamai walikuwa Nadabu na Abishuri. 29 Na jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, ambaye baada ya muda alimzalia Abani na Molidi. 30 Na wana wa Nadabu+ walikuwa Seledi na Apaimu. Lakini Seledi alikufa bila kuwa na wana. 31 Na wana wa Apaimu walikuwa Ishi. Na wana wa Ishi walikuwa Sheshani; na wana wa Sheshani,+ Alai. 32 Na wana wa Yada ndugu ya Shamai walikuwa Yetheri na Yonathani. Lakini Yetheri alikufa bila kuwa na wana. 33 Na wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hao wakawa wana wa Yerahmeeli.
34 Na Sheshani+ hakuwa na wana wowote, ila mabinti. Sasa Sheshani alikuwa na mtumishi Mmisri+ ambaye jina lake lilikuwa Yarha. 35 Basi Sheshani akampa Yarha mtumishi wake binti yake awe mke wake, ambaye baada ya muda alimzalia Atai. 36 Naye Atai akamzaa Nathani. Naye Nathani akamzaa Zabadi.+ 37 Naye Zabadi akamzaa Eflali. Naye Eflali akamzaa Obedi. 38 Naye Obedi akamzaa Yehu. Naye Yehu akamzaa Azaria. 39 Naye Azaria akamzaa Helezi. Naye Helezi akamzaa Eleasa. 40 Naye Eleasa akamzaa Sismai. Naye Sismai akamzaa Shalumu. 41 Naye Shalumu akamzaa Yekamia. Naye Yekamia akamzaa Elishama.
42 Na wana wa Kalebu+ ndugu ya Yerahmeeli walikuwa Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa baba ya Zifu, na wana wa Maresha baba ya Hebroni. 43 Na wana wa Hebroni walikuwa Kora na Tapua na Rekemu na Shema. 44 Naye Shema akamzaa Rahamu baba ya Yorkeamu. Naye Rekemu akamzaa Shamai. 45 Na mwana wa Shamai alikuwa Maoni; na Maoni alikuwa baba ya Beth-suri.+ 46 Na Efa suria wa Kalebu, yeye alimzaa Harani na Mosa na Gazezi. Harani naye akamzaa Gazezi. 47 Na wana wa Yahdai walikuwa Regemu na Yothamu na Geshani na Peleti na Efa na Shaafu. 48 Na Maaka, suria wa Kalebu, yeye alizaa Sheberi na Tirhana. 49 Baada ya muda akamzaa Shaafu baba ya Madmana,+ Sheva baba ya Makbena na baba ya Gibea.+ Na binti ya Kalebu+ alikuwa Aksa.+ 50 Hao wakawa wana wa Kalebu.
Wana wa Huru+ mzaliwa wa kwanza wa Efratha:+ Shobali+ baba ya Kiriath-yearimu,+ 51 Salma baba ya Bethlehemu,+ Harefu baba ya Beth-gaderi. 52 Na Shobali+ baba ya Kiriath-yearimu akaja kuwa na wana: Haroe, nusu ya Menuhothi. 53 Na familia za Kiriath-yearimu zilikuwa Waithri+ na Waputhu na Washumathi na Wamishra. Wasorathi+ na Waeshtaoli+ walitoka kwa hao. 54 Wana wa Salma walikuwa Bethlehemu+ na Wanetofa,+ Atroth-beth-yoabu na nusu ya Wamanahathi, Wazori. 55 Na familia za waandishi waliokaa katika Yabesi+ zilikuwa Watirathi, Washimea, Wasukathi. Hao walikuwa Wakeni+ waliotokana na Hamathi baba ya nyumba ya Rekabu.+
3 Na hawa wakawa wana wa Daudi+ aliowazaa akiwa kule Hebroni:+ Amnoni+ mzaliwa wa kwanza, wa Ahinoamu+ mwanamke Myezreeli,+ Danieli wa pili, wa Abigaili+ mwanamke Mkarmeli,+ 2 Absalomu+ wa tatu, mwana wa Maaka+ binti ya Talmai+ mfalme wa Geshuri,+ Adoniya+ wa nne, mwana wa Hagithi,+ 3 Shefatia wa tano, wa Abitali,+ Ithreamu wa sita, wa Egla+ mke wake. 4 Kulikuwa na wana sita aliowazaa akiwa Hebroni; naye akaendelea kutawala huko miaka saba na miezi sita, naye akatawala katika Yerusalemu miaka 33.+
5 Naye aliwazaa hawa katika Yerusalemu:+ Shimea+ na Shobabu+ na Nathani+ na Sulemani,+ wanne wa Bath-sheba+ binti ya Amieli,+ 6 na Ibhari+ na Elishama+ na Elifeleti,+ 7 na Noga na Nefegi na Yafia,+ 8 na Elishama+ na Eliada na Elifeleti,+ tisa, 9 wana wote wa Daudi mbali na wana wa masuria, na Tamari+ dada yao.
10 Na mwana wa Sulemani alikuwa Rehoboamu,+ Abiya+ mwana wake, Asa+ mwana wake, Yehoshafati+ mwana wake, 11 Yehoramu mwana wake,+ Ahazia+ mwana wake, Yehoashi+ mwana wake, 12 Amazia+ mwana wake, Azaria+ mwana wake, Yothamu+ mwana wake, 13 Ahazi+ mwana wake, Hezekia+ mwana wake, Manase+ mwana wake, 14 Amoni+ mwana wake, Yosia+ mwana wake. 15 Na wana wa Yosia walikuwa Yohanani mzaliwa wa kwanza, Yehoyakimu+ wa pili, Sedekia+ wa tatu, Shalumu wa nne. 16 Na wana wa Yehoyakimu walikuwa Yekonia+ mwana wake, Sedekia mwana wake. 17 Na wana wa Yekonia akiwa mfungwa walikuwa Shealtieli+ mwana wake 18 na Malkiramu na Pedaya na Shenazari, Yekamia, Hoshama na Nedabia. 19 Na wana wa Pedaya walikuwa Zerubabeli+ na Shimei; na wana wa Zerubabeli walikuwa Meshulamu na Hanania (na Shelomithi alikuwa dada yao); 20 na Hashuba na Oheli na Berekia na Hasadia, Yushab-hesedi, watano. 21 Na wana wa Hanania walikuwa Pelatia+ na Yeshaya, wana wa Yeshaya ni Refaya, wana wa Refaya ni Arnani, wana wa Arnani ni Obadia, wana wa Obadia ni Shekania; 22 na wana wa Shekania ni Shemaya, na wana wa Shemaya ni Hatushi na Igali na Baria na Nearia na Shafati, sita. 23 Na wana wa Nearia walikuwa Elioenai na Hizkia na Azrikamu, watatu. 24 Na wana wa Elioenai walikuwa Hodavia na Eliashibu na Pelaya na Akubu na Yohanani na Delaya na Anani, saba.
4 Wana wa Yuda walikuwa Perezi,+ Hezroni+ na Karmi+ na Huru+ na Shobali.+ 2 Naye Reaya+ mwana wa Shobali, yeye alikuwa ni baba ya Yahathi; naye Yahathi akamzaa Ahumai na Lahadi. Hizo ndizo zilizokuwa familia za Wasorathi.+ 3 Na hawa ndio waliokuwa wana wa baba ya Etamu:+ Yezreeli+ na Ishma na Idbashi, (na jina la dada yao lilikuwa Haselelponi,) 4 na Penueli baba ya Gedori+ na Ezeri baba ya Husha. Hao ndio waliokuwa wana wa Huru+ mzaliwa wa kwanza wa Efratha baba ya Bethlehemu.+ 5 Na Ashuri+ baba ya Tekoa+ alikuwa na wake wawili, Hela na Naara. 6 Baada ya muda Naara akamzalia Ahuzamu na Heferi na Temeni na Haahashtari. Hao ndio waliokuwa wana wa Naara. 7 Na wana wa Hela walikuwa Serethi, Ishari na Ethnani. 8 Kosi naye akazaa Anubu na Zobeba na familia za Aharheli mwana wa Harumi.
9 Naye Yabesi+ akaja kuheshimika+ kuliko ndugu zake; na mama yake ndiye aliyemwita jina Yabesi, akisema: “Nimemzaa kwa maumivu.”+ 10 Na Yabesi akaanza kumwita Mungu+ wa Israeli, akisema: “Hakika ukinibariki+ na kwa kweli upanue eneo langu+ na mkono+ wako uwe pamoja nami, nawe uniokoe kutoka katika msiba,+ ili huo usipate kunidhuru,+ —” Basi Mungu akatimiza yale ambayo yeye alikuwa ameomba.+
11 Naye Kelubu ndugu ya Shuha akamzaa Mehiri, aliyekuwa baba ya Eshtoni. 12 Naye Eshtoni akazaa Beth-rafa na Pasea na Tehina baba ya Ir-nahashi. Hao ndio waliokuwa wanaume wa Reka. 13 Na wana wa Kenasi+ walikuwa Othnieli+ na Seraya, na wana wa Othnieli, Hathathi. 14 Meonothai naye akamzaa Ofra. Seraya naye akamzaa Yoabu baba ya Ge-harashimu; kwa maana wao walikuwa mafundi.+
15 Na wana wa Kalebu+ mwana wa Yefune+ walikuwa Iru, Ela na Naamu; na wana wa Ela ni Kenasi. 16 Na wana wa Yehaleleli walikuwa Zifu na Zifa, Tiria na Asareli. 17 Na wana wa Ezra walikuwa Yetheri na Meredi na Eferi na Yaloni; naye akazaa Miriamu na Shamai na Ishba baba ya Eshtemoa.+ 18 Naye mke wake Myahudi, yeye alizaa Yeredi baba ya Gedori na Heberi baba ya Soko na Yekuthieli baba ya Zanoa. Na hao ndio waliokuwa wana wa Bithia binti ya Farao, ambaye Meredi alimchukua.
19 Na wana wa mke wa Hodia, dada ya Nahamu, walikuwa baba ya Keila+ Mgarmi, na Eshtemoa Mmaakathi. 20 Na wana wa Shimoni walikuwa Amnoni na Rina, Ben-hanani na Tiloni. Na wana wa Ishi walikuwa Zohethi na Ben-zohethi.
21 Wana wa Shela+ mwana wa Yuda walikuwa Eri baba ya Leka na Laada baba ya Maresha na familia za nyumba ya wafumaji wa vitambaa laini+ wa nyumba ya Ashbea; 22 na Yokimu na wanaume wa Kozeba na Yoashi na Sarafi, waliochukua wake Wamoabu,+ na Yashubi-lehemu. Na hayo maneno ni ya mapokeo ya kale.+ 23 Hao ndio waliokuwa wafinyanzi+ na wakaaji wa Netaimu na Gedera. Walikaa huko pamoja na mfalme katika kazi yake.+
24 Wana wa Simeoni walikuwa Nemueli+ na Yamini,+ Yaribu, Zera, Shauli,+ 25 Shalumu mwana wake, Mibsamu mwana wake, Mishma mwana wake. 26 Na wana wa Mishma walikuwa Hamueli mwana wake, Zakuri mwana wake, Shimei mwana wake. 27 Na Shimei alikuwa na wana kumi na sita na binti sita; lakini ndugu zake hawakuwa na wana wengi, wala hakuna yoyote ya familia zao iliyokuwa na wana wengi kama wana wa Yuda.+ 28 Nao wakaendelea kukaa katika Beer-sheba+ na Molada+ na Hasar-shuali+ 29 na katika Bilha+ na katika Esemu+ na katika Toladi+ 30 na katika Bethueli+ na katika Horma+ na katika Siklagi+ 31 na katika Beth-markabothi na katika Hasar-susimu+ na katika Beth-biri na katika Shaaraimu.+ Hayo yalikuwa ndiyo majiji yao mpaka Daudi alipotawala.
32 Na makao yao yalikuwa Etamu na Aini, Rimoni na Tokeni na Ashani,+ majiji matano. 33 Na makao yao yote yaliyozunguka majiji hayo yalikuwa mpaka Baali.+ Hayo ndiyo yaliyokuwa makao yao na maandikisho yao ya kiukoo kwa ajili yao. 34 Na Meshobabu na Yamleki na Yosha mwana wa Amazia, 35 na Yoeli na Yehu mwana wa Yoshibia mwana wa Seraya mwana wa Asieli, 36 na Elioenai na Yaakoba na Yeshohaya na Asaya na Adieli na Yesimieli na Benaya, 37 na Ziza mwana wa Shifi mwana wa Aloni mwana wa Yedaya mwana wa Shimri mwana wa Shemaya. 38 Hawa walioingia kwa majina ndio waliokuwa wakuu kati ya familia zao,+ na nyumba ya mababu zao ikaongezeka kwa wingi. 39 Nao wakaenda kwenye mwingilio wa Gedori, hata upande wa mashariki wa lile bonde, ili kutafutia makundi yao malisho. 40 Mwishowe wakapata malisho manono na mazuri,+ na nchi ilikuwa pana sana na haikuwa na usumbufu+ wowote ila starehe; kwa maana wale waliokaa huko nyakati za zamani walikuwa wa Hamu.+ 41 Na hawa walioandikwa kwa majina yao wakaingia katika siku za Hezekia+ mfalme wa Yuda, wakapiga+ mahema ya Wahamu na Meunimu waliokuwa huko, hivi kwamba wakawaangamiza+ mpaka leo hii; nao wakaanza kukaa mahali pao, kwa sababu kulikuwa na malisho+ kwa ajili ya makundi yao huko.
42 Na kutoka kwao kulikuwa na baadhi ya wana wa Simeoni walioenda katika Mlima Seiri,+ watu mia tano, pamoja na Pelatia na Nearia na Refaya na Uzieli wana wa Ishi wakiwa mbele yao. 43 Nao wakawapiga mabaki ya Amaleki+ waliokuwa wameponyoka, nao wakaendelea kukaa huko mpaka leo hii.
5 Na wana wa Rubeni+ mzaliwa wa kwanza wa Israeli—kwa maana yeye alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza;+ lakini kwa kuwa alikitia unajisi kitanda cha baba yake,+ haki yake akiwa mzaliwa wa kwanza ilipewa wana wa Yosefu+ mwana wa Israeli, hivi kwamba yeye hakuandikishwa kiukoo kwa ajili ya haki ya mzaliwa wa kwanza. 2 Kwa maana Yuda+ alikuwa mkuu kati ya ndugu zake, na kiongozi alitoka kwake;+ lakini haki ya mzaliwa wa kwanza ilikuwa ya Yosefu+ — 3 wana wa Rubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa Hanoki+ na Palu,+ Hezroni na Karmi.+ 4 Wana wa Yoeli walikuwa Shemaya mwana wake, Gogu mwana wake, Shimei mwana wake, 5 Mika mwana wake, Reaya mwana wake, Baali mwana wake, 6 Beera mwana wake, ambaye Tilgath-pilneseri+ mfalme wa Ashuru alimpeleka uhamishoni, yeye akiwa mkuu wa Warubeni. 7 Na ndugu zake kulingana na familia zao katika maandikisho ya kiukoo+ kulingana na wazao wao walikuwa, Yeieli akiwa kichwa, na Zekaria, 8 na Bela mwana wa Azazi mwana wa Shema mwana wa Yoeli+ —alikuwa akikaa katika Aroeri+ mpaka Nebo+ na Baal-meoni.+ 9 Hata upande wa mashariki alikaa mpaka mahali ambapo mtu huingilia nyikani kwenye mto Efrati,+ kwa kuwa mifugo yao ilikuwa imekuwa mingi sana katika nchi ya Gileadi.+ 10 Na katika siku za Sauli walipigana na Wahagri,+ walioanguka kwa mkono wao; basi wakakaa katika mahema yao katika nchi yote upande wa mashariki wa Gileadi.
11 Na wana wa Gadi+ mbele yao, walikaa katika nchi ya Bashani+ mpaka Saleka.+ 12 Yoeli alikuwa ndiye kichwa, Shafamu wa pili, na Yanai na Shafati katika Bashani. 13 Na ndugu zao wa nyumba ya mababu zao walikuwa Mikaeli na Meshulamu na Sheba na Yorai na Yakani na Zia na Eberi, saba. 14 Hawa ndio waliokuwa wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi; 15 Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, kichwa cha nyumba ya mababu zao. 16 Nao wakaendelea kukaa katika Gileadi,+ katika Bashani+ na miji yake ya kandokando+ na katika viwanja vyote vya malisho vya Sharoni mpaka miisho yake. 17 Wote walikuwa wameandikishwa kiukoo katika siku za Yothamu+ mfalme wa Yuda na katika siku za Yeroboamu+ mfalme wa Israeli.
18 Kwa habari ya wana wa Rubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase; kati ya wale waliokuwa watu mashujaa,+ wanaume wanaochukua ngao na upanga na kupinda upinde na kuzoezwa katika vita, kulikuwa na 44,760 wanaoingia jeshini.+ 19 Nao wakaanza kupigana na Wahagri,+ na Yeturi+ na Nafishi+ na Nodabu. 20 Nao wakaja kusaidiwa kupigana nao, hivi kwamba Wahagri na wale wote waliokuwa pamoja nao wakatiwa mkononi mwao, kwa maana walikuwa wameomba msaada+ kutoka kwa Mungu katika vita, naye akakubali kusihiwa awape kibali kwa sababu walimtegemea.+ 21 Nao wakateka mifugo yao,+ ngamia zao 50,000, na kondoo 250,000, na punda 2,000, na nafsi za binadamu 100,000.+ 22 Kwa maana kulikuwa na wengi ambao walianguka wakiwa wameuawa, kwa sababu pigano lilikuwa la Mungu wa kweli.+ Nao wakaendelea kukaa mahali pao mpaka wakati wa ule uhamisho.+
23 Kwa habari ya wana wa nusu ya kabila la Manase,+ walikaa katika nchi kutoka Bashani+ mpaka Baal-hermoni+ na Seniri+ na Mlima Hermoni.+ Nao wakawa wengi sana. 24 Na hawa ndio waliokuwa vichwa vya nyumba ya mababu zao: Eferi na Ishi na Elieli na Azrieli na Yeremia na Hodavia na Yahdieli, wanaume waliokuwa mashujaa, watu wenye nguvu, wanaume wenye sifa, vichwa vya nyumba ya mababu zao. 25 Nao wakaanza kutenda kwa ukosefu wa uaminifu kumwelekea Mungu wa mababu zao, wakawa wakifanya uasherati+ na miungu+ ya vikundi vya watu wa nchi hiyo, ambao Mungu alikuwa ameangamiza kutoka mbele yao. 26 Kwa hiyo Mungu wa Israeli akachochea roho+ ya Pulu+ mfalme wa Ashuru,+ roho ya Tilgath-pilneseri+ mfalme wa Ashuru, hivi kwamba akawapeleka uhamishoni+ Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase, akawaleta mpaka Hala+ na Habori na Hara na mto Gozani waendelee kuwako mpaka leo hii.
6 Wana wa Lawi+ walikuwa Gershoni,+ Kohathi+ na Merari.+ 2 Na wana wa Kohathi walikuwa Amramu,+ Ishari+ na Hebroni+ na Uzieli.+ 3 Na wana wa Amramu+ walikuwa Haruni+ na Musa,+ na Miriamu.+ Na wana wa Haruni walikuwa Nadabu+ na Abihu,+ Eleazari+ na Ithamari.+ 4 Eleazari+ naye akamzaa Finehasi.+ Finehasi akamzaa Abishua.+ 5 Naye Abishua akamzaa Buki; naye Buki akamzaa Uzi.+ 6 Naye Uzi akamzaa Zeraya; naye Zeraya akamzaa Merayothi.+ 7 Merayothi akamzaa Amaria; naye Amaria akamzaa Ahitubu.+ 8 Naye Ahitubu akamzaa Sadoki;+ naye Sadoki akamzaa Ahimaazi.+ 9 Naye Ahimaazi akamzaa Azaria. Naye Azaria akamzaa Yohanani. 10 Naye Yohanani akamzaa Azaria.+ Yeye ndiye aliyekuwa kuhani katika nyumba ambayo Sulemani alijenga katika Yerusalemu.
11 Na Azaria akamzaa Amaria.+ Naye Amaria akamzaa Ahitubu.+ 12 Naye Ahitubu akamzaa Sadoki.+ Naye Sadoki akamzaa Shalumu. 13 Naye Shalumu akamzaa Hilkia.+ Naye Hilkia akamzaa Azaria. 14 Naye Azaria akamzaa Seraya.+ Naye Seraya akamzaa Yehosadaki.+ 15 Naye Yehosadaki ndiye aliyeenda wakati Yehova alipopeleka Yuda na Yerusalemu uhamishoni kwa mkono wa Nebukadneza.
16 Wana wa Lawi+ walikuwa Gershomu, Kohathi na Merari. 17 Na haya ndiyo majina ya wana wa Gershomu: Libni+ na Shimei.+ 18 Na wana wa Kohathi+ walikuwa Amramu+ na Ishari na Hebroni na Uzieli.+ 19 Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi.+
Na hizi ndizo zilizokuwa familia za Walawi kulingana na mababu zao:+ 20 Ya Gershomu, Libni+ mwana wake, Yahathi mwana wake, Zima mwana wake, 21 Yoa+ mwana wake, Ido mwana wake, Zera mwana wake, Yeatherai mwana wake. 22 Wana wa Kohathi walikuwa Aminadabu mwana wake, Kora+ mwana wake, Asiri mwana wake, 23 Elkana mwana wake na Ebiasafu+ mwana wake na Asiri mwana wake; 24 Tahathi mwana wake, Urieli mwana wake, Uzia mwana wake, na Shauli mwana wake. 25 Na wana wa Elkana+ walikuwa Amasai na Ahimothi. 26 Kwa habari ya Elkana, wana wa Elkana walikuwa Zofai+ mwana wake na Nahathi mwana wake, 27 Eliabu+ mwana wake, Yerohamu mwana wake, Elkana+ mwana wake. 28 Na wana wa Samweli+ walikuwa Yoeli mzaliwa wa kwanza na wa pili Abiya.+ 29 Wana wa Merari walikuwa Mali,+ Libni mwana wake, Shimei mwana wake, Uza mwana wake, 30 Shimea mwana wake, Hagia mwana wake, Asaya mwana wake.
31 Na hawa ndio ambao Daudi+ aliwapa vyeo kwa ajili ya kuongoza uimbaji katika nyumba ya Yehova baada ya Sanduku kupata mahali pa kupumzika.+ 32 Nao wakawa wahudumu+ katika kuimba+ mbele ya maskani ya hema la mkutano mpaka Sulemani alipoijenga nyumba ya Yehova katika Yerusalemu;+ nao wakaendelea kufanya utumishi wao kulingana na utume wao.+ 33 Na hawa ndio waliohudumu na pia wana wao: Wa wana wa Wakohathi Hemani+ mwimbaji, mwana wa Yoeli,+ mwana wa Samweli,+ 34 mwana wa Elkana,+ mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli,+ mwana wa Toa, 35 mwana wa Sufu,+ mwana wa Elkana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai, 36 mwana wa Elkana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania, 37 mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu,+ mwana wa Kora,+ 38 mwana wa Ishari,+ mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli.
39 Kwa habari ya Asafu+ ndugu yake, aliyekuwa akihudumu upande wake wa kuume, Asafu alikuwa mwana wa Berekia,+ mwana wa Shimea, 40 mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya, 41 mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya, 42 mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei, 43 mwana wa Yahathi,+ mwana wa Gershomu,+ mwana wa Lawi.
44 Kwa habari ya wana wa Merari+ ndugu zao upande wa mkono wa kushoto, palikuwa na Ethani+ mwana wa Kishi,+ mwana wa Abdi, mwana wa Maluku, 45 mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia, 46 mwana wa Amzi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri, 47 mwana wa Mali, mwana wa Mushi,+ mwana wa Merari,+ mwana wa Lawi.
48 Na ndugu zao Walawi+ ndio waliokabidhiwa kwa ajili ya utumishi+ wote wa maskani ya nyumba ya Mungu wa kweli. 49 Na Haruni+ na wanawe walikuwa wakifukiza moshi wa dhabihu+ juu ya madhabahu ya toleo la kuteketezwa+ na juu ya madhabahu ya uvumba+ kwa ajili ya kazi yote ya vitu vitakatifu zaidi na kufanya upatanisho+ kwa ajili ya Israeli,+ kulingana na yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu wa kweli alikuwa ameamuru. 50 Na hawa ndio waliokuwa wana wa Haruni:+ Eleazari+ mwana wake, Finehasi+ mwana wake, Abishua+ mwana wake, 51 Buki mwana wake, Uzi mwana wake, Zeraya+ mwana wake, 52 Merayothi+ mwana wake, Amaria mwana wake, Ahitubu+ mwana wake, 53 Sadoki+ mwana wake, Ahimaazi+ mwana wake.
54 Na haya ndiyo yaliyokuwa makao yao kulingana na kambi zao zilizozungushiwa ukuta katika eneo lao,+ kwa ajili ya wana wa Haruni wa familia ya Wakohathi,+ kwa maana kura ilikuwa imekuwa yao. 55 Basi wakawapa Hebroni+ katika nchi ya Yuda, pamoja na viwanja vyake vya malisho kulizunguka pande zote. 56 Na shamba la jiji na makao+ yake wakampa Kalebu+ mwana wa Yefune.+ 57 Nao wakawapa wana wa Haruni majiji ya makimbilio,+ Hebroni,+ pamoja na Libna+ na viwanja vyake vya malisho na Yatiri+ na Eshtemoa+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, 58 na Hileni+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, Debiri+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, 59 na Ashani+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Beth-shemeshi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho; 60 na kutoka katika kabila la Benyamini, Geba+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Alemethi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Anathothi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho. Majiji yao yote yalikuwa majiji kumi na matatu+ kati ya familia zao.
61 Na kwa wana waliobaki wa Kohathi wakawapa kutoka katika familia ya hilo kabila, kutoka katika ile nusu ya kabila, nusu ya Manase, majiji kumi+ kwa kura.
62 Na kwa wana wa Gershomu+ kulingana na familia zao wakawapa kutoka katika kabila la Isakari+ na kutoka katika kabila la Asheri+ na kutoka katika kabila la Naftali+ na kutoka katika kabila la Manase+ katika Bashani, majiji kumi na matatu.
63 Nao wakawapa wana wa Merari+ kulingana na familia zao kutoka katika kabila la Rubeni+ na kutoka katika kabila la Gadi+ na kutoka katika kabila la Zabuloni+ kwa kura majiji kumi na mawili.
64 Hivyo wana wa Israeli wakawapa Walawi+ majiji hayo pamoja na viwanja vyake vya malisho.+ 65 Tena, kwa kura wakatoa kutoka katika kabila la wana wa Yuda+ na kutoka katika kabila la wana wa Simeoni+ na kutoka katika kabila la wana wa Benyamini+ majiji haya, ambayo waliyaita kulingana na majina.
66 Na baadhi ya familia za wana wa Kohathi zilikuwa na majiji ya eneo lao kutoka katika kabila la Efraimu.+ 67 Basi wakawapa majiji ya makimbilio, Shekemu+ pamoja na viwanja vyake vya malisho katika eneo lenye milima la Efraimu, na Gezeri+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, 68 na Yokmeamu+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Beth-horoni+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, 69 na Aiyaloni+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Gath-rimoni+ pamoja na viwanja vyake vya malisho; 70 na kutoka katika nusu ya kabila la Manase, Aneri+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Bileamu+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, kwa familia ya wana wa Kohathi waliobaki.+
71 Na kwa wana wa Gershomu+ wakawapa kutoka katika familia ya nusu ya kabila la Manase, Golani+ katika Bashani pamoja na viwanja vyake vya malisho na Ashtarothi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho; 72 na kutoka katika kabila la Isakari, Kedeshi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Daberathi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, 73 na Ramothi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Anemu+ pamoja na viwanja vyake vya malisho; 74 na kutoka katika kabila la Asheri, Mashali pamoja na viwanja vyake vya malisho na Abdoni+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, 75 na Hukoki+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Rehobu+ pamoja na viwanja vyake vya malisho; 76 na kutoka katika kabila la Naftali,+ Kedeshi+ katika Galilaya+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Hamoni pamoja na viwanja vyake vya malisho na Kiriathaimu+ pamoja na viwanja vyake vya malisho.
77 Na kwa wana wa Merari waliobaki kutoka katika kabila la Zabuloni+ wakawapa Rimono+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, Tabori pamoja na viwanja vyake vya malisho, 78 na katika eneo la Yordani kule Yeriko upande wa mashariki wa Yordani, kutoka katika kabila la Rubeni,+ Beseri+ katika nyika pamoja na viwanja vyake vya malisho na Yahazi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, 79 na Kedemothi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Mefaathi+ pamoja na viwanja vyake vya malisho; 80 na kutoka katika kabila la Gadi,+ Ramothi+ katika Gileadi pamoja na viwanja vyake vya malisho na Mahanaimu+ pamoja na viwanja vyake vya malisho, 81 na Heshboni+ pamoja na viwanja vyake vya malisho na Yazeri+ pamoja na viwanja vyake vya malisho.
7 Basi wana wa Isakari walikuwa Tola+ na Pua,+ Yashubu na Shimroni,+ wanne. 2 Na wana wa Tola walikuwa Uzi na Refaya na Yerieli na Yahmai na Ibsamu na Shemueli, vichwa vya nyumba ya mababu zao. Kwa Tola kulikuwa na mashujaa, wanaume wenye nguvu, kulingana na wazao wao. Hesabu yao katika siku za Daudi+ ilikuwa 22,600. 3 Na wana wa Uzi walikuwa Izrahia; na wana wa Izrahia walikuwa Mikaeli na Obadia na Yoeli, Ishia, , watano, wote wakiwa ni vichwa. 4 Na pamoja nao kwa wazao wao, kulingana na nyumba ya mababu zao, kulikuwa na vikosi vya jeshi vya vita, 36,000, kwa kuwa walikuwa na wake wengi na wana.+ 5 Na ndugu zao wa familia zote za Isakari walikuwa mashujaa,+ wanaume wenye nguvu, 87,000 kulingana na maandikisho yao yote ya kiukoo.+
6 Wana wa Benyamini+ walikuwa Bela+ na Bekeri+ na Yediaeli,+ watatu. 7 Na wana wa Bela+ walikuwa Esboni na Uzi na Uzieli na Yerimothi na Iri, watano, vichwa vya nyumba ya mababu zao, mashujaa, wanaume wenye nguvu; na maandikisho yao ya kiukoo+ yalikuwa 22,034. 8 Na wana wa Bekeri walikuwa Zemira na Yoashi na Eliezeri na Elioenai na Omri na Yeremothi na Abiya na Anathothi na Alemethi, wote hao walikuwa wana wa Bekeri. 9 Na maandikisho yao ya kiukoo+ kulingana na wazao wao kuhusiana na vichwa vya nyumba ya mababu zao, mashujaa, wanaume wenye nguvu, yalikuwa 20,200. 10 Na wana wa Yediaeli+ walikuwa Bilhani; na wana wa Bilhani walikuwa Yeushi na Benyamini na Ehudi na Kenaana na Zethani na Tarshishi na Ahishahari. 11 Hao wote ndio waliokuwa wana wa Yediaeli, kulingana na vichwa vya mababu zao, mashujaa,+ wanaume wenye nguvu, 17,200 wanaoingia katika jeshi kwa vita.
12 Na Shupimu+ na Hupimu+ walikuwa wana wa Ire;+ na Hushimu, wana wa Aheri.
13 Wana wa Naftali+ walikuwa Yahzieli+ na Guni+ na Yezeri na Shalumu,+ wana wa Bilha.+
14 Wana wa Manase+ walikuwa Asrieli, ambaye suria wake, Msiria, alizaa. (Mwanamke huyo alimzaa Makiri+ baba ya Gileadi. 15 Naye Makiri akachukua mke kwa ajili ya Hupimu na kwa ajili ya Shupimu, na jina la dada yake lilikuwa Maaka.) Na jina la wa pili lilikuwa Selofehadi,+ lakini Selofehadi alikuwa na mabinti.+ 16 Baada ya muda Maaka, mke wa Makiri, akazaa mwana, akamwita jina lake Pereshi; na jina la ndugu yake lilikuwa Shereshi; na wanawe walikuwa Ulamu na Rekemu. 17 Na wana wa Ulamu walikuwa Bedani. Hao ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase. 18 Na dada yake alikuwa Hamolekethi. Aliwazaa Ishodi na Abiezeri+ na Mala. 19 Na wana wa Shemida walikuwa Ahiani na Shekemu na Likhi na Aniamu.
20 Na wana wa Efraimu+ walikuwa Shuthela+ na Beredi mwana wake na Tahathi mwana wake na Eleada mwana wake na Tahathi mwana wake, 21 na Zabadi mwana wake na Shuthela mwana wake na Ezeri na Eleadi. Na watu wa Gathi+ waliozaliwa katika nchi wakawaua kwa sababu waliteremka kuja kuchukua mifugo yao. 22 Na Efraimu baba yao akaomboleza siku nyingi,+ na ndugu zake wakawa wakija kumfariji. 23 Baadaye akalala na mke wake, naye akapata mimba,+ akazaa mwana. Lakini akamwita jina lake Beria, kwa sababu mwanamke huyo alikuwa katika nyumba yake kukiwa na msiba.+ 24 Na binti yake alikuwa Sheera, naye akajenga Beth-horoni,+ ya chini+ na ya juu,+ na Uzen-sheera. 25 Na kulikuwa na Refa mwana wake, na Reshefu, na Tela mwana wake, na Tahani mwana wake, 26 Ladani mwana wake, Amihudi mwana wake, Elishama mwana wake, 27 Nuni+ mwana wake, Yehoshua+ mwana wake.
28 Na miliki yao na makao yao yalikuwa Betheli+ na miji yake ya kandokando na, upande wa mashariki, Naarani+ na, upande wa magharibi, Gezeri+ na miji yake ya kandokando, na Shekemu+ na miji yake ya kandokando mpaka Gaza na miji yake ya kandokando; 29 na kando ya wana wa Manase, Beth-sheani+ na miji yake ya kandokando, Taanaki+ na miji yake ya kandokando, Megido+ na miji yake ya kandokando, Dori+ na miji yake ya kandokando. Wana wa Yosefu+ mwana wa Israeli walikaa humo.
30 Wana wa Asheri+ walikuwa Imna+ na Ishva na Ishvi+ na Beria;+ na Sera alikuwa dada yao. 31 Na wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba ya Birzaithi. 32 Heberi naye akazaa Yafleti na Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao. 33 Na wana wa Yafleti walikuwa Pasaki na Bimhali na Ashvathi. Hao ndio waliokuwa wana wa Yafleti. 34 Na wana wa Shemeri walikuwa Ahi na Roga, Yehuba na Aramu. 35 Na wana wa Helemu ndugu yake walikuwa Sofa na Imna na Sheleshi na Amali. 36 Wana wa Sofa walikuwa Sua na Harneferi na Shuali na Beri na Imra, 37 Beseri na Hodi na Shama na Shilsha na Ithrani na Beera. 38 Na wana wa Yetheri walikuwa Yefune na Pispa na Ara. 39 Na wana wa Ula walikuwa Ara na Hanieli na Risia. 40 Hao wote ndio waliokuwa wana wa Asheri, vichwa+ vya nyumba ya mababu, mashujaa,+ wanaume wenye nguvu, waliochaguliwa, vichwa vya wakuu; na maandikisho yao ya kiukoo+ yalikuwa katika jeshi kwa ajili ya vita. Hesabu yao ilikuwa watu 26,000.+
8 Benyamini+ naye akamzaa Bela+ mzaliwa wake wa kwanza, Ashbeli+ wa pili, Ahara+ wa tatu, 2 Noha+ wa nne na Rafa wa tano. 3 Na Bela akawa na wana, Adari na Gera+ na Abihudi, 4 na Abishua na Naamani na Ahoa, 5 na Gera na Shefufani+ na Huramu.+ 6 Na hawa ndio waliokuwa wana wa Ehudi. Hawa ndio waliokuwa vichwa vya nyumba za mababu vya wakaaji wa Geba,+ nao wakawapeleka uhamishoni katika Manahathi. 7 Na Naamani na Ahiya; na Gera—yeye ndiye aliyewapeleka uhamishoni, naye akamzaa Uza na Ahihudi. 8 Shaharaimu naye akazaa wana katika uwanda+ wa Moabu baada ya kuwafukuza. Wake zake walikuwa Hushimu na Baara. 9 Naye kupitia Hodeshi mke wake, akazaa Yobabu na Sibia na Mesha na Malkamu, 10 na Yeuzi na Sakia na Mirma. Hao walikuwa wanawe, vichwa vya nyumba za mababu.
11 Naye kupitia Hushimu akazaa Abitubu na Elpaali. 12 Na wana wa Elpaali walikuwa Eberi na Mishamu na Shemedi, aliyejenga Ono+ na Lodi+ na miji yake ya kandokando, 13 na Beria na Shema. Hao walikuwa vichwa vya nyumba za mababu, za wakaaji wa Aiyaloni.+ Hao ndio waliofukuza wakaaji wa Gathi. 14 Na kulikuwa na Ahio, Shashaki na Yeremothi, 15 na Zebadia na Aradi na Ederi, 16 na Mikaeli na Ishpa na Yoha, wana wa Beria,+ 17 na Zebadia na Meshulamu na Hizki na Heberi, 18 na Ishmerai na Izlia na Yobabu, wana wa Elpaali, 19 na Yakimu na Zikri na Zabdi, 20 na Elienai na Zilethai na Elieli, 21 na Adaya na Beraya na Shimrathi, wana wa Shimei,+ 22 na Ishpani na Eberi na Elieli, 23 na Abdoni na Zikri na Hanani, 24 na Hanania na Elamu na Anthothiya, 25 na Ifdeya na Penueli, wana wa Shashaki, 26 na Shamsherai na Sheharia na Athalia, 27 na Yaareshia na Eliya na Zikri, wana wa Yerohamu. 28 Hao walikuwa vichwa vya nyumba za mababu kwa wazao wao, wanaume walio vichwa. Hao ndio waliokaa katika Yerusalemu.+
29 Na baba ya Gibeoni,+ Yeieli, alikaa katika Gibeoni, na jina la mke wake lilikuwa Maaka.+ 30 Na mwana wake, mzaliwa wa kwanza, alikuwa Abdoni, na Suri na Kishi na Baali na Nadabu,+ 31 na Gedori na Ahio na Zekeri.+ 32 Miklothi naye akamzaa Shimea.+ Na hao kwa kweli ndio waliokaa mbele ya ndugu zao katika Yerusalemu pamoja na ndugu zao.
33 Neri+ naye akamzaa Kishi;+ naye Kishi akamzaa Sauli;+ naye Sauli akamzaa Yonathani+ na Malki-shua+ na Abinadabu+ na Eshbaali.+ 34 Na mwana wa Yonathani alikuwa Merib-baali.+ Merib-baali naye akamzaa Mika.+ 35 Na wana wa Mika walikuwa Pithoni na Meleki na Tarea+ na Ahazi. 36 Ahazi naye akamzaa Yehoada; naye Yehoada akazaa Alemethi na Azmavethi na Zimri. Naye Zimri akamzaa Mosa; 37 Naye Mosa akamzaa Binea, Rafa+ mwana wake, Eleasa mwana wake, Aseli mwana wake. 38 Na Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo yaliyokuwa majina yao: Azrikamu, Bokeru na Ishmaeli na Shearia na Obadia na Hanani. Hao wote ndio waliokuwa wana wa Aseli. 39 Na wana wa Esheki ndugu yake walikuwa Ulamu mzaliwa wake wa kwanza, Yeushi wa pili na Elifeleti wa tatu. 40 Na wana wa Ulamu wakawa mashujaa,+ wanaume wenye nguvu, wanaopinda upinde,+ walio na wana wengi+ na wajukuu, watu 150. Hao wote walitoka katika wana wa Benyamini.
9 Kwa habari ya Waisraeli wote, wao waliandikishwa kiukoo;+ na tazama, wameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli. Na Yuda wakapelekwa uhamishoni+ kule Babiloni kwa sababu walikosa uaminifu. 2 Na wakaaji wa kwanza waliokuwa katika miliki zao katika majiji yao walikuwa Waisraeli,+ makuhani,+ Walawi+ na Wanethini.+ 3 Na sehemu ya wana wa Yuda+ na sehemu ya wana wa Benyamini+ na sehemu ya wana wa Efraimu na wa Manase walikaa Yerusalemu:+ 4 Uthai mwana wa Amihudi mwana wa Omri mwana wa Imri mwana wa Bani, wa wana wa Perezi+ mwana wa Yuda.+ 5 Na wa Washilo,+ Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe. 6 Na wa wana wa Zera,+ Yeueli, na ndugu zao 690.
7 Na wa wana wa Benyamini, Salu mwana wa Meshulamu mwana wa Hodavia mwana wa Hasenua, 8 na Ibneya mwana wa Yerohamu, na Ela mwana wa Uzi mwana wa Mikri, na Meshulamu mwana wa Shefatia mwana wa Reueli mwana wa Ibniya. 9 Na ndugu zao kulingana na wazao wao walikuwa 956. Hao wote walikuwa wanaume waliokuwa vichwa vya upande wa akina baba kulingana na nyumba za mababu zao.
10 Na wa makuhani kulikuwa na Yedaya na Yehoyaribu na Yakini,+ 11 na Azaria+ mwana wa Hilkia mwana wa Meshulamu mwana wa Sadoki mwana wa Merayothi mwana wa Ahitubu, kiongozi wa nyumba ya Mungu wa kweli, 12 na Adaya mwana wa Yerohamu mwana wa Pashuri mwana wa Malkiya, na Maasai mwana wa Adieli mwana wa Yahzera mwana wa Meshulamu mwana wa Meshilemithi+ mwana wa Imeri, 13 na ndugu zao, vichwa vya nyumba ya mababu zao, 1,760, wanaume wenye nguvu+ kwa ajili ya kazi ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli.
14 Na wa Walawi kulikuwa na Shemaya mwana wa Hashubu+ mwana wa Azrikamu mwana wa Hashabia kutoka kwa wana wa Merari; 15 na Bakbakari, Hereshi na Galali, na Matania+ mwana wa Mika+ mwana wa Zikri+ mwana wa Asafu,+ 16 na Obadia mwana wa Shemaya+ mwana wa Galali mwana wa Yeduthuni,+ na Berekia mwana wa Asa mwana wa Elkana, aliyekuwa akikaa katika makao ya Wanetofa.+
17 Na watunza-malango+ walikuwa Shalumu+ na Akubu na Talmoni na Ahimani na kichwa alikuwa ndugu yao Shalumu, 18 na mpaka wakati huo alikuwa katika lango la mfalme+ upande wa mashariki. Hawa ndio waliokuwa watunza-malango wa kambi za wana wa Lawi.+ 19 Na Shalumu mwana wa Kore mwana wa Ebiasafu+ mwana+ wa Kora+ na ndugu zake wa nyumba ya baba yake Wakora,+ juu ya kazi ya utumishi, watunza-milango+ ya hema, na baba zao juu ya kambi ya Yehova, watunzaji wa njia ya kuingilia. 20 Na Finehasi+ mwana wa Eleazari+ ndiye aliyekuwa kiongozi juu yao hapo zamani. Yehova alikuwa pamoja naye.+ 21 Zekaria+ mwana wa Meshelemia ndiye aliyekuwa mtunza-lango wa mwingilio wa hema la mkutano.
22 Wote waliochaguliwa kuwa watunza-malango kwenye milango walikuwa mia mbili kumi na wawili. Walikuwa katika makao+ yao kulingana na maandikisho yao ya kiukoo.+ Daudi+ na Samweli mwonaji+ waliwaagiza hao rasmi katika vyeo vyao vya kutegemewa.+ 23 Na hao na wana wao walikuwa juu ya malango ya nyumba ya Yehova, ile nyumba ya hema, kwa ajili ya utumishi wa ulinzi.+ 24 Hao watunza-malango walikuja kuwa katika zile pande nne, upande wa mashariki,+ wa magharibi,+ wa kaskazini+ na wa kusini.+ 25 Na ndugu zao katika makao yao walipaswa kuingia kwa siku saba,+ pindi kwa pindi, pamoja na hao. 26 Kwa maana kulikuwa na wanaume wanne wenye nguvu katika vyeo vya kutegemewa. Walikuwa Walawi, nao walisimamia vyumba vya kulia+ chakula na hazina+ za nyumba ya Mungu wa kweli. 27 Nao wakawa wakikaa usiku wote kuizunguka pande zote nyumba ya Mungu wa kweli; kwa maana utumishi wa ulinzi+ ulikuwa juu yao, nao walisimamia ufunguo, ili kufungua asubuhi baada ya asubuhi.+
28 Na baadhi yao walisimamia vyombo+ vya utumishi, kwa kuwa walivileta ndani kulingana na hesabu nao walivitoa nje kulingana na hesabu. 29 Na baadhi yao walikuwa wanaume waliowekwa juu ya vyombo na juu ya vyombo vyote vitakatifu +na juu ya unga laini+ na divai+ na mafuta+ na ubani+ na mafuta ya zeri.+ 30 Na baadhi ya wana wa makuhani walikuwa watengenezaji wa mchanganyiko wa marhamu+ ya mafuta ya zeri. 31 Na Matithia wa Walawi, aliyekuwa mzaliwa wa kwanza wa Shalumu,+ Mkora, alikuwa katika cheo cha kutegemewa akiwa juu ya vitu vilivyookwa katika vikaango.+ 32 Na baadhi ya wana wa Wakohathi, ndugu zao, walikuwa wakisimamia mkate wa tabaka,+ ili kuutayarisha kila sabato.+
33 Na hawa ndio waliokuwa waimbaji,+ vichwa vya upande wa baba vya Walawi katika vyumba vya kulia chakula,+ wale ambao hawakupangwa katika zamu;+ kwa maana walikuwa na wajibu wa kuwa kazini mchana na usiku.+ 34 Hawa ndio waliokuwa vichwa vya upande wa baba vya Walawi kwa wazao wao, wanaume waliokuwa vichwa. Hao ndio waliokaa katika Yerusalemu.+
35 Na baba ya Gibeoni,+ Yeieli, alikuwa akikaa Gibeoni. Na jina la mke wake lilikuwa Maaka. 36 Na mwana wake, mzaliwa wa kwanza, alikuwa Abdoni, na Suri na Kishi na Baali na Neri na Nadabu, 37 na Gedori na Ahio na Zekaria+ na Miklothi. 38 Miklothi naye akamzaa Shimeamu. Nao kwa kweli ndio waliokaa mbele ya ndugu zao katika Yerusalemu pamoja na ndugu zao. 39 Neri+ naye akamzaa Kishi;+ naye Kishi akamzaa Sauli;+ naye Sauli akamzaa Yonathani+ na Malki-shua+ na Abinadabu+ na Eshbaali.+ 40 Na mwana wa Yonathani alikuwa Merib-baali.+ Merib-baali naye akamzaa Mika.+ 41 Na wana wa Mika walikuwa Pithoni na Meleki na Tahrea na Ahazi.+ 42 Ahazi naye akamzaa Yara; naye Yara akazaa Alemethi na Azmavethi na Zimri. Naye Zimri akamzaa Mosa. 43 Mosa naye akamzaa Binea na Refaya+ mwana wake, Eleasa mwana wake, Aseli mwana wake. 44 Na Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo yaliyokuwa majina yao: Azrikamu, Bokeru na Ishmaeli na Shearia na Obadia na Hanani. Hao ndio waliokuwa wana wa Aseli.+
10 Nao Wafilisti+ wakawapiga Israeli; na watu wa Israeli wakaanza kukimbia kutoka mbele ya Wafilisti, wakaendelea kuanguka wakiwa wameuawa katika Mlima Gilboa.+ 2 Na Wafilisti wakaendelea kumfuatilia kwa ukaribu sana Sauli na wanawe; na Wafilisti wakawapiga na kuwaua Yonathani+ na Abinadabu+ na Malki-shua,+ wana wa Sauli.+ 3 Na pigano likawa kali juu ya Sauli; na mwishowe wanaopiga mishale kwa kutumia upinde wakampata, na hao wapiga-mishale wakamuumiza.+ 4 Ndipo Sauli akamwambia mchukua-silaha wake:+ “Chomoa upanga wako,+ unichome nao, ili watu hawa wasiotahiriwa+ wasije kunitendea vibaya.”+ Naye mchukua-silaha wake hakutaka,+ kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akachukua upanga, akauangukia.+ 5 Wakati yule mchukua-silaha wake alipoona kwamba Sauli amekufa, ndipo yeye pia akauangukia upanga, akafa.+ 6 Basi Sauli na wanawe watatu wakafa,+ na wote wa nyumba yake wakafa pamoja. 7 Wakati watu wote wa Israeli waliokuwa katika nchi tambarare ya chini walipoona kwamba wamekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, ndipo wakaanza kuyaacha majiji yao na kukimbia;+ kisha Wafilisti wakaingia na kuanza kukaa ndani yake.
8 Na kesho yake ikawa kwamba, Wafilisti walipokuja kuwavua+ waliouawa, wakamkuta Sauli na wanawe wameanguka juu ya Mlima Gilboa.+ 9 Nao wakamvua na kuchukua kichwa+ chake na silaha zake na kutuma wajumbe kotekote katika nchi ya Wafilisti ili kuzijulisha+ sanamu zao+ pamoja na watu. 10 Mwishowe wakaweka silaha zake katika nyumba ya mungu wao,+ na fuvu lake la kichwa wakalifunga kwenye nyumba ya Dagoni.+
11 Na watu wote wa Yabeshi+ katika Gileadi wakasikia yote ambayo Wafilisti walikuwa wamemtendea Sauli.+ 12 Basi wanaume wote mashujaa wakaondoka na kuchukua maiti ya Sauli na maiti za wanawe, wakazileta mpaka Yabeshi na kuizika mifupa yao chini ya ule mti mkubwa+ katika Yabeshi;+ nao wakafunga+ kwa siku saba.
13 Basi Sauli akafa kwa sababu alikosa uaminifu kwa kutenda bila imani+ juu ya Yehova kuhusu lile neno la Yehova ambalo hakuwa ameshika na pia kwa sababu ya kuuliza kutoka kwa mwenye kuwasiliana na pepo.+ 14 Naye hakuuliza kutoka kwa Yehova.+ Kwa hiyo akamuua na kumpa Daudi mwana wa Yese ufalme.+
11 Baada ya muda Waisraeli+ wote wakajikusanya pamoja kwa Daudi katika Hebroni,+ wakisema: “Tazama! Sisi ni mfupa wako na nyama yako.+ 2 Jana na juzi vilevile, hata Sauli alipokuwa mfalme, wewe ndiye uliyeongoza Israeli kuwatoa na kuwaingiza;+ na Yehova, Mungu wako, alikuambia, ‘Wewe utawachunga+ watu wangu Israeli, nawe utakuwa kiongozi+ juu ya watu wangu Israeli.’” 3 Basi wanaume wote wazee wa Israeli wakaja kwa mfalme katika Hebroni na Daudi akafanya agano nao katika Hebroni mbele za Yehova; kisha wakamtia mafuta+ Daudi awe mfalme juu ya Israeli, kulingana na neno+ la Yehova kupitia kwa Samweli.+
4 Baadaye Daudi na Israeli wote wakaenda Yerusalemu,+ yaani, Yebusi,+ ambapo Wayebusi+ ndio waliokuwa wakaaji wa nchi hiyo. 5 Na wakaaji wa Yebusi wakaanza kumwambia Daudi: “Wewe hutaingia humu.”+ Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni,+ yaani, Jiji la Daudi.+ 6 Hivyo Daudi akasema: “Yeyote atakayewapiga+ Wayebusi kwanza, atakuwa kichwa na mkuu.” Na Yoabu+ mwana wa Seruya akapanda kwanza, naye akawa kichwa. 7 Na Daudi akaanza kukaa katika mahali pagumu kufikiwa.+ Ndiyo maana walipaita Jiji la Daudi.+ 8 Naye akaanza kujenga jiji hilo kuzunguka pande zote, kuanzia Kilima mpaka zile sehemu zenye kuzunguka, lakini Yoabu akazitengeneza+ zile sehemu nyingine za jiji. 9 Na Daudi akaendelea kuwa mkuu zaidi na zaidi,+ kwa maana Yehova wa majeshi alikuwa pamoja naye.+
10 Basi hawa ndio vichwa vya wale wanaume wenye nguvu+ wa Daudi, walioshikamana naye kwa nguvu katika ufalme wake pamoja na Israeli wote, kumfanya kuwa mfalme kulingana na neno la Yehova+ kuhusu Israeli. 11 Na hii ndiyo orodha ya wale wanaume wenye nguvu waliokuwa wa Daudi: Yashobeamu+ mwana wa Mhakmoni, kichwa cha wale watatu. Alikuwa akitikisa mkuki wake juu ya watu mia tatu waliouawa kwa wakati mmoja.+ 12 Na baada yake alikuwa Eleazari+ mwana wa Dodo, Mwahohi.+ Alikuwa kati ya wale wanaume watatu wenye nguvu.+ 13 Yeye ndiye aliyekuwa na Daudi kule Pas-damimu,+ ambapo Wafilisti walikuwa wamejikusanya kwa ajili ya vita. Basi palikuwa na eneo la shamba lililojaa shayiri, na watu wakawa wamekimbia kwa sababu ya Wafilisti.+ 14 Lakini yeye akasimama katikati ya lile shamba, akalikomboa, naye akaendelea kuwapiga na kuwaua Wafilisti, hivi kwamba Yehova akaokoa+ kwa wokovu mkubwa.+
15 Na watatu kati ya wale 30+ waliokuwa vichwa wakashuka kwenda mwambani, kwa Daudi katika pango la Adulamu,+ huku kambi ya Wafilisti ikiwa imepigwa katika nchi tambarare ya chini ya Refaimu.+ 16 Na wakati huo Daudi alikuwa katika mahali palipo pagumu kufikiwa;+ na wakati huo kambi ya kijeshi ya Wafilisti+ ilikuwa katika Bethlehemu. 17 Baada ya muda Daudi akaonyesha tamaa yake na kusema: “Laiti ningekunywa+ maji kutoka katika tangi la Bethlehemu+ lililoko langoni!” 18 Ndipo wale watatu wakaingia kwa nguvu katika kambi ya Wafilisti, wakateka maji kutoka katika lile tangi la Bethlehemu lililoko langoni, wakaja wakiwa wameyachukua na kumletea Daudi.+ Naye Daudi hakukubali kuyanywa, bali akayamwaga mbele za Yehova.+ 19 Naye akaendelea kusema: “Ni jambo lisiloweza kuwaziwa kwangu, kwa habari ya Mungu wangu, nifanye hivi! Je, ninywe damu+ ya watu hawa kwa kuhatarisha nafsi zao? Kwa maana waliyaleta kwa kuhatarisha nafsi zao.” Naye hakukubali kuyanywa.+ Hayo ndiyo mambo ambayo wale wanaume watatu wenye nguvu walifanya.
20 Naye Abishai+ ndugu ya Yoabu,+ yeye alikuwa kichwa cha wale watatu; naye alitikisa mkuki wake juu ya watu 300 waliouawa, naye alikuwa na sifa kama wale watatu. 21 Kati ya hao watatu yeye alikuwa mashuhuri zaidi kuliko hao wengine wawili, naye akawa mkuu wao; ingawa hivyo hakufikia+ kuwa kati ya wale watatu wa kwanza.
22 Naye Benaya+ mwana wa Yehoyada+ mwana wa mwanamume shujaa, aliyefanya matendo mengi katika Kabzeeli,+ yeye mwenyewe alipiga na kuwaua wale wana wawili wa Arieli wa Moabu; naye alishuka, akapiga na kumuua simba+ ndani ya shimo la maji katika siku ya kuanguka kwa theluji. 23 Naye ndiye aliyempiga na kumuua yule mwanamume Mmisri, mwanamume aliyekuwa mkubwa isivyo kawaida, mwenye urefu wa mikono mitano.+ Na mkononi mwa yule Mmisri kulikuwa na mkuki+ kama mti wa wafumaji wa nguo; na bado yeye alishuka kumwendea akiwa na fimbo, akaunyakua ule mkuki kutoka mkononi mwa yule Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.+ 24 Benaya mwana wa Yehoyada alifanya mambo hayo, naye alikuwa na jina kati ya wale wanaume watatu wenye nguvu. 25 Ingawa yeye alikuwa mashuhuri kuliko wale 30, hakufikia daraja la wale watatu wa kwanza.+ Hata hivyo, Daudi alimweka juu ya walinzi wake.+
26 Kwa habari ya wanaume wenye nguvu wa majeshi, kulikuwa na Asaheli+ ndugu ya Yoabu, Elhanani+ mwana wa Dodo wa Bethlehemu. 27 Shamothi+ Mharori, Helezi Mpeloni,+ 28 Ira+ mwana wa Ikeshi Mtekoa, Abiezeri Mwanathothi,+ 29 Sibekai+ Mhusha, Ilai Mwahohi,+ 30 Maharai+ Mnetofa,+ Heledi+ mwana wa Baana Mnetofa, 31 Ithai mwana wa Ribai+ wa Gibea+ wa wana wa Benyamini,+ Benaya Mpirathoni,+ 32 Hurai kutoka katika mabonde ya mto ya Gaashi,+ Abieli Mwarbathi, 33 Azmavethi Mbaharumu,+ Eliaba Mshaalboni, 34 wana wa Hashemu Mgizoni, Yonathani+ mwana wa Shagee Mharari, 35 Ahiamu mwana wa Sakari+ Mharari, Elifali+ mwana wa Uru, 36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni, 37 Hezro Mkarmeli,+ Naarai mwana wa Ezbai, 38 Yoeli ndugu ya Nathani,+ Mibhari mwana wa Hagri, 39 Seleki Mwamoni, Naharai Mberothi, mchukua-silaha wa Yoabu mwana wa Seruya, 40 Ira Mwithri, Garebu+ Mwithri, 41 Uria+ Mhiti,+ Zabadi mwana wa Alai, 42 Adina mwana wa Shiza Mrubeni, kichwa cha Warubeni, ambaye 30 walikuwa pamoja naye; 43 Hanani mwana wa Maaka, na Yoshafati Mmithini, 44 Uziya Mwashtarothi, Shama na Yeieli, wana wa Hothamu Mwaroeri, 45 Yediaeli mwana wa Shimri, na Yoha ndugu yake, Mtisi, 46 Elieli Mmahawi, na Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, na Ithma Mmoabu. 47 Elieli na Obedi na Yaasieli Mmesoba.
12 Na hawa ndio waliomjia Daudi kule Siklagi+ alipokuwa angali chini ya vizuizi kwa sababu ya Sauli+ mwana wa Kishi; nao walikuwa kati ya wale wanaume wenye nguvu,+ wasaidizi katika vita, 2 wenye upinde, wanaotumia mkono wa kuume na kutumia mkono wa kushoto+ wakiwa na mawe+ au wakiwa na mishale+ katika upinde.+ Walikuwa wa ndugu za Sauli, wa Benyamini. 3 Kulikuwa na kichwa Ahiezeri na Yoashi wana wa Shemaa Mgibea,+ na Yezieli na Peleti wana wa Azmavethi,+ na Baraka na Yehu Mwanathothi,+ 4 na Ishmaya Mgibeoni,+ mwanamume mwenye nguvu kati ya wale 30+ na aliye juu ya wale 30; na Yeremia na Yahazieli na Yohanani na Yozabadi Mgedera,+ 5 Eluzai na Yerimothi na Bealia na Shemaria na Shefatia Mharifu, 6 Elkana na Ishia na Azareli na Yoezeri na Yashobeamu, Wakora,+ 7 na Yoela na Zebadia wana wa Yerohamu wa Gedori.
8 Na palikuwa na baadhi ya Wagadi waliojitenga kuwa upande wa Daudi katika mahali palipo pagumu kufikiwa nyikani,+ mashujaa, wanaume wenye nguvu, wanaume wa jeshi kwa ajili ya vita, wenye ngao kubwa na mkuki tayari,+ ambao nyuso zao zilikuwa nyuso za simba,+ nao walikuwa na mwendo kama swala juu ya milima.+ 9 Ezeri ndiye aliyekuwa kichwa, Obadia wa pili, Eliabu wa tatu, 10 Mishmana wa nne, Yeremia wa tano, 11 Atai wa sita, Elieli wa saba, 12 Yohanani wa nane, Elzabadi wa tisa, 13 Yeremia wa kumi, Makbanai wa kumi na moja. 14 Hao walikuwa wa wana wa Gadi,+ vichwa vya jeshi. Aliye mdogo zaidi alikuwa sawa na mia moja, na aliye mkubwa zaidi alikuwa sawa na elfu moja.+ 15 Hao ndio waliovuka Yordani+ katika mwezi wa kwanza mto ulipokuwa umefurika kingo zake,+ kisha wakawafukuza wale wote wa nchi tambarare za chini, kuelekea upande wa mashariki na upande wa magharibi.
16 Na baadhi ya wana wa Benyamini na Yuda wakaja kwa Daudi, katika mahali palipo pagumu kufikiwa.+ 17 Ndipo Daudi akatoka mbele yao, akajibu na kuwaambia: “Ikiwa mmenijia kwa amani+ ili kunisaidia, moyo wangu utaungana nanyi.+ Lakini ikiwa ni kunisaliti kwa adui zangu wakati hakuna kosa lolote mikononi mwangu,+ Mungu+ wa mababu zetu na aone hilo na kulinyoosha.”+ 18 Na roho+ ikamfunika Amasai, kichwa cha wale 30:
“Sisi ni wako, Ee Daudi, nasi tuko pamoja nawe,+ Ee mwana wa Yese.
Amani, amani iwe yako, na amani kwa yule anayekusaidia,
Kwa maana Mungu wako amekusaidia.”+
Basi Daudi akawapokea, akawaweka kati ya vichwa vya vikosi.+
19 Na kulikuwa na baadhi ya watu wa Manase waliotorokea kwa Daudi alipokuja na Wafilisti+ juu ya Sauli kwa ajili ya vita; lakini hakuwasaidia, kwa sababu baada ya kushauriana, wakuu wa muungano+ wa Wafilisti walimfukuza, wakisema: “Atatoroka amwendee Sauli bwana wake na kuhatarisha vichwa vyetu.”+ 20 Alipokuja Siklagi,+ Adna na Yozabadi na Yediaeli na Mikaeli na Yozabadi na Elihu na Zilethai, vichwa+ vya maelfu wa Manase walitoroka kutoka kwa Manase na kumwendea. 21 Nao wakamsaidia Daudi kupigana na kile kikundi cha waporaji,+ kwa sababu wote hao walikuwa mashujaa, wanaume wenye nguvu,+ nao wakawa wakuu katika jeshi; 22 kwa maana watu walizidi kumjia+ Daudi siku kwa siku ili kumsaidia, mpaka ilipokuwa kambi kubwa,+ kama kambi ya Mungu.+
23 Na hizi ndizo zilizokuwa hesabu za vichwa vya walioandaliwa kwa ajili ya jeshi ambao walimjia Daudi kule Hebroni+ ili kumpa ufalme+ wa Sauli kulingana na agizo la Yehova.+ 24 Wana wa Yuda waliokuwa wakichukua ngao kubwa na mkuki walikuwa 6,800, waliotayarishwa kwa ajili ya jeshi. 25 Wa wana wa Simeoni mashujaa, wanaume wenye nguvu wa jeshi walikuwa 7,100.
26 Wa wana wa Walawi 4,600. 27 Na Yehoyada alikuwa ndiye kiongozi+ wa wana wa Haruni,+ naye alikuwa pamoja na watu 3,700. 28 Pia Sadoki+ kijana, shujaa mwenye nguvu, na nyumba ya mababu zake, wakuu 22.
29 Na wa wana wa Benyamini,+ ndugu za Sauli,+ walikuwa 3,000, na mpaka wakati huo hesabu iliyo kubwa kati yao walikuwa wakiilinda kwa makini nyumba ya Sauli. 30 Na wa wana wa Efraimu walikuwa 20,800, mashujaa, wanaume wenye nguvu,+ wanaume wenye sifa, kulingana na nyumba za mababu zao.
31 Na wa nusu ya kabila la Manase+ walikuwa 18,000 waliochaguliwa kwa majina waje kumfanya Daudi kuwa mfalme. 32 Na wa wana wa Isakari+ walio na ujuzi wa jinsi ya kutambua nyakati+ ili kujua yale ambayo Israeli wanapaswa kufanya,+ walikuwa 200 wa kwao, na ndugu zao wote walifuata maagizo yao. 33 Wa Zabuloni+ wale wanaoingia jeshini, wanaojipanga kivita pamoja na silaha zote za vita, walikuwa 50,000, nao wakawa wakimiminika kwa Daudi bila kuwa na mioyo miwili. 34 Na wa Naftali+ walikuwa wakuu 1,000, na pamoja nao wenye ngao kubwa na mkuki walikuwa 37,000. 35 Na wa Wadani wale wanaojipanga kivita walikuwa 28,600. 36 Na wa Asheri+ wale wanaoingia jeshini ili kujipanga kivita walikuwa 40,000.
37 Na kutoka ng’ambo ya Yordani+ wa Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase na silaha zote za kijeshi walikuwa 120,000. 38 Hao wote walikuwa wanaume wa vita, wakimiminika pamoja kujipanga katika vikosi vya kupigana; walikuja kwa moyo kamili+ huko Hebroni ili kumfanya Daudi kuwa mfalme juu ya Israeli wote; na pia waliobaki wa Israeli walikuwa na moyo mmoja kwa ajili ya kumfanya Daudi kuwa mfalme.+ 39 Nao wakaendelea kuwa hapo pamoja na Daudi siku tatu, wakila na kunywa,+ kwa kuwa ndugu zao walikuwa wamewafanyia matayarisho. 40 Na pia wale waliokuwa karibu nao, hata mpaka Isakari+ na Zabuloni+ na Naftali,+ wakawa wakileta chakula juu ya punda+ na juu ya ngamia na juu ya nyumbu na juu ya ng’ombe, vyakula vya unga,+ keki za tini zilizoshinikizwa+ na keki za zabibu kavu+ na divai+ na mafuta+ na ng’ombe+ na kondoo+ kwa wingi sana, kwa maana kulikuwa na shangwe+ katika Israeli.
13 Na Daudi akashauriana na wakuu wa maelfu na wa mamia na kila kiongozi;+ 2 na Daudi akaliambia kutaniko lote la Israeli: “Ikiwa vema kwenu na kukubalika kwa Yehova, Mungu wetu, na tutume watu kwa ndugu zetu waliobaki katika nchi zote za Israeli+ na pamoja nao makuhani+ na Walawi+ katika majiji+ yao yenye viwanja vya malisho, ili wajikusanye pamoja kwetu. 3 Nasi tulete sanduku+ la Mungu wetu kwetu.” Kwa maana hawakuwa wamelitunza katika siku za Sauli.+ 4 Basi kutaniko lote wakasema ifanywe hivyo, kwa maana jambo hilo lilionekana kuwa jema machoni pa watu wote.+ 5 Basi Daudi akakusanya+ Israeli wote kuanzia mto wa Misri+ mpaka maingilio ya Hamathi,+ ili kulileta sanduku+ la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu.+
6 Na Daudi na Israeli wote wakapanda kwenda mpaka Baala,+ Kiriath-yearimu katika Yuda, ili kuleta kutoka huko sanduku la Mungu wa kweli, Yehova, anayekaa juu ya makerubi,+ ambalo jina lake limeitwa juu yake. 7 Hata hivyo, wakapandisha sanduku la Mungu wa kweli juu ya gari jipya la kukokotwa+ kutoka katika nyumba ya Abinadabu, na Uza na Ahio+ walikuwa wakiliongoza lile gari. 8 Na Daudi na Israeli wote walikuwa wakisherehekea+ mbele za Mungu wa kweli kwa nguvu kamili na kwa nyimbo+ na kwa vinubi+ na kwa vinanda+ na kwa matari+ na kwa matoazi na kwa tarumbeta.+ 9 Nao mwishowe wakaja mpaka uwanja wa kupuria wa Kidoni,+ na sasa Uza akanyoosha mkono wake ili kulishika lile Sanduku,+ kwa maana wale ng’ombe karibu waliangushe. 10 Ndipo hasira ya Yehova ikamwakia Uza, hivi kwamba akampiga kwa sababu alikuwa ameunyoosha mkono wake juu ya lile Sanduku,+ naye akafa hapo mbele za Mungu.+ 11 Na Daudi akakasirika+ kwa sababu Yehova alikuwa amemlipukia Uza, na mahali hapo pakaitwa Peres-uza mpaka leo hii.
12 Naye Daudi akamwogopa Mungu wa kweli siku hiyo,+ akisema: “Nitaliletaje sanduku la Mungu wa kweli kwangu?”+ 13 Na Daudi hakulileta Sanduku kwake katika Jiji la Daudi, bali alilichukua, akalipeleka kando kwenye nyumba ya Obed-edomu,+ Mgathi.+ 14 Nalo sanduku la Mungu wa kweli likaendelea kukaa pamoja na nyumba ya Obed-edomu, nyumbani kwake+ kwa miezi mitatu; na Yehova akazidi kuibariki+ nyumba ya Obed-edomu na vitu vyake vyote.
14 Na Hiramu+ mfalme wa Tiro+ akatuma wajumbe kwa Daudi na mierezi+ na wajenzi wa kuta na wafanyakazi wa miti ili wamjengee nyumba.+ 2 Na Daudi akajua kwamba Yehova alikuwa amemfanya imara+ kuwa mfalme juu ya Israeli, kwa maana ufalme wake ulikuwa umeinuliwa sana kwa ajili ya watu wake Israeli.+
3 Na Daudi akaendelea kuchukua wake+ zaidi katika Yerusalemu, na Daudi akazaa wana na mabinti zaidi.+ 4 Na haya ndiyo majina ya watoto wake aliopata katika Yerusalemu: Shamua+ na Shobabu,+ Nathani+ na Sulemani,+ 5 na Ibhari+ na Elishua na Elpeleti,+ 6 na Noga na Nefegi+ na Yafia, 7 na Elishama+ na Beeliada na Elifeleti.+
8 Na Wafilisti wakasikia kwamba Daudi ametiwa mafuta awe mfalme juu ya Israeli wote.+ Ndipo Wafilisti wote wakaja kumtafuta Daudi.+ Daudi aliposikia habari hizo, akatoka na kwenda kupigana nao. 9 Nao Wafilisti wakaingia na kuendelea kuvamia katika nchi tambarare ya chini ya Refaimu.+ 10 Naye Daudi akaanza kumuuliza Mungu,+ akisema: “Je, nipande kwenda kupigana na Wafilisti, na je, hakika utawatia mkononi mwangu?” Ndipo Yehova akamwambia: “Panda uende, nami hakika nitawatia mkononi mwako.” 11 Kwa hiyo Daudi akapanda kwenda Baal-perasimu+ naye akawapiga na kuwaua huko. Ndipo Daudi akasema: “Mungu wa kweli amepenya katikati ya adui zangu kupitia kwa mkono wangu kama pengo lililofanyizwa na maji.” Ndiyo sababu walipaita mahali hapo+ jina Baal-perasimu. 12 Basi wakaiacha miungu yao huko.+ Ndipo Daudi akatoa amri, nayo ikateketezwa motoni.+
13 Baadaye Wafilisti wakavamia tena katika nchi tambarare ya chini.+ 14 Ndipo Daudi akamuuliza+ tena Mungu wa kweli, na sasa Mungu wa kweli akamwambia: “Usipande kuwafuatilia. Zunguka uende, usiende moja kwa moja kuwashambulia, nawe uwajie mbele ya miti ya mibaka.+ 15 Na iwe kwamba, utakaposikia sauti ya mwendo juu ya miti ya mibaka,+ ndipo utoke, uingie katika pigano,+ kwa sababu Mungu wa kweli atakuwa ametoka kwenda mbele yako+ kuipiga kambi ya Wafilisti.” 16 Basi Daudi akafanya kama vile Mungu wa kweli alivyokuwa amemwamuru,+ nao wakaipiga kambi ya Wafilisti kutoka Gibeoni+ mpaka Gezeri.+ 17 Na sifa+ ya Daudi ikaanza kuenea katika nchi zote, na Yehova akatia hofu yake juu ya mataifa yote.+
15 Naye akaendelea kujijengea nyumba+ katika Jiji la Daudi; naye akatayarisha mahali+ kwa ajili ya sanduku la Mungu wa kweli na kulisimamishia hema. 2 Ndipo Daudi aliposema: “Mtu yeyote asilibebe sanduku la Mungu wa kweli isipokuwa Walawi, kwa maana Yehova amewachagua hao ili walibebe sanduku la Yehova+ na kumhudumia+ mpaka wakati usio na kipimo.” 3 Kisha Daudi akawakutanisha Israeli wote katika Yerusalemu+ ili kulipandisha sanduku+ la Yehova mpaka mahali pake ambapo alikuwa amelitayarishia.
4 Na Daudi akawakusanya wana wa Haruni+ na Walawi; 5 wa wana wa Kohathi, Urieli+ mkuu na ndugu zake, 120; 6 wa wana wa Merari,+ Asaya+ mkuu na ndugu zake, 220; 7 wa wana wa Gershomu,+ Yoeli+ mkuu na ndugu zake, 130; 8 wa wana wa Elisafani,+ Shemaya+ mkuu na ndugu zake, 200; 9 wa wana wa Hebroni, Elieli mkuu na ndugu zake, 80; 10 wa wana wa Uzieli,+ Aminadabu mkuu na ndugu zake, 112. 11 Tena, Daudi akawaita Sadoki+ na Abiathari+ makuhani, na Walawi Urieli,+ Asaya+ na Yoeli,+ Shemaya+ na Elieli+ na Aminadabu, 12 naye akawaambia: “Ninyi ndio vichwa+ vya upande wa baba vya Walawi. Jitakaseni,+ ninyi na ndugu zenu, nanyi mlipandishe sanduku la Yehova, Mungu wa Israeli mpaka mahali ambapo nimelitayarishia. 13 Kwa sababu mara ya kwanza hamkufanya hivyo,+ Yehova, Mungu wetu, alitulipukia,+ kwa kuwa hatukumtafuta kulingana na desturi.”+ 14 Basi makuhani na Walawi wakajitakasa+ ili walipandishe sanduku la Yehova, Mungu wa Israeli.
15 Ndipo wana wa Walawi wakaanza kulibeba+ sanduku la Mungu wa kweli, kama Musa alivyoamuru kwa amri ya Yehova, juu ya mabega yao na fimbo zikiwa juu yao.+ 16 Daudi akawaambia wakuu wa Walawi wawaweke ndugu zao waimbaji+ wakiwa na vyombo vya nyimbo,+ vinanda+ na vinubi+ na matoazi,+ wakipiga kwa sauti ili sauti ya kushangilia itokee.
17 Basi Walawi wakamweka Hemani+ mwana wa Yoeli na, kati ya ndugu zake, Asafu+ mwana wa Berekia; na, kati ya ndugu zao wana wa Merari, Ethani+ mwana wa Kushaya; 18 na pamoja nao ndugu zao wa mgawanyo wa pili,+ Zekaria,+ Beni na Yaazieli na Shemiramothi na Yehieli na Uni, Eliabu na Benaya na Maaseya na Matithia na Elifelehu na Mikneya, na Obed-edomu+ na Yeieli watunza-malango, 19 na waimbaji Hemani,+ Asafu+ na Ethani, wakiwa na matoazi ya shaba ili kuyapiga kwa sauti;+ 20 na Zekaria na Azieli+ na Shemiramothi na Yehieli na Uni na Eliabu na Maaseya na Benaya wakiwa na vinanda vilivyorekebishwa kupatana na sauti ya Alamothi,+ 21 na Matithia+ na Elifelehu na Mikneya na Obed-edomu na Yeieli na Azazia wakiwa na vinubi+ vilivyorekebishwa kupatana na Sheminithi,+ wawe viongozi; 22 na Kenania+ mkuu wa Walawi juu ya uchukuzi, yeye akitoa maagizo katika kuchukua, kwa maana alikuwa mwenye ujuzi;+ 23 na Berekia na Elkana watunza-malango+ kwa ajili ya Sanduku; 24 na Shebania na Yoshafati na Nethaneli na Amasai na Zekaria na Benaya na Eliezeri makuhani wakizipiga tarumbeta+ kwa sauti kubwa mbele ya sanduku la Mungu wa kweli, na Obed-edomu na Yehia watunza-malango wa Sanduku.
25 Na Daudi+ na wale wanaume wazee wa Israeli+ na wakuu+ wa maelfu wakatembea kando ili kulipandisha sanduku la agano la Yehova kutoka katika nyumba ya Obed-edomu+ kwa kushangilia.+ 26 Na ikawa kwamba wakati Mungu wa kweli alipowasaidia+ Walawi wakiwa wamelichukua sanduku la agano la Yehova, wakatoa dhabihu ng’ombe-dume saba wachanga na kondoo-dume saba.+ 27 Naye Daudi alikuwa amevaa koti lisilo na mikono la kitambaa laini, na pia Walawi wote waliochukua Sanduku na waimbaji na Kenania+ mkuu wa uchukuzi wa waimbaji;+ lakini Daudi alikuwa amevaa efodi+ ya kitani. 28 Na Waisraeli wote walikuwa wakilipandisha sanduku la agano la Yehova kwa sauti za shangwe+ na kwa kupiga baragumu+ na kwa tarumbeta+ na kwa matoazi,+ wakipiga kwa sauti kubwa vinanda na vinubi.+
29 Na ikawa kwamba wakati sanduku la agano+ la Yehova lilipokuja mpaka Jiji la Daudi, Mikali,+ binti ya Sauli, akaangalia chini kutoka dirishani, akamwona Mfalme Daudi akirukaruka na kusherehekea;+ naye akaanza kumdharau+ moyoni mwake.
16 Hivyo wakaliingiza ndani sanduku la Mungu wa kweli+ na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamishia;+ nao wakaanza kutoa matoleo ya kuteketezwa na dhabihu za ushirika mbele za Mungu wa kweli.+ 2 Daudi alipomaliza kulitoa lile toleo la kuteketezwa+ na dhabihu za ushirika,+ akaanza kuwabariki+ watu katika jina la Yehova.+ 3 Zaidi ya hayo, akawagawia+ Waisraeli wote, mwanamume na mwanamke vilevile, kila mmoja mkate mmoja wa mviringo na keki ya tende na keki ya zabibu kavu. 4 Ndipo akawaweka baadhi ya Walawi+ mbele ya sanduku la Yehova wawe wahudumu;+ ili wakumbushe+ na pia wamshukuru+ na kumsifu+ Yehova, Mungu wa Israeli, 5 Asafu+ akiwa kichwa, na wa pili kwake Zekaria, na Yeieli na Shemiramothi na Yehieli na Matithia na Eliabu na Benaya na Obed-edomu na Yeieli,+ wakiwa na vyombo vya aina ya vinanda na vinubi,+ na Asafu+ akiwa na matoazi akiyapiga kwa sauti,+ 6 na Benaya na Yahazieli makuhani wakiwa na tarumbeta+ daima mbele ya sanduku la agano la Mungu wa kweli.
7 Ndipo katika siku hiyo Daudi alitoa mchango+ kwa mara ya kwanza ili kumshukuru+ Yehova kupitia kwa Asafu+ na ndugu zake:
8 “Mshukuruni Yehova;+ liitieni jina lake,+
Yajulisheni matendo yake katikati ya vikundi vya watu!+
12 Kumbukeni matendo yake ya ajabu ambayo ameyafanya,+
Miujiza yake na maamuzi ya hukumu ya kinywa chake,+
13 Enyi uzao wa Israeli mtumishi wake,+
Enyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+
14 Yeye ni Yehova Mungu wetu;+ maamuzi yake ya hukumu yako duniani pote.+
15 Kumbukeni agano lake mpaka wakati usio na kipimo,+
Neno ambalo aliamuru, mpaka vizazi elfu,+
16 Agano ambalo alifanya na Abrahamu,+
Na ahadi yake yenye kiapo aliyomwapia Isaka.+
17 Kiapo ambacho alikiendeleza kikiwa sharti kwa Yakobo,+
Kama agano lenye kudumu kwa Israeli mpaka wakati usio na kipimo,+
18 Akisema, ‘Nitakupa wewe nchi ya Kanaani,+
Kuwa fungu la urithi wenu.’+
20 Nao wakaendelea kutembea kutoka kwa taifa moja mpaka kwa taifa lingine,+
Na kutoka katika ufalme mmoja mpaka kwa kikundi kingine cha watu.+
24 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa,
Matendo yake ya ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.
26 Kwa maana miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu isiyo na thamani.+
Lakini Yehova, alizifanya mbingu.+
29 Mhesabieni Yehova utukufu wa jina lake,+
Chukueni zawadi na mwingie mbele zake.+
Mwinamieni Yehova katika pambo takatifu.+
30 Iweni na maumivu makali kwa sababu yake, enyi nyote watu wa dunia!
Pia nchi yenye kuzaa imefanywa imara:
Kamwe haitatikiswa.+
33 Na wakati uleule miti ya msituni na ishangilie kwa ajili ya Yehova,+
Kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+
34 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema,+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+
35 Na mseme, ‘Utuokoe, Ee Mungu wa wokovu wetu,+
Na utukusanye pamoja na kutukomboa kutoka kwa mataifa,+
Ili tulishukuru jina lako takatifu,+ ili tukusifu kwa shangwe.+
36 Na abarikiwe Yehova Mungu wa Israeli, kutoka wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo.’”+
Na watu wote wakasema, “Amina!” na sifa kwa Yehova.+
37 Kisha akawaacha hapo Asafu+ na ndugu zake mbele ya sanduku la agano la Yehova ili wahudumu+ daima mbele ya lile Sanduku, kulingana na takwa la kila siku;+ 38 na Obed-edomu na ndugu zake, 68, na Obed-edomu mwana wa Yeduthuni na Hosa kuwa watunza-malango; 39 na Sadoki+ kuhani na ndugu zake makuhani mbele ya maskani ya Yehova katika mahali pa juu palipokuwa katika Gibeoni,+ 40 ili watoe matoleo ya kuteketezwa kwa Yehova juu ya madhabahu ya toleo la kuteketezwa daima asubuhi na jioni na kwa ajili ya yote ambayo yameandikwa katika sheria ya Yehova ambayo aliamuru Israeli;+ 41 na pamoja nao Hemani+ na Yeduthuni na wale watu wengine wachaguliwa waliowekwa+ kwa majina ili wamshukuru Yehova,+ kwa sababu “fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo”;+ 42 na pamoja nao Hemani+ na Yeduthuni,+ wapige tarumbeta+ na matoazi na vyombo vya wimbo wa Mungu wa kweli; na wana+ wa Yeduthuni langoni. 43 Na watu wote wakaanza kwenda kila mmoja nyumbani kwake.+ Basi Daudi akaenda ili kuibariki nyumba yake mwenyewe.
17 Na ikawa kwamba mara tu Daudi alipoanza kukaa katika nyumba yake mwenyewe,+ Daudi akamwambia Nathani+ nabii: “Tazama, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi,+ lakini sanduku+ la agano la Yehova linakaa ndani ya vitambaa vya mahema.”+ 2 Basi Nathani akamwambia Daudi: “Kila jambo lililo moyoni mwako lifanye,+ kwa kuwa Mungu wa kweli yupo pamoja nawe.”+
3 Na ikawa kwamba usiku huo neno+ la Mungu likamjia Nathani, likisema: 4 “Nenda, ukamwambie Daudi mtumishi wangu, ‘Yehova amesema hivi: “Si wewe utakayenijengea mimi nyumba ya kukaa.+ 5 Kwa maana sijakaa katika nyumba tangu siku nilipowapandisha Israeli mpaka leo hii,+ bali nilikaa hema kwa hema na kutoka maskani+ moja mpaka nyingine.+ 6 Wakati wote ambao nilitembea+ katika Israeli yote, je, nilisema hata neno moja na mmoja wa waamuzi wa Israeli ambao niliamuru wawachunge watu wangu, nikisema, ‘Kwa nini hamjanijengea nyumba ya mierezi?’”’+
7 “Na sasa utamwambia Daudi mtumishi wangu hivi, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Mimi mwenyewe nilikuchukua kutoka katika viwanja vya malisho ili uache kufuata kundi+ na uwe kiongozi+ juu ya watu wangu Israeli. 8 Nami nitakuwa pamoja nawe popote utakapotembea,+ nami nitawakatilia mbali adui+ zako wote kutoka mbele yako, nami hakika nitakufanyia jina+ kama jina la wakuu walio duniani.+ 9 Nami hakika nitachagua mahali kwa ajili ya watu wangu Israeli na kuwapanda,+ nao hakika watakaa mahali walipo, nao hawatasumbuliwa tena; na wana wa ukosefu wa uadilifu+ hawatawachosha tena kama walivyofanya hapo mwanzoni,+ 10 tangu zile siku nilipoweka waamuzi+ wawasimamie watu wangu Israeli. Nami hakika nitawatiisha adui zako wote.+ Nami ninakuambia, ‘Pia Yehova atakujengea nyumba.’+
11 “‘“Na itakuwa kwamba siku zako zitakapokuwa zimetimia ili uende kuwa na mababu zako,+ mimi nitainua uzao wako baada yako ambao utakuwa mmoja wa wana wako,+ nami kwa kweli nitaufanya imara ufalme wake.+ 12 Yeye ndiye atakayenijengea nyumba,+ nami hakika nitakifanya imara kiti chake cha ufalme mpaka wakati usio na kipimo.+ 13 Mimi mwenyewe nitakuwa baba yake,+ na yeye mwenyewe atakuwa mwanangu;+ na fadhili zangu zenye upendo sitaziondoa kwake+ kama vile nilivyoziondoa kwa yule aliyekutangulia.+ 14 Nami nitamsimamisha katika nyumba+ yangu na katika ufalme+ wangu mpaka wakati usio na kipimo, na kiti chake cha ufalme+ kitadumu mpaka wakati usio na kipimo.”’”
15 Basi Nathani akamwambia Daudi kulingana na maneno hayo yote na kulingana na maono hayo yote.+
16 Kisha Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Yehova+ na kusema: “Mimi ni nani,+ Ee Yehova Mungu, na nyumba yangu+ ni nini hata ukanileta kufikia hapa?+ 17 Kana kwamba hili ni jambo dogo machoni pako,+ Ee Mungu,+ na bado unasema habari za nyumba ya mtumishi wako mpaka wakati mrefu ujao,+ na umeniangalia kulingana na hali ya mtu anayepanda cheo,+ Ee Yehova, Mungu. 18 Daudi anaweza kukuambia nini zaidi kwa habari ya kumheshimu mtumishi wako,+ kwa kuwa wewe mwenyewe unamjua vema mtumishi wako?+ 19 Ee Yehova, kwa ajili ya mtumishi wako na kwa kupatana na moyo wako mwenyewe+ umeyafanya mambo haya yote makuu kwa kujulisha juu ya mafanikio makuu yote.+ 20 Ee Yehova, hakuna mwingine kama wewe,+ wala hakuna Mungu ila wewe+ kwa habari ya yote ambayo tumeyasikia kwa masikio yetu. 21 Na kuna taifa gani lingine duniani lililo kama watu wako Israeli,+ ambao Mungu wa kweli alikwenda kujikombolea mwenyewe wawe kikundi cha watu,+ ili kujipa jina la mafanikio makubwa+ na mambo yenye kuogopesha kwa kuyafukuza mataifa+ kutoka mbele ya watu wako ambao umewakomboa kutoka Misri? 22 Nawe ukawafanya watu wako Israeli kuwa watu wako+ mpaka wakati usio na kipimo, na wewe mwenyewe, Ee Yehova, ukawa Mungu wao.+ 23 Na sasa, Ee Yehova, lile neno ambalo umesema kumhusu mtumishi wako na kuihusu nyumba yake na liwe la kuaminika mpaka wakati usio na kipimo, na ufanye kama ulivyosema. 24 Jina+ lako na liwe la kuaminika na liwe kuu+ mpaka wakati usio na kipimo, kusema, ‘Yehova wa majeshi,+ Mungu wa Israeli,+ ni Mungu wa Israeli,’+ na acha nyumba ya Daudi mtumishi wako idumu mbele zako.+ 25 Kwa maana wewe mwenyewe, Mungu wangu, umemfunulia mtumishi wako kusudi la kumjengea nyumba.+ Ndiyo sababu mtumishi wako amepata nafasi ya kusali mbele zako. 26 Na sasa, Ee Yehova, wewe ndiye Mungu wa kweli,+ nawe unaahidi wema huu kuhusu mtumishi wako.+ 27 Na sasa ujichukulie wajibu na kuibariki nyumba ya mtumishi wako ili iendelee mpaka wakati usio na kipimo mbele zako;+ kwa maana wewe mwenyewe, Ee Yehova, umebariki, nayo imebarikiwa mpaka wakati usio na kipimo.”+
18 Na ikawa baadaye kwamba Daudi akawapiga Wafilisti+ na kuwatiisha na kuchukua Gathi+ na miji yake ya kandokando kutoka mkononi mwa Wafilisti. 2 Kisha akapiga Moabu, na Wamoabu+ wakawa watumishi wa Daudi wenye kuleta ushuru.+
3 Na Daudi akampiga Hadadezeri+ mfalme wa Soba+ kule Hamathi+ alipokuwa akienda zake kuweka mamlaka yake kwenye mto Efrati.+ 4 Tena, Daudi akateka kutoka kwake magari 1,000 na wapanda-farasi 7,000 na watu 20,000 wanaoenda kwa miguu.+ Ndipo Daudi akakata mishipa ya magoti+ ya farasi wote wa magari,+ lakini akawaacha wabaki kati yao farasi 100 wa magari. 5 Wakati Siria ya Damasko walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba,+ Daudi akapiga watu 22,000 kati ya Wasiria. 6 Kisha Daudi akaweka kambi za kijeshi katika Siria ya Damasko,+ na Wasiria wakawa watumishi wa Daudi wenye kuleta ushuru.+ Na Yehova akaendelea kumpa Daudi wokovu popote alipoenda.+ 7 Tena, Daudi akazichukua zile ngao za mviringo+ za dhahabu zilizokuwa kwa watumishi wa Hadadezeri, akazileta Yerusalemu.+ 8 Na Daudi akachukua shaba nyingi sana kutoka katika Tibhathi+ na Kuni, majiji ya Hadadezeri. Sulemani aliitumia kutengeneza ile bahari ya shaba+ na zile nguzo+ na vyombo vya shaba.+
9 Wakati Tou mfalme wa Hamathi+ aliposikia kwamba Daudi amepiga jeshi lote la Hadadezeri+ mfalme wa Soba, 10 ndipo akamtuma haraka Hadoramu+ mwana wake kwa Mfalme Daudi aulize hali yake na kumpongeza kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumpiga (kwa maana Hadadezeri alikuwa amezoea kupigana na Tou,) naye alikuwa na aina zote za vyombo vya dhahabu na fedha+ na shaba. 11 Vyombo hivyo pia Mfalme Daudi akavitakasa+ kwa Yehova, pamoja na ile fedha na dhahabu ambayo alikuwa amechukua kutoka kwa mataifa yote,+ kutoka Edomu na kutoka Moabu+ na kutoka kwa wana wa Amoni+ na kutoka kwa Wafilisti+ na kutoka kwa Amaleki.+
12 Naye Abishai+ mwana wa Seruya,+ akawapiga Waedomu katika Bonde la Chumvi,+ watu kumi na nane elfu. 13 Basi akaweka kambi za kijeshi katika Edomu, na Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi.+ Na Yehova akaendelea kumwokoa Daudi popote alipoenda.+ 14 Na Daudi akaendelea kutawala juu ya Israeli yote,+ naye akaendelea kutoa uamuzi wa hukumu na uadilifu kwa ajili ya watu wake wote.+ 15 Na Yoabu mwana wa Seruya alikuwa juu ya jeshi;+ na Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi alikuwa karani. 16 Na Sadoki+ mwana wa Ahitubu na Ahimeleki+ mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shausha+ alikuwa mwandishi. 17 Na Benaya+ mwana wa Yehoyada+ alikuwa juu ya Wakerethi+ na Wapelethi;+ na wana wa Daudi walikuwa wa kwanza katika cheo kando ya mfalme.+
19 Na ikawa kwamba baadaye Nahashi+ mfalme wa wana wa Amoni akafa, na mwana wake akaanza kutawala mahali pake.+ 2 Ndipo Daudi akasema: “Nitamwonyesha fadhili zenye upendo+ Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinionyesha fadhili zenye upendo.”+ Basi Daudi akatuma wajumbe ili kumfariji kwa sababu ya baba yake, na watumishi wa Daudi wakaingia katika nchi ya wana wa Amoni+ kwa Hanuni ili kumfariji. 3 Hata hivyo, wakuu wa wana wa Amoni wakamwambia Hanuni: “Je, Daudi anamheshimu baba yako machoni pako kwa kutuma kwako wafariji? Je, watumishi wake hawakuja kwako+ ili kuchunguza kwa ukamili na kufanya mapinduzi na kuipeleleza nchi?”+ 4 Kwa hiyo Hanuni akawachukua wale watumishi wa Daudi,+ akawanyoa,+ akakata nusu ya mavazi yao mpaka kwenye matako yao,+ akawaacha waende zao.+ 5 Baadaye watu wakaenda, wakamwambia Daudi kuhusu wale watu; naye akatuma watu mara moja kwenda kuwapokea, kwa sababu watu hao walikuwa wamefedheheshwa sana; na mfalme akaendelea kusema: “Kaeni katika Yeriko+ mpaka ndevu zenu ziote kabisa. Ndipo mrudi.”
6 Baada ya muda, wana wa Amoni wakaona kuwa wamenuka+ machoni pa Daudi, na Hanuni+ na wana wa Amoni wakatuma talanta 1,000 za fedha+ ili kukodi magari+ na wapanda-farasi kutoka Mesopotamia na kutoka Aram-maaka+ na kutoka Soba.+ 7 Basi wakajikodishia magari 32,000+ na mfalme wa Maaka na watu wake.+ Ndipo wakaja na kupiga kambi mbele ya Medeba;+ nao wana wa Amoni wakakusanyika kutoka katika majiji yao, wakaja sasa kwa ajili ya vita.
8 Wakati Daudi aliposikia habari hizo, akatuma haraka Yoabu+ na jeshi lote na wanaume wenye nguvu.+ 9 Nao wana wa Amoni wakaanza kutoka, wajipange katika vikosi vya vita kwenye mwingilio wa jiji, na wale wafalme+ waliokuwa wamekuja walikuwa peke yao uwanjani.
10 Yoabu alipoona mashambulio yamekuja juu yake kutoka upande wa mbele na kutoka upande wa nyuma, mara moja akachagua baadhi ya wanaume bora katika Israeli na kuwapanga ili wakutane na Wasiria.+ 11 Na wale watu wengine waliobaki akawaweka mkononi mwa Abishai+ ndugu yake, ili wajipange kukutana na wana wa Amoni.+ 12 Naye akasema: “Ikiwa Wasiria+ watakuwa na nguvu mno kuliko mimi, basi wewe utaniokoa;+ lakini ikiwa wana wa Amoni watakuwa na nguvu mno kuliko wewe, mimi pia nitakuja kukuokoa.+ 13 Uwe na nguvu,+ ili tujionyeshe kuwa hodari kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya majiji ya Mungu wetu;+ naye Yehova atafanya yaliyo mema machoni pake mwenyewe.”+
14 Ndipo Yoabu na watu waliokuwa pamoja naye wakasonga mbele kuwaelekea Wasiria vitani,+ nao wakakimbia+ kutoka mbele yake. 15 Basi wana wa Amoni wakaona kwamba Wasiria wamekimbia, nao pia wakakimbia+ kutoka mbele ya Abishai ndugu yake, kisha wakaingia ndani ya jiji. Baadaye Yoabu akaingia Yerusalemu.+
16 Wasiria walipoona kwamba wameshindwa+ mbele ya Israeli, wakatuma wajumbe na kuwatoa Wasiria waliokuwa katika eneo la ule Mto,+ na Shofaki mkuu wa jeshi la Hadadezeri akiwa mbele yao.
17 Daudi alipoletewa habari hiyo, akakusanya mara moja Israeli wote na kuvuka Yordani, akaja kwao, akajipanga kupigana nao.+ Daudi alipojipanga katika vikosi vya vita ili kukutana na Wasiria, wao wakaanza kupigana naye. 18 Lakini Wasiria wakakimbia+ kwa sababu ya Israeli; na Daudi akaua kati ya Wasiria waendesha-gari elfu saba na watu 40,000 wanaoenda kwa miguu, naye akamuua Shofaki mkuu wa jeshi.+ 19 Wakati watumishi wa Hadadezeri walipoona kwamba wameshindwa mbele ya Israeli,+ wakafanya amani mara moja na Daudi, wakaanza kumtumikia;+ na Siria hawakutaka kujaribu tena kuwaokoa wana wa Amoni.+
20 Na ikawa kwamba mwanzoni mwa mwaka,+ wakati ambapo wafalme hufanya mashambulizi,+ Yoabu akaongoza jeshi la mapambano,+ akaiharibu nchi ya wana wa Amoni, akaenda kuzingira Raba,+ Daudi alipokuwa anakaa katika Yerusalemu; na Yoabu akapiga+ Raba na kulibomoa. 2 Lakini Daudi akaliondoa taji la Malkamu kutoka juu ya kichwa chake,+ naye akakuta likiwa na uzito wa talanta moja ya dhahabu, na ndani yake mlikuwa na mawe ya thamani; nalo likaja kuwa juu ya kichwa cha Daudi. Na nyara za jiji lile ambazo alileta zilikuwa nyingi sana.+ 3 Na watu waliokuwa ndani yake akawatoa nje, akawatia kwenye kazi+ ya kukata mawe kwa misumeno na ya vifaa vya chuma vyenye ncha kali na ya mashoka;+ na hivyo ndivyo Daudi alivyoyafanya majiji yote ya wana wa Amoni. Mwishowe Daudi na watu wote wakarudi Yerusalemu.
4 Na ikawa kwamba baada ya hayo vita vikaanza kutokea na Wafilisti+ kule Gezeri.+ Ndipo Sibekai+ Mhusha akampiga Sipai wa wale waliozaliwa kwa Refaimu,+ hivi kwamba wakashindwa.
5 Na kukawa na vita tena na Wafilisti; na Elhanani+ mwana wa Yairi akampiga Lahmi ndugu ya Goliathi+ Mgathi, ambaye mpini wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa wafumaji wa nguo.+
6 Na kukawa na vita tena katika Gathi,+ wakati kulipokuwa na mtu mwenye ukubwa usio wa kawaida,+ ambaye vidole vyake vya mikono na vidole vyake vya miguu vilikuwa sita sita, jumla 24;+ naye pia alikuwa amezaliwa kwa Refaimu.+ 7 Naye akaendelea kudhihaki+ Israeli. Mwishowe Yonathani mwana wa Shimea+ ndugu ya Daudi akampiga na kumuua.
8 Hao ndio waliokuwa wamezaliwa kwa Refaimu+ katika Gathi;+ nao wakaanguka+ kwa mkono wa Daudi na kwa mkono wa watumishi wake.
21 Na Shetani akasimama kushindana na Israeli, akamchochea+ Daudi ahesabu Israeli. 2 Basi Daudi akamwambia Yoabu+ na wakuu wa watu: “Nendeni, mkahesabu+ Israeli kutoka Beer-sheba+ mpaka Dani,+ mniletee nipate kujua hesabu yao.”+ 3 Lakini Yoabu akasema: “Yehova na aongeze watu wake wawe wengi mara mia kuliko walivyo.+ Ee bwana wangu mfalme, je, wao wote si watumishi wa bwana wangu? Kwa nini bwana wangu anatafuta jambo hili?+ Kwa nini awe sababu ya hatia kwa Israeli?”
4 Hata hivyo, neno la mfalme+ likamshinda Yoabu, hivi kwamba Yoabu akatoka,+ akatembea katika Israeli yote, kisha akaja Yerusalemu.+ 5 Kisha Yoabu akampa Daudi hesabu ya watu walioandikishwa; na Israeli wote wakawa jumla ya wanaume milioni moja na mia moja elfu wenye kutumia upanga,+ na Yuda wanaume 470,000 wenye kutumia upanga. 6 Naye hakuandikisha kati yao Lawi na Benyamini,+ kwa sababu neno la mfalme lilimchukiza Yoabu.
7 Basi jambo hilo lilikuwa baya machoni pa Mungu wa kweli,+ kwa hiyo akapiga Israeli. 8 Basi Daudi akamwambia Mungu wa kweli: “Nimetenda dhambi sana+ kwa kuwa nimefanya jambo hili. Na sasa, tafadhali, acha kosa la mtumishi wako lipitilie mbali;+ kwa maana nimetenda kwa upumbavu sana.”+ 9 Na Yehova akamwambia Gadi,+ mwonaji wa Daudi,+ na kusema: 10 “Nenda, umwambie Daudi, ukisema, ‘Yehova amesema hivi: “Kuna mambo matatu ambayo ninayaelekeza kwako.+ Jichagulie mwenyewe moja kati ya hayo, ili nikutendee hilo.”’”+ 11 Basi Gadi akaja, akaingia kwa Daudi,+ akamwambia: “Yehova amesema hivi, ‘Jichagulie moja, 12 kama kuwe na njaa+ kwa miaka mitatu; au miezi mitatu wapinzani wako wakufagilie mbali na upanga wa adui+ zako ukufikie, au siku tatu kuwe na upanga wa Yehova,+ tauni,+ katika nchi, huku malaika wa Yehova akileta uharibifu+ katika eneo lote la Israeli.’ Na sasa uone ni jibu gani nitakalompelekea Yeye aliyenituma.” 13 Kwa hiyo Daudi akamwambia Gadi: “Ni jambo lenye kunitaabisha sana. Tafadhali, acha nianguke mkononi mwa Yehova,+ kwa maana rehema zake ni nyingi;+ lakini usiache nianguke mkononi mwa mwanadamu.”+
14 Ndipo Yehova akaleta tauni+ katika Israeli, hivi kwamba watu 70,000 wakaanguka katika Israeli.+ 15 Tena, Mungu wa kweli akatuma malaika katika Yerusalemu ili kuliangamiza;+ na mara tu alipoanza kuleta maangamizi, Yehova akaona hilo, akaanza kujuta kuhusu msiba ule;+ na kwa hiyo akamwambia yule malaika aliyekuwa akiangamiza: “Imetosha!+ Sasa angusha mkono wako.” Na yule malaika wa Yehova alikuwa amesimama karibu na uwanja wa kupuria wa Ornani+ Myebusi.+
16 Daudi alipoinua macho yake, akamwona malaika+ wa Yehova amesimama kati ya dunia na mbingu, mkononi mwake akiwa na upanga uliochomolewa+ ukiwa umenyooshwa kuelekea Yerusalemu; na Daudi na wanaume wazee, wakiwa wamevaa nguo za magunia,+ wakaanguka kifudifudi mara moja.+ 17 Na Daudi akamwambia Mungu wa kweli: “Je, si mimi niliyesema watu wahesabiwe, na je, si mimi niliyetenda dhambi na bila shaka kufanya ubaya?+ Lakini kondoo hawa,+ wamefanya nini? Tafadhali, Ee Yehova, Mungu wangu, acha mkono wako uje juu yangu na nyumba ya baba yangu; bali si juu ya watu wako,+ kwa kupigwa na tauni.”
18 Naye malaika wa Yehova akamwambia Gadi+ amwambie Daudi apande kwenda kumsimamishia Yehova madhabahu kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani Myebusi.+ 19 Basi Daudi akapanda kulingana na neno la Gadi ambalo alikuwa amesema katika jina la Yehova.+ 20 Na wakati huo, Ornani+ akageuka, akamwona yule malaika; na wanawe wanne waliokuwa pamoja naye walikuwa wamejificha. Sasa Ornani alikuwa akipura ngano. 21 Na Daudi akaja mpaka kwa Ornani. Ornani alipotazama na kumwona Daudi,+ akatoka haraka nje ya uwanja wa kupuria, akamwinamia Daudi kifudifudi. 22 Ndipo Daudi akamwambia Ornani: “Nipe mahali pa uwanja wa kupuria, ili nimjengee Yehova madhabahu hapo. Unipe kwa pesa kamili,+ ili tauni+ ikomeshwe juu ya watu.” 23 Lakini Ornani akamwambia Daudi: “Uchukue uwe wako,+ na bwana wangu mfalme afanye lililo jema machoni pake mwenyewe. Tazama, natoa ng’ombe+ kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa na chombo cha kupuria+ kwa ajili ya kuni+ na ngano kuwa toleo la nafaka. Natoa vyote.”+
24 Hata hivyo, Mfalme Daudi akamwambia Ornani: “Hapana, bali bila shaka nitaununua kwa pesa kamili,+ kwa sababu sitachukua kilicho chako nimpe Yehova ili kutoa matoleo ya kuteketezwa bila gharama.” 25 Kwa hiyo Daudi akampa Ornani kwa ajili ya mahali hapo shekeli za dhahabu zenye uzito wa mia sita.+ 26 Ndipo Daudi akamjengea Yehova madhabahu+ hapo na kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika, naye akamwitia Yehova,+ambaye sasa alimjibu kwa moto+ kutoka mbinguni juu ya madhabahu ya toleo la kuteketezwa. 27 Tena, Yehova akampa amri yule malaika,+ naye akarudisha upanga katika ala yake. 28 Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Yehova amemjibu kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani Myebusi, yeye akaendelea kutoa dhabihu hapo.+ 29 Lakini ile maskani ya Yehova ambayo Musa alikuwa ameitengeneza katika nyika na ile madhabahu ya toleo la kuteketezwa, vilikuwa wakati huo katika mahali pa juu kule Gibeoni.+ 30 Na Daudi alikuwa hajaweza kwenda mbele yake ili kutafuta shauri kwa Mungu, kwa maana alikuwa ameogopa+ kwa sababu ya upanga wa malaika wa Yehova.
22 Ndipo Daudi akasema: “Hii ndiyo nyumba+ ya Yehova, Mungu wa kweli, na hii ndiyo madhabahu+ kwa ajili ya toleo la kuteketezwa kwa ajili ya Israeli.”
2 Sasa Daudi akasema wakaaji wote wageni+ walio katika nchi ya Israeli wakusanywe, kisha akawaweka kuwa wachongaji wa mawe+ ili wachonge mawe ya mraba+ kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu wa kweli. 3 Na Daudi akatayarisha chuma kwa wingi sana kwa ajili ya misumari ya milango ya malango na kwa ajili ya vibanio, na pia shaba nyingi isiyoweza kupimwa uzito,+ 4 na pia mbao za mierezi+ zisizo na hesabu; kwa maana Wasidoni+ na Watiro+ walimletea Daudi mbao za mierezi kwa wingi sana. 5 Kwa hiyo Daudi akasema: “Sulemani mwanangu ni mchanga na mwororo,+ na ile nyumba itakayojengewa Yehova inapaswa kuwa yenye utukufu+ zaidi kwa ajili ya uzuri+ wenye heshima kwa nchi zote. Basi, acha mimi nimfanyie matayarisho.” Hivyo Daudi akafanya matayarisho kwa wingi sana kabla ya kifo chake.+
6 Tena akamwita Sulemani mwana wake ili ampe amri ya kumjengea nyumba Yehova, Mungu wa Israeli. 7 Naye Daudi akamwambia Sulemani mwana wake: “Kwa habari yangu, nilitaka sana moyoni+ mwangu kujenga nyumba kwa ajili ya jina+ la Yehova, Mungu wangu. 8 Lakini neno la Yehova lilikuja dhidi yangu, na kusema, ‘Umemwaga damu nyingi sana,+ nawe umepigana vita vikubwa.+ Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ kwa kuwa umemwaga damu nyingi sana duniani mbele zangu. 9 Tazama! Utazaa mwana.+ Yeye atakuwa mtu mtulivu, nami nitampa pumziko kutoka kwa adui zake wote pande zote;+ kwa maana jina lake litakuwa Sulemani,+ nami nitaleta juu ya Israeli amani+ na utulivu katika siku zake. 10 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ naye atakuwa mwanangu,+ nami nitakuwa baba+ yake. Nami hakika nitakifanya imara kiti cha ufalme+ wake juu ya Israeli mpaka wakati usio na kipimo.’
11 “Sasa, mwanangu, Yehova na awe pamoja nawe, nawe upate mafanikio, ujenge nyumba ya Yehova, Mungu wako, kama alivyosema kukuhusu wewe.+ 12 Ila tu Yehova akupe busara na uelewaji,+ naye akupe amri kuhusu Israeli ili kuishika sheria ya Yehova, Mungu wako.+ 13 Hivyo utapata mafanikio+ ukiangalia kutenda masharti+ na maamuzi ya hukumu+ ambayo Yehova alimwamuru+ Musa kuhusu Israeli. Uwe hodari na mwenye nguvu.+ Usiogope+ wala usiingiwe na hofu.+ 14 Na tazama, wakati wa mateso+ yangu nimetayarisha kwa ajili ya nyumba ya Yehova talanta mia moja elfu za dhahabu+ na talanta milioni moja za fedha, na hakuna namna ya kupima uzito wa shaba+ na chuma+ kwa sababu zimekuwa nyingi sana; nami nimetayarisha mbao na mawe, lakini utaviongeza vitu hivyo. 15 Nawe una wafanyakazi wengi sana, wachongaji wa mawe na wafanyakazi wa mawe+ na kila mwenye ustadi katika kila namna ya kazi.+ 16 Hakuna namna yoyote ya kuhesabu dhahabu, fedha na shaba na chuma.+ Simama, utende,+ na Yehova awe pamoja nawe.”+
17 Tena Daudi akawaamuru wakuu wote wa Israeli wamsaidie Sulemani mwana wake: 18 “Je, Yehova, Mungu wenu, hayuko pamoja nanyi,+ na je, hakuwapa pumziko kuzunguka pande zote?+ Kwa maana ametia mkononi mwangu wakaaji wa nchi, na nchi imetiishwa mbele za Yehova+ na mbele ya watu wake. 19 Basi kazeni mioyo yenu na nafsi+ zenu kumuuliza Yehova, Mungu wenu,+ na msimame, mjenge patakatifu+ pa Yehova, Mungu wa kweli,+ ili kuleta sanduku+ la agano la Yehova na vyombo vitakatifu vya Mungu wa kweli katika nyumba iliyojengwa kwa ajili ya jina+ la Yehova.”
23 Na Daudi alikuwa amezeeka+ na kushiba siku, basi akamfanya Sulemani+ mwana wake kuwa mfalme juu ya Israeli. 2 Ndipo akawakusanya wakuu+ wote wa Israeli na makuhani+ na Walawi.+ 3 Basi Walawi wakahesabiwa kuanzia umri wa miaka 30 na zaidi;+ na hesabu yao, kichwa kwa kichwa, mwanamume kwa mwanamume, ikawa 38,000. 4 Kati ya hao kwa ajili ya kuwa wasimamizi juu ya kazi ya nyumba ya Yehova kulikuwa na 24,000; na 6,000 kuwa maofisa+ na waamuzi;+ 5 na watunza-malango+ 4,000 na watu 4,000 wenye kutoa sifa+ kwa Yehova kwa vyombo+ ambavyo Daudi alisema “Nimevitengeneza kwa ajili ya kutoa sifa.”
6 Kisha Daudi akawagawa katika migawanyo+ kwa wana wa Lawi,+ kwa Gershoni, Kohathi na Merari. 7 Kwa Wagershoni, Ladani na Shimei. 8 Wana wa Ladani walikuwa Yehieli+ akiwa kichwa na Zethamu na Yoeli,+ watatu. 9 Wana wa Shimei walikuwa Shelomothi na Hazieli na Harani, watatu. Hao ndio waliokuwa vichwa vya upande wa baba kwa ajili ya Ladani. 10 Na wana wa Shimei walikuwa Yahathi, Zina na Yeushi na Beria. Hao wanne ndio waliokuwa wana wa Shimei. 11 Naye Yahathi akawa kichwa, Ziza wa pili. Nao Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo wakawa nyumba moja ya ukoo wa upande wa baba+ kwa ajili ya tabaka moja rasmi.
12 Wana wa Kohathi+ walikuwa Amramu, Ishari,+ Hebroni+ na Uzieli,+ wanne. 13 Wana wa Amramu walikuwa Haruni+ na Musa.+ Lakini Haruni akatengwa+ ili atakase Patakatifu Zaidi,+ yeye na wanawe mpaka wakati usio na kipimo, kufukiza moshi wa dhabihu+ mbele za Yehova, kumhudumia+ na kutangaza baraka+ katika jina lake mpaka wakati usio na kipimo. 14 Naye Musa yule mtu wa Mungu wa kweli,+ wanawe waliendelea kuhesabiwa kati ya kabila la Walawi.+ 15 Wana wa Musa walikuwa Gershomu+ na Eliezeri.+ 16 Wana wa Gershomu walikuwa Shebueli+ akiwa kichwa. 17 Na wana wa Eliezeri wakawa ni Rehabia+ akiwa kichwa; na Eliezeri hakupata kuwa na wana wengine, lakini wana wa Rehabia wakawa wengi mno. 18 Wana wa Ishari+ walikuwa Shelomithi+ akiwa ndiye mwanamume aliye kichwa. 19 Wana wa Hebroni walikuwa Yeria akiwa kichwa, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu na Yekameamu+ wa nne. 20 Wana wa Uzieli+ walikuwa Mika akiwa kichwa na Ishia wa pili.
21 Wana wa Merari+ walikuwa Mali na Mushi.+ Wana wa Mali walikuwa Eleazari+ na Kishi. 22 Lakini Eleazari akafa; naye hakuwa amepata wana, isipokuwa mabinti. Basi wana wa Kishi ndugu zao wakawachukua wawe wake zao.+ 23 Wana wa Mushi walikuwa Mali na Ederi na Yeremothi,+ watatu.
24 Hawa ndio waliokuwa wana wa Lawi kulingana na nyumba za baba zao,+ vichwa vya upande wa akina baba, kulingana na watu wao waliopewa utume, katika hesabu ya majina, kwa vichwa vyao, wafanyakazi kwa ajili ya utumishi+ wa nyumba ya Yehova, kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi.+ 25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema: “Yehova, Mungu wa Israeli, amewapa watu wake pumziko,+ naye atakaa Yerusalemu mpaka wakati usio na kipimo.+ 26 Na pia Walawi hawataibeba tena maskani au chochote kati ya vyombo vyake kwa ajili ya utumishi wake.”+ 27 Kwa maana kwa maneno+ ya mwisho ya Daudi hao ndio waliokuwa hesabu ya wana wa Lawi kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi. 28 Kwa maana utendaji wao ulikuwa chini ya mwelekezo wa wana wa Haruni+ kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Yehova juu ya nyua+ na juu ya vyumba vya kulia chakula+ na juu ya utakaso wa kila kitu kitakatifu+ na kazi ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli, 29 kwa ajili ya mkate wa tabaka+ na kwa ajili ya unga laini+ wa toleo la nafaka na kwa ajili ya mkate mwembamba+ usio na chachu+ na kwa ajili ya keki za kuoka+ na kwa ajili ya unga wa kukandwa uliochanganywa+ na kwa ajili ya vipimo vyote vya wingi na ukubwa;+ 30 na kwa ajili ya kusimama+ kila asubuhi+ ili kumshukuru+ na kumsifu+ Yehova, na wakati wa jioni vivyo hivyo; 31 na kwa ajili ya kila toleo la dhabihu za kuteketezwa kwa Yehova katika sabato,+ katika miezi mipya+ na katika majira ya sherehe,+ kufuatilia hesabu kulingana na kanuni zenye kuzihusu, daima mbele za Yehova. 32 Nao wakafanya ulinzi wa hema la mkutano na ulinzi+ wa mahali patakatifu+ na ulinzi wa wana wa Haruni ndugu zao kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Yehova.+
24 Basi wana wa Haruni walikuwa na migawanyo yao. Wana wa Haruni walikuwa Nadabu+ na Abihu,+ Eleazari+ na Ithamari.+ 2 Hata hivyo, Nadabu na Abihu+ walikufa kabla ya baba yao,+ nao hawakuwa na wana wowote, bali Eleazari+ na Ithamari wakaendelea kuwa makuhani. 3 Na Daudi, na Sadoki+ kutoka kwa wana wa Eleazari, na Ahimeleki+ kutoka kwa wana wa Ithamari wakawafanya wawe migawanyo kwa ajili ya cheo chao katika utumishi wao.+ 4 Lakini wana wa Eleazari wakaonekana kuwa na wanaume wengi waliokuwa vichwa kuliko wana wa Ithamari. Basi wakawagawa kwa wana wa Eleazari, wawe vichwa vya nyumba za ukoo wao wa upande wa baba, kumi na sita, na kwa wana wa Ithamari, wawe vichwa vya nyumba zao za ukoo wa upande wa baba, wanane.
5 Tena, wakawagawa kwa kura,+ hawa pamoja na wale, kwa maana kulipaswa kuwa na wakuu wa mahali patakatifu+ na wakuu wa Mungu wa kweli kutoka kwa wana wa Eleazari na kutoka kwa wana wa Ithamari. 6 Ndipo Shemaya mwana wa Nethaneli mwandishi+ wa Walawi akawaandika mbele ya mfalme na wakuu na Sadoki+ kuhani na Ahimeleki+ mwana wa Abiathari+ na vichwa vya baba za makuhani na vya Walawi,+ nyumba moja ya ukoo wa upande wa baba ikichaguliwa kwa ajili ya Eleazari+ na moja ikichaguliwa kwa ajili ya Ithamari.+
7 Na kura ikatoka: ya kwanza ya Yehoyaribu;+ ya pili ya Yedaya, 8 ya 3 ya Harimu, ya 4 ya Seorimu, 9 ya 5 ya Malkiya, ya 6 ya Miyamini, 10 ya 7 ya Hakozi, ya 8 ya Abiya,+ 11 ya 9 ya Yeshua, ya 10 ya Shekania, 12 ya 11 ya Eliashibu, ya 12 ya Yakimu, 13 ya 13 ya Hupa, ya 14 ya Yeshebeabu, 14 ya 15 ya Bilga, ya 16 ya Imeri, 15 ya 17 ya Heziri, ya 18 ya Hapisesi, 16 ya 19 ya Pethahia, ya 20 ya Yehezkeli, 17 ya 21 ya Yakini, ya 22 ya Gamuli, 18 ya 23 ya Delaya, ya 24 ya Maazia.
19 Hivi ndivyo vilivyokuwa vyeo+ vyao kwa ajili ya utumishi wao,+ kuingia katika nyumba ya Yehova kulingana na haki yao+ inayostahiliwa kwa mkono wa Haruni babu yao, kama vile Yehova, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
20 Na wa wana wa Lawi waliobaki, wa wana wa Amramu+ kulikuwa na Shubaeli;+ wa wana wa Shubaeli, Yehdeya; 21 wa Rehabia:+ wa wana wa Rehabia, Ishia akiwa kichwa; 22 wa Waishari,+ Shelomothi;+ wa wana wa Shelomothi, Yahathi; 23 na wana wa Hebroni,+ Yeria+ akiwa kichwa, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, Yekameamu wa nne. 24 Wana wa Uzieli, Mika; wa wana wa Mika,+ Shamiri. 25 Ndugu ya Mika alikuwa Ishia; wa wana wa Ishia, Zekaria.
26 Wana wa Merari+ walikuwa Mali+ na Mushi;+ wana wa Yaazia, Beno. 27 Wana wa Merari: Wa Yaazia, Beno na Shohamu na Zakuri na Ibri. 28 Wa Mali, Eleazari, ambaye hakupata wana wowote.+ 29 Wa Kishi: wana wa Kishi walikuwa Yerahmeeli. 30 Na wana wa Mushi walikuwa Mali+ na Ederi na Yerimothi.+
Hao ndio waliokuwa wana wa Walawi kulingana na nyumba za ukoo wa upande wa baba+ zao. 31 Nao wenyewe pia wakapiga kura+ sawasawa na walivyofanya ndugu zao wana wa Haruni mbele ya Daudi mfalme, na Sadoki na Ahimeleki na vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba vya makuhani na vya Walawi. Na kwa habari ya nyumba za ukoo wa upande wa baba,+ aliye kichwa alikuwa sawasawa na ndugu yake mdogo.
25 Tena Daudi na wakuu+ wa vikundi vya utumishi+ wakatenga kwa ajili ya utumishi sehemu ya wana wa Asafu, Hemani+ na Yeduthuni+ wenye kutoa unabii kwa vinubi,+ kwa vinanda+ na kwa matoazi.+ Na kutoka katika hesabu yao kukawa na wanaume rasmi kwa ajili ya utumishi wao. 2 Wa wana wa Asafu, Zakuri na Yosefu+ na Nethania na Asharela,+ wana wa Asafu chini ya amri ya Asafu+ mwenye kutoa unabii chini ya mfalme. 3 Wa Yeduthuni:+ wana wa Yeduthuni, Gedalia+ na Zeri+ na Yeshaya,+ na Shimei, Hashabia na Matithia,+ sita, chini ya amri ya Yeduthuni baba yao, aliyekuwa akitoa unabii akiwa na kinubi kwa ajili ya kumshukuru na kumsifu Yehova.+ 4 Wa Hemani:+ wana wa Hemani, Bukia,+ Matania,+ Uzieli,+ Shebueli na Yerimothi, Hanania,+ Hanani, Eliatha,+ Gidalti+ na Romamti-ezeri,+ Yoshbekasha,+ Malothi,+ Hothiri,+ Mahaziothi. 5 Hawa wote ndio waliokuwa wana wa Hemani, mwonaji+ wa mfalme katika mambo ya Mungu wa kweli ili ainue pembe yake; basi Mungu wa kweli akampa Hemani wana kumi na wanne na binti watatu.+ 6 Hawa wote ndio waliokuwa chini ya amri ya baba yao katika nyimbo kwenye nyumba ya Yehova, wakiwa na matoazi,+ vinanda+ na vinubi+ kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli.
Chini ya amri ya mfalme kulikuwa Asafu na Yeduthuni na Hemani.+
7 Na hesabu yao pamoja na ndugu zao waliozoezwa nyimbo kwa Yehova,+ wote wakiwa wajuzi,+ ikawa 288. 8 Basi wakapiga kura+ kuhusu vitu vinavyopaswa kutunzwa, mdogo akiwa sawasawa na mkubwa,+ mwenye ujuzi+ pamoja na mwenye kujifunza.
9 Na kura ikatoka: ya kwanza ya Asafu kwa ajili ya Yosefu,+ ya pili ya Gedalia+ (yeye na ndugu zake na wanawe walikuwa 12); 10 ya tatu ya Zakuri,+ wanawe na ndugu zake, 12; 11 ya 4 ya Izri,+ wanawe na ndugu zake, 12; 12 ya 5 ya Nethania,+ wanawe na ndugu zake, 12; 13 ya 6 ya Bukia, wanawe na ndugu zake, 12; 14 ya 7 ya Yesharela,+ wanawe na ndugu zake, 12; 15 ya 8 ya Yeshaya, wanawe na ndugu zake, 12; 16 ya 9 ya Matania, wanawe na ndugu zake, 12; 17 ya 10 ya Shimei, wanawe na ndugu zake, 12; 18 ya 11 ya Azareli,+ wanawe na ndugu zake, 12; 19 ya 12 ya Hashabia, wanawe na ndugu zake, 12; 20 ya 13, ya Shubaeli,+ wanawe na ndugu zake, 12; 21 ya 14, ya Matithia, wanawe na ndugu zake, 12; 22 ya 15, ya Yeremothi, wanawe na ndugu zake, 12; 23 ya 16, ya Hanania, wanawe na ndugu zake, 12; 24 ya 17, ya Yoshbekasha, wanawe na ndugu zake, 12; 25 ya 18, ya Hanani, wanawe na ndugu zake, 12; 26 ya 19, ya Malothi, wanawe na ndugu zake, 12; 27 ya 20, ya Eliatha, wanawe na ndugu zake, 12; 28 ya 21, ya Hothiri, wanawe na ndugu zake, 12; 29 ya 22, ya Gidalti, wanawe na ndugu zake, 12; 30 ya 23, ya Mahaziothi,+ wanawe na ndugu zake, 12; 31 ya 24, ya Romamti-ezeri,+ wanawe na ndugu zake, 12.
26 Kwa ajili ya migawanyo ya watunza-malango:+ Wa Wakora,+ Meshelemia+ mwana wa Kore wa wana wa Asafu. 2 Na Meshelemia alikuwa na wana: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne, 3 Elamu wa tano, Yehohanani wa sita, Elieho-enai wa saba. 4 Na Obed-edomu+ alikuwa na wana: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu na Sakari wa nne na Nethaneli wa tano, 5 Amieli wa sita, Isakari wa saba, Peulethai wa nane; kwa maana Mungu alikuwa amembariki.+
6 Naye Shemaya mwana wake alizaa wana waliokuwa watawala wa nyumba ya baba yao, kwa kuwa walikuwa wanaume wenye uwezo, wenye nguvu. 7 Wana wa Shemaya, Othni na Refaeli na Obedi, Elzabadi, ambaye ndugu zake walikuwa wanaume wenye uwezo, Elihu na Semakia. 8 Hawa wote ndio waliokuwa wa wana wa Obed-edomu, wao na wana wao na ndugu zao, wanaume wenye uwezo na wenye mamlaka kwa ajili ya utumishi, 62 wa Obed-edomu. 9 Na Meshelemia+ alikuwa na wana na ndugu, wanaume wenye uwezo, kumi na wanane. 10 Na Hosa wa wana wa Merari alikuwa na wana. Shimri ndiye aliyekuwa kichwa, kwa maana hakuwa mzaliwa wa kwanza+ lakini baba yake akamweka kuwa kichwa;+ 11 Hilkia wa pili, Tebalia wa tatu, Zekaria wa nne. Wana wote na ndugu za Hosa walikuwa kumi na watatu.
12 Kati ya hii migawanyo ya watunza-malango, wanaume walio vichwa walikuwa na kazi sawasawa na ndugu zao walivyokuwa nayo,+ kuhudumu katika nyumba ya Yehova. 13 Basi wakapiga kura+ kwa ajili ya mdogo sawasawa na kwa mkubwa kulingana na nyumba za ukoo wa upande wa baba+ zao, kwa ajili ya malango mbalimbali. 14 Ndipo kura ya upande wa mashariki ikamwangukia Shelemia.+ Kwa ajili ya Zekaria+ mwana wake, mshauri+ mwenye busara, walipiga kura, na kura yake ikawa upande wa kaskazini.+ 15 Obed-edomu akawa na yake upande wa kusini, na wanawe+ wakawa na maghala.+ 16 Shupimu na Hosa+ wakawa na yao upande wa magharibi karibu na Lango la Shalekethi kando ya njia kuu inayopanda kwenda juu, kikundi cha ulinzi+ kikilingana na kikundi cha ulinzi;+ 17 upande wa mashariki kulikuwa na Walawi sita; upande wa kaskazini kila siku, wanne; upande wa kusini kila siku,+ wanne; na kwa ajili ya maghala,+ wawili wawili; 18 kwa ajili ya roshani upande wa magharibi, wanne kando ya njia kuu,+ wawili kwenye roshani. 19 Hiyo ilikuwa migawanyo ya watunza-malango ya wana wa Wakora+ na ya wana wa Merari.+
20 Kwa habari ya Walawi, Ahiya alikuwa juu ya hazina+ za nyumba ya Mungu wa kweli na juu ya hazina za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu.+ 21 Wana wa Ladani,+ wana wa Mgershoni wa Ladani; walio vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba wa Ladani Mgershoni, Yehieli.+ 22 Wana wa Yehieli, Zethamu na Yoeli+ ndugu yake, walikuwa juu ya hazina+ za nyumba ya Yehova. 23 Kwa ajili ya Waamramu, kwa ajili ya Waishari, kwa ajili ya Wahebroni, kwa ajili ya Wauzieli,+ 24 hata Shebueli+ mwana wa Gershomu mwana wa Musa alikuwa kiongozi juu ya maghala. 25 Kwa habari ya ndugu zake, wa Eliezeri+ kulikuwa na Rehabia+ mwana wake na Yeshaya mwana wake na Yoramu mwana wake na Zikri mwana wake na Shelomothi mwana wake. 26 Huyu Shelomothi na ndugu zake walikuwa juu ya hazina zote za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu,+ ambavyo Daudi+ mfalme na walio vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba,+ na wakuu wa maelfu na wa mamia, na wakuu wa jeshi walikuwa wamevifanya kuwa vitakatifu. 27 Walikuwa wamefanya vitu kuwa vitakatifu kutoka katika vita+ na kutoka katika nyara+ ili kuidumisha nyumba ya Yehova. 28 Na pia vyote ambavyo Samweli mwonaji+ na Sauli mwana wa Kishi na Abneri+ mwana wa Neri na Yoabu+ mwana wa Seruya+ walikuwa wamevifanya kuwa vitakatifu. Chochote ambacho mtu alikifanya kuwa kitakatifu kilikuwa chini ya Shelomithi na ndugu zake.
29 Wa Waishari,+ Kenania na wanawe walikuwa kwa ajili ya shughuli za nje+ wakiwa maofisa na waamuzi+ juu ya Israeli.
30 Wa Wahebroni,+ Hashabia na ndugu zake, wanaume wenye uwezo,+ elfu moja na mia saba, walikuwa juu ya usimamizi wa Israeli katika eneo la Yordani upande wa magharibi kwa ajili ya kazi yote ya Yehova na kwa ajili ya utumishi wa mfalme. 31 Wa Wahebroni, Yeriya+ alikuwa kichwa cha Wahebroni kulingana na vizazi vyao kulingana na mababu zao. Walitafutwa katika mwaka wa 40+ wa ufalme wa Daudi, nao mashujaa, wanaume wenye nguvu wakapatikana kati yao huko Yazeri+ katika Gileadi.+ 32 Na ndugu zake, wanaume wenye uwezo,+ walikuwa elfu mbili na mia saba, walio vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba.+ Basi Daudi mfalme akawapa mgawo kuwa juu ya Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Wamanase,+ kwa ajili ya kila jambo la Mungu wa kweli na jambo+ la mfalme.
27 Kwa habari ya wana wa Israeli kulingana na hesabu yao, walio vichwa vya nyumba za ukoo wa upande wa baba+ na wakuu+ wa maelfu na wa mamia+ na maofisa wao waliomhudumia+ mfalme katika kila jambo la ile migawanyo ya wale walioingia na kutoka mwezi kwa mwezi kwa miezi yote ya mwaka, katika kila mgawanyo kulikuwa na watu 24,000.
2 Juu ya mgawanyo wa kwanza wa mwezi wa kwanza kulikuwa na Yashobeamu+ mwana wa Zabdieli, na katika mgawanyo wake kulikuwa na watu 24,000. 3 Baadhi ya wana wa Perezi+ aliye kichwa cha wakuu wote wa vikundi vya utumishi walikuwa kwa ajili ya mwezi wa kwanza. 4 Na juu ya mgawanyo wa mwezi wa pili kulikuwa na Dodai+ Mwahohi+ na mgawanyo wake, na Miklothi ndiye aliyekuwa kiongozi, na katika mgawanyo wake kulikuwa na watu 24,000. 5 Mkuu wa kikundi cha tatu cha utumishi kwa ajili ya mwezi wa tatu alikuwa ni Benaya+ mwana wa Yehoyada+ mkuu wa makuhani, na katika mgawanyo wake kulikuwa na watu 24,000. 6 Huyo Benaya+ alikuwa mwanamume mwenye nguvu wa wale 30+ na juu ya wale 30; na juu ya mgawanyo wake kulikuwa na Amizabadi mwana wake. 7 Wa nne kwa ajili ya mwezi wa nne alikuwa Asaheli,+ ndugu ya Yoabu,+ na Zebadia mwana wake baada yake, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 8 Mkuu wa tano kwa ajili ya mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi+ Mwizrahia, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 9 Wa sita kwa ajili ya mwezi wa sita alikuwa Ira+ mwana wa Ikeshi+ Mtekoa,+ na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 10 Wa saba kwa ajili ya mwezi wa saba alikuwa Helezi+ Mpeloni,+ wa wana wa Efraimu, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 11 Wa nane kwa ajili ya mwezi wa nane alikuwa Sibekai+ Mhusha wa Wazera,+ na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 12 Wa tisa kwa ajili ya mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri+ Mwanathothi+ wa Wabenyamini, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 13 Wa kumi kwa ajili ya mwezi wa kumi alikuwa Maharai+ Mnetofa wa Wazera,+ na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 14 Wa kumi na moja kwa ajili ya mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya+ Mpirathoni wa wana wa Efraimu,+ na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000. 15 Wa kumi na mbili kwa ajili ya mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai+ Mnetofa, wa Othnieli, na katika mgawanyo wake walikuwa 24,000.
16 Na juu ya makabila ya Israeli,+ wa Warubeni, Eliezeri mwana wa Zikri ndiye aliyekuwa kiongozi; wa Wasimeoni, Shefatia mwana wa Maaka; 17 wa Lawi, Hashabia mwana wa Kemueli; wa Haruni, Sadoki;+ 18 wa Yuda, Elihu,+ mmoja wa ndugu za Daudi;+ wa Isakari, Omri mwana wa Mikaeli; 19 wa Zabuloni, Ishmaya mwana wa Obadia; wa Naftali, Yerimothi mwana wa Azrieli; 20 wa wana wa Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia; wa nusu ya kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaya; 21 wa nusu ya kabila la Manase katika Gileadi, Ido mwana wa Zekaria; wa Benyamini, Yaasieli mwana wa Abneri;+ 22 wa Dani, Azareli mwana wa Yerohamu. Hao walikuwa wakuu+ wa makabila ya Israeli.
23 Na Daudi hakuhesabu wale waliokuwa na umri wa miaka 20 kurudi chini, kwa sababu Yehova alikuwa ameahidi kufanya Israeli kuwa wengi kama nyota za mbinguni.+ 24 Yoabu+ mwana wa Seruya alikuwa ameanza kuhesabu, lakini hakumaliza;+ na kwa sababu hiyo kukawa na ghadhabu+ juu ya Israeli, na hesabu hiyo haikuwekwa katika hesabu ya mambo ya siku za Mfalme Daudi.
25 Na juu ya hazina za mfalme+ kulikuwa na Azmavethi mwana wa Adieli. Na juu ya hazina katika shamba,+ katika majiji+ na katika vijiji na katika minara kulikuwa na Yonathani mwana wa Uzia. 26 Na juu ya wafanyakazi shambani,+ kwa ajili ya kulima udongo, kulikuwa na Ezri mwana wa Kelubu. 27 Na juu ya mashamba ya mizabibu+ kulikuwa na Shimei Mrama; na juu ya vitu vilivyokuwa katika mashamba ya mizabibu kwa ajili ya akiba za divai kulikuwa na Zabdi Mshifi. 28 Na juu ya mashamba ya mizeituni na mikuyu+ iliyokuwa katika Shefela+ kulikuwa na Baal-hanani Mgederi; na juu ya akiba ya mafuta+ kulikuwa na Yoashi. 29 Na juu ya mifugo iliyokuwa ikilisha katika Sharoni+ kulikuwa na Shitrai Msharoni; na juu ya mifugo katika nchi tambarare za chini kulikuwa na Shafati mwana wa Adlai. 30 Na juu ya ngamia+ kulikuwa na Obili Mwishmaeli;+ na juu ya punda-jike kulikuwa na Yehdeya Mmeronothi. 31 Na juu ya makundi kulikuwa na Yazizi Mhagri. Hao wote ndio waliokuwa wakuu wa mali za Mfalme Daudi.
32 Na Yonathani,+ mpwa wa Daudi, alikuwa mshauri, mwanamume mwenye uelewaji,+ naye alikuwa mwandishi pia; na Yehieli mwana wa Hakmoni+ alikuwa pamoja na wana wa mfalme.+ 33 Na Ahithofeli+ alikuwa mshauri+ wa mfalme; na Hushai+ Mwarki,+ alikuwa rafiki ya mfalme.+ 34 Na baada ya Ahithofeli kulikuwa na Yehoyada mwana wa Benaya+ na Abiathari;+ na Yoabu+ alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.
28 Na Daudi akakusanya katika Yerusalemu wakuu+ wote wa Israeli, wakuu+ wa makabila na wakuu+ wa migawanyo ya wale wanaomhudumia mfalme na wakuu wa maelfu+ na wakuu wa mamia+ na wakuu wa mali+ zote na mifugo+ ya mfalme na wa wanawe,+ pamoja na maofisa wa makao+ ya mfalme na wanaume wenye nguvu,+ kila mwanamume shujaa, mwenye nguvu. 2 Kisha Daudi mfalme akasimama kwa miguu yake na kusema:
“Nisikilizeni, ndugu zangu na watu wangu. Nilitaka sana moyoni mwangu+ kujenga nyumba ya kupumzika kwa ajili ya sanduku la agano la Yehova na kama kiti cha miguu+ cha Mungu wetu, nami nikawa nimefanya matayarisho ya kujenga.+ 3 Naye Mungu wa kweli akaniambia, ‘Hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu;+ kwa maana wewe ni mtu wa vita, nawe umemwaga damu.’+ 4 Basi Yehova, Mungu wa Israeli, alinichagua mimi kutoka katika nyumba yote ya baba yangu+ niwe mfalme+ juu ya Israeli mpaka wakati usio na kipimo; kwa maana alimchagua Yuda awe kiongozi,+ na katika nyumba ya Yuda aliichagua nyumba ya baba yangu,+ na kati ya wana wa baba yangu,+ alinikubali mimi,+ ili kunifanya niwe mfalme juu ya Israeli yote; 5 na kati ya wanangu wote (kwa maana wana ambao Yehova amenipa ni wengi)+ ndipo akamchagua Sulemani+ mwanangu aketi kwenye kiti cha ufalme+ wa Yehova juu ya Israeli.
6 “Tena akaniambia, ‘Sulemani mwana wako ndiye atakayejenga nyumba yangu+ na nyua zangu; kwa maana nimemchagua yeye kuwa mwanangu,+ nami nitakuwa baba yake.+ 7 Nami kwa hakika nitaufanya imara ufalme wake+ mpaka wakati usio na kipimo ikiwa ataazimia kwa nguvu kushika amri+ zangu na maamuzi yangu ya hukumu,+ kama ilivyo leo hii.’ 8 Na sasa, mbele ya macho ya Israeli wote, kutaniko la Yehova,+ na masikioni pa Mungu wetu,+ iweni waangalifu na mtafute amri zote za Yehova, Mungu wenu, ili mpate kuimiliki nchi hii nzuri,+ na mpate kuipitisha kuwa urithi kwa wana wenu baada yenu mpaka wakati usio na kipimo.
9 “Nawe, Sulemani mwanangu, mjue+ Mungu wa baba yako, umtumikie+ kwa moyo kamili+ na kwa nafsi yenye shangwe;+ kwa maana Yehova anaichunguza mioyo yote,+ naye anatambua kila mwelekeo wa fikira.+ Ukimtafuta, ataacha umpate;+ lakini ukimwacha,+ atakutupa mbali milele.+ 10 Ona, sasa, kwa maana Yehova mwenyewe amekuchagua wewe ujenge nyumba iwe patakatifu. Uwe hodari na utende.”+
11 Na Daudi akampa Sulemani mwana wake ramani ya ujenzi+ wa ukumbi+ na ya nyumba zake na ya maghala+ yake na madari+ yake na ya vyumba vyake vya ndani vyenye giza na nyumba ya kifuniko cha upatanisho;+ 12 ile ramani ya ujenzi ya kila kitu aliyoipata kwa kuongozwa na roho+ kwa ajili ya nyua+ za nyumba ya Yehova na ya vyumba vyote vya kulia chakula+ pande zote, ya hazina za nyumba ya Mungu wa kweli na ya hazina za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu;+ 13 na kwa ajili ya migawanyo+ ya makuhani na ya Walawi na kwa ajili ya kazi zote za utumishi wa nyumba ya Yehova na ya vyombo vyote vya utumishi wa nyumba ya Yehova; 14 ya dhahabu kulingana na uzito, dhahabu kwa ajili ya vyombo vyote vya utumishi mbalimbali, ya vyombo vyote vya fedha kulingana na uzito, ya vyombo+ vyote vya utumishi mbalimbali; 15 na uzito kwa ajili ya vinara vya taa+ vya dhahabu na taa zake za dhahabu, kulingana na uzito wa vinara mbalimbali vya taa na taa zake, na ya vinara vya fedha kulingana na uzito wa kinara cha taa na taa zake kulingana na utumishi wa vinara mbalimbali vya taa; 16 na dhahabu kulingana na uzito kwa ajili ya meza za mkate wa tabaka,+ kwa ajili ya meza mbalimbali, na fedha kwa ajili ya meza za fedha; 17 na nyuma na mabakuli+ na mitungi ya dhahabu safi, na ya mabakuli madogo ya dhahabu+ kulingana na uzito wa mabakuli madogo mbalimbali, na ya mabakuli madogo ya fedha kulingana na uzito wa mabakuli madogo mbalimbali; 18 na kwa madhabahu ya uvumba+ dhahabu safi kulingana na uzito na kwa ajili ya mfano wa gari,+ yaani, wale makerubi+ wa dhahabu kwa ajili ya kutandaza mabawa yao na kusitiri sanduku la agano la Yehova. 19 “Alitoa ufahamu kwa ajili ya kitu hicho chote kwa njia ya maandishi+ kutoka kwa mkono wa Yehova juu yangu, kwa ajili ya kazi zote za ile ramani ya ujenzi.”+
20 Naye Daudi akaendelea kumwambia Sulemani mwana wake: “Uwe hodari+ na mwenye nguvu nawe utende. Usiogope+ wala usiwe na hofu,+ kwa maana Yehova Mungu, Mungu wangu, yuko pamoja nawe.+ Hatakutupa+ wala kukuacha mpaka itakapomalizika kazi yote ya utumishi wa nyumba ya Yehova. 21 Na tazama, hii ndiyo migawanyo ya makuhani+ na ya Walawi+ kwa ajili ya utumishi wote wa nyumba ya Mungu wa kweli; na kila mtu ambaye ni mwenye kupenda+ na mwenye ustadi kwa ajili ya utumishi+ wote yuko pamoja nawe katika kazi yote, na pia wakuu+ na watu wote, kwa ajili ya maneno yako yote.”
29 Basi Daudi mfalme akaliambia kutaniko lote:+ “Sulemani mwanangu, ambaye Mungu amemchagua,+ ni mchanga+ na mwororo, lakini kazi ni kubwa; kwa kuwa jumba hilo la kifalme si la mwanadamu,+ bali ni la Yehova Mungu. 2 Nami kulingana na nguvu zangu zote,+ nimetayarisha+ kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu dhahabu+ kwa ajili ya kazi ya dhahabu, na fedha kwa ajili ya kazi ya fedha, na shaba kwa ajili ya kazi ya shaba, chuma+ kwa ajili ya kazi ya chuma, na mbao+ kwa ajili ya kazi ya mbao; mawe ya shohamu,+ na mawe ya kupangwa kwa saruji ngumu, na mawe maridadi ya mviringo, na kila jiwe la thamani, na mawe ya alabasta kwa wingi sana. 3 Na kwa kuwa ninapendezwa+ na nyumba ya Mungu wangu, bado kuna mali yangu ya pekee,+ dhahabu na fedha; naitoa kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu, kuongezea vyote ambavyo nimetayarisha kwa ajili ya hiyo nyumba takatifu:+ 4 talanta elfu tatu za dhahabu, za dhahabu ya Ofiri,+ na talanta elfu saba za fedha iliyosafishwa, kwa ajili ya kufunika kuta za hizo nyumba; 5 za dhahabu kwa ajili ya kazi ya dhahabu, na za fedha kwa ajili ya kazi ya fedha na kwa ajili ya kazi yote ya kufanywa kwa mkono wa mafundi. Na ni nani anayejitolea kuujaza mkono wake leo kwa zawadi kwa ajili ya Yehova?”+
6 Na wakuu+ wa nyumba za ukoo wa baba+ na wakuu+ wa makabila ya Israeli na wakuu wa maelfu+ na wa mamia+ na wakuu wa shughuli+ za mfalme wakajitolea. 7 Basi wakatoa kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli dhahabu yenye thamani ya talanta elfu tano na dariki elfu kumi na fedha yenye thamani ya talanta elfu kumi na shaba yenye thamani ya talanta kumi na nane elfu na chuma yenye thamani ya talanta mia moja elfu.+ 8 Na watu wowote waliokuwa na mawe yoyote wakayatoa kwa ajili ya hazina ya nyumba ya Yehova chini ya amri ya Yehieli+ Mgershoni.+ 9 Na watu wakashangilia kutokana na matoleo yao ya hiari waliyotoa, kwa maana walimtolea Yehova matoleo ya hiari kwa moyo kamili;+ na hata Daudi mfalme akashangilia kwa shangwe kubwa.+
10 Basi Daudi akambariki+ Yehova mbele ya macho ya kutaniko+ lote na Daudi akasema: “Na ubarikiwe,+ Ee Yehova, Mungu wa Israeli+ baba yetu, kutoka wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo. 11 Ee Yehova, ukuu+ ni wako na nguvu+ na uzuri+ na utukufu+ na heshima;+ kwa maana kila kitu mbinguni na duniani ni chako.+ Ufalme+ ni wako, Ee Yehova, Wewe unayejiinua kuwa kichwa juu ya wote.+ 12 Utajiri+ na utukufu+ hutokana na wewe, nawe unatawala+ kila kitu; na mkononi mwako mna nguvu+ na uwezo,+ na mkononi mwako mna uwezo wa kufanya kuwa na ukuu+ na kuwapa wote nguvu.+ 13 Na sasa, Ee Mungu wetu, tunakushukuru+ na kulisifu+ jina lako zuri.+
14 “Ingawa hivyo, mimi ni nani,+ na watu wangu ni nani, hata tuwe na nguvu za kutoa matoleo ya hiari hivi?+ Kwa maana kila kitu hutoka kwako,+ nasi tumekupa kutoka katika mkono wako mwenyewe. 15 Kwa maana sisi ni wakaaji wageni mbele zako na wahamiaji+ sawa na mababu zetu. Siku zetu duniani+ ni kama kivuli wala hakuna tumaini. 16 Ee Yehova, Mungu wetu, wingi huu wote ambao tumetayarisha ili kukujengea nyumba kwa ajili ya jina lako takatifu, umetoka mkononi mwako, nao wote ni mali yako.+ 17 Nami ninajua vema, Ee Mungu wangu, kwamba wewe ni mchunguzaji wa moyo,+ nawe unafurahia unyoofu.+ Nami katika unyoofu wa moyo wangu, nimetoa kwa hiari vitu hivi vyote, na sasa watu wako waliopo hapa nimefurahi kuona wakikutolea matoleo kwa hiari. 18 Ee Yehova, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli mababu zetu,+ shika hili mpaka wakati usio na kipimo kama mwelekeo wa fikira za moyo wa watu wako,+ na uelekeze moyo wao kwako.+ 19 Na Sulemani mwanangu umpe moyo kamili+ ili ashike amri+ zako, shuhuda+ zako na masharti+ yako, afanye kila jambo, na kulijenga jumba+ hili la kifalme ambalo nimelifanyia matayarisho.”+
20 Na Daudi akaendelea kuliambia kutaniko lote:+ “Sasa mbarikini+ Yehova, Mungu wenu.” Nalo kutaniko lote wakambariki Yehova, Mungu wa mababu zao, wakainama+ na kumsujudia+ Yehova na mfalme. 21 Nao wakaendelea kutoa dhabihu+ kwa Yehova na kutoa matoleo ya kuteketezwa+ kwa Yehova siku ya pili yake, ng’ombe-dume wachanga elfu moja, kondoo-dume elfu moja, wana-kondoo dume elfu moja na matoleo yao ya kinywaji,+ dhabihu nyingi sana kwa ajili ya Israeli wote.+ 22 Nao wakaendelea kula na kunywa mbele za Yehova siku hiyo kwa shangwe kubwa;+ nao kwa mara ya pili wakamfanya Sulemani mwana wa Daudi kuwa mfalme,+ wakamtia mafuta kwa Yehova awe kiongozi+ na pia Sadoki+ awe kuhani. 23 Na Sulemani akaanza kuketi juu ya kiti cha ufalme cha Yehova+ akiwa mfalme mahali pa Daudi baba yake, akafanikiwa,+ na Israeli wote walikuwa wakimtii. 24 Nao wakuu+ wote na wanaume wenye nguvu+ na pia wana wote wa Mfalme Daudi,+ wakajitiisha kwa Sulemani mfalme. 25 Na Yehova akaendelea kumfanya Sulemani kuwa mkuu zaidi+ mbele ya macho ya Israeli wote na kuweka juu yake heshima ya kifalme ambayo haikuwa imepata kuwa juu ya mfalme yeyote kabla yake juu ya Israeli.+
26 Naye Daudi mwana wa Yese, akatawala juu ya Israeli yote;+ 27 na siku alizotawala juu ya Israeli zilikuwa miaka 40.+ Katika Hebroni alitawala miaka 7,+ na katika Yerusalemu alitawala miaka 33.+ 28 Mwishowe akafa mwenye umri mwema wa uzeeni,+ ameshiba siku, utajiri+ na utukufu;+ na Sulemani mwana wake akaanza kutawala mahali pake.+ 29 Na mambo ya Daudi mfalme, ya kwanza na ya mwisho, yameandikwa katika maneno ya Samweli mwonaji+ na katika maneno ya nabii Nathani+ na katika maneno ya Gadi+ mwonaji, 30 pamoja na ufalme wake wote na nguvu zake na nyakati+ ambazo zilikuwa zimepita juu yake na juu ya Israeli na juu ya falme zote za nchi.+