Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 2 Wafalme 1:1-25:30
  • Kitabu cha Pili cha Wafalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitabu cha Pili cha Wafalme
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Kitabu cha Pili cha Wafalme

Kitabu cha Pili cha Wafalme

au, kulingana na Septuajinti ya Kigiriki, KITABU CHA NNE CHA WAFALME

1 Na Moabu+ wakaanza kuiasi+ Israeli baada ya kifo cha Ahabu.+

2 Kisha Ahazia akaanguka chini+ kupitia tundu lililo katika chumba chake cha darini+ kilichokuwa katika Samaria, naye akawa mgonjwa. Kwa hiyo akatuma wajumbe, akawaambia: “Nendeni, muulizeni+ Baal-zebubu+ mungu wa Ekroni+ ikiwa nitapona ugonjwa huu.”+ 3 Naye malaika+ wa Yehova akamwambia Eliya, Mtishbi:+ “Ondoka, nenda ukutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaambie, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu+ kabisa katika Israeli ndipo mnaenda kumuuliza Baal-zebubu mungu wa Ekroni? 4 Kwa hiyo basi Yehova amesema hivi: “Hutashuka kutoka katika kitanda ulichopanda, kwa sababu utakufa hakika.”’”+ Kisha Eliya akaenda zake.

5 Wale wajumbe waliporudi kwake, akawaambia mara moja: “Kwa nini mmerudi?” 6 Basi wakamwambia: “Pana mtu aliyekuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Nendeni, rudini kwa mfalme aliyewatuma, nanyi mkamwambie: “Yehova amesema hivi,+ ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu kabisa katika Israeli ndipo unatuma watu kumuuliza Baal-zebubu mungu wa Ekroni? Kwa hiyo, hutashuka kutoka katika kitanda ulichopanda, kwa sababu utakufa hakika.’”’”+ 7 Kwa hiyo akawaambia: “Yule mtu aliyekuja kukutana nanyi na kisha akasema nanyi maneno haya alikuwa na sura gani?” 8 Basi wakamwambia: “Alikuwa mtu mwenye vazi la manyoya,+ na mshipi wa ngozi umefungwa kiunoni mwake.”+ Mara moja akasema: “Alikuwa Eliya, Mtishbi.”

9 Naye akatuma kwake mkuu wa 50 akiwa na 50 wake.+ Alipopanda kwake, tazama, alikuwa ameketi juu ya kilele cha mlima. Basi akamwambia: “Ewe mtu wa Mungu wa kweli,+ mfalme amesema, ‘Shuka.’” 10 Lakini Eliya akajibu na kumwambia yule mkuu wa 50: “Naam, ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto+ na ushuke kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na 50 wako.” Na moto ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na wale 50 wake.+

11 Kwa hiyo akatuma tena mkuu mwingine wa 50 akiwa na 50 wake.+ Naye akajibu na kumwambia: “Ewe mtu wa Mungu wa kweli, mfalme amesema hivi, ‘Shuka haraka.’”+ 12 Lakini Eliya akajibu na kuwaambia: “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu wa kweli, moto na ushuke kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na 50 wako.” Na moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na wale 50 wake.

13 Naye akatuma tena mkuu wa tatu wa 50 akiwa na 50 wake.+ Lakini yule mkuu wa tatu wa 50 akapanda, akaja na kupiga magoti+ mbele ya Eliya, akaanza kumwomba+ kibali kwa bidii na kumwambia: “Ewe mtu wa Mungu wa kweli, tafadhali acha nafsi+ yangu na nafsi ya hawa watumishi wako 50 iwe na thamani+ machoni pako. 14 Tazama, moto ulishuka kutoka mbinguni, ukawateketeza+ wale wakuu wawili wa kwanza wa 50 na wale 50 wao, lakini sasa acha nafsi yangu iwe na thamani machoni pako.”

15 Ndipo malaika wa Yehova akamwambia Eliya: “Shuka, uende pamoja naye. Usiogope kwa sababu yake.”+ Basi akasimama, akashuka na kwenda pamoja naye kwa mfalme. 16 Kisha akamwambia: “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu umewatuma wajumbe+ kumuuliza Baal-zebubu mungu wa Ekroni,+ je, ni kwa sababu hakuna Mungu kabisa katika Israeli wa kuuliza neno lake? Basi hutashuka kutoka katika kitanda ambacho umepanda, kwa maana utakufa hakika.’” 17 Naye akafa mwishowe,+ kulingana na neno+ la Yehova alilosema Eliya; na Yehoramu+ akaanza kutawala mahali pake, katika mwaka wa pili wa Yehoramu+ mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, kwa sababu hakuwa amepata mwana.

18 Na mambo mengine ya Ahazia+ aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli?

2 Na ikawa kwamba Yehova alipokuwa karibu kumchukua Eliya+ katika dhoruba ya upepo kwenda juu kuelekea mbinguni,+ Eliya na Elisha+ wakaondoka Gilgali.+ 2 Na Eliya akaanza kumwambia Elisha: “Keti hapa, tafadhali, kwa sababu Yehova amenituma niende mpaka Betheli.” Lakini Elisha akasema: “Kama Yehova anavyoishi+ na kama nafsi yako inavyoishi,+ mimi sitakuacha.”+ Basi wakashuka kwenda Betheli.+ 3 Ndipo wana wa manabii+ waliokuwa katika Betheli wakamjia Elisha na kumwambia: “Je, kweli unajua kwamba leo Yehova anamchukua bwana wako asiwe kichwa juu yako?”+ Naye akasema: “Mimi pia najua vema jambo hilo.+ Kaeni kimya.”

4 Sasa Eliya akamwambia: “Elisha, tafadhali keti hapa, kwa sababu Yehova amenituma Yeriko.”+ Lakini yeye akasema: “Kama Yehova anavyoishi na kama nafsi yako inavyoishi, mimi sitakuacha.” Basi wakaenda mpaka Yeriko. 5 Ndipo wana wa manabii waliokuwa katika Yeriko wakamkaribia Elisha na kumwambia: “Je, kweli unajua kwamba leo Yehova anamchukua bwana wako asiwe kichwa juu yako?” Naye akasema: “Mimi pia najua vema jambo hilo. Kaeni kimya.”+

6 Sasa Eliya akamwambia: “Tafadhali, keti hapa, kwa sababu Yehova amenituma Yordani.”+ Lakini akasema: “Kama Yehova anavyoishi na kama nafsi yako inavyoishi, mimi sitakuacha.”+ Basi wote wawili wakaendelea mbele. 7 Na palikuwa na watu 50 wa wana wa manabii walioenda na kuendelea kusimama wakiwa umbali wa kuonekana;+ lakini wale wawili wakasimama kando ya Yordani. 8 Ndipo Eliya akachukua vazi lake rasmi,+ akalifunga, akapiga maji, nayo mwishowe yakagawanyika huku na huku, hivi kwamba wote wawili wakavuka juu ya nchi kavu.+

9 Na ikawa kwamba mara walipokuwa wamevuka, Eliya akamwambia Elisha: “Omba lile ninalopaswa kukutendea kabla sijachukuliwa kutoka kwako.”+ Naye Elisha akasema: “Tafadhali, sehemu mbili+ za roho+ yako zije kwangu.”+ 10 Kwa hiyo akasema: “Umeomba+ jambo gumu. Ukiniona wakati nitakapochukuliwa kutoka kwako, itakuwa hivyo kwako; lakini kama sivyo, haitakuwa hivyo.”

11 Na ikawa kwamba walipokuwa wanatembea, wakizungumza huku wakitembea, tazama! gari+ la vita lenye moto na farasi wenye moto, nao wakawatenganisha hao wawili; na Eliya akaanza kupanda katika ile dhoruba ya upepo kuelekea mbinguni.+ 12 Wakati huo wote Elisha alikuwa akiona jambo hilo, naye alikuwa analia hivi: “Baba yangu, baba+ yangu, gari la vita la Israeli na wapanda-farasi wake!”+ Naye hakumwona tena. Basi akachukua mavazi yake mwenyewe, akayararua vipande viwili.+ 13 Kisha akalichukua lile vazi+ rasmi la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwake, akarudi na kusimama kando ya ukingo wa Yordani. 14 Ndipo akachukua lile vazi rasmi la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwake, akayapiga yale maji+ na kusema: “Yuko wapi Yehova Mungu wa Eliya, naam, Yeye?”+ Alipoyapiga maji, ndipo mwishowe yakagawanyika huku na huku, hivi kwamba Elisha akavuka.

15 Wakati wana wa manabii waliokuwa katika Yeriko walipomwona akiwa umbali fulani, wakaanza kusema: “Roho+ ya Eliya imetua juu ya Elisha.” Basi wakaja kumpokea, wakamwinamia.+ 16 Nao wakamwambia: “Tazama, sasa, watumishi wako wanao wanaume 50 mashujaa. Tafadhali acha waende, wamtafute bwana wako. Labda roho+ ya Yehova imemwinua na kisha ikamtupa juu ya mmoja wa milima au katika moja la mabonde.” Lakini akasema: “Msiwatume.” 17 Nao wakaendelea kumsihi mpaka akaona haya, hivi kwamba akasema: “Watumeni.” Sasa wakawatuma watu 50; nao wakaendelea kutafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata. 18 Waliporudi kwake, alikuwa anakaa katika Yeriko.+ Ndipo akawaambia: “Je, sikuwaambia, ‘Msiende’?”

19 Baada ya muda watu wa jiji lile wakamwambia Elisha: “Tazama, mahali lilipo jiji hili ni pazuri,+ kama bwana wangu anavyoona; lakini maji+ ni mabaya, na nchi inasababisha mimba ziharibike.”+ 20 Kwa hiyo akasema: “Nileteeni bakuli dogo jipya, mweke chumvi ndani yake.” Basi wakalileta kwake. 21 Kisha akatoka na kwenda kwenye chemchemi ya yale maji, akatupa chumvi ndani yake+ na kusema: “Yehova amesema hivi, ‘Ninafanya maji haya kuwa yenye afya.+ Hayatatokeza tena kifo wala kuharibika mimba.’” 22 Na maji yale yangali yameponywa mpaka leo hii,+ kulingana na neno alilosema Elisha.

23 Naye akapanda kutoka hapo mpaka Betheli.+ Alipokuwa akipanda njiani, tazama, palikuwa na wavulana+ wadogo waliotoka katika jiji, nao wakaanza kumdhihaki,+ wakazidi kumwambia: “Nenda juu, wewe kipara!+ Nenda juu, wewe kipara!” 24 Mwishowe akageuka nyuma, akawaona, naye akawalaani+ katika jina la Yehova. Ndipo dubu-jike+ wawili wakatoka katika vichaka, wakaanza kuwararua vipande-vipande watoto 42 kati yao.+ 25 Naye akaendelea kutoka hapo mpaka Mlima Karmeli,+ na kutoka hapo akarudi Samaria.

3 Naye Yehoramu+ mwana wa Ahabu akawa mfalme juu ya Israeli katika Samaria mwaka wa kumi na nane wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, akaendelea kutawala miaka kumi na miwili. 2 Naye akaendelea kutenda yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ ila tu si kama baba yake+ wala kama mama yake, bali aliondoa nguzo takatifu+ ya Baali ambayo baba yake alikuwa ametengeneza.+ 3 Ila tu alishikamana na dhambi za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, ambazo kwa hizo alisababisha Israeli kutenda dhambi.+ Hakuziacha.

4 Naye Mesha+ mfalme wa Moabu akawa mfugaji wa kondoo, akamlipa mfalme wa Israeli wana-kondoo mia moja elfu na kondoo-dume mia moja elfu ambao hawajakatwa manyoya. 5 Na ikawa kwamba mara tu Ahabu alipokufa,+ mfalme wa Moabu akaanza kumwasi+ mfalme wa Israeli. 6 Basi Mfalme Yehoramu akaondoka Samaria siku hiyo, akawakusanya+ Israeli wote. 7 Tena akatuma kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda, akisema: “Mfalme wa Moabu ameniasi. Je, utaenda pamoja nami kuwapiga vita Moabu?” Naye akasema: “Nitaenda.+ Mimi ni sawa na wewe; watu wangu ni sawa na watu wako;+ farasi wangu ni sawa na farasi wako.” 8 Naye akaendelea kusema: “Je, tutapanda kupitia njia gani hasa?” Akasema: “Kupitia njia ya nyika ya Edomu.”+

9 Na mfalme wa Israeli na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu+ wakaenda, wakazidi kwenda kwa siku saba, na kukawa hakuna maji kwa ajili ya hiyo kambi na kwa ajili ya wanyama wa kufugwa waliokuwa wakifuata hatua zao. 10 Mwishowe mfalme wa Israeli akasema: “Ni jambo la kusikitisha kwamba Yehova amewakusanya wafalme hawa watatu ili kuwatia mkononi mwa Moabu!”+ 11 Kwa hiyo Yehoshafati akasema:+ “Je, hakuna nabii wa Yehova hapa?+ Basi na tumuulize Yehova kupitia yeye.”+ Na mmoja wa watumishi wa mfalme wa Israeli akajibu na kusema: “Pana Elisha+ mwana wa Shafati, aliyemimina maji juu ya mikono ya Eliya.”+ 12 Ndipo Yehoshafati akasema: “Huyu ana neno la Yehova.” Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati na mfalme wa Edomu wakashuka kwake.

13 Na Elisha akamwambia mfalme wa Israeli: “Nina nini nawe?+ Nenda kwa manabii+ wa baba yako na kwa manabii wa mama yako.” Lakini mfalme wa Israeli akamwambia: “Hapana, kwa maana Yehova amewaita wafalme hawa watatu ili kuwatia mkononi mwa Moabu.”+ 14 Naye Elisha akasema: “Kama anavyoishi Yehova wa majeshi+ ambaye ninasimama mbele zake, kama haingekuwa kwamba ninaufikiria uso wa Yehoshafati mfalme wa Yuda,+ nisingekutazama wala kukuona wewe.+ 15 Na sasa nileteeni mpiga-kinanda.”+ Na ikatukia kwamba mara tu yule mpiga-kinanda alipopiga, mkono+ wa Yehova ukawa juu yake. 16 Naye akaendelea kusema: “Yehova amesema hivi, ‘Hili bonde la mto lijazwe mitaro;+ 17 kwa maana Yehova amesema hivi: “Ninyi hamtaona upepo, wala kuona mvua kubwa; ingawa hivyo, lile bonde la mto litajazwa maji,+ nanyi mtakunywa kutoka ndani yake,+ ninyi na mifugo yenu na wanyama wenu wa kufugwa.”’ 18 Na hili kwa kweli litakuwa jambo dogo machoni pa Yehova,+ naye kwa hakika atatia Moabu mkononi mwenu.+ 19 Nanyi bomoeni kila jiji lenye ngome+ na kila jiji bora, mkauangushe+ kila mti mzuri,+ mkazibe mabubujiko yote ya maji, na kuiharibu kwa mawe kila sehemu nzuri ya shamba.”

20 Na ikawa kwamba asubuhi,+ wakati wa kutolewa kwa toleo la nafaka,+ tazama! maji yalikuwa yakija kutoka upande wa Edomu, nayo nchi ikajaa maji.

21 Nao Wamoabu wote wakasikia kwamba hao wafalme wamekuja kupigana nao. Kwa hiyo wakakusanya watu kutoka kati ya wote waliojifunga+ mshipi na kwenda juu, nao wakaanza kusimama mpakani. 22 Walipoamka asubuhi na mapema, jua likamulika juu ya yale maji, hivi kwamba Wamoabu kutoka upande wa pili wakaona yale maji kuwa ni mekundu kama damu. 23 Nao wakaanza kusema: “Hii ni damu! Hakika wafalme wale wamepigwa kwa upanga, nao wakaanza kupigana na kuuana. Basi, sasa, chukueni nyara,+ enyi Moabu!” 24 Walipoingia katika kambi ya Israeli,+ ndipo Waisraeli wakasimama mara moja, wakaanza kuwapiga Wamoabu hivi kwamba wakakimbia kutoka mbele yao.+ Basi wakaingia katika Moabu, wakiwapiga na kuwaua Wamoabu walipokuwa wakija. 25 Na yale majiji wakayabomoa,+ nao wakatupa kila mmoja jiwe lake na kujaza kila sehemu nzuri ya shamba; wakaziba kila bubujiko la maji,+ wakaangusha kila mti mzuri,+ mpaka wakaacha tu ndani yake mawe ya Kir-haresethi;+ na wapiga-kombeo wakaanza kulizunguka na kulipiga.

26 Mfalme wa Moabu alipoona kwamba pigano limekuwa na nguvu kumshinda, ndipo mara moja akachukua pamoja naye watu mia saba wenye kutumia upanga ili wapenye mpaka kwa mfalme wa Edomu;+ lakini hawakuweza. 27 Mwishowe akamchukua mwana wake mzaliwa wa kwanza ambaye angetawala mahali pake, akamtoa+ kuwa dhabihu ya kuteketezwa juu ya ukuta. Na pakawa na ghadhabu kubwa juu ya Israeli, hivi kwamba wakaondoka, wakamwacha na kurudi katika nchi yao.

4 Basi palikuwa na mwanamke fulani wa wake za wana+ wa manabii aliyemlilia Elisha, akisema: “Mtumishi wako, mume wangu, amekufa; nawe unajua vema kwamba mtumishi wako aliendelea kumwogopa+ Yehova, na mkopeshaji+ amekuja kuwachukua watoto wangu wawili wawe watumwa wake.” 2 Kwa hiyo Elisha akamwambia: “Nikufanyie nini?+ Niambie; una nini nyumbani?” Naye akasema: “Mjakazi wako hana chochote nyumbani ila mtungi wenye mdomo wa mafuta.”+ 3 Ndipo yeye akasema: “Nenda, ujiombee vyombo kutoka nje, kutoka kwa jirani zako wote, vyombo vitupu. Usijizuie kwa kuchukua vichache. 4 Nawe uende ufunge mlango nyuma yako na wana wako, nawe umimine katika vyombo hivyo vyote, na uweke kando vile vilivyojaa.” 5 Basi akaenda zake kutoka kwake.

Alipofunga mlango nyuma yake na wanawe, wakawa wakimletea karibu vile vyombo, naye akawa akimimina.+ 6 Na ikawa kwamba mara tu vyombo vile vilipojaa, akamwambia mwana wake: “Niletee karibu tena chombo kingine.”+ Lakini akamwambia: “Hakuna chombo kingine.” Ndipo yale mafuta yakakoma.+ 7 Kwa hiyo akaingia na kumwambia yule mtu wa Mungu wa kweli, naye sasa akasema: “Nenda, uza hayo mafuta ulipe madeni yako,+ nawe pamoja na wana wako mtaishi kwa kile kitakachobaki.”+

8 Na ikawa kwamba siku moja Elisha akapita kwenda Shunemu,+ palipokuwa na mwanamke mmoja mashuhuri, na mwanamke huyo akaanza kumshurutisha+ ale mkate. Na ikawa kwamba kila mara alipopita hapo, akawa akiingia hapo ili ale mkate. 9 Mwishowe akamwambia mume wake:+ “Tazama, sasa, najua vema kwamba ni mtu mtakatifu wa Mungu+ anayepita kwetu kila mara. 10 Tafadhali, acha tutengeneze chumba kidogo cha darini+ kwenye ukuta, tumwekee humo kitanda na meza na kiti na kinara cha taa;+ na itatukia kwamba kila mara anapoingia kwetu, anaweza kuingia humo.”+

11 Na ikawa kwamba siku moja kama kawaida yake, aliingia humo na kwenda katika kile chumba cha darini, akalala humo. 12 Basi akamwambia Gehazi+ mtumishi wake: “Mwite huyo mwanamke Mshunamu.”+ Kwa hiyo akamwita ili asimame mbele yake. 13 Kisha akamwambia huyo mtumishi wake: “Tafadhali, mwambie hivi, ‘Tazama, umejinyima kwa ajili yetu kwa kujinyima huku kote.+ Ufanyiwe nini?+ Je, kuna lolote la kusema kwa mfalme+ au kwa mkuu+ wa jeshi kwa ajili yako?’” Ndipo mwanamke huyo akasema: “Ninakaa kati ya watu wangu mwenyewe.”+ 14 Naye akaendelea kusema: “Kwa hiyo afanyiwe nini mwanamke huyu?” Sasa Gehazi akasema: “Kwa kweli, hana mwana,+ na mume wake ni mzee.” 15 Mara moja akasema: “Mwite.” Basi akamwita, naye akasimama mlangoni. 16 Kisha akasema: “Mwaka ujao wakati huu uliowekwa utakuwa unamkumbatia mwana.”+ Lakini mwanamke huyo akasema: “Hapana, bwana wangu, ewe mtu wa Mungu wa kweli! Usimwambie uwongo mjakazi wako.”

17 Hata hivyo, mwaka uliofuata, yule mwanamke akapata mimba akazaa mwana+ wakati huu uliowekwa, kama Elisha alivyokuwa amemwambia.+ 18 Na yule mtoto akaendelea kukua, halafu siku moja akaenda nje kama kawaida kwa baba yake pamoja na wavunaji.+ 19 Naye akaendelea kumwambia baba yake: “Kichwa changu, kichwa changu!”+ Mwishowe akamwambia mtumishi wake: “Mchukue, umpeleke kwa mama yake.”+ 20 Basi akamchukua, akampeleka kwa mama yake. Naye akaendelea kukaa juu ya magoti yake mpaka katikati ya mchana, na mwishowe akafa.+ 21 Ndipo akapanda, akamlaza juu ya kitanda+ cha yule mtu wa Mungu wa kweli,+ akamfungia mlango na kutoka nje. 22 Sasa akamwita mume wake na kusema: “Tafadhali, niletee mmoja wa watumishi na mmoja wa punda-jike, na acha nimkimbilie yule mtu wa Mungu wa kweli, kisha nirudi.”+ 23 Lakini mume wake akasema: “Kwa nini unaenda kwake leo? Si mwezi mpya+ wala sabato.” Hata hivyo akasema: “Ni sawa.” 24 Basi akamtandika yule punda-jike+ na kumwambia mtumishi wake: “Endesha punda, uende mbele. Kwa ajili yangu usiache kuendesha isipokuwa nikuambie hivyo.”

25 Naye akaenda, akafika kwa yule mtu wa Mungu wa kweli katika Mlima Karmeli. Na ikawa kwamba mara tu yule mtu wa Mungu wa kweli alipomwona kule mbele, mara moja akamwambia Gehazi mtumishi+ wake: “Tazama! ni yule mwanamke Mshunamu. 26 Tafadhali, sasa kimbia ili umpokee na kumwambia, ‘Je, wewe ni salama? Je, mume wako ni salama? Je, mtoto ni salama?’” Naye akasema: “Ni salama.” 27 Alipomjia yule mtu wa Mungu wa kweli katika mlima, mara moja akamshika miguu yake.+ Ndipo Gehazi akaja karibu ili amsukume aondoke,+ lakini mtu wa Mungu wa kweli+ akasema: “Mwache,+ kwa maana nafsi yake ina uchungu+ ndani yake; na Yehova amenificha+ jambo hilo wala hakuniambia.” 28 Sasa akasema: “Je, niliomba mwana kupitia kwa bwana wangu? Je, mimi sikusema, ‘Usiniongoze kwenye tumaini la uwongo’?”+

29 Mara moja akamwambia Gehazi:+ “Jifunge viuno+ vyako, uchukue fimbo+ yangu mkononi mwako, uende. Ukikutana na yeyote, usimsalimu;+ na yeyote akikusalimu, usimjibu. Nawe uitie fimbo yangu juu ya uso wa huyo mvulana.”+ 30 Kwa hiyo mama ya mvulana akasema: “Kama Yehova anavyoishi+ na kama nafsi yako inavyoishi,+ mimi sitakuacha.”+ Kwa hiyo akaondoka, akaenda pamoja naye. 31 Na Gehazi mwenyewe akaenda mbele yao, kisha akaitia fimbo juu ya uso wa yule mvulana, lakini hapakuwa na sauti yoyote wala majibu.+ Basi akarudi kumpokea na kumwambia: “Huyo mvulana hakuamka.”+

32 Mwishowe Elisha akaingia katika hiyo nyumba, na, tazama, huyo mvulana alikuwa amekufa, amelazwa juu ya kitanda chake.+ 33 Ndipo akaingia ndani, akafunga mlango nyuma yao wawili,+ akaanza kusali kwa Yehova.+ 34 Mwishowe akaenda juu, akajilaza juu ya yule mtoto,+ akakitia kinywa chake juu ya kinywa chake, na macho yake juu ya macho yake, na mikono yake juu ya mikono yake, akaendelea kuinama juu yake, na hatua kwa hatua mwili wa mtoto ukawa na joto. 35 Kisha akaanza kutembea tena ndani ya nyumba, mara moja huku mara moja kule, halafu akaenda juu, akainama juu yake. Na yule mvulana akaanza kupiga chafya mara saba, kisha mvulana huyo akafungua macho yake.+ 36 Sasa akamwita Gehazi na kusema: “Mwite huyo mwanamke Mshunamu.”+ Basi akamwita, naye akaingia kwake. Kisha akasema: “Mchukue mwana wako.”+ 37 Naye akaingia, akaanguka miguuni pake, akamwinamia mpaka chini,+ kisha akamchukua mwana wake, akatoka nje.+

38 Na Elisha mwenyewe akarudi Gilgali,+ na kulikuwa na njaa+ katika nchi. Baada ya muda, wana+ wa manabii walipokuwa wamekaa mbele yake,+ akamwambia mtumishi+ wake: “Tia kile chungu kikubwa cha kupikia, uwatokosee mchuzi wana wa manabii.”+ 39 Basi mtu fulani akatoka, akaenda shambani kuchuma miholi,+ naye akapata mzabibu-mwitu na kuchuma maboga kutoka huo, akajaza vazi lake, kisha akaja na kuyakatakata vipande ndani ya chungu cha mchuzi, kwa maana hawakuwa wanayafahamu. 40 Baadaye wakapakua ili watu wale. Na ikawa kwamba, mara tu walipoula ule mchuzi, wakalia na kuanza kusema: “Kuna kifo ndani ya chungu hiki,+ Ee mtu wa Mungu wa kweli.”+ Nao hawakuweza kula. 41 Kwa hiyo akasema: “Basi leteni unga.” Baada ya kuutupa ndani ya kile chungu, akaendelea kusema: “Wapakulieni watu ili wale.” Na hakuna chochote chenye kudhuru kilichokuwa ndani ya kile chungu.+

42 Na palikuwa na mtu aliyekuja kutoka Baal-shalisha,+ naye akamletea+ yule mtu wa Mungu wa kweli mkate wa matunda ya kwanza yaliyoiva,+ mikate 20 ya shayiri,+ na nafaka mpya katika mfuko wake wa mkate. Ndipo akasema: “Wape watu ili wale.”+ 43 Hata hivyo, mtu wake mwenye kumhudumia akasema: “Nitawekaje hiki mbele ya watu mia moja?”+ Naye akasema: “Wape watu ili wale, kwa maana Yehova amesema hivi, ‘Kitaliwa na kutakuwa na masalio.’”+ 44 Basi akakiweka mbele yao, nao wakaanza kula, nao wakawa na masalio kulingana na neno la Yehova.+

5 Basi mtu fulani Naamani,+ mkuu wa jeshi la mfalme wa Siria, alikuwa mwanamume mkuu mbele ya bwana wake naye aliheshimiwa, kwa sababu Yehova alikuwa amewapa Siria wokovu kupitia yeye;+ na mwanamume huyo alikuwa ni mwanamume shujaa, mwenye nguvu, ingawa alikuwa na ukoma. 2 Na Wasiria walikuwa wametoka wakiwa vikundi vya waporaji,+ nao wakamchukua mateka msichana mmoja mdogo+ kutoka katika nchi ya Israeli, naye akaja kuwa mbele ya mke wa Naamani. 3 Baada ya muda msichana huyo akamwambia+ bimkubwa wake: “Laiti bwana wangu angekuwa mbele ya nabii+ aliye katika Samaria! Hapo ndipo angemponya ukoma+ wake.” 4 Kwa hiyo mtu fulani akaenda, akampa bwana wake habari, na kusema: “Yule msichana anayetoka katika nchi ya Israeli alisema+ hivi na vile.”

5 Ndipo mfalme wa Siria akasema: “Anza safari! Haya njoo, nami nipeleke barua kwa mfalme wa Israeli.” Basi akaenda, akachukua mkononi+ mwake talanta kumi za fedha na vipande elfu sita vya dhahabu+ na mavazi+ kumi. 6 Naye akamletea mfalme wa Israeli ile barua,+ kusema: “Na sasa wakati barua hii inapokufikia, tazama, ninamtuma Naamani mtumishi wangu, ili umponye ukoma wake.” 7 Na ikawa kwamba mara tu mfalme wa Israeli aliposoma ile barua, mara moja akayararua+ mavazi yake na kusema: “Je, mimi ni Mungu,+ ili kuua au kuhifadhi hai?+ Kwa maana mtu huyu anatuma mtu kwangu ili nimponye ukoma wake; kwa maana angalieni, tafadhali, mwone jinsi anavyotafuta ugomvi nami.”+

8 Na ikawa kwamba mara tu Elisha mtu wa Mungu wa kweli aliposikia kwamba mfalme wa Israeli ameyararua mavazi yake,+ mara moja akatuma kwa mfalme, na kusema: “Kwa nini uliyararua mavazi yako? Tafadhali, mwache aje kwangu ili ajue kwamba kuna nabii katika Israeli.”+ 9 Basi Naamani akaja na farasi zake na magari yake ya vita, akasimama katika mlango wa nyumba ya Elisha. 10 Hata hivyo, Elisha akatuma mjumbe kwake, kusema: “Nenda kule, uoge+ mara saba+ katika Yordani ili nyama yako irudi kwako;+ na uwe safi.” 11 Ndipo Naamani akaudhika,+ akaanza kwenda zake na kusema: “Tazama, nilikuwa nimesema moyoni mwangu,+ ‘Atakuja nje kabisa kwangu na kwa hakika atasimama na kuliitia jina la Yehova Mungu wake, na kutikisa mkono wake huku na huku juu ya mahali pale, na kumponya mwenye ukoma.’ 12 Je, Abana na Farpari, mito ya Damasko,+ si bora kuliko maji+ yote ya Israeli? Je, siwezi kuoga ndani yake na kuwa safi?”+ Kwa hiyo akageuka, akaenda zake kwa ghadhabu.+

13 Sasa watumishi wake wakakaribia, wakamwambia: “Baba yangu,+ kama nabii angelikuambia jambo kubwa, je, wewe hungelifanya? Basi si zaidi, kwa kuwa alikuambia, ‘Oga, uwe safi’?” 14 Ndipo akashuka, akaanza kujitumbukiza katika Yordani mara saba kulingana na neno la yule mtu wa Mungu wa kweli;+ kisha nyama yake ikarudi kama nyama ya mvulana mdogo,+ naye akawa safi.+

15 Ndipo akarudi kwa yule mtu wa Mungu wa kweli,+ yeye na kambi yake yote, akaenda, akasimama mbele yake na kusema: “Tazama, sasa, hakika ninajua kwamba hakuna Mungu yeyote mahali pengine popote duniani isipokuwa katika Israeli.+ Na sasa, tafadhali pokea zawadi ya kubariki+ kutoka kwa mtumishi wako.” 16 Hata hivyo, yeye akasema: “Kama Yehova anavyoishi+ ambaye nimesimama mbele zake, sitaipokea.”+ Naye akaanza kumsihi aipokee, lakini akazidi kukataa. 17 Mwishowe Naamani akasema: “Tafadhali, kama sivyo, mtumishi wako na apewe udongo,+ mzigo wa nyumbu wawili; kwa sababu mtumishi wako hatatoa tena toleo la kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine yoyote isipokuwa kwa Yehova.+ 18 Katika jambo hili Yehova na amsamehe mtumishi wako: Bwana wangu atakapoingia katika nyumba ya Rimoni+ ili kuinama humo, naye anajiegemeza+ juu ya mkono wangu, nami nilazimike kuinama+ nyumbani mwa Rimoni, nitakapoinama nyumbani mwa Rimoni, tafadhali, Yehova na amsamehe mtumishi wako kwa habari hii.”+ 19 Naye akamwambia: “Nenda kwa amani.”+ Basi akaenda zake kutoka kwake kwa umbali mkubwa kutoka nchi hiyo.

20 Ndipo Gehazi+ mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu wa kweli+ akasema: “Tazama, bwana wangu amemwachilia Naamani,+ huyu Msiria kwa kutopokea mkononi mwake vitu alivyoleta. Kama Yehova anavyoishi,+ nitakimbia nimfuate, nichukue kitu fulani kutoka kwake.”+ 21 Na Gehazi akaanza kumfuatilia Naamani. Naamani alipoona mtu akikimbia nyuma yake, akashuka mara moja kutoka katika gari lake ili kumpokea, kisha akasema: “Je, ni salama?”+ 22 Naye akasema: “Ni salama. Bwana+ wangu amenituma,+ kusema, ‘Tazama! Vijana wawili wamenijia sasa hivi kutoka katika eneo lenye milima la Efraimu, kutoka kwa wana wa manabii.+ Tafadhali, wape talanta moja ya fedha na mavazi mawili.’”+ 23 Basi Naamani akasema: “Haya, chukua talanta mbili.” Naye akaendelea kumhimiza+ na mwishowe akafunga talanta mbili za fedha katika mifuko miwili, pamoja na mavazi mawili, akawapa watumishi wake wawili, ili wavibebe mbele yake.

24 Alipokuja Ofeli, akavichukua mara moja kutoka mkononi mwao, akaviweka nyumbani+ na kuwaacha wale watu waende zao. Basi wakaenda zao. 25 Naye mwenyewe akaingia na kusimama mbele ya bwana wake.+ Sasa Elisha akamwambia: “Umetoka wapi, Gehazi?” Lakini akasema: “Mtumishi wako hakwenda mahali popote hata kidogo.”+ 26 Ndipo akamwambia: “Je, moyo wangu haukukufuata wakati yule mtu alipogeuka na kushuka kutoka katika gari lake ili kukupokea? Je, ni wakati wa kupokea fedha au kupokea mavazi au mashamba ya mizeituni au ya mizabibu au kondoo au ng’ombe au watumishi wa kiume na wajakazi?+ 27 Basi ukoma+ wa Naamani utakushika wewe na uzao wako mpaka wakati usio na kipimo.”+ Mara moja akaondoka mbele yake, mwenye ukoma akiwa mweupe kama theluji.+

6 Na wana+ wa manabii wakaanza kumwambia Elisha: “Tazama, sasa! Mahali+ tunapokaa mbele yako ni padogo+ mno kwetu. 2 Tafadhali, acha twende mpaka Yordani, tuchukue kila mmoja wetu nguzo kutoka hapo, tujijengee+ hapo mahali pa kukaa.” Basi akasema: “Nendeni.” 3 Na mmoja wao akasema: “Njoo, tafadhali, uende pamoja na watumishi wako.” Basi akasema: “Mimi nitaenda.” 4 Kwa hiyo akaenda pamoja nao, na mwishowe wakafika Yordani, wakaanza kukata miti.+ 5 Na ikawa kwamba mtu fulani alikuwa akikata mti wake, na kichwa cha shoka+ kikaanguka majini. Naye akaanza kulia na kusema: “Ole wangu bwana wangu,+ kwa maana lilikuwa la kuazimwa!”+ 6 Ndipo yule mtu wa Mungu wa kweli akasema: “Kimeanguka wapi?” Basi akamwonyesha mahali pale. Akakata kipande cha mti mara moja, akakitupa hapo, akafanya kile kichwa cha shoka kielee.+ 7 Sasa akasema: “Kiinue.” Akanyoosha mkono wake mara moja, akakichukua.

8 Na mfalme wa Siria,+ kwa upande wake, akahusika katika vita juu ya Israeli. Basi akashauriana na watumishi wake,+ akisema: “Mtapiga kambi nami mahali fulani na fulani.”+ 9 Ndipo yule mtu wa Mungu wa kweli+ akatuma watu kwa mfalme wa Israeli, na kusema: “Jilinde usipitie mahali hapa,+ kwa sababu hapo ndipo Wasiria wanaposhukia.”+ 10 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akatuma watu mahali ambapo yule mtu wa Mungu wa kweli alikuwa amemwambia.+ Naye akamwonya,+ akakaa mbali na hapo, si mara moja wala mara mbili.

11 Basi moyo wa mfalme wa Siria ukawa na ghadhabu juu ya jambo hilo,+ kwa hiyo akawaita watumishi wake na kuwaambia: “Je, hamniambii ni nani kati ya walio wetu ambaye yuko upande wa mfalme wa Israeli?”+ 12 Ndipo mmoja wa watumishi wake akasema: “Hakuna yeyote, bwana wangu mfalme, lakini ni Elisha+ nabii aliye katika Israeli ndiye humwambia+ mfalme wa Israeli mambo ambayo wewe husema katika chumba chako cha kulala cha ndani.”+ 13 Kwa hiyo akasema: “Nendeni mwone mahali alipo, ili nitume watu kumchukua.”+ Baadaye akaletewa habari, kusema: “Tazama, yuko katika Dothani.”+ 14 Mara moja akapeleka huko farasi na magari ya vita na jeshi kubwa;+ nao wakaja wakati wa usiku na kulizunguka jiji lile.

15 Wakati mhudumu+ wa yule mtu wa Mungu wa kweli alipoamka asubuhi na mapema, akaenda nje, na, tazama, hapo jeshi lilikuwa limelizunguka jiji kwa farasi na magari ya vita. Mara moja mtumishi wake akamwambia: “Ole, bwana wangu!+ Tutafanya nini?” 16 Lakini yeye akasema: “Usiogope,+ kwa maana wale walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.”+ 17 Na Elisha akaanza kusali+ na kusema: “Ee Yehova, tafadhali fungua macho yake,+ ili aone.” Mara moja Yehova akafungua macho ya yule mtumishi, hivi kwamba akaona; na, tazama! lile eneo lenye milima lilikuwa limejaa farasi na magari ya vita+ ya moto kumzunguka Elisha pande zote.+

18 Walipoanza kushuka kumwendea, Elisha akaendelea kusali kwa Yehova na kusema: “Tafadhali, lipige taifa hili kwa upofu.”+ Basi yeye akawapiga kwa upofu kulingana na neno la Elisha. 19 Sasa Elisha akawaambia: “Hii siyo njia, na hili silo lile jiji. Nifuateni, na acheni niwaongoze kwa yule mtu mnayemtafuta.” Hata hivyo, akawaongoza kwenda Samaria.+

20 Na ikawa kwamba mara walipofika Samaria, ndipo Elisha akasema: “Ee Yehova, fungua macho yao ili waone.”+ Yehova akafungua macho yao mara moja, nao wakaona; na, tazama, walikuwa katikati ya Samaria. 21 Sasa mfalme wa Israeli akamwambia Elisha mara alipowaona: “Je, niwapige, je, niwapige,+ baba yangu?”+ 22 Lakini akasema: “Usiwapige. Je, unawapiga wale ambao wewe umewachukua mateka kwa upanga wako na kwa upinde wako?+ Weka mkate na maji mbele yao ili wale na kunywa,+ waende kwa bwana wao.” 23 Basi akawaandalia karamu kubwa; nao wakaanza kula na kunywa, kisha akawaacha, wakaenda zao kwa bwana wao. Na vikundi vya waporaji vya Wasiria havikurudi+ tena hata mara moja katika nchi ya Israeli.

24 Na ikawa kwamba baadaye Ben-hadadi mfalme wa Siria akakusanya kambi yake yote, akapanda na kulizingira+ Samaria. 25 Baada ya muda njaa kali ikatokea katika Samaria,+ na, tazama! walilizingira mpaka kichwa cha punda+ kikawa na thamani ya vipande 80 vya fedha, na sehemu ya nne ya kipimo cha kabi cha mavi+ ya njiwa ikawa na thamani ya vipande 5 vya fedha. 26 Na ikawa kwamba mfalme wa Israeli alipokuwa akipita juu ya ukuta, mwanamke fulani akamlilia, akisema: “Okoa, Ee bwana wangu mfalme!”+ 27 Naye akasema: “Yehova asipokuokoa wewe, mimi nitakuokoa kutoka chanzo gani?+ ni kutoka uwanja wa kupuria au ni kutoka divai au shinikizo la mafuta?” 28 Na mfalme akaendelea kumwambia tena: “Una nini?” Kwa hiyo mwanamke huyo akasema: “Huyu mwanamke aliniambia, ‘Mtoe mwana wako ili tumle leo, na mwanangu tutamla kesho.’+ 29 Basi tukampika+ mwanangu, tukamla.+ Kisha nikamwambia kesho yake, ‘Mtoe mwana wako ili tumle.’ Lakini akamficha mwana wake.”

30 Na ikawa kwamba mara mfalme alipoyasikia maneno ya mwanamke yule, mara moja akayararua+ mavazi yake; na kwa vile alikuwa akipita juu ya ukuta, watu wakaona, na, tazama! ndani alikuwa amevaa nguo za magunia juu ya mwili wake. 31 Naye akaendelea kusema: “Mungu na anifanyie hivyo, naye azidishe hilo, kichwa cha Elisha mwana wa Shafati kikiendelea kusimama juu yake leo!”+

32 Na Elisha alikuwa ameketi ndani ya nyumba yake mwenyewe, na wanaume wazee walikuwa wameketi pamoja naye,+ alipotuma mtu kutoka mbele yake. Kabla ya yule mjumbe kuingia kwake, yeye akawaambia wale wanaume wazee: “Je, mmeona jinsi ambavyo huyu mwana wa muuaji+ ametuma watu kukiondoa kichwa changu? Angalieni: mara mjumbe yule atakapofika, fungeni mlango, nanyi mtamsukuma nyuma kwa mlango. Je, sauti+ ya miguu ya bwana wake haiko nyuma yake?” 33 Alipokuwa bado anasema nao, tazama, yule mjumbe akawa anashuka kumjia, na mfalme akasema: “Tazama, huu ni msiba kutoka kwa Yehova.+ Kwa nini niendelee kumngojea Yehova?”+

7 Basi Elisha akasema: “Sikilizeni neno la Yehova.+ Yehova amesema hivi, ‘Kesho karibu na wakati kama huu kipimo kimoja cha sea cha unga laini kitakuwa na thamani ya shekeli moja, na vipimo viwili vya sea vya shayiri vitakuwa na thamani ya shekeli moja katika lango la Samaria.’”+ 2 Ndipo amiri msaidizi ambaye mfalme alijiegemeza+ juu ya mkono wake akamjibu mtu wa Mungu wa kweli na kusema: “Ikiwa Yehova angefanya madirisha mbinguni,+ je, jambo hili lingetokea?”+ Naye akasema: “Tazama, wewe unaliona hilo kwa macho yako,+ lakini wewe hutakula kutokana nalo.”+

3 Na palikuwa na watu wanne wenye ukoma, waliokuwa katika mwingilio wa lango;+ nao wakaanza kuambiana: “Kwa nini tunaketi hapa mpaka tufe? 4 Kama tukisema, ‘Tuingie katika jiji,’ wakati kuna njaa katika jiji, pia tutakufa humo.+ Nasi tukiketi hapa, pia tutakufa. Basi sasa njooni, tuivamie kambi ya Wasiria. Wakituhifadhi hai, tutaishi; lakini wakituua, basi tutakufa.”+ 5 Kwa hiyo wakaondoka wakati wa giza la jioni ili waingie katika kambi ya Wasiria; nao wakafika mpaka kandokando ya kambi ya Wasiria, na, tazama! hakuna yeyote aliyekuwako.

6 Na Yehova alikuwa amefanya kambi ya Wasiria isikie+ sauti ya magari ya vita, sauti ya farasi, sauti ya jeshi kubwa,+ hivi kwamba wakaambiana: “Tazama! Mfalme wa Israeli amekodi juu yetu wafalme wa Wahiti+ na wafalme wa Misri+ ili waje juu yetu!” 7 Wakaondoka mara moja, wakakimbia katika giza la jioni,+ wakaacha mahema yao na farasi+ zao na punda zao—ile kambi kama ilivyokuwa—nao wakaendelea kukimbia kwa ajili ya nafsi+ yao.

8 Wale wenye ukoma walipofika kandokando ya ile kambi, ndipo wakaingia ndani ya hema moja, wakaanza kula na kunywa na kuchukua kutoka humo fedha na dhahabu na mavazi, wakaenda kuvificha. Kisha wakarudi na kuingia katika hema lingine, wakachukua vitu kutoka humo na kwenda kuvificha.+

9 Mwishowe wakaanza kuambiana: “Jambo tunalofanya si sawa. Leo ni siku ya habari njema!+ Tukisitasita, na tungojee mpaka nuru ya asubuhi, hatia itatupata pia.+ Basi sasa njooni, tuingie, tupeleke habari nyumbani kwa mfalme.” 10 Basi wakaenda, wakawaita watunza-malango+ wa jiji na kuwaletea habari, wakisema: “Tuliingia katika kambi ya Wasiria, na, tazama! hapakuwa na mtu yeyote humo wala sauti ya mwanadamu, lakini farasi peke yao waliofungwa na punda waliofungwa na mahema kama walivyoyaacha.”+ 11 Mara moja wale watunza-malango wakaita na kupeleka habari ndani nyumbani kwa mfalme.

12 Mfalme akasimama mara moja wakati wa usiku, akawaambia watumishi+ wake: “Tafadhali, acheni niwaambie yale ambayo Wasiria wametufanyia.+ Wanajua vema kwamba tuna njaa;+ na basi walitoka kambini ili wajifiche shambani,+ wakisema, ‘Watatoka jijini, nasi tutawakamata wakiwa hai, nasi tutaingia jijini.’” 13 Ndipo mmoja wa watumishi wake akajibu na kusema: “Tafadhali, acha wachukue farasi watano kati ya wale waliobaki ambao wamebaki jijini.+ Tazama! Wao ni sawa na umati wote wa Israeli ambao umebaki ndani yake. Tazama! Wao ni kama umati wote wa Israeli ambao umeangamia.+ Nasi tutume watu tuone.” 14 Kwa hiyo wakachukua magari mawili pamoja na farasi na mfalme akawatuma kuifuata kambi ya Wasiria, akisema: “Nendeni mwone.” 15 Ndipo wakawafuata mpaka Yordani; na tazama! njia yote ilijaa mavazi na vyombo+ ambavyo Wasiria walikuwa wamevitupa walipokuwa wanakimbia.+ Kisha wale wajumbe wakarudi na kumletea mfalme habari.

16 Na watu wakaenda na kuipora+ kambi ya Wasiria; basi kipimo kimoja cha sea cha unga laini kikawa na thamani ya shekeli moja, na vipimo viwili vya sea vya shayiri vikawa na thamani ya shekeli moja, kulingana na lile neno+ la Yehova. 17 Na mfalme alikuwa amemweka yule amiri msaidizi ambaye alikuwa amejiegemeza+ juu ya mkono wake asimamie njia ya lango; na watu wakaendelea kumkanyaga+ katika njia ya lango, hata akafa, kama alivyokuwa amesema yule mtu wa Mungu wa kweli,+ aliposema wakati mfalme aliposhuka kumjia. 18 Basi ikawa kama alivyosema yule mtu wa Mungu wa kweli kwa mfalme, akisema: “Vipimo viwili vya sea vya shayiri vyenye thamani ya shekeli moja na kipimo kimoja cha sea cha unga laini chenye thamani ya shekeli moja ndivyo itakavyokuwa kesho wakati kama huu katika njia ya lango la Samaria.”+ 19 Lakini yule amiri msaidizi akamjibu mtu wa Mungu wa kweli na kusema: “Hata ikiwa Yehova angefanya madirisha mbinguni, je, ingeweza kutokea kulingana na neno hili?”+ Naye akasema: “Tazama, wewe unaliona hilo kwa macho yako, lakini wewe hutakula kutokana nalo.”+ 20 Basi ikawa hivyo kwake,+ wakati watu walipoendelea kumkanyaga+ katika njia ya lango, hata akafa.

8 Na Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye alikuwa amemfufua mwana wake,+ na kusema: “Ondoka uende, wewe pamoja na nyumba yako, ukae ugenini popote unapoweza kukaa ugenini;+ kwa kuwa Yehova ametangaza kuwe na njaa,+ na zaidi ya hayo, itakuja juu ya nchi kwa miaka saba.”+ 2 Basi yule mwanamke akaondoka, akafanya kulingana na neno la yule mtu wa Mungu wa kweli, akaenda,+ yeye pamoja na nyumba yake,+ akaanza kukaa ugenini katika nchi ya Wafilisti+ kwa miaka saba.

3 Na ikawa kwamba mwishoni mwa miaka saba yule mwanamke akarudi kutoka katika nchi ya Wafilisti, akaenda kumlilia mfalme+ kwa ajili ya nyumba yake na kwa ajili ya shamba lake. 4 Sasa mfalme alikuwa akisema na Gehazi+ mtumishi wa yule mtu wa Mungu wa kweli, kusema: “Tafadhali, nisimulie mambo yote makuu ambayo Elisha amefanya.”+ 5 Na ikawa kwamba alipokuwa akimsimulia mfalme jinsi alivyokuwa amemfufua mtu aliyekufa,+ tazama, yule mwanamke aliyekuwa amemfufulia mwana wake alikuwa akimlilia mfalme kwa ajili ya nyumba yake na kwa ajili ya shamba+ lake. Mara moja Gehazi akasema: “Bwana+ wangu mfalme, huyu ndiye yule mwanamke, na huyu ndiye mwana wake ambaye Elisha alimfufua.” 6 Ndipo mfalme akamuuliza yule mwanamke, naye akamsimulia hadithi ile.+ Kisha mfalme akampa mwanamke huyo ofisa wa makao ya mfalme,+ akisema: “Rudisha mali yote ya mwanamke huyu na mazao yote ya shamba lake tangu siku alipotoka katika nchi mpaka sasa.”+

7 Na Elisha akaenda Damasko;+ na Ben-hadadi+ mfalme wa Siria alikuwa mgonjwa. Basi akaletewa habari, ikisema: “Yule mtu wa Mungu+ wa kweli amefika hapa.” 8 Kwa hiyo mfalme akamwambia Hazaeli:+ “Chukua zawadi+ mkononi mwako, nenda umpokee yule mtu wa Mungu wa kweli, nawe uulize+ Yehova kupitia kwake, na kusema, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’” 9 Basi Hazaeli akaenda kumpokea, akachukua zawadi mkononi mwake, naam, kila namna ya kitu chema cha Damasko, mzigo wa ngamia 40, akaja na kusimama mbele yake, akasema: “Mwana+ wako, Ben-hadadi, mfalme wa Siria, amenituma kwako, kusema, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’” 10 Ndipo Elisha akamwambia: “Nenda, mwambie, ‘Utapona hakika,’ na Yehova amenionyesha+ kwamba atakufa hakika.”+ 11 Naye akamkazia macho, akayakaza mpaka akaona haya. Kisha yule mtu wa Mungu wa kweli akaanza kulia.+ 12 Kwa hiyo Hazaeli akasema: “Kwa nini bwana wangu analia?” Naye akasema: “Kwa sababu ninajua vema mabaya+ utakayowatendea wana wa Israeli. Utateketeza kwa moto mahali pao penye ngome, na wanaume wao walio bora utawaua kwa upanga, na watoto wao utawavunja vipande-vipande,+ na wanawake wao wenye mimba utawapasua.”+ 13 Basi Hazaeli akasema: “Mtumishi wako ni nani, ambaye ni mbwa+ tu, ndipo aweze kufanya jambo hili kuu?” Lakini Elisha akasema: “Yehova amenionyesha wewe kuwa mfalme juu ya Siria.”+

14 Kisha akatoka kwa Elisha, akaenda kwa bwana wake, ambaye sasa alimuuliza: “Elisha alikuambia nini?” Naye akasema: “Aliniambia, ‘Hakika utapona.’”+ 15 Na ikawa kwamba kesho yake akachukua tandiko lenye mapambo, akalichovya ndani ya maji, akalifunika juu ya uso wake,+ hata akafa.+ Na Hazaeli+ akaanza kutawala mahali pake.

16 Na katika mwaka wa tano wa Yehoramu+ mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Yehoshafati alipokuwa mfalme wa Yuda, Yehoramu+ mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda akawa mfalme. 17 Alikuwa na umri wa miaka 32 alipoanza kuwa mfalme, naye akatawala miaka 8 katika Yerusalemu.+ 18 Naye akaendelea kutembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ kama walivyofanya wale wa nyumba ya Ahabu;+ kwa maana binti ya Ahabu ndiye aliyekuwa mke wake,+ naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova. 19 Na Yehova hakutaka kuharibu Yuda+ kwa sababu ya Daudi mtumishi wake,+ kama alivyokuwa ameahidi kumpa taa,+ yeye na wanawe sikuzote.

20 Katika siku zake Edomu+ waliasi kutoka chini ya mkono wa Yuda, nao wakaweka mfalme+ atawale juu yao. 21 Basi Yehoramu akavuka mpaka Sairi, pia magari yote pamoja naye. Na ikawa kwamba yeye akaondoka wakati wa usiku, akawapiga na kuwaua Waedomu waliokuwa wamemzunguka na wale wakuu wa magari; na watu wakakimbia kwenda katika mahema yao. 22 Lakini Edomu wakaendelea kuasi kutoka chini ya mkono wa Yuda mpaka leo hii. Wakati huo ndipo Libna+ wakaanza kuasi.

23 Na mambo mengine ya Yehoramu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 24 Mwishowe Yehoramu akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ Na Ahazia+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

25 Katika mwaka wa kumi na mbili wa Yehoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akawa mfalme.+ 26 Ahazia alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye akatawala mwaka mmoja katika Yerusalemu.+ Na jina la mama yake lilikuwa Athalia+ mjukuu wa Omri+ mfalme wa Israeli. 27 Naye akaendelea kutembea katika njia ya nyumba ya Ahabu,+ akazidi kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ kama nyumba ya Ahabu, kwa maana alikuwa mtu wa jamaa ya nyumba ya Ahabu kupitia ndoa.+ 28 Basi akaenda pamoja na Yehoramu mwana wa Ahabu kupigana vita na Hazaeli+ mfalme wa Siria kule Ramothi-gileadi,+ lakini Wasiria wakampiga+ Yehoramu. 29 Kwa hiyo Yehoramu+ mfalme akarudi Yezreeli+ ili apone yale majeraha waliyomtia Wasiria kule Rama alipopigana na Hazaeli mfalme wa Siria. Naye Ahazia+ mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka ili amwone Yehoramu mwana wa Ahabu katika Yezreeli, kwa maana alikuwa mgonjwa.

9 Na Elisha nabii akamwita mmoja wa wana+ wa manabii, kisha akamwambia: “Jifunge viuno+ vyako uchukue chupa+ hii ya mafuta mkononi mwako, uende Ramothi-gileadi.+ 2 Utakapoingia humo, mwone Yehu+ mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi humo; nawe uingie ndani na kumsimamisha kutoka katikati ya ndugu zake, umwingize katika chumba cha ndani kabisa.+ 3 Nawe uchukue chupa ya mafuta uyamimine juu ya kichwa+ chake na kusema, ‘Yehova amesema hivi: “Ninakutia mafuta+ uwe mfalme+ juu ya Israeli.”’ Nawe ufungue mlango, ukimbie, wala usingoje.”

4 Na yule mtumishi, mtumishi wa nabii, akaondoka kwenda Ramothi-gileadi. 5 Alipoingia, tazama, wakuu wa majeshi walikuwa wameketi. Akasema: “Nina neno kwa ajili yako,+ ewe mkuu.” Ndipo Yehu akasema: “Ni kwa ajili ya nani kati yetu sote?” Kisha akasema: “Kwa ajili yako, ewe mkuu.” 6 Basi akasimama, akaingia ndani ya nyumba; naye akamimina yale mafuta juu ya kichwa chake na kumwambia: “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Ninakutia mafuta uwe mfalme+ juu ya watu wa Yehova,+ yaani, juu ya Israeli. 7 Nawe uipige nyumba ya Ahabu bwana wako, nami lazima nilipize kisasi+ damu ya watumishi wangu manabii na damu ya watumishi wote wa Yehova mkononi mwa Yezebeli.+ 8 Na nyumba yote ya Ahabu lazima iangamie; nami nitakatilia mbali kutoka kwa Ahabu+ mtu yeyote anayekojoa ukutani+ na yeyote asiye na uwezo na asiye na thamani+ katika Israeli. 9 Nami nitaifanya nyumba ya Ahabu kuwa kama nyumba ya Yeroboamu+ mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha+ mwana wa Ahiya. 10 Na mbwa watamla+ Yezebeli katika sehemu ya shamba kule Yezreeli, wala hakuna atakayemzika.’” Kisha akafungua mlango, akakimbia.+

11 Ndipo Yehu akatoka nje, akawaendea watumishi wa bwana wake, nao wakaanza kumuuliza: “Je, ni salama?+ Kwa nini huyu mwenda-wazimu+ alikuja kwako?” Lakini akawaambia: “Ninyi mnajua vema mtu huyo na namna yake ya kuongea.” 12 Lakini wakasema: “Si kweli! Tafadhali tuambie.” Ndipo akasema: “Aliniambia hivi na vile, akisema, ‘Yehova amesema hivi: “Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.”’”+ 13 Kwa hiyo wakafanya haraka, kila mmoja wao akachukua vazi+ lake na kulitandika chini yake juu ya zile ngazi zilizo wazi, nao wakaanza kupiga baragumu,+ wakisema: “Yehu amekuwa mfalme!”+ 14 Na Yehu+ mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi+ akapanga hila+ juu ya Yehoramu.

Na Yehoramu alikuwa akilinda kule Ramothi-gileadi,+ yeye na Israeli wote, kwa sababu ya Hazaeli+ mfalme wa Siria. 15 Baadaye Yehoramu+ mfalme akarudi kule Yezreeli+ ili apone yale majeraha ambayo Wasiria walimtia alipopigana na Hazaeli mfalme wa Siria.+

Sasa Yehu akasema: “Nafsi yenu ikikubali,+ msiache yeyote akimbie kutoka jijini na kupeleka habari Yezreeli.” 16 Na Yehu akaanza kupanda, akaenda Yezreeli; kwa maana Yehoramu alikuwa amelala huko, na Ahazia+ mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka kwenda kumwona Yehoramu. 17 Na mlinzi+ alikuwa amesimama juu ya mnara+ katika Yezreeli,+ naye akaona umati unaosukasuka wa watu wa Yehu alipokuwa akija, naye akasema mara moja: “Ninaona umati unaosukasuka wa watu.” Ndipo Yehoramu akasema: “Chukua askari mpanda-farasi, umtume awapokee, naye aseme, ‘Je, kuna amani?’”+ 18 Basi mpanda-farasi akaenda kumpokea na kusema: “Mfalme amesema hivi, ‘Je, kuna amani?’” Lakini Yehu akasema: “Una nini na ‘amani’?+ Nenda nyuma yangu!”

Na yule mlinzi+ akaendelea kutoa habari, akisema: “Yule mjumbe aliwafikia, lakini hakurudi.” 19 Kwa hiyo akatuma mpanda-farasi wa pili, ambaye, alipowafikia, alisema: “Mfalme amesema hivi, ‘Je, kuna amani?’” Lakini Yehu akasema: “Una nini na ‘amani’?+ Nenda nyuma yangu!”

20 Na yule mlinzi akaendelea kutoa habari, akisema: “Aliwafikia, lakini hakurudi; na uendeshaji ule ni kama uendeshaji wa Yehu+ mjukuu wa Nimshi,+ kwa maana yeye huendesha kiwazimu.”+ 21 Ndipo Yehoramu akasema: “Fungeni!”+ Basi gari lake la vita likafungwa, na Yehoramu mfalme wa Israeli na Ahazia+ mfalme wa Yuda wakatoka, kila mmoja wao akiwa ndani ya gari lake la vita. Walipoendelea kwenda kumpokea Yehu, wakamkuta katika sehemu ya shamba la Nabothi,+ Myezreeli.

22 Na ikawa kwamba mara tu Yehoramu alipomwona Yehu, mara moja akasema: “Je, kuna amani, Yehu?” Lakini yeye akasema: “Kunaweza kuwa na amani+ gani wakati kungali na uasherati wa Yezebeli+ mama yako na ulozi wake mwingi?”+ 23 Mara moja Yehoramu akageuka kwa mikono yake, ili akimbie, na kumwambia Ahazia: “Kuna udanganyifu,+ Ahazia!” 24 Na Yehu akatia upinde+ mkononi mwake, akampiga Yehoramu katikati ya mikono, hivi kwamba ule mshale ukatokea moyoni mwake, naye akaanguka ndani ya gari lake la vita.+ 25 Sasa akamwambia Bidkari amiri msaidizi wake:+ “Mwinue; mtupe katika ile sehemu ya shamba la Nabothi, Myezreeli;+ kwa maana kumbuka: Mimi na wewe tulikuwa tukiendesha makundi ya magari ya farasi nyuma ya Ahabu baba yake, na Yehova akatangaza+ hivi juu yake: 26 ‘ “Hakika niliona jana damu+ ya Nabothi na damu ya wanawe,”+ asema Yehova, “nami hakika nitakulipa+ wewe katika sehemu hii ya shamba,” asema Yehova.’ Basi sasa, mwinue; mtupe katika ile sehemu ya shamba kulingana na neno la Yehova.”+

27 Na Ahazia+ mfalme wa Yuda akaona hilo, akaanza kukimbia kupitia njia ya bustani ya nyumba.+ (Baadaye Yehu akamfuatilia na kusema: “Yeye pia! Mpigeni!” Kwa hiyo wakampiga alipokuwa ndani ya gari kwenye njia inayopanda kwenda Guri, lililo kando ya Ibleamu.+ Naye akaendelea kukimbia kwenda Megido,+ akafa huko.+ 28 Ndipo watumishi wake wakambeba ndani ya gari mpaka Yerusalemu, na hivyo wakamzika katika kaburi lake pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ 29 Na ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja wa Yehoramu+ mwana wa Ahabu kwamba Ahazia+ alianza kuwa mfalme juu ya Yuda.)

30 Mwishowe Yehu akafika Yezreeli,+ na Yezebeli+ akasikia habari hizo. Naye akapaka macho yake wanja+ na kukipamba kichwa chake,+ akatazama chini kupitia dirishani.+ 31 Na Yehu akaingia kupitia lango. Basi yule mwanamke akasema: “Je, mambo yalimwendea sawa Zimri,+ aliyemuua bwana wake?” 32 Basi akainua uso wake kuelekea lile dirisha na kusema: “Ni nani aliye pamoja nami? Ni nani?”+ Mara moja maofisa+ wawili au watatu wa makao ya mfalme wakaangalia chini kumtazama. 33 Basi akasema: “Mwangusheni!”+ Ndipo wakamwangusha huyo mwanamke, na sehemu ya damu yake ikamwagika juu ya ukuta na juu ya farasi; naye akamkanyaga-kanyaga.+ 34 Kisha akaingia ndani, akala na kunywa na kisha kusema: “Tafadhali, mshughulikieni mtu huyu aliyelaaniwa+ na mkamzike, kwa maana yeye ni binti ya mfalme.”+ 35 Walipoenda kumzika, hawakupata chochote chake isipokuwa fuvu la kichwa na miguu na viganja vya mikono.+ 36 Waliporudi na kumwambia, ndipo akasema: “Hilo ni neno la Yehova alilosema kupitia+ mtumishi wake Eliya, Mtishbi, kusema, ‘Katika sehemu ya shamba la Yezreeli mbwa wataila nyama ya Yezebeli.+ 37 Na maiti ya Yezebeli itakuwa kama mbolea+ juu ya uso wa shamba katika sehemu ya shamba la Yezreeli, ili wasiseme: “Huyu ni Yezebeli.”’”+

10 Basi Ahabu alikuwa na wana 70+ katika Samaria.+ Kwa hiyo Yehu akaandika barua, akazituma Samaria kwa wakuu+ wa Yezreeli, wanaume wazee+ na watunzaji wa Ahabu, na kusema: 2 “Basi, sasa, wakati ule barua hii inapowafikia ninyi, mnao wana wa bwana wenu pamoja nanyi, na mnayo magari ya vita na farasi+ pamoja nanyi na jiji lenye ngome na silaha. 3 Nanyi mwone ni nani aliye bora zaidi na mnyoofu zaidi kati ya wana wa bwana wenu, mkamweke yeye juu ya kiti cha ufalme cha baba yake.+ Halafu mpiganie nyumba ya bwana wenu.”

4 Nao wakaogopa sana, wakaanza kusema: “Tazama! Wafalme wawili+ hawakusimama mbele yake, nasi tutasimamaje?”+ 5 Kwa hiyo yule aliyekuwa juu ya nyumba na yule aliyekuwa juu ya jiji na wanaume wazee na watunzaji+ wakatuma ujumbe kwa Yehu, wakisema: “Sisi ni watumishi wako, na kila jambo unalotuambia tutafanya. Hatutamfanya yeyote kuwa mfalme. Fanya yaliyo mema machoni pako.”

6 Ndipo akawaandikia barua ya pili, na kusema: “Ikiwa ninyi ni wangu,+ nanyi mnaitii sauti yangu, chukueni vichwa vya hao wana+ wa bwana wenu, mje kwangu kesho wakati kama huu katika Yezreeli.”+

Basi wana wa mfalme, watu 70, walikuwa na wanaume mashuhuri wa jiji waliokuwa wakiwalea. 7 Na ikawa kwamba mara tu barua ile ilipowafikia, wakawachukua wale wana wa mfalme na kuwachinja, watu 70,+ kisha wakaviweka vichwa vyao ndani ya vikapu, wakampelekea kule Yezreeli. 8 Kisha yule mjumbe+ akaingia na kumwambia: “Wamevileta vichwa+ vya wana wa mfalme.” Kwa hiyo akasema: “Viwekeni katika mafungu mawili kwenye mwingilio wa lango mpaka asubuhi.”+ 9 Na ikawa kwamba wakati wa asubuhi akaondoka. Kisha akasimama tuli na kuwaambia watu wote: “Ninyi ni waadilifu.+ Tazama, mimi mwenyewe nilipanga hila+ juu ya bwana wangu, nami nikamuua;+ lakini ni nani aliyewapiga na kuwaua hawa wote? 10 Basi jueni kwamba hakuna neno lolote la Yehova litakaloanguka chini+ bila kutimizwa ambalo Yehova amesema juu ya nyumba ya Ahabu;+ na Yehova mwenyewe amefanya aliyoyasema kupitia Eliya mtumishi wake.”+ 11 Tena Yehu akaendelea kuwapiga na kuwaua wote waliobaki wa nyumba ya Ahabu katika Yezreeli na watu wake wote walio mashuhuri+ na rafiki zake na makuhani+ wake, mpaka alipokuwa amewaangamiza watu wake wote, bila kuacha mwokokaji yeyote abaki.+

12 Naye akasimama na kuingia, kisha akaenda zake Samaria. Nyumba ya kufungia ya wachungaji ilikuwa njiani. 13 Na Yehu akakutana na ndugu+ za Ahazia+ mfalme wa Yuda. Alipowaambia, “Ninyi ni nani?” ndipo wakasema: “Sisi ni ndugu za Ahazia, nasi tuko njiani kwenda kuuliza kama ni salama kwa wana wa mfalme na kwa wana wa malkia.” 14 Mara moja akasema: “Wakamateni wakiwa hai!”+ Kwa hiyo wakawakamata wakiwa hai, wakawachinja kando ya tangi la maji la ile nyumba ya kufungia, watu 42, naye hakumwacha hata mmoja wao abaki.+

15 Alipokuwa akienda kutoka hapo, akakutana na Yehonadabu+ mwana wa Rekabu+ akija kumpokea. Alipombariki,+ akamwambia: “Je, moyo wako ni mnyoofu kunielekea mimi, kama vile moyo wangu ulivyo kuuelekea moyo wako?”+

Ndipo Yehonadabu akasema: “Ndiyo.”

“Ikiwa ndivyo, nipe mkono wako.”

Kwa hiyo akampa mkono wake. Basi akampandisha ndani ya gari pamoja naye.+ 16 Kisha akasema: “Enda pamoja nami, utazame jinsi ambavyo sivumilii ushindani+ wowote kumwelekea Yehova.” Nao wakaendelea kumwendesha pamoja naye katika gari lake la vita. 17 Mwishowe akafika Samaria. Sasa akaanza kuwapiga na kuwaua wote waliobaki wa Ahabu katika Samaria, mpaka akawaangamiza,+ kulingana na neno la Yehova alilomwambia Eliya.+

18 Tena Yehu akakusanya watu wote na kuwaambia: “Ahabu alimwabudu Baali kwa kiwango kidogo tu.+ Lakini Yehu atamwabudu kwa kiwango kikubwa. 19 Basi sasa waiteni kwangu manabii+ wote wa Baali, waabudu+ wake wote na makuhani+ wake wote. Msiache hata mmoja akose kuwapo, kwa sababu nina dhabihu kubwa kwa ajili ya Baali. Yeyote atakayekosa kuwapo hataendelea kuishi.” Kwa habari ya Yehu, yeye alitenda kwa ujanja,+ kusudi awaharibu waabudu wa Baali.

20 Na Yehu akaendelea kusema: “Takaseni kusanyiko kuu kwa ajili ya Baali.” Basi wakalitangaza. 21 Kisha Yehu akatuma ujumbe katika Israeli yote,+ hivi kwamba waabudu wote wa Baali wakaja. Hakuna hata mmoja aliyebaki ambaye hakuja. Nao wakaendelea kuingia katika nyumba ya Baali,+ na nyumba ya Baali ikajaa kutoka mwisho mpaka mwisho. 22 Sasa akamwambia yule aliyesimamia chumba cha nguo: “Toa mavazi kwa ajili ya waabudu wote wa Baali.” Basi akawatolea mavazi. 23 Ndipo Yehu akaingia na Yehonadabu+ mwana wa Rekabu katika nyumba ya Baali. Sasa akawaambia waabudu wa Baali: “Tafuteni kwa uangalifu mhakikishe kwamba hamna hapa ndani pamoja nanyi waabudu wowote wa Yehova, isipokuwa tu waabudu wa Baali.”+ 24 Mwishowe wakaingia ili kutoa dhabihu na matoleo ya kuteketezwa, na Yehu akaweka watu 80 upande wa nje ili wawepo kwa ajili yake, naye akaendelea kusema: “Mtu yeyote atakayeponyoka kati ya watu ninaotia mikononi mwenu, nafsi ya huyo mtu itakuwa badala ya nafsi ya yule mwingine.”+

25 Na ikawa kwamba mara tu alipomaliza kutoa lile toleo la kuteketezwa, Yehu akawaambia mara moja wale wakimbiaji na maamiri wasaidizi: “Ingieni ndani, wapigeni na kuwaua! Msiache hata mmoja atoke nje.”+ Na wale wakimbiaji na maamiri wasaidizi+ wakaanza kuwapiga na kuwaua kwa makali ya upanga na kuwatupa nje, nao wakazidi kwenda mpaka kwenye jiji la nyumba ya Baali. 26 Kisha wakazitoa nje nguzo takatifu+ za nyumba ya Baali na kuteketeza+ kila moja kwa moto. 27 Tena wakabomoa nguzo takatifu ya Baali+ na kuibomoa nyumba ya Baali,+ nao wakaitenga iwe choo+ mpaka leo hii.

28 Kwa hiyo Yehu akaangamiza Baali kutoka katika Israeli. 29 Ni dhambi tu za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, alizosababisha Israeli kutenda dhambi,+ ambazo Yehu hakugeuka asizifuate, yaani, wale ndama wa dhahabu+ ambao mmoja alikuwa katika Betheli na mwingine katika Dani.+ 30 Basi Yehova akamwambia Yehu: “Kwa kuwa umetenda vema kwa kufanya yaliyo sawa machoni pangu,+ nawe umeitendea nyumba ya Ahabu+ kulingana na yote yaliyokuwa moyoni mwangu, wana, kufikia kizazi cha nne, wataketi kwa ajili yako juu ya kiti cha ufalme cha Israeli.”+ 31 Na Yehu hakuwa mwangalifu ili atembee katika sheria ya Yehova, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote.+ Yeye hakugeuka kutoka katika dhambi za Yeroboamu alizosababisha Israeli kutenda dhambi.+

32 Siku hizo Yehova akaanza kukatilia mbali Israeli kipande kimoja baada ya kingine; na Hazaeli+ akaendelea kuwapiga katika eneo lote la Israeli, 33 kutoka Yordani kuelekea mashariki, nchi yote ya Gileadi,+ Wagadi+ na Warubeni+ na Wamanase,+ kutoka Aroeri,+ lililoko kando ya bonde la mto la Arnoni, naam, Gileadi na Bashani.+

34 Na mambo mengine ya Yehu na yote aliyofanya na uwezo wake wote, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 35 Mwishowe Yehu akalala pamoja na mababu+ zake, nao wakamzika katika Samaria; na Yehoahazi+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake. 36 Na siku ambazo Yehu alitawala juu ya Israeli zilikuwa miaka 28 katika Samaria.

11 Basi kwa habari ya Athalia+ mama ya Ahazia,+ yeye aliona kwamba mwana wake amekufa. Kwa hiyo akasimama, akauangamiza uzao wote wa ufalme.+ 2 Hata hivyo, Yehosheba+ binti ya Mfalme Yehoramu, dada ya Ahazia, akamchukua Yehoashi+ mwana wa Ahazia, akamwiba kutoka kati ya wana wa mfalme waliopaswa kuuawa, naam, yeye na mlezi wake mwanamke, akamwingiza katika chumba cha ndani cha vitanda, nao wakaendelea kumficha+ kutoka machoni pa Athalia, naye hakuuawa. 3 Naye akaendelea kuwa pamoja na mwanamke huyo mafichoni katika nyumba ya Yehova kwa miaka sita, Athalia alipokuwa akitawala juu ya nchi.+

4 Na katika mwaka wa saba Yehoyada+ akatuma watu, kisha akawachukua wakuu wa mamia wa walinzi Wakari+ na wa wakimbiaji+ na kuwaleta kwake katika nyumba ya Yehova, akafanya agano+ pamoja nao na kuwaapisha+ katika nyumba ya Yehova, kisha akawaonyesha mwana wa mfalme. 5 Naye akawaamuru, akisema: “Hivi ndivyo mtakavyofanya: Sehemu ya tatu kati yenu mtaingia siku ya sabato na kuweka ulinzi mkali juu ya nyumba ya mfalme;+ 6 na sehemu ya tatu watakuwa kwenye Lango+ la Msingi, na sehemu ya tatu watakuwa katika lango nyuma ya wakimbiaji; nanyi mweke ulinzi mkali juu ya nyumba+ kwa zamu. 7 Na kuna migawanyo miwili kati yenu ambayo yote inatoka siku ya sabato, nao lazima waweke ulinzi mkali juu ya nyumba ya Yehova kwa ajili ya mfalme. 8 Nanyi mnapaswa kumzunguka mfalme pande zote, kila mmoja akiwa na silaha zake mkononi mwake; na yeyote atakayeingia katikati ya vikosi atauawa. Nanyi mwendelee kuwa na mfalme anapotoka nje na anapoingia ndani.”

9 Na wale wakuu wa mamia+ wakafanya kulingana na yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa ameamuru. Basi kila mmoja wao akachukua watu wake waliokuwa wakiingia wakati wa sabato,+ pamoja na wale waliokuwa wakitoka nje wakati wa sabato, kisha wakamjia Yehoyada kuhani. 10 Sasa kuhani akawapa wale wakuu wa mamia mikuki na ngao za mviringo zilizokuwa za Mfalme Daudi, ambazo zilikuwa katika nyumba ya Yehova.+ 11 Na wakimbiaji+ wakaendelea kusimama kila mmoja akiwa na silaha zake mkononi mwake, kuanzia upande wa kuume wa nyumba mpaka upande wa kushoto wa nyumba, kando ya madhabahu+ na kando ya nyumba, pande zote karibu na mfalme. 12 Kisha akamtoa nje mwana+ wa mfalme, akamvika taji+ na ule Ushuhuda;+ na basi wakamfanya kuwa mfalme+ na kumtia mafuta.+ Nao wakaanza kupiga makofi+ na kusema: “Mfalme na aishi!”+

13 Athalia aliposikia sauti ya watu wakikimbia, mara moja akaingia kwa watu katika nyumba ya Yehova.+ 14 Kisha akaona, na tazama, mfalme alikuwa amesimama kando ya nguzo+ kama ilivyo desturi, na wakuu na tarumbeta+ kando ya mfalme, na watu wote wa nchi wakishangilia+ na kupiga tarumbeta. Athalia+ akayararua mavazi yake mara moja, akaanza kulia: “Ni hila! Ni hila!”+ 15 Lakini Yehoyada kuhani akawaamuru wakuu wa mamia, watu waliochaguliwa wa jeshi,+ na kuwaambia: “Mwondoeni katikati ya vikosi, na yeyote atakayemfuata, auawe kwa upanga!”+ Kwa maana kuhani yule alikuwa amesema: “Asiuawe ndani ya nyumba ya Yehova.” 16 Basi wakamkamata, akafika kando ya njia ya mlango wa farasi+ wa nyumba ya mfalme,+ naye akauawa huko.+

17 Ndipo Yehoyada akafanya agano+ kati ya Yehova+ na mfalme+ na watu, ili kwamba wajionyeshe kuwa watu wa Yehova; na pia kati ya mfalme na watu.+ 18 Kisha watu wote wa nchi wakaenda kwenye nyumba ya Baali, wakazibomoa madhabahu zake;+ nao wakazivunja kabisa+ sanamu zake, nao, mbele ya zile madhabahu,+ wakamuua Matani+ kuhani wa Baali.

Na kuhani akaweka waangalizi juu ya nyumba ya Yehova.+ 19 Tena akawachukua wakuu wa mamia na walinzi Wakari+ na wakimbiaji+ na watu wote wa nchi, ili wamshushe mfalme kutoka katika nyumba ya Yehova; nao wakaja polepole kupitia njia ya lango+ la wakimbiaji mpaka kwenye nyumba ya mfalme; naye akaanza kuketi juu ya kiti cha wafalme.+ 20 Na watu wote wa nchi wakaendelea kushangilia;+ nalo jiji halikuwa na usumbufu, nao walikuwa wamemuua Athalia kwa upanga nyumbani kwa mfalme.+

21 Yehoashi+ alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.+

12 Katika mwaka wa 7 wa Yehu,+ Yehoashi+ akawa mfalme, naye akatawala miaka 40 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Sibia kutoka Beer-sheba. 2 Na Yehoashi akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova siku zake zote ambazo Yehoyada kuhani alimfundisha.+ 3 Ni mahali pa juu peke yake ndipo hapakuondolewa.+ Watu walikuwa wangali wanatoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu.

4 Na Yehoashi akawaambia makuhani:+ “Pesa zote kwa ajili ya matoleo+ matakatifu zinazoletwa katika nyumba ya Yehova,+ pesa ambazo kila mtu hukadiriwa,+ pesa kwa ajili ya nafsi kulingana na kadirio la thamani+ ya mtu mmoja-mmoja, pesa zote ambazo kila mmoja anaazimia moyoni kuleta nyumbani kwa Yehova,+ 5 makuhani na wazichukue, kila mmoja kutoka kwa mtu wanayefahamiana naye;+ nao warekebishe mipasuko ya nyumba popote panapopatikana mpasuko wowote.”+

6 Na ikawa kwamba kufikia mwaka wa 23 wa Mfalme Yehoashi, makuhani hawakuwa wamerekebisha mipasuko ya nyumba.+ 7 Kwa hiyo Mfalme Yehoashi akamwita Yehoyada+ kuhani na makuhani, akawaambia: “Kwa nini hamrekebishi mipasuko ya nyumba? Basi sasa, msichukue pesa zaidi kutoka kwa watu mnaofahamiana nao, bali mzitoe kwa ajili ya mipasuko ya nyumba.”+ 8 Ndipo makuhani wakakubali wasichukue pesa zaidi kutoka kwa watu na kutorekebisha mipasuko ya nyumba.

9 Basi Yehoyada kuhani akachukua sanduku,+ akatoboa tundu katika kifuniko chake, akaliweka kando ya madhabahu upande wa kuume mtu anapoingia ndani ya nyumba ya Yehova, na makuhani, watunza-malango,+ wakaweka humo pesa+ zote zilizokuwa zikiletwa katika nyumba ya Yehova. 10 Na ikawa kwamba mara tu walipoona kuna pesa nyingi sana katika lile sanduku, mwandishi+ wa mfalme na kuhani mkuu wakawa wakija, nao wakazifunga na kuhesabu pesa zilizokuwa zikipatikana kwenye nyumba ya Yehova.+ 11 Na zile pesa ambazo zilikuwa zimehesabiwa, wakaziweka mikononi mwa wafanyakazi+ waliowekwa kwenye nyumba ya Yehova. Wao nao wakazilipa kwa wafanyakazi wa mbao na kwa wajenzi waliokuwa wakifanya kazi katika nyumba ya Yehova, 12 na kwa waashi na kwa wachongaji wa mawe,+ na kwa ajili ya kununua mbao na mawe yaliyochongwa kwa ajili ya kurekebisha mipasuko ya nyumba ya Yehova na kwa ajili ya vyote vilivyotumiwa kwenye nyumba ili kuirekebisha.

13 Ila tu kuhusiana na nyumba ya Yehova hawakutengeneza beseni za fedha, mikasi ya taa,+ mabakuli,+ tarumbeta,+ chombo chochote cha dhahabu na chombo cha fedha kutokana na zile pesa zilizokuwa zikiletwa katika nyumba ya Yehova;+ 14 kwa maana walikuwa wakiwapa wale wafanyakazi, nao walizitumia kurekebisha nyumba ya Yehova.+ 15 Nao hawakuwa wakitoza hesabu+ wale watu ambao mkononi mwao pesa zilitiwa ili kuwapa wale wafanyakazi,+ kwa sababu walikuwa wakifanya kazi kwa uaminifu.+ 16 Na pesa za matoleo ya hatia+ na pesa za matoleo ya dhambi, hazikuwa zikiletwa katika nyumba ya Yehova. Kwa hiyo zikawa za makuhani.+

17 Ndipo ikawa kwamba Hazaeli+ mfalme wa Siria akapanda kwenda kupigana na Gathi,+ akaliteka, kisha Hazaeli akaelekeza uso+ wake apande kwenda juu ya Yerusalemu.+ 18 Kwa hiyo Yehoashi mfalme wa Yuda akachukua matoleo yote matakatifu+ ambayo Yehoshafati na Yehoramu na Ahazia mababu zake, wafalme wa Yuda, walikuwa wameyatakasa na matoleo yake mwenyewe matakatifu na dhahabu yote iliyoonekana katika hazina za nyumba ya Yehova na nyumba ya mfalme, akavipeleka+ kwa Hazaeli mfalme wa Siria. Basi akaondoka juu ya Yerusalemu.

19 Na mambo mengine ya Yehoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 20 Hata hivyo, watumishi+ wake wakasimama na kuungana katika hila,+ wakampiga na kumuua Yehoashi katika nyumba+ ya Kilima,+ katika njia inayoshuka kwenda Sila. 21 Na Yozakari mwana wa Shimeathi na Yehozabadi+ mwana wa Shomeri, watumishi wake, ndio waliompiga, hata akafa. Basi wakamzika pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi; na Amazia+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

13 Katika mwaka wa 23 wa Yehoashi+ mwana wa Ahazia+ mfalme wa Yuda, Yehoahazi+ mwana wa Yehu+ akawa mfalme juu ya Israeli katika Samaria kwa miaka 17. 2 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ akaifuatilia dhambi ya Yeroboamu+ mwana wa Nebati, aliyosababisha Israeli kutenda dhambi.+ Hakugeuka aiache. 3 Na hasira+ ya Yehova ikawaka juu ya Israeli, hivi kwamba akawatia mkononi mwa Hazaeli+ mfalme wa Siria na mkononi mwa Ben-hadadi+ mwana wa Hazaeli siku zao zote.

4 Baada ya muda Yehoahazi akautuliza+ uso wa Yehova, hata Yehova akamsikiliza;+ kwa maana alikuwa ameona kukandamizwa kwa Israeli,+ kwa sababu mfalme wa Siria alikuwa amewakandamiza.+ 5 Basi Yehova akawapa Israeli mwokozi,+ hata wakatoka chini ya mkono wa Siria, na wana wa Israeli wakaendelea kukaa katika nyumba zao kama hapo mwanzoni.+ 6 (Isipokuwa tu hawakuacha dhambi ya nyumba ya Yeroboamu, aliyosababisha Israeli watende dhambi.+ Alitembea katika hiyo;+ na hata mti mtakatifu+ ulisimama katika Samaria.) 7 Kwa maana hakuwa amemwachia Yehoahazi watu wowote isipokuwa wapanda-farasi 50 na magari 10 na watu 10,000 wanaoenda kwa miguu,+ kwa sababu mfalme wa Siria alikuwa amewaharibu,+ ili awafanye kuwa kama mavumbi wakati wa kupura.+

8 Na mambo mengine ya Yehoahazi na yote aliyoyafanya na uwezo wake, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 9 Mwishowe Yehoahazi akalala pamoja na mababu zake, nao wakamzika katika Samaria;+ na Yehoashi+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

10 Katika mwaka wa 37 wa Yehoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi akawa mfalme juu ya Israeli katika Samaria kwa miaka 16. 11 Naye akaendelea kutenda yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+ Hakuziacha dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, alizosababisha Israeli kutenda dhambi.+ Alitembea katika hizo.

12 Na mambo mengine ya Yehoashi na yote aliyoyafanya na uwezo wake na jinsi alivyopigana+ na Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 13 Mwishowe Yehoashi akalala pamoja na mababu zake, na Yeroboamu+ akaketi juu ya kiti chake cha ufalme. Naye Yehoashi akazikwa katika Samaria pamoja na wafalme wa Israeli.+

14 Naye Elisha+ alikuwa ameshikwa na ugonjwa ambao ulikuwa wa kumuua.+ Basi Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kuja kwake, akaanza kulia juu ya uso wake, akisema: “Baba yangu,+ baba yangu, gari la vita la Israeli na wapanda-farasi wake!”+ 15 Na Elisha akamwambia: “Chukua upinde na mishale.” Basi akachukua upinde na mishale. 16 Naye akaendelea kumwambia mfalme wa Israeli: “Weka mkono kwenye upinde.” Basi akaweka mkono wake kwenye upinde, halafu Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono+ ya mfalme. 17 Ndipo akasema: “Fungua dirisha la upande wa mashariki.” Basi akalifungua. Mwishowe Elisha akasema: “Piga!” Basi akapiga. Sasa akasema: “Mshale wa wokovu wa Yehova, naam, mshale wa wokovu+ juu ya Siria! Nawe hakika utaipiga Siria kule Afeki+ kufikia hatua ya kuimaliza.”

18 Naye akaendelea kusema: “Chukua mishale.” Basi akaichukua. Kisha akamwambia mfalme wa Israeli: “Piga chini.” Basi akapiga mara tatu halafu akaacha.+ 19 Na yule mtu wa Mungu wa kweli+ akamkasirikia; kwa hiyo akasema: “Ilikupasa upige mara tano au mara sita! Kama ingekuwa hivyo, ungeipiga Siria kufikia hatua ya kuimaliza, lakini sasa utaipiga Siria mara tatu.”+

20 Kisha Elisha akafa, nao wakamzika.+ Na palikuwa na vikundi vya waporaji+ vya Wamoabu+ waliokuja kwa ukawaida katika nchi mwanzoni mwa mwaka. 21 Na ikawa kwamba walipokuwa wakimzika mtu, tazama, wakaona kikundi cha waporaji. Wakamtupa mara moja yule mtu ndani ya kaburi la Elisha, wakaenda zao. Mtu yule alipoigusa mifupa ya Elisha, akawa hai+ mara moja na kusimama kwa miguu+ yake.

22 Kwa habari ya Hazaeli+ mfalme wa Siria, yeye aliwakandamiza+ Israeli siku zote za Yehoahazi. 23 Hata hivyo, Yehova akawapa kibali+ na kuwaonea rehema+ na kuwageukia kwa ajili ya agano+ lake na Abrahamu,+ Isaka+ na Yakobo;+ naye hakutaka kuwaangamiza,+ wala hakuwatupilia mbali kutoka mbele za uso wake mpaka sasa. 24 Mwishowe Hazaeli mfalme wa Siria akafa, na Ben-hadadi mwana wake akaanza kutawala mahali pake. 25 Na Yehoashi mwana wa Yehoahazi akachukua tena kutoka mkononi mwa Ben-hadadi mwana wa Hazaeli yale majiji aliyokuwa amechukua kutoka mkononi mwa Yehoahazi baba yake katika vita. Yehoashi akampiga mara tatu, naye akayarudisha majiji ya Israeli.+

14 Katika mwaka wa pili wa Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda, akawa mfalme. 2 Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 29 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Yehoadini+ wa Yerusalemu. 3 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa manyoofu machoni pa Yehova,+ ila tu si kama Daudi babu yake.+ Akafanya kulingana na yote ambayo Yehoashi baba yake alifanya.+ 4 Ni mahali pa juu peke yake ndipo hapakuondolewa.+ Watu walikuwa bado wanatoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu.+ 5 Na ikawa kwamba mara tu ufalme ulipokuwa umeimarishwa mkononi mwake, akaanza kuwapiga na kuwaua+ wale watumishi wake waliompiga na kumuua mfalme, baba yake.+ 6 Naye hakuwaua wana wa wale waliompiga na kumuua, kulingana na yale ambayo yameandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa ambayo Yehova aliamuru, akisema:+ “Akina baba wasiuawe kwa sababu ya wana, na wana wasiuawe kwa sababu ya akina baba; bali kila mmoja auawe kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe.”+ 7 Yeye aliwapiga na kuwaua Waedomu+ katika Bonde la Chumvi,+ watu elfu kumi, akateka Sela katika vita hivyo, na jina lake likaitwa Yoktheeli mpaka leo hii.

8 Kisha wakati huo Amazia aliwatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli, na kusema: “Haya njoo. Tutazamane uso kwa uso.”+ 9 Ndipo Yehoashi mfalme wa Israeli akatuma ujumbe kwa Amazia mfalme wa Yuda, na kusema: “Gugu lenye miiba lililokuwa katika Lebanoni lilituma ujumbe kwa mwerezi+ uliokuwa katika Lebanoni, na kusema, ‘Mpe mwanangu binti yako awe mke wake.’ Hata hivyo, mnyama wa mwituni aliyekuwa katika Lebanoni akapita karibu, akalikanyaga lile gugu lenye miiba.+ 10 Bila shaka umepiga+ Edomu, na moyo wako umekuinua.+ Furahia heshima+ yako na ukae nyumbani kwako mwenyewe. Kwa nini, basi, ujiingize katika mzozo+ chini ya hali zisizofaa+ hata uanguke, wewe na Yuda pamoja nawe?” 11 Na Amazia hakusikiliza.+

Basi Yehoashi mfalme wa Israeli akapanda, nao wakatazamana uso kwa uso,+ yeye na Amazia mfalme wa Yuda, kule Beth-shemeshi,+ ya Yuda. 12 Na Yuda wakashindwa mbele ya Israeli,+ hata wakaanza kukimbia, kila mmoja kwenda katika hema lake. 13 Naye Yehoashi mfalme wa Israeli akamkamata Amazia mfalme wa Yuda mwana wa Yehoashi mwana wa Ahazia kule Beth-shemeshi, kisha wakaja Yerusalemu, naye akabomoa shimo katika ukuta wa Yerusalemu katika Lango la Efraimu+ mpaka kwenye Lango la Pembeni,+ urefu wa mikono mia nne. 14 Naye akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika nyumba ya Yehova+ na katika hazina za nyumba ya mfalme na mateka, kisha akarudi Samaria.

15 Na mambo mengine ya Yehoashi, yale aliyoyafanya na uwezo wake na jinsi alivyopigana na Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 16 Mwishowe Yehoashi akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa katika Samaria+ pamoja na wafalme wa Israeli, na Yeroboamu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

17 Na Amazia+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda akaendelea kuishi kwa miaka kumi na mitano+ baada ya kifo cha Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli. 18 Na mambo mengine ya Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda?+ 19 Baadaye wakaungana katika hila+ juu yake katika Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi;+ lakini wakatuma watu kumfuatilia huko Lakishi, wakamuua huko.+ 20 Kwa hiyo wakambeba juu ya farasi, naye akazikwa+ katika Yerusalemu pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ 21 Ndipo watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria,+ wakati huo akiwa na umri wa miaka kumi na sita,+ nao wakamfanya kuwa mfalme mahali pa Amazia+ baba yake. 22 Yeye alijenga Elathi+ na kulirudisha kwa Yuda baada ya mfalme kulala pamoja na mababu zake.

23 Katika mwaka wa 15 wa Amazia mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli akawa mfalme katika Samaria kwa miaka 41. 24 Naye akaendelea kutenda yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova. Hakuacha dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, alizosababisha Israeli kutenda dhambi.+ 25 Yeye ndiye aliyerudisha mpaka wa Israeli kutoka mwingilio wa Hamathi+ hadi kwenye bahari ya Araba,+ kulingana na neno la Yehova, Mungu wa Israeli, aliyesema kupitia Yona+ mtumishi wake, mwana wa Amitai, nabii aliyetoka Gath-heferi.+ 26 Kwa maana Yehova alikuwa ameyaona mateso machungu sana ya Israeli.+ Hapakuwa na yeyote asiye na uwezo wala yeyote asiye na thamani, wala hapakuwa na msaidizi kwa ajili ya Israeli.+ 27 Na Yehova alikuwa ameahidi kwamba hatafutilia mbali jina la Israeli kutoka chini ya mbingu.+ Basi akawaokoa+ kupitia mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.

28 Kwa habari ya mambo mengine ya Yeroboamu na yote ambayo aliyafanya na uwezo wake, jinsi alivyopigana na jinsi alivyorudisha Damasko+ na Hamathi+ kwa Yuda katika Israeli, je, hayakuandikwa katika kitabu cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 29 Mwishowe Yeroboamu akalala pamoja na mababu zake, pamoja na wafalme wa Israeli, na Zekaria+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

15 Katika mwaka wa 27 wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria+ mwana wa Amazia+ mfalme wa Yuda akawa mfalme. 2 Alikuwa na umri wa miaka 16 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 52 katika Yerusalemu.+ Na jina la mama yake lilikuwa Yekolia wa Yerusalemu. 3 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa manyoofu machoni pa Yehova, kulingana na yote ambayo Amazia baba yake alikuwa amefanya.+ 4 Ni mahali pa juu peke yake ambapo hapakuondolewa.+ Watu walikuwa bado wanatoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu.+ 5 Mwishowe Yehova akamletea mfalme pigo,+ naye akaendelea kuwa mwenye ukoma+ mpaka siku ya kufa kwake, naye akaendelea kukaa katika nyumba yake akiwa ameondolewa wajibu wake,+ huku Yothamu+ mwana wa mfalme akiwa juu ya nyumba, akiwahukumu+ watu wa nchi. 6 Na mambo mengine ya Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 7 Baadaye Azaria akalala pamoja na mababu zake,+ nao wakamzika pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi; na Yothamu mwana wake akaanza kutawala mahali pake.+

8 Katika mwaka wa 38 wa Azaria+ mfalme wa Yuda, Zekaria+ mwana wa Yeroboamu akawa mfalme juu ya Israeli katika Samaria kwa miezi 6. 9 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, kama walivyofanya mababu zake.+ Hakuacha dhambi za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, alizosababisha Israeli kutenda dhambi.+ 10 Ndipo Shalumu mwana wa Yabeshi akapanga hila+ juu yake, akampiga+ katika Ibleamu,+ akamuua, akaanza kutawala mahali pake. 11 Na mambo mengine ya Zekaria, tazama, yameandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli. 12 Hilo lilikuwa ni neno la Yehova+ alilokuwa amemwambia Yehu, akisema:+ “Wana,+ mpaka kizazi cha nne, wataketi kwa ajili yako juu ya kiti cha ufalme cha Israeli.” Na ikawa hivyo.+

13 Kwa habari ya Shalumu mwana wa Yabeshi, alikuwa mfalme katika mwaka wa 39 wa Uzia+ mfalme wa Yuda, naye akaendelea kutawala kwa mwezi mmoja kamili katika Samaria.+ 14 Ndipo Menahemu+ mwana wa Gadi akapanda kutoka Tirsa,+ akaja Samaria na kumpiga Shalumu+ mwana wa Yabeshi katika Samaria na kumuua; naye akaanza kutawala mahali pake. 15 Na mambo mengine ya Shalumu na hila+ yake aliyopanga, tazama, yameandikwa katika kitabu cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli. 16 Wakati huo ndipo Menahemu alipopiga Tifsa na vyote vilivyokuwa ndani yake na eneo lake kutoka Tirsa, kwa sababu haukufunguliwa, naye akaupiga. Akapasua wanawake wote wenye mimba+ wa eneo hilo.

17 Katika mwaka wa 39+ wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme juu ya Israeli kwa miaka 10 katika Samaria. 18 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+ Hakuziacha dhambi zote za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, alizosababisha Israeli kutenda dhambi,+ siku zake zote. 19 Pulu+ mfalme wa Ashuru+ akaingia katika nchi. Basi Menahemu akampa+ Pulu talanta elfu moja za fedha,+ ili mikono yake iwe pamoja naye kuimarisha ufalme mkononi mwake.+ 20 Kwa hiyo Menahemu akaleta fedha ile kwa gharama ya Israeli, kwa gharama ya mashujaa wote, wanaume wenye nguvu,+ ili kumpa mfalme wa Ashuru shekeli 50 za fedha kwa kila mwanamume. Basi mfalme wa Ashuru akarudi, naye hakukaa humo nchini. 21 Na mambo mengine ya Menahemu+ na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 22 Mwishowe Menahemu akalala pamoja na mababu zake, na Pekahia+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

23 Katika mwaka wa 50 wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme juu ya Israeli katika Samaria kwa miaka miwili.+ 24 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+ Hakuziacha dhambi za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, alizosababisha Israeli kutenda dhambi.+ 25 Ndipo Peka+ mwana wa Remalia amiri msaidizi+ wake akapanga hila+ juu yake, akampiga katika Samaria katika mnara wa makao wa nyumba ya mfalme+ pamoja na Argobu na Arie, na pamoja naye palikuwa watu 50 wa wana wa Gileadi. Basi akamuua na kuanza kutawala mahali pake. 26 Na mambo mengine ya Pekahia na yote aliyoyafanya, tazama, yameandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli.

27 Katika mwaka wa 52 wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka+ mwana wa Remalia+ akawa mfalme juu ya Israeli katika Samaria kwa miaka 20. 28 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+ Hakuziacha dhambi za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, alizosababisha Israeli watende dhambi.+ 29 Katika siku za Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-pileseri+ mfalme wa Ashuru+ aliingia na kuchukua Iyoni+ na Abel-beth-maaka+ na Yanoa na Kedeshi+ na Hasori+ na Gileadi+ na Galilaya,+ nchi yote ya Naftali,+ akawachukua na kuwapeleka uhamishoni katika Ashuru.+ 30 Mwishowe Hoshea+ mwana wa Ela akafanya hila+ juu ya Peka mwana wa Remalia, akampiga na kumuua;+ naye akaanza kutawala mahali pake katika mwaka wa 20 wa Yothamu+ mwana wa Uzia. 31 Na mambo mengine ya Peka na yote aliyoyafanya, tazama, yameandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli.

32 Katika mwaka wa pili wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu+ mwana wa Uzia+ mfalme wa Yuda akawa mfalme. 33 Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 16 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Yerusha binti ya Sadoki.+ 34 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova.+ Akafanya kulingana na yote ambayo Uzia baba yake alikuwa amefanya.+ 35 Isipokuwa tu mahali pa juu hapakuondolewa. Watu walikuwa bado wanatoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu.+ Yeye ndiye aliyejenga lango la juu la nyumba ya Yehova.+ 36 Na yale mambo mengine ya Yothamu, aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda?+ 37 Katika siku hizo Yehova alianza kuleta+ juu ya Yuda, Resini+ mfalme wa Siria na Peka+ mwana wa Remalia. 38 Mwishowe Yothamu akalala pamoja na mababu zake, akazikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi babu yake;+ na Ahazi+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

16 Katika mwaka wa kumi na saba wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi+ mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda akawa mfalme. 2 Ahazi alikuwa na umri wa miaka 20 alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu miaka 16; naye hakufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, Mungu wake, kama Daudi babu yake.+ 3 Naye akaendelea kutembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ na hata akampitisha mwana wake mwenyewe katika moto,+ kulingana na machukizo+ ya mataifa ambayo Yehova aliyafukuza kwa sababu ya wana wa Israeli. 4 Naye akaendelea kutoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu+ na juu ya vilima+ na chini ya kila mti wenye majani mengi.+

5 Ndipo Resini+ mfalme wa Siria na Peka+ mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaja juu ya Yerusalemu katika vita na kumzingira Ahazi, lakini hawakuweza kupigana.+ 6 Ndipo Resini mfalme wa Siria akarudisha Elathi+ kwa Edomu, kisha akawaondoa Wayahudi kutoka Elathi; nao Waedomu wakaingia katika Elathi, wakaendelea kukaa humo mpaka leo hii. 7 Kwa hiyo Ahazi akatuma wajumbe kwa Tiglath-pileseri+ mfalme wa Ashuru, na kusema: “Mimi ni mtumishi+ wako na mwana wako. Njoo uniokoe+ kutoka mkononi mwa mfalme wa Siria na kutoka mkononi mwa mfalme wa Israeli, ambao wanasimama kunishambulia.” 8 Basi Ahazi akachukua fedha na dhahabu iliyokuwa katika nyumba ya Yehova na katika hazina za nyumba ya mfalme,+ akamtumia mfalme wa Ashuru rushwa.+ 9 Ndipo mfalme wa Ashuru akamsikiliza na mfalme wa Ashuru akaenda Damasko+ na kuliteka,+ akapeleka watu wake uhamishoni kule Kiri,+ naye akamuua Rezini.+

10 Kisha Mfalme Ahazi+ akaenda kukutana na Tiglath-pileseri+ mfalme wa Ashuru kule Damasko, naye akaiona madhabahu+ iliyokuwa katika Damasko. Kwa hiyo Mfalme Ahazi akamtumia Uriya kuhani muundo wa ile madhabahu na kielelezo chake kuhusiana na muundo wake wote.+ 11 Na Uriya+ kuhani akaanza kujenga madhabahu.+ Uriya kuhani akaijenga kulingana na yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ametuma kutoka Damasko, akingojea wakati ambapo Mfalme Ahazi angekuja kutoka Damasko. 12 Mfalme alipokuja kutoka Damasko, ndipo mfalme alipoona ile madhabahu; naye mfalme akaikaribia ile madhabahu+ na kutoa matoleo juu yake.+ 13 Naye akaendelea kutoa toleo lake la kuteketezwa+ na kufukiza moshi+ wa toleo lake la nafaka+ na kumimina toleo lake la kinywaji+ na kunyunyiza damu ya matoleo yake ya ushirika juu ya ile madhabahu. 14 Naye akaleta madhabahu ya shaba+ iliyokuwa mbele za Yehova kutoka mbele ya nyumba, kutoka katikati ya madhabahu yake na nyumba ya Yehova,+ na kuiweka upande wa kaskazini wa madhabahu yake. 15 Na Mfalme Ahazi akatoa amri, naam, kwa Uriya+ kuhani, akisema: “Fukiza toleo la kuteketezwa la asubuhi+ juu ya ile madhabahu kubwa, pia toleo la nafaka la jioni+ na toleo la kuteketezwa la mfalme+ na toleo lake la nafaka na toleo la kuteketezwa la watu wote wa nchi na toleo lao la nafaka na matoleo yao ya kinywaji; na damu yote ya toleo la kuteketezwa na damu yote ya dhabihu unyunyize juu yake. Nayo ile madhabahu ya shaba nitaifikiria.” 16 Na Uriya+ kuhani akafanya kulingana na yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameamuru.+

17 Zaidi ya hayo, Mfalme Ahazi akakata+ vipande-vipande kuta za pembeni+ za yale mabehewa,+ akaziondoa beseni+ juu yake; naye akashusha ile bahari+ kutoka juu ya wale ng’ombe-dume wa shaba+ waliokuwa chini yake, kisha akaiweka juu ya sakafu ya mawe. 18 Na jengo lililofunikwa kwa ajili ya sabato ambalo walikuwa wamejenga katika nyumba na njia ya mfalme ya kuingilia ya nje akalihamisha kutoka katika nyumba ya Yehova kwa sababu ya mfalme wa Ashuru.

19 Na yale mambo mengine ya Ahazi, yale aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 20 Mwishowe Ahazi akalala pamoja na mababu zake, akazikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi;+ na Hezekia+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

17 Katika mwaka wa kumi na mbili wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea+ mwana wa Ela akawa mfalme katika Samaria+ juu ya Israeli kwa miaka tisa. 2 Naye akaendelea kutenda yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, ila tu si kama wafalme wa Israeli waliomtangulia.+ 3 Shalmanesa+ mfalme wa Ashuru+ alipanda kuja kupigana naye, na Hoshea akawa mtumishi wake, akaanza kumlipa ushuru.+ 4 Hata hivyo, mfalme wa Ashuru akatambua kuna hila+ ndani ya Hoshea, kwa vile alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri+ naye hakuleta ushuru kwa mfalme wa Ashuru kama katika miaka ya hapo mwanzoni. Basi mfalme wa Ashuru akamfungia ndani na kuendelea kumfunga kifungoni.+

5 Na mfalme wa Ashuru akapanda kuja juu ya nchi yote na kupanda kuja mpaka Samaria, akalizingira+ kwa miaka mitatu. 6 Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru aliliteka Samaria+ kisha akapeleka Israeli uhamishoni+ katika Ashuru, akaendelea kuwakalisha katika Hala+ na katika Habori kando ya mto Gozani+ na katika majiji ya Wamedi.+

7 Na ikawa kwamba kwa sababu wana wa Israeli walimtendea dhambi+ Yehova, Mungu wao, aliyewapandisha kutoka katika nchi ya Misri kutoka chini ya mkono wa Farao mfalme wa Misri,+ nao wakaanza kuogopa miungu mingine;+ 8 nao wakaendelea kutembea katika sheria+ za mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya wana wa Israeli, na katika sheria za wafalme wa Israeli ambazo walikuwa wametunga; 9 na wana wa Israeli wakatafuta mambo ambayo hayakuwa sawa kumwelekea Yehova Mungu wao,+ wakaendelea kujijengea mahali pa juu+ katika majiji yao yote, kuanzia mnara+ wa walinzi mpaka jiji lenye ngome; 10 nao wakaendelea kujisimamishia nguzo takatifu+ na miti mitakatifu+ juu ya kila kilima+ kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi;+ 11 na hapo katika mahali pote pa juu wakaendelea kufukiza moshi wa dhabihu sawa na mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyapeleka uhamishoni kwa sababu yao, nao wakaendelea kutenda mambo mabaya ili kumtia uchungu+ Yehova;

12 Nao wakaendelea kutumikia sanamu za mavi,+ ambazo Yehova alikuwa amewaambia hivi kuzihusu: “Msifanye jambo hili”;+ 13 na Yehova akaendelea kuonya+ Israeli+ na Yuda+ kupitia manabii+ wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni kutoka katika njia zenu mbaya,+ mshike amri+ zangu, sheria+ zangu, kulingana na sheria+ yote niliyowaamuru mababu+ zenu na ambayo nimepeleka kwenu kupitia watumishi wangu manabii”;+ 14 nao hawakusikiliza lakini wakaendelea kufanya shingo zao kuwa ngumu+ kama shingo za mababu zao ambao hawakuonyesha imani+ katika Yehova Mungu wao; 15 nao wakaendelea kukataa masharti yake na agano+ lake alilofanya na mababu zao na vikumbusho+ vyake alivyokuwa amewaonya navyo, nao wakaendelea kufuata sanamu za ubatili+ nao wenyewe wakawa ubatili,+ naam, kwa kuiga mataifa yaliyowazunguka pande zote, ambao Yehova alikuwa amewaamuru wasifanye kama wao;+

16 Nao wakaendelea kuacha amri+ zote za Yehova, Mungu wao, wakajitengenezea sanamu za kuyeyushwa,+ ndama wawili,+ na kutengeneza mti mtakatifu,+ nao wakaanza kuliinamia jeshi lote la mbinguni+ na kutumikia Baali;+ 17 nao wakaendelea kuwapitisha motoni+ wana wao na binti zao na kufanya uaguzi+ na kutafuta ishara za bahati,+ nao wakaendelea kujiuza+ ili kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, ili kumtia uchungu;+

18 Kwa hiyo Yehova akakasirikia+ Israeli sana, hivi kwamba akawaondoa machoni pake.+ Hakuacha yeyote abaki isipokuwa kabila la Yuda peke yake.+

19 Hata Yuda hawakushika amri za Yehova, Mungu wao,+ lakini walianza kutembea katika sheria za Israeli+ ambazo walitunga. 20 Basi Yehova akaukataa uzao+ wote wa Israeli, akaendelea kuwatesa na kuwatia mkononi mwa waporaji, mpaka alipowatupilia mbali kutoka mbele zake.+ 21 Kwa maana alirarua Israeli kutoka katika nyumba ya Daudi, nao wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme; na Yeroboamu+ akawatenga Israeli wasimfuate Yehova, naye akawasababisha watende dhambi kubwa.+ 22 Na wana wa Israeli wakatembea katika dhambi zote za Yeroboamu alizokuwa ametenda.+ Hawakuziacha, 23 mpaka Yehova alipoondoa Israeli kutoka mbele za macho yake,+ kama alivyokuwa amesema kupitia kwa watumishi wake wote manabii.+ Basi Israeli wakatoka katika udongo wao wenyewe, wakaenda uhamishoni katika Ashuru mpaka leo hii.+

24 Basi mfalme wa Ashuru akaleta watu kutoka Babiloni+ na Kutha na Ava+ na Hamathi+ na Sefarvaimu,+ akawakalisha katika majiji ya Samaria+ badala ya wana wa Israeli; nao wakaanza kumiliki Samaria na kukaa katika majiji yake. 25 Na ikawa kwamba walipoanza kukaa humo, hawakumwogopa+ Yehova. Kwa hiyo Yehova akatuma simba+ katikati yao, nao wakaja kuwa wauaji katikati yao. 26 Basi wakatuma neno kwa mfalme wa Ashuru, na kusema: “Mataifa ambayo umepeleka uhamishoni na kuwakalisha katika majiji ya Samaria hawajui dini ya Mungu wa nchi hiyo, hivi kwamba yeye anazidi kutuma simba katikati yao;+ na tazama! wanawaua, kwa vile hakuna wowote wanaojua dini ya Mungu wa nchi hiyo.”

27 Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru, akisema: “Pelekeni huko mmoja wa makuhani+ mliopeleka uhamishoni kutoka huko, ili aende na kukaa huko, awafundishe dini ya Mungu wa nchi hiyo.” 28 Basi mmoja wa makuhani ambaye walikuwa wamempeleka uhamishoni kutoka Samaria akaja na kuanza kukaa katika Betheli,+ naye akawa mwalimu wao kuhusu jinsi wanavyopaswa kumwogopa Yehova.+

29 Hata hivyo, kila taifa tofauti likajifanyia mungu wake mwenyewe,+ ambaye walimweka katika nyumba ya mahali pa juu ambapo Wasamaria walikuwa wamejenga, kila taifa tofauti, katika majiji yao ambamo walikuwa wakikaa. 30 Na watu wa Babiloni wakatengeneza Sukoth-benothi, na watu wa Kuthi+ wakatengeneza Nergali, na watu wa Hamathi wakatengeneza Ashima. 31 Nao Waavi+ wakatengeneza Nibhazi na Tartaki; na Wasefarvaimu+ wakawa wakiwateketeza wana wao motoni+ kwa Adrameleki na Anameleki miungu ya Sefarvaimu. 32 Nao wakawa wakimwogopa Yehova, wakaanza kujifanyia makuhani+ wa mahali pa juu kutoka kwa watu wa kawaida, wakawa watendaji kwa ajili yao katika nyumba ya mahali pa juu. 33 Wakawa wakimwogopa Yehova,+ lakini wakaiabudu miungu yao wenyewe,+ kulingana na dini ya yale mataifa ambayo kutoka katikati yao waliwapeleka uhamishoni.+

34 Mpaka leo hii wanafanya kulingana na dini zao za kwanza.+ Hapakuwa na yeyote aliyemwogopa Yehova+ wala yeyote aliyefanya kulingana na masharti yake na maamuzi yake ya hukumu+ na sheria+ na amri+ ambazo Yehova aliwaamuru wana wa Yakobo,+ ambaye jina lake alilifanya kuwa Israeli;+ 35 wakati Yehova alipofanya agano+ pamoja nao na kuwaamuru, akisema: “Msiogope miungu mingine,+ wala msiinamie wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu.+ 36 Lakini Yehova, aliyewapandisha ninyi kutoka katika nchi ya Misri kwa nguvu kubwa na kwa mkono ulionyooshwa,+ Yeye ndiye mnayepaswa kuogopa,+ nanyi mnapaswa kumwinamia+ yeye, nanyi mnapaswa kumtolea yeye dhabihu.+ 37 Na yale masharti+ na maamuzi ya hukumu+ na sheria na amri alizowaandikia,+ muwe waangalifu kuzitenda sikuzote;+ nanyi msiogope miungu mingine. 38 Na lile agano ambalo nimefanya pamoja nanyi, msilisahau;+ nanyi msiogope miungu mingine.+ 39 Lakini ni Yehova,+ Mungu wenu, mnayepaswa kumwogopa, kwa maana yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mkononi mwa adui+ zenu wote.”

40 Nao hawakutii, lakini walitenda kulingana na dini yao ya kwanza.+ 41 Na hayo mataifa yakawa yakimwogopa Yehova,+ lakini yakazitumikia sanamu zao za kuchongwa. Na wana wao pamoja na wajukuu wao, wanatenda mpaka leo hii kama tu mababu zao walivyotenda.

18 Na ikawa katika mwaka wa tatu wa Hoshea+ mwana wa Ela mfalme wa Israeli kwamba Hezekia+ mwana wa Ahazi+ mfalme wa Yuda akawa mfalme. 2 Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 29 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Abi binti ya Zekaria.+ 3 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova,+ kulingana na yote ambayo Daudi babu yake alikuwa amefanya.+ 4 Yeye ndiye aliyeondoa mahali pa juu+ na kuzivunja vipande-vipande zile nguzo takatifu+ na kukata ule mti mtakatifu+ na kumponda vipande-vipande yule nyoka wa shaba+ ambaye Musa alitengeneza;+ kwa maana mpaka siku hizo wana wa Israeli walikuwa wameendelea kumfukizia moshi wa dhabihu,+ naye alikuwa akiitwa sanamu+ ya nyoka wa shaba. 5 Alimtegemea Yehova Mungu wa Israeli;+ na baada yake hapakuwa na yeyote kama yeye kati ya wafalme wote wa Yuda,+ hata wale waliomtangulia.+ 6 Naye akaendelea kushikamana na Yehova.+ Hakugeuka kando na kuacha kumfuata, bali aliendelea kuzishika amri zake ambazo Yehova alimwamuru Musa.+ 7 Na Yehova akawa pamoja naye.+ Popote ambapo alienda, alitenda kwa busara;+ naye alimwasi mfalme wa Ashuru wala hakumtumikia.+ 8 Yeye ndiye aliyewapiga Wafilisti+ mpaka Gaza+ na pia maeneo yake, kuanzia ule mnara+ wa walinzi mpaka kwenye jiji lenye ngome.

9 Na ikawa katika mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, yaani, mwaka wa saba wa Hoshea+ mwana wa Ela mfalme wa Israeli, kwamba Shalmanesa+ mfalme wa Ashuru akapanda kuja juu ya Samaria, akaanza kulizingira.+ 10 Nao wakaliteka+ mwishoni mwa miaka mitatu; katika mwaka wa sita wa Hezekia, yaani, mwaka wa tisa wa Hoshea mfalme wa Israeli, Samaria likatekwa.+ 11 Kisha mfalme wa Ashuru+ akapeleka Israeli uhamishoni+ katika Ashuru, akawakalisha katika Hala+ na katika Habori+ kando ya mto Gozani na katika majiji ya Wamedi,+ 12 kwa sababu hawakuisikiliza+ sauti ya Yehova Mungu wao, bali waliendelea kuvunja agano lake,+ naam, yote ambayo Musa+ mtumishi wa Yehova aliamuru.+ Hawakusikiliza wala kutenda.

13 Na katika mwaka wa kumi na nne wa Mfalme Hezekia, Senakeribu+ mfalme wa Ashuru+ akapanda kuja juu ya majiji yote yenye ngome ya Yuda na kuyateka. 14 Kwa hiyo Hezekia mfalme wa Yuda akatuma ujumbe kwa mfalme wa Ashuru kule Lakishi, na kusema: “Nimetenda dhambi. Rudi nyuma, utoke juu yangu. Lolote utakalonitwika, nitalichukua.”+ Basi mfalme wa Ashuru akaweka juu ya Hezekia mfalme wa Yuda talanta+ 300 za fedha na talanta 30 za dhahabu. 15 Kwa hiyo Hezekia akatoa fedha yote iliyopatikana katika nyumba ya Yehova+ na katika hazina za nyumba ya mfalme.+ 16 Wakati huo Hezekia akaing’oa milango ya hekalu la Yehova+ na miimo ambayo Hezekia mfalme wa Yuda alikuwa ameifunika,+ kisha akampa mfalme wa Ashuru.

17 Na mfalme wa Ashuru+ akatuma Tartani+ na Rabsarisi na Rabshake+ kutoka Lakishi+ kwa Mfalme Hezekia katika Yerusalemu, wakiwa na jeshi kubwa mpaka Yerusalemu. Basi wakapanda, wakaja na kusimama tuli kando ya lile bomba+ la kidimbwi cha juu,+ kilicho kwenye njia kuu ya uwanja wa mfuaji wa nguo.+ 18 Nao wakaanza kumwita mfalme, lakini Eliakimu+ mwana wa Hilkia, aliyekuwa juu ya hiyo nyumba, na Shebna+ mwandishi na Yoa mwana wa Asafu karani, wakatoka nje, wakawajia.

19 Basi Rabshake+ akawaambia: “Tafadhali, mwambieni Hezekia, ‘Mfalme mkuu,+ mfalme wa Ashuru, amesema hivi: “Ni tumaini gani hili ambalo umelitegemea?+ 20 Wewe umesema (lakini hilo ni neno la midomo), ‘Kuna mashauri+ na nguvu kwa ajili ya vita.’ Sasa umeweka tegemeo lako katika nani, hivi kwamba ukaniasi+ mimi? 21 Sasa tazama! umeweka tegemeo lako katika usaidizi wa tete hili lililopondeka,+ Misri,+ ambalo, mtu akiliegemea, hakika litaingia mkononi mwake na kuuchoma. Hivyo ndivyo Farao+ mfalme wa Misri alivyo kwa wote wanaomtegemea. 22 Nanyi mkiniambia, ‘Tumeweka tegemeo+ letu katika Yehova,+ Mungu wetu,’ je, yeye siye ambaye mahali pake pa juu+ na madhabahu zake Hezekia+ ameondoa, huku akiwaambia Yuda na Yerusalemu, ‘Mnapaswa kuinama mbele ya madhabahu hii katika Yerusalemu’?”’+ 23 Basi sasa, tafadhali, mpeni dhamana+ bwana wangu mfalme wa Ashuru, nami niwape farasi elfu mbili tuone ikiwa mnaweza kuweka wapanda-farasi juu yao.+ 24 Unawezaje, basi, kugeuza nyuma uso wa gavana mmoja wa watumishi wadogo zaidi wa bwana wangu,+ na huku wewe unategemea Misri kwa ajili ya magari+ na kwa ajili ya wapanda-farasi?+ 25 Sasa je, nimekuja juu ya mahali hapa ili kupaharibu bila kupewa mamlaka kutoka kwa Yehova? Yehova mwenyewe aliniambia,+ ‘Nenda juu ya nchi hii, nawe lazima uiharibu.’”

26 Ndipo Eliakimu+ mwana wa Hilkia na Shebna+ na Yoa+ wakamwambia Rabshake:+ “Tafadhali, sema na watumishi wako katika lugha+ ya Kisiria, kwa maana tunaweza kusikia; wala usiseme nasi katika lugha+ ya Wayahudi masikioni mwa wale watu walio juu ya ukuta.” 27 Lakini Rabshake akawaambia: “Je, bwana wangu amenituma kusema maneno haya kwenu na kwa bwana wenu? Je, si kwa wale watu ambao wameketi juu ya ukuta, ili wale mavi+ yao wenyewe na kunywa mkojo wao wenyewe pamoja nanyi?”+

28 Na Rabshake akaendelea kusimama na kuita kwa sauti kubwa katika lugha ya Wayahudi;+ naye akaendelea kusema: “Sikieni neno la mfalme mkuu,+ mfalme wa Ashuru. 29 Mfalme amesema hivi, ‘Msiache Hezekia awadanganye ninyi, kwa maana hawezi kuwakomboa kutoka mkononi mwangu.+ 30 Wala msiache Hezekia awafanye ninyi mkamtegemee Yehova,+ na kusema: “Hakika Yehova atatukomboa,+ na jiji hili halitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 31 Msimsikilize Hezekia; kwa maana mfalme wa Ashuru amesema hivi: “Salimuni amri kwangu, mtoke nje mje kwangu, mle kila mtu kutokana na mzabibu wake mwenyewe na kila mtu kutokana na mtini+ wake mwenyewe na mnywe kila mtu maji ya tangi+ lake mwenyewe, 32 mpaka nije na kuwachukua ninyi na kwa kweli niwapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe,+ nchi yenye nafaka na divai mpya, nchi yenye mkate+ na mashamba ya mizabibu,+ nchi yenye mizeituni ya mafuta na asali;+ nanyi mwendelee kuishi, msije mkafa. Nanyi msimsikilize Hezekia, kwa maana anawashawishi ninyi, akisema, ‘Yehova mwenyewe atatukomboa.’+ 33 Je, kila mmoja wa miungu ya mataifa ameikomboa+ kwa vyovyote nchi yake mwenyewe kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?+ 34 Iko wapi miungu ya Hamathi+ na Arpadi?+ Iko wapi miungu ya Sefarvaimu,+ Hena+ na Iva?+ Je, imekomboa Samaria kutoka mkononi mwangu?+ 35 Ni miungu gani kati ya miungu yote ya nchi ambayo imeikomboa nchi yao kutoka mkononi mwangu,+ hivi kwamba Yehova akomboe Yerusalemu kutoka mkononi mwangu?”’”+

36 Na watu wakaendelea kukaa kimya+ wala hawakumjibu+ neno lolote, kwa maana amri ya mfalme ilisema: “Hampaswi kumjibu.”+ 37 Lakini Eliakimu+ mwana wa Hilkia, aliyekuwa juu ya hiyo nyumba, na Shebna+ mwandishi na Yoa+ mwana wa Asafu karani wakaja kwa Hezekia, mavazi yao yakiwa yameraruliwa,+ wakamwambia maneno ya Rabshake.

19 Na ikawa kwamba mara tu Mfalme Hezekia+ aliposikia, mara moja akayararua mavazi yake,+ akavaa nguo za magunia,+ akaingia ndani ya nyumba ya Yehova.+ 2 Na zaidi ya hayo, akamtuma Eliakimu,+ aliyekuwa juu ya hiyo nyumba, na Shebna+ mwandishi na wanaume wazee wa makuhani wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa Isaya+ nabii, mwana wa Amozi.+ 3 Nao wakamwambia: “Hezekia amesema hivi, ‘Leo ni siku ya taabu+ na ya kemeo+ na ya dharau yenye dhihaka;+ kwa maana wana wamefika mpaka kwenye mlango wa tumbo la uzazi,+ na hakuna nguvu za kuzaa.+ 4 Pengine Yehova Mungu wako atayasikia+ maneno yote ya Rabshake, ambaye mfalme wa Ashuru bwana wake alimtuma ili kumdhihaki+ Mungu aliye hai, naye kwa kweli atamtoza hesabu kwa ajili ya maneno ambayo Yehova, Mungu wako, ameyasikia.+ Nawe uinue sala+ kwa ajili ya mabaki+ ambao wanapatikana.’”

5 Basi watumishi wa Mfalme Hezekia wakaingia kwa Isaya.+ 6 Ndipo Isaya akawaambia: “Mwambieni bwana wenu, ‘Yehova amesema hivi:+ “Usiogope+ kwa sababu ya maneno uliyosikia ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamesema vibaya kunihusu.+ 7 Tazama, ninatia roho+ ndani yake, naye atasikia habari+ na kurudi katika nchi yake mwenyewe; nami hakika nitamwangusha kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.”’”+

8 Baada ya hapo Rabshake+ akarudi na kumkuta mfalme wa Ashuru akipigana na Libna;+ kwa maana alikuwa amesikia kwamba ameondoka Lakishi.+ 9 Alisikia ikisemwa hivi kumhusu Tirhaka mfalme wa Ethiopia: “Tazama, amekuja kupigana nawe.” Kwa hiyo akatuma wajumbe+ tena kwa Hezekia, na kusema: 10 “Mwambieni hivi Hezekia mfalme wa Yuda, ‘Usiache Mungu unayemtegemea akudanganye,+ na kusema: “Yerusalemu+ halitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 11 Tazama! Wewe mwenyewe umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru walizitendea nchi zote kwa kuziangamiza;+ na je, wewe mwenyewe utakombolewa?+ 12 Je, miungu+ ya mataifa ambayo mababu zangu waliharibu imeyakomboa, naam, Gozani+ na Harani+ na Resefu na wana wa Edeni+ waliokuwa katika Tel-asari?+ 13 Yuko wapi—mfalme wa Hamathi+ na mfalme wa Arpadi+ na mfalme wa majiji ya Sefarvaimu, Hena na Iva?’”+

14 Ndipo Hezekia akaichukua ile barua kutoka mkononi mwa wale wajumbe, akaisoma,+ kisha Hezekia akaenda katika nyumba ya Yehova, akaitandaza mbele za Yehova.+ 15 Na Hezekia akaanza kusali+ mbele za Yehova na kusema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli,+ unayeketi juu ya makerubi,+ wewe peke yako ndiye Mungu wa kweli wa falme+ zote za dunia.+ Wewe mwenyewe umezifanya mbingu+ na dunia.+ 16 Tega sikio lako, Ee Yehova, usikie.+ Fungua macho yako,+ Ee Yehova, uone, na uyasikie maneno ya Senakeribu ambayo ametuma ili kumdhihaki+ Mungu aliye hai. 17 Ee Yehova, ni kweli kwamba wafalme wa Ashuru wameharibu mataifa na nchi zao.+ 18 Nao wameiteketeza miungu yao kwa moto, kwa sababu hiyo haikuwa miungu,+ bali kazi ya mikono ya mwanadamu,+ miti na mawe; hivi kwamba wakaiharibu. 19 Na sasa, Ee Yehova Mungu wetu,+ tafadhali, utuokoe+ kutoka mkononi mwake, ili falme zote za dunia zijue kwamba wewe, Ee Yehova, ndiye Mungu peke yako.”+

20 Na Isaya mwana wa Amozi akatuma habari kwa Hezekia, na kusema: “Yehova, Mungu wa Israeli amesema hivi,+ ‘Nimeisikia+ sala+ ambayo umenitolea kumhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru. 21 Yehova amesema neno hili juu yake:

“Bikira, binti Sayuni, amekudharau,+ amekudhihaki.+

Binti Yerusalemu+ ametikisa kichwa+

chake nyuma yako.

22 Umemdhihaki+ nani na kusema vibaya+ juu

yake?

Nawe umepaaza sauti+

yako juu ya nani

Na kuinua macho+ yako juu?

Ni juu ya Mtakatifu wa Israeli!+

23 Umemdhihaki Yehova kupitia wajumbe+ wako, nawe unasema,+

‘Kwa wingi wa magari yangu ya vita+ mimi mwenyewe—

Mimi hakika nitapanda vilele vya maeneo yenye milima,+

Sehemu za mbali zaidi za Lebanoni;+

Nami nitaikata mierezi+ yake iliyotukuka, miberoshi+ yake iliyo bora.

Nami nitaingia mahali pake pa mwisho pa kukaa, msitu wa shamba lake la matunda.+

24 Mimi hakika nitachimba na kunywa maji mageni,

Nami nitaikausha mifereji yote ya Nile ya Misri kwa nyayo za miguu yangu.’+

25 Je, hujasikia?+ Tangu nyakati za zamani za kale ndilo nitakalofanya.+

Tangu siku zilizopita nimelifanya.+

Sasa nitalitimiza.+

Nawe utafanya majiji yenye ngome yawe ukiwa kama marundo ya mabomoko.+

26 Na wakaaji wao watakuwa na mikono minyonge;+

Wataingiwa na hofu tupu na kuona aibu.+

Watakuwa kama majani ya shambani na majani mabichi yaliyo laini,+

Majani ya dari,+ kunapokuwa na kuunguzwa mbele ya upepo wa mashariki.+

27 Nami najua vema+ kuketi kwako kimya na kuondoka+ kwako na kuingia kwako,

Na kujichochea kwako juu yangu,+

28 Kwa sababu kujichochea kwako juu yangu+ na kunguruma kwako kumepanda mpaka ndani ya masikio yangu.+

Nami hakika nitatia kulabu yangu puani mwako na lijamu yangu katikati ya midomo yako,+

Nami hakika nitakurudisha kupitia njia ile uliyoijia.”+

29 “‘Na hii itakuwa ndiyo ishara kwa ajili yako:+ Mimea inayochipuka kutokana na mbegu zilizoanguka+ italiwa mwaka huu, na katika mwaka wa pili nafaka inayochipuka yenyewe; lakini katika mwaka wa tatu pandeni mbegu,+ na mvune na mpande mashamba ya mizabibu na kula mazao yake.+ 30 Na wale watakaoponyoka wa nyumba ya Yuda, wale wanaobaki,+ hakika watatia mizizi kwenda chini na kuzaa matunda kwenda juu.+ 31 Kwa maana mabaki watatoka katika Yerusalemu,+ na wale wanaoponyoka katika Mlima Sayuni.+ Bidii+ ya Yehova wa majeshi itatenda hayo.

32 “‘Ndiyo sababu Yehova amesema hivi kumhusu mfalme wa Ashuru:+ “Hataingia katika jiji+ hili wala hatapiga mshale+ humo wala kulikabili kwa ngao wala kujenga juu yake boma la kulizingira.+ 33 Atarudi kupitia ile njia aliyoijia, naye hataingia ndani ya jiji hili, asema Yehova.+ 34 Nami hakika nitalilinda+ jiji hili ili kuliokoa kwa ajili yangu mwenyewe+ na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”’”+

35 Na ikawa kwamba usiku huo malaika wa Yehova alitoka, akapiga na kuwaua watu 185,000 katika kambi+ ya Waashuru.+ Watu walipoamka asubuhi na mapema, tazama, wote walikuwa mizoga iliyokufa.+ 36 Kwa hiyo Senakeribu+ mfalme wa Ashuru akaondoka, akaenda, akarudi,+ akaanza kukaa katika Ninawi.+ 37 Na ikawa kwamba alipokuwa akiinama nyumbani mwa Nisroki+ mungu wake,+ Adrameleki na Shareza, wanawe yeye mwenyewe, wakampiga na kumuua kwa upanga,+ nao wakakimbia, wakaenda katika nchi ya Ararati.+ Na Esar-hadoni+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

20 Katika siku hizo Hezekia akawa mgonjwa kufikia hatua ya kufa.+ Basi Isaya+ mwana wa Amozi nabii akaingia kwake na kumwambia: “Yehova amesema hivi, ‘Wape amri watu wa nyumba yako,+ kwa maana wewe hakika utakufa wala hutaishi.’”+ 2 Ndipo akageuza uso wake kuelekea ukuta,+ akaanza kusali kwa Yehova,+ akisema: 3 “Nakuomba, Ee Yehova, tafadhali ukumbuke+ jinsi nilivyotembea+ mbele zako kwa ukweli+ na kwa moyo mkamilifu,+ nami nimetenda yaliyokuwa mema machoni pako.”+ Na Hezekia akaanza kulia sana.+

4 Na ikawa kwamba Isaya hakuwa amefika katika ua wa kati, wakati neno la Yehova lilipomjia,+ na kusema: 5 “Rudi, umwambie Hezekia kiongozi+ wa watu wangu, ‘Yehova, Mungu+ wa Daudi babu yako, amesema hivi: “Nimeisikia+ sala+ yako. Nimeyaona machozi+ yako. Tazama, ninakuponya.+ Siku ya tatu utapanda kwenda katika nyumba ya Yehova.+ 6 Na hakika mimi nitaongeza miaka kumi na mitano kwa siku zako, nami nitakukomboa wewe pamoja na jiji hili kutoka katika mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitalilinda+ jiji hili kwa ajili yangu mwenyewe na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”’”+

7 Na Isaya akaendelea kusema: “Chukueni keki ya tini kavu zilizoshinikizwa.”+ Basi wakaichukua na kuitia juu ya lile jipu,+ kisha akapona+ hatua kwa hatua.

8 Wakati huo, Hezekia akamwambia Isaya: “Kuna ishara+ gani kwamba Yehova ataniponya nami hakika nitapanda siku ya tatu kwenda katika nyumba ya Yehova?” 9 Isaya akasema: “Hii ndiyo ishara+ kwa ajili yako kutoka kwa Yehova kwamba Yehova atatenda neno ambalo amesema: Je, kivuli kiende mbele vipandio kumi vya ngazi au kirudi nyuma vipandio kumi?” 10 Ndipo Hezekia akasema: “Ni jambo rahisi kivuli kwenda mbele vipandio kumi, wala si kwamba kivuli kirudi nyuma vipandio kumi.”+ 11 Kwa hiyo Isaya nabii akaanza kumwita Yehova; naye akafanya kile kivuli ambacho kilikuwa kimeshuka kirudi nyuma juu ya vile vipandio, yaani, juu ya vile vipandio vya ngazi ya Ahazi, vipandio kumi kurudi nyuma.+

12 Wakati huo Berodak-baladani+ mwana wa Baladani mfalme wa Babiloni+ alimtumia Hezekia barua+ na zawadi; kwa maana alikuwa amesikia kwamba Hezekia alikuwa mgonjwa. 13 Na Hezekia akawasikiliza na kuwaonyesha nyumba yake yote ya hazina,+ fedha na dhahabu+ na mafuta ya zeri+ na mafuta mazuri na ghala lake la silaha na vyote vilivyokuwa katika hazina zake. Hakuna kitu chochote ambacho Hezekia hakuwaonyesha katika nyumba yake na katika mamlaka yake yote.+

14 Baada ya hapo Isaya nabii akaingia kwa Mfalme Hezekia na kumwambia:+ “Watu hawa walisema nini nao walitoka wapi wakaja kwako?”+ Kwa hiyo Hezekia akasema: “Walitoka katika nchi ya mbali, kutoka Babiloni.” 15 Akaendelea kusema: “Waliona nini ndani ya nyumba yako?” Naye Hezekia akasema: “Waliona kila kitu kilicho ndani ya nyumba yangu. Hakuna chochote ambacho sikuwaonyesha katika hazina zangu.”+

16 Sasa Isaya akamwambia Hezekia: “Sikia neno la Yehova,+ 17 ‘ “Tazama! Siku zinakuja, na vyote vilivyo ndani ya nyumba+ yako na ambavyo mababu zako wameweka akiba mpaka leo hii vitachukuliwa kwenda Babiloni.+ Hakuna chochote kitakachobaki,”+ Yehova amesema. 18 “Na baadhi ya wana wako mwenyewe watakaotoka kwako ambao utawazaa, watachukuliwa+ na kuwa maofisa wa makao+ ya mfalme katika jumba la mfalme wa Babiloni.”’”+

19 Ndipo Hezekia akamwambia Isaya: “Neno la Yehova ambalo umesema ni jema.”+ Naye akaendelea kusema: “Je, sivyo, ikiwa amani na kweli+ zitaendelea kuwapo katika siku zangu?”+

20 Na mambo mengine ya Hezekia na nguvu zake zote na jinsi alivyotengeneza kile kidimbwi+ na bomba+ la maji kisha akaleta maji ndani ya jiji, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 21 Mwishowe Hezekia akalala pamoja na mababu+ zake; na Manase+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

21 Manase+ alikuwa na umri wa miaka 12 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 55 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Hefziba. 2 Naye akafanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ kulingana na machukizo ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa amefukuza kutoka mbele ya wana wa Israeli. 3 Kwa hiyo akajenga tena mahali pa juu ambapo Hezekia baba yake alikuwa amepaharibu,+ akasimamisha madhabahu kwa ajili ya Baali na kutengeneza mti mtakatifu, kama alivyofanya Ahabu+ mfalme wa Israeli; naye akaanza kuliinamia+ jeshi lote la mbinguni+ na kulitumikia.+ 4 Naye akajenga madhabahu katika nyumba ya Yehova,+ ambayo Yehova alikuwa amesema hivi kuihusu: “Nitaweka jina langu katika Yerusalemu.”+ 5 Naye akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni+ katika nyua mbili za nyumba ya Yehova.+ 6 Naye akampitisha motoni mwana wake mwenyewe,+ naye akafanya uchawi,+ akatafuta ishara za bahati na kufanyiza wenye kuwasiliana na pepo+ na wajuzi wa kubashiri+ matukio. Alifanya kwa kiasi kikubwa yale yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, na kumtia uchungu.

7 Na zaidi, akaweka sanamu ya kuchongwa+ ya mti mtakatifu aliyokuwa ametengeneza katika nyumba+ ambayo Yehova alikuwa amemwambia Daudi na Sulemani mwana wake hivi: “Katika nyumba hii na katika Yerusalemu, ambalo nimelichagua kutoka katika makabila yote ya Israeli, nitaliweka jina langu mpaka wakati usio na kipimo.+ 8 Nami sitafanya tena mguu wa Israeli utoke katika nchi niliyowapa mababu zao,+ mradi tu wawe waangalifu kufanya kulingana na yote ambayo nimewaamuru,+ naam, kuhusiana na sheria yote ambayo mtumishi wangu Musa aliwaamuru.” 9 Nao hawakusikiliza,+ lakini Manase akaendelea kuwashawishi wafanye yaliyokuwa mabaya+ kuliko yale mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyaangamiza kutoka mbele ya wana wa Israeli.

10 Na Yehova akaendelea kusema kupitia watumishi wake manabii,+ akisema: 11 “Kwa sababu Manase+ mfalme wa Yuda amefanya machukizo+ haya, ametenda kwa uovu zaidi kuliko yote waliyotenda Waamori+ waliomtangulia, naye akasababisha Yuda watende dhambi+ kwa sanamu zake za mavi. 12 Ndiyo sababu Yehova, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta msiba juu ya Yerusalemu+ na Yuda, ambao yeyote akiusikia masikio yake mawili yatawasha.+ 13 Nami nitanyoosha juu ya Yerusalemu kamba ya kupimia+ iliyotumika juu ya Samaria+ na pia timazi iliyotumiwa juu ya nyumba ya Ahabu;+ nami nitafuta+ kabisa Yerusalemu kama vile mtu anavyofuta kabisa bakuli lisilo na mkono, akilifuta kabisa na kulipindua.+ 14 Nami nitaacha mabaki+ ya urithi+ wangu na kuwatia mkononi mwa adui zao, nao watakuwa vitu vya kuporwa na kunyakuliwa na adui zao wote,+ 15 kwa sababu walifanya yaliyokuwa mabaya machoni pangu nao waliendelea kunitia uchungu tangu siku ile mababu zao walipotoka Misri mpaka leo hii.’”+

16 Manase pia alimwaga kwa wingi sana damu isiyo na hatia,+ mpaka alipolijaza Yerusalemu kutoka mwisho huu mpaka mwisho ule, mbali na dhambi yake aliyosababisha Yuda kutenda dhambi kwa kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+ 17 Na mambo mengine ya Manase na yote aliyoyafanya na dhambi yake aliyotenda, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 18 Mwishowe Manase akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa katika bustani ya nyumba yake, katika bustani ya Uza;+ na Amoni mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

19 Amoni+ alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka miwili+ katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Meshulemethi binti ya Haruzi kutoka Yotba. 20 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, kama alivyofanya Manase baba yake.+ 21 Naye akaendelea kutembea katika njia yote ambayo baba yake alitembea,+ naye akaendelea kuzitumikia sanamu za mavi+ ambazo baba yake alitumikia na kuziinamia. 22 Basi akamwacha Yehova,+ Mungu wa mababu zake, naye hakutembea katika njia ya Yehova.+ 23 Mwishowe watumishi wa Amoni wakampangia hila na kumuua+ mfalme ndani ya nyumba yake mwenyewe. 24 Lakini watu wa nchi wakawapiga na kuwaua wale wote waliompangia hila+ Mfalme Amoni. Kisha watu wa nchi wakamfanya Yosia+ mwana wake kuwa mfalme mahali pake. 25 Na mambo mengine ya Amoni, yale aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 26 Kwa hiyo wakamzika katika kaburi lake ndani ya bustani ya Uza;+ na Yosia+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

22 Yosia+ alikuwa na umri wa miaka 8 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 31 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Yedida binti ya Adaya kutoka Boskathi.+ 2 Naye akafanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova+ na kutembea katika njia yote ya Daudi babu yake,+ naye hakugeuka kando upande wa kuume wala wa kushoto.+

3 Na ikawa katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yosia kwamba mfalme akamtuma Shafani+ mwana wa Azalia mwana wa Meshulamu mwandishi kwenye nyumba ya Yehova, akisema: 4 “Nenda kwa Hilkia+ kuhani mkuu,+ naye ajumlishe pesa+ zinazoletwa katika nyumba ya Yehova+ ambazo watunza-milango+ wamekusanya kutoka kwa watu; 5 nao wazitie mkononi mwa wale wanaofanya kazi,+ waliochaguliwa, katika nyumba ya Yehova, ili wawape wale wanaofanya kazi waliomo katika nyumba ya Yehova ili kurekebisha mipasuko ya nyumba,+ 6 mafundi na wajenzi na waashi, na kununua mbao na mawe yaliyochongwa ili kuirekebisha nyumba.+ 7 Isipokuwa tu hesabu isifanywe ya zile pesa zinazotiwa mkononi mwao,+ kwa maana wanafanya kazi kwa uaminifu.”+

8 Baadaye Hilkia+ kuhani mkuu akamwambia Shafani+ mwandishi:+ “Nimepata kile kitabu chenyewe cha sheria+ katika nyumba ya Yehova.” Basi Hilkia akampa Shafani kile kitabu, naye akaanza kukisoma. 9 Kisha Shafani mwandishi akaingia kwa mfalme, akamjibu mfalme na kusema: “Watumishi wako wamemimina pesa ambazo zilikuwa ndani ya nyumba, nao wanaendelea kuzitia katika mkono wa wale wanaofanya kazi, wale waliochaguliwa, katika nyumba ya Yehova.”+ 10 Na Shafani mwandishi akaendelea kumwambia mfalme, akisema: “Hilkia kuhani amenipa kitabu+ fulani.” Na Shafani akaanza kukisoma mbele ya mfalme.

11 Na ikawa kwamba mara tu mfalme alipoyasikia maneno ya kile kitabu cha ile sheria, akayararua mavazi+ yake mara moja. 12 Kisha mfalme akawaamuru Hilkia kuhani na Ahikamu+ mwana wa Shafani na Akbori mwana wa Mikaya na Shafani mwandishi na Asaya+ mtumishi wa mfalme, akisema: 13 “Nendeni, muulizeni+ Yehova kwa ajili yangu na kwa ajili ya watu na kwa ajili ya Yuda wote kuhusu maneno ya kitabu hiki ambacho kimepatikana; kwa maana ghadhabu ya Yehova+ ni kubwa ambayo imewashwa juu yetu kwa sababu mababu+ zetu hawakuyasikiliza maneno ya kitabu hiki kwa kutenda kulingana na yote ambayo yameandikwa kutuhusu.”+

14 Basi Hilkia kuhani na Ahikamu na Akbori na Shafani na Asaya wakaenda kwa Hulda nabii,+ mke wa Shalumu mwana wa Tikva mwana wa Harhasi, mtunzaji wa mavazi,+ kwa kuwa alikuwa akikaa katika Yerusalemu katika eneo la pili; nao wakaanza kusema naye.+ 15 Naye akawaambia: “Yehova, Mungu wa Israeli, amesema hivi,+ ‘Mwambieni hivi mtu ambaye amewatuma ninyi kwangu: 16 “Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta msiba+ juu ya mahali hapa na juu ya wakaaji+ wake, naam, maneno+ yote ya kile kitabu ambacho mfalme wa Yuda amesoma;+ 17 kwa sababu wameniacha na kwenda kuifukizia moshi wa dhabihu miungu mingine+ ili kunitia uchungu kwa kazi zote za mikono yao,+ na ghadhabu yangu imewashwa juu ya mahali hapa wala haitazimwa.’”’+ 18 Na kwa habari ya mfalme wa Yuda anayewatuma mkamuulize Yehova, mwambieni hivi, ‘Yehova, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Kuhusu yale maneno ambayo umeyasikia,+ 19 kwa sababu moyo+ wako ulikuwa mwororo hivi kwamba ukajinyenyekeza+ kwa sababu ya Yehova uliposikia yale ambayo nimesema juu ya mahali hapa na wakaaji wake ili pawe kitu cha kushangaza na laana,+ nawe ukayararua+ mavazi yako, ukaanza kulia mbele zangu, mimi, naam, mimi nimesikia,” asema Yehova.+ 20 “Ndiyo sababu tazama, nitakukusanya+ wewe kwa mababu zako, nawe hakika utakusanywa kwenye uwanja wa kaburi lako kwa amani,+ na macho yako hayatauona msiba wote ninaouleta juu ya mahali hapa.”’” Nao wakamletea mfalme jibu lile.

23 Kisha mfalme akatuma watu, nao wakakusanya kwake wanaume wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.+ 2 Ndipo mfalme akapanda kwenda katika nyumba ya Yehova, na pia wanaume wote wa Yuda na wakaaji wote wa Yerusalemu pamoja naye, na pia makuhani+ na manabii na watu wote, kuanzia wadogo mpaka wakubwa;+ naye akaanza kusoma+ masikioni mwao maneno yote ya kile kitabu+ cha agano+ kilichokuwa kimepatikana katika nyumba ya Yehova.+ 3 Na mfalme akaendelea kusimama kando ya nguzo+ na kulifanya agano+ mbele za Yehova, ili kutembea+ kwa kumfuata Yehova na kushika amri+ zake na shuhuda+ zake na sheria+ zake kwa moyo+ wote na kwa nafsi+ yote kwa kuyatenda maneno ya agano hili yaliyoandikwa katika kitabu hiki.+ Basi watu wote wakachukua msimamo wao katika agano lile.+

4 Na mfalme akawaamuru Hilkia+ kuhani mkuu na makuhani wa daraja la pili na watunza-milango+ waondoe katika hekalu la Yehova vyombo vyote vilivyotengenezwa kwa ajili ya Baali+ na kwa ajili ya mti mtakatifu+ na kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni.+ Ndipo akaviteketeza kwa moto nje ya Yerusalemu kwenye matuta ya Kidroni,+ naye akayapeleka mavumbi yake kule Betheli.+ 5 Naye akawaondoa kazini makuhani wa miungu ya kigeni, ambao wafalme wa Yuda walikuwa wameweka ili wapate kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu katika majiji ya Yuda na ujirani wa Yerusalemu, na pia wale wanaofukiza moshi wa dhabihu kwa Baali,+ kwa jua na kwa mwezi na kwa makundi-nyota ya unajimu na kwa jeshi lote la mbinguni.+ 6 Tena akauondoa mti mtakatifu+ katika nyumba ya Yehova mpaka nje ya Yerusalemu, kwenye bonde la mto la Kidroni, akauteketeza+ kwa moto katika bonde la mto la Kidroni na kuusaga ukawa mavumbi, akayatupa mavumbi yake juu ya makaburi+ ya wana wa watu. 7 Tena akazibomoa nyumba za wanaume makahaba wa hekaluni+ waliokuwa katika nyumba ya Yehova, mahali ambapo wanawake walikuwa wakifuma vihekalu vya mahema kwa ajili ya ule mti mtakatifu.

8 Kisha akaleta makuhani wote kutoka katika majiji ya Yuda, ili apafanye pasifae kwa ibada mahali pa juu ambapo makuhani walifukiza moshi wa dhabihu, kuanzia Geba+ mpaka Beer-sheba;+ naye akabomoa mahali pa juu pa malango yaliyokuwa katika mwingilio wa lango la Yoshua, mkuu wa jiji, ambapo palikuwa upande wa kushoto mtu anapoingia katika lango la jiji. 9 Makuhani+ wa mahali pa juu tu ndio hawakupanda mpaka kwenye madhabahu ya Yehova katika Yerusalemu, lakini walikula keki zisizo na chachu+ katikati ya ndugu zao. 10 Naye akafanya Tofethi+ pasifae kwa ibada, mahali palipo katika bonde la wana wa Hinomu,+ ili yeyote asipitishe motoni mwana wake wala binti yake+ kwa Moleki.+ 11 Na zaidi ya hayo, akafanya wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wametoa kwa ajili ya jua wakome kuingia katika nyumba ya Yehova kupitia chumba cha kulia+ chakula cha Nathan-meleki ofisa wa makao ya mfalme, kilichokuwa katika roshani; naye akateketeza kwa moto magari ya jua.+ 12 Na madhabahu zilizokuwa juu ya paa ya chumba cha dari+ cha Ahazi ambazo wafalme wa Yuda walitengeneza, na madhabahu+ ambazo Manase alitengeneza katika nyua mbili za nyumba ya Yehova, mfalme akazibomoa, kisha akaziponda hapo, naye akatupa mavumbi yake katika bonde la mto la Kidroni. 13 Na mahali pa juu palipokuwa mbele+ ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa Mlima wa Uharibifu, ambapo Sulemani+ mfalme wa Israeli alijenga kwa ajili ya Ashtorethi+ chukizo la Wasidoni na kwa ajili ya Kemoshi+ chukizo la Moabu na kwa ajili ya Milkomu+ chukizo la wana wa Amoni, mfalme akapafanya pasifae kwa ibada. 14 Naye akavunja+ vipande-vipande zile nguzo takatifu, akaikata miti mitakatifu na mahali pake akajaza mifupa ya binadamu. 15 Na pia madhabahu iliyokuwa katika Betheli,+ mahali pa juu ambapo Yeroboamu+ mwana wa Nebati alitengeneza, ambaye alisababisha Israeli watende dhambi,+ hata akabomoa hiyo madhabahu na pale mahali pa juu. Kisha akapateketeza kwa moto mahali pa juu; akapasaga pakawa mavumbi na kuuteketeza kwa moto ule mti mtakatifu.

16 Yosia alipogeuka, akayaona makaburi yaliyokuwa hapo mlimani. Kwa hiyo akatuma watu kuichukua mifupa kutoka katika makaburi hayo, akaiteketeza+ kwa moto juu ya ile madhabahu, ili aifanye isifae kwa ibada, kulingana na neno la Yehova+ alilotangaza+ yule mtu wa Mungu wa kweli, aliyetangaza mambo hayo. 17 Kisha akasema: “Lile jiwe la kaburi ninaloona pale ni gani?” Ndipo watu wa jiji lile wakamwambia: “Ni kaburi+ la yule mtu wa Mungu wa kweli aliyekuja kutoka Yuda,+ akatangaza mambo haya ambayo umefanya juu ya madhabahu ya Betheli.”+ 18 Kwa hiyo akasema: “Acheni apumzike.+ Yeyote asiisumbue mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na mifupa ya yule nabii+ aliyetoka katika Samaria.

19 Na pia nyumba+ zote za mahali pa juu zilizokuwa katika majiji+ ya Samaria ambazo wafalme+ wa Israeli walijenga ili kusababisha uchungu+ Yosia akaziondoa, naye akazitendea kulingana na matendo yote aliyotenda kule Betheli.+ 20 Basi akawatoa dhabihu juu ya hizo madhabahu makuhani+ wote wa mahali pa juu waliokuwa pale, akateketeza kwa moto mifupa ya binadamu juu yake.+ Ndipo akarudi Yerusalemu.

21 Basi mfalme akawaamuru watu wote, akisema: “Fanyeni pasaka+ kwa Yehova, Mungu wenu, kulingana na yale yaliyoandikwa katika kitabu hiki cha agano.”+ 22 Kwa maana pasaka kama hii haikuwa imefanywa kuanzia siku za waamuzi waliokuwa wamehukumu Israeli,+ wala siku zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.+ 23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yosia pasaka hii ilifanywa kwa Yehova katika Yerusalemu.+

24 Na pia wenye kuwasiliana na pepo+ na wajuzi wa kubashiri+ matukio na terafimu+ na sanamu za mavi+ na machukizo+ yote yaliyokuwa yametokea katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, Yosia akaondoa, ili atende maneno ya sheria+ yaliyoandikwa katika kile kitabu+ ambacho Hilkia kuhani alipata katika nyumba ya Yehova.+ 25 Na hapakuwa na mfalme kama yeye aliyemtangulia ambaye alirudi+ kwa Yehova kwa moyo wake wote na kwa nafsi yake yote+ na kwa nguvu zake zote, kulingana na sheria yote ya Musa; wala baada yake hapajatokea yeyote aliye kama yeye.

26 Hata hivyo, Yehova hakugeuka aiache hasira yake kali inayowaka, hiyo hasira yake ambayo iliwaka juu ya Yuda+ kwa sababu ya mambo yote yenye kutia uchungu ambayo Manase alisababisha watie uchungu.+ 27 Lakini Yehova akasema: “Nitaondoa Yuda+ pia mbele za macho yangu,+ kama nilivyoondoa Israeli;+ nami nitalikataa jiji hili ambalo nimechagua, naam, Yerusalemu, na nyumba ambayo nimesema hivi kuihusu, ‘Jina langu litaendelea kuwa humo.’”+

28 Kwa habari ya mambo mengine ya Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 29 Katika siku zake Farao Neko+ mfalme wa Misri alipanda kuja kwa mfalme wa Ashuru kando ya mto Efrati,+ na Mfalme Yosia akaenda kukutana naye;+ lakini akamuua+ kule Megido+ mara tu alipomwona. 30 Basi watumishi wake wakamsafirisha katika gari kutoka Megido akiwa amekufa, wakamleta Yerusalemu,+ wakamzika katika kaburi lake. Kisha watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi+ mwana wa Yosia wakamtia mafuta na kumfanya kuwa mfalme mahali pa baba yake.

31 Yehoahazi+ alikuwa na umri wa miaka 23 alipoanza kutawala, naye akatawala miezi mitatu katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 32 Naye akaanza kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, kulingana na yote ambayo mababu zake walifanya.+ 33 Na Farao Neko+ akamtia kifungoni+ kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi, ili kumzuia asitawale katika Yerusalemu, kisha akaitoza+ nchi talanta mia moja za fedha+ na talanta moja ya dhahabu.+ 34 Zaidi ya hayo, Farao Neko akamfanya Eliakimu+ mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa Yosia baba yake na kulibadili jina lake kuwa Yehoyakimu; naye akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafa huko mwishowe.+ 35 Na Yehoyakimu akampa Farao fedha+ na dhahabu. Ila tu aliitoza nchi kodi,+ ili atoe fedha kwa agizo la Farao. Kulingana na kiwango cha kodi cha kila mmoja+ akatoza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi, ili kumpa Farao Neko.

36 Yehoyakimu+ alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 11 katika Yerusalemu.+ Na jina la mama yake lilikuwa Zebida binti ya Pedaya kutoka Ruma. 37 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya+ machoni pa Yehova, kulingana na yote ambayo mababu zake walifanya.+

24 Katika siku zake Nebukadneza+ mfalme wa Babiloni akapanda, na kwa hiyo Yehoyakimu akawa mtumishi+ wake kwa miaka mitatu. Hata hivyo, yeye aligeuka na kumwasi. 2 Na Yehova akaanza kuleta juu yake vikundi vya waporaji vya Wakaldayo+ na vikundi vya waporaji vya Wasiria na vikundi vya waporaji vya Wamoabu+ na vikundi vya waporaji vya wana wa Amoni, naye akaendelea kuwaleta juu ya Yuda ili kuiangamiza, kulingana na neno la Yehova+ alilokuwa amesema kupitia watumishi wake manabii. 3 Hayo yalitendeka juu ya Yuda kwa agizo la Yehova tu, ili kuiondoa+ mbele za macho yake kwa sababu ya dhambi za Manase,+ kulingana na yote aliyokuwa ameyafanya; 4 na pia kwa sababu ya damu isiyo na hatia+ aliyokuwa amemwaga, hivi kwamba akalijaza Yerusalemu damu isiyo na hatia, na Yehova hakukubali kutoa msamaha.+

5 Na yale mambo mengine ya Yehoyakimu+ na yote aliyoyatenda, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 6 Mwishowe Yehoyakimu akalala pamoja na mababu zake,+ na Yehoyakini mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

7 Na mfalme wa Misri hakuja tena kamwe+ kutoka katika nchi yake,+ kwa maana mfalme wa Babiloni alikuwa amechukua vyote vilivyokuwa vya mfalme wa Misri+ kuanzia bonde la mto+ la Misri mpaka mto Efrati.+

8 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala miezi mitatu katika Yerusalemu.+ Na jina la mama yake lilikuwa Nehushta binti ya Elnathani wa Yerusalemu. 9 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, kulingana na yote aliyofanya baba yake.+ 10 Wakati huo watumishi wa Nebukadneza mfalme wa Babiloni walipanda mpaka Yerusalemu, hivi kwamba jiji hilo likazingirwa.+ 11 Na Nebukadneza mfalme wa Babiloni akaja juu ya jiji hilo, watumishi wake walipokuwa wanalizingira.+

12 Mwishowe Yehoyakini mfalme wa Yuda akatoka kumwendea mfalme wa Babiloni,+ yeye pamoja na mama+ yake na watumishi wake na wakuu wake na maofisa wake wa makao ya mfalme; na mfalme wa Babiloni akamchukua katika mwaka wake wa nane+ wa kuwa mfalme. 13 Ndipo akaondoa hapo hazina zote za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mfalme,+ akakata vipande-vipande vyombo vyote vya dhahabu+ ambavyo Sulemani mfalme wa Israeli alikuwa ametengeneza katika hekalu la Yehova, kama Yehova alivyokuwa amesema. 14 Naye akapeleka uhamishoni+ Yerusalemu yote na wakuu+ wote na wanaume mashujaa wote, wenye nguvu+—akapeleka uhamishoni watu elfu kumi—na pia kila fundi+ na mjenzi wa maboma. Hakuna yeyote aliyeachwa nyuma isipokuwa watu wa tabaka ya chini+ wa nchi. 15 Ndivyo alivyompeleka Yehoyakini+ uhamishoni Babiloni;+ na mama+ ya mfalme na wake za mfalme na maofisa wake wa makao+ ya mfalme na watu wa kwanza kabisa wa nchi akawapeleka wakiwa watu waliohamishwa kutoka Yerusalemu mpaka Babiloni. 16 Kwa habari ya wale wanaume mashujaa wote, elfu saba, na mafundi na wajenzi wa maboma, elfu moja, wanaume wote wenye nguvu wenye kupigana vita, mfalme wa Babiloni aliwapeleka uhamishoni mpaka Babiloni.+ 17 Tena mfalme wa Babiloni+ akamfanya Matania ndugu ya baba yake+ kuwa mfalme mahali pake. Kisha akabadili jina lake kuwa Sedekia.+

18 Sedekia+ alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 11 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 19 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, kulingana na yote aliyokuwa amefanya Yehoyakimu.+ 20 Kwa maana hayo yalitendeka katika Yerusalemu na katika Yuda kwa sababu ya hasira+ ya Yehova, mpaka alipokuwa amewatupa kutoka mbele za macho yake.+ Na Sedekia akaanza kumwasi mfalme wa Babiloni.+

25 Na ikawa kwamba katika mwaka wa tisa+ wa kuwa kwake mfalme, katika mwezi wa kumi,+ siku ya kumi ya mwezi huo, Nebukadneza+ mfalme wa Babiloni akaja,+ ndiyo, yeye pamoja na jeshi lake lote, juu ya Yerusalemu, akaanza kupiga kambi juu yake na kujenga juu yake ukuta wa kulizingira pande zote.+ 2 Na jiji likazingirwa mpaka mwaka wa kumi na moja wa Mfalme Sedekia. 3 Katika siku ya tisa+ ya mwezi wa nne njaa+ ilikuwa kali ndani ya jiji, na hapakuwa na mkate+ kwa ajili ya watu wa nchi. 4 Na jiji likabomolewa,+ na watu wote wa vita wakakimbia wakati wa usiku kupitia njia ya lango lililo kati ya zile kuta mbili kando ya bustani ya mfalme,+ huku Wakaldayo+ wakiwa wamelizunguka jiji pande zote; naye mfalme akaanza kwenda+ kuelekea upande wa Araba.+ 5 Na jeshi la Wakaldayo+ likamfuatilia mfalme, nao wakamfikia+ katika nchi tambarare za jangwa la Yeriko;+ na jeshi lake lote likatawanyika kutoka upande wake. 6 Ndipo wakamkamata mfalme+ na kumleta kwa mfalme wa Babiloni kule Ribla,+ ili watangaze uamuzi wa hukumu juu yake. 7 Nao wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake,+ naye akayapofusha macho ya Sedekia,+ kisha akamfunga kwa pingu za shaba,+ akampeleka Babiloni.+

8 Na katika mwezi wa tano, siku ya saba ya mwezi huo, yaani, mwaka wa kumi na tisa+ wa Mfalme Nebukadneza mfalme wa Babiloni, Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi, mtumishi wa mfalme wa Babiloni, aliingia ndani ya Yerusalemu.+ 9 Naye akaiteketeza nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme+ na nyumba zote za Yerusalemu;+ na nyumba ya kila mtu mkuu akaiteketeza kwa moto.+ 10 Na jeshi lote la Wakaldayo lililokuwa pamoja na mkuu wa walinzi likazibomoa kuta za Yerusalemu, kuzunguka pande zote.+ 11 Na wale watu wengine+ walioachwa nyuma katika jiji na wale waliokimbia, wakamwendea mfalme wa Babiloni na ule umati mwingine, Nebuzaradani mkuu wa walinzi akawapeleka uhamishoni.+ 12 Na wengine kati ya watu wa hali ya chini+ wa nchi, yule mkuu wa walinzi akawaacha wabaki wakiwa watunza-mizabibu na wafanyakazi wa kulazimishwa.+ 13 Na zile nguzo+ za shaba zilizokuwa katika nyumba ya Yehova, na yale mabehewa+ na ile bahari ya shaba,+ vitu vilivyokuwa katika nyumba ya Yehova, Wakaldayo wakavivunja vipande-vipande na kuichukua shaba yake kuipeleka Babiloni.+ 14 Nao wakachukua makopo na sepetu na mikasi ya taa na vikombe na vyombo+ vyote vya shaba walivyokuwa wakitumia kuhudumu. 15 Na mkuu wa walinzi akachukua vyetezo na mabakuli yaliyokuwa ya dhahabu+ halisi na yale yaliyokuwa ya fedha halisi.+ 16 Kwa habari ya zile nguzo mbili, ile bahari moja na yale mabehewa ambayo Sulemani alikuwa ametengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yehova, hapakuwa na namna ya kujua uzito wa shaba ya vyombo hivyo vyote.+ 17 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa mikono kumi na minane,+ na lile kombe+ juu yake lilikuwa la shaba; na urefu wa lile kombe ulikuwa mikono mitatu; na kamba za nyavu na makomamanga+ kuzunguka pande zote juu ya lile kombe, hivyo vyote, vilikuwa shaba; na nguzo ya pili ilikuwa vivyo hivyo juu ya zile kamba za nyavu.

18 Zaidi ya hayo, yule mkuu wa walinzi akamchukua Seraya+ mkuu wa makuhani na Sefania+ kuhani wa pili na watunza-milango+ watatu; 19 naye akachukua kutoka jijini ofisa mmoja wa makao ya mfalme ambaye alikuwa na amri juu ya watu wa vita, na watu 5 kutoka kwa wale wenye kuingia kwa mfalme waliopatikana jijini; na mwandishi wa mkuu wa jeshi, mwenye kuwakusanya watu wa nchi, na watu 60 kati ya watu wa nchi waliopatikana katika jiji;+ 20 kisha Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi akawachukua,+ na kuwapeleka kwa mfalme wa Babiloni kule Ribla.+ 21 Na mfalme wa Babiloni akawapiga na kuwaua+ kule Ribla katika nchi ya Hamathi.+ Hivyo Yuda wakaenda uhamishoni kutoka katika nchi yao.+

22 Kwa habari ya wale watu+ walioachwa nyuma katika nchi ya Yuda, ambao Nebukadneza mfalme wa Babiloni alikuwa ameacha, akaweka juu yao Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani.+ 23 Wakati wakuu wote wa majeshi,+ wao pamoja na watu wao, waliposikia kwamba mfalme wa Babiloni amemchagua Gedalia, wakamwendea mara moja Gedalia kule Mispa,+ yaani, Ishmaeli mwana wa Nethania na Yohanani mwana wa Karea na Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yaazania mwana wa yule Mmaakathi, wao pamoja na watu wao. 24 Ndipo Gedalia akawaapia+ wao pamoja na watu wao, akawaambia: “Msiogope kuwa watumishi wa Wakaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babiloni, na itakuwa vema kwenu.”+

25 Na ikawa kwamba katika mwezi wa saba,+ Ishmaeli+ mwana wa Nethania mwana wa Elishama wa uzao wa kifalme akaja, na pia watu kumi pamoja naye, nao wakampiga Gedalia,+ akafa, na pia wale Wayahudi na Wakaldayo waliokuwa pamoja naye katika Mispa.+ 26 Ndipo watu wote, kuanzia mdogo mpaka mkubwa, na wakuu wa majeshi wakaondoka, wakaingia Misri;+ kwa maana waliogopa kwa sababu ya Wakaldayo.+

27 Na ikawa kwamba katika mwaka wa 37 wa uhamisho wa Yehoyakini+ mfalme wa Yuda, katika mwezi wa 12, siku ya 27 ya mwezi huo, Evil-merodaki+ mfalme wa Babiloni, katika mwaka wa kuwa kwake mfalme, akakiinua kichwa+ cha Yehoyakini mfalme wa Yuda kutoka katika nyumba ya kifungo; 28 naye akaanza kusema naye mambo mema, kisha akakiweka kiti chake cha ufalme juu zaidi ya vile viti vya wafalme waliokuwa pamoja naye katika Babiloni.+ 29 Naye akamvua mavazi yake ya gerezani;+ naye akala mkate+ daima mbele yake siku zote za maisha yake. 30 Nayo posho+ yake, alipewa posho daima kutoka kwa mfalme, kila siku kama inavyostahili, siku zote za maisha yake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki