Kitabu cha Kwanza cha Wafalme
au, kulingana na Septuajinti ya Kigiriki, KITABU CHA TATU CHA WAFALME
1 Basi Mfalme Daudi alikuwa amezeeka,+ amesonga katika siku; nao wakawa wakimfunika kwa mavazi, lakini akawa hapati joto. 2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia: “Acha wamtafutie mfalme msichana, bikira,+ kwa ajili ya bwana wangu mfalme, naye atamhudumia+ mfalme, awe mtunzaji+ wake; alale kifuani+ pako, na bwana wangu mfalme atapata joto.”+ 3 Nao wakamtafuta msichana mrembo katika eneo lote la Israeli, na mwishowe wakampata Abishagi,+ Mshunamu,+ wakamleta kwa mfalme. 4 Na huyo msichana alikuwa mrembo zaidi;+ naye akawa mtunzaji wa mfalme, akaendelea kumhudumia, na mfalme hakuwa na uhusiano wa kingono pamoja naye.
5 Wakati huo Adoniya+ mwana wa Hagithi+ alikuwa akijiinua,+ akisema: “Ni mimi nitakayetawala nikiwa mfalme!”+ Naye akajitengenezea gari pamoja na wapanda-farasi 50 wanaokimbia mbele yake.+ 6 Na baba yake hakuumiza hisia zake wakati wowote kwa kusema: “Kwa nini umefanya hivi?”+ Naye pia alikuwa na umbo zuri sana,+ na mama yake alimzaa baada ya Absalomu. 7 Naye akashirikiana na Yoabu mwana wa Seruya na Abiathari+ kuhani, nao wakaanza kumsaidia wakiwa wafuasi wa Adoniya.+ 8 Lakini Sadoki+ kuhani na Benaya+ mwana wa Yehoyada na Nathani+ nabii na Shimei+ na Rei na wale wanaume wenye nguvu+ wa Daudi, hawakushirikiana+ na Adoniya.
9 Mwishowe Adoniya akafanya dhabihu+ ya kondoo na ng’ombe na vinono karibu na lile jiwe la Zohelethi, lililoko kando ya En-rogeli,+ akawaalika ndugu zake wote wana wa mfalme+ na wanaume wote wa Yuda watumishi wa mfalme; 10 naye hakumwalika Nathani nabii na Benaya na wale wanaume wenye nguvu na Sulemani ndugu yake. 11 Sasa Nathani+ akamwambia Bath-sheba,+ mama ya Sulemani:+ “Je, hujasikia kwamba Adoniya mwana wa Hagithi+ amekuwa mfalme, na bwana wetu Daudi hajui habari hizo hata kidogo? 12 Sasa, njoo tafadhali, nikupe shauri kwa uzito.+ Nawe uiokoe nafsi yako mwenyewe na nafsi ya mwana wako Sulemani.+ 13 Nenda uingie kwa Mfalme Daudi, umwambie, ‘Je, si wewe, bwana wangu mfalme, uliyemwapia kijakazi wako, ukisema: “Sulemani mwana wako ndiye atakayekuwa mfalme baada yangu, naye ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme”?+ Basi kwa nini Adoniya amekuwa mfalme?’ 14 Tazama! Wakati utakapokuwa bado unasema na mfalme, ndipo mimi nitaingia nyuma yako, nami nitayathibitisha maneno yako.”+
15 Kwa hiyo Bath-sheba akaingia kwa mfalme katika chumba cha ndani,+ na mfalme alikuwa mzee sana,+ na Abishagi,+ Mshunamu, alikuwa akimhudumia mfalme. 16 Ndipo Bath-sheba akainama na kumsujudia+ mfalme, naye mfalme akasema: “Unaomba jambo gani?”+ 17 Basi akamwambia: “Bwana wangu,+ wewe ndiye uliyemwapia kijakazi wako kwa Yehova Mungu wako hivi, ‘Sulemani mwana wako ndiye atakayekuwa mfalme baada yangu, naye ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme.’+ 18 Na sasa, tazama! Adoniya+ amekuwa mfalme, na sasa bwana wangu mfalme hajui hata kidogo habari hizo.+ 19 Naye ametoa dhabihu za ng’ombe na vinono na kondoo kwa wingi sana, akawaalika wana wote wa mfalme+ na Abiathari+ kuhani na Yoabu+ mkuu wa jeshi; lakini hakumwalika Sulemani mtumishi wako.+ 20 Nawe bwana wangu mfalme—macho+ ya Israeli wote yako juu yako, uwaambie ni nani atakayeketi juu ya kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake.+ 21 Na hakika itatukia kwamba mara tu bwana wangu mfalme atakapolala pamoja na mababu zake,+ mimi na mwanangu Sulemani tutaonwa kuwa wahalifu.”
22 Na tazama! alipokuwa bado anasema na mfalme, nabii Nathani akaingia.+ 23 Mara moja wakamwambia mfalme, wakisema: “Tazama, nabii Nathani!” Kisha akaingia mbele ya mfalme, akamsujudia mfalme kifudifudi.+ 24 Ndipo Nathani akasema: “Bwana wangu mfalme, je, ni wewe mwenyewe uliyesema, ‘Adoniya ndiye atakayekuwa mfalme baada yangu, naye ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme’?+ 25 Kwa maana leo ameshuka ili atoe dhabihu+ ya ng’ombe na vinono na kondoo kwa wingi sana, na kuwaalika wana wote wa mfalme na wakuu wa jeshi na Abiathari kuhani;+ na tazama, wanakula na kunywa mbele yake na kusema, ‘Mfalme Adoniya na aishi!’+ 26 Lakini hakunialika mimi mtumishi wako, mimi na Sadoki+ kuhani na Benaya+ mwana wa Yehoyada na Sulemani mtumishi wako.+ 27 Ikiwa jambo hili limetokana na bwana wangu mfalme, basi hukumjulisha mtumishi wako+ ni nani anayepaswa kuketi juu ya kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake.”
28 Mfalme Daudi akajibu na kusema: “Niitieni Bath-sheba.”+ Basi akaingia mbele ya mfalme na kusimama mbele ya mfalme. 29 Na mfalme akaapa+ na kusema: “Kama Yehova anavyoishi+ aliyeikomboa+ nafsi+ yangu kutoka katika taabu zote,+ 30 kama vile ambavyo nilikuapia kwa Yehova, Mungu wa Israeli, nikisema, ‘Sulemani mwana wako ndiye atakayekuwa mfalme baada yangu, naye ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme mahali pangu!’ hivyo ndivyo nitakavyofanya leo hii.”+ 31 Ndipo Bath-sheba akainama kifudifudi, akamsujudia+ mfalme na kusema: “Bwana wangu Mfalme Daudi na aishi mpaka wakati usio na kipimo!”+
32 Mara moja Mfalme Daudi akasema: “Niitieni Sadoki+ kuhani na Nathani nabii na Benaya+ mwana wa Yehoyada.” Basi wakaingia mbele ya mfalme. 33 Na mfalme akawaambia: “Chukueni watumishi+ wa bwana wenu, mkampandishe Sulemani mwanangu juu ya nyumbu-jike wangu,+ mkamshushe mpaka Gihoni.+ 34 Na Sadoki kuhani na Nathani nabii wamtie mafuta+ huko awe mfalme juu ya Israeli; nanyi pigeni baragumu+ na kusema, ‘Mfalme Sulemani na aishi!’+ 35 Nanyi mje mkiwa mnamfuata, naye aingie na kuketi juu ya kiti changu cha ufalme; naye atakuwa mfalme mahali pangu, nami nitampa utume wa kuwa kiongozi juu ya Israeli na juu ya Yuda.” 36 Mara moja Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme na kusema: “Amina!+ Yehova, Mungu wa bwana wangu mfalme na aseme vivyo hivyo.+ 37 Kama vile Yehova alivyokuwa pamoja na bwana wangu mfalme,+ basi na awe na Sulemani+ vivyo hivyo, na akifanye kiti chake cha ufalme kiwe kikuu+ kuliko kiti cha ufalme cha bwana wangu Mfalme Daudi.”
38 Na Sadoki+ kuhani na Nathani+ nabii na Benaya+ mwana wa Yehoyada na Wakerethi+ na Wapelethi+ wakashuka, wakampandisha Sulemani juu ya nyumbu-jike wa Mfalme Daudi,+ kisha wakamleta mpaka Gihoni.+ 39 Kisha Sadoki kuhani akachukua pembe ya mafuta+ kutoka katika hema,+ akamtia mafuta+ Sulemani; nao wakaanza kupiga baragumu, na watu wote wakaanza kusema kwa sauti: “Mfalme Sulemani na aishi!”+ 40 Kisha watu wote wakapanda wakiwa wanamfuata, na watu walikuwa wakipiga filimbi+ na kushangilia kwa shangwe kubwa,+ hivi kwamba dunia+ ikapasuka kwa sababu ya kelele zao.
41 Na Adoniya na wote walioalikwa ambao walikuwa pamoja naye wakasikia habari hizo, wakati walipokuwa wamemaliza kula.+ Yoabu aliposikia sauti ya baragumu, mara moja akasema: “Kelele hizo za jiji lenye fujo+ zinamaanisha nini?” 42 Alipokuwa bado anasema, tazama, Yonathani+ mwana wa Abiathari kuhani akaja. Ndipo Adoniya akasema: “Ingia ndani, kwa maana wewe ni mwanamume mwenye nguvu, nawe unaleta habari njema.”+ 43 Lakini Yonathani akajibu na kumwambia Adoniya: “Hapana! Bwana wetu Mfalme Daudi amemfanya Sulemani kuwa mfalme.+ 44 Na mfalme alituma pamoja naye Sadoki kuhani na Nathani nabii na Benaya mwana wa Yehoyada na Wakerethi na Wapelethi, nao wakampandisha juu ya nyumbu-jike wa mfalme.+ 45 Kisha Sadoki kuhani na Nathani nabii wakamtia mafuta kuwa mfalme+ katika Gihoni; halafu wakaja kutoka huko wakishangilia, na jiji limejaa fujo. Hizo ndizo kelele mlizosikia.+ 46 Na zaidi ya hayo, Sulemani ameketi juu ya kiti cha ufalme.+ 47 Na tena watumishi wa mfalme wameingia ili kumtakia mema bwana wetu Mfalme Daudi, wakisema, ‘Mungu wako na alifanye jina la Sulemani kuwa na fahari kuliko jina lako, na akifanye kiti chake cha ufalme kuwa kikuu kuliko kiti chako cha ufalme!’+ Ndipo mfalme akainama juu ya kitanda.+ 48 Na hivi pia ndivyo alivyosema mfalme, ‘Abarikiwe+ Yehova, Mungu wa Israeli, ambaye leo ametoa mtu wa kuketi juu ya kiti changu cha ufalme, macho yangu yakiwa yanaona jambo hilo!’”+
49 Na wale wote walioalikwa ambao walikuwa pamoja na Adoniya wakaanza kutetemeka na kusimama, na kila mmoja akaenda njia yake.+ 50 Naye Adoniya akaogopa kwa sababu ya Sulemani. Kwa hiyo akasimama, akaenda zake, akazishika pembe za madhabahu.+ 51 Baada ya muda Sulemani akaletewa habari, zikisema: “Tazama, Adoniya amemwogopa Mfalme Sulemani; na tazama, ameshika pembe za madhabahu, akisema, ‘Mfalme Sulemani na aniapie kwanza kabisa kwamba hatamuua mtumishi wake kwa upanga.’” 52 Naye Sulemani akasema: “Ikiwa atakuwa mwanamume shujaa, unywele wake hata mmoja+ hautaanguka chini; lakini ikiwa ubaya utapatikana ndani yake,+ basi yeye atakufa.”+ 53 Basi Mfalme Sulemani akatuma watu, nao wakamshusha kutoka juu ya madhabahu. Kisha akaingia na kumwinamia Mfalme Sulemani; halafu Sulemani akamwambia: “Nenda nyumbani mwako.”+
2 Na mwishowe siku za kufa kwa Daudi zikakaribia;+ naye akamwamuru Sulemani mwana wake, akisema: 2 “Mimi ninaenda katika njia ya dunia yote,+ nawe uwe na nguvu+ na ujionyeshe kuwa mwanamume.+ 3 Nawe lazima ushike wajibu wako kwa Yehova, Mungu wako, kwa kutembea katika njia+ zake, kwa kushika sheria zake, amri zake na maamuzi yake ya hukumu+ na shuhuda zake, kulingana na yaliyoandikwa katika sheria ya Musa,+ ili utende kwa busara katika kila jambo unalofanya na kila mahali unapoenda; 4 ili Yehova atimize neno lake alilosema kunihusu mimi,+ akisema, ‘Wana+ wako wakitunza njia yao kwa kutembea+ mbele zangu katika kweli+ kwa moyo wao wote+ na kwa nafsi yao yote, hakuna mwanamume wa kwako atakayekatiliwa mbali asiketi juu ya kiti cha ufalme cha Israeli.’+
5 “Nawe mwenyewe pia unajua vema jinsi Yoabu mwana wa Seruya alivyonitendea+ kwa jinsi alivyowatendea wakuu wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri+ mwana wa Neri na Amasa+ mwana wa Yetheri,+ alipowaua na kumwaga damu+ ya vita wakati wa amani na kutia damu ya vita katika mshipi wake uliokuwa kiunoni mwake na katika viatu vyake vilivyokuwa miguuni mwake. 6 Nawe utende kulingana na hekima yako,+ na usiache mvi zake zishuke kwa amani+ katika Kaburi.*+
7 “Nawe uwaonyeshe fadhili zenye upendo wana wa Barzilai+ Mgileadi, nao wawe kati ya wale wanaokula mezani pako;+ kwa maana hivyo ndivyo walivyonikaribia+ wakati nilipokimbia mbele ya Absalomu ndugu yako.+
8 “Na tazama, Shimei+ mwana wa Gera, Mbenyamini, kutoka Bahurimu+ yupo pamoja nawe, naye ndiye aliyenilaani kwa laana kali+ siku ile nilipokuwa nikienda Mahanaimu;+ naye ndiye aliyeshuka kuja kunipokea kwenye Yordani,+ hivi kwamba nikamwapia kwa Yehova, nikisema, ‘Mimi sitakuua kwa upanga.’+ 9 Na sasa usimwache bila adhabu,+ kwa maana wewe ni mtu mwenye hekima+ na unajua vema jinsi unavyopaswa kumtendea, nawe lazima ushushe katika Kaburi* mvi+ zake kwa damu.”+
10 Ndipo Daudi akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa katika Jiji la Daudi.+ 11 Na siku ambazo Daudi alitawala juu ya Israeli zilikuwa miaka 40.+ Katika Hebroni+ alitawala miaka 7,+ na katika Yerusalemu alitawala miaka 33.+
12 Naye Sulemani akaketi juu ya kiti cha ufalme cha Daudi baba yake;+ na hatua kwa hatua ufalme wake ukafanywa kuwa imara sana.+
13 Kisha Adoniya mwana wa Hagithi akamjia Bath-sheba,+ mama ya Sulemani. Na mama huyo akasema: “Je, unakuja kwa amani?”+ naye akajibu: “Ni kwa amani.” 14 Naye akaendelea kusema: “Nina jambo fulani kwa ajili yako.” Basi akamwambia: “Sema.”+ 15 Naye akaendelea hivi: “Wewe mwenyewe unajua vema kwamba ufalme ulipaswa kuwa wangu, na Israeli wote walikuwa wamenielekezea uso ili niwe mfalme;+ lakini ufalme ukageuka, ukawa wa ndugu yangu, kwa maana ni kutokana na Yehova kwamba ukawa wake.+ 16 Na sasa ninakuomba jambo moja. Usiugeuzie mbali uso wangu.”+ Basi akamwambia: “Sema.” 17 Naye akaendelea kusema: “Tafadhali, mwambie Sulemani mfalme (kwa maana hataugeuzia mbali uso wako) kwamba anipe Abishagi,+ Mshunamu,+ awe mke wangu.” 18 Ndipo Bath-sheba akasema: “Vema! Mimi mwenyewe nitasema na mfalme kwa ajili yako.”
19 Basi Bath-sheba akaingia kwa Mfalme Sulemani ili aseme naye kwa ajili ya Adoniya.+ Mara moja mfalme akasimama+ ili kumpokea, akamwinamia.+ Kisha akaketi juu ya kiti chake cha ufalme na kumwekea mama ya mfalme kiti cha ufalme, ili aketi upande wake wa kuume.+ 20 Naye akasema: “Nina ombi moja dogo ninalotoa kwako. Usiugeuzie mbali uso wangu.” Basi mfalme akamwambia: “Toa ombi hilo, mama yangu; kwa maana sitaugeuzia mbali uso wako.” 21 Naye akaendelea kusema: “Acha Abishagi, Mshunamu, apewe Adoniya ndugu yako awe mke wake.” 22 Ndipo Mfalme Sulemani akajibu na kumwambia mama yake: “Na kwa nini unaomba Abishagi Mshunamu kwa ajili ya Adoniya? Mwombee pia ufalme+ (kwa sababu yeye ni ndugu yangu aliye mkubwa wangu),+ naam, kwa ajili yake na kwa ajili ya Abiathari+ kuhani na kwa ajili ya Yoabu+ mwana wa Seruya.”+
23 Kwa hiyo Mfalme Sulemani akaapa kwa Yehova, akisema: “Mungu na anitendee hivyo, naye azidishe jambo hilo,+ ikiwa Adoniya hakusema jambo hili dhidi ya nafsi yake mwenyewe.+ 24 Na sasa, kama Yehova anavyoishi+ ambaye amenifanya imara+ na kuendelea kuniketisha juu ya kiti cha ufalme cha Daudi baba yangu+ na ambaye alinifanyia nyumba+ kama vile ambavyo amesema,+ leo Adoniya atauawa.”+ 25 Mara moja Mfalme Sulemani akamtuma Benaya+ mwana wa Yehoyada; akamshambulia, naye akafa.+
26 Na mfalme akamwambia Abiathari+ kuhani: “Nenda Anathothi+ kwenye mashamba yako! Kwa maana unastahili kufa;+ lakini leo hii sitakuua, kwa sababu ulilichukua sanduku la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova+ mbele ya Daudi baba yangu,+ na kwa sababu ulipata mateso wakati wote ambao baba yangu alipata mateso.”+ 27 Basi Sulemani akamfukuza Abiathari asiwe kuhani wa Yehova, ili kutimiza neno la Yehova alilokuwa amesema juu ya nyumba ya Eli+ katika Shilo.+
28 Na habari hiyo ikamfikia Yoabu+—kwa maana Yoabu alikuwa na mwelekeo wa kumfuata Adoniya,+ ingawa hakuwa na mwelekeo wa kumfuata Absalomu+—na Yoabu akakimbia kwenda katika hema+ la Yehova, akashikilia kwa nguvu pembe za madhabahu.+ 29 Kisha Mfalme Sulemani akaambiwa: “Yoabu amekimbia akaenda katika hema la Yehova, na tazama, yupo kando ya madhabahu.” Kwa hiyo Sulemani akamtuma Benaya mwana wa Yehoyada, akisema: “Nenda, mshambulie!”+ 30 Basi Benaya akaingia katika hema la Yehova na kumwambia: “Mfalme amesema hivi, ‘Toka nje!’” Lakini akasema: “Hapana! Kwa maana hapa+ ndipo nitakapokufa.” Ndipo Benaya akamletea mfalme neno, na kusema: “Hivi ndivyo Yoabu amesema, na hivi ndivyo alivyonijibu.” 31 Kisha mfalme akamwambia: “Fanya kama alivyosema, mshambulie; nawe umzike na kuondoa juu yangu na juu ya nyumba ya baba yangu damu+ ambayo Yoabu alimwaga isivyostahili.+ 32 Na Yehova atarudisha damu yake juu ya kichwa chake mwenyewe,+ kwa sababu aliwashambulia watu wawili walio waadilifu na bora kuliko yeye mwenyewe,+ naye akawaua kwa upanga, wakati baba yangu Daudi hakuwa amejua habari hizo,+ yaani, Abneri+ mwana wa Neri mkuu wa jeshi la Israeli+ na Amasa+ mwana wa Yetheri mkuu wa jeshi la Yuda.+ 33 Na damu yao lazima irudi juu ya kichwa cha Yoabu na juu ya kichwa cha uzao wake mpaka wakati usio na kipimo;+ lakini kwa ajili ya Daudi+ na kwa ajili ya uzao wake na kwa ajili ya nyumba yake na kwa ajili ya kiti chake cha ufalme, kutakuwa na amani mpaka wakati usio na kipimo kutoka kwa Yehova.”+ 34 Kisha Benaya mwana wa Yehoyada akapanda,+ akamshambulia na kumuua;+ naye akazikwa karibu na nyumba yake mwenyewe nyikani. 35 Ndipo mfalme akamweka Benaya+ mwana wa Yehoyada mahali pake juu ya jeshi;+ na mfalme akamweka Sadoki kuwa kuhani mahali pa Abiathari.+
36 Mwishowe mfalme akatuma watu na kumwita Shimei,+ akamwambia: “Jijengee nyumba katika Yerusalemu, nawe lazima ukae humo wala usitoke kwenda mahali hapa na pale. 37 Na itatukia kwamba siku utakapotoka na kuvuka bonde la mto la Kidroni,+ ujue bila shaka kwamba utakufa hakika.+ Hatia ya damu kwa ajili yako itakuwa juu ya kichwa chako mwenyewe.”+ 38 Kwa hiyo Shimei akamwambia mfalme: “Neno hili ni jema. Mtumishi wako atafanya vile ambavyo bwana wangu mfalme amesema.” Na Shimei akaendelea kukaa katika Yerusalemu siku nyingi.
39 Na ikawa mwishoni mwa miaka mitatu kwamba watumwa+ wawili wa Shimei wakakimbia, wakaenda kwa Akishi+ mwana wa Maaka mfalme wa Gathi;+ na watu wakaja kumwambia Shimei, wakisema: “Tazama! Watumwa wako wako kule Gathi.” 40 Shimei akaondoka mara moja, akatandika punda wake, akaenda Gathi kwa Akishi kuwatafuta watumwa wake; kisha Shimei akaenda, akawaleta watumwa wake kutoka Gathi. 41 Kisha Sulemani akaambiwa: “Shimei ametoka Yerusalemu akaenda Gathi na amerudi.” 42 Ndipo mfalme akatuma na kumwita+ Shimei na kumwambia: “Je, sikukuweka chini ya kiapo kwa Yehova na kukuonya,+ nikisema, ‘Siku utakapotoka kwenda nje na utakapoenda hapa na pale ujue bila shaka kwamba utakufa hakika,’ na je, wewe hukuniambia, ‘Neno ambalo nimesikia ni jema’?+ 43 Kwa nini basi, hukushika kiapo cha Yehova+ na amri ambayo nilikuagiza kwa uzito?”+ 44 Naye mfalme akaendelea kumwambia Shimei: “Wewe mwenyewe unajua vema mabaya yote ambayo moyo wako unajua vema kwamba ulimtendea Daudi baba yangu;+ na Yehova hakika atarudisha mabaya yako juu ya kichwa chako mwenyewe.+ 45 Lakini Mfalme Sulemani atabarikiwa,+ na kiti cha ufalme cha Daudi kitafanywa imara mbele za Yehova milele.”+ 46 Basi mfalme akamwamuru Benaya mwana wa Yehoyada, naye akatoka akamshambulia, akafa.+
Na ufalme ukafanywa imara mkononi mwa Sulemani.+
3 Na Sulemani akafanya mapatano ya ndoa+ pamoja na Farao mfalme wa Misri, akamchukua binti ya Farao,+ akamleta katika Jiji la Daudi,+ mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake mwenyewe+ na nyumba ya Yehova+ na ukuta wa Yerusalemu kuzunguka pande zote.+ 2 Ila tu watu walikuwa wakitoa dhabihu katika mahali pa juu,+ kwa maana nyumba haikuwa imejengwa kwa ajili ya jina la Yehova mpaka siku hizo.+ 3 Na Sulemani akaendelea kumpenda Yehova+ kwa kutembea katika sheria za Daudi baba yake.+ Ila tu alikuwa akitoa dhabihu kwa ukawaida na kufukiza matoleo katika mahali pa juu.+
4 Basi mfalme akaenda Gibeoni+ ili kutoa dhabihu huko, kwa maana huko ndiko kulikokuwa mahali pa juu pakuu.+ Sulemani akatoa dhabihu elfu moja za kuteketezwa juu ya madhabahu ile.+ 5 Yehova akamtokea Sulemani katika ndoto+ usiku kule Gibeoni;+ na Mungu akasema: “Omba kile ninachopaswa kukupa.”+ 6 Kwa hiyo Sulemani akasema: “Wewe mwenyewe umemwonyesha fadhili kuu zenye upendo+ mtumishi wako Daudi baba yangu kulingana na alivyotembea mbele zako katika kweli na katika uadilifu+ na katika unyoofu wa moyo kwako; nawe ukaendelea kushika hizi fadhili kuu zenye upendo kwake, hivi kwamba ukampa mwana wa kuketi juu ya kiti chake cha ufalme kama ilivyo leo hii.+ 7 Na sasa, Yehova Mungu wangu, wewe mwenyewe umemfanya mtumishi wako kuwa mfalme mahali pa Daudi baba yangu, nami ni mvulana mdogo tu.+ Sijui jinsi ya kutoka na jinsi ya kuingia.+ 8 Na mtumishi wako yupo katikati ya watu wako ambao umewachagua,+ watu wengi ambao hawana hesabu wala hawawezi kuhesabiwa kwa kuwa ni wengi.+ 9 Nawe umpe mtumishi wako moyo mtiifu ili awahukumu+ watu wako, atambue kati ya mema na mabaya;+ kwa maana ni nani anayeweza kuwahukumu+ hawa watu wako walio wagumu?”+
10 Na jambo hilo likapendeza machoni pa Yehova, kwa sababu Sulemani alikuwa ameomba jambo hilo.+ 11 Na Mungu akaendelea kumwambia: “Kwa kuwa umeomba jambo hili, wala hukujiombea siku nyingi wala utajiri+ wala kuomba nafsi ya adui zako, nawe umejiombea uelewaji wa kusikia kesi,+ 12 tazama! Hakika nitafanya kulingana na maneno yako.+ Tazama! Mimi hakika nitakupa moyo wenye hekima na wenye uelewaji,+ hivi kwamba hakuna mmoja kama wewe ambaye amekuwako kabla yako, na baada yako hatasimama mwingine kama wewe.+ 13 Na pia nitakupa yale ambayo hukuomba,+ utajiri+ na utukufu pia, hivi kwamba hatakuwapo yeyote kati ya wafalme aliye kama wewe, siku zako zote.+ 14 Nawe ukitembea katika njia zangu kwa kushika masharti+ yangu na amri zangu, kama Daudi baba yako alivyotembea,+ mimi pia nitazirefusha siku zako.”+
15 Wakati Sulemani alipoamka,+ tazama, ilikuwa ni ndoto. Ndipo akaja Yerusalemu, akasimama mbele ya sanduku+ la agano la Yehova, akatoa dhabihu za kuteketezwa na kutoa matoleo ya ushirika,+ akaandaa karamu+ kwa ajili ya watumishi wake wote.+
16 Wakati huo wanawake wawili, makahaba,+ wakaingia kwa mfalme na kusimama mbele yake.+ 17 Ndipo mmoja wa hao wanawake akasema: “Nakuomba radhi, bwana wangu,+ mimi na mwanamke huyu tunakaa katika nyumba moja, nami nilizaa mtoto karibu naye ndani ya nyumba ile. 18 Na ikawa kwamba, katika siku ya tatu baada ya mimi kuzaa, huyu mwanamke pia akazaa. Nasi tulikuwa pamoja. Hapakuwa na mgeni pamoja nasi katika nyumba, hapakuwa yeyote ila sisi wawili katika nyumba. 19 Baadaye mwana wa mwanamke huyu akafa usiku, kwa sababu alimlalia. 20 Kwa hiyo akaamka katikati ya usiku, akamchukua mwanangu kutoka kando yangu wakati kijakazi wako alipokuwa amelala usingizi, akamlaza kifuani pake, na mwana wake mfu akamlaza kifuani pangu. 21 Nilipoamka asubuhi ili kumnyonyesha+ mwanangu, tazama, alikuwa amekufa. Kwa hiyo nikamchunguza kwa makini asubuhi, na tazama! yeye hakuwa mwanangu niliyemzaa.” 22 Lakini yule mwanamke mwingine akasema: “Hapana, lakini mwanangu ndiye aliye hai na mwana wako ndiye aliyekufa!” Wakati huo wote mwanamke huyu alikuwa akisema: “Hapana, lakini mwana wako ndiye aliyekufa na mwanangu ndiye aliye hai.” Nao wakaendelea kusema mbele ya mfalme.+
23 Mwishowe mfalme akasema: “Huyu anasema, ‘Huyu ni mwanangu, aliye hai, na mwana wako ndiye aliyekufa!’ na yule naye anasema, ‘Hapana, lakini mwana wako ndiye aliyekufa na mwanangu ndiye aliye hai!’” 24 Na mfalme akaendelea kusema:+ “Nileteeni upanga.” Basi wakaleta upanga mbele ya mfalme. 25 Naye mfalme akasema: “Mkateni vipande viwili mtoto aliye hai, na nusu moja mkampe huyu mwanamke mmoja na ile nusu nyingine mkampe huyu mwingine.” 26 Mara moja yule mwanamke ambaye mwana wake ndiye aliyekuwa hai akamwambia mfalme (kwa sababu hisia zake za ndani+ ziliamshwa kumhusu mwana wake,+ hivi kwamba akasema): “Nakuomba radhi,+ bwana wangu! Mpeni yeye mtoto aliye hai. Usimuue kamwe.” Wakati huo wote yule mwanamke mwingine alikuwa akisema: “Yeye hatakuwa wangu wala hatakuwa wako. Mkateni!”+ 27 Ndipo mfalme akajibu na kusema: “Mpeni yule mtoto aliye hai, wala msimuue hata kidogo. Yeye ndiye mama yake.”
28 Na Israeli wote wakasikia habari za uamuzi huo wa hukumu+ ambao mfalme alikuwa ametoa; nao wakaogopa kwa sababu ya mfalme,+ kwa maana waliona kwamba hekima+ ya Mungu ilikuwa ndani yake ili afanye uamuzi wa hukumu.
4 Na Mfalme Sulemani akaendelea kuwa mfalme juu ya Israeli yote.+ 2 Na hawa ndio waliokuwa wakuu+ wake: Azaria mwana wa Sadoki,+ kuhani; 3 Elihorefu na Ahiya, wana wa Shisha, waandishi;+ Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi, karani; 4 na Benaya+ mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya jeshi,+ na Sadoki na Abiathari+ walikuwa makuhani; 5 na Azaria mwana wa Nathani+ alikuwa juu ya wasaidizi, na Zabudi mwana wa Nathani alikuwa kuhani, rafiki+ ya mfalme; 6 na Ahishari alikuwa juu ya nyumba, na Adoniramu+ mwana wa Abda, juu ya wale walioandikishwa kufanya kazi ya kulazimishwa.+
7 Na Sulemani alikuwa na wasaidizi kumi na wawili juu ya Israeli yote, nao walimwandalia chakula mfalme na nyumba yake. Kila mmoja alikuwa na daraka la kuandaa chakula mwezi mmoja katika mwaka.+ 8 Na haya yalikuwa majina yao: Mwana wa Huru, katika eneo lenye milima la Efraimu;+ 9 mwana wa Dekeri, kule Makazi na kule Shaalbimu+ na Beth-shemeshi+ na Elon-beth-hanani; 10 mwana wa Hesedi, kule Arubothi (alikuwa na Soko na nchi yote ya Heferi);+ 11 mwana wa Abinadabu, safu yote ya milima ya Dori+ (Tafathi, binti ya Sulemani, akawa mke wake); 12 Baana mwana wa Ahiludi, kule Taanaki+ na Megido+ na Beth-sheani+ yote, ambayo iko kando ya Sarethani+ chini ya Yezreeli,+ kutoka Beth-sheani mpaka Abel-mehola+ mpaka eneo la Yokmeamu;+ 13 mwana wa Geberi, kule Ramothi-gileadi+ (alikuwa na vijiji vya mahema vya Yairi+ mwana wa Manase, vilivyoko Gileadi;+ alikuwa na eneo la Argobu,+ lililoko Bashani:+ majiji makubwa 60 yenye kuta na mapingo ya shaba); 14 Ahinadabu mwana wa Ido, kule Mahanaimu;+ 15 Ahimaazi, kule Naftali+ (yeye pia alimchukua Basemathi, binti ya Sulemani, awe mke wake);+ 16 Baana mwana wa Hushai, kule Asheri+ na Bealothi; 17 Yehoshafati mwana wa Parua, kule Isakari;+ 18 Shimei+ mwana wa Ela, kule Benyamini;+ 19 Geberi mwana wa Uri, katika nchi ya Gileadi,+ nchi ya Sihoni+ mfalme wa Waamori,+ na ya Ogu+ mfalme wa Bashani,+ na palikuwa na msaidizi mmoja juu ya wale wasaidizi wengine wote waliokuwa katika nchi hiyo.
20 Yuda na Israeli walikuwa wengi, kama chembe za mchanga ulio kando ya bahari kwa wingi,+ wakila na kunywa na kushangilia.+
21 Naye Sulemani alikuwa mtawala juu ya falme zote kutoka ule Mto+ hadi kwenye nchi ya Wafilisti na hadi kwenye mpaka wa Misri. Walikuwa wakileta zawadi na kumtumikia Sulemani siku zote za maisha yake.+
22 Na chakula cha Sulemani cha kila siku kwa ukawaida kilikuwa vipimo 30 vya kori+ vya unga laini na vipimo 60 vya kori vya unga, 23 ng’ombe 10 wanono na ng’ombe 20 waliolishwa na kondoo 100, mbali na paa+ kadhaa na swala+ na kulungu na kuku waliononeshwa. 24 Kwa maana alikuwa akitawala kila kitu upande huu wa ule Mto,+ kuanzia Tifsa mpaka Gaza,+ naam, wafalme wote upande huu wa ule Mto;+ naye akawa na amani+ katika maeneo yake yote, kuzunguka pande zote. 25 Na Yuda+ na Israeli wakaendelea kukaa salama,+ kila mtu chini ya mzabibu wake mwenyewe na chini ya mtini wake mwenyewe,+ kuanzia Dani mpaka Beer-sheba,+ siku zote za Sulemani.
26 Na Sulemani akawa na vibanda 40,000 vya farasi+ kwa ajili ya magari+ yake na wapanda-farasi 12,000.
27 Na hao wasimamizi+ wakamletea chakula Mfalme Sulemani na kila mtu aliyekuja mezani pa Mfalme Sulemani, kila mmoja katika mwezi wake. Hawakuacha kitu kipunguke. 28 Nao wakaendelea kuleta mahali popote palipopatikana shayiri na majani kwa ajili ya farasi+ na kwa ajili ya farasi wenye mbio, kila mmoja kulingana na utume wake.+
29 Na Mungu akaendelea kumpa Sulemani hekima+ na uelewaji+ kwa wingi sana na ukunjufu wa moyo,+ kama mchanga ulio kando ya bahari.+ 30 Na hekima ya Sulemani ilikuwa pana+ zaidi kuliko hekima ya watu wengine wote wa Mashariki+ na kuliko hekima yote ya Misri.+ 31 Naye alikuwa na hekima zaidi kuliko mwanadamu mwingine yeyote, kuliko Ethani+ Mwezra, na Hemani+ na Kalkoli+ na Darda wana wa Maholi; na sifa yake ikaenea katika mataifa yote yanayozunguka pande zote.+ 32 Naye alikuwa na uwezo wa kusema methali elfu tatu,+ na nyimbo+ zake zikawa elfu moja na tano. 33 Naye alikuwa akisema kuhusu miti, kuanzia mwerezi ulio katika Lebanoni+ mpaka mhisopo+ unaomea juu ya ukuta; na alikuwa akisema kuhusu wanyama+ na kuhusu viumbe vinavyoruka+ na kuhusu vitu vyenye kutambaa+ na kuhusu samaki.+ 34 Na watu kutoka katika vikundi vyote vya watu wakazidi kuja kuisikia hekima ya Sulemani,+ naam, kutoka kwa wafalme wote wa dunia waliokuwa wamesikia habari za hekima yake.+
5 Na Hiramu+ mfalme wa Tiro+ akatuma watumishi+ wake kwa Sulemani, kwa maana alikuwa amesikia kwamba walikuwa wamemtia yeye mafuta kuwa mfalme mahali pa baba yake; kwa kuwa sikuzote Hiramu alimpenda Daudi.+ 2 Naye Sulemani akatuma watu kwa Hiramu, akisema:+ 3 “Wewe mwenyewe unajua vema kwamba Daudi baba yangu hakuweza kujenga nyumba kwa jina la Yehova, Mungu wake, kwa sababu ya vita+ walivyomzunguka navyo pande zote, mpaka Yehova alipowaweka chini ya miguu yake. 4 Na sasa Yehova Mungu wangu amenipa pumziko kuzunguka pande zote.+ Hakuna mpinzani, wala hakuna jambo baya linalotendeka.+ 5 Na tazama, ninafikiria kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu,+ kama vile Yehova alivyomwahidi Daudi baba yangu, akisema, ‘Mwana wako ambaye nitamweka katika kiti chako cha ufalme mahali pako, yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu.’+ 6 Na sasa amuru kwamba wanikatie mierezi kutoka Lebanoni;+ na watumishi wangu watakuwa pamoja na watumishi wako, nami nitakupa mishahara ya watumishi wako kulingana na yote utakayosema, kwa maana wewe mwenyewe unajua vema kwamba sisi hatuna yeyote anayejua kukata miti kama Wasidoni.”+
7 Na ikawa kwamba mara tu Hiramu+ aliposikia maneno ya Sulemani, akaanza kushangilia sana, naye akasema: “Yehova amebarikiwa+ leo kwa maana amempa Daudi mwana mwenye hekima+ juu ya watu hawa wengi sana!”+ 8 Basi Hiramu akatuma watu kwa Sulemani, akisema: “Nimesikia yale uliyotuma kwangu. Mimi nami nitafanya yote yanayokupendeza kwa habari ya mbao za mierezi na mbao za miberoshi.+ 9 Watumishi wangu watazishusha kutoka Lebanoni+ kwenda baharini; nami nitaziweka katika vyelezo vya magogo ili zisafirishwe baharini mpaka mahali ambapo utanijulisha;+ nami nitazifungua pale, nawe utazichukua; na kufanya mapendezi yangu kwa kutoa chakula kwa ajili ya nyumba yangu.”+
10 Hivyo Hiramu akampa Sulemani mbao za mierezi na mbao za miberoshi kulingana na mapendezi yake yote. 11 Naye Sulemani akampa Hiramu vipimo 20,000 vya kori+ vya ngano viwe chakula kwa ajili ya nyumba yake na vipimo 20 vya kori vya mafuta yaliyopondwa.+ Hivyo ndivyo vitu ambavyo Sulemani alimpa Hiramu mwaka baada ya mwaka.+ 12 Naye Yehova akampa Sulemani hekima, kama vile alivyokuwa amemwahidi;+ na pakawa na amani kati ya Hiramu na Sulemani, nao wawili wakafanya agano.
13 Na Mfalme Sulemani akaendelea kuwaleta wale wote walioandikishwa kufanya kazi ya kulazimishwa kutoka katika Israeli yote; na wale walioandikishwa kufanya kazi ya kulazimishwa+ jumla yao ikawa watu 30,000. 14 Naye akawa akiwapeleka Lebanoni kwa zamu za 10,000 kwa mwezi. Wakaendelea kukaa katika Lebanoni kwa mwezi mmoja, na kwa miezi miwili nyumbani kwao;+ na Adoniramu+ alikuwa juu ya wale walioandikishwa+ kufanya kazi ya kulazimishwa.+ 15 Na Sulemani akawa na+ wabeba-mizigo+ 70,000 na wachongaji wa mawe+ 80,000 mlimani,+ 16 mbali na wasimamizi+ wa kifalme wa Sulemani waliokuwa juu ya kazi, wasimamizi wa kazi+ 3,300 juu ya watu waliokuwa wakifanya kazi. 17 Basi mfalme akaamuru kwamba wachimbe mawe makubwa, mawe yenye bei ghali,+ ili kuweka msingi+ wa nyumba kwa mawe yaliyochongwa.+ 18 Kwa hiyo wajenzi wa Sulemani na wajenzi wa Hiramu na Wagebali+ wakachonga mawe, nao wakaendelea kutayarisha mbao na mawe ili kuijenga nyumba.
6 Na ikawa kwamba katika mwaka wa 480 baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri,+ katika mwaka wa nne,+ katika mwezi wa Zivu,+ yaani, mwezi wa pili,+ baada ya Sulemani kuwa mfalme juu ya Israeli, akaanza kumjengea Yehova nyumba.+ 2 Na nyumba ambayo Mfalme Sulemani alimjengea+ Yehova ilikuwa na urefu wa mikono 60,+ na upana wa mikono 20, na kimo cha mikono 30.+ 3 Na ukumbi+ ulio mbele ya hekalu la nyumba ulikuwa na urefu wa mikono 20, mbele ya upana wa nyumba. Ulikuwa na kina cha mikono 10, mbele ya nyumba.
4 Naye akatengeneza madirisha ya nyumba hiyo, yenye viunzi vinavyozidi kuwa vyembamba.+ 5 Tena akajenga kando ya ukuta jengo la kando lenye kuzunguka pande zote, kando ya kuta za nyumba kuzunguka pande zote lile hekalu na kile chumba cha ndani kabisa,+ akatengeneza vyumba vya kando+ kuzunguka pande zote. 6 Chumba cha ubavuni cha chini kabisa kilikuwa na upana wa mikono mitano, na kile cha katikati kilikuwa na upana wa mikono sita, na kile cha tatu kilikuwa na upana wa mikono saba; kwa maana kulikuwa na vitegemezo+ alivyotia katika nyumba ile katika upande wa nje kuzunguka pande zote, ili kitu chochote kisishikanishwe na kuta za nyumba.+
7 Na wakati nyumba ile ilipokuwa ikijengwa, ilijengwa kwa mawe ya machimbo+ yaliyomalizika tayari; na sauti ya nyundo na mashoka na vifaa vyovyote vya chuma haikusikika katika nyumba+ ile ilipokuwa ikijengwa. 8 Mwingilio+ wa chumba cha ubavuni cha chini kabisa ulikuwa upande wa kuume wa nyumba, nao wakawa wakipanda mpaka kwenye kile cha katikati kwa ngazi inayopinda-pinda, na kupanda kutoka katika kile cha katikati mpaka kwenye kile cha tatu. 9 Tena akaendelea kujenga nyumba ile ili aikamilishe,+ na kufunika ndani ya nyumba ile kwa nguzo na safu za mbao za mierezi.+ 10 Na tena akajenga vile vyumba+ vyenye urefu wa mikono mitano vikiwa kwenye ubavu wa ile nyumba yote, navyo vikaunganishwa na nyumba kwa mbao+ za mierezi.
11 Wakati huo neno la Yehova likamjia Sulemani,+ na kusema:+ 12 “Kwa habari ya nyumba hii unayojenga, kama ukitembea katika sheria+ zangu na kutenda maamuzi yangu ya hukumu+ na kushika amri zangu zote kwa kutembea ndani yake,+ mimi pia hakika nitakutimizia neno nililomwambia Daudi baba yako;+ 13 nami hakika nitakaa katikati ya wana wa Israeli,+ wala sitawaacha watu wangu Israeli.”+
14 Na Sulemani akaendelea kujenga ile nyumba ili aikamilishe.+ 15 Naye akajenga kuta za ndani za nyumba kwa mbao za mierezi. Kuanzia sakafu ya nyumba mpaka kwenye maboriti ya dari akaifunika kwa mbao ndani; naye akaifunika sakafu ya nyumba kwa mbao za miberoshi.+ 16 Tena akajenga mikono 20 pande za nyuma za ile nyumba kwa mbao za mierezi, kuanzia kwenye sakafu mpaka kwenye maboriti, naye akaijengea ndani kile chumba cha ndani kabisa,+ pale Patakatifu Zaidi.+ 17 Na nyumba ile ilikuwa ya mikono 40, yaani, lile hekalu+ lililokuwa mbele yake.+ 18 Na mbao za mierezi ndani ya nyumba zilikuwa na mapambo ya michongo yenye umbo la kibuyu+ na shada za maua.+ Yote ilikuwa ya mierezi; halikuonekana jiwe lolote.
19 Naye akatayarisha ndani kile chumba cha ndani kabisa+ kilicho katikati ya ile nyumba, ili kuweka humo lile sanduku+ la agano+ la Yehova. 20 Na kile chumba cha ndani kabisa kilikuwa na urefu wa mikono 20, na upana wa mikono 20,+ na kimo cha mikono 20; naye akakifunika kwa dhahabu safi,+ na kuifunika madhabahu+ kwa mbao za mwerezi. 21 Na Sulemani akaendelea kuifunika+ nyumba ndani kwa dhahabu safi,+ na kupitisha minyororo ya dhahabu+ mbele ya kile chumba cha ndani kabisa,+ na kukifunika kwa dhahabu. 22 Naye akaifunika nyumba yote kwa dhahabu,+ mpaka nyumba yote ilipokamilika; na madhabahu+ yote iliyokuwa upande wa kile chumba cha ndani kabisa akaifunika kwa dhahabu.+
23 Tena akafanya katika kile chumba cha ndani kabisa makerubi+ wawili wa mbao za mfuta, kila mmoja akiwa na urefu wa mikono kumi.+ 24 Na bawa moja la kerubi lilikuwa mikono mitano, na lile bawa lingine la kerubi lilikuwa mikono mitano. Ilikuwa mikono kumi kuanzia ncha ya bawa lake mpaka ncha ya bawa lake lingine.+ 25 Na yule kerubi wa pili alikuwa mikono kumi. Hao makerubi wawili walikuwa na kipimo kilekile na umbo lilelile. 26 Kimo cha kerubi mmoja kilikuwa mikono kumi, na yule kerubi mwingine vivyo hivyo pia. 27 Kisha akawaweka wale makerubi ndani ya ile nyumba ya ndani, hivi kwamba wakayanyoosha mabawa ya hao makerubi.+ Basi bawa la kerubi mmoja likafika kwenye ukuta na bawa la yule mwingine likafika kwenye ule ukuta mwingine; na mabawa yao yalikuwa kuelekea katikati ya nyumba, bawa kwa bawa yakigusana.+ 28 Tena akawafunika makerubi hao kwa dhahabu.+
29 Na kuta zote kuzunguka ile nyumba akazichonga kwa michongo ya makerubi+ na maumbo ya mitende+ na michongo ya maua,+ ndani na nje; 30 naye akafunika kwa dhahabu sakafu+ ya ile nyumba, ndani na nje. 31 Na mwingilio wa kile chumba cha ndani kabisa akaufanya kwa milango+ ya mbao za mfuta:+ nguzo za kando, miimo ya milango na sehemu ya tano. 32 Na ile milango miwili ilikuwa ya mbao za mfuta, naye akachonga juu yake michongo ya makerubi na maumbo ya mitende na michoro ya maua, naye akaifunika kwa dhahabu; kisha akafua ile dhahabu juu ya wale makerubi na yale maumbo ya mitende. 33 Na hivyo ndivyo alivyofanya kwa ajili ya mwingilio wa hekalu, miimo ya milango ya mbao za mfuta, mraba. 34 Na ile milango miwili ilikuwa ya mbao za mberoshi.+ Zile sehemu mbili za mlango mmoja zilifunguka zikiwa juu ya maegemeo, na zile sehemu mbili za ule mlango mwingine zikafunguka zikiwa juu ya maegemeo.+ 35 Naye akachonga makerubi na maumbo ya mitende na michoro ya maua, na kufunika dhahabu iliyonyooshwa juu ya mifano hiyo.+
36 Naye akaendelea kujenga ua wa ndani+ kwa mistari mitatu+ ya mawe yaliyochongwa na mstari mmoja wa nguzo za mwerezi.
37 Katika mwaka wa nne msingi+ wa nyumba ya Yehova ukawekwa, katika mwezi wa Zivu;+ 38 na katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa Buli, yaani, mwezi wa nane, nyumba ikakamilika+ kuhusiana na mambo yake yote na ramani yake yote;+ hivi kwamba alitumia miaka saba kuijenga.
7 Na Sulemani akajenga nyumba yake mwenyewe kwa miaka kumi na mitatu,+ hivi kwamba akaimaliza nyumba yake yote.+
2 Naye akaanza kuijenga Nyumba ya Msitu wa Lebanoni+ yenye urefu wa mikono 100, na upana wa mikono 50, na kimo cha mikono 30, juu ya mistari minne ya nguzo za mierezi, na palikuwa na nguzo+ za mierezi juu ya zile nguzo. 3 Nayo ilifunikwa kwa mbao za mierezi+ juu ya mataruma yaliyokuwa juu ya zile nguzo 45. Palikuwa na 15 kwa kila mstari. 4 Nayo madirisha yenye viunzi, yalikuwa ya mistari mitatu, na palikuwa na mwanya wa mwangaza+ kuelekeana na mwanya wa mwangaza katika mistari mitatu. 5 Na miingilio yote na miimo ya milango ilikuwa imefanywa kuwa mraba na kiunzi,+ na pia sehemu ya mbele ya ule mwanya wa mwangaza kuelekeana na mwanya wa mwangaza katika mistari mitatu.
6 Na Ukumbi wa Nguzo akaufanya kuwa na urefu wa mikono 50, na upana wake mikono 30; na ukumbi mwingine ulikuwa mbele yake na nguzo na paa mbele yake.
7 Nao Ukumbi wa Kiti cha Ufalme+ ambapo alikuwa afanyie hukumu, akaufanya ukumbi wa hukumu;+ nao wakaufunika kwa mbao za mwerezi kuanzia kwenye sakafu mpaka kwenye maboriti.+
8 Na kuhusu ile nyumba yake ambamo alikuwa akae, katika ule ua mwingine,+ ilikuwa mbali na ile nyumba ya Ukumbi. Ilikuwa hivyo katika muundo. Na palikuwa na nyumba kama Ukumbi huu ambayo alimjengea binti ya Farao,+ ambaye Sulemani alikuwa amemchukua.
9 Hizi zote zilikuwa za mawe ghali+ kulingana na vipimo, yaliyokatwa, yakachongwa kwa misumeno ya mawe, ndani na nje, na kutoka katika msingi mpaka kwenye kigongo cha ukuta, na upande wa nje mpaka kwenye ule ua mkuu.+ 10 Na yale mawe ghali yaliyowekwa kuwa msingi yalikuwa mawe makubwa, mawe ya mikono kumi, na mawe ya mikono minane. 11 Na upande wa juu palikuwa na mawe ghali kulingana na vipimo, yaliyochongwa, na pia mbao za mierezi. 12 Nao ua mkuu kuuzunguka ulikuwa na mistari mitatu+ ya mawe yaliyochongwa na mstari mmoja wa nguzo za mierezi; na vivyo hivyo pia kwa ajili ya ua wa ndani+ wa nyumba+ ya Yehova, na kwa ajili ya ukumbi+ wa nyumba.
13 Naye Mfalme Sulemani akatuma watu na kumleta Hiramu+ kutoka Tiro. 14 Yeye alikuwa mwana wa mwanamke mjane kutoka katika kabila la Naftali, na baba yake alikuwa mwanamume Mtiro,+ fundi wa shaba;+ naye alikuwa amejaa hekima na uelewaji+ na ujuzi kwa ajili ya kufanya kila kazi ya kutumia shaba. Basi akaja kwa Mfalme Sulemani, akaanza kufanya kazi yake yote.
15 Kisha akatengeneza nguzo mbili za shaba,+ kila nguzo ikiwa na urefu wa mikono kumi na minane, na kamba ya urefu wa mikono kumi na miwili ingeweza kupima kuzunguka kila moja ya hizo nguzo mbili.+ 16 Naye akafanya makombe mawili ili kuyaweka juu ya vilele vya zile nguzo, yaliyoyeyushwa katika shaba.+ Kombe moja lilikuwa na urefu wa mikono mitano, na lile kombe lingine lilikuwa na urefu wa mikono mitano. 17 Palikuwa na nyavu katika kamba za nyavu, mapambo yaliyopindwa-pindwa katika minyororo,+ kwa ajili ya makombe yaliyokuwa juu ya vilele vya nguzo;+ saba kwa ajili ya kombe moja, na saba kwa ajili ya lile kombe lingine. 18 Naye akatengeneza makomamanga na mistari miwili kuzunguka kikundi kimoja cha kamba za nyavu ili kufunika yale makombe yaliyokuwa juu ya nguzo; naye akafanya vivyo hivyo kwa lile kombe lingine.+ 19 Na yale makombe yaliyokuwa juu ya zile nguzo kwenye ukumbi yalikuwa ya muundo wa mayungiyungi,+ ya urefu wa mikono minne. 20 Na makombe yalikuwa juu ya zile nguzo mbili, pia karibu na kando ya tumbo lililokuwa linashikanisha zile kamba za nyavu; na palikuwa na makomamanga+ mia mbili katika mistari kuzunguka pande zote juu ya kila kombe.
21 Naye akasimamisha nguzo+ za ukumbi+ wa hekalu. Basi akasimamisha nguzo ya kuume na kuiita jina Yakini, kisha akasimamisha nguzo ya kushoto na kuiita jina Boazi. 22 Na juu ya vilele vya zile nguzo palikuwa na muundo wa maua ya mayungiyungi. Na mwishowe kazi ya zile nguzo ikamalizika.
23 Naye akatengeneza bahari ya kuyeyushwa+ ya mikono 10 kutoka ukingo wake mmoja mpaka ukingo wake mwingine, iliyo mviringo pande zote; na kimo chake kilikuwa mikono 5, na kamba ya urefu wa mikono 30 ingeweza kuizunguka pande zote.+ 24 Na palikuwa na mapambo+ yenye umbo la kibuyu+ chini ya ukingo wake pande zote, yakiwa yameizunguka pande zote, kumi katika kipimo cha urefu wa mkono mmoja, yakiwa yameizunguka bahari pande zote,+ na mistari miwili ya mapambo yenye umbo la kibuyu yakiwa yamefanyizwa katika myeyusho wake. 25 Ilikuwa imesimama juu ya ng’ombe-dume kumi na wawili,+ watatu wakitazama kaskazini, na watatu wakitazama magharibi, na watatu wakitazama kusini, na watatu wakitazama mashariki; na hiyo bahari ilikuwa juu yao, na sehemu zao za nyuma zote zilielekea upande wa katikati.+ 26 Na unene wake ulikuwa upana wa kiganja kimoja;+ na ukingo wake ulikuwa kama muundo wa ukingo wa kikombe, ua la yungiyungi.+ Ingeweza kuchukua+ vipimo elfu mbili vya bathi.+
27 Naye akatengeneza yale mabehewa kumi+ ya shaba, kila behewa likiwa na urefu wa mikono minne, na upana wa mikono minne, na kimo cha mikono mitatu. 28 Na huu ulikuwa ndio muundo wa mabehewa hayo: yalikuwa na kuta za pembeni, na hizo kuta za pembeni zilikuwa kati ya mitarimbo. 29 Na juu ya kuta za pembeni zilizokuwa kati ya ile mitarimbo palikuwa na simba,+ ng’ombe-dume+ na makerubi,+ na juu ya ile mitarimbo ilikuwa hivyo. Juu na chini ya wale simba na wale ng’ombe-dume palikuwa na shada+ katika kazi inayoning’inia. 30 Na palikuwa na magurudumu manne ya shaba kwenye kila behewa, na ekseli za shaba; na sehemu zake nne za pembeni zilikuwa maegemeo yake. Maegemeo yalikuwa chini ya beseni, yakiwa yamefanyizwa kwa shada kuanzia kwa moja mpaka lile lingine. 31 Na kinywa chake kutoka ndani mpaka kwenye maegemeo na kwenda juu kilikuwa urefu wa mikono [?]; na kinywa chake kilikuwa cha mviringo, muundo wa kinara cha urefu wa mkono mmoja na nusu, na pia juu ya kinywa chake palikuwa na michongo. Na kuta zao za pembeni zilikuwa za mraba, si mviringo. 32 Na yale magurudumu manne yalikuwa chini ya zile kuta za pembeni, na yale maegemeo ya magurudumu yalikuwa kando ya behewa; na kimo cha kila gurudumu kilikuwa mkono mmoja na nusu. 33 Na muundo wa yale magurudumu ulikuwa kama muundo wa gurudumu la gari.+ Maegemeo yake na mizingo yake na njukuti zake na vinu vyake, vyote vilikuwa vimeyeyushwa. 34 Na palikuwa na maegemeo manne juu ya pembe nne za kila behewa; maegemeo yake yalikuwa kitu kimoja na lile behewa. 35 Na juu ya lile behewa palikuwa na kinara chenye kimo cha nusu mkono, chote kikiwa mviringo; na juu ya lile behewa pande zake na kuta zake za pembeni zilikuwa kitu kimoja na hicho. 36 Tena juu ya mabamba ya pande zake na juu ya kuta zake za pembeni akachonga+ makerubi, simba na maumbo ya mitende kulingana na nafasi iliyo wazi ya kila kimoja, na shada kuzunguka pande zote.+ 37 Hivi ndivyo alivyoyafanya yale mabehewa kumi;+ yote yalikuwa ya myeyusho mmoja,+ kipimo kimoja, umbo moja.
38 Naye akatengeneza beseni+ 10 za shaba. Kila beseni ingeweza kujazwa kwa vipimo 40 vya bathi. Kila beseni ilikuwa na urefu wa mikono 4. Palikuwa na beseni moja juu ya kila behewa kwa ajili ya yale mabehewa 10. 39 Kisha akaweka mabehewa matano upande wa kuume wa nyumba, na matano upande wa kushoto wa nyumba;+ nayo bahari akaiweka upande wa kuume wa nyumba upande wa mashariki, kuelekea kusini.+
40 Na mwishowe Hiramu+ akatengeneza beseni+ na sepetu+ na mabakuli.+ Baadaye Hiramu akamaliza+ kufanya kazi yote ambayo alimfanyia Mfalme Sulemani kuhusiana na nyumba ya Yehova: 41 Zile nguzo+ mbili na yale makombe+ mawili yenye umbo la bakuli yaliyokuwa juu ya zile nguzo mbili, na zile kamba mbili za nyavu+ za kufunika yale makombe mawili ya mviringo yaliyokuwa juu ya zile nguzo, 42 na yale makomamanga+ mia nne kwa ajili ya zile kamba mbili za nyavu, mistari miwili ya makomamanga kwa kila kamba ya nyavu, ili kufunika yale makombe mawili yenye umbo la bakuli yaliyokuwa juu ya zile nguzo mbili; 43 na yale mabehewa+ kumi na zile beseni+ kumi juu ya yale mabehewa, 44 na ile bahari moja+ na wale ng’ombe-dume kumi na wawili chini ya ile bahari;+ 45 na makopo na sepetu na mabakuli na vyombo hivi vyote,+ ambavyo Hiramu alivitengeneza kutoka kwa shaba iliyong’arishwa kwa ajili ya Mfalme Sulemani kwa ajili ya nyumba ya Yehova. 46 Katika Wilaya ya Yordani+ ndipo Mfalme alipoyeyusha katika kalibu ya udongo wa mfinyanzi, kati ya Sukothi+ na Sarethani.+
47 Naye Sulemani akaacha hivyo vyombo+ vyote bila kupimwa uzito kwa sababu vilikuwa vingi mno ajabu.+ Uzito wa ile shaba haukujulikana.+ 48 Na Sulemani mwishowe akavitengeneza vyombo vyote vya nyumba ya Yehova, madhabahu+ ya dhahabu na meza+ ambayo mkate wa wonyesho ulikuwa juu yake, ya dhahabu, 49 na vinara vya taa,+ vitano upande wa kuume na vitano upande wa kushoto mbele ya kile chumba cha ndani kabisa, vya dhahabu safi,+ na maua+ na taa+ na mikasi ya tambi,+ vyote hivyo vya dhahabu, 50 na beseni na mikasi ya taa+ na mabakuli+ na vikombe+ na vyetezo,+ vya dhahabu safi, na matundu kwa ajili ya milango+ ya nyumba ya ndani, yaani, pale Patakatifu Zaidi, na kwa ajili ya milango+ ya nyumba ya hekalu,+ ya dhahabu.
51 Mwishowe kazi yote ambayo Mfalme Sulemani alipaswa kufanya kuhusiana na nyumba ya Yehova ikamalizika;+ na Sulemani akaanza kuingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa amevifanya kuwa vitakatifu;+ fedha na dhahabu na vyombo akaviweka katika hazina za nyumba ya Yehova.+
8 Wakati huo Sulemani+ akaanza kuwakusanya+ wanaume wazee+ wa Israeli, vichwa vyote vya makabila,+ wakuu wa baba,+ wa wana wa Israeli, waende kwa Mfalme Sulemani katika Yerusalemu, ili kulileta sanduku la agano+ la Yehova kutoka katika Jiji la Daudi,+ yaani, Sayuni.+ 2 Basi wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Sulemani katika mwezi wa Ethanimu katika sherehe,+ yaani, mwezi wa saba.+ 3 Basi wanaume wote wazee wa Israeli wakaja, na makuhani wakaanza kulichukua+ Sanduku.+ 4 Nao wakalipandisha sanduku la Yehova na hema+ la mkutano+ na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa katika hema; na makuhani na Walawi+ wakavipandisha.+ 5 Na Mfalme Sulemani na kusanyiko lote la Israeli pamoja naye, wale waliokutana naye kwa wakati uliowekwa, walikuwa mbele ya lile Sanduku, wakitoa dhabihu+ za kondoo na ng’ombe ambao hawangeweza kuhesabiwa kwa sababu ya wingi.+
6 Ndipo makuhani wakaliingiza ndani mahali pake lile sanduku+ la agano la Yehova, mpaka kwenye chumba cha ndani kabisa cha nyumba, pale Patakatifu Zaidi, mpaka chini ya mabawa ya wale makerubi.+
7 Kwa kuwa makerubi walikuwa wamenyoosha mabawa yao juu ya mahali pa lile Sanduku, hivi kwamba makerubi wakawa wamelifunika Sanduku na miti yake kutoka juu.+ 8 Lakini ile miti+ ilikuwa mirefu, hivi kwamba ncha za miti hiyo zilionekana kutoka Patakatifu mbele ya kile chumba cha ndani kabisa, lakini hazikuonekana nje. Nayo iko hapo mpaka leo hii.+ 9 Hamkuwa na chochote ndani ya lile Sanduku ila yale mabamba mawili+ ya mawe ambayo Musa aliweka+ humo kule Horebu, wakati Yehova alipokuwa amemaliza kufanya agano+ na wana wa Israeli walipokuwa wakitoka katika nchi ya Misri.+
10 Na ikawa kwamba makuhani walipoondoka mahali patakatifu, wingu+ likaijaza nyumba ya Yehova. 11 Na makuhani+ hawakuweza kusimama ili kufanya huduma+ yao kwa sababu ya lile wingu, kwa maana utukufu+ wa Yehova uliijaza nyumba ya Yehova.+ 12 Ndipo wakati ule Sulemani akasema: “Yehova mwenyewe alisema kwamba atakaa katika giza zito.+ 13 Nimefanikiwa kukujengea nyumba ya makao yaliyoinuliwa,+ mahali palipofanywa imara+ ili ukae humo mpaka wakati usio na kipimo.”+
14 Kisha mfalme akageuza uso wake, akaanza kulibariki+ kutaniko lote la Israeli, huku kutaniko lote la Israeli likiwa limesimama. 15 Naye akaendelea kusema: “Amebarikiwa Yehova+ Mungu wa Israeli, aliyesema kwa kinywa chake mwenyewe na Daudi+ baba yangu na kwa mkono wake mwenyewe ametimiza,+ akisema, 16 ‘Kuanzia ile siku niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua+ jiji kutoka katika makabila yote ya Israeli ili kujenga nyumba+ ili jina langu+ likae humo; lakini nitamchagua Daudi awe juu ya watu wangu Israeli.’+ 17 Na likawa jambo lililo moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli.+ 18 Lakini Yehova akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu lilikuwa jambo lililo moyoni mwako kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu, ulifanya vema, kwa sababu lilikuwa jambo lililo moyoni mwako.+ 19 Ila tu wewe mwenyewe hutaijenga nyumba hiyo, lakini mwana wako atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayeijenga nyumba kwa ajili ya jina langu.’+ 20 Na Yehova akatimiza neno lake alilokuwa amesema,+ ili nisimame mahali pa Daudi baba yangu na kuketi juu ya kiti cha ufalme cha Israeli,+ kama Yehova alivyosema, na ili nijenge nyumba kwa ajili ya jina la Yehova, Mungu wa Israeli,+ 21 na ili nipate kuchagua mahali hapo kwa ajili ya lile Sanduku ambamo mna agano+ la Yehova alilofanya na mababu zetu alipokuwa akiwatoa katika nchi ya Misri.”
22 Na Sulemani akaanza kusimama mbele ya madhabahu+ ya Yehova mbele ya kutaniko lote la Israeli, naye sasa akanyoosha mikono yake kuelekea mbinguni;+ 23 naye akaendelea kusema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli,+ hakuna Mungu kama wewe+ juu mbinguni wala chini duniani, anayeshika agano na fadhili zenye upendo+ kwa watumishi wako+ wanaotembea mbele zako kwa moyo wao wote,+ 24 wewe ambaye umemtimizia mtumishi wako Daudi baba yangu yale uliyomwahidi, hivi kwamba ukatoa hiyo ahadi kwa kinywa chako mwenyewe, na kwa mkono wako mwenyewe umetimiza, kama ilivyo leo hii.+ 25 Na sasa, Ee Yehova Mungu wa Israeli, umtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu yale uliyomwahidi, ukisema, ‘Mwanamume wa kwako hatakatiliwa mbali mbele zangu asiketi juu ya kiti cha ufalme cha Israeli,+ ikiwa tu wana wako wataangalia njia yao kwa kutembea mbele zangu kama vile ambavyo wewe umetembea mbele zangu.’ 26 Na sasa, Ee Mungu wa Israeli, tafadhali acha ahadi+ uliyomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu itimie.
27 “Lakini, je, kweli Mungu atakaa duniani?+ Tazama! Mbingu,+ ndiyo, mbingu za mbingu,+ haziwezi kukutosha;+ jinsi gani basi, nyumba hii+ ambayo nimeijenga! 28 Nawe ugeuke kuielekea sala+ ya mtumishi wako na ombi lake la kutaka kibali,+ Ee Yehova Mungu wangu, kusikiliza kilio cha kusihi na sala ambayo mtumishi wako anatoa mbele zako leo;+ 29 ili macho yako yafunguliwe+ kuielekea nyumba hii usiku na mchana, kuelekea mahali ambapo ulisema hivi kupahusu, ‘Jina langu litakuwa hapo,’+ ili kusikiliza sala ambayo mtumishi wako anatoa kuelekea mahali hapa.+ 30 Nawe usikilize ombi la kutaka kibali+ la mtumishi wako na la watu wako Israeli ambalo wanasali kuelekea mahali hapa; nawe usikilize katika makao yako, mbinguni,+ nawe usikie na kusamehe.+
31 “Mwanadamu anapomtendea dhambi mwanadamu mwenzake,+ naye amlaani ili kumtia chini ya wajibu wa laana hiyo,+ naye kwa kweli aingie katika laana hiyo mbele ya madhabahu yako katika nyumba hii, 32 basi na usikie ukiwa mbinguni, nawe utende na kuwahukumu watumishi wako kwa kumtangaza yule mwovu kuwa mwovu kwa kutia njia yake juu ya kichwa chake mwenyewe,+ na kwa kumtangaza mwadilifu+ kuwa mwadilifu kwa kumpa kulingana na uadilifu wake.+
33 “Watu wako Israeli wakishindwa mbele ya adui,+ kwa sababu walizidi kukutendea dhambi,+ nao kwa kweli warudi kwako+ na kulisifu jina lako+ na kusali+ na kutoa ombi la kutaka kibali kwako katika nyumba hii,+ 34 basi na usikie ukiwa mbinguni, nawe usamehe dhambi ya watu wako Israeli+ nawe uwarudishe+ katika nchi uliyowapa mababu zao.+
35 “Mbingu ikifungwa hivi kwamba hakuna mvua inayonyesha,+ kwa sababu waliendelea kukutendea dhambi,+ nao kwa kweli wasali kuelekea mahali hapa+ na kulisifu jina lako, nao wageuke kutoka katika dhambi yao, kwa sababu uliendelea kuwatesa,+ 36 basi na usikie ukiwa mbinguni, nawe usamehe dhambi ya watumishi wako, naam, ya watu wako Israeli, kwa sababu unawafundisha+ njia nzuri wanayopaswa kutembea ndani yake;+ nawe unyeshe mvua+ juu ya nchi yako ambayo umewapa watu wako kuwa fungu la urithi.
37 “Njaa+ ikitokea katika nchi, tauni+ ikitokea, kukitokea joto lenye kuunguza, ukungu,+ nzige,+ mende;+ adui yao akiwazingira katika nchi ya malango yao—pigo la namna yoyote, ugonjwa wa namna yoyote— 38 sala yoyote,+ ombi lolote la kutaka kibali+ ambalo huenda likatolewa na mwanadamu au la watu wako wote Israeli,+ kwa sababu wanajua kila mmoja wao pigo la moyo wake mwenyewe,+ nao wanyooshe mikono yao kuelekea nyumba hii,+ 39 basi na usikie ukiwa mbinguni,+ makao yako yaliyofanywa imara,+ nawe usamehe+ na kutenda+ na kumpa kila mmoja kulingana na njia zake zote,+ kwa sababu unaujua moyo wake+ (kwa maana ni wewe peke yako unayejua vema moyo wa wanadamu wote);+ 40 kusudi wakuogope+ siku zote ambazo wako hai juu ya uso wa nchi ambayo uliwapa mababu zetu.+
41 “Na pia kwa mgeni,+ ambaye si sehemu ya watu wako Israeli na ambaye anatoka katika nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako+ 42 (kwa maana watasikia habari za jina lako kuu+ na za mkono wako wenye nguvu+ na za mkono wako ulionyooshwa), naye kwa kweli aje na kusali kuelekea nyumba hii,+ 43 basi na usikilize ukiwa mbinguni, makao yako yaliyofanywa imara,+ nawe ufanye kulingana na yote ambayo mgeni huyo anakuomba;+ kusudi watu wote wa dunia wajue jina lako+ ili wakuogope kama vile watu wako Israeli wanavyokuogopa, na ili wajue kwamba jina lako limeitwa juu ya nyumba hii ambayo nimeijenga.+
44 “Watu wako wakitoka kwenda vitani+ kupigana na adui yao katika njia ambayo unawatuma,+ nao hakika wasali+ kwa Yehova kuelekea upande wa jiji ambalo umelichagua+ na nyumba ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako,+ 45 basi usikie ukiwa mbinguni sala yao na ombi lao la kutaka kibali, nawe ufanye hukumu kwa ajili yao.+
46 “Nao wakikutendea dhambi+ (kwa sababu hakuna mwanadamu asiyetenda dhambi),+ nawe uwakasirikie na kuwatia mkononi mwa adui, na wenye kuwateka wawachukue mateka na kuwapeleka katika nchi ya adui iliyo mbali au iliyo karibu;+ 47 nao warudiwe na fahamu zao katika nchi ile ambayo wamechukuliwa mateka,+ nao hakika warudi+ na kutoa kwako ombi+ la kutaka kibali katika nchi ya watekaji wao,+ wakisema, ‘Tumetenda dhambi+ na kukosea,+ tumetenda uovu’;+ 48 nao kwa kweli warudi kwako kwa moyo wao wote+ na kwa nafsi yao yote katika nchi ya adui zao waliowachukua mateka, nao wasali kwako kuelekea upande ilipo nchi yao ambayo uliwapa mababu zao, jiji ambalo umelichagua na nyumba ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako;+ 49 basi usikie ukiwa mbinguni, makao yako yaliyofanywa imara,+ sala yao na ombi lao la kutaka kibali, nawe ufanye hukumu kwa ajili yao,+ 50 nawe uwasamehe+ watu wako ambao walikutendea dhambi+ na makosa+ yao yote ambayo walikukosea;+ nawe uwafanye waonyeshwe huruma+ na watekaji wao nao wawahurumie 51 (kwa maana wao ni watu wako na urithi wako,+ ulioutoa katika Misri,+ kutoka ndani ya tanuru ya chuma),+ 52 ili macho yako yafunguliwe kuelekea ombi la mtumishi wako la kutaka kibali na kuelekea ombi la kutaka kibali+ la watu wako Israeli, kwa kuwasikiliza kwa mambo yote ambayo wanakuomba.+ 53 Kwa maana wewe mwenyewe uliwatenga wawe urithi wako kutoka katika vikundi vyote vya watu wa dunia,+ kama vile ulivyosema kupitia mtumishi wako Musa+ ulipokuwa ukiwatoa mababu zetu kutoka Misri, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
54 Na ikawa kwamba mara tu Sulemani alipomaliza kusali kwa Yehova kwa sala hii yote na ombi la kutaka kibali, akasimama kutoka mbele ya ile madhabahu ya Yehova, hapo alipokuwa amepiga magoti+ na mikono yake ikiwa imenyooshwa kuelekea mbinguni;+ 55 naye akaanza kusimama+ na kulibariki+ kutaniko lote la Israeli kwa sauti kubwa, akisema: 56 “Abarikiwe Yehova,+ ambaye amewapa watu wake Israeli mahali pa kupumzika kulingana na yote ambayo ameahidi.+ Halikupungua hata neno moja+ kati ya ahadi zake zote nzuri ambazo ameahidi kupitia Musa mtumishi wake.+ 57 Yehova Mungu wetu na awe pamoja nasi+ kama vile alivyokuwa pamoja na mababu zetu.+ Yeye asituache wala asitutupe,+ 58 ili aelekeze moyo wetu+ kwake ili tutembee katika njia zake zote+ na kushika amri+ zake na masharti+ yake na maamuzi yake ya hukumu,+ ambayo aliwaamuru mababu zetu. 59 Na haya maneno yangu ambayo nimeomba kutaka kibali mbele za Yehova yawe karibu+ na Yehova Mungu wetu, mchana na usiku, ili afanye hukumu kwa ajili ya mtumishi wake na hukumu kwa ajili ya watu wake Israeli kama ambavyo huenda ikahitajika+ siku baada ya siku; 60 ili kusudi vikundi vyote vya watu duniani wajue+ kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli.+ Hakuna mwingine.+ 61 Na moyo wenu uwe kamili+ kwa Yehova, Mungu wetu, kwa kutembea katika masharti yake na kwa kushika amri zake kama ilivyo leo hii.”
62 Na mfalme na Israeli wote pamoja naye wakatoa dhabihu kuu mbele za Yehova.+ 63 Na Sulemani akaanza kutoa dhabihu za ushirika+ alizopasa kumtolea Yehova, ng’ombe 22,000 na kondoo 120,000,+ ili mfalme na wana wote wa Israeli waizindue+ nyumba ya Yehova. 64 Siku hiyo mfalme alilazimika kutakasa sehemu ya katikati ya ua ulio mbele ya nyumba ya Yehova,+ kwa sababu ilimpasa atoe hapo dhabihu ya kuteketezwa na toleo la nafaka na vipande vyenye mafuta vya dhabihu za ushirika; kwa maana ile madhabahu ya shaba+ iliyoko mbele za Yehova ilikuwa ndogo mno isiweze kuchukua ile dhabihu ya kuteketezwa na toleo la nafaka na vipande vya mafuta+ vya dhabihu za ushirika. 65 Na Sulemani akaifanya sherehe hiyo wakati huo,+ na Israeli wote pamoja naye, kutaniko kubwa+ kuanzia maingilio ya Hamathi+ kushuka mpaka kwenye bonde la mto la Misri,+ mbele za Yehova, Mungu wetu, siku saba na tena siku nyingine saba,+ siku kumi na nne. 66 Katika siku ya nane akawaacha watu waende zao;+ nao wakaanza kumbariki mfalme na kwenda kwenye nyumba zao, wakishangilia+ na kufurahi moyoni+ mwao kutokana na wema+ wote ambao Yehova alikuwa ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na kwa ajili ya Israeli watu wake.
9 Na ikawa kwamba mara tu Sulemani alipokuwa amemaliza kujenga nyumba+ ya Yehova na nyumba ya mfalme+ na kila kitu chenye kutamanika cha Sulemani ambacho alipendezwa kukifanya,+ 2 ndipo Yehova akamtokea Sulemani mara ya pili, kama vile alivyokuwa amemtokea kule Gibeoni.+ 3 Na Yehova akaendelea kumwambia: “Nimeisikia sala+ yako na ombi lako la kutaka kibali ambalo uliomba kibali mbele zangu. Nimeitakasa+ nyumba hii ambayo umejenga kwa kuweka jina+ langu humo mpaka wakati usio na kipimo; na macho+ yangu na moyo wangu utakuwa humo sikuzote.+ 4 Na wewe, ikiwa utatembea+ mbele zangu, kama Daudi+ baba yako alivyotembea, kwa utimilifu+ wa moyo na kwa unyoofu+ kwa kutenda kulingana na yote ambayo nimekuamuru,+ nawe uyashike masharti+ yangu na maamuzi yangu ya hukumu,+ 5 mimi pia nitakifanya imara kiti cha ufalme wako juu ya Israeli mpaka wakati usio na kipimo, kama nilivyomwahidi Daudi baba yako, nikisema, ‘Hakuna mwanamume wa kwako atakayekatiliwa mbali asiketi juu ya kiti cha ufalme cha Israeli.’+ 6 Ninyi na wana wenu hakika mkigeuka mwache kunifuata+ na mkose kushika amri zangu na masharti yangu ambayo nimeweka mbele yenu, nanyi mwende na kuitumikia miungu mingine+ na kuiinamia, 7 mimi pia nitawakatilia mbali Israeli kutoka juu ya uso wa nchi ambayo nimewapa;+ na ile nyumba ambayo nimeitakasa kwa ajili ya jina langu nitaitupa kutoka mbele zangu,+ na Israeli hakika watakuwa neno la kimethali+ na shutuma kati ya vikundi vyote vya watu. 8 Na nyumba hii itakuwa marundo ya mabomoko.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao+ naye atapiga mluzi na kusema, ‘Kwa sababu gani Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+ 9 Nao watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova Mungu wao, aliyekuwa amewatoa mababu zao katika nchi ya Misri,+ nao wakashikamana na miungu mingine+ na kuiinamia na kuitumikia. Ndiyo sababu Yehova alileta juu yao msiba huu wote.’”+
10 Na ikawa kwamba mwishoni mwa miaka 20, muda ambao Sulemani alitumia kujenga zile nyumba mbili, nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme,+ 11 (Hiramu+ mfalme wa Tiro alikuwa amemsaidia Sulemani+ kwa mbao za mierezi na mbao za miberoshi na kwa kumletea dhahabu nyingi kama alivyopenda,)+ kwamba wakati huo Mfalme Sulemani akampa Hiramu majiji 20 katika nchi ya Galilaya.+ 12 Basi Hiramu akatoka Tiro kwenda kuyaona majiji ambayo Sulemani alikuwa amempa, nayo hayakuwa sawa machoni pake.+ 13 Kwa hiyo akasema: “Haya ni majiji gani uliyonipa, ndugu yangu?” Nayo yakaitwa Nchi ya Kabuli mpaka leo hii.
14 Na wakati huo Hiramu akamtumia mfalme talanta 120 za dhahabu.+
15 Sasa hii ndiyo hesabu ya wale walioandikishwa kufanya kazi ya kulazimishwa+ ambao Mfalme Sulemani aliandikisha ili kujenga nyumba ya Yehova+ na nyumba yake mwenyewe na Kilima+ na ukuta+ wa Yerusalemu na Hasori+ na Megido+ na Gezeri.+ 16 (Farao mfalme wa Misri alikuwa amekuja na kuliteka Gezeri na kuliteketeza kwa moto, naye akawaua Wakanaani+ waliokaa katika hilo jiji. Basi akampa binti yake,+ mke wa Sulemani, kama zawadi ya kuagana.) 17 Na Sulemani akaanza kujenga Gezeri na Beth-horoni ya Chini,+ 18 na Baalathi+ na Tamari nyikani, katika nchi, 19 na majiji yote yenye maghala+ yaliyokuwa yamekuwa ya Sulemani na majiji ya magari na majiji ya wapanda-farasi,+ na vitu vyenye kutamanika vya Sulemani+ ambavyo alitamani kujenga katika Yerusalemu na katika Lebanoni na katika nchi yote ya mamlaka yake. 20 Na watu wote waliobaki kutoka kwa Waamori,+ Wahiti,+ Waperizi,+ Wahivi+ na Wayebusi,+ ambao hawakuwa sehemu ya wana wa Israeli,+ 21 wana wao waliobaki baada yao katika nchi, ambao wana wa Israeli walishindwa kuangamiza,+ Sulemani akaendelea kuwaandikisha kwa ajili ya kazi ya kulazimishwa ya kitumwa mpaka leo hii.+ 22 Na Sulemani hakumfanya yeyote kati ya wana wa Israeli kuwa mtumwa;+ kwa maana wao walikuwa ndio mashujaa wa vita na watumishi wake na wakuu wake na maamiri wasaidizi wake na wakuu wa waendesha-magari wake na wakuu wa wapanda-farasi wake.+ 23 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa wasaidizi waliokuwa juu ya kazi ya Sulemani, 550, wasimamizi wa kazi juu ya watu waliokuwa wakifanya kazi.+
24 Hata hivyo, binti ya Farao+ akatoka katika Jiji la Daudi+ akaenda kwenye nyumba yake mwenyewe, ambayo mfalme alikuwa amemjengea. Wakati huo ndipo Sulemani alipokijenga Kilima.+
25 Na Sulemani akaendelea, mara tatu+ katika mwaka, kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika juu ya madhabahu aliyomjengea Yehova,+ na moshi wa dhabihu ukafukizwa katika madhabahu,+ iliyokuwa mbele za Yehova; naye akaimaliza nyumba.+
26 Na palikuwa na kundi la meli ambazo Mfalme Sulemani aliunda katika Esion-geberi,+ lililoko kando ya Elothi,+ kando ya Bahari Nyekundu katika nchi ya Edomu.+ 27 Na Hiramu akaendelea kutuma watumishi wake kwa lile kundi la meli,+ wanamaji, wenye ujuzi wa bahari, pamoja na watumishi wa Sulemani. 28 Nao wakaenda Ofiri+ na kuchukua kutoka huko talanta 420 za dhahabu,+ wakamletea Mfalme Sulemani.
10 Basi malkia wa Sheba+ alikuwa akisikia habari za Sulemani kuhusiana na jina la Yehova.+ Kwa hiyo akaenda kumjaribu kwa maswali yenye kutatanisha.+ 2 Mwishowe akafika Yerusalemu pamoja na msafara wenye kuvutia sana,+ ngamia+ wenye kuchukua mafuta ya zeri+ na dhahabu nyingi sana na mawe ya thamani; naye akaingia kwa Sulemani, na malkia huyo akaanza kumwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake.+ 3 Naye Sulemani akamwambia mambo yake yote.+ Hakuna jambo lolote lililofichwa kwa mfalme ambalo hakumwambia yule malkia.+
4 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Sulemani+ na ile nyumba ambayo alikuwa amejenga,+ 5 na chakula cha meza yake+ na kuketi kwa watumishi wake na utumishi wa mezani wa wale wenye kumhudumia na mavazi yao na vinywaji vyake+ na dhabihu zake za kuteketezwa alizotoa kwa ukawaida katika nyumba ya Yehova, basi haikubaki roho yoyote ndani ya malkia.+ 6 Kwa hiyo akamwambia mfalme: “Ni la kweli neno lile nililosikia katika nchi yangu kuhusu mambo yako na kuhusu hekima yako.+ 7 Nami sikuyaamini maneno hayo mpaka nilipokuja ili nijionee kwa macho yangu mwenyewe; na tazama! sikuwa nimeambiwa hata nusu.+ Umezidi katika hekima na mafanikio, mambo yale niliyoyasikia.+ 8 Watu wako ni wenye furaha;+ ni wenye furaha+ hawa watumishi wako wanaosimama mbele yako daima, wakiisikiliza hekima yako!+ 9 Na abarikiwe Yehova Mungu wako,+ ambaye amependezwa+ nawe, akakuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli;+ kwa sababu Yehova anawapenda Israeli mpaka wakati usio na kipimo,+ hivi kwamba akakuchagua wewe uwe mfalme+ ili kufanya uamuzi wa hukumu+ na uadilifu.”+
10 Ndipo akampa+ mfalme talanta 120 za dhahabu+ na mafuta mengi sana ya zeri+ na mawe ya thamani. Hayakuletwa kamwe tena mafuta ya zeri yaliyo mengi kama yale ambayo malkia wa Sheba alimpa Mfalme Sulemani.
11 Na kundi la meli la Hiramu+ lililochukua dhahabu kutoka Ofiri+ likaleta pia kutoka Ofiri mbao za misandali+ kwa wingi sana na mawe ya thamani.+ 12 Na mfalme akatengeneza kwa zile mbao za misandali vitegemeo kwa ajili ya nyumba ya Yehova+ na kwa ajili ya nyumba ya mfalme, na pia vinubi+ na vinanda+ kwa ajili ya waimbaji. Mbao za misandali kama hizo hazijaletwa wala kuonekana mpaka leo hii.
13 Naye Mfalme Sulemani mwenyewe akampa malkia wa Sheba vyote vilivyompendeza, ambavyo aliomba, zaidi ya vitu alivyompa kulingana na ukunjufu wa mkono+ wa Mfalme Sulemani. Baada ya hayo akageuka, akaenda katika nchi yake, yeye pamoja na watumishi wake.+
14 Na uzito wa dhahabu+ iliyoletwa kwa Sulemani katika mwaka mmoja ulijumlika kuwa talanta 666 za dhahabu,+ 15 zaidi ya zile zilizoletwa na wasafiri na faida kutoka kwa wafanya-biashara na wafalme+ wote wa Waarabu+ na magavana wa nchi.
16 Na Mfalme Sulemani akatengeneza ngao kubwa mia mbili za dhahabu iliyochanganywa+ (akaweka shekeli mia sita za dhahabu kwenye kila ngao kubwa),+ 17 na ngao ndogo mia tatu za dhahabu iliyochanganywa (akaweka mina tatu za dhahabu kwenye kila ngao ndogo).+ Kisha mfalme akaziweka katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni.+
18 Tena mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha ufalme+ cha pembe za tembo+ na kukifunika kwa dhahabu safi.+ 19 Kulikuwa na vipandio sita vilivyoelekea kwenye kile kiti cha ufalme, na kile kiti kilikuwa na paa la mviringo nyuma yake, na kulikuwa na mikono ya kiti upande huu na upande ule kando ya mahali pa kuketi, na simba+ wawili walisimama kando ya ile mikono ya kiti.+ 20 Na kulikuwa na simba kumi na wawili waliosimama hapo juu ya vile vipandio sita, upande huu na upande ule. Hakuna ufalme mwingine wowote uliokuwa na kiti kilichotengenezwa hivyo.+
21 Na vyombo vyote vya kunywea vya Mfalme Sulemani vilikuwa vya dhahabu, na vyombo vyote vya Nyumba ya Msitu wa Lebanoni+ vilikuwa vya dhahabu safi.+ Hapakuwa na kitu chochote cha fedha; fedha haikuhesabiwa kuwa kitu katika siku za Sulemani. 22 Kwa maana mfalme alikuwa na kundi la meli za Tarshishi+ baharini pamoja na kundi la meli za Hiramu. Mara moja kila miaka mitatu kundi la meli za Tarshishi zilikuja zikiwa zimebeba dhahabu+ na fedha, pembe za tembo,+ na sokwe na tausi.
23 Basi Mfalme Sulemani alikuwa mkuu katika utajiri+ na hekima+ kuliko wafalme wengine wote wa dunia. 24 Na watu wote wa dunia walikuwa wakiutafuta uso wa Sulemani ili wasikie hekima yake ambayo Mungu alikuwa ametia moyoni mwake.+ 25 Nao walikuwa wakileta kila mmoja zawadi yake,+ vyombo vya fedha+ na vyombo vya dhahabu na mavazi na silaha+ na mafuta ya zeri, farasi na nyumbu,+ kama kawaida ya kila mwaka.+
26 Na Sulemani akaendelea kukusanya magari na farasi wengi zaidi; naye akawa na magari elfu moja na mia nne na farasi+ kumi na mbili elfu, naye akaviweka vitu hivyo katika majiji ya magari na karibu na mfalme katika Yerusalemu.+
27 Na mfalme akafanya fedha iliyomo Yerusalemu kuwa kama mawe,+ akafanya mierezi iwe kama mikuyu iliyoko Shefela kwa wingi.+
28 Na farasi wa Sulemani walisafirishwa kutoka Misri, na wanabiashara wa mfalme wakawa wakichukua kundi la farasi kwa bei fulani.+ 29 Na kwa kawaida gari lilikuwa likija na kusafirishwa kutoka Misri kwa vipande 600 vya fedha, na farasi kwa vipande 150; na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa wafalme wote wa Wahiti+ na wafalme wote wa Siria. Walikuwa wakisafirisha vitu kupitia hao.
11 Na Mfalme Sulemani akawapenda wake+ wengi wageni pamoja na binti ya Farao,+ wanawake Wamoabu,+ Waamoni,+ Waedomu,+ Wasidoni+ na Wahiti,+ 2 kutoka kwa mataifa ambayo Yehova alikuwa amewaambia wana wa Israeli: “Msiingie kati yao,+ nao wasije kati yenu; kwa hakika watageuza moyo wenu uifuate miungu yao.”+ Hao ndio Sulemani alishikamana+ nao na kuwapenda. 3 Naye akawa na wake mia saba, binti za kifalme, na masuria mia tatu; na mwishowe wake zake wakaugeuza+ moyo wake. 4 Na ikawa kwamba wakati Sulemani alipokuwa mzee,+ wake zake wakawa wameugeuza+ moyo wake ukaifuata miungu mingine;+ na moyo wake haukuwa mkamilifu+ kwa Yehova Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake. 5 Na Sulemani akaanza kufuata Ashtorethi,+ mungu wa kike wa Wasidoni na kufuata Milkomu,+ chukizo la Waamoni. 6 Na Sulemani akaanza kufanya yaliyokuwa mabaya+ machoni pa Yehova, naye hakumfuata Yehova kikamilifu kama Daudi baba yake.+
7 Ndipo Sulemani akajenga mahali pa juu+ kwa ajili ya Kemoshi,+ chukizo+ la Moabu juu ya mlima+ uliokuwa mbele+ ya Yerusalemu, na kwa ajili ya Moleki, chukizo la wana wa Amoni. 8 Naye akawafanyia hivyo wake zake wote wa kigeni+ waliokuwa wakifukiza moshi na kutoa dhabihu kwa miungu yao.+
9 Na Yehova akamkasirikia+ Sulemani, kwa sababu moyo wake ulikuwa umegeuka ukamwacha Yehova Mungu wa Israeli,+ yeye aliyemtokea mara mbili.+ 10 Na katika jambo hilo alikuwa amemwamuru asiifuate miungu mingine;+ lakini hakushika yale ambayo Yehova alikuwa ameamuru. 11 Sasa Yehova akamwambia Sulemani: “Kwa sababu umefanya jambo hili wala hukushika agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako, nami nitampa mtumishi wako.+ 12 Hata hivyo, sitafanya jambo hilo katika siku zako,+ kwa ajili ya Daudi baba yako.+ Nitaurarua kutoka mkononi mwa mwana wako.+ 13 Ila tu sitaurarua ufalme wote.+ Nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu+ na kwa ajili ya Yerusalemu ambalo nimelichagua.”+
14 Na Yehova akaanza kusimamisha mtu wa kumpinga+ Sulemani,+ yaani, Hadadi, Mwedomu, wa uzao wa mfalme. Yeye alikuwa katika Edomu.+ 15 Na ikawa, Daudi alipopiga Edomu,+ wakati Yoabu mkuu wa jeshi alipokuja kuzika waliouawa, kwamba alijaribu kumpiga na kumuua kila mwanamume katika Edomu.+ 16 (Kwa maana Yoabu na Israeli wote walikaa huko miezi sita mpaka alipokuwa amemkatilia mbali kila mwanamume katika Edomu.) 17 Na Hadadi akakimbia, yeye na wanaume fulani Waedomu wa watumishi wa baba yake pamoja naye, kwenda Misri, Hadadi alipokuwa mvulana mdogo. 18 Basi wakaondoka Midiani,+ wakaingia Parani na kuchukua pamoja nao watu kutoka Parani,+ wakaenda Misri kwa Farao mfalme wa Misri, kisha akampa nyumba. Pia akampa mkate, na kumpa shamba. 19 Na Hadadi akaendelea kupata kibali+ sana machoni pa Farao, hivi kwamba akampa mke,+ dada ya mke wake mwenyewe, dada ya Tapenesi aliyekuwa malkia. 20 Baada ya muda dada ya Tapenesi akamzalia Genubathi mwana wake, na Tapenesi akamwachisha kunyonya+ katika nyumba ya Farao; na Genubathi akaendelea kukaa katika nyumba ya Farao kati ya wana wa Farao.
21 Na Hadadi akasikia akiwa Misri kwamba Daudi amelala pamoja na mababu zake+ na kwamba Yoabu mkuu wa jeshi amekufa.+ Basi Hadadi akamwambia Farao: “Acha niende zangu,+ niende katika nchi yangu.” 22 Lakini Farao akamwambia: “Una uhitaji wa nini ukiwa pamoja nami hivi kwamba unatafuta kwenda katika nchi yako?” Naye akasema: “Hakuna; lakini inakupasa uniache niende tu.”
23 Na Mungu akamsimamishia mpinzani+ mwingine, yaani, Rezoni mwana wa Eliada, aliyekuwa amekimbia kutoka kwa Hadadezeri+ mfalme wa Soba+ bwana wake. 24 Naye akazidi kukusanya watu upande wake, akawa mkuu wa kikundi cha waporaji, Daudi alipowaua watu wa Soba.+ Basi wakaenda Damasko,+ wakaanza kukaa humo na kuanza kutawala katika Damasko. 25 Naye akawa mpinzani wa Israeli siku zote za Sulemani,+ na jambo hilo kuongezea yale madhara ambayo Hadadi alifanya; naye akawachukia sana+ Israeli alipokuwa akitawala juu ya Siria.
26 Na palikuwa na Yeroboamu+ mwana wa Nebati, Mwefraimu, kutoka katika Sereda, mtumishi wa Sulemani,+ na jina la mama yake lilikuwa Serua, mwanamke mjane. Yeye pia akaanza kunyoosha mkono wake juu ya mfalme.+ 27 Na hii ndiyo sababu alinyoosha mkono wake juu ya mfalme: Sulemani alikuwa amekijenga Kilima.+ Alikuwa ameziba pengo la Jiji la Daudi baba yake.+ 28 Sasa Yeroboamu alikuwa mwanamume shujaa, mwenye nguvu.+ Sulemani alipoona kwamba huyo kijana alikuwa mfanyakazi mwenye bidii,+ ndipo akamfanya mwangalizi+ juu ya utumishi wote wa lazima+ wa nyumba ya Yosefu.+ 29 Na ikawa kwamba wakati huo Yeroboamu akatoka katika Yerusalemu, na Ahiya,+ Mshilo,+ nabii, akamkuta njiani, na Ahiya alikuwa amevaa vazi jipya; na hao wawili walikuwa peke yao shambani. 30 Basi Ahiya akashika lile vazi jipya alilokuwa amelivaa, akalirarua+ vipande kumi na viwili.+ 31 Naye akamwambia Yeroboamu:
“Chukua wewe vipande kumi; kwa maana Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Tazama, ninaurarua ufalme kutoka mkononi mwa Sulemani, nami hakika nitakupa wewe makabila kumi.+ 32 Na kabila moja+ ndilo litakalobaki likiwa lake kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi+ na kwa ajili ya Yerusalemu,+ jiji ambalo nimelichagua kutoka katika makabila yote ya Israeli. 33 Sababu ni kwamba wameniacha,+ wakaanza kuinama mbele ya Ashtorethi,+ mungu wa kike wa Wasidoni, na Kemoshi,+ mungu wa Moabu na Milkomu,+ mungu wa wana wa Amoni; nao hawakutembea katika njia zangu kwa kufanya yaliyo sawa machoni pangu na sheria zangu na maamuzi yangu ya hukumu kama Daudi baba yake. 34 Lakini sitauchukua ufalme wote kutoka mkononi mwake, kwa sababu nitamweka kuwa mkuu siku zote za maisha yake, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu niliyemchagua,+ kwa sababu alizishika amri zangu na sheria zangu. 35 Nami kwa hakika nitauchukua ufalme kutoka mkononi mwa mwana wake na kukupa wewe, naam, makabila kumi.+ 36 Nami nitampa mwana wake kabila moja, ili Daudi mtumishi wangu aendelee kuwa na taa sikuzote mbele zangu katika Yerusalemu,+ jiji ambalo nimejichagulia ili kuweka jina langu humo.+ 37 Nami nitakuchukua wewe, nawe hakika utatawala juu ya yote ambayo nafsi yako inatamani,+ nawe hakika utakuwa mfalme juu ya Israeli. 38 Na itatukia kwamba, ukitii yote ambayo nitakuamuru, nawe utembee katika njia zangu na kwa kweli ufanye yaliyo sawa machoni pangu kwa kushika sheria zangu na amri zangu, kama Daudi mtumishi wangu alivyofanya,+ mimi pia nitakuwa pamoja nawe,+ nami nitakujengea nyumba yenye kudumu, kama nilivyomjengea Daudi,+ nami nitakupa Israeli. 39 Nami nitaufedhehesha uzao wa Daudi kwa sababu ya jambo hili,+ ila tu si sikuzote.’”+
40 Na Sulemani akaanza kutafuta kumuua Yeroboamu.+ Kwa hiyo Yeroboamu akaondoka, akakimbia+ kwenda Misri kwa Shishaki+ mfalme wa Misri, naye akaendelea kukaa katika Misri mpaka Sulemani alipokufa.
41 Na mambo mengine ya Sulemani na yote aliyofanya na hekima yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha mambo ya Sulemani? 42 Na siku ambazo Sulemani alitawala katika Yerusalemu juu ya Israeli yote zilikuwa miaka 40.+ 43 Kisha Sulemani akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa katika Jiji la Daudi+ baba yake; na Rehoboamu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
12 Na Rehoboamu+ akaenda Shekemu, kwa maana Israeli wote walikuja kumfanya kuwa mfalme huko Shekemu.+ 2 Na ikawa kwamba mara tu Yeroboamu+ mwana wa Nebati aliposikia habari hizo alipokuwa angali Misri (kwa maana alikuwa amekimbia kwa sababu ya Mfalme Sulemani, ili Yeroboamu akae Misri),+ 3 ndipo wakatuma watu, wakamwita. Baada ya hapo Yeroboamu na kutaniko lote la Israeli wakaja na kuanza kuzungumza na Rehoboamu, wakisema:+ 4 “Baba yako aliifanya nira yetu kuwa ngumu, na sasa wewe ufanye utumishi mgumu wa baba yako na nira yake nzito+ aliyoweka juu yetu kuwa rahisi,+ nasi tutakutumikia.”+
5 Ndipo akawaambia: “Nendeni zenu kwa siku tatu, kisha mrudi tena kwangu.”+ Basi watu wakaenda zao. 6 Na Mfalme Rehoboamu akaanza kushauriana na wanaume wazee+ waliomhudumia Sulemani baba yake alipokuwa angali hai, akisema: “Mnatoa shauri gani la kuwajibu watu hawa?”+ 7 Basi wakasema naye, wakimwambia: “Leo ukitaka kukubali kuwa mtumishi wa watu hawa na kuwatumikia kikweli,+ uwajibu na kusema nao kwa maneno mema;+ nao hakika watakuwa watumishi wako sikuzote.”+
8 Hata hivyo, akaliacha shauri la wanaume wazee walilomshauri, naye akaanza kushauriana na vijana waliokua pamoja naye,+ waliokuwa wakimhudumia.+ 9 Naye akawaambia: “Mnatoa shauri gani+ ili tuwajibu watu hawa ambao wamesema nami, wakiniambia, ‘Ifanye nira ambayo baba yako aliweka juu yetu iwe rahisi’?”+ 10 Ndipo wale vijana waliokuwa wamekua pamoja naye wakamwambia, wakisema: “Waambie+ hivi watu hawa ambao wamesema nawe, ‘Baba yako aliifanya nira yetu kuwa nzito, lakini wewe ifanye iwe rahisi juu yetu’; wewe waambie hivi, ‘Kidole changu kidogo kwa hakika kitakuwa kinene kuliko kiuno cha baba yangu.+ 11 Na sasa baba yangu aliweka juu yenu nira nzito; lakini mimi nitaizidisha nira yenu.+ Baba yangu aliwatia ninyi adabu kwa fimbo, lakini mimi nitawatia adabu kwa mijeledi.’”+
12 Na Yeroboamu na watu wote wakamjia Rehoboamu siku ya tatu, kama mfalme alivyosema: “Rudini kwangu siku ya tatu.”+ 13 Na mfalme akaanza kuwajibu watu kwa ukali,+ akaliacha shauri la wanaume wazee waliomshauri.+ 14 Naye akasema nao kulingana na lile shauri la vijana,+ akisema: “Baba yangu aliifanya nira yenu kuwa nzito, lakini mimi nitaizidisha nira yenu. Baba yangu aliwatia ninyi adabu kwa fimbo, lakini mimi nitawatia adabu kwa mijeledi.”+ 15 Na mfalme hakuwasikiliza watu,+ kwa sababu Yehova ndiye aliyeongoza mambo,+ ili atimize neno+ lake ambalo Yehova alimwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya+ Mshilo.
16 Israeli wote walipoona kwamba mfalme hakuwasikiliza, ndipo watu wakamjibu mfalme, wakisema: “Tuna fungu gani katika Daudi?+ Wala hakuna urithi katika mwana wa Yese. Haya, nenda kwa miungu yako,+ Ee Israeli. Sasa angalia nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi!”+ Kwa hiyo Israeli wakaanza kwenda katika mahema yao. 17 Naye Rehoboamu akaendelea kutawala juu ya wana wa Israeli waliokuwa wakikaa katika majiji ya Yuda.+
18 Basi Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu,+ aliyekuwa juu ya wale walioandikishwa kufanya kazi ya kulazimishwa,+ lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe,+ naye akafa. Na Mfalme Rehoboamu akafaulu kupanda katika gari, akakimbia kwenda Yerusalemu. 19 Na Waisraeli wakaendeleza maasi+ yao juu ya nyumba ya Daudi mpaka leo hii.+
20 Na ikawa kwamba mara tu Israeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, mara moja wakatuma watu kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya kuwa mfalme juu ya Israeli yote.+ Hakuna yeyote aliyekuwa mfuasi wa nyumba ya Daudi isipokuwa kabila la Yuda peke yake.+
21 Rehoboamu alipofika Yerusalemu,+ mara moja akakutanisha nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini,+ wanaume bora 180,000 kwa ajili ya vita, ili wapigane na nyumba ya Israeli, ili kumrudishia ufalme Rehoboamu mwana wa Sulemani. 22 Ndipo neno la Mungu wa kweli likamjia Shemaya+ mtu wa Mungu wa kweli,+ na kusema: 23 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani mfalme wa Yuda na nyumba yote ya Yuda na Benyamini na wale watu wengine, 24 ‘Yehova amesema hivi: “Msipande kwenda kupigana na ndugu zenu wana wa Israeli.+ Mrudi kila mmoja nyumbani kwake, kwa maana jambo hili limetokea kwa mwongozo wangu.”’”+ Basi wakalitii neno la Yehova,+ wakarudi nyumbani kulingana na neno la Yehova.+
25 Na Yeroboamu akajenga Shekemu+ katika eneo lenye milima la Efraimu, akakaa humo. Kisha akatoka huko, akajenga Penueli.+ 26 Na Yeroboamu akaanza kusema moyoni mwake:+ “Sasa ufalme utarudi kwa nyumba ya Daudi.+ 27 Watu hawa wakiendelea kwenda kutoa dhabihu katika nyumba ya Yehova huko Yerusalemu,+ moyo wa watu hawa pia utarudi kwa bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda; nao hakika wataniua+ na kurudi kwa Rehoboamu mfalme wa Yuda.” 28 Basi mfalme akafanya shauri,+ akatengeneza ndama wawili wa dhahabu+ na kuwaambia watu: “Ni vigumu mno kwenu kwenda Yerusalemu. Tazama, huyu ni Mungu wenu,+ enyi Israeli, aliyewatoa ninyi katika nchi ya Misri.”+ 29 Kisha akaweka mmoja kule Betheli,+ na mwingine akamweka kule Dani.+ 30 Na jambo hilo likaja kusababisha dhambi,+ na watu wakaanza kwenda mpaka kule Dani mbele ya yule aliyekuwa huko.
31 Naye akaanza kujenga nyumba ya mahali pa juu+ na kuweka makuhani kutoka kwa watu wa kawaida, ambao hawakuwa wa wana wa Lawi.+ 32 Na Yeroboamu akafanya sherehe katika mwezi wa nane siku ya kumi na tano ya mwezi huo, kama ile sherehe iliyokuwa katika Yuda,+ ili atoe matoleo juu ya madhabahu aliyokuwa ameijenga kule Betheli, ya kutoa dhabihu kwa wale ndama aliotengeneza; naye akaweka makuhani Betheli+ wahudumu mahali pa juu alipokuwa amejenga. 33 Naye akaanza kutoa matoleo juu ya ile madhabahu aliyokuwa amejenga Betheli, siku ya kumi na tano katika mwezi wa nane, mwezi ambao yeye mwenyewe alijibunia;+ naye akafanya sherehe kwa ajili ya wana wa Israeli na kutoa matoleo juu ya madhabahu ili kufukiza moshi wa dhabihu.+
13 Na tazama, palikuwa na mtu+ wa Mungu aliyekuwa amekuja kutoka Yuda kwa neno+ la Yehova ili kwenda Betheli, Yeroboamu alipokuwa amesimama kando ya madhabahu+ ili kufukiza moshi wa dhabihu.+ 2 Ndipo akaipaazia sauti ile madhabahu kwa neno la Yehova, akasema: “Ee madhabahu, madhabahu, Yehova amesema hivi, ‘Tazama! Mwana aliyezaliwa katika nyumba ya Daudi, ambaye jina lake ni Yosia!+ Naye atawatoa juu yako wawe dhabihu wale makuhani wa mahali pa juu wanaofukiza moshi wa dhabihu juu yako, naye atateketeza mifupa ya watu juu yako.’”+ 3 Naye akatoa ishara+ siku hiyo, akisema: “Hii ndiyo ishara ambayo Yehova amesema: Tazama! Madhabahu imepasuka, na majivu yenye mafuta yaliyo juu yake yatamwagika.”
4 Na ikawa kwamba mara tu mfalme aliposikia neno la yule mtu wa Mungu wa kweli alilokuwa ametangaza juu ya ile madhabahu katika Betheli, mara moja Yeroboamu akanyoosha mkono wake kutoka katika madhabahu, akisema: “Mkamateni!”+ Mara moja mkono wake aliomnyooshea ukapooza, naye hakuweza kuurudisha nyuma kwake.+ 5 Na ile madhabahu ikapasuka hivi kwamba majivu yenye mafuta yakamwagika kutoka katika madhabahu, kulingana na ile ishara ambayo yule mtu wa Mungu wa kweli alitoa kwa neno la Yehova.+
6 Ndipo mfalme akajibu na kumwambia yule mtu wa Mungu wa kweli: “Tafadhali, utulize uso wa Yehova Mungu wako, na kusali kwa ajili yangu ili nirudishiwe mkono wangu.”+ Basi yule mtu wa Mungu wa kweli akautuliza+ uso wa Yehova hivi kwamba mkono wa mfalme ukarudishwa kwake, nao ukawa kama pale mwanzoni.+ 7 Na mfalme akaendelea kumwambia yule mtu wa Mungu wa kweli: “Njoo pamoja nami twende nyumbani ule chakula,+ nami nikupe zawadi.”+ 8 Lakini yule mtu wa Mungu wa kweli akamwambia mfalme: “Hata ukinipa nusu ya nyumba yako,+ siwezi kwenda pamoja nawe+ na kula mkate au kunywa maji mahali hapa. 9 Kwa maana hivyo ndivyo yeye alivyoniamuru kwa neno la Yehova, akisema, ‘Usile mkate+ wala usinywe maji, nawe usirudi kwa njia ile uliyoiendea.’” 10 Naye akaanza kwenda kupitia njia nyingine, wala hakurudi kwa njia ile aliyoipitia kuja Betheli.
11 Na nabii+ fulani mzee alikuwa akikaa Betheli, na wanawe wakaja na kumsimulia kazi yote ambayo yule mtu wa Mungu wa kweli alikuwa amefanya siku hiyo katika Betheli na yale maneno aliyomwambia mfalme, nao wakaendelea kumsimulia baba yao. 12 Ndipo baba yao akawaambia: “Basi alienda kupitia njia gani?” Kwa hiyo wanawe wakamwonyesha ile njia ambayo yule mtu wa Mungu wa kweli aliyetoka Yuda alipitia akienda. 13 Sasa akawaambia wanawe: “Nitandikieni punda.” Basi wakamtandikia punda,+ naye akampanda na kwenda.
14 Naye akaanza kumfuata yule mtu wa Mungu wa kweli, akamkuta ameketi chini ya ule mti mkubwa.+ Ndipo akamwambia: “Je, wewe ndiye yule mtu wa Mungu wa kweli ambaye ametoka Yuda?”+ naye akasema: “Ni mimi.” 15 Naye akaendelea kumwambia: “Njoo pamoja nami nyumbani, ule mkate.” 16 Lakini akasema: “Siwezi kurudi pamoja nawe wala kuingia pamoja nawe, nami siwezi kula mkate wala kunywa maji pamoja nawe mahali hapa.+ 17 Kwa maana nimeambiwa kwa neno la Yehova,+ ‘Usile mkate wala usinywe maji huko. Usirudi tena kupitia njia ile uliyoiendea.’”+ 18 Kwa hiyo akamwambia: “Mimi pia ni nabii kama wewe, na malaika+ alisema nami kwa neno la Yehova hivi, ‘Mrudishe pamoja nawe nyumbani kwako ili ale mkate na anywe maji.’” (Alimdanganya.)+ 19 Basi akarudi pamoja naye ili ale mkate nyumbani kwake na anywe maji.+
20 Na ikawa kwamba walipokuwa wameketi mezani, neno+ la Yehova likamjia yule nabii aliyekuwa amemrudisha; 21 naye akaanza kumwambia kwa sauti yule mtu wa Mungu wa kweli aliyekuwa ametoka Yuda, na kusema: “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu uliasi+ agizo la Yehova wala hukushika amri ambayo Yehova Mungu wako alikuamuru,+ 22 lakini ulirudi ili ule mkate na kunywa maji mahali ambapo alikuambia: “Usile mkate wala usinywe maji,” maiti yako haitaingia katika makaburi ya mababu zako.’”+
23 Na ikawa kwamba baada ya huyo kula mkate na kunywa maji, mara moja akamtandikia punda, yaani, yule nabii aliyekuwa amemrudisha. 24 Naye akaanza kwenda zake. Baadaye simba+ akamkuta barabarani na kumuua,+ nayo maiti yake ikatupwa barabarani. Na yule punda akasimama kando yake, na simba akasimama kando ya ile maiti. 25 Na tazama, palikuwa na watu wakipita, nao wakaiona ile maiti imetupwa barabarani na simba amesimama kando ya maiti. Ndipo wakaingia na kusema habari hizo katika jiji ambamo yule nabii mzee alikuwa akikaa.
26 Yule nabii ambaye alikuwa amemrudisha akiwa njiani aliposikia habari hizo, mara moja akasema: “Huyo ni yule mtu wa Mungu wa kweli aliyeasi agizo la Yehova;+ na kwa hiyo Yehova alimkabidhi kwa simba, ili amvunje na kumuua, kulingana na neno la Yehova alilomwambia.”+ 27 Naye akaendelea kuwaambia wanawe, akisema: “Nitandikieni punda.” Basi wakamtandikia.+ 28 Kisha akaondoka, akakuta ile maiti imetupwa barabarani na punda na simba wamesimama kando ya maiti ile. Yule simba hakuwa ameila ile maiti, wala hakuwa amemsaga punda.+ 29 Na yule nabii akaibeba maiti ya yule mtu wa Mungu wa kweli na kuiweka juu ya punda, akairudisha. Basi akaja jijini mwa yule nabii mzee ili kumwombolezea na kumzika. 30 Kwa hiyo akaiweka maiti katika kaburi lake mwenyewe; nao wakaendelea kumwombolezea:+ “Ole wako, ndugu yangu!” 31 Na ikawa kwamba baada ya kumzika akawaambia wanawe: “Nitakapokufa mnizike katika kaburi ambamo yule mtu wa Mungu wa kweli amezikwa. Wekeni mifupa yangu kando ya mifupa yake.+ 32 Kwa maana bila shaka litatimia+ neno lile alilotangaza kwa neno la Yehova juu ya ile madhabahu+ iliyoko Betheli na juu ya nyumba zote za mahali pa juu+ zilizo katika majiji ya Samaria.”+
33 Baada ya jambo hilo Yeroboamu hakugeuka kutoka katika njia yake mbaya, bali alianza kuweka tena makuhani wa mahali pa juu kutoka kwa watu wa kawaida.+ Na mtu yeyote aliyependa jambo hilo, akawa anaujaza mkono wake nguvu,+ akisema: “Na awe mmoja wa makuhani wa mahali pa juu.” 34 Na katika jambo hilo kukawa na kisababishi cha dhambi kwa nyumba ya Yeroboamu+ nayo ikawa sababu ya kuwafutilia mbali na kuwaangamiza kutoka katika uso wa nchi.+
14 Na wakati huo Abiya mwana wa Yeroboamu akawa mgonjwa.+ 2 Kwa hiyo Yeroboamu akamwambia mke wake: “Tafadhali, ondoka, ujibadili sura,+ ili wasijue kuwa wewe ni mke wa Yeroboamu, uende Shilo. Tazama! Huko ndiko aliko Ahiya+ nabii. Yeye ndiye aliyesema kunihusu mimi habari za kuwa mfalme juu ya watu hawa.+ 3 Nawe uchukue mkononi mwako mikate+ kumi na keki zilizonyunyiziwa kitu na chupa+ ya asali, nawe uingie kwake.+ Yeye ndiye atakayekuambia litakalompata mvulana huyu.”+
4 Na mke wa Yeroboamu akafanya hivyo. Basi akaondoka na kwenda Shilo,+ akaja katika nyumba ya Ahiya. Basi Ahiya alikuwa hawezi kuona, kwa maana macho yake yalikuwa yameganda kwa sababu ya umri wake.+
5 Na Yehova alikuwa amemwambia Ahiya: “Tazama, mke wa Yeroboamu anakuja kuomba neno kutoka kwako kuhusu mwana wake; kwa maana ni mgonjwa. Umwambie hivi na hivi. Na itatukia kwamba mara tu atakapofika, atakuwa anajifanya asiweze kutambuliwa.”+
6 Na ikawa kwamba mara tu Ahiya aliposikia sauti ya miguu yake alipokuwa akija mlangoni, akaanza kusema: “Ingia, ewe mke wa Yeroboamu.+ Kwa nini unajifanya usitambuliwe, wakati mimi ninatumwa kwako na ujumbe mkali? 7 Nenda, mwambie Yeroboamu, ‘Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi: “Kwa sababu nilikusimamisha kutoka katikati ya watu wako, ili nikufanye kiongozi juu ya watu wangu Israeli,+ 8 nami nikaurarua+ ufalme kutoka katika nyumba ya Daudi na kukupa wewe, nawe hujawa kama mtumishi wangu Daudi, aliyeshika amri zangu na kunifuata kwa moyo wake wote kwa kufanya yaliyokuwa sawa tu machoni pangu,+ 9 bali ukaanza kutenda vibaya zaidi kuliko wale wote waliokutangulia, nawe ukajitengenezea mungu mwingine+ na sanamu za kuyeyushwa+ ili kunitia uchungu,+ nawe umenitupa mimi nyuma ya mgongo wako;+ 10 kwa sababu hiyo tazama, nitaleta msiba juu ya nyumba ya Yeroboamu, nami kwa hakika nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu yeyote anayekojoa ukutani,+ asiye na uwezo na asiye na thamani katika Israeli;+ nami kwa kweli nitafagia kabisa nikiifuata nyumba ya Yeroboamu,+ kama vile mtu anavyoondoa mavi mpaka yanapokuwa yameondolewa.+ 11 Mtu yeyote wa Yeroboamu atakayekufa jijini, mbwa watamla;+ na yule atakayekufa shambani, ndege wa angani watamla,+ kwa sababu Yehova mwenyewe amesema hayo.”’
12 “Na wewe, ondoka, nenda nyumbani kwako. Miguu yako itakapoingia jijini huyo mtoto atakufa hakika. 13 Na Israeli wote kwa hakika watamwombolezea+ na kumzika, kwa sababu huyu peke yake wa Yeroboamu ndiye atakayezikwa kaburini; kwa maana jambo fulani jema kwa Yehova Mungu wa Israeli limeonekana ndani yake katika nyumba ya Yeroboamu.+ 14 Na hakika Yehova atajisimamishia mfalme+ juu ya Israeli atakayeikatilia mbali nyumba ya Yeroboamu siku ile iliyotajwa, na namna gani ikiwa ni sasa hivi?+ 15 Na kwa kweli Yehova atawapiga Israeli, kama vile tu tete linavyoyumba-yumba majini;+ naye atawang’oa+ Israeli kutoka katika nchi hii nzuri+ aliyowapa mababu zao, naye atawatawanya+ ng’ambo ya ule Mto,+ kwa sababu walitengeneza miti yao mitakatifu,+ na hivyo kumtia uchungu+ Yehova. 16 Naye atawatoa Israeli+ kwa sababu ya dhambi za Yeroboamu alizotenda na ambazo kupitia hizo alisababisha Israeli watende dhambi.”+
17 Ndipo mke wa Yeroboamu akaondoka, akaenda zake, akafika Tirsa.+ Alipokuwa akikaribia mlango wa nyumba, yule mvulana akafa. 18 Kwa hiyo wakamzika, na Israeli wote wakaanza kumwombolezea, kulingana na neno la Yehova alilosema kupitia mtumishi wake Ahiya nabii.
19 Na mambo mengine ya Yeroboamu, jinsi alivyopiga vita+ na jinsi alivyotawala, tazama, yameandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli. 20 Na siku ambazo Yeroboamu alitawala zilikuwa miaka 22, kisha akalala pamoja na mababu zake;+ na Nadabu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
21 Naye Rehoboamu+ mwana wa Sulemani, alikuwa mfalme katika Yuda. Rehoboamu alikuwa na umri wa miaka 41 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 17 katika Yerusalemu, jiji+ ambalo Yehova alichagua kutoka katika makabila+ yote ya Israeli ili kuweka humo jina lake.+ Na jina la mama yake lilikuwa Naama Mwamoni.+ 22 Na Yuda wakaendelea kutenda yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ hivi kwamba wakamchochea+ kuwa na wivu kuliko mambo yote ambayo mababu zao walikuwa wamefanya kwa dhambi zao ambazo walitenda.+ 23 Nao pia wakaendelea kujijengea mahali pa juu+ na nguzo takatifu+ na miti mitakatifu+ juu ya kila kilima kirefu+ na chini ya kila mti wenye majani mengi.+ 24 Na hata mwanamume kahaba wa hekaluni alikuwa katika nchi.+ Walitenda kulingana na machukizo yote ya mataifa ambao Yehova alikuwa amewafukuza mbele ya wana wa Israeli.+
25 Na ikawa kwamba katika mwaka wa tano wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki+ mfalme wa Misri akapanda kushambulia Yerusalemu. 26 Naye akachukua hazina za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mfalme;+ naye akachukua kila kitu.+ Naye akachukua ngao zote za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.+ 27 Basi Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba mahali pake, akaziweka chini ya wakuu wa wakimbiaji,+ walinzi wa mlango wa nyumba ya mfalme.+ 28 Na ikawa ikitukia kwamba, kila mara mfalme akija katika nyumba ya Yehova, wakimbiaji walizichukua, nao walizirudisha katika chumba cha walinzi cha wakimbiaji.+
29 Na mambo mengine ya Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya nyakati za wafalme wa Yuda? 30 Na vita vikatokea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu sikuzote.+ 31 Mwishowe Rehoboamu akalala pamoja na mababu zake, akazikwa na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ Na jina la mama yake lilikuwa Naama, Mwamoni.+ Na Abiyamu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
15 Na katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yeroboamu+ mwana wa Nebati,+ Abiyamu akawa mfalme juu ya Yuda.+ 2 Akatawala miaka mitatu katika Yerusalemu; na jina la mama yake lilikuwa Maaka+ mjukuu wa Abishalomu.+ 3 Naye akaendelea kutembea katika dhambi zote za baba yake alizotenda kabla yake; na moyo wake haukuwa mkamilifu+ kwa Yehova Mungu wake, kama moyo wa Daudi babu yake.+ 4 Kwa maana, kwa ajili ya Daudi,+ Yehova Mungu wake alimpa taa+ katika Yerusalemu kwa kumsimamisha mwana wake baada yake na kuendelea kulisimamisha Yerusalemu,+ 5 kwa sababu Daudi alifanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, naye hakugeuka kando kutoka katika jambo lolote ambalo Yeye alikuwa amemwamuru siku zote za maisha yake,+ ila tu katika ile habari ya Uria, Mhiti.+ 6 Na vita vikatokea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote za maisha yake.+
7 Na mambo mengine ya Abiyamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? Palikuwa na vita pia vilivyotokea kati ya Abiyamu na Yeroboamu.+ 8 Mwishowe Abiyamu akalala pamoja na mababu zake, nao wakamzika katika Jiji la Daudi;+ na Asa+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
9 Katika mwaka wa 20 wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa alitawala akiwa mfalme wa Yuda. 10 Naye akatawala miaka 41 katika Yerusalemu; na jina la nyanya yake lilikuwa Maaka+ mjukuu wa Abishalomu.+ 11 Na Asa akafanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, kama Daudi babu yake.+ 12 Basi akawaondoa wanaume makahaba wa hekaluni kutoka katika nchi,+ akaondoa sanamu zote za mavi+ ambazo mababu zake walikuwa wametengeneza.+ 13 Na hata Maaka+ nyanya yake, mfalme alimwondoa asiwe malkia,+ kwa sababu alikuwa ametengeneza sanamu yenye kutisha kwa ajili ya mti mtakatifu; kisha Asa akaikata sanamu yake yenye kutisha,+ akaiteketeza kwa moto+ katika bonde la mto la Kidroni.+ 14 Naye hakuondoa+ mahali pa juu.+ Hata hivyo, moyo wa Asa ulikuwa mkamilifu kwa Yehova siku zake zote.+ 15 Naye akaanza kuingiza ndani ya nyumba ya Yehova vitu ambavyo baba yake alivifanya kuwa vitakatifu na vitu ambavyo yeye mwenyewe alivifanya kuwa vitakatifu, fedha na dhahabu na vyombo.+
16 Na vita vikawa kati ya Asa na Baasha+ mfalme wa Israeli siku zao zote. 17 Basi Baasha mfalme wa Israeli alikuja kupigana na Yuda na kuanza kujenga Rama,+ asimruhusu mtu yeyote kutoka nje wala kuingia ndani kwa Asa mfalme wa Yuda.+ 18 Ndipo Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imebaki katika hazina za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mfalme, akaitia mkononi mwa watumishi wake; na Mfalme Asa akawatuma waende kwa Ben-hadadi+ mwana wa Tabrimoni mwana wa Hezioni, mfalme wa Siria,+ aliyekuwa akikaa Damasko,+ akisema: 19 “Kuna agano kati yangu na wewe, kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi+ ya fedha na dhahabu. Njoo, vunja agano lako na Baasha mfalme wa Israeli, ili aondoke kwangu.”+ 20 Basi Ben-hadadi akamsikiliza Mfalme Asa, akatuma wakuu wake wa majeshi kushambulia majiji ya Israeli, wakapiga Iyoni+ na Dani+ na Abel-beth-maaka+ na Kinerethi yote, na hata nchi yote ya Naftali.+ 21 Na ikawa kwamba mara tu Baasha aliposikia habari hizo, mara moja akaacha kujenga Rama,+ akaendelea kukaa kule Tirsa.+ 22 Naye Mfalme Asa akaita Yuda+ wote—hakuna yeyote aliyeachwa—nao wakachukua mawe ya Rama na miti yake, ambayo Baasha alikuwa ametumia kujenga; na kwa vitu hivyo Mfalme Asa akaanza kujenga Geba+ katika Benyamini, na Mispa.+
23 Na mambo mengine yote ya Asa na uwezo wake wote na yote aliyoyafanya na majiji aliyoyajenga, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? Ila tu kwamba wakati wa kuzeeka+ kwake miguu yake ikawa na ugonjwa.+ 24 Mwishowe Asa akalala pamoja na mababu zake,+ naye akazikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi babu yake;+ na Yehoshafati+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
25 Naye Nadabu+ mwana wa Yeroboamu akawa mfalme juu ya Israeli katika mwaka wa pili wa Asa mfalme wa Yuda; naye akaendelea kutawala juu ya Israeli miaka miwili. 26 Naye akaendelea kutenda yaliyokuwa mabaya+ machoni pa Yehova, akaendelea kutembea katika njia ya baba yake+ na katika dhambi yake ambayo kwa hiyo alisababisha Israeli kutenda dhambi.+ 27 Na Baasha+ mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akaanza kupanga hila juu yake; naye Baasha akampiga na kumuua kule Gibethoni,+ jiji la Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli wote walipokuwa wakilizingira Gibethoni. 28 Kwa hiyo Baasha akamuua katika mwaka wa tatu wa Asa mfalme wa Yuda, akaanza kutawala mahali pake.+ 29 Na ikawa kwamba mara tu alipokuwa mfalme, akaipiga nyumba yote ya Yeroboamu. Hakuacha yeyote wa Yeroboamu anayepumua abaki mpaka alipokuwa amewaangamiza, kulingana na neno la Yehova alilosema kupitia mtumishi wake Ahiya Mshilo,+ 30 kwa sababu ya dhambi za Yeroboamu ambazo kupitia hizo alisababisha Israeli kutenda dhambi+ na kwa kutia uchungu kwake alikomtia uchungu Yehova Mungu wa Israeli.+ 31 Na mambo mengine ya Nadabu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 32 Na vita vikatokea kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zao zote.+
33 Katika mwaka wa tatu wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme juu ya Israeli yote kule Tirsa kwa miaka 24.+ 34 Naye akaendelea kutenda yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ akaendelea kutembea katika njia ya Yeroboamu+ na katika dhambi yake ambayo kupitia hiyo alisababisha Israeli kutenda dhambi.+
16 Ndipo neno la Yehova likamjia Yehu+ mwana wa Hanani+ juu ya Baasha, akisema: 2 “Kwa vile nilikusimamisha kutoka mavumbini+ ili nikufanye kiongozi juu ya watu wangu Israeli,+ lakini ukaanza kutembea katika njia ya Yeroboamu+ na hivyo kusababisha watu wangu Israeli watende dhambi kwa kunitia uchungu kwa dhambi zao,+ 3 tazama, ninafagia kabisa nikimfuata Baasha na nyumba yake, nami nitaifanya nyumba yake iwe kama nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati.+ 4 Mtu yeyote wa Baasha anayekufa jijini mbwa watamla; na mtu wake yeyote anayekufa shambani ndege wa mbinguni watamla.”+
5 Na mambo mengine ya Baasha na yale aliyoyafanya na nguvu zake, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 6 Mwishowe Baasha akalala pamoja na mababu zake, akazikwa kule Tirsa;+ na Ela mwana wake akaanza kutawala mahali pake. 7 Na pia kupitia Yehu mwana wa Hanani nabii, neno la Yehova lilikuja juu ya Baasha na nyumba yake,+ kwa sababu ya ubaya wote aliotenda machoni pa Yehova kwa kumtia uchungu+ kwa kazi za mikono yake,+ ili iwe kama nyumba ya Yeroboamu, na pia kwa sababu alimpiga na kumuua.+
8 Katika mwaka wa 26 wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akawa mfalme juu ya Israeli kule Tirsa kwa miaka miwili. 9 Na Zimri+ mtumishi wake, mkuu wa nusu ya magari, akaanza kupanga hila juu yake, alipokuwa kule Tirsa akinywa+ na kulewa nyumbani kwa Arsa, aliyekuwa juu ya nyumba+ kule Tirsa. 10 Na Zimri akaingia, akampiga na kumuua+ katika mwaka wa 27 wa Asa mfalme wa Yuda, naye akaanza kutawala mahali pake. 11 Na ikawa kwamba wakati alipoanza kutawala, mara tu alipoketi katika kiti chake cha ufalme, akaipiga nyumba yote ya Baasha. Hakuacha abaki mtu yeyote wa kwake anayekojoa ukutani+ wala walipiza-kisasi wake wa damu+ wala rafiki zake. 12 Hivyo ndivyo Zimri alivyoiangamiza nyumba yote ya Baasha,+ kulingana na neno la Yehova+ alilokuwa amesema juu ya Baasha kupitia Yehu nabii,+ 13 kwa sababu ya dhambi zote za Baasha na dhambi za Ela+ mwana wake ambazo walitenda na ambazo kupitia hizo walisababisha Israeli kutenda dhambi kwa kumtia uchungu Yehova Mungu wa Israeli, kwa sanamu zao za ubatili.+ 14 Na mambo mengine ya Ela na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli?
15 Katika mwaka wa 27 wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akawa mfalme kwa siku 7+ kule Tirsa, watu walipokuwa wamepiga kambi juu ya Gibethoni,+ jiji la Wafilisti. 16 Baada ya muda watu waliokuwa wamepiga kambi wakasikia habari, zikisema: “Zimri amepanga hila na pia akampiga na kumuua mfalme.” Basi Israeli wote wakamfanya Omri,+ mkuu wa jeshi, kuwa mfalme juu ya Israeli siku hiyo katika kambi. 17 Sasa Omri na Israeli wote pamoja naye wakapanda kutoka Gibethoni, wakaanza kuzingira+ Tirsa. 18 Na ikawa kwamba mara tu Zimri alipoona kwamba jiji limetekwa, akaingia katika mnara wa makao wa nyumba ya mfalme, akaiteketeza kwa moto nyumba ya mfalme juu yake mwenyewe, hivi kwamba akafa,+ 19 kwa ajili ya dhambi zake alizotenda kwa kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova+ kwa kutembea katika njia ya Yeroboamu na katika dhambi yake aliyotenda kwa kusababisha Israeli watende dhambi.+ 20 Na mambo mengine ya Zimri na hila yake aliyopanga, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli?
21 Wakati huo ndipo watu wa Israeli walianza kujigawanya kuwa sehemu mbili.+ Kuna sehemu moja ya watu waliokuwa wafuasi wa Tibni mwana wa Ginathi, ili kumfanya kuwa mfalme, na sehemu ile nyingine wafuasi wa Omri. 22 Mwishowe watu waliokuwa wakimfuata Omri wakawashinda watu waliokuwa wakimfuata Tibni mwana wa Ginathi; kwa hiyo Tibni akafa, na Omri akaanza kutawala.
23 Katika mwaka wa 31 wa Asa mfalme wa Yuda, Omri akawa mfalme juu ya Israeli kwa miaka 12. Akatawala miaka 6 kule Tirsa. 24 Naye akanunua mlima wa Samaria kutoka kwa Shemeri kwa talanta mbili za fedha, naye akaanza kujenga juu ya huo mlima na kuita jina la jiji alilolijenga Samaria,+ kulingana na jina la Shemeri bwana wa ule mlima. 25 Na Omri akazidi kutenda yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, akatenda yaliyokuwa mabaya zaidi kuliko wote waliomtangulia.+ 26 Naye akatembea katika njia yote ya Yeroboamu mwana wa Nebati+ na katika dhambi yake ambayo kupitia hiyo alisababisha Israeli kutenda dhambi kwa kumtia uchungu Yehova Mungu wa Israeli, kwa sanamu zao za ubatili.+ 27 Na mambo mengine ya Omri, yale aliyoyafanya na nguvu zake alizotumia kutenda, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 28 Mwishowe Omri akalala pamoja na mababu zake, akazikwa Samaria; na Ahabu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
29 Naye Ahabu mwana wa Omri alikuwa mfalme juu ya Israeli katika mwaka wa 38 wa Asa mfalme wa Yuda; na Ahabu mwana wa Omri akaendelea kutawala juu ya Israeli katika Samaria+ kwa miaka 22. 30 Na Ahabu mwana wa Omri akatenda mabaya zaidi machoni pa Yehova kuliko wote waliomtangulia.+ 31 Na ikawa kana kwamba lilikuwa ni jambo dogo zaidi+ kwake kutembea katika dhambi za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, sasa akamchukua Yezebeli+ binti ya Ethbaali, mfalme wa Wasidoni,+ kuwa mke wake+ naye akaanza kwenda kumtumikia Baali+ na kumwinamia. 32 Tena akamsimamishia Baali madhabahu katika nyumba+ ya Baali aliyoijenga kule Samaria. 33 Na Ahabu akatengeneza mti mtakatifu;+ na Ahabu akafanya mengi zaidi ya kumtia uchungu+ Yehova Mungu wa Israeli, kuliko wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.
34 Katika siku zake Hieli Mbetheli akajenga Yeriko. Kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa kwanza yeye aliuweka msingi wake, na kwa kufiwa na Segubu mwana wake aliye mdogo zaidi yeye aliisimamisha milango yake, kulingana na neno la Yehova alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.+
17 Na Eliya+ Mtishbi kutoka kwa wakaaji wa Gileadi+ akamwambia Ahabu: “Kama anavyoishi+ Yehova Mungu wa Israeli, ambaye ninasimama mbele zake,+ miaka hii hakutakuwa na umande wala mvua,+ isipokuwa kwa agizo la neno langu!”+
2 Basi neno+ la Yehova likamjia, na kusema: 3 “Ondoka hapa, ugeuke, ushike njia kwenda upande wa mashariki, ujifiche+ kwenye bonde la mto la Kerithi lililoko mashariki mwa Yordani. 4 Na itatukia kwamba unapaswa kunywa+ kutoka katika hilo bonde la mto, nami nitawaamuru kunguru+ wakuletee chakula huko.”+ 5 Naye akaenda mara moja na kufanya kulingana na neno la Yehova,+ na kwa hiyo akaenda, akaanza kukaa kando ya lile bonde la mto la Kerithi lililoko mashariki mwa Yordani. 6 Na kunguru wakamletea mkate na nyama wakati wa asubuhi na mkate na nyama wakati wa jioni, naye akaendelea kunywa maji katika lile bonde la mto.+ 7 Lakini ikawa kwamba baada ya siku kadhaa, lile bonde la mto likakauka,+ kwa sababu mvua haikuwa imenyesha juu ya dunia.
8 Basi neno la Yehova likamjia, na kusema:+ 9 “Ondoka, nenda Sarefathi,+ wa Sidoni, nawe ukae huko. Tazama! Nitamwamuru mwanamke fulani huko, mjane, akupe chakula.” 10 Basi akaondoka, akaenda Sarefathi, akafika kwenye mwingilio wa jiji; na tazama! mwanamke, mjane, alikuwa hapo akikusanya kuni. Basi akamwita na kumwambia yule mwanamke: “Tafadhali, niletee maji kidogo katika chombo ninywe.”+ 11 Mwanamke huyo alipoanza kwenda kuyaleta, akamwita na kumwambia: “Tafadhali, niletee kipande cha mkate+ mkononi mwako.” 12 Ndipo mwanamke yule akasema: “Kama anavyoishi Yehova Mungu wako,+ mimi sina keki yoyote ya mviringo,+ isipokuwa mkono mmoja tu+ wa unga katika mtungi mkubwa na mafuta kidogo+ katika mtungi mdogo; na tazama, ninakusanya kuni chache, nami nitaenda kutayarisha kitu kwa ajili yangu na mwanangu, nasi tutakula chakula hicho na kufa.”+
13 Ndipo Eliya akamwambia: “Usiogope.+ Nenda, fanya kulingana na neno lako. Ila tu unitayarishie kwanza keki ndogo ya mviringo kutokana na kile kilichopo,+ nawe uniletee hiyo, na unaweza kutayarisha kitu kwa ajili yako na mwana wako baadaye. 14 Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Ule mtungi mkubwa wa unga hautamalizika, na ule mtungi mdogo wa mafuta hautapungua mpaka siku Yehova atakapoleta mvua juu ya uso wa nchi.’”+ 15 Basi akaenda na kufanya kulingana na neno la Eliya; na mwanamke yule akaendelea kula, yeye pamoja na Eliya na nyumba ya yule mwanamke, kwa siku nyingi.+ 16 Ule mtungi mkubwa wa unga haukumalizika, wala ule mtungi mdogo wa mafuta haukupungua,+ kulingana na neno la Yehova alilokuwa amesema kupitia Eliya.
17 Na ikawa kwamba baada ya mambo hayo mwana wa yule mwanamke, bimkubwa wa ile nyumba, akawa mgonjwa, na ugonjwa wake ukawa mkali sana hivi kwamba hapakuwa na pumzi iliyobaki ndani yake.+ 18 Ndipo akamwambia Eliya: “Nina nini nawe,+ Ee mtu wa Mungu wa kweli? Umekuja kwangu ili kurudisha kumbukumbu la kosa langu+ na kumuua mwanangu.” 19 Lakini akamwambia: “Nipe mwana wako.” Kisha akamchukua kutoka kifuani pake, akampeleka juu katika chumba cha darini,+ alipokuwa akikaa, akamlaza juu ya kitanda chake mwenyewe.+ 20 Naye akaanza kumwita Yehova na kusema: “Ee Yehova Mungu wangu,+ je, tena unaleta mabaya juu ya mjane ninayekaa naye kwa kumuua mwana wake?” 21 Naye akajinyoosha juu ya yule mtoto+ mara tatu na kumwita Yehova na kusema: “Ee Yehova, Mungu wangu, tafadhali, irudishe nafsi+ ya mtoto huyu ndani yake.” 22 Mwishowe Yehova akaisikiliza sauti ya Eliya,+ hivi kwamba nafsi ya yule mtoto ikarudi ndani yake, akawa hai.+ 23 Basi Eliya akamchukua mtoto huyo, akamshusha kutoka katika kile chumba cha darini, akamleta katika nyumba na kumpa mama yake; na kisha Eliya akasema: “Tazama, mwana wako yuko hai.”+ 24 Ndipo yule mwanamke akamwambia Eliya: “Kwa kweli sasa najua kwamba wewe ni mtu wa Mungu+ na kwamba neno la Yehova kinywani mwako ni la kweli.”+
18 Na ikawa kwamba baada ya siku nyingi neno la Yehova likamjia Eliya katika mwaka wa tatu, na kusema: “Nenda, jionyeshe kwa Ahabu, kwa kuwa nimeazimia kunyesha mvua+ juu ya uso wa nchi.”+ 2 Basi Eliya akaenda kujionyesha kwa Ahabu, njaa ilipokuwa kali+ katika Samaria.
3 Wakati huo Ahabu akamwita Obadia, aliyekuwa akiisimamia nyumba.+ (Basi Obadia alikuwa amejionyesha kuwa mtu anayemwogopa+ Yehova sana. 4 Na ikawa kwamba Yezebeli+ alipowakatilia mbali manabii+ wa Yehova, Obadia aliwachukua manabii 100, akawaficha wakiwa vikundi viwili vya watu 50 pangoni, naye akawapa mkate na maji.)+ 5 Na Ahabu akamwambia Obadia: “Tembea katika nchi kwenye mabubujiko yote ya maji na kwenye mabonde yote ya mito. Labda tutapata majani mabichi,+ ili tuwahifadhi hai farasi na nyumbu na ili wanyama zaidi wasiangamie.”+ 6 Kwa hiyo wakagawana nchi ambayo wangepita katikati yake. Ahabu akaenda peke yake kupitia njia moja, na Obadia akaenda peke yake kupitia njia nyingine.+
7 Obadia alipoendelea kusafiri njiani, tazama, Eliya akija kumpokea.+ Mara moja akamtambua, akaanguka kifudifudi,+ akasema: “Je, ni wewe, bwana wangu+ Eliya?” 8 Naye akamwambia: “Ni mimi. Nenda, mwambie bwana wako,+ ‘Tazama, Eliya yupo hapa.’” 9 Lakini akasema: “Nimetenda dhambi gani+ ndipo umtie mtumishi wako mkononi mwa Ahabu, aniue? 10 Kama anavyoishi Yehova Mungu wako,+ hakuna taifa wala ufalme ambapo bwana wangu hajawatuma watu wakutafute. Waliposema, ‘Hayupo hapa,’ akafanya ufalme na taifa kuapa kwamba hawakuweza kukupata.+ 11 Na sasa unasema, ‘Nenda, mwambie bwana wako: “Tazama, Eliya yupo hapa.”’ 12 Na hakika itatukia kwamba, mimi nikiondoka kwako, ndipo roho+ ya Yehova itakapokuchukua na kukupeleka mahali ambapo mimi sitajua; nami nitakuwa nimekuja kumwambia Ahabu, naye hatakupata, naye hakika ataniua,+ kwa kuwa mtumishi wako amemwogopa Yehova tangu ujana wake.+ 13 Je, bwana wangu hakuambiwa yale niliyofanya wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yehova, jinsi nilivyowaficha baadhi ya manabii wa Yehova, watu 100 wakiwa vikundi viwili vya watu 50 pangoni,+ nikaendelea kuwapa mkate na maji?+ 14 Na sasa unasema, ‘Nenda, mwambie bwana wako: “Tazama, Eliya yupo hapa.”’ Naye hakika ataniua.”+ 15 Hata hivyo, Eliya akasema: “Kama anavyoishi+ Yehova wa majeshi+ ambaye ninasimama mbele zake, leo nitajionyesha kwake.”
16 Basi Obadia akaenda kukutana na Ahabu, akamwambia; na kwa hiyo Ahabu akaenda kukutana na Eliya.
17 Na ikawa kwamba, mara tu Ahabu alipomwona Eliya, mara moja Ahabu akamwambia: “Je, ni wewe, mtu unayeleta taabu juu ya Israeli?”+
18 Naye akasema: “Mimi sikuleta taabu juu ya Israeli,+ lakini ni wewe na nyumba ya baba yako,+ kwa sababu ninyi mmeziacha amri za Yehova,+ nawe ukaanza kufuata Mabaali.+ 19 Na sasa tuma watu, unikusanyie Israeli wote katika Mlima Karmeli+ na pia wale manabii 450 wa Baali+ na wale manabii 400 wa ule mti mtakatifu,+ wanaokula mezani pa Yezebeli.”+ 20 Na Ahabu akatuma watu kati ya wana wote wa Israeli, akawakusanya wale manabii+ katika Mlima Karmeli.
21 Kisha Eliya akawakaribia watu wote na kusema: “Mtayumba-yumba juu ya maoni mawili tofauti mpaka wakati gani?+ Ikiwa Yehova ndiye Mungu wa kweli, mfuateni yeye;+ lakini ikiwa ni Baali, mfuateni yeye.” Na watu hawakumjibu neno lolote. 22 Na Eliya akaendelea kuwaambia watu: “Mimi tu nimebaki nikiwa nabii wa Yehova,+ mimi peke yangu, nao manabii wa Baali ni watu 450. 23 Sasa na watupe sisi ng’ombe-dume wachanga wawili, nao wajichagulie ng’ombe-dume mmoja mchanga, wamkate vipande-vipande na kumweka juu ya kuni, lakini wasiziwashe moto. Na mimi nitamtayarisha yule ng’ombe mchanga mwingine, nami nitamweka juu ya kuni, lakini sitaziwasha moto. 24 Nanyi mliitie jina la mungu wenu,+ nami, kwa upande wangu, nitaliitia jina la Yehova; na itatukia kwamba yule Mungu wa kweli atakayejibu kupitia moto,+ huyo ndiye Mungu wa kweli.”+ Kwa hiyo watu wote wakajibu na kusema: “Jambo hili ni jema.”
25 Sasa Eliya akawaambia manabii wa Baali: “Jichagulieni ng’ombe mchanga mmoja, halafu mkamtayarishe kwanza, kwa sababu ninyi ndio wengi; nanyi mliitie jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.” 26 Basi wakamchukua yule ng’ombe mchanga aliyewapa. Kisha wakamtayarisha, nao wakaendelea kuliitia jina la Baali kutoka asubuhi mpaka katikati ya mchana, wakisema: “Ee Baali, tupe jibu!” Lakini hapakuwa na sauti yoyote,+ wala hakuna yeyote aliyetoa jibu.+ Nao wakazidi kurukaruka kuizunguka madhabahu waliyokuwa wameitengeneza. 27 Na ikawa kwamba ilipofika katikati ya mchana Eliya akaanza kuwafanyia dhihaka+ na kusema: “Iteni kwa sauti kubwa, kwa maana yeye ni mungu;+ kwa maana lazima iwe ana kazi fulani, naye ana kinyesi+ na lazima aende chooni.+ Au pengine amelala usingizi naye anapaswa kuamka!”+ 28 Nao wakaanza kuita kwa sauti yao yote, wakijikatakata+ kwa visu na mikuki kulingana na desturi yao, mpaka walipojitiririsha damu. 29 Na ikawa kwamba mara tu mchana ulipokwisha nao wakazidi kutenda kama manabii+ mpaka wakati wa kutolewa kwa toleo la nafaka, hapakuwa na sauti yoyote, wala hapakuwa na yeyote aliyejibu, wala aliyewasikiliza.+
30 Mwishowe Eliya akawaambia watu wote: “Nikaribieni.” Basi watu wote wakamkaribia. Kisha akatengeneza ile madhabahu ya Yehova iliyokuwa imebomoka.+ 31 Basi Eliya akachukua mawe kumi na mawili, kulingana na hesabu ya makabila ya wana wa Yakobo, ambaye neno la Yehova lilikuwa limemjia,+ likisema: “Jina lako litakuwa Israeli.”+ 32 Naye akafanyiza mawe yakawa madhabahu+ kwa jina la Yehova,+ akachimba mtaro wenye ukubwa wa kama sehemu inayopandwa vipimo viwili vya sea vya mbegu, kuizunguka madhabahu yote. 33 Kisha akapanga kwa utaratibu zile kuni,+ akamkata yule ng’ombe mchanga vipande-vipande na kumweka juu ya zile kuni. Sasa akasema: “Jazeni maji mitungi mikubwa minne, myamwage juu ya toleo la kuteketezwa na juu ya kuni.” 34 Kisha akasema: “Fanyeni hivyo tena.” Basi wakafanya hivyo tena. Lakini akasema: “Fanyeni hivyo mara ya tatu.” Basi wakafanya hivyo mara ya tatu. 35 Kwa hiyo maji yakaizunguka ile madhabahu yote, na pia ule mtaro akaujaza maji.
36 Na ikawa kwamba wakati+ wa kutolewa kwa toleo la nafaka, Eliya nabii akaanza kukaribia na kusema: “Ee Yehova Mungu wa Abrahamu,+ Isaka+ na Israeli,+ leo na ijulikane kwamba wewe ni Mungu katika Israeli+ na mimi ni mtumishi wako na ni kwa neno+ lako nimefanya mambo haya yote. 37 Unijibu, Ee Yehova, unijibu, ili watu hawa wajue kwamba wewe, Yehova,+ ndiye Mungu wa kweli na wewe mwenyewe umeugeuza moyo wao urudi.”+
38 Ndipo moto+ wa Yehova ukashuka, ukala lile toleo la kuteketezwa+ na zile kuni na mawe na mavumbi, nao ukaramba maji yaliyokuwa katika mtaro.+ 39 Watu wote walipoona jambo lile, wakaanguka kifudifudi+ mara moja, na kusema: “Yehova ndiye Mungu wa kweli! Yehova ndiye Mungu wa kweli!” 40 Kisha Eliya akawaambia: “Wakamateni manabii wa Baali! Msiache hata mmoja wao aponyoke!” Ndipo wakawakamata mara moja, na Eliya akawashusha mpaka kwenye bonde la mto la Kishoni,+ akawaua huko.+
41 Sasa Eliya akamwambia Ahabu: “Panda ukale na kunywa;+ kwa maana kuna kishindo cha machafuko ya mvua kubwa.”+ 42 Na Ahabu akapanda, akaenda zake kula na kunywa. Naye Eliya akapanda juu ya Karmeli na kuanza kuchutama chini,+ akaweka uso wake katikati ya magoti yake.+ 43 Kisha akamwambia mtumishi wake: “Nenda juu, tafadhali. Tazama upande wa bahari.” Basi akaenda juu, akatazama na kisha akasema: “Hakuna kitu chochote.” Naye akaendelea kusema, “Rudi,” mara saba.+ 44 Na ikawa kwamba mara ya saba akasema: “Tazama! Pana wingu dogo kama kiganja cha mkono wa mwanadamu linalopanda kutoka baharini.”+ Sasa akasema: “Nenda juu, mwambie Ahabu, ‘Funga gari!+ Nawe ushuke ili mvua kubwa isikuzuie!’” 45 Na ikawa kwamba wakati huo mbingu zikatiwa giza kwa mawingu na upepo+ na mvua kubwa sana ikaanza kunyesha.+ Na Ahabu akaendelea kupanda gari, akaenda zake Yezreeli.+ 46 Na mkono wa Yehova ukawa juu ya Eliya,+ hivi kwamba akajifunga viuno,+ naye akakimbia mbele ya Ahabu mpaka Yezreeli.+
19 Kisha Ahabu+ akamwambia Yezebeli+ mambo yote ambayo Eliya alikuwa amefanya na mambo yote kuhusu namna alivyowaua manabii wote kwa upanga.+ 2 Ndipo Yezebeli akatuma mjumbe kwa Eliya, akisema: “Miungu na ifanye hivyo,+ nayo izidishe jambo hilo,+ ikiwa wakati kama huu hapo kesho sitaifanya nafsi yako iwe kama nafsi ya kila mmoja wao!” 3 Naye akaogopa. Basi akaondoka, akaanza kwenda kwa ajili ya nafsi yake,+ akafika Beer-sheba,+ jiji la Yuda.+ Kisha akamwacha mtumishi wake huko. 4 Naye mwenyewe akaingia nyikani safari ya siku moja, mwishowe akafika na kuketi chini ya mretemu fulani.+ Naye akaanza kuomba kwamba nafsi yake ife na kusema: “Inatosha! Sasa, Ee Yehova, iondoe nafsi yangu,+ kwa maana mimi si bora kuliko mababu zangu.”
5 Mwishowe akalala chini, akashikwa na usingizi chini ya ule mretemu.+ Lakini, tazama! Malaika+ akamgusa.+ Ndipo akamwambia: “Amka, ule.” 6 Alipoangalia, na tazama, pale karibu na kichwa chake palikuwa na keki ya mviringo+ juu ya mawe yenye moto na gudulia la maji. Naye akaanza kula na kunywa, kisha akalala chini tena. 7 Baadaye yule malaika+ wa Yehova akarudi mara ya pili, akamgusa na kusema: “Amka, ule, kwa maana safari ni ndefu mno kwako.”+ 8 Basi akaamka, akala na kunywa, naye akazidi kwenda katika nguvu za chakula kile kwa siku 40,+ mchana na usiku, mpaka Horebu, mlima wa Mungu wa kweli.+
9 Mwishowe hapo akaingia pangoni,+ ili alale humo usiku; na tazama! palikuwa na neno la Yehova kwa ajili yake, nalo likamwambia: “Una kazi gani hapa, Eliya?”+ 10 Naye akasema: “Nimekuwa na wivu+ kwelikweli kwa ajili ya Yehova Mungu wa majeshi; kwa maana wana wa Israeli wameliacha agano lako,+ wamezibomoa+ madhabahu zako, nao wamewaua manabii wako kwa upanga,+ hivi kwamba ni mimi peke yangu nimebaki;+ nao wanaanza kuitafuta nafsi yangu ili kuiondoa.”+ 11 Lakini likasema: “Toka, usimame juu ya mlima mbele za Yehova.”+ Na tazama! Yehova alikuwa anapita karibu,+ na upepo mkubwa na wenye nguvu ukawa unapasua milima na kuvunja miamba mbele za Yehova.+ (Yehova hakuwa katika upepo ule.) Na baada ya upepo ule kukawa na tetemeko.+ (Yehova hakuwa katika lile tetemeko.) 12 Na baada ya lile tetemeko kukawa na moto.+ (Yehova hakuwa katika moto ule.) Na baada ya moto ule kukawa na sauti tulivu, ya chini.+ 13 Na ikawa kwamba mara tu Eliya alipoisikia, akafunika uso wake mara moja katika vazi lake rasmi,+ akatoka nje, akasimama mlangoni pa lile pango; na tazama! palikuwa na sauti kwa ajili yake, nayo ikamwambia: “Una kazi gani hapa, Eliya?”+ 14 Naye akasema: “Nimekuwa na wivu kwelikweli kwa ajili ya Yehova Mungu wa majeshi; kwa maana wana wa Israeli wameliacha agano lako,+ wamezibomoa madhabahu zako, nao wamewaua manabii wako kwa upanga, hivi kwamba ni mimi peke yangu nimebaki; nao wanaanza kuitafuta nafsi yangu ili kuiondoa.”+
15 Sasa Yehova akamwambia: “Nenda, rudi katika nyika ya Damasko;+ nawe uingie na kumtia mafuta+ Hazaeli+ kuwa mfalme juu ya Siria. 16 Na Yehu+ mjukuu wa Nimshi+ umtie mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli; na Elisha+ mwana wa Shafati kutoka Abel-mehola+ umtie mafuta kuwa nabii mahali pako.+ 17 Na itatukia kwamba yule atakayepona upanga+ wa Hazaeli, Yehu atamuua;+ na yule atakayepona upanga wa Yehu, Elisha atamuua.+ 18 Nami nimewaacha watu elfu saba wabaki katika Israeli,+ magoti yote ambayo hayakumwinamia Baali,+ na kila kinywa ambacho hakikumbusu.”+
19 Basi akaondoka hapo, akamkuta Elisha mwana wa Shafati akilima+ na jozi kumi na mbili za wanyama mbele yake, naye akiwa na ile ya kumi na mbili. Basi Eliya akavuka mpaka pale alipokuwa, akalitupa vazi lake rasmi+ juu yake. 20 Ndipo akawaacha wale ng’ombe, akakimbia kumfuata Eliya na kusema: “Tafadhali, acha nimbusu baba yangu na mama yangu.+ Kisha nitakufuata.” Naye akamwambia: “Nenda, rudi; kwa maana mimi nimekufanyia nini?” 21 Kwa hiyo akarudi, akaacha kumfuata na kisha akachukua jozi moja ya wale ng’ombe na kuwatoa dhabihu,+ na kwa kutumia vifaa+ vya wale ng’ombe, akatokosa nyama yao, akawapa watu, nao wakaanza kula. Kisha akaondoka, akaanza kumfuata Eliya, naye akaanza kumhudumia.+
20 Naye Ben-hadadi+ mfalme wa Siria akakusanya majeshi yake yote na pia wafalme 32 pamoja naye+ na farasi+ na magari,+ akapanda kwenda kuzingira+ Samaria+ na kupigana nalo. 2 Kisha akatuma wajumbe+ kwa Ahabu mfalme wa Israeli katika jiji. Naye akamwambia: “Ben-hadadi amesema hivi, 3 ‘Fedha yako na dhahabu yako ni yangu, na wake zako na wana wako, wale wenye sura nzuri zaidi, ni wangu.’”+ 4 Ndipo mfalme wa Israeli akajibu na kusema: “Bwana wangu mfalme, kulingana na neno lako, mimi ni wako na vyote vilivyo vyangu.”+
5 Baadaye wajumbe wakarudi na kusema: “Ben-hadadi amesema hivi, ‘Nilituma watu kwako, kusema: “Fedha yako na dhahabu yako na wake zako na wana wako utanipa. 6 Lakini wakati kama huu kesho nitawatuma watumishi wangu kwako, nao watachunguza kwa makini nyumba yako na nyumba za watumishi wako; na itatukia kwamba kila kitu kinachotamanika+ machoni pako watakitia mkononi mwao, nao watakichukua.”’”
7 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaita wanaume wazee wa nchi+ na kusema: “Tafadhali angalieni, oneni kwamba mtu huyu anatafuta msiba;+ kwa maana alituma watu kwangu kuchukua wake zangu na wanangu na fedha yangu na dhahabu yangu, nami sikumnyima vitu hivyo.” 8 Ndipo wanaume wazee na watu wote wakamwambia: “Usitii, wala usikubali.” 9 Kwa hiyo akawaambia wajumbe wa Ben-hadadi: “Mwambieni bwana wangu mfalme, ‘Yote uliyowatuma watu kwanza ukiyataka kwa mtumishi wako nitafanya; lakini jambo hili siwezi kulifanya.’” Basi wale wajumbe wakaenda zao, wakampelekea neno.
10 Sasa Ben-hadadi akatuma watu kwake na kusema: “Miungu+ na inifanyie hivyo, nayo izidishe jambo hilo,+ ikiwa mavumbi ya Samaria yatatosha mikono ya watu wote wanaonifuata!”+ 11 Naye mfalme wa Israeli akajibu na kusema: “Mwambieni hivi, ‘Mtu anayejifunga mshipi+ asijisifu kama yeye anayejifungua mshipi.’”+ 12 Na ikawa kwamba mara tu aliposikia neno hilo, wakati yeye na wale wafalme walipokuwa wakinywa+ katika vibanda, mara moja akawaambia watumishi wake: “Jitayarisheni!” Nao wakaanza kujitayarisha kulishambulia jiji.
13 Na tazama! nabii fulani akamkaribia Ahabu mfalme wa Israeli,+ kisha akasema: “Yehova amesema hivi,+ ‘Je, umeuona umati huu wote mkubwa? Tazama, nitautia mkononi mwako leo, nawe hakika utajua kwamba mimi ni Yehova.’”+ 14 Ndipo Ahabu akasema: “Kupitia nani?” naye akasema: “Yehova amesema hivi, ‘Kupitia vijana wa wakuu wa wilaya za utawala.’” Mwishowe akasema: “Ni nani atakayeanza pambano la vita?” naye akasema: “Ni wewe!”
15 Naye akaanza kuwahesabu wale vijana wa wakuu wa wilaya za utawala, nao wakawa 232;+ na baada yao akawahesabu watu wote, wana wote wa Israeli, 7,000. 16 Nao wakaanza kutoka katikati ya mchana wakati Ben-hadadi alipokuwa akinywa na kulewa+ katika vibanda, yeye pamoja na wale wafalme, wale wafalme 32 waliokuwa wakimsaidia. 17 Wakati wale vijana+ wa wakuu wa wilaya za utawala walipotoka kwanza, mara moja Ben-hadadi akatuma watu; nao wakaja na kumwambia, wakisema: “Kuna watu ambao wametoka katika Samaria.” 18 Ndipo akasema: “Hata kama wametoka kwa ajili ya amani, wakamateni wakiwa hai; au kama wametoka kwa ajili ya vita, wakamateni wakiwa hai.”+ 19 Na hao ndio waliotoka katika jiji, wale vijana wa wakuu wa wilaya za utawala na majeshi yaliyokuwa nyuma yao. 20 Nao wakaanza kumpiga na kumuua kila mmoja mtu wake; na Wasiria+ wakaanza kukimbia,+ na Israeli wakawafuatilia, lakini Ben-hadadi mfalme wa Siria akakimbia akiwa juu ya farasi pamoja na wapanda-farasi. 21 Lakini mfalme wa Israeli akatoka, akazidi kuwapiga na kuwaua wale farasi na magari,+ naye akawapiga Wasiria kwa mauaji makuu.
22 Baadaye yule nabii+ akamkaribia mfalme wa Israeli na kumwambia: “Nenda, jitie nguvu+ na ujue na kuona utakalofanya;+ kwa maana mwanzoni mwa mwaka mfalme wa Siria atakuja kukushambulia.”+
23 Na watumishi wa mfalme wa Siria wakamwambia: “Mungu wao ni Mungu wa milima.+ Ndiyo sababu walikuwa na nguvu kutushinda. Basi, na tupigane nao katika nchi tambarare, tuone kama hatutakuwa na nguvu kuwashinda. 24 Nawe ufanye hivi: Ondoa wafalme,+ kila mmoja kutoka mahali pake, na uweke magavana mahali pao.+ 25 Nawe ujihesabie jeshi linalolingana na jeshi lililoanguka kutoka upande wako, kukiwa na farasi kwa farasi na gari kwa gari; nasi tupigane nao katika nchi tambarare, tuone kama hatutakuwa na nguvu kuwashinda.”+ Basi akasikiliza sauti yao, akafanya vivyo hivyo.
26 Na ikawa kwamba mwanzoni mwa mwaka Ben-hadadi akawakusanya Wasiria+ na kupanda mpaka Afeki+ ili kupigana na Israeli. 27 Nao wana wa Israeli wakakusanywa na kuandaliwa,+ wakaanza kwenda kukutana nao; na wana wa Israeli wakaenda katika kambi mbele yao kama vikundi vidogo viwili vya mbuzi, na Wasiria, kwa upande wao, wakaijaza dunia.+ 28 Kisha yule mtu wa Mungu wa kweli+ akakaribia na kumwambia mfalme wa Israeli, naam, akasema: “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu Wasiria wamesema: “Yehova ni Mungu wa milima, wala si Mungu wa nchi tambarare za chini,” nitautia mkononi mwako umati huu wote mkubwa,+ nanyi mtajua hakika kwamba mimi ni Yehova.’”+
29 Nao wakaendelea kukaa kambini siku saba, hawa wakiwa mbele ya wale.+ Na ikawa kwamba katika siku ya saba lile pambano la kivita likaanza; na wana wa Israeli wakawapiga na kuwaua Wasiria, watu mia moja elfu wanaoenda kwa miguu, katika siku moja. 30 Na wale waliobaki wakakimbia mpaka Afeki,+ katika jiji; na ukuta ukaanguka juu ya watu 27,000 waliokuwa wamebaki.+ Naye Ben-hadadi akakimbia,+ mwishowe akafika jijini, akaingia katika chumba cha ndani kabisa.+
31 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia: “Tazama, sasa, tumesikia kwamba wafalme wa nyumba ya Israeli ni wafalme walio na fadhili zenye upendo.+ Tafadhali, acha tuchukue nguo za magunia+ katika viuno+ vyetu na kamba juu ya vichwa vyetu, nasi twende kwa mfalme wa Israeli. Pengine atahifadhi hai nafsi yako.”+ 32 Basi wakajifunga nguo za magunia katika viuno vyao, na kamba zikiwa juu ya vichwa vyao, wakaja kwa mfalme wa Israeli na kusema: “Mtumishi wako Ben-hadadi amesema, ‘Tafadhali, acha nafsi yangu iishi.’” Naye akasema: “Je, yeye angali hai bado? Yeye ni ndugu yangu.” 33 Basi hao watu+ wakaliona jambo hilo kuwa ni ishara ya bahati na bila kukawia wakaliona kuwa ni uamuzi wake mwenyewe, nao wakaendelea kusema: “Ben-hadadi ni ndugu yako.” Kwa hiyo akasema: “Haya, mleteni.” Ndipo Ben-hadadi akaenda kwake; naye akampandisha garini mara moja.+
34 Sasa Ben-hadadi akamwambia: “Majiji+ ambayo baba yangu aliyachukua kutoka kwa baba yako nitayarudisha; nawe utajipa barabara katika Damasko kama vile baba yangu alivyojipa katika Samaria.”
“Nami nitakuacha uende zako kwa agano.”+
Kwa hiyo akafanya agano naye na kumwacha aende zake.
35 Na mtu fulani wa wana wa manabii+ akamwambia rafiki yake kwa neno+ la Yehova: “Tafadhali, nipige.” Lakini yule mtu akakataa kumpiga. 36 Kwa hiyo akamwambia: “Kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Yehova, tazama, unaondoka kwangu, na hakika simba atakupiga na kukuua.” Kisha akaondoka kando yake, na simba+ akamkuta, akampiga na kumuua.+
37 Naye akamkuta mtu mwingine tena na kusema: “Tafadhali, nipige.” Basi yule mtu akampiga, akampiga na kumtia majeraha.
38 Ndipo yule nabii akaenda, akasimama tuli akimngojea mfalme kando ya barabara, naye akakaa akiwa amejibadilisha sura+ kwa kujifunga kitambaa juu ya macho yake. 39 Na ikawa kwamba mfalme alipokuwa anapita, akamwita mfalme na kusema:+ “Mtumishi wako alienda mahali palipo na pigano kali sana; na tazama! mtu fulani alikuwa akitoka katika uwanja wa mapigano, kisha akaniletea mtu na kusema, ‘Mlinde mtu huyu. Akitoweka kwa vyovyote, nafsi+ yako itachukua mahali pa nafsi+ yake, kama sivyo utapima talanta moja ya fedha.’+ 40 Na ikawa kwamba mtumishi wako alipokuwa akitenda mambo hapa na pale, tazama, yule mtu alitoweka.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwambia: “Hivyo ndivyo ilivyo hukumu yako mwenyewe. Wewe mwenyewe umeamua.”+ 41 Ndipo akavua haraka kile kitambaa kutoka juu ya macho yake, na mfalme wa Israeli akamtambua, kwamba alikuwa ni mmoja wa manabii.+ 42 Sasa akamwambia: “Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu umemwachilia kutoka mkononi mwako mtu niliyetengewa kwa ajili ya maangamizi,+ lazima nafsi+ yako ichukue mahali pa nafsi yake, na watu wako mahali pa watu wake.’”+ 43 Hivyo mfalme wa Israeli akaenda zake nyumbani kwake, akiwa mwenye kinyongo na mwenye huzuni,+ akafika Samaria.+
21 Na ikawa kwamba baada ya mambo hayo palikuwa na shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli, lililokuwa kule Yezreeli,+ kando ya jumba la mfalme Ahabu, mfalme wa Samaria. 2 Kwa hiyo Ahabu akamwambia Nabothi: “Nipe+ shamba lako la mizabibu,+ ili liwe bustani+ yangu ya mboga,+ kwa maana liko karibu na nyumba yangu; nami nitakupa mahali pake shamba la mizabibu lililo bora kuliko hilo. Au ikiwa vema machoni pako,+ nitakupa pesa kama bei yake.” 3 Lakini Nabothi akamwambia Ahabu: “Ni jambo lisilowaziwa+ kwangu, kwa maoni ya Yehova,+ kwamba mimi nikupe fungu la urithi la mababu zangu.”+ 4 Hivyo Ahabu akaenda nyumbani kwake, akiwa mwenye kinyongo na mwenye huzuni kwa sababu ya lile neno ambalo Nabothi Myezreeli alikuwa amemwambia, aliposema: “Sitakupa fungu la urithi la mababu zangu.” Kisha akalala kitandani pake, akakaa akiwa amegeuza uso wake,+ naye hakula mkate.
5 Mwishowe Yezebeli+ mke wake akaingia kwake na kusema naye: “Kwa nini roho yako imehuzunika,+ nawe huli mkate?” 6 Naye akamwambia: “Ni kwa sababu nilisema na Nabothi Myezreeli, nikamwambia, ‘Nipe shamba lako la mizabibu, nikupe pesa. Au, ukipenda, acha nikupe shamba lingine la mizabibu mahali pake.’ Lakini akasema, ‘Sitakupa shamba langu la mizabibu.’”+ 7 Ndipo Yezebeli mke wake akamwambia: “Je, ni wewe unayetawala ukiwa mfalme juu ya Israeli?+ Amka, ule mkate na moyo wako ufurahi. Mimi mwenyewe nitakupa shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli.”+ 8 Basi mwanamke huyo akaandika barua+ kwa jina la Ahabu, akazitia muhuri+ kwa muhuri wa mfalme, akatuma barua hizo kwa wanaume wazee+ na watu wenye vyeo waliokuwa katika jiji lake, wakikaa na Nabothi. 9 Lakini akaandika katika barua hizo, akisema:+ “Tangazeni watu wafunge, mkamketishe Nabothi mbele ya watu. 10 Nanyi mwaketishe watu wawili,+ watu wasiofaa kitu,+ mbele yake, nao watoe ushahidi juu yake,+ wakisema, ‘Umemlaani Mungu na mfalme!’+ Nanyi mtoeni nje na kumpiga kwa mawe ili afe.”+
11 Basi watu wa jiji lake, wanaume wazee na watu wenye vyeo waliokuwa wakikaa katika jiji lake, wakafanya kama vile Yezebeli alivyokuwa ametuma ujumbe kwao, kama ilivyoandikwa katika zile barua alizowatumia.+ 12 Wakatangaza watu wafunge+ na kumketisha Nabothi mbele ya watu. 13 Ndipo watu wawili, watu wasiofaa kitu, wakaingia, wakaketi mbele yake; kisha wale watu wasiofaa kitu wakaanza kutoa ushahidi juu yake, yaani, Nabothi, mbele ya watu, wakisema: “Nabothi amemlaani Mungu na mfalme!”+ Kisha wakamtoa nje hadi mipakani mwa jiji, wakampiga kwa mawe, akafa.+ 14 Sasa wakatuma ujumbe kwa Yezebeli, wakisema: “Nabothi amepigwa kwa mawe, akafa.”+
15 Na ikawa kwamba mara tu Yezebeli aliposikia kwamba Nabothi amepigwa kwa mawe akafa, mara moja Yezebeli akamwambia Ahabu: “Ondoka, miliki shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli,+ ambalo alikataa kukupa kwa pesa; kwa maana Nabothi hayuko hai tena, bali amekufa.” 16 Na ikawa kwamba mara tu Ahabu aliposikia kwamba Nabothi amekufa, Ahabu akaondoka mara moja ili ashuke kwenda katika lile shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli, alimiliki.+
17 Na neno la Yehova+ likamjia Eliya+ Mtishbi, likisema: 18 “Ondoka, nenda ukutane na Ahabu mfalme wa Israeli, aliye katika Samaria.+ Tazama, yupo katika shamba la mizabibu la Nabothi, mahali ambapo ameenda kulimiliki. 19 Nawe unapaswa kumwambia, ukisema, ‘Yehova amesema hivi: “Je, umeua+ na pia ukamiliki?”’+ Nawe unapaswa kumwambia, ukisema, ‘Yehova amesema hivi: “Mahali+ ambapo mbwa waliiramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba damu yako, ndiyo, damu yako.”’”+
20 Na Ahabu akamwambia Eliya: “Je, umenipata, ewe adui yangu?”+ naye akasema: “Nimekupata. ‘Kwa sababu umejiuza ili kufanya yaliyo mabaya machoni pa Yehova,+ 21 tazama, ninaleta msiba juu yako;+ nami nitafagia kabisa nikikufuata nyuma yako+ na kukatilia mbali kutoka kwa Ahabu yeyote anayekojoa ukutani+ na asiye na uwezo na asiye na thamani katika Israeli. 22 Nami nitaifanya nyumba yako kuwa kama nyumba ya Yeroboamu+ mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha+ mwana wa Ahiya, kwa ajili ya kosa ambalo umekosea, kisha kusababisha Israeli kutenda dhambi.’+ 23 Na pia Yehova amesema hivi kuhusu Yezebeli, ‘Mbwa watamla Yezebeli katika uwanja wa shamba la Yezreeli.+ 24 Mtu yeyote wa Ahabu anayekufa jijini mbwa watamla; na yeyote anayekufa shambani ndege wa mbinguni watamla.+ 25 Hakuna kamwe mtu yeyote ambaye amepata kuwa kama Ahabu,+ aliyejiuza ili kufanya yaliyo mabaya machoni pa Yehova, ambaye Yezebeli+ mke wake alimchochea.+ 26 Naye akatenda kwa njia yenye kuchukiza sana kwa kufuata sanamu za mavi,+ kama yale yote ambayo Waamori walikuwa wametenda, ambao Yehova aliwafukuza kutoka mbele ya wana wa Israeli.’”+
27 Na ikawa kwamba mara tu Ahabu alipoyasikia maneno hayo, akayararua mavazi yake, akavaa nguo za magunia+ mwilini mwake; naye akaanza kufunga, akaendelea kulala katika nguo za magunia, akatembea kwa huzuni.+ 28 Na neno la Yehova likamjia Eliya, Mtishbi, likisema: 29 “Je, umeona jinsi ambavyo Ahabu amejinyenyekeza kwa ajili yangu?+ Kwa sababu amejinyenyekeza kwa ajili yangu, sitauleta ule msiba katika siku zake.+ Katika siku za mwana wake nitauleta msiba ule juu ya nyumba yake.”+
22 Na kwa miaka mitatu wakaendelea kuishi bila vita kati ya Siria na Israeli. 2 Na ikawa kwamba katika mwaka wa tatu, Yehoshafati+ mfalme wa Yuda akashuka, akaenda kwa mfalme wa Israeli. 3 Ndipo mfalme wa Israeli akawaambia watumishi wake: “Je, kweli hamjui kwamba Ramothi-gileadi+ ni jiji letu? Na bado tunasitasita kulichukua kutoka mkononi mwa mfalme wa Siria.” 4 Naye akamwambia Yehoshafati: “Je, utaenda pamoja nami kupigana kule Ramothi-gileadi?”+ Ndipo Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli: “Mimi ni sawa na wewe. Watu wangu ni sawa na watu wako.+ Farasi zangu ni sawa na farasi zako.”
5 Hata hivyo, Yehoshafati akaendelea kumwambia mfalme wa Israeli: “Tafadhali, kwanza kabisa uliza+ neno la Yehova.” 6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawakusanya manabii pamoja,+ karibu watu mia nne, akawaambia: “Je, niende kupiga vita juu ya Ramothi-gileadi, au nijiepushe?” Nao wakaanza kusema: “Panda uende,+ na Yehova atalitia jiji hilo mkononi mwa mfalme.”
7 Lakini Yehoshafati akasema: “Je, hayupo hapa tena nabii wa Yehova? Basi na tuulize kupitia yeye.”+ 8 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Bado kuna mtu mmoja ambaye tunaweza kumuuliza Yehova kupitia yeye;+ lakini hakika mimi ninamchukia,+ kwa maana yeye hatoi unabii wa mambo mema kunihusu mimi, ila mabaya+—Mikaya mwana wa Imla.” Hata hivyo, Yehoshafati akasema: “Mfalme asiseme jambo kama hilo.”+
9 Basi mfalme wa Israeli akamwita ofisa+ fulani wa makao ya mfalme na kusema: “Mlete haraka Mikaya mwana wa Imla.”+ 10 Sasa mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi kila mmoja juu ya kiti chake cha ufalme, wakiwa wamevaa mavazi ya kifalme,+ katika uwanja wa kupuria kwenye mwingilio wa lango la Samaria; na manabii wote walikuwa wakitenda kama manabii mbele yao.+ 11 Ndipo Sedekia mwana wa Kenaana akajitengenezea pembe za chuma na kusema: “Yehova amesema hivi,+ ‘Kwa kutumia hizi utawasukuma Wasiria mpaka uwaangamize.’”+ 12 Na wale manabii wengine wote walikuwa wakitoa unabii kama huo, wakisema: “Panda uende Ramothi-gileadi, upate mafanikio; na Yehova hakika atalitia jiji lile mkononi mwa mfalme.”+
13 Na yule mjumbe aliyeenda kumwita Mikaya akamwambia, akisema: “Tazama, sasa! Maneno ya manabii kwa kauli moja ni mema kwa mfalme. Tafadhali, neno lako na liwe kama neno la mmoja wao, nawe useme mema.”+ 14 Lakini Mikaya akasema: “Kama Yehova anavyoishi,+ lile ambalo Yehova ataniambia, hilo ndilo nitakalosema.”+ 15 Ndipo akaingia kwa mfalme, naye mfalme akamwambia: “Mikaya, je, twende kupiga vita juu ya Ramothi-gileadi, au tujiepushe?” Mara moja akamwambia: “Panda uende na kufanikiwa; na Yehova atalitia mkononi mwa mfalme.”+ 16 Kwa hiyo mfalme akamwambia: “Ninakuapisha mara ngapi kwamba usiniambie jambo lolote ila kweli katika jina la Yehova?”+ 17 Basi akasema: “Hakika ninawaona Israeli wote wametawanyika+ juu ya milima, kama kondoo wasio na mchungaji.+ Na Yehova akasema: ‘Hawa hawana mabwana. Kila mmoja na arudi kwa amani nyumbani kwake.’”+
18 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Je, sikukuambia, ‘Hatatoa unabii wa mambo mema kunihusu, ila tu mabaya’?”+
19 Naye akaendelea kusema: “Basi sikia neno la Yehova:+ Hakika ninamwona Yehova ameketi juu ya kiti chake cha ufalme+ na jeshi lote la mbinguni limesimama kando yake, upande wake wa kuume na upande wake wa kushoto.+ 20 Na Yehova akasema, ‘Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili apande kwenda na kuanguka huko Ramothi-gileadi?’ Na huyu akaanza kusema hivi, na yule akasema vile.+ 21 Mwishowe roho+ fulani akaja na kusimama mbele za Yehova, akasema, ‘Mimi nitamdanganya.’ Ndipo Yehova akamwambia, ‘Kwa njia gani?’+ 22 Naye akasema, ‘Nitaenda, nami nitakuwa roho ya udanganyifu katika kinywa cha manabii+ wake wote.’ Kwa hiyo akasema, ‘Utamdanganya, na tena, utashinda.+ Nenda, ukafanye hivyo.’+ 23 Na sasa tazama, Yehova ametia roho ya udanganyifu katika vinywa vya hawa manabii wako wote;+ lakini Yehova mwenyewe ametangaza msiba juu yako.”+
24 Sasa Sedekia mwana wa Kenaana akakaribia, akampiga Mikaya kwenye shavu+ na kusema: “Ni katika njia gani hasa roho ya Yehova ilinipita mimi ikaenda kusema na wewe?”+ 25 Kwa hiyo Mikaya akasema: “Tazama! Utaona ni njia gani siku ile utakapoingia katika chumba cha ndani kabisa+ ili ujifiche.”+ 26 Ndipo mfalme wa Israeli akasema: “Mchukue Mikaya, umrudishe kwa Amoni mkuu wa jiji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.+ 27 Nawe useme, ‘Mfalme amesema hivi:+ “Mtieni mtu huyu katika kizuizi,+ mkamlishe kwa posho iliyopunguzwa ya mkate+ na maji yaliyopunguzwa mpaka nitakapokuja kwa amani.”’”+ 28 Basi Mikaya akasema: “Ukirudi kwa amani kwa vyovyote, Yehova hakusema nami.”+ Naye akaongezea: “Sikieni, enyi watu wote.”+
29 Na mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakapanda kwenda mpaka Ramothi-gileadi.+ 30 Sasa mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Mimi nitajibadili sura na kuingia vitani,+ lakini wewe vaa mavazi yako.”+ Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadili sura,+ akaingia vitani.+ 31 Naye mfalme wa Siria alikuwa amewaamuru wale wakuu 32+ wa magari yake, akisema: “Msipigane na mdogo wala na mkuu, ila na mfalme wa Israeli peke yake.”+ 32 Na ikawa kwamba mara tu wale wakuu wa magari walipomwona Yehoshafati, wakaambiana: “Hakika yeye ndiye mfalme wa Israeli.”+ Basi wakageuka juu yake kupigana; na Yehoshafati akaanza kulia apewe msaada.+ 33 Na ikawa kwamba mara tu wale wakuu wa magari walipoona kwamba yeye hakuwa mfalme wa Israeli, mara moja wakarudi, wakaacha kumfuata.+
34 Na palikuwa na mtu aliyepinda upinde bila kujua, lakini akampiga mfalme wa Israeli katikati ya viungio na vazi la chuma, naye akamwambia mwendesha-gari+ wake: “Geuza mkono wako, uniondoe katika kambi, kwa sababu nimeumizwa vibaya.” 35 Na pigano likazidi kuwa kali siku hiyo, na ikawa lazima kumweka mfalme akiwa amesimama katika gari akiwaelekea Wasiria, na mwishowe akafa+ jioni; na damu ya lile jeraha ikaendelea kumwagika upande wa ndani wa lile gari la vita.+ 36 Na sauti kuu ikaanza kusikika katika kambi karibu na wakati wa kutua kwa jua, ikisema: “Kila mtu aende katika jiji lake, na kila mtu aende katika nchi yake!”+ 37 Basi mfalme akafa. Alipoletwa Samaria, ndipo wakamzika mfalme katika Samaria.+ 38 Nao wakaanza kuliosha lile gari la vita kando ya kidimbwi cha Samaria, na mbwa wakairamba damu yake+ (na makahaba waliogea hapo), kulingana na neno la Yehova alilokuwa amesema.+
39 Na mambo mengine ya Ahabu na yote aliyofanya na ile nyumba ya pembe za tembo+ aliyoijenga na majiji yote aliyoyajenga, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Israeli? 40 Mwishowe Ahabu akalala pamoja na mababu zake;+ na Ahazia+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
41 Naye Yehoshafati+ mwana wa Asa, alianza kutawala juu ya Yuda akiwa mfalme katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli. 42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka 35 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 25 katika Yerusalemu; na jina la mama yake lilikuwa Azuba binti ya Shilhi. 43 Naye akaendelea kutembea katika njia yote ya Asa baba yake. Hakugeuka kando kutoka katika njia hiyo, kwa kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova.+ Ila tu mahali pa juu hapakuondolewa. Watu walikuwa bado wanatoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu.+ 44 Na Yehoshafati akaendeleza uhusiano wa amani pamoja na mfalme wa Israeli.+ 45 Na mambo mengine ya Yehoshafati na nguvu ambazo alitenda nazo na namna alivyopigana vita, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda? 46 Naye akaondoa katika nchi wale wanaume makahaba+ waliokuwa wamebaki katika siku za Asa baba yake.+
47 Na katika Edomu+ hapakuwa na mfalme yeyote; msaidizi alikuwa mfalme.+
48 Naye Yehoshafati akajenga meli za Tarshishi+ ziende Ofiri kuchukua dhahabu; lakini hazikuenda, kwa sababu meli hizo zilivunjika huko Esion-geberi.+ 49 Wakati huo ndipo Ahazia mwana wa Ahabu alipomwambia Yehoshafati: “Acha watumishi wangu waende na watumishi wako katika hizo meli,” lakini Yehoshafati hakukubali.+
50 Mwishowe Yehoshafati akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi+ babu yake; na Yehoramu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
51 Naye Ahazia+ mwana wa Ahabu, alikuwa mfalme juu ya Israeli kule Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye akaendelea kutawala juu ya Israeli kwa miaka miwili. 52 Naye akaendelea kutenda yaliyokuwa mabaya+ machoni pa Yehova, akaendelea kutembea katika njia ya baba yake+ na katika njia ya mama yake+ na katika njia ya Yeroboamu+ mwana wa Nebati, aliyesababisha Israeli kutenda dhambi.+ 53 Naye akaendelea kumtumikia Baali+ na kumwinamia, naye akaendelea kumtia uchungu+ Yehova Mungu wa Israeli, kulingana na yote ambayo baba yake alikuwa amefanya.
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.