Kitabu cha Pili cha Samweli
au, kulingana na Septuajinti ya Kigiriki, KITABU CHA PILI CHA WAFALME
1 Na ikawa baada ya kifo cha Sauli, na wakati Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwapiga Waamaleki,+ kwamba Daudi akaendelea kukaa siku mbili katika Siklagi.+ 2 Na ikawa kwamba katika siku ya tatu, tazama! mtu+ fulani alikuwa anakuja kutoka katika kambi, kutoka kwa Sauli, mavazi yake yakiwa yameraruliwa+ na mavumbi yakiwa juu ya kichwa chake;+ na ikawa alipomjia Daudi, akaanguka chini+ mara moja na kulala kifudifudi.
3 Naye Daudi akamwambia: “Umetoka wapi?” naye akamjibu: “Nimekimbia kutoka katika kambi ya Israeli.” 4 Na Daudi akaendelea kumwambia: “Mambo yaliendaje? Niambie tafadhali.” Naye akasema: “Watu wamekimbia kutoka vitani na pia watu wengi wameanguka, wakafa,+ na hata Sauli+ na Yonathani+ mwana wake wamekufa pia.” 5 Kisha Daudi akamuuliza yule kijana aliyekuwa akimpasha habari: “Unajuaje hakika kwamba Sauli amekufa, na pia Yonathani mwana wake?”+ 6 Ndipo yule kijana aliyekuwa akimpasha habari akasema: “Nilijikuta katika Mlima Gilboa+ bila kutazamia, na tazama, Sauli alikuwa amejiegemeza kwenye mkuki wake;+ na tazama! waendesha-magari na wapanda-farasi walikuwa wamemfikia.+ 7 Alipogeuka nyuma na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Mimi hapa!’ 8 Naye akaendelea kuniambia, ‘Wewe ni nani?’ nami nikamwambia, ‘Mimi ni Mwamaleki.’+ 9 Kisha akasema, ‘Tafadhali, simama juu yangu, na kwa hakika uniue, kwa maana ganzi imenishika, kwa sababu nafsi+ yangu yote ingali ndani yangu.’ 10 Basi nikasimama juu yake na kwa hakika nikamuua,+ kwa maana nilijua kwamba hangeishi baada ya kuanguka. Kisha nikachukua taji+ lililokuwa juu ya kichwa chake na kikuku kilichokuwa kwenye mkono wake, ili nivilete kwa bwana wangu hapa.”
11 Ndipo Daudi akashika mavazi yake akayararua,+ na pia watu wote waliokuwa pamoja naye wakafanya hivyo. 12 Nao wakaanza kuomboleza na kulia+ na kufunga+ mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na kwa ajili ya Yonathani mwana wake na kwa ajili ya watu wa Yehova na kwa ajili ya nyumba ya Israeli,+ kwa sababu walikuwa wameanguka kwa upanga.
13 Basi Daudi akamwambia yule kijana aliyekuwa akimpasha habari: “Unatoka wapi wewe?” naye akajibu: “Mimi ni mwana wa mkaaji mgeni, Mwamaleki.”+ 14 Kisha Daudi akamwambia: “Kwa nini hukuogopa+ kunyoosha mkono wako umwangamize mtiwa-mafuta+ wa Yehova?” 15 Kwa hiyo Daudi akamwita mmoja wa vijana na kumwambia: “Sogea karibu. Mpige.” Basi akampiga, naye akafa.+ 16 Ndipo Daudi akamwambia: “Hatia yako ya damu na iwe juu ya kichwa chako mwenyewe,+ kwa sababu kinywa chako mwenyewe kimetoa ushuhuda juu yako,+ kusema, ‘Mimi mwenyewe kwa hakika nilimuua mtiwa-mafuta wa Yehova.’”+
17 Na Daudi akaimba wimbo huu wa huzuni+ kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwana wake+ 18 na kusema kwamba wana wa Yuda+ wafundishwe “Upinde.”+ Tazama! Umeandikwa katika kitabu cha Yashari:+
19 “Ee Israeli, uzuri umeuawa katika mahali pako pa juu.+
Lo! Jinsi walivyoanguka wanaume wenye nguvu!
20 Msiseme hayo katika Gathi;+
Msiyatangaze katika barabara za Ashkeloni,+
Binti za Wafilisti wasije wakashangilia,
Binti za watu wasiotahiriwa wasije wakafurahi.+
21 Enyi milima ya Gilboa,+ umande wowote, wala mvua yoyote isinyeshe juu yenu, wala kusiwe na mashamba ya michango mitakatifu;+
Kwa sababu ngao ya wenye uwezo ilichafuliwa hapo,
Ngao ya Sauli, hata kukawa hakuna yoyote iliyotiwa mafuta.+
22 Kutoka kwa damu ya waliouawa, kutoka kwa mafuta ya wenye uwezo,
Upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma,+
Na upanga wa Sauli haukurudi bila mafanikio.+
23 Sauli na Yonathani,+ watu wenye kupendwa na wenye kupendeza wakati wa maisha yao,
Nao hawakutenganishwa katika kifo chao.+
Walikuwa wepesi kuliko tai,+
Walikuwa wenye nguvu kuliko simba.+
24 Enyi binti za Israeli, mlilieni Sauli,
Aliyewavika nguo nyekundu kwa umaridadi,
Aliyeweka mapambo ya dhahabu juu ya mavazi yenu.+
25 Lo! Jinsi wenye nguvu walivyoanguka katikati ya pigano!+
Yonathani ameuawa juu ya mahali pako pa juu!+
26 Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu,
Ulinipendeza sana.+
Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu sana kuliko upendo kutoka kwa wanawake.+
2 Na ikawa baadaye kwamba Daudi akamuuliza Yehova,+ akisema: “Je, nipande kwenda katika moja la majiji ya Yuda?” Ndipo Yehova akamwambia: “Panda uende.” Na Daudi akaendelea kusema: “Nipande kwenda wapi?” Ndipo akasema: “Hebroni.”+ 2 Basi Daudi akaenda huko na wake zake wawili pia, Ahinoamu+ Myezreeli, na Abigaili+ mke wa Nabali Mkarmeli. 3 Na Daudi akawaleta wale watu+ waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na nyumba yake; nao wakaanza kukaa katika majiji ya eneo la Hebroni. 4 Ndipo watu wa Yuda+ wakaja, wakamtia Daudi mafuta+ hapo awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda.+
Nao wakaja kumwambia Daudi, wakisema: “Watu wa Yabesh-gileadi ndio waliomzika Sauli.” 5 Basi Daudi akatuma wajumbe kwa watu wa Yabesh-gileadi+ na kuwaambia: “Mbarikiwe na Yehova,+ kwa kuwa mmeonyesha hizi fadhili zenye upendo+ kwa bwana wenu, kwa Sauli, kwa maana mlimzika.+ 6 Na sasa Yehova na awaonyeshe ninyi fadhili zenye upendo+ na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema huu kwa sababu mmefanya jambo hili.+ 7 Na sasa mikono yenu na ijitie nguvu na muwe wanaume mashujaa,+ kwa sababu Sauli bwana wenu amekufa, na nyumba ya Yuda wamenitia mimi mafuta niwe mfalme+ juu yao.”
8 Lakini Abneri+ mwana wa Neri mkuu wa jeshi lililokuwa la Sauli, alimchukua Ish-boshethi,+ mwana wa Sauli, akamvusha mpaka Mahanaimu,+ 9 akamfanya kuwa mfalme juu ya Gileadi+ na Waashuri na Yezreeli+ na juu ya Efraimu+ na Benyamini+ na juu ya Israeli yote. 10 Ish-boshethi, mwana wa Sauli, alikuwa na umri wa miaka 40 alipokuwa mfalme juu ya Israeli, naye akatawala akiwa mfalme kwa miaka miwili. Ni nyumba ya Yuda+ peke yao ndio waliomfuata Daudi. 11 Na hesabu ya siku ambazo Daudi alikuwa mfalme katika Hebroni juu ya nyumba ya Yuda ikawa miaka saba na miezi sita.+
12 Baada ya muda Abneri mwana wa Neri na watumishi wa Ish-boshethi, mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu+ kwenda Gibeoni.+ 13 Naye Yoabu+ mwana wa Seruya+ na watumishi wa Daudi wakaondoka na baadaye wakakutana pamoja kando ya kidimbwi cha Gibeoni; nao wakaendelea kuketi, hawa upande huu wa kile kidimbwi na wale upande ule wa kile kidimbwi. 14 Mwishowe Abneri akamwambia Yoabu: “Tafadhali, acha vijana wasimame, wapambane mbele yetu.” Naye Yoabu akasema: “Acha wasimame.” 15 Basi wakasimama, wakavuka kwa hesabu yao, kumi na wawili wa Benyamini na Ish-boshethi,+ mwana wa Sauli, na kumi na wawili kutoka kwa watumishi wa Daudi. 16 Ndipo wakaanza kukamatana kwa vichwa, huku upanga wa kila mmoja ukiwa katika ubavu wa mwenzake, nao wakaanguka pamoja. Na mahali hapo pakaitwa Helkath-hasurimu, napo ni katika Gibeoni.+
17 Na mapigano yakawa magumu mno siku hiyo, na mwishowe Abneri+ pamoja na watu wa Israeli wakashindwa mbele ya watumishi wa Daudi. 18 Basi wale wana watatu wa Seruya+ walikuwa hapo, Yoabu+ na Abishai+ na Asaheli;+ na Asaheli alikuwa mwepesi kwa miguu yake, kama mmoja wa swala+ walio porini. 19 Na Asaheli akamfuatilia Abneri, naye hakwenda upande wa kuume wala wa kushoto, aache kumfuatilia Abneri. 20 Baada ya muda Abneri akatazama nyuma na kusema: “Je, ni wewe, Asaheli?” naye akasema: “Ni mimi.” 21 Ndipo Abneri akamwambia: “Geuka upande wako wa kuume au wa kushoto, umkamate mmoja wa vijana awe wako na uchukue kile utakachovua+ kutoka kwake kiwe chako.” Na Asaheli hakutaka kugeuka kando, aache kumfuatilia. 22 Kwa hiyo Abneri akamwambia tena Asaheli: “Geuza mwendo wako, acha kunifuatilia. Kwa nini nikupige ufe na kuanguka chini?+ Hapo, basi, ningewezaje kuinua uso wangu kumwelekea Yoabu ndugu yako?” 23 Lakini akaendelea kukataa kugeuka kando; ndipo Abneri akampiga tumboni+ kwa ncha ya nyuma ya mkuki, hata mkuki ukatokea upande wake wa nyuma; akaanguka hapo, akafa papo hapo. Na ikawa kwamba watu wote waliofika mahali ambapo Asaheli alianguka kisha akafa wakawa wakisimama tuli.+
24 Na Yoabu na Abishai wakamfuatilia Abneri. Na jua lilipokuwa likitua wakafika katika kilima cha Ama, kilicho mbele ya Gia kwenye njia ya nyika ya Gibeoni.+ 25 Ndipo wana wa Benyamini wakakusanyika nyuma ya Abneri, wakawa kundi moja, wakaendelea kusimama juu ya kilima kimoja. 26 Kisha Abneri akamwita Yoabu na kusema: “Je, upanga utakula+ bila kukoma? Je, hujui hakika kwamba uchungu ndio utakaotokea mwishowe?+ Basi, itachukua muda gani kabla hujawaambia watu warudi nyuma, waache kuwafuatilia ndugu zao?”+ 27 Naye Yoabu akasema: “Kama Mungu wa kweli anavyoishi,+ kama usingalisema,+ ni wakati wa asubuhi tu ndipo watu wangaliondolewa, kila mmoja aache kumfuatilia ndugu yake.” 28 Basi Yoabu akapiga baragumu,+ kisha watu wote wakasimama, wakaacha kuwafuatilia Israeli, wala hawakurudi tena kupigana upya.
29 Naye Abneri na watu wake wakapiga mwendo kupitia Araba+ usiku huo wote, wakavuka Yordani,+ wakapiga mwendo kuupitia mtaro mzima, mwishowe wakafika Mahanaimu.+ 30 Naye Yoabu akageuka, akaacha kumfuatilia Abneri, akaanza kuwakusanya watu wote pamoja. Na watumishi wa Daudi walipungukiwa na watu kumi na tisa pamoja na Asaheli. 31 Na watumishi wa Daudi walikuwa wamepiga watu wa Benyamini na wa Abneri—walikuwa watu 360 waliokufa.+ 32 Nao wakamchukua Asaheli,+ wakamzika katika kaburi la baba yake,+ katika Bethlehemu.+ Kisha Yoabu na watu wake wakapiga mwendo usiku kucha, na nuru ikawapambazukia Hebroni.+
3 Na vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi vikawa vya muda mrefu;+ na Daudi akazidi kupata nguvu,+ nayo nyumba ya Sauli ikazidi kupungua.+
2 Wakati huo Daudi akazaa wana+ katika Hebroni,+ na mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Amnoni+ kupitia Ahinoamu+ mwanamke Myezreeli. 3 Na mwana wake wa pili alikuwa Kileabu+ kupitia Abigaili+ mke wa Nabali Mkarmeli, na wa tatu alikuwa Absalomu+ mwana wa Maaka binti ya Talmai+ mfalme wa Geshuri. 4 Na wa nne alikuwa Adoniya+ mwana wa Hagithi,+ na wa tano alikuwa Shefatia+ mwana wa Abitali. 5 Na wa sita alikuwa Ithreamu+ kupitia Egla, mke wa Daudi. Hao ndio ambao Daudi alizaa katika Hebroni.
6 Na ikawa kwamba vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi vilipokuwa vikiendelea, Abneri+ alikuwa akiendelea kuimarisha cheo chake katika nyumba ya Sauli. 7 Basi Sauli alikuwa na suria ambaye jina lake lilikuwa Rispa,+ binti ya Aya.+ Baadaye Ish-boshethi+ akamwambia Abneri: “Kwa nini ulilala na suria+ wa baba yangu?” 8 Ndipo Abneri akakasirika+ sana kwa sababu ya maneno ya Ish-boshethi, akasema: “Je, mimi ni kichwa cha mbwa+ wa Yuda? Leo ninaendelea kuonyesha fadhili zenye upendo kwa nyumba ya baba yako, kwa ndugu zake na rafiki zake wa kibinafsi, nami sikukuacha uanguke mkononi mwa Daudi; na bado leo unanitoza hesabu kwa sababu ya kosa linalohusu mwanamke. 9 Basi Mungu na amfanyie Abneri hivyo, naye azidishe jambo hilo,+ ikiwa, kama vile Yehova alivyomwapia Daudi,+ sivyo nitakavyomtendea, 10 ili kuuhamisha ufalme kutoka katika nyumba ya Sauli na kukiweka kiti cha ufalme cha Daudi juu ya Israeli na juu ya Yuda kuanzia Dani mpaka Beer-sheba.”+ 11 Naye hakuweza kusema hata neno moja zaidi ili kumjibu Abneri, kwa sababu ya kumwogopa.+
12 Papo hapo Abneri akatuma wajumbe kwa Daudi, akisema: “Je, nchi hii ni ya nani?” na kuongezea: “Fanya agano lako pamoja nami, na tazama! mkono wangu utakuwa pamoja nawe ili kuwageuza Israeli wote wawe upande wako.”+ 13 Naye akasema: “Vema! Mimi nitafanya agano pamoja nawe. Ila tu kuna jambo moja ambalo ninaomba kwako, nikisema, ‘Huwezi kuuona uso wangu,+ isipokuwa kwanza umlete Mikali,+ binti ya Sauli, utakapokuja kuuona uso wangu.’” 14 Zaidi ya hayo, Daudi akatuma wajumbe kwa Ish-boshethi,+ mwana wa Sauli, akisema: “Mtoe mke wangu Mikali, niliyemchumbia kwa magovi+ mia moja ya Wafilisti.” 15 Kwa hiyo Ish-boshethi akatuma watu, wakamchukua kutoka kwa mume wake, Paltieli+ mwana wa Laishi. 16 Lakini mume wake akaendelea kutembea pamoja naye, akilia huku akimfuata mpaka Bahurimu.+ Ndipo Abneri akamwambia: “Nenda, rudi!” Hivyo akarudi.
17 Wakati huo Abneri akawa amepashana habari na wanaume wazee wa Israeli, akisema: “Jana na juzi+ pia mlikuwa mkimtafuta Daudi awe mfalme juu yenu. 18 Na sasa chukueni hatua, kwa maana Yehova mwenyewe alimwambia Daudi, ‘Kwa mkono wa Daudi+ mtumishi wangu nitawaokoa watu wangu Israeli kutoka katika mkono wa Wafilisti na kutoka katika mkono wa adui zao wote.’” 19 Kisha Abneri akasema pia masikioni mwa Benyamini,+ halafu pia Abneri akaenda kusema masikioni mwa Daudi kule Hebroni yote yaliyokuwa mema machoni pa Israeli na machoni pa nyumba yote ya Benyamini.
20 Abneri alipokuja kwa Daudi kule Hebroni, na watu 20 pamoja naye, Daudi alimfanyia Abneri karamu+ na pia wale watu waliokuwa pamoja naye. 21 Ndipo Abneri akamwambia Daudi: “Niache niondoke, niende kukusanya pamoja Israeli wote kwa bwana wangu mfalme, ili wafanye agano pamoja nawe, nawe hakika utakuwa mfalme juu ya wote ambao nafsi yako inatamani.”+ Basi Daudi akamwacha Abneri aende zake, naye akaenda zake kwa amani.+
22 Na tazama, watumishi wa Daudi na Yoabu walikuwa wakirudi kutoka kufanya uvamizi, na nyara+ waliyoleta ilikuwa nyingi. Lakini Abneri hakuwa na Daudi katika Hebroni, kwa maana alikuwa amemwacha aende zake, naye alikuwa njiani akienda zake kwa amani. 23 Na Yoabu+ na jeshi lote lililokuwa pamoja naye wakaingia, nao wakampa Yoabu habari, wakisema: “Abneri+ mwana wa Neri+ alikuja kwa mfalme, naye akamwacha aende zake, naye yuko njiani anaenda zake kwa amani.” 24 Kwa hiyo Yoabu akaingia kwa mfalme na kusema: “Umefanya nini?+ Tazama! Abneri amekuja kwako. Kwa nini umemwacha aende zake, akafanikiwa kwenda zake? 25 Unamjua vema Abneri mwana wa Neri, kwamba alikuja kukupumbaza, apate kujua kutoka kwako na kuingia kwako+ na kujua kila jambo unalofanya.”+
26 Basi Yoabu akatoka mbele ya Daudi, akatuma wajumbe wamfuate Abneri, nao wakamrudisha+ akiwa kwenye tangi la maji la Sira; na Daudi hakujua jambo hilo. 27 Abneri aliporudi Hebroni,+ Yoabu akampeleka kando ndani ya lango ili aseme naye kimyakimya.+ Hata hivyo, hapo akampiga tumboni,+ hata akafa kwa sababu ya damu ya Asaheli+ ndugu yake. 28 Wakati Daudi aliposikia habari hizo baadaye, mara moja akasema: “Kwa maoni ya Yehova, mimi na ufalme wangu hatuna hatia ya damu+ ya Abneri mwana wa Neri mpaka wakati usio na kipimo. 29 Na ianguke na kurudi juu ya kichwa+ cha Yoabu na juu ya nyumba yote ya baba yake, wala asikose katika nyumba ya Yoabu+ mwanamume anayetokwa na mtiririko+ au mwenye ukoma+ au mwanamume anayeshika gurudumu linalozunguka la kusokota nyuzi+ au anayeanguka kwa upanga au mwenye uhitaji wa mkate!”+ 30 Na Yoabu na Abishai+ ndugu yake, walimuua Abneri+ kwa sababu alikuwa amemuua Asaheli ndugu yao kule Gibeoni katika mapigano.+
31 Kisha Daudi akamwambia Yoabu na watu wote waliokuwa pamoja naye: “Rarueni mavazi yenu,+ na mvae nguo za magunia,+ mlie mbele ya Abneri.” Hata mfalme Daudi akatembea nyuma ya kile kitanda. 32 Nao wakafanya mazishi ya Abneri katika Hebroni; na mfalme akapaaza sauti yake, akalia kando ya kaburi la Abneri, na watu wote wakalia.+ 33 Na mfalme akamwimbia Abneri na kusema:
“Je, Abneri afe kifo kama cha mtu asiye na akili?+
Na miguu yako haikutiwa katika pingu za shaba.+
Umeanguka kama yule anayeanguka mbele ya wana wa ukosefu wa uadilifu.”+
Ndipo watu wote wakamlilia+ tena.
35 Baadaye watu wote wakaja kumpa Daudi mkate+ wa kufariji siku ileile, lakini Daudi akaapa, akisema: “Mungu na anifanyie hivyo+ na kuzidisha jambo hilo, nikionja mkate au kitu chochote kabla ya jua kutua!”+ 36 Na watu wote wakaona, na jambo hilo likawa jema machoni pao. Kama ilivyo kwa kila jambo ambalo mfalme alifanya, lilikuwa jema machoni pa watu wote.+ 37 Na watu wote na Israeli wote wakajua siku hiyo kwamba kuuawa kwa Abneri mwana wa Neri hakukutokana na mfalme.+ 38 Na mfalme akaendelea kuwaambia watumishi wake: “Je, hamjui kwamba ni mkuu na ni mtu mkubwa ambaye ameanguka katika Israeli leo?+ 39 Nami leo niko dhaifu ingawa nimetiwa mafuta+ niwe mfalme, na watu hawa, wana wa Seruya,+ ni wakali mno kwangu.+ Yehova na amlipe mwenye kufanya mabaya kulingana na ubaya wake mwenyewe.”+
4 Wakati mwana+ wa Sauli aliposikia kwamba Abneri amekufa katika Hebroni,+ ndipo mikono yake ikalegea+ na Waisraeli wote wakavurugika. 2 Na palikuwa na watu wawili, wakuu wa vikundi vya waporaji,+ waliokuwa wa mwana wa Sauli, jina la mmoja lilikuwa Baana na jina la mwingine lilikuwa Rekabu, wana wa Rimoni Mbeerothi, wa wana wa Benyamini; kwa maana Beerothi+ pia lilikuwa likihesabiwa kuwa sehemu ya Benyamini. 3 Na Wabeerothi wakakimbia wakaenda Gitaimu,+ nao wakawa wakaaji wageni hapo mpaka leo hii.
4 Basi Yonathani,+ mwana wa Sauli, alikuwa na mwana mwenye kulemaa miguu.+ Alikuwa na umri wa miaka mitano wakati habari juu ya Sauli na Yonathani ilipofika kutoka Yezreeli;+ na mlezi wake akamchukua, akakimbia, lakini ikawa kwamba huyo mwanamke alipokuwa akikimbia akiwa na wasiwasi ili aponyoke, ndipo mtoto huyo akaanguka na kulemaa. Na jina lake lilikuwa Mefiboshethi.+
5 Na wana wa Rimoni Mbeerothi, Rekabu na Baana, wakaenda na kufika katika nyumba ya Ish-boshethi+ mchana, wakati ambapo kulikuwa na joto jingi, alipokuwa analala usingizi wa mchana. 6 Nao wakaingia katika nyumba kama watu wanaochukua ngano, kisha wakampiga tumboni;+ na Rekabu na Baana+ ndugu yake wakakimbia bila kugunduliwa. 7 Wakati walipoingia katika ile nyumba, alikuwa amelala kitandani mwake katika chumba chake cha kulala cha ndani, ndipo wakampiga, wakamuua,+ kisha wakakikata kichwa+ chake na kukichukua, wakatembea barabarani mpaka Araba usiku kucha. 8 Mwishowe wakamletea Daudi kichwa cha Ish-boshethi,+ akiwa Hebroni, wakamwambia mfalme: “Tazama, kichwa cha Ish-boshethi mwana wa Sauli adui+ yako aliyeitafuta nafsi yako;+ lakini leo hii Yehova amemlipizia kisasi+ bwana wangu mfalme juu ya Sauli na uzao wake.”
9 Hata hivyo, Daudi akawajibu Rekabu na Baana ndugu yake, wana wa Rimoni Mbeerothi, na kuwaambia: “Kama Yehova anavyoishi,+ aliyeikomboa+ nafsi+ yangu kutoka katika kila taabu,+ 10 mtu fulani aliponiletea habari,+ akisema, ‘Tazama, Sauli amekufa,’ naye machoni pake mwenyewe akawa kama mtu anayeleta habari njema, hata hivyo, mimi nilimkamata nikamuua+ katika Siklagi ingawa nilistahili kumpa ada ya mjumbe; 11 si zaidi sana wakati watu waovu+ wamemuua mtu mwadilifu nyumbani mwake mwenyewe katika kitanda chake? Na je, sasa nisiitake damu yake kutoka mikononi mwenu,+ na je, nisiwaondoe ninyi kutoka duniani?”+ 12 Basi Daudi akawaamuru vijana, nao wakawaua,+ wakaikata mikono yao na miguu yao na kuwatundika+ kando ya kidimbwi kilicho katika Hebroni; nao wakakichukua kichwa cha Ish-boshethi, wakakizika katika kaburi la Abneri kule Hebroni.+
5 Baada ya muda makabila yote ya Israeli yakaja kwa Daudi+ katika Hebroni+ na kusema: “Tazama! Sisi ni mfupa wako na nyama yako.+ 2 Jana na juzi vilevile,+ Sauli alipokuwa mfalme juu yetu, ni wewe uliyeongoza Israeli katika kuwatoa na kuwaingiza.+ Na Yehova alikuambia, ‘Wewe utawachunga+ watu wangu Israeli, nawe utakuwa kiongozi+ juu ya Israeli.’” 3 Basi wanaume wote wazee+ wa Israeli wakaja kwa mfalme katika Hebroni, na Mfalme Daudi akafanya agano+ nao katika Hebroni mbele za Yehova; kisha wakamtia mafuta+ Daudi awe mfalme juu ya Israeli.+
4 Daudi alikuwa na umri wa miaka 30 alipoanza kuwa mfalme. Akatawala kwa miaka 40+ akiwa mfalme. 5 Katika Hebroni alitawala akiwa mfalme juu ya Yuda kwa miaka 7 na miezi 6;+ na katika Yerusalemu+ akatawala akiwa mfalme kwa miaka 33 juu ya Israeli yote na Yuda. 6 Basi mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu kupigana na Wayebusi+ wanaokaa katika nchi, nao wakaanza kumwambia Daudi: “Wewe hutaingia humu, lakini bila shaka vipofu na vilema watakufukuza,”+ wao walikuwa wakifikiri: “Daudi hataingia humu.” 7 Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni,+ yaani, Jiji la Daudi.+ 8 Hivyo Daudi akasema siku hiyo: “Yeyote atakayewapiga Wayebusi,+ basi, kwa kutumia mfereji wa chini kwa chini wa maji,+ na akutane na vilema pamoja na vipofu, wenye kuchukiza nafsi ya Daudi!” Ndiyo sababu wao husema: “Kipofu na kilema hawataingia katika nyumba.” 9 Na Daudi akaanza kukaa katika ngome hiyo, nayo ikaitwa Jiji la Daudi; na Daudi akaanza kujenga kuzunguka pande zote kuanzia Kilima+ na kuelekea ndani. 10 Kwa hiyo Daudi akaendelea kuwa mkuu zaidi na zaidi,+ na Yehova Mungu wa majeshi+ alikuwa pamoja naye.+
11 Na Hiramu+ mfalme wa Tiro akatuma wajumbe+ kwa Daudi, na pia mierezi+ na wafanyakazi wa miti na wafanyakazi wa mawe ya kuta, nao wakaanza kumjengea Daudi nyumba.+ 12 Na Daudi akajua kwamba Yehova alikuwa amemfanya imara kuwa mfalme juu ya Israeli+ na kwamba alikuwa ameuinua+ ufalme wake kwa ajili ya watu wake Israeli.+
13 Wakati huo Daudi akaendelea kuchukua masuria+ na wake+ zaidi kutoka katika Yerusalemu baada ya kutoka Hebroni; naye Daudi akaendelea kuzaa wana na mabinti zaidi. 14 Na haya ndiyo majina ya wale ambao alizaa katika Yerusalemu: Shamua+ na Shobabu+ na Nathani+ na Sulemani,+ 15 na Ibhari na Elishua+ na Nefegi+ na Yafia,+ 16 na Elishama+ na Eliada na Elifeleti.+
17 Na Wafilisti wakasikia kwamba walikuwa wamemtia mafuta Daudi awe mfalme juu ya Israeli.+ Ndipo Wafilisti wote wakaja kumtafuta Daudi. Daudi aliposikia habari hizo, akashuka, akatoka na kwenda mahali palipo pagumu kufikiwa.+ 18 Nao Wafilisti wakaingia na kuendelea kutembea huku na huku katika nchi tambarare ya chini ya Refaimu.+ 19 Naye Daudi akaanza kumuuliza+ Yehova, akisema: “Je, nipande kwenda kupigana na Wafilisti? Je, utawatia mkononi mwangu?” Ndipo Yehova akamwambia Daudi: “Panda uende, kwa maana bila shaka nitawatia Wafilisti mikononi mwako.”+ 20 Kwa hiyo Daudi akaja Baal-perasimu,+ na Daudi akawapiga na kuwaua huko. Ndipo akasema: “Yehova amepenya katikati ya adui+ zangu mbele yangu, kama pengo lililofanyizwa na maji.” Ndiyo sababu alipaita mahali hapo jina Baal-perasimu.+ 21 Basi wakaziacha sanamu+ zao huko, kwa hiyo Daudi na watu wake wakazichukua.+
22 Baadaye Wafilisti wakaja tena+ na kutembea huku na huku katika nchi tambarare ya chini ya Refaimu.+ 23 Ndipo Daudi akamuuliza+ Yehova, lakini yeye akasema: “Usipande kwenda. Zunguka uende nyuma yao, nawe uje juu yao mbele ya miti ya mibaka.+ 24 Na iwe kwamba, utakaposikia sauti ya mwendo juu ya miti ya mibaka, ndipo utende bila kusita,+ kwa sababu wakati huo Yehova atakuwa ametoka kwenda mbele yako kuipiga kambi ya Wafilisti.”+ 25 Basi Daudi akafanya hivyo, kama Yehova alivyokuwa amemwamuru,+ naye akawapiga+ Wafilisti kutoka Geba+ mpaka Gezeri.+
6 Na Daudi akawakusanya tena wanaume wote bora wa Israeli,+ 30,000. 2 Kisha Daudi na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaondoka, wakaenda Baale-yuda+ ili kuleta kutoka hapo sanduku+ la Mungu wa kweli, ambalo juu yake jina+ limeitwa, jina la Yehova wa majeshi,+ anayeketi juu ya makerubi.+ 3 Hata hivyo, wakalipandisha sanduku la Mungu wa kweli juu ya gari jipya la kukokotwa,+ ili walichukue kutoka katika nyumba ya Abinadabu,+ iliyokuwa juu ya mlima; na Uza na Ahio,+ wana wa Abinadabu, walikuwa wakiliongoza lile gari jipya.
4 Hivyo wakalichukua kutoka katika nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya mlima—pamoja na sanduku la Mungu wa kweli; na Ahio alikuwa akitembea mbele ya lile Sanduku. 5 Na Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wakisherehekea mbele za Yehova kwa namna zote za vyombo vya mbao za mberoshi na kwa vinubi+ na kwa vinanda+ na kwa matari+ na kwa matasa na kwa matoazi.+ 6 Nao mwishowe wakaja mpaka uwanja wa kupuria wa Nakoni, na sasa Uza+ akanyoosha mkono wake kwenye lile sanduku la Mungu wa kweli, akalishika,+ kwa maana wale ng’ombe karibu waliangushe. 7 Ndipo hasira+ ya Yehova ikamwakia Uza, na Mungu wa kweli akampiga+ hapo kwa sababu ya hilo tendo lisilo la heshima kwa Mungu, naye akafa hapo karibu na lile sanduku la Mungu wa kweli.+ 8 Na Daudi akakasirika kwa sababu Yehova alikuwa amemlipukia Uza, na mahali hapo pakaitwa Peres-uza mpaka leo hii.+ 9 Naye Daudi akamwogopa Yehova+ siku hiyo, akaanza kusema: “Sanduku la Yehova litakujaje kwangu?”+ 10 Na Daudi hakutaka kulileta kwake sanduku la Yehova katika Jiji la Daudi.+ Kwa hiyo Daudi akaagiza lipelekwe kando kwenye nyumba ya Obed-edomu,+ Mgathi.+
11 Nalo sanduku la Yehova likaendelea kukaa katika nyumba ya Obed-edomu Mgathi miezi mitatu; na Yehova akazidi kumbariki+ Obed-edomu na nyumba+ yake yote. 12 Mwishowe Mfalme Daudi akaletewa habari, kusema: “Yehova ameibariki nyumba ya Obed-edomu na vitu vyake vyote kwa sababu ya lile sanduku la Mungu wa kweli.” Kwa hiyo Daudi akaenda, akalitoa lile sanduku la Mungu wa kweli kutoka katika nyumba ya Obed-edomu, akaliweka katika Jiji la Daudi kwa kushangilia.+ 13 Na ikawa kwamba wakati wachukuzi+ wa lile sanduku la Yehova walipokuwa wamepiga hatua sita, akatoa mara moja dhabihu ya ng’ombe na kinono.+
14 Naye Daudi alikuwa anacheza dansi mbele za Yehova kwa nguvu zake zote, na wakati huo wote Daudi alikuwa amejifunga efodi+ ya kitani. 15 Na Daudi na nyumba yote ya Israeli wakawa wanalipandisha sanduku+ la Yehova kwa sauti za shangwe+ na sauti za baragumu.+ 16 Na ikawa kwamba wakati sanduku la Yehova lilipokuja ndani ya Jiji la Daudi, Mikali,+ binti ya Sauli, akaangalia chini kutoka dirishani, akamwona Mfalme Daudi akiruka na kucheza dansi huku na huku mbele za Yehova; naye akaanza kumdharau+ moyoni+ mwake. 17 Kwa hiyo wakaliingiza ndani sanduku la Yehova na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamishia;+ kisha Daudi akatoa dhabihu za kuteketezwa+ na dhabihu za ushirika+ mbele za Yehova. 18 Daudi alipomaliza kutoa zile dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika, akawabariki+ watu katika jina la Yehova+ wa majeshi. 19 Zaidi ya hayo, akawagawia+ watu wote, umati wote wa Israeli, mwanamume na mwanamke vilevile, kila mmoja keki ya mkate ya mviringo na keki ya tende na keki ya zabibu kavu,+ kisha watu wote wakaenda, kila mmoja nyumbani kwake.
20 Basi Daudi akarudi kuwabariki watu wa nyumba yake mwenyewe,+ na Mikali,+ binti ya Sauli, akatoka nje kumpokea Daudi na kusema: “Lo! Jinsi mfalme wa Israeli alivyojitukuza leo+ wakati alipojifunua leo mbele ya macho ya vijakazi wa watumishi wake, kama vile mmoja wa watu wapumbavu anavyojifunua!”+ 21 Lakini Daudi akamwambia Mikali: “Ilikuwa mbele za Yehova, aliyenichagua mimi badala ya baba yako na nyumba yake yote, akanipa amri+ niwe kiongozi juu ya Israeli, watu wa Yehova, nami nitasherehekea mbele za Yehova.+ 22 Nami nitajipuuza hata zaidi kuliko hivi,+ nitajishusha machoni pangu mwenyewe; nami nimeamua kujitukuza pamoja na wale vijakazi uliowataja.”+ 23 Basi, kwa habari ya Mikali,+ binti ya Sauli, hakupata mtoto yeyote mpaka siku ya kifo chake.
7 Na ikawa kwamba, mfalme alipokaa katika nyumba yake mwenyewe+ na Yehova akawa amempa pumziko kutoka kwa adui zake wote kuzunguka pande zote,+ 2 ndipo mfalme alipomwambia Nathani+ nabii: “Tazama, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi,+ lakini sanduku la Mungu wa kweli linakaa katikati ya vitambaa vya mahema.”+ 3 Basi Nathani akamwambia mfalme: “Kila jambo lililo moyoni mwako—nenda,+ lifanye, kwa sababu Yehova yupo pamoja nawe.”
4 Na ikawa kwamba usiku huo neno+ la Yehova likamjia Nathani, likisema: 5 “Nenda, ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Yehova amesema hivi: “Je, utanijengea nyumba, nikae ndani?+ 6 Kwa maana sijakaa katika nyumba tangu siku nilipowaleta wana wa Israeli wapande kutoka Misri mpaka leo hii,+ bali sikuzote nilitembea+ katika hema+ na katika maskani.+ 7 Wakati wote ambao nimetembea katikati ya wana wote wa Israeli,+ je, kuna neno lolote ambalo niliambia moja la makabila ya Israeli,+ nililoamuru kuwachunga watu wangu Israeli, nikisema, ‘Kwa nini hamkunijengea nyumba ya mierezi?’”’ 8 Na sasa utamwambia Daudi mtumishi wangu hivi, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Mimi mwenyewe nilikuchukua kutoka katika viwanja vya malisho ili uache kufuata kundi+ na uwe kiongozi+ juu ya watu wangu Israeli. 9 Nami nitakuwa pamoja nawe popote utakapokwenda,+ nami nitawakatilia mbali adui zako wote kutoka mbele yako;+ nami hakika nitakufanyia jina kuu,+ kama jina la wakuu walio duniani. 10 Nami hakika nitachagua mahali+ kwa ajili ya watu wangu Israeli na kuwapanda,+ nao hakika watakaa mahali walipo, nao hawatasumbuliwa tena; na wana wa ukosefu wa uadilifu hawatawatesa tena kama walivyofanya hapo mwanzoni,+ 11 kuanzia siku nilipoweka waamuzi+ wawasimamie watu wangu Israeli; nami nitakupa pumziko kutoka kwa adui zako wote.+
“‘“Na Yehova amekuambia kwamba Yehova atakujengea nyumba.+ 12 Wakati siku zako zitakapotimia,+ nawe ulale pamoja na mababu zako,+ ndipo nitakapoinua uzao wako baada yako, ambao utatoka ndani ya viuno vyako; nami kwa kweli nitaufanya imara ufalme wake.+ 13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ nami hakika nitakifanya imara kiti cha ufalme wake mpaka wakati usio na kipimo.+ 14 Mimi mwenyewe nitakuwa baba yake,+ na yeye mwenyewe atakuwa mwanangu.+ Atakapofanya makosa, nitamkaripia kwa fimbo+ ya wanadamu na kwa mapigo ya wana wa Adamu. 15 Na fadhili zangu zenye upendo hazitaondoka juu yake kama vile nilivyoziondoa juu ya Sauli,+ ambaye nilimwondoa kwa ajili yako. 16 Na nyumba yako na ufalme wako hakika zitakuwa imara mpaka wakati usio na kipimo mbele yako; nacho kiti chako cha ufalme kitafanywa imara mpaka wakati usio na kipimo.”’”+
17 Basi Nathani akamwambia Daudi kulingana na maneno hayo yote na kulingana na maono hayo yote.+
18 Kwa hiyo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Yehova na kusema: “Mimi ni nani,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova? Na nyumba yangu ni nini hata ukanileta kufikia hapa? 19 Kana kwamba hilo ni jambo dogo machoni pako, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, na bado pia unasema habari za nyumba ya mtumishi wako mpaka wakati mrefu ujao; na hii ndiyo sheria iliyotolewa kwa ajili ya wanadamu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ 20 Na Daudi anaweza kuongeza na kukuambia nini zaidi, kwa kuwa wewe mwenyewe unamjua vema mtumishi wako,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova? 21 Kwa ajili ya neno lako+ na kupatana na moyo wako mwenyewe,+ wewe umefanya mambo haya yote makuu ili umjulishe mtumishi wako.+ 22 Hiyo ndiyo maana wewe kwa kweli ni mkuu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova; kwa kuwa hakuna mwingine kama wewe,+ wala hakuna Mungu ila wewe+ kati ya wote ambao tumewasikia kwa masikio yetu. 23 Na kuna taifa gani moja duniani lililo kama watu wako Israeli,+ ambao Mungu alikwenda kujikombolea mwenyewe wawe kikundi cha watu+ wake na kujipa jina+ na kuwafanyia mambo makubwa na yenye kuogopesha+—kufukuza mataifa na miungu yao kwa ajili ya watu wako, ambao umejikombolea+ mwenyewe kutoka Misri? 24 Nawe ulijifanyia imara watu wako Israeli+ kuwa watu wako mpaka wakati usio na kipimo; na wewe mwenyewe, Ee Yehova, umekuwa Mungu wao.+
25 “Na sasa, Yehova Mungu, lile neno ambalo umesema kumhusu mtumishi wako na kuihusu nyumba yake ulifanye mpaka wakati usio na kipimo na ufanye kama ulivyosema.+ 26 Jina lako mwenyewe na liwe kuu mpaka wakati usio na kipimo,+ kusema, ‘Yehova wa majeshi ni Mungu juu ya Israeli,’+ na acha nyumba ya mtumishi wako Daudi ifanywe imara mbele zako.+ 27 Kwa maana wewe, Yehova wa majeshi Mungu wa Israeli, umemfunulia mtumishi wako katika sikio, ukisema, ‘Nitakujengea nyumba.’+ Ndiyo sababu mtumishi wako amejipa moyo kusali kwako kwa sala hii.+ 28 Na sasa, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, wewe ndiye Mungu wa kweli; na maneno yako yawe kweli,+ kwa kuwa unamwahidi mtumishi wako wema huu.+ 29 Na sasa ujichukulie wajibu, na kuibariki+ nyumba ya mtumishi wako ili iendelee mpaka wakati usio na kipimo mbele zako;+ kwa maana wewe mwenyewe, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, umeahidi, na kutokana na baraka yako, acha nyumba ya mtumishi wako ibarikiwe mpaka wakati usio na kipimo.”+
8 Na ikawa baadaye kwamba Daudi akawapiga Wafilisti+ na kuwatiisha,+ na Daudi akachukua Metheg-ama kutoka mkononi mwa Wafilisti.
2 Naye akawapiga Wamoabu+ pia na kuwapima kwa kamba, akiwalaza chini kwenye udongo, ili apime kamba mbili awaue, na kamba moja kamili ya kuwahifadhi hai;+ na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi+ wa kuleta ushuru.+
3 Na Daudi akampiga Hadadezeri+ mwana wa Rehobu mfalme wa Soba+ alipokuwa akienda zake kurudisha mamlaka yake kwenye mto Efrati.+ 4 Naye Daudi akateka kutoka kwake wapanda-farasi 1,700 na watu 20,000 wanaoenda kwa miguu;+ na Daudi akakata mishipa ya magoti+ ya farasi+ wote wa magari, lakini akawaacha wabaki kati yao farasi 100 wa magari.
5 Wakati Siria ya Damasko+ walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, ndipo Daudi akapiga watu 22,000 kati ya Wasiria.+ 6 Zaidi ya hayo, Daudi akaweka kambi za kijeshi+ katika Siria ya Damasko; na Wasiria wakawa watumishi wa Daudi wa kuleta ushuru.+ Na Yehova akaendelea kumwokoa Daudi popote alipoenda.+ 7 Tena, Daudi akazichukua zile ngao za mviringo+ za dhahabu zilizokuwa kwa watumishi wa Hadadezeri, akazileta Yerusalemu. 8 Na Mfalme Daudi akachukua shaba nyingi mno kutoka Beta na Berothai, majiji ya Hadadezeri.+
9 Basi Toi mfalme wa Hamathi+ akasikia kwamba Daudi amepiga jeshi lote la Hadadezeri.+ 10 Kwa hiyo Toi akamtuma Yoramu mwana wake kwa Mfalme Daudi aulize hali yake+ na kumpongeza kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumpiga (kwa maana Hadadezeri alikuwa amezoea kupigana na Toi); na mkononi mwake alikuwa na vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu na vyombo vya shaba.+ 11 Vyombo hivyo pia Mfalme Daudi akavitakasa kwa Yehova, pamoja na ile fedha na dhahabu ambayo alikuwa ameitakasa kutoka kwa mataifa yote ambayo alikuwa ameyatiisha,+ 12 kutoka Siria na kutoka Moabu+ na kutoka kwa wana wa Amoni na kutoka kwa Wafilisti+ na kutoka kwa Amaleki+ na kutoka kwa nyara za Hadadezeri mwana wa Rehobu mfalme wa Soba.+ 13 Na Daudi akajifanyia jina aliporudi kutoka kuwapiga Waedomu katika Bonde la Chumvi+—watu kumi na nane elfu.+ 14 Naye akaweka kambi za kijeshi katika Edomu.+ Katika Edomu yote akaweka kambi za kijeshi, na Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi;+ na Yehova akaendelea kumwokoa Daudi popote alipoenda.+
15 Na Daudi akaendelea kutawala juu ya Israeli+ yote; na Daudi akaendelea kutoa uamuzi wa hukumu na uadilifu+ kwa ajili ya watu wake wote.+ 16 Na Yoabu+ mwana wa Seruya alikuwa juu ya jeshi; na Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi alikuwa karani. 17 Na Sadoki+ mwana wa Ahitubu na Ahimeleki+ mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Seraya alikuwa mwandishi. 18 Na Benaya+ mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi+ na Wapelethi.+ Nao wana wa Daudi, wakawa makuhani.+
9 Na Daudi akasema: “Je, bado kuna yeyote aliyebaki wa nyumba ya Sauli, ili nimwonyeshe fadhili zenye upendo+ kwa ajili ya Yonathani?”+ 2 Basi nyumba ya Sauli ilikuwa na mtumishi ambaye jina lake lilikuwa Siba.+ Kwa hiyo wakamwita, akaja kwa Daudi, ndipo mfalme akamwambia: “Je, wewe ni Siba?” naye akasema: “Mimi ni mtumishi wako.” 3 Na mfalme akaendelea kusema: “Je, hakuna kabisa mtu wa nyumba ya Sauli, ili nimwonyeshe fadhili zenye upendo za Mungu?”+ Hivyo Siba akamwambia mfalme: “Bado kuna mwana wa Yonathani, mwenye kulemaa miguu.”+ 4 Kisha mfalme akamwambia: “Yuko wapi?” Kwa hiyo Siba akamwambia mfalme: “Tazama! Yuko katika nyumba ya Makiri+ mwana wa Amieli kule Lo-debari.”+
5 Mara moja Mfalme Daudi akatuma ujumbe kumchukua kutoka katika nyumba ya Makiri mwana wa Amieli kule Lo-debari. 6 Wakati Mefiboshethi mwana wa Yonathani mwana wa Sauli alipoingia kwa Daudi, akaanguka mara moja kifudifudi, akasujudu.+ Ndipo Daudi akasema: “Mefiboshethi!” naye akajibu: “Mimi hapa, mtumishi wako.” 7 Na Daudi akaendelea kumwambia: “Usiogope, kwa maana hakika nitakuonyesha fadhili zenye upendo+ kwa ajili ya Yonathani baba yako;+ nami nitakurudishia mashamba+ yote ya Sauli babu yako, nawe utakula mkate mezani pangu sikuzote.”+
8 Basi akasujudu na kusema: “Mtumishi wako ni nani, hata ukageuza uso wako kuelekea mbwa aliyekufa+ kama mimi?” 9 Sasa mfalme akamwita Siba, mtumishi wa Sauli, akamwambia: “Kila kitu ambacho kilikuwa cha Sauli na cha nyumba yake yote,+ nampa mjukuu wa bwana wako. 10 Nawe umlimie udongo, wewe na wana wako na watumishi wako, nawe utayakusanya mavuno, nayo yatakuwa chakula kwa walio wa mjukuu wa bwana wako, nao watakula; lakini Mefiboshethi, mjukuu wa bwana wako, atakula mkate mezani pangu sikuzote.”+
Basi Siba alikuwa na wana 15 na watumishi 20.+ 11 Kwa hiyo Siba akamwambia mfalme: “Mtumishi wako atafanya kulingana na yote ambayo mfalme bwana wangu anamwamuru mtumishi wake; lakini Mefiboshethi+ anakula mezani pangu kama mmoja wa wana wa mfalme.” 12 Mefiboshethi alikuwa na mwana mchanga ambaye jina lake lilikuwa Mika,+ na wote waliokuwa wakikaa katika nyumba ya Siba walikuwa watumishi wa Mefiboshethi. 13 Na Mefiboshethi alikuwa anakaa katika Yerusalemu, kwa maana alikuwa akila sikuzote mezani pa mfalme;+ naye alikuwa amelemaa miguu yote miwili.+
10 Na ikawa kwamba baadaye mfalme wa wana wa Amoni+ akafa, na Hanuni mwana wake akaanza kutawala badala yake.+ 2 Ndipo Daudi akasema: “Nitamwonyesha fadhili zenye upendo Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonionyesha fadhili zenye upendo.”+ Basi Daudi akatuma ujumbe kupitia kwa watumishi+ wake ili kumfariji kwa sababu ya baba yake, na watumishi wa Daudi wakaingia katika nchi ya wana wa Amoni. 3 Hata hivyo, wakuu wa wana wa Amoni wakamwambia Hanuni bwana wao: “Je, Daudi anamheshimu baba yako machoni pako kwa kutuma kwako wafariji? Je, Daudi hakuwatuma watumishi wake kwako ili kulichunguza jiji na kulipeleleza+ na kulipindua?”+ 4 Kwa hiyo Hanuni akawachukua wale watumishi wa Daudi, akanyoa nusu ya ndevu zao,+ akakata nusu ya mavazi yao mpaka kwenye matako yao, akawaacha waende zao.+ 5 Baadaye watu wakamletea Daudi habari hiyo, naye akatuma watu mara moja kwenda kuwapokea, kwa sababu watu hao walikuwa wamefedheheshwa sana; na mfalme akaendelea kusema: “Kaeni katika Yeriko+ mpaka ndevu zenu ziote kabisa. Ndipo mrudi.”
6 Baada ya muda wana wa Amoni wakaona kuwa wamenuka+ machoni pa Daudi, na wana wa Amoni wakatuma ujumbe na kukodisha Wasiria wa Beth-rehobu+ na Wasiria wa Soba,+ watu 20,000 wanaoenda kwa miguu, na mfalme wa Maaka,+ watu 1,000, na Ishtobu, watu 12,000. 7 Wakati Daudi aliposikia habari hizo, akatuma Yoabu na jeshi lote na wanaume wenye nguvu.+ 8 Nao wana wa Amoni wakaanza kutoka, wajipange katika vikosi vya vita kwenye mwingilio wa lango, pia Wasiria wa Soba na wa Rehobu,+ na Ishtobu na Maaka wakiwa peke yao uwanjani.+
9 Yoabu alipoona mashambulio yamekuja juu yake kutoka upande wa mbele na kutoka upande wa nyuma, mara moja akachagua baadhi ya wanaume bora+ katika Israeli na kuwapanga ili wakutane na Wasiria. 10 Na wale watu wengine waliobaki akawaweka mkononi mwa Abishai+ ndugu yake, ili awapange wakutane na wana wa Amoni.+ 11 Naye akasema: “Ikiwa Wasiria watakuwa na nguvu mno kuliko mimi, basi wewe utaniokoa; lakini ikiwa wana wa Amoni watakuwa na nguvu mno kuliko wewe, mimi pia nitakuja kukuokoa.+ 12 Uwe na nguvu, ili tujionyeshe kuwa hodari+ kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya majiji ya Mungu wetu;+ naye Yehova atafanya yaliyo mema machoni pake mwenyewe.”+
13 Ndipo Yoabu na watu waliokuwa pamoja naye wakasonga kwenda kupigana na Wasiria, nao wakakimbia kutoka mbele yake.+ 14 Basi wana wa Amoni wakaona kwamba Wasiria wamekimbia, nao wakakimbia kutoka mbele ya Abishai, kisha wakaingia ndani ya jiji.+ Halafu Yoabu akarudi kutoka kwa wana wa Amoni, akaja Yerusalemu.+
15 Wasiria walipoona kwamba wameshindwa mbele ya Israeli, wakajikusanya pamoja. 16 Basi Hadadezeri+ akatuma watu na kuleta Wasiria waliokuwa katika eneo la ule Mto;+ kisha wakaja mpaka Helamu, naye Shobaki+ mkuu wa jeshi la Hadadezeri akiwa mbele yao.
17 Daudi alipoletewa habari hiyo, akakusanya mara moja Israeli wote na kuvuka Yordani, akaja mpaka Helamu. Sasa Wasiria wakajipanga ili kukutana na Daudi, wakaanza kupigana naye.+ 18 Na Wasiria wakakimbia+ kutoka mbele ya Israeli; na Daudi akaua kati ya Wasiria waendesha-magari+ 700 na wapanda-farasi 40,000, naye akampiga Shobaki mkuu wa jeshi, hata akafa huko.+ 19 Wakati wafalme+ wote, watumishi wa Hadadezeri, walipoona kwamba wameshindwa mbele ya Israeli,+ wakafanya amani mara moja na Israeli, wakaanza kuwatumikia;+ na Wasiria waliogopa kujaribu tena kuwaokoa wana wa Amoni.+
11 Na ikawa kwamba mwanzoni mwa mwaka,+ wakati ambapo wafalme hufanya mashambulizi,+ Daudi akamtuma Yoabu na watumishi wake pamoja naye na Israeli wote, ili wawaangamize wana wa Amoni+ na kuzingira Raba,+ Daudi alipokuwa anakaa Yerusalemu.
2 Na ikawa wakati wa jioni kwamba Daudi akaamka kutoka kitandani mwake, akatembea huku na huku juu ya dari+ ya nyumba ya mfalme; na kutoka juu ya dari akamwona+ mwanamke akioga, na mwanamke huyo alikuwa mwenye sura nzuri sana.+ 3 Ndipo Daudi akatuma watu na kuuliza habari za mwanamke+ huyo, na mtu fulani akasema: “Je, huyu si Bath-sheba,+ binti ya Eliamu,+ mke wa Uria+ Mhiti?”+ 4 Kisha Daudi akatuma wajumbe ili yeye amchukue.+ Basi mwanamke huyo akaja, akaingia kwake,+ akalala naye,+ wakati alipokuwa akijitakasa kutoka katika uchafu wake.+ Baadaye mwanamke huyo akarudi nyumbani kwake.
5 Na mwanamke huyo akapata mimba. Basi akatuma ujumbe na kumwambia Daudi: “Nina mimba.” 6 Kwa hiyo Daudi akatuma ujumbe kwa Yoabu, akisema: “Mtume kwangu Uria Mhiti.” Basi Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi. 7 Uria alipokuja kwake, Daudi akaanza kuuliza hali ya Yoabu na hali ya watu na hali ya vita. 8 Mwishowe Daudi akamwambia Uria: “Shuka, nenda nyumbani kwako, uoshe miguu yako.”+ Basi Uria akatoka katika nyumba ya mfalme, na zawadi ya fadhili ya mfalme ikaletwa nyuma yake. 9 Hata hivyo, Uria akalala mlangoni pa nyumba ya mfalme pamoja na watumishi wengine wote wa bwana wake, naye hakushuka kwenda nyumbani kwake mwenyewe. 10 Kwa hiyo wakamwambia Daudi: “Uria hakushuka kwenda nyumbani kwake.” Ndipo Daudi akamwambia Uria: “Umefika kutoka safarini, sivyo? Kwa nini hukushuka kwenda nyumbani kwako?” 11 Ndipo Uria akamwambia Daudi: “Lile Sanduku+ na Israeli na Yuda wanakaa katika vibanda, na Yoabu bwana wangu na watumishi wa bwana wangu+ wanapiga kambi juu ya uso wa pori, nami—niende nyumbani kwangu kula na kunywa na kulala na mke wangu?+ Kama unavyoishi na kama nafsi yako inavyoishi,+ sitafanya jambo hili!”
12 Ndipo Daudi akamwambia Uria: “Kaa hapa leo pia, nami kesho nitakuacha uende.” Kwa hiyo Uria akaendelea kukaa Yerusalemu siku hiyo na pia siku iliyofuata. 13 Zaidi ya hayo, Daudi akamwita ili ale chakula na kunywa mbele yake. Basi akamfanya alewe.+ Hata hivyo, akatoka nje jioni na kulala kitandani mwake pamoja na watumishi wa bwana wake, wala hakushuka kwenda nyumbani kwake. 14 Na ikawa asubuhi kwamba Daudi akamwandikia Yoabu barua,+ akaituma kwa mkono wa Uria. 15 Kwa hiyo akaandika katika barua hiyo, akisema:+ “Mwekeni Uria mbele ya mashambulio makali zaidi ya kivita,+ nanyi mtoke nyuma yake, apigwe, afe.”+
16 Na ikawa, Yoabu alipokuwa akililinda jiji, akamweka Uria mahali ambapo alijua kwamba kuna wanaume mashujaa.+ 17 Wanaume wa jiji walipotoka nje na kupigana na Yoabu, ndipo baadhi ya watu, watumishi wa Daudi, wakaanguka na pia Uria Mhiti akafa.+ 18 Sasa Yoabu akatuma habari kwa Daudi kuhusu habari zote za vita. 19 Naye akamwamuru mjumbe, akisema: “Mara utakapomaliza kumwambia mfalme habari zote za vita, 20 basi na itukie kwamba ghadhabu ya mfalme ikiwaka naye akuambie, ‘Kwa nini mlienda karibu sana na jiji kupigana? Je, hamkujua kwamba watapiga mishale kutoka juu ya ukuta? 21 Ni nani aliyempiga Abimeleki+ mwana wa Yerubeshethi?+ Je, hakuwa mwanamke aliyemtupia jiwe la juu la kusagia+ kutoka juu ya ukuta, hivi kwamba akafa kule Thebesi?+ Kwa nini mlienda karibu sana na ukuta?’ ndipo nawe useme, ‘Mtumishi wako Uria Mhiti alikufa pia.’”+
22 Basi yule mjumbe akaenda, akaja na kumwambia Daudi mambo yote ambayo Yoabu alikuwa amemtuma. 23 Na yule mjumbe akaendelea kumwambia Daudi: “Watu wale walikuwa na nguvu kuliko sisi, nao wakatoka kuja juu yetu shambani; lakini tukaendelea kuwakaza mpaka kwenye mwingilio wa lango. 24 Na wapiga-mishale wakaendelea kuwapiga watumishi wako kutoka juu ya ukuta,+ hivi kwamba baadhi ya watumishi wa mfalme wakafa; na mtumishi wako Uria Mhiti akafa pia.”+ 25 Ndipo Daudi akamwambia yule mjumbe: “Utamwambia Yoabu, ‘Usiache jambo hili liwe baya machoni pako, kwa maana upanga humla+ huyu na pia yule. Zidisha pigano lako juu ya jiji hilo, uliangushe.’+ Nawe umtie moyo.”
26 Na mke wa Uria akasikia kwamba Uria mume wake amekufa, naye akaanza kumlilia+ mume wake.+ 27 Kipindi cha kuomboleza+ kilipokuwa kimepita, mara moja Daudi akatuma watu na kumchukua yule mwanamke, akamleta katika nyumba yake, naye akawa mke wake.+ Baada ya muda akamzalia mwana, lakini lile jambo ambalo Daudi alikuwa amefanya likawa baya+ machoni pa Yehova.+
12 Na Yehova akamtuma Nathani+ kwa Daudi. Basi akaja, akaingia kwake+ na kumwambia: “Palikuwa na wanaume wawili waliokuwa katika jiji moja, mmoja alikuwa tajiri na yule mwingine alikuwa maskini. 2 Yule mwanamume tajiri alikuwa na kondoo na ng’ombe wengi sana;+ 3 lakini yule mwanamume maskini hakuwa na chochote isipokuwa mwana-kondoo jike mmoja, aliye mdogo, ambaye alikuwa amenunua.+ Naye alikuwa akimhifadhi hai, na huyo kondoo alikuwa akikua pamoja naye na wanawe, wote pamoja. Kondoo huyo alikuwa akila tonge lake, na kunywa kutoka katika kikombe chake, naye alikuwa akilala kifuani pake, na kondoo huyo akawa kama binti kwake. 4 Baada ya muda, mgeni akaja kwa yule mwanamume tajiri, lakini hakuchukua kutoka kati ya kondoo zake na ng’ombe zake ili kumwandalia yule msafiri aliyekuja kwake. Kwa hiyo akachukua yule mwana-kondoo jike wa yule mwanamume maskini, akamwandalia yule mtu aliyekuja kwake.”+
5 Ndipo hasira ya Daudi ikamwakia sana yule mwanamume,+ naye akamwambia Nathani: “Kama Yehova anavyoishi,+ mtu huyo aliyefanya hivyo anastahili kufa!+ 6 Na kuhusu yule mwana-kondoo jike, atamlipa+ mara nne,+ kwa sababu yeye amefanya jambo hili na kwa sababu hakuwa na huruma.”+
7 Ndipo Nathani akamwambia Daudi: “Wewe mwenyewe ndiye yule mwanamume! Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Mimi nilikutia mafuta+ uwe mfalme juu ya Israeli, nami nilikukomboa+ kutoka mkononi mwa Sauli. 8 Nami nilikuwa tayari kukupa nyumba ya bwana wako+ na wake za bwana wako+ kifuani pako, na kukupa nyumba ya Israeli na ya Yuda.+ Na kama hayo hayakutosha, nilikuwa tayari kukuongezea vitu kama hivyo na pia vitu vingine.+ 9 Kwa nini umelidharau neno la Yehova kwa kufanya yaliyo mabaya+ machoni pake? Uria Mhiti umempiga kwa upanga,+ nawe ukamchukua mke wake awe mke wako,+ naye ukamuua kwa upanga wa wana wa Amoni. 10 Na sasa upanga+ hautaondoka nyumbani mwako mpaka wakati usio na kipimo,+ kwa sababu ulinidharau mimi, ukamchukua mke wa Uria Mhiti, awe mke wako.’ 11 Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta msiba juu yako kutoka katika nyumba yako mwenyewe;+ nami nitawachukua wake zako chini ya macho yako mwenyewe na kumpa mwanamume mwenzako,+ naye atalala na wake zako chini ya macho ya jua hili.+ 12 Ingawa wewe ulitenda katika siri,+ kwa upande wangu mimi, nitafanya jambo hili mbele ya Israeli+ wote na mbele ya jua.’”+
13 Basi Daudi akamwambia+ Nathani: “Nimemtendea Yehova dhambi.”+ Kwa hiyo Nathani akamwambia Daudi: “Yehova naye ameacha dhambi yako ipite.+ Hutakufa.+ 14 Ingawa hivyo, kwa kuwa bila shaka hukumheshimu Yehova+ kwa jambo hili, pia yule mwana, uliyemzaa, atakufa hakika.”+
15 Kisha Nathani akaenda zake nyumbani kwake.
Na Yehova akampiga+ yule mtoto ambaye mke wa Uria alikuwa amemzalia Daudi, akawa mgonjwa. 16 Na Daudi akaanza kumtafuta Mungu wa kweli kwa ajili ya yule mvulana, Daudi akafunga kabisa,+ akaingia ndani, akakesha usiku na kulala chini kwenye udongo.+ 17 Basi wanaume wazee wa nyumba yake wakasimama juu yake ili wamwinue kutoka chini, lakini yeye hakukubali, wala hakula mkate+ pamoja nao. 18 Na ikawa katika siku ya saba yule mtoto akafa. Nao watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia kwamba mtoto amekufa; kwa maana walisema: “Tazama! Mtoto alipokuwa hai hatukusema naye, wala yeye hakuisikiliza sauti yetu; basi tunawezaje kumwambia, ‘Mtoto amekufa’? Ndipo hakika atafanya jambo baya.”
19 Daudi alipoona kwamba watumishi wake wananong’onezana, Daudi akaanza kutambua kwamba yule mtoto amekufa. Kwa hiyo Daudi akawaambia watumishi wake: “Je, mtoto amekufa?” Wakasema: “Amekufa.” 20 Ndipo Daudi akasimama kutoka chini, akaoga, akajipaka+ mafuta, akabadili nguo zake za kujitanda, naye akaja nyumbani+ kwa Yehova, akasujudu;+ kisha akaja nyumbani mwake na kutoa ombi, nao wakaweka mara moja mkate mbele yake, akaanza kula. 21 Basi watumishi wake wakamwambia: “Ni nini maana ya jambo hili ambalo umefanya? Ulifunga na ulikuwa ukimlilia mtoto alipokuwa hai; na mara tu mtoto alipokufa ukasimama, ukaanza kula mkate.” 22 Naye akasema: “Nilifunga,+ nikawa nikilia+ mtoto alipokuwa bado hai, kwa sababu nilisema, ‘Ni nani anayejua kama Yehova huenda akanipa kibali, na hakika mtoto aishi?’+ 23 Sasa kwa kuwa amekufa, kwa nini nifunge? Je, ninaweza kumrudisha tena?+ Mimi nitakwenda kwake,+ lakini yeye hatarudi kwangu.”+
24 Na Daudi akaanza kumfariji Bath-sheba mke wake.+ Na zaidi ya hayo, akaingia kwake, akalala naye. Baada ya muda akazaa mwana,+ naye akaitwa jina lake Sulemani.+ Na Yehova akampenda mwana huyo.+ 25 Basi akamtuma Nathani+ na kumwita jina lake Yedidia, kwa ajili ya Yehova.
26 Na Yoabu+ akaendelea kupigana na Raba+ jiji la wana wa Amoni, akateka jiji la ufalme ule. 27 Basi Yoabu akatuma wajumbe kwa Daudi na kusema: “Nimepigana na Raba.+ Pia nimeliteka jiji la maji. 28 Na sasa kusanya watu waliobaki, upige kambi juu ya jiji hilo, uliteke; ili isiwe ni mimi mwenye kuliteka, na jiji hilo liitwe kwa jina langu.”
29 Basi Daudi akawakusanya watu wote, akaenda Raba, akapigana nao na kuliteka. 30 Naye akachukua taji la Malkamu kutoka juu ya kichwa chake,+ ambalo uzito wake ulikuwa talanta moja ya dhahabu, pamoja na mawe ya thamani; nalo likaja kuwa juu ya kichwa cha Daudi. Na nyara+ za jiji lile ambazo alileta zilikuwa nyingi sana. 31 Na watu waliokuwa ndani yake, akawatoa nje ili awatie kwenye kazi ya kukata mawe kwa misumeno na ya vifaa vya chuma vyenye ncha kali+ na ya mashoka ya chuma, naye akawafanya watumike kufyatua matofali. Na hivyo ndivyo alivyoyafanya majiji yote ya wana wa Amoni. Mwishowe Daudi na watu wote wakarudi Yerusalemu.
13 Na ikawa baada ya mambo hayo kwamba Absalomu+ mwana wa Daudi alikuwa na dada mwenye sura nzuri ambaye jina lake lilikuwa Tamari,+ na Amnoni+ mwana wa Daudi akampenda.+ 2 Jambo hilo likamhuzunisha sana Amnoni hivi kwamba akawa mgonjwa+ kwa sababu ya Tamari dada yake, kwa sababu alikuwa bikira, na ilikuwa vigumu machoni+ pa Amnoni kumfanya jambo lolote.+ 3 Basi Amnoni alikuwa na rafiki ambaye jina lake lilikuwa Yehonadabu,+ mwana wa Shimea,+ ndugu ya Daudi; na Yehonadabu alikuwa mwanamume mwenye hekima sana. 4 Kwa hiyo akamwambia: “Kwa nini wewe, mwana wa mfalme, una huzuni hivi, asubuhi baada ya asubuhi? Je, hutaki kuniambia?”+ Ndipo Amnoni akamwambia: “Ninampenda Tamari dada+ ya Absalomu ndugu yangu.”+ 5 Hivyo Yehonadabu akamwambia: “Lala kitandani mwako, ujifanye mgonjwa.+ Na baba yako atakuja kukuona, nawe umwambie, ‘Tafadhali, acha Tamari dada yangu aingie ndani, anipe mkate kama mgonjwa, naye atayarishe mkate wa kufariji chini ya macho yangu ili niuone, nami nile kutoka mkononi mwake.’”+
6 Basi Amnoni akalala, akajifanya mgonjwa,+ na kwa hiyo mfalme akaingia ndani kumwona. Ndipo Amnoni akamwambia mfalme: “Tafadhali, acha Tamari dada yangu aingie ndani, aniokee keki mbili zenye umbo la moyo chini ya macho yangu, ili nile mkate kama mgonjwa kutoka mkononi mwake.” 7 Kwa hiyo Daudi akatuma ujumbe kwa Tamari nyumbani, akisema: “Tafadhali, nenda kwa nyumba ya Amnoni ndugu yako, umtayarishie mkate wa kufariji.” 8 Basi Tamari akaenda nyumbani kwa Amnoni+ ndugu yake alipokuwa amelala. Kisha akachukua unga wa kukandwa, akaukanda, akatayarisha hizo keki chini ya macho yake, akaoka keki zenye umbo la moyo. 9 Mwishowe akachukua kikaango kikubwa, akapakua mbele yake, lakini Amnoni akakataa kula na kusema: “Ondoeni watu wote kwangu!”+ Ndipo kila mtu akaondoka kwake.
10 Kisha Amnoni akamwambia Tamari: “Leta mkate wa kufariji katika chumba cha ndani, ili niule kama mgonjwa kutoka mkononi mwako.” Basi Tamari akachukua zile keki zenye umbo la moyo ambazo alikuwa ametayarisha, akazileta ndani kwa Amnoni ndugu yake katika chumba cha ndani. 11 Wakati alipomkaribia ili ale, yeye akamkamata+ mara moja na kumwambia: “Njoo, lala nami,+ dada yangu.”+ 12 Hata hivyo, yeye akamwambia: “Hapana, ndugu yangu! Usinifedheheshe;+ kwa maana si kawaida kufanya hivi katika Israeli.+ Usifanye upumbavu huu wenye kufedhehesha.+ 13 Na mimi, je, nitapeleka wapi shutuma yangu? Na wewe utakuwa kama mmoja wa wanaume wasio na akili katika Israeli. Na sasa, tafadhali, sema na mfalme; kwa maana hatakuzuilia mimi.” 14 Naye hakukubali kuisikiliza sauti yake, bali akatumia nguvu kubwa kuliko zake, akamfedhehesha+ na kulala naye.+ 15 Na Amnoni akaanza kumchukia kwa chuki kubwa sana, kwa sababu chuki aliyomchukia ilikuwa kubwa kuliko upendo aliompenda, hata Amnoni akamwambia: “Ondoka, nenda zako!” 16 Naye akamwambia: “Hapana, ndugu yangu; kwa maana ubaya huu wa kunifukuza ni mkubwa kuliko ule ubaya ambao umenitendea!” Lakini hakukubali kumsikiliza.
17 Kwa hiyo akamwita mtumishi wake aliyemhudumia na kusema: “Tafadhali, mtoe huyu mtu kwangu, aende nje, ukaufunge mlango nyuma yake.” 18 (Basi alikuwa amevaa kanzu yenye mistari-mistari;+ kwa maana hivyo ndivyo binti za mfalme, mabikira, walivyokuwa wakivaa pamoja na makoti yasiyo na mikono.) Basi yule mtu wake wa kumhudumia akamtoa nje kabisa, akaufunga mlango nyuma yake. 19 Ndipo Tamari akatia majivu+ juu ya kichwa chake, akairarua ile kanzu yenye mistari-mistari aliyokuwa amevaa; naye akaweka mikono yake juu ya kichwa chake,+ akatembea akienda zake, akitembea huku akilia.
20 Kwa hiyo Absalomu+ ndugu yake akamwambia: “Je, Amnoni+ ndugu yako ndiye aliyekuwa nawe? Na sasa, dada yangu, nyamaza. Yeye ni ndugu yako.+ Usiweke moyo wako juu ya jambo hili.” Na Tamari akaanza kuishi katika nyumba ya Absalomu ndugu yake, huku akitengwa na ushirika wa wengine. 21 Na Mfalme Daudi akasikia habari ya mambo hayo yote,+ naye akakasirika sana.+ 22 Na Absalomu hakumwambia Amnoni jambo baya wala jema; kwa kuwa Absalomu alimchukia+ Amnoni kwa sababu alikuwa amemfedhehesha Tamari dada yake.
23 Na ikawa, baada ya miaka miwili kamili, Absalomu akawa na watu wenye kukata manyoya ya kondoo+ kule Baal-hasori, karibu na Efraimu;+ naye Absalomu akawaalika wana wote wa mfalme.+ 24 Basi Absalomu akaingia kwa mfalme na kusema: “Tazama, sasa, mtumishi wako ana watu wenye kukata manyoya ya kondoo! Tafadhali, acha mfalme na watumishi wake pia, aende pamoja na mtumishi wako.” 25 Lakini mfalme akamwambia Absalomu: “Hapana, mwanangu! Tafadhali usiache sisi sote twende, ili tusiwe mzigo kwako.” Ingawa alizidi kumhimiza,+ hakukubali kwenda, bali akambariki.+ 26 Mwishowe Absalomu akasema: “Kama si wewe, tafadhali acha Amnoni ndugu yangu aende pamoja nasi.”+ Ndipo mfalme akamwambia: “Kwa nini aende pamoja nawe?” 27 Na Absalomu akaanza kumhimiza,+ hata akamruhusu Amnoni na wana wote wa mfalme waende pamoja naye.
28 Kisha Absalomu akawaamuru watumishi wake, akisema: “Tafadhali, angalieni kwamba mara tu moyo wa Amnoni utakapochangamka kwa divai,+ nami niwaambie, ‘Mpigeni Amnoni!’ Ndipo ninyi mtakapomuua. Msiogope.+ Je, mimi sikuwaamuru? Iweni na nguvu, na muwe wanaume mashujaa.” 29 Na watumishi wa Absalomu wakamtendea Amnoni kama vile Absalomu alivyokuwa ameamuru;+ na wana wengine wote wa mfalme wakaondoka, wakapanda kila mmoja nyumbu wake, wakakimbia. 30 Na ikawa kwamba, walipokuwa njiani, Daudi akaletewa habari, kusema: “Absalomu amewapiga na kuwaua wana wote wa mfalme, na hapana hata mmoja wao amebaki.” 31 Ndipo mfalme akasimama, akazirarua nguo zake,+ akalala chini,+ na watumishi wake wote wakasimama kando, mavazi yao yakiwa yameraruliwa.+
32 Hata hivyo, Yehonadabu+ mwana wa Shimea,+ ndugu ya Daudi, akajibu na kusema: “Bwana wangu asifikiri kwamba wamewaua vijana wote walio wana wa mfalme, kwa maana ni Amnoni peke yake ndiye amekufa,+ kwa sababu kwa agizo la Absalomu limekuwa kama jambo ambalo limewekwa+ kuanzia siku ile alipomfedhehesha+ Tamari dada yake.+ 33 Na sasa bwana wangu mfalme asiliweke neno hili moyoni mwake, kusema, ‘Wana wote wa mfalme wamekufa’; bali ni Amnoni peke yake aliyekufa.”
34 Wakati huo Absalomu naye akakimbia.+ Baadaye yule kijana, mlinzi,+ akainua macho yake, na tazama! kulikuwa na watu wengi wakija barabarani nyuma yake kando ya ubavu wa mlima. 35 Ndipo Yehonadabu+ akamwambia mfalme: “Tazama! Wana wa mfalme wameingia. Imetokea kulingana na neno la mtumishi wako.”+ 36 Na ikawa, mara tu alipomaliza kusema, tazama, wana wa mfalme wakaingia, nao wakaanza kupaaza sauti zao na kulia; na hata mfalme na watumishi wake wote wakalia kilio kikubwa sana. 37 Lakini Absalomu akakimbia apate kwenda kwa Talmai+ mwana wa Amihudi mfalme wa Geshuri.+ Na Daudi akaendelea kumwombolezea+ mwana wake siku zote. 38 Lakini Absalomu akakimbia, akafika Geshuri;+ naye akakaa huko miaka mitatu.
39 Mwishowe nafsi ya Daudi, mfalme, ikatamani kwenda kwa Absalomu; kwa maana alikuwa amejifariji kumhusu Amnoni, kwa sababu alikuwa amekufa.
14 Basi Yoabu+ mwana wa Seruya+ akapata kujua kwamba moyo wa mfalme ulimwelekea Absalomu.+ 2 Kwa hiyo Yoabu akatuma ujumbe huko Tekoa,+ na kutoka huko akamchukua mwanamke mwenye hekima+ na kumwambia: “Tafadhali, omboleza, nawe tafadhali uvae mavazi ya maombolezo, na usijipake mafuta;+ nawe uwe kama mwanamke ambaye amekuwa akiomboleza siku nyingi kwa ajili ya mtu aliyekufa.+ 3 Nawe uingie kwa mfalme, useme naye neno hili.” Basi Yoabu akatia maneno hayo kinywani mwake.+
4 Na yule mwanamke Mtekoa akaingia kwa mfalme, akaanguka kifudifudi,+ akasujudu na kusema: “Okoa,+ Ee mfalme!” 5 Kwa hiyo mfalme akamwambia: “Una jambo gani?” Naye akasema: “Mimi ni mwanamke mjane,+ kwa kuwa mume wangu amekufa. 6 Na mjakazi wako alikuwa na wana wawili, na hao wawili wakaanza kupambana shambani,+ na hapakuwa na mkombozi+ wa kuwatenganisha. Mwishowe mmoja akampiga mwenzake, akamuua. 7 Na tazama, familia yote wamesimama juu ya mjakazi wako, nao wanaendelea kusema, ‘Mtoe yule aliyempiga ndugu yake, ili tumuue kwa sababu ya nafsi ya ndugu+ yake aliyemuua,+ nasi tumwangamize hata mrithi!’ Nao hakika watazima mng’ao wa makaa yangu ambao umebaki, naye mume wangu hatakuwa na jina wala baki juu ya uso wa nchi.”+
8 Ndipo mfalme akamwambia yule mwanamke: “Nenda nyumbani kwako, nami nitatoa amri kukuhusu.”+ 9 Basi yule mwanamke Mtekoa akamwambia mfalme: “Kosa liwe juu yangu, na pia juu ya nyumba ya baba yangu,+ Ee mfalme, lakini mfalme na kiti chake cha ufalme hawana hatia.” 10 Naye mfalme akaendelea kusema: “Yeyote akisema nawe, umlete kwangu, naye hatakudhuru tena kamwe.” 11 Lakini akasema: “Tafadhali, mfalme na amkumbuke Yehova Mungu wako,+ ili mlipiza-kisasi wa damu+ asilete uharibifu sikuzote, na kwamba wasimwangamize mwanangu.” Naye mfalme akasema: “Kama Yehova anavyoishi,+ hata unywele mmoja+ wa mwana wako hautaanguka chini.” 12 Basi yule mwanamke akasema: “Tafadhali, acha mjakazi+ wako aseme neno+ na bwana wangu mfalme.” Kwa hiyo mfalme akasema: “Sema!”+
13 Na yule mwanamke akaendelea kusema: “Kwa nini basi, umewaza jinsi hii+ dhidi ya watu wa Mungu?+ Mfalme anaposema neno hili, yeye ni kama mtu aliye na hatia,+ kwa kuwa mfalme hamrudishi mtu wake aliyefukuzwa.+ 14 Kwa maana sisi tutakufa hakika,+ tutakuwa kama maji yanayomwagwa chini kwenye udongo, ambayo hayawezi kukusanywa. Lakini Mungu hataondolea mbali nafsi hata moja,+ naye amefikiria sababu zinazofanya yule aliyefukuzwa asifukuzwe kwake. 15 Na kwa vile sasa nimeingia ili kusema neno hili na mfalme bwana wangu, ni kwa sababu watu walinitia woga. Basi mjakazi wako akasema, ‘Tafadhali, acha niseme na mfalme. Labda mfalme atatenda kulingana na neno la kijakazi wake. 16 Kwa sababu mfalme alisikiliza ili kumkomboa kijakazi wake kutoka mkononi mwa mtu anayetafuta kuniangamiza mimi na mwanangu wa pekee kutoka katika urithi aliotoa Mungu,’+ 17 ndipo mjakazi wako akasema, ‘Tafadhali, acha neno la bwana wangu mfalme liwe la kutuliza.’ Kwa maana bwana wangu mfalme ni kama malaika+ wa Mungu wa kweli, ili kutofautisha mema na mabaya,+ na Yehova Mungu wako awe pamoja nawe.”
18 Mfalme akajibu na kumwambia yule mwanamke: “Tafadhali, usinifiche jambo ambalo ninakuuliza.”+ Na yule mwanamke akasema: “Tafadhali, bwana wangu mfalme na aseme.” 19 Na mfalme akaendelea kusema: “Je, mkono wa Yoabu+ upo pamoja nawe katika mambo haya yote?”+ Ndipo yule mwanamke akajibu na kusema: “Kama inavyoishi nafsi yako,+ Ee bwana wangu mfalme, hakuna mtu anayeweza kwenda upande wa kuume wala wa kushoto kutoka kwa yote ambayo bwana wangu mfalme amesema; kwa maana mtumishi wako Yoabu ndiye aliyeniamuru, naye ndiye aliyetia maneno haya yote katika kinywa cha mjakazi wako.+ 20 Mtumishi wako Yoabu amefanya jambo hili ili abadili sura ya jambo lile, lakini bwana wangu ana hekima kama hekima ya malaika+ wa Mungu wa kweli, hivi kwamba ajue yote yaliyo duniani.”
21 Basi mfalme akamwambia Yoabu: “Tazama, sasa, hakika nitafanya jambo hili.+ Basi nenda, mrudishe yule kijana Absalomu.”+ 22 Ndipo Yoabu akaanguka kifudifudi, akasujudu na kumbariki mfalme;+ kisha Yoabu akasema: “Leo mtumishi wako amejua kwamba nimepata kibali machoni pako,+ Ee bwana wangu mfalme, kwa maana mfalme ametenda kulingana na neno la mtumishi wake.” 23 Kisha Yoabu akaondoka, akaenda Geshuri,+ akamleta Absalomu Yerusalemu.+ 24 Hata hivyo, mfalme akasema: “Acha ageuke, aende katika nyumba yake, lakini hatauona uso wangu.”+ Basi Absalomu akageuka, akaenda nyumbani kwake, wala hakuuona uso wa mfalme.
25 Basi, kwa kulinganisha na Absalomu, hakuna mwanamume aliyekuwa na sura nzuri+ sana katika Israeli yote kuweza kusifiwa sana hivyo. Hakuwa na kasoro yoyote, kuanzia wayo wa mguu wake mpaka kipaji cha kichwa chake. 26 Na aliponyoa kichwa chake—naye alikuwa akikinyoa mwishoni mwa kila mwaka; kwa kuwa nywele zilikuwa nzito+ sana juu yake, alizinyoa—alipima uzito wa nywele za kichwa chake, shekeli mia mbili kulingana na jiwe la mizani la kifalme. 27 Na Absalomu akazaa wana watatu+ na binti mmoja ambaye jina lake lilikuwa Tamari. Alikuwa mwanamke mrembo zaidi.+
28 Na Absalomu akaendelea kukaa Yerusalemu miaka miwili kamili, naye hakuuona uso wa mfalme.+ 29 Basi Absalomu akatuma ujumbe kumwita Yoabu ili amtume kwa mfalme, naye hakukubali kuja kwake. Ndipo akatuma ujumbe tena, mara ya pili, naye hakukubali kuja. 30 Mwishowe akawaambia watumishi wake: “Tazameni, sehemu ya shamba la Yoabu iliyo kando ya shamba langu, na hapo ana shayiri. Nendeni, mwiteketeze kwa moto.”+ Basi watumishi wa Absalomu wakaiteketeza kwa moto ile sehemu ya shamba.+ 31 Ndipo Yoabu akaondoka, akaja kwa Absalomu nyumbani na kumwambia: “Kwa nini watumishi wako waliiteketeza sehemu ya shamba langu?” 32 Kwa hiyo Absalomu akamwambia Yoabu: “Tazama! Nilituma ujumbe kwako, nikisema, ‘Njoo hapa nikutume kwa mfalme, kusema: “Kwa nini nimekuja kutoka Geshuri?+ Ingalikuwa afadhali kama bado ningalikuwa kule. Na sasa acha niuone uso wa mfalme, na ikiwa ndani yangu mna kosa lolote,+ basi na aniue.”’”
33 Kwa hiyo Yoabu akaingia kwa mfalme na kumwambia. Ndipo akamwita Absalomu, ambaye sasa aliingia kwa mfalme, akamsujudia, akaanguka kifudifudi mbele ya mfalme; kisha mfalme akambusu Absalomu.+
15 Na ikawa baada ya mambo hayo kwamba Absalomu akaagiza atengenezewe gari, pamoja na farasi na watu 50 wenye kukimbia mbele yake.+ 2 Na Absalomu akaamka mapema,+ akasimama upande ule wa barabara unaoelekea langoni.+ Na ikawa kwamba, mtu yeyote akiwa na kesi ya kuja kwa mfalme ili iamuliwe,+ Absalomu alikuwa akimwita na kusema: “Wewe ni mtu wa kutoka jiji gani?” naye akasema: “Mtumishi wako anatoka katika moja la makabila ya Israeli.” 3 Naye Absalomu humwambia: “Tazama, mambo yako ni mema na manyoofu; lakini hakuna yeyote wa kutoka kwa mfalme anayekusikiliza.”+ 4 Na Absalomu husema: “Laiti mimi ningewekwa kuwa mwamuzi katika nchi,+ ili kila mtu aliye na kesi au hukumu aje kwangu! Ndipo hakika ningemtendea haki.”+
5 Pia ilikuwa ikitukia kwamba mtu alipomkaribia ili kumwinamia, alinyoosha mkono wake na kumshika+ na kumbusu. 6 Na Absalomu akaendelea kuwafanyia jambo kama hilo Waisraeli wote waliokuwa wakija kwa mfalme ili kuamuliwa; na Absalomu akaendelea kuiba mioyo ya watu wa Israeli.+
7 Na ikawa kwamba mwishoni mwa miaka 40, Absalomu akamwambia mfalme: “Tafadhali, acha niende, nitimize katika Hebroni+ nadhiri yangu niliyoifanya rasmi kwa Yehova.+ 8 Kwa maana mtumishi wako alifanya nadhiri+ rasmi nilipokuwa nikikaa Geshuri+ katika Siria, nikisema, ‘Hakika Yehova akinirudisha Yerusalemu, ndipo nitakapomtolea Yehova utumishi.’”+ 9 Basi mfalme akamwambia: “Nenda kwa amani.”+ Naye akaondoka, akaenda Hebroni.
10 Sasa Absalomu akatuma wapelelezi+ katika nchi yote ya Israeli, akisema: “Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, ninyi pia mseme, ‘Absalomu amekuwa mfalme+ katika Hebroni!’”+ 11 Basi watu mia mbili walikuwa wameenda pamoja na Absalomu kutoka Yerusalemu, wakiwa wameitwa na kwenda bila habari,+ nao hawakujua jambo hata moja. 12 Na zaidi ya hayo, alipotoa dhabihu, Absalomu akatuma watu kumchukua Ahithofeli+ Mgiloni,+ mshauri wa Daudi,+ kutoka katika Gilo+ jiji lake. Na hila+ hiyo ikaendelea kupata nguvu, na hesabu ya watu ikaendelea kuongezeka+ sikuzote kwa Absalomu.
13 Baada ya muda mleta-habari akaja kwa Daudi, akisema: “Moyo+ wa watu wa Israeli umekuwa nyuma ya Absalomu.” 14 Mara moja Daudi akawaambia watumishi wake wote waliokuwa pamoja naye katika Yerusalemu: “Simameni, tukimbie;+ kwa maana hatutaponyoka kwa sababu ya Absalomu! Nendeni upesi, asije akaharakisha, akatufikia na kututendea mabaya na kulipiga jiji kwa makali ya upanga!”+ 15 Ndipo watumishi wa mfalme wakamwambia mfalme: “Kulingana na yote ambayo bwana wetu mfalme atachagua, tazama, sisi ni watumishi wako.”+ 16 Basi mfalme akatoka, pamoja na watu wote wa nyumbani mwake wakimfuata miguuni pake,+ na mfalme akawaacha wanawake kumi, masuria,+ ili waitunze nyumba. 17 Na mfalme akaendelea kutoka pamoja na watu wote wakimfuata miguuni pake; nao wakaja kusimama kule Beth-merhaki.
18 Na watumishi wake wote walikuwa wakivuka kando yake; na Wakerethi wote na Wapelethi+ wote na Wagathi+ wote, watu mia sita waliokuwa wamemfuata kutoka Gathi,+ walikuwa wakivuka mbele ya uso wa mfalme. 19 Ndipo mfalme akamwambia Itai+ Mgathi: “Kwa nini wewe pia uende pamoja nasi? Rudi,+ ukae na mfalme; kwa maana wewe ni mgeni, na tena, wewe ni mhamishwa kutoka mahali pako. 20 Ulikuja jana tu na je, leo nikufanye utange-tange+ pamoja nasi, uende wakati ninapoenda na popote ninapoenda? Rudi, na uwachukue ndugu zako urudi pamoja nao, na Yehova akuonyeshe fadhili zenye upendo+ na uaminifu!”+ 21 Lakini Itai akamjibu mfalme na kusema: “Kama Yehova anavyoishi na kama anavyoishi+ bwana wangu mfalme, mahali atakapokuwa bwana wangu mfalme, iwe ni kifo ama ni uzima, hapo ndipo mtumishi wako atakapokuwa!”+ 22 Kwa hiyo Daudi akamwambia Itai:+ “Nenda uvuke.” Basi Itai Mgathi akavuka, na pia watu wake wote na watoto wadogo wote waliokuwa pamoja naye.
23 Na watu wote wa nchi wakalia kwa sauti kubwa,+ na watu wote wakavuka, na mfalme alikuwa amesimama kando ya bonde la mto la Kidroni,+ na watu wote wakavuka kwenye barabara pana inayoelekea nyikani. 24 Na tazama, pia Sadoki+ alikuwapo na Walawi+ wote pamoja naye wakiwa wamelichukua+ sanduku+ la agano la Mungu wa kweli; nao wakaliweka chini sanduku la Mungu wa kweli kando ya Abiathari+ mpaka watu wote walipomaliza kuvuka kutoka jijini. 25 Lakini mfalme akamwambia Sadoki: “Rudisha jijini+ sanduku+ la Mungu wa kweli. Nikipata kibali machoni pa Yehova, hakika atanirudisha na kuniruhusu nilione na pia makao yake.+ 26 Lakini akisema, ‘Sikupendezwa nawe,’ basi, mimi hapa, na anifanyie yaliyo mema machoni pake.”+ 27 Na mfalme akaendelea kumwambia Sadoki kuhani: “Wewe ni mwonaji, sivyo?+ Rudi jijini kwa amani, na pia Ahimaazi mwana wako na Yonathani+ mwana wa Abiathari, wana wenu wawili, pamoja nanyi. 28 Tazama, nitangoja kando ya vivuko vya nyikani mpaka neno la kunipasha habari lije kutoka kwenu.”+ 29 Basi Sadoki na Abiathari wakarudisha sanduku la Mungu wa kweli Yerusalemu, nao wakaendelea kukaa huko.
30 Naye Daudi alikuwa akipanda kupitia mpando wa Mizeituni,+ akilia alipokuwa akipanda, kichwa chake kikiwa kimefunikwa;+ naye alikuwa akitembea miguu wazi, na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafunika vichwa vyao, kila mmoja wao, wakapanda juu, wakalia walipokuwa wakipanda.+ 31 Na Daudi akaletewa habari, iliyosema: “Ahithofeli yupo kati ya wale wanaopanga hila+ na Absalomu.”+ Ndipo Daudi akasema:+ “Tafadhali, Ee Yehova,+ badili shauri la Ahithofeli liwe upumbavu!”+
32 Na ikawa kwamba Daudi alipofika kwenye kilele ambapo kwa kawaida watu walikuwa wakimwinamia Mungu, tazama, Hushai+ Mwarki,+ akija kumpokea, kanzu yake ikiwa imeraruliwa na kukiwa na vumbi kichwani pake.+ 33 Hata hivyo, Daudi akamwambia: “Ukivuka kwenda pamoja nami, hakika utakuwa mzigo kwangu.+ 34 Lakini ukirudi jijini nawe umwambie Absalomu, ‘Mimi ni mtumishi wako, Ee mfalme. Nilikuwa mtumishi wa baba yako wakati ule, naam mimi, lakini sasa mimi, naam mimi, ni mtumishi wako,’+ ndipo utavunja+ shauri la Ahithofeli kwa ajili yangu. 35 Je, Sadoki na Abiathari, makuhani, hawako huko pamoja nawe?+ Na itatukia kwamba kila jambo ambalo huenda ukalisikia kutoka katika nyumba ya mfalme, utamwambia Sadoki na Abiathari, makuhani.+ 36 Tazama! Huko pamoja nao kuna wana wao wawili, Ahimaazi+ wa Sadoki na Yonathani+ wa Abiathari; nanyi mwatumie hao kuniletea kila jambo ambalo huenda mkalisikia.” 37 Basi Hushai, rafiki+ ya Daudi, akaingia jijini. Absalomu+ naye akaingia Yerusalemu.
16 Daudi alipokuwa amevuka mbele kidogo ya kile kilele,+ tazama, Siba+ mtumishi wa Mefiboshethi+ alikuwa akija kumpokea, akiwa na punda wawili+ waliotandikwa, na juu yao kulikuwa na mikate+ mia mbili na keki mia moja za zabibu kavu+ na mizigo mia moja ya matunda ya wakati wa kiangazi+ na mtungi mkubwa wa divai.+ 2 Basi mfalme akamwambia Siba: “Vitu hivi vinamaanisha nini kwa upande wako?”+ Ndipo Siba akasema: “Hawa punda ni kwa ajili ya nyumba ya mfalme ili wawapande, na hii mikate na mzigo wa matunda ya wakati wa kiangazi ni kwa ajili ya vijana+ ili wale, na divai ni kwa ajili ya mwenye kuchoka+ nyikani+ ili anywe.” 3 Mfalme akasema: “Na mwana wa bwana wako yuko wapi?”+ Ndipo Siba akamwambia mfalme: “Tazama, anakaa Yerusalemu; kwa maana alisema, ‘Leo nyumba ya Israeli watanirudishia utawala wa kifalme wa baba yangu.’”+ 4 Basi mfalme akamwambia Siba: “Tazama! Mali yote ya Mefiboshethi ni yako.”+ Na Siba akasema: “Mimi ninainama.+ Na nipate kibali machoni pako, bwana wangu mfalme.”
5 Na Mfalme Daudi akaenda mpaka Bahurimu,+ na tazama! palikuwa na mtu anatoka huko, wa familia ya nyumba ya Sauli, na jina lake lilikuwa Shimei,+ mwana wa Gera, akiwa anatoka na kulaani huku akiwa anatoka.+ 6 Naye akaanza kumtupia Daudi mawe, na watumishi wote wa Mfalme Daudi; na watu wote na wanaume wote wenye nguvu walikuwa upande wake wa kuume na wa kushoto. 7 Na Shimei akalaani akisema: “Ondoka, ondoka, wewe mtu mwenye hatia ya damu+ na asiyefaa kitu!+ 8 Yehova amerudisha juu yako hatia yote ya damu kwa ajili ya nyumba ya Sauli ambaye umetawala ukiwa mfalme mahali pake; na Yehova anautia ufalme mkononi mwa Absalomu mwana wako. Na sasa tazama, umo katika msiba wako, kwa sababu wewe ni mtu mwenye hatia ya damu!”+
9 Mwishowe Abishai mwana wa Seruya+ akamwambia mfalme: “Kwa nini huyu mbwa mfu+ amlaani bwana wangu mfalme?+ Tafadhali acha nivuke, niende nikiondoe kichwa chake.”+ 10 Lakini mfalme akasema: “Nina nini nanyi,+ enyi wana wa Seruya?+ Mwacheni alaani+ hivyo, kwa sababu Yehova amemwambia,+ ‘Mlaani Daudi!’ Basi ni nani anayepaswa kusema, ‘Kwa nini ulifanya hivyo?’”+ 11 Na Daudi akaendelea kumwambia Abishai na watumishi wake wote: “Tazama, mwanangu mwenyewe, ambaye ametoka katika viuno vyangu, anaitafuta nafsi yangu;+ si zaidi sasa Mbenyamini huyu!+ Mwacheni alaani, kwa maana Yehova amemwambia hivyo! 12 Labda Yehova ataona+ kwa jicho lake, na Yehova atanirudishia wema badala ya laana yake leo hii.”+ 13 Kwa hiyo Daudi na watu wake wakazidi kusonga mbele barabarani, Shimei naye akiwa anatembea kando ya mlima, akitembea kando yake ili alaani;+ naye akaendelea kutupa mawe akiwa kando yake, naye alitupa mavumbi mengi sana.+
14 Mwishowe mfalme na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika, wakiwa wamechoka. Basi wakajiburudisha huko.+
15 Lakini Absalomu na watu wote, wanaume wa Israeli, wakaingia Yerusalemu;+ na Ahithofeli+ alikuwa pamoja naye. 16 Na ikawa kwamba mara Hushai+ Mwarki,+ rafiki ya Daudi,+ alipoingia kwa Absalomu, Hushai akamwambia Absalomu: “Mfalme na aishi!+ Mfalme na aishi!” 17 Ndipo Absalomu akamwambia Hushai: “Hizi ndizo fadhili zako zenye upendo kwa mwenzako, sivyo? Kwa nini hukuenda pamoja na mwenzako?”+ 18 Kwa hiyo Hushai akamwambia Absalomu: “Sivyo; lakini yeye ambaye Yehova amemchagua na pia watu hawa na wanaume wote wa Israeli, nitakuwa wake, nami nitakaa pamoja naye. 19 Nami nitasema kwa mara ya pili, Mimi nitamtumikia nani? Je, si mbele ya mwana wake? Kama vile nilivyotumika mbele ya baba yako, ndivyo nitakavyokuwa mbele yako.”+
20 Baadaye Absalomu akamwambia Ahithofeli: “Toeni shauri lenu.+ Tufanye nini?” 21 Ndipo Ahithofeli akamwambia Absalomu: “Lala na masuria wa baba yako,+ aliowaacha nyuma kuitunza nyumba.+ Na Israeli wote hakika watasikia kwamba umenuka+ mbele ya baba yako,+ na mikono+ ya wote walio pamoja nawe itapata nguvu.” 22 Basi wakamsimamishia Absalomu hema juu ya dari,+ naye Absalomu akaanza kulala na masuria wa baba yake+ mbele ya macho ya Israeli wote.+
23 Na shauri la Ahithofeli, aliloshauri siku hizo, lilikuwa kama inavyokuwa wakati mtu ameuliza juu ya neno la Mungu wa kweli. Hivyo ndivyo lilivyokuwa shauri+ lote la Ahithofeli+ kwa Daudi na pia kwa Absalomu.
17 Naye Ahithofeli akamwambia Absalomu: “Tafadhali, acha nichague watu kumi na mbili elfu, niondoke na kumfuatilia Daudi usiku wa leo.+ 2 Nami nitamfikia wakati yeye amechoka na mikono yake ina unyonge,+ nami nitamtetemesha; na watu wote walio pamoja naye watakimbia, nami nitampiga na kumuua mfalme akiwa peke yake.+ 3 Nami nitawarudisha kwako watu wote. Kurudi kwa watu wote kunategemea mtu unayemtafuta; na watu wote watakuwa na amani.” 4 Na neno hilo likawa sawa machoni pa Absalomu+ na machoni pa wanaume wazee wote wa Israeli.
5 Hata hivyo, Absalomu akasema: “Tafadhali, mwiteni Hushai+ Mwarki, pia, nasi tusikie maneno yaliyo kinywani mwake pia.” 6 Basi Hushai akaingia kwa Absalomu. Ndipo Absalomu akamwambia: “Ahithofeli amesema hivi na vile. Je, tutende kulingana na neno lake? Ikiwa sivyo, wewe useme.” 7 Ndipo Hushai akamwambia Absalomu: “Shauri ambalo Ahithofeli ametoa si jema wakati huu!”+
8 Na Hushai akaendelea kusema: “Wewe mwenyewe unajua vema kwamba baba yako na wanaume wake ni wenye nguvu,+ nao wana uchungu wa nafsi,+ kama dubu-jike ambaye amepoteza watoto wake porini;+ na baba yako ni shujaa wa vita,+ naye hatalala usiku akiwa pamoja na watu. 9 Tazama! Sasa amejificha+ katika moja la mashimo au katika moja ya mahali penginepo; na hakika itatukia kwamba, mara atakapowaangukia mwanzoni, yeye anayesikia hayo atayasikia na kusema, ‘Watu wanaomfuata Absalomu wameshindwa!’ 10 Na hata mwanamume shujaa ambaye moyo wake ni kama moyo wa simba+ hakika atayeyuka katika udhaifu;+ kwa maana Israeli wote wanajua kwamba baba yako ni mwanamume mwenye nguvu+ na pia wale wanaume mashujaa walio pamoja naye.+ 11 Mimi natoa shauri hili: Acha Israeli wote wakusanyike kwako bila kukosa, kutoka Dani mpaka Beer-sheba,+ kama mchanga ulio kando ya bahari kwa wingi,+ nawe binafsi uende katika pigano.+ 12 Nasi tuje juu yake katika moja ya mahali ambapo atapatikana,+ nasi tutakuja juu yake kama umande+ unavyoanguka juu ya nchi; na hakika hatabaki hata mmoja kati yake na watu wote walio pamoja naye. 13 Naye akiingia ndani ya jiji fulani, Israeli wote watachukua kamba mpaka kwenye jiji hilo, nasi tutalivuta mpaka kwenye bonde la mto, lisibaki hata jiwe moja humo.”+
14 Ndipo Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Hushai Mwarki ni bora+ kuliko shauri la Ahithofeli!” Na Yehova alikuwa ametoa amri+ shauri la Ahithofeli livunjwe+ ingawa lilikuwa jema,+ ili Yehova alete msiba+ juu ya Absalomu.
15 Baadaye Hushai akamwambia Sadoki+ na Abiathari, makuhani: “Ahithofeli alimshauri Absalomu na wanaume wazee wa Israeli hivi na vile; nami nikashauri hivi na vile. 16 Na sasa tuma ujumbe haraka na umwambie Daudi,+ ukisema, ‘Usiku wa leo usilale katika nchi tambarare za jangwa la nyikani, lakini wewe pia usikose kuvuka,+ ili mfalme na watu wote walio pamoja naye wasije wakamezwa.’”+
17 Kwa kuwa Yonathani+ na Ahimaazi+ walikuwa wamesimama katika En-rogeli,+ mjakazi fulani akaenda, akawaambia. Basi wakaondoka, kwa kuwa iliwapasa kumwambia Mfalme Daudi; kwa maana haikuwezekana waonekane wakiingia jijini. 18 Hata hivyo, kijana fulani akawaona, akamwambia Absalomu. Basi hao wawili wakaenda mbio, wakaja kwenye nyumba ya mtu fulani katika Bahurimu,+ aliyekuwa na kisima katika ua wake; nao wakashuka ndani ya kisima hicho. 19 Kisha yule mwanamke akachukua kifuniko, akakitandaza juu ya uso wa kile kisima na kurundika juu yake nafaka iliyovunjwa;+ wala halikujulikana jambo lolote. 20 Sasa watumishi wa Absalomu wakaja kwa mwanamke yule nyumbani kwake na kusema: “Ahimaazi na Yonathani wako wapi?” Kwa hiyo yule mwanamke akawaambia: “Walipita hapa wakaenda kwenye maji.”+ Ndipo wakaendelea kutafuta, nao hawakuwapata,+ kisha wakarudi Yerusalemu.
21 Na ikawa kwamba baada ya kuondoka kwao, ndipo wakatoka ndani ya kile kisima, wakaenda, wakamweleza Daudi na kumwambia Daudi: “Ondokeni, vukeni juu ya maji mbiombio; kwa maana hivi ndivyo Ahithofeli alivyotoa shauri+ juu yenu.” 22 Mara moja Daudi akaondoka na pia watu wote waliokuwa pamoja naye, nao wakaendelea kuvuka Yordani mpaka kulipopambazuka asubuhi,+ mpaka kulipokuwa hakuna hata mmoja ambaye hakuwa amevuka Yordani.
23 Naye Ahithofeli akaona kwamba haikutendwa kulingana na shauri lake,+ naye akatandika punda, akaondoka na kwenda nyumbani kwake katika jiji lake.+ Kisha akawapa nyumba yake+ amri halafu akajinyonga,+ akafa.+ Basi akazikwa+ katika makaburi ya mababu zake.
24 Na Daudi akaja Mahanaimu,+ naye Absalomu akavuka Yordani, yeye na watu wote wa Israeli pamoja naye. 25 Na Amasa+ ndiye ambaye Absalomu aliweka mahali pa Yoabu+ juu ya jeshi; na Amasa alikuwa mwana wa mtu ambaye jina lake lilikuwa Ithra,+ Mwisraeli, aliyelala na Abigaili,+ binti ya Nahashi, dada ya Seruya, mama ya Yoabu. 26 Na Israeli na Absalomu wakapiga kambi katika nchi ya Gileadi.+
27 Na ikawa kwamba, mara tu Daudi alipofika Mahanaimu, Shobi mwana wa Nahashi kutoka Raba+ la wana wa Amoni,+ na Makiri+ mwana wa Amieli+ kutoka Lo-debari, na Barzilai+ Mgileadi, kutoka Rogelimu+ 28 wakaleta vitanda na beseni na vyombo vya mfinyanzi, na ngano na shayiri na unga+ na nafaka iliyochomwa+ na maharagwe mapana+ na dengu+ na nafaka iliyokauka; 29 na asali+ na siagi+ na kondoo na maziwa ya ng’ombe yaliyoganda, wakaleta kwa ajili ya Daudi na kwa ajili ya watu waliokuwa pamoja naye ili wale,+ kwa maana walisema: “Watu wana njaa nao wamechoka na wana kiu nyikani.”+
18 Na Daudi akawahesabu watu waliokuwa pamoja naye na kuweka juu yao wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia.+ 2 Na zaidi ya hayo, Daudi akapeleka sehemu ya tatu+ ya watu iwe chini ya mkono wa Yoabu+ na sehemu ya tatu chini ya mkono wa Abishai+ mwana wa Seruya, ndugu ya Yoabu,+ na sehemu ya tatu chini ya mkono wa Itai+ Mgathi. Kisha mfalme akawaambia watu: “Mimi pia hakika nitaenda pamoja nanyi.” 3 Lakini watu wakasema: “Usitoke kwenda nje,+ kwa maana tukikimbia, hawataweka moyo wao juu yetu;+ na nusu yetu tukifa, hawataweka moyo wao juu yetu, kwa sababu thamani yako ni kama elfu kumi kati yetu;+ na sasa ingekuwa bora ututumikie kwa kutupa msaada+ ukiwa jijini.” 4 Basi mfalme akawaambia: “Lolote lililo jema machoni penu nitafanya.”+ Na mfalme akaendelea kusimama kando ya lango,+ na watu wote wakatoka kwa mamia yao na kwa maelfu yao.+ 5 Na mfalme akaendelea kuwaamuru Yoabu na Abishai na Itai, akisema: “Mtendeeni yule kijana Absalomu kwa upole+ kwa ajili yangu.” Na watu wote wakasikia mfalme alipowaamuru wale wakuu wote kuhusiana na jambo la Absalomu.
6 Na watu wakaendelea kwenda nje kukutana na Israeli; na pigano likawa katika msitu wa Efraimu.+ 7 Mwishowe watu wa Israeli+ wakashindwa+ hapo mbele ya watumishi wa Daudi, na mauaji hapo yakawa makubwa siku hiyo, ya watu 20,000. 8 Na pigano hapo likaenea katika nchi yote yenye kuonekana. Zaidi ya hayo, huo msitu ulikula watu wengi kuliko wale walioliwa na upanga siku hiyo.
9 Mwishowe Absalomu akajikuta mbele ya watumishi wa Daudi. Na Absalomu alikuwa amepanda nyumbu, na yule nyumbu akaja chini ya mtandao wa matawi ya mti mkubwa mno, hivi kwamba kichwa chake kikakwama kabisa katika ule mti mkubwa, naye akainuliwa juu kati ya mbingu na dunia,+ na yule nyumbu aliyekuwa chini yake akapita, akazidi kwenda mbele. 10 Ndipo mtu fulani akaona hayo, akamwambia Yoabu+ na kusema: “Tazama! Nimemwona Absalomu akiwa amening’inia katika mti mkubwa.” 11 Ndipo Yoabu akamwambia yule mtu aliyekuwa akimpasha habari: “Wewe uliona, kwa nini basi hukumpiga, aanguke chini hapo? Ndipo ningekuwa na wajibu wa kukupa vipande kumi vya fedha na mshipi.”+ 12 Lakini mtu huyo akamwambia Yoabu: “Hata kama mkononi mwangu ningekuwa na vipande elfu moja vya fedha, mimi singenyoosha mkono wangu juu ya mwana wa mfalme; kwa maana mfalme alikuamuru wewe na Abishai na Itai masikioni mwetu, akisema, ‘Hata kama wewe ni nani, lindeni yule kijana, Absalomu.’+ 13 Kama sivyo ningeitendea nafsi yake hila na mambo hayo yote hayangefichwa kutoka kwa mfalme,+ nawe mwenyewe ungesimama kando.” 14 Ndipo Yoabu akasema: “Acha nisijikawize hivi mbele yako!” Basi akachukua mkononi mwake mikuki midogo mitatu, akaichoma+ ndani ya moyo wa Absalomu alipokuwa bado hai+ katikati ya ule mti mkubwa. 15 Kisha watumishi kumi wenye kuchukua silaha za Yoabu wakaja, wakampiga Absalomu ili wamuue.+ 16 Sasa Yoabu akapiga baragumu,+ ili watu warudi, waache kufuatilia Israeli; kwa maana Yoabu alikuwa amewazuia watu. 17 Mwishowe wakamchukua Absalomu, wakamtupa msituni ndani ya shimo kubwa, wakarundika juu yake fungu kubwa sana la mawe.+ Lakini Israeli wote wakakimbia, kila mtu akaenda nyumbani kwake.
18 Sasa Absalomu, alipokuwa angali hai, alikuwa amechukua na kujisimamishia nguzo,+ ambayo ipo katika Nchi Tambarare ya Chini ya Mfalme,+ kwa maana alisema: “Sina mwana ili kuweka jina langu katika kumbukumbu.”+ Basi akaiita nguzo hiyo kwa jina+ lake mwenyewe, nayo inaendelea kuitwa Mnara wa Ukumbusho wa Absalomu mpaka leo hii.
19 Naye Ahimaazi+ mwana wa Sadoki akasema: “Tafadhali, acha nikimbie, nimpelekee mfalme habari hizi, kwa sababu Yehova amemhukumu ili amweke huru kutoka mkononi mwa adui zake.”+ 20 Lakini Yoabu akamwambia: “Wewe si mtu wa kupeleka habari leo, nawe utapeleka habari hizo siku nyingine; lakini leo usipeleke habari hizi, kwa sababu mwana wa mfalme amekufa.”+ 21 Ndipo Yoabu akamwambia Mkushi:+ “Nenda, mwambie mfalme yale ambayo umeona.” Kwa hiyo yule Mkushi akamwinamia Yoabu, akaanza kukimbia. 22 Basi Ahimaazi mwana wa Sadoki akamwambia tena Yoabu: “Tafadhali, sasa acha lolote litakalotokea litokee, acha mimi pia nikimbie nyuma ya yule Mkushi.” Hata hivyo, Yoabu akasema: “Kwa nini wewe ukimbie, mwanangu, na hakuna habari zozote kwa ajili yako?” 23 Na bado akasema: “Acha sasa litakalotokea litokee, acha nikimbie.” Basi akamwambia: “Kimbia!” Ndipo Ahimaazi akaanza kukimbia kupitia njia ya ile Wilaya,+ na mwishowe akampita yule Mkushi.
24 Basi Daudi alikuwa ameketi kati ya yale malango mawili.+ Na wakati huo mlinzi+ akaenda juu ya paa ya lango kando ya ukuta. Baada ya muda akainua macho yake, akaona, na tazama! palikuwa na mtu anakimbia akiwa peke yake. 25 Kwa hiyo yule mlinzi akaita na kumwambia mfalme, kisha mfalme akasema: “Ikiwa yuko peke yake, kuna habari kinywani mwake.” Naye akazidi kuja, akaendelea kusogea karibu. 26 Sasa mlinzi akaona mtu mwingine akiwa anakimbia. Kwa hiyo mlinzi akamwita mtunza-lango na kusema: “Tazama! Mtu mwingine anakimbia akiwa peke yake!” naye mfalme akasema: “Huyo pia ni mleta-habari.” 27 Na mlinzi akaendelea kusema: “Ninaona kwamba namna ya kukimbia ya yule wa kwanza ni kama namna ya kukimbia+ ya Ahimaazi+ mwana wa Sadoki,” naye mfalme akasema: “Huyu ni mtu mwema,+ naye hakika anakuja na habari njema.”+ 28 Mwishowe Ahimaazi akaita na kumwambia mfalme: “Ni vema!” Ndipo akamwinamia mfalme kifudifudi. Naye akaendelea kusema: “Abarikiwe+ Yehova Mungu wako, ambaye amewatoa+ watu walionyoosha mkono wao juu ya bwana wangu mfalme!”
29 Hata hivyo, mfalme akasema: “Je, mambo ni mema kwa yule kijana Absalomu?” Naye Ahimaazi akasema: “Niliona ghasia kubwa wakati Yoabu alipotuma mtumishi wa mfalme na mtumishi wako, nami sikujua ni ya nini.”+ 30 Kwa hiyo mfalme akasema: “Ondokea kando, simama pale.” Basi akaondokea kando, akasimama tuli.
31 Na tazama, yule Mkushi+ akaingia, na huyo Mkushi akaanza kusema: “Acha bwana wangu mfalme apokee habari, kwa maana Yehova amekuhukumu leo ili kukuweka huru kutoka mkononi mwa wote wanaosimama juu yako.”+ 32 Lakini mfalme akamwambia Mkushi: “Je, mambo ni mema kwa yule kijana Absalomu?” Ndipo Mkushi akasema: “Adui za bwana wangu mfalme na wote waliosimama juu yako kwa uovu na wawe kama yule kijana.”+
33 Ndipo mfalme akahuzunika, akaenda juu katika chumba cha dari+ juu ya njia ya lango, akaanza kulia; naye alisema hivi akiwa anatembea: “Mwanangu Absalomu, mwanangu, mwanangu+ Absalomu! Laiti mimi mwenyewe ningekufa badala yako, Absalomu mwanangu, mwanangu!”+
19 Baadaye Yoabu akaletewa habari hii: “Tazama! Mfalme analia, naye anaendelea kuomboleza juu ya Absalomu.”+ 2 Basi wokovu wa siku ile ukawa pindi ya watu wote kuomboleza, kwa sababu watu walisikia ikisemwa siku hiyo: “Mfalme ameona uchungu kwa sababu ya mwana wake.” 3 Nao watu wakaanza kujificha na kuingia jijini siku hiyo,+ kama vile watu wanavyojificha wakati wanapofedheheka kwa sababu ya kukimbia vitani. 4 Naye mfalme akajifunika uso, na mfalme akaendelea kulia kwa sauti kubwa: “Mwanangu Absalomu! Absalomu mwanangu, mwanangu!”+
5 Mwishowe Yoabu akaingia kwa mfalme nyumbani na kusema: “Leo umeaibisha uso wa watumishi wako wote, walioiokoa nafsi yako leo+ na nafsi ya wana+ wako na binti+ zako na nafsi ya wake+ zako na nafsi ya masuria wako,+ 6 kwa kuwapenda wale wanaokuchukia na kuwachukia wale wanaokupenda; kwa maana leo umejulisha kwamba wakuu na watumishi si kitu kwako, kwa sababu mimi najua vema leo kwamba kama Absalomu angelikuwa hai na sisi sote wengine tungelikuwa wafu leo, basi hiyo ingelikuwa ni sawa machoni pako. 7 Na sasa ondoka, toka nje, useme moja kwa moja kwenye moyo+ wa watumishi wako, kwa sababu mimi naapa kwa Yehova kwamba, usipotoka, hakuna hata mtu mmoja atakayebaki pamoja nawe usiku wa leo;+ na jambo hilo kwa hakika litakuwa baya zaidi kwako kuliko madhara yote ambayo yamekupata kuanzia ujana wako mpaka sasa.” 8 Basi mfalme akaondoka, akaketi langoni,+ nao wakawapa watu wote habari hiyo, wakisema: “Tazama, mfalme ameketi langoni.” Na watu wote wakaanza kuja mbele ya mfalme.
Lakini Israeli walikuwa wamekimbia kila mmoja kwenda nyumbani kwake.+ 9 Na watu wote wakaja kuhusika katika ugomvi katika makabila yote ya Israeli, wakisema: “Mfalme ndiye aliyetuokoa kutoka mkononi mwa adui zetu,+ na yeye ndiye aliyetuokoa mkononi mwa Wafilisti; na sasa amekimbia kutoka katika nchi mbele ya Absalomu.+ 10 Naye Absalomu, tuliyemtia mafuta awe juu yetu,+ amekufa vitani.+ Basi sasa kwa nini hamfanyi lolote kumrudisha mfalme?”+
11 Basi Mfalme Daudi akatuma ujumbe kwa Sadoki+ na Abiathari,+ makuhani, akisema: “Semeni na wanaume wazee wa Yuda+ hivi, ‘Kwa nini ninyi muwe wa mwisho kumrudisha mfalme nyumbani kwake, wakati neno la Israeli wote limemfikia mfalme nyumbani kwake? 12 Ninyi ni ndugu zangu; ninyi ni mfupa na nyama yangu.+ Basi kwa nini muwe wa mwisho kumrudisha mfalme?’ 13 Nanyi mwambieni Amasa,+ ‘Je, wewe si mfupa wangu na nyama yangu? Basi Mungu na anifanyie hivyo na kuzidisha+ jambo hilo ikiwa hutakuwa mkuu wa jeshi mbele yangu sikuzote badala ya Yoabu.’”+
14 Naye akaanza kuelekeza moyo wa watu wote wa Yuda wakawa kama mtu mmoja,+ hivi kwamba wakampelekea mfalme neno hili: “Rudi, wewe na watumishi wako wote.”
15 Naye mfalme akaanza kurudi, akafika Yordani. Nao Yuda wakaja Gilgali+ ili kwenda kumpokea mfalme, wamvushe mfalme Yordani. 16 Ndipo Shimei+ mwana wa Gera,+ Mbenyamini, aliyetoka Bahurimu,+ akafanya haraka, akashuka pamoja na watu wa Yuda ili kumpokea Mfalme Daudi. 17 Na palikuwa na watu 1,000 pamoja naye kutoka Benyamini. (Na pia Siba+ mtumishi wa nyumba ya Sauli na wanawe 15+ na watumishi wake 20 walikuwa pamoja naye, nao wakafaulu kufika Yordani mbele ya mfalme. 18 Naye akavuka kivuko+ ili kuivusha nyumba ya mfalme na kufanya yaliyo mema machoni pake.) Naye Shimei mwana wa Gera akaanguka chini mbele ya mfalme alipokuwa karibu kuvuka Yordani.+ 19 Akamwambia mfalme: “Bwana wangu asinihesabie kosa, nawe usikumbuke kosa ambalo mtumishi wako alifanya+ siku ile bwana wangu alipotoka Yerusalemu, hivi kwamba mfalme aweke hilo moyoni mwake.+ 20 Kwa maana mtumishi wako anajua vema kwamba mimi ndiye niliyetenda dhambi; na kwa hiyo leo mimi hapa nimekuja wa kwanza kati ya nyumba yote ya Yosefu+ ili nishuke kumpokea bwana wangu mfalme.”
21 Mara moja Abishai,+ mwana wa Seruya,+ akajibu na kusema: “Je, Shimei hapaswi kuuawa kwa sababu hiyo, kwa maana alimlaani mtiwa-mafuta wa Yehova?”+ 22 Lakini Daudi akasema: “Nina nini nanyi,+ ninyi wana wa Seruya, kwamba muwe leo mpinzani+ wangu? Je, yeyote atauawa leo katika Israeli?+ Kwa maana, je, sijui vema kwamba leo mimi ni mfalme juu ya Israeli?” 23 Ndipo mfalme akamwambia Shimei: “Hutakufa.” Naye mfalme akamwapia.+
24 Na Mefiboshethi+ mjukuu wa Sauli akashuka kuja kumpokea mfalme; naye hakuwa ametunza miguu+ yake wala kutunza masharubu+ yake wala kufua mavazi yake tangu siku ile mfalme alipoondoka mpaka siku ile alipokuja kwa amani. 25 Na ikawa kwamba alipokuja Yerusalemu kumpokea mfalme, ndipo mfalme akamwambia: “Kwa nini hukwenda pamoja nami, Mefiboshethi?” 26 Naye akasema: “Bwana wangu mfalme, mtumishi wangu+ ndiye aliyenidanganya. Kwa maana mtumishi wako alikuwa amesema, ‘Acha nijitandikie punda-jike ili nimpande, niende pamoja na mfalme,’ kwa maana mtumishi wako ni kilema.+ 27 Kwa hiyo akamchongea+ mtumishi wako kwa bwana wangu mfalme. Lakini bwana wangu mfalme ni kama malaika+ wa Mungu wa kweli, na basi ufanye yaliyo mema machoni pako. 28 Kwa maana nyumba yote ya baba yangu ingelikuwa si kitu ila kuhukumiwa kifo mbele ya bwana wangu mfalme, na hata hivyo ulimweka mtumishi wako kati ya wale wanaokula mezani pako.+ Basi bado nina nini kama dai la haki la kumlilia+ zaidi mfalme?”
29 Hata hivyo, mfalme akamwambia: “Kwa nini bado unaendelea kusema maneno yako? Mimi nasema, Wewe na Siba mgawane hayo mashamba.”+ 30 Ndipo Mefiboshethi akamwambia mfalme: “Acha ayachukue yote,+ kwa vile sasa bwana wangu mfalme amekuja kwa amani nyumbani kwake.”
31 Naye Barzilai+ Mgileadi akashuka kutoka Rogelimu ili apite mpaka Yordani pamoja na mfalme, apate kumsindikiza mpaka Yordani. 32 Na Barzilai alikuwa mzee sana, akiwa na umri wa miaka 80;+ naye alimwandalia mfalme chakula alipokuwa akikaa Mahanaimu,+ kwa maana alikuwa mwanamume mkuu+ sana. 33 Basi mfalme akamwambia Barzilai: “Wewe vuka pamoja nami, nami nitakuandalia chakula wewe pamoja nami katika Yerusalemu.”+ 34 Lakini Barzilai akamwambia mfalme: “Siku za miaka ya maisha yangu ni ngapi, ili kwamba niende Yerusalemu pamoja na mfalme? 35 Mimi leo nina umri wa miaka 80.+ Je, ninaweza kutambua kati ya jema na baya, au je, mtumishi wako anaweza kuonja ladha ya kile ninachokula na kile ninachokunywa,+ au je, ninaweza kusikiliza+ tena sauti za waimbaji wa kiume na wa kike?+ Kwa nini basi mtumishi wako awe mzigo+ tena kwa bwana wangu mfalme? 36 Kwa maana ni umbali kidogo tu ambao mtumishi wako ameweza kumleta mfalme mpaka Yordani, na kwa nini mfalme anilipe thawabu hii?+ 37 Tafadhali, acha mtumishi wako arudi, na acha nife+ katika jiji langu karibu na kaburi la baba yangu na mama yangu.+ Lakini, tazama, mtumishi wako Kimhamu.+ Acha avuke pamoja na bwana wangu mfalme; nawe umfanyie yaliyo mema machoni pako.”
38 Basi mfalme akasema: “Kimhamu atavuka pamoja nami, nami nitamfanyia yaliyo mema machoni pako; na yote ambayo utaamua kuweka juu yangu nitakufanyia.” 39 Sasa watu wote wakaanza kuvuka Yordani, naye mfalme akavuka; lakini mfalme akambusu+ Barzilai na kumbariki,+ kisha akarudi mahali pake. 40 Mfalme alipovuka kwenda Gilgali,+ Kimhamu alivuka pamoja naye, na pia watu wote wa Yuda, na pia nusu ya watu wa Israeli, ili wamvushe mfalme.
41 Na, tazama! watu wote wa Israeli walikuwa wakimjia mfalme, nao wakamwambia mfalme: “Kwa nini+ ndugu zetu watu wa Yuda walikuiba ili wamlete mfalme na nyumba yake na watu wote wa Daudi pamoja naye kuvuka Yordani?”+ 42 Ndipo watu wote wa Yuda wakawajibu watu wa Israeli: “Kwa sababu mfalme ni mtu wa karibu wa jamaa yetu;+ na kwa nini mmekasirika kwa ajili ya jambo hili? Je, sisi tumekula kwa gharama ya mfalme, au je, tumepewa zawadi?”
43 Hata hivyo, watu wa Israeli wakawajibu watu wa Yuda na kusema: “Sisi tuna sehemu kumi katika mfalme,+ hivi kwamba hata katika Daudi sisi ni zaidi kuliko ninyi. Kwa nini, basi, mmetutendea kwa dharau, na kwa nini jambo letu halikuwa la kwanza+ sisi tumrudishe mfalme wetu?” Lakini neno la watu wa Yuda likawa kali zaidi kuliko neno la watu wa Israeli.
20 Basi palikuwa na mtu asiyefaa kitu,+ ambaye jina lake lilikuwa Sheba,+ mwana wa Bikri, Mbenyamini; naye akapiga baragumu+ na kusema: “Hatuna fungu lolote katika Daudi, nasi hatuna urithi wowote katika mwana wa Yese.+ Kila mmoja na aende kwa miungu yake,+ Ee Israeli!” 2 Basi watu wote wa Israeli wakaanza kupanda, wakaacha kumfuata Daudi ili wamfuate Sheba mwana wa Bikri;+ lakini watu wa Yuda wakashikamana na mfalme wao kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.+
3 Mwishowe Daudi akaja nyumbani kwake katika Yerusalemu.+ Ndipo mfalme akawachukua wale wanawake kumi,+ masuria aliokuwa amewaacha nyuma kuitunza nyumba, akawaweka katika nyumba ya ulinzi, lakini akaendelea kuwapa chakula. Naye hakulala nao+ tena, lakini wakaendelea kufungiwa kabisa mpaka siku walipokufa, wakiwa wajane wenye mume aliye hai.
4 Basi mfalme akamwambia Amasa:+ “Wakusanye watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe usimame hapa.” 5 Kwa hiyo Amasa akaenda kukusanya Yuda pamoja; lakini akaja baada ya muda uliowekwa ambao alikuwa amemwekea. 6 Ndipo Daudi akamwambia Abishai:+ “Sasa Sheba+ mwana wa Bikri atakuwa mbaya kwetu kuliko Absalomu.+ Wewe wachukue watumishi+ wa bwana wako, umfuatilie, asije akajipatia majiji yenye ngome na kukimbia kutoka machoni petu.” 7 Basi watu wa Yoabu+ na Wakerethi+ na Wapelethi+ na wanaume wote wenye nguvu wakatoka ili wamfuatilie; nao wakatoka nje ya Yerusalemu ili wamfuatilie Sheba mwana wa Bikri. 8 Walikuwa karibu na lile jiwe kubwa lililo katika Gibeoni,+ naye Amasa+ akaja kuwapokea. Sasa Yoabu alikuwa amejifunga, amevaa vazi; naye alikuwa amefunga upanga kiunoni mwake, ukiwa katika ala yake. Naye akaenda mbele, nao ukaanguka.
9 Na Yoabu akamwambia Amasa: “Je, mambo ni mema kwako, ndugu yangu?”+ Ndipo mkono wa kuume wa Yoabu ukashika ndevu za Amasa ili ambusu.+ 10 Lakini Amasa hakuwa mwangalifu juu ya ule upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu; naye akamchoma+ nao tumboni, na matumbo yake yakamwagika chini, wala hakuhitaji kurudia kufanya hivyo tena. Basi akafa. Na Yoabu na Abishai ndugu yake wakamfuatilia Sheba mwana wa Bikri.
11 Na mmoja wa vijana wa Yoabu akasimama juu yake na kusema: “Yeyote ambaye amependezwa na Yoabu na yeyote ambaye ni wa Daudi,+ na amfuate Yoabu!” 12 Wakati huo wote Amasa alikuwa akigaagaa katika damu+ katikati ya njia kuu. Mtu yule alipoona kwamba watu wote walisimama tuli, akamwondoa Amasa kutoka katika ile njia kuu mpaka kwenye shamba. Mwishowe akamfunika vazi, kwa sababu aliona kwamba kila mtu aliyefika kwake alisimama tuli.+ 13 Mara tu alipokuwa amemwondoa katika ile njia kuu, kila mtu akapita, akimfuata Yoabu ili kumfuatilia Sheba+ mwana wa Bikri.
14 Na Sheba akapita kati ya makabila yote ya Israeli mpaka jiji la Abeli la Beth-maaka.+ Nao Wabikri wote wakakutanika pamoja, nao pia wakaingia nyuma yake.
15 Nao wakaja, wakamzingira katika Abeli la Beth-maaka, wakatengeneza boma la kulizingira jiji hilo,+ kwa kuwa lilikuwa ndani ya boma. Na watu wote waliokuwa pamoja na Yoabu walikuwa wanauchimbua ukuta, ili kuubomoa. 16 Na mwanamke fulani mwenye hekima+ akaanza kuita kutoka jijini: “Sikilizeni, sikilizeni! Tafadhali, mwambieni Yoabu, ‘Njoo karibu mpaka hapa, nami niseme na wewe.’” 17 Basi akaenda karibu naye, ndipo mwanamke huyo akasema: “Je, wewe ni Yoabu?” naye akasema: “Mimi ndiye.” Ndipo mwanamke huyo akamwambia: “Yasikilize maneno ya kijakazi wako.”+ Naye akasema: “Ninasikiliza.” 18 Mwanamke huyo akaendelea kusema: “Sikuzote walikuwa wakisema katika nyakati za kale hivi, ‘Na waulize katika Abeli, na hakika ndivyo watakavyolimaliza jambo hili.’ 19 Mimi nawakilisha wenye kufanya amani+ na waaminifu+ wa Israeli. Unatafuta kuua jiji+ na mama katika Israeli. Kwa nini uumeze+ urithi+ wa Yehova?” 20 Kwa hiyo Yoabu akajibu na kusema: “Ni jambo lisiloweza kuwaziwa kwangu, kwamba nimeze na kuharibu. 21 Jambo hili haliko hivyo, lakini mtu fulani kutoka eneo lenye milima la Efraimu,+ ambaye jina lake ni Sheba+ mwana wa Bikri, amenyoosha mkono wake juu ya Mfalme Daudi.+ Ninyi mtoeni yeye peke yake,+ nami nitaondoka juu ya jiji hili.”+ Ndipo yule mwanamke akamwambia Yoabu: “Tazama! Utatupiwa kichwa chake+ kupitia ukutani!”
22 Mara moja yule mwanamke akaenda kwa watu wote kwa hekima yake,+ nao wakakikata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri, wakamtupia Yoabu. Basi akapiga baragumu,+ nao wakatawanyika kutoka kwenye jiji lile, kila mmoja akaenda nyumbani kwake; naye Yoabu akarudi Yerusalemu kwa mfalme.
23 Na Yoabu alikuwa juu ya jeshi+ lote la Israeli; na Benaya+ mwana wa Yehoyada+ alikuwa juu ya Wakerethi+ na juu ya Wapelethi.+ 24 Na Adoramu+ alikuwa juu ya wale walioandikishwa kufanya kazi ya kulazimishwa; na Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi alikuwa karani. 25 Na Sheva+ alikuwa mwandishi,+ na Sadoki+ na Abiathari+ walikuwa makuhani. 26 Na Ira, Myairi, pia akawa kuhani+ wa Daudi.
21 Basi kukawa na njaa+ katika siku za Daudi kwa miaka mitatu, mwaka baada ya mwaka; naye Daudi akatafuta shauri mbele za uso wa Yehova. Kisha Yehova akasema: “Kuna hatia ya damu juu ya Sauli na juu ya nyumba yake, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”+ 2 Kwa hiyo mfalme akawaita Wagibeoni+ na kuongea nao. (Kama ilivyo, Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, bali walikuwa mabaki ya Waamori;+ na wana wa Israeli walikuwa wamewaapia,+ lakini Sauli akatafuta kuwapiga+ ili kuwaua alipoona wivu+ kwa sababu ya wana wa Israeli na Yuda.) 3 Na Daudi akawaambia Wagibeoni: “Niwatendee nini, nami nitafanya upatanisho+ kwa kutumia nini, ili muubariki urithi+ wa Yehova?” 4 Kwa hiyo Wagibeoni wakamwambia: “Si jambo la fedha wala dhahabu+ kwetu kwa habari ya Sauli na nyumba yake, wala si juu yetu kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Naye akasema: “Lolote mtakalosema nitawafanyia.” 5 Ndipo wakamwambia mfalme: “Mtu aliyetuangamiza+ na kupanga+ kutumaliza tusiishi katika eneo lolote la Israeli, 6 na tupewe watu saba kati ya wanawe;+ nasi tuwaweke mbele+ za Yehova katika Gibea+ la Sauli, aliyechaguliwa na Yehova.”+ Basi mfalme akasema: “Mimi mwenyewe nitawatoa.”
7 Hata hivyo, mfalme akamhurumia Mefiboshethi+ mwana wa Yonathani mwana wa Sauli kwa sababu ya kile kiapo+ cha Yehova kilichokuwa kati yao, kati ya Daudi na Yonathani mwana wa Sauli. 8 Basi mfalme akawachukua wale wana wawili wa Rispa+ binti ya Aya aliyemzalia Sauli, Armoni na Mefiboshethi, na wale wana watano wa Mikali+ binti ya Sauli ambao alimzalia Adrieli+ mwana wa Barzilai, Mmeholathi. 9 Ndipo akawatia mkononi mwa Wagibeoni, nao wakawaweka kwenye mlima mbele za Yehova,+ hivi kwamba hao saba wakaanguka pamoja; nao waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mwanzoni mwa mavuno ya shayiri.+ 10 Hata hivyo, Rispa binti ya Aya+ akachukua nguo ya gunia,+ akajitandikia juu ya mwamba tangu mwanzo wa mavuno mpaka maji yalipomwagika juu yao kutoka mbinguni;+ naye hakuruhusu ndege+ wa mbinguni watue juu yao wakati wa mchana wala wanyama wa mwituni+ wakati wa usiku.
11 Mwishowe Daudi akaletewa habari+ za mambo ambayo Rispa binti ya Aya, suria wa Sauli, alikuwa amefanya. 12 Kwa hiyo Daudi akaenda, akachukua mifupa ya Sauli+ na mifupa ya Yonathani mwana wake kutoka kwa wenye mashamba wa Yabesh-gileadi,+ ambao walikuwa wameiiba kutoka katika kiwanja cha watu wote cha Beth-shani,+ mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika+ siku ambayo Wafilisti walimpiga na kumuua Sauli juu ya Gilboa.+ 13 Naye akaleta kutoka huko mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwana wake; tena wakaikusanya mifupa ya wale watu waliowekwa mbele zake.+ 14 Kisha wakazika mifupa ya Sauli na Yonathani mwana wake katika nchi ya Benyamini huko Sela+ katika kaburi la Kishi+ baba yake, ili wafanye kila jambo ambalo mfalme alikuwa ameamuru. Basi Mungu akakubali kusihiwa kwa ajili ya nchi baada ya mambo hayo.+
15 Na Wafilisti+ wakaja kupigana vita tena na Israeli. Basi Daudi na watumishi wake pamoja naye wakashuka na kupigana na Wafilisti; naye Daudi akachoka. 16 Na Ishbi-benobu, aliyekuwa mmoja wa wale waliozaliwa kwa Refaimu,+ ambaye uzito wa mkuki+ wake ulikuwa shekeli mia tatu za shaba na ambaye alikuwa amejifunga upanga mpya, akafikiria kumpiga na kumuua Daudi. 17 Basi Abishai+ mwana wa Seruya akaja mara moja kumsaidia,+ akampiga yule Mfilisti na kumuua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia, wakisema: “Usiende tena pamoja nasi vitani,+ usije ukaizima+ taa+ ya Israeli!”
18 Na ikawa kwamba baada ya hayo vita vikatokea tena na Wafilisti katika Gobu. Ndipo Sibekai+ Mhusha+ akampiga Safu, aliyekuwa mmoja wa wale waliozaliwa kwa Refaimu.+
19 Na vita vikatokea tena na Wafilisti katika Gobu, na Elhanani+ mwana wa Yaare-oregimu Mbethlehemu, akampiga Goliathi Mgathi, ambaye mpini wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa wafumaji wa nguo.+
20 Na vita vikatokea tena katika Gathi,+ wakati kulipokuwa na mtu mwenye ukubwa usio wa kawaida, mwenye vidole 6 katika kila mmoja wa mikono yake na vidole 6 katika kila mmoja wa miguu yake, jumla yake 24; naye pia alikuwa amezaliwa kwa Refaimu.+ 21 Naye akaendelea kudhihaki+ Israeli. Mwishowe Yonathani+ mwana wa Shimei,+ ndugu ya Daudi, akampiga na kumuua.
22 Hao wanne walikuwa wamezaliwa kwa Refaimu katika Gathi;+ nao wakaanguka kwa mkono wa Daudi na kwa mkono wa watumishi wake.+
22 Na Daudi akamwambia Yehova maneno ya wimbo+ huu siku ambayo Yehova alikuwa amemkomboa kutoka katika mkono wa adui+ zake wote na kutoka katika mkono wa Sauli;+ 2 naye akasema:
“Yehova ni mwamba+ wangu na ngome+ yangu na Mwokoaji wangu.+
3 Mungu wangu ni mwamba+ wangu. Nitamkimbilia,
Ngao+ yangu na pembe+ yangu ya wokovu, kilele+ changu salama,
Na mahali pangu pa kukimbilia,+ Mwokozi+ wangu; unaniokoa kutoka katika jeuri.+
5 Kwa maana mashuu yanayosababisha kifo yalinizunguka;+
Kulikuwa na mafuriko ya ghafula ya watu wasiofaa kitu yaliyoendelea kuniogopesha.+
7 Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,+
Nami niliendelea kumwita Mungu wangu.+
Ndipo kutoka katika hekalu lake akaisikia sauti yangu,+
Kilio changu cha kuomba msaada kikaingia masikioni mwake.+
8 Nayo dunia ikaanza kutikisika na kutetemeka;+
Misingi ya mbingu ikasukasuka,+
Nayo ikatikisika-tikisika kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
9 Moshi ukapanda katika mianzi ya pua yake, na moto kutoka kinywani mwake ukaendelea kuteketeza;+
Makaa yakawaka moto kutoka kwake.+
11 Naye akaja akiwa amepanda juu ya kerubi,+ akaja akiwa anaruka;
Naye akaonekana juu ya mabawa ya roho.+
13 Kutoka katika mwangaza mbele yake yakawaka makaa yanayowaka ya moto.+
16 Na sakafu za vijito vya bahari zikaonekana,+
Misingi ya nchi yenye kuzaa+ ikafunuliwa,
Kwa kemeo la Yehova, kwa mlipuko wa pumzi ya pua yake.+
18 Alikuwa akinikomboa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+
Kutoka kwa wale wanaonichukia; kwa sababu walikuwa na nguvu kuliko mimi.+
20 Naye akanitoa nje mpaka mahali penye nafasi tele;+
Alikuwa akiniokoa, kwa sababu alikuwa amependezwa nami.+
23 Kwa maana maamuzi yake yote ya hukumu+ yako mbele yangu;
Na kwa habari ya sheria zake, sitageuka kando kuziacha.+
26 Kwa mtu mshikamanifu utatenda kwa ushikamanifu;+
Kwa mtu asiye na kosa, mwenye nguvu, utatenda kwa njia isiyo na kosa;+
30 Kwa maana kwa msaada wako ninaweza kukimbiza kikundi cha waporaji;+
Kwa msaada wa Mungu wangu ninaweza kuupanda ukuta.+
31 Mungu wa kweli, njia yake ni kamilifu;+
Neno la Yehova limetakaswa.+
Yeye ni ngao kwa wale wote wanaomkimbilia.+
34 Anaifanya miguu yangu iwe kama ile ya paa;+
Na kwenye mahali palipo juu kwa ajili yangu yeye huendelea kunisimamisha.+
37 Utafanyiza nafasi kubwa ya kutosha kwa ajili ya hatua zangu zilizo chini yangu;+
Navyo vifundo vya miguu yangu hakika havitatetemeka.+
39 Nami nitawaangamiza na kuwavunja vipande-vipande,+ ili wasisimame;+
Nao wataanguka chini ya miguu yangu.+
41 Nao adui zangu, utanipa upande wa nyuma wa shingo yao;+
Wale wanaonichukia vikali—nitawanyamazisha pia.+
43 Nami nitawatwanga wawe laini kama mavumbi ya udongo;
Nitawaponda kama matope ya barabarani;+
Nitawapiga niwalaze.
44 Nawe utanifanya niponyoke lawama ya watu wangu.+
Utanilinda niwe kiongozi wa mataifa;+
Watu ambao sikujua—watanitumikia.+
48 Mungu wa kweli ndiye Mpaji wa matendo ya kisasi kwangu+
Na ndiye anayeshusha vikundi vya watu chini yangu,+
49 Na ndiye anayeniondoa kwa adui zangu.+
Nawe utaniinua juu ya wale wanaosimama dhidi yangu;+
Utanikomboa kutoka kwa mtu mwenye vitendo vya jeuri.+
51 Yule anayefanya matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake+
Na kuonyesha fadhili zenye upendo kwa mtiwa-mafuta wake,+
Kwa Daudi na kwa uzao wake mpaka wakati usio na kipimo.”+
23 Na haya ndiyo maneno ya mwisho ya Daudi:+
“Neno la Daudi mwana wa Yese,+
Na neno la mwanamume aliyeinuliwa juu,+
Mtiwa-mafuta+ wa Mungu wa Yakobo,
Na mwenye kupendeza wa muziki+ wa Israeli.
3 Mungu wa Israeli alisema,
Mwamba wa Israeli aliniambia,+
‘Wakati yeye anayetawala juu ya wanadamu ni mwadilifu,+
Akitawala kwa kumwogopa Mungu,+
4 Basi ni kama nuru ya asubuhi, jua linapoangaza,
Asubuhi isiyo na mawingu.+
Kutokana na mwangaza, kutokana na mvua, majani hutoka katika nchi.’+
5 Kwa maana je, sivyo ilivyo nyumba yangu kwa Mungu?+
Kwa sababu amenipa agano+ linalodumu mpaka wakati usio na kipimo,
Likiwa limepangwa kwa utaratibu katika kila kitu na likiwa salama.+
Kwa sababu ndilo wokovu+ wangu wote na kupendezwa kwangu kwote,
Je, hiyo siyo sababu atalifanya likue?+
6 Lakini watu wasiofaa kitu+ hufukuziwa mbali,+ wote, kama miti ya miiba;+
Kwa maana haipaswi kuchukuliwa kwa mkono.
7 Mtu anapoigusa
Anapaswa kuwa na silaha kamili za chuma na mpini wa mkuki,
Nayo itateketezwa kabisa kwa moto.”+
8 Haya ndiyo majina ya wale wanaume wenye nguvu+ waliokuwa wa Daudi: Yosheb-bashebethi+ Mtakemoni, kichwa cha wale watatu. Alikuwa akitikisa mkuki wake juu ya watu mia nane waliouawa kwa wakati mmoja. 9 Na baada yake Eleazari+ mwana wa Dodo+ mwana wa Ahohi alikuwa kati ya wale wanaume watatu wenye nguvu ambao walikuwa na Daudi walipowadhihaki Wafilisti. Walikuwa wamejikusanya hapo kwa ajili ya vita, na kwa hiyo watu wa Israeli wakarudi nyuma.+ 10 Yeye ndiye aliyesimama, akawapiga na kuwaua Wafilisti mpaka mkono wake ukachoka na mkono wake ukaendelea kuushika upanga,+ hivi kwamba Yehova akatimiza wokovu mkuu siku hiyo;+ lakini nao watu wakarudi nyuma yake ili tu wawavue nyara wale waliopigwa na kuuawa.+
11 Na baada yake kulikuwa na Shamma mwana wa Agee, Mharari.+ Nao Wafilisti wakajikusanya kule Lehi, ambapo palikuwa na eneo la shamba lililojaa dengu;+ na watu wakakimbia kwa sababu ya Wafilisti. 12 Lakini yeye akasimama katikati ya lile shamba, akalikomboa, naye akaendelea kuwapiga na kuwaua Wafilisti, hivi kwamba Yehova akatimiza wokovu mkubwa.+
13 Na watatu kati ya wale 30 waliokuwa vichwa+ wakashuka, wakaja kwa Daudi wakati wa mavuno, katika pango la Adulamu;+ na kijiji cha mahema cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika nchi tambarare ya chini ya Refaimu.+ 14 Na wakati huo Daudi alikuwa katika mahali palipo pagumu kufikiwa;+ na wakati huo kituo cha mbele+ cha Wafilisti kilikuwa katika Bethlehemu. 15 Baada ya muda Daudi akaonyesha tamaa yake na kusema: “Laiti ningekunywa maji kutoka katika tangi la Bethlehemu lililoko langoni!”+ 16 Ndipo wale wanaume watatu wenye nguvu wakaingia kwa nguvu katika kambi ya Wafilisti, wakateka maji kutoka katika lile tangi la Bethlehemu lililoko langoni, wakaja wakiwa wameyachukua na kumletea Daudi;+ naye hakukubali kuyanywa, bali akayamwaga+ mbele za Yehova. 17 Naye akaendelea kusema: “Ni jambo lisiloweza kuwaziwa kwangu,+ Ee Yehova, kwamba nifanye hivi! Je, ninywe damu+ ya watu wanaoenda kwa kuhatarisha nafsi zao?” Naye hakukubali kuyanywa.
Hayo ndiyo mambo ambayo wale wanaume watatu wenye nguvu walifanya.
18 Naye Abishai+ ndugu ya Yoabu mwana wa Seruya,+ alikuwa kichwa cha wale 30, naye alitikisa mkuki wake juu ya watu 300 waliouawa, naye alikuwa na sifa kama wale watatu.+ 19 Ingawa alikuwa mashuhuri kuliko hata wale wengine 30, naye akawa mkuu wao, hakufikia daraja la wale watatu wa kwanza.+
20 Naye Benaya+ mwana wa Yehoyada+ mwana wa mwanamume shujaa, aliyefanya matendo mengi katika Kabzeeli,+ yeye mwenyewe alipiga na kuwaua wale wana wawili wa Arieli wa Moabu; naye alishuka, akapiga na kumuua simba+ ndani ya shimo la maji katika siku ya kuanguka kwa theluji.+ 21 Naye ndiye aliyempiga na kumuua yule mwanamume Mmisri aliyekuwa mkubwa isivyo kawaida.+ Ingawa mkononi mwa yule Mmisri kulikuwa na mkuki, bado yeye alishuka kumwendea akiwa na fimbo, akaunyakua ule mkuki kutoka mkononi mwa yule Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.+ 22 Benaya+ mwana wa Yehoyada alifanya mambo hayo; naye alikuwa na sifa kama wale wanaume watatu wenye nguvu.+ 23 Ingawa yeye alikuwa mashuhuri hata kuliko wale 30, hakufikia daraja la wale watatu; lakini Daudi alimweka awe kati ya walinzi wake.+
24 Asaheli+ ndugu ya Yoabu alikuwa kati ya wale 30; Elhanani+ mwana wa Dodo wa Bethlehemu, 25 Shamma+ Mharodi, Elika Mharodi, 26 Helezi+ Mpeleti, Ira+ mwana wa Ikeshi+ Mtekoa, 27 Abiezeri+ Mwanathothi,+ Mebunai Mhusha,+ 28 Salmoni Mwahohi,+ Maharai+ Mnetofa, 29 Helebu+ mwana wa Baana Mnetofa, Itai+ mwana wa Ribai wa Gibea wa wana wa Benyamini, 30 Benaya+ Mpirathoni, Hidai wa mabonde ya mto ya Gaashi,+ 31 Abi-alboni Mwarbathi, Azmavethi+ Mbarhumu, 32 Eliaba Mshaalboni, wana wa Yasheni, Yonathani,+ 33 Shamma Mharari, Ahiamu,+ mwana wa Sharari Mharari, 34 Elifeleti mwana wa Ahasbai mwana wa yule Mmaakathi, Eliamu mwana wa Ahithofeli+ Mgiloni, 35 Hezro+ Mkarmeli, Paarai Mwarabi, 36 Igali mwana wa Nathani+ wa Soba, Bani Mgadi, 37 Seleki+ Mwamoni, Naharai Mbeerothi, wachukua-silaha wa Yoabu mwana wa Seruya, 38 Ira Mwithri,+ Garebu+ Mwithri, 39 Uria+ Mhiti—jumla ya watu 37.
24 Tena+ hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli, wakati mtu fulani alipomchochea Daudi juu yao, akisema: “Nenda, uhesabu+ Israeli na Yuda.” 2 Basi mfalme akamwambia Yoabu,+ mkuu wa majeshi aliyekuwa pamoja naye: “Tafadhali, tembea katika makabila yote ya Israeli, kutoka Dani mpaka Beer-sheba,+ nanyi mwandikishe watu,+ nami kwa hakika nitaijua hesabu ya watu.”+ 3 Lakini Yoabu akamwambia mfalme: “Yehova Mungu wako na aongeze watu wawe wengi mara mia kuliko walivyo wakati macho ya bwana wangu mfalme yanapoliona jambo hilo. Hata hivyo, kwa nini bwana wangu mfalme amependezwa na jambo hili?”+
4 Mwishowe neno la mfalme likamshinda+ Yoabu na wakuu wa majeshi. Basi Yoabu na wakuu wa majeshi wakatoka mbele ya mfalme, wakaenda kuwaandikisha+ watu wa Israeli. 5 Ndipo wakavuka Yordani, wakapiga kambi katika Aroeri+ upande wa kuume wa jiji lililoko katikati ya bonde la mto, kuelekea Wagadi,+ na kwenda Yazeri.+ 6 Kisha wakafika mpaka Gileadi+ na nchi ya Tahtim-hodshi, wakaendelea mpaka Dani-yaani nao wakazunguka mpaka Sidoni.+ 7 Ndipo wakafika kwenye ngome ya Tiro+ na majiji yote ya Wahivi+ na ya Wakanaani, nao wakafika ncha ya mwisho katika Negebu+ ya Yuda kule Beer-sheba.+ 8 Kwa hiyo wakaenda wakizunguka katika nchi yote, nao wakaja Yerusalemu mwisho wa miezi 9 na siku 20. 9 Kisha Yoabu akampa mfalme hesabu ya watu walioandikishwa;+ na Israeli wakawa jumla ya wanaume mashujaa mia nane elfu wenye kutumia upanga, na wanaume wa Yuda wakawa mia tano elfu.+
10 Na moyo wa Daudi ukaanza kumpiga+ baada ya kuwahesabu watu. Basi Daudi akamwambia Yehova: “Nimetenda dhambi+ sana kwa lile ambalo nimefanya. Na sasa, Yehova, tafadhali acha kosa la mtumishi wako lipitilie mbali;+ kwa maana nimetenda kwa upumbavu sana.”+ 11 Wakati Daudi alipoamka asubuhi, neno la Yehova likamjia Gadi+ nabii, mwonaji+ wa Daudi, na kusema: 12 “Nenda, umwambie Daudi, ‘Yehova amesema hivi: “Ninakuwekea mambo matatu.+ Jichagulie mwenyewe moja kati ya hayo ili nikutendee hilo.”’”+ 13 Basi Gadi akaingia kwa Daudi, akamwambia:+ “Je, njaa ikujie katika nchi yako kwa miaka saba,+ au miezi mitatu ya wewe kukimbia mbele ya adui zako,+ wakikufuatilia, au kuwe na siku tatu za tauni katika nchi yako?+ Sasa ujue na uone jibu nitakalompelekea Yeye aliyenituma.” 14 Kwa hiyo Daudi akamwambia Gadi: “Ni jambo lenye kunitaabisha sana. Tafadhali, acha tuanguke mkononi mwa Yehova,+ kwa maana rehema zake ni nyingi;+ lakini usiniache nianguke mkononi mwa mwanadamu.”+
15 Ndipo Yehova akaleta tauni+ katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka wakati uliowekwa, hivi kwamba kati ya watu kutoka Dani mpaka Beer-sheba+ watu 70,000 wakafa.+ 16 Na malaika+ akaendelea kunyoosha mkono wake kuelekea Yerusalemu ili kuliangamiza; na Yehova akaanza kujuta+ kuhusu msiba ule, na kwa hiyo akamwambia yule malaika aliyekuwa akiwaangamiza watu: “Imetosha! Sasa angusha mkono wako.” Na yule malaika wa Yehova alikuwa karibu na uwanja wa kupuria wa Arauna+ Myebusi.+
17 Na Daudi akamwambia Yehova, wakati alipomwona yule malaika aliyekuwa akiwapiga na kuwaua watu, ndiyo, akasema: “Tazama, mimi ndiye niliyetenda dhambi, nami ndiye niliyefanya kosa; lakini kondoo+ hawa—wamefanya nini? Tafadhali, acha mkono wako uje juu yangu+ na juu ya nyumba ya baba yangu.”
18 Baadaye Gadi akaingia kwa Daudi siku hiyo na kumwambia: “Nenda, umsimamishie Yehova madhabahu kwenye uwanja wa kupuria wa Arauna Myebusi.”+ 19 Na Daudi akaanza kupanda, kulingana na neno la Gadi, kulingana na alivyoamuru Yehova.+ 20 Wakati Arauna alipotazama chini, akamwona mfalme na watumishi wake wakimjia, mara moja Arauna akatoka nje, akamwinamia+ mfalme kifudifudi.+ 21 Kisha Arauna akasema: “Kwa nini bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Ndipo Daudi akasema: “Ili kununua+ kutoka kwako uwanja wa kupuria kwa ajili ya kumjengea Yehova madhabahu, ili tauni+ ikomeshwe juu ya watu.” 22 Lakini Arauna akamwambia Daudi: “Acha bwana wangu mfalme auchukue+ na afanye toleo la kilicho chema machoni pake. Tazama, ng’ombe ni hawa kwa ajili ya toleo la kuteketezwa na chombo cha kupuria na vifaa vya ng’ombe kwa ajili ya kuni.+ 23 Ee mfalme, Arauna anampa mfalme kila kitu.” Na Arauna akaendelea kumwambia mfalme: “Yehova Mungu wako na akufurahie.”+
24 Hata hivyo, mfalme akamwambia Arauna: “Hapana, bali bila shaka nitaununua kutoka kwako kwa bei fulani;+ nami sitamtolea Yehova Mungu wangu matoleo ya kuteketezwa bila gharama.”+ Basi Daudi akaununua+ ule uwanja wa kupuria na wale ng’ombe kwa shekeli 50 za fedha. 25 Na Daudi akamjengea Yehova madhabahu+ hapo na kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika, na Yehova akakubali kusihiwa+ kwa ajili ya nchi, hivi kwamba ile tauni ikakomeshwa juu ya Israeli.
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.