Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 1 Samweli 1:1-31:13
  • Kitabu cha Kwanza cha Samweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitabu cha Kwanza cha Samweli
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Kitabu cha Kwanza cha Samweli

Kitabu cha Kwanza cha Samweli

au, kulingana na Septuajinti ya Kigiriki, KITABU CHA KWANZA CHA WAFALME

1 Na palikuwa na mtu wa Ramathaim-sofimu+ wa eneo lenye milima la Efraimu,+ na jina lake lilikuwa Elkana,+ mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu, mwana wa Tohu, mwana wa Sufu,+ Mwefraimu. 2 Naye alikuwa na wake wawili, jina la mmoja lilikuwa Hana, na jina la yule mwingine lilikuwa Penina. Na Penina akaja kuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na watoto.+ 3 Na mtu huyo akawa akipanda kutoka jiji lake mwaka baada ya mwaka ili kusujudu+ na kutoa dhabihu kwa Yehova wa majeshi huko Shilo.+ Na hapo ndipo wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi,+ walikuwa makuhani kwa Yehova.+

4 Na ikafika siku ambapo Elkana alitoa dhabihu, naye akawapa mafungu Penina mke wake na wanawe na binti zake wote;+ 5 lakini akampa Hana fungu moja. Hata hivyo, alimpenda Hana.+ Lakini Yehova alikuwa amefunga tumbo lake la uzazi.+ 6 Na yule mke mwenzake alimsumbua+ mno pia hata kumfadhaisha kwa sababu Yehova alikuwa amefunga tumbo lake la uzazi. 7 Naye akawa akifanya hivyo mwaka baada ya mwaka,+ kila mara alipopanda kwenda katika nyumba ya Yehova.+ Akawa akimsumbua hivyo, hivi kwamba akawa akilia na kukataa kula. 8 Naye Elkana mume wake akamwambia: “Hana, kwa nini unalia, na kwa nini huli chakula, na kwa nini moyo wako unahisi vibaya?+ Je, mimi si bora kwako kuliko wana kumi?”+

9 Ndipo Hana akasimama baada ya wao kula huko Shilo na baada ya kunywa, huku Eli kuhani akiwa ameketi juu ya kiti kilicho kando ya mwimo wa mlango wa hekalu+ la Yehova. 10 Na huyo mwanamke alikuwa na uchungu katika nafsi,+ akaanza kusali+ kwa Yehova na kulia sana.+ 11 Naye akaweka nadhiri,+ akisema: “Ee Yehova wa majeshi, ikiwa hakika utayaona mateso ya kijakazi+ wako, nawe kwa kweli unikumbuke,+ na ikiwa hutamsahau kijakazi wako na kwa kweli umpe kijakazi wako uzao wa kiume, mimi nitamtoa kwa Yehova siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita juu ya kichwa chake.”+

12 Na ikatukia kwamba, alipokuwa akisali kwa muda mrefu+ mbele za Yehova, Eli alikuwa anakitazama kinywa chake. 13 Lakini Hana alikuwa akisema moyoni mwake;+ midomo yake tu ndiyo ilikuwa ikitetemeka, na sauti yake haikusikika. Lakini Eli alimdhania kuwa amelewa.+ 14 Kwa hiyo Eli akamwambia: “Utaendelea kujiendesha kama mlevi mpaka wakati gani?+ Iondolee mbali divai yako.” 15 Ndipo Hana akajibu na kusema: “Hapana, bwana wangu! Mimi ni mwanamke aliyekazwa sana rohoni; nami sijanywa divai wala kileo, bali ninamwaga nafsi yangu mbele za Yehova.+ 16 Usimdhanie kijakazi wako kuwa mwanamke asiyefaa kitu,+ kwa maana ni kutokana na wingi wa mahangaiko yangu na usumbufu wangu kwamba nimesema mpaka sasa.”+ 17 Ndipo Eli akajibu na kusema: “Nenda kwa amani,+ naye Mungu wa Israeli akupe ombi lako ambalo umemwomba.”+ 18 Naye akasema: “Mjakazi wako na apate kibali machoni pako.”+ Ndipo mwanamke huyo akaenda zake, akala chakula,+ na uso wake haukuonyesha tena kuhangaika.+

19 Ndipo wakaamka asubuhi na mapema na kusujudu mbele za Yehova, baadaye wakarudi, wakaja nyumbani kwao huko Rama.+ Basi Elkana akalala+ na Hana mke wake, na Yehova akaanza kumkumbuka.+ 20 Kwa hiyo ikawa mwishoni mwa mwaka kwamba Hana akachukua mimba, akamzaa mwana, akamwita jina+ lake Samweli, kwa maana alisema, “Nimemwomba kutoka kwa Yehova.”+

21 Baada ya muda yule mtu, Elkana, akapanda pamoja na nyumba yake yote kwenda kumtolea Yehova dhabihu+ ya kila mwaka na toleo lake la nadhiri.+ 22 Lakini Hana hakupanda,+ kwa maana alikuwa amemwambia mume wake: “Mara mvulana huyu atakapoachishwa kunyonya,+ nitampeleka, naye ataonekana mbele za Yehova na kukaa huko mpaka wakati usio na kipimo.”+ 23 Ndipo Elkana mume+ wake akamwambia: “Fanya inavyoonekana vema machoni pako.+ Kaa nyumbani mpaka utakapomwachisha kunyonya. Ila tu Yehova na alitimize neno lake.”+ Basi mwanamke huyo akakaa nyumbani, akaendelea kumnyonyesha mwana wake mpaka alipomwachisha kunyonya.+

24 Kwa hiyo mara tu alipomwachisha kunyonya, akapanda pamoja naye, pamoja na ng’ombe-dume wa miaka mitatu na efa moja ya unga na mtungi mkubwa wa divai,+ naye akaingia ndani ya nyumba ya Yehova katika Shilo.+ Na huyo mvulana alikuwa pamoja naye. 25 Kisha wakamchinja yule ng’ombe na kumleta yule mvulana kwa Eli.+ 26 Ndipo akasema: “Nakuomba radhi, bwana wangu! Kama inavyoishi nafsi+ yako, bwana wangu, mimi ndiye yule mwanamke aliyekuwa amesimama pamoja nawe mahali hapa ili kusali kwa Yehova.+ 27 Ilikuwa kuhusu mvulana huyu kwamba nilisali ili Yehova anipe ombi+ langu nililomwomba.+ 28 Na mimi nimemwazima Yehova+ mvulana huyu. Siku zote atakazokuwapo, yeye ni mtu aliyeombwa kwa ajili ya Yehova.”

Naye Elkana akainama hapo mbele za Yehova.+

2 Naye Hana akasali+ na kusema:

“Moyo wangu unafurahi katika Yehova,+

Pembe yangu kweli imeinuliwa katika Yehova.+

Kinywa changu kimepanuliwa juu ya adui zangu,

Kwa maana ninashangilia katika wokovu kutoka kwako.+

 2 Hakuna aliye mtakatifu kama Yehova, kwa maana hakuna mwingine isipokuwa wewe;+

Na hakuna mwamba ulio kama Mungu wetu.+

 3 Ninyi msiseme kwa majivuno sana,

Msiache jambo lolote litoke vinywani mwenu bila kuzuiwa,+

Kwa maana Yehova ni Mungu wa ujuzi,+

Naye hupima matendo kwa njia ya haki.+

 4 Wanaume wenye nguvu wanaopiga upinde wamejawa na woga,+

Lakini wale wanaojikwaa hujizungusha nguvu katika viuno.+

 5 Walioshiba lazima wajikodishe kwa ajili ya mkate,+

Lakini wenye njaa hakika hawapati njaa tena.+

Hata aliye tasa amezaa saba,+

Lakini yeye aliyekuwa na wana wengi amedhoofika.+

 6 Yehova ni Mwenye Kuua na Mwenye Kuhifadhi uhai,+

Ni Mwenye Kushusha mpaka katika Kaburi,*+ na Yeye huinua.+

 7 Yehova ni Mwenye Kuleta Umaskini+ na Mwenye Kutajirisha,+

Ni Mwenye Kushusha, pia Mwenye Kuinua,+

 8 Ni Mwenye Kuinua mtu wa hali ya chini kutoka mavumbini;+

Humwinua maskini kutoka katika shimo la majivu,+

Ili awafanye wakae pamoja na watu wenye vyeo; naye huwapa urithi+ wa kiti cha ufalme cha utukufu.+

Kwa maana nguzo za dunia+ ni za Yehova,

Naye huiweka nchi yenye kuzaa juu ya hizo.

 9 Yeye hulinda miguu ya washikamanifu wake;+

Lakini kwa habari ya waovu, wao wananyamazishwa katika giza,+

Kwa maana si kwamba mwanadamu hushinda kwa ukuu wa nguvu.+

10 Wale wanaoshindana na Yehova wataingiwa na woga;+

Atanguruma juu yao kutoka mbinguni.+

Yehova mwenyewe ataihukumu miisho ya dunia,+

Ili ampe mfalme wake nguvu,+

Ili ainue pembe ya mtiwa-mafuta wake.”+

11 Basi Elkana akaenda Rama nyumbani kwake; na yule mvulana akawa mhudumu+ wa Yehova mbele ya Eli kuhani.

12 Basi wana wa Eli walikuwa watu wasiofaa kitu;+ hawakumtambua Yehova.+ 13 Na kwa habari ya haki inayostahiliwa ya makuhani kutoka kwa watu,+ wakati ambapo mtu yeyote alipokuwa akitoa dhabihu, mtumishi wa kuhani alikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake, nyama ilipoanza tu kutokota,+ 14 na kuutia kwa nguvu ndani ya beseni au chungu cha kupikia chenye mikono miwili au sufuria au chungu cha kupikia chenye mkono mmoja. Chochote ambacho uma huo ulichukua kutoka ndani, kuhani alijichukulia. Hivyo ndivyo walivyofanya katika Shilo kwa Waisraeli wote waliokuja huko.+ 15 Pia, hata kabla ya kufukiza moshi wa mafuta,+ mtumishi wa kuhani alikuwa akija na kumwambia mtu anayetoa dhabihu: “Nipe nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani ili apokee kutoka kwako nyama mbichi wala si ile iliyotokoswa.”+ 16 Wakati mtu huyo angemwambia: “Acha kwanza wafukize moshi wa mafuta.+ Kisha ujichukulie chochote ambacho nafsi yako inatamani,”+ yeye hakika alisema: “Hapana, lazima unipe sasa; ikiwa sivyo, nitaichukua kwa nguvu!”+ 17 Na dhambi ya watumishi hao ikaja kuwa kubwa sana mbele za Yehova;+ kwa kuwa watu hao hawakuliheshimu toleo la Yehova.+

18 Naye Samweli alikuwa akihudumu+ mbele za Yehova, akiwa mvulana, amejifunga efodi ya kitani.+ 19 Pia, mama yake alikuwa akimfanyizia koti dogo lisilo na mikono, na kumletea mwaka baada ya mwaka alipopanda pamoja na mume wake ili kutoa dhabihu ya kila mwaka.+ 20 Na Eli akambariki+ Elkana na mke wake, akasema: “Yehova na akupe uzao kutoka kwa mke huyu badala ya kile kitu cha kuazima, ambacho Yehova aliazimwa.”+ Nao wakaenda kwao. 21 Basi Yehova akageuza fikira zake kwa Hana,+ akachukua mimba, akazaa wana watatu na binti wawili.+ Na yule mvulana Samweli akaendelea kukua akiwa na Yehova.+

22 Na Eli alikuwa amezeeka sana, naye alikuwa ameyasikia+ yote ambayo wanawe walizidi kuwatendea+ Israeli wote na jinsi walivyokuwa wakilala na wanawake+ waliokuwa wakitumikia katika mwingilio wa hema la mkutano.+ 23 Naye alikuwa akiwaambia:+ “Kwa nini mnazidi kufanya mambo kama haya?+ Kwa maana mambo ninayoyasikia kuhusu ninyi kutoka kwa watu wote ni mabaya.+ 24 Hapana,+ wanangu, kwa sababu habari ninazosikia si nzuri, ambazo watu wa Yehova wanaeneza.+ 25 Mwanadamu akifanya dhambi juu ya mwanadamu,+ Mungu atakuwa mwamuzi wake;+ lakini mwanadamu akifanya dhambi juu ya Yehova,+ ni nani atakayetoa sala kwa ajili yake?”+ Lakini hawakuisikiliza sauti ya baba+ yao, kwa sababu sasa Yehova alitaka kuwaua.+ 26 Na wakati huo wote mvulana Samweli alikuwa akiendelea kukua na kupendwa na Yehova na vilevile na wanadamu.+

27 Na mtu wa Mungu+ akamjia Eli na kumwambia: “Yehova amesema hivi, ‘Je, kweli sikujifunua kwa nyumba ya babu yako walipokuwa Misri wakiwa watumwa kwa nyumba ya Farao?+ 28 Naye alichaguliwa kwa ajili yangu kutoka kwa makabila yote ya Israeli,+ awe kuhani na kupanda juu ya madhabahu+ yangu ili afukize moshi wa dhabihu, avae efodi mbele zangu, ili niipe nyumba ya babu yako matoleo yote ya wana wa Israeli yaliyotolewa kwa njia ya moto.+ 29 Kwa nini mnaendelea kuipiga teke dhabihu+ yangu na toleo langu ambalo nimeamuru katika makao yangu,+ nawe unaendelea kuwaheshimu wana wako kuliko mimi kwa ninyi kujinenepesha+ kutokana na sehemu bora zaidi za kila toleo la watu wangu Israeli?+

30 “‘Kwa sababu hiyo, hili ndilo neno la Yehova Mungu wa Israeli: “Hakika nilisema, Nyumba yako na nyumba ya babu yako, watatembea mbele zangu daima.”+ Lakini sasa hili ndilo neno la Yehova: “Ni jambo lisilowaziwa kwangu, kwa sababu wale wanaoniheshimu+ nitawaheshimu,+ na wale wanaonidharau watahesabiwa kuwa si kitu.”+ 31 Tazama! Siku zinakuja ambazo hakika nitaukata mkono wako na mkono wa nyumba ya babu yako, ili kusiweko kamwe na mzee katika nyumba yako.+ 32 Nawe kwa kweli utamwona adui katika makao yangu kati ya mema yote yanayofanyiwa Israeli;+ wala hakutakuwako kamwe na mzee katika nyumba yako. 33 Hata hivyo, kuna mwanamume wa kwako ambaye sitamkatilia mbali asiwe kwenye madhabahu yangu ili kuyafanya macho yako yafifie na kuidhoofisha nafsi yako; lakini hesabu kubwa ya nyumba yako watakufa wote kwa upanga wa wanadamu.+ 34 Na hii ndiyo ishara kwako itakayokuja kwa wana wako wawili, Hofni na Finehasi:+ Wote wawili watakufa katika siku moja.+ 35 Nami hakika nitajiinulia kuhani+ mwaminifu. Atafanya kupatana na yaliyo katika moyo wangu na yaliyo katika nafsi yangu; nami nitamjengea nyumba inayodumu, naye atatembea mbele ya mtiwa-mafuta+ wangu siku zote. 36 Na itatukia kwamba yeyote atakayebaki+ katika nyumba yako atakuja na kumwinamia kwa ajili ya malipo ya pesa na mkate wa mviringo, naye atasema: “Tafadhali, niweke katika kimoja cha vyeo vya kikuhani ili nile kipande cha mkate.”’”+

3 Wakati huo wote mvulana Samweli alikuwa akimhudumia+ Yehova mbele ya Eli, na neno kutoka kwa Yehova+ lilikuwa limekuwa haba siku hizo;+ hakuna maono+ yoyote yaliyokuwa yakienezwa kotekote.

2 Na ikawa kwamba siku hiyo Eli alikuwa amelala mahali pake, na macho yake yalikuwa yameanza kuingia giza;+ hakuweza kuona. 3 Na taa ya Mungu ilikuwa haijazimwa bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu+ la Yehova, palipokuwa sanduku la Mungu. 4 Na Yehova akaanza kumwita Samweli. Naye akasema: “Mimi hapa.”+ 5 Naye akakimbia, akaenda kwa Eli na kusema: “Mimi hapa, kwa maana umeniita.” Lakini yeye akasema: “Sikukuita. Lala tena.” Basi akaenda, akalala. 6 Na Yehova akaita tena: “Samweli!”+ Naye Samweli akaamka, akaenda kwa Eli na kusema: “Mimi hapa, kwa maana umeniita.” Lakini yeye akasema: “Sikukuita, mwanangu.+ Lala tena.” 7 (Lakini Samweli alikuwa bado hajamjua Yehova, na neno la Yehova lilikuwa bado halijaanza kufunuliwa kwake.)+ 8 Basi Yehova akaita tena mara ya tatu: “Samweli!” Naye akaamka, akaenda kwa Eli na kusema: “Mimi hapa, kwa maana haikosi kwamba umeniita.”

Naye Eli akaanza kutambua kwamba Yehova ndiye aliyekuwa akimwita yule mvulana. 9 Kwa hiyo Eli akamwambia Samweli: “Nenda, ulale, na itatukia kwamba akikuita, useme hivi, ‘Sema, Yehova, kwa maana mtumishi wako anasikiliza.’” Basi Samweli akaenda, akalala mahali pake.

10 Ndipo Yehova akaja na kusimama hapo, akaita kama katika zile nyakati za kwanza: “Samweli, Samweli!” Ndipo Samweli akasema: “Sema, kwa maana mtumishi wako anasikiliza.”+ 11 Na Yehova akaendelea kumwambia Samweli: “Tazama! Ninafanya+ jambo katika Israeli ambalo yeyote akilisikia, masikio yake mawili yatawasha.+ 12 Siku hiyo nitamtimizia Eli yote ambayo nimesema kwa habari ya nyumba yake, kutoka mwanzo mpaka mwisho.+ 13 Nawe unapaswa kumwambia kwamba naihukumu nyumba yake+ mpaka wakati usio na kipimo kwa sababu ya kosa ambalo amelijua,+ kwa sababu wanawe wanamlaani Mungu,+ lakini yeye hakuwakemea.+ 14 Na hiyo ndiyo sababu nimeiapia nyumba ya Eli kwamba adhabu ya kosa la nyumba ya Eli haitaondolewa kwa dhabihu wala kwa toleo mpaka wakati usio na kipimo.”+

15 Naye Samweli akaendelea kulala mpaka asubuhi. Kisha akafungua milango ya nyumba ya Yehova.+ Na Samweli akaogopa kumwambia Eli maono hayo.+ 16 Lakini Eli akamwita Samweli na kusema: “Samweli, mwanangu!” Naye akasema: “Mimi hapa.” 17 Naye akaendelea kusema: “Ni neno gani alilosema nawe? Tafadhali usinifiche hilo.+ Mungu na akufanyie hivyo naye aliongezee+ hilo ukinificha neno moja kati ya maneno yote ambayo amekuambia.” 18 Basi Samweli akamwambia maneno hayo yote, wala hakumficha lolote. Ndipo yeye akasema: “Ni Yehova. Na afanye yaliyo mema machoni pake.”+

19 Na Samweli akaendelea kukua, na Yehova akawa pamoja naye,+ wala hakuacha neno lake lolote lianguke chini.+ 20 Na Israeli wote kutoka Dani mpaka Beer-sheba+ wakajua kwamba Samweli ndiye aliyewekwa kuwa nabii wa Yehova.+ 21 Na Yehova akatokea tena+ katika Shilo, kwa kuwa Yehova alijifunua kwa Samweli katika Shilo kwa neno lake Yehova.+

4 Na neno la Samweli likaendelea kuwajia Israeli wote.

Ndipo Israeli wakatoka ili kukutana na Wafilisti katika pigano; nao wakapiga kambi kando ya Ebenezeri,+ Wafilisti nao wakapiga kambi katika Afeki.+ 2 Na Wafilisti wakajipanga+ ili kukutana na Israeli, na pigano hilo likaenda vibaya, hivi kwamba Israeli wakashindwa mbele ya Wafilisti,+ ambao waliwapiga na kuwaua karibu watu elfu nne katika pigano uwanjani. 3 Watu walipokuja kambini, wanaume wazee wa Israeli wakaanza kusema: “Kwa nini Yehova alitushinda leo mbele ya Wafilisti?+ Na tujichukulie kutoka Shilo sanduku la agano la Yehova,+ ili lije katikati yetu na kutuokoa kutoka mkononi mwa adui zetu.” 4 Basi watu wakatuma ujumbe huko Shilo na kuchukua kutoka huko sanduku la agano la Yehova wa majeshi, anayeketi juu ya makerubi.+ Na wale wana wawili wa Eli walikuwa hapo pamoja na sanduku la agano la Mungu wa kweli, yaani, Hofni na Finehasi.+

5 Na ikawa kwamba mara sanduku la agano la Yehova lilipoingia katika kambi, Waisraeli wote wakaanza kupiga kelele kubwa,+ hata dunia ikavurugika. 6 Nao Wafilisti pia wakasikia sauti ya kelele hizo, wakaanza kusema: “Hii sauti ya hizi kelele kubwa+ katika kambi ya Waebrania inamaanisha nini?” Mwishowe wakaja kujua kwamba sanduku la Yehova lilikuwa limekuja katika kambi. 7 Nao Wafilisti wakaogopa, kwa sababu walisema: “Mungu ameingia kambini!”+ Basi wakasema: “Ole wetu, kwa maana jambo kama hili halijatokea kamwe tangu hapo mwanzoni! 8 Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka katika mkono wa huyu Mungu mtukufu? Huyu ndiye Mungu aliyepiga Misri kwa kila namna ya mauaji katika nyika.+ 9 Mjionyeshe kuwa hodari na kujiendesha kama wanaume, enyi Wafilisti, ili msije kuwatumikia Waebrania kama vile wao walivyowatumikia ninyi;+ mjiendeshe kama wanaume, mkapigane!” 10 Basi Wafilisti wakapigana, na Israeli wakashindwa,+ nao wakakimbia kila mmoja kwenda katika hema lake;+ na mauaji hayo yakawa makubwa sana,+ hivi kwamba katika Israeli wakaanguka watu 30,000 wenye kwenda kwa miguu.+ 11 Nalo sanduku la Mungu likatekwa,+ na wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakafa.+

12 Na mtu fulani wa Benyamini akakimbia kutoka katika uwanja wa mapigano, akafika Shilo siku hiyo huku mavazi yake yakiwa yameraruliwa,+ na mavumbi yakiwa juu ya kichwa chake.+ 13 Alipofika, Eli alikuwa amekalia kiti kando ya barabara, akitazama, kwa kuwa moyo wake ulikuwa ukitetemeka kwa sababu ya lile sanduku la Mungu wa kweli.+ Na yule mtu akaenda kutoa habari jijini, na jiji lote likaanza kulia. 14 Na Eli akasikia sauti za vilio hivyo. Basi akasema: “Sauti ya machafuko haya inamaanisha nini?”+ Yule mtu akafanya haraka ili aingie na kumpa Eli habari. 15 (Basi Eli alikuwa na umri wa miaka 98, na macho yake yalikuwa yameganda, asiweze kuona.)+ 16 Na yule mtu akamwambia Eli: “Mimi ndiye ninayetoka katika uwanja wa mapigano, nami—nimekimbia leo kutoka katika uwanja wa mapigano.” Naye akasema: “Ni jambo gani limetendeka, mwanangu?” 17 Basi yule mleta-habari akajibu na kusema: “Israeli wamekimbia mbele ya Wafilisti, na pia watu wameshindwa vibaya sana;+ hata wana wako wawili wamekufa pia—Hofni na Finehasi+—nalo sanduku la Mungu wa kweli limetekwa.”+

18 Na ikawa kwamba mara alipotaja sanduku la Mungu wa kweli, akaanguka nyuma kutoka kwenye kiti kando ya lango, na shingo yake ikavunjika, akafa, kwa sababu mwanamume huyo alikuwa mzee tena mzito; naye alikuwa amehukumu Israeli kwa miaka 40. 19 Na binti-mkwe wake, mke wa Finehasi, alikuwa na mimba karibu na kuzaa, naye akasikia habari kwamba sanduku la Mungu wa kweli limetekwa na kwamba baba-mkwe wake na mume wake wamekufa. Kwa hiyo akainama, akaanza kuzaa, kwa sababu uchungu wake ulimjia bila kutazamiwa.+ 20 Na karibu na wakati wa kifo chake, wanawake waliokuwa wamesimama kando yake wakaanza kusema: “Usiogope, kwa maana umezaa mwana.”+ Naye hakujibu wala kuweka moyo wake juu ya maneno hayo. 21 Lakini akamwita mvulana huyo jina Ikabodi,+ akisema: “Utukufu umeondoka katika Israeli kwenda uhamishoni,”+ hayo alisema kuhusu sanduku la Mungu wa kweli lililotekwa na kuhusu baba-mkwe wake na mume wake.+ 22 Basi akasema: “Utukufu umeondoka katika Israeli kwenda uhamishoni,+ kwa sababu sanduku la Mungu wa kweli limetekwa.”+

5 Basi Wafilisti wakalichukua lile sanduku+ la Mungu wa kweli, wakalibeba kutoka Ebenezeri mpaka Ashdodi.+ 2 Na Wafilisti wakalichukua sanduku la Mungu wa kweli, wakaliingiza ndani ya nyumba ya Dagoni na kulisimamisha kando ya Dagoni.+ 3 Kisha Waashdodi wakaamka mapema kesho yake, na tazama, Dagoni alikuwa ameanguka kifudifudi mbele ya sanduku la Yehova.+ Basi wakamchukua Dagoni na kumrudisha mahali pake.+ 4 Walipoamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, tazama, Dagoni alikuwa ameanguka kifudifudi mbele ya sanduku la Yehova, huku kichwa cha Dagoni na mikono yake miwili ikiwa imekatwa, mpaka kwenye kizingiti.+ Ni sehemu yenye umbo la samaki peke yake ndiyo iliyoachwa ikiwa juu yake. 5 Ndiyo sababu makuhani wa Dagoni na wote wanaoingia katika nyumba ya Dagoni hawakikanyagi kizingiti cha Dagoni katika Ashdodi mpaka leo hii.

6 Na mkono wa Yehova+ ukawa mzito juu ya Waashdodi, naye akaanza kusababisha wasiwasi mkubwa na kuwapiga kwa bawasiri,+ yaani, Ashdodi na maeneo yake. 7 Na watu wa Ashdodi wakaona kwamba iko hivyo, ndipo wakasema: “Msiache sanduku la Mungu wa Israeli likae pamoja nasi, kwa sababu mkono wake umekuwa mzito juu yetu na juu ya Dagoni mungu wetu.”+ 8 Basi wakawatuma watu wawakusanye kwao wakuu wote wa muungano wa Wafilisti, wakasema: “Tutalifanyia nini sanduku la Mungu wa Israeli?” Mwishowe wakasema: “Acheni sanduku la Mungu wa Israeli lizunguke kwenda Gathi.”+ Basi wakalibeba sanduku la Mungu wa Israeli kwa kuzunguka mpaka huko.

9 Na ikawa kwamba walipokuwa wamezunguka kulileta huko, mkono wa Yehova+ ukaja kuwa juu ya jiji hilo na kuleta mvurugo mkubwa sana, naye akaanza kuwapiga watu wa jiji, kuanzia mdogo hata mkubwa, na bawasiri+ zikaanza kulipuka juu yao. 10 Basi wakalipeleka sanduku la Mungu wa kweli mpaka Ekroni.+ Na ikawa kwamba mara tu sanduku la Mungu wa kweli lilipofika Ekroni, Waekroni wakaanza kulia, wakisema: “Wamelileta sanduku la Mungu wa Israeli kwangu kwa kuzunguka ili waniue mimi na watu wangu!”+ 11 Kwa hiyo wakatuma watu wakawakusanya wakuu wote wa muungano wa Wafilisti na kusema: “Ondoeni sanduku la Mungu wa Israeli, lirudi mahali pake, ili lisiniue mimi na watu wangu.” Kwa maana mvurugo wa kuleta kifo ulikuwa umetokea katika jiji zima;+ mkono wa Mungu wa kweli ulikuwa umekuwa mzito sana huko,+ 12 na watu ambao hawakufa walikuwa wamepigwa na bawasiri.+ Na kilio+ cha jiji hilo cha kuomba msaada kikaendelea kupanda mpaka mbinguni.

6 Na sanduku+ la Yehova lilikuwa katika eneo la Wafilisti kwa miezi saba. 2 Nao Wafilisti wakawaita makuhani na waaguzi,+ wakisema: “Tulifanyie nini sanduku la Yehova? Tuambieni tunapaswa kulirudisha mahali pake likiwa pamoja na nini.” 3 Nao wakasema: “Ikiwa mnalirudisha sanduku la Mungu wa Israeli, msilirudishe bila toleo, kwa maana kwa vyovyote mnapaswa kumrudishia toleo la hatia.+ Ndipo mtakapoponywa, nanyi mtajua kwa nini mkono wake haukuondoka juu yenu.” 4 Ndipo wakasema: “Tunapaswa kumrudishia toleo gani la hatia?” Nao wakasema: “Kulingana na hesabu ya wakuu wa muungano+ wa Wafilisti, bawasiri tano za dhahabu na panya watano wa dhahabu, kwa maana kila mmoja wenu na wakuu wenu wa muungano wana tauni ileile. 5 Nanyi mfanye sanamu za bawasiri zenu na sanamu za panya+ wenu wanaoiharibu nchi, na kumpa utukufu+ Mungu wa Israeli. Labda atapunguza uzito wa mkono wake kutoka juu yenu na juu ya mungu wenu na juu ya nchi yenu.+ 6 Pia, kwa nini mfanye mioyo yenu kuwa migumu kama vile Misri na Farao walivyofanya mioyo yao kuwa migumu?+ Je, haikuwa ni mara tu Yeye alipowatendea vikali+ ndipo walipowaachilia waende zao, nao wakaenda zao?+ 7 Na sasa chukueni na kutengeneza gari jipya la kukokotwa,+ na ng’ombe wawili wanaonyonyesha, ambao hawajawekwa nira+ yoyote juu yao, nanyi mwafunganishe ng’ombe hao na lile gari, nanyi mwarudishe ndama wao nyumbani ili wasiwafuate. 8 Na mlichukue sanduku la Yehova mliweke juu ya lile gari, na vile vyombo vya dhahabu+ ambavyo mtamrudishia kama toleo la hatia+ mviweke ndani ya sanduku kando yake. Nanyi mnapaswa kuliacha liende, nalo linapaswa kwenda. 9 Nanyi mnapaswa kutazama: likipanda barabara inayoelekea kwenye eneo lake, kuelekea Beth-shemeshi,+ basi yeye ndiye ametutendea huu uovu mkubwa; lakini kama sivyo, tutajua kwamba haukuwa mkono wake uliotugusa; bali ni msiba+ tu uliotuangukia.”

10 Na watu wakafanya hivyo. Kwa hiyo wakachukua ng’ombe wawili wanaonyonyesha, wakawafunganisha na lile gari, na ndama wao wakawafungia nyumbani. 11 Kisha wakaliweka sanduku la Yehova juu ya lile gari,+ na pia lile sanduku na wale panya wa dhahabu na sanamu za bawasiri zao. 12 Na wale ng’ombe wakaanza kwenda mbele moja kwa moja kwenye barabara inayoelekea Beth-shemeshi.+ Wakaenda katika ile njia kuu moja, huku wakilia wakiwa wanaenda, nao hawakugeuka kando upande wa kuume wala wa kushoto. Wakati huohuo wale wakuu wa muungano+ wa Wafilisti walikuwa wakitembea nyuma yao hadi kwenye mpaka wa Beth-shemeshi. 13 Na watu wa Beth-shemeshi walikuwa wakivuna mavuno ya ngano+ katika nchi tambarare ya chini. Walipoinua macho yao na kuona lile Sanduku, wakaanza kushangilia kwa kuliona. 14 Nalo gari likaja katika shamba la Yoshua Mbeth-shemeshi, likasimama pale, ambapo palikuwa na jiwe kubwa. Nao wakaanza kupasua mbao za lile gari, na kuwatoa wale ng’ombe+ kuwa toleo la kuteketezwa kwa Yehova.+

15 Nao Walawi+ wakalishusha sanduku la Yehova na lile sanduku lililokuwa pamoja nalo, ambamo ndani yake mlikuwa vile vyombo vya dhahabu, wakaliweka juu ya lile jiwe kubwa. Na watu wa Beth-shemeshi+ wakatoa matoleo ya kuteketezwa, wakaendelea kumtolea Yehova dhabihu siku hiyo.

16 Na wale wakuu watano wa muungano+ wa Wafilisti wakaona hayo, nao wakarudi Ekroni siku hiyo. 17 Basi hizi ndizo bawasiri za dhahabu ambazo Wafilisti walirudisha kuwa toleo la hatia kwa Yehova:+ kwa ajili ya Ashdodi+ moja, kwa ajili ya Gaza+ moja, kwa ajili ya Ashkeloni+ moja, kwa ajili ya Gathi+ moja, kwa ajili ya Ekroni+ moja. 18 Na wale panya wa dhahabu walilingana na hesabu ya majiji yote ya Wafilisti ya wale wakuu watano wa muungano, kuanzia jiji lenye ngome mpaka kijiji cha nchi iliyo wazi.

Na lile jiwe kubwa ambalo juu yake waliweka sanduku la Yehova ni ushahidi mpaka leo hii katika shamba la Yoshua, Mbeth-shemeshi. 19 Naye akawapiga watu wa Beth-shemeshi,+ kwa maana walikuwa wamelitazama sanduku la Yehova. Basi kati ya watu akapiga na kuua watu 70​—​watu 50,000​—​kisha watu wakaanza kuomboleza kwa sababu Yehova alikuwa amewapiga watu hao kwa mauaji makubwa.+ 20 Na zaidi, watu wa Beth-shemeshi wakasema: “Ni nani atakayeweza kusimama mbele za Yehova, huyu Mungu mtakatifu,+ naye ataondoka kwetu aende kwa nani?”+ 21 Mwishowe wakatuma wajumbe kwa wakaaji wa Kiriath-yearimu,+ wakisema: “Wafilisti wamelirudisha sanduku la Yehova. Shukeni. Mlichukue na kulipandisha kwenu.”+

7 Basi watu wa Kiriath-yearimu+ wakaja, nao wakalipandisha sanduku la Yehova na kuliingiza katika nyumba ya Abinadabu+ juu ya kilima, nao wakamtakasa Eleazari mwana wake ili alinde sanduku la Yehova.

2 Na ikawa kwamba tangu siku ambayo hilo Sanduku lilikaa katika Kiriath-yearimu, siku zikaendelea kuongezeka, nazo zikawa jumla ya miaka 20, na nyumba yote ya Israeli wakamwombolezea Yehova.+ 3 Na Samweli akaiambia nyumba yote ya Israeli: “Ikiwa mnarudi kwa Yehova+ kwa mioyo yenu yote, ondoeni miungu ya kigeni iliyo katikati yenu+ na pia zile sanamu za Ashtorethi,+ nanyi mwelekeze mioyo yenu kwa Yehova bila kuyumba-yumba, mkamtumikie yeye peke yake,+ naye atawakomboa kutoka mkono wa Wafilisti.”+ 4 Kwa hiyo wana wa Israeli wakaondoa Mabaali+ na sanamu za Ashtorethi,+ wakaanza kumtumikia Yehova peke yake.

5 Kisha Samweli akasema: “Kusanyeni Israeli+ wote katika Mispa,+ ili nisali+ kwa Yehova kwa ajili yenu.” 6 Basi wakakusanyika pamoja kule Mispa, nao wakachota maji na kuyamwaga mbele za Yehova na kufunga siku hiyo.+ Nao wakaanza kusema huko: “Tumemtendea dhambi Yehova.”+ Naye Samweli akawahukumu+ wana wa Israeli katika Mispa.

7 Na Wafilisti wakaja kusikia kwamba wana wa Israeli wamekusanyika Mispa, na wale wakuu wa muungano+ wa Wafilisti wakapanda juu ya Israeli. Wana wa Israeli waliposikia habari hizo, wakaanza kuogopa kwa sababu ya Wafilisti.+ 8 Kwa hiyo wana wa Israeli wakamwambia Samweli: “Usikae kimya kwa ajili yetu ukose kumwomba Yehova Mungu wetu msaada,+ atukomboe kutoka mkono wa Wafilisti.” 9 Ndipo Samweli akachukua mwana-kondoo anayenyonya, akamtoa kwa Yehova kuwa toleo la kuteketezwa,+ toleo zima; na Samweli akaanza kumwomba Yehova msaada kwa ajili ya Israeli,+ naye Yehova akamjibu.+ 10 Na ikawa kwamba Samweli alipokuwa akitoa lile toleo la kuteketezwa, Wafilisti wakasonga karibu ili kupigana na Israeli. Na huko Yehova akafanya kuwe na mngurumo wa sauti kubwa+ siku hiyo juu ya Wafilisti, ili awavuruge;+ nao wakashindwa mbele ya Israeli.+ 11 Ndipo watu wa Israeli wakafanya mashambulizi kutoka Mispa na kuwafuatilia Wafilisti, wakaendelea kuwapiga mpaka upande wa kusini wa Beth-kari. 12 Kisha Samweli akachukua jiwe+ na kulisimamisha kati ya Mispa na Yeshana, akaliita jina Ebenezeri. Basi akasema: “Yehova ametusaidia mpaka sasa.”+ 13 Kwa hiyo Wafilisti wakatiishwa, wala hawakuingia tena katika eneo la Israeli;+ na mkono wa Yehova ukaendelea kuwa juu ya Wafilisti siku zote za Samweli.+ 14 Na yale majiji ambayo Wafilisti walikuwa wameyachukua kutoka kwa Israeli yakaendelea kurudi kwa Israeli kutoka Ekroni mpaka Gathi, na Israeli wakayakomboa maeneo ya majiji hayo kutoka mkono wa Wafilisti.

Na kukawa na amani kati ya Israeli na Waamori.+

15 Na Samweli akaendelea kuhukumu Israeli siku zote za maisha yake.+ 16 Naye akasafiri mwaka baada ya mwaka na kufanya mzunguko wa Betheli+ na Gilgali+ na Mispa+ na kuhukumu Israeli+ katika sehemu hizo zote. 17 Lakini alikuwa akirudi Rama,+ kwa sababu nyumba yake ilikuwa huko, naye akahukumu Israeli huko. Naye akamjengea Yehova madhabahu huko.+

8 Na ikawa kwamba mara Samweli alipokuwa amezeeka, akawaweka+ wanawe kuwa waamuzi wa Israeli. 2 Basi jina la mwana wake mzaliwa wa kwanza lilikuwa Yoeli,+ na jina la wa pili Abiya;+ walikuwa wakihukumu katika Beer-sheba. 3 Na wanawe hawakutembea katika njia zake,+ bali walikuwa na mwelekeo wa kufuata faida isiyo ya haki+ na wakawa wakikubali rushwa+ na kupotosha hukumu.+

4 Baada ya muda wanaume wazee wote wa Israeli+ wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli katika Rama 5 na kumwambia: “Tazama! Wewe mwenyewe umezeeka, lakini wana wako hawakutembea katika njia zako. Basi sasa tuchagulie mfalme+ wa kutuhukumu sisi kama mataifa mengine yote.” 6 Lakini jambo hilo lilikuwa baya machoni pa Samweli kwa vile walikuwa wamesema: “Tupe mfalme atuhukumu,” na Samweli akaanza kusali kwa Yehova.+ 7 Ndipo Yehova akamwambia Samweli:+ “Sikiliza sauti ya watu kuhusu mambo yote wanayokuambia;+ kwa maana hawakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi nisiwe mfalme+ juu yao. 8 Kulingana na matendo yao yote ambayo wametenda tangu siku nilipowatoa kutoka Misri+ mpaka leo hii kwa kuwa walizidi kuniacha+ na kuitumikia miungu mingine,+ hivyo ndivyo wanavyokutendea wewe pia. 9 Basi sasa sikiliza sauti yao. Ila tu, unapaswa kuwaonya kwa uzito, nawe ni lazima uwaambie kile ambacho ni haki ya mfalme atakayetawala juu yao.”+

10 Basi Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakimwomba awape mfalme maneno yote ya Yehova. 11 Naye akasema: “Hili ndilo litakalokuwa fungu ambalo ni haki+ ya mfalme atakayetawala juu yenu: Atawachukua wana wenu+ na kuwaweka kama wanawe katika magari+ yake na kati ya wapanda-farasi+ wake, na baadhi yao watakimbia mbele ya magari+ yake; 12 na kujichagulia wakuu wawe juu ya watu 1,000+ na wakuu wawe juu ya watu 50,+ na baadhi yao wamlimie+ na kuvuna mavuno+ yake na kutengeneza silaha zake za vita+ na vyombo vya magari yake.+ 13 Naye atachukua binti zenu wawe wachanganyaji wa marhamu na wapishi na waokaji.+ 14 Na mashamba yenu na mizabibu+ yenu na mizeituni+ yenu, iliyo bora zaidi, atachukua na kuwapa watumishi wake. 15 Na kutoka nafaka ya mashamba yenu na mazao ya mashamba yenu ya mizabibu atachukua sehemu ya kumi,+ naye atawapa maofisa+ wake wa makao ya mfalme na watumishi wake. 16 Atachukua watumishi wenu wanaume na wajakazi wenu na mifugo yenu iliyo bora zaidi, na punda wenu, naye atawatumia kwa kazi yake.+ 17 Atachukua sehemu ya kumi kutoka makundi+ yenu, nanyi mtakuwa watumishi wake. 18 Nanyi mtalia siku hiyo kwa sababu ya mfalme wenu,+ ambaye mlijichagulia wenyewe, lakini Yehova hatawajibu siku hiyo.”+

19 Hata hivyo, watu wakakataa kuisikiliza sauti ya Samweli+ na kusema: “Hapana, bali mfalme atakuwa juu yetu. 20 Na sisi pia, lazima tuwe kama mataifa mengine yote,+ na mfalme wetu lazima atuhukumu na kwenda mbele yetu na kupigana vita vyetu.” 21 Naye Samweli akasikiliza maneno yote ya watu hao; kisha akayasema masikioni mwa Yehova.+ 22 Naye Yehova akamwambia Samweli: “Sikiliza sauti yao, nawe ufanye mfalme awatawale.”+ Basi Samweli akawaambia watu wa Israeli: “Kila mmoja aende kwenye jiji lake.”

9 Basi palikuwa na mtu wa Benyamini, na jina lake lilikuwa Kishi,+ mwana wa Abieli, mwana wa Zerori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia, Mbenyamini,+ mtu mwenye nguvu ya mali.+ 2 Naye alikuwa na mwana ambaye jina lake lilikuwa Sauli,+ kijana na mwenye sura nzuri, wala hakuwako mwanamume yeyote wa wana wa Israeli aliyekuwa na sura nzuri kuliko yeye; kutoka kwenye mabega yake kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wote.+

3 Na punda-jike+ za Kishi baba ya Sauli wakapotea. Basi Kishi akamwambia Sauli mwana wake: “Tafadhali, chukua pamoja nawe mmoja wa watumishi, uondoke, uende kuwatafuta hao punda-jike.” 4 Naye akaenda, akipita katika eneo lenye milima la Efraimu,+ akaendelea, akapita katika nchi ya Shalisha,+ wala hawakuwapata. Nao wakaendelea, wakapita katika nchi ya Shaalimu, lakini hawakuwa huko. Naye akaendelea, akapita katika nchi ya Wabenyamini, wala hawakuwapata.

5 Nao wakaingia katika nchi ya Sufu; na Sauli akamwambia mtumishi wake aliyekuwa pamoja naye: “Haya njoo, turudi, ili baba yangu asije akaacha kufikiri juu ya punda-jike na kuanza kuhangaika juu yetu.”+ 6 Lakini yeye akamwambia: “Tafadhali, tazama! Kuna mtu wa Mungu+ katika jiji hili, na mtu huyo anaheshimiwa. Kila jambo analosema hutimia bila kukosa.+ Na twende huko sasa. Labda anaweza kutuambia njia yetu tunayopaswa kuiendea.” 7 Ndipo Sauli akamwambia mtumishi wake: “Na tukienda, tutampelekea mtu huyo nini?+ kwa maana mkate umekwisha katika vyombo vyetu, wala hakuna zawadi+ yoyote ya kumpelekea huyo mtu wa Mungu wa kweli. Tuna nini pamoja nasi?” 8 Basi mtumishi akamjibu Sauli tena na kusema: “Tazama! Kuna sehemu ya nne ya shekeli+ ya fedha mkononi mwangu, nami nitampa huyo mtu wa Mungu wa kweli, naye atatuambia njia yetu.” 9 (Nyakati za kale katika Israeli, mtu alikuwa akisema hivi akienda kumtafuta Mungu: “Haya njooni, na twende kwa mwonaji.”+ Kwa maana nabii wa leo alikuwa akiitwa mwonaji nyakati za kale.) 10 Ndipo Sauli akamwambia mtumishi wake: “Neno lako ni jema.+ Haya njoo, twende.” Nao wakaenda zao kwenye jiji lile alilokuwamo mtu wa Mungu wa kweli.

11 Walipokuwa wakipanda kwenda jijini, wakakuta wasichana wakitoka kwenda kuteka maji.+ Basi wakawauliza: “Je, mwonaji+ yuko mahali hapa?” 12 Nao wakawajibu na kusema: “Ndiyo. Tazama! Yuko mbele yenu. Fanyeni haraka sasa, kwa sababu amekuja jijini leo, kwa maana leo kuna dhabihu+ kwa ajili ya watu katika mahali pa juu.+ 13 Mara mtakapoingia jijini, mtamkuta moja kwa moja kabla hajapanda kwenda mahali pa juu ili ale chakula; kwa kuwa watu hawawezi kula mpaka aje, kwa maana yeye ndiye anayeibariki dhabihu.+ Baadaye wale walioalikwa hula. Basi sasa pandeni—sasa hivi mtampata.” 14 Nao wakapanda kwenda jijini. Walipokuwa wakiingia katikati ya jiji, tazama, Samweli alikuwa anatoka nje kuja kuwapokea ili kupanda kwenda mahali pa juu.

15 Naye Yehova alikuwa amefunua sikio+ la Samweli ile siku iliyotangulia kuja kwa Sauli, akisema: 16 “Karibu wakati kama huu kesho nitatuma mtu kwako kutoka katika nchi ya Benyamini,+ nawe umtie mafuta+ awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli; naye atawaokoa watu wangu kutoka mkononi mwa Wafilisti,+ kwa sababu nimeona mateso ya watu wangu, kwa maana kilio chao kimenifikia.”+ 17 Na Samweli akamwona Sauli, naye Yehova akamjibu: “Huyu ndiye mtu niliyekuambia, ‘Huyu ndiye atakayewazuia watu wangu wasipite mipaka.’”+

18 Ndipo Sauli akamkaribia Samweli katikati ya lango na kusema: “Tafadhali niambie, Nyumba ya mwonaji iko wapi?” 19 Naye Samweli akamjibu Sauli na kusema: “Mimi ndiye mwonaji. Panda mbele yangu, uende mahali pa juu, nanyi mtakula pamoja nami leo,+ nami nitawaacha mwende zenu asubuhi, nami nitakuambia mambo yote yaliyo moyoni mwako.+ 20 Na wale punda-jike uliowapoteza siku tatu zilizopita,+ usitie moyo+ wako juu yao, kwa maana wamepatikana. Na je, vitu vyote vyenye kutamanika vya Israeli ni vya nani?+ Je, si vyako na vya nyumba yote ya baba yako?” 21 Ndipo Sauli akajibu na kusema: “Je, mimi si Mbenyamini wa kutoka katika kabila dogo zaidi+ kati ya makabila ya Israeli,+ na je, familia yangu si dhaifu zaidi kati ya familia zote za kabila la Benyamini?+ Basi kwa nini umeniambia jambo kama hili?”+

22 Ndipo Samweli akamchukua Sauli na mtumishi wake, akawaleta katika jumba la kulia chakula, akawapa viti mbele+ ya wale walioalikwa; nao walikuwa karibu watu 30. 23 Baadaye Samweli akamwambia mpishi: “Leta lile fungu nililokupa, ambalo juu yake nilikuambia hivi, ‘Liweke kando yako.’” 24 Kwa hiyo yule mpishi akainua ule mguu na ile nyama iliyokuwa juu yake, akauweka mbele ya Sauli. Naye akasema tena: “Kilichowekwa akiba ndicho hiki. Kiweke mbele yako. Ule, kwa maana wamekuwekea hicho akiba mpaka wakati uliowekwa ili ule pamoja na wale walioalikwa.” Basi Sauli akala pamoja na Samweli siku hiyo. 25 Kisha wakashuka kutoka mahali pa juu,+ wakaenda jijini, naye akaendelea kusema na Sauli darini.+ 26 Nao wakaamka mapema na ikawa, mara kulipopambazuka, Samweli akamwita Sauli juu darini, akisema: “Simama, nikuache uende zako.” Basi Sauli akasimama na wote wawili, yeye na Samweli, wakatoka nje. 27 Walipokuwa wakishuka ukingoni mwa jiji, Samweli akamwambia Sauli: “Mwambie mtumishi+ apite mbele yetu”—basi akapita—“nawe simama tuli sasa ili nikuambie neno la Mungu.”

10 Ndipo Samweli akachukua chupa+ ya mafuta na kuyamimina juu ya kichwa chake, akambusu+ na kusema: “Je, si kwa sababu Yehova amekutia mafuta uwe kiongozi+ juu ya urithi wake?+ 2 Utakapoondoka kwangu leo hakika utakuta watu wawili karibu na kaburi la Raheli+ katika eneo la Benyamini katika Selsa, nao watakuambia, ‘Wale punda-jike ambao ulienda kutafuta wamepatikana, lakini sasa baba yako ameacha habari za wale punda-jike+ naye anawahangaikia ninyi, akisema: “Nitafanya nini kwa ajili ya mwanangu?”’+ 3 Nawe utapita kutoka hapo na kusonga mbele zaidi, uje mpaka kwenye ule mti mkubwa wa Tabori, na hapo wanaume watatu watakutana nawe, wakipanda kwenda kwa Mungu wa kweli katika Betheli,+ mmoja akiwa amebeba wana-mbuzi+ watatu na mwingine akiwa amebeba mikate mitatu ya mviringo+ na mwingine akiwa amebeba mtungi mkubwa wa divai.+ 4 Na watauliza habari za hali yako+ na kukupa mikate miwili, nawe uikubali kutoka mkononi mwao. 5 Ni baada ya hapo kwamba utakuja kwenye kilima cha Mungu wa kweli,+ palipo na kambi ya kijeshi+ ya Wafilisti. Na itakuwa kwamba wakati utakapokuja hapo kwenye jiji, utakutana na kikundi cha manabii+ wakishuka kutoka mahali pa juu,+ na mbele yao kukiwa na kinanda+ na tari+ na filimbi+ na kinubi,+ huku wakisema kama manabii. 6 Na roho+ ya Yehova hakika itaanza kutenda kazi juu yako, kisha utasema kama nabii+ pamoja nao, nawe utabadilishwa uwe mtu mwingine. 7 Na itakuwa kwamba ishara+ hizo zitakapokuja juu yako, jifanyie lile ambalo mkono wako unaweza,+ kwa sababu Mungu wa kweli yupo pamoja nawe.+ 8 Nawe ushuke mbele yangu kwenda Gilgali;+ na tazama! ninashuka kuja kwako ili nitoe dhabihu za kuteketezwa, ili nitoe dhabihu za ushirika.+ Uendelee kungojea siku saba+ mpaka nitakapokujia, nami hakika nitakujulisha yale unayopaswa kufanya.”

9 Na ikawa kwamba mara tu alipogeuza bega lake aende zake kutoka kwa Samweli, Mungu akaanza kuubadili moyo wake uwe mwingine;+ na ishara+ hizo zote zikatimia siku hiyo. 10 Basi wakatoka hapo wakaenda kwenye kilima, na tazama, kulikuwa na kikundi cha manabii kikija kumpokea; ndipo mara moja roho ya Mungu ikaanza kutenda kazi juu yake,+ naye akaanza kusema kama nabii+ katikati yao. 11 Na ikawa kwamba wakati watu wote waliokuwa wakimjua hapo zamani walipomwona, tazama! alikuwa akitoa unabii pamoja na manabii. Basi watu wakaambiana: “Ni nini hili lililompata mwana wa Kishi? Je, Sauli pia yumo kati ya manabii?”+ 12 Ndipo mtu mmoja kutoka hapo akajibu na kusema: “Lakini baba yao ni nani?” Ndiyo sababu kumekuwa na neno la kimethali:+ “Je, Sauli pia yumo kati ya manabii?”

13 Mwishowe akamaliza kusema kama nabii, akaja mahali pa juu. 14 Baadaye ndugu ya baba ya Sauli akamwambia yeye na mtumishi wake: “Mlienda wapi?” Naye akasema: “Kuwatafuta wale punda-jike,+ nasi tukaendelea kwenda ili tuone, lakini hawakuwapo. Basi tukaenda kwa Samweli.” 15 Kisha ndugu ya baba ya Sauli akasema: “Tafadhali niambieni, Samweli aliwaambia nini?” 16 Sauli naye akamwambia ndugu ya baba yake: “Alituambia kwa uhakika kwamba wale punda-jike walikuwa wamepatikana.” Lakini yeye hakumwambia lile jambo la ufalme, ambalo Samweli alikuwa amesema.+

17 Na Samweli akawaita watu pamoja waje mbele za Yehova kule Mispa+ 18 na kuwaambia wana wa Israeli: “Yehova, Mungu wa Israeli amesema hivi,+ ‘Mimi ndiye niliyewatoa Israeli kutoka Misri nami nikawakomboa ninyi kutoka mkono wa Misri+ na kutoka mkono wa falme zote zilizokuwa zikiwakandamiza ninyi.+ 19 Lakini ninyi—leo mmemkataa Mungu+ wenu ambaye alikuwa mwokozi wenu kutoka katika maovu yenu yote na taabu zenu, nanyi mkasema: “Hapana, bali uweke mfalme juu yetu.” Basi sasa simameni mbele za Yehova kulingana na makabila+ yenu na kulingana na maelfu yenu.’”

20 Basi Samweli akafanya makabila yote ya Israeli yakaribie,+ nalo kabila la Benyamini likachaguliwa.+ 21 Kisha akafanya kabila la Benyamini likaribie kulingana na familia zao, ndipo familia ya Wamatri ikachaguliwa.+ Mwishowe Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa.+ Nao wakamtafuta, lakini hakupatikana. 22 Kwa hiyo wakamuuliza+ tena Yehova: “Je, mtu huyo amekwisha kuja hapa?” Ndipo Yehova akasema: “Tazama, amejificha+ kati ya mizigo.” 23 Basi wakakimbia na kumchukua kutoka hapo. Aliposimama katikati ya watu, alikuwa mrefu kuliko watu wengine wote kuanzia mabega yake na kwenda juu.+ 24 Ndipo Samweli akawaambia watu wote: “Je, mmemwona yule ambaye Yehova amemchagua,+ kwamba hakuna yeyote kama yeye kati ya watu wote?” Nao watu wote wakaanza kupiga kelele na kusema: “Mfalme na aishi!”+

25 Kwa hiyo Samweli akasema na watu kuhusu fungu ambalo ni haki ya ufalme+ na kuandika hayo katika kitabu na kukiweka mbele za Yehova. Kisha Samweli akawaacha watu wote waende zao, kila mmoja nyumbani kwake. 26 Bali Sauli akaenda nyumbani kwake kule Gibea,+ na wanaume mashujaa ambao Mungu alikuwa amegusa mioyo yao wakaenda pamoja naye.+ 27 Lakini watu wasiofaa kitu+ wakasema: “Huyu atatuokoa vipi?”+ Basi wakamdharau,+ wala hawakumletea zawadi yoyote.+ Lakini yeye akaendelea kuwa kama mtu asiyeweza kusema.+

11 Na Nahashi Mwamoni+ akapanda na kupiga kambi juu ya Yabeshi+ katika Gileadi. Kwa hiyo watu wote wa Yabeshi wakamwambia Nahashi: “Fanya agano pamoja nasi ili tukutumikie.”+ 2 Ndipo Nahashi Mwamoni akawaambia: “Nitafanya agano pamoja nanyi kwa sharti hili, kwa sharti la kung’oa+ kila jicho lenu la kuume, nami ni lazima niweke jambo hilo kuwa shutuma juu ya Israeli wote.”+ 3 Nao wanaume wazee wa Yabeshi wakamwambia: “Tupatie muda wa siku saba, nasi tutatuma wajumbe katika eneo lote la Israeli, na, ikiwa hatutapata mwokozi,+ ndipo tutalazimika kuja kwako.” 4 Baadaye hao wajumbe wakaja Gibea+ la Sauli na kusema maneno hayo masikioni mwa watu, na watu wote wakaanza kupaaza sauti zao na kulia.+

5 Lakini tazama, Sauli akija nyuma ya mifugo yake kutoka shambani, naye Sauli akasema: “Watu wana nini, kwamba walie?” Wakaanza kumsimulia maneno ya wale watu wa Yabeshi. 6 Na roho+ ya Mungu ikaanza kutenda kazi juu ya Sauli alipoyasikia maneno hayo, hasira yake ikawaka sana.+ 7 Kwa hiyo akachukua ng’ombe-dume wawili, akawakata vipande-vipande, akavipeleka katika eneo lote la Israeli+ kwa mkono wa wajumbe, akisema: “Yeyote kati yetu ambaye hatatoka akiwa mfuasi wa Sauli na Samweli, ng’ombe zake watafanywa hivi!”+ Na hofu+ ya Yehova+ ikaanza kuwashika watu hivi kwamba wakatoka kama mtu mmoja.+ 8 Ndipo akahesabu+ watu hao katika Bezeki, na wana wa Israeli wakawa jumla ya 300,000, na watu wa Yuda 30,000. 9 Basi wakawaambia wale wajumbe ambao walikuwa wamekuja: “Hivi ndivyo mtakavyowaambia watu wa Yabeshi katika Gileadi, ‘Kesho mtapata wokovu wakati wa jua kali.’”+ Basi wale wajumbe wakaja na kuwaambia watu wa Yabeshi, nao wakaanza kushangilia. 10 Kwa hiyo watu wa Yabeshi wakasema: “Kesho tutawajia ninyi, nanyi mtutendee kulingana na yote yaliyo mema machoni  penu.”+

11 Na ikawa kesho yake kwamba Sauli+ akaweka watu katika vikosi vitatu;+ nao wakaingia katikati ya kambi wakati wa kesha la kuamkia asubuhi+ na kuwapiga Waamoni+ mpaka wakati siku ilipokuwa na jua kali. Na baadhi yao walipoonekana kuwa wamebaki, ndipo wakatawanywa, wala hawakubaki watu wawili wakiwa pamoja kati yao.+ 12 Na watu wakaanza kumwambia Samweli: “Ni nani wanaosema, ‘Je, Sauli atakuwa mfalme juu yetu?’+ Watoeni watu hao, ili tuwaue.”+ 13 Hata hivyo, Sauli akasema: “Mtu yeyote asiuawe leo,+ kwa maana leo Yehova ametimiza wokovu katika Israeli.”+

14 Baadaye Samweli akawaambia watu: “Njooni, twende Gilgali,+ ili tuufanye upya ufalme huko.”+ 15 Basi watu wote wakaenda Gilgali, kisha wakamfanya Sauli kuwa mfalme mbele za Yehova katika Gilgali. Ndipo wakatoa huko dhabihu za ushirika mbele za Yehova,+ na Sauli na watu wote wa Israeli wakaendelea kushangilia huko kwa hali ya juu sana.+

12 Mwishowe Samweli akawaambia Israeli wote: “Tazama, nimesikiliza sauti yenu kuhusu mambo yote ambayo mmeniambia,+ kwamba nifanye mfalme atawale juu yenu.+ 2 Na sasa tazameni, mfalme anatembea mbele yenu!+ Lakini mimi nimezeeka+ nami nina mvi,+ na tazameni, wanangu wako pamoja nanyi,+ nami nimetembea mbele yenu tangu ujana wangu mpaka leo hii.+ 3 Mimi hapa. Leteni jibu kinyume changu mbele za Yehova na mbele ya mtiwa-mafuta+ wake: Nimechukua ng’ombe wa nani au nimechukua punda wa nani+ au nimempunja nani au nimemponda nani au nimepokea kutoka kwa mkono wa nani pesa za hongo ili nizitumie kufunga macho yangu?+ Nami nitawarudishia ninyi.”+ 4 Nao wakasema: “Wewe hukutupunja, wala kutuponda, wala kupokea chochote kutoka mkononi mwa mtu hata mmoja.”+ 5 Basi akawaambia: “Yehova ni shahidi dhidi yenu, na mtiwa-mafuta+ wake ni shahidi leo kwamba hamkupata chochote mkononi mwangu.”+ Nao wakasema: “Yeye ni shahidi.”

6 Na Samweli akaendelea kuwaambia watu hao: “Yehova ni shahidi, aliyewatumia Musa na Haruni, na ambaye aliwaleta mababu zenu kutoka nchi ya Misri.+ 7 Basi sasa simameni, nami nitawahukumu ninyi mbele za Yehova na kuwasimulia matendo yote ya uadilifu+ ya Yehova ambayo amewafanyia ninyi na mababu zenu.

8 “Mara Yakobo alipokuwa ameingia Misri+ nao mababu zenu wakaanza kumwomba Yehova msaada,+ Yehova aliwatuma Musa+ na Haruni, ili wawaongoze mababu zenu watoke Misri na kuwakalisha mahali hapa.+ 9 Nao wakamsahau Yehova, Mungu wao,+ naye akawauza+ mkononi mwa Sisera+ mkuu wa jeshi la Hasori na mkononi mwa Wafilisti+ na mkononi mwa mfalme wa Moabu,+ nao wakaendelea kupiga vita juu yao. 10 Nao wakaanza kumwomba Yehova msaada,+ wakisema, ‘Tumetenda dhambi,+ kwa maana tumemwacha Yehova ili tutumikie Mabaali+ na sanamu za Ashtorethi;+ basi sasa utukomboe+ kutoka mkono wa adui zetu, ili tukutumikie.’ 11 Ndipo Yehova akamtuma Yerubaali+ na Bedani na Yeftha+ na Samweli,+ akawakomboa kutoka mkono wa adui zenu pande zote, ili mkae kwa amani.+ 12 Mlipoona kwamba Nahashi+ mfalme wa wana wa Amoni amekuja kupigana nanyi, mkaniambia tena na tena, ‘Hapana, bali ni mfalme ndiye atakayetawala juu yetu!’+ ingawa wakati huo wote Yehova Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.+ 13 Na sasa tazameni, mfalme mliyemchagua, ambaye mliomba;+ na tazameni, Yehova ameweka mfalme juu yenu.+ 14 Mkimwogopa+ Yehova na kumtumikia+ na kuitii sauti yake+ kwelikweli, nanyi msipoliasi+ agizo la Yehova, ninyi pamoja na mfalme atakayetawala juu yenu mtakuwa wafuasi wa Yehova, Mungu wenu. 15 Lakini msipoisikiliza sauti ya Yehova,+ na ikiwa kwelikweli mtaliasi agizo la Yehova,+ hakika mkono wa Yehova utakuwa kinyume chenu na baba zenu.+ 16 Sasa, pia, simameni mwone jambo hili kubwa ambalo Yehova anafanya mbele ya macho yenu. 17 Je, leo si mavuno ya ngano?+ Nitamwomba+ Yehova ili alete mngurumo na mvua;+ ndipo mjue na kuona kwamba uovu wenu ni mwingi+ ambao mmefanya machoni pa Yehova kwa kujiombea mfalme.”

18 Ndipo Samweli akamwita Yehova,+ naye Yehova akaleta mngurumo na mvua siku hiyo,+ hivi kwamba watu wote wakawaogopa sana Yehova na Samweli. 19 Na watu wote wakaanza kumwambia Samweli: “Sali+ kwa Yehova Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, kwa maana hatutaki kufa; kwa sababu tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu zote kwa kujiombea mfalme.”

20 Basi Samweli akawaambia watu: “Msiogope.+ Ninyi—mmefanya uovu huu wote. Ila tu msigeuke kando mwache kumtumikia Yehova,+ nanyi lazima mmtumikie Yehova kwa moyo wenu wote.+ 21 Nanyi msigeuke kando ili kufuata vitu visivyo vya kweli+ ambavyo havina faida+ yoyote na ambavyo havikomboi, kwa sababu hivyo ni vitu visivyo vya kweli. 22 Kwa maana Yehova hatawaacha+ watu wake kwa ajili ya jina lake kuu,+ kwa sababu Yehova ameamua mwenyewe kuwafanya ninyi kuwa watu wake.+ 23 Nami pia, kwa upande wangu, ni jambo lisilowaziwa, kwamba nimtendee Yehova dhambi kwa kuacha kusali kwa ajili yenu;+ nami nitawafundisha+ ninyi katika njia iliyo njema+ na iliyo sawa. 24 Ila tu mwogopeni+ Yehova, nanyi mkamtumikie katika kweli kwa moyo wenu wote;+ kwa maana angalieni jinsi amewafanyia mambo makuu.+ 25 Lakini mkifanya yaliyo mabaya bila kujali, ninyi pamoja na mfalme wenu+ mtafagiliwa mbali.”+

13 Sauli alikuwa na umri wa miaka [?] alipoanza kutawala,+ naye akatawala miaka miwili juu ya Israeli. 2 Na Sauli akajichagulia watu elfu tatu katika Israeli; na elfu mbili walikuwa pamoja na Sauli huko Mikmashi+ na katika eneo lenye milima la Betheli, na elfu moja wakawa pamoja na Yonathani+ huko Gibea+ la Benyamini, naye akawaacha watu wale wengine waende zao, kila mmoja kwenye hema lake. 3 Ndipo Yonathani akaipiga kambi ya kijeshi+ ya Wafilisti+ iliyokuwa katika Geba;+ nao Wafilisti wakasikia habari hizo. Naye Sauli akapiga baragumu+ nchini kote, akisema: “Waebrania na wasikie!” 4 Na Israeli wote wakasikia habari: “Sauli ameipiga kambi ya kijeshi ya Wafilisti, na sasa Israeli wamekuwa harufu mbaya+ kwa Wafilisti.” Basi watu wakakusanywa pamoja, wamfuate Sauli huko Gilgali.+

5 Nao Wafilisti, kwa upande wao, wakakusanyika pamoja ili kupigana na Israeli, magari ya vita 30,000+ na wapanda-farasi 6,000 na watu wengi kama chembe za mchanga kando ya bahari;+ nao wakaondoka, wakapanda na kupiga kambi katika Mikmashi upande wa mashariki wa Beth-aveni.+ 6 Na watu wa Israeli wakaona kwamba wako katika shida kali,+ kwa sababu watu walikuwa wamebanwa sana; na watu wakajificha katika mapango+ na mashimo na miamba na ngome na mashimo ya maji. 7 Hata Waebrania wakavuka Yordani+ kwenda katika nchi ya Gadi+ na Gileadi. Lakini Sauli alikuwa bado katika Gilgali, na watu wote wakamfuata wakitetemeka.+ 8 Naye akaendelea kungojea siku saba mpaka wakati uliowekwa ambao Samweli alikuwa amesema;+ na Samweli hakuja Gilgali, na watu wakawa wanatawanyika kutoka kwake. 9 Mwishowe Sauli akasema: “Leteni karibu nami dhabihu ya kuteketezwa na dhabihu za ushirika.” Basi akaitoa dhabihu ya kuteketezwa.+

10 Na ikawa kwamba mara alipokuwa amemaliza kuitoa dhabihu ya kuteketezwa, tazama, Samweli alikuwa anaingia. Basi Sauli akatoka kwenda kumpokea na kumbariki.+ 11 Ndipo Samweli akasema: “Umefanya nini?”+ Naye Sauli akasema: “Niliona kwamba watu wametawanyika kutoka kwangu,+ nawe hukuja katika siku zilizowekwa,+ na Wafilisti walikuwa wakikusanyika pamoja huko Mikmashi,+ 12 basi nikasema moyoni mwangu,+ ‘Sasa Wafilisti watashuka juu yangu katika Gilgali, nami sijautuliza uso wa Yehova.’ Kwa hiyo nikajilazimisha,+ nikaitoa dhabihu ya kuteketezwa.”

13 Ndipo Samweli akamwambia Sauli: “Umetenda kipumbavu.+ Hukuishika amri+ ya Yehova Mungu wako ambayo alikuamuru,+ kwa sababu, kama ungeishika, Yehova angeufanya ufalme wako juu ya Israeli kuwa imara mpaka wakati usio na kipimo. 14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu.+ Yehova atajitafutia mtu anayekubalika kwa moyo wake;+ na Yehova atamweka kuwa kiongozi+ juu ya watu wake, kwa sababu wewe hukushika yale aliyokuamuru Yehova.”+

15 Kisha Samweli akaondoka, akaenda zake kutoka Gilgali mpaka Gibea la Benyamini, naye Sauli akawahesabu watu, wale waliokuwa bado pamoja naye, karibu watu mia sita.+ 16 Na Sauli na Yonathani mwana wake na watu waliokuwa bado pamoja nao walikuwa wakikaa katika Geba+ la Benyamini. Nao Wafilisti walikuwa wamepiga kambi katika Mikmashi.+ 17 Na vikosi vya waporaji vikawa vikifanya mashambulizi kutoka katika kambi ya Wafilisti vikiwa vikosi vitatu.+ Kikosi kimoja kikawa kikigeukia kwenye barabara inayoenda Ofra,+ mpaka nchi ya Shuali, 18 na kile kikosi kingine kikawa kikigeukia kwenye barabara ya Beth-horoni,+ na kile kikosi cha tatu kikawa kikigeukia kwenye barabara iliyo kwenye mpaka ulio upande wa bonde la Seboimu, kuelekea nyikani.

19 Basi hakuonekana fundi wa chuma yeyote katika nchi yote ya Israeli, kwa sababu Wafilisti walikuwa wamesema: “Ili Waebrania wasitengeneze upanga wala mkuki.”+ 20 Na Waisraeli wote wakawa wakishuka kwenda kwa Wafilisti ili wanolewe kila mmoja wao jembe lake au jembetezo lake au shoka lake au mundu wake.+ 21 Na bei ya kunoa ikawa ni pimu moja kwa majembe na kwa majembetezo na kwa vifaa vyenye meno matatu na kwa mashoka na kwa kuimarisha mchokoo wa ng’ombe.+ 22 Na ikawa katika siku ya pigano kwamba haukuonekana upanga+ wala mkuki mkononi mwa mtu yeyote aliyekuwa pamoja na Sauli na Yonathani; lakini kukapatikana mmoja uliokuwa wa Sauli+ na wa Yonathani mwana wake.

23 Basi kituo cha mbele+ cha Wafilisti kikawa kikishambulia kuingia katika kipito cha mfereji cha Mikmashi.+

14 Na ikawa siku moja kwamba Yonathani+ mwana wa Sauli alimwambia mtumishi aliyechukua silaha zake: “Njoo tuvuke, twende kwenye kituo cha mbele cha Wafilisti walio pale ng’ambo.” Lakini hakumwambia baba yake jambo hilo.+ 2 Na Sauli alikuwa akikaa mipakani mwa Gibea+ chini ya mkomamanga ulio katika Migroni; na watu waliokuwa pamoja naye walikuwa karibu wanaume mia sita.+ 3 (Na Ahiya mwana wa Ahitubu,+ ndugu ya Ikabodi,+ mwana wa Finehasi,+ mwana wa Eli,+ kuhani wa Yehova katika Shilo,+ alikuwa ameibeba efodi.)+ Nao watu hawakujua kwamba Yonathani alikuwa ameenda. 4 Basi kati ya zile njia ambazo Yonathani alitafuta kuvukia kwenda juu ya kituo cha mbele+ cha Wafilisti, kulikuwa na mwamba ulio na umbo la jino upande huu na mwamba ulio na umbo la jino upande ule mwingine, na jina la ule mmoja lilikuwa ni Bosesi na jina la ule mwingine lilikuwa ni Sene. 5 Hilo jino moja lilikuwa ni nguzo upande wa kaskazini kuelekea Mikmashi,+ na lile lingine lilikuwa upande wa kusini kuelekea Geba.+

6 Basi Yonathani akamwambia yule mtumishi, mchukua-silaha wake: “Haya njoo, na tuvuke, twende kwenye kituo cha mbele cha wanaume hawa wasiotahiriwa.+ Labda Yehova atatenda kwa ajili yetu, kwa maana hakuna kizuizi chochote kwa Yehova kuokoa kwamba ni kwa wengi au ni kwa wachache.”+ 7 Ndipo mchukua-silaha wake akamwambia: “Fanya lolote lililo moyoni mwako. Enda popote unapotaka. Tazama, mimi nipo pamoja nawe kulingana na moyo wako.”+ 8 Ndipo Yonathani akasema: “Tazama, tunavuka kwenda kwa watu wale, nasi tujionyeshe kwao. 9 Wakituambia hivi, ‘Simameni tuli mpaka tukutane nanyi!’ ndipo tutakaposimama mahali tulipo, nasi tusipande kwenda walipo. 10 Lakini wakisema hivi, ‘Njooni juu yetu!’ ndipo tutakapopanda, kwa sababu hakika Yehova atawatia mkononi mwetu, na hii itakuwa ndiyo ishara kwetu.”+

11 Basi hao wawili wakajionyesha kwenye kituo cha mbele cha Wafilisti. Nao Wafilisti wakasema: “Tazama, Waebrania wanatoka katika matundu walimojificha.”+ 12 Kwa hiyo watu wa kituo hicho cha mbele wakamjibu Yonathani na mchukua-silaha wake na kusema: “Njooni hapa juu tulipo, na sisi tutawaonyesha jambo fulani!”+ Mara moja Yonathani akamwambia mchukua-silaha wake: “Nifuate, kwa kuwa hakika Yehova atawatia mkononi mwa Israeli.”+ 13 Naye Yonathani akaendelea kupanda kwa mikono+ yake na miguu yake, na mchukua-silaha wake akimfuata; nao wakaanza kuanguka mbele ya Yonathani,+ na mchukua-silaha wake akawa akiwaua nyuma yake.+ 14 Na yale mauaji ya kwanza ambayo Yonathani na mchukua-silaha wake waliwapiga yakawa watu karibu 20 ndani ya nafasi inayolingana na karibu nusu ya uwanja unaoweza kulimwa na ng’ombe wawili.

15 Ndipo tetemeko+ likatokea katika kambi iliyo shambani na katikati ya watu wote wa kile kituo cha mbele; na hata lile jeshi la waporaji+ likatetemeka, na dunia ikaanza kutetemeka,+ nalo likawa ni tetemeko kutoka kwa Mungu.+ 16 Na walinzi wa Sauli waliokuwa katika Gibea+ la Benyamini wakaona hayo, na tazama! machafuko hayo yalienea pande zote.+

17 Ndipo Sauli akawaambia watu waliokuwa pamoja naye: “Tafadhali, fanyeni hesabu, mwone ni nani ambaye ametoka kwetu.” Walipohesabu, tazama! Yonathani na mchukua-silaha wake hawakuwepo. 18 Basi Sauli akamwambia Ahiya:+ “Lilete karibu sanduku la Mungu wa kweli!”+ (Kwa maana siku hiyo sanduku la Mungu wa kweli lilikuwa pamoja na wana wa Israeli.)+ 19 Na ikawa kwamba Sauli alipokuwa akisema na kuhani,+ yale machafuko yaliyokuwa katika kambi ya Wafilisti yakazidi kuendelea, yakawa makubwa zaidi na zaidi. Ndipo Sauli akamwambia yule kuhani: “Rudisha mkono wako.” 20 Hivyo Sauli na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaitwa nje.+ Wakaenda mpaka kwenye pigano, na tazama, upanga wa kila mmoja ulikuwa umeinuka juu ya mtu na mwenzake;+ machafuko yalikuwa makubwa sana. 21 Na wale Waebrania waliokuwa wamekuwa mali ya Wafilisti+ kama hapo zamani na waliokuwa wamepanda pamoja nao kuingia katika kambi iliyozunguka pande zote, hata wao pia wakawa upande wa Israeli ambao walikuwa pamoja na Sauli na Yonathani. 22 Na pia watu wote wa Israeli waliokuwa wamejificha+ katika eneo lenye milima la Efraimu wakasikia kwamba Wafilisti wamekimbia, nao pia wakawafuatilia kwa ukaribu vitani. 23 Na Yehova akawaokoa+ Israeli siku hiyo, na pigano hilo likavuka mpaka Beth-aveni.+

24 Na watu wa Israeli walikuwa wamebanwa sana siku hiyo, na bado Sauli akawaapisha watu,+ akisema: “Alaaniwe mtu yeyote atakayekula mkate kabla ya jioni na mpaka niwe nimejilipiza kisasi+ juu ya adui zangu!” Na hakuna yeyote kati ya watu aliyeonja mkate.+

25 Na wale wote wa nchi hiyo wakaingia msituni, nayo asali+ ikawa usoni pa nchi. 26 Watu walipoingia msituni, tazama! asali ilikuwa ikidondoka,+ lakini hakuna yeyote aliyenyoosha mkono wake kuuleta kinywani pake, kwa sababu watu waliogopa kile kiapo.+ 27 Lakini Yonathani hakusikia wakati baba yake alipowaapisha watu,+ kwa hiyo akanyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake, akaichovya ndani ya lile sega la asali na kuurudisha mkono wake kinywani pake, na macho yake yakaanza kung’aa.+ 28 Ndipo mmoja wa wale watu akajibu na kusema: “Baba yako aliwaapisha watu kwa uzito, akisema, ‘Alaaniwe mtu yule atakayekula mkate leo!’”+ (Nao watu wakaanza kuchoka.)+ 29 Hata hivyo, Yonathani akasema: “Baba yangu ameleta taabu+ katika nchi. Tafadhali, angalieni jinsi macho yangu yalivyong’aa kwa sababu ya kuonja hii asali kidogo.+ 30 Si zaidi sana kama watu wangalikula+ leo kutokana na nyara ya adui zao waliyopata!+ Kwa hiyo sasa mauaji juu ya Wafilisti yamekuwa si makubwa.”+

31 Na siku hiyo wakaendelea kuwapiga Wafilisti kutoka Mikmashi+ mpaka Aiyaloni,+ na watu wakachoka sana.+ 32 Na watu wakaanza kukimbilia nyara kwa pupa+ na kuchukua kondoo na ng’ombe na ndama na kuwachinja juu ya nchi, na wale watu wakaanza kula pamoja na damu.+ 33 Basi wakamwambia Sauli, wakisema: “Tazama! Watu wanamtendea dhambi Yehova kwa kula pamoja na damu.”+ Naye akasema: “Mmetenda kwa hila. Kwanza kabisa, viringisheni kwangu jiwe kubwa.” 34 Kisha Sauli akasema: “Tawanyikeni kati ya watu, nanyi mkawaambie, ‘Kila mmoja wenu alete karibu nami ng’ombe wake na kila mmoja kondoo wake, mchinje na mle mahali hapa, wala msimtendee dhambi Yehova kwa kula pamoja na damu.’”+ Basi watu wote wakaleta karibu kila mmoja ng’ombe aliyekuwa mkononi mwake usiku huo, wakawachinjia mahali hapo. 35 Na Sauli akamjengea Yehova madhabahu.+ Kuanzia na hiyo, akaanza kumjengea Yehova madhabahu.+

36 Baadaye Sauli akasema: “Na tushuke kuwafuatilia Wafilisti wakati wa usiku, tuwapore mpaka mapambazuko ya asubuhi,+ nasi tusiache hata mmoja kati yao.”+ Nao wakasema: “Lolote lililo jema machoni pako, fanya.” Ndipo kuhani akasema: “Na tukaribie hapa kwa Mungu wa kweli.”+ 37 Na Sauli akaanza kumuuliza Mungu: “Je, nishuke kuwafuatilia Wafilisti?+ Je, utawatia mkononi mwa Israeli?”+ Naye hakumjibu siku hiyo.+ 38 Basi Sauli akasema: “Njooni hapa karibu,+ enyi wakuu wote wa watu,+ mhakikishe na mwone ni jinsi gani dhambi hii imetokea leo. 39 Kwa maana, kama anavyoishi Yehova, ambaye ni Mkombozi wa Israeli, hata kama iko katika Yonathani mwanangu, yeye atakufa hakika.”+ Lakini hakuna yeyote aliyemjibu kati ya watu wote. 40 Kisha akawaambia tena Israeli wote: “Ninyi mtakuwa upande mmoja, nami na Yonathani mwanangu—tutakuwa upande wa pili.” Ndipo watu wakamwambia Sauli: “Fanya yaliyo mema machoni pako.”+

41 Na Sauli akamwambia Yehova: “Ee Mungu wa Israeli, utoe Thumimu!”+ Ndipo Yonathani na Sauli wakachukuliwa, nao watu wakaondoka.+ 42 Basi Sauli akasema: “Pigeni kura+ kuamua kati yangu na Yonathani mwanangu.” Ndipo Yonathani akachukuliwa. 43 Kisha Sauli akamwambia Yonathani: “Niambie, Umefanya nini?”+ Basi Yonathani akamwambia na kusema: “Kwa kweli nilionja asali kidogo kwenye ncha ya fimbo iliyo mkononi mwangu.+ Mimi hapa! Na nife!”

44 Ndipo Sauli akasema: “Mungu na afanye hivyo naye azidishe hilo,+ ikiwa hutakufa hakika,+ Yonathani.” 45 Lakini watu wakamwambia Sauli: “Je, Yonathani afe, ambaye ametimiza wokovu+ huu mkubwa katika Israeli? Ni jambo lisilowaziwa!+ Kama anavyoishi Yehova,+ hakuna hata unywele mmoja+ wa kichwa chake utakaoanguka chini; kwa maana alifanya kazi na Mungu leo.”+ Hivyo watu wakamkomboa+ Yonathani, naye hakufa.

46 Basi Sauli akarudi, akaacha kuwafuata Wafilisti, na Wafilisti wakaenda kwao.+

47 Naye Sauli akachukua ufalme juu ya Israeli,+ akaanza kupiga vita kuzunguka pande zote juu ya adui zake wote, juu ya Moabu+ na juu ya wana wa Amoni+ na juu ya Edomu+ na juu ya wafalme wa Soba+ na juu ya Wafilisti;+ na mahali popote alipogeukia, akawatendea kama waliohukumiwa kuwa na hatia.+ 48 Naye akatenda kishujaa,+ akapiga Amaleki+ na kukomboa Israeli kutoka mkononi mwa mporaji wao.

49 Na wana wa Sauli wakawa ni Yonathani+ na Ishvi na Malki-shua,+ na majina ya binti zake wawili, jina la yule aliyezaliwa kwanza lilikuwa Merabu+ na jina la yule mdogo lilikuwa Mikali.+ 50 Na jina la mke wa Sauli lilikuwa Ahinoamu binti ya Ahimaazi, na jina la mkuu wa jeshi lake lilikuwa Abneri+ mwana wa Neri, ndugu ya baba ya Sauli. 51 Na Kishi+ alikuwa baba ya Sauli, na Neri+ baba ya Abneri alikuwa mwana wa Abieli.

52 Na vita vikaendelea kuwa vikali juu ya Wafilisti siku zote za Sauli.+ Na kila mara Sauli alipomwona mwanamume yeyote mwenye nguvu au mwanamume yeyote shujaa, alimchukua ili awe pamoja naye.+

15 Ndipo Samweli akamwambia Sauli: “Yehova alinituma mimi nikutie mafuta+ uwe mfalme juu ya watu wake Israeli, basi sasa isikilize sauti ya maneno ya Yehova.+ 2 Yehova wa majeshi amesema hivi,+ ‘Lazima nitoze hesabu+ yale ambayo Amaleki alimfanyia Israeli alipompinga njiani alipokuwa akipanda kutoka Misri.+ 3 Sasa nenda, umpige Amaleki,+ umwangamize+ pamoja na vitu vyote alivyo navyo, usimhurumie, nawe uwaue,+ mwanamume na mwanamke, mtoto na mtoto anayenyonya,+ ng’ombe pamoja na kondoo, ngamia pamoja na punda.’”+ 4 Basi Sauli akawaita watu na kuwahesabu katika Telaimu,+ watu mia mbili elfu wanaoenda kwa miguu na watu elfu kumi wa Yuda.+

5 Naye Sauli akaja mpaka jiji la Amaleki, akavizia kando ya bonde la mto. 6 Wakati huohuo, Sauli akawaambia Wakeni:+ “Nendeni, ondokeni,+ shukeni kutoka katikati ya Waamaleki, nisije nikawafagilia mbali ninyi pamoja nao. Ninyi mliwatendea fadhili zenye upendo wana wote wa Israeli+ walipokuwa wakipanda kutoka Misri.”+ Basi hao Wakeni wakaondoka katikati ya Amaleki. 7 Baada ya hilo Sauli akapiga Amaleki+ kutoka Havila+ mpaka Shuri,+ lililoko mbele ya Misri. 8 Naye akamkamata Agagi+ mfalme wa Amaleki akiwa hai, na watu wengine wote akawaangamiza kwa makali ya upanga.+ 9 Lakini Sauli na watu wakamhurumia Agagi na wanyama bora zaidi wa kundi na mifugo+ na walio wanono na kondoo-dume na vyote vilivyokuwa bora, nao hawakutaka kuwaangamiza.+ Lakini vitu vyote vilivyokuwa vyenye kudharaulika na vyenye kukataliwa, wakaviangamiza.

10 Basi neno la Yehova likamjia Samweli, likisema: 11 “Ninajuta+ kwamba nimemfanya Sauli kuwa mfalme, kwa sababu amegeuka+ asinifuate mimi, naye hakutenda maneno yangu.”+ Nalo jambo hilo likawa lenye kumtaabisha Samweli,+ akaendelea kumlilia Yehova usiku kucha.+ 12 Kisha Samweli akaamka mapema ili akutane na Sauli asubuhi. Lakini Samweli akaletewa habari, kusema: “Sauli alikuja Karmeli,+ na tazama! alikuwa akijisimamishia mnara wa ukumbusho,+ kisha akageuka, akavuka na kushuka mpaka Gilgali.” 13 Mwishowe Samweli akamjia Sauli, naye Sauli akaanza kumwambia: “Umebarikiwa+ na Yehova. Nimelitimiza neno la Yehova.”+ 14 Lakini Samweli akasema: “Basi maana yake nini hii sauti ya kundi ninayoisikia masikioni mwangu, na sauti ya mifugo ninayoisikia?”+ 15 Naye Sauli akasema: “Wamewaleta kutoka kwa Waamaleki, kwa sababu watu+ waliwahurumia wanyama walio bora zaidi wa kundi na mifugo, kwa kusudi la kutoa dhabihu kwa Yehova, Mungu wako;+ lakini vitu vilivyobaki tumeviangamiza.” 16 Ndipo Samweli akamwambia Sauli: “Acha! Nami nitakuambia yale ambayo Yehova aliniambia usiku wa jana.”+ Basi akamwambia: “Sema!”

17 Na Samweli akaendelea kusema: “Je, haikuwa wakati ulipokuwa mdogo machoni pako mwenyewe+ kwamba ukawa kichwa cha makabila ya Israeli, na Yehova akakutia mafuta+ uwe mfalme juu ya Israeli? 18 Baadaye Yehova akakupa kazi na kusema, ‘Nenda, uwaangamize wale watenda-dhambi,+ Waamaleki, nawe upigane nao mpaka utakapokuwa umewaangamiza.’+ 19 Basi kwa nini hukuitii sauti ya Yehova, bali ukakimbilia nyara kwa pupa,+ ukafanya yaliyo mabaya machoni pa Yehova?”+

20 Hata hivyo, Sauli akamwambia Samweli: “Lakini mimi nimeitii+ sauti ya Yehova kwa kuwa nilienda kufanya kazi ambayo Yehova alikuwa amenituma, nami nikamleta Agagi+ mfalme wa Amaleki, lakini Amaleki nimemwangamiza.+ 21 Nao watu+ wakachukua kutoka katika nyara kondoo na ng’ombe, walio bora zaidi kati yao kama kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuangamizwa, ili wamtolee+ Yehova, Mungu wako dhabihu katika Gilgali.”+

22 Naye Samweli akasema: “Je, Yehova hupendezwa sana na matoleo ya kuteketezwa+ na dhabihu kuliko kuitii sauti ya Yehova? Tazama! Kutii+ ni bora kuliko dhabihu,+ na kusikiliza kuliko mafuta+ ya kondoo-dume; 23 kwa maana uasi+ ni sawa na dhambi ya uaguzi,+ na kwenda kwa kimbelembele ni sawa na kutumia nguvu za uchawi na terafimu.+ Kwa kuwa umelikataa neno la Yehova,+ basi yeye pia amekukataa wewe usiwe mfalme.”+

24 Ndipo Sauli akamwambia Samweli: “Nimetenda dhambi;+ kwa kuwa nimevunja agizo la Yehova na maneno yako, kwa sababu niliwaogopa watu+ na kwa hiyo nikaitii sauti yao. 25 Na sasa, tafadhali, isamehe+ dhambi yangu, na urudi pamoja nami ili nisujudu+ mbele za Yehova.” 26 Lakini Samweli akamwambia Sauli: “Sitarudi pamoja nawe, kwa kuwa umelikataa neno la Yehova, naye Yehova amekukataa wewe usiendelee kuwa mfalme juu ya Israeli.”+ 27 Naye Samweli alipokuwa akigeuka akikaribia kwenda, akaukamata haraka upindo wa koti lake lisilo na mikono, lakini likararuka.+ 28 Ndipo Samweli akamwambia: “Yehova ameurarua+ utawala wa kifalme wa Israeli kutoka kwako leo, naye hakika atampa mwenzako ambaye ni bora kuliko wewe.+ 29 Na zaidi ya hayo, Mtukufu wa Israeli+ hatasema uwongo,+ wala Yeye hataona majuto, kwa maana Yeye si mtu wa udongo hata aone majuto.”+

30 Naye akasema: “Nimetenda dhambi. Tafadhali sasa, niheshimu+ mbele ya wanaume wazee wa watu wangu na mbele ya Israeli nawe urudi pamoja na mimi, nami nitamsujudia Yehova, Mungu wako.”+ 31 Basi Samweli akarudi nyuma ya Sauli, na Sauli akamsujudia Yehova. 32 Baada ya hayo Samweli akasema: “Mleteni Agagi mfalme wa Amaleki karibu nami.” Ndipo Agagi akaenda kwake kwa kusitasita, na Agagi akaanza kusema moyoni mwake: “Kwa kweli uchungu wa kifo umeondoka.” 33 Hata hivyo, Samweli akasema: “Kama vile upanga wako+ ulivyofanya wanawake kufiwa na watoto, vivyo hivyo mama+ yako atafiwa zaidi na watoto kati ya wanawake.”+ Kwa hiyo Samweli akamkata Agagi vipande-vipande mbele za Yehova katika Gilgali.+

34 Basi Samweli akaenda zake huko Rama, naye Sauli akapanda kwenda nyumbani kwake katika Gibea+ la Sauli. 35 Na Samweli hakumwona Sauli tena mpaka siku ya kifo chake, kwa maana Samweli alikuwa akimwombolezea+ Sauli. Naye Yehova akajuta kwamba alikuwa amemfanya Sauli kuwa mfalme juu ya Israeli.+

16 Mwishowe Yehova akamwambia Samweli: “Ni mpaka wakati gani utamwombolezea Sauli,+ huku mimi, kwa upande mwingine, nimemkataa asitawale akiwa mfalme juu ya Israeli?+ Jaza pembe yako mafuta,+ nawe uende. Nitakutuma kwa Yese+ Mbethlehemu, kwa maana nimejipatia mfalme kati ya wanawe.”+ 2 Lakini Samweli akasema: “Nawezaje kwenda? Mara Sauli atakaposikia habari hizo, ataniua hakika.”+ Na Yehova akaendelea kusema: “Chukua ng’ombe mchanga wa mifugo pamoja nawe, nawe useme, ‘Nimekuja kumtolea Yehova dhabihu.’+ 3 Na umwite Yese aje kwenye dhabihu; nami, kwa upande wangu, nitakujulisha unalopaswa kufanya,+ nawe unitilie mafuta+ yule nitakayekuonyesha.”

4 Na Samweli akafanya yale ambayo Yehova alisema. Alipokuja Bethlehemu,+ wanaume wazee wa jiji wakaanza kutetemeka+ walipokutana naye, nao wakasema: “Je, kuja kwako kunamaanisha amani?”+ 5 Naye akasema: “Kunamaanisha amani. Nimekuja kumtolea Yehova dhabihu. Jitakaseni,+ nanyi mje pamoja nami kwenye dhabihu.” Ndipo akamtakasa Yese na wanawe, kisha akawaita waje kwenye dhabihu. 6 Na ikawa kwamba walipokuwa wakiingia naye akamwona Eliabu,+ mara moja akasema: “Hakika mtiwa-mafuta wake yuko mbele za Yehova.” 7 Lakini Yehova akamwambia Samweli: “Usiangalie sura yake wala urefu+ wa umbo lake, kwa maana nimemkataa. Kwa kuwa Mungu haoni kama mwanadamu anavyoona,+ kwa maana mwanadamu huona kile kinachoonekana kwa macho,+ lakini Yehova huona jinsi moyo+ ulivyo.” 8 Ndipo Yese akamwita Abinadabu,+ akampitisha mbele ya Samweli, lakini akasema: “Yehova hakumchagua huyu pia.” 9 Kisha Yese akampitisha Shamma,+ lakini akasema: “Yehova hakumchagua huyu pia.” 10 Basi Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli; na bado Samweli akamwambia Yese: “Yehova hakuwachagua hawa.”

11 Mwishowe Samweli akamwambia Yese: “Je, hawa ndio wavulana wote?” Naye akasema: “Aliye mdogo zaidi ameachwa mpaka sasa,+ na tazama! analisha kondoo.”+ Kwa hiyo Samweli akamwambia Yese: “Tuma watu, wamlete, kwa sababu hatutaketi kula chakula mpaka atakapokuja hapa.” 12 Basi akatuma watu, naye akaletwa. Naye alikuwa mwekundu,+ kijana mwenye macho yenye kupendeza na mwenye sura nzuri. Ndipo Yehova akasema: “Simama, mtie mafuta, kwa maana huyu ndiye!”+ 13 Basi Samweli akachukua ile pembe ya mafuta,+ akamtia mafuta katikati ya ndugu zake. Na roho ya Yehova ikaanza kutenda kazi juu ya Daudi kuanzia siku hiyo na kuendelea.+ Baadaye Samweli akasimama, akaenda zake mpaka Rama.+

14 Na roho ya Yehova ikaondoka+ juu ya Sauli, nayo roho mbaya+ kutoka kwa Yehova ikamtia hofu. 15 Na watumishi wa Sauli wakaanza kumwambia: “Tazama, roho mbaya ya Mungu inakutia hofu. 16 Tafadhali basi, bwana wetu na aamuru watumishi wako walio mbele yako kwamba watafute mtu mwenye ustadi,+ anayepiga kinubi.+ Na itatukia kwamba wakati roho mbaya ya Mungu inapokuja juu yako, yeye atakipiga kwa mkono wake, na mambo yatakuendea vema.” 17 Basi Sauli akawaambia watumishi wake: “Tafadhali, nipeni mtu anayejua kukipiga vema, kisha mkamlete kwangu.”+

18 Na mmoja wa watumishi akajibu na kusema: “Tazama! Nimeona jinsi mwana fulani wa Yese Mbethlehemu alivyo mwenye ustadi wa kukipiga,+ naye ni shujaa,+ mwanamume mwenye nguvu,+ na mwanamume wa vita na msemaji mwenye akili+ na mwanamume mwenye umbo zuri,+ na Yehova yupo pamoja naye.”+ 19 Kwa hiyo Sauli akatuma wajumbe kwa Yese na kusema: “Mtume kwangu Daudi mwana wako, aliye pamoja na kundi.”+ 20 Basi Yese akachukua punda, mkate na kiriba cha ngozi+ cha divai na mwana-mbuzi, na kuvituma kwa Sauli kwa mkono wa Daudi mwana wake.+ 21 Kwa hiyo Daudi akamjia Sauli na kumtumikia;+ naye akampenda sana, kisha akawa mchukua-silaha wake.+ 22 Basi Sauli akatuma watu kwa Yese, akisema: “Tafadhali, acha Daudi aendelee kunitumikia, kwa kuwa amepata kibali machoni pangu.” 23 Na ikatukia kwamba wakati roho ya Mungu ilipokuja juu ya Sauli, Daudi alichukua kinubi na kukipiga kwa mkono wake; ndipo Sauli akapata faraja na mambo yakamwendea vema, na ile roho mbaya ikaondoka juu yake.+

17 Na Wafilisti+ wakakusanya kambi zao kwa ajili ya vita. Walipokusanyika pamoja huko Soko,+ ambalo ni jiji la Yuda, ndipo wakapiga kambi kati ya Soko na Azeka,+ katika Efes-damimu.+ 2 Naye Sauli na watu wa Israeli wakakusanyika pamoja na kupiga kambi katika nchi tambarare ya chini ya Ela,+ nao wakajipanga kivita ili kukutana na Wafilisti. 3 Nao Wafilisti walikuwa wamesimama juu ya mlima upande huu, na Waisraeli walikuwa wamesimama juu ya mlima upande ule, na bonde lilikuwa katikati yao.

4 Na bingwa fulani akatoka katika kambi za Wafilisti, na jina lake lilikuwa Goliathi,+ kutoka Gathi,+ urefu wake ulikuwa mikono sita na shubiri moja.+ 5 Na kulikuwa na kofia ya shaba juu ya kichwa chake, naye alikuwa amevaa vazi la chuma, lenye mabamba yanayoingiana, na uzito wa vazi lake la chuma+ ulikuwa shekeli elfu tano za shaba. 6 Na kulikuwa na mabamba ya shaba juu ya miguu yake na fumo la shaba+ kati ya mabega yake. 7 Na mpini wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa wafumaji wa nguo,+ na kichwa cha mkuki wake kilikuwa shekeli mia sita za chuma; na mchukuzi wa ngao kubwa alikuwa akitembea mbele yake. 8 Halafu akasimama tuli, akaanza kuviita vikosi vya Israeli+ na kuwaambia: “Kwa nini mnatoka kujipanga kivita? Je, mimi si Mfilisti nanyi je, si watumishi+ wa Sauli? Jichagulieni mwanamume, naye ashuke, anijie. 9 Akiweza kupigana nami na kunipiga, ndipo sisi tutakapokuwa watumishi wenu. Lakini nikimweza na kumpiga, ndipo ninyi pia mtakapokuwa watumishi wetu, nanyi mtatutumikia.”+ 10 Na Mfilisti huyo akaendelea kusema: “Mimi ninavitukana+ vikosi vya Israeli leo. Nipeni mwanamume, tupigane naye!”+

11 Wakati Sauli+ na Israeli wote waliposikia hayo maneno ya yule Mfilisti, wakaingiwa na hofu na kuogopa sana.+

12 Basi Daudi alikuwa mwana wa yule Mwefrathi+ kutoka Bethlehemu ya Yuda ambaye jina lake lilikuwa Yese. Naye alikuwa na wana wanane.+ Na katika siku za Sauli mtu huyo alikuwa tayari ni mzee kati ya watu. 13 Na wale wana watatu wakubwa zaidi wa Yese wakaenda. Walimfuata Sauli kwenda vitani,+ na majina ya wanawe watatu walioenda vitani ni Eliabu+ mzaliwa wa kwanza, na mwana wake wa pili Abinadabu+ na wa tatu Shamma.+ 14 Na Daudi ndiye aliyekuwa mdogo zaidi,+ na wale watatu wakubwa zaidi wakamfuata Sauli.

15 Naye Daudi alikuwa akienda na kurudi kutoka kwa Sauli ili kuchunga kondoo+ za baba yake katika Bethlehemu. 16 Na yule Mfilisti akaendelea kuja mbele wakati wa asubuhi na mapema na wakati wa jioni na kusimama mahali pake kwa siku 40.

17 Ndipo Yese akamwambia Daudi mwana wake: “Tafadhali, wapelekee ndugu zako hii efa ya nafaka iliyochomwa+ na hii mikate kumi, uwapelekee ndugu zako haraka kambini. 18 Na haya mafungu kumi ya maziwa umpelekee mkuu wa elfu yao;+ pia, uangalie hali njema ya ndugu zako,+ nawe uchukue ishara kutoka kwao.” 19 Wakati huohuo, Sauli pamoja nao na pia wanaume wengine wote wa Israeli walikuwa katika nchi tambarare ya chini ya Ela,+ wakipigana na Wafilisti.+

20 Hivyo Daudi akaamka asubuhi na mapema, akawaacha kondoo mkononi mwa mtunzaji, akavichukua vitu vile, akaenda kama Yese alivyokuwa amemwamuru.+ Alipofika kwenye uwanja wa kambi,+ majeshi yalikuwa yakienda katika uwanja wa mapigano,+ nao wakapiga kelele za vita. 21 Na Israeli na Wafilisti wakaanza kujipanga, kikosi kikutane na kikosi. 22 Mara moja Daudi akaiacha mizigo+ aliyokuwa nayo mkononi mwa mtunzaji wa mizigo,+ na kwenda mbio kwenye uwanja wa mapigano. Alipofika, akaanza kuuliza juu ya hali ya ndugu zake.+

23 Alipokuwa akisema nao, tazama, yule bingwa, ambaye jina lake lilikuwa Goliathi+ Mfilisti kutoka Gathi,+ alikuwa akipanda kutoka katika vikosi vya Wafilisti, akaanza kusema maneno yaleyale kama hapo mwanzoni,+ na Daudi akasikiliza. 24 Nao wanaume wote wa Israeli, walipomwona yule mwanamume, wakakimbia kwa sababu yake, wakaogopa sana.+ 25 Na wanaume wa Israeli wakaanza kusema: “Je, mmemwona huyu mwanamume anayepanda? Anapanda ili kuwatukana+ Israeli. Na itatukia kwamba, mtu yule atakayempiga, mfalme atamtajirisha kwa utajiri mwingi sana, naye atampa binti yake,+ kisha ataiweka huru nyumba ya baba yake katika Israeli.”+

26 Na Daudi akaanza kuwaambia watu waliokuwa wamesimama karibu naye: “Atafanyiwa nini mtu atakayempiga yule Mfilisti+ pale na kuondolea mbali shutuma kutoka juu ya Israeli?+ Kwani huyu Mfilisti asiyetahiriwa+ ni nani hata avitukane+ vikosi vya Mungu aliye hai?”+ 27 Nao watu wakamwambia maneno yaleyale ya kwanza, wakisema: “Hivi ndivyo atakavyofanyiwa mtu atakayempiga.” 28 Na Eliabu+ ndugu yake mkubwa zaidi akasikia alipokuwa akisema na watu wale, nayo hasira ya Eliabu ikawaka juu ya Daudi,+ hivi kwamba akasema: “Kwa nini umeshuka kuja huku? Nawe uliacha mkononi mwa nani wale kondoo wachache nyikani?+ Mimi najua vema kimbelembele chako na ubaya wa moyo wako,+ kwa sababu umeshuka kwa kusudi la kuona pigano.”+ 29 Naye Daudi akasema: “Sasa nimefanya nini? Je, halikuwa neno tu?”+ 30 Ndipo akageuka kutoka kando yake, kuelekea kwa mtu mwingine, kisha akasema neno lilelile kama hapo mwanzoni,+ na watu hao wakampa jibu lilelile kama hapo mwanzoni.+

31 Kwa hiyo maneno aliyoyasema Daudi yakasikiwa, nao wakayasema mbele ya Sauli. Basi akatuma watu aletwe. 32 Naye Daudi akamwambia Sauli: “Usiache moyo wa mtu yeyote uzimie ndani yake.+ Mtumishi wako ataenda na kupigana na huyu Mfilisti.”+ 33 Lakini Sauli akamwambia Daudi: “Wewe huwezi kwenda juu ya huyu Mfilisti kupigana naye,+ kwa maana wewe ni mvulana tu,+ naye ni mwanamume wa vita tangu uvulana wake.” 34 Na Daudi akaendelea kumwambia Sauli: “Mtumishi wako alikuwa mchungaji wa baba yake kati ya kundi, na simba akaja,+ na pia dubu, na kila mmoja akamchukua kondoo kutoka katika kundi. 35 Nami nikamfuata nyuma yake na kumpiga+ na kuokoa kutoka kinywani mwake. Wakati alipoanza kupigana nami, nikazikamata ndevu zake, nikampiga, nikamuua. 36 Mtumishi wako alimuua simba na dubu vilevile; na huyu Mfilisti+ asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa hao, kwa kuwa amevitukana+ vikosi+ vya Mungu aliye hai.”+ 37 Ndipo Daudi akaongeza: “Yehova, aliyenikomboa kutoka katika makucha ya simba na kutoka katika makucha ya dubu, yeye ndiye atakayenikomboa kutoka mkononi mwa huyu Mfilisti.”+ Kwa hiyo Sauli akamwambia Daudi: “Nenda, na Yehova awe pamoja nawe.”+

38 Basi Sauli akamvika Daudi mavazi yake, akaweka kofia ya shaba juu ya kichwa chake, halafu akamvika vazi la chuma. 39 Kisha Daudi akafunga upanga wake juu ya mavazi yake, akaanza kwenda, lakini hakuweza, kwa sababu hakuwa amevijaribu vitu hivyo. Mwishowe Daudi akamwambia Sauli: “Mimi siwezi kwenda nikiwa nimevaa vitu hivi, kwa maana sijavijaribu bado.” Kwa hiyo Daudi akavivua.+ 40 Naye akachukua fimbo yake mkononi mwake, akajichagulia mawe matano, yaliyo laini kabisa, kutoka katika bonde la mto, akayatia katika mfuko wake wa mchungaji ambao ulikuwa mkoba wake, na kombeo+ lilikuwa mkononi mwake. Akaanza kumkaribia yule Mfilisti.

41 Naye yule Mfilisti akaanza kuja, akamkaribia Daudi zaidi na zaidi, na yule mtu aliyechukua ile ngao kubwa alikuwa mbele yake. 42 Sasa yule Mfilisti alipotazama na kumwona Daudi, akaanza kumdharau+ kwa sababu alikuwa mvulana tu,+ mwekundu,+ na mwenye sura nzuri.+ 43 Kwa hiyo Mfilisti akamwambia Daudi: “Je, mimi ni mbwa+ hivi kwamba unijie na fimbo?” Basi huyo Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.+ 44 Na huyo Mfilisti akaendelea kumwambia Daudi: “Wewe nikaribie tu, nyama yako nitawapa ndege wa mbinguni na wanyama wa mwituni.”+

45 Naye Daudi akamwambia yule Mfilisti: “Unakuja kwangu ukiwa na upanga na mkuki na fumo,+ lakini mimi naja kwako nikiwa na jina la Yehova wa majeshi,+ Mungu wa vikosi vya Israeli, ambaye umemtukana.+ 46 Leo Yehova atakutia mkononi mwangu,+ nami hakika nitakupiga na kukiondoa kichwa chako juu yako; nami leo nitawapa ndege wa mbinguni na wanyama-mwitu wa dunia mizoga ya kambi ya Wafilisti;+ na watu wa dunia yote watajua kwamba kuna Mungu aliye wa Israeli.+ 47 Na kutaniko hili lote watajua kwamba Yehova haokoi kwa upanga wala kwa mkuki,+ kwa sababu vita ni vya Yehova,+ naye atawatia ninyi mkononi mwetu.”+

48 Na itatukia kwamba huyo Mfilisti akasimama, akazidi kuja na kukaribia zaidi na zaidi ili akutane na Daudi, na Daudi akaanza kufanya haraka na kukimbia kuelekea kwenye uwanja wa mapigano ili akutane na yule Mfilisti.+ 49 Ndipo Daudi akatia mkono wake ndani ya mfuko wake, akachukua jiwe kutoka humo, akalitupa kwa kombeo, hivi kwamba akampiga+ yule Mfilisti katika paji la uso wake, na lile jiwe likapenya ndani ya paji la uso wake, naye akaanguka kifudifudi.+ 50 Basi Daudi, akiwa na kombeo na jiwe, akawa mwenye nguvu zaidi kuliko yule Mfilisti, akampiga Mfilisti na kumuua; na hakuna upanga uliokuwa mkononi mwa Daudi.+ 51 Na Daudi akaendelea kukimbia, akasimama juu ya yule Mfilisti. Halafu akachukua upanga wake+ na kuuchomoa kutoka ndani ya ala yake, na kumuua kabisa alipoutumia kukikata kichwa chake.+ Nao Wafilisti wakaona kwamba mwanamume wao mwenye nguvu amekufa, nao wakaanza kukimbia.+

52 Basi wanaume wa Israeli na Yuda wakasimama, wakaanza kupiga kelele na kuwafuatilia+ Wafilisti mpaka bondeni,+ mpaka malango ya Ekroni,+ na Wafilisti waliotiwa majeraha ya kufisha wakazidi kuanguka juu ya njia inayotoka Shaaraimu,+ mpaka Gathi na mpaka Ekroni. 53 Baadaye wana wa Israeli wakarudi kutoka katika kuwafuatilia vikali Wafilisti, wakapora+ kambi zao.

54 Ndipo Daudi akachukua kichwa+ cha yule Mfilisti, akakileta Yerusalemu, na silaha zake akaziweka katika hema lake.+

55 Basi wakati ule Sauli alipomwona Daudi akienda kukutana na yule Mfilisti, alimwambia Abneri+ mkuu wa jeshi: “Huyu mvulana+ ni mwana wa nani,+ Abneri?” Abneri naye akasema: “Kwa uhai wa nafsi yako, Ee mfalme, sijui kabisa!” 56 Kwa hiyo mfalme akasema: “Wewe uliza mvulana huyo ni mwana wa nani.” 57 Basi, mara Daudi aliporudi kutoka katika kumpiga yule Mfilisti, Abneri akamchukua, akamleta mbele ya Sauli, akiwa na kichwa+ cha yule Mfilisti mkononi mwake. 58 Sauli sasa akamwambia: “Wewe mvulana, wewe ni mwana wa nani?” naye Daudi akasema: “Mimi ni mwana wa mtumishi wako Yese+ Mbethlehemu.”+

18 Na ikawa kwamba, mara tu alipomaliza kusema na Sauli, nafsi ya Yonathani+ ikashikamana+ na nafsi ya Daudi, na Yonathani akaanza kumpenda kama nafsi yake mwenyewe.+ 2 Ndipo Sauli akamchukua siku hiyo, naye hakumruhusu arudi nyumbani kwa baba yake.+ 3 Na Yonathani na Daudi wakafanya agano,+ kwa maana alimpenda kama nafsi yake mwenyewe.+ 4 Zaidi ya hayo, Yonathani akavua koti lake lisilo na mikono alilokuwa amevaa, akampa Daudi, na pia mavazi yake, na hata upanga wake na upinde wake na mshipi wake. 5 Naye Daudi akaanza kutoka. Popote ambapo Sauli alikuwa akimtuma, alitenda kwa busara,+ hivi kwamba Sauli akamweka juu ya watu wa vita;+ na ikaonekana vema machoni pa watu wote na pia machoni pa watumishi wa Sauli.

6 Na ikawa kwamba walipokuwa wakiingia, wakati Daudi aliporudi kutoka katika kuwapiga Wafilisti, wanawake wakaanza kutoka katika majiji yote ya Israeli wakiimba+ na kucheza dansi ili kumpokea Sauli, mfalme, wakiwa na matari,+ kwa kushangilia+ na wakiwa na udi. 7 Na wale wanawake waliokuwa wakisherehekea wakawa wakiitikia na kusema:

“Sauli amepiga maelfu yake,

Na Daudi makumi ya maelfu yake.”+

8 Na Sauli akaanza kukasirika sana,+ na neno hilo lilikuwa baya kwa maoni yake, hivi kwamba akasema: “Wamempa Daudi makumi ya maelfu, lakini mimi wamenipa maelfu, basi inabaki tu apewe ufalme!”+ 9 Basi Sauli akawa akimtilia Daudi shaka tangu siku hiyo na kuendelea.+

10 Na ikawa kesho yake+ kwamba roho mbaya ya Mungu ikaanza kutenda kazi juu ya Sauli,+ hivi kwamba akatenda kama nabii+ ndani ya nyumba, huku Daudi akipiga muziki kwa mkono wake,+ kama katika siku za hapo zamani; na mkuki ulikuwa mkononi mwa Sauli.+ 11 Ndipo Sauli akautupa mkuki+ na kusema: “Nitampigilia Daudi ukutani!”+ lakini Daudi akakwepa kutoka mbele yake, mara mbili.+ 12 Na Sauli akaanza kumwogopa+ Daudi kwa maana Yehova alikuwa pamoja naye,+ lakini alikuwa amemwacha Sauli.+ 13 Kwa hiyo Sauli akamwondoa katika ushirika wake,+ akamweka kuwa mkuu wa watu elfu kwa ajili yake; naye akatoka na kuingia kwa ukawaida mbele ya watu.+ 14 Na Daudi alikuwa akitenda kwa busara+ katika njia zake zote, na Yehova alikuwa pamoja naye.+ 15 Na Sauli akaendelea kuona kwamba yeye anatenda kwa busara sana,+ hivi kwamba akamwogopa. 16 Na Israeli na Yuda wote wakampenda Daudi, kwa maana alikuwa akitoka na kuingia mbele yao.

17 Mwishowe Sauli akamwambia Daudi: “Huyu hapa Merabu binti yangu mkubwa zaidi.+ Yeye ndiye nitakayekupa awe mke wako.+ Ila tu jionyeshe kwangu kuwa shujaa na upigane vita vya Yehova.”+ Lakini Sauli alisema moyoni mwake hivi: “Mkono wangu usije juu yake, lakini mkono wa Wafilisti uje juu yake.”+ 18 Ndipo Daudi akamwambia Sauli: “Mimi ni nani na watu wa ukoo wangu ni nani, familia ya baba yangu, katika Israeli, hata niwe mwana-mkwe wa mfalme?”+ 19 Hata hivyo, ikawa kwamba wakati Daudi alipopaswa kupewa Merabu, binti ya Sauli, Adrieli+ Mmeholathi+ alikuwa tayari amepewa Merabu, kuwa mke wake.

20 Basi Mikali,+ binti ya Sauli, alikuwa anampenda Daudi, nao wakamletea Sauli habari hiyo, na jambo hilo likampendeza. 21 Kwa hiyo Sauli akasema: “Nitampa yeye ili awe mtego kwake,+ na ili mkono wa Wafilisti uje juu yake.” Basi Sauli akamwambia Daudi: “Utafanya nami mapatano ya ndoa leo kwa mmoja wa hao wanawake wawili.” 22 Zaidi ya hayo, Sauli akawaamuru watumishi wake: “Semeni hivi na Daudi kisiri, ‘Tazama! Mfalme amependezwa nawe, na watumishi wake wote wamekupenda wewe. Basi sasa fanya mapatano ya ndoa na mfalme.’” 23 Ndipo watumishi wa Sauli wakaanza kusema maneno hayo masikioni mwa Daudi, lakini Daudi akasema: “Je, ni jambo rahisi machoni penu kufanya mapatano ya ndoa na mfalme, na huku mimi ni mtu maskini,+ mwenye heshima ndogo?”+ 24 Kisha watumishi wa Sauli wakamletea habari, wakisema: “Daudi alisema hivi na hivi.”

25 Kwa hiyo Sauli akasema: “Mwambieni Daudi hivi, ‘Mfalme hapendezwi na pesa za mahari,+ lakini anapendezwa na magovi+ mia moja ya Wafilisti, ili ajilipize kisasi+ juu ya adui za mfalme.’” Lakini Sauli alikuwa amepanga hila kwamba Daudi aanguke kwa upanga mkononi mwa Wafilisti. 26 Basi watumishi wake wakampelekea Daudi habari hiyo, naye Daudi akapendezwa na jambo hilo, la kufanya mapatano ya ndoa+ na mfalme, na siku hazikuwa bado zimekwisha. 27 Kwa hiyo Daudi akaondoka pamoja na watu wake, akapiga+ watu mia mbili kati ya Wafilisti, na Daudi akaleta magovi yao,+ akampa mfalme hesabu yake kamili, ili kufanya mapatano ya ndoa na mfalme. Naye Sauli akampa Mikali binti yake awe mke wake.+ 28 Na Sauli akaona na kujua kwamba Yehova alikuwa pamoja na Daudi.+ Naye Mikali, binti ya Sauli, alimpenda yeye.+ 29 Na Sauli akaogopa zaidi tena kwa sababu ya Daudi, Sauli akawa adui ya Daudi sikuzote.+

30 Nao wakuu+ wa Wafilisti wakawa wakitoka, na ikawa kwamba kadiri walivyotoka mara nyingi ndivyo Daudi alivyotenda kwa busara+ zaidi kati ya watumishi wote wa Sauli; na jina lake likaja kuwa lenye thamani sana.+

19 Mwishowe Sauli akamwambia Yonathani mwana wake na watumishi wake wote habari za kumuua Daudi.+ 2 Lakini Yonathani mwana wa Sauli alipendezwa sana na Daudi.+ Kwa hiyo Yonathani akamwambia Daudi, akisema: “Sauli baba yangu anatafuta kukuua. Basi sasa jilinde, tafadhali, wakati wa asubuhi, nawe ukae mahali pa siri na ujifiche.+ 3 Nami, kwa upande wangu, nitatoka na kusimama kando ya baba yangu katika shamba mahali utakapokuwa, nami nitasema na baba yangu kwa ajili yako, kisha nitaona litakalofanyika, nami hakika nitakuambia.”+

4 Basi Yonathani akasema vema+ kumhusu Daudi kwa Sauli baba yake na kumwambia: “Mfalme asitende dhambi+ juu ya Daudi mtumishi wake, kwa maana yeye hakutenda dhambi kwako wewe na kazi zake zimekuwa nzuri sana kwako wewe.+ 5 Naye alitia nafsi yake mkononi mwake,+ na kumpiga yule Mfilisti,+ hivi kwamba Yehova akatimiza wokovu+ mkubwa kwa ajili ya Israeli wote. Wewe uliona jambo hilo, ukaanza kushangilia. Basi kwa nini utende dhambi juu ya damu isiyo na hatia kwa kumfanya Daudi auawe+ bila sababu?”+ 6 Ndipo Sauli akaitii sauti ya Yonathani, na Sauli akaapa: “Kama Yehova anavyoishi,+ yeye hatauawa.” 7 Baadaye Yonathani akamwita Daudi na Yonathani akamwambia maneno hayo yote. Kisha Yonathani akampeleka Daudi kwa Sauli, naye akaendelea kuwa mbele yake kama hapo mwanzoni.+

8 Baada ya muda, vita vikatokea tena; na Daudi akafanya mashambulizi na kupigana na Wafilisti, akawapiga kwa mauaji makubwa,+ wakakimbia kutoka mbele yake.+

9 Na roho mbaya+ ya Yehova ikaja juu ya Sauli alipokuwa ameketi nyumbani mwake, mkuki ukiwa mkononi mwake, huku Daudi akipiga muziki kwa mkono wake. 10 Basi Sauli akatafuta kumpigilia Daudi ukutani+ kwa mkuki, lakini akakwepa+ kutoka mbele ya Sauli, hivi kwamba akaupigilia mkuki ule ndani ya ukuta. Naye Daudi akakimbia ili aponyoke usiku huo.+ 11 Baadaye Sauli akatuma wajumbe+ kwa nyumba ya Daudi ili wailinde na kumuua asubuhi;+ lakini Mikali mke wake akamwambia Daudi, akisema: “Usipoiponya nafsi yako usiku wa leo, kesho utakuwa mtu aliyeuawa.” 12 Mara moja Mikali akamteremsha Daudi kupitia dirishani, ili aende, akimbie na kuponyoka.+ 13 Ndipo Mikali akachukua sanamu ya terafimu+ na kuiweka kwenye kitanda, akaweka wavu wa manyoya ya mbuzi penye kichwa chake, kisha akaifunika kwa vazi.

14 Basi Sauli akatuma wajumbe wamchukue Daudi, lakini mke wake akasema: “Ni mgonjwa.”+ 15 Kwa hiyo Sauli akatuma hao wajumbe wamwone Daudi, akisema: “Mleteni kwangu akiwa katika hicho kitanda chake, nimuue.”+ 16 Wajumbe hao walipoingia, na tazama, kulikuwa na ile sanamu ya terafimu kitandani na wavu wa manyoya ya mbuzi mahali pa kichwa chake. 17 Kwa hiyo Sauli akamwambia Mikali: “Kwa nini ulinidanganya+ hivi, hata ukamwacha adui yangu+ aende zake, aponyoke?” Naye Mikali akamwambia Sauli: “Yeye mwenyewe aliniambia, ‘Niache niende! Kwa nini nikuue?’”

18 Na Daudi akakimbia, akaponyoka,+ akaenda kwa Samweli huko Rama.+ Naye akamwambia mambo yote ambayo Sauli alikuwa amemfanyia. Ndipo yeye na Samweli wakaenda zao, wakaanza kukaa katika Naiothi.+ 19 Mwishowe habari ikamfikia Sauli, ikisema: “Tazama! Daudi yuko huko Naiothi katika Rama.” 20 Mara moja Sauli akatuma wajumbe wamkamate Daudi. Nao walipowaona walio wazee kati ya manabii wakitoa unabii, na Samweli akiwa amesimama katika cheo chake juu yao, roho+ ya Mungu ikaja juu ya wale wajumbe wa Sauli, nao pia wakaanza kutenda kama manabii.+

21 Walipomwambia Sauli habari hizo, mara moja akatuma wajumbe wengine, nao pia wakaanza kutenda kama manabii. Basi Sauli akatuma tena wajumbe wengine, kikundi cha tatu, nao pia wakaanza kutenda kama manabii. 22 Mwishowe yeye pia akaenda Rama. Alipofika kwenye tangi kubwa la maji lililo katika Seku, akaanza kuuliza na kusema: “Samweli na Daudi wako wapi?” Nao wakasema: “Wako Naiothi+ katika Rama.” 23 Naye akaendelea na safari yake kutoka hapo mpaka Naiothi katika Rama, na roho+ ya Mungu ikaja juu yake, ndiyo, juu yake, naye akaendelea kutembea na kutenda kama nabii mpaka alipoingia Naiothi katika Rama. 24 Naye pia akavua mavazi yake na kutenda, yeye pia, kama nabii mbele ya Samweli, akalala ameanguka chini akiwa uchi mchana huo wote na usiku huo wote.+ Hiyo ndiyo sababu walianza kusema: “Je, Sauli pia yumo kati ya manabii?”+

20 Na Daudi akakimbia+ kutoka Naiothi katika Rama. Hata hivyo, akaja na kusema mbele ya Yonathani: “Nimefanya nini?+ Kosa langu ni nini, nami nimetenda dhambi gani mbele ya baba yako, kwa maana anaitafuta nafsi yangu?” 2 Naye akamwambia: “Ni jambo lisilowaziwa!+ Hutakufa. Tazama! Baba yangu hatafanya jambo kubwa wala jambo dogo, asilifunue sikioni mwangu;+ na kwa nini baba yangu anifiche jambo hilo?+ Hilo halitendeki.” 3 Lakini Daudi akaapa+ tena na kusema: “Hakika baba yako anajua kwamba nimepata kibali machoni pako,+ na hivyo atasema, ‘Yonathani asijue jambo hili, asije akaumia moyoni.’ Lakini, kwa kweli, kama Yehova anavyoishi+ na kama nafsi yako inavyoishi,+ kuna kama hatua moja tu kati yangu na kifo!”+

4 Na Yonathani akaendelea kumwambia Daudi: “Lolote ambalo nafsi yako itasema nitakufanyia.” 5 Ndipo Daudi akamwambia Yonathani: “Tazama! Kesho ni mwezi mpya,+ nami lazima niketi pamoja na mfalme kwenye mlo; nawe uniache niende, nami nitajificha+ shambani mpaka jioni siku ya tatu. 6 Na baba yako akinikosa kwa vyovyote, ndipo useme, ‘Daudi aliniomba kwa bidii ruhusa ya kutokuwepo ili akimbie kwenda Bethlehemu+ jiji lake, kwa maana kuna dhabihu ya kila mwaka huko kwa ajili ya familia yote.’+ 7 Yeye akisema hivi, ‘Ni vema!’ hilo litamaanisha amani kwa mtumishi wako. Lakini akikasirika kwa vyovyote, ujue kwamba ameazimia jambo baya.+ 8 Nawe umwonyeshe mtumishi wako fadhili zenye upendo,+ kwa maana umemwingiza mtumishi wako pamoja nawe katika agano+ la Yehova. Lakini kama kuna kosa ndani yangu,+ wewe mwenyewe niue, kwa nini kunipeleka kwa baba yako?”

9 Kwa hiyo Yonathani akasema: “Hilo ni jambo lisilowaziwa kukuhusu! Lakini nikijua kwa vyovyote kwamba baba yangu ameazimia uovu uje juu yako, je, sitakuambia jambo hilo?”+ 10 Ndipo Daudi akamwambia Yonathani: “Ni nani atakayeniambia ikiwa baba yako huenda akujibu neno kali?” 11 Naye Yonathani akamwambia Daudi: “Wewe njoo tu, twende shambani.” Basi wote wawili wakaenda shambani. 12 Na Yonathani akaendelea kumwambia Daudi: “Yehova Mungu wa Israeli+ na awe shahidi+ kwamba nitampima baba yangu karibu wakati kama huu hapo kesho, au siku ya tatu, na ikiwa ana mwelekeo mwema kwa Daudi, je, hapo sitatuma neno kwako na kufunua habari hizo sikioni mwako? 13 Kwa hiyo Yehova na amtendee Yonathani hivyo na kuzidi,+ ikiwa, itakuwa vema kwa baba yangu kukutendea uovu, nami nisikufunulie habari hizo sikioni mwako na kukuacha uende zako, nawe hakika usiende kwa amani. Yehova na awe pamoja nawe,+ kama vile alivyokuwa pamoja na baba yangu.+ 14 Na wewe je, ikiwa nitakuwa hai bado,+ ndiyo, je, hutanionyesha fadhili zenye upendo za Yehova, ili nisife?+ 15 Nawe hutakatilia mbali fadhili zako zenye upendo zisiwe na nyumba yangu mpaka wakati usio na kipimo.+ Wala, wakati Yehova atakapokatilia mbali adui za Daudi, kila mmoja kutoka usoni pa nchi, 16 jina la Yonathani halitakatiliwa mbali kutoka katika nyumba ya Daudi.+ Na lazima Yehova atalitaka mkononi mwa adui za Daudi.” 17 Basi Yonathani akamwapia tena Daudi kwa sababu ya upendo wake kwake; kwa maana alimpenda jinsi alivyoipenda nafsi yake mwenyewe.+

18 Na Yonathani akaendelea kumwambia: “Kesho ni mwezi mpya,+ nawe utakosekana, kwa sababu kiti chako kitakuwa wazi. 19 Na hakika utakosekana sana siku ya tatu; nawe uje mahali ulipojificha+ ile siku ya kazi, ukae karibu na hili jiwe hapa. 20 Nami nitapiga mishale mitatu upande mmoja wa jiwe hili, niitupe mahali nitakapotaka kuelekea shabaha. 21 Na tazama! nitamtuma mtumishi, nikisema, ‘Nenda, tafuta ile mishale.’ Nikimwambia mtumishi waziwazi hivi, ‘Tazama! Mishale iko upande huu wako, ichukue,’ ndipo uje, kwa maana hilo linamaanisha amani kwako, wala hakuna jambo, kama Yehova anavyoishi.+ 22 Lakini nikimwambia hivi huyo mvulana, ‘Tazama! Mishale iko mbali zaidi kutoka kwako,’ basi nenda, kwa kuwa Yehova amekutuma uende zako. 23 Na kuhusu neno hili ambalo tumesema+ mimi na wewe, tazama, Yehova na awe kati yangu na wewe mpaka wakati usio na kipimo.”+

24 Ndipo Daudi akajificha shambani.+ Nao mwezi mpya ukafika, naye mfalme akaketi kula mlo.+ 25 Na mfalme alikuwa ameketi katika kiti chake kama katika zile nyakati nyingine, katika kiti kilicho kando ya ukuta; na Yonathani alikuwa anamwelekea, na Abneri+ alikuwa ameketi kando ya Sauli, lakini mahali pa Daudi palikuwa wazi. 26 Na Sauli hakusema lolote siku hiyo, kwa maana alisema moyoni mwake: “Jambo fulani limetokea, naye si safi,+ kwa kuwa hajatakaswa.” 27 Na ikawa kwamba, katika siku iliyofuata mwezi mpya, katika siku ya pili, mahali pa Daudi paliendelea kuwa wazi. Kwa hiyo Sauli akamwambia Yonathani mwana wake: “Kwa nini mwana wa Yese+ hakuja kwenye mlo jana wala leo?” 28 Basi Yonathani akamjibu Sauli: “Daudi aliniomba kwa bidii ruhusa ya kutokuwepo ili aende Bethlehemu.+ 29 Naye akaendelea kusema, ‘Tafadhali niache niende, kwa maana tuna dhabihu ya familia jijini, na ndugu yangu mwenyewe ndiye aliyeniamuru. Basi sasa, ikiwa nimepata kibali machoni pako, acha niende kisirisiri, ili niwaone ndugu zangu.’ Ndiyo sababu hakuja kwenye meza ya mfalme.” 30 Ndipo hasira+ ya Sauli ikawaka juu ya Yonathani naye akamwambia: “Wewe mwana wa mjakazi mwasi,+ je, mimi sijui vema kwamba unamchagua mwana wa Yese, kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya sehemu za siri za mama yako?+ 31 Kwa maana siku zote ambazo mwana wa Yese atakuwa hai katika nchi, wewe na ufalme wako hutasimama imara.+ Basi sasa tuma watu umlete kwangu, kwa maana amekusudiwa kufa.”+

32 Hata hivyo, Yonathani akamjibu Sauli baba yake na kumwambia: “Kwa nini auawe?+ Amefanya nini?”+ 33 Ndipo Sauli akamtupia mkuki, ili ampige;+ na Yonathani akajua kwamba baba yake alikuwa ameazimia kumuua Daudi.+ 34 Mara moja Yonathani akasimama kutoka mezani akiwa na hasira kali,+ naye hakula mkate katika siku ya pili baada ya mwezi mpya, kwa maana alikuwa ameumizwa moyoni kwa habari ya Daudi,+ kwa sababu baba yake mwenyewe alikuwa amemfedhehesha.+

35 Na ikawa asubuhi kwamba Yonathani akatoka kwenda zake katika lile shamba mahali alipoagana kukutana na Daudi,+ na mtumishi kijana alikuwa pamoja naye. 36 Naye akamwambia mtumishi wake: “Tafadhali kimbia, tafuta ile mishale ninayopiga.”+ Mtumishi akakimbia, naye akapiga mshale ili umpite, uende mbele yake. 37 Mtumishi yule alipofika mahali pa mshale aliokuwa amepiga Yonathani, Yonathani akaanza kuita kutoka nyuma ya mtumishi na kusema: “Je, mshale hauko mbali zaidi na wewe?”+ 38 Naye Yonathani akaendelea kuita kutoka nyuma ya mtumishi: “Upesi! Fanya haraka! Usisimame tuli!” Na yule mtumishi wa Yonathani akaiokota ile mishale, kisha akarudi kwa bwana wake. 39 Lakini mtumishi huyo hakujua lolote; ila Yonathani na Daudi peke yao ndio waliojua jambo hilo. 40 Kisha Yonathani akampa mtumishi wake silaha zake na kumwambia: “Nenda, zipeleke jijini.”

41 Yule mtumishi akaenda. Naye Daudi akasimama kutoka hapo karibu na upande wa kusini. Kisha akaanguka kifudifudi+ na kuinama mara tatu; nao wakaanza kubusiana+ na kuliliana, mpaka ikawa Daudi ndiye aliyelia zaidi.+ 42 Na Yonathani akaendelea kumwambia Daudi: “Nenda kwa amani,+ kwa maana tumeapa,+ sisi wawili, katika jina la Yehova, tukisema, ‘Yehova na awe kati yangu na wewe na kati ya uzao wangu na uzao wako mpaka wakati usio na kipimo.’”+

Basi Daudi akaondoka, akaenda zake, na Yonathani akarudi jijini.

21 Baadaye Daudi akafika Nobu+ kwa Ahimeleki+ kuhani; naye Ahimeleki akaanza kutetemeka alipokutana na Daudi, kisha akamwambia: “Kwa nini uko peke yako, wala hakuna yeyote aliye pamoja nawe?”+ 2 Ndipo Daudi akamwambia Ahimeleki kuhani: “Mfalme mwenyewe aliniamuru kuhusu habari fulani,+ naye akaniambia, ‘Usiache yeyote ajue lolote kuhusu habari ninayokutuma na kuhusu yale ambayo nimekuamuru.’ Nami nimefanya mapatano ya kukutana mahali fulani pamoja na vijana. 3 Basi sasa, ikiwa kuna mikate mitano pamoja nawe, nipe mkononi mwangu, au chochote kinachoweza kupatikana.”+ 4 Lakini yule kuhani akamjibu Daudi na kusema: “Hakuna mkate wa kawaida mkononi mwangu, lakini kuna mkate mtakatifu;+ ikiwa tu hao vijana wamejiepusha na wanawake.”+ 5 Kwa hiyo Daudi akamjibu kuhani na kumwambia: “Wanawake wamekaa mbali nasi kama ilivyokuwa hapo mwanzoni nilipotoka,+ na viungo vya hao vijana vingali ni vitakatifu, ingawa utume wenyewe ni wa kawaida. Na je, si zaidi leo, mtu anapokuwa mtakatifu katika kiungo chake?” 6 Basi kuhani akampa kilicho kitakatifu,+ kwa sababu hakukuwa na mkate mwingine hapo isipokuwa mkate wa wonyesho uliokuwa umeondolewa mbele za Yehova+ ili kuweka mkate mpya hapo, siku ambayo uliondolewa.

7 Basi mmoja wa watumishi wa Sauli alikuwa hapo siku hiyo, akiwa amezuiliwa+ mbele za Yehova, na jina lake lilikuwa Doegi+ Mwedomu,+ mkuu wa wachungaji wa Sauli.+

8 Na Daudi akamwambia tena Ahimeleki: “Je, hakuna chochote hapa kwako, mkuki au upanga? Kwa kuwa sikuchukua mkononi mwangu upanga wangu wala silaha zangu, kwa sababu jambo hili la mfalme lilikuwa la haraka.” 9 Ndipo kuhani akasema: “Upanga wa Goliathi+ yule Mfilisti, uliyempiga katika nchi tambarare ya chini ya Ela+—huu hapa, umefungwa katika nguo ya kujitanda, nyuma ya efodi.+ Ikiwa unataka kuuchukua, uchukue, kwa sababu hakuna silaha nyingine yoyote isipokuwa upanga huu.” Naye Daudi akasema tena: “Hakuna upanga mwingine kama huo. Unipe huo.”

10 Kisha Daudi akaondoka, akaendelea kukimbia+ kwa sababu ya Sauli siku hiyo, mwishowe akafika kwa Akishi mfalme wa Gathi.+ 11 Nao watumishi wa Akishi wakaanza kumwambia: “Je, huyu si Daudi mfalme+ wa ile nchi? Je, haikuwa kwa huyu ambaye waliendelea kuitikia kwa kucheza dansi,+ wakisema,

‘Sauli amepiga maelfu yake,

Na Daudi makumi ya maelfu yake’?”+

12 Na Daudi akaanza kuyaweka maneno hayo moyoni mwake, naye akaogopa+ sana kwa sababu ya Akishi mfalme wa Gathi. 13 Kwa hiyo akabadili+ utimamu wake wa akili machoni pao,+ akaanza kujifanya mwenda-wazimu mkononi mwao naye akawa akitia alama kwenye milango ya lango na kuyaacha mate yake yatiririke juu ya ndevu zake. 14 Mwishowe Akishi akawaambia watumishi wake: “Tazameni, mtu huyu anatenda kama mwenda-wazimu. Kwa nini mmemleta kwangu? 15 Je, nimekosa watu walio na wazimu, hivi kwamba mkamleta huyu atende kiwenda-wazimu mbele yangu? Je, huyu anapaswa kuingia nyumbani mwangu?”

22 Basi Daudi akaondoka huko,+ na kukimbilia+ pango+ la Adulamu;+ na ndugu zake na nyumba yote ya baba yake wakasikia habari hiyo, nao wakaondoka, wakashuka kumwendea huko. 2 Na watu wote wenye taabu+ na watu wote waliokuwa na mtu anayewadai deni+ na watu wote waliokuwa na uchungu ndani ya nafsi+ wakaanza kukusanyika pamoja kwake,+ akawa mkuu juu yao;+ na watu mia nne wakaja kuwa pamoja naye.

3 Baadaye Daudi akaondoka huko akaenda Mispe katika Moabu, akamwambia mfalme wa Moabu:+ “Tafadhali, acha baba yangu na mama+ yangu wakae pamoja nanyi mpaka nitakapojua yale ambayo Mungu atanitendea.” 4 Basi akawapa makao mbele ya mfalme wa Moabu, nao wakaendelea kukaa pamoja naye siku zote ambazo Daudi alikuwa mahali pasipoweza kufikiwa.+

5 Baada ya muda, nabii Gadi+ akamwambia Daudi: “Usiendelee kukaa mahali pasipoweza kufikiwa. Nenda zako, unapaswa kurudi katika nchi ya Yuda.”+ Kwa hiyo Daudi akaenda zake, akaingia katika msitu wa Herethi.

6 Na Sauli akasikia kwamba Daudi na wale watu waliokuwa pamoja naye wameonekana. Wakati huo Sauli alikuwa ameketi katika Gibea chini ya mkwaju+ ulio katika mahali pa juu akiwa na mkuki+ wake mkononi mwake, na watumishi wake wote walikuwa wamemzunguka. 7 Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake waliokuwa wamemzunguka: “Tafadhali, sikilizeni, enyi Wabenyamini. Je, mwana wa Yese+ atawapa ninyi nyote mashamba na mizabibu?+ Je, atawaweka nyote kuwa wakuu wa maelfu+ na wakuu wa mamia? 8 Kwa maana mmepanga hila, ninyi nyote, juu yangu; wala hakuna yeyote anayenifunulia masikioni+ mwangu wakati mwanangu mwenyewe anapofanya agano+ na mwana wa Yese, wala hakuna yeyote kati yenu anayenisikitikia na kunifunulia masikioni mwangu kwamba mwanangu mwenyewe amemwinua mtumishi wangu juu yangu kuwa mviziaji kama ilivyo leo hii.”

9 Ndipo Doegi+ Mwedomu, aliyekuwa juu ya watumishi wa Sauli, akajibu na kusema: “Nilimwona mwana wa Yese akija Nobu kwa Ahimeleki+ mwana wa Ahitubu.+ 10 Naye akauliza+ Yehova kwa ajili yake; akampa vyakula,+ akampa upanga+ wa Goliathi yule Mfilisti.” 11 Mara moja mfalme akatuma watu wamwite Ahimeleki mwana wa Ahitubu kuhani na nyumba yote ya baba yake, makuhani waliokuwa katika Nobu.+ Basi wote wakaja kwa mfalme.

12 Sasa Sauli akasema: “Tafadhali, sikiliza, wewe mwana wa Ahitubu!” naye akasema: “Mimi hapa, bwana wangu.” 13 Na Sauli akaendelea kumwambia: “Kwa nini ninyi mmepanga hila juu yangu,+ wewe na mwana wa Yese, kwa kumpa yeye mkate na upanga, na kumuuliza Mungu kwa ajili yake, ili asimame juu yangu kama mviziaji kama ilivyo leo hii?”+ 14 Ndipo Ahimeleki akamjibu mfalme na kusema: “Na ni nani aliye kama Daudi kati ya watumishi wako wote,+ mwaminifu,+ pia mwana-mkwe+ wa mfalme na mkuu juu ya walinzi wako, na mwenye kuheshimiwa nyumbani mwako?+ 15 Je, ni leo nimeanza kumuuliza Mungu+ kwa ajili yake? Ni jambo lisilowaziwa kwangu! Mfalme asiweke jambo lolote juu ya mtumishi wake wala juu ya nyumba nzima ya baba yangu, kwa maana, kwa habari hizi, mtumishi wako hakujua jambo lolote liwe ni kubwa au dogo.”+

16 Lakini mfalme akasema: “Hakika utakufa,+ Ahimeleki, wewe pamoja na nyumba yote ya baba yako.”+ 17 Kwa hiyo mfalme akawaambia wakimbiaji+ waliokuwa wamesimama kumzunguka: “Geukeni, mkawaue makuhani wa Yehova, kwa sababu mkono wao pia uko pamoja na Daudi na kwa sababu walijua kwamba yeye ni mkimbizi wala hawakunifunulia habari hiyo!”+ Lakini wale watumishi wa mfalme hawakutaka kunyoosha mkono wao ili kuwashambulia makuhani wa Yehova.+ 18 Mwishowe mfalme akamwambia Doegi:+ “Wewe geuka, uwashambulie makuhani!” Mara moja Doegi Mwedomu+ akageuka yeye mwenyewe na kuwashambulia hao makuhani, na siku hiyo akawaua+ watu 85 wenye kuvaa efodi+ ya kitani. 19 Akapiga kwa makali ya upanga hata Nobu+ jiji la hao makuhani, mwanamume na mwanamke vilevile, mtoto na vilevile mtoto anayenyonya na ng’ombe na punda na kondoo kwa makali ya upanga.

20 Hata hivyo, mwana mmoja wa Ahimeleki mwana wa Ahitubu, ambaye jina lake lilikuwa Abiathari,+ akaponyoka, akakimbia amfuate Daudi. 21 Naye Abiathari akamjulisha Daudi: “Sauli amewaua makuhani wa Yehova.” 22 Ndipo Daudi akamwambia Abiathari: “Nilijua vema siku ile,+ kwa sababu Doegi Mwedomu alikuwa hapo, kwamba bila shaka atamwambia Sauli.+ Mimi binafsi nimeikosea kila nafsi ya nyumba ya baba yako. 23 Wewe kaa pamoja nami. Usiogope, kwa kuwa yeyote anayeitafuta nafsi yangu anaitafuta nafsi yako, kwa kuwa wewe ni mtu unayehitaji kulindwa pamoja nami.”+

23 Baada ya muda wakamletea Daudi habari, wakisema: “Tazama, Wafilisti wanapiga vita juu ya Keila,+ nao wanapora viwanja vya kupuria.”+ 2 Ndipo Daudi akamuuliza+ Yehova, akisema: “Je, niende, na je, niwapige hawa Wafilisti?” Na Yehova akamwambia Daudi: “Nenda, nawe uwapige Wafilisti, uokoe Keila.” 3 Lakini watu wa Daudi wakamwambia: “Tazama! tunaogopa tukiwa hapa katika Yuda,+ nasi tukienda Keila kupigana na vikosi vya Wafilisti tutaogopa hata zaidi!”+ 4 Kwa hiyo Daudi akauliza tena kutoka kwa Yehova.+ Sasa Yehova akamjibu na kusema: “Ondoka, shuka uende Keila, kwa sababu nitawatia Wafilisti mkononi mwako.”+ 5 Basi Daudi akaenda pamoja na watu wake mpaka Keila, akapigana na Wafilisti na kuchukua mifugo yao, lakini akawapiga wao kwa mauaji makubwa; na Daudi akawa mwokozi wa wakaaji wa Keila.+

6 Sasa ikawa kwamba Abiathari+ mwana wa Ahimeleki alipokimbia kwenda kwa Daudi kule Keila, alishuka na efodi+ mkononi mwake. 7 Baada ya muda, Sauli akajulishwa: “Daudi amekuja Keila.”+ Naye Sauli akaanza kusema: “Mungu amemuuza mkononi mwangu,+ kwa maana amejifungia kwa kuingia katika jiji lenye milango na mapingo.” 8 Kwa hiyo Sauli akawaita watu wote kwenda vitani, washuke mpaka Keila, wamzingire Daudi na watu wake. 9 Naye Daudi akaja kujua kwamba Sauli alikuwa akitunga madhara+ juu yake. Basi akamwambia Abiathari kuhani: “Ilete efodi hapa.”+ 10 Na Daudi akaendelea kusema: “Ee Yehova, Mungu wa Israeli,+ mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anatafuta kuja Keila ili aliharibu jiji kwa sababu yangu.+ 11 Je, wenye mashamba wa Keila watanitia mkononi mwake? Je, Sauli atashuka kuja kulingana na habari ambazo mtumishi wako amesikia? Ee Yehova, Mungu wa Israeli, tafadhali umwambie mtumishi wako.” Ndipo Yehova akasema: “Atashuka.”+ 12 Naye Daudi akaendelea kusema: “Je, wenye mashamba wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwa Sauli?” Naye Yehova akasema: “Watakutia.”+

13 Mara moja Daudi akasimama pamoja na watu wake, karibu watu mia sita,+ wakatoka katika Keila, wakaendelea kutembea mahali popote ambapo waliweza kutembea. Naye Sauli akajulishwa kwamba Daudi aliponyoka kutoka Keila, basi akaacha kwenda. 14 Na Daudi akaanza kukaa nyikani, katika mahali palipo pagumu kufikiwa, naye akaendelea kukaa katika eneo lenye milima katika nyika ya Zifu.+ Na Sauli akaendelea kumtafuta sikuzote,+ naye Mungu hakumtia mkononi mwake.+ 15 Na Daudi akaendelea kuogopa kwa sababu Sauli alikuwa ametoka ili kuitafuta nafsi yake, Daudi alipokuwa katika nyika ya Zifu kule Horeshi.+

16 Sasa Yonathani mwana wa Sauli akasimama, akaenda kwa Daudi kule Horeshi, ili autie nguvu+ mkono wake kuhusiana na Mungu.+ 17 Naye akamwambia: “Usiogope;+ kwa kuwa mkono wa Sauli baba yangu hautakupata, na wewe utakuwa mfalme+ juu ya Israeli, na mimi nitakuwa wa pili kwako; na Sauli baba yangu pia anajua jambo hilo.”+ 18 Ndipo hao wawili wakafanya agano+ mbele za Yehova; na Daudi akaendelea kukaa katika Horeshi, naye Yonathani akaenda nyumbani kwake.

19 Baadaye watu wa Zifu+ wakaenda kwa Sauli kule Gibea,+ wakisema: “Je, Daudi hajifichi+ karibu nasi katika mahali palipo pagumu kufikiwa kule Horeshi,+ katika kilima cha Hakila,+ kilicho upande wa kuume wa Yeshimoni?+ 20 Basi sasa, kulingana na tamaa yote ya nafsi yako+ ya kushuka, Ee mfalme, shuka, na sehemu yetu itakuwa ni kumtia yeye mkononi mwa mfalme.”+ 21 Ndipo Sauli akasema: “Ninyi ni wabarikiwa wa Yehova,+ kwa maana mmenihurumia. 22 Tafadhali nendeni, vumilieni tena kidogo tu, mhakikishe na mwone mahali pake ambapo mguu wake utakuja—yeyote aliyemwona hapo—kwa maana nimeambiwa kwamba bila shaka yeye ni mjanja.+ 23 Angalieni na kuhakikisha kuhusu mahali pote pa kujificha ambapo yeye hujificha; nanyi mrudi kwangu mkiwa na huo ushuhuda, nami nitaenda pamoja nanyi; na itatukia kwamba, ikiwa yupo katika nchi hiyo, nitamtafuta kwa uangalifu kati ya maelfu+ yote ya Yuda.”

24 Kwa hiyo wakaondoka, wakaenda Zifu+ kumtangulia Sauli, huku Daudi na watu wake wakiwa katika nyika ya Maoni+ katika Araba+ upande wa kusini wa Yeshimoni. 25 Baadaye Sauli akaja na watu wake kumtafuta.+ Walipomjulisha Daudi, mara moja akashuka kwenda kwenye mwamba,+ naye akaendelea kukaa katika nyika ya Maoni. Sauli aliposikia habari hiyo, akaenda kumfuatilia+ Daudi katika nyika ya Maoni. 26 Mwishowe Sauli akaja upande huu wa mlima, na Daudi na watu wake wakawa upande mwingine wa mlima huo. Basi Daudi akafanya haraka kuondoka+ kwa sababu ya Sauli; wakati huo wote Sauli na watu wake walikuwa wakimzunguka Daudi na watu wake ili kuwakamata.+ 27 Lakini mjumbe fulani akamjia Sauli, akisema: “Fanya haraka uende, kwa maana Wafilisti wameivamia nchi!” 28 Ndipo Sauli akageuka, akaacha kumfuatilia Daudi,+ akaenda kukutana na Wafilisti. Ndiyo sababu wamepaita mahali hapo Mwamba wa Migawanyiko.

29 Ndipo Daudi akapanda kutoka huko, akaenda kukaa katika mahali palipo pagumu kufikiwa kule En-gedi.+

24 Na ikawa kwamba mara tu Sauli aliporudi baada ya kuwafuatilia Wafilisti,+ wakamletea habari, wakisema: “Tazama! Daudi yuko katika nyika ya En-gedi.”+

2 Na Sauli akachukua watu elfu tatu waliochaguliwa+ kutoka katika Israeli yote kwenda kumtafuta Daudi+ na watu wake juu ya miamba iliyo wazi ya mbuzi wa milimani.+ 3 Mwishowe akafika kwenye mazizi ya mawe ya kondoo kando ya barabara, mahali ambapo palikuwa na pango. Basi Sauli akaingia ndani kwenda haja,+ huku Daudi na watu wake wakiwa katika sehemu za nyuma kabisa za pango hilo,+ wakiwa wameketi. 4 Na watu wa Daudi wakaanza kumwambia: “Hii ndiyo siku ambayo Yehova anakuambia, ‘Tazama! Ninamtia adui yako mkononi mwako,+ nawe umtendee kama inavyoonekana vema machoni pako.’”+ Kwa hiyo Daudi akasimama, akakata kimyakimya upindo wa koti lisilo na mikono la Sauli. 5 Lakini baadaye moyo wa Daudi ukaendelea kumchoma+ kwa sababu alikuwa amekata upindo wa lile koti la Sauli. 6 Basi akawaambia watu wake: “Ni jambo lisilowaziwa kwangu, kwa maoni ya Yehova, kwamba nimfanyie bwana wangu jambo hili, mtiwa-mafuta+ wa Yehova, kwa kunyoosha mkono wangu juu yake, kwa kuwa yeye ni mtiwa-mafuta wa Yehova.”+ 7 Kwa hiyo Daudi akawatawanya watu wake kwa maneno hayo, naye hakuwaruhusu wamshambulie Sauli.+ Naye Sauli akainuka kutoka katika lile pango na kwenda zake.

8 Basi Daudi akainuka baadaye, akatoka nje ya lile pango na kumwita Sauli, akisema: “Bwana wangu+ mfalme!” Ndipo Sauli akatazama nyuma, naye Daudi akainama kifudifudi,+ akasujudu. 9 Na Daudi akaendelea kumwambia Sauli: “Kwa nini unayasikiliza maneno ya watu,+ wakisema, ‘Tazama! Daudi anatafuta kukudhuru’? 10 Tazama, leo macho yako yameona jinsi Yehova alivyokutia leo mkononi mwangu ndani ya pango; na mtu fulani alisema nikuue,+ lakini nikakusikitikia, nikasema, ‘Sitanyoosha mkono wangu juu ya bwana wangu, kwa maana yeye ni mtiwa-mafuta+ wa Yehova.’ 11 Basi ona baba yangu,+ ndiyo, ona mkononi mwangu upindo wa koti lako lisilo na mikono, kwa sababu nilipokata upindo wa koti lako, sikukuua. Ujue na kuona kwamba hakuna ubaya+ wowote wala maasi mkononi mwangu, nami sikutenda dhambi juu yako, huku wewe ukiivizia nafsi yangu ili kuiondolea mbali.+ 12 Yehova na ahukumu kati yangu na wewe;+ na Yehova anilipizie kisasi+ kutoka kwako, lakini mkono wangu mwenyewe hautakuja juu yako.+ 13 Kama vile inavyosema methali ya watu wa kale, ‘Katika waovu uovu utatoka,’+ lakini mkono wangu mwenyewe hautakuja juu yako. 14 Je, mfalme wa Israeli ametoka nje kumfuata nani? Unamfuatilia nani? Mbwa aliyekufa?+ Kiroboto mmoja?+ 15 Na Yehova atakuwa mwamuzi, naye atahukumu kati yangu na wewe, naye ataona na kufanya kesi+ kwa ajili yangu na kunihukumu ili kuniweka huru kutoka mkononi mwako.”

16 Na ikawa kwamba, mara tu Daudi alipomaliza kumwambia Sauli maneno hayo, Sauli akasema: “Je, hii ni sauti yako, Daudi mwanangu?”+ Naye Sauli akapaaza sauti yake, akalia.+ 17 Naye akamwambia Daudi: “Wewe ni mwadilifu kuliko mimi,+ kwa maana wewe ndiye umenitendea mema,+ nami ndiye nimekutendea uovu. 18 Nawe umefunua leo mema ambayo umenitendea kwa maana Yehova alinitia mkononi mwako,+ nawe hukuniua. 19 Kwa maana, mtu akimpata adui yake, je, atamwacha ashike njia aende zake salama?+ Basi Yehova mwenyewe atakupa thawabu ya mema,+ kwa kuwa leo umenitendea hivyo. 20 Na sasa tazama! Najua vema bila shaka kwamba wewe utatawala ukiwa mfalme,+ na kwamba ufalme wa Israeli utadumu mkononi mwako. 21 Basi sasa niapie kwa Yehova+ kwamba hutaukatilia mbali uzao wangu baada yangu na kwamba hutaliangamiza jina langu kutoka katika nyumba ya baba yangu.”+ 22 Kwa hiyo Daudi akamwapia Sauli, kisha Sauli akaenda nyumbani kwake.+ Naye Daudi na watu wake wakapanda, wakaenda mahali palipo pagumu kufikiwa.+

25 Baadaye Samweli+ akafa; na Israeli wote wakakusanyika pamoja, wakamwombolezea+ na kumzika karibu na nyumba yake huko Rama.+ Kisha Daudi akaondoka, akashuka kwenda katika nyika ya Parani.+

2 Sasa palikuwa na mtu fulani katika Maoni,+ na kazi yake ilikuwa katika Karmeli.+ Na mtu huyo alikuwa mkuu sana, naye alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja; naye alikuwa na kazi ya kukata+ kondoo zake manyoya kule Karmeli. 3 Na jina la mtu huyo lilikuwa Nabali,+ na jina la mke wake lilikuwa Abigaili.+ Naye mke huyo alikuwa mwenye busara+ njema na mrembo wa umbo, lakini mume alikuwa mkali na mwenye matendo mabaya;+ naye alikuwa Mkalebu.+ 4 Basi Daudi akasikia akiwa nyikani kwamba Nabali alikuwa akikata kondoo zake manyoya.+ 5 Kwa hiyo Daudi akatuma wanaume kumi vijana, na Daudi akawaambia hao vijana: “Pandeni, mwende Karmeli, mfike kwa Nabali, mkamuulize kwa jina langu kuhusu hali yake.+ 6 Nanyi mkamwambie ndugu yangu hivi, ‘Wema uwe kwako+ na pia wema uwe kwa nyumba yako na wema uwe kwa vyote ulivyo navyo. 7 Na sasa nimesikia kwamba una wakataji-manyoya. Sasa wachungaji wako walikuwa pamoja nasi.+ Hatukuwasumbua,+ wala hakuna chochote chao ambacho kilipotea siku zote walizokuwa katika Karmeli. 8 Waulize hao vijana wako, nao watakuambia, ndipo vijana wangu wapate kibali machoni pako, kwa kuwa tumekuja siku nzuri. Tafadhali, wape watumishi wako na Daudi mwana wako chochote ambacho mkono wako unaweza kupata.’”+

9 Basi wale vijana wa Daudi wakaja na kumwambia Nabali kulingana na maneno hayo yote katika jina la Daudi na kisha wakangoja. 10 Lakini Nabali akawajibu watumishi wa Daudi na kusema: “Daudi ni nani,+ na mwana wa Yese ni nani? Siku hizi watumishi wanaotoroka, kila mmoja kutoka mbele ya bwana wake, wamekuwa wengi.+ 11 Na je, nichukue mkate+ wangu na maji yangu na nyama yangu ambayo nimewachinjia wakataji-manyoya wangu na kuwapa watu ambao sijui hata wanatoka wapi?”+

12 Kwa hiyo vijana wa Daudi wakageuka, wakarudi, wakamletea habari kulingana na maneno hayo yote. 13 Mara hiyo Daudi akawaambia watu wake: “Kila mtu ajifunge upanga wake!”+ Basi kila mtu akajifunga upanga wake na pia Daudi akajifunga upanga wake; wakaanza kupanda nyuma ya Daudi, karibu watu mia nne, huku mia mbili wakibaki kando ya mizigo.+

14 Na wakati huohuo, mmoja wa vijana akaleta habari kwa Abigaili, mke wa Nabali, akisema: “Tazama! Daudi alituma wajumbe kutoka nyikani ili kumtakia bwana wetu mema, lakini akawakemea kwa sauti kali.+ 15 Na watu hao walikuwa wema sana kwetu, nao hawakutusumbua, nasi hatukupoteza hata kitu kimoja siku zote za kutembea kwetu tukiwa shambani.+ 16 Walikuwa ukuta+ kutuzunguka wakati wa usiku na wakati wa mchana, siku zote tulipokuwa pamoja nao, tukichunga kundi. 17 Na sasa ujue na kuona jambo la kufanya, kwa maana msiba umeazimiwa+ juu ya bwana wetu na juu ya nyumba yake yote, kwa maana yeye ni mtu asiyefaa kitu+ sana hata mtu hawezi kusema naye.”

18 Mara moja Abigaili+ akafanya haraka, akachukua mikate mia mbili na mitungi miwili mikubwa ya divai+ na kondoo watano+ na vipimo vitano vya sea vya nafaka iliyochomwa+ na keki mia moja za zabibu kavu+ na keki mia mbili za tini zilizoshinikizwa,+ akazipakia juu ya punda. 19 Kisha akawaambia vijana wake: “Piteni mbele yangu.+ Tazama! Naja nyuma yenu.” Lakini hakumwambia Nabali mume wake jambo lolote.

20 Na ikatukia kwamba alipokuwa amempanda punda+ na kushuka kwenye mlima kisiri, tazama, kumbe, Daudi na watu wake walikuwa wakishuka kuja kukutana naye. Basi akakutana nao. 21 Naye Daudi alikuwa amesema: “Ni kwa ajili ya kukatishwa tamaa tu kwamba nililinda kila kitu cha mtu huyu nyikani wala hakuna hata kitu kimoja kati ya vyote vilivyo vyake ambacho kilipotea,+ na bado ananilipa uovu kwa ajili ya wema.+ 22 Basi Mungu na awafanyie hivyo adui za Daudi na kuzidisha+ ikiwa nitaacha abaki kufikia asubuhi+ yeyote kati ya wote walio wake anayekojoa ukutani.”+

23 Abigaili alipomwona Daudi, akafanya haraka mara moja, akashuka kutoka juu ya yule punda, akaanguka kifudifudi mbele ya Daudi, akainama+ chini. 24 Kisha akaanguka miguuni pake+ na kusema: “Kosa na liwe juu yangu mwenyewe,+ Ee bwana wangu; na, tafadhali mwache kijakazi wako aseme masikioni mwako,+ nawe uyasikilize maneno ya kijakazi wako. 25 Tafadhali, bwana wangu asiweke moyo wake juu ya mtu huyu asiyefaa kitu,+ Nabali, kwa maana, kama lilivyo jina lake, ndivyo alivyo yeye. Nabali ndilo jina lake, na ukosefu wake wa akili uko pamoja naye.+ Lakini mimi kijakazi wako, sikuwaona wale vijana wa bwana wangu uliokuwa umewatuma. 26 Basi sasa, bwana wangu, kama anavyoishi Yehova+ na kama inavyoishi nafsi yako,+ Yehova amekuzuia+ usiingie katika hatia ya damu+ na kufanya mkono wako mwenyewe ukuokoe.+ Basi sasa adui zako na wale wanaotafuta kumdhuru bwana wangu na wawe kama Nabali.+ 27 Na sasa zawadi hii ya baraka+ ambayo kijakazi wako amemletea bwana wangu, ipewe wale vijana wanaotembea katika hatua+ za bwana wangu. 28 Tafadhali, samehe makosa ya kijakazi wako,+ kwa maana bila shaka Yehova atamfanyia bwana wangu nyumba inayodumu,+ kwa maana bwana wangu anapigana vita vya Yehova;+ na ubaya hautapatikana ndani yako siku zako zote.+ 29 Wakati mwanadamu atakaposimama ili kukufuatilia na kuitafuta nafsi yako, nafsi ya bwana wangu itakuwa imefungwa katika mfuko wa uzima+ pamoja na Yehova Mungu wako;+ lakini nafsi ya adui zako yeye ataitupa mbali kama kutoka ndani ya tundu la kombeo.+ 30 Na itatukia kwamba, kwa kuwa Yehova atamfanyia bwana wangu mema kukuelekea kulingana na yote ambayo amesema, hakika atakuweka kuwa kiongozi juu ya Israeli.+ 31 Na usiache hili liwe kwako sababu ya kufadhaika wala kikwazo kwa moyo wa bwana wangu, kwa kumwaga damu bila sababu+ na pia kwa kuacha mkono wa bwana wangu mwenyewe umwokoe.+ Na hakika Yehova atamfanyia mema bwana wangu, nawe utamkumbuka+ kijakazi wako.”

32 Ndipo Daudi akamwambia Abigaili: “Abarikiwe Yehova Mungu wa Israeli,+ aliyekutuma leo unipokee! 33 Busara yako na ibarikiwe,+ nawe ubarikiwe, ambaye umenizuia leo nisiingie katika hatia ya damu+ na kuacha mkono wangu mwenyewe uniokoe.+ 34 Na, kwa upande mwingine, kama anavyoishi Yehova Mungu wa Israeli, ambaye amenizuia nisikudhuru wewe,+ kama hungelifanya haraka ili uje kunipokea,+ kufikia wakati wa nuru ya asubuhi hangelibaki kwa Nabali mtu yeyote anayekojoa ukutani.”+ 35 Kwa hiyo Daudi akapokea kutoka mkononi mwake vitu ambavyo alikuwa amemletea, naye akamwambia: “Panda uende kwa amani+ nyumbani kwako. Tazama, nimeisikiliza sauti yako na kukufikiria+ wewe.”

36 Baadaye Abigaili akaingia kwa Nabali, na tazama, mwanamume huyo alikuwa akifanya karamu katika nyumba yake, karamu kama ile ya mfalme;+ na moyo wa Nabali ulikuwa ukichangamka ndani yake, naye alikuwa amelewa+ kabisa; na kufikia nuru ya asubuhi mke hakuweza kumwambia jambo lolote, liwe ni dogo au kubwa. 37 Na ikawa kwamba asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, mke wake akamwambia mambo hayo yote. Na moyo+ wa mwanamume huyo ukafa ndani yake, naye akawa kama jiwe. 38 Baada ya hapo karibu siku kumi zikapita, ndipo Yehova akampiga+ Nabali, naye akafa.

39 Basi Daudi akasikia kwamba Nabali amekufa, kwa hiyo akasema: “Abarikiwe Yehova, ambaye amefanya kesi+ ya shutuma+ yangu ili kuniweka huru kutoka mkononi mwa Nabali na ambaye amemzuia mtumishi wake asifanye ubaya,+ na Yehova ameurudisha ubaya wa Nabali juu ya kichwa chake mwenyewe!”+ Kisha Daudi akatuma watu na kumwambia Abigaili kwamba alipenda kumchukua awe mke wake.+ 40 Basi watumishi wa Daudi wakamjia Abigaili kule Karmeli na kumwambia hivi: “Daudi ametutuma kwako tukuchukue uwe mke wake.” 41 Mara moja akasimama, akainama kifudifudi,+ akasema: “Tazama, mimi ni kijakazi wako, niwe mjakazi wa kuosha miguu+ ya watumishi wa bwana wangu.”+ 42 Kisha Abigaili+ akafanya haraka, akaondoka, akapanda punda+ pamoja na wanawali wake watano wakiwa wanatembea nyuma yake; akaenda pamoja na wajumbe wa Daudi, na kisha akawa mke wake.

43 Daudi pia alikuwa amemchukua Ahinoamu+ kutoka Yezreeli;+ na hao wanawake wawili wakaja kuwa wake zake.+

44 Lakini Sauli alikuwa amemkabidhi Mikali+ binti yake, mke wa Daudi, kwa Palti+ mwana wa Laishi, aliyetoka Galimu.+

26 Baada ya muda watu wa Zifu+ wakamjia Sauli kule Gibea,+ wakisema: “Je, Daudi hajifichi katika kilima cha Hakila,+ kinachoelekeana na Yeshimoni?”+ 2 Naye Sauli akaondoka,+ akashuka, akaenda katika nyika ya Zifu, na watu elfu tatu+ walikuwa pamoja naye, watu waliochaguliwa wa Israeli, kumtafuta Daudi katika nyika ya Zifu. 3 Na Sauli akapiga kambi katika kilima cha Hakila, kinachoelekeana na Yeshimoni, kando ya barabara, naye Daudi alikuwa akikaa nyikani. Naye akaona kwamba Sauli amemfuata nyikani. 4 Basi Daudi akatuma wapelelezi+ ili ajue kama kweli Sauli amekuja. 5 Baadaye Daudi akasimama, akaenda mahali ambapo Sauli alikuwa amepiga kambi, na Daudi akaona mahali ambapo Sauli alikuwa amelala, na pia Abneri+ mwana wa Neri mkuu wa jeshi lake; na Sauli alikuwa amelala katika uwanja wa kambi,+ watu wakiwa wamepiga kambi kumzunguka. 6 Ndipo Daudi akamwambia Ahimeleki Mhiti,+ na Abishai+ mwana wa Seruya,+ ndugu ya Yoabu: “Ni nani atakayeshuka aende pamoja nami kwa Sauli kambini?” Naye Abishai akasema: “Mimi nitashuka pamoja nawe.”+ 7 Na Daudi akaondoka pamoja na Abishai kwenda kwa wale watu wakati wa usiku; na tazama! Sauli alikuwa amelala katika uwanja wa kambi, huku mkuki wake ukiwa umechomekwa chini penye kichwa chake, na Abneri na watu walikuwa wamelala kumzunguka.

8 Sasa Abishai akamwambia Daudi: “Mungu leo amemtia adui yako mkononi mwako.+ Tafadhali sasa, acha nimpigilie chini kwa mkuki mara moja tu, nami sitafanya hivyo mara mbili.” 9 Hata hivyo, Daudi akamwambia Abishai: “Usimwangamize, kwani ni nani amepata kunyoosha mkono wake juu ya mtiwa-mafuta wa Yehova,+ naye akabaki bila hatia?”+ 10 Na Daudi akasema tena: “Kama Yehova anavyoishi,+ Yehova mwenyewe atampiga;+ au siku yake itakuja+ naye atakufa, au ataanguka vitani,+ na kufagiliwa mbali.+ 11 Ni jambo lisilowaziwa+ kwangu, kwa maoni ya Yehova,+ kwamba ninyooshe mkono wangu+ juu ya mtiwa-mafuta wa Yehova!+ Kwa hiyo, tafadhali sasa, chukua mkuki ulio karibu na kichwa chake na lile gudulia la maji, nasi twende zetu.” 12 Basi Daudi akachukua ule mkuki na lile gudulia la maji kutoka pale karibu na kichwa cha Sauli, kisha wakaondoka; na hakuna yeyote aliyeona+ wala yeyote aliyeangalia wala yeyote aliyeamka, kwa maana wote walikuwa wamelala, kwa sababu walikuwa wameshikwa na usingizi mzito+ kutoka kwa Yehova. 13 Ndipo Daudi akapita, akaenda upande ule mwingine, akasimama kwenye kilele cha mlima akiwa umbali fulani, nafasi iliyokuwa kati yao ilikuwa ni kubwa.

14 Naye Daudi akaanza kuwaita watu na Abneri mwana wa Neri, akisema: “Je, hutajibu, Abneri?” Kwa hiyo Abneri+ akajibu na kusema: “Wewe ni nani ambaye umemwita mfalme?” 15 Na Daudi akaendelea kumwambia Abneri: “Je, wewe si mwanamume? Na ni nani aliye kama wewe katika Israeli? Kwa nini, basi, hukumlinda bwana wako mfalme? Kwa sababu mmoja wa watu aliingia ili kumwangamiza mfalme bwana wako.+ 16 Jambo hili ambalo umefanya si jema. Kama Yehova anavyoishi,+ ninyi mnastahili kufa,+ kwa sababu hamkumlinda+ bwana wenu, mtiwa-mafuta wa Yehova.+ Na sasa ona mahali ulipo mkuki wa mfalme na gudulia la maji+ vilivyokuwa karibu na kichwa chake.”

17 Naye Sauli akaanza kutambua sauti ya Daudi na kusema: “Je, hii ni sauti yako, Daudi mwanangu?”+ Naye Daudi akasema: “Ni sauti yangu, bwana wangu mfalme.” 18 Naye akaongeza kusema: “Kwa nini bwana wangu anamfuatilia mtumishi wake,+ kwani nimefanya nini, na kuna ubaya gani mkononi mwangu?+ 19 Na sasa, tafadhali, bwana wangu mfalme na ayasikilize maneno ya mtumishi wake: Ikiwa ni Yehova aliyekuchochea juu yangu, na anuse harufu ya toleo la nafaka.+ Lakini ikiwa ni wanadamu,+ wamelaaniwa mbele za Yehova,+ kwa sababu leo wamenifukuza nisione kuwa nimeshikamana na urithi wa Yehova,+ wakisema, ‘Nenda, tumikia miungu mingine!’+ 20 Na sasa usiache damu yangu imwagike chini mbele za uso wa Yehova;+ kwa maana mfalme wa Israeli ametoka kwenda kutafuta kiroboto mmoja,+ kama vile mtu anavyomfukuza kwale juu ya milima.”+

21 Naye Sauli akasema: “Nimetenda dhambi.+ Rudi, Daudi mwanangu, kwa maana sitakudhuru tena, kwa sababu ya ukweli wa kwamba nafsi yangu imekuwa na thamani+ machoni pako leo. Tazama! Nimetenda kipumbavu, nami nimekosea sana.” 22 Ndipo Daudi akajibu na kusema: “Tazama, mkuki wa mfalme ni huu, basi mmoja wa vijana na aje, auchukue. 23 Na Yehova ndiye atakayemlipa kila mmoja uadilifu+ wake na uaminifu wake, kwa kuwa Yehova leo alikutia mkononi mwangu, nami sikutaka kunyoosha mkono wangu juu ya mtiwa-mafuta wa Yehova.+ 24 Na tazama! kama vile nafsi yako ilivyokuwa yenye thamani machoni pangu leo hii, vivyo hivyo nafsi yangu na iwe yenye thamani machoni pa Yehova,+ ili anikomboe kutoka katika taabu yote.”+ 25 Ndipo Sauli akamwambia Daudi: “Ubarikiwe, Daudi mwanangu. Bila shaka utafanya kazi nawe bila shaka utakuwa mshindi.”+ Daudi akaenda zake; lakini Sauli akarudi kwake.+

27 Hata hivyo, Daudi akasema moyoni mwake: “Sasa mkono wa Sauli utanifagilia mbali siku moja. Hakuna jambo bora kwangu kuliko kuponyoka+ bila shaka, niende katika nchi ya Wafilisti;+ na Sauli atakata tamaa ya kunitafuta tena katika eneo lote la Israeli,+ nami nitaponyoka kutoka mkononi mwake.” 2 Basi Daudi akaondoka, yeye pamoja na watu mia sita+ waliokuwa pamoja naye, akavuka kwenda kwa Akishi+ mwana wa Maoki, mfalme wa Gathi. 3 Na Daudi akaendelea kukaa na Akishi katika Gathi, yeye pamoja na watu wake, kila mmoja na nyumba yake,+ Daudi na wake zake wawili, Ahinoamu+ Myezreeli na Abigaili,+ mke wa Nabali Mkarmeli. 4 Baada ya muda Sauli akapelekewa habari kwamba Daudi alikuwa amekimbia kwenda Gathi, kwa hiyo hakwenda kumtafuta tena.+

5 Ndipo Daudi akamwambia Akishi: “Ikiwa sasa nimepata kibali machoni pako, na wanipe mahali katika moja la majiji ya mashambani, ili nikae huko; kwa nini mtumishi wako akae katika jiji la kifalme pamoja nawe?” 6 Basi Akishi akampa Siklagi+ siku hiyo. Ndiyo sababu Siklagi limekuwa la wafalme wa Yuda mpaka leo hii.

7 Na hesabu ya siku ambazo Daudi alikaa katika nchi ya mashambani ya Wafilisti ikawa mwaka mmoja na miezi minne.+ 8 Na Daudi akapanda pamoja na watu wake ili wavamie Wageshuri+ na Wagirzi na Waamaleki;+ kwa maana walikuwa wakikaa katika nchi iliyoanzia Telamu+ mpaka Shuri+ na kushuka mpaka nchi ya Misri. 9 Naye Daudi akaipiga nchi, lakini hakuhifadhi hai mwanamume wala mwanamke;+ naye akachukua makundi na mifugo na punda na ngamia na mavazi, kisha akarudi, akaja kwa Akishi. 10 Ndipo Akishi akasema: “Mlivamia wapi leo?” Naye Daudi akasema:+ “Upande wa kusini wa Yuda+ na upande wa kusini wa Wayerahmeeli+ na upande wa kusini wa Wakeni.”+ 11 Na kuhusu mwanamume na mwanamke, Daudi hakuhifadhi hai yeyote ili kuwaleta Gathi, akisema: “Wasije wakatusema kwa maneno haya, ‘Hivi ndivyo Daudi alivyofanya.’”+ (Na hii imekuwa kawaida yake siku zote ambazo aliishi katika nchi ya mashambani ya Wafilisti.) 12 Kwa hiyo Akishi akamwamini+ Daudi, akisema moyoni mwake: “Bila shaka amenuka katikati ya watu wake Israeli;+ naye atakuwa mtumishi wangu mpaka wakati usio na kipimo.”

28 Na ikawa katika siku hizo kwamba Wafilisti wakaanza kukusanya kambi zao kwa ajili ya jeshi ili kufanya vita juu ya Israeli.+ Basi Akishi akamwambia Daudi: “Bila shaka unajua kwamba unapaswa kwenda pamoja nami kambini, wewe na watu wako.”+ 2 Kwa hiyo Daudi akamwambia Akishi: “Ndiyo sababu wewe mwenyewe unajua lile ambalo mtumishi wako anapaswa kufanya.” Basi Akishi akamwambia Daudi: “Ndiyo sababu nitakuweka kuwa mlinzi wa kichwa changu sikuzote.”+

3 Basi Samweli alikuwa amekufa, na Israeli wote walikuwa wamemwombolezea, wakamzika katika Rama jiji lake.+ Naye Sauli alikuwa amewaondolea mbali kutoka katika nchi wenye kuwasiliana na pepo na wajuzi wa kubashiri matukio.+

4 Na Wafilisti wakakusanyika, wakaja na kupiga kambi katika Shunemu.+ Kwa hiyo Sauli akakusanya pamoja Israeli wote nao wakapiga kambi katika Gilboa.+ 5 Sauli alipoona kambi ya Wafilisti, akaogopa, na moyo wake ukaanza kutetemeka sana.+ 6 Ingawa Sauli alikuwa akimuuliza Yehova,+ lakini Yehova hakumjibu kamwe,+ ama kwa ndoto+ ama kwa Urimu+ ama kwa manabii.+ 7 Mwishowe Sauli akawaambia watumishi wake: “Nitafutieni mwanamke ambaye ni stadi wa kuwasiliana na pepo,+ nami nitaenda kwake nitafute shauri kutoka kwake.” Ndipo watumishi wake wakamwambia: “Tazama! Kuna mwanamke katika En-dori ambaye ni stadi wa kuwasiliana na pepo.”+

8 Kwa hiyo Sauli akajibadili sura+ na kuvaa mavazi mengine, akaenda, yeye na watu wawili pamoja naye; nao wakafika kwa yule mwanamke usiku.+ Sasa akasema: “Tafadhali, nifanyie uaguzi+ kwa kuwasiliana na pepo, unipandishie yule nitakayemtaja kwako.” 9 Hata hivyo, yule mwanamke akamwambia: “Tazama, wewe mwenyewe unajua vema yale ambayo Sauli alifanya, jinsi alivyowakatilia mbali kutoka katika nchi wenye kuwasiliana na pepo na wajuzi wa kubashiri matukio.+ Kwa nini, basi, unatenda kama mtu anayeitegea nafsi yangu mtego ili ufanye niuawe?”+ 10 Mara moja Sauli akamwapia kwa Yehova, akisema: “Kama Yehova anavyoishi,+ hutapata hatia ya kosa katika jambo hili!” 11 Ndipo yule mwanamke akasema: “Nikupandishie nani?” Naye akasema: “Nipandishie Samweli.”+ 12 Wakati yule mwanamke alipomwona “Samweli,”+ akaanza kupiga kelele kwa sauti yake yote; na mwanamke huyo akamwambia Sauli: “Kwa nini umenidanganya, kwa kuwa wewe mwenyewe ndiye Sauli?” 13 Lakini mfalme akamwambia: “Usiogope, lakini uliona nini?” Mwanamke huyo akaendelea kumwambia Sauli: “Niliona mungu+ akipanda juu kutoka katika dunia.” 14 Mara moja akamuuliza huyo mwanamke: “Ana umbo gani?” naye akasema: “Ni mwanamume mzee anayepanda juu, naye amevaa koti lisilo na mikono.”+ Ndipo Sauli akatambua kwamba huyo alikuwa ni “Samweli,”+ naye akainama kifudifudi, akasujudu.

15 Naye “Samweli” akaanza kumwambia Sauli: “Kwa nini umenisumbua kwa kufanya nipandishwe?”+ Na Sauli akasema: “Niko katika dhiki kali sana,+ kwa kuwa Wafilisti wanapigana nami, na Mungu ameniacha+ wala hakunipa jibu tena, ama kwa manabii ama kwa ndoto;+ ndiyo sababu ninakuita unijulishe jambo nitakalofanya.”+

16 Na “Samweli” akaendelea kusema: “Kwa nini, basi, unaniuliza mimi, wakati ambapo Yehova mwenyewe amekuacha+ na kwamba yeye ni adui yako?+ 17 Na Yehova atajifanyia kama vile alivyosema kupitia mimi, na Yehova ataurarua ufalme kutoka mkononi mwako,+ na kumpa mwenzako Daudi.+ 18 Kwa vile hukusikiliza sauti ya Yehova,+ nawe hukutekeleza hasira yake inayowaka juu ya Amaleki,+ ndiyo sababu hakika Yehova atakutendea jambo hili leo. 19 Na Yehova atatia Israeli pia pamoja na wewe mkononi mwa Wafilisti,+ na kesho+ wewe na wana wako+ mtakuwa pamoja nami. Hata kambi ya Israeli, Yehova ataitia mkononi mwa Wafilisti.”+

20 Ndipo Sauli akaanguka chini upesi akiwa amejilaza chini mwili mzima, akaogopa sana kwa sababu ya maneno ya “Samweli.” Pia, kukawa hakuna nguvu zozote ndani yake, kwa sababu alikuwa hajala chakula mchana mzima na usiku mzima. 21 Sasa yule mwanamke akamjia Sauli, akaona kwamba alikuwa na wasiwasi sana. Kwa hiyo akamwambia: “Tazama, mjakazi wako ameitii sauti yako, nami nikaitia nafsi yangu mkononi mwangu+ na kuyatii maneno uliyoniambia. 22 Na sasa, tafadhali, wewe pia uitii sauti ya mjakazi wako; na acha niweke mbele yako kipande cha mkate, nawe ule, ili upate nguvu, kwa sababu utaenda zako.” 23 Lakini akakataa na kusema: “Sitakula.” Hata hivyo, watumishi wake na pia yule mwanamke wakazidi kumsihi. Mwishowe akaitii sauti yao, akainuka kutoka chini na kuketi juu ya kiti. 24 Basi yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenoneshwa+ nyumbani. Kwa hiyo akamchinja haraka,+ akachukua unga, akaukanda na kuoka keki zisizo na chachu. 25 Kisha akampakulia Sauli na watumishi wake, nao wakala. Ndipo wakaondoka, wakaenda zao usiku huo.+

29 Na Wafilisti+ wakakusanya kambi zao zote kule Afeki, huku Waisraeli wakipiga kambi kando ya bubujiko lililo katika Yezreeli.+ 2 Na wakuu wa muungano wa Wafilisti+ walikuwa wakipita kwa mamia na kwa maelfu, na Daudi na watu wake walikuwa wakipita baadaye pamoja na Akishi.+ 3 Nao wakuu wa Wafilisti wakaanza kusema: “Hawa Waebrania+ wanataka nini?” Naye Akishi akawaambia wakuu wa Wafilisti: “Je, huyu si Daudi mtumishi wa Sauli mfalme wa Israeli, aliyekuwa pamoja nami hapa mwaka mmoja au miwili,+ nami sijapata+ndani yake jambo hata moja tangu siku ile alipotoroka kuja kwangu mpaka leo hii?” 4 Nao wakuu wa Wafilisti wakamghadhibikia; na wakuu Wafilisti wakaendelea kumwambia: “Mrudishe mtu huyo,+ mwache arudi mahali ulipompa; wala usiache ashuke pamoja nasi kwenda vitani, asije akawa mpinzani+ wetu katika vita. Na je, mtu huyu atajipatia kibali kwa bwana wake jinsi gani? Je, si kwa vichwa vya watu wetu? 5 Je, huyu si Daudi ambaye waliendelea kuitikia katika kucheza dansi, wakisema, ‘Sauli amepiga maelfu yake, na Daudi makumi ya maelfu yake’?”+

6 Basi Akishi+ akamwita Daudi na kumwambia: “Kama Yehova anavyoishi,+ wewe ni mnyoofu, na kutoka kwako na kuingia kwako+ pamoja nami katika kambi kumekuwa kwema machoni pangu;+ kwa maana sijapata ubaya ndani yako tangu siku ile ulipokuja kwangu mpaka leo hii.+ Lakini machoni pa wakuu wa muungano+ wewe si mwema. 7 Na sasa rudi, uende kwa amani, usije ukafanya jambo lolote baya machoni pa wakuu wa muungano wa Wafilisti.” 8 Hata hivyo, Daudi akamwambia Akishi: “Kwani nimefanya nini,+ nawe umepata nini ndani ya mtumishi wako tangu siku ile nilipokuja mbele yako mpaka leo hii,+ ili nisije na kupigana na adui za bwana wangu mfalme?” 9 Ndipo Akishi akajibu na kumwambia Daudi: “Najua vema kwamba umekuwa mwema machoni pangu, kama malaika wa Mungu.+ Ila wakuu wa Wafilisti ndio wamesema, ‘Asipande pamoja nasi kwenda vitani.’ 10 Na sasa ondokeni asubuhi na mapema pamoja na watumishi wa bwana wako waliokuja nawe; nanyi mwondoke asubuhi na mapema wakati kutakapokuwa kumewapambazukia. Kisha mwende zenu.”+

11 Basi Daudi akaondoka mapema, yeye na watu wake, ili waende asubuhi+ na kurudi katika nchi ya Wafilisti; nao Wafilisti wakapanda, wakaenda Yezreeli.+

30 Na ikawa kwamba, wakati Daudi na watu wake walipokuwa wakija Siklagi+ siku ya tatu, Waamaleki+ wakavamia upande wa kusini na pia Siklagi; wakapiga Siklagi, wakaliteketeza kwa moto, 2 nao wakachukua mateka wanawake+ na vyote vilivyokuwa ndani yake, kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi. Hawakumuua yeyote, bali waliwachukua na kwenda zao. 3 Daudi alipokuja jijini na watu wake, tazama, jiji lilikuwa limeteketezwa kwa moto, na wake zao na wana wao na binti zao walikuwa wamechukuliwa mateka. 4 Na Daudi na watu waliokuwa pamoja naye wakaanza kupaaza sauti zao, wakalia,+ mpaka nguvu za kuendelea kulia zilipokwisha ndani yao. 5 Na wake wawili wa Daudi walikuwa wamechukuliwa mateka, Ahinoamu+ Myezreeli, na Abigaili+ mke wa Nabali Mkarmeli. 6 Naye Daudi akataabika sana,+ kwa sababu watu walisema apigwe kwa mawe;+ kwa maana nafsi za watu wote zilikuwa zimeingiwa na uchungu;+ kila mmoja kwa sababu ya wanawe na binti zake. Basi Daudi akajitia nguvu kwa Yehova Mungu wake.+

7 Hivyo Daudi akamwambia Abiathari+ kuhani, mwana wa Ahimeleki: “Tafadhali ilete hapa efodi.”+ Naye Abiathari akamletea Daudi ile efodi. 8 Daudi akaanza kumuuliza Yehova,+ akisema: “Je, nikifuatilie kikundi hiki cha waporaji? Je, nitawafikia?”+ Ndipo akamwambia: “Nenda, uwafuatilie, kwa maana bila shaka utawafikia, nawe bila shaka utaleta ukombozi.”+

9 Mara moja Daudi akaondoka, yeye pamoja na wale watu mia sita+ waliokuwa naye, wakaenda mpaka bonde la mto la Besori, na watu ambao walipaswa kuachwa nyuma wakasimama tuli. 10 Na Daudi akaendelea kufuatilia,+ yeye pamoja na watu mia nne, lakini watu mia mbili waliokuwa wamechoka sana wasiweze kuvuka lile bonde la mto la Besori+ wakasimama tuli.

11 Nao wakakuta mtu, Mmisri,+ shambani. Basi wakampeleka kwa Daudi na kumpa mkate ale, na kumpa maji anywe. 12 Zaidi ya hayo, wakampa kipande cha keki ya tini zilizoshinikizwa na keki mbili za zabibu kavu.+ Ndipo akala na roho+ yake ikarudi kwake; kwa maana hakuwa amekula mkate wala kunywa maji kwa siku tatu, mchana na usiku. 13 Sasa Daudi akamwambia: “Wewe ni wa nani, nawe unatoka wapi?” naye akasema: “Mimi ni mtumishi Mmisri, mtumwa wa mtu Mwamaleki, lakini bwana wangu aliniacha kwa sababu nilishikwa na ugonjwa siku tatu zilizopita.+ 14 Sisi ndio tuliovamia upande wa kusini wa Wakerethi+ na nchi ya Yuda na upande wa kusini wa Kalebu;+ nasi tukateketeza Siklagi kwa moto.” 15 Naye Daudi akamwambia: “Je, utaniongoza, nishuke mpaka kwenye hiki kikundi cha waporaji?” Naye akasema: “Niapie+ kwa Mungu kwamba hutaniua, wala kunitia mkononi mwa bwana wangu,+ nami nitakuongoza, ushuke mpaka kwenye hiki kikundi cha waporaji.”

16 Basi akamwongoza, akashuka,+ na tazama, walikuwa wameenea bila utaratibu juu ya uso wote wa nchi, wakila na kunywa na kufanya karamu+ kwa sababu ya nyara yote kubwa ambayo walikuwa wamechukua kutoka katika nchi ya Wafilisti na nchi ya Yuda.+ 17 Na Daudi akawapiga kuanzia giza la asubuhi mpaka jioni, apate kuwaangamiza; wala hakuna mtu kati yao aliyeponyoka+ ila vijana mia nne waliopanda ngamia na kukimbia. 18 Naye Daudi akakomboa vyote ambavyo Waamaleki walikuwa wamechukua,+ na Daudi akakomboa wake zake wawili. 19 Na hakuna kitu chochote chao kilichokosekana, kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi na wana na mabinti na kuanzia nyara, mpaka chochote ambacho walikuwa wamejichukulia.+ Daudi alirudisha kila kitu. 20 Basi Daudi akachukua makundi yote na mifugo, ambayo waliitanguliza mbele ya ile mifugo mingine. Kisha wakasema: “Hii ni nyara ya Daudi.”+

21 Mwishowe Daudi akawafikia wale wanaume mia mbili+ ambao walikuwa wamechoka sana wasiweze kwenda na Daudi, na ambao waliwaacha waketi kando ya bonde la mto la Besori; nao wakatoka kuja kumpokea Daudi na kuwapokea watu waliokuwa pamoja naye. Daudi alipowakaribia watu hao, akaanza kuwauliza hali yao. 22 Hata hivyo, kila mtu mbaya na asiyefaa kitu+ kati ya watu walioenda pamoja na Daudi akajibu na kuzidi kusema: “Kwa kuwa hawakwenda pamoja nasi, hatutawapa nyara yoyote ambayo tumekomboa, isipokuwa kila mmoja atapewa mke wake na wanawe, wawachukue na kwenda.” 23 Lakini Daudi akasema: “Ndugu zangu, msifanye hivyo na vitu ambavyo Yehova ametupa sisi,+ kwa kuwa alitulinda+ na kukitia mkononi mwetu kile kikundi cha waporaji kilichokuja juu yetu.+ 24 Na ni nani atakayewasikiliza kwa neno hili? Kwa maana kama lilivyo fungu la yule aliyeshuka kwenda vitani ndivyo litakavyokuwa fungu la yule aliyeketi kando ya mizigo.+ Wote watapata fungu pamoja.”+ 25 Na ikawa kwamba kuanzia siku hiyo na kuendelea, akaliweka hilo kuwa sharti na uamuzi wa hukumu+ kwa ajili ya Israeli mpaka leo hii.

26 Wakati Daudi alipofika Siklagi, akapeleka sehemu ya nyara kwa wanaume wazee wa Yuda, rafiki zake,+ akisema: “Tazameni, hii ni zawadi+ ya baraka kwa ajili yenu kutoka katika nyara za adui za Yehova.” 27 Kwa wale waliokuwa Betheli,+ na kwa wale waliokuwa Ramothi+ la kusini, na kwa wale waliokuwa Yatiri,+ 28 na kwa wale waliokuwa Aroeri, na kwa wale waliokuwa Sifmothi, na kwa wale waliokuwa Eshtemoa,+ 29 na kwa wale waliokuwa Rakali, na kwa wale waliokuwa katika majiji ya Wayerahmeeli,+ na kwa wale waliokuwa katika majiji ya Wakeni,+ 30 na kwa wale waliokuwa Horma,+ na kwa wale waliokuwa Borashani,+ na kwa wale waliokuwa Athaki, 31 na kwa wale waliokuwa Hebroni,+ na mahali pote ambapo Daudi alikuwa ametembea, yeye pamoja na watu wake.

31 Basi Wafilisti walikuwa wakipigana na Israeli,+ na watu wa Israeli wakaanza kukimbia kutoka mbele ya Wafilisti, nao wakaendelea kuanguka, wakiwa wameuawa+ katika Mlima Gilboa.+ 2 Na Wafilisti wakaendelea kumfuatilia kwa ukaribu sana Sauli na wanawe; na mwishowe Wafilisti wakawapiga na kuwaua Yonathani+ na Abinadabu+ na Malki-shua,+ wana wa Sauli. 3 Na pigano likawa kali juu ya Sauli, na mwishowe wapiga-mishale, wapiga-upinde, wakampata, na hao wapiga-mishale wakamuumiza vibaya.+ 4 Ndipo Sauli akamwambia mchukua-silaha wake: “Chomoa upanga wako,+ unichome nao, ili watu hawa wasiotahiriwa+ wasije na kunichoma na kunitendea vibaya.” Naye mchukua-silaha wake hakutaka,+ kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akachukua upanga, akauangukia.+ 5 Wakati yule mchukua-silaha wake alipoona kwamba Sauli amekufa,+ ndipo yeye pia akauangukia upanga wake mwenyewe, akafa pamoja naye.+ 6 Basi Sauli na wanawe watatu na mchukua-silaha wake, watu wake wote, wakafa pamoja siku hiyo.+ 7 Wakati watu wa Israeli waliokuwa katika eneo la nchi tambarare ya chini na waliokuwa katika eneo la Yordani walipoona kwamba watu wa Israeli wamekimbia, na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, ndipo wakaanza kuyaacha majiji na kukimbia,+ kisha Wafilisti wakaingia na kuanza kukaa ndani yake.+

8 Na kesho yake ikawa kwamba, Wafilisti walipokuja kuwavua waliouawa,+ wakamkuta Sauli na wanawe watatu wameanguka juu ya Mlima Gilboa.+ 9 Nao wakakata kichwa+ chake na kuvua silaha zake na kutuma wajumbe kotekote katika nchi ya Wafilisti ili kuzijulisha+ nyumba za sanamu+ zao pamoja na watu. 10 Mwishowe wakaweka silaha+ zake katika nyumba za sanamu za Ashtorethi,+ nao wakafunga maiti yake kwenye ukuta wa Beth-shani.+ 11 Na kumhusu yeye, wakaaji wa Yabesh-gileadi+ wakasikia yale ambayo Wafilisti walikuwa wamemtendea Sauli. 12 Mara moja wanaume wote mashujaa wakaondoka, wakaenda usiku kucha, wakachukua maiti ya Sauli na maiti za wanawe kutoka katika ukuta wa Beth-shani, wakaja mpaka Yabeshi na kuziteketeza kwa moto hapo.+ 13 Kisha wakachukua mifupa yao,+ na kuizika+ chini ya mkwaju+ ulio katika Yabeshi, nao wakafunga kwa siku saba.+

[Maelezo ya Chini]

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki