KULINGANA NA YOHANA
1 Hapo mwanzo Neno alikuwako,+ naye Neno alikuwa pamoja na Mungu,+ na Neno alikuwa mungu.*+ 2 Mwanzoni yeye alikuwa pamoja na Mungu. 3 Vitu vyote vilikuja kuwako kupitia kwake,+ na bila yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuja kuwako.
Kile ambacho kimekuja kuwako 4 kupitia kwake kilikuwa uzima, na uzima ulikuwa nuru ya wanadamu.+ 5 Nuru inang’aa gizani,+ lakini giza halijaishinda.
6 Kuna mtu aliyetumwa akiwa mwakilishi wa Mungu; jina lake lilikuwa Yohana.+ 7 Mtu huyo alikuja akiwa shahidi, ili atoe ushahidi kuhusu nuru,+ ili watu wa namna zote waamini kupitia kwake. 8 Yeye hakuwa nuru hiyo,+ bali alikuja kutoa ushahidi kuhusu nuru hiyo.
9 Nuru ya kweli inayowaangazia watu wa aina zote ilikuwa karibu kuja ulimwenguni.+ 10 Alikuwa ulimwenguni,+ nao ulimwengu ulikuja kuwako kupitia kwake,+ lakini ulimwengu haukumjua. 11 Alikuja nyumbani kwake mwenyewe, lakini watu wake mwenyewe hawakumkubali. 12 Hata hivyo, wale wote waliompokea, aliwapa mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu,+ kwa sababu walikuwa na imani* katika jina lake.+ 13 Nao hawakuzaliwa kutokana na damu, wala mapenzi ya mwili au mapenzi ya mwanadamu, bali kutokana na Mungu.+
14 Kwa hiyo Neno akawa mwili,+ akakaa kati yetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu ulio kama wa mwana mzaliwa pekee+ kutoka kwa baba; naye alikuwa amejaa kibali cha Mungu* na kweli. 15 (Yohana alitoa ushahidi kumhusu, ndiyo, alisema kwa sauti kubwa: “Huyu ndiye niliyesema kumhusu, ‘Yule anayekuja nyuma yangu amenitangulia, kwa maana alikuwapo kabla yangu.’”)+ 16 Kwa maana sote tulipokea kutokana na wingi alio nao, hata fadhili zisizostahiliwa juu ya fadhili zisizostahiliwa. 17 Kwa sababu Sheria ilitolewa kupitia Musa,+ lakini fadhili zisizostahiliwa+ na kweli zilikuja kupitia Yesu Kristo.+ 18 Hakuna mwanadamu ambaye amemwona Mungu wakati wowote;+ mungu mzaliwa pekee+ aliye kando ya Baba,*+ ndiye ameeleza kumhusu.+
19 Huu ndio ushahidi aliotoa Yohana, Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu wakamuulize: “Wewe ni nani?”+ 20 Naye akakiri na hakukana, akisema: “Mimi siye Kristo.” 21 Nao wakamuuliza: “Basi, wewe ni nani? Je, wewe ndiye Eliya?”+ Akajibu: “Mimi siye.” “Je, wewe ndiye yule Nabii?”+ Akajibu: “Hapana!” 22 Kwa hiyo wakamwambia: “Wewe ni nani? Tuambie ili tupate jibu la kuwapa wale waliotutuma. Unasema nini juu yako mwenyewe?” 23 Akasema: “Mimi ni mtu anayepaza sauti nyikani, ‘Nyoosheni njia ya Yehova,’*+ kama alivyosema nabii Isaya.”+ 24 Sasa wale waliotumwa walitoka kwa Mafarisayo. 25 Basi wakamuuliza: “Kwa nini unabatiza ikiwa wewe si Kristo au Eliya au yule Nabii?” 26 Yohana akawajibu: “Mimi ninabatiza katika maji. Kuna mtu aliyesimama miongoni mwenu msiyemjua, 27 yule anayekuja nyuma yangu, ambaye sistahili kufungua kamba za viatu vyake.”+ 28 Mambo hayo yalifanyika huko Bethania ng’ambo ya Yordani, ambako Yohana alikuwa akibatiza watu.+
29 Siku iliyofuata alimwona Yesu akimjia, naye akasema: “Ona, Mwanakondoo+ wa Mungu ambaye huondoa dhambi+ ya ulimwengu!+ 30 Huyu ndiye niliyesema kumhusu: ‘Nyuma yangu anakuja mwanamume ambaye amenitangulia, kwa sababu alikuwapo kabla yangu.’+ 31 Hata mimi sikumjua, lakini nilikuja kubatiza katika maji ili afunuliwe kwa Israeli.”+ 32 Yohana pia alitoa ushahidi akisema: “Niliona roho ikishuka kama njiwa kutoka mbinguni, nayo ikakaa juu yake.+ 33 Hata mimi sikumjua, bali Yule aliyenituma nikabatize katika maji aliniambia: ‘Yeyote ambaye utaona roho ikishuka na kukaa juu yake,+ huyo ndiye anayebatiza kwa roho takatifu.’+ 34 Mimi nimeona, nami nimetoa ushahidi kwamba huyo ndiye Mwana wa Mungu.”+
35 Tena siku iliyofuata, Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili kati ya wanafunzi wake. 36 Alipomtazama Yesu akipita akasema: “Ona, Mwanakondoo+ wa Mungu!” 37 Wanafunzi hao wawili walipomsikia akisema hivyo, wakamfuata Yesu. 38 Ndipo Yesu akageuka na alipowaona wakimfuata, akawauliza: “Mnatafuta nini?” Wakamwambia: “Rabi (neno ambalo linapotafsiriwa linamaanisha, “Mwalimu”), unakaa wapi?” 39 Akawaambia: “Njooni, nanyi mtaona.” Basi wakaenda na kuona mahali alipokuwa akikaa, nao wakakaa pamoja naye siku hiyo; ilikuwa karibu saa kumi.* 40 Andrea,+ ndugu ya Simoni Petro alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia mambo aliyosema Yohana na kumfuata Yesu. 41 Kwanza alimpata Simoni ndugu yake na kumwambia: “Tumempata Masihi”+ (neno ambalo linapotafsiriwa linamaanisha, “Kristo”), 42 kisha akampeleka kwa Yesu. Yesu akamtazama na kumwambia: “Wewe ni Simoni+ mwana wa Yohana; utaitwa Kefa” (linalotafsiriwa kuwa, “Petro”).+
43 Siku iliyofuata Yesu alitaka kwenda Galilaya. Basi akamkuta Filipo+ na kumwambia: “Njoo uwe mfuasi wangu.” 44 Filipo alitoka Bethsaida, jiji walilotoka Andrea na Petro. 45 Filipo akamkuta Nathanaeli+ na kumwambia: “Tumempata yule ambaye Musa, katika Sheria, na Manabii waliandika kumhusu: Yesu, mwana wa Yosefu,+ kutoka Nazareti.” 46 Lakini Nathanaeli akamuuliza: “Je, kitu chochote kizuri kinaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamjibu: “Njoo uone.” 47 Yesu alipomwona Nathanaeli akija, akasema hivi kumhusu: “Ona, Mwisraeli kwa hakika ambaye hamna udanganyifu ndani yake.”+ 48 Nathanaeli akamuuliza: “Umenijuaje?” Yesu akamjibu: “Nilikuona ulipokuwa chini ya mtini, kabla ya Filipo kukuita.” 49 Nathanaeli akamwambia: “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mfalme wa Israeli.”+ 50 Yesu akasema: “Je, unaamini kwa sababu nimekuambia nilikuona chini ya mtini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.” 51 Kisha akamwambia: “Kwa kweli ninawaambia, mtaona mbingu imefunguliwa na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka kwa Mwana wa binadamu.”+
2 Basi siku ya tatu kulikuwa na karamu ya ndoa katika Kana ya Galilaya, na mama ya Yesu alikuwa huko. 2 Yesu na wanafunzi wake pia walikuwa wamealikwa kwenye karamu hiyo ya ndoa.
3 Divai ilipopungua mama ya Yesu akamwambia: “Hawana divai.” 4 Lakini Yesu akamjibu: “Mwanamke, jambo hilo linatuhusuje mimi na wewe?* Bado saa yangu haijafika.” 5 Mama yake akawaambia wahudumu: “Fanyeni lolote atakalowaambia.” 6 Kulikuwa na mitungi sita ya maji hapo kulingana na sheria za utakaso za Wayahudi,+ kila mmoja ulikuwa na uwezo wa kuchukua vipimo* viwili au vitatu vya maji. 7 Yesu akawaambia: “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza pomoni. 8 Akawaambia: “Choteni kidogo na kumpelekea msimamizi wa karamu.” Basi wakampelekea. 9 Msimamizi wa karamu alipoonja maji yaliyokuwa yamegeuzwa kuwa divai, bila kujua divai ilitoka wapi (lakini wahudumu waliokuwa wamechota maji hayo walijua), akamwita bwana harusi 10 akamwambia: “Kila mtu hutoa divai nzuri kwanza, kisha hutoa divai hafifu wakati ambapo watu wameingiwa na kileo. Lakini wewe umehifadhi divai nzuri mpaka sasa.” 11 Yesu alifanya muujiza huo wake wa kwanza katika Kana ya Galilaya, kwa hiyo akaonyesha utukufu wake,+ na wanafunzi wake wakamwamini.
12 Baada ya hayo, Yesu, mama yake, ndugu zake,+ na wanafunzi wake wakashuka kwenda Kapernaumu,+ lakini hawakukaa huko siku nyingi.
13 Pasaka+ ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, basi Yesu akapanda kwenda Yerusalemu. 14 Alipoingia hekaluni akakuta watu wakiuza ng’ombe, kondoo, na njiwa,+ pia, wale waliobadili pesa walikuwa kwenye viti vyao. 15 Basi akatengeneza mjeledi wa kamba na kuwafukuza hekaluni wote waliokuwa na kondoo na ng’ombe, akamwaga sarafu za wale waliobadili pesa na kupindua meza zao.+ 16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa: “Ondoeni vitu hivi hapa! Acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”*+ 17 Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba imeandikwa: “Bidii kwa ajili ya nyumba yako itanila.”+
18 Kwa hiyo, Wayahudi wakamuuliza: “Utatuonyesha ishara gani,+ kwa maana unafanya mambo haya?” 19 Yesu akawajibu: “Libomoeni hekalu hili, na kwa siku tatu nitalisimamisha.”+ 20 Kisha Wayahudi wakasema: “Hekalu hili lilijengwa kwa miaka 46, je, wewe utalisimamisha kwa siku tatu?” 21 Lakini alikuwa akizungumza kuhusu hekalu la mwili wake.+ 22 Hata hivyo, alipofufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka alikuwa akisema jambo hilo,+ nao wakaamini andiko na maneno ambayo Yesu alikuwa amesema.
23 Hata hivyo, alipokuwa Yerusalemu kwenye sherehe ya Pasaka, watu wengi wakamwamini, kwa sababu waliona miujiza aliyokuwa akifanya. 24 Lakini Yesu alijihadhari nao kwa sababu aliwajua wote 25 na hakuhitaji mtu yeyote atoe ushahidi kuhusu mwanadamu, kwa maana alijua kilicho ndani ya mwanadamu.+
3 Kulikuwa na Farisayo aliyeitwa Nikodemo,+ mtawala wa Wayahudi. 2 Alienda kwa Yesu usiku+ na kumwambia: “Rabi,+ tunajua kwamba wewe ni mwalimu na umetoka kwa Mungu, kwa maana hakuna anayeweza kufanya miujiza+ kama unayofanya isipokuwa Mungu awe pamoja naye.”+ 3 Yesu akamwambia: “Kwa kweli ninakuambia, mtu asipozaliwa tena,*+ hawezi kuuona Ufalme wa Mungu.”+ 4 Nikodemo akamuuliza: “Mtu akiwa mzee anawezaje kuzaliwa tena? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake mara ya pili na kuzaliwa, sivyo?” 5 Yesu akajibu: “Kwa kweli ninakuambia, mtu asipozaliwa kwa maji+ na roho,+ hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu. 6 Kile ambacho kimezaliwa kwa mwili ni mwili, na kile ambacho kimezaliwa kwa roho ni roho. 7 Usishangae kwa sababu nimekuambia: Lazima ninyi mzaliwe tena. 8 Upepo huvuma mahali unapotaka, nawe unasikia ukivuma, lakini hujui mahali unapotoka wala mahali unapoenda. Ndivyo alivyo kila mtu ambaye amezaliwa kwa roho.”+
9 Nikodemo akamuuliza: “Mambo haya yanawezekanaje?” 10 Yesu akamjibu: “Je, wewe ni mwalimu wa Israeli na bado hujui mambo haya? 11 Kwa kweli ninakuambia, yale tunayojua tunayasema, na yale ambayo tumeyaona tunatoa ushahidi kuyahusu, lakini ninyi hampokei ushahidi tunaotoa. 12 Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani na bado hamyaamini, mtawezaje kuamini nikiwaambia mambo ya mbinguni? 13 Isitoshe, hakuna mtu aliyepanda kwenda mbinguni+ ila yule aliyeshuka kutoka mbinguni,+ yaani, Mwana wa binadamu. 14 Kama vile Musa alivyoinua nyoka nyikani,+ ndivyo Mwana wa binadamu atakavyoinuliwa,+ 15 ili kila mtu anayemwamini apate uzima wa milele.+
16 “Kwa maana, Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa pekee,+ ili kila mtu anayemwamini* asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.+ 17 Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe kupitia kwake.+ 18 Yeyote anayemwamini* hatahukumiwa.+ Yeyote ambaye hamwamini amehukumiwa tayari, kwa sababu hana imani* katika jina la Mwana mzaliwa pekee wa Mungu.+ 19 Basi huu ndio msingi wa hukumu: kwamba nuru imekuja ulimwenguni,+ lakini watu wamependa giza badala ya nuru, kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. 20 Kwa maana yeyote ambaye huzoea kutenda mambo maovu huchukia nuru na haji kwenye nuru, ili matendo yake yasikaripiwe.* 21 Lakini yeyote ambaye hufanya yaliyo ya kweli huja kwenye nuru,+ ili matendo yake yafunuliwe kwamba yamefanywa kulingana na Mungu.”
22 Baada ya mambo haya, Yesu na wanafunzi wake wakaenda katika maeneo ya mashambani ya Yudea, naye akakaa pamoja nao huko kwa muda fulani, akiwabatiza watu.+ 23 Lakini Yohana pia alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu, kwa sababu kulikuwa na maji mengi huko,+ na watu walikuwa wakija na kubatizwa;+ 24 kwa maana bado Yohana hakuwa amefungwa gerezani.+
25 Wanafunzi wa Yohana walibishana na Myahudi fulani kuhusu utakaso. 26 Kwa hiyo wakaja kwa Yohana na kumwambia: “Rabi, mtu aliyekuwa pamoja nawe ng’ambo ya Yordani, ambaye ulitoa ushahidi kumhusu,+ anabatiza na watu wote wanaenda kwake.” 27 Yohana akawaambia: “Mtu hawezi kupokea kitu chochote isipokuwa awe amepewa kutoka mbinguni. 28 Ninyi wenyewe mlishuhudia kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo,+ bali, nimetumwa nimtangulie.’+ 29 Yule aliye na bibi harusi ndiye bwana harusi.+ Hata hivyo, rafiki ya bwana harusi, anaposimama na kumsikia, anashangilia sana kwa sababu ya sauti ya bwana harusi. Kwa hiyo shangwe yangu imekamilishwa. 30 Huyo lazima aendelee kuongezeka, lakini mimi lazima niendelee kupungua.”
31 Yule anayetoka juu+ yuko juu ya watu wote. Yule anayetoka duniani, ni wa kutoka duniani na husema kuhusu mambo ya duniani. Yule anayetoka mbinguni, yuko juu ya watu wote.+ 32 Yeye hutoa ushahidi kuhusu mambo aliyoona na kusikia,+ lakini hakuna mtu anayekubali ushahidi wake.+ 33 Yeyote ambaye ameukubali ushahidi wake ametia muhuri wake* kwamba Mungu ni wa kweli.+ 34 Yule ambaye Mungu amemtuma husema maneno ya Mungu,+ kwa maana Mungu hutoa roho yake kwa wingi.* 35 Baba anampenda Mwana+ naye amekabidhi vitu vyote mkononi mwake.+ 36 Yule anayemwamini Mwana ana uzima wa milele;+ yule asiyemtii Mwana hataona uzima,+ bali ghadhabu ya Mungu hukaa juu yake.+
4 Bwana alipojua kwamba Mafarisayo walikuwa wamesikia kuwa Yesu alikuwa akifanya na kubatiza+ wanafunzi wengi kuliko Yohana— 2 ingawa Yesu hakubatiza bali wanafunzi wake ndio waliokuwa wakibatiza— 3 akaondoka Yudea na kuelekea tena Galilaya. 4 Lakini alipaswa kupitia Samaria. 5 Basi akafika katika jiji moja la Samaria linaloitwa Sikari, lililokuwa karibu na shamba ambalo Yakobo alimpa Yosefu+ mwana wake. 6 Kisima cha Yakobo kilikuwa hapo.+ Basi Yesu, kwa kuwa alikuwa amechoka kwa sababu ya safari, akaketi kando ya kisima hicho.* Ilikuwa karibu saa sita.*
7 Mwanamke Msamaria akaja kuteka maji. Yesu akamwambia: “Naomba maji ninywe.” 8 (Kwa maana wanafunzi wake walikuwa wameenda jijini kununua chakula.) 9 Kwa hiyo mwanamke huyo Msamaria akamuuliza: “Wewe ni Myahudi, nami ni mwanamke Msamaria, unawezaje kuniomba maji ya kunywa?” (Kwa maana Wayahudi hawashirikiani na Wasamaria.)+ 10 Yesu akamjibu: “Kama ungejua zawadi ya bure inayotoka kwa Mungu+ na ni nani ambaye anakuambia, ‘Naomba maji ninywe,’ ungemwomba, naye angekupa maji yaliyo hai.”+ 11 Akamwambia: “Bwana, huna hata ndoo ya kutekea maji, na kisima ni kirefu. Basi, umeyatoa wapi hayo maji yaliyo hai? 12 Je, wewe ni mkuu kuliko babu yetu Yakobo, aliyetupatia kisima hiki ambacho yeye pamoja na wanawe na mifugo yake walikunywa maji yake?” 13 Yesu akamjibu: “Kila mtu anayekunywa maji haya atakuwa na kiu tena. 14 Yeyote atakayekunywa maji nitakayompa hatakuwa na kiu kamwe,+ kwa sababu maji ambayo nitampa yatakuwa kama chemchemi ya maji ndani yake, inayobubujika ili kumpa uzima wa milele.”+ 15 Yule mwanamke akamwambia: “Bwana, nipe maji hayo ili nisiwe na kiu tena wala nisiendelee kuja hapa kuteka maji.”
16 Yesu akamwambia: “Nenda ukamwite mume wako uje naye hapa.” 17 Mwanamke huyo akajibu: “Sina mume.” Yesu akamwambia: “Umesema kweli kwamba huna mume. 18 Kwa maana umekuwa na waume watano, na mwanamume uliye naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.” 19 Yule mwanamke akamwambia: “Bwana, ninaona kwamba wewe ni nabii.+ 20 Mababu zetu waliabudu katika mlima huu, lakini ninyi mnasema tunapaswa kumwabudu Mungu huko Yerusalemu.”+ 21 Yesu akamwambia: “Mwanamke, niamini, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu wala kule Yerusalemu. 22 Ninyi mnaabudu msichokijua;+ sisi tunaabudu tunachokijua, kwa sababu wokovu huanza kwa Wayahudi.+ 23 Hata hivyo, saa inakuja, nayo ipo sasa, ambayo waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana kwa kweli, Baba anawatafuta watu wa namna hiyo wamwabudu.+ 24 Mungu ni Roho,+ na wale wanaomwabudu lazima wamwabudu kwa roho na kweli.”+ 25 Huyo mwanamke akamwambia: “Ninajua kwamba Masihi anakuja, anayeitwa Kristo. Atakapokuja, atatutangazia mambo yote waziwazi.” 26 Yesu akamwambia: “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”+
27 Ndipo wanafunzi wake wakaja, wakashangaa kwa sababu alikuwa akiongea na mwanamke. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyemuuliza: “Unatafuta nini?” au, “Kwa nini unaongea naye?” 28 Basi, yule mwanamke akauacha mtungi wake wa maji akaenda jijini na kuwaambia watu: 29 “Twendeni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichofanya. Je, inawezekana kwamba yeye ndiye Kristo?” 30 Wakatoka jijini wakaenda kumwona Yesu.
31 Wakati huohuo wanafunzi walikuwa wakimhimiza: “Rabi,+ kula.” 32 Lakini akawaambia: “Nina chakula ambacho hamkijui.” 33 Kwa hiyo wanafunzi wakaambiana: “Hakuna mtu aliyemletea chakula, sivyo?” 34 Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma+ na kuimaliza kazi yake.+ 35 Je, ninyi hamsemi kwamba bado kuna miezi minne kabla ya mavuno? Tazama! Ninawaambia: Inueni macho yenu mtazame mashamba, kwamba ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.+ Tayari 36 mvunaji anapokea mshahara na anakusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili mpandaji na mvunaji washangilie pamoja.+ 37 Basi, maneno haya ni ya kweli: Mmoja ni mpandaji na mwingine ni mvunaji. 38 Niliwatuma mkavune kile ambacho hamkufanyia kazi. Wengine wamefanya kazi, nanyi mmefaidika kutokana na kazi yao.”
39 Wasamaria wengi kutoka jiji hilo wakamwamini Yesu kwa sababu yule mwanamke alitoa ushahidi kwa kusema: “Aliniambia mambo yote niliyofanya.”+ 40 Basi Wasamaria walipomjia, wakamwomba akae pamoja nao, naye akakaa huko siku mbili. 41 Kwa hiyo, wengi zaidi wakaamini waliposikia mambo aliyosema , 42 nao wakamwambia yule mwanamke: “Hatuamini kwa sababu tu ya maneno yako; kwa maana sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba kwa hakika mtu huyu ndiye mwokozi wa ulimwengu.”+
43 Baada ya siku hizo mbili akaondoka na kwenda Galilaya. 44 Hata hivyo, Yesu alitoa ushahidi kwamba nabii haheshimiwi katika nchi yake.+ 45 Kwa hiyo, alipofika Galilaya, Wagalilaya wakamkaribisha, kwa sababu walikuwa wameona mambo yote aliyofanya huko Yerusalemu kwenye sherehe,+ kwa maana wao pia walikuwa wameenda kwenye sherehe.+
46 Kisha Yesu akaja tena Kana ya Galilaya, ambako alikuwa amegeuza maji kuwa divai.+ Basi kulikuwa na ofisa fulani wa mfalme ambaye mwana wake alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu. 47 Mtu huyu aliposikia kwamba Yesu ametoka Yudea na kuja Galilaya, akamwendea na kumwomba ashuke kwenda kumponya mwanawe, kwa maana alikuwa karibu kufa. 48 Lakini, Yesu akamwambia: “Msipoona ishara na maajabu, hamtaamini kamwe.”+ 49 Yule ofisa wa mfalme akamwambia: “Bwana, twende kabla mwanangu hajafa.” 50 Yesu akamwambia: “Rudi nyumbani; mwanao yuko hai.”+ Yule mtu akaamini maneno ambayo Yesu alimwambia, akaondoka. 51 Lakini akiwa njiani akakutana na watumwa wake, wakamwambia kwamba mwanawe yuko hai.* 52 Kwa hiyo akawauliza saa ambayo alipata nafuu. Wakamjibu: “Alipona homa jana saa saba.”* 53 Kwa hiyo yule baba akajua ilikuwa saa ileile ambayo Yesu alimwambia: “Mwanao yuko hai.”+ Basi yeye na watu wote wa nyumbani kwake wakaamini. 54 Huo ulikuwa muujiza wa pili+ ambao Yesu alifanya alipotoka Yudea na kwenda Galilaya.
5 Baada ya hayo kulikuwa na sherehe+ ya Wayahudi, na Yesu akapanda kwenda Yerusalemu. 2 Huko Yerusalemu kwenye Lango la Kondoo+ kulikuwa na dimbwi lililoitwa kwa Kiebrania Bethzatha, lenye safu tano za nguzo. 3 Wagonjwa wengi, vipofu, vilema, na wenye viungo vilivyopooza walikuwa wamelala hapo. 4* —— 5 Lakini hapo palikuwa na mtu fulani aliyekuwa mgonjwa kwa miaka 38. 6 Yesu alipomwona mtu huyo amelala hapo, na akijua kwamba alikuwa mgonjwa kwa muda mrefu, akamuuliza: “Je, unataka kupona?”+ 7 Mgonjwa huyo akamjibu: “Bwana, sina mtu wa kuniweka ndani ya dimbwi maji yanapotibuliwa, lakini ninapotaka kuingia, mtu mwingine huingia kabla yangu.” 8 Yesu akamwambia: “Simama! Chukua mkeka wako,* utembee.”+ 9 Mtu huyo akapona mara moja, akabeba mkeka wake* na kuanza kutembea.
Hiyo ilikuwa siku ya Sabato. 10 Basi Wayahudi wakaanza kumwambia mtu huyo aliyeponywa: “Ni Sabato, hupaswi kubeba mkeka.”*+ 11 Lakini akawajibu: “Yule aliyeniponya aliniambia, ‘Beba mkeka* wako utembee.’” 12 Wakamuuliza: “Ni nani huyo aliyekuambia, ‘Beba mkeka wako utembee’?” 13 Lakini mwanamume huyo aliyeponywa hakujua ni nani, kwa maana Yesu alikuwa ameingia katika umati uliokuwa hapo.
14 Baadaye, Yesu alimkuta hekaluni akamwambia: “Ona, sasa umepona. Usifanye dhambi tena, ili usipatwe na jambo baya zaidi.” 15 Yule mtu akaenda na kuwaambia Wayahudi kwamba Yesu ndiye aliyemponya. 16 Kwa hiyo Wayahudi walikuwa wakimtesa Yesu, kwa sababu alikuwa akifanya mambo hayo siku ya Sabato. 17 Lakini akawajibu: “Baba yangu anaendelea kufanya kazi mpaka sasa, nami ninaendelea kufanya kazi.”+ 18 Basi Wayahudi wakazidi kutafuta njia ya kumuua, kwa sababu hakuwa tu akivunja Sabato bali pia alikuwa akimwita Mungu Baba yake,+ akijifanya kuwa sawa na Mungu.+
19 Kwa hiyo, Yesu akawajibu: “Kwa kweli ninawaambia, Mwana hawezi kufanya hata jambo moja kwa uamuzi wake mwenyewe, ila tu lile analomwona Baba akifanya.+ Kwa maana mambo yote ambayo Baba hufanya, vivyo hivyo Mwana hufanya mambo hayo. 20 Kwa maana Baba anampenda Mwana+ na humwonyesha mambo yote anayofanya, naye atamwonyesha kazi kubwa kuliko hizi, ili ninyi mshangae.+ 21 Kwa maana kama vile Baba anavyowafufua wafu na kuwafanya kuwa hai,+ ndivyo Mwana pia anavyowafanya kuwa hai wale anaotaka.+ 22 Kwa maana Baba hamhukumu mtu yeyote kamwe, bali amemkabidhi Mwana kazi yote ya kuhukumu,+ 23 ili wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Yeyote ambaye hamheshimu Mwana hamheshimu Baba aliyemtuma.+ 24 Kwa kweli ninawaambia, yeyote ambaye husikia neno langu na kumwamini Yule aliyenituma ana uzima wa milele,+ naye hahukumiwi bali amevuka kutoka katika kifo na kuingia kwenye uzima.+
25 “Kwa kweli ninawaambia, saa inakuja, nayo imefika, ambapo wafu wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale ambao wamesikiliza wataishi. 26 Kwa maana kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe,*+ ndivyo pia amemruhusu Mwana awe na uzima ndani yake mwenyewe.+ 27 Naye amempa mamlaka ya kuhukumu,+ kwa sababu yeye ndiye Mwana wa binadamu.+ 28 Msishangazwe na jambo hili, kwa maana saa inakuja ambayo wote walio katika makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake+ 29 na kutoka, wale waliotenda mema kwenye ufufuo wa uzima, na wale waliozoea kutenda maovu kwenye ufufuo wa hukumu.+ 30 Siwezi kufanya jambo lolote kwa uamuzi wangu mwenyewe. Kama vile ninavyosikia, ndivyo ninavyohukumu; na hukumu yangu ni ya uadilifu+ kwa sababu sitafuti mapenzi yangu mwenyewe, bali mapenzi ya yule aliyenituma.+
31 “Ikiwa mimi peke yangu ndiye ninayetoa ushahidi juu yangu mwenyewe, ushahidi wangu si wa kweli.+ 32 Kuna mwingine anayetoa ushahidi kunihusu, nami ninajua ushahidi anaotoa kunihusu ni wa kweli.+ 33 Mmewatuma watu kwa Yohana, naye ametoa ushahidi kuhusu kweli.+ 34 Hata hivyo, sikubali ushahidi wa mwanadamu, bali ninasema mambo haya ili mwokolewe. 35 Mtu huyo alikuwa taa inayowaka na kung’aa, na kwa wakati mfupi mlikuwa tayari kufurahia sana mwangaza wake.+ 36 Lakini nina ushahidi mkubwa kuliko wa Yohana, kwa maana kazi ambazo Baba yangu alinipa nitimize, yaani, kazi hizi ninazofanya zinatoa ushahidi kwamba Baba alinituma.+ 37 Naye Baba aliyenituma ametoa ushahidi kunihusu.+ Ninyi hamjasikia sauti yake wakati wowote wala kuona umbo lake,+ 38 nanyi hamna neno lake ndani yenu, kwa sababu hammwamini yule ambaye alimtuma.
39 “Mnayachunguza Maandiko+ mkifikiri mtapata uzima wa milele kupitia Maandiko hayo; nayo* ndiyo yanayotoa ushahidi kunihusu.+ 40 Hata hivyo, hamtaki kuja kwangu+ ili mpate uzima. 41 Mimi sikubali utukufu kutoka kwa wanadamu, 42 lakini ninajua kwamba hamna upendo wa Mungu ndani yenu. 43 Nimekuja katika jina la Baba yangu, lakini hamnikubali. Ikiwa mtu mwingine angekuja kwa jina lake mwenyewe, mngemkubali. 44 Mnawezaje kuniamini, huku mkipeana utukufu ninyi wenyewe lakini hamtafuti utukufu unaotoka kwa Mungu wa pekee?+ 45 Msifikiri kwamba nitawashtaki kwa Baba. Kuna yule anayewashtaki, Musa,+ ambaye mmeweka tumaini lenu kwake. 46 Kwa kweli, ikiwa mngemwamini Musa mngeniamini pia, kwa sababu aliandika kunihusu.+ 47 Lakini ikiwa hamwamini mambo aliyoandika, mnawezaje kuamini mambo ninayosema?”
6 Baada ya hapo Yesu akavuka Bahari ya Galilaya, au Tiberia.+ 2 Na umati mkubwa sana ulikuwa ukimfuata,+ kwa sababu walikuwa wakiona ishara za miujiza alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.+ 3 Basi Yesu akapanda mlimani, akaketi huko pamoja na wanafunzi wake. 4 Sasa Pasaka,+ ile Sherehe ya Wayahudi, ilikuwa imekaribia. 5 Yesu alipoinua macho yake na kuona umati mkubwa ukija, akamuuliza Filipo: “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?”+ 6 Hata hivyo, aliuliza swali hilo ili kumjaribu, kwa maana alijua jambo alilokuwa karibu kufanya. 7 Filipo akamjibu: “Mikate ya dinari* 200 haiwezi kutosha hata tukimpa kila mmoja wao kipande kidogo.” 8 Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu ya Simoni Petro, akamwambia: 9 “Hapa kuna mvulana mdogo aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Je, hivi vitawatosha watu wengi hivi?”+
10 Yesu akasema: “Waambieni watu waketi.” Basi mahali hapo palikuwa na nyasi nyingi, nao watu wakaketi, karibu wanaume 5,000.+ 11 Yesu akaichukua ile mikate, akatoa shukrani, kisha akawagawia wale waliokuwa wameketi hapo; pia akafanya vivyo hivyo na wale samaki wadogo, watu wote wakala na kushiba. 12 Waliposhiba akawaambia wanafunzi wake: “Kusanyeni vipande vilivyobaki, ili chochote kisipotee.” 13 Basi wakakusanya vipande vilivyobaki wakajaza vikapu 12 baada ya watu kula kutokana na ile mikate mitano ya shayiri.
14 Watu walipoona muujiza aliofanya, wakaanza kusema: “Kwa kweli huyu ndiye Nabii aliyepaswa kuja ulimwenguni.”+ 15 Kisha Yesu akijua walitaka kuja kumkamata wamfanye awe mfalme, akaondoka+ tena akaenda mlimani akiwa peke yake.+
16 Ilipofika jioni, wanafunzi wake wakashuka kwenda baharini,+ 17 wakapanda mashua ili wavuke bahari kwenda Kapernaumu. Sasa giza lilikuwa limeingia na bado Yesu hakuwa pamoja nao.+ 18 Pia, bahari ikaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa ukivuma.+ 19 Hata hivyo, walipokuwa wamepiga makasia umbali wa karibu kilomita tano au sita,* wakamwona Yesu akitembea juu ya bahari akiikaribia mashua, nao wakaogopa. 20 Lakini akawaambia: “Ni mimi; msiogope!”+ 21 Basi walitaka kumbeba Yesu kwenye mashua, na mara moja mashua ikafika kwenye nchi kavu mahali walipokuwa wakienda.+
22 Siku iliyofuata umati wa watu waliokuwa wamebaki ng’ambo ya bahari hawakuona mashua nyingine hapo ila mashua moja tu ndogo, na kwamba Yesu hakuwa amepanda kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake, bali wanafunzi walikuwa wameondoka peke yao. 23 Hata hivyo, mashua kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali ambapo walikula mikate baada ya Bwana kutoa shukrani. 24 Basi umati ulipoona kwamba Yesu na wanafunzi wake hawapo, wakapanda mashua zao wakaenda Kapernaumu kumtafuta Yesu.
25 Walipompata ng’ambo ya bahari wakamuuliza: “Rabi,+ ulifika hapa wakati gani?” 26 Yesu akawajibu: “Kwa kweli ninawaambia, hamnitafuti kwa sababu mliona ishara, bali kwa sababu mlikula mikate mkashiba.+ 27 Msifanye kazi kwa ajili ya chakula kinachoharibika, bali kwa ajili ya chakula kinachodumu kufikia uzima wa milele,+ ambacho Mwana wa binadamu atawapa ninyi; kwa maana Baba, Mungu mwenyewe, amemtia muhuri wake wa kibali.”+
28 Basi wakamuuliza: “Tufanye nini ili tutimize kazi za Mungu?” 29 Yesu akawajibu: “Hii ndiyo kazi ya Mungu, kwamba mmwamini* yule aliyemtuma.”+ 30 Basi wakamwambia: “Utafanya ishara gani,+ ili tuone na kukuamini? Unafanya kazi gani? 31 Mababu zetu walikula mana nyikani,+ kama ilivyoandikwa: ‘Aliwapa mkate kutoka mbinguni ili wale.’”+ 32 Kisha Yesu akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia, Musa hakuwapa mkate kutoka mbinguni, lakini Baba yangu anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni. 33 Kwa maana mkate wa Mungu ni yule anayeshuka kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.” 34 Kwa hiyo wakamwambia: “Bwana, tupe mkate huo sikuzote.”
35 Yesu akawaambia: “Mimi ndio mkate wa uzima. Yeyote anayekuja kwangu hatapata njaa kamwe, na yeyote anayeniamini hatapata kiu kamwe.+ 36 Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona na bado hamwamini.+ 37 Wote anaonipa Baba watakuja kwangu, nami sitamfukuza kamwe yeyote anayekuja kwangu;+ 38 kwa maana sikushuka kutoka mbinguni+ kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi ya yule aliyenituma.+ 39 Haya ndiyo mapenzi ya yule aliyenituma, kwamba nisipoteze yeyote kati ya wote alionipa, bali niwafufue+ katika siku ya mwisho. 40 Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Baba yangu, kwamba kila mtu anayemtambua Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele,+ nami nitamfufua+ siku ya mwisho.”
41 Kisha Wayahudi wakaanza kunung’unika kwa sababu alisema: “Mimi ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”+ 42 Nao wakaanza kusema: “Je, huyu si Yesu mwana wa Yosefu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua?+ Sasa anawezaje kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?” 43 Yesu akawaambia: “Acheni kunung’unika miongoni mwenu. 44 Hakuna mtu anayeweza kuja kwangu isipokuwa Baba aliyenituma amvute,+ nami nitamfufua siku ya mwisho.+ 45 Imeandikwa katika Manabii: ‘Wote watafundishwa na Yehova.’*+ Kila mtu ambaye amemsikiliza Baba na kujifunza huja kwangu. 46 Hakuna mwanadamu yeyote ambaye amemwona Baba,+ ila yule aliyetoka kwa Mungu; huyo amemwona Baba.+ 47 Kwa kweli ninawaambia, yeyote anayeamini ana uzima wa milele.+
48 “Mimi ndio mkate wa uzima.+ 49 Mababu zenu walikula mana nyikani na bado wakafa.+ 50 Huu ndio mkate unaoshuka kutoka mbinguni, ili yeyote anayeula asife. 51 Mimi ndio mkate ulio hai ambao ulishuka kutoka mbinguni. Yeyote akila mkate huu ataishi milele; na kwa kweli, mkate nitakaotoa ni mwili wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”+
52 Kisha Wayahudi wakaanza kubishana wakiulizana: “Mtu huyu anawezaje kutupatia mwili wake tule?” 53 Basi Yesu akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia, msipokula mwili wa Mwana wa binadamu na kunywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.+ 54 Yeyote akila mwili wangu na kunywa damu yangu ana uzima wa milele, nami nitamfufua+ siku ya mwisho; 55 kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. 56 Yeyote anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu hubaki katika muungano nami, nami katika muungano naye.+ 57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma nami ninaishi kwa sababu ya Baba, vivyo hivyo yule anayekula mwili wangu, ataishi kwa sababu yangu.+ 58 Huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni. Si kama vile walivyokula mababu zenu na bado wakafa. Yeyote anayekula mkate huu ataishi milele.”+ 59 Alisema mambo haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi* huko Kapernaumu.
60 Waliposikia hivyo, wengi kati ya wanafunzi wake wakasema: “Maneno hayo yanashtua; ni nani anayeweza kuyasikiliza?” 61 Lakini Yesu, akitambua kwamba wanafunzi wake walikuwa wakinung’unika kuhusu hilo, akawaambia: “Je, jambo hili limewakwaza? 62 Basi, itakuwaje mtakapomwona Mwana wa binadamu akipanda kurudi kule alikotoka?+ 63 Roho ndiyo inayotokeza uzima;+ mwili hauna faida hata kidogo. Maneno niliyowaambia ni roho na ni uzima.+ 64 Lakini kuna wengine kati yenu ambao hawaamini.” Kwa maana tangu mwanzo Yesu aliwajua wale ambao hawakuamini na yule ambaye angemsaliti.+ 65 Akaendelea kusema: “Ndiyo sababu nimewaambia, hakuna mtu anayeweza kuja kwangu isipokuwa aruhusiwe na Baba.”+
66 Kwa sababu hiyo, wengi kati ya wanafunzi wake wakarudi kwenye mambo yaliyo nyuma+ nao hawakumfuata tena. 67 Basi Yesu akawauliza wale 12: “Je, ninyi pia mnataka kwenda?” 68 Simoni Petro akamjibu: “Bwana, tutaenda kwa nani?+ Wewe una maneno ya uzima wa milele.+ 69 Tumeamini na tumejua kwamba wewe ndiye Mtakatifu wa Mungu.”+ 70 Yesu akawaambia: “Niliwachagua ninyi 12, sivyo?+ Lakini mmoja wenu ni mchongezi.”*+ 71 Kwa kweli, alikuwa akizungumza kumhusu Yuda mwana wa Simoni Iskariote, ambaye angemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale 12.+
7 Baada ya mambo hayo Yesu aliendelea kusafiri* huko Galilaya, kwa maana hakutaka kwenda Yudea kwa sababu Wayahudi walitaka kumuua.+ 2 Hata hivyo, Sherehe ya Vibanda ya Wayahudi,+ ilikuwa imekaribia. 3 Basi ndugu zake+ wakamwambia: “Ondoka hapa uende Yudea, ili wanafunzi wako pia waone kazi unazofanya. 4 Kwa maana mtu yeyote anayetaka kujulikana hadharani hafanyi jambo lolote kisiri. Ikiwa unafanya mambo haya jionyeshe kwa ulimwengu.” 5 Kwa kweli, ndugu zake hawakuwa wakimwamini.*+ 6 Basi Yesu akawaambia: “Bado wakati wangu haujafika,+ lakini wakati wenu upo sikuzote. 7 Ulimwengu hauna sababu ya kuwachukia ninyi, lakini unanichukia mimi kwa sababu ninatoa ushahidi kuuhusu kwamba matendo yake ni maovu.+ 8 Ninyi nendeni kwenye sherehe; mimi bado siendi kwenye sherehe hiyo, kwa sababu bado wakati wangu haujafika kikamili.”+ 9 Basi baada ya kuwaambia mambo hayo, akabaki Galilaya.
10 Lakini ndugu zake walipopanda kwenda kwenye sherehe, yeye pia alienda, lakini kisiri. 11 Basi Wayahudi wakaanza kumtafuta kwenye sherehe wakiuliza: “Yuko wapi yule mtu?” 12 Kulikuwa na minong’ono mingi kumhusu katika umati. Baadhi yao walisema: “Yeye ni mtu mwema.” Nao wengine wakasema: “Hapana. Anaupotosha umati.”+ 13 Bila shaka, hakuna mtu aliyesema waziwazi kumhusu kwa sababu waliwaogopa Wayahudi.+
14 Sherehe ilipofika katikati, Yesu akapanda kuingia hekaluni na kuanza kufundisha. 15 Wayahudi wakashangaa na kuulizana: “Mtu huyu alipataje ujuzi wa Maandiko,*+ ingawa hajafundishwa shuleni?”*+ 16 Naye Yesu akawaambia: “Mambo ninayofundisha si yangu, bali ni ya yule aliyenituma.+ 17 Mtu yeyote anayetamani kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho haya yanatoka kwa Mungu+ au ninasema mambo niliyojitungia. 18 Mtu anayesema mambo aliyojitungia anajitafutia utukufu; lakini mtu anayetafuta utukufu wa yule aliyemtuma,+ huyo ni wa kweli, na hana ukosefu wowote wa uadilifu ndani yake. 19 Musa aliwapa Sheria,+ sivyo? Lakini hakuna yeyote kati yenu anayetii Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”+ 20 Umati ukamwambia: “Wewe una roho mwovu. Ni nani anayetaka kukuua?” 21 Yesu akawajibu: “Nilifanya jambo moja tu, nyote mkashangaa. 22 Kwa hiyo Musa aliwapa tohara+—si kwamba inatoka kwa Musa, bali inatoka kwa mababu+—nanyi mnamtahiri mtu siku ya sabato. 23 Ikiwa mtu hutahiriwa siku ya sabato ili Sheria ya Musa isivunjwe, mbona mnanikasirikia sana kwa sababu nilimponya mtu siku ya sabato+ naye akapona kabisa? 24 Acheni kuhukumu kwa kutazama sura ya nje tu, bali hukumuni kwa uadilifu.”+
25 Kisha baadhi ya wakaaji wa Yerusalemu wakaanza kusema: “Huyu ndiye mtu wanayetaka kumuua, sivyo?+ 26 Na bado oneni! anazungumza hadharani, na hawamwambii chochote. Je, kweli watawala wametambua kwa hakika kwamba huyu ndiye Kristo? 27 Hata hivyo, tunajua mtu huyu ametoka wapi;+ lakini Kristo atakapokuja, hakuna mtu atakayejua alikotoka.” 28 Kisha Yesu alipokuwa akifundisha hekaluni akasema kwa sauti kubwa: “Ninyi mnanijua na pia mnajua nilikotoka. Nami sikuja kwa uamuzi wangu mwenyewe,+ lakini Yule aliyenituma ni halisi, nanyi hammjui.+ 29 Mimi ninamjua,+ kwa sababu mimi ni mwakilishi kutoka kwake, naye Ndiye aliyenituma.” 30 Basi wakaanza kutafuta njia ya kumkamata,+ lakini hakuna aliyeweza kumkamata, kwa sababu saa yake haikuwa imefika.+ 31 Hata hivyo, wengi katika umati walimwamini,+ nao wakaanza kusema: “Kristo atakapokuja, je, atafanya ishara nyingi kuliko alizofanya mtu huyu?”
32 Mafarisayo walisikia umati ukinong’onezana mambo hayo kumhusu, nao wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakawatuma maofisa wamkamate. 33 Kisha Yesu akasema: “Nitakuwa pamoja nanyi kwa muda mfupi kisha nitarudi kwa Yule aliyenituma.+ 34 Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nilipo hamwezi kuja.”+ 35 Kwa hiyo, Wayahudi wakaanza kuulizana: “Mtu huyu anakusudia kwenda wapi, hivi kwamba hatutampata? Je, anakusudia kwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki ili awafundishe Wagiriki? 36 Anamaanisha nini anaposema, ‘Mtanitafuta, lakini hamtanipata, na mahali nilipo hamwezi kuja’?”
37 Katika siku ya mwisho, siku kuu ya sherehe,+ Yesu alisimama na kusema kwa sauti kubwa: “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe maji.+ 38 Yeyote anayeniamini, kama andiko linavyosema: ‘Vijito vya maji ya uzima vitatiririka kutoka ndani yake.’”+ 39 Hata hivyo, alikuwa akizungumza kuhusu roho, ambayo wale waliomwamini walikuwa karibu kupokea; kwa maana kufikia wakati huo hawakuwa wamepokea roho,+ kwa sababu bado Yesu hakuwa ametukuzwa.+ 40 Baadhi ya watu katika umati waliosikia maneno hayo wakaanza kusema: “Kwa kweli huyu ndiye Nabii.”+ 41 Wengine walikuwa wakisema: “Huyu ndiye Kristo.”+ Lakini wengine wakasema: “Kristo hatakuja kutoka Galilaya, sivyo?+ 42 Je, andiko halisemi kwamba Kristo atatoka katika uzao wa Daudi+ na atatoka Bethlehemu,+ kijiji alichoishi Daudi?”+ 43 Basi kukatokea mgawanyiko kumhusu katika umati. 44 Hata hivyo, baadhi yao walitaka kumkamata, lakini hakuna yeyote aliyemkamata.
45 Kisha wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo. Wakawauliza: “Kwa nini hamkumleta?” 46 Maofisa wakajibu: “Hakuna mtu mwingine yeyote ambaye amewahi kuzungumza hivyo.”+ 47 Nao Mafarisayo wakawauliza: “Je, ninyi pia mmepotoshwa? 48 Je, kuna yeyote kati ya watawala au Mafarisayo ambaye amemwamini?+ 49 Lakini umati huu usiojua Sheria ni watu waliolaaniwa.” 50 Nikodemo, aliyekuwa amemwendea hapo mwanzoni, na ambaye pia alikuwa mmoja wao akawaambia: 51 “Kulingana na Sheria yetu, kabla ya kumhukumu mtu, tunapaswa kumsikiliza ili tujue anachofanya, sivyo?”+ 52 Wakamjibu: “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Chunguza uone kwamba hakuna nabii atakayeinuliwa kutoka Galilaya.”*
8 12 Kisha Yesu akawaambia tena: “Mimi ndiye nuru ya ulimwengu.+ Yeyote anayenifuata hatatembea kamwe gizani, bali atakuwa na nuru+ ya uzima.” 13 Basi Mafarisayo wakamwambia: “Wewe unatoa ushahidi juu yako mwenyewe; ushahidi wako si wa kweli.” 14 Yesu akawajibu: “Hata ikiwa ninatoa ushahidi juu yangu mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli, kwa sababu ninajua nilikotoka na ninakoenda.+ Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakoenda. 15 Ninyi mnahukumu kulingana na mwili;*+ mimi simhukumu mtu yeyote kamwe. 16 Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya kweli, kwa sababu siko peke yangu, bali Baba aliyenituma yuko pamoja nami.+ 17 Pia, katika Sheria yenu imeandikwa: ‘Ushahidi wa watu wawili ni wa kweli.’+ 18 Mimi ninatoa ushahidi juu yangu mwenyewe, na Baba aliyenituma hutoa ushahidi kunihusu.”+ 19 Kisha wakamuuliza: “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu: “Ninyi hamnijui mimi wala Baba yangu.+ Kama mngenijua mimi, mngemjua Baba yangu pia.”+ 20 Alisema maneno hayo katika chumba cha hazina+ alipokuwa akifundisha hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata, kwa sababu saa yake haikuwa imefika.+
21 Kwa hiyo, akawaambia tena: “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, na bado mtakufa katika dhambi zenu.+ Ninakoenda hamwezi kuja.”+ 22 Basi Wayahudi wakaanza kuulizana: “Je, atajiua? Kwa sababu anasema, ‘Ninakoenda hamwezi kuja.’” 23 Akaendelea kuwaambia: “Ninyi mnatoka katika makao ya chini; mimi ninatoka katika makao ya juu.+ Ninyi mnatoka katika ulimwengu huu; mimi sitoki katika ulimwengu huu. 24 Ndiyo maana niliwaambia: Mtakufa katika dhambi zenu. Kwa maana msipoamini kwamba mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu.” 25 Kwa hiyo wakaanza kumuuliza: “Wewe ni nani?” Yesu akawajibu: “Kwa nini hata ninazungumza nanyi? 26 Nina mambo mengi ya kusema kuwahusu na mengi ya kuhukumu. Kwa hakika, Yule aliyenituma ni wa kweli, na mambo niliyoyasikia kutoka kwake ninayasema ulimwenguni.”+ 27 Hawakuelewa kwamba alikuwa akiwaambia kumhusu Baba. 28 Kisha Yesu akasema: “Baada ya kumwinua Mwana wa binadamu,+ ndipo mtakapojua kwamba mimi ndiye+ na kwamba sifanyi jambo lolote kwa uamuzi wangu mwenyewe;+ bali mambo ambayo Baba amenifundisha, ndiyo ninayosema. 29 Na Yule aliyenituma yuko pamoja nami; naye hakuniacha peke yangu, kwa sababu sikuzote mimi hufanya mambo yanayompendeza.”+ 30 Alipokuwa akisema mambo hayo, wengi wakamwamini.
31 Basi Yesu akawaambia Wayahudi waliokuwa wamemwamini: “Mkikaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, 32 nanyi mtaijua kweli,+ nayo kweli itawaweka ninyi huru.”+ 33 Wakamjibu: “Sisi ni uzao wa Abrahamu na hatujawahi kuwa watumwa wa mtu yeyote. Kwa nini basi unasema tutakuwa huru?” 34 Yesu akawajibu: “Kwa kweli ninawaambia, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.+ 35 Isitoshe, mtumwa habaki nyumbani milele; lakini mwana hubaki milele. 36 Kwa hiyo, Mwana akiwaweka ninyi huru, kwa kweli mtakuwa huru. 37 Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini mnataka kuniua, kwa sababu neno langu halifanyi maendeleo kati yenu. 38 Ninasema mambo niliyoona nilipokuwa na Baba yangu,+ lakini ninyi mnafanya mambo mliyosikia kutoka kwa baba yenu.” 39 Wakamwambia: “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia: “Kama mngekuwa watoto wa Abrahamu,+ mngefanya kazi za Abrahamu. 40 Lakini sasa mnataka kuniua, mimi ambaye nimewaambia kweli niliyosikia kutoka kwa Mungu.+ Abrahamu hakufanya hivyo. 41 Mnafanya kazi za baba yenu.” Wakamwambia: “Hatukuzaliwa kutokana na uasherati;* tuna Baba mmoja tu, Mungu.”
42 Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda,+ kwa maana nilitoka kwa Mungu nami nipo hapa. Sikuja kwa uamuzi wangu mwenyewe, bali Yeye ndiye aliyenituma.+ 43 Kwa nini hamwelewi mambo ninayosema? Kwa sababu hamwezi kusikiliza neno langu. 44 Ninyi mmetoka kwa baba yenu Ibilisi, nanyi mnataka kufanya tamaa za baba yenu.+ Alikuwa muuaji alipoanza,*+ naye hakusimama imara katika kweli, kwa sababu kweli haimo ndani yake. Anaposema uwongo, yeye husema kulingana na mwelekeo wake mwenyewe, kwa sababu yeye ni mwongo na ndiye baba ya uwongo.+ 45 Lakini kwa sababu mimi ninawaambia kweli, hamniamini. 46 Ni nani kati yenu anayeweza kunihukumu kwamba nina dhambi? Ikiwa ninasema kweli, kwa nini hamniamini? 47 Yule anayetoka kwa Mungu husikiliza maneno ya Mungu.+ Kwa sababu hiyo, ninyi hamsikilizi, kwa kuwa hamtoki kwa Mungu.”+
48 Wayahudi wakamjibu: “Je, hatusemi kweli tunaposema, ‘Wewe ni Msamaria+ na una roho mwovu’?”+ 49 Yesu akajibu: “Mimi sina roho mwovu bali ninamheshimu Baba yangu, lakini ninyi mnanivunjia heshima. 50 Hata hivyo, mimi sijitafutii utukufu;+ kuna Yule anayetafuta na kuhukumu. 51 Kwa kweli ninawaambia, yeyote akishika maneno yangu, hataona kifo kamwe.”+ 52 Wayahudi wakamwambia: “Sasa tunajua una roho mwovu. Abrahamu alikufa, na manabii vilevile, lakini wewe unasema, ‘Yeyote akishika maneno yangu hataonja kifo kamwe.’ 53 Wewe si mkuu kuliko Abrahamu baba yetu ambaye alikufa, sivyo? Manabii pia walikufa. Unafikiri wewe ni nani?” 54 Yesu akajibu: “Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye mnasema ni Mungu wenu, ndiye anayenitukuza.+ 55 Ninyi bado hamjamjua,+ lakini mimi ninamjua.+ Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi. Lakini mimi ninamjua, na ninalishika neno lake. 56 Baba yenu Abrahamu alishangilia sana tazamio la kuona siku yangu, naye aliiona na kushangilia.”+ 57 Kisha Wayahudi wakamuuliza: “Wewe hujafika umri wa miaka 50, na bado umemwona Abrahamu?” 58 Yesu akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia, mimi nimekuwapo kabla Abrahamu hajakuwapo.”+ 59 Ndipo wakaokota mawe ili wampige, lakini Yesu akajificha na kuondoka hekaluni.
9 Yesu alipokuwa akipita alimwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa. 2 Kisha wanafunzi wake wakamuuliza: “Rabi,+ ni nani aliyetenda dhambi, ni mtu huyu au ni wazazi wake, hivi kwamba akazaliwa kipofu?” 3 Yesu akajibu: “Mtu huyu hakutenda dhambi wala wazazi wake, bali ilikuwa hivyo ili kazi za Mungu zifunuliwe katika kisa chake.+ 4 Lazima tufanye kazi za Yule aliyenituma kukiwa bado mchana;+ usiku unakuja ambapo hakuna mtu atakayeweza kufanya kazi. 5 Maadamu nimo ulimwenguni, mimi ndiye nuru ya ulimwengu.”+ 6 Baada ya kusema mambo hayo, akatema mate chini akafanyiza tope kwa mate, na kumpaka mtu huyo kwenye macho+ 7 na kumwambia: “Nenda ukanawe katika dimbwi la Siloamu” (linalotafsiriwa kuwa “Aliyetumwa”). Naye akaenda na kunawa, akarudi akiwa anaona.+
8 Basi majirani na watu waliokuwa wakimwona akiombaomba wakaanza kuulizana: “Je, huyu si yule mtu aliyekuwa akiketi akiombaomba?” 9 Baadhi yao walikuwa wakisema: “Ni yeye.” Wengine walikuwa wakisema: “Hapana, lakini anafanana naye.” Yule mtu akaendelea kusema: “Ni mimi.” 10 Basi wakamuuliza: “Macho yako yalifunguliwaje?” 11 Akajibu: “Mtu anayeitwa Yesu alifanyiza tope akanipaka kwenye macho kisha akaniambia, ‘Nenda mpaka Siloamu ukanawe.’+ Basi nikaenda, nikanawa, nikaanza kuona.” 12 Ndipo wakamuuliza: “Yuko wapi mtu huyo?” Akasema: “Sijui.”
13 Wakampeleka kwa Mafarisayo mtu huyo ambaye zamani alikuwa kipofu. 14 Ikawa kwamba siku ambayo Yesu alifanyiza tope na kuyafungua macho ya mtu huyo+ ilikuwa Sabato.+ 15 Basi wakati huo Mafarisayo wakaanza kumuuliza jinsi alivyoanza kuona. Akawaambia: “Alinipaka tope kwenye macho yangu, nami nikanawa, sasa ninaona.” 16 Kisha baadhi ya Mafarisayo wakaanza kusema: “Mtu huyo hatoki kwa Mungu, kwa sababu hashiki Sabato.”+ Wengine wakasema: “Mtenda dhambi anawezaje kufanya ishara kama hizo?”+ Basi kukawa na mgawanyiko kati yao.+ 17 Wakamuuliza tena yule mtu aliyekuwa kipofu: “Unasemaje kumhusu kwa kuwa wewe ndiye uliyefunguliwa macho?” Akajibu: “Yeye ni nabii.”
18 Hata hivyo, Wayahudi hawakuamini kwamba alikuwa kipofu na sasa alikuwa anaona. Basi wakawaita wazazi wake 19 wakawauliza: “Je, huyu ni mwana wenu ambaye mnasema alizaliwa kipofu? Basi, imekuwaje kwamba sasa anaona?” 20 Wazazi wake wakajibu: “Tunajua kwamba huyu ni mwana wetu na alizaliwa akiwa kipofu. 21 Lakini hatujui jinsi alivyoanza kuona, wala hatujui mtu aliyemfungua macho. Muulizeni. Yeye ni mtu mzima. Anaweza kujieleza.” 22 Wazazi wake walisema hivyo kwa sababu waliogopa Wayahudi,+ kwa maana tayari Wayahudi walikuwa wamekubaliana kwamba mtu yeyote ambaye angemkiri kuwa ndiye Kristo, angefukuzwa katika sinagogi.+ 23 Ndiyo maana wazazi wake walisema: “Yeye ni mtu mzima, muulizeni.”
24 Basi wakamwita mara ya pili yule mtu aliyekuwa kipofu na kumwambia: “Mpe Mungu utukufu; tunajua mtu huyu ni mtenda dhambi.” 25 Akawajibu: “Kama yeye ni mtenda dhambi mimi sijui. Ninachojua ni kwamba nilikuwa kipofu, lakini sasa ninaona.” 26 Kisha wakamuuliza: “Alikufanyia nini? Aliyafunguaje macho yako?” 27 Akawajibu: “Tayari nimewaambia, lakini hamkusikiliza. Kwa nini mnataka kusikia tena? Je, ninyi pia mnataka kuwa wanafunzi wake?” 28 Ndipo wakamwambia kwa dharau: “Wewe ni mwanafunzi wa mtu huyo, lakini sisi ni wanafunzi wa Musa. 29 Tunajua kwamba Mungu alizungumza na Musa; lakini mtu huyu, hatujui alikotoka.” 30 Yule mtu akawajibu: “Kwa kweli inashangaza kwamba hamjui alikotoka, ingawa ndiye aliyefungua macho yangu. 31 Tunajua kwamba Mungu hawasikilizi watenda dhambi,+ lakini humsikiliza mtu yeyote anayemwogopa na kufanya mapenzi yake.+ 32 Tangu zamani haijasikiwa kamwe mtu yeyote ameyafungua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu. 33 Kama mtu huyu hakutoka kwa Mungu, hangeweza kufanya lolote.”+ 34 Wakamwambia: “Wewe ulizaliwa katika dhambi, na bado unajaribu kutufundisha?” Kwa hiyo, wakamfukuza!+
35 Yesu akasikia kwamba walikuwa wamemfukuza mtu huyo. Basi alipompata akamuuliza: “Je, unamwamini Mwana wa binadamu?” 36 Yule mtu akauliza: “Bwana, huyo ni nani, niambie ili nimwamini?” 37 Yesu akamwambia: “Tayari umemwona, na kwa kweli, yeye ndiye anayezungumza nawe.” 38 Akasema: “Ninamwamini, Bwana.” Naye akamsujudia.* 39 Kisha Yesu akasema: “Nilikuja ulimwenguni kwa ajili ya hukumu hii, ili wale wasioona waweze kuona+ na wale wanaoona wawe vipofu.”+ 40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye waliposikia mambo hayo wakamuuliza: “Je, sisi pia ni vipofu?” 41 Yesu akawaambia: “Kama mngekuwa vipofu, hamngekuwa na dhambi. Lakini sasa mnasema, ‘Tunaona.’ Dhambi yenu inabaki.”+
10 “Kwa kweli ninawaambia, mtu asiyeingia katika zizi la kondoo kupitia mlango, bali anapanda na kuingia kupitia njia nyingine, ni mwizi na mporaji.+ 2 Lakini yule anayeingia kupitia mlango ndiye mchungaji wa kondoo.+ 3 Mlinzi wa mlango humfungulia,+ nao kondoo huisikiliza sauti yake.+ Naye huwaita kondoo wake kwa majina na kuwatoa nje. 4 Baada ya kuwatoa kondoo wake wote nje, yeye huwatangulia, nao kondoo humfuata kwa sababu wanaijua sauti yake. 5 Hawatamfuata mgeni kamwe bali watamkimbia, kwa sababu hawajui sauti ya wageni.” 6 Yesu aliwaambia mfano huo, lakini hawakuelewa alichokuwa akiwaambia.
7 Basi Yesu akasema tena: “Kwa kweli ninawaambia, mimi ndiye mlango wa kondoo.+ 8 Wote ambao wamekuja wakidai kwamba wao ni mimi, ni wezi na waporaji; lakini kondoo hawakuwasikiliza. 9 Mimi ndiye mlango; yeyote anayeingia kupitia kwangu ataokolewa, naye ataingia na kutoka na kupata malisho.+ 10 Mwizi huja kuiba, kuua, na kuangamiza.+ Mimi nimekuja ili wapate uzima na waupate kwa wingi. 11 Mimi ndiye mchungaji mwema;+ mchungaji mwema huutoa uhai wake* kwa ajili ya kondoo.+ 12 Mtu wa kuajiriwa, ambaye si mchungaji na ambaye kondoo si wake, anapomwona mbwamwitu akija yeye huwaacha kondoo na kukimbia—naye mbwamwitu huwanyakua na kuwatawanya— 13 kwa sababu yeye ni mtu wa kuajiriwa naye hawajali kondoo. 14 Mimi ndiye mchungaji mwema. Ninawajua kondoo wangu nao kondoo wangu wananijua,+ 15 kama Baba anavyonijua mimi, nami ninavyomjua Baba;+ na ninatoa uhai wangu* kwa ajili ya kondoo.+
16 “Nami nina kondoo wengine, ambao si wa zizi hili;+ hao pia nitawaleta, nao wataisikiliza sauti yangu, nao watakuwa kundi moja, mchungaji mmoja.+ 17 Kwa sababu hiyo, Baba ananipenda,+ kwa kuwa ninautoa uhai wangu*+ ili niupate tena. 18 Hakuna mtu anayeuchukua kutoka kwangu, bali ninautoa kwa hiari yangu. Nina mamlaka ya kuutoa, nami nina mamlaka ya kuupokea tena.+ Nilipokea amri hii kutoka kwa Baba yangu.”
19 Kisha mgawanyiko ukatokea tena kati ya Wayahudi+ kwa sababu ya maneno hayo. 20 Wengi wao walikuwa wakisema: “Ana roho mwovu naye ana wazimu. Kwa nini mnamsikiliza?” 21 Wengine wakasema: “Haya si maneno ya mtu mwenye roho mwovu. Je, roho mwovu anaweza kufungua macho ya vipofu?”
22 Wakati huo kulikuwa na Sherehe ya Wakfu huko Yerusalemu. Ulikuwa wakati wa majira ya baridi kali, 23 na Yesu alikuwa akitembea hekaluni kwenye safu ya nguzo za Sulemani.+ 24 Kisha Wayahudi wakamzunguka na kuanza kumwambia: “Utaendelea kutuhangaisha* mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo, tuambie waziwazi.” 25 Yesu akawajibu: “Niliwaambia, na bado hamwamini. Kazi ninazofanya katika jina la Baba yangu, zinatoa ushahidi kunihusu.+ 26 Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si kondoo wangu.+ 27 Kondoo wangu husikiliza sauti yangu, nami ninawajua, nao hunifuata.+ 28 Mimi ninawapa uzima wa milele,+ nao hawataharibiwa kamwe, wala hakuna atakayewanyakua kutoka mkononi mwangu.+ 29 Kile ambacho Baba yangu amenipa ni chenye thamani kuliko vitu vingine vyote, na hakuna anayeweza kuwanyakua kutoka mkononi mwa Baba.+ 30 Mimi na Baba ni kitu kimoja.”*+
31 Wayahudi wakaokota mawe tena ili wampige. 32 Yesu akawajibu: “Niliwaonyesha kazi nyingi nzuri kutoka kwa Baba. Kati ya kazi hizo, ni ipi inayofanya mtake kunipiga mawe?” 33 Wayahudi wakamjibu: “Tunakupiga mawe, si kwa sababu ya kazi njema, bali umekufuru;+ kwa maana ingawa wewe ni mwanadamu, unajifanya mungu.” 34 Yesu akawajibu: “Je, haijaandikwa katika Sheria yenu, ‘Mimi nilisema: “Ninyi ni miungu”’?*+ 35 Ikiwa aliwaita ‘miungu’+ wale ambao neno la Mungu lilikuja dhidi yao—na bado andiko haliwezi kubatilishwa— 36 je, mnaniambia mimi ambaye Baba alinitakasa na kunituma ulimwenguni, ‘Unakufuru,’ kwa sababu nilisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu’?+ 37 Kama sifanyi kazi za Baba yangu, msiniamini. 38 Lakini ikiwa ninazifanya, hata ingawa hamniamini mimi, basi iweni na imani katika kazi hizo,+ ili mjue na kuendelea kujua kwamba Baba yuko katika muungano nami, nami niko katika muungano na Baba.”+ 39 Basi wakajaribu tena kumkamata; lakini akawakwepa.
40 Kisha akaenda tena ng’ambo ya Yordani mpaka mahali ambapo mwanzoni Yohana alikuwa akibatiza watu,+ naye akakaa huko. 41 Watu wengi wakamjia na kuanza kusema: “Yohana hakufanya ishara hata moja, lakini mambo yote aliyosema kumhusu mtu huyu yalikuwa ya kweli.”+ 42 Na watu wengi hapo wakamwamini Yesu.
11 Mtu fulani aliyeitwa Lazaro alikuwa mgonjwa; aliishi Bethania, kijiji cha Maria na Martha+ dada yake. 2 Huyo Maria ndiye aliyempaka Bwana mafuta yenye marashi na kufuta miguu yake kwa nywele zake;+ Lazaro, ndugu yake ndiye aliyekuwa mgonjwa. 3 Basi dada zake wakamtumia Yesu ujumbe wakisema: “Bwana, ona! yule unayempenda ni mgonjwa.” 4 Lakini Yesu aliposikia hilo akasema: “Lengo la ugonjwa huu si kusababisha kifo, bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu,+ ili Mwana wa Mungu atukuzwe kupitia huo.”
5 Basi Yesu aliwapenda Martha na dada yake na Lazaro. 6 Hata hivyo, aliposikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali alipokuwa kwa siku mbili zaidi. 7 Baada ya hayo, akawaambia wanafunzi: “Twendeni tena Yudea.” 8 Wanafunzi wakamwambia: “Rabi,+ juzijuzi tu Wayudea walitaka kukupiga mawe,+ nawe unarudi huko tena?” 9 Yesu akajibu: “Kuna saa 12 za mchana, sivyo?+ Yeyote akitembea mchana hatajikwaa, kwa sababu anaona mwangaza wa ulimwengu huu. 10 Lakini ikiwa yeyote anatembea usiku, atajikwaa kwa sababu hana nuru ndani yake.”
11 Baada ya kusema hayo, akawaambia: “Rafiki yetu Lazaro amelala usingizi,+ lakini ninasafiri kwenda huko ili kumwamsha.” 12 Kisha wanafunzi wakamwambia: “Bwana, ikiwa amelala usingizi, atapona.” 13 Hata hivyo, Yesu alikuwa akizungumza kuhusu kifo cha Lazaro. Lakini walifikiri anasema kuhusu kupumzika katika usingizi. 14 Ndipo Yesu akawaambia waziwazi: “Lazaro amekufa,+ 15 nami ninashangilia kwa ajili yenu kwamba sikuwapo, ili mwamini. Lakini twendeni kwake.” 16 Kwa hiyo Tomasi, aliyeitwa Pacha, akawaambia wanafunzi wenzake: “Sisi pia, twendeni tukafe pamoja naye.”+
17 Yesu alipofika, alikuta kwamba tayari Lazaro alikuwa kaburini* kwa siku nne. 18 Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa kilomita tatu hivi.* 19 Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kwa Martha na Maria ili kuwafariji kwa sababu ya kufiwa na ndugu yao. 20 Martha aliposikia Yesu anakuja, alienda kumlaki; lakini Maria+ alibaki nyumbani. 21 Kisha Martha akamwambia Yesu: “Bwana, kama ungekuwa hapa ndugu yangu hangekufa. 22 Lakini hata sasa ninajua kwamba chochote utakachomwomba Mungu, Mungu atakupa.” 23 Yesu akamwambia: “Ndugu yako atafufuka.” 24 Martha akamwambia: “Ninajua atafufuka katika ufufuo+ siku ya mwisho.” 25 Yesu akamwambia: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.+ Yule anayeniamini, hata akifa, ataishi tena; 26 na kila mtu aliye hai na ananiamini hatakufa kamwe.+ Je, unaamini hilo?” 27 Akamwambia: “Ndiyo Bwana, ninaamini kwamba wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, yule anayekuja ulimwenguni.” 28 Baada ya kusema hayo, Martha akaenda kumwita Maria dada yake, akamwambia faraghani: “Mwalimu+ amefika naye anakuita.” 29 Aliposikia hilo, akasimama upesi, akamwendea.
30 Yesu hakuwa ameingia kijijini, bado alikuwa mahali alipokutana na Martha. 31 Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji, walipomwona akisimama upesi na kuondoka, wakamfuata wakidhani kwamba alikuwa akienda kulia kwenye kaburi.*+ 32 Maria alipofika mahali alipokuwa Yesu na kumwona, akaanguka miguuni pake na kumwambia: “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.” 33 Yesu alipomwona akilia na Wayahudi waliokuja pamoja naye wakilia pia, akaugua moyoni* na kutaabika. 34 Akauliza: “Mmemlaza wapi?” Wakamjibu: “Bwana, njoo uone.” 35 Yesu akatokwa na machozi.+ 36 Ndipo Wayahudi wakaanza kusema: “Ona jinsi alivyompenda!” 37 Lakini baadhi yao wakauliza: “Je, mtu huyu aliyemfungua macho yule kipofu+ hangeweza kuzuia huyu asife?”
38 Kisha baada ya Yesu kuugua tena moyoni, akaja kwenye lile kaburi.* Kwa kweli, lilikuwa pango lililofunikwa kwa jiwe. 39 Yesu akasema: “Liondoeni jiwe.” Martha, dada ya yule aliyekufa akamwambia: “Bwana, kufikia sasa lazima awe ananuka, kwa maana ni siku nne.” 40 Yesu akamwambia: “Je, sikukuambia kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”+ 41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Kisha Yesu akatazama mbinguni+ na kusema: “Baba, ninakushukuru kwa sababu umenisikia. 42 Kwa kweli, ninajua kwamba sikuzote wewe hunisikia; lakini nilisema kwa ajili ya umati waliosimama kunizunguka, ili waamini kwamba ulinituma.”+ 43 Baada ya kusema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro, njoo huku nje!”+ 44 Mtu huyo aliyekuwa amekufa akatoka, miguu na mikono yake ikiwa imefungwa kwa vitambaa, na uso wake ukiwa umefungwa kwa kitambaa. Yesu akawaambia: “Mfungueni, mmwache aende.”
45 Kwa hiyo, Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kwa Maria, wakamwamini Yesu walipoona alichofanya,+ 46 lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia jambo ambalo Yesu alikuwa amefanya. 47 Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya Sanhedrini na kusema: “Tutafanya nini, kwa kuwa mtu huyu anafanya ishara nyingi?+ 48 Tukimwacha aendelee, watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja na kuchukua mahali petu* na taifa letu.” 49 Lakini mmoja wao aitwaye Kayafa,+ aliyekuwa kuhani mkuu mwaka huo, akawaambia: “Ninyi hamjui chochote, 50 na hamwelewi kwamba ni kwa faida yenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu kuliko taifa lote liangamizwe.” 51 Lakini hakusema hivyo kwa kujitungia; bali kwa sababu alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, alitoa unabii kwamba Yesu angekufa kwa ajili ya taifa, 52 na si kwa ajili ya taifa tu, bali pia ili awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika kotekote. 53 Basi tangu siku hiyo wakapanga njama ili kumuua.
54 Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alienda katika eneo lililo karibu na nyika, katika jiji linaloitwa Efraimu,+ naye akakaa huko pamoja na wanafunzi. 55 Sasa Pasaka+ ya Wayahudi ilikuwa karibu na watu wengi kutoka mashambani walipanda kwenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili wajitakase kisherehe. 56 Walikuwa wakimtafuta Yesu, nao wakawa wakiulizana wakiwa wamesimama hekaluni: “Mnaonaje? Je, kweli atakuja kwenye sherehe?” 57 Lakini wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa agizo kwamba ikiwa mtu yeyote angejua mahali alipo Yesu, alipaswa kuwajulisha ili wamkamate.
12 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu akafika Bethania, alikoishi Lazaro+ ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka kwa wafu. 2 Basi, wakamwandalia mlo wa jioni huko, na Martha alikuwa akiwahudumia,+ lakini Lazaro alikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wakila* pamoja na Yesu. 3 Kisha Maria akachukua ratili* moja ya mafuta yenye marashi, nardo halisi, ghali sana, akammiminia Yesu miguuni na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba ikajaa harufu ya mafuta yenye marashi.+ 4 Lakini Yuda Iskariote,+ mmoja wa wanafunzi wake aliyekuwa karibu kumsaliti akasema: 5 “Kwa nini mafuta haya yenye marashi hayangeuzwa kwa dinari* 300 na maskini wapewe pesa hizo?” 6 Hakusema hivyo kwa sababu aliwahangaikia maskini, bali kwa sababu alikuwa mwizi, naye ndiye aliyetunza sanduku la pesa na alikuwa akiiba pesa zilizowekwa humo. 7 Kisha Yesu akawaambia: “Mwacheni afanye hivyo kwa ajili ya matayarisho ya siku ya mazishi yangu.+ 8 Kwa maana maskini mnao sikuzote,+ lakini mimi hamtakuwa nami sikuzote.”+
9 Wakati huohuo, umati mkubwa wa Wayahudi ukajua kwamba alikuwa huko, nao ukaja, si kwa sababu ya Yesu tu, bali pia ili kumwona Lazaro aliyekuwa amefufuliwa kutoka kwa wafu.+ 10 Sasa wakuu wa makuhani wakapanga njama ili kumuua Lazaro pia, 11 kwa kuwa Wayahudi wengi walikuwa wakienda huko na kumwamini Yesu kwa sababu ya Lazaro.+
12 Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye sherehe, ukasikia kwamba Yesu alikuwa akija Yerusalemu. 13 Basi wakachukua matawi ya mitende na kutoka nje kwenda kumlaki, nao wakaanza kusema kwa sauti kubwa: “Tunaomba umwokoe! Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova,*+ Mfalme wa Israeli!”+ 14 Yesu alipompata mwanapunda, akaketi juu yake,+ kama ilivyoandikwa: 15 “Usiogope binti ya Sayuni. Tazama! Mfalme wako anakuja, akiwa ameketi juu ya mwanapunda.”+ 16 Mwanzoni, wanafunzi wake hawakuelewa mambo hayo, lakini Yesu alipotukuzwa,+ wakakumbuka kwamba mambo hayo yalikuwa yameandikwa kumhusu na kwamba walimtendea mambo hayo.+
17 Umati uliokuwa pamoja naye alipomwita Lazaro kutoka kaburini*+ na kumfufua kutoka kwa wafu ukaendelea kutoa ushahidi.+ 18 Kwa sababu hiyo pia, umati ukaenda kumlaki kwa sababu ulisikia alikuwa amefanya muujiza huo. 19 Basi Mafarisayo wakaambiana: “Mnaona, hamjafaulu hata kidogo. Tazama! Ulimwengu wote umemfuata.”+
20 Sasa kulikuwa na baadhi ya Wagiriki miongoni mwa wale waliokuja kuabudu kwenye sherehe. 21 Basi, wakamjia Filipo+ aliyetoka Bethsaida ya Galilaya, wakaanza kumwomba: “Bwana, tunataka kumwona Yesu.” 22 Filipo akaenda kumwambia Andrea, kisha wote wawili wakaja na kumwambia Yesu.
23 Lakini Yesu akawajibu: “Saa imefika ya Mwana wa binadamu kutukuzwa.+ 24 Kwa kweli ninawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka kwenye udongo na kufa, hubaki ikiwa mbegu moja tu; lakini ikifa,+ huzaa matunda mengi. 25 Yeyote anayeupenda sana uhai wake* huuangamiza, lakini yeyote anayeuchukia uhai wake*+ katika ulimwengu huu ataulinda kwa ajili ya uzima wa milele.+ 26 Ikiwa yeyote anataka kunihudumia, basi anifuate na mahali nilipo ndipo mhudumu wangu atakapokuwa pia.+ Ikiwa yeyote anataka kunihudumia, Baba atamheshimu. 27 Sasa ninataabika,*+ nami niseme nini? Baba, niokoe kutoka katika saa hii.+ Hata hivyo, ndiyo sababu nimekuja kwenye saa hii. 28 Baba, litukuze jina lako.” Ndipo sauti+ ikasikika kutoka mbinguni ikisema: “Nimelitukuza nami nitalitukuza tena.”+
29 Umati uliokuwa umesimama hapo ulisikia sauti hiyo ukaanza kusema kumekuwa na mngurumo. Nao wengine wakasema: “Malaika ameongea naye.” 30 Yesu akajibu: “Sauti hii imesikika, si kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu. 31 Sasa ulimwengu huu unahukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu+ huu atatupwa nje.+ 32 Na bado mimi, nikiinuliwa kutoka duniani,+ nitawavuta watu wa namna zote kwangu.” 33 Kwa kweli alisema hivyo ili kuonyesha ni kifo cha aina gani alikuwa karibu kufa.+ 34 Kisha umati ukamwambia: “Tulisikia kutoka katika Sheria kwamba Kristo hudumu milele.+ Kwa nini unasema kwamba lazima Mwana wa binadamu ainuliwe?+ Huyo Mwana wa binadamu ni nani?” 35 Basi Yesu akawaambia: “Nuru itakuwa miongoni mwenu kwa muda kidogo zaidi. Tembeeni wakati bado mna nuru, ili giza lisiwazidi nguvu; yeyote anayetembea katika giza hajui anakoenda.+ 36 Wakati mna nuru, iweni na imani* katika nuru ili muwe wana wa nuru.”+
Yesu alisema mambo hayo, kisha akaenda kujificha mbali nao. 37 Ingawa alikuwa amefanya ishara nyingi sana mbele yao, hawakuwa wakimwamini, 38 ili maneno haya aliyosema nabii Isaya yatimizwe: “Yehova,* ni nani ambaye ameamini jambo alilosikia kutoka kwetu?*+ Na mkono wa Yehova,* umefunuliwa kwa nani?”+ 39 Wao hawakuamini kwa sababu pia Isaya alisema: 40 “Ameyapofusha macho yao naye ameifanya mioyo yao iwe migumu, ili wasione kwa macho yao na kuelewa kwa mioyo yao na kugeuka nami niwaponye.”+ 41 Isaya alisema mambo haya kwa sababu aliona utukufu wake, naye alisema kumhusu.+ 42 Hata hivyo, watawala wengi kwa kweli walimwamini,+ lakini hawakumkiri kwa sababu waliwaogopa Mafarisayo, ili wasifukuzwe katika sinagogi;+ 43 kwa maana waliupenda utukufu wa wanadamu kuliko utukufu wa Mungu.+
44 Hata hivyo, Yesu akasema kwa sauti kubwa: “Yeyote anayeniamini, haniamini mimi tu bali pia Yule aliyenituma;+ 45 na yeyote anayeniona mimi anamwona pia Yule aliyenituma.+ 46 Nimekuja nikiwa nuru ulimwenguni,+ ili kila mtu anayeniamini asibaki gizani.+ 47 Lakini ikiwa yeyote anasikia maneno yangu na hayashiki, simhukumu; kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.+ 48 Yeyote anayenipuuza na hapokei maneno yangu, ana wa kumhukumu. Neno ambalo nimesema ndilo litakalomhukumu katika siku ya mwisho. 49 Kwa maana sijasema kwa uamuzi wangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma amenipa amri kuhusu jambo la kutangaza na la kusema.+ 50 Pia, ninajua kwamba amri yake inamaanisha uzima wa milele.+ Kwa hiyo, mambo ninayosema, ninasema kama Baba alivyoniambia.”+
13 Sasa, kwa sababu alijua kabla ya sherehe ya Pasaka kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba+ ilikuwa imefika,+ Yesu akiwa amewapenda walio wake ulimwenguni, aliwapenda mpaka mwisho.+ 2 Walipokuwa wakila mlo wa jioni, tayari Ibilisi alikuwa ameweka wazo la kumsaliti Yesu+ ndani ya moyo wa Yuda Iskariote,+ mwana wa Simoni. 3 Basi, Yesu akijua kwamba Baba alikuwa ameviweka vitu vyote mikononi mwake na kwamba alikuja kutoka kwa Mungu na alikuwa akienda kwa Mungu,+ 4 akasimama kutoka kwenye mlo wa jioni na kuyaweka kando mavazi yake ya nje. Naye akachukua taulo, akajifunga kiunoni.+ 5 Akatia maji kwenye beseni, akaanza kuiosha miguu ya wanafunzi na kuikausha kwa taulo aliyokuwa amejifunga kiunoni. 6 Kisha akamfikia Simoni Petro. Petro akamuuliza: “Bwana, unaosha miguu yangu?” 7 Yesu akamjibu: “Ninalofanya huelewi sasa, lakini utaelewa baada ya mambo haya.” 8 Petro akamwambia: “Hutaosha kamwe miguu yangu.” Yesu akamjibu: “Nisipokuosha,+ wewe huna sehemu pamoja nami.” 9 Simoni Petro akamwambia: “Bwana, usioshe miguu yangu tu, bali pia mikono na kichwa changu.” 10 Yesu akamwambia: “Yeyote ambaye ameoga hahitaji kuoshwa zaidi ya miguu yake, yuko safi kabisa. Nanyi mko safi, lakini sio nyote.” 11 Kwa maana alimjua mtu aliyekuwa akimsaliti.+ Ndiyo sababu alisema: “Sio nyote mlio safi.”
12 Baada ya kuosha miguu yao na kuvaa mavazi yake ya nje, akaketi mezani tena akawaambia: “Je, mnaelewa jambo ambalo nimewafanyia? 13 Ninyi huniita, ‘Mwalimu,’ na, ‘Bwana,’ nanyi hamjakosea, kwa maana ndivyo nilivyo.+ 14 Kwa hiyo, ingawa mimi ni Bwana na Mwalimu, niliiosha miguu yenu,+ basi ninyi pia mnapaswa* kuoshana miguu.+ 15 Kwa maana nimewawekea kielelezo, ili mfanye kama nilivyowafanyia.+ 16 Kwa kweli ninawaambia, mtumwa si mkuu kuliko bwana wake, wala yule aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma. 17 Ikiwa mnajua mambo haya, mtakuwa wenye furaha mkiyatenda.+ 18 Sisemi kuwahusu ninyi nyote; ninawajua wale ambao nimewachagua. Lakini ilikuwa hivyo ili andiko hili litimizwe:+ ‘Yule aliyekuwa akila mkate wangu amekiinua kisigino chake dhidi yangu.’*+ 19 Kuanzia sasa na kuendelea ninawaambia kabla jambo hilo halijatokea, ili litakapotokea mwamini kwamba mimi ndiye.+ 20 Kwa kweli ninawaambia, yeyote anayempokea yule ninayemtuma ananipokea mimi pia,+ na yeyote anayenipokea, anampokea pia Yule aliyenituma.”+
21 Baada ya kusema mambo hayo, Yesu akataabika rohoni, naye akatoa ushahidi akisema: “Kwa kweli ninawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”+ 22 Wanafunzi wakaanza kutazamana, bila kujua alikuwa akisema kuhusu nani.+ 23 Mmoja wa wanafunzi ambaye Yesu alimpenda,+ alikuwa ameketi mezani karibu na* Yesu. 24 Kwa hiyo, Simoni Petro akamwonyesha huyo ishara kwa kichwa na kumwambia: “Tuambie anasema kuhusu nani.” 25 Basi mwanafunzi huyo akaegemea nyuma kifuani pa Yesu na kumuuliza: “Bwana, ni nani?”+ 26 Yesu akajibu: “Ni yule ambaye nitampa kipande cha mkate ninachochovya.”+ Basi, akachovya kipande cha mkate, kisha akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. 27 Baada ya Yuda kuchukua kipande hicho cha mkate, Shetani akamwingia.+ Kwa hiyo, Yesu akamwambia: “Kile unachofanya, kifanye upesi zaidi.” 28 Lakini hakuna hata mmoja kati ya wale waliokuwa wameketi mezani aliyejua kwa nini alimwambia hivyo. 29 Kwa kuwa Yuda alikuwa akitunza sanduku la pesa,+ baadhi yao walifikiri Yesu alikuwa akimwambia, “Nunua vitu tunavyohitaji kwa ajili ya sherehe,” au kwamba anapaswa kuwapa maskini kitu fulani. 30 Kwa hiyo, baada ya kupokea kipande cha mkate, mara moja akatoka nje. Ilikuwa usiku.+
31 Kwa hiyo alipoondoka, Yesu akasema: “Sasa Mwana wa binadamu ametukuzwa,+ na Mungu ametukuzwa kuhusiana naye. 32 Mungu mwenyewe atamtukuza,+ naye atamtukuza mara moja. 33 Watoto wadogo, nipo pamoja nanyi muda kidogo zaidi. Mtanitafuta; na kama nilivyowaambia Wayahudi, ninawaambia ninyi pia, ‘Ninakoenda hamwezi kuja.’+ 34 Ninawapa ninyi amri mpya, kwamba mpendane; kama vile ambavyo nimewapenda,+ nanyi mpendane vivyo hivyo.+ 35 Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu—mkiwa na upendo miongoni mwenu.”+
36 Simoni Petro akamuuliza: “Bwana, unaenda wapi?” Yesu akajibu: “Ninakoenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”+ 37 Petro akamwambia: “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Nitatoa uhai wangu* kwa ajili yako.”+ 38 Yesu akajibu: “Je, utatoa uhai wako* kwa ajili yangu? Kwa kweli ninakuambia, kabla ya jogoo kuwika utanikana mara tatu.”+
14 “Mioyo yenu isitaabike.+ Iweni na imani* katika Mungu;+ iweni na imani pia katika mimi. 2 Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi. Kama sivyo, ningewaambia kwa maana ninaenda zangu kuwatayarishia mahali.+ 3 Pia, nikienda na kuwatayarishia mahali, nitakuja tena nami nitawapokea nyumbani kwangu, ili mahali nilipo, ninyi pia muwe hapo.+ 4 Nanyi mnajua njia ya mahali ninakoenda.”
5 Tomasi+ akamwambia: “Bwana, sisi hatujui unakoenda. Tunawezaje kuijua njia?”
6 Yesu akamwambia: “Mimi ndiye njia+ na kweli+ na uzima.+ Hakuna mtu anayekuja kwa Baba bila kupitia kwangu.+ 7 Kama ninyi mngenijua, mngemjua Baba yangu pia; tangu sasa na kuendelea ninyi mnamjua na mmemwona.”+
8 Filipo akamwambia: “Bwana, tuonyeshe Baba na hilo linatutosha.”
9 Yesu akamwambia: “Je, hata baada ya kuwa pamoja nanyi kwa muda mrefu hivyo, bado Filipo hujanijua? Yeyote ambaye ameniona mimi amemwona Baba pia.+ Kwa nini unasema, ‘Tuonyeshe Baba’? 10 Je, huamini kwamba mimi nimo katika muungano pamoja na Baba, naye Baba yumo katika muungano pamoja nami?+ Mambo ninayowaambia sisemi kwa kujitungia,+ bali Baba ambaye hukaa katika muungano pamoja nami anafanya kazi zake. 11 Iweni na imani kwamba nimo katika muungano pamoja na Baba na Baba yumo katika muungano pamoja nami; kama sivyo, iweni na imani kwa sababu ya kazi zenyewe.+ 12 Kwa kweli ninawaambia, yeyote anayeniamini atafanya pia kazi ambazo mimi hufanya; naye atafanya kazi kubwa kuliko hizi,+ kwa sababu ninaenda zangu kwa Baba.+ 13 Pia, lolote mtakaloomba katika jina langu nitalifanya, ili Baba atukuzwe kuhusiana na Mwana.+ 14 Mkiomba jambo lolote katika jina langu, nitalifanya.
15 “Ikiwa mnanipenda, mtazishika amri zangu.+ 16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa msaidizi* mwingine awe pamoja nanyi milele,+ 17 roho ya ile kweli,+ ambayo ulimwengu hauwezi kuipokea, kwa sababu hauioni wala kuijua.+ Ninyi mnaijua, kwa sababu hiyo hukaa pamoja nanyi na imo ndani yenu. 18 Sitawaacha ninyi mayatima. Ninakuja kwenu.+ 19 Bado muda kidogo nao ulimwengu hautaniona tena, lakini ninyi mtaniona,+ kwa sababu ninaishi, nanyi mtaishi. 20 Siku hiyo mtajua kwamba nimo katika muungano pamoja na Baba yangu nanyi mumo katika muungano pamoja nami, nami nimo katika muungano pamoja nanyi.+ 21 Yeyote aliye na amri zangu na kuzishika, huyo ndiye anayenipenda. Na yeyote anayenipenda atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujionyesha waziwazi kwake.”
22 Yuda,+ sio Yuda Iskariote, akamuuliza: “Bwana, imekuwaje kwamba unakusudia kujionyesha waziwazi kwetu bali si kwa ulimwengu?”
23 Yesu akamjibu: “Ikiwa yeyote ananipenda, atalishika neno langu,+ naye Baba yangu atampenda, nasi tutakuja kwake na kukaa pamoja naye.+ 24 Yeyote asiyenipenda hayashiki maneno yangu. Neno mnalolisikia si langu, bali ni la Baba aliyenituma.+
25 “Nimewaambia mambo haya nikiwa bado pamoja nanyi. 26 Lakini msaidizi, roho takatifu, ambayo Baba ataituma katika jina langu, hiyo itawafundisha mambo yote na kuwakumbusha mambo yote niliyowaambia.+ 27 Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu.+ Siwapi amani kwa njia ile ambayo ulimwengu huitoa. Mioyo yenu isitaabike wala kuogopa. 28 Mlisikia nikiwaambia, ‘Ninaenda, nami nitakuja tena kwenu.’ Kama mngenipenda, mngeshangilia kwamba ninaenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.+ 29 Kwa hiyo sasa nimewaambia kabla jambo hilo halijatokea, ili litakapotokea mwamini.+ 30 Sitasema nanyi tena mambo mengi, kwa maana mtawala wa ulimwengu+ anakuja, naye hana uwezo juu yangu.*+ 31 Lakini, ili ulimwengu ujue kwamba ninampenda Baba, ninafanya kama vile Baba alivyoniamuru.+ Simameni tuondoke hapa.
15 “Mimi ndiye mzabibu wa kweli, naye Baba yangu ndiye mkulima. 2 Yeye huliondoa kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda, naye hulisafisha kila tawi linalozaa matunda, ili lizae matunda zaidi.+ 3 Tayari ninyi ni safi kwa sababu ya neno ambalo nimewaambia.+ 4 Kaeni katika muungano pamoja nami, nami nitakaa katika muungano pamoja nanyi. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda likiwa peke yake lisipobaki katika mzabibu, vivyo hivyo hamwezi kuzaa matunda msipokaa katika muungano pamoja nami.+ 5 Mimi ndiye mzabibu; nanyi ndio matawi. Yeyote anayekaa katika muungano pamoja nami, nami katika muungano pamoja naye, huyo huzaa matunda mengi;+ kwa maana bila mimi hamwezi kufanya lolote kamwe. 6 Ikiwa yeyote hakai katika muungano pamoja nami, atatupwa kama tawi kisha atakauka. Nao watu hukusanya matawi hayo na kuyatupa ndani ya moto, nayo huteketea. 7 Mkikaa katika muungano pamoja nami, na maneno yangu yakae ndani yenu, ombeni chochote mnachotaka nanyi mtapewa.+ 8 Baba yangu hutukuzwa kwa jambo hili, kwamba mwendelee kuzaa matunda mengi na kujithibitisha kuwa wanafunzi wangu.+ 9 Kama vile Baba alivyonipenda,+ ndivyo nimewapenda ninyi; kaeni katika upendo wangu. 10 Mkishika amri zangu, mtakaa katika upendo wangu, kama vile ambavyo nimeshika amri za Baba na kukaa katika upendo wake.
11 “Nimewaambia mambo haya, ili shangwe yangu iwe ndani yenu na shangwe yenu ijae.+ 12 Hii ndiyo amri yangu, kwamba mpendane kama vile nilivyowapenda.+ 13 Hakuna mtu aliye na upendo mkuu kuliko huu, kwamba mtu atoe uhai wake* kwa ajili ya rafiki zake.+ 14 Ninyi ni rafiki zangu ikiwa mnafanya mambo ninayowaamuru.+ 15 Siwaiti ninyi tena watumwa, kwa sababu mtumwa hajui mambo ambayo bwana wake hufanya. Lakini nimewaita rafiki, kwa sababu nimewajulisha mambo yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu. 16 Ninyi hamkunichagua, bali mimi niliwachagua na kuwaweka rasmi mwende na kuendelea kuzaa matunda na kwamba matunda yenu yadumu, ili hata mkimwomba Baba jambo lolote katika jina langu, awape.+
17 “Mambo haya ninawaamuru, kwamba mpendane.+ 18 Ikiwa ulimwengu unawachukia, kumbukeni kwamba umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.+ 19 Kama mngekuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungependa kilicho chake. Sasa kwa sababu ninyi si sehemu ya ulimwengu,+ bali nimewachagua kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukia.+ 20 Kumbukeni neno nililowaambia: Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia;+ ikiwa wamelishika neno langu, watalishika lenu pia. 21 Lakini watawatendea mambo yote haya kwa ajili ya jina langu, kwa sababu hawamjui Yule aliyenituma.+ 22 Kama singekuja na kuzungumza nao, hawangekuwa na dhambi.+ Lakini sasa hawana kisingizio kwa ajili ya dhambi yao.+ 23 Anayenichukia mimi anamchukia Baba+ yangu pia. 24 Kama singefanya kati yao kazi ambazo hakuna mwingine aliyezifanya, hawangekuwa na dhambi;+ lakini sasa wameniona, nao wamenichukia mimi na pia Baba yangu. 25 Lakini hilo lilifanyika ili kutimiza neno lililoandikwa katika Sheria yao: ‘Walinichukia bila sababu.’+ 26 Atakapokuja msaidizi ambaye nitawatumia kutoka kwa Baba, roho ya ile kweli,+ inayotoka kwa Baba, huyo atatoa ushahidi kunihusu;+ 27 nanyi, mtatoa ushahidi,+ kwa sababu mmekuwa pamoja nami tangu mwanzoni.
16 “Nimewaambia mambo haya ili msikwazike. 2 Watu watawafukuza katika masinagogi.+ Kwa kweli, saa inakuja ambayo kila mtu atakayewaua+ atafikiri kwamba amemtolea Mungu utumishi mtakatifu. 3 Lakini watafanya mambo haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.+ 4 Hata hivyo, nimewaambia mambo haya ili saa yake itakapofika, mkumbuke kwamba niliwaambia.+
“Sikuwaambia mambo haya mwanzoni, kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi. 5 Lakini sasa ninaenda kwa Yule aliyenituma;+ na bado hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza, ‘Unaenda wapi?’ 6 Lakini kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejaa huzuni.+ 7 Hata hivyo, ninawaambia ukweli, ninaenda zangu kwa faida yenu. Kwa maana nisipoenda, msaidizi+ hatakuja kwenu; lakini nikienda, nitamtuma kwenu. 8 Naye atakapokuja atauthibitishia waziwazi ulimwengu kuhusu dhambi na kuhusu uadilifu na kuhusu hukumu: 9 kwanza kuhusu dhambi,+ kwa sababu hawaniamini;*+ 10 kisha kuhusu uadilifu, kwa sababu ninaenda kwa Baba nanyi hamtaniona tena; 11 pia kuhusu hukumu, kwa sababu mtawala wa ulimwengu huu amehukumiwa.+
12 “Bado nina mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili kwa sasa. 13 Hata hivyo, huyo* atakapokuja, roho ya ile kweli,+ atawaongoza ninyi kwenye kweli yote, kwa maana hatasema kwa uamuzi wake mwenyewe, bali atasema mambo anayosikia, naye atawatangazia mambo yanayokuja.+ 14 Huyo atanitukuza,+ kwa sababu atawatangazia mambo aliyopokea kutoka kwangu.+ 15 Vitu vyote alivyo navyo Baba ni vyangu.+ Ndiyo sababu nilisema huyo atawatangazia mambo aliyopokea kutoka kwangu. 16 Baada ya muda kidogo hamtaniona tena,+ na baada ya muda kidogo mtaniona.”
17 Ndipo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana: “Anamaanisha nini anapotuambia, ‘Baada ya muda kidogo hamtaniona, na tena, baada ya muda kidogo mtaniona,’ na, ‘kwa sababu ninaenda kwa Baba’?” 18 Basi walikuwa wakisema: “Anamaanisha nini anaposema, ‘muda kidogo’? Hatuelewi anachozungumzia.” 19 Yesu alijua kwamba walitaka kumuuliza, basi akawaambia: “Je, mnaulizana hivyo kwa sababu nilisema: ‘Baada ya muda kidogo hamtaniona, na tena, baada ya muda kidogo mtaniona’? 20 Kwa kweli ninawaambia, mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utashangilia; mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa shangwe.+ 21 Mwanamke anapokuwa akizaa anahisi huzuni kwa sababu saa yake imefika, lakini baada ya kumzaa mtoto hakumbuki tena dhiki hiyo kwa sababu anashangilia kwamba mtu amezaliwa ulimwenguni. 22 Basi, ninyi pia mnahuzunika sasa; lakini nitawaona tena na mioyo yenu itashangilia+ na hakuna mtu atakayeondoa shangwe yenu. 23 Siku hiyo hamtaniuliza swali lolote. Kwa kweli ninawaambia, mkimwomba Baba jambo lolote,+ atawapa katika jina langu.+ 24 Kufikia sasa hamjaomba hata jambo moja katika jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili shangwe yenu iwe kamili.
25 “Nimewaambia mambo haya kwa mifano. Saa inakuja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mifano, bali nitawaeleza waziwazi kumhusu Baba. 26 Siku hiyo mtamwomba Baba katika jina langu; ninaposema hivyo, simaanishi kwamba nitawaombea ninyi. 27 Kwa maana Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mmenipenda+ na mmeamini kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wa Mungu.+ 28 Nilikuja nikiwa mwakilishi wa Baba, nami nimekuja ulimwenguni. Sasa ninaondoka ulimwenguni, nami ninarudi kwa Baba.”+
29 Wanafunzi wake wakamwambia: “Ona! Sasa unazungumza waziwazi, nawe hutumii mifano. 30 Sasa tunafahamu kwamba unajua mambo yote na huhitaji kuulizwa swali na mtu yeyote. Kwa hiyo, tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.” 31 Yesu akawajibu: “Je, sasa mnaamini? 32 Tazama! Saa inakuja, na kwa kweli imefika, wakati kila mmoja wenu atatawanyika na kwenda nyumbani kwake, nanyi mtaniacha peke yangu.+ Lakini siko peke yangu, kwa sababu Baba yuko pamoja nami.+ 33 Nimewaambia mambo haya ili kupitia kwangu muwe na amani.+ Ulimwenguni mtapata dhiki, lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu.”+
17 Yesu akasema mambo hayo, kisha akatazama mbinguni na kusema: “Baba, saa imefika. Mtukuze mwana wako ili mwana wako akutukuze,+ 2 kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili,*+ ili awape uzima wa milele+ wote ambao umempa.+ 3 Uzima wa milele ndio huu,+ wakujue wewe,* Mungu wa pekee wa kweli,+ na yule uliyemtuma, Yesu Kristo.+ 4 Nimekutukuza duniani,+ kwa kuwa nimemaliza kazi uliyonipa nifanye.+ 5 Sasa Baba, nitukuze kando yako kwa utukufu niliokuwa nao kando yako kabla ya ulimwengu kuwako.+
6 “Nimelifunua* jina lako kwa watu ulionipa kutoka ulimwenguni.+ Walikuwa wako, nawe ukanipa, nao wamelishika* neno lako. 7 Sasa wamejua kwamba vitu vyote ulivyonipa vimetoka kwako; 8 kwa sababu nimewapa maneno uliyonipa,+ nao wameyakubali na kwa hakika wamejua kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wako,+ nao wameamini kwamba ulinituma.+ 9 Ninaomba kwa ajili yao; siombi kwa ajili ya ulimwengu, bali ninawaombea wale ulionipa, kwa sababu ni wako; 10 na vitu vyangu vyote ni vyako na vyako ni vyangu,+ nami nimetukuzwa kati yao.
11 “Mimi simo tena ulimwenguni, bali wao wamo ulimwenguni,+ nami ninakuja kwako. Baba Mtakatifu, walinde+ kwa sababu ya jina lako ambalo umenipa, ili wawe kitu kimoja* kama vile sisi tulivyo kitu kimoja.*+ 12 Nilipokuwa pamoja nao nilikuwa nikiwatunza+ kwa sababu ya jina lako ambalo umenipa; nami nimewalinda na hakuna hata mmoja wao aliyeangamizwa+ ila yule mwana wa maangamizi,+ ili andiko litimizwe.+ 13 Lakini sasa ninakuja kwako, nami ninasema mambo haya ulimwenguni ili wapate kikamili shangwe niliyo nayo.+ 14 Nimewapa neno lako, lakini ulimwengu umewachukia, kwa sababu wao si sehemu ya ulimwengu,+ kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.
15 “Sikuombi uwatoe ulimwenguni, bali uwalinde kwa sababu ya yule mwovu.+ 16 Wao si sehemu ya ulimwengu,+ kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.+ 17 Watakase* kupitia ile kweli;+ neno lako ni kweli.+ 18 Kama ulivyonituma ulimwenguni, mimi pia nimewatuma ulimwenguni.+ 19 Nami ninajitakasa kwa ajili yao, ili wao pia watakaswe kupitia ile kweli.
20 “Ninaomba si kwa ajili ya hawa tu, bali pia wale wanaoniamini kupitia neno lao, 21 ili wote wawe kitu kimoja,+ kama vile ambavyo wewe Baba umo katika muungano nami, nami nimo katika muungano nawe,+ ili wao pia wawe katika muungano nasi, ili ulimwengu uamini kwamba ulinituma. 22 Nimewapa utukufu ambao umenipa, ili wawe kitu kimoja kama vile sisi tulivyo kitu kimoja.+ 23 Mimi katika muungano nao nawe katika muungano nami, ili wakamilishwe wawe kitu kimoja,* ili ulimwengu ujue kwamba ulinituma na uliwapenda wao kama vile ulivyonipenda. 24 Baba, ninataka wale ambao umenipa wawe pamoja nami mahali nilipo,+ ili waone utukufu wangu ambao umenipa, kwa sababu ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu.+ 25 Baba Mwadilifu, kwa kweli, ulimwengu haujakujua wewe,+ lakini mimi ninakujua,+ na hawa wamejua kwamba ulinituma. 26 Nimewajulisha jina lako nami nitalijulisha,+ ili upendo ulionipenda uwe ndani yao nami katika muungano pamoja nao.”+
18 Baada ya kusema mambo hayo, Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake, wakavuka Bonde la Kidroni*+ na kufika kwenye bustani, naye akaingia humo pamoja nao.+ 2 Sasa Yuda msaliti wake alijua mahali hapo, kwa sababu mara nyingi Yesu alikutana hapo na wanafunzi wake. 3 Basi Yuda akaja na kikosi cha wanajeshi, maofisa wa wakuu wa makuhani na wa Mafarisayo, wakafika hapo wakiwa na mienge, taa, na silaha.+ 4 Kisha Yesu akijua mambo yote ambayo yangempata, akawakaribia na kuwauliza: “Mnamtafuta nani?” 5 Wakamjibu: “Yesu Mnazareti.”+ Akawaambia: “Ni mimi.” Basi Yuda msaliti wake, alikuwa pia amesimama pamoja nao.+
6 Hata hivyo, Yesu alipowaambia, “Ni mimi,” wakarudi nyuma na kuanguka chini.+ 7 Basi akawauliza tena: “Mnamtafuta nani?” Wakasema: “Yesu Mnazareti.” 8 Yesu akajibu: “Niliwaambia ni mimi. Basi, ikiwa mnanitafuta mimi, waacheni wanaume hawa waende.” 9 Hilo lilitimiza maneno aliyokuwa amesema: “Kati ya wale ulionipa, sikumpoteza hata mmoja.”+
10 Simoni Petro alikuwa na upanga, basi akauchomoa na kumpiga mtumwa wa kuhani mkuu na kumkata sikio la kulia.+ Jina la mtumwa huyo lilikuwa Malko. 11 Hata hivyo, Yesu akamwambia Petro: “Rudisha upanga ndani ya ala yake.+ Je, sipaswi kukinywa kikombe ambacho Baba amenipa?”+
12 Ndipo wanajeshi na kamanda wa jeshi na maofisa wa Wayahudi wakamkamata Yesu na kumfunga. 13 Kwanza wakampeleka kwa Anasi, kwa maana alikuwa baba mkwe wa Kayafa,+ ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo.+ 14 Kwa kweli, Kayafa ndiye aliyewashauri Wayahudi kwamba ilikuwa kwa faida yao mtu mmoja afe kwa ajili ya watu.+
15 Sasa Simoni Petro na mwanafunzi mwingine wakamfuata Yesu.+ Mwanafunzi huyo alijulikana na kuhani mkuu, naye akaingia pamoja na Yesu ndani ya ua wa kuhani mkuu, 16 lakini Petro alikuwa amesimama nje kwenye mlango.* Basi yule mwanafunzi mwingine, aliyejulikana na kuhani mkuu, akatoka nje na kuzungumza na mlinzi wa mlango, akamwingiza Petro ndani. 17 Basi kijakazi, aliyekuwa mlinzi wa mlango, akamuuliza Petro: “Wewe pia ni mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu, sivyo?” Petro akajibu: “Hapana.”+ 18 Sasa wale watumwa na maofisa walikuwa wamesimama kuzunguka moto wa makaa waliokuwa wameuwasha, kwa sababu kulikuwa na baridi nao walikuwa wakiota moto. Petro pia alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.
19 Basi mkuu wa makuhani akamuuliza Yesu kuhusu wanafunzi wake na kuhusu mafundisho yake. 20 Yesu akamjibu: “Nimezungumza na ulimwengu hadharani. Sikuzote nilifundisha katika sinagogi na hekaluni,+ ambapo Wayahudi wote hukusanyika, nami sikusema jambo lolote kwa siri. 21 Kwa nini unaniuliza? Waulize wale waliosikia nilichowaambia. Ona! Hawa wanajua nilichosema.” 22 Baada ya kusema hivyo, mmoja wa maofisa aliyekuwa amesimama hapo karibu akampiga Yesu kofi usoni+ na kusema: “Je, hivyo ndivyo unavyomjibu mkuu wa makuhani?” 23 Yesu akamjibu: “Ikiwa nimesema vibaya, toa ushahidi kuhusu kosa hilo; lakini ikiwa nimesema jambo lililo sawa, kwa nini unanipiga?” 24 Kisha Anasi akaagiza Yesu apelekwe kwa kuhani mkuu Kayafa,+ akiwa amefungwa.
25 Sasa Simoni Petro alikuwa amesimama hapo akiota moto. Ndipo wakamwambia: “Wewe pia ni mmoja wa wanafunzi wake, sivyo?” Akakana na kusema: “Hapana.”+ 26 Mmoja wa watumwa wa kuhani mkuu, aliyekuwa mtu wa ukoo wa yule aliyekatwa sikio+ na Petro, akasema: “Nilikuona katika bustani pamoja naye, sivyo?” 27 Hata hivyo, Petro akakana tena, na papo hapo jogoo akawika.+
28 Kisha wakamtoa Yesu kwa Kayafa na kumpeleka kwenye makao ya gavana.+ Ilikuwa asubuhi mapema. Lakini wao hawakuingia ndani ya makao ya gavana, ili wasitiwe unajisi+ kwa sababu walitaka kula mlo wa Pasaka. 29 Basi Pilato akatoka nje na kuwauliza: “Mna mashtaka gani kumhusu mtu huyu?” 30 Wakamjibu: “Kama mtu huyu hangekuwa mkosaji,* hatungemkabidhi kwako.” 31 Basi Pilato akawaambia: “Mchukueni mkamhukumu kulingana na sheria yenu.”+ Wayahudi wakamwambia: “Si halali kwetu kumuua mtu yeyote.”+ 32 Hilo lilitimiza maneno aliyosema Yesu ili kuonyesha angekufa kifo cha aina gani.+
33 Basi Pilato akaingia tena ndani ya makao ya gavana, akamwita Yesu na kumuuliza: “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?”+ 34 Yesu akajibu: “Je, unauliza hivyo kwa kujitungia, au uliambiwa na watu wengine kunihusu?” 35 Pilato akajibu: “Mimi si Myahudi, sivyo? Taifa lako na wakuu wa makuhani wamekukabidhi kwangu. Ulifanya nini?” 36 Yesu akajibu:+ “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.+ Kama Ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania ili nisitiwe mikononi mwa Wayahudi.+ Lakini, kama ilivyo, Ufalme wangu hautoki katika chanzo hiki.” 37 Basi Pilato akamuuliza: “Kwa hiyo, wewe ni mfalme?” Yesu akajibu: “Wewe mwenyewe unasema kwamba mimi ni mfalme.+ Nimezaliwa kwa ajili ya hili, na kwa ajili ya hili nimekuja ulimwenguni, ili nitoe ushahidi kuhusu kweli.+ Kila mtu aliye upande wa kweli huisikiliza sauti yangu.” 38 Pilato akamuuliza: “Kweli ni nini?”
Baada ya kusema hivyo, akatoka nje tena na kuwaambia Wayahudi: “Sijampata na kosa lolote.+ 39 Isitoshe, mna desturi kwamba niwafungulie mtu siku ya Pasaka.+ Basi, mnataka niwafungulie Mfalme wa Wayahudi?” 40 Wakasema tena kwa sauti kubwa: “Si mtu huyu, bali Baraba!” Baraba alikuwa mwizi.+
19 Kisha Pilato akamchukua Yesu, akampiga mijeledi.+ 2 Nao wanajeshi wakasokota taji la miiba kisha wakamvisha kichwani, pia wakamvisha joho la zambarau,+ 3 nao walikuwa wakija na kumwambia: “Salamu,* ewe Mfalme wa Wayahudi!” Pia walikuwa wakimpiga makofi usoni.+ 4 Pilato akatoka nje tena na kuwaambia: “Ona! Namtoa nje kwenu ili mjue kwamba sijampata na kosa lolote.”+ 5 Basi Yesu akatoka nje, akiwa amevaa taji la miiba na joho la zambarau. Naye Pilato akawaambia: “Tazama! Mwanamume!” 6 Hata hivyo, wakuu wa makuhani na maofisa walipomwona, wakasema kwa sauti kubwa: “Atundikwe mtini! Atundikwe mtini!”*+ Pilato akawaambia: “Mchukueni mkamuue* ninyi wenyewe, kwa maana mimi sijampata na kosa lolote.”+ 7 Wayahudi wakamjibu: “Sisi tuna sheria, na kulingana na sheria anapaswa kufa,+ kwa sababu alijifanya kuwa mwana wa Mungu.”+
8 Pilato aliposikia maneno yao, akaogopa hata zaidi, 9 akaingia tena ndani ya makao ya gavana akamuuliza Yesu: “Umetoka wapi?” Lakini Yesu hakumjibu.+ 10 Basi Pilato akamuuliza: “Unakataa kuzungumza nami? Je, hujui kwamba nina mamlaka ya kukufungua na mamlaka ya kukuua?”* 11 Yesu akamjibu: “Wewe hungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu kama hungepewa kutoka juu. Ndiyo maana mtu aliyenitia mikononi mwako ana dhambi kubwa zaidi.”
12 Kwa sababu hiyo, Pilato akaendelea kutafuta njia ya kumfungua, lakini Wayahudi wakasema kwa sauti kubwa: “Ukimfungua mtu huyu, wewe si rafiki ya Kaisari. Kila mtu anayejifanya mfalme anasema vibaya kumhusu* Kaisari.”+ 13 Baada ya kusikia maneno hayo, Pilato akamtoa Yesu nje, naye akaketi kwenye kiti cha hukumu mahali panapoitwa Sakafu ya Jiwe, au katika Kiebrania, Gabatha. 14 Sasa ilikuwa siku ya Matayarisho+ ya Pasaka; karibu saa sita.* Naye akawaambia Wayahudi: “Oneni! Mfalme wenu!” 15 Hata hivyo, wakasema kwa sauti kubwa: “Mwondoe! Mwondoe! Atundikwe mtini!”* Pilato akawaambia: “Je, mnataka nimuue mfalme wenu?” Wakuu wa makuhani wakajibu: “Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.” 16 Kisha akamkabidhi kwao ili auawe kwenye mti.+
Basi wakamchukua Yesu. 17 Yesu akabeba mti wake wa mateso,* akaenda mahali panapoitwa Fuvu la Kichwa,+ au Golgotha katika Kiebrania.+ 18 Hapo wakamtundika mtini,+ na watu wawili kando yake, mmoja kulia na mwingine kushoto, naye Yesu katikati yao.+ 19 Pilato akaandika pia tangazo na kuliweka juu ya huo mti wa mateso.* Liliandikwa: “Yesu Mnazareti Mfalme wa Wayahudi.”+ 20 Wayahudi wengi walilisoma tangazo hilo, kwa sababu mahali ambapo Yesu alitundikwa mtini palikuwa karibu na jiji, nalo liliandikwa katika Kiebrania, Kilatini, na Kigiriki. 21 Hata hivyo, wakuu wa makuhani wa Wayahudi wakamwambia Pilato: “Usiandike, ‘Mfalme wa Wayahudi,’ andika kwamba alisema, ‘Mimi ni Mfalme wa Wayahudi.’ ” 22 Pilato akajibu: “Yale ambayo nimeandika, nimeandika.”
23 Baada ya wanajeshi kumtundika Yesu kwenye mti, wakachukua mavazi yake ya nje na kuyagawanya vipande vinne, kila askari kipande kimoja, na pia wakachukua vazi la ndani. Lakini vazi la ndani halikuwa na mshono, lilikuwa limefumwa kutoka juu mpaka chini. 24 Basi wakaambiana: “Tusilirarue, badala yake tupige kura ili tuamue litakuwa la nani.”+ Hilo lilitimiza andiko linalosema: “Waligawana mavazi yangu, na wakalipigia kura vazi langu.”+ Kwa kweli, hivyo ndivyo walivyofanya wale wanajeshi.
25 Hata hivyo, kando ya mti wa mateso* wa Yesu, walikuwa wamesimama mama yake+ na dada ya mama yake; Maria mke wa Klopa na Maria Magdalene.+ 26 Basi, Yesu alipomwona mama yake na mwanafunzi ambaye alimpenda+ wamesimama karibu, akamwambia mama yake: “Mwanamke, ona! Mwanao!” 27 Kisha akamwambia mwanafunzi huyo: “Ona! Mama yako!” Na tangu saa hiyo mwanafunzi huyo akamchukua Maria na kumpeleka nyumbani kwake.
28 Baada ya hayo, Yesu alipojua kwamba kufikia sasa mambo yote yalikuwa yametimizwa, akasema: “Nina kiu,”+ na hivyo akatimiza andiko. 29 Hapo palikuwa na chombo kilichojaa divai kali. Basi wakaweka sifongo iliyojaa divai kali juu ya kijiti cha hisopo* na kukileta karibu na mdomo wake.+ 30 Baada ya kuipokea ile divai kali, Yesu akasema: “Imetimizwa!”+ akainamisha kichwa chake akakata pumzi.*+
31 Kwa kuwa ilikuwa siku ya Matayarisho,+ ili miili hiyo isibaki kwenye miti ya mateso+ siku ya Sabato, (kwa maana siku hiyo ya Sabato ilikuwa kuu),+ Wayahudi walimwomba Pilato aagize miguu yao ivunjwe na miili iondolewe. 32 Basi, wanajeshi wakaja na kuvunja miguu ya wale watu wawili waliokuwa wametundikwa mtini kando ya Yesu. 33 Lakini walipomfikia Yesu, waliona kwamba tayari amekufa, kwa hiyo hawakuivunja miguu yake. 34 Lakini mwanajeshi mmoja akauchoma ubavu wa Yesu kwa mkuki,+ na mara moja damu na maji vikatoka. 35 Na yule aliyeona hilo ametoa ushahidi huu, nao ushahidi wake ni wa kweli, na anajua kwamba anachosema ni kweli, ili ninyi pia mwamini.+ 36 Kwa kweli, mambo hayo yalitendeka ili kutimiza andiko linalosema: “Hakuna mfupa wake hata mmoja utakaovunjwa.”*+ 37 Pia, andiko lingine linasema: “Watamtazama yule waliyemchoma.”+
38 Baada ya mambo hayo Yosefu wa Arimathea, aliyekuwa mwanafunzi wa Yesu lakini kwa siri kwa sababu aliwaogopa Wayahudi,+ akamwomba ruhusa Pilato ili auondoe mwili wa Yesu, naye Pilato akamruhusu. Basi akaja na kuuondoa mwili huo.+ 39 Nikodemo,+ yule mtu aliyemjia usiku mara ya kwanza, akaja pia akiwa amebeba mchanganyiko* wa manemane na udi, wenye uzito wa karibu ratili* mia moja.+ 40 Basi wakauchukua mwili wa Yesu na kuufunga kwa vitambaa vya kitani pamoja na manukato,+ kulingana na desturi ya mazishi ya Wayahudi. 41 Ilitukia kwamba kulikuwa na bustani mahali alipouawa,* na katika bustani hiyo kulikuwa na kaburi*+ jipya ambamo hakuna mtu alikuwa amewahi kulazwa. 42 Kwa sababu ilikuwa siku ya Matayarisho+ ya Wayahudi na kaburi lilikuwa hapo karibu, wakamlaza Yesu humo.
20 Siku ya kwanza ya juma, Maria Magdalene alienda mapema kwenye kaburi,*+ kulipokuwa bado na giza, naye akaona jiwe limeondolewa kwenye kaburi.*+ 2 Basi akakimbia kwenda kwa Simoni Petro na yule mwanafunzi mwingine, ambaye Yesu alimpenda,+ naye akawaambia: “Wamemwondoa Bwana kaburini,+ nasi hatujui wamemlaza wapi.”
3 Ndipo Petro na yule mwanafunzi mwingine wakaelekea kaburini. 4 Wote wawili wakaanza kukimbia pamoja, lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia upesi kuliko Petro akatangulia kufika kwenye kaburi. 5 Akainama, akaona vitambaa vya kitani hapo chini,+ lakini hakuingia ndani. 6 Ndipo Simoni Petro akaja akimfuata, akaingia kaburini. Naye akaona vile vitambaa vya kitani hapo chini. 7 Kitambaa ambacho Yesu alikuwa amefungwa kichwani hakikuwa pamoja na vitambaa vingine bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa kando. 8 Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyetangulia kufika kwenye kaburi akaingia pia, naye akaona na kuamini. 9 Kwa maana bado hawakuwa wameelewa andiko linalosema kwamba lazima afufuliwe kutoka kwa wafu.+ 10 Basi wanafunzi hao wakarudi nyumbani kwao.
11 Hata hivyo, Maria akaendelea kusimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia, akainama kutazama ndani ya kaburi, 12 naye akaona malaika wawili+ waliovaa mavazi meupe wakiwa wameketi mahali ulipokuwa umelazwa mwili wa Yesu, mmoja kichwani na mwingine miguuni. 13 Nao wakamuuliza: “Mwanamke, kwa nini unalia?” Akawajibu: “Wamemwondoa Bwana wangu, nami sijui wamemlaza wapi.” 14 Baada ya kusema hayo, akageuka na kumwona Yesu akiwa amesimama hapo, lakini hakutambua kwamba ni Yesu.+ 15 Yesu akamuuliza: “Mwanamke, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Maria, akifikiri kwamba ni mtunza-bustani, akamwambia: “Bwana, ikiwa umemchukua, niambie umemlaza wapi, nami nitamwondoa.” 16 Yesu akamwita: “Maria!” Alipogeuka akasema kwa Kiebrania: “Raboni!” (maana yake “Mwalimu!”) 17 Yesu akamwambia: “Acha kuning’ang’ania, kwa maana bado sijapanda kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu,+ nawe uwaambie, ‘Ninapanda kwenda kwa Baba yangu+ na Baba yenu na kwa Mungu wangu+ na Mungu wenu.’” 18 Maria Magdalene akaenda na kuwaambia wanafunzi: “Nimemwona Bwana!” Kisha akawaambia alichoambiwa na Yesu.+
19 Ilipofika jioni siku hiyo, siku ya kwanza ya juma, milango ikiwa imefungwa mahali ambapo wanafunzi walikuwa kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi, Yesu akaja na kusimama katikati yao na kuwaambia: “Na muwe na amani.”+ 20 Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake.+ Basi wanafunzi wakashangilia walipomwona Bwana.+ 21 Yesu akawaambia tena: “Na muwe na amani.+ Kama vile ambavyo Baba amenituma,+ mimi pia ninawatuma ninyi.”+ 22 Baada ya kusema hivyo akapuliza juu yao na kuwaambia: “Pokeeni roho takatifu.+ 23 Mkimsamehe mtu yeyote dhambi zake, atasamehewa; msipomsamehe mtu yeyote dhambi zake, hatasamehewa.”
24 Lakini Tomasi,+ mmoja wa wale 12, aliyeitwa Pacha, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja. 25 Basi wale wanafunzi wengine walikuwa wakimwambia: “Tumemwona Bwana!” Lakini akawaambia: “Nisipoona alama za misumari kwenye mikono yake na kutia kidole changu katika alama hizo kisha niutie mkono wangu ubavuni mwake,+ sitaamini kamwe.”
26 Basi, siku nane baadaye wanafunzi wake walikuwa tena ndani ya nyumba, na Tomasi alikuwa pamoja nao. Yesu akaja, ingawa milango ilikuwa imefungwa, naye akasimama katikati yao na kusema: “Na muwe na amani.”+ 27 Kisha akamwambia Tomasi: “Weka kidole chako hapa, uone mikono yangu, na ulete mkono wako uguse ubavu wangu, ili uache kuwa na shaka* bali uamini.” 28 Tomasi akamjibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!” 29 Yesu akamwambia: “Je, umeamini kwa sababu umeniona? Wenye furaha ni wale ambao wanaamini ingawa bado hawajaona.”
30 Kwa kweli, Yesu alifanya pia miujiza mingine mingi mbele ya wanafunzi, ambayo haijaandikwa katika kitabu hiki cha kukunjwa.+ 31 Lakini mambo haya yameandikwa ili mwamini kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa sababu ya kuamini, mpate uzima kupitia jina lake.+
21 Baada ya mambo hayo, Yesu alijifunua* tena kwa wanafunzi kwenye Bahari ya Tiberia. Alijifunua katika njia hii. 2 Simoni Petro, Tomasi (aliyeitwa Pacha),+ Nathanaeli+ kutoka Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo,+ na wanafunzi wake wengine wawili, walikuwa pamoja. 3 Simoni Petro akawaambia: “Ninaenda kuvua samaki.” Wakamwambia: “Sisi pia tutaenda nawe.” Basi wakaenda, wakapanda mashua, lakini usiku huo hawakuvua chochote.+
4 Hata hivyo, kulipoanza kupambazuka, Yesu alisimama kando ya bahari, lakini wanafunzi hawakutambua ni Yesu.+ 5 Basi Yesu akawauliza: “Watoto, mna chakula chochote?”* Wakamjibu: “Hapana!” 6 Akawaambia: “Utupeni wavu upande wa kulia wa mashua, nanyi mtapata.” Basi wakautupa, lakini wakashindwa kuuvuta kwa sababu samaki walikuwa wengi sana.+ 7 Ndipo mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda+ akamwambia Petro: “Ni Bwana!” Simoni Petro, aliposikia kwamba ni Bwana, akavaa* vazi lake la nje kwa maana alikuwa uchi,* akajitumbukiza baharini. 8 Lakini wale wanafunzi wengine wakaja katika ile mashua ndogo, wakiukokota wavu wenye samaki wengi kwa maana hawakuwa mbali na nchi kavu, walikuwa umbali wa mita 90* hivi.
9 Walipofika ufuoni wakaona moto wa makaa na juu yake palikuwa na samaki na mkate. 10 Yesu akawaambia: “Leteni baadhi ya samaki mliowavua sasa hivi.” 11 Basi Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuuvuta hadi ufuoni wavu uliojaa samaki wakubwa 153. Ingawa walikuwa wengi sana wavu haukupasuka. 12 Yesu akawaambia: “Njooni mpate kiamshakinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyekuwa na ujasiri wa kumuuliza: “Wewe ni nani?” kwa sababu walijua ni Bwana. 13 Yesu akaja, akachukua mkate na kuwapa, na samaki vilevile. 14 Sasa hiyo ilikuwa mara ya tatu+ Yesu kuwatokea wanafunzi baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu.
15 Baada ya kupata kiamshakinywa, Yesu akamuuliza Simoni Petro: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda kuliko hawa?” Petro akamjibu: “Ndiyo, Bwana, unajua ninakupenda.” Yesu akamwambia: “Lisha wanakondoo wangu.”+ 16 Akamuuliza mara ya pili: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda?” Petro akamjibu: “Ndiyo, Bwana, unajua ninakupenda.” Yesu akamwambia: “Chunga kondoo wangu wadogo.”+ 17 Akamuuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda?” Petro akahuzunika kwamba alimuuliza mara ya tatu: “Je, unanipenda?” Kwa hiyo akamjibu: “Bwana, wewe unajua mambo yote; unajua kwamba ninakupenda.” Yesu akamwambia: “Lisha kondoo wangu wadogo.+ 18 Kwa kweli ninakuambia, ulipokuwa kijana, ulikuwa unavaa mwenyewe na kutembea kokote ulikotaka. Lakini utakapozeeka, utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvalisha na kukupeleka usikotaka.” 19 Alisema hivyo ili kuonyesha angemtukuza Mungu kwa kifo cha namna gani. Baada ya kusema hayo, akamwambia: “Endelea kunifuata.”+
20 Petro alipogeuka, akamwona mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda+ akiwafuata, yule ambaye kwenye mlo wa jioni alikuwa ameegemea nyuma kifuani pa Yesu, akamuuliza: “Bwana, ni nani anayekusaliti?” 21 Basi alipomwona, Petro akamuuliza Yesu: “Bwana, namna gani kuhusu mtu huyu?” 22 Yesu akamwambia: “Ikiwa ni mapenzi yangu akae mpaka nije, hilo linakuhusuje? Wewe endelea kunifuata.” 23 Basi habari ikaenea miongoni mwa akina ndugu kwamba mwanafunzi huyo hatakufa. Hata hivyo, Yesu hakumwambia kwamba hatakufa, bali alisema: “Ikiwa ni mapenzi yangu akae mpaka nije, hilo linakuhusuje?”
24 Huyo ndiye mwanafunzi+ anayetoa ushahidi huu kuhusu mambo haya, na ambaye aliyaandika mambo haya, nasi tunajua kwamba ushahidi wake ni wa kweli.
25 Kwa kweli, pia kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa kirefu, nadhani ulimwengu haungekuwa na nafasi ya kuviweka vitabu vya kukunjwa ambavyo vingeandikwa.+
Au “alikuwa wa kimungu.”
Au “walionyesha imani.”
Au “alijaa fadhili zisizostahiliwa.”
Au “kifuani pa Baba.” Inamaanisha mahali pa heshima ya pekee au pendeleo.”
Angalia Nyongeza A5.
Yaani, karibu saa 10 jioni.
Tnn., “Nina nini nawe, mwanamke?” Hii ni nahau au msemo unaoonyesha kukataa jambo. Matumizi ya neno “mwanamke” hayaonyeshi ukosefu wa heshima.
Yaelekea kipimo hicho kilikuwa bathi iliyokuwa sawa na lita 22. Angalia Nyongeza B14.
Au “soko.”
Au labda, “asipozaliwa kutoka juu.”
Au “anayeonyesha kwamba anamwamini.”
Au “anayeonyesha imani.”
Au “haonyeshi imani.”
Au “yasifunuliwe.”
Au “amethibitisha.”
Au “hatoi roho kwa kipimo.”
Au “chemchemi hiyo; au mabubujiko hayo.”
Yaani, karibu saa 6 mchana.
Au “alikuwa anapata nafuu.”
Yaani, karibu saa 7 mchana.
Angalia Nyongeza A3.
Au “kitanda chako.”
Au “kitanda chake.”
Au “kitanda.”
Au “kitanda.”
Au “alivyo na zawadi ya uhai ndani yake mwenyewe.”
Yaani, Maandiko.
Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “karibu stadia 25 au 30.” Angalia Nyongeza B14.
Au “mwonyeshe imani katika.”
Angalia Nyongeza A5.
Au “kusanyiko la watu wote.”
Au “ibilisi.”
Au “kutembea.”
Au “wakionyesha kwamba wanamwamini.”
Tnn., “maandishi.”
Yaani, shule za kirabi.
Baadhi ya hati za kale zinazoaminika hazina mstari wa 53 hadi sura ya 8 mstari wa 11.
Au “kwa viwango vya wanadamu.”
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Au “tangu mwanzoni.”
Au “akamwinamia.”
Au “nafsi yake.”
Au “nafsi yangu.”
Au “nafsi yangu.”
Au “kuhangaisha nafsi zetu.”
Au “tuna umoja.”
Au “ni kama mungu.”
Au “kwenye kaburi la ukumbusho.”
Tnn., “stadia 15 hivi.” Angalia Nyongeza B14.
Au “kaburi la ukumbusho.”
Tnn., “rohoni.”
Au “kaburi la ukumbusho.”
Yaani, hekalu.
Au “wameketi mezani.”
Yaani, ratili ya Kiroma, karibu gramu 327. Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza A5.
Au “kwenye kaburi la ukumbusho.”
Au “anayeipenda sana nafsi yake.”
Au “anayeichukia nafsi yake.”
Au “nafsi yangu inataabika.”
Au “onyesheni imani.”
Angalia Nyongeza A5.
Au “ujumbe wetu?”
Angalia Nyongeza A5.
Au “mna wajibu wa.”
Au “amenigeuka.”
Tnn., “kifuani pa.”
Au “nafsi yangu.”
Au “nafsi yako.”
Au “Onyesheni imani.”
Au “mfariji.”
Au “hana nguvu juu yangu.”
Au “nafsi yake.”
Au “hawaonyeshi kwamba wananiamini.”
Maneno “huyo” na “naye” katika mstari wa 13 na 14 yanarejelea “msaidizi” aliyetajwa katika mstari wa 7. Yesu alitumia neno “msaidizi” (ambalo lina jinsia ya kiume katika Kigiriki) alipoipa roho takatifu sifa ya mtu ingawa ni nguvu isiyo na utu, na katika Kigiriki haina jinsia ya kiume wala ya kike.
Au “wanadamu wote; watu wote.”
Au “waendelee kupata ujuzi juu yako wewe.”
Au “Nimelijulisha.”
Au “wamelitii.”
Au “wawe na umoja.”
Au “tulivyo na umoja.”
Au “Uwaweke kando; Uwafanye wawe watakatifu.”
Au “waunganishwe kikamili.”
Au “bonde la majira ya baridi kali la Kidroni.”
Au “mwingilio.”
Au “mhalifu.”
Au “Uheshimiwe.”
Au “Auawe kwenye mti! Auawe kwenye mti!”
Au “mkamuue kwenye mti.”
Au “kukuua kwenye mti?”
Au “anampinga.”
Yaani, karibu saa 6 mchana.
Au “Auawe kwenye mti!”
Angalia Kamusi, “Mti wa mateso.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “akafa.”
Au “utakaopondwa.”
Au labda, “mchanganyiko uliosokotwa.”
Yaani, ratili ya Kiroma. Angalia Nyongeza B14.
Au “alipouawa kwenye mti.”
Au “kaburi la ukumbusho.”
Au “kaburi la ukumbusho.”
Au “kaburi la ukumbusho.”
Tnn., “kuwa asiyeamini.”
Au “aliwatokea.”
Au “samaki wowote.”
Au “akajifunga.”
Au “alikuwa amevaa mavazi machache.”
Karibu futi 300. Tnn., “mikono 200 hivi.” Angalia Nyongeza B14.