Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • nwt Methali 1:1-31:31
  • Methali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Methali
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Methali

METHALI

1 Methali za Sulemani+ mwana wa Daudi,+ mfalme wa Israeli:+

 2 Ili mtu ajifunze* hekima+ na nidhamu;

Ili aelewe maneno ya hekima;

 3 Ili apate nidhamu+ inayoleta ufahamu,

Uadilifu,+ busara,*+ na unyoofu;*

 4 Ili kumfanya mjinga awe mwerevu;+

Ili kumpa kijana ujuzi na uwezo wa kufikiri.+

 5 Mtu mwenye hekima husikiliza na kujifunza zaidi;+

Mtu mwenye uelewaji hupata mwelekezo stadi*+

 6 Ili kuelewa methali na fumbo,*

Maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.+

 7 Kumwogopa* Yehova ndio mwanzo wa ujuzi.+

Ni wapumbavu tu wanaodharau hekima na nidhamu.+

 8 Mwanangu, sikiliza nidhamu ya baba yako,+

Wala usiyaache mafundisho* ya mama yako.+

 9 Ni shada linalovutia kwenye kichwa chako+

Na pambo maridadi shingoni mwako.+

10 Mwanangu, watenda dhambi wakijaribu kukushawishi, usikubali.+

11 Wakisema: “Njoo twende.

Acha tuvizie ili kumwaga damu.

Tutajificha na kuwashambulia bila sababu watu wasio na hatia.

12 Tutawameza wakiwa hai kama Kaburi* linavyomeza,

Wazima-wazima, kama wale wanaoshuka shimoni.

13 Na tunyakue mali zao zote zenye thamani;

Nyumba zetu tutazijaza nyara.

14 Unapaswa kujiunga nasi,*

Nasi sote tutagawana sawasawa vitu tunavyoiba.”*

15 Mwanangu, usiwafuate.

Iepushe miguu yako na njia yao.+

16 Kwa maana miguu yao hukimbilia kutenda uovu;

Wanaenda haraka kumwaga damu.+

17 Kwa kweli ni kazi bure kutandaza wavu huku ndege akitazama.

18 Ndio sababu wanavizia ili kumwaga damu;

Wanajificha ili wawaue* wengine.

19 Hizo ndizo njia za wale wanaotafuta faida isiyo ya haki,

Ambayo itawaangamiza wale wanaoipata.+

20 Hekima ya kweli+ hupaza sauti kubwa barabarani.+

Huendelea kuinua sauti yake katika viwanja vya jiji.+

21 Hupaza sauti kwenye makutano ya barabara zenye watu wengi.

Nayo husema hivi kwenye malango ya jiji:+

22 “Ninyi wajinga mtaendelea kuupenda ujinga mpaka lini?

Nanyi wadhihaki mtaendelea kufurahia dhihaka mpaka lini?

Nanyi wapumbavu mtaendelea kuchukia ujuzi mpaka lini?+

23 Sikilizeni karipio langu.*+

Ndipo nitakapowamiminia roho yangu;

Nitawajulisha maneno yangu.+

24 Kwa sababu niliwaita, lakini mkaendelea kukataa,

Niliunyoosha mkono wangu, lakini hakuna yeyote aliyejali,+

25 Mliendelea kupuuza ushauri wangu wote

Na kukataa karipio langu,

26 Mimi pia nitawacheka mtakapopatwa na msiba;

Nitawadhihaki jambo mnaloogopa litakapokuja,+

27 Jambo mnaloogopa litakapokuja kama dhoruba,

Na msiba wenu utakapofika kama upepo wa dhoruba,

Wakati dhiki na taabu zitakapowapata.

28 Wakati huo wataendelea kuniita, lakini sitajibu;

Watanitafuta kwa bidii, lakini hawatanipata,+

29 Kwa sababu walichukia ujuzi,+

Nao hawakuchagua kumwogopa Yehova.+

30 Walikataa ushauri wangu;

Waliyadharau makaripio yangu yote.

31 Basi watapata matokeo* ya njia yao,+

Nao watashiba kabisa mashauri yao* wenyewe.

32 Kwa maana upotovu wa wajinga utawaua,

Na kutojali kwa wapumbavu kutawaangamiza.

33 Lakini yule anayenisikiliza ataishi kwa usalama+

Naye hatahangaishwa na woga wa msiba.”+

2 Mwanangu, ukiyakubali maneno yangu

Na kuhifadhi amri zangu kama hazina,+

 2 Kwa kutega sikio lako usikilize hekima+

Na kuuelekeza moyo wako upate utambuzi;+

 3 Pia, ukiuita uelewaji kwa sauti+

Na kupaza sauti yako upate utambuzi;+

 4 Ukiendelea kuutafuta kama fedha,*+

Na kuendelea kuutafuta sana kama hazina zilizofichika;+

 5 Ndipo utakapoelewa kumwogopa Yehova,+

Nawe utapata ujuzi kumhusu Mungu.+

 6 Kwa maana Yehova mwenyewe hutoa hekima;+

Na kinywani mwake hutoka ujuzi na utambuzi.

 7 Huwahifadhia wanyoofu hekima inayotumika;

Yeye ni ngao kwa wanaotembea kwa utimilifu.+

 8 Huvilinda vijia vya haki,

Naye atailinda njia ya washikamanifu wake.+

 9 Ndipo utakapoelewa lililo la uadilifu na la haki na lililo sawa,

Njia yote ya lililo jema.+

10 Hekima inapoingia moyoni mwako+

Na ujuzi kupendeza nafsi* yako,+

11 Uwezo wa kufikiri utakukinga,+

Na utambuzi utakulinda,

12 Ili kukuokoa kutoka kwenye njia mbaya,

Kutoka kwa mtu anayesema mambo mapotovu,+

13 Kutoka kwa wale wanaoviacha vijia vya unyoofu

Ili watembee katika njia za giza,+

14 Kutoka kwa wale wanaoshangilia kutenda mabaya,

Wanaofurahia upotovu wa uovu,

15 Wale ambao vijia vyao vimepinda

Na ambao mwenendo wao wote ni wenye hila.

16 Utakuokoa kutoka kwa mwanamke aliyepotoka,*

Kutoka kwa maneno laini* ya mwanamke mwasherati,*+

17 Anayemwacha rafiki wa karibu* wa ujana wake+

Na kusahau agano la Mungu wake;

18 Kwa maana nyumba yake huzama katika kifo,

Na vijia vyake* huongoza kwa wale waliokufa ambao hawana uwezo.+

19 Hakuna yeyote anayelala naye* atakayerudi,

Wala hawatarudi kwenye vijia vya uzima.+

20 Basi fuata njia ya watu wema

Na ubaki kwenye vijia vya waadilifu,+

21 Kwa maana ni wanyoofu tu watakaokaa duniani,

Na wasio na lawama* ndio watakaobaki ndani yake.+

22 Lakini waovu, wataangamizwa kutoka duniani,+

Na wenye hila watang’olewa kutoka ndani yake.+

3 Mwanangu, usisahau mafundisho* yangu,

Na moyo wako ushike amri zangu,

 2 Kwa sababu zitakuongezea siku nyingi

Na miaka ya uhai na amani.+

 3 Usiruhusu upendo mshikamanifu na uaminifu* zikuache.+

Zifunge shingoni mwako;

Ziandike kwenye kibao cha moyo wako;+

 4 Ndipo utakapopata kibali na ufahamu mzuri

Machoni pa Mungu na wanadamu.+

 5 Mtumaini Yehova+ kwa moyo wako wote,

Wala usitegemee* uelewaji wako mwenyewe.+

 6 Katika njia zako zote mtambue yeye,+

Naye atavinyoosha vijia vyako.+

 7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe.+

Mwogope Yehova na ujiepushe na uovu.

 8 Hilo litaponya mwili wako*

Na kuiburudisha mifupa yako.

 9 Mheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye thamani,+

Kwa mavuno ya kwanza ya* mazao* yako yote;+

10 Ndipo maghala yako yatakapojazwa kabisa,+

Na mitungi yako itafurika* divai mpya.

11 Mwanangu, usikatae nidhamu ya Yehova,+

Wala usichukie karipio lake,+

12 Kwa maana Yehova huwakaripia wale anaowapenda,+

Kama baba anavyomkaripia mwana anayempenda.+

13 Mwenye furaha ni mtu anayepata hekima+

Na mtu anayepata utambuzi;

14 Kupata hekima ni bora kuliko kupata fedha,

Na kuipata kama faida ni bora kuliko kupata dhahabu.+

15 Ni yenye thamani kuliko marijani;*

Hakuna chochote unachotamani kinachoweza kulinganishwa nayo.

16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kulia;

Na katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na utukufu.

17 Njia zake zinapendeza,

Na vijia vyake vyote vina amani.+

18 Ni mti wa uzima kwa wale wanaoishika,

Na wale wanaoishika kwa nguvu wataitwa wenye furaha.+

19 Yehova aliuweka msingi wa dunia kwa hekima.+

Aliziimarisha kabisa mbingu kwa utambuzi.+

20 Kwa ujuzi wake vilindi vya maji vilitenganishwa

Na anga zenye mawingu zilidondosha umande.+

21 Mwanangu, zisiondoke machoni pako.*

Ilinde hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri;

22 Zitakupa uzima

Na kuwa pambo shingoni mwako;

23 Ndipo utakapotembea kwa usalama katika njia yako,

Na mguu wako hautajikwaa kamwe.*+

24 Unapolala, hutaogopa;+

Utalala, na usingizi wako utakuwa mtamu.+

25 Hutaogopa tisho lolote la ghafla+

Wala dhoruba inayowajia waovu.+

26 Kwa maana Yehova atathibitika kuwa chanzo cha uhakika wako;+

Ataulinda mguu wako usinaswe.+

27 Usiwanyime mema wale unaopaswa kuwatendea mema*+

Ikiwa una uwezo wa kuwasaidia.*+

28 Usimwambie jirani yako, “Nenda; rudi baadaye! Nitakupa kesho,”

Ikiwa unaweza kumpa kitu hicho sasa.

29 Usipange kumdhuru jirani yako+

Anayejihisi akiwa salama mkiwa pamoja.

30 Usigombane na mtu bila sababu+

Ikiwa hajakutendea jambo lolote baya.+

31 Usimwonee wivu mtu mkatili+

Wala kuchagua yoyote kati ya njia zake,

32 Kwa maana Yehova humchukia mtu mwenye hila,+

Lakini ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.+

33 Laana ya Yehova iko juu ya nyumba ya mwovu,+

Lakini huyabariki makao ya mwadilifu.+

34 Kwa maana yeye huwadhihaki wale wanaodhihaki,+

Lakini huwaonyesha kibali wapole.+

35 Wenye hekima watarithi heshima,

Lakini wapumbavu hutukuza aibu.+

4 Wanangu, sikilizeni nidhamu ya baba;+

Sikilizeni kwa makini ili mpate uelewaji,

 2 Kwa maana nitawapa mafundisho mema;

Msiache mafundisho* yangu.+

 3 Nilikuwa mwana halisi wa baba yangu+

Na mama yangu alinipenda sana.+

 4 Baba alinifundisha na kusema: “Moyo wako na ushike kabisa maneno yangu.+

Shika amri zangu, uendelee kuishi.+

 5 Jipatie hekima, jipatie uelewaji.+

Usisahau, wala usiache ninayosema.

 6 Usiiache, nayo itakukinga.

Ipende, nayo itakulinda.

 7 Hekima ndilo jambo muhimu zaidi,*+ kwa hiyo jipatie hekima,

Pamoja na vyote unavyojipatia, jipatie uelewaji.+

 8 Ithamini sana, nayo itakukweza.+

Itakuheshimu kwa sababu unaikumbatia.+

 9 Itakuvika shada lenye kuvutia kichwani;

Itakupamba kwa taji maridadi.”

10 Mwanangu, sikiliza maneno yangu na uyakubali,

Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.+

11 Nitakufundisha katika njia ya hekima;+

Nitakuongoza katika vijia vya unyoofu.+

12 Unapotembea, hatua zako hazitazuiwa;

Na ukikimbia, hutajikwaa.

13 Shika kabisa nidhamu; usiiache.+

Ilinde, kwa maana ni uzima wako.+

14 Usiingie katika kijia cha waovu,

Wala usitembee katika njia ya watu wabaya.+

15 Iepuke, usiifuate;+

Jiepushe nayo, pita mbali nayo.+

16 Kwa maana hawawezi kulala wasipotenda uovu.

Hawapati usingizi wasipomwangusha mtu.

17 Wanajilisha mkate wa uovu,

Na kunywa divai ya ukatili.

18 Lakini kijia cha waadilifu ni kama nuru nyangavu ya asubuhi

Inayong’aa zaidi na zaidi mpaka mchana kamili.+

19 Njia ya waovu ni kama giza;

Hawajui ni nini kinachowafanya wajikwae.

20 Mwanangu, sikiliza maneno yangu;

Sikiliza kwa makini* ninayokwambia.

21 Yasiondoke machoni pako;

Yaweke ndani kabisa moyoni mwako,+

22 Kwa maana ni uzima kwa wale wanaoyapata+

Na afya kwa mwili wao wote.

23 Ulinde moyo wako kuliko vitu vyote unavyolinda,+

Kwa maana humo ndimo zinamotoka chemchemi za uzima.

24 Jiepushe kabisa na maneno yaliyopotoka,+

Na ujitenge mbali na mazungumzo yenye hila.

25 Macho yako yanapaswa kutazama mbele moja kwa moja,

Naam, yakaze macho yako* moja kwa moja mbele yako.+

26 Lainisha* mapito ya miguu yako,+

Na njia zako zote zitakuwa thabiti.

27 Usielekee kulia wala kushoto.+

Iepushe miguu yako na lililo ovu.

5 Mwanangu, sikiliza hekima yangu.

Sikiliza kwa makini* utambuzi wangu,+

 2 Ili uweze kuulinda uwezo wako wa kufikiri

Na kuulinda ujuzi kwa midomo yako.+

 3 Kwa maana midomo ya mwanamke aliyepotoka* inadondoka kama sega la asali,+

Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta.+

 4 Lakini mwishowe ni mchungu kama pakanga+

Na mwenye makali kama upanga unaokata kwa pande zote mbili.+

 5 Miguu yake hushuka kwenye kifo.

Hatua zake huongoza moja kwa moja Kaburini.*

 6 Hakazii fikira kijia cha uzima.

Huyumbayumba katika njia yake, lakini hajui inakoelekea.

 7 Sasa, wanangu, nisikilizeni

Nanyi msiache ninayosema.

 8 Kaeni mbali naye;

Msiukaribie mlango wa nyumba yake,+

 9 Ili msiwape wengine heshima yenu+

Wala kuvuna miaka ya ukatili;+

10 Ili wageni wasimalize mali* zenu+

Na vitu mlivyopata kwa jasho viende katika nyumba ya mgeni.

11 La sivyo, mtalia kwa uchungu mwishoni mwa maisha yenu

Nyama na mwili wenu vitakapodhoofika+

12 Nanyi mseme: “Jinsi nilivyochukia nidhamu!

Jinsi moyo wangu ulivyodharau karipio!

13 Sikusikiliza sauti ya wakufunzi wangu

Wala kuwasikiliza kwa makini walimu wangu.

14 Nimefika ukingoni mwa maangamizi kamili

Katikati ya kutaniko lote.”*+

15 Kunywa maji ya tangi lako mwenyewe

Na maji yanayotiririka* kutoka katika kisima chako mwenyewe.+

16 Je, chemchemi zako zitawanywe nje,

Na vijito vyako vya maji katika viwanja vya jiji?+

17 Na yawe yako peke yako,

Wala si ya wageni pamoja nawe.+

18 Chemchemi yako na ibarikiwe,*

Na ushangilie pamoja na mke wa ujana wako,+

19 Paa jike anayependeza, mbuzi wa mlimani* anayevutia.+

Matiti yake na yakuridhishe* nyakati zote.

Upendo wake na ukusisimue daima.+

20 Basi mwanangu, kwa nini usisimuliwe na mwanamke aliyepotoka*

Au kukikumbatia kifua cha mwanamke mwasherati?*+

21 Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele ya macho ya Yehova;

Yeye huvichunguza vijia vyake vyote.+

22 Mwovu hunaswa na makosa yake mwenyewe,

Naye atashikwa na kamba za dhambi yake mwenyewe.+

23 Atakufa kwa sababu ya utovu wa nidhamu

Na kupotea njia kwa sababu ya upumbavu wake uliopita kiasi.

6 Mwanangu, ikiwa umemdhamini* jirani yako,+

Ikiwa umempa mkono* mtu usiyemjua,+

 2 Ikiwa umenaswa na ahadi yako,

Ukakamatwa na maneno ya kinywa chako,+

 3 Mwanangu, fanya hivi ili ujiokoe,

Kwa maana umeanguka mikononi mwa jirani yako:

Nenda ujinyenyekeze mwenyewe na kumsihi haraka jirani yako.+

 4 Usiruhusu macho yako yapate usingizi,

Wala kope zako kusinzia.

 5 Jiokoe kama swala kutoka mikononi mwa mwindaji,

Kama ndege kutoka mikononi mwa mwindaji wa ndege.

 6 Mwendee chungu, ewe mvivu;+

Zichunguze njia zake uwe na hekima.

 7 Ingawa hana kamanda, ofisa, au mtawala,

 8 Yeye hutayarisha chakula chake wakati wa kiangazi,+

Na kukusanya chakula chake wakati wa mavuno.

 9 Ewe mvivu, utaendelea kulala hapo mpaka lini?

Utaamka lini kutoka katika usingizi wako?

10 Lala kidogo, sinzia kidogo,

Kunja mikono kidogo ili upumzike,+

11 Na umaskini wako utakuja kama jambazi,

Na uhitaji wako kama mwanamume mwenye silaha.+

12 Mtu mwovu asiyefaa kitu huzurura-zurura akisema maneno mapotovu;+

13 Hukonyeza jicho lake,+ hutoa ishara kwa mguu wake, na kuashiria kwa vidole vyake.

14 Kwa moyo uliopotoka,

Sikuzote anapanga njama za uovu+ na kueneza ugomvi.+

15 Kwa hiyo, msiba wake utakuja ghafla;

Atavunjwa mara moja naye hataweza kupona.+

16 Kuna vitu sita ambavyo Yehova anachukia;

Naam, vitu saba vinavyomchukiza:

17 Macho ya kiburi,+ ulimi wa uwongo,+ na mikono inayomwaga damu isiyo na hatia,+

18 Moyo unaopanga njama za uovu,+ na miguu inayokimbilia haraka uovu,

19 Shahidi wa uwongo anayesema uwongo kila anapopumua,+

Na mtu yeyote anayepanda ugomvi miongoni mwa ndugu.+

20 Mwanangu, shika amri ya baba yako,

Wala usiyaache mafundisho* ya mama yako.+

21 Zifunge daima kuzunguka moyo wako;

Zifunge shingoni mwako.

22 Unapotembea huku na huku, itakuongoza;

Unapolala, itakulinda;

Na unapoamka, itaongea nawe.*

23 Kwa maana amri hiyo ni taa,+

Na sheria ni nuru,+

Na makaripio ya nidhamu ndiyo njia ya uzima.+

24 Yatakulinda dhidi ya mwanamke mwovu,+

Dhidi ya ulimi unaoshawishi wa mwanamke mwasherati.*+

25 Usiutamani urembo wake moyoni mwako+

Wala kukubali akunase kwa macho yake yanayovutia,

26 Kwa maana kahaba humfanya mtu abaki tu na kipande cha mkate,+

Lakini mke wa mwanamume mwingine huuwinda uhai wenye* thamani.

27 Je, mtu anaweza kukusanya moto kwenye kifua chake na mavazi yake yasiungue?+

28 Au je, mtu anaweza kutembea juu ya makaa yanayowaka moto na miguu yake isiungue?

29 Ndivyo ilivyo kwa mtu yeyote anayelala na mke wa jirani yake;

Hakuna yeyote anayemgusa mwanamke huyo atakayekosa kuadhibiwa.+

30 Watu hawamdharau mwizi

Akiiba ili ajishibishe* anapokuwa na njaa.

31 Lakini akipatikana, atalipa mara saba;

Atatoa vitu vyote vyenye thamani vya nyumba yake.+

32 Mtu yeyote anayefanya uzinzi na mwanamke hana busara;*

Yule anayefanya hivyo anajiangamiza mwenyewe.+

33 Atapata tu majeraha na kuvunjiwa heshima,+

Na aibu yake haitafutiliwa mbali.+

34 Kwa maana wivu humfanya mume awake hasira;

Hataonyesha huruma anapolipiza kisasi.+

35 Hatakubali fidia* yoyote;

Hutamtuliza, hata ukimpa zawadi kubwa kadiri gani.

7 Mwanangu, shika maneno yangu,

Na uzihifadhi amri zangu kama hazina.+

 2 Shika amri zangu uishi;+

Linda mafundisho* yangu kama mboni ya jicho lako.

 3 Zifunge juu ya vidole vyako;

Ziandike kwenye kibao cha moyo wako.+

 4 Iambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”

Na uuite uelewaji “mtu wangu wa ukoo,”

 5 Ili vikulinde dhidi ya mwanamke aliyepotoka,*+

Dhidi ya mwanamke mwasherati* na maneno yake laini.*+

 6 Kutoka kwenye dirisha la nyumba yangu,

Nilitazama chini kupitia viunzi vya dirisha langu,

 7 Na nilipokuwa nikiwachunguza wajinga,*

Nilitambua miongoni mwa vijana, kijana fulani mwanamume asiye na busara.*+

 8 Alipita barabarani karibu na njia panda anapoishi mwanamke huyo,

Naye akashika njia inayoelekea nyumbani kwa mwanamke huyo

 9 Jioni wakati wa gizagiza,+

Usiku na giza linapoingia.

10 Kisha nikamwona mwanamke akija kukutana naye,

Akiwa amevaa kama* kahaba,+ mwenye moyo mjanja.

11 Mwanamke mwenye kelele na mkaidi.+

Hakai* kamwe nyumbani mwake.

12 Mara yuko nje, mara yuko katika viwanja vya jiji,

Ananyemelea karibu na kila njia panda.+

13 Kisha anamkamata kwa nguvu kijana huyo na kumpiga busu;

Bila aibu, mwanamke huyo anamwambia:

14 “Nililazimika kutoa dhabihu za ushirika.+

Leo nilitimiza nadhiri zangu.

15 Ndiyo sababu nimekuja kukupokea,

Kukutafuta, nami nimekupata!

16 Nimetandika matandiko bora kitandani mwangu,

Kitani cha Misri chenye rangi mbalimbali.+

17 Nimenyunyiza manemane, udi, na mdalasini kitandani mwangu.+

18 Njoo, tunywe na kushiba upendo mpaka asubuhi;

Na tujifurahishe kwa mahaba,

19 Kwa maana mume wangu hayuko nyumbani;

Amesafiri mbali.

20 Alibeba mfuko wa pesa,

Naye hatarudi mpaka siku ya mwezi mpevu.”

21 Anampotosha kwa ushawishi mkubwa.+

Anamtongoza kwa maneno laini.

22 Ghafla kijana huyo anamfuata, kama ng’ombe dume anayeenda machinjioni,

Kama mjinga anayeenda kuadhibiwa katika mikatale,*+

23 Mpaka mshale unapochoma ini lake;

Kama ndege anayekimbia kuingia mtegoni, hajui kwamba hilo litamgharimu uhai wake.*+

24 Na sasa, wanangu, nisikilizeni;

Sikilizeni kwa makini maneno ninayosema.

25 Msiruhusu moyo wenu ugeuke na kufuata njia zake.

Msipotee njia na kufuata vijia vyake,+

26 Kwa maana amewaangamiza wengi,+

Na wale aliowaua ni wengi sana.+

27 Nyumba yake huongoza Kaburini;*

Hushuka chini kwenye vyumba vya ndani vya kifo.

8 Je, hekima haipazi sauti?

Je, utambuzi hauinui sauti yake?+

 2 Kwenye sehemu zilizoinuka+ pembeni mwa barabara,

Husimama kwenye makutano ya barabara.

 3 Karibu na malango yanayoelekea jijini,

Kwenye njia zinazoelekea milangoni,

Huendelea kulia kwa sauti kubwa:+

 4 “Ninawaita, enyi watu, ninawaita;

Ninampazia sauti kila mtu.*

 5 Enyi wajinga, jifunzeni werevu;+

Enyi wapumbavu, jipatieni moyo wenye uelewaji.*

 6 Sikilizeni, kwa maana ninayosema ni muhimu,

Midomo yangu husema yaliyo sawa;

 7 Kwa maana kinywa changu husema ukweli kwa sauti ya chini,

Na midomo yangu huchukia jambo ovu.

 8 Maneno yote ya kinywa changu ni ya uadilifu.

Hakuna neno hata moja lililopinda wala kupotoka.

 9 Yote yako wazi kabisa kwa mtu mwenye utambuzi

Nayo ni sawa kwa wale ambao wamepata ujuzi.

10 Chukueni nidhamu yangu badala ya fedha,

Na ujuzi badala ya dhahabu bora zaidi,+

11 Kwa maana hekima ni bora kuliko marijani;*

Vitu vingine vyote vinavyotamanika haviwezi kulinganishwa nayo.

12 Mimi, hekima, ninakaa pamoja na werevu;

Nimepata ujuzi na uwezo wa kufikiri.+

13 Kumwogopa Yehova humaanisha kuchukia uovu.+

Ninachukia kujikweza na kiburi+ na njia ya uovu na maneno mapotovu.+

14 Nina ushauri mzuri na hekima inayotumika;+

Uelewaji+ na nguvu+ ni vyangu.

15 Kwa msaada wangu wafalme huendelea kutawala,

Na maofisa wakuu hutunga sheria za uadilifu.+

16 Kwa msaada wangu wakuu huendelea kutawala,

Na viongozi huhukumu kwa uadilifu.

17 Ninawapenda wale wanaonipenda,

Na wale wanaonitafuta watanipata.+

18 Nina utajiri na utukufu,

Mali inayodumu* na uadilifu.

19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, hata kuliko dhahabu safi,

Na mazao yangu ni bora kuliko fedha bora kabisa.+

20 Mimi hutembea katika kijia cha uadilifu,

Katikati ya vijia vya haki;

21 Mimi huwapa urithi mwingi wale wanaonipenda,

Nami huyajaza maghala yao.

22 Yehova aliniumba mwanzoni mwa njia yake,+

Mwanzo kabisa wa kazi zake za zamani za kale.+

23 Niliimarishwa tangu nyakati za kale,*+

Tangu mwanzoni, nyakati za mapema kabla ya dunia kuwepo.+

24 Wakati ambapo hakukuwa na vilindi vya maji,+ nilizaliwa,*

Wakati ambapo hakukuwa na chemchemi zilizofurika maji.

25 Kabla milima haijawekwa mahali pake,

Kabla ya vilima, nilizaliwa,

26 Wakati ambapo hakuwa ameiumba dunia na mashamba yake

Wala mabonge ya kwanza ya udongo.

27 Alipozitayarisha mbingu,+ nilikuwepo;

Alipouweka upeo* juu ya maji,+

28 Alipoyafanya imara mawingu yaliyo juu,

Alipojenga msingi wa chemchemi za vilindini,

29 Alipoiwekea bahari sheria

Kwamba maji yake yasipite agizo lake,+

Alipoiweka* misingi ya dunia,

30 Wakati huo nilikuwa kando yake nikiwa mfanyakazi stadi.+

Mimi ndiye aliyenipenda sana+ siku baada ya siku;

Nilishangilia mbele zake wakati wote;+

31 Nilishangilia dunia yake inayokaliwa,

Nami niliwapenda sana wanadamu.

32 Na sasa, wanangu, nisikilizeni;

Naam, wenye furaha ni wale wanaoshika njia zangu.

33 Sikilizeni nidhamu+ muwe na hekima,

Msiipuuze kamwe.

34 Mwenye furaha ni mtu anayenisikiliza

Kwa kuja mapema* milangoni pangu siku baada ya siku,

Kwa kusubiri karibu na miimo ya milango yangu;

35 Kwa maana anayenipata mimi atapata uzima,+

Naye hupata kibali kutoka kwa Yehova.

36 Lakini anayenipuuza anajidhuru mwenyewe,*

Na wale wanaonichukia wanapenda kifo.”+

9 Hekima ya kweli imejenga nyumba yake;

Imechonga nguzo zake saba.

 2 Imetayarisha kabisa nyama yake;*

Imechanganya divai yake;

Imepanga pia meza yake.

 3 Imewatuma vijakazi wake

Ili waite kwa sauti kutoka vileleni juu ya jiji:+

 4 “Yeyote ambaye ni mjinga, na aje humu.”

Humwambia yule asiye na busara:*

 5 “Njoo, ule mkate wangu

Na unywe divai niliyochanganya.

 6 Acha ujinga wako* uishi;+

Tembea moja kwa moja katika njia ya uelewaji.”+

 7 Anayemrekebisha mtu mwenye dhihaka hualika aibu,+

Na yeyote anayemkaripia mtu mwovu ataumia.

 8 Usimkaripie mtu mwenye dhihaka, kwa maana atakuchukia.+

Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.+

 9 Mfundishe mwenye hekima, naye atazidi kuwa na hekima.+

Mfundishe mwadilifu, naye atazidi kuelimika.

10 Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima,+

Na kumjua Aliye Mtakatifu Zaidi+ ni uelewaji.

11 Kwa maana nitafanya siku zako ziwe nyingi,+

Na miaka ya maisha yako itaongezwa.

12 Ukipata hekima, unapata hekima kwa faida yako mwenyewe,

Lakini ukiwa mwenye dhihaka, utaibeba dhihaka hiyo peke yako.

13 Mwanamke mpumbavu ana kelele.+

Yeye ni mjinga na hajui chochote.

14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake

Kwenye kiti sehemu zilizoinuka jijini,+

15 Akiwaita kwa sauti wale wanaopita karibu naye,

Waendao moja kwa moja kwenye njia yao:

16 “Yeyote ambaye ni mjinga, aje hapa.”

Huwaambia wale wasio na busara:*+

17 “Maji yaliyoibwa ni matamu,

Na chakula kinacholiwa sirini kinapendeza.”+

18 Lakini hawajui kwamba wale waliokufa ambao hawana uwezo wako hapo,

Na kwamba wageni wake wamo katika vina vya Kaburi.*+

10 Methali za Sulemani.+

Mwana mwenye hekima humfanya baba yake ashangilie,+

Lakini mwana mpumbavu ni huzuni kwa mama yake.

 2 Hazina zilizopatikana kwa uovu hazitakuwa na faida yoyote,

Lakini uadilifu ndio unaookoa kutoka katika kifo.+

 3 Yehova hatamwacha mwadilifu akae njaa,+

Lakini atawanyima waovu wanachotamani.

 4 Mikono milegevu italeta umaskini,+

Lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.+

 5 Mwana anayetenda kwa ufahamu hukusanya mazao wakati wa kiangazi,

Lakini mwana anayetenda kwa aibu analala usingizi mzito wakati wa mavuno.+

 6 Baraka ziko juu ya kichwa cha mwadilifu,+

Lakini kinywa cha mwovu hufunika ukatili.

 7 Kumbukumbu* ya mwadilifu itabarikiwa,+

Lakini jina la mwovu litaoza.+

 8 Mwenye hekima moyoni atakubali mafundisho,*+

Lakini mtu anayezungumza maneno ya upumbavu atakanyagiwa chini.+

 9 Anayetembea kwa utimilifu atatembea kwa usalama,+

Lakini anayepotosha njia zake atajulikana.+

10 Anayekonyeza jicho lake kwa hila husababisha huzuni,+

Na yule anayezungumza maneno ya upumbavu atakanyagiwa chini.+

11 Kinywa cha mwadilifu ni chemchemi ya uzima,+

Lakini kinywa cha mwovu hufunika ukatili.+

12 Chuki ndiyo inayochochea ugomvi,

Lakini upendo hufunika makosa yote.+

13 Hekima hupatikana kwenye midomo ya mtu mwenye utambuzi,+

Lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa mtu asiye na busara.*+

14 Watu wenye hekima huhifadhi ujuzi kama hazina,+

Lakini kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.+

15 Mali ya* tajiri ni jiji lake lenye ngome.

Ufukara wa maskini ndio unaowaangamiza.+

16 Kazi ya mwadilifu huongoza kwenye uzima;

Lakini mazao ya mwovu huongoza kwenye dhambi.+

17 Anayetii nidhamu ni kijia kinachoelekea kwenye uzima,*

Lakini anayepuuza karipio huwapotosha wengine.

18 Anayeficha chuki yake husema uwongo,+

Na yule anayeeneza habari zinazodhuru* ni mpumbavu.

19 Maneno yanapokuwa mengi, makosa hayawezi kuepukwa,+

Lakini yeyote anayedhibiti midomo yake anatenda kwa busara.+

20 Ulimi wa mwadilifu ni kama fedha bora kabisa,+

Lakini moyo wa mwovu una thamani ndogo.

21 Midomo ya mwadilifu huwalisha* wengi,+

Lakini wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa ufahamu.+

22 Baraka ya Yehova ndiyo inayomtajirisha mtu,+

Naye haichanganyi na maumivu.*

23 Kutenda mambo ya aibu ni kama mchezo kwa mpumbavu,

Lakini hekima ni ya mtu mwenye utambuzi.+

24 Anachoogopa mwovu kitamjia;

Lakini tamaa ya mwadilifu itatoshelezwa.+

25 Dhoruba ikipita, mwovu hatakuwepo tena,+

Lakini mwadilifu ni msingi milele.+

26 Kama siki kwenye meno na moshi machoni,

Ndivyo alivyo mtu mvivu kwa yule anayemtuma.*

27 Kumwogopa Yehova hurefusha maisha,+

Lakini miaka ya waovu itafupishwa.+

28 Matarajio ya* waadilifu huleta shangwe,+

Lakini tumaini la waovu litatokomea.+

29 Njia ya Yehova ni ngome kwa mtu asiye na lawama,+

Lakini ni maangamizi kwa watenda maovu.+

30 Mwadilifu hataangushwa kamwe,+

Lakini waovu hawataendelea kukaa duniani.+

31 Kinywa cha mwadilifu huzaa* hekima,

Lakini ulimi uliopotoka utaangamizwa.

32 Midomo ya mwadilifu inajua mambo yanayopendeza,

Lakini kinywa cha waovu kimepotoka.

11 Mizani ya uwongo* humchukiza Yehova,

Lakini kipimo sahihi* humfurahisha.+

 2 Kimbelembele kinapokuja, aibu itafuata,+

Lakini wenye kiasi wana hekima.+

 3 Utimilifu wa wanyoofu ndio unaowaongoza,+

Lakini ujanja wa wenye hila utawaangamiza.+

 4 Mali haitakuwa* na faida yoyote siku ya ghadhabu,+

Lakini uadilifu ndio utakaookoa kutoka katika kifo.+

 5 Uadilifu wa mtu asiye na lawama hukinyoosha kijia chake,

Lakini mwovu ataanguka kwa sababu ya uovu wake mwenyewe.+

 6 Uadilifu wa wanyoofu utawaokoa,+

Lakini wenye hila watanaswa na tamaa zao wenyewe.+

 7 Mtu mwovu anapokufa, tumaini lake hutokomea;

Na matarajio aliyokuwa nayo kwa kutegemea nguvu zake hutokomea pia.+

 8 Mwadilifu huokolewa kutoka katika taabu,

Na mwovu huingia humo badala yake.+

 9 Kwa kinywa chake mwasi imani* humwangamiza jirani yake,

Lakini kwa ujuzi waadilifu huokolewa.+

10 Wema wa watu waadilifu hulifanya jiji lishangilie,

Na waovu wanapoangamia, kunakuwa na kelele za shangwe.+

11 Jiji hukwezwa kwa sababu ya baraka ya mtu mnyoofu,+

Lakini kinywa cha waovu hulibomoa.+

12 Mtu yeyote asiye na busara* humdharau jirani yake,

Lakini mtu mwenye utambuzi wa kweli hukaa kimya.+

13 Mchongezi huzurura-zurura akifunua mazungumzo ya siri,+

Lakini mtu anayeaminika* hutunza siri.*

14 Mwelekezo stadi* unapokosekana, watu huanguka,

Lakini washauri wengi huleta mafanikio.*+

15 Yeyote anayemwekea dhamana ya mkopo* mtu asiyemjua hakika ataumia,+

Lakini yeyote anayeepuka* kumpa mkono ili kumdhamini atakuwa salama.

16 Mwanamke mwenye fadhili* hupata utukufu,+

Lakini watu wasio na huruma hujitwalia utajiri.

17 Mtu mwenye fadhili* hujinufaisha,*+

Lakini mtu mkatili hujiletea shida.*+

18 Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu,+

Lakini mtu anayepanda uadilifu hupata thawabu ya kweli.+

19 Anayetetea uadilifu kwa uthabiti atapata uzima,+

Lakini anayefuatia uovu anaelekea kwenye kifo.

20 Waliopotoka moyoni wanamchukiza Yehova,+

Lakini wale ambao njia yao haina lawama humfurahisha.+

21 Uwe na hakika kuhusu hili:* Mtu mwovu hatakosa kuadhibiwa,+

Lakini watoto wa mwadilifu wataponyoka.

22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe

Ndivyo alivyo mwanamke mrembo anayekataa busara.

23 Tamaa ya waadilifu huongoza kwenye mema,+

Lakini tumaini la waovu huongoza kwenye ghadhabu.

24 Mtu mmoja hutoa kwa ukarimu* na kupata vitu vingi zaidi;+

Mtu mwingine huwanyima wengine wanachostahili, lakini anakuwa maskini.+

25 Mtu mkarimu atapata ufanisi,*+

Na yule anayewaburudisha wengine* yeye mwenyewe ataburudishwa.+

26 Watu watamlaani anayeficha nafaka,

Lakini watambariki anayeiuza.

27 Anayetafuta kwa bidii kutenda mema hutafuta kibali,+

Lakini anayetafuta uovu—kwa hakika atapatwa na uovu.+

28 Anayeutumaini utajiri wake ataanguka,+

Lakini waadilifu watasitawi kama majani.+

29 Yeyote anayewaletea taabu* watu wa nyumbani mwake atarithi upepo,+

Na mpumbavu atakuwa mtumishi wa mtu mwenye hekima moyoni.

30 Tunda la mwadilifu ni mti wa uzima,+

Na yule anayeziteka* nafsi* ni mwenye hekima.+

31 Ikiwa, kwa hakika, mtu mwadilifu duniani huthawabishwa,

Sembuse mwovu na mtenda dhambi!+

12 Anayependa nidhamu anapenda ujuzi,+

Lakini anayechukia karipio hana akili.*+

 2 Mtu mwema hupata kibali cha Yehova,

Lakini Yeye humhukumu mtu anayepanga njama za uovu.+

 3 Hakuna mtu anayekuwa salama kwa kutenda uovu,+

Lakini waadilifu hawatang’olewa kamwe.

 4 Mke mwema* ni taji kwa mume wake,+

Lakini mke anayetenda kwa aibu ni kama uozo katika mifupa ya mume wake.+

 5 Mawazo ya waadilifu ni ya haki,

Lakini mwongozo wa waovu hudanganya.

 6 Maneno ya waovu huvizia ili kuua,*+

Lakini kinywa cha wanyoofu huwaokoa.+

 7 Waovu wanapoangamizwa, hawako tena,

Lakini nyumba ya mwadilifu itaendelea kusimama.+

 8 Mtu husifiwa kwa sababu ya busara ya kinywa chake,+

Lakini mtu aliye na moyo uliopotoka atatendewa kwa dharau.+

 9 Ni afadhali usiheshimiwe sana lakini uwe na mtumishi

Kuliko kujitukuza mwenyewe na ukose chakula.*+

10 Mwadilifu huwatunza wanyama anaowafuga,*+

Lakini hata rehema ya waovu ni ukatili.

11 Anayelima shamba lake atakuwa na chakula tele,+

Lakini anayefuatia vitu visivyo na maana hana busara.*

12 Mtu mwovu hutamani kitu kilichokamatwa na watu wengine waovu,

Lakini mzizi wa waadilifu huzaa matunda.

13 Mwovu hunaswa na mazungumzo yake ya dhambi,+

Lakini mwadilifu huokoka kutoka katika taabu.

14 Mtu hushiba mema kwa sababu ya matunda ya maneno yake,*+

Na kazi ya mikono yake itamthawabisha.

15 Njia ya mpumbavu ni sawa machoni pake mwenyewe,+

Lakini mwenye hekima hukubali ushauri.*+

16 Mjinga huonyesha papo hapo* kwamba ameudhika,+

Lakini mtu mwerevu hupuuza* matusi.

17 Anayetoa ushahidi kwa uaminifu atasema ukweli,*

Lakini shahidi wa uwongo husema mambo ya udanganyifu.

18 Maneno yanayosemwa bila kufikiri huchoma kama upanga,

Lakini ulimi wa mwenye hekima huponya.+

19 Midomo inayosema ukweli itadumu milele,+

Lakini ulimi unaosema uwongo utadumu kwa muda mfupi tu.+

20 Udanganyifu umo moyoni mwa wale wanaopanga njama zinazodhuru,

Lakini wale wanaositawisha* amani wana shangwe.+

21 Hakuna madhara yatakayompata mwadilifu,+

Lakini waovu watapatwa na misiba mingi.+

22 Midomo inayosema uwongo humchukiza Yehova,+

Lakini wanaotenda kwa uaminifu humfurahisha.

23 Mtu mwerevu hufunika mambo anayojua,

Lakini moyo wa mjinga hububujika ujinga.+

24 Mkono wa wenye bidii utatawala,+

Lakini mikono milegevu italazimishwa kufanya kazi za utumwa.+

25 Mahangaiko yaliyo moyoni mwa mtu huulemea moyo,*+

Lakini neno jema huuchangamsha.+

26 Mwadilifu hutafuta malisho yake,

Lakini njia ya waovu huwapotosha.

27 Watu wavivu hawakimbizi mawindo,+

Lakini bidii ni hazina ya mtu yenye thamani.

28 Kijia cha uadilifu huongoza kwenye uzima;+

Kando ya kijia hicho hakuna kifo.

13 Mwana mwenye hekima hukubali nidhamu ya baba yake,+

Lakini mwenye dhihaka hasikilizi kemeo.*+

 2 Mtu atakula mema kwa sababu ya matunda ya maneno yake,*+

Lakini tamaa hasa* ya wenye hila ni ukatili.

 3 Anayelinda kinywa chake anaulinda uhai wake,*+

Lakini anayefungua wazi midomo yake ataangamia.+

 4 Kuna vitu anavyotamani sana mtu mvivu, ingawa hana chochote,+

Lakini mwenye bidii atatoshelezwa kikamili.*+

 5 Mwadilifu huchukia uwongo,+

Lakini matendo ya waovu huleta aibu na fedheha.

 6 Uadilifu humlinda mtu ambaye njia yake haina hatia,+

Lakini uovu humshusha mtenda dhambi.

 7 Kuna mtu anayejifanya tajiri ingawa hana chochote;+

Kuna mtu anayejifanya maskini ingawa ana mali nyingi.

 8 Utajiri ni fidia ya uhai wa mtu,+

Lakini maskini hata hawatishwi.*+

 9 Nuru ya waadilifu hung’aa kwa uangavu,*+

Lakini taa ya waovu itazimwa.+

10 Kimbelembele husababisha mzozo tu,+

Lakini hekima ni ya wale wanaotafuta ushauri.*+

11 Mali inayopatikana haraka* itapungua,+

Lakini mali ya yule anayeikusanya kidogo kidogo* itaongezeka.

12 Matarajio yaliyoahirishwa* hufanya moyo uwe mgonjwa,+

Lakini tamaa inayotoshelezwa ni mti wa uzima.+

13 Yeyote anayedharau mafundisho* atalipia adhabu yake,+

Lakini anayeheshimu amri atathawabishwa.+

14 Mafundisho* ya mwenye hekima ni chemchemi ya uzima+

Humwepusha mtu na mitego ya kifo.

15 Ufahamu ulio makini huleta kibali,

Lakini njia ya wenye hila ni ngumu sana.

16 Mtu mwerevu hutenda kwa ujuzi,+

Lakini mjinga hufunua ujinga wake mwenyewe.+

17 Mjumbe mwovu huanguka taabani,+

Lakini mjumbe mwaminifu huleta maponyo.+

18 Yeyote anayepuuza nidhamu huwa maskini na kupata aibu,

Lakini anayekubali kurekebishwa* atatukuzwa.+

19 Tamaa inapotoshelezwa ni tamu kwa mtu,*+

Lakini wapumbavu huchukia kuacha uovu.+

20 Anayetembea na wenye hekima atakuwa na hekima,+

Lakini anayeshirikiana na wapumbavu ataumia.+

21 Msiba huwafuatia watenda dhambi,+

Lakini ufanisi huwathawabisha waadilifu.+

22 Mtu mwema huwaachia urithi wajukuu wake,

Lakini mali ya mtenda dhambi itawekwa akiba kwa ajili ya mwadilifu.+

23 Shamba la maskini lililolimwa huzaa chakula kingi,

Lakini linaweza* kufagiliwa mbali na ukosefu wa haki.

24 Yeyote anayeizuia fimbo yake* anamchukia mwanawe,+

Lakini yule anayempenda humtia nidhamu kwa bidii.*+

25 Mwadilifu hula na kutosheleza hamu* yake,+

Lakini tumbo la waovu liko tupu.+

14 Mwanamke ambaye kwa kweli ana hekima huijenga nyumba yake,+

Lakini aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

 2 Mtu anayetembea kwa unyoofu wake anamwogopa Yehova,

Lakini yule ambaye njia zake ni zenye hila* humdharau Yeye.

 3 Fimbo ya kiburi imo kinywani mwa mpumbavu,

Lakini midomo ya wenye hekima itawalinda.

 4 Mahali pasipo na ng’ombe, hori ni safi,

Lakini nguvu za ng’ombe dume huleta mavuno mengi.

 5 Shahidi mwaminifu hatasema uwongo,

Lakini shahidi wa uwongo husema uwongo kila anapopumua.+

 6 Mtu mwenye dhihaka hutafuta hekima lakini haipati kamwe,

Lakini ujuzi humjia kwa urahisi mtu aliye na uelewaji.+

 7 Kaa mbali na mtu mpumbavu,

Kwa maana hutapata ujuzi katika midomo yake.+

 8 Kwa hekima, mtu mwerevu huelewa njia anayofuata,

Lakini wapumbavu hudanganywa* na ujinga wao.+

 9 Wajinga hufanyia mzaha hatia,*+

Lakini wanyoofu wako tayari kufanya mapatano.*

10 Moyo hujua uchungu wake wenyewe,*

Na hakuna mgeni yeyote anayeweza kushiriki shangwe yake.

11 Nyumba ya mwovu itaharibiwa,+

Lakini hema la mnyoofu litasitawi.

12 Kuna njia inayoonekana kuwa sawa machoni pa mtu,+

Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+

13 Hata katika kicheko moyo unaweza kuhisi maumivu,

Na shangwe inaweza kuishia katika huzuni.

14 Mtu aliyepotoka moyoni atavuna matokeo ya njia zake,+

Lakini mtu mwema huvuna thawabu ya matendo yake.+

15 Mjinga* huamini kila neno,

Lakini mwerevu hutafakari kila hatua.+

16 Mwenye hekima hujihadhari na kuepuka uovu,

Lakini mpumbavu hajali,* naye anajiamini kupita kiasi.

17 Yule anayekasirika upesi hutenda kipumbavu,+

Lakini mtu anayechanganua mambo* huchukiwa.

18 Mjinga* atarithi upumbavu,

Lakini werevu huvikwa ujuzi kama taji.+

19 Watu wabaya watalazimika kuinama chini mbele ya watu wema,

Na waovu watainama katika malango ya waadilifu.

20 Maskini huchukiwa hata na majirani zake,+

Lakini tajiri ana marafiki wengi.+

21 Anayemdharau jirani yake anatenda dhambi,

Lakini yeyote anayewahurumia watu wa hali ya chini ni mwenye furaha.+

22 Je, wale wanaopanga njama zinazodhuru hawatapotea njia?

Lakini wanaokusudia kutenda mema watapata upendo mshikamanifu na uaminifu.+

23 Kila aina ya kazi ngumu ina faida,

Lakini maneno matupu huleta umaskini.+

24 Taji la wenye hekima ni mali yao;

Lakini ujinga wa wapumbavu ni ujinga tu.+

25 Shahidi wa kweli huokoa uhai,*

Lakini shahidi mdanganyifu husema uwongo kila anapopumua.

26 Anayemwogopa Yehova humtumaini kwa uthabiti,+

Na woga huo utakuwa kimbilio kwa watoto wake.+

27 Kumwogopa Yehova ni chemchemi ya uzima,

Humwepusha mtu na mitego ya kifo.

28 Umati wa watu ni fahari ya mfalme,+

Lakini mtawala asiye na raia huangamia.

29 Mtu asiyekasirika upesi ana utambuzi mwingi,+

Lakini asiye na subira hudhihirisha upumbavu.+

30 Moyo mtulivu huupa mwili uzima,*

Lakini wivu huozesha mifupa.+

31 Anayempunja mtu wa hali ya chini anamtukana Muumba wake,+

Lakini yeyote anayewahurumia maskini humtukuza Mungu.+

32 Mtu mwovu ataangamizwa na uovu wake mwenyewe,

Lakini mwadilifu atapata kimbilio katika utimilifu wake.+

33 Hekima hutulia katika moyo wa mtu mwenye uelewaji,+

Lakini miongoni mwa wapumbavu ni lazima ijitangaze.

34 Uadilifu hulikweza taifa,+

Lakini dhambi hulifedhehesha taifa.

35 Mfalme hufurahishwa na mtumishi anayetenda kwa ufahamu,+

Lakini hasira yake huwaka dhidi ya yule anayetenda kwa aibu.+

15 Jibu la upole* hutuliza hasira,+

Lakini neno kali* huchochea hasira.+

 2 Ulimi wa mwenye hekima hutumia vizuri ujuzi,+

Lakini kinywa cha mpumbavu hububujika ujinga.

 3 Macho ya Yehova yako kila mahali,

Yakiwaangalia waovu na wema.+

 4 Ulimi mtulivu* ni mti wa uzima,+

Lakini maneno yaliyopotoka hukatisha tamaa.*

 5 Mjinga hudharau nidhamu ya baba yake,+

Lakini mwerevu hukubali kurekebishwa.*+

 6 Nyumba ya mwadilifu ina hazina tele,

Lakini mazao* ya mwovu humletea taabu.+

 7 Midomo ya wenye hekima hueneza ujuzi,+

Lakini moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.+

 8 Dhabihu ya waovu humchukiza Yehova,+

Lakini sala ya wanyoofu humfurahisha Yeye.+

 9 Yehova huchukia njia ya mwovu,+

Lakini humpenda mtu anayefuatia uadilifu.+

10 Nidhamu huonekana kuwa mbaya* kwa mtu anayeiacha njia,+

Lakini yeyote anayechukia karipio atakufa.+

11 Kaburi* na mahali pa maangamizi* viko wazi kabisa machoni pa Yehova.+

Sembuse mioyo ya wanadamu!+

12 Mtu mwenye dhihaka hampendi anayemrekebisha.*+

Hatatafuta ushauri kutoka kwa wenye hekima.+

13 Moyo wenye shangwe hufanya uso uchangamke,

Lakini maumivu ya moyo huiponda roho.+

14 Moyo wenye uelewaji hutafuta ujuzi,+

Lakini kinywa cha wapumbavu hula* ujinga.+

15 Siku zote za mtu anayeteseka ni mbaya,+

Lakini mtu aliye na moyo mchangamfu* huwa na karamu daima.+

16 Ni afadhali kuwa na vichache na kumwogopa Yehova+

Kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na mahangaiko.*+

17 Ni afadhali kula mboga za majani mahali penye upendo+

Kuliko kula ng’ombe dume aliyenoneshwa* mahali penye chuki.+

18 Mtu mwenye hasira kali huchochea mzozo,+

Lakini mtu asiyekasirika upesi hutuliza ugomvi.+

19 Njia ya mvivu ni kama uzio wa miiba,+

Lakini kijia cha wanyoofu ni kama barabara iliyosawazika.+

20 Mwana mwenye hekima humfanya baba yake ashangilie,+

Lakini mtu mpumbavu humdharau mama yake.+

21 Mtu asiye na busara* hufurahia ujinga,+

Lakini mtu mwenye utambuzi huenda mbele moja kwa moja.+

22 Mipango huvunjika watu wasiposhauriana,*

Lakini mambo hufanikiwa kupitia washauri wengi.+

23 Mtu hushangilia anapotoa jibu linalofaa,*+

Na neno linalosemwa wakati unaofaa—ni jema sana!+

24 Kwa mwenye ufahamu kijia cha uzima huelekea juu,+

Ili kumwepusha na Kaburi* lililo chini.+

25 Yehova ataibomoa nyumba ya mtu mwenye kiburi,+

Lakini ataulinda mpaka wa mjane.+

26 Yehova huchukia njama za mtu mwovu,+

Lakini maneno yanayopendeza ni safi Kwake.+

27 Mtu anayepata faida isiyo ya haki huwaletea taabu* watu wa nyumba yake mwenyewe,+

Lakini anayechukia rushwa ataendelea kuishi.+

28 Moyo wa mwadilifu hutafakari kabla ya kujibu,*+

Lakini kinywa cha waovu hububujika mambo mabaya.

29 Yehova yuko mbali sana na waovu,

Lakini huisikia sala ya waadilifu.+

30 Macho yanayong’aa* huufanya moyo ushangilie;

Habari njema huitia nguvu mifupa.*+

31 Mtu anayesikiliza karipio la uzima

Hutulia miongoni mwa wenye hekima.+

32 Yeyote anayekataa nidhamu anaudharau uhai wake,*+

Lakini yeyote anayesikiliza karipio hupata uelewaji.*+

33 Kumwogopa Yehova ni mazoezi ya kupata hekima,+

Na kabla ya utukufu kuna unyenyekevu.+

16 Mtu huyatayarisha mawazo ya moyo wake,*

Lakini jibu analotoa* hutoka kwa Yehova.+

 2 Njia zote za mwanadamu huonekana kuwa sawa* machoni pake,+

Lakini Yehova huchunguza nia.*+

 3 Mkabidhi Yehova lolote unalofanya,*+

Na mipango yako itafanikiwa.

 4 Yehova amefanya kila kitu kitimize kusudi lake,

Hata waovu kwa ajili ya siku ya msiba.+

 5 Kila mtu mwenye kiburi moyoni humchukiza Yehova.+

Uwe na hakika kwamba* hatakosa kuadhibiwa.

 6 Kwa upendo mshikamanifu na uaminifu, kosa husamehewa,+

Na kwa kumwogopa Yehova mtu hujiepusha na uovu.+

 7 Yehova anapofurahia njia za mtu,

Huwafanya hata maadui wake wawe na amani naye.+

 8 Afadhali kuwa na kidogo pamoja na uadilifu+

Kuliko kuwa na mapato mengi pasipo haki.+

 9 Mtu anaweza kupanga njia yake moyoni mwake,

Lakini Yehova ndiye anayezielekeza hatua zake.+

10 Uamuzi ulioongozwa na roho* unapaswa kuwa katika midomo ya mfalme;+

Hapaswi kamwe kusaliti haki.+

11 Mizani na vipimo vya unyoofu hutoka kwa Yehova;

Mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ni kazi yake.+

12 Matendo maovu huwachukiza wafalme,+

Kwa maana kiti cha ufalme huimarishwa kabisa kwa uadilifu.+

13 Maneno ya uadilifu huwafurahisha wafalme.

Wanampenda mtu anayeongea kwa unyoofu.+

14 Ghadhabu ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo,+

Lakini mtu mwenye hekima huituliza.*+

15 Katika nuru ya uso wa mfalme kuna uzima;

Kibali chake ni kama wingu la mvua wakati wa masika.+

16 Jinsi lilivyo jambo bora kupata hekima kuliko dhahabu!+

Ni bora kuchagua uelewaji kuliko fedha.+

17 Barabara kuu ya wanyoofu huepuka uovu.

Yeyote anayelinda njia yake huhifadhi uhai wake.*+

18 Kiburi hutangulia kuanguka kwa kishindo,

Na roho ya majivuno hutangulia kujikwaa.+

19 Ni afadhali kuwa mnyenyekevu*+ miongoni mwa wapole

Kuliko kugawana nyara na watu wenye kiburi.

20 Mtu anayeonyesha ufahamu katika jambo atapata mafanikio,*

Na mwenye furaha ni yule anayemtumaini Yehova.

21 Watu wenye hekima moyoni wataitwa watu wenye uelewaji,+

Na mtu anayeongea kwa fadhili* huongeza ushawishi.+

22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa walio nao,

Lakini wajinga hutiwa nidhamu kwa ujinga wao wenyewe.

23 Moyo wa mwenye hekima hukipatia kinywa chake ufahamu+

Na huongeza ushawishi kwenye maneno yake.

24 Maneno yanayopendeza ni sega la asali,

Ni matamu kwa nafsi* nayo huponya mifupa.+

25 Kuna njia inayoonekana kuwa sawa machoni pa mtu,

Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+

26 Hamu ya chakula* ya mfanyakazi humfanya afanye kazi kwa bidii

Kwa sababu njaa yake* humchochea kuendelea kufanya kazi.+

27 Mtu asiyefaa kitu huchimbua lililo ovu;+

Na maneno yake ni kama moto unaounguza.+

28 Mfanya fujo* husababisha mgawanyiko,+

Na mchongezi huwatenganisha marafiki wa karibu.+

29 Mtu mkatili humshawishi jirani yake

Na kumwongoza katika njia isiyofaa.

30 Hukonyeza jicho lake anapopanga njama zinazodhuru.

Huibanabana midomo yake pamoja anapotekeleza hila.

31 Mvi ni taji la umaridadi*+

Zinapopatikana katika njia ya uadilifu.+

32 Mtu asiyekasirika upesi+ ni bora kuliko mwanamume mwenye nguvu,

Na mtu anayedhibiti hasira yake* ni bora kuliko mtu anayelishinda jiji.+

33 Kura hupigwa mapajani,+

Lakini kila uamuzi unaofanywa kwa kura hiyo hutoka kwa Yehova.+

17 Ni afadhali kipande kikavu cha mkate mahali penye amani*+

Kuliko nyumba iliyojaa karamu* pamoja na ugomvi.+

 2 Mtumishi mwenye ufahamu atamtawala mwana anayetenda kwa aibu;

Atapokea urithi kama ndugu za mwana huyo.

 3 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,+

Lakini Yehova ndiye mchunguzaji wa mioyo.+

 4 Mtu mwovu husikiliza maneno yanayoumiza,

Na mtu mdanganyifu husikiliza ulimi unaodhuru.+

 5 Yeyote anayemdhihaki maskini anamtukana Muumba wake,+

Na yeyote anayeshangilia msiba wa mwingine hatakosa kuadhibiwa.+

 6 Wajukuu ni taji kwa waliozeeka,

Na akina baba* ni utukufu wa wana* wao.

 7 Maneno manyoofu* hayamfai mpumbavu.+

Sembuse maneno ya uwongo kwa mtawala!*+

 8 Zawadi ni kama kito chenye thamani kwa* aliye nayo;+

Humletea mafanikio, kila mahali anapoenda.+

 9 Yeyote anayesamehe* kosa hutafuta upendo,+

Lakini yule anayeendelea kuongea kuhusu jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.+

10 Kemeo humgusa moyo zaidi mtu mwenye uelewaji+

Kuliko kumpiga mpumbavu mara mia moja.+

11 Mtu mwovu hutafuta uasi tu,

Lakini mjumbe mkatili atatumwa kumwadhibu.+

12 Ni afadhali kukutana na dubu aliyenyang’anywa watoto wake

Kuliko kukutana na mtu mpumbavu katika ujinga wake.+

13 Mtu yeyote akilipa uovu kwa wema,

Uovu hautaondoka katika nyumba yake.+

14 Kuanzisha vita ni kama kufungua lango la mafuriko;*

Kabla ugomvi haujalipuka, ondoka.+

15 Yeyote anayetangaza kwamba mwovu hana hatia na yeyote anayemshutumu mwadilifu+

—Wote wawili wanamchukiza Yehova.

16 Kuna faida gani kwa mpumbavu kuwa na uwezo wa kupata hekima

Ilhali hana moyo wa kuipata?*+

17 Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote+

Naye ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.+

18 Mtu ambaye hana busara* humpa mwingine mkono na kukubali

Kuweka dhamana mbele ya jirani yake.+

19 Mtu anayependa ugomvi anapenda dhambi.+

Yeyote anayeliinua juu lango lake anaalika msiba.+

20 Mtu aliyepotoka moyoni hatapata mafanikio,*+

Na yule anayesema maneno ya udanganyifu ataanguka kwenye maangamizi.

21 Baba anayezaa mtoto mpumbavu atahuzunika;

Na baba ya mtoto asiye na akili hana shangwe.+

22 Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri,*+

Lakini roho iliyopondeka humfyonza mtu nguvu.*+

23 Mtu mwovu atachukua rushwa kwa siri*

Ili apotoshe njia ya haki.+

24 Hekima iko mbele kabisa ya uso wa mtu mwenye utambuzi,

Lakini macho ya mpumbavu hutangatanga mpaka kwenye miisho ya dunia.+

25 Mwana mpumbavu humletea huzuni baba yake

Na kumletea maumivu ya moyo* yule aliyemzaa.+

26 Si vema kumwadhibu* mwadilifu,

Na kuwapiga viboko watu wanaoheshimiwa si jambo linalofaa.

27 Mtu mwenye ujuzi huyazuia maneno yake,+

Na mtu mwenye utambuzi atabaki mtulivu.*+

28 Hata mjinga anayekaa kimya ataonwa kuwa mwenye hekima,

Na yule anayefunga midomo yake, ataonwa kuwa mwenye utambuzi.

18 Yeyote anayejitenga na wengine anafuatia tamaa zake mwenyewe za kichoyo;

Hukataa* hekima yote inayotumika.

 2 Mtu mpumbavu hapendezwi na uelewaji;

Anaona ni afadhali afunue yaliyo moyoni mwake.+

 3 Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pia,

Na aibu huja pamoja na fedheha.+

 4 Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina.+

Chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.

 5 Si vema kumpendelea mwovu+

Wala kumnyima haki mtu mwadilifu.+

 6 Maneno ya mpumbavu husababisha ugomvi,+

Na kinywa chake hualika kipigo.+

 7 Kinywa cha mpumbavu ndicho kinachomwangamiza,+

Na midomo yake ni mtego kwa uhai wake.*

 8 Maneno ya mchongezi ni kama matonge matamu;*+

Humezwa na kushuka tumboni moja kwa moja.+

 9 Yeyote aliye mvivu katika kazi yake

Ni ndugu ya mtu mharibifu.+

10 Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu.+

Mwadilifu hukimbilia humo na kupata ulinzi.*+

11 Mali ya tajiri ni jiji lake lenye ngome;

Ni kama ukuta wa ulinzi katika mawazo yake.+

12 Kabla ya kuanguka kwa kishindo moyo wa mtu huwa na kiburi,+

Na kabla ya utukufu kuna unyenyekevu.+

13 Yeyote anayejibu kabla ya kusikia ukweli wa mambo,

Huo ni upumbavu na aibu kwake.+

14 Roho ya mtu inaweza kumtegemeza anapokuwa mgonjwa,+

Lakini ni nani anayeweza kustahimili roho iliyopondeka?*+

15 Moyo wa mtu mwenye uelewaji hupata ujuzi,+

Na sikio la mwenye hekima hujitahidi kupata ujuzi.

16 Zawadi ya mwanadamu humfungulia njia;+

Humwezesha kufika mbele ya watu mashuhuri.

17 Mtu wa kwanza kuwasilisha kesi yake huonekana kuwa sahihi,+

Mpaka mwingine anapokuja na kumuuliza maswali.*+

18 Kupiga kura hukomesha mizozo+

Na kukata maneno kati ya* wapinzani wenye nguvu.

19 Ndugu aliyekosewa ni mgumu kuliko jiji lenye ngome,+

Na kuna mizozo ambayo ni kama makomeo ya ngome.+

20 Tumbo la mtu litajazwa matunda ya maneno yake;*+

Atashiba mazao ya midomo yake.

21 Kifo na uhai viko katika nguvu za ulimi;+

Wale wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.+

22 Anayepata mke mwema amepata kitu chema,+

Naye hupata kibali cha* Yehova.+

23 Maskini husihi anapoongea,

Lakini tajiri hujibu kwa ukali.

24 Kuna marafiki walio tayari kuangamizana,+

Lakini kuna rafiki anayeshikamana na mtu kwa ukaribu kuliko ndugu.+

19 Ni afadhali kuwa maskini na kutembea kwa utimilifu+

Kuliko kuwa mpumbavu na kusema uwongo.+

 2 Mtu asiye na ujuzi si mtu mzuri,+

Na mtu anayetenda bila kufikiri* anatenda dhambi.

 3 Ujinga wa mtu ndio unaopotosha njia yake,

Kisha moyo wake unamkasirikia vikali Yehova.

 4 Mali huwavuta marafiki wengi,

Lakini maskini ataachwa hata na rafiki yake.+

 5 Shahidi anayesema uwongo hatakosa kuadhibiwa,+

Na yule anayesema uwongo kila anapopumua hataponyoka.+

 6 Wengi hujipendekeza kwa mtu maarufu,*

Na kila mtu ni rafiki ya yule anayetoa zawadi.

 7 Ndugu wote wa mtu maskini humchukia;+

Marafiki zake humwepuka hata zaidi!+

Huwafuatia ili awasihi, lakini hakuna yeyote anayemsikiliza.

 8 Yeyote anayepata busara* anajipenda mwenyewe.*+

Yeyote anayethamini utambuzi kama hazina atapata mafanikio.*+

 9 Shahidi anayesema uwongo hatakosa kuadhibiwa,

Na yule anayesema uwongo kila anapopumua ataangamia.+

10 Mjinga hastahili kuishi maisha ya anasa;

Sembuse mtumishi kuwatawala wakuu!+

11 Ufahamu wa mtu hakika hutuliza hasira yake,+

Na ni fahari kwake kuachilia* kosa.+

12 Ghadhabu ya mfalme ni kama mngurumo wa simba,*+

Lakini kibali chake ni kama umande juu ya majani.

13 Mwana mpumbavu humletea shida baba yake,+

Na mke mgomvi* ni kama paa ambalo haliachi kamwe kuvuja.+

14 Nyumba na mali hurithiwa kutoka kwa akina baba,

Lakini mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.+

15 Uvivu huleta usingizi mzito,

Na mtu mzembe atakaa njaa.+

16 Anayeshika amri anaulinda uhai wake;*+

Asiyejali njia zake atakufa.+

17 Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova,+

Naye Atamlipa* kwa anayotenda.+

18 Mtie nidhamu mtoto* wako wakati bado kuna tumaini,+

Nawe usiwajibike kwa* kifo chake.+

19 Mtu mwenye hasira kali atalipia adhabu;

Ukijaribu kumwokoa, utalazimika kufanya hivyo tena na tena.+

20 Sikiliza mashauri na ukubali nidhamu,+

Ili uwe na hekima wakati wako ujao.+

21 Moyo wa mwanadamu una mipango mingi,

Lakini shauri* la Yehova ndilo litakalodumu.+

22 Kinachomfanya mtu awe mwenye kutamanika ni upendo wake mshikamanifu;+

Na ni afadhali kuwa maskini kuliko kuwa mwongo.

23 Kumwogopa Yehova huongoza kwenye uzima;+

Yule aliye na woga huo atakuwa na pumziko jema, hatapatwa na madhara.+

24 Mvivu huutumbukiza* mkono wake katika bakuli la karamu,

Lakini hata hashughuliki kuurudisha kinywani mwake.+

25 Mpige mwenye dhihaka,+ ili mjinga awe mwerevu,+

Mkaripie mwenye uelewaji ili aongeze ujuzi wake.+

26 Yule anayemtendea vibaya baba yake na kumfukuza mama yake

Ni mwana anayeleta aibu na fedheha.+

27 Mwanangu, ukiacha kusikiliza nidhamu,

Utatangatanga mbali na maneno ya ujuzi.

28 Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki haki,+

Na kinywa cha waovu hubugia uovu.+

29 Hukumu inawangojea wadhihaki,+

Na mgongo wa wapumbavu unangojea mapigo.+

20 Divai ni mdhihaki,+ kileo ni vurugu;+

Yeyote anayepotoshwa navyo hana hekima.+

 2 Kutisha* kwa mfalme ni kama mngurumo wa simba;*+

Yeyote anayemkasirisha anauhatarisha uhai wake mwenyewe.+

 3 Ni heshima kwa mtu kujiepusha na ugomvi,+

Lakini kila mjinga atajitumbukiza humo.+

 4 Mvivu halimi katika majira ya baridi kali,

Kwa hiyo atakuwa akiombaomba wakati wa mavuno, wakati hana chochote.*+

 5 Mawazo* yaliyo moyoni mwa mtu ni kama maji yenye kina,

Lakini mtu mwenye utambuzi huyateka.

 6 Watu wengi hutangaza upendo wao mshikamanifu,

Lakini ni nani anayeweza kumpata mtu mwaminifu?

 7 Mwadilifu anatembea kwa utimilifu wake.+

Watoto* wake wanaokuja baada yake watakuwa na furaha.+

 8 Mfalme anapoketi kwenye kiti cha ufalme ili kuhukumu,+

Hupepeta uovu wote kwa macho yake.+

 9 Ni nani anayeweza kusema: “Nimeusafisha moyo wangu;+

Mimi ni safi kutokana na dhambi yangu”?+

10 Vipimo vya udanganyifu na mizani za uwongo*

—Vyote viwili humchukiza Yehova.+

11 Hata mtoto* hujulikana kwa matendo yake,

Kama tabia yake ni safi na ya unyoofu.+

12 Sikio linalosikia na jicho linaloona

—Yehova ameviumba vyote viwili.+

13 Usipende usingizi, la sivyo utakuwa maskini.+

Fungua macho yako, nawe utashiba mkate.+

14 “Si kizuri, si kizuri!” asema mnunuzi;

Kisha anaenda zake na kujigamba.+

15 Kuna dhahabu, pia kuna marijani* kwa wingi,

Lakini midomo ya ujuzi ni kitu chenye thamani.+

16 Chukua vazi la mtu ikiwa amemwekea dhamana mtu asiyemjua;+

Chukua dhamana kutoka kwake ikiwa alimfanyia hivyo mwanamke mgeni.*+

17 Mkate uliopatikana kwa udanganyifu ni mtamu kwa mtu,

Lakini baadaye kinywa chake kitajaa changarawe.+

18 Kwa mashauriano,* mipango itafanikiwa,*+

Na kwa mwelekezo stadi* pigana vita vyako.+

19 Mchongezi huzurura-zurura akifunua mazungumzo ya siri;+

Usishirikiane na mtu anayependa kupiga porojo.*

20 Yeyote anayemtukana baba yake na mama yake,

Taa yake itazimwa giza litakapoingia.+

21 Urithi unaopatikana kwa pupa mwanzoni

Hautakuwa baraka mwishoni.+

22 Usiseme: “Nitalipiza uovu!”+

Mtumaini Yehova,+ naye atakuokoa.+

23 Vipimo vya udanganyifu vinamchukiza* Yehova,

Na mizani za uwongo si nzuri.

24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova;+

Mwanadamu anawezaje kuelewa njia yake mwenyewe?*

25 Ni mtego kwa mtu kutangaza haraka-haraka, “Ni kitakatifu!”+

Kisha anachunguza baadaye alichoweka nadhiri.+

26 Mfalme mwenye hekima huwapepeta waovu+

Na kuwakanyaga kwa gurudumu la kupuria.+

27 Pumzi ya mtu ni taa ya Yehova,

Inayochunguza kikamili utu wake wa ndani kabisa.

28 Upendo mshikamanifu na uaminifu humlinda mfalme;+

Kwa upendo mshikamanifu anadumisha kiti chake cha ufalme.+

29 Utukufu wa vijana ni nguvu zao,+

Na fahari ya wazee ni mvi zao.+

30 Michubuko na majeraha huondolea mbali* uovu,+

Na mapigo husafisha utu wa ndani kabisa wa mtu.

21 Moyo wa mfalme ni kama vijito vya maji mkononi mwa Yehova.+

Yeye huuelekeza mahali popote anapopenda.+

 2 Njia zote za mwanadamu huonekana kuwa sawa machoni pake,+

Lakini Yehova huichunguza mioyo.*+

 3 Kutenda mambo manyoofu na ya haki

Humpendeza Yehova zaidi kuliko dhabihu.+

 4 Macho ya kiburi na moyo wenye majivuno

—Taa inayowaongoza waovu ni dhambi.+

 5 Mipango ya wenye bidii hakika huleta mafanikio,*+

Lakini wote walio na haraka kwa hakika watakuwa maskini.+

 6 Kupata hazina kwa ulimi unaosema uwongo

Ni kama ukungu unaotoweka, mtego unaoangamiza.*+

 7 Ukatili wa waovu utawafagilia mbali,+

Kwa maana wanakataa kutenda haki.

 8 Njia ya mtu mwenye hatia imepinda,

Lakini matendo ya mtu safi yamenyooka.+

 9 Ni afadhali kuishi pembeni juu ya paa

Kuliko kuishi katika nyumba moja na mke mgomvi.*+

10 Mtu mwovu hutamani maovu;+

Hamtendei kwa fadhili jirani yake.+

11 Mwenye dhihaka anapoadhibiwa, asiye na uzoefu hupata hekima zaidi,

Na mtu mwenye hekima anapopata ufahamu, anapata ujuzi.*+

12 Aliye Mwadilifu huichunguza nyumba ya mwovu;

Huwapindua waovu na kuwaangamiza.+

13 Yeyote anayeziba sikio lake asisikie kilio cha mtu wa hali ya chini

Yeye mwenyewe ataita naye hatajibiwa.+

14 Zawadi ya siri hutuliza hasira,+

Na rushwa iliyofichwa* hutuliza ghadhabu kali.

15 Mwadilifu hushangilia kutenda haki,+

Lakini hilo ni jambo baya sana kwa watenda maovu.

16 Mtu anayetangatanga kutoka kwenye njia ya ufahamu

Atapumzika katika kundi la wale waliokufa ambao hawana uwezo.+

17 Anayependa raha* atakuwa maskini;+

Anayependa divai na mafuta hatakuwa tajiri.

18 Mwovu ni fidia ya mwadilifu,

Na mwenye hila atachukuliwa badala ya mnyoofu.+

19 Ni afadhali kuishi nyikani

Kuliko kuishi na mke mgomvi* anayekasirika haraka.+

20 Hazina yenye thamani na mafuta hupatikana katika nyumba ya mwenye hekima,+

Lakini mtu mpumbavu atatumia vibaya* vitu alivyo navyo.+

21 Yeyote anayefuatia uadilifu na upendo mshikamanifu

Atapata uzima, uadilifu, na utukufu.+

22 Mtu mwenye hekima anaweza kupanda katika* jiji la watu wenye nguvu

Na kudhoofisha nguvu wanazotumaini.+

23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wake

Anajiepusha na taabu.+

24 Mtu mwenye kimbelembele, anayejigamba kwa kiburi, hivyo ndivyo unavyomwita

Mtu anayetenda kwa kimbelembele bila kujali.+

25 Anachotamani mtu mvivu kitamuua,

Kwa maana mikono yake inakataa kufanya kazi.+

26 Anatamani kwa pupa mchana kutwa,

Lakini mwadilifu hutoa, hawanyimi wengine chochote.+

27 Dhabihu ya mwovu inachukiza.+

Sembuse anapoitoa akiwa na nia ovu!*

28 Shahidi anayesema uwongo ataangamia,+

Lakini mtu anayesikiliza atatoa ushahidi kwa mafanikio.*

29 Mtu mwovu huvaa uso wa ushupavu,+

Lakini njia ya mtu mnyoofu ni hakika.*+

30 Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumpinga Yehova.+

31 Farasi hutayarishwa kwa ajili ya siku ya vita,+

Lakini wokovu ni wa Yehova.+

22 Ni afadhali kuchagua jina jema* kuliko mali nyingi;+

Kuheshimiwa* ni bora kuliko fedha na dhahabu.

 2 Matajiri na maskini wanafanana katika jambo hili:*

Yehova aliwaumba wote.+

 3 Mtu mwerevu huona hatari na kujificha,

Lakini wajinga husonga mbele na kupata madhara.*

 4 Unyenyekevu na kumwogopa Yehova huleta

Utajiri na utukufu na uzima.+

 5 Miiba na mitego iko kwenye njia ya mtu aliyepotoka,

Lakini yeyote anayethamini uhai wake* hukaa mbali nayo.+

 6 Mzoeze mvulana* njia anayopaswa kuifuata;+

Hata atakapozeeka hataiacha.+

 7 Tajiri humtawala maskini,

Na mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji.+

 8 Yeyote anayepanda uovu atavuna msiba,+

Na fimbo ya ghadhabu yake itaangamia.+

 9 Mtu mkarimu* atabarikiwa,

Kwa maana chakula chake humgawia maskini.+

10 Mfukuze mtu mwenye dhihaka,

Na ugomvi utatoweka;

Mizozo* na matusi yatakoma.

11 Mtu anayependa moyo safi na ambaye husema maneno yenye fadhili

Atakuwa rafiki ya mfalme.+

12 Macho ya Yehova huulinda ujuzi,

Lakini Yeye huyapindua maneno ya wenye hila.+

13 Mvivu anasema: “Kuna simba nje!

Nitauawa katikati ya uwanja wa jiji!”+

14 Kinywa cha wanawake waliopotoka* ni shimo refu.+

Anayeshutumiwa na Yehova ataanguka ndani yake.

15 Ujinga umefungwa katika moyo wa mvulana,*+

Lakini fimbo ya nidhamu ndiyo itakayouondolea mbali.+

16 Anayempunja maskini ili aongeze mali yake+

Na yule anayewapa zawadi matajiri

Mwishowe watakuwa maskini.

17 Tega sikio lako usikie maneno ya wenye hekima,+

Ili uufanye moyo wako uzingatie ujuzi wangu,+

18 Kwa maana inapendeza kuyahifadhi ndani yako kabisa,+

Ili yote yawe midomoni mwako daima.+

19 Ili umtegemee Yehova,

Ninakupa ujuzi leo.

20 Je, tayari sijakuandikia,

Na kukupa mashauri na ujuzi,

21 Ili nikufundishe maneno ya kweli yanayotegemeka,

Uweze kumpelekea habari sahihi yule aliyekutuma?

22 Usimwibie mtu maskini kwa kuwa ni maskini,+

Wala usimkandamize mtu wa hali ya chini katika lango la jiji,+

23 Kwa maana Yehova mwenyewe atawatetea+

Naye atawaangamiza wanaowapunja.

24 Usiwe na urafiki na mtu mwenye hasira kali

Wala kushirikiana na mtu anayekasirika upesi,

25 Ili usijifunze kamwe njia zake

Na kujitia mtegoni.+

26 Usiwe miongoni mwa wale wanaopeana mikono wanapotoa dhamana,

Wanaoweka dhamana kwa ajili ya mikopo.+

27 Ikiwa huna kitu cha kulipa,

Kitanda chako kitavutwa na kuchukuliwa ukiwa umekilalia!

28 Usiisogeze alama ya kale ya mpaka

Iliyowekwa na mababu zako.+

29 Je, umemwona mtu aliye stadi katika kazi yake?

Atasimama mbele ya wafalme;+

Hatasimama mbele ya watu wa kawaida.

23 Ukiketi kula pamoja na mfalme,

Chunguza kwa makini kilicho mbele yako;

 2 Tia kisu kwenye koo lako*

Ikiwa una hamu kubwa ya chakula.*

 3 Usivitamani vyakula vyake vitamu,

Kwa maana ni vyakula vya udanganyifu.

 4 Usijichoshe kupata utajiri.+

Acha, na uonyeshe uelewaji.*

 5 Ukiutupia jicho, haupo,+

Kwa maana hakika utaota mabawa kama ya tai na kuruka mbali angani.+

 6 Usile chakula cha mtu mchoyo;*

Usivitamani vyakula vyake vitamu,

 7 Kwa maana yeye ni kama mtu anayeweka hesabu.*

“Kula na kunywa,” anakuambia, lakini sivyo anavyomaanisha.*

 8 Utatapika matonge uliyokula

Nawe utakuwa umepoteza maneno yako ya kumsifu.

 9 Usiongee masikioni mwa mpumbavu,+

Kwa maana ataidharau hekima ya maneno yako.+

10 Usiisogeze alama ya kale ya mpaka+

Wala kuingia katika shamba la mayatima.

11 Kwa maana Mtetezi* wao ana nguvu;

Atawatetea dhidi yako.+

12 Ufanye moyo wako uzingatie nidhamu

Na sikio lako maneno ya ujuzi.

13 Usimnyime mvulana* nidhamu.+

Ukimpiga kwa fimbo, hatakufa.

14 Unapaswa kumpiga kwa fimbo,

Ili umwokoe asiingie Kaburini.*

15 Mwanangu, ikiwa moyo wako utakuwa na hekima,

Basi moyo wangu mimi utashangilia.+

16 Utu wangu wa ndani utashangilia

Midomo yako inaposema mambo yaliyo sawa.

17 Moyo wako usiwaonee wivu watenda dhambi,+

Bali mwogope Yehova mchana kutwa,+

18 Kwa maana ndipo utakapokuwa na wakati ujao+

Na tumaini lako halitafutiliwa mbali.

19 Mwanangu, sikiliza uwe na hekima,

Na uuelekeze moyo wako katika njia inayofaa.

20 Usiwe miongoni mwa watu wanaokunywa divai nyingi mno,+

Miongoni mwa wale wanaokula nyama kwa pupa,+

21 Kwa maana mlevi na mlafi watakuwa maskini,+

Na kusinzia kutamvika mtu matambara.

22 Msikilize baba yako aliyekuzaa,

Wala usimdharau mama yako kwa sababu tu amezeeka.+

23 Inunue* kweli wala usiiuze kamwe,+

Pia hekima na nidhamu na uelewaji.+

24 Baba ya mtu mwadilifu hakika atakuwa na shangwe;

Na baba anayemzaa mwana mwenye hekima atamfurahia.

25 Baba yako na mama yako watafurahi,

Na mama aliyekuzaa atakuwa na shangwe.

26 Mwanangu, nipe moyo wako,

Na macho yako yapendezwe na njia zangu.+

27 Kwa maana kahaba ni shimo refu,

Na mwanamke mwasherati* ni kisima chembamba.+

28 Hunyemelea kama mnyang’anyi;+

Huongeza idadi ya wanaume wasio waaminifu.

29 Ni nani mwenye ole? Ni nani aliye na wasiwasi?

Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani anayelalamika?

Ni nani aliye na majeraha bila sababu? Ni nani aliye na macho mazito?*

30 Ni wale wanaoshinda kwenye divai;+

Wale wanaotafuta* divai iliyochanganywa.

31 Usiitazame rangi nyekundu ya divai

Inapong’aa katika kikombe na kushuka taratibu,

32 Kwa maana mwishowe huuma kama nyoka,

Nayo hutoa sumu kama nyoka kipiri.

33 Macho yako yataona mambo ya ajabu,

Na moyo wako utasema mambo yaliyopotoka.+

34 Nawe utakuwa kama mtu anayelala katikati ya bahari,

Kama mtu anayelala juu ya mlingoti wa meli.

35 Utasema: “Wamenipiga, lakini sikuhisi chochote.*

Walinipiga, lakini sikujua.

Nitaamka lini?+

Nahitaji kinywaji kingine.”*

24 Usiwaonee wivu waovu,

Wala usitamani kushirikiana nao,+

 2 Kwa maana moyo wao hutafakari ukatili,

Na midomo yao huongea kuhusu kuwataabisha wengine.

 3 Nyumba* hujengwa kwa hekima,+

Na kwa utambuzi hufanywa iwe salama.

 4 Kwa ujuzi vyumba hujazwa

Kila aina ya hazina zenye thamani na zinazopendeza.+

 5 Mtu mwenye hekima ana nguvu,+

Na kwa ujuzi mtu huzidisha nguvu zake.

 6 Kwa mwelekezo stadi* utapigana vita vyako,+

Na kupitia washauri wengi kuna ushindi.*+

 7 Mjinga hawezi kupata hekima ya kweli;+

Hana lolote la kusema katika lango la jiji.

 8 Yeyote anayepanga njama ya uovu

Ataitwa stadi wa kupanga hila.+

 9 Njama za upumbavu* ni dhambi,

Na watu humchukia mwenye dhihaka.+

10 Ukivunjika moyo siku ya taabu,*

Nguvu zako zitakuwa chache.

11 Waokoe wale wanaopelekwa kwenye kifo,

Na uwazuie wale wanaopepesuka wakielekea kuchinjwa.+

12 Ukisema: “Lakini hatukujua jambo hili,”

Je, Yule anayeichunguza mioyo* hatatambua hilo?+

Naam, Yule anayekutazama atajua

Naye atamlipa kila mwanadamu kulingana na matendo yake.+

13 Mwanangu, kula asali, kwa sababu ni njema;

Asali ya sega ni tamu kinywani.

14 Vivyo hivyo, jua kwamba hekima ina manufaa kwako.*+

Ukiipata, utakuwa na wakati ujao

Na tumaini lako halitafutiliwa mbali.+

15 Usivizie kwa uovu karibu na makao ya mtu mwadilifu;

Usiharibu mahali pake pa kupumzikia.

16 Kwa maana mwadilifu anaweza kuanguka mara saba, lakini atainuka tena,+

Lakini waovu watakwazwa na msiba.+

17 Adui yako akianguka, usishangilie,

Na akijikwaa, usiruhusu moyo wako uwe na shangwe;+

18 La sivyo, Yehova ataona jambo hilo naye hatafurahi,

Naye ataiondoa hasira yake kumwelekea.*+

19 Usifadhaike* kwa sababu ya waovu;

Usiwaonee wivu watu waovu,

20 Kwa maana mtu yeyote mwovu hana wakati ujao;+

Taa ya waovu itazimwa.+

21 Mwanangu, mwogope Yehova na mfalme.+

Nawe usishirikiane na waasi,*+

22 Kwa maana msiba wao utatokea ghafla.+

Ni nani anayejua jinsi wote wawili* watakavyowaangamiza?+

23 Haya pia ni maneno ya wenye hekima:

Kuonyesha upendeleo katika hukumu si jambo zuri.+

24 Yeyote anayemwambia mtu mwovu, “Wewe ni mwadilifu,”+

Atalaaniwa na watu na kushutumiwa na mataifa.

25 Lakini mambo yatawaendea vema wale wanaomkaripia;+

Watapata baraka ya vitu vyema.+

26 Watu wataibusu midomo ya mtu anayejibu kwa unyoofu.*+

27 Tayarisha kazi yako ya nje, na utayarishe kila kitu shambani;

Kisha uijenge nyumba* yako.

28 Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako pasipo msingi.+

Usiitumie midomo yako kuwadanganya wengine.+

29 Usiseme: “Nitamtendea kama tu alivyonitendea;

Nitamlipiza kwa sababu ya mambo aliyonitendea.”*+

30 Nilipita karibu na shamba la mtu mvivu,+

Karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na busara.*

31 Niliona limejaa magugu;

Ardhi ilifunikwa na miiba,

Na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.+

32 Nilitazama hilo na kulitia moyoni;

Nililiona na kujifunza somo hili:*

33 Lala kidogo, sinzia kidogo,

Kunja mikono kidogo ili upumzike,

34 Na umaskini wako utakuja kama jambazi,

Na uhitaji wako kama mwanamume mwenye silaha.+

25 Hizi pia ni methali za Sulemani+ zilizonakiliwa* na watu wa Hezekia+ mfalme wa Yuda:

 2 Ni utukufu wa Mungu kutunza jambo likiwa siri,+

Na utukufu wa wafalme ni kulichunguza jambo kabisa.

 3 Kama mbingu zilivyo juu na kama dunia ilivyo na kina,

Ndivyo moyo wa wafalme usivyochunguzika.

 4 Ondoa takataka katika fedha,

Nayo itakuwa safi kabisa.+

 5 Mwondoe mtu mwovu mbele ya mfalme,

Na kiti chake cha ufalme kitaimarishwa kabisa katika uadilifu.+

 6 Usijiheshimu mwenyewe mbele ya mfalme,+

Wala usijiingize miongoni mwa watu mashuhuri,+

 7 Kwa maana ni afadhali yeye akuambie, “Njoo hapa juu,”

Kuliko akuaibishe mbele ya mkuu.+

 8 Usiharakishe kupeleka kesi mahakamani,

Kwa maana utafanya nini baadaye jirani yako akikuaibisha?+

 9 Suluhisha jambo hilo na jirani yako,+

Lakini usifunue uliyoambiwa sirini,*+

10 Ili anayesikiliza asikuaibishe

Nawe ueneze habari mbaya ambayo haiwezi* kubatilishwa.

11 Kama matofaa ya dhahabu yaliyonakshiwa kwenye vyombo vya fedha

Ndivyo lilivyo neno linalosemwa wakati unaofaa.+

12 Kama kipuli cha dhahabu na pambo la dhahabu bora

Ndivyo alivyo mkaripiaji mwenye hekima kwa sikio linalosikia.+

13 Kama baridi ya theluji siku ya mavuno

Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wanaomtuma,

Kwa maana yeye humburudisha bwana wake.+

14 Kama mawingu na upepo usioleta mvua

Ndivyo alivyo mtu anayejigamba kwamba atatoa zawadi lakini haitoi kamwe.*+

15 Kwa subira kamanda hushawishiwa,

Na ulimi laini* unaweza kuvunja mfupa.+

16 Ukipata asali, kula kiasi kinachokutosha,

Kwa maana ukiila kupita kiasi, huenda ukaitapika.+

17 Mguu wako na uwe haba katika nyumba ya jirani yako,

Ili asikuchoke na kukuchukia.

18 Kama rungu la vita na upanga na mshale mkali

Ndivyo alivyo mtu anayetoa ushahidi wa uwongo dhidi ya jirani yake.+

19 Kama jino lililovunjika au mguu unaochechemea

Ndivyo ilivyo kumtumaini mtu asiyetegemeka* nyakati za taabu.

20 Kama mtu anayevua nguo siku ya baridi

Na kama siki iliyomwagwa kwenye magadi

Ndivyo alivyo mtu anayeuimbia nyimbo moyo wenye huzuni.+

21 Ikiwa adui yako* ana njaa, mpe mkate ale;

Ikiwa ana kiu, mpe maji anywe,+

22 Kwa maana utakuwa unakusanya makaa ya mawe yanayowaka juu ya kichwa chake,*+

Na Yehova atakuthawabisha.

23 Upepo wa kaskazini huleta mvua,

Na ulimi unaopiga porojo huleta uso wenye hasira.+

24 Ni afadhali kuishi pembeni juu ya paa

Kuliko kuishi katika nyumba moja na mke mgomvi.*+

25 Kama maji baridi kwa nafsi* iliyochoka

Ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.+

26 Kama chemchemi yenye matope na kisima kilichochafuliwa

Ndivyo alivyo mtu mwadilifu anayekubali kumfuata* mtu mwovu.

27 Si vizuri kula asali nyingi mno,+

Wala si utukufu kujitafutia utukufu wako mwenyewe.+

28 Kama jiji lililobomolewa, lisilo na ukuta,

Ndivyo alivyo mtu asiyeweza kuidhibiti hasira yake.*+

26 Kama theluji wakati wa kiangazi na mvua wakati wa mavuno,

Ndivyo heshima isivyomfaa mpumbavu.+

 2 Kama ndege alivyo na sababu ya kukimbia na mbayuwayu kuruka,

Ndivyo laana isivyokuja bila sababu nzuri.*

 3 Mjeledi ni wa farasi, lijamu ni ya punda,+

Na fimbo ni ya mgongo wa watu wapumbavu.+

 4 Usimjibu mpumbavu kulingana na ujinga wake,

Ili usiwe kama yeye.*

 5 Mjibu mpumbavu kulingana na ujinga wake,

Ili asifikiri kwamba ana hekima.+

 6 Kama mtu anayeilemaza miguu yake na kujidhuru mwenyewe*

Ndivyo alivyo mtu anayemkabidhi mambo mpumbavu.

 7 Kama miguu inayochechemea* ya walemavu,

Ndivyo ilivyo methali kinywani mwa watu wapumbavu.+

 8 Kama jiwe linavyofungwa kwenye kombeo,

Ndivyo ilivyo kumpa utukufu mtu mpumbavu.+

 9 Kama mmea wa miiba mkononi mwa mlevi,

Ndivyo ilivyo methali kinywani mwa watu wapumbavu.

10 Kama mpiga mishale anayemjeruhi yeyote yule,*

Ndivyo alivyo mtu anayemwajiri mpumbavu au wapita njia.

11 Kama mbwa anayerudia matapishi yake,

Ndivyo mpumbavu anavyorudia ujinga wake.+

12 Je, umemwona mtu anayefikiri ana hekima?+

Kuna tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwa mtu huyo.

13 Mvivu anasema: “Kuna mwanasimba barabarani,

Kuna simba katika uwanja wa jiji!”+

14 Mlango huzunguka-zunguka katika bawaba zake,*

Na mvivu hugeuka-geuka kitandani mwake.+

15 Mvivu huutumbukiza* mkono wake katika bakuli la karamu,

Lakini amechoka sana kuurudisha kinywani mwake.+

16 Mvivu hufikiri kwamba ana hekima zaidi

Kuliko watu saba wanaojibu kwa busara.

17 Kama mtu anayemkamata mbwa masikio

Ndivyo alivyo mpita njia anayekasirishwa na* ugomvi usiomhusu.+

18 Kama mwenda wazimu anayetupa vishale vinavyowaka moto, mishale, na kifo*

19 Ndivyo alivyo mtu anayemhadaa jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”+

20 Pasipo na kuni moto huzimika,

Na pasipo na mchongezi, ugomvi hukoma.+

21 Kama makaa yanavyoongezwa kwenye makaa yanayozimika na kuni zinavyoongezwa motoni,

Ndivyo mtu mgomvi anavyochochea ugomvi.+

22 Maneno ya mchongezi ni kama matonge matamu;*

Humezwa na kushuka tumboni moja kwa moja.+

23 Kama fedha inayopakwa juu ya chombo cha udongo

Ndivyo yalivyo maneno ya upendo yanayotoka katika* moyo mwovu.+

24 Anayewachukia wengine huficha chuki hiyo kwa midomo yake,

Lakini ndani amesitiri udanganyifu.

25 Ingawa anaongea kwa fadhili, usimwamini,

Kwa maana kuna mambo saba yanayochukiza moyoni mwake.*

26 Ingawa chuki yake imefichwa kwa udanganyifu,

Uovu wake utafunuliwa kutanikoni.

27 Anayechimba shimo ataanguka ndani yake,

Na yeyote anayebingirisha jiwe—litamrudia.+

28 Ulimi unaosema uwongo huwachukia watu uliowaponda,

Na kinywa kinachosifusifu huleta uharibifu.+

27 Usijigambe kuhusu kesho,

Kwa maana hujui siku italeta nini.*+

 2 Acha mtu mwingine* akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe;

Wengine,* wala si midomo yako mwenyewe.+

 3 Jiwe ni zito na mchanga ni mzito sana,

Lakini usumbufu unaosababishwa na mjinga ni mzito kuliko vyote viwili.+

 4 Kuna ukatili wa ghadhabu na mafuriko ya hasira,

Lakini ni nani anayeweza kustahimili wivu?+

 5 Karipio la wazi ni afadhali kuliko upendo uliofichwa.+

 6 Majeraha yanayosababishwa na rafiki ni ya uaminifu,+

Lakini mabusu ya adui ni mengi.*

 7 Yule aliyetosheleza hamu yake hukataa* asali ya sega,

Lakini kwa mwenye njaa, hata kilicho kichungu ni kitamu.

 8 Kama ndege anayeenda* mbali kutoka kwenye kiota chake

Ndivyo alivyo mtu anayetangatanga mbali kutoka nyumbani kwake.

 9 Mafuta na uvumba huufanya moyo ushangilie;

Ndivyo ulivyo urafiki mtamu unaochipuka kutokana na shauri la unyoofu.*+

10 Usimwache rafiki yako au rafiki ya baba yako,

Wala usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku ya msiba wako;

Ni afadhali jirani aliye karibu kuliko ndugu aliye mbali.+

11 Uwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie,+

Ili niweze kumjibu yule anayenidhihaki.+

12 Mtu mwerevu huona hatari na kujificha,+

Lakini wajinga husonga mbele na kupata madhara.*

13 Chukua vazi la mtu ikiwa amemdhamini mtu asiyemjua;

Chukua dhamana kutoka kwake ikiwa alimfanyia hivyo mwanamke mgeni.*+

14 Mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kubwa asubuhi na mapema,

Itaonwa kuwa laana.

15 Mke mgomvi* ni kama paa linalovuja maji mfululizo siku ya mvua.+

16 Yeyote anayeweza kumzuia anaweza kuuzuia upepo

Naye anaweza kuyakamata mafuta kwa mkono wake wa kulia.

17 Kama chuma kinavyonoa chuma,

Ndivyo mtu anavyomnoa* rafiki yake.+

18 Anayeutunza mtini atakula matunda yake,+

Na anayemtunza bwana wake ataheshimiwa.+

19 Kama maji yanavyoonyesha* uso wa mtu,

Ndivyo moyo wa mtu unavyoonyesha* moyo wa mwingine.

20 Kaburi na mahali pa maangamizi* havitosheki kamwe,+

Wala macho ya mwanadamu hayatosheki kamwe.

21 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,+

Vivyo hivyo mtu hupimwa kwa sifa anayopokea.*

22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi*

Kama nafaka iliyopondwa katika kinu,

Upumbavu wake hautamtoka.

23 Unapaswa kujua vizuri hali ya kundi lako.

Watunze vizuri* kondoo wako,+

24 Kwa maana mali haidumu milele,+

Wala taji halidumu vizazi vyote.

25 Majani mabichi hutoweka, na majani mapya huchipuka,

Na majani ya milimani yanakusanywa.

26 Wanakondoo dume hukupatia mavazi yako,

Na mbuzi dume hukupatia malipo ya shamba.

27 Nawe utakuwa na maziwa ya mbuzi yanayotosha kukulisha wewe,

Kuilisha familia yako, na kuwategemeza vijakazi wako.

28 Waovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayewakimbiza,

Lakini waadilifu wana ujasiri kama simba.*+

 2 Kunapokuwa na uovu* nchini, nchi inakuwa na kiongozi mmoja baada ya mwingine,+

Lakini kwa msaada wa mtu mwenye utambuzi na ujuzi, kiongozi atadumu kwa muda mrefu.+

 3 Mtu maskini anayempunja mtu wa hali ya chini+

Ni kama mvua inayofagilia mbali chakula chote.

 4 Wale wanaoiacha sheria humsifu mtu mwovu,

Lakini wale wanaoishika sheria huwakasirikia.+

 5 Waovu hawawezi kuelewa haki,

Lakini wale wanaomtafuta Yehova wanaweza kuelewa mambo yote.+

 6 Ni afadhali maskini anayetembea kwa utimilifu wake

Kuliko tajiri ambaye njia zake zimepotoka.+

 7 Mwana mwenye uelewaji hushika sheria,

Lakini rafiki ya walafi humwaibisha baba yake.+

 8 Anayezidisha mali zake kwa faida+ na riba

Humkusanyia yule anayemtendea maskini kwa fadhili.+

 9 Anayekataa kusikiliza sheria

—Hata sala yake inachukiza.+

10 Anayempotosha mnyoofu afuate njia ya uovu ataanguka katika shimo lake mwenyewe,+

Lakini wasio na lawama watarithi kilicho chema.+

11 Tajiri hujiona mwenyewe kuwa mwenye hekima,+

Lakini mtu maskini aliye na utambuzi anaweza kumchunguza kabisa.+

12 Waadilifu wanaposhinda, kuna utukufu mwingi,

Lakini waovu wanapopata mamlaka, watu hujificha.+

13 Anayefunika makosa yake hatafanikiwa,+

Lakini yeyote anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+

14 Mwenye furaha ni mtu aliye chonjo sikuzote,*

Lakini yeyote anayeufanya moyo wake kuwa mgumu ataanguka katika msiba.+

15 Kama simba anayenguruma na dubu anayeshambulia

Ndivyo alivyo mtawala mwovu anayewatawala watu wasio na uwezo.+

16 Kiongozi asiye na utambuzi hutumia vibaya mamlaka yake,+

Lakini mtu anayechukia faida isiyo ya haki atarefusha maisha yake.+

17 Mtu aliyelemewa na hatia ya damu kwa sababu ya kumuua mwingine* ataendelea kukimbia mpaka kaburini.*+

Mtu yeyote asimsaidie.

18 Anayetembea bila kosa ataokolewa,+

Lakini yule ambaye njia zake zimepotoka ataanguka ghafla.+

19 Anayelima ardhi yake atakuwa na chakula kingi,*

Lakini anayefuatia vitu visivyo na thamani atakuwa na umaskini wa kutosha.+

20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi,+

Lakini anayeharakisha kupata utajiri hatabaki bila hatia.+

21 Si vema kuonyesha upendeleo;+

Lakini mtu anaweza kukosea kwa sababu ya kipande cha mkate.

22 Mtu mwenye wivu* hujitahidi sana kupata mali,

Lakini hajui kwamba umaskini utamkumba.

23 Yeyote anayemkaripia mwingine+ hatimaye atapata kibali zaidi+

Kuliko mtu anayesifusifu kwa ulimi wake.

24 Yeyote anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Si kosa,”+

Ni rafiki ya mtu anayesababisha uharibifu.+

25 Mtu mwenye pupa* huchochea mgawanyiko,

Lakini yeyote anayemtegemea Yehova atapata ufanisi.*+

26 Yeyote anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu,+

Lakini anayetembea kwa hekima ataponyoka.+

27 Yeyote anayewapa maskini hatakosa chochote,+

Lakini yule anayewafumbia macho atapata laana nyingi.

28 Waovu wanapopata mamlaka, mtu hujificha,

Lakini wanapoangamia, waadilifu huongezeka.+

29 Mtu anayeifanya shingo yake kuwa ngumu baada ya kukaripiwa sana+

Atavunjwa kwa ghafla, naye hataweza kupona.+

 2 Waadilifu wanapokuwa wengi, watu hushangilia,

Lakini mwovu anapotawala, watu hulia kwa maumivu.+

 3 Mtu anayependa hekima humfanya baba yake ashangilie,+

Lakini rafiki ya makahaba hutumia vibaya mali yake.+

 4 Kwa haki mfalme huleta uthabiti nchini,+

Lakini mtu anayetafuta rushwa huiharibu.

 5 Mtu anayemsifusifu jirani yake

Anautandaza wavu wa kuinasa miguu yake.+

 6 Kosa la mtu mbaya humnasa yeye mwenyewe,+

Lakini mwadilifu hupaza sauti kwa shangwe na kufurahi.+

 7 Mwadilifu hujali haki za kisheria za maskini,+

Lakini mwovu hajali kamwe.+

 8 Watu wanaojigamba huuwasha moto mji,+

Lakini wenye hekima hutuliza hasira.+

 9 Mtu mwenye hekima anapobishana na mpumbavu,

Kutakuwa na kelele na dhihaka, lakini hawataridhika.+

10 Watu wenye kiu ya damu humchukia mtu yeyote asiye na hatia,*+

Nao hujaribu kumuua mnyoofu.*

11 Mtu mpumbavu humwaga hisia zake zote,*+

Lakini mwenye hekima huzizuia kwa utulivu.+

12 Mtawala anaposikiliza uwongo,

Watumishi wake wote watakuwa waovu.+

13 Maskini na mkandamizaji wanafanana katika jambo hili:*

Yehova huyapa nuru macho ya wote wawili.*

14 Mfalme anapowahukumu maskini kwa haki,+

Kiti chake cha ufalme kitakuwa salama daima.+

15 Fimbo* na karipio hufunza hekima,+

Lakini mtoto aliyeachiliwa humwaibisha mama yake.

16 Waovu wanapoongezeka, uovu huongezeka,

Lakini waadilifu watawaona wakianguka.+

17 Mtie nidhamu mwana wako naye atakupumzisha;

Atakufurahisha sana.+

18 Wakati hakuna maono,* watu hufanya wapendavyo,+

Lakini wenye furaha ni wale wanaoishika sheria.+

19 Mtumishi hatakubali kurekebishwa kwa maneno,

Kwa maana ingawa anaelewa, hatii.+

20 Je, umemwona mtu anayeongea bila kufikiri?+

Kuna tumaini zaidi kwa mjinga kuliko yeye.+

21 Mtumishi akibembelezwa tangu ujana wake,

Baadaye atakuwa mtu asiye na shukrani.

22 Mtu anayekasirika upesi huchochea ugomvi;+

Yeyote aliye mwepesi wa ghadhabu hufanya makosa mengi.+

23 Kiburi cha mtu kitamnyenyekeza,+

Lakini yeyote aliye mnyenyekevu rohoni atapata utukufu.+

24 Rafiki ya mwizi hujichukia mwenyewe.

Huenda akasikia tangazo la kutoa ushahidi,* lakini hatoi habari yoyote.+

25 Kuwaogopa* wanadamu ni mtego,+

Lakini yule anayemtumaini Yehova atalindwa.+

26 Watu wengi hutaka kukutana na* mfalme,

Lakini mtu hupata haki kutoka kwa Yehova.+

27 Mtu asiyetenda haki humchukiza mwadilifu,+

Lakini yule ambaye njia yake imenyooka humchukiza mwovu.+

30 Ujumbe mzito wa Aguri mwana wa Yake, aliomwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.

 2 Mimi ni mjinga kuliko mtu yeyote yule,+

Nami sina uelewaji ambao mwanadamu anapaswa kuwa nao.

 3 Sijajifunza hekima,

Nami sina ujuzi kumhusu Aliye Mtakatifu Zaidi.

 4 Ni nani amepanda mbinguni kisha akashuka?+

Ni nani ameukusanya upepo katika viganja vyake viwili?

Ni nani ameyafunga maji katika vazi lake?+

Ni nani ameimarisha* miisho yote ya dunia?+

Jina lake ni nani nalo jina la mwana wake ni nani—ikiwa unajua?

 5 Kila neno la Mungu ni safi.+

Yeye ni ngao kwa wale wanaomkimbilia.+

 6 Usiongeze chochote katika maneno yake,+

La sivyo atakukaripia,

Nawe utathibitika kuwa mwongo.

 7 Ninakuomba mambo mawili.

Usininyime mambo hayo kabla sijafa.

 8 Yaondolee mbali nami mambo yasiyo ya kweli na ya uwongo.+

Usinipe umaskini wala utajiri.

Acha nile tu fungu langu la chakula,+

 9 Ili nisishibe na kukukana na kusema, “Yehova ni nani?”+

Wala usiruhusu niwe maskini, niibe na kuliaibisha* jina la Mungu wangu.

10 Usimchongee mtumishi kwa bwana wake,

La sivyo atakulaani, nawe utapatikana na hatia.+

11 Kuna kizazi kinachomtukana baba yao

Nacho hakimbariki mama yao.+

12 Kuna kizazi kinachojiona kuwa safi+

Lakini hakijasafishwa uchafu wake.*

13 Kuna kizazi chenye macho yaliyojaa kiburi

Na ambacho macho yake yanatazama kwa majivuno mengi!+

14 Kuna kizazi ambacho meno yake ni mapanga

Na ambacho mataya yake ni visu vya kuchinjia;

Wanawanyafua watu wa hali ya chini duniani

Na maskini kutoka miongoni mwa wanadamu.+

15 Ruba wana mabinti wawili wanaolia, “Nipe! Nipe!”

Kuna vitu vitatu visivyotosheka,

Vinne ambavyo havisemi kamwe, “Inatosha!”

16 —Kaburi*+ na tumbo lisiloweza kuzaa,

Nchi iliyonyimwa maji,

Na moto ambao kamwe hausemi, “Inatosha!”

17 Jicho linalomdhihaki baba na kudharau kumtii mama+

—Kunguru wa bondeni* wataling’oa,

Na tai wachanga watalila.+

18 Kuna mambo matatu yanayozidi ufahamu wangu,*

Na manne ambayo siyaelewi:

19 Njia ya tai angani,

Njia ya nyoka juu ya mwamba,

Njia ya meli baharini,

Na njia ya mwanamume pamoja na mwanamwali.

20 Hii ndiyo njia ya mwanamke mzinzi:

Anakula, anajipangusa kinywa;

Kisha anasema, “Sijafanya kosa lolote.”+

21 Kuna mambo matatu yanayoitetemesha dunia

Na mambo manne ambayo haiwezi kuvumilia:

22 Mtumwa anapotawala akiwa mfalme,+

Mjinga anaposhiba kupita kiasi,

23 Mwanamke anayechukiwa* anapoolewa,

Na kijakazi anapochukua nafasi ya bimkubwa wake.+

24 Kuna vitu vinne duniani ambavyo ni miongoni mwa vitu vidogo zaidi,

Lakini vina hekima ya kisilika:*+

25 Chungu si viumbe wenye nguvu,*

Lakini wanatayarisha chakula chao wakati wa kiangazi.+

26 Wibari*+ si viumbe wenye nguvu,*

Lakini wanajenga nyumba zao kwenye majabali.+

27 Nzige+ hawana mfalme,

Lakini wote husonga mbele kwa mpangilio.*+

28 Mjusi+ hushika kwa miguu yake,

Naye huingia katika jumba la mfalme.

29 Kuna viumbe watatu wenye mwendo unaovutia,

Wanne wenye mwendo wa madaha:

30 Simba, mnyama mwenye nguvu zaidi kuliko wanyama wote,

Ambaye hamkimbii yeyote;+

31 Mbwa mwindaji; mbuzi dume;

Na mfalme aliye pamoja na jeshi lake.

32 Ikiwa umejikweza kwa ujinga+

Au ikiwa umepanga kufanya hivyo,

Funika kinywa chako kwa mkono wako.+

33 Kwa maana kama vile kusukasuka maziwa kunavyotokeza siagi

Na kufinya pua kunavyofanya damu itoke,

Ndivyo kuchochea hasira kunavyotokeza ugomvi.+

31 Maneno ya Mfalme Lemueli, ujumbe mzito ambao mama yake alimpa ili kumfundisha:+

 2 Nikwambie nini, ewe mwanangu,

Niseme nini, ewe mwana wa tumbo langu,

Nikwambie nini, ewe mwana wa nadhiri zangu?+

 3 Usiwape wanawake nguvu zako,+

Wala kufuata njia zinazowaangamiza wafalme.+

 4 Si vema kwa wafalme, ewe Lemueli,

Si vema kwa wafalme kunywa divai

Wala watawala kuuliza, “Kiko wapi kinywaji changu?”+

 5 Ili wasinywe na kusahau maagizo

Na kupotosha haki za watu wa hali ya chini.

 6 Wape kileo watu wanaoangamia+

Na divai wale wanaoteseka vikali.*+

 7 Acha wanywe na kusahau umaskini wao;

Na wasikumbuke tena taabu yao.

 8 Watetee wasioweza kuzungumza;

Tetea haki za wote wanaoangamia.+

 9 Sema waziwazi na uhukumu kwa uadilifu;

Tetea haki za* watu wa hali ya chini na maskini.+

א [Aleph]

10 Ni nani anayeweza kumpata mke mwema?*+

Thamani yake inazidi kabisa thamani ya marijani.*

ב [Beth]

11 Mume wake humwamini kutoka moyoni,

Na mume huyo hakosi chochote chenye thamani.

ג [Gimel]

12 Humthawabisha mume wake kwa mema, wala si kwa mabaya,

Sikuzote za maisha yake.

ד [Daleth]

13 Hujipatia sufu na kitani;

Hufurahia kufanya kazi kwa mikono yake.+

ה [He]

14 Yeye ni kama meli za mfanyabiashara,+

Huleta chakula chake kutoka mbali.

ו [Waw]

15 Pia yeye huamka kabla ya mapambazuko,

Na kuwaandalia chakula watu wa nyumbani mwake

Na kuwapa mafungu vijakazi wake.+

ז [Zayin]

16 Hulikazia fikira shamba na kulinunua;

Hupanda shamba la mizabibu kwa jasho lake.*

ח [Heth]

17 Hujitayarisha kwa ajili ya kazi ngumu,*+

Naye huitia nguvu mikono yake.

ט [Teth]

18 Huhakikisha kwamba biashara yake ina faida;

Taa yake haizimiki usiku.

י [Yod]

19 Mikono yake hushika kijiti cha kusokotea uzi,

Na mikono yake hushika gurudumu la mfumaji.+

כ [Kaph]

20 Humnyooshea mkono mtu wa hali ya chini,

Huwafumbulia maskini mikono yake.+

ל [Lamed]

21 Wakati wa theluji hana wasiwasi kuhusu watu wa nyumbani mwake,

Kwa sababu watu wote wa nyumbani mwake wamevaa mavazi yenye joto.*

מ [Mem]

22 Hujitengenezea matandiko ya kufunika kitanda.

Mavazi yake ni ya kitani na sufu ya zambarau.

נ [Nun]

23 Mume wake anajulikana sana kwenye malango ya jiji,+

Ambapo huketi pamoja na wazee wa nchi.

ס [Samekh]

24 Hufuma nguo za kitani* na kuziuza

Na kuwauzia mishipi wafanyabiashara.

ע [Ayin]

25 Amevaa nguvu na fahari,

Naye huutazamia wakati ujao kwa uhakika.*

פ [Pe]

26 Hufumbua kinywa chake kwa hekima;+

Sheria ya fadhili iko* kwenye ulimi wake.

צ [Tsade]

27 Huangalia shughuli za nyumbani mwake,

Naye hali mkate wa uvivu.+

ק [Qoph]

28 Watoto wake husimama na kumtangaza kuwa mwenye furaha;

Mume wake husimama na kumsifu.

ר [Resh]

29 Kuna wanawake wengi walio wema,*

Lakini wewe—wewe umewapita wote hao.

ש [Shin]

30 Sura nzuri inaweza kudanganya, na huenda urembo ukatoweka upesi,*+

Lakini mwanamke anayemwogopa Yehova atasifiwa.+

ת [Taw]

31 Mpeni thawabu kwa mambo anayofanya,*+

Kazi zake na zimsifu kwenye malango ya jiji.+

Au “ajue.”

Au “jambo lililo la haki.”

Au “kutokuwa na ubaguzi.”

Au “mwongozo wenye hekima.”

Au “mfano.”

Au “Kumheshimu.”

Au “usiiache sheria.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “Liweke fungu lako pamoja na letu.”

Au “tutakuwa na mfuko mmoja (kibeti kimoja).”

Au “waangamize nafsi za.”

Au “Geukeni ninapowakaripia.”

Tnn., “watakula matunda.”

Au “njama zao; mipango yao.”

Yaani, madini ya fedha.

Angalia Kamusi.

Tnn., “mgeni.” Ni wazi kwamba ni mgeni machoni pa Mungu kwa sababu ya upotovu wa maadili.

Au “maneno yenye ushawishi.”

Tnn., “mgeni.” Ni wazi kwamba ni mgeni machoni pa Mungu kwa sababu ya upotovu wa maadili.

Au “mume.”

Tnn., “mapito yake.”

Tnn., “anayeingia kwake.”

Au “wanaoshika utimilifu.”

Au “sheria.”

Au “ukweli.”

Tnn., “usiegemee.”

Tnn., “kitovu chako.”

Au “vitu vilivyo bora vya.”

Au “mapato.”

Au “mashinikizo yako ya divai yatafurika.”

Angalia Kamusi.

Ni wazi kwamba mstari huu unarejelea sifa za Mungu zinazotajwa katika mistari iliyotangulia.

Au “hautagonga kamwe kitu chochote.”

Au “wale wanaostahili.”

Au “Ikiwa mkono wako una nguvu za kusaidia.”

Au “sheria.”

Au “la msingi.”

Tnn., “Yategee sikio.”

Au “macho yako yanayong’aa.”

Au labda, “Chunguza kwa makini.”

Tnn., “Utegee sikio.”

Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “nguvu.”

Tnn., “Katikati ya kusanyiko na kutaniko.”

Au “baridi.”

Au “Chanzo chako cha maji na kibarikiwe.”

Au “mbuzi mwitu.”

Au “yakuleweshe.”

Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.

Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.

Tnn., “umemwekea dhamana.”

Yaani, Unapomdhamini.

Au “usiiache sheria.”

Au “itakufundisha.”

Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.

Au “huiwinda nafsi yenye.”

Au “aijaze nafsi yake.”

Tnn., “amepungukiwa moyoni.”

Au “ridhaa.”

Au “sheria.”

Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.

Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.

Au “yenye ushawishi.”

Au “wasio na uzoefu.”

Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”

Au “Akiwa na mavazi ya.”

Tnn., “Miguu yake haikai.”

Au “pingu.”

Au “nafsi yake.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “kila mwanadamu.”

Tnn., “eleweni moyo.”

Angalia Kamusi.

Au “Kanuni zilizorithiwa.”

Au “zamani za kale.”

Au “nilizaliwa kana kwamba kwa uchungu wa kuzaa.”

Tnn., “Alipopiga duara.”

Au “Alipotunga sheria kuhusu.”

Au “Kwa kukesha.”

Au “anaidhuru nafsi yake.”

Tnn., “Amechinja nyama yake.”

Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”

Au “Waache wajinga.”

Tnn., “waliopungukiwa moyoni.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “Sifa.”

Tnn., “amri.”

Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”

Au “Kitu chenye thamani cha.”

Au labda, “yuko kwenye kijia kinachoelekea kwenye uzima.”

Au “uvumi unaodhuru.”

Au “huwaongoza.”

Au “huzuni; dhiki.”

Au “mwajiri wake.”

Au “Tumaini la.”

Au “huzaa tunda la.”

Au “udanganyifu.”

Au “jiwe kamili la kupimia.”

Au “Vitu vyenye thamani havitakuwa.”

Au “mtu anayemkataa Mungu.”

Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”

Tnn., “mwaminifu rohoni.”

Tnn., “hufunika jambo.”

Au “Mwongozo wenye hekima.”

Au “wokovu.”

Au “rehani.”

Tnn., “anayechukia.”

Au “anayevutia.”

Au “Mtu mwenye upendo mshikamanifu.”

Au “huitendea mema nafsi yake.”

Au “aibu.”

Tnn., “Mkono kwa mkono.”

Tnn., “hutawanya.”

Tnn., “atanenepeshwa.”

Tnn., “anayewanywesha wengine kwa ukarimu.”

Au “aibu.”

Au “anayezishawishi.”

Angalia Kamusi.

Au “hana ufahamu.”

Au “mwenye uwezo.”

Tnn., “huvizia ili kumwaga damu.”

Tnn., “mkate.”

Au “huitunza nafsi ya mnyama anayemfuga.”

Tnn., “amepungukiwa moyoni.”

Tnn., “kinywa chake.”

Au “mashauri.”

Au “siku hiyohiyo.”

Tnn., “hufunika.”

Tnn., “mambo ya uadilifu.”

Tnn., “Lakini washauri wa.”

Au “humfanya ashuke moyo.”

Au “rekebisho.”

Tnn., “kinywa chake.”

Au “Lakini nafsi hasa.”

Au “anailinda nafsi yake.”

Tnn., “atanenepeshwa.”

Tnn., “hawasikii kemeo lolote.”

Tnn., “hushangilia.”

Au “wanaoshauriana.”

Au “Mali inayotokana na ubatili.”

Tnn., “anayekusanya kwa mkono.”

Au “Tumaini lililoahirishwa.”

Au “neno.”

Au “Sheria.”

Au “karipio.”

Au “nafsi.”

Au “anaweza.”

Au “asiyetoa nidhamu; adhabu.”

Au labda, “bila kukawia.”

Au “nafsi.”

Au “zimepotoka.”

Au labda, “wapumbavu huwadanganya wengine.”

Au “hufanya mzaha wanapoambiwa wafanye marekebisho.”

Au “Lakini kuna nia njema kati ya wanyoofu.”

Au “uchungu wa nafsi yake.”

Au “Asiye na uzoefu.”

Au “ana hasira kali.”

Au “mwenye uwezo wa kufikiri.”

Au “Asiye na uzoefu.”

Au “nafsi.”

Au “afya.”

Au “tulivu.”

Au “linaloumiza.”

Au “Ulimi unaoponya.”

Tnn., “huiponda roho.”

Au “karipio.”

Au “mapato.”

Au “kali.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “na Abadoni.”

Au “anayemkaripia.”

Au “hufuatia.”

Au “mzuri.”

Au “vurugu.”

Tnn., “aliyelishwa kwenye hori.”

Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”

Au “watu wasipokuwa na mazungumzo ya siri.”

Tnn., “hushangilia jibu la kinywa chake.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “aibu.”

Au “hufikiria kwa uangalifu jinsi ya kujibu; hufikiria kabla ya kuongea.”

Au “Kumtupia mtu jicho kwa uchangamfu.”

Tnn., “huinenepesha mifupa.”

Au “anaidharau nafsi yake.”

Tnn., “moyo.”

Tnn., “Mipangilio ya moyo ni ya mtu.”

Au “jibu linalofaa.” Tnn., “jibu la ulimi.”

Tnn., “safi.”

Tnn., “huzichunguza roho.”

Tnn., “Mvingirishie Yehova kazi zako.”

Tnn., “Mkono kwa mkono.”

Au “Uamuzi ulioongozwa na Mungu.”

Au “huiepuka.”

Au “nafsi yake.”

Tnn., “na roho ya upole.”

Tnn., “mema.”

Au “Na maneno yanayovutia.” Tnn., “Na utamu wa midomo.”

Au “Yana ladha tamu.” Angalia Kamusi.

Au “Nafsi.”

Tnn., “mdomo wake.”

Au “Mpanga njama.”

Au “utukufu.”

Tnn., “anayetawala roho yake.”

Au “utulivu.”

Tnn., “dhabihu.”

Au “wazazi.”

Au “watoto.”

Au “mazuri.”

Au “kiongozi.”

Au “ni kito kinachomletea kibali.”

Tnn., “anayefunika.”

Au “kufungulia maji bwawani.” Tnn., “kufungulia maji.”

Au “Ilhali hana busara?”

Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”

Tnn., “mema.”

Au “humsaidia mtu kupona.”

Au “huikausha kabisa mifupa.”

Tnn., “rushwa kutoka kifuani.”

Tnn., “Na kumletea uchungu.”

Au “kumtoza faini.”

Tnn., “atabaki na roho iliyotulia.”

Au “Hudharau.”

Au “nafsi yake.”

Au “vitu vinavyomezwa kwa pupa.”

Tnn., “na kuinuliwa juu,” yaani, hawezi kufikiwa, yuko salama.

Au “iliyokata tamaa kabisa?”

Au “kumhoji.”

Tnn., “Na kuwatenganisha.”

Tnn., “kinywa chake.”

Au “nia njema ya.”

Tnn., “anayetembea haraka.”

Au “mkarimu.”

Tnn., “moyo.”

Au “anaipenda nafsi yake.”

Tnn., “mema.”

Tnn., “kupita.”

Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”

Au “msumbufu.”

Au “anailinda nafsi yake.”

Au “Atamthawabisha.”

Au “mwana.”

Au “usitamani.”

Au “kusudi.”

Tnn., “huuzika.”

Au “Kuogopesha.”

Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”

Au labda, “Atatazama wakati wa mavuno lakini hatapata chochote.”

Au “Makusudio.” Tnn., “Mashauri.”

Tnn., “Wana.”

Au “Mawe mawili ya kupimia yaliyo tofauti na vyombo viwili vya kupimia vilivyo tofauti.”

Au “mvulana.”

Angalia Kamusi.

Au “mgeni.”

Au “mashauri.”

Au “itaimarishwa.”

Au “mwongozo wenye hekima.”

Au “anayeshawishi kwa midomo yake.”

Au “Mawe mawili ya kupimia yaliyo tofauti yanamchukiza.”

Au “njia ya kufuata.”

Au “husugua na kuondoa.”

Au “huzichunguza nia.”

Au “manufaa.”

Au labda, “kwa wale wanaotafuta kifo.”

Au “msumbufu.”

Au “anajua la kufanya.”

Tnn., “iliyo kifuani.”

Au “anasa.”

Au “msumbufu.”

Tnn., “atavimeza.”

Au “kulishinda.”

Au “akiwa na mwenendo wa aibu!”

Tnn., “atazungumza milele.”

Au “mtu mnyoofu huifanya njia yake iwe hakika.”

Au “sifa njema.” Tnn., “jina.”

Tnn., “Kibali.”

Tnn., “hukutana.”

Au “adhabu.”

Au “nafsi yake.”

Au “mtoto; kijana.”

Tnn., “Aliye na jicho zuri.”

Au “Kesi.”

Tnn., “wageni.”

Au “mtoto; kijana.”

Au “Jizuie.”

Au “una nafsi iliyojaa tamaa.”

Au labda, “Acha kufuata uelewaji wako mwenyewe.”

Au “cha yeyote mwenye jicho ovu.”

Au “anayehesabu katika nafsi yake.”

Tnn., “moyo wake hauko pamoja nawe.”

Tnn., “Mkombozi.”

Au “mtoto; kijana.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “Jipatie.”

Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.

Au “macho yaliyochoka.”

Au “wanaokusanyika ili kuonjaonja.”

Au “sikuhisi uchungu.”

Au “Nitaitafuta divai tena.”

Au “Familia.”

Au “mwongozo wenye hekima.”

Au “wokovu.”

Au “Njama za mpumbavu.”

Au “nyakati za taabu.”

Au “anayechunguza nia.”

Au “ni tamu kwa nafsi yako.”

Yaani, yule adui.

Au “Usiwake hasira.”

Au “wale wanaotaka mabadiliko.”

Yaani, Yehova na mfalme.

Au labda, “Kujibu kwa unyoofu ni kama kumbusu mtu.”

Au “familia.”

Au “Nitamlipa sawasawa na matendo yake.”

Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”

Tnn., “Nilipokea nidhamu.”

Au “zilizonakiliwa na kukusanywa.”

Au “usifunue siri za wengine.”

Au “uvumi unaodhuru ambao hauwezi.”

Tnn., “kuhusu zawadi ya uwongo.”

Au “mpole.”

Au labda, “mtu mwenye hila.”

Tnn., “anayekuchukia.”

Yaani, kupunguza uadui wake na kuyeyusha ugumu wake.

Au “msumbufu.”

Angalia Kamusi.

Au “anayekubaliana na.” Tnn., “anayepepesuka mbele ya.”

Au “asiyeweza kuizuia roho yake.”

Au labda, “Ndivyo laana isiyostahiliwa isivyompata mtu.”

Au “Ili usilingane naye.”

Tnn., “kunywa ukatili.”

Au “inayoning’inia.”

Au “anayemjeruhi kila mtu.”

Au “maegemeo yake.”

Tnn., “huuzika.”

Au labda, “anayejiingiza katika.”

Au “mishale inayoua.”

Au “vitu vinavyomezwa kwa pupa.”

Tnn., “Ndivyo ilivyo midomo yenye shauku pamoja na.”

Au “Kwa maana moyo wake unachukiza kabisa.”

Tnn., “itazaa nini.”

Tnn., “mtu asiyekujua.”

Tnn., “Wageni.”

Au labda, “si ya unyoofu; ni ya kulazimishwa.”

Tnn., “huikanyagia chini.”

Au “anayekimbia.”

Au “shauri la nafsi.”

Au “adhabu.”

Au “mgeni.”

Au “msumbufu.”

Tnn., “anavyounoa uso wa.”

Au “yanavyoakisi.”

Au “unavyoakisi.”

Au “Sheoli na Abadoni.”

Au “Vivyo hivyo mtu hulingana na sifa yake.”

Au “mtwangio.”

Au “Uweke moyo kwa; Wakazie uangalifu.”

Au “mwanasimba.”

Au “uasi.”

Au “anayeogopa nyakati zote.”

Au “aliyelemewa na damu ya nafsi.”

Au “shimoni.”

Tnn., “mkate mwingi.”

Au “pupa.”

Au labda, “Nafsi yenye kiburi.”

Tnn., “atanenepeshwa.”

Au “lawama.”

Au labda, “Lakini mnyoofu hujaribu kuulinda uhai wake.”

Tnn., “roho yake yote.”

Tnn., “hukutana pamoja.”

Yaani, Huwapa uhai.

Au “Nidhamu; Adhabu.”

Au “maono ya kinabii; ufunuo.”

Au “kiapo kinachohusisha laana.”

Au “Kutetemeshwa na.”

Au labda, “kutafuta kibali cha.” Tnn., “kuutafuta uso wa.”

Tnn., “ameinua.”

Au “kulishambulia.”

Tnn., “kinyesi chake.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “korongoni.”

Au “ambayo ni ya ajabu sana kwangu.”

Au “ambaye hapendwi.”

Au “hekima kupindukia.”

Tnn., “si taifa lenye nguvu.”

Au “Pelele.”

Tnn., “si taifa lenye nguvu.”

Au “vikundi-vikundi.”

Au “wenye uchungu nafsini.”

Au “Tetea kesi ya.”

Au “mwenye uwezo; bora.”

Angalia Kamusi.

Au “kwa mapato yake.” Tnn., “kutokana na matunda ya mikono yake.”

Tnn., “Hufunga nguvu kiunoni mwake.”

Tnn., “mavazi mawili-mawili.”

Au “nguo za ndani.”

Au “huucheka wakati ujao.”

Au “Mafundisho ya upendo yako; Sheria ya upendo mshikamanifu iko.”

Au “mwenye uwezo; bora.”

Au “ukawa ubatili.”

Tnn., “Mpeni baadhi ya matunda ya mikono yake.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki