Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Ufunuo 1:1-22:21
  • Ufunuo kwa Yohana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufunuo kwa Yohana
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Ufunuo kwa Yohana

Ufunuo kwa Yohana

1 Ufunuo+ kupitia Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa,+ kuwaonyesha watumwa+ wake mambo ambayo lazima yatendeke upesi.+ Naye alimtuma malaika+ wake na kupitia yeye akautoa kwa njia ya ishara+ kwa mtumwa wake Yohana,+ 2 aliyetoa ushahidi kuhusu neno ambalo Mungu alitoa+ na kuhusu ushahidi ambao Yesu Kristo alitoa,+ naam, kuhusu mambo yote aliyoyaona. 3 Mwenye furaha+ ni yeye anayesoma kwa sauti+ na wale wanaosikia maneno ya unabii huu,+ na wanaoshika mambo yaliyoandikwa humo;+ kwa maana wakati uliowekwa uko karibu.+

4 Yohana kwa makutaniko saba+ yaliyo katika wilaya ya Asia:

Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa “Yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja,”+ na kutoka kwa zile roho saba+ zilizo mbele ya kiti chake cha ufalme, 5 na kutoka kwa Yesu Kristo, “Shahidi Mwaminifu,”+ “Mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,”+ na “Mtawala wa wafalme wa dunia.”+

Kwake yeye anayetupenda+ na aliyetufungua kutoka katika dhambi zetu kupitia damu yake mwenyewe+— 6 naye alitufanya tuwe ufalme,+ makuhani+ kwa Mungu na Baba yake—ndiyo, kwake yeye na kuwe utukufu na nguvu milele.+ Amina.

7 Tazama! Anakuja na mawingu,+ na kila jicho litamwona,+ na wale waliomchoma;+ na makabila yote ya dunia yatajipiga-piga kwa huzuni kwa sababu yake.+ Ndiyo, Amina.

8 “Mimi ndiye Alfa na Omega,”+ asema Yehova Mungu, “Yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja,+ Mweza-Yote.”+

9 Mimi Yohana, ndugu yenu na mshiriki pamoja nanyi katika dhiki+ na ufalme+ na uvumilivu+ kwa kushirikiana na Yesu,+ nilikuja kuwa katika kisiwa kinachoitwa Patmo kwa sababu ya kusema juu ya Mungu na kutoa ushahidi kumhusu Yesu.+ 10 Kwa uongozi wa roho+ nilikuja kuwa+ katika siku ya Bwana,+ nami nikasikia nyuma yangu sauti yenye nguvu+ kama ile ya tarumbeta, 11 ikisema: “Yale unayoona yaandike+ katika kitabu cha kukunjwa kisha uyatume kwa yale makutaniko saba,+ katika Efeso+ na katika Smirna+ na katika Pergamamu+ na katika Thiatira+ na katika Sardi+ na katika Filadelfia+ na katika Laodikia.”+

12 Nami nikageuka ili nione sauti iliyokuwa ikisema nami, na, nilipokuwa nimegeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu,+ 13 na katikati ya vinara hivyo vya taa palikuwa na mtu kama mwana wa binadamu,+ aliyevikwa vazi lililofika chini miguuni, na aliyefungwa kifuani mshipi wa dhahabu. 14 Zaidi ya hayo, kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe,+ kama theluji, na macho yake kama mwali wa moto;+ 15 na miguu yake ilikuwa kama shaba safi+ inapowaka katika tanuru; na sauti+ yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi. 16 Na katika mkono wake wa kuume kulikuwa na nyota saba,+ na kutoka katika kinywa chake upanga mkali, mrefu na wenye makali kuwili+ ulikuwa umechomoka, na sura yake ilikuwa kama jua linapoangaza katika nguvu zake.+ 17 Nami nilipomwona, nikaanguka kana kwamba nimekufa miguuni pake.

Naye akaweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope.+ Mimi ndiye wa Kwanza+ na wa Mwisho,+ 18 na aliye hai;+ nami nilikufa,+ lakini, tazama! ninaishi milele na milele,+ nami nina funguo za kifo+ na za Kaburi.*+ 19 Kwa hiyo andika mambo uliyoyaona, na mambo yaliyopo na mambo yatakayotendeka baada ya haya.+ 20 Kwa habari ya siri takatifu ya zile nyota saba+ ulizoona juu ya mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu:+ Zile nyota saba zinamaanisha wale malaika wa yale makutaniko saba, na vile vinara saba vya taa vinamaanisha makutaniko saba.+

2 “Kwa malaika+ wa kutaniko katika Efeso+ andika: Haya ndiyo mambo anayosema yeye ambaye anashika zile nyota saba+ katika mkono wake wa kuume, yeye anayetembea katikati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu,+ 2 ‘Mimi nayajua matendo yako,+ na kazi yako ya jasho na uvumilivu, na kwamba huwavumilii watu wabaya, na kwamba uliwajaribu+ wale wanaosema kwamba wao ni mitume,+ lakini wao sio, nawe uliwaona kuwa waongo. 3 Wewe pia unaonyesha uvumilivu,+ nawe umestahimili kwa ajili ya jina langu+ nawe hujachoka.+ 4 Hata hivyo, nina jambo hili dhidi yako, kwamba umeacha upendo uliokuwa nao mwanzoni.+

5 “ ‘Kwa hiyo kumbuka umeanguka kutoka wapi, nawe utubu+ na kufanya yale matendo ya mwanzoni. Usipofanya hivyo, mimi ninakuja kwako,+ nami nitakiondoa kinara chako cha taa+ kutoka mahali pake, usipotubu. 6 Ingawa hivyo, una hili, kwamba unachukia+ matendo ya madhehebu ya Nikolao,+ ambayo mimi pia ninayachukia. 7 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho+ inayaambia makutaniko: Yule ambaye atashinda+ nitampa ruhusa ya kula matunda kutokana na ule mti wa uzima,+ ulio katika paradiso ya Mungu.’

8 “Na kwa malaika+ wa kutaniko katika Smirna andika: Haya ndiyo mambo anayosema, ‘wa Kwanza na wa Mwisho,’+ aliyekufa na akawa hai tena,+ 9 ‘Ninajua dhiki na umaskini wako—lakini wewe ni tajiri+—na kufuru la wale wanaosema kwamba wao wenyewe ni Wayahudi,+ lakini sivyo walivyo bali wao ni sinagogi la Shetani.+ 10 Usiogope mateso ambayo yanakaribia kukupata.+ Tazama! Ibilisi+ ataendelea kuwatupa gerezani baadhi yenu ili mjaribiwe kwa ukamili,+ na ili muwe na dhiki+ siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufikia kifo,+ nami nitakupa taji la uzima.+ 11 Yeye aliye na sikio na asikie+ yale ambayo roho+ inayaambia makutaniko: Yeye atakayeshinda,+ kifo cha pili+ hakitamdhuru hata kidogo.’

12 “Na kwa malaika wa kutaniko katika Pergamamu andika: Haya ndiyo mambo anayosema yeye aliye na ule upanga mkali, mrefu na wenye makali kuwili,+ 13 ‘Ninajua mahali unapokaa, yaani, mahali kilipo kiti cha ufalme cha Shetani; na bado unaendelea kulishika sana jina langu,+ nawe hukukana imani yako katika mimi+ hata katika siku za Antipa, shahidi+ wangu, aliye mwaminifu, aliyeuawa+ kando yenu, mahali anapokaa Shetani.

14 “ ‘Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako, kwamba unao hapo wale wanaolishika sana fundisho la Balaamu,+ aliyemfundisha Balaki+ kuweka kikwazo mbele ya wana wa Israeli, ili wale vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na kufanya uasherati.+ 15 Vivyo hivyo, wewe pia una wale wanaolishika sana fundisho la madhehebu ya Nikolao.+ 16 Kwa hiyo tubu.+ Usipofanya hivyo, mimi ninakuja kwako upesi, nami nitapigana nao vita+ kwa ule upanga mrefu wa kinywa changu.+

17 “ ‘Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko:+ Yeye atakayeshinda+ nitampa sehemu ya mana+ iliyofichwa, nami nitampa jiwe dogo jeupe la mviringo, na juu ya jiwe hilo jina+ jipya likiwa limeandikwa ambalo hakuna yeyote anayelijua ila yule anayelipokea.’+

18 “Na kwa malaika wa kutaniko katika Thiatira+ andika: Haya ndiyo mambo ambayo Mwana+ wa Mungu anasema, yeye ambaye macho yake ni kama mwali wa moto,+ na miguu yake ni kama shaba safi,+ 19 ‘Mimi nayajua matendo yako, na upendo+ wako na imani na huduma na uvumilivu wako, na kwamba matendo+ yako ya hivi karibuni yanazidi yale ya zamani.+

20 “ ‘Hata hivyo, nina hili dhidi yako, kwamba unamvumilia yule mwanamke Yezebeli,+ anayejiita mwenyewe nabii, naye anafundisha+ na kuwapotosha watumwa wangu+ wafanye uasherati+ na kula vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu.+ 21 Nami nilimpa wakati wa kutubu,+ lakini yeye hataki kutubu uasherati+ wake. 22 Tazama! niko karibu kumtupa katika kitanda cha ugonjwa, na wale wanaofanya uzinzi pamoja naye katika dhiki kuu, wasipotubu matendo yake. 23 Nami nitawaua watoto wake kwa pigo lenye kufisha, hivi kwamba makutaniko yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza figo na mioyo, nami nitawapa ninyi mmoja-mmoja kulingana na matendo yenu.+

24 “ ‘Hata hivyo, ninawaambia wale wengine kati yenu walio katika Thiatira, wale wote wasio na fundisho hili, wale ambao hawakujua “mambo mazito ya Shetani,”+ kama wanavyosema: Mimi siweki juu yenu mzigo mwingine wowote.+ 25 Hata hivyo, shikeni sana lile mlilo nalo+ mpaka nije. 26 Na yeye atakayeshinda na kushika matendo yangu mpaka mwisho+ nitampa mamlaka juu ya mataifa,+ 27 naye atawachunga watu kwa fimbo ya chuma+ hivi kwamba watavunjwa vipande-vipande kama vyombo vya udongo,+ kama vile nilivyopokea kutoka kwa Baba yangu, 28 nami nitampa nyota ya asubuhi.+ 29 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho+ inayaambia makutaniko.’+

3 “Na kwa malaika+ wa kutaniko katika Sardi andika: Haya ndiyo mambo anayosema yeye aliye na zile roho saba+ za Mungu na zile nyota saba,+ ‘Mimi nayajua matendo yako, kwamba una jina kuwa uko hai, lakini umekufa.+ 2 Uwe mwenye kulinda,+ na uyatie nguvu+ mambo yanayobaki yaliyokuwa tayari kufa, kwa maana mimi sikuona matendo yako kuwa yamefanywa kwa ukamili mbele za Mungu wangu.+ 3 Kwa hiyo, endelea kukazia akilini jinsi ulivyopokea+ na jinsi ulivyosikia, nawe uendelee kulishika,+ na utubu.+ Hakika usipoamka,+ nitakuja kama mwizi,+ nawe hutajua hata kidogo saa nitakayokuja juu yako.+

4 “ ‘Hata hivyo, una majina+ machache katika Sardi ambayo hayakutia unajisi+ mavazi yao ya nje, nao watatembea pamoja nami wakiwa na mavazi meupe,+ kwa sababu wanastahili.+ 5 Yeye atakayeshinda+ atapambwa hivyo mavazi meupe ya nje;+ nami sitalifuta kwa vyovyote jina lake kutoka katika kitabu cha uzima,+ bali nitalikiri jina lake mbele za Baba+ yangu na mbele ya malaika+ zake. 6 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho+ inayaambia makutaniko.’

7 “Na kwa malaika+ wa kutaniko katika Filadelfia andika: Haya ndiyo mambo anayosema yeye aliye mtakatifu,+ aliye wa kweli,+ aliye na ufunguo wa Daudi,+ ambaye hufungua hivi kwamba hakuna yeyote atakayefunga, na ambaye hufunga hivi kwamba hakuna yeyote anayefungua, 8 ‘Mimi nayajua matendo yako+—tazama! nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa,+ ambao hakuna yeyote anayeweza kuufunga—kwamba una nguvu kidogo, nawe ulilishika neno langu na hukulikana jina langu.+ 9 Tazama! Nitawatoa wale wa sinagogi la Shetani wanaosema ni Wayahudi,+ lakini sivyo walivyo bali wanasema uwongo+—tazama! nitawafanya waje na kusujudu+ mbele ya miguu yako na kuwafanya wajue kwamba nimekupenda wewe. 10 Kwa sababu ulilishika neno juu ya uvumilivu+ wangu, mimi pia nitakulinda+ kutokana na ile saa ya jaribu itakayokuja juu ya dunia nzima inayokaliwa, ili kuwatia katika jaribu wale wanaokaa duniani.+ 11 Mimi ninakuja upesi.+ Endelea kushika sana kile ulicho nacho,+ ili yeyote asilichukue taji+ lako.

12 “ ‘Yeye atakayeshinda—nitamfanya kuwa nguzo+ katika hekalu+ la Mungu wangu,+ naye hataondoka ndani yake tena kwa vyovyote, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu na jina la jiji la Mungu wangu, Yerusalemu+ jipya linaloshuka kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na lile jina langu jipya.+ 13 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho+ inayaambia makutaniko.’

14 “Na kwa malaika wa kutaniko katika Laodikia+ andika: Haya ndiyo mambo anayosema Amina,+ shahidi+ mwaminifu+ na wa kweli,+ mwanzo wa uumbaji wa Mungu,+ 15 ‘Mimi nayajua matendo yako, kwamba wewe si baridi wala si moto. Laiti ungalikuwa baridi au moto. 16 Kwa hiyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu na si moto+ wala si baridi,+ nitakutapika kutoka kinywani mwangu. 17 Kwa sababu unasema: “Mimi ni tajiri,+ nimejipatia utajiri na sihitaji kitu chochote hata kidogo,” lakini hujui kwamba wewe ni mwenye taabu na wa kusikitikiwa na maskini na kipofu+ na uchi, 18 ninakushauri ununue kutoka kwangu dhahabu+ iliyosafishwa kwa moto ili uwe tajiri, na mavazi meupe ya nje ili uvikwe na kwamba aibu ya uchi wako isifunuliwe,+ na dawa ya macho ya kupaka katika macho+ yako ili upate kuona.

19 “ ‘Wale wote ninaowapenda, mimi huwakaripia na kuwatia nidhamu.+ Kwa hiyo uwe mwenye bidii na utubu.+ 20 Tazama! Nimesimama mlangoni+ na kupiga hodi. Mtu yeyote akiisikia sauti yangu na kuufungua mlango,+ nitaingia ndani ya nyumba yake na kula mlo wa jioni pamoja naye, yeye naye pamoja nami. 21 Yeye atakayeshinda+ nitampa ruhusa ya kuketi pamoja nami katika kiti changu cha ufalme,+ kama vile nilivyoshinda na kuketi+ pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha ufalme.+ 22 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho+ inayaambia makutaniko.’ ”+

4 Baada ya mambo haya nikaona, na, tazama! mlango uliofunguliwa mbinguni, na sauti ya kwanza niliyoisikia ilikuwa kama ya tarumbeta,+ ikisema nami, ikiniambia: “Panda uje huku,+ nami nitakuonyesha mambo ambayo lazima yatendeke.”+ 2 Baada ya mambo haya mara moja nikawa katika nguvu za roho: na, tazama! kiti cha ufalme+ kilikuwa mahali pake mbinguni,+ na kuna yule aliyeketi juu ya kile kiti cha ufalme.+ 3 Na yule aliyeketi, kuonekana kwake+ ni kama jiwe la yaspi+ na jiwe jekundu la thamani, na upinde wa mvua+ ambao kuonekana kwake ni kama zumaridi+ unakizunguka kile kiti cha ufalme.

4 Na kuzunguka kile kiti cha ufalme pande zote kulikuwa na viti vya ufalme 24, na juu ya viti hivyo vya ufalme+ niliona wameketi wazee+ 24+ waliovikwa mavazi meupe ya nje,+ na juu ya vichwa vyao kulikuwa na mataji ya dhahabu.+ 5 Na umeme+ na sauti na ngurumo+ zinatoka katika kile kiti cha ufalme; na taa+ saba za moto zinawaka mbele ya kile kiti cha ufalme, na hizo zinamaanisha zile roho saba+ za Mungu. 6 Na mbele ya kile kiti cha ufalme kuna kitu mfano wa bahari kama kioo,+ kama fuwele.

Na katikati ya kile kiti cha ufalme na kuzunguka kile kiti kuna viumbe hai+ wanne ambao wamejaa macho mbele na nyuma. 7 Na kiumbe hai wa kwanza ni kama simba,+ na kiumbe hai wa pili ni kama ng’ombe-dume+ mchanga, na kiumbe hai wa tatu+ ana uso kama wa mwanadamu, na kiumbe hai wa nne+ ni kama tai+ anayeruka. 8 Na kwa habari ya wale viumbe hai wanne,+ kila mmoja wao ana mabawa sita;+ kuzunguka pande zote na chini yao wamejaa macho.+ Nao hawapumziki mchana na usiku huku wakisema: “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova+ Mungu, Mweza-Yote,+ aliyekuwako+ na aliyeko na anayekuja.”

9 Na wakati wowote hao viumbe hai wanapompa utukufu na heshima na shukrani+ Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme,+ Yule anayeishi milele na milele,+ 10 wale wazee 24+ huanguka chini mbele za Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme na kumwabudu+ Yule anayeishi milele na milele, nao hutupa mataji yao mbele ya kile kiti, wakisema: 11 “Unastahili, Ee Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu+ na heshima+ na nguvu,+ kwa sababu uliumba vitu vyote,+ na kwa sababu ya mapenzi+ yako vilikuwako navyo vikaumbwa.”+

5 Nami nikaona katika mkono wa kuume wa Yule aliyeketi juu ya kile kiti cha ufalme+ kitabu cha kukunjwa kilichoandikwa ndani na upande wa nyuma,+ kimefungwa+ kabisa kwa mihuri saba. 2 Nami nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kubwa: “Ni nani anayestahili kukifungua kile kitabu cha kukunjwa na kufungua mihuri yake?” 3 Lakini hapakuwa na hata mmoja, wala mbinguni wala juu ya dunia wala chini ya dunia, aliyeweza kukifungua kitabu hicho cha kukunjwa au kutazama ndani yake. 4 Nami nikalia sana kwa sababu hakuna yeyote aliyepatikana kuwa anastahili kukifungua kitabu hicho cha kukunjwa au kutazama ndani yake.+ 5 Lakini mmoja wa wale wazee akaniambia: “Acha kulia. Tazama! Simba ambaye ni wa kabila la Yuda,+ mzizi+ wa Daudi,+ ameshinda+ ili akifungue kitabu hicho cha kukunjwa na mihuri yake saba.”

6 Nami nikamwona mwana-kondoo,+ kana kwamba alikuwa amechinjwa,+ akiwa amesimama katikati ya kile kiti cha ufalme+ na ya wale viumbe hai wanne na katikati ya wale wazee,+ akiwa na pembe saba na macho saba, macho ambayo yanamaanisha roho+ saba za Mungu ambazo zimetumwa katika dunia nzima. 7 Naye akaenda na mara moja akakichukua kutoka katika mkono wa kuume wa Yule aliyeketi juu ya kile kiti cha ufalme.+ 8 Na alipokichukua kile kitabu cha kukunjwa, wale viumbe hai wanne na wale wazee 24+ wakaanguka chini mbele ya Mwana-Kondoo, kila mmoja akiwa na kinubi+ na mabakuli ya dhahabu yaliyokuwa yamejaa uvumba,+ na huo uvumba unamaanisha sala+ za watakatifu. 9 Nao wanaimba wimbo mpya,+ wakisema: “Wewe unastahili kukichukua kile kitabu cha kukunjwa na kufungua mihuri yake, kwa sababu ulichinjwa na kwa damu+ yako ukamnunulia+ Mungu+ watu kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa, 10 nawe ukawafanya kuwa ufalme+ na makuhani+ kwa Mungu wetu,+ nao watatawala wakiwa wafalme+ juu ya dunia.”

11 Nami nikaona, nami nikasikia sauti ya malaika wengi kuzunguka kile kiti cha ufalme na wale viumbe hai na wale wazee, na hesabu yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu+ na maelfu ya maelfu,+ 12 wakisema kwa sauti kubwa: “Mwana-Kondoo aliyechinjwa+ anastahili kupokea uwezo na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.”+

13 Na kila kiumbe kilicho mbinguni na juu ya dunia na chini ya dunia+ na juu ya bahari, na vitu vyote vilivyo ndani ya hivyo, nikasikia vikisema: “Kwake Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme+ na kwa Mwana-Kondoo+ kuwe na baraka na heshima+ na utukufu+ na nguvu milele na milele.” 14 Na wale viumbe hai wanne wakasema: “Amina!” na wale wazee+ wakaanguka chini na kuabudu.+

6 Naye Mwana-Kondoo+ alipofungua mmoja wa ile mihuri saba,+ nikaona, na kumsikia mmoja wa wale viumbe hai+ wanne akisema kwa sauti kama ya ngurumo: “Njoo!”+ 2 Nami nikaona, na, tazama! farasi mweupe;+ na yule anayeketi+ juu yake alikuwa na upinde;+ naye akapewa taji,+ naye akaenda akishinda+ na kukamilisha ushindi wake.+

3 Naye alipofungua muhuri wa pili, nikamsikia kiumbe hai wa pili+ akisema: “Njoo!” 4 Na mwingine akatokea, farasi mwenye rangi ya moto; na yeye anayeketi juu yake akapewa ruhusa ya kuondoa amani duniani ili wauane; naye akapewa upanga mkubwa.+

5 Naye+ alipofungua muhuri wa tatu, nikamsikia kiumbe hai wa tatu+ akisema: “Njoo!” Nami nikaona, na, tazama! farasi mweusi; na yeye anayeketi juu yake alikuwa na mizani+ mkononi mwake. 6 Nami nikasikia sauti kana kwamba ni katikati+ ya wale viumbe hai wanne+ ikisema: “Kibaba cha ngano kwa dinari+ moja, na vibaba vitatu vya shayiri kwa dinari moja; wala usidhuru mafuta ya zeituni na divai.”+

7 Naye alipofungua muhuri wa nne, nikasikia sauti ya kiumbe hai wa nne+ akisema: “Njoo!” 8 Nami nikaona, na, tazama! farasi wa rangi ya kijivu; na yeye anayeketi juu yake alikuwa na jina Kifo. Na Kaburi*+ lilikuwa likimfuata kwa ukaribu. Nao wakapewa mamlaka juu ya sehemu ya nne ya dunia, ili kuua kwa upanga+ mrefu na kwa upungufu wa chakula+ na kwa pigo lenye kufisha na kwa wanyama-mwitu+ wa dunia.

9 Naye alipofungua muhuri wa tano, nikaona chini ya madhabahu+ nafsi+ za wale waliouawa+ kwa sababu ya neno la Mungu na kwa sababu ya kazi ya ushahidi+ waliyokuwa nayo. 10 Nao wakalia kwa sauti kubwa, wakisema: “Utajizuia mpaka wakati gani, Bwana Mwenye Enzi Kuu+ mtakatifu na wa kweli,+ kuhukumu+ na kulipiza kisasi cha damu+ yetu juu ya wale wanaokaa duniani?” 11 Na kila mmoja wao akapewa kanzu nyeupe;+ nao wakaambiwa wapumzike tena muda kidogo, mpaka ijazwe pia hesabu ya watumwa wenzao na ndugu zao waliokuwa karibu kuuawa+ kama vile wao pia walivyouawa.

12 Nami nikaona alipofungua muhuri wa sita, na tetemeko kubwa la nchi likatokea; na jua likawa jeusi kama gunia+ la manyoya, na mwezi mzima ukawa kama damu,+ 13 na nyota za mbinguni zikaanguka duniani, kama vile mtini unaotikiswa na upepo mkali unavyozitupa tini zake mbichi. 14 Na mbingu ikaondoka kama kitabu cha kukunjwa kinachokunjwa,+ na kila mlima na kila kisiwa vikaondolewa mahali pake.+ 15 Na wafalme wa dunia na wenye daraja la juu na viongozi wa kijeshi na matajiri na wenye nguvu na kila mtumwa na kila mtu huru wakajificha katika mapango na katika miamba+ ya milima. 16 Nao wanaendelea kuiambia milima na miamba: “Tuangukieni,+ mtufiche kutoka usoni pa Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme+ na kutoka kwenye ghadhabu ya Mwana-Kondoo,+ 17 kwa sababu siku kuu+ ya ghadhabu+ yao imekuja, na ni nani anayeweza kusimama?”+

7 Baada ya hayo nikaona malaika+ wanne wamesimama juu ya pembe nne za dunia, wakizishika sana zile pepo+ nne za dunia, ili upepo wowote usivume juu ya dunia au juu ya bahari au juu ya mti wowote.+ 2 Nami nikamwona malaika mwingine akipanda kutoka mashariki,+ akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai;+ naye akapaaza sauti kubwa kwa wale malaika wanne waliopewa ruhusa kuidhuru dunia na bahari, 3 akisema: “Msiidhuru dunia au bahari au miti, mpaka baada ya sisi kuwatia muhuri+ watumwa wa Mungu wetu katika mapaji ya nyuso zao.”+

4 Nami nikaisikia hesabu ya wale waliotiwa muhuri, 144,000,+ waliotiwa muhuri kutoka kila kabila+ la wana wa Israeli:+

5 Kutoka kabila la Yuda+ kumi na mbili elfu waliotiwa muhuri;

kutoka kabila la Rubeni+ kumi na mbili elfu;

kutoka kabila la Gadi+ kumi na mbili elfu;

6 kutoka kabila la Asheri+ kumi na mbili elfu;

kutoka kabila la Naftali+ kumi na mbili elfu;

kutoka kabila la Manase+ kumi na mbili elfu;

7 kutoka kabila la Simeoni+ kumi na mbili elfu;

kutoka kabila la Lawi+ kumi na mbili elfu;

kutoka kabila la Isakari+ kumi na mbili elfu;

8 kutoka kabila la Zabuloni+ kumi na mbili elfu;

kutoka kabila la Yosefu+ kumi na mbili elfu;

kutoka kabila la Benyamini+ kumi na mbili elfu waliotiwa muhuri.+

9 Baada ya mambo haya nikaona, na, tazama! umati mkubwa,+ ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka mataifa+ yote na makabila na vikundi vya watu+ na lugha,+ wamesimama mbele ya kiti cha ufalme+ na mbele ya Mwana-Kondoo, wamevikwa kanzu nyeupe;+ na kulikuwa na matawi ya mitende+ mikononi mwao. 10 Nao wanaendelea kupaaza sauti kubwa, wakisema: “Wokovu unatoka kwa Mungu wetu,+ anayeketi juu ya kiti cha ufalme,+ na Mwana-Kondoo.”+

11 Na malaika+ wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha ufalme na wale wazee+ na wale viumbe hai wanne,+ nao wakaanguka kifudifudi mbele ya kile kiti cha ufalme na kumwabudu Mungu,+ 12 wakisema: “Amina! Baraka na utukufu na hekima na kutoa shukrani na heshima na uwezo na nguvu+ ziwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amina.”+

13 Na mmoja wa wale wazee+ akajibu, akaniambia: “Hawa waliovaa kanzu nyeupe,+ wao ni nani nao walitoka wapi?” 14 Basi nikamwambia mara moja: “Bwana wangu, wewe ndiye unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wale wanaotoka katika ile dhiki kuu,+ nao wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe+ katika damu+ ya Mwana-Kondoo. 15 Ndiyo sababu wako mbele+ ya kile kiti cha ufalme cha Mungu; nao wanamtolea utumishi mtakatifu+ mchana na usiku katika hekalu lake; na Yule anayeketi juu ya kiti cha ufalme+ atatandaza hema+ lake juu yao. 16 Hawatakuwa na njaa tena wala kuwa na kiu tena, wala jua halitawachoma wala joto lolote lenye kuunguza,+ 17 kwa sababu Mwana-Kondoo,+ aliye katikati ya kile kiti cha ufalme, atawachunga,+ na kuwaongoza kwenye chemchemi za maji+ ya uzima. Na Mungu atafuta kila chozi katika macho yao.”+

8 Naye+ alipofungua muhuri wa saba,+ kimya kikatokea mbinguni kwa karibu nusu saa. 2 Nami nikawaona wale malaika saba+ wanaosimama mbele za Mungu, nao wakapewa tarumbeta saba.

3 Na malaika mwingine akafika na kusimama kwenye madhabahu,+ akiwa na chombo cha uvumba cha dhahabu; naye akapewa kiasi kikubwa cha uvumba+ ili autoe pamoja na sala za watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu ambayo ilikuwa mbele ya kile kiti cha ufalme. 4 Na moshi wa uvumba huo ukapanda kutoka katika mkono wa huyo malaika pamoja na sala+ za watakatifu mbele za Mungu. 5 Lakini mara moja malaika huyo akachukua kile chombo cha uvumba, akakijaza sehemu ya moto+ wa madhabahu na kukitupa duniani.+ Na ngurumo+ zikatokea na sauti na umeme+ na tetemeko la nchi.+ 6 Na wale malaika saba wenye tarumbeta+ saba+ wakajitayarisha kuzipiga.

7 Na wa kwanza akaipiga tarumbeta yake. Na kukatukia mvua ya mawe na moto+ uliochangamana na damu, nao ukatupwa duniani; na sehemu ya tatu ya dunia ikateketezwa,+ na sehemu ya tatu ya miti ikateketezwa, na mimea yote mibichi+ ikateketezwa.

8 Na malaika wa pili akaipiga tarumbeta yake. Na kitu fulani kama mlima+ mkubwa unaowaka moto kikatupwa ndani ya bahari.+ Na sehemu ya tatu ya bahari ikawa damu;+ 9 na sehemu ya tatu ya viumbe vilivyo katika bahari ambavyo vina nafsi vikafa,+ na sehemu ya tatu ya mashua ikavunjwa-vunjwa.

10 Na malaika wa tatu akaipiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa inayowaka kama taa ikaanguka kutoka mbinguni,+ nayo ikaanguka juu ya sehemu ya tatu ya mito na juu ya chemchemi za maji.+ 11 Na jina la nyota hiyo ni Pakanga. Na sehemu ya tatu ya maji ikageuka kuwa pakanga, na wengi kati ya wanadamu wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yalikuwa yamefanywa kuwa machungu.+

12 Na malaika wa nne akaipiga tarumbeta yake. Na sehemu ya tatu ya jua ikapigwa na sehemu ya tatu ya mwezi na sehemu ya tatu ya nyota, ili sehemu ya tatu ya hizo itiwe giza+ na mchana usiwe na nuru kwa sehemu yake ya tatu,+ na usiku vivyo hivyo.

13 Nami nikaona, nami nikasikia tai+ akiruka katikati ya mbingu+ akisema kwa sauti kubwa: “Ole, ole, ole+ wao wanaokaa duniani kwa sababu ya mipigo mingine ya tarumbeta ya wale malaika watatu walio karibu kuzipiga tarumbeta zao!”+

9 Na malaika wa tano akaipiga tarumbeta yake.+ Nami nikaona nyota+ iliyokuwa imeanguka kutoka mbinguni mpaka duniani, naye akapewa ufunguo+ wa shimo la abiso.+ 2 Naye akalifungua shimo la abiso, na moshi+ ukapanda kutoka katika shimo lile kama moshi wa tanuru kubwa,+ na jua likatiwa giza,+ pia hewa, kwa moshi wa shimo lile. 3 Na nzige+ wakaja juu ya dunia kutoka katika moshi huo; nao wakapewa mamlaka, mamlaka ileile kama ya nge+ wa dunia. 4 Nao wakaambiwa wasidhuru majani ya dunia wala mmea wowote wala mti wowote, isipokuwa tu wale wanadamu wasio na muhuri wa Mungu juu ya mapaji ya nyuso zao.+

5 Na nzige hao walipewa ruhusa, si wawaue, bali kwamba hawa wateswe+ miezi mitano, na mateso juu yao yalikuwa kama kuteswa na nge+ wakati anapomuuma mwanadamu. 6 Na katika siku hizo wanadamu watatafuta kifo+ lakini hawatakipata kwa vyovyote, nao watatamani kufa lakini kifo kitazidi kuwakimbia.

7 Na mfano wa nzige hao ulikuwa kama farasi+ waliotayarishwa kwa ajili ya pigano; na juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu kilichoonekana kama mataji yaliyo mfano wa dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanaume,+ 8 lakini walikuwa na nywele kama nywele za wanawake.+ Na meno yao yalikuwa kama ya simba;+ 9 nao walikuwa na mabamba ya kifuani+ kama mabamba ya kifuani ya chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari+ ya farasi wengi wakikimbia kwenda katika pigano.+ 10 Pia, wana mikia na miiba kama nge;+ na katika mikia yao kuna mamlaka yao ya kuumiza wanadamu miezi mitano. 11 Wana mfalme juu yao, yule malaika wa abiso.+ Katika Kiebrania jina lake ni Abadoni, lakini katika Kigiriki ana jina Apolioni.+

12 Ole mmoja umepita. Tazama! Ole+ mbili zaidi zinakuja baada ya mambo haya.

13 Na malaika+ wa sita akaipiga tarumbeta+ yake. Nami nikaisikia sauti+ moja kutoka katika zile pembe za madhabahu+ ya dhahabu iliyo mbele za Mungu 14 ikimwambia malaika wa sita, aliyekuwa na tarumbeta: “Wafungue malaika+ wanne waliofungwa+ kwenye mto mkubwa Efrati.”+ 15 Na wale malaika wanne wakafunguliwa, ambao wametayarishwa kwa ajili ya ile saa na siku na mwezi na mwaka, kuua sehemu ya tatu ya wanadamu.

16 Na hesabu ya majeshi ya askari wapanda-farasi ilikuwa makumi mawili ya maelfu ya makumi ya maelfu: niliisikia hesabu yao. 17 Na hivi ndivyo nilivyowaona wale farasi katika maono, na wale walioketi juu yao: walikuwa na mabamba ya kifuani ya rangi nyekundu ya moto na ya bluu ya hayasinthi na ya manjano ya kiberiti; na vichwa vya farasi wale vilikuwa kama vichwa vya simba,+ na katika vinywa vyao ukatoka moto na moshi na kiberiti.+ 18 Kwa hayo mapigo matatu sehemu ya tatu ya wanadamu waliuawa, kutokana na ule moto na moshi na kiberiti vilivyotoka katika vinywa vyao. 19 Kwa maana mamlaka ya farasi wale imo katika vinywa vyao na katika mikia yao; kwa maana mikia yao ni kama nyoka+ na ina vichwa, nao wanadhuru kwa kutumia hivyo.

20 Lakini wale wanadamu wengine ambao hawakuuawa kwa yale mapigo hawakutubu matendo ya mikono yao,+ ili kwamba wasiabudu roho waovu+ na sanamu za dhahabu na fedha+ na shaba na mawe na miti, ambazo haziwezi kuona wala kusikia wala kutembea;+ 21 nao hawakutubu mauaji+ yao wala mazoea yao ya kuwasiliana na pepo+ wala uasherati wao wala wizi wao.

10 Nami nikamwona malaika+ mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni, amepambwa wingu,+ na upinde wa mvua ulikuwa juu ya kichwa chake, na uso wake ulikuwa kama jua,+ na miguu+ yake ilikuwa kama nguzo za moto, 2 na mkononi mwake alikuwa na kitabu kidogo cha kukunjwa kilichofunguliwa. Naye akaweka mguu wake wa kuume juu ya bahari, lakini ule wa kushoto juu ya dunia,+ 3 naye akapaaza kilio kwa sauti kubwa kama vile simba+ anaponguruma. Na alipopaaza kilio, zile ngurumo+ saba zikatoa sauti zao.

4 Basi zile ngurumo saba ziliposema, nilikuwa karibu kuandika; lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema: “Yatie muhuri mambo+ ambayo zile ngurumo saba zilisema, nawe usiyaandike hayo.” 5 Na yule malaika niliyemwona amesimama juu ya bahari na juu ya dunia akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni,+ 6 naye akaapa kwa Yule anayeishi+ milele na milele,+ aliyeiumba mbingu na vitu vilivyo ndani yake na dunia+ na vitu vilivyo ndani yake na bahari na vitu vilivyo ndani yake:+ “Hakutakuwa tena na kukawia;+ 7 bali katika siku za kupiga kwa yule malaika wa saba,+ akiwa karibu kuipiga tarumbeta yake,+ ile siri takatifu+ ya Mungu kulingana na habari njema aliyowatangazia watumwa wake mwenyewe manabii+ itamalizika.”

8 Na ile sauti+ niliyosikia kutoka mbinguni inasema nami tena na kuniambia: “Nenda, kichukue kile kitabu cha kukunjwa kilichofunguliwa ambacho kimo mkononi mwa malaika ambaye amesimama juu ya bahari na juu ya dunia.”+ 9 Nami nikaenda zangu kwa yule malaika na kumwambia anipe kile kitabu kidogo cha kukunjwa. Naye akaniambia: “Kichukue, ukile,+ nacho kitalitia tumbo lako uchungu, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.” 10 Nami nikakichukua kile kitabu kidogo cha kukunjwa kutoka mkononi mwa yule malaika kisha nikakila,+ nacho kinywani mwangu kilikuwa kitamu kama asali;+ lakini nilipokuwa nimekila, tumbo langu likatiwa uchungu. 11 Nao wakaniambia: “Lazima utoe unabii tena kuhusiana na vikundi vya watu na mataifa na lugha na wafalme wengi.”+

11 Nami nikapewa utete unaofanana na fimbo+ aliposema: “Simama upime patakatifu pa hekalu+ la Mungu na madhabahu na wale wanaoabudu ndani yake. 2 Lakini kwa habari ya ua ulio nje+ ya patakatifu pa hekalu, utupe nje kabisa wala usiupime, kwa sababu mataifa+ wamepewa huo, nao watalikanyagia chini ya miguu lile jiji takatifu+ kwa miezi 42.+ 3 Nami nitawafanya mashahidi wangu wawili+ watoe unabii+ kwa siku 1,260 wakiwa wamevikwa nguo za magunia.”+ 4 Hao wanafananishwa na ile mizeituni miwili+ na vile vinara viwili vya taa+ nao wamesimama mbele za Bwana wa dunia.+

5 Na yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwateketeza adui zao;+ na yeyote akitaka kuwadhuru, lazima atauawa kwa njia hiyo. 6 Hawa wana mamlaka ya kufunga mbingu+ ili mvua isinyeshe+ katika siku zao za kutoa unabii, nao wana mamlaka juu ya maji ili kuyageuza kuwa damu+ na kuipiga dunia kwa kila namna ya mapigo mara nyingi kama vile wanavyopenda.

7 Na wakiisha kumaliza kutoa ushahidi wao, yule mnyama-mwitu anayepanda kutoka katika abiso+ atapigana vita nao na kuwashinda na kuwaua.+ 8 Na maiti zao zitakuwa juu ya njia pana ya lile jiji kubwa ambalo katika maana ya kiroho linaitwa Sodoma+ na Misri, ambako pia Bwana wao alitundikwa mtini.+ 9 Na wale kati ya vikundi vya watu na makabila na lugha na mataifa+ watazitazama maiti zao kwa siku tatu na nusu,+ wala hawaziachi maiti zao zilazwe kaburini. 10 Na wale wanaokaa duniani wanashangilia+ juu yao na kujifurahisha, na watapelekeana zawadi,+ kwa sababu hao manabii wawili waliwatesa wale wanaokaa duniani.

11 Na baada ya zile siku tatu na nusu+ roho ya uhai kutoka kwa Mungu ikaingia ndani yao,+ nao wakasimama kwa miguu yao, na woga mkubwa ukawaingia wale waliokuwa wakiwatazama. 12 Nao wakasikia sauti kubwa+ kutoka mbinguni ikiwaambia: “Pandeni mje huku.”+ Nao wakapanda kuingia mbinguni katika wingu, na adui zao wakawatazama. 13 Na katika saa hiyo tetemeko kubwa la nchi likatokea, na sehemu ya kumi+ ya jiji ikaanguka; na watu elfu saba wakauawa na tetemeko hilo la nchi, na wale wengine wakawa na hofu na kumpa utukufu Mungu wa mbinguni.+

14 Ole wa pili+ umepita. Tazama! Ole wa tatu unakuja upesi.

15 Na malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake.+ Na sauti kubwa zikatokea mbinguni, zikisema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana+ wetu na wa Kristo+ wake, naye atatawala akiwa mfalme milele na milele.”+

16 Na wale wazee 24+ waliokuwa wameketi juu ya viti vyao vya ufalme mbele za Mungu wakaanguka kifudifudi+ na kumwabudu Mungu,+ 17 wakisema: “Tunakushukuru wewe,+ Yehova Mungu, Mweza-Yote,+ Yeye aliyeko+ na aliyekuwako, kwa sababu umechukua nguvu zako kuu+ na kuanza kutawala ukiwa mfalme.+ 18 Lakini mataifa wakawa na ghadhabu, nayo ghadhabu yako mwenyewe ikaja, na wakati uliowekwa kwa ajili ya kuhukumiwa kwa wafu, na kuwapa thawabu+ watumwa wako manabii+ na watakatifu na wale wanaoliogopa jina lako, wadogo kwa wakubwa,+ na kuwaharibu+ wale wanaoiharibu dunia.”+

19 Na patakatifu pa hekalu la Mungu palipo mbinguni+ pakafunguliwa, na sanduku+ la agano lake likaonekana katika patakatifu pa hekalu lake.+ Na kukatokea umeme na sauti na ngurumo na tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.

12 Na ishara+ kubwa ilionekana mbinguni, mwanamke+ aliyepambwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake palikuwa na taji la nyota kumi na mbili, 2 naye alikuwa na mimba. Naye analia akiwa katika maumivu+ na katika uchungu wake wa kuzaa.

3 Na ishara nyingine ilionekana mbinguni, na, tazama! joka+  mkubwa wa rangi ya moto, mwenye vichwa saba na pembe kumi na mataji saba juu ya vichwa vyake; 4 na mkia+ wake unakokota sehemu ya tatu ya nyota+ za mbinguni, naye akazitupa chini mpaka duniani.+ Na huyo joka mkubwa akaendelea kusimama mbele ya yule mwanamke+ aliyekuwa karibu kuzaa,+ ili, atakapozaa, ammeze+ mtoto wake.

5 Na mwanamke yule akamzaa mwana,+ mwanamume, atakayechunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.+ Na mtoto wake akanyakuliwa mpaka kwa Mungu na kwenye kiti chake cha ufalme.+ 6 Na mwanamke yule akakimbilia nyikani,+ ambapo ana mahali palipotayarishwa na Mungu, ili wamlishe+ hapo siku 1,260.+

7 Na vita vikatokea ghafula mbinguni: Mikaeli+ na malaika zake wakapigana na yule joka mkubwa, naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana 8 lakini hakushinda, wala mahali hapakupatikana mbinguni kwa ajili yao tena. 9 Kwa hiyo yule joka+ mkubwa akatupwa chini, yule nyoka wa zamani,+ yeye anayeitwa Ibilisi+ na Shetani,+ anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa;+ akatupwa chini duniani,+ na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye. 10 Nami nikaisikia sauti kubwa mbinguni ikisema:

“Sasa kumekuwa na wokovu+ na nguvu+ na ufalme wa Mungu wetu+ na mamlaka ya Kristo wake,+ kwa sababu mshtaki wa ndugu zetu ametupwa chini, anayewashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu!+ 11 Nao wakamshinda+ kwa sababu ya damu ya Mwana-Kondoo+ na kwa sababu ya neno la kutoa kwao ushahidi,+ nao hawakupenda nafsi+ zao hata walipokabili kifo. 12 Kwa sababu hiyo furahini, enyi mbingu nanyi mnaokaa ndani yake!+ Ole+ wa dunia na wa bahari,+ kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.”+

13 Sasa yule joka mkubwa alipoona kwamba ametupwa chini duniani,+ alimtesa yule mwanamke+ aliyezaa mtoto mwanamume. 14 Lakini yule mwanamke akapewa mabawa mawili ya tai mkubwa,+ ili aruke kwenda nyikani+ mahali pake; hapo ndipo anapolishwa+ kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati+ mbali na uso wa yule nyoka.+

15 Naye nyoka akatapika maji+ kama mto kutoka katika kinywa chake nyuma ya yule mwanamke, ili kumzamisha kwa mto huo.+ 16 Lakini dunia ikaja kumsaidia mwanamke,+ nayo dunia ikafungua kinywa chake na kuumeza mto ambao yule joka mkubwa aliutapika kutoka katika kinywa chake. 17 Na yule joka mkubwa akawa na ghadhabu kumwelekea yule mwanamke,+ naye akaenda zake kupigana vita na wale waliobaki wa uzao wake, wanaoshika amri za Mungu na walio na kazi ya kutoa ushahidi+ kumhusu Yesu.

13 Naye akasimama tuli juu ya mchanga+ wa bahari.

Nami nikaona mnyama-mwitu+ akipanda kutoka katika bahari,+ mwenye pembe kumi+ na vichwa saba,+ na mataji kumi juu ya pembe zake, lakini juu ya vichwa vyake majina yenye makufuru.+ 2 Basi yule mnyama-mwitu niliyemwona alikuwa kama chui,+ lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu,+ na kinywa chake kilikuwa kama kinywa cha simba.+ Na yule joka+ mkubwa akampa huyo mnyama nguvu zake na kile kiti chake cha ufalme na mamlaka kubwa.+

3 Nami nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimechinjwa mpaka kufa, lakini pigo lake la kifo+ likapona, na dunia yote ikamfuata yule mnyama-mwitu kwa mshangao. 4 Nao wakamwabudu yule joka mkubwa kwa sababu alimpa yule mnyama-mwitu mamlaka, nao wakamwabudu mnyama-mwitu kwa maneno haya: “Ni nani aliye kama huyu mnyama-mwitu, na ni nani anayeweza kupigana naye?” 5 Naye akapewa kinywa kinachosema mambo makuu+ na makufuru,+ naye akapewa mamlaka ya kutenda kwa miezi 42.+ 6 Naye akafungua kinywa chake kwa kumkufuru+ Mungu, kulikufuru jina lake na makao yake, hata wale wanaokaa mbinguni.+ 7 Naye akapewa ruhusa+ ya kupigana vita na watakatifu na kuwashinda,+ naye akapewa mamlaka juu ya kila kabila na watu na lugha na taifa. 8 Na wale wote wanaokaa duniani watamwabudu; hakuna jina la hata mmoja wao limeandikwa katika kitabu cha kukunjwa+ cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa,+ tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.+

9 Ikiwa yeyote ana sikio, na asikie.+ 10 Ikiwa yeyote amekusudiwa kwenda utekwani, yeye huenda zake utekwani.+ Ikiwa yeyote ataua kwa upanga, yeye lazima atauawa kwa upanga.+ Hapa ndipo panapomaanisha uvumilivu+ na imani+ ya watakatifu.+

11 Nami nikamwona mnyama-mwitu+ mwingine akipanda kutoka katika dunia,+ naye alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akaanza kusema kama joka+ mkubwa. 12 Naye anatumia mamlaka yote ya yule mnyama-mwitu+ wa kwanza machoni pake. Naye huifanya dunia na wale wanaokaa ndani yake wamwabudu yule mnyama-mwitu wa kwanza, ambaye pigo lake la kifo lilipona.+ 13 Naye hufanya ishara+ kubwa, hivi kwamba hata yeye hufanya moto ushuke kutoka mbinguni mpaka duniani machoni pa wanadamu.

14 Naye huwapotosha wale wanaokaa duniani, kwa sababu ya ishara alizopewa ruhusa kufanya machoni pa yule mnyama-mwitu, huku akiwaambia wale wanaokaa duniani wafanye sanamu+ ya yule mnyama-mwitu aliyekuwa na pigo+ la upanga na bado akarudi kwenye uzima. 15 Naye akapewa ruhusa kuipa pumzi ile sanamu ya mnyama-mwitu, hivi kwamba ile sanamu ya mnyama-mwitu iseme na pia kufanya wauawe wale wote ambao hawakutaka hata kidogo kuiabudu ile sanamu+ ya mnyama-mwitu.

16 Naye huwalazimisha watu wote,+ wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, kwamba wawape hao alama katika mkono wao wa kuume au juu ya paji la uso wao,+ 17 na kwamba mtu yeyote asiweze kununua au kuuza isipokuwa mtu aliye na ile alama, jina+ la yule mnyama-mwitu au namba ya jina lake.+ 18 Hapa ndipo hekima inapohitajiwa: Yeye aliye na akili na apige hesabu ya namba ya yule mnyama-mwitu, kwa maana ni namba ya mwanadamu;+ na namba yake ni 666.+

14 Nami nikaona, na, tazama! Mwana-Kondoo+ amesimama juu ya Mlima Sayuni,+ na pamoja naye 144,000+ wakiwa na jina lake na jina la Baba+ yake limeandikwa juu ya mapaji ya nyuso zao. 2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi+ na kama sauti ya ngurumo kubwa; na sauti niliyosikia ilikuwa kama ya waimbaji ambao wanafuatanisha sauti zao kwa kinubi+ wakivipiga vinubi vyao. 3 Nao wanaimba+ kana kwamba ni wimbo mpya+ mbele ya kile kiti cha ufalme na mbele ya wale viumbe hai wanne+ na wale wazee;+ na hakuna yeyote aliyeweza kujifunza kikamili wimbo ule ila wale 144,000,+ ambao wamenunuliwa+ kutoka duniani. 4 Hao ndio wale ambao hawakujitia unajisi na wanawake;+ kwa kweli, wao ni mabikira.+ Hao ndio wale wanaoendelea kumfuata Mwana-Kondoo popote anapoenda.+ Hao walinunuliwa+ kutoka kati ya wanadamu wakiwa matunda ya kwanza+ kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo, 5 na hamna uwongo uliopatikana katika vinywa vyao;+ wao hawana dosari.+

6 Nami nikamwona malaika mwingine akiruka katikati ya mbingu,+ naye alikuwa na habari njema+ ya milele ili aitangaze kuwa habari za furaha kwa wale wanaokaa duniani, na kwa kila taifa na kabila na lugha na watu,+ 7 akisema kwa sauti kubwa: “Mwogopeni Mungu+ na kumpa utukufu,+ kwa sababu saa ya hukumu yake imefika,+ na kwa hiyo mwabuduni Yeye aliyezifanya+ mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.”+

8 Na mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema: “Ameanguka! Babiloni+ Mkubwa ameanguka,+ yeye aliyeyafanya mataifa yote yanywe kutokana na divai+ ya hasira ya uasherati wake!”+

9 Na malaika mwingine, wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kubwa: “Yeyote akimwabudu yule mnyama-mwitu+ na sanamu yake,+ na kupokea alama juu ya paji la uso wake au juu ya mkono wake,+ 10 yeye pia atakunywa kutokana na divai ya hasira ya Mungu inayomwagwa bila kuchanganywa na kitu ndani ya kikombe cha ghadhabu yake,+ naye atateswa+ kwa moto na kiberiti+ machoni pa malaika watakatifu na machoni pa Mwana-Kondoo. 11 Na moshi wa kuteswa kwao unapanda milele na milele,+ nao hawana pumziko mchana na usiku, wale wanaomwabudu yule mnyama-mwitu na sanamu yake, na yeyote anayepokea alama+ ya jina lake. 12 Hapa ndipo panapomaanisha uvumilivu kwa watakatifu,+ wale wanaoshika amri za Mungu+ na imani+ kwa Yesu.”

13 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema: “Andika: Wenye furaha ni wafu+ wanaokufa katika muungano na Bwana+ tangu wakati huu na kuendelea.+ Ndiyo, roho inasema, acheni wapumzike kutokana na kazi zao za jasho, kwa maana mambo waliyotenda yanaambatana nao moja kwa moja.”

14 Nami nikaona, na, tazama! wingu jeupe, na mtu fulani kama mwana wa binadamu+ ameketi juu ya wingu lile, mwenye taji la dhahabu+ juu ya kichwa chake na mundu mkali mkononi mwake.

15 Na malaika mwingine akatokea katika patakatifu pa hekalu, akimpaazia sauti kubwa yule anayeketi juu ya lile wingu: “Tia ndani mundu wako uvune,+ kwa sababu saa imekuja ya kuvuna, kwa maana mavuno+ ya dunia yameiva kabisa.”+ 16 Na yule aliyeketi juu ya wingu akatia ndani mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.

17 Na bado malaika mwingine akatokea katika patakatifu pa hekalu palipo mbinguni,+ yeye, pia, akiwa na mundu mkali.

18 Na bado malaika mwingine akatokea katika madhabahu naye alikuwa na mamlaka juu ya moto.+ Naye akapaaza sauti kubwa akamwita yule aliyekuwa na mundu mkali, akisema: “Tia ndani mundu wako mkali ukusanye vishada vya mzabibu wa dunia,+ kwa sababu zabibu zake zimeiva.” 19 Na yule malaika+ akatia ndani mundu wake katika dunia na kuukusanya mzabibu+ wa dunia, naye akautupa ndani ya shinikizo kubwa la divai la hasira ya Mungu.+ 20 Na lile shinikizo la divai likakanyagiwa nje ya jiji,+ na damu ikatoka katika lile shinikizo la divai hata kufikia juu kwenye lijamu za farasi,+ kwa umbali wa stadia elfu moja mia sita.+

15 Nami nikaona ishara+ nyingine mbinguni, kubwa na ya ajabu sana, malaika saba+ wenye mapigo saba.+ Hayo ndiyo ya mwisho, kwa sababu kupitia hayo hasira+ ya Mungu inamalizika.+

2 Nami nikaona kitu mfano wa bahari+ kama kioo iliyochangamana na moto, na wale wanaotokea wakiwa washindi+ kutoka kwa yule mnyama-mwitu na kutoka kwa ile sanamu+ yake na kutoka kwa ile namba+ ya jina lake wakiwa wamesimama kando ya ule mfano wa bahari+ kama kioo, wakiwa na vinubi+ vya Mungu. 3 Nao wanaimba wimbo wa Musa+ mtumwa wa Mungu na wimbo wa Mwana-Kondoo,+ wakisema:

“Matendo yako ni makuu na ya ajabu,+ Yehova Mungu, Mweza-Yote.+ Njia zako ni za uadilifu na za kweli,+ Mfalme wa umilele.+ 4 Ni nani ambaye kwa kweli hatakuogopa wewe,+ Yehova,+ na kulitukuza jina lako,+ kwa sababu wewe peke yako ni mshikamanifu?+ Kwa maana mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako,+ kwa sababu amri zako za uadilifu zimefunuliwa.”+

5 Na baada ya mambo haya nikaona, na patakatifu pa hema+ la ushahidi+ pakafunguliwa mbinguni,+ 6 na wale malaika saba+ wenye mapigo saba+ wakatokea katika patakatifu, wamevikwa kitani safi,+ chenye kung’aa nao wamefungwa vifuani mwao mishipi ya dhahabu. 7 Na mmoja wa wale viumbe hai wanne+ akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa hasira ya Mungu,+ anayeishi milele na milele.+ 8 Na patakatifu pakajawa na moshi kwa sababu ya utukufu wa Mungu+ na kwa sababu ya nguvu zake, na hakuna yeyote aliyeweza kuingia katika patakatifu mpaka yalipomalizika yale mapigo saba+ ya wale malaika saba.

16 Nami nikasikia sauti+ kubwa kutoka katika patakatifu ikiwaambia wale malaika saba: “Nendeni mkamwage yale mabakuli saba ya hasira+ ya Mungu ndani ya dunia.”

2 Na yule wa kwanza+ akaenda zake na kumwaga bakuli lake ndani ya dunia.+ Na kidonda chenye kuumiza na kilicho hatari+ kikaja juu ya wale wanadamu waliokuwa na alama ya yule mnyama-mwitu+ na waliokuwa wakiiabudu sanamu yake.+

3 Na yule wa pili+ akamwaga bakuli lake ndani ya bahari.+ Nayo ikawa damu+ kama ya mwanadamu aliyekufa, na kila nafsi iliyo hai ikafa, ndiyo, vitu vilivyo ndani ya bahari.+

4 Na yule wa tatu+ akamwaga bakuli lake ndani ya mito+ na chemchemi za maji. Nazo zikawa damu.+ 5 Nami nikamsikia malaika aliye juu ya maji akisema: “Wewe, Ambaye uko na uliyekuwako,+ Mshikamanifu,+ wewe ni mwadilifu, kwa sababu umetoa maamuzi haya,+ 6 kwa sababu waliimwaga damu ya watakatifu na ya manabii,+ nawe umewapa damu+ wanywe. Wanastahili hilo.”+ 7 Nami nikaisikia madhabahu ikisema: “Ndiyo, Yehova Mungu, Mweza-Yote,+ maamuzi yako ya hukumu ni ya kweli na ya uadilifu.”+

8 Na yule wa nne+ akamwaga bakuli lake juu ya jua; na jua likapewa ruhusa ya kuwaunguza+ wanadamu kwa moto. 9 Na wale wanadamu wakaunguzwa kwa joto kubwa, lakini wakalikufuru jina+ la Mungu, aliye na mamlaka+ juu ya mapigo haya, nao hawakutubu ili wampe utukufu.+

10 Na yule wa tano akamwaga bakuli lake juu ya kiti cha ufalme cha yule mnyama-mwitu.+ Na ufalme wake ukatiwa giza,+ nao wakaanza kuzitafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu yao, 11 lakini wakamkufuru+ Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu yao na kwa sababu ya vidonda vyao, nao hawakutubu matendo yao.

12 Na yule wa sita+ akamwaga bakuli lake juu ya mto mkubwa Efrati,+ na maji yake yakakauka,+ ili njia itayarishwe kwa ajili ya wafalme+ wanaotoka mashariki.

13 Nami nikaona maneno machafu matatu yaliyoongozwa na roho+ ambayo yalionekana kama vyura+ yakitoka katika kinywa cha yule joka+ mkubwa na kutoka katika kinywa cha yule mnyama-mwitu+ na kutoka katika kinywa cha yule nabii wa uwongo.+ 14 Hayo, kwa kweli, ni maneno yanayoongozwa+ na roho waovu nayo yanafanya ishara,+ nayo yanakwenda kwa wafalme+ wa dunia nzima inayokaliwa,+ ili kuwakusanya pamoja kwa vita+ vya ile siku kuu+ ya Mungu Mweza-Yote.+

15 “Tazama! Ninakuja kama mwizi.+ Mwenye furaha ni yule anayekaa macho+ na kutunza mavazi yake ya nje, ili asipate kutembea akiwa uchi na watu waitazame aibu yake.”+

16 Nayo yakawakusanya pamoja mahali panapoitwa katika Kiebrania Har-Magedoni.+

17 Na yule wa saba akamwaga bakuli lake juu ya hewa.+ Ndipo sauti+ kubwa ikatokea katika patakatifu kutoka katika kile kiti cha ufalme, ikisema: “Imekuwa!” 18 Na umeme na sauti na ngurumo zikatokea, na kukatokea tetemeko kubwa la nchi+ la namna ambayo haijatokea tangu wanadamu walipokuja kuwa duniani,+ tetemeko la nchi+ lenye kuenea sana, lililo kubwa sana. 19 Na lile jiji kubwa+ likapasuka na kuwa sehemu tatu, na majiji ya mataifa yakaanguka; na Babiloni Mkubwa+ akakumbukwa machoni pa Mungu, ili kumpa kikombe cha divai cha hasira ya ghadhabu yake.+ 20 Pia, kila kisiwa kikakimbia, na milima haikupatikana.+ 21 Na mvua kubwa ya mawe+ iliyo na kila jiwe lenye uzito wa karibu talanta moja ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu, na wale wanadamu wakamkufuru+ Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe,+ kwa sababu pigo lake lilikuwa kubwa isivyo kawaida.

17 Na mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na mabakuli saba+ akaja, akasema nami, akaniambia: “Njoo, nitakuonyesha hukumu juu ya yule kahaba+ mkubwa anayekaa juu ya maji mengi,+ 2 ambaye wafalme wa dunia walifanya uasherati naye,+ na wale ambao hukaa katika dunia walileweshwa kwa divai ya uasherati wake.”+

3 Naye akanichukua katika nguvu za roho+ kuingia nyikani. Nami nikamwona mwanamke ameketi juu ya mnyama-mwitu+ mwenye rangi nyekundu aliyejaa majina ya makufuru+ na aliyekuwa na vichwa saba+ na pembe kumi. 4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo za rangi ya zambarau+ na nyekundu,+ naye alikuwa amepambwa dhahabu na jiwe la thamani na lulu+ na mkononi mwake alikuwa na kikombe cha dhahabu+ kilichojaa machukizo+ na mambo machafu ya uasherati wake.+ 5 Na juu ya paji la uso wake jina, fumbo,+ lilikuwa limeandikwa: “Babiloni Mkubwa, mama wa makahaba+ na wa machukizo ya dunia.”+ 6 Nami nikaona kwamba yule mwanamke amelewa damu+ ya watakatifu na damu ya mashahidi wa Yesu.+

Basi, nilipomwona nilishangaa kwa mshangao mkubwa.+ 7 Na kwa hiyo yule malaika akaniambia: “Kwa nini ulishangaa? Nitakuambia fumbo la yule mwanamke+ na la yule mnyama-mwitu anayembeba na aliye na vichwa saba na pembe kumi:+ 8 Mnyama-mwitu uliyemwona alikuwako,+ lakini hayuko, na bado yuko karibu kupanda kutoka katika abiso,+ naye ataenda kwenye uharibifu. Na watakapoona jinsi yule mnyama-mwitu alivyokuwako, lakini hayuko, na bado atakuwapo, wale wanaokaa duniani watamsifu kwa mshangao, lakini majina yao hayakuandikwa kwenye kile kitabu cha kukunjwa cha uzima+ tangu kuwekwa kwa msingi wa ulimwengu.+

9 “Hapa ndipo inapohitajiwa akili yenye hekima:+ Vile vichwa saba+ vinamaanisha milima saba,+ ambapo yule mwanamke huketi juu. 10 Na kuna wafalme saba: watano wameanguka,+ mmoja yuko,+ yule mwingine bado hajafika,+ lakini atakapofika lazima adumu kwa muda mfupi.+ 11 Na yule mnyama-mwitu aliyekuwako lakini hayuko,+ yeye mwenyewe pia ni mfalme wa nane, lakini anatokana na wale saba, naye anaenda zake kwenye uharibifu.

12 “Na zile pembe kumi ulizoona zinamaanisha wafalme kumi,+ ambao bado hawajapokea ufalme, lakini wanapokea mamlaka wakiwa wafalme saa moja pamoja na yule mnyama-mwitu. 13 Hawa wana wazo moja, na kwa hiyo wanampa yule mnyama-mwitu nguvu na mamlaka yao.+ 14 Hawa watapigana na Mwana-Kondoo,+ lakini, kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme,+ Mwana-Kondoo atawashinda.+ Pia, wale walioitwa na waliochaguliwa na walio waaminifu pamoja naye watawashinda.”+

15 Naye ananiambia: “Yale maji uliyoyaona, ambapo yule kahaba anaketi, yanamaanisha vikundi vya watu na umati na mataifa na lugha.+ 16 Na zile pembe kumi+ ulizoona, na yule mnyama-mwitu,+ hawa watamchukia yule kahaba+ na kumfanya kuwa ukiwa na uchi, nao watakula sehemu zake zenye nyama na kumteketeza kabisa kwa moto.+ 17 Kwa maana Mungu alitia hilo ndani ya mioyo yao ili kutekeleza wazo lake,+ kutekeleza lile wazo lao moja kwa kumpa yule mnyama-mwitu ufalme wao,+ mpaka maneno ya Mungu yatakapokwisha kutimizwa.+ 18 Na yule mwanamke+ uliyemwona anamaanisha lile jiji kubwa lililo na ufalme juu ya wafalme wa dunia.”+

18 Baada ya mambo haya nikamwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka+ kubwa; na dunia ikaangazwa nuru kutokana na utukufu wake.+ 2 Naye akapaaza kilio kwa sauti yenye nguvu,+ akisema: “Ameanguka! Babiloni Mkubwa ameanguka,+ naye amekuwa makao ya roho waovu na mahali pa kuvizia pa kila pumzi+ chafu na mahali pa kuvizia pa kila ndege mchafu na mwenye kuchukiwa!+ 3 Kwa kuwa mataifa yote yameanguka yakiwa majeruhi kwa sababu ya divai ya hasira ya uasherati wake,+ na wafalme wa dunia walifanya uasherati+ naye, na wanabiashara+ wa dunia wanaosafiri walikuwa matajiri kutokana na nguvu za anasa yake isiyo na aibu.”+

4 Nami nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: “Tokeni kwake, watu wangu,+ ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake,+ na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya mapigo yake. 5 Kwa maana dhambi zake zimekusanyika pamoja mpaka mbinguni,+ naye Mungu amekumbuka matendo yake yasiyo ya haki.+ 6 Mlipeni sawa na vile yeye mwenyewe alivyolipa,+ na mtendeeni mara mbili ya hivyo, ndiyo, mara mbili ya hesabu ya mambo aliyoyatenda;+ katika kikombe+ ambacho ndani yake alitia mchanganyiko mtilieni+ mchanganyiko mara mbili+ ya hivyo. 7 Kwa kadiri alivyojitukuza mwenyewe na kuishi katika anasa isiyo na aibu, kwa kadiri hiyo mpeni mateso na maombolezo.+ Kwa maana moyoni mwake anaendelea kusema, ‘Ninaketi nikiwa malkia,+ nami si mjane,+ nami sitaona maombolezo kamwe.’+ 8 Hiyo ndiyo sababu katika siku moja mapigo+ yake yatakuja, kifo na kuomboleza na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto,+ kwa sababu Yehova Mungu, aliyemhukumu, ni mwenye nguvu.+

9 “Na wafalme+ wa dunia waliofanya uasherati pamoja naye na kuishi katika anasa isiyo na aibu watalia na kujipiga-piga wenyewe kwa huzuni juu yake,+ wanapoutazama moshi+ kutokana na kuungua kwake, 10 huku wao wakisimama mbali kwa sababu ya woga wao wa kuteseka kwake na kusema,+ ‘Ole, ole, wewe jiji kubwa,+ Babiloni wewe jiji lenye nguvu, kwa sababu katika saa moja hukumu yako imefika!’+

11 “Pia, wanabiashara+ wa dunia wanaosafiri wanalia na kuomboleza juu yake,+ kwa sababu hakuna yeyote wa kununua tena mali zao zilizojaa, 12 mali zilizojaa+ za dhahabu na fedha na jiwe la thamani na lulu na kitani bora na zambarau na hariri na vitambaa vyekundu; na kila kitu cha miti iliyotiwa manukato na kila namna ya kitu cha pembe ya tembo na kila namna ya kitu kinachotokana na miti ya thamani zaidi na cha shaba na cha chuma na cha marumaru;+ 13 pia mdalasini na kiungo cha Kihindi na uvumba na mafuta yenye marashi na ubani na divai na mafuta ya zeituni na unga laini na ngano na ng’ombe na kondoo, na farasi na magari na watumwa na nafsi za binadamu.+ 14 Ndiyo, tunda zuri ambalo nafsi yako ilitamani+ limeondoka kwako, na vitu vyote vitamu na vitu vyenye fahari vimeangamia kutoka kwako, na watu hawatavipata tena kamwe.+

15 “Wanabiashara+ wanaosafiri wa vitu hivyo, waliopata utajiri kutokana naye, watasimama mbali kwa sababu ya woga wao juu ya kuteseka kwake na kulia na kuomboleza,+ 16 wakisema, ‘Ole, ole—lile jiji kubwa,+ lililovikwa kitani bora na zambarau na kitambaa chekundu, na kupambwa kitajiri kwa mapambo ya dhahabu na mawe ya thamani na lulu,+ 17 kwa sababu katika saa moja mali nyingi hivyo zimefanywa ukiwa!’+

“Na kila kapteni wa meli na kila mtu ambaye husafiri baharini mahali popote,+ na mabaharia na wale wote ambao hupata riziki baharini, walisimama mbali+ 18 na kupaaza kilio walipokuwa wakiutazama moshi uliotokana na kuteketezwa kwake na kusema, ‘Ni jiji gani lililo kama lile jiji kubwa?’+ 19 Nao wakatupa mavumbi juu ya vichwa+ vyao na kupaaza kilio, wakilia na kuomboleza,+ na kusema, ‘Ole, ole,—lile jiji kubwa, ambalo wale wote walio na mashua baharini+ walikuwa matajiri+ kwa sababu ya utajiri wake mkubwa, kwa sababu katika saa moja amefanywa ukiwa!’+

20 “Furahini juu yake, enyi mbingu,+ pia ninyi watakatifu+ na ninyi mitume+ na ninyi manabii, kwa sababu Mungu amemtoza adhabu ya hukumu kwa ajili yenu!”+

21 Na malaika mwenye nguvu akainua jiwe kama jiwe kubwa la kusagia+ na kulitupa ndani ya bahari,+ akisema: “Hivi ndivyo Babiloni lile jiji kubwa litakavyotupwa chini kwa mtupo wa kasi sana, naye hatapatikana tena.+ 22 Na sauti ya waimbaji ambao hufuatanisha sauti zao kwa kinubi na ya wanamuziki na ya wapiga-filimbi na ya wapiga-tarumbeta haitasikiwa tena kamwe ndani yako,+ na hakuna fundi wa kazi yoyote atakayepatikana ndani yako tena kamwe, na hakuna sauti ya jiwe la kusagia itakayosikiwa tena kamwe ndani yako, 23 na hakuna nuru ya taa itakayoangaza tena kamwe ndani yako, na hakuna sauti ya bwana-arusi na bibi-arusi itakayosikiwa tena kamwe ndani yako;+ kwa sababu wanabiashara+ wako wanaosafiri walikuwa ndio watu wenye daraja la juu+ wa dunia, kwa maana mataifa yote yalipotoshwa kwa mazoea yako ya kuwasiliana na pepo.+ 24 Ndiyo, ndani yake ilipatikana damu+ ya manabii+ na ya watakatifu+ na ya wale wote ambao wameuawa juu ya dunia.”+

19 Baada ya mambo haya nikasikia kitu kama sauti kubwa ya umati mkubwa mbinguni.+ Walisema: “Msifuni Yah!+ Wokovu+ na utukufu na nguvu ni za Mungu wetu,+ 2 kwa sababu hukumu zake ni za kweli na za uadilifu.+ Kwa maana ametekeleza hukumu juu ya yule kahaba mkubwa aliyeiharibu dunia kwa uasherati wake, naye amelipiza kisasi damu ya watumwa wake mkononi mwake.”+ 3 Na mara moja, kwa mara ya pili wakasema:+ “Msifuni Yah! Na moshi kutoka kwake unaendelea kupanda milele na milele.”+

4 Na wale wazee 24+ na wale viumbe hai wanne+ wakaanguka chini na kumwabudu Mungu anayeketi+ juu ya kiti cha ufalme, na kusema: “Amina! Msifuni Yah!”+

5 Pia, sauti ikatoka katika kile kiti cha ufalme na kusema: “Muwe mkimsifu Mungu wetu, enyi nyote watumwa wake,+ ambao mnamwogopa, wadogo kwa wakubwa.”+

6 Nami nikasikia kitu kama sauti ya umati mkubwa na kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo nzito. Wakasema: “Msifuni Yah,+ kwa sababu Yehova Mungu wetu, Mweza-Yote,+ ameanza kutawala akiwa mfalme.+ 7 Acheni tushangilie na kuwa wenye shangwe mno, na tumpe yeye utukufu,+ kwa sababu ndoa+ ya Mwana-Kondoo imefika+ na mke wake amejitayarisha.+ 8 Ndiyo, amepewa ruhusa ya kupambwa kitani bora, changavu, safi, kwa maana hicho kitani bora humaanisha matendo ya uadilifu ya watakatifu.”+

9 Naye ananiambia: “Andika: Wenye furaha ni wale walioalikwa+ kwenye mlo wa jioni wa ndoa ya Mwana-Kondoo.”+ Pia, ananiambia: “Hayo ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”+ 10 Ndipo nikaanguka chini mbele ya miguu yake ili kumwabudu yeye.+ Lakini yeye ananiambia: “Uwe mwangalifu! Usifanye hivyo!+ Mimi ni mtumwa mwenzako tu na wa ndugu zako walio na kazi ya kutoa ushahidi kumhusu Yesu.+ Mwabudu Mungu;+ kwa maana kutoa ushahidi kumhusu Yesu ndilo kusudi la unabii.”+

11 Nami nikaona mbingu imefunguliwa, na, tazama! farasi mweupe.+ Na yeye aliyeketi juu yake anaitwa Mwaminifu+ na wa Kweli,+ naye anahukumu na kufanya vita kwa uadilifu.+ 12 Macho yake ni mwali wa moto,+ na juu ya kichwa chake kuna vilemba vingi.+ Ana jina+ lililoandikwa ambalo hakuna yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe, 13 naye amepambwa vazi la nje lililonyunyiziwa damu,+ na jina analoitwa ni Neno la Mungu.+ 14 Pia, majeshi yaliyokuwa mbinguni yalikuwa yakimfuata juu ya farasi weupe, nayo yalikuwa yamevikwa kitani bora cheupe, safi. 15 Na upanga mrefu mkali unachomoza kutoka kinywani mwake,+ ili ayapige mataifa nao, naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.+ Yeye anakanyaga pia shinikizo la divai+ ya hasira ya ghadhabu ya Mungu+ Mweza-Yote. 16 Na juu ya vazi lake la nje, juu ya paja lake, ana jina ambalo limeandikwa, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.+

17 Nikaona pia malaika amesimama katika jua, naye akapaaza kilio kwa sauti kubwa na kuwaambia ndege+ wote wanaoruka katikati ya mbingu: “Njooni hapa, mkusanyike pamoja kwenye mlo mkubwa wa jioni wa Mungu, 18 ili mpate kula sehemu zenye nyama za wafalme na sehemu zenye nyama+ za viongozi wa kijeshi na sehemu zenye nyama za watu wenye nguvu+ na sehemu zenye nyama za farasi+ na za wale wanaoketi juu yao, na sehemu zenye nyama za wote, za watu huru na vilevile za watumwa na za wadogo na wakubwa.”

19 Nami nikamwona yule mnyama-mwitu+ na wafalme+ wa dunia na majeshi yao wamekusanyika pamoja ili kupigana vita+ na yule anayeketi juu ya farasi+ na jeshi lake. 20 Na yule mnyama-mwitu+ akakamatwa, na yule nabii wa uwongo+ pamoja naye, aliyefanya mbele yake ishara+ alizotumia kuwapotosha wale waliopokea alama+ ya yule mnyama-mwitu na wale wanaoitolea sanamu+ yake ibada. Wakiwa bado hai, wote wawili walitupwa ndani ya ziwa la moto linalowaka kwa kiberiti.+ 21 Lakini wale wengine wakauawa kabisa kwa ule upanga mrefu wa yule anayeketi juu ya farasi,+ upanga uliochomoza kinywani mwake.+ Na ndege+ wote wakashiba+ sehemu zao zenye nyama.+

20 Nami nikamwona malaika akishuka kutoka mbinguni mwenye ufunguo wa abiso+ na mnyororo mkubwa mkononi mwake. 2 Naye akamkamata yule joka+ mkubwa, yule nyoka wa zamani,+ ambaye ni Ibilisi+ na Shetani,+ na kumfunga kwa miaka elfu. 3 Naye akamtupa ndani ya abiso+ na kuifunga na kuitia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena mpaka ile miaka elfu itakapokwisha. Baada ya mambo hayo yeye atafunguliwa kwa muda kidogo.+

4 Nami nikaona viti vya ufalme,+ na kulikuwa na wale walioketi juu yake, nao wakapewa mamlaka ya kuhukumu.+ Ndiyo, niliona nafsi za wale waliouawa kwa shoka kwa ajili ya ushahidi waliotoa kumhusu Yesu na kwa ajili ya kusema juu ya Mungu, na wale ambao hawakumwabudu yule mnyama-mwitu+ wala sanamu+ yake na ambao hawakupokea ile alama juu ya paji la uso wao na juu ya mkono wao.+ Nao wakawa hai na kutawala wakiwa wafalme+ pamoja na Kristo kwa miaka elfu. 5 (Wale wafu+ wengine hawakuwa hai mpaka ile miaka elfu ilipokwisha.)+ Huo ndio ufufuo wa kwanza.+ 6 Mwenye furaha+ na mtakatifu+ ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; kifo cha pili+ hakina mamlaka juu ya hao,+ bali watakuwa makuhani+ wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka elfu.+

7 Sasa mara tu ile miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa kutoka katika gereza lake, 8 naye ataenda kuyapotosha yale mataifa yaliyo katika pembe nne za dunia, Gogu na Magogu, kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita. Hesabu yao ni kama mchanga wa bahari.+ 9 Nao wakasonga juu ya upana wa dunia na kuizunguka kambi ya watakatifu+ na lile jiji+ linalopendwa. Lakini moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza.+ 10 Na Ibilisi+ aliyekuwa akiwapotosha alitupwa ndani ya lile ziwa la moto na kiberiti, ambamo wote wawili, yule mnyama-mwitu+ na yule nabii wa uwongo, tayari walikuwa;+ nao watateswa mchana na usiku milele na milele.

11 Nami nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na yeye aliyeketi juu yake.+ Dunia na mbingu zikakimbia kutoka mbele zake,+ na mahali popote hapakupatikana kwa ajili ya hizo. 12 Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo,+ wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima.+ Na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao.+ 13 Na bahari ikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi* vikawatoa wale wafu+ waliokuwa ndani yake, nao walihukumiwa kila mmoja kulingana na matendo yake.+ 14 Na kifo+ na Kaburi* vikatupwa ndani ya lile ziwa la moto. Hili linamaanisha kifo cha pili,+ lile ziwa la moto.+ 15 Zaidi ya hayo, yeyote ambaye hakupatikana ameandikwa katika kile kitabu cha uzima+ alitupwa ndani ya lile ziwa la moto.+

21 Nami nikaona mbingu mpya+ na dunia mpya;+ kwa maana mbingu+ ya kwanza na dunia+ ya kwanza zilikuwa zimepitilia mbali, na bahari+ haipo tena. 2 Nikaona pia lile jiji takatifu,+ Yerusalemu Jipya, likishuka kutoka mbinguni+ kwa Mungu na limetayarishwa kama bibi-arusi+ aliyepambwa kwa ajili ya mume wake.+ 3 Ndipo nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha ufalme ikisema: “Tazama! Hema+ la Mungu liko pamoja na wanadamu, naye atakaa+ pamoja nao, nao watakuwa watu wake.+ Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.+ 4 Naye atafuta kila chozi+ kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena,+ wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.+ Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”+

5 Na Yule aliyeketi juu ya kiti cha ufalme+ akasema: “Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.”+ Pia, anasema: “Andika, kwa sababu maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.” 6 Naye akaniambia: “Yamekuwa! Mimi ndiye Alfa na Omega, mwanzo na mwisho.+ Kwa yeyote aliye na kiu mimi nitampa maji bure kutoka kwenye chemchemi ya maji ya uzima.+ 7 Yeyote anayeshinda atarithi vitu hivi, nami nitakuwa Mungu wake+ naye atakuwa mwanangu.+ 8 Lakini kwa habari ya waoga na wale wasio na imani+ na wale wenye kuchukiza katika uchafu+ wao na wauaji+ na waasherati+ na wale wanaozoea kuwasiliana na pepo na waabudu-sanamu+ na waongo+ wote, fungu lao litakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto+ na kiberiti.+ Hili linamaanisha kifo cha pili.”+

9 Na akaja mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na mabakuli saba yaliyojaa mapigo saba ya mwisho,+ naye akasema nami na kuniambia: “Njoo hapa, nitakuonyesha bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo.”+ 10 Kwa hiyo akanichukua katika nguvu za roho mpaka kwenye mlima mkubwa na mrefu sana,+ naye akanionyesha lile jiji takatifu+ Yerusalemu likishuka kutoka mbinguni kwa Mungu+ 11 na likiwa na utukufu wa Mungu.+ Mwangaza wake ulikuwa kama jiwe la thamani zaidi, kama jiwe la yaspi lenye kung’aa kwa uangavu kama fuwele.+ 12 Lilikuwa na ukuta+ mkubwa na mrefu sana nalo lilikuwa na malango kumi na mawili, na kwenye hayo malango malaika kumi na wawili, na majina yalikuwa yameandikwa ambayo ni yale ya makabila kumi na mawili ya wana wa Israeli.+ 13 Upande wa mashariki kulikuwa na malango matatu, na upande wa kaskazini malango matatu, na upande wa kusini malango matatu, na upande wa magharibi malango matatu.+ 14 Ukuta wa jiji lile pia ulikuwa na mawe ya msingi+ kumi na mawili, na juu ya hayo majina kumi na mawili ya mitume+ kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.

15 Basi yeye aliyekuwa akisema nami alikuwa ameshika utete wa dhahabu kuwa kipimio,+ ili alipime jiji lile na malango yake na ukuta wake.+ 16 Na jiji linakaa mraba, na urefu wake ni mkubwa kama upana wake. Naye akalipima jiji+ kwa utete, stadia elfu kumi na mbili; urefu wake na upana wake na kimo chake ni sawa. 17 Pia, akapima ukuta wake, mikono 144, kulingana na kipimo cha mwanadamu, na wakati huohuo cha malaika. 18 Basi muundo wa ukuta wake ulikuwa yaspi,+ na jiji lilikuwa dhahabu safi kama kioo safi. 19 Misingi+ ya ukuta wa jiji ilikuwa imepambwa kwa kila namna ya jiwe la thamani:+ msingi wa kwanza ulikuwa yaspi,+ wa pili yakuti,+ wa tatu kalkedoni, wa nne zumaridi,+ 20 wa tano sardoniksi, wa sita sardio, wa saba krisolito,+ wa nane beroli, wa tisa topazi,+ wa kumi krisopraso, wa kumi na moja hayasinthi, wa kumi na mbili amethisto.+ 21 Pia, yale malango kumi na mawili yalikuwa lulu kumi na mbili; kila moja la malango lilifanyizwa kwa lulu moja.+ Na njia pana ya jiji ilikuwa dhahabu safi, kama kioo kiangavu.

22 Nami sikuona hekalu ndani yake,+ kwa maana Yehova+ Mungu Mweza-Yote+ ndiye hekalu lake,+ na pia Mwana-Kondoo.+ 23 Na jiji lile halihitaji jua wala mwezi kuliangaza, kwa maana utukufu wa Mungu ulilitia nuru,+ na taa yake ilikuwa yule Mwana-Kondoo.+ 24 Na mataifa yatatembea kwa njia ya nuru yake,+ na wafalme wa dunia wataleta utukufu wao ndani yake.+ 25 Na malango yake hayatafungwa hata kidogo wakati wa mchana,+ kwa maana usiku hautakuwa humo.+ 26 Nao wataleta utukufu na heshima ya mataifa ndani yake.+ 27 Lakini kitu chochote kisicho kitakatifu na yeyote anayeendelea kutenda chukizo+ na uwongo+ hataingia ndani yake hata kidogo;+ watakaoingia ni wale tu walioandikwa katika kile kitabu cha kukunjwa cha uzima cha Mwana-Kondoo.+

22 Naye akanionyesha mto wa maji ya uzima,+ mwangavu kama fuwele, ukitiririka kutoka katika kiti cha ufalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo+ 2 ukiteremka kupitia katikati ya njia yake pana. Na upande huu wa mto na upande ule kulikuwa na miti+ ya uzima yenye kuzaa mazao kumi na mawili ya matunda, ikitoa matunda yake kila mwezi.+ Na majani ya miti ile yalikuwa ya kuponya mataifa.+

3 Na humo haitakuwapo laana yoyote tena.+ Bali kiti cha ufalme cha Mungu+ na cha Mwana-Kondoo+ kitakuwa katika jiji hilo, na watumwa wake watamtolea utumishi mtakatifu;+ 4 nao watauona uso wake,+ na jina lake litakuwa juu ya mapaji ya nyuso zao.+ 5 Pia, usiku hautakuwapo tena,+ na hawana uhitaji wa nuru ya taa wala hawana nuru ya jua, kwa sababu Yehova Mungu ataangaza nuru+ yake juu yao, nao watatawala wakiwa wafalme milele na milele.+

6 Naye akaniambia: “Maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli;+ ndiyo, Yehova Mungu wa maneno ya manabii yaliyoongozwa na roho+ alimtuma malaika wake ili kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo lazima yatendeke upesi.+ 7 Na, tazama! mimi ninakuja upesi.+ Mwenye furaha ni yeyote anayeshika maneno ya unabii wa kitabu hiki cha kukunjwa.”+

8 Basi, mimi Yohana ndiye niliyekuwa nikisikia na kuona mambo haya. Na nilipokuwa nimesikia na kuona, nikaanguka chini kuabudu+ mbele ya miguu ya yule malaika aliyekuwa akinionyesha mambo haya. 9 Lakini yeye akaniambia: “Uwe mwangalifu! Usifanye hivyo! Mimi ni mtumwa mwenzako tu na wa ndugu zako walio manabii+ na wa wale wanaoshika maneno ya kitabu hiki cha kukunjwa. Mwabudu Mungu.”+

10 Pia yeye akaniambia: “Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki cha kukunjwa, kwa maana wakati uliowekwa uko karibu.+ 11 Yeye anayetenda ukosefu wa uadilifu, na azidi kutenda ukosefu wa uadilifu;+ na mwenye uchafu azidi kufanywa mwenye uchafu;+ lakini mwadilifu+ na azidi kufanya uadilifu, na mtakatifu azidi kufanywa kuwa mtakatifu.+

12 “ ‘Tazama! Mimi ninakuja upesi,+ na thawabu+ ninayotoa ipo pamoja nami, ili kumlipa kila mmoja kulingana na matendo yake.+ 13 Mimi ndiye Alfa na Omega,+ wa kwanza na wa mwisho,+ mwanzo na mwisho. 14 Wenye furaha ni wale wanaofua kanzu zao,+ ili wawe na mamlaka ya kwenda kwenye miti ya uzima+ na kwamba waweze kuingia katika jiji kupitia malango yake.+ 15 Nje kuna mbwa+ na wale wenye mazoea ya kuwasiliana na pepo+ na waasherati+ na wauaji na waabudu-sanamu na kila mtu anayependezwa na uwongo+ na kuendelea kuutenda.’

16 “ ‘Mimi, Yesu, nilimtuma malaika wangu kuwatolea ninyi ushahidi juu ya mambo haya kwa ajili ya yale makutaniko. Mimi ndiye mzizi+ na uzao+ wa Daudi, na nyota nyangavu ya asubuhi.’ ”+

17 Na roho+ na bibi-arusi+ huendelea kusema: “Njoo!” Na yeyote anayesikia na aseme: “Njoo!”+ Na yeyote anayeona kiu aje;+ yeyote anayetaka achukue maji ya uzima bure.+

18 “Ninamtolea ushahidi kila mtu anayesikia maneno ya unabii wa kitabu hiki cha kukunjwa: Yeyote akiongeza+ kwenye mambo haya, Mungu atamwongezea mapigo+ yaliyoandikwa katika kitabu hiki; 19 na yeyote akiondoa lolote kutoka katika maneno ya kitabu cha unabii huu, Mungu ataondoa fungu lake kutoka katika ile miti ya uzima+ na kutoka katika lile jiji takatifu,+ mambo ambayo yameandikwa katika kitabu hiki cha kukunjwa.

20 “Yeye anayetoa ushahidi juu ya mambo haya asema, ‘Ndiyo; mimi ninakuja upesi.’ ”+

“Amina! Njoo, Bwana Yesu.”

21 Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo na ziwe pamoja na watakatifu.+

[Maelezo ya Chini]

Hadesi. Tazama Nyongeza 4.

Hadesi. Tazama Nyongeza 4.

Hadesi. Tazama Nyongeza 4.

Hadesi. Tazama Nyongeza 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki