Mambo ya Walawi
1 Yehova akamwita Musa, akasema naye kutoka katika hema la mkutano,+ akamwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli,+ nawe utawaambia, ‘Ikiwa mtu fulani kati yenu atatoa toleo kwa Yehova kutoka katika wanyama wa kufugwa, mtatoa toleo lenu kutoka katika mifugo na kutoka katika kundi.
3 “‘Ikiwa toleo lake ni toleo la kuteketezwa+ kutoka katika mifugo, atamtoa dume, asiye na kasoro.+ Atamtoa kwenye mwingilio wa hema la mkutano kwa hiari yake mwenyewe mbele za Yehova.+ 4 Naye ataweka mkono wake juu ya kichwa cha toleo hilo la kuteketezwa, nalo litakubaliwa+ kwa neema ili afanye upatanisho kwa ajili yake.+
5 “‘Kisha yule ng’ombe-dume mchanga atachinjwa mbele za Yehova; na wana wa Haruni, makuhani,+ wataitoa damu na kuinyunyiza damu hiyo kwenye madhabahu kuizunguka pande zote,+ madhabahu iliyo kwenye mwingilio wa hema la mkutano. 6 Nalo toleo la kuteketezwa litachunwa ngozi na kukatwa katika vipande vyake.+ 7 Na wana wa Haruni, makuhani, watawasha moto kwenye madhabahu+ na kuweka kuni kwa utaratibu kwenye moto.+ 8 Na wana wa Haruni, makuhani, watavipanga vile vipande+ kwa utaratibu, kichwa na mafuta juu ya kuni zilizo katika moto ulio kwenye madhabahu. 9 Na matumbo+ yake na miguu yake itaoshwa kwa maji; naye kuhani atafukiza vyote hivyo kwenye madhabahu viwe toleo la kuteketezwa, toleo linalotolewa kwa njia ya moto lililo na harufu ya kumtuliza Yehova.+
10 “‘Na ikiwa toleo lake linatoka katika kundi,+ kutoka kati ya wana-kondoo dume au mbuzi, wa kiume,+ asiye na kasoro, ndiye atakayemtoa kuwa toleo la kuteketezwa.+ 11 Naye atachinjwa kando ya madhabahu kuelekea kaskazini mbele za Yehova, nao wana wa Haruni, makuhani, watainyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.+ 12 Naye atamkata katika vipande vyake na kichwa chake na mafuta yake, naye kuhani ataviweka kwa utaratibu juu ya kuni zilizo katika moto ulio kwenye madhabahu.+ 13 Naye atayaosha matumbo+ na miguu+ kwa maji; naye kuhani atatoa vyote hivyo na kuvifukiza+ kwenye madhabahu. Ni toleo la kuteketezwa, toleo linalotolewa kwa njia ya moto lililo na harufu ya kumtuliza Yehova.+
14 “‘Hata hivyo, ikiwa toleo lake la kuteketezwa kwa Yehova ni toleo linalotoka kati ya ndege, basi atatoa toleo lake kutoka kati ya njiwa-tetere+ au hua wachanga.+ 15 Naye kuhani atamtoa kwenye madhabahu na kukikongonyoa+ kichwa chake na kumfukiza kwenye madhabahu, lakini damu yake itamwagwa kando ya madhabahu. 16 Naye ataondoa gole lake na manyoya yake na kuyatupa kando ya madhabahu, upande wa mashariki, mahali pa majivu yenye mafuta.+ 17 Naye atampasua kwenye mabawa yake. Hatamgawanya.+ Kisha kuhani atamfukiza kwenye madhabahu juu ya kuni zilizo katika moto. Ni toleo la kuteketezwa,+ toleo linalotolewa kwa njia ya moto lililo na harufu ya kumtuliza Yehova.+
2 “‘Sasa ikiwa nafsi fulani itamtolea Yehova toleo la nafaka,+ toleo lake litakuwa la unga laini;+ naye atamimina mafuta juu yake na kutia ubani juu yake. 2 Naye atauleta kwa wana wa Haruni, makuhani, naye kuhani atachukua kipimo cha mkono mmoja wa unga huo laini na mafuta yake pamoja na ubani wake wote; naye ataufukiza uwe kumbukumbu+ lake kwenye madhabahu, kama toleo linalotolewa kwa njia ya moto lililo na harufu ya kumtuliza Yehova. 3 Na kilichobaki kutokana na lile toleo la nafaka ni cha Haruni na wanawe,+ kama kitu kitakatifu+ zaidi kutoka katika matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto.
4 “‘Na ikiwa utatoa toleo la nafaka la kitu kilichookwa jikoni, kinapaswa kuwa cha unga laini, keki za mviringo+ zilizotiwa mafuta zisizo na chachu, au mkate mwembamba uliotiwa mafuta+ usio na chachu.+
5 “‘Na ikiwa toleo lako ni toleo la nafaka kutoka katika kiokeo,+ litakuwa la unga laini uliotiwa mafuta, usio na chachu. 6 Litavunjwa vipande-vipande, nawe utamimina mafuta juu yake.+ Ni toleo la nafaka.
7 “‘Na ikiwa toleo lako ni toleo la nafaka kutoka katika sufuria ya kukaangia, litafanywa kwa unga laini pamoja na mafuta. 8 Nawe utaleta kwa Yehova toleo hilo la nafaka lililofanywa kwa vitu hivyo; nalo litatolewa kwa kuhani naye atalileta karibu na madhabahu. 9 Naye kuhani atachukua sehemu ya toleo hilo la nafaka kuwa kumbukumbu+ lake na kuifukiza kwenye madhabahu, kuwa toleo linalotolewa kwa njia ya moto lililo na harufu ya kumtuliza Yehova.+ 10 Na kilichobaki kutoka katika toleo hilo la nafaka ni cha Haruni na wanawe, kama kitu kitakatifu zaidi cha matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto.+
11 “‘Hakuna toleo lolote la nafaka ambalo mtamtolea Yehova litakalofanywa kuwa kitu kilichotiwa chachu,+ kwa sababu hamtafukiza unga wowote uliokandwa wenye chachu wala asali yoyote, kuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.
12 “‘Likiwa ni toleo la mazao ya kwanza,+ mtamtolea Yehova vitu hivyo, navyo visiletwe juu ya madhabahu viwe harufu ya kutuliza.
13 “‘Na kila toleo kati ya toleo lako la nafaka utalikoleza kwa chumvi;+ wala usikubali chumvi ya agano+ la Mungu wako ikosekane kwenye toleo lako la nafaka. Pamoja na kila toleo lako utatoa chumvi.
14 “‘Na ikiwa utamtolea Yehova toleo la nafaka la matunda ya kwanza yaliyoiva, utatoa masuke mabichi yaliyookwa kwa moto, chenga-chenga za nafaka mpya, kuwa toleo la matunda yako ya kwanza yaliyoiva.+ 15 Nawe utatia mafuta juu yake na kuweka ubani juu yake. Ni toleo la nafaka.+ 16 Naye kuhani atafukiza kumbukumbu+ lake, yaani, sehemu ya chenga-chenga zake na mafuta, pamoja na ubani wake wote, kuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.
3 “‘Na ikiwa toleo lake ni dhabihu ya ushirika,+ ikiwa analitoa kutoka kati ya mifugo, wa kiume au wa kike, atamtoa yule asiye na kasoro+ mbele za Yehova. 2 Naye atauweka mkono wake juu ya kichwa+ cha toleo lake, nalo litachinjwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano; nao wana wa Haruni, makuhani, watainyunyiza damu yake kwenye madhabahu kuizunguka pande zote. 3 Naye atatoa sehemu ya dhabihu hiyo ya ushirika kuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, yaani, mafuta+ yanayofunika matumbo, naam, mafuta yote yaliyo juu ya matumbo,+ 4 na zile figo mbili+ na mafuta yaliyo juu yake, sawa na yale yaliyo juu ya viuno. Na kile kipasho kilicho juu ya ini, atakiondoa pamoja na figo. 5 Nao wana wa Haruni+ wataifukiza+ kwenye madhabahu, juu ya toleo la kuteketezwa lililo juu ya kuni+ zilizo katika moto, kuwa toleo linalotolewa kwa njia ya moto lililo na harufu ya kumtuliza+ Yehova.
6 “‘Na ikiwa toleo lake linatoka kati ya kundi kwa ajili ya dhabihu ya ushirika kwa Yehova, wa kiume au wa kike, atamtoa yule asiye na kasoro.+ 7 Ikiwa anamtoa kondoo-dume mchanga awe toleo lake, basi atamtoa mbele za Yehova.+ 8 Naye atauweka mkono wake juu ya kichwa+ cha toleo lake, nalo litachinjwa+ mbele ya hema la mkutano; nao wana wa Haruni watainyunyiza damu yake kwenye madhabahu kuizunguka pande zote. 9 Na kutoka katika dhabihu ya ushirika atatoa mafuta yake kuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+ Mkia wote wenye mafuta+ ndio atakaoutoa karibu na uti wa mgongo, na mafuta yanayofunika matumbo, ndiyo, mafuta yote yaliyo juu ya matumbo,+ 10 na zile figo mbili na yale mafuta yaliyo juu yake, yale yaliyo juu ya viuno. Na kile kipasho+ kilicho juu ya ini, atakiondoa pamoja na figo. 11 Na kuhani atavifukiza+ kwenye madhabahu kama chakula,+ toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.
12 “‘Na ikiwa toleo lake ni mbuzi,+ basi atamtoa mbele za Yehova. 13 Naye atauweka mkono wake juu ya kichwa chake,+ naye atachinjwa+ mbele ya hema la mkutano; nao wana wa Haruni watainyunyiza damu yake kwenye madhabahu kuizunguka pande zote. 14 Na kutokana naye atatoa toleo lake, kuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, mafuta yanayofunika matumbo, naam, mafuta yote yaliyo juu ya matumbo,+ 15 na zile figo mbili na mafuta yaliyo juu yake, yale yaliyo juu ya viuno. Na kile kipasho kilicho juu ya ini, atakiondoa pamoja na hizo figo. 16 Naye kuhani atavifukiza juu ya madhabahu kama chakula, toleo linalotolewa kwa njia ya moto kuwa harufu ya kutuliza. Mafuta yote ni ya Yehova.+
17 “‘Ni sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili ya vizazi vyenu, katika makao yenu yote: msile mafuta yoyote wala damu+ yoyote.’”
4 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, uwaambie, ‘Ikiwa nafsi itatenda dhambi+ bila kukusudia+ katika yoyote kati ya mambo ambayo Yehova ameamuru yasifanywe, na kwa kweli afanye moja kati ya mambo hayo:
3 “‘Kuhani, aliyetiwa mafuta,+ akitenda dhambi+ na kuleta hatia juu ya watu, basi, kwa ajili ya dhambi yake ambayo ametenda,+ atamtolea Yehova ng’ombe-dume mchanga ambaye hana kasoro, kuwa toleo la dhambi. 4 Naye atamleta ng’ombe huyo kwenye mwingilio wa hema la mkutano+ mbele za Yehova na kuuweka mkono wake juu ya kichwa cha ng’ombe huyo,+ naye atamchinja ng’ombe huyo mbele za Yehova. 5 Naye kuhani, aliyetiwa mafuta,+ atachukua sehemu ya damu ya ng’ombe huyo na kuileta ndani ya hema la mkutano; 6 naye kuhani atachovya kidole+ chake ndani ya damu hiyo na kutapanya sehemu ya damu hiyo mara saba+ mbele za Yehova mbele ya pazia la mahali patakatifu. 7 Naye kuhani atatia sehemu ya damu hiyo juu ya pembe+ za madhabahu ya uvumba uliotiwa manukato mbele za Yehova, iliyo ndani ya hema la mkutano, na damu yote iliyobaki ya ng’ombe huyo ataimimina kwenye msingi+ wa madhabahu ya toleo la kuteketezwa, iliyo kwenye mwingilio wa hema la mkutano.
8 “‘Na mafuta yote ya ng’ombe huyo wa toleo la dhambi atayaondoa kutoka kwake, mafuta yanayofunika matumbo, ndiyo, mafuta yote yaliyo juu ya matumbo,+ 9 na zile figo mbili na mafuta yaliyo juu yake, yale yaliyo juu ya viuno. Nacho kipasho kilicho juu ya ini, atakiondoa pamoja na figo.+ 10 Kitakuwa kama kile kilichoondolewa kutoka kwa yule ng’ombe-dume wa dhabihu ya ushirika.+ Naye kuhani atavifukiza kwenye madhabahu ya toleo la kuteketezwa.+
11 “‘Lakini ngozi ya ng’ombe-dume huyo na nyama yake yote pamoja na kichwa chake na miguu yake na matumbo yake na mavi yake,+ 12 atamtoa ng’ombe mzima mpaka nje ya kambi+ katika mahali safi ambapo yale majivu yenye mafuta+ humwagwa, naye atamteketeza juu ya kuni kwenye moto.+ Mahali ambapo majivu yenye mafuta humwagwa, anapaswa kuteketezwa hapo.
13 “‘Na kusanyiko lote la Israeli likifanya kosa+ na jambo hilo limefichwa machoni pa kutaniko ya kwamba wamefanya moja kati ya mambo yote ambayo Yehova ameamuru yasifanywe na kwa hiyo wamekuwa na hatia,+ 14 nayo dhambi ambayo wamefanya kinyume cha moja kati ya mambo hayo imejulikana,+ basi kutaniko litatoa ng’ombe-dume mchanga kwa ajili ya toleo la dhambi na kumleta mbele ya hema la mkutano. 15 Na wanaume wazee wa kusanyiko wataweka mikono yao juu ya kichwa cha ng’ombe+ huyo mbele za Yehova, na ng’ombe huyo atachinjwa mbele za Yehova.
16 “‘Kisha kuhani, aliyetiwa mafuta,+ ataleta sehemu ya damu ya ng’ombe-dume huyo ndani ya hema la mkutano.+ 17 Naye kuhani atachovya kidole chake katika sehemu ya damu hiyo na kuitapanya mara saba mbele za Yehova mbele ya pazia.+ 18 Naye atatia sehemu ya damu hiyo juu ya pembe za madhabahu+ iliyo mbele za Yehova, ambayo imo ndani ya hema la mkutano; na damu yote inayobaki ataimimina kwenye msingi wa madhabahu ya toleo la kuteketezwa,+ iliyo kwenye mwingilio wa hema la mkutano. 19 Naye atachukua mafuta yake yote, na kuyafukiza kwenye madhabahu.+ 20 Naye atamfanya huyo ng’ombe-dume kama alivyomfanya yule ng’ombe mwingine wa toleo la dhambi. Hivyo ndivyo atakavyomfanya; naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yao, ndipo watasamehewa. 21 Naye atamtoa huyo ng’ombe mpaka nje ya kambi na kumteketeza, kama alivyomteketeza ng’ombe-dume wa kwanza.+ Ni toleo la dhambi kwa ajili ya kutaniko.+
22 “‘Mkuu+ anapotenda dhambi naye afanye bila kukusudia moja kati ya mambo yote ambayo Yehova Mungu wake ameamuru yasifanywe,+ na kwa hiyo amekuwa na hatia, 23 au amejulishwa dhambi yake ambayo amefanya kinyume cha amri,+ basi atamleta mwana-mbuzi dume+ ambaye hana kasoro, awe toleo lake. 24 Naye atauweka mkono wake juu ya kichwa+ cha mwana-mbuzi huyo na kumchinja katika mahali ambapo toleo la kuteketezwa huchinjiwa kwa ukawaida mbele za Yehova.+ Hilo ni toleo la dhambi.+ 25 Naye kuhani atachukua sehemu ya damu ya toleo la dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe+ za madhabahu hiyo ya toleo la kuteketezwa, naye ataimimina damu yake inayobaki kwenye msingi wa madhabahu ya toleo la kuteketezwa. 26 Naye atayafukiza mafuta yake yote kwenye madhabahu kama yale mafuta ya dhabihu ya ushirika;+ naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa ajili ya dhambi zake,+ naye atasamehewa.
27 “‘Na ikiwa nafsi yoyote kati ya watu wa nchi itatenda dhambi bila kukusudia kwa kufanya moja kati ya mambo ambayo Yehova anaamuru yasifanywe nayo iwe na hatia,+ 28 au amejulishwa dhambi yake ambayo ametenda, basi atamtoa mwana-mbuzi jike+ ambaye hana kasoro, awe toleo lake kwa ajili ya dhambi ambayo amefanya. 29 Naye ataweka mkono wake juu ya kichwa+ cha toleo la dhambi na kulichinja toleo la dhambi katika mahali pale pale pa toleo la kuteketezwa.+ 30 Naye kuhani atachukua sehemu ya damu yake kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe+ za madhabahu ya toleo la kuteketezwa, naye ataimimina damu yake yote inayobaki kwenye msingi wa madhabahu.+ 31 Naye atayaondoa mafuta yake yote,+ kama mafuta yalivyoondolewa kwenye dhabihu ya ushirika;+ naye kuhani atayafukiza kwenye madhabahu yawe harufu ya kumtuliza Yehova;+ naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.+
32 “‘Lakini ikiwa atamleta mwana-kondoo+ awe toleo lake la dhambi, atamleta mwana-kondoo jike ambaye hana kasoro.+ 33 Naye atauweka mkono wake juu ya kichwa cha toleo la dhambi na kumchinja awe toleo la dhambi katika mahali pale ambapo toleo la kuteketezwa huchinjiwa.+ 34 Naye kuhani atachukua sehemu ya damu hiyo ya toleo la dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya toleo la kuteketezwa,+ naye ataimimina damu yake yote inayobaki kwenye msingi wa madhabahu. 35 Naye atayaondoa mafuta yake yote kama mafuta ya mwana-kondoo dume wa dhabihu ya ushirika yanavyoondolewa kwa ukawaida, naye kuhani atayafukiza kwenye madhabahu juu ya matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto;+ naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa ajili ya dhambi ambayo amefanya, naye atasamehewa.+
5 “‘Ikiwa nafsi+ inatenda dhambi kwa kuwa amesikia laana+ ya hadharani naye ni shahidi au ameiona au amepata kujua juu yake, asipotoa habari,+ ndipo atakapojibu kwa sababu ya kosa lake.
2 “‘Au nafsi inapogusa kitu kisicho safi, iwe ni mzoga wa mnyama-mwitu asiye safi au mzoga wa mnyama wa kufugwa asiye safi au mzoga wa kiumbe kinachozaana kwa wingi kisicho safi,+ ingawa ulikuwa umefichwa machoni pake,+ bado yeye si safi naye amekuwa na hatia.+ 3 Au ikiwa anagusa uchafu wa mwanadamu kuhusiana na uchafu+ wowote wake ambao huenda ukamfanya asiwe safi, ingawa ulikuwa umefichwa machoni pake, na hata hivyo yeye mwenyewe amepata kujua, basi amekuwa na hatia.
4 “‘Au ikiwa nafsi inaapa kiasi cha kusema kwa midomo yake bila kufikiri+ kwamba itende uovu+ au kufanya mema kuhusiana na jambo lolote ambalo huenda mtu huyo akasema bila kufikiri katika ahadi yenye kiapo,+ ingawa lilikuwa limefichwa machoni pake, na hata hivyo yeye mwenyewe amepata kulijua, basi amekuwa na hatia kuhusiana na moja kati ya mambo hayo.
5 “‘Na itakuwa kwamba ikiwa anakuwa na hatia kwa sababu ya moja kati ya mambo hayo, ndipo atakapoungama+ jinsi ambavyo ametenda dhambi. 6 Naye ataleta toleo lake la hatia+ mbele za Yehova kwa ajili ya dhambi yake ambayo ametenda, yaani, wa kike kutoka katika kundi, mwana-kondoo jike au mwana-mbuzi jike,+ kwa ajili ya toleo la dhambi; naye kuhani atamfanyia upatanisho kwa ajili ya dhambi yake.+
7 “‘Hata hivyo, ikiwa hana uwezo wa kutoa kondoo,+ basi atamletea Yehova njiwa-tetere+ wawili au hua wawili wachanga wawe toleo lake la hatia+ kwa ajili ya dhambi ambayo ametenda, mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi na mmoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa. 8 Naye atawaleta kwa kuhani, ambaye kwanza atamtoa yule wa toleo la dhambi na kukongonyoa+ kichwa chake upande wa mbele wa shingo yake, lakini asikikate kabisa. 9 Naye atatapanya sehemu ya damu ya toleo la dhambi kando ya madhabahu, lakini damu inayobaki itaachwa itiririke kwenye msingi wa madhabahu.+ Hilo ni toleo la dhambi. 10 Na yule mwingine atamtoa kuwa toleo la kuteketezwa kulingana na utaratibu wa kawaida;+ naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa sababu ya dhambi yake ambayo ametenda, naye atasamehewa.+
11 “‘Sasa ikiwa hana uwezo+ wa kutoa njiwa-tetere wawili au hua wawili wachanga, basi ataleta sehemu ya kumi ya efa+ ya unga laini kwa ajili ya toleo la dhambi, uwe toleo lake la dhambi. Naye hatatia mafuta+ juu yake wala hataweka ubani juu yake, kwa maana ni toleo la dhambi.+ 12 Naye atauleta kwa kuhani, naye kuhani atachukua kipimo cha mkono mmoja uwe kumbukumbu+ lake naye ataufukiza kwenye madhabahu juu ya toleo la Yehova linalotolewa kwa njia ya moto.+ Hilo ni toleo la dhambi.+ 13 Naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa sababu ya dhambi yake ambayo ametenda, yoyote kati ya dhambi hizo, naye atasamehewa; nao utakuwa wa kuhani+ sawa na toleo la nafaka.’”
14 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 15 “Ikiwa nafsi inajiendesha kwa njia isiyo ya uaminifu kwa kutenda dhambi bila kukusudia juu ya mambo matakatifu ya Yehova,+ basi atamtolea Yehova kondoo-dume ambaye hana kasoro kutoka katika kundi, awe toleo lake la hatia,+ kulingana na ile thamani iliyokadiriwa ya shekeli za fedha,+ kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, kuwa toleo la hatia. 16 Naye atalipa kwa ajili ya dhambi ambayo amepatendea mahali patakatifu naye ataongeza juu yake sehemu yake ya tano,+ naye atampa kuhani, ili kuhani afanye upatanisho+ kwa ajili yake kwa kutumia yule kondoo-dume wa toleo la hatia, naye atasamehewa.+
17 “Na ikiwa nafsi inatenda dhambi kwa kuwa anafanya moja kati ya mambo ambayo Yehova anaamuru yasifanywe, ingawa hakujua,+ hata hivyo amekuwa na hatia na lazima atajibu kwa sababu ya kosa lake.+ 18 Naye atamleta kondoo-dume ambaye hana kasoro kutoka katika kundi kulingana na thamani iliyokadiriwa, kwa ajili ya toleo la hatia,+ kwa kuhani; naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake kwa sababu ya kosa alilofanya bila kukusudia, ingawa yeye mwenyewe hakujua, naye atasamehewa.+ 19 Hilo ni toleo la hatia.+ Hakika amekuwa na hatia dhidi ya Yehova.”
6 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Ikiwa nafsi inatenda dhambi, kwa kujiendesha kwa njia isiyo ya uaminifu kwa Yehova+ naye amdanganye+ mwenzake juu ya kitu fulani alicho nacho au arbuni iliyo mkononi mwake+ au kumnyang’anya, au ampunje mwenzake,+ 3 au apate kitu kilichopotea+ naye adanganye kuhusu kitu hicho na kuapa kwa uwongo+ juu ya jambo lolote kati ya mambo yote ambayo huenda mtu huyo akafanya na kutenda dhambi kutokana nayo; 4 basi itakuwa kwamba akitenda dhambi na kuwa na hatia,+ lazima atarudisha kile kitu alichopata kwa unyang’anyi au alichopata kwa upokonyaji ambacho amechukua kwa kupunja au kitu alicho nacho ambacho alipewa au kitu kilichopotea ambacho amekipata, 5 au kitu chochote ambacho huenda akaapa juu yake kwa uwongo, naye atatoa malipo+ kwa ajili yake kwa kiwango chake kamili, naye ataongezea juu yake sehemu yake ya tano. Siku ambayo hatia yake itahakikishwa atampa mwenyewe kitu hicho. 6 Naye atamletea Yehova toleo la hatia, kondoo-dume ambaye hana kasoro+ kutoka katika kundi kulingana na thamani iliyokadiriwa, kwa ajili ya toleo la hatia,+ kwa kuhani. 7 Naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake mbele za Yehova, naye atasamehewa lolote ambalo huenda akafanya kati ya mambo yote hayo, nalo limfanye awe na hatia.”
8 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 9 “Mwamuru Haruni na wanawe, na kusema, ‘Hii ndiyo sheria ya toleo la kuteketezwa:+ Toleo la kuteketezwa litakuwa kwenye jiko juu ya madhabahu usiku kucha mpaka asubuhi, nao moto wa madhabahu utawashwa ndani yake. 10 Naye kuhani atajivika nguo yake rasmi ya kitani,+ naye atavaa ile suruali+ ya kitani mwilini mwake. Kisha atayachukua yale majivu yenye mafuta+ ya toleo la kuteketezwa ambayo huteketezwa kwa moto kwa ukawaida juu ya madhabahu, naye atayaweka kando ya madhabahu. 11 Naye atayavua mavazi+ yake na kuvaa mavazi mengine, naye atayachukua yale majivu yenye mafuta mpaka mahali safi nje ya kambi.+ 12 Na huo moto kwenye madhabahu utaendelea kuwaka juu yake. Usizimike. Naye kuhani atateketeza kuni+ juu yake asubuhi baada ya asubuhi na kuweka kwa utaratibu toleo la kuteketezwa juu yake, naye atafukiza vile vipande vyenye mafuta vya dhabihu ya ushirika juu yake.+ 13 Moto+ utawaka daima kwenye madhabahu. Usizimike.
14 “‘Hii ndiyo sheria ya toleo la nafaka:+ Ninyi wana wa Haruni, litoeni mbele za Yehova mbele ya madhabahu. 15 Na mmoja wao atachukua kipimo cha mkono mmoja wa huo unga laini wa toleo la nafaka na sehemu ya mafuta yake na ubani wote ulio juu ya toleo hilo la nafaka, naye ataufukiza kwenye madhabahu uwe harufu ya kutuliza ya kumbukumbu+ lake kwa Yehova. 16 Na ule unaobaki, Haruni na wanawe wataula.+ Utaliwa kama keki zisizo na chachu+ katika mahali patakatifu. Wataula kwenye ua wa hema la mkutano. 17 Hautaokwa pamoja na kitu chochote kilichotiwa chachu.+ Nimeutoa uwe fungu lao kutoka katika matoleo yangu yanayotolewa kwa njia ya moto.+ Ni kitu kitakatifu zaidi,+ kama lile toleo la dhambi na kama lile toleo la hatia. 18 Kila mwanamume+ kati ya wana wa Haruni ataula. Ni posho kutoka katika matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto, mpaka wakati usio na kipimo+ katika vizazi vyenu vyote. Chochote kitakachoyagusa kitakuwa kitakatifu.’”
19 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 20 “Hili ndilo toleo+ la Haruni na wanawe ambalo watamtolea Yehova siku ya kutiwa mafuta kwake:+ sehemu ya kumi ya efa+ ya unga laini uwe toleo la nafaka+ daima, nusu yake asubuhi na nusu yake jioni. 21 Utatolewa pamoja na mafuta kwenye kiokeo.+ Utauleta ukiwa umechanganywa vizuri. Utatoa vitumbua vya toleo la nafaka vipande-vipande viwe harufu ya kumtuliza Yehova. 22 Na kuhani, aliyetiwa mafuta badala yake kati ya wanawe,+ atatoa toleo hilo. Ni sharti mpaka wakati usio na kipimo: Hilo toleo zima litafukizwa+ kwa Yehova. 23 Na kila toleo la nafaka la kuhani+ litakuwa toleo zima. Halitaliwa.”
24 Naye Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 25 “Sema na Haruni na wanawe, na kuwaambia, ‘Hii ndiyo sheria ya toleo la dhambi:+ Katika mahali+ ambapo toleo la kuteketezwa huchinjiwa kwa ukawaida, toleo la dhambi litachinjwa mbele za Yehova. Ni kitu kitakatifu zaidi.+ 26 Kuhani ambaye hutoa toleo hilo kwa ajili ya dhambi atalila.+ Katika mahali patakatifu+ litaliwa katika ua+ wa hema la mkutano.
27 “‘Chochote ambacho huenda kikagusa nyama yake kitakuwa kitakatifu,+ na mtu yeyote akitapanya damu yake juu ya vazi,+ utakioshea katika mahali patakatifu kile ambacho ametapanya damu juu yake.+ 28 Na chombo cha udongo+ ambamo huenda likatokosewa ndani yake kitavunjwa. Lakini ikiwa lilitokoswa katika chombo cha shaba, basi kitaparuzwa na kuoshwa kwa maji.
29 “‘Kila mwanamume kati ya makuhani atalila.+ Ni kitu kitakatifu zaidi.+ 30 Hata hivyo, toleo lolote la dhambi ambalo sehemu ya damu+ yake itaingizwa katika hema la mkutano ili kufanya upatanisho katika mahali patakatifu, halitaliwa. Litateketezwa kwa moto.
7 “‘Nayo hii ndiyo sheria ya toleo la hatia:+ Ni kitu kitakatifu zaidi.+ 2 Katika mahali+ ambapo toleo la kuteketezwa huchinjiwa kwa ukawaida, hapo watachinja toleo la hatia, na damu+ yake atainyunyiza+ juu ya madhabahu kuizunguka pande zote. 3 Nayo mafuta yake yote,+ atatoa ule mkia wenye mafuta na mafuta yanayofunika matumbo, 4 na zile figo mbili na mafuta yaliyo juu yake sawa na yale yaliyo juu ya viuno. Na kile kipasho kilicho juu ya ini, atakiondoa pamoja na figo.+ 5 Naye kuhani atavifukiza kwenye madhabahu viwe toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+ Ni toleo la hatia. 6 Litaliwa na kila mwanamume kati ya makuhani.+ Katika mahali patakatifu litaliwa. Ni kitu kitakatifu zaidi.+ 7 Kama toleo la dhambi lilivyo, ndivyo na toleo la hatia lilivyo. Kuna sheria moja kwa matoleo hayo.+ Litakuwa la kuhani ambaye atafanya upatanisho kwa toleo hilo.
8 “‘Naye kuhani anayetoa toleo la kuteketezwa la mtu yeyote, ngozi+ ya toleo la kuteketezwa ambalo mtu huyo ameleta kwa kuhani itakuwa yake.
9 “‘Na kila toleo la nafaka ambalo huenda likaokwa kwenye jiko+ na kila moja lililotayarishwa kwenye sufuria ya kukaangia+ na kwenye kiokeo+ ni la kuhani anayelitoa. Litakuwa lake.+ 10 Bali kila toleo lililotiwa mafuta+ au lililo kavu+ litakuwa la wana wote wa Haruni, la mmoja sawa na mwingine.
11 “‘Sasa hii ndiyo sheria ya dhabihu ya ushirika+ ambayo mtu yeyote atamtolea Yehova: 12 Ikiwa anaitoa ili kuonyesha shukrani,+ basi ataitoa pamoja na dhabihu ya shukrani ya keki za mviringo zisizo na chachu ambazo zimetiwa mafuta na mikate myembamba isiyo na chachu iliyopakwa mafuta+ na unga laini uliochanganywa vizuri ukiwa keki za mviringo zilizotiwa mafuta. 13 Atatoa toleo lake pamoja na ile dhabihu ya shukrani ya dhabihu zake za ushirika na kuziambatanisha na keki za mviringo za mkate wenye chachu.+ 14 Na kutoka katika hiyo atatoa moja kati ya kila toleo liwe fungu takatifu kwa Yehova;+ nalo litakuwa la kuhani+ anayenyunyiza damu ya dhabihu za ushirika. 15 Nayo nyama ya dhabihu ya shukrani ya dhabihu zake za ushirika italiwa siku yake ya kutoa toleo. Hataweka akiba yoyote ya nyama hiyo mpaka asubuhi.+
16 “‘Na ikiwa dhabihu ya toleo lake ni toleo la nadhiri+ au la hiari,+ italiwa siku atakayoitoa dhabihu yake, na kesho yake kilichobaki kinaweza kuliwa. 17 Lakini nyama inayobaki ya dhabihu katika siku ya tatu, itateketezwa kwa moto.+ 18 Hata hivyo, ikiwa nyama yoyote ya dhabihu yake ya ushirika italiwa katika siku ya tatu, yule anayeitoa hatapata kibali.+ Haitahesabiwa kwake.+ Itakuwa kitu kichafu, nayo nafsi ambayo itakula sehemu yake itajibu kwa kosa lake.+ 19 Nayo nyama itakayogusa kitu chochote kisicho safi+ isiliwe. Itateketezwa kwa moto. Kuhusu nyama ile nyingine, kila mtu aliye safi anaweza kuila nyama hiyo.
20 “‘Nayo nafsi inayokula nyama ya dhabihu ya ushirika, ambayo ni ya Yehova, wakati ambapo uchafu wake uko juu yake, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.+ 21 Na ikiwa nafsi itagusa kitu chochote kisicho safi, uchafu wa mwanadamu+ au mnyama asiye safi+ au kitu chochote chenye kuchukiza kisicho safi,+ naye ale sehemu ya nyama ya dhabihu ya ushirika, ambayo ni ya Yehova, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.’”
22 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 23 “Sema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Msile mafuta+ yoyote ya ng’ombe-dume au mwana-kondoo dume au ya mbuzi. 24 Sasa mafuta ya mzoga ambao tayari umekufa na mafuta ya mnyama aliyeraruliwa+ vipande-vipande yanaweza kutumiwa kwa ajili ya kitu kingine chochote kinachoweza kufikiriwa, lakini ninyi msiyale hata kidogo. 25 Kwa maana mtu yeyote anayekula mafuta kutoka kwa mnyama anayemtoa awe toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, nafsi inayokula itakatiliwa mbali+ na watu wake.
26 “‘Wala msile damu+ yoyote mahali popote mnapokaa, iwe ni ya ndege au ya mnyama. 27 Nafsi yoyote inayokula damu yoyote, nafsi hiyo itakatiliwa mbali+ na watu wake.’”
28 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 29 “Sema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Mtu anayemtolea Yehova dhabihu yake ya ushirika atamletea Yehova toleo lake kutoka katika dhabihu yake ya ushirika.+ 30 Mikono yake italeta yale mafuta+ yaliyo kwenye kidari yawe toleo la Yehova linalotolewa kwa njia ya moto. Atayaleta pamoja na kidari hicho ili akitikise huku na huku kikiwa toleo la kutikisa+ mbele za Yehova. 31 Naye kuhani atayafukiza+ mafuta kwenye madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Haruni na wanawe.+
32 “‘Nanyi mtampa kuhani mguu wa kuume uwe fungu+ takatifu kutoka katika dhabihu zenu za ushirika. 33 Kati ya wana wa Haruni, yule atakayeitoa damu ya dhabihu ya ushirika na yale mafuta, ule mguu wa kuume utakuwa fungu lake.+ 34 Kwa maana kidari cha toleo la kutikisa+ na mguu wa lile fungu takatifu navichukua kutoka kwa wana wa Israeli kutoka katika dhabihu zao za ushirika, nami nitampa Haruni kuhani na wanawe kutoka kwa wana wa Israeli, kama sharti mpaka wakati usio na kipimo.
35 “‘Hili ndilo lililokuwa fungu la kuhani la Haruni na fungu la kuhani la wanawe kutoka katika matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto, katika siku ambayo aliwatoa+ watumikie wakiwa makuhani kwa Yehova, 36 kama vile Yehova alivyokuwa ameamuru wapewe katika siku ya kutiwa mafuta+ kwao kutoka kati ya wana wa Israeli. Ni kanuni mpaka wakati usio na kipimo katika vizazi vyao.’”+
37 Hii ndiyo sheria inayohusu toleo la kuteketezwa,+ toleo la nafaka+ na toleo la dhambi+ na toleo la hatia+ na dhabihu ya kuweka rasmi+ na dhabihu ya ushirika,+ 38 kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa kwenye Mlima Sinai+ katika siku aliyowaamuru wana wa Israeli wamtolee Yehova matoleo yao katika nyika ya Sinai.+
8 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Mchukue Haruni na wanawe pamoja naye+ na yale mavazi+ na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta+ na yule ng’ombe-dume wa toleo la dhambi+ na wale kondoo-dume wawili na kile kikapu cha keki zisizo na chachu,+ 3 nawe ukutanishe kusanyiko lote+ kwenye mwingilio wa hema la mkutano.”+
4 Ndipo Musa akafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru, nalo kusanyiko likakutanika kwenye mwingilio+ wa hema la mkutano. 5 Sasa Musa akaliambia kusanyiko: “Hili ndilo jambo ambalo Yehova ametoa amri lifanywe.”+ 6 Basi Musa akawaleta karibu Haruni na wanawe na kuwaosha+ kwa maji.+ 7 Baada ya hayo akamvika kanzu+ na kumfunga ukumbuu+ na kumvika lile koti lisilo na mikono+ na kumvika efodi+ na kumfunga kwa mshipi+ wa ile efodi na kuufunga imara kwa mshipi huo. 8 Kisha akamvika kile kifuko cha kifuani+ na kutia Urimu na Thumimu+ ndani ya kifuko hicho. 9 Kisha akakiweka kilemba+ juu ya kichwa chake na kuweka juu ya kile kilemba upande wa mbele bamba linalong’aa la dhahabu, ile ishara takatifu ya wakfu,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
10 Sasa Musa akachukua yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta, akaitia mafuta ile maskani+ na vyote vilivyokuwa ndani yake na kuvitakasa. 11 Kisha akatapanya sehemu yake mara saba kwenye madhabahu na kuitia mafuta madhabahu+ na vyombo vyake vyote na ile beseni na kinara chake ili kuvitakasa. 12 Mwishowe akamimina sehemu ya mafuta hayo ya kutia mafuta juu ya kichwa cha Haruni na kumtia mafuta ili kumtakasa.+
13 Halafu Musa akawaleta karibu wana wa Haruni+ na kuwavika kanzu na kuwafunga ukumbuu+ na kuwafunga valio la kichwani,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
14 Halafu akamwongoza ng’ombe-dume+ wa toleo la dhambi na Haruni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa+ cha yule ng’ombe wa toleo la dhambi. 15 Naye Musa akamchinja+ na kuichukua damu+ yake na kuitia kwa kidole chake juu ya pembe za madhabahu kuizunguka pande zote na kuitakasa madhabahu kutokana na dhambi, lakini ile damu nyingine akaimimina kwenye msingi wa madhabahu, apate kuitakasa ili afanye upatanisho+ juu yake. 16 Kisha akachukua mafuta yote yaliyokuwa kwenye matumbo, na kipasho cha ini na figo mbili na mafuta yake naye Musa akayafukiza juu ya madhabahu.+ 17 Naye akamteketeza kwa moto yule ng’ombe-dume pamoja na ngozi yake na nyama yake na mavi yake nje ya kambi,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
18 Sasa akamleta karibu kondoo-dume wa toleo la kuteketezwa, naye Haruni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.+ 19 Kisha Musa akamchinja na kuinyunyiza damu yake juu ya madhabahu kuizunguka pande zote.+ 20 Naye akamkata kondoo huyo vipande-vipande,+ naye Musa akakifukiza kichwa na vile vipande na yale mafuta. 21 Naye akaosha matumbo na miguu kwa maji, na Musa akamfukiza kondoo mzima juu ya madhabahu.+ Lilikuwa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya harufu ya kutuliza.+ Lilikuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
22 Kisha akamleta karibu kondoo-dume wa pili, yule kondoo wa kuweka rasmi,+ naye Haruni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo. 23 Baada ya hayo Musa akamchinja na kuchukua sehemu ya damu yake na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la Haruni na kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.+ 24 Kisha Musa akawaleta karibu wana wa Haruni na kutia sehemu ya damu kwenye ncha ya sikio lao la kuume na kwenye kidole gumba chao cha mkono wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha mguu wao wa kuume; lakini Musa akainyunyiza ile damu iliyobaki juu ya madhabahu kuizunguka pande zote.+
25 Kisha akachukua yale mafuta na ule mkia mnono na mafuta yote yaliyokuwa kwenye matumbo,+ na kipasho cha ini na zile figo mbili na mafuta yake na mguu wa kuume.+ 26 Na kutoka katika kikapu cha keki zisizo na chachu kilichokuwa mbele za Yehova akachukua keki moja ya mviringo isiyo na chachu+ na keki moja ya mviringo ya mkate uliotiwa mafuta+ na mkate mmoja mwembamba.+ Halafu akaviweka juu ya vile vipande vyenye mafuta na ule mguu wa kuume. 27 Baada ya hayo akaviweka vyote hivyo juu ya mikono ya Haruni na mikono ya wanawe na kuanza kuvitikisa huku na huku vikiwa toleo la kutikisa mbele za Yehova.+ 28 Kisha Musa akavichukua kutoka mikononi mwao na kuvifukiza kwenye madhabahu juu ya lile toleo la kuteketezwa.+ Hivyo vilikuwa dhabihu ya kuweka rasmi+ kwa ajili ya harufu ya kutuliza.+ Lilikuwa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+
29 Naye Musa akachukua kidari+ na kukitikisa huku na huku kikiwa toleo la kutikisa mbele za Yehova.+ Kutoka katika yule kondoo-dume wa kuweka rasmi kikawa fungu+ la Musa, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
30 Baada ya hayo Musa akachukua sehemu ya mafuta yanayotumiwa kutia mafuta+ na sehemu ya damu iliyokuwa juu ya madhabahu na kuvitapanya juu ya Haruni na mavazi yake na juu ya wanawe na mavazi ya wanawe. Basi akamtakasa+ Haruni na mavazi yake na wanawe+ na mavazi ya wanawe.
31 Kisha Musa akamwambia Haruni na wanawe: “Itokoseni+ nyama kwenye mwingilio wa hema la mkutano, na hapo ndipo mtakapoila+ na mkate ulio katika kile kikapu cha kuweka rasmi, kama vile nilivyopewa amri, kusema, ‘Haruni na wanawe wataila.’ 32 Na kinachobaki cha ile nyama na ule mkate mtakiteketeza kwa moto.+ 33 Nanyi msitoke nje ya mwingilio wa hema la mkutano kwa siku saba,+ mpaka siku ya kutimia kwa siku za kuwekwa kwenu rasmi, kwa sababu itachukua siku saba kuujaza mkono wenu nguvu.+ 34 Kama vile ambavyo imefanywa leo, Yehova ameamuru ifanywe hivyo ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.+ 35 Nanyi mtakaa katika mwingilio wa hema la mkutano mchana na usiku kwa siku saba,+ nanyi mtashika kesha la lazima la Yehova,+ msije mkafa; kwa maana hivyo ndivyo nimeamriwa.”
36 Naye Haruni na wanawe wakafanya mambo yote ambayo Yehova alikuwa amewaamuru kupitia Musa.
9 Na ikawa kwamba katika siku ya nane,+ Musa akamwita Haruni na wanawe na wanaume wazee wa Israeli. 2 Kisha akamwambia Haruni: “Jichukulie ndama mchanga awe toleo la dhambi+ na kondoo-dume awe toleo la kuteketezwa,+ ambao hawana kasoro, nawe uwatoe mbele za Yehova.+ 3 Lakini kwa wana wa Israeli utasema, na kuwaambia, ‘Jichukulieni mbuzi-dume+ kwa ajili ya toleo la dhambi na ndama na mwana-kondoo dume,+ kila mmoja wao mwenye umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa, 4 na ng’ombe-dume na kondoo-dume kwa ajili ya dhabihu za ushirika+ ili uwatoe dhabihu mbele za Yehova, na toleo la nafaka+ lililotiwa mafuta, kwa sababu leo ndio wakati ambao Yehova atawatokea ninyi.’”+
5 Basi wakapeleka vitu ambavyo Musa alikuwa ameamuru mbele ya hema la mkutano. Halafu kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Yehova.+ 6 Naye Musa akasema: “Hili ndilo jambo ambalo Yehova amewaamuru mfanye, ili utukufu wa Yehova uwatokee ninyi.”+ 7 Halafu Musa akamwambia Haruni: “Nenda karibu na madhabahu, utoe toleo lako la dhambi+ na toleo lako la kuteketezwa, nawe ufanye upatanisho+ kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya nyumba yako; na utoe toleo la watu+ na kufanya upatanisho+ kwa ajili yao, kama vile Yehova alivyoamuru.”
8 Haruni akaenda mara moja karibu na madhabahu na kumchinja yule ndama wa toleo la dhambi aliyekuwa kwa ajili yake.+ 9 Kisha wana wa Haruni wakampa damu+ naye akachovya kidole chake katika damu+ hiyo na kuitia juu ya pembe za madhabahu,+ na ile damu nyingine iliyobaki akaimimina kwenye msingi wa madhabahu. 10 Naye akafukiza juu ya madhabahu+ mafuta+ na figo na kipasho cha ini kutoka katika lile toleo la dhambi, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa. 11 Naye akaiteketeza kwa moto nyama na ngozi nje ya kambi.+
12 Kisha akachinja toleo la kuteketezwa nao wana wa Haruni wakampa damu naye akainyunyiza juu ya madhabahu kuizunguka pande zote.+ 13 Nao wakampa toleo la kuteketezwa likiwa vipande-vipande na kile kichwa, naye akavifukiza juu ya madhabahu.+ 14 Na zaidi, akaosha matumbo na miguu na kuvifukiza juu ya lile toleo la kuteketezwa kwenye madhabahu.+
15 Kisha akatoa lile toleo la watu+ na kumchukua yule mbuzi wa toleo la dhambi aliyekuwa kwa ajili ya watu na kumchinja na kutoa toleo la dhambi kama yule wa kwanza. 16 Halafu akatoa lile toleo la kuteketezwa na kulitoa kwa kufuatia utaratibu wa kawaida.+
17 Kisha akatoa lile toleo la nafaka+ na kuujaza mkono wake sehemu ya toleo hilo na kulifukiza juu ya madhabahu, mbali na lile toleo la kuteketezwa la asubuhi.+
18 Baada ya hayo akamchinja yule ng’ombe-dume na yule kondoo-dume wa dhabihu ya ushirika+ aliyekuwa kwa ajili ya watu. Halafu wana wa Haruni wakampa damu naye akainyunyiza juu ya madhabahu kuizunguka.+ 19 Navyo vile vipande vyenye mafuta+ vya yule ng’ombe-dume na ule mkia mnono+ wa yule kondoo-dume na yale mafuta yanayofunika na zile figo na kile kipasho cha ini, 20 sasa wakaviweka vile vipande vyenye mafuta juu ya vidari,+ kisha akavifukiza vipande hivyo vyenye mafuta juu ya madhabahu. 21 Lakini vidari na ule mguu wa kuume, Haruni alivitikisa huku na huku vikiwa toleo la kutikisa+ mbele za Yehova, kama vile Musa alivyoamuru.
22 Kisha Haruni akainua mikono yake kuelekea watu, akawabariki,+ naye akashuka+ baada ya kutoa toleo la dhambi na toleo la kuteketezwa na dhabihu za ushirika. 23 Mwishowe Musa na Haruni wakaingia ndani ya hema la mkutano, kisha wakatoka nje na kuwabariki watu.+
Ndipo utukufu wa Yehova+ ukawatokea watu wote, 24 na moto ukatoka mbele za Yehova+ nao ukaanza kuteketeza lile toleo la kuteketezwa na vile vipande vyenye mafuta juu ya madhabahu. Watu wote walipoona hilo, wakaanza kupaaza sauti+ zao nao wakaanguka kifudifudi.
10 Baadaye Nadabu na Abihu,+ wana wa Haruni, wakachukua na kuleta kila mmoja wao chetezo+ chake na kutia moto ndani yake na kutia uvumba+ juu yake, nao wakaanza kumtolea Yehova moto haramu,+ ambao hakuwa amewaamuru. 2 Ndipo moto ukatoka mbele za Yehova na kuwateketeza,+ hivi kwamba wakafa mbele za Yehova.+ 3 Ndipo Musa akamwambia Haruni: “Hivi ndivyo Yehova amesema, ‘Na nitakaswe+ kati ya wale walio karibu nami,+ nami nitukuzwe mbele ya uso wa watu wote.’”+ Naye Haruni akakaa kimya.
4 Basi Musa akamwita Mishaeli na Elsafani, wana wa Uzieli,+ ndugu ya baba ya Haruni, akawaambia: “Njooni karibu, wachukueni ndugu zenu kutoka mbele ya mahali patakatifu mpaka nje ya kambi.”+ 5 Basi wakakaribia na kuwachukua wakiwa na kanzu zao mpaka nje ya kambi, kama vile Musa alivyokuwa amesema.
6 Kwa hiyo Musa akamwambia Haruni na Eleazari na Ithamari wale wanawe wengine: “Msiache vichwa vyenu vikose kuwa nadhifu,+ wala msiyararue mavazi yenu, msije mkafa wala asije akalikasirikia kusanyiko lote;+ lakini ndugu zenu wa nyumba yote ya Israeli watalilia kule kuteketeza, ambako Yehova aliteketeza. 7 Nanyi msitoke katika mwingilio wa hema la mkutano msije mkafa,+ kwa sababu mafuta ya Yehova yanayotumiwa kutia mafuta yako juu yenu.”+ Basi wakafanya kulingana na neno la Musa.
8 Naye Yehova akasema na Haruni, na kumwambia: 9 “Usinywe divai wala kileo,+ wewe na wanao pamoja nawe, mnapoingia ndani ya hema la mkutano, msije mkafa. Hiyo ni sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili ya vizazi vyenu, 10 na ili kufanya tofauti kati ya kitu kitakatifu na kile najisi na kati ya kitu kisicho safi na kilicho safi,+ 11 na ili kuwafundisha wana wa Israeli+ masharti yote ambayo Yehova amesema kupitia Musa.”
12 Ndipo Musa akasema na Haruni na wanawe waliobaki, yaani, Eleazari na Ithamari: “Chukueni toleo la nafaka+ lililobaki kutoka katika matoleo ya Yehova yaliyotolewa kwa njia ya moto na mle pasipo kutiwa chachu karibu na madhabahu, kwa sababu hilo ni kitu kitakatifu zaidi.+ 13 Nanyi mtakula katika mahali patakatifu,+ kwa maana ndilo posho lenu na posho la wana wenu kutoka kwa matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto; kwa maana hivyo ndivyo nimeamriwa. 14 Nanyi mtakula kile kidari cha toleo la kutikisa+ na ule mguu wa lile fungu takatifu+ katika mahali safi, wewe na wanao na binti zako pamoja nawe,+ kwa sababu vimetolewa kuwa posho lako na posho la wanao kutoka katika dhabihu za ushirika za wana wa Israeli. 15 Watauleta mguu wa lile fungu takatifu na kile kidari cha toleo la kutikisa+ pamoja na matoleo yanayotolewa kwa njia ya moto, ya vile vipande vyenye mafuta, ili kutikisa toleo la kutikisa huku na huku, mbele za Yehova; nalo litakuwa posho+ mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili yako na wanao pamoja nawe, kama vile Yehova ameamuru.”
16 Naye Musa akamtafuta sana huyo mbuzi wa toleo la dhambi,+ na, tazama! alikuwa ameteketezwa kabisa. Basi akawaka hasira kuwaelekea Eleazari na Ithamari, wana wa Haruni waliokuwa wamebaki, na kusema: 17 “Kwa nini hamkula lile toleo la dhambi katika mahali palipo patakatifu,+ kwa kuwa ni kitu kitakatifu zaidi naye amewapa ninyi mpate kujibu kwa ajili ya kosa la kusanyiko ili kufanya upatanisho kwa ajili yao mbele za Yehova?+ 18 Tazama! damu yake haijaletwa ndani katika mahali patakatifu.+ Mlipaswa kula toleo hilo katika mahali patakatifu, kama vile nilivyokuwa nimeamriwa.”+ 19 Basi Haruni akasema na Musa: “Tazama! Leo wametoa toleo lao la dhambi na toleo lao la kuteketezwa mbele za Yehova,+ kisha mambo haya yameanza kunipata; na ikiwa ningekuwa nimekula toleo la dhambi leo, je, jambo hilo lingekuwa jema machoni pa Yehova?”+ 20 Musa aliposikia hilo, ndipo hilo likawa jema machoni pake.
11 Na Yehova akasema na Musa na Haruni, akiwaambia: 2 “Semeni na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Hiki ndicho kiumbe hai ambacho mnaweza kula+ kati ya wanyama wote walio kwenye uso wa dunia: 3 Kila kiumbe kati ya wanyama chenye ukwato uliopasuka na chenye mwanya kwenye ukwato na kinachocheua, hicho ndicho mnachoweza kula.+
4 “‘Ila hiki ndicho ambacho hamtakula kati ya wacheuaji na wenye ukwato uliopasuka: ngamia, kwa sababu ni mcheuaji lakini hana ukwato uliopasuka. Huyo si safi kwenu.+ 5 Pia wibari,+ kwa sababu ni mcheuaji lakini hana ukwato uliopasuka. Huyo si safi kwenu. 6 Pia sungura,+ kwa sababu ni mcheuaji lakini hana ukwato uliopasuka. Huyo si safi kwenu. 7 Pia nguruwe,+ kwa sababu ana ukwato uliopasuka naye ana mwanya kwenye ukwato, lakini yeye mwenyewe hacheui. Huyo si safi kwenu. 8 Msile yoyote kati ya nyama zao, wala msiguse mizoga yao.+ Hao si safi kwenu.+
9 “‘Hiki ndicho mnachoweza kula kati ya kila kitu kilicho majini:+ Kila kitu chenye mapezi na magamba+ majini, katika bahari na katika mito, hivyo mnaweza kula. 10 Na kila kitu katika bahari na katika mito ambacho hakina mapezi na magamba, kati ya kila kiumbe kinachozaana kwa wingi cha majini na kati ya kila nafsi hai iliyo majini, hivyo ni vitu vyenye kuchukiza kwenu. 11 Naam, vitakuwa chukizo kwenu. Msile yoyote kati ya nyama zao,+ nanyi mtaichukia mizoga yao. 12 Kila kitu majini ambacho hakina mapezi na magamba ni chukizo kwenu.
13 “‘Navyo hivi ndivyo mtakavyovichukia kati ya viumbe vinavyoruka.+ Visiliwe. Hivyo ni chukizo: tai+ na furukombe na tai-mzoga mweusi, 14 na mwewe mwekundu na mwewe mweusi+ kulingana na aina yake, 15 na kila kunguru+ kulingana na aina yake, 16 na mbuni+ na bundi na shakwe na kipanga kulingana na aina yake, 17 na bundi mdogo na mnandi na bundi mwenye masikio marefu,+ 18 na bata-maji na mwari na tai-mzoga,+ 19 na korongo, kulastara kulingana na aina yake na hudihudi na popo.+ 20 Kila kiumbe chenye mabawa kinachozaana kwa wingi ambacho hutembea kwa miguu minne ni chukizo kwenu.+
21 “‘Ila hiki ndicho mnachoweza kula kati ya viumbe vyote vyenye mabawa vinavyozaana kwa wingi ambavyo hutembea kwa miguu minne, vile vyenye miguu ya kuruka juu ya miguu yao, ili kuruka nayo juu ya dunia. 22 Hawa ndio mnaoweza kula kati yao: nzige mwenye kuhama+ kulingana na aina yake, na nzige anayeweza kuliwa+ kulingana na aina yake, na nyenje kulingana na aina yake na panzi+ kulingana na aina yake. 23 Na kila kiumbe kingine chenye mabawa kinachozaana kwa wingi chenye miguu minne ni chukizo+ kwenu. 24 Basi kupitia kwao mtajifanya wenyewe msiwe safi. Kila mtu anayegusa mizoga yao atakuwa asiye safi mpaka jioni.+ 25 Na kila mtu anayebeba wowote kati ya mizoga yao atayafua+ mavazi yake, naye atakuwa asiye safi mpaka jioni.
26 “‘Na mnyama yeyote ambaye ana ukwato uliopasuka lakini hana mwanya wala si mcheuaji, hao si safi kwenu. Kila mtu anayewagusa hao atakuwa si safi.+ 27 Na kila kiumbe kinachotembea kwa miguu yenye makucha kati ya viumbe hai vinavyoenda kwa miguu minne, hao si safi kwenu. Kila mtu anayeigusa mizoga yao atakuwa asiye safi mpaka jioni. 28 Naye anayeibeba mizoga+ yao atafua mavazi yake,+ naye atakuwa asiye safi mpaka jioni. Hao si safi kwenu.
29 “‘Nacho hiki ndicho kisicho safi kwenu kati ya viumbe vinavyozaana kwa wingi ambavyo hujaa duniani:+ fuko na panya anayeruka+ na mjusi kulingana na aina yake, 30 na mjusi kafiri na mjusi mkubwa na mjusi wa majini na mjusi wa mchangani na kinyonga. 31 Hao si safi kwenu kati ya viumbe vyote vinavyozaana kwa wingi.+ Kila mtu anayevigusa viumbe hivyo vikiwa vimekufa atakuwa asiye safi mpaka jioni.+
32 “‘Sasa chochote ambacho yeyote kati yao ataangukia akiwa amekufa kitakuwa kisicho safi, kiwe ni chombo cha mbao+ au nguo au ngozi+ au nguo ya gunia.+ Chombo chochote ambacho hutumiwa kwa njia fulani kitatiwa katika maji, nacho kitakuwa kisicho safi mpaka jioni halafu kitakuwa safi. 33 Nacho chombo chochote cha udongo+ ambacho yeyote kati yao ataanguka ndani yake, chochote kilicho ndani yake kitakuwa kisicho safi, nanyi mtakivunja.+ 34 Chakula cha namna yoyote ambacho huenda kikaliwa kitakachopata maji kutoka katika chombo hicho kitakuwa kisicho safi, na kinywaji chochote ambacho kinaweza kunywewa katika chombo chochote kitakuwa kisicho safi. 35 Na kila kitu ambacho juu yake huenda wowote kati ya mizoga yao ukaangukia kitakuwa kisicho safi. Iwe ni jiko au kinara cha mtungi, kitavunjwa. Vitu hivyo si safi, navyo vitakuwa si safi kwenu. 36 Ila tu bubujiko na shimo la maji yaliyozuiliwa ndiyo yatakayoendelea kuwa safi, lakini mtu yeyote anayegusa mizoga yao atakuwa asiye safi. 37 Na wowote wa mizoga ukianguka juu ya mbegu yoyote ya mmea wa kupandwa, ni safi. 38 Lakini ikiwa maji yatatiwa juu ya mbegu na kitu fulani cha mizoga yao kianguke juu yake, si safi kwenu.
39 “‘Sasa, ikiwa mnyama yeyote aliye wenu kwa ajili ya chakula atakufa, mtu anayeugusa mzoga wake atakuwa asiye safi mpaka jioni.+ 40 Naye anayekula+ sehemu yoyote ya mzoga wake atayafua mavazi yake, naye atakuwa asiye safi mpaka jioni; naye anayeubeba mzoga wake atayafua mavazi yake, naye atakuwa asiye safi mpaka jioni. 41 Na kila kiumbe kinachozaana kwa wingi ambacho kinajaa duniani ni chukizo.+ Kisiliwe. 42 Nacho kiumbe chochote ambacho hutembea kwa tumbo+ na kiumbe chochote ambacho hutembea kwa miguu yote minne au hesabu yoyote kubwa ya miguu ya viumbe vyote vinavyozaana kwa wingi ambavyo vinajaa duniani, msivile, kwa sababu hivyo ni chukizo.+ 43 Msifanye nafsi zenu ziwe zenye kuchukiza kutokana na kiumbe chochote kinachozaana kwa wingi ambacho kinajaa, wala msijifanye kuwa wasio safi kutokana nao na kupata kuwa wasio safi kutokana nao.+ 44 Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wenu;+ nanyi mtajitakasa wenyewe nanyi mtakuwa watakatifu,+ kwa sababu mimi ni mtakatifu.+ Kwa hiyo msifanye nafsi zenu kuwa zisizo safi kutokana na kiumbe chochote kinachozaana kwa wingi ambacho hutembea juu ya dunia. 45 Kwa maana mimi ni Yehova anayewaongoza ninyi kutoka katika nchi ya Misri ili kujionyesha kuwa Mungu kwenu;+ nanyi mtakuwa watakatifu,+ kwa sababu mimi ni mtakatifu.+
46 “‘Hiyo ndiyo sheria juu ya mnyama na kiumbe kinachoruka na kila nafsi hai ambayo hutembea majini+ na kuhusu kila nafsi inayojazana duniani, 47 ili kufanya tofauti+ kati ya kisicho safi na kilicho safi na kati ya kiumbe hai kinachoweza kuliwa na kiumbe hai kisichopasa kuliwa.’”
12 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Ikiwa mwanamke atachukua mimba+ na kuzaa mtoto wa kiume, atakuwa asiye safi kwa siku saba; kama vile katika siku za uchafu wakati anapokuwa na hedhi atakuwa asiye safi.+ 3 Na siku ya nane ngozi ya govi la mtoto huyo itatahiriwa.+ 4 Kwa siku 33 zaidi mwanamke huyo atakaa katika damu ya utakaso. Asiguse kitu chochote kilicho kitakatifu, wala asiingie mahali patakatifu mpaka kutimia kwa siku za utakaso wake.+
5 “‘Sasa, ikiwa atazaa mtoto wa kike, basi atakuwa asiye safi kwa siku 14, kama vile wakati wa kuwa na hedhi. Kwa siku 66 zaidi atakaa katika damu ya utakaso wake. 6 Kisha zitakapotimia siku za utakaso wake kwa ajili ya mwana au binti ataleta mwana-kondoo dume katika mwaka wake wa kwanza kwa ajili ya toleo la kuteketezwa+ na hua mchanga au njiwa-tetere+ kwa ajili ya toleo la dhambi kwenye mwingilio wa hema la mkutano kwa kuhani. 7 Naye atalitoa mbele za Yehova na kufanya upatanisho kwa ajili ya mwanamke huyo, naye atakuwa safi kutokana na chemchemi ya damu yake.+ Hiyo ndiyo sheria juu ya mwanamke anayezaa mtoto wa kiume au wa kike. 8 Lakini ikiwa hana uwezo wa kutosha wa kutoa kondoo, basi atachukua njiwa-tetere wawili au hua wachanga wawili,+ mmoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa na yule mwingine kwa ajili ya toleo la dhambi, naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake, naye atakuwa safi.’”
13 Na Yehova akasema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 2 “Ikiwa ngozi ya mwili wa mtu itatokeza upele au kigaga+ au doa na kukua katika ngozi ya mwili wake na kuwa pigo la ukoma,+ basi ataletwa kwa Haruni kuhani au kwa mmoja wa wanawe walio makuhani.+ 3 Naye kuhani ataliangalia lile pigo lililo katika ngozi ya mwili.+ Nywele zilizo katika pigo hilo zikigeuka na kuwa nyeupe na pigo lionekane kuwa limepenya chini ya ngozi ya mwili wake, ni pigo la ukoma. Naye kuhani atalitazama, naye atamtangaza kuwa asiye safi. 4 Lakini ikiwa doa ni jeupe katika ngozi ya mwili wake nalo halionekani kuwa limepenya chini ya ngozi yake na nywele zake hazijageuka na kuwa nyeupe, basi kuhani atamtenga+ mwenye pigo hilo siku saba. 5 Naye kuhani atamtazama siku ya saba, na ikiwa pigo hilo linaonekana kuwa limekoma, pigo hilo halijaenea katika ngozi, kuhani atamtenga+ pia siku nyingine saba.
6 “Naye kuhani atamtazama katika siku ya saba mara ya pili, na ikiwa pigo limefifia nalo pigo halijaenea katika ngozi, kuhani atamtangaza pia kuwa safi. Lilikuwa kigaga. Naye atayafua mavazi yake na kuwa safi. 7 Lakini ikiwa pasipo shaka kigaga hicho kimeenea katika ngozi baada ya kuonekana mbele ya kuhani ili kuthibitisha utakaso wake, basi atajionyesha tena mara ya pili mbele ya kuhani,+ 8 naye kuhani atatazama; na ikiwa kigaga hicho kimeenea katika ngozi, basi kuhani huyo atamtangaza kuwa asiye safi. Ni ukoma.+
9 “Ikiwa pigo la ukoma litatokea katika mtu, ataletwa kwa kuhani. 10 Naye kuhani atatazama;+ na ikiwa kuna upele mweupe katika ngozi nao umegeuza nywele kuwa nyeupe na ubichi wa nyama iliyo hai+ upo kwenye upele huo, 11 huo ni ukoma wa kudumu+ katika ngozi ya mwili wake; naye kuhani atamtangaza kuwa asiye safi. Hapaswi kumtenga,+ kwa kuwa yeye si safi. 12 Sasa ikiwa pasipo shaka ukoma huo unatokea katika ngozi, nao ukoma ufunike ngozi yote ya mtu mwenye pigo hilo toka kichwani pake mpaka miguuni pake na kuonekana kikamili machoni pa kuhani; 13 naye kuhani ametazama nao ukoma umeufunika mwili wake wote, basi atalitangaza pigo hilo kuwa safi. Lote limegeuka kuwa jeupe. Yeye ni safi. 14 Lakini siku ambayo nyama mbichi itaonekana ndani yake, atakuwa najisi. 15 Naye kuhani+ ataiona nyama hai, naye atamtangaza kuwa asiye safi. Hiyo nyama hai si safi. Ni ukoma.+ 16 Au ikiwa nyama hai itarudi na kubadilika kuwa nyeupe, ndipo atakuja kwa kuhani. 17 Naye kuhani atamtazama,+ na ikiwa pigo hilo limebadilika na kuwa jeupe, ndipo kuhani atalitangaza pigo hilo kuwa safi. Yeye ni safi.
18 “Na kuhusu nyama, ikiwa jipu+ litatokea katika ngozi yake nalo lipone, 19 na mahali pa jipu patokee upele mweupe au doa jekundu-jeupe, ndipo atajionyesha kwa kuhani. 20 Naye kuhani atatazama,+ na ikiwa linaonekana kuwa limepenya chini ya ngozi na nywele zake zimegeuka na kuwa nyeupe, ndipo kuhani atamtangaza kuwa asiye safi. Ni pigo la ukoma. Limetokea katika jipu. 21 Lakini kuhani akilitazama, na, tazama sasa, hakuna nywele nyeupe ndani yake wala halijapenya chini ya ngozi na limefifia, kuhani atamtenga+ siku saba. 22 Na ikiwa pasipo shaka limeenea katika ngozi, ndipo kuhani huyo atamtangaza kuwa asiye safi. Ni pigo. 23 Lakini doa likibaki mahali pake, halijaenea, ni jipu lenye kuwasha;+ naye kuhani atamtangaza kuwa safi.+
24 “Au ikiwa ngozi ya mwili itakuwa na kovu kutokana na moto, na ubichi wa nyama wa kovu hilo uwe doa jekundu-jeupe au jeupe, 25 ndipo kuhani atalitazama; na ikiwa nywele zimegeuka na kuwa nyeupe katika doa hilo nalo linaonekana kuwa limepenya chini ya ngozi, ni ukoma. Umetokea katika kovu hilo, naye kuhani atamtangaza kuwa asiye safi. Ni pigo la ukoma. 26 Lakini ikiwa kuhani ataliangalia, na, tazama sasa, hakuna nywele nyeupe katika doa hilo nalo halijapenya chini ya ngozi nalo limefifia, ndipo kuhani atamtenga siku saba. 27 Naye kuhani atamtazama katika siku ya saba. Ikiwa pasipo shaka limeenea katika ngozi, ndipo kuhani atamtangaza kuwa asiye safi. Ni pigo la ukoma. 28 Lakini doa hilo likibaki mahali pake, halijaenea katika ngozi nalo limefifia, ni upele wa kovu; naye kuhani atamtangaza kuwa safi, kwa sababu ni kovu lenye kuwasha.
29 “Na mwanamume au mwanamke, ikiwa atapata pigo kwenye kichwa au kwenye kidevu, 30 ndipo kuhani+ ataliona pigo hilo; na ikiwa linaonekana kuwa limepenya chini ya ngozi, nazo nywele ni za manjano na ni chache ndani yake, ndipo kuhani atamtangaza kuwa asiye safi. Ni kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida.+ Ni ukoma wa kichwa au wa kidevu. 31 Lakini ikiwa kuhani ataliona pigo la kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida, na, tazama! linaonekana kuwa halijapenya chini ya ngozi wala hakuna nywele nyeusi hapo, ndipo kuhani atamtenga+ mwenye pigo la kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida kwa siku saba.+ 32 Naye kuhani atalitazama pigo hilo katika siku ya saba; na ikiwa kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida hakujaenea, wala hakuna nywele za manjano ambazo zimekuwa hapo na kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida+ hakujapenya chini ya ngozi, 33 ndipo atanyolewa, lakini hatapanyoa mahali palipoanguka nywele isivyo kawaida;+ naye kuhani atamtenga siku nyingine saba huyo mtu ambaye nywele zimeanguka isivyo kawaida.
34 “Naye kuhani atatazama kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida katika siku ya saba; na ikiwa kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida hakujaenea katika ngozi, wala haionekani kwamba kumepenya chini ya ngozi, ndipo kuhani atamtangaza kuwa safi,+ naye atayafua mavazi yake na kuwa safi. 35 Lakini ikiwa pasipo shaka kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida kunaenea katika ngozi baada ya kuthibitishwa kwa utakaso wake, 36 ndipo kuhani+ atamwona; na ikiwa kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida kumeenea katika ngozi, kuhani hana haja ya kuchunguza nywele za manjano; yeye si safi. 37 Lakini ikiwa kwa kuonekana kwake, kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida kumesimama na nywele nyeusi zimeota hapo, kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida kumepona. Yeye ni safi, naye kuhani atamtangaza kuwa safi.+
38 “Na mwanamume au mwanamke, ikiwa madoa+ yatatokea katika ngozi ya mwili wao, madoa meupe, 39 ndipo kuhani+ atatazama; na ikiwa madoa hayo katika ngozi ya mwili wao ni ya rangi nyeupe iliyofifia, ni upele usio na madhara. Umetokea katika ngozi. Yeye ni safi.
40 “Naye mwanamume, ikiwa kichwa chake kitaanza kuwa na upara,+ ni upara. Yeye ni safi. 41 Na ikiwa kichwa chake kitakuwa na upara upande wa mbele, ni upara wa paji la uso. Yeye ni safi. 42 Lakini ikiwa pigo jekundu-jeupe litatokea katika upara wa utosi au wa paji la uso, ni ukoma unaotokea katika upara wa utosi wake au paji lake la uso. 43 Naye kuhani+ atamtazama; na ikiwa kuna upele wa pigo jekundu-jeupe katika upara wa utosi wake au wa paji lake la uso unaoonekana kama ukoma katika ngozi ya mwili, 44 yeye ni mwenye ukoma. Yeye si safi. Kuhani atamtangaza kuwa asiye safi. Pigo lake lipo kichwani pake. 45 Naye mwenye ukoma ambaye ana pigo ndani yake, mavazi yake yatararuliwa,+ na kichwa chake kisitunzwe,+ naye anapaswa kufunika masharubu+ yake na kupaaza sauti, ‘Si safi, si safi!’+ 46 Siku zote ambazo pigo hilo litakuwa ndani yake atakuwa si safi. Yeye si safi. Atakaa akiwa ametengwa. Makao yake yatakuwa nje ya kambi.+
47 “Kwa habari ya vazi, ikiwa pigo la ukoma litatokea ndani yake, iwe ni ndani ya vazi la sufu au ni ndani ya vazi la kitani, 48 au ndani ya mtande+ au ndani ya mshindio wa kitani na wa sufu, au ndani ya ngozi au ndani ya chochote kilichotengenezwa kwa ngozi,+ 49 nalo pigo la rangi ya kijani-manjano au la rangi nyekundu-nyekundu litokee ndani ya vazi hilo au ndani ya ngozi au ndani ya mtande au ndani ya mshindio au ndani ya chombo chochote cha ngozi, ni pigo la ukoma, nalo lazima lionyeshwe kwa kuhani. 50 Naye kuhani+ ataona pigo hilo, naye atalitenga+ pigo hilo siku saba. 51 Atakapokuwa ameliona pigo hilo katika siku ya saba, ya kwamba pigo hilo limeenea katika vazi au katika mtande au katika mshindio+ au katika ngozi ambayo inaweza kutumiwa kwa ajili ya matumizi yoyote, pigo hilo ni ukoma hatari.+ Si safi. 52 Naye atateketeza vazi hilo au mtande huo au mshindio huo katika sufu hiyo au katika kitani+ hicho, au chombo chochote cha ngozi ambamo pigo hilo linaweza kutokea, kwa sababu ni ukoma hatari.+ Utateketezwa katika moto.
53 “Lakini ikiwa kuhani anatazama, na, tazama sasa, pigo hilo halijaenea katika vazi au katika mtande au katika mshindio au katika chombo chochote cha ngozi,+ 54 kuhani pia ataamuru waoshe kile ambacho ndani yake mna pigo hilo, naye atalitenga mara ya pili kwa siku saba. 55 Naye kuhani atatazama pigo hilo baada ya kuoshwa, na ikiwa kuonekana kwa pigo hilo hakujabadilika na bado pigo hilo halijaenea, si safi. Utaliteketeza katika moto. Ni tundu lililo chini katika kiraka kilichochanika upande wa ndani au wa nje.
56 “Lakini ikiwa kuhani ametazama, na, tazama sasa, pigo limefifia baada ya kuoshwa, ndipo atalirarua kutoka katika vazi au ngozi au mtande au mshindio. 57 Hata hivyo, ikiwa bado linaonekana katika vazi au katika mtande au katika mshindio+ au katika chombo chochote cha ngozi, linatokea. Utakiteketeza+ motoni chochote kile ambacho ndani yake mna pigo hilo. 58 Nalo vazi au mtande au mshindio au chombo chochote cha ngozi ambacho utaosha, pigo litakapokuwa limetoweka kutoka kwake, kitaoshwa tena mara ya pili; nacho kitakuwa safi.
59 “Hiyo ndiyo sheria ya pigo la ukoma katika vazi la sufu au kitani,+ au katika mtande au katika mshindio, au katika chombo chochote cha ngozi, ili kukitangaza kuwa safi au kukitangaza kuwa si safi.”
14 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Hii itakuwa sheria ya mwenye ukoma+ katika siku ya kuthibitisha utakaso wake, atakapoletwa kwa kuhani.+ 3 Naye kuhani atatoka nje ya kambi, na kuhani atatazama; na ikiwa pigo la ukoma limepona+ katika yule mwenye ukoma, 4 ndipo kuhani atatoa amri; naye atachukua ndege wawili walio safi+ na mti wa mwerezi+ na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili+ na hisopo+ ili kujitakasa. 5 Naye kuhani atatoa amri, na yule ndege mmoja atauawa katika chombo cha udongo juu ya maji yanayotiririka.+ 6 Naye yule ndege aliye hai, atamchukua na huo mti wa mwerezi na kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na hisopo, naye atavichovya pamoja na yule ndege aliye hai katika damu ya huyo ndege aliyeuawa juu ya maji yanayotiririka. 7 Kisha ataitapanya+ mara saba+ juu ya yule anayejitakasa kutokana na ukoma naye atamtangaza kuwa safi,+ naye atamwachilia ndege aliye hai aruke kwenda zake porini.+
8 “Na yule anayejitakasa atayafua mavazi+ yake na kunyoa nywele zake zote na kuoga+ katika maji naye atakuwa safi, kisha baadaye ataingia kambini. Naye atakaa nje ya hema lake kwa siku saba.+ 9 Na itakuwa kwamba katika siku ya saba atanyoa nywele zake zote zilizo kichwani+ pake na kwenye kidevu chake na nyusi zake. Naam, atanyoa nywele zake zote, naye atayafua mavazi yake na kuoga mwili wake katika maji; naye atakuwa safi.
10 “Na katika siku ya nane+ atachukua wana-kondoo dume wawili ambao hawana kasoro na mwana-kondoo jike mmoja ambaye hana kasoro,+ katika mwaka wake wa kwanza, na sehemu tatu za kumi za efa ya unga laini kuwa toleo la nafaka+ lililotiwa mafuta na logi moja ya mafuta;+ 11 na kuhani anayemtangaza kuwa safi atamleta mtu huyo anayejitakasa, na vitu hivyo, mbele za Yehova katika mwingilio wa hema la mkutano. 12 Naye kuhani atamchukua yule mwana-kondoo dume na kumtoa kwa ajili ya toleo la hatia+ pamoja na ile logi+ moja ya mafuta naye atavitikisa huku na huku kama toleo la kutikisa+ mbele za Yehova. 13 Naye atamchinja yule mwana-kondoo dume mahali+ ambapo lile toleo la dhambi na toleo la kuteketezwa huchinjiwa kwa kawaida, katika mahali patakatifu,+ kwa sababu, kama vile toleo la dhambi, vivyo hivyo toleo la hatia ni la kuhani.+ Ni kitu kitakatifu zaidi.
14 “Naye kuhani atachukua sehemu ya damu ya toleo la hatia, naye kuhani ataitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayejitakasa na kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.+ 15 Naye kuhani atachukua kiasi fulani cha ile logi+ ya mafuta na kuyamimina kwenye kiganja cha mkono wa kushoto wa kuhani. 16 Naye kuhani atachovya kidole chake cha kuume ndani ya mafuta yaliyo katika mkono wake wa kushoto naye atatapanya sehemu ya mafuta hayo kwa kidole chake mara saba+ mbele za Yehova. 17 Nayo yale mafuta mengine yaliyo kwenye mkono wake atatia sehemu yake kwenye ncha ya sikio la yule anayejitakasa na kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume juu ya ile damu ya toleo la hatia.+ 18 Na mafuta yanayobaki yaliyo kwenye mkono wa kuhani atayatia kwenye kichwa cha yule anayejitakasa, naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake mbele za Yehova.
19 “Naye kuhani atatoa toleo la dhambi+ na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule anayejitakasa kutokana na uchafu wake, na baadaye atachinja lile toleo la kuteketezwa. 20 Naye kuhani atatoa toleo la kuteketezwa na toleo la nafaka+ juu ya madhabahu, naye kuhani+ atafanya upatanisho kwa ajili yake;+ naye atakuwa safi.+
21 “Hata hivyo, ikiwa yeye ni wa hali ya chini+ naye hana mapato ya kutosha,+ basi atachukua mwana-kondoo dume mmoja akiwa toleo la hatia kwa ajili ya toleo la kutikisa ili kufanya upatanisho kwa ajili yake na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliotiwa mafuta ukiwa toleo la nafaka na logi ya mafuta, 22 na njiwa-tetere+ wawili au hua wawili wachanga, kulingana na mapato yake, na mmoja atakuwa toleo la dhambi na yule mwingine atakuwa toleo la kuteketezwa. 23 Na siku ya nane+ atawaleta ili kuthibitisha utakaso+ wake kwa kuhani katika mwingilio wa hema la mkutano+ mbele za Yehova.
24 “Naye kuhani atamchukua yule mwana-kondoo dume wa toleo la hatia+ na ile logi ya mafuta, naye kuhani atavitikisa huku na huku vikiwa toleo la kutikisa mbele za Yehova.+ 25 Naye atamchinja yule kondoo-dume mchanga wa toleo la hatia, naye kuhani atachukua sehemu ya damu ya toleo la hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayejitakasa na kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.+ 26 Naye kuhani atamimina sehemu ya mafuta hayo kwenye kiganja cha mkono wa kushoto wa kuhani.+ 27 Naye kuhani atatapanya+ kwa kidole chake cha kuume sehemu ya mafuta yaliyo katika mkono wake wa kushoto mara saba mbele za Yehova. 28 Naye kuhani atatia sehemu ya mafuta hayo yaliyo katika mkono wake kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayejitakasa na kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume juu ya mahali penye ile damu ya toleo la hatia.+ 29 Na yatakayobaki kati ya yale mafuta yaliyo katika mkono wa kuhani, atayatia kwenye kichwa+ cha yule anayejitakasa ili kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Yehova.
30 “Naye atamtoa mmoja wa wale njiwa-tetere au wa wale hua wachanga anaoweza kuwapata,+ 31 mmoja wa hao anaoweza kuwapata akiwa toleo la dhambi+ na yule mwingine akiwa toleo la kuteketezwa+ pamoja na toleo la nafaka; naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili ya yule anayejitakasa mbele za Yehova.
32 “Hiyo ndiyo sheria kwa ajili ya yule aliyekuwa na pigo la ukoma ambaye huenda asiwe na uwezo wakati wa kuthibitisha utakaso wake.”
33 Naye Yehova akasema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 34 “Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani,+ ambayo ninawapa ninyi iwe mali yenu,+ nami niweke pigo la ukoma katika nyumba ya nchi mtakayoimiliki,+ 35 basi mwenye nyumba hiyo atakuja na kumwambia kuhani, na kusema, ‘Kitu fulani kama pigo kimenitokea katika nyumba.’ 36 Naye kuhani atatoa maagizo, nao wataondoa vitu katika nyumba hiyo kabla kuhani hajaingia kuliona pigo, asije akatangaza kila kitu kilicho katika nyumba hiyo kuwa si safi; kisha kuhani ataingia na kuiona nyumba hiyo. 37 Atakapokuwa ameliona pigo hilo, ndipo ikiwa pigo liko katika kuta za nyumba hiyo, pamoja na mibonyeo ya rangi ya kijani-manjano au ya rangi nyekundu-nyekundu, nayo yaonekana kuwa imepenya ndani ya uso wa ukuta, 38 ndipo kuhani atatoka nje ya mlango wa nyumba hiyo naye ataitenga+ nyumba hiyo kwa siku saba.
39 “Naye kuhani atarudi katika siku ya saba na kutazama;+ na ikiwa pigo hilo limeenea katika kuta za nyumba hiyo, 40 ndipo kuhani atatoa maagizo, nao watayang’oa+ mawe ambayo ndani yake mna pigo hilo, nao watayatupa nje ya jiji katika mahali pasipo safi. 41 Naye atafanya nyumba hiyo ikwanguliwe kotekote upande wa ndani, nao watamwaga saruji ya udongo ambao wamekwangua nje ya jiji katika mahali pasipo safi. 42 Nao watachukua mawe mengine na kuyaingiza mahali pa yale mawe ya zamani; naye atafanya saruji tofauti ya udongo ichukuliwe, naye atafanya nyumba hiyo ipigwe lipu.
43 “Hata hivyo, ikiwa pigo hilo litarudi nalo litokee katika nyumba hiyo baada ya kuyang’oa mawe hayo na baada ya kuikwangua nyumba hiyo na kuipiga lipu, 44 ndipo kuhani+ ataingia ndani na kutazama; na ikiwa pigo hilo limeenea katika nyumba hiyo, ni ukoma hatari+ ulio katika nyumba hiyo. Si safi. 45 Naye atafanya nyumba hiyo ibomolewe pamoja na mawe yake na mbao zake na saruji yote ya udongo ya nyumba hiyo, naye atafanya vichukuliwe nje ya jiji mpaka mahali pasipo safi.+ 46 Lakini yeyote atakayeingia ndani ya nyumba hiyo siku yoyote ya kutengwa+ kwake, atakuwa asiye safi mpaka jioni;+ 47 na yeyote anayelala katika nyumba hiyo atayafua mavazi yake,+ na yeyote anayekula katika nyumba hiyo atayafua mavazi yake.
48 “Hata hivyo, ikiwa kuhani ataingia na kuangalia, na, tazama sasa, pigo halijaenea katika nyumba baada ya kuipiga lipu nyumba hiyo, basi kuhani ataitangaza nyumba hiyo kuwa safi, kwa sababu pigo hilo limepona.+ 49 Na ili kuitakasa nyumba hiyo kutokana na dhambi atachukua ndege wawili+ na mti wa mwerezi+ na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili+ na hisopo. 50 Naye atamuua ndege mmoja katika chombo cha udongo juu ya maji yanayotiririka.+ 51 Naye atauchukua ule mti wa mwerezi na ile hisopo+ na kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kuvichovya katika damu ya yule ndege aliyeuawa juu ya maji yanayotiririka, naye ataitapanya+ kuelekea nyumba hiyo mara saba.+ 52 Naye ataitakasa nyumba hiyo kutokana na dhambi kwa damu ya yule ndege na yale maji yanayotiririka na yule ndege aliye hai na ule mti wa mwerezi na ile hisopo na kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili. 53 Naye atamwacha yule ndege aliye hai aende zake nje ya jiji mpaka porini naye atafanya upatanisho+ kwa ajili ya nyumba hiyo; nayo itakuwa safi.
54 “Hiyo ndiyo sheria juu ya pigo la ukoma+ na juu ya kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida+ 55 na juu ya ukoma wa vazi+ na katika nyumba, 56 na juu ya upele na kigaga na doa,+ 57 ili kutoa maagizo+ wakati kitu fulani si safi na wakati kitu fulani ni safi. Hiyo ndiyo sheria juu ya ukoma.”+
15 Na Yehova akaendelea kusema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, nanyi mtawaambia, ‘Ikiwa mwanamume yeyote ana mtiririko unaotoka+ katika kiungo chake cha uzazi, kile kinachomtoka si safi. 3 Nao huu utakuwa uchafu wake kutokana na kinachomtoka: Iwe kiungo chake cha uzazi kimetiririka kwa mtiririko unaotoka au kiungo chake cha uzazi kimezuiliwa kutokana na mtiririko wake unaotoka, huo ni uchafu wake.
4 “‘Kitanda chochote ambacho yule mwenye mtiririko unaotoka atalalia kitakuwa si safi, na chombo chochote ambacho atakalia kitakuwa si safi. 5 Na mtu ambaye atagusa kitanda chake atayafua mavazi yake, naye ataoga katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni.+ 6 Na yeyote atakayeketi juu ya chombo chochote ambacho yule mwenye mtiririko unaotoka alikuwa amekalia atayafua+ mavazi yake, naye ataoga katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni. 7 Na yeyote atakayegusa mwili wa mtu mwenye mtiririko unaotoka+ atayafua mavazi yake, naye ataoga katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni.+ 8 Na ikiwa mtu mwenye mtiririko unaotoka atamtemea mate mtu aliye safi, ndipo atayafua mavazi yake na kuoga katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni. 9 Na matandiko+ yoyote ambayo yule mwenye mtiririko unaotoka alikuwa ameyapanda yatakuwa si safi. 10 Na mtu yeyote atakayegusa chochote kilicho chini yake atakuwa asiye safi mpaka jioni; naye atakayevichukua atayafua mavazi yake, naye ataoga katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni. 11 Na mtu yeyote ambaye yule mwenye mtiririko unaotoka+ atamgusa kabla hajanawa mikono yake katika maji atayafua mavazi yake katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni. 12 Na chombo cha udongo ambacho yule mwenye mtiririko unaotoka atagusa kitavunjwa;+ na chombo chochote cha mbao+ kitaoshwa katika maji.
13 “‘Sasa, ikiwa yule mwenye mtiririko unaotoka atakuwa safi kutokana na mtiririko wake unaotoka, basi atajihesabia siku saba kwa ajili ya utakaso+ wake, naye atayafua mavazi yake na kuoga mwili wake katika maji yanayotiririka;+ naye atakuwa safi. 14 Na katika siku ya nane atajichukulia njiwa-tetere+ wawili au hua wawili wachanga, naye atakuja mbele za Yehova kwenye mwingilio wa hema la mkutano na kumpa kuhani. 15 Naye kuhani atawatoa, mmoja kuwa toleo la dhambi na yule mwingine kuwa toleo la kuteketezwa;+ naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Yehova kuhusiana na mtiririko wake unaotoka.
16 “‘Sasa, mwanamume akitokwa na shahawa,+ basi ataoga mwili wake wote katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni. 17 Na vazi lolote na ngozi yoyote ambazo shahawa iliyotoka itakuwa juu yake zitafuliwa katika maji nazo zitakuwa si safi mpaka jioni.+
18 “‘Naye mwanamke ambaye mwanamume atalala naye na kutokwa na shahawa, wataoga katika maji na kuwa wasio safi+ mpaka jioni.
19 “‘Na ikiwa mwanamke ana mtiririko unaotoka, nao mtiririko wake unaotoka katika mwili wake uwe ni damu,+ ataendelea kwa siku saba kuwa katika uchafu+ wake wa hedhi,+ na yeyote atakayemgusa atakuwa asiye safi mpaka jioni. 20 Na kitu chochote ambacho atalalia katika uchafu wake wa hedhi kitakuwa si safi,+ na kila kitu ambacho atakalia kitakuwa si safi. 21 Na mtu yeyote anayegusa kitanda chake atayafua mavazi yake, naye ataoga katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni.+ 22 Na mtu yeyote atakayegusa chombo chochote alichokuwa akikalia atayafua mavazi yake, naye ataoga katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni.+ 23 Na ikiwa alikuwa amekalia kitanda au chombo kingine, kwa kukigusa+ atakuwa asiye safi mpaka jioni. 24 Na ikiwa mwanamume atalala naye na uchafu wake wa hedhi uwe juu yake,+ ndipo atakuwa asiye safi kwa siku saba, na kitanda chochote ambacho mwanamume huyo huenda akalalia kitakuwa si safi.
25 “‘Naye mwanamke, ikiwa mtiririko unaotoka wa damu yake utatiririka kwa siku nyingi+ wakati ambapo si wakati wa kawaida wa uchafu wake wa hedhi,+ au ikiwa atakuwa na mtiririko mrefu kuliko uchafu wake wa hedhi, siku zote za mtiririko wake unaotoka usio safi zitakuwa kama siku za uchafu wake wa hedhi. Yeye si safi. 26 Kitanda chochote ambacho huenda atalalia katika yoyote ya siku za mtiririko wake unaotoka kitakuwa kwake kitanda cha uchafu wa hedhi,+ na chombo chochote ambacho huenda atakalia kitakuwa si safi kama ule uchafu wake wa hedhi. 27 Na mtu yeyote atakayevigusa+ atakuwa asiye safi, naye atayafua mavazi yake na kuoga katika maji na kuwa asiye safi mpaka jioni.
28 “‘Hata hivyo, ikiwa amekuwa safi kutokana na mtiririko wake unaotoka, atajihesabia pia siku saba, kisha atakuwa safi.+ 29 Na katika siku ya nane atajichukulia njiwa-tetere+ wawili au hua wawili wachanga, naye atawaleta kwa kuhani katika mwingilio wa hema la mkutano.+ 30 Naye kuhani atamfanya mmoja kuwa toleo la dhambi na yule mwingine kuwa toleo la kuteketezwa;+ naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake mbele za Yehova kuhusiana na mtiririko wake unaotoka ambao si safi.
31 “‘Nanyi mtawatenga wana wa Israeli kutoka kwa uchafu wao, wasije wakafa katika uchafu wao kwa kuinajisi maskani yangu, iliyo katikati yao.+
32 “‘Hiyo ndiyo sheria juu ya mwanamume aliye na mtiririko unaotoka+ na mwanamume ambaye ametokwa na shahawa+ na kuwa asiye safi kutokana nayo; 33 na mwanamke aliye na hedhi+ katika uchafu wake, na mtu yeyote aliye na mtiririko wake unaotoka,+ awe mwanamume au mwanamke, na awe ni mwanamume anayelala na mwanamke asiye safi.’”
16 Na Yehova akasema na Musa baada ya kifo cha wana wawili wa Haruni, waliokufa kwa sababu ya kukaribia kwao mbele za Yehova.+ 2 Na Yehova akamwambia Musa: “Sema na Haruni ndugu yako, asiwe akija nyakati zote katika mahali patakatifu+ ndani ya pazia,+ mbele ya kifuniko kilicho juu ya Sanduku, asije akafa;+ kwa sababu nitaonekana katika wingu+ juu ya kifuniko+ hicho.
3 “Haruni ataingia pamoja na vitu hivi katika mahali patakatifu:+ pamoja na ng’ombe-dume mchanga kwa ajili ya toleo la dhambi+ na kondoo-dume kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.+ 4 Anapaswa kuvaa ile kanzu takatifu ya kitani,+ nayo ile suruali+ ya kitani itakuwa mwilini mwake, naye atajifunga kwa ukumbuu+ wa kitani na kujivika kile kilemba+ cha kitani. Hayo ni mavazi matakatifu.+ Naye atauosha mwili wake katika maji+ na kuyavaa.
5 “Na kutoka katika kusanyiko la wana wa Israeli+ atachukua wana-mbuzi dume wawili kwa ajili ya toleo la dhambi+ na kondoo-dume mmoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.+
6 “Naye Haruni atamtoa yule ng’ombe-dume wa toleo la dhambi, aliye kwa ajili yake,+ naye atafanya upatanisho+ kwa ajili yake mwenyewe+ na nyumba yake.+
7 “Naye atawachukua wale mbuzi wawili na kuwasimamisha mbele za Yehova kwenye mwingilio wa hema la mkutano. 8 Na Haruni atapiga kura+ juu ya mbuzi hao wawili, kura moja kwa ajili ya Yehova na ile nyingine kwa ajili ya Azazeli.+ 9 Naye Haruni atamtoa yule mbuzi ambaye kura+ ilimwangukia kwa ajili ya Yehova, naye atamfanya kuwa toleo la dhambi.+ 10 Lakini yule mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Azazeli atasimamishwa akiwa hai mbele za Yehova ili kufanya upatanisho kwa ajili yake, ili kumpeleka+ nyikani+ kwa ajili ya Azazeli.
11 “Na Haruni atamtoa yule ng’ombe-dume wa toleo la dhambi, aliye kwa ajili yake, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na nyumba yake; naye atamchinja ng’ombe-dume huyo wa toleo la dhambi, aliye kwa ajili yake.+
12 “Naye atachukua chetezo+ kilichojaa makaa yanayowaka moto kutoka katika madhabahu+ mbele za Yehova, na mikono yake yote miwili+ ikiwa imejaa uvumba uliotiwa manukato,+ naye atavileta ndani ya pazia.+ 13 Pia atautia uvumba juu ya moto mbele za Yehova,+ nalo wingu la uvumba litafunika kifuniko cha Sanduku,+ kilicho juu ya ule Ushuhuda,+ asije akafa.
14 “Naye atachukua sehemu ya damu ya ng’ombe-dume+ na kuitapanya kwa kidole chake mbele ya kifuniko upande wa mashariki, naye atatapanya+ sehemu ya damu hiyo kwa kidole chake mara saba mbele ya kifuniko.+
15 “Naye atamchinja yule mbuzi wa toleo la dhambi, aliye kwa ajili ya watu,+ naye ataileta damu yake ndani ya pazia+ na kufanya na hiyo damu+ sawa na vile alivyofanya na ile damu ya ng’ombe-dume; naye ataitapanya kukielekea kifuniko na mbele ya kifuniko.
16 “Naye atafanya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu kuhusiana na uchafu+ wa wana wa Israeli na kuhusiana na maasi yao katika dhambi zao zote;+ na hivyo ndivyo anavyopaswa kufanya kwa ajili ya hema la mkutano, linalokaa pamoja nao katikati ya uchafu wao.
17 “Na mtu mwingine yeyote asiwemo katika hema la mkutano tangu anapoingia ndani ili kufanya upatanisho mpaka atakapotoka nje; naye atafanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe+ na kwa ajili ya nyumba yake na kwa ajili ya kutaniko lote la wana wa Israeli.+
18 “Naye atatoka nje kwenda kwenye madhabahu,+ iliyo mbele za Yehova, na kufanya upatanisho kwa ajili yake, naye atachukua sehemu ya damu ya yule ng’ombe-dume na sehemu ya damu ya yule mbuzi na kuitia juu ya pembe za ile madhabahu kuizunguka pande zote.+ 19 Pia atatapanya+ sehemu ya damu juu yake kwa kidole chake mara saba na kuisafisha na kuitakasa kutokana na uchafu wa wana wa Israeli.
20 “Atakapokuwa amemaliza kufanya upatanisho+ kwa ajili ya mahali patakatifu na lile hema la mkutano na ile madhabahu, atamtoa pia yule mbuzi aliye hai.+ 21 Na Haruni ataweka mikono yake miwili+ juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai na kuungama+ juu yake makosa+ yote ya wana wa Israeli na maasi yao yote na dhambi+ zao zote, naye atayaweka juu ya kichwa cha yule mbuzi+ na kumpeleka mpaka nyikani+ kwa mkono wa mtu aliye tayari.+ 22 Naye mbuzi huyo atachukua juu yake mwenyewe makosa+ yao yote mpaka katika nchi ya jangwa,+ naye atampeleka mbuzi huyo nyikani.+
23 “Naye Haruni ataingia katika hema la mkutano na kuvua yale mavazi ya kitani aliyokuwa amevaa alipoingia mahali patakatifu, naye atayaweka hapo chini.+ 24 Naye ataoga mwili wake katika maji+ katika mahali patakatifu+ na kuvaa mavazi+ yake na kutoka nje na kutoa toleo lake la kuteketezwa+ na toleo la kuteketezwa la watu+ na kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu.+ 25 Naye atayafukiza mafuta ya toleo la dhambi juu ya madhabahu.+
26 “Na yule+ aliyempeleka yule mbuzi kwa ajili ya Azazeli,+ atayafua mavazi yake, naye ataoga mwili wake katika maji,+ kisha anaweza kuingia kambini.
27 “Hata hivyo, yule ng’ombe-dume wa toleo la dhambi na yule mbuzi wa toleo la dhambi, ambao damu yao ililetwa ndani ili kufanya upatanisho, atawapeleka mpaka nje ya kambi; nao watateketeza ngozi zao na nyama yao na mavi yao katika moto.+ 28 Na yule aliyewateketeza atayafua mavazi yake, naye ataoga mwili wake katika maji, kisha anaweza kuingia kambini.
29 “Na itakuwa sheria mpaka wakati usio na kipimo kwenu ninyi:+ Katika mwezi wa saba, siku ya kumi ya mwezi huo,+ mtazitesa nafsi zenu,+ nanyi msifanye kazi yoyote,+ iwe ni mwenyeji au mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni katikati yenu. 30 Kwa maana katika siku hii upatanisho+ utafanywa kwa ajili yenu ili kuwatangaza kuwa safi. Mtakuwa safi kutokana na dhambi zenu zote mbele za Yehova.+ 31 Ni sabato+ ya pumziko kamili kwenu, nanyi mtazitesa nafsi zenu. Ni sheria mpaka wakati usio na kipimo.
32 “Naye kuhani atakayetiwa mafuta+ na ambaye mkono wake utajazwa nguvu ili kutenda akiwa kuhani,+ atakayemfuata+ baba yake, atafanya upatanisho naye atavaa yale mavazi ya kitani.+ Hayo ni mavazi matakatifu.+ 33 Naye atafanya upatanisho kwa ajili ya patakatifu zaidi,+ na kwa ajili ya hema+ la mkutano na kwa ajili ya madhabahu+ atafanya upatanisho; na kwa ajili ya makuhani na kwa ajili ya watu wote wa kutaniko atafanya upatanisho.+ 34 Na hiyo itakuwa sheria kwenu mpaka wakati usio na kipimo,+ ili kufanya upatanisho kwa ajili ya wana wa Israeli kuhusu dhambi zao zote mara moja kwa mwaka.”+
Basi akafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
17 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na Haruni na wanawe na wana wote wa Israeli, nawe uwaambie, ‘Hili ndilo jambo ambalo Yehova ameamuru, na kusema:
3 “‘“Mtu yeyote wa nyumba ya Israeli atakayemchinja ng’ombe-dume au mwana-kondoo dume au mbuzi katika kambi au atakayemchinja nje ya kambi 4 naye asimlete kwenye mwingilio wa hema la mkutano+ ili kumtoa awe toleo kwa Yehova mbele ya maskani ya Yehova, mtu huyo atahesabiwa kuwa na hatia ya damu. Amemwaga damu, naye mtu huyo lazima akatiliwe mbali kutoka katikati ya watu wake,+ 5 ili kwamba wana wa Israeli walete dhabihu zao, wanazozitoa dhabihu katika uwanja,+ nao watazileta kwa Yehova kwenye mwingilio wa hema la mkutano kwa kuhani,+ nao watatoa dhabihu hizo zikiwa dhabihu za ushirika kwa Yehova.+ 6 Naye kuhani atainyunyiza damu juu ya madhabahu+ ya Yehova kwenye mwingilio wa hema la mkutano, naye atayafukiza mafuta+ yawe harufu ya kumtuliza Yehova.+ 7 Kwa hiyo hawapaswi tena kutoa dhabihu zao kwa wale roho waovu wenye umbo la mbuzi+ wanaofanya uasherati+ pamoja nao. Hiyo itakuwa sheria kwenu mpaka wakati usio na kipimo, katika vizazi vyenu vyote.”’
8 “Nawe utawaambia, ‘Mtu yeyote wa nyumba ya Israeli au mkaaji mgeni yeyote ambaye huenda akawa anakaa akiwa mgeni katikati yenu anayetoa toleo la kuteketezwa+ au dhabihu 9 naye asiilete kwenye mwingilio wa hema la mkutano ili kuitoa kwa Yehova,+ mtu huyo lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.+
10 “‘Na mtu yeyote wa nyumba ya Israeli au mkaaji mgeni yeyote anayekaa akiwa mgeni katikati yenu atakayekula namna yoyote ya damu,+ nitauweka uso wangu dhidi ya nafsi+ hiyo inayokula damu, nami hakika nitamkatilia mbali kutoka katikati ya watu wake. 11 Kwa maana nafsi ya mwili iko katika damu,+ nami mwenyewe nimeiweka juu ya madhabahu ili ninyi mfanye upatanisho+ kwa ajili ya nafsi zenu, kwa sababu damu+ ndiyo hufanya upatanisho+ kupitia nafsi iliyo ndani yake. 12 Ndiyo sababu nimewaambia wana wa Israeli: “Nafsi yoyote kati yenu isile damu na mkaaji mgeni yeyote anayekaa akiwa mgeni katikati yenu+ hapaswi kula damu.”+
13 “‘Na mtu yeyote kati ya wana wa Israeli au mkaaji mgeni yeyote anayekaa akiwa mgeni katikati yenu ambaye katika kuwinda anamkamata mnyama-mwitu au ndege anayeweza kuliwa, basi ataimwaga damu+ yake na kuifunika kwa mavumbi.+ 14 Kwa maana nafsi ya kila namna ya mwili ni damu yake kwa nafsi iliyo ndani yake. Basi niliwaambia wana wa Israeli: “Hamtakula damu ya mwili wa namna yoyote, kwa sababu nafsi ya kila mwili wa namna yoyote iko katika damu yake.+ Mtu yeyote atakayeila atakatiliwa mbali.”+ 15 Nayo nafsi yoyote itakayokula mwili uliokufa tayari au kitu kilichoraruliwa na mnyama-mwitu,+ awe ni mwenyeji au mkaaji mgeni, basi atayafua mavazi yake na kuoga katika maji na kuwa asiye safi+ mpaka jioni; naye atakuwa safi. 16 Lakini ikiwa hatayafua naye hataoga mwili wake, basi atajibu kwa kosa lake.’”+
18 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu.+ 3 Jinsi inavyofanya nchi ya Misri ambamo mlikaa, msifanye;+ na jinsi inavyofanya nchi ya Kanaani, ambamo nitawaleta, msifanye;+ na katika sheria zao msitembee. 4 Maamuzi yangu ya hukumu+ mtayatenda, na sheria+ zangu mtazishika ili kutembea katika hizo.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu. 5 Nanyi mtazishika sheria zangu na maamuzi yangu ya hukumu, ambazo ikiwa mtu atazifanya, yeye pia ataishi kwa hizo.+ Mimi ni Yehova.+
6 “‘Yeyote kati yenu asimkaribie mtu yeyote wa jamaa yake, wa kimwili, wa karibu ili kufunua uchi.+ Mimi ni Yehova. 7 Uchi wa baba yako+ na uchi wa mama yako usiufunue. Yeye ni mama yako. Usiufunue uchi wake.
8 “‘Uchi wa mke wa baba yako usiufunue.+ Ni uchi wa baba yako.
9 “‘Nao uchi wa dada yako, binti ya baba yako au binti ya mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo hiyo au amezaliwa nje, usiufunue uchi wao.+
10 “‘Nao uchi wa binti ya mwana wako au binti ya binti yako, usiufunue uchi wao, kwa sababu wao ni uchi wako.
11 “‘Nao uchi wa binti ya mke wa baba yako, uzao wa baba yako, kwa kuwa yeye ni dada yako, usiufunue uchi wake.
12 “‘Uchi wa dada ya baba yako usiufunue. Yeye ana uhusiano wa damu na baba yako.+
13 “‘Uchi wa dada ya mama yako usiufunue, kwa sababu yeye ana uhusiano wa damu na mama yako.
14 “‘Uchi wa ndugu ya baba yako usiufunue. Usimkaribie mke wake. Yeye ni shangazi yako.+
15 “‘Uchi wa binti-mkwe+ wako usiufunue. Yeye ni mke wa mwana wako. Usiufunue uchi wake.
16 “‘Uchi wa mke wa ndugu yako+ usiufunue. Ni uchi wa ndugu yako.
17 “‘Uchi wa mwanamke na binti yake usiufunue.+ Binti ya mwana wake na binti ya binti yake usimchukue ili kuufunua uchi wake. Wao wana uhusiano wa damu. Ni mwenendo mpotovu.+
18 “‘Nawe usimchukue mwanamke pamoja na dada yake awe mshindani+ ili kuufunua uchi wake, yaani, pamoja naye akiwa angali hai.
19 “‘Nawe usimkaribie mwanamke wakati wa hedhi+ ya uchafu wake ili kuufunua uchi wake.+
20 “‘Nawe usimpe mke wa mwenzako shahawa inayokutoka awe asiye safi kutokana nayo.+
21 “‘Nawe usiuruhusu uzao wako wowote utolewe+ kwa Moleki.+ Usilitie unajisi+ jina la Mungu wako kwa njia hiyo. Mimi ni Yehova.+
22 “‘Nawe usilale na mwanamume+ kama vile unavyolala na mwanamke.+ Ni jambo lenye kuchukiza.
23 “‘Nawe usimpe mnyama yeyote shahawa+ yako awe asiye safi kutokana nayo, na mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kuungana naye.+ Ni kuvunja jambo lililo la asili.
24 “‘Msijifanye wenyewe kuwa wasio safi kwa lolote la mambo hayo, kwa sababu kwa mambo yote hayo mataifa ninayoyafukuza kutoka mbele yenu yamejifanya yenyewe kuwa si safi.+ 25 Kwa hiyo nchi si safi, nami nitaleta adhabu kwa ajili ya kosa lake juu yake, nayo nchi itawatapika wakaaji wake.+ 26 Nanyi mtazishika sheria zangu na maamuzi yangu ya hukumu,+ nanyi msifanye lolote la mambo hayo yenye kuchukiza, iwe ni mwenyeji au mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni katikati yenu.+ 27 Kwa maana mambo yote hayo yenye kuchukiza, watu wa nchi waliokuwa mbele yenu wameyafanya,+ hivi kwamba nchi si safi. 28 Ndipo nchi haitawatapika ninyi kwa sababu ya kuitia kwenu unajisi kama vile itakavyoyatapika mataifa yaliyokuwa mbele yenu.+ 29 Ikiwa mtu yeyote atafanya lolote la mambo yote hayo yenye kuchukiza, basi nafsi zinazoyafanya zitakatiliwa mbali kutoka katikati ya watu wao.+ 30 Nanyi mtatimiza wajibu wenu kwangu ili kutoendeleza yoyote kati ya desturi hizo zenye kuchukiza ambazo zimeendelezwa mbele yenu,+ ili msijifanye kuwa wasio safi kutokana nazo. Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”
19 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na kusanyiko lote la wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Muwe watakatifu,+ kwa sababu mimi Yehova Mungu wenu ni mtakatifu.+
3 “‘Kila mmoja wenu anapaswa kumwogopa mama yake na baba yake,+ nazo sabato zangu mnapaswa kuzishika.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu. 4 Msigeukie miungu isiyo na thamani,+ wala msijifanyie miungu ya kuyeyushwa.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.
5 “‘Sasa ikiwa mtamtolea Yehova dhabihu ya ushirika,+ mtaitoa ili mjipatie kibali.+ 6 Inapaswa kuliwa siku ile mnayotoa dhabihu na kesho yake, lakini kitakachobaki mpaka siku ya tatu kitateketezwa kwa moto.+ 7 Hata hivyo, ikiwa kwa vyovyote kitaliwa siku ya tatu, ni kitu kichafu.+ Hakitapokewa kwa kibali.+ 8 Naye atakayekila atajibu kwa kosa lake,+ kwa sababu amekitia unajisi kitu kitakatifu cha Yehova; nayo nafsi hiyo itakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake.
9 “‘Na mnapovuna mavuno ya nchi yenu, msivune kabisa ukingo wa shamba lenu, nayo masalio ya mavuno yenu msiyaokote.+ 10 Pia, usikusanye masalio+ ya shamba lako la mizabibu, wala usiokote zabibu zilizotawanyika za shamba lako la mizabibu. Ziache kwa ajili ya mwenye kuteseka na mkaaji mgeni.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.
11 “‘Msiibe,+ wala msidanganye,+ wala msitendeane kwa uwongo mtu yeyote na mwenzake.+ 12 Na msiape uwongo kwa jina langu,+ ili msilitie unajisi jina la Mungu wenu. Mimi ni Yehova. 13 Usimpunje+ mwenzako, wala usinyang’anye.+ Usikae na mshahara wa mfanyakazi wa kukodiwa usiku kucha mpaka asubuhi.+
14 “‘Usimlaani kiziwi, na mbele ya kipofu usiweke kikwazo;+ nawe umwogope Mungu wako.+ Mimi ni Yehova.
15 “‘Msifanye ukosefu wa haki katika hukumu. Usiwatendee watu wa hali ya chini kwa njia ya ubaguzi,+ wala usimpendelee mtu mkuu.+ Utamhukumu mwenzako kwa haki.
16 “‘Usizunguke katikati ya watu wako ili kuchongea.+ Usisimame dhidi ya damu ya mwenzako.+ Mimi ni Yehova.
17 “‘Usimchukie ndugu yako moyoni mwako.+ Lazima umkaripie mwenzako,+ usije ukachukua dhambi pamoja naye.
18 “‘Usilipize kisasi+ wala usiwe na kinyongo juu ya wana wa watu wako;+ nawe mpende mwenzako kama wewe mwenyewe.+ Mimi ni Yehova.
19 “‘Mtazishika sheria zangu: Usiwafanye wanyama wako wa kufugwa wa aina mbili wazaane. Usilipande shamba lako aina mbili za mbegu,+ nawe usivae vazi la aina mbili za nyuzi, zilizochanganywa.+
20 “‘Sasa mwanamume akilala na mwanamke na shahawa imtoke, wakati ambapo yeye ni mjakazi aliyewekwa kwa ajili ya mwanamume mwingine, naye hajakombolewa kwa njia yoyote wala hajapewa uhuru, adhabu itatolewa. Watu hao wasiuawe, kwa sababu hakuwa amewekwa huru. 21 Naye atamletea Yehova toleo lake la hatia kwenye mwingilio wa hema la mkutano, kondoo-dume wa toleo la hatia.+ 22 Naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa yule kondoo-dume wa toleo la hatia mbele za Yehova kwa ajili ya dhambi yake ambayo alitenda; naye atasamehewa dhambi yake ambayo alitenda.+
23 “‘Na ikiwa mnaingia katika nchi, na kuupanda mti wowote kwa ajili ya chakula, mtayaona matunda yake kuwa machafu kama “govi” lake. Kwa miaka mitatu utakuwa haujatahiriwa kwenu. Hayataliwa. 24 Lakini katika mwaka wa nne matunda+ yake yote yatakuwa kitu kitakatifu cha kusherehekea kwa kushangilia kwa Yehova.+ 25 Na katika mwaka wa tano mnaweza kula matunda yake ili kujiongezea mazao yake.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.
26 “‘Msile kitu chochote pamoja na damu.+
“‘Msitafute ishara za bahati,+ wala msifanye uchawi.+
27 “‘Msikate ndevu zenu ziwe fupi kuzunguka pande zote, wala usiharibu ncha ya ndevu zako.+
28 “‘Na msijikatekate mwili wenu kwa ajili ya nafsi iliyokufa,+ wala msijitie alama ya chanjo. Mimi ni Yehova.
29 “‘Usimtie unajisi binti yako kwa kumfanya kahaba,+ ili nchi isifanye ukahaba na hivyo nchi ijae maadili mapotovu.+
30 “‘Sabato zangu mtazishika,+ nanyi mtapaheshimu patakatifu pangu.+ Mimi ni Yehova.
31 “‘Msiwaendee wenye kuwasiliana na pepo,+ wala msitafute shauri la wajuzi wa kubashiri matukio,+ ili kutiwa unajisi nao. Mimi ni Yehova Mungu wenu.
32 “‘Unapaswa kusimama mbele ya mtu mwenye mvi,+ nawe umwonyeshe ufikirio mtu mzee,+ nawe umwogope Mungu wako.+ Mimi ni Yehova.
33 “‘Na ikiwa mkaaji mgeni anakaa pamoja nawe akiwa mgeni katika nchi yenu, msimtendee vibaya.+ 34 Yule mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni pamoja nanyi atakuwa kwenu kama mwenyeji wenu; nawe utampenda kama wewe mwenyewe,+ kwa maana mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.
35 “‘Msikose kufanya haki katika kuhukumu,+ katika kupima, katika kupima uzito+ au katika kupima vitu vya majimaji. 36 Mtakuwa na mizani sahihi, vipimo sahihi,+ kipimo sahihi cha efa na kipimo sahihi cha hini. Mimi ni Yehova Mungu wenu, ambaye nimewatoa ninyi katika nchi ya Misri. 37 Kwa hiyo mtazishika sheria zangu zote na maamuzi yangu yote ya hukumu, nanyi mtazifanya.+ Mimi ni Yehova.’”
20 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Utawaambia wana wa Israeli, ‘Mtu yeyote wa wana wa Israeli, na mkaaji mgeni yeyote anayekaa akiwa mgeni katika Israeli, anayempa Moleki+ yeyote kati ya uzao wake, lazima auawe. Watu wa nchi watampiga kwa mawe mpaka afe. 3 Mimi nami, nitauweka uso wangu juu ya mtu huyo, nami nitamkatilia mbali kutoka katikati ya watu wake,+ kwa sababu amempa Moleki baadhi ya uzao wake kwa kusudi la kupatia unajisi mahali pangu patakatifu+ na kulitia unajisi jina langu takatifu.+ 4 Na ikiwa watu wa nchi hiyo hawatamuua kwa kuyaficha macho yao kimakusudi yasimwone mtu huyo anapompa Moleki yeyote kati ya uzao wake,+ 5 basi mimi nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu huyo na familia yake,+ nami nitamkatilia mbali yeye na wote wanaofanya uasherati pamoja naye katika kufanya uasherati+ na Moleki watoke katikati ya watu wao.
6 “‘Nayo nafsi inayowaendea wenye kuwasiliana na pepo+ na wajuzi wa kubashiri+ matukio ili kufanya uasherati nao, nitauweka uso wangu juu ya nafsi hiyo na kumkatilia mbali kutoka katikati ya watu wake.+
7 “‘Nanyi mtajitakasa na kuwa watakatifu,+ kwa sababu mimi ni Yehova Mungu wenu. 8 Nanyi mtazishika sheria zangu na kuzitenda.+ Mimi ni Yehova, ninayewatakasa ninyi.+
9 “‘Ikiwa kutakuwa na mtu yeyote anayemlaani baba yake na mama yake,+ lazima auawe.+ Ni baba yake na mama yake ambao amewalaani. Damu yake mwenyewe iko juu yake.+
10 “‘Sasa mwanamume anayefanya uzinzi na mke wa mwanamume mwingine ni mwanamume anayefanya uzinzi na mke wa mwenzake.+ Lazima auawe, mwanamume huyo mzinzi na vilevile mwanamke huyo mzinzi.+ 11 Na mwanamume anayelala na mke wa baba yake ameufunua uchi wa baba yake.+ Lazima wote wawili wauawe. Damu yao wenyewe iko juu yao. 12 Na mwanamume akilala na binti-mkwe wake, lazima wote wawili wauawe.+ Wamevunja jambo la asili. Damu yao wenyewe iko juu yao.+
13 “‘Na mwanamume akilala na mwanamume sawa na vile mtu anavyolala na mwanamke, wote wawili wamefanya jambo lenye kuchukiza.+ Lazima wauawe. Damu yao wenyewe iko juu yao.
14 “‘Na mwanamume akimchukua mwanamke pamoja na mama yake, ni mwenendo mpotovu.+ Watamteketeza yeye na wao katika moto,+ ili mwenendo mpotovu+ usiendelee katikati yenu.
15 “‘Na mwanamume akimpa mnyama shahawa yake imtokayo,+ lazima auawe, nanyi mtamuua mnyama huyo. 16 Na mwanamke akimkaribia mnyama yeyote ili kuungana+ naye, mtamuua mwanamke huyo na mnyama huyo. Lazima wauawe. Damu yao wenyewe iko juu yao.
17 “‘Na mwanamume akimchukua dada yake, binti ya baba yake au binti ya mama yake, naye auone uchi wake, naye dada yake auone uchi wake, ni aibu.+ Kwa hiyo watakatiliwa mbali kutoka machoni pa wana wa watu wao. Ni uchi wa dada yake ambao ameufunua. Atajibu kwa kosa lake.
18 “‘Na mwanamume akilala na mwanamke mwenye hedhi na kuufunua uchi wake, ameifunua chemchemi yake, naye mwanamke huyo ameifichua chemchemi ya damu yake.+ Kwa hiyo wote wawili watakatiliwa mbali kutoka katikati ya watu wao.
19 “‘Nao uchi wa dada ya mama yako+ na dada ya baba yako+ usiufunue, kwa sababu mtu atakuwa ameufunua uhusiano wake wa damu.+ Watajibu kwa kosa lao. 20 Na mwanamume anayelala na mke wa ndugu ya baba yake ameufunua uchi wa ndugu ya baba yake.+ Watajibu kwa dhambi yao. Watakufa bila kupata mtoto.+ 21 Na mtu akimchukua mke wa ndugu yake, ni chukizo.+ Ni uchi wa ndugu yake ambao ameufunua. Watakuwa bila mtoto.
22 “‘Nanyi mtazishika sheria+ zangu zote na maamuzi yangu yote ya hukumu+ na kuzifanya, ili nchi nitakayowaingiza mkae ndani yake isije ikawatapika ninyi.+ 23 Nanyi msitembee katika sheria za mataifa ambayo nitayafukuza kutoka mbele yenu,+ kwa sababu wamefanya mambo hayo yote nami nayachukia.+ 24 Ndipo nikawaambia ninyi:+ “Ninyi mtaimiliki nchi yao, nami nitawapa ninyi ili mwimiliki, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu, ambaye nimewatenga kutoka kwa vikundi vya watu.”+ 25 Nanyi mtatofautisha mnyama aliye safi na asiye safi na kutofautisha ndege aliye safi na asiye safi;+ nanyi msizifanye nafsi zenu kuwa zenye kuchukiza+ kupitia mnyama na ndege na kitu chochote ambacho hutembea juu ya nchi ambacho nimekitenga kwa ajili yenu kwa kuvitangaza kuwa si safi. 26 Nanyi mtakuwa watakatifu kwangu,+ kwa sababu mimi Yehova ni mtakatifu;+ nami ninawatenga kutoka kwa vikundi vya watu ili muwe wangu.+
27 “‘Naye mwanamume au mwanamke atakayekuwa na roho ya kuwasiliana na pepo au roho ya kubashiri,+ lazima wauawe.+ Watawapiga hao kwa mawe na kuwaua. Damu yao wenyewe iko juu yao.’”+
21 Na Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Ongea na makuhani, wana wa Haruni, nawe uwaambie, ‘Kwa ajili ya nafsi iliyokufa, mtu yeyote asijitie unajisi katikati ya watu wake.+ 2 Lakini kwa ajili ya mtu mwenye uhusiano wa damu aliye karibu naye, kwa ajili ya mama yake na kwa ajili ya baba yake na kwa ajili ya mwana wake na kwa ajili ya binti yake na kwa ajili ya ndugu yake 3 na kwa ajili ya dada yake, bikira aliye karibu naye, ambaye hajawa wa mwanamume, kwa ajili yake anaweza kujitia unajisi. 4 Hatajitia unajisi kwa ajili ya mwanamke mwenye mume katikati ya watu wake ili kujitia unajisi. 5 Hawataweka upara juu ya vichwa+ vyao, na ncha ya ndevu zao hawatanyoa,+ na katika mwili wao hawatafanya mkato.+ 6 Watakuwa watakatifu kwa Mungu wao,+ nao hawatalitia unajisi jina la Mungu wao,+ kwa sababu wao ndio wanaotoa matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto, mkate wa Mungu wao;+ nao watakuwa watakatifu.+ 7 Kahaba+ au mwanamke aliyenajisiwa hawatamwoa; na mwanamke aliyetalikiwa+ kutoka kwa mume wake hawatamwoa,+ kwa sababu yeye ni mtakatifu kwa Mungu wake. 8 Basi utamtakasa,+ kwa sababu yeye ni mtu anayeutoa mkate wa Mungu wako. Atakuwa mtakatifu kwako,+ kwa sababu mimi Yehova, ninayewatakasa ninyi, mimi ni mtakatifu.+
9 “‘Sasa ikiwa binti ya kuhani atajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamtia unajisi baba yake. Binti huyo atateketezwa katika moto.+
10 “‘Naye kuhani mkuu wa ndugu zake ambaye kichwa chake kimemiminiwa mafuta+ na ambaye mkono wake umejazwa nguvu ili kuvaa yale mavazi,+ hatakiacha kichwa chake bila kutunzwa,+ wala hatayararua mavazi yake.+ 11 Naye hatakuja mahali penye nafsi yoyote iliyokufa.+ Kwa ajili ya baba yake na mama yake hatajitia unajisi. 12 Pia hatatoka nje ya patakatifu wala kupatia unajisi patakatifu pa Mungu wake,+ kwa sababu ishara ya wakfu, yale mafuta ya Mungu wake yanayotumiwa kutia mafuta,+ yako juu yake. Mimi ni Yehova.
13 “‘Naye atamwoa mwanamke katika ubikira wake.+ 14 Na mwanamke mjane au aliyetalikiwa na yule aliyenajisiwa, kahaba, asimwoe yeyote kati ya hawa, lakini aoe bikira kutoka kwa watu wake awe mke wake. 15 Naye hatautia unajisi uzao wake kati ya watu wake,+ kwa sababu mimi ni Yehova ninayemtakasa.’”+
16 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 17 “Sema na Haruni, na kumwambia, ‘Mtu yeyote wa uzao wako katika vizazi vyao vyote ambaye ana kasoro+ asije karibu ili kuutoa mkate wa Mungu wake.+ 18 Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye kasoro, asikaribie: mtu aliye kipofu au kilema au mwenye pua iliyokatika au mwenye kiungo kimoja kilicho kirefu mno,+ 19 au mtu aliyevunjika mguu au aliyevunjika mkono, 20 au mwenye kijongo au aliyekonda au mwenye ugonjwa wa macho au mwenye vigaga au mwenye mba au aliyevunjwa mapumbu yake.+ 21 Mtu yeyote wa uzao wa Haruni kuhani ambaye ana kasoro hatakaribia ili kutoa matoleo ya Yehova kwa njia ya moto.+ Kuna kasoro ndani yake. Hatakaribia ili kuutoa mkate wa Mungu wake.+ 22 Anaweza kula mkate wa Mungu wake kutoka kati ya vitu vitakatifu zaidi+ na kutoka kati ya vitu vitakatifu.+ 23 Hata hivyo, hatakaribia pazia,+ wala hatakaribia madhabahu,+ kwa sababu kuna kasoro ndani yake;+ naye hatapatia unajisi patakatifu pangu,+ kwa kuwa mimi ni Yehova ninayewatakasa wao.’”+
24 Basi Musa akasema na Haruni na wanawe na wana wote wa Israeli.
22 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na Haruni na wanawe, kwamba wajitenge na vitu vitakatifu vya wana wa Israeli nao wasilitie unajisi jina langu takatifu+ katika vitu ambavyo wananitakasia.+ Mimi ni Yehova. 3 Waambie, ‘Katika vizazi vyenu vyote mtu yeyote wa uzao wenu wote atakayekaribia vitu vitakatifu, ambavyo wana wa Israeli watamtakasia Yehova, wakati ambapo uchafu wake ungali juu yake,+ nafsi hiyo itakatiliwa mbali kutoka mbele zangu. Mimi ni Yehova. 4 Hakuna mtu yeyote wa uzao wa Haruni wakati ambapo ana ukoma+ au mtiririko unaotoka+ atakayekula vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi,+ wala yule atakayegusa mtu yeyote asiye safi kwa nafsi iliyokufa+ au mtu ambaye shahawa itamtoka,+ 5 wala mtu atakayegusa kitu chochote kinachozaana kwa wingi ambacho si safi kwake+ au atakayemgusa mtu asiye safi kwake kuhusiana na uchafu wake wowote.+ 6 Nafsi itakayogusa kitu chochote cha vitu hivyo itakuwa si safi mpaka jioni naye hatakula kitu chochote katika vitu vitakatifu, lakini ataoga mwili wake katika maji.+ 7 Jua likiisha kutua, yeye pia atakuwa safi, na baadaye anaweza kula sehemu ya vitu vitakatifu, kwa sababu ni mkate wake.+ 8 Pia hatakula mwili wowote uliokufa tayari au kitu chochote kilichoraruliwa na wanyama-mwitu na kuwa asiye safi kutokana nacho.+ Mimi ni Yehova.
9 “‘Nao watashika wajibu wao kwangu, wasije wakachukua dhambi kwa sababu yake nao wakafa+ kwa sababu yake kwa sababu walikuwa wakivitia unajisi. Mimi ni Yehova ninayewatakasa wao.
10 “‘Na hakuna mgeni yeyote atakayekula kitu chochote kilicho kitakatifu.+ Hakuna mkaaji aliye pamoja na kuhani wala mfanyakazi wa kukodiwa atakayekula kitu chochote kilicho kitakatifu. 11 Lakini ikiwa kuhani atanunua nafsi, akifanya ununuzi kwa pesa zake, anaweza kushiriki kukila. Nao watumwa waliozaliwa katika nyumba yake, wanaweza kushiriki kuula mkate wake.+ 12 Na ikiwa binti ya kuhani atakuwa wa mwanamume aliye mgeni, yeye binti huyo hatakula mchango wa vitu vitakatifu. 13 Lakini ikiwa binti ya kuhani atakuwa mjane au kutalikiwa akiwa hana uzao, naye arudi nyumbani kwa baba yake kama katika ujana wake,+ anaweza kula sehemu ya mkate wa baba yake;+ lakini hakuna mgeni yeyote atakayeula.
14 “‘Sasa ikiwa mtu atakula kitu kitakatifu bila kukusudia,+ basi ataongeza sehemu yake ya tano+ juu yake naye atampa kuhani hicho kitu kitakatifu. 15 Kwa hiyo hawatatia unajisi vitu vitakatifu vya wana wa Israeli, ambavyo huenda wakamchangia Yehova,+ 16 na kuwafanya wapate adhabu ya hatia kwa sababu ya kula kwao vitu vyao vitakatifu; kwa maana mimi ni Yehova ninayewatakasa wao.’”
17 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 18 “Sema na Haruni na wanawe na wana wote wa Israeli, nawe uwaambie, ‘Mtu yeyote wa nyumba ya Israeli au mkaaji mgeni katika Israeli anayetoa toleo lake,+ kwa ajili ya nadhiri+ yao yoyote au kwa ajili ya matoleo yao ya hiari,+ ambayo huenda wakamtolea Yehova kwa ajili ya toleo la kuteketezwa, 19 ili kupata kibali+ kwa ajili yenu, lazima awe hana kasoro,+ wa kiume kutoka katikati ya mifugo, katikati ya wana-kondoo dume au katikati ya mbuzi. 20 Kitu chochote chenye kasoro hamtakitoa,+ kwa sababu hakitawaletea ninyi kibali.
21 “‘Na ikiwa mtu atamtolea Yehova dhabihu ya ushirika+ ili kulipa nadhiri+ au kama toleo la hiari, atakuwa asiye na kasoro katikati ya mifugo au kundi, ili kupata kibali. Kasoro yoyote isiwe ndani yake. 22 Hakuna dhabihu yoyote iliyo na upofu au mvunjiko au mkato au chunjua au vigaga au mba,+ yeyote kati ya hao msimtolee Yehova, wala hakuna toleo lolote linalotolewa kwa njia ya moto+ kutoka kati ya hao mtakaloweka juu ya madhabahu ya Yehova. 23 Na kuhusu ng’ombe-dume au kondoo mwenye kiungo kirefu mno au kifupi mno,+ unaweza kumtoa awe toleo la hiari; lakini kwa ajili ya nadhiri hatapokewa kwa kibali. 24 Lakini mwenye mapumbu+ yaliyominywa au yaliyovunjwa au yaliyong’olewa au yaliyokatwa hamtamtolea Yehova, na katika nchi yenu hamtawatoa. 25 Na yeyote kati ya hao kutoka katika mkono wa mgeni hamtamtoa awe mkate wa Mungu wenu, kwa sababu uharibifu wao umo ndani yao. Kuna kasoro+ ndani yao. Hawatakubaliwa kwa ajili yenu nanyi mpate kibali.’”+
26 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 27 “Ng’ombe-dume au mwana-kondoo dume au mbuzi akizaliwa, basi atakaa na mama yake siku saba,+ lakini kuanzia siku ya nane na kuendelea atapokewa kwa kibali kama toleo, toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto. 28 Naye ng’ombe na kondoo, hamtamchinja yeye pamoja na mtoto wake katika siku moja.+
29 “Na ikiwa mtatoa dhabihu ya shukrani kwa Yehova,+ mtaitoa ili kupata kibali kwa ajili yenu. 30 Katika siku hiyo italiwa.+ Hamtaacha yoyote mpaka asubuhi.+ Mimi ni Yehova.
31 “Nanyi mtazishika amri zangu na kuzitenda.+ Mimi ni Yehova. 32 Nanyi hamtalitia unajisi jina langu takatifu,+ nami nitatakaswa katikati ya wana wa Israeli.+ Mimi ni Yehova ninayewatakasa ninyi,+ 33 Mimi ninayewatoa katika nchi ya Misri ili kujionyesha kuwa Mungu kwenu.+ Mimi ni Yehova.”
23 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, nawe uwaambie, ‘Sherehe za majira+ za Yehova ambazo mtatangaza+ ni mikusanyiko mitakatifu. Hizi ndizo sherehe zangu za majira:
3 “‘Siku sita kazi inaweza kufanywa, lakini katika siku ya saba ni sabato ya pumziko kamili,+ mkusanyiko mtakatifu. Hamtafanya kazi ya aina yoyote. Ni sabato kwa Yehova katika makao yenu yote.+
4 “‘Hizi ndizo sherehe za majira+ za Yehova, mikusanyiko mitakatifu,+ ambazo mtatangaza katika wakati wake uliowekwa:+ 5 Katika mwezi wa kwanza, katika siku ya kumi na nne ya mwezi huo,+ katikati ya zile jioni mbili ni pasaka+ kwa Yehova.
6 “‘Na katika siku ya kumi na tano ya mwezi huu ni sherehe kwa Yehova ya keki zisizo na chachu.+ Kwa siku saba mtakula keki zisizo na chachu.+ 7 Katika siku ya kwanza mtafanya mkusanyiko mtakatifu.+ Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote. 8 Lakini mtatoa toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto kwa siku saba. Katika siku ya saba kutakuwa na mkusanyiko mtakatifu. Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote.’”
9 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 10 “Sema na wana wa Israeli, nawe uwaambie, ‘Mwishowe mtakapoingia katika nchi ambayo nitawapa ninyi, nanyi mtakapokuwa mmevuna mavuno yake, mtaleta pia mganda wa matunda ya kwanza+ ya mavuno yenu kwa kuhani. 11 Naye atautikisa huo mganda huku na huku,+ mbele za Yehova ili kupata kibali kwa ajili yenu. Siku itakayofuata sabato kuhani atautikisa huku na huku. 12 Na katika siku ambayo mganda wenu utatikiswa huku na huku mtamtoa mwana-kondoo dume ambaye hana kasoro, aliye katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa kwa Yehova; 13 na kama toleo lake la nafaka, sehemu mbili za kumi za efa ya unga laini uliotiwa mafuta, kama toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, harufu ya kutuliza; na kama toleo lake la kinywaji, sehemu ya nne ya hini ya divai. 14 Nanyi hamtakula mkate wowote wala nafaka iliyochomwa wala nafaka mpya mpaka siku hiyo,+ mpaka mtakapoleta toleo la Mungu wenu. Ni sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa vizazi vyenu vyote katika makao yenu yote.
15 “‘Nanyi mtajihesabia toka siku inayofuata sabato, toka siku ya kuleta kwenu ule mganda wa toleo la kutikisa, sabato 7.+ Zitakuwa kamili. 16 Mpaka siku inayofuata sabato ya 7 mtahesabu, siku 50,+ nanyi mtamtolea Yehova toleo jipya la nafaka.+ 17 Kutoka katika makao yenu mtaleta mikate+ miwili iwe toleo la kutikisa. Itakuwa ya sehemu mbili za kumi za efa ya unga laini. Itaokwa ikiwa imetiwa chachu,+ kama matunda ya kwanza yaliyoiva kwa Yehova.+ 18 Nanyi mtatoa pamoja na mikate hiyo wana-kondoo dume+ saba ambao hawana kasoro, kila mmoja mwenye umri wa mwaka mmoja, na ng’ombe-dume mmoja mchanga na kondoo-dume wawili. Watakuwa toleo la kuteketezwa kwa Yehova pamoja na toleo lao la nafaka na matoleo yao ya vinywaji yanayotolewa kwa njia ya moto, yenye harufu ya kumtuliza Yehova. 19 Nanyi mtamtoa mwana-mbuzi+ mmoja awe toleo la dhambi na wana-kondoo dume wawili, kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja, wawe dhabihu ya ushirika.+ 20 Naye kuhani atawatikisa huku na huku+ pamoja na ile mikate ya matunda ya kwanza yaliyoiva, kama toleo la kutikisa mbele za Yehova, pamoja na wale wana-kondoo dume wawili. Hivyo vitakuwa vitu vitakatifu kwa Yehova kwa ajili ya kuhani.+ 21 Nanyi mtatoa tangazo+ siku hiyo; kutakuwa na mkusanyiko mtakatifu kwa ajili yenu. Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote. Ni sheria mpaka wakati usio na kipimo katika makao yenu yote kwa vizazi vyenu vyote.
22 “‘Na wakati mnapovuna mavuno ya nchi yenu, hutamaliza kabisa ukingo wa shamba lako unapovuna, na masalio ya mavuno yako hutaokota.+ Utayaacha kwa ajili ya watu wenye kuteseka+ na mkaaji mgeni.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”
23 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 24 “Sema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Katika mwezi wa saba,+ siku ya kwanza ya mwezi huo, mtakuwa na pumziko kamili, ukumbusho kwa kupiga tarumbeta,+ mkusanyiko mtakatifu.+ 25 Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote, nanyi mtamtolea Yehova toleo linalotolewa kwa njia ya moto.’”
26 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 27 “Hata hivyo, katika siku ya kumi ya mwezi huu wa saba ni siku ya upatanisho.+ Mtafanya mkusanyiko mtakatifu, nanyi mtazitesa nafsi+ zenu na kumtolea Yehova toleo+ linalotolewa kwa njia ya moto. 28 Nanyi hamtafanya kazi ya aina yoyote siku hiyo, kwa sababu ni siku ya upatanisho ili kufanya upatanisho+ kwa ajili yenu mbele za Yehova Mungu wenu; 29 kwa sababu kila nafsi ambayo haitateseka siku hiyo itakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake.+ 30 Nayo nafsi yoyote itakayofanya kazi ya aina yoyote siku hiyo, mimi nitaiharibu nafsi hiyo itoke katikati ya watu wake.+ 31 Hamtafanya kazi ya aina yoyote.+ Ni sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili ya vizazi vyenu katika makao yenu yote. 32 Ni sabato ya pumziko kamili kwenu,+ nanyi mtazitesa+ nafsi zenu katika siku ya tisa ya mwezi huo wakati wa jioni. Toka jioni mpaka jioni mtaishika sabato.”
33 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 34 “Sema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huu wa saba ni sherehe ya vibanda muda wa siku saba kwa Yehova.+ 35 Siku ya kwanza ni mkusanyiko mtakatifu. Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote. 36 Siku saba mtamtolea Yehova toleo linalotolewa kwa njia ya moto. Siku ya nane mtakuwa na mkusanyiko mtakatifu,+ nanyi mtamtolea Yehova toleo linalotolewa kwa njia ya moto. Ni kusanyiko kuu. Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote.
37 “‘Hizi ndizo sherehe za majira+ za Yehova mtakazotangaza kuwa mikusanyiko mitakatifu,+ kwa ajili ya kumtolea Yehova toleo linalotolewa kwa njia ya moto:+ toleo la kuteketezwa+ na toleo la nafaka+ la dhabihu na matoleo ya vinywaji+ kulingana na ratiba ya kila siku, 38 mbali na sabato za Yehova+ na mbali na zawadi+ zenu na mbali na matoleo yenu ya nadhiri+ na mbali na matoleo yenu ya hiari,+ ambayo mtamtolea Yehova. 39 Hata hivyo, katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakapokuwa mmeyakusanya mazao ya nchi, mtasherehekea sherehe+ ya Yehova siku saba.+ Katika siku ya kwanza ni pumziko kamili na katika siku ya nane ni pumziko kamili.+ 40 Nanyi mtajichukulia katika siku ya kwanza tunda la miti yenye fahari, matawi ya mitende+ na matawi ya miti yenye majani mengi na mierebi ya bonde la mto, nanyi mtashangilia+ mbele za Yehova Mungu wenu siku saba. 41 Nanyi mtaisherehekea kama sherehe kwa Yehova siku saba katika mwaka.+ Kama sheria mpaka wakati usio na kipimo katika vizazi vyenu, mtaisherehekea katika mwezi wa saba. 42 Na katika vibanda mtakaa siku saba.+ Wenyeji wote katika Israeli watakaa katika vibanda,+ 43 ili vizazi vyenu vipate kujua+ kwamba niliwafanya wana wa Israeli wakae katika vibanda nilipokuwa nikiwatoa katika nchi ya Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”
44 Basi Musa akawaambia wana wa Israeli juu ya sherehe+ za majira za Yehova.
24 Na Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta safi ya zeituni zilizopondwa kwa ajili ya mwanga,+ ili kuiwasha taa daima.+ 3 Nje ya pazia la Ushuhuda katika hema la mkutano Haruni ataiweka kwa utaratibu toka jioni mpaka asubuhi mbele za Yehova daima. Ni sheria mpaka wakati usio na kipimo katika vizazi vyenu vyote. 4 Juu ya kinara cha taa+ cha dhahabu safi ataziweka taa+ kwa utaratibu mbele za Yehova daima.+
5 “Nawe utachukua unga laini na kuuoka uwe keki kumi na mbili za mviringo. Kila keki itafanyizwa kwa sehemu mbili za efa. 6 Nawe utaziweka katika vikundi viwili vya tabaka, sita katika kikundi kimoja cha tabaka,+ juu ya meza ya dhahabu safi mbele za Yehova.+ 7 Nawe utaweka ubani safi juu ya kila kikundi cha tabaka, nao utakuwa mkate kwa ajili ya kumbukumbu,+ toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto. 8 Katika siku moja ya sabato baada ya nyingine atauweka kwa utaratibu mbele za Yehova daima.+ Ni agano pamoja na wana wa Israeli mpaka wakati usio na kipimo. 9 Nao utakuwa wa Haruni na wa wanawe,+ nao wataula katika mahali patakatifu,+ kwa sababu ni kitu kitakatifu zaidi kwa ajili yake kutoka kwa matoleo ya Yehova yanayotolewa kwa njia ya moto, kama sharti mpaka wakati usio na kipimo.”
10 Sasa mwana wa mwanamke Mwisraeli, ambaye, hata hivyo, alikuwa mwana wa mwanamume Mmisri,+ akatoka kwenda katikati ya wana wa Israeli, naye yule mwana wa mwanamke Mwisraeli akaanza kupambana+ na mwanamume Mwisraeli kambini. 11 Naye yule mwana wa mwanamke Mwisraeli akaanza kulitukana lile Jina+ na kulilaani.+ Basi wakamleta kwa Musa.+ Basi jina la mama yake lilikuwa Shelomithi, binti ya Dibri wa kabila la Dani. 12 Ndipo wakamtia kifungoni+ mpaka kuwe na tangazo lililo wazi kulingana na neno la Yehova.+
13 Na Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 14 “Mtoe nje ya kambi+ yule aliyelaani; na wale wote waliomsikia wataweka mikono+ yao juu ya kichwa chake, nalo kusanyiko lote litampiga kwa mawe.+ 15 Nawe utasema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Ikiwa mtu yeyote atamlaani Mungu wake, basi atajibu kwa dhambi yake. 16 Kwa hiyo lazima yule mtukanaji wa jina la Yehova auawe.+ Lazima kusanyiko lote limpige kwa mawe. Mkaaji mgeni hali kadhalika mwenyeji atauawa kwa kulitukana lile Jina.+
17 “‘Na ikiwa mtu ataipiga nafsi yoyote ya mwanadamu kiasi cha kuiua, lazima atauawa.+ 18 Naye mwenye kuipiga nafsi ya mnyama wa kufugwa kiasi cha kuiua atalipa, nafsi kwa nafsi.+ 19 Na ikiwa mtu atamtia mwenzake kasoro, basi kama vile tu ambavyo yeye amefanya, ndivyo atakavyofanywa.+ 20 Mfupa uliovunjika kwa mfupa uliovunjika, jicho kwa jicho, jino kwa jino; aina ileile ya kasoro ambayo huenda akamtia mtu, hiyo ndiyo atakayotiwa.+ 21 Naye mwenye kumpiga mnyama kiasi cha kumuua+ atalipa,+ lakini mwenye kumpiga mwanadamu kiasi cha kumuua atauawa.+
22 “‘Uamuzi mmoja wa hukumu utatumika kwenu. Mkaaji mgeni atakuwa sawa na mwenyeji,+ kwa sababu mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+
23 Kisha Musa akasema na wana wa Israeli, nao wakamtoa nje ya kambi yule aliyekuwa amelaani, wakampiga kwa mawe.+ Basi wana wa Israeli wakafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
25 Na Yehova akazidi kusema na Musa kwenye Mlima Sinai, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, nawe uwaambie, ‘Mwishowe mtakapoingia katika nchi nitakayowapa ninyi,+ ndipo nchi hiyo itakaposhika sabato kwa Yehova.+ 3 Miaka sita utapanda mbegu katika shamba lako, na miaka sita utakata matawi ya shamba lako la mizabibu, nawe utakusanya mazao ya nchi.+ 4 Lakini katika mwaka wa saba kutakuwa na sabato ya pumziko kamili kwa ajili ya nchi hiyo,+ sabato kwa Yehova. Shamba lako hutalipanda mbegu, nalo shamba lako la mizabibu hutalikata matawi. 5 Mimea inayochipuka kutokana na mbegu zilizoanguka za mavuno yako hutavuna, na zabibu za mzabibu wako ambao haujakatwa matawi usikusanye. Kutakuwa na mwaka wa pumziko kamili kwa ajili ya nchi. 6 Nayo sabato ya nchi itakuwa chakula kwa ajili yenu, kwa ajili yako na mtumwa wako na kijakazi wako na mfanyakazi wako wa kukodiwa na mkaaji anayekaa pamoja nawe, wale wanaokaa wakiwa wakaaji wageni pamoja nawe, 7 na kwa ajili ya mnyama wako wa kufugwa na mnyama-mwitu aliye katika nchi yako. Mazao yake yote yatakuwa ndiyo chakula.
8 “‘Nawe utajihesabia sabato 7 za miaka, miaka 7 mara 7, na siku za sabato 7 za miaka zitakuwa miaka 49 kwa ajili yako. 9 Nawe utafanya baragumu ya sauti+ kubwa ivume katika mwezi wa saba siku ya kumi ya mwezi huo;+ katika siku ya upatanisho+ mtaifanya baragumu hiyo ivume katika nchi yenu yote. 10 Nanyi mtautakasa mwaka wa 50 na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakaaji wake wote.+ Itakuwa Yubile+ kwenu, nanyi mtarudi kila mmoja kwenye miliki yake nanyi mtarudi kila mmoja kwa familia yake.+ 11 Mwaka wa 50 utakuwa Yubile kwenu.+ Hamtapanda mbegu wala kuvuna mimea ya nchi inayochipuka kutokana na mbegu zilizoanguka wala kukusanya zabibu kutoka katika mizabibu ambayo haijakatwa matawi.+ 12 Kwa maana huo ni Yubile. Utakuwa kitu kitakatifu kwenu. Mnaweza kula kutoka shambani kile ambacho nchi inazaa.+
13 “‘Katika mwaka huu wa Yubile mtarudi kila mmoja kwenye miliki yake.+ 14 Sasa ikiwa mtamuuzia mwenzenu mali au kununua kutoka katika mkono wa mwenzenu, msikoseane.+ 15 Kwa hesabu ya miaka iliyo baada ya Yubile utanunua kutoka kwa mwenzako; kwa hesabu ya miaka ya mazao atakuuzia.+ 16 Kulingana na hesabu kubwa ya miaka ataongeza thamani yake ya ununuzi,+ na kulingana na uchache wa miaka atapunguza thamani yake ya ununuzi, kwa sababu hesabu ya mazao ndiyo anayokuuzia. 17 Na mtu yeyote kati yenu asimkosee mwenzake,+ nawe umwogope Mungu wako,+ kwa sababu mimi ni Yehova Mungu wenu.+ 18 Kwa hiyo mtazishika sheria zangu na kufuata maamuzi yangu ya hukumu na kuyatenda. Ndipo mtakapokaa katika nchi hiyo kwa usalama.+ 19 Nayo nchi itatoa mazao yake,+ nanyi mtakula na kushiba na kukaa kwa usalama juu yake.+
20 “‘Lakini ikiwa mtasema: “Tutakula nini katika mwaka wa saba kwa kuwa huenda tusipande mbegu wala kukusanya mazao yetu?”+ 21 ndipo hakika nitaamuru baraka zangu kwa ajili yenu katika mwaka wa sita, nayo itatoa mazao yake kwa ajili ya miaka mitatu.+ 22 Nanyi mtapanda mbegu mwaka wa nane na mtakula kutokana na mazao ya zamani mpaka mwaka wa tisa. Mtakula yale ya zamani mpaka mazao yake yaingie.
23 “‘Kwa hiyo nchi haitauzwa milele,+ kwa sababu nchi ni yangu.+ Kwa maana ninyi ni wakaaji wageni na wahamiaji kwa maoni yangu.+ 24 Na katika nchi yenu yote mnayoimiliki mtaipa nchi haki ya kununuliwa na kurudishwa.+
25 “‘Ikiwa ndugu yako atakuwa maskini na alazimike kuuza sehemu ya miliki yake, mkombozi wa jamaa yake ya karibu atakuja pia na kununua na kurudisha kile ambacho ndugu yake aliuza.+ 26 Na ikiwa mtu yeyote hatakuwa na mkombozi nao mkono wake mwenyewe upate faida naye apate kiasi cha kutosha kuikomboa, 27 pia atahesabu miaka tangu alipoiuza naye atarudisha pesa zinazosalia kwa mtu aliyemuuzia, naye atarudi kwenye miliki yake.+
28 “‘Lakini ikiwa mkono wake haupati kiasi cha kutosha kumrudishia, alichokiuza kitaendelea kuwa mkononi mwa mnunuzi wake mpaka mwaka wa Yubile;+ nacho kitarudishwa katika Yubile, naye atarudi katika miliki yake.+
29 “‘Sasa ikiwa mtu atauza nyumba ya kukaa katika jiji lenye ukuta, haki yake ya kuikomboa itaendelea pia mpaka mwaka umalizike tangu alipoiuza; haki yake ya kukomboa+ itaendelea kwa mwaka mzima. 30 Lakini ikiwa haitanunuliwa na kurudishwa kabla ya ule mwaka mzima kutimia kwa ajili yake, nyumba hiyo iliyo katika jiji lenye ukuta itasimama milele ikiwa mali ya mnunuzi katika vizazi vyake. Haitarudishwa katika Yubile. 31 Hata hivyo, nyumba za makao ambayo hayana ukuta kuyazunguka zitahesabiwa kama sehemu ya mashamba ya nchi. Haki ya kukomboa+ itaendelea kwa ajili yake, na katika Yubile+ itarudishwa.
32 “‘Na kuhusu majiji ya Walawi pamoja na nyumba za majiji ya miliki yao,+ haki ya kukomboa itaendelea mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili ya Walawi.+ 33 Na mahali ambapo mali ya Walawi hainunuliwi tena, nyumba iliyouzwa katika jiji la miliki yake itatoka pia katika Yubile;+ kwa sababu nyumba za majiji ya Walawi ni miliki yao katikati ya wana wa Israeli.+ 34 Tena, kiwanja cha malisho+ cha majiji yao kisiuzwe, kwa sababu hicho ni miliki mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili yao.
35 “‘Na ikiwa ndugu yako atakuwa maskini na kwa hiyo ni dhaifu kifedha karibu nawe,+ utamtegemeza pia.+ Kama mkaaji mgeni na kama mhamiaji,+ ataendelea kukaa akiwa hai pamoja nawe. 36 Usichukue faida na riba kutoka kwake,+ lakini umwogope Mungu wako;+ naye ndugu yako ataendelea kukaa akiwa hai pamoja nawe. 37 Hutampa pesa zako kwa faida,+ wala hutampa chakula chako kwa riba. 38 Mimi ni Yehova Mungu wenu, aliyewatoa ninyi katika nchi ya Misri ili kuwapa nchi ya Kanaani,+ ili nijionyeshe kuwa Mungu wenu.+
39 “‘Na ikiwa ndugu yako atakuwa maskini karibu nawe naye alazimike kujiuza kwako,+ usimtumie kama mfanyakazi katika utumishi wa kitumwa.+ 40 Atakuwa pamoja nawe kama mfanyakazi wa kukodiwa,+ kama mhamiaji. Atakutumikia mpaka mwaka wa Yubile. 41 Naye ataondoka kwako, yeye na wanawe pamoja naye, naye atarudi kwa familia yake, naye atarudi kwa miliki ya mababu zake.+ 42 Kwa maana wao ni watumwa wangu niliowatoa kutoka katika nchi ya Misri.+ Hawatajiuza kama vile mtumwa anavyouzwa. 43 Hutamkanyagia chini kwa uonevu,+ nawe utamwogopa Mungu wako.+ 44 Na kuhusu mtumwa wako na kijakazi wako atakayekuwa wako kutoka katika mataifa yanayowazunguka ninyi, kutoka kwao ninyi mnaweza kununua mtumwa au kijakazi. 45 Na pia kutoka kwa wana wa wahamiaji wanaokaa wakiwa wageni pamoja nanyi,+ kutoka kwao mnaweza kuwanunua, na kutoka katika familia zao zilizo pamoja nanyi, waliozaliwa kwao katika nchi yenu; nao watakuwa miliki yenu. 46 Nanyi mtawapitisha wawe urithi kwa wana wenu baada yenu ili wawarithi kama miliki mpaka wakati usio na kipimo.+ Mnaweza kuwatumia kama wafanyakazi, lakini juu ya ndugu zenu wana wa Israeli, msikanyagane, kwa uonevu.+
47 “‘Lakini ikiwa mkono wa mkaaji mgeni au mhamiaji aliye pamoja nawe utakuwa na mali, na ndugu yako amekuwa maskini karibu nawe naye alazimike kujiuza kwa mkaaji mgeni au mhamiaji aliye pamoja nawe, au kwa mshiriki wa familia ya huyo mkaaji mgeni, 48 baada ya kujiuza mwenyewe,+ haki ya kukomboa itaendelea katika kisa chake.+ Mmoja wa ndugu zake anaweza kumnunua.+ 49 Au ndugu ya baba yake au mwana wa ndugu ya baba yake anaweza kumnunua, au mtu wa jamaa yake ya kimwili mwenye uhusiano wa damu,+ mtu wa familia yake, anaweza kumnunua tena.
“‘Au ikiwa mkono wake mwenyewe umepata mali, basi mwenyewe atajinunua.+ 50 Naye atafanya hesabu na mnunuzi wake tangu mwaka aliojiuza mpaka mwaka wa Yubile,+ na pesa za ununuzi wake zitalingana na hesabu ya miaka.+ Ataendelea kuwa pamoja naye jinsi ambavyo siku za kazi za mfanyakazi wa kukodiwa huhesabiwa.+ 51 Ikiwa bado kuna miaka mingi, atalipa bei yake ya ukombozi kulingana nayo kutoka katika pesa zake za ununuzi. 52 Lakini ikiwa ni miaka michache tu inayobaki mpaka mwaka wa Yubile,+ basi mwenyewe atajipigia hesabu. Kulingana na miaka yake atalipa bei yake ya ukombozi. 53 Ataendelea kuwa pamoja naye kama mfanyakazi wa kukodiwa+ mwaka baada ya mwaka. Hatamkanyagia chini kwa uonevu+ mbele ya macho yako. 54 Hata hivyo, ikiwa hawezi kujinunua kwa masharti hayo, atatoka katika mwaka wa Yubile,+ yeye na wanawe pamoja naye.
55 “‘Kwa maana wana wa Israeli ni watumwa wangu.+ Wao ni watumwa wangu niliowatoa katika nchi ya Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.+
26 “‘Msijifanyie miungu isiyo na thamani,+ wala msijisimamishie sanamu ya kuchongwa+ au nguzo takatifu, wala msiweke jiwe kuwa sanamu katika+ nchi yenu ili kuliinamia;+ kwa maana mimi ni Yehova Mungu wenu. 2 Mtazishika sabato+ zangu na kupaheshimu patakatifu pangu. Mimi ni Yehova.
3 “‘Mkiendelea kutembea katika sheria zangu na kushika amri zangu na kuzifuata,+ 4 hakika mimi pia nitawapa ninyi manyunyu yenu ya mvua wakati wake unaofaa,+ nayo nchi itatoa mazao yake,+ nao mti wa shambani utatoa matunda yake.+ 5 Na hakika kupura kwenu kutafikia ukusanyaji wenu wa zabibu, nao ukusanyaji wa zabibu utafikia upandaji wa mbegu; na hakika mtakula mkate wenu na kushiba+ na kukaa kwa usalama katika nchi yenu.+ 6 Nami nitaweka amani katika nchi,+ nanyi mtalala, pasipo yeyote wa kuwatetemesha;+ nami nitamkomesha katika nchi+ mnyama-mwitu mwenye madhara, nao upanga hautapita katika nchi yenu.+ 7 Na hakika ninyi mtawafuatilia adui+ zenu, nao wataanguka kwa upanga mbele yenu. 8 Na hakika watano kati yenu watawafukuza mia, na mia kati yenu watawafukuza elfu kumi, nao adui zenu wataanguka kwa upanga mbele yenu.+
9 “‘Nami nitageuka kwenu+ na kuwawezesha kuzaana na kuwazidisha ninyi,+ nami nitatimiza agano langu pamoja nanyi.+ 10 Na hakika mtakula vitu vya zamani vya mwaka uliotangulia,+ nanyi mtatoa nje vitu vya zamani kabla ya vitu vipya. 11 Na hakika mimi nitaweka maskani yangu katikati yenu,+ nayo nafsi yangu haitawachukia ninyi.+ 12 Na hakika mimi nitatembea katikati yenu na kujionyesha kuwa Mungu wenu,+ nanyi mtajionyesha kuwa watu wangu.+ 13 Mimi ni Yehova Mungu wenu, niliyewatoa katika nchi ya Misri ili msiwe watumwa kwao,+ nami nikavunja nira zenu na kuwafanya mtembee mkiwa wima.+
14 “‘Hata hivyo, ikiwa hamtanisikiliza wala kutenda amri zote hizi,+ 15 na ikiwa mtazikataa sheria zangu,+ na ikiwa nafsi zenu zitachukia maamuzi yangu ya hukumu hivi kwamba zisitende amri zangu zote, mfikie hatua ya kulivunja agano langu,+ 16 ndipo mimi nitawafanyia yanayofuata, na katika kutoa adhabu hakika nitaleta juu yenu usumbufu kwa kifua kikuu+ na homa kali, kufanya macho yafifie+ na kuifanya nafsi idhoofike.+ Nanyi mtapanda mbegu yenu bure, kwa maana adui zenu hakika wataila.+ 17 Na hakika mimi nitauweka uso wangu juu yenu, nanyi hakika mtashindwa mbele ya adui zenu;+ nao wale wanaowachukia ninyi watawakanyagia chini,+ nanyi kwa kweli mtakimbia wakati ambapo hakuna mtu yeyote anayewafuatilia.+
18 “‘Lakini ikiwa hamtanisikiliza ijapokuwa mambo yote hayo, ndipo nitawatia adabu mara saba zaidi kwa sababu ya dhambi zenu.+ 19 Nami nitakivunja kiburi cha nguvu zenu na kuzifanya mbingu zenu ziwe kama chuma+ na nchi yenu iwe kama shaba. 20 Nazo nguvu zenu zitatumika bure, kwa maana nchi yenu haitatoa mazao yake,+ nao mti wa dunia hautatoa matunda yake.+
21 “‘Lakini ikiwa mtaendelea kutembea kwa kunipinga nanyi msitake kunisikiliza mimi, ndipo nitakapoleta juu yenu mapigo mara saba zaidi kulingana na dhambi zenu.+ 22 Nami nitatuma wanyama wa mwituni katikati yenu,+ nao hakika watawaua watoto+ wenu na kukatilia mbali wanyama wenu wa kufugwa na kupunguza hesabu yenu, nazo barabara zenu kwa kweli zitakuwa ukiwa.+
23 “‘Hata hivyo, ikiwa kwa mambo hayo hamtakubali mimi niwarekebishe+ na iwe kwamba ni lazima tu mtembee kwa kunipinga, 24 ndipo mimi, naam, mimi nitatembea kwa kuwapinga;+ nami, naam, mimi nitawapiga mara saba kwa sababu ya dhambi zenu.+ 25 Nami hakika nitaleta juu yenu upanga unaolipiza kisasi+ kwa ajili ya agano;+ na hakika ninyi mtajikusanya katika majiji yenu, nami hakika nitaleta tauni katikati yenu,+ nanyi mtatiwa mkononi mwa adui.+ 26 Nitakapokuwa nimevunja fimbo zenu ambazo huning’inizwa mikate ya mviringo,+ kwa kweli wanawake kumi wataoka mkate wenu katika jiko moja na kuwarudishia mkate wenu kulingana na uzito;+ nanyi mtakula bali hamtashiba.+
27 “‘Hata hivyo, ikiwa pamoja na hayo hamtanisikiliza na iwe kwamba ni lazima tu mtembee kwa kunipinga,+ 28 ndipo nitakapotembea kwa kuwapinga vikali,+ na mimi, naam, mimi nitawatia adabu mara saba kwa sababu ya dhambi zenu.+ 29 Kwa hiyo mtakula nyama ya wana wenu, nanyi mtakula nyama ya binti zenu.+ 30 Na hakika mimi nitaangamiza mahali penu patakatifu pa juu+ na kuvikatilia mbali vinara vyenu vya uvumba na kuilaza mizoga yenu wenyewe juu ya mizoga ya sanamu zenu za mavi;+ nayo nafsi yangu itawachukia ninyi.+ 31 Nami nitayatia majiji yenu kwenye upanga+ na kufanya ukiwa patakatifu penu,+ wala sitanusa harufu zenu za kutuliza.+ 32 Nami nitaifanya nchi iwe ukiwa,+ nao adui zenu wanaokaa ndani yake wataitazama kwa mshangao.+ 33 Nami nitawatawanya ninyi katikati ya mataifa,+ nami nitauchomoa upanga nyuma yenu;+ nayo nchi yenu itakuwa ukiwa,+ na majiji yenu yatakuwa bomoko lenye ukiwa.
34 “‘Na wakati huo nchi italipa sabato zake siku zote za kukaa kwake ukiwa, huku ninyi mkiwa katika nchi ya adui zenu. Wakati huo nchi itashika sabato, kwa maana lazima ilipe sabato zake.+ 35 Siku zote za kukaa kwake ukiwa itashika sabato, kwa sababu haikushika sabato wakati wa sabato zenu mlipokuwa mkikaa juu yake.
36 “‘Nao wale wanaobaki katikati yenu,+ hakika nitatia woga mioyoni mwao katika nchi za adui zao; na sauti ya jani linalopeperushwa itawafukuza, nao kwa kweli watakimbia kama wanavyoukimbia upanga na kuanguka pasipo mtu yeyote kufuatilia.+ 37 Na hakika wao watajikwaa juu ya mmoja na mwenzake kana kwamba ni kutokana na upanga pasipo mtu yeyote kufuatilia, nanyi hamtakuwa na uwezo wowote wa kusimama na kuwapinga adui zenu.+ 38 Nanyi mtaangamia katikati ya mataifa,+ nayo nchi ya adui zenu itawala ninyi. 39 Na wale watakaobaki kati yenu, wataoza+ kabisa kwa sababu ya kosa lao katika nchi za adui zenu. Naam, kwa sababu ya makosa ya baba zao,+ pamoja nao wataoza kabisa. 40 Na hakika wao wataungama kosa lao wenyewe+ na kosa la baba zao katika ukosefu wao wa uaminifu walipojiendesha kwa njia isiyo ya uaminifu kunielekea mimi, naam, wakati ambapo walitembea kwa kunipinga.+ 41 Hata hivyo, mimi nilitembea kwa kuwapinga,+ na nikalazimika kuwaleta katika nchi ya adui zao.+
“‘Labda wakati huo moyo wao ambao haujatahiriwa+ utanyenyekezwa,+ na wakati huo watalipia kosa lao. 42 Nami nitalikumbuka agano langu pamoja na Yakobo;+ na hata agano langu pamoja na Isaka+ na hata agano langu pamoja na Abrahamu+ nitalikumbuka, nayo nchi nitaikumbuka. 43 Wakati wote huo walipoiacha nchi na ilipokuwa ikilipa sabato zake+ huku ikikaa ukiwa bila wao, nao wenyewe walikuwa wakilipia kosa lao,+ kwa sababu, naam kwa sababu, walikuwa wameyakataa maamuzi yangu ya hukumu,+ nazo nafsi zao zilikuwa zimechukia sheria zangu.+ 44 Na hata hivyo pamoja na yote hayo, huku wakiendelea kukaa katika nchi ya adui zao, hakika sitawakataa+ wala kuwachukia+ ili kuwaangamiza, na kulivunja agano+ langu pamoja nao; kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao. 45 Nami nitakumbuka kwa ajili yao lile agano la mababu+ zao ambao niliwatoa katika nchi ya Misri machoni pa mataifa,+ ili nijionyeshe kuwa Mungu wao. Mimi ni Yehova.’”
46 Hayo ndiyo masharti na maamuzi ya hukumu+ na sheria ambazo Yehova aliweka kati yake na wana wa Israeli katika Mlima Sinai kupitia Musa.+
27 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, nawe uwaambie, ‘Ikiwa mtu atamwekea Yehova nadhiri ya pekee+ kwa kumtolea Yehova nafsi kulingana na thamani iliyokadiriwa, 3 nayo thamani iliyokadiriwa iwe ya mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 mpaka miaka 60, basi thamani iliyokadiriwa itakuwa shekeli 50 za fedha kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 4 Lakini ikiwa ni mwanamke, basi thamani iliyokadiriwa itakuwa shekeli 30. 5 Na ikiwa umri ni kuanzia miaka 5 mpaka miaka 20, basi thamani iliyokadiriwa ya mwanamume itakuwa shekeli 20 na kwa ajili ya mwanamke itakuwa shekeli 10. 6 Na ikiwa umri ni kuanzia mwezi mmoja mpaka miaka mitano, basi thamani iliyokadiriwa ya mwanamume itakuwa shekeli tano+ za fedha na kwa ajili ya mwanamke thamani iliyokadiriwa itakuwa shekeli tatu za fedha.
7 “‘Sasa ikiwa umri ni kuanzia miaka 60 na zaidi, ikiwa ni mwanamume, basi thamani iliyokadiriwa itakuwa shekeli 15 na kwa ajili ya mwanamke itakuwa shekeli 10. 8 Lakini ikiwa amekuwa maskini mno kwa ajili ya ile thamani iliyokadiriwa,+ ndipo atakapomsimamisha mtu huyo mbele ya kuhani, naye kuhani atakadiria thamani yake.+ Kulingana na anachoweza+ yule mwenye kuweka nadhiri, kuhani atakadiria thamani yake.
9 “‘Na ikiwa ni mnyama kama yule ambaye mtu humtolea Yehova, kila kitu ambacho atampa Yehova kitakuwa kitu kitakatifu.+ 10 Hataweka kingine mahali pake, wala kukibadili chema kwa kibaya au kibaya kwa chema. Lakini ikiwa ni lazima akibadili, mnyama kwa mnyama, basi lazima hicho chenyewe na kile kitakachobadilishwa nacho vitakuwa kitu kitakatifu. 11 Na ikiwa ni mnyama yeyote asiye safi+ kama yule ambaye mtu hawezi kumtoa katika toleo kwa Yehova,+ basi lazima amsimamishe mnyama huyo mbele ya kuhani.+ 12 Naye kuhani atamkadiria thamani yake iwapo ni mzuri au mbaya. Kulingana na thamani iliyokadiriwa na kuhani,+ ndivyo atakavyokuwa. 13 Lakini ikiwa anataka kumnunua, basi atatoa sehemu yake ya tano+ kwa kuongezea ile thamani iliyokadiriwa.
14 “‘Sasa ikiwa mtu ataitakasa nyumba yake iwe kitu kitakatifu kwa Yehova, basi kuhani atakadiria thamani yake iwapo ni nzuri au mbaya.+ Kulingana na kadirio la kuhani ambalo ataikadiria, ndivyo itakavyogharimu. 15 Lakini ikiwa mtakasaji anataka kuinunua nyumba yake, basi atatoa sehemu ya tano ya thamani iliyokadiriwa kwa kuongezea thamani hiyo;+ nayo itakuwa yake.
16 “‘Na ikiwa ni sehemu ya shamba lililo mali yake+ ambalo mtu anataka kulitakasa kwa Yehova, basi thamani itakadiriwa kulingana na mbegu yake: ikiwa ni homeri+ moja ya mbegu ya shayiri, basi kwa shekeli 50 za fedha. 17 Ikiwa atalitakasa shamba lake kuanzia mwaka wa Yubile+ na kuendelea, litagharimu kulingana na thamani iliyokadiriwa. 18 Na ikiwa atalitakasa shamba lake baada ya Yubile, basi kuhani atafanya hesabu ya bei kulingana na miaka inayobaki mpaka mwaka wa Yubile inayofuata, na kiasi fulani kitapunguzwa kutoka katika thamani iliyokadiriwa.+ 19 Lakini ikiwa mtakasaji wake atalinunua shamba hilo, basi atatoa sehemu ya tano ya pesa ya thamani iliyokadiriwa kwa kuongezea thamani hiyo, nalo litaendelea kuwa lake.+ 20 Sasa ikiwa hatalinunua shamba hilo lakini shamba hilo liuziwe mtu mwingine, halitanunuliwa na kurudishwa tena. 21 Na wakati shamba hilo litakapotoka katika Yubile litakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova, kama shamba lililotolewa wakfu.+ Kuhani atalimiliki.+
22 “‘Na ikiwa atamtakasia Yehova shamba alilolinunua ambalo si sehemu ya shamba lililo mali yake,+ 23 basi kuhani atamfanyia hesabu ya kadirio la thamani mpaka mwaka wa Yubile, naye atatoa thamani iliyokadiriwa katika siku hiyo.+ Ni kitu kitakatifu kwa Yehova.+ 24 Katika mwaka wa Yubile shamba hilo litarudi kwa mtu aliyelinunua kutoka kwake, kwa mtu ambaye shamba hilo ni mali yake.+
25 “‘Sasa kila thamani itakadiriwa kwa shekeli ya mahali patakatifu. Shekeli itakuwa gera 20.+
26 “‘Ila mzaliwa wa kwanza kati ya wanyama, anayezaliwa akiwa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya Yehova,+ mtu yeyote asimtakase. Awe ni ng’ombe au kondoo, ni wa Yehova.+ 27 Na ikiwa ni mmoja wa wanyama wasio safi+ naye ni lazima amkomboe kulingana na thamani iliyokadiriwa, basi atatoa sehemu yake ya tano kwa kuongezea juu yake.+ Lakini ikiwa hatanunuliwa, basi atauzwa kulingana na thamani iliyokadiriwa.
28 “‘Ila tu hakuna kitu chochote kilichotolewa wakfu ambacho huenda mtu akamtolea Yehova kwa ajili ya uharibifu+ kutoka katikati ya vyote vilivyo vyake, iwe ni kutoka kwa wanadamu au wanyama au kutoka katika shamba lililo mali yake, kitakachouzwa, wala hakuna aina yoyote ya kitu kilichotolewa ambacho kitanunuliwa.+ Hicho ni kitu kitakatifu zaidi kwa Yehova. 29 Hakuna mtu yeyote ambaye huenda akawa ametengwa kwa ajili ya kuharibiwa kutoka kati ya wanadamu atakayekombolewa.+ Lazima auawe.+
30 “‘Na kila sehemu ya kumi+ ya nchi, kutoka katika mbegu ya nchi na tunda la mti, ni ya Yehova. Ni kitu kitakatifu kwa Yehova. 31 Na ikiwa mtu anataka kununua sehemu yake yoyote ya kumi, atatoa sehemu yake ya tano kwa kuongezea juu ya hiyo.+ 32 Na kwa kila sehemu ya kumi ya mifugo na ya kundi, kila kitu ambacho hupita chini ya bakora,+ kichwa cha kumi kitakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova. 33 Hatamchunguza iwapo ni mzuri au mbaya, wala hatambadilisha. Lakini akimbadilisha, hicho chenyewe na kile kilichobadilishwa nacho vitakuwa kitu kitakatifu.+ Hatanunuliwa.’”
34 Hizo ndizo amri+ ambazo Yehova alimpa Musa kuwa amri kwa wana wa Israeli katika Mlima Sinai.+