Hesabu
1 Naye Yehova akasema na Musa katika nyika ya Sinai,+ kwenye hema la mkutano,+ siku ya kwanza ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili wa kutoka kwao nchini Misri,+ naye akamwambia: 2 “Chukueni hesabu+ ya kusanyiko lote la wana wa Israeli kulingana na familia zao, kulingana na nyumba ya baba zao, kwa hesabu ya majina, wanaume wote, kichwa kwa kichwa kati yao, 3 kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi,+ kila mtu anayeingia jeshini katika Israeli.+ Mtawaandikisha kulingana na majeshi yao, wewe na Haruni.
4 “Na wanaume fulani watakuwa pamoja nanyi, mwanamume mmoja kwa kabila moja; kila mmoja ni kichwa cha nyumba ya baba zake.+ 5 Na haya ndiyo majina ya wanaume watakaosimama pamoja nanyi: Wa Rubeni,+ Elisuri+ mwana wa Shedeuri; 6 wa Simeoni,+ Shelumieli+ mwana wa Zurishadai; 7 wa Yuda,+ Nashoni+ mwana wa Aminadabu; 8 wa Isakari,+ Nethaneli+ mwana wa Zuari; 9 wa Zabuloni,+ Eliabu+ mwana wa Heloni; 10 wa wana wa Yosefu:+ wa Efraimu,+ Elishama mwana wa Amihudi; wa Manase,+ Gamalieli mwana wa Pedazuri; 11 wa Benyamini,+ Abidani+ mwana wa Gidioni; 12 wa Dani,+ Ahiezeri+ mwana wa Amishadai; 13 wa Asheri,+ Pagieli+ mwana wa Okrani; 14 wa Gadi,+ Eliasafu+ mwana wa Deueli;+ 15 wa Naftali,+ Ahira+ mwana wa Enani. 16 Hao ndio walioitwa wa kusanyiko, wakuu+ wa makabila ya baba zao. Hao ndio vichwa vya maelfu ya Israeli.”+
17 Basi Musa na Haruni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wametajwa kwa majina. 18 Nao wakakutanisha kusanyiko lote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, ili uzao+ wao utambuliwe kwa habari ya familia zao katika nyumba ya baba zao, kulingana na hesabu ya majina, kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi,+ kichwa kwa kichwa kati yao, 19 kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa; naye akawaandikisha+ katika nyika ya Sinai.
20 Na wana wa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao, kukawa kulingana na hesabu ya majina, kichwa kwa kichwa kati yao, wanaume wote wenye umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 21 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Rubeni walikuwa 46,500.+
22 Wa wana wa Simeoni,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao, watu wake walioandikishwa kulingana na hesabu ya majina, kichwa kwa kichwa kati yao, wanaume wote wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 23 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Simeoni walikuwa 59,300.+
24 Wa wana wa Gadi,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 25 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Gadi+ walikuwa 45,650.+
26 Wa wana wa Yuda,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 27 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Yuda walikuwa 74,600.+
28 Wa wana wa Isakari,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 29 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Isakari walikuwa 54,400.+
30 Wa wana wa Zabuloni,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 31 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Zabuloni walikuwa 57,400.+
32 Wa wana wa Yosefu: wa wana wa Efraimu,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 33 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Efraimu+ walikuwa 40,500.+
34 Wa wana wa Manase,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 35 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Manase walikuwa 32,200.+
36 Wa wana wa Benyamini,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 37 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Benyamini walikuwa 35,400.+
38 Wa wana wa Dani,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 39 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Dani walikuwa 62,700.+
40 Wa wana wa Asheri,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 41 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Asheri walikuwa 41,500.+
42 Wa wana wa Naftali,+ kuzaliwa kwao kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini, 43 wale walioandikishwa kati yao wa kabila la Naftali walikuwa 53,400.+
44 Hao ndio walioandikishwa, ambao Musa aliandikisha, pamoja na Haruni na wakuu wa Israeli, wanaume kumi na wawili. Waliwakilisha kila mmoja nyumba ya baba zake. 45 Na wale wote walioandikishwa wa wana wa Israeli kulingana na nyumba ya baba zao kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kila mtu anayeingia jeshini katika Israeli, wakawa, 46 naam, wale wote walioandikishwa wakawa 603,550.+
47 Hata hivyo, Walawi+ kulingana na kabila la baba zao hawakuandikishwa kati yao.+ 48 Kwa hiyo Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 49 “Ni kabila la Lawi tu ambalo hutaandikisha, na hesabu yao usiichukue kati ya wana wa Israeli.+ 50 Na wewe mwenyewe uweke rasmi Walawi juu ya maskani ya Ushuhuda+ na juu ya vyombo vyake vyote na juu ya kila kitu kilicho chake.+ Wao wenyewe wataichukua maskani na vyombo vyake vyote,+ nao wenyewe watahudumu+ kwenye hiyo maskani; nao watapiga kambi kuizunguka maskani.+ 51 Na wakati maskani hiyo inapoondoka, Walawi wataishusha; na wakati maskani hiyo inapopiga kambi,+ Walawi wataisimamisha; na mgeni yeyote anayekaribia anapaswa kuuawa.+
52 “Na wana wa Israeli watapiga kambi kila mmoja kulingana na kambi yake, na kila mtu kulingana na mgawanyo+ wake wa makabila matatu kwa majeshi yao. 53 Nao Walawi watapiga kambi kuizunguka maskani ya Ushuhuda, ili ghadhabu+ yoyote isizuke juu ya kusanyiko la wana wa Israeli; nao Walawi watashika utumishi wa maskani ya Ushuhuda.”+
54 Na wana wa Israeli wakafanya kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru Musa. Walifanya vivyo hivyo.+
2 Sasa Yehova akasema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 2 “Wana wa Israeli watapiga kambi, kila mtu kulingana na mgawanyo wake wa makabila matatu,+ kando ya alama za nyumba ya baba zao. Watapiga kambi kuzunguka pande zote mbele ya hema la mkutano.
3 “Na wale wanaopiga kambi upande wa mashariki kuelekea mapambazuko ya jua watakuwa mgawanyo wa makabila matatu ya kambi ya Yuda kwa majeshi yao, na mkuu wa wana wa Yuda ni Nashoni+ mwana wa Aminadabu. 4 Na jeshi lake na wale walioandikishwa kati yao ni 74,600.+ 5 Na wale wanaopiga kambi kando yake watakuwa kabila la Isakari,+ na mkuu wa wana wa Isakari ni Nethaneli+ mwana wa Zuari. 6 Na jeshi lake na watu wake walioandikishwa ni 54,400.+ 7 Na kabila la Zabuloni; na mkuu wa wana wa Zabuloni ni Eliabu+ mwana wa Heloni. 8 Na jeshi lake na watu wake walioandikishwa ni 57,400.+
9 “Watu wote walioandikishwa wa kambi ya Yuda ni 186,400 kwa majeshi yao. Wanapaswa kuondoka kwanza.+
10 “Ule mgawanyo wa makabila matatu wa Rubeni+ utakuwa kuelekea kusini kwa majeshi yao, na mkuu wa wana wa Rubeni ni Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 11 Na jeshi lake na watu wake walioandikishwa ni 46,500.+ 12 Na wale wanaopiga kambi kando yake watakuwa kabila la Simeoni, na mkuu wa wana wa Simeoni ni Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 13 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 59,300.+ 14 Na kabila la Gadi; na mkuu wa wana wa Gadi ni Eliasafu+ mwana wa Reueli. 15 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 45,650.+
16 “Watu wote walioandikishwa wa kambi ya Rubeni ni 151,450 kwa majeshi yao, nao wanapaswa kuondoka wakiwa wa pili.+
17 “Hema la mkutano+ litakapoondoka, kambi ya Walawi+ itakuwa katikati ya kambi hizo.
“Kama vile watakavyopiga kambi, ndivyo watakavyoondoka,+ kila mmoja mahali pake, kulingana na mgawanyo wao wa makabila matatu.
18 “Mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya Efraimu+ kwa majeshi yao utakuwa kuelekea magharibi, na mkuu wa wana wa Efraimu ni Elishama+ mwana wa Amihudi. 19 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 40,500.+ 20 Na kando yake kutakuwa na kabila la Manase,+ na mkuu wa wana wa Manase ni Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 21 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 32,200.+ 22 Na kabila la Benyamini;+ na mkuu wa wana wa Benyamini ni Abidani+ mwana wa Gidioni. 23 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 35,400.+
24 “Watu wote walioandikishwa wa kambi ya Efraimu ni 108,100 kwa majeshi yao, nao wanapaswa kuondoka wakiwa wa tatu.+
25 “Mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya Dani utakuwa kuelekea kaskazini kwa majeshi yao, na mkuu wa wana wa Dani ni Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 26 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 62,700.+ 27 Na wale wanaopiga kambi kando yake ni kabila la Asheri, na mkuu wa wana wa Asheri ni Pagieli+ mwana wa Okrani. 28 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 41,500.+ 29 Na kabila la Naftali;+ na mkuu wa wana wa Naftali ni Ahira+ mwana wa Enani. 30 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 53,400.+
31 “Watu wote walioandikishwa wa kambi ya Dani ni 157,600. Wanapaswa kuondoka wakiwa wa mwisho+—kulingana na mgawanyo wao wa makabila matatu.”
32 Hao ndio watu walioandikishwa wa wana wa Israeli kulingana na nyumba ya baba zao; wote walioandikishwa wa kambi hizo kwa majeshi yao walikuwa 603,550.+ 33 Lakini Walawi hawakuandikishwa+ katikati ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa. 34 Na wana wa Israeli wakafanya kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru Musa.+ Hivyo ndivyo walivyopiga kambi kwa migawanyo yao ya makabila matatu,+ na hivyo ndivyo walivyoondoka,+ kila mmoja kwa familia zake kulingana na nyumba ya baba zake.
3 Sasa hivi ndivyo vilivyokuwa vizazi vya Haruni na Musa katika siku ambayo Yehova alisema na Musa katika Mlima Sinai.+ 2 Nayo haya ndiyo yaliyokuwa majina ya wana wa Haruni: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu,+ Eleazari+ na Ithamari.+ 3 Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya wana wa Haruni, makuhani waliotiwa mafuta ambao mikono yao ilijazwa nguvu watumikie wakiwa makuhani.+ 4 Hata hivyo, Nadabu na Abihu walikufa mbele za Yehova walipotoa moto haramu+ mbele za Yehova katika nyika ya Sinai; nao hawakuwa na wana wowote. Lakini Eleazari+ na Ithamari+ waliendelea kutumikia wakiwa makuhani pamoja na Haruni baba yao.
5 Na Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 6 “Leta kabila la Lawi+ karibu, nawe utawasimamisha mbele ya Haruni kuhani, nao watamhudumia.+ 7 Nao watashika wajibu wao kwake na wajibu wao kwa kusanyiko lote mbele ya hema la mkutano katika kutimiza utumishi wa maskani. 8 Nao watatunza vyombo+ vyote vya hema la mkutano, naam, wajibu wa wana wa Israeli katika kutimiza utumishi wao wa maskani.+ 9 Nawe utawakabidhi Walawi kwa Haruni na wanawe. Wao ni watu waliokabidhiwa, aliokabidhiwa kutoka kwa wana wa Israeli.+ 10 Nawe utawaweka rasmi Haruni na wanawe, nao lazima wautunze ukuhani+ wao; na mgeni yeyote atakayekaribia atauawa.”+
11 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 12 “Mimi nami, tazama! nawachukua Walawi kutoka katikati ya wana wa Israeli badala ya wazaliwa wa kwanza+ wote wanaofungua tumbo la uzazi la wana wa Israeli; nao Walawi watakuwa wangu. 13 Kwa maana kila mzaliwa wa kwanza ni wangu.+ Katika siku niliyompiga na kumuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri+ nilijitakasia kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli kuanzia mwanadamu mpaka mnyama.+ Wanapaswa kuwa wangu. Mimi ni Yehova.”
14 Na Yehova akazidi kusema na Musa katika nyika ya Sinai,+ na kumwambia: 15 “Waandikishe wana wa Lawi kulingana na nyumba ya baba zao kulingana na familia zao. Kila mwanamume kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi utamwandikisha.”+ 16 Naye Musa akaanza kuwaandikisha kwa agizo la Yehova, kama vile alivyokuwa ameamriwa. 17 Nao hawa ndio waliokuwa wana wa Lawi+ kulingana na majina yao: Gershoni na Kohathi na Merari.+
18 Sasa haya ndiyo yaliyokuwa majina ya wana wa Gershoni kulingana na familia zao: Libni na Shimei.+
19 Nao wana wa Kohathi+ kulingana na familia zao walikuwa Amramu na Ishari,+ Hebroni na Uzieli.
20 Na wana wa Merari+ kulingana na familia zao walikuwa Mali+ na Mushi.+
Hizi ndizo zilizokuwa familia za Walawi kulingana na nyumba ya baba zao.
21 Za Gershoni zilikuwa familia ya Walibni+ na familia ya Washimei.+ Hizo ndizo zilizokuwa familia za Wagershoni. 22 Watu wao walioandikishwa walikuwa kulingana na hesabu ya wanaume wote kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi.+ Watu wao walioandikishwa walikuwa 7,500.+ 23 Familia za Wagershoni zilikuwa nyuma ya maskani.+ Zilikuwa zimepiga kambi upande wa magharibi. 24 Na mkuu wa nyumba ya ukoo wa upande wa baba kwa ajili ya Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli. 25 Na wajibu wa wana wa Gershoni+ katika hema la mkutano ulikuwa maskani na lile hema,+ kifuniko+ chake na kisitiri+ cha mwingilio wa hema la mkutano, 26 na mapazia+ ya ua na kisitiri+ cha mwingilio wa ua ulioizunguka maskani na madhabahu, na kamba+ zake za hema, kwa ajili ya utumishi wake wote.
27 Na za Kohathi zilikuwa familia ya Waamramu na familia ya Waishari na familia ya Wahebroni na familia ya Wauzieli. Hizo ndizo zilizokuwa familia za Wakohathi.+ 28 Kati ya hesabu ya wanaume kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 8,600, waliokuwa wakitimiza wajibu wa mahali patakatifu.+ 29 Familia za wana wa Kohathi zilikuwa zimepiga kambi upande wa maskani kuelekea kusini.+ 30 Na mkuu wa nyumba ya ukoo wa upande wa baba kwa ajili ya familia za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.+ 31 Na wajibu+ wao ulikuwa ni lile Sanduku+ na meza+ na kinara cha taa+ na madhabahu+ na vyombo+ vya mahali patakatifu ambavyo wangevitumia kuhudumu na kisitiri,+ na utumishi wake wote.
32 Na mkuu wa wakuu wa wana wa Lawi alikuwa Eleazari+ mwana wa Haruni kuhani, aliyekuwa mwangalizi wa wale waliokuwa wakitimiza wajibu wa mahali patakatifu.
33 Za Merari zilikuwa familia ya Wamali+ na familia ya Wamushi.+ Hizo ndizo zilizokuwa familia za Merari.+ 34 Na watu wao walioandikishwa kwa hesabu ya wanaume wote kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 6,200.+ 35 Na mkuu wa nyumba ya ukoo wa upande wa baba kwa ajili ya familia za Merari alikuwa Zurieli mwana wa Abihaili. Walipiga kambi upande wa maskani kuelekea kaskazini.+ 36 Na uangalizi ambao wana wa Merari walipewa uwe wajibu wao ulikuwa kusimamia viunzi+ vya maskani na fito+ zake na nguzo+ zake na vikalio vyake na vyombo+ vyake vyote na utumishi+ wake wote, 37 na nguzo+ za ua pande zote na vikalio+ vyake na vigingi vya hema na kamba zake za hema.
38 Na wale wanaopiga kambi mbele ya maskani kuelekea mashariki, mbele ya hema la mkutano kuelekea mapambazuko ya jua, walikuwa Musa na Haruni na wanawe, wale waliokuwa wakitimiza wajibu wa patakatifu,+ kama wajibu wa wana wa Israeli. Na mgeni yeyote ambaye angekaribia angeuawa.+
39 Watu wote walioandikishwa wa Walawi ambao Musa na Haruni waliandikisha kwa agizo la Yehova kulingana na familia zao, wanaume wote kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi, walikuwa 22,000.
40 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Waandikishe wanaume wote wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi,+ na uchukue hesabu ya majina yao. 41 Nawe utawachukua Walawi kwa ajili yangu—mimi ni Yehova—mahali pa wazaliwa wote wa kwanza katikati ya wana wa Israeli,+ na wanyama wa kufugwa wa Walawi mahali pa wazaliwa wote wa kwanza kati ya wanyama wa kufugwa wa wana wa Israeli.”+ 42 Na Musa akaanza, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru, kuandikisha wazaliwa wote wa kwanza katikati ya wana wa Israeli. 43 Na wanaume wote wazaliwa wa kwanza kulingana na hesabu ya majina kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi kati ya watu wao walioandikishwa wakawa 22,273.
44 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 45 “Chukua Walawi mahali pa wazaliwa wote wa kwanza kati ya wana wa Israeli, na wanyama wa kufugwa wa Walawi mahali pa wanyama wao wa kufugwa; na Walawi watakuwa wangu.+ Mimi ni Yehova. 46 Na kama bei ya fidia+ ya wale 273 kutoka kwa wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli, wale wanaowazidi Walawi,+ 47 utachukua shekeli 5 kwa ajili ya kila mtu.+ Katika shekeli ya mahali patakatifu utaichukua. Shekeli moja ni gera 20.+ 48 Nawe utawapa Haruni na wanawe pesa hizo zikiwa bei ya fidia ya wale wanaowazidi.” 49 Kwa hiyo Musa akachukua pesa za ukombozi kutoka kwa wale waliozidi bei ya fidia ya Walawi. 50 Alichukua pesa hizo kutoka kwa wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli, shekeli 1,365, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 51 Kisha Musa akawapa Haruni na wanawe hizo pesa za bei ya fidia kulingana na amri ya Yehova, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
4 Yehova sasa akasema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 2 “Wana wa Kohathi+ kati ya wana wa Lawi watahesabiwa, kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao, 3 kuanzia umri wa miaka 30+ na zaidi mpaka miaka 50,+ wale wote wanaoingia katika kikundi+ cha utumishi ili kufanya kazi katika hema la mkutano.
4 “Huu ndio utumishi wa wana wa Kohathi katika hema la mkutano.+ Ni kitu kitakatifu zaidi: 5 Na Haruni na wanawe wataingia ndani wakati ambapo kambi inaondoka, nao watalishusha pazia lenye kusitiri+ na kulifunika sanduku+ la ushuhuda kwa pazia hilo. 6 Nao wataweka kifuniko cha ngozi za sili+ juu yake na kutandaza kitambaa kizima cha uzi wa bluu juu na kutia miti yake.+
7 “Nao watatandika kitambaa cha bluu juu ya meza+ ya mkate wa wonyesho, nao wataweka juu yake sahani+ na vikombe na mabakuli+ na mitungi ya toleo la kinywaji; na ule mkate+ wa daima utakaa juu yake. 8 Nao watatandika kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili+ juu yake, nao watakifunika kwa kifuniko cha ngozi za sili+ na kuitia miti+ yake. 9 Nao watachukua kitambaa cha bluu na kukifunika kinara cha taa+ cha mwanga na taa+ zake na mikasi+ yake ya tambi na vyetezo+ vyake na vyombo+ vyake vyote vya mafuta wanavyotumia kwa ukawaida kukihudumia. 10 Nao watakiweka pamoja na vyombo vyake vyote katika kifuniko cha ngozi za sili+ na kukiweka juu ya ufito. 11 Na juu ya madhabahu ya dhahabu+ watatandika kitambaa cha bluu, nao wataifunika kwa kifuniko cha ngozi za sili+ na kuiitia miti+ yake. 12 Nao watachukua vyombo+ vyote vya huduma ambavyo wanavitumia kwa ukawaida kuhudumu katika mahali patakatifu, nao watavitia katika kitambaa cha bluu na kuvifunika kwa kifuniko cha ngozi za sili+ na kuviweka juu ya ufito.
13 “Nao watayaondoa majivu yenye mafuta ya madhabahu+ na kutandika kitambaa cha sufu kilichotiwa rangi ya zambarau juu yake. 14 Nao watatia juu yake vyombo vyake vyote ambavyo wao huvitumia kuihudumia kwa ukawaida, vyetezo, nyuma na sepetu na mabakuli, vyombo vyote vya madhabahu;+ nao watatandika juu yake kifuniko cha ngozi za sili na kuitia miti+ yake.
15 “Naye Haruni na wanawe watamaliza kufunika mahali patakatifu+ na vyombo+ vyote vya mahali patakatifu wakati kambi inapoondoka, kisha wana wa Kohathi watakuja ili kuvichukua,+ lakini hawapaswi kugusa+ mahali patakatifu wasije wakafa. Vitu hivyo ni mzigo wa wana wa Kohathi katika hema la mkutano.+
16 “Na uangalizi+ wa Eleazari mwana wa Haruni kuhani utakuwa juu ya mafuta+ ya mwanga na uvumba uliotiwa manukato+ na lile toleo la nafaka la daima+ na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta,+ uangalizi wa maskani yote na vyote vilivyo ndani yake, yaani, mahali patakatifu na vyombo vyake.”
17 Na Yehova akazidi kusema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 18 “Usiache familia ya Wakohathi+ ikatiliwe mbali kutoka kati ya Walawi. 19 Lakini wafanyie jambo hili ili waendelee kuishi wala wasife kwa sababu ya kukaribia kwao vitu vilivyo vitakatifu zaidi.+ Haruni na wanawe wataingia ndani, nao watawapa mgawo kila mmoja wao kwenye utumishi wake na kwenye mzigo wake. 20 Nao hawapaswi kuingia ndani ili kuviona vitu vitakatifu hata kwa kitambo kidogo, na iwe lazima wafe.”+
21 Kisha Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 22 “Wana wa Gershoni+ watahesabiwa, naam, wao kulingana na nyumba ya baba zao kulingana na familia zao. 23 Kuanzia umri wa miaka 30 na zaidi mpaka miaka 50 utawaandikisha,+ wote wanaokuja kuingia katika kikundi cha utumishi ili kutoa utumishi katika hema la mkutano. 24 Huu ndio utumishi wa familia za Wagershoni unaohusu kutumikia na unaohusu uchukuzi.+ 25 Nao watachukua vitambaa+ vya mahema ya maskani na hema la mkutano,+ kifuniko+ chake na kifuniko cha ngozi ya sili+ kilicho juu yake, na kile kisitiri+ cha mwingilio wa hema la mkutano, 26 na mapazia+ ya ua na kisitiri+ cha mwingilio wa lango la ua unaozunguka maskani na madhabahu pande zote, na kamba zake za hema na vyombo vyake vyote vya utumishi, na vitu vyote vinavyotumiwa kwa ukawaida kufanya kazi. Ndivyo watakavyotumikia. 27 Kwa agizo la Haruni na wanawe+ utumishi wote wa wana wa Wagershoni+ utafanywa kuhusiana na mizigo yao yote na utumishi wao wote, nanyi mtawapa migawo ya mizigo yao yote kulingana na wajibu. 28 Huo ndio utumishi wa familia za wana wa Wagershoni+ katika hema la mkutano, na utumishi wao wa lazima uko chini ya mkono wa Ithamari+ mwana wa Haruni kuhani.
29 “Nao wana wa Merari,+ utawaandikisha kulingana na familia zao katika nyumba ya baba zao. 30 Kuanzia umri wa miaka 30 na zaidi mpaka miaka 50 utawaandikisha, wote wanaoingia katika kikundi cha utumishi ili kutoa utumishi wa hema la mkutano.+ 31 Na huu ndio wajibu wao, mzigo wao,+ kulingana na utumishi wao wote katika hema la mkutano: vile viunzi vya mbao+ vya maskani na fito+ zake na nguzo+ zake na vikalio+ vyake, 32 na nguzo+ za ua kuzunguka pande zote na vikalio+ vyake na vigingi+ vyake vya hema na kamba zake za hema pamoja na vifaa vyake vyote na utumishi wake wote. Na kulingana na majina yao utawapa mgawo wa vifaa ambao ni wajibu wao, uwe mzigo wao.+ 33 Huu ndio utumishi wa familia za wana wa Merari+ kulingana na utumishi wao wote katika hema la mkutano, chini ya mkono wa Ithamari mwana wa Haruni kuhani.”+
34 Na Musa na Haruni na wakuu+ wa kusanyiko wakawaandikisha wana wa Wakohathi+ kulingana na familia zao na kulingana na nyumba ya baba zao, 35 kuanzia umri wa miaka 30+ na zaidi mpaka miaka 50,+ wote walioingia katika kikundi cha utumishi kwa ajili ya utumishi katika hema la mkutano.+ 36 Na walioandikishwa kati yao kulingana na familia zao wakawa 2,750.+ 37 Hao ndio walioandikishwa+ wa familia za Wakohathi, wale wote wanaotumikia katika hema la mkutano, ambao Musa na Haruni waliwaandikisha kwa agizo la Yehova kupitia Musa.
38 Nao walioandikishwa kati ya wana wa Gershoni+ kulingana na familia zao na kulingana na nyumba ya baba zao, 39 kuanzia umri wa miaka 30 na zaidi mpaka miaka 50, wote ambao waliingia katika kikundi cha utumishi kwa ajili ya utumishi katika hema la mkutano,+ 40 wale walioandikishwa kati yao kulingana na familia zao, kulingana na nyumba ya baba zao, wakawa 2,630.+ 41 Hao ndio walioandikishwa kati ya familia za wana wa Gershoni, wale wote wanaotumikia katika hema la mkutano, ambao Musa na Haruni waliandikisha kwa agizo la Yehova.+
42 Nao walioandikishwa wa familia za wana wa Merari kulingana na familia zao, kulingana na nyumba ya baba zao, 43 kuanzia umri wa miaka 30 na zaidi mpaka miaka 50, wote wanaoingia katika kikundi cha utumishi kwa ajili ya utumishi wa hema la mkutano,+ 44 wale walioandikishwa kati yao kulingana na familia zao wakawa 3,200.+ 45 Hao ndio walioandikishwa kati ya familia za wana wa Merari, ambao Musa na Haruni waliandikisha kwa agizo la Yehova kupitia Musa.+
46 Wote walioandikishwa ambao Musa na Haruni na wakuu wa Israeli waliwaandikisha kuwa Walawi kulingana na familia zao na kulingana na nyumba ya baba zao, 47 kuanzia umri wa miaka 30 na zaidi mpaka miaka 50,+ wote wanaokuja kutoa utumishi mgumu na utumishi wa kubeba mizigo katika hema la mkutano,+ 48 walioandikishwa kati yao wakawa 8,580.+ 49 Kwa agizo la Yehova waliandikishwa kupitia Musa, kila mmoja kulingana na utumishi wake na mzigo wake; nao waliandikishwa kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.+
5 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Amuru wana wa Israeli kwamba wamtoe nje ya kambi kila mtu mwenye ukoma+ na kila mtu mwenye mtiririko unaotoka+ na kila mtu asiye safi kutokana na nafsi iliyokufa.+ 3 Awe mwanamume au mwanamke mnapaswa kumtoa nje.+ Mnapaswa kumtoa nje ya kambi, ili wasije wakachafua+ kambi za wale ambao ninakaa katikati yao.”+ 4 Nao wana wa Israeli wakafanya hivyo, naam, wakawatoa nje ya kambi. Kama vile Yehova alivyokuwa amemwambia Musa, ndivyo wana wa Israeli walivyofanya.
5 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 6 “Sema na wana wa Israeli, ‘Kwa habari ya mwanamume au mwanamke, ikiwa watatenda yoyote kati ya dhambi za wanadamu kwa kufanya tendo la kumkosea uaminifu Yehova, nafsi hiyo pia imekuwa na hatia.+ 7 Nao lazima waungame+ dhambi yao ambayo wametenda, naye lazima alipie hatia yake kwa ukamili wake, pia aongeze sehemu yake ya tano juu yake,+ naye lazima ampe yule ambaye alimtendea kosa. 8 Lakini ikiwa huyo aliyetendewa kosa hana mtu wa jamaa ya karibu wa kulipwa yale malipo ya hatia, yale malipo ya hatia yanayorudishwa kwa Yehova yatakuwa ya kuhani, isipokuwa yule kondoo-dume wa upatanisho ambaye atamtumia kufanya upatanisho kwa ajili yake.+
9 “‘Na kila mchango+ wa vitu vyote vitakatifu+ vya wana wa Israeli, ambavyo watapeleka kwa kuhani, vitakuwa vyake.+ 10 Na vitu vitakatifu vya kila mmoja vitakuwa vyake mwenyewe. Chochote kile ambacho mtu atampa kuhani, hicho kitakuwa chake.’”
11 Na Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 12 “Sema na wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Ikiwa mke wa mtu yeyote atageuka kando, yaani, kwa kufanya tendo la kumkosea uaminifu,+ 13 na kwa kweli mwanamume mwingine alale naye na kutokwa na shahawa,+ nalo limefichwa machoni pa mume wake+ nalo halijagunduliwa, naye mwanamke huyo amejitia unajisi lakini hakuna shahidi juu yake, naye hajakamatwa; 14 na roho ya wivu+ imempata mume wake, naye ameutilia shaka uaminifu wa mke wake, na mwanamke huyo kwa kweli amejitia unajisi, au roho ya wivu imempata mume wake, naye ameutilia shaka uaminifu wa mke wake, lakini yeye kwa kweli hajajitia unajisi; 15 basi mwanamume huyo lazima amlete mke wake kwa kuhani+ na kuleta toleo lake pamoja naye, sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Hatamimina mafuta juu yake wala kuweka ubani+ juu yake, kwa sababu ni toleo la nafaka la wivu, toleo la ukumbusho linaloleta kosa kwenye kumbukumbu.
16 “‘Naye kuhani lazima amlete huyo mwanamke mbele na kumfanya asimame mbele za Yehova.+ 17 Naye kuhani atachukua maji matakatifu katika chombo cha udongo, naye kuhani atachukua sehemu ya mavumbi yaliyo kwenye sakafu ya maskani, naye atayatia katika maji. 18 Naye kuhani atamsimamisha mwanamke huyo mbele za Yehova na kufungua nywele za kichwa cha mwanamke huyo na kutia kwenye viganja vya mkono wake lile toleo la nafaka la ukumbusho, yaani, toleo la nafaka la wivu,+ na katika mkono wa kuhani kutakuwa na maji machungu yanayoleta laana.+
19 “‘Naye kuhani lazima amwapishe, naye atamwambia mwanamke huyo: “Ikiwa hakuna mwanamume yeyote ambaye amelala nawe na ikiwa hujageuka kando katika uchafu wowote huku ukiwa chini ya mume wako,+ uwe huru na madhara ya maji haya machungu yanayoleta laana. 20 Lakini wewe, ikiwa umegeuka kando ukiwa chini ya mume wako+ na ikiwa umejitia unajisi na mwanamume fulani ametia ndani yako shahawa zake zilizomtoka,+ isipokuwa mume wako,—” 21 Kuhani huyo sasa atamwapisha mwanamke huyo kwa kiapo kinachohusisha kulaani,+ naye kuhani atamwambia mwanamke huyo: “Yehova na akuweke kuwa laana na kiapo katikati ya watu wako, kwa Yehova kulifanya paja+ lako lianguke, na tumbo lako livimbe. 22 Na maji haya yanayoleta laana yataingia kwenye matumbo yako na kulifanya tumbo lako livimbe na paja lako lianguke.” Naye mwanamke huyo atasema: “Amina! Amina!”
23 “‘Naye kuhani ataandika laana hizo katika kitabu+ na kuzifutilia+ mbali kwenye yale maji machungu. 24 Naye atamnywesha yule mwanamke maji hayo machungu yanayoleta laana,+ nayo maji yanayoleta laana yataingia ndani yake kama kitu kichungu. 25 Na kuhani atachukua toleo la nafaka+ la wivu kutoka katika mkono wa mwanamke huyo na kutikisa toleo hilo la nafaka huku na huku mbele za Yehova, naye atalileta karibu na madhabahu. 26 Naye kuhani atachukua sehemu ya toleo la nafaka iwe kumbukumbu+ yake naye ataifukiza juu ya madhabahu, kisha atamnywesha yule mwanamke maji hayo. 27 Baada ya kumnywesha maji hayo, itatukia pia kwamba ikiwa amejitia unajisi kwa kufanya tendo la kukosa uaminifu kwa mume wake,+ ndipo maji yanayoleta laana yataingia ndani yake kama kitu kichungu, nalo tumbo lake litavimba, nalo paja lake litaanguka, na mwanamke huyo atakuwa laana katikati ya watu wake.+ 28 Hata hivyo, ikiwa mwanamke huyo hajajitia unajisi bali yeye ni safi, basi atakuwa huru asipate adhabu hiyo;+ naye atatiwa mimba kwa shahawa.
29 “‘Hiyo ndiyo sheria juu ya wivu,+ mahali ambapo mwanamke anageuka kando+ huku akiwa chini ya mume wake,+ naye anajitia unajisi, 30 au katika kisa cha mwanamume anayepata roho ya wivu, naye amtilie shaka mke wake juu ya uaminifu wake; naye atamsimamisha mke wake mbele za Yehova, naye kuhani atatimiza sheria yote hiyo kumwelekea. 31 Naye mwanamume huyo atakuwa hana hatia ya kosa, bali mke huyo atajibu kwa kosa lake.’”
6 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli nawe utawaambia, ‘Mwanamume au mwanamke akiweka nadhiri ya pekee ya kuishi akiwa Mnadhiri+ kwa Yehova, 3 anapaswa kujiepusha na divai na kileo. Hatakunywa siki ya divai au siki ya kileo,+ wala kunywa maji yoyote yanayotengenezwa kutokana na zabibu, wala kula zabibu zikiwa mbichi au zikiwa zimekauka. 4 Siku zote za Unadhiri wake hatakula kitu chochote kinachotengenezwa kutokana na mzabibu wa divai, kuanzia zabibu ambazo hazijaiva mpaka maganda.
5 “‘Siku zote za nadhiri ya Unadhiri wake wembe wowote usipite juu ya kichwa chake;+ mpaka siku ambazo ametengwa kwa ajili ya Yehova zitimie, atakuwa mtakatifu kwa kuacha mashungi+ ya nywele za kichwa chake yakue. 6 Siku zote za kutengwa kwake kwa ajili ya Yehova asikaribie nafsi yoyote iliyokufa.+ 7 Hata kwa ajili ya baba yake au mama yake au ndugu yake au dada yake asijitie unajisi watakapokufa,+ kwa sababu ishara ya Unadhiri wake kwa Mungu wake iko juu ya kichwa chake.
8 “‘Siku zote za Unadhiri wake atakuwa mtakatifu kwa Yehova. 9 Lakini ikiwa yeyote anayekufa atakufa ghafula kando yake+ hivi kwamba awe amekitia unajisi kichwa cha Unadhiri wake, basi lazima anyoe+ kichwa chake katika siku ya kuthibitisha utakaso wake. Katika siku ya saba anapaswa kukinyoa. 10 Na katika siku ya nane atamletea kuhani njiwa-tetere wawili au hua wawili wachanga kwenye mwingilio wa hema la mkutano.+ 11 Naye kuhani atamtoa mmoja kama toleo la dhambi+ na yule mwingine kama toleo la kuteketezwa+ na kufanya upatanisho kwa ajili yake, kwa kuwa ametenda dhambi kwa sababu ya ile nafsi iliyokufa. Ndipo atakitakasa kichwa chake siku hiyo. 12 Naye ataishi kama Mnadhiri+ kwa Yehova kwa siku za Unadhiri wake, naye ataleta mwana-kondoo dume aliye katika mwaka wake wa kwanza awe toleo la hatia;+ nazo siku zile za kwanza hazitahesabiwa kwa sababu aliunajisi Unadhiri wake.
13 “‘Sasa hii ndiyo sheria kumhusu Mnadhiri: Katika siku ambayo siku za Unadhiri wake zitatimia,+ ataletwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano. 14 Naye atamtolea Yehova toleo lake, kondoo-dume mmoja asiye na kasoro, aliye katika mwaka wake wa kwanza awe toleo la kuteketezwa+ na mwana-kondoo jike asiye na kasoro, aliye katika mwaka wake wa kwanza awe toleo la dhambi+ na kondoo-dume mmoja asiye na kasoro awe dhabihu ya ushirika,+ 15 na kikapu cha keki za mviringo+ zisizo na chachu, za unga laini, zilizotiwa mafuta,+ na mikate myembamba iliyotiwa mafuta,+ na toleo lake la nafaka+ na matoleo yake ya kinywaji.+ 16 Na kuhani atayatoa mbele za Yehova na kutoa toleo lake la dhambi na toleo lake la kuteketezwa.+ 17 Naye atamtolea Yehova yule kondoo-dume akiwa dhabihu ya ushirika+ pamoja na kile kikapu cha keki zisizo na chachu; naye kuhani atatoa toleo lake la nafaka+ pamoja na toleo lake la kinywaji.
18 “‘Na huyo Mnadhiri atanyoa+ kichwa chake cha Unadhiri wake kwenye mwingilio wa hema la mkutano, naye atachukua nywele za kichwa cha Unadhiri wake na kuzitia katika moto ulio chini ya dhabihu ya ushirika. 19 Naye kuhani atachukua bega lililotokoswa+ kutoka kwa yule kondoo-dume na keki moja ya mviringo isiyo na chachu kutoka kwenye kile kikapu, na mkate mwembamba+ mmoja usio na chachu, na kuvitia mikononi mwa huyo Mnadhiri baada ya ishara yake ya Unadhiri kunyolewa. 20 Naye kuhani atavitikisa huku na huku viwe toleo la kutikisa mbele za Yehova.+ Ni kitu kitakatifu kwa kuhani huyo, pamoja na kidari+ cha lile toleo la kutikisa na mguu wa mchango.+ Na baadaye Mnadhiri huyo anaweza kunywa divai.+
21 “‘Hiyo ndiyo sheria juu ya Mnadhiri+ ambaye ataweka nadhiri—toleo lake kwa Yehova juu ya Unadhiri wake, mbali na vile anavyoweza kupata. Kulingana na nadhiri yake atakayoweka, ndivyo anavyopaswa kufanya kwa sababu ya sheria ya Unadhiri wake.’”
22 Kisha Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 23 “Sema na Haruni na wanawe, na kuwaambia, ‘Hivi ndivyo mtakavyowabariki+ wana wa Israeli, na kuwaambia:
24 “Yehova na akubariki+ na kukutunza.+
25 Yehova na aufanye uso wake ung’ae kukuelekea,+ na akupe kibali.+
26 Yehova na ainue uso wake kukuelekea+ na kukupa amani.”’+
27 Nao wataweka jina+ langu juu ya wana wa Israeli, ili mimi mwenyewe nipate kuwabariki wao.”+
7 Sasa ikawa kwamba katika siku ambayo Musa alimaliza kuisimamisha maskani,+ aliitia mafuta+ na kuitakasa pamoja na vyombo vyake vyote na madhabahu na vyombo vyake vyote. Hivyo akavitia mafuta na kuvitakasa.+ 2 Ndipo wakuu wa Israeli,+ vichwa vya nyumba ya upande wa baba zao, wakatoa toleo,+ wao wakiwa wakuu wa makabila na wakisimamia wale walioandikishwa, 3 nao wakaleta toleo lao mbele za Yehova, magari sita yaliyofunikwa na ng’ombe kumi na wawili, gari moja kwa ajili ya wakuu wawili na ng’ombe-dume mmoja kwa ajili ya kila mmoja; nao wakatoa toleo hilo mbele ya maskani. 4 Ndipo Yehova akamwambia Musa: 5 “Kubali vitu hivyo kutoka kwao, kwa maana vitatumika kuendeleza utumishi wa hema la mkutano, nawe utawapa Walawi vitu hivyo, kila mmoja kulingana na utumishi wake mwenyewe.”
6 Basi Musa akayakubali hayo magari na wale ng’ombe, akawapa Walawi. 7 Magari mawili na ng’ombe wanne akawapa wana wa Gershoni kulingana na utumishi wao,+ 8 na magari manne na ng’ombe wanane kwa wana wa Merari kulingana na utumishi wao,+ chini ya mkono wa Ithamari mwana wa Haruni kuhani.+ 9 Lakini wana wa Kohathi hakuwapa chochote, kwa sababu utumishi wa mahali patakatifu ulikuwa juu yao.+ Walifanya uchukuzi wao kwa mabega yao.+
10 Sasa wakuu wakatoa toleo lao wakati wa kuzinduliwa+ kwa madhabahu katika siku ya kutiwa kwake mafuta, nao wakuu wakatoa toleo lao mbele ya madhabahu. 11 Basi Yehova akasema na Musa: “Mkuu mmoja katika siku moja na mkuu mwingine katika siku nyingine ndivyo watakavyotoa toleo lao kwa ajili ya kuzinduliwa kwa madhabahu.”+
12 Basi yule aliyetoa toleo lake katika siku ya kwanza akawa Nashoni+ mwana wa Aminadabu wa kabila la Yuda. 13 Nalo toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu,+ vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 14 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba;+ 15 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 16 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 17 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Nashoni mwana wa Aminadabu.+
18 Katika siku ya pili Nethaneli+ mwana wa Zuari, mkuu wa Isakari, akatoa toleo. 19 Naye akatoa toleo lake la sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 20 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba; 21 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 22 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 23 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Nethaneli mwana wa Zuari.
24 Katika siku ya tatu kulikuwa na mkuu wa wana wa Zabuloni, Eliabu+ mwana wa Heloni. 25 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka; 26 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba; 27 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 28 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 29 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Eliabu mwana wa Heloni.+
30 Katika siku ya nne kulikuwa na mkuu wa wana wa Rubeni, Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 31 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 32 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba; 33 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 34 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 35 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Elisuri mwana wa Shedeuri.+
36 Katika siku ya tano kulikuwa na mkuu wa wana wa Simeoni, Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 37 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 38 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba; 39 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 40 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 41 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Shelumieli mwana wa Zurishadai.+
42 Katika siku ya sita kulikuwa na mkuu wa wana wa Gadi, Eliasafu+ mwana wa Deueli. 43 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 44 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba;+ 45 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 46 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 47 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Eliasafu mwana wa Deueli.+
48 Katika siku ya saba kulikuwa na mkuu wa wana wa Efraimu, Elishama+ mwana wa Amihudi. 49 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 50 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba; 51 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 52 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 53 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Elishama mwana wa Amihudi.+
54 Katika siku ya nane kulikuwa na mkuu wa wana wa Manase, Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 55 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 56 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba;+ 57 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 58 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 59 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Gamalieli mwana wa Pedazuri.+
60 Katika siku ya tisa kulikuwa na mkuu+ wa wana wa Benyamini, Abidani+ mwana wa Gidioni. 61 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 62 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba; 63 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 64 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 65 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Abidani mwana wa Gidioni.+
66 Katika siku ya kumi kulikuwa na mkuu wa wana wa Dani, Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 67 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 68 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba; 69 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 70 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 71 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Ahiezeri mwana wa Amishadai.+
72 Katika siku ya kumi na moja kulikuwa na mkuu wa wana wa Asheri, Pagieli+ mwana wa Okrani. 73 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 74 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba;+ 75 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 76 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 77 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Pagieli mwana wa Okrani.+
78 Katika siku ya kumi na mbili kulikuwa na mkuu wa wana wa Naftali, Ahira+ mwana wa Enani. 79 Toleo lake lilikuwa sahani moja ya fedha, uzito wake ukiwa shekeli 130, bakuli moja la fedha la shekeli 70 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vyote viwili vikiwa vimejaa unga laini uliotiwa mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 80 kikombe kimoja cha dhahabu cha shekeli kumi, kilichojaa uvumba;+ 81 ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, mwana-kondoo dume mmoja katika mwaka wake wa kwanza, kwa ajili ya toleo la kuteketezwa;+ 82 mwana-mbuzi mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 83 na kwa ajili ya toleo la ushirika+ ng’ombe wawili, kondoo-dume watano, mbuzi-dume watano, wana-kondoo dume watano kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la Ahira mwana wa Enani.+
84 Hili ndilo lililokuwa toleo la kuzindua+ madhabahu katika siku ya kutiwa kwake mafuta, kwa upande wa wakuu+ wa Israeli: sahani 12 za fedha, mabakuli+ 12 ya fedha, vikombe 12 vya dhahabu; 85 shekeli 130 kwa kila sahani ya fedha, na shekeli 70 kwa kila bakuli, na fedha yote ya vyombo hivyo ikiwa shekeli 2,400 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu;+ 86 vile vikombe+ 12 vya dhahabu vilivyojaa uvumba vikiwa shekeli 10 kila kikombe kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, dhahabu yote ya vikombe ikiwa shekeli 120; 87 ng’ombe wote kwa ajili ya toleo la kuteketezwa+ wakiwa ng’ombe-dume 12, kondoo-dume 12, wana-kondoo dume 12 kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja na matoleo yao ya nafaka,+ na wana-mbuzi 12 kwa ajili ya toleo la dhambi;+ 88 na ng’ombe wote wa dhabihu ya ushirika+ walikuwa ng’ombe-dume 24, kondoo-dume 60, mbuzi-dume 60, wana-kondoo dume 60 kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hilo ndilo lililokuwa toleo la kuzindua+ madhabahu baada ya kutiwa kwake mafuta.+
89 Sasa wakati wowote ambapo Musa aliingia ndani ya hema la mkutano ili kusema naye,+ ndipo aliposikia sauti ikizungumza naye toka juu ya kifuniko+ kilichokuwa juu ya sanduku la ushuhuda, kutoka katikati ya wale makerubi+ wawili; naye akasema naye.
8 Na Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na Haruni, nawe utamwambia, ‘Wakati wowote unapowasha taa, zile taa saba zitaangaza eneo lililo mbele ya kinara.’”+ 3 Naye Haruni akaanza kufanya hivyo. Akawasha taa zake kwa ajili ya eneo lililo mbele ya kinara cha taa,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa. 4 Sasa huu ndio uliokuwa ufundi wa kinara cha taa. Kilikuwa cha dhahabu iliyofuliwa. Kuanzia sehemu zake za kando na mpaka kwenye maua yake kilikuwa kimefuliwa.+ Kulingana na maono+ ambayo Yehova alikuwa amemwonyesha Musa, ndivyo alivyokuwa amekitengeneza kinara cha taa.
5 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 6 “Wachukue Walawi kutoka kati ya wana wa Israeli, nawe uwatakase.+ 7 Na hivi ndivyo unavyopaswa kuwafanyia ili kuwatakasa: Tapanya maji ya kutakasa dhambi juu yao,+ na wapitishe wembe juu ya mwili+ wao wote nao wayafue mavazi+ yao na kujitakasa.+ 8 Kisha wachukue ng’ombe-dume+ mchanga na toleo lake la nafaka+ la unga laini uliotiwa mafuta, nawe utachukua ng’ombe-dume mwingine mchanga kwa ajili ya toleo la dhambi.+ 9 Nawe utawasimamisha Walawi mbele ya hema la mkutano na kukutanisha kusanyiko lote la wana wa Israeli.+ 10 Nawe utawasimamisha Walawi mbele za Yehova, nao wana wa Israeli wataweka+ mikono yao juu ya Walawi.+ 11 Na Haruni atawasogeza Walawi huku na huku mbele za Yehova kama toleo la kutikisa+ kutoka kwa wana wa Israeli, nao wataendeleza utumishi wa Yehova.+
12 “Kisha Walawi wataweka mikono yao juu ya vichwa vya wale ng’ombe-dume.+ Baada ya jambo hilo, mtoe mmoja awe toleo la dhambi na yule mwingine awe toleo la kuteketezwa kwa Yehova ili kufanya upatanisho+ kwa ajili ya Walawi. 13 Nawe utawasimamisha Walawi mbele ya Haruni na wanawe na kuwasogeza huku na huku kama toleo la kutikisa kwa Yehova. 14 Nawe utawatenga Walawi kutoka katikati ya wana wa Israeli, nao Walawi watakuwa wangu.+ 15 Na baadaye Walawi wataingia ndani ili kutumikia katika hema la mkutano.+ Kwa hiyo utawatakasa na kuwasogeza huku na huku kama toleo la kutikisa.+ 16 Kwa maana wao ni watu waliokabidhiwa, niliokabidhiwa mimi kati ya wana wa Israeli.+ Badala ya wale wote wanaofungua tumbo la uzazi, wazaliwa wote wa kwanza kati ya wana wa Israeli,+ nitawachukua kwa ajili yangu mwenyewe. 17 Kwa maana kila mzaliwa wa kwanza kati ya wana wa Israeli ni wangu, kati ya mwanadamu na kati ya mnyama.+ Katika siku niliyompiga na kumuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri+ niliwatakasa hao kwa ajili yangu.+ 18 Nami nitawachukua Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza kati ya wana wa Israeli.+ 19 Nami nitamkabidhi Haruni na wanawe hao Walawi wakiwa watu waliokabidhiwa katikati ya wana wa Israeli,+ ili kuendeleza utumishi wa wana wa Israeli katika hema la mkutano+ na kufanya upatanisho kwa ajili ya wana wa Israeli, ili pigo lolote lisitukie katikati ya wana wa Israeli+ kwa sababu wana wa Israeli wanapakaribia mahali patakatifu.”
20 Naye Musa na Haruni na kusanyiko lote la wana wa Israeli wakawafanyia Walawi hivyo. Kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru Musa kuhusu Walawi, hivyo ndivyo wana wa Israeli walivyowafanyia. 21 Basi Walawi wakajitakasa+ na kufua mavazi yao, kisha Haruni akawasogeza huku na huku kama toleo la kutikisa mbele za Yehova.+ Halafu Haruni akafanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.+ 22 Mara tu baada ya jambo hilo Walawi wakaingia ndani ili kuendeleza utumishi wao katika hema la mkutano mbele ya Haruni na wanawe.+ Kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa kuhusu Walawi, ndivyo walivyowafanyia.
23 Sasa Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 24 “Jambo hili linawahusu Walawi: Kuanzia umri wa miaka 25 na zaidi, ataingia katika ushirika katika utumishi wa hema la mkutano. 25 Lakini baada ya umri wa miaka 50 atatoka katika ushirika wa utumishi naye hatatumikia tena. 26 Naye atawahudumia ndugu zake katika hema la mkutano kwa kutimiza wajibu huo, lakini hatatoa utumishi wowote. Utawafanyia Walawi hivyo katika wajibu wao mbalimbali.”+
9 Na Yehova akasema na Musa katika nyika ya Sinai katika mwaka wa pili baada ya kuondoka kwao katika nchi ya Misri, katika mwezi wa kwanza,+ na kumwambia: 2 “Sasa wana wa Israeli watatayarisha dhabihu ya pasaka+ katika wakati wake uliowekwa.+ 3 Katika siku ya kumi na nne ya mwezi huu katikati ya zile jioni mbili+ mtaitayarisha katika wakati wake uliowekwa. Kulingana na sheria zake zote na utaratibu wake wote wa kawaida mtaitayarisha.”+
4 Basi Musa akawaambia wana wa Israeli waitayarishe dhabihu ya pasaka. 5 Basi wakaitayarisha dhabihu ya pasaka katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi huo katikati ya zile jioni mbili, katika nyika ya Sinai. Kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru Musa, ndivyo wana wa Israeli walivyofanya.+
6 Sasa kukawa na watu ambao walikuwa wamekuwa najisi kwa sababu ya nafsi+ ya binadamu hivi kwamba hawakuweza kuitayarisha dhabihu ya pasaka katika siku hiyo. Kwa hiyo wakaenda mbele ya Musa na Haruni katika siku hiyo.+ 7 Kisha watu hao wakamwambia: “Tumekuwa najisi kwa sababu ya nafsi ya binadamu. Kwa nini tuzuiwe kumtolea Yehova toleo+ katika wakati wake uliowekwa katikati ya wana wa Israeli?” 8 Ndipo Musa akawaambia: “Simameni hapo, acheni nisikie jambo ambalo Yehova ataamuru juu yenu.”+
9 Ndipo Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 10 “Sema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Ingawa huenda mtu yeyote kati yenu au wa vizazi vyenu akawa najisi kwa sababu ya nafsi+ au ameenda safari ya mbali, yeye pia lazima atamtayarishia Yehova dhabihu ya pasaka. 11 Katika mwezi wa pili,+ siku ya kumi na nne katikati ya zile jioni mbili, wataitayarisha. Wataila pamoja na keki zisizo na chachu na mboga chungu.+ 12 Hawapaswi kuacha chochote mpaka asubuhi,+ wala hawapaswi kuvunja mfupa wowote ulio ndani yake.+ Wanapaswa kuitayarisha kulingana na sheria yote ya pasaka.+ 13 Lakini wakati ambapo mtu alikuwa safi au hakuwa ameenda safari naye alipuuza kuitayarisha dhabihu ya pasaka, basi lazima nafsi hiyo itakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake,+ kwa sababu haikutoa toleo la Yehova katika wakati wake uliowekwa. Mtu huyo atajibu kwa sababu ya dhambi yake.+
14 “‘Na ikiwa mkaaji mgeni atakuwa akikaa pamoja nanyi akiwa mgeni, yeye pia atamtayarishia Yehova dhabihu ya pasaka.+ Anapaswa kufanya kulingana na sheria ya pasaka na kulingana na utaratibu wake wa kawaida.+ Kutakuwa na sheria moja kwa ajili yenu, kwa ajili ya mkaaji mgeni na kwa ajili ya mwenyeji wa nchi.’”+
15 Sasa katika siku ya kusimamisha maskani+ wingu lilifunika maskani ya hema la Ushuhuda,+ lakini wakati wa jioni kitu kilichoonekana kama moto+ kilikaa juu ya maskani hiyo mpaka asubuhi. 16 Hivyo ndivyo ilivyoendelea daima: Wingu liliifunika wakati wa mchana, na kitu kilichoonekana kama moto wakati wa usiku.+ 17 Na wakati wowote wingu hilo lilipoinuka kutoka juu ya hema, wana wa Israeli walikuwa wakiondoka mara moja baada yake,+ na mahali ambapo wingu hilo lilikuwa likikaa, hapo ndipo wana wa Israeli walipokuwa wakipiga kambi.+ 18 Wana wa Israeli walikuwa wakiondoka kwa agizo la Yehova, na kupiga kambi kwa agizo la Yehova.+ Siku zote ambazo wingu hilo lilikaa juu ya maskani, walikaa katika kambi. 19 Na wakati ambapo wingu hilo lilirefusha kukaa kwake juu ya maskani hiyo siku nyingi, wana wa Israeli pia walishika wajibu wao kwa Yehova kwamba wasiondoke.+ 20 Na nyakati fulani wingu hilo lilikaa siku chache juu ya maskani. Walikuwa wakipiga kambi kwa agizo+ la Yehova, na kuondoka kwa agizo la Yehova. 21 Na nyakati fulani wingu+ hilo lilikaa kuanzia jioni mpaka asubuhi; na wingu hilo liliondoka wakati wa asubuhi, nao wakaondoka. Iwe wingu hilo liliinuka mchana au usiku, wao pia waliondoka.+ 22 Iwe wingu hilo lilirefusha kukaa kwake juu ya maskani kwa siku mbili au mwezi au siku zaidi, wana wa Israeli waliendelea kukaa katika kambi nao hawakuwa wakiondoka, lakini lilipoinuka waliondoka.+ 23 Walipiga kambi kwa agizo la Yehova, na kuondoka kwa agizo la Yehova. Walishika wajibu+ wao kwa Yehova kufuatia agizo la Yehova kupitia Musa.+
10 Na Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Jifanyie tarumbeta+ mbili za fedha. Utazifua, nawe utazitumia kuliita+ kusanyiko na kwa ajili ya kuzivunja kambi. 3 Nao watazipiga zote mbili, nalo kusanyiko lote litakutana nawe kwenye mwingilio wa hema la mkutano.+ 4 Na ikiwa watapiga moja tu, ndipo wakuu wakiwa vichwa vya maelfu ya Israeli watakutana nawe kama ilivyopangwa.+
5 “Nanyi mtapiga mvumo unaopanda na kushuka, nazo kambi za wale wanaopiga kambi upande wa mashariki+ zitaondoka. 6 Nanyi mtapiga mvumo unaopanda na kushuka kwa mara ya pili, nazo kambi za wale wanaopiga kambi upande wa kusini+ zitaondoka. Watapiga mvumo unaopanda na kushuka kila mara moja kati yazo inapoondoka.
7 “Sasa wakati wa kuita kutaniko pamoja, mtapiga,+ lakini hamtapiga mvumo unaopanda na kushuka. 8 Nao wana wa Haruni, kuhani, watazipiga tarumbeta,+ nazo zitakuwa sheria kwa ajili yenu mpaka wakati usio na kipimo katika vizazi vyenu.
9 “Na ikiwa mtaingia vitani katika nchi yenu kupigana na mkandamizaji anayewasumbua ninyi,+ mnapaswa pia kutoa mwito wa vita kwa tarumbeta+ nanyi hakika mtakumbukwa mbele za Yehova Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.+
10 “Na katika siku ya kushangilia+ kwenu na katika majira yenu ya sherehe+ na mwanzoni mwa miezi yenu,+ mtapiga tarumbeta juu ya matoleo yenu ya kuteketezwa+ na dhabihu zenu za ushirika;+ nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Yehova Mungu wenu. Mimi ni Yehova Mungu wenu.”+
11 Sasa ikawa kwamba katika mwaka wa pili, katika mwezi wa pili, siku ya 20 katika mwezi huo,+ lile wingu likainuka kutoka juu ya maskani+ ya Ushuhuda. 12 Nao wana wa Israeli wakaanza kuondoka katika namna ya kuondoka+ kwao kutoka katika nyika ya Sinai, nalo wingu likakaa katika nyika ya Parani.+ 13 Nao wakaanza kuondoka kwa mara ya kwanza, kulingana na agizo la Yehova kupitia Musa.+
14 Kwa hiyo ule mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya wana wa Yuda ndio ulioondoka kwanza kabisa, kwa majeshi yao,+ naye Nashoni+ mwana wa Aminadabu alikuwa juu ya jeshi la mgawanyo huo. 15 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Isakari kulikuwa na Nethaneli+ mwana wa Zuari. 16 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Zabuloni kulikuwa na Eliabu mwana wa Heloni.+
17 Nayo maskani ikashushwa,+ nao wana wa Gershoni+ na wana wa Merari,+ wakiwa wachukuzi wa maskani wakaondoka.
18 Nao ule mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya Rubeni+ ukaondoka, kwa majeshi yao, naye Elisuri+ mwana wa Shedeuri alikuwa juu ya jeshi lake. 19 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Simeoni+ kulikuwa na Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 20 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Gadi kulikuwa na Eliasafu+ mwana wa Deueli.
21 Nao Wakohathi wakiwa wachukuzi wa patakatifu+ wakaondoka, kwa maana watakuwa wameisimamisha maskani kufikia wakati wa kuja kwao.
22 Na ule mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya wana wa Efraimu+ ukaondoka, kwa majeshi yao, naye Elishama+ mwana wa Amihudi alikuwa juu ya jeshi lake. 23 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Manase+ kulikuwa na Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 24 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Benyamini+ kulikuwa na Abidani+ mwana wa Gidioni.
25 Na ule mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya wana wa Dani+ ukaondoka ukifanyiza kikosi cha nyuma cha ulinzi+ kwa ajili ya kambi zote, kwa majeshi yao, naye Ahiezeri+ mwana wa Amishadai alikuwa juu ya jeshi lake. 26 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Asheri+ kulikuwa na Pagieli+ mwana wa Okrani. 27 Na juu ya jeshi la kabila la wana wa Naftali+ kulikuwa na Ahira+ mwana wa Enani. 28 Hivyo ndivyo wana wa Israeli walivyoondoka, kwa majeshi yao, walipokuwa wakiondoka.+
29 Ndipo Musa akamwambia Hobabu mwana wa Reueli+ Mmidiani, baba-mkwe wa Musa: “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Yehova alisema, ‘Nitawapa ninyi.’+ Nenda pamoja nasi, nasi hakika tutakutendea mema,+ kwa sababu Yehova amesema mema juu ya Israeli.”+ 30 Lakini akamwambia: “Sitaenda pamoja nanyi, bali nitaenda katika nchi yangu+ mwenyewe na kwa jamaa zangu.” 31 Basi akasema: “Tafadhali, usituache, kwa sababu unajua vema mahali ambapo tunaweza kupiga kambi nyikani, utakuwa macho yetu. 32 Na itakuwa kwamba ikiwa utaenda pamoja nasi,+ naam, itakuwa kwamba wema ambao Yehova atatutendea, sisi nasi tutakutendea wewe.”
33 Kwa hiyo wakapiga mwendo kutoka mlima wa Yehova+ safari ya siku tatu, nalo sanduku la agano+ la Yehova lilikuwa likipiga mwendo mbele yao kwa safari ya siku tatu ili kutafuta mahali pa kupumzika kwa ajili yao.+ 34 Nalo wingu+ la Yehova lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipokuwa wakipiga mwendo kutoka katika kambi.
35 Na ikawa kwamba Sanduku lilipokuwa likiondoka, Musa alikuwa akisema: “Usimame, Ee Yehova, adui zako na watawanyike;+ na wale wanaokuchukia vikali wakimbie toka mbele zako.”+ 36 Na lilipopumzika, alikuwa akisema: “Urudi, Ee Yehova, kwa makumi ya maelfu ya maelfu ya Israeli.”+
11 Sasa watu wakawa kama watu wenye jambo baya la kulalamika masikioni mwa Yehova.+ Yehova alipolisikia jambo hilo, hasira yake ikawaka, nao moto wa Yehova ukaanza kuwaka juu yao na kuteketeza wengine kati yao katika mwisho wa kambi.+ 2 Watu walipoanza kumlilia Musa, ndipo yeye akamwomba Yehova dua,+ nao moto ukapoa. 3 Na jina la mahali hapo likaitwa Tabera,+ kwa sababu moto wa Yehova ulikuwa umewaka juu yao.
4 Nao umati uliochangamana+ uliokuwa katikati yao ukaonyesha tamaa ya uchoyo,+ na wana wa Israeli pia wakaanza kulia tena na kusema: “Ni nani atakayetupa nyama tule?+ 5 Jinsi tunavyokumbuka samaki tuliokuwa tukila bure huko Misri,+ matango na matikiti-maji na vitunguu vya majani na vitunguu na vitunguu saumu! 6 Lakini sasa nafsi yetu imekauka. Macho yetu hayaoni chochote isipokuwa mana.”+
7 Mana+ ilikuwa kama mbegu ya mgiligilani+ nayo ilionekana kama ulimbo wa bedola.+ 8 Watu walitawanyika na kuiokota+ na kuisaga katika mawe ya kusaga ya mkononi au kuitwanga katika kinu, nao waliitokosa katika vyungu vya kupikia+ au kuifanya kuwa keki za mviringo, nayo ladha yake ilikuwa kama ladha ya keki tamu iliyotiwa mafuta.+ 9 Na umande uliposhuka juu ya kambi usiku, mana ilishuka juu yake.+
10 Na Musa akawasikia watu wakilia katika familia zao, kila mtu kwenye mwingilio wa hema lake. Na hasira ya Yehova ikaanza kuwaka sana,+ na machoni pa Musa lilikuwa jambo baya.+ 11 Ndipo Musa akamwambia Yehova: “Kwa nini umemsababishia mtumishi wako uovu, na kwa nini sijapata kibali machoni pako, kwa kuuweka mzigo wa watu wote hawa juu yangu?+ 12 Je, nilichukua mimba ya watu hawa wote? Je, ni mimi niliyewazaa, hivi kwamba uniambie, ‘Wabebe kifuani pako,+ kama vile mwanamume mlezi anavyombeba mtoto anayenyonya,’+ mpaka katika nchi uliyowaapia mababu zao?+ 13 Nitatoa wapi nyama ya kuwapa watu wote hawa? Kwa maana wananililia daima, na kusema, ‘Tupe nyama, tule!’ 14 Mimi siwezi, mimi peke yangu, kuwabeba watu wote hawa, kwa sababu ni wazito mno kwangu.+ 15 Kwa hiyo ikiwa hivi ndivyo unavyonifanyia, tafadhali niue kabisa,+ ikiwa nimepata kibali machoni pako, wala usiache niutazame msiba wangu.”
16 Basi Yehova akamwambia Musa: “Nikusanyie wanaume 70 kati ya wanaume wazee wa Israeli,+ ambao unajua kwamba ni wanaume wazee wa watu na maofisa wao,+ nawe utawapeleka kwenye hema la mkutano, nao watasimama hapo pamoja nawe. 17 Nami nitashuka chini+ na kusema nawe huko;+ nami nitaondoa sehemu ya roho+ iliyo juu yako na kuiweka juu yao, nao watakusaidia kuubeba mzigo wa watu ili usiubebe, wewe peke yako.+ 18 Nawe utawaambia watu hao, ‘Jitakaseni kwa ajili ya kesho,+ kwa maana hakika mtakula nyama, kwa sababu mmelia masikioni mwa Yehova,+ na kusema: “Ni nani atakayetupa nyama tule, kwa maana mambo yalituendea vema huko Misri?”+ Na Yehova hakika atawapa nyama, nanyi kwa kweli mtakula.+ 19 Mtakula, si siku moja wala siku 2 wala siku 5 wala siku 10 wala siku 20, 20 bali mwezi mzima, mpaka itokee kwenye mianzi ya pua zenu nayo iwe chukizo kwenu,+ kwa sababu tu mlimkataa Yehova, aliye katikati yenu, nanyi mlilia mbele zake, na kusema: “Kwa nini tumetoka Misri?”’”+
21 Ndipo Musa akasema: “Watu nilio katikati yao ni wanaume mia sita elfu+ wanaotembea kwa miguu, hata hivyo wewe—wewe umesema, ‘Nitawapa nyama, nao hakika watakula kwa mwezi mzima’! 22 Je, mifugo na makundi yatachinjwa kwa ajili yao, ili iwatoshe?+ Au samaki wote wa baharini watakamatwa kwa ajili yao, ili iwatoshe?”
23 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Je, mkono wa Yehova ni mfupi?+ Sasa utaona ikiwa ninalosema litatukia kwako au hapana.”+
24 Kisha Musa akatoka na kusema na watu maneno ya Yehova. Naye akakusanya wanaume 70 kutoka kwa wanaume wazee wa watu na kuwasimamisha kulizunguka hema pande zote.+ 25 Ndipo Yehova akashuka katika wingu,+ akasema naye,+ akachukua sehemu ya roho+ iliyokuwa juu yake na kuiweka juu ya kila mmoja wa wale wanaume wazee 70. Na ikawa kwamba mara tu roho hiyo ilipotua juu yao, ndipo wakaanza kutenda kama manabii; lakini hawakufanya hivyo tena.+
26 Sasa kulikuwa na wawili kati ya wanaume hao waliobaki katika kambi. Jina la mmoja wao lilikuwa Eldadi, na jina la yule mwingine lilikuwa Medadi. Nayo roho ikaanza kushuka juu yao, kwa maana walikuwa kati ya wale walioandikwa, lakini hawakuwa wameenda kwenye hema. Basi wakaanza kutenda kama manabii katika kambi. 27 Na mwanamume mmoja kijana akakimbia na kumletea Musa habari na kusema: “Eldadi na Medadi wanatenda kama manabii katika kambi!” 28 Ndipo Yoshua mwana wa Nuni, mhudumu+ wa Musa tangu ujana wake, akajibu na kusema: “Bwana wangu Musa, wazuie!”+ 29 Hata hivyo, Musa akamwambia: “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Hapana, laiti watu wote wa Yehova wangekuwa manabii, kwa sababu Yehova angeiweka roho yake juu yao!”+ 30 Baadaye Musa akaondoka, akaenda kambini, yeye na wale wanaume wazee wa Israeli.
31 Na upepo+ ukavuma kutoka kwa Yehova na kuanza kusukuma kware kutoka baharini+ na kuwaangusha juu ya kambi karibu safari ya siku moja kwenda upande huu na karibu safari ya siku moja kwenda upande ule, pande zote kuizunguka kambi, na karibu kimo cha mikono miwili juu ya uso wa dunia. 32 Ndipo watu wakasimama siku hiyo mchana kutwa na usiku kucha na kesho yake mchana kutwa nao wakaendelea kuokota kware. Yeye aliyeokota kidogo zaidi alikusanya homeri+ kumi, nao wakawatandaza katika eneo kubwa pande zote za kambi kwa ajili yao. 33 Nyama hiyo ilikuwa ingali bado katikati ya meno yao,+ kabla haijatafunwa, wakati hasira ya Yehova ilipowaka+ juu ya watu hao, na Yehova akaanza kuwapiga watu kwa mauaji makubwa sana.+
34 Jina la mahali hapo likaitwa Kibroth-hataava,+ kwa sababu hapo waliwazika watu walioonyesha tamaa ya uchoyo.+ 35 Kutoka Kibroth-hataava watu wakafunga safari kuelekea Haserothi, nao wakaendelea kukaa Haserothi.+
12 Sasa Miriamu na Haruni wakaanza kusema dhidi ya Musa kwa sababu ya mke Mkushi ambaye alikuwa amemchukua, kwa sababu alikuwa amemchukua mke Mkushi.+ 2 Nao wakawa wakisema: “Je, Yehova amesema kupitia Musa tu? Je, hajasema kupitia sisi pia?”+ Na Yehova alikuwa akisikiliza.+ 3 Naye mtu huyu Musa alikuwa mpole+ zaidi kuliko watu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.
4 Ndipo ghafula Yehova akawaambia Musa na Haruni na Miriamu: “Tokeni, ninyi watatu, mwende kwenye hema la mkutano.” Basi hao watatu wakatoka. 5 Kisha Yehova akashuka katika nguzo ya wingu+ na kusimama kwenye mwingilio wa hema na kuwaita Haruni na Miriamu. Nao wakaenda nje. 6 Naye akasema: “Sikieni maneno yangu, tafadhali. Kungalikuwa na nabii kati yenu kwa ajili ya Yehova, ningalijijulisha kwake katika maono.+ Ningalisema naye katika ndoto.+ 7 Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu Musa!+ Amekabidhiwa nyumba yangu yote.+ 8 Mimi husema naye kinywa kwa kinywa,+ na hivyo kumwonyesha, wala si kwa vitendawili;+ naye huona sura ya Yehova.+ Kwa nini, basi, hamkuogopa kusema juu ya mtumishi wangu, juu ya Musa?”+
9 Nayo hasira ya Yehova ikawaka juu yao, naye akaenda zake. 10 Nalo wingu likageuka na kutoka juu ya hema, na, tazama! Miriamu alikuwa amepigwa kwa ukoma mweupe kama theluji.+ Ndipo Haruni akageuka kumwelekea Miriamu, na, tazama! alikuwa amepigwa kwa ukoma.+ 11 Mara moja Haruni akamwambia Musa: “Nakuomba radhi, bwana wangu! Tafadhali, usituhesabie dhambi ambayo tumetenda kwa upumbavu na ambayo tumefanya!+ 12 Tafadhali, usimwache aendelee kuwa kama mtu aliyekufa,+ ambaye nyama yake wakati wa kutoka kwake katika tumbo la uzazi la mama yake imeliwa nusu!” 13 Na Musa akaanza kumlilia Yehova, na kusema: “Ee Mungu, tafadhali! Mponye, tafadhali!”+
14 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Ikiwa baba yake angemtemea mate+ moja kwa moja usoni pake, je, hangefedheheshwa siku saba? Na atengwe+ siku saba nje ya kambi,+ kisha apokewe ndani baadaye.”+ 15 Kwa hiyo Miriamu akatengwa nje ya kambi siku saba,+ nao watu hawakuondoka mpaka Miriamu alipopokewa ndani. 16 Kisha watu wakaondoka Haserothi+ na kupiga kambi katika nyika ya Parani.+
13 Sasa Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Tuma watu kwa ajili yako wapate kuipeleleza nchi ya Kanaani, ninayowapa wana wa Israeli.+ Mtamtuma mtu mmoja kwa ajili ya kila kabila la baba yake, kila mmoja wao mkuu+ kati yao.”
3 Basi Musa akawatuma kutoka katika nyika ya Parani+ kwa agizo la Yehova. Wanaume wote hao walikuwa vichwa vya wana wa Israeli. 4 Na haya ndiyo majina yao: Wa kabila la Rubeni, Shamua mwana wa Zakuri; 5 wa kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori; 6 wa kabila la Yuda, Kalebu+ mwana wa Yefune; 7 wa kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu; 8 wa kabila la Efraimu, Hoshea+ mwana wa Nuni; 9 wa kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu; 10 wa kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi; 11 wa kabila la Yosefu,+ kwa ajili ya kabila la Manase,+ Gadi mwana wa Susi; 12 wa kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali; 13 wa kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli; 14 wa kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofsi; 15 wa kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki. 16 Hayo ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma wakaipeleleze nchi. Na huyo Hoshea mwana wa Nuni, Musa akamwita Yehoshua.+
17 Musa alipokuwa akiwatuma kuipeleleza nchi ya Kanaani, aliwaambia: “Pandeni hapa na kuingia Negebu,+ nanyi mtapanda na kuingia katika eneo lenye milima.+ 18 Nanyi mtaona jinsi nchi ilivyo+ na watu wanaokaa humo, ikiwa wana nguvu au ni dhaifu, ikiwa ni wachache au ni wengi; 19 na jinsi nchi wanayokaa ndani yake ilivyo, iwapo ni nzuri au ni mbaya, na jinsi majiji wanayokaa ndani yake yalivyo, iwapo ni katika kambi au ni katika ngome; 20 Na jinsi nchi ilivyo, iwapo ni nono au imekonda,+ iwapo kuna miti ndani yake au hakuna. Nanyi mjionyeshe kuwa hodari+ na kuchukua baadhi ya matunda ya nchi hiyo.” Sasa siku hizo zilikuwa siku za matunda yaliyoiva ya kwanza ya zabibu.+
21 Basi wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka katika nyika ya Zini+ mpaka Rehobu+ mpaka mahali pa kuingilia pa Hamathi.+ 22 Walipopanda kuingia Negebu,+ ndipo wakafika Hebroni.+ Sasa Ahimani, Sheshai na Talmai,+ wale waliozaliwa kwa Anaki+ walikuwa huko. Hebroni+ lilikuwa limejengwa miaka saba kabla ya Soani+ la Misri. 23 Walipofika kwenye bonde la mto la Eshkoli,+ wakakata chipukizi lenye kishada kimoja cha zabibu.+ Na wawili kati ya wanaume hao wakalichukua kwa ufito, na pia baadhi ya makomamanga+ na baadhi ya tini. 24 Wakapaita mahali hapo bonde la mto la Eshkoli,+ kwa sababu ya kile kishada ambacho wana wa Israeli walikata kutoka huko.
25 Mwishowe, mwishoni mwa siku 40+ wakarudi kutoka kuipeleleza nchi. 26 Basi wakatembea na kuja kwa Musa na Haruni na kusanyiko lote la wana wa Israeli katika nyika ya Parani, huko Kadeshi.+ Nao wakaleta neno kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya nchi. 27 Nao wakampa habari na kusema: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo kwa kweli inatiririka maziwa na asali,+ na haya ni matunda yake.+ 28 Hata hivyo, mambo ya hakika ni kwamba watu wanaokaa katika nchi hiyo ni wenye nguvu, na majiji yenye ngome ni makubwa sana;+ na, pia, wazao wa Anaki tuliwaona huko.+ 29 Waamaleki+ wanakaa katika nchi ya Negebu,+ na Wahiti na Wayebusi+ na Waamori+ wanakaa katika eneo lenye milima, na Wakanaani+ wanakaa kando ya bahari na kando ya ukingo wa Yordani.”
30 Ndipo Kalebu+ akajaribu kuwatuliza watu mbele ya Musa naye akasema: “Na tupande moja kwa moja, nasi tutaimiliki, kwa sababu kwa hakika tunaweza kuishinda.”+ 31 Lakini wale watu waliopanda pamoja naye wakasema: “Hatuwezi kupanda kupigana na watu hao, kwa sababu ni wenye nguvu kuliko sisi.”+ 32 Nao wakazidi kuwaletea wana wa Israeli habari mbaya+ juu ya nchi waliyokuwa wameipeleleza, na kusema: “Ile nchi, tuliyoipitia ili kuipeleleza, ni nchi ambayo inakula wakaaji wake; na watu wote tuliowaona katikati yake ni watu wenye ukubwa usio wa kawaida.+ 33 Na humo tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki,+ waliotoka kwa Wanefili; hivi kwamba sisi tukawa machoni petu wenyewe kama panzi, na machoni pao sisi tukawa vivyo hivyo.”+
14 Ndipo kusanyiko lote likapaaza sauti zao, nao watu wakazidi kupaaza sauti zao na kulia+ usiku kucha. 2 Na wana wote wa Israeli wakaanza kunung’unika juu ya Musa na Haruni,+ na kusanyiko lote likaanza kusema dhidi yao: “Laiti tungalikufa katika nchi ya Misri, au laiti tungalikufa katika nyika hii! 3 Na kwa nini Yehova anatuleta kwenye nchi hii ili tuanguke kwa upanga?+ Wake zetu na watoto wetu wadogo watakuwa nyara.+ Je, si afadhali kwetu turudi Misri?”+ 4 Hata wakaambiana: “Na tuchague kiongozi, nasi turudi Misri!”+
5 Ndipo Musa na Haruni wakaanguka kifudifudi+ mbele ya kutaniko lote la kusanyiko la wana wa Israeli. 6 Na Yoshua mwana wa Nuni+ na Kalebu mwana wa Yefune,+ ambao ni kati ya wale walioipeleleza nchi hiyo, wakayararua mavazi yao,+ 7 nao wakaliambia kusanyiko lote la wana wa Israeli hivi: “Nchi tuliyoipitia ili kuipeleleza ni nchi nzuri sana, sana.+ 8 Ikiwa Yehova amependezwa nasi,+ basi kwa hakika atatuingiza katika nchi hii na kutupa sisi, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ 9 Ila tu msimwasi Yehova;+ nanyi msiwaogope watu wa nchi hiyo,+ kwa maana wao ni mkate kwetu. Ulinzi wao umegeuka kutoka juu yao,+ na Yehova yuko pamoja nasi.+ Msiwaogope.”+
10 Hata hivyo, kusanyiko lote likasema wapigwe kwa mawe.+ Na utukufu wa Yehova ukaonekana juu ya hema la mkutano machoni pa wana wote wa Israeli.+
11 Mwishowe Yehova akamwambia Musa: “Watu hawa wataendelea kunitendea bila heshima+ mpaka wakati gani,+ nao watakosa kuniamini mpaka wakati gani ijapokuwa ishara zote ambazo nilifanya katikati yao?+ 12 Acha niwapige kwa tauni na kuwafukuzia mbali, na acha nikufanye wewe kuwa taifa kubwa zaidi na lenye nguvu zaidi kuliko wao.”+
13 Lakini Musa akamwambia Yehova: “Ndipo hakika Wamisri watasikia kwamba kwa nguvu zako uliwaongoza watu hawa kutoka katikati yao.+ 14 Nao hakika watawaambia wakaaji wa nchi hii. Wamesikia kwamba wewe ni Yehova katikati ya watu hawa,+ ambaye umeonekana uso kwa uso.+ Wewe ni Yehova, nalo wingu lako linasimama juu yao, nawe unaenda mbele yao katika nguzo ya wingu wakati wa mchana na katika nguzo ya moto wakati wa usiku.+ 15 Ukiwaua watu hawa kama mtu mmoja,+ ndipo mataifa ambayo yamesikia juu ya sifa yako watasema hivi, 16 ‘Kwa sababu Yehova hakuweza kuwaleta watu hawa katika nchi ambayo aliwaapia, aliwaua nyikani.’+ 17 Na sasa, tafadhali, nguvu zako na ziwe kuu,+ Ee Yehova, kama ulivyonena, na kusema, 18 ‘Yehova, si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ anayesamehe kosa na ubaya,+ lakini ambaye kwa vyovyote hatakosa kuadhibu,+ anayeleta adhabu kwa ajili ya kosa la baba juu ya wana, juu ya kizazi cha tatu na juu ya kizazi cha nne.’+ 19 Usamehe, tafadhali, kosa la watu hawa kulingana na ukuu wa fadhili zako zenye upendo, na kama vile ambavyo umewasamehe watu hawa tangu Misri na kuendelea mpaka sasa.”+
20 Ndipo Yehova akasema: “Ninasamehe kulingana na neno lako.+ 21 Na, kwa upande mwingine, kama ninavyoishi, dunia yote itajaa utukufu wa Yehova.+ 22 Lakini watu wote ambao wamekuwa wakiuona utukufu+ wangu na ishara+ zangu ambazo nimefanya katika Misri na nyikani na bado wakaendelea kunijaribu+ mara kumi hizi, nao hawakuisikiliza sauti yangu,+ 23 hawataiona kamwe nchi ambayo niliwaapia baba zao, naam, wale wote wanaonitendea bila heshima hawataiona.+ 24 Naye mtumishi wangu Kalebu,+ kwa sababu roho iliyo tofauti ilionekana kuwa pamoja naye, naye aliendelea kunifuata kikamilifu,+ nitamwingiza katika nchi ambamo ameenda, na wazao wake wataimiliki.+ 25 Huku Waamaleki na Wakanaani+ wakiwa wanakaa katika nchi tambarare ya chini, geukeni kesho na kuondoka ili mpige mwendo kuelekea nyikani kupitia njia ya Bahari Nyekundu.”+
26 Naye Yehova akasema na Musa na Haruni, na kumwambia: 27 “Kusanyiko hili lenye uovu litaendelea kuwa na manung’uniko haya ambayo linaendeleza juu yangu mpaka wakati gani?+ Nimesikia manung’uniko ya wana wa Israeli wanayonung’unika juu yangu.+ 28 Waambie, ‘ “Kama ninavyoishi,” asema Yehova, “ikiwa sitawafanyia ninyi vile ambavyo mmesema masikioni mwangu!+ 29 Katika nyika hii mizoga yenu itaanguka,+ naam, wote kati ya hesabu yenu ya walioandikishwa kuanzia miaka 20 na zaidi, ninyi ambao mmenung’unika juu yangu.+ 30 Nanyi hamtaingia katika nchi ambayo niliinua mkono wangu katika kiapo+ ya kwamba nitakaa pamoja nanyi, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+
31 “‘“Nao watoto wenu wadogo mliosema watakuwa nyara,+ hao pia hakika nitawaingiza, nao kwa kweli wataijua nchi ambayo mmeikataa.+ 32 Lakini mizoga yenu wenyewe itaanguka katika nyika hii.+ 33 Na wana wenu watakuwa wachungaji nyikani+ kwa miaka 40, nao watajibu kwa sababu ya matendo yenu ya uasherati,+ mpaka mizoga yenu itakapofikia mwisho wake nyikani.+ 34 Kwa hesabu ya siku mlizoipeleleza nchi hiyo, siku 40,+ siku moja kwa mwaka mmoja, siku moja kwa mwaka mmoja,+ mtajibu kwa sababu ya makosa yenu miaka 40,+ kwa maana lazima mjue maana ya mimi kutenganishwa nanyi.+
35 “‘“Mimi Yehova nimesema hakika hilo ndilo nitakalolitendea kusanyiko hili lote lenye uovu,+ wale ambao wamekusanyika pamoja dhidi yangu: Katika nyika hii watafikia mwisho wao, na humo watakufa.+ 36 Na wale wanaume ambao Musa aliwatuma kuipeleleza nchi na ambao, waliporudi, walianza kulifanya kusanyiko lote linung’unike juu yangu, kwa kuleta habari mbaya juu ya nchi hiyo,+ 37 naam, wanaume walioleta habari mbaya juu ya nchi watakufa kwa tauni mbele za Yehova.+ 38 Lakini Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune wataendelea kuishi, kati ya wale wanaume walioenda kuipeleleza nchi.”’”+
39 Musa alipowaambia wana wote wa Israeli maneno hayo, ndipo watu wakaanza kuomboleza sana.+ 40 Na zaidi ya hayo, wakaamka asubuhi na mapema na kujaribu kwenda juu ya mlima, wakisema: “Tazama, sisi tutapanda mpaka mahali ambapo Yehova alitaja. Kwa maana tumetenda dhambi.”+ 41 Lakini Musa akasema: “Kwa nini mnavunja agizo la Yehova?+ Lakini jambo hilo halitafanikiwa. 42 Msipande, kwa sababu Yehova hayuko katikati yenu, msije mkashindwa mbele ya adui zenu.+ 43 Kwa maana Waamaleki na Wakanaani wako huko mbele yenu;+ nanyi hakika mtaanguka kwa upanga, kwa sababu mligeuka na kuacha kumfuata Yehova, Yehova hataendelea kuwa pamoja nanyi.”+
44 Hata hivyo, wakafanya kimbelembele kupanda mpaka juu ya mlima,+ lakini sanduku la agano la Yehova na Musa hawakuondoka katikati ya kambi.+ 45 Ndipo Waamaleki+ na Wakanaani waliokuwa wakikaa katika mlima huo wakashuka na kuanza kuwapiga nao wakawatawanya mpaka Horma.+
15 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Mwishowe mtakapoingia katika nchi ya makao yenu, ambayo nitawapa,+ 3 nanyi mtamtolea Yehova toleo linalotolewa kwa njia ya moto,+ toleo la kuteketezwa+ au dhabihu ili kufanya nadhiri ya pekee au kwa hiari+ au wakati wa sherehe zenu za majira,+ ili kumfanyia Yehova harufu yenye kutuliza,+ kutoka katika mifugo au kutoka katika kundi; 4 yule anayetoa toleo lake pia atamtolea Yehova toleo la nafaka la unga laini,+ sehemu ya kumi ya efa, uliotiwa sehemu ya nne ya hini ya mafuta. 5 Nawe utatoa divai iwe toleo la kinywaji,+ sehemu ya nne ya hini, pamoja na lile toleo la kuteketezwa au kwa ajili ya dhabihu ya kila mwana-kondoo dume. 6 Au kwa ajili ya kondoo-dume utatoa toleo la nafaka la sehemu mbili za kumi za unga laini, uliotiwa sehemu ya tatu ya hini ya mafuta. 7 Nawe utatoa divai iwe toleo la kinywaji, sehemu ya tatu ya hini, kama harufu ya kumtuliza Yehova.
8 “‘Lakini ikiwa utatoa dume la mifugo liwe toleo la kuteketezwa+ au dhabihu ili kuweka nadhiri+ ya pekee au dhabihu za ushirika kwa Yehova,+ 9 mtu atatoa pia pamoja na yule dume wa mifugo, toleo la nafaka+ la sehemu tatu za kumi za unga laini, uliotiwa nusu hini ya mafuta. 10 Nawe unapaswa kutoa divai iwe toleo la kinywaji,+ nusu hini, kama toleo linalotolewa kwa njia ya moto, lenye harufu ya kumtuliza Yehova. 11 Hivyo ndivyo inavyopaswa kufanywa kwa ajili ya kila ng’ombe-dume au kwa ajili ya kila kondoo-dume au kwa ajili ya kichwa kimoja kati ya mwana-kondoo dume au kati ya mbuzi. 12 Hesabu yoyote ile mtakayotoa, hivyo ndivyo mnavyopaswa kufanya kwa ajili ya kila mmoja kulingana na hesabu yao. 13 Kila mwenyeji anapaswa kuwatoa hao kwa njia hiyo katika kutoa toleo linalotolewa kwa njia ya moto, lenye harufu ya kumtuliza Yehova.+
14 “‘Na ikiwa mkaaji mgeni atakaa pamoja nanyi akiwa mgeni au mtu aliye katikati yenu kwa vizazi vyenu, naye atoe toleo linalotolewa kwa njia ya moto, lenye harufu ya kumtuliza Yehova, kama vile mnavyopaswa kufanya, ndivyo anavyopaswa kufanya.+ 15 Ninyi mlio wa kutaniko na yule mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni mtakuwa na sheria moja.+ Itakuwa sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili ya vizazi vyenu. Mkaaji mgeni atakuwa sawa nanyi mbele za Yehova.+ 16 Kutakuwa na sheria moja na uamuzi mmoja wa hukumu kwa ajili yenu na kwa ajili ya mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni pamoja nanyi.’”+
17 Na Yehova akaendelea kumwambia Musa, na kusema: 18 “Sema na wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Mtakapoingia katika nchi ambamo nitawapeleka ninyi,+ 19 itatukia kwamba mtakapokula mkate wowote wa nchi hiyo,+ mtamtolea Yehova mchango. 20 Mtatoa mchango wa mazao ya kwanza+ ya unga wenu wenye chenga-chenga ukiwa keki za mviringo. Kama ulivyo mchango wa uwanja wa kupuria ndivyo mtakavyoutoa mchango huo. 21 Sehemu ya mazao ya kwanza ya unga wenu wenye chenga-chenga mtaitoa ikiwa mchango kwa Yehova katika vizazi vyenu vyote.
22 “‘Sasa ikiwa mtafanya kosa bila kukusudia nanyi mkose kushika amri zote hizi,+ ambazo Yehova amemwambia Musa, 23 yote ambayo Yehova amewaamuru ninyi kupitia Musa tangu siku ambayo Yehova alitoa amri na kuendelea kwa ajili ya vizazi vyenu, 24 ndipo itatukia kwamba ikiwa limefanywa mbali na macho ya kusanyiko kwa kukosea bila kukusudia, kusanyiko lote litatoa ng’ombe-dume mchanga awe toleo la kuteketezwa kwa ajili ya harufu ya kumtuliza Yehova, na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji kulingana na utaratibu wa kawaida,+ na mwana-mbuzi mmoja awe toleo la dhambi.+ 25 Naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili ya kusanyiko lote la wana wa Israeli, nao watasamehewa; kwa sababu lilikuwa kosa ambalo hawakukusudia,+ nao walileta mbele za Yehova toleo linalotolewa kwa njia ya moto kwa Yehova na toleo lao la dhambi kwa ajili ya kosa lao ambalo hawakukusudia. 26 Nalo kusanyiko lote la wana wa Israeli na mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni katikati yao litasamehewa,+ kwa sababu watu wote hao walifanya kosa bila kukusudia.
27 “‘Na ikiwa nafsi yoyote itatenda dhambi bila kukusudia,+ basi itatoa mbuzi-jike katika mwaka wake wa kwanza awe toleo la dhambi.+ 28 Naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya nafsi hiyo iliyofanya kosa kwa kutenda dhambi mbele za Yehova bila kukusudia, ili kuifanyia upatanisho, naye atasamehewa.+ 29 Kama ilivyo kwa mwenyeji kati ya wana wa Israeli na mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni katikati yao, kutakuwa na sheria moja kwenu juu ya kufanya jambo bila kukusudia.+
30 “‘Lakini nafsi inayofanya jambo kwa kukusudia,+ awe ni mwenyeji au mkaaji mgeni, aseme vibaya juu ya Yehova,+ katika hali hiyo nafsi hiyo lazima ikatiliwe mbali kutoka katikati ya watu wake.+ 31 Kwa sababu ni neno la Yehova ambalo amedharau+ na ni amri yake ambayo amevunja,+ nafsi hiyo lazima itakatiliwa mbali.+ Kosa lake mwenyewe liko juu yake.’”+
32 Wana wa Israeli walipokuwa nyikani, siku moja walimkuta mtu akikusanya kuni siku ya sabato.+ 33 Ndipo wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Musa na Haruni na kusanyiko lote. 34 Kwa hiyo wakamtia kifungoni,+ kwa sababu haikuwa imeelezwa waziwazi afanywe nini.
35 Baada ya muda Yehova akamwambia Musa: “Mtu huyo lazima auawe,+ kusanyiko lote litampiga kwa mawe nje ya kambi.”+ 36 Basi kusanyiko lote likamtoa nje ya kambi na kumpiga kwa mawe mpaka akafa, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
37 Naye Yehova akaendelea kumwambia Musa: 38 “Sema na wana wa Israeli, nawe utawaambia wajifanyie upindo wenye nyuzinyuzi kwenye miisho ya nguo zao katika vizazi vyao vyote, nao wataweka uzi wa bluu juu ya upindo wenye nyuzinyuzi wa miisho ya nguo,+ 39 ‘Nao utakuwa upindo wenye nyuzinyuzi kwa ajili yenu, nanyi mtauona na kukumbuka amri+ zote za Yehova na kuzishika, wala hamtaifuata mioyo yenu na macho yenu,+ ambayo mnayafuata katika uasherati.+ 40 Kusudi ni kwamba mpate kukumbuka na kushika amri zangu zote na kuwa watakatifu kwa Mungu wenu.+ 41 Mimi ni Yehova Mungu wenu, ambaye nimewatoa katika nchi ya Misri ili niwe Mungu wenu.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+
16 Na Kora+ mwana wa Ishari,+ mwana wa Kohathi,+ mwana wa Lawi,+ akaondoka, pamoja na Dathani+ na Abiramu+ wana wa Eliabu,+ na Oni mwana wa Pelethi, wana wa Rubeni.+ 2 Nao wakasimama mbele ya Musa, wao na watu 250 kati ya wana wa Israeli, wakuu wa kusanyiko, walioitwa kutoka kati ya mkutano, wanaume wenye sifa. 3 Basi wakakutana dhidi ya+ Musa na Haruni na kuwaambia: “Imetosha, kwa sababu kusanyiko lote, wote hao ni watakatifu+ na Yehova yuko katikati yao.+ Kwa nini, basi, mjiinue wenyewe juu ya kutaniko la Yehova?”+
4 Musa aliposikia jambo hilo mara moja akaanguka kifudifudi. 5 Ndipo akasema na Kora na kusanyiko lake lote, na kuwaambia: “Asubuhi Yehova atajulisha ni nani aliye wake+ na ni nani aliye mtakatifu+ na ni nani anayeweza kumkaribia,+ na yeyote atakayemchagua+ huyo atamkaribia. 6 Fanyeni hivi: Chukueni vyetezo+ kwa ajili yenu, Kora na kusanyiko+ lake lote, 7 na mtie moto ndani yake na kutia uvumba juu yake mbele za Yehova kesho, na itatukia kwamba mtu ambaye Yehova atamchagua,+ yeye ndiye mtakatifu. Imetosha, enyi wana wa Lawi!”+
8 Na Musa akaendelea kumwambia Kora: “Sikilizeni, tafadhali, enyi wana wa Lawi. 9 Je, ni jambo dogo sana kwenu ya kwamba Mungu wa Israeli amewatenga+ ninyi mbali na kusanyiko la Israeli ili kuwaleta ninyi kwake mpate kuendeleza utumishi wa maskani ya Yehova na kusimama mbele ya kusanyiko ili kuwahudumia,+ 10 na kwamba amewaleta karibu ninyi na ndugu zenu wote wana wa Lawi? Basi, je, ni lazima pia ninyi mjaribu kunyakua ukuhani?+ 11 Kwa sababu hiyo wewe na kusanyiko lako lote wanaokusanyika pamoja mnampinga Yehova.+ Na Haruni, yeye ni nani hata mnung’unike juu yake?”+
12 Baadaye Musa akatuma watu wawaite Dathani na Abiramu+ wana wa Eliabu, lakini wakasema: “Sisi hatutakuja!+ 13 Je, ni jambo dogo sana kwamba umetuleta kutoka katika nchi inayotiririka maziwa na asali ili kutuua nyikani,+ hivi kwamba ujaribu pia kujifanya mkuu juu yetu kabisa?+ 14 Kama ilivyo, hujatuleta katika nchi inayotiririka maziwa na asali,+ upate kutupa urithi wa shamba na shamba la mizabibu. Je, macho ya watu hawa ndiyo unayotaka kutoboa? Sisi hatutakuja!”
15 Basi Musa akakasirika sana na kumwambia Yehova: “Usigeuke ili kutazama toleo lao la nafaka.+ Hata punda-dume mmoja sijachukua kutoka kwao, wala sijamuumiza mmoja wao.”+
16 Ndipo Musa akamwambia Kora:+ “Wewe na kusanyiko lako lote, muwepo mbele za Yehova+ kesho, wewe na wao na Haruni. 17 Na kila mmoja achukue chetezo chake, nanyi mtie uvumba juu yake na kuleta kila mmoja chetezo chake mbele za Yehova, vyetezo 250, na wewe na Haruni kila mmoja chetezo chake.” 18 Basi wakachukua kila mmoja chetezo chake, wakatia moto juu yake, wakatia uvumba juu yake, wakasimama kwenye mwingilio wa hema la mkutano pamoja na Musa na Haruni. 19 Kora alipokuwa amekusanya kusanyiko+ lote pamoja dhidi yao kwenye mwingilio wa hema la mkutano, ndipo utukufu wa Yehova ukalitokea kusanyiko+ lote.
20 Sasa Yehova akasema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 21 “Jitengeni+ wenyewe kutoka katikati ya kusanyiko hili, nipate kuwaangamiza+ wao mara moja.” 22 Ndipo wakaanguka kifudifudi na kusema: “Ee Mungu, Mungu wa roho za kila namna ya mwili,+ je, mtu mmoja tu atatenda dhambi nawe ulikasirikie kusanyiko lote?”+
23 Basi Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 24 “Sema na kusanyiko, na kuwaambia, ‘Ondokeni kuzunguka pande zote za maskani za Kora, Dathani na Abiramu!’”+
25 Kisha Musa akaondoka na kwenda kwa Dathani na Abiramu, na wanaume wazee+ wa Israeli wakaenda pamoja naye. 26 Ndipo akasema na kusanyiko, na kuwaambia: “Geukeni kando, tafadhali, kutoka mbele ya mahema ya watu hawa waovu wala msiguse chochote kilicho chao,+ msije mkafagiliwa mbali katika dhambi yao yote.” 27 Wakaondoka mara moja kutoka mbele ya maskani ya Kora, Dathani na Abiramu, kutoka pande zote, nao Dathani na Abiramu wakatoka nje, wakasimama kwenye mwingilio wa mahema yao,+ pamoja na wake zao, na wana wao na watoto wao wadogo.
28 Ndipo Musa akasema: “Kwa jambo hili mtajua kwamba Yehova amenituma nifanye matendo yote haya,+ kwamba si kutoka moyoni mwangu mwenyewe:+ 29 Ikiwa watu hawa watakufa kifo cha wanadamu wote na kwamba adhabu iletwe juu yao kulingana na adhabu ya wanadamu wote,+ basi si Yehova aliyenituma mimi.+ 30 Lakini ikiwa ni kitu fulani kilichoumbwa ambacho Yehova ataumba,+ nayo nchi ifungue kinywa chake na kuwameza+ na kila kitu kilicho chao, nao washuke chini wakiwa hai mpaka katika Kaburi,*+ ndipo hakika mtajua kwamba watu hawa wamemtendea Yehova bila heshima.”+
31 Na ikawa kwamba mara tu alipomaliza kusema maneno hayo, nchi iliyokuwa chini yao ikaanza kupasuka na kutengana.+ 32 Nayo dunia ikafungua kinywa chake na kuwameza wao na nyumba zao na wanadamu wote waliokuwa wa Kora na mali zote.+ 33 Kwa hiyo wakashuka chini, na wote waliokuwa wao, wakiwa hai mpaka katika Kaburi,* nayo dunia ikawafunika,+ hivi kwamba wakaangamia kutoka katikati ya kutaniko.+ 34 Na Waisraeli wote waliokuwa wamewazunguka wakakimbia kwa sababu ya kilio chao, kwa maana walianza kusema: “Tunaogopa kwamba huenda dunia ikatumeza sisi!”+ 35 Na moto ukaja kutoka kwa Yehova+ na kuwateketeza wale wanaume 250 waliokuwa wakitoa uvumba.+
36 Sasa Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 37 “Mwambie Eleazari mwana wa Haruni kuhani kwamba achukue vyetezo+ hivyo kutoka katika moto, ‘Nawe utawanye moto pale; kwa maana ni vitakatifu, 38 naam, vyetezo vya wanaume hao waliozitendea dhambi nafsi zao wenyewe.+ Nao watavifanya viwe mabamba membamba ya madini ya kutanda madhabahu,+ kwa sababu walivitoa mbele za Yehova, hivi kwamba vikawa vitakatifu; navyo vitakuwa ishara kwa wana wa Israeli.’”+ 39 Basi Eleazari kuhani akachukua vile vyetezo vya shaba,+ ambavyo wale waliokuwa wameteketezwa walikuwa wametoa, nao wakavifua vikawa vya kutanda madhabahu, 40 kuwa ukumbusho kwa wana wa Israeli, kusudi mgeni+ yeyote ambaye si uzao wa Haruni asikaribie ili kufukiza uvumba mbele za Yehova,+ wala yeyote asiwe kama Kora na kusanyiko lake,+ kama vile Yehova alivyokuwa amesema naye kupitia Musa.
41 Na kesho yake kusanyiko lote la wana wa Israeli likaanza kunung’unika juu ya Musa na Haruni,+ na kusema: “Ninyi, ninyi mmewaua watu wa Yehova.” 42 Na ikawa kwamba kusanyiko lilipokuwa limekutanika dhidi ya Musa na Haruni, ndipo walipogeuka kulielekea hema la mkutano; na, tazama! wingu likalifunika, nao utukufu wa Yehova ukaanza kutokea.+
43 Naye Musa na Haruni wakaja mbele ya hema la mkutano.+ 44 Ndipo Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 45 “Ondokeni kutoka katikati ya kusanyiko hili, nipate kuliangamiza mara moja.”+ Ndipo wakaanguka kifudifudi.+ 46 Kisha Musa akamwambia Haruni: “Chukua chetezo utie ndani yake moto kutoka juu ya madhabahu+ na kutia uvumba nawe uende kwenye kusanyiko haraka na kufanya upatanisho kwa ajili yao,+ kwa sababu hasira imetoka usoni pa Yehova.+ Pigo limeanza!” 47 Haruni akakichukua mara moja, kama vile Musa alivyokuwa amesema, naye akakimbia kuingia katikati ya kutaniko; na, tazama! pigo lilikuwa limeanza katikati ya watu. Basi akatia uvumba juu yake na kuanza kufanya upatanisho kwa ajili ya watu. 48 Naye akaendelea kusimama katikati ya wafu na walio hai.+ Mwishowe tauni hiyo ikakomeshwa.+ 49 Nao waliokufa kutokana na tauni hiyo wakajumlika kuwa elfu kumi na nne na mia saba, mbali na wale waliokufa kwa sababu ya Kora. 50 Mwishowe Haruni aliporudi kwa Musa kwenye mwingilio wa hema la mkutano, tauni hiyo ilikuwa imekomeshwa.
17 Sasa Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli nawe uchukue kutoka kwao fimbo+ moja kwa ajili ya kila nyumba ya ukoo wa upande wa baba kutoka kwa wakuu+ wao wote, kulingana na nyumba ya baba yao, fimbo kumi na mbili. Utaandika jina la kila mmoja katika fimbo yake. 3 Na jina la Haruni utaliandika katika fimbo ya Lawi, kwa sababu kuna fimbo moja kwa ajili ya kichwa cha nyumba ya baba zao. 4 Nawe utaziweka katika hema la mkutano mbele ya Ushuhuda+ huo, mahali ambapo mimi huwatokea ninyi kwa ukawaida.+ 5 Na itatukia kwamba mtu nitakayemchagua,+ fimbo yake itachipuka, nami nitakomesha manung’uniko+ ya wana wa Israeli juu yangu, ambayo wananung’unika juu yenu.”+
6 Basi Musa akasema na wana wa Israeli, na wakuu wao wote wakampa fimbo kwa ajili ya kila mkuu, fimbo moja kwa kila mkuu, kulingana na nyumba ya baba zao, fimbo kumi na mbili;+ nayo fimbo ya Haruni ilikuwa kati ya fimbo zao.+ 7 Ndipo Musa akaziweka fimbo hizo mbele za Yehova katika hema la Ushuhuda.+
8 Na ikawa kwamba kesho yake wakati ambapo Musa aliingia ndani ya hema la Ushuhuda, tazama! fimbo ya Haruni kwa ajili ya nyumba ya Lawi ilikuwa imechipuka, nayo ilikuwa ikitokeza matumba na maua yanayochanua nayo ilikuwa na lozi zilizoiva. 9 Ndipo Musa akatoa nje fimbo zote kutoka mbele za Yehova na kuziweka mbele ya wana wote wa Israeli, nao wakatazama na kuchukua kila mtu fimbo yake mwenyewe.
10 Basi Yehova akamwambia Musa: “Irudishe fimbo+ ya Haruni mbele ya Ushuhuda huo iwe kitu cha kuwekwa kama ishara+ kwa wana wa uasi,+ ili manung’uniko yao yakome juu yangu, wasije wakafa.” 11 Musa akafanya mara moja kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru. Alifanya vivyo hivyo.
12 Nao wana wa Israeli wakaanza kumwambia Musa hivi: “Sasa bila shaka tutakata pumzi, bila shaka tutaangamia, sisi sote tutaangamia bila shaka.+ 13 Mtu yeyote anayekaribia,+ anayekuja karibu na maskani ya Yehova, atakufa!+ Je, ni lazima tukate pumzi kwa njia hii?”+
18 Na Yehova akamwambia Haruni: “Wewe na wana wako na nyumba ya baba yako pamoja nawe mtajibu kwa sababu ya kosa dhidi ya patakatifu,+ na wewe na wana wako pamoja nawe mtajibu kwa sababu ya kosa dhidi ya ukuhani wenu.+ 2 Na uwalete karibu, pia, ndugu zako wa kabila la Lawi, ukoo wa baba yako, pamoja nawe, wapate kuungana nawe na wapate kukuhudumia wewe,+ wewe na wana wako pamoja nawe, mbele ya hema la Ushuhuda.+ 3 Nao watashika wajibu wao kwako na wajibu wao kwa hema lote.+ Ila wasikaribie vyombo vya mahali patakatifu na madhabahu wasije wakafa,+ wao wala ninyi. 4 Nao wataungana nawe na watashika wajibu wao kwa hema la mkutano kuhusu utumishi wote wa hema, wala mgeni yeyote asiwakaribie ninyi.+ 5 Nanyi mtashika wajibu wenu kwa mahali patakatifu+ na wajibu wenu kwa madhabahu,+ ili hasira+ zaidi isitokee juu ya wana wa Israeli. 6 Na mimi, tazama! mimi nimewachukua ndugu zenu, Walawi, kutoka katikati ya wana wa Israeli,+ wawe zawadi kwenu,+ kama wale waliokabidhiwa kwa Yehova ili kuendeleza utumishi wa hema la mkutano.+ 7 Na wewe na wana wako pamoja nawe mnapaswa kuulinda ukuhani wenu juu ya kila shughuli ya madhabahu na juu ya kile kilicho ndani ya pazia;+ nanyi mtatoa utumishi.+ Nitawapa ukuhani wenu kama utumishi wa zawadi, na mgeni atakayesogea karibu lazima auawe.”+
8 Na Yehova akazidi kumwambia Haruni: “Mimi nami, tazama! nimekupa wewe utunzaji wa michango inayotolewa kwa ajili yangu.+ Vitu vyote vitakatifu vya wana wa Israeli nimekupa wewe na wana wako viwe fungu, viwe posho mpaka wakati usio na kipimo.+ 9 Hilo litakuwa lenu kutoka katika vitu vitakatifu zaidi, kutoka katika toleo linalotolewa kwa njia ya moto, kila toleo lao pamoja na kila toleo lao la nafaka+ na kila toleo lao la dhambi+ na kila toleo lao la hatia,+ ambalo watanirudishia. Ni kitu kitakatifu zaidi kwa ajili yako na wana wako. 10 Utakula katika mahali patakatifu zaidi.+ Kila mwanamume atakula.+ Kitakuwa kitu kitakatifu kwako.+ 11 Na hiki ni chako: mchango+ wa zawadi yao pamoja na matoleo yote ya kutikisa+ ya wana wa Israeli. Nimekupa wewe na wana wako na binti zako pamoja nawe vitu hivyo,+ viwe posho mpaka wakati usio na kipimo. Kila mtu aliye safi katika nyumba yako anaweza kula.+
12 “Vyote vilivyo bora katika mafuta na vyote vilivyo bora katika divai mpya na nafaka, matunda yao ya kwanza,+ ambayo watampa Yehova, nimekupa wewe.+ 13 Matunda yaliyoiva ya kwanza katika vyote vilivyo katika nchi yao, ambayo watamletea Yehova, yatakuwa yako.+ Kila mtu aliye safi katika nyumba yako anaweza kula.
14 “Kila kitu kilichotolewa katika Israeli kinapaswa kuwa chako.+
15 “Kila kitu kinachofungua tumbo la uzazi,+ cha kila namna yenye mwili, ambacho watamtolea Yehova, kati ya wanadamu na kati ya wanyama, kinapaswa kuwa chako. Hata hivyo, unapaswa kumkomboa mzaliwa wa kwanza wa wanadamu;+ na mzaliwa wa kwanza wa mnyama ambaye si safi unapaswa kumkomboa.+ 16 Na kwa bei ya ukombozi kwa ajili yake kuanzia umri wa mwezi mmoja na kuendelea utamkomboa, kwa thamani iliyokadiriwa, shekeli 5 za fedha kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.+ Ni gera 20.+ 17 Ila tu ng’ombe-dume aliye mzaliwa wa kwanza au mwana-kondoo dume aliye mzaliwa wa kwanza au mbuzi aliye mzaliwa wa kwanza hutawakomboa.+ Hao ni kitu kitakatifu. Damu+ yao unapaswa kuinyunyiza juu ya madhabahu, na mafuta yao utayafukiza kama toleo linalotolewa kwa njia ya moto ili kuwa harufu ya kumtuliza Yehova.+ 18 Na nyama yao itakuwa yako. Kama vile kidari cha toleo la kutikisa na kama ule mguu wa kuume, inapaswa kuwa yako.+ 19 Michango yote mitakatifu,+ ambayo wana wa Israeli watamchangia Yehova, nimekupa wewe na wana wako na binti zako pamoja nawe, iwe posho lenu mpaka wakati usio na kipimo.+ Ni agano la chumvi mpaka wakati usio na kipimo mbele za Yehova kwa ajili yako na kwa ajili ya uzao wako pamoja nawe.”+
20 Na Yehova akaendelea kumwambia Haruni: “Katika nchi yao hutakuwa na urithi, wala hakuna fungu lolote litakalokuwa lako katikati yao.+ Mimi ni fungu lako na urithi wako katikati ya wana wa Israeli.+
21 “Na kwa wana wa Lawi, tazama! nimewapa kila sehemu ya kumi+ katika Israeli iwe urithi wao kwa sababu ya utumishi wao wanaofanya, utumishi wa hema la mkutano. 22 Na wana wa Israeli wasikaribie tena hema la mkutano wasije wakawa na hatia ya dhambi na kufa.+ 23 Nao Walawi wenyewe wataendeleza utumishi wa hema la mkutano, nao ndio wanaopaswa kujibu kwa kosa lao.+ Ni sheria mpaka wakati usio na kipimo katika vizazi vyenu vyote kwamba katikati ya wana wa Israeli hawapaswi kupata urithi.+ 24 Kwa maana ile sehemu ya kumi ya wana wa Israeli, ambayo watamchangia Yehova kuwa mchango, nimewapa Walawi kuwa urithi. Ndiyo sababu nimewaambia, ‘Katikati ya wana wa Israeli hawapaswi kupata urithi.’”+
25 Ndipo Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 26 “Na wewe utasema na Walawi, nawe utawaambia, ‘Mtapokea kutoka kwa wana wa Israeli sehemu ya kumi ambayo nimewapa ninyi kutoka kwao kwa ajili ya urithi wenu,+ nanyi mtatoa mchango wenu kutoka katika hiyo uwe mchango kwa Yehova wa sehemu ya kumi ya hiyo sehemu ya kumi.+ 27 Na utahesabiwa kwenu kuwa mchango wenu, kama ile nafaka ya uwanja wa kupuria+ na kama yale mazao kamili ya shinikizo la divai au la mafuta. 28 Na kwa njia hiyo ninyi wenyewe mtachanga mchango wenu kwa Yehova kutoka katika sehemu zenu zote za kumi ambazo mtapokea kutoka kwa wana wa Israeli, na katika hizo mtamtolea Yehova mchango kwa Haruni kuhani. 29 Katika zawadi zote mtakazopewa, mtachanga kila namna ya mchango kwa Yehova, ule ulio bora zaidi,+ uwe kitu kitakatifu kutoka kwao.’
30 “Nawe utawaambia, ‘Mnapochanga vilivyo bora kutoka kwa hivyo,+ ndipo itahesabiwa kwa Walawi kama mazao ya uwanja wa kupuria na kama mazao ya shinikizo la divai au la mafuta. 31 Nanyi mtakula vitu hivyo kila mahali, ninyi na nyumba yenu, kwa sababu ni malipo yenu kwa ajili ya utumishi wenu katika hema la mkutano.+ 32 Nanyi msijiletee hatia ya dhambi mnapochanga vilivyo bora katika hivyo, wala msitie unajisi vitu vitakatifu vya wana wa Israeli, msije mkafa.’”+
19 Na Yehova akasema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 2 “Hii ni amri ya sheria ambayo Yehova ameamuru, na kusema, ‘Waambie wana wa Israeli kwamba wakuchukulie ng’ombe mwekundu aliye timamu+ ambaye hana kasoro yoyote na ambaye hajafungwa nira yoyote.+ 3 Nanyi mtamkabidhi Eleazari kuhani, naye atampeleka nje ya kambi, naye atachinjwa mbele yake. 4 Kisha Eleazari kuhani atachukua sehemu ya damu yake kwa kidole chake na kuitapanya sehemu ya damu yake moja kwa moja kuelekea hema la mkutano mara saba.+ 5 Na ng’ombe huyo atateketezwa motoni mbele ya macho yake. Ngozi yake na nyama yake na damu yake pamoja na mavi yake vitateketezwa.+ 6 Naye kuhani atachukua mti wa mwerezi+ na hisopo+ na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili+ na kuvitupa katikati ya moto unaomteketeza ng’ombe. 7 Naye kuhani atayafua mavazi yake na kuoga mwili wake katika maji, na baadaye anaweza kuingia kambini; lakini yule kuhani atakuwa si safi mpaka jioni.
8 “‘Na yule aliyemteketeza atayafua mavazi yake katika maji na kuoga mwili wake katika maji,+ naye atakuwa asiye safi mpaka jioni.
9 “‘Na mwanamume aliye safi atayakusanya majivu+ ya ng’ombe huyo na kuyaweka nje ya kambi katika mahali safi; nayo yatatumika kama kitu cha kuwekwa kwa ajili ya yale maji ya kutakasa kwa wana wa Israeli.+ Ni toleo la dhambi. 10 Na yule anayekusanya majivu ya yule ng’ombe atayafua mavazi yake na kuwa asiye safi mpaka jioni.+
“‘Nayo itakuwa sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa wana wa Israeli na mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni katikati yao.+ 11 Yeyote atakayegusa maiti ya nafsi+ yoyote ya binadamu atakuwa asiye safi siku saba.+ 12 Mtu huyo anapaswa kujitakasa kwa maji hayo siku ya tatu,+ na siku ya saba atakuwa safi. Lakini ikiwa hatajitakasa siku ya tatu, basi siku ya saba hatakuwa safi. 13 Kila mtu atakayegusa maiti, nafsi ya mtu yeyote atakayekufa, na ambaye hatajitakasa, ameitia unajisi maskani ya Yehova,+ nayo nafsi hiyo lazima ikatiliwe mbali kutoka katika Israeli.+ Kwa sababu maji ya kutakasa+ hayakunyunyizwa juu yake, anaendelea kuwa asiye safi. Uchafu wake bado uko juu yake.+
14 “‘Hii ndiyo sheria ikiwa mtu atakufa ndani ya hema: Kila mtu atakayeingia katika hema hilo, na kila mtu aliye ndani ya hema hilo, atakuwa asiye safi siku saba. 15 Na kila chombo+ kilichofunguliwa ambacho hakina kifuniko kilichofunikwa si safi. 16 Na kila mtu ambaye huko shambani atagusa mtu aliyeuawa kwa upanga+ au maiti au mfupa+ wa mtu au kaburi atakuwa asiye safi siku saba. 17 Nao watachukua kwa ajili ya yule asiye safi sehemu ya mavumbi ya moto wa toleo la dhambi na kutia maji yanayotiririka juu ya mavumbi katika chombo. 18 Ndipo mtu aliye safi+ atachukua hisopo+ na kuichovya ndani ya maji yale na kuyatapanya juu ya hema na vyombo vyote na nafsi zote zilizokuwa hapo na juu ya yule aliyegusa mfupa au mtu aliyeuawa au maiti au kaburi. 19 Na yule mtu aliye safi atayatapanya juu ya yule asiye safi siku ya tatu na siku ya saba na kumtakasa kutokana na dhambi yake siku ya saba;+ naye atayafua mavazi yake na kuoga katika maji, naye atakuwa safi jioni.
20 “‘Lakini mtu asiye safi na ambaye hatajitakasa, basi, nafsi hiyo lazima ikatiliwe mbali+ kutoka katikati ya kutaniko, kwa sababu amepatia unajisi patakatifu pa Yehova. Maji ya kutakasa hayakunyunyizwa juu yake. Yeye si safi.
21 “‘Nayo itatumika kama sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili yao, kwamba yule anayetapanya maji kwa ajili ya kutakasa anapaswa kuyafua mavazi yake,+ pia yule anayegusa maji ya kutakasa. Atakuwa asiye safi mpaka jioni. 22 Na kitu chochote ambacho huenda yule mtu asiye safi atakigusa kitakuwa kisicho safi,+ nayo nafsi itakayokigusa itakuwa najisi mpaka jioni.’”+
20 Nao wana wa Israeli, kusanyiko lote, wakaingia katika nyika ya Zini+ katika mwezi wa kwanza, nao watu wakakaa Kadeshi.+ Hapo ndipo Miriamu+ alipofia na hapo ndipo alipozikwa.
2 Sasa hapakuwa na maji kwa ajili ya kusanyiko hilo,+ nao wakaanza kukutanika pamoja dhidi ya Musa na Haruni.+ 3 Nao watu wakagombana+ na Musa na kusema: “Laiti tungalikufa wakati ndugu zetu walipokufa mbele za Yehova!+ 4 Na kwa nini ninyi mmeleta kutaniko la Yehova katika nyika hii ili sisi na wanyama wetu wa kubeba mizigo tufie huko?+ 5 Na kwa nini mmetuongoza kutoka Misri na kutuleta katika mahali hapa pabaya?+ Si mahali pa mbegu na tini na mizabibu na makomamanga,+ wala hapana maji ya kunywa.” 6 Ndipo Musa na Haruni wakatoka mbele ya kutaniko wakaenda kwenye mwingilio wa hema la mkutano na kuanguka kifudifudi,+ nao utukufu wa Yehova ukaanza kuwatokea.+
7 Ndipo Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 8 “Ichukue fimbo+ na kuliita kusanyiko pamoja, wewe na Haruni ndugu yako, nanyi mtauambia mwamba mbele ya macho yao ili kwa kweli utoe maji yake; nawe utawatolea maji kutoka katika mwamba na kuwapa maji kusanyiko na wanyama wao wa kubeba mizigo.”+
9 Basi Musa akachukua fimbo kutoka mbele za Yehova,+ kama vile alivyokuwa amemwamuru. 10 Kisha Musa na Haruni wakaliita kutaniko pamoja mbele ya mwamba, naye akawaambia: “Sikieni, sasa, enyi waasi!+ Je, tuwatolee ninyi maji katika mwamba huu?”+ 11 Halafu Musa akainua mkono wake na kuupiga mwamba mara mbili kwa fimbo yake; na maji mengi yakaanza kutoka, nalo kusanyiko na wanyama wao wa kubeba mizigo wakaanza kunywa.+
12 Baadaye Yehova akawaambia Musa na Haruni: “Kwa sababu hamkuonyesha imani kwangu ili kunitakasa+ mbele ya macho ya wana wa Israeli, kwa hiyo ninyi hamtaliingiza kutaniko hili katika nchi ambayo hakika nitawapa wao.”+ 13 Hayo ndiyo maji ya Meriba,+ kwa sababu wana wa Israeli waligombana na Yehova, hivi kwamba akatakaswa katikati yao.
14 Basi Musa akatuma wajumbe kutoka Kadeshi mpaka kwa mfalme wa Edomu:+ “Hivi ndivyo ndugu yako Israeli+ amesema, ‘Wewe mwenyewe unajua vema magumu yote ambayo yametupata.+ 15 Na baba zetu walishuka Misri,+ nasi tukaendelea kukaa Misri siku nyingi;+ nao Wamisri wakaanza kutudhuru sisi na baba zetu.+ 16 Mwishowe tukamlilia Yehova+ naye akaisikia sauti yetu na kumtuma malaika,+ akatutoa Misri; na tazama, tuko hapa Kadeshi, jiji lililo kwenye mpaka wa eneo lako. 17 Acha tupite, tafadhali, katika nchi yako. Hatutapita katika shamba wala katika shamba la mizabibu, wala hatutakunywa maji ya kisima. Katika njia ya mfalme tutapiga mwendo.+ Hatutageuka kuelekea kuume wala kuelekea kushoto,+ mpaka tutakapokuwa tumepita katikati ya eneo lako.’”
18 Hata hivyo, Edomu akamwambia: “Hutapita katikati yangu, nisije nikatoka nje nikiwa na upanga ili nikutane nawe.” 19 Nao wana wa Israeli wakamwambia: “Kwa njia kuu tutaenda; na ikiwa mimi na mifugo yangu tutakunywa maji yako, nitalipa thamani yake.+ Sitaki kitu chochote ila kupita kwa miguu yangu.”+ 20 Bado akasema: “Hutapita.”+ Kisha Edomu+ akatoka nje ili kukutana naye akiwa na watu wengi sana na mkono wenye nguvu. 21 Basi Edomu akakataa kumpa Israeli ruhusa ya kupita katikati ya eneo lake.+ Kwa hiyo Israeli akageuka na kumwacha.+
22 Na wana wa Israeli, kusanyiko lote, wakaondoka Kadeshi+ nao wakafika Mlima Hori.+ 23 Kisha Yehova akawaambia Musa na Haruni jambo hili katika Mlima Hori karibu na mpaka wa nchi ya Edomu: 24 “Haruni atakusanywa kwa watu wake,+ kwa maana hataingia katika nchi ambayo nitawapa wana wa Israeli, kwa sababu ninyi mliasi agizo langu kuhusiana na maji ya Meriba.+ 25 Wachukue Haruni na Eleazari mwana wake, uwalete juu kwenye Mlima Hori. 26 Nawe umvue Haruni mavazi yake,+ nawe utamvika Eleazari+ mwana wake mavazi hayo; naye Haruni atakusanywa, naye atakufa huko.”+
27 Basi Musa akafanya kama vile Yehova alivyokuwa ameamuru; nao wakapanda Mlima Hori mbele ya macho ya kusanyiko lote. 28 Kisha Musa akamvua Haruni mavazi yake na kumvika Eleazari mwana wake mavazi hayo, kisha Haruni akafa huko juu ya mlima huo.+ Naye Musa na Eleazari wakashuka kutoka mlimani. 29 Nalo kusanyiko lote likapata kuona kwamba Haruni alikuwa amekata pumzi, na nyumba yote ya Israeli ikaendelea kumlilia Haruni siku 30.+
21 Sasa yule Mkanaani, mfalme wa Aradi,+ aliyekaa Negebu,+ akapata kusikia kwamba Israeli alikuwa amekuja kupitia njia ya Atharimu, naye akaanza kupigana na Israeli na kuchukua baadhi yao kuwa mateka. 2 Basi Israeli akaweka nadhiri kwa Yehova na kusema:+ “Hakika ukiwatia watu hawa mkononi mwangu, mimi pia hakika nitayaangamiza majiji yao.”+ 3 Kwa hiyo Yehova akaisikiliza sauti ya Israeli na kuwakabidhi Wakanaani; nao wakawaangamiza wao na majiji yao. Kisha wakapaita mahali hapo Horma.+
4 Walipoendelea kusafiri kutoka Mlima Hori+ wakipitia njia ya Bahari Nyekundu ili kuizunguka nchi ya Edomu,+ nafsi ya watu ikaanza kuchoka kwa sababu ya ile njia. 5 Nao watu wakaendelea kusema dhidi ya Mungu+ na Musa:+ “Kwa nini mmetutoa Misri ili tufe nyikani?+ Kwa maana hakuna mkate wala maji,+ nayo nafsi yetu imeuchukia huu mkate wa kudharaulika.”+ 6 Basi Yehova akatuma nyoka wenye sumu+ katikati ya watu, nao wakawa wakiwauma watu, hivi kwamba watu wengi wa Israeli wakafa.+
7 Mwishowe watu wakamjia Musa na kusema: “Tumetenda dhambi,+ kwa sababu tumesema dhidi ya Yehova na dhidi yako. Tutetee kwa Yehova awaondoe nyoka hawa juu yetu.”+ Naye Musa akawatetea watu.+ 8 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Jifanyie nyoka mkali na kumweka juu ya nguzo ya ishara. Na itatukia kwamba wakati mtu yeyote ameumwa, basi atamtazama na hivyo ataendelea kuwa hai.”+ 9 Mara moja Musa akafanya nyoka wa shaba+ na kumweka juu ya nguzo ya ishara;+ na ikawa kwamba nyoka alipomuuma mtu naye akamtazama+ yule nyoka wa shaba, ndipo alipoendelea kuwa hai.+
10 Kisha wana wa Israeli wakaondoka na kupiga kambi Obothi.+ 11 Kisha wakaondoka Obothi na kupiga kambi Iye-abarimu,+ katika nyika inayoelekea upande wa mbele wa Moabu, kuelekea mashariki. 12 Kutoka huko wakasafiri na kupiga kambi kando ya bonde la mto la Zeredi.+ 13 Kutoka huko wakasafiri na kupiga kambi katika eneo la Arnoni,+ lililo katika nyika inayosambaa kutoka katika mpaka wa Waamori; kwa maana Arnoni ni mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori. 14 Ndiyo sababu imesemwa katika kitabu cha Vita vya Yehova:
“Vahebu katika Sufa na mabonde ya mito ya Arnoni, 15 na mdomo wa mabonde ya mito, ambao umejipinda kuelekea kiti cha Ari+ na kuegemea juu ya mpaka wa Moabu.”
16 Kisha kutoka huko hadi Beeri.+ Hicho ndicho kisima ambacho Yehova alimwambia hivi Musa juu yake: “Wakusanye watu, niwape maji.”+
18 Kisima, wakuu walikichimba. Watu wenye vyeo kati ya watu walikichimba,
Kwa fimbo ya kiongozi,+ kwa fimbo zao wenyewe.”
Kisha kutoka nyikani mpaka Matana. 19 Na kutoka Matana mpaka Nahalieli, na kutoka Nahalieli mpaka Bamothi.+ 20 Na kutoka Bamothi mpaka katika bonde lililo katika uwanja wa Moabu,+ kwenye kichwa cha Pisga,+ nalo linachomoza kuelekea uso wa Yeshimoni.+
21 Sasa Israeli akatuma wajumbe kwa Sihoni+ mfalme wa Waamori, na kusema: 22 “Acha nipite katikati ya nchi yako. Hatutageuka kando kuingia katika shamba wala katika shamba la mizabibu. Hatutakunywa maji ya kisima chochote. Kwenye barabara ya mfalme tutapiga mwendo mpaka tutakapokuwa tumepita katikati ya eneo lako.”+ 23 Naye Sihoni hakumruhusu Israeli apite katikati ya eneo lake,+ bali Sihoni akawakusanya watu wake wote na kwenda kukutana na Israeli nyikani, naye akaja kule Yahazi+ na kuanza kupigana na Israeli. 24 Ndipo Israeli akampiga kwa makali ya upanga+ na kuitwaa nchi+ yake kutoka Arnoni+ hadi Yaboki,+ karibu na wana wa Amoni; kwa sababu Yazeri+ ndio mpaka wa wana wa Amoni.+
25 Basi Israeli akayachukua majiji hayo yote, naye Israeli akaanza kukaa katika majiji yote ya Waamori,+ katika Heshboni+ na miji yake yote ya kandokando. 26 Kwa maana Heshboni lilikuwa jiji la Sihoni.+ Yeye alikuwa mfalme wa Waamori,+ naye ndiye aliyepigana na mfalme wa Moabu zamani na kuichukua nchi yake yote kutoka mkononi mwake mpaka Arnoni.+ 27 Ndiyo sababu waimbaji wa mafungu ya shairi la kufanya mzaha walisema:
“Njoo katika Heshboni.
Jiji la Sihoni na lijengwe na kuonekana kuwa limefanywa imara.
28 Kwa maana moto umetoka Heshboni,+ mwali wa moto kutoka katika mji wa Sihoni.
Umeteketeza Ari+ la Moabu, wanaomiliki mahali pa juu pa Arnoni.
29 Ole wako, Moabu! Hakika mtaangamia, enyi watu wa Kemoshi!+
Hakika atawafanya wanawe kama watu walioponyoka na binti zake kuwa utekwani mkononi mwa mfalme wa Waamori, Sihoni.
30 Kwa hiyo na tuwapige mishale.
Hakika Heshboni ataangamia mpaka Diboni,+
Nao wanawake mpaka Nofa, wanaume mpaka Medeba.”+
31 Na Israeli akaanza kukaa katika nchi ya Waamori.+ 32 Ndipo Musa akatuma watu fulani wakapeleleze Yazeri.+ Kwa hiyo wakateka miji yake ya kandokando na kuwaondolea mbali Waamori waliokuwa humo.+ 33 Baada ya hapo wakageuka, wakapanda wakipitia njia ya Bashani.+ Ndipo Ogu+ mfalme wa Bashani akatoka nje ili kukutana nao, yeye pamoja na watu wake wote, katika vita vya Edrei.+ 34 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Usimwogope,+ kwa maana nitamtia yeye na watu wake wote na nchi yake mkononi mwako;+ nawe utamtendea kama vile ulivyomtendea Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekuwa akikaa Heshboni.”+ 35 Basi wakampiga yeye pamoja na wanawe na watu wake wote, mpaka ikawa hakuna mwokokaji aliyebaki kwake;+ nao wakaitwaa nchi yake.+
22 Ndipo wana wa Israeli wakaondoka na kupiga kambi kwenye nchi tambarare za jangwa la Moabu+ ng’ambo ya Yordani kutoka Yeriko. 2 Na Balaki+ mwana wa Sipori akaona mambo yote ambayo Israeli alikuwa amewatendea Waamori. 3 Na Moabu akawaogopa sana watu hao, kwa sababu walikuwa wengi; na Moabu akaanza kuhofu na kuchukizwa kwa sababu ya wana wa Israeli.+ 4 Na Moabu akawaambia wanaume wazee wa Midiani:+ “Sasa hili kutaniko litaramba mazingira yenu yote kama ng’ombe anavyoramba majani ya shambani.”
Na Balaki+ mwana wa Sipori alikuwa mfalme wa Moabu wakati huo hasa. 5 Sasa akatuma wajumbe kwa Balaamu+ mwana wa Beori huko Pethori,+ kando ya Mto+ wa nchi ya wana wa watu wake, aitwe, na kusema: “Tazama! Watu wametoka Misri. Tazama! Wameijaza nchi kwa kadiri ambayo mtu anaweza kuona,+ nao wanakaa mbele yangu. 6 Basi sasa njoo, tafadhali; uwalaani+ watu hawa kwa ajili yangu, kwa maana ni wenye nguvu kuliko mimi. Huenda nitaweza kuwapiga nami niwafukuze kutoka katika nchi; kwa maana najua vema kwamba yule unayembariki ni mtu aliyebarikiwa naye yule unayemlaani, amelaaniwa.”+
7 Basi wanaume wazee wa Moabu na wanaume wazee wa Midiani wakasafiri wakiwa na malipo ya uaguzi+ mikononi mwao nao wakaenda kwa Balaamu+ na kumwambia maneno ya Balaki. 8 Ndipo akawaambia: “Kaeni hapa usiku wa leo, nami nitawajibu ninyi kama vile tu Yehova atakavyosema nami.”+ Basi wakuu wa Moabu wakakaa pamoja na Balaamu.
9 Ndipo Mungu akamjia Balaamu na kusema:+ “Wanaume hawa walio pamoja nawe ni nani?” 10 Kwa hiyo Balaamu akamwambia Mungu wa kweli: “Balaki+ mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, amewatuma kwangu, na kusema, 11 ‘Tazama! Watu wanaotoka Misri, nao wanaifunika dunia kufikia upeo wa macho.+ Sasa njoo, uwalaani kwa ajili yangu.+ Huenda nitaweza kupigana nao na kuwafukuza.’” 12 Lakini Mungu akamwambia Balaamu: “Usiende pamoja nao. Usiwalaani watu hao,+ kwa maana wamebarikiwa.”+
13 Kisha Balaamu akaondoka asubuhi na kuwaambia wakuu wa Balaki: “Nendeni katika nchi yenu, kwa sababu Yehova amekataa kuniruhusu niende pamoja nanyi.” 14 Kwa hiyo wakuu wa Moabu wakaondoka, wakamjia Balaki na kusema: “Balaamu amekataa kuja pamoja nasi.”+
15 Hata hivyo, Balaki akatuma tena wakuu wengine, wengi zaidi na wenye kuheshimika zaidi kuliko wale wa kwanza. 16 Nao wakaja kwa Balaamu na kumwambia: “Hivi ndivyo ambavyo Balaki mwana wa Sipori amesema, ‘Tafadhali, usizuiliwe kuja kwangu. 17 Kwa maana hakika nitakuheshimu wewe sana,+ na kila kitu ambacho utaniambia nitafanya.+ Kwa hiyo njoo, tafadhali. Walaani watu hawa kwa ajili yangu.’” 18 Lakini Balaamu akajibu na kuwaambia watumishi wa Balaki: “Hata kama Balaki angenipa nyumba yake ikiwa imejaa fedha na dhahabu, singeweza kupita agizo la Yehova Mungu wangu, ili kufanya jambo dogo au kubwa.+ 19 Basi sasa ninyi pia kaeni hapa, tafadhali, usiku wa leo nipate kujua Yehova ataniambia nini zaidi.”+
20 Ndipo Mungu akamjia Balaamu usiku na kumwambia: “Ikiwa wanaume hao wamekuja kukuita, ondoka, nenda pamoja nao. Lakini neno nitakalosema nawe ndilo tu utakalosema.”+ 21 Kisha Balaamu akaondoka asubuhi, akamtandika punda-jike wake, akaenda pamoja na wakuu wa Moabu.+
22 Nayo hasira ya Mungu ikaanza kuwaka kwa sababu alikuwa akienda; na malaika wa Yehova akasimama barabarani ili kumzuia.+ Naye alikuwa amepanda juu ya punda-jike wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye. 23 Na yule punda akamwona malaika wa Yehova akiwa amesimama barabarani, upanga wake uliochomolewa ukiwa mkononi mwake;+ na yule punda akajaribu kugeuka kando kutoka barabarani aende shambani, lakini Balaamu akaanza kumpiga punda ili kumgeuza na kumrudisha barabarani. 24 Naye malaika wa Yehova akaendelea kusimama katika hiyo njia nyembamba katikati ya mashamba ya mizabibu, yenye ukuta wa mawe upande huu na ukuta wa mawe upande ule. 25 Naye punda-jike huyo akaendelea kumwona malaika wa Yehova na kuanza kujifinyia ukutani na hivyo kuufinya mguu wa Balaamu ukutani; naye akazidi kumpiga.
26 Sasa malaika wa Yehova akapita tena na kusimama mahali pembamba, ambapo hapakuwa na njia ya kugeuka kuume wala kushoto. 27 Punda huyo alipomwona malaika wa Yehova akalala chini, chini ya Balaamu; hivi kwamba hasira ya Balaamu ikawaka,+ naye akaendelea kumpiga punda kwa fimbo yake. 28 Mwishowe Yehova akafungua kinywa cha punda+ huyo naye akamwambia Balaamu: “Nimekutendea nini hivi kwamba umenipiga mara tatu hizi?”+ 29 Ndipo Balaamu akamwambia punda huyo: “Ni kwa sababu umenitendea bila huruma. Laiti ningalikuwa na upanga mkononi mwangu, kufikia sasa ningalikuwa nimekuua!”+ 30 Kisha yule punda-jike akamwambia Balaamu: “Je, mimi si punda wako ambaye umepanda maisha yako yote mpaka leo hii? Je, nimezoea kukutendea hivi?”+ Akajibu: “Hapana!” 31 Na Yehova akafungua macho+ ya Balaamu, naye akamwona malaika wa Yehova amesimama katika barabara na upanga wake uliochomolewa ukiwa mkononi mwake. Mara moja akainama chini na kujilaza kifudifudi.
32 Ndipo malaika wa Yehova akamwambia: “Kwa nini umempiga punda wako mara hizi tatu? Tazama! Mimi—mimi nimekuja kukuzuia, kwa sababu njia yako imekwenda moja kwa moja kinyume cha mapenzi yangu.+ 33 Naye punda aliniona na kujaribu kugeuka kando mbele yangu mara tatu hizi.+ Tuseme asingekuwa amegeuka kando kutoka mbele yangu! Kufikia sasa ningekuwa nimekuua,+ lakini yeye ningemhifadhi hai.” 34 Ndipo Balaamu akamwambia malaika wa Yehova: “Nimetenda dhambi,+ kwa sababu sikujua kwamba ni wewe uliyekuwa umesimama barabarani ili kukutana nami. Basi sasa, ikiwa ni vibaya machoni pako, acha nirudi zangu.” 35 Lakini malaika wa Yehova akamwambia Balaamu: “Nenda pamoja na wanaume hao;+ nawe hutasema lolote isipokuwa lile neno nitakalokuambia.”+ Naye Balaamu akaendelea kwenda pamoja na wakuu wa Balaki.
36 Balaki aliposikia kwamba Balaamu amekuja, mara moja akatoka ili kumpokea katika jiji la Moabu, lililo kwenye ukingo wa Arnoni, lililo mwishoni mwa eneo hilo.+ 37 Ndipo Balaki akamwambia Balaamu: “Je, kwa kweli sikutuma watu wakuite? Kwa nini hukuja kwangu? Je, kwa kweli mimi siwezi kukuheshimu wewe kwelikweli?”+ 38 Basi Balaamu akamwambia Balaki: “Tazama, nimekuja kwako sasa. Je, nitaweza kusema jambo fulani?+ Neno ambalo Mungu atatia kinywani mwangu ndilo nitakalosema.”+
39 Kwa hiyo Balaamu akaenda pamoja na Balaki nao wakafika Kiriath-husothi. 40 Na Balaki akatoa dhabihu ng’ombe na kondoo+ na kupeleka sehemu yake kwa Balaamu na wale wakuu waliokuwa pamoja naye. 41 Na ikawa kwamba asubuhi Balaki akamchukua Balaamu na kumleta mpaka Bamoth-baali,+ ili kutoka huko awaone watu wote.+
23 Kisha Balaamu akamwambia Balaki: “Nijengee mahali hapa madhabahu saba+ na unitayarishie mahali hapa ng’ombe-dume saba na kondoo-dume saba.” 2 Balaki akafanya mara moja kama vile Balaamu alivyokuwa amesema. Kisha Balaki na Balaamu wakatoa ng’ombe-dume mmoja na kondoo-dume mmoja juu ya kila madhabahu.+ 3 Na Balaamu akamwambia Balaki: “Simama kando ya toleo lako la kuteketezwa,+ nami niende. Labda Yehova atawasiliana nami na kukutana nami.+ Ndipo lolote atakalonionyesha, hakika nitakuambia.” Basi akaenda kwenye kilima kilicho wazi.
4 Mungu alipowasiliana na Balaamu,+ Balaamu akamwambia: “Niliweka madhabahu saba katika mistari, nami nikatoa ng’ombe-dume mmoja na kondoo-dume mmoja juu ya kila madhabahu.”+ 5 Basi Yehova akatia neno katika kinywa cha Balaamu+ na kusema: “Rudi kwa Balaki, na hili ndilo utakalosema.”+ 6 Basi akarudi kwake, na, tazama! yeye na wakuu wote wa Moabu walikuwa wamesimama kando ya toleo lake la kuteketezwa. 7 Kisha akaanza neno lake la kimethali+ na kusema:
“Kutoka Aramu+ Balaki mfalme wa Moabu alijaribu kuniongoza,
Kutoka katika milima ya mashariki:
‘Njoo, mlaani Yakobo kwa ajili yangu.
Naam, njoo, washutumu Israeli.’+
8 Ningewezaje kuwalaani wale ambao Mungu hajawalaani?+
Nami ningewezaje kuwashutumu wale ambao Yehova hajawashutumu?+
9 Kwa maana kutoka juu ya miamba nawaona wao,
Na kutoka vilimani nawatazama wao.
Wakiwa kikundi cha watu wanaendelea kukaa wakiwa wamejitenga,+
Nao hawajihesabu katikati ya mataifa.+
10 Ni nani ambaye amehesabu chembe za mavumbi ya Yakobo+
Na ni nani ambaye amehesabu sehemu ya nne ya Israeli?
Nafsi yangu na ife kifo cha wanyoofu,+
Na mwisho wangu na uwe kama ule wao mwishowe.”+
11 Hapo Balaki akamwambia Balaamu: “Umenitendea nini? Nilikuchukua ili uwalaani adui zangu, na, tazama, umewabariki kwelikweli.”+ 12 Naye akajibu na kusema: “Je, lolote ambalo Yehova ametia katika kinywa changu silo ninalopaswa kuwa mwangalifu kulisema?”+
13 Ndipo Balaki akamwambia: “Njoo, tafadhali, pamoja nami mpaka mahali pengine ambapo unaweza kuwaona. Ila utauona mwisho wao tu, nawe hutawaona+ wote. Nawe uwalaani kwa ajili yangu kutoka huko.”+ 14 Basi akampeleka mpaka uwanja wa Sofimu, mpaka juu ya Pisga,+ na kujenga madhabahu saba na kutoa ng’ombe-dume mmoja na kondoo-dume mmoja juu ya kila madhabahu.+ 15 Kisha akamwambia Balaki: “Simama hapa kando ya toleo lako la kuteketezwa, na mimi nami acha niwasiliane naye pale.” 16 Basi Yehova akawasiliana na Balaamu na kutia neno katika kinywa chake na kusema:+ “Rudi kwa Balaki,+ na hili ndilo utakalosema.” 17 Basi akaja kwake, na, tazama! alikuwa amesimama kando ya toleo lake la kuteketezwa, na wakuu wa Moabu pamoja naye. Ndipo Balaki akamwambia: “Yehova amesema nini?” 18 Basi akaanza neno lake la kimethali na kusema:+
“Ondoka, Balaki, usikilize.
Tega sikio kwangu, Ee mwana wa Sipori.+
19 Mungu si mwanadamu kwamba aseme uwongo,+
Wala si mwana wa binadamu kwamba ajute.+
Je, yeye mwenyewe amelisema naye hatalitenda,
Na je, yeye amesema naye hatalitimiza?+
21 Hajatazama nguvu zozote za uchawi+ juu ya Yakobo,
Wala hajaona taabu yoyote juu ya Israeli.
Yehova Mungu wake yuko pamoja naye,+
Na sauti ya mfalme iko katikati yake.
23 Kwa maana hakuna apizo lolote la bahati mbaya juu ya Yakobo,+
Wala uaguzi wowote juu ya Israeli.+
Na wakati huu inaweza kusemwa juu ya Yakobo na Israeli,
‘Mungu ametenda nini!’+
24 Tazama, kikundi cha watu kitasimama kama simba,
Na kama simba kitajiinua.+
Hakitalala chini mpaka kile mawindo,
Na damu ya waliouawa kitakunywa.”+
25 Hapo Balaki akamwambia Balaamu: “Ikiwa, kwa upande mmoja, huwezi kumlaani hata kidogo, basi, kwa upande mwingine, hupaswi kumbariki hata kidogo.” 26 Naye Balaamu akajibu na kumwambia Balaki: “Je, sikusema nawe, na kukuambia, ‘Yote ambayo Yehova atasema ndiyo nitakayotenda’?”+
27 Ndipo Balaki akamwambia Balaamu: “Njoo, tafadhali. Acha nikupeleke mahali pengine tena. Labda itakuwa sawa machoni pa Mungu wa kweli ili upate kuwalaani kwa ajili yangu kutoka huko.”+ 28 Kwa hiyo Balaki akamchukua Balaamu mpaka juu ya Peori, unaoelekea Yeshimoni.+ 29 Kisha Balaamu+ akamwambia Balaki: “Nijengee mahali hapa madhabahu saba na unitayarishie mahali hapa ng’ombe-dume saba na kondoo-dume saba.”+ 30 Basi Balaki akafanya kama vile Balaamu alivyokuwa amesema, naye akatoa ng’ombe-dume mmoja na kondoo-dume mmoja kwenye kila madhabahu.+
24 Balaamu alipoona kwamba ilikuwa vema machoni pa Yehova kubariki Israeli, hakuenda kama zile mara nyingine+ na kutafuta ishara zozote za bahati mbaya,+ bali alielekeza uso wake nyikani. 2 Balaamu alipoinua macho yake na kumwona Israeli akikaa kulingana na makabila yake,+ ndipo roho ya Mungu ikaja juu yake.+ 3 Basi akaanza neno lake la kimethali+ na kusema:
“Neno la Balaamu mwana wa Beori,
Na neno la mwanamume jicho likiwa limefunguliwa,+
4 Neno la mtu anayesikia maneno ya Mungu,+
Aliyeona maono ya Mweza-Yote+
Alipokuwa akianguka chini macho yakiwa yamefunguliwa:+
5 Ni yenye kupendeza kama nini mahema yako, Ee Yakobo, maskani zako, Ee Israeli!+
6 Yameenea mbali kama mabonde ya mto,+
Kama bustani kando ya mto.+
Kama mimea ya udi ambayo Yehova amepanda,
Kama mierezi kando ya maji.+
7 Maji yanatiririka kutoka katika ndoo zake mbili za ngozi,
Na mbegu yake iko kando ya maji mengi.+
Mfalme+ wake pia atakuwa juu kuliko Agagi,+
Na ufalme wake utainuliwa juu.+
8 Mungu anamleta kutoka Misri;
Ule mwendo mwepesi wa ng’ombe-dume wa mwituni ni wake.+
Atayateketeza mataifa, wakandamizaji wake,+
Na mifupa yao ataitafuna-tafuna,+ naye atawavunja vipande-vipande kwa mishale yake.+
9 Aliinama chini, akalala kama simba,
Na, kama simba, ni nani anayethubutu kumwamsha?+
Wale wanaokubariki ndio waliobarikiwa,+
Nao wale wanaokulaani ndio waliolaaniwa.”+
10 Ndipo hasira ya Balaki ikawaka juu ya Balaamu naye akapiga makofi,+ naye Balaki akamwambia Balaamu: “Nilikuita ili uwalaani+ adui zangu, na, tazama! umewabariki kabisa mara hizi tatu. 11 Basi sasa kimbia uende kwako. Nilikuwa nimesema moyoni mwangu kwamba nitakuheshimu wewe,+ lakini, tazama! Yehova amekuzuilia usipate heshima.”
12 Naye Balaamu akamwambia Balaki: “Je, sikuwaambia wajumbe wako uliowatuma kwangu na kusema, 13 ‘Hata ikiwa Balaki angenipa nyumba yake iliyojaa fedha na dhahabu, singeweza kupita agizo la Yehova na kufanya jambo jema au baya kutoka moyoni mwangu mwenyewe. Lolote lile ambalo Yehova atasema ndilo nitakalosema’?+ 14 Na sasa, tazama, naenda zangu kwa watu wangu. Njoo, acha nikushauri+ wewe mambo ambayo watu hawa watawatendea watu wako baadaye katika siku za mwisho.”+ 15 Kwa hiyo akaanza neno lake la kimethali+ na kusema:
“Neno la Balaamu mwana wa Beori,
Na neno la mwanamume jicho likiwa limefunguliwa,+
16 Neno la yule anayesikia maneno ya Mungu,+
Na yule anayejua ujuzi wa Aliye Juu Zaidi—
Maono ya Mweza-Yote aliyaona+
Alipokuwa akianguka chini macho yake yakiwa yamefunguliwa:+
Nitamtazama, bali si karibu.
Nyota+ itatokea katika Yakobo,
Na fimbo ya enzi itainuka katika Israeli.+
Naye atavunja vipaji vya kichwa cha Moabu+
Na fuvu la kichwa cha wana wote wa fujo ya vita.
19 Na kutoka katika Yakobo mtu ataenda akitiisha,+
Naye atamharibu mwokokaji yeyote kutoka katika jiji.”+
20 Alipomwona Amaleki, akaendeleza neno lake la kimethali na kusema:+
“Amaleki alikuwa wa kwanza wa mataifa,+
Lakini mwisho wake baadaye utakuwa kuangamia kwake.”+
21 Alipowaona Wakeni,+ akaendeleza neno lake la kimethali na kuendelea kusema:
“Makao yako ni yenye kudumu, na makao yako yamewekwa juu ya mwamba.
22 Lakini kutakuwa na mtu wa kuteketeza Kayini.+
Itachukua muda mrefu kadiri gani mpaka Ashuru atakapokuchukua mateka?”+
23 Naye akaendeleza neno lake la kimethali na kuendelea kusema:
“Ole! Ni nani atakayeokoka wakati Mungu atakapolisababisha?+
24 Na kutakuwako meli kutoka pwani ya Kitimu,+
Nazo hakika zitatesa Ashuru,+
Nazo zitatesa Eberi kwelikweli.
Lakini yeye pia ataangamia mwishowe.”
25 Kisha Balaamu akaondoka, akaenda na kurudi kwake.+ Na Balaki pia akaenda zake.
25 Sasa Israeli alikuwa akikaa Shitimu.+ Ndipo watu wakaanza kufanya uasherati na binti za Moabu.+ 2 Na wanawake hao wakaja kuwaita watu waende kwenye dhabihu za miungu yao,+ nao watu wakaanza kula na kuinamia miungu yao.+ 3 Kwa hiyo Israeli akajishikamanisha na Baali wa Peori;+ nayo hasira ya Yehova ikaanza kuwaka juu ya Israeli.+ 4 Basi Yehova akamwambia Musa: “Chukua wote walio vichwa vya watu nawe uwaanike mbele za Yehova kuelekea jua, ili hasira inayowaka ya Yehova+ igeukie mbali na Israeli.” 5 Ndipo Musa akawaambia waamuzi wa Israeli:+ “Kila mmoja wenu awaue+ watu wake ambao wameshikamana na Baali wa Peori.”
6 Lakini, tazama! mwanamume+ mmoja kati ya wana wa Israeli akaja, naye alikuwa akimleta mwanamke Mmidiani+ karibu na ndugu zake, mbele ya macho ya Musa na mbele ya macho ya kusanyiko lote la wana wa Israeli, walipokuwa wakilia kwenye mwingilio wa hema la mkutano. 7 Finehasi+ mwana wa Eleazari mwana wa Haruni kuhani alipoona hilo, akainuka mara moja kutoka katikati ya kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake. 8 Kisha akamfuata yule mwanamume wa Israeli ndani ya hema lenye kuba na kuwachoma wote wawili, mwanamume huyo wa Israeli na mwanamke huyo kupitia sehemu zake za uzazi. Ndipo tauni ikakomeshwa kutoka kwa wana wa Israeli.+ 9 Nao waliokufa kutokana na tauni hiyo walijumlika kuwa 24,000.+
10 Kisha Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 11 “Finehasi+ mwana wa Eleazari mwana wa Haruni kuhani ameigeuzia mbali ghadhabu+ yangu kutoka juu ya wana wa Israeli kwa kutovumilia kwake ushindani wowote kunielekea mimi katikati yao,+ hivi kwamba sikuwaangamiza wana wa Israeli kwa kusisitiza kwangu kwamba watu wajitoe kikamili.+ 12 Kwa sababu hiyo, ‘Tazama, nampa yeye agano langu la amani. 13 Nalo litatumika kama agano la ukuhani mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili yake na uzao wake baada yake,+ kwa kuwa hakuvumilia ushindani wowote kumwelekea Mungu+ wake naye alifanya upatanisho kwa ajili ya wana wa Israeli.’”+
14 Jina la mwanamume huyo Mwisraeli aliyepigwa na kuuawa pamoja na yule mwanamke Mmidiani lilikuwa Zimri mwana wa Salu, mkuu+ wa nyumba ya ukoo wa upande wa baba ya Wasimeoni. 15 Nalo jina la mwanamke Mmidiani aliyepigwa na kuuawa lilikuwa Kozbi binti ya Suri;+ huyo alikuwa kichwa katika ukoo wa nyumba ya upande wa baba yake katika Midiani.+
16 Baadaye Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 17 “Wamidiani na wasumbuliwe, nanyi mtawapiga,+ 18 kwa sababu wanawasumbua ninyi kwa matendo yao ya ujanja+ ambayo wamewatendea ninyi kwa ujanja katika lile jambo la Peori+ na katika lile jambo la Kozbi+ binti ya mkuu wa Midiani, dada yao ambaye alipigwa na kuuawa+ katika ile siku ya tauni kuhusu lile jambo la Peori.”+
26 Na ikawa kwamba baada ya tauni hiyo,+ Yehova akamwambia hivi Musa na Eleazari mwana wa Haruni kuhani: 2 “Chukueni hesabu ya kusanyiko lote la wana wa Israeli kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kulingana na nyumba ya baba zao, wale wote wanaoingia jeshini katika Israeli.”+ 3 Naye Musa na Eleazari+ kuhani wakaanza kusema nao katika nchi tambarare za jangwa la Moabu+ kando ya Mto Yordani huko Yeriko,+ na kuwaambia: 4 “Chukueni hesabu yao kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.”+
Sasa wana wa Israeli waliotoka nchi ya Misri walikuwa: 5 Rubeni, mzaliwa wa kwanza+ wa Israeli; wana wa Rubeni: Wa Hanoki+ familia ya Wahanoki; wa Palu+ familia ya Wapalu; 6 wa Hezroni+ familia ya Wahezroni; wa Karmi+ familia ya Wakarmi. 7 Hizo ndizo zilizokuwa familia za Warubeni, nao walioandikishwa kati yao walijumlika kuwa 43,730.+
8 Na mwana wa Palu alikuwa Eliabu. 9 Nao wana wa Eliabu: Nemueli na Dathani na Abiramu. Dathani+ huyu na Abiramu+ walikuwa watu walioitwa na kusanyiko, ambao walipambana na Musa na Haruni katika kusanyiko la Kora,+ walipopambana na Yehova.
10 Ndipo dunia ikafungua kinywa chake na kuwameza.+ Naye Kora, alikufa kwenye kifo cha kusanyiko wakati ambapo moto uliwateketeza watu 250.+ Nao wakaja kuwa mfano.+ 11 Hata hivyo, wana wa Kora hawakufa.+
12 Wana wa Simeoni+ kulingana na familia zao: wa Nemueli+ familia ya Wanemueli; wa Yamini+ familia ya Wayamini; wa Yakini+ familia ya Wayakini; 13 wa Zera familia ya Wazera; wa Shauli+ familia ya Washauli. 14 Hizo ndizo zilizokuwa familia za Wasimeoni: 22,200.+
15 Wana wa Gadi+ kulingana na familia zao: Wa Sefoni familia ya Wasefoni; wa Hagi familia ya Wahagi; wa Shuni familia ya Washuni; 16 wa Ozni familia ya Waozni; wa Eri familia ya Waeri; 17 wa Arodi familia ya Waarodi; wa Areli+ familia ya Waareli. 18 Hizo ndizo zilizokuwa familia za wana wa Gadi, za walioandikishwa kati yao: 40,500.+
19 Wana wa Yuda+ walikuwa Eri+ na Onani.+ Hata hivyo, Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani.+ 20 Nao wana wa Yuda wakawa, kulingana na familia zao: Wa Shela+ familia ya Washela; wa Perezi+ familia ya Waperezi; wa Zera+ familia ya Wazera. 21 Nao wana wa Perezi wakawa: Wa Hezroni+ familia ya Wahezroni; wa Hamuli+ familia ya Wahamuli. 22 Hizo ndizo zilizokuwa familia za Yuda,+ za walioandikishwa kati yao: 76,500.+
23 Wana wa Isakari+ kulingana na familia zao walikuwa: Wa Tola+ familia ya Watola; wa Puva familia ya Wapuni; 24 wa Yashubu familia ya Wayashubu; wa Shimroni+ familia ya Washimroni. 25 Hizo ndizo zilizokuwa familia za Isakari, za walioandikishwa kati yao: 64,300.+
26 Wana wa Zabuloni+ kulingana na familia zao walikuwa: Wa Seredi familia ya Waseredi; wa Eloni familia ya Waeloni; wa Yahleeli+ familia ya Wayahleeli. 27 Hizo ndizo zilizokuwa familia za Wazabuloni, za walioandikishwa kati yao: 60,500.+
28 Wana wa Yosefu+ kulingana na familia zao walikuwa Manase na Efraimu.+ 29 Wana wa Manase+ walikuwa: Wa Makiri+ familia ya Wamakiri. Naye Makiri akamzaa Gileadi.+ Wa Gileadi familia ya Wagileadi. 30 Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi: Wa Yezeri+ familia ya Wayezeri; wa Heleki familia ya Waheleki; 31 wa Asrieli familia ya Waasrieli; wa Shekemu familia ya Washekemu; 32 wa Shemida+ familia ya Washemida; wa Heferi+ familia ya Waheferi. 33 Sasa Selofehadi mwana wa Heferi hakuwa na wana, bali binti,+ na majina ya binti za Selofehadi yalikuwa Mala na Noa, Hogla, Milka na Tirsa.+ 34 Hizo ndizo zilizokuwa familia za Manase, nao walioandikishwa kati yao walikuwa 52,700.+
35 Hawa ndio waliokuwa wana wa Efraimu+ kulingana na familia zao: Wa Shuthela+ familia ya Washuthela; wa Bekeri familia ya Wabekeri; wa Tahani+ familia ya Watahani. 36 Nao hawa ndio wana wa Shuthela: Wa Erani familia ya Waerani. 37 Hizo ndizo zilizokuwa familia za wana wa Efraimu,+ za walioandikishwa kati yao: 32,500. Hao ndio waliokuwa wana wa Yosefu kulingana na familia zao.+
38 Wana wa Benyamini+ kulingana na familia zao walikuwa: Wa Bela+ familia ya Wabela; wa Ashbeli+ familia ya Waashbeli; wa Ahiramu familia ya Waahiramu; 39 wa Shefufamu familia ya Washufamu; wa Hufamu+ familia ya Wahufamu. 40 Wana wa Bela wakawa Ardi na Naamani:+ Wa Ardi familia ya Waardi; wa Naamani familia ya Wanaamani. 41 Hao ndio waliokuwa wana wa Benyamini+ kulingana na familia zao, nao walioandikishwa kati yao walikuwa 45,600.+
42 Hawa ndio waliokuwa wana wa Dani+ kulingana na familia zao: Wa Shuhamu familia ya Washuhamu. Hizo ndizo zilizokuwa familia za Dani+ kulingana na familia zao. 43 Familia zote za Washuhamu, za walioandikishwa kati yao, walikuwa 64,400.+
44 Wana wa Asheri+ kulingana na familia zao walikuwa: Wa Imna+ familia ya Waimna; wa Ishvi+ familia ya Waishvi; wa Beria familia ya Waberia; 45 wa wana wa Beria: Wa Heberi familia ya Waheberi; wa Malkieli+ familia ya Wamalkieli. 46 Nalo jina la binti ya Asheri lilikuwa Sera.+ 47 Hizo ndizo zilizokuwa familia za wana wa Asheri,+ za walioandikishwa kati yao: 53,400.+
48 Wana wa Naftali+ kulingana na familia zao walikuwa: Wa Yahzeeli+ familia ya Wayahzeeli; wa Guni+ familia ya Waguni; 49 wa Yezeri+ familia ya Wayezeri; wa Shilemu+ familia ya Washilemu. 50 Hizo ndizo zilizokuwa familia za Naftali+ kulingana na familia zao, nao walioandikishwa kati yao walikuwa 45,400.+
51 Hawa ndio walioandikishwa kati ya wana wa Israeli: 601,730.+
52 Kisha Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 53 “Kwa hawa nchi itagawanywa kwa ajili ya urithi kulingana na hesabu ya majina yao.+ 54 Kulingana na hesabu kubwa utaongeza urithi wa mtu, na kulingana na uchache utapunguza urithi wa mtu.+ Kila urithi wa mtu utatolewa kulingana na watu wake walioandikishwa. 55 Nchi itagawanywa kwa kura+ tu. Kulingana na majina ya makabila ya baba zao watapata urithi. 56 Kwa uamuzi wa kura urithi wa mtu utagawanywa kati ya walio wengi na walio wachache.”
57 Sasa hawa ndio walioandikishwa wa Walawi+ kulingana na familia zao: Wa Gershoni+ familia ya Wagershoni; wa Kohathi+ familia ya Wakohathi; wa Merari+ familia ya Wamerari. 58 Hizi ndizo zilizokuwa familia za Walawi: familia ya Walibni,+ familia ya Wahebroni,+ familia ya Wamali,+ familia ya Wamushi,+ familia ya Wakora.+
Na Kohathi+ akamzaa Amramu.+ 59 Nalo jina la mke wa Amramu lilikuwa Yokebedi,+ binti ya Lawi, ambaye mke wake alimzalia Lawi katika Misri. Baada ya muda akamzalia Amramu Haruni na Musa na Miriamu dada yao.+ 60 Kisha Haruni akazaa Nadabu na Abihu,+ Eleazari na Ithamari.+ 61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa kwa sababu ya kutoa moto haramu mbele za Yehova.+
62 Nao walioandikishwa kati yao wakawa 23,000, wanaume wote kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi.+ Kwa maana hawakuandikishwa katikati ya wana wa Israeli,+ kwa sababu hawakupaswa kupewa urithi wowote katikati ya wana wa Israeli.+
63 Hawa ndio walioandikishwa na Musa na Eleazari kuhani walipowaandikisha wana wa Israeli katika nchi tambarare za jangwa la Moabu kando ya Yordani huko Yeriko.+ 64 Lakini kati ya hao hakukuwa na mtu kati ya wale walioandikishwa na Musa na Haruni kuhani wakati ambapo waliwaandikisha wana wa Israeli katika nyika ya Sinai.+ 65 Kwa maana Yehova alikuwa amesema hivi juu yao: “Lazima watakufa nyikani.”+ Kwa hiyo hakubaki mtu yeyote kati yao isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+
27 Ndipo binti za Selofehadi+ mwana wa Heferi mwana wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase,+ wa familia za Manase mwana wa Yosefu, wakaja karibu. Na haya ndiyo yaliyokuwa majina ya binti zake: Mala, Noa na Hogla na Milka na Tirsa.+ 2 Nao wakasimama mbele ya Musa na mbele ya Eleazari kuhani+ na mbele ya wakuu na kusanyiko lote kwenye mwingilio wa hema la mkutano, na kusema: 3 “Baba yetu alikufa nyikani,+ wala hakuwa katikati ya lile kusanyiko, yaani, wale waliojipanga dhidi ya Yehova katika kusanyiko la Kora,+ bali alikufa kutokana na dhambi yake mwenyewe;+ naye hakuwa na wana wowote wa kiume. 4 Kwa nini jina la baba yetu liondolewe kutoka katikati ya familia yake kwa sababu hakuwa na mwana?+ Tupe miliki katikati ya ndugu za baba yetu.”+ 5 Ndipo Musa akaiweka kesi yao mbele za Yehova.+
6 Kisha Yehova akamwambia Musa hivi: 7 “Binti za Selofehadi wanasema jambo lililo sawa. Wape miliki ya urithi katikati ya ndugu za baba yao, nawe utaupitisha urithi wa baba yao kwao.+ 8 Nawe utasema na wana wa Israeli, na kuwaambia, ‘Ikiwa mtu yeyote atakufa bila kuwa na mwana, mtaupitisha urithi wake kwa binti yake. 9 Na ikiwa hana binti, mtawapa ndugu zake urithi wake. 10 Na ikiwa hana ndugu, mtawapa ndugu za baba yake urithi wake. 11 Na ikiwa baba yake hana ndugu, mtampa urithi wake mtu wa familia yake aliye wa karibu zaidi na mwenye uhusiano wa damu,+ naye atauchukua. Nayo itatumika kama sheria kulingana na uamuzi wa hukumu kwa ajili ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.’”
12 Basi Yehova akamwambia Musa: “Nenda juu katika mlima huu wa Abarimu,+ ukaone nchi ambayo hakika nitawapa wana wa Israeli.+ 13 Ukiisha kuiona, ndipo utakusanywa kwa watu wako,+ naam, wewe, kama vile Haruni ndugu yako alivyokusanywa,+ 14 kwa sababu ninyi mliasi agizo langu katika nyika ya Zini kusanyiko lilipogombana,+ juu ya kunitakasa+ kando ya maji mbele ya macho yao. Hayo ndiyo maji ya Meriba+ huko Kadeshi+ katika nyika ya Zini.”+
15 Kisha Musa akasema na Yehova, na kumwambia: 16 “Yehova Mungu wa roho+ za namna zote za mwili+ na aweke rasmi juu ya kusanyiko mwanamume+ 17 ambaye atatoka nje mbele yao na ambaye ataingia ndani mbele yao na ambaye atawatoa nje na ambaye atawaingiza ndani,+ ili kusanyiko la Yehova lisiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”+ 18 Kwa hiyo Yehova akamwambia Musa: “Jichukulie Yoshua mwana wa Nuni, mwanamume ambaye ndani yake mna roho,+ nawe utaweka mkono wako juu yake;+ 19 nawe umsimamishe mbele ya Eleazari kuhani na mbele ya kusanyiko lote, nawe umpe utume mbele ya macho yao.+ 20 Nawe utatia sehemu ya utukufu wako juu yake,+ ili kusanyiko lote la wana wa Israeli lipate kumsikiliza yeye.+ 21 Naye atasimama mbele ya Eleazari kuhani, naye atauliza+ kwa ajili yake kulingana na hukumu ya Urimu+ mbele za Yehova. Kwa agizo lake watatoka nje na kwa agizo lake wataingia ndani, yeye na wana wote wa Israeli pamoja naye na kusanyiko lote.”
22 Naye Musa akafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru. Kwa hiyo akamchukua Yoshua na kumsimamisha mbele ya Eleazari+ kuhani na mbele ya kusanyiko lote 23 na kuweka mikono yake juu yake na kumpa utume,+ kama vile Yehova alivyokuwa amesema kupitia Musa.+
28 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Waamuru wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Muwe waangalifu na kunitolea toleo langu, mkate wangu,+ kwa ajili ya matoleo yangu yanayotolewa kwa njia ya moto yakiwa harufu ya kunituliza,+ kwenye nyakati zake zilizowekwa.’+
3 “Nawe utawaambia, ‘Hili ndilo toleo linalotolewa kwa njia ya moto ambalo mtamtolea Yehova: wana-kondoo dume ambao hawana kasoro wenye umri wa mwaka mmoja, wawili kila siku wakiwa toleo la kuteketezwa daima.+ 4 Mwana-kondoo dume mmoja utamtoa asubuhi, na yule mwana-kondoo dume mwingine utamtoa katikati ya zile jioni mbili,+ 5 pamoja na sehemu ya kumi ya efa+ ya unga laini ukiwa toleo la nafaka+ lililotiwa sehemu ya nne ya hini ya mafuta yaliyopondwa;+ 6 lile toleo la kuteketezwa la daima,+ lililotolewa kwenye Mlima Sinai likiwa harufu ya kutuliza, toleo lililotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto,+ 7 pamoja na toleo lake la kinywaji,+ sehemu ya nne ya hini kwa kila mwana-kondoo dume.+ Mimina katika mahali patakatifu lile toleo la kinywaji la kileo+ kwa Yehova. 8 Nawe utamtoa yule mwana-kondoo dume mwingine katikati ya zile jioni mbili. Pamoja na toleo lilelile la nafaka kama lile la asubuhi na pamoja na toleo lake lilelile la kinywaji utalitoa likiwa toleo linalotolewa kwa njia ya moto, toleo lenye harufu ya kumtuliza Yehova.+
9 “‘Hata hivyo, siku ya sabato+ kutakuwa wana-kondoo dume wawili ambao hawana kasoro wenye umri wa mwaka mmoja na vipimo viwili vya sehemu ya kumi ya unga laini ukiwa toleo la nafaka lililotiwa mafuta, pamoja na toleo lake la kinywaji, 10 likiwa toleo la kuteketezwa la sabato katika sabato yake, pamoja na lile toleo la kuteketezwa la daima+ na toleo lake la kinywaji.+
11 “‘Na mwanzoni mwa miezi yenu mtamtolea Yehova toleo la kuteketezwa la ng’ombe-dume wawili wachanga na kondoo-dume mmoja, wana-kondoo dume saba ambao hawana kasoro kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja,+ 12 na vipimo vitatu vya sehemu ya kumi ya unga laini ukiwa toleo la nafaka+ lililotiwa mafuta kwa ajili ya kila ng’ombe-dume na vipimo viwili vya sehemu ya kumi ya unga laini ukiwa toleo la nafaka lililotiwa mafuta kwa ajili ya kondoo-dume mmoja,+ 13 na kipimo kimoja cha sehemu ya kumi ya unga laini ukiwa toleo la nafaka lililotiwa mafuta kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume, likiwa toleo la kuteketezwa, harufu ya kutuliza,+ toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto. 14 Na kama matoleo yao ya kinywaji watatoa nusu+ ya hini ya divai kwa ajili ya ng’ombe-dume na sehemu ya tatu+ ya hini kwa ajili ya kondoo-dume na sehemu ya nne+ ya hini kwa ajili ya mwana-kondoo dume. Hilo ndilo toleo la kuteketezwa la kila mwezi katika mwezi wake kwa ajili ya miezi ya mwaka.+ 15 Pia, mwana-mbuzi+ mmoja atatolewa akiwa toleo la dhambi kwa Yehova kwa kuongezea lile toleo la kuteketezwa la daima pamoja na toleo lake la kinywaji.+
16 “‘Na katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi huo, itakuwa pasaka ya Yehova.+ 17 Na siku ya kumi na tano ya mwezi huu itakuwa sherehe. Keki zisizo na chachu zitaliwa kwa siku saba.+ 18 Katika siku ya kwanza kutakuwako mkusanyiko mtakatifu.+ Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote.+ 19 Nanyi mtatoa toleo linalotolewa kwa njia ya moto, toleo la kuteketezwa+ kwa Yehova, ng’ombe-dume wawili wachanga na kondoo-dume mmoja na wana-kondoo dume saba kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja.+ Wanapaswa kuwa wasio na kasoro kwa ajili yenu.+ 20 Na kama matoleo yao ya nafaka+ ya unga laini uliotiwa mafuta mtatoa vipimo vitatu vya sehemu ya kumi kwa ajili ya ng’ombe-dume na vipimo viwili vya sehemu ya kumi+ kwa ajili ya kondoo-dume. 21 Utatoa kipimo kimoja cha sehemu ya kumi+ kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo dume saba; 22 na mbuzi mmoja wa toleo la dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.+ 23 Mbali na lile toleo la kuteketezwa la asubuhi, ambalo ni kwa ajili ya toleo la kuteketezwa+ la daima,+ mtayatoa hayo. 24 Mtatoa matoleo kama hayo kila siku kwa zile siku saba kuwa mkate,+ toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto,+ lenye harufu ya kumtuliza Yehova. Litatolewa pamoja na toleo la kuteketezwa la daima, na toleo lake la kinywaji. 25 Na siku ya saba mtafanya mkusanyiko mtakatifu.+ Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote.+
26 “‘Na katika siku ya matunda yaliyoiva ya kwanza,+ mtakapomtolea Yehova toleo la nafaka mpya, katika sherehe yenu ya majuma+ mtafanya mkusanyiko mtakatifu. Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote.+ 27 Nanyi mtatoa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya harufu ya kumtuliza Yehova, ng’ombe-dume wawili wachanga, kondoo-dume mmoja, wana-kondoo dume saba kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja;+ 28 na kama toleo lao la nafaka la unga laini uliotiwa mafuta, vipimo vitatu vya sehemu ya kumi kwa ajili ya kila ng’ombe-dume, vipimo viwili vya sehemu ya kumi+ kwa ajili ya yule kondoo-dume, 29 kipimo kimoja cha sehemu ya kumi+ vivyo hivyo kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo dume saba; 30 mwana-mbuzi mmoja ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.+ 31 Mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima pamoja na toleo lake la nafaka mtawatoa.+ Watakuwa wasio na kasoro kwenu,+ pamoja na matoleo yao ya kinywaji.+
29 “‘Na katika mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi huo, mtafanya mkusanyiko mtakatifu.+ Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote.+ Itakuwa siku ya kupiga tarumbeta kwenu.+ 2 Nanyi mtatoa toleo la kuteketezwa kuwa harufu ya kumtuliza Yehova, ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, wana-kondoo dume saba, kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 3 na toleo lao la nafaka la unga laini uliotiwa mafuta, vipimo vitatu vya sehemu ya kumi kwa ajili ya yule ng’ombe-dume, vipimo viwili vya sehemu ya kumi kwa ajili ya yule kondoo-dume,+ 4 na kipimo kimoja cha sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mmoja kati ya wale wana-kondoo saba;+ 5 na mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu;+ 6 mbali na lile toleo la kuteketezwa+ la kila mwezi na toleo lake la nafaka+ na lile toleo la kuteketezwa la daima+ na toleo lake la nafaka,+ pamoja na matoleo yake ya kinywaji,+ kulingana na utaratibu wa kawaida kwa ajili yake, kuwa harufu ya kutuliza, toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+
7 “‘Na katika siku ya kumi ya mwezi huu mtafanya mkusanyiko mtakatifu,+ nanyi mtazitesa nafsi zenu.+ Hampaswi kufanya kazi yoyote.+ 8 Nanyi mtamtolea Yehova toleo la kuteketezwa, lenye harufu ya kutuliza, ng’ombe-dume mmoja mchanga, kondoo-dume mmoja, wana-kondoo dume saba kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja.+ Watakuwa wasio na kasoro kwa ajili yenu.+ 9 Na likiwa toleo lao la nafaka la unga laini uliotiwa mafuta vipimo vitatu vya sehemu ya kumi kwa ajili ya yule ng’ombe-dume, vipimo viwili vya sehemu ya kumi kwa ajili ya yule kondoo-dume mmoja,+ 10 kipimo kimoja cha sehemu ya kumi vivyo hivyo kwa ajili ya kila mmoja wa wale wana-kondoo saba;+ 11 mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi, mbali na lile toleo la dhambi la upatanisho+ na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka, pamoja na matoleo yake ya kinywaji.+
12 “‘Na katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba+ mtafanya mkusanyiko mtakatifu.+ Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote,+ nanyi mtamfanyia Yehova sherehe kwa siku saba.+ 13 Nanyi mtatoa toleo la kuteketezwa,+ toleo linalotolewa kwa njia ya moto, lenye harufu ya kumtuliza Yehova, ng’ombe-dume wachanga kumi na watatu, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Watakuwa wasio na kasoro.+ 14 Na toleo lao la nafaka la unga laini uliotiwa mafuta vipimo vitatu vya sehemu ya kumi kwa ajili ya kila ng’ombe-dume kati ya wale ng’ombe-dume kumi na watatu, vipimo viwili vya sehemu ya kumi kwa ajili ya kila kondoo-dume kati ya wale kondo-dume wawili,+ 15 na kipimo kimoja cha sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume kati ya wale wana-kondoo kumi na wanne;+ 16 na mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi, mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima, toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
17 “‘Na katika siku ya pili ng’ombe-dume wachanga kumi na wawili, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 18 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 19 na mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka, pamoja na matoleo yake ya kinywaji.+
20 “‘Na katika siku ya tatu ng’ombe-dume kumi na mmoja, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 21 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida; 22 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.
23 “‘Na katika siku ya nne ng’ombe-dume kumi, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 24 toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 25 na mwana-mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa+ la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
26 “‘Na katika siku ya tano ng’ombe-dume tisa, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 27 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 28 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
29 “‘Na katika siku ya sita ng’ombe-dume wanane, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 30 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 31 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na matoleo yake ya kinywaji.+
32 “‘Na katika siku ya saba ng’ombe-dume saba, kondoo-dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wanne kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 33 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya wale ng’ombe-dume, wale kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 34 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
35 “‘Na katika siku ya nane mtafanya kusanyiko kuu.+ Hamtafanya kazi ngumu ya aina yoyote.+ 36 Nanyi mtatoa toleo la kuteketezwa, toleo linalotolewa kwa njia ya moto, lenye harufu ya kumtuliza Yehova, ng’ombe-dume mmoja, kondoo-dume mmoja, wana-kondoo dume saba kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja, ambao hawana kasoro;+ 37 na toleo lao la nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ kwa ajili ya yule ng’ombe-dume, yule kondoo-dume na wale wana-kondoo kwa hesabu yao kulingana na utaratibu wa kawaida;+ 38 na mbuzi mmoja akiwa toleo la dhambi,+ mbali na lile toleo la kuteketezwa la daima na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
39 “‘Hayo mtamtolea Yehova kwenye sherehe zenu za majira,+ mbali na matoleo yenu ya nadhiri+ na matoleo yenu ya hiari+ yakiwa matoleo yenu ya kuteketezwa+ na matoleo yenu ya nafaka+ na matoleo yenu ya kinywaji+ na dhabihu zenu za ushirika.’”+ 40 Naye Musa akaongea na wana wa Israeli kulingana na kila jambo ambalo Yehova alikuwa amemwamuru Musa.+
30 Ndipo Musa akasema na vichwa+ vya makabila ya wana wa Israeli, na kuwaambia: “Hili ndilo neno ambalo Yehova ameamuru: 2 Ikiwa mwanamume ataweka nadhiri+ kwa Yehova au ikiwa ataapa kiapo+ ili kufunga nadhiri ya kujiepusha+ juu ya nafsi yake, hapaswi kulivunja neno lake.+ Anapaswa kufanya kulingana na yote ambayo yametoka kinywani mwake.+
3 “Na ikiwa mwanamke ataweka nadhiri kwa Yehova+ au akijifunga kwa nadhiri ya kujiepusha katika nyumba ya baba yake wakati wa ujana wake, 4 na kwa kweli baba yake asikie nadhiri yake au nadhiri yake ya kujiepusha ambayo amefunga juu ya nafsi yake, na baba yake akae kimya kumwelekea, nadhiri zake zote zitasimama pia, na kila nadhiri ya kujiepusha+ ambayo amefunga juu ya nafsi yake itasimama. 5 Lakini ikiwa baba yake amemkataza katika siku ya kusikia kwake nadhiri zake zote au nadhiri zake za kujiepusha ambazo amefunga juu ya nafsi yake, haitasimama, bali Yehova atamsamehe, kwa sababu baba yake alimkataza.+
6 “Hata hivyo, ikiwa yeye ana mume, nayo nadhiri yake iko juu yake+ au ile ahadi ya midomo yake, iliyotolewa bila kufikiri, iko juu ya nafsi yake, 7 na kwa kweli mume wake asikie na kukaa kimya kumwelekea siku ya kusikia kwake, nadhiri zake zitasimama au nadhiri zake za kujiepusha ambazo amefunga juu ya nafsi yake zitasimama.+ 8 Lakini ikiwa mume wake atamkataza katika siku ya kusikia kwake,+ yeye pia ameifuta nadhiri yake iliyokuwa juu yake au ile ahadi ya midomo yake, iliyotolewa bila kufikiri, ambayo aliifunga juu ya nafsi yake, na Yehova atamsamehe.+
9 “Kuhusu nadhiri ya mjane au mwanamke aliyepewa talaka, kila jambo ambalo amefunga juu ya nafsi yake litasimama dhidi yake.
10 “Hata hivyo, ikiwa ameweka nadhiri au amefunga nadhiri ya kujiepusha juu ya nafsi yake kwa kiapo+ katika nyumba ya mume wake, 11 na mume wake awe amesikia jambo hilo na kukaa kimya kumwelekea, hakumkataza; na nadhiri zake zote zitasimama au nadhiri yoyote ya kujiepusha ambayo amefunga juu ya nafsi yake itasimama. 12 Lakini ikiwa mume wake amezifuta kabisa katika siku ya kusikia kwake maneno yoyote ya midomo yake yakiwa nadhiri zake au nadhiri ya kujiepusha ya nafsi yake, hazitasimama.+ Mume wake amezifuta, na Yehova atamsamehe.+ 13 Nadhiri yoyote au kiapo chochote cha kujiepusha ili kuitesa nafsi,+ mume wake atakiimarisha au mume wake atakifuta. 14 Lakini ikiwa mume wake atakaa kimya kabisa kumwelekea siku baada ya siku, yeye ameziimarisha pia nadhiri zake zote au nadhiri zake zote za kujiepusha zilizo juu yake.+ Amezithibitisha kwa sababu alikaa kimya kumwelekea siku alipozisikia. 15 Na ikiwa atazifuta kabisa baada ya yeye kuzisikia, kwa kweli pia analichukua kosa la mke wake.+
16 “Hayo ndiyo masharti ambayo Yehova alimwamuru Musa yawe kati ya mume na mke wake,+ kati ya baba na binti yake wakati wa ujana wake katika nyumba ya baba yake.”+
31 Kisha Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Lipiza kisasi+ kwa ajili ya wana wa Israeli juu ya Wamidiani.+ Baadaye utakusanywa kwa watu wako.”+
3 Basi Musa akasema na watu, na kuwaambia: “Tayarisheni wanaume kati yenu kwa ajili ya jeshi, watumiwe kupiga Midiani ili kulipiza kisasi cha Yehova juu ya Midiani.+ 4 Watu elfu moja wa kila kabila kati ya makabila yote ya Israeli mtawatuma katika jeshi.” 5 Kwa hiyo kutoka kati ya maelfu+ ya Israeli watu elfu moja katika kabila walipewa mgawo, kumi na mbili elfu waliotayarishwa kwa ajili ya jeshi.+
6 Ndipo Musa akawatuma, watu elfu moja wa kila kabila, kwenye jeshi, wao na Finehasi+ mwana wa Eleazari kuhani kwenye jeshi, na vile vyombo vitakatifu na zile tarumbeta+ za kupiga mbiu zilikuwa mkononi mwake. 7 Nao wakapigana vita na Midiani, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa, nao wakamuua kila mwanamume.+ 8 Nao wakawaua wafalme wa Midiani pamoja na wengine waliouawa, yaani, Evi na Rekemu na Suri na Huru na Reba, wale wafalme watano wa Midiani;+ nao wakamuua Balaamu+ mwana wa Beori kwa upanga. 9 Lakini wana wa Israeli wakawachukua mateka wanawake wa Midiani na watoto wao wadogo;+ na wanyama wao wote wa kufugwa na mifugo yao yote na riziki yao yote wakaipora. 10 Nayo majiji yao yote walimokuwa wamefanya makao na kambi zao zenye kuta wakaziteketeza kwa moto.+ 11 Nao wakachukua nyara+ zote na kuteka nyara binadamu na wanyama wote wa kufugwa. 12 Nao wakamletea Musa na Eleazari kuhani na kusanyiko la wana wa Israeli mateka na nyara na vitu vilivyoporwa, mpaka kambini, mpaka nchi tambarare za jangwa la Moabu,+ kando ya Yordani huko Yeriko.
13 Ndipo Musa na Eleazari kuhani na wakuu wote wa kusanyiko wakatoka nje ili wakutane nao nje ya kambi. 14 Na Musa akaanza kuwa na ghadhabu kwa sababu ya wale wanaume waliowekwa rasmi wa majeshi ya vita,+ wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia waliokuwa wakiingia kutoka katika safari hiyo ya kijeshi. 15 Kwa hiyo Musa akawaambia: “Je, mmemhifadhi hai kila mwanamke?+ 16 Tazama! Hao ndio, kupitia kwa neno la Balaamu, waliowashawishi wana wa Israeli kukosa uaminifu+ kwa Yehova juu ya lile jambo la Peori,+ hivi kwamba tauni ikaja juu ya kusanyiko la Yehova.+ 17 Na sasa ueni kila mtoto wa kiume, na kumuua kila mwanamke ambaye amefanya ngono na mtu kwa kulala na mwanamume.+ 18 Na mwahifadhi hai kwa ajili yenu watoto wote kati ya wanawake ambao hawajajua tendo la kulala na mwanamume.+ 19 Nanyi mpige kambi nje ya kambi siku saba. Kila mtu ambaye ameua nafsi+ na kila mtu ambaye amegusa mtu aliyeuawa,+ mtajitakasa+ katika siku ya tatu na katika siku ya saba, ninyi na mateka wenu. 20 Na kila vazi na kila chombo cha ngozi na kila kitu kilichotengenezwa kwa manyoya ya mbuzi na kila chombo cha mbao mtajitakasia kutoka katika dhambi.”+
21 Ndipo Eleazari kuhani akawaambia wanaume wa jeshi waliokuwa wameenda kwenye pigano: “Hii ndiyo amri ya sheria ambayo Yehova amemwamuru Musa, 22 ‘Ni dhahabu na fedha, shaba, chuma, bati na risasi tu, 23 kila kitu ambacho hustahimili moto, ndicho mtakachokipitisha motoni,+ nacho kitakuwa safi. Ila kinapaswa kutakaswa kwa kutumia maji ya kutakasa.+ Na kila kitu ambacho hakiwezi kustahimili moto mtakipitisha katika maji.+ 24 Nanyi mtayafua mavazi yenu katika siku ya saba na kuwa safi, na baadaye mtaweza kuingia ndani ya kambi.’”+
25 Na Yehova akamwambia Musa hivi: 26 “Chukua hesabu ya nyara, mateka ya binadamu na pia ya wanyama wa kufugwa, wewe na Eleazari kuhani na vichwa vya baba za kusanyiko. 27 Nawe utagawa nyara katika sehemu mbili kati ya wale walioshiriki katika pigano ambao walitoka nje kufunga safari na wale wengine wote wa kusanyiko.+ 28 Nawe utachukua iwe kodi+ kwa ajili ya Yehova kutoka kwa wanaume wa vita waliotoka nje kwenda safarini nafsi moja kati ya mia tano, ya binadamu na ya mifugo na ya punda na ya kundi. 29 Kutoka katika nusu yao utachukua na kumpa Eleazari kuhani wawe mchango wa Yehova.+ 30 Na kutoka katika nusu ya wana wa Israeli utachukua mmoja kati ya 50, kati ya binadamu, kati ya mifugo, kati ya punda na kati ya kundi, kati ya kila namna ya wanyama wa kufugwa, nawe utawapa Walawi,+ watunzaji wa wajibu wa maskani ya Yehova.”+
31 Na Musa na Eleazari kuhani wakafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa. 32 Na nyara, mabaki ya vitu vilivyoporwa ambavyo watu wa ile safari walikuwa wamechukua vikiwa nyara, zikajumlika kuwa kundi la wanyama 675,000, 33 na mifugo 72,000, 34 na punda 61,000. 35 Nazo nafsi+ za binadamu kutoka kati ya wanawake ambao hawakuwa wamejua tendo la kulala na mwanamume,+ nafsi zote zilikuwa 32,000. 36 Na ile nusu iliyokuwa fungu la wale waliotoka kwenda safarini hesabu yake ilijumlika kuwa kundi la wanyama 337,500. 37 Nayo kodi+ ya Yehova kutoka katika kundi ikajumlika kuwa 675. 38 Na kati ya wanyama wa mifugo kulikuwa na 36,000, nayo kodi juu yao kwa ajili ya Yehova ilikuwa 72. 39 Nao punda walikuwa 30,500, nayo kodi juu yao kwa ajili ya Yehova ilikuwa 61. 40 Nazo nafsi za binadamu zilikuwa 16,000, nayo kodi juu yao kwa ajili ya Yehova ilikuwa nafsi 32. 41 Ndipo Musa akampa Eleazari kuhani ile kodi iwe mchango wa Yehova,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.+
42 Na kutoka katika ile nusu ya wana wa Israeli, ambayo Musa aligawa kutoka katika ile mali ya wanaume waliopiga vita: 43 Sasa nusu ya kusanyiko kutoka katika kundi ilijumlika kuwa 337,500, 44 na ya mifugo, 36,000 45 na punda, 30,500, 46 na nafsi za binadamu, 16,000. 47 Kisha Musa akachukua kutoka katika ile nusu ya wana wa Israeli ile ya kutolewa katika 50, ya binadamu na ya wanyama wa kufugwa, na kuwapa Walawi,+ watunzaji wa wajibu+ wa maskani ya Yehova, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
48 Nao watu waliowekwa rasmi ambao walikuwa wa yale maelfu ya jeshi,+ wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia,+ wakamkaribia Musa, 49 na kumwambia Musa: “Watumishi wako wamechukua hesabu ya wanaume wa vita walio chini ya usimamizi wetu wala hakuna hata mmoja aliyesemwa kuwa anakosekana kwetu.+ 50 Kwa hiyo na tutoe kila mmoja kile ambacho amepata kiwe toleo la Yehova,+ vyombo vya dhahabu, mikufu ya mguuni, na vikuku, pete za muhuri,+ vipuli, na mapambo ya kike,+ ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zetu mbele za Yehova.”
51 Basi Musa na Eleazari kuhani wakakubali dhahabu hiyo kutoka kwao,+ vito vyote. 52 Nayo dhahabu yote ya mchango ambayo walimchangia Yehova ikajumlika kuwa shekeli 16,750, kutoka kwa wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia. 53 Wanaume wa jeshi walikuwa wamepora vitu kila mmoja kwa ajili yake mwenyewe.+ 54 Basi Musa na Eleazari kuhani wakaikubali dhahabu hiyo kutoka kwa wakuu wa maelfu na kwa wakuu wa mamia na kuileta ndani ya hema la mkutano iwe ukumbusho+ kwa wana wa Israeli mbele za Yehova.
32 Sasa wana wa Rubeni+ na wana wa Gadi+ wakawa na mifugo mingi, mingi sana, kwa kweli. Nao wakaanza kuiona nchi ya Yazeri+ na nchi ya Gileadi, na, tazama! mahali hapo palikuwa mahali pa mifugo. 2 Basi wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakaja na kumwambia Musa na Eleazari kuhani na wakuu wa kusanyiko, jambo hili: 3 “Atarothi+ na Diboni+ na Yazeri na Nimra+ na Heshboni+ na Eleale+ na Sebamu na Nebo+ na Beoni,+ 4 nchi ambayo Yehova alishinda+ mbele ya kusanyiko la Israeli, ni nchi ya mifugo, nao watumishi wako wana mifugo.”+ 5 Nao wakaendelea kusema: “Ikiwa tumepata kibali machoni pako, acheni watumishi wako wapewe nchi hiyo iwe miliki yao. Usitufanye tuvuke Yordani.”+
6 Basi Musa akawaambia wana wa Gadi na wana wa Rubeni: “Je, ndugu zenu wataenda vitani huku ninyi mkiendelea kukaa hapa?+ 7 Na kwa nini mwavunje moyo wana wa Israeli wasivuke kuingia katika nchi ambayo hakika Yehova atawapa wao? 8 Hivyo ndivyo baba zenu walivyofanya+ nilipowatuma kutoka Kadesh-barnea+ wakaione nchi. 9 Walipoenda kwenye bonde la mto la Eshkoli+ na kuiona nchi, ndipo walipowavunja moyo wana wa Israeli, ili wasiingie katika nchi ambayo kwa hakika Yehova angewapa.+ 10 Basi hasira ya Yehova ikawaka siku hiyo hivi kwamba akaapa,+ na kusema, 11 ‘Wanaume waliotoka Misri kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi+ hawatauona udongo ambao niliwaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo,+ kwa sababu hawakunifuata kabisa, 12 isipokuwa Kalebu+ mwana wa Yefune Mkenizi na Yoshua+ mwana wa Nuni, kwa sababu wamemfuata Yehova kikamilifu.’ 13 Basi hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli naye akawafanya watange-tange nyikani miaka 40,+ mpaka kizazi chote kilichokuwa kikifanya uovu machoni pa Yehova kikafikia mwisho wake.+ 14 Na tazama, ninyi mmesimama mahali pa baba zenu kama kundi la watu wenye dhambi ili kuizidisha hasira ya Yehova+ inayowaka juu ya Israeli. 15 Ikiwa mtageuka na kuacha kumfuata,+ yeye naye pia bila shaka atawaacha wao tena wakae muda mrefu zaidi nyikani,+ nanyi mtakuwa mmewatendea kwa uharibifu watu hawa wote.”+
16 Baadaye wakamkaribia na kusema: “Acha tujenge hapa mazizi ya mawe ya makundi kwa ajili ya mifugo yetu na majiji kwa ajili ya watoto wetu wadogo. 17 Lakini sisi wenyewe tutaenda tayari tukiwa tumejipanga kivita+ mbele ya wana wa Israeli mpaka tutakapokuwa tumewafikisha mahali pao, nao watoto wetu wadogo watakaa katika majiji yenye ngome mbali na uso wa wakaaji wa nchi. 18 Hatutarudi katika nyumba zetu mpaka wana wa Israeli watakapokuwa wamemiliki nchi, kila mmoja akiwa na urithi wake mwenyewe.+ 19 Kwa maana hatutapata urithi pamoja nao kuanzia upande wa Yordani na ng’ambo, kwa sababu urithi wetu umetujia upande wa Yordani kuelekea mashariki.”+
20 Basi Musa akawaambia: “Ikiwa mtafanya hivyo, ikiwa mtajitayarisha mbele za Yehova kwa ajili ya vita,+ 21 na kila mmoja wenu aliye tayari kwa kweli atavuka Yordani mbele za Yehova, mpaka atakapokuwa amewafukuzia mbali adui zake kutoka mbele zake,+ 22 na nchi iwe imetiishwa mbele za Yehova,+ kisha mrudi baadaye,+ ninyi pia mtajionyesha kuwa mko huru na hatia juu ya Yehova na juu ya Israeli; nayo nchi hii itakuwa miliki yenu mbele za Yehova.+ 23 Lakini ikiwa hamtafanya hivyo, mtakuwa mmemtendea Yehova dhambi.+ Na kwa hiyo jueni kwamba dhambi yenu itawafikia ninyi.+ 24 Jijengeeni majiji kwa ajili ya watoto wenu wadogo na mazizi ya mawe kwa ajili ya makundi yenu, nanyi mnapaswa kufanya jambo lililotoka kinywani mwenu.”+
25 Ndipo wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakamwambia Musa hivi: “Watumishi wako watafanya kama vile bwana wangu anavyoamuru.+ 26 Watoto wetu wadogo, wake zetu, mifugo yetu na wanyama wetu wote wa kufugwa watakaa huko katika majiji ya Gileadi,+ 27 lakini watumishi wako watavuka, kila mtu aliye tayari kwa ajili ya jeshi,+ mbele za Yehova kwa ajili ya vita, kama vile bwana wangu anavyosema.”
28 Basi Musa akatoa amri juu yao kwa Eleazari kuhani na Yoshua mwana wa Nuni na vichwa vya upande wa baba vya makabila ya wana wa Israeli. 29 Kwa hiyo Musa akawaambia: “Ikiwa wana wa Gadi na wana wa Rubeni watavuka pamoja nanyi Yordani, kila mtu aliye tayari kwa ajili ya vita,+ mbele za Yehova, nayo nchi itiishwe mbele yenu, basi ninyi mtawapa nchi ya Gileadi iwe miliki yao.+ 30 Lakini wasipovuka wakiwa tayari pamoja nanyi, basi watapewa makao katikati yenu katika nchi ya Kanaani.”+
31 Ndipo wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakajibu, na kusema: “Jambo ambalo Yehova amewaambia watumishi wako ndivyo tutakavyofanya.+ 32 Sisi wenyewe tutavuka tukiwa tayari mbele za Yehova mpaka nchi ya Kanaani,+ na miliki ya urithi wetu itakuwa pamoja nasi upande huu wa Yordani.”+ 33 Basi Musa akawapa, yaani, wana wa Gadi+ na wana wa Rubeni+ na nusu ya kabila la Manase+ mwana wa Yosefu, ufalme wa Sihoni+ mfalme wa Waamori na ufalme wa Ogu+ mfalme wa Bashani, nchi ya majiji yake katika maeneo, na majiji ya nchi kuzunguka pande zote.
34 Na wana wa Gadi wakajenga Diboni+ na Atarothi+ na Aroeri,+ 35 na Atroth-shofani na Yazeri+ na Yogbeha,+ 36 na Beth-nimra+ na Beth-harani,+ majiji yenye ngome,+ na mazizi ya mawe ya makundi.+ 37 Na wana wa Rubeni wakajenga Heshboni+ na Eleale+ na Kiriathaimu,+ 38 na Nebo+ na Baal-meoni+—majina yao yakiwa yamebadilishwa—na Sibma; nao wakaanza kuyaita kwa majina yao wenyewe majiji waliyojenga.
39 Nao wana wa Makiri+ mwana wa Manase wakapiga mwendo mpaka Gileadi, wakaliteka, wakawafukuzia mbali Waamori waliokuwamo. 40 Basi Musa akampa Makiri mwana wa Manase, Gileadi, naye akakaa humo.+ 41 Na Yairi mwana wa Manase akapiga mwendo, akateka vijiji vyao vya mahema, naye akaanza kuviita Hawoth-yairi.+ 42 Naye Noba akapiga mwendo, akaliteka Kenathi+ na miji yake ya kandokando; naye akaanza kuliita Noba kwa jina lake mwenyewe.
33 Hivi ndivyo vilivyokuwa vituo vya wana wa Israeli waliotoka nchi ya Misri+ kwa majeshi+ yao kwa mkono wa Musa na Haruni.+ 2 Naye Musa akaendelea kuandika mahali walipoondoka, kulingana na vituo vyao kwa agizo la Yehova; navyo hivi ndivyo vilivyokuwa vituo vyao kutoka mahali pamoja walipoondoka mpaka pengine:+ 3 Nao wakaondoka Ramesesi+ katika mwezi wa kwanza, katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza.+ Siku ileile iliyofuata pasaka+ wana wa Israeli wakatoka kwa mkono ulioinuliwa mbele ya macho ya Wamisri wote.+ 4 Wakati wote huo, Wamisri walikuwa wakiwazika wale ambao Yehova alikuwa amewapiga katikati yao, yaani, wazaliwa wote wa kwanza;+ na juu ya miungu yao Yehova alikuwa amefanya hukumu.+
5 Kwa hiyo wana wa Israeli wakaondoka Ramesesi,+ wakapiga kambi Sukothi.+ 6 Kisha wakaondoka Sukothi, wakapiga kambi Ethamu,+ ambapo pako ukingoni mwa nyika. 7 Halafu wakaondoka Ethamu, wakageuka na kurudi nyuma kuelekea Pihahirothi,+ ambapo panaelekeana na Baal-sefoni;+ nao wakapiga kambi mbele ya Migdoli.+ 8 Halafu wakaondoka Pihahirothi, wakapita katikati ya bahari+ mpaka nyikani,+ wakaendelea kupiga mwendo safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu,+ wakapiga kambi Mara.+
9 Kisha wakaondoka Mara wakaja Elimu.+ Sasa katika Elimu kulikuwa na mabubujiko 12 ya maji na mitende 70. Kwa hiyo wakapiga kambi huko. 10 Kisha wakaondoka Elimu, wakapiga kambi kando ya Bahari Nyekundu. 11 Baada ya hapo wakaondoka katika Bahari Nyekundu, wakapiga kambi katika nyika ya Sini.+ 12 Halafu wakaondoka katika nyika ya Sini, wakapiga kambi Dofka. 13 Baadaye wakaondoka Dofka, wakapiga kambi Alushi. 14 Kisha wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu.+ Na huko kukawa hakuna maji ya kunywa kwa ajili ya watu. 15 Baada ya hapo wakaondoka Refidimu, wakapiga kambi katika nyika ya Sinai.+
16 Halafu wakaondoka katika nyika ya Sinai, wakapiga kambi Kibroth-hataava.+ 17 Kisha wakaondoka Kibroth-hataava, wakapiga kambi Haserothi.+ 18 Baada ya hapo wakaondoka Haserothi, wakapiga kambi Rithma. 19 Kisha wakaondoka Rithma, wakapiga kambi Rimon-peresi. 20 Halafu wakaondoka Rimon-peresi, wakapiga kambi Libna. 21 Baadaye wakaondoka Libna, wakapiga kambi Risa. 22 Kisha wakaondoka Risa, wakapiga kambi Kehelatha. 23 Halafu wakaondoka Kehelatha, wakapiga kambi katika Mlima Sheferi.
24 Baada ya hapo wakaondoka Mlima Sheferi, wakapiga kambi+ Harada. 25 Halafu wakaondoka Harada, wakapiga kambi Makelothi. 26 Kisha wakaondoka+ Makelothi, wakapiga kambi Tahathi. 27 Baada ya hapo wakaondoka Tahathi, wakapiga kambi Tera. 28 Halafu wakaondoka Tera, wakapiga kambi Mithka. 29 Baadaye wakaondoka Mithka, wakapiga kambi Hashmona. 30 Kisha wakaondoka Hashmona, wakapiga kambi Moserothi. 31 Halafu wakaondoka Moserothi, wakapiga kambi Bene-yaakani.+ 32 Baada ya hapo wakaondoka Bene-yaakani, wakapiga kambi Hor-hagidgadi. 33 Kisha wakaondoka Hor-hagidgadi, wakapiga kambi Yotbata.+ 34 Baadaye wakaondoka Yotbata, wakapiga kambi Abrona. 35 Halafu wakaondoka Abrona, wakapiga kambi Esion-geberi.+ 36 Baada ya hapo wakaondoka Esion-geberi, wakapiga kambi katika nyika ya Zini,+ yaani, Kadeshi.
37 Baadaye wakaondoka Kadeshi, wakapiga kambi katika Mlima Hori,+ kwenye mpaka wa nchi ya Edomu. 38 Naye Haruni kuhani akapanda katika Mlima Hori kwa agizo la Yehova, akafa huko katika mwaka wa 40 tangu wana wa Israeli walipotoka katika nchi ya Misri, katika mwezi wa 5, siku ya kwanza ya mwezi huo.+ 39 Naye Haruni alikuwa na umri wa miaka 123 alipokufa kwenye Mlima Hori.
40 Sasa yule Mkanaani, mfalme wa Aradi,+ alipokuwa akikaa katika Negebu,+ katika nchi ya Kanaani, akapata kusikia juu ya kuja kwa wana wa Israeli.
41 Baada ya muda wakaondoka katika Mlima Hori,+ wakapiga kambi Salmona. 42 Baada ya hapo wakaondoka Salmona, wakapiga kambi Punoni. 43 Kisha wakaondoka Punoni, wakapiga kambi Obothi.+ 44 Halafu wakaondoka Obothi, wakapiga kambi Iye-abarimu kwenye mpaka wa Moabu.+ 45 Baadaye wakaondoka Iyimu, wakapiga kambi Dibon-gadi.+ 46 Baada ya hapo wakaondoka Dibon-gadi, wakapiga kambi Almon-diblathaimu. 47 Halafu wakaondoka Almon-diblathaimu,+ wakapiga kambi katika milima ya Abarimu+ mbele ya Nebo.+ 48 Mwishowe wakaondoka katika milima ya Abarimu, wakapiga kambi katika nchi tambarare za jangwa la Moabu+ kando ya Yordani, kule Yeriko. 49 Nao wakaendelea kukaa katika kambi kando ya Yordani kutoka Beth-yeshimothi+ mpaka Abel-shitimu+ katika nchi tambarare za jangwa la Moabu.
50 Na Yehova akasema na Musa katika nchi tambarare za jangwa la Moabu kando ya Yordani, kule Yeriko,+ na kumwambia: 51 “Sema na wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Mtavuka Yordani kuingia katika nchi ya Kanaani.+ 52 Nanyi mnapaswa kuwafukuzia mbali wakaaji wote wa nchi hiyo kutoka mbele yenu na kuharibu maumbo yao yote ya mawe,+ nanyi mnapaswa kuziharibu sanamu zao zote za madini ya kuyeyusha,+ na mnapaswa kupaharibu mahali pao pote patakatifu.+ 53 Nanyi mtaimiliki nchi na kukaa humo, kwa sababu hakika nitawapa ninyi nchi hiyo mpate kuimiliki.+ 54 Nanyi mtaigawa nchi hiyo kwa ajili yenu iwe miliki kwa kura+ kulingana na familia zenu.+ Kwake aliye na hesabu kubwa mtaongeza urithi wake, na kwake aliye mchache mtaupunguza urithi wake.+ Mahali ambapo kura itamtokea, hapo patakuwa pake.+ Kulingana na makabila ya baba zenu mnapaswa kumiliki nchi.+
55 “‘Hata hivyo, ikiwa hamtawafukuzia mbali wakaaji wa nchi hiyo kutoka mbele yenu,+ basi wale mtakaoacha watakuwa kama michomo katika macho yenu na kama miiba ubavuni mwenu, nao watawasumbua katika nchi ambamo mtakuwa mkikaa.+ 56 Na itatukia kwamba kama vile nilivyokusudia kuwatendea hao, ndivyo nitakavyowatendea ninyi.’”+
34 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Waamuru wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Mnaingia katika nchi ya Kanaani.+ Hiyo ndiyo nchi itakayowaangukia kwa urithi,+ nchi ya Kanaani kulingana na mipaka yake.+
3 “‘Na upande wenu wa kusini utakuwa kutoka nyika ya Zini kando ya Edomu,+ nao mpaka wenu wa kusini utakuwa kutoka mwisho wa Bahari ya Chumvi+ upande wa mashariki. 4 Nao mpaka wenu utabadilika kutoka kusini mwa mpando wa Akrabimu+ na kuvuka hadi Zini, nao mwisho wake utakuwa kusini mwa Kadesh-barnea;+ nao utatoka Hasar-adari+ na kuvuka hadi Asimoni. 5 Nao mpaka utabadilika hapo Asimoni hadi kwenye bonde la mto la Misri,+ na mwisho wake utakuwa katika ile Bahari.+
6 “‘Nao mpaka wenu wa magharibi,+ utakuwa Bahari Kuu na nchi ya pwani. Huo utakuwa mpaka wenu wa magharibi.
7 “‘Sasa huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini: Kutoka Bahari Kuu mtatia alama kufika Mlima Hori+ uwe mpaka wenu. 8 Kutoka Mlima Hori mtatia mpaka alama hadi mahali pa kuingilia pa Hamathi,+ na mwisho wa mpaka utakuwa Sedadi.+ 9 Nao mpaka utaenda hadi Zifroni, nao mwisho wake utakuwa Hasar-enani.+ Huo utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
10 “‘Halafu mtatia alama mpaka wenu wa mashariki kutoka Hasar-enani hadi Shefamu. 11 Na mpaka huo utashuka kutoka Shefamu hadi Ribla upande wa mashariki wa Aini, nao mpaka utashuka hadi mteremko wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.+ 12 Nao mpaka utashuka hadi Yordani, na mwisho wake utakuwa katika Bahari ya Chumvi.+ Hiyo itakuwa nchi+ yenu kulingana na mipaka yake kuizunguka pande zote.’”
13 Kwa hiyo Musa akawaamuru wana wa Israeli, na kusema: “Hii ndiyo nchi mtakayojigawia kwa kura+ iwe miliki, kama vile ambavyo Yehova ameamuru ili kuyapa yale makabila tisa na nusu.+ 14 Kwa maana kabila la wana wa Warubeni kulingana na nyumba za baba zao na kabila la wana wa Wagadi kulingana na nyumba za baba zao tayari wamechukua, na nusu ya kabila la Manase tayari wamechukua urithi wao.+ 15 Yale makabila mawili na nusu tayari yamechukua urithi wao kutoka katika eneo la Yordani kando ya Yeriko upande wa mashariki kuelekea mashariki.”+
16 Na Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 17 “Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowagawia ninyi nchi iwe miliki, Eleazari+ kuhani na Yoshua mwana wa Nuni.+ 18 Nanyi mtachukua mkuu mmoja kutoka katika kila kabila ili kuigawa nchi iwe miliki.+ 19 Nayo haya ndiyo majina ya wanaume hao: Wa kabila la Yuda,+ Kalebu mwana wa Yefune;+ 20 na wa kabila la wana wa Simeoni,+ Shemueli mwana wa Amihudi; 21 wa kabila la Benyamini,+ Elidadi mwana wa Kisloni; 22 na wa kabila la wana wa Dani,+ mkuu mmoja, Buki mwana wa Yogli; 23 wa wana wa Yosefu,+ wa kabila la wana wa Manase,+ mkuu mmoja, Hanieli mwana wa Efodi; 24 na wa kabila la wana wa Efraimu,+ mkuu mmoja, Kemueli mwana wa Shiftani; 25 na wa kabila la wana wa Zabuloni,+ mkuu mmoja, Elisafani mwana wa Parnaki; 26 na wa kabila la wana wa Isakari,+ mkuu mmoja, Paltieli mwana wa Azani; 27 na wa kabila la wana wa Asheri,+ mkuu mmoja, Ahihudi mwana wa Shelomi; 28 na wa kabila la wana wa Naftali,+ mkuu mmoja, Pedaheli mwana wa Amihudi.” 29 Hao ndio watu ambao Yehova aliwaamuru wawafanye wana wa Israeli waimiliki nchi katika nchi ya Kanaani.+
35 Na Yehova akaendelea kusema na Musa kwenye nchi tambarare za jangwa la Moabu kando ya Yordani,+ huko Yeriko, na kumwambia: 2 “Wape wana wa Israeli amri ya kwamba lazima wawape Walawi majiji+ wakae humo kutoka katika urithi wa miliki yao, nao watawapa Walawi kiwanja cha malisho cha majiji kuzunguka pande zote.+ 3 Na majiji hayo yatatumika kwao kuwa makao yao, navyo viwanja vyao vya malisho vitakuwa kwa ajili ya wanyama wao wa kufugwa na mali zao na kwa ajili ya wanyama-mwitu wao wote. 4 Na viwanja vya malisho vya majiji hayo, ambayo mtawapa Walawi, vitakuwa kutoka katika ukuta wa jiji kuelekea nje kipimo cha mikono elfu moja kuzunguka pande zote. 5 Nanyi mtapima nje ya jiji upande wa mashariki mikono elfu mbili na upande wa kusini mikono elfu mbili na upande wa magharibi mikono elfu mbili na upande wa kaskazini mikono elfu mbili, jiji likiwa katikati. Hicho kitatumika kwao kama kiwanja cha malisho cha majiji hayo.
6 “Haya ndiyo majiji mtakayowapa Walawi: majiji 6 ya makimbilio,+ ambayo mtatoa ili muuaji akimbilie humo,+ na mbali na hayo mtatoa majiji mengine 42. 7 Majiji yote mtakayowapa Walawi yatakuwa majiji 48, hayo pamoja na viwanja vyake vyote vya malisho.+ 8 Majiji mtakayotoa yatatoka katika miliki ya wana wa Israeli.+ Kutoka kwa wengi mtachukua mengi, na kutoka kwa wachache mtachukua machache.+ Kila mmoja kulingana na urithi wake atakaochukua uwe miliki, atawapa Walawi sehemu ya majiji yake.”
9 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 10 “Sema na wana wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Mtavuka Yordani na kuingia katika nchi ya Kanaani.+ 11 Nanyi mtachagua majiji yatakayowafaa ninyi. Yatatumika kwenu yakiwa majiji ya makimbilio, naye muuaji atakayeipiga nafsi na kuiua bila kukusudia lazima akimbilie humo.+ 12 Na majiji hayo yatatumika kwenu yakiwa makimbilio ili kumkimbia mlipiza-kisasi cha damu,+ kusudi muuaji asife mpaka asimame mbele ya kusanyiko kwa ajili ya hukumu.+ 13 Nayo majiji mtakayotoa, yale majiji sita ya makimbilio, yatakuwa kwa ajili yenu. 14 Mtatoa majiji matatu upande huu wa Yordani,+ na majiji matatu mtatoa katika nchi ya Kanaani.+ Yatatumika yakiwa majiji ya makimbilio. 15 Majiji hayo sita yatatumika yakiwa kimbilio kwa wana wa Israeli na kwa mkaaji mgeni+ na kwa mhamiaji aliye kati yao, ili mtu yeyote ambaye ataipiga nafsi na kuiua bila kukusudia akimbilie humo.+
16 “‘Sasa ikiwa amempiga kwa chombo cha chuma akafa, yeye ni muuaji wa kukusudia.+ Lazima muuaji huyo wa kukusudia auawe.+ 17 Na ikiwa alimpiga kwa jiwe dogo ambalo lingeweza kumuua naye afe, yeye ni muuaji wa kukusudia. Lazima muuaji huyo wa kukusudia auawe. 18 Na ikiwa alimpiga kwa chombo kidogo cha mbao ambacho kingeweza kumuua naye afe, yeye ni muuaji wa kukusudia. Lazima muuaji huyo wa kukusudia auawe.
19 “‘Mlipiza-kisasi+ cha damu ndiye atakayemuua huyo muuaji wa kukusudia. Hapo atakapokutana naye atamuua. 20 Na ikiwa alikuwa akimsukuma+ kwa sababu ya chuki au ikiwa amemvizia+ na kumtupia kitu ili afe, 21 au ikiwa kwa uadui amempiga kwa mkono wake ili afe, lazima mpigaji huyo atauawa. Yeye ni muuaji wa kukusudia. Mlipiza-kisasi cha damu atamuua yule muuaji wa kukusudia akimkuta.+
22 “‘Lakini ikiwa alimsukuma bila uadui wowote au kumtupia chombo chochote pasipo kumvizia,+ 23 au jiwe lolote ambalo lingeweza kumuua pasipo yeye kumwona, au kumwangushia, naye afe, naye hakuwa adui yake wala hakuwa akitafuta kumdhuru, 24 ndipo kusanyiko litahukumu kati ya yule mpigaji na yule mlipiza-kisasi cha damu kulingana na hukumu hizi.+ 25 Nalo kusanyiko+ lazima limkomboe muuaji asiyekusudia kutoka mkononi mwa mlipiza-kisasi cha damu, nalo kusanyiko litamrudisha katika jiji lake la makimbilio alilokuwa amekimbilia, naye atakaa humo mpaka kifo cha kuhani mkuu aliyetiwa mafuta kwa kutumia mafuta matakatifu.+
26 “‘Lakini ikiwa muuaji asiyekusudia atatoka nje ya mipaka ya jiji la makimbilio ambalo amekimbilia, 27 naye mlipiza-kisasi+ cha damu amkute nje ya mpaka wa lile jiji la makimbilio, na yule mlipiza-kisasi cha damu amuue yule muuaji asiyekusudia, yeye hana hatia ya damu. 28 Kwa maana alipaswa kukaa katika jiji la makimbilio mpaka kifo cha kuhani mkuu,+ na baada ya kifo cha kuhani mkuu yule muuaji asiyekusudia anaweza kurudi katika nchi iliyo miliki yake. 29 Nazo hizo zitatumika kuwa sheria za hukumu kwa ajili yenu katika vizazi vyenu vyote katika makao yenu yote.
30 “‘Kila mwenye kupiga nafsi na kuiua anapaswa kuuawa akiwa muuaji wa kukusudia+ kwa kinywa cha mashahidi,+ na shahidi mmoja hawezi kutoa ushuhuda juu ya nafsi ili afe. 31 Nanyi hampaswi kuchukua fidia kwa ajili ya nafsi ya muuaji wa kukusudia anayestahili kufa,+ kwa maana lazima auawe.+ 32 Nanyi hampaswi kuchukua fidia kwa ajili ya mtu ambaye amekimbia kwenda katika jiji lake la makimbilio, ili arudi kukaa katika nchi kabla ya kifo cha kuhani mkuu.
33 “‘Nanyi msiichafue nchi mliyo ndani yake; kwa sababu damu ndiyo inayoichafua nchi,+ na kwa ajili ya nchi hakuwezi kuwa na upatanisho kuhusu damu ambayo imemwagwa juu yake isipokuwa kwa damu ya yule anayeimwaga.+ 34 Wala msiitie unajisi nchi ambayo mnakaa ndani yake, ambayo mimi ninakaa katikati yake; kwa maana mimi Yehova ninakaa katikati ya wana wa Israeli.’”+
36 Nao vichwa vya upande wa baba vya familia ya wana wa Gileadi mwana wa Makiri+ mwana wa Manase wa familia za wana wa Yosefu wakakaribia na kusema mbele ya Musa na wakuu, vichwa vya upande wa baba vya wana wa Israeli, 2 na kusema: “Yehova alimwamuru bwana wangu awape wana wa Israeli nchi iwe urithi kwa kura;+ naye bwana wangu aliamriwa na Yehova kwamba urithi wa Selofehadi ndugu yetu awape binti zake.+ 3 Ikiwa yeyote wa wana wa yale makabila mengine ya wana wa Israeli atawachukua wawe wake zao, urithi wa wanawake hao utaondolewa pia kutoka katika urithi wa baba zetu na kuongezwa katika urithi wa kabila watakaloingia, hivi kwamba utaondolewa katika kura ya urithi wetu.+ 4 Sasa Yubile+ ikitukia kwa ajili ya wana wa Israeli, urithi wa wanawake hao utaongezwa kwenye urithi wa kabila watakaloingia; hivi kwamba urithi wao utaondolewa katika urithi wa kabila la baba zetu.”
5 Ndipo Musa akawaamuru wana wa Israeli kwa agizo la Yehova, na kusema: “Kabila la wana wa Yosefu linasema jambo lililo sawa. 6 Hili ndilo neno ambalo Yehova ameamuru kwa ajili ya binti za Selofehadi,+ na kusema, ‘Kwa yeyote atakayekuwa mwema machoni pao wanaweza kuwa wake zake. Ila tu wanapaswa kuwa wake katika familia ya kabila la baba zao.+ 7 Na hakuna urithi wowote wa wana wa Israeli unaopaswa kuzunguka kutoka kabila moja mpaka kabila lingine, kwa sababu wana wa Israeli wanapaswa kushikamana kila mmoja wao na urithi wa kabila la mababu zake. 8 Na kila binti atakayepata miliki ya urithi kutoka katika makabila ya wana wa Israeli, anapaswa kuwa mke katika mojawapo ya familia za kabila la baba yake,+ ili wana wa Israeli wapate miliki kila mmoja katika urithi wa mababu zake. 9 Wala hakuna urithi unaopaswa kuzunguka kutoka katika kabila moja mpaka lingine, kwa sababu makabila ya wana wa Israeli yanapaswa kushikamana kila mmoja na urithi wake mwenyewe.’”
10 Kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa, hivyo ndivyo binti za Selofehadi walivyofanya.+ 11 Basi Mala, Tirsa na Hogla na Milka na Noa, binti za Selofehadi,+ wakawa wake za wana wa ndugu za baba yao. 12 Wakawa wake za baadhi ya familia za wana wa Manase mwana wa Yosefu, ili urithi wao uendelee kuwa pamoja na kabila la familia ya baba yao.
13 Hizi ndizo amri+ na maamuzi ya hukumu ambayo Yehova aliwaamuru wana wa Israeli kupitia Musa, katika nchi tambarare za jangwa la Moabu kando ya Yordani, huko Yeriko.+
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.