Kumbukumbu la Torati
1 Haya ndiyo maneno ambayo Musa aliwaambia Israeli wote katika eneo la Yordani+ nyikani, katika nchi tambarare za jangwa mbele ya Sufi, katikati ya Parani+ na Tofeli na Labani na Haserothi+ na Dizahabu, 2 mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kupitia njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-barnea.+ 3 Na ikawa kwamba katika mwaka wa 40,+ katika mwezi wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi huo, Musa akasema na wana wa Israeli kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru kwa ajili yao, 4 baada ya kumshinda Sihoni+ mfalme wa Waamori, aliyekuwa akikaa kule Heshboni, na Ogu+ mfalme wa Bashani, aliyekuwa akikaa kule Ashtarothi,+ katika Edrei.+ 5 Katika eneo la Yordani nchini Moabu, Musa akaanza kuifafanua sheria hii,+ na kusema:
6 “Yehova Mungu wetu alisema nasi katika Horebu,+ na kutuambia hivi, ‘Mmekaa muda mrefu vya kutosha katika eneo hili lenye milima.+ 7 Geukeni mfunge safari, mwende kwenye eneo lenye milima la Waamori+ na kwa jirani zao wote katika Araba,+ lile eneo lenye milima+ na Shefela na Negebu+ na pwani ya bahari,+ nchi ya Wakanaani,+ na Lebanoni,+ mpaka ule mto mkubwa, mto Efrati.+ 8 Tazama, naiweka nchi hiyo mbele yenu. Ingieni mwimiliki nchi ambayo Yehova aliwaapia baba zenu, Abrahamu, Isaka+ na Yakobo,+ kwamba atawapa wao na uzao wao baada yao.’+
9 “Nami nikawaambia hivi wakati huo, ‘Mimi peke yangu siwezi kuwabeba ninyi.+ 10 Yehova Mungu wenu amewazidisha ninyi, na tazama, ninyi leo ni kama nyota za mbinguni kwa wingi.+ 11 Yehova Mungu wa mababu zenu na awaongeze+ mara elfu moja zaidi ya jinsi mlivyo, naye na awabariki+ ninyi kama vile alivyowaahidi ninyi.+ 12 Mimi peke yangu ninawezaje kuubeba uzito wenu na mzigo wenu na ugomvi wenu?+ 13 Tafuteni watu wenye hekima na busara+ na uzoefu+ wa makabila yenu, ili niwaweke wawe vichwa juu yenu.’+ 14 Ndipo mkanijibu na kusema, ‘Jambo ambalo umesema tufanye ni jema.’ 15 Basi nikawachukua vichwa vya makabila yenu, wanaume wenye hekima na uzoefu, na kuwaweka kuwa vichwa juu yenu, wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia na wakuu wa 50 na wakuu wa makumi na maofisa wa makabila yenu.+
16 “Nami nikawaamuru waamuzi wenu wakati huo, na kusema, ‘Mnaposikiliza kesi kati ya ndugu zenu, hukumuni kwa uadilifu+ kati ya mtu na ndugu yake au mkaaji mgeni wake.+ 17 Msipendelee katika hukumu.+ Msikilizeni mdogo sawa na mkubwa.+ Msiogope kwa sababu ya mwanadamu,+ kwa maana hukumu ni ya Mungu;+ na kesi ambayo ni ngumu mno kwenu, nileteeni, nami nitaisikiliza.’+ 18 Nami nikawaamuru ninyi wakati huo mambo yote mnayopaswa kufanya.
19 “Halafu tukaondoka Horebu na kupiga mwendo kupitia nyika yote hiyo iliyo kuu na yenye kutia woga,+ ambayo mmeiona, kupitia eneo lenye milima la Waamori,+ kama vile Yehova Mungu wetu alivyokuwa ametuamuru; na mwishowe tukafika Kadesh-barnea.+ 20 Sasa nikawaambia ninyi, ‘Mmefika kwenye eneo lenye milima la Waamori, ambalo Yehova Mungu wetu anatupa sisi.+ 21 Tazama, Yehova Mungu wako ameitia nchi hiyo mikononi mwako.+ Panda, ukaimiliki, kama vile Yehova Mungu wa mababu zako alivyokuambia.+ Usiogope, wala usiingiwe na hofu.’+
22 “Hata hivyo, ninyi nyote mkanikaribia na kusema, ‘Acha tutume watu mbele yetu, wakaipeleleze nchi kwa ajili yetu, watuletee neno kuhusu njia ambayo tutaipitia kwenda katika majiji tutakayoyafikia.’+ 23 Basi, jambo hilo likawa jema machoni pangu, hivi kwamba nikachukua wanaume kumi na wawili kati yenu, mmoja kwa ajili ya kila kabila.+ 24 Kisha wakageuka na kupanda eneo lenye milima,+ wakafika kwenye bonde la mto la Eshkoli,+ wakapeleleza. 25 Nao wakachukua sehemu ya matunda ya nchi+ hiyo mkononi mwao na kutuletea, nao wakaja na kutuletea neno na kusema, ‘Nchi ambayo Yehova Mungu wetu anatupa sisi ni nzuri.’+ 26 Lakini hamkutaka kwenda,+ nanyi mkaanza kujiendesha kwa kuliasi agizo la Yehova Mungu wenu.+ 27 Nanyi mkanung’unika katika mahema yenu na kusema, ‘Kwa sababu Yehova alituchukia,+ ndiyo maana alitutoa katika nchi ya Misri+ atutie mkononi mwa Waamori, ili kutuangamiza.+ 28 Tunapanda kwenda wapi? Ndugu zetu wameufanya moyo wetu uyeyuke,+ kwa kusema: “Tuliona huko watu wakubwa zaidi na warefu zaidi kuliko sisi,+ majiji makubwa na yaliyotiwa ngome mpaka mbinguni+ na pia wale wana wa Waanaki.”’+
29 “Kwa hiyo nikawaambia ninyi, ‘Msishtuke wala kuogopa kwa sababu yao.+ 30 Yehova Mungu wenu ndiye anayeenda mbele yenu. Atawapigania ninyi+ kulingana na yote ambayo aliwafanyia ninyi katika Misri chini ya macho yenu wenyewe,+ 31 na katika nyika,+ mahali ambapo uliona jinsi Yehova Mungu wako alivyokuchukua+ kama vile mtu anavyomchukua mwana wake, katika njia yote mliyoitembea mpaka mlipokuja hapa.’+ 32 Lakini ijapokuwa mlikuwa na neno hilo ninyi hamkuwa na imani katika Yehova Mungu wenu,+ 33 aliyekuwa akienda mbele yenu njiani ili kupeleleza mahali kwa ajili yenu ili mpige kambi,+ kwa moto wakati wa usiku ili mwione njia mnayopaswa kuitembea na kwa wingu wakati wa mchana.+
34 “Wakati wote huo Yehova alisikia sauti ya maneno yenu. Basi akakasirika, akaapa,+ na kusema, 35 ‘Hakuna hata mmoja kati ya watu hawa wa kizazi hiki kiovu atakayeiona ile nchi nzuri niliyoapa ya kwamba nitawapa baba zenu,+ 36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune.+ Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wanawe nchi ile aliyoikanyaga, kwa sababu amemfuata Yehova kikamili.+ 37 (Hata mimi Yehova alinikasirikia kwa sababu yenu, na kusema, ‘Wewe pia hutaingia humo.+ 38 Yoshua mwana wa Nuni, anayesimama mbele yako, ndiye atakayeingia humo.’+ Yeye amempa nguvu,+ kwa sababu atawafanya Israeli wairithi.) 39 Nao watoto wenu ambao mlisema hivi juu yao: “Watakuwa nyara!”+ na wana wenu ambao leo hawajui jema wala baya, hao wataingia humo, nami nitawapa hiyo, nao wataimiliki. 40 Nanyi wenyewe, badilini njia mnayoelekea, mtoke nyikani kupitia njia ya Bahari Nyekundu.’+
41 “Ndipo mlipojibu na kuniambia, ‘Tumemtendea dhambi Yehova.+ Sisi—sisi tutapanda na kupigana kulingana na yote ambayo Yehova Mungu wetu ametuamuru!’ Basi mkajifunga, kila mmoja, silaha zake za vita nanyi mkaliona kuwa jambo rahisi kupanda mlimani.+ 42 Lakini Yehova akaniambia, ‘Waambie: “Msipande kwenda kupigana, kwa sababu mimi simo katikati yenu;+ msije mkashindwa mbele ya adui zenu.”’+ 43 Basi nikasema nanyi, nanyi hamkusikiliza bali mkaanza kujiendesha kwa kumwasi+ Yehova na kuwaka hasira, nanyi mkajaribu kwenda juu mlimani.+ 44 Ndipo Waamori waliokuwa wakikaa katika mlima huo wakatoka ili kukutana nanyi nao wakawafuatilia ninyi,+ kama vile nyuki wanavyofanya, na kuwatawanya ninyi huko Seiri mpaka Horma.+ 45 Baada ya jambo hilo mkarudi na kuanza kulia mbele za Yehova, lakini Yehova hakuisikiliza sauti yenu,+ wala hakuwategea ninyi sikio.+ 46 Basi mkaendelea kukaa kule Kadeshi siku nyingi, siku nyingi kadiri mlivyokaa huko.+
2 “Kisha tukageuka na kuondoka kuelekea nyikani kupitia njia ya Bahari Nyekundu, kama vile Yehova alivyokuwa amesema nami;+ nasi tukauzunguka Mlima Seiri kwa siku nyingi. 2 Mwishowe Yehova akaniambia hivi, 3 ‘Mmeuzunguka mlima huu muda mrefu vya kutosha.+ Geukeni mwelekee kaskazini. 4 Nawe uwaamuru watu, na kusema: “Mnapita kando ya mpaka wa ndugu zenu,+ wana wa Esau,+ ambao wanakaa Seiri,+ nao wataogopa kwa sababu yenu,+ nanyi lazima muwe waangalifu sana. 5 Msigombane nao, kwa sababu sitawapa ninyi sehemu ya nchi yao hata upana wa wayo wa mguu; kwa sababu nimempa Esau Mlima Seiri uwe miliki yake.+ 6 Chakula mtakachonunua kutoka kwao kwa pesa, mtakula; na pia maji mtakayonunua kutoka kwao kwa pesa, mtakunywa.+ 7 Kwa maana Yehova Mungu wako amekubariki wewe katika kila tendo la mkono wako.+ Anajua vema juu ya kutembea kwako katika nyika hii kuu. Miaka hii 40+ Yehova Mungu wako amekuwa pamoja nawe. Hukukosa kitu chochote.”’+ 8 Basi tukapita mbali na ndugu zetu, wana wa Esau,+ wanaokaa Seiri, kutoka njia ya Araba,+ kutoka Elathi na kutoka Esion-geberi.+
“Kisha tukageuka na kupitia njia ya nyika ya Moabu.+ 9 Ndipo Yehova akaniambia, ‘Usimsumbue Moabu wala kupigana vita naye, kwa sababu sitakupa wewe sehemu yoyote ya nchi yake iwe miliki yako, kwa maana wana wa Loti+ nimewapa Ari+ iwe miliki yao. 10 (Waemi+ walikaa humo nyakati za kale, watu wakubwa na wengi sana na warefu kama Waanaki.+ 11 Nao Warefaimu,+ wao pia walionwa kama Waanaki,+ na Wamoabu walikuwa wakiwaita Waemi. 12 Nao Wahori+ walikaa Seiri nyakati za kale, na wana wa Esau+ wakawafukuza na kuwaangamiza kutoka mbele yao, wakakaa mahali pao,+ kama vile Israeli atakavyoitendea nchi iliyo miliki yake, ambayo hakika Yehova atawapa.) 13 Wakati huu ondokeni mshike njia na kuvuka bonde la mto la Zeredi.’ Basi tukavuka bonde la mto la Zeredi.+ 14 Na siku tulizotembea kutoka Kadesh-barnea mpaka tulipovuka bonde la mto la Zeredi zilikuwa miaka 38, mpaka kizazi chote cha wanaume wa vita kilipokuwa kimefikia mwisho wake kutoka katika kambi, kama vile Yehova alivyokuwa amewaapia.+ 15 Na mkono+ wa Yehova pia ulikuwa juu yao ili kuwafadhaisha kutoka katika kambi, mpaka walipofikia mwisho wao.+
16 “Na ikawa kwamba mara tu wanaume hao wa vita walipokwisha kufa wote kutoka kati ya watu,+ 17 Yehova akazidi kusema nami, na kuniambia hivi, 18 ‘Leo utapita karibu na eneo la Moabu, yaani, Ari,+ 19 nawe utakaribia mbele ya wana wa Amoni. Usiwasumbue wala usigombane nao, kwa sababu sitakupa sehemu yoyote ya nchi ya wana wa Amoni iwe miliki yako, kwa maana nimewapa wana wa Loti iwe miliki yao.+ 20 Hiyo pia ilikuwa ikionwa kuwa nchi ya Warefaimu.+ (Warefaimu walikaa humo nyakati za kale, nao Waamoni walikuwa wakiwaita hao Wazamzumi. 21 Walikuwa wakubwa na wengi sana na watu warefu kama Waanaki;+ naye Yehova akawaangamiza+ kutoka mbele yao, ili wapate kuwafukuza na kukaa mahali pao; 22 kama vile alivyowafanyia wana wa Esau, wanaokaa Seiri,+ wakati ambapo aliwaangamiza Wahori+ kutoka mbele yao, ili wapate kuwafukuza na kukaa mahali pao mpaka leo hii. 23 Nao Waavi,+ waliokuwa wakikaa katika makao yaliyoko mpaka Gaza,+ Wakaftori,+ waliotoka Kaftori,+ wakawaangamiza, ili wapate kukaa mahali pao.)
24 “‘Ondokeni, mshike njia na kuvuka bonde la mto la Arnoni.+ Tazama, nimemtia mkononi mwako Sihoni+ mfalme wa Heshboni, yule Mwamori. Kwa hiyo anza kumiliki nchi yake, na kupigana vita naye. 25 Leo nitaanza kutia hofu kwa ajili yako na woga kwa ajili yako mbele ya watu chini ya mbingu zote, ambao watasikia habari juu yako; nao watafadhaika na kuwa na maumivu kama yale ya kuzaa kwa sababu yako.’+
26 “Ndipo nikatuma wajumbe kutoka katika nyika ya Kedemothi+ mpaka kwa Sihoni+ mfalme wa Heshboni wakiwa na maneno ya amani,+ na kusema, 27 ‘Niruhusu nipite katika nchi yako. Nitatembea barabarani tu. Sitageuka kuume wala kushoto.+ 28 Chakula utakachoniuzia kwa pesa, ndicho nitakachokula; na maji utakayonipa kwa pesa, ndiyo nitakayokunywa. Ila tu uniruhusu nipite kwa miguu yangu,+ 29 kama vile wana wa Esau wanaokaa Seiri+ na Wamoabu+ wanaokaa Ari walivyonifanyia, mpaka nitakapokuwa nimevuka Yordani na kuingia nchi ambayo Yehova Mungu wetu anatupa sisi.’+ 30 Naye Sihoni mfalme wa Heshboni hakuturuhusu tupite katikati yake, kwa sababu Yehova Mungu wako alikuwa ameiacha roho yake iwe kaidi+ na moyo wake uwe mgumu, ili amtie mkononi mwako kama ilivyo leo hii.+
31 “Ndipo Yehova akaniambia, ‘Tazama, nimeanza kumtia Sihoni na nchi yake mkononi mwako. Anza kuimiliki nchi yake.’+ 32 Sihoni alipotoka nje, yeye na watu wake wote, ili kukutana nasi vitani huko Yahazi,+ 33 ndipo Yehova Mungu wetu alipomtia mkononi mwetu,+ hivi kwamba tukamshinda yeye+ na wanawe na watu wake wote. 34 Nasi tukateka majiji yake yote wakati huo na kuangamiza+ kila jiji, wanaume na wanawake na watoto wadogo. Hatukuacha mwokokaji yeyote. 35 Ila wanyama wa kufugwa ndio tuliochukua wawe nyara zetu, pamoja na nyara za majiji tuliyokuwa tumeteka.+ 36 Toka Aroeri,+ jiji lililo kando ya ukingo wa bonde la mto la Arnoni, na lile jiji lililo katika bonde la mto, mpaka Gileadi, hakukuwa na mji wowote uliokuwa juu sana kwetu.+ Yehova Mungu wetu aliitia yote mkononi mwetu. 37 Ila wewe hukwenda karibu na nchi ya wana wa Amoni,+ ukingo mzima wa bonde la mto la Yaboki,+ wala majiji ya eneo lenye milima, wala kitu chochote ambacho juu yake Yehova Mungu wetu alikuwa ametoa amri.
3 “Kisha tukageuka na kupanda kupitia njia ya Bashani. Ndipo Ogu+ mfalme wa Bashani akatoka nje, yeye na watu wake wote, ili kukutana nasi katika pigano huko Edrei.+ 2 Basi Yehova akaniambia, ‘Usimwogope,+ kwa maana nitamtia yeye na watu wake wote na nchi yake mkononi mwako; nawe utamtendea kama vile ulivyomtendea Sihoni+ mfalme wa Waamori, aliyekuwa akikaa kule Heshboni.’ 3 Basi Yehova Mungu wetu akamtia mkononi mwetu pia Ogu mfalme wa Bashani pamoja na watu wake wote, nasi tukaendelea kumpiga mpaka akawa hana mwokokaji aliyebaki.+ 4 Nasi tukateka majiji yake yote wakati huo. Hakukuwa na mji wowote ambao hatukuuchukua kutoka kwao, majiji 60,+ eneo lote la Argobu,+ ufalme wa Ogu katika Bashani.+ 5 Majiji yote hayo yalikuwa yametiwa ngome ya ukuta mrefu, milango na mapingo, mbali na miji mingi sana ya mashambani. 6 Hata hivyo, tuliwaangamiza,+ kama vile tulivyomtendea Sihoni mfalme wa Heshboni, kwa kuangamiza kila jiji, mwanamume, mwanamke na watoto wadogo.+ 7 Na wanyama wote wa kufugwa na nyara za majiji tukachukua kuwa nyara kwa ajili yetu wenyewe.+
8 “Nasi tukaendelea kuchukua wakati huo ile nchi kutoka mkononi mwa wale wafalme wawili wa Waamori+ waliokuwa katika eneo la Yordani, kutoka katika bonde la mto la Arnoni+ mpaka Mlima Hermoni;+ 9 (Wasidoni walikuwa wakiuita Hermoni Sirioni,+ nao Waamori walikuwa wakiuita Seniri,)+ 10 majiji yote ya nchi tambarare ya juu na Gileadi yote na Bashani yote mpaka Saleka+ na Edrei,+ majiji ya ufalme wa Ogu katika Bashani. 11 Kwa maana Ogu mfalme wa Bashani ndiye tu aliyebaki kati ya mabaki ya Warefaimu.+ Tazama! Sanduku lake lilikuwa sanduku la chuma. Je, haliko kule Raba+ kwa wana wa Amoni? Urefu wake ni mikono tisa, na upana wake ni mikono minne, kwa mkono wa mwanadamu. 12 Nasi tukaitwaa nchi hii wakati huo; kutoka Aroeri,+ kando ya bonde la Arnoni, na nusu ya eneo lenye milima la Gileadi, na majiji yake nimewapa Warubeni na Wagadi.+ 13 Na ile Gileadi+ nyingine na Bashani+ yote ya ufalme wa Ogu nimewapa nusu ya kabila la Manase. Eneo lote la Argobu+ la Bashani yote, je, haliitwi nchi ya Warefaimu?+
14 “Yairi+ mwana wa Manase alichukua eneo lote la Argobu+ hadi mpaka wa Wageshuri+ na Wamaakathi,+ naye akaviita vijiji hivyo vya Bashani kwa jina lake mwenyewe, Hawoth-yairi,+ mpaka leo hii. 15 Na Makiri+ nimempa Gileadi.+ 16 Na Warubeni+ na Wagadi nimewapa kutoka Gileadi+ hadi kwenye bonde la mto la Arnoni, mpaka ukiwa ni katikati ya lile bonde la mto, hadi Yaboki, lile bonde la mto lililo mpakani mwa wana wa Amoni;+ 17 na Araba na Yordani na ule mpaka, kutoka Kinerethi+ hadi bahari ya Araba, Bahari ya Chumvi,+ chini ya mteremko wa Pisga+ kuelekea mashariki.
18 “Basi nikawaamuru ninyi wakati huo, na kusema, ‘Yehova Mungu wenu amewapa nchi hii mpate kuimiliki. Mtavuka, mkiwa tayari na silaha, mbele ya ndugu zenu, wana wa Israeli, wanaume wote mashujaa.+ 19 Ila wake zenu na watoto wenu na mifugo yenu (najua kwamba mna kiasi kikubwa cha mifugo) wataendelea kukaa katika majiji yenu ambayo nimewapa ninyi,+ 20 mpaka Yehova atakapowapa ndugu zenu pumziko, kama ninyi, nao pia wawe wamemiliki nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa ng’ambo ya Yordani; ndipo mtakaporudi, kila mmoja kwenda kwenye miliki yake ambayo nimewapa ninyi.’+
21 “Nami nikamwamuru Yoshua+ wakati huo, na kusema, ‘Macho yako yanaona yote ambayo Yehova Mungu wako amewafanyia wafalme hao wawili. Hivyo ndivyo Yehova atakavyozifanyia falme zote ambazo mnavuka kuziendea huko.+ 22 Msiwaogope, kwa maana Yehova Mungu wenu Ndiye anayewapigania ninyi.’+
23 “Nami nikamwomba Yehova kibali wakati huo, na kusema, 24 ‘Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, wewe mwenyewe umeanza kumfanya mtumishi wako aone ukuu+ wako na mkono wako wenye nguvu,+ kwa maana ni nani aliye mungu mbinguni au duniani ambaye hutenda matendo kama yako na utendaji wenye nguvu kama wako?+ 25 Acha nivuke, tafadhali, niione hiyo nchi nzuri+ iliyo ng’ambo ya Yordani, eneo hilo zuri lenye milima+ na Lebanoni.’+ 26 Na Yehova akaendelea kuwa na ghadhabu juu yangu kwa sababu yenu+ wala hakunisikiliza; lakini Yehova aliniambia, ‘Imetosha! Usiseme nami tena kamwe juu ya jambo hili. 27 Panda juu ya Pisga,+ uinue macho yako kuelekea magharibi na kaskazini na kusini na mashariki, uone kwa macho yako, kwa maana wewe hutavuka huu mto Yordani.+ 28 Nawe umpe Yoshua utume+ na kumtia moyo na kumwimarisha, kwa maana yeye ndiye atakayevuka+ mbele ya watu hawa naye ndiye atakayewafanya warithi nchi utakayoiona.’+ 29 Wakati wote huo tulikuwa tukikaa katika lile bonde mbele ya Beth-peori.+
4 “Na sasa, Ee Israeli, sikilizeni masharti na maamuzi ya hukumu ninayowafundisha ninyi kufanya, ili mpate kuishi+ na kwa kweli mpate kuingia na kuimiliki nchi ambayo Yehova Mungu wa mababu zenu anawapa ninyi. 2 Nanyi msiongeze kwenye neno ninalowaamuru ninyi, wala msiondoe lolote kutoka katika hilo,+ ili mzishike amri za Yehova Mungu wenu ninazowaamuru ninyi.
3 “Macho yenu wenyewe ndiyo yaliyoona mambo ambayo Yehova alifanya katika kile kisa cha Baali wa Peori,+ kwamba kila mtu aliyemfuata Baali wa Peori ndiye ambaye Yehova Mungu wako aliangamiza kutoka katikati yako.+ 4 Lakini ninyi mnaoshikamana+ na Yehova Mungu wenu, nyote mko hai leo. 5 Tazama! nimewafundisha masharti+ na maamuzi ya hukumu,+ kama vile ambavyo Yehova Mungu wangu ameniamuru mimi, ili ninyi mfanye hivyo katikati ya nchi ambayo mnaenda kuimiliki. 6 Nanyi mtazishika na kuzifanya, kwa sababu hiyo ni hekima+ kwenu na uelewaji+ kwenu mbele ya macho ya vikundi vya watu watakaosikia juu ya masharti yote haya, nao watasema, ‘Taifa hili kubwa bila shaka ni watu wenye hekima na wenye uelewaji.’+ 7 Kwa maana ni taifa+ gani kubwa ambalo lina miungu iliyo karibu nalo kama Yehova Mungu wetu alivyo tunapomwitia nyakati zote?+ 8 Na kuna taifa gani kubwa lenye masharti na maamuzi ya hukumu ya uadilifu kama sheria yote hii ninayoweka mbele yenu leo?+
9 “Ila jiangalie na kuitunza vema nafsi yako,+ ili usisahau mambo ambayo macho yako yameona,+ nayo yasiondoke moyoni mwako siku zote za maisha yako;+ nawe utawajulisha mambo hayo wana wako na wajukuu wako,+ 10 siku ambayo ulisimama mbele za Yehova Mungu wako katika Horebu,+ wakati ambapo Yehova aliniambia, ‘Kutanisha watu pamoja kwangu ili niwafanye wasikie maneno yangu,+ ili wapate kujifunza kuniogopa+ mimi siku zote walizo hai juu ya nchi na ili wawafundishe wana wao.’+
11 “Kwa hiyo mkaja karibu na kusimama chini ya mlima, nao mlima ulikuwa ukiwaka moto mpaka katikati ya mbingu; kulikuwa na giza, wingu na weusi mzito.+ 12 Naye Yehova akaanza kusema nanyi kutoka katikati ya moto.+ Sauti ya maneno ndiyo mliyokuwa mkiisikia, bali hamkuwa mkiona umbo+ lolote—mlisikia sauti tu.+ 13 Naye akawajulisha ninyi agano+ lake, alilowaamuru mtende—yale Maneno Kumi,+ kisha akayaandika juu ya mabamba mawili ya mawe.+ 14 Na Yehova aliniamuru mimi wakati huo niwafundishe masharti na maamuzi ya hukumu, ili ninyi myatende katika nchi ambayo mnavuka ili kuimiliki.+
15 “Nanyi mjiangalie vema nafsi zenu,+ kwa sababu hamkuona umbo+ lolote katika siku ambayo Yehova alisema nanyi katika Horebu kutoka katikati ya moto, 16 ili msitende kwa uharibifu+ wala msijifanyie wenyewe sanamu ya kuchongwa, umbo la mfano wowote, mfano wa mwanamume au mwanamke,+ 17 mfano wa mnyama yeyote aliye duniani,+ mfano wa ndege yeyote mwenye mabawa ambaye huruka mbinguni,+ 18 mfano wa kitu chochote kinachotembea kwenye nchi, mfano wa samaki+ yeyote aliye katika maji chini ya dunia; 19 wala usije ukayainua macho yako mbinguni na kuona jua na mwezi na nyota, jeshi lote la mbinguni, nawe upate kushawishiwa na kuviinamia na kuvitumikia,+ vile ambavyo Yehova Mungu wako amegawia vikundi vyote vya watu chini ya mbingu nzima.+ 20 Lakini ninyi ndio watu ambao Yehova alichukua apate kuwatoa nje ya tanuru ya chuma,+ toka nje ya Misri, ili muwe watu wa mali ya kibinafsi kwake+ kama ilivyo leo hii.
21 “Na Yehova akaniwakia hasira kwa sababu yenu,+ hivi kwamba akaapa kwamba sitavuka Yordani wala kuingia katika ile nchi nzuri ambayo Yehova Mungu wako anakupa iwe urithi wako.+ 22 Kwa maana ninakufa katika nchi hii.+ Sivuki Yordani, lakini ninyi mnavuka, nanyi mtaimiliki nchi hiyo nzuri. 23 Jiangalieni msije mkasahau agano la Yehova Mungu wenu ambalo alifanya pamoja nanyi+ na msijifanyie sanamu ya kuchongwa, umbo la kitu chochote ambacho juu yake Yehova Mungu wako amekuamuru.+ 24 Kwa maana Yehova Mungu wako ni moto unaoteketeza,+ Mungu anayetaka watu wajitoe kikamili.+
25 “Ikiwa utakuwa baba ya wana na wajukuu nanyi mmekaa muda mrefu katika nchi na kutenda kwa uharibifu+ na kufanya sanamu ya kuchongwa,+ umbo la kitu chochote, na kufanya uovu machoni pa Yehova Mungu+ wako na kumtia uchungu, 26 leo nachukua mbingu na dunia ili ziwe mashahidi dhidi yenu,+ ya kwamba hakika mtaangamia haraka kutoka katika nchi ambayo mnavuka Yordani ili mwimiliki. Hamtarefusha siku zenu juu yake, kwa sababu hakika mtaangamizwa.+ 27 Na Yehova atawatawanya ninyi katikati ya watu,+ nanyi mtabaki hesabu chache+ katikati ya mataifa ambayo Yehova atayafukuzia mbali. 28 Na huko mtalazimika kuitumikia miungu mingine,+ kazi ya mikono ya mwanadamu, miti na mawe,+ ambayo haiwezi kuona wala kusikia wala kula wala kunusa.+
29 “Mkimtafuta Yehova Mungu wenu mkiwa huko, hakika mtampata pia,+ kwa sababu utauliza kumhusu kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote.+ 30 Utakapokuwa katika dhiki kali na maneno yote haya yawe yamekupata mwishoni mwa siku hizo, basi utarudi kwa Yehova Mungu+ wako na kuisikiliza sauti yake.+ 31 Kwa maana Yehova Mungu wako ni Mungu mwenye rehema.+ Hatakutupa wala kukuharibu wala kulisahau agano+ la mababu zako ambalo aliwaapia.
32 “Sasa uliza, tafadhali, juu ya siku za zamani+ zilizokuwapo kabla yako, kutoka siku ambayo Mungu alimuumba mwanadamu duniani+ na kutoka mwisho mmoja wa mbingu mpaka mwisho mwingine wa mbingu, Je, jambo lolote kubwa kama hili lilitokezwa au jambo lolote kama hili lilisikiwa?+ 33 Je, kundi lingine lolote la watu limesikia sauti ya Mungu ikisema kutoka katikati ya moto jinsi ambavyo wewe mwenyewe umeisikia, nao wakaendelea kuishi?+ 34 Au je, Mungu alijaribu kuja kuchukua taifa kwa ajili yake mwenyewe kutoka kati ya taifa lingine kwa uthibitisho,+ kwa ishara+ na kwa miujiza+ na kwa vita+ na kwa mkono wenye nguvu+ na kwa mkono ulionyooshwa+ na kwa woga mkuu+ kama yote ambayo Yehova Mungu wenu amewafanyia ninyi katika Misri mbele ya macho yako? 35 Wewe—wewe umeonyeshwa, ili upate kujua kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli;+ hakuna mwingine isipokuwa yeye.+ 36 Kutoka mbinguni alikufanya usikie sauti yake ili kukurekebisha; na duniani alikufanya uone moto wake mkuu, nayo maneno yake uliyasikia kutoka katikati ya moto huo.+
37 “Na hata hivyo unaendelea kuishi, kwa sababu aliwapenda mababu zako hivi kwamba akachagua uzao wao baada yao+ na kukuleta kutoka Misri mbele za macho yake kwa nguvu zake kuu,+ 38 ili kuyafukuzia mbali mataifa makubwa zaidi na yenye nguvu zaidi kuliko wewe kutoka mbele yako, ili akulete ndani, akupe nchi yao iwe urithi kama ilivyo leo hii.+ 39 Nawe unajua vema leo, nawe ukumbuke moyoni mwako kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli mbinguni juu na duniani chini.+ Hakuna mwingine.+ 40 Nawe lazima uyashike masharti yake+ na amri zake ninazokuamuru leo, ili mambo yakuendee vema wewe+ na wana wako baada yako, na ili urefushe siku zako juu ya nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa,+ sikuzote.”
41 Wakati huo Musa akatenga majiji matatu upande wa Yordani kuelekea mashariki,+ 42 ili akimbilie humo yule atakayemuua mwenzake bila kujua,+ ikiwa hakuwa akimchukia hapo kwanza;+ naye atakimbilia moja la majiji hayo naye ataishi,+ 43 yaani, Beseri+ katika nyika kwenye nchi tambarare ya juu kwa ajili ya Warubeni, na Ramothi+ katika Gileadi kwa ajili ya Wagadi, na Golani+ katika Bashani kwa ajili ya Wamanase.+
44 Sasa hii ndiyo sheria+ ambayo Musa aliweka mbele ya wana wa Israeli. 45 Huu ndio ushuhuda+ na masharti+ na maamuzi ya hukumu+ ambayo Musa aliwaambia wana wa Israeli walipokuwa wakitoka Misri, 46 katika eneo la Yordani katika bonde mbele ya Beth-peori,+ katika nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekuwa akikaa Heshboni,+ ambaye Musa na wana wa Israeli walimshinda walipokuwa wakitoka Misri.+ 47 Nao wakaimiliki nchi yake na nchi ya Ogu+ mfalme wa Bashani, wale wafalme wawili wa Waamori waliokuwa katika eneo la Yordani kuelekea mashariki, 48 kutoka Aroeri,+ jiji lililoko ukingoni mwa bonde la mto la Arnoni, mpaka Mlima Sioni, yaani, Hermoni,+ 49 na Araba+ yote katika eneo la Yordani kuelekea mashariki, na mpaka bahari ya Araba+ chini ya miteremko ya Pisga.+
5 Na Musa akaita Israeli+ wote na kuwaambia: “Sikia, Ee Israeli, masharti na maamuzi ya hukumu+ ambayo ninasema masikioni mwenu leo, nanyi mjifunze hayo na kuwa waangalifu kuyatenda.+ 2 Yehova Mungu wetu alifanya agano pamoja nasi katika Horebu.+ 3 Yehova hakufanya agano hili pamoja na mababu zetu, bali pamoja nasi, sisi sote tulio hai hapa leo. 4 Uso kwa uso Yehova alisema pamoja nanyi katika mlima kutoka katikati ya moto.+ 5 Mimi nilikuwa nimesimama katikati ya Yehova na ninyi wakati huo+ ili kuwaambia neno la Yehova, (kwa maana mliogopa kwa sababu ya moto nanyi hamkupanda juu mlimani,)+ na kusema,
6 “‘Mimi ni Yehova Mungu wako,+ niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya watumwa.+ 7 Usiwe kamwe na miungu mingine dhidi ya uso wangu.+
8 “‘Usijifanyie sanamu ya kuchongwa,+ umbo+ lolote lililo kama kitu chochote kilicho mbinguni juu au kilicho duniani chini au kilicho katika maji chini ya dunia. 9 Usiviinamie wala kufanywa uvitumikie,+ kwa sababu mimi Yehova Mungu wako ni Mungu anayetaka watu wajitoe kikamili,+ ninayeleta adhabu kwa ajili ya kosa la akina baba juu ya wana na juu ya kizazi cha tatu na juu ya kizazi cha nne, kwa wale wanaonichukia;+ 10 lakini ninayeonyesha fadhili zenye upendo kwa kizazi cha elfu kwa wale wanaonipenda na wanaoshika amri zangu.+
11 “‘Usilitumie jina la Yehova Mungu wako katika njia ya ubatili,+ kwa maana Yehova hatamwacha bila kumwadhibu, yeyote ambaye analitumia jina lake kwa njia isiyofaa.+
12 “‘Kwa kuishika siku ya sabato ili kuiona kuwa takatifu, kama vile Yehova Mungu wako alivyokuamuru,+ 13 utatoa utumishi nawe utafanya kazi yako yote kwa siku sita.+ 14 Lakini siku ya saba ni sabato kwa Yehova Mungu wako.+ Usifanye kazi yoyote,+ wewe wala mwana wako wala binti yako wala mtumishi wako wala kijakazi wako wala ng’ombe wako wala mkaaji mgeni wako aliye ndani ya malango yako,+ ili mtumishi wako na kijakazi wako wapate kupumzika kama wewe.+ 15 Nawe ukumbuke kwamba ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri+ na Yehova Mungu wako akakutoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa.+ Ndiyo sababu Yehova Mungu wako alikuamuru uendelee kuishika siku ya sabato.+
16 “‘Mheshimu baba yako na mama yako,+ kama vile ambavyo Yehova Mungu wako amekuamuru; ili siku zako zipate kuwa ndefu na ili mambo yakuendee vema+ katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe.
20 “‘Wala usimshuhudie mwenzako uwongo.+
21 “‘Wala usimtamani mke wa mwenzako.+ Wala usitamani kwa uchoyo nyumba ya mwenzako, shamba lake au mtumishi wake au kijakazi wake, ng’ombe wake au punda wake au kitu chochote cha mwenzako.’+
22 “Yehova aliliambia kutaniko lenu lote Maneno hayo katika mlima kutoka katikati ya ule moto,+ lile wingu na ule weusi mzito, kwa sauti kubwa, naye hakuongeza lolote; kisha akayaandika juu ya mabamba mawili ya mawe na kunipa mimi.+
23 “Na ikawa kwamba mara tu mlipoisikia sauti kutoka katikati ya lile giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto,+ ninyi mlikuja karibu nami, vichwa vyote vya makabila yenu na wanaume wenu wazee. 24 Ndipo mkasema, ‘Tazama, Yehova Mungu wetu ametuonyesha utukufu wake na ukuu wake, nasi tumeisikia sauti yake kutoka katikati ya moto.+ Leo tumeona kwamba Mungu anaweza kusema na mwanadamu naye aendelee kuishi.+ 25 Na sasa kwa nini tufe, kwa maana moto huu mkubwa unaweza kututeketeza?+ Tukiisikia tena sauti ya Yehova Mungu wetu, hakika sisi tutakufa.+ 26 Kwa maana ni nani mwenye mwili wa nyama ambaye ameisikia sauti ya Mungu aliye hai+ ikisema kutoka katikati ya moto kama tulivyofanya sisi, naye akaendelea kuishi? 27 Wewe mwenyewe nenda karibu, usikie yote ambayo Yehova Mungu wetu atasema; nawe ndiye utakayesema nasi yote ambayo Yehova Mungu wetu atasema nawe,+ nasi hakika tutasikiliza na kuyatenda.’
28 “Kwa hiyo Yehova akaisikia sauti ya maneno yenu mliposema nami, naye Yehova akaniambia, ‘Nimeisikia sauti ya maneno ya watu hawa, yale ambayo wamekuambia. Wamefanya vema katika yote waliyosema.+ 29 Laiti wangaliusitawisha moyo wao huu uniogope+ na kushika amri zangu zote sikuzote,+ ili mambo yawaendee vema, wao na wana wao mpaka wakati usio na kipimo!+ 30 Nenda ukawaambie: “Rudini nyumbani kwenye mahema yenu.” 31 Nawe usimame hapa pamoja nami, nami nitasema nawe amri zote na masharti na maamuzi ya hukumu ambayo utawafundisha+ na ambayo watafanya katika nchi nitakayowapa waimiliki.’ 32 Nanyi mtakuwa waangalifu kufanya kama vile ambavyo Yehova Mungu wenu amewaamuru ninyi.+ Msigeuke kuume wala kushoto.+ 33 Katika njia yote ambayo Yehova Mungu wenu amewaamuru ninyi, mnapaswa kutembea,+ ili mpate kuishi na ili mambo yawaendee ninyi vema+ nanyi mpate kurefusha siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.
6 “Sasa hizi ndizo amri, masharti na maamuzi ya hukumu ambayo Yehova Mungu wenu ameamuru mfundishwe,+ ili myatende katika nchi mnayovuka ili kuimiliki; 2 upate kumwogopa+ Yehova Mungu wako ili kushika sheria zake zote na amri zake ambazo ninakuamuru wewe, wewe na mwana wako na mjukuu wako,+ siku zote za maisha yako, na ili siku zako ziwe ndefu.+ 3 Nawe usikilize, Ee Israeli, nawe uwe mwangalifu kuzitenda,+ ili mambo yakuendee vema+ nanyi mpate kuwa wengi sana, kama vile ambavyo Yehova Mungu wa mababu zako amekuahidi wewe,+ kuhusu nchi inayotiririka maziwa na asali.
4 “Sikiliza, Ee Israeli: Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja.+ 5 Nawe lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo+ wako wote na kwa nafsi+ yako yote na kwa nguvu+ zako zote. 6 Na maneno haya ninayokuamuru leo lazima yawe moyoni mwako;+ 7 nawe uyakazie kwa mwana wako+ na kuyasema unapoketi katika nyumba yako na unapotembea barabarani na unapolala+ na unapoamka. 8 Nawe uyafunge kama ishara kwenye mkono wako,+ na yawe kama utepe wa kipaji katikati ya macho yako;+ 9 nawe uyaandike juu ya miimo ya mlango wa nyumba yako na juu ya malango yako.+
10 “Na itatukia kwamba Yehova Mungu wako atakapokuleta katika nchi ambayo aliwaapia mababu zako Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwamba atakupa,+ majiji makubwa na yenye kupendeza ambayo wewe hukuyajenga,+ 11 na nyumba zilizojaa vitu vyote vizuri na ambazo hukuzijaza, na mashimo ya maji yaliyochimbwa ambayo hukuyachimba, mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hukuipanda, nawe utakapokuwa umekula na kushiba,+ 12 jiangalie usije ukamsahau+ Yehova, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya watumwa. 13 Unapaswa kumwogopa Yehova Mungu wako,+ nawe unapaswa kumtumikia yeye,+ nawe unapaswa kuapa kwa jina lake.+ 14 Usiifuate miungu mingine, miungu yoyote ya vikundi vya watu wanaowazunguka pande zote,+ 15 (kwa maana Yehova Mungu wako aliye katikati yako ni Mungu anayetaka watu wajitoe kikamili,)+ hasira ya Yehova isije ikawaka juu yako,+ naye akuangamize kutoka katika uso wa nchi.+
16 “Msimjaribu Yehova Mungu wenu,+ vile mlivyomjaribu huko Masa.+ 17 Mnapaswa kuzishika kwa vyovyote amri za Yehova Mungu+ wenu na ushuhuda+ wake na masharti+ yake ambayo amekuamuru.+ 18 Nawe ufanye yaliyo sawa na yaliyo mema machoni pa Yehova, ili mambo yakuendee vema+ wewe, nawe kwa kweli upate kuingia na kuimiliki ile nchi nzuri ambayo Yehova amewaapia mababu zako,+ 19 kwa kuwasukumia mbali adui zako wote toka mbele yako, kama vile ambavyo Yehova ameahidi.+
20 “Ikiwa mwana wako atakuuliza katika siku fulani wakati ujao,+ akisema, ‘Ushuhuda na masharti na maamuzi ya hukumu ambayo Yehova Mungu wetu amewaamuru ninyi yanamaanisha nini?’ 21 ndipo utakapomwambia mwana wako, ‘Tulikuwa watumwa kwa Farao katika Misri, lakini Yehova alitutoa Misri kwa mkono wenye nguvu.+ 22 Basi Yehova akaendelea kuweka ishara na miujiza,+ kubwa na zenye kuleta msiba, juu ya Misri, juu ya Farao na juu ya nyumba yake yote mbele ya macho yetu.+ 23 Naye akatutoa huko ili atulete hapa, atupe nchi ambayo alikuwa amewaapia mababu zetu.+ 24 Basi Yehova akatuamuru tushike masharti yote haya,+ tumwogope Yehova Mungu wetu kwa ajili ya hali njema yetu sikuzote,+ ili tupate kuendelea kuwa hai kama ilivyo leo hii.+ 25 Nayo itamaanisha uadilifu kwetu,+ kwamba tuwe waangalifu kutenda amri yote hii mbele za Yehova Mungu wetu, kama vile ambavyo ametuamuru.’+
7 “Wakati ambapo Yehova Mungu wako mwishowe atakuingiza katika nchi ambayo unaenda kuimiliki,+ pia ataondolea mbali mataifa yenye hesabu kubwa ya watu toka mbele yako,+ Wahiti+ na Wagirgashi+ na Waamori+ na Wakanaani+ na Waperizi+ na Wahivi+ na Wayebusi,+ mataifa saba yenye hesabu kubwa ya watu na yenye nguvu kuliko wewe.+ 2 Na Yehova Mungu wako hakika atawatia hao mkononi mwako, nawe utawashinda.+ Unapaswa kuwaangamiza.+ Usifanye agano lolote pamoja nao wala kuwaonyesha kibali chochote.+ 3 Nawe usifanye mapatano yoyote ya ndoa pamoja nao. Binti yako usimpe mwana wake, wala binti yake usimchukue kwa ajili ya mwana wako.+ 4 Kwa maana atamgeuza mwana wako aache kunifuata, nao watatumikia miungu mingine;+ na hasira ya Yehova itawaka kwelikweli juu yenu, naye hakika atakuangamiza haraka.+
5 “Kwa upande mwingine, hivi ndivyo mtakavyowafanyia: Madhabahu zao mtazibomoa,+ nazo nguzo zao takatifu mtazivunja,+ nayo miti yao mitakatifu+ mtaikata,+ na sanamu zao za kuchongwa mtaziteketeza kwa moto.+ 6 Kwa maana ninyi ni watu watakatifu kwa Yehova Mungu wenu.+ Ni ninyi ambao Yehova Mungu amewachagua ninyi muwe watu wake, mali ya pekee, kutoka kati ya vikundi vyote vya watu vilivyo kwenye uso wa nchi.+
7 “Yehova hakuwaonyesha upendo hivi kwamba akawachagua kwa sababu mlikuwa kikundi chenye hesabu kubwa zaidi ya watu kuliko vikundi vyote,+ kwa maana ninyi ndio mliokuwa kikundi chenye watu wachache zaidi.+ 8 Lakini ilikuwa kwa sababu Yehova aliwapenda ninyi,+ na kwa sababu ya kushika ile ahadi yenye kiapo aliyowaapia mababu zenu,+ ndiyo sababu Yehova aliwatoa nje kwa mkono wenye nguvu,+ apate kuwakomboa ninyi kutoka katika nyumba ya watumwa,+ kutoka katika mkono wa Farao mfalme wa Misri. 9 Nawe unajua vema kwamba Yehova Mungu wako ndiye Mungu wa kweli,+ yule Mungu mwaminifu,+ anayeshika agano+ na fadhili zenye upendo kwa wale wanaompenda na wale wanaoshika amri zake mpaka vizazi elfu,+ 10 lakini anayemlipa usoni pake yule anayemchukia kwa kumwangamiza.+ Hatasitasita kuelekea yule anayemchukia; atamlipa usoni pake. 11 Nawe utashika amri na masharti na maamuzi ya hukumu ninayokuamuru leo kwa kuyatenda.+
12 “Na itatukia kwamba, kwa sababu mnaendelea kusikiliza maamuzi haya ya hukumu na kuyashika na kuyatekeleza,+ Yehova Mungu wako atakutimizia lile agano+ na fadhili zenye upendo ambazo aliwaapia mababu zako.+ 13 Naye hakika atakupenda na kukubariki+ na kukuzidisha+ na kubariki uzao wa tumbo lako+ na mazao ya udongo wako,+ nafaka yako na divai yako mpya na mafuta yako, watoto wa ng’ombe wako na uzao wa kundi lako,+ kwenye nchi aliyowaapia mababu zako ya kwamba atakupa wewe.+ 14 Utakuwa kikundi cha watu kilichobarikiwa zaidi kuliko vikundi vingine vyote.+ Katikati yako hapatakuwa na mwanamume au mwanamke asiye na uzao, wala katikati ya wanyama wako wa kufugwa.+ 15 Na Yehova atakuondolea kila ugonjwa; na yale magonjwa mabaya ya Misri unayoyajua,+ hatayaweka juu yako, naye atayaweka juu ya wote wanaokuchukia. 16 Nawe utawaangamiza watu wote ambao Yehova Mungu wako anawatia mkononi mwako.+ Jicho lako lisiwasikitikie;+ wala usiitumikie miungu yao,+ kwa sababu jambo hilo litakuwa mtego kwako.+
17 “Ikiwa utasema moyoni mwako, ‘Mataifa haya yana watu wengi mno kwangu. Nitawezaje kuyafukuzia mbali?’+ 18 usiwaogope.+ Kumbuka kabisa yale ambayo Yehova Mungu wako alimtendea Farao na Misri yote,+ 19 ule uthibitisho mkubwa ambao macho yako yaliona,+ na zile ishara na miujiza+ na ule mkono wenye nguvu+ na ule mkono ulionyooshwa+ ambao Yehova Mungu wako aliutumia kukutoa huko.+ Hivyo ndivyo Yehova Mungu wako atakavyowatendea watu wote unaoogopa mbele yao.+ 20 Na Yehova Mungu wako pia atapeleka juu yao hisia ya kuvunjika moyo,+ mpaka wale waliobaki+ na waliojificha mbele yako waangamie. 21 Usishtuke kwa sababu yao, kwa maana Yehova Mungu wako yuko katikati yako,+ Mungu mkuu na mwenye kuogopesha.+
22 “Na Yehova Mungu wako atayasukumia mbali mataifa haya toka mbele yako kidogo kidogo.+ Hutaruhusiwa kuwamaliza kabisa upesi, wanyama wa mwituni wasije wakaongezeka dhidi yako. 23 Na Yehova Mungu wako atawatia mkononi mwako na kuwashinda kabisa kwa ushindi mkubwa, mpaka wawe wameangamizwa.+ 24 Naye atawatia wafalme wao mkononi mwako,+ nawe lazima uyaharibu majina yao toka chini ya mbingu.+ Hakuna mtu atakayesimama imara dhidi yako,+ mpaka utakapokuwa umewaangamiza.+ 25 Sanamu za kuchongwa za miungu yao mtaziteketeza kwa moto.+ Usitamani fedha na dhahabu iliyo juu yake,+ wala usiichukue kwa ajili yako,+ usije ukanaswa nayo;+ kwa maana hizo ni chukizo+ kwa Yehova Mungu wako. 26 Nawe usilete chukizo katika nyumba yako nawe uwe kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuangamizwa kama kitu hicho. Kinai kitu hicho na kukichukia kabisa,+ kwa sababu ni kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuangamizwa.+
8 “Kila amri ninayokuamuru leo muwe waangalifu kuishika,+ ili mpate kuendelea kuishi+ na kuongezeka, mwingie na kuimiliki nchi ambayo Yehova aliwaapia mababu zenu.+ 2 Nawe uikumbuke njia yote ambayo Yehova Mungu wako alikutembeza miaka hii 40 nyikani,+ ili kukunyenyekeza,+ kukujaribu+ apate kujua yaliyokuwa moyoni mwako,+ iwapo utashika amri zake au hapana. 3 Kwa hiyo alikunyenyekeza, akakuacha ukae na njaa,+ akakulisha mana,+ ambayo hukuwa umeijua wala baba zako hawakuwa wameijua; ili kukufanya ujue kwamba mwanadamu haishi kwa mkate tu bali mwanadamu huishi kwa kila neno la kinywa cha Yehova.+ 4 Nguo yako ya kujitanda haikuchakaa, wala mguu wako haukuvimba miaka hii 40.+ 5 Nawe unajua vema kwa moyo wako mwenyewe kwamba kama vile mtu anavyomrekebisha mwana wake, ndivyo Yehova Mungu wako alikuwa akikurekebisha.+
6 “Nawe ushike amri za Yehova Mungu wako kwa kutembea katika njia zake+ na kwa kumwogopa.+ 7 Kwa maana Yehova Mungu wako anakuleta katika nchi nzuri,+ nchi yenye mabonde ya mito yenye maji, mabubujiko na vilindi vya maji kutoka katika nchi tambarare ya bonde+ na katika eneo lenye milima, 8 nchi ya ngano na shayiri na mizabibu na tini na makomamanga,+ nchi ya mizeituni ya mafuta na asali,+ 9 nchi ambamo hutakula mkate kwa uhaba, ambamo hutakosa chochote, nchi ambayo mawe yake ni chuma na ambayo kutoka katika milima yake utachimba shaba.
10 “Utakapokuwa umekula na kushiba,+ wewe pia unapaswa kumbariki+ Yehova Mungu wako kwa ajili ya mema ya nchi ambayo amekupa.+ 11 Jiangalie usije ukamsahau+ Yehova Mungu wako kwa kutozishika amri zake na maamuzi yake ya hukumu na sheria zake ambazo ninakuamuru leo;+ 12 usije ukala na kushiba kwelikweli, ukajenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake,+ 13 na mifugo yako na kundi lako likaongezeka, na fedha na dhahabu zikakuongezekea, na vyote vilivyo vyako vikaongezeka; 14 nao moyo wako uinuke juu,+ na umsahau Yehova Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya watumwa;+ 15 aliyekutembeza katika ile nyika kubwa na yenye kuogopesha,+ iliyo na nyoka wenye sumu+ na nge na nchi kame ambayo haina maji; ambaye alikutolea maji katika jiwe gumu;+ 16 aliyekulisha mana+ nyikani, ambayo baba zako hawakuwa wameijua, apate kukunyenyekeza+ na kukujaribu ili akutendee mema siku zako za baadaye;+ 17 nawe useme moyoni mwako, ‘Nguvu zangu mwenyewe na uwezo kamili wa mkono wangu mwenyewe zimenifanyizia mali hii.’+ 18 Nawe umkumbuke Yehova Mungu wako, kwa sababu yeye ndiye anayekupa nguvu za kufanyiza mali;+ ili kutimiza agano lake ambalo aliwaapia mababu zako, kama ilivyo leo hii.+
19 “Na itatukia kwamba ikiwa utamsahau Yehova Mungu wako hata kidogo nawe ufuate miungu mingine na kuitumikia na kuiinamia, nashuhudia juu yenu leo kwamba ninyi mtaangamia kabisa.+ 20 Kama yale mataifa ambayo Yehova anaangamiza kutoka mbele yenu, hivyo ndivyo mtakavyoangamia, kwa sababu ninyi hamtaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu.+
9 “Sikia, Ee Israeli, leo unavuka Yordani+ uingie ndani na kuyafukuza mataifa makubwa zaidi na yenye nguvu zaidi kuliko wewe,+ majiji makubwa na yenye ngome zinazofika mbinguni,+ 2 watu wakubwa na warefu, wana wa Waanaki,+ ambao umejua na kusikia ikisemwa juu yao, ‘Ni nani anayeweza kusimama imara mbele ya wana wa Anaki?’ 3 Nawe unajua vema leo kwamba Yehova Mungu wako anavuka mbele yako.+ Yeye ni moto unaoteketeza.+ Atawaangamiza hao,+ na yeye mwenyewe atawatiisha mbele yenu; nanyi mtawafukuza na kuwaharibu haraka, kama vile ambavyo Yehova amesema nanyi.+
4 “Usiseme hivi moyoni mwako wakati ambapo Yehova Mungu wako atawasukumia mbali kutoka mbele yako, ‘Kwa sababu ya uadilifu wangu mwenyewe Yehova amenileta ndani niimiliki nchi hii,’+ ingawa ni kwa sababu ya uovu wa mataifa haya kwamba Yehova anawafukuzia mbali kutoka mbele yako.+ 5 Hutaimiliki nchi yao kwa sababu ya uadilifu+ wako wala kwa sababu ya unyoofu wa moyo wako;+ kwa kweli, Yehova anayafukuzia mbali mataifa haya kutoka mbele yako+ kwa sababu ya uovu wao, na ili kulitimiza neno ambalo Yehova aliwaapia mababu zako, Abrahamu,+ Isaka+ na Yakobo.+ 6 Nawe ni lazima ujue kwamba Yehova Mungu wako hakupi wewe nchi hii nzuri uimiliki kwa sababu ya uadilifu wako; kwa maana ninyi ni watu wenye shingo ngumu.+
7 “Kumbuka: Usisahau jinsi ambavyo umemchokoza Yehova Mungu wako nyikani.+ Tangu siku uliyotoka katika nchi ya Misri mpaka mlipofika mahali hapa ninyi mmekuwa wenye tabia ya kumwasi Yehova.+ 8 Hata katika Horebu mlimfanya Yehova akasirike hivi kwamba Yehova akapandwa na hasira kufikia hatua ya kuwaangamiza ninyi.+ 9 Nilipoenda juu mlimani nikapokee yale mabamba ya mawe,+ mabamba ya agano ambalo Yehova alikuwa amefanya pamoja nanyi,+ nami nikaendelea kukaa mlimani siku 40, mchana na usiku,+ (sikula mkate wala kunywa maji,) 10 kisha Yehova akanipa yale mabamba mawili ya mawe yaliyoandikwa kwa kidole cha Mungu;+ na maneno yote ambayo Yehova alikuwa amesema nanyi katika mlima kutoka katikati ya moto katika siku ya kutaniko, yalikuwa juu yake.+ 11 Na ikawa kwamba mwishoni mwa zile siku 40, mchana na usiku, Yehova akanipa yale mabamba mawili ya mawe, mabamba ya agano;+ 12 na Yehova akaniambia, ‘Ondoka, shuka upesi kutoka hapa, kwa sababu watu wako uliowatoa Misri wametenda kwa uharibifu.+ Wamegeuka kando upesi kutoka katika njia ambayo niliwaamuru. Wamejifanyia wenyewe sanamu ya kuyeyushwa.’+ 13 Naye Yehova akaniambia hivi, ‘Nimewaona watu hawa, na, tazama! ni watu wenye shingo ngumu.+ 14 Niache nipate kuwaangamiza+ na kufagilia mbali jina lao kutoka chini ya mbingu,+ na acha nikufanye wewe kuwa taifa lenye nguvu zaidi na lenye hesabu kubwa zaidi ya watu kuliko walivyo.’+
15 “Kisha nikageuka na kushuka kutoka mlimani, huku mlima ukiwaka moto;+ na yale mabamba mawili ya agano yalikuwa katika mikono yangu miwili.+ 16 Halafu nikaangalia, na tazama, ninyi mlikuwa mmemtendea dhambi Yehova Mungu wenu! Mlikuwa mmejifanyia wenyewe ndama wa kuyeyushwa.+ Mlikuwa mmegeuka kando upesi kutoka katika njia ambayo Yehova alikuwa amewaamuru ninyi.+ 17 Ndipo nikashika yale mabamba mawili, nikayatupa chini kutoka katika mikono yangu miwili, nikayavunja mbele ya macho yenu.+ 18 Nami nikajilaza kifudifudi mbele za Yehova, kama mara ya kwanza, siku 40, mchana na usiku. Sikula mkate wala kunywa maji,+ kwa sababu ya dhambi zenu zote mlizokuwa mmetenda kwa kutenda uovu machoni pa Yehova ili kumtia uchungu.+ 19 Kwa maana niliogopa kwa sababu ya hasira kali ambayo Yehova alikuwa ameghadhibika kuwaelekea ninyi kufikia hatua ya kuwaangamiza ninyi.+ Hata hivyo, Yehova alinisikiliza pia wakati huo.+
20 “Yehova pia akamkasirikia sana Haruni kufikia hatua ya kumwangamiza;+ lakini niliomba dua+ pia kwa ajili ya Haruni wakati huo. 21 Nayo dhambi yenu mliyoitenda, yule ndama,+ nilimchukua, nikamteketeza katika moto na kumponda-ponda, nikamsaga kabisa mpaka akawa mavumbi laini; kisha nikayatupa mavumbi yake katika mto unaoteremka kutoka mlimani.+
22 “Na zaidi ya hayo, huko Tabera+ na huko Masa+ na huko Kibroth-hataava+ mlimkasirisha Yehova.+ 23 Na Yehova alipowatuma kutoka Kadesh-barnea,+ na kusema, ‘Pandeni mwimiliki nchi ambayo nitawapa ninyi!’ ndipo mkaasi agizo la Yehova Mungu wenu,+ nanyi hamkumwamini+ wala hamkuisikiliza sauti yake.+ 24 Mmejionyesha kuwa wenye tabia ya kumwasi Yehova+ tangu siku niliyowajua ninyi.
25 “Kwa hiyo nikaendelea kujilaza kifudifudi mbele za Yehova siku 40, mchana na usiku,+ kwa maana nilijilaza kifudifudi hivyo kwa sababu Yehova alizungumza juu ya kuwaangamiza ninyi.+ 26 Nami nikaanza kuomba dua+ kwa Yehova na kusema, ‘Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, usiwaharibu watu wako, mali yako binafsi,+ uliowakomboa kwa ukuu wako, ambao uliwatoa Misri+ kwa mkono wenye nguvu.+ 27 Uwakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaka na Yakobo.+ Usiugeuze uso wako kuelekea ugumu wa watu hawa na uovu wao na dhambi yao,+ 28 ili nchi+ uliyotutoa ndani yake isije ikasema: “Kwa sababu Yehova hakuweza kuwaingiza katika nchi aliyokuwa amewaapia, na kwa sababu aliwachukia, ndiyo maana aliwatoa ili apate kuwaua nyikani.”+ 29 Wao pia ni watu wako na mali yako+ binafsi ambayo ulitoa kwa nguvu zako kuu na kwa mkono wako ulionyooshwa.’+
10 “Wakati huo Yehova aliniambia, ‘Jichongee mabamba mawili ya mawe kama yale ya kwanza,+ nawe uje kwangu juu mlimani, nawe utajitengenezea sanduku la mbao.+ 2 Nami nitaandika juu ya mabamba hayo yale maneno yaliyokuwa kwenye yale mabamba ya kwanza, ambayo uliyavunja, nawe utayaweka ndani ya sanduku hilo.’ 3 Kwa hiyo nikatengeneza sanduku la mbao za mshita, nikachonga mabamba mawili ya mawe kama yale ya kwanza+ na kupanda juu mlimani, nayo yale mabamba mawili yalikuwa mkononi mwangu. 4 Kisha akaandika juu ya yale mabamba maandishi yaleyale kama ya kwanza,+ yale Maneno Kumi,+ ambayo Yehova alisema nanyi mlimani toka katikati ya moto+ katika siku ya kutaniko;+ kisha Yehova akanipa hayo. 5 Ndipo nikageuka, nikashuka kutoka mlimani+ na kuweka yale mabamba katika sanduku nililokuwa nimetengeneza, ili yapate kukaa humo, kama vile ambavyo Yehova alikuwa ameniamuru.+
6 “Nao wana wa Israeli wakaondoka Beerothi Bene-yaakani+ wakielekea Mosera. Huko Haruni akafa, naye akazikwa huko;+ na Eleazari mwana wake akawa kuhani badala yake.+ 7 Kutoka huko wakaondoka kuelekea Gudgoda, na kutoka Gudgoda kuelekea Yotbata,+ nchi yenye mabonde ya mito yenye maji yanayotiririka.
8 “Wakati huo Yehova alitenga kabila la Lawi+ ili lichukue sanduku la agano la Yehova,+ lisimame mbele za Yehova ili kumhudumia+ na kubariki katika jina lake mpaka leo hii.+ 9 Ndiyo sababu Lawi hana fungu na urithi pamoja na ndugu zake.+ Yehova ndiye urithi wake, kama vile Yehova Mungu wako alivyokuwa amemwambia.+ 10 Na mimi—mimi nilikaa mlimani kama siku za kwanza, siku 40, mchana na usiku,+ naye Yehova akanisikiliza pia katika pindi hiyo.+ Yehova hakutaka kukuharibu wewe.+ 11 Ndipo Yehova akaniambia, ‘Ondoka, nenda mbele ya watu ili watoke, wapate kuingia na kuimiliki nchi ambayo nimewaapia mababu zao kwamba nitawapa wao.’+
12 “Na sasa, Ee Israeli, Yehova Mungu wako anataka nini kutoka kwako+ ila kumwogopa+ Yehova Mungu wako, ili kutembea katika njia zake zote+ na kumpenda+ yeye na kumtumikia Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote;+ 13 kuzishika amri za Yehova na sheria+ zake ninazokuamuru wewe leo, kwa faida yako?+ 14 Tazama, mbingu, naam, mbingu za mbingu,+ dunia+ na vyote vilivyomo, ni mali ya Yehova. 15 Ila Yehova alishikamana na mababu zako na kuwapenda, hivi kwamba akachagua uzao wao baada yao,+ naam, ninyi, kutoka kati ya vikundi vyote vya watu, kama ilivyo leo hii. 16 Nanyi mtatahiri govi la mioyo+ yenu wala msifanye shingo zenu kuwa ngumu tena.+ 17 Kwa maana Yehova Mungu wenu ni Mungu wa miungu+ na Bwana wa mabwana,+ Mungu mkuu, mwenye nguvu na mwenye kuogopesha,+ asiyemtendea yeyote kwa upendeleo+ wala kukubali rushwa,+ 18 anayetekeleza haki kwa ajili ya mvulana asiye na baba na mjane+ na kumpenda mkaaji mgeni+ ili kumpa mkate na nguo ya kujitanda. 19 Ninyi pia lazima mumpende mkaaji mgeni,+ kwa maana mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.+
20 “Unapaswa kumwogopa Yehova Mungu wako.+ Unapaswa kumtumikia yeye,+ nawe unapaswa kushikamana naye,+ na kwa jina lake unapaswa kutoa ahadi zenye kiapo.+ 21 Yeye ndiye unayepaswa kumsifu,+ naye ni Mungu wako, ambaye amekutendea wewe mambo haya makuu na yenye kuogopesha ambayo macho yako yameona.+ 22 Mababu zako walishuka kuingia Misri+ wakiwa na nafsi 70, na sasa Yehova Mungu wako amekufanya kama nyota za mbinguni kwa wingi.+
11 “Nawe umpende Yehova Mungu+ wako na kushika wajibu wako kwake na sheria zake na maamuzi yake ya hukumu+ na amri zake sikuzote. 2 Nanyi mnajua vema leo (kwa maana mimi sihutubii wana wenu ambao hawajajua wala hawajaona nidhamu ya Yehova+ Mungu wenu, ukuu wake,+ mkono wake wenye nguvu+ na mkono wake ulionyooshwa,+ 3 wala ishara zake na matendo yake aliyotenda katikati ya Misri+ kwa Farao mfalme wa Misri na kwa nchi yake yote; 4 wala mambo aliyotendea majeshi ya Misri, farasi zake na magari yake ya vita ambao dhidi ya nyuso zao aliyafanya maji ya Bahari Nyekundu yafurike walipokuwa wakiwafuatilia,+ na Yehova akawaangamiza mpaka leo hii;+ 5 wala mambo aliyowatendea ninyi nyikani mpaka mlipokuja mahali hapa; 6 wala mambo aliyowatendea Dathani na Abiramu+ wana wa Eliabu mwana wa Rubeni, wakati dunia ilipofungua kinywa chake na kuwameza pamoja na nyumba zao na mahema yao na kila kitu kilichokuwako ambacho kilipiga hatua na kuwafuata katikati ya Israeli yote);+ 7 kwa maana macho yenu ndiyo yaliyoona matendo hayo makubwa ya Yehova ambayo aliyatenda.+
8 “Nanyi mtashika amri yote ninayowaamuru leo,+ ili muwe na nguvu na mpate kuingia na kuimiliki nchi ambayo mnavuka ili kuimiliki,+ 9 na ili mrefushe siku zenu+ kwenye udongo ambao Yehova aliwaapia mababu zenu kwamba atawapa wao na uzao wao,+ nchi inayotiririka maziwa na asali.+
10 “Kwa maana ile nchi unayoenda kuimiliki si kama nchi ya Misri mliyotoka, mahali ambapo ulikuwa ukipanda mbegu yako nawe ulikuwa ukimwagilia maji kwa mguu wako, kama bustani ya mboga. 11 Lakini nchi mnayovuka ili kuimiliki ni nchi yenye milima na nchi tambarare za mabonde.+ Inakunywa maji ya mvua ya mbinguni; 12 nchi ambayo Yehova Mungu wako anaitunza. Macho+ ya Yehova Mungu wako yako juu yake daima, toka mwanzo wa mwaka mpaka mwisho wa mwaka.
13 “Na itatukia kwamba ikiwa mtatii amri+ zangu ninazowaamuru ninyi leo ili kumpenda Yehova Mungu wenu na kumtumikia kwa moyo wenu wote na kwa nafsi yenu yote,+ 14 mimi pia nitatoa mvua kwa ajili ya nchi yenu katika wakati wake uliowekwa,+ mvua ya vuli na mvua ya masika,+ nawe kwa kweli utakusanya nafaka yako na divai yako tamu na mafuta yako. 15 Nami nitatokeza majani katika shamba lako kwa ajili ya wanyama wa kufugwa,+ nawe kwa kweli utakula na kushiba.+ 16 Jiangalieni mioyo yenu isije ikashawishiwa,+ nanyi mgeuke kando na kuabudu miungu mingine na kuiinamia,+ 17 na hasira ya Yehova iwake juu yenu, naye afunge mbingu hivi kwamba mvua yoyote isitokee+ nayo nchi isitoe mazao yake nanyi mwangamie haraka kutoka katika nchi nzuri ambayo Yehova anawapa ninyi.+
18 “Nanyi mtatia maneno haya yangu katika moyo wenu+ na nafsi yenu na kuyafunga kama ishara juu ya mkono wenu, nayo yatakuwa kama utepe wa kipaji katikati ya macho yenu.+ 19 Pia mtawafundisha wana wenu, ili kusema juu yake unapoketi katika nyumba yako na unapotembea barabarani na unapolala na unapoamka.+ 20 Nawe utayaandika juu ya miimo ya mlango wa nyumba yako na kwenye malango yako,+ 21 ili siku zenu na siku za wana wenu ziwe nyingi+ juu ya nchi ambayo Yehova aliwaapia mababu zenu kwamba atawapa,+ kama siku za mbingu juu ya dunia.+
22 “Kwa maana ikiwa mtaishika kabisa amri yote hii+ ninayowaamuru ninyi ili kuifanya, kumpenda Yehova Mungu wenu,+ kutembea katika njia zake+ na kushikamana naye,+ 23 Yehova pia atayafukuzia mbali mataifa yote haya kwa sababu yenu,+ nawe hakika utayafukuza mataifa yaliyo makubwa zaidi na yenye watu wengi zaidi kuliko wewe.+ 24 Kila mahali ambapo wayo wa mguu wenu utakanyaga patakuwa penu.+ Mpaka wenu utakuwa kutoka nyikani hadi Lebanoni, kutoka ule Mto, mto Efrati, hadi bahari ya magharibi.+ 25 Hakuna mtu atakayesimama imara dhidi yenu.+ Yehova Mungu wenu atatia mbele ya uso wa nchi+ yote ambayo mtaikanyaga hofu kwa ajili yenu na woga kwa ajili yenu kama vile alivyowaahidi ninyi.
26 “Tazama, ninaweka mbele yenu leo baraka na laana:+ 27 baraka, ikiwa mtatii amri za Yehova Mungu+ wenu ninazowaamuru ninyi leo; 28 na laana,+ ikiwa hamtatii amri za Yehova Mungu+ wenu nanyi mgeuke kutoka katika njia ambayo ninawaamuru ninyi juu yake leo, ili kufuata miungu mingine ambayo hamjaijua.
29 “Na itatukia kwamba wakati Yehova Mungu wako atakapokuleta ndani ya nchi ambayo utaimiliki,+ utatoa pia baraka juu ya Mlima Gerizimu+ na laana juu ya Mlima Ebali.+ 30 Je, haiko upande wa Yordani kuelekea upande wa magharibi, katika nchi ya Wakanaani wanaokaa Araba,+ mbele ya Gilgali,+ kando ya ile miti mikubwa ya More?+ 31 Kwa maana mnavuka Yordani mwingie ndani kuimiliki nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa ninyi, nanyi mtaimiliki na kukaa ndani yake.+ 32 Nanyi muwe waangalifu ili kutimiza masharti yote na maamuzi ya hukumu+ ninayoweka mbele yenu leo.+
12 “Haya ndiyo masharti+ na maamuzi ya hukumu+ ambayo mnapaswa kuwa waangalifu kuyatimiza+ katika nchi ambayo Yehova Mungu wa mababu zenu atawaruhusu kuimiliki, siku zote mtakazokuwa hai kwenye nchi hiyo.+ 2 Mnapaswa kuangamiza kabisa+ mahali pote ambapo mataifa mnayoyafukuza yameitumikia miungu yao, juu ya milima mirefu na vilima na chini ya kila mti wenye majani mengi.+ 3 Nanyi mtabomoa madhabahu+ zao na kuvunja-vunja nguzo zao takatifu,+ nanyi mtaiteketeza miti yao mitakatifu+ katika moto na kukata sanamu za kuchongwa+ za miungu yao, nanyi mtayaharibu majina yao kutoka mahali hapo.+
4 “Msimfanyie hivyo Yehova Mungu wenu,+ 5 lakini mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua kutoka katika makabila yenu yote ili kuliweka jina lake hapo, kulifanya likae, hapo ndipo mtapatafuta, nanyi mje hapo.+ 6 Na hapo mtaleta matoleo yenu ya kuteketezwa na dhabihu+ zenu na sehemu zenu za kumi+ na mchango wa mkono wenu+ na matoleo yenu ya nadhiri+ na matoleo yenu ya hiari+ na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yenu na wa kundi lenu.+ 7 Na hapo mtakula mbele za Yehova Mungu+ wenu na kushangilia katika kazi zenu zote,+ ninyi na nyumba zenu, kwa sababu Yehova Mungu wako amekubariki.
8 “Msifanye kulingana na mambo yote ambayo tunafanya hapa leo, kila mmoja lolote linaloonekana kuwa sawa machoni pake mwenyewe,+ 9 kwa sababu bado hamjaingia katika mahali pa kupumzika+ na urithi ambao Yehova Mungu wako anakupa wewe. 10 Nanyi mtavuka Yordani+ na kukaa katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa iwe miliki,+ naye atawapa pumziko kutokana na adui zenu wanaowazunguka, nanyi hakika mtakaa kwa usalama.+ 11 Na itatukia kwamba mahali+ ambapo Yehova Mungu wenu atachagua ili jina lake likae hapo ndipo mtakapoleta vyote ambavyo ninawaamuru leo, matoleo yenu ya kuteketezwa+ na dhabihu zenu, na sehemu zenu za kumi+ na mchango+ wa mkono wenu na kila kilicho bora cha matoleo yenu ya nadhiri+ ambayo mtamwekea nadhiri Yehova. 12 Nanyi mtashangilia mbele za Yehova Mungu wenu,+ ninyi na wana wenu na binti zenu na watumishi wenu na vijakazi wenu na Mlawi aliye ndani ya malango yenu, kwa sababu hana fungu wala urithi pamoja nanyi.+ 13 Jiangalie usije ukatoa matoleo yako ya kuteketezwa katika mahali pengine popote utakapoona.+ 14 Bali katika mahali ambapo Yehova atachagua katika moja la makabila yako ndipo utakapotoa matoleo yako ya kuteketezwa, na hapo ndipo utakapofanya yote ninayokuamuru wewe.+
15 “Ila wakati wowote ambapo nafsi yako inatamani, unaweza kuchinja,+ nawe utakula nyama kulingana na baraka ya Yehova Mungu wako ambayo amekupa wewe, ndani ya malango yako yote. Asiye safi+ pamoja na aliye safi wataweza kula, kama swala na kama paa.+ 16 Ila tu damu msile.+ Utaimwaga kwenye udongo kama maji.+ 17 Hutaruhusiwa kula ndani ya malango yako sehemu ya kumi ya nafaka+ yako au ya divai yako mpya au ya mafuta yako au mzaliwa wa kwanza wa mifugo+ yako na wa kundi lako au yoyote ya matoleo yako ya nadhiri utakayoweka nadhiri au matoleo yako ya hiari+ au mchango wa mkono wako.+ 18 Lakini mbele za Yehova Mungu wako utaila, katika mahali ambapo Yehova Mungu wako atachagua,+ wewe na mwana wako na binti yako na mtumishi wako na kijakazi wako na Mlawi aliye ndani ya malango yako; nawe utashangilia+ mbele za Yehova Mungu wako katika kazi zako zote. 19 Jiangalie usije ukamwacha Mlawi+ siku zako zote kwenye nchi yako.
20 “Wakati ambapo Yehova Mungu wako atalipanua eneo lako,+ kama vile ambavyo amekuahidi,+ nawe hakika utasema, ‘Acha nile nyama,’ kwa sababu nafsi yako inatamani kula nyama, wakati wowote ambapo nafsi yako inatamani unaweza kula nyama.+ 21 Ikiwa mahali ambapo Yehova Mungu wako atachagua kuweka jina lake+ hapo patakuwa mbali nawe, basi utachinja sehemu ya mifugo yako au sehemu ya kundi lako ambalo Yehova amekupa wewe, kama vile ambavyo nimekuamuru wewe, nawe utakula ndani ya malango yako wakati wowote ambapo nafsi yako inaitamani.+ 22 Kama vile tu swala na paa huliwa, ndivyo utakavyoila:+ asiye safi+ na aliye safi pamoja unaweza kuila. 23 Ila tu uazimie kwa uthabiti usile damu,+ kwa sababu damu ndiyo nafsi+ nawe usile nafsi pamoja na nyama. 24 Usiile. Uimwage kwenye udongo kama maji.+ 25 Usiile, ili mambo yakuendee vema+ wewe na wana wako baada yako, kwa sababu utafanya yaliyo sawa machoni pa Yehova.+ 26 Vitu vyako vitakatifu+ tu ndivyo vitakavyokuwa vyako, na matoleo yako ya nadhiri+ utayachukua, nawe utakuja mahali ambapo Yehova atachagua.+ 27 Nawe utatoa matoleo yako ya kuteketezwa,+ nyama na damu,+ juu ya madhabahu ya Yehova Mungu wako; na damu ya dhabihu zako itamiminwa juu ya madhabahu ya Yehova+ Mungu wako, bali nyama unaweza kula.
28 “Uwe mwangalifu, nawe utii maneno yote haya ambayo ninakuamuru wewe,+ ili mambo yakuendee vema+ wewe na wana wako baada yako mpaka wakati usio na kipimo, kwa sababu utafanya yaliyo mema na sawa machoni pa Yehova Mungu wako.+
29 “Yehova Mungu wako atakapoyakatilia mbali kutoka mbele yako mataifa ambayo unaenda kuyafukuza,+ utayafukuza na kukaa katika nchi yao.+ 30 Jiangalie usije ukanaswa na kuwafuata,+ baada ya wao kuangamizwa kutoka mbele yako, nawe usije ukauliza kuhusu miungu yao, na kusema, ‘Mataifa haya yalikuwa yakiitumikiaje miungu yao? Nami, naam, mimi nitafanya vivyo hivyo.’ 31 Usimfanyie hivyo Yehova Mungu wako,+ kwa maana kila kitu kinachochukiza kwa Yehova, ambacho anachukia wameifanyia miungu yao, kwa maana hata wana wao na binti zao wao huwateketeza motoni kwa ukawaida kwa ajili ya miungu yao.+ 32 Kila neno ninalowaamuru ninyi ndilo mtakalokuwa waangalifu kulifanya.+ Msiongeze juu yake wala kuondoa kutoka kwake.+
13 “Ikiwa nabii+ au mwotaji wa ndoto+ atainuka katikati yenu naye awape ishara au kitu cha ajabu,+ 2 nayo ishara hiyo au kitu hicho cha ajabu kiwe kweli alichokuambia,+ akisema, ‘Na tuifuate miungu mingine, ambayo wewe hukuijua, nasi tuitumikie,’ 3 usisikilize maneno ya nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawajaribu+ apate kujua ikiwa ninyi mnampenda Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi yenu yote.+ 4 Mnapaswa kumfuata Yehova Mungu wenu, nanyi mnapaswa kumwogopa yeye, nanyi mnapaswa kuzishika amri zake, nanyi mnapaswa kuisikiliza sauti yake, nanyi mnapaswa kumtumikia yeye, nanyi mnapaswa kushikamana naye.+ 5 Na nabii+ huyo au mwotaji huyo wa ndoto atauawa,+ kwa sababu amesema maasi juu ya Yehova Mungu wenu, ambaye aliwatoa ninyi katika nchi ya Misri na amekukomboa kutoka katika nyumba ya watumwa, ili kukugeuza kutoka katika njia ambayo Yehova Mungu wako amekuamuru kuitembea;+ nawe utaondolea mbali kilicho kiovu kutoka katikati yako.+
6 “Ikiwa ndugu yako, mwana wa mama yako, au mwana wako au binti yako au mke wako mpendwa au mwenzako aliye kama nafsi yako mwenyewe,+ atajaribu kukushawishi kwa siri, akisema, ‘Twende tukaitumikie miungu mingine,’+ ambayo hukuijua, wewe wala mababu zako, 7 baadhi ya miungu ya watu wanaowazunguka ninyi pande zote, wale walio karibu nawe au wale walio mbali nawe, kutoka mwisho mmoja wa nchi mpaka mwisho mwingine wa nchi, 8 usikubali nia yake wala kumsikiliza,+ wala jicho lako lisimsikitikie,+ wala usione huruma, wala kumficha kwa kumlinda; 9 bali lazima umuue.+ Mkono wako utakuwa wa kwanza kuja juu yake ili kumuua, nao mkono wa watu wote baadaye.+ 10 Nawe utampiga kwa mawe, naye atakufa,+ kwa sababu alijaribu kukugeuza mbali na Yehova Mungu wako, ambaye amekutoa katika nchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya watumwa.+ 11 Ndipo Israeli wote watasikia na kuogopa, nao hawatafanya tena jambo lolote kama jambo hilo baya kati yako.+
12 “Ikiwa utasikia ikisemwa katika moja la majiji yako, ambayo Yehova Mungu wako anakupa ukae humo, 13 ‘Watu wasiofaa kitu wametokea katikati yako+ ili wajaribu kuwageuzia mbali wakaaji wa jiji lao,+ kwa kusema: “Twende tukaitumikie miungu mingine,” ambayo hamjaijua,’ 14 mtatafuta na kupeleleza na kuuliza habari kabisa;+ na ikiwa jambo hili limethibitika kuwa kweli, jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa katikati yako, 15 lazima utawapiga wakaaji wa jiji hilo kwa makali ya upanga.+ Uliharibu+ pamoja na kila kitu kilicho ndani yake, na wanyama wake wa kufugwa kwa makali ya upanga. 16 Na nyara zake zote utakusanya katikati ya kiwanja chake cha watu wote, nawe utaliteketeza jiji+ hilo kwa moto pamoja na nyara zake zote kama toleo zima la kuteketezwa kwa Yehova Mungu wako, nalo litakuwa rundo la mabomoko mpaka wakati usio na kipimo.+ Halipaswi kujengwa tena kamwe. 17 Na kitu chochote kisishikamane na mkono wako kutoka katika kitu kilichofanywa kuwa kitakatifu kwa marufuku,+ ili Yehova ageukie mbali kutoka kwa hasira yake inayowaka+ naye awape ninyi rehema,+ naye awaonyeshe rehema na kuwazidisha, kama vile alivyowaapia mababu zenu.+ 18 Kwa maana unapaswa kuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kushika amri+ zake zote ambazo ninakuamuru leo, ili kufanya yaliyo sawa machoni pa Yehova Mungu wako.+
14 “Ninyi ni wana wa Yehova Mungu wenu.+ Msijikatekate+ wala kujitia upara+ kwenye mapaji ya nyuso zenu kwa ajili ya mtu aliyekufa. 2 Kwa maana ninyi ni watu watakatifu+ kwa Yehova Mungu wenu, naye Yehova amewachagua ninyi muwe watu wake, mali ya pekee,+ kutoka kati ya vikundi vyote vya watu vilivyo kwenye uso wa nchi.
3 “Usile kitu chenye kuchukiza cha namna yoyote.+ 4 Hii ndiyo aina ya wanyama mnaoweza kula:+ ng’ombe, kondoo na mbuzi, 5 paa+ na swala na kulungu na mbuzi-mwitu na palahala na kondoo-mwitu na paa-mbuzi; 6 na kila mnyama mwenye ukwato uliopasuka na ambaye ana mpasuko kwenye kwato mbili, mnyama anayecheua kati ya wanyama.+ Huyo mnaweza kumla. 7 Aina hii tu ndiyo ambayo hampaswi kula kati ya wale wanaocheua au wenye ukwato uliopasuka, wenye mwatuko: ngamia+ na sungura+ na wibari,+ kwa sababu hao hucheua lakini hawana ukwato uliopasuka. Hao si safi kwenu. 8 Nguruwe+ pia, kwa sababu ana ukwato uliopasuka lakini hacheui. Huyo si safi kwenu. Msile yoyote ya nyama yao, na mizoga yao msiiguse.+
9 “Aina hii kutoka kati ya kila kitu kilicho majini mnaweza kula: Kila kitu chenye mapezi na magamba mnaweza kula.+ 10 Na kila kitu ambacho hakina mapezi wala magamba msile.+ Hicho si safi kwenu.
11 “Ndege yeyote aliye safi mnaweza kula. 12 Lakini hawa ndio ndege ambao hampaswi kuwala: tai na furukombe na tai-mzoga mweusi,+ 13 na mwewe mwekundu na mwewe mweusi+ na ndege-mbua kulingana na aina yake; 14 na kila kunguru+ kulingana na aina yake; 15 na mbuni+ na bundi na shakwe na kipanga kulingana na aina yake; 16 na bundi mdogo na bundi mwenye masikio marefu+ na bata-maji, 17 na mwari+ na tai-mzoga na mnandi, 18 na korongo na kulastara kulingana na aina yake, na hudihudi na popo.+ 19 Na kila kiumbe kinachozaana kwa wingi chenye mabawa si safi kwenu.+ Havipaswi kuliwa. 20 Kiumbe chochote safi kinachoruka mnaweza kula.
21 “Msile mwili wowote uliokufa tayari.+ Mkaaji mgeni aliye ndani ya malango yako unaweza kumpa mwili huo, naye ataula; au mwili huo unaweza kuuziwa mgeni, kwa sababu wewe ni kikundi cha watu watakatifu kwa Yehova Mungu wako.
“Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.+
22 “Lazima utatoa sehemu ya kumi ya mazao yako yote ya mbegu yako, yanayotoka shambani mwaka baada ya mwaka.+ 23 Na mbele za Yehova Mungu wako, katika mahali ambapo atachagua ili jina lake likae hapo, utakula sehemu ya kumi ya nafaka yako,+ divai yako mpya na mafuta yako na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yako na wa kundi lako;+ ili ujifunze kumwogopa Yehova Mungu wako sikuzote.+
24 “Sasa ikiwa safari itakuwa ndefu mno kwako,+ kwa sababu hutaweza kuichukua, kwa kuwa mahali ambapo Yehova Mungu wako atachagua kuweka jina lake+ patakuwa mbali mno nawe, (kwa sababu Yehova Mungu wako atakubariki,)+ 25 basi utaigeuza kuwa pesa, nawe utafunga pesa hizo katika mkono wako na kusafiri mpaka mahali ambapo Yehova Mungu wako atapachagua. 26 Nawe utatoa pesa hizo kwa ajili ya chochote ambacho nafsi yako itatamani+ kati ya ng’ombe na kondoo na mbuzi na divai na kileo+ na kitu chochote ambacho huenda nafsi yako ikakuomba; nawe utakula huko mbele za Yehova Mungu wako na kushangilia,+ wewe na nyumba yako. 27 Na Mlawi aliye ndani ya malango yako, hutamwacha,+ kwa maana yeye hana fungu wala urithi pamoja nawe.+
28 “Mwishoni mwa miaka mitatu utatoa sehemu yote ya kumi ya mazao yako ya mwaka huo,+ nawe utaiweka ndani ya malango yako. 29 Naye Mlawi,+ kwa sababu hana fungu wala urithi pamoja nawe, na mkaaji mgeni+ na mvulana asiye na baba na mjane,+ walio ndani ya malango yako, watakuja, nao watakula na kujishibisha; ili Yehova Mungu wako apate kukubariki+ katika kila tendo+ la mkono wako ambalo utafanya.
15 “Mwishoni mwa kila miaka saba mtaachilia huru. 2 Nayo hii ndiyo namna ya kuachilia huru:+ kila mkopeshaji ataachilia huru deni ambalo amemkopesha mwenzake. Hatamkaza mwenzake au ndugu yake afanye malipo,+ kwa sababu kuachilia huru kwa ajili ya Yehova lazima kutangazwe.+ 3 Mgeni+ unaweza kumkaza afanye malipo; lakini chochote kilicho chako kitakachokuwa na ndugu yako, mkono wako na ukiachilie huru. 4 Hata hivyo, mtu yeyote asije kuwa maskini katikati yako, kwa sababu hakika Yehova atakubariki+ katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa iwe urithi, uimiliki,+ 5 ikiwa tu hutakosa kuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wako nawe uwe mwangalifu kufanya amri yote hii ninayokuamuru leo.+ 6 Kwa maana hakika Yehova Mungu wako atakubariki kama vile alivyokuahidi, nawe utayakopesha+ mataifa mengi kwa rehani, lakini wewe mwenyewe hutakopa; nawe utatawala juu ya mataifa mengi, lakini hayo hayatatawala juu yako.+
7 “Ikiwa mmoja wa ndugu zako atakuwa maskini kati yako katika moja la majiji yako, katika nchi yako ambayo Yehova Mungu wako anakupa, usiufanye moyo wako kuwa mgumu wala kuufunga mkono wako kumwelekea ndugu yako aliye maskini.+ 8 Kwa maana unapaswa kumfungulia mkono kwa ukarimu+ nawe umkopeshe kwa rehani kwa kadiri anayohitaji, kile anachopungukiwa. 9 Jiangalie neno baya lisije likawa moyoni mwako,+ na kusema, ‘Mwaka wa saba, mwaka wa kuachilia huru, umekaribia,’+ nalo jicho lako likose ukarimu kumwelekea ndugu yako aliye maskini,+ nawe usimpe chochote, naye amlilie Yehova juu yako,+ nayo iwe dhambi kwako.+ 10 Unapaswa kumpa hata iweje,+ nao moyo wako usiwe mchoyo unapompa, maana kwa sababu hiyo Yehova Mungu wako atakubariki katika kila tendo lako na katika kila kazi unayofanya.+ 11 Kwa maana maskini hatakosa kamwe kuwako katika nchi.+ Ndiyo sababu ninakuamuru, na kusema, ‘Unapaswa kuufungua mkono wako kwa ukarimu kwa ndugu yako anayeteseka na aliye maskini katika nchi yako.’+
12 “Ikiwa utauziwa ndugu yako, mwanamume Mwebrania au mwanamke Mwebrania,+ naye amekutumikia kwa miaka sita, basi katika mwaka wa saba utamruhusu aondoke kwako kama mtu aliyewekwa huru.+ 13 Na ikiwa utamruhusu aondoke kwako kama mtu aliyewekwa huru, usimwache aondoke mikono mitupu.+ 14 Usikose kumtayarishia kitu fulani kutoka katika kundi lako na uwanja wako wa kupuria na mafuta yako na shinikizo lako la divai. Kama vile ambavyo Yehova Mungu wako amekubariki, unapaswa kumpa vivyo hivyo.+ 15 Nawe ukumbuke kwamba ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri na Yehova Mungu wako alikukomboa.+ Ndiyo sababu ninakuamuru jambo hili leo.
16 “Na itatukia kwamba ikiwa atakuambia, ‘Sitakuacha!’ kwa sababu anakupenda wewe na nyumba yako, kwa maana mambo yalikuwa yakimwendea vema alipokuwa pamoja nawe,+ 17 utachukua msumari na kuupenyeza kwenye sikio lake na kwenye mlango, naye atakuwa mtumwa wako mpaka wakati usio na kipimo.+ Nawe utamfanyia kijakazi wako vivyo hivyo. 18 Lisiwe jambo gumu machoni pako unapomruhusu aondoke katika ushirika wako akiwa mtu aliyewekwa huru;+ kwa sababu kwa thamani mara mbili ya mfanyakazi wa kukodiwa+ alikutumikia kwa miaka sita, na Yehova Mungu wako amekubariki katika kila kitu ambacho ulikuwa ukifanya.+
19 “Kila mwanamume mzaliwa wa kwanza atakayezaliwa katika mifugo yako na katika kundi lako utamtakasa kwa Yehova Mungu wako.+ Usifanye utumishi wowote na mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe-dume wako, wala kukata manyoya ya mzaliwa wa kwanza wa kundi lako.+ 20 Utamla mbele za Yehova Mungu wako mwaka baada ya mwaka katika mahali ambapo Yehova Mungu wako atapachagua,+ wewe na nyumba yako. 21 Na ikiwa atakuwa na kasoro, awe kilema au kipofu, kasoro yoyote mbaya, usimtoe dhabihu kwa Yehova Mungu wako.+ 22 Ndani ya malango yako utamla, asiye safi na aliye safi pamoja,+ kama yule swala na kama yule paa.+ 23 Ila tu usile damu.+ Utaimwaga kwenye udongo kama maji.+
16 “Mwezi wa Abibu+ na uadhimishwe, nawe utasherehekea pasaka kwa Yehova Mungu wako,+ kwa sababu katika mwezi wa Abibu Yehova Mungu wako alikutoa Misri wakati wa usiku.+ 2 Nawe utatoa dhabihu ya pasaka kwa Yehova Mungu wako,+ mnyama wa kundi na wa mifugo,+ katika mahali ambapo Yehova atapachagua kuweka jina lake.+ 3 Usile chochote chenye chachu pamoja nayo kwa siku saba.+ Utakula pamoja nayo keki zisizo na chachu, mkate wa mateso, kwa sababu ulitoka katika nchi ya Misri kwa haraka,+ ili ukumbuke siku ya kutoka kwako katika nchi ya Misri siku zote za maisha yako.+ 4 Na unga wowote uliokandwa wenye chachu usionekane pamoja nawe katika eneo lako lote kwa siku saba,+ wala nyama yoyote, ambayo utaitoa dhabihu katika jioni ya siku ya kwanza, isikae usiku kucha mpaka asubuhi.+ 5 Hutaruhusiwa kutoa dhabihu ya pasaka katika lolote la majiji yako ambayo Yehova anakupa wewe. 6 Bali mahali ambapo Yehova Mungu wako atapachagua ili jina lake likae,+ hapo utatoa dhabihu ya pasaka wakati wa jioni mara tu baada ya jua kutua,+ wakati uliowekwa wa kutoka kwenu Misri. 7 Nanyi mtapika na kula+ katika mahali ambapo Yehova Mungu wenu atapachagua,+ na wakati wa asubuhi mtageuka na kwenda kwenye mahema yenu. 8 Siku sita mtakula keki zisizo na chachu; na siku ya saba kutakuwako kusanyiko kuu kwa Yehova Mungu wenu.+ Hamtafanya kazi yoyote.
9 “Mtajihesabia majuma saba. Tangu wakati ambapo mundu unawekwa kwa mara ya kwanza kwenye nafaka inayosimama utaanza kuhesabu majuma saba.+ 10 Halafu utasherehekea sherehe ya majuma kwa Yehova Mungu wako,+ kulingana na toleo la hiari la mkono wako ambalo utatoa, kama vile Yehova Mungu wako atakavyokuwa amekubariki.+ 11 Nawe utashangilia mbele za Yehova Mungu wako,+ wewe na mwana wako na binti yako na mtumishi wako na kijakazi wako na Mlawi aliye ndani ya malango yako na mkaaji mgeni+ na mvulana asiye na baba+ na mjane,+ walio katikati yako, katika mahali ambapo Yehova Mungu wako atapachagua ili jina lake likae.+ 12 Nawe utakumbuka kwamba ulikuwa mtumwa katika Misri,+ nawe utashika na kutimiza masharti haya.+
13 “Sherehe ya vibanda+ utaisherehekea kwa ajili yako mwenyewe kwa siku saba wakati ambapo unakusanya kutoka katika uwanja wako wa kupuria na mafuta yako na shinikizo la divai. 14 Nawe utashangilia wakati wa sherehe yako,+ wewe na mwana wako na binti yako na mtumishi wako na kijakazi wako na Mlawi na mkaaji mgeni na mvulana asiye na baba na mjane, walio ndani ya malango yako. 15 Siku saba utamfanyia Yehova Mungu wako sherehe+ katika mahali ambapo Yehova atapachagua, kwa sababu Yehova Mungu wako atakubariki+ katika mazao yako yote na katika kila tendo la mkono wako, nawe utakuwa na shangwe kwelikweli.+
16 “Mara tatu katika mwaka kila mwanamume wa kwako ataonekana mbele za Yehova Mungu wako katika mahali ambapo atapachagua:+ katika sherehe ya keki zisizo na chachu+ na katika sherehe ya majuma+ na katika sherehe ya vibanda,+ na mtu yeyote asionekane mbele za Yehova mikono mitupu.+ 17 Zawadi ya mkono wa kila mtu itakuwa kulingana na baraka za Yehova Mungu wako ambazo amekupa wewe.+
18 “Utaweka waamuzi+ na maofisa+ kwa ajili yako ndani ya malango yote ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe kulingana na makabila yako, nao watawahukumu watu kwa hukumu ya uadilifu. 19 Usipotoshe hukumu.+ Usipendelee+ wala kukubali rushwa, kwa maana rushwa hupofusha macho ya wenye hekima+ na hupotoa maneno ya waadilifu. 20 Haki—haki utaifuatilia,+ ili upate kuendelea kuwa hai nawe umiliki nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe.+
21 “Usijipandie aina yoyote ya mti ili uwe mti mtakatifu karibu na madhabahu ya Yehova Mungu wako ambayo utajifanyia.+
22 “Wala usijisimamishie nguzo takatifu,+ kitu ambacho Yehova Mungu wako anakichukia kwelikweli.+
17 “Usimtolee Yehova Mungu wako dhabihu ya ng’ombe-dume au kondoo mwenye kasoro, kitu chochote kibaya; kwa sababu ni chukizo kwa Yehova Mungu wako.+
2 “Ikiwa atapatikana katikati yako katika moja la majiji yako ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe, mwanamume au mwanamke atakayekuwa na mazoea ya kufanya mabaya machoni pa Yehova Mungu wako na kuvunja agano lake,+ 3 naye aende na kuabudu miungu mingine na kuinamia hiyo au jua au mwezi au jeshi lote la mbinguni,+ jambo ambalo sijaamuru,+ 4 nawe umeambiwa, ukasikia, ukatafuta kabisa, na, tazama! jambo hilo limethibitishwa kuwa kweli,+ jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa katika Israeli! 5 utamtoa nje ya malango yako mwanamume huyo au mwanamke huyo ambaye amefanya jambo hilo baya, naam, mwanamume huyo au mwanamke huyo, nawe utampiga kwa mawe mtu huyo, naye lazima afe.+ 6 Kwa kinywa cha mashahidi wawili au cha mashahidi watatu+ anayekufa atauawa. Hatauawa kwa kinywa cha shahidi mmoja.+ 7 Mkono wa mashahidi kwanza kabisa unapaswa kuja juu yake ili kumuua, na mkono wa watu wote baadaye;+ nawe utakiondolea mbali kilicho kibaya kutoka katikati yako.+
8 “Ikiwa jambo la uamuzi wa hukumu litakuwa lisilo la kawaida kwako,+ ambamo damu imemwagwa,+ ambamo dai halali limezushwa,+ au tendo lenye jeuri limefanywa, mambo ya mzozo,+ ndani ya malango yako, utaondoka pia na kwenda mahali ambapo Yehova Mungu wako atapachagua,+ 9 nawe utaenda kwa makuhani+ Walawi, na kwa mwamuzi+ atakayekuwa akitenda siku hizo, nawe utauliza, nao watakupa neno la uamuzi wa hukumu.+ 10 Kisha utafanya kulingana na lile neno watakalokupa kutoka mahali hapo ambapo Yehova atachagua; nawe utakuwa mwangalifu kufanya kulingana na yote watakayokuagiza. 11 Kulingana na sheria watakayokuonyesha, na kulingana na uamuzi wa hukumu watakaokuambia, unapaswa kufanya.+ Usigeuke kando ya neno watakalokupa, upande wa kuume au upande wa kushoto.+ 12 Na mtu atakayejiendesha kwa kimbelembele kwa kutomsikiliza kuhani anayesimama ili kuhudumu hapo kwa Yehova Mungu wako au kwa mwamuzi,+ mtu huyo lazima afe;+ nawe utaondolea mbali kilicho kibaya kutoka Israeli.+ 13 Nao watu wote watasikia na kuogopa,+ nao hawatatenda kwa kimbelembele tena.
14 “Mwishowe utakapoingia katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe, nawe uwe umeimiliki na kukaa ndani yake,+ nawe uwe umesema, ‘Acha niweke mfalme juu yangu kama mataifa yote yanayonizunguka’;+ 15 utaweka juu yako mfalme ambaye Yehova Mungu wako atachagua.+ Kutoka katikati ya ndugu zako utaweka mfalme juu yako. Hutaruhusiwa kuweka juu yako mgeni ambaye si ndugu yako. 16 Ila tu asiongeze farasi kwa ajili yake,+ wala kuwafanya watu warudi Misri ili kuongeza farasi;+ huku Yehova amewaambia ninyi, ‘Msirudi kamwe tena katika njia hii.’ 17 Pia asizidishe wake kwa ajili yake, ili moyo wake usigeuke kando;+ wala asijiongezee sana fedha na dhahabu.+ 18 Na itatukia kwamba atakapoketi kwenye kiti chake cha ufalme, atajiandikia katika kitabu nakala ya sheria hii kutoka katika ile iliyo mkononi mwa makuhani Walawi.+
19 “Naye atakaa nacho, na kukisoma siku zote za maisha yake,+ kusudi ajifunze kumwogopa Yehova Mungu wake ili apate kushika maneno yote ya sheria hii na masharti haya kwa kuyafanya;+ 20 ili moyo wake usijiinue juu ya ndugu zake+ naye asigeuke kando kutoka kwenye amri kwenda upande wa kuume au upande wa kushoto,+ ili arefushe siku zake juu ya ufalme wake,+ yeye na wanawe katikati ya Israeli.
18 “Hakuna fungu au urithi pamoja na Israeli litakalokuja kuwa la makuhani, Walawi,+ kabila zima la Lawi. Matoleo yanayotolewa kwa njia ya moto kwa Yehova, naam, urithi wake, watayala.+ 2 Kwa hiyo hakuna urithi utakaokuja kuwa wake katikati ya ndugu zake. Yehova ndiye urithi wake,+ kama vile alivyosema naye.
3 “Sasa hii itaendelea kuwa haki wanayostahili makuhani kutoka kwa watu, kutoka kwa wale wanaotoa dhabihu, iwe ni ng’ombe-dume au kondoo: Mtu atampa kuhani mfupa wa bega na mataya na tumbo. 4 Sehemu ya kwanza ya nafaka yako, divai yako mpya na mafuta yako na sufu yako ya kwanza iliyokatwa ya kundi lako unapaswa kumpa.+ 5 Kwa maana yeye ndiye ambaye Yehova Mungu wako amechagua kutoka kati ya makabila yako yote, asimame ili kuhudumu katika jina la Yehova, yeye na wanawe, sikuzote.+
6 “Na ikiwa Mlawi ataenda nje ya moja la majiji yako ya Israeli yote, ambapo alikaa kwa muda,+ naye aje kwa sababu ya tamaa yoyote ya nafsi yake mpaka mahali ambapo Yehova atapachagua,+ 7 atahudumu pia katika jina la Yehova Mungu wake sawa na ndugu zake wote, Walawi, wanaosimama hapo mbele za Yehova.+ 8 Atakula fungu linalolingana,+ mbali na kile anachopata kutokana na vitu anavyouza kati ya mali za mababu zake.
9 “Utakapokuwa umeingia katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe, usijifunze kufanya kulingana na machukizo ya mataifa hayo.+ 10 Asipatikane ndani yako yeyote anayempitisha mwana wake au binti yake katikati ya moto,+ yeyote anayefanya uaguzi,+ mwenye kufanya uchawi+ au yeyote anayetafuta ishara za bahati+ au mlozi,+ 11 au anayefunga wengine kwa kuwatakia maovu+ au yeyote anayetafuta shauri kwa mwenye kuwasiliana na pepo+ au mjuzi wa kubashiri matukio+ au yeyote anayeuliza habari kutoka kwa wafu.+ 12 Kwa maana kila mtu anayefanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova, na kwa sababu ya machukizo hayo, Yehova Mungu wako anawafukuza kutoka mbele yako.+ 13 Utajionyesha kuwa huna kosa kwa Yehova Mungu wako.+
14 “Kwa maana mataifa haya unayoyafukuza yalikuwa yakiwasikiliza wale wanaofanya uchawi+ na wale wanaoagua;+ lakini wewe, Yehova Mungu wako hajakupa kitu chochote kama hicho.+ 15 Nabii kutoka katikati yako mwenyewe, kutoka kwa ndugu zako, kama mimi, ndiye ambaye Yehova Mungu wako atakuinulia—ninyi mnapaswa kumsikiliza yeye+— 16 kulingana na yote uliyomwomba Yehova Mungu wako huko Horebu katika ile siku ya kutaniko,+ na kusema ‘Usiache nisikie tena sauti ya Yehova Mungu wangu, na huu moto mkubwa usiache niuone tena, nisije nikafa.’+ 17 Ndipo Yehova akaniambia, ‘Wamefanya vema katika kusema walilosema.+ 18 Nitawainulia wao nabii kutoka katikati ya ndugu zao, kama wewe;+ nami nitaweka maneno yangu katika kinywa chake,+ naye atasema nao yote nitakayomwamuru.+ 19 Na itatukia kwamba mtu ambaye hatasikiliza maneno yangu ambayo atayasema katika jina langu, mimi mwenyewe nitamtaka ajibu.+
20 “Hata hivyo, nabii atakayethubutu kusema katika jina langu neno ambalo sijamwamuru kusema+ au atakayesema katika jina la miungu mingine,+ nabii huyo lazima afe.+ 21 Na ikiwa utasema moyoni mwako: “Tutajuaje neno ambalo Yehova hajasema?”+ 22 Nabii anaposema katika jina la Yehova na neno hilo lisitukie au lisitimie, hilo ndilo neno ambalo Yehova hakusema.+ Kwa kimbelembele nabii huyo alilisema. Usimwogope.’+
19 “Yehova Mungu wako atakapokatilia mbali mataifa+ ambayo nchi yao Yehova Mungu wako anakupa wewe, nawe uwe umewafukuza na kukaa katika majiji yao na nyumba zao,+ 2 utatenga majiji matatu kwa ajili yako katikati ya nchi yako ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe uimiliki.+ 3 Utajitayarishia njia, nawe utagawa katika sehemu tatu lile eneo la nchi yako ambayo Yehova Mungu wako alikupa wewe iwe mali yako, nayo itakuwa kwa ajili ya muuaji yeyote, akimbilie humo.+
4 “Sasa hii ndiyo hukumu ya muuaji atakayekimbilia humo na ambaye ataishi: Anapompiga na kumuua mwenzake bila kujua naye hakuwa akimchukia hapo kwanza;+ 5 au anapoenda na mwenzake msituni kukusanya kuni, na mkono wake umeinuliwa ili kugonga kwa shoka ili kuukata mti, nacho chuma kiwe kimechomoka kutoka katika mpini wa mbao,+ na kiwe kimemgonga mwenzake naye akafa, yeye mwenyewe atakimbilia moja la majiji hayo naye ataishi.+ 6 Kama sivyo mlipiza-kisasi+ cha damu, kwa sababu moyo wake una moto, anaweza kumfuatilia muuaji, amfikie, kwa kuwa njia ni ndefu; naye anaweza kuipiga nafsi yake na kuiua, ingawa hakuna hukumu ya kifo+ kwa ajili yake, kwa sababu hakuwa akimchukia hapo kwanza. 7 Ndiyo sababu ninakuamuru wewe, na kusema, ‘Utajitengea majiji matatu.’+
8 “Na ikiwa Yehova Mungu wako atalipanua eneo lako kulingana na jambo alilowaapia mababu zako,+ naye amekupa wewe nchi yote aliyoahidi kuwapa mababu zako,+ 9 kwa sababu utaishika amri yote hii ninayokuamuru wewe leo kwa kuifanya, kumpenda Yehova Mungu wako na kutembea katika njia zake sikuzote,+ basi utajiongezea majiji mengine matatu kwa majiji haya matatu,+ 10 ili damu isiyo na hatia+ isimwagwe katikati ya nchi yako ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe iwe urithi, na hatia yoyote ya damu isiwe juu yako.+
11 “Lakini ikiwa kutakuwako mtu anayemchukia+ mwenzake, naye amemvizia, akainuka juu yake, akaipiga nafsi yake na kuiua naye amekufa,+ na mtu huyo amekimbilia moja la majiji hayo, 12 ndipo wanaume wazee wa jiji lake watatuma watu na kumchukua kutoka humo, nao watamtia mkononi mwa mlipiza-kisasi cha damu, naye lazima afe.+ 13 Jicho lako lisimsikitikie,+ nawe lazima uondolee mbali hatia ya damu isiyo na hatia kutoka katika Israeli,+ ili uwe na mema.
14 “Usisogeze nyuma alama za mpaka wa mwenzako,+ wakati ambapo mababu watakuwa wameweka mipaka katika urithi wako ambao utarithi katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe uimiliki.
15 “Shahidi mmoja asiinuke juu ya mtu kuhusu kosa au dhambi yoyote,+ kuhusu dhambi yoyote ambayo huenda akafanya. Kwa kinywa cha mashahidi wawili au kwa kinywa cha mashahidi watatu jambo hilo litathibitishwa vizuri.+ 16 Ikiwa shahidi anayepanga hila ya jeuri atainuka juu ya mtu na kuleta shtaka la maasi juu yake,+ 17 ndipo watu hao wawili wenye mzozo watakaposimama mbele za Yehova, mbele ya makuhani na waamuzi watakaokuwa wakitenda siku hizo.+ 18 Na waamuzi watatafuta kabisa,+ na ikiwa shahidi huyo ni shahidi wa uwongo naye ameleta shtaka la uwongo juu ya ndugu yake, 19 ndipo mtakapomfanyia kama vile alivyompangia ndugu yake hila,+ nawe utaondolea mbali kilicho kibaya kutoka katikati yako.+ 20 Kwa hiyo wale wanaobaki watasikia na kuogopa, nao hawatafanya tena kamwe jambo baya kama hilo katikati yako.+ 21 Na jicho lako lisisikitike:+ nafsi itakuwa kwa nafsi, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.+
20 “Ikiwa utaenda katika pigano juu ya adui zako nawe uone farasi na magari ya vita,+ watu wengi kuliko wewe, usiwaogope; kwa maana Yehova Mungu wako yuko pamoja nawe,+ aliyekutoa katika nchi ya Misri.+ 2 Na itatukia kwamba mtakapokuwa mmekaribia pigano, ndipo kuhani atakapokaribia na kusema na watu.+ 3 Naye atawaambia, ‘Sikieni, Ee Israeli, mnakaribia leo kupigana na adui zenu. Msiache mioyo yenu iogope.+ Msiogope na kukimbia kwa wasiwasi au kutetemeka kwa sababu yao,+ 4 kwa maana Yehova Mungu wenu anapiga mwendo pamoja nanyi ili kupigana kwa ajili yenu juu ya adui zenu apate kuwaokoa ninyi.’+
5 “Maofisa+ pia watasema na watu, na kuwaambia, ‘Ni nani ambaye amejenga nyumba mpya naye hajaizindua? Na aende na kurudi nyumbani kwake, asije akafa vitani na mwanamume mwingine aizindue.+ 6 Na ni nani ambaye amepanda shamba la mizabibu naye hajaanza kutumia matunda yake? Na aende na kurudi nyumbani kwake, asije akafa vitani na mwanamume mwingine akaanza kutumia matunda yake.+ 7 Na ni nani ambaye amemchumbia mwanamke naye hajamchukua? Na aende na kurudi nyumbani kwake,+ asije akafa vitani na mwanamume mwingine amchukue mwanamke huyo.’ 8 Nao maofisa watazidi kusema na watu na kuwaambia, ‘Ni nani mwoga na mwenye moyo dhaifu?+ Na aende na kurudi nyumbani kwake, asije akasababisha mioyo ya ndugu zake iyeyuke kama moyo wake mwenyewe.’+ 9 Na itatukia kwamba wakati ambapo maofisa hao watakuwa wamemaliza kusema na watu, ndipo watakapoweka pia wakuu wa majeshi mbele ya watu.
10 “Ikiwa utakaribia jiji ili kupigana nalo, utalitangazia pia masharti ya amani.+ 11 Na itatukia kwamba ikiwa litakutolea jibu la amani nalo limekufungulia, itatukia pia kwamba watu wote watakaopatikana ndani yake watakuwa wako kwa ajili ya kazi ya kulazimishwa, nao watakutumikia.+ 12 Lakini lisipofanya amani pamoja nawe,+ nalo lifanye vita pamoja nawe, nawe ulazimike kulizingira, 13 Yehova Mungu wako hakika atalitia mkononi mwako, nawe utampiga kila mwanamume aliye ndani yake kwa makali ya upanga.+ 14 Utapora kwa ajili yako+ wanawake tu na watoto wadogo+ na wanyama wa kufugwa+ na kila kitu kitakachokuwa jijini, nyara zake zote; nawe utakula nyara za adui zako, ambao Yehova Mungu wako amekupa wewe.+
15 “Hivyo ndivyo utakavyoyafanyia majiji yote yaliyo mbali sana nawe ambayo si majiji ya mataifa haya. 16 Ni katika majiji ya watu hawa tu ambayo Yehova anakupa yawe urithi ambayo hutaacha hai chochote kinachopumua,+ 17 kwa sababu lazima utawaangamiza, Wahiti na Waamori, Wakanaani na Waperizi, Wahivi na Wayebusi,+ kama vile ambavyo Yehova Mungu wako amekuamuru; 18 ili wasiwafundishe kulingana na machukizo yao yote, ambayo wameifanyia miungu yao, nanyi mumtendee dhambi Yehova Mungu wenu.+
19 “Ikiwa utazingira jiji siku nyingi kwa kupigana nalo ili kuliteka, usiharibu miti yake kwa kutumia shoka juu yake; kwa maana utakula kutokana nayo, nawe usiikate na kuiangusha,+ kwani mti wa shamba je, ni mtu ndipo uuzingire? 20 Ila mti ambao wewe unajua kwamba si mti wa chakula, huo ndio unaopaswa kuharibu, nawe utaukata na kujenga mazingiwa+ juu ya jiji linalofanya vita nawe, mpaka lianguke.
21 “Ikiwa mtu atapatikana akiwa ameuawa katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa uimiliki, akiwa ameanguka uwanjani, na haijajulikana ni nani aliyempiga na kumuua,+ 2 wanaume wako wazee na waamuzi+ wako watatoka nje na kupima mpaka kwenye majiji yanayomzunguka mtu aliyeuawa; 3 na itakuwa ni lile jiji lililo karibu zaidi na yule aliyeuawa. Nao wanaume wazee wa jiji hilo watamchukua ng’ombe mchanga kutoka kati ya mifugo ambaye hajafanya kazi, ambaye hajavuta nira; 4 na wanaume wazee wa jiji hilo watampeleka ng’ombe huyo mpaka kwenye bonde la mto wenye maji yanayotiririka ambapo kidesturi hapakuwa na kulima wala kupanda mbegu, nao watavunja shingo ya ng’ombe huyo mchanga katika bonde hilo la mto.+
5 “Na makuhani wana wa Lawi watakaribia, kwa sababu hao ndio Yehova Mungu wako amechagua wamhudumie+ na kulisifu+ jina la Yehova na ambao kwa kinywa chao kila mzozo juu ya kila tendo lenye jeuri, wapasa kuondolewa mbali.+ 6 Kisha wanaume wote wazee wa jiji hilo walio karibu zaidi na mtu aliyeuawa wataosha mikono yao+ juu ya yule ng’ombe mchanga, ambaye shingo yake ilivunjwa katika lile bonde la mto; 7 nao watajibu na kusema, ‘Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona ikimwagwa.+ 8 Usiihesabie watu wako Israeli, ambao ulikomboa,+ Ee Yehova, wala usiweke katikati ya watu wako Israeli hatia ya damu isiyo na hatia.’+ Na wasihesabiwe hatia hiyo ya damu. 9 Na wewe—wewe utaondolea mbali hatia ya damu kutoka katikati yako,+ kwa sababu utafanya yaliyo sawa machoni pa Yehova.+
10 “Ikiwa utaenda vitani kupigana na adui zako na Yehova Mungu wako awe amewatia mkononi mwako+ nawe uwachukue mateka;+ 11 nawe uone kati ya mateka hao mwanamke mwenye umbo zuri, nawe ushikamane naye+ na kumchukua awe mke wako, 12 ndipo utakapomleta ndani ya nyumba yako. Lazima anyoe kichwa chake,+ atunze kucha zake, 13 na kuvua nguo ya kujitanda ya utekwa wake, akae katika nyumba yako, amlilie baba yake na mama yake kwa mwezi mzima;+ na baada ya jambo hilo utalala naye, nawe utamchukua awe bibi-arusi wako, naye atakuwa mke wako. 14 Na itatukia kwamba ikiwa hukupendezwa naye, basi utamwacha aende zake,+ kama inavyopenda nafsi yake mwenyewe; lakini hutamuuza kamwe kwa ajili ya pesa. Usimwonee+ baada ya kumfedhehesha.
15 “Ikiwa mwanamume atakuwa na wake wawili, mmoja anayependwa na mwingine anayechukiwa, nao, yule anayependwa na yule anayechukiwa, wamzalie wana, na iwe kwamba mwana mzaliwa wa kwanza ni wa yule anayechukiwa,+ 16 pia itatukia kwamba katika siku ambayo atawapa wanawe urithi wa vitu alivyo navyo, hataruhusiwa kumfanya mwana wa yule anayependwa awe mzaliwa wake wa kwanza kwa hasara ya mwana wa yule anayechukiwa, mzaliwa wa kwanza.+ 17 Kwa maana anapaswa kumtambua mwana wa yule anayechukiwa kuwa mzaliwa wa kwanza kwa kumpa sehemu mbili za kila kitu alicho nacho,+ kwa sababu huyo ndiye mwanzo wa nguvu zake za uzazi.+ Haki ya cheo cha mzaliwa wa kwanza ni yake.+
18 “Ikiwa mtu atakuwa na mwana ambaye ni mkaidi na mwasi,+ awe hasikilizi sauti ya baba yake au sauti ya mama yake,+ nao wamemrekebisha bali yeye hawasikilizi,+ 19 baba yake na mama yake watamshika na kumtoa nje mpaka kwa wanaume wazee wa jiji lake na kwenye lango la mahali pake,+ 20 nao watawaambia wanaume wazee wa jiji lake, ‘Huyu mwana wetu ni mkaidi na mwasi; hasikilizi sauti yetu,+ ni mlafi+ na mlevi.’+ 21 Ndipo watu wote wa jiji watampiga kwa mawe, naye lazima afe. Kwa hiyo mtaondolea mbali kilicho kibaya kutoka kati yenu, na Israeli wote watasikia na kuogopa kwelikweli.+
22 “Na ikiwa mtu atakuwa na dhambi inayostahili hukumu ya kifo, naye ameuawa,+ nawe umemtundika juu ya mti,+ 23 maiti yake isibaki usiku kucha juu ya mti;+ bali kwa vyovyote utamzika siku hiyo, kwa sababu mtu aliyetundikwa ni kitu kilicholaaniwa na Mungu;+ nawe usiitie unajisi nchi yako, ambayo Yehova Mungu wako anakupa iwe urithi.+
22 “Usimwone ng’ombe wa ndugu yako au kondoo wake akipotea njia nawe uwaache kimakusudi.+ Kwa vyovyote unapaswa kuwarudisha kwa ndugu yako.+ 2 Na ikiwa ndugu yako hayuko karibu nawe na wewe hujamjua, utamleta mnyama huyo nyumbani mwako, naye atakaa nawe mpaka ndugu yako awe amemtafuta. Nawe utamrudisha kwake.+ 3 Hivyo ndivyo pia utakavyofanya na punda wake, na hivyo ndivyo utakavyofanya na nguo yake ya kujitanda, na hivyo ndivyo utakavyofanya na kitu chochote kilichopotea cha ndugu yako, kinachopotea kutoka kwake na ambacho umepata. Hutaruhusiwa kukiacha.
4 “Usimwone punda wa ndugu yako au ng’ombe wake akianguka barabarani nawe uwaache kimakusudi. Kwa vyovyote unapaswa kuwasaidia na kuwainua.+
5 “Vazi lolote la mwanamume lisivaliwe na mwanamke, wala mwanamume asivae nguo ya kujitanda ya mwanamke;+ kwa maana mtu yeyote anayefanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova Mungu wako.
6 “Ikiwa kiota cha ndege kitakuwa mbele yako njiani, katika mti wowote au chini kikiwa na vifaranga+ au mayai, naye mama anakalia vifaranga au mayai, usimchukue mama pamoja na watoto.+ 7 Kwa vyovyote unapaswa kumwacha mama aende zake, lakini unaweza kuchukua watoto; ili mambo yapate kukuendea vema wewe, nawe urefushe siku zako.+
8 “Ikiwa utajenga nyumba mpya, pia utafanya ukuta wa ukingoni kwa ajili ya dari lako,+ ili usiletee nyumba yako hatia ya damu kwa sababu mtu anaweza kuanguka kutoka hapo.
9 “Usipande shamba lako la mizabibu aina mbili za mbegu,+ mazao kamili ya mbegu hiyo ambayo huenda ukapanda na mazao ya shamba la mizabibu yasije yakatwaliwa na patakatifu.
10 “Usilime kwa ng’ombe-dume na punda pamoja.+
11 “Usivae kitu kilichochanganywa cha sufu na kitani pamoja.+
12 “Utajifanyia shada kwenye miisho minne ya mavazi yako ambayo wewe hujifunika nayo.+
13 “Ikiwa mwanamume atamchukua mwanamke, alale naye, na aje kumchukia,+ 14 naye awe amemshtaki mwanamke huyo kuwa mwenye matendo yenye sifa mbaya na kuleta jina baya+ juu yake, naye amesema, ‘Mwanamke huyu nimemchukua, nikamkaribia, nami sikupata uthibitisho wa ubikira ndani yake’;+ 15 baba ya msichana huyo na mama yake wataleta uthibitisho wa ubikira wa msichana huyo kwa wanaume wazee wa jiji hilo kwenye lango lake;+ 16 naye baba ya msichana atawaambia wanaume wazee, ‘Nilimpa mwanamume huyu binti yangu awe mke wake, naye akamchukia.+ 17 Na tazama, anamshtaki juu ya matendo yenye sifa mbaya,+ na kusema: “Nimepata kujua kwamba binti yako hana uthibitisho wa ubikira.”+ Sasa huu ndio uthibitisho wa ubikira wa binti yangu.’ Nao watatandaza nguo hiyo ya kujitanda mbele ya wanaume wazee wa jiji hilo. 18 Nao wanaume wazee+ wa jiji hilo watamchukua mwanamume huyo na kumtia nidhamu.+ 19 Nao watamtoza shekeli mia moja na kumpa baba ya msichana huyo, kwa sababu alileta jina baya juu ya bikira wa Israeli;+ naye ataendelea kuwa mke wake. Hataruhusiwa kumtaliki siku zake zote.
20 “Hata hivyo, ikiwa jambo hilo limeonekana kuwa kweli, uthibitisho wa ubikira haukupatikana ndani ya msichana huyo,+ 21 watamtoa nje msichana huyo kwenye mlango wa nyumba ya baba yake, nao watu wa jiji lake watampiga kwa mawe, naye lazima afe, kwa sababu amefanya upumbavu wenye kufedhehesha+ katika Israeli kwa kufanya ukahaba katika nyumba ya baba yake.+ Kwa hiyo lazima utaondolea mbali lililo baya kutoka katikati yako.+
22 “Ikiwa mwanamume atapatikana akilala na mwanamke aliye na mume,+ wote wawili watauawa pamoja, yule mwanamume anayelala na mwanamke pamoja na huyo mwanamke.+ Kwa hiyo lazima utaondolea mbali lililo baya kutoka katika Israeli.+
23 “Ikiwa kulikuwa na msichana bikira aliyechumbiwa na mwanamume,+ na mwanamume fulani akamkuta jijini na kulala naye,+ 24 mtawatoa wote wawili mpaka kwenye lango la jiji na kuwapiga kwa mawe, nao lazima wafe, yule msichana kwa sababu hakupiga mayowe jijini, na yule mwanamume kwa sababu alimfedhehesha mke wa mwenzake.+ Kwa hiyo lazima utaondolea mbali lililo ovu kutoka katikati yako.+
25 “Hata hivyo, ikiwa mwanamume huyo alimkuta uwanjani msichana huyo aliyechumbiwa, naye mwanamume huyo akamkamata na kulala naye, mwanamume huyo aliyelala naye atakufa yeye peke yake, 26 naye yule msichana msimfanye lolote. Msichana huyo hana dhambi inayostahili kifo, kwa sababu kama vile mtu humwinukia mwenzake na kumuua,+ naam, nafsi, ndivyo ilivyo katika hali hii. 27 Kwa maana alimkuta uwanjani. Msichana aliyechumbiwa alipiga mayowe, lakini hakukuwa na mtu wa kumwokoa.
28 “Na mwanamume akimkuta msichana, bikira ambaye hajachumbiwa, naye kwa kweli amkamate na kulala naye,+ nao wapatikane,+ 29 mwanamume aliyelala naye atampa baba ya msichana shekeli 50,+ naye msichana huyo atakuwa mke wake kwa sababu mwanamume huyo alimfedhehesha. Hataruhusiwa kumtaliki siku zake zote.+
30 “Mwanamume yeyote hapaswi kumchukua mke wa baba yake, asije akaufunua upindo wa nguo ya baba yake.+
23 “Mwanamume yeyote aliyefanywa towashi+ kwa kuvunjwa mapumbu+ au kwa kukatwa uume wake asiingie katika kutaniko la Yehova.
2 “Mwana-haramu+ yeyote asiingie katika kutaniko la Yehova. Hata kufikia kizazi cha kumi mtu yeyote wake asiingie katika kutaniko la Yehova.
3 “Mwamoni au Mmoabu yeyote asiingie katika kutaniko la Yehova.+ Hata kufikia kizazi cha kumi mtu yeyote wao asiingie katika kutaniko la Yehova mpaka wakati usio na kipimo, 4 kwa sababu hawakuja kuwasaidia+ kwa mkate na maji njiani mlipokuwa mkitoka Misri,+ na kwa sababu walimkodi juu yako Balaamu yule mwana wa Beori kutoka Pethori ya Mesopotamia, ili akulaani.+ 5 Na Yehova Mungu wako hakutaka kumsikiliza Balaamu;+ lakini Yehova Mungu wako kwa ajili yako aligeuza ile laana ikawa baraka,+ kwa sababu Yehova Mungu wako alikupenda.+ 6 Usifanyie kazi amani yao na ufanisi wao siku zako zote mpaka wakati usio na kipimo.+
7 “Usimchukie Mwedomu, kwa maana yeye ni ndugu yako.+
“Usimchukie Mmisri, kwa maana ulikuwa mkaaji mgeni katika nchi yake.+ 8 Wana ambao huenda wakazaliwa wakiwa kizazi cha tatu wanaweza kuingia wenyewe katika kutaniko la Yehova.
9 “Ikiwa utaenda nje kambini kupigana na adui zako, ndipo utajiepusha na kila jambo baya.+ 10 Ikiwa kati yako kutakuwa na mwanamume ambaye haendelei kuwa safi, kwa sababu ya uchafuzi ambao hutukia usiku,+ atatoka nje ya kambi. Hataingia katikati ya kambi.+ 11 Na itatukia kwamba jioni inapofika ataoga kwa maji, na wakati wa kutua kwa jua anaweza kuingia katikati ya kambi.+ 12 Na mahali pa faragha panapaswa kuwapo kwa ajili ya matumizi yako nje ya kambi, nawe utaenda nje huko. 13 Nawe unapaswa kuwa na kijiti cha kuchimbia kwa ajili ya matumizi yako pamoja na vifaa vyako, na itatukia kwamba utakapochutama nje, utachimba shimo pia kwa hicho na kugeuka na kufunika mavi yako.+ 14 Kwa maana Yehova Mungu wako anatembea ndani ya kambi yako ili kukukomboa+ na kuwatia adui zako mkononi mwako;+ na kambi yako lazima iwe takatifu,+ ili asione kitu chochote kisichofaa ndani yako naye ageuke na kuacha kuandamana nawe.+
15 “Usimtie mtumwa mkononi mwa bwana wake anapomkimbia bwana wake na kuja kwako.+ 16 Ataendelea kukaa pamoja nawe katikati yako katika mahali popote atakapochagua katika moja la majiji yako,+ popote anapopenda. Usimtendee vibaya.+
17 “Yeyote kati ya binti za Israeli asiwe kahaba wa hekaluni,+ wala yeyote kati ya wana wa Israeli asiwe kahaba wa hekaluni.+ 18 Usilete malipo+ ya kahaba au bei ya mbwa+ ndani ya nyumba ya Yehova Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu hao ni chukizo kwa Yehova Mungu wako, naam, wote wawili.
19 “Usimfanye ndugu yako alipe faida,+ faida juu ya pesa, faida juu ya chakula,+ faida juu ya kitu chochote ambacho mtu anaweza kudai faida. 20 Unaweza kumlipiza mgeni+ faida, lakini ndugu yako usimfanye alipe faida;+ ili Yehova Mungu wako akubariki katika kazi zako zote katika nchi ambayo unaenda kuimiliki.+
21 “Ikiwa utaweka nadhiri kwa Yehova+ Mungu wako, usikawie kuitimiza,+ kwa sababu Yehova Mungu wako lazima ataitaka kutoka kwako, nayo kwa kweli itakuwa dhambi kwako.+ 22 Lakini ikiwa utaepuka kuweka nadhiri, haitakuwa dhambi kwako.+ 23 Maneno ya midomo yako utayatimiza,+ nawe lazima ufanye kama vile ambavyo umeweka nadhiri kwa Yehova Mungu wako kama toleo la hiari ambalo ulisema kwa kinywa chako.+
24 “Ikiwa utaingia katika shamba la mizabibu la mwenzako, utakula zabibu zinazotosha kuishibisha nafsi yako tu, lakini usitie zozote katika chombo chako.+
25 “Ikiwa utaenda kwenye nafaka ya mwenzako inayosimama, utachuma masuke yaliyoiva tu kwa mkono wako, lakini usiusogeze mundu huku na huku juu ya nafaka inayosimama ya mwenzako.+
24 “Mwanamume akimchukua mwanamke na kumfanya awe mke wake, pia itatukia kwamba ikiwa hatapata kibali machoni pake kwa sababu amepata kitu fulani kisichofaa katika mwanamke huyo,+ atamwandikia pia cheti cha talaka+ na kukitia mkononi mwake na kumfukuza kutoka katika nyumba yake.+ 2 Naye ataondoka katika nyumba ya mwanamume huyo, akawe mke wa mwanamume mwingine.+ 3 Ikiwa yule mwanamume wa mwisho amekuja kumchukia naye amemwandikia cheti cha talaka, akakitia mkononi mwake na kumfukuza kutoka katika nyumba yake, au ikiwa yule mwanamume wa mwisho aliyemchukua awe mke wake atakufa, 4 yule mume wa kwanza aliyemfukuza hataruhusiwa kumchukua tena awe mke wake baada ya mwanamke huyo kutiwa unajisi;+ kwa maana hilo ni chukizo mbele za Yehova, nawe usiingize katika dhambi nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe iwe urithi.
5 “Ikiwa mwanamume atamchukua mwanamke mpya,+ hapaswi kwenda jeshini, wala asitwikwe jambo lingine lolote. Ataachwa akae katika nyumba yake kwa mwaka mmoja, naye amfanye mke wake ambaye amemwoa ashangilie.+
6 “Mtu yeyote asitwae kuwa rehani jiwe la kusagia la mkononi au jiwe lake la juu la kusagia,+ kwa sababu ni nafsi anayoitwaa kuwa rehani.
7 “Ikiwa mtu atapatikana akiteka nyara+ nafsi ya ndugu zake wa wana wa Israeli, naye amemtendea kwa uonevu na kumuuza,+ mteka-nyara huyo lazima afe. Nawe lazima uondolee mbali lililo baya kutoka katikati yako.+
8 “Jilinde katika pigo la ukoma,+ ujitunze vizuri na kufanya yote ambayo makuhani Walawi watawaagiza ninyi.+ Kama vile nilivyowaamuru, muwe waangalifu kufanya.+ 9 Jambo ambalo Yehova Mungu wako alimtendea Miriamu njiani mlipokuwa mkija kutoka Misri lapasa kukumbukwa.+
10 “Ikiwa utamkopesha mwenzako mkopo wa namna yoyote,+ usiingie katika nyumba yake ili kuchukua kutoka kwake kitu ambacho amekiweka kuwa rehani.+ 11 Unapaswa kusimama nje, na mtu ambaye unamkopesha atakuletea hiyo rehani nje. 12 Na ikiwa mtu huyo yuko katika taabu, hupaswi kwenda kulala na rehani yake.+ 13 Kwa vyovyote unapaswa kumrudishia rehani hiyo mara tu baada ya jua kutua,+ naye ataenda kulala na vazi lake,+ naye atakubariki;+ nalo hilo litamaanisha uadilifu kwako mbele za Yehova Mungu wako.+
14 “Hupaswi kumpunja mfanyakazi wa kukodiwa aliye katika taabu na aliye maskini, awe wa ndugu zako au wa wakaaji wageni wako walio katika nchi yako, ndani ya malango yako.+ 15 Katika siku yake utampa malipo yake,+ nalo jua lisitue juu yake, kwa sababu yeye yuko katika taabu naye anaiinua nafsi yake kwa malipo yake; ili asimlilie Yehova juu yako,+ na iwe dhambi kwako.+
16 “Akina baba wasiuawe kwa sababu ya watoto, na watoto wasiuawe kwa sababu ya akina baba.+ Kila mmoja atauawa kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe.+
17 “Hupaswi kupotosha hukumu ya mkaaji mgeni+ au ya mvulana asiye na baba,+ nawe hupaswi kutwaa vazi la mjane kama rehani.+ 18 Nawe lazima ukumbuke kwamba ulikuwa mtumwa katika Misri, na Yehova Mungu wako alikukomboa kutoka huko.+ Ndiyo sababu ninakuamuru ufanye jambo hili.
19 “Ikiwa utavuna mavuno ya shamba lako,+ nawe umesahau mganda shambani, hupaswi kurudi kuuchukua. Huo utakaa kwa ajili ya mkaaji mgeni, kwa ajili ya mvulana asiye na baba na kwa ajili ya mjane;+ ili Yehova Mungu wako akubariki katika kila tendo la mkono wako.+
20 “Ikiwa utachuma mzeituni wako, usipitie matawi yake tena. Huo wapaswa kukaa hivyo kwa ajili ya mkaaji mgeni, kwa ajili ya mvulana asiye na baba na kwa ajili ya mjane.+
21 “Ikiwa utakusanya zabibu za shamba lako la mizabibu, hupaswi kurudi na kukusanya masalio tena. Yatabaki hivyo kwa ajili ya mkaaji mgeni, kwa ajili ya mvulana asiye na baba na kwa ajili ya mjane. 22 Nawe utakumbuka kwamba ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri.+ Ndiyo sababu ninakuamuru ufanye jambo hili.+
25 “Ikiwa mzozo utatokea kati ya watu,+ nao wamejitokeza kwa ajili ya hukumu,+ watawahukumu na kumtangaza mwadilifu kuwa mwadilifu na mwovu kuwa mwovu.+ 2 Na itatukia kwamba ikiwa yule mwovu anastahili kupigwa,+ atalazwa kifudifudi na mwamuzi na kupigwa+ mbele yake kwa hesabu inayolingana na tendo lake baya. 3 Anaweza kumpiga kwa mapigo 40. Asiongeze lolote, asije akaendelea kumpiga kwa mapigo mengi zaidi ya hayo+ naye ndugu yako afedheheke machoni pako.
4 “Hupaswi kumfunga kinywa ng’ombe-dume anapopura.+
5 “Ikiwa ndugu wanakaa pamoja na mmoja wao awe amekufa bila kuwa na mwana wa kiume, mke wa yule aliyekufa asiwe wa mwanamume mgeni wa nje. Ndugu-mkwe wake anapaswa kumwendea, naye lazima amchukue awe mke wake na kufanya ndoa ya ndugu-mkwe pamoja naye.+ 6 Na itatukia kwamba mzaliwa wa kwanza atakayemzaa ataendeleza jina la ndugu yake aliyekufa,+ ili jina lake lisifutwe kutoka katika Israeli.+
7 “Sasa ikiwa mwanamume huyo hapendezwi kumchukua mjane wa ndugu yake, mjane wa ndugu yake ataenda langoni kwa wanaume wazee+ na kusema, ‘Ndugu ya mume wangu amekataa kuhifadhi jina la ndugu yake katika Israeli. Hakukubali kufanya ndoa ya ndugu-mkwe pamoja nami.’ 8 Nao wanaume wazee wa jiji lake watamwita na kusema naye, naye atasimama na kusema, ‘Sikupendezwa kumchukua.’+ 9 Ndipo mjane wa ndugu yake atamkaribia mbele ya macho ya wanaume wazee, avue kiatu cha mwanamume huyo kutoka mguuni+ pake, amtemee mate usoni,+ ajibu na kusema, ‘Hivyo ndivyo inavyopaswa kufanyiwa mwanamume ambaye hatajenga nyumba ya ndugu yake.’+ 10 Nalo jina lake litaitwa katika Israeli ‘Nyumba ya yule ambaye kiatu chake kilivuliwa.’
11 “Ikiwa wanaume wawili watapambana pamoja, na mke wa mmoja awe amekuja karibu ili kumkomboa mume wake kutoka mkononi mwa yule anayempiga, naye ameunyoosha mkono wake na kumkamata sehemu zake za siri,+ 12 basi lazima utaukata mkono wa mwanamke huyo. Jicho lako lisiwe na huruma.+
13 “Hupaswi kuwa na aina mbili za mawe ya mizani katika mfuko wako,+ kubwa na dogo. 14 Hupaswi kuwa na aina mbili za vipimo vya efa+ nyumbani mwako, kikubwa na kidogo. 15 Utaendelea kuwa na kipimo cha uzito kilicho sahihi na cha haki. Utaendelea kuwa na kipimo cha efa kilicho sahihi na cha haki, ili siku zako ziwe ndefu kwenye nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe.+ 16 Kwa maana kila mtu anayefanya mambo haya, kila anayefanya ukosefu wa haki, ni chukizo kwa Yehova Mungu wako.+
17 “Jambo ambalo Amaleki alikutendea njiani mlipokuwa mkitoka Misri, likumbukwe,+ 18 jinsi alivyokukuta njiani naye akaanza kupiga upande wa nyuma wale wote waliokuwa wanajikokota nyuma yako, nawe ulikuwa umeishiwa na nguvu na kuchoka; naye hakumwogopa Mungu.+ 19 Na itatukia kwamba wakati ambapo Yehova Mungu wako atakuwa amekupumzisha kutokana na adui zako wanaokuzunguka pande zote katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa iwe urithi ili uimiliki,+ utafutilia mbali jina la Amaleki kutoka chini ya mbingu.+ Hupaswi kusahau.
26 “Na itatukia kwamba mwishowe utakapoingia katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa iwe urithi, nawe umeimiliki na kukaa ndani yake,+ 2 utachukua pia sehemu ya matunda ya kwanza ya mazao ya udongo, ambayo utaleta ndani kutoka katika nchi yako ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe, nawe utayatia katika kikapu na kwenda mahali ambapo Yehova+ Mungu wako atachagua ili jina lake likae hapo.+ 3 Nawe utakuja kwa kuhani+ atakayekuwa akitenda katika siku hizo na kumwambia, ‘Lazima nitoe habari leo kwa Yehova Mungu wako kwamba nimekuja katika nchi ambayo Yehova aliwaapia mababu zetu kwamba atatupa sisi.’+
4 “Naye kuhani atachukua kile kikapu kutoka mkononi mwako na kukiweka mbele ya madhabahu ya Yehova Mungu wako. 5 Nawe utajibu na kusema mbele za Yehova Mungu wako, ‘Baba yangu alikuwa Msiria+ anayeangamia; naye akashuka kwenda Misri+ na kukaa huko akiwa mgeni akiwa na hesabu ndogo sana;+ lakini huko akawa taifa kubwa, lenye nguvu na lenye watu wengi.+ 6 Nao Wamisri wakaanza kututendea vibaya na kututesa na kuweka utumwa mgumu juu yetu.+ 7 Nasi tukaanza kumlilia Yehova Mungu wa mababu zetu,+ naye Yehova akaisikia sauti yetu+ na kutazama mateso yetu na taabu yetu na kukandamizwa kwetu.+ 8 Mwishowe Yehova akatuleta kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu+ na mkono ulionyooshwa+ na kwa woga+ mkuu na kwa ishara na miujiza.+ 9 Kisha akatuleta mahali hapa na kutupa sisi nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ 10 Na sasa, tazama, nimeleta matunda ya kwanza ya mazao ya nchi ambayo Yehova amenipa mimi.’+
“Utayaweka mbele za Yehova Mungu wako na kuinama chini mbele za Yehova Mungu wako.+ 11 Nawe utashangilia+ mema yote ambayo Yehova Mungu wako amekupa wewe na nyumba yako, wewe na Mlawi na mkaaji mgeni aliye katikati yako.+
12 “Unapomaliza kutoa zaka ya sehemu yote ya kumi+ ya mazao yako katika mwaka wa tatu,+ mwaka wa sehemu ya kumi, utampa Mlawi pia, mkaaji mgeni, mvulana asiye na baba na mjane, nao wataila ndani ya malango yako na kujishibisha.+ 13 Nawe utasema mbele za Yehova Mungu wako, ‘Nimeondolea mbali kilicho kitakatifu kutoka katika nyumba nami pia nimempa Mlawi na mkaaji mgeni, na mvulana asiye na baba na mjane,+ kulingana na amri yako yote ambayo umenipa mimi. Sijavunja amri zako, wala sijasahau.+ 14 Sijaila wakati wa kuomboleza kwangu, wala sijaondoa sehemu yake yoyote nikiwa si safi, wala sijatoa sehemu yake yoyote kwa ajili ya yeyote aliyekufa. Nimeisikiliza sauti ya Yehova Mungu wangu. Nimefanya kulingana na yote ambayo umeniamuru. 15 Utazame chini kutoka katika makao yako matakatifu,+ mbinguni, na kuwabariki watu wako Israeli+ na udongo ambao umetupa sisi, kama vile ulivyowaapia mababu zetu,+ nchi inayotiririka maziwa na asali.’+
16 “Leo Yehova Mungu wako anakuamuru utimize haya masharti na maamuzi ya hukumu;+ nawe utazishika na kuzitimiza kwa moyo+ wako wote na nafsi yako yote.+ 17 Yehova umemfanya aseme leo kwamba atakuwa Mungu wako unapotembea katika njia zake na kushika masharti+ yake na amri+ zake na maamuzi yake ya hukumu+ na kusikiliza sauti+ yake. 18 Naye Yehova, amekufanya useme leo kwamba utakuwa kikundi cha watu wake, mali ya pekee,+ kama vile alivyokuahidi,+ na kwamba utashika amri zake zote, 19 na kwamba atakuweka wewe juu kuliko mataifa mengine yote ambayo ameyafanya,+ hilo likitokeza sifa na heshima na uzuri, huku ukijithibitisha kuwa kikundi cha watu kilicho kitakatifu kwa Yehova Mungu wako,+ kama vile ambavyo ameahidi.”
27 Na Musa pamoja na wanaume wazee wa Israeli wakawaamuru watu, na kusema: “Kila amri ninayowaamuru ninyi leo, itashikwa.+ 2 Na itatukia kwamba katika siku ambayo mtavuka Yordani+ kuingia katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe, utajiwekea pia mawe makubwa na kuyapaka chokaa. 3 Nawe utaandika juu yake maneno yote ya sheria hii+ utakapokuwa umevuka,+ ili uingie katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe, nchi inayotiririka maziwa na asali, kulingana na yale ambayo Yehova Mungu wa mababu zako amesema nawe.+ 4 Na itatukia kwamba mtakapokuwa mmevuka Yordani, mtayasimamisha mawe hayo, kama ninavyowaamuru ninyi leo, katika Mlima Ebali,+ nawe utayapaka chokaa.+ 5 Pia utamjengea Yehova Mungu wako madhabahu huko, madhabahu ya mawe. Usitumie chombo cha chuma juu yake.+ 6 Kwa mawe mazima utaijenga madhabahu ya Yehova Mungu wako, nawe utamtolea Yehova Mungu wako matoleo ya kuteketezwa juu yake.+ 7 Nawe utatoa dhabihu za ushirika+ na kuzila huko,+ nawe utashangilia mbele za Yehova Mungu wako.+ 8 Nawe utaandika juu ya mawe hayo maneno yote ya sheria hii,+ na kuyafanya yawe wazi kabisa.”+
9 Ndipo Musa na makuhani Walawi wakasema na Israeli wote, na kuwaambia: “Kaa kimya, usikilize, Ee Israeli. Leo umekuwa kikundi cha watu wa Yehova Mungu wako.+ 10 Nawe uisikilize sauti ya Yehova Mungu wako na kutimiza amri+ zake na masharti+ yake, ninayokuamuru leo.”
11 Naye Musa akaendelea kuwaamuru watu katika siku hiyo, na kusema: 12 “Wanaofuata ndio watakaosimama ili kuwabariki watu kwenye Mlima Gerizimu+ wakati ambapo mtakuwa mmevuka Yordani: Simeoni na Lawi na Yuda na Isakari na Yosefu na Benyamini. 13 Na wanaofuata ndio watakaosimama kwa ajili ya laana+ kwenye Mlima Ebali:+ Rubeni, Gadi na Asheri na Zabuloni, Dani na Naftali. 14 Nao Walawi watamjibu kila mtu wa Israeli na kusema kwa sauti iliyopaazwa:+
15 “‘Amelaaniwa mtu ambaye anafanya sanamu ya kuchongwa+ au sanamu ya kuyeyushwa,+ kitu kinachochukiza kwa Yehova,+ kilichotengenezwa kwa mikono ya mfanyakazi wa mbao na chuma,+ na ambaye amekiweka mafichoni.’ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)+
16 “‘Amelaaniwa yule ambaye humtendea baba yake au mama yake kwa dharau.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
17 “‘Amelaaniwa yule ambaye huisogeza nyuma alama ya mpaka wa mwenzake.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
18 “‘Amelaaniwa yule ambaye humpotosha kipofu njiani.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
19 “‘Amelaaniwa yule ambaye hupotosha+ hukumu+ ya mkaaji mgeni,+ mvulana asiye na baba na mjane.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
20 “‘Amelaaniwa yule ambaye hulala na mke wa baba yake, kwa sababu ameufunua upindo wa nguo ya baba yake.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
21 “‘Amelaaniwa yule ambaye hulala na mnyama yeyote.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
22 “‘Amelaaniwa yule ambaye hulala na dada yake, binti ya baba yake au binti ya mama yake.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
23 “‘Amelaaniwa yule ambaye hulala na mama-mkwe wake.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
24 “‘Amelaaniwa yule ambaye kutoka mafichoni humpiga na kumuua mwenzake.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
25 “‘Amelaaniwa yule ambaye hukubali rushwa ili kuipiga na kuiua nafsi, wakati ambapo hiyo ni damu isiyo na hatia.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
26 “‘Amelaaniwa yule ambaye hatayatimiza maneno ya sheria hii kwa kuyafanya.’+ (Nao watu wote watajibu na kusema, ‘Amina!’)
28 “Na itatukia kwamba ikiwa hakika utaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kuwa mwangalifu kutenda amri zake zote ninazokuamuru leo,+ Yehova Mungu wako atakuweka juu, juu ya mataifa mengine yote ya dunia.+ 2 Nazo baraka hizi zote zitakujia na kukufikia,+ kwa sababu umeendelea kuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wako:
3 “Utabarikiwa jijini,+ nawe utabarikiwa shambani.+
4 “Utabarikiwa uzao wa tumbo+ lako na mazao ya udongo wako na uzao wa mnyama wako wa kufugwa,+ mtoto wa ng’ombe wako na uzao wa kundi lako.+
5 “Kitabarikiwa kikapu+ chako na kikandio chako.+
6 “Utabarikiwa unapoingia ndani, na utabarikiwa unapotoka nje.+
7 “Yehova atawafanya adui zako wanaoinuka juu yako washindwe mbele yako.+ Kwa njia moja watakuja juu yako, lakini kwa njia saba watakimbia kutoka mbele yako.+ 8 Yehova atakuagizia baraka kwenye maghala yako ya chakula+ na kila kazi unayofanya,+ naye hakika atakubariki katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe. 9 Yehova atakuweka kuwa kikundi chake kitakatifu cha watu,+ kama vile alivyokuapia,+ kwa sababu uliendelea kushika amri+ za Yehova Mungu wako, nawe umetembea katika njia zake. 10 Na vikundi vyote vya watu wa dunia vitalazimika kuona kwamba jina la Yehova limeitwa juu yako,+ nao kwa kweli watakuogopa wewe.+
11 “Yehova pia atakufanya ufurike kwelikweli kwa ufanisi katika uzao wa tumbo+ lako na uzao wa wanyama wako wa kufugwa na mazao ya udongo wako,+ katika udongo ambao Yehova aliwaapia mababu zako kwamba atakupa wewe.+ 12 Yehova atakufungulia ghala lake zuri, mbingu, ili kunyesha mvua juu ya nchi yako katika majira+ yake na kubariki kila tendo la mkono wako;+ nawe hakika utakopesha mataifa mengi, hali wewe mwenyewe hutakopa.+ 13 Na Yehova kwa kweli atakuweka kuwa kichwa wala si mkia; nawe utakuwa juu tu,+ wala hutakuwa chini, kwa sababu unaendelea kutii amri+ za Yehova Mungu wako, ambazo ninakuamuru wewe leo ili uzishike na kuzifanya. 14 Nawe usigeuke kando ya maneno yote ninayowaamuru ninyi leo, upande wa kuume au upande wa kushoto,+ kutembea kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia.+
15 “Na itatukia kwamba ikiwa hutasikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kuwa mwangalifu kutenda amri yake yote na kanuni zake ninazokuamuru wewe leo, laana hizi zote zitakujia pia na kukufikia:+
16 “Utalaaniwa jijini,+ nawe utalaaniwa shambani.+
17 “Kitalaaniwa kikapu+ chako na kikandio+ chako.
18 “Utalaaniwa uzao wa tumbo lako+ na mazao ya udongo wako,+ mtoto wa ng’ombe wako na uzao wa kundi lako.+
19 “Utalaaniwa unapoingia ndani, nawe utalaaniwa unapotoka nje.+
20 “Yehova ataituma laana+ juu yako, kuvurugika+ na kemeo+ katika kila hatua unayochukua unayojaribu kutimiza, mpaka uwe umeharibiwa na kuangamizwa haraka, kwa sababu ya ubaya wa mazoea yako kwa kuwa umeniacha mimi.+ 21 Yehova atasababisha tauni ishikamane nawe mpaka awe amekuangamiza kutoka katika nchi ambayo unaenda kuimiliki.+ 22 Yehova atakupiga kwa kifua kikuu+ na homa kali na mchonyoto na joto la homa na upanga+ na kuunguza+ na ukungu,+ navyo vitakufuatilia mpaka utakapokuwa umeangamia. 23 Anga zako zilizo juu ya kichwa chako pia zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma.+ 24 Yehova atanyesha ungaunga na vumbi kama mvua ya nchi yako. Kutoka mbinguni itakuja juu yako mpaka utakapokuwa umeangamizwa kabisa. 25 Yehova atakufanya ushindwe mbele ya adui zako.+ Utatoka nje kwa njia moja kwenda juu yao, lakini kwa njia saba utakimbia kutoka mbele yao; nawe utakuwa kitu chenye kuogopesha kwa falme zote za dunia.+ 26 Na maiti yako itakuwa chakula kwa ajili ya kila kiumbe kinachoruka cha mbinguni na kwa mnyama wa porini, pasipo mtu yeyote wa kuwatetemesha.+
27 “Yehova atakupiga kwa jipu la Misri+ na bawasiri na ukurutu na upele wa ngozi, nawe hutaweza kupona magonjwa hayo. 28 Yehova atakupiga kwa wazimu+ na kupoteza uwezo wa kuona+ na kuchanganyikiwa kwa moyo.+ 29 Nawe kwa kweli utakuwa mtu anayepapasa-papasa katikati ya mchana, kama vile kipofu anavyopapasa-papasa gizani,+ nawe hutafanya njia zako zifanikiwe; nawe utakuwa mtu tu ambaye sikuzote hupunjwa na kunyang’anywa, pasipo mtu wa kukuokoa.+ 30 Utamchumbia mwanamke, lakini mwanamume mwingine atamlala kinguvu.+ Utajenga nyumba, lakini hutakaa ndani yake.+ Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutaanza kutumia matunda yake.+ 31 Ng’ombe-dume wako atachinjwa hapo mbele ya macho yako—lakini hutakula sehemu yoyote yake. Utanyang’anywa punda wako mbele ya uso wako—lakini hatarudi kwako. Kondoo wako watapewa adui zako—lakini hutakuwa na mwokozi yeyote.+ 32 Wana wako na binti zako watapewa watu wengine+ na macho yako yakitazama na kuwatamani sikuzote—lakini mikono yako itakuwa haina nguvu.+ 33 Mazao ya udongo wako na mazao yako yote yataliwa na watu ambao hukuwajua;+ nawe utakuwa mtu aliyepunjwa na kupondwa sikuzote.+ 34 Nawe utatiwa wazimu kwa kuona kwa macho yako mambo ambayo utaona.+
35 “Yehova atakupiga kwa jipu hatari kwenye magoti yote mawili na miguu yote miwili, ambalo hutaweza kupona, kutoka wayo wa mguu wako mpaka utosi wa kichwa chako.+ 36 Yehova atakufanya wewe na mfalme wako ambaye umemweka juu yako mpige mwendo+ mpaka taifa ambalo hukujua, wala wewe wala mababu zako; na huko utalazimika kuitumikia miungu mingine, ya miti na ya mawe.+ 37 Nawe utakuwa kitu cha kushangaza,+ neno la kimethali+ na shutuma kati ya vikundi vyote vya watu ambao Yehova atakuongoza kwao.
38 “Utapeleka mbegu nyingi shambani, lakini utakusanya chache,+ kwa sababu nzige wataimeza.+ 39 Mashamba ya mizabibu utayapanda na hakika utayapalilia, lakini pia hutakunywa divai yoyote wala kukusanya chochote,+ kwa sababu mdudu atazila.+ 40 Pia utakuwa na mizeituni katika eneo lako, lakini hutajipaka mafuta yoyote, kwa sababu zeituni zako zitaanguka.+ 41 Utazaa wana na mabinti, lakini hawataendelea kuwa wako, kwa sababu wataenda utekwani.+ 42 Miti yako yote na mazao ya udongo wako wadudu wenye kuvuma watamiliki. 43 Mkaaji mgeni aliye katikati yako ataendelea kupanda zaidi na zaidi juu yako, lakini wewe—wewe utaendelea kushuka chini zaidi na zaidi.+ 44 Yeye ndiye atakayekukopesha, lakini wewe—wewe hutamkopesha.+ Yeye atakuwa kichwa, lakini wewe—wewe utakuwa mkia.+
45 “Na laana zote hizo+ hakika zitakujia na kukufuata na kukufikia mpaka utakapokuwa umeangamizwa,+ kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kushika amri zake na kanuni zake alizokuamuru.+ 46 Nazo zitaendelea kuwa juu yako na uzao wako kama ishara na kitu cha ajabu mpaka wakati usio na kipimo,+ 47 kwa sababu hukumtumikia Yehova Mungu wako kwa kushangilia na shangwe+ ya moyo kwa ajili ya wingi wa kila kitu.+ 48 Nawe utalazimika kuwatumikia adui+ zako ambao Yehova atawatuma juu yako kwa njaa+ na kiu na uchi na uhitaji wa kila kitu; naye hakika ataweka nira ya chuma katika shingo yako mpaka atakapokuwa amekuangamiza wewe.+
49 “Yehova atainua juu yako taifa la mbali, kutoka mwisho wa dunia,+ kama vile tai anavyorukia windo,+ taifa ambalo lugha yake hutaielewa,+ 50 taifa lenye sura kali,+ ambalo halitapendelea mwanamume mzee wala kumwonyesha kibali kijana.+ 51 Nao hakika watakula uzao wa wanyama wako wa kufugwa na mazao ya udongo wako mpaka utakapokuwa umeangamizwa,+ nao hawatakuachia nafaka yoyote, divai mpya au mafuta, mtoto wa ng’ombe wako au uzao wa kundi lako, mpaka watakapokuwa wamekuangamiza.+ 52 Nao kwa kweli watakuzingira ndani ya malango yako yote mpaka kuta zako ndefu na zenye ngome ambazo unazitumaini zitakapoanguka katika nchi yako yote, naam, hakika watakuzingira ndani ya malango yako katika nchi yako yote, ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe.+ 53 Ndipo utalazimika kula uzao wa tumbo lako, nyama ya wana wako na binti zako,+ ambao Yehova Mungu wako amekupa wewe, kwa sababu ya mbano na mkazo ambao adui yako atakusonga nao.
54 “Naye mwanamume aliye mwororo sana na aliye laini kati yako, jicho+ lake litakuwa na mwelekeo mwovu kwa ndugu yake na mke wake anayetunzwa kwa upendo na mabaki ya wanawe aliobaki nao, 55 ili asimpe yeyote kati yao nyama yoyote ya wanawe ambayo atakula, kwa kuwa hana chochote alichobaki nacho kwa sababu ya mbano na mkazo ambao adui yako atakusonga nao ndani ya malango yako yote.+ 56 Naye mwanamke aliye mwororo sana na aliye laini kati yako ambaye hakujaribu kamwe kuuweka wayo wa mguu wake kwenye udongo kwa kuwa alikuwa laini na kwa sababu ya wororo wake,+ jicho lake litakuwa na mwelekeo mwovu kwa mume wake anayetunzwa kwa upendo na mwana wake na binti yake, 57 naam, kuelekea kondo la nyuma linalotoka katikati ya miguu yake na kuelekea wanawe ambao amewazaa,+ kwa sababu atawala katika siri kwa sababu ya uhitaji wa kila kitu kwa sababu ya mbano na mkazo ambao adui yako atakusonga nao ndani ya malango yako.+
58 “Ikiwa hutakuwa mwangalifu kutimiza maneno yote ya sheria hii ambayo yameandikwa katika kitabu+ hiki ili kuliogopa hili jina tukufu+ na lenye kuogopesha,+ naam,Yehova,+ Mungu wako, 59 ndipo hakika Yehova atayafanya mapigo yako na mapigo ya uzao wako yawe makali sana, mapigo makuu na yenye kudumu kwa muda mrefu,+ na magonjwa hatari na yenye kudumu kwa muda mrefu.+ 60 Naye atarudisha juu yako magonjwa yote ya Misri ambayo ulihofu mbele yake, nayo yatajishikilia kwako.+ 61 Tena, ugonjwa wowote na pigo lolote ambalo halijaandikwa katika kitabu cha sheria hii, Yehova ataleta hayo juu yako mpaka uwe umeangamizwa. 62 Nanyi mtaachwa na hesabu ndogo sana,+ ijapokuwa mmekuwa kama nyota za mbinguni kwa wingi,+ kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wako.
63 “Na itatukia kwamba kama vile Yehova alivyokuwa na furaha juu yenu ili kuwafanyia mema na kuwazidisha ninyi,+ ndivyo Yehova atakavyokuwa na furaha juu yenu ili kuwaharibu ninyi na kuwaangamiza ninyi;+ nanyi mtang’olewa kutoka katika nchi mnayoenda kuimiliki.+
64 “Na Yehova atakutawanya katikati ya vikundi vyote vya watu kutoka mwisho mmoja wa dunia mpaka mwisho mwingine wa dunia,+ na huko utalazimika kuitumikia miungu mingine ambayo hukuijua, wala wewe wala mababu zako, miti na mawe.+ 65 Na kati ya mataifa hayo hutakuwa na starehe yoyote,+ wala hakutakuwa na mahali popote pa kupumzika kwa ajili ya wayo wa mguu wako; naye Yehova kwa kweli atakupa huko moyo wa kutetemeka+ na kufifia kwa macho+ na kukata tamaa kwa nafsi. 66 Nawe hakika utakuwa katika hatari kubwa zaidi ya maisha yako na kuwa katika hofu usiku na mchana, nawe hutakuwa na hakika ya uhai wako.+ 67 Wakati wa asubuhi utasema, ‘Laiti ingekuwa jioni!’ na jioni utasema, ‘Laiti ingekuwa asubuhi!’ kwa sababu ya hofu ya moyo wako, hofu ambayo utakuwa nayo na kwa sababu ya kuona kwa macho yako mambo ambayo utayaona.+ 68 Na hakika Yehova atakurudisha Misri kwa meli katika njia ambayo nilikuambia hivi kuihusu, ‘Hutaiona tena kamwe,’+ nanyi mtalazimika kujiuza huko kwa adui zenu kuwa watumwa na vijakazi,+ lakini hakutakuwa na mtu wa kuwanunua.”
29 Haya ndiyo maneno ya agano ambalo Yehova alimwamuru Musa afanye pamoja na wana wa Israeli katika nchi ya Moabu mbali na lile agano alilofanya pamoja nao katika Horebu.+
2 Naye Musa akaita Israeli wote na kuwaambia: “Ninyi ndio mlioona yote ambayo Yehova alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao na watumishi wake wote na nchi yake yote,+ 3 maonyesho makubwa ambayo macho yako yaliona,+ hizo ishara+ kuu na miujiza.+ 4 Na bado Yehova hajawapa ninyi moyo wa kujua na macho ya kuona na masikio ya kusikia mpaka leo hii.+ 5 ‘Nilipokuwa nikiwaongoza ninyi kwa miaka 40 nyikani,+ mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na kiatu chako hakikuchakaa kwenye mguu wako.+ 6 Mkate hamkula,+ na divai na kileo hamkunywa, ili mjue kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’ 7 Mwishowe mkaja mahali hapa, na Sihoni mfalme wa Heshboni+ na Ogu+ mfalme wa Bashani wakatoka kukutana nasi katika pigano, lakini tukawashinda.+ 8 Baada ya hilo tukachukua nchi yao na kuwapa Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase iwe urithi.+ 9 Basi lazima mshike maneno ya agano hili na kuyatenda, ili kila kitu mnachofanya kiwe na matokeo mazuri.+
10 “Ninyi nyote mmesimama mbele za Yehova Mungu wenu, vichwa vya makabila yenu, wanaume wenu wazee na maofisa wenu, kila mtu wa Israeli,+ 11 watoto wenu, wake+ zenu, na mkaaji wako mgeni+ aliye katikati ya kambi yako, kuanzia mkusanya-kuni wako mpaka mteka-maji+ wako, 12 ili uingie katika agano+ la Yehova Mungu wako na kiapo chake, ambalo Yehova Mungu wako anafanya pamoja nawe leo;+ 13 kwa kusudi la kukusimamisha wewe leo kuwa kikundi chake cha watu+ na kwamba yeye ajionyeshe kuwa Mungu wako,+ kama vile ambavyo amekuahidi wewe na kama vile ambavyo amewaapia mababu zako Abrahamu,+ Isaka+ na Yakobo.+
14 “Sasa si ninyi peke yenu ninaofanya pamoja nanyi agano hili na kiapo hiki,+ 15 bali ni pamoja na yule anayesimama nasi hapa leo mbele za Yehova Mungu wetu na pamoja na wale ambao hawako hapa pamoja nasi leo;+ 16 (kwa maana ninyi wenyewe mnajua vema jinsi tulivyokaa katika nchi ya Misri na jinsi tulivyopita katikati ya mataifa ambayo mlipita katikati yake.+ 17 Nanyi mlikuwa mkiona vitu vyao vyenye kuchukiza na sanamu zao za mavi,+ miti na mawe, fedha na dhahabu, zilizokuwa ndani yake;) 18 ili pasiwe kati yenu mwanamume au mwanamke au familia au kabila ambalo moyo wake leo unageuka mbali na Yehova Mungu wetu ili kwenda na kuitumikia miungu ya mataifa hayo;+ ili kusiwe kati yenu mzizi unaozaa tunda la mti wenye sumu na pakanga.+
19 “Na itatukia kwamba wakati ambapo mtu atakuwa amesikia maneno ya kiapo hiki,+ naye amejibariki moyoni mwake, na kusema, ‘Nitakuwa na amani,+ ijapokuwa nitatembea katika ukaidi wa moyo wangu,’+ kwa kusudi la kumfagilia mbali aliyenyweshwa maji vizuri pamoja na mwenye kiu, 20 Yehova hatataka kumsamehe,+ lakini hasira ya Yehova+ na ukali+ wake utatoa moshi juu ya mtu huyo,+ na kiapo chote ambacho kimeandikwa katika kitabu hiki+ hakika kitamkalia, na Yehova kwa kweli atafutilia mbali jina lake kutoka chini ya mbingu. 21 Basi Yehova atamtenga+ kwa ajili ya msiba mbali na makabila yote ya Israeli kupatana na kiapo chote cha agano ambacho kimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
22 “Nacho kizazi cha wakati ujao, wana wenu watakaoinuka baada yenu, watalazimika kusema, pia mgeni atakayekuja kutoka katika nchi ya mbali, naam, wakati ambapo wameona mapigo ya nchi hiyo na magonjwa yake ambayo Yehova ameifanya iugue,+ 23 kiberiti na chumvi+ na kuwaka,+ hivi kwamba nchi yake yote haitapandwa, wala kuchipuka, wala mmea wowote hautachipuka ndani yake, kama maangamizi ya Sodoma na Gomora,+ Adma+ na Seboiimu,+ ambayo Yehova aliangamiza katika hasira yake na katika ghadhabu yake;+ 24 naam, mataifa yote yatalazimika kusema, ‘Kwa nini Yehova aliitendea hivi nchi hii?+ Joto la hasira hii kuu ni la nini?’ 25 Ndipo watalazimika kusema, ‘Ni kwa sababu waliliacha agano+ la Yehova Mungu wa mababu zao, ambalo alifanya pamoja nao alipowatoa katika nchi ya Misri.+ 26 Nao walienda na kuitumikia miungu mingine na kuiinamia, miungu ambayo hawakuwa wameijua naye hakuwa amewapa.+ 27 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka juu ya nchi hiyo kwa kuleta juu yake laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki.+ 28 Basi Yehova akawang’oa kutoka katika udongo wao kwa hasira+ na ghadhabu na ukali mwingi na kuwatupa katika nchi nyingine kama ilivyo kufikia leo hii.’+
29 “Mambo yaliyofichwa+ ni ya Yehova Mungu wetu, bali mambo yaliyofunuliwa+ ni yetu na wana wetu mpaka wakati usio na kipimo, ili tupate kuyatimiza maneno yote ya sheria hii.+
30 “Na itatukia kwamba wakati ambapo maneno yote haya yatakuja juu yako, baraka+ na laana,+ ambazo nimeweka mbele yako, nawe umeyarudisha moyoni+ mwako kati ya mataifa yote ambako Yehova Mungu wako amekutawanya,+ 2 nawe utakapokuwa umerudi kwa Yehova Mungu wako+ na kusikiliza sauti yake kulingana na yote ninayokuamuru leo, wewe na wana wako, kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote,+ 3 ndipo Yehova Mungu wako atakaporudisha mateka+ wako pia na kukuonyesha rehema+ na kukukusanya tena kutoka kwa vikundi vyote vya watu ambako Yehova Mungu wako amekutawanya.+ 4 Ikiwa watu wako waliotawanywa watakuwa kwenye mwisho wa mbingu, kutoka huko Yehova Mungu wako atakukusanya na kutoka huko atakuchukua.+ 5 Yehova Mungu wako kwa kweli atakuleta katika nchi ambayo baba zako walimiliki, nawe utaimiliki; naye kwa kweli atakufanyia mema na kukuzidisha wewe kuliko baba zako.+ 6 Na Yehova Mungu wako atautahiri moyo wako+ na moyo wa uzao wako,+ ili wewe umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote kwa ajili ya uhai wako.+ 7 Na Yehova Mungu wako hakika ataweka viapo hivi vyote juu ya adui zako na wale wanaokuchukia, ambao wamekutesa.+
8 “Na wewe, utageuka uisikilize sauti ya Yehova na kufanya amri zake zote ninazokuamuru leo.+ 9 Na Yehova Mungu wako kwa kweli atakufanya uwe na wingi kupita kiasi katika kila kazi ya mkono wako,+ katika uzao wa tumbo lako na katika uzao wa wanyama wako wa kufugwa+ na mazao ya udongo wako,+ na kutokeza ufanisi;+ kwa sababu Yehova atakuwa na furaha tena juu yako kwa mema, kama vile alivyokuwa na furaha juu ya mababu zako;+ 10 kwa maana utaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wako ili uzishike amri zake na sheria zake zilizoandikwa katika kitabu hiki cha sheria,+ kwa sababu utarudi kwa Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na nafsi yako yote.+
11 “Kwa maana amri hii ninayokuamuru leo si ngumu mno kwako, wala haiko mbali.+ 12 Haiko mbinguni, hata useme, ‘Ni nani atakayepanda kwa ajili yetu mpaka mbinguni ailete kwetu, atuwezeshe kuisikia ili tuifanye?’+ 13 Wala haiko ule upande mwingine wa bahari, hata useme, ‘Ni nani atakayevuka kwa ajili yetu mpaka ule upande mwingine wa bahari ailete kwetu, atuwezeshe kuisikia ili tuifanye?’ 14 Kwa maana neno hilo liko karibu sana nawe, katika kinywa chako mwenyewe na katika moyo wako mwenyewe,+ ili ulifanye.+
15 “Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mema, na kifo na mabaya.+ 16 Ikiwa utazisikiliza amri za Yehova Mungu wako, ninazokuamuru leo, ili kumpenda Yehova Mungu wako,+ kutembea katika njia zake na kushika amri+ zake na kanuni zake na maamuzi yake ya hukumu,+ ndipo hakika utakapoendelea kuwa hai+ na kuongezeka, na Yehova Mungu wako atakubariki katika nchi unayoenda kuimiliki.+
17 “Lakini moyo wako ukigeukia mbali nawe usisikilize,+ na hakika ushawishiwe na kuinamia miungu mingine na kuitumikia,+ 18 nawaambia ninyi leo kwamba hakika mtaangamia.+ Hamtarefusha siku zenu katika nchi mnayovuka Yordani ili kuimiliki. 19 Nachukua mbingu na dunia kuwa mashahidi juu yenu leo,+ kwamba nimeweka uzima na kifo mbele yako,+ baraka+ na laana;+ nawe lazima uchague uzima ili uendelee kuwa hai,+ wewe na uzao wako,+ 20 kwa kumpenda Yehova Mungu wako,+ kwa kuisikiliza sauti yake na kwa kushikamana naye;+ kwa maana yeye ni uhai wako na urefu wa siku zako,+ ili ukae katika nchi ambayo Yehova aliwaapia mababu zako Abrahamu, Isaka na Yakobo kwamba atawapa wao.”+
31 Ndipo Musa akaenda na kusema na Israeli wote maneno haya 2 na kuwaambia: “Leo mimi nina umri wa miaka 120.+ Sitaruhusiwa tena kutoka nje na kuingia ndani,+ kama vile Yehova alivyoniambia, ‘Wewe hutavuka mto huu wa Yordani.’+ 3 Yehova Mungu wako ndiye anayevuka mbele yako.+ Yeye mwenyewe atayaangamiza mataifa haya kutoka mbele yako, na wewe lazima uyafukuzie mbali.+ Yoshua ndiye anayevuka mbele yako,+ kama alivyosema Yehova. 4 Na hakika Yehova atawatendea wao kama alivyowatendea Sihoni+ na Ogu,+ wafalme wa Waamori, na nchi yao, alipowaangamiza hao.+ 5 Na Yehova amewatia mkononi mwenu,+ nanyi lazima mwatendee kulingana na amri yote ambayo nimewaamuru ninyi.+ 6 Iweni hodari na wenye nguvu.+ Usiogope wala kushtuka mbele yao,+ kwa sababu Yehova Mungu wako ndiye anayepiga mwendo pamoja nawe. Hatakutupa wala kukuacha kabisa.”+
7 Na Musa akamwita Yoshua na kumwambia mbele ya macho ya Israeli wote: “Uwe hodari na mwenye nguvu,+ kwa sababu wewe—wewe utawaingiza watu hawa katika nchi ambayo Yehova aliwaapia mababu zao kwamba atawapa, na wewe mwenyewe utawapa iwe urithi.+ 8 Na Yehova ndiye anayepiga mwendo mbele yako. Yeye mwenyewe ataendelea kuwa pamoja nawe.+ Hatakutupa wala kukuacha kabisa. Usiogope wala usiingiwe na hofu.”+
9 Ndipo Musa akaandika sheria hii+ na kuwapa makuhani wana wa Lawi,+ wachukuaji wa sanduku la agano la Yehova,+ na kuwapa wanaume wote wazee wa Israeli. 10 Na Musa akawaamuru, na kusema: “Mwishoni mwa kila miaka saba, katika wakati uliowekwa wa mwaka wa kuachilia huru,+ katika sherehe ya vibanda,+ 11 wakati ambapo Israeli wote watakuja kuuona uso wa Yehova+ Mungu wako katika mahali atakapopachagua,+ utaisoma sheria hii mbele ya Israeli wote masikioni mwao.+ 12 Wakutanishe watu,+ wanaume na wanawake na watoto wadogo na mkaaji mgeni aliye ndani ya malango yako, ili wasikilize na ili wajifunze,+ kwa maana ni lazima wamwogope Yehova Mungu+ wenu na kuwa waangalifu kuyatimiza maneno yote ya sheria hii. 13 Na wana wao ambao hawakujua wanapaswa kusikiliza,+ nao lazima wajifunze kumwogopa Yehova Mungu wenu siku zote ambazo ninyi mnakaa juu ya nchi ambayo mnavuka Yordani ili kuimiliki.”+
14 Baada ya jambo hilo Yehova akamwambia Musa: “Tazama! Siku za kufa kwako zimekaribia.+ Mwite Yoshua, na usimame katika hema la mkutano, ili nimpe utume.”+ Basi Musa na Yoshua wakaenda na kusimama katika hema la mkutano.+ 15 Ndipo Yehova akaonekana katika hema katika nguzo ya wingu, na hiyo nguzo ya wingu ikaanza kusimama kwenye mlango wa hema.+
16 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Tazama! Unalala pamoja na mababu zako;+ na hakika watu hawa watainuka+ na kufanya uasherati na miungu migeni ya nchi wanayoiendea,+ kati yao, nao hakika wataniacha+ na kuvunja agano langu ambalo nimefanya pamoja nao.+ 17 Ndipo hasira yangu itakapowaka kwelikweli juu yao katika siku hiyo,+ nami hakika nitawaacha+ na kuuficha uso wangu mbali nao,+ nao watakuwa kitu cha kuteketezwa; na misiba mingi na taabu zitakuja juu yao,+ nao watalazimika kusema siku hiyo, ‘Je, misiba hii haikuja juu yetu kwa sababu Mungu wetu hayuko katikati yetu?’+ 18 Mimi nami, nitauficha kabisa uso wangu katika siku hiyo kwa sababu ya ubaya wote ambao wameutenda, kwa sababu wameigeukia miungu mingine.+
19 “Na sasa jiandikieni wenyewe wimbo huu+ na kuwafundisha wana wa Israeli.+ Uwekeni katika vinywa vyao ili wimbo huu upate kuwa shahidi wangu juu ya wana wa Israeli.+ 20 Kwa maana nitawaleta katika nchi ambayo nimewaapia mababu zao,+ inayotiririka maziwa na asali,+ nao hakika watakula+ na kushiba na kunenepa+ na kuigeukia miungu mingine,+ nao kwa kweli wataitumikia na kunitendea bila heshima na kulivunja agano langu.+ 21 Na itatukia kwamba wakati ambapo misiba mingi na taabu zitawajia,+ wimbo huu lazima pia utashuhudia mbele yao, kwa sababu haupaswi kusahauliwa katika vinywa vya uzao wao, kwa maana najua vema mwelekeo wao+ wanaousitawisha leo kabla sijawaingiza katika nchi niliyowaapia.”
22 Kwa hiyo Musa akaandika wimbo huu katika siku hiyo, ili awafundishe wana wa Israeli.+
23 Naye akampa utume Yoshua mwana wa Nuni+ na kusema: “Uwe hodari na mwenye nguvu,+ kwa sababu wewe—wewe utawaingiza wana wa Israeli katika nchi ambayo nimewaapia,+ na mimi mwenyewe nitaendelea kuwa pamoja nawe.”
24 Na ikawa kwamba mara tu Musa alipomaliza kuandika maneno ya sheria hii katika kitabu mpaka yakaisha,+ 25 Musa akaanza kuwaamuru Walawi, wachukuaji wa sanduku la agano la Yehova,+ na kusema: 26 “Mkichukue kitabu hiki cha sheria,+ nanyi mkiweke kando ya sanduku+ la agano la Yehova Mungu wenu, nacho kitashuhudia hapo juu yenu.+ 27 Kwa maana mimi—mimi najua vema uasi+ wenu na shingo yenu ngumu.+ Ikiwa wakati ambapo ningali hai pamoja nanyi leo, mmekuwa wenye tabia ya kumwasi Yehova,+ itakuwaje basi baada ya kifo changu! 28 Nikutanishie wanaume wote wazee wa makabila yenu na maofisa wenu,+ na acheni niseme masikioni mwao maneno haya, na acheni nichukue mbingu na dunia ziwe mashahidi dhidi yao.+ 29 Kwa maana najua vema kwamba baada ya kifo changu hakika mtatenda kwa uharibifu,+ nanyi hakika mtageuka kando kutoka katika njia ambayo nimewaamuru ninyi; na msiba+ lazima utawaangukia mwishoni mwa siku hizo, kwa sababu mtafanya yaliyo mabaya machoni pa Yehova ili kumtia uchungu kwa kazi za mikono yenu.”+
30 Naye Musa akasema masikioni mwa kutaniko lote la Israeli maneno ya wimbo huu mpaka yakaisha:+
2 Mafundisho yangu yatatiririka kama mvua,+
Maneno yangu yatadondoka kama umande,+
Kama mvua ya rasharasha juu ya majani+
Na kama manyunyu mengi juu ya mimea+
4 Yeye Mwamba, kazi zake ni kamilifu,+
Kwa maana njia zake zote ni haki.+
Mungu wa uaminifu,+ ambaye hana ukosefu wowote wa haki;+
Yeye ni mwadilifu na mnyoofu.+
6 Je, Yehova ndiye mnayeendelea kumfanyia hivi,+
Enyi watu wajinga na ambao hawana hekima?+
Je, yeye si Baba yenu aliyewazaa,+
Yeye aliyewafanyiza ninyi na kuwaimarisha?+
Fikirieni miaka iliyopita kutoka kizazi mpaka kizazi;
Muulize baba yako, naye anaweza kukuambia;+
Wanaume wenu wazee, nao wanaweza kukuambia.+
8 Wakati Aliye Juu Zaidi alipoyapa mataifa urithi,+
Alipowatenganisha wana wa Adamu,+
Ndipo alipoweka mpaka wa vikundi vya watu+
Kuhusiana na hesabu ya wana wa Israeli.+
10 Alimpata katika nchi ya nyika,+
Na katika jangwa tupu, lenye kulia.+
Alianza kumzunguka,+ kumtunza,+
Kumlinda kama mboni ya jicho lake.+
11 Kama vile tai anavyokitikisa kiota chake,
Anavyoelea angani juu ya watoto wake,+
Anavyotandaza mabawa yake, na kuwachukua,
Anavyowachukua kwenye manyoya yake,+
12 Ndivyo Yehova peke yake alivyoendelea kumwongoza,+
Na hapakuwa na mungu yeyote wa kigeni pamoja naye.+
13 Aliendelea kumfanya apande juu ya mahali pa juu pa dunia,+
Hivi kwamba akala mazao ya shamba.+
Naye akaendelea kumfanya anyonye asali kutoka katika mwamba,+
Na mafuta kutoka katika jiwe gumu;+
14 Siagi ya mifugo na maziwa ya kundi+
Pamoja na mafuta ya kondoo-dume,
Na kondoo-dume, uzao wa Bashani, na mbuzi-dume+
Pamoja na mafuta ya figo ya ngano;+
Nawe uliendelea kunywa kama divai damu ya zabibu.+
15 Yeshuruni+ alipoanza kunenepa, ndipo akapiga teke.+
Umepata mafuta, umekuwa mnene, umeshiba mno.+
Basi akamwacha Mungu, aliyemfanya,+
Na kumdharau Mwamba+ wa wokovu wake.
16 Walianza kumchochea awe na wivu+ kwa miungu migeni;+
Kwa mambo yenye kuchukiza waliendelea kumtia uchungu.+
17 Waliwatolea dhabihu roho waovu, wala si Mungu,+
Miungu ambayo hawakuijua,+
Mipya iliyokuja hivi karibuni,+
Ambayo mababu zenu hawakuifahamu.
18 Mwamba aliyekuzaa wewe, ulimsahau,+
Nawe ukaanza kumwondoa Mungu katika kumbukumbu, yule anayekutokeza kwa uchungu wa kuzaa.+
19 Yehova alipoona hilo, ndipo akawadharau wao,+
Kwa sababu ya usumbufu uliosababishwa na wanawe na binti zake.
20 Kwa hiyo akasema, ‘Acha niufiche uso wangu kutoka kwao,+
Acha nione mwisho wao utakuwaje baadaye.
Kwa maana wao ni kizazi chenye upotovu,+
Wana ambao ndani yao hamna uaminifu.+
21 Wao wamenichochea niwe na wivu kwa kile ambacho si mungu;+
Wameniudhi kwa sanamu zao za ubatili;+
Na mimi, nitawachochea wawe na wivu kwa kile ambacho si kikundi cha watu;+
Kwa taifa jinga nitawatia uchungu.+
22 Kwa maana moto umewashwa katika hasira yangu+
Nao utateketeza mpaka katika Kaburi,* mahali pa chini zaidi,+
Nao utateketeza dunia na mazao yake+
Nao utawasha misingi ya milima.+
24 Watachoka kutokana na njaa+ na kuliwa na homa kali+
Na maangamizi machungu.+
Na meno ya wanyama nitatuma juu yao,+
Kwa sumu ya watambaazi wa mavumbini.+
25 Nje upanga utawasababishia vifo,+
Na ndani woga,+
Wa kijana na bikira,+
Anayenyonya pamoja na mwanamume mwenye mvi.+
26 Ningalikuwa nimesema: “Nitawatawanya,+
Nitalifanya jina lao likome kutoka katikati ya watu wanaoweza kufa,”+
27 Isingalikuwa kwa sababu niliogopa usumbufu kutoka kwa adui,+
Kwamba wapinzani wao wangaliweza kuelewa vibaya,+
Ili waseme: “Mkono wetu umeshinda,+
Na si Yehova aliyefanya mambo haya yote.”+
29 Laiti wangalikuwa wenye hekima!+ Ndipo wangalifikiria hili kwa uzito.+
Wangaliufikiria mwisho wao baadaye.+
Haingewezekana isipokuwa Mwamba wao awe amewauza+
Na Yehova awe amewatoa.
Zabibu zao ni zabibu za sumu,
Vishada vyao ni vichungu.+
35 Kisasi ni changu, na malipo.+
Katika wakati uliowekwa mguu wao utasogea kwa kuyumba-yumba,+
Kwa maana siku ya maafa yao iko karibu,+
Na matukio yanafanya haraka kujitayarisha kwa ajili yao.’+
36 Kwa maana Yehova atawahukumu watu wake+
Naye atajuta juu ya watumishi wake,+
Kwa sababu ataona kwamba tegemeo limetoweka
Na aliyeko tu ni mtu asiye na uwezo na asiye na thamani.
38 Iliyokuwa ikila mafuta ya dhabihu zao,+
Ili kunywa divai ya matoleo yao ya kinywaji?+
Na isimame na kuwasaidia ninyi.+
Na iwe mahali pa maficho kwa ajili yenu.+
39 Oneni sasa kwamba mimi—mimi ndiye+
Na hakuna miungu pamoja nami.+
Mimi huua, nami hufanya hai.+
Nimejeruhi vikali,+ na mimi—mimi nitaponya,+
Na hakuna anayenyakua kutoka mkononi mwangu.+
40 Kwa maana mimi nainua mkono wangu kuelekea mbinguni kwa kiapo,+
Nami ninasema: “Kama nilivyo hai mpaka wakati usio na
kipimo,”+
41 Kwa kweli nikiunoa upanga wangu unaometameta,+
Na mkono wangu ushike hukumu,+
Nitawalipa kisasi wapinzani wangu+
Na kutoa malipo kwa wale wanaonichukia vikali.+
42 Nitailewesha mishale yangu kwa damu,+
Nao upanga wangu utakula nyama,+
Kwa damu ya waliouawa na mateka,
Kwa vichwa vya viongozi wa adui.’+
43 Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake,+
Kwa maana atalipiza kisasi damu ya watumishi wake,+
Naye atawalipa kisasi adui zake+
Naye kwa kweli atafanya upatanisho kwa ajili ya nchi ya watu wake.”
44 Basi Musa akaja na kusema maneno yote ya wimbo huu masikioni mwa watu,+ yeye na Hoshea mwana wa Nuni.+ 45 Baada ya Musa kumaliza kuwaambia Israeli wote maneno yote hayo, 46 ndipo akawaambia: “Tieni mioyo yenu katika maneno yote ninayosema kwa kuwaonya ninyi leo,+ ili muwaamuru wana wenu wawe waangalifu kufanya maneno yote ya sheria hii.+ 47 Kwa maana hilo si neno lisilo na thamani kwenu,+ bali linamaanisha uhai wenu,+ na kwa neno hili mnaweza kurefusha siku zenu juu ya udongo ambao mnavuka Yordani ili kuumiliki.”+
48 Na Yehova akasema na Musa siku hiyohiyo, na kumwambia: 49 “Panda juu ya mlima huu wa Abarimu,+ Mlima Nebo,+ ulio katika nchi ya Moabu, mbele ya Yeriko, nawe uione nchi ya Kanaani, ninayowapa wana wa Israeli waimiliki.+ 50 Kisha ufe katika mlima utakaopanda, na kukusanywa kwa watu wako,+ kama vile Haruni ndugu yako alivyokufa katika Mlima Hori+ na kukusanywa kwa watu wake; 51 Kwa sababu ninyi mlitenda isivyofaa kunielekea mimi+ katikati ya wana wa Israeli kwenye maji ya Meriba+ ya Kadeshi katika nyika ya Zini; kwa sababu ninyi hamkunitakasa mimi katikati ya wana wa Israeli.+ 52 Kwa maana kutoka mbali utaiona nchi, lakini hutaingia katika nchi ninayowapa wana wa Israeli.”+
33 Sasa hii ndiyo baraka+ ambayo Musa mtu wa Mungu wa kweli+ aliwabariki nayo wana wa Israeli kabla ya kifo chake. 2 Naye akasema:
“Yehova—alikuja kutoka Sinai,+
Naye akamulika juu yao kutoka Seiri.+
Aliangaza kutoka katika eneo lenye milima la Parani,+
Naye alikuwa pamoja na makumi ya maelfu ya watakatifu,+
Mashujaa wao kwenye mkono wake wa kuume.+
3 Pia alikuwa akiwatunza kwa upendo watu wake;+
Watakatifu wao wote wako mkononi mwako.+
Na wao—wao waliegama miguuni pako;+
Walianza kupokea baadhi ya maneno yako.+
5 Naye akawa mfalme katika Yeshuruni,+
Wakati ambapo walio vichwa vya watu walikusanyika pamoja,+
Hesabu kamili ya makabila ya Israeli.+
7 Nayo hii ndiyo iliyokuwa baraka ya Yuda,+ alipoendelea kusema:
“Usikie, Ee Yehova, sauti ya Yuda,+
Nawe umlete kwa watu wake.
Mikono yake imeshindania kilicho chake;
Nawe uwe msaidizi juu ya wapinzani wake.”+
“Thumimu yako na Urimu+ yako ni vyake mtu aliye mshikamanifu kwako,+
Uliyemjaribu huko Masa.+
Ulianza kushindana naye kando ya maji ya Meriba,+
9 Mtu aliyemwambia baba yake na mama yake, ‘Mimi sijamwona.’
Hata ndugu zake hakuwatambua,+
Na wanawe hakuwajua.
Kwa maana walilishika neno lako,+
Na agano lako waliendelea kulishika.+
10 Na wamfundishe Yakobo hukumu zako+
Na Israeli sheria yako.+
Na watoe uvumba mbele za mianzi ya pua yako+
Na toleo zima kwenye madhabahu yako.+
11 Bariki, Ee Yehova, nguvu zake,+
Na ufurahie utendaji wa mikono yake.+
Waumize vikali viunoni mwao wale wanaoinuka juu yake,+
Na wale wanaomchukia vikali, ili wasiinuke.”+
“Mpendwa+ wa Yehova na akae katika usalama kando yake,+
Anapomkinga siku nzima,+
Naye lazima akae katikati ya mabega yake.”+
“Nchi yake na ibarikiwe daima na Yehova+
Kwa vitu bora vya mbinguni, kwa umande,+
Na kwa kilindi cha maji kilicho chini,+
14 Na kwa vitu bora, mazao ya jua,+
Na kwa vitu bora, mazao ya mwezi.+
15 Na kwa vilivyo bora kabisa kutoka katika milima ya mashariki,+
Na kwa vitu bora vya vilima vyenye kudumu mpaka wakati usio na kipimo,
16 Na kwa vitu bora vya dunia na vitu vinavyoijaza,+
Na kwa kibali cha Yule anayekaa katika kichaka cha miiba.+
Na vije juu ya kichwa cha Yosefu+
Na juu ya utosi wa kichwa cha yule aliyechaguliwa kutoka kati ya ndugu zake.+
17 Kama mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe-dume ndivyo fahari yake ilivyo,+
Na pembe zake ni pembe za ng’ombe-dume wa mwituni.+
Atasukuma vikundi vya watu kwa pembe hizo+
Wote pamoja mpaka miisho ya dunia,
Nao ni makumi ya maelfu ya Efraimu,+
Nao ni maelfu ya Manase.”
19 Wataita vikundi vya watu mlimani.
Huko watatoa dhabihu za uadilifu.+
Kwa maana watanyonya mali nyingi ya bahari+
Na akiba zilizofichika za mchanga.”
“Amebarikiwa yule anayepanua mipaka ya Gadi.+
Yeye atakaa kama simba,+
Naye atararua mkono, naam, utosi wa kichwa.+
21 Naye atajichagulia sehemu ya kwanza,+
Kwa maana huko fungu la mpaji-sheria linahifadhiwa.+
Na walio vichwa vya watu watajikusanya pamoja.
Hakika atautimiza uadilifu wa Yehova
Na maamuzi yake ya hukumu pamoja na Israeli.”
“Aliyebarikiwa na wana ni Asheri.+
Na awe aliyekubaliwa na ndugu zake,+
Na yule anayechovya mguu wake katika mafuta.+
25 Chuma na shaba ni makufuli ya lango lako,+
Na kulingana na siku zako ndivyo yalivyo matembezi yako ya starehe.
26 Hakuna aliye kama Mungu wa kweli+ wa Yeshuruni,+
Anayepanda juu ya mbingu ili kukusaidia+
Na juu ya anga zenye kutanda mawingu katika adhama yake.+
27 Mungu wa nyakati za kale ni mahali pa kujificha,+
Na chini kuna mikono yenye kudumu mpaka wakati usio na kipimo.+
Naye atawafukuzia mbali adui zako toka mbele yako,+
Naye atasema, ‘Waangamize!’+
28 Na Israeli atakaa katika usalama,+
Chemchemi ya Yakobo peke yake,+
Katika nchi ya nafaka na divai mpya.+
Naam, mbingu zake zitatiririsha umande.+
Ni nani aliye kama wewe,+
Kikundi cha watu kinachofurahia wokovu wa Yehova,+
Aliye ngao ya msaada wako,+
Na Yule aliye upanga wako wa adhama?+
Kwa hiyo adui zako watatetemeka mbele yako,+
Na wewe—utapakanyaga mahali pao pa juu.”+
34 Kisha Musa akatoka katika nchi tambarare za jangwa la Moabu na kuingia katika Mlima Nebo,+ mpaka juu ya Pisga,+ mbele ya Yeriko.+ Naye Yehova akamwonyesha nchi yote, Gileadi mpaka Dani,+ 2 na Naftali yote na nchi ya Efraimu na Manase na nchi yote ya Yuda mpaka bahari ya magharibi,+ 3 na Negebu+ na Wilaya,+ nchi tambarare ya bonde la Yeriko, jiji la mitende,+ mpaka Soari.+
4 Na Yehova akamwambia: “Hii ndiyo nchi ambayo nilimwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo, na kusema, ‘Nitaupa uzao wako.’+ Nimekufanya uione kwa macho yako mwenyewe, kwa maana wewe hutavuka kuingia huko.”+
5 Baada ya hilo Musa mtumishi wa Yehova+ akafa huko katika nchi ya Moabu kulingana na agizo la Yehova.+ 6 Naye akamzika katika bonde katika nchi ya Moabu mbele ya Beth-peori,+ na hakuna mtu ambaye amepata kujua kaburi lake mpaka leo hii.+ 7 Naye Musa alikuwa na umri wa miaka 120 wakati wa kifo chake.+ Jicho lake halikuwa limeingia giza,+ na nguvu zake hazikuwa zimepotea.+ 8 Na wana wa Israeli wakamlilia Musa kwenye nchi tambarare za jangwa la Moabu kwa siku 30.+ Mwishowe siku za kulia za kipindi cha kumwombolezea Musa zikamalizika.
9 Na Yoshua mwana wa Nuni alikuwa amejaa roho ya hekima,+ kwa kuwa Musa alikuwa ameweka mkono wake juu yake;+ na wana wa Israeli wakaanza kumsikiliza nao wakafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.+ 10 Lakini hajainuka kamwe nabii katika Israeli aliye kama Musa,+ ambaye Yehova alimjua uso kwa uso,+ 11 kuhusiana na ishara zote na miujiza yote ambayo Yehova alimtuma afanye katika nchi ya Misri kwa Farao na watumishi wake wote na nchi yake yote,+ 12 na kuhusiana na mkono wote wenye nguvu na hofu kuu yote ambayo Musa alifanya ionekane mbele ya macho ya Israeli wote.+
[Maelezo ya Chini]
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.