Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Kutoka 1:1-40:38
  • Kutoka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoka
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Kutoka

Kutoka

1 Na haya ndiyo majina ya wana wa Israeli walioingia Misri pamoja na Yakobo; walioingia kila mwanamume na nyumba yake:+ 2 Rubeni,+ Simeoni,+ Lawi+ na Yuda,+ 3 Isakari,+ Zabuloni+ na Benyamini,+ 4 Dani+ na Naftali,+ Gadi+ na Asheri.+ 5 Nafsi zote zilizotoka katika kiuno+ cha Yakobo zikawa nafsi 70, lakini tayari Yosefu alikuwa Misri.+ 6 Mwishowe Yosefu akafa,+ na pia ndugu zake wote na kizazi hicho chote. 7 Na wana wa Israeli wakazaa na kuanza kujaa; nao wakazidi kuongezeka na kuwa wenye nguvu zaidi kwa kiwango kisicho cha kawaida, hivi kwamba wakaijaza nchi.+

8 Baada ya muda mfalme mpya ambaye hakumjua Yosefu akainuka juu ya Misri.+ 9 Naye akawaambia watu wake: “Tazama! Watu wa wana wa Israeli ni wengi zaidi na wenye nguvu kuliko sisi.+ 10 Haya! Na tuwatendee kwa werevu,+ wasije wakaongezeka, na iwe kwamba, vita vikizuka juu yetu, basi hakika wao watajiunga na wale wanaotuchukia na kupigana nasi na kutoka katika nchi hii.”

11 Basi wakaweka juu yao wakuu wa kazi ya kulazimishwa kusudi wawakandamize katika kazi yao ya kubeba mizigo;+ nao wakajenga majiji ili yawe maghala kwa ajili ya Farao, yaani, Pithomu na Raamsesi.+ 12 Lakini kadiri walivyowakandamiza, ndivyo walivyozidi kuongezeka na ndivyo walivyozidi kuenea kotekote, hivi kwamba wakahofu na kuchukizwa kwa sababu ya wana wa Israeli.+ 13 Kwa hiyo Wamisri wakawatumikisha wana wa Israeli chini ya uonevu.+ 14 Nao wakazidi kuyafanya maisha yao yawe machungu kwa utumwa mgumu wa kutengeneza saruji ya udongo+ na matofali na kwa kila namna ya utumwa shambani,+ ndiyo, kila namna ya utumwa wao ambao kwa huo waliwatumia wakiwa watumwa chini ya uonevu.+

15 Baadaye mfalme wa Misri akawaambia wazalishaji+ Waebrania, ambao jina la mmoja wao lilikuwa Shifra na jina la yule mwingine lilikuwa Pua, 16 ndiyo, hata akawaambia: “Mnapowasaidia wanawake Waebrania kuzaa nanyi mpate kuwaona kwenye kiti cha kuzalia, ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni; lakini ikiwa ni binti, basi na aishi.” 17 Hata hivyo, wazalishaji hao walimwogopa Mungu wa kweli,+ nao hawakufanya kama vile mfalme wa Misri alivyokuwa amewaambia,+ bali walikuwa wakiwahifadhi hai watoto wa kiume.+ 18 Baada ya muda mfalme wa Misri akawaita wazalishaji hao na kuwaambia: “Kwa nini mmefanya jambo hili, ya kwamba mliwahifadhi hai watoto wa kiume?”+ 19 Nao wazalishaji wakamwambia Farao: “Kwa sababu wanawake Waebrania si kama wanawake Wamisri. Kwa sababu wao ni wenye nguvu, wao huwa tayari wamezaa kabla mzalishaji hajaingia kwao.”

20 Kwa hiyo Mungu akawatendea vema wazalishaji hao;+ na watu wakazidi kuongezeka na kuwa wengi zaidi na kuwa wenye nguvu sana. 21 Na ikawa kwamba kwa sababu wazalishaji walikuwa wamemwogopa Mungu wa kweli, baadaye akawapa familia.+ 22 Mwishowe Farao akawaamuru watu wake wote, na kusema: “Kila mwana anayezaliwa mtamtupa kwenye mto Nile, lakini kila binti mtamhifadhi hai.”+

2 Wakati huohuo, mwanamume fulani wa nyumba ya Lawi alimchukua binti mmoja wa Lawi.+ 2 Naye mwanamke huyo akapata mimba, akazaa mwana. Alipoona jinsi alivyokuwa mwenye sura ya kupendeza, akamficha+ kwa miezi mitatu.+ 3 Alipokuwa hawezi tena kuendelea kumficha,+ akamchukulia safina ya mafunjo, akaipaka lami na bereu,+ akamweka mtoto huyo ndani yake na kuiweka katikati ya matete+ kando ya mto Nile. 4 Na zaidi ya hayo, dada yake akasimama umbali fulani apate kuona kile ambacho angetendewa.+

5 Baada ya muda, binti ya Farao akaja kuoga katika Mto Nile, nao wanawake wa kumhudumia walikuwa wakitembea kando ya Mto Nile. Naye akaiona ile safina katikati ya matete. Mara moja akamtuma kijakazi wake aende akailete.+ 6 Alipoifungua akamwona yule mtoto, na tazama, mvulana huyo alikuwa akilia. Kwa hiyo akamwonea huruma,+ ingawa alisema: “Huyu ni mmoja wa watoto wa Waebrania.” 7 Kisha dada ya mtoto huyo akamwambia binti ya Farao: “Je, niende nikakuitie mwanamke anayenyonyesha kutoka kati ya wanawake Waebrania apate kukunyonyeshea mtoto huyu?” 8 Basi binti ya Farao akamwambia: “Nenda!” Naye mwanamwali huyo akaenda mara moja na kumwita mama ya mtoto huyo.+ 9 Ndipo binti ya Farao akamwambia: “Mchukue mtoto huyu, uninyonyeshee, nami nitakupa malipo+ yako.” Kwa hiyo mwanamke huyo akamchukua mtoto na kumnyonyesha. 10 Naye mtoto akakua. Kisha akamleta kwa binti ya Farao, hivi kwamba akawa mwana kwake;+ naye akamwita jina lake Musa na kusema: “Ni kwa sababu nimemtoa majini.”+

11 Sasa ikawa kwamba katika siku hizo, Musa alipozidi kuwa na nguvu, akatoka nje kwenda kwa ndugu zake apate kutazama mizigo waliyokuwa wakibeba;+ naye akamwona Mmisri fulani akimpiga Mwebrania fulani, mmoja wa ndugu zake.+ 12 Kwa hiyo akatazama huku na huku akaona kwamba hapakuwa na mtu yeyote karibu. Kisha akampiga Mmisri huyo na kumuua, halafu akamficha ndani ya mchanga.+

13 Hata hivyo, akatoka siku iliyofuata, na tazama, wanaume wawili Waebrania walikuwa wakipambana. Basi akamwambia mwenye kosa: “Kwa nini umpige mwenzako?”+ 14 Naye akamwambia: “Ni nani aliyekuweka wewe rasmi kuwa mkuu na mwamuzi juu yetu?+ Je, unakusudia kuniua kama vile ulivyomuua yule Mmisri?”+ Sasa Musa akaogopa na kusema: “Hakika jambo hilo limejulikana!”+

15 Baadaye Farao akasikia juu ya jambo hilo, naye akajaribu kumuua Musa;+ lakini Musa akakimbia+ toka kwa Farao apate kuishi katika nchi ya Midiani;+ naye akaketi kando ya kisima. 16 Sasa kuhani+ wa Midiani alikuwa na binti saba, na kama kawaida wakaja kuteka maji na kuijaza mifereji ili kulinywesha kundi la baba yao.+ 17 Na kama kawaida wachungaji wakaja na kuwafukuzia mbali. Kwa hiyo Musa akasimama na kuwasaidia wanawake hao na kulinywesha kundi lao.+ 18 Basi walipofika nyumbani kwa Reueli+ baba yao, akasema kwa mshangao: “Imekuwaje mmefika nyumbani upesi sana leo?” 19 Nao wakasema: “Mmisri+ fulani alitukomboa kutoka katika mkono wa wachungaji na, zaidi ya hayo, kwa kweli alitutekea maji ili kulinywesha kundi.” 20 Kisha akawaambia binti zake: “Lakini yeye yuko wapi? Kwa nini mmemwacha nyuma mwanamume huyo? Mwiteni, apate kula mkate.”+ 21 Baada ya hayo Musa akakubali kukaa na mtu huyo, naye akampa Musa Sipora+ binti yake. 22 Baadaye Sipora akazaa mwana, naye Musa akamwita jina lake Gershomu,+ kwa sababu, alisema: “Nimekuwa mkaaji mgeni katika nchi ya kigeni.”+

23 Na ikawa kwamba wakati wa siku hizo nyingi, mwishowe mfalme wa Misri akafa,+ lakini wana wa Israeli wakaendelea kuugua kwa sababu ya utumwa na kulia kwa kulalamika,+ nacho kilio chao cha kuomba msaada kikaendelea kupaa juu kwa Mungu wa kweli kwa sababu ya utumwa huo.+ 24 Mwishowe Mungu akasikia+ kuugua+ kwao naye Mungu akalikumbuka agano lake pamoja na Abrahamu, Isaka na Yakobo.+ 25 Basi Mungu akawatazama wana wa Israeli naye Mungu akaona.

3 Naye Musa akawa mchungaji wa kundi la Yethro,+ kuhani wa Midiani, aliyekuwa mwana-mkwe wake.+ Alipokuwa akiliongoza kundi kuelekea upande wa magharibi wa nyika, mwishowe akafika kwenye mlima wa Mungu wa kweli,+ Horebu.+ 2 Ndipo malaika wa Yehova akamtokea katika mwali wa moto katikati ya mti wa miiba.+ Alipoendelea kuangalia, tazama, ule mti wa miiba ulikuwa ukiwaka moto lakini haukuwa ukiteketea. 3 Ndipo Musa akasema: “Acha nigeuke nichunguze ajabu hii kubwa, kwa nini mti wa miiba hauteketei.”+ 4 Yehova alipoona kwamba alikuwa amegeuka achunguze, Mungu akamwita mara moja toka katikati ya ule mti wa miiba na kusema: “Musa! Musa!” naye akajibu: “Mimi hapa.”+ 5 Kisha akasema: “Usikaribie hapa. Vua viatu vyako kutoka miguuni, kwa sababu mahali ambapo umesimama ni udongo mtakatifu.”+

6 Naye akaendelea kusema: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.”+ Kisha Musa akauficha uso wake, kwa sababu aliogopa kumtazama Mungu wa kweli. 7 Naye Yehova akaongezea: “Pasipo shaka nimeyaona mateso ya watu wangu walio Misri, nami nimesikia kilio chao kwa sababu ya wale wanaowalazimisha kufanya kazi; kwa sababu nayajua vizuri maumivu waliyo nayo.+ 8 Nami ninashuka ili kuwakomboa kutoka katika mkono wa Wamisri+ na kuwatoa katika nchi hiyo mpaka kwenye nchi nzuri na kubwa, nchi inayotiririka maziwa na asali,+ kwa Wakanaani na Wahiti na Waamori na Waperizi na Wahivi na Wayebusi.+ 9 Na sasa, tazama! kilio cha wana wa Israeli kimenifikia, nami nimeona pia ukandamizaji ambao Wamisri wanatumia kuwakandamiza.+ 10 Na sasa njoo, nikutume kwa Farao, nawe uwatoe watu wangu wana wa Israeli kutoka Misri.”+

11 Hata hivyo, Musa akamwambia Mungu wa kweli: “Mimi ni nani hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli kutoka Misri?”+ 12 Naye akajibu: “Kwa sababu nitakuwa pamoja nawe,+ nayo hii ndiyo ishara kwako ya kwamba mimi ndiye niliyekutuma:+ Baada ya kuwatoa watu hao Misri, ninyi mtamtumikia Mungu wa kweli kwenye mlima huu.”+

13 Hata hivyo, Musa akamwambia Mungu wa kweli: “Tuseme nimefika kwa wana wa Israeli nami niwaambie, ‘Mungu wa mababu zenu amenituma kwenu,’ nao waniambie, ‘Jina lake ni nani?’+ Nitawaambia nini?” 14 Ndipo Mungu akamwambia Musa: “NITAKUWA KILE NITAKACHOKUWA.”+ Naye akaongeza kusema: “Hivi ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli, ‘NITAKUWA amenituma kwenu.’”+ 15 Kisha Mungu akamwambia Musa tena:

“Hivi ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli, ‘Yehova Mungu wa mababu zenu, Mungu wa Abrahamu,+ Mungu wa Isaka+ na Mungu wa Yakobo,+ amenituma kwenu.’ Hilo ndilo jina langu mpaka wakati usio na kipimo,+ na huo ndio ukumbusho wangu kwa kizazi baada ya kizazi.+ 16 Wewe nenda, uwakusanye wanaume wazee wa Israeli, na kuwaambia, ‘Yehova Mungu wa mababu zenu amenitokea,+ Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, na kusema: “Hakika nitaelekeza fikira+ kwenu na kwa yale mnayotendewa katika Misri. 17 Na kwa hiyo nasema, Nitawatoa katika mateso+ ya Wamisri na kuwapeleka mpaka nchi ya Wakanaani na Wahiti na Waamori+ na Waperizi na Wahivi na Wayebusi,+ mpaka nchi inayotiririka maziwa na asali.”’+

18 “Nao hakika wataisikiliza sauti yako,+ nawe utakuja, wewe pamoja na wanaume wazee wa Israeli, kwa Mfalme wa Misri, nanyi mtamwambia, ‘Yehova Mungu wa Waebrania+ amewasiliana nasi,+ na sasa tunataka kwenda, tafadhali, safari ya siku tatu nyikani, nasi tunataka kumtolea dhabihu Yehova Mungu wetu.’+ 19 Nami, naam, mimi najua vema kwamba mfalme wa Misri hatawapa ruhusa ya kwenda isipokuwa kupitia kwa mkono wenye nguvu.+ 20 Nami nitaunyoosha mkono+ wangu na kuipiga Misri kwa matendo yangu yote ya ajabu nitakayoyafanya katikati yake; kisha atawaruhusu mwondoke.+ 21 Nami nitawapa watu hawa kibali machoni pa Wamisri; na hakika itakuwa kwamba mtakapoenda, hamtaenda mikono mitupu.+ 22 Na kila mwanamke atamwomba jirani yake na mwanamke mgeni aliye katika nyumba yake, vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu na nguo za kujitanda, nanyi mtawatwika wana wenu na binti zenu; nanyi mtawaacha Wamisri bila chochote.”+

4 Hata hivyo, Musa akajibu na kusema: “Lakini tuseme hawaniamini wala hawaisikilizi sauti yangu,+ kwa sababu watasema, ‘Yehova hakukutokea.’” 2 Ndipo Yehova akamwambia: “Ni nini hicho kilicho mkononi mwako?” naye akajibu: “Fimbo.”+ 3 Kisha akasema: “Itupe chini.” Basi akaitupa chini, nayo ikawa nyoka;+ na Musa akaanza kumkimbia. 4 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Nyoosha mkono wako umkamate kwenye mkia.” Basi akaunyoosha mkono wake, akamkamata, naye akawa fimbo mkononi mwake. 5 “Ili kwamba,” kama alivyosema, “wapate kuamini ya kwamba Yehova Mungu wa mababu zao,+ Mungu wa Abrahamu,+ Mungu wa Isaka+ na Mungu wa Yakobo,+ amekutokea.”+

6 Kisha Yehova akamwambia tena: “Tia mkono wako, tafadhali, ndani ya mkunjo wa juu wa vazi lako.” Basi akautia mkono wake ndani ya mkunjo huo. Alipouchomoa, tazama, mkono wake ulikuwa umepatwa na ukoma kama theluji!+ 7 Kisha akasema: “Rudisha mkono wako ndani ya mkunjo wa juu wa vazi lako.” Basi akaurudisha mkono wake ndani ya mkunjo huo. Alipouchomoa kutoka katika mkunjo huo, tazama, ulikuwa umerudishwa ukawa kama sehemu nyingine ya mwili wake!+ 8 “Na itakuwa kwamba,” kama alivyosema, “ikiwa hawatakuamini wala kuisikiliza sauti ya ishara ya kwanza, basi hakika wataiamini sauti ya ishara hiyo ya baadaye.+ 9 Hata hivyo, itakuwa kwamba, ikiwa hawataziamini ishara hizo mbili wala kuisikiliza sauti yako,+ basi utachukua maji kutoka katika Mto Nile na kuyamwaga kwenye nchi kavu; nayo maji utakayochukua kutoka katika Mto Nile hakika yatakuwa, ndiyo, kwa kweli yatakuwa damu juu ya nchi kavu.”+

10 Ndipo Musa akamwambia Yehova: “Nakuomba radhi, Yehova, lakini mimi si msemaji mzuri, tangu jana wala tangu kabla ya hapo wala tangu uliposema na mtumishi wako, kwa maana kinywa changu ni kizito na ulimi wangu ni mzito.”+ 11 Ndipo Yehova akamwambia: “Ni nani aliyekifanya kinywa kwa ajili ya mwanadamu au ni nani ambaye humfanya mtu kuwa bubu au kiziwi au mwenye kuona vizuri au kipofu? Je, si mimi, Yehova?+ 12 Basi sasa, nenda, nami nitakuwa pamoja na kinywa chako nami nitakufundisha unayopaswa kusema.”+ 13 Lakini akasema: “Nakuomba radhi, Yehova, lakini tuma, tafadhali, kupitia mkono wa yule utakayemtuma.” 14 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Musa naye akasema: “Je, Haruni Mlawi si ndugu yako?+ Najua kwamba anaweza kuongea kwelikweli. Na tena, tazama, yuko njiani akija kukupokea. Atakapokuona, hakika atashangilia moyoni mwake.+ 15 Nawe utasema naye na kuyaweka maneno hayo kinywani mwake;+ nami nitakuwa pamoja na kinywa chako na kinywa chake,+ nami nitawafundisha mambo mtakayofanya.+ 16 Naye atasema na watu kwa ajili yako; na itakuwa kwamba yeye atatumikia akiwa kinywa kwako,+ nawe utatumikia ukiwa Mungu kwake.+ 17 Nayo fimbo hii utaichukua mkononi mwako ili uitumie kufanya zile ishara.”+

18 Basi Musa akarudi kwa Yethro baba-mkwe wake na kumwambia:+ “Nataka kwenda, tafadhali, nirudi kwa ndugu zangu walio Misri ili nione kama wangali hai.”+ Kwa hiyo Yethro akamwambia Musa: “Nenda kwa amani.”+ 19 Kisha Yehova akamwambia Musa huko Midiani: “Nenda, rudi Misri, kwa sababu watu wote waliokuwa wakiiwinda nafsi yako wamekufa.”+

20 Ndipo Musa akamchukua mke wake na wanawe na kuwapandisha juu ya punda, naye akarudi katika nchi ya Misri. Na zaidi, Musa akaichukua ile fimbo ya Mungu wa kweli mkononi mwake.+ 21 Naye Yehova akamwambia Musa: “Ukisha kwenda na kurudi Misri hakikisha umefanya miujiza yote ambayo nimeitia mkononi mwako mbele ya Farao.+ Mimi nami, nitauacha moyo wake uwe mkaidi;+ naye hatawaruhusu watu waende zao.+ 22 Nawe utamwambia Farao, ‘Hivi ndivyo Yehova amesema: “Israeli ni mwanangu, mzaliwa wangu wa kwanza.+ 23 Nami nakuambia wewe: Mruhusu mwanangu aende zake ili anitumikie. Lakini iwapo utakataa kumruhusu aende zake, tazama, nitamuua mwana wako, mzaliwa wako wa kwanza.”’”+

24 Sasa ikawa kwamba walipokuwa barabarani, mahali pa kulala,+ Yehova akakutana naye,+ naye akawa akitafuta njia ya kumuua.+ 25 Mwishowe Sipora+ akachukua jiwe gumu na kukata govi+ la mwanawe, akalifanya liguse miguu yake, na kusema: “Ni kwa sababu wewe ni bwana-arusi wa damu kwangu.” 26 Basi akamwachilia. Ndipo akasema: “Bwana-arusi wa damu,” kwa sababu ya tohara.

27 Kisha Yehova akamwambia Haruni: “Nenda ukakutane na Musa nyikani.”+ Basi akaenda akakutana naye katika mlima wa Mungu wa kweli,+ akambusu. 28 Naye Musa akamwambia Haruni maneno yote ya Yehova, aliyekuwa amemtuma,+ na ishara zote alizokuwa amemwamuru kufanya.+ 29 Kisha Musa na Haruni wakaenda na kuwakusanya wanaume wote wazee wa wana wa Israeli.+ 30 Ndipo Haruni akasema maneno yote ambayo Yehova alikuwa amemwambia Musa,+ naye akafanya ishara+ machoni pa watu. 31 Kwa hiyo watu wakaamini.+ Waliposikia kwamba Yehova alikuwa amewaelekezea fikira+ wana wa Israeli na kwamba alikuwa ameyaona mateso yao,+ ndipo wakainama na kusujudu.+

5 Na baadaye Musa na Haruni wakaingia ndani na kumwambia Farao:+ “Hivi ndivyo Yehova Mungu wa Israeli amesema, ‘Waruhusu watu wangu waende zao, wakanifanyie sherehe nyikani.’”+ 2 Lakini Farao akasema: “Yehova ni nani,+ hivi kwamba mimi niitii sauti yake na kuwaruhusu Israeli waende zao?+ Simjui Yehova hata kidogo+ na tena sitawaruhusu Israeli waende zao.”+ 3 Hata hivyo, wakaendelea kusema: “Mungu wa Waebrania amewasiliana nasi.+ Tunataka kwenda, tafadhali, safari ya siku tatu nyikani na kumtolea dhabihu Yehova Mungu wetu;+ ikiwa sivyo huenda akatupiga kwa tauni au kwa upanga.”+ 4 Ndipo mfalme wa Misri akawaambia: “Kwa nini, Musa na Haruni, mnawafanya watu waache kazi zao?+ Nendeni mkabebe mizigo yenu!”+ 5 Naye Farao akaendelea kusema: “Tazama! Watu wa nchi hii sasa ni wengi,+ nanyi kwa kweli mnawaachisha kubeba mizigo.”+

6 Siku hiyo, mara moja Farao akawaamuru wale waliokuwa wakiwalazimisha watu kufanya kazi na maofisa+ wao, na kusema: 7 “Msikusanye nyasi ili kuwapa watu watengeneze matofali+ kama hapo zamani. Acheni wao wenyewe waende kujikusanyia nyasi. 8 Tena, jumla ya matofali yanayohitajiwa waliyokuwa wakiyatengeneza hapo zamani, mtazidi kuwadai. Msiwapunguzie hata kidogo, kwa sababu wanalegea.+ Ndiyo sababu wanalia, wakisema, ‘Tunataka kwenda, tunataka kumtolea Mungu wetu dhabihu!’+ 9 Utumishi na uwe mzito juu ya watu hao na waufanyie kazi, wala wasisikilize maneno ya uwongo.”+

10 Basi wale waliokuwa wakiwalazimisha watu kufanya kazi+ na maofisa wao wakatoka na kuwaambia watu: “Hivi ndivyo Farao amesema, ‘Siwapi ninyi nyasi tena. 11 Ninyi wenyewe nendeni, jitafutieni nyasi, popote mtakapoipata, kwa sababu utumishi wenu hautapunguzwa hata kidogo.’”+ 12 Kwa hiyo watu wakatawanyika kotekote nchini Misri ili kukusanya majani makavu kuwa nyasi. 13 Na wale waliokuwa wakiwalazimisha kufanya kazi wakawa wakiwahimiza,+ wakisema: “Malizeni kazi zenu, kila mmoja kazi yake, siku baada ya siku, kama wakati ambapo nyasi ilikuwa ikipatikana.”+ 14 Baadaye maofisa+ wa wana wa Israeli, ambao wasimamizi wa kazi wa Farao walikuwa wamewaweka juu yao, wakapigwa,+ wakiambiwa: “Kwa nini hamkumaliza kazi yenu mliyoamriwa ya kutengeneza matofali+ kama hapo zamani, jana na pia leo?”+

15 Basi maofisa+ wa wana wa Israeli wakaingia ndani na kuanza kumlilia Farao, na kusema: “Kwa nini unawatendea hivi watumishi wako? 16 Watumishi wako hawapewi nyasi yoyote na bado wanatuambia, ‘Tengenezeni matofali!’ na tazama, watumishi wako wanapigwa, hali watu wako mwenyewe ndio wenye makosa.”+ 17 Lakini yeye akasema: “Mnalegea, mnalegea!+ Ndiyo sababu mnasema, ‘Tunataka kwenda, tunataka kumtolea Yehova dhabihu.’+ 18 Na sasa nendeni, mkafanye utumishi! Ingawa hamtapewa nyasi yoyote, bado mtatengeneza jumla ya matofali iliyowekwa.”+

19 Ndipo maofisa wa wana wa Israeli wakajiona ya kwamba wamo katika hali mbaya iliposemwa:+ “Msipunguze hata kidogo kiwango cha matofali yanayotengenezwa na mtu kwa siku.”+ 20 Kisha wakakutana na Musa na Haruni,+ waliokuwa wamesimama hapo ili wakutane nao walipokuwa wakitoka kwa Farao. 21 Wakawaambia mara moja: “Yehova na awatazame ninyi na kuhukumu,+ kwa kuwa mmetufanya tunuke vibaya+ mbele ya Farao na mbele ya watumishi wake kwa kuutia upanga mkononi mwao watuue.”+ 22 Kisha Musa akamgeukia Yehova+ na kusema: “Yehova, kwa nini umesababisha uovu uwapate watu hawa?+ Kwa nini umenituma mimi?+ 23 Kwa maana tangu wakati nilipoenda mbele ya Farao ili kusema katika jina lako,+ amewafanyia watu hawa uovu,+ nawe hujawakomboa watu wako hata kidogo.”+

6 Basi Yehova akamwambia Musa: “Sasa utaona nitakayomtendea Farao,+ maana kwa sababu ya mkono wenye nguvu atawaruhusu waende zao na kwa sababu ya mkono wenye nguvu atawafukuza watoke katika nchi yake.”+

2 Naye Mungu akaendelea kusema na Musa na kumwambia: “Mimi ni Yehova.+ 3 Nami nilikuwa nikimtokea Abrahamu,+ Isaka+ na Yakobo+ kama Mungu Mweza-Yote,+ lakini kuhusu jina langu Yehova+ sikujifanya nijulikane+ kwao. 4 Na pia nilifanya agano pamoja nao niwape nchi ya Kanaani, nchi ya makao yao ya kigeni walimokaa wakiwa wageni.+ 5 Nami, naam mimi, nimesikia kuugua kwa wana wa Israeli,+ ambao Wamisri wanawatumikisha, nami ninalikumbuka agano langu.+

6 “Kwa hiyo waambie wana wa Israeli, ‘Mimi ni Yehova, nami hakika nitawatoa chini ya mizigo ya Wamisri na kuwakomboa kutoka katika utumwa wao,+ nami kwa kweli nitawaokoa ninyi kwa mkono ulionyooshwa na kwa hukumu kubwa.+ 7 Nami hakika nitawachukua kwangu muwe watu wangu,+ nami kwa kweli nitakuwa Mungu kwenu;+ nanyi hakika mtajua kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu anayewatoa kutoka chini ya mizigo ya Misri.+ 8 Nami hakika nitawaingiza katika nchi ambayo niliuinua mkono wangu katika kiapo+ kwamba nitampa Abrahamu, Isaka na Yakobo; nami kwa kweli nitawapa ninyi iwe mali yenu.+ Mimi ni Yehova.’”+

9 Baadaye Musa akawaambia wana wa Israeli maneno hayo, lakini hawakumsikiliza Musa kwa sababu ya kuvunjika moyo na kwa sababu ya utumwa mgumu.+

10 Ndipo Yehova akaongea na Musa, na kusema: 11 “Ingia ndani, mwambie Farao, mfalme wa Misri,+ kwamba inampasa awaruhusu wana wa Israeli waondoke katika nchi yake.”+ 12 Hata hivyo, Musa akasema mbele za Yehova, na kumwambia: “Tazama! Wana wa Israeli hawakunisikiliza;+ Farao atawezaje kunisikiliza,+ kwa maana mimi sijatahiriwa midomo?”+ 13 Lakini Yehova akaendelea kusema na Musa na Haruni na kuitoa amri kupitia kwao kwa wana wa Israeli na kwa Farao, mfalme wa Misri, ili kuwatoa wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri.+

14 Hawa ndio vichwa vya nyumba za baba zao: Wana wa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli,+ walikuwa Hanoki na Palu, Hezroni na Karmi.+ Hizo ndizo familia za Rubeni.+

15 Nao wana wa Simeoni walikuwa Yemueli na Yamini na Ohadi na Yakini na Zohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.+ Hizo ndizo familia za Simeoni.+

16 Na haya ndiyo majina ya wana wa Lawi,+ kulingana na ukoo wa familia yao:+ Gershoni na Kohathi na Merari.+ Nayo miaka ya maisha ya Lawi ilikuwa miaka 137.

17 Wana wa Gershoni walikuwa Libni na Shimei,+ kulingana na familia zao.+

18 Na wana wa Kohathi walikuwa Amramu na Ishari na Hebroni na Uzieli.+ Nayo miaka ya maisha ya Kohathi ilikuwa miaka 133.

19 Na wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi.+

Hizo ndizo zilizokuwa familia za Walawi, kulingana na ukoo wa familia yao.+

20 Sasa Amramu alimchukua Yokebedi dada ya baba yake awe mke wake.+ Baadaye akamzalia Haruni na Musa.+ Nayo miaka ya maisha ya Amramu ilikuwa miaka 137.

21 Na wana wa Ishari walikuwa Kora+ na Nefegi na Zikri.

22 Na wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli na Elsafani na Sithri.+

23 Sasa Haruni alimchukua Elisheba, binti ya Aminadabu, dada ya Nashoni,+ awe mke wake. Baadaye akamzalia Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.+

24 Na wana wa Kora walikuwa Asiri na Elkana na Abiasafu.+ Hizo ndizo zilizokuwa familia za Wakora.+

25 Na Eleazari, mwana wa Haruni,+ alijichukulia mmoja wa binti za Putieli awe mke wake. Baadaye akamzalia Finehasi.+

Hao ndio vichwa vya upande wa baba vya Walawi, kulingana na familia zao.+

26 Huyo ndiye Haruni na Musa ambao Yehova aliwaambia:+ “Watoeni wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri kulingana na majeshi yao.”+ 27 Wao ndio waliokuwa wakisema na Farao, mfalme wa Misri, ili kuwatoa wana wa Israeli kutoka Misri.+ Huyo ndiye Musa na Haruni.

28 Na ikawa siku ambayo Yehova alisema na Musa katika nchi ya Misri,+ 29 kwamba Yehova aliongea na Musa, na kusema: “Mimi ni Yehova.+ Mwambie Farao mfalme wa Misri kila jambo ninalokuambia.” 30 Kisha Musa akasema mbele za Yehova: “Tazama! Mimi sijatahiriwa midomo, basi Farao atawezaje kunisikiliza mimi?”+

7 Kwa hiyo Yehova akamwambia Musa: “Tazama, nimekufanya wewe kuwa Mungu kwa Farao,+ na Haruni ndugu yako atakuwa nabii wako.+ 2 Wewe—wewe utasema mambo yote nitakayokuamuru;+ naye Haruni ndugu yako atamwambia Farao,+ naye lazima awaruhusu wana wa Israeli waondoke nchini mwake.+ 3 Mimi nami, nitauacha moyo wa Farao uwe mkaidi,+ nami hakika nitazidisha ishara zangu na miujiza yangu katika nchi ya Misri.+ 4 Na Farao hatawasikiliza ninyi;+ nami nitalazimika kuuweka mkono wangu juu ya Misri na kuleta majeshi yangu,+ watu wangu,+ wana wa Israeli,+ kutoka katika nchi ya Misri kwa hukumu kubwa.+ 5 Na Wamisri hakika watajua kwamba mimi ni Yehova wakati ambapo nitaunyoosha mkono wangu juu ya Misri,+ nami kwa kweli nitawatoa wana wa Israeli kutoka katikati yao.”+ 6 Na Musa na Haruni wakafanya kama vile Yehova alivyokuwa amewaamuru.+ Walifanya vivyo hivyo.+ 7 Na Musa alikuwa na umri wa miaka 80 naye Haruni alikuwa na umri wa miaka 83 wakati waliposema na Farao.+

8 Sasa Yehova akamwambia Musa na Haruni: 9 “Ikiwa Farao atanena nanyi, na kusema, ‘Jifanyieni muujiza,’+ basi utamwambia Haruni, ‘Chukua fimbo yako,+ uitupe chini mbele ya Farao.’ Itakuwa nyoka mkubwa.”+ 10 Kwa hiyo Musa na Haruni wakaingia ndani kwa Farao na kufanya sawasawa na vile ambavyo Yehova alikuwa ameamuru. Basi Haruni akaitupa chini fimbo yake mbele ya Farao na watumishi wake nayo ikawa nyoka mkubwa. 11 Hata hivyo, Farao pia aliwaita watu wenye hekima na walozi;+ na makuhani wa Misri wenye kufanya uchawi nao pia wakafanya jambo hilo hilo kwa ufundi wao wa uchawi.+ 12 Kwa hiyo kila mmoja wao akatupa chini fimbo yake, nazo zikawa nyoka wakubwa; lakini fimbo ya Haruni ikameza fimbo zao. 13 Bado, moyo wa Farao ukawa mkaidi,+ naye hakuwasikiliza, kama Yehova alivyokuwa amesema.

14 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Moyo wa Farao ni mgumu.+ Amekataa kuwaruhusu watu waende zao.+ 15 Nenda kwa Farao asubuhi. Tazama! Anaenda majini!+ Nawe usimame mahali ili kukutana naye kwenye ukingo wa Mto Nile,+ nayo fimbo iliyogeuka na kuwa nyoka uichukue mkononi mwako.+ 16 Nawe utamwambia, ‘Yehova Mungu wa Waebrania amenituma kwako,+ na kusema: “Waruhusu watu wangu waende zao wakanitumikie nyikani,”+ lakini, tazama, wewe hujatii mpaka sasa. 17 Hivi ndivyo Yehova amesema:+ “Kwa hili utajua kwamba mimi ni Yehova.+ Tazama, ninayapiga maji yaliyo katika Mto Nile+ kwa fimbo niliyo nayo mkononi, nayo hakika yatageuka na kuwa damu.+ 18 Na samaki walio katika Mto Nile watakufa,+ nao Mto Nile utanuka kwelikweli,+ nao Wamisri hawatakuwa na hamu hata kidogo ya kunywa maji kutoka katika Mto Nile.”’”+

19 Baadaye Yehova akamwambia Musa: “Mwambie Haruni, ‘Ichukue fimbo yako na kuunyoosha mkono+ wako juu ya maji ya Misri, juu ya mito yao, juu ya mifereji yao ya Nile na juu ya madimbwi yao yenye matete+ na juu ya maji yao yote yaliyozuiliwa, ili yawe damu.’ Na hakika damu itakuwa katika nchi yote ya Misri na katika vyombo vya mbao na katika vyombo vya mawe.” 20 Musa na Haruni wakafanya hivyo mara moja,+ kama vile Yehova alivyokuwa ameamuru,+ naye akainua fimbo na kuyapiga maji ya Mto Nile machoni pa Farao na watumishi wake,+ nayo maji yote yaliyokuwa katika Mto Nile yakageuzwa kuwa damu.+ 21 Na samaki waliokuwa katika Mto Nile wakafa,+ nao Mto Nile ukaanza kunuka; nao Wamisri hawakuweza kunywa maji kutoka katika Mto Nile;+ na damu ikawa katika nchi yote ya Misri.

22 Hata hivyo, makuhani wa Misri wenye kufanya uchawi wakafanya jambo hilo hilo kwa ufundi wao wa siri;+ hivi kwamba moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi,+ naye hakuwasikiliza, kama vile Yehova alivyokuwa amesema.+ 23 Basi Farao akageuka na kuingia nyumbani mwake, naye hakuuruhusu moyo wake ufikirie jambo hilo kwa uzito.+ 24 Na Wamisri wote wakaanza kuchimba kuuzunguka Mto Nile wakitafuta maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji yoyote ya Mto Nile.+ 25 Na siku saba zikatimia baada ya Yehova kuupiga Mto Nile.

8 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Ingia kwa Farao, nawe umwambie, ‘Hivi ndivyo Yehova amesema: “Waruhusu watu wangu waende zao ili wanitumikie.+ 2 Na ikiwa utaendelea kukataa kuwaruhusu waende zao, tazama, nitaleta pigo la vyura+ katika eneo lako lote. 3 Nao Mto Nile utajaa vyura, nao hakika watapanda na kuingia ndani ya nyumba yako na ndani ya chumba chako cha ndani cha kulala na juu ya kitanda chako na ndani ya nyumba za watumishi wako na juu ya watu wako na ndani ya majiko yako na ndani ya vyombo vyako vya kukandia unga.+ 4 Na vyura hao watakuja juu yako na juu ya watu wako na juu ya watumishi wako wote.”’”+

5 Baadaye Yehova akamwambia Musa: “Mwambie Haruni, ‘Nyoosha mkono wako pamoja na fimbo+ yako juu ya mito, mifereji ya Nile na madimbwi yenye matete na kuwafanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.’” 6 Ndipo Haruni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, na vyura wakaanza kuja juu na kuifunika nchi ya Misri. 7 Hata hivyo, makuhani wenye kufanya uchawi wakafanya jambo hilo hilo kwa ufundi wao wa siri na kuwafanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.+ 8 Mwishowe Farao akawaita Musa na Haruni na kusema: “Msihi Yehova+ ili awaondoe vyura hawa kutoka kwangu na kwa watu wangu, kwa maana nataka kuwaruhusu watu waende zao, wakamtolee Yehova dhabihu.”+ 9 Kisha Musa akamwambia Farao: “Jitwalie utukufu kutoka kwangu na kusema ni wakati gani nitakaposihi kwa ajili yako na watumishi wako na watu wako ili kuwaondolea mbali hao vyura kutoka kwenu na nyumbani mwenu. Watabaki katika Mto Nile tu.” 10 Naye akajibu: “Kesho.” Basi akasema: “Itakuwa kulingana na neno lako, ili ujue kwamba hakuna mwingine yeyote aliye kama Yehova Mungu wetu,+ 11 kwa kuwa hakika vyura wataondoka kwako na nyumbani mwako na kuondoka kwa watumishi wako na watu wako. Watabaki katika Mto Nile tu.”+

12 Basi Musa na Haruni wakaondoka kwa Farao, naye Musa akamlilia Yehova+ kwa sababu ya vyura hao ambao Yeye alikuwa ameweka juu ya Farao. 13 Kisha Yehova akafanya kulingana na neno la Musa,+ na vyura wakaanza kufa kutoka katika nyumba, nyua na mashamba. 14 Nao wakawakusanya, mafungu mafungu, nayo nchi ikaanza kunuka.+ 15 Farao alipoona kwamba kitulizo kilikuwa kimetokea, akaufanya moyo wake uwe mgumu;+ naye hakuwasikiliza wao, kama vile Yehova alivyokuwa amesema.+

16 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Mwambie Haruni, ‘Inyooshe fimbo+ yako na kuyapiga mavumbi ya dunia, nayo yatakuwa chawa katika nchi yote ya Misri.’” 17 Nao wakafanya hivyo. Kwa hiyo Haruni akaunyoosha mkono wake pamoja na fimbo yake na kuyapiga mavumbi ya dunia, nao chawa wakawa juu ya wanadamu na wanyama. Mavumbi yote ya dunia yakawa chawa katika nchi yote ya Misri.+ 18 Nao makuhani wenye kufanya uchawi wakajaribu kufanya vivyo hivyo kwa ufundi wao wa siri,+ ili kutokeza chawa, lakini hawakuweza.+ Na chawa hao wakawa juu ya wanadamu na wanyama. 19 Basi makuhani wenye kufanya uchawi wakamwambia Farao: “Ni kidole+ cha Mungu!”+ Lakini moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi,+ naye hakuwasikiliza, kama vile Yehova alivyokuwa amesema.

20 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Amka asubuhi na mapema usimame mbele ya Farao.+ Tazama! Anatoka kwenda majini! Nawe utamwambia, ‘Hivi ndivyo Yehova amesema: “Waruhusu watu wangu waende zao ili wanitumikie.+ 21 Lakini ikiwa hutawaruhusu watu wangu waende zao, tazama, nitatuma mainzi+ juu yako na watumishi wako na watu wako na ndani ya nyumba zako; nazo nyumba za Wamisri zitajaa mainzi, na pia nchi ambayo wako juu yake. 22 Na siku hiyo hakika nitaifanya nchi ya Gosheni ambapo watu wangu wanakaa iwe tofauti, kwamba inzi yeyote asiwe huko;+ ili upate kujua kwamba mimi ni Yehova katikati ya dunia.+ 23 Nami kwa kweli nitaweka mpaka kati ya watu wangu na watu wako.+ Kesho ishara hii itatokea.”’”

24 Naye Yehova akafanya hivyo; na makundi makubwa ya mainzi yakaanza kuvamia nyumba ya Farao na nyumba za watumishi wake na nchi yote ya Misri.+ Nchi ikaharibika kwa sababu ya mainzi hao.+ 25 Mwishowe Farao akawaita Musa na Haruni na kusema: “Nendeni, mtoleeni Mungu wenu dhabihu nchini.”+ 26 Lakini Musa akasema: “Haikubaliki kufanya hivyo, kwa sababu tutamtolea Yehova Mungu wetu dhabihu ya kitu ambacho ni chukizo kwa Wamisri.+ Tuseme tungetoa dhabihu ya kitu ambacho ni chukizo machoni pa Wamisri; je, hawangetupiga kwa mawe? 27 Tutaenda safari ya siku tatu nyikani nasi hakika tutamtolea Yehova Mungu wetu dhabihu sawasawa na alivyotuambia.”+

28 Farao sasa akasema: “Mimi—mimi nitawaruhusu mwende zenu,+ nanyi kwa kweli mtamtolea dhabihu Yehova Mungu wenu nyikani.+ Ila tu msiende mbali sana. Sihi kwa ajili yangu.”+ 29 Ndipo Musa akasema: “Tazama, naondoka kwako, nami kwa kweli nitamsihi Yehova, na hakika mainzi wataondoka kwa Farao, kwa watumishi wake na kwa watu wake kesho. Ila Farao asifanye mchezo tena kwa kukataa kuwaruhusu watu waende zao kumtolea Yehova dhabihu.”+ 30 Kisha Musa akaondoka mbele ya Farao na kumsihi Yehova.+ 31 Basi Yehova akafanya kulingana na neno la Musa,+ na mainzi wakaondoka kwa Farao, kwa watumishi wake na kwa watu wake.+ Hakuna hata mmoja aliyebaki. 32 Hata hivyo, Farao akaufanya moyo wake uwe mgumu wakati huu pia wala hakuwaruhusu watu waende zao.+

9 Kwa hiyo Yehova akamwambia Musa: “Ingia ndani kwa Farao, umwambie,+ ‘Hivi ndivyo Yehova Mungu wa Waebrania amesema: “Waruhusu watu wangu waende zao wapate kunitumikia. 2 Lakini ukiendelea kukataa kuwaruhusu waende zao nawe ukiendelea kuwazuia,+ 3 tazama! mkono wa Yehova+ utakuja juu ya mifugo+ yako iliyo shambani. Kutakuwa na tauni kali sana+ juu ya farasi, punda, ngamia, mifugo na makundi. 4 Na Yehova hakika atafanya tofauti kati ya mifugo ya Israeli na mifugo ya Misri, wala hakuna chochote cha wana wa Israeli kitakachokufa.”’”+ 5 Tena, Yehova akaweka wakati, na kusema: “Kesho Yehova atafanya jambo hilo katika nchi.”+

6 Basi Yehova akafanya jambo hilo siku iliyofuata, na aina zote za mifugo ya Wamisri zikaanza kufa;+ lakini hakuna mnyama yeyote kati ya mifugo ya wana wa Israeli aliyekufa. 7 Kisha Farao akatuma watu, na, tazama! hakuna hata mnyama mmoja kati ya mifugo ya Israeli aliyekuwa amekufa. Hata hivyo, moyo wa Farao ukaendelea kuwa mgumu,+ naye hakuwaruhusu watu waende zao.

8 Kisha Yehova akawaambia Musa na Haruni: “Chukueni masizi kutoka katika tanuru,+ yaliyojaa kwenye mikono yote miwili, naye Musa ayarushe kuelekea mbinguni mbele ya macho ya Farao. 9 Nayo yatakuwa mavumbi juu ya nchi yote ya Misri, nayo yatakuwa majipu yanayopasuka na yenye malengelenge+ juu ya mwanadamu na mnyama katika nchi yote ya Misri.”

10 Basi wakachukua masizi ya tanuru na kusimama mbele ya Farao, naye Musa akayarusha kuelekea mbinguni, nayo yakawa majipu yenye malengelenge,+ yanayopasuka juu ya mwanadamu na mnyama. 11 Nao makuhani wenye kufanya uchawi hawakuweza kusimama mbele ya Musa kutokana na majipu, kwa sababu makuhani hao na Wamisri wote walikuwa wamepata majipu hayo.+ 12 Lakini Yehova akauacha moyo wa Farao uwe mkaidi, naye hakuwasikiliza, kama vile Yehova alivyokuwa amemwambia Musa.+

13 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Amka asubuhi na mapema usimame mbele ya Farao,+ nawe umwambie, ‘Hivi ndivyo Yehova Mungu wa Waebrania amesema: “Waruhusu watu wangu waende zao wapate kunitumikia.+ 14 Kwa maana wakati huu ninatuma mapigo yangu yote juu ya moyo wako na juu ya watumishi wako na watu wako, ili upate kujua kwamba hakuna yeyote aliye kama mimi katika dunia yote.+ 15 Kwa maana kufikia sasa ningalikuwa nimenyoosha mkono wangu nipate kukupiga wewe na watu wako kwa tauni ili ufutiliwe mbali kutoka duniani.+ 16 Lakini, kwa kweli, kwa sababu hii nimekuacha uendelee kuwako,+ ili kukuonyesha nguvu zangu na ili nifanye jina langu litangazwe katika dunia yote.+ 17 Je, bado unajiendesha kwa majivuno juu ya watu wangu kwa kutowaruhusu waende zao?+ 18 Tazama, kesho wakati kama huu nitafanya mvua kubwa sana ya mawe inyeshe, mvua ambayo haijapata kunyesha Misri tangu siku ilipowekwa msingi mpaka sasa.+ 19 Na sasa tuma watu, uingize mifugo yako yote na vitu vyote vilivyo vyako shambani mahali pa kujikinga. Na kuhusu mwanadamu na mnyama yeyote atakayepatikana shambani, bila kuingia nyumbani, mvua hiyo ya mawe+ itawaangukia, nao watakufa.”’”

20 Yeyote aliyeogopa neno la Yehova kati ya watumishi wa Farao aliwakimbiza watumishi wake na mifugo wake ndani ya nyumba,+ 21 lakini yeyote ambaye moyo wake haukujali neno la Yehova aliwaacha watumishi wake na mifugo yake shambani.+

22 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Nyoosha mkono+ wako kuelekea mbinguni, ili mvua ya mawe+ ipate kunyesha juu ya nchi yote ya Misri, juu ya mwanadamu na mnyama na mimea yote ya shambani katika nchi ya Misri.” 23 Kwa hiyo Musa akainyoosha fimbo yake kuelekea mbinguni; na Yehova akatoa mingurumo na mvua ya mawe,+ na moto ulikuwa ukishuka chini mpaka duniani, naye Yehova akafanya mvua ya mawe iendelee kunyesha juu ya nchi ya Misri. 24 Basi mvua ya mawe ikanyesha, nao moto ukiwaka-waka katikati ya mvua ya mawe. Ilikuwa nzito sana, hivi kwamba haikuwa imetokea yoyote kama hiyo katika nchi yote ya Misri tangu ilipokuwa taifa.+ 25 Nayo mvua ya mawe ikapiga nchi yote ya Misri. Mvua ya mawe ikapiga kila kitu kilichokuwa shambani, kuanzia mwanadamu mpaka mnyama, na kila aina ya mimea ya shambani; nayo ikavunja-vunja namna zote za miti ya shambani.+ 26 Ila tu katika nchi ya Gosheni, ambako wana wa Israeli walikuwa, hakukuwa na mvua yoyote ya mawe.+

27 Mwishowe Farao akawatuma watu wawaite Musa na Haruni, naye akawaambia: “Nimetenda dhambi wakati huu.+ Yehova ni mwadilifu,+ na mimi na watu wangu tumekosea. 28 Msihi Yehova ili mingurumo hii ya Mungu na mvua yake ya mawe+ ziishie hapo. Ndipo nitakuwa tayari kuwaruhusu mwende zenu, nanyi hamtaendelea kukaa zaidi.” 29 Basi Musa akamwambia: “Mara tu nitakapoondoka jijini nitamnyooshea Yehova mikono yangu.+ Mingurumo itakoma nayo mvua ya mawe haitaendelea tena, ili upate kujua kwamba dunia ni ya Yehova.+ 30 Na wewe, pamoja na watumishi wako, tayari ninajua kwamba hata wakati huo hamtaonyesha woga wowote kwa sababu ya Yehova Mungu.”+

31 Kama ilivyokuwa, kitani na shayiri zilikuwa zimepigwa, kwa sababu shayiri ilikuwa na masuke nacho kitani kilikuwa na matumba ya maua.+ 32 Lakini ngano na kusemethi+ hazikuwa zimepigwa, kwa sababu majira yake yalikuwa hayajafika. 33 Sasa Musa akaondoka jijini kutoka kwa Farao, akamnyooshea Yehova mikono yake, nayo mingurumo na mvua ya mawe zikaanza kukoma na mvua haikunyesha juu ya dunia.+ 34 Farao alipoona kwamba mvua na mawe ya mvua na mingurumo zilikuwa zimekoma, akatenda dhambi tena na kuufanya moyo wake uwe mgumu,+ yeye na watumishi wake. 35 Nao moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi, naye hakuwaruhusu wana wa Israeli waende zao, kama vile Yehova alivyokuwa amesema kupitia Musa.+

10 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Ingia ndani kwa Farao, kwa sababu mimi—mimi nimeuacha moyo wake na mioyo ya watumishi wake iwe migumu,+ ili niweke ishara zangu hizi mbele yake,+ 2 na ili upate kutangaza masikioni mwa mwana wako na mwana wa mwana wako jinsi ambavyo nimeshughulika vikali na Misri na ishara zangu ambazo nimesimamisha katikati yao;+ nanyi hakika mtajua kwamba mimi ni Yehova.”+

3 Basi Musa na Haruni wakaingia ndani kwa Farao na kumwambia: “Hivi ndivyo Yehova Mungu wa Waebrania amesema, ‘Utaendelea kukataa kujitiisha kwangu mpaka wakati gani?+ Waruhusu watu wangu waende zao ili wanitumikie. 4 Kwa maana ikiwa utaendelea kukataa kuwaruhusu watu wangu waende zao, tazama, kesho nitaleta nzige ndani ya mipaka yako.+ 5 Nao watafunika uso wa dunia unaoonekana wala haitawezekana kuiona dunia; nao watakula kilichobaki, kile ambacho mvua ya mawe iliwaachia ninyi, nao watakula miti yenu yote inayochipuka shambani.+ 6 Nazo nyumba zako na nyumba za watumishi wako wote na nyumba za Misri yote zitajaa kwa kadiri ambayo baba zako na baba za baba zako hawajapata kuona tangu siku za kuwako kwao juu ya nchi mpaka leo hii.’”+ Kisha akageuka na kuondoka kwa Farao.+

7 Baada ya hapo watumishi wa Farao wakamwambia: “Mtu huyu ataendelea kuwa mtego+ kwetu mpaka wakati gani? Waruhusu watu waende zao ili wamtumikie Yehova Mungu wao. Je, bado hujajua kwamba Misri imeangamia?”+ 8 Kwa hiyo Musa na Haruni wakarudishwa kwa Farao, naye akawaambia: “Nendeni, mkamtumikie Yehova Mungu wenu.+ Ni nani hasa wanaoenda?” 9 Ndipo Musa akasema: “Tutaenda pamoja na vijana wetu na wazee wetu. Tutaenda pamoja na wana wetu na binti+ zetu, pamoja na kondoo zetu na ng’ombe zetu,+ kwa maana tuna sherehe ya kumfanyia Yehova.”+ 10 Naye akawajibu: “Na iwe hivyo, kwamba Yehova yuko pamoja nanyi wakati nitakapowaruhusu ninyi na watoto wenu mwende zenu!+ Tazama, tofauti na hilo, mna lengo la kufanya jambo baya.+ 11 Hapana! Nendeni, tafadhali, ninyi wanaume, mkamtumikie Yehova, kwa sababu hilo ndilo mnalotaka kupata.” Ndipo wakafukuzwa kutoka mbele ya Farao.+

12 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Unyooshe+ mkono wako juu ya nchi ya Misri kwa ajili ya nzige, ili waje juu ya nchi ya Misri na kula mimea yote ya nchi, kila kitu ambacho ile mvua ya mawe iliacha.”+ 13 Mara moja Musa akainyoosha fimbo yake juu ya nchi ya Misri, naye Yehova akafanya upepo wa mashariki+ uvume juu ya nchi siku hiyo yote na usiku wote. Asubuhi ikafika nao upepo wa mashariki ukawaleta hao nzige. 14 Nao nzige wakaanza kuja juu ya nchi yote ya Misri na kutua juu ya eneo lote la Misri.+ Walikuwa wenye kulemea sana.+ Kabla yao hawakuwa wametokea kamwe jinsi hiyo nzige wengine kama wao, wala hakutatokea wowote kamwe jinsi hiyo baada yao. 15 Nao wakaufunika uso unaoonekana wa nchi+ yote, nayo nchi ikawa na giza;+ nao wakawa wakila mimea yote ya nchi na matunda yote ya miti ambayo ile mvua ya mawe ilikuwa imeacha;+ wala hakikubaki chochote cha kijani kibichi juu ya miti wala juu ya mimea ya shambani katika nchi yote ya Misri.+

16 Basi Farao akawaita haraka haraka Musa na Haruni na kusema: “Nimemtendea dhambi Yehova Mungu wenu na ninyi pia.+ 17 Na sasa mnisamehe,+ tafadhali, dhambi yangu mara hii moja tu na kumsihi+ Yehova Mungu wenu apate kuniondolea pigo hili lenye kufisha.” 18 Basi akaondoka kwa Farao na kumsihi Yehova.+ 19 Kisha Yehova akageuza upepo mkali sana wa magharibi, nao ukawaondolea mbali nzige hao na kuwapeleka katika Bahari Nyekundu. Hakuna nzige hata mmoja aliyeachwa abaki katika eneo lote la Misri. 20 Hata hivyo, Yehova akauacha moyo wa Farao uwe mkaidi,+ naye hakuwaruhusu wana wa Israeli waende zao.

21 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Unyooshe mkono wako kuelekea mbinguni,+ ili giza lipate kutokea juu ya nchi ya Misri nalo giza liweze kuguswa.” 22 Mara moja Musa akanyoosha mkono wake kuelekea mbinguni, na giza zito likaanza kutokea katika nchi yote ya Misri kwa siku tatu.+ 23 Hawakuonana, wala hakuna yeyote kati yao aliyeondoka mahali pake kwa siku tatu; lakini kwa wana wote wa Israeli kulikuwa na nuru katika makao yao.+ 24 Kisha Farao akamwita Musa na kusema: “Nendeni, mkamtumikie Yehova.+ Ni kondoo zenu na ng’ombe zenu tu watakaozuiwa. Watoto wenu pia wanaweza kwenda pamoja nanyi.”+ 25 Lakini Musa akasema: “Wewe mwenyewe pia utatupa mikononi mwetu dhabihu na matoleo ya kuteketezwa, kwa maana tutavitoa kwa Yehova Mungu wetu.+ 26 Na mifugo yetu pia itaenda pamoja nasi.+ Hakuna hata ukwato utakaoruhusiwa kubaki, kwa sababu ni kutoka kati yao kwamba tutachukua baadhi yao ili kumwabudu Yehova Mungu wetu,+ nasi wenyewe hatujui tutakachotoa katika ibada kwa Yehova mpaka tufike huko.”+ 27 Ndipo Yehova akauacha moyo wa Farao uwe mkaidi, wala hakukubali kuwaruhusu waende zao.+ 28 Basi Farao akamwambia: “Toka mbele yangu!+ Jiangalie! Usijaribu kuuona uso wangu tena, kwa sababu siku utakayouona uso wangu utakufa.”+ 29 Ndipo Musa akasema: “Kama ambavyo umesema na iwe. Sitajaribu kuuona uso wako tena.”+

11 Na Yehova akamwambia Musa: “Nitaleta pigo moja zaidi juu ya Farao na Misri. Halafu atawaruhusu mwende zenu kutoka hapa.+ Wakati atakapowaruhusu mwende zenu nyote kabisa, atawafukuza kutoka hapa.+ 2 Sasa, sema masikioni mwa watu, kwamba kila mwanamume na amwombe mwenzake na kila mwanamke na amwombe mwenzake vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu.”+ 3 Basi Yehova akawapa watu kibali machoni pa Wamisri.+ Mwanamume huyo Musa pia alikuwa mkuu sana katika nchi ya Misri, machoni pa watumishi wa Farao na machoni pa watu.+

4 Na Musa akasema: “Hivi ndivyo Yehova amesema, ‘Karibu na katikati ya usiku hivi nitaingia katikati ya Misri,+ 5 na kila mzaliwa wa kwanza+ katika nchi ya Misri atakufa, tokea mzaliwa wa kwanza wa Farao anayeketi juu ya kiti chake cha ufalme hata mzaliwa wa kwanza wa mjakazi aliye kwenye jiwe la kusagia la mkononi na kila mzaliwa wa kwanza wa mnyama.+ 6 Na hakika kutatokea kilio kikubwa katika nchi yote ya Misri, ambacho namna yake haijatokea kamwe, na ambacho namna yake haitatokea kamwe.+ 7 Lakini hakuna mbwa yeyote atakayeuchezesha ulimi wake kwa bidii dhidi ya yeyote wa wana wa Israeli, kuanzia mwanadamu hata mnyama;+ ili mpate kujua kwamba Yehova anaweza kufanyiza tofauti kati ya Wamisri na wana wa Israeli.’+ 8 Na hakika hawa watumishi wako wote watanijia na kusujudu mbele yangu,+ na kusema, ‘Nenda, wewe na watu wote wanaofuata hatua zako.’ Na baada ya hapo mimi nitaondoka.” Kisha akaondoka mbele ya Farao akiwaka hasira.

9 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Farao hatawasikiliza ninyi,+ ili miujiza yangu iongezeke katika nchi ya Misri.”+ 10 Na Musa na Haruni wakafanya miujiza yote hiyo mbele ya Farao;+ lakini Yehova alikuwa akiuacha moyo wa Farao uwe mkaidi, hivi kwamba hakuwaruhusu wana wa Israeli waende zao kutoka katika nchi yake.+

12 Yehova akasema na Musa na Haruni katika nchi ya Misri: 2 “Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu. Utakuwa mwezi wa kwanza wa mwaka kwenu.+ 3 Sema na kusanyiko lote la Israeli, na kuwaambia, ‘Siku ya kumi ya mwezi huu watajichukulia kila mmoja kondoo+ kwa ajili ya nyumba ya mababu, kondoo mmoja kwa kila nyumba. 4 Lakini ikiwa nyumba hiyo ni ndogo sana kwa kondoo huyo, basi yeye na jirani yake aliye karibu watamwingiza nyumbani mwake kulingana na hesabu ya nafsi; mtafanya hesabu ya kila mmoja kulingana na ulaji wake kuhusiana na kondoo huyo. 5 Kondoo huyo anapaswa kuwa asiye na kasoro,+ dume, mwenye umri wa mwaka mmoja, kwa ajili yenu.+ Mnaweza kumchagua kutoka kati ya wana-kondoo dume au kutoka kati ya mbuzi. 6 Naye ataendelea kukaa chini ya ulinzi wenu mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi huu,+ nalo kutaniko zima la kusanyiko la Israeli litamchinja katikati ya zile jioni mbili.+ 7 Nao watachukua sehemu ya damu na kuipaka juu ya miimo miwili ya mlango na sehemu ya juu ya mlango wa nyumba ambamo watamla.+

8 “‘Nao wataila hiyo nyama usiku huu.+ Wataila ikiwa imechomwa kwa moto pamoja na keki zisizo na chachu+ na pia mboga chungu za majani.+ 9 Msile yoyote ya hiyo ikiwa mbichi au ikiwa imetokoswa, ikiwa imepikwa ndani ya maji, bali ikiwa imechomwa kwa moto, kichwa chake pamoja na miguu yake na matumbo yake. 10 Nanyi hamtaacha yoyote mpaka asubuhi, lakini yoyote itakayobaki mpaka asubuhi mtaiteketeza kwa moto.+ 11 Na hivi ndivyo mtakavyokula, viuno vyenu vikiwa vimefungwa mshipi,+ viatu+ vikiwa miguuni penu na fimbo yenu mkononi mwenu; nanyi mtaila haraka haraka. Ni pasaka ya Yehova.+ 12 Nami nitapita katikati ya nchi ya Misri usiku huu+ na kumpiga kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri, kuanzia mwanadamu hata mnyama;+ nami nitatekeleza hukumu+ juu ya miungu yote ya Misri. Mimi ni Yehova.+ 13 Na damu hiyo itakuwa ishara yenu juu ya nyumba mtakazokuwamo; nami nitaiona damu hiyo na kupita juu yenu,+ nalo pigo halitakuja juu yenu kama uharibifu ninapoipiga nchi ya Misri.

14 “‘Na siku hii itakuwa ukumbusho kwenu, nanyi mtaisherehekea ikiwa sherehe kwa Yehova katika vizazi vyenu vyote. Nanyi mtaisherehekea kama sheria mpaka wakati usio na kipimo. 15 Siku saba mtakula keki zisizo na chachu. Ndiyo, siku ya kwanza mtaondoa unga uliokandwa wenye chachu kutoka katika nyumba zenu, kwa sababu mtu yeyote anayekula kitu kilicho na chachu, kuanzia siku ya kwanza mpaka siku ya saba,+ nafsi hiyo itakatiliwa mbali kutoka katika Israeli.+ 16 Na siku ya kwanza kutakuwa na mkusanyiko mtakatifu kwa ajili yenu, na siku ya saba mkusanyiko mtakatifu.+ Hakuna kazi yoyote itakayofanywa katika siku hizo.+ Ila tu kile ambacho kila nafsi inahitaji kula, hicho tu kinaweza kufanywa kwa ajili yenu.+

17 “‘Nanyi lazima mshike sherehe ya keki zisizo na chachu,+ kwa sababu siku hiyo hiyo nitayatoa majeshi yenu kutoka katika nchi ya Misri. Nanyi mtaishika siku hiyo katika vizazi vyenu vyote, kama sheria mpaka wakati usio na kipimo. 18 Katika mwezi wa kwanza, siku ya 14 ya mwezi huo, wakati wa jioni mtakula keki zisizo na chachu mpaka siku ya 21 ya mwezi wakati wa jioni.+ 19 Siku saba unga wowote uliokandwa wenye chachu usipatikane katika nyumba zenu, kwa sababu mtu yeyote anayeonja kitu kilicho na chachu, awe mkaaji mgeni au mwenyeji wa nchi,+ nafsi hiyo itakatiliwa mbali kutoka katika kusanyiko la Israeli.+ 20 Hamtakula kitu chochote kilicho na chachu. Katika makao yenu yote mtakula keki zisizo na chachu.’”

21 Papo hapo Musa akawaita wanaume wote wazee wa Israeli+ na kuwaambia: “Toeni na kujichukulia kondoo na mbuzi kulingana na familia zenu, na kuchinja mnyama wa pasaka.+ 22 Nanyi mtachukua tawi la hisopo+ na kulichovya katika damu iliyo ndani ya beseni na kuipaka sehemu ya juu ya mlango na juu ya ile miimo miwili ya mlango kwa kiasi fulani cha damu iliyo kwenye beseni; na yeyote kati yenu asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi. 23 Kisha Yehova atakapopita katikati ili kuwaletea pigo Wamisri na kuiona damu kwenye sehemu ya juu ya mlango na kwenye ile miimo miwili ya mlango, hakika Yehova atapita juu ya mlango, naye hataruhusu uharibifu uingie ndani ya nyumba zenu na kuwaletea pigo.+

24 “Nanyi mtashika jambo hili kama sharti+ kwa ajili yenu na wana wenu mpaka wakati usio na kipimo.+ 25 Na itakuwa kwamba mtakapoingia katika nchi ambayo Yehova atawapa, kama alivyosema, basi mtaendelea kuufanya utumishi huu.+ 26 Na itakuwa kwamba wana wenu watakapowaambia, ‘Utumishi huu unamaanisha nini kwenu?’+ 27 ndipo mtakaposema, ‘Ni dhabihu ya pasaka kwa Yehova,+ aliyepita juu ya nyumba za wana wa Israeli huko Misri alipowaletea Wamisri pigo, lakini akazikomboa nyumba zetu.’”

Kisha watu hao wakainama na kusujudu.+ 28 Kisha wana wa Israeli wakaenda na kufanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa na Haruni.+ Wakafanya vivyo hivyo.

29 Na ikawa kwamba katikati ya usiku Yehova akampiga kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri,+ kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao anayeketi juu ya kiti cha ufalme kufikia mzaliwa wa kwanza wa mateka aliye gerezani, na kila mzaliwa wa kwanza wa mnyama.+ 30 Kisha Farao akaamka usiku, yeye na watumishi wake wote na Wamisri wengine wote; na kukaanza kutokea kilio kikubwa kati ya Wamisri,+ kwa sababu hapakuwa na nyumba yoyote ambamo hamkuwa na mtu aliyekufa. 31 Ndipo akamwita+ Musa na Haruni mara moja wakati wa usiku na kusema: “Simameni, tokeni kati ya watu wangu, ninyi na wale wana wengine wa Israeli, na mwende, mkamtumikie Yehova, kama mlivyosema.+ 32 Chukueni makundi yenu na mifugo yenu, kama mlivyosema,+ na mwende. Pia, mnibariki mimi vilevile.”

33 Na Wamisri wakaanza kuwahimiza watu ili wawafukuze haraka+ kutoka katika nchi hiyo, “kwa sababu,” walisema, “sisi sote ni kana kwamba tumekufa!”+ 34 Basi watu wakachukua unga wao wa kukandwa kabla haujachacha, pamoja na vikandio vyao vikiwa vimefungwa katika nguo zao za kujitanda begani mwao. 35 Na wana wa Israeli wakafanya kulingana na neno la Musa, wakawaomba Wamisri vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu na nguo za kujitanda.+ 36 Naye Yehova akawapa watu hao kibali machoni pa Wamisri,+ hivi kwamba hao wakawapa walichoomba;+ nao wakawaacha Wamisri bila chochote.+

37 Na wana wa Israeli wakaondoka Ramesesi+ kuelekea Sukothi,+ kufikia hesabu ya wanaume mia sita elfu wanaotembea kwa miguu, bila kuhesabu watoto.+ 38 Na jamii kubwa iliyochangamana+ pia ikaenda pamoja nao, na makundi na mifugo vilevile, kundi la wanyama wengi sana. 39 Nao wakaanza kuoka unga uliokandwa waliokuwa wameuchukua kutoka Misri uwe keki za mviringo, keki zisizo na chachu, kwa sababu haukuwa umechacha, kwa sababu walikuwa wamefukuzwa kutoka Misri nao hawakuweza kukawia na pia hawakuwa wamejitayarishia vyakula vyovyote.+

40 Na kukaa kwa wana wa Israeli, waliokuwa wamekaa+ katika Misri,+ kulikuwa miaka 430.+ 41 Na ikawa kwamba mwishoni mwa ile miaka 430, naam, ikawa kwamba siku hiyo hiyo majeshi yote ya Yehova yakatoka katika nchi ya Misri.+ 42 Ni usiku wa kuadhimishwa kuhusiana na Yehova kwa kuwatoa katika nchi ya Misri. Kuhusiana na Yehova usiku huu ni usiku wa kuadhimishwa kwa wana wote wa Israeli katika vizazi vyao.+

43 Na Yehova akamwambia Musa na Haruni: “Hii ndiyo sheria ya pasaka:+ Hakuna mgeni yeyote atakayeila.+ 44 Lakini palipo na mtumwa yeyote aliyenunuliwa kwa pesa, utamtahiri.+ Ndipo atashiriki kuila. 45 Mhamiaji na mfanyakazi wa kukodiwa hatakula. 46 Italiwa katika nyumba moja. Hutatoa nyama yoyote nje ya nyumba hiyo na kuipeleka mahali fulani nje. Wala hamtavunja mfupa wake wowote ndani yake.+ 47 Kusanyiko lote la Israeli litaisherehekea.+ 48 Na ikiwa mkaaji mgeni anakaa pamoja nawe akiwa mgeni naye atasherehekea pasaka kwa Yehova, kila mwanamume wa kwake na atahiriwe.+ Ndipo apate kukaribia ili kuisherehekea; na awe kama mwenyeji wa nchi. Bali mwanamume yeyote ambaye hajatahiriwa asipate kuila. 49 Sheria moja itakuwapo kwa ajili ya mwenyeji na kwa ajili ya mkaaji mgeni anayekaa akiwa mgeni katikati yenu.”+

50 Basi wana wote wa Israeli wakafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa na Haruni. Walifanya vivyo hivyo.+ 51 Na ikawa siku hiyo hiyo kwamba Yehova akawatoa wana wa Israeli pamoja na majeshi+ yao kutoka katika nchi ya Misri.

13 Na Yehova akanena zaidi na Musa, na kusema: 2 “Nitakasie kila mzaliwa wa kwanza wa kiume anayefungua kila tumbo la uzazi kati ya wana wa Israeli, kati ya wanadamu na wanyama. Ni wangu.”+

3 Naye Musa akawaambia watu: “Na ikumbukwe siku hii ambayo mlitoka Misri,+ katika nyumba ya watumwa, kwa sababu kwa nguvu za mkono Yehova aliwatoa hapa.+ Basi chochote kilicho na chachu kisiliwe.+ 4 Leo mnaondoka katika mwezi wa Abibu.+ 5 Na itakuwa kwamba Yehova atakapokuwa amekuingiza katika nchi ya Wakanaani na Wahiti na Waamori na Wahivi na Wayebusi,+ ambayo aliwaapia mababu zako kuwa atakupa,+ nchi inayotiririka maziwa na asali,+ ndipo utatoa utumishi huu katika mwezi huu. 6 Siku saba utakula keki zisizo na chachu,+ na katika siku ya saba ni sherehe kwa Yehova.+ 7 Keki zisizo na chachu zitaliwa kwa siku hizo saba;+ na chochote kilicho na chachu kisionekane kwako,+ wala unga wowote uliokandwa wenye chachu usionekane kwako ndani ya mipaka yako yote.+ 8 Nawe utamwambia mwana wako siku hiyo, na kusema, ‘Ni kwa sababu ya jambo ambalo Yehova amenifanyia nilipotoka Misri.’+ 9 Nayo itatumika kwako kama ishara mkononi mwako na ukumbusho katikati ya macho yako,+ ili sheria ya Yehova iwe katika kinywa chako;+ kwa sababu kwa mkono wenye nguvu Yehova alikutoa Misri.+ 10 Nawe lazima uishike sheria hii kwa wakati wake uliowekwa mwaka baada ya mwaka.+

11 “Na itakuwa kwamba wakati Yehova anapokuingiza katika nchi ya Wakanaani,+ kama alivyokuapia wewe na mababu zako,+ na wakati anapokupa hiyo, 12 ndipo lazima umtoe kila anayefungua tumbo la uzazi kwa ajili ya Yehova,+ na kila mzaliwa wa kwanza, mtoto wa mnyama,+ ambaye atakuwa mali yako. Walio wa kiume ni wa Yehova.+ 13 Na kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa kondoo, nawe usipomkomboa, basi utaivunja shingo yake.+ Na kila mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu kati ya wana wako utamkomboa.+

14 “Na itakuwa kwamba ikiwa mwana wako atakuuliza baadaye,+ na kusema, ‘Hili linamaanisha nini?’ basi utamwambia, ‘Kwa nguvu za mkono, Yehova alitutoa Misri,+ katika nyumba ya watumwa.+ 15 Na ikawa kwamba Farao alipoonyesha ukaidi kwa kukataa kuturuhusu twende zetu,+ ndipo Yehova akamuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri,+ kuanzia mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu kufikia mzaliwa wa kwanza wa mnyama.+ Ndiyo sababu mimi ninamtolea Yehova dhabihu wote wa kiume wanaofungua tumbo la uzazi,+ na kila mzaliwa wa kwanza wa wanangu ninamkomboa.’+ 16 Nayo itatumika kuwa ishara mkononi mwako na utepe wa kipaji katikati ya macho yako,+ kwa sababu kwa nguvu za mkono Yehova alitutoa Misri.”+

17 Na ikawa kwamba wakati Farao alipowaruhusu watu waende zao, Mungu hakuwaongoza kupitia njia ya nchi ya Wafilisti kwa kuwa tu ilikuwa karibu, kwa maana Mungu alisema: “Huenda hao watu watajuta watakapoona vita nao hakika watarudi Misri.”+ 18 Basi Mungu akawafanya watu wazunguke kupitia njia ya nyika ya Bahari Nyekundu.+ Hata hivyo wana wa Israeli walitoka nchini Misri wakiwa wamejipanga kivita.+ 19 Na Musa akaichukua mifupa ya Yosefu pamoja naye, kwa sababu alikuwa amewafanya wana wa Israeli waape rasmi, na kusema: “Bila shaka Mungu atawaelekezea ninyi fikira,+ nanyi lazima mwichukue mifupa yangu kutoka hapa pamoja nanyi.”+ 20 Nao wakaondoka Sukothi na kupiga kambi katika Ethamu ukingoni mwa nyika.+

21 Naye Yehova alikuwa akienda mbele yao wakati wa mchana katika nguzo ya wingu ili kuwaongoza njiani,+ na wakati wa usiku katika nguzo ya moto ili kuwapa nuru ya kwenda wakati wa mchana na wakati wa usiku.+ 22 Ile nguzo ya wingu haikuondoka mbele ya watu wakati wa mchana wala ile nguzo ya moto wakati wa usiku.+

14 Sasa Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, kwamba warudi na kupiga kambi mbele ya Pihahirothi katikati ya Migdoli na bahari, kukabili Baal-sefoni.+ Mbele yake mtapiga kambi kando ya bahari. 3 Kisha Farao hakika atasema kuhusu wana wa Israeli, ‘Wanatanga-tanga nchini kwa kuvurugika. Nyika imewazingira.’+ 4 Kwa hiyo, kwa kweli nitauacha moyo wa Farao uwe mkaidi,+ naye hakika atawafuatilia wao nami nitajipatia utukufu kupitia kwa Farao na majeshi yake yote;+ nao Wamisri watajua hakika kwamba mimi ni Yehova.”+ Basi wakafanya vivyo hivyo.

5 Baadaye mfalme wa Misri akaambiwa kwamba watu walikuwa wamekimbia na kwenda zao. Mara moja moyo wa Farao na watu wake vilevile ukabadilika kuhusiana na watu,+ kwa hiyo wakasema: “Tumefanya nini, kwa kuwaruhusu Waisraeli waende zao, waache kuwa watumwa+ wetu?” 6 Kwa hiyo akatayarisha magari yake ya vita, na kuwachukua watu wake pamoja naye.+ 7 Naye akachukua magari mia sita yaliyochaguliwa+ na yale magari mengine yote ya Misri na mashujaa wa vita juu ya kila moja la magari hayo. 8 Basi Yehova akauacha moyo wa Farao mfalme wa Misri uwe mkaidi,+ naye akawafuatilia wana wa Israeli, huku wana wa Israeli wakienda kwa mkono ulioinuliwa.+ 9 Nao Wamisri wakawafuatilia, na farasi wote wa magari wa Farao na askari wake wapanda-farasi+ na majeshi yake wakawafikia walipokuwa wamepiga kambi kando ya bahari, karibu na Pihahirothi, kukabili Baal-sefoni.+

10 Farao alipokaribia, wana wa Israeli wakaanza kuinua macho yao, na tazama, Wamisri walikuwa wakipiga mwendo wakiwafuatilia; na wana wa Israeli wakaogopa sana na kuanza kumlilia Yehova.+ 11 Nao wakamwambia Musa: “Je, ni kwa sababu hakuna makaburi yoyote huko Misri ndiyo sababu umetuleta hapa ili tufie nyikani?+ Ni nini hiki ambacho umetutendea kwa kutuongoza kutoka Misri? 12 Je, hili silo neno tulilokuambia huko Misri, tukisema, ‘Tuache, tuwatumikie Wamisri’? Kwa maana ni afadhali kwetu tuwatumikie Wamisri kuliko kufa nyikani.”+ 13 Kisha Musa akawaambia watu: “Msiogope.+ Simameni imara muuone wokovu wa Yehova, atakaowafanyia ninyi leo.+ Kwa maana Wamisri mnaowaona leo hamtawaona tena, hasha, hamtawaona tena kamwe.+ 14 Yehova mwenyewe atawapigania ninyi,+ nanyi wenyewe mtakaa kimya.”

15 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Kwa nini unaendelea kunililia?+ Waambie wana wa Israeli kwamba wanapaswa kuvunja kambi. 16 Wewe nawe, inua fimbo+ yako na kuunyoosha mkono wako juu ya bahari, uitenganishe,+ ili wana wa Israeli wapate kupita katikati ya bahari juu ya nchi kavu.+ 17 Mimi nami, tazama, nitaiacha mioyo ya Wamisri iwe mikaidi,+ ili waingie kuwafuatilia wao nami nijipatie utukufu kupitia kwa Farao na majeshi yake yote, magari yake ya vita na askari wake wapanda-farasi.+ 18 Na Wamisri hakika watajua kwamba mimi ni Yehova nitakapojipatia utukufu kupitia kwa Farao, magari yake ya vita na askari wake wapanda-farasi.”+

19 Ndipo malaika+ wa Mungu wa kweli aliyekuwa akienda mbele ya kambi ya Israeli akaondoka na kwenda nyuma, nayo nguzo ya wingu ikaondoka mbele yao na kusimama nyuma yao.+ 20 Kwa hiyo ikaingia katikati ya kambi ya Wamisri na kambi ya Israeli.+ Kwa upande mmoja ikawa wingu pamoja na giza. Kwa upande ule mwingine ikawa ikiuangaza usiku.+ Nacho kikundi hiki hakikukaribia kikundi kile usiku kucha.

21 Sasa Musa akanyoosha mkono wake juu ya bahari;+ naye Yehova akaanza kuifanya bahari irudi nyuma kwa upepo wenye nguvu wa mashariki usiku kucha na kuligeuza bonde la bahari liwe nchi kavu,+ nayo maji yalikuwa yakitenganishwa.+ 22 Mwishowe wana wa Israeli wakapita katikati ya bahari juu ya nchi kavu,+ huku maji yakiwa ukuta kwao mkono wao wa kuume na wa kushoto.+ 23 Na Wamisri wakaanza kufuatilia, nao farasi wote wa Farao, magari yake ya vita na askari wake wapanda-farasi wakaanza kuingia baada yao,+ kuingia katikati ya bahari. 24 Na ikawa kwamba wakati wa kesha la kuamkia asubuhi, Yehova akaanza kuiangalia kambi ya Wamisri kutoka ndani ya nguzo ya moto na wingu,+ naye akaivuruga+ kambi ya Wamisri. 25 Naye akawa akiyaondoa magurudumu kutoka kwenye magari yao hivi kwamba wakawa wakiyaendesha kwa shida;+ nao Wamisri wakaanza kusema: “Na tukimbie tusikaribie Israeli hata kidogo, kwa sababu hakika Yehova anawapigania dhidi ya Wamisri.”+

26 Mwishowe Yehova akamwambia Musa: “Unyooshe mkono wako juu ya bahari,+ ili maji yarudi juu ya Wamisri, magari yao ya vita na askari wao wapanda-farasi.” 27 Mara moja Musa akaunyoosha mkono wake juu ya bahari, nayo bahari ikaanza kurudia hali yake ya kawaida asubuhi ikikaribia. Wakati wote huo Wamisri walikuwa wakikimbia wasikutane nayo, lakini Yehova akawakung’uta Wamisri katikati ya bahari.+ 28 Nayo maji yakaendelea kurudi.+ Mwishowe yakafunika magari ya vita na askari wapanda-farasi wa majeshi yote ya Farao na ambao walikuwa wameingia baharini kuwafuatilia.+ Hakuna hata mmoja kati yao aliyebaki.+

29 Nao wana wa Israeli, walitembea juu ya nchi kavu katikati ya sakafu ya bahari,+ nayo maji yalikuwa kwao ukuta mkono wao wa kuume na wa kushoto.+ 30 Basi siku hiyo Yehova akaokoa Israeli kutoka kwa mkono wa Wamisri,+ na Israeli wakawaona Wamisri wakiwa wamekufa kando ya bahari.+ 31 Israeli wakauona pia ule mkono mkuu ambao Yehova aliufanya utende juu ya Wamisri; nao watu wakaanza kumwogopa Yehova na kuwa na imani katika Yehova na katika Musa mtumishi wake.+

15 Wakati huo Musa na wana wa Israeli wakaanza kumwimbia Yehova wimbo huu na kusema yafuatayo:+

“Acheni nimwimbie Yehova, kwa maana ametukuzwa sana.+

Farasi na mpandaji wake amewatupa baharini.+

 2 Nguvu zangu na uwezo wangu ni Yah,+ kwa maana yeye ndiye wokovu wangu.+

Huyu ndiye Mungu wangu, nami nitamsifu;+ Mungu wa baba yangu,+ nami nitamwinua juu.+

3 Yehova ni mtu wa vita+ anayetenda kiume. Yehova ndilo jina lake.+

 4 Ametupa magari ya Farao na majeshi yake baharini.+

Na mashujaa wake wa vita walio bora wamezamishwa katika Bahari Nyekundu.+

 5 Maji yenye kututumuka yaliwafunika;+ wakashuka ndani ya vilindi kama jiwe.+

 6 Mkono wako wa kuume, Ee Yehova, unajionyesha kuwa wenye nguvu katika uwezo,+

Mkono wako wa kuume, Ee Yehova, unaweza kumvunja-vunja adui.+

7 Na katika wingi wa ukuu wako wewe unaweza kuwatupa chini wale wanaosimama juu yako;+

Wewe unaituma hasira yako inayowaka, nayo inawateketeza kama majani makavu.+

 8 Na kwa pumzi kutoka katika mianzi ya pua+ yako maji yalirundamana;

Yalisimama tuli kama bwawa la mafuriko;

Maji yenye kututumuka yaligandamana katika moyo wa bahari.

 9 Adui alisema, ‘Nitafuatilia!+ Nitafikia!+

Nitagawa nyara!+ Nafsi yangu itajawa nazo!

Nitauchomoa upanga wangu! Mkono wangu utawafukuzia mbali!’+

10 Ulipuliza kwa pumzi yako,+ bahari ikawafunika;+

Walizama kama risasi katika maji makuu.+

11 Ni nani kati ya miungu aliye kama wewe, Ee Yehova?+

Ni nani aliye kama wewe, unayejionyesha kuwa mwenye nguvu katika utakatifu?+

Unayestahili kuogopwa+ kwa nyimbo za sifa,+ Unayefanya mambo ya ajabu.+

12 Uliunyoosha mkono wako wa kuume,+ nayo dunia ikawameza.+

13 Wewe katika fadhili zako zenye upendo umewaongoza watu ambao umewakomboa;+

Wewe katika nguvu zako hakika utawaongoza mpaka kwenye makao yako matakatifu.+

14 Vikundi vya watu vitasikia,+ vitafadhaika;+

Uchungu wa kuzaa+ utawashika wakaaji wa Ufilisti.

15 Wakati huo mashehe wa Edomu kwa kweli watasumbuka;

Nao wadhalimu wa Moabu, kutetemeka kutawashika.+

Wakaaji wote wa Kanaani kwa kweli watavunjika moyo.+

16 Woga na hofu zitaanguka juu yao.+

Kwa sababu ya ukuu wa mkono wako watatulia kama jiwe,

Mpaka watu wako+ wapite, Ee Yehova,

Mpaka watu ambao umewatokeza+ wapite.+

17 Utawaleta na kuwapanda katika mlima wa urithi wako,+

Mahali palipofanywa imara ambapo umetayarisha ili ukae,+ Ee Yehova,

Patakatifu,+ Ee Yehova, ambapo mikono yako imepafanya imara.

18 Yehova atatawala akiwa mfalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+

19 Farasi wa Farao+ pamoja na magari yake ya vita na askari wake wapanda-farasi walipoingia baharini,+

Ndipo Yehova alipoyarudisha maji ya bahari juu yao,+

Huku wana wa Israeli wakitembea juu ya nchi kavu katikati ya bahari.”+

20 Naye Miriamu nabii, dada ya Haruni,+ akachukua tari mkononi mwake;+ na wanawake wote wakaanza kutoka pamoja naye wakiwa na matari na kucheza dansi.+ 21 Naye Miriamu akawa akiwaitikia wanaume:+

“Mwimbieni Yehova,+ kwa maana ametukuzwa sana.+

Farasi na mpandaji wake amewatupa baharini.”+

22 Baadaye Musa akaondoa Israeli kutoka katika Bahari Nyekundu nao wakaenda katika nyika ya Shuri+ na kupiga mwendo kwa siku tatu nyikani, lakini hawakupata maji.+ 23 Mwishowe wakafika Mara,+ lakini hawakuweza kunywa maji ya Mara kwa sababu yalikuwa machungu. Ndiyo sababu alipaita jina Mara.+ 24 Nao watu wakaanza kunung’unika juu ya Musa,+ na kusema: “Tutakunywa nini?” 25 Kisha yeye akamlilia Yehova.+ Basi Yehova akamwelekeza kwenye mti fulani, naye akautupa ndani ya maji nayo maji yakawa matamu.+

Hapo Yeye akawawekea sharti na kesi ya kuhukumia na hapo akawatia katika jaribu.+ 26 Naye akasema: “Ikiwa utaisikiliza kwa makini sauti ya Yehova Mungu wako na kufanya lililo sawa machoni pake na kutega sikio usikie amri zake na kushika masharti yake yote,+ sitaweka juu yako yoyote ya magonjwa yale niliyoweka juu ya Wamisri;+ kwa sababu mimi ni Yehova anayekuponya.”+

27 Baada ya hapo wakafika Elimu, ambapo palikuwa na mabubujiko 12 ya maji na mitende 70.+ Basi wakapiga kambi hapo kando ya maji hayo.

16 Baadaye wakaondoka Elimu,+ nalo kusanyiko zima la wana wa Israeli mwishowe likafika katika nyika ya Sini,+ iliyo katikati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili baada ya kutoka kwao katika nchi ya Misri.

2 Nalo kusanyiko zima la wana wa Israeli likaanza kunung’unika juu ya Musa na Haruni huko nyikani.+ 3 Na wana wa Israeli wakawa wakiwaambia: “Laiti tungekufa+ kwa mkono wa Yehova katika nchi ya Misri tulipokuwa tukiketi kando ya vyungu vya nyama,+ tulipokuwa tukila mkate na kushiba, kwa sababu ninyi mmetutoa na kutuleta nyikani ili kuliua kutaniko lote kwa njaa.”+

4 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Tazama, nitawanyeshea mkate kutoka mbinguni;+ nao watu watatoka nje na kuokota kila mtu kiasi chake siku baada ya siku,+ ili nipate kuwajaribu iwapo watatembea katika sheria yangu au hapana.+ 5 Na itakuwa kwamba katika siku ya sita+ watatayarisha kile watakacholeta ndani, nacho kitakuwa mara mbili ya kile ambacho wao huokota siku baada ya siku.”+

6 Kwa hiyo Musa na Haruni wakawaambia wana wote wa Israeli: “Wakati wa jioni hakika mtajua kwamba Yehova ndiye aliyewatoa ninyi katika nchi ya Misri.+ 7 Na asubuhi kwa kweli mtauona utukufu wa Yehova,+ kwa sababu amesikia manung’uniko yenu juu ya Yehova. Na sisi ni nani hivi kwamba mnung’unike juu yetu?” 8 Naye Musa akaendelea kusema: “Itakuwa hivyo wakati ambapo Yehova atawapa jioni nyama ya kula na asubuhi mkate wa kuwashibisha, kwa sababu Yehova amesikia manung’uniko yenu mnayonung’unika juu yake. Na sisi ni nani? Manung’uniko yenu si juu yetu, bali ni juu ya Yehova.”+

9 Naye Musa akamwambia Haruni: “Liambie kusanyiko zima la wana wa Israeli, ‘Njooni karibu mbele za Yehova, kwa sababu ameyasikia manung’uniko yenu.’”+ 10 Kisha ikawa kwamba mara tu baada ya Haruni kusema na kusanyiko zima la wana wa Israeli, wakageuka na kutazama kuelekea nyikani, na, tazama! utukufu wa Yehova ukaonekana katika wingu.+

11 Naye Yehova akazidi kunena na Musa, na kusema: 12 “Nimeyasikia manung’uniko ya wana wa Israeli.+ Sema nao, na kuwaambia, ‘Katikati ya zile jioni mbili mtakula nyama na asubuhi mtashiba mkate;+ nanyi hakika mtajua kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+

13 Basi ikawa kwamba wakati wa jioni kware+ wakaanza kuja na kuifunika kambi, na asubuhi kulikuwa kumetokea utando wa umande kuizunguka kambi.+ 14 Baada ya muda ule utando wa umande ukawa mvuke, na tazama, juu ya uso wa nyika kulikuwa na kitu laini chenye chembechembe,+ laini kama sakitu+ juu ya dunia. 15 Wana wa Israeli walipokiona, wakaanza kusemezana: “Ni nini hiki?” Kwa maana hawakujua kilikuwa nini. Basi Musa akawaambia: “Ni mkate ambao Yehova amewapa ninyi uwe chakula.+ 16 Hili ndilo neno ambalo Yehova ameamuru, ‘Okoteni kiasi chake, kila mmoja kulingana na kiasi anachoweza kula. Mtachukua kipimo cha omeri+ kwa ajili ya kila mtu kulingana na hesabu ya nafsi ambazo kila mmoja wenu anazo katika hema lake.’” 17 Nao wana wa Israeli wakaanza kufanya hivyo; nao wakakiokota, baadhi yao wakakusanya kingi na wengine wakakusanya kichache. 18 Walipokipima kwa omeri, yule aliyekusanya kingi hakuwa na ziada na yule aliyekusanya kichache hakuwa na upungufu.+ Walikiokota kila mmoja kulingana na kiasi anachoweza kula.

19 Kisha Musa akawaambia: “Mtu yeyote asiache chochote mpaka asubuhi.”+ 20 Lakini hawakumsikiliza Musa. Wakati ambapo watu fulani waliacha kiasi fulani mpaka asubuhi, kilitokeza wadudu na kunuka;+ hivi kwamba Musa aliwakasirikia.+ 21 Nao wakawa wakikiokota asubuhi baada ya asubuhi,+ kila mmoja kulingana na alichoweza kula. Jua lilipokuwa kali, kiliyeyuka.

22 Na ikawa kwamba katika siku ya sita waliokota mara mbili ya kiasi cha mkate,+ vipimo viwili vya omeri kwa kila mtu. Kwa hiyo wakuu wote wa kusanyiko wakaja na kumjulisha Musa. 23 Basi akawaambia: “Ndivyo Yehova amesema. Kesho kutakuwa na kushika sabato, sabato takatifu kwa Yehova.+ Mnachoweza kuoka, okeni, na mnachoweza kutokosa, tokoseni,+ na ziada yote iliyopo jiwekeeni akiba kiwe kitu cha kuwekwa mpaka asubuhi.” 24 Basi wakakiweka akiba mpaka asubuhi, kama vile Musa alivyokuwa ameamuru; nacho hakikunuka wala funza hawakutokea ndani yake.+ 25 Kisha Musa akasema: “Kuleni hiki leo, kwa sababu leo ni sabato+ kwa Yehova. Leo hamtakipata uwanjani. 26 Siku sita mtakiokota, lakini siku ya saba ni sabato.+ Siku hiyo hakuna chochote kitakachofanyizwa.” 27 Hata hivyo, ikawa kwamba katika siku ya saba baadhi ya watu walitoka nje kwenda kukiokota, lakini hawakupata chochote.

28 Basi Yehova akamwambia Musa: “Ninyi watu mtaendelea kukataa kushika amri zangu na sheria zangu mpaka wakati gani?+ 29 Kumbukeni kwamba Yehova amewapa ninyi sabato.+ Ndiyo sababu anawapa siku ya sita mkate wa siku mbili. Endeleeni kukaa kila mmoja mahali pake.+ Mtu yeyote asitoke mahali pake siku ya saba.” 30 Na watu wakaishika sabato siku ya saba.+

31 Na nyumba ya Israeli ikaanza kukiita jina lake “mana.” Nacho kilikuwa cheupe kama mbegu za mgiligilani, na ladha yake ilikuwa kama ya keki bapa zenye asali.+ 32 Kisha Musa akasema: “Hili ndilo neno ambalo Yehova ameamuru, ‘Kijazeni kwenye kipimo cha omeri kiwe kitu cha kuwekwa katika vizazi vyenu vyote,+ ili wapate kuona mkate niliowalisha ninyi nyikani nilipokuwa nikiwatoa katika nchi ya Misri.’”+ 33 Kwa hiyo Musa akamwambia Haruni: “Chukua mtungi, uweke omeri moja kamili ya mana na kuiweka mbele za Yehova iwe kitu cha kuwekwa katika vizazi vyenu vyote.”+ 34 Sawasawa na vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa, Haruni akaiweka mbele ya ule Ushuhuda+ iwe kitu cha kuwekwa. 35 Nao wana wa Israeli wakala mana miaka 40,+ mpaka walipofika katika nchi inayokaliwa.+ Walikula mana mpaka walipofika mpakani mwa nchi ya Kanaani.+ 36 Omeri ni sehemu ya kumi ya kipimo cha efa.

17 Nalo kusanyiko lote la wana wa Israeli likaondoka katika nyika ya Sini+ hatua kwa hatua, kulingana na agizo la Yehova,+ nao wakapiga kambi katika Refidimu.+ Lakini hapakuwa na maji ya kunywa kwa ajili ya watu.

2 Na watu wakaanza kugombana na Musa na kusema:+ “Tupe maji tunywe.” Lakini Musa akawaambia: “Kwa nini mnagombana na mimi? Kwa nini mnaendelea kumjaribu Yehova?”+ 3 Na watu wakaendelea kuwa na kiu ya maji wakiwa huko, na watu wakaendelea kunung’unika juu ya Musa na kusema: “Kwa nini umetutoa Misri ili kutuua kwa kiu sisi na wana wetu na mifugo yetu?”+ 4 Mwishowe Musa akamlilia Yehova, na kusema: “Nitafanya nini na watu hawa? Bado muda kidogo nao watanipiga kwa mawe!”+

5 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Pita mbele ya watu+ na uchukue pamoja nawe baadhi ya wanaume wazee wa Israeli na fimbo yako ambayo uliitumia kupiga maji ya Mto Nile.+ Ichukue mkononi mwako nawe uendelee kutembea. 6 Tazama! Nitasimama mbele yako juu ya mwamba huko Horebu. Nawe utaupiga mwamba huo, na maji yatatoka ndani yake, na watu watayanywa.”+ Kisha Musa akafanya hivyo machoni pa wanaume wazee wa Israeli. 7 Basi akapaita mahali hapo jina Masa+ na Meriba,+ kwa sababu ya kugombana kwa wana wa Israeli na kwa sababu ya kumjaribu Yehova,+ na kusema: “Je, Yehova yuko katikati yetu au hapana?”+

8 Nao Waamaleki+ wakaja na kupigana na Israeli huko Refidimu.+ 9 Ndipo Musa akamwambia Yoshua:+ “Tuchagulie wanaume, nawe uende+ ukapigane na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilima, nikiwa na fimbo ya Mungu wa kweli mkononi mwangu.”+ 10 Kisha Yoshua akafanya kama vile Musa alivyokuwa amemwambia,+ ili kupigana na Waamaleki; na Musa, Haruni na Huru+ wakapanda mpaka juu ya kilima.

11 Na ikawa kwamba mara tu Musa alipoinua mkono wake juu, Waisraeli wakawa na nguvu zaidi;+ lakini mara tu alipoushusha mkono wake, Waamaleki wakawa na nguvu zaidi. 12 Mikono ya Musa ilipokuwa mizito, walichukua jiwe wakaliweka chini yake, naye akalikalia; naye Haruni na Huru wakaitegemeza mikono yake, mmoja upande huu na yule mwingine upande ule, hivi kwamba mikono yake ikawa imara mpaka jua lilipotua. 13 Basi Yoshua akawashinda kabisa Amaleki na watu wake kwa makali ya upanga.+

14 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Andika hili katika kitabu+ liwe ukumbusho na uliseme masikioni mwa Yoshua, ‘Nitafutilia mbali kabisa ukumbusho wa Amaleki toka chini ya mbingu.’”+ 15 Naye Musa akajenga madhabahu na kuiita jina Yehova-nisi, 16 na kusema: “Kwa sababu kuna mkono dhidi ya kiti cha ufalme+ cha Yah,+ Yehova atakuwa na vita na Amaleki kizazi baada ya kizazi.”+

18 Sasa Yethro kuhani wa Midiani, baba-mkwe wa Musa,+ akasikia mambo yote ambayo Mungu alikuwa ameyafanya kwa ajili ya Musa na kwa ajili ya Israeli watu wake, jinsi Yehova alivyokuwa amewatoa Israeli kutoka Misri.+ 2 Basi Yethro, baba-mkwe wa Musa, akamchukua Sipora, mke wa Musa, baada ya kuachwa aende zake, 3 na wanawe wawili,+ ambao jina la mmoja wao lilikuwa Gershomu,+ “kwa sababu,” akasema, “nimekuwa mkaaji mgeni katika nchi ya kigeni”; 4 nalo jina la yule mwingine lilikuwa Eliezeri,+ “kwa sababu,” kama alivyosema, “Mungu wa baba yangu ni msaidizi wangu kwa kuwa alinikomboa kutokana na upanga wa Farao.”+

5 Basi Yethro, baba-mkwe wa Musa, pamoja na wanawe na mke wake wakamjia Musa huko nyikani ambako alikuwa amepiga kambi, kwenye mlima wa Mungu wa kweli.+ 6 Kisha akatuma neno kwa Musa: “Mimi, baba-mkwe wako, Yethro,+ nimekuja kwako, na pia mke wako na wanawe wawili pamoja naye.” 7 Mara moja Musa akatoka kwenda kumpokea baba-mkwe wake, naye akajilaza kifudifudi mbele yake na kumbusu;+ na kila mmoja wao akaanza kuuliza jinsi yule mwingine alivyokuwa akiendelea. Kisha wakaingia hemani.

8 Naye Musa akaanza kumsimulia baba-mkwe wake yote ambayo Yehova alikuwa amemtendea Farao na Misri kwa sababu ya Israeli,+ na magumu yote yaliyokuwa yamewapata njiani,+ na bado Yehova alikuwa akiwakomboa.+ 9 Kisha Yethro akawa na furaha kwa sababu ya mema yote ambayo Yehova alikuwa ametenda kwa ajili ya Israeli kwa kuwa alikuwa amewakomboa kutoka katika mkono wa Misri.+ 10 Basi Yethro akasema: “Na abarikiwe Yehova, ambaye amewakomboa kutoka katika mkono wa Misri na kutoka katika mkono wa Farao, na ambaye amewakomboa watu kutoka katika mkono wa Misri.+ 11 Sasa najua kwamba Yehova ni mkuu kuliko miungu+ mingine yote kwa sababu ya jambo hili walilotenda kwa kimbelembele dhidi yao.” 12 Kisha Yethro, baba-mkwe wa Musa, akachukua toleo la kuteketezwa na dhabihu kwa ajili ya Mungu;+ naye Haruni na wanaume wote wazee wa Israeli wakaja kula mkate pamoja na baba-mkwe wa Musa, mbele za Mungu wa kweli.+

13 Na ikawa kwamba siku iliyofuata, Musa akaketi chini kama kawaida ili ahukumu watu,+ nao watu wakasimama mbele ya Musa tangu asubuhi mpaka jioni. 14 Naye baba-mkwe wa Musa akaona yote aliyokuwa akiyatenda kwa ajili ya watu. Basi akasema: “Ni shughuli ya aina gani hii unayotenda kwa ajili ya watu? Kwa nini ni wewe peke yako unayeendelea kuketi, na watu wote wanaendelea kusimama mbele yako tangu asubuhi mpaka jioni?” 15 Ndipo Musa akamwambia baba-mkwe wake: “Kwa sababu watu huendelea kunijia ili kuuliza habari kutoka kwa Mungu.+ 16 Ikitokea kwamba wana kesi ambayo imezuka,+ hiyo lazima ije kwangu, nami lazima niamue kati ya upande mmoja na ule mwingine, nami lazima nijulishe maamuzi ya Mungu wa kweli na sheria zake.”+

17 Ndipo baba-mkwe wa Musa akamwambia: “Si vema jinsi unavyofanya. 18 Utachoka, wewe na watu hawa walio pamoja nawe, kwa sababu shughuli hii ni mzigo mkubwa mno kwako.+ Wewe huwezi kuifanya peke yako.+ 19 Sasa sikiliza sauti yangu.+ Nitakushauri, na Mungu atakuwa pamoja nawe.+ Wewe mwenyewe uwe mwakilishi kwa ajili ya watu mbele za Mungu wa kweli,+ na wewe mwenyewe utaleta kesi hizo mbele za Mungu wa kweli.+ 20 Nawe utawaonya juu ya masharti na sheria,+ nawe utawajulisha njia wanayopaswa kuitembea na kazi wanayopaswa kuifanya.+ 21 Lakini wewe mwenyewe unapaswa kuchagua kutoka kati ya watu wote wanaume wenye uwezo,+ wanaomwogopa Mungu,+ wanaume wenye kutegemeka,+ wanaochukia faida isiyo ya haki;+ na lazima uwaweke hao juu yao wawe wakuu juu ya maelfu,+ wakuu juu ya mamia, wakuu juu ya 50, na wakuu juu ya makumi.+ 22 Nao watawahukumu watu kwenye kila pindi inayofaa; na itakuwa kwamba kila kesi kubwa watakuletea wewe,+ lakini kila kesi ndogo wao wenyewe wataishughulikia wakiwa waamuzi. Kwa hiyo jirahisishie mambo, nao wataubeba mzigo pamoja nawe.+ 23 Ukifanya jambo hilo hasa, naye Mungu amekuamuru, hapo ndipo hakika utakapoweza kulistahimili na, zaidi ya hilo, watu hawa wataenda mahali pao wenyewe kwa amani.”+

24 Musa akaisikiliza sauti ya baba-mkwe wake mara moja na kufanya yote aliyokuwa amesema.+ 25 Naye Musa akachagua wanaume wenye uwezo kutoka Israeli lote na kuwapa vyeo vya kuwa vichwa juu ya watu,+ kuwa wakuu wa maelfu, wakuu wa mamia, wakuu wa 50 na wakuu wa makumi. 26 Nao wakawahukumu watu katika kila pindi inayofaa. Kesi ngumu walikuwa wakimletea Musa,+ lakini kila kesi ndogo wao wenyewe waliishughulikia wakiwa waamuzi. 27 Kisha Musa akamsindikiza baba-mkwe wake,+ naye akaenda zake kwenye nchi yake.

19 Katika mwezi wa tatu baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri,+ siku hiyo hiyo, wakaingia katika nyika ya Sinai.+ 2 Nao wakaanza safari kutoka Refidimu,+ wakaingia katika nyika ya Sinai, wakapiga kambi nyikani;+ nao Israeli wakapiga kambi hapo mbele ya mlima.+

3 Naye Musa akapanda kwenda kwa Mungu wa kweli, na Yehova akaanza kumwita toka mlimani,+ na kusema: “Hivi ndivyo utakavyoiambia nyumba ya Yakobo na kuwaambia wana wa Israeli, 4 ‘Ninyi wenyewe mmeona niliyowatendea Wamisri,+ ili nipate kuwachukua ninyi juu ya mabawa ya tai na kuwaleta kwangu.+ 5 Na sasa ikiwa mtaitii+ sauti yangu kabisa na kulishika kwa kweli agano+ langu, ndipo hakika mtakapokuwa mali yangu ya pekee kutoka kati ya vikundi vingine vyote vya watu,+ kwa sababu dunia nzima ni yangu.+ 6 Na ninyi wenyewe mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’+ Hayo ndiyo maneno utakayowaambia wana wa Israeli.”

7 Basi Musa akaja na kuwaita wanaume wote wazee+ kati ya watu na kuweka mbele yao maneno hayo yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru.+ 8 Kisha watu wote wakajibu kwa pamoja na kusema: “Yote ambayo Yehova amesema tuko tayari kuyafanya.”+ Mara moja Musa akarudi na kumwambia Yehova maneno ya watu.+ 9 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Tazama! Nitakujia katika wingu lenye giza,+ ili watu wapate kusikia ninaposema nawe,+ ili wapate kukuamini wewe pia mpaka wakati usio na kipimo.”+ Kisha Musa akamwambia Yehova maneno ya watu.

10 Na Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Nenda kwa watu, ukawatakase leo na kesho, nao wafue nguo zao za kujitanda.+ 11 Na wawe tayari kwa ajili ya siku ya tatu, kwa sababu katika siku ya tatu Yehova atashuka chini mbele ya macho ya watu wote juu ya Mlima Sinai.+ 12 Nawe uwawekee watu mipaka pande zote, na kusema, ‘Jihadharini juu ya kupanda mlimani, wala msiguse ukingo wake. Mtu yeyote atakayeugusa mlima hakika atauawa.+ 13 Mkono wowote usimguse, kwa maana lazima atapigwa kwa mawe au kwa mshale. Iwe ni mnyama au mwanadamu, hataishi.’+ Pembe ya kondoo+ itakapopigwa wao wenyewe wanaweza kuja mpaka kwenye mlima.”

14 Kisha Musa akateremka kutoka mlimani, akawaendea watu, naye akaanza kuwatakasa watu; nao wakaanza kufua nguo zao za kujitanda.+ 15 Kwa hiyo akawaambia watu: “Jitayarisheni+ siku hizi tatu. Ninyi wanaume msimkaribie mwanamke.”+

16 Na katika siku ya tatu kulipokuwa asubuhi, mingurumo na umeme zikaanza kutokea,+ na wingu zito+ juu ya mlima na sauti kubwa sana ya pembe,+ hivi kwamba watu wote waliokuwa kambini wakaanza kutetemeka.+ 17 Basi Musa akawatoa watu nje ya kambi ili wakutane na Mungu wa kweli, nao wakasimama kwenye sehemu ya chini ya mlima.+ 18 Nao Mlima Sinai ukatoa moshi kila mahali,+ kwa kuwa Yehova alikuwa ameshuka juu yake katika moto;+ na moshi wake ukawa ukipaa kama moshi wa tanuru,+ na mlima wote ulikuwa ukitetemeka sana.+ 19 Sauti ya pembe ilipozidi kuwa kubwa, Musa akaanza kusema, naye Mungu wa kweli akaanza kumjibu kwa sauti.+

20 Basi Yehova akashuka chini kwenye Mlima Sinai, juu ya kilele cha mlima. Kisha Yehova akamwita Musa aje kwenye kilele cha mlima, naye Musa akaenda juu.+ 21 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Shuka, uwaonye watu, wasijaribu kupenya kwa Yehova ili kumwona na wengi wao walazimike kuanguka.+ 22 Nao makuhani pia ambao humkaribia Yehova kwa ukawaida wajitakase,+ ili Yehova asilipuke juu yao.”+ 23 Ndipo Musa akamwambia Yehova: “Watu hawawezi kuja kwenye Mlima Sinai, kwa sababu wewe mwenyewe tayari ulituonya, na kusema, ‘Wekeni mipaka kwa ajili ya mlima na kuufanya kuwa mtakatifu.’”+ 24 Hata hivyo, Yehova akamwambia: “Nenda, teremka, nawe uje juu, wewe na Haruni pamoja nawe; bali usiache makuhani na watu wapenye na kuja kwa Yehova, ili asije akalipuka juu yao.”+ 25 Basi Musa akateremka kwa watu na kuwaambia.+

20 Na Mungu akaanza kunena maneno haya yote, na kusema:+

2 “Mimi ni Yehova Mungu wako,+ ambaye nimekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya watumwa.+ 3 Usiwe na miungu mingine+ yoyote dhidi ya uso wangu.

4 “Usijifanyie sanamu ya kuchongwa wala umbo lililo kama kitu chochote kilicho juu mbinguni wala kilicho chini duniani wala kilicho ndani ya maji chini ya dunia.+ 5 Usiviinamie wala kushawishiwa kuvitumikia,+ kwa sababu mimi Yehova Mungu wako ni Mungu anayetaka watu wajitoe kikamili,+ na ambaye huleta adhabu juu ya wana kwa sababu ya kosa la akina baba, juu ya kizazi cha tatu na juu ya kizazi cha nne, kwa wale wanaonichukia;+ 6 lakini huonyesha fadhili zenye upendo kuelekea kizazi cha elfu kwa wale wanaonipenda na kuzishika amri zangu.+

7 “Usilitumie jina la Yehova Mungu wako kwa njia isiyofaa,+ kwa maana Yehova hatamwacha bila kuadhibiwa yule anayelitumia jina lake kwa njia isiyofaa.+

8 “Kwa kuikumbuka siku ya sabato ili kuiona kuwa takatifu,+ 9 utafanya utumishi nawe uifanye kazi yako yote kwa siku sita.+ 10 Lakini siku ya saba ni sabato kwa Yehova Mungu wako.+ Usifanye kazi yoyote, wewe wala mwana wako wala binti yako, mtumwa wako wala kijakazi wako wala mnyama wako wa kufugwa wala mgeni wako aliye ndani ya malango yako.+ 11 Kwa maana katika siku sita Yehova alizifanya mbingu na dunia, bahari na kila kilichomo,+ naye akaanza kupumzika siku ya saba.+ Ndiyo sababu Yehova aliibariki siku ya sabato na kuifanya kuwa takatifu.+

12 “Mheshimu baba yako na mama yako+ ili siku zako zipate kuwa ndefu juu ya nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe.+

13 “Usiue.+

14 “Usifanye uzinzi.+

15 “Usiibe.+

16 “Usishuhudie kwa uwongo ukiwa shahidi dhidi ya mwenzako.+

17 “Usiitamani nyumba ya mwenzako. Usimtamani mke wa mwenzako,+ wala mtumwa wake wala kijakazi wake wala ng’ombe-dume wake wala punda wake wala chochote cha mwenzako.”+

18 Sasa watu wote walikuwa wakiona ile mingurumo na miwako ya umeme na sauti ya baragumu na mlima ukitoa moshi. Watu walipoona hilo, ndipo wakatetemeka na kusimama mbali.+ 19 Nao wakaanza kumwambia Musa: “Wewe sema nasi, nasi tusikie; lakini Mungu asiseme nasi tusije tukafa.”+ 20 Basi Musa akawaambia watu: “Msiogope, kwa sababu Mungu wa kweli amekuja ili kuwatia ninyi katika jaribu,+ na ili kumwogopa yeye, kuendelee kuwa mbele ya nyuso zenu ili ninyi msije mkatenda dhambi.”+ 21 Na watu wakaendelea kusimama mbali, bali Musa akaenda karibu na lile wingu kubwa jeusi mahali alipokuwa Mungu wa kweli.+

22 Naye Yehova akaendelea kumwambia Musa:+ “Hivi ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli, ‘Ninyi wenyewe mmeona kwamba nilisema nanyi kutoka mbinguni.+ 23 Msifanye miungu ya fedha pamoja nami, wala msijifanyie miungu ya dhahabu.+ 24 Utanifanyia madhabahu ya udongo,+ nawe utatoa juu yake dhabihu za matoleo yako ya kuteketezwa na dhabihu zako za ushirika, kundi lako na mifugo yako.+ Katika kila mahali ambapo nitalifanya jina langu likumbukwe nitakuja kwako, nami hakika nitakubariki.+ 25 Na ikiwa utanifanyia madhabahu ya mawe, usiijenge kwa mawe yaliyochongwa. Ikiwa utatumia tindo juu yake, basi utaitia unajisi.+ 26 Nawe usipande juu ya madhabahu yangu kwa ngazi, ili sehemu zako za siri zisifunuliwe juu yake.’

21 “Nayo haya ndiyo maamuzi ya hukumu utakayoweka mbele yao:+

2 “Ikiwa utamnunua mtumwa+ Mwebrania, atakuwa mtumwa kwa miaka sita, lakini mwaka wa saba ataondoka kama mtu aliyewekwa huru bila malipo.+ 3 Ikiwa ataingia akiwa peke yake, ataondoka akiwa peke yake. Ikiwa ana mke, basi mke wake ataondoka pamoja naye. 4 Ikiwa bwana wake atampa mke, naye amzalie wana na mabinti, huyo mke na watoto wake watakuwa wa bwana wake+ naye ataondoka akiwa peke yake.+ 5 Lakini ikiwa mtumwa huyo atasisitiza kusema, ‘Nampenda bwana wangu kwelikweli, mke wangu na wanangu; sitaki kuondoka kama mtu aliyewekwa huru,’+ 6 basi bwana wake atamleta karibu na Mungu wa kweli naye atamleta kwenye mlango au kwenye mwimo wa mlango; naye bwana wake atalichoma sikio lake na kulitoboa kwa sindano, naye atakuwa mtumwa wake mpaka wakati usio na kipimo.+

7 “Ikiwa mtu atamuuza binti yake awe kijakazi,+ hataondoka kama vile wanaume watumwa wanavyoondoka. 8 Ikiwa hapendezi machoni pa bwana wake hivi kwamba hamfanyi kuwa suria+ bali anamfanya akombolewe, hatakuwa na haki ya kumuuza kwa watu wa kigeni katika kumtendea kwake kwa hila. 9 Na ikiwa atamfanya awe wa mwana wake, atamtendea kulingana na haki wanazostahili mabinti.+ 10 Ikiwa atajichukulia mke mwingine, chakula chake, mavazi yake+ na haki yake ya ndoa+ hazitapunguzwa. 11 Ikiwa hatampa mambo hayo matatu, basi kijakazi huyo ataondoka bure, bila kulipa pesa.

12 “Yule anayempiga mtu na kumuua lazima atauawa.+ 13 Lakini ikiwa mtu hakuvizia naye Mungu wa kweli aruhusu jambo hilo litokee mkononi mwake,+ basi nitakuwekea mahali anapoweza kukimbilia.+ 14 Na ikiwa mtu atawaka hasira juu ya mwenzake kufikia hatua ya kumuua kwa kutumia hila,+ utamwondoa hata kwenye madhabahu yangu akafe.+ 15 Naye anayempiga baba yake na mama yake lazima auawe.+

16 “Naye anayemteka nyara mtu+ na kumuuza+ au ambaye mikononi mwake huyo aliyetekwa amepatikana lazima auawe.+

17 “Naye anayemlaani baba yake na mama yake lazima atauawa.+

18 “Na watu wakianza ugomvi na mmoja wao ampige mwenzake kwa jiwe au jembe naye asife bali alazimike kuendelea kukaa kitandani mwake; 19 ikiwa atasimama na kutembea nje ya milango kwa kitu fulani cha kumtegemeza, basi yule aliyempiga hatapata adhabu; atalipa kwa ajili tu ya wakati uliopotea wa mtu huyo wa kufanya kazi mpaka awe amepona kabisa.

20 “Na ikiwa mtu atampiga+ mtumwa wake au kijakazi wake kwa fimbo naye kwa kweli afe chini ya mkono wake, lazima huyo atalipizwa kisasi.+ 21 Hata hivyo, akikaa kwa siku moja au siku mbili, hatalipizwa kisasi, kwa sababu yeye ni pesa zake.

22 “Na ikiwa watu watapambana nao kwa kweli wamuumize sana mwanamke mwenye mimba nao watoto+ wake watoke lakini kifo kisitokee, atadaiwa alipie hasara kulingana na kile ambacho mume wa mwanamke huyo atamdai; naye atakitoa kupitia kwa waamuzi.+ 23 Lakini kifo kikitokea, basi utatoa nafsi kwa nafsi,+ 24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,+ 25 alama kwa alama, jeraha kwa jeraha, pigo kwa pigo.+

26 “Na ikiwa mtu atalipiga jicho la mtumwa wake au jicho la kijakazi wake na kwa kweli aliharibu vibaya, atamwacha aende zake kama mtu aliyewekwa huru ili kulipia jicho lake.+ 27 Na ikiwa ni jino la mtumwa wake au jino la kijakazi wake ndilo ameng’oa, atamwacha aende zake kama mtu aliyewekwa huru ili kulipia jino lake.

28 “Na ikiwa ng’ombe-dume atampiga kwa pembe mwanamume au mwanamke naye afe, lazima ng’ombe-dume huyo atapigwa kwa mawe,+ lakini nyama yake isiliwe; na mwenye ng’ombe-dume huyo hatapata adhabu. 29 Lakini ikiwa ng’ombe-dume huyo alikuwa na zoea la kupiga kwa pembe tangu zamani na mwenye ng’ombe-dume huyo alionywa bali hakumzuia, naye amuue mwanamume au mwanamke, ng’ombe-dume huyo atapigwa kwa mawe na pia mwenye ng’ombe-dume huyo atauawa. 30 Ikiwa atadaiwa fidia, basi atatoa bei ya ukombozi kwa ajili ya nafsi yake kulingana na yote atakayodaiwa.+ 31 Ikiwa ng’ombe-dume huyo alimpiga mwana au alimpiga binti, mwenye ng’ombe-dume atatendewa kulingana na uamuzi huu wa hukumu.+ 32 Ikiwa aliyepigwa ni mtumwa au ni kijakazi, mwenye ng’ombe-dume atamlipa bwana wake bei ya shekeli 30,+ naye ng’ombe-dume atapigwa kwa mawe.

33 “Na mtu akifunua shimo, au mtu akichimba shimo naye asilifunike, na ng’ombe-dume au punda aanguke ndani yake,+ 34 mwenye shimo hilo anapaswa kulipa.+ Bei hiyo atamlipa mwenye mnyama, naye mnyama aliyekufa atakuwa wake. 35 Na ikiwa ng’ombe-dume wa mtu atamuumiza ng’ombe-dume wa mtu mwingine naye afe, basi watamuuza ng’ombe-dume aliye hai na kugawana pesa zilizolipwa kwa ajili yake; naye yule aliyekufa pia watagawana.+ 36 Au ikiwa ilijulikana kwamba ng’ombe-dume huyo alikuwa na zoea la kupiga kwa pembe lakini mwenye ng’ombe-dume huyo hakumzuia,+ basi lazima atalipa+ ng’ombe-dume kwa ng’ombe-dume, naye aliyekufa atakuwa wake.

22 “Na mtu akiiba ng’ombe-dume au kondoo na kumchinja au kumuuza, atalipa watano kutoka katika mifugo kwa ajili ya ng’ombe-dume huyo na wanne kutoka katika kundi kwa ajili ya kondoo huyo.+

2 (“Mwizi+ akipatikana akifanya tendo la kuvunja+ ili kuingia naye apigwe na kuuawa, hakuna hatia ya damu kwa ajili yake.+ 3 Ikiwa jua limeangaza juu yake, basi kuna hatia ya damu kwa ajili yake.)

“Lazima alipe. Ikiwa hana chochote, basi atauzwa kwa ajili ya vitu alivyoiba.+ 4 Vitu vilivyoibwa vikipatikana pasipo shaka mikononi mwake, ng’ombe-dume, punda, na kondoo, wakiwa hai, atalipa mara mbili.

5 “Mtu akilisha katika shamba au shamba la mizabibu naye aache wanyama wake wa kubeba mizigo wakale katika shamba lingine, atalipa+ kwa yaliyo bora ya shamba lake mwenyewe au kwa yaliyo bora ya shamba lake mwenyewe la mizabibu.

6 “Moto ukienea na kushika miiba, nayo miganda au nafaka inayosimama au shamba liteketee,+ yule aliyeuanzisha moto huo lazima alipie kilichoteketea.

7 “Mtu akimpa mwenzake pesa au vitu amwekee,+ navyo viibiwe kutoka katika nyumba ya mtu huyo, mwizi huyo akipatikana, atalipa mara mbili.+ 8 Mwizi huyo asipopatikana, basi mwenye nyumba hiyo ataletwa karibu na Mungu wa kweli+ ili kuona ikiwa hakutia mkono wake juu ya vitu vya mwenzake. 9 Kuhusu kesi yoyote ya ukosaji,+ inayohusu ng’ombe-dume, punda, kondoo, vazi, kitu chochote kilichopotea ambacho huenda akasema hivi juu yake ‘Ndicho hiki!’ kesi yao wote wawili italetwa mbele za Mungu wa kweli.+ Yule ambaye Mungu atamtangaza kuwa mwovu atamlipa mwenzake mara mbili.+

10 “Mtu akimpa mwenzake punda au ng’ombe-dume au kondoo au mnyama yeyote wa kufugwa ili aweke, naye mnyama huyo afe au alemae au achukuliwe bila mtu yeyote kuona, 11 kiapo+ kwa jina la Yehova kinapaswa kifanywe kati yao wawili ya kwamba yeye hakutia mkono wake juu ya mali za mwenzake;+ na mwenyewe lazima akubali, na yule mwingine hatalipa. 12 Lakini ikiwa kwa kweli wataibiwa kutoka kwake, atamlipa mwenyewe.+ 13 Ikiwa kwa kweli atararuliwa na mnyama-mwitu,+ atamleta awe ushuhuda.+ Hatalipia kitu kilichoraruliwa na mnyama-mwitu.

14 “Lakini mtu yeyote akimwomba mwenzake kitu fulani,+ nacho kilemae au kife kama mwenyewe hayupo pamoja nacho, lazima atalipa.+ 15 Ikiwa mwenyewe yupo pamoja nacho, hatalipa. Ikiwa ni cha kukodi, lazima hasara itiwe ndani ya kodi yake.

16 “Sasa, mwanamume akimshawishi bikira ambaye hajachumbiwa, na alale naye,+ lazima atamchukua awe mke wake kwa ile bei ya kununua.+ 17 Baba yake akikataa kabisa kumpa yeye, mwanamume huyo atalipa pesa hizo kwa kiwango cha bei ya kununua mabikira.+

18 “Usimhifadhi hai mwanamke mlozi.+

19 “Mtu yeyote anayelala na mnyama lazima atauawa.+

20 “Mtu anayetoa dhabihu kwa miungu yoyote isipokuwa kwa Yehova peke yake ataangamizwa.+

21 “Na usimtendee vibaya mkaaji mgeni wala kumkandamiza,+ kwa sababu ninyi mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.+

22 “Msimtese mjane yeyote wala mvulana asiye na baba.+ 23 Mkimtesa hata kidogo, naye anililie hata kidogo, sitakosa kukisikia kilio chake;+ 24 nayo hasira yangu itawaka kwelikweli,+ nami hakika nitawaua kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane, nao wana wenu watakuwa wavulana wasio na baba.+

25 “Ukiwakopesha watu wangu pesa, mwenye kuteseka aliye kando yako,+ usiwe kwake kama mla-riba. Msimtoze faida.+

26 “Ukichukua vazi la mwenzako kuwa rehani,+ yakupasa ulirudishe kwake wakati wa kutua kwa jua. 27 Kwa maana hilo ndilo vazi pekee la kujifunika alilo nalo.+ Ndiyo nguo yake ya kujitanda ili kuifunika ngozi yake. Atalalia nini? Na itakuwa kwamba atanililia, nami hakika nitasikia, kwa sababu mimi ni mwenye neema.+

28 “Usimlaani Mungu+ wala kumlaani mkuu kati ya watu wako.+

29 “Mazao yako kamili na ziada ya shinikizo lako usitoe kwa kusitasita.+ Mzaliwa wa kwanza wa wana wako utanipa mimi.+ 30 Hivi ndivyo utakavyofanya kuhusu ng’ombe-dume wako na kondoo wako:+ Siku saba atakaa na mama yake.+ Siku ya nane unipe mimi.

31 “Nanyi lazima muwe watu watakatifu kwangu;+ nanyi msile nyama shambani ambayo imeraruliwa na mnyama-mwitu.+ Mtawatupia mbwa nyama hiyo.+

23 “Usieneze habari isiyo ya kweli.+ Usishirikiane na mtu mwovu kwa kuwa shahidi anayepanga jeuri.+ 2 Usiufuate umati kwa ajili ya makusudio maovu;+ wala usishuhudie juu ya ubishi ili kugeuka kando pamoja na umati kwa kusudi la kupotosha haki.+ 3 Na kwa ajili ya mtu wa hali ya chini, usionyeshe upendeleo katika ubishi wake.+

4 “Ukikutana na ng’ombe-dume au punda wa adui yako akipotea, lazima umrudishe kwake.+ 5 Ukimwona punda wa mtu anayekuchukia akiwa amelala chini ya mzigo wake, basi lazima ujizuie usimwache. Lazima utamfungua pamoja naye.+

6 “Usipotoshe uamuzi wa hukumu wa mtu wako aliye maskini katika ubishi wake.+

7 “Utakaa mbali na neno la uwongo.+ Nawe usimuue mtu asiye na hatia na yule aliye mwadilifu, kwa maana sitamtangaza mwovu kuwa mwadilifu.+

8 “Usikubali rushwa, kwa maana rushwa hupofusha watu wanaoona vizuri na inaweza kupotosha maneno ya watu waadilifu.+

9 “Nawe usimkandamize mkaaji mgeni,+ kwa maana ninyi wenyewe mmeijua nafsi ya mkaaji mgeni, kwa sababu mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.+

10 “Na kwa miaka sita utapanda mbegu katika shamba lako nawe utakusanya mazao yake.+ 11 Lakini mwaka wa saba utaliacha bila kulimwa nawe utaliacha lipumzike,+ nao maskini wa watu wako watakula kutokana nalo; nacho kile ambacho wataacha kitaliwa na wanyama wa mwituni.+ Hivyo ndivyo utakavyofanya na shamba lako la mizabibu na shamba lako la mizeituni.

12 “Siku sita utafanya kazi yako;+ lakini siku ya saba utaacha, ili ng’ombe-dume wako na punda wako wapate kupumzika na mwana wa kijakazi wako na mkaaji mgeni wapate kujiburudisha.+

13 “Nanyi mtajilinda kuhusiana na yote hayo ambayo nimewaambia ninyi;+ nanyi msilitaje jina la miungu mingine. Lisisikiwe kinywani mwako.+

14 “Mara tatu kwa mwaka utanifanyia sherehe.+ 15 Utaishika sherehe ya keki zisizo na chachu.+ Utakula keki zisizo na chachu+ siku saba, kama vile ambavyo nimekuamuru, wakati uliowekwa katika mwezi wa Abibu,+ kwa sababu katika mwezi huo ulitoka Misri. Nao wasionekane mbele zangu mikono mitupu.+ 16 Pia, sherehe ya mavuno ya matunda ya kwanza yaliyoiva+ ya kazi zenu, ya vitu mnavyopanda shambani;+ na sherehe ya kukusanya mwishoni mwa mwaka, wakati ambapo mnakusanya kazi zenu kutoka shambani.+ 17 Pindi tatu katika mwaka kila mwanamume wa kwako ataonekana mbele za uso wa Bwana wa kweli, Yehova.+

18 “Msitoe dhabihu damu ya dhabihu yangu pamoja na kitu kilicho na chachu. Nayo mafuta ya sherehe yangu yasikae usiku kucha mpaka asubuhi.+

19 “Yaliyo bora zaidi kati ya matunda ya kwanza yaliyoiva ya udongo wako utayaleta katika nyumba ya Yehova Mungu wako.+

“Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.+

20 “Tazama, ninamtuma malaika+ mbele yako ili akuongoze barabarani na kukuingiza mahali ambapo nimetayarisha.+ 21 Jiangalie kwa sababu yake na kuitii sauti yake. Usijiendeshe kwa kumwasi yeye, kwa maana hatawasamehe kosa lenu;+ kwa sababu jina langu limo ndani yake. 22 Hata hivyo, ukiitii sauti yake kabisa na kwa kweli ufanye yote nitakayosema,+ basi hakika nitawaonyesha adui zako uadui na kuwasumbua wale wanaokusumbua.+ 23 Kwa maana malaika wangu ataenda mbele yako naye kwa kweli atakuongoza kwa Waamori na Wahiti na Waperizi na Wakanaani, na Wahivi na Wayebusi, nami hakika nitawafutilia hao mbali.+ 24 Usiinamie miungu yao wala kuchochewa kuitumikia, wala usifanyize chochote kilicho kama kazi zao,+ bali lazima utawaangusha nawe lazima uzivunje nguzo zao takatifu.+ 25 Nanyi mtamtumikia Yehova Mungu wenu,+ naye hakika ataubariki mkate wako na maji yako;+ nami kwa kweli nitageuzia mbali ugonjwa kutoka katikati yako.+ 26 Wala hakutakuwa na mwanamke ambaye mimba yake itatoka wala mwanamke tasa katika nchi yako.+ Nitafanya hesabu ya siku zako itimie.+

27 “Na nitatuma mbele yako hali ya kuniogopa,+ nami hakika nitawavuruga watu wote utakaoingia katikati yao, nami kwa kweli nitakupa shingo za adui zako wote.+ 28 Nami nitaituma mbele yako hisia ya kuvunjika moyo,+ nayo itawafukuzia mbali Wahivi, Wakanaani na Wahiti kutoka mbele yako.+ 29 Sitawafukuza kutoka mbele yako kwa mwaka mmoja, ili nchi isiwe mahame yenye ukiwa nao wanyama wa mwituni waongezeke kwelikweli juu yako.+ 30 Nitawafukuza kutoka mbele yako hatua kwa hatua, mpaka uongezeke na kuimiliki nchi hiyo kabisa.+

31 “Nami nitauweka mpaka wako kutoka Bahari Nyekundu hadi bahari ya Wafilisti na kutoka nyikani hadi kwenye Mto;+ kwa sababu nitawaweka wakaaji wa nchi hiyo mikononi mwenu, na hakika wewe utawafukuzia mbali kutoka mbele yako.+ 32 Hutafanya agano pamoja nao au miungu yao.+ 33 Wasikae katika nchi yako, wasije wakakufanya unitendee dhambi. Ikiwa utaitumikia miungu yao, itakuwa mtego kwako.”+

24 Naye akamwambia Musa: “Panda uende kwa Yehova, wewe na Haruni, Nadabu na Abihu+ na wanaume wazee 70+ wa Israeli, nanyi mtainama mkiwa mbali. 2 Naye Musa peke yake atamkaribia Yehova; lakini wao wasikaribie, wala watu wasipande kwenda pamoja naye.”+

3 Kisha Musa akaja na kuwasimulia watu maneno yote ya Yehova na maamuzi yote ya hukumu,+ nao watu wote wakajibu kwa sauti moja na kusema: “Maneno yote ambayo Yehova amesema tuko tayari kuyafanya.”+ 4 Basi Musa akaandika maneno yote ya Yehova.+ Kisha akaamka asubuhi na mapema na kujenga kwenye sehemu ya chini ya huo mlima madhabahu na nguzo kumi na mbili zinazolingana na yale makabila kumi na mawili ya Israeli.+ 5 Baadaye akawatuma vijana kati ya wana wa Israeli nao wakatoa dhabihu za kuteketezwa na kutoa ng’ombe-dume wakiwa dhabihu, kama dhabihu za ushirika+ kwa Yehova. 6 Kisha Musa akachukua nusu ya damu na kuitia katika mabakuli,+ na nusu ya damu akainyunyiza juu ya madhabahu.+ 7 Mwishowe akachukua kitabu cha agano+ na kukisoma katika masikio ya watu.+ Kisha wakasema: “Yote ambayo Yehova amesema tuko tayari kuyafanya na kuyatii.”+ 8 Basi Musa akaichukua damu na kuinyunyiza juu ya watu+ na kusema: “Tazama, hii ndiyo damu ya agano+ ambalo Yehova amefanya pamoja nanyi kuhusu maneno yote haya.”

9 Na Musa na Haruni, Nadabu na Abihu na watu 70 kati ya wanaume wazee wa Israeli wakapanda juu, 10 nao wakamwona Mungu wa Israeli.+ Na chini ya miguu yake palikuwa na kitu kilichofanana na mawe bapa ya yakuti na kama mbingu kwa kutakata.+ 11 Naye hakuunyoosha mkono wake juu ya wale wanaume mashuhuri kati ya wana wa Israeli,+ bali walipata maono ya Mungu wa kweli,+ wakala na kunywa.+

12 Sasa Yehova akasema na Musa: “Njoo kwangu juu mlimani, ukae huko, kwa maana nataka kukupa mabamba ya mawe na sheria na amri ambayo nitaiandika ili kuwafundisha wao.”+ 13 Basi Musa na Yoshua mhudumu wake wakasimama, naye Musa akapanda kwenda juu katika mlima wa Mungu wa kweli.+ 14 Lakini alikuwa amewaambia wale wanaume wazee: “Ninyi tungojeeni mahali hapa mpaka turudi kwenu.+ Na, tazama! Haruni na Huru+ wako pamoja nanyi. Yeyote aliye na kesi, na awaendee.”+ 15 Basi Musa akaenda juu katika mlima, huku wingu likiufunika mlima huo.+

16 Na utukufu+ wa Yehova ukaendelea kukaa juu ya Mlima Sinai,+ nalo wingu likaendelea kuufunika kwa siku sita. Mwishowe katika siku ya saba akamwita Musa kutoka katikati ya lile wingu.+ 17 Na machoni pa wana wa Israeli, kuonekana kwa utukufu wa Yehova kulikuwa kama moto+ wenye kuteketeza juu ya kilele cha mlima. 18 Kisha Musa akaingia katikati ya wingu na kwenda juu katika mlima.+ Naye Musa akakaa mlimani siku 40, mchana na usiku.+

25 Naye Yehova akasema na Musa,+ na kumwambia: 2 “Sema na wana wa Israeli, kwamba wanichukulie mchango: Kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake unamchochea ninyi mtauchukua mchango wangu.+ 3 Na huu ndio mchango ambao mtauchukua kutoka kwao: dhahabu+ na fedha+ na shaba,+ 4 na uzi wa bluu, na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau, na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, na kitani bora, na manyoya ya mbuzi,+ 5 na ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu, na ngozi za sili, na mbao za mshita;+ 6 mafuta ya mwanga,+ mafuta ya zeri+ kwa ajili ya kutia mafuta+ na kwa ajili ya uvumba uliotiwa manukato;+ 7 na mawe ya shohamu na mawe ya kuwekwa kwenye efodi+ na kwenye kile kifuko cha kifuani.+ 8 Nao watanifanyia patakatifu, kwa maana mimi nitakaa katikati yao.+ 9 Kulingana na yote ninayokuonyesha wewe kuwa mfano wa maskani na mfano wa vyombo vyake vyote, hivyo ndivyo mtakavyoifanya.+

10 “Nao watafanya Sanduku la mbao za mshita,+ mikono miwili na nusu urefu wake na mkono mmoja na nusu upana wake na mkono mmoja na nusu kimo chake. 11 Nawe utalifunika kwa dhahabu safi.+ Utalifunika upande wa ndani na wa nje, nawe utalifanyia ukingo wa dhahabu kuzunguka juu yake pande zote.+ 12 Nawe utatengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili yake na kuziweka juu ya miguu yake minne, pete mbili upande wake mmoja na pete mbili upande wake mwingine.+ 13 Nawe utafanya miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.+ 14 Nawe utaitia miti hiyo kwenye zile pete zilizo kwenye pande za Sanduku ili kuitumia kulibeba Sanduku. 15 Miti hiyo itakaa kwenye pete za Sanduku. Haitaondolewa.+ 16 Nawe utaweka katika Sanduku hilo ushuhuda nitakaokupa.+

17 “Nawe utafanya kifuniko cha dhahabu safi, mikono miwili na nusu urefu wake na mkono mmoja na nusu upana wake.+ 18 Nawe utafanya makerubi wawili wa dhahabu. Utawafanya kwa kazi ya kufua kwenye miisho miwili ya kifuniko.+ 19 Na ufanye kerubi mmoja mwisho huu na kerubi mmoja mwisho ule.+ Juu ya kifuniko mtawafanya makerubi hao kwenye miisho yake miwili. 20 Na makerubi hao watakuwa wamenyoosha mabawa yao kuelekea juu, wakifunika kifuniko hicho kwa mabawa yao, nyuso zao zikielekeana.+ Nyuso za makerubi hao zitaelekea kifuniko. 21 Nawe utakiweka kifuniko+ hicho juu ya Sanduku, na ndani ya Sanduku utaweka ushuhuda nitakaokupa. 22 Nami nitakutokea hapo na kusema nawe toka juu ya kifuniko+ hicho, toka katikati ya wale makerubi wawili walio juu ya sanduku la ushuhuda, naam, yote nitakayokuamuru wewe kwa ajili ya wana wa Israeli.+

23 “Nawe utafanya meza+ ya mbao za mshita, mikono miwili urefu wake na mkono mmoja upana wake na mkono mmoja na nusu kimo chake. 24 Nawe utaifunika kwa dhahabu safi, nawe utaifanyia ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.+ 25 Nawe utaifanyia mzingo wa upana wa kiganja kuizunguka pande zote, nawe utafanya ukingo wa dhahabu kwa ajili ya mzingo wake kuizunguka pande zote.+ 26 Nawe utaifanyia pete nne za dhahabu na kuziweka pete hizo kwenye pembe nne za miguu yake minne.+ 27 Hizo pete zitakuwa karibu na mzingo ili kutegemeza miti ya kuibeba meza hiyo.+ 28 Nawe utafanya miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu, nao wataitumia kuibeba meza hiyo.+

29 “Nawe utafanya sahani zake na vikombe vyake na mitungi yake na mabakuli yake watakayotumia katika kumimina matoleo ya kinywaji. Utavifanya kutokana na dhahabu safi.+ 30 Nawe utauweka mkate wa wonyesho juu ya meza hiyo mbele zangu daima.+

31 “Nawe utafanya kinara cha taa cha dhahabu safi. Hicho kinara cha taa kitafanyizwa kwa kazi ya kufua.+ Msingi wake, matawi yake, vikombe vyake, vifundo vyake na maua yake vitatoka kwake. 32 Na matawi sita yatatoka pande zake, matawi matatu ya kinara cha taa kutoka upande wake mmoja na matawi matatu ya kinara cha taa kutoka ule upande wake mwingine.+ 33 Vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vitakuwa kwenye kila moja la matawi yaliyoko upande mmoja, vifundo na maua vikifuatana, na vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi kwenye kila moja la matawi yaliyoko upande ule mwingine, vifundo na maua vikifuatana.+ Hivyo ndivyo ilivyo kwa matawi sita yanayotoka katika kile kinara cha taa. 34 Na kwenye kinara cha taa kuna vikombe vinne vyenye umbo la maua ya mlozi, vifundo vyake na maua yake vikifuatana.+ 35 Na kile kifundo kilicho chini ya matawi mawili chatoka kwake na kifundo kilicho chini ya yale matawi mawili mengine chatoka kwake na kifundo kilicho chini ya matawi mengine mawili chatoka kwake, kwa ajili ya yale matawi sita yanayotoka katika kinara.+ 36 Vifundo vyake na matawi yake vitatoka kwake. Vyote ni kitu kimoja kilichofuliwa, cha dhahabu safi.+ 37 Nawe utakifanyia taa saba; na taa hizo zitawashwa, nazo zitaangaza juu ya eneo lililo mbele yake.+ 38 Na mikasi yake ya tambi na vyetezo vyake ni vya dhahabu safi.+ 39 Atakifanya hicho pamoja na vyombo vyake vyote kwa talanta ya dhahabu safi. 40 Na uhakikishe kwamba umezifanya kulingana na mfano ulioonyeshwa mlimani.+

26 “Nayo maskani mtaifanya kwa vitambaa kumi vya mahema,+ kwa vitambaa vya kitani bora kilichosokotwa na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili.+ Kwa makerubi,+ kazi ya mtarizi, utavifanya. 2 Urefu wa kila kitambaa cha hema utakuwa mikono 28 na upana wa kila kitambaa utakuwa mikono 4. Vitambaa hivyo vyote vitakuwa na kipimo kimoja.+ 3 Vitambaa vitano vitafanyiza mfuatano, kimoja kikiwa kimeunganishwa na kingine, na vitambaa vitano vitafanyiza mfuatano, kimoja kikiwa kimeunganishwa na kingine.+ 4 Nawe utafanya vitanzi vya uzi wa bluu kwenye upindo wa kile kitambaa kimoja kilicho mwisho wa mfuatano; nawe utafanya vivyo hivyo kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pale pengine pa kuungania.+ 5 Utafanya vitanzi 50 kwenye kitambaa kimoja, na vitanzi 50 utavifanya kwenye mwisho wa kitambaa kilicho mahali pale pengine pa kuungania, vitanzi vikikabiliana.+ 6 Nawe utafanya kulabu 50 za dhahabu na kuviunganisha vitambaa hivyo, kimoja kwa kingine, kwa kulabu hizo, navyo vitakuwa maskani moja.+

7 “Nawe utafanya nguo za manyoya ya mbuzi+ kwa ajili ya hema juu ya maskani. Utafanya vitambaa kumi na moja vya mahema. 8 Urefu wa kila kitambaa utakuwa mikono+ 30, na upana wa kila kitambaa utakuwa mikono 4. Vitambaa vyote 11 vitakuwa na kipimo kimoja. 9 Nawe utaviunganisha vitambaa vitano pamoja, na vitambaa sita pamoja,+ nawe utakikunja mara mbili kile kitambaa cha sita kilicho upande wa mbele wa hema. 10 Nawe utafanya vitanzi 50 kwenye upindo wa kile kitambaa kimoja, cha nje kabisa kwenye ule mfuatano, na vitanzi 50 kwenye upindo wa kitambaa kilicho mahali pale pengine pa kuungania. 11 Nawe utafanya kulabu 50 za shaba+ na kuzitia kulabu hizo kwenye vile vitanzi na kuliunganisha lile hema pamoja, nalo litakuwa kitu kimoja.+ 12 Nacho kitambaa kitakachobaki kitakuwa cha kuning’inia. Nusu ya kitambaa cha hema kitakachobaki kitaning’inia upande wa nyuma wa maskani. 13 Na mkono mmoja wa upande huu na mkono mmoja wa upande ule wa kile kinachobakia katika urefu wa vitambaa utakuwa wa kuning’inia pande za maskani, ili kuifunika upande huu na upande ule.

14 “Nawe utafanya kifuniko cha hilo hema, kifuniko cha ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko cha ngozi za sili upande wa juu.

15 “Nawe utafanya viunzi+ vya mbao za mshita kwa ajili ya maskani hiyo, vinavyosimama mwishoni. 16 Urefu wa kiunzi utakuwa mikono kumi, nao upana wa kila kiunzi utakuwa mkono mmoja na nusu. 17 Kila kiunzi kitakuwa na ndimi mbili zilizounganishwa pamoja. Hivyo ndivyo utakavyofanya na viunzi vyote vya maskani. 18 Nawe utavifanya viunzi vya mbao kwa ajili ya maskani, viunzi 20 kwa ajili ya upande unaokabili Negebu, upande wa kusini.

19 “Nawe utafanya vikalio+ 40 vya fedha chini ya vile viunzi 20; vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja pamoja na ndimi zake mbili, na vikalio viwili chini ya kile kiunzi kingine pamoja na ndimi zake mbili. 20 Na kwa ajili ya upande ule mwingine wa maskani, upande wa kaskazini, viunzi 20,+ 21 na vikalio vyake 40 vya fedha, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja na vikalio vingine viwili chini ya kile kiunzi kingine.+ 22 Na kwa ajili ya sehemu za nyuma za maskani kuelekea upande wa magharibi utafanya viunzi sita.+ 23 Nawe utafanya viunzi viwili viwe miimo ya pembeni ya maskani+ katika sehemu zake mbili za nyuma. 24 Navyo vitakuwa pacha sehemu ya chini, navyo vitakuwa pacha mpaka juu ya kila moja kwenye pete ya kwanza. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa ajili ya vyote viwili. Vitakuwa miimo miwili ya pembeni. 25 Na kutakuwa na viunzi vinane na vikalio vyake vya fedha, vikalio kumi na sita, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja na vikalio viwili chini ya kile kiunzi kingine.

26 “Nawe utafanya miti ya mshita,+ mitano kwa ajili ya viunzi vya mbao vya upande mmoja wa maskani, 27 na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya upande ule mwingine wa maskani na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya upande wa maskani kwa ajili ya zile pande mbili za nyuma kuelekea upande wa magharibi.+ 28 Nao mti wa katikati ulio katikati ya viunzi utatoka mwisho mmoja mpaka mwingine.

29 “Nawe utavifunika vile viunzi vya mbao kwa dhahabu,+ na pete zake utazifanya kwa dhahabu ili zitegemeze ile miti; nawe utaifunika miti hiyo kwa dhahabu. 30 Nawe utaisimamisha maskani kulingana na ramani yake ambayo umeonyeshwa mlimani.+

31 “Nawe utafanya pazia+ la uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa. Atalifanya likiwa na makerubi,+ kazi ya mtarizi. 32 Nawe utaliweka juu ya nguzo nne za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Misumari yake itakuwa ya dhahabu. Zinakaa juu ya vikalio vinne vya fedha. 33 Nawe utaliweka pazia chini ya kulabu na kulileta sanduku la ushuhuda+ ndani ya hilo pazia; nalo pazia litawatenganishia Patakatifu+ na Patakatifu Zaidi.+ 34 Nawe utakiweka kifuniko juu ya sanduku la ushuhuda katika Patakatifu Zaidi.

35 “Nawe utaiweka meza nje ya pazia, na kinara cha taa+ kitakuwa upande tofauti na hiyo meza, kitakuwa upande wa maskani kuelekea kusini; nayo meza utaiweka upande wa kaskazini. 36 Nawe utafanya kisitiri+ kwa ajili ya mlango wa hema, kisitiri cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani safi kilichosokotwa, kazi ya mfumaji. 37 Nawe utakifanyizia kile kisitiri nguzo tano za mshita na kuzifunika kwa dhahabu. Vibanio vyake vitakuwa vya dhahabu. Nawe utavitengenezea vikalio vitano vya shaba.

27 “Nawe utafanya madhabahu ya mbao za mshita, mikono mitano urefu wake na mikono mitano upana wake. Madhabahu+ hiyo itakuwa mraba, na kimo chake kitakuwa mikono mitatu. 2 Nawe utafanya pembe+ zake kwenye ncha zake nne. Pembe zake zitatoka kwake, nawe utaifunika kwa shaba.+ 3 Nawe utafanya makopo yake ya kuondolea majivu yake yenye mafuta, na sepetu zake, na mabakuli yake, na nyuma zake, na vyetezo vyake; nawe utavifanya vyombo vyake vyote kwa shaba.+ 4 Nawe utaifanyia kiunzi cha fito, mtandao wa fito+ za shaba; nawe utafanya pete nne za shaba juu ya mtandao huo kwenye miisho yake minne. 5 Nawe utauweka chini ya ukingo wa madhabahu, chini upande wa ndani, nao mtandao huo utakuwa kuelekea katikati ya madhabahu.+ 6 Nawe utafanya miti kwa ajili ya madhabahu, miti yake ikiwa ya mshita, nawe utaifunika kwa shaba.+ 7 Nayo miti yake itaingizwa kwenye zile pete, nayo miti itakuwa kwenye zile pande mbili za madhabahu wakati wa kuibeba.+ 8 Utaifanya iwe sanduku la mbao lenye uwazi. Kama vile alivyokuonyesha mlimani, ndivyo watakavyoifanya.+

9 “Nawe utafanya ua+ wa maskani. Upande kuelekea Negebu, kuelekea kusini, ua utakuwa na mapazia ya kitani bora kilichosokotwa,+ urefu wa upande mmoja ukiwa mikono mia moja. 10 Nazo nguzo zake 20 na vikalio vyake 20 vitakuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vitakuwa vya fedha.+ 11 Ndivyo pia utakavyokuwa upande wa kaskazini kwa urefu, mapazia yakiwa mikono 100 kwa urefu, nazo nguzo zake 20 na vikalio vyake 20 vitakuwa vya shaba, misumari ya nguzo na viungo vyake vitakuwa vya fedha.+ 12 Nao upana wa ua, upande wa magharibi mapazia yatakuwa mikono 50, nguzo zake zikiwa 10 na vikalio vyake vikiwa 10.+ 13 Nao upana wa ua upande wa mashariki kuelekea macheo ya jua utakuwa mikono 50.+ 14 Na kutakuwako na mikono kumi na mitano ya mapazia upande mmoja, nguzo zake zitakuwa tatu navyo vikalio vyake vitakuwa vitatu.+ 15 Nao upande ule mwingine kutakuwako mikono kumi na mitano ya mapazia, nguzo zake zitakuwa tatu na vikalio vyake vitakuwa vitatu.+

16 “Na kwa ajili ya lango la ua kutakuwa na kisitiri chenye urefu wa mikono 20, cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kazi ya mfumaji,+ nguzo zake zikiwa 4 na vikalio vyake 4.+ 17 Nguzo zote za ua kuzunguka pande zote zitakazwa kwa vifaa vya fedha, navyo vibanio vyake vitakuwa vya fedha lakini vikalio vyake vitakuwa vya shaba.+ 18 Urefu wa ua utakuwa mikono 100,+ nao upana utakuwa mikono 50, nacho kimo kitakuwa mikono 5, ya kitani bora kilichosokotwa, navyo vikalio vyake vitakuwa vya shaba. 19 Navyo vyombo vyote vya hiyo maskani katika utumishi wake wote, na misumari yake yote ya mahema, na misumari yote ya ua itakuwa ya shaba.+

20 “Nawe utawaamuru wana wa Israeli wakupe mafuta safi ya zeituni zilizopondwa kwa ajili ya mwanga, ili kuziwasha taa daima.+ 21 Katika hema la mkutano, nje ya pazia+ lililo kando ya ule Ushuhuda, Haruni na wanawe watauweka kwa utaratibu tangu asubuhi mpaka jioni mbele za Yehova.+ Itakuwa sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa vizazi vyao,+ itakayotekelezwa na wana wa Israeli.+

28 “Na wewe, mlete karibu nawe Haruni ndugu yako na wanawe pamoja naye kutoka katikati ya wana wa Israeli ili awe kuhani kwangu,+ Haruni,+ Nadabu na Abihu,+ Eleazari na Ithamari,+ wana wa Haruni. 2 Nawe utafanya mavazi matakatifu kwa ajili ya Haruni ndugu yako, kwa utukufu na uzuri.+ 3 Na wewe mwenyewe utasema na wote wenye hekima walio na moyo ambao nimeujaza roho ya hekima,+ nao watayafanya mavazi ya Haruni ili kumtakasa, ili awe kuhani kwangu.+

4 “Na haya ndiyo mavazi watakayoyafanya: kifuko cha kifuani,+ na efodi+ na koti lisilo na mikono+ na kanzu yenye mirabamiraba, kilemba+ na ukumbuu;+ nao watafanya mavazi matakatifu kwa ajili ya Haruni ndugu yako na wanawe, ili awe kuhani kwangu. 5 Na wao wenyewe wataichukua dhahabu na ule uzi wa bluu na ile sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kile kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kile kitani bora.

6 “Nao watafanya efodi ya dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kazi ya mtarizi.+ 7 Nayo itakuwa na vipande viwili vya begani vitakavyounganishwa kwenye miisho yake miwili, nayo itaunganishwa.+ 8 Nao mshipi,+ ulio juu yake ili kufunga kwa kuikaza, kulingana na ufundi wake, utakuwa wa vifaa vyake, wa dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.

9 “Nawe utachukua mawe mawili ya shohamu+ na kuchonga+ majina ya wana wa Israeli juu yake,+ 10 majina sita juu ya jiwe moja na yale majina mengine sita yanayobaki juu ya lile jiwe lingine kulingana na utaratibu wa kuzaliwa kwao.+ 11 Kwa kazi ya fundi wa mawe, kwa mchongo wa muhuri, utayachonga kwenye yale mawe mawili majina ya wana wa Israeli.+ Yakiwa yametiwa katika mapambo ya dhahabu ndivyo utakavyoyafanya.+ 12 Nawe utayaweka yale mawe mawili juu ya vile vipande vya begani vya efodi yawe mawe ya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli;+ naye Haruni atayachukua majina yao mbele za Yehova kwenye vipande vyake viwili vya begani ili kuwa ukumbusho. 13 Nawe utafanya mapambo ya dhahabu, 14 na minyororo miwili ya dhahabu safi.+ Utaifanya kama nyuzi, kwa ufundi wa kamba; nawe utaiunganisha ile minyororo iliyo kama kamba kwenye yale mapambo.+

15 “Nawe utakifanya kifuko cha kifuani cha hukumu+ kwa ufundi wa mtarizi. Sawa na ufundi wa efodi utakifanya. Utakifanya kwa dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.+ 16 Kinapaswa kuwa mraba kinapokunjwa, urefu wake ukiwa shubiri moja na upana wake ukiwa shubiri moja.+ 17 Nawe utakijaza kwa mawe, kukiwa na mistari minne ya mawe.+ Mstari wa zabarijadi,+ topazi+ na zumaridi+ ndio mstari wa kwanza. 18 Nao mstari wa pili utakuwa feruzi,+ yakuti+ na yaspi.+ 19 Nao mstari wa tatu utakuwa jiwe la leshemi, akiki+ na amethisti.+ 20 Nao mstari wa nne utakuwa krisolito,+ shohamu+ na yashefi. Matundu ya dhahabu yanapaswa kuwa katika vijazio vyake.+ 21 Na hayo mawe yatakuwa kulingana na majina ya wana wa Israeli, wale kumi na wawili kulingana na majina yao.+ Kwa michongo ya muhuri yatakuwa, kila moja kulingana na jina lake, kwa ajili ya yale makabila kumi na mawili.+

22 “Nawe utafanya juu ya kile kifuko cha kifuani minyororo yenye shada, iliyosokotwa kama kamba, ya dhahabu safi.+ 23 Nawe utafanya pete mbili za dhahabu juu ya kile kifuko cha kifuani,+ nawe utaziweka hizo pete mbili kwenye miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani. 24 Nawe utazitia zile kamba mbili za dhahabu kwenye zile pete mbili zilizo kwenye miisho ya kile kifuko cha kifuani.+ 25 Nawe utaitia ile miisho miwili ya zile kamba mbili katika yale mapambo mawili, nawe utaitia katika vile vipande vya begani vya efodi, upande wake wa mbele.+ 26 Nawe utafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani kwenye upindo wake ulioko upande unaoielekea efodi, upande wa ndani.+ 27 Nawe utafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka juu ya vile vipande viwili vya begani vya efodi upande wa chini, mbele yake, karibu na mahali inapounganikia, juu ya mshipi wa efodi.+ 28 Nao watakifunga kifuko cha kifuani kwa pete zake kwenye zile pete za efodi kwa uzi wa bluu, ili kiwe juu ya mshipi wa efodi nacho kifuko cha kifuani kisiondoke juu ya efodi.+

29 “Naye Haruni atayachukua majina ya wana wa Israeli kwenye kile kifuko cha kifuani cha hukumu juu ya moyo wake anapoingia Patakatifu ili uwe ukumbusho mbele za Yehova daima. 30 Nawe utaweka Urimu+ na Thumimu ndani ya kile kifuko cha kifuani cha hukumu, nazo zitakuwa juu ya moyo wa Haruni anapoingia mbele za Yehova; naye Haruni atachukua hukumu+ za wana wa Israeli juu ya moyo wake mbele za Yehova daima.

31 “Nawe utalifanya koti lote lisilo na mikono la efodi kwa uzi wa bluu.+ 32 Nalo litakuwa na sehemu iliyo wazi katikati yake upande wa juu. Sehemu hiyo iliyo wazi itakuwa na ukingo wa kuizunguka pande zote, kazi ya mfumaji. Sehemu hiyo itakuwa kama ile sehemu wazi ya vazi la chuma, ili isipate kuraruliwa.+ 33 Nawe utafanya kwenye upindo wake makomamanga ya uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, kwenye upindo wake kuuzunguka pande zote, na kengele+ za dhahabu katikati yake pande zote; 34 kengele ya dhahabu na komamanga, kengele ya dhahabu na komamanga juu ya upindo wa koti lisilo na mikono kulizunguka pande zote.+ 35 Nalo litakuwa juu ya Haruni ili apate kuhudumu, nayo sauti kutoka kwake itasikiwa anapoingia ndani ya patakatifu mbele za Yehova na anapotoka nje, ili asife.+

36 “Nawe utafanya bamba linalong’aa la dhahabu safi na kulichonga kwa michongo ya muhuri, ‘Utakatifu ni wa Yehova.’+ 37 Nawe utalikaza kwa uzi wa bluu, nalo litakuwa juu ya kilemba.+ Litakuwa upande wa mbele wa kilemba. 38 Nalo litakuwa kwenye paji la uso wa Haruni, naye Haruni atatoa jibu kwa ajili ya kosa linalofanywa juu ya vyombo vitakatifu,+ ambavyo wana wa Israeli watatakasa, yaani, zawadi zao zote takatifu; nalo litakaa kwenye paji la uso wake daima, ili kupata kibali kwa ajili yao+ mbele za Yehova.

39 “Nawe utafuma kanzu ya kitani bora yenye mirabamiraba na kufanya kilemba cha kitani bora,+ nawe utafanya ukumbuu,+ kazi ya mfumaji.

40 “Nao wana wa Haruni utawafanyia kanzu,+ nawe utawafanyia ukumbuu kila mmoja wao, nawe utawafanyia mavalio ya kichwani+ kwa utukufu na uzuri.+ 41 Na kwa vitu hivyo wewe utamvika Haruni ndugu yako na wanawe pamoja naye, nawe utawatia mafuta+ na kuijaza mikono yao nguvu+ na kuwatakasa, nao watakuwa makuhani kwangu. 42 Na uwafanyie suruali za kitani ili kuufunika mwili ulio uchi.+ Zianzie kiunoni mpaka kwenye mapaja. 43 Nazo zitavaliwa na Haruni na wanawe wanapoingia kwenye hema la mkutano au wanapoenda karibu na madhabahu ili kuhudumu katika mahali patakatifu, ili wasifanye kosa na kufa hakika. Ni sheria mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili yake na uzao wake baada yake.+

29 “Na hili ndilo jambo utakalowafanyia ili kuwatakasa wapate kuwa makuhani kwangu: Mchukue ng’ombe-dume mchanga, na kondoo-dume wawili,+ wasio na kasoro,+ 2 na mkate usio na chachu na keki za mviringo zisizo na chachu, ambazo zimetiwa mafuta na mkate mwembamba usio na chachu, uliotiwa mafuta.+ Utavifanya kutokana na unga laini wa ngano. 3 Nawe utavitia kwenye kikapu na kuvitoa vikiwa ndani ya kikapu,+ hali kadhalika yule ng’ombe-dume na wale kondoo-dume wawili.

4 “Nawe utawaweka Haruni na wanawe kwenye mlango+ wa hema la mkutano, nawe utawaosha kwa maji.+ 5 Kisha utayachukua yale mavazi+ na kumvika Haruni kwa kanzu na koti lisilo na mikono la efodi na kwa efodi na kifuko cha kifuani, nawe utamfunga hicho kwa kukaza kwa mshipi wa efodi.+ 6 Nawe utakiweka kilemba juu ya kichwa chake na kuiweka ile ishara takatifu ya wakfu juu ya kilemba.+ 7 Nawe utachukua mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na kuyamimina+ juu ya kichwa chake na kumtia mafuta.+

8 “Ndipo utakapowaleta wanawe karibu, nawe utawavika kanzu.+ 9 Nawe utawafunga ukumbuu, Haruni pamoja na wanawe, nawe utawafunga valio la kichwani; nao ukuhani utakuwa wao, hiyo ikiwa ni sheria mpaka wakati usio na kipimo.+ Basi utajaza nguvu mkono wa Haruni na mkono wa wanawe.+

10 “Sasa utamtoa yule ng’ombe-dume mbele ya hema la mkutano, na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ng’ombe-dume.+ 11 Nawe utamchinja huyo ng’ombe-dume mbele za Yehova, kwenye mlango wa hema la mkutano.+ 12 Nawe utachukua sehemu ya damu+ ya huyo ng’ombe-dume na kuiweka kwa kidole chako juu ya zile pembe za madhabahu,+ na damu yote inayobaki utaimimina chini ya madhabahu.+ 13 Nawe utayachukua mafuta yote+ yanayofunika matumbo,+ na kile kipasho kilicho juu ya ini,+ na zile figo mbili na mafuta yaliyo juu yake, nawe utavifukiza juu ya madhabahu.+ 14 Lakini nyama ya ng’ombe-dume na ngozi yake na mavi yake utaviteketeza kwa moto nje ya kambi.+ Hilo ni toleo la dhambi.

15 “Kisha utamchukua kondoo-dume mmoja,+ naye Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.+ 16 Nawe utamchinja kondoo huyo na kuichukua damu yake na kuinyunyiza kuzunguka pande zote juu ya madhabahu.+ 17 Nawe utamkata kondoo huyo katika vipande vyake mbalimbali, na kuyaosha matumbo+ yake na miguu yake na kuviweka vipande vyake pamoja hata kichwa chake. 18 Nawe utamfukiza kondoo huyo mzima juu ya madhabahu. Hilo ni toleo la kuteketezwa+ kwa Yehova, harufu yenye kutuliza.+ Ni toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.

19 “Kisha utamchukua yule kondoo-dume mwingine, naye Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.+ 20 Nawe utamchinja kondoo huyo na kuchukua sehemu ya damu yake na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la Haruni na kwenye ncha ya sikio la kuume la wanawe na kwenye kidole gumba cha mkono wao wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha mguu wao wa kuume,+ nawe utainyunyiza damu hiyo kuzunguka pande zote juu ya madhabahu. 21 Nawe utachukua sehemu ya damu hiyo iliyo kwenye madhabahu na sehemu ya mafuta yanayotumiwa kutia mafuta,+ nawe utayatapanya juu ya Haruni na mavazi yake na juu ya wanawe na mavazi ya wanawe walio pamoja naye, ili yeye na mavazi yake na wanawe na mavazi ya wanawe walio pamoja naye yapate kuwa matakatifu kwelikweli.+

22 “Nawe utachukua kutoka kwa kondoo-dume huyo mafuta na ule mkia mnono+ na yale mafuta yanayofunika matumbo, na kipasho cha ini, na zile figo mbili na mafuta yaliyo juu yake, na mguu wa kuume,+ kwa maana huyo ni kondoo wa kuweka rasmi;+ 23 Pia mkate wa mviringo na keki ya mviringo ya mkate uliotiwa mafuta na mkate mwembamba kutoka katika kile kikapu cha keki zisizo na chachu kilicho mbele za Yehova.+ 24 Nawe utaviweka vyote hivyo kwenye mikono ya Haruni na kwenye mikono ya wanawe,+ nawe utavitikisa huku na huku vikiwa toleo la kutikisa mbele za Yehova.+ 25 Nawe utavichukua kutoka katika mikono yao na kuvifukiza juu ya madhabahu juu ya toleo la kuteketezwa viwe harufu ya kutuliza mbele za Yehova.+ Ni toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.+

26 “Nawe utachukua kidari cha yule kondoo-dume wa kuweka rasmi,+ aliye wa Haruni, na kukitikisa huku na huku kikiwa toleo la kutikisa mbele za Yehova, nacho kitakuwa fungu lako. 27 Nawe utakitakasa kidari+ cha toleo la kutikisa na ule mguu wa fungu takatifu ambao ulitikiswa na ambao ulichangiwa kutoka katika yule kondoo-dume wa kuweka rasmi,+ kutoka katika kile kilichokuwa cha Haruni na kutoka katika kile kilichokuwa cha wanawe. 28 Nacho kitakuwa cha Haruni na wanawe kulingana na sharti mpaka wakati usio na kipimo, litakalofanywa na wana wa Israeli, kwa sababu hicho ni fungu takatifu;+ nacho kitakuwa fungu takatifu litakalotolewa na wana wa Israeli. Kutoka katika dhabihu zao za ushirika+ hilo ndilo fungu lao takatifu kwa Yehova.

29 “Nayo mavazi matakatifu+ yaliyo ya Haruni yatatumiwa na wanawe+ baada yake ili kuwatia mafuta+ wakiwa wameyavaa na kuijaza mikono yao nguvu wakiwa wameyavaa.+ 30 Kuhani atakayechukua mahali pake kutoka kati ya wanawe na atakayeingia katika hema la mkutano ili kuhudumu katika mahali patakatifu atayavaa kwa siku saba.+

31 “Nawe utamchukua yule kondoo-dume wa kuweka rasmi, nawe utaitokosa nyama yake katika mahali patakatifu.+ 32 Naye Haruni na wanawe wataila+ nyama ya kondoo huyo na mkate ulio katika kikapu kwenye mlango wa hema la mkutano. 33 Nao watakula vitu ambavyo vimetumiwa kufanya upatanisho ili kuijaza mikono yao nguvu, ili kuwatakasa.+ Lakini mgeni asivile, kwa maana ni vitakatifu.+ 34 Na ikiwa nyama yoyote ya dhabihu ya kuweka rasmi na mkate wowote utabaki mpaka asubuhi, basi utateketeza kwa moto kitakachobaki.+ Kisiliwe, kwa sababu ni kitu kitakatifu.

35 “Nawe utamfanyia Haruni na wanawe hivyo kulingana na yote ambayo nimekuamuru wewe.+ Utachukua siku saba ili kuijaza mikono yao nguvu.+ 36 Nawe utamtoa ng’ombe-dume wa toleo la dhambi kila siku kwa ajili ya upatanisho,+ nawe utaitakasa madhabahu kutokana na dhambi kwa kufanya upatanisho juu yake, nawe utaitia mafuta+ ili kuitakasa. 37 Utachukua siku saba kufanya upatanisho juu ya madhabahu, nawe utaitakasa+ ili iwe madhabahu takatifu zaidi.+ Mtu yeyote atakayegusa madhabahu hiyo atakuwa mtakatifu.+

38 “Na hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu hiyo: wana-kondoo dume kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja, wawili kila siku daima.+ 39 Nawe utamtoa mwana-kondoo dume mmoja asubuhi,+ na kumtoa yule mwana-kondoo dume mwingine kati ya zile jioni mbili.+ 40 Na sehemu ya kumi ya kipimo cha efa ya unga laini+ uliotiwa sehemu ya nne ya hini ya mafuta yaliyopondwa, na toleo la kinywaji+ la sehemu ya nne ya hini ya divai, vitatolewa kwa ajili ya yule mwana-kondoo dume wa kwanza. 41 Nawe utamtoa yule mwana-kondoo dume wa pili kati ya zile jioni mbili. Pamoja na toleo la nafaka+ kama lile la asubuhi na pamoja na toleo la kinywaji kama lake, utamtoa awe harufu ya kutuliza, toleo linalotolewa kwa Yehova kwa njia ya moto. 42 Ni toleo la daima+ la kuteketezwa katika vizazi vyenu vyote kwenye mwingilio wa hema la mkutano mbele za Yehova, ambapo nitajitokeza kwenu ili kusema nanyi hapo.+

43 “Nami nitajitokeza hapo kwa wana wa Israeli, napo hakika patatakaswa kwa utukufu wangu.+ 44 Nami nitalitakasa hema la mkutano na madhabahu; nami nitamtakasa+ Haruni na wanawe ili wawe makuhani kwangu. 45 Nami nitakaa katikati ya wana wa Israeli, nami nitakuwa Mungu wao.+ 46 Nao hakika watajua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao, aliyewatoa katika nchi ya Misri ili nikae kati yao.+ Mimi ni Yehova Mungu wao.+

30 “Nawe utafanya madhabahu iwe mahali pa kufukizia uvumba;+ utaifanya kwa mbao za mshita. 2 Urefu wa mkono mmoja na upana wa mkono mmoja, itakuwa mraba, nacho kimo chake kitakuwa mikono miwili. Pembe zake zikiwa zimechomoka kutoka kwake.+ 3 Nawe utaifunika kwa dhahabu safi, sehemu yake ya juu na sehemu zake za kando kuzunguka pande zote na pembe zake; nawe utaifanyia ukingo wa dhahabu kuzunguka pande zote.+ 4 Pia utaifanyia pete mbili za dhahabu. Chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili utazifanya, kwenye pande zake mbili zinazoelekeana, kwa kuwa zitakuwa za kutegemeza ile miti ya kuibebea.+ 5 Nawe utafanya miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.+ 6 Nawe utaiweka mbele ya pazia lililo karibu na sanduku la ushuhuda,+ mbele ya kifuniko kilicho juu ya ule Ushuhuda, mahali ambapo nitajitokeza kwako.+

7 “Naye Haruni atafukiza+ uvumba uliotiwa manukato+ juu yake. Asubuhi kwa asubuhi, anapotayarisha taa,+ ataufukiza.⁠ 8 Naye Haruni anapowasha taa katikati ya zile jioni mbili, ataufukiza. Ni uvumba wa daima mbele za Yehova katika vizazi vyenu vyote. 9 Hamtatoa juu yake uvumba haramu+ au toleo la kuteketezwa au toleo la nafaka; wala hamtamimina toleo la kinywaji juu yake. 10 Naye Haruni atafanya upatanisho juu ya pembe zake mara moja kwa mwaka.+ Kwa sehemu ya damu ya toleo la dhambi+ la upatanisho ataifanyia upatanisho mara moja kwa mwaka katika vizazi vyenu. Ni takatifu zaidi kwa Yehova.”

11 Na Yehova akaendelea kunena na Musa, na kusema: 12 “Wakati wowote unapowahesabu wana wa Israeli,+ basi kila mmoja wao atamtolea Yehova fidia kwa ajili ya nafsi yake wakati wa kuhesabiwa kwao,+ ili kusiwe na pigo juu yao wakati wa kuhesabiwa kwao.+ 13 Hiki ndicho watakachotoa wale wote wanaopita kwa wale waliohesabiwa: nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.+ Gera 20 zinatoshana na shekeli moja. Nusu shekeli ndio mchango kwa Yehova.+ 14 Kila mtu anayepita kuingia upande wa wale walioandikishwa kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi atatoa mchango wa Yehova.+ 15 Tajiri asitoe zaidi, naye mtu wa hali ya chini asitoe kidogo kuliko hiyo nusu shekeli,+ kusudi amtolee Yehova mchango ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu.+ 16 Nawe utachukua pesa za fedha za upatanisho kutoka kwa wana wa Israeli na kuzitoa kwa ajili ya utumishi wa hema la mkutano,+ ili kwa kweli uwe ukumbusho mbele za Yehova na wana wa Israeli, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu.”

17 Naye Yehova akazidi kusema na Musa, na kumwambia: 18 “Utafanya beseni ya shaba na kinara chake cha shaba, ya kuoshea,+ nawe utaiweka kati ya hema la mkutano na ile madhabahu na kutia maji ndani yake.+ 19 Naye Haruni na wanawe wataosha mikono yao na miguu yao kwenye beseni hiyo.+ 20 Wanapoingia kwenye hema la mkutano wataoga kwa maji wasije wakafa, au wanapoenda karibu na madhabahu kuhudumia ili kumfukizia Yehova toleo linalotolewa kwa njia ya moto.+ 21 Nao wataosha mikono yao na miguu yao wasije wakafa,+ nalo litakuwa ni sharti kwao mpaka wakati usio na kipimo, kwake yeye na uzao wake katika vizazi vyao vyote.”+

22 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 23 “Wewe nawe, jichukulie manukato bora zaidi:+ vipimo 500 vya matone ya manemane+ iliyoganda, na mdalasini+ wenye harufu tamu nusu ya kiasi hicho, vipimo 250, na kane+ yenye harufu tamu, vipimo 250, 24 na kida,+ vipimo 500 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu,+ na mafuta ya zeituni, hini moja.+ 25 Kisha utafanya kutokana nayo mafuta matakatifu ya kutia mafuta, marhamu, mchanganyiko wa kazi ya mtengenezaji wa marhamu.+ Yatakuwa mafuta matakatifu ya kutia mafuta.+

26 “Nawe utayatumia kutia mafuta lile hema la mkutano+ na lile sanduku la ushuhuda, 27 na ile meza na vyombo vyake vyote na kile kinara na vyombo vyake na ile madhabahu ya uvumba, 28 na ile madhabahu ya toleo la kuteketezwa na vyombo vyake vyote na ile beseni pamoja na kinara chake. 29 Nawe utavitakasa ili kwa kweli viwe vitakatifu zaidi.+ Yeyote atakayevigusa atakuwa mtakatifu.+ 30 Nawe utamtia mafuta Haruni+ na wanawe,+ nawe utawatakasa watende wakiwa makuhani kwangu.+

31 “Nawe utanena na wana wa Israeli, na kusema, ‘Haya yataendelea kuwa kwangu mafuta matakatifu ya kutia mafuta, wakati wa vizazi vyenu vyote.+ 32 Hayatapakwa kwenye ngozi ya mwanadamu, na kwa mchanganyiko wake usifanye mengine yoyote kama hayo. Ni kitu kitakatifu. Yataendelea kuwa kitu kitakatifu kwenu. 33 Mtu yeyote anayetengeneza marhamu kama hayo na kumtia mgeni sehemu ya mafuta hayo atakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake.’”+

34 Naye Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Jichukulie manukato:+ matone ya natafi na shekelethi na kelbena iliyotiwa manukato na ubani+ safi. Kutakuwa na kipimo kimoja cha kila moja. 35 Nawe utayafanya yawe uvumba,+ mchanganyo wa viungo, kazi ya mtengenezaji wa marhamu, uliotiwa chumvi,+ safi, kitu kitakatifu. 36 Nawe utaponda sehemu yake iwe unga laini na kutia kiasi chake fulani mbele ya ule Ushuhuda katika hema la mkutano,+ nitakapojitokeza kwako.+ Yatakuwa matakatifu zaidi kwenu. 37 Nao uvumba ambao wewe utaufanya kwa mchanganyiko huo, ninyi hampaswi kuufanya kwa ajili yenu wenyewe.+ Kwa ajili yenu utaendelea kuwa kitu kitakatifu kwa Yehova.+ 38 Yeyote atakayefanya wowote ulio kama huo ili kufurahia harufu yake atakatiliwa mbali+ kutoka kwa watu wake.”

31 Naye Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumwambia: 2 “Ona, ninamwita kwa jina Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda.+ 3 Nami nitamjaza roho ya Mungu katika hekima na katika uelewaji na katika ujuzi na katika kila aina ya ufundi,+ 4 kwa ajili ya kubuni vyombo, kwa ajili ya kufanya kazi ya dhahabu na fedha na shaba,+ 5 na katika kazi ya mawe ili kuyapamba+ na katika kazi ya mbao ili kufanya kila aina ya vifaa.+ 6 Mimi nami, tazama! Ninamweka pamoja naye Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani,+ na katika moyo wa kila mwenye hekima ninaweka hekima, ili kwa kweli wapate kufanya kila kitu ambacho nimekuamuru:+ 7 lile hema la mkutano+ na lile Sanduku+ kwa ajili ya ushuhuda na kifuniko kilicho juu yake,+ na vyombo vyote vya lile hema, 8 na ile meza na vyombo vyake,+ na kile kinara cha dhahabu safi na vyombo vyake vyote,+ na ile madhabahu ya uvumba,+ 9 na ile madhabahu ya toleo la kuteketezwa na vyombo vyake vyote,+ na ile beseni na kinara chake,+ 10 na yale mavazi yaliyofumwa na yale mavazi matakatifu kwa ajili ya Haruni kuhani na yale mavazi ya wanawe kwa ajili ya kutenda wakiwa makuhani;+ 11 na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba uliotiwa manukato kwa ajili ya patakatifu.+ Kulingana na kila jambo ambalo nimekuamuru, watafanya.”

12 Naye Yehova akazidi kusema na Musa: 13 “Wewe nawe, nena na wana wa Israeli, na kusema, ‘Hasa sabato zangu, mtazishika,+ kwa maana ni ishara kati yangu na ninyi katika vizazi vyenu ili mpate kujua kwamba mimi Yehova ninawatakasa ninyi.+ 14 Nanyi lazima mwishike sabato, kwa maana ni kitu kitakatifu kwenu.+ Mtu atakayeinajisi hakika atauawa.+ Ikiwa mtu yeyote atafanya kazi siku hiyo, basi nafsi hiyo itakatiliwa mbali toka katikati ya watu wake.+ 15 Siku sita kazi inaweza kufanywa, lakini siku ya saba ni sabato ya pumziko kamili.+ Ni kitu kitakatifu kwa Yehova. Mtu yeyote atakayefanya kazi siku ya sabato hakika atauawa. 16 Nao wana wa Israeli lazima waishike sabato, ili kuitimiza sabato katika vizazi vyao. Ni agano mpaka wakati usio na kipimo.+ 17 Kati yangu na wana wa Israeli ni ishara mpaka wakati usio na kipimo,+ kwa sababu katika siku sita Yehova alizifanya mbingu na dunia na katika siku ya saba alipumzika naye akaanza kujiburudisha.’”+

18 Sasa mara tu alipomaliza kusema naye kwenye Mlima Sinai alimpa Musa mabamba mawili ya ule Ushuhuda,+ mabamba ya mawe ambayo juu yake yaliandikwa kwa kidole cha Mungu.+

32 Wakati huo watu wakaona kwamba Musa alikuwa akichukua muda mrefu kushuka kutoka mlimani.+ Basi watu wakakutanika kumzunguka Haruni na kumwambia: “Simama, tufanyie mungu atakayeenda mbele yetu,+ kwa sababu huyo Musa, yule mtu aliyetuongoza kutoka katika nchi ya Misri,+ hakika hatujui lililompata.” 2 Basi Haruni akawaambia: “Ng’oeni vipuli vya dhahabu+ vilivyo katika masikio ya wake zenu, ya wana wenu na ya binti zenu mniletee.” 3 Nao watu wote wakaanza kung’oa vipuli vya dhahabu vilivyokuwa katika masikio yao na kuvileta kwa Haruni. 4 Kisha akaichukua dhahabu hiyo toka mikononi mwao, naye akaifanya+ kwa kifaa cha kuchongea na kuifanya kuwa sanamu ya kuyeyushwa ya ndama.+ Nao wakaanza kusema: “Huyu ndiye Mungu wako, Ee Israeli, aliyekuongoza kutoka nchi ya Misri.”+

5 Haruni alipoona hilo, akajenga madhabahu mbele yake. Mwishowe Haruni akatangaza na kusema: “Kutakuwa na sherehe kwa ajili ya Yehova kesho.” 6 Basi siku iliyofuata wakaamka mapema, nao wakaanza kutoa matoleo ya kuteketezwa na kutoa dhabihu za ushirika. Baada ya hayo watu wakaketi ili wale na kunywa. Kisha wakasimama wapate kujifurahisha.+

7 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Nenda, shuka, kwa sababu watu wako ambao uliwaongoza kutoka nchi ya Misri wametenda kwa uharibifu.+ 8 Wamegeuka kando haraka kutoka katika njia niliyowaamuru waende.+ Wamejifanyia sanamu ya kuyeyushwa ya ndama na wanaendelea kuiinamia na kuitolea dhabihu na kusema, ‘Huyu ndiye Mungu wako, Ee Israeli, aliyekuongoza kutoka nchi ya Misri.’”+ 9 Naye Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Nimewatazama watu hawa na, kumbe, ni watu wenye shingo ngumu.+ 10 Basi sasa, niache, ili hasira yangu iwake juu yao nami niwaangamize,+ nami nikufanye wewe kuwa taifa kubwa.”+

11 Naye Musa akaanza kuutuliza uso wa Yehova Mungu+ wake na kusema: “Kwa nini, Ee Yehova, hasira+ yako iwake juu ya watu wako ambao uliwatoa katika nchi ya Misri kwa nguvu kuu na kwa mkono wenye nguvu? 12 Kwa nini Wamisri+ waseme, ‘Aliwatoa kwa nia mbaya ili awaue katikati ya milima na kuwaangamiza kutoka katika uso wa nchi’?+ Geukia mbali uiache hasira yako inayowaka+ na ujute+ kuhusu uovu huo juu ya watu wako. 13 Wakumbuke Abrahamu, Isaka na Israeli watumishi wako, uliowaapia kwa jina lako mwenyewe,+ kwa kuwa uliwaambia, ‘nitauzidisha uzao wenu kama nyota za mbinguni,+ nayo nchi hii yote ambayo nimeichagua, nitaupa uzao+ wenu, ili kwa kweli wapate kuimiliki mpaka wakati usio na kipimo.’”+

14 Naye Yehova akaanza kujuta juu ya ule uovu aliokuwa amesema kwamba atawafanyia watu wake.+

15 Kisha Musa akageuka na kushuka kutoka mlimani+ akiwa na yale mabamba mawili ya Ushuhuda+ mkononi mwake, mabamba yaliyoandikwa pande zote mbili. Yaliandikwa upande huu na upande ule. 16 Nayo mabamba hayo yalikuwa kazi ya Mungu, nayo maandishi yalikuwa maandishi ya Mungu yaliyochongwa juu ya mabamba hayo.+ 17 Naye Yoshua akaanza kuzisikia kelele za watu kwa sababu ya kupaaza kwao sauti, naye akamwambia Musa: “Kuna kelele za pigano+ kambini.” 18 Lakini akasema:

“Si sauti ya kuimba kwa sababu ya tendo lenye nguvu,+

Wala si sauti ya kuimba kwa sababu ya kushindwa;

Ni sauti ya uimbaji mwingine ninayoisikia.”

19 Basi ikawa kwamba mara tu alipoikaribia kambi naye akaweza kuiona ile ndama+ na zile dansi, hasira ya Musa ikaanza kuwaka, naye akayatupa mara moja yale mabamba mawili kutoka mkononi mwake na kuyavunja-vunja chini ya mlima.+ 20 Kisha akaichukua ile ndama waliyokuwa wameifanya naye akaiteketeza kwa moto na kuipondaponda mpaka ikawa laini,+ kisha akaitawanya juu ya maji+ na kuwalazimisha wana wa Israeli wanywe.+ 21 Kisha Musa akamwambia Haruni: “Watu hawa walikufanya nini hivi kwamba umeleta dhambi kubwa juu yao?” 22 Basi Haruni akasema: “Hasira ya bwana wangu isiwake. Wewe mwenyewe unawajua vema watu hawa, ya kwamba wana mwelekeo mwovu.+ 23 Basi waliniambia, ‘Tufanyie mungu atakayeenda mbele yetu,+ kwa sababu huyo Musa, yule mtu aliyetuongoza kutoka katika nchi ya Misri, hakika hatujui lililompata.’ 24 Basi nikawaambia, ‘Ni nani walio na dhahabu yoyote? Waing’oe kutoka kwao wanipe.’ Nami nikaitupa motoni na ndama hii ikatokea.”

25 Naye Musa akaona kwamba watu walikuwa wamejiachilia, kwa sababu Haruni alikuwa amewaachilia+ ili kuwa fedheha kati ya wapinzani wao.+ 26 Kisha Musa akasimama katika lango la kambi na kusema: “Ni nani aliye upande wa Yehova? Na aje kwangu!”+ Nao wana wote wa Lawi wakaanza kujikusanya kwake. 27 Sasa akawaambia: “Hivi ndivyo Yehova Mungu wa Israeli amesema, ‘Kila mmoja wenu na auweke upanga wake kwenye paja lake. Piteni kati na kurudi toka lango mpaka lango katika kambi na kuua kila mtu ndugu yake na kila mtu mwenzake na kila mtu rafiki yake.’”+ 28 Nao wana wa Lawi+ wakafanya kama vile Musa alivyokuwa amesema, hivi kwamba walianguka kati ya watu siku hiyo watu wapatao elfu tatu. 29 Naye Musa akasema: “Ujazeni mkono wenu leo nguvu kwa ajili ya Yehova,+ kwa sababu kila mmoja wenu yuko dhidi ya mwana wake mwenyewe na ndugu+ yake mwenyewe, na kwamba apate kuweka baraka juu yenu leo.”+

30 Na ikawa kwamba siku ileile iliyofuata, Musa akawaambia watu: “Ninyi—ninyi mmetenda dhambi kubwa,+ na sasa nitapanda kwenda kwa Yehova. Huenda nitaweza kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.”+ 31 Basi Musa akarudi kwa Yehova, akasema: “Ah, watu hawa wametenda dhambi kubwa, kwa kuwa wamejifanyia mungu wa dhahabu!+ 32 Lakini sasa ikiwa utasamehe dhambi yao,+—na ikiwa sivyo, nifute,+ tafadhali, kutoka katika kitabu+ chako ambacho umeandika.” 33 Hata hivyo, Yehova akamwambia Musa: “Yeyote ambaye amenitendea dhambi, nitamfutilia mbali kutoka katika kitabu changu.+ 34 Na sasa, njoo, waongoze watu kwenda mahali nilipokuambia juu yake. Tazama! Malaika wangu ataenda mbele yako,+ na siku ile nitakayoleta adhabu hakika mimi nitaleta adhabu juu yao kwa sababu ya dhambi yao.”+ 35 Naye Yehova akaanza kuwaletea watu hao pigo kwa sababu walikuwa wameifanya ile ndama, ambayo Haruni alikuwa ameifanya.+

33 Na Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Nenda, ondoka hapa, wewe na watu uliowaongoza kutoka nchi ya Misri,+ mpaka kwenye nchi ambayo nilimwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo, na kusema, ‘Nitaupa uzao wako.’+ 2 Nami nitamtuma malaika mbele yako+ na kuwafukuza Wakanaani, Waamori, na Wahiti na Waperizi, Wahivi na Wayebusi;+ 3 kwenye nchi inayotiririka maziwa na asali,+ kwa maana sitaenda katikati yenu, kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu,+ nisije nikawaangamiza njiani.”+

4 Watu waliposikia neno hilo baya, wakaanza kuomboleza;+ wala hakuna yeyote kati yao aliyevaa mapambo yake. 5 Na Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Waambie wana wa Israeli, ‘Ninyi ni watu wenye shingo ngumu.+ Kwa kitambo kidogo+ ningeweza kuingia katikati yenu na kuwaangamiza. Sasa vueni mapambo yenu myaweke chini, kwa maana nataka kujua jambo nitakalowatendea ninyi.’”+ 6 Na wana wa Israeli wakavua mapambo yao kuanzia Mlima Horebu+ na kuendelea.

7 Musa naye akalichukua hema lake na kulipiga nje ya kambi, mbali na kambi; naye akaliita hema la mkutano. Na ikawa kwamba yeyote aliyekuwa akiuliza+ habari kutoka kwa Yehova alikuwa akienda nje kwenye hema la mkutano, lililokuwa nje ya kambi. 8 Na ikatukia kwamba mara tu Musa alipoenda nje kwenye hema, watu wote waliinuka,+ nao wakasimama kila mmoja kwenye mlango wa hema lake mwenyewe, nao wakamtazama Musa mpaka alipoingia ndani ya hema. 9 Pia ikatukia kwamba mara tu Musa alipokuwa ameingia ndani ya hema, ile nguzo ya wingu+ ilishuka chini, nayo ikasimama kwenye mwingilio wa hema na yeye akasema+ na Musa. 10 Na watu wote wakaiona ile nguzo ya wingu+ ikisimama kwenye mwingilio wa hema, nao watu wote wakasimama na kuinama kila mmoja kwenye mwingilio wa hema lake mwenyewe.+ 11 Naye Yehova akasema na Musa uso kwa uso,+ kama vile mwanadamu anavyosema na mwenzake. Aliporudi kambini, mhudumu wake+ Yoshua, mwana wa Nuni,+ akiwa mtumishi, hakuwa akiondoka katikati ya hema.

12 Sasa Musa akamwambia Yehova: “Angalia, wewe unaniambia, ‘Waongoze watu hawa,’ lakini hujanijulisha yule ambaye utamtuma pamoja nami. Na zaidi ya hayo, wewe mwenyewe umesema, ‘Ninakujua wewe kwa jina+ na, mbali na hayo, umepata kibali machoni pangu.’ 13 Na sasa, tafadhali, ikiwa nimepata kibali machoni pako,+ nijulishe, tafadhali, njia zako,+ nipate kukujua, ili nipate kibali machoni pako. Na ukumbuke kwamba taifa hili ni watu wako.”+ 14 Basi akasema: “Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe+ nami hakika nitakupa wewe pumziko.”+ 15 Ndipo akamwambia: “Ikiwa wewe mwenyewe hutakwenda pamoja nami, usituongoze kutoka hapa. 16 Na sasa itajulikana jinsi gani kwamba nimepata kibali machoni pako, mimi na watu wako? Je, si kwa wewe kwenda pamoja nasi,+ kwa kuwa mimi na watu wako tumefanywa tofauti na watu wengine wote walio juu ya uso wa nchi?”+

17 Naye Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Jambo hili, pia, ambalo umesema, nitalifanya,+ kwa sababu wewe umepata kibali machoni pangu nami nakujua wewe kwa jina.” 18 Ndipo akasema: “Nionyeshe, tafadhali, utukufu wako.”+ 19 Lakini akasema: “Mimi mwenyewe nitaupitisha wema wangu wote mbele ya uso wako,+ nami nitalitangaza jina la Yehova mbele yako;+ nami nitamwonyesha kibali yeyote ambaye ninataka kumwonyesha kibali, nami nitamwonyesha rehema yeyote ambaye ninataka kumwonyesha rehema.”+ 20 Naye akaongezea: “Huwezi kuuona uso wangu, kwa sababu hakuna mwanadamu anayeweza kuniona na bado aishi.”+

21 Naye Yehova akazidi kusema: “Tazama, pana mahali kando yangu, nawe utasimama juu ya mwamba. 22 Na itakuwa kwamba utukufu wangu utakapokuwa ukipita nitakutia katika shimo ndani ya mwamba, nami nitaweka mkono wangu juu yako uwe kisitiri mpaka niwe nimepita. 23 Kisha nitauondoa mkono wangu, nawe kwa kweli utauona mgongo wangu. Lakini uso wangu hautaonekana.”+

34 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Jichongee mabamba mawili ya mawe kama yale ya kwanza,+ nami nitaandika juu ya mabamba hayo maneno yaliyokuwa kwenye yale mabamba ya kwanza,+ ambayo uliyavunja-vunja.+ 2 Nawe ujitayarishe kwa ajili ya asubuhi, kwa kuwa asubuhi utapanda Mlima Sinai na kusimama kando yangu huko juu ya mlima.+ 3 Lakini mtu yeyote asipande pamoja nawe, na pia, mtu mwingine yeyote asionekane kotekote katika mlima.+ Tena, kundi lolote wala mifugo yoyote isilishe mbele ya mlima huo.”+

4 Basi Musa akachonga mabamba mawili ya mawe kama yale ya kwanza na kuamka asubuhi na mapema, akaenda juu katika Mlima Sinai, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru, naye alikuwa ameyachukua yale mabamba mawili ya mawe mikononi mwake. 5 Naye Yehova akashuka+ katika wingu, akasimama huko pamoja naye na kulitangaza jina la Yehova.+ 6 Na Yehova akapita karibu mbele ya uso wake na kutangaza: “Yehova, Yehova, Mungu mwenye rehema+ na neema,+ si mwepesi wa hasira+ naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo+ na kweli,+ 7 anayehifadhi fadhili zenye upendo kwa ajili ya maelfu,+ anayesamehe kosa na ubaya na dhambi,+ lakini kwa vyovyote hatakosa kuadhibu,+ anayeleta adhabu kwa ajili ya kosa la akina baba juu ya wana na juu ya wajukuu, juu ya kizazi cha tatu na juu ya kizazi cha nne.”+

8 Mara moja Musa akafanya haraka kuinama chini na kusujudu.+ 9 Kisha akasema: “Ikiwa, sasa, nimepata kibali machoni pako, Ee Yehova, tafadhali, Yehova na aende pamoja nasi katikati yetu,+ kwa sababu ni watu wenye shingo ngumu,+ nawe utusamehe kosa letu na dhambi yetu,+ nawe utuchukue tuwe mali yako.”+ 10 Naye akasema: “Tazama, ninafanya agano: Mbele ya watu wako wote nitafanya mambo ya ajabu ambayo hayajapata kuumbwa kamwe katika dunia yote wala kati ya mataifa yote;+ na watu wote ambao unakaa katikati yao kwa kweli wataiona kazi ya Yehova, kwa sababu ni jambo lenye kuogopesha ambalo ninakutendea.+

11 “Wewe kwa upande wako shika ninalokuamuru leo.+ Tazama, ninawafukuza toka mbele yako Waamori na Wakanaani na Wahiti na Waperizi na Wahivi na Wayebusi.+ 12 Jiangalie usije ukafanya agano pamoja na wakaaji wa nchi hiyo unayoiendea,+ isije ikawa mtego katikati yako.+ 13 Lakini madhabahu zao mtazibomoa, nazo nguzo zao takatifu mtazivunja, nayo miti yao mitakatifu mtaikata.+ 14 Kwa maana hutamsujudia mungu mwingine,+ kwa sababu Yehova, ambaye jina lake ni Wivu, yeye ni Mungu mwenye wivu;+ 15 usije ukafanya agano na wakaaji wa nchi hiyo, kwa maana hakika watafanya uasherati na miungu+ yao na kutolea miungu yao dhabihu,+ na mtu fulani hakika atakualika, nawe hakika utakula sehemu ya dhabihu yake.+ 16 Ndipo utakapolazimika kuwachukua baadhi ya binti zao kwa ajili ya wana wako,+ na binti zao hakika watafanya uasherati na miungu yao na kuwafanya wana wako wafanye uasherati na miungu yao.+

17 “Usijifanyie miungu ya sanamu ya kuyeyushwa.+

18 “Sherehe ya keki zisizo na chachu utaishika.+ Utakula keki zisizo na chachu, kama vile nilivyokuamuru, siku saba kwenye ule wakati uliowekwa katika mwezi wa Abibu,+ kwa sababu ni katika mwezi wa Abibu kwamba ulitoka Misri.

19 “Kila kitu ambacho kinafungua kwanza tumbo la uzazi ni changu,+ nayo mifugo yako yote, mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe-dume na wa kondoo.+ 20 Naye mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa kondoo.+ Lakini ikiwa hutamkomboa, basi utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza wa wana wako utamkomboa.+ Nao wasionekane mbele zangu mikono mitupu.+

21 “Siku sita utafanya kazi, bali siku ya saba utaishika sabato.+ Wakati wa kulima na wakati wa kuvuna utaishika sabato.+

22 “Nawe utaiendeleza sherehe yako ya majuma kwa matunda ya kwanza yaliyoiva ya mavuno ya ngano,+ na sherehe ya kukusanya mwishoni mwa mwaka.+

23 “Mara tatu katika mwaka kila mwanamume wa kwako ataonekana+ mbele za Bwana wa kweli, Yehova, Mungu wa Israeli. 24 Kwa maana nitayafukuzia mbali mataifa toka mbele yako,+ nami nitalipanua eneo lako;+ wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati utakapokuwa ukienda kuuona uso wa Yehova Mungu wako mara tatu kwa mwaka.+

25 “Usichinje, pamoja na kitu kilicho na chachu, damu ya dhabihu yangu.+ Nayo dhabihu ya sherehe ya pasaka isikae usiku kucha mpaka asubuhi.+

26 “Matunda ya kwanza yaliyoiva yaliyo bora+ zaidi ya udongo wako utayaleta kwenye nyumba ya Yehova Mungu wako.+

“Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”+

27 Naye Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Jiandikie maneno haya,+ kwa sababu ninafanya agano pamoja nawe na Israeli kupatana na maneno haya.”+ 28 Naye akaendelea kuwa huko pamoja na Yehova siku 40, mchana na usiku. Hakula mkate wala hakunywa maji.+ Naye akaandika juu ya yale mabamba maneno ya lile agano, yale Maneno Kumi.+

29 Sasa ikawa kwamba Musa alipoteremka kutoka katika Mlima Sinai, yale mabamba mawili ya Ushuhuda yalikuwa mkononi mwa Musa aliposhuka kutoka mlimani,+ naye Musa hakujua kwamba ngozi ya uso wake ilikuwa ikitoa miale kwa sababu alikuwa amesema naye.+ 30 Haruni na wana wote wa Israeli walipomwona Musa, lo, tazama! ngozi ya uso wake ilitoa miale nao wakaogopa kumkaribia.+

31 Naye Musa akawaita. Basi Haruni na wakuu wote katikati ya kusanyiko wakarudi kwake, na Musa akaanza kusema nao. 32 Mara baada ya hapo wana wote wa Israeli wakamkaribia, naye akaanza kuwaamuru mambo yote ambayo Yehova alikuwa amesema naye juu ya Mlima Sinai.+ 33 Musa alipomaliza kusema nao, alikuwa akiweka utaji juu ya uso wake.+ 34 Lakini Musa alipokuwa akiingia ndani mbele za Yehova kusema naye, alikuwa akiutoa utaji mpaka wakati wa kutoka kwake nje.+ Naye akatoka nje na kusema na wana wa Israeli mambo aliyokuwa akiamriwa.+ 35 Nao wana wa Israeli wakauona uso wa Musa, kwamba ngozi ya uso wa Musa ilitoa miale;+ naye Musa akaurudisha utaji juu ya uso wake mpaka alipoingia ndani kusema naye.+

35 Baadaye Musa akaita kusanyiko lote la wana wa Israeli na kuwaambia: “Haya ndiyo maneno ambayo Yehova ameamuru yafanywe:+ 2 Siku sita kazi inaweza kufanywa,+ lakini siku ya saba itakuwa kitu kitakatifu kwenu, sabato ya pumziko kamili kwa Yehova. Mtu yeyote anayefanya kazi siku hiyo atauawa.+ 3 Msiwashe moto katika makao yenu yoyote katika siku ya sabato.”

4 Naye Musa akaendelea kusema na kusanyiko lote la wana wa Israeli: “Hili ndilo neno ambalo Yehova ameamuru, na kusema, 5 ‘Kutoka katikati yenu toeni mchango kwa ajili ya Yehova.+ Kila mtu mwenye moyo wenye nia+ na aulete ukiwa mchango wa Yehova, yaani, dhahabu na fedha na shaba+ 6 na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora na manyoya ya mbuzi+ 7 na ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu na ngozi za sili na mbao za mshita 8 na mafuta kwa ajili ya mwanga na mafuta ya zeri kwa ajili ya mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na kwa ajili ya uvumba uliotiwa manukato+ 9 na mawe ya shohamu na mawe ya kupamba kwa ajili ya efodi+ na kwa ajili ya kifuko cha kifuani.+

10 “‘Na wote wenye moyo wa hekima+ katikati yenu na waje na kufanya yote ambayo Yehova ameamuru, 11 yaani, ile maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, kulabu zake na mbao zake za viunzi, miti yake, nguzo zake na vikalio vyake; 12 lile Sanduku+ na miti+ yake, kifuniko+ na pazia+ la kisitiri; 13 ile meza+ na miti yake na vyombo vyake vyote na mkate wa wonyesho;+ 14 na kile kinara cha taa+ cha kuangaza na vyombo vyake na taa zake na yale mafuta+ ya kuangaza; 15 na ile madhabahu ya uvumba+ na miti yake; na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba uliotiwa manukato;+ na kile kisitiri cha mwingilio kwa ajili ya mwingilio wa maskani; 16 ile madhabahu+ ya toleo la kuteketezwa na kile kiunzi cha shaba kwa ajili yake, miti yake na vyombo vyake vyote; ile beseni+ na kinara chake; 17 yale mapazia ya ua,+ nguzo zake na vikalio vyake; na kile kisitiri cha lango la ua; 18 ile misumari ya hema la maskani na ile misumari ya hema la ua na kamba zake;+ 19 yale mavazi+ yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika patakatifu, yale mavazi matakatifu+ kwa ajili ya Haruni kuhani na yale mavazi ya wanawe kwa ajili ya kutenda wakiwa makuhani.’”

20 Basi kusanyiko lote la wana wa Israeli likaondoka mbele ya Musa. 21 Kisha wakaja, kila mtu ambaye moyo wake ulimsukuma,+ nao wakaleta, kila mtu ambaye roho yake ilimchochea, mchango wa Yehova kwa ajili ya kazi ya hema la mkutano na kwa ajili ya utumishi wake wote na kwa ajili ya yale mavazi matakatifu. 22 Nao wakaendelea kuja, wanaume pamoja na wanawake, kila mtu mwenye moyo wenye nia. Wakaleta bizimu na vipuli na pete na mapambo ya kike, aina zote za vyombo vya dhahabu, yaani, kila mtu aliyemtolea Yehova toleo la kutikisa la dhahabu.+ 23 Na wote waliokuwa na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora na manyoya ya mbuzi na ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu na ngozi za sili, wakaleta.+ 24 Wale wote wanaochanga mchango wa fedha na shaba wakaleta mchango wa Yehova, nao wale wote waliokuwa na mbao za mshita kwa ajili ya kazi yote ya utumishi wakazileta.

25 Na wanawake wote waliokuwa wenye hekima ya moyo+ wakasokota kwa mikono yao, nao wakawa wakileta nyuzi zilizosokotwa za ule uzi wa bluu na ile sufu iliyotiwa rangi ya zambarau, kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kile kitani bora. 26 Na wanawake wote ambao mioyo yao iliwasukuma kwa hekima wakasokota manyoya ya mbuzi.

27 Nao wakuu wakaleta mawe ya shohamu na mawe ya mapambo kwa ajili ya ile efodi na kile kifuko cha kifuani,+ 28 na yale mafuta ya zeri na yale mafuta ya kuangaza na ya kutia mafuta na ya uvumba uliotiwa manukato.+ 29 Kila mwanamume na kila mwanamke ambao mioyo yao iliwachochea kuleta kitu fulani kwa ajili ya kazi yote ambayo Yehova alikuwa ameamuru ifanywe kupitia kwa Musa akafanya hivyo; wana wa Israeli wakaleta toleo la hiari kwa Yehova.+

30 Kisha Musa akawaambia wana wa Israeli: “Tazama, Yehova amemwita kwa jina Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda. 31 Naye akamjaza roho ya Mungu katika hekima, katika uelewaji na katika ujuzi na katika kila aina ya ufundi 32 na kwa ajili ya kubuni vyombo, kwa ajili ya kazi ya dhahabu na fedha na shaba,+ 33 na katika kazi ya mawe ya kupambia na katika kazi ya mbao ili kufanya vifaa sanifu vya kila namna.+ 34 Naye ametia moyoni mwake apate kufundisha, yeye na Oholiabu+ mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani. 35 Amewajaza hekima ya moyo+ ili kufanya kazi yote ya fundi na ya mtarizi+ na ya mfumaji wa uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau, wa kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora, na ya mfumaji wa nguo, watu wanaofanya kila namna ya kazi na kubuni vyombo.

36 “Na Bezaleli atafanya kazi, pia Oholiabu+ na kila mtu mwenye moyo wa hekima ambaye Yehova amempa hekima+ na uelewaji+ wa mambo haya ili kujua jinsi ya kufanya kazi yote ya utumishi mtakatifu kulingana na yote ambayo Yehova ameamuru.”+

2 Naye Musa akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye moyo wa hekima ambaye Yehova alikuwa ametia hekima+ moyoni mwake, kila mtu ambaye moyo wake ulimsukuma kwenda kufanya kazi.+ 3 Kisha wakachukua toka mbele ya Musa michango+ yote ambayo wana wa Israeli walikuwa wameleta kwa ajili ya kazi ya utumishi mtakatifu ili kuifanya, na, hao wa mwisho, bado walimletea matoleo ya hiari asubuhi kwa asubuhi.

4 Na wote wenye hekima waliokuwa wakiifanya kazi yote takatifu wakaanza kuja, mtu mmoja baada ya mwingine, kutoka katika kazi yao waliyokuwa wakiifanya, 5 na kumwambia Musa: “Watu wanaleta vitu vingi zaidi kuliko vinavyohitajiwa kwa utumishi kwa ajili ya kazi ambayo Yehova ameamuru ifanywe.” 6 Basi Musa akaamuru kwamba tangazo litolewe kambini, na kusema: “Wanaume na wanawake, msitoe vitu zaidi kwa ajili ya mchango mtakatifu.” Basi watu wakazuiliwa wasilete. 7 Navyo vitu hivyo vikawa vya kutosha kwa ajili ya kazi yote iliyopasa kufanywa, na kuzidi.

8 Na wote wenye moyo wa hekima+ kati ya wale waliokuwa wakifanya kazi hiyo wakaifanya maskani,+ vile vitambaa kumi vya mahema vya kitani bora kilichosokotwa na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili; pamoja na makerubi, kazi ya mtarizi, akavifanya. 9 Urefu wa kila kitambaa cha hema ulikuwa mikono 28, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono 4. Vitambaa vyote hivyo vilikuwa na kipimo kimoja. 10 Kisha akaunganisha vitambaa vitano pamoja,+ na vile vitambaa vingine vitano akaviunganisha pamoja. 11 Kisha akafanya vitanzi vya uzi wa bluu kwenye upindo wa kitambaa kilicho mahali pa kuungania. Akafanya vivyo hivyo kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pale pengine pa kuungania.+ 12 Akafanya vitanzi 50 kwenye kitambaa kimoja, akafanya vitanzi 50 kwenye mwisho wa kitambaa kilichokuwa mahali pale pengine pa kuungania, vitanzi hivyo vikiwa vinaelekeana.+ 13 Mwishowe akafanya kulabu 50 za dhahabu na kuviunganisha vitambaa hivyo pamoja kwa kulabu hizo, hivi kwamba hiyo ikawa maskani moja.+

14 Naye akafanya vitambaa vya mahema vya manyoya ya mbuzi kwa ajili ya hema lililo juu ya maskani. Vitambaa kumi na moja ndivyo alivyofanyiza.+ 15 Urefu wa kila kitambaa ulikuwa mikono 30, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono 4. Vitambaa hivyo 11 vilikuwa na kipimo kimoja.+ 16 Kisha akaunganisha vitambaa vitano pamoja na vile vitambaa vingine sita pamoja.+ 17 Kisha akafanya vitanzi 50 kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pa kuungania, naye akafanya vitanzi 50 kwenye upindo wa kile kitambaa kingine kilichoungana nacho.+ 18 Kisha akafanya kulabu 50 za shaba kwa ajili ya kuliunganisha hilo hema pamoja liwe kipande kimoja.+

19 Naye akafanya kifuniko cha hema kutokana na ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko kutokana na ngozi za sili,+ upande wa juu.+

20 Kisha akafanya viunzi vya mbao vya maskani kutokana na mbao za mshita,+ vilivyosimama upande wa mwisho. 21 Urefu wa kiunzi ulikuwa mikono kumi, nao upana wa kila kiunzi ulikuwa mkono mmoja na nusu.+ 22 Kila kiunzi kilikuwa na ndimi mbili zilizounganishwa. Hivyo ndivyo alivyofanya viunzi vyote vya maskani.+ 23 Basi akafanya viunzi vya maskani, viunzi 20 kwa ajili ya upande unaoikabili Negebu, kuelekea kusini.+ 24 Naye akafanya vikalio 40 vya fedha viwe chini ya vile viunzi 20, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja pamoja na ndimi zake mbili na vikalio vingine viwili chini ya kiunzi kingine pamoja na ndimi zake mbili.+ 25 Na kwa ajili ya ule upande mwingine wa maskani, upande wa kaskazini, akafanya viunzi 20+ 26 na vikalio vyake 40 vya fedha, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja na vikalio viwili chini ya kiunzi kingine.+

27 Na kwa ajili ya zile pande za nyuma za maskani kuelekea magharibi akafanya viunzi sita.+ 28 Naye akafanya viunzi viwili viwe miimo ya pembeni ya maskani kwenye pande zake mbili za nyuma.+ 29 Nayo ilikuwa pacha upande wa chini nayo ikawa pacha mpaka juu ya kila moja kwenye pete ya kwanza. Hivyo ndivyo alivyoifanya yote miwili, ile miimo ya pembeni.+ 30 Basi vikajumlika kuwa viunzi vinane na vikalio vyake kumi na sita vya fedha, vikalio viwili kando ya vikalio viwili chini ya kila kiunzi.+

31 Naye akafanya miti ya mshita, mitano kwa ajili ya viunzi vya upande mmoja wa maskani+ 32 na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya upande ule mwingine wa maskani na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya maskani kwa ajili ya zile pande mbili za nyuma za magharibi.+ 33 Kisha akafanya mti wa katikati upitie katikati ya vile viunzi toka mwisho mmoja mpaka ule mwingine.+ 34 Naye akavifunika vile viunzi kwa dhahabu, akafanyiza pete zake za dhahabu ziwe vitegemezo kwa ajili ya ile miti, akaifunika ile miti kwa dhahabu.+

35 Naye akafanya pazia+ la uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa. Akalitia makerubi kwa kazi ya mtarizi.+ 36 Kisha akalifanyia nguzo nne za mshita na kuzifunika kwa dhahabu, vibanio vyake vikiwa vya dhahabu, na kutengeneza vikalio vinne vya fedha kwa ajili yake.+ 37 Naye akafanya kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema kutokana na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kazi ya mfumaji,+ 38 na nguzo zake tano na vibanio vyake. Naye akavifunika vilele vyake na viungo vyake kwa dhahabu, lakini vile vikalio vyake vitano vilikuwa vya shaba.+

37 Sasa Bezaleli+ akafanya Sanduku+ la mbao za mshita. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.+ 2 Kisha akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje na kulifanyia ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote.+ 3 Kisha akalitengenezea pete nne za dhahabu, za juu ya miguu yake minne, pete mbili upande wake mmoja na pete mbili upande wake mwingine.+ 4 Kisha akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.+ 5 Halafu akaitia miti hiyo kwenye zile pete zilizo pande za Sanduku ili kulibeba Sanduku.+

6 Naye akafanya kifuniko+ cha dhahabu safi. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake.+ 7 Kisha akafanya makerubi wawili wa dhahabu. Kwa kazi ya kufua akawafanya kwenye miisho yote miwili ya kifuniko.+ 8 Kerubi mmoja kwenye mwisho ule, na yule kerubi mwingine kwenye mwisho huu. Aliwafanya makerubi juu ya kifuniko kwenye miisho yote miwili.+ 9 Nao wakawa makerubi wanaonyoosha mabawa yao mawili kuelekea juu, wakisitiri kifuniko kwa mabawa yao,+ nazo nyuso zao zilikuwa zikielekeana. Nyuso za makerubi hao zilielekea kifuniko hicho.+

10 Naye akafanya meza ya mbao za mshita.+ Mikono miwili urefu wake, na mkono mmoja upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.+ 11 Halafu akaifunika kwa dhahabu safi na kufanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.+ 12 Kisha akafanya mzingo wa upana wa kiganja kuizunguka na kufanya ukingo wa dhahabu kwa ajili ya mzingo wake kuizunguka pande zote.+ 13 Tena, akatengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili yake na kuziweka pete hizo kwenye zile pembe nne zilizokuwa kwa ajili ya ile miguu minne.+ 14 Pete hizo zilikuwa karibu na ule mzingo, ili kutegemeza ile miti ya kuibeba meza hiyo.+ 15 Halafu akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu ili kuibeba ile meza.+ 16 Baada ya hilo akafanya kutokana na dhahabu safi vile vyombo vilivyo juu ya meza, sahani zake na vikombe vyake na mabakuli yake na mitungi yake iliyotumiwa kumimina matoleo ya kinywaji.+

17 Kisha akafanya kinara cha taa+ cha dhahabu safi. Kwa kazi ya kufua akakifanya kinara cha taa. Pande zake na matawi yake, vikombe vyake, mafundo yake na maua yake vikatokea kwake.+ 18 Na matawi sita yalikuwa yakitoka kwenye pande zake, matawi matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye upande wake mmoja na matawi mengine matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye ule upande wake mwingine.+ 19 Vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kikundi kimoja cha matawi, vifundo na maua yakifuatana; na vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kile kikundi kingine cha matawi, vifundo na maua yakifuatana. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa yale matawi sita yaliyokuwa yakitoka katika kile kinara cha taa.+ 20 Na kwenye kile kinara cha taa kulikuwa na vikombe vinne vyenye umbo la maua ya mlozi, vifundo vyake na maua yake yakifuatana.+ 21 Na kile kifundo chini ya matawi mawili kilitoka kwake, na kifundo kilicho chini ya yale matawi mengine mawili kilitoka kwake, na kifundo kingine kilicho chini ya matawi mengine mawili zaidi kilitoka kwake, kwa ajili ya matawi sita yanayotoka katika kinara.+ 22 Vifundo vyake na matawi yake vilitoka kwake. Vyote vilikuwa kitu kimoja cha kazi ya kufua, cha dhahabu safi.+ 23 Kisha akafanya taa zake saba na mikasi ya tambi zake na vyetezo vyake kutokana na dhahabu safi.+ 24 Alikifanya kwa talanta ya dhahabu safi, hicho pamoja na vyombo vyake vyote.

25 Sasa akafanya madhabahu ya uvumba+ kutokana na mbao za mshita.+ Mkono mmoja urefu wake na mkono mmoja upana wake, ikiwa mraba, na mikono miwili kimo chake. Pembe zake zilitoka kwake.+ 26 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, upande wake wa juu na pande zake za kando kuizunguka na pembe zake, naye akafanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.+ 27 Naye akaifanyia pete mbili za dhahabu chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili, kwenye pande zake mbili zinazoelekeana, za kutegemeza ile miti ya kuibeba.+ 28 Kisha akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.+ 29 Tena akafanya yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta+ na ule uvumba safi uliotiwa manukato,+ kazi ya mtengenezaji wa marhamu.

38 Naye akafanya madhabahu ya toleo la kuteketezwa kwa mbao za mshita. Mikono mitano urefu wake, na mikono mitano upana wake, ilikuwa mraba, na mikono mitatu kimo chake.+ 2 Halafu akafanya pembe zake+ kwenye zile ncha zake nne. Pembe zake zilitoka kwake. Kisha akaifunika kwa shaba.+ 3 Baada ya hilo akavifanya vyombo vyote vya madhabahu, yale makopo na zile sepetu na yale mabakuli, zile nyuma na vile vyetezo. Vyombo vyake vyote alivifanya kwa shaba.+ 4 Tena akaifanyia madhabahu kiunzi cha fito, mtandao wa shaba, chini ya ukingo wake, chini kuelekea katikati yake.+ 5 Halafu akatengeneza pete nne kwenye ile miisho minne karibu na kile kiunzi cha shaba, ili kuitegemeza ile miti. 6 Baada ya hilo akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa shaba.+ 7 Kisha akaitia ile miti kwenye zile pete zilizo pande za madhabahu ili kuibeba.+ Akaifanya kuwa sanduku la mbao lenye uwazi.+

8 Kisha akafanya beseni ya shaba+ na kinara chake cha shaba, kwa kutumia vioo vya watumishi wanawake ambao walifanya utumishi uliopangwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano.+

9 Naye akafanya ule ua.+ Upande unaokabili Negebu, kuelekea kusini, mapazia ya ua yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa, kwa mikono mia moja.+ 10 Nguzo zake 20 na vikalio vyake 20 vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.+ 11 Pia, kwa ajili ya upande wa kaskazini kulikuwa na mikono 100. Nguzo zake 20 na vikalio vyake 20 vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.+ 12 Lakini kwa ajili ya upande wa magharibi mapazia yalikuwa mikono 50. Nguzo zake zilikuwa 10 na vikalio vyake 10.+ Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha. 13 Na kwa ajili ya upande wa mashariki kuelekea macheo ya jua kulikuwa na mikono 50.+ 14 Mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano kwa upande mmoja. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.+ 15 Na kwa ajili ya upande ule mwingine, huu na ule, wa lango la ua, mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.+ 16 Mapazia yote ya ua kuzunguka pande zote yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa. 17 Navyo vikalio vya nguzo vilikuwa vya shaba. Vibanio vya vikalio na viungo vyake vilikuwa vya fedha navyo vilifunikwa kwa shaba sehemu ya juu, na kulikuwa na viungo vya shaba kwa ajili ya nguzo zote za ua.+

18 Nacho kisitiri cha lango la ua kilikuwa kazi ya mfumaji, cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa,+ na urefu wake ulikuwa mikono 20, nacho kimo kotekote kilikuwa mikono 5 sawasawa na mapazia ya ua.+ 19 Na nguzo zake nne na vikalio vyake vinne vilikuwa vya shaba. Misumari yake ilikuwa ya fedha na utando wa vichwa vyake na viungo vyake ulikuwa wa fedha. 20 Na misumari yote ya hema kwa ajili ya maskani na kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote ilikuwa ya shaba.+

21 Hivi ndivyo vitu vilivyohesabiwa vya maskani, maskani ya Ushuhuda,+ vilivyohesabiwa kwa amri ya Musa, kuwa utumishi wa Walawi+ chini ya uongozi wa Ithamari+ mwana wa Haruni kuhani. 22 Naye Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda alifanya yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru Musa. 23 Na pamoja naye alikuwa Oholiabu+ mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, fundi na mtarizi na mfumaji wa uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora.

24 Dhahabu yote iliyotumiwa kwa ajili ya kazi katika kazi yote ya mahali patakatifu ikawa jumla ya dhahabu ya toleo la kutikisa,+ talanta 29 na shekeli 730 kulingana na shekeli+ ya mahali patakatifu.+ 25 Nayo fedha ya wale walioandikishwa kati ya kusanyiko ilikuwa talanta 100 na shekeli 1,775 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 26 Ile nusu shekeli kwa ajili ya mtu mmoja ilikuwa nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, kwa kila mtu aliyekuwa akipita kuingia upande wa wale waliokuwa wameandikishwa kuanzia miaka 20 na zaidi,+ jumla ya watu 603,550.+

27 Na talanta mia moja za fedha zilitumiwa kutengeneza vikalio vya mahali patakatifu na vikalio vya lile pazia. Vikalio mia moja vilitoshana na talanta mia moja, talanta moja kwa kikalio kimoja.+ 28 Na kutokana na zile shekeli 1,775 alifanyiza vibanio vya nguzo na kuvifunika sehemu yake ya juu na kuviunganisha pamoja.

29 Nayo shaba ya toleo la kutikisa ilikuwa talanta 70 na shekeli 2,400. 30 Naye akaitumia kufanya vile vikalio vya mwingilio wa hema la mkutano na ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, na vyombo vyote vya madhabahu, 31 na vile vikalio vya ua kuzunguka pande zote, na vile vikalio vya lango la ua, na misumari yote ya maskani na misumari+ yote ya ua kuzunguka pande zote.

39 Na kutokana na ule uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili+ wakafanya mavazi+ yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu.+ Basi wakafanya yale mavazi matakatifu+ yaliyokuwa kwa ajili ya Haruni, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

2 Basi akaifanya ile efodi+ ya dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa. 3 Kisha wakafua mabamba ya dhahabu yawe mabamba membamba, naye akakata nyuzi za kufuma pamoja na ule uzi wa bluu na ile sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kile kitani bora, kama kazi ya mtarizi.+ 4 Wakaifanyia vipande vya begani vilivyounganishwa. Iliunganishwa kwenye miisho yake miwili. 5 Nao mshipi, uliokuwa juu yake ili kuifunga, ulikuwa wa kitambaa kilekile kulingana na ufundi wake, wa dhahabu, uzi wa bluu, na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

6 Kisha wakafanya mawe ya shohamu+ yaliyopangwa kwenye mapambo ya dhahabu, yaliyochongwa kwa michoro ya muhuri kulingana na majina ya wana wa Israeli.+ 7 Basi akayaweka kwenye vile vipande vya begani vya efodi yawe mawe ya ukumbusho+ kwa ajili ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa. 8 Kisha akafanya kile kifuko cha kifuani+ kwa ufundi wa mtarizi, kama ule ufundi wa efodi, kutokana na dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.+ 9 Kilikuwa mraba kilipokunjwa. Walikifanya kile kifuko cha kifuani, kinapokunjwa, shubiri moja urefu wake na shubiri moja upana wake.+ 10 Kisha wakakijaza kwa mistari minne ya mawe. Mstari wa zabarijadi, topazi na zumaridi ulikuwa mstari wa kwanza.+ 11 Nao mstari wa pili+ ulikuwa feruzi, yakuti+ na yaspi.+ 12 Nao mstari wa tatu+ ulikuwa jiwe la leshemi, akiki na amethisti. 13 Nao mstari wa nne+ ulikuwa krisolito na shohamu+ na yashefi. Yaliwekwa katika mapambo ya dhahabu katika mahali pake. 14 Na mawe hayo yalikuwa kulingana na majina ya wana wa Israeli. Yalikuwa kumi na mawili kulingana na majina yao, kwa michongo ya muhuri, kila moja kulingana na jina lake kwa ajili ya yale makabila kumi na mawili.+

15 Nao wakafanya juu ya kile kifuko cha kifuani minyororo yenye mashada, msokoto wa kamba, wa dhahabu safi.+ 16 Kisha wakafanya mapambo mawili ya dhahabu na pete mbili za dhahabu na kuziweka hizo pete mbili kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani.+ 17 Baada ya hilo wakapitisha zile kamba mbili za dhahabu kwenye zile pete mbili zilizo kwenye miisho ya kile kifuko cha kifuani.+ 18 Nao wakapitisha ile miisho miwili ya zile kamba mbili kwenye yale mapambo mawili. Halafu wakaiweka juu ya vile vipande vya begani vya efodi, mbele yake.+ 19 Kisha wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani kwenye upindo wake ulio upande unaoelekea ile efodi upande wa ndani.+ 20 Halafu wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka juu ya vile vipande viwili vya begani vya efodi upande wake wa chini, sehemu yake ya mbele, karibu na mahali pake pa kuungania, juu ya ule mshipi wa efodi.+ 21 Mwishowe wakakifunga kile kifuko cha kifuani kwa pete zake kwenye zile pete za efodi kwa uzi wa bluu, ili kipate kuwa juu ya mshipi wa efodi na kile kifuko cha kifuani kisiondoke juu ya efodi, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.+

22 Kisha akafanya lile koti lisilo na mikono+ la efodi, ufundi wa mfumaji, lote la uzi wa bluu. 23 Na sehemu wazi ya hilo koti ilikuwa katikati yake, kama sehemu wazi ya vazi la chuma. Sehemu hiyo iliyo wazi ilikuwa na ukingo kuizunguka pande zote ili isiraruke.+ 24 Halafu wakafanya kwenye upindo wa hilo koti makomamanga ya uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, vilivyosokotwa pamoja.+ 25 Na zaidi, wakafanya kengele za dhahabu safi na kuziweka kengele hizo katikati ya makomamanga+ kwenye upindo wa lile koti kuzunguka pande zote, katikati ya makomamanga; 26 kengele na komamanga, kengele na komamanga kwenye upindo wa hilo koti kuzunguka pande zote,+ kwa ajili ya kuhudumu, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

27 Kisha wakafanya zile kamba za kitani bora,+ ufundi wa mfumaji, kwa ajili ya Haruni na wanawe, 28 na kile kilemba+ cha kitani bora na yale mavalio ya kichwani+ ya mapambo ya kitani bora na zile suruali+ za kitani bora kilichosokotwa, 29 na ule ukumbuu+ wa kitani bora kilichosokotwa na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, kazi ya mfumaji, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

30 Mwishowe wakafanya lile bamba linalong’aa, ishara takatifu ya wakfu, kutokana na dhahabu safi na kuandika juu yake maandishi kwa mchongo wa muhuri: “Utakatifu ni wa Yehova.”+ 31 Kisha wakalitia uzi wa bluu ili waliweke juu ya kile kilemba upande wa juu,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

32 Basi kazi ya ile maskani ya hema la mkutano ikafikia mwisho wake, kwa maana wana wa Israeli waliendelea kufanya kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru Musa.+ Walifanya vivyo hivyo.

33 Nao wakaileta maskani+ kwa Musa, lile hema+ pamoja na vyombo vyake vyote,+ kulabu+ zake, viunzi vyake vya mbao,+ miti+ yake na nguzo zake na vikalio+ vyake, 34 na kifuniko chake cha ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi+ nyekundu na kifuniko chake cha ngozi za sili+ na pazia la kisitiri,+ 35 na sanduku+ la ushuhuda na miti+ yake na kifuniko,+ 36 meza,+ vyombo vyake vyote+ na ule mkate wa wonyesho, 37 kile kinara cha taa+ cha dhahabu safi, taa zake, ule mstari wa taa,+ na vyombo vyake vyote+ na yale mafuta ya kuangazia,+ 38 na madhabahu+ ya dhahabu na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta+ na ule uvumba uliotiwa manukato+ na kile kisitiri+ kwa ajili ya mwingilio wa hema, 39 ile madhabahu+ ya shaba na kile kiunzi+ chake cha shaba, miti+ yake na vyombo vyake vyote,+ ile beseni+ na kinara+ chake, 40 mapazia+ ya ua, nguzo+ zake na vikalio+ vyake na kile kisitiri+ kwa ajili ya lango la ua, kamba+ zake za hema na misumari+ yake ya hema na vyombo vyote+ kwa ajili ya utumishi wa maskani, kwa ajili ya hema la mkutano, 41 yale mavazi+ yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika patakatifu, yale mavazi matakatifu+ kwa ajili ya Haruni kuhani na mavazi ya wanawe ya kutumikia wakiwa makuhani.+

42 Kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru Musa, hivyo ndivyo wana wa Israeli walivyoufanya utumishi wote.+ 43 Naye Musa akaiona ile kazi yote, na, tazama! walikuwa wameifanya kama vile Yehova alivyokuwa ameamuru. Hivyo ndivyo walivyokuwa wamefanya. Basi Musa akawabariki.+

40 Kisha Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Katika siku ya mwezi wa kwanza,+ siku ya kwanza ya mwezi, utaisimamisha maskani ya hema la mkutano.+ 3 Nawe utaliweka sanduku la ushuhuda+ ndani yake na kufunga kwa pazia+ njia ya kuingia penye Sanduku. 4 Nawe utaileta meza+ ndani na kuweka kwa utaratibu mpangilio wake, nawe utakileta ndani kile kinara cha taa+ na kuziwasha taa zake.+ 5 Nawe utaiweka madhabahu ya dhahabu kwa ajili ya uvumba+ mbele ya sanduku la ushuhuda na kuweka kile kisitiri cha mwingilio wa maskani mahali pake.+

6 “Nawe utaweka ile madhabahu+ ya matoleo ya kuteketezwa mbele ya mwingilio wa maskani ya hema la mkutano, 7 nawe utaweka ile beseni katikati ya hema la mkutano na ile madhabahu na kutia maji ndani yake.+ 8 nawe utaweka ua+ kuzunguka pande zote na kuweka kile kisitiri+ cha lango la ua. 9 Nawe utachukua yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na kuitia mafuta+ maskani na vyote vilivyomo ndani yake,+ nawe utaitakasa pamoja na vyombo vyake vyote, nayo itakuwa kitu kitakatifu. 10 Nawe utaitia mafuta madhabahu ya toleo la kuteketezwa na vyombo vyake vyote na kuitakasa madhabahu+ hiyo, nayo itakuwa madhabahu takatifu zaidi.+ 11 Nawe utaitia mafuta ile beseni na kinara chake na kuitakasa.

12 “Kisha utamleta Haruni na wanawe karibu na mwingilio wa hema la mkutano na kuwaosha kwa maji.+ 13 Nawe utamvisha Haruni mavazi matakatifu+ na kumtia mafuta+ na kumtakasa, naye atatenda akiwa kuhani kwangu. 14 Baada ya hilo utawaleta wanawe karibu, nawe utawavika kanzu.+ 15 Nawe lazima utawatia mafuta kama vile ulivyomtia mafuta baba yao,+ nao lazima watanitumikia wakiwa makuhani, na kutiwa kwao mafuta lazima kutumike kwao kwa kuendelea kukiwa ukuhani mpaka wakati usio na kipimo katika vizazi vyao.”+

16 Naye Musa akafanya kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru.+ Alifanya vivyo hivyo.

17 Basi ikawa kwamba katika mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili, siku ya kwanza ya mwezi, maskani ilisimamishwa.+ 18 Musa alipoisimamisha maskani, aliweka vikalio+ vyake chini na kuweka viunzi vyake vya mbao+ na kuweka miti+ yake na kusimamisha nguzo+ zake. 19 Halafu akatandaza lile hema+ juu ya maskani na kuweka kifuniko+ cha hema juu yake, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

20 Baada ya hilo akachukua ule Ushuhuda+ na kuuweka katika Sanduku+ na kuiweka ile miti+ kwenye lile Sanduku na kuweka kile kifuniko+ juu ya lile Sanduku.+ 21 Halafu akaleta lile Sanduku ndani ya maskani na kuweka lile pazia+ la kusitiri mahali pake na kufunga njia ya kuingia penye sanduku la ushuhuda,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

22 Kisha akaiweka meza+ katika lile hema la mkutano upande wa maskani kuelekea kaskazini nje ya lile pazia, 23 naye akapanga mstari wa mikate+ juu yake mbele za Yehova, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

24 Halafu akaweka kile kinara cha taa+ ndani ya hema la mkutano mbele ya ile meza, upande wa maskani kuelekea kusini. 25 Kisha akawasha zile taa+ mbele za Yehova, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

26 Kisha akaweka ile madhabahu ya dhahabu+ ndani ya hema la mkutano mbele ya lile pazia, 27 ili afukize juu yake uvumba uliotiwa manukato,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

28 Mwishowe akaweka kile kisitiri+ cha mwingilio wa maskani mahali pake.

29 Naye akaweka ile madhabahu+ ya toleo la kuteketezwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano, ili atoe juu yake toleo la kuteketezwa+ na toleo la nafaka, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

30 Halafu akaweka ile beseni kati ya hema la mkutano na ile madhabahu na kutia ndani yake maji ya kuosha.+ 31 Naye Musa na Haruni na wanawe wakaosha mikono yao na miguu yao hapo. 32 Walipoingia kwenye hema la mkutano na walipoenda karibu na ile madhabahu, walikuwa wakioga,+ kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.

33 Mwishowe akaweka ua+ kuizunguka pande zote ile maskani na ile madhabahu na kuweka kisitiri cha lango la ua.+

Basi Musa akaimaliza kazi. 34 Nalo wingu+ likaanza kulifunika hema la mkutano, na utukufu wa Yehova ukaijaza maskani. 35 Naye Musa hakuweza kuingia ndani ya hema la mkutano, kwa sababu wingu+ lilikaa juu yake na utukufu wa Yehova uliijaza maskani.+

36 Na wakati ambapo wingu hilo lilikuwa likiinuka kutoka juu ya maskani wana wa Israeli walikuwa wakivunja kambi katika hatua zao zote za safari.+ 37 Hata hivyo, ikiwa wingu hilo halikuinuka, basi hawakuwa wakivunja kambi mpaka siku ambayo liliinuka.+ 38 Kwa maana wingu la Yehova lilikuwa juu ya maskani wakati wa mchana, na moto ulikuwa juu yake wakati wa usiku machoni pa nyumba yote ya Israeli katika hatua zao zote za safari.+

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki