HESABU
1 Na Yehova akazungumza na Musa katika nyika ya Sinai,+ kwenye hema la mkutano,+ siku ya kwanza ya mwezi wa pili katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchini Misri.+ Akamwambia: 2 “Wahesabu+ Waisraeli wote,* kila mmoja wao* kulingana na familia yake, kulingana na ukoo wake,* orodhesha majina ya wanaume wote. 3 Wewe na Haruni mnapaswa kuwaandikisha watu wote wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi+ wanaoweza kutumikia katika jeshi la Israeli, kulingana na vikosi vyao.*
4 “Mchukueni mwanamume mmoja kutoka katika kila kabila, kila mmoja wao anapaswa kuwa kiongozi wa ukoo wake.*+ 5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia ninyi: kutoka kabila la Rubeni, Elisuri+ mwana wa Shedeuri; 6 kabila la Simeoni, Shelumieli+ mwana wa Zurishadai; 7 kabila la Yuda, Nashoni+ mwana wa Aminadabu; 8 kabila la Isakari, Nethaneli+ mwana wa Zuari; 9 kabila la Zabuloni, Eliabu+ mwana wa Heloni; 10 wana wa Yosefu: kabila la Efraimu,+ Elishama mwana wa Amihudi; kabila la Manase, Gamalieli mwana wa Pedazuri; 11 kabila la Benjamini, Abidani+ mwana wa Gidioni; 12 kabila la Dani, Ahiezeri+ mwana wa Amishadai; 13 kabila la Asheri, Pagieli+ mwana wa Okrani; 14 kabila la Gadi, Eliasafu+ mwana wa Deueli; 15 kabila la Naftali, Ahira+ mwana wa Enani. 16 Hao ndio waliochaguliwa miongoni mwa Waisraeli. Hao ndio wakuu+ wa makabila ya baba zao, viongozi wa maelfu katika Israeli.”+
17 Basi Musa na Haruni wakawachukua wanaume hao waliotajwa majina. 18 Wakawakusanya Waisraeli wote siku ya kwanza ya mwezi wa pili, ili kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi aandikishwe kulingana na jina lake, familia yake, na ukoo wake,*+ 19 kama Yehova alivyomwamuru Musa. Basi akawaandikisha katika nyika ya Sinai.+
20 Wana wa Rubeni, wazao wa mzaliwa wa kwanza wa Israeli,+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 21 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Rubeni walikuwa 46,500.
22 Wazao wa Simeoni+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 23 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Simeoni walikuwa 59,300.
24 Wazao wa Gadi+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 25 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Gadi walikuwa 45,650.
26 Wazao wa Yuda+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 27 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Yuda walikuwa 74,600.
28 Wazao wa Isakari+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 29 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Isakari walikuwa 54,400.
30 Wazao wa Zabuloni+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 31 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Zabuloni walikuwa 57,400.
32 Wazao wa Yosefu kupitia Efraimu+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 33 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Efraimu walikuwa 40,500.
34 Wazao wa Manase+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 35 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Manase walikuwa 32,200.
36 Wazao wa Benjamini+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 37 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Benjamini walikuwa 35,400.
38 Wazao wa Dani+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 39 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Dani walikuwa 62,700.
40 Wazao wa Asheri+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 41 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Asheri walikuwa 41,500.
42 Wazao wa Naftali+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 43 wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Naftali walikuwa 53,400.
44 Hao ndio walioandikishwa na Musa na Haruni na wale wakuu 12 wa Israeli, kila mmoja wao aliwakilisha ukoo wake.* 45 Waisraeli wote wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambao wangeweza kutumikia katika jeshi la Israeli waliandikishwa kulingana na ukoo wao,* 46 watu wote walioandikishwa walikuwa 603,550.+
47 Lakini Walawi+ hawakuandikishwa pamoja nao, kulingana na makabila ya baba zao.+ 48 Basi Yehova akamwambia Musa: 49 “Ni kabila la Lawi tu ambalo hutaliandikisha, nawe hupaswi kuwahesabu pamoja na Waisraeli wengine.+ 50 Unapaswa kuwaweka rasmi Walawi wasimamie hema la Ushahidi+ na vyombo vyake vyote na kila kitu kilichomo.+ Watabeba hema hilo na vyombo vyake vyote,+ nao watalitunza+ na kupiga kambi kulizunguka.+ 51 Wakati wowote hema hilo linapohamishwa, Walawi ndio wanaopaswa kulifungua;+ na wakati linaposimamishwa, Walawi ndio wanaopaswa kulisimamisha; na mtu yeyote asiye na idhini* akilikaribia anapaswa kuuawa.+
52 “Kila Mwisraeli anapaswa kupiga hema lake katika kambi aliyogawiwa, kila mwanamume kulingana na kundi lake la makabila matatu,*+ kulingana na kikosi chake.* 53 Walawi wanapaswa kupiga kambi kuzunguka hema la Ushahidi, ili hasira yangu isiwawakie Waisraeli;+ na lazima Walawi wawajibike kulitunza* hema la Ushahidi.”+
54 Waisraeli walifanya mambo yote ambayo Yehova alimwamuru Musa. Hivyo ndivyo walivyofanya.
2 Yehova akamwambia hivi Musa na Haruni: 2 “Waisraeli wanapaswa kupiga kambi mahali ambapo kundi lao la makabila matatu+ limegawiwa, kila mtu karibu na alama ya ukoo wake.* Wanapaswa kupiga kambi kuelekeana na hema la mkutano, kuzunguka pande zake zote.
3 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Yuda litapiga kambi upande wa mashariki, upande wa mapambazuko ya jua, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Yuda ni Nashoni+ mwana wa Aminadabu. 4 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 74,600.+ 5 Kabila la Isakari litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Isakari ni Nethaneli+ mwana wa Zuari. 6 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 54,400.+ 7 Kisha kabila la Zabuloni; mkuu wa wana wa Zabuloni ni Eliabu+ mwana wa Heloni. 8 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 57,400.+
9 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Yuda ni 186,400. Wanapaswa kuwa wa kwanza kuondoka.+
10 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Rubeni+ litapiga kambi upande wa kusini, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Rubeni ni Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 11 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 46,500.+ 12 Kabila la Simeoni litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Simeoni ni Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 13 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 59,300.+ 14 Kisha kabila la Gadi; mkuu wa wana wa Gadi ni Eliasafu+ mwana wa Reueli. 15 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 45,650.+
16 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Rubeni ni 151,450, nao wanapaswa kuwa wa pili kuondoka.+
17 “Hema la mkutano linapohamishwa,+ kambi ya Walawi inapaswa kuwa katikati ya kambi nyingine zote.
“Wote wanapaswa kusafiri kwa kufuata utaratibu uleule wanaofuata wanapopiga kambi,+ kila mtu mahali pake, kulingana na makundi yao ya makabila matatu-matatu.
18 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Efraimu litapiga kambi upande wa magharibi, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Efraimu ni Elishama+ mwana wa Amihudi. 19 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 40,500.+ 20 Kabila la Manase+ litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Manase ni Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 21 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 32,200.+ 22 Kisha kabila la Benjamini; mkuu wa wana wa Benjamini ni Abidani+ mwana wa Gideoni. 23 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 35,400.+
24 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Efraimu ni 108,100, nao wanapaswa kuwa wa tatu kuondoka.+
25 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Dani litapiga kambi upande wa kaskazini, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Dani ni Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 26 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 62,700.+ 27 Kabila la Asheri litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Asheri ni Pagieli+ mwana wa Okrani. 28 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 41,500.+ 29 Kisha kabila la Naftali; mkuu wa wana wa Naftali ni Ahira+ mwana wa Enani. 30 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 53,400.+
31 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Dani ni 157,600. Wanapaswa kuwa wa mwisho kuondoka,+ kulingana na kundi lao lenye makabila matatu.”
32 Hao ndio Waisraeli walioandikishwa kulingana na koo zao;* watu wote walioandikishwa katika kambi hizo ili kuwa wanajeshi walikuwa 603,550.+ 33 Lakini kama Yehova alivyomwamuru Musa, Walawi hawakuandikishwa+ pamoja na Waisraeli wengine.+ 34 Waisraeli walifanya mambo yote ambayo Yehova alimwamuru Musa. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi kulingana na makundi yao ya makabila matatu,+ na hivyo ndivyo walivyokuwa wakiondoka,+ kila mmoja kulingana na familia yake na ukoo wake.*
3 Basi hawa ndio waliokuwa wazao wa* Haruni na Musa siku ambayo Yehova alizungumza na Musa kwenye Mlima Sinai.+ 2 Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni: Nadabu mzaliwa wa kwanza, Abihu,+ Eleazari,+ na Ithamari.+ 3 Hayo ndiyo majina ya wana wa Haruni waliotiwa mafuta ili watumikie wakiwa makuhani.+ 4 Hata hivyo, Nadabu na Abihu walikufa mbele za Yehova walipomtolea Yehova moto haramu+ katika nyika ya Sinai, nao hawakuwa na wana wowote. Lakini Eleazari+ na Ithamari+ waliendelea kutumikia wakiwa makuhani pamoja na Haruni baba yao.
5 Kisha Yehova akamwambia Musa, 6 “Walete watu wa kabila la Lawi+ mbele ya kuhani Haruni ili wamhudumie.+ 7 Watatimiza wajibu wao wa kumtumikia na kuwatumikia Waisraeli wote mbele ya hema la mkutano kwa kufanya kazi za hema la ibada. 8 Watatunza vyombo vyote+ vya hema la mkutano na kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia Waisraeli kwa kufanya kazi za hema la ibada.+ 9 Utawakabidhi Walawi kwa Haruni na wanawe. Ni watu waliokabidhiwa, ambao Haruni amekabidhiwa kutoka kati ya Waisraeli.+ 10 Unapaswa kumweka rasmi Haruni na wanawe ili watekeleze majukumu yao ya ukuhani,+ na mtu yeyote asiye na idhini* atakayekaribia mahali patakatifu anapaswa kuuawa.”+
11 Yehova akaendelea kumwambia Musa, 12 “Tazama! Mimi nawachukua Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya wazaliwa wote wa kwanza* wa Waisraeli;+ Walawi watakuwa wangu. 13 Kwa maana kila mzaliwa wa kwanza ni wangu.+ Siku niliyomuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri+ nilijitakasia kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli kuanzia mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu mpaka wa mnyama.+ Watakuwa wangu. Mimi ni Yehova.”
14 Yehova akaendelea kuzungumza na Musa katika nyika ya Sinai,+ akamwambia: 15 “Waandikishe wana wa Lawi kila mmoja kulingana na ukoo wake* na familia yake. Unapaswa kumwandikisha kila mwanamume, kuanzia mtoto wa umri wa mwezi mmoja na zaidi.”+ 16 Kwa hiyo Musa akawaandikisha kama alivyoagizwa na Yehova, kama alivyoamriwa. 17 Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi, na Merari.+
18 Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni kulingana na familia zao: Libni na Shimei.+
19 Wana wa Kohathi kulingana na familia zao walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli.+
20 Wana wa Merari kulingana na familia zao walikuwa Mali+ na Mushi.+
Hizo ndizo zilizokuwa familia za Walawi kila mmoja kulingana na ukoo wake.*
21 Familia ya Walibni+ na familia ya Washimei zilitokana na Gershoni. Hizo ndizo zilizokuwa familia za Wagershoni. 22 Wanaume wao wote walioandikishwa kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 7,500.+ 23 Familia za Wagershoni zilipiga kambi nyuma ya hema la ibada+ upande wa magharibi. 24 Mkuu wa ukoo* wa Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli. 25 Majukumu ya wana wa Gershoni+ katika hema la mkutano yalikuwa kutunza hema lenyewe pamoja+ na kifuniko chake,+ pazia+ la mlango wa hema la mkutano, 26 mapazia ya ua yanayoning’inia,+ pazia la mlango wa ua+ linalozunguka hema la ibada na madhabahu, kamba za hema, na utumishi wote uliohusiana na vitu hivyo.
27 Familia ya Waamramu, familia ya Waishari, familia ya Wahebroni, na familia ya Wauzieli zilitokana na Kohathi. Hizo ndizo zilizokuwa familia za Wakohathi.+ 28 Wanaume wote kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 8,600; jukumu lao lilikuwa kutunza mahali patakatifu.+ 29 Familia za wana wa Kohathi zilipiga kambi upande wa kusini wa hema la ibada.+ 30 Mkuu wa ukoo* wa familia za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.+ 31 Majukumu yao yalikuwa kutunza Sanduku la Agano,+ meza,+ kinara cha taa,+ madhabahu,+ vyombo+ vilivyotumiwa katika utumishi wa mahali patakatifu, pazia,+ na utumishi wote uliohusiana na vitu hivyo.+
32 Kiongozi wa wakuu wa Walawi alikuwa Eleazari+ mwana wa kuhani Haruni, naye aliwasimamia wale waliokuwa na majukumu ya kufanya kazi mahali patakatifu.
33 Familia ya Wamali na familia ya Wamushi zilizotokana na Merari. Hizo ndizo zilizokuwa familia za Merari.+ 34 Wanaume wote walioandikishwa kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 6,200.+ 35 Mkuu wa ukoo* wa familia za Merari alikuwa Zurieli mwana wa Abihaili. Walipiga kambi upande wa kaskazini wa hema la ibada.+ 36 Wana wa Merari walikuwa na majukumu ya kusimamia viunzi+ vya hema la ibada, fito zake,+ nguzo zake,+ vikalio vyake, vyombo vyake vyote,+ na utumishi wote uliohusiana na vitu hivyo,+ 37 na pia nguzo zote zilizozunguka ua na vikalio vyake,+ vigingi vya hema, na kamba za hema hilo.
38 Musa na Haruni na wanawe walipiga kambi mbele ya hema la ibada upande wa mashariki, upande wa mapambazuko ya jua. Walikuwa na wajibu wa kutunza mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu yeyote asiye na idhini* ambaye angekaribia mahali patakatifu angeuawa.+
39 Wanaume wote Walawi wenye umri wa kuanzia mwezi mmoja na zaidi walioandikishwa na Musa na Haruni kulingana na familia zao, kama Yehova alivyoagiza, walikuwa 22,000.
40 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Waandikishe wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa Waisraeli kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi,+ wahesabu na kuorodhesha majina yao. 41 Wachukue Walawi kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli,+ mimi ni Yehova, chukua pia mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa mifugo ya Waisraeli.”+ 42 Ndipo Musa akawaandikisha wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli kama Yehova alivyomwamuru. 43 Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume walioandikishwa kwa majina kuanzia umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 22,273.
44 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 45 “Wachukue Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli, chukua pia mifugo ya Walawi badala ya mifugo ya Waisraeli, na Walawi watakuwa wangu. Mimi ni Yehova. 46 Ili kulipia bei ya fidia+ ya wale wazaliwa wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wanazidi idadi ya Walawi,+ 47 chukua shekeli tano* kwa ajili ya kila mmoja wao,+ kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.* Shekeli moja ni sawa na gera 20.*+ 48 Utampa Haruni na wanawe pesa hizo ambazo ni bei ya fidia ya wale wanaozidi idadi yao.” 49 Kwa hiyo Musa akachukua pesa za ukombozi kutoka kwa wale waliozidi idadi ya wale waliofidiwa na Walawi. 50 Alichukua pesa hizo kutoka kwa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, shekeli 1,365, kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu. 51 Kisha Musa akampa Haruni na wanawe pesa hizo za fidia kulingana na neno la* Yehova, kama Yehova alivyomwamuru Musa.
4 Yehova akamwambia hivi Musa na Haruni: 2 “Mnapaswa kuwahesabu wana wa Kohathi+ miongoni mwa wana wa Lawi, kulingana na familia zao na koo zao,* 3 wote wenye umri wa miaka 30+ hadi 50+ walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano.+
4 “Huu ndio utumishi wa wana wa Kohathi katika hema la mkutano.+ Unahusiana na vitu vitakatifu kabisa: 5 Wakati wa kuvunja kambi, Haruni na wanawe wataingia na kulishusha pazia linaloning’inia mbele ya sanduku la Ushahidi+ na kulifunika kwa pazia hilo.+ 6 Wataweka kifuniko cha ngozi ya sili juu yake na kutandaza juu yake kitambaa cha bluu, halafu wataingiza fito za kubebea+ sanduku hilo.
7 “Pia watafunika meza ya mikate ya wonyesho+ kwa kitambaa cha bluu, na juu yake wataweka sahani, vikombe, mabakuli, na magudulia ya toleo la kinywaji;+ mikate ya wonyesho ambayo huwa juu ya meza hiyo daima+ inapaswa kubaki juu yake. 8 Watafunika vitu hivyo kwa kitambaa chekundu na juu yake wataweka kifuniko cha ngozi ya sili na kuingiza fito za kuibeba.+ 9 Kisha watachukua kitambaa cha bluu na kukifunika kinara cha taa+ pamoja na taa zake,+ koleo zake, vyetezo vyake,+ na vyombo vyake vyote vya kuwekea mafuta. 10 Nao wataweka kinara hicho pamoja na vyombo vyake vyote ndani ya ngozi ya sili na kukiweka juu ya ufito wa kubebea. 11 Kisha watatandaza kitambaa cha bluu juu ya madhabahu ya dhahabu+ na kuifunika kwa kifuniko cha ngozi ya sili, halafu wataingiza fito za kuibeba.+ 12 Nao watachukua vyombo vyote+ wanavyotumia kwa ukawaida wanapohudumu mahali patakatifu na kuviweka ndani ya kitambaa cha bluu na kuvifunika kwa kifuniko cha ngozi ya sili, kisha wataviweka juu ya ufito wa kubebea.
13 “Wataondoa majivu* yaliyo kwenye madhabahu+ na kutandaza kitambaa cha sufu cha zambarau juu ya madhabahu hiyo. 14 Kisha wataweka juu yake vyombo vyake vyote wanavyotumia kuhudumu kwenye madhabahu: vyetezo, nyuma,* sepetu, na mabakuli, vyombo vyote vya madhabahu;+ watatandaza juu yake kifuniko cha ngozi ya sili na kuingiza fito za kuibeba.+
15 “Ni lazima Haruni na wanawe wamalize kufunika mahali patakatifu+ na vyombo vyote vya mahali patakatifu kabla ya watu kuanza safari. Kisha wana wa Kohathi watakuja kuvibeba,+ lakini hawapaswi kugusa vitu vitakatifu, la sivyo watakufa.+ Wana wa Kohathi ndio walio na jukumu la kubeba vitu vya hema la mkutano.
16 “Eleazari+ mwana wa kuhani Haruni ana jukumu la kusimamia mafuta kwa ajili ya taa,+ uvumba uliotiwa manukato,+ toleo la kawaida la nafaka, na mafuta yanayotumiwa kutia mafuta.+ Ndiye anayesimamia hema lote la ibada na vitu vyote vilivyomo, pamoja na mahali patakatifu na vyombo vyake.”
17 Yehova akaendelea kumwambia Musa na Haruni: 18 “Msiache familia za Wakohathi+ ziangamizwe kutoka miongoni mwa Walawi. 19 Lakini fanyeni jambo hili ili waendelee kuishi nao wasife kwa sababu ya kukaribia vitu vitakatifu kabisa.+ Haruni na wanawe wataingia humo na kumgawia kila mmoja wao kazi yake na vitu anavyopaswa kubeba. 20 Hawapaswi kuingia hemani na kuona vitu vitakatifu hata kwa muda mfupi, la sivyo watakufa.”+
21 Kisha Yehova akamwambia Musa: 22 “Wana wa Gershoni+ wanapaswa kuhesabiwa kulingana na koo zao* na familia zao. 23 Utawaandikisha wanaume wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano. 24 Huu ndio utumishi ambao watu wa familia za Wagershoni wamegawiwa kufanya na vitu wanavyopaswa kubeba:+ 25 Watabeba vitambaa vya hema la ibada,+ hema la mkutano, kifuniko chake na kifuniko cha ngozi ya sili kilicho juu yake,+ pazia la mlango wa hema la mkutano,+ 26 mapazia ya ua yanayoning’inia,+ pazia la mlango wa ua+ unaozunguka hema la ibada na madhabahu, kamba za hema hilo na vyombo vyake vyote, na vitu vyote vinavyotumiwa katika utumishi wa hema la ibada. Hiyo ndiyo kazi waliyogawiwa. 27 Haruni na wanawe watasimamia utumishi wote wa Wagershoni+ pamoja na vitu wanavyopaswa kubeba; utawapa jukumu la kubeba vitu hivyo vyote. 28 Huo ndio utumishi utakaofanywa na familia za Wagershoni katika hema la mkutano;+ watasimamiwa na Ithamari+ mwana wa kuhani Haruni.
29 “Utawaandikisha wana wa Merari+ kulingana na familia zao na ukoo wao.* 30 Utawaandikisha wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano. 31 Ni jukumu lao kubeba+ vitu vifuatavyo vinavyohusiana na utumishi wao katika hema la mkutano: viunzi+ vya hema la ibada, fito zake,+ nguzo zake,+ vikalio vyake;+ 32 nguzo+ za ua unaozunguka pande zote, vikalio vyake,+ vigingi vyake vya hema,+ na kamba za hema hilo pamoja na vifaa vyake vyote na utumishi wote unaohusiana na hema la ibada. Utamgawia kila mmoja wao kwa jina vifaa anavyopaswa kubeba. 33 Hivyo ndivyo familia za wana wa Merari+ zitakavyotumikia katika hema la mkutano chini ya usimamizi wa Ithamari mwana wa kuhani Haruni.”+
34 Kisha Musa na Haruni na wakuu+ wa Israeli wakawaandikisha wana wa Kohathi+ kulingana na familia zao na ukoo wao,* 35 wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano.+ 36 Wote walioandikishwa kulingana na familia zao walikuwa 2,750.+ 37 Hao ndio walioandikishwa kutoka katika familia za Wakohathi, wote walitumikia katika hema la mkutano. Musa na Haruni waliwaandikisha kama Yehova alivyoagiza kupitia Musa.+
38 Wana wa Gershoni+ waliandikishwa kulingana na familia zao na ukoo wao,* 39 wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano. 40 Wote walioandikishwa kulingana na familia zao na ukoo wao* walikuwa 2,630.+ 41 Hao ndio walioandikishwa kutoka katika familia za wana wa Gershoni, wote walitumikia katika hema la mkutano. Musa na Haruni waliwaandikisha kama Yehova alivyoagiza.+
42 Wana wa Merari waliandikishwa kulingana na familia zao na ukoo wao,* 43 wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano.+ 44 Wote walioandikishwa kulingana na familia zao walikuwa 3,200.+ 45 Hao ndio walioandikishwa kutoka katika familia za wana wa Merari, ambao waliandikishwa na Musa na Haruni kama Yehova alivyoagiza kupitia Musa.+
46 Musa na Haruni na wakuu wa Israeli waliwaandikisha Walawi hao wote kulingana na familia zao na koo zao;* 47 walikuwa na umri wa miaka 30 hadi miaka 50, na wote waligawiwa kazi ya kutumikia katika hema la mkutano na kubeba mizigo ya hema hilo.+ 48 Wote walioandikishwa walikuwa 8,580.+ 49 Waliandikishwa kama Yehova alivyoagiza kupitia Musa, kila mmoja wao kulingana na utumishi wake na mzigo aliopaswa kubeba; waliandikishwa kama Yehova alivyomwamuru Musa.
5 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 2 “Waamuru Waisraeli wamtoe nje ya kambi kila mtu mwenye ukoma+ na kila mtu anayetokwa na umajimaji+ na kila mtu aliyejichafua kwa kumgusa mtu aliyekufa.*+ 3 Mnapaswa kumtoa nje awe ni mwanamume au mwanamke. Mnapaswa kuwatoa nje ya kambi watu hao ili wasichafue+ kambi za wale ninaokaa* kati yao.”+ 4 Basi Waisraeli wakafanya hivyo, wakawatoa nje ya kambi. Waisraeli wakafanya kama Yehova alivyomwambia Musa.
5 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 6 “Waambie Waisraeli, ‘Mwanamume au mwanamke akitenda dhambi yoyote ya kibinadamu na kukosa kuwa mwaminifu kwa Yehova, mtu huyo ana* hatia.+ 7 Ni lazima aungame+ dhambi aliyotenda na alipe malipo kamili kwa ajili ya hatia yake na kuongeza sehemu ya tano ya malipo hayo;+ atampa yule aliyemkosea. 8 Lakini ikiwa mtu aliyekosewa hana mtu wa karibu wa ukoo atakayepokea malipo hayo, yanapaswa kurudishwa kwa Yehova nayo yatakuwa ya kuhani, isipokuwa kondoo dume wa dhabihu ya kufunika dhambi atakayetolewa kufunika dhambi yake.+
9 “‘Kila mchango mtakatifu+ kutoka kwa Waisraeli unaoletwa kwa kuhani utakuwa wake.+ 10 Vitu vitakatifu vya kila mtu vitaendelea kuwa vyake mwenyewe. Kitu chochote ambacho mtu anampa kuhani kitakuwa cha kuhani.’”
11 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 12 “Waambie Waisraeli, ‘Hivi ndivyo mtakavyofanya mke wa mtu yeyote akipotoka na kukosa uaminifu kwa mume wake 13 na mwanamume mwingine afanye naye ngono,+ lakini mume wake hajui jambo hilo na halijagunduliwa, kwa hiyo mwanamke huyo amejichafua lakini hakuna shahidi wa kumshtaki, naye hajakamatwa: 14 Iwe mume wake ana wivu na anatilia shaka uaminifu wa mke wake aliyejichafua, au iwe ana wivu na anatilia shaka uaminifu wa mke wake ingawa hajajichafua, 15 ni lazima mwanamume huyo ampeleke mke wake kwa kuhani pamoja na toleo kwa ajili yake, yaani, sehemu ya kumi ya kipimo cha efa* ya unga wa shayiri. Hapaswi kumimina mafuta juu ya toleo hilo wala kutia ubani juu yake, kwa sababu ni toleo la nafaka la wivu, toleo la nafaka ambalo ni kumbukumbu la hatia.
16 “‘Kuhani atamleta mwanamke huyo na kumsimamisha mbele za Yehova.+ 17 Kisha kuhani atatia maji matakatifu katika chombo cha udongo na kuchukua kiasi kidogo cha mavumbi kutoka kwenye sakafu ya hema la ibada na kuyatia katika maji hayo. 18 Baada ya kuhani kumsimamisha mwanamke huyo mbele za Yehova, atafungua nywele za mwanamke huyo na kuweka katika mikono ya mwanamke huyo lile toleo la nafaka la kumbukumbu, yaani, toleo la nafaka la wivu,+ huku kuhani akiwa ameshika mkononi yale maji machungu yanayoleta laana.+
19 “‘Kisha kuhani atamwapisha mwanamke huyo akisema: “Ikiwa hujafanya ngono na mwanamume mwingine ukiwa chini ya mamlaka ya mume wako+ wala hujapotoka au kujichafua, basi maji haya machungu yanayoleta laana yasikudhuru. 20 Lakini ikiwa umepotoka ukiwa chini ya mamlaka ya mume wako na kujichafua kwa kufanya ngono na mwanamume mwingine+ ambaye si mume wako—” 21 Basi kuhani atamwapisha mwanamke huyo kiapo chenye laana, na kumwambia: “Yehova na akufanye uwe mfano wa laana na kiapo miongoni mwa watu wako, Yehova na akufanye uwe tasa* na tumbo lako livimbe. 22 Maji haya yanayoleta laana yataingia katika matumbo yako na kufanya tumbo lako livimbe nawe utakuwa tasa.”* Kisha mwanamke huyo atasema: “Amina! Amina!”*
23 “‘Halafu kuhani ataandika laana hizo katika kitabu na kuziosha kwenye maji machungu ili zifutike. 24 Kisha atamnywesha mwanamke huyo maji hayo machungu yanayoleta laana, na maji hayo yanayoleta laana yataingia mwilini mwake na kusababisha maumivu makali. 25 Kuhani atachukua toleo la nafaka la wivu+ kutoka mikononi mwa mwanamke huyo na kulitikisa kwenda mbele na nyuma mbele za Yehova, kisha atalileta karibu na madhabahu. 26 Halafu kuhani atachukua mkono mmoja wa toleo la nafaka ili kuwa dhabihu ya kumbukumbu na kuliteketeza juu ya madhabahu ili lifuke moshi,+ kisha atamnywesha mwanamke huyo maji hayo. 27 Baada ya mwanamke huyo kunyweshwa maji hayo, ikiwa amejichafua na kukosa uaminifu kwa mume wake, maji yanayoleta laana yataingia mwilini mwake na kusababisha maumivu makali, na tumbo lake litavimba naye atakuwa tasa,* na mwanamke huyo atakuwa mfano wa laana miongoni mwa watu wake. 28 Hata hivyo, ikiwa mwanamke huyo hajajichafua, naye ni safi, basi hatapata madhara, ataweza kupata mimba na kuzaa watoto.
29 “‘Hiyo ndiyo sheria kuhusu wivu+ inayopaswa kufuatwa mwanamke akipotoka na kujichafua akiwa chini ya mamlaka ya mume wake, 30 au ikiwa mwanamume ana wivu na anatilia shaka uaminifu wa mke wake; mwanamume huyo atamsimamisha mke wake mbele za Yehova, naye kuhani atamtendea mwanamke huyo kulingana na sheria hii yote. 31 Mwanamume huyo hatakuwa na hatia, lakini mke wake ataadhibiwa kwa sababu ya kosa lake.’”
6 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 2 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Mwanamume au mwanamke akiweka nadhiri ya pekee ya kuishi akiwa Mnadhiri*+ kwa Yehova, 3 anapaswa kujiepusha na divai na vinywaji vingine vyenye kileo. Hapaswi kunywa siki ya divai au siki ya kitu chochote chenye kileo.+ Hapaswi kamwe kunywa maji ya zabibu, wala kula zabibu zilizotoka kuchumwa au zilizokaushwa. 4 Siku zote atakazokuwa Mnadhiri hapaswi kula kitu chochote kinachotokana na mzabibu, kuanzia zabibu ambazo hazijaiva mpaka maganda yake.
5 “‘Siku zote atakazokuwa Mnadhiri hakuna wembe utakaogusa kichwa chake.+ Ataendelea kuwa mtakatifu kwa kuacha nywele za kichwa chake ziwe ndefu mpaka siku alizojitenga kwa ajili ya Yehova zitakapokwisha. 6 Siku zote alizojitenga kwa ajili ya Yehova hapaswi kumkaribia mtu aliyekufa.* 7 Hata baba yake au mama yake au ndugu yake au dada yake akifa, hapaswi kujichafua,+ kwa sababu ishara ya kwamba yeye ni Mnadhiri kwa Mungu iko juu ya kichwa chake.
8 “‘Atakuwa mtakatifu kwa Yehova siku zote atakazokuwa Mnadhiri. 9 Lakini mtu akifa ghafla kando yake+ na kuchafua nywele zake ambazo ni ishara ya kwamba amejitenga kwa ajili ya Mungu,* ni lazima anyoe kichwa chake+ siku anapothibitisha utakaso wake. Anapaswa kukinyoa siku ya saba. 10 Na siku ya nane anapaswa kumpelekea kuhani njiwa tetere wawili au hua wawili wachanga kwenye mlango wa hema la mkutano. 11 Kuhani atamtoa ndege mmoja kuwa dhabihu ya dhambi na mwingine kuwa dhabihu ya kuteketezwa ili kufunika dhambi aliyotenda+ kwa kumgusa mtu aliyekufa.* Kisha anapaswa kutakasa kichwa chake siku hiyo. 12 Ni lazima ajitenge tena kwa ajili ya Yehova na kuanza upya siku za Unadhiri wake, naye ataleta mwanakondoo dume wa mwaka mmoja kuwa dhabihu ya hatia. Hata hivyo, zile siku za awali hazitahesabiwa kwa sababu aliuchafua Unadhiri wake.
13 “‘Hii ndiyo sheria inayomhusu Mnadhiri: Atakapomaliza siku zake za kuwa Mnadhiri,+ ataletwa kwenye mlango wa hema la mkutano. 14 Akiwa hapo atamtolea Yehova dhabihu zake: mwanakondoo dume wa mwaka mmoja asiye na kasoro kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa,+ mwanakondoo jike wa mwaka mmoja asiye na kasoro kwa ajili ya dhabihu ya dhambi,+ kondoo dume mmoja asiye na kasoro kwa ajili ya dhabihu ya ushirika,+ 15 kikapu cha mikate ya mviringo isiyo na chachu na iliyookwa kwa unga laini uliochanganywa na mafuta, mikate myembamba isiyo na chachu na iliyopakwa mafuta, na toleo la nafaka+ na matoleo ya vinywaji ya dhabihu hizo.+ 16 Kuhani atatoa vitu hivyo mbele za Yehova na kutoa dhabihu ya dhambi na dhabihu ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu huyo. 17 Kisha atamtolea Yehova kondoo dume kwa ajili ya dhabihu ya ushirika pamoja na kikapu cha mikate isiyo na chachu, pia atatoa toleo la nafaka+ pamoja na toleo la kinywaji la dhabihu hiyo.
18 “‘Halafu ni lazima Mnadhiri huyo anyoe nywele za kichwa chake*+ kwenye mlango wa hema la mkutano, naye atachukua nywele hizo za Unadhiri wake na kuzitia katika moto ulio chini ya dhabihu ya ushirika. 19 Kisha kuhani atachukua mguu wa mbele uliochemshwa+ wa yule kondoo dume, mkate mmoja wa mviringo usio na chachu kutoka katika kile kikapu, na mkate mmoja mwembamba usio na chachu, na kuviweka mikononi mwa Mnadhiri huyo baada ya nywele zake za Unadhiri kunyolewa. 20 Halafu kuhani atavitikisa vitu hivyo kwenda mbele na nyuma vikiwa toleo la kutikiswa mbele za Yehova.+ Ni vitu vitakatifu kwa kuhani, pamoja na kidari cha toleo la kutikiswa na mguu uliotolewa kama mchango.+ Baada ya hayo, Mnadhiri huyo anaweza kunywa divai.
21 “‘Hii ndiyo sheria inayomhusu Mnadhiri+ anayeweka nadhiri: Akiweka nadhiri na iwe kwamba anaweza kumtolea Yehova toleo ambalo halihitajiwi katika kutimiza Unadhiri wake, ni lazima atimize nadhiri yake kulingana na sheria ya Unadhiri wake.’”
22 Kisha Yehova akamwambia Musa: 23 “Mwambie hivi Haruni na wanawe: ‘Hivi ndivyo mtakavyowabariki+ Waisraeli. Waambieni:
24 “Yehova na awabariki+ na kuwalinda.
25 Yehova na awaangazie nuru ya uso wake,+ na kuwapa kibali chake.
26 Yehova na ainue uso wake kuwaelekea na kuwapa amani.”’+
27 Ni lazima waliweke jina langu juu ya Waisraeli,+ ili niwabariki Waisraeli.”+
7 Siku ambayo Musa alimaliza kutengeneza hema la ibada,+ alilitia mafuta+ na kulitakasa pamoja na vyombo vyake vyote, na madhabahu na vyombo vyake vyote.+ Baada ya kuvitia mafuta na kuvitakasa vitu hivyo,+ 2 wakuu wa Israeli,+ viongozi wa koo zao,* wakaleta matoleo. Wakuu hao wa makabila waliosimamia kazi ya kuwaandikisha watu 3 wakamletea Yehova matoleo yao; walileta magari sita yaliyofunikwa na pia ng’ombe dume 12, gari moja kutoka kwa kila wakuu wawili na ng’ombe dume mmoja kutoka kwa kila mkuu; wakaleta vitu hivyo mbele ya hema la ibada. 4 Yehova akamwambia Musa: 5 “Pokea vitu hivyo kutoka kwao, kwa maana vitatumiwa katika utumishi wa hema la mkutano, nawe unapaswa kuwapa Walawi vitu hivyo, utampa kila mmoja kulingana na mahitaji ya kazi yake.”
6 Basi Musa akapokea magari hayo pamoja na ng’ombe na kuwapa Walawi. 7 Aliwapa wana wa Gershoni magari mawili na ng’ombe dume wanne kulingana na mahitaji ya kazi yao;+ 8 akawapa wana wa Merari magari manne na ng’ombe dume wanane kulingana na mahitaji ya kazi yao, chini ya usimamizi wa Ithamari mwana wa kuhani Haruni.+ 9 Lakini hakuwapa chochote wana wa Kohathi kwa sababu majukumu yao yalihusisha kutumikia mahali patakatifu,+ nao walibeba vitu vitakatifu mabegani.+
10 Basi wakuu wakaleta matoleo yao siku ya kuzindua*+ madhabahu na kuitia mafuta. Wakuu walipoleta matoleo yao mbele ya madhabahu, 11 Yehova akamwambia Musa: “Kila siku, mkuu mmoja ataleta matoleo yake kwa ajili ya kuizindua madhabahu.”
12 Yule aliyeleta matoleo yake siku ya kwanza alikuwa Nashoni+ mwana wa Aminadabu wa kabila la Yuda. 13 Alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130* na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,*+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 14 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba;* 15 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 16 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 17 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Nashoni mwana wa Aminadabu.+
18 Siku ya pili, Nethaneli+ mwana wa Zuari, mkuu wa Isakari, alileta matoleo yake. 19 Alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 20 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 21 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 22 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 23 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Nethaneli mwana wa Zuari.
24 Siku ya tatu, mkuu wa wana wa Zabuloni, Eliabu+ mwana wa Heloni, 25 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 26 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 27 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 28 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 29 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Eliabu+ mwana wa Heloni.
30 Siku ya nne, mkuu wa wana wa Rubeni, Elisuri+ mwana wa Shedeuri, 31 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 32 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 33 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 34 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 35 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Elisuri+ mwana wa Shedeuri.
36 Siku ya tano, mkuu wa wana wa Simeoni, Shelumieli+ mwana wa Zurishadai, 37 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 38 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 39 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 40 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 41 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Shelumieli+ mwana wa Zurishadai.
42 Siku ya sita, mkuu wa wana wa Gadi, Eliasafu+ mwana wa Deueli, 43 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 44 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 45 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 46 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 47 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Eliasafu+ mwana wa Deueli.
48 Siku ya saba, mkuu wa wana wa Efraimu, Elishama+ mwana wa Amihudi, 49 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 50 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 51 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 52 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 53 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Elishama+ mwana wa Amihudi.
54 Siku ya nane, mkuu wa wana wa Manase, Gamalieli+ mwana wa Pedazuri, 55 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 56 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 57 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 58 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 59 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Gamalieli+ mwana wa Pedazuri.
60 Siku ya tisa, mkuu+ wa wana wa Benjamini, Abidani+ mwana wa Gidioni, 61 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 62 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 63 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 64 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 65 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Abidani+ mwana wa Gidioni.
66 Siku ya kumi, mkuu wa wana wa Dani, Ahiezeri+ mwana wa Amishadai, 67 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 68 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 69 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 70 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 71 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Ahiezeri+ mwana wa Amishadai.
72 Siku ya 11, mkuu wa wana wa Asheri, Pagieli+ mwana wa Okrani, 73 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 74 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 75 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 76 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 77 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Pagieli+ mwana wa Okrani.
78 Siku ya 12, mkuu wa wana wa Naftali, Ahira+ mwana wa Enani, 79 alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 80 kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 81 ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 82 mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 83 na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Ahira+ mwana wa Enani.
84 Haya ndiyo matoleo ya kuzindua+ madhabahu yaliyoletwa na wakuu wa Israeli siku ilipotiwa mafuta: sahani 12 za fedha, mabakuli 12 ya fedha, vikombe 12 vya dhahabu;+ 85 kila sahani ya fedha ilikuwa na uzito wa shekeli 130, na kila bakuli lilikuwa na uzito wa shekeli 70, fedha yote iliyotengeneza vyombo hivyo ilikuwa na uzito wa shekeli 2,400 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu;+ 86 vile vikombe 12 vya dhahabu vilivyojaa uvumba vilikuwa na uzito wa shekeli 10 kila kikombe kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu, dhahabu yote iliyotengeneza vikombe hivyo ilikuwa na uzito wa shekeli 120. 87 Ng’ombe dume wote walioletwa kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa walikuwa 12, pia kondoo dume 12, wanakondoo dume 12 kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja na matoleo yao ya nafaka, na wanambuzi 12 kwa ajili ya dhabihu ya dhambi; 88 na ng’ombe dume wote walioletwa kwa ajili ya dhabihu ya ushirika walikuwa 24, pia kondoo dume 60, mbuzi dume 60, na wanakondoo dume 60 kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo matoleo yaliyotolewa kwa ajili ya kuizindua+ madhabahu baada ya kuitia mafuta.+
89 Kila mara Musa alipoingia katika hema la mkutano kuongea na Mungu,+ alisikia sauti ikizungumza naye kutoka juu ya kifuniko+ cha sanduku la Ushahidi, kutoka katikati ya wale makerubi wawili;+ Mungu aliongea naye.
8 Yehova akamwambia Musa: 2 “Mwambie hivi Haruni: ‘Unapowasha taa, taa hizo saba zinapaswa kuangaza upande wa mbele wa kinara cha taa.’”+ 3 Basi Haruni akafanya hivi: Akawasha taa hizo ili ziangaze upande wa mbele wa kinara cha taa,+ kama Yehova alivyomwamuru Musa. 4 Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa nyundo+ kwa kutumia dhahabu; kuanzia shina lake mpaka maua yake, kilitengenezwa kwa nyundo. Kinara hicho cha taa kilitengenezwa kulingana na maono+ ambayo Yehova alikuwa amemwonyesha Musa.
5 Yehova akazungumza tena na Musa, akamwambia: 6 “Wachukue Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli, uwatakase.+ 7 Hivi ndivyo unavyopaswa kuwatakasa: Wanyunyizie maji ya kutakasa dhambi, na ni lazima wajinyoe mwili mzima kwa wembe, wafue mavazi yao, na kujitakasa.+ 8 Kisha watachukua ng’ombe dume mchanga+ na toleo lake la nafaka+ la unga laini uliochanganywa na mafuta, nawe utachukua ng’ombe dume mwingine mchanga kwa ajili ya dhabihu ya dhambi.+ 9 Utawapeleka Walawi mbele ya hema la mkutano na kuwakusanya Waisraeli wote.+ 10 Utakapowapeleka Walawi mbele za Yehova, Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.+ 11 Ni lazima Haruni awatoe* Walawi mbele za Yehova kama toleo la kutikiswa+ kutoka kwa Waisraeli, nao watatekeleza utumishi wa Yehova.+
12 “Kisha Walawi wataweka mikono yao juu ya vichwa vya wale ng’ombe dume.+ Kisha watamtolea Yehova ng’ombe dume mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi na mwingine kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa ili kufunika dhambi+ zao. 13 Nawe utawasimamisha Walawi mbele ya Haruni na wanawe na kuwatoa* kwa Yehova kama toleo la kutikiswa. 14 Ni lazima uwatenge Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli, nao Walawi watakuwa wangu.+ 15 Kisha Walawi wataingia ndani ya hema la mkutano ili kutumikia. Hivyo ndivyo unavyopaswa kuwatakasa na kuwatoa* kama toleo la kutikiswa. 16 Kwa maana wao ni watu waliokabidhiwa, niliokabidhiwa kutoka miongoni mwa Waisraeli. Nitawachukua hao kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wote wa kwanza* wa Waisraeli.+ 17 Kwa maana kila mzaliwa wa kwanza miongoni mwa Waisraeli ni wangu, awe mwanadamu au mnyama.+ Niliwatakasa ili wawe wangu siku niliyomuua kila mzaliwa wa kwanza nchini Misri.+ 18 Nitawachukua Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa Waisraeli. 19 Nitampa Haruni na wanawe Walawi hao wakiwa watu waliokabidhiwa kutoka miongoni mwa Waisraeli, ili watumikie katika hema la mkutano+ kwa niaba ya Waisraeli na kutoa dhabihu ya kufunika dhambi za Waisraeli, na ili Waisraeli wasipatwe na pigo lolote+ kwa sababu wao hukaribia mahali patakatifu.”
20 Musa na Haruni na Waisraeli wote wakawatendea Walawi mambo hayo. Waisraeli waliwatendea Walawi kulingana na mambo yote ambayo Yehova alimwamuru Musa awatendee. 21 Basi Walawi wakajitakasa na kufua mavazi yao,+ kisha Haruni akawatoa* kama toleo la kutikiswa mbele za Yehova.+ Halafu Haruni akatoa dhabihu ya kufunika dhambi zao ili kuwatakasa.+ 22 Baada ya hayo, Walawi waliingia ili kutumikia katika hema la mkutano chini ya usimamizi wa Haruni na wanawe. Waliwatendea kama Yehova alivyomwamuru Musa kuhusu Walawi.
23 Sasa Yehova akamwambia Musa: 24 “Jambo hili linawahusu Walawi: Mwanamume mwenye umri wa miaka 25 na zaidi atajiunga na wale wanaotumikia katika hema la mkutano. 25 Lakini baada ya umri wa miaka 50 atastaafu, hataendelea na utumishi huo. 26 Anaweza kuwasaidia ndugu zake wanaotumikia katika hema la mkutano, lakini hapaswi kupewa kazi humo. Hivyo ndivyo utakavyofanya kuhusu Walawi na majukumu yao.”+
9 Yehova akazungumza na Musa katika nyika ya Sinai katika mwezi wa kwanza+ wa mwaka wa pili baada ya wao kutoka nchini Misri, akamwambia: 2 “Waisraeli wanapaswa kutayarisha dhabihu ya Pasaka+ wakati wake uliopangwa.+ 3 Siku ya 14 ya mwezi huo kabla ya giza kuingia,* mnapaswa kuitayarisha wakati wake uliopangwa. Mnapaswa kuitayarisha kulingana na sheria zake zote na utaratibu wake wote uliowekwa.”+
4 Basi Musa akawaambia Waisraeli waitayarishe dhabihu ya Pasaka. 5 Kwa hiyo wakaitayarisha dhabihu ya Pasaka katika nyika ya Sinai katika mwezi wa kwanza, siku ya 14 ya mwezi huo kabla ya giza kuingia.* Waisraeli walifanya mambo yote ambayo Yehova alimwamuru Musa.
6 Sasa watu fulani hawakuwa safi kwa sababu waligusa mtu aliyekufa,+ hivyo hawangeweza kuitayarisha dhabihu ya Pasaka siku hiyo. Kwa hiyo wakaenda kumwona Musa na Haruni siku hiyo,+ 7 wakamwambia Musa: “Sisi si safi kwa sababu tumemgusa mtu aliyekufa. Kwa nini tukatazwe kumtolea Yehova dhabihu kwa wakati uliopangwa pamoja na Waisraeli wengine?”+ 8 Ndipo Musa akawaambia: “Ngojeni hapo, acheni nione Yehova ataamuru nini kuwahusu.”+
9 Yehova akamwambia Musa: 10 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Mtu yeyote miongoni mwenu au miongoni mwa vizazi vyenu vijavyo akijichafua kwa kumgusa mtu aliyekufa+ au akisafiri mbali, bado anapaswa kumtayarishia Yehova dhabihu ya Pasaka. 11 Watu hao wanapaswa kuitayarisha katika mwezi wa pili,+ siku ya 14 kabla ya giza kuingia.* Wanapaswa kuila pamoja na mikate isiyo na chachu na mboga chungu.+ 12 Hawapaswi kuacha chochote mpaka asubuhi,+ wala hawapaswi kuvunja mfupa wowote wa dhabihu hiyo.+ Wanapaswa kuitayarisha kulingana na sheria zote za Pasaka. 13 Lakini ikiwa mtu alikuwa safi au hakuwa amesafiri naye amepuuza kuitayarisha dhabihu ya Pasaka, ni lazima mtu huyo auawe kutoka kati ya watu wake+ kwa sababu hakumtolea Yehova dhabihu hiyo kwa wakati wake uliopangwa. Mtu huyo ataadhibiwa kwa sababu ya dhambi yake.
14 “‘Ikiwa unaishi na mgeni, anapaswa pia kumtayarishia Yehova dhabihu ya Pasaka.+ Anapaswa kuitayarisha kulingana na sheria na utaratibu uliowekwa wa Pasaka.+ Ninyi nyote mtafuata sheria moja, mkaaji mgeni pamoja na mwenyeji wa nchi.’”+
15 Siku ambayo hema la ibada lilijengwa,+ wingu lilifunika hema la ibada, yaani, hema la Ushahidi, lakini wakati wa jioni kitu kilichoonekana kama moto kilikaa juu ya hema hilo mpaka asubuhi.+ 16 Hivi ndivyo ilivyokuwa kila siku: Wingu hilo lilifunika hema wakati wa mchana, na kitu kilichoonekana kama moto kilikaa juu ya hema wakati wa usiku.+ 17 Kila mara wingu hilo lilipoinuka kutoka juu ya hema, Waisraeli waliondoka bila kukawia,+ na mahali ambapo wingu hilo lilisimama, hapo ndipo Waisraeli walipopiga kambi.+ 18 Waisraeli waliondoka kwa agizo la Yehova, na kwa agizo la Yehova walipiga kambi.+ Waliendelea kupiga kambi muda wote ambao wingu hilo lilikaa juu ya hema la ibada. 19 Wingu hilo lilipokaa juu ya hema la ibada kwa siku nyingi, Waisraeli walimtii Yehova nao hawakuondoka.+ 20 Nyakati nyingine wingu hilo lilikaa juu ya hema la ibada kwa siku chache. Waliendelea kupiga kambi kwa agizo la Yehova, na kwa agizo la Yehova waliondoka. 21 Nyakati fulani wingu hilo lilikaa juu ya hema la ibada kuanzia jioni mpaka asubuhi tu, na wingu hilo lilipoinuka asubuhi, waliondoka. Iwe liliinuka mchana au usiku, waliondoka.+ 22 Iwe ni kwa siku mbili, mwezi mmoja, au muda mrefu zaidi, muda wote ambao wingu hilo lilikaa juu ya hema la ibada, Waisraeli waliendelea kupiga kambi nao hawakuondoka. Lakini lilipoinuka waliondoka. 23 Walipiga kambi kwa agizo la Yehova, na kwa agizo la Yehova waliondoka. Walitimiza wajibu wao kwa Yehova kama Yehova alivyowaagiza kupitia Musa.
10 Kisha Yehova akamwambia Musa: 2 “Jitengenezee tarumbeta mbili+ za fedha; zitengeneze kwa kutumia nyundo, nawe uzitumie kuwakusanya watu na kuvunja kambi. 3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, ni lazima Waisraeli wote wakusanyike mbele yako kwenye mlango wa hema la mkutano.+ 4 Tarumbeta moja tu ikipigwa, ni wakuu peke yao watakaokusanyika mbele yako, yaani, viongozi wa maelfu katika Israeli.+
5 “Mkipiga tarumbeta kwa mlio unaobadilika-badilika, wale wanaopiga kambi upande wa mashariki+ wanapaswa kuanza safari. 6 Mkipiga tarumbeta mara ya pili kwa mlio unaobadilika-badilika, wale wanaopiga kambi upande wa kusini+ wanapaswa kuanza safari. Tarumbeta inapaswa kupigwa kwa njia hiyo kila mara kambi moja inapoanza safari.
7 “Mnapowakusanya watu wote, mnapaswa kuzipiga tarumbeta+ kwa mlio usiobadilika-badilika. 8 Wana wa Haruni, makuhani, wanapaswa kuzipiga tarumbeta;+ na hiyo itakuwa sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote.
9 “Ikiwa maadui wanaowakandamiza watawashambulia katika nchi yenu, mnapaswa kupiga mwito wa vita kwa tarumbeta hizo,+ na Yehova Mungu wenu atawakumbuka na kuwaokoa kutoka kwa maadui wenu.
10 “Pia, katika siku zenu za kushangilia+—wakati wa sherehe zenu+ na mwanzoni mwa miezi yenu—mtazipiga tarumbeta hizo mnapotoa* dhabihu zenu za kuteketezwa+ na dhabihu zenu za ushirika;+ zitanifanya mimi Mungu wenu niwakumbuke. Mimi ni Yehova Mungu wenu.”+
11 Basi katika mwaka wa pili, mwezi wa pili, siku ya 20 ya mwezi huo,+ lile wingu liliinuka kutoka juu ya hema+ la Ushahidi. 12 Kwa hiyo Waisraeli wakaanza kuondoka katika nyika ya Sinai kulingana na utaratibu uliowekwa wa kuondoka,+ na wingu hilo likasimama katika nyika ya Parani.+ 13 Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwao kuondoka kama Yehova alivyokuwa amewaagiza kupitia Musa.+
14 Kwa hiyo kundi la makabila matatu katika kambi ya wana wa Yuda liliondoka kwanza kulingana na vikosi vyake,* na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Nashoni+ mwana wa Aminadabu. 15 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Isakari alikuwa Nethaneli+ mwana wa Zuari. 16 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Zabuloni alikuwa Eliabu+ mwana wa Heloni.
17 Hema la ibada lilipofunguliwa,+ wana wa Gershoni+ na wana wa Merari,+ waliobeba hema hilo, walianza safari.
18 Kisha kundi la makabila matatu katika kambi ya Rubeni liliondoka kulingana na vikosi vyake,* na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 19 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Simeoni alikuwa Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 20 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Gadi alikuwa Eliasafu+ mwana wa Deueli.
21 Kisha Wakohathi, waliobeba vyombo vya mahali patakatifu,+ wakaondoka. Hema la ibada lilipaswa kusimamishwa kabla hawajafika.
22 Kisha kundi la makabila matatu katika kambi ya wana wa Efraimu liliondoka kulingana na vikosi vyake,* na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Elishama+ mwana wa Amihudi. 23 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Manase alikuwa Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 24 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Benjamini alikuwa Abidani+ mwana wa Gidioni.
25 Kisha kundi la makabila matatu katika kambi ya wana wa Dani liliondoka kulingana na vikosi vyake,* nao walikuwa kikosi cha nyuma cha kulinda kambi zote, na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 26 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Asheri alikuwa Pagieli+ mwana wa Okrani. 27 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Naftali alikuwa Ahira+ mwana wa Enani. 28 Huo ndio utaratibu ambao Waisraeli na vikosi vyao walifuata* kila mara walipoanza safari.+
29 Kisha Musa akamwambia Hobabu mwana wa Reueli,*+ Mmidiani, baba mkwe wake: “Tunaenda mahali ambapo Yehova alisema, ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’+ Basi twende pamoja,+ nasi tutakutendea mema, kwa sababu Yehova ameahidi kuwapa Waisraeli mambo mema.”+ 30 Lakini akamwambia: “Sitaenda. Nitarudi katika nchi yangu na kwa watu wangu wa ukoo.” 31 Musa akamwambia: “Tafadhali usituache, kwa maana unajua mahali tunapopaswa kupiga kambi nyikani, nawe unaweza kutuonyesha njia.* 32 Ukienda pamoja nasi,+ jambo lolote jema ambalo Yehova atatutendea, bila shaka tutakutendea wewe pia.”
33 Basi wakasafiri kwa siku tatu kutoka kwenye mlima wa Yehova,+ na sanduku+ la agano la Yehova lilisafirishwa mbele yao kwa siku hizo tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.+ 34 Nalo wingu la Yehova+ lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka mahali walipokuwa wamepiga kambi.
35 Kila mara Sanduku hilo lilipoanza kusafirishwa, Musa alisema: “Inuka, Ee Yehova,+ acha maadui wako watawanyike, na wale wanaokuchukia wakimbie kutoka mbele zako.” 36 Na lilipowekwa chini, alisema: “Rudi, Ee Yehova, kwa maelfu yasiyohesabika* ya Waisraeli.”+
11 Sasa watu wakaanza kulalamika kwa uchungu mbele za Yehova. Yehova aliposikia malalamiko yao, alikasirika sana, na moto kutoka kwa Yehova ukaanza kuwateketeza na kuwaangamiza baadhi ya watu waliokuwa kandokando ya kambi. 2 Watu walipoanza kumlilia Musa, alimwomba Yehova dua,+ nao moto ukazimika. 3 Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Tabera,* kwa sababu moto kutoka kwa Yehova uliwateketeza watu.+
4 Kisha umati wa watu waliochangamana nao*+ ukaanza kutamani chakula kwa pupa,+ basi Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema: “Ni nani atakayetupatia nyama tule?+ 5 Tunakumbuka sana samaki wa bure tuliokuwa tukila nchini Misri, pamoja na matango, matikiti, vitunguu vya majani, vitunguu maji, na vitunguu saumu!+ 6 Lakini sasa tunadhoofika. Hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana.”+
7 Kwa kweli, mana+ ilikuwa kama mbegu za giligilani,+ na ilionekana kama utomvu wa mbedola. 8 Watu walikuwa wakienda kila mahali kuiokota, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia au waliitwanga kwenye kinu. Halafu waliichemsha katika vyungu vya kupikia au waliitumia kuoka mikate ya mviringo,+ na ladha yake ilikuwa kama ladha ya keki tamu iliyookwa kwa mafuta. 9 Umande ulipoanguka kambini usiku, mana pia ilianguka pamoja na umande huo.+
10 Musa akawasikia watu wakilia katika kila familia, kila mtu kwenye mlango wa hema lake. Basi Yehova akakasirika sana,+ na Musa pia akachukizwa sana na jambo hilo. 11 Kisha Musa akamwambia Yehova: “Kwa nini unanitesa mimi mtumishi wako? Kwa nini hupendezwi nami, hivi kwamba umenitwika mzigo wa watu wote hawa?+ 12 Je, ni mimi niliyebeba mimba ya watu hawa wote? Je, ni mimi niliyewazaa ndiyo sababu unaniambia, ‘Wabebe kifuani pako, kama mlezi* anavyombeba mtoto mchanga,’ na kuwapeleka katika nchi uliyoapa kwamba utawapa mababu zao?+ 13 Nitapata wapi nyama ya kuwapa watu hawa wote? Kwa sababu wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’ 14 Siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu; ni mzigo mzito sana kwangu.+ 15 Ikiwa utaendelea kunitendea hivi, tafadhali niue sasa hivi.+ Ikiwa nimepata kibali machoni pako, usiache niendelee kutaabika.”
16 Yehova akamjibu Musa: “Nikusanyie wanaume 70 miongoni mwa wazee wa Israeli, wanaume ambao unajua kwamba ni wazee na maofisa wa watu,+ nawe uwapeleke kwenye hema la mkutano, na kuwaagiza wasimame hapo pamoja nawe. 17 Nitashuka+ na kuzungumza nawe hapo,+ nami nitachukua kiasi fulani cha roho+ iliyo juu yako na kuiweka juu yao, nao watakusaidia kubeba mzigo wa watu hawa ili usiubebe peke yako.+ 18 Unapaswa kuwaambia watu, ‘Jitakaseni kwa ajili ya kesho,+ kwa maana hakika mtakula nyama, kwa sababu Yehova amewasikia mkilia+ na kusema: “Ni nani atakayetupatia nyama tule? Hali yetu ilikuwa nzuri zaidi nchini Misri.”+ Hakika Yehova atawapa nyama, nanyi mtaila.+ 19 Hamtaila kwa siku moja tu, au siku 2, au siku 5, au siku 10, au hata siku 20, 20 bali kwa mwezi mzima, mpaka itakapotokea kwenye mianzi ya pua zenu na kuwachukiza,+ kwa sababu mlimkataa Yehova aliye kati yenu, nanyi mlilia mbele zake mkisema: “Kwa nini tumetoka Misri?”’”+
21 Kisha Musa akasema: “Niko miongoni mwa wanaume 600,000+ wanaotembea kwa miguu, nawe unasema, ‘Nitawapa nyama, nao watakula nyama ya kutosha kwa mwezi mzima’! 22 Je, makundi mazima ya kondoo na ng’ombe yakichinjwa, yatawatosha? Au samaki wote wa baharini wakivuliwa, je, watawatosha?”
23 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Je, mkono wa Yehova ni mfupi?+ Sasa utaona ikiwa jambo ninalosema litatimia kwako au la.”
24 Basi Musa akatoka na kuwaambia watu maneno ya Yehova. Akawakusanya wanaume 70 miongoni mwa wazee wa watu na kuwaagiza wasimame kuzunguka hema la mkutano.+ 25 Kisha Yehova akashuka katika wingu+ na kuzungumza naye,+ akachukua kiasi fulani cha roho+ iliyokuwa juu yake na kuiweka juu ya kila mmoja wa wale wazee 70. Na mara tu roho hiyo iliposhuka juu yao, wakaanza kutenda kama manabii,*+ lakini hawakufanya hivyo tena.
26 Wawili kati ya wanaume hao walibaki kambini. Mmoja aliitwa Eldadi na mwingine Medadi. Na roho ikaanza kushuka juu yao, kwa maana walikuwa kati ya wale ambao majina yao yalikuwa yameandikwa lakini hawakwenda kwenye hema la mkutano. Basi wakaanza kutenda kama manabii kambini. 27 Mwanamume mmoja kijana akakimbia na kumwambia Musa: “Eldadi na Medadi wanatenda kama manabii kambini!” 28 Ndipo Yoshua+ mwana wa Nuni, aliyekuwa mtumishi wa Musa tangu ujanani, akasema: “Bwana wangu Musa, wakataze!”+ 29 Lakini Musa akamwambia: “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Usifanye hivyo, laiti watu wote wa Yehova wangekuwa manabii na laiti Yehova angeweka roho yake juu yao!” 30 Baadaye Musa akarudi kambini pamoja na wazee wa Israeli.
31 Kisha upepo kutoka kwa Yehova ukavuma ghafla na kuanza kuleta kware kutoka baharini na kuwaangusha kotekote kambini,+ kwenye eneo la umbali wa siku moja hivi kila upande kuzunguka kambi, wakafikia kimo cha mikono miwili* hivi kutoka ardhini. 32 Basi siku hiyo yote, mchana na usiku wote, na siku nzima iliyofuata waliendelea kuokota kware. Hakuna aliyeokota chini ya homeri kumi,* nao waliwaanika kila mahali kambini. 33 Lakini nyama ilipokuwa ingali katikati ya meno yao, kabla hawajaitafuna, hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya watu, na Yehova akaanza kuwapiga watu kwa maangamizi makubwa sana.+
34 Kwa hiyo wakapaita mahali hapo Kibroth-hataava,*+ kwa sababu hapo ndipo walipowazika watu waliokuwa na tamaa na pupa.+ 35 Kutoka Kibroth-hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi+ na kukaa huko.
12 Miriamu na Haruni wakaanza kusema vibaya kumhusu Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa, kwa maana Musa alikuwa ameoa mwanamke Mkushi.+ 2 Walikuwa wakisema: “Je, Yehova amezungumza kupitia Musa peke yake? Je, hajazungumza kupitia sisi pia?”+ Na Yehova alikuwa akisikiliza.+ 3 Basi Musa alikuwa mtu mpole zaidi kuliko watu wote*+ duniani.
4 Kwa ghafla Yehova akamwambia Musa, Haruni, na Miriamu: “Ninyi watatu, nendeni kwenye hema la mkutano.” Basi wote watatu wakaenda. 5 Yehova akashuka katika nguzo ya wingu+ na kusimama kwenye mlango wa hema la mkutano, akamwita Haruni na Miriamu. Wote wawili wakaenda mbele. 6 Ndipo akawaambia: “Tafadhali, sikilizeni maneno yangu. Ikiwa nabii wangu, mimi Yehova, angekuwa miongoni mwenu, ningejitambulisha kwake katika maono,+ nami ningeongea naye katika ndoto.+ 7 Lakini sijafanya hivyo kuhusiana na mtumishi wangu Musa! Nimemkabidhi nyumba yangu yote.*+ 8 Mimi huongea naye uso kwa uso,*+ waziwazi, wala si kwa mafumbo; naye huona uwepo wangu, mimi Yehova. Kwa nini, basi, hamkuogopa kusema vibaya kumhusu Musa, mtumishi wangu?”
9 Kwa hiyo hasira ya Yehova ikawaka dhidi yao, naye akaenda zake. 10 Lile wingu likaondoka juu ya hema, na tazama! Miriamu alikuwa amepigwa kwa ukoma mweupe kama theluji.+ Kisha Haruni akageuka na kumtazama Miriamu, akaona kwamba alikuwa amepigwa kwa ukoma.+ 11 Mara moja Haruni akamwambia Musa: “Nakusihi, bwana wangu! Tafadhali, usituadhibu kwa sababu ya dhambi hii! Tumetenda kwa upumbavu. 12 Tafadhali, usimwache aendelee kuwa kama mtu aliyezaliwa akiwa amekufa, ambaye nusu ya mwili wake imeoza!” 13 Basi Musa akaanza kumlilia Yehova, akisema: “Ee Mungu, tafadhali mponye! Tafadhali!”+
14 Yehova akamjibu Musa: “Ikiwa baba yake angemtemea mate usoni moja kwa moja, je, hangeaibika kwa siku saba? Acha atengwe nje ya kambi kwa siku saba,+ kisha anaweza kurudishwa kambini.” 15 Kwa hiyo Miriamu akatengwa nje ya kambi kwa siku saba,+ na watu hawakuendelea na safari hadi Miriamu aliporudishwa kambini. 16 Kisha watu wakaondoka Haserothi+ na kuanza kupiga kambi katika nyika ya Parani.+
13 Yehova akamwambia Musa: 2 “Watume wanaume wakaipeleleze nchi ya Kanaani ninayowapa Waisraeli. Mtume mwanamume mmoja kutoka katika kila kabila la baba yake, kila mmoja wao anapaswa kuwa mkuu+ katika kabila lake.”+
3 Basi Musa akawatuma kutoka katika nyika ya Parani+ kama Yehova alivyomwagiza. Wanaume hao wote walikuwa viongozi wa Waisraeli. 4 Haya ndiyo majina yao: kutoka katika kabila la Rubeni, Shamua mwana wa Zakuri; 5 kutoka katika kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori; 6 kutoka katika kabila la Yuda, Kalebu+ mwana wa Yefune; 7 kutoka katika kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu; 8 kutoka katika kabila la Efraimu, Hoshea+ mwana wa Nuni; 9 kutoka katika kabila la Benjamini, Palti mwana wa Rafu; 10 kutoka katika kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi; 11 kutoka katika kabila la Yosefu,+ kwa ajili ya kabila la Manase,+ Gadi mwana wa Susi; 12 kutoka katika kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali; 13 kutoka katika kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli; 14 kutoka katika kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofsi; 15 kutoka katika kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki. 16 Hayo ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kuipeleleza nchi. Musa alimpa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.*+
17 Musa alipokuwa akiwatuma kuipeleleza nchi ya Kanaani, aliwaambia: “Pandeni mwingie Negebu, na kwenda juu kwenye eneo lenye milima.+ 18 Chunguzeni mwone nchi hiyo ilivyo+ na kama watu wanaoishi humo ni wenye nguvu au dhaifu, wengi au wachache, 19 na kama nchi hiyo ni nzuri au ni mbaya na kama majiji wanamoishi ni kambi au ni ngome. 20 Chunguzeni ikiwa ni nchi tajiri au maskini,+ ina miti au haina. Ni lazima muwe jasiri+ na kuchukua baadhi ya matunda ya nchi hiyo.” Ulikuwa wakati wa kuiva kwa zabibu za kwanza.+
21 Basi wakaenda na kuipeleleza nchi kuanzia nyika ya Zini+ hadi Rehobu+ mpaka Lebo-hamathi.*+ 22 Walipopanda na kuingia Negebu, walifika Hebroni,+ ambako Ahimani, Sheshai, na Talmai,+ wazao wa Anaki+ waliishi. Sasa, Jiji la Hebroni lilijengwa miaka saba kabla ya jiji la Soani lililoko Misri. 23 Walipofika kwenye Bonde la Eshkoli,+ walikata tawi lenye kishada kimoja cha zabibu, na wanaume wawili wakalibeba kwa ufito pamoja na makomamanga kadhaa na tini.+ 24 Wakapaita mahali hapo Bonde la Eshkoli*+ kwa sababu ya kishada ambacho Waisraeli walikata kutoka huko.
25 Baada ya kuipeleleza nchi kwa siku 40,+ wanaume hao walirudi. 26 Walirudi kwa Musa, Haruni, na Waisraeli wote katika nyika ya Parani, huko Kadeshi.+ Wakawaletea habari Waisraeli wote na kuwaonyesha matunda ya nchi hiyo. 27 Hivi ndivyo walivyomwambia Musa: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, na kwa kweli inatiririka maziwa na asali,+ na haya ndiyo matunda yake.+ 28 Lakini watu wanaoishi katika nchi hiyo wana nguvu, na majiji yao yenye ngome ni makubwa sana. Tuliona pia wazao wa Anaki huko.+ 29 Waamaleki+ wanaishi katika nchi ya Negebu,+ nao Wahiti, Wayebusi,+ na Waamori+ wanaishi katika eneo lenye milima, na Wakanaani+ wanaishi karibu na bahari+ na kwenye kingo za Yordani.”
30 Kisha Kalebu akajaribu kuwatuliza watu waliosimama mbele ya Musa kwa kuwaambia: “Twendeni mara moja, na bila shaka tutaimiliki, kwa maana kwa hakika tunaweza kuishinda.”+ 31 Lakini wanaume waliopanda huko pamoja naye wakasema: “Hatuwezi kwenda kupigana na watu hao, kwa sababu wana nguvu kuliko sisi.”+ 32 Nao wakaendelea kuwapa Waisraeli habari mbaya+ kuhusu nchi waliyoipeleleza, wakisema: “Nchi tuliyoenda kuipeleleza ni nchi inayowameza wakaaji wake, na watu wote tuliowaona huko ni wakubwa isivyo kawaida.+ 33 Na huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki,+ wazao wa Wanefili, tulijiona kuwa kama panzi mbele yao, na ndivyo walivyotuona.”
14 Basi Waisraeli wote wakalia kwa sauti na kutokwa na machozi usiku kucha.+ 2 Waisraeli wote wakaanza kumnung’unikia Musa na Haruni,+ na wote wakawalalamikia wakisema: “Laiti tungalifia katika nchi ya Misri, au laiti tungalifia hapa nyikani! 3 Kwa nini Yehova anatuleta kwenye nchi hii ili tuuawe kwa upanga?+ Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka.+ Je, si afadhali turudi Misri?”+ 4 Hata waliambiana: “Na tuchague kiongozi, turudi Misri!”+
5 Ndipo Musa na Haruni wakaanguka chini kifudifudi mbele ya Waisraeli wote waliokuwa wamekusanyika. 6 Yoshua+ mwana wa Nuni na Kalebu+ mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwa watu walioipeleleza nchi, wakayararua mavazi yao, 7 na kuwaambia hivi Waisraeli wote: “Nchi tuliyoenda kuipeleleza ni nchi nzuri sana, nzuri kwelikweli.+ 8 Ikiwa Yehova amependezwa nasi, kwa hakika atatuingiza katika nchi hii na kutupatia iwe yetu, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ 9 Lakini msimwasi Yehova, nanyi msiwaogope watu wa nchi hiyo,+ kwa maana tutawashinda kwa urahisi.* Ulinzi wao umeondolewa, na Yehova yuko pamoja nasi.+ Msiwaogope.”
10 Hata hivyo, Waisraeli wote wakasema wapigwe mawe.+ Lakini utukufu wa Yehova ukatokea juu ya hema la mkutano machoni pa Waisraeli wote.+
11 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Watu hawa wataendelea kunidharau mpaka lini,+ watakataa kuniamini mpaka lini licha ya miujiza yote niliyofanya miongoni mwao?+ 12 Acha niwapige kwa ugonjwa hatari* na kuwafukuza, na acha nikufanye wewe kuwa taifa kubwa zaidi na lenye nguvu zaidi kuliko wao.”+
13 Lakini Musa akamwambia Yehova: “Kisha Wamisri, ambao kati yao uliwatoa watu hawa kwa nguvu zako, watasikia habari hizo,+ 14 nao watawaambia wakaaji wa nchi hii. Wakaaji hao pia wamesikia kwamba wewe, Yehova, uko miongoni mwa watu hawa,+ nawe umewatokea uso kwa uso.+ Wewe ni Yehova, na wingu lako limesimama juu yao, nawe unawatangulia katika nguzo ya wingu wakati wa mchana na katika nguzo ya moto wakati wa usiku.+ 15 Ukiwaua watu hawa wote mara moja, mataifa ambayo yamesikia sifa zako yatasema, 16 ‘Yehova alishindwa kuwapeleka watu hawa katika nchi ambayo aliapa kuwa angewapa ndiyo sababu aliwachinja nyikani.’+ 17 Sasa, Ee Yehova, tafadhali, acha nguvu zako kuu zionekane, kama ulivyoahidi uliposema, 18 ‘Mimi Yehova, si mwepesi wa hasira, nina upendo mwingi mshikamanifu,*+ ninasamehe makosa na uovu, lakini sikosi kamwe kuwaadhibu wenye hatia, ninawaadhibu wana na wajukuu kufikia kizazi cha tatu na cha nne kwa sababu ya makosa ya baba zao.’+ 19 Tafadhali, wasamehe watu hawa dhambi zao kulingana na upendo wako mwingi mshikamanifu, kama ambavyo umekuwa ukiwasamehe tangu walipotoka Misri mpaka sasa.”+
20 Basi Yehova akasema: “Nimewasamehe kama ulivyoomba.+ 21 Lakini, kwa hakika kama niishivyo, dunia yote itajaa utukufu wa Yehova.+ 22 Hata hivyo, hakuna mtu hata mmoja aliyeona utukufu wangu na miujiza+ niliyofanya nchini Misri na nyikani ambaye bado ananijaribu+ mara hizi kumi na kukataa kusikiliza sauti yangu+ 23 ataiona nchi niliyoapa kwamba nitawapa baba zao. Hakuna mtu hata mmoja anayenidharau atakayeiona.+ 24 Lakini kwa sababu mtumishi wangu Kalebu+ alikuwa na roho tofauti naye aliendelea kunifuata kwa moyo wote, kwa hakika nitamwingiza katika nchi aliyoenda kuipeleleza, na wazao wake wataimiliki.+ 25 Kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani+ wanaishi bondeni, kesho geukeni mwelekee nyikani kupitia njia ya Bahari Nyekundu.”+
26 Kisha Yehova akamwambia Musa na Haruni: 27 “Umati huu wa watu waovu utaendelea kuninung’unikia mpaka lini?+ Nimesikia manung’uniko ya Waisraeli juu yangu.+ 28 Waambie, ‘“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Yehova, “nitawatendea mambo yaleyale niliyosikia mkisema!+ 29 Maiti zenu zitaanguka katika nyika hii,+ naam, ninyi nyote mlioninung’unikia, kila mtu aliyeandikishwa mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi.+ 30 Hakuna hata mmoja wenu atakayeingia katika nchi niliyoapa kwamba mtaishi ndani yake,+ isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+
31 “‘“Na watoto wenu ambao mlisema kwamba watakuwa mateka,+ nitawaingiza katika nchi ambayo mmeikataa, nao wataijua.+ 32 Lakini maiti zenu zitaanguka katika nyika hii. 33 Wana wenu watakuwa wachungaji nyikani kwa miaka 40,+ nao lazima wateseke kwa sababu ya matendo yenu ya kukosa uaminifu* mpaka mtu wenu wa mwisho atakapofia nyikani.+ 34 Mtateseka kwa sababu ya makosa yenu kwa miaka 40,+ sawa na siku 40+ ambazo mliipeleleza nchi, yaani, siku moja kwa mwaka mmoja, siku moja kwa mwaka mmoja, kwa maana mtajionea matokeo ya kunipinga mimi.*
35 “‘“Mimi, Yehova, nimesema. Hivi ndivyo nitakavyoutendea umati huu wa watu waovu, ambao umekusanyika pamoja dhidi yangu: Wataishia humu nyikani, naam, watafia humu.+ 36 Wanaume ambao Musa aliwatuma kuipeleleza nchi, wakaleta habari mbaya kuhusu nchi hiyo na kufanya Waisraeli wote wamnung’unikie Musa,+ 37 naam, wanaume hao walioleta habari mbaya kuhusu nchi hiyo watauawa mbele za Yehova.+ 38 Lakini Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwa wanaume walioenda kuipeleleza nchi, ndio watakaoendelea kuishi.”’”+
39 Musa alipowaambia Waisraeli wote maneno hayo, watu walianza kuomboleza kwa uchungu mwingi. 40 Hata waliamka asubuhi na mapema na kujaribu kupanda juu mlimani, wakisema: “Tuko tayari kupanda mpaka mahali ambapo Yehova alituambia, kwa maana tumetenda dhambi.”+ 41 Lakini Musa akawaambia: “Kwa nini mnakiuka agizo la Yehova? Hamtafanikiwa. 42 Msipande kwenda huko, kwa sababu Yehova hayuko pamoja nanyi; mtashindwa na maadui wenu.+ 43 Kwa maana Waamaleki na Wakanaani watakabiliana nanyi huko,+ nao watawaangamiza kwa upanga. Kwa sababu mliacha kumfuata Yehova, Yehova hatakuwa pamoja nanyi.”+
44 Hata hivyo, kwa kimbelembele wakapanda kuelekea mlimani,+ lakini sanduku la agano la Yehova lilibaki katikati ya kambi, na Musa pia alibaki.+ 45 Ndipo Waamaleki na Wakanaani walioishi kwenye mlima huo wakashuka na kuanza kuwashambulia, wakawatawanya mpaka Horma.+
15 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 2 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Hatimaye mtakapoingia katika nchi ninayowapa mwishi ndani yake,+ 3 na kumtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto kutoka kati ya mifugo au kundi—iwe ni dhabihu ya kuteketezwa+ au dhabihu ya kutimiza nadhiri ya pekee au toleo la hiari+ au dhabihu mnayotoa wakati wa sherehe zenu za majira,+ ili kumtolea Yehova harufu inayompendeza*+— 4 ni lazima pia mtu anayetoa dhabihu yake amtolee Yehova sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja* ya unga laini+ uliochanganywa na robo ya hini* ya mafuta ili iwe toleo la nafaka. 5 Pia mnapaswa kutoa robo ya kipimo cha hini ya divai ili iwe toleo la kinywaji; mtaitoa pamoja na dhabihu ya kuteketezwa+ au pamoja na dhabihu ya kila mwanakondoo dume. 6 Au mtatoa kondoo dume pamoja na sehemu mbili za kumi za kipimo cha efa moja ya unga laini uliochanganywa na sehemu ya tatu ya hini ya mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka. 7 Nanyi mnapaswa kutoa sehemu ya tatu ya hini ya divai ili iwe toleo la kinywaji lenye harufu inayompendeza* Yehova.
8 “‘Lakini mkimtolea Yehova mnyama dume kutoka katika mifugo yenu ili awe dhabihu ya kuteketezwa+ au dhabihu ya kutimiza nadhiri ya pekee+ au dhabihu za ushirika,+ 9 mnapaswa kumtoa mnyama dume huyo pamoja na sehemu tatu za kumi za kipimo cha efa moja ya unga laini uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka.+ 10 Mnapaswa pia kutoa nusu ya hini ya divai ili iwe toleo la kinywaji+ linalochomwa kwa moto lenye harufu inayompendeza* Yehova. 11 Hivyo ndivyo mnavyopaswa kumtoa kila ng’ombe dume au kila kondoo dume au kila mwanakondoo dume au mbuzi dume. 12 Haidhuru mnatoa wanyama wangapi, mnapaswa kutoa vitu hivyo pamoja na kila mnyama mnayemtoa, kulingana na idadi yao. 13 Hivyo ndivyo kila Mwisraeli mwenyeji anavyopaswa kutoa dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.
14 “‘Ikiwa mgeni anayeishi nanyi au mtu mwingine ambaye ameishi pamoja nanyi kwa muda mrefu atatoa pia dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayompendeza* Yehova, anapaswa kufanya kama mnavyofanya.+ 15 Ninyi pamoja na mgeni anayeishi miongoni mwenu mtafuata sheria zilezile. Itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyenu vyote. Ninyi pamoja na mgeni mtakuwa sawa mbele za Yehova.+ 16 Ninyi na mgeni anayeishi miongoni mwenu mtafuata sheria zilezile na amri zilezile.’”*
17 Yehova akaendelea kumwambia Musa, 18 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka 19 nanyi mle chakula chochote cha* nchi hiyo,+ mnapaswa kumtolea Yehova kiasi fulani kama mchango. 20 Mtatoa mchango wa mazao ya kwanza+ ya mikate ya mviringo iliyookwa kwa unga wenu ambao haujakobolewa. Mtautoa kama mchango unaotoka katika uwanja wa kupuria nafaka. 21 Baadhi ya mazao ya kwanza ya unga wenu ambao haujakobolewa mtamtolea Yehova mchango katika vizazi vyenu vyote.
22 “‘Sasa mkifanya kosa, nanyi mkose kushika amri hizi zote ambazo mimi, Yehova, nimempa Musa, 23 mambo yote ambayo mimi, Yehova, nimewaamuru ninyi kupitia Musa katika vizazi vyenu tangu siku ambayo mimi Yehova niliamuru, 24 na ikiwa kosa hilo lilifanywa bila kukusudia na bila kusanyiko lote kujua, basi ni lazima kusanyiko lote litoe dhabihu ya kuteketezwa ya ng’ombe dume mchanga ili iwe harufu inayompendeza* Yehova, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji kulingana na utaratibu wa kawaida,+ na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi.+ 25 Kuhani atatoa dhabihu ya kufunika dhambi ya kusanyiko lote la Waisraeli, nao watasamehewa,+ kwa sababu lilikuwa kosa, nao walimletea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto na kuleta dhabihu yao ya dhambi mbele za Yehova kwa ajili ya kosa lao. 26 Kusanyiko lote la Waisraeli pamoja na wageni wanaokaa miongoni mwao watasamehewa kosa hilo kwa sababu watu wote walihusika.
27 “‘Mtu yeyote akifanya dhambi bila kukusudia, atatoa mbuzi jike wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi.+ 28 Kisha kuhani atatoa dhabihu ili mtu aliyetenda dhambi mbele za Yehova bila kukusudia asamehewe dhambi yake, yaani, atamtolea dhabihu ya kufunika dhambi yake, na mtu huyo atasamehewa.+ 29 Waisraeli wenyeji na pia wageni wanaoishi miongoni mwao watafuata sheria zilezile zinazomhusu mtu anayetenda kosa bila kukusudia.+
30 “‘Lakini mtu anayetenda kosa kimakusudi,+ awe ni mwenyeji au mgeni, anamkufuru Yehova, naye lazima auawe. 31 Kwa kuwa amedharau neno la Yehova na kuvunja amri yake, ni lazima mtu huyo auawe.+ Ataadhibiwa kwa sababu ya kosa lake.’”*+
32 Waisraeli walipokuwa nyikani, walimkuta mtu fulani akiokota kuni siku ya Sabato.+ 33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Musa na Haruni na Waisraeli wote. 34 Wakamtia kifungoni+ kwa sababu sheria haikusema waziwazi mtu huyo afanyiwe nini.
35 Basi Yehova akamwambia Musa: “Ni lazima mtu huyo auawe,+ Waisraeli wote watampiga mawe nje ya kambi.”+ 36 Basi Waisraeli wote wakamtoa nje ya kambi, wakampiga mawe na kumuua, kama Yehova alivyomwamuru Musa.
37 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 38 “Waambie Waisraeli wajitengenezee upindo wa nyuzinyuzi kwenye ncha za mavazi yao katika vizazi vyao vyote, nao watashona uzi wa bluu juu ya upindo huo wa nyuzinyuzi.+ 39 ‘Mnapaswa kutengeneza upindo huo wa nyuzinyuzi ili muuone na kukumbuka amri zote za Yehova na kuzishika.+ Msifuate mioyo yenu na macho yenu, ambayo yanawaongoza kwenye ukahaba wa kiroho.+ 40 Upindo huo utawasaidia kukumbuka, nanyi mtashika amri zangu zote na kuwa watakatifu kwangu mimi Mungu wenu.+ 41 Mimi ni Yehova Mungu wenu, niliyewatoa nchini Misri ili nijithibitishe kuwa Mungu wenu.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+
16 Kisha Kora+ mwana wa Ishari,+ mwana wa Kohathi,+ mwana wa Lawi,+ akaungana na Dathani na Abiramu wana wa Eliabu,+ na Oni mwana wa Pelethi, wazao wa Rubeni.+ 2 Nao, pamoja na wanaume 250 Waisraeli, wakuu wa kusanyiko, wanaume maarufu waliowekwa rasmi wakaanza kumpinga Musa. 3 Basi wakakusanyika dhidi ya+ Musa na Haruni na kuwaambia: “Mmetuchosha! Kusanyiko lote ni takatifu,+ watu wote, na Yehova yuko miongoni mwao.+ Basi, kwa nini mnajikweza juu ya kutaniko la Yehova?”
4 Musa aliposikia jambo hilo, mara moja akaanguka chini kifudifudi. 5 Kisha akamwambia Kora na watu wote waliomuunga mkono, “Asubuhi Yehova ataonyesha ni nani aliye wake+ na ni nani aliye mtakatifu na ni nani anayepaswa kumkaribia,+ na yeyote atakayemchagua+ ndiye atakayemkaribia. 6 Fanyeni hivi: Wewe Kora na wote wanaokuunga mkono,+ chukueni vyetezo,+ 7 kesho wekeni moto ndani yake na kutia uvumba juu yake mbele za Yehova, na mtu ambaye Yehova atamchagua,+ ndiye mtakatifu. Ninyi wana wa Lawi+ mmevuka mpaka!”
8 Kisha Musa akamwambia Kora: “Sikilizeni, tafadhali, ninyi wana wa Lawi. 9 Je, mnaona ni jambo dogo sana kwenu kwamba Mungu wa Israeli amewateua ninyi miongoni mwa Waisraeli+ wote na kuwaruhusu mumkaribie ili kutumikia katika hema la Yehova la ibada na kusimama mbele ya Waisraeli wote ili kuwahudumia,+ 10 na kuwaleta karibu naye ninyi pamoja na ndugu zenu wote, wana wa Lawi? Je, ni lazima pia mjaribu kunyakua ukuhani?+ 11 Kwa sababu hiyo, wewe na watu wote wanaokuunga mkono mnampinga Yehova. Haruni ni nani hivi kwamba mnung’unike kumhusu?”+
12 Baadaye Musa akatuma ujumbe ili Dathani na Abiramu+ wana wa Eliabu waitwe, lakini wakasema: “Hatutakuja! 13 Je, unafikiri ni jambo dogo kututoa katika nchi inayotiririka maziwa na asali ili utuue nyikani?+ Sasa, je, unataka kujifanya kiongozi mwenye mamlaka kamili juu yetu?* 14 Isitoshe, hujatuleta katika nchi yoyote inayotiririka maziwa na asali+ wala kutupatia urithi wa mashamba au shamba la mizabibu. Je, unataka kutoboa macho ya watu hawa? Sisi hatutakuja!”
15 Basi Musa akakasirika sana na kumwambia Yehova: “Usikubali toleo lao la nafaka. Sijachukua hata punda mmoja kutoka kwao, wala sijamdhuru mtu yeyote kati yao.”+
16 Kisha Musa akamwambia Kora: “Kesho, fika mbele za Yehova, wewe pamoja na watu wote wanaokuunga mkono, wewe na watu hao pamoja na Haruni. 17 Kila mmoja wenu anapaswa kuchukua chetezo chake na kuweka uvumba juu yake, na kila mmoja atapeleka chetezo chake mbele za Yehova, vyetezo 250, pia wewe na Haruni mtapeleka kila mmoja chetezo chake.” 18 Basi kila mmoja wao akachukua chetezo chake, akaweka moto na uvumba juu yake na kusimama kwenye mlango wa hema la mkutano pamoja na Musa na Haruni. 19 Kora alipokuwa amewakusanya watu wote waliomuunga mkono+ kwenye mlango wa hema la mkutano ili kumpinga Musa na Haruni, utukufu wa Yehova ukawatokea watu wote waliokusanyika.+
20 Kisha Yehova akamwambia Musa na Haruni, 21 “Jitengeni na kikundi hiki, ili nikiangamize mara moja.”+ 22 Ndipo Musa na Haruni wakaanguka chini kifudifudi na kusema: “Ee Mungu, Mungu wa roho ya watu wote,*+ je, dhambi ya mtu mmoja ikufanye uwakasirikie watu wote waliokusanyika?”+
23 Basi Yehova akamwambia Musa, 24 “Waambie hivi watu wote: ‘Ondokeni karibu na mahema ya Kora, Dathani, na Abiramu!’”+
25 Kisha Musa akaondoka na kwenda kwa Dathani na Abiramu, na wazee+ wa Israeli wakaenda pamoja naye. 26 Musa akawaambia hivi watu wote: “Tafadhali, ondokeni karibu na mahema ya watu hawa waovu wala msiguse kitu chochote ambacho ni mali yao, msije mkafagiliwa mbali kwa sababu ya dhambi yao yote.” 27 Mara moja wakaondoka karibu na mahema ya Kora, Dathani, na Abiramu, wakaondoka kila upande, kisha Dathani na Abiramu wakatoka nje, wakasimama kwenye mlango wa mahema yao pamoja na wake zao, wana wao, na watoto wao wachanga.
28 Halafu Musa akasema: “Hivi ndivyo mtakavyojua kwamba Yehova amenituma nifanye mambo haya yote, na kwamba sijayatunga moyoni mwangu:* 29 Watu hawa wakifa kama wanavyokufa wanadamu wengine wote na kuadhibiwa kama wanadamu wengine wote, basi Yehova hajanituma.+ 30 Lakini Yehova akiwatendea jambo lisilo la kawaida, ardhi ifunguke* na kuwameza watu hawa pamoja na vitu vyao vyote, nao waingie Kaburini* wakiwa hai, mtajua kwa hakika kwamba wamemdharau Yehova.”
31 Mara tu alipomaliza kusema maneno hayo yote, ardhi ikafunguka chini yao.+ 32 Naam, dunia ikafunguka* na kuwameza watu hao pamoja na familia zao na watu wote wa Kora+ na mali zao zote. 33 Kwa hiyo watu hao pamoja na watu wao wote wakaingia Kaburini* wakiwa hai, dunia ikawafunika, nao wakaangamia kutoka kati ya kutaniko.+ 34 Waisraeli wote waliokuwa wamewazunguka waliposikia vilio vyao wakakimbia wakisema: “Tunaogopa dunia itatumeza!” 35 Kisha moto ukashuka kutoka kwa Yehova+ na kuwateketeza wale wanaume 250 waliokuwa wakifukiza uvumba.+
36 Kisha Yehova akamwambia Musa, 37 “Mwambie Eleazari mwana wa kuhani Haruni achukue vyetezo+ hivyo kutoka motoni kwa sababu ni vitakatifu. Mwambie pia autawanye moto huo mbali kidogo na mahali hapo. 38 Vyetezo vya wanaume waliouawa kwa sababu ya dhambi yao vinapaswa kunyooshwa ili viwe mabamba membamba ya kufunika madhabahu,+ kwa sababu walivipeleka mbele za Yehova, navyo vikawa vitakatifu. Vinapaswa kuwa onyo kwa Waisraeli.”+ 39 Basi kuhani Eleazari akachukua vyetezo vya shaba vilivyoletwa na wale wanaume waliokuwa wameteketezwa, akavipiga na kuvinyoosha ili vifunike madhabahu, 40 kama Yehova alivyomwambia kupitia Musa. Viliwakumbusha Waisraeli kwamba mtu yeyote asiye na idhini* ambaye si mzao wa Haruni hapaswi kukaribia madhabahu ili kumfukizia Yehova+ uvumba na kwamba mtu yeyote asiwe kama Kora na wale waliomuunga mkono.+
41 Siku iliyofuata, kusanyiko lote la Waisraeli likaanza kumnung’unikia Musa na Haruni,+ likisema: “Ninyi wawili mmewaua watu wa Yehova.” 42 Watu wote walipokuwa wamekusanyika dhidi ya Musa na Haruni, waligeuka kuelekea hema la mkutano, na tazama! wingu lilifunika hema hilo, na utukufu wa Yehova ukaanza kuonekana.+
43 Musa na Haruni wakaenda mbele ya hema la mkutano,+ 44 na Yehova akamwambia Musa, 45 “Ninyi wanaume, jitengeni na kusanyiko hili ili niliangamize mara moja.”+ Ndipo Musa na Haruni wakaanguka chini kifudifudi.+ 46 Kisha Musa akamwambia Haruni, “Chukua chetezo uweke moto ndani yake kutoka katika madhabahu+ na uweke uvumba juu yake, nawe uende haraka kwao na kuufukiza ili dhambi yao ifunikwe,+ kwa sababu Yehova amekasirika. Pigo limeanza!” 47 Mara moja Haruni akachukua chetezo, kama Musa alivyomwambia, akakimbia katikati ya kusanyiko hilo, na pigo lilikuwa limeanza kuwaathiri watu. Basi akaweka uvumba juu ya chetezo, akaanza kuufukiza ili dhambi yao ifunikwe. 48 Akaendelea kusimama katikati ya watu waliokufa na walio hai, hatimaye pigo hilo likaisha. 49 Watu waliokufa kutokana na pigo hilo walikuwa 14,700, bila kuwahesabu wale waliokufa kwa sababu ya Kora. 50 Mwishowe Haruni aliporudi kwa Musa kwenye mlango wa hema la mkutano, pigo hilo lilikuwa limekomeshwa.
17 Kisha Yehova akamwambia Musa, 2 “Zungumza na Waisraeli na uchukue kutoka kwao fimbo moja kwa ajili ya kila kabila, kutoka kwa wakuu wa kila kabila,+ jumla ya fimbo 12. Andika jina la kila mmoja wao kwenye fimbo yake. 3 Unapaswa kuandika jina la Haruni kwenye fimbo ya Lawi, kwa sababu kuna fimbo moja kwa ajili ya kiongozi wa kila kabila. 4 Ziweke fimbo hizo ndani ya hema la mkutano mbele ya sanduku la Ushahidi,+ mahali ambapo mimi hukutokea kwa ukawaida.+ 5 Na fimbo ya mtu nitakayemchagua+ itachipua, nami nitakomesha manung’uniko ya Waisraeli dhidi yangu,+ ambayo pia wanakunung’unikia.”+
6 Basi Musa akazungumza na Waisraeli, na wakuu wao wote wakampa fimbo—fimbo moja kutoka kwa kila mkuu wa kabila, fimbo 12—nayo fimbo ya Haruni ilikuwa kati ya fimbo zao. 7 Kisha Musa akaziweka fimbo hizo mbele za Yehova katika hema la Ushahidi.
8 Siku iliyofuata, Musa alipoingia katika hema la Ushahidi, aliona fimbo ya Haruni ya kabila la Lawi imetokeza matumba nayo ilikuwa ikichanua maua na kuzaa matunda ya lozi yaliyoiva. 9 Kisha Musa akazichukua fimbo zote kutoka mbele za Yehova na kuzileta mbele ya Waisraeli wote. Wakazitazama na kila mkuu akachukua fimbo yake.
10 Halafu Yehova akamwambia Musa, “Irudishe fimbo ya Haruni+ mbele ya sanduku la Ushahidi ili iwekwe kuwa onyo+ kwa wana wa kuasi,+ ili manung’uniko yao dhidi yangu yakome na ili wasife.” 11 Mara moja Musa akafanya kama Yehova alivyomwamuru. Hivyo ndivyo alivyofanya.
12 Kisha Waisraeli wakamwambia Musa, “Sasa tutakufa, bila shaka tutaangamia, sisi sote tutaangamia! 13 Hata mtu yeyote atakayekaribia hema la Yehova la ibada atakufa!+ Je, ni lazima sote tufe kwa njia hiyo?”+
18 Kisha Yehova akamwambia Haruni, “Wewe na wana wako na ukoo wako* mtawajibika ikiwa kosa lolote litafanywa dhidi ya mahali patakatifu,+ na wewe na wana wako mtawajibika ikiwa kosa lolote litafanywa dhidi ya ukuhani wenu.+ 2 Pia walete ndugu zako wa kabila la Lawi, kabila la mababu zako, ili wajiunge nawe na kukuhudumia wewe+ pamoja na wanao mbele ya hema la Ushahidi.+ 3 Wanapaswa kutimiza majukumu utakayowapa na utumishi wa hema lote.+ Hata hivyo, hawapaswi kukaribia vyombo vya mahali patakatifu na madhabahu, ili wewe pamoja nao msife.+ 4 Watajiunga nawe na kutimiza majukumu yao kuhusiana na hema la mkutano na utumishi wote katika hema hilo, na mtu yeyote asiye na idhini* hapaswi kuwakaribia ninyi.+ 5 Ni lazima mtimize majukumu yenu ya mahali patakatifu+ na madhabahu,+ ili ghadhabu+ yangu isije tena juu ya Waisraeli. 6 Mimi mwenyewe nimewachukua ndugu zenu, Walawi, kutoka miongoni mwa Waisraeli na kuwakabidhi ninyi kama zawadi.+ Wamekabidhiwa kwa Yehova ili watumikie katika hema la mkutano.+ 7 Wewe na wanao mna wajibu wa kufanya kazi za ukuhani zinazohusu madhabahu na vitu vilivyo nyuma ya pazia,+ nanyi mtatimiza utumishi huo.+ Nimewapa utumishi wa ukuhani kama zawadi, na mtu yeyote asiye na idhini* atakayekaribia mahali patakatifu anapaswa kuuawa.”+
8 Yehova akaendelea kumwambia Haruni: “Mimi mwenyewe nilikuweka usimamie michango ninayoletewa.+ Nimekupa wewe na wanao sehemu ya vitu vyote vitakatifu vinavyotolewa kama mchango na Waisraeli ili viwe posho yenu ya kudumu.+ 9 Hivi ndivyo vitakavyokuwa vitu vyenu kutoka katika matoleo yote matakatifu kabisa yanayochomwa kwa moto: matoleo yao yote, kutia ndani matoleo yao ya nafaka+ na dhabihu zao za dhambi+ na dhabihu zao za hatia+ wanazoniletea. Ni vitu vitakatifu kabisa kwako na wanao. 10 Mtavila vitu hivyo mahali patakatifu zaidi.+ Kila mwanamume anaweza kuvila. Vitakuwa vitu vitakatifu kwenu.+ 11 Vitu hivi pia vitakuwa vyenu: zawadi ambazo Waisraeli wanatoa kuwa mchango+ pamoja na matoleo yao yote ya kutikiswa.+ Nimekupa wewe na wanao na mabinti wako vitu hivyo ili viwe posho yenu ya kudumu.+ Kila mtu aliye safi katika nyumba yako anaweza kula.+
12 “Mafuta yote bora na divai yote mpya na nafaka, mazao yao ya kwanza,+ ambayo wanampa Yehova, ninakupa wewe.+ 13 Mazao yote ya kwanza yaliyokomaa ya ardhi yao, ambayo watamletea Yehova, yatakuwa yako.+ Kila mtu aliye safi katika nyumba yako anaweza kula.
14 “Kila kitu kilichotolewa kwa ajili yangu* katika Israeli kinapaswa kuwa chako.+
15 “Kila mzaliwa wa kwanza wa viumbe wote walio hai,+ ambaye watanitolea mimi Yehova, awe ni mwanadamu au mnyama, anapaswa kuwa wako. Hata hivyo, ni lazima uwakomboe wazaliwa wa kwanza wa wanadamu,+ na unapaswa pia kuwakomboa wazaliwa wa kwanza wa wanyama wasio safi.+ 16 Unapaswa kumkomboa mzaliwa wa kwanza kwa bei ya ukombozi akiwa na umri wa kuanzia mwezi mmoja na zaidi, kwa thamani iliyokadiriwa ya shekeli tano za fedha,*+ kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.* Ni gera 20.* 17 Lakini hupaswi kumkomboa+ ng’ombe dume ambaye ni mzaliwa wa kwanza au mwanakondoo dume ambaye ni mzaliwa wa kwanza au mbuzi ambaye ni mzaliwa wa kwanza. Hao ni watakatifu. Unapaswa kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu,+ na mafuta yao unapaswa kuyateketeza ili yafuke moshi yakiwa dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.+ 18 Nyama yao itakuwa yako. Itakuwa yako sawa na kidari cha toleo la kutikiswa na mguu wa kulia.+ 19 Michango yote mitakatifu ambayo Waisraeli watamchangia Yehova,+ nimekupa wewe na wanao na mabinti wako, ili iwe posho yenu ya kudumu.+ Ni agano la chumvi linalodumu* mbele za Yehova kwa ajili yako na wazao wako.”
20 Yehova akaendelea kumwambia Haruni: “Hutakuwa na urithi katika nchi yao, wala hutakuwa na sehemu ya* ardhi miongoni mwao.+ Mimi ni fungu lako na urithi wako miongoni mwa Waisraeli.+
21 “Ona kwamba nimewapa wana wa Lawi kila sehemu ya kumi+ katika Israeli iwe urithi wao kwa sababu ya utumishi wao, utumishi wa hema la mkutano. 22 Waisraeli wasikaribie tena hema la mkutano ili wasitende dhambi na kufa. 23 Ni Walawi tu watakaotumikia katika hema la mkutano, na ndio watakaowajibika kwa ajili ya makosa yao.+ Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kwamba hawapaswi kuchukua urithi miongoni mwa Waisraeli.+ 24 Kwa maana nimewapa Walawi sehemu ya kumi ambayo Waisraeli wananitolea mchango, mimi Yehova, ili iwe urithi wao. Ndiyo sababu nimewaambia, ‘Hawapaswi kuchukua urithi miongoni mwa Waisraeli.’”+
25 Kisha Yehova akamwambia Musa, 26 “Unapaswa kuwaambia hivi Walawi: ‘Mtapokea kutoka kwa Waisraeli sehemu ya kumi ambayo nimewapa ninyi kutoka kwao ili iwe urithi wenu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova mchango wa sehemu ya kumi kutoka katika sehemu hiyo ya kumi.+ 27 Sehemu hiyo itahesabiwa kuwa mchango wenu, itaonwa kama nafaka kutoka katika uwanja wa kupuria+ au divai yote inayotoka katika shinikizo la divai au mafuta yote yanayotoka katika shinikizo la mafuta. 28 Kwa njia hiyo mtamtolea Yehova mchango kutoka katika sehemu zote za kumi mnazopokea kutoka kwa Waisraeli, na kutoka kwa sehemu hizo mnapaswa kumtolea Yehova mchango na kumpa kuhani Haruni. 29 Mtamtolea Yehova michango yote kutoka katika zawadi bora zaidi mnazopokea,+ ambazo ni takatifu.’
30 “Nawe unapaswa kuwaambia, ‘Mnapotoa vitu bora zaidi kutoka katika zawadi hizo kuwa mchango, mchango huo wa Walawi utaonwa kama nafaka kutoka katika uwanja wa kupuria na kama divai inayotoka katika shinikizo la divai au mafuta yanayotoka katika shinikizo la mafuta. 31 Ninyi na familia zenu mnaweza kula vitu hivyo mahali popote kwa sababu ni malipo kwa ajili ya utumishi wenu katika hema la mkutano.+ 32 Hamtakuwa na hatia ya dhambi maadamu mnanitolea vitu bora kutoka katika zawadi hizo, nanyi hampaswi kuchafua vitu vitakatifu vya Waisraeli, msije mkafa.’”+
19 Yehova akamwambia tena Musa na Haruni, 2 “Hii ndiyo sheria ambayo mimi Yehova nimeamuru, ‘Waambieni Waisraeli wawaletee ng’ombe mwekundu ambaye hana kasoro yoyote+ na ambaye hajawahi kufungwa nira. 3 Mtampa kuhani Eleazari ng’ombe huyo, naye atampeleka nje ya kambi na kuchinjwa mbele yake. 4 Kisha kuhani Eleazari atachukua kwa kidole chake kiasi kidogo cha damu ya ng’ombe huyo na kuinyunyiza mara saba kuelekea upande wa mbele wa hema la mkutano.+ 5 Kisha ng’ombe huyo atateketezwa mbele ya macho yake. Ngozi yake na nyama yake na damu yake pamoja na mavi yake yatateketezwa.+ 6 Halafu kuhani atachukua tawi la mwerezi, tawi la hisopo,+ na kitambaa chekundu na kutupa vitu hivyo katika moto unaomteketeza ng’ombe huyo. 7 Kisha kuhani atafua mavazi yake na kuoga kwenye maji, halafu anaweza kurudi kambini; lakini kuhani huyo hatakuwa safi mpaka jioni.
8 “‘Mtu aliyemteketeza ng’ombe huyo atafua mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni.
9 “‘Mtu aliye safi atayakusanya majivu ya ng’ombe huyo+ na kuyapeleka mahali safi nje ya kambi, yatahifadhiwa na Waisraeli ili yatumiwe kutengenezea maji ya kutakasa.+ Ni dhabihu ya dhambi. 10 Yule anayekusanya majivu ya ng’ombe huyo atafua mavazi yake, na hatakuwa safi mpaka jioni.
“‘Hiyo itakuwa sheria ya kudumu kwa Waisraeli na wageni wanaoishi miongoni mwao.+ 11 Mtu yeyote anayemgusa mtu aliyekufa* hatakuwa safi kwa siku saba.+ 12 Mtu huyo anapaswa kujitakasa kwa maji hayo siku ya tatu, na siku ya saba atakuwa safi. Lakini asipojitakasa siku ya tatu, hatakuwa safi siku ya saba. 13 Mtu yeyote anayemgusa mtu aliyekufa lakini hajitakasi amechafua hema la Yehova la ibada,+ na ni lazima mtu huyo auawe kutoka katika Israeli.+ Kwa sababu hajanyunyiziwa maji ya kutakasa,+ ataendelea kuwa mchafu. Yeye bado ni mchafu.
14 “‘Hii ndiyo sheria kuhusu mtu anayefia ndani ya hema: Kila mtu anayeingia katika hema hilo na kila mtu aliyekuwa ndani ya hema hilo wakati huo, hatakuwa safi kwa siku saba. 15 Kila chombo kilichofunuliwa ambacho kifuniko chake hakijafungwa kwa kamba si safi.+ 16 Kila mtu aliye uwanjani anayemgusa mtu aliyeuawa kwa upanga au maiti au mfupa wa mtu au kaburi hatakuwa safi kwa siku saba.+ 17 Kwa ajili ya mtu huyo asiye safi, watachukua majivu ya dhabihu ya dhambi iliyoteketezwa na kuyamiminia maji ya kijito katika chombo. 18 Kisha mtu aliye safi+ atachukua tawi la hisopo+ na kulichovya ndani ya maji hayo na kunyunyizia hema na vyombo vyote na watu waliokuwa ndani ya hema hilo na mtu aliyegusa mfupa au mtu aliyeuawa au maiti au kaburi. 19 Siku ya tatu na siku ya saba, mtu aliye safi atamnyunyizia maji hayo mtu asiye safi na kumtakasa dhambi yake siku ya saba;+ kisha atafua mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye atakuwa safi jioni.
20 “‘Lakini mtu asiye safi ambaye hatajitakasa ni lazima auawe kutoka kutanikoni+ kwa sababu amechafua mahali patakatifu pa Yehova. Kwa kuwa hakunyunyiziwa maji ya kutakasa, yeye si safi.
21 “‘Hii itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yao: Yule anayenyunyiza maji ya kutakasa+ anapaswa kufua mavazi yake, na yule anayegusa maji ya kutakasa hatakuwa safi mpaka jioni. 22 Kitu chochote kinachoguswa na mtu asiye safi hakitakuwa safi, na mtu anayekigusa hatakuwa safi mpaka jioni.’”+
20 Katika mwezi wa kwanza, Waisraeli wote walifika katika nyika ya Zini, wakaanza kukaa Kadeshi.+ Miriamu+ akafa na kuzikwa huko.
2 Mahali hapo hapakuwa na maji kwa ajili ya Waisraeli,+ basi wakakusanyika dhidi ya Musa na Haruni. 3 Watu wakagombana na Musa+ wakisema: “Laiti tungekufa ndugu zetu walipokufa mbele za Yehova! 4 Kwa nini mmelileta kutaniko la Yehova katika nyika hii ili sisi na mifugo yetu tufie humu?+ 5 Na kwa nini mlitutoa Misri na kutuleta mahali hapa paovu?+ Huku hakuna mbegu na tini na mizabibu na makomamanga, wala hakuna maji ya kunywa.”+ 6 Basi Musa na Haruni wakatoka mbele yao na kwenda kwenye mlango wa hema la mkutano, wakaanguka chini kifudifudi, na utukufu wa Yehova ukaanza kuwatokea.+
7 Kisha Yehova akamwambia Musa, 8 “Ichukue ile fimbo, kisha wewe na Haruni ndugu yako muwakusanye watu wote, halafu uzungumze na mwamba mbele ya macho yao ili utoe maji, nawe utatoa maji katika mwamba huo na kuwapa watu wote pamoja na mifugo yao maji ya kunywa.”+
9 Kwa hiyo, Musa akachukua fimbo kutoka mbele za Yehova,+ kama Alivyomwamuru. 10 Basi Musa na Haruni wakawakusanya watu wote mbele ya mwamba huo, akawaambia, “Sikilizeni sasa, enyi waasi! Je, ni lazima tuwatolee maji katika mwamba huu?”+ 11 Ndipo Musa akainua mkono wake na kuupiga mwamba huo mara mbili kwa fimbo yake, na maji mengi yakaanza kububujika, watu wakaanza kunywa pamoja na mifugo yao.+
12 Baadaye Yehova akamwambia hivi Musa na Haruni: “Kwa sababu hamkuonyesha kwamba mna imani kwangu na kunitakasa mbele ya Waisraeli, hamtawaingiza watu hawa katika nchi ambayo nitawapa.”+ 13 Hayo ndiyo maji ya Meriba,*+ mahali ambapo Waisraeli waligombana na Yehova, naye akawathibitishia kwamba yeye ni mtakatifu.
14 Kisha Musa akawatuma wajumbe kutoka Kadeshi ili waende kwa mfalme wa Edomu,+ wamwambie: “Ndugu yako Israeli+ anasema hivi: ‘Unajua vizuri matatizo yote tuliyopata. 15 Baba zetu walienda Misri,+ nasi tuliishi Misri kwa miaka mingi,*+ nao Wamisri walitutesa sisi na baba zetu.+ 16 Mwishowe tulimlilia Yehova,+ naye akasikia kilio chetu na kumtuma malaika;+ akatutoa Misri, na sasa tuko hapa Kadeshi, jiji linalopakana na eneo lako. 17 Tafadhali turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutapita katika mashamba yenu au shamba lolote la mizabibu, nasi hatutakunywa maji ya kisima chochote. Tutafuata Barabara ya Mfalme bila kugeuka kulia au kushoto mpaka tutakapokuwa tumepita katika eneo lako.’”+
18 Hata hivyo, mfalme wa Edomu akamwambia, “Usipite katika eneo letu. Ukipita, nitatoka na kukushambulia kwa upanga.” 19 Basi Waisraeli wakamwambia, “Tutafuata barabara kuu, na ikiwa sisi na mifugo yetu tutakunywa maji yako, tutalipa.+ Sisi tunataka tu kupita kwa miguu, hatutaki kitu kingine chochote.”+ 20 Lakini bado akasema, “Hamtapita.”+ Ndipo mfalme wa Edomu akatoka ili kumshambulia akiwa na watu wengi na jeshi lenye nguvu.* 21 Basi mfalme wa Edomu akakataa kuwaruhusu Waisraeli wapite katika eneo lake; kwa hiyo Waisraeli wakageuka na kumwacha.+
22 Waisraeli wote wakaondoka Kadeshi na kufika kwenye Mlima Hori.+ 23 Kisha Yehova akamwambia hivi Musa na Haruni kwenye Mlima Hori karibu na mpaka wa nchi ya Edomu: 24 “Haruni atakufa na kuzikwa kama watu wake walivyozikwa.*+ Hataingia katika nchi nitakayowapa Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili mliasi agizo nililowapa kuhusu maji ya Meriba.+ 25 Mchukue Haruni na Eleazari mwanawe, uwalete juu kwenye Mlima Hori. 26 Mvue Haruni mavazi yake+ umvishe Eleazari+ mwanawe, kisha Haruni atafia huko.”*
27 Basi Musa akafanya kama Yehova alivyomwamuru, nao wakapanda Mlima Hori watu wote wakiwatazama. 28 Kisha Musa akamvua Haruni mavazi yake na kumvisha Eleazari mwanawe. Baada ya hayo, Haruni akafa juu ya mlima huo.+ Kisha Musa na Eleazari wakateremka kutoka mlimani. 29 Waisraeli wote walipoona kwamba Haruni amekufa, nyumba yote ya Israeli ikamwombolezea Haruni kwa siku 30.+
21 Mfalme Mkanaani wa Aradi,+ aliyeishi Negebu, aliposikia kwamba Waisraeli walipitia njia ya Atharimu, aliwashambulia na kuwateka baadhi yao. 2 Kwa hiyo Waisraeli wakamwekea Yehova nadhiri hii: “Ukiwatia watu hawa mikononi mwetu, bila shaka tutayaangamiza majiji yao.” 3 Kwa hiyo Yehova akawasikiliza Waisraeli na kuwatia Wakanaani mikononi mwao, Waisraeli wakawaangamiza pamoja na majiji yao. Basi wakapaita mahali hapo Horma.*+
4 Walipoendelea na safari yao kutoka Mlima Hori+ kupitia njia ya Bahari Nyekundu ili kuizunguka nchi ya Edomu,+ watu wakachoshwa na safari. 5 Na watu wakaendelea kumnung’unikia Mungu na Musa,+ wakisema: “Kwa nini mmetutoa Misri ili tufe nyikani? Hakuna chakula wala maji,+ nasi tumeuchukia mkate huu unaochukiza.”+ 6 Basi Yehova akaleta nyoka wenye sumu* katikati ya watu, na nyoka hao wakawauma sana hivi kwamba Waisraeli wengi wakafa.+
7 Kwa hiyo watu wakaja kwa Musa na kumwambia: “Tumetenda dhambi kwa kumnung’unikia Yehova na wewe pia.+ Msihi Yehova atuondolee nyoka hawa.” Basi Musa akamsihi Mungu kwa niaba ya watu.+ 8 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Tengeneza mfano wa nyoka mwenye sumu na uuweke juu ya nguzo. Mtu yeyote akiumwa na nyoka, ni lazima autazame mfano huo ili aendelee kuishi.” 9 Mara moja Musa akatengeneza nyoka wa shaba+ na kumweka juu ya nguzo,+ na mtu yeyote aliyeumwa na nyoka na kumtazama nyoka huyo wa shaba, aliendelea kuishi.+
10 Kisha Waisraeli wakaendelea na safari na kupiga kambi Obothi.+ 11 Halafu wakaondoka Obothi na kupiga kambi Iye-abarimu,+ katika nyika inayoelekeana na Moabu, upande wa mashariki. 12 Kutoka huko wakasafiri na kupiga kambi karibu na Bonde la Zeredi.+ 13 Wakaondoka huko na kupiga kambi katika eneo la Arnoni,+ lililo katika nyika inayoanzia kwenye mpaka wa Waamori, kwa maana eneo la Arnoni ni mpaka wa Moabu, kati ya Wamoabu na Waamori. 14 Ndiyo sababu kitabu cha Vita vya Yehova kinasema kuhusu “Jiji la Vahebu katika eneo la Sufa na mabonde* ya Arnoni, 15 na miteremko ya mabonde, inayofika katika mji wa Ari na kufika kwenye mpaka wa Moabu.”
16 Kisha wakasafiri mpaka Beeri. Ni kwenye kisima hicho ambapo Yehova alimwambia Musa hivi: “Wakusanye watu, niwape maji.”
17 Wakati huo, Waisraeli waliimba wimbo huu:
“Bubujika, Ee kisima!—Kiimbieni!*
18 Kisima kilichochimbwa na wakuu, kilichochimbwa na watu mashuhuri,
Kwa fimbo ya kiongozi na kwa fimbo zao wenyewe.”
Kisha wakatoka nyikani na kwenda Matana, 19 kutoka Matana mpaka Nahalieli, na kutoka Nahalieli mpaka Bamothi.+ 20 Wakatoka Bamothi na kwenda kwenye bonde lililo katika eneo la Moabu,+ juu ya Pisga,+ linaloelekeana na Yeshimoni.*+
21 Sasa Waisraeli wakawatuma wajumbe wakamwambie hivi Sihoni mfalme wa Waamori:+ 22 “Turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutageuka na kuingia katika mashamba yenu au shamba lolote la mizabibu. Hatutakunywa maji ya kisima chochote. Tutafuata Barabara ya Mfalme mpaka tutakapokuwa tumepita katika eneo lako.”+ 23 Lakini Sihoni hakuwaruhusu Waisraeli wapitie katika eneo lake. Badala yake, Sihoni akawakusanya watu wake wote kwenda kuwashambulia Waisraeli nyikani, akafika Yahazi na kuanza kupigana nao.+ 24 Lakini Waisraeli wakamshinda kwa upanga+ na kumiliki nchi yake+ kuanzia Arnoni+ mpaka Yaboki,+ karibu na Waamoni, kwa sababu jiji la Yazeri+ linapakana na eneo la Waamoni.+
25 Basi Waisraeli wakachukua majiji hayo yote, wakaanza kuishi katika majiji yote ya Waamori,+ huko Heshboni na miji yake yote. 26 Kwa maana Heshboni lilikuwa jiji la Sihoni, mfalme wa Waamori ambaye alikuwa amepigana na mfalme wa Moabu na kuchukua nchi yake yote mpaka Arnoni. 27 Ndiyo maana watu walitunga shairi hili la dhihaka:
“Njooni Heshboni.
Jiji la Sihoni na lijengwe na kuimarishwa kabisa.
28 Kwa maana moto ulitoka Heshboni, mwali wa moto ulitoka katika mji wa Sihoni.
Umeteketeza jiji la Ari la Moabu, mabwana wa milima ya Arnoni.
29 Ole wako, Moabu! Mtaangamizwa, enyi watu wa Kemoshi!+
Huwafanya wanawe kuwa wakimbizi na binti zake kuwa mateka wa Sihoni, mfalme wa Waamori.
30 Acheni tuwapige mishale;
Heshboni litaangamizwa mpaka Diboni;+
Acheni tuliharibu kabisa mpaka Nofa;
Moto utasambaa mpaka Medeba.”+
31 Basi Waisraeli wakaanza kuishi katika nchi ya Waamori. 32 Kisha Musa akawatuma watu fulani wakapeleleze Yazeri.+ Wakateka miji yake na kuwafukuza Waamori waliokuwa humo. 33 Halafu wakageuka na kupanda kupitia njia ya Bashani. Ndipo Ogu+ mfalme wa Bashani akatoka pamoja na watu wake wote ili kupigana vita nao huko Edrei.+ 34 Yehova akamwambia Musa: “Usimwogope,+ kwa maana nitamtia mikononi mwako pamoja na watu wake wote na nchi yake,+ nawe utamtendea kama ulivyomtendea Sihoni mfalme wa Waamori, aliyeishi Heshboni.”+ 35 Basi wakaendelea kumshambulia pamoja na wanawe na watu wake wote hivi kwamba hakuna mtu yeyote kati ya watu wake aliyeokoka,+ nao wakaichukua nchi yake.+
22 Kisha Waisraeli wakaondoka na kupiga kambi kwenye jangwa tambarare la Moabu ng’ambo ya Yordani kutoka Yeriko.+ 2 Sasa Balaki+ mwana wa Sipori aliona mambo yote ambayo Waisraeli waliwatendea Waamori, 3 na Wamoabu wakawaogopa sana Waisraeli, kwa sababu walikuwa wengi sana; naam, Wamoabu wakafadhaika kwa hofu kwa sababu ya Waisraeli.+ 4 Basi Wamoabu wakawaambia wazee wa Midiani:+ “Sasa umati huu utaramba eneo letu lote kama ng’ombe dume anavyokula nyasi shambani.”
Balaki mwana wa Sipori ndiye aliyekuwa mfalme wa Moabu wakati huo. 5 Aliwatuma wajumbe kwa Balaamu mwana wa Beori huko Pethori,+ karibu na Mto Efrati katika nchi yake. Alimwambia hivi: “Sasa, kuna watu ambao wametoka Misri. Wamejaa kila mahali duniani,*+ na wanakaa papa hapa karibu nami. 6 Basi, tafadhali, njoo uwalaani watu hawa kwa niaba yangu,+ kwa maana wana nguvu kuliko mimi. Huenda nikawashinda na kuwafukuza kutoka nchini, kwa maana najua vema kwamba yule unayembariki amebarikiwa na yule unayemlaani amelaaniwa.”
7 Basi wazee wa Moabu na wazee wa Midiani wakachukua malipo ya uaguzi* na kwenda kumwona Balaamu,+ wakamwambia maneno ya Balaki. 8 Ndipo Balaamu akawaambia: “Laleni hapa usiku wa leo, nami nitawajulisha jambo lolote ambalo Yehova ataniambia.” Hivyo wakuu wa Moabu wakakaa na Balaamu.
9 Kisha Mungu akamtokea Balaamu na kumuuliza:+ “Wanaume hawa walio pamoja nawe ni nani?” 10 Balaamu akamwambia Mungu wa kweli: “Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, amenitumia ujumbe akisema, 11 ‘Watu wanaotoka Misri wamejaa kila mahali duniani.* Sasa njoo uwalaani kwa niaba yangu.+ Huenda nikapigana nao na kuwafukuza.’” 12 Lakini Mungu akamwambia Balaamu: “Usiende na wanaume hawa. Usiwalaani watu hao, kwa maana wamebarikiwa.”+
13 Balaamu akaamka asubuhi na kuwaambia wakuu wa Balaki: “Rudini katika nchi yenu, kwa maana Yehova amenikataza kwenda pamoja nanyi.” 14 Kwa hiyo wakuu wa Moabu wakaondoka, wakarudi kwa Balaki na kumwambia: “Balaamu amekataa kuja pamoja nasi.”
15 Hata hivyo, Balaki akawatuma tena wakuu wengine, wengi zaidi na wenye kuheshimika zaidi kuliko wale wa kwanza. 16 Wakafika kwa Balaamu na kumwambia: “Balaki mwana wa Sipori anasema hivi: ‘Tafadhali, usiruhusu chochote kikuzuie kuja kwangu, 17 kwa maana nitakuthawabisha sana, nami nitafanya chochote utakachoniambia. Njoo tafadhali, uwalaani watu hawa kwa niaba yangu.’” 18 Lakini Balaamu akawaambia watumishi wa Balaki: “Hata Balaki akinipa nyumba yake mwenyewe iliyojaa fedha na dhahabu, siwezi kukiuka jambo lolote ambalo Yehova Mungu wangu ameniagiza nifanye, liwe jambo dogo au kubwa.+ 19 Lakini tafadhalini, laleni hapa usiku wa leo pia, ili nijue Yehova ataniambia jambo gani lingine.”+
20 Kisha Mungu akamtokea Balaamu usiku na kumwambia: “Ikiwa wanaume hao wamekuja kukuita, nenda pamoja nao. Lakini utasema tu maneno nitakayokwambia.”+ 21 Basi Balaamu akaamka asubuhi, akaweka matandiko juu ya punda wake na kwenda pamoja na wakuu wa Moabu.+
22 Lakini Mungu akakasirika sana kwa sababu Balaamu alikuwa akienda, na malaika wa Yehova akasimama njiani ili kumzuia. Sasa Balaamu alikuwa amepanda juu ya punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye. 23 Punda huyo alipomwona malaika wa Yehova amesimama njiani akiwa ameshika upanga uliochomolewa, alijaribu kutoka njiani ili aingie shambani. Lakini Balaamu akaanza kumpiga punda huyo ili arudi njiani. 24 Ndipo malaika wa Yehova akasimama kwenye kijia chembamba katikati ya mashamba mawili ya mizabibu, na kulikuwa na ukuta wa mawe upande huu na huu wa kijia hicho. 25 Punda alipomwona malaika wa Yehova, akaanza kujisukumiza ukutani na kuubana mguu wa Balaamu ukutani, na Balaamu akaanza kumpiga tena.
26 Sasa malaika wa Yehova akaenda mbele tena na kusimama mahali pembamba ambapo hapakuwa na nafasi ya kugeuka kulia au kushoto. 27 Punda alipomwona malaika wa Yehova, akalala chini Balaamu akiwa mgongoni, basi Balaamu akakasirika sana na kuendelea kumpiga punda kwa fimbo yake. 28 Mwishowe Yehova akamfanya punda huyo aongee,*+ akamuuliza Balaamu: “Nimekutendea nini hivi kwamba umenipiga mara tatu?”+ 29 Balaamu akamjibu hivi punda huyo: “Ni kwa sababu umenifanya mjinga. Ningekuwa na upanga mkononi, ningekuua!” 30 Kisha punda akamwambia Balaamu: “Je, mimi si punda wako ambaye amekubeba maisha yako yote mpaka leo? Je, nimewahi kukutendea hivi?” Balaamu akajibu: “Hapana!” 31 Ndipo Yehova akayafungua macho ya Balaamu,+ naye akamwona malaika wa Yehova amesimama njiani akiwa ameshika upanga uliochomolewa. Papo hapo Balaamu akainama chini na kusujudu.
32 Malaika wa Yehova akamwambia: “Kwa nini umempiga punda wako mara tatu? Mimi mwenyewe nimekuja kukuzuia kwa sababu njia yako haipatani na mapenzi yangu.+ 33 Punda aliniona na kujaribu kunikwepa mara hizo tatu.+ Kama hangenikwepa ningekuwa nimekuua na kumwacha yeye akiwa hai.” 34 Balaamu akamwambia malaika wa Yehova: “Nimetenda dhambi, kwa sababu sikujua kwamba ni wewe uliyesimama njiani ili kunizuia. Na sasa ikiwa hufurahii jambo hili, mimi nitarudi.” 35 Lakini malaika wa Yehova akamwambia Balaamu: “Nenda pamoja na wanaume hao, lakini utasema tu maneno nitakayokwambia.” Basi Balaamu akaendelea na safari pamoja na wakuu wa Balaki.
36 Balaki aliposikia kwamba Balaamu amefika, alitoka nje mara moja kumpokea katika jiji la Moabu, kwenye ukingo wa Arnoni, katika mpaka wa Moabu. 37 Balaki akamuuliza Balaamu: “Je, sikuwatuma wajumbe wakuite uje kwangu? Kwa nini hukuja? Je, ulidhani siwezi kukuthawabisha kwelikweli?”+ 38 Balaamu akamjibu hivi Balaki: “Sasa nimekuja kwako. Lakini, je, nitaruhusiwa kusema jambo lolote? Ninaweza kusema tu maneno ambayo Mungu anatia kinywani mwangu.”+
39 Kwa hiyo Balaamu akaenda pamoja na Balaki, wakafika Kiriath-husothi. 40 Balaki akatoa dhabihu za ng’ombe na kondoo, naye akamgawia Balaamu na wakuu waliokuwa pamoja naye. 41 Asubuhi Balaki akamchukua Balaamu na kwenda naye Bamoth-baali; akiwa huko aliweza kuwaona Waisraeli wote.+
23 Kisha Balaamu akamwambia Balaki: “Jenga madhabahu saba mahali hapa,+ nawe unitayarishie ng’ombe dume saba na kondoo dume saba.” 2 Mara moja Balaki akafanya kama Balaamu alivyomwambia. Kisha Balaki na Balaamu wakatoa dhabihu ya ng’ombe dume mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.+ 3 Halafu Balaamu akamwambia Balaki: “Kaa hapa karibu na dhabihu yako ya kuteketezwa, nami nitaenda. Labda Yehova atawasiliana nami. Jambo lolote atakalonifunulia, nitakwambia.” Basi akaenda juu ya kilima kilicho wazi.
4 Ndipo Mungu akawasiliana na Balaamu,+ Balaamu akamwambia: “Nilijenga safu za madhabahu saba na kutoa dhabihu ya ng’ombe dume mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.” 5 Yehova akatia maneno haya katika kinywa cha Balaamu:+ “Rudi kwa Balaki, na hili ndilo utakalosema.” 6 Basi akarudi na kumkuta Balaki na wakuu wote wa Moabu wakiwa wamesimama karibu na dhabihu yake ya kuteketezwa. 7 Kisha akasema maneno haya ya kishairi:+
“Balaki mfalme wa Moabu amenileta kutoka Aramu,+
Kutoka katika milima ya mashariki:
‘Njoo umlaani Yakobo kwa niaba yangu.
Naam, njoo uwashutumu Waisraeli.’+
8 Ninawezaje kuwalaani watu ambao Mungu hajawalaani?
Ninawezaje kuwashutumu wale ambao Yehova hajawashutumu?+
9 Kutoka juu ya miamba ninawaona,
Na kutoka vilimani ninawatazama.
Acha nife kifo cha watu wanyoofu,
Na mwisho wangu uwe kama wao.”
11 Ndipo Balaki akamwambia Balaamu: “Kwa nini umenitendea hivi? Nilikuleta ili uwalaani maadui wangu, lakini badala yake umewabariki tu.”+ 12 Balaamu akasema: “Je, sipaswi kusema neno lolote ambalo Yehova anatia kinywani mwangu?”+
13 Balaki akamwambia: “Tafadhali, twende mahali pengine ambapo unaweza kuwaona. Utaona baadhi yao; hutawaona wote. Ukiwa huko walaani kwa niaba yangu.”+ 14 Kwa hiyo akampeleka kwenye uwanja wa Sofimu, juu ya Pisga,+ naye akajenga madhabahu saba na kutoa dhabihu ya ng’ombe dume mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.+ 15 Kisha Balaamu akamwambia Balaki: “Kaa hapa karibu na dhabihu yako ya kuteketezwa ninapoenda pale kuwasiliana Naye.” 16 Basi Yehova akawasiliana na Balaamu na kutia neno hili kinywani mwake:+ “Rudi kwa Balaki, na hili ndilo utakalosema.” 17 Basi akarudi na kumkuta Balaki akisubiri karibu na dhabihu yake ya kuteketezwa, na wakuu wa Moabu walikuwa pamoja naye. Balaki akamuuliza: “Yehova amesema nini?” 18 Kisha Balaamu akasema maneno haya ya kishairi:+
“Inuka, Balaki, usikilize.
Nisikilize, ewe mwana wa Sipori.
Akisema jambo, je, hatalitenda?
Akinena jambo, je, hatalitimiza?+
21 Havumilii nguvu zozote za uchawi dhidi ya Yakobo,
Wala haruhusu taabu yoyote impate Israeli.
Yehova Mungu wake yuko pamoja nao,+
Nao humsifu kwa sauti kubwa kuwa mfalme wao.
Yeye ni kama pembe za fahali mwitu.+
Sasa inaweza kusemwa hivi kumhusu Yakobo na Israeli:
‘Tazameni mambo ambayo Mungu ametenda!’
Hawatalala chini mpaka wale mawindo
Na kunywa damu ya waliouawa.”
25 Ndipo Balaki akamwambia Balaamu: “Ikiwa huwezi kamwe kuwalaani, basi usiwabariki pia.” 26 Balaamu akamwambia Balaki: “Je, sikukwambia, ‘Nitafanya mambo yote ambayo Yehova anasema’?”+
27 Ndipo Balaki akamwambia Balaamu: “Tafadhali njoo nikupeleke mahali pengine. Labda Mungu wa kweli atakubali uwalaani kwa niaba yangu kutoka mahali hapo.”+ 28 Basi Balaki akampeleka Balaamu juu ya Mlima Peori, unaoelekeana na Yeshimoni.*+ 29 Kisha Balaamu akamwambia Balaki: “Jenga madhabahu saba mahali hapa, nawe unitayarishie ng’ombe dume saba na kondoo dume saba.”+ 30 Kwa hiyo Balaki akafanya kama Balaamu alivyomwambia, naye akatoa dhabihu ya ng’ombe dume mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.
24 Balaamu alipoona kwamba Yehova alifurahia* kuwabariki Waisraeli, hakwenda tena kutafuta ishara za msiba,+ bali aliugeuza uso wake kutazama nyikani. 2 Balaamu alipotazama na kuwaona Waisraeli wakiwa wamepiga kambi kulingana na makabila yao,+ roho ya Mungu ikamjia.+ 3 Kisha akasema maneno haya ya kishairi:+
“Maneno ya Balaamu mwana wa Beori,
Na maneno ya mwanamume ambaye macho yake yamefunguliwa,
4 Maneno ya mtu anayesikia neno la Mungu,
Aliyeona maono ya Mweza-Yote,
Aliyeinama chini macho yakiwa yamefumbuliwa:+
6 Yameenea mbali kama mabonde,+
Kama bustani kando ya mto,
Kama mimea ya udi iliyopandwa na Yehova,
Kama mierezi kando ya maji.
7 Maji yanaendelea kutiririka kutoka katika ndoo zake mbili za ngozi,
8 Mungu anamtoa Misri;
Yeye ni kama pembe za fahali mwitu kwa Waisraeli.
Atayala mataifa, wale wanaomkandamiza,+
Na mifupa yao ataitafuna-tafuna, naye atawapasua-pasua kwa mishale yake.
9 Amejikunyata, amelala chini kama simba,
Na kama simba, ni nani anayethubutu kumwamsha?
Wale wanaokubariki wamebarikiwa,
Na wale wanaokulaani wamelaaniwa.”+
10 Ndipo Balaki akamkasirikia sana Balaamu. Akapiga makofi kwa dharau na kumwambia Balaamu: “Nilikuita uwalaani maadui wangu,+ badala yake umewabariki mara tatu. 11 Sasa rudi nyumbani mara moja. Nilitaka kukuthawabisha sana,+ lakini Yehova amekunyima thawabu.”
12 Balaamu akamwambia Balaki: “Je, sikuwaambia hivi wajumbe uliowatuma kwangu: 13 ‘Hata Balaki akinipa nyumba yake mwenyewe iliyojaa fedha na dhahabu, siwezi kwa hiari yangu* kukiuka jambo lolote ambalo Yehova ameniagiza nifanye, liwe jambo zuri au baya. Nitasema tu jambo ambalo Yehova ataniambia’?+ 14 Na sasa naenda kwa watu wangu. Njoo nikwambie* mambo ambayo watu hawa watawatendea watu wako wakati ujao.”* 15 Kwa hiyo akasema maneno haya ya kishairi:+
“Maneno ya Balaamu mwana wa Beori,
Na maneno ya mwanamume ambaye macho yake yamefunguliwa,+
16 Maneno ya mtu anayesikia neno la Mungu,
Na yule anayemjua Aliye Juu Zaidi,
Aliona maono ya Mweza-Yote
Alipokuwa akiinama chini macho yake yakiwa yamefunguliwa:
17 Nitamwona, lakini si sasa;
Nitamtazama, lakini si hivi karibuni.
Naye hakika atapasua paji la uso la Moabu+
Na fuvu la kichwa la wana wote wa vurugu.
20 Alipowaona Waamaleki, aliendelea kusema maneno yake ya kishairi:
21 Alipowaona Wakeni,+ aliendelea kusema maneno yake ya kishairi:
“Makao yenu yako salama, yamejengwa juu ya mwamba.
22 Lakini mtu fulani atawateketeza Wakeni.*
Ni muda gani unaobaki kabla ya Ashuru kuwachukua mateka?”
23 Akaendelea kusema maneno yake ya kishairi:
“Lo! Ni nani atakayeokoka Mungu atakapofanya hivyo?
Lakini wao pia wataangamia* kabisa.”
25 Kisha Balaamu+ akaondoka na kurudi kwake. Balaki pia akaenda zake.
25 Waisraeli walipokuwa wakikaa Shitimu,+ watu walianza kufanya uasherati na mabinti wa Moabu.+ 2 Wanawake hao waliwaalika kwenye dhabihu za miungu yao,+ nao watu wakaanza kula na kuinamia miungu yao.+ 3 Kwa hiyo Waisraeli wakashiriki katika kumwabudu* Baali wa Peori,+ na hasira ya Yehova ikawaka dhidi yao. 4 Yehova akamwambia Musa: “Wachukue viongozi wote wa watu hawa na uwatundike kweupe kabisa wakati wa mchana* mbele za Yehova, ili hasira kali ya Yehova isiendelee kuwaka dhidi ya Waisraeli.” 5 Kisha Musa akawaambia hivi waamuzi wa Israeli:+ “Kila mmoja wenu awaue watu wake walioshiriki katika kumwabudu* Baali wa Peori.”+
6 Lakini wakati huo, Mwisraeli fulani akamleta mwanamke Mmidiani+ karibu na ndugu zake Waisraeli huku Musa na Waisraeli wote wakitazama walipokuwa wakilia kwenye mlango wa hema la mkutano. 7 Finehasi+ mwana wa Eleazari mwana wa kuhani Haruni alipoona jambo hilo, aliinuka mara moja kutoka kati ya Waisraeli waliokusanyika, akachukua mkuki. 8 Kisha akamfuata mwanamume huyo Mwisraeli mpaka hemani, akawachoma mkuki wote wawili, nao ukapenya kwenye viungo vya uzazi vya mwanamke huyo. Ndipo pigo lililowapata Waisraeli likakomeshwa.+ 9 Watu waliokufa kutokana na pigo hilo walikuwa 24,000.+
10 Kisha Yehova akamwambia Musa: 11 “Finehasi+ mwana wa Eleazari mwana wa kuhani Haruni amezuia ghadhabu yangu dhidi ya Waisraeli kwa sababu hakuvumilia ushindani wowote dhidi yangu miongoni mwao.+ Kwa hiyo sijawaangamiza Waisraeli licha ya kwamba ninasisitiza watu waniabudu mimi peke yangu.+ 12 Kwa hiyo mwambie, ‘Ninafanya agano langu la amani pamoja naye. 13 Nalo litakuwa agano la ukuhani wa kudumu kwa ajili yake na wazao wake,+ kwa maana hakuvumilia ushindani wowote kumwelekea Mungu wake,+ naye alifanya dhambi ya Waisraeli ifunikwe.’”
14 Sasa, mwanamume huyo Mwisraeli aliyeuawa pamoja na mwanamke Mmidiani aliitwa Zimri mwana wa Salu, mkuu wa ukoo* wa Wasimeoni. 15 Mwanamke Mmidiani aliyeuawa aliitwa Kozbi binti ya Suri;+ Suri alikuwa kiongozi wa koo* za nyumba fulani huko Midiani.+
16 Baadaye Yehova akamwambia Musa: 17 “Wachokozeni Wamidiani na kuwaangamiza,+ 18 kwa sababu wamekuwa wakiwachokoza kwa hila zao kama ilivyokuwa kule Peori+ na pia kuhusiana na Kozbi binti ya mkuu wa Midiani, dada yao aliyeuawa+ wakati pigo lilipotokea kwa sababu ya mambo yaliyotokea Peori.”+
26 Baada ya pigo hilo,+ Yehova akamwambia hivi Musa na Eleazari mwana wa kuhani Haruni: 2 “Wahesabuni Waisraeli wote wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi, kulingana na koo zao,* wahesabuni wote wanaoweza kutumikia katika jeshi la Israeli.”+ 3 Basi Musa na kuhani Eleazari+ wakawaambia watu hivi katika jangwa tambarare la Moabu+ karibu na Yordani huko Yeriko:+ 4 “Wahesabuni watu wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi, kama Yehova alivyomwamuru Musa.”+
Kwa hiyo Waisraeli waliotoka nchini Misri walikuwa: 5 Rubeni,+ mzaliwa wa kwanza wa Israeli; wana wa Rubeni+ walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu; 6 kutoka kwa Hezroni, ukoo wa Wahezroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi. 7 Hizo ndizo zilizokuwa koo za Warubeni, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 43,730.+
8 Mwana wa Palu alikuwa Eliabu. 9 Na wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani, na Abiramu. Huyu ndiye Dathani na Abiramu, wakuu wa Waisraeli ambao walimpinga Musa+ na Haruni na kujiunga na kikundi cha Kora+ kilichompinga Yehova.+
10 Kisha dunia ikafunguka* na kuwameza. Lakini Kora alikufa pamoja na watu waliomuunga mkono moto ulipowateketeza watu 250.+ Wakawa onyo kwa wengine.+ 11 Hata hivyo, wana wa Kora hawakufa.+
12 Wana wa Simeoni+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka kwa Yakini, ukoo wa Wayakini; 13 kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli. 14 Hizo ndizo zilizokuwa koo za Wasimeoni: walikuwa 22,200.+
15 Wana wa Gadi+ kulingana na koo zao: kutoka kwa Sefoni, ukoo wa Wasefoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni; 16 kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri; 17 kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli. 18 Hizo ndizo zilizokuwa koo za wana wa Gadi, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 40,500.+
19 Wana wa Yuda+ walikuwa Eri na Onani.+ Hata hivyo, Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani.+ 20 Na wana wa Yuda kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela,+ ukoo wa Washela; kutoka kwa Perezi,+ ukoo wa Waperezi; kutoka kwa Zera,+ ukoo wa Wazera. 21 Na wana wa Perezi walikuwa: kutoka kwa Hezroni,+ ukoo wa Wahezroni; kutoka kwa Hamuli,+ ukoo wa Wahamuli. 22 Hizo ndizo zilizokuwa koo za Yuda, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 76,500.+
23 Wana wa Isakari+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola,+ ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuni; 24 kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni. 25 Hizo ndizo zilizokuwa koo za Isakari, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 64,300.+
26 Wana wa Zabuloni+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yahleeli, ukoo wa Wayahleeli. 27 Hizo ndizo zilizokuwa koo za Wazabuloni, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 60,500.+
28 Wana wa Yosefu+ kulingana na koo zao walikuwa Manase na Efraimu.+ 29 Wana wa Manase+ walikuwa: kutoka kwa Makiri,+ ukoo wa Wamakiri; naye Makiri alikuwa baba ya Gileadi;+ kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi. 30 Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi: kutoka kwa Yezeri, ukoo wa Wayezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki; 31 kutoka kwa Asrieli, ukoo wa Waasrieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu; 32 kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi. 33 Sasa Selofehadi mwana wa Heferi hakuwa na watoto wa kiume, alikuwa na mabinti tu,+ na majina ya mabinti wa Selofehadi+ ni Mala, Noa, Hogla, Milka, na Tirsa. 34 Hizo ndizo zilizokuwa koo za Manase, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 52,700.+
35 Hawa ndio waliokuwa wana wa Efraimu+ kulingana na koo zao: kutoka kwa Shuthela,+ ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani. 36 Na hawa ndio wana wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani. 37 Hizo ndizo zilizokuwa koo za wana wa Efraimu, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 32,500.+ Hao ndio waliokuwa wana wa Yosefu kulingana na koo zao.
38 Wana wa Benjamini+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela,+ ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu; 39 kutoka kwa Shefufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu. 40 Wana wa Bela ni Ardi na Naamani:+ kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani. 41 Hao ndio waliokuwa wana wa Benjamini kulingana na koo zao, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 45,600.+
42 Hawa ndio waliokuwa wana wa Dani+ kulingana na koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizo ndizo zilizokuwa koo za Dani kulingana na wazao wao. 43 Watu walioandikishwa kutoka katika koo zote za Washuhamu walikuwa 64,400.+
44 Wana wa Asheri+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia; 45 kutoka kwa wana wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli. 46 Binti ya Asheri aliitwa Sera. 47 Hizo ndizo zilizokuwa koo za wana wa Asheri, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 53,400.+
48 Wana wa Naftali+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Yahzeeli, ukoo wa Wayahzeeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni; 49 kutoka kwa Yezeri, ukoo wa Wayezeri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu. 50 Hizo ndizo zilizokuwa koo za Naftali kulingana na wazao wao, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 45,400.+
51 Wanaume wote Waisraeli walioandikishwa walikuwa 601,730.+
52 Kisha Yehova akamwambia Musa hivi: 53 “Watu hao wanapaswa kugawiwa urithi wa nchi kulingana na orodha ya majina.*+ 54 Unapaswa kuyapa makundi makubwa urithi mkubwa, na makundi madogo urithi mdogo.+ Kila kundi linapaswa kupewa urithi wake kulingana na idadi ya watu walioorodheshwa. 55 Hata hivyo, nchi inapaswa kugawanywa kwa kura.+ Watu wanapaswa kupokea urithi wao kulingana na majina ya makabila ya baba zao. 56 Kila urithi utagawanywa kwa kura, na makundi makubwa na madogo yatapewa urithi wao.”
57 Sasa hawa ndio Walawi walioandikishwa+ kulingana na koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi,+ ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari. 58 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni,+ ukoo wa Wahebroni,+ ukoo wa Wamali,+ ukoo wa Wamushi,+ ukoo wa Wakora.+
Kohathi alikuwa baba ya Amramu.+ 59 Na mke wa Amramu alikuwa Yokebedi,+ binti ya Lawi; Yokebedi alizaliwa nchini Misri. Naye alimzalia Amramu, Haruni na Musa na Miriamu dada yao.+ 60 Kisha Haruni akamzaa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.+ 61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa kwa sababu ya kumtolea Yehova moto haramu.+
62 Wanaume wote wenye umri wa kuanzia mwezi mmoja na zaidi walioandikishwa walikuwa 23,000.+ Hawakuandikishwa pamoja na Waisraeli wengine,+ kwa sababu hawakupaswa kupewa urithi miongoni mwa Waisraeli.+
63 Hao ndio walioandikishwa na Musa na kuhani Eleazari walipowaandikisha Waisraeli katika jangwa tambarare la Moabu karibu na Yordani huko Yeriko. 64 Lakini hakuna hata mmoja wao aliyeandikishwa na Musa na kuhani Haruni wakati walipowahesabu Waisraeli katika nyika ya Sinai.+ 65 Kwa maana Yehova alikuwa amesema hivi kuwahusu: “Ni lazima wafe nyikani.”+ Kwa hiyo hakuna mwanamume hata mmoja kati yao aliyebaki isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+
27 Kisha mabinti wa Selofehadi,+ mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, wa koo za Manase mwana wa Yosefu, wakaja. Mabinti hao waliitwa Mala, Noa, Hogla, Milka, na Tirsa. 2 Wakasimama mbele ya Musa, kuhani Eleazari, mbele ya wakuu,+ na mbele ya Waisraeli wote kwenye mlango wa hema la mkutano, wakasema: 3 “Baba yetu alikufa nyikani, lakini hakuwa miongoni mwa kikundi kilichojiunga na Kora kumpinga Yehova,+ bali alikufa kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe naye hakuwa na mtoto yeyote wa kiume. 4 Kwa nini jina la baba yetu lipotee kutoka katika ukoo wake kwa sababu hakuwa na mtoto wa kiume? Tupe urithi miongoni mwa ndugu za baba yetu.” 5 Kwa hiyo Musa akawasilisha kesi yao mbele za Yehova.+
6 Basi Yehova akamwambia Musa hivi: 7 “Mabinti wa Selofehadi wanasema ukweli. Kwa vyovyote vile unapaswa kuwapa urithi miongoni mwa ndugu za baba yao na urithi wa baba yao.+ 8 Nawe uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mtu akifa bila kuacha mtoto wa kiume, mtampa binti yake urithi wake. 9 Na ikiwa hana binti, mtawapa ndugu zake urithi wake. 10 Na ikiwa hana ndugu, mtawapa ndugu za baba yake urithi wake. 11 Na ikiwa baba yake hana ndugu, mtampa urithi wake mtu wa karibu zaidi wa ukoo aliye na uhusiano wa damu naye. Uamuzi huu utakuwa sheria kwa Waisraeli, kama Yehova alivyomwamuru Musa.’”
12 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Panda mlima huu wa Abarimu,+ uione nchi nitakayowapa Waisraeli.+ 13 Baada ya kuiona, utakufa pia na kuzikwa pamoja na watu wako,*+ kama Haruni ndugu yako alivyozikwa,+ 14 kwa sababu Waisraeli walipokuwa wakigombana nami katika nyika ya Zini, mliasi agizo langu la kunitakasa mbele yao nilipowapa maji.+ Hayo ndiyo maji ya Meriba+ huko Kadeshi+ katika nyika ya Zini.”+
15 Kisha Musa akamwambia hivi Yehova: 16 “Yehova, Mungu anayewapa watu wote uhai,* naomba umchague mwanamume atakayewasimamia watu hawa 17 ili awatangulie na kuwaongoza katika mambo yote, ili watu hawa wa Yehova wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.” 18 Kwa hiyo Yehova akamwambia Musa: “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mwanamume aliye na roho,* na uweke mikono yako juu yake.+ 19 Kisha umsimamishe mbele ya kuhani Eleazari na mbele ya watu wote, nawe umweke kuwa kiongozi.+ 20 Utampa sehemu ya mamlaka* yako,+ ili Waisraeli wote wamsikilize.+ 21 Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atatumia Urimu+ kujua uamuzi wa Yehova kwa niaba yake. Kwa agizo lake, yeye na Waisraeli wote na watu wengine wote watatoka, na kwa agizo lake wataingia ndani.”
22 Kwa hiyo Musa akafanya kama Yehova alivyomwamuru. Akamchukua Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na mbele ya watu wote, 23 akaweka mikono yake juu yake na kumweka kuwa kiongozi,+ kama Yehova alivyosema kupitia Musa.+
28 Kisha Yehova akamwambia Musa, 2 “Waamuru hivi Waisraeli: ‘Hakikisheni kwamba mnanitolea toleo langu, chakula changu.* Ni lazima mnitolee kwa wakati uliowekwa dhabihu zangu zinazoteketezwa zenye harufu inayonipendeza.’*+
3 “Nawe uwaambie, ‘Hii ndiyo dhabihu inayochomwa kwa moto ambayo mtamtolea Yehova: mtatoa kwa ukawaida kila siku wanakondoo dume wawili wasio na kasoro wenye umri wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa.+ 4 Mtamtoa mwanakondoo dume mmoja asubuhi, na mwanakondoo dume wa pili mtamtoa jioni kabla ya giza kuingia,*+ 5 pamoja na toleo la nafaka la sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja* ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini* ya mafuta ya zeituni zilizopondwa.+ 6 Ni dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida,+ iliyoanzishwa kwenye Mlima Sinai, dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova, 7 pamoja na toleo lake la kinywaji la robo ya hini kwa ajili ya kila mwanakondoo dume.+ Mimineni kileo mahali patakatifu kikiwa toleo la kinywaji mbele za Yehova. 8 Nanyi mtamtoa mwanakondoo dume wa pili jioni kabla ya giza kuingia.* Mtamtoa pamoja na toleo la nafaka kama lile lililotolewa asubuhi pamoja na toleo lake la kinywaji. Mtamtoa akiwa dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.+
9 “‘Hata hivyo, siku ya Sabato,+ mnapaswa kutoa wanakondoo dume wawili wasio na kasoro wenye umri wa mwaka mmoja pamoja na toleo la nafaka la sehemu mbili za kumi za kipimo cha efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta, pamoja na toleo lake la kinywaji. 10 Hiyo ndiyo dhabihu ya kuteketezwa ya Sabato, pamoja na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida pamoja na toleo lake la kinywaji.+
11 “‘Mwanzoni mwa kila mwezi* mtamtolea Yehova dhabihu ya kuteketezwa ya ng’ombe dume wawili wachanga, kondoo dume mmoja, wanakondoo dume saba wasio na kasoro wote wa umri wa mwaka mmoja,+ 12 na toleo la nafaka la sehemu tatu za kumi za vipimo vya unga laini uliochanganywa na mafuta+ kwa ajili ya kila ng’ombe dume na toleo la nafaka la sehemu mbili za kumi za vipimo vya unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya kondoo dume mmoja,+ 13 na toleo la nafaka la sehemu moja ya kumi ya kipimo cha unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya kila mwanakondoo dume; mtavitoa vitu hivyo vikiwa dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza*+ Yehova. 14 Na matoleo ya kinywaji ya dhabihu hiyo yanapaswa kuwa nusu ya hini ya divai kwa ajili ya ng’ombe dume+ na sehemu ya tatu ya hini kwa ajili ya kondoo dume+ na robo ya hini kwa ajili ya mwanakondoo dume.+ Hiyo ndiyo dhabihu ya kuteketezwa inayopaswa kutolewa kila mwezi kwa mwaka mzima. 15 Pia, mwanambuzi mmoja anapaswa kutolewa kwa Yehova ili kuwa dhabihu ya dhambi; atatolewa na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida pamoja na toleo lake la kinywaji.
16 “Siku ya 14 ya mwezi wa kwanza, itakuwa Pasaka ya Yehova.+ 17 Na siku ya 15 ya mwezi huo, kutakuwa na sherehe. Mikate isiyo na chachu italiwa kwa siku saba.+ 18 Katika siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu. 19 Nanyi mtamtolea Yehova dhabihu ya kuteketezwa inayochomwa kwa moto ya ng’ombe dume wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wote wa umri wa mwaka mmoja. Mnapaswa kutoa wanyama wasio na kasoro.+ 20 Mnapaswa kuwatoa pamoja na matoleo ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;+ sehemu tatu za kumi kwa ajili ya ng’ombe dume na sehemu mbili za kumi kwa ajili ya kondoo dume mmoja. 21 Mtatoa sehemu moja ya kumi kwa ajili ya kila mwanakondoo dume kati ya wale wanakondoo dume saba, 22 na pia mbuzi mmoja ili kuwa dhabihu ya dhambi kwa ajili ya kufunika dhambi zenu. 23 Mtatoa vitu hivyo pamoja na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa asubuhi kwa ukawaida. 24 Mtatoa vitu hivyo kama chakula* kwa njia ileile kila siku kwa siku saba, ni dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova. Inapaswa kutolewa na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida pamoja na toleo lake la kinywaji. 25 Siku ya saba mtakuwa na kusanyiko takatifu.+ Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.+
26 “‘Siku ya mavuno ya kwanza yaliyokomaa,+ mnapomtolea Yehova nafaka iliyotoka kuvunwa+ katika sherehe yenu ya majuma,+ mnapaswa kuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.+ 27 Mtatoa ng’ombe dume wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wote wa umri wa mwaka mmoja kuwa dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayompendeza* Yehova,+ 28 pamoja na toleo la nafaka la unga laini uliochanganywa na mafuta; sehemu tatu za kumi kwa ajili ya kila ng’ombe dume, na sehemu mbili za kumi kwa ajili ya kondoo dume mmoja, 29 sehemu moja ya kumi kwa ajili ya kila mwanakondoo dume kati ya wale wanakondoo dume saba, 30 na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya kufunika dhambi zenu.+ 31 Mtatoa vitu hivyo pamoja na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida pamoja na toleo lake la nafaka. Mtatoa wanyama wasio na kasoro,+ pamoja na matoleo yao ya kinywaji.
29 “‘Na siku ya kwanza ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.+ Mnapaswa kupiga tarumbeta siku hiyo.+ 2 Mtatoa ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, wanakondoo dume saba wote wa mwaka mmoja kuwa dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayompendeza* Yehova, wanyama wote hawapaswi kuwa na kasoro, 3 pamoja na toleo la nafaka la unga laini uliochanganywa na mafuta; sehemu tatu za kumi kwa ajili ya ng’ombe dume, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya kondoo dume, 4 na sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mwanakondoo dume kati ya wale wanakondoo dume saba, 5 na mwanambuzi dume mmoja ili kuwa dhabihu ya dhambi kwa ajili ya kufunika dhambi zenu. 6 Mtatoa vitu hivyo pamoja na dhabihu ya kuteketezwa ya kila mwezi na toleo lake la nafaka+ na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida pamoja na toleo lake la nafaka+ na matoleo yake ya kinywaji,+ mkifuata utaratibu wa kawaida wa kutoa dhabihu hizo, ili iwe dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.
7 “‘Na siku ya kumi ya mwezi huo wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu,+ nanyi mnapaswa kujitesa.* Hampaswi kufanya kazi yoyote.+ 8 Mtamtoa ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wote wa umri wa mwaka mmoja kuwa dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayompendeza* Yehova; wanyama wote hawapaswi kuwa na kasoro.+ 9 Mtawatoa pamoja na toleo lao la nafaka la unga laini uliochanganywa na mafuta; sehemu tatu za kumi kwa ajili ya ng’ombe dume, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya kondoo dume mmoja, 10 sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mwanakondoo dume kati ya wale wanakondoo dume saba, 11 na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya dhambi inayotolewa kwa ajili ya kufunika dhambi+ na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na matoleo yake ya kinywaji.
12 “‘Na siku ya 15 ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu, nanyi mnapaswa kumfanyia Yehova sherehe kwa siku saba.+ 13 Mtatoa ng’ombe dume wachanga 13, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja kuwa dhabihu inayochomwa+ kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova; wanyama wote hawapaswi kuwa na kasoro.+ 14 Mtawatoa pamoja na toleo lao la nafaka la unga laini uliochanganywa na mafuta; sehemu tatu za kumi kwa ajili ya kila ng’ombe dume kati ya wale ng’ombe dume 13, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya kila kondoo dume kati ya wale kondoo dume 2, 15 na sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mwanakondoo dume kati ya wale wanakondoo dume 14, 16 na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
17 “‘Na siku ya pili mtatoa ng’ombe dume wachanga 12, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 18 na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 19 na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na matoleo yake ya kinywaji.+
20 “‘Na siku ya tatu mtatoa ng’ombe dume 11, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 21 na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 22 na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
23 “‘Na siku ya nne mtatoa ng’ombe dume 10, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 24 na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 25 na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
26 “‘Na siku ya tano mtatoa ng’ombe dume 9, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 27 na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 28 na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
29 “‘Na siku ya sita mtatoa ng’ombe dume 8, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 30 na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 31 na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na matoleo yake ya kinywaji.+
32 “‘Na siku ya saba mtatoa ng’ombe dume 7, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 33 na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 34 na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
35 “‘Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.+ 36 Mtatoa ng’ombe dume mmoja, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wote wa mwaka mmoja kuwa dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova, wanyama wote hawapaswi kuwa na kasoro,+ 37 na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya huyo ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 38 na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+
39 “‘Mtamtolea Yehova dhabihu hizo wakati wa sherehe zenu za majira,+ mbali na dhabihu zenu za nadhiri+ na matoleo yenu ya hiari+ yakiwa dhabihu zenu za kuteketezwa;+ na pia matoleo yenu ya nafaka+ na matoleo yenu ya kinywaji+ na dhabihu zenu za ushirika.’”+ 40 Musa aliwaambia Waisraeli mambo yote ambayo Yehova alimwamuru.
30 Kisha Musa akawaambia hivi viongozi+ wa makabila ya Israeli: “Yehova ameamuru hivi: 2 Mwanamume akimwekea Yehova nadhiri+ au akiapa+ kuweka nadhiri ya kujinyima kitu fulani,* hapaswi kuvunja ahadi yake.+ Anapaswa kufanya kila jambo aliloapa kufanya.+
3 “Na binti anayeishi katika nyumba ya baba yake akimwekea Yehova nadhiri au akiweka nadhiri ya kujinyima kitu fulani 4 na baba yake akisikia nadhiri yake au nadhiri aliyoweka ya kujinyima lakini asimpinge, basi ni lazima atimize nadhiri zake zote, kutia ndani kila nadhiri aliyoweka ya kujinyima kitu fulani. 5 Lakini baba yake akimkataza baada ya kusikia kwamba binti yake ameweka nadhiri au nadhiri za kujinyima kitu fulani, basi hatatimiza nadhiri hizo. Yehova atamsamehe kwa sababu baba yake alimkataza.+
6 “Hata hivyo, binti huyo akiolewa baada ya kuweka nadhiri au kuahidi kujinyima kitu fulani bila kufikiri 7 na mume wake akisikia nadhiri yake lakini asimpinge siku anayosikia kuhusu nadhiri hiyo, basi ni lazima binti huyo atimize nadhiri zake au nadhiri alizoweka za kujinyima kitu fulani. 8 Lakini mume wake akimkataza siku anayosikia kuhusu nadhiri hiyo, mume huyo anaweza kufuta nadhiri hiyo au ahadi ambayo mke wake aliweka bila kufikiri,+ na Yehova atamsamehe mke huyo.
9 “Lakini mjane au mwanamke aliyetalikiwa akiweka nadhiri, atatimiza kila jambo ambalo aliahidi.
10 “Hata hivyo, ikiwa mwanamke aliweka nadhiri au nadhiri ya kujinyima kitu fulani akiwa katika nyumba ya mume wake 11 na mume wake alisikia nadhiri yake lakini hakumpinga wala kumkataza, basi ni lazima atimize nadhiri zake au nadhiri yoyote aliyoweka ya kujinyima kitu fulani. 12 Lakini ikiwa mume wake alifuta kabisa nadhiri zozote au nadhiri yoyote ya kujinyima ya mke wake siku aliposikia kuzihusu, mke wake hatatimiza nadhiri hizo.+ Mume wake alizifuta, na Yehova atamsamehe mke huyo. 13 Mume wake anapaswa kukubali au kufuta kiapo chochote au nadhiri yoyote ya kujinyima kitu fulani. 14 Lakini ikiwa mume wake hampingi siku baada ya siku, basi amekubali viapo vyote au nadhiri zote za kujinyima za mke wake. Anakubaliana nazo kwa sababu hakumpinga siku alipomsikia akiweka nadhiri hizo. 15 Lakini mume wake akizifuta baadaye, baada ya siku aliyozisikia, atakuwa na hatia kwa kosa la mke wake.+
16 “Hizo ndizo sheria ambazo* Yehova alimwamuru Musa kuhusu mume na mke wake, na kuhusu baba na binti yake anayeishi nyumbani kwa baba yake.”
31 Kisha Yehova akamwambia Musa: 2 “Walipize kisasi+ Wamidiani+ kwa sababu ya mambo waliyowatendea Waisraeli. Baadaye utakufa na kuzikwa pamoja na watu wako.”*+
3 Basi Musa akawaambia watu hivi: “Watayarisheni wanaume wakapigane* na Wamidiani na kulipiza kisasi cha Yehova dhidi yao. 4 Mtapeleka jeshini wanaume 1,000 kutoka katika kila kabila la Israeli.” 5 Kwa hiyo wanaume 1,000 kutoka katika kila kabila miongoni mwa maelfu ya Waisraeli,+ jumla ya wanaume 12,000, walitayarishwa kwa ajili ya vita.
6 Kisha Musa akawatuma vitani wanaume 1,000 kutoka katika kila kabila, wakiwa pamoja na Finehasi+ mwana wa kuhani Eleazari aliyebeba mkononi mwake vyombo vitakatifu na tarumbeta za kutangaza mwito.+ 7 Walipigana na Wamidiani, kama Yehova alivyomwamuru Musa, wakawaua wanaume wote. 8 Miongoni mwa watu waliouawa kulikuwepo wafalme watano wa Midiani, yaani, Evi, Rekemu, Suri, Huru, na Reba. Pia, walimuua kwa upanga Balaamu+ mwana wa Beori. 9 Lakini Waisraeli waliwachukua mateka wanawake wa Midiani na watoto wao. Walichukua pia wanyama wao wote, naam, mifugo yao yote, na mali zao zote. 10 Waliteketeza majiji yote ambamo Wamidiani waliishi na kambi zao zote.* 11 Wakachukua nyara zote na mateka wote, wanadamu na wanyama. 12 Wakamletea Musa na kuhani Eleazari na Waisraeli wote mateka hao na nyara hizo kambini, katika jangwa tambarare la Moabu,+ karibu na Yordani huko Yeriko.
13 Kisha Musa na kuhani Eleazari na wakuu wote wa Waisraeli wakatoka ili kukutana nao nje ya kambi. 14 Lakini Musa alikasirishwa sana na wanaume waliowekwa kusimamia jeshi, yaani, wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia waliokuwa wakirudi kutoka vitani. 15 Musa akawauliza: “Kwa nini mmewaacha hai wanawake wote? 16 Kumbukeni kwamba hao ndio waliochochewa na Balaamu kuwashawishi Waisraeli wakose uaminifu+ kwa Yehova kule Peori,+ na kuwaletea pigo watu wa Yehova.+ 17 Sasa muueni kila mtoto wa kiume na kila mwanamke ambaye amewahi kufanya ngono na mwanamume. 18 Lakini msiwaue wasichana wote ambao hawajawahi kufanya ngono na mwanamume.+ 19 Nanyi mnapaswa kupiga kambi nje ya kambi kwa siku saba. Kila mtu miongoni mwenu ambaye amemuua mtu na kila mtu ambaye amemgusa mtu aliyeuawa+ anapaswa kujitakasa+ siku ya tatu na siku ya saba, ninyi na mateka wenu. 20 Mnapaswa pia kutakasa kutokana na dhambi kila vazi, kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kila kitu kilichotengenezwa kwa manyoya ya mbuzi, na kila kitu kilichotengenezwa kwa mbao.”
21 Ndipo kuhani Eleazari akawaambia wanaume walioenda vitani: “Hii ndiyo sheria ambayo Yehova amempa Musa, 22 ‘Ni dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, na madini ya risasi tu, 23 yaani, kila kitu kinachoweza kustahimili moto, ndicho mnachopaswa kupitisha motoni, nacho kitakuwa safi. Hata hivyo, kinapaswa pia kusafishwa kwa maji ya kutakasa.+ Kila kitu ambacho hakiwezi kustahimili moto, mnapaswa kukitakasa kwa maji. 24 Nanyi mnapaswa kufua mavazi yenu siku ya saba na kuwa safi, kisha mnaweza kuingia kambini.’”+
25 Tena Yehova akamwambia Musa hivi: 26 “Wewe pamoja na kuhani Eleazari na viongozi wa koo* za Waisraeli hesabuni nyara zote, kutia ndani wanadamu na wanyama waliotekwa. 27 Gaweni nyara hizo katika mafungu mawili, ili wanajeshi walioenda vitani wapate fungu moja na Waisraeli wengine fungu lingine.+ 28 Kutoka kwa wanajeshi walioenda vitani, mtachukua nafsi* moja kutoka kwa kila nafsi 500 za wanadamu, za ng’ombe, za punda, na kondoo ili iwe kodi ya Yehova. 29 Mnapaswa kuchukua nafsi hizo kutoka katika fungu lao na kumpa kuhani Eleazari kama mchango kwa Yehova.+ 30 Kutoka katika fungu ambalo Waisraeli watapewa, mnapaswa kuchukua nafsi moja kutoka kwa kila nafsi 50 za wanadamu, za ng’ombe, za punda, za kondoo, na za kila aina ya mnyama wa kufugwa, na kuwapa Walawi,+ wanaotimiza majukumu katika hema la Yehova la ibada.”+
31 Basi Musa na kuhani Eleazari wakafanya kama Yehova alivyomwamuru Musa. 32 Nyara na vitu vyote ambavyo watu walichukua vitani ni kondoo 675,000, 33 ng’ombe 72,000, 34 na punda 61,000. 35 Wanawake ambao hawakuwa wamefanya ngono na mwanamume+ walikuwa wanawake* 32,000. 36 Na nusu iliyokuwa fungu la wale walioenda vitani ilikuwa kondoo 337,500. 37 Kondoo 675 kati yao walichukuliwa ili kuwa kodi kwa Yehova. 38 Pia, kulikuwa na ng’ombe 36,000, na ng’ombe 72 kati yao walichukuliwa ili kuwa kodi kwa Yehova. 39 Punda walikuwa 30,500, na punda 61 kati yao walichukuliwa ili kuwa kodi kwa Yehova. 40 Wanadamu walikuwa 16,000, na 32 kati yao walichukuliwa ili kuwa kodi kwa Yehova. 41 Kisha Musa akampa kuhani Eleazari kodi hiyo iwe mchango wa Yehova,+ kama Yehova alivyomwamuru Musa.
42 Ile nusu waliyopewa Waisraeli ambayo Musa aliitenga na nusu waliyopewa wanajeshi walioenda vitani, 43 ilikuwa kondoo 337,500, 44 ng’ombe 36,000, 45 punda 30,500, 46 na wanadamu 16,000. 47 Kisha kutoka katika nusu hiyo ambayo ni fungu la Waisraeli, Musa alichukua nafsi moja kutoka kwa kila nafsi 50 za wanadamu na za wanyama akawapa Walawi+ waliotimiza majukumu katika hema la Yehova la ibada,+ kama Yehova alivyomwamuru Musa.
48 Kisha wanaume waliowekwa kusimamia maelfu ya wanajeshi,+ yaani, wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia, wakamfikia Musa, 49 na kumwambia: “Sisi watumishi wako tumewahesabu wanajeshi walio chini ya usimamizi wetu, na hakuna hata mmoja wao anayekosekana.+ 50 Kwa hiyo mruhusu kila mmoja wetu atoe vitu alivyopata ili viwe vya Yehova, yaani, vitu vya dhahabu, mikufu ya miguuni, bangili, pete za muhuri, vipuli, na vito vingine, ili Yehova afunike dhambi zetu.”
51 Basi Musa na kuhani Eleazari wakapokea dhahabu hiyo kutoka kwao, naam, vito vyote. 52 Dhahabu yote ambayo wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia walimtolea Yehova mchango ilikuwa shekeli 16,750.* 53 Kila mwanajeshi alikuwa amejichukulia nyara. 54 Musa na kuhani Eleazari walipokea dhahabu hiyo kutoka kwa wakuu wa maelfu na wakuu wa mamia na kuileta katika hema la mkutano ili iwe kumbukumbu mbele za Yehova kwa ajili ya Waisraeli.
32 Sasa wana wa Rubeni+ na wana wa Gadi+ walikuwa na mifugo mingi sana, wakaona kwamba eneo la Yazeri+ na eneo la Gileadi yalikuwa maeneo mazuri kwa mifugo. 2 Basi wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakaja kwa Musa, kuhani Eleazari, na wakuu wa Waisraeli na kuwaambia hivi: 3 “Atarothi, Diboni, Yazeri, Nimra, Heshboni,+ Eleale, Sebamu, Nebo,+ na Beoni,+ 4 maeneo ambayo Yehova aliyashinda mbele ya Waisraeli,+ ni maeneo mazuri kwa mifugo, nasi watumishi wenu tuna mifugo mingi.”+ 5 Wakaendelea kusema, “Ikiwa sisi watumishi wenu tumepata kibali machoni penu, tupeni maeneo haya tuyamiliki. Msituvushe ng’ambo ya Mto Yordani.”
6 Lakini Musa akawaambia hivi wana wa Gadi na wana wa Rubeni: “Je, ndugu zenu wataenda vitani huku ninyi mkiendelea kukaa hapa? 7 Kwa nini muwavunje moyo Waisraeli wasivuke kuingia katika nchi ambayo kwa hakika Yehova atawapa? 8 Hivyo ndivyo baba zenu walivyofanya nilipowatuma kutoka Kadesh-barnea wakaione ile nchi.+ 9 Walipofika kwenye Bonde la Eshkoli+ na kuiona nchi hiyo, waliwavunja moyo Waisraeli wasiingie katika nchi ambayo Yehova angewapa.+ 10 Yehova aliwaka hasira siku hiyo na kuapa hivi:+ 11 ‘Wanaume waliotoka Misri wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi hawataiona nchi+ ambayo niliapa kwamba nitampa Abrahamu, Isaka, na Yakobo,+ kwa sababu hawakunifuata kwa moyo wote— 12 isipokuwa Kalebu+ mwana wa Yefune, Mkenizi, na Yoshua+ mwana wa Nuni, kwa sababu wamenifuata mimi Yehova kwa moyo wote.’+ 13 Basi hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli naye akawafanya watangetange nyikani kwa miaka 40,+ mpaka kizazi chote kilichokuwa kikifanya maovu machoni pa Yehova kilipoangamia.+ 14 Na sasa ninyi mmekuwa kama baba zenu, kundi la watenda dhambi wanaozidisha hasira kali ya Yehova dhidi ya Waisraeli. 15 Mkigeuka na kuacha kumfuata, kwa hakika atawaacha tena watu hawa nyikani, nanyi mtasababisha watu hawa wote waangamizwe.”
16 Baadaye wakaja tena kwake na kumwambia: “Turuhusu tujenge hapa mazizi ya mawe kwa ajili ya mifugo yetu na majiji kwa ajili ya watoto wetu. 17 Lakini sisi tutaendelea kuwa tayari kwa ajili ya vita+ na tutakuwa mstari wa mbele mpaka tutakapowafikisha Waisraeli mahali pao, wakati huo watoto wetu watakaa katika majiji yenye ngome, wakiwa salama kutoka kwa wakaaji wa nchi. 18 Hatutarudi katika nyumba zetu mpaka kila Mwisraeli atakaporithi eneo lake.+ 19 Kwa maana hatutapokea urithi wowote pamoja nao katika eneo lote lililo ng’ambo ya Yordani, kwa sababu tumepokea urithi wetu upande wa mashariki wa Yordani.”+
20 Musa akawaambia: “Ikiwa mtafanya hivi: Ikiwa mtachukua silaha mbele za Yehova kwa ajili ya vita;+ 21 na ikiwa kila mmoja wenu atachukua silaha na kuvuka Yordani mbele za Yehova anapowafukuza maadui wake kutoka mbele zake+ 22 mpaka mtakaposhinda na kuichukua nchi mbele za Yehova,+ mnaweza kurudi+ nanyi hamtakuwa na hatia mbele za Yehova na Waisraeli. Ndipo Yehova atakapokubali mmiliki nchi hii.+ 23 Lakini msipofanya hivyo, mtakuwa mmemtendea dhambi Yehova. Nanyi mjue kwamba mtaadhibiwa kwa sababu ya dhambi yenu. 24 Kwa hiyo mnaweza kujenga majiji kwa ajili ya watoto wenu na mazizi kwa ajili ya mifugo yenu,+ lakini ni lazima mfanye mambo mliyoahidi.”
25 Wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakamwambia Musa hivi: “Bwana wetu, sisi watumishi wako tutafanya kama unavyotuamuru. 26 Watoto wetu, wake zetu, mifugo yetu, na wanyama wetu wote watabaki hapa katika majiji ya Gileadi,+ 27 lakini sisi watumishi wako tutavuka, kila mwanamume aliyechukua silaha ili kupigana vita mbele za Yehova,+ kama unavyosema bwana wetu.”
28 Basi Musa akampa kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo* za makabila ya Waisraeli amri kuwahusu. 29 Musa akawaambia hivi: “Ikiwa wana wa Gadi na wana wa Rubeni watavuka Yordani pamoja nanyi, yaani, kila mwanamume aliyechukua silaha ili kupigana vita mbele za Yehova, nanyi mshinde na kuchukua eneo hilo, basi mtawapa eneo la Gileadi ili walimiliki.+ 30 Lakini ikiwa hawatachukua silaha na kuvuka pamoja nanyi, basi wataishi pamoja nanyi katika nchi ya Kanaani.”
31 Basi wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakajibu: “Sisi watumishi wako tutafanya mambo ambayo Yehova ametuambia. 32 Tutachukua silaha na kuvuka mbele za Yehova kuingia nchi ya Kanaani,+ lakini urithi wetu utakuwa upande huu wa Yordani.” 33 Hivyo Musa akawapa—wana wa Gadi, wana wa Rubeni,+ na nusu ya kabila la Manase+ mwana wa Yosefu—ufalme wa Sihoni+ mfalme wa Waamori na ufalme wa Ogu+ mfalme wa Bashani, maeneo hayo na majiji yaliyokuwemo na pia majiji jirani.
34 Wana wa Gadi wakajenga* Diboni,+ Atarothi,+ Aroeri,+ 35 Atroth-shofani, Yazeri,+ Yogbeha,+ 36 Beth-nimra,+ Beth-harani,+ majiji yenye ngome, na mazizi ya mawe kwa ajili ya mifugo. 37 Nao wana wa Rubeni wakajenga Heshboni,+ Eleale,+ Kiriathaimu,+ 38 Nebo,+ na Baal-meoni+—majina ya majiji hayo yalibadilishwa—na Sibma; nao wakaanza kuyapa majina mapya majiji waliyojenga upya.
39 Wana wa Makiri+ mwana wa Manase walishambulia eneo la Gileadi, wakaliteka, na kuwafukuza Waamori waliokaa humo. 40 Kwa hiyo Musa akampa Makiri mwana wa Manase, Gileadi, akaanza kukaa katika eneo hilo.+ 41 Na Yairi mwana wa Manase akawashambulia wakaaji wa eneo hilo na kuteka vijiji vyao vya mahema, akaviita Hawoth-yairi.*+ 42 Naye Noba akashambulia na kuliteka jiji la Kenathi na miji yake, naye akaliita Noba, jina lake mwenyewe.
33 Waisraeli walipiga kambi katika vituo vifuatavyo walipotoka nchini Misri+ kulingana na vikosi vyao*+ wakiongozwa na Musa na Haruni.+ 2 Musa aliandika kila kituo katika safari yao kama Yehova alivyomwagiza, na hivi ndivyo vituo vya safari yao, kituo baada ya kituo:+ 3 Waliondoka Ramesesi+ siku ya 15 ya mwezi wa kwanza.+ Siku hiyohiyo baada ya Pasaka,+ Waisraeli waliondoka kwa ujasiri* huku Wamisri wote wakiwatazama. 4 Wakati huo, Wamisri walikuwa wakiwazika wazaliwa wao wote wa kwanza ambao Yehova aliwaangamiza,+ kwa kuwa Yehova alikuwa ametekeleza hukumu dhidi ya miungu yao.+
5 Kwa hiyo Waisraeli wakaondoka Ramesesi na kupiga kambi Sukothi.+ 6 Kisha wakaondoka Sukothi na kupiga kambi Ethamu,+ kwenye ukingo wa nyika. 7 Halafu wakaondoka Ethamu, wakageuka na kurudi Pihahirothi, mbele ya Baal-sefoni,+ wakapiga kambi karibu na Migdoli.+ 8 Kisha wakaondoka Pihahirothi na kupita katikati ya bahari+ mpaka nyikani,+ wakaendelea kusafiri kwa siku tatu katika nyika ya Ethamu+ na kupiga kambi huko Mara.+
9 Kisha wakaondoka Mara na kufika Elimu. Huko Elimu kulikuwa na chemchemi 12 za maji na mitende 70, kwa hiyo wakapiga kambi mahali hapo.+ 10 Halafu wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari Nyekundu. 11 Kisha wakaondoka kando ya Bahari Nyekundu na kupiga kambi katika nyika ya Sini.+ 12 Halafu wakaondoka katika nyika ya Sini na kupiga kambi Dofka. 13 Baadaye wakaondoka Dofka na kupiga kambi Alushi. 14 Kisha wakaondoka Alushi na kupiga kambi Refidimu,+ ambapo hapakuwa na maji ya kunywa. 15 Halafu wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika nyika ya Sinai.+
16 Wakaondoka katika nyika ya Sinai na kupiga kambi Kibroth-hataava.+ 17 Kisha wakaondoka Kibroth-hataava na kupiga kambi Haserothi.+ 18 Baada ya hapo wakaondoka Haserothi na kupiga kambi Rithma. 19 Kisha wakaondoka Rithma na kupiga kambi Rimon-peresi. 20 Halafu wakaondoka Rimon-peresi na kupiga kambi Libna. 21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi Risa. 22 Kisha wakaondoka Risa na kupiga kambi Kehelatha. 23 Halafu wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Kisha wakaondoka kwenye Mlima Sheferi na kupiga kambi Harada. 25 Halafu wakaondoka Harada na kupiga kambi Makelothi. 26 Kisha wakaondoka+ Makelothi na kupiga kambi Tahathi. 27 Halafu wakaondoka Tahathi na kupiga kambi Tera. 28 Kisha wakaondoka Tera na kupiga kambi Mithka. 29 Baadaye wakaondoka Mithka na kupiga kambi Hashmona. 30 Kisha wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi. 31 Halafu wakaondoka Moserothi na kupiga kambi Bene-yaakani.+ 32 Kisha wakaondoka Bene-yaakani na kupiga kambi Hor-hagidgadi. 33 Halafu wakaondoka Hor-hagidgadi na kupiga kambi Yotbata.+ 34 Baadaye wakaondoka Yotbata na kupiga kambi Abrona. 35 Kisha wakaondoka Abrona na kupiga kambi Esion-geberi.+ 36 Kisha wakaondoka Esion-geberi na kupiga kambi katika nyika ya Zini,+ yaani, Kadeshi.
37 Baadaye wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori,+ mpakani mwa nchi ya Edomu. 38 Kisha kuhani Haruni akapanda juu ya Mlima Hori kwa agizo la Yehova, akafa huko siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa 40 tangu Waisraeli walipotoka nchini Misri.+ 39 Haruni alikuwa na umri wa miaka 123 alipokufa juu ya Mlima Hori.
40 Basi mfalme wa Aradi,+ Mkanaani, aliyekuwa akiishi Negebu katika nchi ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Baada ya muda wakaondoka kwenye Mlima Hori+ na kupiga kambi Salmona. 42 Kisha wakaondoka Salmona na kupiga kambi Punoni. 43 Halafu wakaondoka Punoni na kupiga kambi Obothi.+ 44 Wakaondoka Obothi na kupiga kambi Iye-abarimu kwenye mpaka wa Moabu.+ 45 Baadaye wakaondoka Iyimu* na kupiga kambi Dibon-gadi.+ 46 Kisha wakaondoka Dibon-gadi na kupiga kambi Almon-diblathaimu. 47 Halafu wakaondoka Almon-diblathaimu na kupiga kambi kwenye milima ya Abarimu+ karibu na Nebo.+ 48 Mwishowe wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi katika jangwa tambarare la Moabu karibu na Yordani huko Yeriko.+ 49 Wakaendelea kupiga kambi kandokando ya Mto Yordani kuanzia Beth-yeshimothi mpaka Abel-shitimu,+ katika jangwa tambarare la Moabu.
50 Yehova akazungumza na Musa katika jangwa tambarare la Moabu karibu na Yordani huko Yeriko, akamwambia: 51 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Mnavuka Mto Yordani kuingia katika nchi ya Kanaani.+ 52 Ni lazima muwafukuze wakaaji wote wa nchi hiyo kutoka mbele yenu na kuharibu sanamu zao zote za mawe+ na sanamu zao zote za chuma,*+ nanyi mnapaswa kuharibu mahali pao pote patakatifu palipo juu.+ 53 Mtaimiliki nchi hiyo na kuishi humo, kwa maana hakika nitawapa nchi hiyo ili mwimiliki.+ 54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kura+ na kuimiliki kulingana na familia zenu. Kundi kubwa litapokea urithi mkubwa zaidi na kikundi kidogo kitapokea urithi mdogo.+ Kila mtu atapokea urithi wake mahali ambapo kura yake itaangukia. Mtapokea urithi wenu wa nchi kulingana na makabila ya baba zenu.+
55 “‘Hata hivyo, msipowafukuza wakaaji wa nchi hiyo kutoka mbele yenu,+ basi wale mtakaoruhusu wabaki watakuwa kama vibanzi katika macho yenu na kama miiba kwenye mbavu zenu, nao watawasumbua katika nchi mtakayoishi.+ 56 Nami nitawatendea ninyi mambo niliyokusudia kuwatendea wao.’”+
34 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 2 “Wape Waisraeli maagizo haya: ‘Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani,+ nchi mtakayoirithi, hii ndiyo itakayokuwa mipaka ya nchi hiyo ya Kanaani.+
3 “‘Mpaka wenu wa kusini utaanzia nyika ya Zini kando ya Edomu, na upande wa mashariki mpaka huo wa kusini utaanzia mwisho wa Bahari ya Chumvi.+ 4 Kisha mpaka huo utapinda na kwenda upande wa kusini wa mwinuko wa Akrabimu,+ nao utaendelea mpaka Zini na kuishia upande wa kusini wa Kadesh-barnea.+ Kisha utaenda Hasar-adari+ na kuendelea mpaka Asimoni. 5 Mpaka huo utapinda huko Asimoni na kuelekea kwenye Bonde la Misri na kuishia kwenye Bahari ya Mediterania.+
6 “‘Mpaka wenu wa magharibi utakuwa Bahari Kuu* na pwani. Huo utakuwa mpaka wenu wa magharibi.+
7 “‘Huu ndio utakaokuwa mpaka wenu wa kaskazini: Mtaweka alama kuanzia Bahari Kuu mpaka Mlima Hori.+ 8 Kutoka Mlima Hori mtaweka alama mpaka Lebo-hamathi,*+ nao utaishia Sedadi.+ 9 Kisha utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hasar-enani.+ Huo utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
10 “‘Kisha mtaweka alama ya mpaka wenu wa mashariki kuanzia Hasar-enani hadi Shefamu. 11 Mpaka huo utaanzia Shefamu hadi Ribla, upande wa mashariki wa Aini, nao utashuka na kuvuka mteremko wa mashariki wa Bahari ya Kinerethi.*+ 12 Kisha utaendelea mpaka Yordani na kuishia kwenye Bahari ya Chumvi.+ Hiyo ndiyo itakayokuwa nchi yenu+ na mipaka inayoizunguka.’”
13 Kwa hiyo Musa akawapa Waisraeli maagizo haya: “Hiyo ndiyo nchi mtakayoigawanya kwa kura na kuimiliki,+ kama Yehova alivyoamuru kwamba makabila tisa na nusu yapewe nchi hiyo. 14 Kwa maana kabila la Rubeni kulingana na koo zao,* kabila la Gadi kulingana na koo zao,* na nusu ya kabila la Manase tayari yamechukua urithi wao.+ 15 Makabila hayo mawili na nusu tayari yamechukua urithi wao upande wa mashariki wa Yordani karibu na Yeriko, upande wa mapambazuko ya jua.”+
16 Yehova akaendelea kumwambia Musa, 17 “Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowagawia nchi ili mwimiliki: kuhani Eleazari+ na Yoshua+ mwana wa Nuni. 18 Nanyi mtachukua mkuu mmoja kutoka katika kila kabila ili awasaidie kuigawanya nchi mtakayorithi.+ 19 Haya ndiyo majina ya wanaume hao: kutoka kabila la Yuda,+ Kalebu+ mwana wa Yefune; 20 kutoka kabila la wana wa Simeoni,+ Shemueli mwana wa Amihudi; 21 kutoka kabila la Benjamini,+ Elidadi mwana wa Kisloni; 22 kutoka kabila la wana wa Dani,+ mkuu mmoja, Buki mwana wa Yogli; 23 kutoka kwa wana wa Yosefu,+ kwa ajili ya kabila la wana wa Manase,+ mkuu mmoja, Hanieli mwana wa Efodi; 24 kutoka kabila la wana wa Efraimu,+ mkuu mmoja, Kemueli mwana wa Shiftani; 25 kutoka kabila la wana wa Zabuloni,+ mkuu mmoja, Elisafani mwana wa Parnaki; 26 kutoka kabila la wana wa Isakari,+ mkuu mmoja, Paltieli mwana wa Azani; 27 kutoka kabila la wana wa Asheri,+ mkuu mmoja, Ahihudi mwana wa Shelomi, 28 na kutoka kabila la wana wa Naftali,+ mkuu mmoja, Pedaheli mwana wa Amihudi.” 29 Hao ndio wanaume ambao Yehova aliamuru wawagawie Waisraeli ardhi katika nchi ya Kanaani.+
35 Yehova akaendelea kuzungumza na Musa katika jangwa tambarare la Moabu karibu na Yordani+ huko Yeriko, akamwambia: 2 “Waagize Waisraeli wawape Walawi majiji ya kuishi kutoka katika urithi watakaomiliki,+ nao wanapaswa kuwapa Walawi malisho yanayozunguka majiji hayo.+ 3 Wataishi katika majiji hayo, na malisho hayo yatakuwa ya mifugo yao, na ya mali zao, na wanyama wao wengine wote. 4 Malisho ya majiji mtakayowapa Walawi yatakuwa na upana wa mikono 1,000* kila upande kutoka kwenye ukuta wa jiji. 5 Mtapima nje ya jiji mikono 2,000 upande wa mashariki, mikono 2,000 upande wa kusini, mikono 2,000 upande wa magharibi, na mikono 2,000 upande wa kaskazini; jiji litakuwa katikati. Hayo ndiyo yatakayokuwa malisho ya majiji yao.
6 “Majiji mtakayowapa Walawi yatakuwa majiji 6 ya makimbilio+ ili mtu anayemuua mwenzake akimbilie humo,+ pia mtawapa majiji mengine 42. 7 Mtawapa Walawi jumla ya majiji 48 pamoja na malisho yake.+ 8 Majiji mtakayowapa yatatoka katika urithi wa Waisraeli.+ Mtachukua majiji mengi kutoka kwa makabila makubwa na majiji machache kutoka kwa makabila madogo.+ Kila kabila litawapa Walawi baadhi ya majiji yake kulingana na urithi ambao litapokea.”
9 Yehova akaendelea kumwambia Musa, 10 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Mnavuka Mto Yordani kuingia katika nchi ya Kanaani.+ 11 Mnapaswa kuchagua majiji yatakayowafaa ninyi ili yawe majiji ya makimbilio ili mtu anayemuua mwenzake bila kukusudia akimbilie humo.+ 12 Majiji hayo yatakuwa mahali penu pa kukimbilia kutoka kwa mtu anayelipiza kisasi cha damu,+ ili muuaji asiuawe kabla ya kesi yake kusikilizwa mbele ya kusanyiko.+ 13 Majiji sita ya makimbilio mtakayotoa yatatumiwa kwa kusudi hilo. 14 Mtatoa majiji matatu upande huu wa Yordani+ na majiji matatu katika nchi ya Kanaani+ ili yawe majiji ya makimbilio. 15 Majiji hayo sita yatakuwa majiji ya makimbilio kwa ajili ya Waisraeli, kwa ajili ya wageni,+ na kwa ajili ya wahamiaji wanaoishi miongoni mwenu, ili mtu yeyote anayemuua mwenzake bila kukusudia akimbilie humo.+
16 “‘Lakini ikiwa mtu amempiga mwenzake kwa kifaa cha chuma na kumuua, yeye ni muuaji. Lazima muuaji huyo auawe.+ 17 Ikiwa alimpiga kwa jiwe ambalo linaweza kuua, na mtu huyo akafa, aliyempiga ni muuaji. Lazima muuaji huyo auawe. 18 Ikiwa alimpiga kwa kifaa cha mbao kinachoweza kuua, na mtu huyo akafa, aliyempiga ni muuaji. Lazima muuaji huyo auawe.
19 “‘Mwenye kulipiza kisasi cha damu ndiye atakayemuua muuaji. Atakapokutana naye, atamuua yeye mwenyewe. 20 Ikiwa mtu anayemchukia mwenzake anamsukuma au kumtupia kitu fulani kwa nia mbaya* na kumuua,+ 21 au kwa sababu ya chuki anampiga kwa mkono na kumuua, ni lazima mtu huyo aliyempiga auawe. Yeye ni muuaji. Mtu anayelipiza kisasi cha damu atamuua muuaji huyo atakapokutana naye.
22 “‘Lakini ikiwa alimsukuma au kumtupia kitu chochote na kumuua bila kukusudia au bila chuki na bila nia mbaya,*+ 23 au ikiwa alimwangushia jiwe bila kumwona na mtu huyo akafa, lakini hakuwa adui yake au hakukusudia kumdhuru, 24 basi watu wanapaswa kuhukumu kati ya muuaji na mtu anayelipiza kisasi cha damu, kwa kufuata sheria hizo.+ 25 Kisha watu watamwokoa muuaji kutoka mikononi mwa mtu anayelipiza kisasi cha damu na kumrudisha katika jiji lake la makimbilio alimokuwa amekimbilia, naye atakaa humo mpaka kuhani mkuu aliyetiwa mafuta matakatifu+ atakapokufa.
26 “‘Lakini muuaji akitoka nje ya mpaka wa jiji la makimbilio alimokimbilia, 27 kisha mtu anayelipiza kisasi cha damu ampate nje ya mpaka wa jiji la makimbilio na kumuua, mtu huyo anayelipiza kisasi cha damu hatakuwa na hatia ya damu. 28 Kwa maana ni lazima muuaji akae katika jiji lake la makimbilio mpaka kuhani mkuu atakapokufa. Lakini baada ya kuhani mkuu kufa, muuaji anaweza kurudi katika ardhi anayomiliki.+ 29 Mtatumia sheria hizo kuhukumu katika vizazi vyenu vyote mahali popote mnapoishi.
30 “‘Yeyote anayemuua mtu* anapaswa kuuawa kama muuaji+ ikiwa kuna ushahidi kutoka kwa mashahidi;+ lakini hakuna mtu atakayeuawa* kwa ushahidi wa mtu mmoja tu. 31 Hampaswi kuchukua fidia yoyote kwa ajili ya uhai wa* muuaji anayestahili kufa, kwa maana ni lazima auawe.+ 32 Nanyi hampaswi kuchukua fidia kwa ajili ya mtu aliyekimbilia katika jiji lake la makimbilio na hivyo kumruhusu arudi kuishi katika ardhi yake kabla ya kuhani mkuu kufa.
33 “‘Msiichafue nchi mnayoishi ndani yake, kwa sababu damu inachafua nchi,+ na hakuna msamaha kwa ajili ya damu iliyomwagwa nchini isipokuwa kwa kumwaga damu ya yule aliyeimwaga.+ 34 Msiitie unajisi nchi mnayoishi ndani yake, ambamo ninakaa; kwa maana mimi, Yehova, ninakaa miongoni mwa Waisraeli.’”+
36 Viongozi wa familia za wazao wa Gileadi mwana wa Makiri+ mwana wa Manase wa koo za wana wa Yosefu wakaja kuzungumza na Musa na wakuu, yaani, viongozi wa makabila ya Waisraeli. 2 Wakawaambia: “Yehova alimwamuru bwana wetu awagawie Waisraeli nchi kwa kura+ ili wairithi; na bwana wetu aliamriwa na Yehova achukue urithi wa Selofehadi ndugu yetu na kuwapa binti zake.+ 3 Lakini wakiolewa na wanaume wa kabila lingine la Waisraeli, urithi wa wanawake hao utaondolewa kutoka katika urithi wa baba zetu na kuongezwa kwenye urithi wa kabila ambamo wataolewa, kwa hiyo urithi huo utaondolewa kutoka katika urithi wetu tuliopokea kwa kura. 4 Waisraeli wanapofanya Mwadhimisho wa Miaka 50,+ urithi wa wanawake hao utaongezwa kwenye urithi wa kabila walimoolewa, na hivyo urithi wao utaondolewa kutoka katika urithi wa kabila la baba zetu.”
5 Ndipo Musa akawaamuru hivi Waisraeli kama Yehova alivyoagiza: “Kabila la wana wa Yosefu linasema ukweli. 6 Yehova ameamuru hivi kuhusu mabinti wa Selofehadi: ‘Wanaweza kuolewa na mtu yeyote wampendaye. Lakini wanapaswa kuolewa na mwanamume anayetoka katika ukoo wa kabila la baba yao. 7 Hakuna urithi wa Waisraeli unaopaswa kuhamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila lingine, kwa sababu Waisraeli wanapaswa kushikilia urithi wa kabila la mababu zao. 8 Na kila binti aliye na urithi miongoni mwa makabila ya Waisraeli anapaswa kuolewa na mzao wa kabila la baba yake,+ ili Waisraeli waendelee kumiliki urithi wa mababu zao. 9 Hakuna urithi unaopaswa kuhamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila lingine, kwa sababu makabila ya Waisraeli yanapaswa kushikilia urithi wao.’”
10 Mabinti wa Selofehadi walifanya kama Yehova alivyomwamuru Musa.+ 11 Basi Mala, Tirsa, Hogla, Milka, na Noa, mabinti wa Selofehadi,+ waliolewa na wana wa ndugu za baba yao. 12 Wakawa wake za wanaume kutoka katika koo za Manase mwana wa Yosefu, ili urithi wao ubaki katika kabila la baba yao.
13 Hizo ndizo amri na sheria ambazo* Yehova aliwapa Waisraeli kupitia Musa katika jangwa tambarare la Moabu karibu na Yordani, huko Yeriko.+
Tnn., “wana wote wa Israeli.”
Au “kila kichwa.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “mgeni yeyote,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.
Au “alama yake.”
Tnn., “jeshi lake.”
Au “kulilinda; kutumikia katika.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “hivi ndivyo vilivyokuwa vizazi vya.”
Tnn., “mgeni yeyote,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.
Au “kila kifungua mimba.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “Mgeni yeyote,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Au “shekeli takatifu.”
Gera moja ilikuwa na uzito wa gramu 0.57. Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “kinywa cha.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “majivu yenye mafuta,” yaani, majivu yaliyojaa mafuta ya dhabihu.
Wingi wa kifaa kinachoitwa uma.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “kugusa nafsi iliyokufa.” Angalia Kamusi.
Au “ninaopiga hema.”
Au “nafsi hiyo ina.”
Sehemu ya kumi ya efa ilikuwa sawa na lita 2.2 au kilogramu 1.3 hivi. Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “afanye paja lako lidhoofike.” Inaonekana msemo huu unarejelea viungo vya uzazi.
Tnn., “na paja lako litadhoofika.” Inaonekana msemo huu unarejelea viungo vya uzazi.
Au “Na iwe hivyo! Na iwe hivyo!”
Tnn., “na paja lake litadhoofika.” Inaonekana msemo huu unarejelea viungo vya uzazi.
Katika Kiebrania ni na·zirʹ, linalomaanisha “Aliyetengwa; Aliyewekwa Wakfu; Aliyewekwa Kando.”
Au “kuikaribia nafsi iliyokufa.” Angalia Kamusi.
Au “kutia unajisi kichwa cha Unadhiri wake.”
Au “kugusa nafsi iliyokufa.”
Au “kichwa cha Unadhiri wake.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “kuweka wakfu.”
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Au “shekeli takatifu.”
Au “bakuli dogo lenye uzito wa shekeli 10, lililojaa uvumba.”
Tnn., “awatikise,” yaani, awafanye waende mbele na nyuma.
Tnn., “kuwatikisa,” yaani, kuwafanya waende mbele na nyuma.
Tnn., “kuwatikisa,” yaani, kuwafanya waende mbele na nyuma.
Au “kila kifungua mimba.”
Tnn., “akawatikisa,” yaani, akawafanya waende mbele na nyuma.
Tnn., “katikati ya zile jioni mbili.”
Tnn., “katikati ya zile jioni mbili.”
Tnn., “katikati ya zile jioni mbili.”
Tnn., “juu ya.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yao yalifuata.”
Yaani, Yethro.
Tnn., “kuwa macho yetu.”
Au “makumi ya maelfu kwa maelfu.”
Maana yake “Kuteketea,” yaani, moto mkali.
Inaonekana ni watu ambao hawakuwa Waisraeli.
Au “mlezi wa kiume.”
Au “wakaanza kutabiri.”
Mkono mmoja ulilingana na sentimita 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Homeri ni kipimo sawa na lita 220. Angalia Nyongeza B14.
Maana yake “Makaburi ya Watu Wenye Tamaa.”
Au “mnyenyekevu zaidi, kuliko mtu mwingine yeyote.”
Tnn., “Anajithibitisha mwenyewe kuwa mwaminifu katika nyumba yangu yote.”
Tnn., “kinywa kwa kinywa.”
Au “Yehoshua,” linalomaanisha Yehova Ni Wokovu.
Au “njia ya kuingia Hamathi.”
Maana yake “Kishada cha Zabibu.”
Tnn., “wao ni mkate kwetu.”
Au “tauni.”
Au “fadhili nyingi zenye upendo.”
Tnn., “ya ukahaba.”
Au “ya kuwa maadui wangu.”
Au “inayomtuliza.”
Sehemu ya kumi ya efa ilikuwa sawa na lita 2.2 au kilogramu 1.3 hivi. Angalia Nyongeza B14.
Hini ilikuwa sawa na lita 3.67. Angalia Nyongeza B14.
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Tnn., “maamuzi yaleyale ya hukumu.”
Tnn., “mkate wowote wa.”
Au “inayomtuliza.”
Tnn., “Kosa lake litakuwa juu ya kichwa chake.”
Au “kupiga ubwana juu yetu.”
Tnn., “roho za miili yote.”
Au “si matakwa yangu mwenyewe.”
Tnn., “ifungue kinywa chake.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “ikafungua kinywa chake.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “mgeni yeyote.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “mgeni yeyote,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.
Tnn., “mgeni yeyote,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.
Yaani, kila kitu kilichofanywa kuwa kitakatifu kwa Mungu kwa kuwa hakiwezi kukombolewa au kuchukuliwa tena.
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Au “shekeli takatifu.”
Gera moja ilikuwa na uzito wa gramu 0.57. Angalia Nyongeza B14.
Au “inayomtuliza.”
Yaani, agano linalodumu na lisilobadilika.
Au “fungu la.”
Au “nafsi iliyokufa ya mwanadamu yeyote.” Angalia Kamusi.
Maana yake “Kugombana.”
Tnn., “siku nyingi.”
Tnn., “mkono wenye nguvu.”
Tnn., “atakusanywa kwa watu wake.” Huu ni msemo wa kishairi unaorejelea kifo.
Tnn., “atakusanywa na kufia huko.”
Maana yake “Kuangamiza.”
Tnn., “wenye moto.”
Au “makorongo.”
Au “Kiitikieni.”
Au labda, “jangwa; nyika.”
Au “nchini.”
Au “ubashiri.”
Au “nchini.”
Tnn., “akakifungua kinywa cha huyo punda jike.”
Au “anayejuta.”
Au “ubashiri.”
Au labda, “jangwa; nyika.”
Tnn., “lilikuwa jambo jema machoni pa Yehova.”
Au “uzao wake umepandwa.”
Tnn., “kutoka moyoni mwangu.”
Au “nikupe ushauri kuhusu.”
Au “siku za mwisho.”
Tnn., “ataliteketeza Kaini.”
Tnn., “yeye pia ataangamia.”
Au “wakashikamana na.”
Au “juani.”
Au “walioshikamana na.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “ikafungua kinywa chake.”
Au “kulingana na idadi ya majina yaliyoorodheshwa.”
Tnn., “utakusanywa pia kwa watu wako.” Huu ni msemo wa kishairi unaorejelea kifo.
Tnn., “Mungu wa roho za miili yote.”
Au “mtazamo unaofaa.”
Au “heshima.”
Au “mkate wangu.”
Au “inayonituliza.”
Tnn., “katikati ya zile jioni mbili.”
Sehemu ya kumi ya efa ilikuwa sawa na lita 2.2 au kilogramu 1.3 hivi. Angalia Nyongeza B14.
Hini ilikuwa sawa na lita 3.67. Angalia Nyongeza B14.
Au “inayomtuliza.”
Tnn., “katikati ya zile jioni mbili.”
Au “inayomtuliza.”
Tnn., “miezi yenu.”
Au “inayomtuliza.”
Tnn., “mkate.”
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Kwa ujumla inaeleweka kwamba “kujitesa” kunamaanisha kujinyima kwa njia mbalimbali, kutia ndani kufunga.
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Au “akijifunga wajibu.”
Au “Hayo ndiyo masharti ambayo.”
Tnn., “utakusanywa kwa watu wako.” Huu ni msemo wa kishairi unaorejelea kifo.
Au “Tayarisheni jeshi likapigane.”
Au “kambi zao zote zilizozingirwa na kuta.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Angalia Kamusi.
Au “nafsi.”
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “wakajenga upya.”
Maana yake “Vijiji vya Mahema vya Yairi.”
Tnn., “majeshi yao.”
Tnn., “mkono ulioinuliwa.”
Huu ni ufupisho wa Iye-abarimu.
Tnn., “za kuyeyushwa.”
Yaani, Mediterania.
Au “njia ya kuingia Hamathi.”
Yaani, ziwa la Genesareti, au Bahari ya Galilaya.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Mkono mmoja ulilingana na sentimita 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “huku akimvizia.”
Tnn., “bila kumvizia.”
Au “anayeua nafsi.”
Au “nafsi itakayouawa.”
Au “nafsi ya.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu ambayo.”