EZEKIELI
1 Katika mwaka wa 30, siku ya tano ya mwezi wa nne, nilipokuwa kando ya mto Kebari+ miongoni mwa watu waliohamishwa,+ mbingu zilifunguliwa nami nikaanza kuona maono ya Mungu. 2 Katika siku ya tano ya mwezi huo—yaani, katika mwaka wa tano wa uhamisho wa mfalme Yehoyakini+— 3 neno la Yehova lilimjia Ezekieli* mwana wa Buzi kuhani akiwa kando ya mto Kebari katika nchi ya Wakaldayo.+ Na huko, mkono wa Yehova ukaja juu yake.+
4 Nilipokuwa nikitazama, nikaona tufani ya upepo+ ikija kutoka kaskazini, na kulikuwa na wingu kubwa na moto unaowakawaka*+ uliozungukwa na nuru nyangavu, na katikati ya ule moto kulikuwa na kitu kilichong’aa kama mchanganyiko wa dhahabu na fedha.+ 5 Katikati yake kulikuwa na mfano wa viumbe hai wanne,+ na kila mmoja wao alifanana na mwanadamu. 6 Kila mmoja wao alikuwa na nyuso nne na mabawa manne.+ 7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, na nyayo za miguu yao zilikuwa kama nyayo za ndama, nayo ilikuwa iking’aa kama shaba iliyong’arishwa.+ 8 Walikuwa na mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yao pande zote nne, na wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa. 9 Mabawa yao yaligusana. Hawakugeuka walipokuwa wakienda; kila mmoja wao alikuwa akienda mbele moja kwa moja.+
10 Nyuso zao zilionekana hivi: Kila mmoja wa viumbe hao wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na uso wa simba+ upande wa kulia, na uso wa ng’ombe dume+ upande wa kushoto, na kila mmoja wa viumbe hao wanne alikuwa na uso+ wa tai.+ 11 Hivyo ndivyo nyuso zao zilivyokuwa. Mabawa yao yalikuwa yamenyooshwa juu yao. Kila mmoja wao alikuwa na mabawa mawili yaliyogusana na mabawa mawili yaliyofunika miili yao.+
12 Kila mmoja wao alikuwa akienda mbele moja kwa moja, walienda popote ambapo roho iliwaelekeza kwenda.+ Hawakugeuka walipokuwa wakienda. 13 Na wale viumbe hai walionekana kama makaa ya moto yanayowaka, na kitu kilichofanana na mienge ya moto mwangavu kilikuwa kikisonga mbele na nyuma katikati ya hao viumbe hai, na radi ilikuwa ikiwakawaka kutoka katika ule moto.+ 14 Na hao viumbe hai walipoenda na kurudi, mwendo wao ulionekana kama radi inayowakawaka.
15 Nilipoendelea kuwatazama hao viumbe hai, niliona gurudumu moja duniani kando ya kila mmoja wa hao viumbe hai wenye nyuso nne.+ 16 Magurudumu hayo na muundo wake yalionekana yaking’aa kama krisolito, na yote manne yalifanana. Na mwonekano wake na muundo wake ni kama gurudumu lililokuwa ndani ya gurudumu.* 17 Yaliposonga, yangeweza kwenda upande wowote kati ya zile pande nne bila kugeuka yalipokuwa yakienda. 18 Mizingo yake ilikuwa juu sana hivi kwamba iliogopesha, na mizingo ya magurudumu yote manne ilikuwa imejaa macho kuizunguka.+ 19 Wakati wowote viumbe hai waliposonga, yale magurudumu yalisonga pamoja nao, na wale viumbe hai walipoinuliwa kutoka duniani, yale magurudumu yaliinuliwa juu pia.+ 20 Walienda popote ambapo roho iliwaelekeza kwenda, popote roho ilipoenda. Magurudumu yaliinuliwa pamoja nao, kwa maana roho iliyokuwa ikitenda katika wale viumbe hai* ilikuwa pia katika yale magurudumu. 21 Waliposonga, magurudumu hayo yalisonga; na waliposimama tuli, nayo yalisimama tuli; na walipoinuliwa juu kutoka duniani, magurudumu yaliinuliwa juu pamoja nao, kwa maana roho iliyokuwa ikitenda katika wale viumbe hai ilikuwa pia katika yale magurudumu.
22 Juu ya vichwa vya wale viumbe hai kulikuwa na mfano wa anga lililometameta kama barafu inayotisha, lililotanda juu ya vichwa vyao.+ 23 Chini ya anga hilo mabawa yao yalikuwa yamenyooka,* moja kuelekea lingine. Kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ya kufunika upande mmoja wa mwili wake na mawili ya kufunika upande mwingine. 24 Niliposikia sauti ya mabawa yao, ilikuwa kama sauti ya maji yenye kishindo, kama sauti ya Mweza-Yote.+ Waliposonga, ilikuwa kama sauti ya jeshi. Waliposimama tuli, waliyashusha mabawa yao.
25 Kulikuwa na sauti juu ya anga lililokuwa juu ya vichwa vyao. (Waliposimama tuli, waliyashusha mabawa yao.) 26 Juu ya anga lililokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu kilichoonekana kama jiwe la yakuti,+ na kilifanana na kiti cha ufalme.+ Kwenye kiti hicho cha ufalme aliketi mmoja aliyeonekana kama mwanadamu.+ 27 Nami nikaona kitu kinachong’aa kama mchanganyiko wa dhahabu na fedha,+ kilichokuwa kama moto unaong’aa kutoka kwenye kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kwenda juu; na kutoka kwenye kiuno chake kwenda chini, nikaona kitu kilichofanana na moto.+ Kulikuwa na mwangaza mkali kumzunguka pande zote 28 kama wa upinde wa mvua+ katika mawingu siku ya mvua. Hivyo ndivyo mwangaza uliozunguka pande zote ulivyoonekana. Ulikuwa kama mwonekano wa utukufu wa Yehova.+ Nilipouona, nikaanguka chini kifudifudi na kuanza kusikia sauti ya mtu akizungumza.
2 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu,* simama kwa miguu yako ili nizungumze nawe.”+ 2 Alipozungumza nami, roho ikaingia ndani yangu na kunifanya nisimame kwa miguu yangu+ ili niweze kumsikia Yule anayezungumza nami.
3 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, ninakutuma kwa watu wa Israeli,+ kwa mataifa yenye kuasi ambayo yameniasi.+ Wao na mababu zao wamenikosea mpaka leo hii.+ 4 Ninakutuma kwa wana wakaidi* na wenye moyo mgumu,+ nawe lazima uwaambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyosema.’ 5 Nao, iwe watasikiliza au watakataa kusikiliza—kwa maana wao ni nyumba ya uasi+—watajua kwa hakika kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.+
6 “Lakini wewe, mwana wa binadamu, usiwaogope,+ na usiogope maneno yao, ingawa umezungukwa na michongoma na miiba*+ na unakaa katikati ya nge. Usiogope maneno yao+ na usitishwe na nyuso zao,+ kwa maana wao ni nyumba ya uasi. 7 Ni lazima uwaambie maneno yangu, iwe watasikiliza au la, kwa maana wao ni waasi.+
8 “Lakini wewe, mwana wa binadamu, sikiliza ninalokuambia. Usiwe mwasi kama nyumba hii ya uasi. Fungua kinywa chako ule ninachokupa.”+
9 Nilipotazama, niliona mkono ulionyooshwa kunielekea,+ na katika mkono huo niliona kitabu cha kukunjwa kilichoandikwa.+ 10 Alipokikunjua mbele yangu, kilikuwa kimeandikwa mbele na nyuma.+ Nyimbo za huzuni na maombolezo na vilio vilikuwa vimeandikwa kwenye kitabu hicho.+
3 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, kula kilicho mbele yako.* Kula kitabu hiki cha kukunjwa, na uende ukazungumze na watu wa nyumba ya Israeli.”+
2 Kwa hiyo nikafungua kinywa changu, naye akanipa kitabu hicho nile. 3 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, kula kitabu hiki ninachokupa, ukijaze tumboni mwako.” Basi nikaanza kukila, nacho kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu.+
4 Akaniambia: “Mwana wa binadamu, nenda miongoni mwa watu wa nyumba ya Israeli uwaambie maneno yangu. 5 Kwa maana hutumwi kwenda kwa watu wanaozungumza lugha isiyoeleweka au lugha isiyojulikana, bali kwa watu wa nyumba ya Israeli. 6 Hutumwi kwa watu wengi wanaozungumza lugha isiyoeleweka au lugha isiyojulikana, ambao maneno yao huwezi kuelewa. Ikiwa ningekutuma kwao, wangekusikiliza.+ 7 Lakini watu wa nyumba ya Israeli watakataa kukusikiliza, kwa maana hawataki kunisikiliza mimi.+ Watu wote wa nyumba ya Israeli wana vichwa vigumu na mioyo migumu.+ 8 Tazama! Nimeufanya uso wako uwe mgumu kama nyuso zao na paji la uso wako liwe gumu kama mapaji ya nyuso zao.+ 9 Nimelifanya paji la uso wako kuwa kama almasi, gumu kuliko jiwe gumu.+ Usiwaogope, wala usitishwe na nyuso zao,+ kwa maana wao ni nyumba ya uasi.”
10 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, yatie moyoni mwako na kuyasikiliza maneno yangu yote nitakayokuambia. 11 Nenda miongoni mwa watu wako waliohamishwa*+ uzungumze nao. Waambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyosema,’ iwe watasikiliza au watakataa kusikiliza.”+
12 Ndipo roho ikanibeba+ nami nikasikia nyuma yangu sauti ya mngurumo mkubwa iliyosema: “Utukufu wa Yehova na usifiwe katika mahali pake.” 13 Nilisikia sauti ya mabawa ya wale viumbe hai yalipokuwa yakigusana,+ na sauti ya magurudumu kando yao,+ na sauti ya mngurumo mkubwa. 14 Nayo roho ikanibeba na kunichukua, nami nikaenda kwa uchungu na kwa ghadhabu ya roho yangu, na mkono wa Yehova ukatulia juu yangu kwa nguvu. 15 Basi nikaenda Tel-abibu kwa watu waliohamishwa, waliokuwa wakikaa kando ya mto Kebari,+ nami nikakaa huko walipokuwa wakikaa; nikakaa miongoni mwao kwa siku saba nikiwa nimepigwa na bumbuazi.+
16 Mwishoni mwa siku saba neno la Yehova likanijia:
17 “Mwana wa binadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa watu wa nyumba ya Israeli;+ nawe unaposikia neno kutoka katika kinywa changu, lazima uwape onyo langu.+ 18 Ninapomwambia mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’ lakini wewe usimwonye, nawe ukatae kumwambia mtu huyo mwovu aiache njia yake ya uovu ili aendelee kuwa hai,+ yeye atakufa kwa sababu ya kosa lake kwa sababu yeye ni mwovu,+ lakini damu yake nitaidai kutoka kwako.*+ 19 Lakini ukimwonya mtu mwovu naye asiuache uovu wake na njia yake ya uovu, yeye atakufa kwa sababu ya kosa lake, lakini wewe kwa hakika utauokoa uhai wako.*+ 20 Lakini mtu mwadilifu anapoacha uadilifu wake na kutenda kosa,* nitaweka kikwazo mbele yake, naye atakufa.+ Ikiwa hukumwonya, atakufa kwa sababu ya dhambi yake na matendo yake ya uadilifu hayatakumbukwa, lakini damu yake nitaidai kutoka kwako.*+ 21 Lakini ikiwa umemwonya mtu mwadilifu asitende dhambi, naye asitende dhambi, kwa hakika ataendelea kuwa hai kwa sababu alionywa,+ na wewe utauokoa uhai wako.”*
22 Nikiwa huko mkono wa Yehova ukanijia, naye akaniambia: “Ondoka, nenda kwenye bonde tambarare, nami nitazungumza nawe huko.” 23 Basi nikaondoka na kwenda kwenye bonde tambarare, na tazama! utukufu wa Yehova ulikuwa huko,+ kama utukufu niliokuwa nimeuona kando ya mto Kebari,+ nami nikaanguka chini kifudifudi. 24 Kisha roho ikaingia ndani yangu na kunifanya nisimame kwa miguu yangu,+ naye akaniambia:
“Nenda, jifungie ndani ya nyumba yako. 25 Lakini wewe mwana wa binadamu, wataweka kamba juu yako na kukufunga nazo ili usiweze kuondoka miongoni mwao. 26 Nami nitaufanya ulimi wako ushikamane na kaakaa la kinywa chako, nawe utakuwa bubu, usiweze kuwakaripia, kwa sababu wao ni nyumba ya uasi. 27 Lakini ninapozungumza nawe nitafungua kinywa chako, nawe lazima uwaambie,+ ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyosema.’ Anayesikiliza na asikilize,+ na anayekataa kusikiliza na akatae, kwa sababu wao ni nyumba ya uasi.+
4 “Na wewe, mwana wa binadamu, chukua tofali na uliweke mbele yako. Uchonge jiji juu yake—Yerusalemu. 2 Lizingire na ujenge ukuta wa kulizingira,+ utengeneze boma la kulizingira,+ upige kambi kulizunguka,+ na kulizungushia mitambo ya kubomolea.+ 3 Chukua kiokeo cha chuma, na ukiweke kuwa ukuta wa chuma kati yako na jiji hilo. Kisha ukaze uso wako dhidi yake, nalo litazingirwa; nawe utalizingira. Hiyo ni ishara kwa watu wa nyumba ya Israeli.+
4 “Kisha ulalie upande wako wa kushoto na uweke hatia ya watu wa nyumba ya Israeli juu yako.*+ Utabeba hatia yao kwa idadi ya siku utakazolalia upande wako wa kushoto. 5 Na mimi nitakupa wewe siku 390, zinazolingana na miaka ya hatia yao,+ nawe utaibeba hatia ya watu wa nyumba ya Israeli. 6 Nawe lazima uzitimize.
“Kisha kwa mara ya pili utalala chini, utalalia upande wako wa kulia, nawe utaibeba hatia ya watu wa nyumba ya Yuda+ kwa siku 40. Nimekupa wewe siku moja kwa mwaka mmoja, siku moja kwa mwaka mmoja. 7 Nawe utauelekeza uso wako kwa jiji la Yerusalemu lililozingirwa,+ mkono wako ukiwa wazi, nawe utatabiri dhidi ya jiji hilo.
8 “Tazama! Nitakufunga kwa kamba ili usiweze kugeuka kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine, mpaka utakapotimiza siku zako za kulizingira.
9 “Na uchukue ngano, shayiri, maharagwe mapana, dengu, mtama, na kusemethi, nawe uvitie katika chombo kimoja na ujitengenezee mkate. Kwa idadi ya siku unazolalia upande wako, siku 390, utaula.+ 10 Utapima na kula shekeli 20* za chakula kwa siku. Utaula nyakati hususa.
11 “Na utakunywa maji kwa kipimo, sehemu ya sita ya hini.* Utayanywa nyakati hususa.
12 “Utaula kama ambavyo ungekula mkate wa mviringo wa shayiri; utauoka mbele ya macho yao, ukitumia mavi ya wanadamu yaliyokauka.” 13 Na Yehova akaendelea kusema: “Hivyo ndivyo Waisraeli watakavyoula mkate wao—usio safi—kati ya mataifa ambako nitawatawanya.”+
14 Ndipo nikasema: “Isiwe hivyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tangu ujana wangu mpaka sasa sijatiwa* unajisi kwa kula nyama ya mnyama ambaye amepatikana amekufa wala mnyama aliyeraruliwa,+ na nyama isiyo safi* haijawahi kuingia kinywani mwangu.”+
15 Basi akaniambia: “Sawa, nitakuruhusu utumie mavi ya ng’ombe badala ya mavi ya wanadamu, nawe utaoka mkate wako juu yake.” 16 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, nitafanya chakula kikosekane* Yerusalemu,+ na kwa wasiwasi mwingi watakula mkate wao kwa kipimo,+ na kwa hofu nyingi watakunywa maji yao kwa kipimo.+ 17 Hili litatukia ili wakose mkate na maji, nao waangaliane kwa mshtuko na kudhoofika kwa sababu ya kosa lao.
5 “Lakini wewe, mwana wa binadamu, chukua upanga mkali ili uutumie kama wembe wa kinyozi. Nyoa kichwa chako na ndevu zako, nawe uchukue mizani, uzipime nywele hizo na kuzigawa katika mafungu. 2 Utaiteketeza theluthi moja ya nywele hizo katika moto ndani ya jiji siku za kuzingira zitakapokamilika.+ Kisha utachukua theluthi nyingine nawe utaipiga kwa upanga kulizunguka jiji pande zote,+ na theluthi ya mwisho utaitawanya kwenye upepo, nami nitauchomoa upanga ili kuwakimbiza.+
3 “Pia utachukua nywele chache na kuzifunga katika pindo za* vazi lako. 4 Na uchukue nyingine na kuzitupa motoni na kuziteketeza. Moto utatokea humo na kuenea katika nyumba yote ya Israeli.+
5 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Huyu ni Yerusalemu. Nimemweka katikati ya mataifa, na nchi zinamzunguka pande zote. 6 Lakini aliasi sheria zangu* na amri zangu, akatenda uovu zaidi kuliko mataifa na nchi zinazomzunguka pande zote.+ Kwa maana wamekataa sheria zangu, nao hawakutembea katika amri zangu.’
7 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu mlikuwa wasumbufu kuliko mataifa yote yanayowazunguka na hamkutembea katika amri zangu au kutenda kulingana na sheria zangu, badala yake mkafuata sheria za mataifa yanayowazunguka pande zote,+ 8 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Sasa niko dhidi yako, Ee jiji,+ na mimi mwenyewe nitatekeleza hukumu katikati yako mbele ya mataifa.+ 9 Nami nitafanya ndani yako mambo ambayo sijawahi kufanya, na ambayo sitafanya tena kwa sababu ya mazoea yako yote yanayochukiza.+
10 “‘“Kwa hiyo akina baba miongoni mwenu watawala wana wao,+ nao wana watawala baba zao, nami nitatekeleza hukumu kati yenu na kuwatawanya kila upande* wale waliobaki kati yenu.”’+
11 “‘Kwa hiyo, kwa hakika, kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘kwa sababu mlipachafua mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu zote zinazochukiza na mazoea yenu yote yanayochukiza,+ mimi pia nitawakataa;* jicho langu halitasikitika, nami sitawahurumia.+ 12 Theluthi yenu moja watakufa kwa ugonjwa hatari au kuangamia kwa njaa kali miongoni mwenu. Na theluthi nyingine watauawa kwa upanga kuwazunguka pande zote.+ Nami nitaitawanya theluthi ya mwisho kila upande,* nami nitauchomoa upanga ili kuwakimbiza.+ 13 Ndipo hasira yangu itakapokoma, na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitaridhika.+ Nitakapomaliza kuwamwagia ghadhabu yangu, watalazimika kujua kwamba mimi, Yehova, ninasisitiza watu waniabudu mimi peke yangu.+
14 “‘Nitakufanya kuwa ukiwa na kitu cha kushutumiwa kati ya mataifa yanayokuzunguka na mbele ya macho ya kila mpita njia.+ 15 Utakuwa kitu cha kushutumiwa na kudharauliwa,+ mfano wa kuonya na tisho kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapotekeleza hukumu dhidi yako kwa hasira na ghadhabu na kwa adhabu kali. Mimi, Yehova, nimesema.
16 “‘Nitawaletea mishale hatari ya njaa kali ili iwaangamize.+ Mishale nitakayowaletea itawaangamiza ninyi. Nitaifanya njaa iwe kali zaidi kwenu kwa kufanya chakula chenu kisipatikane.*+ 17 Nitawaletea njaa kali na wanyama wakali wa mwituni,+ nao watawaua watoto wenu. Ugonjwa hatari na umwagaji wa damu utawalemea, nami nitaleta upanga dhidi yenu.+ Mimi, Yehova, nimesema.’”
6 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako kwenye milima ya Israeli na utabiri dhidi yake. 3 Nawe utasema, ‘enyi milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyoiambia milima, vilima, vijito na mabonde: “Tazameni! Ninaleta upanga dhidi yenu, nami nitaharibu mahali penu pa juu. 4 Madhabahu zenu zitabomolewa na vinara vyenu vya uvumba vitavunjwa,+ na waliouawa kati yenu nitawatupa chini mbele ya sanamu zenu zinazochukiza.*+ 5 Nami nitazitupa maiti za watu wa Israeli mbele ya sanamu zao zinazochukiza, nami nitaitawanya mifupa yenu kuzunguka pande zote za madhabahu zenu.+ 6 Katika makao yenu yote, majiji yataharibiwa+ na mahali pa juu patabomolewa na kuachwa ukiwa.+ Madhabahu zenu zitaharibiwa na kuvunjwa vipandevipande, sanamu zenu zinazochukiza zitaharibiwa, vinara vyenu vya uvumba vitakatwakatwa, na kazi zenu zitafutiliwa mbali. 7 Na wale waliouawa wataanguka katikati yenu,+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+
8 “‘“Lakini nitaacha wengine wabaki, kwa maana baadhi yenu wataponyoka upanga miongoni mwa mataifa mtakapotawanywa katika nchi mbalimbali.+ 9 Na wale watakaoponyoka watanikumbuka kati ya mataifa ambamo watapelekwa mateka.+ Watatambua kwamba nilikuwa nimevunjika moyo kwa sababu ya moyo wao usio na uaminifu* ulioniacha+ na macho yao ambayo yanatamani sana* sanamu zao zinazochukiza.+ Wataaibika na kuchukizwa na mambo yote maovu na yenye kuchukiza ambayo wametenda.+ 10 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova na kwamba vitisho vyangu vya kuwaletea msiba huu havikuwa vya bure.”’+
11 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Piga makofi na upige mguu chini, na uomboleze kwa sababu ya mambo yote maovu na yanayochukiza yaliyofanywa na watu wa nyumba ya Israeli, kwa maana watakufa kwa upanga, kwa njaa kali na kwa ugonjwa hatari.+ 12 Yule aliye mbali sana atakufa kwa ugonjwa hatari, na yule aliye karibu atauawa kwa upanga, na yeyote anayeponyoka mambo hayo na kubaki atakufa kwa njaa kali; nami nitawamwagia kikamili ghadhabu yangu.+ 13 Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova+ wakati waliouawa miongoni mwao watakapotapakaa kati ya sanamu zao zinazochukiza kuzunguka pande zote za madhabahu zao,+ juu ya kila kilima kirefu, juu ya vilele vyote vya milima, na chini ya kila mti wenye majani mengi, na chini ya matawi ya miti mikubwa, mahali ambapo wametoa dhabihu zenye harufu nzuri* ili kuzituliza sanamu zao zote zinazochukiza.+ 14 Nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yao na kuifanya nchi iwe ukiwa, na makao yao yote yatakuwa ukiwa kuliko nyika iliyo karibu na Dibla. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”
7 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Nawe Mwana wa binadamu, hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyoiambia nchi ya Israeli: ‘Mwisho! Mwisho umezifikia pembe nne za nchi. 3 Sasa mwisho umekufikia, nami nitakumwagia hasira yangu, nami nitakuhukumu kulingana na njia zako na kukuadhibu* kwa sababu ya matendo yako yote yanayochukiza. 4 Jicho langu halitakusikitikia; wala sitakuhurumia,+ kwa maana nitakuletea matokeo ya njia zako mwenyewe, nawe utapatwa na madhara ya matendo yako yanayochukiza.+ Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+
5 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Tazama! Msiba, msiba wa pekee, unakuja.+ 6 Mwisho unakuja; mwisho utakuja; utainuka* wenyewe dhidi yako. Tazama! Unakuja. 7 Zamu yako imefika,* wewe unayekaa nchini. Wakati unakuja, siku hiyo iko karibu.+ Kuna vurugu, wala si kelele za shangwe milimani.
8 “‘Hivi karibuni nitakumwagia ghadhabu yangu,+ nami nitakumwagia hasira yangu yote,+ nami nitakuhukumu kulingana na njia zako na kukuadhibu* kwa sababu ya matendo yako yote yanayochukiza. 9 Jicho langu halitakusikitikia; wala sitakuhurumia.+ Kwa maana nitakuletea matokeo ya njia zako mwenyewe, nawe utapatwa na madhara ya matendo yako mwenyewe yanayochukiza. Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi, Yehova, ndiye ninayewapiga.+
10 “‘Tazama, ile siku! Tazama, inakuja!+ Zamu yako imefika;* fimbo imechanua na kimbelembele kimechipuka. 11 Ukatili umesitawi na kuwa fimbo ya uovu.+ Wao wenyewe, mali yao, umati wao, wala umashuhuri wao hautaokoka. 12 Wakati utakuja, siku hiyo itafika. Mnunuzi asishangilie, na muuzaji asiomboleze, kwa maana kuna ghadhabu dhidi ya umati wao wote.*+ 13 Kwa maana muuzaji hatakirudia kitu alichouza, hata uhai wake ukiokolewa, kwa maana maono hayo yanahusu umati wote. Hakuna atakayerudi, na kwa sababu ya kosa lake,* hakuna atakayeokoa uhai wake.
14 “‘Wamepiga tarumbeta+ na kila mtu yuko tayari, lakini hakuna anayeenda vitani, kwa sababu nina ghadhabu dhidi ya umati wote.+ 15 Upanga uko nje,+ na ugonjwa hatari na njaa kali zimo ndani. Yeyote aliye uwanjani atakufa kwa upanga, na njaa kali na ugonjwa hatari vitawameza wale walio jijini.+ 16 Watu wao watakaofanikiwa kuponyoka wataenda milimani, na kama njiwa wa mabondeni, kila mmoja ataomboleza kwa sababu ya kosa lake.+ 17 Mikono yao yote italegea, na magoti yao yote yatadondosha maji.*+ 18 Wamevaa nguo za magunia,+ nao wanatetemeka.* Kila mtu ataaibishwa, na kila kichwa kitakuwa na upara.*+
19 “‘Watatupa fedha yao barabarani, nayo dhahabu yao itawachukiza. Wala fedha yao wala dhahabu yao haitaweza kuwaokoa katika siku ya ghadhabu ya Yehova.+ Hawatashiba,* wala kuyajaza matumbo yao, kwa maana vitu hivyo* vimekuwa kikwazo kinachosababisha kosa lao. 20 Walijivunia urembo wa mapambo yao, nao wakayatumia* kutengeneza mifano yao inayochukiza, sanamu zao zinazochukiza.+ Ndiyo sababu nitaifanya fedha na dhahabu yao kuwa chukizo kwao. 21 Nami nitaitia* mikononi mwa wageni ili waipore na kuwapa waovu wa dunia kuwa nyara, nao wataitia unajisi.
22 “‘Nami nitaugeuza uso wangu kutoka kwao,+ nao watapatia unajisi mahali pangu palipofichika,* na wanyang’anyi wataingia mahali hapo na kupatia unajisi.+
23 “‘Tengeneza mnyororo,*+ kwa maana nchi imejaa hukumu yenye madoa ya damu+ na jiji limejaa ukatili.+ 24 Nami nitaingiza mataifa mabaya kabisa,+ nayo yatamiliki nyumba zao,+ nami nitakikomesha kiburi cha wenye nguvu, na mahali pao patakatifu patatiwa unajisi.+ 25 Maumivu yao yatakapokuja, watatafuta amani lakini haitakuwepo.+ 26 Msiba utakuja juu ya msiba, na habari baada ya habari, na watu watatafuta maono kutoka kwa nabii,+ lakini sheria itatoweka* kutoka kwa kuhani na ushauri* kutoka kwa wazee.+ 27 Mfalme ataomboleza,+ naye mkuu atavaa kukata tamaa,* na mikono ya watu wa nchi itatetemeka kwa hofu. Nitawatendea kulingana na njia zao, nami nitawahukumu kama walivyohukumu. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”+
8 Na katika mwaka wa sita, mwezi wa sita, siku ya tano ya mwezi huo, nilipokuwa nimeketi nyumbani mwangu na wazee wa Yuda walipokuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ulinishika nikiwa hapo. 2 Nilipokuwa nikitazama, niliona umbo lililoonekana kama moto; kulikuwa na moto chini ya kitu kilichoonekana kama kiuno chake,+ na kuanzia kiuno chake kwenda juu, mwonekano wake uling’aa kama mchanganyiko wa dhahabu na fedha.+ 3 Kisha akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono na kuniinua kwa kishungi cha nywele za kichwa changu, na roho ikanibeba katikati ya dunia na mbingu na kunileta Yerusalemu kupitia maono kutoka kwa Mungu, kwenye njia inayoelekea kwenye lango la ndani+ linalotazama kaskazini, mahali ilipokuwa ishara ya* ibada ya sanamu inayochochea wivu.+ 4 Na tazama! utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa hapo,+ kama mwonekano niliokuwa nimeuona katika bonde tambarare.+
5 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, tafadhali inua macho yako kuelekea kaskazini.” Basi nikainua macho yangu kuelekea kaskazini, na huko, upande wa kaskazini wa lango la madhabahu kulikuwa na ishara hii ya* wivu langoni. 6 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, je, unaona mambo mabaya sana na yenye kuchukiza ambayo watu wa nyumba ya Israeli wanafanya hapa,+ mambo yanayonifanya niende mbali sana na mahali pangu patakatifu?+ Lakini utaona mambo yanayochukiza yaliyo mabaya hata zaidi.”
7 Kisha akanileta kwenye mlango wa ua, nami nilipotazama, niliona tundu ukutani. 8 Akaniambia: “Mwana wa binadamu, tafadhali toboa ukuta.” Nami nikautoboa ukuta na kuona mlango. 9 Akaniambia: “Ingia ndani uone mambo maovu na yenye kuchukiza wanayofanya hapa.” 10 Basi nikaingia na kutazama, nikaona mifano mbalimbali ya viumbe wanaotambaa na wanyama wanaochukiza+ na sanamu zote zinazochukiza* za watu wa nyumba ya Israeli;+ zilikuwa zimechongwa ukutani kuzunguka pande zote. 11 Na wazee 70 wa nyumba ya Israeli walikuwa wamesimama mbele ya vitu hivyo, naye Yaazania mwana wa Shafani+ alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja wao alikuwa na chetezo chake mkononi mwake, na wingu la uvumba lenye manukato lilikuwa likipanda juu.+ 12 Akaniambia: “Mwana wa binadamu, je, umeona mambo ambayo wazee wa nyumba ya Israeli wanafanya gizani, kila mmoja akiwa katika vyumba vya ndani ambamo sanamu zake za kuchongwa zimewekwa ili zionekane?* Kwa maana wanasema, ‘Yehova hatuoni. Yehova ameiacha nchi hii.’”+
13 Naye akaendelea kuniambia: “Utaona mambo yanayochukiza yaliyo mabaya hata zaidi ambayo wanafanya.” 14 Basi akanileta kwenye njia inayoelekea kwenye lango la kaskazini la nyumba ya Yehova, na huko nikaona wanawake wameketi wakimlilia mungu Tamuzi.
15 Naye akaendelea kuniambia: “Je, unaona mambo haya, ewe mwana wa binadamu? Utaona mambo yanayochukiza ambayo ni mabaya hata zaidi kuliko haya.”+ 16 Basi akanileta katika ua wa ndani wa nyumba ya Yehova.+ Hapo kwenye mlango wa hekalu la Yehova, katikati ya ukumbi na madhabahu, kulikuwa na wanaume 25 hivi ambao migongo yao ilielekea hekalu la Yehova na nyuso zao zilitazama mashariki; nao walikuwa wakiliinamia jua kuelekea mashariki.+
17 Akaniambia: “Mwana wa binadamu, je, unaona hili? Je, ni jambo dogo sana kwa watu wa nyumba ya Yuda kufanya mambo haya yanayochukiza, kuijaza nchi ukatili+ na kuendelea kunikasirisha? Tazama, wanaidunga pua yangu kwa lile tawi.* 18 Basi nitatenda kwa ghadhabu. Jicho langu halitasikitika; wala sitawahurumia.+ Hata wakilia kwa sauti kubwa masikioni mwangu, sitawasikia.”+
9 Kisha nikamsikia akisema hivi kwa sauti kubwa: “Waiteni wale watakaoliadhibu jiji hili, kila mmoja wao akiwa na silaha yake ya kuangamiza mkononi mwake!”
2 Nikaona wanaume sita wakija kutoka upande wa lango la juu+ linalotazama kaskazini, kila mmoja akiwa na silaha yake ya kuponda mkononi mwake; na kulikuwa na mwanamume mmoja kati yao aliyevaa kitani, akiwa na kidau cha wino cha mwandishi kiunoni,* nao wakaingia ndani na kusimama kando ya madhabahu ya shaba.+
3 Kisha utukufu wa Mungu wa Israeli+ ukainuka kutoka mahali ulipokuwa umetulia juu ya makerubi na kwenda kwenye kizingiti cha mlango wa nyumba hiyo,+ naye akaanza kumwita kwa sauti yule mwanamume aliyevaa kitani, ambaye alikuwa na kidau cha wino cha mwandishi kiunoni. 4 Yehova akamwambia: “Pita kotekote jijini, katika jiji lote la Yerusalemu, nawe uyatie alama mapaji ya nyuso za watu wanaolia kwa uchungu na kwa maumivu makali+ kwa sababu ya mambo yote yanayochukiza yanayofanywa jijini.”+
5 Naye akawaambia wale wengine huku nikisikia: “Piteni kotekote jijini baada yake na kuua. Jicho lenu lisisikitike, wala msiwe na huruma hata kidogo.+ 6 Mnapaswa kuwaua wote kabisa, mzee, kijana, bikira, mtoto mdogo, na wanawake.+ Lakini msimkaribie mtu yeyote aliye na ile alama.+ Mnapaswa kuanzia mahali pangu patakatifu.”+ Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya ile nyumba.+ 7 Kisha akawaambia: “Itieni nyumba unajisi na kuzijaza nyua wale waliouawa.+ Nendeni!” Basi wakaenda na kuwaua watu jijini.
8 Walipokuwa wakiwaua, nilibaki mimi peke yangu, nikaanguka kifudifudi na kupaza sauti: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Je, utawaangamiza Waisraeli wote wanaobaki unapolimwagia ghadhabu yako jiji la Yerusalemu?”+
9 Basi akaniambia: “Kosa la watu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni kubwa sana, kubwa kwelikweli.+ Nchi imejaa umwagaji wa damu,+ nalo jiji limejaa ufisadi.+ Kwa maana wanasema, ‘Yehova ameiacha nchi hii, na Yehova haoni.’+ 10 Lakini mimi, jicho langu halitasikitika; wala sitawahurumia.+ Nitawaletea madhara ya njia yao juu ya kichwa chao wenyewe.”
11 Ndipo nikamwona yule mwanamume aliyevaa kitani, ambaye alikuwa na kidau cha wino kiunoni, akirudi na kuleta habari akisema: “Nimefanya kama ulivyoniamuru.”
10 Nilipokuwa nikitazama, niliona juu ya anga lililokuwa juu ya vichwa vya makerubi kitu kama jiwe la yakuti kikitokea juu yao, nacho kilifanana na kiti cha ufalme.+ 2 Kisha akamwambia yule mwanamume aliyevaa kitani:+ “Ingia katikati ya magurudumu yanayozunguka,+ chini ya makerubi, na ujaze mikono yako miwili makaa yanayowaka+ kutoka katikati ya makerubi na kuyarusha juu ya jiji.”+ Basi akaingia huku nikitazama.
3 Makerubi walikuwa wamesimama upande wa kulia wa ile nyumba mwanamume huyo alipoingia, nalo wingu likajaa katika ua wa ndani. 4 Na utukufu wa Yehova+ ukainuka kutoka kwa makerubi mpaka kwenye kizingiti cha mlango wa nyumba hiyo, na hatua kwa hatua nyumba hiyo ikajaa wingu,+ na ua ulikuwa umejaa mwangaza wa utukufu wa Yehova. 5 Na sauti ya mabawa ya makerubi ilisikika katika ua wa nje, kama sauti ya Mungu Mweza-Yote anapozungumza.+
6 Kisha akamwamuru hivi yule mwanamume aliyevaa kitani: “Chukua moto kutoka katikati ya magurudumu yanayozunguka, kutoka katikati ya makerubi,” naye akaingia na kusimama kando ya gurudumu. 7 Kisha mmoja wa makerubi akaunyoosha mkono wake kuelekea moto uliokuwa katikati ya makerubi.+ Akachukua kiasi fulani na kukiweka kwenye mikono miwili ya yule aliyevaa kitani,+ naye akauchukua na kwenda nje. 8 Makerubi walikuwa na kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yao.+
9 Nilipokuwa nikitazama, niliona magurudumu manne kando ya makerubi, gurudumu moja kando ya kila kerubi, na magurudumu hayo yalionekana yaking’aa kama jiwe la krisolito.+ 10 Kuhusu mwonekano wake, yote manne yalifanana, yalionekana kama gurudumu moja likiwa katikati ya gurudumu lingine. 11 Yaliposonga, yaliweza kwenda upande wowote kati ya zile pande nne bila kugeuka, kwa maana yalikuwa yakienda upande ambao kichwa kilitazama nayo yalienda bila kugeuka. 12 Miili yao yote, migongo yao, mikono yao, mabawa yao, na yale magurudumu, magurudumu ya wote wanne, yalijaa macho kila mahali.+ 13 Kuhusu yale magurudumu, nilisikia sauti ikiyaita, “Magurudumu yanayozunguka!”
14 Kila mmoja wao* alikuwa na nyuso nne. Uso wa kwanza ulikuwa uso wa kerubi, uso wa pili ulikuwa uso wa mwanadamu, wa tatu ulikuwa uso wa simba, na wa nne ulikuwa uso wa tai.+
15 Na wale makerubi walikuwa wakiinuka—walikuwa viumbe hai walewale niliowaona* kwenye mto Kebari+— 16 na wale makerubi waliposonga, magurudumu yalikuwa yakisonga kando yao; na wale makerubi walipoinua juu mabawa yao ili yawe juu sana ya dunia, magurudumu hayo hayakuwa yakigeuka au kuondoka kando yao.+ 17 Waliposimama tuli, nayo yalisimama tuli; nao walipoinuka, yaliinuka pamoja nao, kwa maana roho iliyokuwa ikitenda katika wale viumbe hai* ilikuwa ndani ya magurudumu.
18 Kisha utukufu wa Yehova+ ukaondoka kwenye kizingiti cha mlango wa nyumba na kusimama tuli juu ya makerubi.+ 19 Sasa makerubi wakainua juu mabawa yao na kuinuka kutoka duniani huku nikitazama. Yale magurudumu pia yalikuwa kando yao walipoondoka. Wakasimama katika kizingiti cha lango la mashariki la nyumba ya Yehova, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.+
20 Hao ndio viumbe hai niliokuwa* nimeona chini ya Mungu wa Israeli kwenye mto Kebari,+ basi nikajua kwamba walikuwa makerubi. 21 Wote wanne walikuwa na nyuso nne, mabawa manne, na kitu kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yao.+ 22 Na nyuso zao zilikuwa kama nyuso nilizokuwa nimeona kando ya mto Kebari.+ Kila mmoja wao alikuwa akienda mbele moja kwa moja.+
11 Na roho ikaniinua juu na kunileta kwenye lango la mashariki la nyumba ya Yehova, lango linalotazama mashariki.+ Hapo langoni niliona wanaume 25, na miongoni mwao kulikuwa na Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, wakuu wa watu.+ 2 Kisha Yeye akaniambia: “Mwana wa binadamu, hawa ndio wanaume wanaopanga uovu na kutoa ushauri wa uovu katika* jiji hili. 3 Wanasema, ‘Je, huu si wakati wa kujenga nyumba?+ Jiji* ni chungu cha kupikia,*+ na sisi ni nyama.’
4 “Basi tabiri dhidi yao. Tabiri, mwana wa binadamu.”+
5 Ndipo roho ya Yehova ikaja juu yangu,+ naye akaniambia: “Waambie, ‘Yehova anasema hivi: “Mambo mliyosema ni sahihi, enyi watu wa nyumba ya Israeli, nami ninajua mnachofikiria.* 6 Mmewafanya wengi wafe katika jiji hili, nanyi mmezijaza barabara zake watu waliokufa.”’”+ 7 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Maiti mlizotawanya jijini ndizo nyama, nalo jiji ni chungu cha kupikia.+ Lakini ninyi wenyewe mtatolewa ndani yake.’”
8 “‘Mmeuogopa upanga,+ nami nitauleta upanga dhidi yenu,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 9 ‘Nitawatoa ninyi ndani yake na kuwatia mikononi mwa watu wa nchi ya kigeni na kutekeleza hukumu dhidi yenu.+ 10 Mtauawa kwa upanga.+ Nitawahukumu kwenye mpaka wa Israeli,+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 11 Jiji halitakuwa chungu chenu cha kupikia, nanyi hamtakuwa nyama iliyo ndani yake; nitawahukumu ninyi kwenye mpaka wa Israeli, 12 nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova. Kwa maana hamkutembea katika masharti yangu wala kutenda hukumu zangu,+ bali mmetenda kulingana na hukumu za mataifa yanayowazunguka.’”+
13 Mara tu nilipotabiri, Pelatia mwana wa Benaya akafa, nami nikaanguka chini kifudifudi na kulia kwa sauti: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Je, utawaangamiza Waisraeli wanaobaki?”+
14 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 15 “Mwana wa binadamu, ndugu zako, ndugu zako walio na haki ya kukomboa, pamoja na watu wote wa nyumba ya Israeli, wameambiwa na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Msimkaribie Yehova. Nchi ni yetu; tumepewa ili tuimiliki.’ 16 Kwa hiyo waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ingawa nimewapeleka mbali sana miongoni mwa mataifa, nami nimewatawanya katika nchi hizo,+ baada ya muda mfupi nitakuwa kwao mahali patakatifu katika nchi ambazo wameenda.”’+
17 “Kwa hiyo waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Pia nitawakusanya ninyi kutoka kwa mataifa na kuwakusanya kutoka katika nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawapa nchi ya Israeli.+ 18 Nao watarudi huko na kuondoa humo vitu vyote vinavyochukiza na mazoea yote yanayochukiza.+ 19 Nami nitawapa moyo wenye umoja,*+ nami nitatia roho mpya ndani yao;+ nami nitauondoa moyo wa jiwe katika miili yao+ na kuwapa moyo wa nyama,*+ 20 ili watembee katika sheria zangu na kushika hukumu zangu na kuzitii. Kisha watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.”’
21 “‘“Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeazimia kuendelea kufanya mambo yao yanayochukiza na mazoea yao yanayochukiza, nitawaletea madhara ya njia yao juu ya kichwa chao,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’”
22 Sasa wale makerubi wakayainua juu mabawa yao, na yale magurudumu yalikuwa karibu nao,+ na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.+ 23 Kisha utukufu wa Yehova+ ukapanda kutoka jijini ukasimama juu ya mlima ulio upande wa mashariki wa jiji hilo.+ 24 Kisha roho ikaniinua juu—katika maono kupitia roho ya Mungu—na kunileta kwa watu walio uhamishoni huko Ukaldayo. Kisha maono niliyokuwa nimeyaona yakatoweka. 25 Nami nikaanza kuwaambia watu walio uhamishoni mambo yote ambayo Yehova alikuwa amenionyesha.
12 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, unaishi katika nyumba ya uasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni, na masikio ya kusikia, lakini hawasikii,+ kwa maana wao ni nyumba ya uasi.+ 3 Nawe, mwana wa binadamu, jitayarishie mizigo ya kwenda uhamishoni. Kisha, mchana wakiwa wanatazama, unapaswa kwenda uhamishoni. Toka nyumbani kwako uende uhamishoni mahali pengine huku wakitazama. Labda wataona, ingawa wao ni nyumba ya uasi. 4 Wakati wa mchana toa mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni huku wakitazama, kisha jioni huku wakitazama, uondoke kama mtu anayepelekwa uhamishoni.+
5 “Toboa shimo ukutani huku wakitazama, nawe ubebe mizigo yako na kupitia humo.+ 6 Beba mizigo yako begani huku wakikutazama, nawe uende nayo gizani. Ufunike uso wako ili usiweze kuona chini, kwa maana ninakufanya uwe ishara kwa watu wa nyumba ya Israeli.”+
7 Nikafanya kama nilivyoamriwa. Nikaitoa mizigo yangu nje mchana kama mizigo ya kwenda uhamishoni, na jioni nikatoboa shimo ukutani kwa mkono. Na kulipokuwa na giza, nikachukua mizigo yangu, nikaibeba begani mbele ya macho yao.
8 Asubuhi neno la Yehova likanijia tena likisema: 9 “Mwana wa binadamu, je, watu wa nyumba ya Israeli, nyumba ya uasi, hawakukuuliza, ‘Unafanya nini?’ 10 Waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tangazo hili linamhusu mkuu+ huko Yerusalemu na watu wote wa nyumba ya Israeli walio jijini.”’
11 “Waambie, ‘Mimi ni ishara kwenu.+ Kama vile nilivyotenda, ndivyo watakavyotendewa. Watapelekwa uhamishoni, utekwani.+ 12 Mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani na kuondoka kukiwa na giza. Atatoboa shimo ukutani na kuibeba mizigo yake kupitia humo.+ Ataufunika uso wake ili asione chini.’ 13 Nitautandaza wavu wangu juu yake, naye atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia.+ Kisha nitampeleka Babiloni, kwenye nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona; naye atafia huko.+ 14 Na wote wanaomzunguka, wasaidizi wake na wanajeshi wake, nitawatawanya pande zote;+ nami nitauchomoa upanga ili kuwakimbiza.+ 15 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi hizo. 16 Lakini nitawalinda watu wachache kati yao wasife kwa upanga, njaa kali, na ugonjwa hatari, ili wasimulie kuhusu mazoea yao yote yanayochukiza miongoni mwa mataifa ambamo watapelekwa; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”
17 Nalo neno la Yehova likanijia tena likisema: 18 “Mwana wa binadamu, unapaswa kula mkate wako ukitetemeka na kunywa maji yako ukifadhaika na kuhangaika.+ 19 Waambie watu wa nchi, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anawaambia hivi wakaaji wa Yerusalemu katika nchi ya Israeli: “Watakula mkate wao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa hofu, kwa maana nchi yao itakuwa ukiwa kabisa+ kwa sababu ya ukatili wa wale wote wanaokaa ndani yake.+ 20 Majiji yanayokaliwa yataharibiwa, na nchi itakuwa ukiwa;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’”+
21 Nalo neno la Yehova likanijia tena likisema: 22 “Mwana wa binadamu, ni methali gani hii mliyo nayo katika Israeli, inayosema, ‘Siku zinapita, na maono yote hayatimii’?+ 23 Kwa hiyo waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitafanya msemo huo ukome, nao hawatautumia tena kama methali katika Israeli.”’ Lakini waambie, ‘Siku zimekaribia,+ na maono yote yatatimia.’ 24 Kwa maana hakutakuwa tena na maono ya uwongo au uaguzi* wa udanganyifu katika nyumba ya Israeli.+ 25 ‘“Kwa maana mimi, Yehova, nitasema. Neno lolote nitakalosema litafanywa bila kukawia zaidi.+ Katika siku zenu,+ enyi nyumba ya uasi, nitasema neno na kulitimiza,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’”
26 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 27 “Mwana wa binadamu, hivi ndivyo watu wa* Israeli wanavyosema, ‘Maono anayoona ni ya muda mrefu kutoka sasa, naye anatabiri kuhusu wakati ujao ulio mbali.’+ 28 Kwa hiyo waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “‘Hakuna neno langu lolote litakalokawia; jambo lolote nitakalosema litafanywa,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”’”
13 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli,+ nawe uwaambie hivi wale wanaotunga unabii wao wenyewe:*+ ‘Sikieni neno la Yehova. 3 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ole wao manabii wapumbavu, wanaofuata roho yao wenyewe, ingawa hawajaona chochote!+ 4 Ewe Israeli, manabii wako wamekuwa kama mbweha katika magofu. 5 Hamtaenda mahali palipobomoka katika kuta za mawe ili kuzijenga upya kwa ajili ya watu wa nyumba ya Israeli,+ ili Waisraeli waendelee kusimama vitani katika siku ya Yehova.”+ 6 “Wameona maono ya uwongo na kutabiri uwongo, wale wanaosema, ‘Neno la Yehova ni,’ wakati ambapo Yehova mwenyewe hajawatuma, nao wamengoja neno lao litimie.+ 7 Je, ninyi hamkuona maono ya uwongo, na kutabiri uwongo, mnaposema, ‘Neno la Yehova ni,’ wakati ambapo sijasema lolote?”’
8 “‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “‘Kwa sababu mmesema uwongo na maono yenu ni ya uwongo, mimi niko dhidi yenu,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”+ 9 Mkono wangu uko dhidi ya manabii ambao maono yao ni ya uwongo na wanaotabiri uwongo.+ Nao hawatakuwa miongoni mwa watu ninaowaambia siri zangu; wala hawataandikwa katika orodha ya watu wa nyumba ya Israeli; wala hawatarudi katika nchi ya Israeli; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ 10 Hayo yote ni kwa sababu wamewapotosha watu wangu wakisema, “Kuna amani!” wakati hakuna amani.+ Ukuta dhaifu unapojengwa, wanaupiga lipu kwa chokaa.’*+
11 “Waambie wale wanaopiga lipu kwa chokaa kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itakuja, mvua ya mawe itanyesha,* na dhoruba kali za upepo zitaubomoa.+ 12 Na ukuta huo utakapoanguka mtaulizwa, ‘Chokaa mliyopaka iko wapi?’+
13 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitasababisha dhoruba kali za upepo zilipuke kwa ghadhabu yangu, na mvua kubwa ya mafuriko kwa hasira yangu, na mvua ya mawe kwa ghadhabu inayoangamiza. 14 Nitaubomoa ukuta ambao mmeupiga lipu kwa chokaa na kuuangusha chini ardhini, na msingi wake utafunuliwa. Jiji litakapoanguka, mtaangamia ndani yake; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
15 “‘Nitakapoumwagia ukuta huo ghadhabu yangu yote na kuwamwagia wale walioupiga lipu kwa chokaa, nitawaambia ninyi: “Ukuta haupo tena, na wale wanaoupiga lipu hawapo tena.+ 16 Manabii wa Israeli hawapo tena, wale wanaowatabiria watu wa Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yao, wakati hakuna amani,”’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
17 “Nawe, mwana wa binadamu, uelekeze uso wako dhidi ya mabinti wa watu wako wanaotunga unabii wao wenyewe, nawe utabiri dhidi yao. 18 Waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ole wao wanawake wanaoshona pamoja tepe kwa ajili ya mikono yote* na kutengeneza shela kwa ajili ya vichwa vya kila ukubwa ili kuwinda uhai wa* watu! Je, mnawinda uhai wa* watu wangu na kujaribu kuhifadhi uhai wenu* wenyewe? 19 Je, mtanitia unajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya makonzi ya shayiri na kwa ajili ya makombo ya mkate,+ mkiwaua watu wasiostahili kufa na kuwaacha hai watu wasiostahili kuishi, kwa kuwadanganya watu wangu, wanaosikiliza uwongo wenu?”’+
20 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko dhidi ya tepe zenu enyi wanawake, mnazotumia kuwinda watu* kana kwamba wao ni ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu na kuwafungua watu mnaowawinda kama ndege. 21 Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena windo lenu; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 22 Kwa sababu mmemvunja moyo aliye mwadilifu kwa uwongo wenu+ ingawa mimi mwenyewe sikuwa nimemsababishia taabu,* nanyi mmeiimarisha mikono ya mwovu+ ili asiiache njia yake ya uovu na kuendelea kuishi.+ 23 Kwa hiyo, ninyi wanawake hamtaona tena maono ya uwongo na kufanya uaguzi;*+ nami nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”
14 Na baadhi ya wazee wa Israeli wakaja na kuketi mbele yangu.+ 2 Kisha neno la Yehova likanijia likisema: 3 “Mwana wa binadamu, wanaume hawa wameazimia kufuata sanamu zao zinazochukiza,* nao wameweka kikwazo kinachowafanya watu watende dhambi. Je, niwaruhusu waniombe ushauri?+ 4 Sasa zungumza nao uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ikiwa Mwisraeli ameazimia kufuata sanamu zake zinazochukiza na kuweka kikwazo kinachowafanya watu watende dhambi kisha anaenda kuomba ushauri kutoka kwa nabii, mimi, Yehova, nitamjibu ipasavyo kulingana na sanamu zake nyingi zinazochukiza. 5 Kwa maana nitatia hofu katika mioyo ya watu wa nyumba ya Israeli* kwa sababu wote wameniacha na kuzifuata sanamu zao zinazochukiza.”’+
6 “Basi waambie watu wa nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Rudini na mziache sanamu zenu zinazochukiza na mgeuze nyuso zenu kutoka kwenye mazoea yenu yanayochukiza.+ 7 Kwa maana ikiwa Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi Israeli anajitenga nami na kuazimia kufuata sanamu zake zinazochukiza na kuweka kikwazo kinachowafanya watu watende dhambi, kisha aje kuomba ushauri kutoka kwa nabii wangu,+ mimi, Yehova, nitamjibu mimi mwenyewe. 8 Nitamkataa* mtu huyo na kumfanya awe ishara ya kuonya na methali, nami nitamwangamiza kabisa kutoka kati ya watu wangu;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’
9 “‘Lakini nabii akipumbazwa naye atoe ushauri, ni mimi, Yehova, ambaye nimempumbaza nabii huyo.+ Ndipo nitakapounyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka kwa watu wangu Waisraeli. 10 Nao lazima wataibeba hatia yao; hatia ya mwenye kuomba ushauri itakuwa sawa na hatia ya nabii, 11 ili watu wa nyumba ya Israeli waache kutangatanga mbali nami na kuacha kujichafua kwa makosa yao yote. Nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
12 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 13 “Mwana wa binadamu, ikiwa nchi itanitendea dhambi kwa kukosa uaminifu, nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kufanya chakula kisipatikane*+ na kuleta njaa kali nchini+ na kuwaangamiza kabisa wanadamu na wanyama kutoka humo.”+ 14 “‘Hata ikiwa watu hawa watatu—Noa,+ Danieli,+ na Ayubu+—wangekuwa humo, wangejiokoa wao wenyewe* tu kwa sababu ya uadilifu wao,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
15 “‘Au nikifanya wanyama hatari wa mwituni wapite kotekote nchini na kuwaua watu wengi* na kuifanya nchi iwe ukiwa hivi kwamba hakuna mtu atakayepita humo kwa sababu ya wanyama wa mwituni,+ 16 kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hata ikiwa watu hao watatu wangekuwa humo, hawangewaokoa wana wao wala mabinti wao; wangejiokoa wao wenyewe tu, na nchi ingekuwa ukiwa.’”
17 “‘Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo+ na kusema: “Upanga na upite kotekote nchini,” na kuwaangamiza wanadamu na wanyama kutoka humo,+ 18 hata ikiwa watu hao watatu wangekuwa humo, kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hawangewaokoa wana wao wala mabinti wao; wangejiokoa wao wenyewe tu.’”
19 “‘Au nikileta ugonjwa hatari katika nchi hiyo+ na kuimwagia ghadhabu yangu kwa umwagaji wa damu ili kuwaangamiza wanadamu na wanyama kutoka humo, 20 hata ikiwa Noa,+ Danieli,+ na Ayubu+ wangekuwa humo, kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hawangewaokoa wana wao wala mabinti wao; wangejiokoa wao wenyewe tu kwa sababu ya uadilifu wao.’”+
21 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ndivyo itakavyokuwa nitakapoleta adhabu zangu nne*+—upanga, njaa kali, wanyama hatari wa mwituni, na ugonjwa hatari+—dhidi ya jiji la Yerusalemu ili kuwaangamiza kabisa wanadamu na wanyama kutoka humo.+ 22 Lakini, baadhi ya watu waliobaki humo wataponyoka na kutolewa nje,+ wana na mabinti. Wanakuja kwenu, nanyi mtakapoona njia zao na matendo yao, kwa hakika mtafarijiwa kuhusiana na msiba ambao nilileta dhidi ya Yerusalemu, kuhusu kila jambo ambalo nilitenda dhidi ya jiji hilo.’”
23 “‘Watawafariji mtakapoona njia zao na matendo yao, nanyi mtajua kwamba sikutenda bila sababu yale niliyolazimika kulitendea jiji hilo,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
15 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, mbao za mzabibu hutofautianaje na za mti mwingine wowote au tawi la miti ya msituni? 3 Je, ufito wake unaweza kutumiwa kufanyia kazi? Au je, watu huutumia kutengeneza kijiti cha kuning’inizia vyombo? 4 Tazama! Hutupwa motoni uwe kuni, na moto huchoma miisho yote miwili na kuunguza katikati. Je, sasa unafaa kwa kazi yoyote? 5 Hata ulipokuwa mzima, haungetumiwa kwa chochote. Je, utakuwa na thamani yoyote baada ya kuchomwa na kuunguzwa na moto?”
6 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kama mbao za mzabibu kati ya miti ya msituni, ambazo nimezitoa ziwe kuni kwa ajili ya moto, ndivyo nitakavyoshughulika na wakaaji wa Yerusalemu.+ 7 Nimewakataa.* Wameponyoka kutoka motoni, lakini moto utawateketeza. Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapowakataa.’”*+
8 “‘Nami nitaifanya nchi iwe ukiwa+ kwa sababu wametenda kwa ukosefu wa uaminifu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
16 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, lijulishe Yerusalemu mazoea yake yanayochukiza.+ 3 Nawe utaliambia, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anakuambia hivi Yerusalemu: “Asili yako na kuzaliwa kwako ni katika nchi ya Mkanaani. Baba yako alikuwa Mwamori,+ na mama yako alikuwa Mhiti.+ 4 Kuhusu kuzaliwa kwako, siku uliyozaliwa, kitovu chako hakikukatwa, hukuoshwa kwa maji uwe safi, hukusuguliwa kwa chumvi, wala hukufungwa kwa vitambaa. 5 Hakuna mtu aliyekusikitikia vya kutosha hivi kwamba akakufanyia lolote kati ya mambo hayo. Hakuna mtu aliyekuhurumia. Badala yake, ulitupwa uwanjani kwa sababu ulichukiwa* siku uliyozaliwa.
6 “‘“Nilipokuwa nikipita, nilikuona ukitupatupa mateke katika damu yako, nawe ulipokuwa umelala hapo katika damu yako, nikasema: ‘Endelea kuishi!’ Naam, nilikuambia ukiwa umelala hapo katika damu yako: ‘Endelea kuishi!’ 7 Nilikufanya uwe umati mkubwa sana, kama mimea inayochipuka shambani, nawe ukakua, ukakomaa na kuvaa mapambo bora sana. Matiti yako yakakomaa, na nywele zako zikakua; lakini bado ulikuwa uchi, bila chochote.”’
8 “‘Nilipokuwa nikipita na kukuona, nilitambua kwamba ulikuwa na umri wa kutosha kuonyeshwa upendo. Basi nikatandaza vazi langu juu yako+ na kuufunika uchi wako, nami nikaapa na kufanya agano pamoja nawe,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nawe ukawa wangu. 9 Isitoshe, nilikuosha kwa maji na kuiondoa damu iliyokuwa juu yako na kukupaka mafuta.+ 10 Kisha nikakuvika vazi lililotariziwa na kukupa viatu vya ngozi bora* na kukufunika kwa kitani bora, nami nikakuvika mavazi ya bei ghali. 11 Nikakupamba kwa vito na kutia bangili kwenye mikono yako na mkufu shingoni mwako. 12 Pia nikatia pete ya puani kwenye pua yako na vipuli kwenye masikio yako na taji maridadi kwenye kichwa chako. 13 Ukaendelea kujipamba kwa dhahabu na fedha, na mavazi yako yalikuwa kitani bora, kitambaa cha bei ghali, na vazi lililotariziwa. Ulikula unga laini, asali, na mafuta, nawe ukawa mrembo kupindukia,+ ukastahili kuwa malkia.’”*
14 “‘Sifa zako zikaanza* kuenea kati ya mataifa+ kwa sababu ya urembo wako, kwa maana urembo wako ulikuwa kamili kwa sababu niliweka fahari yangu mwenyewe juu yako,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
15 “‘Lakini ulianza kuutumaini urembo wako,+ nawe ukawa kahaba kwa sababu ya sifa zako.+ Ulimmwagia kila mpita-njia matendo yako ya ukahaba,+ na urembo wako ukawa wake. 16 Ukachukua baadhi ya mavazi yako na kutengeneza mahali pa juu penye rangi mbalimbali ambapo ulifanyia ukahaba+—mambo hayo hayapaswi kufanywa, wala hayapaswi kutendeka kamwe. 17 Pia, ulichukua vito vyako maridadi vilivyotengenezwa* kwa dhahabu na fedha ambayo nilikupatia nawe ukajitengenezea sanamu za kiume na kufanya nazo ukahaba.+ 18 Nawe ukachukua mavazi yako yaliyotariziwa na kuzifunika,* nawe ukazitolea mafuta yangu na uvumba wangu.+ 19 Na mkate wangu niliokuwa nimekupa—uliotengenezwa kwa unga laini, mafuta, na asali niliyokupa ule—uliutoa pia kwa sanamu hizo ukiwa harufu inayopendeza.*+ Hivyo ndivyo ilivyokuwa,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
20 “‘Uliwachukua wana na mabinti wako uliokuwa umenizalia,+ nawe ukawatoa dhabihu kwa sanamu hizo ili waangamizwe+—je, matendo yako ya ukahaba hayajatosha? 21 Uliwachinja wanangu, nawe ukawatoa wawe dhabihu kwa kuwateketeza* motoni.+ 22 Ulipokuwa ukitenda mambo yako yote yanayochukiza na matendo ya ukahaba, hukukumbuka siku za ujana wako ulipokuwa uchi, bila chochote, ukitupatupa mateke katika damu yako. 23 Baada ya uovu wako wote, ole, ole wako,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 24 ‘Ulijijengea kilima na kujitengenezea mahali pa juu katika kila kiwanja cha jiji. 25 Ulijenga mahali pako pa juu sehemu zinazoonekana zaidi za kila barabara, nawe ukaugeuza urembo wako kuwa kitu kinachochukiza kwa kuutoa mwili wako* kwa kila mpita-njia,+ nawe ukazidisha matendo yako ya ukahaba.+ 26 Ulifanya ukahaba na wana wa Misri,+ majirani wako wenye uchu,* nawe ulinikasirisha kwa matendo yako yasiyohesabika ya ukahaba. 27 Sasa nitauleta mkono wangu dhidi yako na kupunguza posho yako ya chakula+ na kukutia mikononi mwa mapenzi* ya wanawake wanaokuchukia,+ mabinti wa Wafilisti, wanawake walioshtushwa na mwenendo wako mchafu.+
28 “‘Kwa kuwa hungeweza kutoshelezwa, ulifanya pia ukahaba na wana wa Ashuru,+ lakini baada ya kufanya nao ukahaba, bado hukutosheka. 29 Basi ukazidisha ukahaba wako kuelekea nchi ya wafanyabiashara* na kuelekea kwa Wakaldayo,+ lakini bado hukutosheka. 30 Jinsi moyo wako ulivyokuwa mgonjwa,’* asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘ulipofanya mambo hayo yote, ukitenda kama kahaba mwenye ushupavu!+ 31 Lakini ulipojenga kilima chako katika sehemu zinazoonekana zaidi za kila barabara na kutengeneza mahali pako pa juu katika kila kiwanja cha jiji, hukuwa kama kahaba, kwa sababu ulikataa malipo yoyote. 32 Wewe ni mke mzinzi anayewachukua wageni badala ya mume wake mwenyewe!+ 33 Watu huwapa zawadi makahaba wote,+ lakini wewe ndiye unayewapa zawadi wote walio na uchu kukuelekea,+ nawe unawapa rushwa ili waje kwako kutoka pande zote ili kufanya ukahaba.+ 34 Wewe ni tofauti kabisa na wanawake wengine wanaofanya ukahaba. Hakuna mtu anayefanya ukahaba kama wewe! Unawalipa watu, nao hawakulipi. Unatenda tofauti kabisa.’
35 “Kwa hiyo, ewe kahaba,+ sikia neno la Yehova. 36 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu uchu wako umemwagwa na uchi wako umefunuliwa ulipokuwa ukifanya ukahaba na wapenzi wako na sanamu zako zote zinazoudhi na kuchukiza*+ ambazo hata ulizitolea dhabihu ya damu ya wanao,+ 37 kwa hiyo ninawakusanya pamoja wapenzi wote ambao umewapa raha, wote uliowapenda na wote uliowachukia. Nitawakusanya pamoja dhidi yako kutoka pande zote na kuwafunulia uchi wako, nao watakuona ukiwa uchi kabisa.+
38 “‘Nami nitakuadhibu kwa hukumu wanayostahili wanawake wazinzi+ na wanawake wanaomwaga damu,+ na damu yako itamwagwa kwa ghadhabu na wivu.+ 39 Nitakutia mikononi mwao, nao watavibomoa vilima vyako, na mahali pako pa juu patabomolewa;+ nao watakuvua mavazi yako+ na kuchukua vito vyako* maridadi+ na kukuacha uchi, bila chochote. 40 Wataleta umati dhidi yako,+ nao watakupiga mawe+ na kukuchinja kwa panga zao.+ 41 Wataziteketeza nyumba zako kwa moto+ na kutekeleza hukumu dhidi yako mbele ya macho ya wanawake wengi; nami nitakomesha ukahaba wako,+ nawe utaacha kutoa malipo. 42 Nitaitosheleza ghadhabu yangu dhidi yako,+ na hasira yangu itakuacha;+ nami nitatulia na sitaendelea kukasirika.’
43 “‘Kwa sababu hukuzikumbuka siku za ujana wako+ nawe umenikasirisha kwa kufanya mambo hayo yote, sasa nitakuletea madhara ya njia zako juu ya kichwa chako mwenyewe,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nawe hutaendelea tena na mwenendo wako mchafu na mazoea yako yote yanayochukiza.
44 “‘Tazama! Kila mtu anayetumia methali ataitumia methali hii kukuhusu: “Kama mama alivyo, ndivyo binti alivyo!”+ 45 Wewe ni binti ya mama yako, aliyemdharau mume wake na watoto wake. Nawe ni dada ya dada zako, waliowadharau waume zao na watoto wao. Mama yenu alikuwa Mhiti, na baba yenu alikuwa Mwamori.’”+
46 “‘Dada yako mkubwa ni Samaria,+ anayekaa upande wako wa kaskazini* pamoja na mabinti zake,*+ na dada yako mdogo, anayekaa upande wako wa kusini,* ni Sodoma+ pamoja na mabinti zake.+ 47 Hukutembea tu katika njia zao na kufuata mazoea yao yanayochukiza, bali pia kwa muda mfupi mwenendo wako ulikuwa mpotovu hata zaidi kuliko mwenendo wao.+ 48 Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘Sodoma dada yako na mabinti zake hawajatenda yale ambayo wewe na mabinti zako mmetenda. 49 Tazama! Hili ndilo lililokuwa kosa la Sodoma dada yako: Yeye pamoja na mabinti zake+ walikuwa na kiburi,+ nao walikuwa na chakula kingi+ na utulivu mwingi;+ hata hivyo hawakuwasaidia walioteseka na maskini.+ 50 Waliendelea kuwa na majivuno+ na kuzidi kutenda mambo yanayochukiza machoni pangu,+ basi nikalazimika kuwaondoa.+
51 “‘Samaria+ hata hakutenda nusu ya dhambi zako. Uliendelea kuzidisha mazoea yako yanayochukiza kuliko yao, hivi kwamba dada zako wakaonekana kuwa waadilifu kwa sababu ya mazoea yako yote yanayochukiza.+ 52 Lazima sasa ubebe fedheha yako kwa kuwa umetetea* tabia za dada zako. Kwa sababu ya dhambi yako ya kutenda mambo yanayochukiza kuliko wao, wao ni waadilifu kuliko wewe. Basi sasa, na uaibike na kubeba fedheha ya kuwafanya dada zako waonekane kuwa waadilifu.’
53 “‘Nami nitawakusanya watu wao waliotekwa, watu waliotekwa wa Sodoma pamoja na mabinti zake na watu waliotekwa wa Samaria pamoja na mabinti zake; na pamoja nao nitawakusanya pia watu wako waliotekwa,+ 54 ili uibebe fedheha yako; nawe utafedheheka kwa sababu ya yale ambayo umefanya kwa kuwafariji. 55 Na dada zako wewe mwenyewe, Sodoma na mabinti zake, watarudia hali yao ya mwanzoni, na Samaria na mabinti zake watarudia hali yao ya mwanzoni, na wewe pamoja na mabinti zako mtarudia hali yenu ya mwanzoni.+ 56 Dada yako Sodoma hakustahili kutajwa nawe katika siku ya fahari yako, 57 kabla uovu wako mwenyewe haujafunuliwa.+ Sasa mabinti wa Siria na majirani zake wanakushutumu, na mabinti wa Wafilisti,+ wote wanaokuzunguka, wanakudharau. 58 Utayabeba madhara ya mwenendo wako mchafu na mazoea yako yanayochukiza,’ asema Yehova.”
59 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Sasa nitakutendea kama ulivyotenda,+ kwa maana ulikidharau kiapo kwa kuvunja agano langu.+ 60 Lakini mimi mwenyewe nitalikumbuka agano nililofanya pamoja nawe katika siku za ujana wako, nami nitafanya agano la kudumu pamoja nawe.+ 61 Utakumbuka tabia yako na kufedheheka+ utakapowakaribisha dada zako, waliokuzidi umri na pia walio na umri mdogo kuliko wako, nami nitakupa wawe mabinti zako, lakini si kwa sababu ya agano lako.’
62 “‘Na mimi mwenyewe nitafanya agano langu pamoja nawe; nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova. 63 Kisha utakumbuka na kuaibika sana usiweze kuufungua mdomo wako kwa sababu ya kufedheheka,+ nitakapofunika dhambi zako licha ya mambo yote ambayo umefanya,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
17 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, tega kitendawili na useme methali kuhusu watu wa nyumba ya Israeli.+ 3 Nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tai mkubwa,+ mwenye mabawa makubwa, na manyoya marefu, na aliyejaa manyoya yenye rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni+ na kuchukua sehemu ya juu ya mwerezi.+ 4 Aliling’oa chipukizi lake lililo juu zaidi na kulileta kwenye nchi ya wafanyabiashara* na kuliweka katika jiji la wafanyabiashara.+ 5 Kisha akachukua baadhi ya mbegu za nchi hiyo+ na kuziweka katika shamba lenye rutuba. Akaipanda mbegu moja kama mti wa mvinje kando ya maji mengi. 6 Basi ikachipuka na kuwa mzabibu mfupi, unaotambaa,+ wenye majani yanayotazama ndani na mizizi inayokua chini yake. Kwa hiyo ukawa mzabibu, ukatokeza machipukizi na kuota matawi.+
7 “‘“Akaja tai mwingine mkubwa,+ mwenye mabawa makubwa na manyoya makubwa.+ Kisha mzabibu huo ukasambaza mizizi yake kwa bidii kumwelekea, mbali na bustani mahali ambapo ulipandwa, nao ukaelekeza majani yake kwake ili aumwagilie maji.+ 8 Ulikuwa tayari umepandwa katika shamba zuri karibu na maji mengi, ili utokeze matawi, uzae matunda, na uwe mzabibu mkubwa.”’+
9 “Sema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Je, utasitawi? Je, mtu fulani hataing’oa mizizi yake+ na kufanya matunda yake yaoze na machipukizi yake yanyauke?+ Utakauka sana hivi kwamba hautahitaji mkono wenye nguvu wala watu wengi ili kuung’oa pamoja na mizizi yake. 10 Ingawa umepandikizwa, je, utasitawi? Je, hautakauka kabisa, utakapopigwa na upepo wa mashariki? Utakauka katika bustani ulikochipuka.”’”
11 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 12 “Tafadhali iambie nyumba ya uasi, ‘Je, hamtambui maana ya mambo haya?’ Sema, ‘Tazama! Mfalme wa Babiloni alikuja Yerusalemu, akamchukua mfalme wake na wakuu wake na kurudi pamoja nao Babiloni.+ 13 Isitoshe, alimchukua mmoja aliyekuwa wa uzao wa*+ kifalme, akafanya naye agano na kumwapisha.+ Kisha akawachukua watu mashuhuri wa nchi,+ 14 ili ufalme huo ushushwe, usiweze kuinuka, ili uendelee kuwapo ikiwa tu utashika agano lake.+ 15 Lakini mwishowe mfalme huyo alimwasi+ kwa kutuma wajumbe wake Misri ili apate farasi+ na jeshi kubwa kutoka huko.+ Je, atafanikiwa? Je, yule anayefanya mambo hayo ataponyoka adhabu? Je, anaweza kuvunja agano na bado aponyoke?’+
16 “‘“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “atafia huko Babiloni, mahali ambapo anaishi mfalme* aliyemweka* kuwa mfalme, ambaye alikidharau kiapo chake na ambaye alilivunja agano lake.+ 17 Na lile jeshi kubwa na wanajeshi wengi wa Farao hawatamsaidia kamwe vitani,+ wakati boma la kuzingira litakapojengwa na kuta za kuzingira zitakapojengwa ili kuangamiza uhai wa* watu wengi. 18 Amedharau kiapo na kuvunja agano. Hata ingawa alitoa ahadi,* amefanya mambo hayo yote, naye hataponyoka.”’
19 “‘Kwa hiyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Kwa hakika kama ninavyoishi, nitamletea juu ya kichwa chake madhara ya kudharau kiapo changu+ na kuvunja agano langu. 20 Nitautandaza wavu wangu juu yake, naye atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia.+ Nitamleta Babiloni na kumhukumu huko kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu alionitendea.+ 21 Wakimbizi wote kati ya wanajeshi wake watauawa kwa upanga, na wale wanaobaki watatawanyika kila upande.*+ Ndipo mtakapolazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.”’+
22 “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitachukua chipukizi kutoka katika kilele cha mwerezi mkubwa+ na kulipanda, kutoka juu ya matawi yake nitakata chipukizi changa,+ nami mwenyewe nitalipanda juu ya mlima mrefu na ulio juu sana.+ 23 Nitalipanda juu ya mlima mrefu wa Israeli; na matawi yake yatakua, nalo litazaa matunda na kuwa mwerezi mkubwa. Na ndege wa kila aina wataishi chini yake na kukaa kwenye kivuli cha majani yake. 24 Na miti yote ya shambani italazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimeushusha ule mti mrefu na kuukweza ule mti mfupi;+ nimeukausha ule mti mbichi na kuufanya mti uliokauka usitawi.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nimefanya hivyo.”’”
18 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Methali hii mnayoisema katika nchi ya Israeli inamaanisha nini, ‘Akina baba wamekula zabibu chachu, lakini meno ya wana ndiyo yanayotiwa ukakasi’?+
3 “‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hamtaendelea kuutaja msemo huo katika Israeli. 4 Tazama! Nafsi zote—ni zangu.* Kama nafsi ya baba ilivyo yangu ndivyo ilivyo nafsi ya mwana—ni zangu. Nafsi* inayotenda dhambi ndiyo itakayokufa.*
5 “‘Ikiwa mtu ni mwadilifu na anatenda haki na uadilifu, 6 naye hali dhabihu zinazotolewa kwa sanamu kwenye milima;+ hazitumaini sanamu zinazochukiza* za watu wa nyumba ya Israeli; hamnajisi mke wa jirani yake+ au kulala na mwanamke aliye katika hedhi;+ 7 hamtesi mtu yeyote,+ bali hurudisha rehani aliyopewa na mtu mwenye deni lake;+ hamnyang’anyi yeyote,+ bali humpa mwenye njaa chakula chake+ na kumfunika kwa vazi aliye uchi;+ 8 hatozi faida wala kutoza riba,+ lakini anajizuia asitende isivyo haki;+ anatekeleza haki ya kweli kati ya mtu na mwenzake;+ 9 naye anaendelea kutembea katika amri zangu na kushika sheria zangu* ili atende kwa uaminifu. Mtu huyo ni mwadilifu na kwa hakika ataendelea kuishi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
10 “‘Lakini ikiwa yeye ni baba ya mwana ambaye ni mnyang’anyi+ au muuaji*+ au anayefanya lolote kati ya mambo haya mengine 11 (ingawa baba yake hajafanya lolote kati ya mambo hayo)—anakula dhabihu zilizotolewa kwa sanamu kwenye milima, anamnajisi mke wa jirani yake, 12 anawatesa wenye uhitaji na maskini,+ anawanyang’anya watu vitu vyao, harudishi kitu kilichowekwa rehani; anatumaini sanamu zinazochukiza,+ anajihusisha na mazoea yanayochukiza,+ 13 ametoza riba na kutoza faida+—basi mwana huyo hataendelea kuishi. Kwa sababu ya mambo hayo yote yanayochukiza aliyofanya, kwa hakika atauawa. Damu yake mwenyewe itakuwa juu yake.
14 “‘Lakini ikiwa baba ana mwana anayeona dhambi zote anazofanya baba yake, na ingawa anaziona, hafanyi mambo kama hayo, 15 hali dhabihu zilizotolewa kwa sanamu kwenye milima; hazitumaini sanamu zinazochukiza za watu wa nyumba ya Israeli; hamnajisi mke wa jirani yake; 16 hamtesi mtu yeyote; habaki na kitu kilichowekwa rehani; hamnyang’anyi mtu kitu chochote; chakula chake mwenyewe anampa mwenye njaa na kumfunika kwa vazi aliye uchi; 17 anaepuka kuwakandamiza maskini; hatozi riba wala kutoza faida; naye anafuata sheria zangu;* ametembea katika amri zangu. Mtu huyo hatakufa kwa sababu ya kosa la baba yake. Kwa hakika ataendelea kuishi. 18 Lakini kwa kuwa baba yake alifanya ulaghai, akamnyang’anya ndugu yake, na kufanya mambo mabaya kati ya watu wake, atakufa kwa sababu ya kosa lake.
19 “‘Nanyi mtasema: “Kwa nini mwana hana hatia kwa sababu ya kosa la baba yake?” Kwa kuwa mwana ametenda mambo ya haki na ya uadilifu, amezishika amri zangu zote na kuzitenda, kwa hakika ataendelea kuishi.+ 20 Nafsi inayotenda dhambi ndiyo itakayokufa.*+ Mwana hatakuwa na hatia kwa sababu ya kosa la baba yake, na baba hatakuwa na hatia kwa sababu ya kosa la mwanawe. Mwadilifu atathawabishwa kwa sababu ya uadilifu wake mwenyewe, na mwovu ataadhibiwa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe.+
21 “‘Sasa mtu mwovu akiziacha dhambi zote alizofanya na kushika amri zangu na kutenda mambo ya haki na ya uadilifu, kwa hakika ataendelea kuishi. Hatakufa.+ 22 Hatahukumiwa kwa kosa lolote alilotenda.*+ Ataendelea kuishi kwa kutenda uadilifu.’+
23 “‘Je, ninafurahia hata kidogo kifo cha mtu mwovu?’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Je, sipendelei kwamba aziache njia zake naye aendelee kuishi?’+
24 “‘Lakini mtu mwadilifu akiacha uadilifu wake na kutenda kosa,* na kufanya mambo yote yanayochukiza wanayofanya waovu, je, ataishi? Hakuna jambo lolote litakalokumbukwa kati ya matendo ya uadilifu aliyotenda.+ Atakufa kwa sababu ya ukosefu wake wa uaminifu na dhambi aliyotenda.+
25 “‘Lakini mtasema: “Njia ya Yehova si ya haki.”+ Tafadhali sikilizeni, enyi watu wa nyumba ya Israeli! Je, ni njia yangu isiyo ya haki?+ Je, si njia zenu ambazo si za haki?+
26 “‘Mtu mwadilifu akiuacha uadilifu wake na kutenda kosa, naye afe kwa sababu ya kosa hilo, atakufa kwa sababu ya kosa lake mwenyewe.
27 “‘Na mtu mwovu akiacha uovu ambao ametenda na kuanza kutenda mambo ya haki na ya uadilifu, atauhifadhi uhai wake* mwenyewe.+ 28 Akitambua na kuacha makosa yote ambayo ametenda, kwa hakika ataendelea kuishi. Hatakufa.
29 “‘Lakini watu wa nyumba ya Israeli watasema: “Njia ya Yehova si ya haki.” Je, ni kweli kwamba ni njia zangu ambazo si za haki, enyi watu wa nyumba ya Israeli?+ Je, si njia zenu ambazo si za haki?’
30 “‘Kwa hiyo, nitamhukumu kila mmoja wenu kulingana na njia zake,+ enyi watu wa nyumba ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Acheni, naam, acheni kabisa makosa yenu yote, ili yasiwe kikwazo kinachowaletea hatia. 31 Jiondoleeni makosa yenu yote mliyofanya+ na mjipatie* moyo mpya na roho mpya,+ kwa nini mfe,+ enyi watu wa nyumba ya Israeli?’
32 “‘Mimi sifurahii kifo cha mtu yeyote,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Kwa hiyo geukeni na kuishi.’”+
19 “Nawe lazima uimbe wimbo wa huzuni* kuhusu wakuu wa Israeli, 2 useme,
‘Mama yako alikuwa nani? Simba jike kati ya simba.
Alilala kati ya wanasimba wenye nguvu* naye akawalea watoto wake.
3 Alimlea mmoja wa watoto wake, akawa mwanasimba mwenye nguvu.+
Naye akajifunza jinsi ya kurarua mawindo,
Akamnyafua hata mwanadamu.
4 Mataifa yalisikia kumhusu na wakamkamata katika shimo lao,
Nao wakamleta kwa kulabu nchini Misri.+
5 Mama huyo alisubiri na hatimaye akaona hakuna tumaini kwamba atarudi.
Basi akamchukua mwingine kati ya watoto wake na kumtuma akiwa mwanasimba mwenye nguvu.
6 Yeye pia alitembea huku na huku kati ya simba, naye akawa mwanasimba mwenye nguvu.
Akajifunza jinsi ya kurarua mawindo, na hata akawanyafua wanadamu.+
7 Akazungukazunguka katika minara yao yenye ngome na kuyaharibu majiji yao,
Hivi kwamba nchi iliyo ukiwa ikajaa sauti ya mngurumo wake.+
8 Mataifa ya wilaya jirani yalikuja dhidi yake ili kuutandaza wavu wao juu yake,
Naye akanaswa katika shimo lao.
9 Wakamweka katika kizimba kwa kulabu na kumpeleka kwa mfalme wa Babiloni.
Wakamfunga huko ili sauti yake isisikike tena kwenye milima ya Israeli.
10 Mama yako alikuwa kama mzabibu+ katika damu yako,* uliopandwa kando ya maji.
Ukazaa matunda na kujaa matawi kwa sababu ya maji mengi.
11 Nao ukatokeza matawi yenye nguvu,* yanayofaa kuwa fimbo za ufalme za watawala.
Ukakua, ukawa mrefu kuliko miti mingine,
Nao ukaonekana kwa sababu ya urefu wake na wingi wa majani yake.
12 Lakini aling’olewa kwa ghadhabu+ na kutupwa chini ardhini,
Na upepo wa mashariki ukayakausha matunda yake.
Matawi yake yenye nguvu yalikatwa yakakauka,+ na moto ukayateketeza.+
13 Sasa amepandwa nyikani,
Katika nchi isiyo na maji na yenye kiu.+
14 Moto ukaenea kutoka kwenye matawi yake* na kuteketeza machipukizi yake na matunda yake,
Na hakuna tawi lenye nguvu lililobaki, hakuna fimbo ya mfalme ya kutawala.+
“‘Huo ni wimbo wa huzuni, nao utatumiwa kama wimbo wa huzuni.’”
20 Katika mwaka wa saba, mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi huo, baadhi ya wazee wa Israeli walikuja na kuketi mbele yangu ili kuniomba ushauri kutoka kwa Yehova. 2 Ndipo neno la Yehova likanijia likisema: 3 “Mwana wa binadamu, zungumza na wazee wa Israeli uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Je, mnakuja kuniomba ushauri? ‘Kwa hakika kama ninavyoishi, sitawajibu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”’
4 “Je, uko tayari kuwahukumu?* Mwana wa binadamu je, uko tayari kuwahukumu? Wajulishe mambo yanayochukiza ambayo mababu zao walifanya.+ 5 Waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Siku nilipoichagua Israeli,+ pia niliuapia* uzao wa* nyumba ya Yakobo, na kujijulisha kwao nchini Misri.+ Naam, niliwaapia na kusema, ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu.’ 6 Siku hiyo niliapa kwamba nitawatoa nchini Misri na kuwapeleka katika nchi niliyokuwa nimeichunguza* kwa ajili yao, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ Nchi hiyo ilikuwa nzuri sana kuliko* nchi zote. 7 Kisha nikawaambia, ‘Lazima kila mmoja wenu atupe vitu vinavyochukiza vilivyo mbele ya macho yake; msijitie unajisi kwa sanamu zinazochukiza* za Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’+
8 “‘“Lakini wakaniasi nao hawakutaka kunisikiliza. Hawakuvitupa vitu vinavyochukiza vilivyokuwa mbele yao, nao walikataa kuziacha sanamu zinazochukiza za Misri.+ Basi nikaahidi kuwamwagia ghadhabu yangu na kuwaletea hasira yangu yote nchini Misri. 9 Lakini nilichukua hatua kwa ajili ya jina langu ili lisichafuliwe mbele ya mataifa ambamo waliishi.+ Nilijijulisha kwao* mbele ya mataifa hayo nilipowatoa* nchini Misri.+ 10 Kwa hiyo nikawatoa nchini Misri na kuwaongoza kuingia nyikani.+
11 “‘“Kisha nikawapa amri zangu na kuwajulisha sheria zangu,*+ ili mtu anayezifuata apate uzima kupitia hizo.+ 12 Pia nikawapa sabato zangu,+ ziwe ishara kati yangu nao,+ ili wajue kwamba mimi, Yehova, ndiye ninayewatakasa.
13 “‘“Lakini watu wa nyumba ya Israeli waliniasi nyikani.+ Hawakutembea katika amri zangu, nao wakakataa sheria zangu,* ambazo mtu akizifuata, atapata uzima kupitia hizo. Walizitia unajisi kabisa sabato zangu. Basi nikaahidi kuwamwagia ghadhabu yangu nyikani ili niwaangamize kabisa.+ 14 Nilichukua hatua kwa ajili ya jina langu mwenyewe ili lisichafuliwe mbele ya mataifa, walioona nikiwatoa* huko.+ 15 Pia nikawaapia wakiwa nyikani kwamba sitawapeleka katika nchi niliyowapa+—nchi inayotiririka maziwa na asali,+ nchi nzuri sana kuliko* nchi zote— 16 kwa sababu walizikataa sheria zangu* na hawakutembea katika amri zangu, nao wakazitia unajisi sabato zangu, kwa maana mioyo yao ilikuwa ikifuata sanamu zao zinazochukiza.+
17 “‘“Lakini niliwasikitikia,* nami sikuwaharibu; sikuwaangamiza kabisa nyikani. 18 Niliwaambia wana wao nyikani,+ ‘Msitembee katika masharti ya mababu zenu+ wala kushika hukumu zao wala kujichafua kwa sanamu zao zinazochukiza. 19 Mimi ni Yehova Mungu wenu. Tembeeni katika amri zangu, na kuzishika sheria zangu,* na kuzifuata.+ 20 Nanyi zitakaseni sabato zangu,+ nazo zitakuwa ishara kati yangu nanyi ili mjue kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’+
21 “‘“Lakini wana hao wakaanza kuniasi.+ Hawakutembea katika amri zangu, nao hawakushika wala kufuata sheria zangu,* ambazo mtu akizifuata, atapata uzima kupitia hizo. Walizitia unajisi sabato zangu. Basi nikaahidi kuwamwagia ghadhabu yangu, na kuwaletea hasira yangu yote nyikani.+ 22 Lakini nilijizuia+ na kuchukua hatua kwa ajili ya jina langu mwenyewe,+ ili lisichafuliwe mbele ya mataifa, walioona nikiwatoa* huko. 23 Pia, niliwaapia nyikani kwamba nitawatawanya miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali,+ 24 kwa sababu hawakufuata sheria zangu* na walikataa amri zangu,+ walizitia unajisi sabato zangu, nao wakafuata* sanamu zinazochukiza za mababu zao.+ 25 Pia, niliwaruhusu wafuate masharti ambayo hayakuwa mazuri na sheria* ambazo hazingewasaidia kupata uzima.+ 26 Nami nikawaacha watiwe unajisi kwa dhabihu zao wenyewe—walipomteketeza* motoni kila mzaliwa wa kwanza+—ili kuwafanya wawe ukiwa, ili wajue kwamba mimi ni Yehova.”’
27 “Basi zungumza na watu wa nyumba ya Israeli, ewe mwana wa binadamu, nawe uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Kwa njia hii pia, mababu zenu walinikufuru kwa kunitendea kwa ukosefu wa uaminifu. 28 Niliwaleta katika nchi niliyoapa kwamba ningewapatia.+ Walipoona vilima vyote virefu na miti yenye majani mengi,+ walianza kutoa dhabihu zao na matoleo yao yanayochukiza. Walitoa harufu inayopendeza* ya dhabihu zao na kumwaga matoleo yao ya vinywaji hapo. 29 Basi nikawauliza, ‘Mahali hapa pa juu mnapoenda panamaanisha nini? (Bado panaitwa Mahali pa Juu mpaka leo hii.)’”’+
30 “Sasa waambie watu wa nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Je, mnajichafua kama mababu zenu walivyofanya kwa kuzifuata sanamu zao zinazochukiza ili kufanya nazo ukahaba wa kiroho?+ 31 Na je, bado mnajichafua mpaka leo hii kwa kuzitolea dhabihu sanamu zenu zote zinazochukiza, mkiwateketeza* motoni wana wenu?+ Je, wakati huohuo ninapaswa kujibu maombi yenu, enyi watu wa nyumba ya Israeli?”’+
“‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘Sitajibu maombi yenu.+ 32 Na jambo mnalofikiria mnaposema, “Na tuwe kama mataifa, kama familia za nchi nyingine, wanaoabudu* miti na mawe,”+ jambo hilo halitatimia kamwe.’”
33 “‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘Nitawatawala nikiwa mfalme kwa mkono wenye nguvu, kwa mkono ulionyooshwa, na kwa ghadhabu kali.+ 34 Kwa mkono wenye nguvu, kwa mkono ulionyooshwa, na kwa ghadhabu kali nitawatoa kati ya mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi ambazo mmetawanywa.+ 35 Nitawapeleka katika nyika ya mataifa na huko nitawahukumu uso kwa uso.+
36 “‘Kama nilivyowahukumu mababu zenu katika nyika ya nchi ya Misri, ndivyo nitakavyowahukumu ninyi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 37 ‘Nitawafanya mpite chini ya fimbo ya mchungaji+ na kuwaleta chini ya wajibu wa* agano. 38 Lakini nitawaondoa waasi kati yenu na wale wanaonitendea dhambi.+ Kwa maana nitawatoa katika nchi wanayokaa wakiwa wageni, lakini hawataingia katika nchi ya Israeli;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
39 “Nanyi, enyi watu wa nyumba ya Israeli, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kila mmoja wenu na aende kuziabudu sanamu zake zinazochukiza.+ Lakini baadaye ikiwa hamtanisikiliza, hamtaweza tena kulichafua jina langu takatifu kwa dhabihu zenu na kwa sanamu zenu zinazochukiza.’+
40 “‘Kwa maana katika mlima wangu mtakatifu, kwenye mlima mrefu wa Israeli,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘ndiko watu wote wa nyumba ya Israeli, wote, watanitumikia nchini.+ Nitafurahishwa nao huko, nami nitadai mnipe michango yenu na matunda ya kwanza ya matoleo yenu, vitu vyenu vyote vitakatifu.+ 41 Kwa sababu ya harufu inayopendeza,* nitafurahishwa nanyi nitakapowatoa kati ya mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi ambazo mmetawanywa;+ nami nitatakaswa kati yenu mbele ya macho ya mataifa.’+
42 “‘Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova+ nitakapowapeleka katika nchi ya Israeli,+ katika nchi ambayo niliapa kwamba nitawapa mababu zenu. 43 Na huko mtakumbuka mwenendo wenu na matendo yenu yote ambayo mlijichafua kupitia hayo,+ nanyi mtajichukia* kwa sababu ya mambo yote mabaya mliyotenda.+ 44 Ndipo mtakapolazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakaposhughulika nanyi kwa ajili ya jina langu,+ si kulingana na mwenendo wenu mwovu au kulingana na matendo yenu yaliyopotoka, enyi watu wa nyumba ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
45 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 46 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako upande wa eneo la kusini na utangaze kuelekea kusini, na uutabirie msitu wa uwanja wa kusini. 47 Uambie msitu wa kusini, ‘Sikia neno la Yehova. Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ninawasha moto dhidi yako,+ nao utateketeza kila mti mbichi na kila mti uliokauka ndani yako. Moto huo unaowaka hautazimwa,+ nao utachoma kila uso, kuanzia kusini mpaka kaskazini. 48 Na kila mwili utaona* kwamba Mimi mwenyewe, Yehova, nimeuwasha moto, ili usizimwe.”’”+
49 Nami nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Wanasema kunihusu, ‘Je, hazungumzi kwa vitendawili?’”*
21 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako Yerusalemu, na utoe tangazo dhidi ya mahali patakatifu, na utabiri dhidi ya nchi ya Israeli. 3 Iambie nchi ya Israeli, ‘Yehova anasema hivi: “Niko dhidi yako, nami nitauchomoa upanga wangu kutoka katika ala yake+ na kumkatilia mbali mwadilifu na mwovu kutoka kati yako. 4 Kwa kuwa nitamkatilia mbali kutoka kati yako mwadilifu na mwovu, upanga wangu utachomolewa kutoka katika ala yake dhidi ya wote wenye mwili,* kutoka kusini mpaka kaskazini. 5 Watu wote watalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimeuchomoa upanga wangu kutoka katika ala yake. Hautarudi tena kamwe.”’+
6 “Nawe, mwana wa binadamu, lia kwa maumivu huku ukitetemeka,* naam, lia kwa uchungu mbele yao.+ 7 Na wakikuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa maumivu?’ utasema, ‘Kwa sababu ya habari fulani.’ Kwa maana hakika itakuja, na kila moyo utayeyuka kwa woga na kila mkono utalegea na kila roho itahuzunika na kila goti litadondosha maji.*+ ‘Tazama! Hakika itakuja—itatokea,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
8 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 9 “Mwana wa binadamu, tabiri, ‘Yehova anasema hivi: “Sema, ‘Upanga! Upanga+ umenolewa, nao umesuguliwa. 10 Umenolewa kwa ajili ya uchinjaji mkubwa; umesuguliwa ili uwakewake kama radi.’”’”
“Je, hatupaswi kushangilia?”
“‘Je, utakataa* fimbo ya ufalme ya mwana wangu mwenyewe,+ kama unavyokataa kila mti?
11 “‘Umetolewa ili usuguliwe na kushikwa mkononi. Upanga huo umenolewa na kusuguliwa, ili utiwe mkononi mwa muuaji.+
12 “‘Mwana wa binadamu, lia kwa sauti na uomboleze,+ kwa maana upanga umekuja dhidi ya watu wangu; uko dhidi ya wakuu wote wa Israeli.+ Na upanga huo utawaangamiza pamoja na watu wangu. Kwa hiyo piga paja lako kwa huzuni. 13 Kwa maana uchunguzi umefanywa,+ na itakuwaje ikiwa upanga utaikataa fimbo ya ufalme? Haitaendelea* kuwapo,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
14 “Nawe, mwana wa binadamu, tabiri na upige makofi na kusema mara tatu, ‘Upanga!’ Ni upanga wa wale waliouawa, upanga wa uchinjaji mkubwa, unaowazunguka.+ 15 Mioyo yao itayeyuka kwa woga+ na wengi wataanguka katika malango ya jiji lao; nitawachinja kwa upanga. Naam, unawakawaka kama radi na umesuguliwa ili kuchinja! 16 Kata kwa makali upande wa kulia! Geukia upande wa kushoto! Nenda popote ambapo makali yako yanaelekezwa! 17 Nami pia nitapiga makofi na kuiridhisha ghadhabu yangu.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.”
18 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 19 “Nawe, mwana wa binadamu, chora njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babiloni utapitia. Zote mbili zitaanzia nchi ileile, na ishara iwekwe* mahali ambapo barabara inatengana ili kuingia katika yale majiji mawili. 20 Unapaswa kuchora njia moja ili upanga ushambulie jiji la Raba+ la Waamoni, na njia nyingine ili ushambulie jiji la Yerusalemu+ lenye ngome, nchini Yuda. 21 Kwa maana mfalme wa Babiloni amesimama ili kufanya uaguzi* kwenye njia panda, mahali ambapo zile barabara mbili zinatengana. Anaitikisa mishale. Anaomba ushauri kutoka kwa sanamu* zake; anachunguza ini. 22 Uaguzi* ulio katika mkono wake wa kulia umeelekezwa Yerusalemu, ili kuweka mitambo ya kubomolea, ili kutoa agizo la kuchinja, ili kupiga kelele za vita, kuweka kwenye malango mitambo ya kubomolea, kujenga boma la kuzingira, kujenga ukuta wa kuzingira.+ 23 Lakini utaonekana kama uaguzi* wa uwongo machoni pa wale* waliowaapia.+ Lakini anakumbuka hatia yao naye atawakamata.+
24 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Mmefanya hatia yenu wenyewe ikumbukwe kwa kuyafunua makosa yenu na kufanya dhambi zenu zionekane katika matendo yenu yote. Kwa kuwa sasa mmekumbukwa, mtachukuliwa kwa nguvu.’*
25 “Lakini siku yako imefika, ewe uliyejeruhiwa vibaya, mkuu mwovu wa Israeli,+ wakati wa adhabu yako ya mwisho. 26 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kiondoe kilemba, na ulivue taji.+ Hili halitabaki kama lilivyo.+ Mwinue aliye chini,+ na umshushe aliye juu.+ 27 Nitaliharibu, nitaliharibu, nitaliharibu. Nalo halitakuwa la mtu yeyote mpaka yule aliye na haki ya kisheria atakapokuja,+ nami nitampa yeye.’+
28 “Nawe, mwana wa binadamu, tabiri, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi kuhusu Waamoni na kuhusu matusi yao.’ Sema, ‘Upanga! Upanga umechomolewa kwa ajili ya kuchinja; umesuguliwa ili kunyafua na kuwakawaka kama radi. 29 Licha ya maono ya uwongo na uaguzi* wa uwongo kuwahusu ninyi, mtarundikwa juu ya waliouawa,* watu waovu ambao siku yao imefika, wakati wa adhabu yao ya mwisho. 30 Urudishe upanga katika ala yake. Nitakuhukumia mahali ulipoumbwa, katika nchi uliyozaliwa. 31 Nitakumwagia ghadhabu yangu. Nitakupulizia moto wa hasira yangu, nami nitakutia mikononi mwa watu wakatili, mafundi wa maangamizi.+ 32 Utakuwa kuni kwa ajili ya moto;+ damu yako mwenyewe itamwagwa nchini, nawe hutakumbukwa tena, kwa maana mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’”
22 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Nawe, mwana wa binadamu, je, uko tayari kulitangazia hukumu* jiji lenye hatia ya damu+ na kulijulisha mambo yake yote yanayochukiza?+ 3 Nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ewe jiji linalomwaga damu+ ndani yake, ambalo wakati wake unakuja,+ linalotengeneza sanamu zinazochukiza* ili kujichafua,+ 4 umwagaji wako wa damu umekufanya uwe na hatia,+ na sanamu zako zinazochukiza zimekufanya usiwe safi.+ Umeharakisha mwisho wa siku zako, na mwisho wa miaka yako umefika. Ndiyo sababu nitakufanya uwe kitu cha kushutumiwa na mataifa na kitu cha kudhihakiwa na nchi zote.+ 5 Nchi zilizo karibu nawe na zile zilizo mbali nawe zitakudhihaki,+ wewe ambaye jina lako si safi na ambaye umejaa msukosuko. 6 Tazama! Kila mkuu wa Israeli aliye miongoni mwako anatumia mamlaka yake kumwaga damu.+ 7 Ndani yako wanamdharau baba yao na mama yao.+ Wanampunja mkaaji mgeni, na kumtesa yatima na mjane.”’”+
8 “‘Unapadharau mahali pangu patakatifu, nawe unazitia unajisi sabato zangu.+ 9 Ndani yako kuna wachongezi wanaokusudia kumwaga damu.+ Ndani yako wanakula dhabihu milimani na kuendeleza mwenendo mchafu ndani yako.+ 10 Ndani yako wanakidharau kitanda cha baba yao,*+ nao wanamnajisi mwanamke asiye safi aliye katika hedhi.+ 11 Ndani yako mwanamume mmoja anatenda kwa njia inayochukiza na mke wa jirani yake,+ mwingine anamnajisi binti mkwe wake mwenyewe kwa mwenendo mchafu,+ na mwingine anamnajisi dada yake, binti ya baba yake mwenyewe.+ 12 Ndani yako wanapokea rushwa ili kumwaga damu.+ Unakopesha kwa riba+ au kwa faida,* nawe unachukua pesa kwa nguvu kutoka kwa majirani zako.+ Naam, umenisahau kabisa,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
13 “‘Tazama! Ninapiga makofi kwa kuwa nimechukizwa na faida isiyo ya haki ambayo umepata na kwa sababu ya matendo yako ya kumwaga damu yaliyo ndani yako. 14 Je, ujasiri* wako utadumu na mikono yako itaendelea kuwa imara katika siku nitakapokuchukulia hatua?+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema, nami nitachukua hatua. 15 Nitakutawanya miongoni mwa mataifa na kukutawanya katika nchi hizo,+ nami nitakomesha uchafu wako.+ 16 Nawe utadharauliwa na mataifa, na utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”+
17 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 18 “Mwana wa binadamu, watu wa nyumba ya Israeli wamekuwa kama takataka isiyo na thamani kwangu. Wote ni shaba na bati na chuma na risasi katika tanuru. Wamekuwa takataka ya fedha.+
19 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa kama takataka isiyo na thamani,+ ninawakusanya pamoja ndani ya Yerusalemu. 20 Kama watu wanavyokusanya fedha na shaba na chuma na risasi na bati katika tanuru ili kuyapulizia moto madini hayo na kuyayeyusha, ndivyo nitakavyowakusanya ninyi kwa hasira yangu na kwa ghadhabu yangu, nami nitawapuliza na kuwayeyusha.+ 21 Nitawakusanya na kuwapuliza kwa moto wa ghadhabu yangu,+ nanyi mtayeyushwa ndani yake.+ 22 Kama fedha inavyoyeyushwa katika tanuru, ndivyo mtakavyoyeyushwa ndani yake; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimewamwagia ghadhabu yangu.’”
23 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 24 “Mwana wa binadamu, iambie hivi nchi hiyo: ‘Wewe ni nchi ambayo haitasafishwa au kunyeshewa mvua katika siku ya ghadhabu. 25 Ndani yake manabii wake wamepanga njama,+ kama simba anayenguruma akirarua mawindo.+ Wanawanyafua watu. Wanachukua hazina na vitu vyenye thamani. Wamewafanya wengi kuwa wajane ndani yake. 26 Makuhani wake wamevunja sheria yangu,+ nao wanaendelea kupatia unajisi mahali pangu patakatifu.+ Hawatofautishi kati ya kitu kitakatifu na cha kawaida,+ hawawajulishi watu kisicho safi na kilicho safi,+ na wanakataa kushika sabato zangu, nami nimechafuliwa kati yao. 27 Wakuu wake walio kati yake ni kama mbwamwitu wanaorarua mawindo; wanamwaga damu na kuua watu* ili wapate faida isiyo ya haki.+ 28 Lakini manabii wake wamepiga lipu matendo yao kwa kutumia chokaa. Wanaona maono ya uwongo na kufanya uaguzi* wa uwongo,+ nao wanasema: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi,” wakati ambapo Yehova mwenyewe hajasema. 29 Watu wa nchi wamewapunja watu na kuwanyang’anya vitu vyao,+ wamewatesa wenye uhitaji na maskini, nao wamempunja mkaaji mgeni na kumnyima haki.’
30 “‘Nilikuwa nikitafuta kati yao mtu ambaye angeurekebisha ukuta wa mawe au asimame mbele yangu katika shimo ukutani kwa ajili ya nchi, ili nisiiangamize,+ lakini sikumpata yeyote. 31 Basi nitawamwagia ghadhabu yangu na kuwaangamiza kabisa kwa moto wa ghadhabu yangu. Nitawaletea madhara ya njia yao juu ya kichwa chao wenyewe,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
23 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, kulikuwa na wanawake wawili waliokuwa mabinti za mama mmoja.+ 3 Wakawa makahaba huko Misri;+ tangu ujana wao walifanya ukahaba. Huko matiti yao yalitomaswa, na vifua vyao vya ubikira vilipapaswa-papaswa. 4 Yule mkubwa aliitwa Ohola,* na dada yake Oholiba.* Wakawa wangu nao wakazaa wana na mabinti. Kuhusu majina yao, Ohola ni Samaria,+ na Oholiba ni Yerusalemu.
5 “Ohola akaanza kufanya ukahaba+ alipokuwa wangu. Aliwatamani kwa uchu wapenzi wake,+ majirani zake Waashuru.+ 6 Walikuwa magavana waliovaa mavazi ya bluu na watawala wasaidizi—wote walikuwa vijana wanaovutia waliopanda farasi wao. 7 Akaendelea kufanya ukahaba na wana wote bora wa Ashuru, naye akajichafua+ kwa sanamu zinazochukiza* za wale aliowatamani kwa uchu. 8 Hakuacha ukahaba aliofanya huko Misri, kwa maana walilala naye alipokuwa kijana, nao walipapasa-papasa kifua chake cha ubikira na kummwagia uchu wao.*+ 9 Basi nikamtia mikononi mwa wapenzi wake, wana wa Ashuru,+ ambao aliwatamani kwa uchu. 10 Waliufunua uchi+ wake na kuwakamata wanawe na mabinti zake,+ naye wakamuua kwa upanga. Akawa na sifa mbaya kati ya wanawake, nao wakatekeleza hukumu dhidi yake.
11 “Dada yake Oholiba alipoona jambo hilo, akawa na uchu mbaya zaidi, na ukahaba wake ulikuwa mbaya kuliko wa dada yake.+ 12 Aliwatamani kwa uchu majirani zake wana wa Ashuru,+ magavana na watawala wasaidizi waliovaa mavazi ya kifahari na waliopanda farasi—wote walikuwa vijana wanaovutia. 13 Alipojichafua, niliona kwamba wote wawili walikuwa wamefuata njia ileile.+ 14 Lakini alizidisha matendo yake ya ukahaba. Aliwaona wanaume waliochongwa ukutani, sanamu za Wakaldayo zilizochongwa na kupakwa rangi nyekundu, 15 wakiwa wamevaa mishipi kiunoni, na vilemba vikubwa kwenye vichwa vyao, nao walikuwa na sura kama za mashujaa, wote walifanana na Wababiloni, waliozaliwa katika nchi ya Wakaldayo. 16 Akaanza kuwatamani kwa uchu mara tu alipowaona, naye akawatuma wajumbe kwao huko Ukaldayo.+ 17 Basi wana wa Babiloni wakaendelea kuja kwenye kitanda chake cha mapenzi, nao wakamchafua kwa uchu wao.* Baada ya kuchafuliwa nao, akawaacha akiwa amechukizwa.
18 “Alipoendelea kufanya ukahaba kwa ushupavu na kufunua uchi wake,+ nilimwacha nikiwa nimechukizwa, kama nilivyomwacha dada yake nikiwa nimechukizwa.+ 19 Naye akaendelea kuzidisha matendo yake ya ukahaba,+ akizikumbuka siku za ujana wake alipofanya ukahaba nchini Misri.+ 20 Aliwatamani kwa uchu kama masuria wa wanaume ambao kiungo chao cha kiume ni kama cha punda na ambao viungo vyao vya uzazi ni kama vya farasi. 21 Ulitamani mwenendo wako mchafu uliokuwa nao ulipokuwa kijana kule Misri+ walipopapasa-papasa kifua chako, matiti ya ujana wako.+
22 “Kwa hiyo, ewe Oholiba, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ninawachochea wale waliokupenda+ ambao uliwaacha ukiwa umechukizwa, nami nitawaleta ili wakushambulie kutoka kila upande,+ 23 wana wa Babiloni+ na Wakaldayo+ wote, wanaume wa Pekodi+ na Shoa na Koa, pamoja na wana wote wa Ashuru. Wote ni vijana wanaovutia, magavana na watawala wasaidizi, mashujaa waliochaguliwa moja kwa moja,* wote wakiwa wamepanda farasi. 24 Watakushambulia kwa magari ya vita na magurudumu yenye kelele pamoja na umati mkubwa wa wanajeshi, pamoja na ngao kubwa na ngao ndogo* na kofia. Watajipanga kukuzunguka, nami nitawapa mamlaka ya kuhukumu, nao lazima wakuhukumu wapendavyo.+ 25 Nitakumwagia ghadhabu yangu, nao watakutendea kwa hasira kali. Watakata pua yako na masikio yako, na watu wako waliobaki watauawa kwa upanga. Watawachukua wana na mabinti zako, na watu wako wanaobaki watateketezwa kabisa kwa moto.+ 26 Watakuvua mavazi yako+ na kuchukua vito vyako* maridadi.+ 27 Nitaukomesha mwenendo wako mchafu na ukahaba wako+ ulioanza nchini Misri.+ Utaacha kuwatazama, na hutaikumbuka Misri tena.’
28 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko karibu kukutia mikononi mwa wale unaowachukia, wale uliowaacha ukiwa umechukizwa.+ 29 Watakutendea kwa chuki na kuchukua kila kitu ulichofanyia kazi kwa jasho+ nao watakuacha ukiwa uchi, bila chochote. Uchi unaoaibisha wa uasherati wako na mwenendo wako mchafu na ukahaba wako utafunuliwa.+ 30 Utatendewa mambo hayo kwa sababu uliyafuata mbio mataifa kama kahaba,+ kwa sababu ulijichafua kwa sanamu zao zinazochukiza.+ 31 Umeifuata njia ileile aliyoifuata dada yako,+ nami nitakiweka kikombe chake mkononi mwako.’+
32 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
‘Utakunywa kikombe kipana na chenye kina cha dada yako,+
Nawe utakuwa kitu cha kuchekwa na kudhihakiwa, na kikombe hicho kina mambo hayo kwa wingi.+
33 Utalemewa na* ulevi na huzuni,
Kikombe cha hofu na ukiwa,
Kikombe cha dada yako, Samaria.
34 Utalazimika kukinywa na kukimaliza kabisa+ na kuviguguna vigae vyake
Kisha utayang’oa matiti yako.
“Kwa maana mimi mwenyewe nimesema,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’
35 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa kuwa umenisahau nawe umenipuuza kabisa,*+ utapata madhara ya mwenendo wako mchafu na matendo yako ya ukahaba.’”
36 Kisha Yehova akaniambia: “Mwana wa binadamu, je, utatangaza hukumu dhidi ya Ohola na Oholiba+ na kuwaonyesha waziwazi mazoea yao yanayochukiza? 37 Wamefanya uzinzi,*+ na mikono yao ina damu. Hawajafanya uzinzi tu na sanamu zao zinazochukiza, bali pia wamewateketeza* motoni wana wao walionizalia, kama chakula cha sanamu zao.+ 38 Isitoshe, hili ndilo wamenifanyia: Walipatia unajisi mahali pangu patakatifu siku hiyo, nao wakazitia unajisi sabato zangu. 39 Baada ya kuwachinja wana wao kama dhabihu kwa sanamu zao zinazochukiza,+ walikuja mahali pangu patakatifu ili kupatia unajisi+ siku hiyohiyo. Hivyo ndivyo walivyofanya ndani ya nyumba yangu mwenyewe. 40 Hata walimtuma mjumbe ili awaite wanaume waje kutoka mbali.+ Walipokuwa wakija, ulioga na kujipaka rangi machoni na kujipamba kwa mapambo.+ 41 Nawe ukaketi kwenye kochi la kifahari+ ambalo mbele yake kuna meza iliyoandaliwa,+ na juu yake uliweka uvumba wangu+ na mafuta yangu.+ 42 Sauti ya umati wa watu waliostarehe ilisikika huko, na miongoni mwao kulikuwa na walevi walioletwa kutoka nyikani. Waliwavisha wanawake bangili kwenye mikono na mataji maridadi kwenye vichwa vyao.
43 “Ndipo nikasema kumhusu yule aliyechakazwa na uzinzi: ‘Sasa ataendelea kufanya ukahaba wake.’ 44 Basi wakaendelea kuingia kwake, kama mtu anavyoenda kwa kahaba. Hivyo ndivyo walivyoenda kwa Ohola na kwa Oholiba, wanawake wenye mwenendo mchafu. 45 Lakini watu waadilifu watamhukumu kwa hukumu ambayo uzinzi+ na umwagaji wa damu unastahili;+ kwa maana wao ni wanawake wazinzi na mikono yao ina damu.+
46 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Jeshi litaletwa liwashambulie na kuwafanya kuwa kitu cha kutisha na kitu cha kuporwa.+ 47 Jeshi hilo litawapiga mawe+ na kuwakatakata kwa panga zao. Watawaua wana wao na mabinti wao+ na kuziteketeza nyumba zao kwa moto.+ 48 Nitakomesha mwenendo wako mchafu nchini, na wanawake wote watajifunza somo nao hawataiga mwenendo wenu mchafu.+ 49 Watawaletea madhara ya mwenendo wenu mchafu na ya dhambi zenu kuhusiana na sanamu zenu zinazochukiza; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’”+
24 Neno la Yehova likanijia tena katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi ya mwezi huo, likisema: 2 “Mwana wa binadamu, andika tarehe hii,* siku hiihii ya leo. Mfalme wa Babiloni ameanza kulishambulia Yerusalemu siku hiihii ya leo.+ 3 Na useme methali* kuhusu nyumba ya uasi, sema hivi kuwahusu:
“‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Weka motoni chungu cha kupikia;* kiweke motoni na utie maji ndani yake.+
4 Weka vipande vya nyama ndani yake,+ kila kipande kizuri,
Paja na bega; kijaze kwa mifupa bora zaidi.
5 Chukua kondoo bora zaidi katika kundi,+ na urundike kuni chini ya chungu kuzunguka pande zote.
Chemsha vipande hivyo, na upike mifupa iliyo ndani yake.’”
6 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
‘Ole wake jiji la umwagaji wa damu,+ chungu cha kupikia chenye kutu, ambacho kutu yake haijaondolewa!
Toeni nyama ndani yake, kipande kwa kipande;+ msizipigie kura.
7 Kwa maana damu yake imo ndani yake;+ aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi.
Hakuimwaga ardhini, ili kuifunika kwa mavumbi.+
8 Ili kuchochea ghadhabu ya kulipiza kisasi,
Nimeiweka damu yake juu ya mwamba ulio wazi, unaong’aa
Ili isifunikwe.’+
9 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
‘Ole wake jiji linalomwaga damu!+
Nitarundika rundo kubwa la kuni.
10 Rundika kuni na uwashe moto,
Chemsha nyama kabisa, umwage mchuzi mzito, na uiache mifupa iungue.
11 Kiweke chungu kisicho na kitu kwenye makaa ili kiwe moto
Ili shaba yake iwe moto kabisa.
Uchafu wake utayeyuka ndani yake,+ na kutu yake itateketezwa.
12 Ni jambo linalokatisha tamaa na kuchosha,
Kwa maana kutu yake nyingi haitatoka.+
Kitupeni motoni pamoja na kutu yake!’
13 “‘Uchafu wako ulisababishwa na mwenendo wako mchafu.+ Nilijaribu kukusafisha lakini hungeweza kuwa safi kutokana na uchafu wako. Hutakuwa safi mpaka ghadhabu yangu dhidi yako itakapotulia.+ 14 Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema. Itatendeka. Nitatenda bila kujizuia, bila huruma, bila kughairi.+ Watakuhukumu kulingana na njia zako na matendo yako,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
15 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 16 “Mwana wa binadamu, kwa pigo moja niko karibu kumwondoa mpenzi wako kutoka kwako.+ Hupaswi kuomboleza;* wala hupaswi kulia wala kutokwa na machozi. 17 Lia kimyakimya kwa maumivu, wala usifanye desturi za kuwaombolezea waliokufa.+ Jifunge kilemba chako,+ na uvae viatu vyako.+ Hupaswi kufunika masharubu yako,*+ na usile mkate ulioletewa na watu wengine.”*+
18 Nami nikazungumza na watu asubuhi, na mke wangu akafa jioni. Basi asubuhi nikafanya kama nilivyoamriwa. 19 Watu walikuwa wakiniuliza: “Je, hutatuambia jinsi mambo haya unayofanya yanavyotuhusu?” 20 Nikawajibu: “Neno la Yehova limenijia likisema, 21 ‘Waambie watu wa nyumba ya Israeli, “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko karibu kupatia unajisi mahali pangu patakatifu,+ chanzo cha fahari yenu kubwa, kitu mnachokipenda sana na tamaa ya moyo wenu.* Wana na mabinti wenu mliowaacha watauawa kwa upanga.+ 22 Nanyi mtalazimika kufanya kama nilivyofanya. Hamtafunika masharubu yenu, nanyi hamtakula mkate mlioletewa na watu wengine.+ 23 Vilemba vyenu vitakuwa kwenye vichwa vyenu na viatu vyenu kwenye miguu yenu. Hamtaomboleza wala kulia. Badala yake mtaoza katika makosa yenu,+ na kila mmoja wenu atamlilia mwenzake kwa maumivu. 24 Ezekieli amekuwa ishara kwenu.+ Mtatenda kama alivyotenda. Jambo hilo litakapotukia, mtalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’”’”
25 “Nawe, mwana wa binadamu, siku nitakapoondoa ngome yao kutoka kwao—kitu maridadi kinachowaletea shangwe, kitu wanachokipenda sana, tamaa ya moyo wao*—pamoja na wana wao na mabinti wao,+ 26 utajulishwa jambo hilo na yule aliyeponyoka.+ 27 Siku hiyo utafungua kinywa chako na kuzungumza na yule aliyeponyoka, nawe hutakuwa tena bubu.+ Utakuwa ishara kwao, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”
25 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako kwa Waamoni,+ na utabiri dhidi yao.+ 3 Unapaswa kusema hivi kuhusu Waamoni, ‘Sikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Kwa sababu ulisema ‘Aha!’ dhidi ya mahali pangu patakatifu wakati palipotiwa unajisi, na dhidi ya nchi ya Israeli ilipofanywa ukiwa, na dhidi ya watu wa nyumba ya Yuda, walipopelekwa uhamishoni, 4 kwa hiyo, ninakutia mikononi mwa Watu wa Mashariki uwe mali yao. Watapiga kambi zao* ndani yako na kusimamisha mahema yao kati yako. Watakula matunda yako, na kunywa maziwa yako. 5 Nitalifanya jiji la Raba+ liwe malisho ya ngamia, na nchi ya Waamoni iwe mahali pa kupumzika kwa ajili ya mifugo; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’”
6 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ulipiga makofi+ na kupiga miguu yako chini nawe ukashangilia kwa dharau kubwa dhidi ya nchi ya Israeli,+ 7 kwa hiyo nitaunyoosha mkono wangu dhidi yako ili nikutie mikononi mwa mataifa uwe kitu cha kuporwa. Nitakukatilia mbali kutoka kati ya mataifa na kukuharibu kutoka katika nchi hizi.+ Nitakuangamiza, nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
8 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu watu wa Moabu+ na Seiri+ wamesema, “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama mataifa mengine yote,” 9 ninauacha wazi mpaka* wa Moabu kwenye majiji yake ya mpakani, uzuri wa* nchi yake, Beth-yeshimothi, Baal-meoni, hadi Kiriathaimu.+ 10 Nitaitoa pamoja na Waamoni kuwa mali ya watu wa Mashariki,+ ili Waamoni wasikumbukwe kati ya mataifa.+ 11 Nami nitatekeleza hukumu katika Moabu,+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
12 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nchi ya Edomu imelipiza kisasi dhidi ya nyumba ya Yuda nayo imepata hatia kubwa kwa kulipiza kisasi dhidi yake;+ 13 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Pia nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya Edomu na kuwaangamiza wanadamu na wanyama waliomo, nami nitaifanya kuwa ukiwa.+ Kuanzia Temani mpaka Dedani, watauawa kwa upanga.+ 14 ‘Nitalipiza kisasi dhidi ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Waisraeli.+ Watawaletea watu wa Edomu hasira yangu na ghadhabu yangu, ili wapatwe na kisasi changu mwenyewe,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”’
15 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ya chuki yao isiyo na mwisho, Wafilisti wamejaribu kwa nia ovu* kulipiza kisasi na kuleta maangamizi.+ 16 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ninaunyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti,+ nami nitawakatilia mbali Wakerethi+ na kuwaangamiza wakaaji wanaobaki wa pwani ya bahari.+ 17 Nitatekeleza matendo makubwa ya kisasi dhidi yao kwa adhabu kali, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoleta kisasi changu dhidi yao.”’”
26 Katika mwaka wa 11, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Yehova lilinijia likisema: 2 “Mwana wa binadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu,+ ‘Aha! Lango la mataifa limevunjwa!+ Kila kitu kitakuja kwangu, nami nitakuwa tajiri kwa sababu ameangamizwa’; 3 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko dhidi yako, Ee Tiro, nami nitayainua mataifa mengi dhidi yako, kama vile bahari inavyoinua mawimbi yake. 4 Wataziharibu kuta za Tiro na kuibomoa minara yake,+ nami nitakwangua udongo na kumfanya awe mwamba ulio wazi, unaong’aa. 5 Atakuwa uwanja wa kukaushia nyavu za kukokotwa katikati ya bahari.’+
“‘Kwa maana mimi mwenyewe nimesema,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘naye ataporwa na mataifa. 6 Na vijiji vyake* vilivyo mashambani vitachinjwa kwa upanga, na watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
7 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ninamleta Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni dhidi ya Tiro kutoka kaskazini;+ yeye ni mfalme wa wafalme,+ akiwa na farasi,+ magari ya vita,+ wapanda farasi, na jeshi lenye wanajeshi* wengi. 8 Ataviangamiza kwa upanga vijiji vyako vilivyo mashambani, naye atajenga ukuta wa kuzingira na kujenga dhidi yako boma la kuzingira na kuinua ngao kubwa dhidi yako. 9 Ataponda kuta zako kwa mtambo wake wa kubomolea,* na kubomoa minara yako kwa mashoka yake.* 10 Farasi wake watakuwa wengi sana hivi kwamba watakufunika kwa mavumbi, na sauti ya wapanda farasi, magurudumu, na magari ya vita itafanya kuta zako zitikisike anapoingia kwenye malango yako, kama wanaume wanaovamia jiji lenye kuta zilizobomolewa. 11 Kwato za farasi wake zitakanyaga-kanyaga barabara zako zote;+ atawaua watu wako kwa upanga, na nguzo zako kubwa zitaporomoka ardhini. 12 Wataiba mali zako, watapora bidhaa zako,+ watabomoa kuta zako, na kubomoa nyumba zako nzuri; kisha watayatupa mawe yako na mbao zako na udongo wako katika maji.’
13 “‘Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na sauti ya vinubi vyako haitasikika tena.+ 14 Nami nitakufanya uwe jiwe lililo wazi, linalong’aa, nawe utakuwa uwanja wa kukaushia nyavu za kukokotwa.+ Hutajengwa tena kamwe, kwa maana mimi mwenyewe, Yehova, nimesema,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
15 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anamwambia Tiro hivi: ‘Je, visiwa havitatetemeka vitakaposikia sauti ya kuanguka kwako, wanaokaribia kufa* watakapokuwa wakilia kwa maumivu makali, na uchinjaji utakapokuwa ukiendelea ndani yako?+ 16 Wakuu wote wa bahari hakika watashuka kutoka kwenye viti vyao vya ufalme na kuvua kanzu zao* na mavazi yao yaliyotariziwa, nao wataanza* kutetemeka. Wataketi chini na kuendelea kutetemeka na kukuangalia kwa mshangao.+ 17 Nao watakuimbia wimbo wa huzuni*+ na kukuambia:
“Jinsi ulivyoangamia,+ wewe uliyekuwa na wakaaji kutoka baharini, jiji lililosifiwa;
Wewe na wakaaji wako mlikuwa wenye nguvu baharini,+
Ukieneza hofu kwa wakaaji wote wa dunia!
18 Visiwa vitatetemeka siku utakapoanguka,
Visiwa vya bahari vitakuwa na wasiwasi utakapoondoka.”’+
19 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitakapokufanya ukiwa kama majiji yasiyokaliwa, nitakapokulemea kwa mawimbi makubwa nawe ufunikwe kwa maji mengi,+ 20 nitakushusha wewe pamoja na wale wanaoshuka shimoni,* kwa watu wa zamani za kale; nitakufanya ukae mahali pa chini zaidi, kama mahali pa zamani palipoachwa ukiwa, pamoja na wale wanaoshuka shimoni,+ ili usikaliwe. Kisha nitaitukuza* nchi ya walio hai.
21 “‘Nitakuletea hofu ya ghafla, nawe hutakuwapo tena.+ Watakutafuta, lakini hutapatikana tena kamwe,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
27 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Nawe, mwana wa binadamu, mwimbie Tiro wimbo wa huzuni,*+ 3 nawe umwambie Tiro,
‘Wewe unayekaa katika malango ya bahari,
Mfanyabiashara wa mataifa ya visiwa vingi,
Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Ee Tiro, wewe mwenyewe umesema, ‘Nina urembo mkamilifu.’+
4 Maeneo yako yamo katikati ya bahari,
Na wajenzi wako wameukamilisha urembo wako.
5 Walitengeneza mbao zako zote kutokana na miberoshi ya Seniri,+
Nao waliuchukua mwerezi kutoka Lebanoni ili kukutengenezea mlingoti.
6 Walitengeneza makasia yako kutokana na mialoni ya Bashani,
Na omo yako ilitengenezwa kwa mvinje na kupambwa ndani kwa pembe za tembo kutoka visiwa vya Kitimu.+
7 Kitani chenye rangi mbalimbali kutoka Misri ndicho kilichokuwa tanga lako,
Na sitaha yako ilifunikwa kwa nyuzi za bluu na sufu ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.+
8 Wakaaji wa Sidoni na Arvadi+ walikuwa wapiga makasia wako.
Watu wako mwenyewe wenye ustadi, Ee Tiro, walikuwa mabaharia wako.+
9 Wanaume wa Gebali+ wenye uzoefu* na ustadi waliziba nyufa zako kwa kalafati.+
Meli zote za baharini na wanamaji wake walikuja kwako kubadilishana bidhaa.
10 Wanaume wa Uajemi, Ludi, na Putu+ walikuwa katika jeshi lako, wanaume wako wa vita.
Walitundika ngao na kofia zao ndani yako, nao walikuletea fahari.
11 Wanaume wa Arvadi katika jeshi lako walisimama juu ya kuta zako pande zote,
Na wanaume jasiri walilinda minara yako.
Walitundika ngao zao za mviringo kuzunguka kuta zako
Nao wakaukamilisha urembo wako.
12 “‘“Watu wa Tarshishi+ walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mwingi.+ Walibadilisha fedha, chuma, bati, na risasi kwa ajili ya bidhaa zako.+ 13 Watu wa Yavani, Tubali,+ na Mesheki+ walifanya nawe biashara, wakibadilisha watumwa+ na vitu vya shaba kwa ajili ya bidhaa zako. 14 Watu wa nyumba ya Togarma+ walibadilisha farasi na farasi wa vita na nyumbu kwa ajili ya bidhaa zako. 15 Watu wa Dedani+ walifanya nawe biashara; uliwaajiri wafanyabiashara kwenye visiwa vingi; walitoa pembe za tembo+ na mbao za mpingo kama ushuru wako. 16 Watu wa Edomu walifanya biashara nawe kwa sababu ya wingi wa bidhaa zako. Walitoa feruzi, sufu ya zambarau, vitambaa vyenye rangi mbalimbali vilivyotariziwa, vitambaa bora, marijani, na zabarijadi ili kubadilishana na bidhaa zako.
17 “‘“Watu wa Yuda na wa nchi ya Israeli walifanya nawe biashara, wakitoa ngano ya Minithi,+ vyakula bora, asali,+ mafuta, na zeri+ ili kubadilishana na bidhaa zako.+
18 “‘“Watu wa Damasko+ walifanya nawe biashara kwa sababu ya wingi wa bidhaa zako na utajiri wako wote, wakibadilishana divai ya Helboni na sufu ya Zahari.* 19 Watu wa Vedani na Yavani kutoka Uzali walitoa chuma kilichofuliwa, kida,* na kane* ili kubadilishana na bidhaa zako. 20 Watu wa Dedani+ walifanya nawe biashara kwa kukupa matandiko ya farasi.* 21 Uliwaajiri Waarabu na wakuu wote wa Kedari,+ waliokuwa wafanyabiashara wa wanakondoo na kondoo dume na mbuzi.+ 22 Wafanyabiashara wa Sheba na Raama+ walibadilishana nawe bidhaa; walitoa kila aina ya manukato bora, mawe yenye thamani, na dhahabu, ili kubadilishana na bidhaa zako.+ 23 Watu wa Harani,+ Kane, Edeni,+ wafanyabiashara wa Sheba,+ Asihuru,+ na Kilmadi walibadilishana nawe bidhaa. 24 Katika soko lako walibadilishana nawe mavazi maridadi, majoho yaliyotengenezwa kwa kitambaa cha bluu na vitambaa vyenye rangi mbalimbali vilivyotariziwa, na mazulia ya rangi mbalimbali, yote yakiwa yamefungwa kabisa kwa kamba.
25 Meli za Tarshishi+ zilisafirisha bidhaa zako katika misafara,
Hivi kwamba ukajaa na kulemewa na mzigo* katikati ya bahari kuu.
26 Wapiga makasia wako wamekuleta katika bahari kuu;
Upepo wa mashariki umekuvunjavunja katikati ya bahari kuu.
27 Utajiri wako, bidhaa zako, mali zako, wanamaji wako, na mabaharia wako,
Wale wanaoziba nyufa zako kwa kalafati, wale wanaofanya biashara ya kubadilishana bidhaa zako,+ na wanaume wote wa vita+
—Umati wote ulio* ndani yako—
Wote watazama katikati ya bahari kuu siku utakayoanguka.+
28 Mabaharia wako watakapolia kwa sauti, maeneo ya pwani yatatetemeka.
29 Wapiga makasia wote, wanamaji, na mabaharia
Watashuka kutoka kwenye meli zao na kusimama kwenye nchi kavu.
30 Watapaza sauti zao na kukulilia kwa uchungu+
Huku wakijirushia mavumbi vichwani na kugaagaa kwenye majivu.
31 Watajitia upara na kuvaa nguo za magunia;
Watakulilia kwa uchungu* na kukuombolezea sana.
32 Katika maombolezo yao watakuimbia wimbo wa huzuni na kukuombolezea wakisema:
‘Ni nani aliye kama Tiro, ambaye sasa amenyamazishwa katikati ya bahari?+
33 Bidhaa zako zilipofika kutoka kwenye bahari kuu, uliyashibisha mataifa mengi.+
Utajiri wako mwingi na bidhaa zako ziliwatajirisha wafalme wa dunia.+
34 Sasa umevunjwavunjwa katika bahari kuu, katika vilindi vya bahari,+
Na bidhaa zako zote na watu wako wamezama pamoja nawe.+
35 Wakaaji wote wa visiwani watakutazama kwa mshangao,+
Nao wafalme wao watatetemeka kwa hofu+—nyuso zao zitakuwa na wasiwasi.
36 Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa watapiga mluzi kwa sababu ya yale yatakayokupata.
Mwisho wako utafika ghafla nao utakuwa mbaya sana,
Nawe hutakuwapo tena kamwe.’”’”+
28 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, mwambie kiongozi wa Tiro, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Kwa sababu moyo wako umekuwa na majivuno,+ unaendelea kusema, ‘Mimi ni mungu.
Ninaketi kwenye kiti cha ufalme cha mungu katikati ya bahari.’+
Lakini wewe ni mwanadamu tu, wewe si mungu,
Ingawa moyoni mwako unahisi kwamba wewe ni mungu.
3 Tazama! Una hekima kuliko Danieli.+
Hujafichwa siri yoyote.
4 Umejitajirisha kwa hekima yako na utambuzi wako,
Nawe unaendelea kukusanya dhahabu na fedha katika hazina zako.+
5 Ustadi wako katika biashara ulikuletea utajiri mwingi,+
Nao moyo wako ukawa na majivuno kwa sababu ya utajiri wako.”’
6 “‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Kwa sababu katika moyo wako unahisi wewe ni mungu,
7 Ninawaleta wageni wakushambulie, walio wakatili zaidi kati ya mataifa,+
Nao watachomoa panga zao na kuuharibu uzuri wa hekima yako
Na kuitia unajisi fahari yako yenye utukufu.+
Nawe utakufa kifo cha kikatili katikati ya bahari kuu.+
9 Je, bado utamwambia yule anayekuua, ‘Mimi ni mungu?’
Utakuwa mwanadamu tu, wala si mungu, mikononi mwa wale wanaokutia unajisi.”’
10 “‘Kwa mkono wa wageni, utakufa kifo cha watu ambao hawajatahiriwa,
Kwa maana mimi mwenyewe nimesema,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
11 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 12 “Mwana wa binadamu, mwimbie mfalme wa Tiro wimbo wa huzuni,* nawe umwambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Ulikuwa mfano wa ukamilifu,*
Ulijaa hekima+ nawe ulikuwa na urembo mkamilifu.+
13 Ulikuwa katika Edeni, bustani ya Mungu.
Ulipambwa kwa kila jiwe lenye thamani
—Zabarijadi, topazi, na yaspi;
krisolito, shohamu, na yashefi; yakuti, feruzi,+ na zumaridi;
Na vifuko na vishikizi vyake vilikuwa vya dhahabu.
Vilitayarishwa siku uliyoumbwa.
14 Nilikuweka kuwa kerubi anayefunika aliyetiwa mafuta.
Ulikuwa kwenye mlima mtakatifu wa Mungu,+ nawe ulitembea-tembea kati ya mawe yenye moto.
15 Hukuwa na kosa katika njia zako tangu siku uliyoumbwa
Mpaka uovu* ulipopatikana ndani yako.+
16 Kwa sababu ya biashara zako nyingi,+
Ulijaa ukatili, nawe ukaanza kutenda dhambi.+
Basi nitakufukuza kutoka kwenye mlima wa Mungu kama kitu kilicho najisi na kukuangamiza,+
Mbali kutoka kwenye mawe ya moto, ewe kerubi unayefunika.
17 Moyo wako ulikuwa na majivuno kwa sababu ya urembo wako.+
Uliipotosha hekima yako kwa sababu ya fahari yako yenye utukufu.+
Nitakutupa chini duniani.+
Nitakufanya uwe kitu cha kutazamwa na wafalme.
18 Kwa sababu ya hatia yako kubwa na ukosefu wako wa unyoofu katika biashara, umepatia unajisi mahali pako patakatifu.
Nitatokeza moto katikati yako, nao utakuteketeza kabisa.+
Nitakufanya uwe majivu juu ya dunia mbele ya wote wanaokutazama.
19 Wale wote waliokujua kati ya mataifa watakutazama kwa mshangao.+
Mwisho wako utafika ghafla nao utakuwa mbaya sana,
Hutakuwapo tena kamwe.”’”+
20 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 21 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako Sidoni,+ nawe utabiri dhidi yake. 22 Nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Niko dhidi yako, Ee Sidoni, nami nitatukuzwa katikati yako;
Na watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapotekeleza hukumu dhidi yake na kutakaswa ndani yake.
23 Nitapeleka ugonjwa hatari humo na damu itatiririka kwenye barabara zake.
Waliouawa wataanguka katikati yake upanga utakapokuja kumshambulia kutoka kila upande;
Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+
24 “‘“Na watu wa nyumba ya Israeli hawatazungukwa tena na michongoma inayodhuru na miiba mikali,+ wale wanaowadhihaki; na watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”’
25 “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitakapowakusanya tena watu wa nyumba ya Israeli kutoka miongoni mwa mataifa walikotawanywa,+ nitatakaswa kati yao machoni pa mataifa.+ Nao watakaa katika nchi yao+ niliyompa mtumishi wangu Yakobo.+ 26 Wataishi huko kwa usalama+ na watajenga nyumba na kupanda mashamba ya mizabibu+ na watakaa kwa usalama nitakapotekeleza hukumu dhidi ya wote wanaowazunguka ambao wanawadhihaki;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao.”’”
29 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya 12 ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia likisema: 2 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako kwa Farao mfalme wa Misri, na utabiri dhidi yake na dhidi ya nchi yote ya Misri.+ 3 Sema maneno haya: ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Niko dhidi yako, Farao mfalme wa Misri,+
Mnyama mkubwa sana wa baharini anayelala kati ya vijito vya mto wake Nile,*+
Ambaye amesema, ‘Mto wangu Nile ni wangu.
Niliutengeneza kwa ajili yangu.’+
4 Lakini nitatia kulabu katika mataya yako na kufanya samaki wa mto wako Nile washikamane na magamba yako.
Nitakutoa katika mto wako Nile pamoja na samaki wa mto wako Nile wanaoshikamana na magamba yako.
5 Nitakuacha jangwani, wewe na samaki wote wa mto wako Nile.
Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa wala kuokotwa.+
Nitakufanya uwe chakula cha wanyama wa mwituni wa dunia na ndege wa angani.+
6 Ndipo wakaaji wote wa Misri watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,
Kwa sababu kwa watu wa nyumba ya Israeli walikuwa kama unyasi* tu, hawakuwategemeza.+
7 Walipokushika mkono, ulipondwa,
Nawe ukafanya wavunjike bega.
Walipojitegemeza kwako, ulivunjika,
Nawe ukafanya miguu yao ipepesuke.”*+
8 “‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ninaleta upanga ukushambulie,+ nami nitamwangamiza mwanadamu na mnyama kutoka ndani yako. 9 Nchi ya Misri itakuwa ukiwa na mahali palipoharibiwa;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, kwa maana umesema,* ‘Mto Nile ni wangu; mimi ndiye niliyeutengeneza.’+ 10 Basi niko dhidi yako na dhidi ya mto wako Nile, nami nitaifanya nchi ya Misri iwe mahali palipoharibiwa na palipokauka, mahame na ukiwa,+ kutoka Migdoli+ hadi Siene+ hadi kwenye mpaka wa Ethiopia. 11 Hakuna mwanadamu wala mnyama wa kufugwa atakayepitia humo kwa miguu,+ nayo haitakaliwa kwa miaka 40. 12 Nitaifanya nchi ya Misri iwe nchi yenye ukiwa kuliko nchi zote, na majiji yake yatakuwa majiji yenye ukiwa kuliko majiji yote kwa miaka 40;+ nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali.”+
13 “‘Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Baada ya miaka 40 nitawakusanya Wamisri kutoka katika mataifa ambako walitawanywa;+ 14 Wamisri waliotekwa nitawarudisha katika nchi ya Pathrosi,+ katika nchi waliyozaliwa, na huko watakuwa ufalme duni. 15 Misri itakuwa chini kuliko zile falme nyingine nayo haitayatawala tena yale mataifa mengine,+ nitawafanya wawe wadogo sana hivi kwamba hawataweza kuyatiisha mataifa mengine.+ 16 Nchi ya Misri haitakuwa tena tegemeo kwa watu wa nyumba ya Israeli,+ bali itawakumbusha tu kosa walilofanya kwa kutafuta msaada kutoka kwa Wamisri. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”’”
17 Sasa katika mwaka wa 27, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia likisema: 18 “Mwana wa binadamu, Mfalme Nebukadneza*+ wa Babiloni aliamuru jeshi lake lifanye kazi kubwa ya kushambulia Tiro.+ Kila kichwa kilitiwa upara, na kila bega lilisuguliwa na kuchubuka ngozi. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kwa ajili ya kazi kubwa aliyofanya ya kuishambulia Tiro.
19 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ninampa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni nchi ya Misri,+ naye atabeba utajiri wake na kuchukua nyara kwa wingi na kuipora; na vitu hivyo vitakuwa malipo ya jeshi lake.’
20 “‘Kama malipo ya kazi kubwa aliyofanya ya kushambulia Tiro, nitampa nchi ya Misri kwa sababu walitenda kwa ajili yangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
21 “Siku hiyo nitaichipusha pembe kwa ajili ya watu wa nyumba ya Israeli,*+ nami nitakupa* nafasi ya kuzungumza kati yao; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”
30 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, tabiri, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Ombolezeni, ‘Ole, ile siku inakuja!’
3 Kwa maana siku hiyo iko karibu, naam, siku ya Yehova iko karibu.+
Itakuwa siku ya mawingu,+ wakati uliowekwa wa mataifa.+
4 Upanga utaishambulia Misri, na Ethiopia itakumbwa na hofu wakati waliouawa watakapoanguka huko Misri;
Utajiri wake umechukuliwa na misingi yake imebomolewa kabisa.+
5 Ethiopia,+ Putu,+ Ludi na watu wote wa mataifa mbalimbali,*
Na Kubu, pamoja na wana wa nchi ya agano,*
Wote watauawa kwa upanga.”’
6 Yehova anasema hivi:
‘Wale wanaoiunga mkono Misri wataangamia pia,
Na nguvu zake zenye kiburi zitashushwa.’+
“‘Kuanzia Migdoli+ mpaka Siene+ watauawa kwa upanga nchini,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 7 ‘Watafanywa kuwa nchi yenye ukiwa zaidi, na majiji yake yatakuwa majiji yaliyoharibiwa kabisa.+ 8 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapowasha moto huko Misri na wote walioungana naye watakapopondwa. 9 Siku hiyo nitawatuma wajumbe katika meli ili kuifanya Ethiopia inayojitumaini itetemeke; watashikwa na hofu katika siku hiyo inayokuja dhidi ya Misri, kwa maana hakika itakuja.’
10 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitauangamiza umati wa Misri kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni.+ 11 Yeye na wanajeshi wake, taifa katili zaidi kati ya mataifa,+ wataletwa ili kuiangamiza nchi. Watachomoa panga zao na kuishambulia Misri na kuijaza nchi watu waliouawa.+ 12 Nitaigeuza mifereji ya Nile+ iwe nchi kavu na kuiuza nchi mikononi mwa watu waovu. Nitaifanya nchi na kila kitu kilichomo kiwe ukiwa kwa mkono wa wageni.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’
13 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitaziangamiza pia sanamu zinazochukiza* na kuiharibu miungu ya ubatili ya Nofu.*+ Hakutakuwa tena na mkuu* anayetoka katika nchi ya Misri, nami nitaweka hofu katika nchi ya Misri.+ 14 Nitalifanya jiji la Pathrosi+ liwe ukiwa na kuwasha moto katika jiji la Soani na kutekeleza hukumu dhidi ya jiji la No.*+ 15 Nitalimwagia ghadhabu yangu jiji la Sini, ngome ya Misri, na kuwaangamiza wakaaji wa jiji la No. 16 Nitawasha moto nchini Misri; na jiji la Sini litashikwa na hofu na jiji la No litapenywa kwa nguvu na Nofu* litashambuliwa kweupe kabisa wakati wa mchana! 17 Wanaume vijana wa Oni* na Pibesethi watauawa kwa upanga, na majiji yatapelekwa utekwani. 18 Kule Tehafnehesi mchana utakuwa na giza nitakapovunja nira za Misri huko.+ Nguvu zake zenye kiburi zitakwisha,+ mawingu yatamfunika, na miji yake itapelekwa utekwani.+ 19 Nitatekeleza hukumu dhidi ya Misri, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”
20 Na katika mwaka wa 11, mwezi wa kwanza, siku ya saba ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia likisema: 21 “Mwana wa binadamu, nimeuvunja mkono wa mfalme Farao wa Misri; hautafungwa upone au kufungwa kwa kitambaa uwe na nguvu za kushika upanga.”
22 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko dhidi ya mfalme Farao wa Misri,+ nami nitaivunja mikono yake, mkono wenye nguvu na ule uliovunjika,+ nami nitaufanya upanga uanguke kutoka mkononi mwake.+ 23 Kisha nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali.+ 24 Nitaitia nguvu mikono ya* mfalme wa Babiloni+ na kuutia upanga wangu mkononi mwake,+ nami nitaivunja mikono ya Farao, naye atalia kwa sauti na kwa maumivu makali kama mtu anayekufa mbele yake.* 25 Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babiloni, lakini mikono ya Farao italegea; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babiloni naye aunyooshe dhidi ya nchi ya Misri.+ 26 Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali,+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”
31 Katika mwaka wa 11, mwezi wa tatu, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia likisema: 2 “Mwana wa binadamu, mwambie mfalme Farao wa Misri na umati wake,+
‘Unafanana na nani katika ukuu wako?
3 Kulikuwa na Mwashuru, mwerezi kule Lebanoni,
Uliokuwa na matawi maridadi kama kichaka chenye kivuli, na uliokuwa mrefu,
Kilele chake kilikuwa mawinguni.
4 Maji yaliufanya uwe mkubwa, chemchemi zenye maji mengi ziliufanya uwe mrefu.
Vijito vilizunguka mahali ulipopandwa;
Mifereji yake iliinywesha maji miti yote ya shambani.
5 Ndiyo sababu ulikuwa mrefu kuliko miti mingine yote ya shambani.
Na vitawi vyake viliongezeka, na matawi yake yakawa marefu
Kwa sababu ya maji mengi ya vijito vyake.
6 Ndege wote wa angani walitengeneza viota kwenye vitawi vyake,
Wanyama wote wa mwituni walizaa chini ya matawi yake,
Na mataifa yote yenye watu wengi yaliishi chini ya kivuli chake.
7 Ukapendeza katika uzuri na urefu wa matawi yake,
Kwa maana mizizi yake ilipenya chini kwenye maji mengi.
8 Hakuna mwerezi mwingine katika bustani ya Mungu+ uliofanana nao.
Hakuna mberoshi uliokuwa na vitawi kama vyake,
Na hakuna mwaramoni uliokuwa na matawi yaliyofanana na yake.
Hakuna mti mwingine katika bustani ya Mungu uliokaribia uzuri wake.
9 Niliufanya upendeze, kwa majani mengi,
Na miti mingine yote ya Edeni, bustani ya Mungu wa kweli, iliuonea wivu.’
10 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ulikuwa* mrefu sana, ukainua kilele chake mawinguni, nao moyo wake ukawa na kiburi kwa sababu ya kimo chake, 11 nitautia mikononi mwa mtawala mwenye nguvu wa mataifa.+ Hakika atauadhibu, nami nitaukataa kwa sababu ya uovu wake. 12 Na wageni, wakatili zaidi kati ya mataifa, wataukata, nao watauacha milimani, nayo majani yake yataanguka katika mabonde yote, na matawi yake yatavunjika na kusambaa katika vijito vyote vya nchi.+ Mataifa yote ya dunia yataondoka kwenye kivuli chake na kuuacha. 13 Ndege wote wa angani wataishi kwenye shina lake lililoanguka, na wanyama wote wa mwituni kwenye matawi yake.+ 14 Itakuwa hivyo ili mti wowote ulio karibu na maji usiwe mrefu sana au usiinue kilele chake mawinguni na kusiwe na mti ulionyweshwa maji mengi utakaofikia kimo chao. Kwa maana miti yote itatiwa mikononi mwa kifo, kwenye nchi iliyo chini, pamoja na wana wa binadamu, wanaoshuka shimoni.’*
15 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Siku utakaposhuka kuingia Kaburini* nitasababisha maombolezo. Kwa hiyo, nitayafunika maji yenye kina na kuvizuia vijito vyake ili maji yake mengi yazuiwe. Nitatia giza Lebanoni kwa sababu yake, nayo miti yote ya shambani itanyauka. 16 Nitayafanya mataifa yatetemeke kwa sauti ya kuanguka kwake nitakapoushusha Kaburini* pamoja na wote wanaoshuka shimoni,* na miti yote ya Edeni,+ miti iliyo bora na iliyo mizuri kabisa ya Lebanoni, miti yote iliyonyweshwa maji mengi, itafarijiwa katika nchi iliyo chini. 17 Wameshuka Kaburini* pamoja naye, kwa wale waliouawa kwa upanga,+ pamoja na wale waliomsaidia* ambao waliishi katika kivuli chake kati ya mataifa.’+
18 “‘Ni mti gani katika Edeni uliofanana nawe kwa utukufu na ukuu?+ Lakini kwa hakika utashushwa pamoja na miti ya Edeni katika nchi iliyo chini. Utalala kati ya wale ambao hawajatahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Itakuwa hivyo kwa Farao na umati wake wote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
32 Na katika mwaka wa 12, mwezi wa 12, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, mwimbie wimbo wa huzuni* mfalme Farao wa Misri, nawe umwambie,
‘Ulikuwa kama mwanasimba* mwenye nguvu wa mataifa,
Lakini umenyamazishwa.
Ulikuwa kama mnyama mkubwa sana wa baharini,+ ukitibua maji katika mito yako,
Ukivuruga maji kwa miguu yako na kuchafua mito.’*
3 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
‘Nitautumia umati wa mataifa mengi kutandaza wavu wangu juu yako,
Nao watakukokota katika wavu wangu wa kukokotwa.
4 Nitakuacha nchini;
Nitakutupa uwanjani.
Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako,
Nami nitawashibisha wanyama wa mwituni wa dunia nzima kwa nyama yako.+
5 Nitaitupa nyama yako juu ya milima
Na kuyajaza mabonde mabaki yako.+
6 Nitailowesha nchi kwa damu yako inayobubujika, mpaka juu ya milima,
Nayo itajaa kwenye vijito.’*
7 ‘Na utakapozimwa nitazifunika mbingu na kuzitia giza nyota zake.
Nitalifunika jua kwa mawingu,
Na mwezi hautatoa nuru yake.+
8 Kwa sababu yako, nitaitia giza mianga yote inayong’aa mbinguni,
Nami nitaifunika nchi yako kwa giza,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
9 ‘Nitaitaabisha mioyo ya mataifa mengi nitakapowapeleka watu wako waliotekwa katika mataifa mengine,
Katika nchi ambazo huzijui.+
10 Nitayafanya mataifa mengi yashikwe na hofu,
Na wafalme wao watatetemeka kwa woga kwa sababu yako nitakapoutikisa upanga wangu mbele yao.
Wataendelea kutetemeka, kila mmoja akihofia uhai wake,
Siku utakayoanguka.’
11 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
‘Upanga wa mfalme wa Babiloni utakushambulia.+
12 Nitaufanya umati wako uuawe kwa panga za mashujaa hodari,
Walio wakatili zaidi kati ya mataifa, wote.+
Watashusha chini kiburi cha Misri, na umati wake wote utaangamizwa.+
13 Nitaiangamiza mifugo yake yote kando ya maji yake mengi,+
Na hakuna mguu wa mwanadamu au ukwato wa mnyama wa kufugwa utakaoyachafua tena.’+
14 ‘Wakati huo nitayasafisha kabisa maji yao,
Nami nitafanya mito yao itiririke kama mafuta,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
15 ‘Nitakapoifanya nchi ya Misri iwe mahame na ukiwa, nchi iliyoporwa vitu vyote vilivyoijaza,+
Nitakapowaua wakaaji wote walio ndani yake,
Watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+
16 Huu ni wimbo wa huzuni, na hakika watu watauimba;
Mabinti wa mataifa watauimba.
Wataiimbia nchi ya Misri na umati wake wote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
17 Kisha katika mwaka wa 12, siku ya 15 ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia likisema: 18 “Mwana wa binadamu, uombolezee umati wa Misri nawe umshushe kwenye nchi iliyo chini, yeye na mabinti wa mataifa yenye nguvu, pamoja na wale wanaoshuka chini shimoni.*
19 “‘Unamzidi nani kwa urembo? Shuka chini, ulale na watu ambao hawajatahiriwa!’
20 “‘Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga.+ Ametiwa mikononi mwa upanga; mkokote pamoja na umati wake wote.
21 “‘Kutoka kwenye vina vya Kaburi* mashujaa hodari zaidi watazungumza naye na wasaidizi wake. Hakika watashuka chini na kulala kama watu ambao hawajatahiriwa, waliouawa kwa upanga. 22 Ashuru yuko huko pamoja na umati wake wote. Makaburi yao yamemzunguka, wote wameuawa kwa upanga.+ 23 Makaburi yake yamo katika vina vya shimo,* na umati wake umezunguka kaburi lake, wote wameuawa kwa upanga, kwa sababu walisababisha hofu katika nchi ya walio hai.
24 “‘Elamu+ yuko huko pamoja na umati wake wote kulizunguka kaburi lake, wote wakiwa wameuawa kwa upanga. Wameshuka chini bila kutahiriwa katika nchi iliyo chini, wale waliosababisha hofu katika nchi ya walio hai. Sasa watabeba aibu yao pamoja na wale wanaoshuka chini shimoni.* 25 Wamemtengenezea kitanda kati ya watu waliouawa, pamoja na umati wake wote kuzunguka makaburi yake. Wote hawajatahiriwa, na waliuawa kwa upanga, kwa sababu walisababisha hofu katika nchi ya walio hai; nao watabeba aibu yao pamoja na wale wanaoshuka chini shimoni.* Amewekwa miongoni mwa wale waliouawa.
26 “‘Watu wa Mesheki na Tubali+ na umati wao* wote wako huko. Makaburi yao yamemzunguka. Wote hawajatahiriwa, wamechomwa kwa upanga, kwa sababu walisababisha hofu katika nchi ya walio hai. 27 Je, hawatalala pamoja na mashujaa hodari waliouawa ambao hawajatahiriwa, ambao walishuka Kaburini* wakiwa na silaha zao za vita? Nao wataweka panga zao chini ya vichwa vyao* na dhambi zao kwenye mifupa yao, kwa sababu mashujaa hawa hodari walisababisha hofu katika nchi ya walio hai. 28 Lakini wewe, utapondwa miongoni mwa watu ambao hawajatahiriwa, nawe utalala pamoja na wale waliouawa kwa upanga.
29 “‘Edomu+ yuko huko, wafalme wake na wakuu wake wote, ambao ingawa walikuwa hodari, walilazwa miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga; wao pia watalala na watu ambao hawajatahiriwa+ na pamoja na wale wanaoshuka chini shimoni.*
30 “‘Wakuu* wote wa kaskazini wako huko, pamoja na Wasidoni wote,+ ambao wameshuka kwa aibu pamoja na waliouawa, ingawa walisababisha hofu kwa nguvu zao. Watalala wakiwa hawajatahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga nao watabeba aibu yao pamoja na wale wanaoshuka chini shimoni.*
31 “‘Farao atawaona hao wote, naye atafarijiwa kwa sababu ya mambo yote yaliyoupata umati wake;+ Farao na jeshi lake lote watauawa kwa upanga,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
32 “‘Kwa kuwa alisababisha hofu katika nchi ya walio hai, Farao na umati wake wote watalazwa ili wapumzike pamoja na watu ambao hawajatahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
33 Na neno la Yehova likanijia likisema: 2 “Mwana wa binadamu, zungumza na wana wa watu wako,+ uwaambie,
“‘Ikiwa nitaleta upanga uishambulie nchi,+ na watu wote wa nchi hiyo wamchukue mtu fulani na kumfanya awe mlinzi wao, 3 naye aone upanga ukija kuishambulia nchi, kisha apige pembe na kuwaonya watu,+ 4 ikiwa mtu atasikia sauti ya pembe lakini asitii onyo,+ nao upanga uje na kumuua,* damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.+ 5 Aliisikia sauti ya pembe, lakini hakutii onyo. Damu yake itakuwa juu yake mwenyewe. Kama angetii onyo, angeokoa uhai wake.*
6 “‘Lakini mlinzi akiuona upanga ukija naye asipige pembe+ na watu wasipate onyo nao upanga uje na kumuua mmoja wao, mtu huyo atakufa kwa sababu ya kosa lake mwenyewe, lakini nitaidai damu yake kutoka kwa mlinzi.’*+
7 “Na wewe, mwana wa binadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa watu wa nyumba ya Israeli; unaposikia neno kutoka katika kinywa changu lazima uwape onyo langu.+ 8 Ninapomwambia mtu mwovu, ‘Wewe mwovu, hakika utakufa!’+ lakini wewe humwonyi waziwazi mtu huyo mwovu ili abadili njia yake, yeye kwa kuwa ni mwovu atakufa kwa sababu ya kosa lake mwenyewe,+ lakini damu yake nitaidai kutoka kwako. 9 Lakini ukimwonya mtu mwovu aiache njia yake naye akatae kubadili njia yake, atakufa kwa sababu ya kosa lake,+ lakini wewe kwa hakika utauokoa uhai wako.*+
10 “Na wewe, mwana wa binadamu, waambie hivi watu wa nyumba ya Israeli: ‘Ninyi mmesema hivi: “Maasi yetu na dhambi zetu zinatulemea sana na kutufanya tudhoofike;+ basi tunawezaje kuendelea kuishi?”’+ 11 Waambie, ‘“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “Mimi sifurahishwi na kifo cha mwovu,+ bali kwamba mtu mwovu abadili njia yake+ na kuendelea kuishi.+ Geukeni, geukeni mziache njia zenu mbaya,+ kwa nini mfe, enyi watu wa nyumba ya Israeli?”’+
12 “Na wewe, mwana wa binadamu, waambie wana wa watu wako, ‘Uadilifu wa mtu mwadilifu hautamwokoa akiasi;+ wala uovu wa mwovu hautamkwaza akiacha uovu wake;+ wala hakuna mtu yeyote mwadilifu atakayeendelea kuishi kwa sababu ya uadilifu wake siku atakayotenda dhambi.+ 13 Ninapomwambia mtu mwadilifu: “Hakika utaendelea kuishi,” naye autumaini uadilifu wake mwenyewe na kutenda kosa,*+ hakuna tendo lolote la uadilifu alilotenda litakalokumbukwa, lakini atakufa kwa sababu ya kosa alilotenda.+
14 “‘Ninapomwambia mtu mwovu: “Hakika utakufa,” naye aiache dhambi yake na kutenda mambo ya haki na ya uadilifu,+ 15 na mtu huyo mwovu arudishe kitu kilichowekwa rehani+ na kulipa vitu alivyomnyang’anya mwingine,+ naye atembee katika sheria za uzima kwa kutotenda kosa, hakika ataendelea kuishi.+ Hatakufa. 16 Hataadhibiwa kwa sababu ya dhambi yoyote aliyotenda.*+ Kwa hakika ataendelea kuishi kwa sababu ya kutenda mambo ya haki na ya uadilifu.’+
17 “Lakini watu wako wamesema, ‘Njia ya Yehova si ya haki,’ ingawa kwa kweli ni njia yao isiyo ya haki.
18 “Mtu mwadilifu akiacha uadilifu wake na kutenda kosa, lazima afe kwa sababu ya kosa hilo.+ 19 Lakini mtu mwovu akiacha uovu wake na kutenda mambo ya haki na ya uadilifu, ataendelea kuishi kwa sababu ya kufanya hivyo.+
20 “Lakini ninyi mnasema, ‘Njia ya Yehova si ya haki.’+ Nitamhukumu kila mmoja wenu kulingana na njia zake, enyi watu wa nyumba ya Israeli.”
21 Mwishowe katika mwaka wa 12, mwezi wa kumi, siku ya tano ya mwezi wa uhamisho wetu, mtu aliyetoroka Yerusalemu alinijia+ na kusema: “Jiji limeangamizwa!”+
22 Basi, jioni ya siku iliyokuwa imetangulia kabla ya mtu huyo aliyetoroka kuja, mkono wa Yehova ulinijia naye akakifungua kinywa changu kabla ya mtu huyo kunijia asubuhi. Kinywa changu kilifunguliwa, nami sikuwa bubu tena.+
23 Kisha neno la Yehova likanijia likisema: 24 “Mwana wa binadamu, wakaaji wa magofu+ haya wanasema hivi kuhusu nchi ya Israeli: ‘Abrahamu alikuwa mtu mmoja tu, hata hivyo aliimiliki nchi hii.+ Lakini sisi ni wengi; kwa hakika tumepewa nchi hii iwe mali yetu.’
25 “Kwa hiyo waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Mnakula chakula pamoja na damu,+ nanyi mnayainua macho yenu kwa sanamu zenu zinazochukiza* na kuendelea kumwaga damu.+ Basi kwa nini mwimiliki nchi hii? 26 Mmeutegemea upanga wenu.+ Mmetenda mambo yanayochukiza, na kila mmoja wenu amemchafua mke wa jirani yake.+ Basi kwa nini mwimiliki nchi hii?”’+
27 “Unapaswa kuwaambia, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Kwa hakika kama ninavyoishi, wale wanaoishi katika magofu watauawa kwa upanga; na wale walio uwanjani nitawafanya wawe chakula cha wanyama wa mwituni; na wale walio katika ngome na mapango watakufa kwa ugonjwa.+ 28 Nitaifanya nchi iwe mahame na ukiwa kabisa,+ na kiburi chake chenye majivuno kitakomeshwa, na milima ya Israeli itafanywa ukiwa,+ na hakuna yeyote atakayepitia humo. 29 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoifanya nchi iwe mahame na ukiwa kabisa+ kwa sababu ya mambo yote yanayochukiza ambayo wamefanya.”’+
30 “Na wewe, mwana wa binadamu, watu wako wanaongea kukuhusu kando ya kuta na kwenye vizingiti vya milango ya nyumba.+ Kila mtu anamwambia ndugu yake, ‘Hebu njoo tusikie neno linalotoka kwa Yehova.’ 31 Watakusanyika na kuketi mbele yako kama watu wangu; nao watasikia maneno yako lakini hawatayatenda.+ Kwa maana wanakusifusifu kwa vinywa vyao* lakini moyo wao una pupa ya kupata faida isiyo ya haki. 32 Tazama! Kwao, wewe ni kama wimbo wa mapenzi, unaoimbwa kwa sauti tamu na kuchezwa kwa ustadi kwa kinanda. Watasikia maneno yako, lakini hakuna yeyote atakayeyatenda. 33 Na yatakapotimia—kwa maana yatatimia—watalazimika kujua kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.”+
34 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, tabiri dhidi ya wachungaji wa Israeli. Tabiri, na uwaambie wachungaji hao, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ole wao wachungaji wa Israeli,+ ambao wamekuwa wakijilisha wenyewe! Je, wachungaji hawapaswi kulilisha kundi?+ 3 Mnakula mafuta, mnajivika wenyewe sufu, nanyi mnamchinja mnyama aliyenona zaidi,+ lakini hamlilishi kundi.+ 4 Hamjawatia nguvu walio dhaifu au kuwaponya wagonjwa au kuwafunga waliojeruhiwa au kuwarudisha waliotangatanga au kuwatafuta waliopotea;+ badala yake, mmewatawala kwa ukali na kwa uonevu.+ 5 Kwa hiyo walitawanyika kwa sababu hakukuwa na mchungaji;+ walitawanyika na kuwa chakula cha kila mnyama wa mwituni. 6 Kondoo wangu waliendelea kutangatanga kwenye milima yote na kwenye kila kilima kirefu; kondoo wangu walitawanyika kotekote duniani, na hakuna aliyewatafuta au kujitahidi kuwapata.
7 “‘“Kwa hiyo, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Yehova: 8 ‘“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “kwa sababu kondoo wangu wamekuwa windo, chakula cha kila mnyama wa mwituni, kwa sababu hapakuwa na mchungaji, nao wachungaji wangu hawakuwatafuta kondoo wangu; badala yake waliendelea kujilisha wenyewe, nao hawakuwalisha kondoo wangu,”’ 9 basi, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Yehova. 10 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko dhidi ya wachungaji, nami nitafanya wawajibike kwa sababu ya kondoo wangu,* nami nitawafukuza ili wasiwalishe* kondoo wangu,+ nao wachungaji hawatajilisha tena. Nitawaokoa kondoo wangu kutoka kinywani mwao, nao hawatakuwa chakula chao tena.’”
11 “‘Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Mimi nipo hapa, na mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo wangu na kuwatunza.+ 12 Nitawatunza kondoo wangu kama mchungaji ambaye amewapata kondoo wake waliotawanyika na kuwalisha.+ Nitawaokoa kutoka katika maeneo yote walikotawanyika siku ya mawingu na giza zito.+ 13 Nitawatoa katika mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi hizo na kuwaleta katika nchi yao na kuwalisha kwenye milima ya Israeli,+ kando ya vijito na kando ya makao yote nchini. 14 Nitawalisha kwenye malisho mazuri, na nchi ambamo watalisha itakuwa kwenye milima mirefu ya Israeli.+ Huko watalala katika nchi yenye malisho mazuri,+ nao watakula kwenye malisho bora juu ya milima ya Israeli.”
15 “‘“Mimi mwenyewe nitawalisha kondoo wangu,+ na mimi mwenyewe nitawalaza,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 16 “Aliyepotea nitamtafuta,+ anayetangatanga nitamrudisha, aliyejeruhiwa nitamfunga, na aliye dhaifu nitamtia nguvu; lakini aliyenona na aliye na nguvu nitamwangamiza. Huyo nitamlisha hukumu.”
17 “‘Kuwahusu ninyi kondoo wangu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Niko karibu kuhukumu kati ya kondoo mmoja na kondoo mwingine, kati ya kondoo dume na mbuzi dume.+ 18 Je, hamtosheki kujilisha kwenye malisho yaliyo bora zaidi? Je, ni lazima myakanyage-kanyage kwa miguu yenu malisho yenu mengine? Na baada ya kunywa maji yaliyo safi zaidi, je, ni lazima myachafue kwa kuyakanyaga-kanyaga kwa miguu yenu? 19 Je, kondoo wangu wanapaswa kujilisha kwa malisho mliyoyakanyaga-kanyaga kwa miguu yenu na kunywa maji yaliyochafuliwa kwa kukanyagwa-kanyagwa kwa miguu yenu?”
20 “‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anawaambia hivi: “Mimi nipo hapa, na mimi mwenyewe nitahukumu kati ya kondoo aliyenona na kondoo aliyekonda, 21 kwa maana kwa ubavu wenu na kwa bega lenu mliendelea kuwasukuma, na kwa pembe zenu mliendelea kuwasukuma wote waliokuwa wagonjwa mpaka mkawatawanya maeneo ya mbali. 22 Nami nitawaokoa kondoo wangu, nao hawataendelea kuwa windo;+ nami nitahukumu kati ya kondoo mmoja na kondoo mwingine. 23 Nami nitamweka mchungaji mmoja juu yao,+ mtumishi wangu Daudi,+ naye atawalisha. Yeye mwenyewe atawalisha na kuwa mchungaji wao.+ 24 Na mimi, Yehova, nitakuwa Mungu wao,+ na mtumishi wangu Daudi atakuwa kiongozi wao. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.+
25 “‘“Nitafanya agano la amani pamoja nao,+ na kuwaondoa kabisa nchini wanyama hatari wa mwituni,+ ili wakae kwa usalama nyikani na kulala misituni.+ 26 Nitawafanya wao na eneo linalozunguka kilima changu kuwa baraka,+ nami nitaifanya mvua inyeshe kwa wakati unaofaa. Baraka zitamwagika kama mvua.+ 27 Miti ya shambani itazaa matunda yake, na udongo utatoa mazao yake,+ nao wataishi kwa usalama nchini. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapozivunja nira zao+ na kuwaokoa kutoka mikononi mwa wale waliowafanya kuwa watumwa. 28 Hawatakuwa windo la mataifa tena, na wanyama wa mwituni wa dunia hawatawanyafua, nao wataishi kwa usalama, na hakuna mtu atakayewaogopesha.+
29 “‘“Nitawatayarishia shamba maarufu,* nao hawatakufa tena kwa njaa kali nchini,+ na hawatafedheheshwa tena na mataifa.+ 30 ‘Nao watalazimika kujua kwamba mimi, Yehova Mungu wao, niko pamoja nao na kwamba wao, watu wa nyumba ya Israeli, ni watu wangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”’
31 “‘Nanyi kondoo wangu,+ kondoo ninaowatunza, ninyi ni wanadamu tu, nami ni Mungu wenu,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
35 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako kwenye eneo lenye milima la Seiri,+ na utabiri dhidi yake.+ 3 Uliambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Niko dhidi yako, ewe eneo lenye milima la Seiri, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya uwe mahame na ukiwa.+ 4 Nitayafanya majiji yako kuwa magofu, nawe utakuwa mahame na ukiwa;+ nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova. 5 Kwa maana ulikuwa na chuki isiyo na mwisho,+ nawe uliwatia Waisraeli mikononi mwa upanga wakati wa msiba wao, wakati wa adhabu yao ya mwisho.”’+
6 “‘Kwa hiyo, kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitakutayarisha kwa ajili ya umwagaji wa damu, na umwagaji wa damu utakufuatia.+ Kwa maana uliichukia damu, umwagaji wa damu utakufuatia.+ 7 Nitalifanya eneo lenye milima la Seiri kuwa mahame na ukiwa,+ nami nitamwangamiza mtu yeyote anayepitia humo na yeyote anayerudi. 8 Nitaijaza milima yake watu waliouawa; na wale waliouawa kwa upanga wataanguka kwenye vilima vyako, katika mabonde yako, na katika vijito vyako vyote. 9 Nitakufanya uwe ukiwa wa kudumu, na majiji yako hayatakaliwa;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
10 “Kwa sababu ulisema, ‘Mataifa haya mawili na nchi hizi mbili zitakuwa zangu, nasi tutazimiliki zote mbili,’+ hata ingawa Yehova mwenyewe alikuwa humo, 11 ‘kwa hiyo kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitakutendea kulingana na hasira ileile na wivu uleule ulioonyesha ulipowachukia;+ nami nitajijulisha miongoni mwao nitakapokuhukumu. 12 Kisha utalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema kuhusu milima ya Israeli, uliposema, “Imefanywa ukiwa nasi tumepewa ili tuinyafue.”* 13 Nanyi mlizungumza kwa kiburi dhidi yangu, na kuzidisha maneno yenu dhidi yangu.+ Niliyasikia yote.’
14 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Dunia yote itashangilia nitakapokufanya uwe mahame na ukiwa. 15 Kama ulivyoshangilia urithi wa watu wa nyumba ya Israeli ulipofanywa ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea.+ Utakuwa magofu yaliyo ukiwa, ewe eneo lenye milima la Seiri, naam, Edomu yote;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”
36 “Nawe, mwana wa binadamu, tabiri kuhusu milima ya Israeli, nawe useme, ‘Enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Yehova. 2 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Adui amesema hivi dhidi yenu, ‘Aha! Hata mahali pa juu pa zamani pamekuwa mali yetu!’”’+
3 “Basi tabiri, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Kwa sababu wamekufanya uwe ukiwa na kukushambulia kutoka kila upande, ili uwe mali ya wale waliookoka* kutoka kati ya mataifa na watu wanaendelea kuzungumza kukuhusu na kukuchongea,+ 4 kwa hiyo, enyi milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyoiambia milima na vilima, vijito na mabonde, magofu yaliyofanywa ukiwa,+ na majiji yaliyoachwa ambayo yameporwa na kudhihakiwa na wale waliookoka kutoka katika mataifa yanayowazunguka;+ 5 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anawaambia hivi: ‘Katika moto wa bidii yangu+ nitawakemea wale waliookoka kutoka katika mataifa na nchi yote ya Edomu, wale ambao kwa shangwe nyingi na kwa dharau kubwa*+ wamechukua nchi yangu na kuifanya kuwa mali yao, ili wachukue malisho yake na kuipora.’”’+
6 “Basi tabiri kuhusu nchi ya Israeli, nawe uiambie milima na vilima, vijito na mabonde, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tazama! Nitazungumza kwa bidii yangu na kwa ghadhabu yangu, kwa sababu mmefedheheshwa na mataifa.”’+
7 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Mimi mwenyewe ninainua mkono wangu na kuapa kwamba mataifa yanayozunguka yatabeba aibu yao wenyewe.+ 8 Lakini ninyi, enyi milima ya Israeli, mtachipusha matawi na kuzaa matunda yenu kwa ajili ya watu wangu Waisraeli,+ kwa maana watarudi hivi karibuni. 9 Kwa maana niko pamoja nanyi, nami nitawageukia, nanyi mtalimwa na kupandwa mbegu. 10 Nitazidisha idadi ya watu wako—nyumba yote ya Israeli, yote—nayo majiji yatakaliwa+ na magofu yatajengwa upya.+ 11 Naam, nitazidisha idadi ya watu wako na mifugo yako;+ wataongezeka na kuzaana. Nami nitafanya ukaliwe kama ilivyokuwa zamani,+ nami nitakufanya usitawi kuliko mwanzoni;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 12 Nitawafanya watu—watu wangu Waisraeli—watembee juu yako, nao watakumiliki.+ Utakuwa urithi wao, nawe hutawafanya wakose watoto tena kamwe.’”+
13 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa kuwa wanawaambia ninyi, “Wewe ni nchi inayowameza watu na kuwaua watoto wa mataifa yako,”’ 14 ‘kwa hiyo, hutawameza tena watu wala kuyafanya mataifa yako yakose watoto,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 15 ‘Sitaruhusu tena utukanwe na mataifa au udhihakiwe na watu,+ nawe hutafanya tena mataifa yako yakwazike,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
16 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 17 “Mwana wa binadamu, watu wa nyumba ya Israeli walipokuwa wakiishi katika nchi yao, waliichafua kwa njia zao na matendo yao.+ Njia zao zilikuwa kama uchafu wa hedhi kwangu.+ 18 Basi nikawamwagia ghadhabu yangu kwa sababu ya damu waliyoimwaga juu ya nchi+ na kwa sababu waliichafua nchi kwa sanamu zao zinazochukiza.*+ 19 Basi nikawatawanya miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali.+ Niliwahukumu kulingana na njia yao na kulingana na matendo yao. 20 Lakini walipoingia katika mataifa hayo, watu walilichafua jina langu takatifu+ kwa kusema hivi kuwahusu: ‘Hawa ndio watu wa Yehova, lakini walilazimika kutoka katika nchi yake.’ 21 Basi nitalihangaikia jina langu takatifu, ambalo watu wa nyumba ya Israeli walilichafua miongoni mwa mataifa ambako walienda.”+
22 “Kwa hiyo, waambie watu wa nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Sifanyi jambo hili kwa ajili yenu, enyi watu wa nyumba ya Israeli, bali kwa ajili ya jina langu takatifu, ambalo ninyi mmelichafua miongoni mwa mataifa ambako mlienda.”’+ 23 ‘Kwa hakika nitalitakasa jina langu kuu,+ ambalo lilichafuliwa miongoni mwa mataifa, ambalo mlilichafua miongoni mwao; nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitakapotakaswa miongoni mwenu mbele ya macho yao. 24 Nitawatoa kutoka kwa mataifa na kuwakusanya kutoka katika nchi zote na kuwaleta katika nchi yenu.+ 25 Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi;+ nami nitawatakasa kutokana na uchafu wenu+ wote na kutokana na sanamu zenu zote zinazochukiza.+ 26 Nitawapa moyo mpya+ na kutia roho mpya ndani yenu.+ Nitauondoa moyo wa jiwe+ kutoka mwilini mwenu na kuwapa moyo wa nyama.* 27 Nitaitia roho yangu ndani yenu, nami nitawafanya mtembee katika masharti yangu,+ nanyi mtashika na kufuata sheria zangu.* 28 Kisha mtakaa katika nchi niliyowapa mababu zenu, nanyi mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.’+
29 “‘Nitawaokoa kutokana na uchafu wenu wote na kuiita nafaka na kuifanya iwe tele, nami sitawaletea njaa kali.+ 30 Nitayafanya matunda ya mti na mazao ya shamba yawe tele, ili msipatwe tena na aibu ya njaa kali miongoni mwa mataifa.+ 31 Kisha mtakumbuka njia zenu ovu na matendo yenu mabaya, nanyi mtajichukia kwa sababu ya hatia yenu na matendo yenu yanayochukiza.+ 32 Lakini jueni jambo hili: Sifanyi hivyo kwa ajili yenu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Badala yake, aibikeni na kufedheheka kwa sababu ya njia zenu, enyi watu wa nyumba ya Israeli.’
33 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Siku nitakayowatakasa kutokana na hatia yenu yote, nitayafanya majiji yakaliwe+ na magofu yajengwe upya.+ 34 Nchi yenye ukiwa, iliyokuwa ukiwa ili kila mtu anayepita aione, italimwa. 35 Na watu watasema: “Nchi iliyokuwa ukiwa imekuwa kama bustani ya Edeni,+ na majiji yaliyokuwa magofu na yaliyokuwa ukiwa na kubomolewa sasa yana ngome na yanakaliwa na watu.”+ 36 Na mataifa yaliyobaki kukuzunguka yatalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimejenga kilichobomolewa, nami nimepanda kilichofanywa ukiwa. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema, nami nimelitenda.’+
37 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitawaruhusu pia watu wa nyumba ya Israeli waniombe niwatendee jambo hili: Nitazidisha idadi ya watu wao kama kundi. 38 Kama kundi la watu watakatifu, kama kundi la Yerusalemu* wakati wa sherehe zake,+ majiji yaliyokuwa magofu yatajaa makundi ya watu;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”
37 Mkono wa Yehova ulikuwa juu yangu, naye Yehova akanichukua kwa roho yake na kuniweka chini katikati ya bonde tambarare,+ nalo lilikuwa limejaa mifupa. 2 Akanizungusha kwenye mifupa hiyo yote, nami nikaona kwamba kulikuwa na mifupa mingi sana katika bonde hilo tambarare, nayo ilikuwa mikavu sana.+ 3 Akaniuliza: “Mwana wa binadamu, je, mifupa hii inaweza kuwa hai?” Nikajibu: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, wewe ndiye unayejua.”+ 4 Basi akaniambia: “Itabirie mifupa hii, uiambie, ‘Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Yehova:
5 “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameiambia hivi mifupa hii: “Nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtakuwa hai.+ 6 Nitaweka kano na nyama juu yenu, nami nitawafunika kwa ngozi na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtakuwa hai; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’”
7 Kisha nikatabiri kama nilivyoamriwa. Mara tu nilipotabiri, nikasikia sauti, sauti ya vitu vinavyogongana, nayo mifupa ikaanza kukaribiana, mfupa kwa mfupa. 8 Kisha nikaona kano na nyama zikija juu yake, na ngozi ikazifunika. Lakini bado hakukuwa na pumzi ndani yake.
9 Kisha akaniambia: “Utabirie upepo. Tabiri, mwana wa binadamu, nawe uuambie upepo, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Njoo kutoka kwenye zile pepo nne, ewe upepo,* nawe uwapulizie watu waliouawa, ili wawe hai.”’”
10 Basi nikatabiri kama alivyoniamuru, nayo pumzi* ikaingia ndani yao, nao wakaanza kuishi na kusimama kwa miguu yao;+ walikuwa jeshi kubwa ajabu.
11 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, mifupa hii ni watu wote wa nyumba ya Israeli.+ Wanasema, ‘Mifupa yetu imekauka, nalo tumaini letu limepotea.+ Tumeangamizwa kabisa.’ 12 Basi tabiri uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitayafungua makaburi yenu+ na kuwainua kutoka katika makaburi yenu, watu wangu, na kuwaleta katika nchi ya Israeli.+ 13 Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoyafungua makaburi yenu na nitakapowainua kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu.”’+ 14 ‘Nitaitia roho yangu ndani yenu,+ nanyi mtakuwa hai, nami nitawafanya mwishi katika nchi yenu; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nimelitenda,’ asema Yehova.”
15 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 16 “Nawe, mwana wa binadamu, chukua kijiti nawe uandike juu yake, ‘Kwa ajili ya Yuda na kwa ajili ya watu wa Israeli walio pamoja naye.’*+ Kisha uchukue kijiti kingine na kuandika juu yake, ‘Kwa ajili ya Yosefu, kijiti cha Efraimu, na watu wote wa nyumba ya Israeli walio pamoja naye.’*+ 17 Kisha viunganishe ili viwe kijiti kimoja tu mkononi mwako.+ 18 Watu wako* watakapokuuliza, ‘Je, hutatuambia mambo haya yanamaanisha nini?’ 19 waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitakichukua kijiti cha Yosefu, kilicho mkononi mwa Efraimu, na makabila ya Israeli yaliyo pamoja naye, nami nitakiunganisha na kijiti cha Yuda; nami nitavifanya viwe kijiti kimoja,+ navyo vitakuwa kijiti kimoja mkononi mwangu.”’ 20 Vijiti utakavyoandika juu yake vinapaswa kuwa mkononi mwako ili wavione.
21 “Kisha uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitawachukua Waisraeli kutoka katika mataifa ambako walienda, nami nitawakusanya pamoja kutoka kila upande na kuwaleta katika nchi yao.+ 22 Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo,+ kwenye milima ya Israeli, na mfalme mmoja atawatawala wote,+ nao hawatakuwa tena mataifa mawili; wala hawatagawanyika tena kuwa falme mbili.+ 23 Hawatajitia unajisi tena kwa sanamu zao zinazochukiza* na kwa matendo yao yanayochukiza na kwa makosa yao yote.+ Nitawaokoa kutoka katika ukosefu wao wote wa uaminifu ambao umewafanya watende dhambi, nami nitawatakasa. Watakuwa watu wangu, nami mwenyewe nitakuwa Mungu wao.+
24 “‘“Mtumishi wangu Daudi atakuwa mfalme wao,+ na wote watakuwa na mchungaji mmoja.+ Watatembea katika sheria zangu* na kuzishika amri zangu kwa uangalifu.+ 25 Wataishi katika nchi niliyompa mtumishi wangu, Yakobo, ambamo mababu zenu waliishi,+ nao watakaa humo milele,+ wao na watoto* wao na watoto wa watoto wao;+ na mtumishi wangu Daudi atakuwa kiongozi* wao milele.+
26 “‘“Nami nitafanya agano la amani pamoja nao;+ litakuwa agano la milele pamoja nao. Nitawaimarisha na kuwafanya wawe wengi+ na kupaweka mahali pangu patakatifu miongoni mwao milele. 27 Hema langu litakuwa* pamoja nao,* nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.+ 28 Na mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi, Yehova, ninawatakasa Waisraeli mahali pangu patakatifu patakapokuwa kati yao milele.”’”+
38 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako dhidi ya Gogu wa nchi ya Magogu,+ kiongozi mkuu* wa Mesheki na Tubali,+ na utabiri dhidi yake.+ 3 Sema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tazama, niko dhidi yako, ewe Gogu, kiongozi mkuu* wa Mesheki na Tubali. 4 Nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako+ na kukutoa pamoja na jeshi lako lote,+ farasi na wapanda farasi, wote wakiwa wamevaa mavazi ya kifahari, kusanyiko kubwa sana lenye ngao kubwa na ngao ndogo,* wote wakiwa na mapanga; 5 Uajemi, Ethiopia, na Putu+ wako pamoja nao, wote wakiwa na ngao ndogo na kofia; 6 Gomeri na wanajeshi wake wote, watu wa nyumba ya Togarma+ kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini, pamoja na wanajeshi wake wote—mataifa mengi yako pamoja nawe.+
7 “‘“Uwe tayari, ujitayarishe, wewe pamoja na majeshi yako yote yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe utakuwa kamanda* wao.
8 “‘“Utakaziwa fikira* baada ya siku nyingi. Katika miaka ya mwisho utaishambulia nchi ambayo watu wake wamerudishwa kutoka kwenye uharibifu wa upanga, waliokusanywa pamoja kutoka katika mataifa mengi, na kuletwa kwenye milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imebaki ukiwa. Wakaaji wa nchi hii walirudishwa kutoka katika mataifa, na wote wanakaa kwa usalama.+ 9 Utawashambulia kama dhoruba nawe utaifunika nchi kama mawingu, wewe na wanajeshi wako wote na mataifa mengi pamoja nawe.”’
10 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Siku hiyo mawazo yataingia moyoni mwako, nawe utapanga njama ya uovu. 11 Utasema: “Nitaivamia nchi yenye vijiji visivyo na ulinzi.*+ Nitawashambulia wale wanaokaa kwa usalama, bila usumbufu, wote wanaoishi katika vijiji visivyolindwa na ukuta, makomeo, au malango.” 12 Ili kupora na kuchukua nyara nyingi, ili kushambulia maeneo yaliyoharibiwa ambayo sasa yanakaliwa na watu+ waliokusanywa kutoka katika mataifa,+ ambao wanajikusanyia utajiri na mali,+ wale wanaoishi katikati ya dunia.
13 “‘Sheba+ na Dedani,+ wafanyabiashara wa Tarshishi+ na mashujaa* wake wote watakuuliza: “Je, unavamia ili upore na kupata nyara nyingi? Je, umekusanya majeshi yako ili kubeba fedha na dhahabu, kuchukua utajiri na mali, ili kuteka nyara nyingi sana?”’
14 “Basi tabiri, mwana wa binadamu, nawe umwambie Gogu, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Siku ambayo watu wangu Waisraeli watakapokuwa wakiishi kwa usalama, je, hutajua jambo hilo?+ 15 Utakuja kutoka mahali pako, kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini,+ wewe pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kusanyiko kubwa, jeshi kubwa sana.+ 16 Kama mawingu yanayoifunika nchi, utawashambulia watu wangu Waisraeli. Katika kipindi cha mwisho cha zile siku, nitakuleta uishambulie nchi yangu+ ili mataifa yanijue nitakapojitakasa mwenyewe kupitia wewe mbele ya macho yao, ewe Gogu.”’+
17 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Je, wewe si yuleyule niliyesema kumhusu katika siku za zamani kupitia watumishi wangu manabii wa Israeli, waliotabiri kwa miaka mingi kwamba utaletwa ili kuwashambulia?’
18 “‘Siku hiyo, siku ambayo Gogu ataishambulia nchi ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘ghadhabu yangu kali itawaka.+ 19 Kwa bidii yangu, kwa moto wa ghadhabu yangu, nitazungumza; na siku hiyo kutakuwa na tetemeko kubwa la ardhi katika nchi ya Israeli. 20 Kwa sababu yangu, samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa mwituni, wanyama wote wanaotambaa juu ya nchi, na wanadamu wote walio duniani watatetemeka, nayo milima itaangushwa chini,+ na miamba itaanguka, na kila ukuta utaporomoka.’
21 “‘Nitauita upanga umshambulie kwenye milima yangu yote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Upanga wa kila mtu utamshambulia ndugu yake mwenyewe.+ 22 Nitamletea hukumu yangu* kwa ugonjwa hatari+ na kwa umwagaji wa damu; nami nitaleta dhidi yake mvua kubwa ya mafuriko na mawe ya mvua+ na moto+ na kiberiti+ na dhidi ya wanajeshi wake na dhidi ya mataifa mengi yaliyo pamoja naye.+ 23 Nami hakika nitajitukuza na kujitakasa na kujijulisha mwenyewe mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
39 “Nawe, mwana wa binadamu, tabiri dhidi ya Gogu,+ umwambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Niko dhidi yako, Gogu, kiongozi mkuu* wa Mesheki na Tubali.+ 2 Nitakugeuza na kukuongoza na kukufanya uje kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini+ na kukuleta kwenye milima ya Israeli. 3 Nitaupiga upinde wako utoke kwenye mkono wako wa kushoto na kufanya mishale yako ianguke kutoka kwenye mkono wako wa kulia. 4 Utaanguka kwenye milima ya Israeli,+ wewe na wanajeshi wako wote na mataifa yatakayokuwa pamoja nawe. Nitakufanya uwe chakula cha kila aina ya ndege wanaowinda na wanyama wa mwituni.”’+
5 “‘Utaanguka uwanjani,+ kwa maana mimi mwenyewe nimesema,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
6 “‘Nami nitatuma moto dhidi ya Magogu na dhidi ya wale wanaokaa visiwani kwa usalama,+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova. 7 Nitalifanya jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Waisraeli, nami sitaruhusu jina langu takatifu lichafuliwe tena; na mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ Mtakatifu katika Israeli.’+
8 “‘Naam, jambo hilo linakuja, nalo litatendeka,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Hiyo ndiyo siku ambayo nimesema kuihusu. 9 Kwa hakika wakaaji wa majiji ya Israeli watatoka nje na kuwasha moto kwa silaha—ngao ndogo* na ngao kubwa, pinde na mishale, rungu za vita* na mikuki. Nao watazitumia kuwasha moto+ kwa miaka saba. 10 Hawatahitaji kukusanya kuni shambani wala kuokota kuni misituni, kwa sababu watatumia silaha hizo kuwasha mioto.’
“‘Watawateka nyara wale waliowateka nyara na kuwapora wale waliokuwa wakiwapora,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
11 “‘Siku hiyo, nitampa Gogu+ kaburi katika Israeli, kwenye bonde la wale wanaosafiri upande wa mashariki wa bahari, nalo litazuia njia ya wale wanaopitia humo. Hapo ndipo watakapomzika Gogu na umati wake wote, nao wataliita Bonde la Hamon-Gogu.*+ 12 Kwa miezi saba watu wa nyumba ya Israeli watawazika ili kuitakasa nchi.+ 13 Watu wote wa nchi watafanya kazi ya kuwazika, na hilo litawaletea umaarufu siku nitakayojitukuza,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
14 Watu watapewa kazi ya kupitapita nchini daima na kuizika miili iliyobaki juu ya dunia, ili kuitakasa dunia. Wataendelea kutafuta kwa miezi hiyo saba. 15 Wale wanaopitapita nchini watakapoona mfupa wa mwanadamu, wataweka alama kando yake. Kisha wale waliopewa kazi ya kuzika watauzika mfupa huo katika Bonde la Hamon-Gogu.+ 16 Na huko pia kutakuwa na jiji linaloitwa Hamona.* Nao wataitakasa nchi.’+
17 “Nawe, mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Waambie ndege wa kila aina na wanyama wote wa mwituni, “Kusanyikeni pamoja na mje. Kusanyikeni kuzunguka dhabihu yangu ninayowatayarishia, dhabihu kubwa kwenye milima ya Israeli.+ Mtakula nyama na kunywa damu.+ 18 Mtakula nyama ya wenye nguvu na kunywa damu ya viongozi wa dunia—kondoo dume, wanakondoo, mbuzi, na ng’ombe dume—wanyama wote waliononeshwa wa Bashani. 19 Mtakula mafuta kwa pupa mpaka mshibe na kunywa damu mpaka mlewe kutokana na dhabihu nitakayowatayarishia.”’
20 “‘Mtashibishwa mezani pangu kwa farasi na waendeshaji wa magari, watu wenye nguvu na kila aina ya mashujaa,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
21 “‘Nitauonyesha wazi utukufu wangu kati ya mataifa, nayo mataifa yote yataona hukumu ambayo nimetekeleza na nguvu nilizoonyesha* kati yao.+ 22 Kuanzia siku hiyo, watu wa nyumba ya Israeli watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao. 23 Nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba watu wa nyumba ya Israeli walipelekwa uhamishoni kwa sababu ya kosa lao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu.+ Basi niliwaficha uso wangu+ na kuwatia mikononi mwa maadui wao,+ na wote wakauawa kwa upanga. 24 Niliwatendea kulingana na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.’
25 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitawarudisha watu wa Yakobo waliotekwa+ na kuwaonyesha rehema watu wote wa nyumba ya Israeli;+ nami nitalitetea jina langu takatifu kwa bidii.*+ 26 Baada ya kufedheheshwa kwa sababu ya ukosefu wao wote wa uaminifu kunielekea,+ watakaa kwa usalama katika nchi yao, na hakuna mtu atakayewaogopesha.+ 27 Nitakapowarudisha kutoka katika mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi za maadui wao,+ mimi pia nitajitakasa miongoni mwao mbele ya macho ya mataifa mengi.’+
28 “‘Watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao nitakapowapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa na kuwarudisha katika nchi yao, bila kumwacha yeyote kati yao huko.+ 29 Sitawaficha uso wangu tena,+ kwa maana nitawamiminia roho yangu watu wa nyumba ya Israeli,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
40 Katika mwaka wa 25 wa uhamisho wetu,+ mwanzoni mwa mwaka, siku ya 10 ya mwezi, katika mwaka wa 14 baada ya jiji kuanguka,+ siku hiyohiyo mkono wa Yehova ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka jijini.+ 2 Kupitia maono kutoka kwa Mungu, alinileta katika nchi ya Israeli na kuniweka juu ya mlima mrefu sana,+ na juu yake kulikuwa na jengo lililoonekana kama jiji, upande wa kusini.
3 Aliponipeleka huko, niliona mtu fulani ambaye alionekana kama shaba.+ Alikuwa na kamba ya kitani na utete wa kupimia* mkononi mwake,+ naye alikuwa amesimama langoni. 4 Mtu huyo akaniambia: “Mwana wa binadamu, tazama kwa uangalifu, sikiliza kwa makini, na ukazie fikira* kila kitu ninachokuonyesha, kwa maana uliletwa hapa kwa sababu hiyo. Waambie watu wa nyumba ya Israeli kila kitu unachoona.”+
5 Nikaona ukuta uliozunguka nje ya hekalu.* Mkononi mwa mtu huyo kulikuwa na utete wa kupimia wenye urefu wa mikono sita (kila mkono ulikuwa umeongezwa urefu wa kiganja kimoja).* Akaanza kupima ukuta, nao ulikuwa na unene wa utete mmoja na urefu wake ulikuwa utete mmoja.
6 Kisha akaja kwenye lango lililotazama mashariki+ na kupanda ngazi zake. Alipopima kizingiti cha lango hilo, upana wake ulikuwa utete mmoja, na upana wa kile kizingiti kingine ulikuwa utete mmoja pia. 7 Kila chumba cha walinzi kilikuwa na urefu wa utete mmoja na upana wa utete mmoja, na kulikuwa na kipimo cha mikono mitano kati ya vyumba vya walinzi.+ Kipimo cha kizingiti cha lango kando ya ukumbi wa lango linalotazama upande wa ndani kilikuwa utete mmoja.
8 Alipima ukumbi wa lango kuelekea ndani, nao ulikuwa utete mmoja. 9 Kisha akapima ukumbi wa lango, nao ulikuwa mikono minane; na akapima nguzo zake za pembeni, nazo zilikuwa mikono miwili; na ukumbi wa lango ulikuwa upande uliotazama ndani.
10 Kulikuwa na vyumba vitatu vya walinzi katika kila upande wa lango la mashariki. Vyumba hivyo vitatu vilikuwa na ukubwa uleule, nazo nguzo za pembeni zilizokuwa pande zote mbili zilikuwa na ukubwa uleule.
11 Kisha akapima upana wa lango, nao ulikuwa mikono 10; na urefu wa lango ulikuwa mikono 13.
12 Eneo lililogawanywa lililokuwa mbele ya vyumba vya walinzi kila upande lilikuwa na kipimo cha mkono mmoja. Vyumba vya walinzi pande zote mbili vilikuwa mikono sita kila kimoja.
13 Kisha akapima lango kutoka kwenye paa la chumba kimoja cha mlinzi* mpaka kwenye paa la kile kingine, na upana wake ulikuwa mikono 25; mlango mmoja ulitazamana na mlango mwingine.+ 14 Kisha akapima nguzo za pembeni, ambazo zilikuwa na urefu wa mikono 60, pia nguzo za pembeni katika malango kuzunguka ua. 15 Urefu kutoka upande wa mbele wa lango mpaka mbele ya ukumbi upande wa ndani wa lango ulikuwa mikono 50.
16 Ndani ya lango, kila upande kwenye vyumba vya walinzi na pia kwenye nguzo zake za pembeni kulikuwa na madirisha yenye viunzi ambavyo ukubwa wake ulipungua kutoka nje kwenda ndani.+ Upande wa ndani wa kumbi ulikuwa pia na madirisha kila upande, na kulikuwa na michongo ya mitende+ kwenye nguzo za pembeni.
17 Kisha akanileta kwenye ua wa nje, nami nikaona vyumba vya kulia chakula,*+ na sakafu iliyozunguka ua. Kulikuwa na vyumba 30 vya kulia chakula kwenye ile sakafu. 18 Urefu wa sakafu iliyokuwa kando ya malango ulikuwa sawa na urefu wa malango—hiyo ilikuwa sakafu ya chini.
19 Kisha akapima umbali* kutoka mbele ya lango la chini mpaka kwenye uzio wa ua wa ndani. Ulikuwa mikono 100 upande wa mashariki na wa kaskazini.
20 Ua wa nje ulikuwa na lango lililotazama kaskazini, naye akapima urefu wake na upana wake. 21 Kulikuwa na vyumba vitatu vya walinzi kila upande. Nguzo zake za pembeni na ukumbi wake ulikuwa na vipimo sawa na lile lango la kwanza. Urefu wake ulikuwa mikono 50 na upana wake mikono 25. 22 Madirisha yake, ukumbi wake, na michongo yake ya mitende+ yalikuwa na ukubwa ulio sawa na yale ya lango la mashariki. Watu wangeweza kuyafikia kwa kupanda ngazi saba, na ukumbi wake ulikuwa mbele yake.
23 Kulikuwa na lango katika ua wa ndani lililotazamana na lango la kaskazini na lingine lililotazamana na lango la mashariki. Alipima urefu kutoka lango moja hadi lingine, nao ulikuwa mikono 100.
24 Kisha akanileta upande wa kusini, nami nikaona lango upande wa kusini.+ Akapima nguzo zake za pembeni na ukumbi wake, nazo zilikuwa na ukubwa ulio sawa na zile nyingine. 25 Kila upande na pia katika ukumbi wake kulikuwa na madirisha, kama madirisha yale mengine. Urefu wake ulikuwa mikono 50 na upana wa mikono 25. 26 Kulikuwa na ngazi saba zilizoelekea langoni,+ na ukumbi wake ulikuwa mbele yake. Nalo lilikuwa na michongo ya mitende kwenye nguzo zake za pembeni, mmoja kila upande.
27 Ua wa ndani ulikuwa na lango lililotazama upande wa kusini, akapima kuelekea kusini kutoka lango moja mpaka lingine, na urefu wake ulikuwa mikono 100. 28 Kisha akanileta kwenye ua wa ndani kupitia lango la kusini; alipolipima lango la kusini, lilikuwa na ukubwa sawa na yale malango mengine. 29 Vyumba vyake vya walinzi, nguzo zake za pembeni, na ukumbi wake ulikuwa na ukubwa sawa na malango mengine. Kulikuwa na madirisha kila upande na pia kwenye ukumbi. Urefu wake ulikuwa mikono 50 na upana wake mikono 25.+ 30 Kulikuwa na kumbi pande zote; zilikuwa na urefu wa mikono 25 na upana wa mikono 5. 31 Ukumbi wake ulitazama ua wa nje, na kulikuwa na michongo ya mitende kwenye nguzo zake za pembeni,+ na ngazi nane zilielekea kwenye lango hilo.+
32 Aliponileta kwenye ua wa ndani kutoka mashariki, alilipima lango, nalo lilikuwa na ukubwa sawa na malango mengine. 33 Vyumba vyake vya walinzi, nguzo zake za pembeni, na ukumbi wake ulikuwa na ukubwa sawa na malango mengine, na kulikuwa na madirisha kila upande na pia kwenye ukumbi. Urefu wake ulikuwa mikono 50 na upana wake mikono 25. 34 Ukumbi wake ulitazama ua wa nje, na kulikuwa na michongo ya mitende kwenye nguzo zake mbili za pembeni, na ngazi nane zilielekea kwenye lango hilo.
35 Kisha akanileta kwenye lango la kaskazini+ naye akalipima; ukubwa wake ulikuwa sawa na malango mengine. 36 Vyumba vyake vya walinzi, nguzo zake za pembeni, na ukumbi wake ulikuwa sawa na malango mengine. Lango hilo lilikuwa na madirisha kila upande. Urefu wake ulikuwa mikono 50 na upana wa mikono 25. 37 Nguzo zake za pembeni zilitazama ua wa nje na kulikuwa na michongo ya mitende kwenye nguzo zake mbili za pembeni, na ngazi nane zilielekea kwenye lango hilo.
38 Kulikuwa na chumba cha kulia chakula pamoja na mlango wake karibu na nguzo za pembeni za malango, mahali ambapo dhabihu nzima za kuteketezwa zilioshewa.+
39 Kulikuwa na meza mbili kila upande wa ukumbi wa lango ambapo wanyama wa dhabihu nzima za kuteketezwa walichinjiwa,+ na wa dhabihu za dhambi,+ na wa dhabihu za hatia.+ 40 Kwenye njia inayopanda kuelekea katika lango la kaskazini, kulikuwa na meza mbili nje ya lango. Kulikuwa pia na meza mbili upande ule mwingine wa ukumbi wa lango. 41 Kulikuwa na meza nne kila upande wa lango—meza nane kwa ujumla—ambapo wanyama wa dhabihu walichinjiwa. 42 Zile meza nne za dhabihu nzima za kuteketezwa zilitengenezwa kwa mawe yaliyochongwa. Zilikuwa na urefu wa mkono mmoja na nusu, upana wa mkono mmoja na nusu, na kimo cha mkono mmoja. Juu yake waliweka vifaa vilivyotumiwa kuwachinjia wanyama wa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu nyingine. 43 Rafu zenye upana wa kiganja kimoja, zilifungwa kuzunguka pande zote za kuta za ndani; na nyama za dhabihu za zawadi ziliwekwa kwenye zile meza.
44 Kulikuwa na vyumba vya kulia chakula vya waimbaji nje ya lango la ndani;+ vilikuwa katika ua wa ndani karibu na lango la kaskazini, vikitazama upande wa kusini. Kulikuwa na chumba kingine cha kulia chakula karibu na lango la mashariki, kilitazama kaskazini.
45 Akaniambia: “Chumba hiki cha chakula kinachotazama upande wa kusini ni cha makuhani walio na jukumu la kutimiza utumishi wa hekaluni.+ 46 Chumba cha kulia chakula kinachotazama upande wa kaskazini ni cha makuhani walio na jukumu la kutimiza utumishi wa madhabahu.+ Hao ni wana wa Sadoki,+ Walawi waliopewa kazi ya kumkaribia Yehova ili kumhudumia.”+
47 Kisha akapima ua wa ndani. Ulikuwa na urefu wa mikono 100 na upana wa mikono 100, mraba. Madhabahu ilikuwa mbele ya hekalu.
48 Kisha akanileta kwenye ukumbi wa hekalu,+ naye akapima nguzo ya pembeni ya ukumbi, nayo ilikuwa mikono mitano upande mmoja na mikono mitano upande wa pili. Upana wa lango ulikuwa mikono mitatu upande mmoja na mikono mitatu upande wa pili.
49 Ukumbi ulikuwa na urefu wa mikono 20 na upana wa mikono 11.* Watu walipanda ngazi ili kufika kwenye ukumbi huo. Kulikuwa na nguzo kwenye miimo ya pembeni, nguzo moja kila upande.+
41 Kisha akanileta kwenye sehemu ya nje ya patakatifu,* naye akapima nguzo za pembeni; zilikuwa na upana wa mikono sita* upande mmoja na mikono sita upande mwingine. 2 Mlango ulikuwa na upana wa mikono kumi, na kuta za pembeni za mlango zilikuwa mikono mitano upande mmoja na mikono mitano upande wa pili. Akapima urefu wake, ambao ulikuwa mikono 40, na upana wake, mikono 20.
3 Kisha akaingia ndani* na kupima nguzo ya pembeni ya mlango, nayo ilikuwa na unene wa mikono miwili, na mlango ulikuwa na upana wa mikono sita. Kuta za pembeni za mlango zilikuwa* mikono saba. 4 Kisha akapima chumba kilichotazamana na sehemu ya nje ya patakatifu, na urefu wake ulikuwa mikono 20, na upana wake mikono 20.+ Naye akaniambia: “Hapa ndipo Patakatifu Zaidi.”+
5 Kisha akapima ukuta wa hekalu, na unene wake ulikuwa mikono sita. Na vyumba vya kando kuzunguka hekalu vilikuwa na upana wa mikono minne.+ 6 Vyumba vya kando vilikuwa na ghorofa tatu, moja juu ya nyingine, na kila ghorofa ilikuwa na vyumba 30. Kulikuwa na vidato kuzunguka pande zote za ukuta wa hekalu ambavyo vilishikilia vyumba vya kando, ili vishikio visiguse ukuta wa hekalu lenyewe.+ 7 Pande zote mbili za hekalu zilikuwa na njia iliyopindapinda* ambayo ilipanuka kadiri ilivyopanda kuelekea vyumba vya juu.+ Upana uliongezeka kutoka ghorofa moja hadi nyingine kadiri mtu alivyopanda kutoka ghorofa ya chini hadi ya juu akipitia ghorofa ya katikati.
8 Nikaona kwamba kulikuwa na jukwaa lililoinuliwa kuzunguka hekalu, na misingi ya vyumba vya kando ilikuwa na urefu wa utete mmoja wa mikono sita mpaka kwenye pembe. 9 Upana wa ukuta wa nje wa vyumba vya kando ulikuwa mikono mitano. Kulikuwa na eneo lililo wazi* kando ya vyumba vya kando vilivyokuwa sehemu ya hekalu.
10 Kati ya hekalu na vile vyumba vya kulia chakula*+ kulikuwa na eneo lenye upana wa mikono 20 kila upande. 11 Kulikuwa na mlango kati ya vyumba vya kando na eneo lililo wazi lililokuwa upande wa kaskazini na mlango mwingine upande wa kusini. Upana wa eneo lililo wazi ulikuwa mikono mitano pande zote.
12 Jengo lililokuwa magharibi likitazama eneo lililo wazi lilikuwa na upana wa mikono 70 na urefu wa mikono 90; ukuta wa jengo hilo ulikuwa na unene wa mikono mitano pande zote.
13 Akapima hekalu, nalo lilikuwa na urefu wa mikono 100. Lile eneo lililo wazi, jengo,* na kuta zake zilikuwa pia na urefu wa mikono 100. 14 Upana wa upande wa mbele wa hekalu uliotazama mashariki na pia wa eneo lililo wazi ulikuwa mikono 100.
15 Akapima urefu wa jengo lililotazama eneo lililo wazi upande wa nyuma, pamoja na mabaraza yake pande zote mbili, na urefu wake ulikuwa mikono 100.
Pia akapima sehemu ya nje ya patakatifu, sehemu ya ndani ya patakatifu,+ na zile kumbi za ua, 16 pia vizingiti, madirisha yenye viunzi ambavyo ukubwa wake ulipungua kutoka nje kwenda ndani,+ na mabaraza yaliyokuwa katika sehemu hizo tatu. Karibu na kizingiti kulikuwa na mbao+ zilizofunika kuta kuanzia sakafuni mpaka kwenye madirisha; nayo madirisha yalikuwa yamefunikwa. 17 Pia alipima sehemu ya juu ya mlango na sehemu ya ndani ya hekalu na nje na kuzunguka ukuta wote. 18 Kulikuwa na michongo ya makerubi+ na pia michongo ya mitende,+ kila mtende ulikuwa kati ya makerubi wawili, na kila kerubi alikuwa na nyuso mbili. 19 Uso wa mwanadamu ulitazama mtende upande mmoja, na uso wa simba* ulitazama mtende upande wa pili.+ Ilichongwa hivyo katika hekalu lote. 20 Kuanzia sakafuni mpaka sehemu iliyo juu ya mlango kulikuwa na michongo ya makerubi na michongo ya mitende kwenye ukuta wa patakatifu.
21 Miimo ya milango* ya patakatifu ilikuwa mraba.+ Mbele ya mahali patakatifu* kulikuwa na kitu kama 22 madhabahu ya mbao+ iliyokuwa na kimo cha mikono mitatu, na urefu wa mikono miwili. Ilikuwa na nguzo za pembeni, na sehemu yake ya chini* na kuta zake zilitengenezwa kwa mbao. Kisha akaniambia: “Hii ndiyo meza iliyo mbele za Yehova.”+
23 Kulikuwa na milango miwili katika sehemu ya nje ya patakatifu na pia mahali patakatifu.+ 24 Milango ilikuwa na bawaba mbili zilizozunguka, bawaba mbili kwa kila mlango. 25 Kulikuwa na michongo ya makerubi na michongo ya mitende kwenye milango ya patakatifu, kama ile iliyokuwa ukutani.+ Pia kulikuwa na kifuniko* cha mbao juu ya upande wa mbele wa ukumbi kwa nje. 26 Pia kulikuwa na madirisha yenye viunzi ambavyo ukubwa wake ulipungua kutoka nje kwenda ndani+ na michongo ya mitende pande zote mbili za ukumbi, pia kwenye vyumba vya kando vya hekalu na vifuniko.
42 Kisha akanipeleka kwenye ua wa nje kuelekea kaskazini.+ Naye akanileta kwenye jengo lenye vyumba vya kulia chakula lililopakana na eneo lililo wazi,+ upande wa kaskazini wa jengo linalofuata.+ 2 Urefu wake katika mlango wa kaskazini ulikuwa mikono 100,* na upana wake mikono 50. 3 Lilikuwa kati ya ua wa ndani, ambao ulikuwa na upana wa mikono 20,+ na sakafu ya ua wa nje. Mabaraza yake yalitazamana na yalikuwa na urefu wa ghorofa tatu. 4 Mbele ya vyumba vya kulia chakula* kulikuwa na njia ya ndani+ yenye upana wa mikono 10 na urefu wa mikono 100,* na milango yake ilitazama kaskazini. 5 Vyumba vya kulia chakula vilivyokuwa juu katika jengo hilo vilikuwa vyembamba kuliko vile vya chini na vya katikati, kwa sababu mabaraza yalichukua nafasi kubwa ya vyumba hivyo. 6 Kwa maana mabaraza yalikuwa na urefu wa ghorofa tatu, lakini hayakuwa na nguzo kama nguzo za nyua. Ndiyo sababu nafasi kubwa zaidi ya vyumba vilivyokuwa juu ilichukuliwa na mabaraza kuliko katika ghorofa ya chini na ya katikati.
7 Ukuta wa nje wa mawe uliokuwa karibu na vyumba vya kulia chakula kuelekea ua wa nje uliotazama vile vyumba vingine vya kulia chakula ulikuwa na urefu wa mikono 50. 8 Kwa maana urefu wa vyumba vya kulia chakula vilivyotazama ua wa nje ulikuwa mikono 50, lakini vile vilivyotazama patakatifu vilikuwa na urefu wa mikono 100. 9 Kulikuwa na njia iliyoelekea kwenye vyumba vya kulia chakula upande wa mashariki kutoka kwenye ua wa nje.
10 Kulikuwa pia na vyumba vya kulia chakula katika* ukuta wa mawe wa ua upande wa mashariki, karibu na eneo lililo wazi na pia jengo.+ 11 Mbele ya vyumba hivyo kulikuwa na njia kama ile ya vyumba vya kulia chakula vya kaskazini.+ Vyumba hivyo vilikuwa na urefu na upana uleule, na milango yake ya kutokea na ramani yake ililingana na ya vyumba vya kaskazini vya kulia chakula. Milango yake 12 ilikuwa kama milango ya vyumba vya kusini vya kulia chakula. Kulikuwa na mlango mahali ambapo njia ilianzia, kabla ya ukuta wa mawe uliokuwa upande wa mashariki, mahali ambapo mtu angeweza kuingilia.+
13 Kisha akaniambia: “Vyumba vya kulia chakula vya kaskazini na vyumba vya kulia chakula vya kusini vinavyopakana na eneo lililo wazi+ ndivyo vyumba vya kulia chakula vilivyo vitakatifu ambamo makuhani wanaomkaribia Yehova hula matoleo matakatifu zaidi.+ Matoleo matakatifu zaidi, toleo la nafaka, dhabihu ya dhambi, na dhabihu ya hatia huwekwa humo, kwa sababu mahali hapo ni patakatifu.+ 14 Makuhani wanapoingia, hawapaswi kutoka mahali patakatifu na kwenda kwenye ua wa nje kabla hawajavua mavazi wanayovaa wanapohudumu,+ kwa sababu ni matakatifu. Watavaa mavazi mengine ili waende katika maeneo ambayo watu wanaruhusiwa kuingia.”
15 Alipomaliza kupima sehemu ya ndani ya hekalu,* akanipeleka nje kupitia lango linalotazama mashariki,+ naye akapima eneo hilo lote.
16 Akapima upande wa mashariki kwa ule utete wa kupimia.* Ulikuwa na urefu wa tete 500 kutoka upande mmoja hadi mwingine, kulingana na utete wa kupimia.
17 Akapima upande wa kaskazini, nao ulikuwa na urefu wa tete 500, kulingana na utete wa kupimia.
18 Akapima upande wa kusini, nao ulikuwa na urefu wa tete 500, kulingana na utete wa kupimia.
19 Akazunguka upande wa magharibi. Akapima urefu wa tete 500 kwa utete wa kupimia.
20 Akapima pande nne za eneo hilo. Lilikuwa na ukuta uliolizunguka pande zote+ uliokuwa na urefu wa tete 500 na upana wa tete 500,+ ili kutenganisha kitu kitakatifu na kitu cha matumizi ya kawaida.+
43 Kisha akanipeleka kwenye lango linalotazama mashariki.+ 2 Hapo nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka mashariki,+ na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji yenye kishindo;+ nayo dunia iling’aa kwa utukufu wake.+ 3 Mambo niliyoona yalikuwa kama maono niliyoona nilipokuja* kuliangamiza jiji, na yalionekana kama mambo niliyoona karibu na mto Kebari;+ nami nikaanguka kifudifudi.
4 Kisha utukufu wa Yehova ukaingia hekaluni* kupitia lango lililotazama mashariki.+ 5 Ndipo roho ikaniinua na kuniingiza kwenye ua wa ndani, nami nikaona kwamba hekalu lilikuwa limejaa utukufu wa Yehova.+ 6 Kisha nikasikia mtu akizungumza nami kutoka katika lile hekalu, na mtu huyo akaja na kusimama kando yangu.+ 7 Akaniambia:
“Mwana wa binadamu, hapa ndipo mahali pa kiti changu cha ufalme+ na mahali pa nyayo za miguu yangu,+ ambapo nitakaa kati ya watu wa Israeli milele.+ Watu wa nyumba ya Israeli hawatalichafua tena jina langu takatifu,+ wao na wafalme wao, kwa ukahaba wao wa kiroho na kwa maiti za wafalme wao wanapokufa. 8 Kwa kuweka kizingiti chao kando ya kizingiti changu na mwimo wa mlango wao kando ya mwimo wa mlango wangu, kukiwa na ukuta tu kati yangu nao,+ walilichafua jina langu takatifu kwa mambo yanayochukiza waliyotenda hivi kwamba nikawaangamiza kabisa kwa hasira yangu.+ 9 Basi sasa na wauweke mbali nami ukahaba wao wa kiroho na maiti za wafalme wao, nami nitakaa miongoni mwao milele.+
10 “Na wewe, mwana wa binadamu, waeleze watu wa nyumba ya Israeli kuhusu hekalu+ ili waaibike kwa sababu ya makosa yao,+ nao wanapaswa kuichunguza ramani yake.* 11 Ikiwa wataaibika kwa sababu ya mambo yote ambayo wamefanya, unapaswa kuwaonyesha ramani ya hekalu, mpangilio wake, na njia zake za kutokea, na za kuingilia.+ Waonyeshe ramani zake zote na maagizo yake, ramani zake na sheria zake, nawe uziandike mbele ya macho yao, ili waone ramani zake zote na kufuata maagizo yake.+ 12 Hii ndiyo sheria ya hekalu. Eneo lote kuzunguka juu ya mlima ni takatifu zaidi.+ Tazama! Hii ndiyo sheria ya hekalu.
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa kipimo cha mikono+ (kila mkono uliongezwa kiganja kimoja).* Sehemu yake ya chini ni mkono mmoja na upana wake mkono mmoja. Ina ukingo ambao upana wake ni shubiri* moja kuzunguka pembeni. Hiyo ndiyo sehemu ya chini ya madhabahu. 14 Kuanzia sehemu ya chini ya sakafu mpaka kwenye kidato cha chini kinachozunguka pande zote ni mikono miwili, na upana wake ni mkono mmoja. Kuanzia kidato kidogo kinachozunguka pande zote mpaka kwenye kidato kikubwa kinachozunguka pande zote ni mikono minne, na upana wake ni mkono mmoja. 15 Jiko la madhabahu lina urefu wa mikono minne, na kutoka kwenye jiko la madhabahu kuelekea juu kuna zile pembe nne.+ 16 Jiko la madhabahu ni la mraba, urefu wake ni mikono 12 na upana wake ni mikono 12.+ 17 Pande nne za kidato kinachozunguka zina urefu wa mikono 14 na upana wa mikono 14; na ukingo unaozunguka ni nusu mkono, na sehemu yake ya chini ni mkono mmoja pande zote.
“Na ngazi zake zinatazama upande wa mashariki.”
18 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Hii ndiyo miongozo ya kufuata madhabahu inapotengenezwa, ili dhabihu nzima za kuteketezwa zitolewe na damu inyunyizwe juu yake.’+
19 “‘Utawapa makuhani Walawi wazao wa Sadoki+ wanaonikaribia ili kunihudumia ng’ombe dume mchanga wa kundi kwa ajili ya dhabihu ya dhambi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 20 ‘Unapaswa kuchukua kiasi fulani cha damu yake na kuitia kwenye zile pembe nne za madhabahu, juu ya ncha nne za kidato kinachozunguka pande zote, na juu ya ukingo unaozunguka pande zote, ili kuitakasa kutokana na dhambi na kufunika dhambi yake.+ 21 Kisha utamchukua yule ng’ombe dume mchanga, ile dhabihu ya dhambi, ili umteketeze mahali palipochaguliwa pa hekalu, nje ya patakatifu.+ 22 Katika siku ya pili utatoa mbuzi dume ambaye hana kasoro kwa ajili ya dhabihu ya dhambi; nao wataitakasa madhabahu kutokana na dhambi kama walivyoitakasa kutokana na dhambi kwa kutumia yule ng’ombe dume mchanga.’
23 “‘Utakapomaliza kuitakasa kutokana na dhambi, utatoa ng’ombe dume mchanga wa kundi ambaye hana kasoro na kondoo dume wa kundi ambaye hana kasoro. 24 Nawe utawaleta kwa Yehova, na makuhani watawanyunyizia chumvi+ na kuwatoa kwa Yehova wakiwa dhabihu nzima ya kuteketezwa. 25 Kwa siku saba utamtoa mbuzi dume kwa ajili ya dhabihu ya dhambi kila siku,+ pia ng’ombe dume mchanga wa mifugo, na kondoo dume kutoka katika kundi; utawatoa wanyama ambao hawana kasoro.* 26 Kwa siku saba watafunika dhambi ya madhabahu, nao wataitakasa na kuiweka tayari. 27 Baada ya siku hizo kwisha, siku ya nane+ na kuendelea, kuhani atatoa dhabihu zenu* nzima za kuteketezwa na dhabihu za ushirika kwenye madhabahu; nami nitafurahishwa nanyi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
44 Akanirudisha kupitia lango la nje la patakatifu lililotazama mashariki,+ nalo lilikuwa limefungwa.+ 2 Ndipo Yehova akaniambia: “Lango hili litabaki likiwa limefungwa. Halipaswi kufunguliwa, na hakuna mwanadamu yeyote atakayelitumia kuingia; kwa maana mimi Yehova, Mungu wa Israeli, nimeingia kupitia lango hilo,+ basi linapaswa kubaki likiwa limefungwa. 3 Hata hivyo, kiongozi ataketi humo ili ale mkate mbele zangu mimi Yehova,+ kwa maana yeye ni kiongozi. Ataingia kupitia ukumbi wa lango, naye atatoka kupitia lango hilo.”+
4 Kisha akanileta kupitia lango la kaskazini mpaka mbele ya hekalu. Nilipotazama nikaona kwamba utukufu wa Yehova ulikuwa umejaa katika hekalu la Yehova.+ Basi nikaanguka chini kifudifudi.+ 5 Ndipo Yehova akaniambia: “Mwana wa binadamu, kaza fikira,* angalia, na usikilize kwa makini nitakayokuambia kuhusu maagizo na sheria za hekalu la Yehova. Tazama kwa makini sana njia ya kuingia hekaluni na njia zote za kutokea patakatifu.+ 6 Utawaambia hivi watu wa nyumba ya Israeli walioasi: ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Matendo yenu yanayochukiza yametosha, enyi watu wa nyumba ya Israeli. 7 Mnapowaleta patakatifu pangu wageni ambao hawajatahiriwa moyoni na mwilini, wanalitia unajisi hekalu langu. Mnatoa mkate wangu, mafuta, na damu, huku agano langu likivunjwa kwa sababu ya matendo yenu yote yanayochukiza. 8 Hamjavitunza vitu vyangu vitakatifu.+ Badala yake mnawapa wengine majukumu ya kuhudumu mahali pangu patakatifu.”’
9 “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Hakuna mgeni yeyote anayeishi Israeli ambaye hajatahiriwa moyoni na mwilini atakayeingia mahali pangu patakatifu.”’
10 “‘Lakini Walawi waliotangatanga na kwenda mbali nami+ Waisraeli waliponiacha ili kufuata sanamu zao zinazochukiza* watapata madhara ya kosa lao. 11 Nao watakuwa wahudumu wa mahali pangu patakatifu ili kusimamia malango ya hekalu+ na kuhudumu hekaluni. Watawachinja wanyama wa dhabihu nzima za kuteketezwa na dhabihu kwa ajili ya watu, nao watasimama mbele ya watu ili kuwahudumia. 12 Kwa sababu waliwahudumia mbele ya sanamu zao zinazochukiza nao wakawa kikwazo na kuwafanya watu wa nyumba ya Israeli watende dhambi,+ ndiyo sababu nimeinua mkono wangu dhidi yao na kuapa,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nao watapata madhara ya kosa lao. 13 Hawatanikaribia ili kunitumikia wakiwa makuhani wangu wala kukaribia kitu chochote kati ya vitu vyangu vitakatifu au vitu vitakatifu kabisa, nao watabeba aibu yao kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza waliyofanya. 14 Lakini nitawapa kazi ya kushughulikia majukumu ya hekalu, kushughulikia utumishi wa hekaluni na mambo yote yanayopaswa kufanywa humo.’+
15 “‘Nao makuhani Walawi, wana wa Sadoki,+ walioshughulikia majukumu ya mahali pangu patakatifu Waisraeli waliponiacha,+ watanikaribia ili kunihudumia, nao watasimama mbele zangu ili kunitolea mafuta+ na damu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 16 ‘Hao ndio watakaoingia mahali pangu patakatifu, nao wataikaribia meza yangu ili kunihudumia,+ nao watatimiza majukumu yangu.+
17 “‘Wanapoingia kwenye malango ya ua wa ndani, wanapaswa kuvaa mavazi ya kitani.+ Hawapaswi kuvaa vazi lolote la sufu wanapohudumu katika malango ya ua wa ndani au wakiwa ndani. 18 Wanapaswa kuvaa vilemba vya kitani kichwani, nao wanapaswa kuvaa suruali fupi za kitani viunoni mwao.+ Hawapaswi kuvaa chochote kitakachofanya watokwe na jasho. 19 Kabla ya kwenda kwenye ua wa nje—ua wa nje mahali palipo na watu—wanapaswa kuyavua mavazi waliyokuwa wamevaa walipokuwa wakihudumu+ na kuyaweka katika vyumba vitakatifu vya kulia chakula.*+ Kisha watavaa mavazi mengine, ili wasije wakawapitishia watu utakatifu* kwa mavazi hayo. 20 Hawapaswi kunyoa kichwa chao+ au kuacha nywele za kichwa chao ziwe ndefu. Wanapaswa kupunguza nywele za vichwa vyao. 21 Makuhani hawapaswi kunywa divai wanapoingia kwenye ua wa ndani.+ 22 Hawapaswi kumwoa mjane au mwanamke aliyetalikiwa;+ lakini wanaweza kumwoa bikira wa uzao wa Israeli au mjane wa kuhani.’+
23 “‘Wanapaswa kuwafundisha watu wangu tofauti kati ya kitu kitakatifu na kitu cha kawaida; nao watawafundisha tofauti kati ya kitu kisicho safi na kitu kilicho safi.+ 24 Wanapaswa kuwa waamuzi katika kesi;+ ni lazima wahukumu kulingana na sheria zangu.*+ Wanapaswa kufuata sheria zangu na amri zangu zinazohusu sherehe zangu zote+ na kuzitakasa sabato zangu. 25 Hawapaswi kumkaribia mwanadamu yeyote aliyekufa, la sivyo hawatakuwa safi. Hata hivyo, wanaweza kujichafua kwa ajili ya baba, mama, mwana, binti, au dada yao ambaye hajaolewa.+ 26 Na baada ya kuhani kutakaswa, wanapaswa kumhesabia siku saba. 27 Siku anayoingia katika mahali patakatifu, katika ua wa ndani, ili kuhudumu katika mahali patakatifu anapaswa kutoa dhabihu yake ya dhambi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
28 “‘Na huu ndio utakaokuwa urithi wao: Mimi ndiye urithi wao.+ Msiwape mali yoyote katika Israeli, kwa maana mimi ndiye mali yao. 29 Wao ndio watakaokula toleo la nafaka,+ dhabihu ya dhambi, na dhabihu ya hatia,+ na kila kitu kilichotolewa katika Israeli kitakuwa chao.+ 30 Matunda yote ya kwanza yaliyo bora na kila aina ya mchango mtakaotoa utakuwa wa makuhani.+ Nanyi mnapaswa kumpatia kuhani mavuno ya kwanza ya unga wenu ambao haujakobolewa.+ Hilo litafanya baraka ikae juu ya nyumba zenu.+ 31 Makuhani hawapaswi kula ndege yeyote au mnyama yeyote aliyepatikana amekufa au kuraruliwa vipandevipande.’+
45 “‘Mtakapoigawa nchi iwe urithi,+ mnapaswa kumtolea Yehova sehemu takatifu ya nchi kuwa mchango.+ Inapaswa kuwa na urefu wa mikono 25,000,* na upana wa mikono 10,000.+ Eneo hilo lote litakuwa* sehemu takatifu. 2 Ndani yake kutakuwa na eneo la mraba la mahali patakatifu lenye urefu wa mikono 500 na upana wa mikono 500,*+ na kila upande litakuwa na malisho yenye kipimo cha mikono 50.+ 3 Na kutoka katika kipimo hicho utapima urefu wa 25,000 na upana wa 10,000, na ndani yake kutakuwa na mahali patakatifu, kitu kitakatifu kabisa. 4 Litakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani,+ wahudumu wa mahali patakatifu, wanaokaribia ili kumhudumia Yehova.+ Patakuwa mahali kwa ajili ya nyumba zao, na mahali patakatifu kwa ajili ya patakatifu.
5 “‘Walawi, wahudumu wa hekaluni, watakuwa na sehemu yenye urefu wa mikono 25,000 na upana wa mikono 10,000,+ nao watamiliki vyumba 20 vya kulia chakula.*+
6 “‘Mnapaswa kutoa sehemu ya jiji yenye urefu wa mikono 25,000 (inayolingana na mchango mtakatifu) na upana wa mikono 5,000.+ Itakuwa ya watu wote wa nyumba ya Israeli.
7 “‘Na kwa ajili ya kiongozi kutakuwa na ardhi pande zote mbili za ule mchango mtakatifu na eneo lililogawiwa jiji. Itapakana na ule mchango mtakatifu na eneo la jiji. Itakuwa upande wa magharibi na upande wa mashariki. Urefu wake kuanzia mpaka wa magharibi hadi mpaka wa mashariki utakuwa sawa na mojawapo ya sehemu za makabila.+ 8 Ardhi hii itakuwa mali yake katika Israeli. Nao viongozi wangu hawatawatesa tena watu wangu,+ nao watawapa nchi watu wa nyumba ya Israeli kulingana na makabila yao.’+
9 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Imetosha, enyi viongozi wa Israeli!’
“‘Acheni ukatili na ukandamizaji, na mtende mambo ya haki na ya uadilifu.+ Acheni kuchukua kwa nguvu mali ya watu wangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 10 ‘Mnapaswa kutumia mizani sahihi na kipimo sahihi cha efa* na kipimo sahihi cha bathi.*+ 11 Kunapaswa kuwa na kipimo hususa cha efa na cha bathi. Kipimo cha bathi kinapaswa kuwa sehemu ya kumi ya homeri* na kipimo cha efa kinapaswa kuwa sehemu ya kumi ya homeri. Homeri ndiyo itakayokuwa kiwango cha kupimia. 12 Shekeli*+ inapaswa kuwa gera 20.* Na shekeli 20 ukijumlisha na shekeli 25 na pia shekeli 15, jumla yake itakuwa mane* moja kwako.’
13 “‘Huu ndio mchango unaopaswa kutoa: sehemu ya sita ya efa kutoka katika kila homeri ya ngano, na sehemu ya sita ya efa kutoka katika kila homeri ya shayiri. 14 Posho ya mafuta inapaswa kupimwa kwa kipimo cha bathi. Bathi ni sehemu ya kumi ya kori* na bathi kumi ni homeri moja, kwa sababu bathi kumi zinalingana na homeri moja. 15 Na kutoka katika kundi la mifugo ya Waisraeli, kondoo mmoja anapaswa kutolewa kwa kila kondoo 200. Hawa watatolewa kwa ajili ya toleo la nafaka,+ dhabihu nzima ya kuteketezwa,+ na dhabihu za ushirika,+ ili kufunika dhambi za watu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
16 “‘Watu wote nchini watatoa mchango huu+ kwa kiongozi wa Israeli. 17 Lakini kiongozi atakuwa na wajibu wa kushughulikia dhabihu nzima za kuteketezwa,+ toleo la nafaka,+ na toleo la kinywaji wakati wa sherehe,+ miezi mipya, Sabato,+ na sherehe zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli.+ Yeye ndiye atakayetoa dhabihu ya dhambi, toleo la nafaka, dhabihu nzima ya kuteketezwa, na dhabihu za ushirika, ili kufunika dhambi za watu wa nyumba ya Israeli.’
18 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi huo, unapaswa kumchukua ng’ombe dume mchanga asiye na kasoro kutoka katika mifugo, nawe utapatakasa mahali patakatifu kutokana na dhambi.+ 19 Kuhani atachukua sehemu ya damu ya dhabihu ya dhambi na kuiweka kwenye mwimo wa mlango wa hekalu,+ juu ya zile pembe nne za ukingo unaozunguka madhabahu, na juu ya mwimo wa lango la ua wa ndani. 20 Hivyo ndivyo utakavyofanya katika siku ya saba ya mwezi kwa sababu ya mtu yeyote anayefanya dhambi bila kukusudia au bila kujua;+ nanyi mtatoa dhabihu ya kufunika dhambi ya hekalu.+
21 “‘Katika mwezi wa kwanza, siku ya 14 ya mwezi huo, mtafanya sherehe ya Pasaka.+ Kwa siku saba mnapaswa kula mikate isiyo na chachu.+ 22 Siku hiyo kiongozi atatoa ng’ombe dume mchanga awe dhabihu ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote nchini.+ 23 Kwa siku saba za sherehe atamtolea Yehova dhabihu nzima ya kuteketezwa ya ng’ombe dume saba wachanga wasio na kasoro na kondoo dume saba wasio na kasoro kila siku kwa siku hizo saba,+ atatoa pia mbuzi dume kila siku awe dhabihu ya dhambi. 24 Pia anapaswa kutoa toleo la nafaka la efa moja kwa ajili ya kila ng’ombe dume mchanga na efa moja kwa ajili ya kila kondoo dume, vilevile hini* moja ya mafuta kwa kila efa.
25 “‘Katika mwezi wa saba, siku ya 15 ya mwezi huo, kwa siku saba wakati wa sherehe,+ anapaswa kutoa dhabihu ileile ya dhambi, dhabihu nzima ya kuteketezwa, toleo la nafaka, na mafuta.’”
46 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Lango la ua wa ndani linalotazama mashariki+ linapaswa kubaki likiwa limefungwa+ kwa siku sita za kazi,+ lakini siku ya Sabato na siku ya mwezi mpya linapaswa kufunguliwa. 2 Kiongozi ataingia ndani kupitia njia ya ukumbi wa lango,+ naye atasimama kando ya mwimo wa lango. Makuhani watatoa dhabihu yake nzima ya kuteketezwa na dhabihu zake za ushirika, naye atainama chini kwenye kizingiti cha lango na kutoka nje. Lakini lango linapaswa kubaki wazi mpaka jioni. 3 Watu wa nchi watainama chini pia mbele za Yehova kwenye kizingiti cha lango hilo siku za Sabato na wakati wa miezi mipya.+
4 “‘Siku ya Sabato kiongozi atamtolea Yehova dhabihu nzima ya kuteketezwa ya wanakondoo dume sita wasio na kasoro na kondoo dume asiye na kasoro.+ 5 Toleo la nafaka litakuwa efa moja* kwa ajili ya yule kondoo dume na chochote anachoweza kutoa kwa ajili ya wale wanakondoo dume, pamoja na hini moja* ya mafuta kwa kila efa.+ 6 Siku ya mwezi mpya atatoa ng’ombe dume mchanga wa kundi asiye na kasoro, wanakondoo sita dume, na kondoo dume mmoja; hawapaswi kuwa na kasoro.+ 7 Atatoa toleo la nafaka la efa moja kwa ajili ya yule ng’ombe dume mchanga, na efa moja kwa ajili ya yule kondoo dume, na chochote anachoweza kutoa kwa ajili ya wale wanakondoo dume. Naye anapaswa kutoa hini moja ya mafuta kwa kila efa.
8 “‘Kiongozi anapoingia, anapaswa kuingia kupitia njia ya ukumbi wa lango, naye anapaswa kutoka kupitia njia hiyohiyo.+ 9 Na watu wa nchi wanapoingia mbele za Yehova wakati wa sherehe,+ wale wanaoingia kupitia lango la kaskazini+ ili kuabudu, wanapaswa kutoka kupitia lango la kusini,+ na wale wanaoingia kupitia lango la kusini wanapaswa kutoka kupitia lango la kaskazini. Mtu yeyote asirudi kupitia lango aliloingilia, kwa maana wanapaswa kutoka kupitia lango lililo upande mwingine. 10 Naye kiongozi aliye miongoni mwao, anapaswa kuingia wanapoingia, na kutoka wanapotoka. 11 Wakati wa sherehe na majira ya sherehe anapaswa kutoa toleo la nafaka la efa moja kwa ajili ya yule ng’ombe dume mchanga, efa moja kwa ajili ya yule kondoo dume, na chochote anachoweza kutoa kwa ajili ya wale wanakondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.+
12 “‘Ikiwa kiongozi atatoa dhabihu nzima ya kuteketezwa+ au dhabihu za ushirika ziwe toleo la hiari kwa Yehova, atafunguliwa lango linalotazama mashariki, naye atatoa dhabihu yake nzima ya kuteketezwa na dhabihu zake za ushirika kama anavyofanya siku ya Sabato.+ Baada ya kutoka nje, lango linapaswa kufungwa.+
13 “‘Kila siku unapaswa kumtoa mwanakondoo dume asiye na kasoro aliye katika mwaka wake wa kwanza awe dhabihu nzima ya kuteketeza kwa Yehova.+ Unapaswa kufanya hivyo kila asubuhi. 14 Pamoja na mwanakondoo huyo, kila asubuhi unapaswa kutoa sehemu ya sita ya efa iwe toleo la nafaka, pamoja na sehemu ya tatu ya hini ya mafuta ili inyunyizwe juu ya unga laini kama toleo la kawaida la nafaka kwa Yehova. Hii ni sheria ya kudumu. 15 Wanapaswa kumtoa mwanakondoo dume, toleo la nafaka, na mafuta kila asubuhi kama dhabihu nzima ya kuteketezwa ya kawaida.’
16 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kiongozi akimpa zawadi kila mmoja wa wanawe iwe urithi, itakuwa mali ya wanawe. Hiyo ni miliki yao waliyorithi. 17 Lakini akimpa mmoja wa watumishi wake zawadi kutoka katika urithi wake, itakuwa yake mpaka mwaka wa uhuru;+ kisha itarudi kwa kiongozi. Urithi wa wanawe tu ndio utakaokuwa wao daima. 18 Kiongozi hapaswi kuchukua urithi wowote wa watu kwa kuwalazimisha waondoke katika mali yao. Anapaswa kuwapa wanawe urithi kutoka kwenye mali yake mwenyewe, ili mtu yeyote miongoni mwa watu wangu asiondolewe kwa lazima katika mali yake.’”
19 Kisha akaniingiza kupitia njia+ iliyokuwa kando ya lango linaloelekea kwenye vyumba vitakatifu vya kulia chakula* vya makuhani, vilivyotazama kaskazini,+ na hapo nikaona mahali upande wa nyuma kuelekea magharibi. 20 Akaniambia: “Hapa ndipo mahali ambapo makuhani watachemshia dhabihu ya hatia na dhabihu ya dhambi na mahali ambapo wataokea toleo la nafaka,+ ili wasibebe chochote na kukipeleka kwenye ua wa nje na kuwapitishia watu utakatifu.”*+
21 Akanitoa nje kwenye ua wa nje na kuniongoza kupitia zile pembe nne za ua, nami nikaona ua kando ya kila pembe ya ua wa nje. 22 Kwenye hizo pembe nne za ua kulikuwa na nyua ndogo, zenye urefu wa mikono 40* na upana wa mikono 30. Nyua zote nne zilikuwa na ukubwa uleule.* 23 Kulikuwa na vidato* kuzunguka nyua zote nne, na chini ya vidato hivyo walijenga sehemu za kuchemshia dhabihu. 24 Kisha akaniambia: “Hizi ndizo nyumba ambamo wahudumu wa hekalu huchemshia dhabihu zinazoletwa na watu.”+
47 Kisha akanirudisha kwenye mlango wa hekalu,+ na hapo nikaona maji yakitiririka kuelekea mashariki kutoka chini ya kizingiti cha hekalu,+ kwa maana upande wa mbele wa hekalu ulitazama mashariki. Maji hayo yalikuwa yakitiririka kutoka chini upande wa kulia wa hekalu, upande wa kusini wa madhabahu.
2 Kisha akaniongoza nje kupitia lango la kaskazini+ na kunizungusha nje mpaka kwenye lango la nje linalotazama upande wa mashariki,+ nikaona maji yakitiririka kutoka upande wa kulia.
3 Mtu huyo alipotoka nje kuelekea mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake,+ alipima mikono 1,000* na kunipitisha katika maji; maji hayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
4 Kisha akapima mikono mingine 1,000 na kunipitisha katika maji, nayo yalifika mpaka kwenye magoti.
Akapima mikono mingine 1,000 na kunipitisha humo, na maji hayo yalifika kiunoni.
5 Alipopima mikono mingine 1,000, maji yalikuwa mengi sana hivi kwamba singeweza kuvuka, kwa maana maji hayo yalikuwa na kina kirefu hivi kwamba mtu angelazimika kuogelea, maji mengi sana ambayo mtu hangeweza kuvuka kwa miguu.
6 Akaniuliza: “Mwana wa binadamu, je, umeona hili?”
Kisha akanitembeza na kunirudisha kwenye ukingo wa kile kijito. 7 Niliporudi, nikaona miti mingi sana pande zote za ukingo wa kile kijito.+ 8 Ndipo akaniambia: “Maji haya yanatiririka kuelekea eneo la mashariki na yanashuka kupitia Araba*+ na kuingia baharini. Yakiingia baharini,+ maji ya bahari yataponywa. 9 Kila mahali ambapo maji hayo yanapita, makundi makubwa ya viumbe walio* hai yataishi. Kutakuwa na samaki wengi, kwa sababu maji hayo yatatiririka* huko. Maji ya baharini yataponywa, na mahali ambapo kijito hicho kinapita, kila kitu kitaishi.
10 “Wavuvi watasimama kando yake kutoka En-gedi+ mpaka En-eglaimu ambako kutakuwa na uwanja wa kukaushia nyavu za kukokotwa. Kutakuwa na samaki wengi wa aina nyingi, kama samaki wa ile Bahari Kuu.*+
11 “Kutakuwa na sehemu zenye majimaji na matope, nazo hazitaponywa. Zitabaki zikiwa sehemu za chumvi.+
12 “Aina zote za miti ya chakula zitakua kwenye kingo zote mbili za hicho kijito. Majani yake hayatanyauka; wala miti hiyo haitakosa kuzaa matunda. Kila mwezi itazaa matunda mapya, kwa sababu maji yake yanatiririka kutoka patakatifu.+ Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatatumiwa kuponya.”+
13 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Hili ndilo eneo ambalo mtayagawia yale makabila 12 ya Israeli kuwa urithi wao wa ardhi, na Yosefu atapata sehemu mbili.+ 14 Nanyi mtairithi na kuigawa kwa usawa.* Niliapa kuwapatia mababu zenu nchi hii,+ na sasa mmegawiwa* ili iwe urithi wenu.
15 “Huu ndio mpaka wa kaskazini wa nchi: Unaanzia ile Bahari Kuu kupitia njia ya Hethloni+ kuelekea Sedadi,+ 16 Hamathi,+ Berotha,+ na Sibraimu, kati ya eneo la Damasko na eneo la Hamathi, hadi Haser-hatikoni, karibu na mpaka wa Haurani.+ 17 Basi mpaka utaanzia baharini hadi Hasar-enoni,+ kwenye mpaka wa Damasko kuelekea kaskazini, pamoja na mpaka wa Hamathi.+ Huo ndio mpaka wa kaskazini.
18 “Upande wa mashariki mpaka huo unapita kati ya Haurani na Damasko na kando ya Yordani kati ya Gileadi+ na nchi ya Israeli. Mnapaswa kupima kutoka mpakani hadi kwenye bahari ya mashariki.* Huo ndio mpaka wa mashariki.
19 “Mpaka wa kusini* utaanzia Tamari hadi kwenye maji ya Meribath-kadeshi,+ kisha utaelekea kwenye lile Korongo* hadi kwenye ile Bahari Kuu.+ Huo ndio mpaka wa kusini.*
20 “Bahari Kuu iko upande wa magharibi, kuanzia kwenye mpaka hadi kwenye eneo lililo ng’ambo ya Lebo-hamathi.*+ Huo ndio mpaka wa magharibi.”
21 “Mnapaswa kugawana nchi hii miongoni mwenu, miongoni mwa makabila 12 ya Israeli. 22 Mnapaswa kuigawa iwe urithi miongoni mwenu wenyewe na kuwagawia wageni wanaoishi pamoja nanyi ambao wamezaa watoto wakati wanaishi miongoni mwenu; nao watakuwa kwenu kama Waisraeli wenyeji. Watapokea urithi pamoja nanyi miongoni mwa makabila ya Israeli. 23 Mnapaswa kumpa mkaaji mgeni urithi katika eneo la kabila analoishi ndani yake,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
48 “Haya ndiyo majina ya makabila hayo, kuanzia mpaka wa kaskazini: Sehemu ya Dani+ inapita kwenye njia ya Hethloni hadi Lebo-hamathi*+ hadi Hasar-enani, kwenye mpaka wa Damasko kuelekea kaskazini kando ya Hamathi;+ nayo inaanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 2 Sehemu ya Asheri+ iko kwenye mpaka wa Dani, kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 3 Sehemu ya Naftali+ iko kwenye mpaka wa Asheri, kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 4 Sehemu ya Manase+ iko kwenye mpaka wa Naftali, kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 5 Sehemu ya Efraimu iko kwenye mpaka wa Manase,+ kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 6 Sehemu ya Rubeni iko kwenye mpaka wa Efraimu,+ kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 7 Sehemu ya Yuda iko kwenye mpaka wa Rubeni,+ kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 8 Kwenye mpaka wa Yuda, kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, mchango mtakaoweka kando unapaswa kuwa na upana wa mikono 25,000,*+ nao unapaswa kulingana na urefu wa zile sehemu nyingine za makabila kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. Patakatifu patakuwa katikati yake.
9 “Mchango mtakaoweka kando kwa ajili ya Yehova utakuwa na urefu wa mikono 25,000 na upana wa mikono 10,000. 10 Huu ndio utakaokuwa mchango mtakatifu kwa ajili ya makuhani.+ Upande wa kaskazini utakuwa mikono 25,000, upande wa magharibi 10,000, na upande wa mashariki 10,000, na upande wa kusini 25,000. Patakatifu pa Yehova patakuwa katikati yake. 11 Patakuwa pa makuhani waliotakaswa kutoka kwa wana wa Sadoki,+ wale walioshughulikia majukumu niliyowapa na ambao hawakuniacha wakati Waisraeli na Walawi waliponiacha.+ 12 Watapokea sehemu ya mchango wa nchi hiyo iliyowekwa kando kuwa kitu kitakatifu kabisa, kwenye mpaka wa Walawi.
13 “Kando tu ya eneo la makuhani, Walawi watakuwa na sehemu yenye urefu wa mikono 25,000, na upana wa mikono 10,000. (Urefu wote utakuwa 25,000 na upana 10,000.) 14 Hawapaswi kuuza, kubadilisha, au kumpa mtu mwingine eneo lolote la sehemu hii bora ya nchi, kwa maana ni kitu kitakatifu kwa Yehova.
15 “Eneo linalobaki lenye upana wa mikono 5,000 lililo kando ya mpaka wenye urefu wa mikono 25,000 litakuwa la matumizi ya kawaida ya jiji,+ kwa ajili ya makao na malisho. Jiji litakuwa katikati yake.+ 16 Hivi ndivyo vipimo vya jiji: Mpaka wa kaskazini mikono 4,500, mpaka wa kusini 4,500, mpaka wa mashariki 4,500, na mpaka wa magharibi 4,500. 17 Malisho ya jiji yatakuwa mikono 250 upande wa kaskazini, 250 upande wa kusini, 250 upande wa mashariki, na 250 upande wa magharibi.
18 “Urefu wa sehemu inayobaki utalingana na mchango mtakatifu,+ upande wa mashariki mikono 10,000, na upande wa magharibi 10,000. Italingana na mchango mtakatifu na mazao yake yatakuwa chakula cha wale wanaolitumikia jiji. 19 Wale wanaolitumikia jiji kutoka katika makabila yote ya Israeli watailima sehemu hiyo.+
20 “Mchango mzima ni mikono 25,000 mraba. Mnapaswa kuuweka kando uwe mchango mtakatifu pamoja na miliki ya jiji.
21 “Sehemu itakayobaki pande zote za mchango mtakatifu na wa miliki ya jiji itakuwa mali ya kiongozi.+ Itakuwa kando ya mipaka yenye urefu wa mikono 25,000 iliyo upande wa mashariki na magharibi wa ule mchango. Italingana na sehemu zinazopakana, na itakuwa ya kiongozi. Mchango mtakatifu na patakatifu pa hekalu patakuwa katikati yake.
22 “Miliki ya Walawi na miliki ya jiji itakuwa kati ya mali ya kiongozi. Eneo la kiongozi litakuwa kati ya mpaka wa Yuda+ na Benjamini.
23 “Na kuhusu makabila yanayobaki, sehemu ya Benjamini inaanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi.+ 24 Sehemu ya Simeoni iko kando ya mpaka wa Benjamini,+ kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 25 Sehemu ya Isakari+ iko kando ya mpaka wa Simeoni, kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 26 Sehemu ya Zabuloni iko kando ya mpaka wa Isakari,+ kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi.+ 27 Sehemu ya Gadi iko kando ya mpaka wa Zabuloni,+ kuanzia mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. 28 Mpaka wa kusini ulio kando ya mpaka wa Gadi utaanzia Tamari+ hadi kwenye maji ya Meribath-kadeshi,+ hadi kwenye lile Korongo*+ na kwenda hadi kwenye ile Bahari Kuu.*
29 “Hii ndiyo nchi ambayo mnapaswa kuigawa iwe urithi wa makabila ya Israeli,+ na hizo ndizo zitakazokuwa sehemu zao,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
30 “Hizi ndizo zitakazokuwa njia za kutokea za jiji: Kipimo cha upande wa kaskazini kitakuwa mikono 4,500.+
31 Malango ya jiji yatapewa majina ya makabila ya Israeli. Kati ya malango matatu ya kaskazini, kuna lango moja la Rubeni, moja la Yuda, na moja la Lawi.
32 Upande wa mashariki utakuwa na urefu wa mikono 4,500, na malango matatu: lango moja la Yosefu, lango moja la Benjamini, na lango moja la Dani.
33 Upande wa kusini utakuwa na urefu wa mikono 4,500, nao utakuwa na malango matatu: lango moja la Simeoni, lango moja la Isakari, na lango moja la Zabuloni.
34 Upande wa magharibi utakuwa na urefu wa mikono 4,500, nao utakuwa na malango matatu: lango moja la Gadi, lango moja la Asheri, na lango moja la Naftali.
35 “Urefu kuzunguka jiji lote utakuwa mikono 18,000. Na jina la jiji hilo kuanzia siku hiyo na kuendelea litakuwa, Yehova Yupo Hapo.”+
Maana yake “Mungu Huimarisha.”
Au “na radi.”
Labda yalikutana katikati kwenye mhimili mmoja katika pembe mraba.
Tnn., “roho ya yule kiumbe hai.”
Au labda, “yalinyooka moja kwa moja.”
“Mwana wa binadamu”; maneno haya yanapatikana mara 93 katika Ezekieli na hapa ndipo yanapopatikana kwa mara ya kwanza.
Au “wenye uso mgumu.”
Au labda, “ingawa watu ni wakaidi, nao ni kama vitu vinavyokudunga.”
Tnn., “kula utakachopata.”
Tnn., “wana wa watu wako.”
Au “nitakufanya uwajibike kwa sababu ya damu yake.”
Au “utaiokoa nafsi yako.”
Au “kutenda jambo lisilo la haki.”
Au “nitakufanya uwajibike kwa sababu ya damu yake.”
Au “utaiokoa nafsi yako.”
Tnn., “juu yake,” yaani, upande wa kushoto wa Ezekieli.
Karibu gramu 230. Angalia Nyongeza B14.
Karibu lita 0.6. Angalia Nyongeza B14.
Au “nafsi yangu haijatiwa.”
Au “mbaya.”
Tnn., “nitazivunja fito za mikate.” Labda ni fito zilizotumiwa kuhifadhia mikate.
Au “marinda ya.”
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Tnn., “kuelekea kila upepo.”
Au “nitawapunguza.”
Tnn., “kuelekea kila upepo.”
Tnn., “kwa kuvunja fito zenu za mikate.” Labda ni fito zilizotumiwa kuhifadhia mikate.
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “uliopotoka kimaadili; wa ukahaba.”
Au “yanayofuatilia kwa upotovu wa kimaadili.”
Au “wametoa harufu zinazovutia.”
Au “kukufanya uwajibike.”
Tnn., “utaamka.”
Au labda, “Shada lako la maua limefika.”
Au “kukufanya uwajibike.”
Au labda, “Shada lako la maua limefika.”
Yaani, wale wanaonunua mali na pia wale wanaouza hawatafaidika, kwa maana wote wataangamizwa.
Au labda, “kwa kosa lake.”
Yaani, watajikojolea kwa sababu ya woga.
Tnn., “wamefunikwa na hofu.”
Yaani, vichwa vyao vitanyolewa kwa sababu ya maombolezo.
Au “Nafsi zao hazitashiba.”
Yaani, fedha yao na dhahabu yao.
Yaani, mapambo ya dhahabu na fedha.
Yaani, fedha yao na dhahabu yao waliyotumia kutengeneza sanamu.
Inaonekana ni sehemu ya ndani zaidi ya mahali patakatifu pa Yehova.
Yaani, minyororo ya utekwa.
Au “mafundisho yatatoweka.”
Au “mashauri.”
Au “ukiwa.”
Au “mfano wa.”
Au “mfano huu wa.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “katika vyumba vya ndani vya sanamu yake bora?”
Inaonekana ni tawi lililotumiwa katika ibada ya sanamu.
Au “chombo cha kuwekea wino cha mwandishi.”
Yaani, kila kerubi.
Tnn., “kilikuwa kile kiumbe hai nilichoona.”
Tnn., “roho ya yule kiumbe hai.”
Tnn., “Huyu ndiye kiumbe hai niliyekuwa.”
Au “dhidi ya.”
Yaani, jiji la Yerusalemu, ambamo Wayahudi walidhani watalindwa.
Au “chungu cha kupikia chenye mdomo mpana.”
Au “mambo yanayokuja katika roho yenu.”
Tnn., “moyo mmoja.”
Yaani, moyo ulio mwepesi kutii mwongozo wa Mungu.
Au “ubashiri.”
Tnn., “nyumba ya.”
Au “wanaotabiri kutoka moyoni mwao wenyewe.”
Yaani, wanajenga ukuta wa ndani ulio dhaifu na kujaribu kuufanya uonekane imara kwa chokaa.
Tnn., “nanyi, enyi mawe ya mvua mtanyesha.”
Yaani, tepe za uchawi zinazovaliwa kwenye viwiko au mkononi.
Au “nafsi za.”
Au “nafsi za.”
Au “nafsi zenu.”
Au “nafsi.”
Au “maumivu.”
Au “ubashiri.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Tnn., “nitawakamata watu wa nyumba ya Israeli katika moyo wao.”
Tnn., “Nitaukaza uso wangu dhidi ya.”
Tnn., “kuvunja fito zake za mikate.” Labda ni fito zilizotumiwa kuhifadhia mikate.
Au “wangeokoa nafsi zao.”
Au “na kuwaua watoto.”
Au “matendo yangu manne ya hukumu yanayodhuru.”
Tnn., “Nimeukaza uso wangu dhidi yao.”
Tnn., “nitakapoukaza uso wangu dhidi yao.”
Au “nafsi yako ilichukiwa.”
Au “ngozi ya sili.”
Au “ukastahili cheo cha kifalme.”
Au “Jina lako likaanza.”
Au “mapambo yako maridadi yaliyotengenezwa.”
Yaani, sanamu za kiume.
Au “inayotuliza.”
Tnn., “kuwapitisha.”
Tnn., “kupanua miguu yako.”
Tnn., “majirani wako wenye mwili mkubwa.”
Au “nafsi.”
Tnn., “nchi ya Kanaani.”
Au “Jinsi moyo wako ulivyokuwa dhaifu.” Au labda, “Jinsi nilivyojawa na ghadhabu dhidi yako.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “mapambo yako.”
Tnn., “upande wako wa kushoto.”
Labda ni miji ya jiji hilo.
Tnn., “upande wako wa kulia.”
Au “umeunga mkono.”
Tnn., “nchi ya Kanaani.”
Tnn., “mbegu ya.”
Yaani, Nebukadneza.
Yaani, Sedekia.
Au “nafsi za.”
Tnn., “aliutoa mkono wake.”
Tnn., “kwa kila upepo.”
Au “Uhai wote—ni wangu.” Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “Mtu anayetenda dhambi ndiye atakayekufa.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Tnn., “mtu anayemwaga damu.”
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Au “Mtu anayetenda dhambi ndiye atakayekufa.”
Tnn., “Kosa lolote alilotenda halitakumbukwa.”
Au “kutenda jambo lisilo la haki.”
Au “ataihifadhi nafsi yake.” Angalia Kamusi.
Tnn., “mjitengenezee.”
Au “wimbo wa maombolezo.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au labda, “kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu.”
Au “fimbo zenye nguvu.”
Au “fimbo zake.”
Au “kuwatangazia hukumu.”
Tnn., “niliinua mkono wangu kwa.”
Tnn., “mbegu ya.”
Au “nimeipeleleza.”
Au “pambo la.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Yaani, Waisraeli.
Yaani, Waisraeli.
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Yaani, Waisraeli.
Au “pambo la.”
Tnn., “waliyakataa maamuzi yangu ya hukumu.”
Tnn., “jicho langu liliwasikitikia.”
Tnn., “kuyashika maamuzi yangu ya hukumu.”
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Yaani, Waisraeli.
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Tnn., “macho yao yakafuata.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu.”
Tnn., “walipompitisha.”
Au “inayotuliza.”
Tnn., “mkiwapitisha.”
Au “wanaohudumia; wanaotumikia.”
Tnn., “katika kifungo cha.”
Au “inayotuliza.”
Tnn., “mtazichukia nyuso zenu.”
Au “watu wote wataona.”
Au “methali?”
Au “watu wote.”
Tnn., “kiuno chako kikitetemeka.”
Yaani, watajikojolea kwa sababu ya woga.
Yaani, upanga wa Yehova.
Au “Fimbo ya ufalme haitaendelea.”
Tnn., “mkono uwekwe.”
Au “ubashiri.”
Tnn., “terafimu.”
Au “Ubashiri.”
Au “ubashiri.”
Yaani, wakaaji wa Yerusalemu.
Tnn., “kwa mkono.”
Au “ubashiri.”
Tnn., “juu ya shingo za waliouawa.”
Tnn., “je, utalihukumu, je, utalihukumu.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Tnn., “wanaufunua uchi wa baba yao.”
Au “kutoza riba ya juu sana.”
Tnn., “moyo.”
Au “nafsi.”
Au “ubashiri.”
Maana yake “Hema Lake.”
Maana yake “Hema Langu Limo Ndani Yake.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “kufanya naye uasherati.”
Au “kwa uasherati wao.”
Tnn., “walioitwa.”
Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.
Au “mapambo yako.”
Au “Utajawa na.”
Tnn., “umenitupa nyuma ya mgongo wako.”
Yaani, uzinzi wa kiroho.
Tnn., “wamewapitisha.”
Tnn., “jina la siku.”
Au “istiari.”
Au “chungu cha kupikia chenye mdomo mpana.”
Au “kukipigapiga kifua chako.”
Au “mdomo wako wa juu.”
Tnn., “mkate wa wanadamu.”
Au “kitu ambacho nafsi yenu inakihurumia.”
Au “nafsi zao.”
Au “kambi zao zenye ukuta.”
Au “mteremko.”
Au “pambo la.”
Au “kwa dharau iliyo katika nafsi yao.”
Tnn., “mabinti zake.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Tnn., “watu.”
Au “mtambo wake wa kushambulia.”
Au “panga zake.”
Tnn., “waliouawa.”
Au “majoho yasiyo na mikono.”
Tnn., “watavikwa.”
Au “wimbo wa maombolezo.”
Au “kaburini.”
Au “nitaipamba.”
Au “wimbo wa maombolezo.”
Tnn., “wanaume wazee.”
Au “sufu ya rangi nyekundu na kijivu.”
Mti wa jamii ya mdalasini.
Utete wenye harufu nzuri.
Au “matandiko yaliyotengenezwa kwa vitambaa vilivyofumwa.”
Au labda, “na utukufu.”
Tnn., “Kutaniko lolote lililo.”
Au “kwa uchungu wa nafsi.”
Au “kaburini.”
Au “wimbo wa maombolezo.”
Tnn., “Ulikuwa ukifunga kielelezo kwa muhuri.”
Au “ukosefu wa uadilifu.”
Kuanzia mstari huu, neno “Nile” linarejelea mto huo na mifereji yake ya kumwagilia mimea maji.
Tnn., “utete.”
Tnn., “viuno vyao vipepesuke.”
Tnn., “amesema.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “nitawapa nguvu watu wa nyumba ya Israeli.”
Yaani, Ezekieli.
Au “wote waliotoka katika mataifa mengine.”
Huenda inarejelea Waisraeli walioungana na Misri.
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “Memfisi.”
Au “kiongozi.”
Yaani, Thebesi.
Au “Memfisi.”
Yaani, Heliopolisi.
Au “nitaongeza nguvu za.”
Yaani, mbele ya mfalme wa Babiloni.
Tnn., “wewe ulikuwa.”
Au “kaburini.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “kaburini.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “mkono wake.”
Au “wimbo wa maombolezo.”
Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”
Tnn., “mito yao.”
Tnn., “Nawe utazijaza sakafu za vijito.”
Au “kaburini.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “kaburi.”
Au “kaburini.”
Au “kaburini.”
Tnn., “wake.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Huenda inarejelea mashujaa waliozikwa wakiwa na panga zao, kwa heshima ya kijeshi.
Au “kaburini.”
Au “Viongozi.”
Au “kaburini.”
Tnn., “kumwondoa.”
Au “nafsi yake.”
Au “nitamfanya mlinzi awajibike kwa sababu ya damu ya mtu huyo.”
Au “utaiokoa nafsi yako.”
Au “kutenda jambo lisilo la haki.”
Tnn., “Hakuna dhambi yoyote aliyotenda itakayokumbukwa.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “wanazungumza kwa tamaa sana.”
Au “nitadai kondoo wangu kutoka mikononi mwao.”
Au “wasiwachunge.”
Tnn., “ili wapate jina.”
Tnn., “tumepewa kama chakula.”
Tnn., “waliobaki.”
Au “dharau katika nafsi.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Yaani, moyo ulio mwepesi kutii mwongozo wa Mungu.
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Au labda, “Kama makundi ya kondoo wa dhabihu huko Yerusalemu.”
Au “pumzi; roho.”
Au “roho.”
Au “wanaoshirikiana naye.”
Au “wanaoshirikiana naye.”
Tnn., “wana wa watu wako.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Tnn., “wana.”
Au “mkuu.”
Au “Makao yangu yatakuwa; Nyumba yangu itakuwa.”
Au “juu yao.”
Au “mkuu wa wakuu.”
Au “mkuu wa wakuu.”
Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.
Tnn., “mlinzi.”
Au “Utaitwa.”
Au “eneo lililo wazi la mashambani.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au “Nitamhukumu.”
Au “mkuu wa wakuu.”
Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.
Au labda, “silaha zenye ncha kali zilizovaliwa mkononi.”
Au “Bonde la Umati wa Gogu.”
Maana yake “Umati.”
Tnn., “mkono nilioonyesha.”
Tnn., “nitajitoa kikamili kwa ajili ya jina langu takatifu.”
Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “uweke moyo wako kwa.”
Tnn., “nyumba.” Neno “hekalu” linatumiwa katika sura ya 40-48 wakati ambapo linarejelea majengo ya hekalu au hekalu lenyewe.
Tnn., “utete wa kupimia wa mikono sita, mkono mmoja na kiganja kimoja.” Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Labda inarejelea sehemu ya juu ya ukuta wa chumba cha mlinzi.
Au “nikaona vyumba.”
Tnn., “upana.”
Au labda, “12.”
Tnn., “hekalu.” Katika sura ya 41 na 42, neno hili linamaanisha sehemu ya nje ya mahali patakatifu (Patakatifu) au sehemu yote ya mahali patakatifu (hekalu kutia ndani Patakatifu na Patakatifu Zaidi).
Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Yaani, kwenye sehemu ya ndani ya mahali patakatifu, au Patakatifu Zaidi.
Tnn., “upana wa mlango ulikuwa.”
Inaonekana inarejelea ngazi za duara.
Inaonekana ni njia nyembamba iliyozunguka hekalu.
Au “vile vyumba.”
Yaani, jengo la upande wa magharibi wa mahali patakatifu.
Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”
Tnn., “Mwimo wa mlango.” Inaonekana maneno haya yanarejelea njia ya kuingia Patakatifu.
Inaonekana inarejelea Patakatifu Zaidi.
Tnn., “urefu wake.”
Au “paa dogo.”
Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Au “vile vyumba.”
Kulingana na Septuajinti ya Kigiriki ni “urefu wa mikono 100.” Maandishi ya Kiebrania yanasema hivi: “Njia ya mkono mmoja.” Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “katika upana wa.”
Tnn., “nyumba ya ndani.”
Angalia Nyongeza B14.
Au labda, “alipokuja.”
Tnn., “kwenye ile nyumba.”
Tnn., “kupima kielelezo chake.”
Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Yaani, upana wa kiganja cha mkono kuanzia kidole gumba hadi kidole kidogo, karibu sentimita 22.2 ( inchi 8.75). Angalia Nyongeza B14.
Au “walio kamili.”
Yaani, za watu.
Tnn., “elekeza moyo wako.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “vile vyumba vitakatifu.”
Tnn., “wasije wakawatakasa watu.”
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Au “Sehemu yote iliyo ndani ya mipaka hiyo itakuwa.”
Tnn., “500 kwa 500.”
Au “vyumba 20.”
Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza B14.
Au “mina.” Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza B14.
Angalia Nyongeza B14.
Au “vyumba vitakatifu.”
Tnn., “kuwatakasa watu.”
Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Au “Zote nne na nyua zake za pembeni zilikuwa na ukubwa uleule.”
Au “safu.”
Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Au “jangwa tambarare.”
Au “nafsi zilizo.”
Tnn., “vijito hivyo viwili vitatiririka.”
Yaani, Bahari ya Mediterania.
Tnn., “mtairithi, kila mtu kama ndugu yake.”
Tnn., “inawaangukia.”
Yaani, Bahari ya Chumvi.
Tnn., “upande wa kusini kuelekea kusini.”
Yaani, Korongo la Misri.
Tnn., “upande wa kusini kuelekea kusini.”
Au “njia ya kuingia Hamathi.”
Au “njia ya kuingia Hamathi.”
Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Yaani, Korongo la Misri.
Yaani, Bahari ya Mediterania.